WAKAZI wa kata ya Mvuha na maeneo jirani wameondokana na safari za hadi kilomita 80 kufuata huduma za benki Morogoro mjini, baada ya kuzinduliwa kwa Tawi la NMB Mvuha ambalo sasa limesogeza huduma za kifedha karibu na wananchi.

Tawi hilo, lililojengwa kwa gharama ya Sh milioni 296, linakuwa la 251 katika mtandao wa NMB unaohudumia zaidi ya wateja milioni 10 nchini. Linawahudumia wananchi, wakulima, wafanyabiashara, Serikali na taasisi mbalimbali.

Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango, alisema tawi hilo pia litatoa elimu kuhusu kupanga matumizi, kuweka akiba, kukopa kwa tija na kutumia huduma za kifedha kwa usalama.

Uzinduzi huo uliongozwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, ambaye aliipongeza NMB kwa kuendelea kusogeza huduma za kifedha mijini na vijijini."Endeleeni kuwafikia na kuwahudumia Watanzania popote walipo,”alisema Bw.Michael.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...