Na. Mwandishi wetu, Pemba
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Tanzania, Mh. Hamad Hassan Chande (Mb), amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) itaendelea kushirikiana katika kuimarisha na kuendeleza sekta ya utalii ili kuchochea maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla

Mhe. Chande amebainisha hayo wakati wa uzinduzi wa Bonanza la Sita la Utalii wa Michezo na Utamaduni Pemba (Tamasha la Pemba Tourisport & Cultural Bonanza 2026) linalolenga kukifungua Kisiwa cha Pemba kiutalii, kuvutia wawekezaji, watalii wa ndani na nje ya nchi kwa kutangaza vivutio vilivyomo kwenye kisiwa hicho.

“Katika siku hizi nne ambazo tamasha hili linaendelea, ikiwa leo ni siku ya mwanzo naamini, watanzania, wenyeji na wageni watanufaika kuona vivutio mbalimbali ambavyo vitatangazwa na wataalamu wetu na kushawishika katika kuongezeka kwa wageni nje ya nchi, na ambao wamekuja mara moja niwaombe sana waje kwa mara ya pili, ya tatu na ya nne” alisema Mhe. Chande

Mhe. Chande, licha ya kuipongeza Kamisheni ya utalii pia ametoa wito kutangaza mazao mapya ya utalii yaliyopo kwenye Kisiwa hicho kwa ubunifu mkubwa kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza na kuongeza pato la taifa kupitia rasilimali zilizopo kwenye kisiwa hicho badala ya kuwa sehemu tu ya kutembelea

Mhe. Chande ameongeza kuwa, moja ya faida kubwa ya tamasha hilo ni kuwapatia vijana jukwaa la kuonesha uwezo wao katika fani mbalimbali ikiwemo michezo, sanaa na utamaduni ikiwa ni nafasi muhimu kwao katika kujiimarisha, kuingia kwenye masoko ya ajira, ubunifu, na kuonesha biashara zao.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Adil George, amesema kuendelea kufanyika kwa bonanza hilo ni utekelezaji wa maelekezo na shabaha ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ya kuleta mageuzi ya kiuchumi katika Kisiwa cha Pemba kupitia sekta ya utalii, michezo na utamaduni.

Bonanza la Utalii wa Michezo na Utamaduni Pemba linatarajiwa kuendelea kuwa chachu ya kuitangaza Pemba, kuimarisha mshikamano wa jamii na kuongeza mchango wa sekta ya utalii katika uchumi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.


Na Mwandishi Wetu

KANISA la Mlima wa Moto la Mikocheni jijini Dar es Salaam, limezindua kongamano la kuombea nchi amani lijulikanalo kama Anza mwaka na Bwana na miongoni mwa yatakayozungumziwa ni ujasiriamali.

Akizungumza leo Kanisani hapo, Askofu wa Kanisa hilo, Rose Mgeta alisema miongoni mwa yatakayofanyika kwenye kongamano hilo la siku nane ni kuombea nchi amani ili isirudi kwenye machafuko ya Oktoba 229 mwaka jana.

Alisema kwenye kongamano hilo vijana pia watafundishwa masuala ya ujasiriamali na biashara ili waweze kutambua fursa na kuzitumia kuondokana na umaskini.

Alisema vijana watakaohudhuria kongamano hilo mbali na neno la Mungu watafundishwa mbinu mbalimbali za kufafuta fedha kama ujasiriamali na namna ya kutumia fursa mbalimbali za kibiashara zilizopo.

Askofu Mgetta alisema maadili kwa sasa yanakwenda kombo hivyo kwenye kongamano hilo watafundisha pia vijana kuzingatia maadili ikiwemo kuheshimu wazazi na watu wanaowazunguka.

“Vijana waishi maisha ya heshima kwa wazazi na watu wanaowazunguka ili wapate heri duniani, kuheshimu wazazi ni Baraka kwa hiyo tutawakumbusha vijana umuhimu wa kuwakumbuka na kuwasaidia vijana,” alisema

Akitoa shukrani zake kwa kufanikiwa kupata ubunge, Mbunge wa Mlimba (CCM), Dk Hellen-Rose Rwakatare aliwataka waumini hao kuomba na kujituma ili waweze kufanikiwa.

“Maandiko matakatifu yanasema usiposhukuru kwa kidogo hutapewa hata hicho kikubwa, nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuibuka na ushindi mkubwa kuanzia kwenye kura za maoni hadi Uchaguzi Mkuu, mnafahamu Mungu amenitendea mengi sana ndani ya miaka miwili,” alisema

“Tulianza mchakato pamoja hapa, tuliomba tukapita kura za maoni, nikaja kuomba tena, nikaenda kwenye uchaguzi mkuu, mungu akanisaidia tena, nilishinda kwa kura nyingi sana kwenye lile jimbo haijawahi kutokea, nilishinda kwa asilimia 95.9,’ alisema

“Namshukuru sana Askofu Rose Mgeta, Askofu Dunstan Maboya kama mnakumbuka aliniombea akaniwekea mikono kichwani akasema Baraka za mama ziko juu yangu, kwa hiyo nawashauri muishi kwa kutenda mema kwasababu mema yataambana na nyinyi,” alisema

“Mama yangu alipanda mbegu, alitenda mema sana kiasi kwamba sisi watoto wake kila tunakopita tunafunguliwa milango, kama unanafasi ya kutenda jema tenda usingoje shukrani hata adui yako mtendee mema, msikimbie kimbie kubadilisha makanisa ombeni mkiwa hapahapa Mungu ni huyu huyu,” alisema

“Ombeni kwa kufuata fomyula msiombe mkiwa mmekaa tu bila kufanyakazi, lile ombi unaloomba simama ukalifanyie kazi, mfano unaomba kazi unakaa nyumbani, hiyo kazi itakukuta nyumbani? Unaomba kuongezewa cheo lakini hufanyi kazi kwa bidii cheo huwezi kupata,” alisema

“Msichana unaomba upate mchumba basi jitahidi upendeze, na mvulana unataka mchumba basi jitahidi uwe na tabia njema ili uweze kujibiwa ombi lako usika kae tu,’ alisema.

“Mungu anasema nitabariki kazi ya mikono yako lakini huwezi kubarikiwa ukiwa umekaa nyumbani, lazima msimame mfanye kazi kwa bidii kwa hiyo lazima msimame kwa dhati na msimame kwa nguvu kuomba” alisema

“Mama yangu hakuwa anapenda umaskini na wengi humu mmeombewa hapa hapa na mmeondokana na umaskini kwa hiyo mnaona hakuna lisilowezekana chini ya madhabahu huu,” alisema












BALOZI wa Shina Namba 8 la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kiburugwa Salumu Abdallah, yuko hoi kitandani kwa mwaka mmoja sasa baada ya nyumba yake kusombwa na mafuriko ya Mfereji wa Shego, ulipo katika kata hiyo wilayani Temeke, mkoani Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Temeke, Hamis Slim, akiongozana na Diwani wa kata hiyo, Rashid Chaburuma pamoja naq viongozi wa Chama, walifika nyumbani kwa Salumu kumjulia hali ambapo ameeleza bado anasumbuliwa na maradhi tangu nyumba yake iliposombwa na maji na kuomba jitihada za kutatua kero hiyo zifanyike.

Slim, alimhakikishia balozi huyo kuwa dhamira kubwa ya kufika katika eneo hilo la Mfereji wa Shego ni baada ya kupokea malalamiko mengi ya wanachama wa CCM, jumuia ya wazazi na wananchi kuhusu adha wanayoipata hasa kipindi cha mvua kutokana na mfereji huo kwa miaka mingi sasa.

“Tumefika hapa kukupa pole kwa sababu ulikuwa mstari wa mbele kueleza kuhusu changamoto ya mfereji huu. Chanzo cha maradhi yako ni baada ya kupata adha ya mafuriko na miongoni mwa nyumba zilizo sombwa ni nyumba yako. Tunakupa pole na tutaendelea kupambana kuhakikisha serikali yetu sikivu tunaishauri kumalizia sehemu ya iliyobaki ya ujenzi wa mradi huo,”amesema Slimu.

Ameeleza awali mfereji huo ulianza kutengenezwa katika Kata ya Charambe na kuishia katika Kata ya Kiburugwa lakini haukumaliziwa hadi Kata ya Mbagala ambapo unaishia Mto Mzinga.

Slimu amesema mvua kubwa iliyoinyesha mwaka jana na mwaka juzi ilisababisha mafuriko yaliyoondoka na nyumba nyingi za wakati wa eneo hilo.

“Ninaamini serikali ya CCM< chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ipo katika utaratibu wa kuboresha mazingira hususan miundombinu. Wananchi wawe watulivu kwa sababu Rais anaendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi yake aliyoitoa ndani ya siku 100,”amesema Slim.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Kiburugwa, Rashid Chabruma, amesema serikali imejipanga kuendeleza ujenzi na ujenzi wa mfereji huo hadi kwa Manganya ambapo jitihada kubwa zimekuwa zikifanywa na Mbunge wa Mbagala Bruchad Kakulu .

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kingugi, Kata ya Kiburugwa, Athumani Magenge, ameeleza Mfereji wa Shego umekuwa adha kubwa kwa wananchi wa Mitaa ya Kingugi, Kwa nyoka na Magenge.

“Eneo hili limeaghiri zaidi ya kaya 300. Wengi walihifadhiwa katika ofisi zetu kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya mvua kubwa kunyesha mwaka jana na mwaka juzi. Zimebaki kilometa tano tu kumalizia ujenzi wa mfereji huyo. Mfereji huu unaendelea kutanuka na kuathiriwa,”amesema.

Ameiomba serikali kuwafikiria wananchi wa Kiburugwa kujenga mfereji huo ili kunusuru wananchi na kuondokana na adha kubwa wanayoipata mvua inapo nyesha.






Na WAF, Dar es Salaam

Serikali ya Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni Nne (4) kwa ajili ya matibabu ya upasuaji wa Mabusha nchini ambapo wananchi wanapata huduma hiyo bila malipo. 

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amesema hayo leo Januari 25, 2026 alipofanya ziara kwenye kambi ya upasuaji Mabusha katika Kituo cha Afya Kilakala, Temeke Jijini Dar es Salaam zoezi linaloendelea kwa wiki tatu sasa.

"Serikali imegharamia zaidi ya Shilingi Bilioni Nne katika huduma hii ambapo Upasuaji huu unafanyika kwa kitaalamu, mgonjwa anapewa dawa za usingizi tu sehemu ambayo anafanyiwa upasuaji na ufahamu wake unakuwa upo kama kawaida na," amesema

Aidha, Dkt. Magembe amesema kuwa tangu kuanza kwa kambi za upasuaji wa mabusha katika Mkoa wa Dar es Salaam, zaidi ya watu 1,300 wamejitokeza kupatiwa huduma. Kati yao, watu 668 walithibitika kuwa na mabusha, na watu 457 wamefanyiwa upasuaji, huku lengo likiwa kuwafikia watu 500 katika vituo vya afya vya Kilakala na Kinondoni.

"Ili kujikinga na magonjwa haya ni muhimu kuzingatia usafi wa mazingira ikiwemo kufukia madimbwi ya maji, kufyeka nyasi katika maeneo yanayotuzunguka ili kuzuia mazalia ya Mbu," amesema

Pia, Dkt. Magembe ametumia fursa hiyo kuwaasa wananchi juu ya umuhimu wa Mfuko wa Bima ya Afya kwa wote kufuatia utekelezaji wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100.

Kwa upande wake Mganga Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Mohammed Mang'una amewataka  wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata huduma hizo kwa kuwa zinatolewa bila malipo ambapo Takwimu zinaonesha kuwa wanaojitokeza zaidi ni wenye umri zaidi ya miaka 45. 

Kambi hiyo inafanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo pia itaendelea katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Morogoro pamoja na Mbeya.





Na Karama Kenyunko, Michuzi TV

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imejipanga kuanzisha bonanza la michezo litakalofanyika kila robo mwaka kwa watumishi wake nchi nzima, ikiwa ni mkakati wa kuimarisha afya ya mwili na akili pamoja na kuongeza ari na mshikamano kazini.

Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, amesema leo Januari 25, 2026, katika viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam, wakati wa bonanza la michezo litakalotumika pia kama jukwaa la kuhamasisha ulipaji kodi na kulinda jamii.

Amesema bonanza hilo linalenga kuwashirikisha watumishi wote wa TRA ili kujenga umoja, afya njema na ari ya kazi, huku akibainisha kuwa litakuwa likifanyika kila robo mwaka katika vituo vyao nchini.

“Hii natamani ifanyike kwa watumishi wote wa TRA. Nadhani tuanze kufanya bonanza kila robo mwaka kwa nchi nzima, tukiwa na maudhui ya kuhamasisha walipaji kodi na kulinda jamii,” alisema Mwenda.

Kamishna Mwenda ameongeza kuwa bonanza hilo limefanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Forodha Duniani, ambayo kilele chake ni leo, ikiwa ni sehemu ya kuthamini kazi kubwa inayofanywa na mawakala wa forodha ya kulinda nchi kupitia mipaka yake.

Bonanza hilo limehusisha michezo mbalimbali ya burudani na ushindani, ukiwemo mchezo wa mpira wa miguu ambapo timu ya maofisa wa TRA iliibuka washindi kwa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya timu ya mawakala wa forodha, katika mchezo uliovuta hisia za watazamaji.

Mbali na mpira wa miguu, michezo mingine iliyochezwa ni pamoja na kuvuta kamba, kukimbiza kuku pamoja na michezo ya karata, hali iliyoleta burudani na kuimarisha mshikamano miongoni mwa washiriki.

Kamishna Mwenda amesema amefurahishwa na mwitikio wa watumishi na ubora wa michezo iliyochezwa, akisisitiza kuwa michezo ni chachu ya afya bora, umoja na utendaji kazi wenye tija.








Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Kinyasi Millya (Mb.) ametembelea Kituo cha Utoaji Huduma kwa Pamoja Mpakani ( One Stop Boarder Post-OSBP ) cha Namanga kilichopo mkoani Arusha Januari 24,2026.

Akitembelea kituoni hapo, Mhe Millya alipokelewa na Meneja wa Mamlaka ya Mapato mkoa wa Arusha Bw. Deogratius Shuma na wawakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Longido na watumishi wa  taasisi 18 za Serikali zinazotoa huduma katima kituo hicho.

Mhe Waziri Milya pia alikutana na viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara mpakani ikiwemo TAFFA, CHAWAMATA, TCCIA,na Wanawake Wajasiliamali Mpakani.

Ziara hiyo ililenga kujionea hali halisi ya utendaji kazi wa Kituo cha Namanga kwa upande wa Tanzania, kukagua miundombinu ya Kituo na utoaji wa huduma hususan katika uendeshaji wa shughuli za pamoja za Forodha katika mwamvuli wa Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza na wadau kituoni hapo Mhe. Millya amesema mpaka wa Namanga ni moja kati ya vituo vikubwa na kitovu cha kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya kutokana na usafirishaji wa bidhaa za viwandani, mazao ya kilimo, huduma za utalii na muingiliano wa wananchi ki fursa kati ya nchi mbili.

Katika mazungumzo na  wadau, Mhe Millya amepokea changamoto zinazokabili ufanisi wa Kituo cha Namanga, aidha wadau wameishukuru Serikali kwa kutembelea kituo hicho na kuonesha imani kubwa katika kutatua changamoto mbalimbali zilizopo na kuboresha miundombinu ili kuleta tija na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya.



















Top News