Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
MSEMAJI wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imepata mafanikio makubwa katika siku 100 za uongozi wake, hususan katika maboresho na ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam, ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo Januari 20, 2026, Msigwa amesema mkutano huo umefanyika katika Bandari ya Dar es Salaam ili kuonesha kwa vitendo kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika kuboresha huduma bandarini, akisisitiza kuwa bandari hiyo ni lango kuu la usafirishaji wa mizigo katika ukanda wa Afrika.

Ameeleza kuwa maboresho hayo yamelenga kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za uendeshaji na kuiweka bandari katika ushindani wa kikanda na kimataifa.

Msigwa amesema katika mwaka wa fedha 2024/2025 bandari za Tanzania zilihudumia kiasi kikubwa cha shehena kutoka nchi jirani ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, Malawi, Uganda na Zimbabwe, jambo linaloonesha nafasi ya kimkakati ya Tanzania katika biashara ya kikanda.

Ameongeza kuwa ushiriki wa sekta binafsi kupitia mikataba kati ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na makampuni ya DP World pamoja na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited umeleta mabadiliko makubwa katika miundombinu na utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa Msigwa, ameeleza kuwa uwekezaji uliofanywa umeongeza uwezo wa Bandari ya Dar es Salaam kuhudumia shehena, ambapo katika mwaka wa fedha 2024/2025 bandari hiyo ilihudumia tani milioni 27.7, sawa na ongezeko la asilimia 17 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.

Aidha, muda wa kuhudumia meli za makasha umepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosaidia kupunguza gharama kwa wafanyabiashara na kuongeza ushindani wa bandari.

Ameongeza kuwa maboresho hayo yamechangia ongezeko la ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja pamoja na kuongeza mapato ya Serikali kupitia kodi za forodha, ambazo zimeongezeka kwa asilimia 17 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025.

Msigwa amesema mafanikio hayo yanaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha mazingira ya biashara na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Msigwa amesema kukamilika kwa miradi ya maboresho ya bandari kutaifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa na uwezo wa kuhudumia meli kubwa za kisasa, kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena hadi tani milioni 30 kwa mwaka na kuimarisha ushindani wa bandari za Tanzania dhidi ya bandari nyingine katika ukanda wa Bahari ya Hindi.

Pia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ili kuhakikisha bandari zinakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

 Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
MRADI wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) unaendelea kubadilisha taswira ya uchumi na maisha ya wananchi katika mikoa inayopitiwa na mradi huo, huku ajira, miundombinu na mapato ya Serikali vikiongezeka kwa kasi kadri utekelezaji unavyokaribia ukingoni.

Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, mradi huo umefikia asilimia 79 ya utekelezaji hadi kufikia Desemba 31, 2025 na unatarajiwa kukamilika Julai 2026.

Hayo ameyasema leo Januari 20, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika bandari ya Dar es Salaam, amesema mbali na umuhimu wake wa kimkakati kwa sekta ya nishati, EACOP umeendelea kuwa chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa Watanzania.

Msigwa amesema kuwa tangu kuanza kwa mradi huo mwaka 2021, Watanzania wamekuwa wanufaika wakuu wa ajira zinazotokana na shughuli za ujenzi wa bomba, vituo vya kusukuma mafuta, matenki, jeti na miundombinu mingine.

"Hadi kufikia Juni 2025, jumla ya ajira 9,194 zilikuwa zimetolewa kwa Watanzania, sawa na asilimia 80 ya lengo la ajira 10,000, ambapo vijana wenye ujuzi wa chini, wa kati na wa juu wamepata fursa za kujipatia kipato na kuongeza maarifa ya kazi." Amesema Msigwa

Ameeleza kuwa mradi huo haukuishia tu kutoa ajira, bali pia umewekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kupitia mafunzo ya ufundi na kitaalamu.

"Vijana wengi wamepata mafunzo kupitia vyuo vya VETA na baadhi yao tayari wameajiriwa, huku wengine wakiandaliwa kuwa waendeshaji wa mradi mara baada ya ujenzi kukamilika."

Hatua hiyo, kwa mujibu wa Msigwa, itaifanya Tanzania kuwa na wataalamu wa ndani watakaosimamia uendeshaji wa mradi kwa miaka ijayo.

Kwa upande wa uchumi wa ndani, Msigwa amesema mradi wa EACOP umeongeza mzunguko wa fedha nchini baada ya kununua bidhaa na huduma zenye thamani ya Shilingi trilioni 1.325 kutoka kwa zaidi ya makampuni 200 ya Kitanzania.

Amesema hatua hiyo imeimarisha biashara za ndani, kuongeza mapato ya wafanyabiashara na kuchochea ukuaji wa uchumi katika maeneo yanayopitiwa na mradi.

Serikali pia imeanza kuvuna matunda ya mradi huo kupitia mapato ya kodi, tozo na malipo mbalimbali, ambapo zaidi ya Shilingi bilioni 50 tayari zimekusanywa.

Msigwa amesema kuwa baada ya mradi kukamilika na kuanza kusafirisha mafuta, Serikali inatarajia kupata mapato ya moja kwa moja yanayokadiriwa kufikia Shilingi trilioni 2.3 kwa kipindi cha miaka 25, jambo litakaloongeza uwezo wa Serikali kugharamia huduma za kijamii na miradi ya maendeleo.

Katika upande wa miundombinu, wananchi wameendelea kunufaika na uboreshaji wa barabara zenye urefu wa kilomita 304 pamoja na ujenzi wa mitandao ya mabomba ya maji safi yenye zaidi ya kilomita 30 katika maeneo mbalimbali ya mradi.

Msigwa amesema barabara hizo zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika shughuli za uzalishaji mali, huku upatikanaji wa maji safi ukiboresha afya na ustawi wa jamii.

Ameongeza kuwa ujenzi wa gati na miundombinu ya kupakilia mafuta katika eneo la Chongoleani mkoani Tanga uko katika hatua za mwisho, hali itakayoongeza shughuli za bandari, ajira na mapato pindi mafuta yatakapoanza kusafirishwa kwenda masoko ya kimataifa.

Msigwa amesema mradi wa EACOP umeonesha kuwa miradi mikubwa ya kimkakati inaweza kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi endapo itasimamiwa vizuri.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika kimataifa ili kuleta tija endelevu kwa Taifa na vizazi vijavyo.
Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeandika historia mpya katika ukusanyaji wa mapato ya Bandari baada ya kuvunja rekodi ya makusanyo, hali inayotajwa kuwa matokeo ya mageuzi ya kiutendaji, matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidigitali na kuimarika kwa ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa biashara.

Akizungumza na waandishi wa habari, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema mapato ya Bandari yameendelea kuongezeka kwa kasi katika Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia maboresho makubwa yaliyofanywa katika usimamizi wa kodi na ufanisi wa utoaji huduma.

Msigwa amebainisha hayo leo Januari 20,2026 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Bandari ya Dar es Salaam amesema kuwa katika kipindi cha Julai hadi Desemba mwaka wa fedha 2025/26, TRA imekusanya mapato makubwa kupitia Bandari, yakichangia kwa kiasi kikubwa kufikia wastani wa makusanyo ya zaidi ya shilingi trilioni 3 (Tatu) kwa mwezi kitaifa.

Ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na kuongezeka kwa shughuli za biashara bandarini, kupungua kwa ucheleweshaji wa mizigo na kuimarika kwa uwazi katika ukusanyaji wa kodi na tozo mbalimbali.

Amesema rekodi hiyo imeimarishwa zaidi mwezi Desemba 2025, ambapo makusanyo ya mapato ya Bandari yalikuwa sehemu ya mchango mkubwa uliowezesha TRA kukusanya jumla ya shilingi trilioni 4.13 kwa mwezi mmoja, kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa hapo awali.

Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali, matumizi ya Mfumo Jumuishi wa Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani (IDRAS) yamekuwa chachu ya mafanikio hayo kwa kuwezesha ufuatiliaji wa miamala ya kikodi kwa wakati halisi, kuunganishwa kwa mifumo ya taasisi husika bandarini na kupunguza mianya ya upotevu wa mapato.

Ameongeza kuwa kupitia mfumo huo, wafanyabiashara na wakala wa forodha wanapata huduma za kikodi kwa saa 24, ikiwa ni pamoja na utoaji wa risiti za kielektroniki, uthibitishaji wa nyaraka na ukumbusho wa moja kwa moja wa majukumu ya kikodi, hatua iliyorahisisha biashara na kuongeza utii wa walipakodi.

Msigwa amesema mafanikio ya TRA katika ukusanyaji wa mapato ya Bandari ni kielelezo cha dhamira ya Serikali ya kuendelea kuboresha mazingira ya biashara, kuongeza ufanisi wa Bandari na kuhakikisha mapato ya umma yanakusanywa kwa uwazi na uadilifu kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo na huduma za kijamii.

Msigwa pia ametoa wito wa kuendeleza nidhamu ya ulipaji kodi ili Tanzania iendelee kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na Bandari zake.

 

Na Mwandishi wetu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amefanya ziara ya kikazi katika Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar (ZFCC) ikiwa ni hatua ya kuimarisha mashirikiano kati ya taasisi hizo mbili katika masuala ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Bi. Ngasongwa alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZFCC, Bi. Aliya Juma ambapo viongozi hao walifanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ustawi wa taasisi hizo na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 14 Januari, 2026 katika ofisi za ZFCC - Zanzibar, Bi. Ngasongwa alisema ushirikiano kati ya taasisi hizo unaendelea kuimarika kupitia utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) yaliyokwisha sainiwa.

"FCC na ZFCC tayari zimeanza kutekeleza kwa vitendo maeneo ya ushirikiano ikiwemo kujengeana uwezo, kubadilishana uzoefu na kufanya ukaguzi wa pamoja ili kudhibiti bidhaa bandia na kulinda haki za watumiaji wa bidhaa au huduma."alisema Bi. Ngasongwa

Katika ziara hiyo, Bi. Ngasongwa pia alikutana na kuzungumza na menejimenti ya ZFCC ambapo walijadili namna ya kuendeleza mpango wa pamoja wa kuboresha mifumo ya utendaji kazi na kubadilishana taarifa.

Kikao hicho cha siku moja kilihitimishwa kwa pande zote mbili kuahidi kuendeleza juhudi za pamoja ili kuhakikisha mazingira ya biashara yanaendelea kuwa shindani, salama na rafiki kwa mlaji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (Mb) leo (Jumanne, Jan. 20, 2026) amekutana Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na kusisitiza umuhimu wa Mfuko kuwekeza katika miradi inayozalisha ajira kwa vijana wa kitanzania.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Makao Makuu ya PSSSF jijini Dodoma, Mhe. Sangu amekumbusha kuwa kwa sasa Serikali inatekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo (DIRA 2025) ambayo, Pamoja na mambo mengine, inasisitiza uwekezaji katika miradi inayozalisha ajira na kuchochea Uchumi.

“Bodi ihakikishe mambo makubwa mawili katika utekelezaji wa miradi – kwanza kuzalisha ajira na pia ajira hizo ziwafikie vijana wa kitanzania kama DIRA 2050 na mipango ya Serikali inavyoelekeza,” amesema Waziri Sangu katika mkutano huo wake wa kwanza na Bodi ya Wadhamini ya PSSSF.

Katika mkutano huo, Menejimenti ya PSSSF nayo ilihudhuria ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Bw. Fortunatus Magambo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSSSF Bi. Joyce Mapunjo, kwa niaba ya Bodi, alimuhakikishia Waziri Sangu kuwa utekelezaji wa majukumu ya Mfuko unaongozwa na Mpango Mkakati uliohuishwa kwa kuzingatia DIRA 20250 na miongozo ya Serikali.

“Tumepokea maelekezo na tutazingatia katika utekelezaji … nikuhakikishie kuwa tuna Mpango Mkakati mpya (2026/2027 - 2030/2031) unaozingatia mipango ya kitaifa na pia tunatumia utaalam na uzoefu wetu kuhakikisha malengo ya Mfuko yanatimia na unaendelea kuwa stahimilivu,” amesema Bi. Mapunjo ambaye ni Katibu Mkuu mstaafu aliyehudumu kwenye Wizara mbalimbali.

Mfuko wa PSSSF ulianzishwa mwaka 2018 kufuatia kuunganishwa kwa iliyokuwa Mifuko ya GEPF, LAPF, PSPF na PPF. Kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Mfuko, PSSSF ina majukumu manne ya kusajili wanachama, kukusanya michango, kuwekeza ili kutunza thamani ya fedha na kulipa mafao mbalimbali kwa wanachama wake.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)
Mwenyekiti  wa wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Joyce Mapunjo, akizungumza katika kikao kazi kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu , Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)
Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu, ,Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) pamoja na Menejimenti ya watumishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)
Na Mwandishi wetu, Eyasi.

Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Karatu, ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Dkt. Lameck Karanga, imekutana na baadhi ya wananchi wa kabila la wahadzabe, kabila ambalo kwao nyama ya nyani ni kipaumbele kikubwa katika maisha yao na kukutana na wadatoga wanaojihusisha na uhunzi ,ziara ambayo imefanyika katika eneo la Eyasi wilayani humo.

Kabila la wahadzabe ambalo linaheshimika kutokana na mila na silka zake za kiasili linaamini kuwa nyama ya nyani ndiyo nyama bora na tamu kuliko zote duniani na limekuwa likimtumia mnyama huyo kama kielelezo muhimu kwa maisha yao huku kabila la wadatoga wakiendelea kutumia zana za kale katika uhunzi wa kufua bidhaa mbalimbali za kitamaduni.

Makabila yote mawili yanapatikana ndani ya jiopaki ya Ngorongoro Lengai inayopatikana wilaya ya Karatu, Ngorongoro na Monduli ,wilaya ambazo baadhi ya maeneo yake yanaunda jiopaki ya kidunia inayojulikana kama Ngorongoro Lengai Global Geopark inayotambuliwa na Shirika la Sayansi,Elimu na Utamaduni ( UNESCO).

Akizungumza na jamii ya makabila hayo Dkt. Lameck Karanga amewapongeza wananchi hao kwa kuendelea kutumisha mila na tamaduni za asili huku wakiwa kielelezo katika utunzaji wa amani na utulivu katika maeneo yao na kuwataka kuendelea kuwa kielelezo bora cha jamii nchini kwani serikali itaendelea kuwalinda na kuboresha shughuli za utalii katika eneo hilo.

Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Utalii na Maendeleo ya jamii wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro bwana Joas Makwati ameeleza kuwa mradi wa Jiopaki ya Ngorongoro unanufaisha jamii zinazokaa ndani na nje ya eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwa kuwa Shughuli za ufugaji, uwindaji na kilimo hutegemea uwepo wa maji uhifadhi wa misitiu ya Ngorongoro.

Kabila la wahadzabe linaloishi pembezoni mwa eneo la Eyasi limekuwa likisifika kutokana na utaalam wake wa kuchoma na kula nyama za nyani jambo ambalo limewafanya wageni kutoka ndani nan je ya nchi kuwatembelea ili kuona jinsi mnyama huyo alivyokuwa tunu kwa kabila hilo.

Nyama ya nyani iliyochomwa vizuri kwa mujibu wa kabila hilo ina vionjo vitamu kutokana na mnyama huyo kula mizizi,matunda na mimea pori ambayo huifanya nyama yake kuwa na ladha ya kuvutia na yenye kuufanya mwili uweze kuhimili magonjwa mbalimbali.











LEO hii ligi ya mabingwa bado inaendelea huku nafasi ya wewe kuondoka na mshindo ikiwa kubwa pale Meridianbet. Tandika jamvi lako na Meridianbet leo ujiweke kwenye nafasi ya washindi sasa.

Mapema kabisa Club Brugge atakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Kairaty Almaty ambao mpaka sasa wana pointi 1 pekee huku wageni wao wakiwa na pointi 4. Takwimu zinaonesha kuwa timu hizi hazijawahi kukutana kwenye mashindano yoyote hii ndio mara ya kwanza. Je nani kushinda leo?. Bashiri hapa.

Nao vijana wa Pep Guardiola Manchester City watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Bodoe/Glimt ambao mpaka sasa hawajashinda mechi yoyote. City wao wapo nafasi ya 4 na ushindi ni muhimu sana kwenye mechi hii. Meridianbet wanampa nafasi kubwa ya kushinda City. Je wewe beti yako unaiweka kwa nani siku ya leo?. Tandika hapa.

Vijana wa Napoli wao wakiwa na matokeo ambayo hayaridhishi watakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Copenhagen ambapo wote wana pointi 7 kwenye msimamo wa Uefa. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye mechi zilizobaki. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Jisajili hapa.

Piga pesa kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mechi kali ni hii ya Inter Milan vs Arsenal ambao ndio vinara wa msimamo wa UEFA kwani mpaka sasa kwenye mechi 6 walizocheza wameshinda zote huku vijana wa Chivu wao wakishinda 4 na kupoteza mbili hadi sasa. Je vijana wa London wataendeleza ushindi wao?. Machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Suka jamvi lako hapa.

Bingwa mara nyingi wa michuano hii Real Madrid watakuwa Santiago Bernabeu kupepetana dhidi ya AS Monaco ya kule Ufaransa ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 19 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 7. Ushindi huu ni muhimu wa Real kwani utawapeleka hadi nafasi ya juu. Je beti yako unaiweka kwa nani leo?. Tengeneza jamvi hapa.

Kwa upande wa Sporting Lisbon wao watamenyana dhidi ya bingwa mtetezi PSG ambao mpaka sasa wapo nafasi ya 3 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 14 na pointi zao 10. Meridianbet wao wanampa bingwa mtetezi nafasi kubwa ya kushinda ugenini. Je wewe unampa nani nafasi ya kushinda?. Jisajili hapa.

Tottenham Host Spurs atamleta kwake Borussia Dortmund ambapo mechi ya mwisho kukutana kati yao ilikuwa ni 2019 ambapo BVB alichapika, hivyo leo hii anataka kulipa kisasi akiwa ugenini. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii pale Meridianbet, hivyo ingia kwenye akaunti yako na ubeti sasa.

Villarreal uso kwa uso dhidi ya Ajax ambao tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni pointi 2 pekee. Timu zote zipo mkiani kwenye ligi ya mabingwa hadi sasa. Meridianbet wameipa mechi hii Odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000 siku ya leo. Jisajili hapa.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela akizungumza wakati kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani katika Kongamano la Uwekezaji mkoani lililofanyika Geita leo Januari 20, 2026.
Mwenyekiti wa Bodi ya MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Dkt. Aziz Mlimaakizungumza wakati kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani katika Kongamano la Uwekezaji mkoani lililofanyika Geita leo Januari 20, 2026.

MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imeendelea na kampeni yake ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani kwa kufanya Kongamano la Uwekezaji mkoani Geita, likiwa na lengo la kuwahamasisha wananchi kushiriki moja kwa moja katika shughuli za uwekezaji na kuondoa dhana potofu kuwa uwekezaji ni kwa wageni pekee.

Kongamano hilo lililofanyika leo Januari 20, 2026 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, lilimshirikisha Mkuu wa Mkoa huo, Martine Shigela, ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Shigela aliipongeza TISEZA kwa juhudi zake za kusogeza elimu ya uwekezaji kwa wananchi wa Geita na kuwahimiza kutumia fursa zilizopo kwa kusajili miradi yao kupitia TISEZA ili kunufaika na vivutio mbalimbali vya kikodi na visivyo vya kikodi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TISEZA, Dkt. Aziz Mlima, amesema Mkoa wa Geita una fursa nyingi za uwekezaji katika sekta mbalimbali na kusisitiza kuwa huu ni wakati sahihi kwa Watanzania kuelimishwa na kushiriki kikamilifu katika uwekezaji ili kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa na kuongeza ajira kwa wananchi.

Katika kongamano hilo, TISEZA pia ilizindua Dawati la Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani, ambalo linalenga kusogeza huduma za uwekezaji karibu na wananchi, kuongeza mwitikio wa Watanzania katika kuwekeza, kurahisisha utatuzi wa changamoto zinazowakabili wawekezaji, kuboresha upatikanaji wa takwimu muhimu za biashara na uwekezaji pamoja na kusimamia ardhi mahsusi kwa uwekezaji ili kuepusha migogoro na uvamizi wa ardhi.

Kwa ujumla, kongamano hilo limekuwa jukwaa muhimu la kuwawezesha wananchi wa Mkoa wa Geita kupata uelewa mpana kuhusu fursa za uwekezaji wa ndani na mchango wao katika kukuza uchumi wa taifa.

Kupitia elimu iliyotolewa pamoja na uzinduzi wa Dawati la Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani, TISEZA imeendelea kuthibitisha dhamira yake ya kuboresha mazingira ya uwekezaji na kuwahamasisha Watanzania kuchukua hatua za moja kwa moja katika uwekezaji.

Kampeni ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani inatarajiwa kutekelezwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara, ikianzia Kanda ya Ziwa watapita katika mikoa sita ambayo ni Mwanza, Geita, Mara, Bukoba, Shinyanga na Simiyu.

Pia wataendelea katika Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Magharibi kwa kushirikiana na Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na vyombo vya habari.


Matukio mbalimbali.
Picha za pamoja.

 Na. Emmanuel Buhohela, Dodoma


Kamati ya kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii imeipongeza Serikali kwa kutatua kwa kiasi kikubwa changamoto ya upungufu wa Watumishi katika Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. 


Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Thimotheo Mzava Jijini Dodoma wakati kamati hiyo ikipewa mafunzo kuhusu Muundo na majukumu ya Wizara na Taasisi zake na kutaka jitihada hizo kuendelezwa ili kuwa na uwiano mzuri wa watumishi katika Taasisi ili ziweze kutekeleza kikamilifu majukumu yake. 



Mhe. Mzava ameongeza kuwa kwa kipindi kilichopita kamati hiyo imekuwa ikipokea malalamiko ya upungufu wa watumishi tofauti na hali ilivyo sasa na kuiopongeza Serikali na kwamba Kamati hiyo ya kudumu ya Bunge inatarajia kuimarika kwa utendaji


Aidha, ameitaka wizara kuendekea kuvitazama na kuviwezesha vyuo vilivyoko chini ya wizara ili kuviwezesha kuzalisha wataalam na kutoa mchango katika sekta ya ajira. 


Baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo waliopata fursa za kutoa ushauri na maelekezo wamesema wako tayari kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuendeleza uhifadhi ili kizazi kijacho kiweze kunufaika na rasilimali hiyo adhimu. 



Akizungumza wakati wa kuhitimisha kikao cha leo Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema Serikali inaendelea kuwa sikivu na kutekeleza majukumu yake ya kusimamia kikamilifu na kuendeleza sekta ya uhifadhi na Utalii ili kuwanufaisha wananchi wote. 


Ameongeza kuwa kutokana na kauli mbiu ya chama cha mapinduzi ya kazi na utu Wizara itaendelea kutekeleza majukumu yake ipasavyo ili kufikia maono ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuacha tabasamu kwa wananchi pindi atakapomaliza muhula wake wa uongozi. Tanzania 


Taasisi zilizowasikisha taarifa zake kwa niaba ya Mhe. Waziri wa Maliasili na Utalii ni Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), Chuo Cha Usimamizi wa Wanyamapori (MWEKA) pamoja na  Chuo Cha Taifa cha Utalii (NCT).



Kikao hicho kimeongozwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Thimotheo Paul Mzava (Mb) na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb.), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu Bw. Nkoba Mabula, Menejimenti ya Wizara, Wakuu wa Taasisi pamoja na vyuo vilivyopo chini ya Wizara.

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma limewahimiza wananchi na watumiaji wa umeme kuhakikisha wanalinda na kutunza miundombinu ya umeme iliyopo katika maeneo yao ili huduma ya umeme iendelee kupatikana kwa uhakika kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Wito huo umetolewa na Afisa Uhusiano Huduma kwa Wateja wa TANESCO mkoani Ruvuma, Alan Njiro, wakati akitoa elimu kwa wananchi wa kijiji cha Selekano kilichopo katika kata ya Liganga, Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akizungumza na wananchi hao ambao vitongoji vyao vimepitiwa na mradi wa REA, Njiro amewataka kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa nguzo, nyaya na miundombinu mingine ya umeme ili kuepuka uharibifu unaoweza kusababisha kukatika kwa huduma ya umeme.

Aidha, amewasisitiza wananchi kuwa waangalifu katika malipo ya kuunganishiwa umeme, akieleza kuwa gharama ya kuunganishiwa umeme vijijini ni shilingi elfu ishirini na saba (27,000) tu, na kuwataka kuepuka kutoa fedha kwa watu kwani malipo yote hufanyika kupitia namba za kumbukumbu ya malipo.

Amesema TANESCO itaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuhakikisha huduma ya umeme inalindwa na inawanufaisha wananchi katika kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.








Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 20,2026 amefanya mazungumzo na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Emmanuel Tutuba, ofisini kwa Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma.


Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, amekutana na uongozi wa Chama cha Mabroka wa Madini Tanzania (CHAMMATA) jijini Dodoma kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili mabroka wa madini nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, pamoja na watendaji wengine kutoka Wizara ya Madini na Tume ya Madini, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali kushirikiana kwa karibu na wadau wa sekta ya madini katika kuendeleza sekta hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wanachama wa CHAMMATA, Mwenyekiti wa chama hicho, Jeremia Kituyo, amewasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili mabroka wa madini, ambapo mara baada ya kusikiliza hoja na maoni yaliyowasilishwa, Naibu Katibu Mkuu Mbibo amewahakikishia viongozi wa CHAMMATA kuwa Serikali itayafanyia kazi mapendekezo hayo kwa kushirikiana na taasisi husika, ili kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Mbibo amesisitiza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wadau wote wa sekta ya madini, wakiwemo wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini, wanafanya kazi katika mazingira rafiki, salama na yenye tija kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Ameongeza kuwa jitihada hizo zinalenga kuongeza uzalishaji, kuimarisha biashara ya madini kwa uwazi na ushindani, pamoja na kuhakikisha mchango wa sekta ya madini unaendelea kukua na kuchangia ipasavyo katika Pato la Taifa na maendeleo ya uchumi wa nchi kwa ujumla.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau wa sekta ya madini wameipongeza Wizara ya Madini kwa kuchukua hatua kubwa za kuwawezesha wananchi, ikiwemo utoaji wa leseni za madini kwa vikundi vya vijana, kuwarasimisha wadau wa madini na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za madini kwa mujibu wa sheria na kanuni za madini.

Aidha, wadau hao wameiomba Wizara ya Madini kuendelea kutoa msaada zaidi, hususan katika kuwaunganisha na Taasisi za Fedha ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo itakayowaongezea uwezo wa mitaji na kuchochea ukuaji wa biashara zao za madini nchini.




Top News