DODOMA | 24 Julai 2026

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kutoka Tanzania Makao Makuu ya CCM, Dodoma, na kuwapongeza kwa dhamana ya kuiwakilisha nchi katika chombo hicho cha kikanda.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo Julai 24,2026, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro,amewahimiza kuendelea kutanguliza maslahi ya Taifa na Jumuiya kwa kudumisha mshikamano, kujenga ushirikiano na wabunge kutoka nchi wanachama katika kuimarisha mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao Tanzania inajivunia kuwa moja wa waasisi wake.

Katibu Mkuu amesisitiza kuwa Chama kina matarajio makubwa kwao na kitaendelea kuwapa ushirikiano wanapotekeleza wajibu wao wa kitaifa na kikanda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...