Na Munir Shemweta, KITETO


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameahidi kupelewa kwa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Kiteto mkoani Manyara.

Dkt Akwilapo alitoa ahadi hiyo leo tarehe 26 Februari 2026 kufuatia kuwasilishwa kwa malalamiko na mwananchi mmoja aliyemueleza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba aliyeko katika ziara mkoani Manyara kuwa, katika wilaya ya kiteto wananchi wamekuwa wakipata shida ya kushughulikiwa mashauri yao ya ardhi kupitia Baraza la Ardhi kutokana na kukosekana kwa mwenyekiti wa Baraza.

Kwa sasa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Kiteto linahudumiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba kutoka Dodoma jambo lililoelezwa kuwa limechangia mashauri kuchukua muda mrefu.

Dkt Akwilapo amesema, suala la Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba Wilaya katika wilaya ya Kiteto tayari limeshamfikia na analifanyia kazi na muda wowote mwenyeikiti atapatikana ndani ya muda mfupi.

‘’Nimemuagiza katibu mkuu aliyefanyie kazi na muda wowote tutapata mwenyekiti mahsusi kwa ajili ya eneo hili’’. Amesema Dkt Akwilapo

Akigeukia suala la migogoro ya ardhi katika wilaya ya Kiteto, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema, migogoro mingi katika wilaya ya Kiteto imesababishwa na ukosefu wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Akwilapo, wilaya ya Kiteto ina jumla ya vijiji 63 na kati ya hivyo vijiji 33 ndivyo vilivyofanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi huku vijiji 22 mpango wake ukiwa umeisha muda wake jambo alilolieleza kuwa, sasa jumla ya vijiji 52 vinahitaji kufanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi.

Amesema, Wizara yake inalifanyia kazi suala hilo na katika mpango wa Bajeti ijayo ya 2026/2026 wameomba fedha na itakapofanikiwa Wizara yake itatekeleza mpango huo kwa kushirikiana na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMA).
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza katika mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026.
Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akiwa pamoja na viongozi wengine wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. Wa pili kulia ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo.
Sehemu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika ziara ya Waziri Mkuu Wilayani Kiteto mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026.
Waziri Mkuu Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba akisalimiana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri alipowasili wilayani Kiteto wakati wa ziara yake mkoani Manyara tarehe 26 Februari 2026. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi.Mwajabu Nyamkomora,akizungumza  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

......

KATIBU Tawala Msaidizi Mkoa wa Dodoma, Mwajabu Nyamkomora, amesema uwajibikaji na uaminifu ni miongoni mwa misingi muhimu inayochochea biashara endelevu na kukuza uchumi wa wananchi.

Bi.Nyamkomora ameyasema hayo  wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara kuhusu shughuli za Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

Amesisitiza kuwa wadau wa biashara wanapaswa kuzingatia maadili hayo ili kujenga mazingira bora ya ushindani wa haki sokoni, hatua itakayoongeza imani kwa wawekezaji na kuimarisha ustawi wa uchumi.

“Biashara endelevu inahitaji uwajibikaji na uaminifu. Bila misingi hiyo, ni vigumu kujenga soko lenye ushindani wa haki na linalomnufaisha mlaji,” amesema Bi. Nyamkomora.

Aidha ameeleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuongeza uelewa wa wadau kuhusu majukumu ya Baraza hilo pamoja na namna ya kulifikia kwa urahisi wanapokumbana na changamoto za kibiashara.

Kwa mujibu wake, elimu hiyo itawasaidia washiriki kutambua njia sahihi za kutatua migogoro inayohusiana na ushindani wa kibiashara na masuala ya udhibiti wa soko, jambo litakalosaidia kuimarisha biashara na kuongeza ufanisi katika shughuli za kiuchumi.

“Kupitia semina hii, kama sekta na wadau wetu muhimu tunaendelea kuimarisha mshikamano, kubadilishana uzoefu na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu,” ameongeza.

Hata hivyo amewataka wadau kujikita katika misingi ya uwajibikaji na uaminifu ili kuvutia uwekezaji unaoendana na kasi ya maendeleo ya Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Bi.Nyamkomora amebainisha kuwa Ofisi ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Baraza la Ushindani kwa kutoa ushirikiano wa kutosha utakaowezesha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo, kwa lengo la kuboresha mazingira ya biashara na kukuza ustawi wa wananchi.

Kwa upande wake, Msajili wa Baraza la Ushindani, Mbegu Kaskasi, amesema kuwa  mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa Baraza kutoa elimu kwa wadau kufuatia maelekezo ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ya kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu majukumu ya taasisi hiyo.

Naye Mkuu wa Idara ya Uchumi wa FCT, Kulwa Msogoti, ameeleza kuwa Baraza hilo ni chombo cha kisheria kinachosikiliza rufaa za ushindani na kulinda maslahi ya wafanyabiashara pamoja na watumiaji wa bidhaa na huduma, kwa lengo la kujenga uchumi shindani na jumuishi nchini.

Nao Baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamesema kuwa mafunzo hayo yamewapa mwanga kuhusu namna ya kufuata taratibu sahihi za kisheria wanapokumbana na changamoto za ushindani au wanaporidhika na maamuzi ya mamlaka za udhibiti.

Semina hiyo ni sehemu ya mkakati wa Baraza la Ushindani wa kuwafikia wadau katika mikoa mbalimbali nchini ili kuongeza uelewa wa sheria za ushindani na kuimarisha utatuzi wa migogoro kwa njia ya kisheria.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akizungumza  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MSAJILI  wa Baraza la Ushindani (FCT), Mbegu Kaskasi,akizungumza  wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu  Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani)  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu  Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani)  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Katibu  Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora (hayupo pichani)  wakati akifungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa  semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma  yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Uchumi FC Bw.Kulwa Msogoti,akiwasilisha mada wakati wa  semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma  yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

MKUU wa Idara ya Sheria FCT Bw.Kunda Mkenda,akiwasilisha mada kuhusu Sheria wakati wa  semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma  yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

AFISA TEHAMA  FCT Athuman Kanyegezi,akiwasilisha mada kuhusu TEHAMA wakati wa  semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma  yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

WADAU mbalimbali wakichangia mada na kutoa ushauri wakati wa  semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) Mkoa wa Dodoma  yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma.

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .

KATIBU Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Dodoma Bi. Mwajabu Nyamkomora,akiwa katika picha ya pamoja na washiriki mara baada ya kufungua semina ya kuwajengea uwezo wadau wa Baraza la Ushindani (FCT) kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika leo Februari 27,2026 jijini Dodoma .


Mbunge wa Jimbo la Kisarawe,Mhe.Dkt. Selemani Jafo, ameendelea kuonesha dhamira yake ya dhati katika kuboresha huduma za afya kupitia kampeni yake ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao”, inayolenga kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati ili kusogeza huduma karibu na wananchi.

Akiwa katika ziara ya kuwashukuru wananchi wa Kitongoji cha Kola, Jafo amechangia tofali 1,500 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati mpya itakayohudumia wakazi wa eneo hilo.

"Mchango huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kupunguza adha ya wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu, hususan wajawazito, watoto na wazee ambao kwa muda mrefu wamekumbana na changamoto ya kukosa huduma za afya karibu na makazi yao."amesema Dkt.Jafo

Akizungumza na wananchi, Dkt.Jafo amesisitiza kuwa afya ni haki ya msingi kwa kila mwananchi na kwamba ni wajibu wa viongozi kuhakikisha huduma hizo zinapatikana kwa urahisi bila usumbufu.

Ameeleza kuwa kampeni ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao” inalenga kukamilisha ujenzi wa zahanati katika kila kijiji ndani ya jimbo hilo, ili kuimarisha ustawi wa jamii na kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika.

Aidha amebainisha kuwa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2020 hadi 2025, aliweza kuhamasisha ujenzi wa zahanati 27 kupitia ushirikiano wa Mfuko wa Jimbo, Halmashauri, Serikali Kuu pamoja na wadau wa maendeleo.

Amesema mafanikio hayo yanatoa msingi imara wa kuendeleza juhudi zaidi katika awamu ijayo.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Masaki, Pili Kondo Chamgui, amempongeza Dkt.Jafo kwa juhudi zake za kuwajali wananchi. Ameeleza kuwa kwa sasa vijiji vyote vya kata hiyo vina zahanati, huku Kituo cha Afya cha Masaki kikiwa kinatoa pia huduma za upasuaji, hatua iliyopunguza kwa kiasi kikubwa rufaa zisizo za lazima.

Ameongeza kuwa ujenzi wa zahanati katika Kitongoji cha Kola utakuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo ambao hulazimika kusafiri zaidi ya kilometa sita kufuata huduma za afya katika kijiji mama cha Kisanga.

Nao,Wananchi wa Kitongoji cha Kola, wameeleza shukrani zao kwa mbunge huyo, wakisema amesikia kilio chao cha muda mrefu cha ukosefu wa huduma za afya karibu na makazi yao. Walisema changamoto hiyo ilikuwa ikiweka maisha yao hatarini hasa wakati wa dharura za kiafya.

Kwa ujumla, kampeni ya “Kila Mtu Atibiwe Kwao” inaendelea kuleta matumaini mapya kwa wananchi wa Kisarawe, huku ushirikiano kati ya viongozi na jamii ukiwa chachu muhimu ya kusogeza huduma bora za afya karibu zaidi na wananchi.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, akimkabidhi cheti cha ushiriki wa Mafunzo ya Usimamizi wa Kimkakati wa Elimu Mwalimu Dennis John Otieno, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) na pia Mkuu wa Shule ya Sekondari Ilboru mkoani Arusha.

Mafunzo hayo ya Uongozi kwa Viongozi wa Elimu na Wakuu wa Shule yamefanyika katika chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo Bagamoyo.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Maulid aliwapongeza washiriki kwa kujituma na kuonesha uzingatiaji mkubwa katika vipindi vya mafunzo. Aliwataka kuyazingatia na kuyatekeleza kwa vitendo maudhui waliyojifunza ili kuleta tija katika usimamizi wa taaluma, malezi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika taasisi zao.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU Mkoa wa Lindi, imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi milioni 16 baada ya kubaini na kuziba mianya ya ubadhirifu katika miradi ya maendeleo na usimamizi wa rasilimali katika kipindi cha Oktoba hadi Disemba 2025.

Kwa Mujibu wa Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoani humo  EMMA ACKIM MWASOGYE alipokuwa anazungumza na wanahabari mapema leo Februari 27,2026 ,Wilaya ya Ruangwa,uchunguzi uliofanyika kwenye vijiji 15 umeimarisha usimamizi wa misitu na kwamba kamati za misitu zimeundwa na kupewa miongozo, hali iliyosaidia kupunguza uvunaji haramu na kuongeza mapato ya vijiji huku wananchi sasa wakishiriki moja kwa moja kulinda rasilimali zao.

Katika hatua nyingine, amesema Taasisi hiyo katika Wilaya ya Nachingwea ilibaini dosari ujenzi wa Kituo cha Afya Luponda ambapo baadhi ya vifaa vya ujenzi havikuwekwa kwenye makadirio ya gharama na baada  ya ushauri wa taasisi hiyo, marekebisho yalifanyika na mradi unaendelea kwa kuzingatia taratibu.

MWASOGYE amebainisha kuwa TAKUKURU Lindi itaendelea kusimamia kwa karibu miradi ya maendeleo na mifumo ya ukusanyaji mapato ili kuhakikisha fedha za umma zinalindwa na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Amesisitiza kuwa ushirikiano wa wananchi ni muhimu katika kufichua vitendo vya rushwa na ubadhirifu, na kuwataka kuendelea kutoa taarifa.





-Katika kipindi cha mwaka 2025 imefikisha Sh.trilioni 4.4 kutoka Sh.trilioni 2.6 

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji na Dhamana(CMSA) imesema Serikali imepata mafanikio makubwa kupitika mifuko ya uwekezaji ya pamoja ambapo katika kipindi cha mwaka 2025 imefikisha Sh. trilioni 4.4 ikilinganishwa na Sh.trilioni 2.6 ya mwaka 2024.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Usimamizi na Uchunguzi wa Mamlaka hiyo Exaud Julius katika hafla wadau wa sekta hiyo kutathimini utendaji wa masoko ya mitaji kwa mwaka uliopita.

“Hatua hiyo imetokana na Serikali kuweka mazingira wezeshi na shirikishi yenye lengo la kukuza na kuendeleza masoko ya mitaji pamoja na matumizi ya tehema.CMSA imepata mafanikio makubwa mwaka 2025, kutokana na ushirikishwaji mzuri wa wadau na sera zinazounga mkono na kuboresha mazingira ya uwekezaji.”

Ameongeza pia matumizi ya teknolojia na ubunifu, ikiwemo kuanzishwa kwa bidhaa mbalimbali za uwekezaji, yamepanua ushiriki wa wawekezaji sokoni.“Tumezindua bidhaa mpya sokoni, ikiwemo Exchange Traded Funds (ETFs), ili kuwapa wateja wetu wigo mpana zaidi wa chaguzi za uwekezaji.”

Amefafanua hatua hiyo  imechangia ongezeko la idadi ya wawekezaji binafsi wanaoshiriki katika soko la mitaji.

Kwa upande wake Meneja wa Utafiti na Uchambuzi kutoka Vertex International Securities Ltd Frank Abel amesema kampuni yao ilianzisha jukwaa hilo ili kuwaleta pamoja wadau wa soko la mitaji, kupitia kupitia mafanikio ya soko na kujadili maendeleo, ikiwemo uzinduzi wa bidhaa mpya kama ETFs.

Ambapo pia ameonesha kuridhishwa na mwenendo mzuri wa soko, huku akibainisha idadi ya wawekezaji imekuwa ikiongezeka kwa kasi.“Ongezeko hili haliko tu kwenye hisa bali pia katika uwekezaji wa pamoja kupitia mifuko ya uwekezaji.”

Aidha ameishukuru Serikali kwa kuunda mazingira mazuri na wezeshi yaliyowawezesha wawekezaji kushiriki kikamilifu katika soko.Kwasasa mtu yeyote anaweza kununua hisa kupitia simu ya mkononi, jambo linalorahisisha uwekezaji zaidi kuliko hapo awali.

Amewahiza Watanzania kuwekeza katika soko la hisa huku wakifanya shughuli zao za kila siku, ikiwemo kupitia mifuko ya uwekezaji wa pamoja na mifumo mingine ya uwekezaji.

Wakati huo huo Geoffrey Malauri ambaye ni Mwenyekiti TISEBA amesema  mwenendo wa soko la hisa unahamasisha, akibainisha kuanzishwa kwa bidhaa mbalimbali sokoni, ikiwemo mifuko ya pensheni.

Amesema ubunifu kupitia majukwaa ya kidijitali umechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uwekezaji wa rejareja.“Kwenye miaka miwili iliyopita, teknolojia ya simu imesaidia kuvutia wawekezaji wapya sokoni, hasa wawekezaji binafsi pamoja na taasisi.”

Hata hivyo amesema kupitia teknolojia ya simu, wawekezaji wanaweza kununua na kuuza hisa kutoka mahali popote walipo.Pia mazingira mazuri na wezeshi pia yamevutia wawekezaji kutoka nje kuwekeza katika soko letu la mitaji.

Amewahimiza Watanzania kuchukua fursa ya mazingira haya rafiki kununua hisa au hati fungani za serikali, huku akiwahimiza wawekezaji wa ndani na nje kuchunguza fursa zilizopo katika masoko ya mitaji.

Pamoja na hayo ongezeko la bidhaa za kifedha sokoni, ikiwemo Exchange Traded Funds (ETFs), limechangia kuongeza uwekezaji katika masoko ya mitaji hapa nchini.











Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauniakizungumza wakati akifungua Semina kwa Wajumbe wa Baraza la WawakilishiZanzibar kuhusu Elimu ya Muungano iliyofanyika katika Ukumbi wa Mkutano waBaraza la Wawakilishi Unguja, Zanzibar, Februari 27, 2026.


MWANDISHI WETU, UNGUJA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Hamad Yussuf Masauni, amewaasa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuelimisha wananchi kuhusu misingi, faida nawajibu wao katika kulinda na kuutetea Muungano,

Pia amewataka Kupinga na kusahihisha upotoshaji wa taarifa kuhusu Muungano, hususanikupitia mikutano ya hadhara na mitandao ya kijamii.

Amesema, kwa kufanya hivyo, Wawakilishi watakuwa mabalozi wa amani, umoja namshikamano wa kitaifa, kusikiliza na kuwasilisha.

Waziri Masauni aliyasema hayo Februari 27,2026 wakati akifungua semina ya elimu yaMuungano kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, ikiwa ni sehemu ya mpango unaoendeleawa kutoa elimu hiyo kwa makundi mbalimbali ya jamii.

Amesema, kwa ujumla Wawakilishi ni nguzo muhimu ya kulinda na kuimarisha Muungano waTanzania kwa kupitia kutunga sheria, kusimamia Serikali na kuelimisha wananchi.

“Wawakilishi mnabeba dhamana ya kihistoria ya kuhakikisha Muungano unaendelea kuwachanzo cha amani, mshikamano wa pande mbili na maendeleo,” alisema

Amesema, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ni nguzo muhimu katika kuendelea kuuelimishana kuulinda Muungano wa Tanzania kwa kuwa wako karibu zaidi na wananchi.

Amesema, Wajumbe hao wana nafasi kubwa ya kuifikisha elimu ya Muungano kwa wananchi kwa sababu wanawakilisha na kukutana na wananchi mara kwa mara katika majimbo yao.

“Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ni nguzo muhimu katika kuulinda Muungano wetu, wanawafikia wananchi wengi zaidi, hivyo wana wajibu wa kueneza elimu ya Muungano katikamaeneo yao,” amesema

Ameeleza kuwa kwa kiasi kikubwa mpango huo unawalenga vijana ili waweze kufahamu fursazilizopo ndani ya Muungano na kuzitumia kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

Amesema, fursa za Muungano ni nyingi, lakini changamoto iliyopo ni kutokuzitangaza nakuzifafanua ipasavyo kwa wananchi.

Kupitia semina hiyo mada mbali mbali zimewasilishwa kama vile Chimbuko, Misingi, Umuhimu wa Muungano, na Upekee wa Muungano.

Amesema, kupitia mada hizo wawakilishi hao watakuza na kuongeza uelewa na kutoa taswirapana juu ya umuhimu wa uwepo wa Muungano na kuibua hamasa ya katika kujenga uzalendowa dhati kwa nchi, kuudumisha na kuuenzi Muungano kwa manufaa ya kizazi cha sasa nakijacho.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Dkt. Richard Muyungi, amesema ofisi hiyo itaendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ilikuhakikisha uelewa wa masuala ya Muungano unaongezeka na kuimarika.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauniakizungumza wakati akifungua Semina kwa Wajumbe wa Baraza la WawakilishiZanzibar kuhusu Elimu ya Muungano iliyofanyika katika Ukumbi wa Mkutano waBaraza la Wawakilishi Unguja, Zanzibar, Februari 27, 2026.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakiwa katika semina kuhusuMuungano iliyofanyika katika Ukumbi wa Mkutano wa Baraza la Wawakilishi Unguja, Zanzibar, Februari 27, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akiwa miongonimwa viongozi walioshiriki semina kuhusu elimu ya Muungano iliyotolewa kwa Wajumbewa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Ukumbi wa Mkutano wa Baraza la Wawakilishi Unguja, Zanzibar, Februari 27, 2026.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Top News