Habari Za Hivi Punde Habari Za Hivi Punde
Soma zaidi NA FARIDA MANGUBE
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mheshimiwa Prof. Riziki Silas Shemdoe (Mb), ameipongeza Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa kazi kubwa ya kuunganisha mawasiliano ya barabara kutoka kijiji hadi kijiji na wilaya hadi wilaya, akisema kuwa jukumu hilo ni gumu na linahitaji weledi, uzalendo na utendaji wa hali ya juu.
Prof. Shemdoe alitoa pongezi hizo alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Isago lenye urefu wa mita 42.6 katika Kata ya Mngeta, Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, mkoani Morogoro, akiwa katika ziara ya kikazi ya tarehe 2 hadi 6 Julai 2026 Mkoani humo.
Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya mradi iliyosomwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emmanuel Ndyamukama, Waziri Shemdoe amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya barabara na madaraja ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi.
"TARURA mmefanya kazi kubwa sana ya kuunganisha wananchi kupitia mtandao wa barabara vijijini. Kazi hii si rahisi; inahitaji utaalamu, kujituma na uwezo wa kufanya kazi katika mazingira magumu. Serikali inatambua mchango wenu na inawapongeza kwa juhudi zenu za kuhakikisha wananchi wanapata huduma za usafiri na usafirishaji wakati wote," amesema Prof. Shemdoe.
Aidha, Waziri huyo aliwataka mkandarasi na mshauri wa mradi kuongeza kasi ya utekelezaji ili mradi ukamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika, huku akisisitiza matumizi sahihi ya fedha za umma na ubora wa kazi zinazotekelezwa.
Mhandisi Emmanuel Ndyamukama ni Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro, amesema mradi wa ujenzi wa Daraja la Isago ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kuboresha miundombinu katika maeneo ya uzalishaji vijijini, kuimarisha uchumi na kuongeza uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na majanga ya asili.
Mkataba wa ujenzi wa daraja hilo ulisainiwa tarehe 15 Desemba 2025 kati ya Katibu Mkuu wa TAMISEMI na kampuni ya ENGISOFT Company Limited kwa thamani ya shilingi bilioni 1.738 (bila kodi), huku usimamizi wa mradi ukifanywa na kampuni za LUPTAN Consults Ltd kwa kushirikiana na Afro Base & ORU Consults.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 42.6, barabara za maingilio zenye urefu wa mita 300, ujenzi wa makalvati mawili pamoja na kuinua tuta katika eneo la mradi.
Utekelezaji ulianza rasmi Januari 1, 2026 na unatarajiwa kukamilika Agosti 30, 2026. Hadi sasa, utekelezaji umefikia asilimia 20, huku mkandarasi akiwa amelipwa malipo ya awali yenye jumla ya shilingi milioni 260.7.
Daraja la Isago linatarajiwa kuunganisha kwa urahisi maeneo ya kilimo kati ya Mngeta na Isago, kurahisisha usafiri wa wananchi kufikia huduma muhimu za elimu, afya na biashara, pamoja na kupunguza athari za mafuriko ambazo zimekuwa zikisababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo.
Mhandisi Ndyamukama imesema mradi umekumbwa na changamoto ya kuchelewa kwa utekelezaji kutokana na mvua kubwa za msimu zilizonyesha mkoani Morogoro na kuathiri baadhi ya shughuli za ujenzi.
Kwa upande wao Watumiaji wa Barabara na wakazi wa Kata ya Mngeta akiwemo Rajabu Sudi amesema kukamilika kwa daraja hilo kutarahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo kwenda sokoni, kupunguza gharama za usafiri na kuongeza fursa za biashara na uwekezaji katika eneo hilo.
Nae Elizabeth Sanga mkazi wa Kijiji cha Isago amesema kwa miaka mingi walikuwa wakipata shida kuvuka eneo hilo kipindi cha mafuriko, hali iliyosababisha wanafunzi kukosa masomo, wagonjwa kushindwa kufika kwenye vituo vya afya kwa wakati na wafanyabiashara kuchelewa kufikisha bidhaa zao sokoni.
Amesema ujenzi wa daraja hilo ni suluhisho la kudumu ambalo litabadilisha maisha ya wakazi wa eneo hilo.
Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limesema litaendelea kuimarisha huduma za mawasiliano nchini kwa kuendeleza matumizi ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kupanua huduma za kidijitali na kuwekeza katika teknolojia za kisasa ili kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa kidijitali.
Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Moremi Marwa, amesema mafanikio yanayoendelea kupatikana ndani ya shirika hilo yametokana na maboresho ya kiutendaji na kibiashara yaliyofanyika katika kipindi cha hivi karibuni, hatua ambayo imewezesha TTCL kuongeza mapato, kupata faida na kuboresha huduma kwa wananchi.
Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Marwa alisema TTCL imeutumia mkutano huo kama jukwaa la kuonesha teknolojia na huduma mbalimbali zinazochochea maendeleo ya uchumi wa kidijitali kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano.
Alisema miongoni mwa huduma zinazotolewa ni intaneti ya kasi ya juu ya Supersonic Speed, kituo cha FTTX Experience Center kinachowawezesha wananchi kujionea matumizi ya teknolojia ya nyumba janja (Smart Home), pamoja na huduma za Cloud Computing kupitia Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data (National ICT Data Centre – NIDC).
Marwa alifafanua kuwa huduma za Cloud Computing zinazotolewa kupitia NIDC zinawapa wateja fursa ya kuhifadhi taarifa na mifumo yao kwa usalama wa hali ya juu bila kulazimika kuwekeza gharama kubwa katika miundombinu ya kuhifadhi data, jambo linalosaidia kuongeza ufanisi wa shughuli za taasisi na biashara.
Akizungumzia utendaji wa shirika hilo, alisema TTCL imepata faida ya takribani shilingi bilioni 23 katika mwaka wa fedha 2024/2025, huku matokeo ya awali ya mwaka wa fedha 2025/2026 yakionyesha kuongezeka kwa mapato, faida na idadi ya wateja wanaotumia huduma za shirika hilo.
Alisema mafanikio hayo yametokana na utekelezaji wa maboresho ya kimkakati yaliyofanywa kufuatia maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha TTCL linaendeshwa kwa misingi ya kibiashara, linaongeza mapato na kuondokana na utegemezi wa hasara.
Marwa alisisitiza kuwa TTCL itaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuboresha miundombinu ya mawasiliano ili kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora, salama na za uhakika zinazochangia maendeleo ya uchumi wa kidijitali na Taifa kwa ujumla.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI ya GF Group imeandika historia kwa kutwaa tuzo ya Banda Bora kwa Ujumla katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa mwaka wa pili mfululizo, mafanikio ambayo yameelezwa kuwa ni matokeo ya ubunifu, nidhamu, mshikamano na kujituma kwa wafanyakazi wake.
Akizungumza na Wafanyakazi pamoja na Wadau Mbalimbali Mkurugenzi Mtendaji wa GF Group Imran Karmali amesema tuzo walioipata ni ushindi ulipatikana sio kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya uthibitisho wa dhamira ya kampuni ya kuwa kinara katika sekta ya magari na viwanda nchini Tanzania.
Amesema kuwa miaka 19 tangu kuanzishwa kwake GF Group kutoka kuwa na maono ya kawaida hadi kuwa miongoni mwa makundi makubwa ya biashara ya magari nchini, ikiwa inawakilisha chapa mbalimbali za kimataifa, kuunganisha magari hapa nchini, kuwekeza katika maendeleo ya watu, kuzalisha ajira na kuchangia ukuaji wa sekta ya viwanda.
Ilielezwa kuwa kampuni hiyo haijikiti tena katika uuzaji wa magari pekee, bali sasa inaunganisha magari nchini, inaleta teknolojia mpya, inajenga uwezo wa wataalamu wa ndani na kuwekeza katika uzalishaji unaoifanya Tanzania kuwa kitovu cha maendeleo ya sekta ya magari.
Aidha, GF Group imetangaza hatua nyingine muhimu ya kihistoria kwa kuanza kuingiza sokoni bidhaa zinazobeba chapa yake yenyewe ya GF, hatua ambayo inaonyesha uwezo wa kampuni hiyo kutengeneza na kukuza bidhaa za Kitanzania zenye ubora wa kimataifa.
Kwa mujibu wa kampuni hiyo, lengo si kutengeneza magari kwa ajili ya Tanzania pekee, bali kuzalisha bidhaa zinazobuniwa kwa mahitaji ya Afrika, kutengenezwa nchini Tanzania na kuaminiwa katika duniani.
Karmali amesema tuzo hiyo haihusu uzuri wa banda pekee, bali ni ishara ya kutambuliwa kwa ubunifu, weledi, maono na uwezo wa kutekeleza mipango mikubwa kwa mafanikio.
Hata hivyo amesema wafanyakazi wa GF Group walihimizwa kuendelea kuwa mabalozi wa kampuni kwa kuhakikisha kila huduma wanayotoa, kila uamuzi wanaoufanya na kila gari wanalolizalisha linaendelea kujenga sifa ya kampuni hiyo ndani na nje ya Tanzania.
Amesema GF Group katika sekta ya magari duniani inaendelea kubadilika kutokana na ujio wa magari ya umeme na teknolojia za kidijitali, hivyo kampuni imejipanga kuwa sehemu ya kuunda mustakabali huo badala ya kuusubiri.
Uongozi huo ulisisitiza kuwa ushindi wa mwaka huu ni hatua moja tu katika safari ndefu ya kujenga kampuni ya Kitanzania inayoweza kushindana na kampuni bora barani Afrika kwa ubora wa bidhaa, ubunifu, uadilifu, uzalishaji wa kisasa na uwezo wa kuunda fursa kwa Watanzania.
Karmali amesema wafanyakazi wote wana mchango wao katika mafanikio hayo huku akiahidi kuendelea kuinua viwango vya utendaji na kuacha urithi utakaowanufaisha vizazi vijavyo.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
JUMLA ya wananchi 1,940 wamepata huduma za uchunguzi wa macho na ushauri wa kitabibu bila malipo katika Banda la MIXX kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika banda hilo, Mtaalamu wa Macho na Huduma kwa Jamii kutoka Taasisi ya Bilal Muslim, Patrick Martine, alisema huduma hiyo imewezesha wananchi kupimwa afya ya macho na kupatiwa miwani bure kulingana na mahitaji yao.
Alisema kati ya wananchi waliopimwa, watu 41 walibainika kuwa na tatizo la mtoto wa jicho na wataendelea kupatiwa matibabu kupitia Taasisi ya Bilal Muslim.
Martine alisema ushirikiano kati ya MIXX na Taasisi ya Bilal Muslim umewezesha wananchi wengi kupata huduma ambazo kwa kawaida zingehitaji gharama kubwa, huku akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo kabla ya maonesho kumalizika.
Aidha, alieleza kuwa baadhi ya changamoto za macho zinazoongezeka kwa sasa zinachangiwa na matumizi ya muda mrefu ya vifaa vya kielektroniki kama televisheni na simu, pamoja na sababu nyingine za kiafya zinazohitaji uchunguzi wa mapema.
Kwa upande wake, Meneja wa Banda la MIXX, Omega Mwakifuna, alisema utoaji wa huduma za macho ni sehemu ya mkakati wa kampuni wa kurudisha kwa jamii kwa kuwasaidia wananchi kupata huduma muhimu za afya bila gharama.
Alisema MIXX itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha wananchi wote watakaotembelea banda hilo na kuhitaji huduma za macho wanapata fursa ya kupimwa na kupatiwa ushauri wa kitaalamu.
Baadhi ya wananchi walionufaika na huduma hiyo wameipongeza MIXX kwa kuwaletea huduma karibu yao.
Mkazi wa Kijichi, Cecilia Kapituka, alisema amepimwa macho na kupatiwa miwani miwili bure, jambo ambalo limemsaidia kupata suluhisho la tatizo lililokuwa likimsumbua kwa muda mrefu.
Naye mkazi wa Mabibo, Daud Bernad, alisema amefurahishwa na huduma hiyo baada ya kupimwa na kupatiwa miwani bila malipo, huku akiwahamasisha wananchi wengine kutembelea Banda la MIXX katika Maonesho ya Sabasaba ili kunufaika na huduma hiyo muhimu.
*Yawahamasisha Wananchi Kutumia Umeme kwa Ufanisi na gharama nafuu
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limewahimiza Watanzania kutembelea banda lake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) ili kujionea teknolojia mbalimbali za kisasa zinazolenga kuboresha matumizi ya umeme kwa usalama, ufanisi na gharama nafuu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Irene Gowele, alisema maonesho ya mwaka huu yamebeba ubunifu unaowawezesha wananchi kujifunza namna teknolojia ya umeme inavyoweza kuboresha maisha yao ya kila siku.
Alisema mbali na shughuli za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme, TANESCO imejikita kuonesha thamani ya matumizi ya umeme katika sekta mbalimbali za maisha na uzalishaji.
Kivutio kikubwa katika banda hilo ni Nyumba Janja (Smart Home), ambayo imewekewa mfumo wa kisasa wa umeme wa kidijitali unaoongeza usalama wa nyumba dhidi ya majanga kama moto, huku ukimruhusu mmiliki kudhibiti vifaa vya umeme akiwa popote duniani kupitia simu ya mkononi.
Gowele alisema mfumo huo humwezesha mtumiaji kuwasha au kuzima vifaa vya umeme kwa njia ya programu maalumu pamoja na kufuatilia kiwango cha umeme kinachotumiwa na kila kifaa, hatua inayosaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na gharama za bili.
Aidha, alisema TANESCO inaendelea kuhamasisha matumizi ya vifaa vinavyotumia umeme kwa ufanisi mkubwa (energy efficient), ambapo nyumba hiyo imewekewa vifaa vinavyotumia kiwango kidogo cha umeme ili kuwaonesha wananchi namna wanavyoweza kupunguza matumizi ya nishati bila kuathiri huduma.
Pia aliwakumbusha wananchi kuhusu mpango wa TANESCO wa kukopesha majiko ya umeme, akisema wanaotembelea banda hilo wanaweza kupata majiko hayo kwa kununua au kwa mkopo kwa kutumia namba ya mita ya umeme pamoja na Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kwa ajili ya uhakiki.
Alieleza kuwa majiko hayo yana ufanisi mkubwa na yana uwezo wa kupika chakula cha Kitanzania kwa gharama ya chini ya shilingi 356 za umeme, hivyo kuwa mbadala wa gharama nafuu ukilinganisha na baadhi ya nishati nyingine za kupikia.
Katika maonesho hayo, wananchi pia wanapata fursa ya kujionea kwa teknolojia ya kidijitali miradi mikubwa ya uzalishaji umeme inayotekelezwa na TANESCO, ikiwemo Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere na Mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu mkoani Shinyanga unaozalisha megawati 50.
Vilevile, banda hilo linatoa elimu kuhusu matumizi ya umeme katika sekta ya usafiri kupitia magari, pikipiki na bajaji zinazotumia umeme, huku TANESCO ikisisitiza kuwa Tanzania ina umeme wa kutosha unaoweza kusaidia wananchi kupunguza gharama za usafiri na kuchangia utunzaji wa mazingira kwa kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa.
"TANESCO imekuja ki-smart Sabasaba mwaka huu. Tunawakaribisha wananchi wote kutembelea banda letu wajifunze, wajionee teknolojia hizi na namna zinavyoweza kuboresha maisha yao huku zikipunguza gharama za matumizi ya nishati," alisema Gowele.
.png)
KILA msimu huwa na hadithi yake, lakini msimu huu wa kiangazi umefika na simulizi ambalo linaweza kubadili maisha ya mashabiki wa kasino mtandaoni. Meridianbet imezindua rasmi mashindano makubwa ya Evoplay Summer Season of Legends, kampeni inayowapa wachezaji nafasi ya kushindania zawadi kubwa zenye thamani ya hadi shilingi bilioni 1.089 za Kitanzania. Kwa dau kuanzia shilingi 600 tu, kila mchezaji ana nafasi ya kuanza safari yake kuelekea kwenye orodha ya mabingwa wa msimu huu.
Katika ulimwengu wa michezo ya kasino, kuna wakati ambapo bahati hukutana na ujasiri, na hapo ndipo hadithi za mabingwa huzaliwa. Mashindano haya ya Evoplay yameundwa mahsusi kwa wapenzi wa ushindani wanaotaka kuona majina yao yakipanda kwenye msimamo. Kila mzunguko unaochezwa huongeza nafasi ya mchezaji kukusanya pointi na kupanda daraja. Mfumo huu wa mashindano unahakikisha kuwa kila sekunde ya mchezo ina maana, kila ushindi una thamani, na kila mchezaji ana nafasi ya kuwa sehemu ya historia mpya ya Meridianbet.
Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba na nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10#.
Msisimko wa mashindano haya unazidi kuongezeka kutokana na mkusanyiko wa michezo maarufu inayoshiriki. Michezo kama Queen of Sirens, Hot Triple Sevens Hold & Win, Imperial Relics: Three Pots, Budai Reels pamoja na Cycle of Luck, zimeandaliwa ili kuwapa washiriki uzoefu wa kipekee unaochanganya burudani, mkakati na matarajio ya ushindi mkubwa. Kila mchezo una hadithi yake, lakini yote yana lengo moja la kumfanya mchezaji kuwa sehemu ya hadithi ya mabingwa.
Tofauti na mashindano mengi ya kawaida, Evoplay Summer Season of Legends imegawanywa katika hatua mbalimbali kila mwezi, jambo linalowapa washiriki nafasi nyingi zaidi za kujaribu bahati zao na kuboresha nafasi zao kwenye uongozi. Kwa vijana wengi wanaopenda burudani ya kidijitali, hii ni nafasi ya kuonesha uwezo wao, kushindana na marafiki zao, na kuandika simulizi mpya za ushindi ambazo zinaweza kukumbukwa kwa muda mrefu.
Kadiri joto la kiangazi linavyoendelea kupanda, ndivyo pia ushindani katika Evoplay Summer Season of Legends unavyozidi kuwa mkali. Meridianbet imefungua mlango kwa kila mchezaji mwenye ndoto ya kuwa bingwa, na sasa ni wakati wa kuchukua hatua. Ingia kwenye mchezo, weka dau lako la kuanzia shilingi 600, kusanya pointi zako, na pambana kupanda kileleni mwa ubao wa viongozi. Msimu huu unaweza kuwa mwanzo wa safari yako ya kuwa legend mpya.

LEO Julai 5, 2026, saa 23:00, Uwanja wa MetLife, New Jersey, utashuhudia pambano kali la michuano ya Dunia kati ya Brazil na Norway. Hii ni mechi ya Raundi ya 16 ambayo inaahidi burudani na mivutano mikubwa. Brazil, yenye mataji matano ya duniani, inatafuta kuvunja rekodi isiyofurahisha ya kutokuwahi kuishinda Norway katika pambano zima la kimataifa.
Kihistoria, Norway ni "kiboko" kwa Brazil, kwa kuwa katika michezo yote minne iliyopita, Brazil haijapata ushindi wowote. Tukio la kukumbukwa zaidi lilifanyika katika mashindano ya Dunia la 1998 huko Ufaransa, ambapo Norway iliibuka na ushindi wa 2-1 baada ya Brazil kuongoza kwa bao la Bebeto, na kufanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora. Rekodi hii inawapa Norway imani kubwa, wakijua wana uwezo wa kuwapa taabu Wabrazil.
Kwa upande wa Brazil, chini ya ufundi wa Carlo Ancelotti, wanaingia mechi hii wakiwa na rekodi nzuri ya kutooshindwa katika mechi zao zote tatu za makundi na ushindi wa 2-1 dhidi ya Japan katika Raundi ya 32. Hata hivyo, wana wasiwasi wa jeraha la kiungo Lucas Paqueta, ambaye ni muhimu katika kuunda mashambulizi na kudhibiti mchezo wa kati.
Ancelotti anatarajiwa kubadilisha mbinu na kucheza kwa tahadhari zaidi, wakizingatia kuziba nafasi na kuzuia mashambulizi ya Norway, hasa wakipinga mipango ya kukabiliana haraka ya Norway na mchezaji wao hatari, Erling Haaland.
Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.
Norway, wanaorejea kwenye michuano ya Dunia baada ya miaka 28, wamekuwa wakiendelea kuonyesha nguvu kubwa ya mashambulizi. Wao ni timu pekee ya Ulaya iliyofuzu kwa rekodi safi ya ushindi nane kwa nane katika mechi za kufuzu, wakifunga mabao 37.
Martin Odegaard ndiye kiungo anayeongoza mashambulizi, wakati Erling
Haaland akiwa na rekodi ya mabao 5 tayari katika michuano hii, anatarajiwa kuwa tishio kwa ulinzi wa Brazil, wakisaidiwa na winga mahiri Antonio Nusa. Jisajili sasa
Hivyo basi, mechi hii ya leo inakuja na uzito mkubwa wa kihistoria na mbinu. Brazil inatafuta kulipa kisasi na kuvunja ukame wa miaka 24 wa kutoshinda taji la Dunia, wakati Norway inatarajia kuendeleza rekodi yao ya kutowahi kushindwa na Brazil na kufanikisha safari yao ya kurudi katika hatua za juu za michuano. Hii ni mechi ambapo mkakati, uvumilivu, na uwezo wa kuzuia makosa makubwa ndio vitaamua.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (CCM) ambaye ni mlezi wa CCM Mkoa wa Dodoma, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameshiriki Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dodoma, kilichofanyika katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dodoma leo tarehe 04 Julai 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jaji. Joseph Sinde Warioba, katika makazi yake, Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam.
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu alama za kiusalama zilizopo kwenye noti za Tanzania ili kuwawezesha kutambua tofauti kati ya Sarafu halali na bandia, sambamba na kuhamasisha utunzaji sahihi wa fedha ili zisiharibike au kuchakaa mapema.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Julai 4, 2026, Afisa kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sarafu BoT, Shadrack Mapunda, amesema taasisi hiyo ina jukumu la kuandaa mahitaji ya sarafu, kuzitengeneza na kuhakikisha zinapatikana kwa kiwango kinachokidhi mahitaji ya uchumi.
Mapunda amesema upangaji wa mahitaji ya fedha huzingatia mambo mbalimbali ikiwemo kasi ya ukuaji wa uchumi, ongezeko la idadi ya watu, maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya utengenezaji wa sarafu, ameongeza kuwa BoT huhifadhi noti na sarafu zilizotengenezwa katika maghala maalumu yaliyopo kwenye ofisi zake saba nchini pamoja na vituo vidogo vya kusambazia fedha kwa kushirikiana na benki za biashara kwenye maeneo ambayo hawana ofisi.
Aidha, amesema BoT imekuwa ikiendesha kampeni za elimu kwa umma kuhusu alama za kiusalama zilizopo kwenye sarafu za Tanzania ili wananchi waweze kuzitambua kwa urahisi na kuepuka kupokea noti bandia katika shughuli zao za kila siku.
Mapunda amesisitiza kuwa sheria za nchi zinakataza mtu yeyote kuharibu sarafu kwa makusudi, akieleza kuwa anayebainika kufanya kitendo hicho anakuwa ametenda kosa na ataadhibiwa kwa kifungo kisichopungua miezi sita, au faini ya kuanzia shilingi 500,000, au adhabu zote mbili kulingana na uamuzi wa mahakama.
Pia amewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba kufika kwenye ofisi za Benki Kuu ya Tanzania ili kupata elimu zaidi kuhusu sarafu za Tanzania, alama zake za kiusalama pamoja na majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na Benki kuu ya Tanzania (BoT).
Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Julai 4, 2026, Afisa kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sarafu BoT, Shadrack Mapunda, amesema taasisi hiyo ina jukumu la kuandaa mahitaji ya sarafu, kuzitengeneza na kuhakikisha zinapatikana kwa kiwango kinachokidhi mahitaji ya uchumi.
Mapunda amesema upangaji wa mahitaji ya fedha huzingatia mambo mbalimbali ikiwemo kasi ya ukuaji wa uchumi, ongezeko la idadi ya watu, maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya utengenezaji wa sarafu, ameongeza kuwa BoT huhifadhi noti na sarafu zilizotengenezwa katika maghala maalumu yaliyopo kwenye ofisi zake saba nchini pamoja na vituo vidogo vya kusambazia fedha kwa kushirikiana na benki za biashara kwenye maeneo ambayo hawana ofisi.
Aidha, amesema BoT imekuwa ikiendesha kampeni za elimu kwa umma kuhusu alama za kiusalama zilizopo kwenye sarafu za Tanzania ili wananchi waweze kuzitambua kwa urahisi na kuepuka kupokea noti bandia katika shughuli zao za kila siku.
Mapunda amesisitiza kuwa sheria za nchi zinakataza mtu yeyote kuharibu sarafu kwa makusudi, akieleza kuwa anayebainika kufanya kitendo hicho anakuwa ametenda kosa na ataadhibiwa kwa kifungo kisichopungua miezi sita, au faini ya kuanzia shilingi 500,000, au adhabu zote mbili kulingana na uamuzi wa mahakama.
Pia amewahimiza wananchi wanaotembelea Maonesho ya Sabasaba kufika kwenye ofisi za Benki Kuu ya Tanzania ili kupata elimu zaidi kuhusu sarafu za Tanzania, alama zake za kiusalama pamoja na majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na Benki kuu ya Tanzania (BoT).
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema imetumia Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu yake, fursa zilizopo katika sekta ya mbolea pamoja na mnyororo wa thamani wa uagizaji, utengenezaji na usambazaji wa mbolea nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Julai 4, 2026, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini wa TFRA, Joshua Ng’ondya, amesema mamlaka hiyo imefika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, umuhimu wa upimaji wa udongo, pamoja na utaratibu wa kujisajili ili kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku.
Amesema kupitia maonesho hayo, wananchi na wafanyabiashara wanapata maelekezo ya namna ya kupata leseni za biashara, kusajili maeneo ya biashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mbolea, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika biashara ya mbolea nchini.
Ng’ondya amesema TFRA ina jukumu la kudhibiti ubora wa mbolea za viwandani na mbolea hai zilizosajiliwa, pamoja na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyotakiwa kabla ya kuingia sokoni na katika mpango wa ruzuku kwa wakulima.
Aidha, ameeleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu kuhusu namna ya kutengeneza, kusajili na kuingiza mbolea sokoni kwa kufuata taratibu zilizowekwa, ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora, salama na zenye tija katika kuongeza uzalishaji wa mazao.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Julai 4, 2026, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini wa TFRA, Joshua Ng’ondya, amesema mamlaka hiyo imefika kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, umuhimu wa upimaji wa udongo, pamoja na utaratibu wa kujisajili ili kunufaika na mpango wa mbolea za ruzuku.
Amesema kupitia maonesho hayo, wananchi na wafanyabiashara wanapata maelekezo ya namna ya kupata leseni za biashara, kusajili maeneo ya biashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mbolea, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika biashara ya mbolea nchini.
Ng’ondya amesema TFRA ina jukumu la kudhibiti ubora wa mbolea za viwandani na mbolea hai zilizosajiliwa, pamoja na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyotakiwa kabla ya kuingia sokoni na katika mpango wa ruzuku kwa wakulima.
Aidha, ameeleza kuwa mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu kuhusu namna ya kutengeneza, kusajili na kuingiza mbolea sokoni kwa kufuata taratibu zilizowekwa, ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea bora, salama na zenye tija katika kuongeza uzalishaji wa mazao.
Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
TAASISI zinazojihusisha na sekta ya ubaharia zimetakiwa kuimarisha ushirikiano ili kuwawezesha wanafunzi wanaohitimu masomo ya ubaharia kupata ajira kwenye meli mbalimbali na kuchangia ukuaji wa sekta hiyo nchini.
Wito huo umetolewa leo Julai 4, 2026 na Kiongozi wa Taasisi ya Mission for Seafarers, Father Johnson Lameck, wakati wa maadhimisho ya Siku Maalumu ya Kuwakumbuka na Kuwaombea Dua Mabaharia waliotangulia mbele za haki.
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Father Lameck alisema Tanzania imejaliwa kuwa na bahari pamoja na fursa nyingi za uchumi wa buluu, hivyo kuna umuhimu wa taasisi zinazohusika na sekta ya ubaharia kushirikiana katika kuwaandaa wahitimu na kuwaunganisha na soko la ajira.
“Hapa nimesikia zipo taasisi mbalimbali. Tuone namna gani tunaweza kushirikiana na wanaosomesha mabaharia na kuwapatia vyeti. Kazi zao ni za meli na shughuli nyingine mbalimbali,” alisema.
Alisema kuna haja ya taasisi hizo kushirikiana na Chuo cha Mabaharia Dar es Salaam (DMI) ili wanafunzi wanaomaliza masomo wapate nafasi za ajira kwenye meli mbalimbali.
“Tuone namna gani tunaweza tukajikondesha na DMI ili wanafunzi hawa wanaomaliza waweze kupata ajira kwenye meli hizo. Hicho ndicho kilio chao kikubwa pale kwetu. Tunafahamu na tunaangalia namna gani tunaweza kusaidia wakapata ajira kwenye meli mbalimbali,” alisema.
Aidha, aliwataka viongozi wa taasisi mbalimbali kuweka mikakati ya pamoja ya kuwawezesha vijana kupitia miradi mbalimbali itakayochochea maendeleo yao na kuimarisha sekta ya ubaharia.
Pia alisisitiza kuwa sekta ya uchumi wa buluu ina fursa kubwa za ajira na maendeleo, akihimiza vijana kuzitumia rasilimali za bahari kujijengea uchumi na kuchangia maendeleo ya taifa.
Kwa upande mwingine, Father Lameck alitoa salamu za pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao baharini na kuwataka Watanzania kuendelea kuwaombea ili wapate faraja na nguvu wanapoendelea kuwakumbuka waliotangulia mbele za haki.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka rekodi mpya katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya jumla ya Shilingi trilioni 37.96 katika mwaka wa fedha 2025/26, sawa na asilimia 105.24 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni 36.07.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, leo Julai 04, 2026 imeeleza kuwa mafanikio hayo katika makusanyo ya kodi ni sawa na ukuaji wa asilimia 17.61 ikilinganishwa na makusanyo ya Shilingi trilioni 32.27 yaliyopatikana katika mwaka wa fedha 2024/25.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na kuendelea kutumia mbinu za kisasa katika usimamizi wa kodi, kuimarisha uzingatiaji wa sheria za kodi pamoja na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Takwimu zinaonyesha kuwa katika miezi yote 12 ya mwaka wa fedha uliomalizika Juni 2026, TRA ilifanikiwa kuvuka malengo ya makusanyo ambapo kwa Mwezi Juni wameweka rekodi mpya kwa kukusanya Shilingi trilioni 4.01, sawa na ufanisi wa asilimia 107.98, huku Januari, Machi na Aprili pia zikifanya vizuri kwa kuvuka malengo yaliyowekwa.
Katika taarifa hiyo, TRA imeeleza kuwa mafanikio hayo yameiwezesha mamlaka hiyo kuweka rekodi mpya nne katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali nchini, hatua inayodhihirisha kuendelea kuimarika kwa mifumo ya kodi na usimamizi wa mapato.
Mamlaka hiyo imewahakikishia wananchi na wadau mbalimbali kuwa itaendelea kuboresha huduma kwa walipakodi, kuimarisha matumizi ya teknolojia na kuhakikisha mapato ya Serikali yanaongezeka kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma za kijamii.
Mafanikio ya TRA yanatarajiwa kuongeza uwezo wa Serikali kutekeleza bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27 kupitia mapato ya ndani, sambamba na kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo ya nje.
TRA yavunja rekodi ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo mbali na kuvuka malengo ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo, TRA pia imeweka rekodi mpya ya kukusanya mapato kwa miezi 24 mfululizo kuanzia Julai 2024 hadi Juni 2026, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mamlaka hiyo.
Katika kipindi hicho, wastani wa ufanisi wa makusanyo umefikia asilimia 104.64.
Aidha, mwezi Desemba 2025 uliweka historia mpya baada ya TRA kukusanya Shilingi trilioni 4.13 ndani ya mwezi mmoja, kiwango kilichovunja rekodi ya awali ya Shilingi trilioni 3.58 iliyowekwa Desemba 2024.
Kwa mwaka wa fedha 2025/26, wastani wa makusanyo ya kila mwezi umefikia Sh. trilioni 3.16, kutoka wastani wa Sh.trilioni 2.69 uliopatikana mwaka 2024/25.
Mafanikio hayo yameelezwa kuwa yametokana na uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kusimamia mageuzi ya ukusanyaji wa mapato kwa kusisitiza utii wa sheria za kodi, kuhamasisha ulipaji wa hiari, kupanua wigo wa walipakodi, kuimarisha matumizi ya mifumo ya TEHAMA na kuhakikisha kodi zinazokusanywa zinatumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika kipindi hicho, TRA imekamilisha ujenzi wa Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani (IDRAS), ulioanza kutumika rasmi Februari 2026. Mfumo huo umeunganishwa na mifumo ya taasisi 52 za umma na taasisi 30 binafsi, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato na kurahisisha utoaji wa huduma kwa walipakodi.
Vilevile, kampeni za kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari zimeendelea kuzaa matunda, ambapo kiwango cha utii wa walipakodi kimeongezeka kutoka asilimia 77.48 mwaka 2020/21 hadi asilimia 85.71 mwaka 2024/25, huku pengo la kodi likipungua hadi asilimia 1.89.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, utekelezaji wa sera za kiuchumi zinazolenga kuhimili misukosuko ya uchumi duniani umechangia kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji na biashara nchini, hali iliyowezesha TRA kufikia ufanisi wa makusanyo wa wastani wa asilimia 105.24 katika mwaka wa fedha 2025/26, sambamba na ukuaji wa mapato wa asilimia 17.61.
Katika taarifa hiyo, TRA imeeleza kuwa mafanikio hayo yameiwezesha mamlaka hiyo kuweka rekodi mpya nne katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali nchini, hatua inayodhihirisha kuendelea kuimarika kwa mifumo ya kodi na usimamizi wa mapato.
Mamlaka hiyo imewahakikishia wananchi na wadau mbalimbali kuwa itaendelea kuboresha huduma kwa walipakodi, kuimarisha matumizi ya teknolojia na kuhakikisha mapato ya Serikali yanaongezeka kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma za kijamii.
Mafanikio ya TRA yanatarajiwa kuongeza uwezo wa Serikali kutekeleza bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27 kupitia mapato ya ndani, sambamba na kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo ya nje.
TRA yavunja rekodi ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo mbali na kuvuka malengo ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo, TRA pia imeweka rekodi mpya ya kukusanya mapato kwa miezi 24 mfululizo kuanzia Julai 2024 hadi Juni 2026, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mamlaka hiyo.
Katika kipindi hicho, wastani wa ufanisi wa makusanyo umefikia asilimia 104.64.
Aidha, mwezi Desemba 2025 uliweka historia mpya baada ya TRA kukusanya Shilingi trilioni 4.13 ndani ya mwezi mmoja, kiwango kilichovunja rekodi ya awali ya Shilingi trilioni 3.58 iliyowekwa Desemba 2024.
Kwa mwaka wa fedha 2025/26, wastani wa makusanyo ya kila mwezi umefikia Sh. trilioni 3.16, kutoka wastani wa Sh.trilioni 2.69 uliopatikana mwaka 2024/25.
Mafanikio hayo yameelezwa kuwa yametokana na uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kusimamia mageuzi ya ukusanyaji wa mapato kwa kusisitiza utii wa sheria za kodi, kuhamasisha ulipaji wa hiari, kupanua wigo wa walipakodi, kuimarisha matumizi ya mifumo ya TEHAMA na kuhakikisha kodi zinazokusanywa zinatumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika kipindi hicho, TRA imekamilisha ujenzi wa Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani (IDRAS), ulioanza kutumika rasmi Februari 2026. Mfumo huo umeunganishwa na mifumo ya taasisi 52 za umma na taasisi 30 binafsi, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato na kurahisisha utoaji wa huduma kwa walipakodi.
Vilevile, kampeni za kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari zimeendelea kuzaa matunda, ambapo kiwango cha utii wa walipakodi kimeongezeka kutoka asilimia 77.48 mwaka 2020/21 hadi asilimia 85.71 mwaka 2024/25, huku pengo la kodi likipungua hadi asilimia 1.89.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, utekelezaji wa sera za kiuchumi zinazolenga kuhimili misukosuko ya uchumi duniani umechangia kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji na biashara nchini, hali iliyowezesha TRA kufikia ufanisi wa makusanyo wa wastani wa asilimia 105.24 katika mwaka wa fedha 2025/26, sambamba na ukuaji wa mapato wa asilimia 17.61.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi baada ya tafiti, kubadilishana uzoefu na stadi mbalimbali kutoka kwa Nchi zenye mbinu bora,teknolojia ya juu pamoja na uzoefu mkubwa wa kukabiliana na uhalifu,Amezindua Programu Maalumu ya Usalama,Maendeleo na Samia ambayo pia itashirikisha hatua za Mafunzo na Vifaa vya Kisasa kutoka nchi zilizoendelea Kiusalama lengo ikiwa ni kuimarisha na kuhusianisha Usalama na masuala ya Amani na Maendeleo Tanzania bara na visiwani .
Waziri Katambi amezindua Programu hiyo leo,jijini Dar es Salam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo akizungumza na mamia ya wafanyabiashara,machinga,madereva bodaboda,mamalishe na babalishe amesema suala la amani na usalama ni jukumu la kikatiba la serikali iliyochaguliwa na wananchi.
Amesisitiza kuwa kipaumbele cha Rais Samia ni Nchi Kwanza, Wananchi kwanza na Uchumi kwanza.
“Wizara hii ina dhamana ya masuala ya Ulinzi na Usalama, ina dhamana ya ulinzi wa kila raia, ina dhamana ya ulinzi wa kila mali ya raia, ina dhamana ya ulinzi wa Rasilimali za Taifa pamoja na mali za Taifa zinazomilikiwa na Umma" alisema Katambi
“Taarifa yoyote,maelezo yoyote,kauli yoyote,uchochezi wa aina yoyote unaolenga kuhatarisha amani ya mtu mmoja ambae ni raia wa Tanzania,sisi kama Serikali kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977 Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao na rasilimali za nchi ni jukumu la Serikali kwa kuhakikisha wananchi wanakua salama kwenye mazingira ya uzalishaji na shughuli za maendeleo”aliongeza Waziri Katambi
Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa wafanyabiashara,bodaboda,machinga,babalishe na mamalishe walisema wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwawekea mazingira sahihi ya kufanya shughuli zao huku wakiweka wazi nia yao ya kutotumika na kikundi cha watu wachache wanaotaka kuchafua amani ya nchi.
Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Ayoub Mohammed Mahmoud,Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo,Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,SACP William Mkonda,Viongozi wa Wafanyabiashara,Bodaboda,Wamachinga,Mamalishe na Babalishe pamoja na wananchi.
Waziri Katambi amezindua Programu hiyo leo,jijini Dar es Salam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo akizungumza na mamia ya wafanyabiashara,machinga,madereva bodaboda,mamalishe na babalishe amesema suala la amani na usalama ni jukumu la kikatiba la serikali iliyochaguliwa na wananchi.
Amesisitiza kuwa kipaumbele cha Rais Samia ni Nchi Kwanza, Wananchi kwanza na Uchumi kwanza.
“Wizara hii ina dhamana ya masuala ya Ulinzi na Usalama, ina dhamana ya ulinzi wa kila raia, ina dhamana ya ulinzi wa kila mali ya raia, ina dhamana ya ulinzi wa Rasilimali za Taifa pamoja na mali za Taifa zinazomilikiwa na Umma" alisema Katambi
“Taarifa yoyote,maelezo yoyote,kauli yoyote,uchochezi wa aina yoyote unaolenga kuhatarisha amani ya mtu mmoja ambae ni raia wa Tanzania,sisi kama Serikali kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977 Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao na rasilimali za nchi ni jukumu la Serikali kwa kuhakikisha wananchi wanakua salama kwenye mazingira ya uzalishaji na shughuli za maendeleo”aliongeza Waziri Katambi
Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa wafanyabiashara,bodaboda,machinga,babalishe na mamalishe walisema wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwawekea mazingira sahihi ya kufanya shughuli zao huku wakiweka wazi nia yao ya kutotumika na kikundi cha watu wachache wanaotaka kuchafua amani ya nchi.
Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Ayoub Mohammed Mahmoud,Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo,Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,SACP William Mkonda,Viongozi wa Wafanyabiashara,Bodaboda,Wamachinga,Mamalishe na Babalishe pamoja na wananchi.
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itakamilisha mchakato wa kuunda Halmashauri ya Mwibara ili kusogeza huduma za Serikali karibu na wananchi na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za kijamii na maendeleo.
Ametoa kauli hiyo leo Julai 4, 2026, alipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Halmashauri ya Mji wa Bunda mkoani Mara, baada ya Mbunge wa Bunda Vijijini, Mhe. Boniface Mwita Getere, kuwasilisha ombi la wananchi la kuanzishwa kwa halmashauri hiyo.
Waziri Mkuu alisema Serikali imepokea hoja hiyo na kutambua umuhimu wake, akibainisha kuwa utaratibu wa kuanzisha halmashauri mpya utaendelea kufuatwa ili kuhakikisha huduma za Serikali zinawafikia wananchi kwa ufanisi zaidi.
"Nimeipokea hoja hii. Serikali ina utaratibu unaofuatwa katika kugawa maeneo ya kiutawala. Nimemuelekeza Mkuu wa Mkoa pamoja na Sekretarieti ya Mkoa kuendelea na mchakato huo ili Serikali iweze kupeleka mapendekezo kwenye mamlaka husika kwa hatua zinazostahili," alisema Waziri Mkuu.
Alisema Serikali imeendelea kutekeleza sera ya kusogeza huduma karibu na wananchi, ndiyo sababu imekuwa ikiendelea kuanzisha maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji wa kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma.
Katika kufafanua hatua za utekelezaji wa Serikali, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange, alisema Serikali itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma katika Wilaya ya Bunda kupitia uwekezaji katika sekta za afya, elimu na miundombinu, huku ikikamilisha hospitali, vituo vya afya na kuongeza watumishi wa sekta ya afya.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, alisema Serikali itaendelea na mpango wa kupanga matumizi bora ya ardhi na kupima vijiji, sambamba na kuimarisha mfumo wa usimamizi wa ardhi ili kudhibiti migogoro ya umiliki na kuhakikisha hati mbili hazitolewi katika eneo moja.
Naye Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, alisema Serikali itaendelea kukamilisha Mradi wa Maji wa Onyamswa pamoja na miradi mingine ya maji katika Bunda, akisisitiza kuwa kipaumbele ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kabla ya ujenzi wa miundombinu ya utawala.
Aidha, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, alisema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Mara, huku wananchi wa maeneo ya mijini yenye sifa za vijijini wakiendelea kunufaika na utaratibu wa kuunganishiwa umeme kwa gharama nafuu.
Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha utawala bora na kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia uanzishwaji wa maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji, sambamba na kuendelea kuwekeza katika sekta za afya, elimu, maji, nishati na miundombinu ya maendeleo.
Ametoa kauli hiyo leo Julai 4, 2026, alipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Halmashauri ya Mji wa Bunda mkoani Mara, baada ya Mbunge wa Bunda Vijijini, Mhe. Boniface Mwita Getere, kuwasilisha ombi la wananchi la kuanzishwa kwa halmashauri hiyo.
Waziri Mkuu alisema Serikali imepokea hoja hiyo na kutambua umuhimu wake, akibainisha kuwa utaratibu wa kuanzisha halmashauri mpya utaendelea kufuatwa ili kuhakikisha huduma za Serikali zinawafikia wananchi kwa ufanisi zaidi.
"Nimeipokea hoja hii. Serikali ina utaratibu unaofuatwa katika kugawa maeneo ya kiutawala. Nimemuelekeza Mkuu wa Mkoa pamoja na Sekretarieti ya Mkoa kuendelea na mchakato huo ili Serikali iweze kupeleka mapendekezo kwenye mamlaka husika kwa hatua zinazostahili," alisema Waziri Mkuu.
Alisema Serikali imeendelea kutekeleza sera ya kusogeza huduma karibu na wananchi, ndiyo sababu imekuwa ikiendelea kuanzisha maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji wa kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma.
Katika kufafanua hatua za utekelezaji wa Serikali, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange, alisema Serikali itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma katika Wilaya ya Bunda kupitia uwekezaji katika sekta za afya, elimu na miundombinu, huku ikikamilisha hospitali, vituo vya afya na kuongeza watumishi wa sekta ya afya.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, alisema Serikali itaendelea na mpango wa kupanga matumizi bora ya ardhi na kupima vijiji, sambamba na kuimarisha mfumo wa usimamizi wa ardhi ili kudhibiti migogoro ya umiliki na kuhakikisha hati mbili hazitolewi katika eneo moja.
Naye Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, alisema Serikali itaendelea kukamilisha Mradi wa Maji wa Onyamswa pamoja na miradi mingine ya maji katika Bunda, akisisitiza kuwa kipaumbele ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kabla ya ujenzi wa miundombinu ya utawala.
Aidha, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, alisema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Mara, huku wananchi wa maeneo ya mijini yenye sifa za vijijini wakiendelea kunufaika na utaratibu wa kuunganishiwa umeme kwa gharama nafuu.
Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha utawala bora na kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia uanzishwaji wa maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji, sambamba na kuendelea kuwekeza katika sekta za afya, elimu, maji, nishati na miundombinu ya maendeleo.
Subscribe to:
Posts (Atom)




.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)













.jpeg)




.jpeg)





