Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amesema Ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya maendeleo ya Afrika  (AfDB), katika miradi ya kimkakati  unaendelea kuimarika jambo linawezesha nchi kukua kiuchumi.

Ameyasema hayo Machi 25, 2026 alipokuwa anapokea nakala za hati za utambulisho za Mwakilishi Mkazi  mpya wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania Bi. Mary Manneko Monyau, katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kombo amesema miradi hiyo imejikita zaidi katika sekta za miundombinu, usafirishaji, na nishati ambazo ni uti wa mgongo wa mabadiliko ya kiuchumi nchini. Ameongeza kuwa kwa sasa Benki hiyo inafadhili miradi 27 ikiwemo  Barabara ya Mzunguko wa Nje ya Dodoma, Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR)  na Mradi wa nyaya za umeme za chini ya bahari unaounganisha visiwa vya Zanzibar, Pemba, na Mafia.

Aidha amempongeza  Bi. Monyau kwa uteuzi wake na kueleza kuwa Serikali ina imani kubwa na uzoefu wake, hususan kutokana na mafanikio aliyoyaonesha alipokuwa Mwakilishi  Mkazi nchini Sudan.

Kwa Upande wake Bi. Monyau amesisitiza kuwa AfDB itajikita zaidi katika kuoanisha mipango yake na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050 ambapo imepania kuongeza upatikanaji wa mitaji na kusaidia miradi inayoinua uhuru wa kifedha wa Tanzania, huku ikizingatia kukuza ajira kwa vijana na miundombinu wezeshi itakayochochea ukuaji wa viwanda na biashara kanda nzima.















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...