Na mwandishi wetu.
Washiriki wa mbio za baiskeli zijulikanazo kama “Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge” kutoka mikoa ya Shinyanga na Mwanza wameendelea kuudhihirisha umma wa wakazi wa kanda ya ziwa na watanzania kwa ujumla kuwa mpaka sasa hawana mpinzani baada ya washiriki wa mbio hizo kuibuka kidedea katika fainali za kumtafuta mshindi wa kanda hiyo.

Washiriki wa mikoa hii miwili wamejinyakulia nafasi zote za juu na hivyo kuwashinda wenzao wa mikoa mingine ya Kanda ya ziwa ikiwemo Kagera, Mara, Geita na Simiyu.

Katika mbio za wanaume za umbali wa kilometa 156.6 kutoka Kahama mpaka Tinde na kisha Kurejea Kahama, mshindi wa mwaka jana Masunga Duba (Mwanza) aliibuka tena kidedea huku nafasi ya pili ikichukuliwa na Lupilya Hamis(Shinyanga) na nafasi ya tatu ikimuendea Kulwa Tuki(Shinyanga), washindi hawa wamejinyakulia kitita cha pesa taslimu Sh1,500.000/- kwa mshindi wa kwanza, Sh1,200.000/= mshindi wa pili na Sh800,000/= kwa mshindi wa tatu.

Kwa upande wa mbio za wanawake za umbali wa kilometa 80, kutoka Kahama mpaka Mwakata Kisha kurejea Kahama, timu ya mkoa wa Mwanza imedhihirisha kuwa wao bado ni mabingwa kwa kuibuka tena washindi wa mbio hizo, huku mshindi wa mbio za Mwaka jana Martha Antony, akiibuka mshindi wa kwanza akifuatiwa na Laulensia Luziba na nafasi ya tatu ikienda kwa Veronica Simon. Washindi hao wamepata zawadi ya pesa taslimu Sh1,200.000/= kwa mshindi wa kwanza, Sh800,000/= mshindi wa pili na Sh600,000/= mshindi wa tatu.
 Mmoja wa washiriki wa mbio hizo akinywa maji wakati wa mashindano hayo.
Mshindi wa mbio za Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge, Masunga Duba aliyeinua mikono akishangilia mara baada ya kumaliza mbio hizo akiwa mbele ya wenzake. Mshindi huyo anatoka mkoa wa Shinyanga.
 Washindi wa mbio za wanawake (kilometa 80). Aliyesimama katikati ni Martha antony ambaye ndio aliibuka mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Laulensia Luzuba, (mwenye mtoto) aliyekuwa mshindi wa pili na Veronica Saimon (wa kwanza kushoto) aliyejinyakulia nafasi ya Tatu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 18, 2015

    Baiskeli ya kwanza ya kisasa inagia zingine swala kichekesho

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...