Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Sempeo Manongi, amesema wafanyabiashara wana jukumu kubwa katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na ustawi wa Taifa kwa ujumla. Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi ni msingi muhimu wa mafanikio ya kiuchumi.
Manongi ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuboresha sera, sheria na kanuni ili kuweka mazingira wezeshi yatakayowawezesha wafanyabiashara kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi. Amesema mifumo ya ushindani wa kibiashara imeimarishwa ili kuhakikisha hakuna upendeleo unaoweza kudhoofisha soko huria.
“Serikali imeweka mazingira mazuri ya ushindani wa kibiashara na inatambua kuwa uchumi wa nchi unategemea usawa kwa wadau wote,” amesema Manongi. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa wafanyabiashara kuzingatia maadili na taratibu zilizowekwa ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.
Aidha, amewahimiza wafanyabiashara kutumia fursa za mafunzo na semina zinazotolewa mara kwa mara na Serikali ili kuongeza uelewa wao kuhusu masuala ya kisheria, ushindani na haki za kibiashara. Amesema elimu hiyo itawasaidia kufanya maamuzi sahihi yatakayokuza biashara zao kwa muda mrefu.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...