BAADHI ya abiria wakidandia lori likiwa katika mwendo katika kijiji Muze,barabara ya Sumbawanga - Mtowisa. barabara hii pamoja na kwamba inapita katika vijiji vilivyopo katika Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga maarufu kwa kilimo cha mpunga, ufuta na mahindi lakini wakazi wake wanalazimika kusafiri katika magari ya mizigo kwa kuwa hakuna mabasi yanayopita huko kutokana na mindombinu ya barabara kuwa mibovu.
Magari mawili madogo yakipishana kwa taabu sana leo, katika njia panda ya kwenda uwanja wa ndege wa Sumbawanga na kitongoji cha Sumbawanga Asilia katika Manispaa ya Sumbawanga , kipande hiki cha barabara kimechimbika na kufanya 'mabwawa' ya maji ambayo hayajafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu hiyo kuhatarisha maisha ya watumiaji wa barabara.
AKINA mama wakiwa wametanda viazi na maboga kando ya barabara ya Sumbawanga - Muze kijijini Muze katika Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga.
WATOTO wanaosoma Shule ya Awali iliyopo katika Shule ya Msingi Mwenge 'A' mjini Sumbawanga wakinywa uji.chakula mashuleni inasemekana huboresha mahudhurio na uelewa kwa wanafunzi (Picha na Mdau Peti Siyame wa Globu ya Jamii -Sumbawanga.)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2012

    Kumbe Sumbawanga kuna maisha bora namna hii? CCM walijitahidi sana. CHADEMA muache kejeli.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...