Kampuni ya mawasiliano ya Halotel Tanzania imezindua rasmi na kwa kishindo ushiriki wake katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu kama SabaSaba, ikiwa na uwepo thabiti unaoambatana na uzoefu wa kipekee wa kidigitali katika banda lake la maonesho.

Ikiwa chini ya kauli mbiu “Teknolojia kutoka Moyoni”, Halotel inaendelea kuonesha dhamira yake ya kuendeleza mageuzi ya kidigitali nchini Tanzania kupitia huduma bunifu za mawasiliano, kidigitali na kifedha zinazolenga kurahisisha maisha ya kila siku na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Wageni wanaotembelea banda la Halotel watapata nafasi ya kujionea suluhisho mbalimbali za kisasa zikiwemo huduma za mtandao wa 5G, huduma ya intaneti ya kasi ya juu ya HaloFibre, suluhisho za kidigitali kwa biashara pamoja na huduma rahisi za kifedha zinazotolewa kupitia HaloPesa.

Kupitia HaloPesa, wateja wanaendelea kufurahia huduma salama, rahisi na zenye ufanisi za kifedha kidigitali zikiwemo kutuma na kupokea fedha, kuweka na kutoa fedha, pamoja na kufanya malipo kwa urahisi, hatua inayochangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha ujumuishaji wa kifedha nchini.

Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya HaloPesa, Halotel imeandaa zawadi maalum, ofa za kipekee na shughuli mbalimbali za kuwashirikisha wateja, zinazolenga kuboresha zaidi uzoefu wa wageni katika kipindi chote cha maonesho.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho katika banda la Halotel, Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara wa Halotel Tanzania, Bw. Abdallah Salum, amesema:

“Saba Saba inatupatia jukwaa muhimu la kuwasiliana moja kwa moja na wateja wetu na kuonesha ubunifu unaoendelea kuboresha maisha yao kupitia teknolojia.”

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Halotel Tanzania, Bi. Tran Thi Thuy Dung, aliendelea kusisitiza dhamira ya kampuni katika ubunifu na maendeleo ya kidigitali akisema:

“Halotel inaendelea kujitolea kuwekeza katika suluhisho bunifu zinazoboresha uzoefu wa wateja na kuharakisha mageuzi ya kidigitali nchini Tanzania. Kupitia maonesho haya, tunawapa wageni nafasi ya kushuhudia kwa vitendo huduma zetu na kuona athari zake halisi katika maisha ya kila siku.”

Kwa upande wa HaloPesa, Meneja wa Masoko, Bi. Aidat Lwiza, alibainisha:

“Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya HaloPesa, tunafuraha kuleta ofa na uzoefu wa kipekee kwa wateja ili kuimarisha zaidi upatikanaji wa huduma za kifedha kidigitali zilizo rahisi na zenye uhakika katika kipindi chote cha maonesho ya SabaSaba.”

Halotel inawaalika wageni wote, wadau na washiriki wa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam kutembelea banda lao na kujionea ubunifu wa huduma pamoja na ofa maalum zitakazopatikana katika kipindi chote cha maonesho kuanzia 28 Juni hadi 13 Julai 2026.
















































Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...