Serikali imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za haraka za kuboresha utendaji wao, ikisisitiza kuwa haitavumilia taasisi zitakazoendelea kuonesha utendaji duni kwa muda mrefu.
Onyo hilo lilitolewa na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, jijini Dar es Salaam Ijumaa, Juni 26, 2026, wakati wa mahojiano maalumu kuelekea Siku ya Gawio itakayofanyika Jumanne, Juni 30, 2026, katika Ikulu ya Dar es Salaam.
Bw. Mchechu alisema taasisi zote zinazostahili kuwasilisha gawio na michango mingine Serikalini zinapaswa kutekeleza wajibu huo kwa wakati, akisisitiza kuwa kushindwa kufanya hivyo ni kuinyima Serikali na wananchi mapato stahiki.
“Mashirika si mali ya bodi za wakurugenzi wala menejimenti; ni mali ya umma zinazosimamiwa na Serikali. Kwa muktadha huo, kurejesha kilicho haki ya wananchi si fadhila, bali ni wajibu,” alionya.
Alisisitiza kuwa viongozi wa taasisi za umma wanapaswa kuhakikisha malengo ya faida wanayopewa yanafikiwa ili kuongeza mchango wa taasisi hizo kwa uchumi wa taifa.
“Lazima taasisi zetu ziyaishi malengo ya faida ambayo huwa tunazipa. Mtu (kiongozi wa taasisi) ambaye ataendelea kushindwa kuleta gawio kwa kipindi kirefu, huyo hatufai,” alionya Bw. Mchechu.
Aidha, alisema gawio na michango mingine inapaswa kutokana na faida au ziada halisi ya taasisi, badala ya kukopa fedha, akisisitiza kuwa kufanya hivyo kunatoa taswira isiyo sahihi kuhusu utendaji wa taasisi.
“Ukikopa ili utoe gawio au mchango mwingine kwa Serikali, unakuwa unamdanganya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na hata nafsi yako mwenyewe,” alisema.
Alipoulizwa iwapo taasisi zitakazoshindwa kufanya vizuri katika utoaji wa gawio mwaka huu zinaweza kufutwa, Bw. Mchechu alisema kufutwa au kuunganishwa kwa taasisi za umma ni mchakato endelevu unaofuata taratibu zilizowekwa, na si uamuzi unaotokana na matokeo ya Siku ya Gawio pekee.
“Hatufuti taasisi kwa sababu ya matokeo ya siku ya gawio. Tunazipa kwanza muda wa kufanya maboresho, na zisipoonyesha mabadiliko ndipo tunachukua hatua stahiki,” alifafanua Bw. Mchechu.
Katika mwaka wa fedha 2024/25, Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) ilikusanya Sh1.028 trilioni kama gawio na michango mingine kutoka kwa taasisi za umma pamoja na kampuni ambazo Serikali ina umiliki wa hisa chache, kiwango kilichoweka rekodi mpya tangu kuanzishwa kwa ofisi hiyo mwaka 1959.
Pamoja na mafanikio hayo, Bw. Mchechu alisema Serikali inaamini bado kuna fursa kubwa ya kuongeza makusanyo kwa kuimarisha utendaji wa taasisi za umma na usimamizi wa uwekezaji wa Serikali.
Akizungumzia matarajio ya siku zijazo, alisema OTR inaamini kuwa maboresho yanayoendelea katika ufanisi wa kiutendaji na kifedha wa taasisi za umma yataonekana katika matokeo ya mwaka huu wa fedha, huku mafanikio zaidi yakitarajiwa katika miaka ijayo.
“Tunategemea tutaanza na nguvu mpya, mwaka huu tutavunja rekodi ya mwaka jana na mwakani tutavunja rekodi ya mwaka huu,” alisema Bw. Mchechu.
Kauli za Bw. Mchechu zinaendana na msimamo wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, ambaye hivi karibuni alionya taasisi na mashirika ya umma yanayoendelea kuonesha utendaji usioridhisha kuwa yako hatarini kufutwa au kuunganishwa endapo hayataboresha utendaji wake.
Prof. Mkumbo alisema haiingii akilini kuona baadhi ya mashirika ya umma yakishindwa kutoa gawio stahiki licha ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali.
Alisema Serikali itazipa taasisi husika muda wa kujirekebisha kabla ya kuchukua maamuzi ya kuziunganisha au kuzifuta pale itakapobidi.
“Ni afadhali kuwa na mashirika machache ya biashara, lakini yanayotoa gawio stahiki kwa Serikali,” alisisitiza Prof. Mkumbo.
Kwa mujibu wa OTR, Serikali inamiliki hisa katika taasisi na kampuni 308, ambapo 91 zinafanya shughuli za kibiashara huku 217 zikitoa huduma za umma.
Prof. Mkumbo alisema Serikali inataka kuona wananchi wakinufaika zaidi na uwekezaji wa Sh92.3 trilioni uliofanywa katika mashirika na taasisi za umma.
Ili kufanikisha azma hiyo, OTR imesema inaendelea kuimarisha usimamizi wa utendaji wa taasisi za umma ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na usimamizi wa uwekezaji.
Bi. Lightness Mauki, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Utendaji, Ufuatiliaji na Tathmini ya Mashirika ya Kibiashara wa OTR, alisema ofisi hiyo imejipanga kuendelea kuimarisha utendaji wa taasisi za umma kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na usimamizi wa uwekezaji.
“Ni imani yetu kuwa usimamizi bora wa utendaji wa taasisi za umma ni msingi wa kuleta mageuzi endelevu katika uendeshaji wa taasisi na mashirika ya umma,” alisema Bi. Mauki.
Alisema usimamizi huo unatarajiwa kuchochea uzalishaji, kukuza uchumi na kuongeza mapato ya kodi na yasiyo ya kodi, hatua itakayoimarisha uwezo wa serikali kutekeleza majukumu yake ya maendeleo na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Kwa upande wake, Bw. David Shambwe, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mashirika Yasiyo ya Kibiashara wa OTR, alisema pamoja na mashirika hayo kutokuwa na lengo la kuzalisha faida, yanapaswa kuonyesha ufanisi katika utoaji wa huduma na matumizi ya rasilimali za umma.
Alisema OTR inaendelea kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini ya utendaji ili kuhakikisha mashirika hayo yanatekeleza majukumu yake kwa ufanisi, uwajibikaji na kwa kuzingatia thamani ya fedha katika matumizi ya rasilimali za Serikali.
“Lengo letu ni kuona mashirika yasiyo ya kibiashara yanatoa huduma bora, zenye tija na zinazokidhi matarajio ya wananchi. Ufanisi wa taasisi hizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha uwekezaji wa Serikali unaleta matokeo chanya kwa maendeleo ya taifa,” alisema Bw. Shambwe.
Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, akizungumza na Mwandishi wa Habari wa Azam TV, Kissa Daniel, wakati wa mahojiano maalum yaliyofanyika Ijumaa iliyopita katika makao makuu ya Ofisi ya Msajili wa Hazina, jijini Dar es Salaam."VETERANI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wamesema wataendelea kuenzi mchango mkubwa wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, marehemu Mohammed Mtulia.
Ahadi hiyo ilitolewa na Veterani Sadick Chamumi, kwa niaba ya Katibu wa Maveterani hao, Mkoa wa Dar es Salaam, walipofika nyumbani kwa marehemu Mzee Mtulia, Mtaa wa Muheza, wilayani Temeke, kuwasilisha rambirambi zao.
"Mzee Mtulia ameacha wasifu mkubwa, hivyo inabidi tujifunze kutoka kwake. Kwa niaba ya Mavetarani wa UVCCM, tunaipa pole familia na tutaendelea kushirikiana nayo,”almesema Chamumi.
Mzee Mtulia alifariki dunia Mei 5, mwaka huu, nyumbani kwake Mtaa wa Mkuranga B, wilayani Temeke.
Naye, Katibu Msaidizi wa Veterani wa UVCCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Justy Mboke, ameeleza Mzee Mtulia enzi za uhai wake alifanya mambo makubwa, hususan kuimarisha mabaraza ya wazee kuanzia ngazi za tawi, kata, wilaya hadi mkoa.
“Mabaraza hayo mpaka hivi sasa yanafanya kazi. Sifa hiyo tutaiheshimu na kuienzi sisi veterani,” amesema.
Kwa upande wake, Katibu wa Baraza la Wazee wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Mzee Mohammed Mbonde, amewashukuru veterani kwa kuwasilisha rambirambi.
“Mzee Mtulia alifundisha upendo, uelewano, kuheshimiana, kuthaminiana na kuvumiliana. Haya ndiyo yalikuwa malezi yake kwetu,” amesema na kuongeza kuwa tukio hilo ni la udugu zaidi na upendo.
Amewaomba wazee hao kuendelea kushirikiana na kushikamana kwa kuwa uzee ni udugu, busara na hekima.
Msemaji wa familia ya marehemu Mtulia,ambaye ni mtoto wa marehemu, Athuman Mtulia, alishukuru veterani kwa kumuenzi Mzee Mtulia, kwa kuwa kitendo hicho kimeleta faraja katika familia.
Veterani ni watu wote ambao wakuliwa TANU Youth Legue na Afro Shiraz Party Legue, waliotikia wito wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere kutaka vijana wajiunge na Jeshi jipya la Tanganyika mwaka 1964 na waliotembea kwa miguu kuunga mkono Azimio la Arusha.
Pia wale wote walioshiriki vita ya Kagera dhidi ya Fashti Nduli Amin na ambao walikuwa vijana wa CCM waliovuka umri kwa mujibu wa kanuni toleo la Mwaka 1978 ukomo wa kuwa kijana wa miaka 35 ni veterani wa Chama.
Dhumuni ni kutayarisha veterani vijana wa kuwa watetezi na walinzi wa CCM na serikali yake kwa vitendo ambapo kariri ya vetenari hao ni Ujamaa na Kujitegemea.
Wizara ya Fedha imetoa wito kwa wananchi, wafanyabiashara, na wadau mbalimbali wa uchumi kutembelea Banda la Maonesho la Wizara ya Fedha, ili kupata huduma zinazotolewa na Wizara kupitia Wizara yenyewe na Taasisi zilizochini yake, hatua inayolenga kuimarisha uwazi na uwajibikaji kati ya Wizara na wananchi.
Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanafanyika katika Viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam, kuanzia Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yakiwa na Kaulimbiu kuu "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania" ikiwa ni sambamba na kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Maonesho hayo.
Lengo kuu la ushiriki wa Wizara na Taasisi zake katika Maonesho hayo ni kusogeza huduma karibu na jamii na kutoa elimu ya kifedha itakayosaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Serikali, usimamizi wa rasilimali za Taifa na fursa na huduma mbalimbali za masomo na kiuchumi zinazopatikana nchini.
Maafisa kutoka Idara na Vitengo mbalimbali vya Wizara ya Fedha na Taasisi zake, wanaoshiriki maadhimisho hayo ni pamoja na Maafisa kutoka Idara ya Bajeti, Idara ya Pensheni, Idara ya Usimamizi wa Sera za Ununuzi wa Umma, Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Idara ya Uchambuzi wa Sera, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Kitengo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi.
Aidha, katika Banda la Wizara ya Fedha, Watumishi kutoka Taasisi mbalimbali za Wizara hiyo, wanapatikana ili kutoa huduma kwa wananchi na wafanyabishara wote, ikiwemo watumishi kutoka Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Mfuko wa uwekezaji wa Utt Amis, Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM), na Soko la Hisa la Dar Es salaam (DSE).
Taasisi nyingine zinazopatikana katika Banda la Wizara ya Fedha ni pamoja na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA), Mfuko wa Self (Self Microfinance), Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), Benki ya Maendeleo (TIB), Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA), Ofisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (TOST) pamoja na Chuo Cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP).
Wananchi wote wanakaribishwa kutembelea Banda hilo, ambapo wataalamu waliobobea kutoka Idara na Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara wapo tayari kutoa huduma na ufafanuzi wa kina kuhusu masuala ya sera za kodi, bajeti kuu ya Serikali, na pamoja na huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara ya Fedha na taasisi zake.
Mwandishi Mwendesha Ofisi Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha, Bi. Masia Msuya, akiwasainisha kitabu cha wageni wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu kuu "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania", yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Afisa Mikopo Wa Hazina Saccoss, Bi. Miriam Msalanga, akitoa elimu kuhusu mikopo inayotolewa na chama hicho, kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu kuu "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania", yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Afisa Hesabu, Huduma za Mfuko Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Juliana Owiso, akitoa maelezo kuhusu uhakiki wa wastaafu, kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu kuu "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania", yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Maafisa wa Wizara ya Fedha, wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yenye Kaulimbiu kuu "Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba ni Fahari ya Tanzania", yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF- Dodoma.)
Kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa daraja la mawe la Kanyunye na ufunguaji wa barabara yenye urefu wa kilomita 2.6 katika kijiji cha Kanyunye, wilayani Newala kumeleta suluhisho la kudumu la usafiri na usafirishaji wa mazao hususani zao la korosho linalozalishwa kwa wingi katika kijiji hicho.
Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea miradi inayotekelezwa na TARURA kupitia mradi wa RISE programu ya kuondoa vikwazo barabarani (Bottleneck), Meneja wa TARURA wilaya ya Newala, Mhandisi Silvester Balama amesema waliibua mradi huo kutokana na changamoto ya mawasiliano ambayo wananchi wa eneo hilo walikuwa wakikabiliana nayo.
"Wakazi wa kijiji hiki wengi ni wakulima wa zao la korosho na ghala lao la kihifadhi korosho zikishavunwa lipo katika kijiji cha Moneka kwa hiyo walikuwa wanapata shida kusafirisha mazao yao kutoka Kanyunye kwenda Moneka kwa sababu ya kukosekana kwa kivuko na barabara" ,amesema Mhandisi Balama.
Ameongeza kuwa ili mazao yao yaweze kufika katika kijiji cha Moneka ambako ndipo lilipo ghala la kihifadhia korosho ilikuwa lazima wazunguke upande mwingine katika vijiji vya wilaya ya Masasi ili waweze kulifikia ghala hilo.
"Uwepo wa kivuko hiki kumesaidia kutoa mazao moja kwa moja kutoka kijiji cha Kanyunye kwenda kijiji cha Moneka ambako kuna ghala lao. Pia kijiji cha Kanyunye hakina shule, shule yao ya msingi ipo kijiji cha Moneka, watoto walikuwa wanapata shida sana namna ya kuvuka kwenye mto huu kwa hiyo baada ya ujenzi huu imekuwa ni ukombozi mkubwa kwao kwa maana sasa watoto wanapita juu na wanawahi kufika shule".
Bi. Zainabu Mohamedi Seif mkazi wa kijiji cha Kanyunye amesema kabla ya ujenzi wa daraja hilo walikuwa wakitembea umbali mrefu kuzifikia huduma za afya hospitali ambayo ipo mjini Newala lakini sasa hivi wanakodi bodaboda tu kwenda Newala kwa wakati na kwa gharama nafuu.
Kwa upande wake, Bw. Mohamed Seif Hussein maarufu mzee Mchomolo amesema wao kama wananchi wamefurahishwa na ujenzi wa daraja hilo na kwamba limewakomboa kwa namna nyingi.
"Hii njia ilikuwa ni ya kichochoro baada ya kutengeneza barabara na kujengwa hili daraja sasa hivi imekuwa barabara maarufu ya kupita sio sisi tu bali hata wenzetu wa kijiji jirani cha Mwanona wameacha kuzunguka huko sasa hivi wanapita barabara hii kwenda Newala, kabla ya hapo tulikuwa tunateseka sana" amesema mzee Mchomola.
Akizungumza kwa niaba ya wabunge hao mbunge wa viti maalum Mhe. Zainab Abdallah ameeleza kuwa katika ziara hiyo wameshuhudia maendeleo yaliyotukuka kuhusu uhifadhi, utalii, Malikale, urithi wa utamaduni na maendeleo ya jamii ambapo vinadhihirisha kuwa Ngorongoro ni kivutio bora cha Utalii Barani Afrika.
“Kuona ni kuamini, jana na leo tumetembelea eneo la hifadhi ya Ngorongoro na tumeona maendeleo makubwa yakifanyika na kwa macho yetu tumeshuhudia idadi kubwa ya watalii waliojawa na nyuso za bashasha na furaha kwa kushuhudia vivutio vilivyopo, mandhari na hali ya hewa ambayo unaipata Ngorongoro pekee”,amesema Mhe. Zainab.
Wabunge katika ziara hiyo walielezwa kuhusiana na historia ya kutokea kwa kreta ya Ngorongoro, chimboko la binadamu wa kale na namna ambavyo mabadiliko ya viumbe mbalimbali yanavyoendelea kutokea kwa nyakati tofauti.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Idara ya maendeleo ya jamii, Gloria Bideberi akizungumza kwa niaba ya kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro, Abdul-Razaq Badru amewapongeza wabunge hao kwa kufanya maamuzi sahihi ya kutembelea hifadhi hiyo yenye vivutio mbalimbali na kuwaomba kuendelea kuwa mabalozi wa kuitangaza Ngorongoro ambayo imepata tuzo ya kuwa chaguo la Wasafiri(Watalii) la kiwango cha Juu cha Ubora mwaka 2026 (Travellers Choice Awards, Best of the best 2026)
Eneo la hifadhi ya Ngorongoro linasifika duniani kutokana na kuwa na ikolojia yenye mchanganyiko wa viumbe mbalimbali kuishi kwa pamoja Ngorongoro kwa miaka mingi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania waendelee kuhimizana kuhusu ulinzi wa Taifa na kamwe wasipuuze viashiria vya uvunjifu wa amani.
"Tuendelee kuhimizana kuhusu suala la ulinzi wa Taifa letu. Ulinzi wa Taifa letu ni wa kila Mtanzania na amani yetu ni ya kila Mtanzania."
"Sasa hivi hatupaswi kupuuzia viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Hatutakiwi kuvipuuza kwa sababu vimetuachia doa," amesema.
Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 28, 2026) katika ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye usharika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida.
Harambee hiyo ambayo ni ya nne kufanyika, ililenga kukusanya sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya kuboresha vituo vya huduma za afya, kuimarisha vituo vya huduma za elimu, utumishi na uinjilisti vya Dayosisi hiyo ambavyo vinapaswa kukamilika ifikapo Desemba, mwaka huu.
Jumla ya sh. bilioni 1.331 zilikusanywa zikiwa ni fedha taslimu na ahadi. Waziri Mkuu amesema sh. milioni 69 zilizobakia, zitakamilishwa ndani ya wiki ijayo kutokana na ahadi zilizotolewa na watu mbalimbali na timu aliyoiunda yeye ili isimamie kukamilishwa kwa ahadi hiyo.
Mapema, akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo, Mkuu wa Kanisa la KKKT, Askofu Dkt. Alex Gehazi Malasusa alisema kupitia harambee hiyo, washarika wamepewa nafasi ya kumrudishia Mungu shukrani kwa ukarimu aliowatendea maishani mwao.
"Kila tunachokifanya kinapaswa kimtukuze Mungu, mali na fedha zetu ziwe za halali, zisitokane na kuwakanyaga wengine. Mali na fedha zetu zitawaliwe na Mungu," alisisitiza.
Naye, Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kati, Dkt. Cyprian Hilinti alisema kanisa hilo linaendelea kutekeleza jukumu la kuwaombea viongozi wa nchi kila Jumapili ikiwemo kuombea amani baina ya kabila na kabila, wakulima na wafugaji na vyama kwa vyama.
"Tunatamani kuona msamaha ukipatikana katika nyanja tofauti. Msamaha ni dawa," alisema.
Alisema tangu waanze harambee hiyo miaka minne iliyopita, majimbo nane yamezaliwa, sharika mpya 27 zimezaliwa, wamepata washarika wapya 17,364 na wachungaji wapya 65.
Kwa upande wa huduma za jamii, Askofu Hilinti alisema wamefanikiwa kusajili shule mpya mbili za sekondari, shule moja ya msingi inayofundisha kwa Kiingereza (English medium) na akatumia fursa hiyo kuwashukuru washarika wote wa Dayosisi hiyo kwa kujitoa kwao katika kipindi chote hicho.



.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)







.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)












.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)




