.jpeg)

Ikulu Zanzibar | 23 Machi 2026
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Ndugu David Nchimbi, aliyeambatana na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, CPA Moremi Marwa, pamoja na ujumbe wao, waliofika kujitambulisha.
Rais Dkt. Mwinyi ameahidi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kushirikiana na TTCL katika kuimarisha mawasiliano Zanzibar kupitia huduma mbalimbali zinazotolewa na Shirika hilo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Ndugu David Nchimbi, amemshukuru Rais Dkt. Mwinyi kwa ushirikiano unaoendelea kati ya Shirika hilo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha huduma za mawasiliano nchini.


.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...