Na Mwandishi Wetu, Morogoro

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu imezindua mfumo mpya wa kisasa wa ramani ya maeneo hatarishi, Tanzania Climate Vulnerability System (TVCVS), unaolenga kubaini mapema maeneo yanayokumbwa na majanga na kusaidia kupunguza athari kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akifungua mafunzo ya mfumo huo tarehe 16 Juni, 2025 katika ukumbi wa Kings Way Hotel, Morogoro, Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Brig. Jen. Hosea Ndagala, alisema mfumo huo utasaidia kufuatilia kwa karibu mabadiliko ya hali ya hewa na kutoa taarifa kwa wakati kwa sekta mbalimbali zilizo hatarini.

Mfumo huo unasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini -TMA, na taasisi nyingine, ukifadhiliwa na IMF na kuendelezwa na Global Center on Adaptation kwa usaidizi wa Masae Analytics.

“Mfumo huu ni sehemu ya juhudi za kitaifa na kimataifa za tahadhari ya mapema. Utasaidia kulinda maisha, mali, na kusaidia mipango bora ya maendeleo,” alisema Brig. Jen. Ndagala.

Washiriki kutoka sekta mbalimbali wamehimizwa kutumia mafunzo hayo kwa vitendo katika kupanga na kutekeleza miradi yao kwa kuzingatia athari za mabadiliko ya tabianchi.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 16.06.2025 amezindua jengo la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Simiyu na kuwataka Watanzania kujenga utamaduni wa kulipa Kodi kwa hiari ili kuiwezesha Nchi kujitegemea kiuchumi.

Rais Samia amesema kujitegemea kiuchumi kunaletwa na Wananchi kupitia Kodi wanazolipa na kuitaka TRA kuendelea kukusanya Kodi kwa njia rafiki kwa wananchi na kuwapatia elimu ya Kodi wananchi ambao hawana uelewa wa masuala ya Kodi.

Amesema kutegemea msaada ni utumwa hivyo TRA kupitia Kodi zinazokusanywa zimekuwa zikitekeleza miradi ya kijamii kama vile kupeleka Maji, Umeme na Huduma za Afya nchi nzima na katika miradi mikubwa ndiyo nchi imekuwa ikikopa au kupata msaada wa kutekeleza.

"Tunataka TRA ikusanye zaidi ndiyo maana tumewaongezea nguvu Kazi na majengo ya kisasa, nendeni mkakusanye kodi kwa njia rafiki, lakini kwa wale masugu na viburi lazima nao wafanywe walipe Kodi kama ilivyo kwa wengine" amesema Rais Samia.

Aidha Rais Samia ameagiza kuongezwa kwa kasi ya ujenzi wa majengo ya TRA ambayo bado hayajakamilika ili yaanze kutoa huduma katika mazingira rafiki.

Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Yusuph Juma Mwenda amesema jengo hilo limegharimu kiasi cha Sh. Bilioni 9.83 na ni miongoni mwa majengo mengine yanayojengwa nchi nzima kwa gharama ya Sh. Bilioni 116.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema jengo hilo na mengine yanayoendelea kujengwa nchini yataongeza utoaji huduma bora kwa Mlipakodi, yataongeza hamasa kwa Watumishi pia yataongeza makusanyo ya Kodi kwa ujumla.

"Mhe. Rais tunashukuru kwa kutupatia fedha za ujenzi wa majengo yote yaliyokamilika na yanayoendelea kujengwa hii itasaidia tuendelee kukusanya Kodi na kuvuka malengo kama ilivyokuwa kwa miezi 11 mfululizo tangu kuanza mwaka wa fedha 2024/2025 pia tunashukuru umetuongezea nguvu Kazi ya Watumishi wapya 1896" Kamishna Mkuu Mwenda amesema.

Kamishna Mkuu Mwenda amesema katika kipindi cha miezi 11 TRA ilitakiwa kukusanya Sh. Trilioni 27.841 lakini imekusanya Sh. Trilioni 28.861 sawa na ufanisi wa asilimia 105 na anatarajia mwezi uliosalia wa June watavuka malengo.






Na Mwandishi Wetu

ZAIDI ya wanafunzi 200 wanatarajiwa kusafiri kwenda masomoni kwenye mataifa mbalimbali kwa mwaka wa masomo wa 2025/2026 hivi karibuni kuanza pitia uratibu wa Global Education Link (GEL).

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa GEL, Abdulmalick Mollel, wakati wa kikao baina ya wanafunzi hao na wazazi wao kuhusu kukamilisha taratibu za safari.

Wanafunzi hao wanatarajiwa kusafiri kwenda masomoni kwa nchi za Uingereza, Canada, Marekani Malaysia, Poland, Uturuki na India.

Kikao hicho kilifanyika ofisini hapo ambacho kililenga kuwaelimisha wanafunzi hao taratibu na kanuni wanazotakiwa kufuata wanapokuwa masomoni nje ya nchi zikiwemo mila, tamaduni na desturi za nchi wanazotarajia kwenda.

“Ni jukumu la GEL kuhakikisha maandalizi yote ya visa na nyaraka zingine zimekamilika na kuhakikisha wanafunzi ambao wameniamini na wazazi wao kuwaelekeza vizuri na jukumu la mwanafunzi ni kusema kozi anayokwenda kusoma,” alisema

“Mwanafunzi atasema anataka kozi gani anataka kusoma nchi gani na atasema anataka kukaa kwenye chumba cha aina gani na mzazi anatakiwa kujiridhisha na kozi na nchi anayokwenda kusoma,” alisema Mollel

“Mzazi unatakiwa kuwa makini sana kuchagua nchi ambayo mtoto wako anakwenda kusoma kwasababu lazima uzingatie uwezo wako wa kiuchumi ili usipeleka mtoto wako halafu mambo yakawa magumu huko mbeleni,” alisema

Mollel alisema kikao kama hicho cha wazazi na wanafunzi kimekuwa kikichambua mila na tamaduni ambazo mwanafunzi anapaswa kuzingatia kulingana na nchi anayotarajia kwenda kusoma ili asikutane na vikwazo anapokuwa nchini humo.

Mollel alisema ni muhimu wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi kujua kupika wenyewe ili kurahisisha maisha ya kukaa nje ya nchi kwani vyuakula vya kununua wakati mwingine ni gharama kubwa.

“Awe mvulana au msichana anapaswa kujua kupika kwasababu huwezi kuwa unakula hotelini kila siku gharama za maisha zitakuwa juu kwa hiyo kama unaishi na rafiki zao mnapangiana zamu za kupika na maisha yanakuwa nafuu kidogo,” alisema Mollel

Kadhalika, Mollel alisema GEL imekuwa ikifuatilia kwa karibu mwenendo wa kitaaluma na tabia kwa wanafunzi wote wanaosafiri kupitia taasisi yake ili kuhakikisha wanahitimu wakiwa na alama nzuri.

Alisema mbali na kufuatilia maendeleo ya taaluma, GEL imekuwa ikifuatilia usalama wa wanafunzi hao nje ya nchi na hata ilivyotokea vita baina ya Urusi na Ukraine GEL ilisimama imara na wanafunzi wote waliokuwa Ukraine walirudi salama nchini.

Mollel alisema ni muhimu kwa wazazi nao kufuatilia kwa karibu maendeleo ya tabia na taaluma ya watoto wao kwani wasipofanya hivyo baadhi wanaweza kudanganya na mwisho wa siku wanashindwa kuhitimu masomo yao.

“Mwanafunzi unapaswa kufuata kile kilichokupeleka kule, umeenda kusoma basi wewe kazi yako ni kusoma achana na starehe na mambo yasiyokuwa ya kitaaluma kwasababu mzazi anajinyima vitu vingi ili wewe usome sasa usipohitimu unamtesa sana mzazi,” alisema

Mmoja wa wazazi walioshiriki kikao hicho, Deogratius Uiso alisema amefurahishwa na maelezo yaliyotolewa na GEL kuhusu fursa za masomo kwenye mataifa mbalimbali duniani na mila na tamaduni.

“Sisi wazazi vikao kama hivi vinatusaidia sana kupata mwanga wa mtoto anapokwenda mfano tumeambiwa kuwa anaweza kukutana na changamoto ya mila na tamaduni ambazo anapaswa kuendana nazo ili kuishi vizuri,” alisema









Na John Mapepele -OR TAMISEMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi nchini kuwaachia watoto wa kike kusoma shule maalum za msingi na sekondari ambazo zimejengwa na Serikali.

Mhe. Rais ametoa kauli hiyo leo, Juni 16, 2025 Mkoani Simiyu alipozindua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Simiyu iliyogharimu takribani bilioni 4.5 ambapo amesema Serikali imejenga shule za aina kila mkoa ili kuwasaidia watoto wa kike.
Amesema Serikali imeamua kujenga shule hizo maalum za sayansi kwa watoto wa kike kwa kuwa walikuwa nyuma katika mkondo wa sayansi.

" Shule hizi zimekuja kama maalum kwa watoto wetu wa kike ili waweze kupata fursa ya kusoma masomo ya Sayansi na kuendelea na masomo ya juu". Amefafanua Mhe. Samia

Mhe Rais amesema katika kuboresha elimu nchini imejenga miundombinu muhimu kama mabweni, madarasa, maabala, nyumba za walimu, viwanja vya michezo na majiko ya kisasa yasiyotumia kuni.


Aidha, amesema pia Serikali inajenga shule maalum kwa watoto wa kiume katika mikoa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Simiyu ambapo amesisitiza kuwa watoto wengine ambao hawatapata fursa ya kuendelea na elimu ya juu wataweza kujiunga na VETA.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amemshukuru Mhe Rais kwa maono yake ya uwekezaji mkubwa katika elimu, afya, miundombinu, na utawala bora hapa nchini.

Mhe. Mchengerwa pia amemshukuru Mhe Rais kwa kuzindua Ofisi ya kisasa ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Ofisi ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi hii leo kabla ya kuzindua shule hiyo.



Amesema zaidi ya bilioni 90 zimetumika kwa ajili ya kujenga Ofisi za Wakuu wa Mikoa 26 hapa nchini.

Mhe. Rais Samia yupo Mkoani Simiyu kwa ziara ya kikazi mbali na kuzindua miradi chini ya Wizara ya TAMISEMI pia amezindua miradi kadhaa ya maendeleo.






Na MWANDISHI WETU- CHALINZE

SERIKALI imesisitiza kuwa imejipanga kuhakikisha kuwa wafugaji nchini wanakuwa na uwezo wa kufanya ufugaji wa kisasa wenye tija zaidi na kuachana na mbinu duni kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa mifugo kutoka ndani na nje ya nchi.

Hayo yasemwa jana Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti, wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Tatu ya Mifugo ya Nchi Tatu 2025 yaliyofanyika katika Kijiji cha Ubena Zomozi, Halmashauri ya Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, ambapo maonesho hayo yamefadhiliwa na Benki ya NMB na kuandaliwa na Kampuni ya Mbogo Ranches, chini ya kaulimbiu: “Kujenga Ushirikiano, Kukuza Kilimo”.

Maonesho hayo yalihudhuriwa na wafugaji kutoka nchi tatu ambazo ni Tanzania, Kenya na Namibia, pamoja na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Isaac Njenga na Kamishna Mkuu wa Namibia, Lebbius Thobias pamoja na waonyeshaji wa vifaa na bidhaa mbalimbali za kilimo kutoka kampuni mbalimbali.

“Asilimia takribani 97 ya ng’ombe nchini ni wa asili, ambao hutoa wastani wa kilo 80 hadi 120 za nyama kwa ng’ombe mmoja, na maziwa ni kati ya lita moja hadi tatu kwa siku kwa kila ng’ombe. Aina hii ya uzalishaji haina tija, ndiyo maana Serikali inashirikiana na wadau mbalimbali kuleta mapinduzi katika sekta hii,” alisema Mnyeti.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya ya Biashara Benki ya NMB, Msolo Mlozi alisema kuwa hadi sasa benki hiyo imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa wafugaji nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo kunenepesha mifugo, kununua chakula bora cha mifugo, kununua aina bora za mifugo na kujenga miundombinu bora ili kuongeza uzalishaji.

“Benki yetu inafahamu changamoto zinazowakumba wafugaji kama vile uhaba wa chakula na maji hasa wakati wa kiangazi, magonjwa ya mifugo, uzalishaji mdogo kutoka kwa mifugo wa asili, na ukosefu wa makazi ya kudumu kwa wafugaji. Kupitia mikopo tunayotoa, wafugaji wanaweza kukuza au kununua chakula cha mifugo, kuchimba visima vya kudumu na kutatua tatizo la ukosefu wa maji, pia kuhudhuria mafunzo mbalimbali ya kuongeza maarifa,” alisema Mlozi

Naye Mkurugenzi wa Mbogo Ranches, Naweed Mulla alisema kuwa maonesho haya yameandaliwa kwa lengo la kuwawezesha wafugaji wa ndani kujifunza mbinu za kisasa kutoka kwa wenzao wa nchi jirani pamoja na kupata fursa ya kununua mifugo bora ya ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku ili kuongeza uzalishaji.

“Tukio hili ni fursa nzuri kwa wafugaji wetu kupata maarifa ya ufugaji wa kisasa na kuyatekeleza. Pia ni jukwaa nzuri kwa washiriki wa nchi zote tatu kuungana na kuendeleza mawasiliano,” alisema.

Kwa nyakati tofauti, Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Isaac Njenga na Kamishna Mkuu wa Namibia, Lebbius Thobias, walisisitiza umuhimu wa nchi hizo tatu kuongeza ushirikiano katika sekta ya mifugo ambayo walisema inatoa fursa nyingi za kiuchumi kwa watu binafsi na kwa taifa kwa ujumla.

“Wakati Rais wetu Dk. Netumbo Nandi Ndaitwah, alipotembelea nchi hii mwezi uliopita, alifanya mazungumzo na Rais Samia Suluhu Hassan, na moja ya mambo waliyoyajadili ni kukuza sekta ya mifugo. Tukio hili ni ishara tosha kuwa sekta ya mifugo inatambuliwa kwa mchango wake muhimu katika maisha yetu ya kila siku,” alisema.

Taiko Tarongei, mfugaji kutoka Ubena, Halmashauri ya Chalinze, alisema kuwa kupitia maonesho hayo amejifunza umuhimu wa kutumia mbinu za kisasa za ufugaji na ameahidi kuzitumia ili kuongeza tija.












Na MWANDISHI WETU

DIWANI wa Kata ya Marumbo, Kisarawe, mkoani Pwani, Msafiri Mpendu, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuifungua kata hiyo  kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kipindi cha miaka mitano.

Ameyasema hayo alipowasilisha  taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Kata ya hiyo kwa mwaka wa fedha 2020 -2025 .

Diwani Mpendu, amesema   zaidi ya sh. milioni 227 zimepelekwa katika sekta ya afya kwenye miradi ya ujenzi wa zahanati, nyumba za watumishi na usambazaji wa mifumo ya maji.

Ameeleza, a katika  sekta ya elimu sh. milioni 239 zilipokelewa na kuelekezwa fedha  katika maendeleo ya miundombinu ya elimu  kama ujenzi wa madarasa, vyoo,majiko  na  ugawaji magodoro kwa wanafunzi.

Akizungumzia  sekta ya maji katika kata hiyo, Mpendu amesema wananchi wamenufaika na uchimbaji wa visima 16 vilivyochimbwa kimkakati.

 “Lengo ni  kuhakikisha visima hivi  vinahudumia idadi kubwa ya watu katika vijiji vyote vya kata hii ya Marumbo, kazi iliyofanywa na serikali pamoja na wadau,”amesema.

Kuhusu miundombinu ya  barabara, Mpendu, amebainisha ibainisha  uboreshaji huo umechochea  kiuchumi na kurahisisha upatikanajiwa huduma za kijamii.

Ameushukuru  Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA)  kuhakikisha barabara muhimu zinapitika kwa urahisi katika misimu yote ya mwaka. 

Kuhusu huduma za kijamii Diwani  Mpendu, amesema hatua zinaendelea kuchukuliwa katika  mpango wa  kuimarisha lishe ambapo  katika kipindi cha miaka mitano  jumla ya ng'ombe 1400 walichinjwa.

“Tuligawa nyama kwa wananchi. Pia tuligawa vyakula mbalimbali katika  familia zenye mahitaji maalumu  kusaidia lishe  hasa kwa watoto,”amesema.

Amesema uwezeshaji huo ulifanywa ni diwani kwa kushirikiana na wafadhili.. 

Mpendu alisema  katika kuinua wanawake,vijana na watu wenye ulemavu  kiuchumi, serikali  chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  ilitoa  kiasi cha sh. milioni 25 ambapo  vikundi vinne katika kata hiyo vimepata  mikopo  ya kuanzisha na kukuza biashara. 

“Kero ya mawasiliano katika kata hii imepatiwa ufumbuzi kwa  kuwekwa minara miwili ya kampuni za simu hali  iliyorahisisha mawasiliano na kufungua fursa ya kukuza uchumi, kurahisisha huduma za kutuma na kupokea fedha tofauti na awali,”ameeleza  Diwani Mpendu.





MJUMBE wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) ya CCM, Ramadhan Mlao, amewataka vijana kujitokeza kuommba ridhaa ya kugombea nafasi mbalimbaliza uongozi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Amesema vijana hawatakiwi kuwa ‘wabena mabegi’ ya wagombea badala yake washiriki kikamilifu katika uchaguzi huo kuwani nafasi za uongozi.

Mlao,aliyasema hayo, Dar es Salaam, alipofungua mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ilala.

“Tunaanza uchaghuzi wa ndani kabla ya kufanya uchaguzi wa nje. Uchaguzi wa ndani kila mwanachama wa CCM anayo haki ya kuchukua fomu na kuomba ridhaa kugombea,”amesema Mlao.

Amewaomba vijana wenye nia na dhamira ya kuomba nafasi kujitokeze kuomba nafasi hizo.

“Chama hiki kiliasisiwa na Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume wakiwa vijana wachanga kabisa.Walipabana kwa dhati wakakijenga. Vijana hatuna namna ya kukaa kando na nafasi hizi zinazo tangazwa,”alieleza.

Amesema, haipendezi vijana kusalia kuwa wapambe wa wagombea na kuwabebea mabegi watia nia.

Aidha aliitaka UVCCM kuwa makini na wana chama watakao jitokeza kuomba ridhaa ya kuombea.

“Watakao chukua fomu kuomba ridhaa ni watu tunaoshi nao katika mitaa yetu.Tunajua tabia zao, mienendo yao na hurka zao. Tusikubali kuingia katika mtego kuchagua mtu ambaye tunapenbdezwa naye sisi tu ikiwa jamii haipendezwi naye,”ameeleza Mlao.

Amebainisha, kura katika uchaguzi wanje hazitapigwa na wana CCM tu bali hata wasio wanachama wa CCM, hivyo ni muhimu kusimamisha mgombea ambaye atakubalika na wote.

“Pia tusisimamishe wagombea ambao tutapata kazi kubwa ya kuwapamba na kuwa nadi.CCM inauzika . Tusipeleke wagombea wasio uzika wakakipa taabu Chama katika kuwa nad,”amesema.

Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Ilala, Juma Mizingu, alieleza, lengo la mafunzo hayo ni kuwandaa vijana kuelekea uchaguzi mkuu.

“Ifikapo Oktoba mwaka huu vijana tunahakikisha Rais Dk. Samia, anapata kura za kishindo. Tunaendelea kujipanga kuhakikisha pia CCM inapata ushindi katika kata zote 36 za Wilaya ya Ilala na majimbo yote matatu,”amesema Mizungu.

Amesema, UVVCM Wilaya ya Ilala inampongeza Rais Dk. Samia, kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani humo ambao ni utekelezaji wa Ilani ya CCM.

“Tumeshuhudia Rais Dk. Samia, akielekeza fedha nyingi katika miradi ya maendeleo. Tunamhakikishia vijana Wilaya ya Ilala tutampa kura za kishindo na tuko tayari kupambania ushindi huu,”ameeleza.




Songea-Ruvuma.

Katika kuadhimisha wiki ya usalama wa miundombinu ya TANESCO, Afisa Usalama Mkuu Msaidizi kutoka Kitengo cha Uzuiaji Makao Makuu ya TANESCO, Shami Yusuph Dunia, ametoa wito kwa wafanyakazi na jamii kushirikiana kwa karibu kuhakikisha ulinzi wa miundombinu ya shirika hilo.

Akizungumza na wafanyakazi wa TANESCO mkoani Ruvuma leo Juni 16, 2025, Dunia amesema kuwa jukumu la kulinda miundombinu ya shirika si la idara ya usalama peke yake, bali linamhusu kila mfanyakazi na mwananchi. Amefafanua kuwa kazi ya usalama ni pamoja na kuzuia na kuchunguza matukio ya uharibifu au wizi wa vifaa vya shirika, hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za umeme kwa ufanisi.

Ameeleza kuwa kwa kuwa TANESCO ni shirika lenye mtandao mpana wa kitaifa, ni vigumu kwa idara ya usalama pekee kukabiliana na vitendo vyote vya kihalifu, hivyo ni muhimu kila mfanyakazi kuhakikisha miundombinu kama njia za kusafirisha umeme, mabwawa, mita, magari ya shirika, na vifaa vingine inalindwa muda wote.

Dunia amesisitiza kuwa jamii nayo ina nafasi muhimu katika mapambano dhidi ya uharibifu wa miundombinu, hasa wakati huu ambapo vitendo vya uharibifu na wizi wa vifaa vya umeme vinaongezeka, ameitaka jamii kuwa walinzi wa mali za umma kwa kutoa taarifa pindi wanaposhuhudia au kupata taarifa za uhalifu.

Aidha, amewatahadharisha wafanyakazi kuhusu kuongezeka kwa matapeli wanaowalaghai wateja kwa kutumia jina la TANESCO, ametoa wito kwa wafanyakazi kuwa walinzi wa wateja kwa kuhakikisha hakuna mtu asiyehusika anayewafikia kabla ya maafisa halali wa shirika, huku akihimiza utoaji wa taarifa haraka kwa uongozi pale vitendo hivyo vinapogundulika.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma, Alan Njiro, amewakumbusha wafanyakazi ngazi ya jamii kutumia elimu waliyopatiwa kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi, amesema watumishi hao ndio wanaokutana na wananchi mara kwa mara, hivyo wana nafasi ya kipekee katika kuwaelimisha kuhusu ulinzi wa miundombinu ya umeme.

Mafanikio ya TANESCO kama mtoa huduma wa umeme nchini yanategemea kwa kiwango kikubwa uimara na usalama wa miundombinu yake. Ushirikiano wa karibu kati ya wafanyakazi, wananchi na uongozi wa shirika ni silaha muhimu katika kuhakikisha miundombinu inalindwa dhidi ya uharibifu na wizi, Kwa pamoja kupitia uzalendo na uwajibikaji, TANESCO inaweza kuimarisha utoaji wa huduma bora na endelevu kwa Watanzania wote.







Denis Mguye, Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Arusha na Mratibu wa Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (ECD), ameona mabadiliko makubwa yakichukua nafasi—mabadiliko yanayobadilisha familia na mustakabali wa jamii katika Mkoa wa Arusha.

“Wanaume sasa wanasimama bega kwa bega na wake zao kliniki—jambo ambalo halikuwazwa kutokea hata miaka michache iliyopita,” anasema.

Ni nini kimechochea mabadiliko haya? Mzazi Hodari, mpango wa miaka miwili wa kipekee unaomaanisha "mzazi bingwa", umewezesha serikali za mitaa, watoa huduma za afya na familia kufafanua upya malezi yenye uwajibikaji, wakigeuza maono kuwa vitendo.

Kwa mara ya kwanza, baadhi ya mamlaka za serikali za mitaa katika Mkoa wa Arusha zinaandaa kujumuisha mikakati ya malezi ya awali ya watoto katika bajeti zao rasmi kuanzia mwaka ujao wa fedha.

Hii ni zaidi ya mabadiliko ya sera—ni ishara ya kujitolea kwa kina.

“Hii si tu kufuata maelekezo,” anasema Mguye. “Ni kutambua kuwa malezi na maendeleo ya mtoto ni kiini cha ustawi wa mkoa.”

Mtazamo huu mpya wa mkoa unalingana na kanuni za Mwongozo wa Uendeshaji na Uwasilishaji wa Mipango ya Ustawi wa Jamii katika Halmashauri (CCSWOPG) uliozinduliwa mwaka 2022, wenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya serikali, wadau, na jamii katika maeneo muhimu ya ustawi wa kijamii, ikiwemo ECD.

Wakati mipango ya awali kama Malezi III iliweka misingi muhimu, timu ya ECD ya Arusha ilitambua kuwa uhamasishaji wa vitendo unaotoka kwa jamii wenyewe ulikuwa muhimu.

Hapo ndipo Mzazi Hodari ulipojitokeza kuwa tofauti. Kupitia mfano wa mtu kwa mtu, ujumbe wa karibu na rasilimali zinazoeleweka, uliwagusa wanajamii moja kwa moja.

“Tumeona kwa macho yetu jinsi mbinu hii inavyowapa wazazi uwezo wa kuleta mabadiliko wao wenyewe,” anasema Mguye. “Sio wataalamu tu wanaozungumza—ni majirani, marafiki na wenzao wakisaidiana.”

Violet Chahe, Mratibu Msaidizi wa Afya ya Uzazi na Mtoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, anasimulia mabadiliko ya mtazamo.

“Sasa tunawaona baba, waliokuwa wamefungwa na mila, si tu kuhudhuria kliniki na wake zao bali pia kucheza na watoto na kushiriki katika malezi nyumbani. Mabadiliko haya, yaliyochochewa na Mzazi Hodari, yanaimarisha familia na kutuhamasisha kupanua afua wilaya nzima.”

Moja ya matokeo yasiyotarajiwa? Waandishi wa habari kuwa mabalozi wa malezi. Kilichoanza kama vipindi vya redio kwenye kituo kimoja kimekua hadi kuwa harakati; sasa vikifikia vituo sita vya redio za jamii, ambapo waandishi wa habari wanaongoza mijadala ya malezi, wakialika wataalamu na kuunda mwelekeo wa mjadala wa umma.

Wengi wameenda zaidi ya kuripoti—wamekuwa mabingwa wa malezi bora wao wenyewe. Mguye anasimulia hadithi za baba waliovutiwa na matangazo haya au kushawishiwa na wake zao kuanza kushiriki. Hata katika maeneo ambayo Mzazi Hodari haujafika rasmi, athari zake zinaonekana zikithibitisha jinsi mazungumzo halisi ya kijamii yanavyosambaa kwa mbali.

Harakati hii imeleta mabadiliko hadi ngazi ya uongozi wa mkoa, ikiathiri sera, vipaumbele, na mtazamo wa jamii kuhusu malezi.

Timu maalum ya mabingwa wa ECD imeibuka katika Sekretarieti ya Mkoa wa Arusha. Baadhi wanatumia maarifa hayo majumbani kwao, na wengine wanaomba vipindi vya malezi kwenye kata wanazozisimamia.

“Ni ule uhalisia wa mbinu ndio unaifanya iwe na nguvu,” anasema Mguye. “Imetengenezwa kwa kuzingatia jamii zetu—ni ya vitendo, yenye heshima, na rahisi kuitumia.”

Zaidi ya vikao rasmi, mazungumzo yanabadilika hata katika maeneo ya kawaida. Makundi ya WhatsApp,yaliyokuwa yakijaa gumzo za kila siku kati ya waendesha bodaboda, wauzaji madukani na wakulima sasa yana mijadala ya lishe, usalama wa watoto, na msaada wa kihisia, yakibadilisha mazungumzo ya kawaida kuwa fursa za kujifunza na kuleta mabadiliko.

Mguye anazungumzia Kinara mmoja wa kiume kutoka jamii ya kimila ambaye awali alichekwa kwa kushiriki katika malezi:

“Watu walimcheka,” anasema Mguye. “Lakini walipoona mabadiliko halisi—watoto wenye afya bora, migogoro michache—walimpa heshima. Leo hii, ni sauti inayoaminika katika jamii yake.”

Kliniki za maeneo mbalimbali nazo zimeona athari.

Familia zinakuja pamoja, wanauliza maswali zaidi, na hufuata maendeleo ya watoto wao kwa karibu. Viashiria vya maendeleo ya awali ya mtoto kwenye kadi za afya vinafikiwa kwa kiwango cha juu zaidi. Wazo kwamba malezi ni jukumu la pamoja halijajulikana tu—limekubalika.

“Mzazi Hodari imeleta mazungumzo kuhusu malezi na mshikamano katika maeneo ambapo hayakuwepo,” anasema Mguye. “Umefanya watu waamini kuwa wanaweza kufanya mambo kwa njia tofauti—na bora zaidi.”

Akielezea mafanikio haya, Mguye anaona taswira ya siku zijazo ambapo mikutano ya robo mwaka italeta pamoja vinara ili kuchambua takwimu, kushiriki hadithi kutoka mashinani, na kupanua mbinu bora katika mkoa wote. Pia anaona fursa za ubunifu katika uhamasishaji, kama vile michezo ya soka ya jamii yenye maudhui ya malezi na maendeleo ya awali ya watoto.

“Hizi ni dalili za mwanzo tu,” anasema. “Lakini kizazi kijacho kitaona matokeo halisi—vijana watakaokua wakiwa na misingi imara, familia zenye afya, na hali ya kujiamini. Hicho ndicho kizazi tunachokilea.”
Dar es Salaam, 14 June 2025 — Standard Chartered Bank Tanzania, in partnership with Nipe Fagio, successfully conducted its annual employee volunteering beach clean-up on Saturday, 14 June 2025, at Rungwe Beach in Dar es Salaam. The event, which drew the participation of over 70 bank staff and their family members, was held in honour of World Environment Day and as part of the Bank’s broader sustainability agenda.

The beach clean-up is a flagship environmental volunteering initiative by Standard Chartered Bank Tanzania, carried out annually for the past several years in collaboration with Nipe Fagio. Each year, the Bank selects a different beach to clean, reaffirming its commitment to promoting environmental stewardship and community engagement.

The event aligns with Standard Chartered Group’s sustainability agenda, which is centred around three pillars: Sustainable Finance , Responsible Company , and Inclusive Communities . Locally, the beach clean-up is part of the Bank’s “Here for Good” brand promise, aiming to reduce environmental impact, raise awareness on plastic pollution, and empower communities to act in preserving natural ecosystems.

Over the past years, Standard Chartered Bank Tanzania has consistently championed sustainability through various initiatives, including transitioning to energy-efficient office solutions, implementing waste reduction strategies, and supporting financial inclusion projects that uplift communities. The Bank has also invested in staff engagement programmes that promote climate awareness and responsible living.

This year’s clean-up at Rungwe Beach resulted in the removal of significant plastic and non-biodegradable waste. Colleagues collected close to 100 bags of waste, amounting to approximately 1 tonne of waste removed from Rungwe Beach shoreline, contributing to the health of Dar es Salaam’s coastal ecosystem, and reinforcing the Bank’s commitment to environmental preservation. This figure, while a notable achievement, also serves as a stark reminder of the urgent and ongoing need for sustained action.

Standard Chartered Bank Tanzania remains dedicated to being a force for good, embedding sustainability into its core operations, and supporting the United Nations Sustainable Development Goals (SDGs), particularly SDG 13 (Climate Action), SDG 14 (Life Below Water), and SDG 17 (Partnerships for the Goals)


Dar es Salaam, Juni 16, 2025 — Kampuni ya Multichoice Tanzania, kupitia huduma yake ya DStv, imethibitisha dhamira yake ya kuendelea kuwa karibu na wateja wake kwa kuzindua kampeni mpya inayojulikana kama "Onja Utamu wa Mitanange", ikilenga kuwawezesha wateja kushuhudia michuano mikubwa ya FIFA kwa bei nafuu.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Masoko wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo, amesema kampeni hiyo inalenga kutoa fursa kwa kila Mtanzania, hasa wapenzi wa michezo, kupata uhondo wa michuano hiyo mikubwa duniani LIVE, kupitia kifurushi cha bei ya chini kabisa cha POA.

“Tunatambua umuhimu wa burudani ya michezo kwa wateja wetu. Kupitia kampeni ya 'Onja Utamu', sasa mteja yeyote akilipia kuanzia kifurushi cha POA, atapata nafasi ya kujionea mechi zote za michuano ya FIFA moja kwa moja, bila kulazimika kubadilisha kifurushi,” amesema Shelukindo.

Ameongeza kuwa lengo kuu ni kuhakikisha hakuna Mtanzania anayekosa kushuhudia burudani hiyo ya kipekee, huku akisisitiza kuwa Multichoice Tanzania itaendelea kuwekeza katika kuhakikisha huduma bora na zenye thamani kwa wateja wake zinapatikana kwa kila mtu — bila kujali uwezo wa kifedha.

Kampeni ya “Onja Utamu wa Mitanange” inakuja wakati ambapo mashabiki wa soka duniani kote wakiwa na hamasa kubwa kuelekea michuano hiyo mikubwa ya FIFA, na hivyo kuwa fursa adhimu kwa familia, marafiki na majirani kukusanyika pamoja na kufurahia burudani kupitia DStv.







Top News