balozi wetu wa kudumu huko umoja wa mataifa mh. balozi dk. augustine mahiga, akiongea na waandishi wa habari jijini dar leo kuhusu ujio wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa mh. ki-moon ban kesho kwa ziara ya siku mbili. kulia ni mwakilishi mkazi wa umoja wa mataifa bongo, oscar fernandez taranco, na kushoto ni ofisa alieambatana na balozi mahiga.
ili kuona video ya mkutano huo:
Sikujua Tanzania tuna "balozi wa kudumu."
ReplyDelete"Tarehe February 25, 2009 8:02 PM, Mtoa Maoni: Banzi
ReplyDeleteSikujua Tanzania tuna "balozi wa kudumu." "
Sasa unajua
"Tarehe February 25, 2009 8:02 PM, Mtoa Maoni: Banzi
ReplyDeleteSikujua Tanzania tuna "balozi wa kudumu." "
Sasa Unajua
Balozi wa kudumu tunae - ila mimi nilipoona Ki-Moon nikafikiri mwanamuziki - rapa...
ReplyDeletebongo kulikoni mbona tunahost wageni wengi hivyo? si tutaishiwa? wangechukua basi hata muda kuja....juzi tuna mgeni toka china, mara japani, sasa UN...tutachacha sana before we know what's up with them .....
ReplyDeleteWewe Banzi na wenzio mwashangaa nini kuweko kwa balozi wa kudumu. Hicho ni cheo ambacho mwakilishi yeyote wa Rais kwenye ofisi ya Umoja wa Mataifa huitwa Permanent Representative yaani Balozi wa kudumu. Haimaanishi kuwa Dr Mahiga kama binafsi yake ni wa kudumu. Hapana ila ile nafasi anayoishikilia ndivyo inavyoitwa. Kwa hiyo anaweza akaondolewa na akapelekwa Banzi na akawa balozi wa kudumu. Mmeelewa sasa?
ReplyDeleteWewe Banzi na wenzio mwashangaa nini kuweko kwa balozi wa kudumu. Hicho ni cheo ambacho mwakilishi yeyote wa Rais kwenye ofisi ya Umoja wa Mataifa huitwa Permanent Representative yaani Balozi wa kudumu. Haimaanishi kuwa Dr Mahiga kama binafsi yake ni wa kudumu. Hapana ila ile nafasi anayoishikilia ndivyo inavyoitwa. Kwa hiyo anaweza akaondolewa na akapelekwa Banzi na akawa balozi wa kudumu. Mmeelewa sasa?
ReplyDeletebalozi wa kuduma,,,mahiga,,
ReplyDeletebela kamwene mnoge,makaasi,wanoge wana uko ku-ulaya,ale bela!ndili ipaa bongo..
ivi ina mana ndo forever yan mtu mwingine hatakiwi kuchaguliwa badala yake???siasa za wapi izo?
nani anamlipa mshahara UN au TZ?
Wewe Anonymous wa Feb 26, 9:59 AM
ReplyDeleteSasa kama Mahiga mwenyewe sio balozi wa maisha ila "kudumu" ni uwepo wa ule ubalozi basi cheo chochote kile duniani tunaweza kukiita cha kudumu, maadam kipo kila siku bila ya kujali nani anakikalia.
Hata Kikwete tunaweza kumuita Rais wa kudumu! Eeeeh, maana cheo chake si kipo bwana, atoke asitoke, cheo chake kipo, au? Kikwete nae ni Rais wa Tanzani wa kudumu?
Kama sio, na Mahiga nae hatuwezi kumuita balozi wa kudumu eti kwa vile kile kiti cha ubalozi ndio cha kudumu.
Kama nakosea nitajie cheo ambacho sio cha kudumu.