Dar es Salaam

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu mchango wa sayansi ya visukuku mimea (Palynology) katika utafiti wa mafuta na gesi asilia kupitia Banda la TPDC kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).

Mtafiti Mwandamizi wa Visukuku Mimea wa TPDC, Bw. Johanes Kakoki, alisema uchambuzi wa visukuku mimea kama dinoflagellates ( viumbe vidogo sana vya majini aina ya planktoni) , chavua (pollen) na mbeguchembe (spores) husaidia kubaini umri wa miamba na uwezo wake wa kuzalisha na kuhifadhi mafuta au gesi asilia.

Aliongeza kuwa taarifa hizo huunganishwa na tafiti za kijiolojia, kijiofizikia na kijiokemia ili kuongeza usahihi wa kubaini maeneo yenye rasilimali za mafuta na gesi, huku teknolojia za kisasa zikiboresha ufanisi wa tafiti na kupunguza gharama.

Kupitia maonesho hayo, TPDC inaendelea kuelimisha wananchi kuhusu hatua za utafiti wa mafuta na gesi asilia na mchango wa tafiti za kisayansi katika maendeleo ya sekta na uchumi wa Taifa.

#Tunaboreshamaishanakuwezeshamaendeleo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...