MKURUGENZI wa Kituo Cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) David Kafulila amesema Muungano wa Tanzania ni wa kipekee barani Afrika kwa kuwa umejengwa juu ya misingi ya watu, na si serikali pekee.

Kupitia ukurasa wake wa X, Kafulila amesema Tanzania inaadhimisha miaka 62 ya Muungano ambao ni wa mataifa mawili huru barani Afrika uliofanikiwa kudumu kwa zaidi ya miongo sita.

Alitolea mifano ya miungano mingine barani Afrika iliyovunjika ndani ya muda mfupi, ikiwemo ule wa Ethiopia na Eritrea (1952-1962), Ghana-Guinea-Mali (1958-1963), na Senegambia (1982-1989).

Siri ya Mafanikio: Udugu na Utamaduni
Kafulila alieleza kuwa tofauti na miungano mingi ya Ulaya kama Umoja wa Ulaya au ya Asia ambayo inategemea zaidi makubaliano ya kiuchumi na kibiashara, Muungano wa Tanzania ulijengwa juu ya misingi imara ya udugu wa damu, lugha ya Kiswahili, na historia ya pamoja ya kijamii.

Jambo hilo, alisema, linaoufanya Muungano wa Tanzania kuwa na umoja wa watu zaidi kuliko umoja wa serikali pekee.

Alimalizia ujumbe wake kwa kusema: Tutazidi kuwakumbuka Nyerere na Karume siku zote kama hii.

Ujumbe huo umechapishwa ikiwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa Aprili 26, 1964.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...