TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, imeendelea na vikao vyake leo Februari 14, 2026 kwa kukutana na Balozi wa Kudumu wa Tanzania Ofisi rasmi za Umoja wa Mataifa huko Geneva, Uswiswi, Dkt Abdallah Possi na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Ufalme wa Ubelgiji na Mkuu wa Ubalozi wa Tanzania kwa Umoja wa Ulaya (EU), Jestas Nyamanga.

Mkutano huo wa Tume na Mabalozi hao umefanyika katika ukumbi wa Tanganyika uliopo jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Tume kukusanya taarifa, maoni na ushauri kutoka kwa viongozi mbalimbali.

Kwa Pamoja Balozi Possi na Balozi Nyamanga walijadili namna matukio ya uvunjifu wa amani yalivyoanza, athari zake kwa wananchi, mali zao na miundombinu, pamoja na mapendekezo ya namna ya kudhibiti na kuzuia matukio kama hayo yasijirudie siku zijazo.

Vilevile, katika mkutano huo hoja zilizojadiliwa zilihusu maeneo ya tathmini ya athari za matukio hayo na ushauri wa hatua za kijamii na kisheria zinazoweza kuchukuliwa ili kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa.

Tume inaendelea kukutana na makundi mbalimbali ikiwemo waathirika wa matukio ya uvunjifu wa amani katika mikoa tofauti nchini, kwa lengo la kukusanya ushahidi na taarifa zitakazoiwezesha kuandaa ripoti ya kina.







 

 

Tuzo hiyo imetolewa tarehe 13 Februari 2026, katika hoteli ya King Jada Dar es Salaam na taasisi ya kimataifa inayojishughulisha na kutoa mafunzo, vyeti, na viwango vya taaluma ya huduma kwa wateja (customer service) na vituo vya kupokea simu (call centers inayoitwa Chartered Institute of Customer Management (CICM) Tanzania. 

Tuzo hii inaonesha namna MSD ilivyoboresha huduma zake kwa wateja kwa hasa za upatikanaji wa bidhaa za afya kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini. 

MSD hadi sasa inahudumia vituo vya kutolea huduma za afya 8,893 nchi nzima, huku vituo vyote vikipelekewa bidhaa hizo hadi mlangoni mara sita kwa mwaka.

Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji Hassan Ali ameeleza kuwa tangu kufanyika kwa maboresho Bohari ya Dawa, bidhaa za aina mbalimbali zimekuwa zikisambazwa kuendana na kasi ya uhitaji wa huduma hizo, ikiwemo mashine za kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo,  mashine za usingizi na hata zile za kuwezesha huduma za afya ya kinywa na meno ambazo huduma zote hutekelezwa kwa kuzingatia misingi ya huduma kwa wateja iliyowekwa.

Ameongeza kuwa MSD ina mifumo ya kisasa ya kuwasiliana na wateja kama  vile Customer Portal, ujumbe wa simu (bulky sms), pamoja na Call Center ambapo zote hizi huwezesha kuwasiliana na wateja na kutatua changamoto mbalimbali.





Na Mwandishi wetu, Ngorongoro.

Kama wewe unahisi Penzi lako linalegalega na kuishiwa Pawa hujachelewa, mshawishi mpenzi, mume au mke wako mje Bustani ya Edeni katika hifadhi ya Ngorongoro. Shuhuda za wanyama wakubwa watano, mandhari ya kuvutia yaliyopambwa na sauti za ndege porini pamoja na harufu nzuri ya maua ya bustani ya Edeni yatalipa Nguvu Penzi lako kwa kulinogesha na kuligongelea Msumari.

Mamia wamejitokeza leo tarehe 14/02/2026,  kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao (Valentine’s Day), wakichagua hifadhi hiyo kama sehemu maalum ya kuonesha mapenzi na kufurahia vivutio vya utalii kwenye kivutio cha utalii namba moja Afrika.

Watalii waliotembelea Ngorongoro  wameshiriki matembezi ya utalii, upigaji picha za kumbukumbu na shughuli mbalimbali zilizowawezesha kufurahia mazingira ya hifadhi kwa namna tofauti na sherehe za mijini. 

Mmoja wa watembezi hao Juma Shemoka na Mpenzi wake Radhia El-had wanaelezaa uzoefu huo umeongeza thamani ya sikukuu hiyo kwa kuunganisha burudani, mapumziko na kujifunza kuhusu uhifadhi wa mazingira na jinsi Wanyamapori wanavyoishi na kuthihirisha thamani ya upendo.

Hivi karibuni mamlaka hiyo ilizindua huduma mpya ya Wedding Tourism, inayowezesha wanandoa na wachumba kufanya harusi, kuvishana pete pamoja na sherehe nyingine za kimahaba ndani ya maeneo ya hifadhi ambapo huduma hiyo inalenga kupanua bidhaa za utalii na kuvutia makundi mapya ya wageni wa ndani na nje ya nchi kufurahia mapenzi ndani ya maeneo tulivu ya hufadhi.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Afisa Masoko Mkuu  Ngorongoro, Michael Makombe, alisema mwitikio mkubwa wa wananchi unaonesha kuwa juhudi za kukuza utalii wa ndani zinaendelea kuleta matokeo chanya. 

Karibu Ngorongoro ambapo maajabu saba yanayojumuisha asili ya binadamu, mazalia ya nyumbu, Kasoko ya Ngorongoro, maisha ya watu, wanyamapori, malikale, Jiolojia na vingine vingi vinakutana katika eneo moja.






 

-Ataka uchunguzi wa matumizi ya fedha na ununuzi wa vifaa hospitalini hapo.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 14, 2026 ameweka jiwe la msingi la Hospitali ya Wilaya Kilindi iliyojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 2.64 ambapo kati ya fedha hizo shilingi 2.51 ni kutoka Serikali Kuu, Shilingi milioni 50 ni za mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi milioni 89.9 ni kutoka Benki ya Dunia 

Ujenzi wa Hospitali hiyo umesaidia kuwapunguzia  wananchi adha na gharama kubwa za matibabu ambazo walilazimika kuzifuata katika Wilaya za jirani.

Pamoja na kuridhishwa na ubora wa majengo katika hospitali hiyo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu amemtaka Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga kufuatilia na kujua ni kwanini idadi ya majengo yaliyopo ni machache kuliko yaliyokusudiwa ikiwa fedha yote ya utekelezaji wa mradi ilitoka.

“Majengo yapo kwenye viwango vizuri, ila fedha iliyokuja ilikuwa ijenge majengo mengi zaidi lakini mmejenga pungufu, fedha nyingine ipo wapi?, michezo ya upotevu wa fedha za Serikali hatuwezi ivumilia”








 

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Mkoa wa Kagera kanali Yahaya Ramadhani  Kido amesema suala la ulinzi na usalama litakuwa kipaumbele chake  cha kwanza kutokana na mkoa huo una mipaka yenye uingiliano mkubwa na nchi jirani.

Katika hafla fupi ya hati ya makabidhiano kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Fatma Mwassa ,Kanali Kido amesema suala la ulinzi na usalama wa nchi sio la kubembelezana isipokuwa Kila mtanazania  anapaswa kutoa taarifa haraka pale anapomtilia mashaka mgeni yeyote anayeingia nchini bila kibari.

"Kagera ni mkoa wa kimkakati nyote mtakuwa mlisikia maagizo ya Mheshimiwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuhusu ulinzi na usalama hivyo naomba vyombo vya usalama tuchukue hatua kukabiliana na wimbi la wahamihaji wanaokimbilia katika mkoa huu kufuga ,kulima kujimilikisha,hii nchi ni yetu na sio Mali ya wageni kutoka nje "amesema.

Aidha amesema  pia kipaumbele chake cha pili ni kuhakikisha miradi ya kimkakati yote inatekelezwa na kukamilika kwa wakati kwani miradi hiyo ndio yenye kuchochea Uchumi kwa wananchi.

“Miradi inayotekelezwa katika halmashauri lazima iendane thamani ya fedha na ikamilike ili kusogeza huduma Bora kwa wananchi wa mkoa wa Kagera.”

Awali kabla ya makabidhiano aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Fatma Mwassa amesema Mkoa wa Kagera unakabiliwa na changamoto ya wahamihaji kutoka nchi za Burundi,Rwanda,Uganda na nchi nyingine za Sudan Na congo 

Amesema kwa mwaka 2024 hadi Novemba 2025 wahamihaji haramu walioingia nchini na kurudishwa walikuwa 17,200 na kati ya hao asilimia 85,ilitoka Burundi ,asilimia 5 Rwanda ,asilimia 5 Uganda na asilimia Nyinginezo .

“İdadi hiyo ni kubwa sana na inahitaji kuchukua hatua za haraka na weledi mkubwa kwani wengi ufata aridhi marisho na vibarua na baadhi wakifika wanaoa na kuolewa.”

Pia amesema mkoa huo unamiradi mingi inayotekelezwa huku akitaja kuwa uchumi wa Kagera kwa miaka mingi  umekwama kutokana na kutokuwa na maamuzi ya kuwaweka vijana katika mpango mkakati wa kuwapatia kipato cha mwaka mzima kupitia sekta za kilimo mifugo na uvuvi na wengi wakitegemea ajira kutoka serikalini.

Fatma Mwassa amewashukuru  wananchi na viongozi kwa ushirikiano na mipango thabiti ya kuendeleza mkoa huo ikiwemo mpango mkakati wa kuwapatia ajira vijana 2,000 Kila halmashauri kupitia Sekta ya kilimo ,mifugo,uvuvi na viwanda.





 



Na Mwandishi wetu - Dodoma

SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa mahusiano nchini kwa lengo la kutambulisha jukumu la sekta hiyo na kukusanya maoni yatakayosaidia kuandaa na kuboresha nyaraka za uimarishaji wa mahusiano.

Akizungumza Februari 13, 2026 jijini Dodoma wakati wa ziara yake katika Makao Makuu ya Baraza la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu imefungua milango kwa wadau wote wakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za dini na vyama vya siasa ili kushirikiana katika kujenga taifa lenye mshikamano.

“Tumekutana kujadili namna ya kuimarisha mahusiano na kuendeleza ushirikiano. Utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unategemea amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa,” alisema Sangu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa NaCoNGO, Jasper Makala, aliishukuru Serikali kwa kuitambua na kuiheshimisha sekta ya mashirika yasiyo ya kiserikali, akisema ziara hiyo imeimarisha mazungumzo na ushirikiano kati ya Serikali na sekta hiyo.

Amesema NaCoNGO itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kulinda amani na kusimamia maadili kupitia mifumo yao ya ndani, ili kuhakikisha mashirika wanachama yanafuata miongozo na taratibu zilizowekwa.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika ambao unaongozwa na Kaulimbiu ya Mwaka 2026 inayosema: “Kuhakikisha Upatikanaji Endelevu wa Maji na Huduma Salama za Usafi wa Mazingira ili Kufikia Malengo ya Ajenda 2063.” Kaulimbiu hiyo inalenga kuhimiza hatua za pamoja za bara katika kuhakikisha usalama wa rasilimali maji, afya ya jamii, na maendeleo endelevu.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia Mheshimiwa Abiy Ahmed pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika, tarehe 14 Februari, 2026 jijini Addis Ababa, Ethiopia.

 

KIGOMA

Baraza la Ushindani(FCT), moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, imeendesha kikao cha kuwajengea uwezo watumiaji wa huduma, wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za ushindani na taratibu za rufaa.

Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Lake Tanganyika Hotel na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara na huduma.

Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Ndg. Deogratias Sangu, aliwataka wananchi kutumia elimu waliyoipata kuelewa haki zao katika ushindani na udhibiti wa soko. Alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani utasaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kujenga mazingira ya Soko yenye usawa na haki.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa FCT, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahim, alisema Baraza lina jukumu la kusikiliza na kuamua rufaa zinazotokana na maamuzi ya Fair Competition Commission (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti wa sekta mbalimbali ikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.

Aliwahimiza wananchi wa Kigoma kulitumia Baraza hilo wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya vyombo husika, akisisitiza kuwa mfumo wa rufaa umewekwa kisheria ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati na kwa uwazi.

“Watu wakijua wapi pa kupata haki, wanapunguza gharama za kuhangaika kutoka sehemu moja ya huduma hadi nyingine,” alisema Mhe. Jaji Ebrahim, akisisitiza kuwa elimu ya sheria ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wananchi na wafanyabiashara kukua kiuchumi.

Wadau waliohudhuria kikao hicho waliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kuimarisha taasisi zinazolinda na kusimamia haki za wafanyabiashara na watumiaji wa huduma.

Walisema juhudi hizo zinaonyesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi kupitia mfumo wa ushindani ulio wazi, shindani na wa haki, unaochochea ukuaji wa biashara na ustawi wa taifa.

     


Top News