SIMON S. KAHEMELE
26th Julai 1965 – 14th Novemba 2014
Ni mwaka mmoja sasa tangu ulipotuacha ghafla katika ajali ya gari. 

Tukiwa tungali na majonzi ya kuondokewa nawe katika ulimwengu huu, mambo mema uliyotufanyia ulipokuwa hai bado yanaendelea kugusa maisha yetu. 

Tunakukumbuka sana kila iitwapo leo na nyakati tulizoshirikiana hazijafutika katika mioyo yetu. Mke wako, familia yako na marafiki zako wanakupenda sana na kusikia upweke kwa kuondokewa nawe. 
Leo tumekusanyika Manda mahali ulipolala, ili kumshukuru na kumtukuza Mungu kwa kutupa zawadi ya maisha yako hapa duniani na kwa kufungua rasmi kanisa (Simon’s Memorial Chapel), hii ikiwa ni ukamilisho wa ndoto uliyokuwa nayo.  
Shukrani za pekee ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki wote walioshirikiana nasi katika kufanikisha ndoto hiyo. Mungu awazidishie pale palipopungua.
 Daima Tunakukumbuka, Pumzika kwa Amani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ni kweli tulikupenda sana, lakini Mwenyezi alikupenda zaidi akakuchukua. RIP Simon.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...