
KATIBU Msaidizi Mkuu Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa CCM, Ndg. Bulugu Magege, leo tarehe 30/09/2025 amekutana na vijana wa Kata ya Mlowo na kuwasisitiza kuhakikisha kura zao zote wanampa Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wa CCM katika ngazi zote.
Katika mazungumzo hayo, Bulugu aliwaeleza vijana kuwa Ilani ya CCM imewapa kipaumbele kikubwa vijana ikiwemo mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri, ajira, elimu bora na uwezeshaji kiuchumi. Alisisitiza kuwa Dkt. Samia ni Rais mwenye upendo mkubwa kwa vijana, anayetamani kuwaona wakibadilisha maisha yao kupitia fursa alizozileta.
Bulugu aliambatana na Ndg. Haji Shabani Mwalimu, Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbozi na Ndg. Noel Donald Mkwemba, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Mkoa wa Songwe. Vijana wa Mlowo walimhakikishia kuwa wako tayari kuhakikisha CCM inapata ushindi wa kishindo ifikapo Oktoba 29, 2025.
#OktobaTunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazoZoteTunawashaKijani
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...