Na Said Mwishehe,Michuzi Blog

-MAMIA ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)ambao ni

Mabalozi wa mashina kutoka Wilaya za Temeke na Kigamboni jijini Dar es Salaam wamesema wanamatumamaini makubwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk.Asha-RoseMigiro

Wamesema Dk.Migiro ameweka historia ya kuwa Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke ndani ya chama hicho na kwa uwezo wake mkubwa katika siasa na uongozi ni wazi chama hicho kimepata Katibu mkuu sahihi.

Wakizungumza leo Januari 7,2026 katika ukumbi wa PTA uliopo Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam mabalozi hao wa shina ambao wamefika kwa ajili kushiriki kikao kazi kilichoandaliwa na Dk.Migoro wamesema wanaamini kupitia kikao hicho watapata maneno ya faraja kutoka kwake.

Balozi wa Shina kutoka Kibada wilayani Kigamboni Mwakibona Jumanne amesema wanamshukuru Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Dk.Migiro kuwa Katibu Mkuu katibu mkuu wa ccm

Aidha amesema wanashukuru Dk.Migiro kwa ujio wake leo kwani atawaambia neno la faraja wana CCM na Watanzania kwa ujumla.

Aidha amesema anaipongeza Serikali kwa kutuliza nchi na mpaka leo hali ni shwari na amani imetewala.”Ingekuwa nchi nyingine hali isingekuwa kama ilivyo na pengine ingeendelea kuharibika zaidi , hivyo tunaiomba Serikali iendelee kuwa na msimamo huo huo kusimamia amani ya nchi.

“Kwa utulivu na amani ndio tunaweza kufanya maendeleo ya nchi ,kijamii na kuhakikisha tunaendelea kupata maendeleo na Tanzania inasonga mbele.”

Kwa upande wake Asia Sadick ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM kutoka Kijiji  cha Wavuvi Kata ya Mtoni amempongeza Mwenyekiti na Rais Dk.Samia kwa kumteua Dk.Migoro kuwa Katibu Mkuu kwani wanamatumaini na hawana shaka na uwezo wake katika uongozi na katika kikao cha leo wanatarajia kupewa ujumbe uliobeba matumaini kwa Taifa la Tanzania.

Katibu Mkuu Dk.Migoro leo anaanza ziara katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo leo Januari 7,2026 atakuwa na kikao kazi na viongozi mbalimbali wakiwemo mabalozi wa mashina katika Wilaya za Temeke na Kigamboni .Kikao hicho kinafanyika ukumbi wa PTA  uliopo viwanja vya Sabasaba jiijini Dar es Salaam 





 

*Mkurugenzi Mtendaji amshukuru Rais Samia miradi 66 ikitelelezwa

Na Said Mwishehe,Michuzi Blog

HALMASHAURI ya Meru mkoani Arusha imetoa shukrani kwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka miradi mbalimbali ya maendeleo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ambapo Halmashauri hiyo imetekeleza miradi 66.

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari waliotembelea miradi ya TASAF inayotekelezwa kupitia OPEC Fund Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwalimu Zainab Makwiya ametumia nafasi hiyo kuelezea kutekelezwa kwa moradi ya TASAF.

“Nawashukuru timu zima ya TASAF kwa kuendelea kutuamini Meru kwa kutupatia miradi ya maendeleo.Halmashauri yetu imekuwa ılığa ya vizuri katika kutekeleza miradi ya TASAF ikiwemo ya miradi ya OPEC.

“Pia niishukuru Serikali yangu inaongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhika haya yote yanayoendelea ndani ya Meru kwasababu hizi ni fedha zinazokuja kwa ajili ya miradi bila Rais kukubali huenda tusingepokea. Kwahiyo tunamshukuru na tunamuomba aendelee kututafutia zaidi ili tutekeleze miradi.

“Ninafahamu jinsi gani halmashauri zilizovyokuwa zinahangaika kutafuta fedha za miradi ya maendeleo hasa ikifika katika kipindi kama hiki cha watoto kwenda shule kidado cha kwanza , darasa la awali na darasa la kwanza.”

Amefafanua kwasasa mambo yamekuwa tofauti kwasababu fedha za halmashauri na washirika wengine TASAF imekuwa mkombozi mkubwa akitolea mfano katika halmashauri yake wanayo miradi mingi ya madarasa ambayo hapo awali wazazi walitakiwa wachangie au Mkurugenzi na mkuu wa wilaya watafute fedha lakini sasa hivi wanachokifanya ni kusimamia tu miradi ikamilike

“Ukiachana na hiyo watoto wa kike walikuwa wanapata shida hasa wale waliokuwa wanakaa mazingira magumu lakini kupitia TASAF wameweza kujenga mabweni ambayo sasa hawatembei tena umbali mrefu wako mabwenini wanapata huduma zote.

“Tukiachana na mabweni katika sekta ya afya tumejenga jengo la afya afya ya mama na mtoto katika Kituo cha afya Mbuguni na jengo limeanza kutumika.Kwahiyo tunashukuru TASAF kwa miradi ambayo imetuletea,”amesema Mwalimu Makwiya.

Ameongeza pia kupitia TASAF wamepata miradi ya nyumba za walimu ambapo kuna baadhi ya shule walimu walikuwa wanateseka yaani wanagawana vyumba ,mwalimu anakaa kwenye chumba kimoja kama amepanga kwani unakuta nyumba ya vyumba vitatu wanakaa walimu watatu.

“Lakini kwa sasa katika maeneo ambayo TASAF imetupatia mradi wa nyumba za walimu leo hii hata ukienda unafurahi maana walimu wanafanya kazi vizuri.

Aidha amesema Halmashauri ya Wilaya ya Meru kazi kubwa inayofanyika ni kilimo, ufugaji na biashara.”Katika kilimo tumepata miradi ya umwagiliaji ambapo sasa hivi tumeongeza uzalishaji,nikitoa mfano Ngabobo ni kwa wamasai lakini wanalima na wanazalisha nyanya na mbogamboga

“Kwa maana hiyo uzalishaji umeongezeka kwani wanapata fedha kupitia kupitia mifugo lakini pia kupitia kilimo na kwa Ngobobo TASAF kupitia mradi wa OPEC imejenga mifereji ambayo kwasasa maji yanakwenda mashambani na wakati huo huo kwa matumizi mengine ya kijamii.

“Hakika TASAF mmetukomboa ndani ya halmashauri ya Meru lakini sio kutukomboa tu mmeleta utulivu kwa familia kwasababu watu walikuwa wanakimbia majumbani.Tumetekeleza miradi ya TASAF kwa kiwango kikubwa hivyo wakati miradi ya TASAF inafika mwisho sisi tulishakamilisha miradi yote.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru mkoani Arusha Mwalimu Zainab Makwiya (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)pamoja na waandishi wa habari waliokuwa katika ziara ya kutembelea miradi ya OPEC iliyopo katika Wilaya hiyo.



Waziri wa Madini , Anthony Mavunde akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) juu ya ushirikishwaji wa watanzania kwenye sekta ya madini nchini

-Mgodi wa North Mara viongozi wake kwa asilimia 100 ni Watanzania


Waziri wa madini,Mh.Antony Mavunde amesema mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara ambao unaendeshwa na kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals umekuwa kinara katika utekelezaji wa sheria na kanuni ya Maudhui ya Ndani (Local Content) ikiwemo upande wa ajira ambapo asilimia 100 ya viongozi wanaoendesha mgodi ni Watanzania.


Mbali na viongozi wa mgodi huo pia Meneja wa Barrick nchini (Country Manager) ni Mtanzania.


Akiongea na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mkakati wa Serikali wa kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo mzima wa sekta ya madini, Mhe. Mavunde amesema kwenye miradi ya madini, amesema kumeshuhudiwa ongezeko la ajira kwa watanzania kutoka ajira 6,668 kati ya ajira 7,003 sawa na asilimia 95 kwa mwaka 2018 hadi kufikia ajira 18,853 kati ya ajira 19,356 sawa na asilimia 97 kufikia Desemba 2024.


Amesema katika nafasi zinazohitaji kupata uzoefu kutokana na kukua kwa teknolojia duniani, kumekuwa na utaratibu wa kisheria wa urithishwaji wa Watanzania kwa nafasi zinazoshikiliwa na Wataalamu wa Kigeni na kutoa mfano wa kampuni ya Barrick kupitia mgodi wake wa North Mara ambapo nafasi zote za juu za uongozi wanaoendesha shughuli kwa weredi mkubwa zinashikiliwa na Watanzania kwa asilimia 100.


Kupitia mkutano huo Waziri Mavunde pia ametangaza rasmi orodha ya Huduma na Bidhaa 20 zinazopaswa kutolewa Migodini kupitia kampuni zinazomilikiwa na watanzania kwa asilimia 100 ikilenga kuongeza wigo wa ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo mzimawa sekta ya madini baada ya kufanywa marekebisho ya Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania kwenye Sekta ya Madini za Mwaka 2018.


"Kwa awamu ya kwanza tarehe 14 Novemba, 2025 Tume ya Madini ilitangaza orodha ya bidhaa na huduma zinazotakiwa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa na kampuni za kitanzania kwa asilimia 100, ambapo kwa mara ya kwanza Tume ya Madini itatatangaza kupitia Kanuni 13A," amesema Waziri Mavunde.


Akizungumzia manunuzi ya huduma na bidhaa kwa kampuni za kitanzania amesema yameongezeka kutoka kiasi cha Shilingi trilioni 1.85 kati ya manunuzi ya huduma na bidhaa za jumla ya kiasi cha Shilingi trilioni 3.01 sawa na asilimia 62 kwa mwaka 2018 hadi kufikia Shilingi trilioni 4.41 ambayo ni sawa na asilimia 88 ya kiasi cha Shilingi trilioni 5.00 ya manunuzi yote yaliyofanyika mwaka 2024.


Pia amesema Serikali inaendelea kufungua wigo kwa ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini na kuongeza manufaa ya rasilimali madini kwa kutenga eneo maalum la uwekezaji la ulipokuwa Mgodi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu la Barrick Buzwagi lenye ukubwa wa ekari 1331, kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa za migodini na kusema tayari viwanda sita vimekwisha jengwa huku wamiliki wa viwanda 15 wakionesha nia ya kujenga viwanda katika eneo hilo.


Waziri Mavunde ameitaka sekta binafsi nchini Tanzania kuchangamkia fursa ya usambazaji wa bidhaa na utoaji wa huduma migodini ili kuhakikisha fedha kiasi kikubwa inabaki nchini Tanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.


Amewasisitiza wawekezaji wote kuzingatia Sheria za madini na utekelezaji wa Kanuni za Ushirikishwaji Watanzania kwenye sekta ya madini sambambamba na kuwataka watanzania kuchangamkia fursa zilizopo katika miradi ya madini ili kukabiliana na changamoto za ajira kwa manufaa ya mtu mmoja mmoja na manufaa ya taifa.



KAMISHNA wa Kamisheni ya Polisi Jamii, CP Faustine Shilogile, amewasili mkoani Mwanza leo, Januari 07, 2026, kwa ziara ya kikazi ambapo anatarajiwa kufungua mafunzo ya siku moja kwa Maafisa wa Polisi Jamii kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mafunzo hayo yatahusisha washiriki ambao ni maafisa wa Polisi Jamii kutoka Mikoa ya Mara, Tarime, Rorya, Simiyu, Geita, Tabora na Shinyanga.

Lengo kuu la mafunzo haya ni kuimarisha mikakati ya kuzuia uhalifu kabla haujatokea na endapo utatokea, usirudiwe tena, kwa mujibu wa mipango iliyowekwa na wadau husika.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuongeza ufanisi wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha usalama na kuendeleza ushirikiano na jamii katika kudhibiti uhalifu.





Washindi na watumiaji wa My Aitel App wajipatia zawadi zao, pia Airtel kutoa garI aina ya Mazda. Watumiaji wa Mtandao huo waaswa kutumia My Artel App kwaajili ya kujipatia zawadi mbalimbali zinazotolewa msimu huu wa sikukuu.

Kutazama video bonyeza hapa



Na Khadija Kalili ,Kibaha

MKURUGENZI wa Kiduli Security Ally Masimike amesema kuwa "awali ya yote anawapongeza wachezaji kwa kucheza mchezo mzuri na suala la kupoteza ni bahati mbaya hivyo wanakwenda kujipanga kuangalia wapi wamekosea ili watakapokuja kucheza katita fainali wanaimani matokeo yatakua mazuri.

"Leo tumecheza fainali ya kwanza na kupoteza lakini tunayo nafasi katika mechi ijayo tuna chukulia hii ni bahati mbaya tunakwenda kuziba upungufu"amesema Kiduli.

Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano ya Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Nasoro Shomvi 'Mbilinyi' ametoa wito kwa wadau wa michezo Mkoa wa Pwani kujitokeza kwa wingi katika fainali ligi darala la tatu ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza ambapo Bagamoyo Sugar ya Bagamoyo wamertoka kifua mbele kwa Kiduli FC ya Kibaha itakayo chezwa tarehe 12 Januari katika Uwanja wa Mwendapole, Kibaha.

Katika machine iliyochezwa jana tarehe 6 Januari 2026 Bagamoyo Sugar wametoka kifua mbele kwa kuongoza 1-0.

Mbilinyi amesema kuwa Ligi hiyo ilikuwa ni kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20.

"Timu ya Soka ya Bagamoyo ya imeifunga Kiduli Fc ya Kibaha kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa Ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Pwani ikiwa ni fainali ya kwanza" amesema Mbilinyi.

Mchezo huo umechezwa kwenye Uwanja wa Mwendapole Kibaha huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa Januari 12 kwenye Uwanja huo huo ikiwa ni fainali ya pili ili kupata bingwa wa Mkoa.

Bingwa wa LigiMkurugenzi wa Kiduli Security Ally Masimike amesema kuwa "awali ya yote anawapongeza wachezaji kwa kucheza mchezo mzuri na suala la kupoteza ni bahati mbaya hivyo wanakwenda kujipanga kuangalia wapi wamekosea ili watakapokuja kucheza katita fainali wanaimani matokeo yatakua mazuri.

"Leo tumecheza fainali ya kwanza na kupoteza lakini tunayo nafasi katika mechi ijayo tuna chukulia hii ni bahati mbaya tunakwenda kuziba upungufu"amesema Kiduli. hiyo atapata Kombe na atawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa.

"Mwaka huu katika fainali tutatoa Kombe kubwa kwa timu itakayoshinda pia kutakua na Mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Timu ya Baberian " amesema Mbilinyi.
Na Said Mwishehe

MRADI wa mfereji wa maji uliojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF)kupitia mradi wa OPEC katika vijiji vitatu vya Ngabobo, Oltepes na Tank katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha umewezesha wananchi wa vijiji hivyo kujikita katika kilimo cha umwagiliaji na hasa nyanya,vitunguu na mbogamboga.

Mradi huo wa umwagiliaji ulioibuliwa katika Vijiji hovyo vitatu vya Ngabobo, Oltepes na Tank ambapo jumla ya wakazi 4,184 wananufaika na mradi wa mfereji huo wa umwagiliaji.

Akizungumza hivi karibuni kuhusu mradi huo wa mfereji uliojengwa kupitia OPEC ,Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Meru Edwin Serumkuma amesema mfereji huo unahudumia hekta za Kilimo 1310 na zaidi ya wakulima 851 wanatumia mfereji huu katika kilimo cha nyanya, vitunguu na mboga mboga.

Pia amesema unatumika kuzalisha mazao ya chakula kama mahindi na maharage huku akifafanua pia maji ya mfereji huo hutiririka kwa mwaka mzima na bila kupungua ambayo vilevile hutumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za binadamu kama kunyweshea mifugo namajumbani.

Kuhusu utekelezaji wa mradi huo amesema uliibuliwa na wananchi wa Vijiji vya Ngabobo, Tank na Oltepeskatika kupitia mikutano maalum katika vijiji vyote uliyofanyika kati ya Januari 21,2025 mpaka Januari 21,2025.

“Mpaka sasa mradi umekamilika na unatumika.Mradi huu umegharimu Sh.401,785,714.26 hadi kukamilika kwake. Jumla ya miradi 9 kila mmoja ukiwa na thamani ya Tshs. 44,642,857.14 imetekelezwa ambapo kila Kijiji kilitekeleza miradi 3.

“Na kila mradi ulitakiwa kujenga km 0.6 hivyo miradi 9 ilitakiwa kujenga Km 5.4, lakini mradi huu una urefu wa kilometa 7.2 na pia limejengwa daraja kubwa la kuvushia wanyama na wananchi ili kupunguza uharibifu wa mfereji.

“Pia vimejengwa vigawa maji 32 katika mfereji wote. Wakati tunatekeleza mradi huu mwaka 2021/2022 Kijiji cha Ngabobo kilipata mradi wa kujenga mita 350 wakafanikiwa kujenga kilometa moja hivyo ukiunganisha mradi wa 2021/2022 jumla mradi huu utakuwa naurefu wa kilometa 8.2. Nguvu za jamii katika mradi huu ilikua ni wananchi wenyewe kujitoa kama vibarau,”amesema Serumkuma.

Kwa upande wake Diwani Kata ya Ngabobo Gabriel Kinua amesema kabla ya mradi huo kulikuwa na changamoto kubwa kwani walikuwa tunatumia mfereji ambao ulikuwa umetengenezwa na wananchi na ulikuwa haujasakafiwa wala kutengenezwa kwa namna yeyote ile

“Hivyo kabla ya mferej kujengwa tulikuwa na changamoto kubwa ya maji hasa miezi ambayo hakuna mvua,mazao yalikuwa yanakauka na watu walikuwa wanalima kwa kiwango kidogo kwasababu maji hayatoshelezi.

“Mradi huu umekuwa na matokeo makubwa kwani tumepunguza muda maji kufika mashambani maji ,haya maji saa moja na nusu inanyesha kwa wakulima wengi.Pia maji yameongezeka kwani yalikuwa yanapotea njiani kwasababu ya mchanga na udongo kufyonza maji lakini kwa sasa maji yameongezeka na hivyo wananchi wanalima kwa wingi

“Kujengwa kwa mfereji huu pia umefanya sasa mazao yameongezeka na hivyo halmashauri inapata ushuru unatokana na mazao ya mbogamboga,”amesisitiza alipokuwa akielezea faida za mradi wa mfereji huo.





Wakazi wa Majengo na Amani Mbezi kwa Msuguli wakiwa wamepanga foleni kuchota maji kwa mmoja ya mwananchi wa mtaa wa pili.

Dar es Salaam Januari 6, 2025: Wakazi wa mitaa ya Majengo na Amani iliyopo Mbezi kwa Msuguli, wameilalamikia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kwa kile walichokitaja kuwa manyanyaso na uzembe wa muda mrefu katika utoaji wa huduma ya maji, hali iliyosababisha maisha yao kuwa magumu kwa kipindi kirefu.

Wakizungumza katika kikao chao cha Mtaa kilichofanyika hivi karibuni, wakazi hao wamesema wamekuwa hawapati maji kwa muda mrefu licha ya kuwepo kwa ratiba ya mgao wa maji iliyotolewa na DAWASA yenyewe, ratiba ambayo kwao haijawahi kutekelezwa ipasavyo.

Mmoja wa wakazi hao, Mama Rhoda, alisema hali ya upatikanaji wa maji katika Mtaa wa Majengo ni ya kusikitisha huku akishangazwa na ukweli kwamba mitaa ya jirani kama Masaki, Malamba Mawili na Kanisa la Udongo inayohudumiwa na kituo cha Kimara imekuwa ikipata maji kwa uhakika.


“Sisi wakazi wa Majengo tumekuwa tukipata maji kwa shida sana. Tunajiuliza, kwa nini sisi tu? Wenzetu wa Masaki na Kanisa la Udongo wanapata maji, yanatoka wapi? Sisi tunaohudumiwa na Kinyerezi kila siku ni hadithi tu,” alisema Mama Rhoda.

Naye Albert Mwemezi alisema DAWASA Kinyerezi imekuwa ikitoa ahadi hewa kwa kudai maji yatatoka siku za Alhamisi, Jumapili na Jumatatu, lakini hakuna utekelezaji zaidi ya maneno ya “kesho”.


Kwa upande wake, Ngosha Jacob, mteja mkubwa wa DAWASA katika eneo hilo anayefyatua matofali alisema upungufu wa maji umeathiri moja kwa moja shughuli za uzalishaji licha ya wao kulipa bili kwa wakati.

“Huduma ya maji ni muhimu sana kwa shughuli zetu za uzalishaji. Inashangaza tunalipa bili kwa wakati lakini huduma hatupati. Huu ni uzembe mkubwa,” alisema Jacob.

Mkazi mwingine, Abdul Shaban, alisema miezi miwili iliyopita aliwasiliana moja kwa moja na Mkurugenzi Mkuu wa DAWASA ambaye alikiri kupokea malalamiko yao na kuahidi kuyafanyia kazi, hata hivyo juhudi hizo hazikuzaa matunda kwani kero hiyo bado haijapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Licha ya Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kuweka kambi katika eneo la Kinyerezi, wakazi wa Majengo na Amani wamesema wamekaa bila maji kwa zaidi ya miezi mitatu hadi minne, hali inayowaacha katika mateso makubwa.

Mkazi mmoja aliyeomba kutotajwa jina lake alisema maji yamekuwa anasa, na kwa sasa wanalazimika kununua maji kwa mkazi mwenye kisima kwa gharama ya shilingi 500 kwa dumu moja.

Mwandishi wa MMG aliyefika eneo la tukio na kujionea hali halisi ya maisha ya wakazi hao, alijaribu kuwasiliana na uongozi wa DAWASA upande wa Kinyerezi lakini hakupata majibu ya moja kwa moja zaidi ya ahadi za “maji yatatoka kesho”.

Wakazi wamesisitiza kuwa kero yao ya maji ilikuwepo hata kabla ya tangazo la mgao wa maji lililotolewa na Waziri wa Maji, wakitaka DAWASA kutoitumia hoja ya uhaba wa maji kama kisingizio.

Akizungumza kwa niaba ya wakazi, Ayoub Rusungu alisema kuna mitaa ya jirani inayopata maji angalau mara mbili kwa wiki, jambo linaloibua maswali juu ya usawa na haki katika utoaji wa huduma.

“Kwa nini mitaa mingine ipate maji mara kwa mara halafu sisi tusipate hata mara moja kwa wiki? Hapa kuna jambo halipo sawa. Kuna mitaa yenye watu wakubwa wanapata maji, sisi wanyonge tunaachwa bila maji kabisa,” alisema Rusungu.

Wakazi hao wametoa wito kwa DAWASA na Wizara ya Maji kuingilia kati kwa haraka ili kutatua kero hiyo ya muda mrefu, wakisema maji ni huduma ya msingi na haki yao ya msingi kama wananchi.

WAPENZI wa kasino na michezo ya mtandaoni, mara baada ya kutamatika kwa msimu wa Halloween, Meridianbet imeendelea kukupatia burudani isiyo na kifani kupitia Trick or Treat Bonanza, mchezo ambao unachanganya ladha iliyopita ya Halloween na fursa za ushindi wa kweli.

Mchezo huu unakukaribisha kwenye Haunted Candy Realm, ulimwengu wa ajabu uliojaa pipi za kuogofya, vishawishi vya kutisha, na zawadi zisizo na kikomo. Kila mzunguko wa mchezo huu ni safari ya msisimko, na mvuto pamoja na ushindi mkubwa unaokuweka kwenye shauku kubwa aswaa.

Kwa nini Trick or Treat Bonanza ni tofauti na michezo mingine mingi? Hii ni kwa sababu ya kuwa na mizunguko ya bure na michezo ya bonasi isiyo na mwisho. Lakini pia vizidishi vya ushindi vipo hadi mara 21,100 ya dau lako.

Mbali na mchezo huu, pia meridianbet wana kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Na kikubwa zaidi kwenye mchezo huu pendwa wa Trick or Treat Bonanza ni kwamba imewekewa njia nyepesi ya kununua bonasi kwa wale wanaopenda kuingia moja kwa moja kwenye ushindi mkubwa, na kila ukinunua bonasi basi unajiweka kwenye nafasi ya kujipatia zawadi nyingi na kubwa ndani ya mchezo.

Shiriki Trick or Treat Bonanza leo na ujionee utamu wa mchezo huu huku ukijongea kuelekea kwenye historia mpya ya ushindi kutoka meridianbet.


JE unajua kuwa ukibashiri na Meridianbet ni rahisi sana kwako kuondoka na mtanange wa maana?. Timu kibao zipo uwanjani kuhakikisha haubaki patupu leo, hivyo tandika jamvi lako la uhakika hapa.

Ligi kuu ya Uingereza, EPL inatarajiwa kuendelea leo hii ambapo Brentford ataumana dhidi ya Sunderland ambao wapo nafasi ya 8 na mwenyeji wake nafasi ya 7. Wote wana pointi sawa hivyo ushindi ni muhimu kwa kila timu siku ya leo. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii siku ya leo. Tandika jamvi hapa.

Mechi nyingine ni hii Everton vs Wolves ambao wamepata ushindi mmoja tuu kwenye ligi japokuwa bado wapo nafasi ya mwisho hadi sasa. The Toffees wanahitaji ushindi kwenye mechi hii pale nyumbani ili wajiweke sawa kwenye msimamo wa ligi. Mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000. Jisajili hapa.

Pia naye Fulham atamenyana dhidi ya Chelsea ambao wametoka kumfukuza kocha wao hadi sasa, huku pia wakiwa wanajitafuta kubakia nafasi 4 za juu kwenye msimamo wa ligi. Mara ya mwisho kukutana hawa wawili, The Blues waliondoka na ushindi mnono pale kwao. Je ni wakati sahihi wa kulipa kisasi?. Bashiri hapa.

Ushindi upo kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa upande wa Manchester City wao wataumana dhidi ya Brighton ambao wapo nafasi ya 10 kwenye msimamo wa ligi. City wapo kwenye mbio za ubingwa na wanahitaji ushindi huu siku ya leo wajiweke sawa kwenye nafasi 4 za juu. ODDS za kibabe zipo mechi hii. Suka jamvi hapa .

Vilevile ligi kuu ya Italia, SERIE A inatarajiwa kuendelea ambapo Bologna ataumana dhidi ya Atalanta ambao wapo nafasi ya 8 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 7 kwenye msimamo wa ligi. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni pointi moja pekee. Je leo hii nani kuibuka na pointi 3?. Jisajili hapa.

Naye Napoli chini ya kocha mkuu Conte atakuwa nyumbani kusaka ushindi dhidi ya Hellas Verona ambao wapo nafasi ya 3 kutoka mwisho, huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi. Nafasi ya kushinda pale Meridianbet amepewa Naples hivyo ingia na ubeti hapa.

Halikadhalika naye Parma atamleta Inter ambao mpaka sasa ndio vinara wa ligi wakiwa mbele kwa pointi moja chini ya anayemfuata. Mgeni anahitaji ushindi siku ya leo ili azidi kukaa kileleni kwenye msimamo wa ligi na kuchukua taji ambalo msimu uliopita walilikosa. Je nani unampa pesa yako ndogo akutajirishe?. Bashiri hapa.

SUPER CUP, kule Hispania pia inatarajiwa kuendelea ambapo FC Barcelona ataumana dhidi ya Athletic Bilbao ambapo mechi ya mwisho kwenye ligi walipokutana, Barca aliondoka na ushindi mnono kabisa. Je kwenye kombe hili Bilbao anaweza akalipa kisasi?. Tandika jamvi hapa.

 

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timontheo Mnzava, amewataka madiwani na wenyeviti wa vijiji kushirikiana kwa karibu katika kutatua migogoro ya ardhi ili kulifanya jimbo hilo kuwa mfano wa matumizi sahihi ya ardhi na kuimarisha amani kwa wananchi.

Mbunge Mnzava ametoa wito huo wakati akiendelea na ziara zake za kukutana na makundi mbalimbali ya jamii, kwa kushirikiana na viongozi wa Chama pamoja na Halmashauri. Katika kikao maalum alichokaa na madiwani pamoja na wenyeviti wa vijiji, walijadili masuala mbalimbali yenye lengo la kuimarisha utawala bora na maendeleo ya wananchi.

Katika kikao hicho, Mhe. Mnzava aliwapongeza madiwani kwa ushindi wao katika uchaguzi na kuwashukuru wenyeviti wa vijiji kwa kushiriki kikamilifu katika kulinda amani wakati wote wa zoezi la uchaguzi, Alisisitiza kuwa mchango wao ulikuwa mkubwa katika kuhakikisha maeneo yao yanabaki salama na yenye mshikamano.

Aidha, aliwakumbusha viongozi hao majukumu yao ya msingi, hususan kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa vitendo, kwa kuzingatia maslahi ya wananchi waliowachagua.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mnzava alikemea vikali vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya mihuri katika maeneo yao, akisisitiza kuwa vitendo hivyo vinadhoofisha uaminifu wa wananchi kwa viongozi wao na kukwamisha haki. Akihitimisha kikao hicho, aliwataka madiwani na wenyeviti wa vijiji kuwa mstari wa mbele katika kulinda na kuitunza amani iliyopo, akisisitiza kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu ya jimbo na taifa kwa ujumla.

000

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wanaodaiwa kuhusika katika matukio tofauti ya mauaji na ukatili wa kijinsia yaliyotokea katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Mkoa Morogoro imesema kuwa Januari 4, 2026 walimkamata Helakimu Joseph Kacheli (50), mkulima na mkazi wa kijiji cha Sesenga, kwa tuhuma za kumuua mkewe, Sofina Alipisini (27), mkulima na mkazi wa Lumbachini.

Inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi baada ya tukio, mtuhumiwa alijaribu kujidhuru lakini aliokolewa na kwa sasa anaendelea na matibabu chini ya ulinzi wa Polisi.

Katika tukio jingine, Januari 5, 2026, jeshi hilo lilimkamata Justine Bernad Thomas (42), mkazi wa kijiji cha Sogeambele, kwa tuhuma za kumuua Machafu Magembe Masanja (42) kufuatia ugomvi uliotokana na mauzo ya mpunga yaliyofanywa bila ridhaa ya marehemu.

Wakati huohuo, wilayani Kilombero, Jeshi la Polisi lilimkamata Andrew Joseph Katanga (33), mkulima na mkazi wa Katindiuka, kwa tuhuma za kufanya ukatili wa kijinsia dhidi ya mwanae wa kumzaa mwenye umri wa miaka 14. Tukio hilo linadaiwa kutokea Desemba 31, 2025, na uchunguzi bado unaendelea.

Kufuatia na matukio hayo Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limetoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi na badala yake kutoa taarifa mapema kwa vyombo vya usalama ili kusaidia kuzuia matukio ya kihalifu kabla hayajaleta madhara makubwa kwa jamii.

Dar es Salaam

Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari na kuwa makini katika kipindi cha msimu wa mvua ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kujaa kwa maji katika maeneo ya miundombinu ya barabara.

Rai hiyo imetolewa na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff, wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Menejimenti ya Wakala, Mameneja wa Mikoa pamoja na Waratibu wa miradi ya dharura kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Seff amesema ni muhimu wananchi kuzingatia alama zote za usalama barabarani katika matumizi ya barabara na kuepuka kuvuka barabara au madaraja yenye maji mengi.

“Ni vyema wananchi kuchukua tahadhari katika maeneo yao au wanapokuwa safarini, endapo daraja limezidiwa na maji wanapaswa kusubiri hadi yapungue hivyo itakua ni njia bora ya kuepusha ajali na kulinda usalama wa miundombinu nchini,” amesisitiza.

Aidha, amewataka wananchi kutoa taarifa mara moja pale panapotokea uharibifu wa miundombinu ya barabara kwenye ofisi za Wilaya, Mikoa au Makao Makuu ya TARURA, ili kuzuia ajali zinazoweza kujitokeza.

Mhandisi Seff ameongeza kuwa kwa maeneo ambayo barabara au daraja limesombwa na maji, wananchi wanapaswa kuwa makini zaidi ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea.









 


Top News