Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga
Elimu ni haki muhimu ya binadamu. Elimu ni nyenzo muhimu ya kumsaidia binadamu kumudu maisha yake. Kwa kutambua hilo, ndiyo maana wazazi na walezi wanapambana sana kusomesha watoto na vijana wao ili kuwawezesha kupata elimu bora ya kuwasaidia katika maisha yao na kutimiza ndoto zao za kimaendeleo walizonazo.
Kazi kubwa na nzuri zimefanyika nchini katika kuboresha sekta ya elimu katika ngazi zote za elimu kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu Ili watoto na vijana wa Kitanzania waweze kupata elimu bora ya kuwasaidia maishani mwao. Mitaala ya ujifunzaji imeboreshwa ili kuwajengea wanafunzi umahiri wa kujitegemea pindi wanapohitimu ngazi mbalimbali za masomo yao.
Ikumbukwe kuwa mabadiliko haya mazuri ya mitaala yamekuja kipindi hiki ambacho wahitimu wengi wana changamoto ya kukosa stadi na ujuzi stahiki wa kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri katika sekta mbalimbali. Ndiyo maana wengi tunapongeza mabadiliko haya ya mitaala kwa ustawi mwema wa wahitimu. Katika elimu ya juu, serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inaratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wanafunzi huku wanufaika wa mikopo hiyo wakiwajibika kuirejesha mikopo hiyo baada ya kuhitimu na kuwa na kipato katika sekta rasmi au isiyo rasmi.
Kwa kutambua changamoto iliyopo kwa baadhi ya wahitimu kukosa ujuzi na stadi mbalimbali, HESLB inashirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo taasisi ya kifedha katika kuhakikisha wanawajengea uwezo wahitimu ili waweze kuajiriwa au kujiajiri ambapo kufanikiwa kwao kunaiwezesha HESLB kukusanya fedha kutoka kwa wahitimu hao lakini pia nchi kupata wataalamu kwa maendeleo.
Mathalani, Februari 18, 2026, katika Ofisi za CRDB Makao Makuu Jijini Dar es Salaam, HESLB iliingia makubaliano ya kushirikiana na CRDB Bank Foundation na kampuni ya Basil Link ili kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu kupata ujuzi wa kidigitali, elimu ya ujasiriamali na elimu ya fedha.
Kwa hakika makubaliano haya ni mwelekeo mzuri katika kuwaandaa wanafunzi wa vyuo vikuu kujitegemea kutokana na mafunzo muhimu watakayoyapata kupitia uwezeshaji utakaofanywa hasa katika kuwa na jicho la kuona fursa za kiuchumi zilizopo.
Kupitia programu hiyo lijulikanalo kwa jina la "Imbeju - SmartElite," wanafunzi wa vyuo watapata mafunzo ya ujasiriamali ili kuweza kujiajiri wenyewe. Aidha, watapata pia elimu ya fedha ambayo ni muhimu sana katika ulimwengu huu wa sasa. Sanjari na hilo, wanafunzi watapata mikopo nafuu na ushauri elekezi wa namna bora ya kuwekeza mikopo hiyo ili ilete tija kiuchumi.
Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Mwambapa alisema "Tunataka kuona vijana wanachangamkia fursa, wanabuni, wanaanzisha biashara na hata kuajiri wengine. Hii si tu kuwasaidia kumaliza chuo, bali kuwaandaa kuingia katika uchumi wa kidigitali wakiwa tayari na ujuzi pamoja na raslimali."
Kwa upande wa Dk. Peter Mmari ambaye ni Mkurugenzi na Upangaji Mikopo wa HESLB amesema "Kupitia mpango huu, wanafunzi wataongeza uwezo wa kutumia mifumo ya kidijitali na watapata fursa ya kujiajiri wakiwa vyuoni au baada ya kuhitimu. Tunaamini wataweza pia kutoa mchango katika kuwainua Watanzania wengine kielimu na kiuchumi."
Kimsingi, vijana wenye vipaji na mawazo bunifu watanufaika na mpango huu huku wakiwezeshwa mitaji na vitendea kazi kama kompyuta. Kwa hakika programu ya Imbeju - Smart Elite, ni mkombozi kwa vijana hasa katika ulimwengu wa uchumi wa kidijitali na biashara.
Na Diana Byera,Karagwe
MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Kagera, Devotha Daniel, ametoa msaada wa Sh. 1,000,000 kwa mtoto Grecseous Raphael mwenye umri wa miezi 4, mkazi wa Kata ya Kihanga, Wilaya ya Karagwe, anayesumbuliwa na uvimbe kichwani
Lengo la msaada huo ni kumuwezesha mtoto huyo kupelekwa Hospitali ya Kanda ya Bugando kwa ajili ya upasuaji.
Mbunge Devotha Daniel ametoa msaada huo ikiwa ni katika kipindi cha kuendelea kusambaza tabasamu kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, amesema alipata taarifa za mtoto huyo kupitia matangazo ya kituo cha redio ya jamii cha Fadeco Radio, ambapo mama wa mtoto alikuwa akiomba msaada kwa wasamaria wema.
“Baada ya kusikia taarifa hizo, niliguswa na kuamua kufika moja kwa moja kwa familia ya mtoto kwa ajili ya kuona hali halisi na kutoa mchango wangu.”
Mbali na msaada huo wa fedha ameahidi kugharamia bima ya afya kwa familia nzima ya mtoto huyo, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na ulinzi wa matibabu.
Kwa upande wake, mama wa mtoto Swaumati Sijaji amemshukuru Mbunge huyo kwa kufika nyumbani kwao na kuwafariji pamoja na kutoa msaada huo ambao utasaidia kumpeleka mtoto waoHospitali ya Kanda ya Bugando kufanyiwa upasuaji wa uvimbe huo.
Hata hivyo familia ya mtoto huyo imesema msaada huo umewapa matumaini mapya ya kuona mtoto wao anapatiwa matibabu stahiki na kurejea katika hali ya kawaida.Hawakutarajia kupata msaada kwa haraka kiasi hicho huku wakimuahidi kumuombea Mbunge huyo ili aendelee kuwahudumia wananchi kwa moyo wa huruma.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Karagwe Georgiana Mkapapa amesema kitendo hicho kinaonesha namna Mbunge huyo alivyo karibu na wananchi wake, na kuwataka wanawake na wananchi kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono na kumuamini katika jitihada zake za kuwatumikia na kuwaletea maendeleo.

Na.Mwandishi Wetu
Taasisi ya Jafo Education Foundation imefadhili jumla ya vijana 51 kusoma katika Chuo cha FDC Kisarawe - Mzenga, kwa lengo la kuwawezesha kupata ujuzi wa fani mbalimbali za ufundi.
Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua miradi na kuzungumza na wananchi katika Kata ya Mzenga, Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Mhe.Dkt. Selemani Jafo, amesema vijana hao 51 watatoka katika kata zote 17 za wilaya hiyo na taasisi hiyo itagharamia ada zao za masomo.
"Hii ni fursa muhimu kwa vijana wa Kisarawe kujipatia ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuajiriwa, hasa katika kipindi hiki ambacho soko la ajira linahitaji wataalamu wenye ujuzi wa vitendo."amesema Dkt. Jafo
Dkt.Jafo amesema kuwa Chuo cha FDC Kisarawe – Mzenga ni chuo kipya kilichojengwa wilayani humo na tayari kinatoa mafunzo katika fani mbalimbali zikiwemo ufundi magari, ushonaji, ujenzi, mapishi, umeme, kompyuta pamoja na mafunzo ya muda mfupi.
Aidha, Dkt. Jafo ameeleza kuwa tangu mwaka 2010 amefanikiwa kusaidia zaidi ya vijana 500 kutoka familia zenye changamoto kusoma katika ngazi mbalimbali, ikiwemo kidato cha tano, astashahada, stashahada na shahada.
Katika kuendeleza juhudi za kukuza elimu ya ufundi, tarehe 20 Februari, Dkt. Jafo kupitia taasisi yake amekabidhi msaada wa vyerehani vinne vya umeme katika chuo hicho, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Samia Suluhu Hassan.
Amesema kuwa dhamira kuu ni kuwawezesha vijana katika fani za ufundi ili kujenga msingi imara wa ajira rasmi na zisizo rasmi, pamoja na kuongeza kasi ya maendeleo katika Wilaya ya Kisarawe.

Na Pamela Mollel, Arusha
Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fedha ujao, hatua inayotajwa kuwa chachu ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, miundombinu na huduma za kijamii.
Bajeti hiyo inatajwa kuwa na neema kubwa kwa wanafunzi wapya zaidi ya 20,000 wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwakani.
Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika juzi, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Baraka Simon, alisema bajeti hiyo imegawanyika katika sehemu kuu mbili.
Alifafanua kuwa kati ya bilioni 75.4 zilizopendekezwa, fedha hizo zimeelekezwa katika miradi ya maendeleo, huku mapato ya ndani yakitarajiwa kuwa shilingi bilioni 9.2.
“Bilioni 75.4 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo, lakini kwa upande wa mapato ya ndani ni bilioni 9.2. Tuna imani kubwa sana na bajeti hii na tunajua italeta mafanikio makubwa sana na itakuwa rafiki kwa wananchi,” alisema.
Katika hatua nyingine, alisema bajeti hiyo imelenga pia kuandaa vyumba zaidi ya 200 vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza watakaoanza masomo mwakani.
Alieleza kuwa mabadiliko yanayotarajiwa katika mfumo wa elimu yataongeza idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza, baada ya wanafunzi wa darasa la sita kuhitimu na kujiunga na ngazi hiyo sambamba na wenzao wengine.
“Mwakani kutakuwa na mabadiliko ya mfumo wa elimu. Wanafunzi wa darasa la sita wakimaliza watajiunga na kidato cha kwanza, lakini hata hao wengine nao wanatakiwa kuingia kidato cha kwanza. Tumejipanga vyema,” aliongeza.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mlangarini, Emanuel Mrema, alisema wanashukuru kwa bajeti hiyo kwani imegusa nyanja zote muhimu zinazohitajika katika jamii.
Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto katika baadhi ya kata, kupitia bajeti hiyo vijiji vyote vitanufaika na miradi ya maendeleo itakayotekelezwa katika mwaka wa fedha ujao.
Kwa ujumla, bajeti hiyo imeibua matumaini mapya kwa wananchi wa Wilaya ya Arusha, huku matarajio makubwa yakiwekwa katika utekelezaji wake ili kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa.
Na Mwandishi Wetu
Wito umetolewa kwa makampuni makubwa ya uchimbaji madini nchini kuwekeza katikakuwawezesha wachimbaji wadogo katika nyanja mbalimbali ikiwemo teknolojia za kisasa na usimikaji wa mifumo ya usalama na afya mahali pa kazi ili kujenga uchumijumuishi unaotokana na sekta ya madini.
Wito huo umetolewa na serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, alipofanya ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria yaUsalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabuwa Geita (GGML).
Waziri Sangu ameipongeza menejimenti ya Mgodi huo kwa kuzalisha ajira nyingi kwaWatanzania ambapo GGML imeajiri jumla ya wafanyakazi 2,366 moja kwa moja na4,629 wameajiriwa kupitia wakandarasi mbalimbali wanatoa huduma katika Mgodi waGGML.
Sambamba na pongezi hizo, Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kazi ameutakaMgodi huo kuhakikisha kwamba shughuli zake zinakuwa na athari chanya katikauchumi wa jamii zinazowazunguka kwa kutoa fursa za kazi za muda mfupi ikiwemokuwezesha miradi mbalimbali ya kijamii.
Aidha, Waziri Sangu ameipongeza GGML kwa kuchagua suala la usalama na afya kwawafanyakazi kuwa tunu yao ya kwanza katika shughuli zao za uchimbaji na uchakatajiwa madini jambo ambalo limewafanya kujenga mifumo madhubuti ya kulinda afya nausalama wa wafanyakazi inayozingatia matumizi ya teknolojia za kisasa.
“Ninawapongeza kwa kuweka usalama na afya kama tunu yenu ya kwanza na hiiimejidhirisha katika wasilisho lenu mlilofanya hapa ambapo masuala ya usalama naafya yamechukua nafasi ya juu zaidi ya biashara mnayofanya,” ameeleza Waziri Sangu na kuongeza:
“Pongezi hizi inastahili pia Taasisi ya OSHA ambayo imekuwa ikiwaongoza katikakutekeleza hayo kupitia usimamizi mzuri wa Sheria Na.5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 na miongozo mbalimbali chini ya sheria hiyo ambayowamekuwa wakiitoa kupitia kaguzi zao za mara kwa mara.”
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita,Hashim Abdallah Komba, amesema OSHA ni miongoni mwa Taasisi zenye msaadamkubwa katika kuwezesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kufanyika kwa tija katikaMkoa wa Geita.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema ziara hiyo, inalenga kuona jinsi OSHA inavyoshirikiana na wadau wake kutekeleza Sheria yaUsalama na Afya mahali pa kazi ambayo dhima yake kuu ni kulinda nguvukazi ya Taifa dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi pamoja na kulinda uwekezaji kupitiakuzuia uharibifu wa mali.
Awali, menejimenti ya GGML iliwasilisha taarifa juu ya shughuli zao iliyoainisha jinsiafya na usalama wa wafanyakazi unavyozingatiwa katika shughuli husika. Miongonimwa masuala yaliyoelezwa katika taarifa hiyo ni pamoja na historia ya mgodi ambapoimeelezwa kuwa madini katika mgodi huo yaligunduliwa mnamo mwaka 1898 nauchimbaji rasmi kuanza mwaka 1999.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkoa wa Geita, Menejimenti ya Mgodi wa Geita na watendaji wa Ofisi yake katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwa ameambatana na watendaji katika Ofisi yake na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita, wakifuatilia wasilisho la taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi huo.





Na Mwandishi Wetu Wetu - DODOMA
Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) imetoa mafunzo ya vipimo kwa wanafunzi wa Dr. Samia Dodoma Secondary School, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi katika biashara na maisha ya kila siku.
Katika zoezi hilo, wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kuhusu dhima na majukumu ya Wakala huo, pamoja na namna unavyolinda maslahi ya watumiaji na wafanyabiashara kwa kuhakikisha vipimo vinakuwa sahihi na vya kuaminika.

Akizungumza baada ya mafunzo hayo, Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa WMA, Veronica Simba, amesema elimu ya vipimo itatolewa katika mikoa yote ya Tanzania Bara ili kuhakikisha wanafunzi wengi zaidi wanapata uelewa wa matumizi sahihi ya vipimo.
Amesema mpango huo unalenga kukuza uelewa wa masuala ya vipimo kwa vijana, sambamba na kuimarisha utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji katika sekta ya biashara nchini.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Dodoma, Said Ibrahim, amesema mafunzo hayo yanaenda sambamba na uanzishwaji wa Klabu za Vipimo mashuleni ili kuendelea kuandaa mabalozi mahiri watakaotoa elimu ya vipimo shuleni na katika jamii kwa ujumla.
“Kwa Dodoma tayari tumeshatoa mafunzo katika shule mbili ambazo ni Shule ya Msingi Mtemi Mazengo na leo tumetoa hapa katika Shule ya Sekondari ya Dkt. Samia Dodoma. Tunaamini mabadiliko katika matumizi ya vipimo sahihi yataongezeka,” amesema Said.

Naye , Mwalimu Mussa Madandi, ambaye pia ni mlezi wa Klabu ya Vipimo shuleni hapo, amesema elimu hiyo wamekuwa wakiifundisha darasani, lakini mafunzo yaliyotolewa na WMA yamewapa wanafunzi nafasi ya kujifunza kwa vitendo, jambo litakalosaidia kuongeza uelewa na kuimarisha matumizi ya vipimo sahihi.
“Vipimo ni somo tunalolifundisha karibu kila darasa, lakini leo wanafunzi wamepata mafunzo kwa vitendo kutoka kwa wataalamu wenyewe. Naamini hali hii itaongeza hamasa ya kuzingatia usahihi katika matumizi ya vipimo na kuwafanya wawe mabalozi wazuri kwa wazazi wao na jamii inayowazunguka,” amesema Mwalimu Madandi.
Mwanafunzi Itabangola Elias amesema elimu hiyo imewasaidia kuelewa namna ya kutambua vipimo sahihi na kujikinga dhidi ya udanganyifu unaoweza kujitokeza katika biashara.
Baada ya mafunzo hayo, wanafunzi walishiriki kujibu maswali mbalimbali kuhusiana na vipimo na shughuli za Wakala huo, ambapo waliofanya vizuri walipatiwa zawadi mbalimbali kama sehemu ya kuwahamasisha kuendelea kujifunza na kuwa mabalozi wa matumizi sahihi ya vipimo katika jamii.






-Ammwagia sifa Rais Dkt Samia kwa Mapinduzi ya elimu
NA MWANDISHI WETU, MBEYA
MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amewataka wahitimu wa kidato cha sita nchini kuwa mabalozi wa nidhamu na uzalendo, huku akibainisha kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ni dhamira ya dhati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutengeneza taifa la wasomi wenye ushindani.
Mhe. Itunda ameyasema hayo jana wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Ivume yaliyofanyika jijini Mbeya.
Sifa kwa Rais Samia na Maboresho ya Miundombinu
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, DC Itunda amempongeza kwa dhati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumwaga mabilioni ya fedha mkoani Mbeya kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa, maabara za kisasa na mabweni.
"Chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Rais Samia, tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa wakati ili kuhakikisha watoto wetu wanasoma katika mazingira bora, jambo ambalo limeongeza morali kwa walimu na kuinua kiwango cha ufaulu," alisema Mhe. Itunda.
Wito wa Nidhamu na Uzalendo kwa Wahitimu
DC Itunda amewahimiza wahitimu hao wa Ivume Sekondari kutolewa macho na mafanikio ya muda mfupi, badala yake wazingatie nidhamu na uzalendo wanapoelekea kwenye ngazi za juu za elimu. Aliwasisitiza kuwa Serikali inawategemea kama nguvu kazi ya baadae ya Taifa.
"Nidhamu ndiyo dira ya mafanikio yenu kuanzia sasa. Tunatarajia muwe mabalozi wazuri wa Ivume na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla kule mwendako. Epukeni vitendo vinavyoweza kuharibu mustakabali wenu na wa Taifa lenu," aliongeza.
Maagizo kwa Waliobaki Shuleni
Kwa upande mwingine, Mhe. Itunda amewataka wanafunzi wanaoendelea na masomo kuongeza bidii na kuzingatia maadili mema, akionya kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo vya utovu wa nidhamu ambavyo vinakwamisha juhudi za kuinua taaluma.
Mapema, Uongozi wa Shule ya Sekondari Ivume uliishukuru Serikali ya Mkoa na Wilaya kwa ushirikiano wa karibu, ukiahidi kuendelea kusimamia taaluma na kulea vijana katika misingi ya uzalendo na uwajibikaji.











.jpeg)




.jpeg)

.jpeg)










.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)