Na Farida Mangube Morogoro

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda, amewataka wananchi walio karibu na vyanzo vya Maji kulinda vyanzo hivyo pamoja na miundombinu ya huduma hiyo.

Ametoa wito wakati akizindua mradi wa maji wa uhifadhi wa chanzo Cha mto Ruvu kupitia ujenzi wa miondombinu ya usambazaji Maji wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unaotarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa vijiji vya Dakawa na Mngazi Halmashauri ya Morogoro.

Amesema Serikali imeendelea kuwekeza fedha nyingi katika sekta ya maji kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi, hivyo ni wajibu wa jamii kuhakikisha miundombinu hiyo inalindwa na kutunzwa ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu.

Mradi huo wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unahusisha uchimbaji wa visima viwili vyenye uwezo wa kuzalisha lita 248,000 za maji kwa saa, ujenzi wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 26, vituo 34 vya kuchotea maji pamoja na matenki mawili yenye uwezo wa kuhifadhi lita 160,000 za maji.

Aidha, mradi huo umejumuisha uwekaji wa pampu za kusukuma maji zenye uwezo wa lita 30,000 kwa saa katika Kijiji cha Mngazi na lita 50,000 kwa saa katika Kijiji cha Dakawa, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kwa uhakika.

Katika kuimarisha matumizi bora ya rasilimali za maji, mradi huo pia umejenga birika la kunyweshea mifugo katika Kitongoji cha Lukenze, Kijiji cha Dakawa, ambalo linatarajiwa kusaidia kupunguza migogoro ya matumizi ya maji kati ya wakulima na wafugaji.

Kwa sasa mradi huo unawanufaisha wananchi 6,453 wa vijiji vya Dakawa na Mngazi, huku idadi ya wanufaika ikitarajiwa kuongezeka na kufikia watu 11,550 ifikapo mwaka 2043.

Mwang’onda alieleza kuridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kushiriki katika uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Baadhi ya wakazi wa vijiji vya Mngazi na Dakawa, akiwemo Kibua Haji na Maua Bunga, walieleza kufurahishwa na utekelezaji wa mradi huo wakisema umesaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa maji iliyokuwa ikiwalazimu kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi na salama.

Wananchi hao waliipongeza Serikali kupitia Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huo na kuomba huduma hiyo kuendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi katika maeneo mengine ya wilaya hiyo.






Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdalla Hamid, ameendelea na ziara yake ya kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Mtwara.

Akiwa katika shughuli za ubanguaji korosho, Ndugu Rabia amesema CCM itaendelea kusimamia na kulinda maslahi ya wakulima wa korosho, akibainisha kuwa zao hilo lina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi na Taifa.

Aidha, ameelekeza kuchimbwa kwa kisima cha maji katika eneo la Mtwanya Juu ili kusaidia shughuli za Kiwanda cha Ubanguaji Korosho.

“Serikali ya CCM haitorudi nyuma katika kulinda maslahi ya mkulima wa korosho. Mkulima anapostawi, Taifa linastawi. Tuendelee kuzalisha kwa wingi na kwa ubora zaidi ili kuongeza tija na manufaa kwa wakulima,” amesema Rabia.











The Office of Former President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr Jakaya Mrisho Kikwete, categorically refutes the false and misleading report currently circulating online, claiming that Dr Kikwete is associated with an alleged investment programme promising Tanzanians guaranteed income through an AI-powered financial platform.

The report claims that thousands of Tanzanians have already benefited from the programme after investing TSh 653,000, with promises of earning more than TSh 9,200,000 per month. These claims are entirely false.

The Office of the Former President wishes to make it absolutely clear that H.E. Dr Jakaya Mrisho Kikwete has never been involved in, endorsed, promoted, or supported any such financial scheme. His office has not authorised the use of his name, image, or reputation in connection with this alleged programme, and it will not engage in such activities.

Members of the public are strongly advised to ignore this false report and to exercise great caution against such fraudulent and illegal schemes. Anyone who comes across similar misleading information should treat it as fake news and avoid sharing, registering, or sending money to any person or platform linked to it.



Mwandishi Wetu, Ngorongoro
SERIKALI itaendelea kuongeza nguvu katika uhifadhi wa wanyamapori aina ya Faru ambao wapo haratini kutoweka kwa kuimarisha Mradi wa Kimkakati wa Uhifadhi wa Faru weupe ili kuongeza chachu ya ongezeko la uhifadhi na utafiti wa wanyamapori waliopo nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hasaan Chande wakati wa hafla maalumu ya kuwaachilia huru Faru weupe 17 waliopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ikiwa ni mradi maalumu uliofadhiliwa kupitia Shirika la Andbeyond kwa ushirikiano na Serikali ya Afrika Kusini

“Kwa kweli mmebuni kitu kizuri ambacho kinaleta tija na ufanisi na kuleta lmaendeleo kwa nchi yoyote, lengo kuu ikiwa ni kuongeza utafiti, uhifadhi na kupata elimu.

"Wako wengi Duniani watakuja kujifunza kupitia Faru hawa weile wakiwa ama ni wanafunzi, au wakufunzi," alisema Mhe. Chande.

Amempongeza na Kumshukuru Mhifadhi namba moja nchini katika uhifadhi na muongoza watalii, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utayari na utashi wake katika uhifadhi huku akiishukuru pia Serikali ya Afrika Kusini kwa ushirikiano mzuri na Tanzania kwa ufadhili wa Faru hao.

Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Alexander Lobora amesema hatua ya kuwaachia huru Faru hao kutoka kwenye uzio imesaidia katika kuongeza wigo wa kupata eneo kubwa zaidi la kujitafutia malisho huku wakihakikishiwa ulinzi kutokana na miundombinu ya ufuatiliaji wa wanyama ndani ya hifadhi

“Kwa niaba ya Sekta ya Utalii kwa ujumla serikali ipo tayari kupokea Faru zaidi kwa awamu ya pili kwa sababu tayari tumejifunza mengi kwa awamu ya kwanza na lengo la Faru hawa kubwa ni uhifadhi kama tulivyosaini Mikataba ya Kimataifa kama nchi kuhusu wanyamapori ambao wapo hatarini kutoweka,” alisema Dkt. Lobora.

Kwa upande wake Kamishina wa Uhifadhi wa Mamalaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw.. Abdul-Razaq Badru amesema, NCAA itaendelea kuimarisha ulinzi mkali kwa kutumia mitambo ya kisasa katika kuwalinda na kuwahifadhi wanyama hao walio hatarini kutoweka kwa ajili ya manufaa ya Taifa na kuongeza mwitikio wa uhifadhi na utafiti kwa kizazi hiki na kijacho.

Naye Mtendaji Mkuu wa Shirika la Anbeyond Bw. Mussa Mathayo amesema awali ulifanya utafiti wa eneo la kuishi Faru hao ili kuwa na afya njema na kujitafutia malisho na kubainisha kuwa shirika hilo lipo tayari kuongeza idadi ya Faru waliosalia ili kufikisha Faru 36 kama ilivyokuwa kwenye mkataba.







Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Energies Tanzania imezindua kituo kipya cha mafuta eneo la Wazo jijini Dar es Salaam huku mkakati wake wake ukiwa ni kuendelea kusogeza huduma za nishati za mafuta na gesi karibu na wananchi.

Akizungumza leo Juni 15,2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kituo hicho,Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Energies Tanzania Iman Mtafya amesema mazingira bora ya uwekezaji yanayofanywa na Serikali katika sekta ya nishati ya mafuta na gesi imewezesha Oryx kuendelea kusogeza upatikanaji wa nishati hizo.

“Oryx ndio tunaongoza kwenye mtandao wa vituo vya mafuta na usambazaji wa gesi na tutaendelea kuiunga mkono serikali katika kuhamasisha matumizi ya nishati na uzinduzi  wa kituo hiki ni mkakati wetu wa kuendelea kusogeza huduma zetu.

“Kwahiyo tunaendelea kuwekeza maeneo mbalimbali na tumeanza hapa Wazo na hivi karibuni tutafungua kituo kingine Dodoma ambacho kitakuwa umbali wa kilometa 40 kutoka Dodoma Mjini.Lengo ni kuonesha kama kampuni tunaendelea kuwafikia wateja kokote walipo, hata vijijini.”

Akieleza zaidi kampuni ya Oryx inajali usalama na katika kituo hicho wametumia teknolojia ya juu  huku akisisitiza pia wanazingatia ubora wa bidhaa zao na Oryx ndio kampuni pekee yenye maabara ya kupima ubora wa bidhaa zao ili kuhakikishia wateja wanapoweka mafuta katika vyombo vya moto yanakuwa yamezingatia ubora.

Mtafya amesema pia kama Serikali inavyoendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji ndio maana unaona na wao wanaendelea kukua kwa panua huduma na sio Dar es Salaam tu bali na mikoani. 

“Mazingira yaliyowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Nishati wawekezaji tunapata msaada mkubwa wa kupanua wigo wa kusogeza huduma karibu na wananchi, katika sekta ya nishati tunaona Waziri wa Nishati anavyoendelea kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya nishati .

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa CDT Oil na CDT Energies Boniphace Nasibu ambaye ndio msimamizi wa kituo hicho katika biashara ya mafuta,vilainishi pamoja na gesi amesema wameangalia jamii inayozunguka eneo hilo na kuona kuna kila sababu ya kusogeza huduma.

“Kituo chetu kipo karibu Madale ambako kuna mashamba ya jeshi,kiwanda cha saruji cha Wazo pamoja na watu wa eneo la Wazo na kwa ujumla tumejiridhisha hapa ni sehemu sahihi ya kuwahakikishia wananchi kupata mafuta na gesi ya kupikia.”

Amewahakikishia wateja wao watapata huduma zote zinazostahili ili wafurahie huduma za Oryx zinazopatikana huku akiishukuru oryx kwa kufanikisha uwepo wa kituo hicho.

Wakati huo huo akizungumza kwa niaba ya wananchi wa eneo la Wazo Sheikh Amani Hamis amesema kufunguliwa kwa kituo hicho mbali ya kusogeza huduma za nishati ya mafuta pamoja na gesi pia imewezesha vijana wa eneo hilo kupata ajira kupitia kituo hicho.

Amesema pia anaishukuru Serikali kwa kutoa fursa kwa wawekezaji kuja kuwekeza nchini na hivyo wawekezaji hao kuwezesha wananchi wa Watanzania kunufaika na uwekezaji huo.


Balozi wa Tanzania nchini China, Dkt. Suleiman Haji Suleiman, ameendelea na ziara yake inayolenga kukutana na wakuu wa vyuo vikuu mbalimbali nchini China ikiwemo Chuo cha Hong Kong Polytechnic University (HKPU) ambapo amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa chuo hicho, Prof Daniel Shek.

Aidha, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa shule za Biashara, Sayansi na Uhandisi na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa kitaaluma kati ya Chuo cha Hong kong polytechnic na Chuo Kikuu cha Sayansi cha Nelson Mandela (NM-AIST) cha jijini Arusha nchini Tanzania.

Balozi Dkt. Haji amesema kupitia ushirikiano huo, HKPU imeonesha utayari wa kusaidia wanafunzi wa Tanzania kupata maarifa na uzoefu wa kimataifa katika maeneo ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), Sayansi, Utafiti, Teknolojia na Uhandisi ambayo ndiyo nguzo muhimu za maendeleo katika dunia ya sasa pamoja na kutoa mafunzo kwa vitendo (Internship) kwa kipindi cha miezi sita hadi mwaka mmoja.

"Pamoja na mambo mengine, ushirikiano huu wa Tanzania na China katika Sekta ya Elimu, utahusisha programu maalumu za kukuza vipaji vya wanafunzi katika nyanja za Sayansi na Teknolojia, Uhandisi na Hisabati, hatua ambayo itasaidia kuandaa kizazi chenye uwezo wa kushindana katika uchumi wa maarifa na ajira za kimataifa," amesema.








Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Serikali imeagiza Jeshi la Polisi pamoja na Madawati ya Jinsia nchini kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria, ikiwa ni pamoja na ushoga, ukahaba na uendeshaji wa madanguro.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, alipokuwa akizungumza Bungeni, ambapo amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16, inayobainisha makosa mbalimbali ya jinai yanayohusiana na makosa ya kijinsia na uendeshaji wa biashara haramu za ngono.

Amesema vifungu vya 139 hadi 147 vya sheria hiyo vinaeleza wazi makosa yanayohusiana na vitendo hivyo, na kwamba mamlaka husika zitaendelea kuchukua hatua mara pale ushahidi wa kutosha utakapopatikana.

Aidha, Waziri Katambi ametoa onyo kwa watu wanaojihusisha na uendeshaji wa madanguro na shughuli za ukahaba, akibainisha kuwa sheria inakataza kumiliki au kunufaika na mapato yatokanayo na biashara hiyo pamoja na kushiriki kwa namna yoyote ile.

Kwa upande wake, Mbunge wa Katavi, Thomas Maganga, alihoji kauli ya Serikali kuhusu kuongezeka kwa matukio ya vitendo vya ushoga katika baadhi ya maeneo ya makazi, akidai kuwa hali hiyo imeanza kujitokeza katika baadhi ya kata na mitaa licha ya uwepo wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, alieleza kuwa vitendo vya ushoga ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za Tanzania, na wahusika wanapaswa kuchukuliwa hatua stahiki za kisheria.

Amesema mchakato wa kushughulikia makosa hayo unahusisha uthibitishaji wa tuhuma, uchunguzi wa kina, upelelezi wa kina wa vyombo vya dola, na hatimaye kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa taratibu za sheria.

KATAMBI amesitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa wahalifu wote wanaobainika kutenda makosa ya jinai wanachukuliwa hatua sawa na wengine wote bila upendeleo, kwa mujibu wa sheria za nchi.


Na Janeth Raphael MichuziTv- Bungeni Dodoma

Serikali ya Tanzania imeeleza mkakati wake wa kuendeleza na kutenga Maeneo Maalum ya Uwekezaji (Special Economic Zones – SEZs) kwa lengo la kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, kupitia uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji na miundombinu wezeshi.

Hayo yameelezwa Bungeni na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt.Pius Chaya

alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Itigi, Yohana Stephen Msita, aliyehoji kuhusu hatua za Serikali katika kutenga ardhi na kulipa fidia kwa ajili ya maeneo hayo ya uwekezaji.

Dkt. Chaya amebainisha kuwa Serikali, kupitia Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), inaendelea kutekeleza mkakati wa kitaifa wa kutambua, kutenga na kuendeleza maeneo ya kimkakati ya uwekezaji kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za Serikali.

Taasisi hizo ni pamoja na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Msajili wa Hazina. Ushirikiano huo unalenga kuhakikisha ardhi inapatikana kwa wakati, fidia inalipwa ipasavyo, na maeneo yanakuwa tayari kwa matumizi ya uwekezaji.

Mkakati huo unahusisha hatua muhimu zikiwemo utambuzi wa maeneo yenye fursa za kimkakati, uandaaji wa mipango kabambe ya matumizi ya ardhi, kufanya upembuzi yakinifu (feasibility studies), pamoja na kushirikisha sekta binafsi katika uendelezaji wa maeneo hayo kwa kujenga miundombinu muhimu kama barabara, maji na umeme.

Kwa mujibu wa Serikali, hadi kufikia Mei 2026, jumla ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi 34 yamekwisha tangazwa katika maeneo mbalimbali nchini. Kati ya hayo, maeneo 16 yako chini ya usimamizi wa TISEZA, 12 yanamilikiwa na sekta binafsi, 4 yanasimamiwa na Halmashauri za Serikali za Mitaa (LGAs), na 2 yanamilikiwa na taasisi za umma.

Serikali pia imeeleza kuwa inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha maeneo hayo yanaendelezwa na kuvutia wawekezaji, ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na ajira nchini.

Aidha, imezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinayalinda maeneo yote yaliyotengwa kwa uwekezaji—ikiwemo yale yaliyolipiwa fidia na yale yanayosubiri malipo—ili kuzuia uvamizi na kupunguza migogoro ya ardhi.

Serikali imesisitiza kuwa ulinzi na usimamizi madhubuti wa maeneo hayo ni msingi muhimu wa mafanikio ya mkakati wa Maeneo Maalum ya Uwekezaji nchini.


Na Janeth Raphael MichuziTv

Serikali imesema itaendelea kuboresha mfumo wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kupitia halmashauri ili kuondoa changamoto za kisheria na kiutendaji zinazowakabili wananchi wanaonufaika na mikopo hiyo.

Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt. festo Ndugange wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas, aliyetaka kujua kama Serikali iko tayari kutoa waraka maalumu wa kurahisisha utoaji wa mikopo kwa wananchi kutokana na changamoto zilizopo.

Dkt Ndugange amesema Serikali imeendelea kusimamia utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri, kwa kuzingatia Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura ya 290 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2024.

Ameeleza kuwa kanuni hizo zimeweka bayana taratibu zote za usimamizi, utoaji, ukopaji na urejeshaji wa mikopo hiyo, jambo ambalo limeongeza uwazi na ufanisi katika utekelezaji wake.

Aidha, Dkt Ndugange amesema mwaka 2025 Serikali ilitoa mwongozo maalumu wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi wa vikundi vinavyonufaika na mikopo hiyo.

Kwa mujibu wa mwongozo huo, majukumu ya kamati mbalimbali zinazoshughulikia mikopo katika ngazi za mikoa na serikali za mitaa yameainishwa wazi, ikiwemo jukumu la kuhakikisha maombi ya mikopo yanachakatwa kwa wakati na walengwa wanapata huduma kwa haraka zaidi.

Katika hatua nyingine ya kuboresha huduma, Serikali imeanzisha mfumo wa kielektroniki wa WEZESHA Portal unaolenga kurahisisha usimamizi na utoaji wa mikopo hiyo pamoja na kuongeza uwazi katika mchakato mzima.

Dkt. Ndugange amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau mbalimbali ili kufanya maboresho zaidi yatakayorahisisha upatikanaji wa mikopo na kuongeza tija kwa makundi maalumu yanayolengwa.

Hatua hizo zinatarajiwa kuongeza ufanisi wa utoaji wa mikopo, kupunguza urasimu na kuwezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotolewa kupitia mikopo ya asilimia 10 ya halmashauri.



MERIDIANBET inaendelea kuwa karibu na wachezaji wake kwa kukuletea mchezo mpya wa kusisimua wa Skyward Deluxe. Jiandae kwa mwezi mzima wa burudani, ushindi na zawadi zinazoshuka kila wakati. Huu ni muda wako wa kucheza, kushinda na kufurahia kila mzunguko kwa kiwango cha juu.

Kupitia promosheni ya Warm-Up na mashindano ya dunia, wachezaji wana nafasi ya kujinyakulia beti za bure kupitia Sky Drops zinazotolewa kila saa. Kila unapocheza, nafasi ya kupata zawadi inaongezeka na kufanya kila dakika kuwa ya thamani zaidi.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Msisimko unaendelea kabla ya mechi kupitia Build-Up Drops, ambapo zawadi maalum hutolewa kwa wachezaji wanaoshiriki mapema. Hii ni fursa ya kuongeza ushindi wako kabla hata ya mpira kuanza kuchezwa.

Mbali na hilo, kuna msimamo wa siku, wiki na mwezi unaokupa nafasi ya kupanda viwango na kushindana na wachezaji wengine. Kadri unavyocheza ndivyo nafasi yako ya kufika kileleni na kujinyakulia zawadi zaidi inavyoongezeka.

Zawadi zote hutolewa moja kwa moja kama beti za bure katika thamani ya pesa kulingana na mchezo wako. Cheza Skyward Deluxe leo ndani ya Meridianbet, chukua ushindi wako na panda kwenye uongozi kila siku.




MCHEZO kati ya Ivory Coast na Ecuador utakaopigwa leo Juni 15 saa 02:00 usiku unatarajiwa kuwa mmoja wa mechi muhimu zaidi za ufunguzi katika Kundi E. Timu zote mbili zinaingia zikiwa na matumaini makubwa ya kufuzu hatua ya mtoano, jambo linalofanya pambano hili kuwa la ushindani mkubwa tangu dakika ya kwanza.

Ecuador inaonekana kuwa na rekodi bora ya hivi karibuni kutokana na uimara wao wa kujilinda, huku Ivory Coast ikijivunia kasi na nguvu ya safu yao ya ushambuliaji. Ivory Coast wanawasili kwenye mchezo huu wakiwa na morali kubwa baada ya kuifunga Ufaransa mabao 2-1 katika mchezo wa maandalizi ya michuano hii mikubwa.

Kikosi cha kocha Emerse Faé kina nyota kama Amad Diallo, Franck Kessié, Ibrahim Sangaré na Ousmane Diomandé ambao wamekuwa uti wa mgongo wa timu hiyo. Ushindi dhidi ya Ufaransa umeonyesha kuwa mabingwa hao wa Afrika wana uwezo wa kushindana na timu kubwa duniani na wanaweza kuleta hatari kubwa kupitia mashambulizi ya kushtukiza.

Kwa upande wa Ecuador, nguvu yao kubwa ipo kwenye safu ya ulinzi. Wakiwa na wachezaji kama Moisés Caicedo, Willian Pacho, Piero Hincapié na Pervis Estupiñán, wamejijengea sifa ya kuwa miongoni mwa timu ngumu zaidi kufungwa mabao. Takwimu zinaonyesha waliruhusu mabao machache sana katika mechi za kufuzu kwenye michuano hii na wameingia mashindanoni wakiwa hawajapoteza kwa muda mrefu. Hata hivyo, changamoto yao kubwa imekuwa ukosefu wa mabao mengi licha ya kuwa na nahodha na mfungaji wao tegemeo Enner Valencia.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kiufundi, mechi hii inaweza kuamuliwa na vita ya eneo la kiungo. Ivory Coast watategemea nguvu za Kessié na Sangaré kuvunja mipango ya Ecuador, huku Ecuador wakimtegemea Caicedo kudhibiti kasi ya mchezo na kusaidia safu ya ulinzi. Timu itakayoshinda mapambano ya katikati ya uwanja inaweza kupata nafasi kubwa ya kutawala mchezo. Kutokana na uimara wa pande zote mbili, nafasi za mabao mengi zinaonekana kuwa ndogo.

Kwa mtazamo wa jumla, huu ni mchezo ambao unaweza kuamua mapema nani atakuwa katika nafasi nzuri ya kuambatana na Ujerumani kuelekea hatua ya mtoano. Ecuador wanaonekana kuwa na ulinzi bora zaidi, lakini Ivory Coast wana faida ya kasi na ubunifu katika safu ya ushambuliaji. Matokeo ya sare yanaonekana kuwa na uwezekano mkubwa, ingawa ushindi mwembamba wa upande wowote hautakuwa wa kushangaza.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, amesema wazalishaji, wafanyabiashara na watoa huduma nchini ni nguzo muhimu katika maendeleo ya uchumi kutokana na mchango wao katika uzalishaji, biashara na utoaji wa huduma mbalimbali na jitihada zao zinapaswa kutambuliwa ili kuhamasisha utendaji bora na kuongeza ushindani wenye tija.


Londo amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa utambuzi wa kampuni bora 100 za chapa za Afrika zinazotengeneza bidhaa zilizoko barani humo, jijini Dar es Salaam.

Amesema serikali inatambua mchango wa Wafanyabiashara na wazalishaji, na ni njia mojawapo ya kuwapa hamasa ya kuendelea kufanya vizuri zaidi katika shughuli zao za kiuchumi.

"Mwaka huu ni wa kihistoria kutokana na kupitishwa kwa bajeti itakayoweka msingi wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kuwa mhimili mkubwa wa ukuaji wa uchumi,hivyo Serikali inaitambua sekta binafsi kama mdau muhimu katika kufanikisha maendeleo ya Taifa",amesema Londo.

Katika hatua nyingine Mhe. Londo amesema Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji na wafanyabiashara ili kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za uzalishaji, biashara na uchumi wa viwanda, ameeleza kuwa hatua hizo zitasaidia kuimarisha uchumi wa wananchi na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Kwa upande wake Mratibu wa tuzo hizo, Deogratius Kilawe, amesema kwamba lengo la kuandaliwa kwa tuzo hizo ni kutengeneza ushindani wa soko kwa bidhaa za Afrika, na kuongeza huduma bora kwa wananchi.

“Mwaka wa nne tunawatambua wazalishaji hao sasa, watu walioshiriki kuwania ni takribani 5,000 hadi kufikia mchakato wa kampuni 500, kutoka katika nchi zaidi ya saba,” amesema Kilawe.







Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kinampanda–Kisana–Kisiriri umeshasainiwa, hatua inayofungua njia ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kubadilisha shughuli za usafiri na uchumi katika maeneo ya Wilaya ya Iramba.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kinampanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu ya upatikanaji wa fedha za mradi huo na kwamba changamoto iliyobaki sasa ni kukamilisha taratibu za kumpata mkandarasi atakayetekeleza ujenzi huo.

“Leo tunavyoongea, mkataba wa upatikanaji wa fedha umeshasainiwa. Kwa hiyo fedha si tatizo tena. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao walishuhudia kusainiwa kwa mkataba huo,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema barabara hiyo itaanzia Kitusha, kupita Kinampanda, Galangala, Kisana na kuunganishwa na Kisiriri kabla ya kuelekea Sibiti, hatua itakayorahisisha mawasiliano na usafirishaji wa watu na bidhaa katika ukanda huo.

Waziri Mkuu amesema mradi huo utatekelezwa kwa kiwango cha kisasa na unatarajiwa kuwa miongoni mwa barabara bora zaidi mkoani Singida.

“Barabara hii huenda ikawa moja ya barabara bora kuliko zote hapa mkoani Singida. Itakuwa ni barabara ya kisasa kweli kweli,” amesema.

Akitoa ufafanuzi wa hatua za utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Singida, Mhandisi Claver Mwinuka amesema tayari mchakato wa kumpata mshauri elekezi unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.

Amesema baada ya kukamilika kwa michoro na nyaraka za zabuni, Serikali itaanza mchakato wa kumpata mkandarasi huku matarajio yakiwa ni mkandarasi huyo kupatikana ifikapo mwezi Septemba mwaka huu.

Mhandisi Mwinuka amesema barabara hiyo ina urefu wa kilometa 38.5 na itajengwa kwa upana wa mita 9.5, tofauti na barabara nyingi za TARURA ambazo hujengwa kwa upana wa mita 8.5.

Aidha, amesema barabara hiyo itakuwa na taa zaidi ya 400 pamoja na vituo vya mabasi vya kisasa vitakavyoboresha huduma za usafiri kwa wananchi.

Wakati huohuo, Dkt. Mwigulu amesema Serikali itaendelea kuimarisha huduma za afya katika Tarafa ya Kinampanda kwa kupeleka gari jipya la wagonjwa (ambulance) katika Kituo cha Afya Kinampanda ndani ya wiki moja hadi mbili.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuboresha huduma za afya kwa wananchi kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Kinampanda kupitia mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya katika kila tarafa.

“Leo kama sehemu ya shukrani, nawaletea ambulance mpya. Itakuwepo hapa kituoni ili iweze kuwasaidia wananchi wa Kinampanda,” amesema.

Aidha, Dkt. Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi amesema Serikali inaendelea na maandalizi ya utekelezaji wa miradi mingine ya barabara katika Wilaya ya Iramba ikiwemo Shelui–Nkongilangi–Tulya–Kidaru, Mtoa–Mtekente–Urugu–Mlandala–Sepuka pamoja na Iguguno–Nduguti–Gumanga–Sibiti ambayo ipo katika hatua mbalimbali za usanifu na maandalizi ya utekelezaji.




Top News