Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza katika mbio za Mwenge wa Uhuru unaotarajia kuwasili jijini humo aprili 13 mwaka huu ukitokea Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo utakimbizwa umbali wa kilometa 392.22 kwenye Wilaya zote tano za mkoa huo ukikagua, kuzimdua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi 35 yenye thamani ya shilingi bilioni 113.5


Akizungumza na waandishi wa habari RC Chalamila amesema shabaha ya mbio za mwenge wa uhuru ni kuleta umoja, mshikamano na udugu baina ya watanzania ambapo amesema aprili 13 baada ya kuwasili utakimbizwa wilayani Ilala, April 14 wilaya ya Kigamboni, April 15 wilaya ya Temeke, April 16 wilaya ya Ubungo na April 17 wilaya ya Kinondoni na April 18 Mkoa utakabidhi Mkoa wa Pwani.


RC Chalamila amesema Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu wa 2026 umebeba ujumbe wa kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa chini ya kauli mbiu isemayo "Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo"


Sanjari na ujumbe wa kudumu wa mbio hizo ambao ni kuimarisha mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, Dawa za Kulevya Lishe, na Rushwa, hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika Wilaya zote ambako Mwenge wa Uhuru utakimbizwa.


Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Albert Chalamila amezungumzia suala la Nishati ya mafuta ya petroli na diseli ambapo amewatoa shaka wananchi na wakazi wa Mkoa  huo kuwa hadi sasa hakuna uhaba wa mafuta  japo kuna changamoto ya ongezeko la bei ya bidhaa hiyo.


Vilevile RC Chalamila ametumia nafasi hiyo kuwataka wanasiasa kuacha kulitumia suala la kuongezeka kwa bei ya mafuta kisiasa kwa suala hilo ni la kidunia kutokana na vita iliyotokea na kusababisha kuongeza bei ya mafuta kwenye Soko la Dunia, mabadiliko ya gharama za uletaji mafuta na mabadiliko ya thamani ya dola huku akisisitiza kuwa Serikali chini ya Rais Dkt Samia inaendelea na mikakati na kuwa na mifumo bora ya kuhifadhi mafuta ili changamoto kama hiyo iwe historia


Aidha Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amezungumzia ziara ya Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba aliyoifanya wiki iliyopita kwenye soko lililoungua moto la Ubungo simu 2000 na kusema kuwa maelekezo aliuoyatoa yanatekelezwa pamoja na yale ualiyotolewa na waziri wa TAMISEMI


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amewataka wananchi wa Mkoa huo kujitokeza katika mbio za Mwenge wa Uhuru unaotarajia kuwasili jijini humo aprili 13 mwaka huu ukitokea Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo utakimbizwa umbali wa kilometa 392.22 kwenye Wilaya zote tano za mkoa huo ukikagua, kuzimdua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi 35 yenye thamani ya shilingi bilioni 113.5


Akizungumza na waandishi wa habari RC Chalamila amesema shabaha ya mbio za mwenge wa uhuru ni kuleta umoja, mshikamano na udugu baina ya watanzania ambapo amesema aprili 13 baada ya kuwasili utakimbizwa wilayani Ilala, April 14 wilaya ya Kigamboni, April 15 wilaya ya Temeke, April 16 wilaya ya Ubungo na April 17 wilaya ya Kinondoni na April 18 Mkoa utakabidhi Mkoa wa Pwani.


RC Chalamila amesema Mwengu wa Uhuru kwa mwaka huu wa 2026 umebeba ujumbe wa kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa chini ya kauli mbiu isemayo "Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo"


Sanjari na ujumbe wa kudumu wa mbio hizo ambao ni kuimarisha mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, Dawa za Kulevya Lishe, na Rushwa, hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika Wilaya zote ambako Mwenge wa Uhuru utakimbizwa.


Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Albert Chalamila amezungumzia suala la Nishati ya mafuta ya petroli na diseli ambapo amewatoa shaka wananchi na wakazi wa Mkoa  huo kuwa hadi sasa hakuna uhaba wa mafuta  japo kuna changamoto ya ongezeko la bei ya bidhaa hiyo.


Vilevile RC Chalamila ametumia nafasi hiyo kuwataka wanasiasa kuacha kulitumia suala la kuongezeka kwa bei ya mafuta kisiasa kwa suala hilo ni la kidunia kutokana na vita iliyotokea na kusababisha kuongeza bei ya mafuta kwenye Soko la Dunia, mabadiliko ya gharama za uletaji mafuta na mabadiliko ya thamani ya dola huku akisisitiza kuwa Serikali chini ya Rais Dkt Samia inaendelea na mikakati na kuwa na mifumo bora ya kuhifadhi mafuta ili changamoto kama hiyo iwe historia


Aidha Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amezungumzia ziara ya Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba aliyoifanya wiki iliyopita kwenye soko lililoungua moto la Ubungo simu 2000 na kusema kuwa maelekezo aliuoyatoa yanatekelezwa pamoja na yale ualiyotolewa na waziri wa TAMISEMI


Na MWANDISHI WETU

WAZIRI  wa  Ujenzii, Abdalllah Ulega, amesema serikali itaendelea kushirikiana kikamilifu na wabunifu majengo kuhakikisha kuwa na miji iliyopangika vyema na manengo salama.

Aidha amewataka wabunifu majengo nchini kuwekeza taaluma yao katika ubunifu kwa kutumia teknolojia  kubwa lakini kwa gharama nafuu.

Ulega ameyasema hayo, mjini Morogoro, alipofungua semina ya siku mbili ya wabunifu majengo kuhusu  upangaji miji na ujenzi wa nyumba bora zinazo zingatia teknolojia ya sasa na zamani (AAT CPD)

Semina hiyo  iimeshirkishs  wataalamu zaidi ya 300 kutoka ndani na nje ya ncjhi imeandaliwa na Chama cha Wabunifu Majengo Tanzania (AAT)

Waziri Ulega amesema fani ya ubunifu majengo ni fani muhimu  hivyo kuwataks wataalamu hao kujitangaza ili jamii iwatambue na kuwatumia.

"Vilevile  nyie ni wanasayansi wazuri. Tumieni  ubunifu wenu kubuni  mambo ya teknolojia  kwa gharama nafuu  itakayo endana na mahitaji na mazingira ya nchi yetu" amesema Ulega.

Amebainisha katika dunia ya sasa wanasayansi wanatumia  teknolojia kubuni vitu  kwa gharama nafuu vinavyo weza kuingia katika ushindani na vitu vya teknojia ya gharama kubwa.

"Hivyo nasisitiza  mtumie ubunifu wenu katika kuisaidia jamii yetu kwa kutumia teknolojia ya gharama nafuu yenye tija," amebainisha.

Pia ameitaka AAT kuitangaza taaluma hii kwani wabunifu majengo wakitumika vyema wanasaidia taifa kuwa na miji bora inayoendelea yenye ujenzi salama na iliyopangika.

"Fani yenu  ni muhimu lakini imefichwa. Huenda imefichwa zaidi  na wahandisi ambao wanafanya kazi zote za ujenzi. Mkijitangaza mkajulikana jamii itawatumia na itaachana pia na kuwatumia vishoka katika ujenzi," ameeleza Waziri Ulega.

Amebainis  serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kushirikiana na wabunifu majengo nchini kwa kuzifanyia marekebisho,sheria na kanuni mbalimbali ili kuketa uwajibikaji bora ma ufanisi.

Aidha ameipongeza  AAT kwa kuandaa semina hiyo  hasa kuwashirikisha wanafunzi wa vyuo na vyu vikuu wanasomea taaluma mbalimbali za kada hiyo ya ujenzi jambo alilosema litaleta tija kwa taifa.

Awali Rais  wa AAT  Mack  T'Chawi, alisema semina hiyo itasaidia kutoa elimu ya namna ya kupanga miji inayobadilika kullngana na teknolojia ya sasa na ya zamani.

Katibu  Mtendaji wa AAT Attie  Ally, alisema katika kuunga mkono jitihada  za Rais Dk. Samia kukiza sekta ya utalii nchini washiriku wa semina hiyo leo watakwenda kutalii katika Mbuga ya Wanyama ya Mikumi mkoani humo.

"AAT tunaujga mkono jitihada za Rais Dk. Samia za kutangaza utalii, hivyo washiriki wote wa semina hii ya kimataifa tutawapeleka  Mikumi kutalii," almesema  Attie.

Washiriki wa semina hiyo wamesema ina tija kubwa kwao katika kubadilishana uzoefu hasa kipindi hiki ambapo miji mingi inaendelea kukua kutokana na ongezeko la watu.






Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuzindua ofisi mpya katika mkoa wa Pwani, na kutoa vyeti na leseni 143 kwa wazalishaji wa bidhaa katika kanda ya mashariki inayojumuisha mikoa ya Pwani, Morogoro na Tanga, Hatua inayolenga kuongeza uzingatiaji wa viwango vya ubora katika uzalishaji wa bidhaa nchini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ofisi hiyo iliyopo katika jengo la Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha, Mkoani Pwani Katibu Tawala Msaidizi wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji mkoani humo, Bi. Ritta Magere, amesema uwepo wa ofisi hiyo utarahisisha kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma kwa wazalishaji, hasa katika mkoa huo wenye zaidi ya viwanda 1,700.

Bi. Magere ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia TBS kwa kuanzisha ofisi hiyo, akieleza kuwa ni hatua muhimu itakayoongeza tija kwa wamiliki wa viwanda na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali katika mkoa wa Pwani na maeneo jirani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi, amesema shirika hilo linaendelea kusogeza huduma kwa jamii ili kupunguza adha ya wazalishaji kusafiri umbali mrefu kwenda Dar es Salaam kufuata huduma, Amesema ofisi ya Pwani itakuwa mbadala rahisi kwa wadau wa kanda hiyo.

Aidha, Dkt. Katunzi ameongeza kuwa TBS ina mpango wa kuanzisha ofisi ndogo katika mkoa wa Morogoro ili kuendelea kuwafikia wadau karibu zaidi, hatua ambayo itasaidia kuokoa muda na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Baadhi ya wazalishaji wa bidhaa, akiwemo Bi. Angela Sanga, wamepongeza uamuzi huo wakisema kuwa utaongeza motisha ya kuzalisha bidhaa zenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko la ndani na kimataifa, huku wakitarajia kunufaika zaidi na huduma zilizo karibu nao.



Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Uingizaji na Usambazaji wa mafuta Jamii ya Petrol nchini ya 'MOIL Energies' imesema imefurahishwa kwa kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ulipaji kodi ya nishati hiyo kabla ya kuyatoa vituoni na kwenda sokoni (BIL)kwa kiasi kikubwa umesaidia kudhibiti 'ujanja ujanja' uliokuwepo hapo awali

Akizungumza Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo nchini, Dkt Sajad Habib Rai amesema wao kama Kampuni ya kwanza nchini kutoa mapendekezo ya kuanzishwa kwa mfumo huo kwa EWURA na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na baadae kuanzishwa rasmi na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), wanajivunia kuona umetekelezwa kwa kuwa dhamira yao ilikuwa kuona huduma ya usambazaji wa mafuta nchini na nje ya nchi unaleta tija kwa Taifa.

"Tumefurahi kuona TRA wameusimamia kikamilifu mfumo huu kwa kuwa unazuia ukwepaji kodi ambao hapo awali ulikuwa ukifanywa na wafanyabiashara, hivi sasa TRA inapata kodi yake mapema kabla ya kuyaingiza mafuta sokoni" amesema Dk Sajad ambaye pia ni Meneja MKAZI wa 'Mansoor Industry Limited'

Hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo huo ambao kwa kiasi kikubwa unalezwa kuleta tija kwa Serikali kwa kuwa umesaidia kudhibiti upotevu wa mapato unaotakana na Kodi za uingizaji wa mafuta hayo nchini.

Kupitia mfumo huo mpya na wa kisasa, kila mwagizaji au muingizaji wa mafuta atalazimika kutaja kiasi cha mafuta alichokiingiza nchini ambapo kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) watayataweka vinasaba kama alama ya kila mwagizaji kwa lengo la kuwatambua wahusika wote na kiasi alichoagiza ili kuwakadiria viwango vya Kodi wanavyopaswa kulipa.

"Nawapongeza TRA kwa kuona tija na umuhimu wa kuutumia mfumo huu, sisi kama wafanyabiashara tunaozingatia taratibu halali za uingizaji na Usambazaji wa mafuta tunaiona kuwa hatua hii ni kubwa na inayostahili kupongezwa kwa kuwa italeletea manufaa Taifa" ameongeza Dkt Sajad

Utaratibu huo wa kikodi unawataka wamiliki wa mafuta hayo kuyalipia kodi kabla ya kuyaingiza sokoni ili yanapoingizwa sokoni yanaendelea na taratibu za uuzwaji hali ambayo inarahisisha usambazaji na kuwafikishia wateja huduma ya mafuta kwa wakati sambamba na kudhibiti kubaki nchini mafuta ambayo kimsingi yanapaswa kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Aidha akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya hivi karibuni katika bohari za kuhifadhia mafuta zilizopo Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Juma Mwenda pamoja na mambo mengine alisema lengo la TRA kuweka utaratibu huo ni kuwezesha biashara kufanyika kwa urahisi na kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali huku akitoa wito kwa wafanyabiashara watakaokutana na changamoto zozote kuwasiliana na TRA.

Pamoja na mambo mengine pia Kamishina Mwenda alisema Mamlaka hiyo pia umeweka utaratibu wa kufanya kazi kwa Saa 24 ili kuharakisha utolewaji wa huduma kwa walipakodi ambao ni waingizaji, wasambazaji na wauzaji wa mafuta hayo.



Mbunge wa Jimbo la Namtumbo na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, amezindua rasmi huduma ya umeme katika vitongoji 15 vya jimbo hilo kupitia mpango wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Uzinduzi huo umefanyika Aprili 10, 2026 katika Kitongoji cha Mtonya na Mandepwende, kilichopo Kata ya Ruinga, ambapo Mheshimiwa Homera amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi endelevu za serikali kuhakikisha wananchi wa maeneo ya vijijini wanapata huduma ya umeme.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Homera alieleza kuwa kuwashwa kwa umeme katika vitongoji hivyo 15 ni mwanzo wa mpango mpana zaidi, ambapo serikali kwa kushirikiana na REA imejipanga kuhakikisha kila mwezi vitongoji vipya vinaunganishwa na huduma ya umeme katika jimbo hilo.

Amesisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha wananchi wote wanapata umeme bila kujali hali ya makazi yao, akieleza kuwa hata nyumba za nyasi au zilizojengwa katika mazingira tofauti zinapaswa kufikiwa na huduma hiyo muhimu.

Kwa upande wake, Deo Nangu, aliyewakilisha Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa REA, Hassan Said, amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.6.

Mradi huo unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme, kuchochea shughuli za kiuchumi, na kuboresha maisha ya wananchi wa Namtumbo kwa ujumla.













TAMASHA la Utalii la Same festival linalofanyika kila mwaka wilayani Same mkoani Kilimanjaro limetajwa kuwa chanzo cha kuchochea idadi ya wageni wanaotembelea hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mhifadhi wa hifadhi hiyo, Kamishna Emmanuel Sisiya katika uzinduzi wa tamasha hilo uliofanyika wilayani Same, ambapo alisema kuwa hapo nyuma wageni waliokuwa wakitembelea hifadhi hiyo walikuwa wachache.

Alisema kuwa, tamasha hilo limekuwa chachu na hamasa kubwa ya kutangaza hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ambapo kabla ya kuanzishwa tamasha hilo idadi ya wageni waliokuwa wakitembelea hifadhi walikuwa wachache lakini kwa sasa wameongezeka ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita walipokea wageni 7700 na katika wageni hao 4000 ni Watanzania.

"Wageni wengi wamechangiwa na hamasa kubwa inayofanywa kupitia tamasha hili la Same Utalii festival na kila anayekuja anakiri kuwa yeye ameifahamu Mkomazi kupitia matamasha mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanyika kuitangaza Mkomazi hivyo nirudishe pongezi kwa Mkuu wa wilaya Kasilda Mgeni kwa kuanzisha tamasha hili " Alisema Kumishna Sisiya.

Aliongeza kuwa, kwa sasa hifadhi hiyo ina fursa ya uwekezaji ambapo yapo maeneo kwa wageni kuja kuwekeza maeneo ya malazi na hoteli kwani wageni wengi wanaofika Same hudai eneo la malazi hayatoshi.

Alisema kuwa, ndani ya hifadhi maeneo ya malazi yaliyopo hayatoshi hivyo sasa ni fursa kwa Watanzania kuwekeza ndani ya hifadhi hiyo.

"Hifadhi ya Mkomazi katika Kanda ya Kaskazini ni ya pili ambapo ukifika utaweza kuwaona wale wanyama wakubwa watano tofauti na hapo katika Kanda ya Kaskazini utaweza kuwaona Serengeti na Ngorongoro lakini kwa urahisi na kwa ukaribu ukitaka kumwona faru mweusi utamwona ndani ya hifadhi ya Mkomazi" alisema.






Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) limetangaza kuwa Maonesho yake ya Tano ya Kitaifa yanatarajiwa kufanyika Oktoba 21 hadi 30, 2026 katika Uwanja wa Magufuli uliopo Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga, yakilenga kuinua uchumi wa wajasiriamali wadogo nchini.

Akizungumza Aprili 10, 2026 na wajasiriamali kuhusu maandalizi ya maonesho hayo, Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Silvester Mpanduji amesema tukio hilo litatoa fursa ya kujifunza mbinu bora za uzalishaji wa bidhaa zenye ubora na ushindani, pamoja na kupanua mitandao ya kibiashara.

Amesema maonesho hayo yatawakutanisha wajasiriamali, taasisi za Serikali na zisizo za kiserikali, pamoja na wadau wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi.

“Maonesho haya yatakuwa jukwaa muhimu kwa wajasiriamali kujitangaza, kupanua masoko, na kujifunza mbinu bora za uzalishaji,” amesema Prof. Mpanduji.

Kwa mujibu wa SIDO, zaidi ya wajasiriamali 600 kutoka Tanzania Bara na Visiwani wanatarajiwa kushiriki, sambamba na taasisi zaidi ya 50 zinazotoa huduma kwa sekta ya viwanda vidogo na vya kati.

Mbali na hilo, washiriki watapata fursa ya kujenga mitandao ya kibiashara, kukutana na wanunuzi na wawekezaji wapya, pamoja na kupata mitaji kupitia taasisi za kifedha.

Aidha, wananchi watapata nafasi ya kujifunza kuhusu bidhaa zinazozalishwa nchini na teknolojia mbalimbali zinazoweza kusaidia kuanzisha viwanda vidogo.

SIDO imewahamasisha wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kushiriki maonesho hayo ili kunufaika na fursa za kibiashara, huku sekta binafsi ikihimizwa kudhamini na kuonesha huduma zao.

Wananchi, hususan vijana na wanawake, wametakiwa kutumia maonesho hayo kama jukwaa la kujifunza namna ya kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Kwa ujumla, maonesho ya SIDO yameendelea kuwa chachu muhimu ya kukuza uchumi wa viwanda nchini kwa kuhamasisha ubunifu, ushindani na upatikanaji wa masoko kwa wazalishaji wa ndani.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, David Lyamongi amesema mkoa huo umejipanga kikamilifu kuhakikisha maonesho hayo yanafanyika kwa ufanisi mkubwa.

Ameeleza kuwa miundombinu ya usafiri, huduma za malazi pamoja na ulinzi na usalama viko katika hali nzuri kwa ajili ya kuhudumia wageni na washiriki.

“Mkoa wa Shinyanga upo tayari kushirikiana na wadau wote kuhakikisha maonesho haya yanafanikiwa na kuleta tija kwa washiriki na wananchi kwa ujumla,” amesema Lyamongi.

Aidha, Uwanja wa Magufuli uliopo Kahama umetajwa kuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya maonesho hayo kutokana na ukubwa wake na urahisi wa kufikika kutoka maeneo mbalimbali ya nchi



















Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo ameshiriki Mkutano wa Tisa wa Bahari ya Hindi, unaofanyika jijini Port Louis, Mauritius Aprili 10 hadi 12, 2026.

Mkutano huo unawakutanisha viongozi wa serikali, wanadiplomasia, wataalamu wa masuala ya usalama wa bahari, pamoja na wadau wa maendeleo kutoka mataifa yanayozunguka Bahari ya Hindi kujadili fursa na changamoto zinazohusiana na usalama wa bahari, biashara, mabadiliko ya tabianchi, pamoja na ushirikiano wa kiuchumi katika ukanda wa Bahari ya Hindi.

Mkutano huo umefunguliwa na Waziri Mkuu wa Mauritius Mheshimiwa Dr. Navinchandra Ramgoolam aliyesisitiza umoja, ushirikiano, na uwajibikaji wa pamoja miongoni mwa mataifa ya Bahari ya Hindi. Ametoa wito kwa nchi kushirikiana kukabiliana na changamoto za pamoja kama vile vitisho vya usalama, mabadiliko ya tabianchi, na maendeleo ya kiuchumi, ili kujenga mustakabali salama, endelevu, na wenye ustawi kwa eneo hilo.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano huo Waziri wa Mambo ya Nje wa India Mheshimiwa Subrahmanyam Jaishankar amesisitiza umuhimu wa ushirikiano imara wa kikanda na uwajibikaji wa pamoja katika Bahari ya Hindi. Alithibitisha dhamira ya India ya kukuza utulivu, maendeleo, ustawi na kuhimiza nchi za bahari ya Hindi kushirikiana katika kukabiliana na changamoto kuu kama usalama wa baharini, mabadiliko ya tabianchi, na maendeleo endelevu ili kuhakikisha eneo lenye amani na ustahimilivu.

Wakati wa Mkutano huo Mhe. Waziri Kombo atashiriki mijadala ya ngazi ya juu, kuelezea umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda na uchumi wa buluu. Balozi Kombo pia atafanya mazungumzo ya pande mbili na mawaziri na viongozi kutoka nchi mbalimbali ili kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na nchi hizo.

Mkutano huo ni jukwaa muhimu la kubadilishana mawazo, uzoefu na kuweka mikakati ya pamoja itakayochochea maendeleo endelevu kwa mataifa yanayozunguka Bahari ya Hindi na dunia kwa ujumla.








Top News