Na Mwandishi Wetu

MFUKO wa Maendeleo ya jamii(TASAF)umeunga mkono juhudi za Serikali katika huduma ya afya kwa kutoa msaada muhimu katika Taasisi ya Saratani Ocean Road jijini Dar es Salaam.

Msaada huo umekabidhiwa leo hospitalini hapo na Meneja rasilimali watu wa mfuko huo Mariam Al- Jabiri kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Shedrack Mziray.

Al-Jabiri ambaye ameambatana na baadhi ya wafanyakazi wa Tasaf amesema Serikali imewekeza nguvu kubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini.

“Msaada huu umelenga kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini,”amesema huku akiwatakia uponyaji wa haraka wagonjwa wote wanaopata matibabu katika taasisi hiyo.

Aidha baadhi wa Wafanyakazi hao wa TASAF wakiongozwa na Meneja huyo wamepata nafasi ya kuwajulia hali wagonjwa hospitalini hapo huku wakiwafariji kwa kuwatia moyo na kufanya sala fupi kuwaombea uponyaji wa haraka.

Kwa upande wake Mwakalishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Ocean Road Dk.Diwani Msemo ameushukuru mfuko wa maendeleo ya jamii kwa msaada huo.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...