Kadiri Watanzania wanavyozidi kuhitaji njia za malipo kidijitali za haraka, salama na rahisi, Benki ya Exim Tanzania imeendelea kuingia katika ubia wa kimkakati wadau mbalimbali ikiwemo The Voice TZ, moja ya maeneo maarufu ya burudani na huduma za chakula, kwa lengo la kurahisisha na kuboresha matumizi ya malipo yasiyotumia fedha taslimu kwa wateja. Huku msimu wa sikukuu ukikaribia, wateja wengi wanatafuta njia za kulipia huduma kwa urahisi, usalama na bila usumbufu wanapofurahia huduma bora za chakula na burudani.

Kupitia ushirikiano huu, wateja wa The Voice TZ sasa wataweza kulipia huduma kwa kutumia kadi za Benki ya Exim au huduma ya Lipa ChapChap, hivyo kuondoa ulazima wa kutumia fedha taslimu, huku wakihakikishiwa miamala ya haraka, salama na yenye uwazi.

Aidha, wateja watakaotumia kadi za Exim watanufaika na punguzo maalum la asilimia 10 kwenye bili zao, hatua inayoongeza thamani ya matumizi yao. Malipo yatathibitishwa papo hapo, na endapo kutatokea hitilafu yoyote, marejesho yatafanyika mara moja. Risiti zitatolewa kupitia ujumbe mfupi wa simu (SMS) au nakala ya karatasi, jambo linaloongeza uaminifu na urahisi kwa wateja.

Akizungumzia ushirikiano huo, Mkuu wa Huduma za Wateja Binafsi wa Benki ya Exim Tanzania, Andrew Lyimo, alisema:

“Huu ushirikiano na The Voice TZ unalenga kurahisisha maisha ya wateja wetu na kuongeza thamani ya huduma wanazopata. Katika kipindi cha sikukuu ambapo sehemu za huduma ya chakula na burudani huwa na wateja wengi, wateja wetu wataweza kufurahia huduma bila usumbufu wa kubeba fedha taslimu au ucheleweshaji wakati wa malipo, huku wakinufaika na faida zaidi wanapotumia kadi za Exim.”

Ili kuhakikisha huduma hizi zinakidhi mahitaji ya wateja, Benki ya Exim imeziweka kwa kuzingatia urahisi wa matumizi, uwazi na uaminifu. Maboresho haya ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa Benki wa kuhamasisha matumizi ya malipo ya kidijitali nchini, kupitia uwekezaji wake katika mifumo ya kidijitali, huduma za kadi na suluhisho la Lipa ChapChap.

Kwa upande wake, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu, alieleza kuwa Benki inaendelea kuweka mteja katikati ya huduma zake:

“Lengo letu kuu ni mteja. Kupitia ushirikiano huu, wateja wataweza kufurahia malipo ya haraka ya ‘tap and go’, marejesho ya papo hapo pale panapotokea hitilafu, pamoja na uwazi wa gharama. Haya yote yanahusu urahisi na kujenga imani katika matumizi ya malipo ya kidijitali, hasa katika vipindi vya msimu wa sikukuu.”

Kupitia ushirikiano huu na The Voice TZ, Benki ya Exim inaunganisha suluhisho zake za kifedha na jukwaa linalokutana moja kwa moja na wateja, kuhakikisha teknolojia inarahisisha uzoefu wa kila siku wa Watanzania.

Naye Mkurugenzi wa Masuala ya Kiufundi wa The Voice TZ, Deogratius Stephen, alizungumzia umuhimu wa ushirikiano huu kwa wateja:

“Benki ya Exim imekuwa mshirika imara kwetu katika nyakati mbalimbali, za mafanikio na changamoto. Leo, tunajivunia kuimarisha zaidi ushirikiano huu kwa kuboresha uzoefu wa wateja wetu. Sasa wanaweza kulipa kwa haraka na kwa usalama, na hivyo kupata muda zaidi wa kufurahia huduma zetu na kusherehekea.”

Mpango huu unatarajiwa si tu kuboresha uzoefu wa wateja katika The Voice TZ, bali pia kuhamasisha matumizi mapana ya suluhisho za malipo ya kidijitali za Benki ya Exim katika maeneo mengine ya huduma na biashara nchini.

Kadri msimu wa sikukuu unavyokaribia, kadi za Benki ya Exim pamoja na huduma ya Lipa ChapChap zinawawezesha Watanzania kufanya malipo kwa urahisi, usalama na bila kubeba fedha taslimu, hivyo kuwapa uhuru zaidi wa kufurahia sherehe zao. Hatua hii inaendana na jitihada za benki kuendelea kuleta suluhisho za kisasa zinazomlenga mteja na kurahisisha huduma za kifedha.










 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...