Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu wa Tatu wa Uganda Mhe. Rukia Isaya Nakadama mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe nchini humo tarehe 12 Mei, 2026. Rais Dkt. Samia amewasili nchini Uganda kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule nchi hiyo, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, zitakazofanyika katika Viwanja vya Kololo Jijini Kampala nchini humo.

Na Janeth Raphael- MichuziTv -Dodoma.

Serikali imesema inaendelea kuchukua hatua mahsusi za kupunguza gharama za uzalishaji wa zao la tumbaku ili kuongeza faida kwa wakulima na kuimarisha mchango wa zao hilo katika uchumi wa nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 12, 2026 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Jacqueline Kainja Andrew, aliyetaka kujua ni lini Serikali itaangalia upya gharama za uzalishaji wa tumbaku ili wakulima waweze kunufaika zaidi na kilimo hicho.

Akijibu swali hilo, Silinde amesema Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa tumbaku, ikiwemo ongezeko la bei za pembejeo, gharama kubwa za nishati inayotumika katika ukaushaji wa tumbaku kama kuni na makaa, pamoja na riba kubwa za mikopo kutoka taasisi za kifedha.

Amesema kupitia Bodi ya Tumbaku kwa kushirikiana na wadau wa sekta hiyo, tayari Serikali imeanza kufanya tathmini ya kina ya muundo wa gharama za uzalishaji ili kubaini maeneo yanayochangia mzigo mkubwa kwa wakulima na namna ya kupunguza gharama hizo.

“Serikali inaangalia maeneo mbalimbali ikiwemo tozo za vyama vya ushirika, gharama za pembejeo pamoja na masharti ya mikopo inayotolewa kwa wakulima wa tumbaku,” amesema Silinde.

Aidha, amesema Serikali tayari imeanza mazungumzo na benki pamoja na taasisi za kifedha zinazotoa mikopo kwa wakulima wa tumbaku ili kujadili uwezekano wa kupunguza riba na gharama nyingine zinazohusiana na huduma za kifedha.

Kwa mujibu wa Silinde, hatua hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wakulima wa tumbaku wanapata faida stahiki kutokana na jasho lao, huku zikilenga kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji wa zao hilo muhimu la biashara nchini.













Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Uganda kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni tarehe 12 Mei, 2026.









NA: MWANDISHI WETU, PANGANI.

Utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu unaozingatia umahiri kwa wanafunzi unaendelea kutekelezwa nchi nzima katika kuhakikisha nchi inazalisha wahitimu wenye uwezo wa kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa.

Katika Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga, Mei 8, 2026, wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo, katika somo la Biashara (Business Studies), wameweza kupika vitafunwa mbalimbali kama chapati, maandazi, sambusa na vitumbua ikiwa ni sehemu ya ujifunzaji kwa vitendo wa uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zilizo katika mazingira yao (local production).

Mwalimu wa somo la Biashara wa shule hiyo, Shija Clement amesema baada ya ujifunzaji wa nadharia wa Mada ya Uzalishaji (Production), wanafunzi wanapaswa kuweka ujifunzaji huo kwa vitendo ili kuwajenga katika umahiri na kujitegemea hata baada ya kuhitimu masomo yao ili pia waweze kujiajiri wenyewe na kuanzisha biashara zao.

"Wanafunzi wanapaswa kuwa na ujuzi fulani wanapohitimu masomo, wanafunzi hawa wamefanya kwa vitendo utengenezaji wa sambusa, chapati, maandazi na vitumbua lakini pia wamewauzia wanafunzi wenzao ili kuangalia kama uzalishaji wao umewapatia faida au hasara," amesema Shija.

Sambamba na hilo, Shija amesema somo la Biashara linahitaji kufanya vitendo zaidi kwa sababu elimu ya biashara inapaswa kuwekwa katika vitendo ili tija ya kupata faida ionekane badala ya kubaki na maarifa ya biashara kichwani pekee.

Katika hatua nyingine, mwanafunzi ambaye ameshiriki kupika vitafunwa hivyo, Fatuma Madaba amesema amefurahia mapishi na ameongeza uelewa wa namna ya kupika vitafunwa hivyo, ujuzi ambao anaweza kutumia hata akimaliza shule katika kujiingizia kipato.

"Nimeongeza kitu kikubwa katika mapishi ya leo, elimu hii ya ujasiriamali tunayofundishwa imenisaidia kunijenga hata baada ya kuhitimu masomo yangu naweza kuingiza kipato," amesema Madaba.

Kwa upande wa Mkuu wa Shule hiyo, Nassoro Gamba, amepongeza ubunifu huo ambao umejikita kuimarisha stadi za umahiri katika ujenzi wa vizazi vyenye kujitegemea katika maisha. Pia, ameahidi kuwa mteja wa kudumu wa bidhaa zao watakazoendelea kuzizalisha shuleni hapo.

Ikumbukwe kuwa somo la Biashara ni miongoni mwa masomo ya lazima kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini, ikiwa ni mkakati wa serikali wa kuzalisha wahitimu wenye maarifa na ujuzi fulani katika kujipatia kipato ili kuepuka kusubiri kuajiriwa.






Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba jana Mei 11, 2026 alishiriki chakula cha jioni cha kitaifa kilichoandaliwa na Rais wa Kenya Dkt. William Ruto kwa heshima ya Wakuu wa Nchi na Serikali wanaoshiriki Mkutano wa Ushirikiano wa Afrika na Ufaransa

Dkt. Mwigulu yupo nchini Kenya akimuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ushirikiano wa Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Lengo la mkutano huo ni kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.

WAZIRI MKUU, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto pamoja na Mke wa Rais wa Kenya, Mama Rachel Ruto, wakati wa chakula cha jioni cha kitaifa kilichoandaliwa kwa heshima ya Wakuu wa Nchi na Serikali wanaoshiriki Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward Summit: Africa–France Partnership for Innovation and Growth) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.




 

Na Nasra Ismail


📍Lwamgasa, Geita

Bodi mpya ya Wakurugenzi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) leo 11 Mei, 2026 imefanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya Shirika hilo iliyoko kanda ya Ziwa. Lengo la ziara hiyo ni kujionea utekelezaji na kuhakikisha miradi inatekelezwa kama ilivyopangwa na kukidhi malengo yaliyowekwa na Shirika.

Wajumbe wa bodi hiyo wametembelea kwanza kituo bora cha mfano kwa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu uliopo katika Kata ya Lwamgasa, Wilaya ya Geita. Mradi huo hutumika kama darasa la kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini kutoka sehemu mbalimbali nchini.

Akizungumza moja ya wajumbe hao Bw. Leonard Chacha, amesema mgodi wa Lwamgasa ni mgodi wa mfano nchini. Amesisitiza kuwa kupitia mgodi huo, wachimbaji wanafundishwa namna bora ya kuchimba kisasa ili kuongeza tija na kuhakikisha usalama wao wakati wa kazi na utunzaji wa mazingira.

Chacha aliongeza kuwa pamoja na mafunzo ya uchimbaji, wachimbaji hao pia huwezeshwa kutumia mashine za kisasa katika uchenjuaji wa madini ya dhahabu. Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwaondoa wachimbaji wadogo kwenye teknolojia duni inayowapotezea madini mengi na kuharibu mazingira.

Katika hatua nyingine ya ziara hiyo, wajumbe wa bodi walitembelea Mgodi wa Dhahabu wa Buckreef ambao STAMICO inauendesha kwa ubia na kampuni ya TRX Gold Corporation. Wajumbe hao walipata wasaa wa kupata taarifa ya mradi na kukagua shughuli mbalimbali za uzalishaji kuanzia uchimbaji hadi uchenjuaji.

Aidha, Wajumbe wa bodi wameridhishwa na hali ya utunzaji wa mazingira katika mgodi wa Buckreef. Wamesema uongozi wa mgodi umeweka mikakati mizuri ya kuhakikisha shughuli za uchimbaji hazileti madhara kwa mazingira yanayozunguka eneo la mradi.

Wilson Mutagwaba, Mjumbe wa Bodi ya STAMICO, amekiri kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa katika mgodi wa Buckreef. Amesema pamoja na utunzaji wa mazingira, suala la usalama mahali pa kazi limepewa kipaumbele kikubwa na wafanyakazi wote wanafuata taratibu za usalama.

Bodi ya Wakurugenzi imeahidi kutoa ushirikiano wa dhati katika kufanikisha shughuli za Shirika na kuendelea kufanya ziara za mara kwa mara katika miradi yote ya STAMICO nchini. Lengo ni kuhakikisha miradi hiyo inakuwa na tija kwa Taifa, inalipa kodi stahiki na inawanufaisha wananchi wanaozunguka maeneo ya miradi hiyo.












KINSHASA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mei 5, 2026 – Mkuu wa Udhibiti wa Airtel Africa na Mwenyekiti wa Kundi la Sera Afrika la GSMA, Bw. Daddy Mukadi, ametoa wito kwa serikali za Afrika kutambua sekta ya mawasiliano ya simu kama nguzo kuu ya uchumi na kutekeleza mageuzi mawili mahususi ya kodi yanayoweza kuharakisha kwa kiasi kikubwa ujumuishaji wa kidijitali barani.

Akizungumza katika toleo la kwanza la mkutano wa États Généraux du Secteur des Postes et Télécommunications uliofanyika Kinshasa, DRC—hafla iliyolenga kuandaa dira ya kimkakati ya sekta ya kidijitali na mawasiliano nchini humo na kuhudhuriwa na Rais Félix Tshisekedi Bw. Mukadi, ambaye pia ni mwanachama wa Kundi la Sera la Kimataifa la GSMA, aliwataka wadau wa serikali na sekta binafsi kufikiria upya nafasi ya mawasiliano ya simu katika maendeleo ya kitaifa.

Alisisitiza kuwa sekta hiyo haipaswi tena kuonekana kama sekta saidizi pekee, bali kama mhimili mkuu wa maendeleo ya uchumi wa bara.
“Sekta ya mawasiliano haiwezi tena kuchukuliwa kama ya kusaidia tu. Sasa ni sekta ya msingi. Sekta zote kuanzia usalama, fedha, usafiri hadi afya zinategemea teknolojia ya kidijitali kwa ukuaji,” alisema.

Kauli zake zinakuja katika wakati muhimu kwa uchumi wa kidijitali barani Afrika. Kwa mujibu wa ripoti ya Mobile Economy Africa 2025 ya GSMA, sekta ya simu ilichangia dola za Marekani bilioni 220 katika uchumi wa Afrika mwaka 2024, sawa na asilimia 7.7 ya Pato la Taifa (GDP), na inatarajiwa kufikia dola bilioni 270 ifikapo mwaka 2030.

Hata hivyo, licha ya mitandao ya simu kufikia asilimia 95 ya watu barani Afrika, takribani asilimia 75 ya wananchi bado hawajaunganishwa na huduma za intaneti—changamoto inayochangiwa zaidi na gharama kubwa za vifaa vya kidijitali.

Kutokana na hali hiyo, Bw. Mukadi alipendekeza maboresho ya sera za umma pamoja na mifumo ya kisheria na udhibiti ili kupanua upatikanaji wa huduma za kidijitali. Alisisitiza kuwa sekta ya mawasiliano inapaswa kutambuliwa kama nguzo ya msingi ya maendeleo ya uchumi, huku wadau wakishirikiana kuongeza uwekezaji, kupanua wigo wa huduma na kupunguza pengo la matumizi ya huduma hizo.

Aidha, alitaja vikwazo vikuu vinavyozuia ujumuishaji wa kidijitali kuwa ni pamoja na gharama za simu janja na ushuru wa uagizaji wa miundombinu ya mawasiliano. Alipendekeza kusamehe ushuru na kodi kwa muda wa miaka miwili hadi mitatu kwa simu janja za bei nafuu (kati ya dola 40 hadi 150) ili kusaidia kupunguza pengo la matumizi.

Pia alipendekeza kuondolewa kwa ushuru wa kuingiza vifaa vya mawasiliano kwa angalau miaka mitatu ili kuchochea upanuzi wa mtandao.

Aliongeza kuwa, hatua hizi “zitasaidia kuleta teknolojia jumuishi na endelevu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii,” akiongeza kuwa zitachochea kasi ya muunganiko, kuboresha upatikanaji wa huduma na kuwezesha watu, biashara na jamii nyingi zaidi kushiriki katika uchumi wa kidijitali.

Alissisitiza kuwa ni muhimu kwa serikali na sekta binafsi kushirikiana kwa karibu kuunda mazingira ya udhibiti yanayochochea ubunifu, kulinda watumiaji na kuhimiza uwekezaji wa muda mrefu.
Dar es Salaam ilishuhudia weekend ya kipekee ya burudani, fashion, elegance na celebration baada ya Serengeti Premium Apple kuandaa mfululizo wa matukio ya kusherehekea Siku ya Mama Duniani yaliyofanyika katika maeneo ya Upper Deck, Hyatt Regency, na Maison Femme.

Wanawake mbalimbali kutoka kwenye taaluma tofauti, sekta za mitindo, ubunifu, lifestyle, media na burudani walijitokeza kwa muonekano wa kuvutia na wa kifahari kusherehekea pamoja na mama zao, marafiki, na wanawake wenzao wanaowapa hamasa kwenye maisha yao ya kila siku.

Kuanzia mitindo ya mavazi ya kuvutia, mionekano ya kipekee, na kufurahia nyakati za kipekee pamoja mpaka kufanya ‘toast’ pamoja na mama zao, weekend hiyo iligeuka kuwa celebration ya kisasa iliyochanganya mitindo, urembo, usasa na kujumuika pamoja katika mazingira ya kipekee yaliyojaa furaha na upendo.

Katika kila location, wageni walipokelewa kwa glass maridadi ya kinywaji cha Serengeti Premium Apple ambacho kimetengezwa hapa nchini na kampuni ya Serengeti Breweries Limited kabla ya kushiriki kwenye #ToastToMoms, moment maalum iliyowapa nafasi ya kuelezea sababu zao za kumsherehekea mama yao au wanawake waliowalea na kuwahamasisha maishani.

Mbali na kusherehekea Siku ya Mama Duniani, experiences hizo pia ziliendelea kuonyesha misingi ya chapa mpya ya Serengeti Premium Apple iliyotengenezwa Tanzania ikiwa na ladha ya hadhi ya kimataifa ambayo ni: ladha yake laini ya apple, yenye kuburudisha na rahisi kufurahia kunywa, kuendelea kusherehekea wanawake wa kisasa wenye kujiamini na hadhi, pamoja na kuvumbua namna mpya za kufurahia mitindo mipya na ya kisasa ya maisha kupitia  nyakati tofauti zinazounganisha watu.

Kupitia mazingira ya kifahari, muziki, mitindo ya mavazi, kufurahia chakula na vinywaji, kujumuika kwa pamoja kupitia nyakati zenye hadhi ya kipekee, Serengeti Premium Apple inaendelea kujitambulisha kama kinywaji kinachowakilisha kizazi cha kisasa cha Watanzania wanaopenda fahari yao, kujumuika kwa pamoja, na kusherehekea maisha kwa namna tofauti.

Kwa wengi waliohudhuria, #ToastToMoms haikuwa tu event ya Mother’s Day, ilikuwa celebration ya womanhood, confidence, style na appreciation.

Sophistication. Bottled.

Stylish women. Beautiful moments. Premium vibes. #ToastToMoms by Serengeti Apple ilikuwa full elegance all weekend.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Wanawake wa kisasa walitokelezea kwa fashion, confidence na classy vibes kusherehekea #ToastToMoms.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Mother’s Day lakini kwa elegance, style na unforgettable vibes.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Wanawake walipendeza. Vibes zilikuwa premium. Serengeti Apple delivered the moment.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Fashion, laughter, beautiful toasts na premium moments — hivyo ndivyo #ToastToMoms ilivyokuwa.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Soft life, stylish moments na celebration za kweli Siku ya Mama Duniani.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Classy looks. Beautiful smiles. Mother’s Day vibes done right.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Elegant women + premium vibes + unforgettable toasts.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple

Weekend ya fashion, vibes na celebrating moms the sophisticated way ikisindikizwa na Serengeti Apple.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple


Wanawake wa Dar walijitokeza kwa confidence, elegance na premium energy kusherehekea Siku ya Mama Duniani na Serengeti Apple.#SerengetiApple #SophisticationBottled #ToastToMoms @serengeti.apple




 

Katika hatua muhimu kwa sekta ya benki nchini  na uongozi wa taasisi za kibiashara barani Afrika, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc, Ruth Zaipuna, anatarajiwa kuzungumza katika Cambridge Africa Business Conference 2026, utakaofanyika Mei 30, 2026 katika Chou cha Biashara cha Cambridge Judge chini ya  Chuo Kikuu cha Cambridge Uingereza.

Katika jukwaa hilo, Zaipuna anatarajiwa kutoa hotuba kuu kuhusu safari ya mageuzi ya NMB na mchango wake katika uchumi wa Tanzania, akieleza namna benki hiyo ilivyokua kutoka katika mizizi ya huduma ndogo za fedha hadi kuwa moja ya taasisi zinazoongoza katika sekta ya fedha nchini.

Mkutano huo wenye kaulimbiu ya “Kujenga Mustakabali wa Afrika: Mitaji, Ubunifu na Ukuaji wa Kiwango cha Bara,” unalenga kujadili nafasi ya Afrika katika kuchochea ukuaji kupitia mitaji, ubunifu na uwezo wa taasisi za Afrika kufanya kazi kwa kiwango cha bara, hususan katika mazingira ya AfCFTA.

Akizungumzia mwaliko huo, Zaipuna alisema ni heshima kwa NMB na Tanzania, akibainisha kuwa safari ya benki hiyo inaonesha kuwa taasisi zinazoongozwa na Waafrika zinaweza kujenga ubora wa kiwango cha dunia huku zikibaki karibu na mahitaji ya wananchi, biashara na vipaumbele vya taifa.





Na Mwandishi Wetu, Masvingo - Zimbabwe.

TANZANIA imesema itaendelea kutumia teknolojia ya Akili Unde (AI) katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza ufanisi wa utoaji wa tahadhari za mapema na kupunguza madhara yanayosababishwa na majanga mbalimbali.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, wakati wa mkutano wa maandalizi ya Mkutano wa Sita wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika Mei 11, 2026 mjini Masvingo, Zimbabwe.

Alisema matumizi ya AI yatasaidia uchakataji na ufuatiliaji wa taarifa mbalimbali zinazoripotiwa kuhusu masuala ya maafa nchini, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa Serikali katika kufanya maamuzi ya haraka wakati wa majanga.

“Matumizi ya teknolojia ya Akili Unde yatawezesha uchambuzi wa taarifa kwa haraka, kutabiri hatari zinazoweza kujitokeza na kusaidia hatua za mapema za kukabiliana na maafa,” alisema Dkt. Yonazi.

Dkt. Yonazi alisema Serikali inaendelea kuweka mkazo katika maeneo muhimu yatakayosaidia kuwa na usimamizi wenye tija wa maafa ikiwemo utafiti wa kisayansi, matumizi sahihi ya Akili Unde, ushirikiano katika uhifadhi wa taarifa za matukio pamoja na matumizi ya menejimenti ya maarifa.

Aidha alisema Tanzania imeendelea kuwa mfano katika ukanda wa Kusini mwa Afrika kutokana na uwezo wake wa kuratibu na kusimamia maafa kwa mafanikio huku ikiendelea kuzuia, kupunguza madhara, kujiandaa na kurejesha hali pindi majanga yanapotokea.

Alifafanua kuwa mafanikio hayo yamechangiwa na uwepo wa Kituo cha Ufuatiliaji wa Mwenendo wa Majanga na Tahadhari ya Mapema ambacho hufanya kazi saa 24 kupokea, kufuatilia na kuchambua taarifa za majanga kwa wakati halisi.

“Kituo cha Operesheni ya Maafa kimekuwa msaada mkubwa kwani kimerahisisha upatikanaji wa taarifa za mapema, uchambuzi wa takwimu za wakati halisi na upangaji wa mikakati ya kurejesha hali pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu namna ya kujiandaa na kukabiliana na maafa,” alisisitiza.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa mkutano wa maandalizi ya Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  uliofanyika tarehe 11 Mei, 2026 Mjini Masvingo Nchini Zimbabwe na kuhudhuriwa na Makatibu Wakuu, Maafisa Waandamizi kutoka nchi kumi na sita wanaoshughulika na masuala ya usimamizi wa maafa. 


Baadhi ya Washiriki wa mkutano wa maandalizi ya Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  uliofanyika tarehe 11 Mei, 2026 Mjini Masvingo Nchini Zimbabwe wakifuatilia mada wakati wa mkutano huo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi (katikati mwenye tai) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya ujumbe alioongozana nao kutoka Tanzania kwa lengo la kushiriki Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  uliofanyika kuanzia tarehe 11 hadi 14Mei, 2026 Mjini Masvingo Nchini Zimbabwe.Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania Nchini Zimbabwe Mhe. CP- Suzan Kaganda na kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig. Jenerali Hosea Ndagala.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)



Top News