Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji, Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (kulia) na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (kushoto), wakiwa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.
Meneja Masoko wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Caleb Majo (kushoto), akitoa elimu kuhusu huduma zinazotolewa na Vodacom Tanzania wakati wa mahojiano maalumu na Azam Media katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini. Wengine ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Alex Bitekeye (wa pili kushoto), Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (wa pili kulia), na Mtangazaji wa Azam Media, Jafar Mponda (kulia).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi (aliyekaa katikati), Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga (aliyekaa kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE, Latifa Khamis (aliyekaa kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa kampuni mbalimbali, akiwemo Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (aliyevaa tisheti nyekundu), muda mfupi baada ya kufungwa kwa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (SABASABA). Vodacom Tanzania Plc ilitambuliwa kama mshirika muhimu wa maonesho hayo baada ya kupewa tuzo mbili; Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kufanikisha maonesho hayo.
Mkuu wa idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (wa sita kulia), na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (wa sita kushoto) wakiwa katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wengine wa Vodacom wakiwa wa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA) muda mfupi baada ya kufungwa rasmi kwa maonesho hayo. Kwa siku zote 13 za maonesho hayo Vodacom Tanzania ilishiriki fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...