Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa Malaigwanani ,wazee na kina mama maarufu wapatao 33 kutoka kata 11 za ndani ya eneo la hifadhi Ngorongoro ili kuwajengea uwezo wa kutambua fursa mpya za kiuchumi.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kamishina Msaidizi Mwandamizi anayeshughulikia huduma za jamii bi Gloria Bideberi amesema lengo la semina hiyo ni kuhakikisha Malaigwanani na wazee hao wanapata elimu ya kutosha kuhusu ujasiriamali na namna ya kutumia fursa zinazopatikana katika maeneo yao.
Bi. Gloria alieleza kwamba elimu hiyo itakwenda sambamba na ziara za kujifunza kwa vitendo, ambapo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ikiwemo kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za maziwa Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga ili kujifunza namna bidhaa zinavyozalishwa, kuendelezwa na kufikishwa katika masoko.
“Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa wananchi hawa wanapata elimu ya kutosha na kuwawezesha kutembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ili kujifunza kwa vitendo zaidi,” alisema Gloria
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika maendeleo endelevu ya eneo la Hifadhi Ngorongoro.




.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...