-Ammwagia sifa Rais Dkt Samia kwa Mapinduzi ya elimu


NA MWANDISHI WETU, MBEYA

MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amewataka wahitimu wa kidato cha sita nchini kuwa mabalozi wa nidhamu na uzalendo, huku akibainisha kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ni dhamira ya dhati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutengeneza taifa la wasomi wenye ushindani.

Mhe. Itunda ameyasema hayo jana wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Ivume yaliyofanyika jijini Mbeya.


Sifa kwa Rais Samia na Maboresho ya Miundombinu

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, DC Itunda amempongeza kwa dhati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumwaga mabilioni ya fedha mkoani Mbeya kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa, maabara za kisasa na mabweni.

"Chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Rais Samia, tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa wakati ili kuhakikisha watoto wetu wanasoma katika mazingira bora, jambo ambalo limeongeza morali kwa walimu na kuinua kiwango cha ufaulu," alisema Mhe. Itunda.

Wito wa Nidhamu na Uzalendo kwa Wahitimu

DC Itunda amewahimiza wahitimu hao wa Ivume Sekondari kutolewa macho na mafanikio ya muda mfupi, badala yake wazingatie nidhamu na uzalendo wanapoelekea kwenye ngazi za juu za elimu. Aliwasisitiza kuwa Serikali inawategemea kama nguvu kazi ya baadae ya Taifa.

"Nidhamu ndiyo dira ya mafanikio yenu kuanzia sasa. Tunatarajia muwe mabalozi wazuri wa Ivume na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla kule mwendako. Epukeni vitendo vinavyoweza kuharibu mustakabali wenu na wa Taifa lenu," aliongeza.

Maagizo kwa Waliobaki Shuleni

Kwa upande mwingine, Mhe. Itunda amewataka wanafunzi wanaoendelea na masomo kuongeza bidii na kuzingatia maadili mema, akionya kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo vya utovu wa nidhamu ambavyo vinakwamisha juhudi za kuinua taaluma.

Mapema, Uongozi wa Shule ya Sekondari Ivume uliishukuru Serikali ya Mkoa na Wilaya kwa ushirikiano wa karibu, ukiahidi kuendelea kusimamia taaluma na kulea vijana katika misingi ya uzalendo na uwajibikaji.





Tarehe 21 Februari 2026, 

Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Kampasi ya Tabora imefanya ziara ya kijamii katika Kituo cha Kulelea Wazee wenye Mahitaji Maalum kilichopo Ipuli, Manispaa ya Tabora. Ziara hiyo ilikuwa ni sehemu ya mikakati ya chuo kuimarisha ushirikiano na jamii.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora, Bi. Asha Churu, kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Kampasi ya Tabora, Dkt. Joseph Mbwillo, wameongoza timu  ya watumishi na wanachuo wa Kampasi ya Tabora kutembelea kituo hicho katika kujali na kusaidia wazee wenye mahitaji maalum.

Lengo kuu la ziara lilikuwa ni kuwapelekea misaada mbalimbali kwa wahitaji hao, ikiwa ni pamoja na mchele, maharage, mafuta ya kupikia na mafuta ya kujipaka, sabuni za kuogea na kufulia, nguo, sukari, mashuka pamoja na nguo katika kuboresha maisha ya wazee hao.

Pamoja na kutoa misaada hiyo, timu hiyo pia ilifanya kazi ya usafi wa mazingira ya makazi ya wazee pamoja na  zoezi la upandaji miti katika eneo hilo kwa lengo la kuimarisha ustawi wao na kuhifadhi mazingira kwa ujumla.

Ziara hii ni sehemu kuelekea kilele cha maadhimisho ya mika 25 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kwa kuonyesha mfano wa jamii inayojali na kuendeleza mazingira kwa manufaa ya wote.








 

 MAMLAKA ya Uteuzi imeongeza muda wa siku arobaini na mbili (42) kuanzia tarehe 20 Februari, 2026 Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 ili Tume iweze kukamilisha uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025 na kuitaka ikamilishe kazi na kuwasilisha Taarifa yake kabla au ifikapo tarehe 3 Aprili, 2026. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa katika gazeti la serikali Tume imeongezewa muda huo ili kutoa fursa na muda wa kutosha kwa kila mwenye taarifa, ushahidi au maoni, aliyepo nchini au nje ya nchi, kuwasiliana na Tume ili kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote, au taasisi yoyote, itakayokosa nafasi ya kusikilizwa. 

Sababu nyingine za kuongeza muda ni pamoja na zifuatazo Wingi na mchanganyiko wa taarifa zilizokusanywa, na zinazoendelea kukusanywa, na Tume ambazo zinahitaji muda zaidi wa kufanyiwa uchambuzi wa kina, Tume kulazimika kutumia Wataalamu (experts) kutoka ndani na nje ya nchi wenye uwezo wa kufanya uchunguzi wa kisayansi, na uchambuzi wa kidijitali wa baadhi ya taarifa na vielelezo kutokana na aina ya matukio na ushahidi uliokusanywa hadi sasa, na unaoendelea kuwasilishwa.

Sababu nyingine ni Tume kubaini mapengo kadhaa katika taarifa na vielelezo vilivyokusanywa hadi sasa hivyo kuhitaji kutafuta au kupata taarifa zaidi ili kukamilisha ushahidi kwa kila hoja inayohusika, Kutoa fursa kwa wadau wachache muhimu ambao kwa sababu mbalimbali bado hawajafika mbele ya Tume, licha ya kupelekewa mialiko zaidi ya mara moja. 

Taarika hiyo imewataja wadau hao kuwa ni pamoja na baadhi ya viongozi wa dini, viongozi wa baadhi ya vyama vya siasa, taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali na watu binafsi na Wingi wa wananchi wengine wanaoendelea kufika mbele ya Tume kuwasilisha taarifa, ushahidi na ushauri wao. 

Kutokana na fursa hiyo ya Tume kuongezewa muda Tume kupitia Mwenyekiti wake Jaji Othuman Chande inatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuwasilisha ushahidi kwenye Tume kwa kutumia njia zote zilizokuwa zimeainishwa awali ambazo ni majadiliano ya ana kwa ana, mawasilisho ya maandishi (written submissions) kwa njia ya posta au tovuti maalumu ya Tume; barua pepe; ujumbe mfupi wa simu (SMS); kujaza dodoso maalumu kwenye mtandao (www.tume.uchunguzi.go.tz), au kwa kupitia mitandao mingine ya kijamii.

Pia tume hiyo imetoa wito maalumu kwa baadhi ya viongozi wa dini, viongozi wa baadhi ya vyama vya siasa, taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali na watu binafsi ambao wamepewa mialiko na Tume lakini bado hawajafika mbele ya Tume kutumia fursa hii kufika au kuwasiliana na Tume kutoa mchango wao katika uchunguzi unaoendelea kwa manufaa ya wananchi, wadau na nchi kwa ujumla.

Taarifa hiyo pia kupitia Gazeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaeleza Umma umuhimu wa kuendelea kuipa Tume ushirikiano ili kuiwezesha kukamilisha kazi yake ya uchunguzi. Kama ilivyokuwa mwanzo, Tume itaendelea kufanya vikao vya wazi (public hearing) isipokuwa pale ambapo mashahidi kwa faida ya usalama wao hawapendi majina yao, sura na taarifa zao zitolewe kwenye vyombo vya habari au mitandao ya kijamii. 

Kwa mujibu wa Mpango Kazi, Tume ilipaswa kuwasilisha Taarifa kabla au ifikapo tarehe 20 Februari 2026 ikiwa ndani ya siku 90, ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 20 Novemba, 2025 mara baada ya kuzinduliwa na Mheshimiwa Rais.





Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James, amesema kuwa uongozi wa mkoa umeweka mkakati mahsusi wa kujenga mfumo thabiti na shirikishi wa kuwawezesha vijana kiuchumi, unaojumuisha mafunzo ya ujuzi, upatikanaji wa mitaji pamoja na kuwatafutia masoko ya uhakika kwa bidhaa na huduma zao.

Akizungumza Februari 20, 2026 katika hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa wajasiriamali iliyofanyika katika Ukumbi wa SIDO, Mhe. Kheri amesema hatua hiyo ni sehemu ya dira ya mkoa kuifanya Iringa kuwa kitovu cha uzalishaji na uongezaji thamani wa rasilimali zilizopo ndani ya mkoa.

Vitendea kazi hivyo vimetolewa kupitia Mradi wa SET (Skills for Employment Tanzania) unaotekelezwa na Swisscontact, ukiwa na lengo la kuwawezesha vijana waliopatiwa mafunzo kuanzisha au kupanua shughuli zao za uzalishaji kwa tija zaidi.

Mhe. Kheri amefafanua kuwa Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira rafiki yanayochochea ushirikiano kati ya sekta ya umma, sekta binafsi na wadau wa maendeleo, jambo linalorahisisha utekelezaji wa mipango ya kuwainua vijana kiuchumi.

Aidha, amebainisha kuwa mkoa wa Iringa una fursa kubwa kutokana na ardhi yake yenye rutuba kwa shughuli za kilimo, rasilimali za misitu pamoja na sekta ya utalii inayokua kwa kasi, na kusisitiza kuwa rasilimali hizo zikitumika ipasavyo zinaweza kuwa chachu ya ajira na ustawi wa vijana wengi zaidi.








Na Mwandishi WETU, Dodoma

BARAZA la Ardhi na Nyumba la Wilaya, Mkoa wa Dodoma limewasikiliza wananchi wa jamii ya Kiiraqw waliofika katika baraza hilo kuwasilisha hoja na ushahidi wao katika mgogoro wa ardhi, wakidai kumiliki kihalali shamba lenye ukubwa wa ekari nane lililopo Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma.

Hatua hiyo imekuja kutokana na maombi ya wadaawa hao ambao ni pande mbili zinazohusika katika shauri hilo, kubainisha kuwa wanakabiliwa na changamoto ya lugha, hali iliyokuwa ikiathiri uwezo wao wa kujitetea na kueleza kwa uwazi hoja zao mbele ya Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mhe. Omary Mbega.

Kutokana na hilo, Baraza lilitoa huduma ya ukalimani kupitia mkalimani, Simon Tlatlaa Emmay, ambaye alitafsiri maelezo yao na kuwawezesha wadaawa hao kufafanua kwa kina madai yao, kuwasilisha ushahidi pamoja na vielelezo muhimu bila kikwazo cha lugha.

Shauri hilo ni Shauri la Ardhi Na. 92 la mwaka 2025, linalomhusu Ekaristi Ngu’nda kama Mleta Maombi dhidi ya Lolote Nanacha na Martin Lolo Nanacha, ambao ni Wajibu Maombi.

Mgogoro huo unahusu umiliki wa shamba lenye ukubwa wa ekari nane lililopo Kitongoji cha Msunjirire, Kijiji cha Zajilwa, Kata ya Zajilwa, Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma.

Katika madai yake, Mleta Maombi anadai kuwa ndiye mmiliki halali wa eneo hilo la ardhi, akieleza kuwa ekari hizo ziliuzwa na Wajibu Maombi kwa utaratibu unaozua mgogoro wa kisheria.

Akizungumza mara baada ya kusikilizwa kwa shauri hilo, mmoja wa Wajibu Maombi, Lolo Nanacha, alisema uwepo wa mkalimani umeimarisha imani yake katika mfumo wa utoaji haki.

“Leo nimejisikia huru kueleza ukweli wangu. Nimeeleweka vizuri, na ninaamini haki itatendeka,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza hilo Omary Mbega, alisisitiza kuwa huduma ya ukalimani ni sehemu muhimu ya kuhakikisha kila mwananchi anapata haki sawa bila kujali tofauti ya lugha au asili yake.

Shauri hilo limeahirishwa hadi Aprili 15, 2026, ambapo mashahidi zaidi watasikilizwa kabla ya kutolewa uamuzi wa mwisho.



WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewapongeza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa kusimamia vizuri mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya Mbatakero na kubakiza ziada ya sh. milioni 4.33.

Ametoa pongezi hizo leo (Jumamosi, Februari 21, 2026) wakati akizungumza na wakazi wa Kata ya Weruweru mara baada ya kuzindua shule mpya ya sekondari ya Mbatakero, wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro ambayo imejengwa kupitia mradi wa SEQUIP.

Viongozi waliopongezwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Dionis Myinga, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai, Edmund Rutaraka, Mhandisi wa Wilaya, Arnold Matandiko na Afisa Elimu wa Wilaya sehemu ya sekondari, Margaret Muro.

Dkt. Mwigulu amesema ujenzi wa shule hiyo unatokana na dhamira ya dhati aliyonayo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuondoa kero zinazowasumbua wananchi. “Tunaposema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa kuna watu huwa hawatuelewi. Lakini hawa waliokuwa wakitembea km. 18 kwenda na kurudi shuleni, wao na wazazi wao wanaelewa zaidi kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Rais wetu.”

“Kama mlivyosikia, Rais Dkt. Samia anapoelezwa kuna shida, anasema viongozi watatue changamoto hiyo, ndicho kilichotokea katika shule hii ambayo wanafunzi walilazimika kutembea umbali mrefu. Katika kipindi cha miaka minne, amejenga zaidi ya shule 1,300 za sekondari na amemaliza kabisa suala lililokuwa linaitwa chaguo la pili (second selection)”.

Mapema, akitoa taarifa ya ujenzi wa shule hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Mhandisi Matandiko alisema ujenzi wake umegharimu sh. milioni 584.28 na kwamba uwepo wa shule hiyo utasaidia kuondoa adha waliyokuwa wanapata wanafunzi wa eneo hilo ya kutembea umbali km. 9 kwenda kwenda sekondari za Roo na Longoi ambazo ziko jirani na kijiji cha Mbatakero.

Alisema shule hiyo mpya ina madarasa nane, jengo la TEHAMA, jengo la utawala, maabara tatu za kemia, fizikia na baiolojia, kisima kimoja na matundu 10 ya vyoo.

Alisema wakati wa ujenzi kulikuwa na kazi zilizofanywa na wananchi ambayo thamani yake ni milioni 2.49 na hivyo kupunguza gharama, hali iliyowezesha wao kubaki na ziada ya sh. milioni 4.33 ambazo walishaomba kibali kwa Mkurugenzi zitumike kununua viti na meza za walimu ambavyo havikuwepo kwenye hela ya mradi

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Bomang’ombe hadi Kikavuchini kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 25.7 na kuzungumza na wananchi.

Meneja wa TARURA Wilaya ya Hai, Mhandishi Kuya Francis alisema ujenzi wa barabara hiyo ulianza Agosti 05, 2024 na unatarajiwa kukamilika Mei 31, 2026. “Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 70 ambapo kazi zilizofanyika ni kuandaa tabaka la kwanza la barabara km 3.5, kuweka lami km 2.5, kujenga makutano ya barabara (roundabout) na kujenga mitaro na vivuko.

Alisema hadi kukamilika kwake mradi huo utagharimu sh. bilioni 2.99 na kwamba hadi sasa wameshapokea sh. milioni 569.73 katika awamu ya kwanza ambapo taratibu za kupokea sh. milioni 861.78 za awamu ya pili zinaendelea



Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akieleza umuhimu wa Baraza la Masoko ya Mitaji katika kutatua changamoto za Masoko wakati wa kikao kati yake na Mwenyekiti wa Baraza la Masoko ya Mitaji Mhe. Jaji Dkt. Ntemi Kilekamajenga, kilichofanyika katika Ofisi za Hazina Ndogo, jijini Dar es Salaam.

Na. Josephine Majura na Peter Haule, WF, Dar es Salaam
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameitaka Mamlaka hiyo kutoa elimu kuhusu Baraza hilo ili wadau wengi waweze kulitumia kutatua changamoto zao.

Mhe. Balozi Omar, ametoa maelekezo hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Baraza la Masoko ya Mitaji ukiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhe. Jaji Dkt. Ntemi Kilekamajenga, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.

Aidha, alieleza dhamira ya Serikali ya kuendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji ili kuvutia mitaji na kukuza maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Masoko ya Mitaji, Mhe. Dkt. Ntemi Kilekamajenga, amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa Baraza hilo ni kuwa na jukwaa maalumu kwa ajili ya usikilizwaji wa migogoro inayohusu Masoko ya Mitaji.

Alisema kuwa Baraza hilo lina Mamlaka pia ya kusikiliza migogoro inayotoka kwenye Soko la bidhaa yakiwemo masuala ya stakabadhi gharani.

Kikao hicho kimehudhuliwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji, Dkt. Martin Kolikoli na Kaimu Kamishna Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha Wizara ya Fedha Bi. Dionisia Mjema.

Na Munir Shemweta, WANMM MUHEZA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Leonard Akwilapo amewaongoza Mawaziri wenzake wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na Ofisi ya Raisi Mipango na Uwekezaji katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 18 Februari 2026 katika ofisi ya Mkuu wa wilaya Muheza mkoa wa Tanga ikiwa ni utekelezaji wa masuala yaliyojitokeza wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

Mawaziri hao ni Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa TAMISEMI na Dkt. Pius Chaya, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji ambao kupitia kikao hicho, kilichohusisha pia wataalamu, viongozi hao walipata fursa ya kuwahoji wananchi walioguswa na migogoro hiyo ya mashamba ya uwekezaji ambayo yaliyofutiwa umiliki mwaka 2016.

Mashamba hayo ni Azimio/ Kilapula Geiglitz, Bwembwera, Kibaranga, Kihuhwi, Lewa pamoja na Saguras yaliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Leonard Akwilapo (wa pili kulia) akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. Wa pili kushoto ni Waziri wa TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe na kulia ni Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya na Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayubu Sebabili.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe (Wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya (Kulia) akisisitiza jambo wakati kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji kwenye wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. Katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian.

 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza Dkt. Jumaa Mhina akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. 




Baadhi ya wananchi walioguswa na mgogoro wa mashamba ya uwekezaji katika halmashauri ya Muheza mkoa wa Tanga wakielezea umiliki wao wa maeneo kwenye mashamba hayo mbele ya mawaziri wakati wa kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji tarehe 18 Februari 2026. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

 


 

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani, Dkt. Selemani Jafo, ametangaza mpango wa kuweka kambi maalum katika eneo la ujenzi wa Daraja la Kitomondo lililopo katika barabara ya Mzenga–Gwata, akilenga kuharakisha ukamilishaji wa mradi huo na kuondoa adha wanazokumbana nazo wananchi hasa nyakati za mvua.

Dkt. Jafo alitoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kata za Mzenga na Mafizi ndani ya Jimbo la Kisarawe, ambapo alikagua maendeleo ya mradi huo na kusikiliza changamoto za wananchi wanaotegemea daraja hilo kwa shughuli za kila siku.

Daraja la Kitomondo linajengwa na kampuni ya Neloyt Tanzania Limited kwa gharama ya shilingi milioni 359.67 chini ya usimamizi wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), hata hivyo ujenzi wake umechelewa kukamilika hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa Mzenga na Mafizi.

Mbunge huyo amesema daraja hilo ni kiungo muhimu kwa wakazi wa kata hizo na vijiji vya Mafizi, Nyani, Gwata na Ving’andi, akieleza kuwa kuchelewa kwake kumeathiri shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo usafiri wa wanafunzi, wagonjwa na wafanyabiashara.

Amesisitiza kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutarahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao na bidhaa, hivyo kuchochea maendeleo katika Jimbo la Kisarawe.

Kwa upande wake, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kisarawe, Eng. Africano Orota, amemhakikishia Dkt. Jafo kuwa wataongeza usimamizi na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.


SOKO la burudani ya michezo ya mtandaoni limepata msukumo mpya baada ya ushirikiano mkubwa kati ya Meridianbet na Expanse Studios, wakileta zawadi ya kipekee kupitia mchezo maarufu wa Zombie Apocalypse. Huu si mchezo wa kawaida ni uzoefu wa kipekee uliobuniwa kwa ubunifu wa hali ya juu, michoro ya kuvutia na msisimko utakaokufanya ushindwe kupepesa macho.

Kupitia ofa hii maalum, wachezaji wanapata fursa ya kucheza mizunguko 100 leo na kesho yake kupokea mizunguko 50 ya bure. Hii ni nafasi adhimu kwa kila mpenda michezo ya sloti kuongeza nafasi ya ushindi huku akifurahia burudani isiyo na kifani. Ni zawadi inayolenga kuwapa wateja thamani halisi na furaha maradufu.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi, Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Mchezo wa Zombie Apocalypse unakupeleka katika ulimwengu wa kusisimua uliojaa changamoto na zawadi kubwa. Kila mzunguko ni nafasi mpya ya ushindi, kila mzunguko ni hatua kuelekea mafanikio. Muunganiko wa teknolojia ya kisasa kutoka Expanse Studios na uzoefu wa Meridianbet katika tasnia ya michezo ya kubashiri umezaa matokeo yanayovutia soko na kuinua viwango vya burudani.

Hii ni zaidi ya ofa, ni mwaliko kwa wachezaji wote kujitosa katika mapinduzi ya michezo ya mtandaoni. Kwa kubonyeza tu na kuanza kucheza, unajiweka kwenye mstari wa ushindi na kuwa sehemu ya wimbi jipya la burudani linalotikisa tasnia.

Usikubali kubaki nyuma wakati wengine wakivuna zawadi. Cheza mizunguko 100 leo na upokee mizunguko 50 ya bure kesho. Jiunge sasa na Meridianbet ushuhudie msisimko wa Zombie Apocalypse, ambapo ushindi wako unaanza kwa uamuzi mmoja tu wa wewe kujaribu.

Na. Vero Ignatus,Arusha.

Serikali imepiga marufuku watumishi wa Uma Kutumia mitandao isiyo rasmi ambayo ni tofauti na ile iliyounganishwa na mfumo wa Serikali mtandao katika kutuma nyaraka na taarifa mbalimbali za serikali kwani si salama kwa usalama wa nchi na wananchi

 Marufuku hiyo imetolewa  l9 April 2026  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya   Rais  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete wakati akifunga kikao kazi cha 6 cha serikali mtandao kilichofanyika kwa siku Tatu mkoani Arusha nakusema kwamba  watumishi wa Umma kutumia mifumo isiyo rasmi ni hatari kwani inasababisha nyaraka za siri za serikali kuonekana mtandaoni. 

Bado tunao wafanyakazi wa Serikali wanatumia Mtandao binafsi kurusha taarifa za Serikali jambo ambalo siyo sawa kwa taarifa hizo za Serikali kuwekwa wazi jambo hilo liwe narufuku kuanzia Leo taarifa za Serikali kutumwa kwa Mtandao binafsi. Alisema

Kikao Kazi hicho  cha siku tatu, kimewakutanisha takribani washiriki 1,000 kutoka sekta za umma na binafsi, na kimejadili kwa kina masuala muhimu yanayohusu ujenzi, uendelezaji na usimamizi wa jitihada za Serikali Mtandao. Ambapo Kupitia mijadala hiyo wamepata fursa ya: Kutathmini utekelezaji wa maazimio ya Kikao Kazi kilichopita,, Kubainisha mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Serikalini,

Pia waliweza Kujadili changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana nazo,Na kuweka maazimio mapya yatakayotuongoza katika hatua zinazofuata za kuendelea kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma za umma kwa njia ya kidijitali.

Kikwete amesema amefarijika kuona kuwa, mijadala yote imejikita katika uzingatiaji wa Sheria, Kanuni,Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, jambo ambalo ni msingi muhimu wa kuhakikisha miradi ya TEHAMA Serikalini inakuwa salama, endelevu na yenye kujali Katika kikao kazi hiki, 

Sambamba na hayo Serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), itatoa tuzo kwa taasisi zilizofanya vizuri katika kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, kwenye utekelezajiwa miradi ya TEHAMA.ambapo  amezipongeza taasisi zote zilizotunukiwa tuzo hizo  na kusema Tuzo hizo si za heshima tu, bali ni chachu ya kuhamasisha ubora, uwajibikaji na uzingatiaji wa misingi ya Serikali Mtandao katika taasisi zote za umma.



Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Kitanzania ya Compact Energies, inayojihusisha na uzalishaji na usambazaji wa vifaa vya kisasa vinavyotumia nishati ya jua, imesema kuwa Tanzania ina nafasi kubwa ya kuleta mageuzi ya kiuchumi kupitia uwekezaji katika teknolojia za uzalishaji wa umeme wa jua kwa matumizi ya majumbani na viwandani.

Akizungumza wakati wa Mkutano wa 5 wa Z-Summit Zanzibar uliomalizika hivi karibuni Visiwani Zanzibar, Meneja wa Masoko na Mauzo wa kampuni hiyo, Bw. Joseph Madata Biseko , alisema kuwa uwekezaji katika uzalishaji wa nishati ya jua utasaidia kupunguza gharama za uzalishaji viwandani na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi.

Aliongeza kuwa matumizi ya nishati ya jua yatasaidia pia kupunguza gharama za maisha kwa wananchi, kwa kuwa ni nishati nafuu na inayopatikana kwa uhakika ikilinganishwa na vyanzo vingine vya umeme vyenye gharama kubwa .

“Uzuri wa umeme wa jua, gharama ni wakati wa kuunganisha tu na hakuna malipo ya mwezi, ukitofautisha na aina nyingine ya nishati,”

“Kampuni yetu imejipanga kutoa suluhisho la changamoto za upatikanaji wa umeme usio wa uhakika kwa kusambaza vifaa vya ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu, ili Watanzania na wawekezaji wa kigeni wanufaike kupitia uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma mbalimbali,” amesema Bw. Biseko

Mkutano huo uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta za utalii, uuzaji wa viwanja na nyumba, pamoja na nishati. Washiriki walitoka katika nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Uganda, Ghana, Nigeria, Tanzania Bara na Zanzibar.

Kupitia jukwaa hilo, kampuni hiyo, iliyoshinda tuzo ya ‘Africa Company of the Year Awards’ katika kipengele cha Makampuni Makubwa Barani Afrika kutoka nchi 26 mwaka 2024, pia ilipata fursa ya kuonesha bidhaa na huduma zake, huku ikisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika nishati jadidifu kama msingi wa maendeleo endelevu ya kiuchumi nchini.



*Atambulisha jukumu jipya la Mahusiano linaloratibiwa na Wizara Yake.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu (Mb.) ametembelea Ofisi za Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) Makao Makuu Februari 19 2026 Jijini Dar es Salaam na kukutana na Viongozi kwa lengo la kujitambulisha na kulitambulisha jukumu jipya la Mahusiano ambalo Ofisi yake imekabidhiwa kuliratibu.

Aidha, Waziri Sangu alipowasili amepokelewa na
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT ) Dkt. Alhad Mussa Salum pamoja na wajumbe wa jumuiya hio.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Sangu alipongeza Jumuiya hiyo kwa mchango wake mkubwa katika kuimarisha amani, umoja na mshikamano nchini kupitia Maridhiano.

Vilevile, alieleza kuwa JMAT imekuwa nguzo muhimu ya maadili na mshikamano wa kijamii kwa kuhimiza maridhiano ya amani, kuvumiliana na kuimarisha mahusiano mema baina ya waumini wa dini mbalimbali.

"Juhudi hizo zimechangia kwa kiasi kikubwa kudumisha utulivu na mshikamano wa kitaifa" amesema Mhe. Sangu.

Aidha, Mhe. Sangu amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za kidini katika kushughulikia changamoto za kijamii, kiuchumi, kisiasa, kikanda na kimataifa hususan malezi bora na maadili mema katika jamii.

Sambamba na hayo, ameihakikishia JMAT kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na Baraza hilo na taasisi mbalimbali kuendeleza agenda ya amani, mshikamano na maendeleo jumuishi.

Kwa upande wake Mwenyekiti Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) Dkt. Alhad Mussa Salum, amempongeza Rais kwa kutambua umuhimu wa Mahusiano na kuanzisha Wizara mahsusi inayoshughulikia mahusiano.

Aidha, ameishukuru Serikali kwa kutambua na kuthamini mchango wa Jumuiya na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha umoja wa kitaifa, amani na mshikamano.

Top News