Na. OWM-KAM Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imewapiga msasa Washiriki kutoka katika Wizara pamoja na Taasisi za Serikali kuhusu Mfumo wa Kielektroniki wa Taarifa za Soko la Ajira (NLMIS) yanayofanyika leo Februari 18, 2026 katika Jengo la OSHA, Jijini Dodoma.

Aidha, Mafunzo hayo yalilenga kuwapatia uwezo katika utoaji Taarifa za ajira wakiwa katika maeneo ya Kazi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yao ya kila Siku.

Akizungumza, Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bi. Alana Nchimbi katika mafunzo, amewataka washiriki kuzingatia mafunzo ya Mfumo huo ili kupata takwimu sahihi za Ajira zinazozalishwa kupitia miradi mbalimbali.

Naye, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bw. Godwin Mpelumbe amesema Taarifa za soko la Ajira zimetengenezwa kwa kupitia vitengo mbalimbali ikiwepo, Ukuzaji Ujuzi, Vyama vya Wafanyakazi, Sheria, Sera na Mikakati ya masuala ya soko la ajira nchini.

Kwa wakati tofauti, washiriki wa mafunzo hayo wamepongeza Serikali kwa kuanzisha mfumo huo na kuomba kutoa Elimu kwa wadau na watumiaji wa mfumo ili kuendelea kupata ujuzi na tija katika utendaji kazi wao.






Na. OWM-KAM Dodoma

Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano imewapiga msasa Washiriki kutoka katika Wizara  pamoja na Taasisi za Serikali kuhusu Mfumo wa Kielektroniki wa Taarifa za Soko la Ajira (NLMIS) yaliyoyofanyika Februari 18, 2026 katika Jengo la OSHA, Jijini Dodoma.

Aidha, Mafunzo hayo yalilenga kuwapatia uwezo katika utoaji Taarifa za ajira wakiwa katika maeneo ya Kazi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yao ya kila Siku.

Akizungumza, Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bi. Alana Nchimbi katika mafunzo, amewataka washiriki kuzingatia mafunzo ya Mfumo huo ili kupata takwimu sahihi za Ajira zinazozalishwa kupitia miradi mbalimbali.

Naye, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bw. Godwin Mpelumbe amesema Taarifa za soko la Ajira zimetengenezwa kwa kupitia vitengo mbalimbali ikiwepo, Ukuzaji Ujuzi, Vyama vya Wafanyakazi, Sheria, Sera na Mikakati ya masuala ya soko la ajira nchini.

Kwa wakati tofauti, washiriki wa mafunzo hayo wamepongeza Serikali kwa kuanzisha mfumo huo na kuomba kutoa Elimu kwa wadau na watumiaji wa mfumo ili kuendelea kupata ujuzi na tija katika utendaji kazi wao.







Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo, amewataka viongozi na makamanda wa vituo vya wakala huo kubadili mtazamo wa uongozi kwa kusikiliza wananchi, kuwaelewa vijana wa ajira mpya na kusimamia migogoro ya rasilimali kwa busara, akisisitiza kuwa ofisi za umma hazina kisingizio cha kuchelewesha majibu kwa wananchi.

Akizungumza leo katika siku ya pili ya Mkutano wa Nne wa Viongozi na Makamanda wa Vituo vya TFS unaoendelea katika Ukumbi wa Hoteli ya Kate, Morogoro, Prof. Silayo alisema mabadiliko ya kijamii na kimazingira yanailazimu TFS kuwa na fikra pana zaidi na mbinu mpya za uongozi na utatuzi wa changamoto.

“Serikali imeweka mwelekeo wa kuwasikiliza wananchi. Hivyo, kila kiongozi wa TFS kwa nafasi yake anapaswa kuwa tayari kusikiliza, kujibu na kutatua changamoto zinazoletwa mezani. Ofisi ni ya Serikali; haijalishi ulikuwepo au hukuwepo wakati tatizo linaanza,” alisisitiza.

Prof. Silayo alisema TFS inapaswa kuendana na kasi ya mabadiliko ya kijamii yanayoathiri mitazamo ya vijana wanaoajiriwa sasa, akibainisha kuwa kizazi kipya kina matarajio tofauti kuhusu mazingira ya kazi.

“Leo kijana anaajiriwa akiwa tayari na matarajio maalum. Hatuwezi kuwachukulia kama wasikilizaji tu; tunapaswa kuwaheshimu, kuwaongoza na kuwajengea motisha,” alisema, akihimiza viongozi wa vituo kuwa tayari kupokea mawazo mapya na kuimarisha mazingira ya kazi yanayozingatia utu na heshima.

Akizungumzia athari za mabadiliko ya tabianchi na shinikizo la kijamii, Prof. Silayo alisema ongezeko la mahitaji ya rasilimali linaweza kuchochea migogoro kati ya wananchi na hifadhi, hivyo akawataka viongozi kusimamia hali hiyo kwa weledi.

Alitoa mfano wa baadhi ya wananchi wanaochoma misitu kwa lengo la kujikinga dhidi ya wanyamapori waharibifu, akisema hatua hizo ni matokeo ya “mikakati ya kuishi” inayotokana na msongo wa kimazingira.

“Hatuwezi kupuuza dalili hizi. Ni lazima tuwafikie wananchi, tuwasikilize na tushirikiane nao kabla madhara hayajawa makubwa,” alisema.

Alibainisha kuwa migogoro haiwezi kuepukika kabisa, bali kinachopaswa kusimamiwa ni kiwango chake na namna ya kuimudu kwa ustahimilivu na majadiliano ya wazi.

Kamishna alisisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za wilaya, mikoa pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama katika operesheni na doria maalum, akisema ushirikiano huo husaidia taasisi kuwa na sauti na ulinzi mpana hata pale maofisa wake wanapokosekana.

Alionya dhidi ya tabia ya kuahirisha utekelezaji wa maazimio ya mikutano, akitaka kila azimio liwe na majibu na hatua za utekelezaji kwa wakati.

“Haiwezekani tuwe na azimio la mwaka mzima halafu leo hatuna jibu. Tatizo linaweza kuwa la mfumo, lakini lisiwe la uzembe wa utendaji,” alionya.

Mkutano huo wa siku tano unajadili utekelezaji wa maazimio ya mwaka uliopita, changamoto za kiutendaji katika vituo vya TFS na mikakati ya kuimarisha uhifadhi endelevu wa misitu na nyuki sambamba na kushirikisha michezo (TFS Bonanza) ambayo vyote vimepewa kaulimbiu ya “One Team, One Dream”.

Akihitimisha hotuba yake, Prof. Silayo alitangaza rasmi kuanza kwa shughuli za siku ya pili ya mkutano huo, akiwataka viongozi hao kutumia fursa hiyo kubadilishana uzoefu na kuimarisha mshikamano katika kusimamia rasilimali za misitu kwa manufaa ya taifa.




 


Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude amezindua rasmi awamu ya pili ya Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (Accountants and Auditors Appeals Board – AAAB) katika hafla iliyofanyika kwa lengo la kuimarisha uwazi, uwajibikaji na weledi katika taaluma ya Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu nchini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo tarehe 18 Februari 2026, CPA Mkude alieleza kuwa bodi hiyo ina jukumu muhimu la kusikiliza na kuamua rufaa zinazowasilishwa na wahasibu na wakaguzi wa hesabu kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya taaluma. Alisisitiza kuwa uzinduzi wa awamu hii ya pili unaashiria kuendelea kwa dhamira ya Serikali ya kuimarisha mifumo ya usimamizi wa fedha za umma na kuhakikisha haki inatendeka kwa pande zote zinazohusika.

“Bodi hii ni mhimili muhimu katika kulinda misingi ya haki, uwazi na taaluma bora. Ni matarajio yetu kuwa wajumbe wa awamu hii ya pili watafanya kazi kwa kuzingatia misingi ya uadilifu na weledi wa hali ya juu,” alisema CPA Mkude.

Aidha, aliwataka wajumbe wa bodi hiyo mpya kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uwajibikaji na weledi ili kuendeleza heshima na hadhi ya taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu nchini, sambamba na kuimarisha imani ya wadau wa sekta ya fedha.

Awamu hii ya pili ya Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) inatarajiwa kuongeza ufanisi katika utatuzi wa rufaa, kuharakisha utoaji wa maamuzi, na kuimarisha zaidi mifumo ya kitaaluma katika kusimamia maadili na viwango vya kazi kwa wahasibu na wakaguzi wa hesabu nchini.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) wakati wa uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa hotel ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) Jaji Mtaafu Sirillius Matupa akizungumza kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo kwa awamu ya Pili.
Mwakilishi wa Msajili wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB)  Gloria Kaaya akizungumza wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo. 
Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude akikabidi vitendea kazi kwa wajumbe wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) wakiongozwa na Mwenyekiti wa AAAB Jaji Mtaafu Sirillius Matupa wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo kwa awamu ya pili.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) pamoja na watumishi kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania (NBAA) wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude wakati wa uzindui wa Bodi hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) Emmy Hudson akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) wakiongozwa na Mwenyekiti wa AAAB Jaji Mtaafu Sirillius Matupa wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo kwa awamu ya pili.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Rufaa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (AAAB) wakiongozwa na Mwenyekiti wa AAAB Jaji Mtaafu Sirillius Matupa pamoja na watumishi kutoka NBAA wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo kwa awamu ya pili.
Benki ya Stanbic kwa kushirikiana na Uwezo Tanzania wamezindua mpango madhubuti wa maktaba za shule unaoanza katika shule za msingi 45 zilizopo Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe, kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa vitabu na vifaa vya kujifunzia vinavyolingana na mtaala mpya wa taifa.

Mpango huu unalenga uanzishwaji wa maktaba hizo pamoja na kutoa vitabu vya hadithi na rasilimali za kielimu zilizobuniwa ili kuimarisha elimu msingi, kukuza ujuzi wa kusoma na kuandika, pamoja na kuongeza ushiriki wa wanafunzi katika madarasa na jamii kwa ujumla.

Kupitia Mpango wa My Village, UWEZO inaunga mkono maktaba za jamii kwa kuimarisha elimu msingi kwa watoto kwa kutoa vitabu vinavyoendana na mtaala wa taifa. Tukio hili la kukabidhi vitabu linaendana na Mpango wa Kitaifa wa Maendeleo ya Elimu wa KKK uliozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 29 Januari. Kwa kuboresha upatikanaji wa vitabu na vifaa vya kujifunzia. mpango huu unachangia kuboresha stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu, pamoja na kuwezesha ufuatiliaji na uungaji mkono wa elimu msingi kwa watoto katika ngazi ya jamii.

Mpango huu unafadhiliwa na Benki ya Stanbic Tanzania. Fedha kutoka Benki ya Stanbic Tanzania zitasaidia ununuzi wa vitabu vinavyoendana na mtaala pamoja na vitabu vya ziada, ambapo inatarajiwa kufaidisha takribani watoto 33,619 kila mwaka kwa kipindi cha miaka 10 hadi 20.

“Ushirikiano huu unaakisi namna Benki ya Stanbic inavyotekeleza uwekezaji wake wa kijamii, kwa kuzingatia miradi yenye manufaa ya moja kwa moja na inayoweza kupimwa matokeo yake. Kama ilivyo kwa programu zetu zilizopita katika sekta ya elimu na maendeleo ya jamii, mpango huu unatuwezesha kukidhi mahitaji halisi ya jamii zetu, na inaendana na kauli mbiu yetu kuwa Tanzania ni nyumbani, na tunachochea ukuaji wake,” amesema Dickson Senzi, Meneja Mwandamizi wa Mahusiano na Mawasiliano, Benki ya Stanbic Tanzania.

Pamoja na Benki ya Stanbic Tanzania, Uwezo Tanzania pia inafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Maktaba ya Taifa ya Tanzania, na wachapishaji wa vitabu wa Mkuki na Nyota. Aidha, uanzishwaji wa maktaba za shule unatarajiwa kuwahamasisha walimu na timu za usimamizi wa shule kushiriki kikamilifu katika juhudi za elimu ngazi ya kijiji kwa kutoa maeneo na miundombinu ya maktaba ndani ya shule. Njia hii itawezesha watoto na wazazi kutembelea maktaba pamoja, na kusaidia usomaji wa vitabu vya mtaala na vile vya ziada shuleni na nyumbani.

Zaidi ya hayo, walimu wanaoshiriki katika mpango huu watapatiwa vijitabu vyenye maudhui ya kujifunzia kusoma, kuandika na kuhesabu, na mahudhurio ya maktaba yatarekodiwa kwa utaratibu maalum. Walimu pia watahamasishwa kuchangia vitabu vingine vinavyopatikana shuleni mwao na kuviongeza katika maktaba za shule.

Mpango huu ni hatua muhimu katika kuboresha matokeo ya elimu msingi, kukuza utamaduni wa kusoma, na kuendeleza ubunifu na fikra pevu miongoni mwa wanafunzi. Kupitia mpango huu, Uwezo Tanzania inathibitisha dhamira yake ya kuhakikisha upatikanaji wa haki wa rasilimali bora za elimu na kuwawezesha wanafunzi kote Tanzania.

Meneja Mwandamizi wa Mahusiano na Mawasiliano, Benki ya Stanbic Tanzania, Dickson Senzi (kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa Uwezo Tanzania, Baraka Mgohamwende (kushoto), wakimkabidhi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Sunday Deogratius, vitabu vilivyofadhiliwa na Benki ya Stanbic kwa ajili ya kuanzisha maktaba 45 katika shule za msingi za Wilaya ya Ludewa. Hafla hiyo fupi ilifanyika jijini Dar es Salaam, jana.








Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akizungumza wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, akisema JamiiAfrica inaamini kuwa bila taarifa sahihi hakuna maamuzi sahihi, ndiyo maana wanashirikiana na Ubalozi wa Uholanzi pamoja na UTPC kuhakikisha waandishi wa habari wanapatiwa mbinu bora za kuhakiki taarifa na kukabiliana na propaganda.

Picha ya kumbukumbu washiriki wa mafunzo

Na Mwandishi wetu - Geita

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi badala ya taarifa potofu, akisisitiza kuwa mapambano dhidi ya upotoshaji wa habari yanahitaji weledi, maadili na matumizi sahihi ya teknolojia.

Akifungua mafunzo maalum kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa Taarifa yaliyofanyika Jumatano, Februari 18, 2026 mjini Geita, Simbaya amesema katika dunia ya sasa yenye wingi wa taarifa, ni rahisi kwa jamii kupotoshwa iwapo waandishi hawatakuwa makini katika uchambuzi na uthibitishaji wa habari.

“Wananchi wanahitaji taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Jukumu la mwandishi ni kuhakikisha jamii inapata ukweli. Ndiyo maana tumeona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya. Nendeni mkatumie elimu hii kwa vitendo. Tunataka muandike habari zenye uwezo wa kubadili jamii na kujenga taifa,” amesema Simbaya.

Ameongeza kuwa UTPC inataka kuona waandishi wakiendelea kushikilia misingi ya maadili ya taaluma yao na kuandika habari zenye tija zisizopotosha umma.

Lengo kuu ni kuwajengea waandishi uwezo wa kukabiliana na changamoto za fake news, misinformation na disinformation ambazo zimekuwa tishio kubwa duniani.

Washiriki wamepatiwa mbinu mbalimbali za uthibitishaji wa habari, ikiwemo matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence – AI), kugundua asili ya picha na video, kulinganisha taarifa na vyanzo vinavyoaminika, pamoja na kusoma zaidi ya vichwa vya habari ili kuepuka kupotoshwa.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa “Ukweli Kwanza” unaolenga kuongeza weledi wa waandishi wa habari na kuimarisha uwezo wa wananchi kupambana na upotoshaji wa taarifa. Kupitia mradi huo, waandishi wanafundishwa mbinu za fact-checking, matumizi sahihi ya teknolojia na namna ya kutambua na kukabiliana na misinformation na disinformation.

Aidha, mradi huo unalenga kuwawezesha waandishi chipukizi, hususan wanawake, kuwa mstari wa mbele katika kulinda ukweli na kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari nchini.

Kupitia mafunzo haya, UTPC na wadau wake wanaamini kuwa waandishi wa habari wataendelea kuwa nguzo muhimu ya ukweli, uwazi na uwajibikaji katika jamii.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uholanzi.

UTPC pia imeshirikiana na taasisi ya JamiiAfrica katika kupata wataalamu wanaoweza kutoa mafunzo haya kwa weledi.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita



















Top News