Na Mwandishi Wetu

Balozi Sita zinazowakilisha nchi zao nchini Tanzania zimeshiriki Tamasha la Piano ya muziki wa Franco Rhumba kwa ajili kupata furaha.

Akizingumza wakati kufungua Tamasha hilo lilofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo nchini Tanzania Jean Pierre Massala amesema kuwa Muziki huo unakuwatanisha kupata furaha pamoja na kujenga umoja .

Amesema kuwa kuwa waandaji wameweza kuona umuhimu kukaa pamoja na kupata furaha kupitia muziki huo ambao unapendwa na Wakongo na Jamii zingine.

Massala amesema kuwa matamasha hayo hayo ni muhimu kwani yanakutanisha watu tofauti ambao wanafanya kujenga umoja wenye furaha.

Kwa upande wa Balozi wa Morocco nchini Tanzania Zakaria El Goumiri. amesema kuwa wameshiriki Tamasha hilo kufurahi na kutaka waandaji waendelee kuandaa kwani linawaweka pamoja

Aidha amesema kuwa furaha za muziki za muziki zinaunganisha makundi mbalimbali kwa kuleta upendo

Mmoja wa waandaji Tamasha hilo Alain Izai amesema kuwa wanashukuru mwitikio walioupata katika Tamasha kwa kuungwa na Balozi Sita Kushiriki mwanzo hadi mwisho.

Izai amesema kuwa wataendelea kuandaa matamasha hayo mara kwa mara katika kutoa burdani kujenga furaha katika nyoyo zao.

Hata hivyo amesema Muziki wa Rhumba unapendwa na kila rika ambapo kazi yao ni kuendelea kutunga katika kuboresha nyimbo za muziki huo.
Kundi cha wasanii wakipata maelezo kwa ajili ya kutoa burdani kwa Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome baada ya  kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania  Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akiwa katika picha ya pamoja baada ya   baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania  Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akikata Keki iliyoandaliwa na Wafanyakazi wa Ubalozi huo wakati alipowasili katika Ofisi ya Ubalozi mara baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania  Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Balozi wa Kenya Nchini Tanzania Catherine Wahome akikabidhiwa Ua kwa ajili ya upendo wakati alipowasili katika Ofisi ya Ubalozi mara baada ya kukabidhi Hati ya Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania  Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Na Mwandishi wetu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeitaka Serikali kuongeza juhudi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyo chini ya Wizara ya Madini ili kuhakikisha inaleta matokeo chanya kwa wananchi na kukuza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa.

Akiwasilisha maoni ya Kamati bungeni Aprili 27, 2026, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Simon Lusengekile, alisisitiza umuhimu wa upangaji na usimamizi makini wa miradi yote ya madini ili ikamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika.

Lusengekile alieleza kuwa Serikali inapaswa kuendelea kutenga rasilimali za kutosha kwa ajili ya miradi hiyo, sambamba na kuimarisha ufuatiliaji wake, hatua itakayosaidia kuongeza ufanisi na tija kwa wananchi.

Alibainisha kuwa usimamizi thabiti wa miradi hiyo utasaidia kuboresha utoaji wa huduma na kuimarisha sekta ya madini, hasa kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayolenga kuongeza thamani ya rasilimali za madini hapa nchini.

“Ni muhimu kwa Wizara kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa umakini mkubwa na kuendana na dira ya maendeleo ya taifa katika sekta ya madini,” alisisitiza Lusengekile.

Katika maoni yake, Kamati pia imehimiza Serikali kuwekeza zaidi katika teknolojia za kisasa za uchenjuaji na uchakataji wa madini, ili kuongeza thamani kabla ya kusafirishwa nje ya nchi, jambo litakalosaidia kuongeza mapato ya taifa.

Aidha, Kamati imeitaka Serikali kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wa sekta hiyo, hatua itakayochochea uwazi, uwajibikaji na utekelezaji wenye tija wa sera na miradi ya maendeleo.

Kwa ujumla, Kamati imeweka bayana kuwa mafanikio ya sekta ya madini yanategemea zaidi usimamizi madhubuti, uwekezaji wa kutosha na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuleta manufaa endelevu kwa Taifa.


Wizara ya Madini imeiomba Bunge kuidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 174.98 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ili kuwezesha utekelezaji wa majukumu yake muhimu ya kusimamia na kuendeleza sekta ya madini nchini.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi bungeni jijini Dodoma leo Aprili 27, 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema bajeti hiyo imelenga kuimarisha ufanisi wa shughuli za wizara pamoja na kuongeza mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.

Kwa mujibu wa maelezo ya waziri huyo, kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 71.51 sawa na asilimia 40.87 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuendeleza miundombinu na kuongeza tija katika sekta hiyo.

Aidha, shilingi bilioni 103.47 sawa na asilimia 59.13 zitatumika kwa matumizi ya kawaida ya wizara na taasisi zake. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 27.36 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi, huku shilingi bilioni 76.11 zikienda katika matumizi mengine ya kiutendaji na uendeshaji wa shughuli za kila siku.

Mavunde amesisitiza kuwa utekelezaji makini wa bajeti hiyo utasaidia kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa maduhuli ya serikali, ambayo yanakadiriwa kufikia shilingi trilioni 1.4, sambamba na kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali madini nchini.

Bajeti hiyo inaelezwa kuwa sehemu muhimu ya mkakati wa serikali wa kuifanya sekta ya madini kuwa moja ya nguzo kuu za ukuaji wa uchumi na chanzo kikubwa cha mapato ya taifa.



Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

WIZARA ya Madini imeweka bayana vipaumbele nane kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ikilenga kuifanya sekta hiyo kuwa mhimili imara wa uchumi wa Taifa kupitia ongezeko la mapato, ajira na usimamizi bora wa rasilimali.

Akiwasilisha mpango wa bajeti bungeni, Waziri wa Madini, Antony Mavunde, alisema serikali imejipanga kuhakikisha sekta ya madini inachangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika ukuaji wa uchumi kwa kuzingatia maeneo muhimu ya kimkakati.

Kipaumbele cha kwanza ni kuimarisha utafiti wa madini nchini. Serikali inalenga kubaini maeneo mapya yenye utajiri wa madini pamoja na kuongeza upatikanaji wa takwimu sahihi zitakazosaidia kuvutia wawekezaji na kuongeza hifadhi ya madini.

Katika hatua ya kuongeza thamani ya rasilimali hizo, kipaumbele cha pili kinahusu kukuza uchakataji wa madini ndani ya nchi. Serikali inalenga kuhakikisha madini mengi zaidi yanachakatwa kabla ya kuuzwa nje, jambo litakaloongeza ajira, mapato ya ndani na thamani ya mauzo ya nje.

Kipaumbele cha tatu kinajikita katika kuongeza ushiriki wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa madini. Hii inahusisha kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo na wa kati ili waweze kushiriki kikamilifu na kunufaika zaidi na rasilimali za nchi.

Sambamba na hilo, kipaumbele cha nne ni kuwawezesha wachimbaji wadogo kwa kuwapatia maeneo rasmi ya uchimbaji, mitaji pamoja na teknolojia ya kisasa. Hatua hii inalenga kuongeza uzalishaji na kupunguza uchimbaji holela usiozingatia sheria.

Kwa upande wa mapato, serikali imeweka mkazo katika kuimarisha udhibiti wa mapato yatokanayo na madini kama kipaumbele cha tano. Lengo ni kudhibiti utoroshaji wa madini na kuhakikisha kodi pamoja na tozo zote zinalipwa ipasavyo.

Kipaumbele cha sita kinahusu kukuza masoko ya madini ndani ya nchi. Serikali inalenga kuhakikisha wachimbaji wanapata masoko ya uhakika yenye uwazi na bei shindani, hali itakayoongeza mapato kwa wachimbaji na taifa kwa ujumla.

Katika kuvutia mitaji zaidi, kipaumbele cha saba ni kuboresha mazingira ya uwekezaji. Serikali imepanga kurahisisha taratibu za utoaji wa leseni pamoja na kuendelea kuweka sera rafiki zitakazowavutia wawekezaji wa ndani na nje.

Hatimaye, kipaumbele cha nane kinahusu kuimarisha usimamizi wa mazingira na usalama migodini. Serikali inalenga kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa kuzingatia sheria, kulinda afya za wachimbaji na kuhifadhi mazingira.

Kwa ujumla, utekelezaji wa vipaumbele hivi unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya madini, kuongeza mchango wake katika pato la Taifa na kuboresha maisha ya Watanzania kupitia ajira na fursa za kiuchumi.





Korogwe, Tanga.

‎Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza utekelezaji wa mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) unaolenga kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga.

‎Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Burhan Ngulungu ambapo amesema kuwa takribani shilingi Bilioni 19 kupitia mradi wa TACTIC zitatumika katika ujenzi wa barabara za lami Km 10.4 na mifereji ya maji ya mvua itakayosaidia kuondoa maji katikati ya mji na kupeleka eneo la mto Pangani.

‎"Kuna barabara itaunganisha stendi ya Kijazi na soko la Kilole, hivyo barabara ikikamilika licha ya kupendezesha mji, wananchi pia wataweza kupata huduma za usafiri na usafishaji, mazingira bora ya kufanyia biashara kwa wajasiriamali na wafanyabiashara na pia kuongeza mapato ya halmashauri ya mji wa Korogwe", amesema.

‎ ‎Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Korogwe mjini CPA. Charles Njama amesema mradi huo unaotarajiwa kujenga barabara katika kata za Bagamoyo, Mgombezi, Mtonga, Manundu, Masuguru na Magunga unakwenda kuleta tabasamu la kudumu kwa wananchi wa Korogwe.

‎"Tunamshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mradi huu, barabara ya NMB-Magunga ni muhimu kwa wananchi wa Korogwe, Handeni, Lushoto na maeneo mengine kwasababu inapeleka wagonjwa hospitali ya Magunga, ikikamilika kwa kiwango cha lami itasaidia wagonjwa kufika hospitali bila usumbufu", amesema.

‎Naye, Mhandisi Charles Kamugisha Mratibu mradi wa TACTIC Korogwe Mji, ameeleza kuwa mradi unatarajiwa kukamilika tarehe 23 Januari, 2027 ambapo unahusisha ujenzi wa barabara ya NMB-Magunga Km 2.7, Bagamoyo-Mgombezi-Kibo Km 6.5, Kijazi Bus Stand-Kilole sokoni Km 1.2 pamoja na mifereji ya maji ya mvua Km 1.43 fedha za mkopo nafuu toka Benki ya Dunia.

‎Vilevile, Mhandisi Zakayo Magoro Meneja wa TARURA wilaya ya Korogwe amesema kuwa TARURA ina mtandao wa barabara za lami Km 16.1 kupitia mradi wa TACTIC zitaongezeka hadi kufikia Km 26.5 ambapo zikikamilika zitapendezesha mji, thamani ya ardhi itapanda na itapunguza gharama za matengenezo ya mara kwa mara.

‎Naye, Bw. Mohamed Dachi mkazi wa kata ya Mgombezi ambaye ni mkulima ameishukuru serikali kwa ujenzi wa barabara ya Bagamoyo hadi Kibo ambapo ikikamilika itaongeza fursa za kibiashara na kiuchumi kwani watasafirisha mazao yao sokoni kwa urahisi.

‎Bw. Salmin Sadala mkazi wa kata ya Manundu ambaye ni mfanyabiashara ndogondogo amesema kuwa baada ya kukamilika kwa mradi huo licha ya mji wa Korogwe kupendeza pia taa zikiwekwa watafanya biashara hadi usiku na kuchochea kukua kwa shughuli za kiuchumi kwa wananchi.


















Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema vijana ndio nguzo kuu ya uendeshaji wa Serikali ya awamu ya sita, akisisitiza kuwa mustakabali wa taifa uko mikononi mwao kutokana na idadi yao kubwa nchini.

Akizungumza katika Kongamano la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi lililofanyika Tunguu, Zanzibar, Rais Samia alisema takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 zinaonyesha wazi kuwa vijana ndio kundi kubwa la Watanzania, hivyo wanapaswa kupewa nafasi pana zaidi katika maamuzi ya maendeleo ya taifa.

Amefafanua kuwa Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuboresha mazingira ya kiuchumi, kijamii na kisiasa ili kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika uongozi na kujenga taifa lenye ushindani.

“Serikali hii inaendeshwa na vijana. Sisi tuliopo juu kazi yetu ni kutoa mwelekeo, kusimamia sera na kurekebisha mifumo ya kisheria pale inapohitajika,” alisema Rais Samia.

Aidha, amebainisha kuwa muundo wa sasa wa Serikali unaonesha dhamira hiyo, ambapo idadi kubwa ya mawaziri na manaibu mawaziri ni vijana. Aliongeza kuwa hata katika vikao vya Baraza la Mawaziri, zaidi ya robo tatu ya wajumbe waliohudhuria walikuwa chini ya umri wa miaka 50.

Rais Samia amesisitiza kuwa hatua hiyo si ya bahati mbaya, bali ni utekelezaji wa dira ya maendeleo ya taifa pamoja na maelekezo ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ambayo inaelekeza kuwekeza nguvu zaidi kwa vijana.

Kwa upande mwingine, aliwataka vijana kote nchini kutumia fursa wanazopewa kwa uwajibikaji, nidhamu na uzalendo, ili kuhakikisha wanachangia kikamilifu katika kukuza uchumi na ustawi wa jamii.












Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, amesisitiza kuwa uendelevu wa Taifa hauwezi kupatikana iwapo wananchi hawatazingatia utunzaji wa mazingira, akieleza kuwa changamoto za mabadiliko ya tabia nchi zinaweza kuathiri ustawi wa jamii na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, katika maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi NaneNane, kata ya Nzuguni, Shekimweri amesema ni muhimu kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda mazingira ili kukabiliana na athari kama ukame.

Katika kuadhimisha Muungano huo, Shekimweri alishiriki zoezi la upandaji miti katika Shule ya Msingi NaneNane, ambapo jumla ya miti 162 imepandwa, ameeleza kuwa idadi hiyo inaashiria miaka ya Muungano na umoja wa Taifa, Aidha, amewataka wanafunzi na walimu kuitunza miti hiyo ili iweze kukua na kuleta manufaa kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Sambamba na hilo, amewataka wananchi kuendelea kuuenzi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kudumisha amani, umoja na mshikamano ulioasisiwa na waasisi wa Taifa la Tanzania, Amesema misingi hiyo inapaswa kuanzia kwa mtu mmoja mmoja, familia, jamii hadi Taifa kwa ujumla.

Aidha, amebainisha kuwa katika kipindi cha miaka 62 ya Muungano, nchi imepiga hatua kubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo afya na usafirishaji. Amesema huduma za afya sasa zinapatikana hadi ngazi ya kata kutokana na upatikanaji wa vifaa tiba, hali iliyopunguza adha ya wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.

Kwa upande wa usafirishaji, amesema maboresho yaliyofanyika yamerahisisha safari, ambapo kwa sasa inawezekana kusafiri kutoka Dodoma kwenda Zanzibar na kurejea siku hiyo hiyo, tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano yalianza Aprili 24, 2026 kwa shughuli mbalimbali ikiwemo usafi kwenye kata zote, mdahalo, maandamano ya amani ya kilomita 6.2 na bonanza la michezo, kabla ya kuhitimishwa Aprili 26, 2026 kwa zoezi la upandaji miti.




Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Manyoni

HOSPITALI ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida imesema hospitali hiyo kwa sasa imekuwa na uwezo mkubwa wa utoaji bora wa huduma za afya kutokana na uwepo wa dawa na vifaa tiba vya kisasa vilivyotolewa na Bohari ya Dawa(MSD).

Kwa mujibu wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni ni kwamba MSD wamepeleka vifaa vya kisasa ambavyo vimewezesha kurahisisha huduma kwa wateja(wagonjwa) ikiwemo mashine yenye uwezo wa kupima sampuli nane kwa wakati mmoja hali ambayo pia imesaidia kupunguza msongamano.

Akizungumza katika ziara ya kikazi iliyoandaliwa na MSD ya kutembelea hospitali hiyo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida Dk.Bwire Robert amesema MSD wamefanya mageuzi makubwa ya kiutendaji katika usambazaji wa dawa na vifaa tiba katika hospitali, vituo vya afya na Zahanati nchini. 

Amesisitiza mabadiliko yaliofanywa na MSD yamewarahisishia wao kama watoa huduma za afya kwa wananchi kufanyakazi zao kwa kujiamini huku malalamiko ya wananchi kuhusu huduma yakipungua kwa kiasi kikubwa.

Dk.Bwire kwa sasa MSD wanafanyakazi kidijitali jambo ambalo linarahisisha mpaka ngazi ya kijiji kutoa oda ya dawa na kufanyiwa kazi ndani ya muda mfupi na hatimaye kupata dawa na vifaa tiba. 

“Kumekuwa na mapinduzi makubwa katika utoaji huduma kutokana na Serikali kuwekeza katika vifaa tiba,  dawa na watoa huduma.”

Akieleza zaidi Dk.Bwire amesema uamuzi wa MSD kuwezesha uwepo wa chumba maalum na vifaa tiba kwa ajili ya kuhudumia watoto njiti umewezesha sasa watoto hao kuhudumiwa vema na kukua bila changamoto yeyote na kusisitiza hivi sasa hata mtoto mwenye gramu 600 wana uhakika atahudumiwa,atakuwa salama.

“MSD imetuletea vifaa maalum vya kuwatunzia watoto njiti na uwepo wa vifaa hivyo tumepunguza vifo vya watoto njiti kwa asilimia 90,haya ni mafanikio makubwa sana katika sekta ya afya.Tunaipongeza Serikali yetu inayoongozwa na Rais Samia kwani kupitia MSD huduma za afya zimekuwa bora na za uhakika.”

Pamoja na hayo amesema pia MSD imewezesha hospitali ya Wilaya ya Hospitali Manyoni kuwa na vifaa vya maabara vya kisasa ikiwemo mashine za UtraSound ya kisasa, mashine za upasuaji, na Mashine ya usingizi . 

Kuhusu vitanda vyenye mashine za kupumulia amesema wanavyo vya kutosha hivyo kwao sio changamoto tena huku akieleza kuwa uamuzi wa MSD kujenga chumba cha kisasa cha kuhifadhia maiti imesaidia miili ya wapendwa wetu kuhifadhiwa sehemu salama katika hospitali hiyo.

Awali Meneja MSD kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa amefafanua kwamba MSD inahudumia  vituo zaidi ya 400 kwa Mkoa wa Singida huku Kanda Nzima ya Kati ikiwemo Mkoa wa Singida, Dodoma na Wilaya ya Kiteto ikiwa na jumla ya vituo zaidi ya 840.

Kwa wa upande wa wananchi wa Wilaya ya Manyoni wameipongeza Serikali kupitia MSD kwa kuendelea kuboresha huduma za afya kwa kuiwezesha Hospitali ya Wilaya kuwa na vifaa tiba vya kisasa sambamba na uhakika wa dawa kwani yale malalamiko ya kukosa huduma hayapo tena.

Wananchi hao walipoulizwa kuhudumiwa katika hospitali za serikali au binafsi wanachagua kwenda wapi wamejibu kwa sasa kimbilio lao ni katika hospitali za serikali kwani hakuna huduma ambayo wanaihitaji wameikosa kwa kuwa kuna kila kitu.






-Asema Rais Dkt. Samia ni kiongozi mbunifu na wa vitendo


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anazungumza na wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam ambapo amefanya ziara ya kikazi ya siku moja.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara unaofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Msimbazi, Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kiongozi wa vitendo na mwenye dhamira ya dhati ya kuwatumikia watanzania kwa kutoa majawabu ya changamoto zinazowakabili.

Aidha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ofisi zote za umma zipo kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania kwa kutoa majawabu ya kero za wananchi.

Awali Mheshimiwa, Dkt. Mwigulu alikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6.

Pia, Mheshimiwa Waziri Mkuu alikagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.














Vyama 12 Vimepongeza ripoti ya tume ya kuchunguza matukio ya tarehe 29 na baada ya uchaguzi iliyowasilishwa na Jaji Chande.

Katika mkutano huo Mhe Doyo alipongeza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kukubaliana na mapendekezo yote yaliyopendekezwa na tume hiyo, aidha Mhe.Doyo amesisitiza pendekezo namba nne na pendekezo namba tano mamlaka husika wayafanyie kazi haraka kuondoa mzozo uliopo wa kisiasa hapa nchini.










Top News