Katika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kutekeleza mageuzi makubwa ya elimu nchini, timu ya Benki ya Exim ikiongozwa na Afisa Mkuu wa Fedha Bw. Shani Kinswaga pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na wa kati Bw. Andrew Lyimo na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw. Stanley Kafu ilikutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Adolf Mkenda.
Kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma, Aprili 27, 2026 kilikuwa na lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Benki ya Exim katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya elimu, zikiwemo fursa za ufadhili wa wanafunzi wa elimu ya juu hususan wanaosomea sayansi ya data (Data Science), akili unde (Artificial Intelligence) na sayansi shirikishi.
Majadiliano hayo pia yaliangazia fursa mbalimbali ikiwemo fursa za ufadhili unaoweza kutolewa na Benki hiyo, hususani kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaochukua masomo ya sayansi ya elimu ya data na akili.



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...