Na Janeth Raphael MichuziTv .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa onyo kali kwa viongozi wapya walioapishwa, akisisitiza kuwa madaraka waliyopewa si ya kujinufaisha wala kujiona bora, bali ni dhamana ya kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na uwajibikaji.

Akizungumza leo katika hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, Rais Samia aliwakumbusha viongozi hao kuwa nafasi walizonazo ni za muda na zinapaswa kutumika kwa manufaa ya umma, si kwa maslahi binafsi.

Amesisitiza umuhimu wa unyenyekevu kwa viongozi, akieleza kuwa ni kosa kubwa kwa yeyote kujivuna au kujiona hawezi kuwajibishwa kwa sababu ya cheo chake. “Madaraka ni dhamana nzito mbele ya Mungu na jamii, hivyo kila kiongozi anapaswa kuyaheshimu na kuyatumia kwa haki,” alionya.

Katika hotuba hiyo, Rais Samia pia ameeleza sababu za kumteua Eveline Munisi kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, licha ya kuwa Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi. Alifafanua kuwa uamuzi huo umetokana na sifa, uzoefu na uwezo aliouona katika wasifu wake wa kitaaluma, akiamini kuwa ana mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa Serikali.

Aidha, Rais Samia alirejea falsafa ya James Mbatia, aliyewahi kusisitiza umuhimu wa “kumhudumia Mama Tanzania,” akisema kauli hiyo inaendelea kuwa chachu ya kuwaunganisha Watanzania bila kujali tofauti zao za kisiasa, kwa lengo la kusukuma mbele maendeleo ya Taifa.

Akizungumzia ajira, Rais Samia alibainisha kuwa Serikali inaendelea kupanua fursa kwa vijana ndani na nje ya nchi. Alieleza kuwa zaidi ya vijana 7,000 tayari wamepata nafasi za ajira nje ya nchi mwaka huu, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda haki na stahili zao wanapokuwa kazini.

Pia aligusia umuhimu wa kuimarisha mahusiano kati ya Serikali, waajiri na wafanyakazi, akisema ushirikiano huo ni msingi wa kudumisha amani mahali pa kazi na kuchochea maendeleo endelevu ya nchi.

Akihitimisha hotuba yake, Rais Samia aliwataka viongozi wote walioapishwa kusimamia majukumu yao kwa uadilifu, weledi na kujituma, ili kuendana na matarajio ya Watanzania na kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa Taifa lenye ustawi.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya aliyekuwa Askofu wa Pili wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma na Katibu Mkuu Mstaafu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Marehemu Askofu Stanford Shauri.

Mazishi hayo yamefanyika katika Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma, Liuli Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais amesema Serikali inatambua mchango mkubwa aliyoutoa Askofu Shauri katika hapa nchini, akiwa ametumikia Serikali za Mitaa kwa zaidi ya miaka 12 pamoja na kuwa katibu mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa zaidi ya miaka 10.

Aidha, Makamu wa Rais amesema Marehemu Askofu Shauri amekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii pamoja na kuendeleza na kuikuza imani ya kikristo nchini.

Amesema ni dhamira ya Serikali kuendeleza yale ambayo Marehemu Askofu Shauri aliyasimamia ikiwemo masuala ya amani na haki.

Makamu wa Rais amewasilisha salamu za pole kwa familia ya marehemu, Kanisa la Anglikana, wakazi wa Ruvuma, Nyasa na wote walioguswa na msiba huo.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Maimbo Mndolwa, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano mzuri iliyonayo na Taasisi za Dini katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi. Ameipongeza Serikali kwa ukarabati wa barabara kutoka Mbambabay hadi Liuli katika Wilaya ya Nyasa ambayo ilikuwa ni changamoto kubwa hali inayodhihirisha kuwajali wananchi wa eneo hilo.














HANDENI, Tanga.
TIMU ya Wataalam kutoka Idara ya Wanyamapori na Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara ya Maliasili na Utalii wameendelea na zoezi la kutoa elimu kuhusu Wanyamapori wakali na waharibifu pamoja na uhifadhi wa mazingira kwa Wanafunzi wa shule za msingi na Sekindari katika Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu katika shule za msingi Mzeri na shule ya sekindari Misima Kiongozi wa Wataalam hao Bw. Nassor Wawa amesema elimu inapotolewa kwa vijana wenye umri mdogo inasaidia kujenga utamaduni wa Uhifadhi sambamba na elimu hiyo kudumu kwa jamii kwa muda mrefu.

Ameongeza kuwa Wanafunzi hao wanapokuwa na uelewa wa kutosha husaidia kuwaelimisha wazazi na jamii kwa ujumla.

Nao baadhi ya Wanafunzi na walimu waliopata mafunzo hayo wameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kutoa elimu hiyo kwani imewaongezea maarifa ya namna ya kuishi na kukabiliana na Wanyamapori wakali na waharibifu pamoja na uhifadhi wa mazingira.

Wameomba elimu hiyo kutolewa mara kwa mara kwa jamii zinazzunguka Hifadhi za Taifa kwa kiwa itasaidia kujenga uwajibikaji wa pamoja.

Elimu hiyo inatolewa kwa wananchi wa Wilaya ya Handeni hususani Wanafunzi wa shule za msingi na sekindari kwa lengo la kuwapa mbinu na maarifa ya kukabiliana na Wanyamapori wakali na waharibifu wanapopita katika makazi yao lakini pia kusaidia uhifadhi.

Walimu nchini wametakiwa kuchukua jukumu kubwa katika kujenga kizazi chenye uelewa wa teknolojia na matumizi sahihi ya mifumo ya kidijitali ili kuiwezesha Tanzania kunufaika kikamilifu na uchumi wa kidijitali.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Kati, Mhandisi Asajile John, wakati wa mkutano na wadau wa elimu uliofanyika Mei 6, 2026 jijini Dodoma, amesema walimu wana nafasi muhimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata maarifa sahihi ya teknolojia tangu ngazi za awali.

Amesisitiza kuwa masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye uwezo wa kushindana katika dunia ya kidijitali, aidha amezihimiza shule kuanzisha vilabu vya kidijitali vitakavyowawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo, kujadiliana na kukuza ubunifu wao.

“Nadhani kama zilivyo Klabu za rushwa, hisabati n.k, nadhani ni wakati sasa wa shule kuanzisha vilabu vya kidijitali ili kuwajengea wanafunzi uelewa mpana wa teknolojia na kuwasaidia kuwa kuwajenga kuanzia ngazi ya awali”.

Akizungumzia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mhandisi Asajile alibainisha kuwa inalenga kufikia angalau asilimia 70 ya Watanzania kuwa na uelewa wa matumizi ya teknolojia ya kidijitali, pamoja na kuhakikisha huduma nyingi zinaunganishwa katika mifumo ya kidijitali ili kuongeza tija.

Katika mkutano huo, pia aliwakumbusha wananchi kuwa makini na matumizi ya simu zao, akieleza kuwa katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu kumekuwepo na takribani majaribio ya uhalifu 9,800 kupitia ujumbe wa “tuma pesa kwa namba hii”.

Ameonya kuwa baadhi ya wahalifu hutumia laini zilizosajiliwa kwa majina ya watu wengine, hivyo wananchi wanapaswa kulinda laini zao kwani usajili wake ni mkataba wa kisheria unaohusisha namba ya NIDA na alama za vidole.

“Laini yako ni jukumu lako, Hakikisha haitumiki vibaya kwani unaweza kujikuta unaingia kwenye matatizo ya kisheria bila sababu,”.

Amehitimisha kwa kusema kuwa matumizi sahihi ya teknolojia ya mawasiliano yanaweza kurahisisha maisha, kuokoa muda na kuongeza ufanisi katika shughuli mbalimbali za maendeleo.




 

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeboresha huduma zake kwa kuwarahisishia wanachama kujisajili, kupata taarifa na kufuatilia mafao yao kupitia simu za mkononi bila kulazimika kufika ofisini.

Akizungumza Mei 6, 2026 jijini Dodoma wakati wa mkutano wa wadau wa elimu wa mkoa huo, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kati Lulyalya Sayi, amesema maboresho hayo yanalenga kumwezesha mchangiaji kukokotoa mafao yake na kufahamu jumla ya michango aliyowasilisha kwa urahisi zaidi.

Ameeleza kuwa mfuko huo ulianzishwa mwaka 2018 na unahudumia watumishi wa umma pamoja na sekta binafsi, kwa mujibu wa Sayi, PSSSF hutoa mafao ya aina mbili ambayo ni mafao ya muda mfupi na mafao ya muda mrefu.

Amesema Mafao ya muda mfupi yanawalenga wanachama wanaokumbwa na changamoto za muda, ikiwemo wanawake waliojifungua, wafanyakazi waliofukuzwa kazi, pamoja na wagonjwa,ambapo wanufaika hupatiwa mafao kuwasaidia kukabiliana na hali hizo.

Kwa upande wa mafao ya muda mrefu, amesema yanahusisha pensheni ya uzeeni kwa wanachama waliochangia kwa angalau miaka 15, na endapo mchangiaji atafariki baada ya kuanza kupokea pensheni, wategemezi wake watanufaika kwa kipindi cha miaka mitatu kupata mafao yake.

Aidha, mafao ya muda mrefu pia yanajumuisha, Mafao ya warithi, kwa wanachama waliotoa mchango kwa angalau miaka 15 lakini wakafariki kabla ya kustaafu wategemezi wao watapatiwa mafao hayo, lakini pia Mafao ya ulemavu, kwa wanachama wanaopata ulemavu kabla ya kufikia umri wa kustaafu, watapata mafao yao ili mradi wawe wamechangia kwa muda unaostahili.

Kwa sasa, wanachama wanaweza kutumia simu janja kuingia kwenye mfumo wa PSSSF (PSSSF Portal) kupitia google na kupata taarifa za michango  yao kwa urahisi badala ya kufika ofisini, amewataka wananchi kuendelea kujisajili na kufurahia huduma za mfuko huo.





Je, umewahi kucheza na kukosa namba zote halafu ukabaki na maumivu ya kupoteza? Sasa Meridianbet wamekuja na jambo jipya kabisa linalobadilisha mchezo. Kupitia huduma ya Lucky Loser, hata ukikosa namba zako zote bado una nafasi ya kushinda na kuselebuka kama mshindi halisi.

Ndiyo, umesoma vizuri. Ukiwa umecheza mchezo wa Win&Go na tiketi yako ikakosa namba zote 6, badala ya kukosa kila kitu, tiketi yako inageuka kuwa ya ushindi. Kupitia Lucky Loser, dau lako linazidishwa mara 30, hii ni nafasi ya kipekee kwa wachezaji wanaopenda ushindi hata pale mambo yanapogeuka.

Vilevile, Michezo mingi zaidi ya kubashiri inaendelea kupatikana ndani ya Meridianbet ikiwa na ODDS kubwa na machaguo mengi zaidi. Kushiriki ni vyepesi kupitia tovuti ya MERIDIANBET au kwa kupiga *149*10#.

Kipengele hiki kinapatikana kwa tiketi zinazochezwa kupitia akaunti ya fedha na zinahusisha kuchagua namba 6 ndani ya mchezo wa Win&Go. Hii ina maana kuwa kila unapocheza, hata kama bahati haiko upande wako mwanzoni, bado una nafasi ya kuondoka na pesa mkononi.

Kwa vijana wanaopenda michezo ya kubahatisha na kushinda, Meridianbet wanaendelea kuthibitisha kuwa wao ni chaguo sahihi. Wanakuja na ubunifu unaokupa nafasi zaidi ya kushinda na kufanya kila mchezo uwe na msisimko wa kipekee.

Usikubali kupitwa na nafasi hii. Ingia Meridianbet, cheza Win&Go na ujionee mwenyewe nguvu ya Lucky Loser. Kwa sababu hapa, hata ukipoteza bado unashinda.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa vikosi vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) vilivyopata miradi ya nishati safi ya kupikia kuwa mabalozi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa jamii zinazowazunguka.

Mwenyekiti Kingu ametoa wito huo leo Mei 5, 2026 wakati wa ziara ya Bodi hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inaayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Kambi ya JKT ya Maramba mkoani Tanga.

Aidha, amesisitiza vijana wanaliopo kwenye kambi hizo za JKT kupatiwa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala ili waweze kutumia ujuzi huo kujiajiri na kuwa mawakala wa kutengeneza mkaa mbadala pindi watakapomaliza mafunzo yao.

Kwa upande wake, akimwakilisha Mkuu wa JKT, Kanali Projest Rutaihwa aliishukuru menejimenti na Bodi ya REA kwa utekelezaji wa miradi nishati safi ya kupikia huku akiahidi kusimamia mradi huo unakuwa endelevu ili kuendelea kulinda mazingira pamoja na afya za wanaoandaa chakula.

Naye Luteni Kanali Thobias Ngailo, Meneja wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka JKT, ameeleza kuwa jumla ya vikosi 22 vimenufaika na fedha zilizotolewa na Serikali kupitia REA ambapo amesema mashine 30 kati ya 60 za kutengeneza mkaa mbadala zimeshasambazwa katika vikosi na zinaendelea kufanya kazi, hatua inayotarajiwa kuongeza uzalishaji na matumizi ya nishati safi kwa kiwango kikubwa. 











Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili katika Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma kushiriki Ibada ya Mazishi ya aliyekuwa Askofu wa Pili wa Anglikana Dayosisi ya Ruvuma na Katibu Mkuu Mstaafu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Marehemu Askofu Stanford Shauri, Ibada inayofanyika Liuli Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma leo tarehe 06 Mei 2026.



Na Mwandishi Wetu.

CHAMA cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato Tanzania (TAREWU) kimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) na Taasisi ya Usimamizi wa Vihatarishi Tanzania (IRMT) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika maendeleo ya kitaaluma na mafunzo ya usimamizi wa vihatarishi.

Makubaliano hayo yamesainiwa jijini Dar es Salaam, yakilenga kuwajengea uwezo wanachama wa TAREWU ili kuongeza ufanisi na tija katika sekta ya ukusanyaji mapato nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa IRMT, CPA Pius Maneno, amesema taasisi yake ipo tayari kutoa mafunzo yenye viwango vya kimataifa na kushirikiana katika kukuza taaluma ya usimamizi wa vihatarishi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAREWU, Lutufyo Mtafya, amesema makubaliano hayo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa mpango mkakati wa chama hicho unaolenga kuwafanya wanachama wake kuwa na ujuzi shindani unaoendana na mabadiliko ya kiuchumi duniani.

Amesema kupitia ushirikiano huo, wanachama watanufaika na programu za mafunzo, ushauri wa kitaalamu pamoja na fursa za kukuza ujuzi katika maeneo ya kisasa ya usimamizi wa vihatarishi.

Naye Katibu wa IRMT, Christopher Njovu, amesema ushirikiano huo utasaidia kuongeza uelewa wa masuala ya vihatarishi katika sekta ya ukusanyaji mapato na kusisitiza umuhimu wa taaluma hiyo katika kulinda rasilimali za taasisi.

Kwa upande wa TAREWU, Katibu wake, Wakili Michael Marere, amesema makubaliano hayo yatakuwa chachu ya maendeleo endelevu kwa wanachama na sekta nzima ya mapato nchini.

TAREWU imeeleza kuwa ina imani ushirikiano huo utafungua ukurasa mpya wa mafanikio, huku IRMT ikiahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa yanafikiwa.



Na Mwandishi wetu

MKUU wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yatakayofanyika kitaifa Mei 8, 2026 katika Kijiji cha Mgusu, Manispaa ya Geita.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, maandalizi ya tukio hilo yamekamilika, huku shughuli za awali zikitarajiwa kuanza Mei 6 hadi 7 kwa kutoa huduma za matibabu kwa punda pamoja na elimu kwa wafugaji na jamii.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa kipindi hicho, kliniki maalumu zitahudumia takribani punda 700 katika maeneo ya Mgusu, Magenge na mji wa Geita. Sambamba na hilo, elimu kuhusu utunzaji bora, lishe na matumizi sahihi ya vifaa vya punda itatolewa ili kuboresha ustawi wa wanyama hao.

"Zaidi ya wanafunzi 3,800 pamoja na wanajamii watanufaika na programu za elimu zitakazowasilishwa kupitia maonesho ya vitendo, sanaa na kampeni za uhamasishaji, lengo likiwa ni kujenga kizazi chenye uelewa wa kulinda rasilimali hiyo muhimu,"ilieleze taarifa hiyo.

Maadhimisho hayo yatakuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa ustawi wa punda, yakiongozwa na kaulimbiu isemayo, “Kulinda Punda wa Afrika ni Wajibu Wetu Sote.” Kaulimbiu hiyo inalenga kuibua uelewa mpana juu ya changamoto zinazowakabili punda na haja ya kuchukua hatua za pamoja kuwalinda.

Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto, ameusifu uwekezaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wa Tanzania unaoendelea jijini Nairobi, akisema ni mfano bora wa matumizi sahihi ya akiba za wanachama katika kukuza uchumi na maendeleo ya kikanda.

Akizungumza Mei 5, 2026 wakati akihutubia Bunge jijini Dodoma, Mhe. Dkt. Ruto alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Tanzania, Bw. Masha Mshomba, kwa usimamizi thabiti wa uwekezaji huo, akibainisha kuwa unaonesha namna bora ya kugeuza akiba za wanachama kuwa miradi yenye tija.

Alisema mradi huo uliopo eneo la Upper Hill, jijini Nairobi, unahusisha ujenzi wa majengo pacha yenye ghorofa 22, unaogharimu takribani dola za Marekani zaidi ya Milioni 51. Mradi huo unatekelezwa kwa kutumia akiba za wanachama wa NSSF Tanzania na unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili.

Mhe. Dkt. Ruto alieleza kuwa uwekezaji huo ni somo muhimu kwa Kenya na mataifa mengine ya Afrika Mashariki kuhusu umuhimu wa kukuza utamaduni wa akiba na uwekezaji kwa maendeleo ya muda mrefu.

“Uwekezaji ni zao la akiba. Huwezi kuwekeza kama huna akiba,” alisisitiza Dkt. Ruto, akihimiza wananchi na taasisi kuzingatia nidhamu ya kuchangia katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mustakabali wa baadaye.

Aidha, alibainisha kuwa nchini Kenya wamefanya maboresho ya mfumo wa hifadhi ya jamii mwaka 2023 baada ya kujifunza kutoka mifumo bora ikiwemo ya Tanzania.

Alieleza kuwa mfumo huo unahitaji mwajiri na mwajiriwa kuchangia kwa pamoja hadi asilimia 20 ya mapato ili kuimarisha usalama wa kifedha kwa wafanyakazi wanapostaafu.

Mhe. Dkt. Ruto alisisitiza kuwa utamaduni wa kujiwekea akiba unapaswa kuendelezwa ndani ya jamii, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kujenga mifumo imara ya hifadhi ya jamii.

Rais Dkt. Ruto pia alisifu mafanikio ya Tanzania katika sekta ya hifadhi ya jamii, akieleza kuwa Kenya inaendelea kujifunza na kuchukua mifano bora kutoka kwa majirani zake.

Katika kuimarisha ushirikiano wa kikanda, alisema anajivunia uhusiano mzuri uliopo kati ya Kenya na Tanzania chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akibainisha kuwa huu ni wakati muhimu katika historia ya mataifa hayo mawili.

Akihitimisha, Dkt. Ruto amesema kuwa kwa sasa kuna hatua kubwa ya kihistoria katika uhusiano wa Kenya na Tanzania, akieleza furaha yake kwa ushirikiano wa karibu kati yake na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema viongozi hao wanafanya kazi kwa pamoja kuwaleta karibu wananchi wa Afrika Mashariki na kuondoa changamoto zilizodumaza maendeleo kwa muda mrefu.

Kauli hiyo inaakisi mwelekeo wa mataifa ya Afrika Mashariki katika kutumia rasilimali zao za ndani kama kichocheo cha ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi.

Rais Dkt. William Ruto anahitimisha ziara rasmi ya siku mbili nchini Tanzania, iliyoanza Mei 4 hadi 5, 2026.






















MCHEZO wa marudiano wa nusu fainali ya UEFA Champions League kati ya Bayern Munich na Paris Saint-Germain unatarajiwa kuwa wa moto mkubwa kufuatia matokeo ya mkondo wa kwanza yaliyomalizika kwa PSG kushinda 5-4.

Huu ni miongoni mwa michezo yenye mabao mengi zaidi katika hatua hii, ukiweka wazi kuwa timu zote mbili zinategemea zaidi nguvu ya ushambuliaji kuliko ulinzi.

Katika mchezo wa kwanza, PSG walionyesha ubora mkubwa hasa kipindi cha pili walipofika hadi kuongoza 5-2, wakiongozwa na nyota wao kama Ousmane Dembélé na Khvicha Kvaratskhelia waliocheza kwa kiwango cha juu na kufunga mabao muhimu. Hata hivyo, Bayern hawakukata tamaa na walirudi kwa kasi wakifunga mabao mawili ya haraka na kufanya matokeo kuwa 5-4, jambo linaloacha mlango wazi kwa mchezo wa pili.

Kiu ya ushindi kwa Bayern Munich itakuwa kubwa zaidi wakicheza nyumbani, kwani wanahitaji ushindi wa angalau bao moja ili kusawazisha au mawili ili kusonga mbele moja kwa moja. Kikosi chao chenye washambuliaji hatari kama Harry Kane, Michael Olise na Luis Díaz tayari kilionyesha uwezo wa kupasua safu ya ulinzi ya PSG, hivyo wana nafasi halisi ya kubadili matokeo.

Kwa upande wa PSG, wataingia wakiwa na faida ndogo lakini yenye thamani kubwa. Kocha Luis Enrique anatarajiwa kuendelea na mfumo wa kushambulia badala ya kujilinda, jambo linaloweza kufanya mchezo huu kuwa wazi tena. Hata hivyo, changamoto kubwa kwao ni udhaifu wa safu ya ulinzi uliodhihirika kwenye mchezo wa kwanza pamoja na uwezekano wa kukosekana kwa baadhi ya wachezaji muhimu kutokana na majeraha.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kiufundi, mechi hii itategemea nani atakuwa na uwiano mzuri kati ya kushambulia na kujilinda. Bayern wanaweza kutumia presha ya mashabiki wao na kasi ya pembeni kuvuruga PSG, huku PSG wakitegemea zaidi mipira ya kushitukiza (counter attack) na ubunifu wa viungo wao. Udhibiti wa kiungo na matumizi sahihi ya nafasi chache vitakuwa silaha kuu kwa timu zote mbili.

Kwa ujumla, mchezo huu unatarajiwa kuwa na ushindani mkali na uwezekano mkubwa wa mabao mengi tena kutokana na historia ya mkondo wa kwanza. Ni pambano la wazi ambalo linaweza kuamuliwa na makosa madogo ya ulinzi au ubora binafsi wa wachezaji. Mashabiki wa soka wanatarajia burudani nyingine kubwa, huku nafasi ya kufuzu fainali ikiwa bado iko wazi kwa pande zote mbili.jisajili.
Na MWANDISHI WETU

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, ametangaza operesheni kali dhidi ya wanaojihusisha na uvujaji wa mapato wilayani humo na kumwagiza Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Aidan Kitare, kuivunja Kikosi Kazi cha Mapato (KKM) kinacho husika na usimamizi wa mapato.

Aidha ametoa onya kali kwa baadhi ya madiwani watakao jaribu kulalamika baada ya kuondolewa au jamaa zao kuondolewa katika kamati hiyo kutokana na kubainika kushiriki katika kuhujumu mapato.Magoti, aliyasema hayo alipohutubia kikao cha Baraza la Madiwani la Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani.

Ameeleza kusikitishwa na uvujaji mkubwa wa mapato katika wilaya hiyo hali inayo kwamisha maendeleo."Watu wana kula kwelikweli. Wanakula vibaya mno halafu wanalalamika. Nataka niwaambie tumefahamiana kwa sababu ya kazi, tofauti na kazi sina udugu nanyie. Tufanye kazi , tumsaidie Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kutekeleza majukumu,"amesema Magoti.

Amesema, dhamira ni kujenga Kisarawe inayo heshimu mali na mapato ya serikali ambapo kama mianya ya uvujaji wa mapato itadhibitiwa wilaya hiyo inaweza kukusanya sh.bilioni 7 tofauti na sh. bilioni 4 inazo kusanya sasa.
"Unakwenda sehemu unakuta waliumu wana kaa chini. Hawana ofisi. Hii ni aibu. Mapato yanaliwa na watu wachache,"amebainisha Magoti.

Amesema ana faili maalumu la wahusika wanao jihusisha kuhujumu mapato pamoja na maeneo yote yanayo tumika."Ninafaili hili hapa. Wahusika wote wanaohujumu mapato. Diwani ukiwa na malalamiko yoyote fika ofisini kwa Mwenyekiti wa Halmashauri au kwa mkurugenzi akulete kwa mkuu wa wilaya na ukibainika unahusika au ndugu yako unaye mtetea anahusika tukakupa ushahidi tutakuchukulia hatua,"amedai Magoti.

Amesema anataarifa za kila mtu aliyeondolewa katika Kikosi Kazi cha Mapato ya halmashauri hiyo kupitia faili maalumu la wahujumu wa mapato.

"Diwani yoyote anaye jua kwamba ndugu yake alikula mapato taarifa zake ninazo humu katika falili.Diwani yoyote atakaye piga kelele nitamkamata,"ameonya Magoti.
Ameeleza, diwani kuwa na ndugu anaye kusanya mapato siyo dhabi bali dhambi ni kumtumia ndugu yake huyo kujipatia mapato na kuibia halmashauri.

"Kwa Mamlaka niliyo nayo ninakuelekeza mkurugenzi kuvunja kikosi hicho hadi kufikia pia ukae na Kamati ya Usalama ya wilaya kuunda kikosi kipya,"amesema
Magoto amesema kikosi hicho kikundwa kikiundwa, kipewe semina na kiingie kazini kutekeleza majukumu ya kukusanya mapato.

Aliongeza; "Na hiki mkurugenzi ndiyo kipimo chako cha kwanza cha kujua unatosha ama utoshoshi. Mimi ndiyo nina vyombo. Hakuna mtu yoyote mwenye vyombo katika wilaya hii. Mkurugenzi usiogope. Mimi ndiyo naweza kusema uwepo au usiwepo kwa hiyo fanya kazi,".

Aidha ameelekeza polisi wilayani humo kumsakama mmiliki mmoja wa jengo la ghorofa jirani na ofisi za halmashauri hiyo ambalo alisema lina husika katika vitendo vya kuhujumu mapato.

"Kuna kijengo cha ghorofa jirani na hapa halmashauri. Mwiteni mmiliki anieleze shughuli zinazofanyika pale hadi saa saba usiku na kuanza kesho usiku (leo) wote watao kuwa pale wakamatwe,"amesema.Ameeleza mmiliki wa jengo hilo ambaye ni mwanamke afikishwe mbele yake kabla ya saa 9:00 alasili jana kujieleza.

Katika hatua nyingine, Magoti alitangaza kufanya operesheni ya kuvunja nyumba zilizojengwa kinyume cha sheria katika eneo la serikali la Homboza na kwamba katika operesheni hiyo aliyo ibatiza jina la Kanyamazongo atawatia mbaloni mabalozi saba wanaopinga jitihada za serikali.

"Hatuhitaji watu wanao hujumu serikali.Pale halmashauri itaingiza shilingi bilioni 5.8. Kuna shule imejengwa pale halmashauri ili nunua eneo lake yenyewe.Ni vitu vya ajabu sana,"amesema .

Aidha Magoti alitaja vizuizi vinavyoongoza kwa kuiba mapato wilayani humo na kuyatorosha kuwa ni Homboza, Kwa Pinda, Kiluvya Kisokwa, Ikuruwi, Kauzeni, Msanga na Masaki.

" Kuna watu wanachukua fedha taslimu pale.Tunaorodha yao humu katika faili. Tutakamata baiskeli, pikipi, magari na kila muhusika,"ameeleza Magoti.
Kuhusu watu wanaouza kiholela maeneo hususan katika eneo la Cha Kenge, Magoti amesema Operesheni Kanyazongo itamkumba kila muhusika.

"Madiwani niwaombe nyie ndiyo viongozi wa kamati za maendeleo za kata kwa hiyo kama eneo lako linauza viwanja kinyume cha utaratibu tutakuhoji,"amesema


















Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Godfrey Eliakimu Mnzava, akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, viongozi wa siasa, pamoja na timu ya wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, amefanya ziara ya kikazi kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopendekezwa kupitiwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mnzava alikagua mradi wa Kituo cha Mafuta cha Mavoa kilichopo Kitongoji cha Njiapanda Magharibi, Kata ya Njiapanda, pamoja na mradi wa Zahanati ya Ghona uliopo Kijiji cha Ghona katika Kata ya Kahe Mashariki. 

Aidha, Mkuu wa Wilaya na timu yake walifika katika Shule ya Sekondari Mwika ambapo ndipo litakapokuwa eneo la mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, eneo ambalo pia Mwenge utajionea programu maalum ya matumizi ya Nishati Safi.

Miradi mingine iliyofanyiwa ukaguzi ni pamoja na ujenzi wa barabara katika Kata ya Kilema Kusini, mradi wa maji wa Kijiji cha Mabungo uliopo Kata ya Kirua Vunjo Kusini, pamoja na mradi wa vijana na uzalishaji wa madini ya ujenzi. 

Vilevile, ziara hiyo ilihusisha ukaguzi wa ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Kimochi na ujenzi wa Shule ya Amali ya Sekondari Chemchem iliyoko Manushi katika Kata ya Kibosho Magharibi.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2026 zinatarajiwa kuingia mkoani Kilimanjaro tarehe 28 Juni 2026 na kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ifikapo tarehe 01 Julai 2026. 

Mwenge huo utaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo.








Top News