Mwenyekiti wa Chama cha Umoja wa Mwanamke wa Thamani, Hajira Bitebo, amewahimiza wanawake kujishughulisha na shughuli za maendeleo na kufanya kazi kwa bidii badala ya kubweteka kukaa nyumbani bila kujituma.

Bitebo amesema mwanamke anapofanya kazi na kujitegemea kiuchumi huweza kusaidia familia na kuchangia maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Kwa upande wake, Katibu wa chama hicho, Blandina Lukindo, amewataka wanawake kujithamini, kujipenda na kujitambua ili kuimarisha nafasi yao katika jamii na kujenga maisha bora kwa familia na taifa kwa ujumla.

Lukindo amesema ni muhimu kwa mwanamke kujithamini na kujipenda kwani hatua hiyo humjengea kujiamini na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha.

Baadhi ya wanawake waliohudhuria mkutano huo wamesema elimu waliyoipata imewapa hamasa ya kujitambua zaidi, kujipenda na kufanya kazi kwa bidii ili kuboresha maisha yao









Na Pamela mollel,Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa juhudi zake za kuhamasisha wanawake kushiriki kikamilifu katika nyanja mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta za utalii na uhifadhi, hatua inayochangia kuongeza usawa wa kijinsia na kuwajengea wanawake ujasiri wa kushika nafasi za uongozi.

Pongezi hizo zimetolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Sekela Mwangota, ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini

Mwangota amesema uongozi wa Rais Samia umefungua fursa zaidi kwa wanawake kuamini uwezo wao, kujitokeza katika nafasi mbalimbali za uongozi na kushiriki kikamilifu katika maamuzi muhimu ya maendeleo ndani ya taasisi na jamii kwa ujumla.

Alitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Machi 8, 2026 katika ukumbi wa Mafao House jijini Arusha, ambapo wanawake wa TANAPA waliungana kuadhimisha siku hiyo muhimu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwangota alisema siku hiyo ni fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii,

Katika hafla hiyo iliyobeba ujumbe wa “Nguvu ya Mwanamke wa TANAPA, Fahari ya Uhifadhi na Utalii,” Mwangota alimkaribisha Mtaalamu wa Itifaki na Mwanadiplomasia Mwandamizi, Omary Kashera, kutoa mada kuhusu nafasi ya wanawake katika uongozi na maendeleo.

Kashera alisema kuwa Siku ya Wanawake Duniani ilianzishwa mwaka 1911 kwa lengo la kupigania haki na usawa wa wanawake duniani.

Alitolea mfano mafanikio ya Rais Samia kama uthibitisho kuwa mwanamke ana uwezo mkubwa wa kuongoza na kushinda changamoto mbalimbali za maisha, huku akimnukuu aliyekuwa Mke wa Rais wa zamani wa Marekani, Michelle Obama akisisitiza kuwa wanawake wanapaswa kuendelea kujiamini na kusonga mbele licha ya changamoto wanazokutana nazo.









Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Njombe.

WAKALA wa Nishati Vijijini(REA) umetoa ruzuku ya Sh.Bilioni 1.63 kwa ajili ya kuwezesha kutekelezwa kwa mradi wa kuzalisha umeme wa maji kilowati 360 wa Ijangwala uliopo katika Wilaya ya Makete mkoani Njombe ambapo umeme huo umeingzwa katika gridi ya Taifa.

Uwepo wa mradi huo wa kuzalisha umeme uliopo Kijiji cha Masisiwe, Kata ya Ukwama wilayani Makete unasimamiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)Dayosisi ya Kusini Kati-Makete baada ya kubuni mradi huo kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya kukosa umeme katika Kanisa hilo na hivyo kutumia mafuta ya dizeli katika kufanya shughuli mbalimbali za kanisa hilo.

Akizungumza leo Machi 10,2026 mbele ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari ambao ni Wanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF),Kaimu Meneja Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji wa Miradi kutoka REA Mhandisi Emmanuel Yessaya amesema fedha ambazo zimetolewa na wakala huo ndizo zimewezesha ujenzi wa miundombinu ya mradi huo wa umeme.

Mhandisi Yessaya amewaeleza Wahariri hao walioko katika ziara ya kutembelea mradi inayosomamiwa au kufadhili na REA,amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi ya uzalishaji umeme inayoungwa mkono na serikali ili kuongeza uzalishaji wa nishati bora.

“Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini REA imetoa fedha yaruzuku ya Sh. bilioni 1.63 ambazo zimetumika katika kufanikisha ujenzi wa miundombinu ya mradi huu ambao kwa sasa unazalisha umeme kilowati 360 ambao unachangia umeme katika gridi ya Taifa.

“Umeme unaozalishwa katika mradi huu umesaidia kwa kiwango kikubwa hapa Wilayani Makete kuwa na umeme wa uhakika.Na kwa Mkoa wa Njombe REA tumefanikishwa kutekelezwa kwa miradi mitano ukiwemo mradi wa umeme wa Ijangwala.”

Aidha amesema Serikali kupitia REA imekuwa ikitoa ruzuku kwa waendelezaji wa miradi ya nishati kuanzia hatua za awali za maandalizi,kugharamia tafiti za awali za uwekezaji kama upembuzi yakinifu, tathmini ya athari za mazingira na maandalizi ya mpango wa biashara.

Pia amesema kupitia Mpango wa Upanuzi wa Umeme Vijijini Tanzania (TREEP), mradi huo ulipata mkopo wa Sh.milioni 922 kwa ajili ya kusaidia shughuli za utekelezaji wake.

“Baadhi ya miundombinu iliyogharamiwa na serikali ni transfoma chochezi ya KVA 500 na njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 0.6 inayounganisha kituo cha mradi na gridi ya taifa.

Awali Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Ijangala, Daud Sanga, amesema sehemu kubwa ya fedha za ujenzi wa mradi huo zimetoka REA na ukweli REA imekuwa msaada mkubwa katika kuutekeleza mradi ambao tayari umeanza kutoa matunda kwa kuuza umeme katika gridi ya taifa na kupata fedha.

Akieleza zaidi amesema miundombinu yote ya mradi huo imekamilika, ikiwemo jengo la kuzalisha umeme, bwawa la maji, mabomba ya kusafirisha maji na kituo cha kupoza umeme.

“Tunashukuru REA kwani tangu mwanzo wa mradi mpaka sasa tumekuwa pamoja katika kila hatua.Kwa kipekee tunaishukuru serikali chini ya uongozi Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha nchi inakuwa na umeme wa uhakika,”amesema Sanga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania(TEF) Deodatus Balile amepongeza kazi kubwa inayofanywa na REA katika kuendelea kutekeleza miradi ya nishati ya umeme vijijini.

“REA wanafanyakazi nzuri sana wameweza kupeleka umeme katika vijiji na kweli hawa REA wanaweza kupewa hata miradi ya maji wakaipeleka vijijini kama walivyofanya kwenye umeme na hilo linawezekana maana katika umeme huku wamefanikiwa sana.”

Balile ameongeza pia ushirikiano kati ya TEF na REA kwa sehemu kubwa unasaidia jamii ya Watanzania kupata taarifa sahihi kuhusu miradi ya nishati inayotekelezwa vijijini.












Na Mwandishi Wetu

SHULE ya Msingi Msasani B imepokea ufadhili wa kukarabati vyoo 12, hatua inayolenga kuboresha usafi na kuunda mazingira salama na yenye afya kwa wanafunzi na walimu.

Msaada huo wenye thamani ya Sh.milioni 15 umetolewa na kampuni ya Strategis Insurance Tanzania Limited kama sehemu ya mchango wake katika maadhimisho ya kimataifa ya Siku ya Wanawake Duniani(IWD), ambayo huadhimishwa kila mwaka Machi 8 ya kila mwaka.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Dkt. Flora Minja amesema mpango huo umechochewa na kaulimbiu ya IWD ya mwaka huu, Give to Gain” (Toa ili Upate), ambayo inahamasisha watu kurudisha fadhila kwa jamii.

Amesema waliamua kusaidia shule hiyo baada ya kubaini hitaji la haraka la kuboresha miundombinu ya vyoo wakati wa ziara yao shuleni hapo.

“Kupitia kaulimbiu ya mwaka huu, ‘Give to Gain,’ tuliona ni muhimu kufanya jambo lenye maana kwa wanafunzi kwa kuchangia kuboresha miundombinu ya usafi ili waweze kusoma katika mazingira safi na salama,” amesema.

Ameongeza ingawa mradi huo unawanufaisha wavulana na wasichana, pia unaakisi dhamira pana ya maadhimisho ya IWD kwa kusaidia kuunda mazingira yanayowawezesha vijana kustawi.

Dkt. Minja pia amesisitiza umuhimu wa kuwawezesha wanawake zaidi kufikia nafasi za juu za uongozi, akibainisha kuwa wanawake bado ni wachache katika ngazi za juu za usimamizi.

“Katika ngazi za juu za uongozi, wanawake bado ni wachache. Sisi tuliopo katika nafasi hizi tunajitahidi kutoa ushauri na kuweka sera zitakazowasaidia wanawake wengine kupanda hadi ngazi za juu za maamuzi,” amesema.

Kwa mujibu wake, kaulimbiu ya mwaka huu pia inawahimiza wanawake walioko katika nafasi za uongozi kuwainua wengine ili katika miaka ijayo kuwe na uwakilishi mkubwa zaidi wa wanawake katika nafasi muhimu za uongozi.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msasani B, Bw. Badru Musoke, ameishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo, akieleza wakati kampuni ilipotembelea shule waliwasilisha maeneo matatu ya kipaumbele yaliyohitaji msaada, ambapo ukarabati wa vyoo uliteuliwa.

“Msaada huu ni muhimu sana. Serikali inafanya juhudi kubwa kuboresha elimu, lakini haiwezi kufanya kila kitu peke yake. Inahitaji msaada wa wadau kama Strategis Insurance,” ameongeza.

Pia amesema ukarabati huo utasaidia kuhakikisha wanafunzi wanapata huduma bora za usafi na salama, ambazo ni muhimu kwa mazingira bora ya kujifunzia. Pia alibainisha kuwa shule inakabiliwa na changamoto ya kuboresha miundombinu ya michezo ili kukuza vipaji vya wanafunzi.

“Lengo letu si kuhakikisha tu wanafunzi wanafanya vizuri kitaaluma, bali pia kukuza vipaji vyao. Tuna uwanja wa michezo, lakini bado haujafikia kiwango tunachotamani. Kama wadau zaidi watajitokeza kutusaidia, itasaidia sana kuuboresha,”amesema.


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akipata maelezo kuhusu hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma kutoka kwa Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael (wa pili kulia). Ziara hiyo imefanyika Machi 09, 2026 Mtumba Dodoma.

************

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya Suma JKT kuongeza kasi ya ujenzi wa Jengo la Ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma.

Dkt. Muyungi amesema hayo Machi 09, 2026 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi hiyo ambapo aliongozana na Viongozi na Menejimenti kwa ajili ya kujionea na hatua iliyofikiwa katika mradi huo.

Amesema mkandarasi wa kampuni ya Suma JKT hana budi kufanya kazi masaa 24 ili kuwezesha maboresho na ukarabati wa baadhi ya maeneo ndani ya jengo ambayo hayajakamilika.

Ameongeza kuwa Ofisi yake haitongeza muda wa kukamilisha mradi huo kwa kuwa ilishafanya hivyo hapo awali na hivyo kumtaka mkandarasi hukakikisha anatumia vyema muda uliopo kuweza kukamilisha na kukabidhi jengo hilo.

“Kamati ya Bunge inatarajia kufanya ziara katika mradi wa jengo hili tarehe 18 Machi mwaka huu, hivyo nawasisitiza kuhakikisha mnakamilisha kazi hii kwa wakati kabla yatarehe hiyo kufika” amesema Dkt. Muyungi.

Aidha Dkt. Muyungi amesema Ofisi yake imetimiza mahitaji yote yaliyohitajika kwa ajili ya kukamilisha mradi wa ujenzi wa jengo hilo ikiwemo malipo ya fedha kwa mkandarasi na ununuzi wa samani mbalimbali.

Pia Dkt. Muyungi amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha anajenga miundombinu yenye mifumo ya kisasa ya uchakataji na usimamizi wa taka ngumu kuweza kutumiakatika jengo hilo pindi litakapokamilika hatua inayolenga kutunza mazingira.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael amesema kampuni itazingatia maelekezo yaliyotolewa na kuyafanyia kazi ili kuhakikisha mradi wa ujenzi wa jengo hilo unakamilika katika muda uliopangwa.

Katika ziara hiyo Dkt. Muyungi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu (Muungano), Bw. Abdallah Hassan Mitawi na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda pamoja na menejementi ya ofisi hiyo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara yake ya  kukagua ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma. Ziara hiyo imeifanya Machi 09, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara yake ya  kukagua ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma. Ziara hiyo imeifanya Machi 09, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Juma Mohamed Salum (kushoto) akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dkt. Richard Muyungi wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma Machi 09, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo kwa Mratibu wa Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi hiyo kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo Machi 9, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akitazama samani mbalimbali zilizopo ndani ya mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa jengo hilo Machi 9, 2026. Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasimali Watu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Paul Masanja.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akikagua mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma Machi 9, 2026. Kushoto ni Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael.

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime

Faida za kuwepo mwekezaji mwenye uwezo, teknolojia za kisasa na mahusiano mazuri na jamii umedhihirika kutokana na Kikosi cha Dharura na Uokoaji (ERT) kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara ambacho kimesaidia kuokoa watu 22 wakiwemo watoto - waliokuwa wamezingirwa na mafuriko na kukwama kwa siku mbili katika kijiji cha Matongo, wilayani Tarime.


Wananchi hao walizingirwa na maji ghafla kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kulazimika kupanda juu ya miti ili kunusuru maisha yao, kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele.


“Tulijitahidi kuokoa maisha yao wote waliokuwa wamezingirwa na maji na hakuna kifo wala majeruhi. Kwa hivyo, lazima tuwashukuru watu wa mgodi walifanya kazi kubwa kwa kushirikiana na timu ya uokoaji ya wilaya na mkoa,” Meja Gowele aliwambia waandishi wa habari.


Alifafanua kuwa kikosi cha uokoaji kutoka mgodi huo ambao unaendeshwa na kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals kilitangulia kwenye eneo la tukio mara baada ya kupata taarifa - kikiwa na boti, magari na vifaa vingine vya kisasa vya uokoaji.


Shughuli za uokoaji zilianza Jumamosi iliyopita saa moja asubuhi hadi saa 12 jioni katika eneo la Mashambani lenye makambi ya wakulima na wafugaji.


“Mimi mwenyewe nilikuwepo tangu mwanzo hadi mwisho na Kamati ya Usalama, pamoja na timu za uokoaji za wilaya na mkoa zikishirikiana na mgodi ambao walitusaidia kwa kutoa vifaa vya kisasa kwa ajili ya uokoaji. Kwa hivyo, tuna kila sababu ya kuwashukuru watu wa mgodi kwa kazi waliyofanya,” alisema Meja Gowele.


Baada ya kuokolewa, wananchi hao walipatiwa huduma ya kwanza na kusaidiwa kurejea kwenye makazi yao katika vijiji mbalimbali wilayani Tarime.


“Baada ya kuwatoa tuliwacheki kuona kama wanahitaji matibabu lakini wengi walikuwa wana njaa na niliagiza wakapata uji na maji,” alisema Mkuu wa Wilaya, Meja Gowele.


Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Matongo, Charles Ryoba, alimshukuru Mkuu wa Wilaya, Gowele na Mgodi wa Barrick North Mara kwa kuchukua hatua za haraka kuokoa watu hao baada ya kuwapa taarifa za tukio hilo.


“Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa Mgodi wa Barrick North Mara kwa namna walivyopokea jambo hii na kufika kwa muda muafaka, hii inadhirisha wazi kuwa mahusinao yetu na Barrick ni mazuri,” alisema Ryoba mara baada ya shughulli za uokoaji kukamilika.


Alizishukuru pia timu za uokoaji za wilaya ya Tarime na mkoa wa Mara kwa kujitokeza kushiriki kuokoa maisha ya wananchi hao bila kukata tamaa.

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime











Top News