-Wananchi kuvuna lita bilioni 21 za maji chini ya ardhi


Na Mwandishi wetu


UTAFITI uliofanywa na Bodi ya Maji ya Wami Ruvu (WRWB) umeonesha kuwepo wa maji lita bilioni 21 za maji chini ya ardhi zitakazotumika kama mbadala wakati wa kipindi cha ukosefu wa maji katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Hatua hiyo muhimu ya WRWB ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya kwanza katika kutafuta vyanzo vipya mbadala vya maji katika kukabiliana na ukosefu wa mji katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani.

Utekelezaji wa uchimbaji wa visima virefu vya maji

mbadala (back up) unatekelezwa na WRWB kwa awamu mbalimbali katika jiji la Dar es salaam na Mkoa wa Pwani kama mbadala wa maji hii ni kutokana na kuwepo kwa vipindi vya ukame jambo ambalo limekuwa likiathiri uvunaji maji katika bonde na kusababisha mgao wa maji katika maeneo ya Pwani na Dar es salaam

Aidha, uchimbaji wa awamu ya kwanza unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Juni 2026.

Kwa mujibu wa mtaalam wa haidrojia kutoka WRWB,Omary Kizulwa alisema bodi imeamua kuwatumia wataalamu wake ili kubaini vyanzo vipya vya maji ili kuondoa kero ya maji katika mikoa ya Pwani na Dar es Salam kwa kuchimba visima mbadala vya kuhifadhi maji katika maeneo mbalimbali.

“Kwa sasa hivi Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu tunafanya tafiti katika jiji la Dar es salaam na Pwani tafiti hizi zinatuwezesha kubaini maeneo ambayo yana vyanzo vya maji chini ya ardhi ili tuweze kuchimba visima” “Visima hivi vitakua kama back up (mbadala) kusaidia kipindi ambapo ukame unapotokea au ambapo hata ukame hamna viweze kutumika katika kutoa huduma ya maji” alisema“Zoezi la utafiti na uchimbaji linaendelea mpaka sasa tumeshafanya utafiti zaidi ya maeneo 40, Maeneo ya Ruvu Juu, Ruvu chini, Kigamboni , Chamazi, Ubungo, Kinondoni na Mburahati” alisema

“Tumeshafanya tafiti na tumeshaweka pointi na hivi sasa tunavyozungumza mitambo ipo site inaendelea na uchimbaji mpaka sasa zaidi ya visima 17 vimechimbwa na baadhi ya visima vimeonesha uwezo mkubwa kutoa maji na ni maji mazuri, mfano eneo la Mburahati tumechimba kisima kikubwa pale kina uwezo wa kutoa maji takribani lita elfu 50,000 mpaka 100,000 kwa saa na visima vingine kama Ilala na visima vya huku Chamazi vina karibia elfu 10,000 mpaka elfu 20,000 na kuendelea”

Aidha mtaalam huyo alisema kuwa Tanzania haina uhaba wa maji huku akibainisha kuwa maji chini ya ardhi ni lita bilioni 21 na maji juu ya ardhi ni lita bilioni 105

MRADI WA KIDUNDA

Aligusia pia mradi wa maji wa kimkakati wa Bwawa la Maji Kidunda unaotekelezwa kwa gharama ya sh.bilioni 336 kuwa utasaidia nao kuhifadhi maji ya juu ya ardhi kipindi ambapo kuna ukame

Kwa mujibu wa serikali Mradi wa Bwawa la Kidunda ni muhimu kwa kuwa utawezesha kukidhi mahitaji ya maji kwa wananchi wanaotarajiwa kuongezeka na kufikianidadi ya watu 11,387,753 ifikapo mwaka 2032, ambapo mahitaji ya maji yanakadiriwa kufikia zaidi ya lita bilioni

1.028 kwa siku. Mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi kutoka kampuni ya Sino Hydro Corporation ya nchini China.

Bwawa la Kidunda, litakalokuwa na ujazo wa lita bilioni 190, litawezesha mitambo ya Ruvu Juu na Ruvu Chini, yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya lita milioni 466 kwa siku, kufanya kazi katika majira yote ya mwaka na hivyo kuondoa upungufu wa maji wakati wa kiangazi.

Mitambo hiyo inahudumia zaidi ya asilimia 80 ya eneo lote la huduma la DAWASA.

Kwa upande wake wakati wa ziara ya kukagua mradi wa Kidunda msishoni mwa mwaka jana Waziri wa Maji Jumaa Aweso alisema nchi nyingi duniani kwa sasa zinakabiliwa na changamoto ya ukameinayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi, hali ambayo pia imeanza kuathiri Tanzania.

Kutokana na hali hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliielekeza Wizara ya Maji kuchukua hatua za haraka na za muda mrefu ili kukabiliana na changamoto hiyo.

“Wizara ya Maji tuliweka mkakati wa muda mfupi jijini Dar es Salaam kwa kuchimba visima vitanovilivyogharimu takribani Sh.bilioni 23.6, sanjari na mkakati wa muda mrefu wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda mkoani Morogoro pamoja na mpango wa kutumia maji ya Mto Rufiji mkoani Pwani ili kuongeza uzalishaji wa maji,” alisema

Alisema kwa sasa mahitaji ya maji kwa Jiji la Dar es Salaam ni takribani lita milioni 534 kwa siku, ilhali changamoto ya ukame ikiathiri kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma ya maji.



Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Yahya Ramadhan Kido amesema Mkoa wa Kagera unaendelea kufanya vizuri katika uzalishaji wa zao la kahawa, huku akibainisha kuwa hadi sasa mkoa huo una jumla ya miche ya kahawa milioni 85 inayotarajiwa kuongeza tija na kuinua uchumi wa wakulima.

Kanali Kido amesema hayo wakati akifungua mkutano wa wadau wa kahawa mkoani Kagera, ambapo ameeleza kuwa Serikali kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali imeendelea kusambaza miche ya kahawa kwa wananchi, huku miche milioni 36.75 ikiwa tayari imetolewa kwa wakulima kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa zao hilo muhimu la biashara.

Amesema katika msimu wa 2025/2026 pekee, miche milioni 13.7 ilisambazwa kwa wakulima kupitia ushirikiano kati ya Bodi ya Kahawa Tanzania, halmashauri, vikundi vya wakulima pamoja na sekta binafsi.

Aidha, ameitaka Bodi ya Kahawa Tanzania kuendelea kusambaza miche zaidi kwa wakulima pamoja na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo, hususan wadudu waharibifu aina ya bungua mweusi ambao wamekuwa wakisababisha hasara kwa baadhi ya wakulima.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania, Primus Kimaryo amesema bado kuna haja kubwa ya kuendelea kutoa elimu kwa wakulima na wafanyabiashara wa zao hilo ili kudhibiti biashara ya kahawa inayofanyika kwa njia za magendo.

Amesema baadhi ya watu wanaojihusisha na biashara hiyo haramu wanatoka ndani ya jamii husika, hali inayochangia upotevu wa mapato kwa wakulima pamoja na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Primus Kimaryo amewataka wafanyabiashara kuachana na vitendo vya kuuza kahawa kwa njia zisizo rasmi, huku akiwataka wakulima kuwa waaminifu kwa kuuza kahawa kupitia mifumo halali ili waweze kunufaika zaidi kiuchumi.

Katika hatua nyingine, amesema Mkoa wa Kagera umeendelea kufanya vizuri katika uzalishaji wa kahawa, ambapo uzalishaji wa kahawa ya maganda umefikia zaidi ya tani elfu 50, hatua inayodhihirisha ukuaji wa sekta hiyo ndani ya mkoa huo.





WAZIRI MKUU, amewahimiza wananchi kuendelea kuiombea Tanzania ili amani, umoja na mshikamano wa kitaifa viendelee kuimarika sambamba na nchi kuendelea kupiga hatua za maendeleo katika sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Amesema hayo leo Jumapili, Mei 17, 2026 aliposhiriki ibada katika (KKKT) Usharika wa Kondoa Mjini, Jimbo la Kondoa, Dayosisi ya Dodoma.

Ibada hiyo iliongozwa na Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Dodoma, pamoja na Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kondoa Mjini na Mkuu wa Jimbo la Kondoa KKKT, .

Waziri Mkuu amesema anaendelea kushirikiana na taasisi za dini nchini akitambua mchango wake katika kujenga jamii yenye maadili, umoja na maendeleo.

“Ujumbe wake kwa wananchi wa Kondoa ni kwamba tuendelee kuiombea nchi yetu ili iendelee kuwa ya amani na kuendelea kupiga hatua za maendeleo,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ikiwemo ujenzi wa daraja la kuingia Kondoa Mjini pamoja na daraja la barabara ya kuelekea Hanang.

“Tumebeba jambo la daraja la kuingia hapa Kondoa Mjini, hilo tutaanza nalo. Lakini la pili ni daraja la kuelekea Hanang ambalo na lenyewe kero yake ni kubwa sana,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya utekelezaji wa mfumo wa elimu ya lazima wa miaka 10 unaotarajiwa kuanza mwaka 2028.

“Hatutakuwa na jambo linaloitwa mtoto amemaliza darasa la saba. Tunaenda kuondoa mfumo wa kuishia darasa la saba ili elimu ya lazima iwe miaka 10,” amesema.

Amesema utekelezaji wa mfumo huo unahitaji ushiriki na hamasa kutoka kwa Watanzania wote kutokana na umuhimu wa mabadiliko hayo katika sekta ya elimu nchini.

Kwa upande wake, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kushirikiana na taasisi za dini nchini.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama yetu , kwa ushirikiano na sisi watu wa imani na viongozi wa dini,” amesema.

Aidha, amesema kanisa linaendelea kumuombea Waziri Mkuu pamoja na viongozi wa Serikali ili waendelee kulitumikia taifa kwa hekima na uadilifu.









Katika bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii, makabila ya Wadatoga na Wahadzabe ambayo ni sehemu ya Jiopaki ya Ngorongoro Lengai walitia nakshi na uturi bajeti  hiyo kwa kumsindikiza waziri wa Maliasili na Utalii  Dkt.Ashatu Kijaji (Mb) kuingia katika ukumbi wa bunge jijini Dodoma.

Wadatoga ni waumini wa kuoa mke zaidi ya mmoja wanaotokana na jamii yao, wana uwezo wa kuoa hadi wake kumi  na kila mke akafurahia utamu wa ndoa kutoka kwa mume wake. 

Kwa Jamii hii kuwa na wake wengi si heshima tu bali unachukuliwa kama uchumi kwa kuwa utapata watoto wengi watakaokusaidia shughuli za kuchunga mifugo, kulima chakula cha familia, kufanya kazi za uhunzi, kujenga maboma ya familia na kutanua ukubwa wa jina la ukoo.

Wadatoga hawaishiwi "Power" kwasababu hawali chipsi mayai, soseji wala Baga, hawatafuti energy wala dawa za Congo,hawana mawazo ya vikoba,ni mwendo wa vyakula vya asili tu kama Ugali, mtama, ulezi, Maharage, mbaazi, viazi vitamu na Maziwa ambapo mafuta ya kupikia hawanunui dukani bali yanatokana na samli  kutoka kwenye maziwa ya Ng'ombe yaliyogandishwa kisha kuchekechwa kwenye kibuyu maalum na kuzalisha mafuta ambayo husafishwa kiasili na kukaa muda  mrefu bila kuharibika.

Kama wewe ni kijana na unataka kuwa na uwezo wa kuwa na wake wengi karibu makumbusho ya Urithi Jiopaki ujue siri ya wadatoga na vyakula vyao vya miaka na mikaka.

Wanajumuiya wa Shirika la INADES Formation Tanzania wamelitaka shirika hilo kubuni miradi ya kilimo itakayosaidia kuwavutia vijana kuingia katika sekta hiyo, wakiamini inaweza kuwa njia ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Wito huo umetolewa jijini Dodoma na Patrick Lameck wakati wa Washa iliyofanyika kuelekea mkutano mkuu wa mwaka wa wanajumuiya na wadau wa shirika hilo, unaoenda sambamba na uchaguzi wa viongozi.

Lameck amesema ili kupanua wigo wa utendaji wa shirika hilo, ni muhimu kuanzishwa kwa miradi ya kilimo itakayowapa vijana fursa ya kushiriki shughuli za uzalishaji na kujiongezea kipato.

Amesema bado vijana wengi wanaogopa kujihusisha na kilimo kutokana na dhana iliyozoeleka kuwa sekta hiyo haina faida, hali inayochangia kupungua kwa ushiriki wao.

“Tunaomba viongozi wetu wabuni miradi ya kilimo, kwa sababu itasaidia kushawishi vijana kujiunga na shughuli hizo na kuboresha maisha yao.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa INADES Formation Tanzania, Jacqueline Nicodemus, amesema wanajumuiya wanapaswa kuwa na mshikamano na ushirikiano ili kuwezesha shirika hilo kufikia malengo na mikakati iliyojiwekea.

Amesema mafanikio ya shirika yatategemea ushiriki wa pamoja wa wanachama katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazopangwa.

“Tunapaswa kuwa kitu kimoja na kushirikiana katika utekelezaji wa mipango yetu ili kuhakikisha shirika linaendelea kupiga hatua.”







 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri (kulia), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
▪️︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala

▪️︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji.

Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa.

“Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao maalumu kitakachowahusisha wakuu wa mikoa pamoja na sekta zinazohusika kutoka maeneo yanayozalisha mazao yanayotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kufanya tathmini ya changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.

“Nitaitisha kikao cha wakuu wa mikoa ya maeneo haya yanayozalisha mazao ambayo wananchi wake wamekuwa wakipata changamoto ili tupate mpango kazi wa namna ya kumaliza tatizo hili,” amesema.

Ametaja baadhi ya mikoa inayohusika kuwa ni Dodoma, Singida, Simiyu, Tabora pamoja na baadhi ya mikoa ya Kusini inayozalisha mazao ya biashara ikiwemo ufuta na dengu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza wanunuzi wa mazao kutumia taasisi za kifedha kupata mikopo badala ya kuwakopesha wakulima kabla ya mauzo ya mazao yao.

“Wenzetu wanaokwenda kununua haya mazao wasiwakope wakulima, wao wakakope benki. Benki ndiyo taasisi zinazotoa mikopo,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mfumo huo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma kwa urahisi na kunufaika ipasavyo na mazao yao.












︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala
︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji.

Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa.

“Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao maalumu kitakachowahusisha wakuu wa mikoa pamoja na sekta zinazohusika kutoka maeneo yanayozalisha mazao yanayotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kufanya tathmini ya changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.

“Nitaitisha kikao cha wakuu wa mikoa ya maeneo haya yanayozalisha mazao ambayo wananchi wake wamekuwa wakipata changamoto ili tupate mpango kazi wa namna ya kumaliza tatizo hili,” amesema.

Ametaja baadhi ya mikoa inayohusika kuwa ni Dodoma, Singida, Simiyu, Tabora pamoja na baadhi ya mikoa ya Kusini inayozalisha mazao ya biashara ikiwemo ufuta na dengu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza wanunuzi wa mazao kutumia taasisi za kifedha kupata mikopo badala ya kuwakopesha wakulima kabla ya mauzo ya mazao yao.

“Wenzetu wanaokwenda kununua haya mazao wasiwakope wakulima, wao wakakope benki. Benki ndiyo taasisi zinazotoa mikopo,” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mfumo huo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma kwa urahisi na kunufaika ipasavyo na mazao yao.
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Kongamano la 13 la Jukwaa la Miji Duniani (13th World Urban Forum) litakalofanyika Baku, Azerbaijan kuanzia tarehe 17-22 Mei 2026.

Kongamano hilo litakalofanyika katika Uwanja wa Olimpiki wa Baku kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Makazi Duniani (UN-Habitat), linabeba kaulimbiu isemayo: “Makazi kwa Dunia: Miji na Jamii Salama na Imara.”

Jukwaa hilo la Miji Duniani litazikutanisha nchi mbalimbali zikijadili na kuweka mikakati ya pamoja ya namna miji inavyoweza kuwa chachu ya kuchochea maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, Kongamano hilo la siku sita litahusisha ushiriki wa viongozi katika ngazi ya Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wataalamu mbalimbali watakaojadili changamoto za kimataifa za makazi pamoja na kukuza maendeleo endelevu ya miji.

Kupitia kongamano hilo la Miji Duniani kutakuwa na mawasilisho na mijadala kutoka kwa Mawaziri ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajia kutoa tamko litakalotolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo.

Mawasilisho na mijada ya mawaziri katika kongamano hilo la Miji Duniani yatatoa fursa kwa Tanzania kujifunza kutoka nchi nyingine mbinu bora zinazoweza kuboresha utekelezaji wa sera mbalimbali za maendeleo pamoja na kutoa uzoefu wake.

Ujumbe wa Tanzania katika Kongamano hilo la Jukwaa la miji Duniani unahusisha pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Profesa Riziki Shemdoe, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Lucy Kabyemera pamoja na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila.


GABORONE, BOTSWANA
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amewasili nchini Botswana leo tarehe 15 Mei 2026 kumwakilisha Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika shughuli za Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Botswana, Hayati Festus Gontebanye Mogae.

Hayati Mogae alifariki dunia tarehe 08 Mei 2026 akiwa na umri wa miaka 86. Mazishi hayo yanatarajiwa kufanyika kesho, tarehe 16 Mei 2026, jijini Gaborone.

Mara baada ya kuwasili nchini humo, Mheshimiwa Dkt. Kikwete alifika katika Ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Botswana ambako alisaini katika Kitabu cha Rambirambi kuenzi mchango mkubwa wa Hayati Mogae kwa taifa la Botswana na bara la Afrika kwa ujumla.

Pichani Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Kikwete anaonekana akisaini kitabu cha rambirambi huku nyuma yake akiwa amesimama Mheshimiwa James Bwana, Balozi wa Tanzania nchini Botswana.

Katika picha ya pili, Mheshimiwa Dkt. Kikwete anaonekana akiwa pamoja na Mheshimiwa Dithapelo Keorapetse, Spika wa Bunge la Botswana, pamoja na Dkt. Gabriel Goitsemodimo Gosiame Malebang, Katibu wa Bunge la Botswana.

Wengine ni Mheshimiwa Balozi James Bwana pamoja na Balozi Mstaafu Dkt. Athalia Molokomme ambaye alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Botswana wakati wa mapokezi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu.
Mkurugenzi Mkuu wa ESRF Profesa Fortunata Makene akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Makutano wa kufungua fursa za uwekezaji utaofanyika mwezi ujao Mjini Arusha.
Mwakilishi Mkazi wa UNDP Shogeki Komatsubara akizungumza kuhusiana nafasi ya UNDP katika ushiriki wa mkutano wa kufungua fursa za uwekezaji katika mkutano utaofanyika Mjini Arusha Juni Mwaka huu.
Baadhi washiriki katika mkutano huo

*Miradi 60 ya Kimkakati Kuwasilishwa Kongamano la Uwekezaji Tanzania

Na Mwandishi Wetu
TANZANIA inatarajia kuwa mwenyeji wa Makutano wa Uwekezaji unaolenga kuvutia uwekezaji wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 2.85 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi ESRF Profesa Fortunata Makene alisema kongamano hilo litafanyika Juni 1 hadi 2, 2026 katika Gran MeliĆ” Arusha mkoani Arusha na Mgeni rasmi Waziri wa Mpingo na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo

Profesa Makene alisema mkutano huo utaunganisha wawekezaji wa kimataifa, taasisi za fedha, wadau wa maendeleo pamoja na waendelezaji wa miradi ya uwekezaji ya serikali iliyokamilisha maandalizi kwa ajili ya kupata mitaji.

Mkutano huo umeratibiwa Kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) ,Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) Tanzania, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji Tanzania (TISEZA) pamoja na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar I(ZIPA).

Aidha, usajili kwa washiriki wa mkutano huo umefunguliwa rasmi ambapo wamiliki wa miradi ya umma, wawekezaji, waendelezaji wa miradi pamoja na taasisi za fedha za maendeleo wametakiwa kujisajili kupitia mfumo rasmi wa TIGF.

Profesa Makene alisema kongamano hilo litawakutanisha viongozi wa serikali, taasisi za fedha, mifuko ya hifadhi ya jamii, wawekezaji binafsi pamoja na taasisi za kifedha kutoka ndani na nje ya nchi.

Alisema lengo kuu ni kuhakikisha mazungumzo ya uwekezaji yanazaa matokeo halisi kupitia miradi 60 iliyopitiwa na kuthibitishwa yenye thamani ya takribani dola bilioni 2.85 za Marekani.

Miradi hiyo inahusisha sekta mbalimbali za kipaumbele ikiwemo utalii na miundombinu ya asili, nishati jadidifu, usafirishaji, uchumi wa buluu Zanzibar, usindikaji wa mazao, miundombinu ya maji pamoja na miradi ya maendeleo ya ngazi za chini.

Waandaji wa kongamano hilo pia wametangaza kuwepo kwa miradi kati ya nane hadi 10 yenye kipaumbele kikubwa inayotarajiwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni 100 za Marekani kila mmoja.

Profesa Makene alisema Tanzania ipo tayari kubadilisha fursa zilizopo kuwa miradi yenye tija ya kibiashara kwa manufaa ya taifa.

“TIGF 2026 ndiyo jukwaa ambalo jumuiya ya wawekezaji wa kimataifa itaweza kupata fursa hizi na kufuatilia kila hatua ya uwekezaji hadi pale makubaliano yatakapokamilika,” alisema Profesa Makene.

Amesema Tanzania inatarajia kunufaika zaidi na uwekezaji endelevu kupitia mkutano huo unaolenga kuharakisha mtiririko wa uwekezaji nchini na kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha uwekezaji barani Afrika.

Aidha, alisema kongamano hilo litakuwa daraja muhimu kati ya vipaumbele vya maendeleo ya taifa na mtaji wa kimataifa unaohitajika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Mataifa Nchini Tanzania (UNDP) Shigeki Komatsubara alisema taasisi hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania katika kukuza maendeleo yanayoendeshwa na uwekezaji.

“UNDP Tanzania ipo tayari kusaidia Tanzania kuwezesha jukwaa linalokidhi viwango vya wawekezaji wa kimataifa,” alisema Komatsubara.

Top News