Na Humphrey Shao , Globu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Madini, Dotto Butiku ameagiza wamiliki wote wa migodi nchini kuzingatia takwa la kutoa huduma kwa jamii katika sehemu ilipo migodi yao kuwa sio ni ombi ni lazima kwa mujibu wa sheria ya Huduma kwa Jamii.
Waziri Biteko amesema hayo alipokuwa kifunga ziara yake katika Wilaya ya Mkuranga ambapo alitembelea katika Mgodi wa Mchanga Mwanadilatu na Kiwanda cha Kioo ambao wanachimba Mchang akatika eneo la Vianzi.
"Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na Marekebisho yake ya mwaka 2017 inamtka kila mwekezaji kuandaa mpango wa huduma kwa jamii na kuupeleka Halmashauri kwa ajili ya kupitishwa lakini tumeona wachimbaji wengi wamekuwa wakifanya vile wanavyotaka wao hivyo tunawaomba wote wawasilishe mpango huo hili wanachi ambao ndio waathirika wakubwa na uchimbaji huo nao wapate faida kwani jambo hili sio la hiari ni lalazima "amesema Waziri Biteko.
Aidha Waziri Biteko ametoa Maagizo kwa Mwekezaji wa Mwekezaji wa Kioo kuwasilisha risiti zote za uuzaji na ununuzi wa mchanga kwa watalaamu wa madini wa Kanda ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro hili waweze kupangiwa kiasi sahii cha Mrabaha unaotakiwa kuingia Serikalini kama kanuni zinavyotaka kulipa pesa kutokana na bei ya mauzo ya Mwisho.
Naibu Waziri wa Madini, Dotto Biteko akizungumza na Wachimbaji wadogo katika Mgodi wa Mchanga wa Mwanadilatu Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani wakati wa Ziara yake ya kukagua migodi na mfumo wa ulipaji mirabaha kwa wachimbaji.
Mmoja wa Wamiliki wa Mgodi wa Mchanga katika Mtaa wa Mwanadilatu Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani Francis Magua akitoa Malalamiko yake mbele ya Naibu waziri wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini katika migodi ya Wilaya hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Juma Abedi akizungumza na Naibu waziri wa Madini juu ya Matatizo yanayofanywa na Muwekezaji wa Kiwanda cha Kioo ambaye anajiusisha na uchimbaji mchanga katika wilaya hiyo.
Naibu Waziri wa Madini,Dotto Biteko akikagua eneo la Kiwanda Cha Kioo ambao wanajihusisha na shughuli ya uchimbaji wa Madini ya Mchanga kwa ajili ya utengenezaji wa Vioo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...