Na Damian Kunambi, Njombe.

Mahakama ya Watoto wilayani Ludewa mkoani Njombe imemhukumu kifungo cha nje cha miezi 4 mtoto mwenye umri wa miaka 14 (jina limehifadhiwa) mkazi wa kijiji cha Shaurimoyo wilayani humo ambaye ni mhitimu wa darasa la saba kwa kosa la kumbaka mtoto (jina lake limehifadhiwa)mwenye umri wa miaka 9 ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza.

Hukumu hiyo imetolewa jana March 14, 2022 na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya hiyo Isaac Ayengo baada ya mtuhumiwa huyo kukiri kutenda kosa hilo.

Aidha Amesema kifungo hicho kitaambatana na kumlipa faini ya shilingi 400,000 muhanga wa tukio hilo kwa kipindi cha miezi minne, mtuhumiwa kuripoti kwa Afisa ustawi wa jamii mara moja kwa wiki kwa kipindi cha miezi minne, mtuhumiwa kutii maelekezo ya Afisa ustawi wa jamii, Mtuhumiwa kuhudhuria shuleni kwaajili ya kuanza kidato cha kwanza, mtuhumiwa kutoingia katika maeneo ya burudani/starehe.

Awali akisomewa shitaka hilo na Mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Asifiwe Asigile mtuhumiwa huyo alidaiwa kuwa mnamo Januari 31, 2022 katika kijiji cha Shaurimoyo majira ya jioni mtoto huyo alitenda kosa hilo ikiwa ni kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya16 marejeo 2019.

Aliendelea kwa kusema kuwa mtuhumiwa huyo alikiri kutenda kosa hilo pamoja na hoja 9 za upande wa Jamhuri na kupelekea kupokea ripoti ya Afisa Ustawi wa jamii iliyohusu makuzi na maisha ya mtuhumiwa huyo huku katika maombolezo yake akisema kuwa ni mara yake ya kwanza hivyo anaomba asamehewe.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...