MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema, TET imejipanga kuhakikisha shule zote za Serikali zinafikiwa na vitabu kabla hazijafunguliwa.

Dkt. Komba ameyasema hayo leo Januari 10, 2026 alipotembelea ghara la TET la kuhifadhia vitabu vya kiada lililopo Mikocheni Jijini Dar es Salaam.

Amesema, tayari Serikali imechapa vitabu ya madarasa yote yanayotekeleza Mtaala ulioboreshwa na vitabu vya kujazia kwa madarasa yaliyoanza kutekeleza Mtaala ulioboreshwa mwaka 2023, pamoja na vitabu vya madarasa yanayoelekea kukamilisha Mtaala wa zamani.

"Mwaka huu wa fedha Serikali imechapa vitabu ya madarasa yote yanayotekeleza Mtaala ulioboreshwa, huku akisisitiza TET imechapa vitabu vya kujazia kwa madarasa yaliyoanza kutekeleza Mtaala ulioboreshwa, pamoja na vitabu vya madarasa yanayoelekea kukamilisha Mtaala wa zamani." Amesema Dkt. Komba.

Aidha, Dkt Komba amesema jumla ya nakala 18,628 ambazo zimejumuhisha Elimu ya Awali, Elimu ya msingi darasa la tano mpaka mpaka la saba, kidato cha kwanza mpaka cha nne pamoja na kidato cha tano mpaka cha sita.

Ameendelea kusema, vitabu hivyo vinavyosambazwa kwa uwiano wa kitabu kimoja, mwanafunzi mmoja na uwiano wa kitabu kimoja wanafunzi watatu.

Pamoja nanhayo Dkt. Komba ameishukuru Serikali ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipatia TET fedha za kutosha kuendelea kuchapa vitabu na kuvisambaza katika halmashauri zote nchini.

Pia, Dkt. Komba ametoa wito kwa walimu kuvitunza vitabu hivyo na kuvitumia kwa usahihi ili kuhakikisha vinaleta tija kwa maendeleo ya elimu nchini.










Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda ameipongeza taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kuendeleza juhudi za kusaidia watoto wa familia zenye uhitaji kwa kugawa sare na vifaa vya shule, akisema hatua hiyo inaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha elimu jumuishi na bora kwa wote.

Mkenda ametoa pongezi hizo wakati wa hafla ya kugawa sare na vifaa vya shule kwa watoto 400 kutoka vituo saba vya makao ya watoto jijini Dar es Salaam vilivyotolewa na taasisi ya LALJI FOUNDATION ikiwa ni sehemu ya taasisi hiyo kuunga mkono juhudi za Serikali kuinua elimu kwa watoto kutoka familia zenye uhitaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkenda amesema hatua hiyo ya kusaidia watoto walio katika mazingira magumu inaonyesha mshikamano wa taasisi binafsi na Serikali katika kuhakikisha elimu inapatikana kwa usawa na bila ubaguzi.

“Watoto hawa sasa watajiunga na wenzao mashuleni wakiwa na furaha na hali ya kujiamini Watakuwa na sare, mabegi, viatu na vifaa vya kujifunzia sawa na wenzao. Hii ni hatua muhimu katika kuondoa unyonge na kuleta matumaini mapya kwa watoto hawa,” alisema Prof. Mkenda.

Kwa upande wake, Kamishna wa Elimu Tanzania Lyabwene Mutahabwa alisema msaada huo utapunguza changamoto zinazowakabili watoto katika kuanza mwaka wa masomo.

“Watoto hawa sasa watahudhuria shuleni kwa wakati, bila kubeba mzigo wa kutafuta sare au vifaa. Hii itaongeza mahudhurio na hatimaye kuongeza ufaulu,” alisema Mutahabwa.

Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir, aliwahimiza Watanzania kutenda matendo ya huruma kwa jamii, hasa kusaidia familia zenye uhitaji.

“Kutoa kwa ajili ya wenye uhitaji ni ibada inayompendeza Mwenyezi Mungu. Wito wangu kwa jamii ni kujitoa kusaidia kadiri ya uwezo wetu, kwani thawabu ni kubwa mbele za Mungu,” alisema Mufti Zubeir.

Kwa upande wake mlezi wa taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohsin LALJI ( Sheni) alieleza kuwa taasisi hiyo itaendelea kusaidia jamii katika sekta ya elimu, afya na ustawi wa jamii, ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii.



Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, amewataka watumishi wa mamlaka hiyo kuendelea kufanya kazi kwa weledi, bidii na ubunifu ili kuhakikisha wanapata matokeo chanya katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa Nusu ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2025/26.

Bw. Mwenda ametoa wito huo Ijumaa, Januari 9, 2026, wakati akihitimisha Mkutano wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa TRA kwa Nusu ya Mwaka wa Fedha 2025/26 uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).

Amesisitiza kuwa jukumu la ukusanyaji wa kodi ni la watumishi wote wa TRA na siyo maafisa kodi pekee, hivyo kila mtumishi anapaswa kutumia weledi, ubunifu na kuzingatia maadili ya kazi ili kufanikisha lengo la TRA la kukusanya Shilingi trilioni 36.066 katika Mwaka wa Fedha 2025/26.

Aidha, Kamishna Mkuu Mwenda amesema ni matarajio yake kuona TRA inakusanya kodi kwa ufanisi mkubwa na hatimaye kuliwezesha Taifa kujitegemea kupitia mapato yake ya ndani.

“Na mimi ninatamani siku moja TRA iiwezeshe nchi yetu kuweza kujitegemea,” alisema Bw. Mwenda.

Akizungumzia mikakati ya ukusanyaji wa mapato kwa Nusu ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2025/26, Bw. Mwenda amesema TRA imejipanga kuendelea kutumia mifumo ya kisasa ya kidijitali, akitaja mfumo wa IDRAS unaotarajiwa kuanza kutumika rasmi Februari 9, 2026.

Mikakati mingine ni pamoja na kupambana na ukwepaji wa kodi, kuzuia magendo, kudhibiti mipaka, kuendelea kujenga uwezo wa watumishi kitaaluma pamoja na kuhakikisha wanapatiwa vifaa stahiki ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Pia, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuiwezesha TRA kupata watumishi wapya, huku akitoa wito kwa viongozi wa mamlaka hiyo kuhakikisha watumishi hao wanasimamiwa ipasavyo ili walete tija katika utendaji kazi wao.

Kwa upande wake, Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amewataka watumishi kuendelea kuboresha huduma kwa walipakodi, kupanua wigo wa walipakodi pamoja na kupambana na mbinu mbalimbali za ukwepaji wa kodi.

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa TRA, Bw. Moshi Jonathan Kabengwe, amewapongeza wajumbe wote walioshiriki mkutano huo na kuwataka kuyatekeleza maazimio yote yaliyofikiwa ili TRA iendelee kuvuka malengo ya makusanyo.

Aidha, amewapongeza watumishi wa TRA wanaotarajiwa kustaafu ndani ya mwaka 2026, akisema wameacha alama chanya katika utendaji wao wa kazi.

Mkutano huo wa siku tano wa tathmini ya utendaji kazi wa TRA kwa Nusu ya Kwanza ya Mwaka wa Fedha 2025/26 uliwashirikisha jumla ya washiriki 477 kutoka ofisi za TRA nchini kote.



Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya TECNO mobile limited imezindua uwanja wa kisasa katika eneo la Mwananyamala ambao utakaokuwa ukitumiwa na vijana na watoto kukuza vipaji vya mpira wa miguu katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam.

TECNO imewekeza nguvu na malengo ya kukuza tasnia ya mpira wa miguu kwa jamii ya kitanzania ikiwamo kujenga viwanja na kukuza vipaji vya vijana chini ya umri wa miaka 17 kwenye soka ikiwa ni hatua ya awali.

Akizungumza leo Januari 10,2026 wakati wa uzinduzi wa uwanja huo uliogharimu zaidi ya shilingi Milioni 70, Meneja wa TECNO nchini Tanzania, Dino Han, alisema kuwa hiyo ni hatua ya kwanza ila kampuni ina mipango thabiti ya kuendelea kuchangi katika maendeleo ya mpira wa miguu nchini Tanzania kwa kujenga viwanja vya kisasa vingi zaidi kupitia mauzo ya bidhaa zake ikiwamo simu za mkononi.

Alitoa shukrani kwa wakazi wa Mwananyamala kwa kukubaliana na jitihada zao za kuboresha kiwanja hicho ambacho kwa sasa kina muonekano wa kisasa.

“Tunawashukuru viongozi wa Serikali pamoja na wazazi wa Mwananyamala kwa kukubali kiwanja hiki kuboreshwa ili kukidhi soka la awali kwa vijana wao, Lengo letu ni kuendeleza mauzo ya bidhaa zetu ili kuboresha viwanja vingine Zaidi,”alisema.

Katika hatua nyingine ya kukuza mpira wa miguu kwa vijana, Meneja huyo alisema kupitia mpango wa Watoto wa Power Tanzania moment watoto 20 wamechaguliwa kujiunga na Academy ya Hornet ya Masaki jijini Dar es Salaam, ambapo watajifunza kwa miezi mitatu, pia wazazi wao watakabidhiwa 3,000,000 kwaajili ya kukidhi mahitaji yao na kuwa motisha ili kuendeleza vipaji vyao.

“Fedha hizi zimetokana na mauzo ya simu ya mwezi Desemba, mwaka jana, kila simu iliyouzwa Sh. 10,000 ilitengwa kwaajili ya kukuza vipaji vya mpira wa miguu, ambapo ilipatikana takriban Sh. 90,000,000,” alisema meneja huyo.

Kwa upande wake Meya wa Kinondoni, Songoro Mnyonge aliishukuru kampuni ya TECNO mobile limited kwa hatua yake ya kukuza soka nchini kwa vijana, huku akizitaka kampuni nyingine na wadau kuwekeza katika soka la vijana.

“TECNO iwe mfano kwa makampuni mengine katika jitihada za kukuza soka letu kuanzia kwa vijana, soka ni ajira na hatunabudi kutengeneza vipaji kuanzia kwa vijana wadogo. Suala la kuboresha miundombinu ya viwanja vyetu ni muhimu sana,”alisema Meya huyo.

Wakati huo huo Juma Hussein, mmoja wa wakazi wa Mwananyamala aliishukuru TECNO kwa hatua ya kuboresha kiwanja hicho akidai kuwa mtaani kuna vipaji vingi vya soka kwa vijana wadogo, ila tatizo ni kukosa viwanja vya kisasa vya kuchezea.

“Tunapokuwa na viwanja kama hivi vingi ni fursa kwa watoto wetu wenye vipaji kuviendeleza. Uwanja huu kabla ya kuboreshwa ulikuwa ni vumbi tupu, ila sasa umewekea kapeti za uzio wa kisasa, ni wajibu wetu kuutunza kwaajili ya vizazi vyetu vijavyo, alisema Hussein

Kijana Khalid Omary, ambaye pia ni mkaazi wa Mwananyamala, aliomba wadau wengine kuendelea kujitokeza katika kuibua vipaji vya soka kwa vijana wadogo. Sisi vijana wenye vipaji vya soka, mtaani tupo wengi ila wakati mwingine tunakosa mtu wa kutushika mkono kama walivyofanya TECNO, tunaomba wadau wazid kujiti kujitokeza,” alisema Omary

Na Seif Mangwangi, Hai

SERIKALI imesema imewekeza kwenye ujenzi wa mradi wa EASTRIP ili kukifanya Chuo cha Ufundi Arusha, kupitia Kituo cha Umahiri Kikuletwa, kuwa kitovu cha mafunzo ya nishati jadidifu (renewable energy) kwa ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Afrika.

Hayo yameelezwa leo 6 Januari 2026 na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa EASTRIP Kikuletwa ulioko Wilaya ya Hai Kilimanjaro.

Wanu amesema kituo hicho cha umahiri cha Kikuletwa ni cha kimkakati kwa sababu kitatoa mafunzo ya vitendo katika uzalishaji wa nishati jadidifu (nishati ya nguvu ya maji, nishati ya nguvu ya jua, nishati nguvu ya upepo, na nishati ya bioanuwai.

“ Aidha kituo hiki kitaandaa na kuwapa ujuzi (skills) vijana watakaofanya kazi katika miradi mikubwa ya kitaifa na kimataifa kama vile Bwawa la Uzalishaji Umeme la Mwalimu Nyerere na kitachochea ushirikiano wa kikanda kwa kupokea wanafunzi na wataalamu kutoka nchi mbalimbali kwa ajili ya mafunzo na tafiti,” amesema.

Ameupongeza uongozi wa chuo cha ufundi Arusha kuongeza idadi ya udahili wa wanafunzi hususani wanawake, “ haya ni mafanikio makubwa sana Kwa nchi yetu, katika kumuinua mtoto wa kike,” amesema

Amesema katika utekelezaji wa Sera ya Elimu 2014 toleo la 2023, Serikali itaendelea kuboresha Chuo cha Ufundi Arusha ili vijana waliochagua mkondo wa amali wapate fursa za kujiunga na Chuo hiki kinachosifika kwa ubora.

Wanu amesema hatua ya Wizara ya Nishati kuunganisha Chuo cha Ufundi Arusha na taasisi ya International Solar Alliance ambayo imeingia makubaliano ya kuanzisha Kituo Maalum cha Rasilimali ya Nishati ya jua ni ya kupongezwa.

“Kituo hiki kitatoa huduma kwa pamoja (one stop Center) kwa ajili ya kujenga uwezo, upimaji (testing), uwekwaji wa viwango (standardization) na uendelezaji wa teknolojia za nishati ya jua. Uwepo wa kituo hiki utachochea maendeleo kwenye uvumbuzi wa vifaa vinavyotumia nishati ya jua hapa nchini,” amesema.

Akitoa taarifa ya chuo cha ufundi Arusha, Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Chacha Musa amesema uwepo wa Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Mafunzo ya Nishati Jadidifu chini ya chuo hicho kutafungua fursa nyingi kwa Chuo, kwa jamii ya Kikuletwa na Taifa.

Amesema chuo kimejipanga kuhamasisha wanafunzi wa kitanzania wanaosoma mkondo wa amali wachague kubobea katika mafunzo ya nishati jadidifu yanayotolewa chuoni hapo katika Kampasi ya Kikuletwa ili kuchangia kuzalisha wataalamu wengi zaidi ambao watashiriki katika utekelezaji wa mkakati wa Serikali wa matumizi ya nishati safi.

“Tutahakikisha kuwa tunatangaza uwepo wa kituo hiki cha umahiri kwa makampuni yanayohusika na uzalishaji wa umeme katika nchi mbalimbali ili watumie kituo hiki kwa ajili ya kuwapatia mafunzo wafanyakazi wao,” amesema.

Amesema hatua hiyo itaiingizia Tanzania fedha za kigeni na kuboresha utoaji wa mafunzo na utajitangaza zaidi kimataifa ili kuwavutia wanafunzi kutoka nchi mbalimbali kuja kupata mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi Kikuletwa.

Profesa Chacha amesema mafunzo yatakayotolewa yatakuwa ya ubora wa hali ya juu kwa kuwa Chuo cha Ufundi Arusha ni miongoni mwa vyuo vichache sana duniani vinavyomiliki mtambo wa kufua umeme kwa nguvu za maji.

“Hatua hii pia italiingizia taifa letu fedha za kigeni, tutaendelea kuimarisha ushirikiano na taasisi na viwanda mbalimbali katika utoaji mafunzo yanayoendana na mahitaji ya soko,” amesema.

Ameishukuru Wizara ya Nishati kwa kuwaunganisha na taasisi ya International Solar Alliance (ISA) ili kuanzisha Kituo Maalum cha Rasilimali za Nishati ya jua.

“ Kituo hiki kitatoa huduma kwa pamoja (one stop Center) kwa ajili ya kujenga uwezo, upimaji (testing), uwekwaji wa viwango (standardization) na uendelezaji wa teknolojia za nishati ya jua. Uwepo wa kituo hiki utachochea maendeleo kwenye uvumbuzi wa vifaa vinavyotumia nishati ya jua,” amesema.

Aidha Profesa Chacha amesema chuo hicho kimepata mafanikio makubwa ikiwemo kufanikiwa kutengeza mitaala mipya ishirini na saba (27) inayokidhi mahitaji ya viwanda katika programu zinazohusiana na nishati jadidifu.

“ Kati ya hizo jumla ya mitaala kumi na mbili (12) imetengenezwa kwa programu za muda mrefu na mitaala kumi na tano (15) katika programu za muda mfupi,” amesema.

Pia amesema jumla ya wakufunzi thelathini na moja (31) wamefanikiwa kupata mafunzo ya viwandani kwa muda wa kuanzia mwezi mmoja na kuendelea ili kuweza kuendana na mabadiliko ya teknolojia na ujuzi unaohitajika katika viwanda.

“ Jumla ya watumishi kumi na tatu (13) wamefanikiwa kupata nafasi za kujifunza katika taasisi mbalimbali za nje ya nchi, Jumla ya makubaliano (memorundum of understanding) kumi na sita (16) na viwanda na taasisi nyingine za kielimu za nje ya nchi imefikiwa,” amesema.

Amesema chuo kimefanikiwa kufanya ufuatiliaji wa wahitimu kila mwaka ambapo katika wahitimu wa mwaka 2024 asilimia 72.5% walifanikiwa kupata ajira katika muda wa miezi sita baada ya kuhitimu na kwa upande wa wahitimu wa kike asilimia 62.6% walifanikiwa kupata ajira katika muda wa miezi sita baada ya kuhitimu.

Mafanikio mengine ni pamoja na chuo hicho kununua baadhi ya fenicha, vifaa, na vitendea kazi ikiwemo vifaa vya maabara ya nishati jadidifu kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo (testing na simulation).

Kuhusu ujenzi wa Miundo Mbinu, Profesa Chacha amesema chuo kimefanikiwa kufanya ujenzi wa majengo kumi na moja (11) katika Kampasi ya Kikuletwa na yameshakamilika.




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mazingira ya kujifunzia kwa kujenga skuli za kisasa zenye hadhi, viwango na ubora unaokidhi mahitaji ya elimu ya karne ya sasa.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Januari 2026 alipofungua Skuli mbili za Ghorofa za Ramadhan Haji Faki iliyopo Gamba, Mkoa wa Kaskazini Unguja, pamoja na Skuli ya Kifundi ya kwa niaba iliyopo Pemba.

Amesema ujenzi wa skuli hizo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuondokana na skuli za mabanda na badala yake kuwa na majengo ya kudumu yanayokidhi viwango vya kisasa vya elimu, jambo litakalosaidia kuongeza ufanisi wa ufundishaji na mafunzo. Aidha, amewahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kutumia kikamilifu fursa ya miundombinu bora iliyowekezwa na Serikali.

Akizungumzia ujenzi wa dakhalia, Rais amesema utasaidia kumaliza changamoto ya wanafunzi kukaa nje ya mazingira ya skuli, hali ambayo imekuwa ikichangia kushusha uwezo wao wa kitaaluma, na kuwasisitiza wanafunzi kutumia fursa hiyo kufanya vizuri katika masomo yao.

Akitoa taarifa ya kitaalamu kuhusu ujenzi wa Skuli ya Gamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Ndg. Khamis Abdalla Said, amesema skuli hiyo imegharimu Shilingi Bilioni 11.2 na imejengwa na Kampuni ya ZECON, ikiwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 800 kwa wakati mmoja. Ameongeza kuwa Skuli ya Kifundi ya Pemba imegharimu Shilingi Bilioni 9.4 na imejengwa na Kampuni ya SALEM Construction.

Skuli hizo zimejengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya Maendeleo ya Kiarabu (BADEA), kama sehemu ya mkakati wa kuimarisha sekta ya elimu na kukuza rasilimali watu Zanzibar.



 

Asema ndio sababu za kumteua Profesa Kabudi kuwa Ofisi ya Rais Ikulu

Na Said Mwishehe,Michuzi TVRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amesema ameteua aliyekuwa Makamu wa Rais Dk.Philip Mpango kuwa Mshauri wake katika uchumi na miradi na aliyekuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuwa mshauri wake katika mambo ya jamii.

Hivyo amesema kutokana na kuwa na washauri hao katika ofisi yake ndio maana ameamua kufanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri kwa kumteua aliyekuwa Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi amemteua kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -Kazi Maalum 

Akizungumza leo Januari 10,2026 Ikulu Dar es Salaam katika hafla ya kuwapongeza wanamichezo mbalimbali wakiwemo timu ya Taifa Stars iliyofanikiwa kuingia 16 Bora katika michuano ya AFCON ,Rais Samia ametumia nafasi hiyo kuelezea sababu ya kumteua Profesa Kabudi kuwa Ikulu.

“Pamoja na kwamba leo ni siku ya kuwapongeza wana michezo waliofanya vizuri kama vijana wangu wa Taifa Stars lakini pia shughuli hii imekuwa wakati maalum kumuaga Profesa Kabudi kutoka kwenye michezo na kuja kwangu Ikulu.

“Imekuwa mapema kubadilisha lakini kwasababu kuendana na siasa za dunia zinavyokwenda ambazo zinajicho chanya kwa Tanzania na nyingine jicho hasi kwa Tanzania.

“Pale Ikulu nahitaji akili iliyopevuka yenye maarifa mapana , uzoefu mkubwa na mtu ambaye yuko vizuri kujieleza na anaweza kulieleza jambo likaeleweka hivyo nimepiga picha serikalini kwangu kote nikasema Profesa Kabudi atanifaa

“Lakini jingine ni kwamba punde hivi nimeteua washauri wa Rais.Nimemteua aliyekuwa Makamu wa Rais kuwa mshauri wa uchumi na miradi na nimemteua aliyekuwa Waziri Mkuu atakuwa ananishauri mambo ya jamii.

“Sasa vile vichwa viwili vikubwa vinahitaji mtu aliyetulia mtulivu anayeweza kwenda nao,hawa watoto wangu wanaweza kujijibia tu ikaja kesi lakini Profesa Kabudi anaweza kwenda nao.

“Kwahiyo hiyo ndio sababu nimchukue Profesa Kabudi Ikulu aje anisaidie kazi lakini nikajipa moyo Mwana FA (Hamis Mwinjuma)na Makonda (Paul Makonda)wanaweza kuindesha Wizara ya Michezo vizuri kwasababu ni Wizara ya vijana na wao ni vijana hivyo wataweza ni vijana kwa vijana wenzao

“Ningesema Makonda afanye kazi na washauri wangu wale watu wangesema mama anamjua vizuri Makonda ? Lakini Makonda kwa vijana wenzie yuko vizur sana na Mwana FA kwa wanamistari wenzie yuko vizuri sana,”amesema Rais Samia akitoa sababu za kumteua Profesa Kabudi kwenda Ikulu.





Waziri Kombo Aagana na Waziri wa Mambo ya Nje wa China
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo, ameagana na mgeni wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mheshimiwa Wang Yi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Wang Yi alikuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kuanzia Januari 9-10 2026. Ziara hiyo ililenga kuimarisha na kuendeleza uhusiano wa kihistoria na wa kimkakati kati ya Tanzania na China.

Akiwa nchini, Mheshimiwa Waziri Wang Yi alifanya mazungumzo ya uwili na mwenyeji wake Mheshimiwa Waziri Kombo na kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kuagana, Mheshimiwa Waziri Kombo alimshukuru Mheshimiwa Waziri Wang Yi na ujumbe wake kwa kuichagua Tanzania kuwa sehemu ya ziara yake na kusisitiza kuwa ziara hiyo imezidi kuimarisha uhusiano wa kindugu, mshikamano na ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na China.

Alisema ni matarajio ya Tanzania kuona makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara hiyo yakitekelezwa kwa vitendo kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Naye Mheshimiwa Wang Yi ameiishukuru Serikali ya Tanzania kwa mapokezi na ukarimu alioupata wakati wa ziara yake na kueleza kuridhishwa na kiwango cha ushirikiano kilichopo na akaahidi kuwa China itaendelea kuwa mshirika wa karibu na wa kuaminika wa Tanzania katika juhudi zake za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.





 Na Pamela Mollel Arusha

Serikali imezitaka taasisi za umma na binafsi nchini kuongeza juhudi katika utoaji wa elimu ya ulinzi wa taarifa binafsi kwa wananchi na watumishi wake, ili kuimarisha faragha, usalama wa taarifa na haki za msingi za wananchi katika mazingira ya uchumi wa kidijitali.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Anjellah Kairuki, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo maalum kwa Maafisa wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi yaliyofanyika jijini Arusha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Kairuki alisema kuwa utoaji wa elimu kwa umma ni nguzo muhimu ya utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, akibainisha kuwa uelewa mdogo wa sheria hiyo unaweza kusababisha ukiukwaji wa faragha na haki za wananchi.

“Maafisa wa ulinzi wa taarifa binafsi mliohitimu leo mna wajibu wa kisheria kuhakikisha elimu ya ulinzi wa taarifa binafsi inatolewa ndani ya taasisi zenu. Serikali haitakubali visingizio vya kutokujua sheria, uzembe au ucheleweshaji wa utekelezaji,” alisema Waziri Kairuki.

Waziri huyo alisisitiza kuwa elimu hiyo inapaswa kutekelezwa kitaifa kwa kushirikiana na taasisi za umma na binafsi pamoja na sekta mbalimbali ikiwemo fedha, mawasiliano, afya, elimu, vyombo vya habari, asasi za kiraia na makundi mengine yote yanayohusika na ukusanyaji au uchakataji wa taarifa binafsi.

Aidha, alieleza kuwa kila Afisa wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi ana wajibu wa kuhakikisha taasisi yake inazingatia kikamilifu kanuni za uhalali, uwazi, matumizi ya taarifa kwa madhumuni mahususi, usalama wa taarifa na heshima ya faragha ya wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Bw. Adadi Mohamed, alisema kuwa Tume itaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kufahamu wajibu na haki zao, akibainisha kuwa uchumi wa kidijitali una uhusiano wa moja kwa moja na sekta ya utalii.

Bw. Adadi alionya kuwa kutotekeleza Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ni sawa na kuweka rehani faragha, usalama na haki za msingi za wananchi wanaohudumiwa na taasisi za umma na binafsi.

“Kukosekana kwa ulinzi wa taarifa binafsi kunahatarisha imani ya wananchi na kudhoofisha maendeleo ya uchumi wa kidijitali,” alisema.

Akielezea lengo la mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Dkt. Emmanuel Mkilia, alisema kuwa mafunzo hayo yalilenga kuwaandaa Maafisa wa rasilimali watu na Maafisa wa Ulinzi wa Taarifa Binafsi wenye uwezo wa kusimamia utekelezaji wa sheria ndani ya taasisi za umma na binafsi.

Dkt. Mkilia alifafanua kuwa kusudio kuu ni kuhakikisha ukusanyaji, uchakataji, uhifadhi na matumizi ya taarifa binafsi vinafanyika kwa kuzingatia kikamilifu matakwa ya Sheria, kanuni na viwango vya kitaaluma vinavyolinda haki ya faragha ya wananchi kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Kwa mujibu wa Tume hiyo, jumla ya taasisi 178 zilishiriki mafunzo hayo, ambapo taasisi 28 zilitoka serikalini, taasisi 38 kutoka sekta ya utalii na taasisi 112 kutoka sekta nyingine mbalimbali zinazojihusisha na ukusanyaji na uchakataji wa taarifa binafsi.









ZANZIBAR, January 10, 2026

Residents of Zanzibar have appealed to the Government, through the Mining Commission, to establish official mineral markets and auction centres in the Isles to enable traders, small-scale miners and investors to conduct mineral business in a transparent, secure and competitive pricing environment.

The appeal was made by members of the public who visited the Mining Commission Pavilion during the ongoing 12th Zanzibar International Trade Fair (ZITF) at Fumba. 

They noted that the absence of formal mineral markets and auction platforms has limited their full participation in mineral trading activities.

The residents said that the establishment of such markets would stimulate Zanzibar’s economic growth, create employment opportunities for youth and women, increase household incomes and curb illegal and informal mineral trade.

Through its pavilion, the Mining Commission is showcasing various investment opportunities across the mineral value chain, including mineral exploration, mining, processing, value addition, mineral trading, as well as the supply of goods and services to mining operations.

The 12th Zanzibar International Trade Fair will continue until January 16, 2026, and members of the public have been invited to visit the Mining Commission Pavilion to receive education, professional guidance and explore fast-growing investment opportunities in Tanzania’s mineral sector.



MERIDIANBET Missions inaleta mtazamo mpya kabisa wa kushiriki michezo ya kasino kwa kugeuza kila hatua ya mchezaji kuwa sehemu ya safari yenye malengo. Mfumo huu unakupa changamoto maalum zinazokusanya pointi kulingana na ushiriki wako, na hivyo kufanya kila mzunguko au mchezo uwe na maana zaidi katika safari yako ya burudani ya kidijitali.

Ndani ya Missions, mchezaji anapewa uhuru wa kuchagua misheni kulingana na mapendeleo yake. Iwe ni slot maarufu kama Gates of Olympia, Ladies Days au michezo mingine chini ya Expanse, kila chaguo linafungua fursa ya kukusanya pointi. Mfumo wa ufuatiliaji uliopo kwenye akaunti yako hukuwezesha kuona maendeleo yako kwa wakati halisi na kujua ulipoelekea.

Jisajili na Meridianbet, cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Kadri unavyoshiriki misheni mbalimbali, pointi zako zinakupandisha kutoka ngazi ya mwanzo hadi viwango vya juu zaidi. Kuanzia Bronze, kupita Silver hadi Gold, kila kiwango kinaashiria uzoefu mpana zaidi. Pointi hizi si za mapambo tu, zinatumika kama sarafu ya kununua vitu na zawadi ndani ya duka maalum la Meridianbet.

Kupitia pointi ulizokusanya, unaweza kuchagua zawadi zinazokufaa zaidi. Kuna chaguo la mizunguko ya bonasi kwa michezo ya kasino, tiketi za bonasi kwa michezo ya ubashiri, hadi zawadi za kiwango cha juu kama vifaa vya kisasa vya kielektroniki. Hii inaifanya Missions kuwa zaidi ya mchezo, ni mfumo wa kuthamini juhudi za mchezaji.

Meridianbet Missions imeundwa kwa ajili ya wale wanaopenda changamoto, mpangilio na malengo yanayoonekana. Kuanzia kujiunga hadi kukamilisha misheni zako, kila hatua inaleta msisimko mpya na motisha ya kuendelea. Mfumo huu unaongeza thamani ya burudani kwa katika kila safari ya mchezaji.

Top News