Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imefanikiwa kukamata dawa za kuelevya aina ya mirungi kilo 106.25 katika wilaya ya Longido mkoani Arusha zikiwa zinasafirishwa kwa gari aina ya Toyota Wish yenye namba ya usajili T 889 DPG.

Akizungumza leo Aprili 14,202 jijini Dar es Salaam Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema katika tukio hilo Diwani wa Kata Kimokouwa Solomon Koholo (38) na Lekaneti Kukuu (38) wanashikiliwa kutokana na tuhuma hizo.

Akifafanua zaidi kutokana na tukio hilo amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu maarufu kutumika kwa namna moja au nyingine katika biashara ya dawa za kulevya ambapo ametumia nafasi hiyo kutoa onyo kuwa mamlaka hiyo haitasita kumchukulia hatua yeyote yule hata awe maarufu kiasi gani.

Mbali na tukio hilo pia amesema katika Mkoa waKilimanjaro, eneo la Himo na Same, zimekatwa kilo 68.3 za mirungi zilizowahusisha watuhumiwa Amin Mazua (58) maarufu kwa jina la Mbaruku na Wilbard Mchau (50).

Akieleza zaidi kuhusu operesheni za mamlaka hiyo amesema sambamba na Sambamba na udhibiti wa mirungi, aina nyingine ya dawa za kulevya zilikamatwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi Mabalozi wanaokwenda kuiwakilisha Tanzania katika Mataifa mbalimbali kutanguliza mbele maslahi ya Taifa ya kiuchumi, kisiasa na kidiplomasia.

Makamu wa Rais amesema hayo, wakati akizungumza na Mabalozi wateule wanaokwenda kuiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mataifa mbalimbali, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma kwa lengo la kuwaaga mabalozi hao.

Amewaasa kuwa wabunifu na kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kutangaza fursa zilizopo nchini na kuwashawishi wawekezaji na wafanyabiashara kuwekeza nchini.

Aidha, amewataka Mabalozi hao kusimamia maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi hiki anachojenga uchumi wa nchi na kuimarisha uhusiano wa kimataifa.

Makamu wa Rais, amewaagiza Mabalozi hao kuhakikisha wanasimamia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi pamoja na miongozo mbalimbali kutoka Serikalini.

Makamu wa Rais amewapongeza Mabalozi hao kwa kuaminiwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwenda kuiwakilisha nchi katika Mataifa mbalimbali na kuwasihi kutumia vema imani hiyo waliyopewa.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Mabalozi, Balozi Mteule wa Tanzania nchini Oman Mhe. Balozi Maulidah Hassan amemshukuru Makamu wa Rais kwa muongozo, maelekezo na ushauri aliyotoa na kuahidi kufanya kazi kwa bidii.

Mabalozi hao wateule waliofika kwaajili ya kuaga kabla ya kwenda kwenye vituo vyao ni pamoja na Mhe. Balozi Mhandisi Zena Ahmed Said (Saudi Arabia) Mhe. Balozi Cyprian Luhemeja (Zambia), Mhe. Balozi Maulidah Hassan (Oman), Mhe. Balozi Salim Othman Hamad (Comoro), Mhe. Balozi Swahiba Mndeme (Sweden), Mhe. Balozi Noel Kaganda (Korea) na Mhe. Balozi Musa Haji Ali, Naibu Mwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York.









Utafiti mpya uliozinduliwa katika Kongamano la Feminist Conversation Space umebaini uwepo wa changamoto kubwa za ufadhili zinazowakabili wasichana na wanaharakati wa masuala ya wanawake (young feminists) katika ukanda wa Afrika Mashariki, hali inayodhoofisha utekelezaji wa shughuli zao licha ya mchango wao mkubwa katika jamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, mwakilishi wa Msichana Initiative Consolata Chikoti alisema kuwa licha ya wanaharakati hao kuwa mstari wa mbele kupigania mabadiliko katika masuala mbalimbali ikiwemo ukatili wa kijinsia, ndoa za utotoni, afya ya uzazi na haki za kiuchumi, bado wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa rasilimali za kifedha. Utafiti huo umeonesha kuwa ukosefu wa ufadhili wa uhakika ni changamoto namba moja, huku mashirika mengi yakishindwa kulipa watumishi, kuendesha miradi au hata kugharamia shughuli za msingi.

Kwa mujibu wa utafiti huo, fedha zinazopatikana mara nyingi huwa za muda mfupi, zisizo endelevu na hazitoshelezi mahitaji, huku baadhi ya ufadhili ukidumu kwa miezi michache tu. Mashirika ya ngazi ya chini na yale ya vijijini yameonekana kuathirika zaidi kutokana na changamoto za kidijitali pamoja na kushindwa kukidhi masharti magumu ya wafadhili kama vile ukaguzi wa hesabu na miundo rasmi ya taasisi.

Takwimu zinaonesha kuwa nchini Kenya, ni asilimia 38 tu ya mashirika yanayopata ufadhili wa ndani na wa kimataifa kwa pamoja, wakati asilimia 33 yanategemea ufadhili wa ndani pekee ambao mara nyingi huwa mdogo.

Aidha, katika ukanda mzima, baadhi ya makundi hasa yanayoshughulikia masuala ya pembezoni hupata chini ya dola 1,000 kwa mwaka licha ya jukumu lao kubwa katika kushughulikia changamoto za kijamii.

Mbali na changamoto za kifedha, utafiti huo pia umebainisha kuwepo kwa vikwazo vya kijamii na kiusalama, ikiwemo upinzani kutoka kwa jamii, vitisho, unyanyasaji wa mtandaoni pamoja na ukosefu wa huduma za afya ya akili kwa wanaharakati hao.

Hata hivyo, wadau wameeleza kuwa pamoja na changamoto hizo, wanaharakati wa kike wameendelea kuonesha uimara kwa kuandaa na kuendesha harakati katika maeneo mbalimbali kwa rasilimali chache lakini kwa dhamira kubwa.

Katika hatua nyingine, uzinduzi huo uliambatana na kutambulishwa kwa Mfuko wa Wasichana na Wanaharakati wa Kike Afrika Mashariki (East African Girls and Young Feminist Fund), unaolenga kubadili mfumo wa ufadhili kwa kuzingatia uaminifu, kusaidia uongozi wa ngazi ya chini na kuleta mageuzi katika utoaji wa rasilimali.

Washiriki wa kongamano hilo walisisitiza umuhimu wa majukwaa ya majadiliano kama Feminist Conversation Space katika kujenga mshikamano, kubadilishana uzoefu na kuimarisha mikakati ya pamoja miongoni mwa wanaharakati.

Licha ya changamoto zilizopo, matumaini yameendelea kuwepo, huku wadau wakisisitiza kuwa mshikamano na juhudi za pamoja ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha harakati za usawa wa kijinsia zinaendelea kukua na kuleta mabadiliko chanya katika jamii.




•Zilifichwa zenye mfumo wa AC na maeneo mengine ya basi hilo

*Ni basi linalofanya safari kati ya Mombasa, Kenya na Dar es Salaam

Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imefanikiwa kukamata dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 101.2 katika la Tabata Kibo jijini Dar es Salaam zikiwa zimefichwa katika basi la abiria aina ya Yutong la kampuni ya Abood lenye namba ya usajili T 181 EMJ lililokuwa likifanya safari kati ya Mombasa, Kenya na Dar es Salaam, Tanzania.

Akizungumza leo Aprili 14,2026 Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya(DCEA) Aretas Lyimo amesema dawa hizo zilifichwa katika maeneo mbalimbali ya basi hilo ikiwemo ndani ya mfumo wa hewa (AC) kwa lengo la kukwepa kugundulika.

Kamishina Jenerali Lyimo amesema watuhumiwa waliokamatwa katika tukio hilo ni dereva wa basi Ramadhan Mohamed (52), Salma Sanga (26) kondakta, Twahilu Athuman (38), Mohamedy Mikidadi (37) na Ibrahim Mohamed (39). Mkoani Pwani kilogramu 419.09 za mirungi zilikamatwa zikiwa zinasafirishwa kuelekea Dar es Salaam.

Akifafanua kuhusu tukio hilo amesema kwa mujibu wa sheria wanaotakiwa kukamatwa ni wale ambao wanatuhumiwa kukutwa na dawa za kulevya lakini kwa kuwa waliokutwa ni dereva na kondakta ndio maana ba basi hilo nalo linashikiliwa na mamlaka hiyo kwa hatua nyingine za kisheria.

Akitoa taarifa kuhusu operesheni iliyofanywa na mamlaka hiyo katika maeneo mbalimbali nchini amesema DCEA) imefanikiwa kukamata jumla ya kilogramu 1,983.31 za dawa mbalimbali za kulevya, kilogramu 3,012.5 na lita 17,960 za kemikali bashirifu, vidonge 286 na chupa 1,001 za dawa tiba zenye asili ya kulevya.

Sambamba na ukamataji huo, ekari 55.5 za mashamba ya bangi ziliteketezwa huku watuhumiwa 77 wakikamatwa kuhusiana na makosa hayo. Katika matukio hayo, magari tisa, pikipiki 12 na bajaji moja vilikamatwa.

Akifafanua amesema uchambuzi wa takwimu umebaini ongezeko la ukamataji wa dawa za kulevya aina ya mirungi, ambapo kilogramu 1,267.12 zilikamatwa, sawa na 64 ya dawa zote zilizokamatwa mwezi huo.

“Hali hii imetokana na mkakati wa Mamlaka kujikita katika operesheni za dawa za kulevya za mashambani baada ya kudhibiti kwa kiasi kikubwa mitandao ya dawa za kulevya za viwandani.Baadhi ya matukio ya ukamataji yaliyofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.” Amesema Kamishna Jenerali Lyimo

Miongoni mwa matukio hayo amesema katika Mkoa wa Mwanza zilikamatwa kilogramu 52 za mirungi katika kizuizi cha barabarani cha Magu pamoja na Bandari ya Mwanza South, ikisafirishwa kwa kutumia gari aina ya Fuso yenye namba ya usajili T 296 APA.

Amesema dawa hizo zilikuwa zimefichwa katikati ya mizigo mingine, ikiwemo mabelo ya nguo za mitumba. Dereva wa gari hilo, Hassan Hassan (37), mkazi wa Mahina Nyamagana alikamatwa.

Aidha, wilayani Misungwi mkoani humo, kilogramu 184.9 za mirungi zilikamatwa zikiwahusisha watuhumiwa Chrispin Shoo (62) na mkewe Esther Pastory (55). Dawa hizo zilibainika ndani ya nyumba na katika vyombo vya usafiri ambavyo ni Gari aina ya Toyota Crown yenye namba ya usajili T 742 EGL, Toyota Wish yenye 2 namba ya usajili T 854 DXB, pamoja na bajaji yenye namba za usajili MC 261 EZV.

Pia amesema mkoani Tanga, zilikamatwa Kilogramu 32.95 za Mirungi ikiwa imefichwa ndani ya mfuko kwa kuchanganywa na maembe. Katika tukio hilo, Seif Omar (38), maarufu kwa jina la Haniwao, mkazi wa Mtaa wa Taifa Barabara ya 13, ambaye pia ni mjumbe wa Serikali ya Mtaa alikamatwa.

Katika operesheni nyingine zilizofanyika mkoani humo, jumla ya Kilogramu 164.01 za Mirungi zilikamatwa katika matukio tofauti.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Mhe. Balozi Stephen Mbundi, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma tarehe 13 Aprili, 2026.
 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao cha ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings 2026) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), iliyoanza Jijini Washington D.C. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba na Viongozi wengine waandamizi wa Serikali na baadhi ya Taasisi zake.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Washington, D.C)


Na Benny Mwaipaja, Washington D.C,Marekani
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amempongeza Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Balozi Elsie Sia Kanza, kwa kusimamia ipasavyo sera ya Diplomasia ya kiuchumi kati ya Tanzania na Marekani, ambapo kiwango cha ufanyaji biashara, uwekezaji na utalii kutoka nchi hizo mbili kimeendelea kukua.

Mhe. Balozi Omar ametoa pongezi hizo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani iliyotolewa na Mhe. Balozi Kanza kwa ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), iliyoanza Jijini Washington D.C.

Alisema kuwa ushirikiano wa Tanzania na Marekani umeendelea kuimarika ambapo nchi inatarajia kunufaika zaidi kutokana na mipango thabiti iliyowekwa na ubalozi ambapo miradi mbalimbali katika sekta za biashara, madini na utalii imeongezeka.

“Tunaona uwekezaji mkubwa unakuja kutoka Marekani na huko tunakokwenda tunategemea utakuwa mkubwa zaidi, ikianza kufunguka miradi mitatu minne na mmoja umeutaja upande wa madini ya niobium tunategemea kufanya vizuri zaidi. hatua ya Marriot kuongeza Hoteli kutoka11 kuelekea hoteli 20 ndani ya kipindi cha miaka mitatu inayokuja, maana yake imani ya wenzetu wa Marekani katika Sekta ya utalii inaendelea kuwa kubwa” Alisema Mhe.Balozi Omar.

Akitoa Taarifa ya utekelezaji wa Majukumu ya Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Balozi Kanza alibainisha kuwa thamani ya biashara kati ya nchi hizo imeendelea kukua kwa kasi, ikiongezeka kutoka dola za Marekani 1.15 bilioni mwaka 2023 hadi dola 1.4 bilioni mwaka 2024, sawa na ongezeko la 22.1%. Pia mauzo ya bidhaa za Tanzania Marekani yaliongezeka kwa asilimia 18 mwaka 2025 licha ya changamoto za kimazingira za biashara.

Programu ya AGOA, iliyokuwa imesitishwa tarehe 30 Septemba 2025, imeongezwa muda wa mwaka mmoja hadi 31 Desemba 2026 baada ya kuishawishi nchi hiyo iongeze muda wa kutekeleza program hiyo yenye manufaa makubwa kwa Tanzania ambapo katika miaka ya hivi karibuni mauzo ya nje ya Tanzania Kupitia AGOA yalifikia asilimia 42.85 huku takribani 95% ya mauzo hayo yakihusiana na nguo.

Kwa upande wa uwekezaji, Mhe. Balozi Dkt. Kanza alisema kuwa Kampuni za Marekani zinaendelea kupanua uwekezaji nchini Tanzania ikiwemo Kampuni ya Marriott iliyopanga kuongeza idadi ya hoteli nchini kutoka 11 hadi 20 ifikapo mwaka 2027, na kampuni ya Visa imezindua ofisi ya biashara nchini.

Pia mkataba wa uwekezaji wa dola za Marekani 300 milioni na Panda Hill Tanzania Limited umefadhiliwa na Denham, ukilenga uzalishaji wa madini aina ya niobium mkoani Songwe unaotarajiwa kuzalisha ajira ya watu takriban 600.

“Katika sekta ya utalii, Marekani imeendelea kuwa chanzo kikuu cha watalii na wawindaji wanaoitembelea Tanzania; idadi ya watalii kutoka Marekani iliongezeka kutoka 118,108 mwaka 2023 hadi takriban 145,000 mwaka 2024, huku zaidi ya 60% ya wawindaji wote wakiwa kutoka Marekani. Filamu ya “The Royal Tour” iliyoigizwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilichangia ongezeko hilo. Alifafanua zaidi Mhe. Balozi Kanza

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba na Viongozi wengine waandamizi wa Serikali na baadhi ya Taasisi zake.

Na Saidi Saidi WMJJWM- Dar Es Salaam
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, amekemea vikali uzushi unaoenezwa na baadhi ya watu wenye nia ya kupotosha jamii kuwa mwanaume akishikwa bega hupoteza sehemu zake za siri (Nyeti)

Dkt. Gwajima amekemea uzushi huo Aprili 12, 2026, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto Anayeishi na Kufanya Kazi Mtaani yaliyofanyika katika Wilaya ya Ubungo, mkoani Dar Es Salaam, yaliyolenga kuhamasisha ulinzi, malezi na ustawi wa watoto.

Akizungumzia uzushi huo, Dkt. Gwajima aliendesha zoezi la wanaume kushikana mabega, wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Albert Msando, ili kuthibitisha ukweli wa madai hayo ambapo mara baada ya zoezi hilo, wanaume walithibitisha kuwa taarifa hizo ni za uongo, kwani hakuna aliyepotelewa nyeti zake.

Aidha, Dkt. Gwajima amewataka wananchi kupuuza uzushi huo na badala yake wajikite katika shughuli za maendeleo na ustawi wa jamii huku akisisitiza umuhimu wa kujenga jamii yenye uelewa sahihi inayoweza kupambanua taarifa za kweli na za upotoshaji ili kuimarisha maendeleo endelevu ya taifa.

Katika hatua nyingine, Dkt. Gwajima amewaelekeza viongozi wa Wizara hiyo kuongeza juhudi za utoaji wa elimu kwa jamii ili kuondoa dhana potofu hiyo, akisisitiza kuwa upotoshaji wa aina hiyo unalenga kupunguza umakini wa wananchi katika ajenda za maendeleo na ustawi wa jamii.


Taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Kigoma Hilltop Hotel, Ahlulybayt Academic Center, Vision 4 All Eye Centre pamoja na Supa Foam imeendesha kambi maalumu ya siku nne ya matibabu ya macho bure kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma.

Kambi hiyo ilifanyika kuanzia tarehe 03 hadi 06 Aprili 2026 katika viwanja vya shule za Ahlulbayt Islamic Center Manispaa ya Kigoma Ujiji, ilitoa huduma mbalimbali muhimu ikiwemo uchunguzi wa macho, ushauri wa kitaalamu, utolewaji wa miwani, huduma za dawa pamoja na upasuaji wa mtoto wa jicho bila malipo.

Akizumza baada ya kukamilika kwa kambi hiyo mlezi wa Taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohsen Lalji amesema Zaidi ya wananchi 6000 walijiotokeza kupata huduma ambapo watu 5079 walifanyiwa uchunguzi wa macho, 2218 walipatiwa miwani ya macho, 518 walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho na watu 3215 walipatiwa dawa za macho huku huduma zote zikitolewa bure bila malipo.

Amesema lengo la kambi hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu kwa wakati na ukaribu zaidi.

Akizindua rasmi kambi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh Balozi Simon Sirro aliipongeza LALJI FOUNDATION na washirika wake kwa jitihada hizo za kuwafikia wananchi na kuwapatia huduma muhimu za matibabu ya macho, hususan kwa wale wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aidha, aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali katika kuboresha huduma za kijamii na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Wakizungumza baada ya kupatiwa huduma, wananchi wengi walieleza kuwa walikuwa hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu ya macho, ikiwemo upasuaji na ununuzi wa miwani, hali iliyowafanya kuendelea kuishi na matatizo ya macho kwa muda mrefu.

Wananchi hao pia waliomba juhudi kama hizi ziendelee kudumishwa ili kuwasaidia watu wengi zaidi, hasa wale wa kipato cha chini ambao bado wanakabiliwa na changamoto ya kumudu gharama za huduma za afya.

Kambi hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za wadau wa maendeleo katika kuhakikisha jamii inapata huduma bora za matibabu ya macho hususan katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kama Kigoma.




Baraza la Wafanyakazi la Nne la Tume ya Ushindani (FCC) limehitimisha kikao chake cha siku mbili kwa kuazimia kuunga mkono rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Miaka Mitano 2026/27-2030/31 unaolenga kutekeleza moja kwa moja Dira ya Taifa ya 2050.

Kikao hicho kilichofanyika tarehe 9 na 10 Aprili, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya Sunset, Manispaa ya Morogoro kiliwakutanisha wajumbe wa Menejimenti na Wawakilishi wa Watumishi kujadili ajenda kuu mbili : Rasimu ya Mpango Mkakati na Rasimu ya Bajeti ya 2026/27

Akifunga baraza hilo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza Bi. Khadija Ngasongwa alisema Mpango Mkakati huo umeandaliwa kwa kuzingatia maono ya Dira ya 2050 ya kuwa na “Uchumi shindani, jumuishi na himilivu unaochochea ustawi wa Watanzania wote”

“Baraza la Wafanyakazi ni jukwaa muhimu la ushirikishwaji. Mpango Mkakati huu tuliojadili ni nyaraka muhimu inayoonesha ramani ya safari ya Tume na unaakisi dhamira yetu ya pamoja ya kuiunga mkono Dira ya 2050 kupitia soko huru, salama kwa mlaji na linalochochea ukuaji wa uchumi shindani ,” alisema Bi. Khadija

Kupitia Azimio la Baraza, watumishi wa FCC wamekubaliana kuunga mkono kikamilifu rasimu ya Mpango Mkakati huo na kushiriki katika utekelezaji wake utakaoanza tarehe 01 Julai, 2026. Maeneo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na kukuza ushindani huru na wa haki, kupambana na bidhaa bandia na kuimarisha ulinzi wa mlaji.

Baraza hilo ambalo hukutana mara mbili kwa mwaka kwa mujibu wa sheria, limeelezwa kuwa chombo muhimu cha kuimarisha mshikamano, uwajibikaji na mawasiliano ya wazi kati ya Menejimenti na Watumishi.

“Kupitia mshikamano huu, tutaongeza ufanisi katika kusimamia ushindani wa haki na kulinda maslahi ya walaji kama sehemu ya mchango wa Tume katika kufanikisha Dira ya Taifa ya 2050,” ilisomeka sehemu ya azimio la baraza.

Uongozi wa Tume umedumisha utamaduni shirikishi katika kujadili masuala ya taasisi kimkakati. Watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya Tume kabla ya rasimu kuidhinishwa na Bodi ya Tume ya Ushindani.

FCC itaendelea kuthamini mchango wa Baraza la Wafanyakazi katika maamuzi ya kimkakati sambamba na azma ya kujenga mazingira bora ya kazi na kutoa huduma bora kwa umma.





















Leo tarehe 13 Aprili saa 22:00, Uwanja wa Old Trafford utakuwa mwenyeji wa pambano la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kati ya Manchester United na Leeds United. Mechi hii inajulikana kwa jina la "War of the Roses" kutokana na uhasama wa kihistoria kati ya mikoa ya Lancashire (Manchester) na Yorkshire (Leeds).

Kwenye msimamo, Manchester United wako nafasi ya 3 wakiwa na pointi 55 baada ya mechi 31, wakiwa na rekodi ya ushindi 15, sare 10 na kupoteza 6 . Kwa upande wa Leeds United, wako nafasi ya 15 wakiwa na pointi 33 baada ya mechi 31, wakiwa na ushindi 7, sare 12 na kushindwa 12 .

Hii ni mechi muhimu kwa United kujiimarisha kwenye nafasi ya kuwania Kombe la Ulaya, na kwa Leeds ni muhimu kukimbia eneo la kushuka daraja kwani wana pointi 3 tu juu ya Tottenham iliyopo nafasi ya 17 .

Mechi hii itasimamiwa na mwamuzi mkuu Paul Tierney anajulikana kuwa mwamuzi mkali, na kwa kuzingatia umuhimu wa mechi hii, nidhamu itakuwa muhimu sana.
a
Kwa upande wa Manchester United, kocha Michael Carrick ndiye anayeongoza timu. Carrick ameweza kujenga timu yenye nguvu ya kushambulia kwa njia mbalimbali. Wachezaji hatari wa United ni pamoja na Benjamin Sesko (mshambuliaji), Bryan Mbeumo (winga), na Bruno Fernandes (kiungo mshambuliaji) . United wana nguvu kubwa katika kuunda nafasi za kufunga, kushambulia kwa mbavu, na kumaliza nafasi .

Kwa upande wa Leeds United, kocha Daniel Farke ndiye anayeongoza. Leeds wana nguvu katika mikondo ya adhabu za moja kwa moja (direct free kicks) na mashambulizi ya mpira wa kona . Wachezaji hatari ni pamoja na Dominic Calvert-Lewin (mshambuliaji) aliye katika kiwango kizuri baada ya kufunga kwenye michezo ya kombe .

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Manchester United wamepokea habari njema ya kurudi kwa Lisandro Martinez ambaye amekosa mechi 5 za mwisho kutokana na jeraha na anatarajiwa kucheza leo . Hii ni nyongeza muhimu hasa akizingatiwa kuwa Harry Maguire hayupo kwa sababu ya kusimikwa kwa kadi nyekundu aliyopata dhidi ya Bournemouth .

Majeruhi wengine wa United ni Matthijs De Ligt (mgongo) ambaye hajacheza tangu Novemba, na Patrick Dorgu (hamstring) ambaye bado hajajiandaa kikamilifu . Benjamin Sesko na Bryan Mbeumo wanatarajiwa kuwa fiti licha ya kukosa mazoezi

Kwa upande wa Leeds, wana wasiwasi wa majeruhi wakiwemo Anton Stach (kiungo) anayekisiwa kuwa na jeraha la ligament kwenye kifundo cha mguu, na Joe Rodon (beki) aliyeumia kwa kuanguka vibaya . Pia, Daniel James anatarajiwa kukosa kutokana na jeraha la adductor . jisajili sasa

Kihistoria, timu hizi zimekutana mara 117, huku Manchester United ikishinda mara 52, Leeds mara 26, na sare 39 . Walipo kutana mwanzoni mwa msimu huu (Januari 2026) ulimalizika kwa sare ya 1-1 kwenye Dimba la Elland Road. United wamekuwa wakitawala kwenye michezo ya hivi karibuni, huku Leeds wakishindwa kufunga katika mechi zao 4 za mwisho za ligi .


Bahati imekuwa ikicheza mchezo wa kujificha, lakini sasa Meridianbet wameleta Leprechaun Wish, mchezo wa sloti unaomlipa kila mtu anayecheza. Hii sio sloti ya kawaida, ni safari ya kwenda Ireland kwenye milima ya kijani kibichi, sarafu za kuvutia, karafuu zilizojaa bahati na kofia za kichawi. Ukicheza, unahisi kama uko kwenye hadithi halisi za Irish.

Kila raundi ina msisimko, maana ndani ya mchezo kuna chungu cha dhahabu kinachokupa scatter, sarafu na alama zingine za kushangaza. Mistari 20 ya kubashiri inakuwezesha kucheza kwa mtindo yako, ukijua kila mchezo unaweza kuleta jackpot. Hapa, hakuna mtu anayechelewa, kila dakika ni nafasi ya kushinda pesa halisi.

Meridianbet wanakupa jukwaa pana la kubashiri, mechi kali za kimataifa hadi michezo ya kasino mtandaoni iliyojaa burudani. Ukiwa na odds zenye ushindani mkubwa, kila tiketi inakuwa na thamani zaidi. Jiunge sasa kupitia tovuti yao au piga *149*10#.

Na kwa wale wanaopenda mambo ya haraka, kuna kipengele cha kununua bonasi. Hii inakupa nguvu ya kuingia moja kwa moja kwenye mchezo wa ushindi. Sasa si lazima usubiri, unaweza kujaribu kila njia na kujaribu bahati yako mara moja. Hii ni nafasi ya kujaribu ushindi mkubwa.

Huu mchezo siyo tu cheza cheza, ni stori ya kushinda, kusherehekea na kujaribu bahati yako. Ireland iko mkononi mwako, na pesa ziko karibu tu. Mchezo mmoja tu, na unaweza kuwa bosi.

Hivyo, usichelewe, ingia Meridianbet, cheza mizunguko yako kadhaa, ufurahie Leprechaun Wish huku bahati ikikufanyia kazi. Hii ni safari ya raha, msisimko na pesa, yote kwa upande wako.



Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ni jambo la kawaida kwa baadhi ya watu kupinga hatua za Serikali, hasa pale maamuzi hayo yanapogusa maslahi yao binafsi—hususan kwa wale waliokuwa wakinufaika kwa njia zisizo halali.

Akizungumza leo jijini Dodoma mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Ntyuka–Mvumi–Kikombo yenye urefu wa kilomita 76, pamoja na kipande cha barabara ya Chololo–Mapinduzi (Makao Makuu ya TPDF) chenye kilomita 5, Dkt. Mwigulu alisema Serikali haitayumbishwa na kelele za wachache wanaopinga mabadiliko yenye manufaa kwa taifa.

Alieleza kuwa mara nyingi watu wanaoguswa na hatua hizo hujipanga kwa kuajiri wengine ili kuishambulia Serikali na viongozi wake kupitia mitandao au majukwaa mbalimbali ya kijamii.

“Watanzania msitishike na hao watu, kwa sababu wanafugwa huko waliko. Ili mikataba yao iendelee, ni lazima waendelee kutukana,” alisisitiza.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa mwenendo huo si wa sasa pekee, bali umekuwepo hata katika awamu zilizopita za uongozi, ambapo baadhi ya watu walikuwa wakitoa kauli za kejeli na mashambulizi dhidi ya viongozi wanaochukua hatua thabiti.

Aidha, amebainisha kuwa hata yeye binafsi amekuwa mhanga wa mashambulizi hayo, akifananisha hali hiyo na mapambano ya kiimani, ambapo wanaosimama kupinga maovu hukumbana na upinzani mkali.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, akisisitiza kuwa juhudi za Serikali ya awamu ya sita zinalenga kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha zinawanufaisha wananchi wote.

Amesisitiza kuwa miradi ya maendeleo kama ujenzi wa barabara hizo ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya Serikali katika kuboresha miundombinu na kukuza uchumi wa nchi.





Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

BANK of Africa Tanzania imezindua programu ya masuluhisho na huduma mahususi za kifedha pamoja na ushauri kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), ikiwa ni jitihada za kuboresha upatikanaji wa mikopo, elimu ya biashara na kukuza ushindani wa biashara nchini.

Uzinduzi wa programu hiyo ulipongezwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, aliyesema kuwa hatua hiyo inalenga kuboresha mahitaji ya kifedha ya wajasiriamali kupitia huduma, mikopo na elimu ya biashara.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika Tawi la Lumumba jijini Dar es Salaam, Tutuba alisema tukio hilo linaashiria hatua muhimu katika kuimarisha masuluhisho ya kifedha kwa SMEs na kukuza sekta binafsi.

“Mpango huu unaonyesha mabadiliko chanya katika sekta ya benki, kutoka mfumo wa ukopeshaji wa jumla kwenda kwenye huduma jumuishi za kifedha zinazolenga mahitaji maalum ya wateja,” alisema.

Aliongeza kuwa SMEs ni uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania, zikichangia takribani asilimia 95 ya biashara zote na asilimia 35 ya Pato la Taifa (GDP), huku zikitoa ajira kwa zaidi ya watu milioni tano.

Aidha, alisema mpango huo unaendana na Mkakati wa Taifa wa Huduma Jumuishi za Fedha (2023–2028) unaolenga kuhakikisha Watanzania wanapata huduma za kifedha nafuu na za kuaminika. Alitaja makundi ya kipaumbele kuwa ni pamoja na wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, wakulima na wavuvi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Bank of Africa Tanzania, Esther Cecil Maruma, alisema mkakati huo umejengwa katika uelewa wa kina wa mahitaji ya SMEs.

“Tunataka kuwezesha biashara kukua kwa kasi, kushindana vyema na kudumu kwa muda mrefu kupitia masuluhisho yanayojibu changamoto zao moja kwa moja,” alisema.

Alieleza kuwa huduma mpya zilizozinduliwa ni pamoja na ufadhili wa ankara (invoice discounting), overdraft, mikopo ya muda mfupi na mrefu, ufadhili wa mali na magari, dhamana, pamoja na huduma za biashara za kimataifa.

Maruma alisisitiza kuwa benki inalenga kuwa mshirika wa kweli wa ukuaji wa biashara, si mtoaji wa mikopo pekee.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji – Biashara, Hamza Cherkaoui, alisema wameboresha huduma ili ziwe rahisi, zenye unyumbufu na zinazoendana na mahitaji halisi ya biashara.

Naye Mjumbe wa Bodi, Waziri Kindamba, aliipongeza benki hiyo kwa ubunifu huo unaolenga kutatua changamoto za wajasiriamali.

Kwa upande wake, mteja wa muda mrefu wa benki hiyo, Mohammed Bahasawan, alisema mpango huo ni fursa muhimu kwa wafanyabiashara kukuza mitaji na biashara zao.

“Nimekuwa mteja wa benki hii kwa miaka mingi, na ninaamini huu ni mwanzo wa suluhisho la changamoto nyingi za wajasiriamali nchini,” alisema.
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Tutuba (katikati), akikata utepe kuzindua Programu ya masuluhisho na huduma mahususi za kifedha na ushauri kwa wafanyabiashara wa kati na wadogo (SMEs)wa Bank of Africa, jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji - Bank of Africa, Esther Cecil Maruma, Mjumbe wa Bodi - Bank of Africa - Mkurugenzi, Waziri Kindamba (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Biashara wa benki hiyo, Hamza Cherkaoui (kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uendeshaji wa Bank of Africa, Wasia Mushi.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha SME wa Bank of Africa, Beatrice Richard, akielezea jambo kwa Mgeni rasimi, Gavana wa Emmanuel Tutupa na Viongozi wa benki hiyo, alipotembelea eneo jipya maalum kwa wateja wa SME wakati wa uzinduzi juzi.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutupa na Mjumbe wa Bodi wa Bank of Africa, Waziri Kindamba na Mkurugenzi Mtendaji - Bank of Africa, Esther Cecil Maruma (kulia walio kaa) wakiwa katika picha ya pamoja na wateja wa benki hiyo, wakati wa uzinduzi wa masuluhisho na huduma mahususi za kifedha na ushauri kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs).

Top News