📍 Chinangali Park, Dodoma
TAWIRI imeendelea kutoa elimu kwa wadau wakiwepo wananchi ambapo wakulima wamepata elimu ya umuhimu wa wadudu katika uhifadhi endelevu wa wanyamapori sambamba na mchango wa wadudu katika kilimo ikiwa ni pamoja na uchavushaji.
Vilevile wananchi wamepata uelewa juu ya juhudi zinazofanywa na TAWIRI chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii za kuwahifadhi wanyamapori kwa kutumia taarifa sahihi za kisayansi.
“tunashukuru kwa elimu nzuri, kabla ya elimu hii nilijua wanyamapori wanakaa porini wanajihudumia lakini leo nimepata uelewa wanyamapori wanatibiwa, wanahesabiwa, wanafuatiliwa mienendo yao kwa kutumia teknolojia”
amesema Enderesa Salla miongoni mwa wananchi waliotembelea banda la TAWIRI
TAWIRI tunawakaribisha wananchi na wadau mbalimbali kuja kupata elimu ya sayansi ya wanyamapori kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza Utalii.

RAIS wa Jamhuri ya Namibia, Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya Kitaifa ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akiwa nchini Rais Dkt. Nandi-Ndaitwah anatarajiwa kufanya mazungumzo ya uwili na mwenyeji wake, Rais Dkt. Samia kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano katika sekta mbalimbali zenye manufaa kwa Wananchi wa Tanzania na Namibia.
Pia Rais Ndaitwah na mwenyeji wake Rais Dk.Samia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano kati ya Nchi hizo mbili.
Aidha pamoja na mambo mengine inaelezwa kwamba ziara hiyo inakwenda kufungua fursa zaidi za kiuchumi kati ya nchi hizo ambazo zimekuwa na urafiki wa kindugu na wa kihistoria kwa muda mrefu.
Akizungumzia ziara hiyo alipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya Rais Ndaitwah, Balozi wa Tanzania nchini Namibia, Caesar Waitara, amesema ziara hiyo ni ishara ya uhusiano wa muda mrefu na wa kihistoria uliopo kati ya mataifa hayo mawili, huku akisisitiza kuwa ziara hiyo inaleta manufaa makubwa katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi.
Balozi Waitara anasema Rais wa Namibia anaitazama Tanzania kama nyumbani kwake kutokana na historia yake ya kuishi nchini kwa miaka sita alipokuwa mwakilishi wa chama cha SWAPO katika nchi za Afrika Mashariki.
Anabainisha kuwa makao yake yalikuwa katika eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam, jambo linaloimarisha zaidi uhusiano wake binafsi na Tanzania.
“Ujio wake unaonyesha jinsi uhusiano kati ya Tanzania na Namibia ulivyo imara na wa muda mrefu. Kila mara anapokuja Tanzania anajisikia kama yuko nyumbani,” anasema Waitara.
Anaeleza kuwa Namibia inaendelea kuthamini mchango wa Tanzania katika harakati za ukombozi wa taifa hilo, hususan kupitia kambi za wapigania uhuru zilizokuwa Kongwa pamoja na msaada wa mafunzo ya kijeshi uliotolewa kwa wapigania uhuru wa Namibia.
Kwa mujibu wa balozi huyo, pamoja na historia ya ukombozi, mataifa hayo sasa yamejikita zaidi katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kupitia biashara, uwekezaji na kubadilishana uzoefu katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Waitara anasema Tanzania inaendelea kusukuma mbele ajenda ya diplomasia ya uchumi kupitia balozi zake nje ya nchi kwa lengo la kuvutia uwekezaji na kufungua fursa za biashara.
Anataja uwekezaji wa Watanzania nchini Namibia kuwa ni mfano wa mafanikio ya ushirikiano huo, ambapo baadhi ya Watanzania wameanzisha biashara na taasisi za elimu.
Anabainisha kuwa kuna chuo kikuu nchini Namibia kinachomilikiwa kwa asilimia 100 na Mtanzania, ambacho kinatoa elimu ya shahada, shahada za uzamili na uzamivu, huku kikiwa na zaidi ya wanafunzi 10,000.
Aidha, Watanzania wengine wanaendelea kufanya biashara mbalimbali nchini humo, wakati WanaNamibia wamewekeza Tanzania katika sekta za utalii na mawasiliano.
Katika kuimarisha mahusiano ya kitamaduni, Waitara anasema ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) umeanza kutoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa njia ya mtandao nchini Namibia.
Anafafanua wanafunzi 26 walihitimu mafunzo ya awali mwaka jana, huku kundi jipya la wanafunzi 40 likitarajiwa kuanza masomo hivi karibuni.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, akizungumzia ziara ya Rais wa Namibia anasisitiza ni uthibitisho kuwa mahusiano ya kihistoria kati ya mataifa hayo sasa yamepanuka na kuwa ushirikiano mkubwa wa kiuchumi.
Anasema maboresho makubwa yaliyofanyika katika Bandari ya Dar es Salaam yanaifanya Tanzania kuwa lango muhimu la biashara kwa nchi nyingi za ukanda wa Kusini mwa Afrika, jambo linaloweza kuongeza ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Namibia.
Wakati Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, anasema mafanikio ya diplomasia ya uchumi hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa usalama.
Ananasisitiza kuwa amani na utulivu wa Tanzania ndiyo msingi unaowezesha viongozi wa kimataifa kutembelea nchi na wawekezaji kuendelea kuwekeza.
“Usalama ni mtaji muhimu wa uchumi. Bila usalama hakuna biashara, hakuna uwekezaji wala maendeleo. Ni jukumu la kila mwananchi kuendelea kuilinda amani ya nchi yetu,” anasema Kamanda Muliro.
Ziara ya Rais wa Namibia nchini Tanzania inatarajiwa kuimarisha zaidi ushirikiano wa kihistoria, kiuchumi na kitamaduni kati ya mataifa hayo mawili, huku ikifungua fursa mpya za biashara, uwekezaji na maendeleo kwa wananchi wa pande zote mbili.
SERIKALI imeitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kujiandaa mapema kukabiliana na mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kiteknolojia yanayotarajiwa katika miaka 30 ijayo, ikieleza kuwa zaidi ya asilimia 70 ya shughuli za kiuchumi zitakuwa zikifanyika kwa njia za kidijitali.
Hayo ameyasema na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Nsubili Joshua, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omary, wakati wa Kongamano la Miaka 30 ya TRA tangu kuanzishwa kwake mwaka 1996, lililoandaliwa na TRA kupitia Chuo cha Kodi.
Joshua alisema mabadiliko ya teknolojia yanayoendelea duniani yanahitaji TRA kuwa mbele ya wakati kwa kuandaa mifumo madhubuti ya usimamizi wa kodi itakayoweza kukusanya mapato kutoka biashara za mtandaoni na huduma zinazovuka mipaka ya nchi.
Alisema pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 30 ya TRA, bado kuna haja ya kuimarisha mifumo ya kodi ili iendane na kasi ya maendeleo ya uchumi wa kidijitali unaotarajiwa kutawala katika miaka ijayo.
“Katika miaka 30 ijayo zaidi ya asilimia 70 ya shughuli za kiuchumi zitafanyika kwa njia za kidijitali hivyo TRA inapaswa kuwa tayari kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kwa ufanisi bila kuathiri mazingira ya biashara na ubunifu,” amesema Joshua.
Alifafanua kuwa lengo la Serikali si kuzuia maendeleo ya teknolojia, bali kuhakikisha kunakuwa na usawa wa kodi na ulinzi wa mapato ya taifa huku mazingira bora ya uwekezaji na ushindani wa haki yakiendelea kudumishwa.
Aidha, aliitaka TRA kuongeza uwekezaji katika matumizi ya akili mnemba (AI), uchambuzi wa takwimu na mifumo ya ufuatiliaji wa miamala kwa wakati halisi ili kubaini mianya ya ukwepaji kodi na kuimarisha uwazi katika ukusanyaji wa mapato.
Joshua alisema matumizi ya teknolojia hizo yatasaidia kugundua udanganyifu mapema, kupunguza mawasiliano yasiyo ya lazima kati ya walipakodi na maafisa wa kodi pamoja na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.
Pia aliitaka TRA kuendelea kubuni mifumo rahisi ya usajili, ukadiriaji na ulipaji kodi kwa sekta isiyo rasmi ikiwemo wafanyabiashara wadogo na wakulima, ili kupanua wigo wa walipakodi na kuongeza mapato ya ndani.
Alisema mafanikio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yatategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa nchi kukusanya mapato ya ndani na kuyasimamia kwa ufanisi, jambo linaloifanya TRA kuwa na jukumu muhimu katika safari ya maendeleo ya taifa.
Joshua alisisitiza kuwa ushirikiano kati ya TRA, wafanyabiashara, watafiti na wadau wengine wa kodi ni muhimu katika kujenga mfumo wa kodi unaoendana na mahitaji ya uchumi wa kisasa na kuhakikisha Tanzania inanufaika kikamilifu na mapinduzi ya teknolojia yanayoendelea duniani.
Kamishina Mkuu wa TRA CPA Yusuph Mwenda akitoa maelezo kuhusiana tangu kuanzishwa mamlaka ya Mapato katika kongamano la miaka 30 tangu Kuanzishwa lililofanyika Ukumbi wa Serena ,jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Nsubili Jushua akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omary wakati akizindua Kongamano la Miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato (TRA) lililofanyika Ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Kodi Profesa Isaya Jairo akizungumza kuhusiana na kuratibu Kongamano hilo kwa lengo kukutanisha wadau kujadiliana miaka 30 ijayo juu utendaji wa TRA.jijini Dar es Salaam.
Picha za pamoja za Makundi katika kongamano la TRAUbena Zomozi; Benki ya NMB imetoa zaidi ya Sh180 bilioni kufadhili wafugaji na biashara katika mnyororo wa thamani wa mifugo, ikiwemo unenepeshaji, uzalishaji wa malisho, ununuzi wa mbegu bora na ujenzi wa miundombinu ya kisasa.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema hayo katika ufunguzi wa Tri-Nations Livestock Expo 2026 uliofanywa na Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, katika viwanja vya Mbogo Ranches, Ubena Zomozi, Chalinze. NMB ni mdhamini mkuu kwa mwaka wa nne mfululizo.
Mponzi alisema mikopo hiyo inatolewa kwa riba nafuu ya asilimia tisa, huku mkakati wa NMB wa agribusiness na agri-wholesale ukilenga kufadhili wafugaji, wazalishaji wa malisho, wanunuzi, wasindikaji na biashara kubwa katika sekta hiyo.
Dk. Nchemba aliwataka wafugaji kutumia elimu na teknolojia inayopatikana katika maonesho hayo kukabiliana na uhaba wa malisho na kuongeza tija.
NMB imesema itaendelea kutoa elimu ya fedha, ushauri wa biashara, mikopo na bima kupitia matawi 248, mawakala zaidi ya 75,000 na huduma za kidijitali ili kusogeza huduma karibu zaidi na wafugaji nchini.
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), mdhamini mkuu wa Ligi ya NBC Championship, imejivunia mafanikio yanayoendelea kushuhudiwa katika mchezo wa soka nchini huku ikikabidhi kombe la ubingwa wa msimu wa 2025/2026 kwa Geita Gold FC, timu iliyotwaa taji hilo baada ya kumaliza ligi ikiwa kileleni kwa alama 77.
Ubingwa huo unaipa Geita Gold FC tiketi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027 sambamba na Kagera Sugar FC iliyomaliza nafasi ya pili kwa alama 71 na hivyo nayo kufuzu kushiriki ligi hiyo.Kombe hilo lilikabidhiwa jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa.
Katika hafla hiyo, Mkuu wa Biashara wa NBC Kanda ya Ziwa, Mafwimbo Bihemo, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, alisema benki hiyo inafurahishwa na namna uwekezaji wake katika soka unavyoendelea kuzaa matokeo chanya kupitia ongezeko la ushindani, kuibuka kwa vipaji vipya na kuimarika kwa viwango vya ligi za ndani.
Alisema NBC, ambayo imewekeza zaidi ya Shilingi bilioni 32 katika udhamini wa Ligi Kuu ya NBC, NBC Championship na Ligi ya Vijana, itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha soka linaendelea kukua na kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.
“Tunawapongeza washiriki wote wa NBC Championship kwa ushindani mkubwa waliouonyesha msimu mzima. Kipekee tunawapongeza Geita Gold FC kwa kutwaa ubingwa na Kagera Sugar FC kwa kufuzu Ligi Kuu ya NBC. Mafanikio haya yanaonyesha kiwango kikubwa cha ushindani kinachoendelea kujengeka katika soka la Tanzania,” alisema Bihemo.
Alisema NBC inaona matokeo ya uwekezaji huo kupitia maendeleo yanayoonekana katika ligi za ndani, kuimarika kwa ushindani wa vilabu na mafanikio yanayozidi kupatikana kwa timu za taifa katika mashindano ya kimataifa.
“Tunajivunia kuona soka la Tanzania likiendelea kupiga hatua. Ushindani unaoanzia ligi za vijana, NBC Championship hadi Ligi Kuu ya NBC umeendelea kuongeza ubora wa mchezo na kuzalisha wachezaji wenye uwezo wa kushindana katika viwango vya juu zaidi. Haya ndiyo matokeo tunayolenga kuyaona kupitia uwekezaji wetu,” aliongeza.
Bihemo alisema NBC itaendelea kuboresha mchango wake kwa wadau wa soka kupitia huduma mbalimbali za kifedha zikiwemo mikopo kwa vilabu, bima za afya kwa wachezaji na benchi la ufundi pamoja na elimu ya fedha inayolenga kuimarisha ustawi wa wadau wa mchezo huo.
Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, aliipongeza NBC kwa mchango wake mkubwa katika kukuza soka la Tanzania kupitia udhamini wa ligi hizo tatu, akibainisha kuwa ushindani wa sasa katika ligi za ndani ni miongoni mwa matokeo makubwa ya uwekezaji huo.
“Leo tunaona NBC Championship ikiwa na ushindani mkubwa kuanzia mwanzo hadi mwisho wa msimu. Vilabu vinaendesha shughuli zake kwa weledi zaidi, vina uwezo wa kusajili wachezaji bora na kujiandaa vizuri kwa mashindano. Haya ni maendeleo makubwa kwa soka letu,” alisema Karia.
Aliwataka Geita Gold FC na Kagera Sugar FC kutumia fursa ya kupanda Ligi Kuu ya NBC kujiimarisha zaidi ili kuongeza ushindani katika ligi hiyo pamoja na kuwekeza katika miundombinu ya viwanja ili mashabiki wao waweze kufurahia mechi za nyumbani katika mazingira bora.
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wa Geita Gold FC, nahodha wa timu hiyo Yusuph Mhilu aliwashukuru mashabiki, viongozi, benchi la ufundi na wadhamini kwa mchango wao katika kufanikisha ubingwa huo.
Alisema timu hiyo inatambua ushindani mkubwa uliopo katika Ligi Kuu ya NBC na tayari imeanza maandalizi ya kuhakikisha inakwenda kutoa ushindani wa kiwango cha juu msimu ujao.
Mkuu wa Biashara wa NBC Kanda ya Ziwa, Mafwimbo Bihemo (mwenye fulana nyeusi) pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia (alievaa kofia) wakiwapongeza wachezaji wa timu ya Geita Gold FC ya mkoani Geita baada ya timu hiyo kukabidhiwa rasmi kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship)msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe hilo ilifanyika jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia (katikati alievaa kofia) akiongoza zoezi la uvalishaji wa medali kwa wachezaji wa timu ya Geita Gold FC ya mkoani Geita baada ya timu hiyo kukabidhiwa rasmi kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship)msimu wa 2025/2026. Hafla ya kukabidhi kombe hilo ilifanyika jana katika Uwanja wa Nyankumbu, Geita, baada ya Geita Gold FC kuhitimisha msimu kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Big Man FC ya Lindi katika mechi iliyoshuhudiwa na mamia ya mashabiki pamoja na viongozi mbalimbali wa soka, serikali na vyama vya siasa

Baadhi ya mashabiki wa Geita Gold FC wakifurafia ubingwa huo.

Haikuwa kazi rahisi! Wachezaji wa Geita Gold FC wakiwa kwenye nyakati tofauti uwanjani.

Vikosi vya Geita Gold FC (juu) na Big Man FC (chini) vilivyokutana kwenye mchezo huo
Muonekano wa kombe la Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) msimu wa 2025/2026
Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na wadau wa maafa nchini katika Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS) tarehe 19 Juni, 2026 Jijini Dodoma.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Nandi-Ndaitwah alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali. Katika mapokezi hayo pia alikuwepo Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini Tanzania, Mhe. Gabriel Sinimbo.
Ziara hiyo inafanyika katika kipindi ambacho Tanzania na Namibia zinaendelea kuimarisha uhusiano wao wa kihistoria uliojengwa katika misingi ya mshikamano wa harakati za ukombozi wa Afrika, urafiki wa muda mrefu na ushirikiano wa karibu katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Akiwa nchini, Mhe. Rais Nandi-Ndaitwah anatarajiwa kufanya mazungumzo ya uwili na mwenyeji wake, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano katika sekta mbalimbali zenye manufaa kwa wananchi wa Tanzania na Namibia. Viongozi hao pia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Ziara hii ya kwanza ya Kitaifa ya Rais Nandi-Ndaitwah nchini Tanzania tangu alipoingia madarakani inaashiria dhamira ya pamoja ya Tanzania na Namibia ya kuendeleza ushirikiano wa kimkakati, kuimarisha diplomasia ya uchumi, pamoja na kukuza biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili.
Ziara hii pia inatarajiwa kutoa fursa ya kuenzi historia ya ushirikiano wa ukombozi kati ya Tanzania na Namibia, huku ikifungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika nyanja mbalimbali za maendeleo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho cha wananchi wa mataifa hayo mawili.











.jpeg)

.jpeg)













.jpeg)
