MAREHEMU MRS.MONICA GRACE MGANGA

Majirani Ndugu na Marafiki zetu wapendwa tunapenda kuwashukuru sana kwa moyo wenu wa huruma na upendo mliotuonyesha katika kipindi kigumu tulichokipitia cha kumpoteza gafla Mama yetu Mpenzi, mmekua mkitufariji kila mara Mwenyezi Mungu awabariki sana,

Haikua rahisi kwetu kuweza kuamini kuwa kipenzi chetu hayuko nasi tena ila kwa msaada wa mugu zilipita saa siku wiki miezi na sasa mwaka mmoja umetimia basi tunaomba mshirikiane na sisi tena katika mkesha siku ya ijumaa ya tarehe 09/07/2010 Nyumbani kwetu Makumbusho kuanzia saa Moja usiku na asubuhi yake tutakua na misa siku ya Jumamosi tarehe 10/07/2010 katika kanisa la Mt Albano upanga saa 3.00 asubuhi na baada ya hapo tutakua na sadaka ndogo ya shukurani ya pamoja hapo hapo kanisani.


Tunawaomba mfike wote muwe pamoja nasi tena kukesha ,kuimba, kusalia na kula pamoja nasi katika kumbukumbu ya Mama yetu Mpenzi
Tunaomba upatapo taarifa hii muarifu na mwingine
Tunawashukuru sana na karibuni sana

Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki sana

Mama Mpenzi tunakukumbuka na Kukuombea kila siku tunakupenda sana na tutakupenda Milele unakumbukwa sana na Mume wako Mpenzi Harold Mganga,Binti zako Jennifer,Angella,Doreen na Miriam. Wakwe zako Robin,John na Amos.Wajukuu zako Joe, Perpetu,Rolenzo, Thomas na Keith

Mwenyezi Mungu ailaze Roho yako Mahali Pema peponi, Amin

Ni Sisi familia ya Mganga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 08, 2010

    Poleni sana sana!!Familia ya Madenge(Yahya,Masoud,Aman,Shaffy na M`ramba)ingawa msiba umetokea mwaka sasa inawapa pole..hatukua na taarifa.....M/Mungu awape uvumilivu.........(amen).

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 08, 2010

    Jamani kina Jeniffer na Angella poleni sana kwa msiba wa mama, nilikuwa namfahamu kwani niliwahi kufanya kazi na wote Jeniffer na angella kwa nyakati tofauti. Namshukuru Mungu kwa kuwapa subira. Atazidi kuwajaalia kuwa na moyo mkuu. Nawatakia ibada njema hapo nyumbani makumbusho.... Amos Msanjila (the same name) - London

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...