Akizungumza wakati wa kikao hicho, RC Makalla amewapongeza TRA kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa Mapato kwa Mwezi huu na kuwaelekeza kuendelea kukusanya mapato kwa mujibu wa sheria pasipo kuwabugudhi wananchi huku akisisitiza utoaji wa elimu kwa walipa Kodi.
Aidha RC Makalla amewataka TANROAD na TARURA kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye Barabara zao na kufanyia ukarabati sehemu zenye changamoto ili kuondokana na kero ya ubovu wa Barabara.
Aidha amewataka kusimamia ipasavyo miradi ya barabara huku akielekeza DMDP kushirikiana na Halmashauri kuweka moundombinu bora ya kuhakikisha masoko yote yaliyojengwa yanaanza kutumika baada ya kubaini masoko mengi yaliyojengwa yamekosa wapangaji.
Pamoja na hayo RC Makalla amewaelekeza TANESCO kuhakikisha inafanyia kazi changamoto ndogondogo zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa mapema kwa wananchi pindi inapotokea matengenezo au hitilafu ili watu wajiandae.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...