Ajali imetokea katika Mgodi wa Dhahabu wa Msasa uliopo Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, baada ya sehemu ya eneo la uchimbaji kuporomoka na kufunika madarura manne yenye namba K 46A, 47A, 48A na 49A.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi – Mbogwe, madarura hayo yalikuwa yamefungwa tangu Machi 27, 2026 kwa ajili ya ukarabati, hata hivyo baadhi ya watu waliingia katika eneo hilo bila kufuata taratibu.


Taarifa imeeleza kuwa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha zimechangia kulegea kwa udongo na kusababisha tukio hilo.


Jitihada za uokoaji zilifanyika na hakuna kifo kilichoripotiwa.


Tume ya Madini imewataka wachimbaji na wananchi kuzingatia taratibu za usalama migodini ili kuepusha ajali kama hizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...