RAIS Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho, yuko Boston, Marekani ambapo anashiriki kutoa mafunzo kwa Mawaziri wakiwemo wa Fedha na wa Mipango kutoka nchi mbalimbali zinazoendelea kupitia Mpango wa Uongozi wa Ngazi ya Mawaziri wa Harvard “Harvard Ministerial Leadership Program” inayoendeshwa na Chuo Kikuu cha Harvard.

Mheshimiwa Rais Mstaafu ni mmoja wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu wanaoshiriki kutoa mafunzo hayo.

Pamoja na Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu, wengine wanaoshiriki kutoa mafunzo hayo ni pamoja na Wakuu wa Taasisi za Kimataifa, Mashirika Binafsi na Wabobezi katika masuala ya sera, uchumi na maendeleo kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Kutoka Tanzania, mafunzo hayo yamehudhuriwa na Mhe. Khamis Mussa Omar, Waziri wa Fedha; Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo, Waziri Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji; na Mhe. Juma Malik Akil, Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...