Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Ndani na Ununuzi wa Pamoja, Joseph Charos akitoa taarifa ya ujenzi wa maabara ya mbolea kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde (hayupo pichani) alipotembelea ofisi ya TFRA Jijini Dar es Salaam tarehe 8 Julai, 2022.
Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Ndani na Ununuzi wa Mbolea kwa Pamoja, Joseph Charos akimkaribisha Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde kwenye jengo la maabara linaloendelea na ujenzi katika eneo la Kilimo III Vetwnari Manispaa ya Temeke Jijini Dar es Salaam leo tarehe 08 Julai, 2022.

 

NAIBU Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde ameuagiza uongozi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania kuhakikisha kuwa ujenzi wa maabara ya mbolea unakamilika kwa wakati.

Ametoa agizo hilo leo Julai 8, 2022 alipotembelea ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) ili kupata taarifa na kuona hatua ya ujenzi wa maabara hiyo ulipofikia.

Naibu Waziri Mavunde amesema kukamilika kwa jengo hilo la maabara kutaifanya Tanzania kuwa na maabara kubwa inayojihusisha na upimaji wa mbolea  Afrika mashariki na kati.

Aidha, ameitaka kamati ya ujenzi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi wa TFRA kuhakikisha wanasimamia ipasavyo upatikanaji wa vifaa vya ujenzi ili ifikapo mwezi Agosti ujenzi wa maabara hiyo uwe umekamilika.

“Suala la ujenzi mwisho iwe mwezi wa saba, mwezi wa nane nitafika ili kuona hatua mliyofikia kwani serikali ina shauku kubwa kuona maabara inafanya kazi hivyo mfanye kazi usiku na mchana”, Mavunde alisisitiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA Dkt. Stephan Ngailo alisema ofisi yake itahakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati kwani kukamilika kwake kuna manufaa kwa nchi, taasisi anayoisimamia na jamii ya watanzania kwa ujumla.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa ma baraaba hiyo Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi na Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji wa Ndani na Ununuzi wa Mbolea kwa Pamoja, Joseph Charos amesema ujenzi umekamilika kwa asilimia 70 na kuwa tayari vifaa vyote kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo vimenunuliwa.

Ujenzi wa maabara hii ni katika kuhakikisha TFRA inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa ikiwa ni pamoja na kufanya uchambuzi wa mbolea na kuzisajili kwa matumizi ya kilimo,  kufanya uchambuzi wa udongo na mimea pamoja na kuitambulisha maabara kimataifa kutokana na uwezo wake katika kuchambua mbolea Afrika Mashariki na Kati.

Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti TFRA Happness Mbelle (kushoto),mjumbe wa kamati ya ujenzi Dkt. Asheri Kalala na Fundi ujenzi wa maabara ya mbolea wakifuatilia maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde (hayupo pichani) alipofanya ziara kujionea hatua za ujenzi wa maabara zilipofikia tarehe 8 Julai, 2022.
Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde (kulia), Mkurugenzi wa   Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt. Stephan Ngailo (katikati), Meneja wa Kitengo cha Manunuzi Josephy Hillary na wajumbe wa kamati ya ujenzi wakielekea linapojengwa jengo la maabara ya mbolea ili kujionea hatua ya ujenzi wa maabara hiyo tarehe 8 Julai, 2022.
Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde (ameshika nguzo) akikagua utengenezaji wa madirisha kwa ajili ya maabara ya mbolea unaoendelea katika eneo la ujenzi jijini Dar es Salaam wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania, Dkt. Stephan Ngailo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...