Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo vya habari nchini kuzingatia kikamilifu masharti ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, hususan wanapoajiri au kuwasainisha mikataba watumishi wa kada ya habari, ili kuepuka migogoro ya kisheria inayoweza kujitokeza baadaye.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, tarehe 20-21 Januari, 2026 wakati wa ziara ya kikazi ya Bodi katika mikoa ya Dodoma na Iringa, ilipotembelea vyombo kadhaa vya habari kwa lengo la kukagua kiwango cha uzingatiaji wa Sheria hiyo kwa watumishi wanaojihusisha na shughuli za kihabari, wakiwemo wahariri, waandishi wa habari, watangazaji, wapiga picha waandaaji na waandishi wa kujitegemea
Akizungumza baada ya ziara hiyo, Wakili Kipangula amesema Bodi imebaini uwepo wa waandishi wenye sifa stahiki kwa mujibu wa Sheria kwenye vyombo hivyo, lakini bado hawajajisajili katika Mfumo wa TAI-HABARI ili kuomba ithibati na vitambulisho vya uandishi wa habari, hali inayoweza kuwaweka waajiri na waajiriwa katika hatari ya kukiuka Sheria.

Ameeleza kuwa ni muhimu kwa waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wote wa kada ya habari wanakuwa wamekamilisha taratibu za usajili na kupata ithibati kabla ya kupewa majukumu au kuajiriwa ili kulinda uhalali wa ajira na kuepuka athari za kisheria.
Aidha, Wakili Kipangula amesema changamoto nyingine iliyobainika katika baadhi ya vyombo vya habari ni malipo madogo ya posho au mishahara kwa waandishi, hali inayohitaji mjadala mpana na mikakati maalum ya pamoja kati ya waajiri, wadau wa habari na Serikali ili kuhakikisha mazingira bora na ya haki ya kazi kwa waandishi wa habari.

Hata hivyo, amepongeza baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari waliobainika kuzingatia kwa umakini masharti ya Sheria, kushughulikia changamoto za waandishi wao kwa uwazi, na kufanya uwekezaji mkubwa unaolenga kujenga mazingira wezeshi, salama na rafiki ya utendaji wa kazi za kihabari.

Kwa mujibu wa Wakili Kipangula, juhudi hizo ni mfano wa kuigwa na zinachangia moja kwa moja katika kulinda hadhi ya taaluma ya habari, kuongeza weledi wa waandishi na kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari kwa jamii.
Benki ya  Absa Tanzania leo imehitimisha rasmi kampeni yake ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa' iliyodumu Kwa miezi mitatu baada ya kufanyika kwa droo ya tatu na ya mwisho katika hafla Iliyofanyika jijini Dar es Salaam, jana. 

Droo ya mwisho imehitimisha kampeni ya miezi mitatu iliyolenga kuwazawadia wateja kwa kufanya miamala  na huduma za kibenki kwa njia za kidijitali ikiwa ni pamoja na matumizi ya kadi, huku ikithibitisha dhamira ya Absa ya kuhimiza miamala salama, rahisi na isiyotumia fedha taslimu.

Katika hafla hiyo, Absa ilifanya droo ya mwisho ya kila mwezi na kutoa jumla ya shilingi milioni 18 za Kitanzania (TZS 18 milioni) kwa wateja watatu walioibuka washindi kutokana na ushiriki wao katika mwezi wa mwisho wa kampeni.

 Washindi hao ni Bw. Abdulrazak Ali Seif (TZS 10 milioni), Bi. Aysha Mbarak Meghji (TZS 5 milioni), na Bw. Gibbons Samuel Katule (TZS 3 milioni). Droo hiyo ilifanyika kwa kuzingatia Masharti na Vigezo vya kampeni na mbele ya mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, ili kuhakikisha uwazi na haki katika mchakato wa uchaguzi wa washindi.

Katika tukio lililosubiriwa kwa hamu zaidi wakati wa kilele cha kampeni hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah aliibuka  Mshindi wa Zawadi Kuu, akiondoka na shilingi milioni 30 za Kitanzania (TZS 30 milioni). Ushindi huo umetokana na matumizi yake ya mara kwa mara ya huduma za benki za kidijitali na kadi za Absa katika kipindi chote cha kampeni, na unaonesha jinsi miamala ya kila siku inaweza kuleta mabadiliko makubwa katika maisha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisisitiza mchango mkubwa wa wateja katika mafanikio ya kampeni hiyo:

“Kampeni hii imekuwa na Manufaa mkubwa kwa wateja wetu tangu mwanzo. Tumehamasishwa kuona jinsi wengi wao wakichangamkia  njia rahisi, salama na zisizotumia fedha taslimu katika kufanya miamala. Play Your Cards Right imeonesha kuwa pale wateja wanapochagua benki ya kidijitali, kila mtu hunufaika, kuanzia urahisi wa huduma hadi kuimarika kwa ujumuishaji wa kifedha.

"Tunawashukuru kwa dhati wateja wetu kwa kuendelea kuiamini Absa na kuwa sehemu ya safari hii.”

Kwa upande wake, Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu (MI & Analytics), Bw. Denis Kessy, alieleza athari pana ya kampeni hiyo:
“Absa tunaamini kuwa kila mteja ana Stori yenye thamani. Kampeni hii imetupa fursa ya kusherehekea Stori hizo, kubwa na ndogo, kwa kuwazawadia wateja wetu kwa kutumia tu huduma zetu za benki.

 Tunapohitimisha kampeni hii leo, tunajivunia si mshindi wa zawadi kuu pekee, bali kila mteja aliyeshiriki.”

Aliendelea kusisitiza ukubwa wa mafanikio ya kampeni hiyo kwa kusema:
“Kupitia kampeni hii, Absa iliwazawadia washindi 72 wa kila wiki, washindi tisa wa kila mwezi na mshindi mmoja wa Zawadi Kuu, kwa jumla ya shilingi milioni 120 za Kitanzania (TZS 120 milioni) zilizorejeshwa kwa wateja wetu.

 Huu ni uthibitisho dhahiri kuwa kuchagua Absa kunalipa.”
Kampeni ya Play Your Cards Right ilikuwa kampeni ya zawadi kwa wateja iliyodumu kwa miezi mitatu kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025, ikiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya malipo ya kidijitali na yasiyotumia fedha taslimu. Wateja walipata nafasi ya kushiriki katika droo za kila wiki na kila mwezi kwa kutumia kadi zao za debit au credit za Absa kupitia malipo ya kuswipe, kutap (tap) au ununuzi mtandaoni.

Kwa kukamilika kwa droo ya mwisho, kampeni ya Play Your Cards Right imefikia tamati rasmi. Washindi waliotangazwa katika droo ya mwisho watatambuliwa rasmi katika hafla maalum ya kukabidhi zawadi itakayofanyika mwezi Februari, na hivyo kuhitimisha kampeni hii kwa namna ya kukumbukwa, ikiwa ni uthibitisho wa dhamira ya Absa ya kuwaweka wateja katikati ya kila zawadi na kila hatua ya safari yake.Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki yaAbsaTanzania, Bw. Aron Luhanga (kushoto), akifanya droo ya mwisho ya kampeni ya benki ya miezi mitatu ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa', jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alijinyakulia zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.Mmoja wa washindi wa kila mwezi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki ya Absa Tanzania iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' Bw. George Kivaria, akichukua tiketi ya bahati nasibu ili kumpata mshindi wa droo Kuu wakati wa droo ya mwisho iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alishinda zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano  wa Benki ya Absa  Tanzania, Bw. Aron Luhanga.Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy (wa tatu kushoto), akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. George Kivaria (wa pili kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy, akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. Mohammed Zulfikar Hemani (kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa', wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga. 

Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO mkoa wa  Ruvuma, Alan Njiro, ametoa wito kwa wateja wa shirika hilo kuhakikisha wanatumia vifaa vya umeme vyenye ubora na vinavyokidhi viwango katika nyumba zao ili kuepuka changamoto na hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya vifaa visivyo na ubora au feki.

Njiro ametoa wito huo akiwa katika Mtaa wa Pambazuko, Kata ya Shule ya Tanga, Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliopitiwa na Mradi wa REA Awamu ya Pili, amehimiza wananchi kununua vifaa vyenye alama za ubora na kutumia mafundi waliosajiliwa na wenye ujuzi wakati wa kusuka miundombinu ya umeme katika nyumba zao.

Kwa upande wake, Afisa Usalama wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma, Paulo Maysoli, amewataka wananchi wa mkoa huo kutunza na kuilinda miundombinu ya umeme dhidi ya uharibifu na vitendo vya wizi, akisisitiza kuwa miundombinu hiyo ni mali ya umma na ni jukumu la kila mwananchi kuilinda na kuitunza.



Aidha, wananchi wa Mtaa wa Pambazuko wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa REA katika mtaa wao, wakieleza kuwa mradi huo utachangia kuboresha maisha yao na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

TANESCO Mkoa wa Ruvuma imewahimiza wananchi kushirikiana na taasisi husika kwa kuzingatia matumizi ya vifaa vya umeme vyenye ubora, kuzingatia ushauri wa kitaalamu na kulinda miundombinu ya umeme, ili kuhakikisha usalama, uendelevu wa huduma ya umeme na maendeleo endelevu katika jamii.




Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeagizwa kuongeza juhudi za udhibiti wa sekta ya fedha kwa lengo la kuwalinda wananchi dhidi ya athari za kukopa katika taasisi zisizo rasmi, hali inayosababisha wengi wao kupoteza mali na rasilimali zao za thamani kutokana na mikopo yenye masharti kandamizi.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (MB), kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula, wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yaliyofanyika tarehe 21 Januari 2026 katika Viwanja vya Usagara mkoani Tanga.

Katika hotuba hiyo, Waziri wa Fedha amebainisha kuwa wananchi wengi wamekuwa wakipata athari mbalimbali kutokana na kukopa fedha katika taasisi zisizo rasmi, hivyo kusisitiza umuhimu wa wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu uhalali wa taasisi za kifedha kabla ya kukopa.

Amehimiza wananchi kusoma na kujiridhisha na mikataba ya mikopo wanayoingia ili kuepuka hasara zinazotokana na kusaini mikataba bila kuelewa masharti yake.

Kwa upande wake, Gavana wa BoT, Bw. Emmanuel Tutuba, kupitia hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Ustawi na Huduma Jumuishi za Fedha, Bw. Kennedy Komba, amesema kuwa katika kutekeleza sera za ujumuishi wa kifedha na kuongeza uwazi, ulinzi na ufikikaji wa huduma kwa watumiaji wa huduma za fedha, hususan kwa wale wenye malalamiko dhidi ya watoa huduma au wanaokosa taarifa kamili kuhusu gharama, tozo na utaratibu wa ukokotoaji wa riba na mikopo, BoT imeanzisha na kuimarisha mifumo mbalimbali.

Mifumo hiyo ni pamoja na mifumo ya uwasilishaji na usimamizi wa malalamiko (SEMA na BOT), kilinganishi cha bei, kikokotoo cha gharama za mikopo, pamoja na utaratibu wa usimamizi shirikishi kwa watoa huduma ndogo za fedha wa kundi la pili, hatua ambazo zimeongeza uwazi, ufanisi na ubora wa huduma za fedha zinazotolewa kwa wananchi kwa kuzingatia matakwa ya sheria na kanuni zilizopo.

Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayofanyika kuanzia tarehe 19 hadi 26 Januari 2026, yanalenga kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya fedha na matumizi ya huduma rasmi za fedha kwa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.



MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema hadi kufikia uzinduzi rasmi wa Mfumo Jumuishi wa Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani (IDRAS) unaotarajiwa kufanyika Februari 9, mwaka huu, jumla ya taasisi 60 zitakuwazimeunganishwa na mfumo huo ili ziweze kutoa huduma kwa wafanyabiashara.

Kamishna wa Kodi za Ndani, Alfred Mlegi amesema hayo leo Januari, 21,2026 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa IDRAS) kwa wafanyabiashara na walipa kodi wote.

Mlegi amesema TRA imetoa mafunzo hayo kwa wafanyabiashara na walipa kodi kabla ya kuanza kutumika kwa mfumo huo ili kuwaongeza uelewa juu ya namna ya kuutumia na kuepuka changamoto.

“Tume­lenga kuunganisha mfumo huu kwenye jumla ya taasisi 300, lakini kwa kuanzia tunaanza na hizi 60 ili ziendelee kutoa huduma ikiwemo kuwasiliana moja kwa moja bila mfanyabiashara au mlipa kodi kufika katika ofisi zetu,” amesema Mlega

Amesema mfumo huo una jumla ya moduli 17, lakini 15 zipo tayari kuanza kufanya kazi isipokuwa mbili za ukaguzi na uchunguzi ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi.

“Mfumo huu ni kwa ajili ya wananchi katika kuwasaidia katika suala la kulipa kodi, kutunza kumbukumbu za bidhaa zilizouzwa au kununuliwa, shughuli zote za mapingamizi pamoja na kukusanya taarifa zitakazotusaidia kufanya makadirio ya kodi na kuondoa malalamiko ya hisia za kubambikiwa kodi,” amesema.

Ameeleza kuwa awali kulikuwa na mifumo mingi iliyokuwa ikitumika kutoa huduma kwa wafanyabiashara hali iliyosababisha usumbufu, hivyo TRA imeamua kuja na mfumo mmoja utakaomsaidia mfanyabiashara kufanya shughuli zote za usimamizi wa kodi.

Ameongeza, “Hapo awali wafanyabiashara wengi walikuwa wakilalamika kuhusu kodi wanazokadiriwa kuwa si sahihi na wengine wakidai tulikuwa tunawabambikia kodi. Kutokana na hitaji la maboresho, tumekuja na mfumo huu kwa sababu unakusanya taarifa nyingi kutoka sehemu mbalimbali, hivyo itakuwa rahisi kufanya makadirio ya kila mfanyabiashara na mlipa kodi. Ndiyo maana leo tunatoa elimu kuhusu mfumo huu.”

Mlega amesema kulikuwepo na malalamiko juu ya matumizi ya mashine za EFD, lakini kupitia mfumo huo hakutakuwa na ulazima wa kuwa na mashine hiyo kwa kuwa mfumo utamwezesha mtumiaji kutoa risiti.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Dar es Salaam, Pendo Lukas amesema wana imani na mfumo huo kwa sababu utaondoa kilio na malalamiko ya wafanyabiashara.

Pendo ametoa wito kwa wafanyabiashara kuukubali mfumo huo pamoja na kuendelea kuwaunga mkono TRA katika kile wanachokifanya cha kumsaidia mfanyabiashara, akisema wanatumia gharama nyingi na muda wao kuhakikisha kila mfanyabiashara anahudumiwa kwa ukaribu na kwa weledi.

“Tuna imani kwa sababu kupitia mafunzo haya kila mfanyabiashara ataweza kujihudumia yeye mwenyewe pamoja na uwazi wa malipo yake kwa kuzingatia ulichotumia ndicho ulipe,” amesema.

Ameishukuru TRA kwa kuboresha mifumo yao kwani imesaidia kodi kuwa rafiki kwa wafanyabiashara, na kwa sasa hawana migogoro wala hawakimbii mamlaka hiyo kama ilivyokuwa hapo awali.



Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, leo Januari 21, 2026 amewasilisha Taarifa ya Taasisi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma.

Kamati hiyo ilipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Nishati na utekelezaji wa Majukumu ya TANESCO


Na Mwandishi wetu, Simanjiro
WAKAZI wawili wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumbaka kwa zamu msichana mwenye umri wa miaka 24.

Pamoja na kumbaka na kumwingilia kinyume cha maumbile msichana huyo pia walimpora simu aina ya Samsung na kumwibia fedha zake Sh70,000.

Hata hivyo, katika hukumu ya kesi hiyo namba 10374/2025 iliyotolewa mji mdogo wa Orkesumet na hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo Nicodemo washtakiwa watatu kati ya watano hawakuwepo mahakama hapo.

Hakimu Nicodemo amewataja washtakiwa Meshack Paulo (23) na Ibrahim Ibu (24) ambao ni wachimbaji wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani walimbaka, kumlawiti.

Amesema washtakiwa hao na wenzao watatu Februari 4, 2025 kwa pamoja walimbaka msichana huyo ambaye ni muhudumu wa bar ya Feri mwenye umri wa miaka 24.

Ameeleza kwamba wakati msichana huyo usiku huo wa saa 8 akitoka kazini akitembea kwenda nyumbani alimuona mshtakiwa wa kwanza Meshack akiwa na pikipiki kisha akampakiza.

Amesema alipakia pikipiki hiyo na walipofika na eneo la karibu na kanisa la Ngurumu ya Upako wakati akipelekwa nyumbani walisimamishwa na watu wengine wanne wakawa watano.

Ameeleza kwamba aliwatambua watu hao kutokana na mwanga wa nishati ya umeme iliyokuwa kwenye eneo la kanisa hilo wakaanza kumkaba.

Ameeleza kwamba katika ushahidi wake msichana huyo akadai kuwa mshtakiwa wa kwanza Meshack alimziba mdomo kisha wakambaka kwa zamu.

Amesema pia washtakiwa hao wakamnyang'anya simu aina ya Samsung yenye thamani ya Sh600,000 na fedha Sh70,000.

Katika utetezi wao mshtakiwa namba moja Meshack alikubali kuwa eneo la tukio ila hakushiriki ubakaji na mshtakiwa wa pili ameeleza kwamba hakuwepo kwenye tukio hilo.

Hata hivyo, hakimu Nicodemo akisoma hukumu hiyo ameeleza kwamba mahakama hiyo imewatia hatiani washtakiwa hao na kuwahukumu miaka 30 kwenda gerezani.

Kocha wa Timu ya Mpira ya Pete ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) akizungumza na wachezaji wa timu wakati wa kipindi cha mapumziko katika mchezo baina yao na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.

MKurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Hanifa Selengu akizungumza jambo na wachezaji wa Timu wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.
Sehemu ya wachezaji wa akiba na benchi la ufundi la Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakifuatilia maelekezo ya kocha wa timu hiyo Bw. Mafuru Buriro wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.
(NA MPIGAPICHA WETU)

TIMU ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) imeendeleza wimbi la ushindi katika mashindano ya Ligi ya Muungano ya mchezo huo yanayoendelea katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar.

Katika matokeo ya mechi ya leo Jumatano Januari 21, 2026, Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais imeiadhibu vikali Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jumla ya magoli 45 dhidi ya 34 katika mchezo ambao Ofisi hiyo ilitawalawa maeneo yote ya mchezo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo, Mchezaji wa Timu hiyo, Bi. Anna Akwilini amesema nidhamu, ushirikiano na kujitumu kwa wachezaji ndio siri kubwa ya mafanikio ya timu hiyo katika mashindano hayo.

“Benchi la ufundi kupitia Kocha amekuwa akiturekebisha kwa makosa madogo madogo na pia hamasa ya mashabiki katika majukwaa imekuwa ikitujengea hali ya kujiamini na kupata hamasa kubwa katika kila mchezo tunaocheza” amesema Akwilini.

Amesema wachezaji wa timu hiyo wamekusudia kuendelea kufanya vizuri zaidi katika michezo yote iliyosalia ili iweze kuibua na ushindi na hatimaye kunyakua ubingwa wa Ligi hiyo ambayo imekuwa na ushindani wa hali ya juu kutoka kwa timu zote.

“Ofisi itahakikisha itajipanga vyema zaidi kwa kufanya usajili wa wachezaji wakati wa Ligi ya mashindano ya mchezo kwa upande wa Tanzania Bara na baadaye kufanya vizuri zaidi katika mashindano ya Muungano” amesema Mwasamale.

Kwa upande wake Kocha wa Timu hiyo, Bw. Mafuru Buriro amesema mechi hiyo ilikuwa ngumu lakini kutokana uimara wa kikosi chake kimeweza kufanya vizuri na kuwa na imejipanga inapata matokeo mazuri katika michezo iliyosalia.

“JKT ni timu iliyokaa pamoja kwa muda mrefu wamezoeana na kupata muda mwingi wa kufanya mazoezi ya pamoja lakini tulitumia uzoefu na bidi ya wachezaji wetu katika kupata ushindi katika mchezo huu” amesema Buriro.

Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 15 Januari mwaka huu yameshirikisha jumla ya Timu 11 ikiwemo Timu 06 kutoka Tanzania Bara na Timu 05 kutoka Zanzibar ambapo yanatarajia kuhitimishwa rasmi tarehe 24 Januari mwaka huu.

 Timu zinazoshiriki Ligi ya Mashindano hayo ni Ofisi ya Makamu wa Rais, JKT, JKU, Mafunzo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Kikosi cha Valantia Zanzibar (KVZ), Polisi Arusha, Dodoma Jiji, Zimamoto na Uhamiaji.




Na Khadija Kalili, Kibaha
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani, leo tarehe 21 Januari 2026, imekabidhi vifaa tiba vya kisasa vya aina mbili kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi, kwa lengo la kusaidia huduma za afya na ukuwaji wa watoto njiti.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika hospitalini hapo, Mkurugenzi wa TAKUKURU Nchini, Crispin Chalamila, ambaye alikuwa mgeni rasmi, alisema kuwa msaada huo umetokana na michango ya hiari ya wafanyakazi wa TAKUKURU nchini, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali katika kupunguza vifo vya watoto njiti.

Chalamila alisema kuwa msaada huo ni muendelezo wa jitihada za Taasisi hiyo katika kusaidia sekta ya afya, akibainisha kuwa hadi sasa vifaa tiba kama hivyo vimekwishakabidhiwa katika hospitali nane zilizopo katika mikoa nane nchini.

“Watumishi wa TAKUKURU kwa pamoja tulikubaliana kuchangia sehemu ya mishahara yetu ili kufanikisha ununuzi wa mashine hizi. Tayari tumekwisha toa msaada katika hospitali nane,” alisema Chalamila.

Aidha, alisema kuwa TAKUKURU itaendelea kutoa michango hiyo katika hospitali mbalimbali nchini, huku akizitaka taasisi nyingine za kiserikali, mashirika binafsi na wananchi kwa ujumla kushirikiana na Serikali katika kupambana na vifo vya watoto wachanga, hususan watoto njiti.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Watoto katika Hospitali ya Tumbi, Dkt. Adelina Rutashobya, alisema kuwa katika mwaka 2025 hospitali hiyo ilipokea watoto 1,393, ambapo watoto 370 sawa na asilimia 27 walizaliwa kabla ya wakati. Aliongeza kuwa watoto 173 waligundulika kuwa na matatizo ya moyo na watoto 61 walifariki dunia.

Dkt. Rutashobya alisema kuwa asilimia 10 ya watoto hao walipewa rufaa kwenda hospitali nyingine, huku asilimia 80.8 wakiruhusiwa baada ya kupata matibabu. Hata hivyo, alibainisha kuwa hospitali hiyo bado inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vifaa tiba na dawa kwa ajili ya watoto njiti.

Alitaja baadhi ya mahitaji hayo kuwa ni pamoja na mashine za uangalizi wa karibu kwa watoto (incubators), mashine za kutoa maji na dawa, pamoja na dawa za kusaidia kukomaza mapafu ya watoto.

Wakati huo huo, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Pwani, Domina Mkama, alisema kuwa Taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Hospitali ya Tumbi katika masuala mbalimbali, ikiwemo utoaji wa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na masuala ya afya.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi, Dkt. Amani Malima, aliushukuru uongozi wa TAKUKURU kwa msaada huo, akisema kuwa vifaa vilivyotolewa ni muhimu katika kuboresha huduma na kuokoa maisha ya watoto njiti, huku akiahidi kuvihifadhi na kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

 

Na Mwandishi wetu, Dodoma


Jumla ya Wapiga Kura 38,151 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa marudio katika Kata za Malangali iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Mkoa wa Rukwa na Mzinga iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amesema hayo leo Januari 21, 2026 jijini Ddodoma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika Kata hizo utakao fanyika Januari 22, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 92 vya Kupigia Kura vitatumika.
 
Aidha, amesema jumla ya wagombea sita (6) kutoka katika vyama vya siasa vitatu (3) wanawania nafasi wazi za udiwani katika maeneo hayo na kuvipongeza vyama vya siasa na wagombea waliojitokeza kushiriki katika uchaguzi huo.
 
“Kati ya wagombea sita (06), wagombea watano (05) sawa na asilimia 83.3 ni wanaume na mgombea mmoja (01) sawa na asilimia 16.7 ni Mwanamke. Kwa namna ya pekee, Tume inavipongeza vyama vilivyoshiriki na wagombea waliojitokeza kushiriki,” alisema Jaji Mwambegele.
 
Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Januari 05, 2026 vimetakiwa kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura.
 
“Wasimamizi wa uchaguzi katika Majimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,” alisema Jaji Mwambegele.
 
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
 
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni. Ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.
 
“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,” alisema Jaji Mwambegele.
 
Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa (NIDA), Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

Kocha wa Timu ya Mpira ya Pete ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)akizungumza na wachezaji wa timu wakati wa kipindi cha mapumziko katika mchezo baina yao na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.


************

Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) imeendeleza wimbi la ushindi katika mashindano ya Ligi ya Muungano ya mchezo huo yanayoendelea katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar.

Katika matokeo ya mechi ya leo Jumatano Januari 21, 2026, Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais imeiadhibu vikali Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jumla ya magoli 45 dhidi ya 34 katika mchezo ambao Ofisi hiyo ilitawalawa maeneo yote ya mchezo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo, Mchezaji wa Timu hiyo, Bi. AnnaAkwilini amesema nidhamu, ushirikiano na kujitumu kwa wachezaji ndio siri kubwa ya mafanikio ya timu hiyo katika mashindano hayo.

“Benchi la ufundi kupitia Kocha amekuwa akiturekebisha kwa makosa madogo madogo na pia hamasa ya mashabiki katika majukwaa imekuwa ikitujengea hali ya kujiamini na kupata hamasa kubwa katika kila mchezo tunaocheza” amesema Akwilini.

Amesema wachezaji wa timu hiyo wamekusudia kuendelea kufanya vizuri zaidi katika michezo yote iliyosalia ili iweze kuibua na ushindi na hatimaye kunyakua ubingwa wa Ligi hiyo ambayo imekuwa na ushindani wa hali ya juu kutoka kwa timu zote.

“Ofisi itahakikisha itajipanga vyema zaidi kwa kufanya usajili wa wachezaji wakati wa Ligi ya mashindano ya mchezo kwa upande wa Tanzania Bara na baadaye kufanya vizuri zaidi katika mashindano ya Muungano” amesema Mwasamale.

Kwa upande wake Kocha wa Timu hiyo, Bw. Mafuru Buriro amesema mechi hiyo ilikuwa ngumu lakini kutokana uimara wa kikosi chake kimeweza kufanya vizuri na kuwa na imejipanga inapata matokeo mazuri katika michezo iliyosalia.

“JKT ni timu iliyokaa pamoja kwa muda mrefu wamezoeana na kupata muda mwingi wa kufanya mazoezi ya pamoja lakini tulitumia uzoefu na bidi ya wachezaji wetu katika kupata ushindi katika mchezo huu” amesema Buriro.

Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 15 Januari mwaka huu yameshirikisha jumla ya Timu 11 ikiwemo Timu 06 kutoka Tanzania Bara na Timu 05 kutoka Zanzibar ambapo yanatarajia kuhitimishwa rasmi tarehe 24 Januari mwaka huu.

Timu zinazoshiriki Ligi ya Mashindano hayo ni Ofisi ya Makamu wa Rais, JKT, JKU, Mafunzo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Kikosi cha Valantia Zanzibar (KVZ), Polisi Arusha, Dodoma Jiji, Zimamoto na Uhamiaji.

Sehemu ya wachezaji wa akiba na benchi la ufundi la Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakifuatilia maelekezo ya kocha watimu hiyo Bw. Mafuru Buriro wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Hanifa Selengu akizungumza jambo na wachezaji wa Timu wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.

(NA MPIGAPICHA WETU)

Accra, Ghana

Tume ya Madini Tanzania imefanya ziara ya kikazi kwa Bodi ya Dhahabu ya Ghana (Ghana Gold Board – GoldBod) jijini Accra, ikiwa na lengo la kujifunza kwa vitendo namna taasisi hiyo ya kipekee imefanikiwa kubadilisha taswira ya biashara ya dhahabu nchini Ghana na kuimarisha mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa.

Ziara hiyo ya mafunzo ya kubadilishana uzoefu (peer learning) imebaini kuwa GoldBod imeweka mifumo madhubuti ya kuwasimamia wachimbaji wadogo na kuwajumuisha katika mfumo rasmi wa biashara ya dhahabu. 

Hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya udanganyifu na utoroshaji wa dhahabu, kuongeza mapato ya serikali na fedha za kigeni, pamoja na kuimarisha akiba ya dhahabu ya Benki ya Ghana.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa GoldBod, Profesa Richard Nunekpeku, amesema kwa kipindi kirefu wachimbaji wadogo walikuwa nje ya mfumo rasmi, hali iliyosababisha upotevu mkubwa wa mapatato kwa serikali.

 Amesema kuanzishwa kwa GoldBod kumewezesha dhahabu yote inayozalishwa kukusanywa na kufanyiwa biashara kwa njia halali, hivyo kuchangia mapato ya taifa, kuongeza akiba ya dhahabu ya Benki ya Ghana na kudumisha uthabiti wa thamani ya fedha ya nchi hiyo.

Katika ziara hiyo, ujumbe wa Tume ya Madini  pia umetembelea kitengo cha Gold Jewelry kilicho chini ya Ghana Gold Board, kinachoshughulikia utengenezaji, uthibitishaji, uwekaji alama za thamani na usafirishaji wa bidhaa za usonara.

 Kitengo hicho kinatajwa kuwa ni hatua muhimu katika kuongeza thamani ya dhahabu nchini Ghana na kuimarisha ushirikiano wa wadau wote katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini.

Ziara hiyo ya kihistoria imeonesha umuhimu wa ushirikiano wa kikanda barani Afrika katika kusimamia rasilimali za madini. Kupitia uzoefu wa GoldBod—bodi pekee yenye mamlaka ya kununua, kuuza, kupima, kuhakiki, kutoa thamani na kusafirisha dhahabu pamoja na madini mengine ya thamani, Tanzania imepata mafunzo muhimu yatakayosaidia kuimarisha mifumo ya usimamizi wa biashara ya madini. Mfano wa Ghana unaonesha kuwa usimamizi thabiti na wa kitaasisi wa sekta ya madini unaweza kuleta manufaa makubwa kwa wananchi na maendeleo ya taifa kwa ujumla.













Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa BoA Bank, Hamza Cherkaoui akimkabidhi cheti cha shukrani kwa wateja wa SME wa Bank of Africa Tanzania.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha SME wa Bank of Africa Tanzania, Beatrice Richard akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa Bank of Africa Tanzania, Hamza Cherkaoui (katikati), akisalimiana na mmoja kati ya wateja waliohudhuria mafunzo ya elimu ya fedha kwa wajasiriamali yaliyoandaliwa na benki hiyo,Jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa Bank of Africa Tanzania, Hamza Cherkaoui, akifungua warsha ya Elimu ya Fedha kwa wajasiriamali (SME Clinic) yenye kaulimbiu “Kuwezesha Ukuaji Pamoja,”iliyofanyika jijini Dar es salaam juzi.
Viongozi na wafanyakazi wa Bank of Africa Tanzania, wakiwa katika picha ya pamoja na wateja wa SME baada ya mafunzo ya elimu ya fedha kwa wajasiriamali (SME Clinic) iliyolenga kutoa mafunzo kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, Dar es Salaam.


BANK of Africa Tanzania imeandaa warsha kwa ajili ya wajasiriamali iitwayo SME Clinic ambayo inalenga kutoa elimu ya masuala ya fedha ili kusaidia ukuaji wa biashara zao nchini kote.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi Mtendaji Biashara wa Bank of Africa Tanzania, Hamza Cherkaoui, alisisitiza umuhimu wa Wajasiriamali katika kukuza uchumi wa Tanzania hasa kwenye masuala ya ajira na kuboresha maisha ya mtu mmoja mmoja. Akieleza dhamira ya benki alisema “Tumejikita kuhakikisha tunawawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kuwapatia maarifa, nyenzo na masuluhisho ya kifedha wanayohitaji ili kuendelea kustawi.”

“Bank of Africa Tanzania tumejikita kuhakikisha tunawapatia wajasiriamali wadogo na wa kati maarifa, nyenzo na masuluhisho ya kifedha wanayohitaji ili kustawi. Kupitia programu kama SME Clinic, tunajenga ushirikiano endelevu na wa kudumu na wateja wetu. Kwa kaulimbiu ya mwaka huu ‘Kuwezesha Ukuaji Pamoja’, tunadhihirisha dira yetu ya kuwa mshirika wa kifedha anayeaminika anayekua sambamba na wateja wake na sekta ya biashara za Tanzania,” alisema.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha SME wa Bank of Africa Tanzania akiongea katika warsha hiyo, alibainisha dhamira ya Benki katika kuwawezesha wajasiriamali kwa kuwapatia maarifa sahihi na suluhisho za kisasa za kifedha. Alieleza kuwa kupitia SME Clinic, benki inalenga kuwajengea uwezo wajasiriamali katika usimamizi bora wa fedha huku ikihamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali ili kurahisisha uendeshaji wa biashara zao.

Beatrice alisema benki inaendelea kutoa huduma rafiki za benki mtandao, ikiwemo BOAWeb/Internet Banking na B-Mobile, sambamba na kutumia mtandao wake mpana wa mawakala kuwafikia wateja popote walipo. Akigusia kaulimbiu ya “Kuwezesha Ukuaji Pamoja,” alisisitiza kuwa Bank of Africa Tanzania si mtoa huduma wa kifedha pekee, bali ni mshirika wa karibu wa wajasiriamali katika safari yao ya ukuaji endelevu na mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa taifa.

Kaulimbiu ya mwaka huu, “Kuwezesha Ukuaji Pamoja”, inadhihirisha dhamira ya kwenda sambamba na wajasiriamali kuhakikisha si tu wanabaki sokoni, bali wanakua kwa njia endelevu na kuchangia kikamilifu maendeleo ya taifa. SME Clinic ya jijini Dar es salaam imewaleta pamoja wajasiriamali, wataalamu wa Bank of Africa Tanzania na wadau wa sekta mbalimbali kwa siku ya mafunzo, kubadilishana mawazo na kukuza ushirikiano.

Warsha hiyo hufanyika kila mwaka na inasisitiza dhamira yake ya utoaji wa elimu ya masuala ya kifedha inayolenga kuwawezesha wajasiriamali na kusaidia ukuaji wa biashara zao nchini kote.

SME Clinic ni sehemu ya Programu ya Elimu ya Fedha ya Bank of Africa Tanzania iliyoanzishwa mwaka 2021 kufuatia Kanuni za Ulinzi wa Watumiaji wa Huduma za Fedha za mwaka 2019. Kifungu cha 19 cha kanuni hizo kinahitaji kila mtoa huduma za kifedha kuandaa programu za elimu ya fedha kwa wateja wake.

Tangu ilipoanzishwa programu hii, imefanikiwa kuendesha warsha hizi (SME Clinics) katika mikoa ya Dar es Salaam,Dodoma, Mwanza na wilayani Kahama na tayari imeweza kuwafikia zaidi ya wateja 800.

Warsha hii pia inalenga kuboresha ujuzi katika usimamizi wa biashara kwa wateja, kuimarisha uhusiano kati ya Bank of Africa Tanzania na wateja wake, na kuhimiza matumizi ya mifumo na teknolojia za kidijitali ili kuongeza ufanisi wa biashara.

Top News