Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni(kushoto) akiteta jambo na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla kabla ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026.


Na Mwandishi Wetu

Unguja:

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefungua semina yaWabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar na kusisitizaumuhimu wa kuimarisha usimamizi na uwajibikaji katika utekelezaji wa Mfuko wa KuchocheaMaendeleo ya Jimbo.

Semina hiyo imefanyika Unguja, Zanzibar Februari 26, 2026 akieleza kuwa Mfuko wa Jimboumechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji wa maji safina salama, umeme, elimu, barabara na kukuza shughuli za biashara katika jamii.

Amesema mfuko huo ulianzishwa kwa lengo la kuwashirikisha wananchi katika kubuni nakutekeleza miradi ya maendeleo inayogusa mahitaji halisi ya majimbo yao, hivyo ni wajibu wawabunge kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kikamilifu ili miradi iwe na tija na uendelevu.

“Serikali inalenga kuwezesha utekelezaji wa miradi ya haraka yenye manufaa kwa wananchi, kuimarisha uwajibikaji na ushiriki wa jamii katika kupanga na kusimamia maendeleo pamoja nakupunguza pengo la maendeleo kati ya maeneo mbalimbali,” amesema Mhe. Abdulla.

Ameeleza licha ya kuwepo kwa sheria na miongozo ya matumizi ya fedha za mfuko huo, badokuna changamoto za usimamizi katika baadhi ya halmashauri zilizosababisha kuibuka kwa hoja za ukaguzi.

Kutokana na changamoto hiyo amewataka watendaji wa halmashauri kusimamia ipasavyo fedhahizo ili kuepuka dosari na kuhakikisha thamani ya fedha inapatikana.

Aidha amezungumzia umuhimu wa kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya marekebisho yaSheria ya Mfuko wa Jimbo ya mwaka 2009, kufuatia maelekezo yaliyotolewa baada yakuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa mfuko kwa mwaka 2023/24 katika Kamati yaKudumu ya Bunge ya TAMISEMI.

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeombwa kuratibu upatikanaji wa maoni kutoka upandewa Zanzibar, hivyo akawahimiza wabunge kutumia semina hiyo kama jukwaa la majadiliano yawazi na kitaalamu kwa lengo la kuboresha mfumo wa mfuko huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema semina hiyo ni hatua muhimu katika kuimarishauelewa wa wabunge kuhusu utekelezaji na usimamizi wa Mfuko wa Jimbo.

Amesema maboresho yanayopendekezwa yanalenga kuhakikisha sheria na miongozo ya mfukoinaendana na hali halisi ya utekelezaji na kuongeza uwazi pamoja na ufanisi katika matumizi yafedha za umma.

Semina hiyo imewakutanisha wabunge kutoka majimbo 50 ya Zanzibar pamoja na viongozi nawatendaji kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, kwa lengo la kujadili kwa kina namna bora ya kuboresha utekelezaji wa Mfuko wa Kuchochea Maendeleo yaJimbo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauniakizungumza wakati wa Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
Baadhi ya Wabunge wakiwa kwenye Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. HemedSuleiman Abdulla.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni(katikati) akimkabidhi zawadi Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla mara baada ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026. Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Kundi la Vijana Kanda ya Pemba Mhe Zainab Abdallah.
Mbunge wa Kundi la Vijana Kanda ya Pemba Mhe Zainab Abdallah (wa kwanza kushoto) akimkabidhi zawadi Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (kulia) mara baada ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026. Wa katikati ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Serikali imesema inatilia mkazo katika ulinzi na usalama wa kidijital ili kulinda miundombinu dhidi ya vitisho vya kimtandao ambavyo vinaweza kutumiwa na wahalifu wa ndani na nje ya nchi na kuhatarisha usalama wa wananchi na mali zao.

Akizungumza jijini Dodoma leo Februari 26, 2026 Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Angella Jasmine Mbelwa Kairuki wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kati ya wizara na sekta binafsi zilizoko chini ya wizara hiyo wakiwemo TCRA na TTCL,

Waziri Kairuki amesema serikali imeamua kuweka mazingira ya kisera, kisheria na miongozo mbalimbali katika ulinzi na usalama wa Huduma za mtandao kwa kuweka sera nzuri ya uwekezaji, akitolea mfano TCRA na TTCL, na kuwa Wajenzi wa minara ya mashirika hiyo ni wakandalasi wa hapa nchini na kuongeza kuwa mamlaka ya mawasiliano Tanzania na taarifa zao zinasaidia kuvutia uwekezaji utakao kuwa wa tija kwa Taifa.

Mheshimiwa Kairuki ameyaasa mashirika yaliyoko chini ya wizara hiyo kukamilisha na kutekeleza mipango kabambe kwa mifumo ya Tehama kwa awamu na hasa sehemu zenye pengo kubwa, kuendeleza kukuza uwekezaji wa sekta binafsi kwa kutoa motisha kuweka sheria nzuri na kuwepo na uwazi wa upatikanaji wa ardhi na leseni,kuimarisha usalama wa kidigiti kupitia sera mafunzo na uwekezaji katika vituo vya ulinzi wa kimtandao na upatikanaji wa watoa huduma kwa makundi dhaifu ili kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uchumi wa kidijitali.

Kwa upande wake Mchumi mkuu wa Tume ya Taifa Mipango Bwana Jordan Matonya masema kuwa Dira inatoa mwongozo mzuri Kitaifa kwa kupanga na kutekeleza na kuleta muundo na maudhui ya Dira ya 2050 na kuwa na uchumi imara, na kuwa na mpango wa miaka mitano mitano huanzia mwaka huu Julai 2026.

Utakaorahisisha upatikanaji wa taarifa wa maeneo muhimu ya kiuwekezaji.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa,akizungumza na waandishi wa habari katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar  Es Salaam leo Februari 26, 2026.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
SERIKALI imesema kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya usafiri wa anga na reli umeongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa ubebaji wa mizigo nchini, huku kila sekta ikiwa na nafasi na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, wakati akifafanua mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati chini ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Februari 26, 2026 kuhusu usafiri wa anga, Msigwa amesema kuwa uwekezaji uliofanywa kupitia Kampuni ya Ndege Tanzania, Air Tanzania Company Limited, umeongeza kwa kasi uwezo wa kubeba mizigo ya kimataifa na kikanda.

Ameeleza kuwa ununuzi wa ndege ya mizigo aina ya Boeing 767-300F pamoja na upanuzi wa safari za kimataifa umewezesha kuongezeka kwa mizigo kutoka tani 2,567 mwaka 2021/22 hadi tani 6,919 mwaka 2024/25.

“Ongezeko hili limechangiwa na upanuzi wa safari za kimataifa, hali iliyorahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo, mifugo, mbogamboga na matunda kwenda masoko ya nje kwa haraka zaidi,” amesema Msigwa, akibainisha kuwa usafiri wa anga una faida ya kasi na unafuu kwa mizigo inayohitaji kuwahi sokoni au inayoharibika haraka.
Kwa upande wa reli, Msigwa amesema kuwa uwekezaji kupitia Shirika la Reli Tanzania umeongeza uwezo mkubwa wa kubeba mizigo kwa wingi na kwa gharama nafuu zaidi. Tangu kuanza kwa huduma za Reli ya Kisasa (SGR), zaidi ya tani 52,305 za mizigo zimesafirishwa hadi Desemba 2025, huku maboresho ya reli ya zamani (MGR) yakiongeza uwezo wa kubeba mizigo mizito kwa kuongeza kiwango cha ekseli kutoka tani 13.5 hadi 18.5.
Amefafanua kuwa tofauti na ATCL inayolenga zaidi mizigo ya thamani kubwa au inayohitaji kufikishwa kwa haraka, reli inalenga mizigo mikubwa na mizito kama saruji, makaa ya mawe, nafaka na bidhaa za viwandani, hususan katika safari za ndani na nchi jirani.

Hata hivyo, Msigwa amesisitiza kuwa sekta hizo mbili zinakamilishana badala ya kushindana.

“ATCL na TRC zinafanya kazi kwa mfumo unaosaidiana. Ndege zinasaidia kufungua masoko ya mbali kwa haraka, wakati reli inahakikisha mizigo inasafirishwa kwa wingi kutoka uzalishaji hadi bandarini au nchi jirani kwa gharama nafuu,” amesema.

Kwa mujibu wa Serikali, wakati ATCL imeongeza mapato ya fedha za kigeni kupitia safari za kimataifa, TRC imeimarisha mnyororo wa thamani wa ndani kwa kuunganisha maeneo ya uzalishaji na bandari, hatua inayochochea biashara ya kikanda na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania.

Kwa ujumla, Msigwa amesema mafanikio hayo yanaakisi mkakati wa Serikali wa kujenga mfumo jumuishi wa usafiri unaounganisha anga, reli na bandari, kwa lengo la kuongeza ufanisi wa ubebaji wa mizigo, kupunguza gharama za usafirishaji na kukuza uchumi wa taifa.



Na Khadija Kalili, Mlandizi
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Abuu Jumaa leo tarehe 25 Februari 2026 amekutana na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi katika mkutano maalumu wa kutoa shukran zake za dhati kwao kwa kumchagua kuwaongoza Jimboni humo.

Mhe.Mbunge Hamoud amesema hayo leo tarehe 25 kwenye mkutano uliofanyika Malandizi Stendi, Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani ambao umehudhuriwa na viongozi kutoka kata sita za Mlandizi Mjini.

"Baada ya miezi mitatu kupita ya uchaguzi leo nimekuja hapa ili niwashkuru kwa kusimama nami kwenyw uchaguzi na kunichagua kuwa mwakilishi wenu kwa mara nyingine tena nasema mimi siyo mjanja sana bali ni Mwenyeezi Mungu Mungu amepanga iwe hivi" amesema Jumaa.

"Nawashukuru sana kwa kunichagua kuwa Mbunge wenu, Wabunge wawili wa Viti Maalumu Asha Baraka na Hawa Mchafu pamoja na Madiwani 14wa kuchaguliwa na wa Viti Maalumu watano haya ni mafanikio makubwa kwa sababu nikiangalia safu yote ni majembe huvyo tupeane muda" amesisitiza Mhe.Jumaa.

Amesema kuwa anawashukuru pia kwa kumchagua Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan pia amewaomba wana CCM kumpa ushirikiano Mhe.Rais Dkt Samia hasa katika kipindi hiki ambacho anakwenda kumalizia ngwe yake ili aweze kutekeleza mambo mengi makubwa katika nchi yetu" amesema Mhe. Jumaa.

"Tunatakiwa wote kwa pamoja tumsaidie Mhe.Rais Dkt. Samia ili tuweze kuifikia Tanzania yenye mafanikio na kicheko kwa wote" amesema Mhe.Mbunge Jumaa.

Aidha Mh.Jumaa ameanza kwa kukutana na Kata sita ambazo ni Mlandizi ,Mtambani,Kawawa,
Mtongani,Janga na Kilangalanga.

Wakati huohuo ametoa ahadi lukuki ikiwa ni pamoja na kujenga maduka makubwa na ya kisasa Shopping Mall,Machinjio, Shule mpya kata ya Janga, atajenga Zahanati Kata ya Kawawa.

Mhe.Jumaa ameongeza kwa kusema kuwa wamekusudia kujenga jengo la Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akisisitiza kwa kusema kuwa Mungu akimjaalia atajenga kwa fedha zake mwenyewe.

"Baadaye tutapita katika ofisi zote za Kata kuangalia changamoto walizo nazo na tutazitatua.

Akizungumza kuhusu uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 2027 amewasisitiza Viongozi wote ambao wanajiona hawana uwezo wa kuongoza wajiengue mapema na kuatafuta warithi wao ikiwa pamoja na kuwaandaa vijana wenye wito ambao wana uwezona watakaowavusha katika uchaguzi huo ujao.
Katika kikao hicho cha Halmashauri Kuu Cha Sita cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kibaha Vijijini kimeongizwa na Mwenyekiti wake Mkali Kanusu ambaye amesisitiza kuwa mwakani atagombea tena katika nafasi hiyo.

"CCM ni Chama kizurikinatulea kinatuheshimisha pia runadhaminika hivyo tunendelee kukijenga kwa makundi kwa maslahi ya Chama chetu hivyo wote kwa sasa tukubaliane kufanya kazi na kushirikiana kwa pamoja.

Mimi ndiyo mwakilishi wa Mhe.Rais Dkt Samia hivyo hata kama hunipendi hunitaki wewe njoo tuzungumze kwa maslahi ya Chama chetu ili wote kwa pamoja tulete maendeleo.

"Nimedhamiria kupambana kupandisha Mamlaka ya Mji ,na jambo linakwenda vizuri katika ngazi za juu ikiwamo Wilaya na Mkoa.
Endapo tutapandishwa hadhi tutapata faida ya Mji kupangika kisasa ,kupata ongezeko katika ruzuku barabara zitajengwa katika kiwango cha lami ,pia ikumbukwe kuwa 2025-26 tumeongoza kwa nchi nzima kwa kukusanya mapato hili ni jambo la kujivunia ,tutamaliza ujenzi wa soko ,stendi ya mabasi tutajenga hoteli kubwa na ya kisasa maegesho ya magari.

Aidha Mhe.Jumaa amezitaja baadhi ya barabara ambazo ziko katika mpango wa kujengwa katika kiwango cha lami ni Chalinze Gwata, Utete, Rufiji na Makofia Mlandizi Mzenga.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani, Selemani Jafo, ameonesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Nyani, Kata ya Mafizi, akieleza kuwa hatua iliyofikiwa inaleta matumaini mapya kwa wananchi.

Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya BROADWAYS ENGINEERING CO LTD una thamani ya shilingi milioni 402.8 na hadi sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji, jambo linaloashiria kuwa upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo si wa muda mrefu tena.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji, mradi unahusisha ujenzi wa mnara wa tanki la maji lenye urefu wa mita 12 na uwezo wa kuhifadhi lita 50,000, pamoja na ujenzi wa vituo vitano vya kuchotea maji na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilometa 16.167.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Dkt. Jafo alimpongeza mkandarasi kwa kufanya kazi kwa kasi na weledi mkubwa, akibainisha kuwa kampuni hiyo imeendelea na kazi hata kabla ya kupokea malipo yoyote, jambo alilolitaja kuwa ni uzalendo na kujitolea kwa maendeleo ya wananchi.

Kutokana na kasi hiyo, Jafo ameiiomba Wizara ya Maji kulipa kiasi cha shilingi milioni 279.1 kwa kazi zilizokamilika ili kumwezesha mkandarasi huyo kuendelea na hatua zilizobaki na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Mbali na mkandarasi, mbunge huyo pia amempongeza Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kisarawe, Mhandisi Evangelista Kahwili, kwa usimamizi makini wa miradi ya maji ndani ya jimbo hilo, akisema nidhamu na ufuatiliaji wa karibu umechangia mafanikio yanayoonekana.

Wananchi wa Nyani na maeneo ya jirani wanatarajia kunufaika na mradi huo mara utakapokamilika, huku wakieleza kuwa utapunguza adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji na kuboresha afya pamoja na shughuli za kiuchumi katika eneo hilo.



▪️Ataka hatua za kinidhamu zichukuliwe licha ya fedha hizo kurejeshwa.

▪️Asisitiza hakuna kufanya ustaarabu kwa wezi wa mali za umma.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amemtaka Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Bahati Haule, kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa ya kila mmoja aliyehusika kuchukua fedha za mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa pamoja na kurejeshwa kwa fedha hizo, ni lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wote waliohusika na mpango huo ili kuimarisha uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma..

Amesema hayo leo Alhamisi (Februari 26, 2026) baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto. Ofisi hiyo itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake, na ujenzi wake umefikia asilimia 85.

“Kamanda wa TAKUKURU, ninataka uniletee taarifa hii kabla sijamaliza ziara yangu katika Mkoa wa Manyara. Ninahitaji taarifa za mtu mmoja mmoja kwa wote waliohusika kuchukua fedha hizo. Hatukutumwa kuja kuchukua fedha za umma, hatua za kinidhamu lazima zichukuliwe,” amesisitiza.

Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa mbali na taarifa hiyo, anataka pia kuwasilishwa taarifa za mapato ya ndani, ikiwemo mapato yatokanayo na minada, zikionyesha namna yanavyokusanywa na kutumika. “Hakuna kuvumilia ubadhirifu wa mali ya umma. Tunataka kila mtu aheshimu fedha za utekelezaji wa miradi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana dhamira ya dhati ya kutatua changamoto za Watanzania, akisisitiza kuwa lengo lake ni kuona maendeleo endelevu yanapatikana nchini.






IKIWA taarifa na elimu ni nyenzo muhimu ya kukabiliana na changamoto za afya ripoti inaeleza waandishi wa habari za afya wanakumbwa na hali inayofanya wasitekeleze wajibu wao unaosaidia ustawi sekta hiyo barani Afrika.

Hayo yameelezwa kwenye ripoti ya mwelekeo wa Vyombo vya Habari vya Afya Afrika 2026, iliyozinduliwa Leo Februari 26, Feb na FINN Partners.

Pia ripoti hiyo inaangazia mwelekeo mpya unaokua wa uandishi wa habari unaozingatia suluhisho na unaoongozwa na Waafrika, ambao unaweza kubadilisha namna masuala ya afya yanavyoripotiwa barani humo.

Ripoti hiyo inatokana na maoni ya waandishi wa habari, wahariri na watetezi kutoka nchi 11 za Afrika, na inatoa taswira halisi ya jinsi habari za afya zinavyoripotiwa pamoja na mahitaji muhimu ya kuimarisha mchango wa vyombo vya habari katika kuboresha matokeo ya afya ya umma.

Waandishi wa habari za afya kwa sasa wanakabiliana na changamoto kadhaa, ikiwemo kupungua kwa ufadhili wa wafadhili, kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza kama saratani, kisukari na matatizo ya afya ya akili, milipuko ya mara kwa mara ya magonjwa ya kuambukiza, pamoja na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa afya. Wakati huo huo, vyumba vya habari vinafanya kazi kwa rasilimali chache, kupungua kwa madawati maalum ya afya, na upatikanaji mdogo wa takwimu sahihi na za wakati.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo Peter FINN, Mwanzilishi Mshirika na Mtendaji Mkuu wa FINN Partners amesema kuwa uandishi wa habari za afya ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha hali ya afya za Waafrika.

“Tuko katika wakati muhimu sana kwa mawasiliano ya afya barani Afrika. Uandishi wa habari unapokosa rasilimali za kutosha, afya ya umma huathirika. Mifumo imara ya afya inahitaji mifumo imara ya vyombo vya habari, na hiyo inamaanisha kuwachukulia waandishi wa habari kama washirika muhimu, si wasambazaji wa taarifa tu.”

Ripoti hiyo pia inaonesha kuwa mabadiliko katika ufadhili wa afya duniani yamekuwa mada kuu katika vyombo vya habari, yakizisukuma nchi kufikiria upya uhuru wa sekta ya afya, ufadhili wa ndani na uzalishaji wa ndani. Wakati huo huo, waandishi wa habari wanajitahidi kutafsiri mabadiliko hayo ya sera na kuyaonesha kwa namna yanavyoathiri maisha halisi ya wananchi.

“Namna masuala ya afya yanavyoripotiwa huathiri imani ya umma, vipaumbele vya sera na hatimaye uimara wa mifumo ya afya,” alisema Maryam Bigdeli, Mtaalamu wa Mifumo ya Afya na aliyewahi kuwa Mwakilishi wa World Health Organization nchini Morocco.

Maryam aliongeza kuwa “Katika kipindi hiki cha mabadiliko ya vipaumbele vya afya duniani na vikwazo vya ufadhili, nchi za Afrika zinapaswa kujikita katika kujenga mifumo imara inayotegemea huduma bora za afya ya msingi, ufadhili endelevu na utawala unaowajibika. Ripoti hii inaonesha umuhimu wa suluhisho za ndani na mjadala unaotegemea ushahidi ili kuhakikisha usawa na uimara wa mifumo ya afya kwa muda mrefu.”

Licha ya changamoto hizo, ripoti imebaini mwelekeo chanya ambapo waandishi wa habari wanazidi kuzingatia uandishi unaotumia takwimu na unaolenga suluhisho, huku ukitoa nafasi kubwa kwa wataalamu na muktadha wa Kiafrika. Waandishi wa habari wanatoa wito kwa wataalamu, watafiti na watendaji wa Kiafrika kunukuliwa zaidi kama vyanzo vikuu vya taarifa, na hivyo kubadilisha taswira ya Afrika kutoka kuwa mhanga wa matatizo hadi kuwa sehemu ya suluhisho.

“Matokeo ya ripoti hii yanaakisi hali halisi tuliyonayo,” alisema Sheriff Bojang, mwandishi wa The Africa Report. “Waandishi wa habari wana hamu kubwa ya kusimulia hadithi zenye athari, lakini wanakabiliwa na ukosefu wa rasilimali na upatikanaji mdogo wa wataalamu wa ndani wanaoaminika. Sasa tunahama kutoka kunukuu tafiti za Magharibi pekee na kuelekea katika kuwasilisha habari za afya kwa muktadha wa ndani. Ripoti hii inatoa mwongozo muhimu kwa mashirika ya afya kusaidia vyombo vya habari ili kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia wananchi.”

Ripoti hiyo inahitimisha kwa kutoa wito kwa serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, wafadhili na sekta binafsi kuwekeza katika uandishi wa habari wa ndani, kuboresha upatikanaji wa takwimu na wataalamu wa Kiafrika, pamoja na kujenga ushirikiano wa muda mrefu unaojengwa juu ya uaminifu ili kuimarisha afya ya umma barani Afrika.


Meneja Mkuu Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA. Ashraph Abdukarim amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Chuo Kikuu cha Agakhan, mazungumzo hayo yamejikita kwenye uwekezaji wa miundombinu na uaznzishaji wa kituo cha kulea watoto katika Soko Kuu la Kariakoo.

CPA. Abdulkarim amewaeleza viongozi hao kuwa shirika limeandaa eneo zuri na kubwa ambalo endapo mwekezaji akijitokeza anaweza kujenga kituo hicho ambacho ujenzi wake ni utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa Februari 8, 2026 alifungua soko hilo rasmi.

CPA. Abdulkarim amebainisha kuwa kinachoendelea kwa sasa ni maandalizi ya michoro na taarifa ya kina kuhusu namna gani kituo hicho kiwe ambapo taarifa hizo zinaandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI baada ya kutembelea eneo hilo wakiwa na wataalam mbalimbali ambao waliambatana na wataalam wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Jiji la Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa ujumbe huo kutoka Chuo Kikuu cha Agakhan, Prof Paschal Ruggajo ameushukuru uongozi wa Shirika la Masoko la Kariakoo kwa kukubali kukutana nao, kwani wanayo nia ya dhati ya kuanzisha kituo hicho kwa kutambua umuhimu wa afya na mazingira salama kwa mama na mtoto.

Naye, Dkt. Mariam Nooran ambaye ni Mkuu wa Idara ya Watoto Chuo Kikuu cha Agakhan ameonesha umuhimu wa kuwa na eneo la kunyonyesha na pia kulea watoto kwa pamoja na kubainisha kuwa yapo mambo mbalimbali yanapaswa kuzingatiwa ikiwemo usafi, usalama na mazingira yanayowapa fursa watoto kucheza.

Ikumbukwe kuwa Shirika la Masoko Kariakoo lilitenga eneo maalum kwa ajili ya wakina mama wanaofanya biashara katika Soko Kuu la Kariakoo kunyonyesha watoto wao, jambo ambalo limepata mwitikio mkubwa kutoka kwa jamii.






Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa salamu za rambirambi kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi OFMCap, kufuatia kifo cha Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo hilo, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, aliyefariki dunia Februari 19, 2026, katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipokuwa akipatiwa matibabu.

Akizungumza Februari 26, 2026 baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, Dar es Salaam, Katibu Mkuu CCM, Dkt. Asha-Rose Migiro, alisema amewasilisha salamu za rambirambi kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Migiro alisema marehemu Kadinali Pengo atakumbukwa kama mchungaji wa faraja na tumaini, kiongozi wa kiroho mwenye hekima, unyenyekevu na msimamo thabiti wa maadili.

Alijipambanua si tu kwa huduma ya Kanisa, bali pia kwa mchango wake katika kuimarisha mshikamano wa kitaifa, maadili ya jamii, malezi ya vijana na uwajibikaji wa viongozi.

“Kadinali Pengo ameacha alama inayodumu ya utumishi wa Mungu, utumishi wa Taifa na utumishi wa jamii. Maisha na mafundisho yake yataendelea kuwa dira kwa vizazi vijavyo,” alisema Dkt. Migiro.

CCM imesema inaliombea Kanisa Katoliki na waumini wote wapate faraja katika kipindi hiki cha maombolezo na Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Kwa mujibu wa ratiba ya mazishi, mwili wa marehemu utawasili Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Februari 27, 2026 kwa ajili ya waumini kutoa heshima zao za mwisho, na Ibada ya Misa ya Mazishi itafanyika Februari 28, 2026 katika Kituo cha Hija Pugu, Dar es Salaam.




Benki ya Exim Tanzania imeandaa hafla ya futari kwa wateja wake jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza na kuimarisha mahusiano yanayojengwa juu ya misingi ya uaminifu, uwajibikaji na maadili ya pamoja.

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki, Bw. Jaffari Matundu, alisema kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ni wakati wa kutafakari na kukumbushana kuwa mafanikio ya kweli hujengwa juu ya maadili thabiti kama vile uaminifu, huruma na uwazi katika utendaji.

Benki ya Exim inathamini mahusiano na wateja wake zaidi ya miamala ya kifedha.

 “Dhamira yetu si kutoa huduma za kifedha pekee, bali kujenga imani, kupanua fursa na kugusa maisha ya watu kwa namna chanya,” alisisitiza.

Katika kuendeleza dhamira ya kuongeza ujumuishi wa kifedha nchini, Benki imeendelea kupanua mtandao wake kwa kufungua matawi katika maeneo ya Kahama, Ubungo na hivi karibuni Paje, huku mipango ikiendelea kuelekea Geita.

 Hatua hiyo inalenga kusogeza huduma karibu zaidi kwa wafanyabiashara, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla.

Aidha, Benki ilithibitisha kuwa itaendelea kuwa mshirika wa kuaminika kwa wateja wake katika safari yao ya ukuaji na maendeleo ya muda mrefu.

“Uaminifu wenu kwetu ndiyo mtaji wetu mkubwa. Kila mara mnapochagua kufanya nasi kazi, mnatuwekea dhamana.

Na dhamana hiyo tunaichukulia kwa uzito na heshima kubwa.” Alisema Bw. Matundu.

Hafla hiyo iliwakutanisha viongozi wa dini, wateja pamoja na wageni waalikwa katika mazingira ya mshikamano, tafakari na kuimarisha ushirikiano kwa maendeleo ya pamoja. @exim_banktz 




 

Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma 

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amewataka wanataaluma wa lishe nchini kutoa elimu sahihi kwa wananchi kwa viwango vinavyokubalika kupitia kwa makundi mbalimbali ikiwemo wana-habari, mama lishe, baba lishe ili jamii ione faida ya uwepo wa wanataaluma hao. 

Dkt. Magembe amesema hayo leo Februari 26, 2026 alipokua anafungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Chama cha Wataalamu wa Lishe Tanzania 2026 uliofanyika katika ukumbi wa Mabeyo Mkoani Dodoma. 

"Sasa hivi, huko kwenye mitandao ya kijamii kuna watu wengi ambao hata hawajui chochote kuhusu lishe, lakini wako bize kila siku kutoa elimu ya lishe kwenye mitandao ya kijamii, mtaani, tusiwaache wale waongee kwa sababu wakati mwengine wanapotosha," amesema Dkt. Magembe 

Amesema, jamii inatakiwa kupata elimu sahihi, ujumbe sahihi, kujua nini na kwa wakati gani chakula kipi kinafaa kuliwa, vitu gani visiliwe na kwa wakati gani, hii itapelekea kupata taifa lenye afya bora. 

Aidha, Dkt. Magembe amewataka wanataaluma hao kufanya tafiti ili kujua tatizo la lishe nchini katika baadhi ya Mikoa na kujua kwa nini matatizo ya lishe yanayofautiana kati ya mkoa mmoja na mwengine. 

"Hakuna taaluma yoyote katika Sekta ya Afya ambayo inaweza kwenda bila tafiti, tunakazi ya kufanya ili tujue tatizo ni nini, kwa nini mikoa yenye uzalishaji wa chakula ndio kuna udumavu," amesema Dkt. Magembe 

katika hatua nyingine Dkt. Magembe ametumia fursa hiyo kuiasa jamii juu ya kupanda miti ya matunda pamoja na bustani za mbogamboga majumbani na hata katika vituo vya afya nchini







Top News