Airtel Tanzania inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuwawezesha vijana kupitia ujuzi wa kidijitali unaozingatia utunzaji wa mazingira. Hii imefanyika kupitia mafunzo ya urejeshaji na ukarabati wa vifaa vya kielektroniki yaliyotolewa wakati wa warsha ya ReFab Dar 2, iliyofanyika jijini Dar es Salaam kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Vijana na Stadi 2026.

Warsha hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano kati ya Dar Teknohama Business Incubator, BUNI Hub, Airtel Fursa Lab na TechStar Innovation Hub. Lengo lilikuwa kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo vikuu, vyuo vya ufundi stadi, wahitimu wa TEHAMA, wajasiriamali na wabunifu ili kupata mafunzo ya vitendo kuhusu ukarabati wa vifaa, usimamizi wa taka za kielektroniki na mbinu salama za urejelezaji.

Katika hatua ya kuimarisha mafunzo hayo, Airtel Tanzania imekabidhi jumla ya kompyuta 35 kwa DTBi. Pia kupitia ushirikiano wa Airtel Fursa Lab na DTBi, zaidi ya vijana na wajasiriamali 5,300 wamenufaika na mafunzo ya ujuzi wa kidijitali, ujasiriamali na uchumi katika vituo vinne vya ubunifu vilivyopo Dar es Salaam na Zanzibar.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Bi. Beatrice Singano alisema kuwa uwekezaji katika vijana ni muhimu kwa ujenzi wa uchumi endelevu wa kidijitali. Alisema kuwa kupitia teknolojia na ujuzi wa vitendo, vijana wanaweza kujiajiri, kutatua changamoto za jamii na kuchangia maendeleo ya taifa huku wakihifadhi mazingira.

Aidha, Airtel Tanzania inaendelea na mradi wa E-Waste Go Green unaolenga kuhamasisha usimamizi salama wa taka za vifaa vya kielektroniki. Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 50 ya minara ya mawasiliano ya Airtel imeunganishwa na umeme wa gridi ya taifa, na asilimia 94 ya taka zinazozalishwa katika shughuli za kampuni hiyo zinarejelezwa kama sehemu ya dhamira ya uwajibikaji wa mazingira.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...