GEITA: Kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu, kukosa ajira si lazima kuwe na maana ya kukosa kabisa fursa za kufanya kazi; wakati mwingine changamoto kubwa ni kukosa maarifa na ujuzi unaowawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa zilizopo.

Hilo ndilo linalolenga kushughulikiwa na Mradi wa BRIDGE Tanzania, unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini, kwa kuwapatia vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu elimu ya msingi na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwawezesha kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, vijana 210 tayari wamepatiwa mafunzo kupitia mradi huo, huku baadhi yao wakianza kutumia ujuzi walioupata katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo sabuni za miche, sabuni za maji na vyakula vya mifugo.


Mafunzo hayo pia yanahusisha kusoma, kuandika, kuhesabu na ujasiriamali, yakilenga kuwajengea vijana uwezo unaoweza kutumika katika maisha yao na katika mazingira ya soko.

Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya (District Steering Committee) ya Mradi wa BRIDGE Tanzania kilichofanyika Nzera, Geita, Mratibu Msaidizi wa Kitaifa wa mradi huo, Adriano Adrian Hyera, alisema hadi sasa vijana 210 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita wamepatiwa mafunzo.

Alisema mradi huo unaweka mkazo katika kuwapa vijana fursa ya kupata maarifa na ujuzi ambao unaweza kuwasaidia kujenga uwezo wa kujitegemea.


“Lengo si kuwapa vijana mafunzo pekee, bali kuwajengea uwezo ambao wataweza kuutumia baada ya mafunzo ili kujipatia kipato na kujitegemea,” alisema Hyera.

Kwa mujibu wa muundo wa mradi, vijana ambao hawakupata fursa ya kukamilisha elimu ya msingi hupewa nafasi ya kujenga uwezo katika kusoma, kuandika na kuhesabu, kabla ya kuendelea na mafunzo ya ujuzi wa vitendo unaoendana na mazingira yao na fursa zinazopatikana katika soko.

Mtazamo huo unaweka msisitizo katika kuunganisha elimu na ujuzi wa vitendo, ili kijana anapomaliza mafunzo asiishie kuwa na maarifa ya darasani pekee, bali awe na uwezo wa kutumia ujuzi huo katika shughuli za uzalishaji na kujiajiri.

Katika utekelezaji wake Geita, mradi unawawezesha vijana kujifunza kwa vitendo na pia unatoa vifaa na mahitaji muhimu kwa ajili ya mafunzo, ili kuwapa nafasi ya kufanya mazoezi ya uzalishaji wakati wa kujifunza.

Baadhi ya vijana walionufaika na programu hiyo wamesema mafunzo yamewajengea uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kuwapa mtazamo mpya kuhusu namna wanavyoweza kutumia ujuzi wao kama njia ya kujipatia kipato.

Ujuzi huo unawapa pia nafasi ya kutengeneza bidhaa ambazo zinaweza kutumika katika jamii na, kwa kuzingatia ubora na mahitaji ya soko, kuwa sehemu ya shughuli zao za kiuchumi.

Kutoka elimu ya msingi hadi ujuzi wa soko

Kwa mtazamo wa mradi, elimu na ujuzi haviwekwi katika maeneo mawili tofauti, bali vinaunganishwa ili kumjengea kijana uwezo wa kutumia maarifa yake katika mazingira halisi.

Baada ya kujenga msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu, kijana hupewa ujuzi wa vitendo unaozingatia eneo analotoka na fursa zinazopatikana katika soko.

Hii inalenga kuwapa vijana ambao hawakumaliza elimu rasmi nafasi ya kupata ujuzi unaoweza kuwasaidia kushindana katika shughuli za kiuchumi pamoja na vijana wengine waliopitia njia rasmi za elimu na mafunzo ya ufundi.

Kwa maana hiyo, BRIDGE Tanzania inalenga kujenga daraja kati ya elimu, ujuzi na soko, badala ya kuishia katika utoaji wa mafunzo pekee.

Vijana wahimizwa kutumia fursa za mikopo

Akizungumzia hatua zinazofuata baada ya mafunzo, Hyera aliwashauri vijana kujiunga katika vikundi vya watu watano ili waweze kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na Halmashauri.

Alisema ushiriki katika vikundi unaweza kuwasaidia vijana kutumia ujuzi walioupata katika shughuli za kiuchumi na kutafuta fursa za kukuza shughuli zao.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa mafunzo wanayopata vijana yanaunganishwa na fursa za mitaji na uzalishaji, ili kuongeza uwezekano wa ujuzi huo kuleta matokeo katika maisha yao.

Majaribio yenye matarajio ya kupanuka

BRIDGE Tanzania ni mpango wa majaribio unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Kaskazini A Unguja.

Mradi una lengo la kuwafikia vijana 3,000 katika kipindi cha miaka mitano, sawa na takribani vijana 600 kila mwaka.

Majaribio hayo yanatoa nafasi ya kutathmini namna ya kuwaunganisha vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu na elimu ya msingi, ujuzi wa vitendo na fursa za kiuchumi.

Matokeo na uzoefu unaopatikana katika maeneo ya utekelezaji utasaidia katika kutathmini namna mfumo huo unavyoweza kuimarishwa na, baada ya tathmini, kupanuliwa katika maeneo mengine nchini.

Tume ya UNESCO katika utekelezaji

Utekelezaji wa BRIDGE Tanzania unaenda sambamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuwawezesha vijana kupata maarifa, ujuzi na fursa za kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa.

Kupitia Tume ya Taifa ya UNESCO, ushirikiano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini umegeuzwa kuwa fursa ya kuwafikia vijana ambao kwa sababu mbalimbali hawapo katika mfumo rasmi wa elimu.

Tume ya Taifa ya UNESCO, kwa jukumu lake la kuratibu, kutathmini na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za UNESCO nchini, inaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuhakikisha programu zinazotekelezwa zinachangia mahitaji na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania.

Kwa BRIDGE Tanzania, msisitizo ni kuhakikisha kijana aliye nje ya mfumo rasmi hapotezi fursa ya kujenga uwezo. Badala yake, anapewa nafasi ya kujifunza, kupata ujuzi na kuutumia katika kujenga maisha yake.

Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya kilichofanyika Nzera, Geita, kilitoa nafasi kwa wadau kupitia utekelezaji wa mradi, mafanikio, changamoto na hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kuongeza manufaa yake kwa vijana.

Kwa vijana hao 210 wa Geita, safari inaanzia katika kujenga msingi wa elimu na ujuzi; lakini lengo kubwa ni kuwawezesha kutumia uwezo huo katika ulimwengu halisi wa kazi, uzalishaji na kujitegemea.

▪️Waziri Mavunde na Waziri Kabamba wakubaliana msingi wa ushirikiano,

▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia na Rais Tshisekedi ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili,

▪️Ushirikiano walenga kurahisisha usafirishaji na biashara ya madini,

▪️Wakubaliana kuweka mikakati ya pamoja kuimarisha ufuatiliaji wa uzalishaji wa madini (traceability),


TIANJIN, CHINA

Pembezoni mwa Mkutano wa Madini wa China uliofanyika Jijini Tianjin, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia  ya Kongo (DRC), Mheshimiwa Louis Watum Kabamba yaliyolenga kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano kwenye sekta ya madini.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika tarehe 11 Septemba, 2026 Waziri Mavunde na mwenzake Mhe. Kabamba walijadiliana kwa kina namna ya kuendeleza sekta ya madini baina ya Nchi zao na hatimaye kuweka msingi ambao utakuwa ni mwanzo wa kuimarisha ushirikiano utakaoleta tija kwa pande zote mbili.

"Leo tumekutana hapa si kwa bahati mbaya, haya ni matokeo ya maelekezo ya viongozi wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mhe. Felix Tshekedi ya kwamba Nchi zetu ni muda muafaka wa kuimarisha ushirikiano kwenye sekta ya madini kwani tunahitajiana na kutegemeana hususan katika masuala ya usafirishaji wa madini" 

"Viongozi wetu wameshatuwekea msingi, sisi kazi yetu ni kuhakikisha tunayaishi maono yao na kuimarisha ushirikiano ambao utakwenda kuongeza tija na kuboresha sekta zetu za madini kuanzia uzalishaji mpaka biashara na uongezaji thamani madini" alisisitiza Waziri Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa ushirikiano baina ya Kongo DRC na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania umelenga kwa kiasi kikubwa kurahisisha ufanyaji wa biashara na usafirishaji wa madini kwa maslahi mapana ya Nchi zetu.

Vilevile, Mavunde alieleza kuwa kwa sasa ni vyema Tanzania na DRC wakaweka mikakati ya pamoja na kuisimamia kwa lengo la kuimarisha ufuatiliaji wa mnyonyoro wa uzalishaji wa madini kuanzia yanapochimbwa mpaka yanapouzwa au kusafirishwa kwenda nje (traceability).

Naye, Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Mhe. Louis Kabamba alishukuru kwa kukutana na mwenzake na kuahidi kuwa, kwa namna yeyote ni vyema kuyaishi maono ya Viongozi wakuu wa Mataifa haya ili kuleta manufaa yanayotarajiwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Aliendelea kusisitiza kuwa ushirikiano baina ya Tanzania na DRC pia utasaidia kubadilishana uzoefu wa namna ya kuendeleza sekta ya madini hususani katika kuwezesha uchimbaji mdogo na kuongeza mapato ya Serikali, hatua ambayo kwa DRC bado wachimbaji wadogo wanachangia kiasi kidogo. Pia, Mhe. Kabamba alisifu maendeleo ya STAMICO na kuomba uzoefu wao usaidie kuimarisha Shirika la Madini la Kongo ili liweze kuzalisha na kujiendesha kwa faida.








Kampeni ya Bonge la Wakala ya CRDB imechochea ushindani mkubwa miongoni mwa mawakala wa benki hiyo huku waliofanya vizuri zaidi katika kuongeza idadi ya miamala wakizawadiwa pikipiki 33 na mashine za POS 55  katika kipindi cha miezi mitano tangu kuanzishwa kwa kampeni hiyo.

Akizungumza mjini Morogoro wakati wa zoezi la kukabidhi zawadi hizo, Mkurugenzi wa Matawi wa CRDB Bank Tanzania, Bonaventura Paul Kiungo, amesema kampeni hiyo imechangia kuongeza mapato ya benki kwa asilimia 8, huku matumizi ya maeneo ya mawakala katika utoaji wa huduma kwa jamii yakifikia asilimia 90.

Amesema hali hiyo imesaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha na kutimiza mahitaji ya wateja katika maeneo mbalimbali nchini.

Katika zoezi hilo, jumla ya pikipiki 33 na mashine za POS 55 zilikabidhiwa kwa mawakala walioibuka washindi baada ya kufanya idadi kubwa ya miamala katika kipindi cha miezi mitano tangu kuanzishwa kwa kampeni ya Bonge la Wakala.

Kiungo amesema utoaji wa zawadi hizo ni sehemu ya malengo ya CRDB ya kuhamasisha mawakala kuongeza juhudi katika utoaji wa huduma na kupanua wigo wa huduma za benki kwa wananchi.

Ameongeza kuwa kampeni hiyo itaendelea kuwa endelevu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo kukuza mtandao wa mawakala na kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa urahisi zaidi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawakala wa CRDB, Abbas Abrahiman, amesema kampeni hiyo imeongeza chachu na ushindani miongoni mwa mawakala, hali ambayo imekuwa na mchango katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja.

Naye Ester Raphael, mmoja wa mawakala walionufaika na zawadi hizo, amesema pikipiki waliyopewa itasaidia kuongeza ufanisi na ubora wa huduma kwa wateja, hasa katika kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

Kampeni ya Bonge la Wakala inalenga kuhamasisha mawakala kuongeza idadi ya miamala, kuboresha huduma na kuchochea matumizi ya huduma za kifedha kupitia mtandao wa mawakala wa CRDB nchini.








Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndg. Abdi Mahmoud Abdi, ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa Hospitali ya Nungwi, Mkoa wa Kaskazini ‘A’, akisema mradi huo utasaidia kutatua changamoto mbalimbali za huduma za afya kwa wananchi wa jimbo hilo.

Ndg. Abdi amesema ujenzi wa hospitali hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, yenye lengo la kuboresha huduma za afya na kuzisogeza karibu zaidi na wananchi.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na viongozi wao kuanzia ngazi ya jimbo hadi taifa, katika kuhakikisha huduma za kijamii, hususan afya, zinaendelea kuboreshwa na kusogezwa karibu na wananchi.

Kwa upande wake, mkandarasi wa mradi huo amesema ujenzi wa kituo hicho cha afya chenye ghorofa mbili umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.






 


SERIKALI Mkoa wa Pwani imetoa wito kwa wataalamu wa maafa kuongeza kasi ya kutoa elimu kwa jamii, hususan wakulima, wafugaji na wananchi wanaoishi maeneo ya mabondeni, kuhusu tahadhari na hatua za kuchukua kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Richard Kayombo, wakati wa kikao cha Kamati ya Wataalamu ya Usimamizi wa Maafa Mkoa wa Pwani, akisisitiza umuhimu wa wananchi kuelewa namna ya kujikinga na kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza.

Kayombo ameeleza Mkoa umeanza maandalizi ya kukabiliana na El Niño, ikiwemo kuimarisha mifumo ya mawasiliano, ufuatiliaji, maandalizi na mwitikio wa haraka, huku akizitaka halmashauri kuanza kusafisha mifereji ya maji katika maeneo mbalimbali .

Kadhalika amefafanua mkoa umetekeleza maelekezo ya Serikali ya kuanzisha Kituo cha Uendeshaji wa Dharura (EOC), kitakachosaidia kukusanya na kuchambua taarifa za majanga, hali ya hewa, maeneo hatarishi na madhara yanayotokea, pamoja na kuratibu shughuli za uokoaji, misaada na utoaji wa taarifa kwa haraka.

Aidha, Kayombo amesema Mkoa unapaswa kuwa na msimamo mmoja katika kutekeleza maelekezo ya Serikali, ikiwemo kutumia fursa ya Pwani kuwa kituo cha kuhifadhi vifaa vya dharura vya miundombinu ya barabara, huku akisisitiza ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama, ikiwemo Jeshi la Polisi na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Kwa upande wake, Mratibu wa Kamati ya Maafa Mkoa wa Pwani, Roseline Kimaro, amesema halmashauri zote tisa na taasisi mbalimbali zimeandaa mikakati ya kukabiliana na El Niño, huku elimu ikiendelea kutolewa kwa wananchi kuhusu kujilinda, kuchukua tahadhari, kupunguza madhara, mwitikio wa haraka na kurejesha huduma pindi athari zitakapotokea.

Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Mipango na Uratibu, Romwald Mwendi, ameeleza Mkoa umejiandaa kwa rasilimali za dharura zikiwemo magari, boti, vifaa vya uokoaji, magari ya wagonjwa, dawa, chakula, maji, mafuta, mahema, ghala la chakula pamoja na vifaa vya mawasiliano.





-Wawabeba wanawake, walemavu


Na George Maziku, Geita

MGODI wa dhahabu wa wachimbaji wadogo wa I.N.K uliopo kijiji cha Ng'andu, kata ya Lugunga, wilaya ya Mbogwe, mkoa wa Geita umewawekea mazingjra mazuri ya kazi vikundi vya wanawake na walemavu wanaofanya kazi katika mgodi huo.

Pia uongozi wa mgodi wa I.N.K ukionvozwa na aliyekuwa mkurugenzi mkuu marehemu Iddi Noor Kajuna na mkurugenzi mwenza Elia Masanja Mcheka umekuwa ukiwapa msaada wa mawe ya dhahabu wanawake na walemavu ili kuwawezesha kuinuka kiuchumi.

Hayo yamesemwa jana na Meneja Mkuu wa mgodi huo Farid Ahmed Lugusha alipozungumza na Michuzi Blog ofisini kwake iliyopo mgodini hapo.

"Mgodi wetu ni tofauti sana na migodi mingine kwa namna tunavyowatendea wanawake na walenavu. Siyo tu kwamba tunawapa fursa ya kujitafutia mgodini kwetu kwa njia ya kuokota mawe ya dhahabu, maarufu kama ukwale lakini pia tunawapa bure mawe aina ya felo ambayo yana kiwango kidogo cha dhahabu ili nao wapate mitaji ya kununulia mawe mazuri ya dhahabu au dhahabu yenyewe", alisema meneja huyo.

Alisema kuwa utaratibu huo umekuwa kama sera ya mgodi wao na akawahakikishia wanawake na walemavu kuwa wataendelea kusaidiwa hata baada ya kifo cha mkurugenzi mkuu marehemu Kajuna.

"Nataka nitumie nafasi hii kuwahakikishia wanawake na walemavu kwamba kifo cha mkurugenzi Kajuna hakiwezi kuathiri msaada waliokuwa wakipewa na mgodi huu. Sisi watendaji tuliobaki tukiongozwa na mkurugenzi aliyebaki mheshimiwa Elia tutaendelea kuwasaidia na kuwashika mkono ili watimize malengo yao ya kujikwamua kiuchumi", alibainisha meneja Lugusha.

Aidha, Lugusha amewataka wanawake, vijana na walemavu wengine wasiokuwa na kazi za kufanya huko majumbani na mitaani, kuja mgodini kwake kujitafutia badala ya kukaa kuilalamikia serikali.

"Napenda kutumia fursa hii ya kutembelewa na vyombo vya habari, kuwaita wanawake, vijana na walemavu kuja katika mgodi wetu kujitafutia, waje wafanye kazi kama wanavyofanya wenzao waliopo hapa, waache kulalamikia serikali wakiwa wamekaa tu bila kufanya kazi, hakuna serikali ya kuwagawia fedha wananchi wake bila kufanya kazi", alisisitiza Lugusha.






Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salumu, akiongoza ujumbe wa jumuiya hiyo kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Septemba 2026, kufuatia kufiwa na mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, tarehe 7 Septemba 2026.

Kwa upande wake, Balozi wa Amani nchini Tanzania, Mess Chengula, alitoa salamu za pole kwa Mhe. Rais, familia na Watanzania kwa ujumla, akiwasihi kuwa na subira na mshikamano katika kipindi hiki cha majonzi.
















Klabu ya Chelsea itakuwa mwenyeji wa Hull City katika mchezo wa Ligi Kuu England (EPL) utakaochezwa leo Jumamosi, Septemba 12, 2026, katika Uwanja wa Stamford Bridge. Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 17:00 jioni.

Chelsea inaingia kwenye mchezo huo ikitafuta kurejea kwenye njia ya ushindi baada ya kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Arsenal katika mchezo uliopita. Licha ya matokeo hayo, Chelsea imeonyesha kiwango kizuri mwanzoni mwa msimu chini ya kocha Xabi Alonso, huku ikionyesha uwezo mzuri katika kujenga mashambulizi.

Kwa upande wa Hull City, timu hiyo inakutana na changamoto ya kucheza ugenini dhidi ya Chelsea. Hull City imeanza msimu ikiwa na kiwango cha ushindani na imeonyesha uimara katika baadhi ya michezo yake ya awali.

Hull City ni miongoni mwa timu mpya katika Ligi Kuu msimu huu baada ya kufuzu kutoka Championship kupitia mchezo wa play-off, ambapo iliifunga Middlesbrough katika fainali. Timu hiyo inarejea Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2016/17.

Historia ya mikutano kati ya timu hizi inaonyesha kuwa Chelsea imekuwa na matokeo mazuri dhidi ya Hull City katika michezo yao ya hivi karibuni. Chelsea haijapoteza katika mikutano yao tisa iliyopita, huku ikishinda michezo yote hiyo.

Mchezo wa Stamford Bridge utakuwa nafasi kwa Chelsea kuendelea kujenga mwenendo mzuri chini ya Alonso, wakati Hull City ikitafuta kupata matokeo yatakayoonyesha uwezo wake wa kushindana katika msimu wake wa kurejea Ligi Kuu.

Taarifa za ratiba, matokeo na takwimu za michezo mbalimbali ya EPL zinapatikana kupitia majukwaa ya taarifa za michezo, ikiwemo Meridianbet, pamoja na vyanzo vingine vya michezo.
DUNIA ya burudani ya mtandaoni imepata sura mpya baada ya Meridianbet kuongeza nguvu kwenye jukwaa lake kwa kumkaribisha Play’n GO, mmoja wa watoa huduma maarufu duniani wa michezo ya kasino ya kisasa. Hatua hiyo imekuja ikiwa na lengo la kuwapa wapenzi wa burudani ya kidijitali uzoefu mpya wenye ubunifu, msisimko na ladha tofauti, huku kila mchezo ukibeba kitu cha kipekee kinachoweza kumfanya mchezaji kufurahia kila hatua ya mchezo.

Kupitia ushirikiano huo, wachezaji wa Meridianbet sasa wanaweza kuingia katika ulimwengu wa michezo iliyobuniwa kwa ubunifu wa hali ya juu na inayochanganya burudani na simulizi zinazovutia. Miongoni mwa michezo inayopatikana ni Book of Dead, Hot Dog Heist, Flying Pigs, Crystal Hall na Cats and Cash, huku kila mmoja ukiwa na muonekano, mtindo na simulizi yake. Hii inamaanisha kuwa badala ya kuwa na chaguo moja la burudani, wachezaji wana nafasi ya kuchagua mchezo unaoendana na ladha yao kila wanapoingia Meridianbet.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kinachofanya Play’n GO kuvutia zaidi ni namna inavyoweka ubunifu katikati ya uzoefu wa mchezaji. Michezo hiyo imeundwa kwa mtindo unaochanganya picha, hadithi na mfumo wa kisasa wa uchezaji, hivyo kufanya kila raundi kuwa sehemu ya tukio linaloendelea. Kwa wapenzi wa burudani wanaotafuta kitu zaidi ya mchezo wa kawaida, ujio huu unafungua mlango wa uzoefu wa kasino unaoweza kuwapeleka kwenye mazingira tofauti, huku msisimko ukiendelea kuongezeka kadri mchezo unavyoendelea.

Meridianbet, kwa upande wake, inaendelea kuweka mkazo kwenye kutoa burudani yenye ubora pamoja na mazingira salama na yanayofurahisha kwa wachezaji wake. Kupitia michezo hii mipya, wachezaji wanapata fursa ya kujaribu bahati zao huku wakifurahia ubunifu wa kiwango cha kimataifa.

Ujio wa Play’n GO ndani ya Meridianbet kwa hakika unaongeza sura mpya kwenye burudani ya mtandaoni, ukiwapa wachezaji nafasi ya kugundua michezo yenye hadithi, ubunifu na msisimko wa aina yake. Kwa wale wanaopenda kujaribu michezo mipya na kufurahia teknolojia ya kisasa ya burudani, hii ni fursa ya kuingia kwenye ulimwengu mpya uliojaa chaguo mbalimbali.
Na Janeth Raphael – MichuziTv

Serikali imeeleza kuwa pamoja na mafanikio yanayoendelea kupatikana katika uhifadhi wa wanyamapori na maliasili, sekta hiyo bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji hatua endelevu, ikiwemo migongano kati ya binadamu na wanyamapori, ujangili, uvamizi wa maeneo ya hifadhi na shoroba pamoja na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesema hayo leo Septemba 11, 2026, wakati akizungumza katika hafla ya kufunga mafunzo kwa marubani wa ndege nyuki (drones) na kukabidhi vitendea kazi, iliyofanyika Mtumba, Dodoma.

Dkt. Kijaji amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuimarisha uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za wanyamapori, lakini ongezeko la migongano kati ya binadamu na wanyamapori bado ni changamoto inayohitaji kupewa kipaumbele kutokana na madhara inayosababisha kwa wananchi, mifugo na mazao.

Amesema matukio hayo yanaweza pia kuathiri mtazamo wa jamii kuhusu uhifadhi wa wanyamapori, hivyo Serikali inaendelea kutafuta njia bora za kuzuia na kudhibiti migongano hiyo kabla haijasababisha madhara makubwa kwa wananchi.

Dkt. Kijaji amesema ujangili na biashara haramu ya nyara na mazao ya misitu ni miongoni mwa changamoto nyingine zinazoendelea kuhatarisha uwepo wa baadhi ya spishi za wanyamapori na uendelevu wa rasilimali za asili.

Amesema upanuzi wa shughuli za kibinadamu, ikiwemo kilimo, ufugaji, uchimbaji wa madini na ujenzi wa makazi katika maeneo yasiyozingatia mipango bora ya matumizi ya ardhi, umeongeza shinikizo katika maeneo ya hifadhi na kutishia kupotea kwa baadhi ya makazi muhimu ya wanyamapori.

Aidha, amesema uvamizi wa shoroba za wanyamapori umeendelea kuwa kikwazo kwa uhamaji wa wanyamapori kutoka eneo moja kwenda jingine, hali inayoweza kuathiri mifumo ya ikolojia inayounganisha maeneo mbalimbali ya hifadhi.

Dkt. Kijaji ametaja pia kuenea kwa mimea vamizi ndani ya maeneo ya hifadhi kuwa changamoto inayopunguza ubora wa makazi na malisho ya wanyamapori, huku mabadiliko ya tabianchi yakichangia ukame, mvua zisizotabirika, mafuriko, upungufu wa maji na uharibifu wa miundombinu ya uhifadhi.

Amesema katika kukabiliana na changamoto hizo, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kitaifa kwa kushirikiana na wananchi na wadau wa uhifadhi, huku ikiongeza matumizi ya teknolojia katika kuboresha usimamizi na ulinzi wa rasilimali hizo.

Dkt. Kijaji amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara imeweka kipaumbele katika kupunguza migongano ya binadamu na wanyamapori kupitia utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Utatuzi wa Migongano ya Binadamu na Wanyamapori wa Miaka 10.

Amesema mkakati huo unalenga kuzuia, kudhibiti na kushughulikia kwa haraka matukio yanayohusisha wanyamapori wakali na waharibifu, ili kupunguza madhara kwa wananchi na kulinda usalama wa jamii.

Ametaja pia Mkakati wa Usimamizi na Uhifadhi wa Tembo wa Miaka 10, unaolenga kuimarisha uhifadhi endelevu wa tembo pamoja na kupunguza athari hasi dhidi ya wanyama hao na makazi yao.

Vilevile, Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Kuongoa na Kurasimisha Shoroba za Wanyamapori wa Miaka Mitano, unaolenga kuimarisha hali ya uhifadhi katika maeneo yanayotumiwa na wanyamapori wanapohama kutoka hifadhi moja kwenda nyingine au kutoka nchi moja kwenda nyingine ndani ya mifumo ikolojia inayovuka mipaka.

Amesema mfumo huo unasaidia mamlaka kupata taarifa kwa haraka na kuchukua hatua za kudhibiti matukio hayo, sambamba na kurahisisha mchakato wa ulipaji wa kifuta jasho au kifuta machozi kwa wananchi walioathirika.

Dkt. Kijaji amesema matumizi ya ndege nyuki (drones) nayo yanaendelea kupewa umuhimu katika ufuatiliaji na usimamizi wa maeneo ya uhifadhi, kwa lengo la kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa taarifa na kuwezesha hatua kuchukuliwa kwa wakati dhidi ya changamoto zinazojitokeza.

Amesisitiza kuwa mafanikio ya uhifadhi hayawezi kutegemea Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, wananchi na wadau wa uhifadhi ili kuhakikisha rasilimali za wanyamapori zinalindwa, zinatunzwa na kunufaisha kizazi cha sasa na kijacho.






DENIS MLOWE, IRINGA


MKURUGENZI wa Bodi ya Maji Bonde la Rufiji, David Munkyala, amesema Serikali imeanza kuchukua hatua za kudumu katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa maji kwa mifugo na migogoro kati ya wakulima na wafugaji katika Tarafa ya Pawaga, Wilaya ya Iringa.

Munkyala amesema hayo wakati akizungumza na wanahabari juu ya hatua zilizochukuliwa na Bodi hiyo katika kuhakikisha wafugaji wanapata maji kwa ajili ya mifugo yao bila kulazimika kuingia katika maeneo ya mashamba au kutumia vyanzo vya maji vilivyopo kwenye maeneo ya miradi ya umwagiliaji.

Amesema changamoto hiyo ilijitokeza zaidi baada ya kuboreshwa kwa Skimu ya Umwagiliaji ya Mkombozi, ambapo awali wafugaji walikuwa wakipeleka mifugo kunywa maji katika maeneo ya mto na mabondeni, lakini baada ya maboresho ya skimu hiyo utaratibu huo ukabadilika na wafugaji kuzuiwa kupeleka mifugo katika maeneo ya mradi.

Munkyala alisema kuwa hali hiyo ilisababisha baadhi ya wafugaji kukosa maeneo mbadala ya kunyweshea mifugo na hivyo kuanza kuingia katika maeneo ya mashamba ya wakulima, jambo lililokuwa likichochea migogoro kati ya makundi hayo.

Amesema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, kutoa maelekezo mwezi Julai mwaka huu ya kutafutwa kwa njia mbadala ya kuwapatia wafugaji maji, Bodi ya Maji Bonde la Rufiji ilifanya utafiti na kuanza utekelezaji wa hatua hiyo kwa kuchimba kisima kirefu katika eneo hilo.

“Tumefanya survey na kuchimba kisima kirefu cha zaidi ya mita 100 na tumefanikiwa kupata maji ya kutosha. Kisima hiki kinatoa takribani lita 15 kwa sekunde, ambayo ni kiwango kikubwa cha maji,” amesema Munkyala.

Ameeleza kuwa lengo la kuchimba kisima hicho lilikuwa ni kuhakikisha wafugaji wanapata maji karibu na maeneo yao, hatua ambayo itasaidia kupunguza migogoro kati yao na wakulima, sambamba na kulinda vyanzo vya maji na mazingira.
Munkyala amesema matumizi ya mito na mabonde kwa ajili ya kunyweshea mifugo yanaweza kusababisha uharibifu wa kingo za mito, mmomonyoko wa udongo na kuongezeka kwa tope kwenye mito, hali ambayo inaweza kupunguza kina cha maji na kuathiri matumizi ya maji kwa shughuli mbalimbali, ikiwemo umwagiliaji na uzalishaji wa nishati.

“Kitendo cha mifugo kwenda mtoni kinaweza kuharibu kingo za mto na kusababisha mmomonyoko wa udongo na udongo huo huingia mtoni na kuongeza matope, jambo ambalo linaweza kupunguza kina cha mto na kuathiri matumizi ya maji kwa shughuli nyingine,” amesema.

Amesema ujio wa Mawaziri wawili wenye dhamana ya sekta ya kilimo pamoja na mifugo na uvuvi katika eneo hilo ni hatua muhimu kwa kuwa wamekuja kujionea utekelezaji wa mradi huo na kutafuta suluhisho la kudumu la changamoto zinazowakabili wakulima na wafugaji.

Munkyala, hatua zilizopendekezwa na Mawaziri hao zimeongeza matumaini ya kumaliza changamoto hiyo, baada ya kuahidi kuongeza miundombinu katika kisima kilichochimbwa pamoja na kuchimba visima vingine vitano kwa ajili ya kuwapatia wananchi na wafugaji maji.

Amesema kati ya visima hivyo, vitatu vinatarajiwa kuanza kuchimbwa kwa haraka na kuwezeshwa kwa miundombinu inayohitajika ili viweze kutumika na wananchi pamoja na wafugaji.

Amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza utegemezi wa mifugo kwenda kwenye mabonde na mito kutafuta maji, hali ambayo imekuwa ikichangia migogoro na uharibifu wa mazingira.

Aidha, amesema Mawaziri hao wameelekeza Halmashauri kuhakikisha zinajenga miundombinu maalumu ya kunyweshea mifugo, huku zikitafutwa pia njia za kuongeza upatikanaji wa malisho kwa wafugaji.

Amesema miongoni mwa mikakati hiyo ni kuwezesha upandaji wa nyasi na kuboresha maeneo ya malisho ili mifugo ipate chakula cha kutosha na kupunguza ulazima wa wafugaji kupeleka mifugo katika maeneo ya mabondeni kwa ajili ya kutafuta maji na malisho.

Munkyala amewashukuru Mawaziri hao kwa kutembelea eneo la mradi na kutoa maelekezo yanayolenga kupata suluhisho la kudumu, akisema hatua hizo zitasaidia kuimarisha mahusiano kati ya wakulima na wafugaji, kulinda mazingira na kuhakikisha rasilimali za maji zinatumika kwa uendelevu.



Nyerere Cycling Tour Imetangaza washirika wa safari ya mwaka huu itakayokuwa na umbali wa kilomita 1,500 hadi Butiama, huku Vodacom Tanzania ikiendelea kuwa mshirika mkuu wa msafara huo, ikishirikiana na Afro Oil, Stanbic Bank Tanzania, BYD, ABC Bicycle, Coca-Cola na Huawei.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Zuweina Farah, alisema Vodacom itaendelea kushirikiana na Nyerere Cycling Tour kama mshirika mkuu, akieleza kuwa ushirikiano huo unaonesha dhamira ya kampuni ya kuendelea kuunga mkono mipango yenye kuleta matokeo chanya kwa jamii nchini.

Alisema Vodacom pia inafurahia kuwapokea washirika wapya ambao ushiriki wao utaongeza thamani katika safari ya mwaka huu na kusaidia kupanua wigo na matokeo ya msafara huo.

Msafara huo utafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 14 Oktoba 2026, ukiwa na mkazo katika elimu, afya na uhifadhi wa mazingira, sambamba na kuhamasisha wanafunzi, hususan wasichana, kushiriki katika michezo ya kuendesha baiskeli.

Katika safari ya mwaka huu, Vodacom wanatarajia kutoa madawati 1,000 kwa shule 10, kukarabati madarasa 40 na kujenga madarasa mapya 10, huku shughuli hizo zikitarajiwa kuwafikia zaidi ya wanafunzi 25,000. Katika safari zilizopita, Nyerere Cycling Tour ilifikia shule 107 na zaidi ya wanafunzi 75,000 walinufaika.

Akizungumzia ushirika wao, Meneja wa Uendelevu wa Stanbic Bank Tanzania, Annette Mkini, alisema benki hiyo itatumia msafara huo kuhamasisha elimu ya fedha kwa wanafunzi na vijana, ili kuwajengea uelewa itakayowasaidia kufanya maamuzi bora kuhusu matumizi na usimamizi wa fedha.

Kwa upande wake, Afro Oil imesema ushiriki wake unatokana na dhamira ya kampuni ya kurudisha kwa jamii, huku Samwel Msonsa kutoka BYD alisema kampuni hiyo itashiriki katika uzalishaji na uhamasishaji wa msafara huo, pamoja na shughuli za uhifadhi wa mazingira ikiwemo upandaji miti.

Msafara huo hadi sasa umesajili waendesha baiskeli 213, huku wengine wakitarajiwa kujiunga njiani. Waendesha baiskeli kutoka nchi 12 wanatarajiwa kushiriki, zikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Malawi, Zambia, Afrika Kusini, Australia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Uholanzi. Aidha, wanawake 23 tayari wamesajiliwa kushiriki katika msafara huo.

Vodacom pia ilitoa taarifa kuhusu Vodacom Coastal Classic, ambayo hadi sasa imeandikisha washiriki 147. Na washindi wa nafasi ya kwanza kwa wanawake na wanaume watapata Sh milioni 10 kila mmoja, nafasi ya pili Sh milioni 7 na nafasi ya tatu Sh milioni 5. Waendesha baiskeli watakaomaliza nafasi ya nne hadi ya kumi watapata Sh milioni 1 kila mmoja.

Vodacom Tanzania imewekeza Sh milioni 160 katika Msafara wa Baiskeli wa Nyerere, huku Vodacom Foundation ikichangia zaidi ya Sh milioni 300 kwa shughuli za kijamii zitakazotekelezwa katika maeneo yatakayopitiwa na msafara huo, ikiwemo uboreshaji wa shule na utoaji wa madawati. Safari hiyo itahitimishwa Butiama, nyumbani kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Washirika wa Nyerere Cycling Tour, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Zuweina Farah (wa nne kulia), ambaye aliwakilisha Vodacom Tanzania PLC kama mdhamini mkuu wa msafara huo, wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano na waandishi wa habari na wadau wa msafara huo uliolenga kutangaza rasmi washirika wa zamani na wapya wa msafara huo. Katika picha kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Afroil, Mohamed Al-Jabry(wa pili kushoto) Meneja wa Uendelevu wa Stanbic Bank Tanzania, Annette Nkini (wa tatu kushoto), Mkuu wa Masoko na Mauzo wa BYD, Samwel Msonsa (wanne kushoto), Mwanzilishi wa Nyerere Cycling Tour, Gabriel Landa, Meneja wa Akaunti wa Vodacom Huawei, Victor Wang, na Katibu Mtendaji wa Coca-Cola Tanzania, Yvette Gadi. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam, Septemba 11, 2026
Baadhi ya washiriki wa msafara wa Nyerere cycling tour wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari na wadau wa msafara huo uliolenga kutangaza rasmi washirika wa zamani na wapya wa msafara huo.

Mwanzilishi wa Nyerere Cycling Tour Gabriel Landa (wa kwanza kulia) akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari na washirika wao. Majadiliano hayo yalihusu namna gani watajumuika katika msafara huo.

Mwanzilishi wa Nyerere Cycling Tour Gabriel Landa akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari na wadau wa msafara. Mkutano huo ulilenga kutangaza rasmi washirika wa zamani na wapya wa msafara huo.
Washirika, Washiriki na Wadau wa Nyerere Cycling Tour wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kuhitimisha mkutano wa waandishi wa habari uliopangwa kwa ajili ya kutangaza rasmi washirika wapya na wa zamani wa msafara huo.

LIGI Kuu ya Hispania (LaLiga) itaendelea na msisimko wake leo, Septemba 11, ambapo Sevilla watawakaribisha Valencia katika uwanja wao wa nyumbani, Estadio Ramón Sánchez Pizjuán, jijini Seville. Mechi hii ya mzunguko wa tano itaanza saa 22:00 usiku,

Sevilla, chini ya uongozi wa kocha Luis García, wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa nafasi ya saba kwenye msimamo wakiwa na pointi saba kutoka mechi nne. Timu hiyo ilianza vizuri kwa ushindi wa nyumbani wa 2-1 dhidi ya Rayo Vallecano, ikafuatiwa na ushindi wa 3-1 ugenini dhidi ya Athletic Club, kabla hali kuanza kubadilika. Baadaye walifungwa 3-1 nyumbani dhidi ya Atletico Madrid, na wikendi iliyopita walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Espanyol huko nje.

Jambo la kushangaza ni kwamba Sevilla walicheza sehemu kubwa ya mchezo huo dhidi ya Espanyol wakiwa na wachezaji kumi tu, na licha ya kuongoza mapema nusu ya pili, walifungwa goli dakika ya 98 na kupoteza ushindi uliokuwa mikononi mwao.

Upande wa pili, hali ni tete zaidi kwa Valencia. Timu ya kocha Carlos Corberán inashika mkia wa msimamo (nafasi ya 20) ikiwa na pointi moja tu kutoka mechi nne, jambo linaloashiria msimu mgumu tangu mwanzo. Katika mchezo wao wa mwisho, Valencia walipigwa vibaya 5-0 nyumbani dhidi ya Barcelona.

Kocha Corberán mwenyewe alikiri hali hiyo baada ya mechi, akisema kwamba dhidi ya timu kubwa kama Barcelona, kila kitu lazima kiende sawasawa ili kupata matokeo mazuri, jambo ambalo halikutokea kwao siku hiyo.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema. Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa sasa Valencia wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa hawajapata ushindi kwa mfululizo wa michezo kadhaa, huku baadhi ya ripoti zikieleza kuwa wana changamoto kubwa ya majeruhi kambini kwao, jambo litakalomfanya Corberán ajitahidi zaidi kupanga kikosi chake ili apate ushindi wa kwanza.

Valencia hawajafungwa katika michezo sita ya mwisho dhidi ya Sevilla, na wameshinda mechi mbili kati ya tatu za mwisho walizokuja uwanjani hapa. Katika mchezo wao wa mwisho msimu uliopita, Valencia walishinda 2-0 ushindi uliothibitisha uwezo wao wa kuizuia Sevilla licha ya kutokuwa na fomu nzuri wakati huo.

Kwa ujumla, hii ni mechi ya "lazima kushinda" kwa pande zote mbili kwa sababu tofauti Sevilla wanataka kurejea kwenye ushindi baada ya wiki mbili za kutofunga, huku Valencia wakitafuta ushindi wao wa kwanza wa msimu ili kutoka chini kabisa ya msimamo.
MASHABIKI wa michezo ya kasino mtandaoni sasa wana sababu nyingine ya kuongeza burudani zao baada ya mchezo mpya Wilder icy fruits kutoka Expanse kuwasili ndani ya Meridianbet. Mchezo huu umebeba ladha mpya ya burudani kupitia mandhari yenye rangi zinazovutia, matunda yenye muonekano wa barafu na mshangao unaoweza kujitokeza wakati wowote. Kwa wachezaji wanaopenda michezo yenye kasi, mvuto na ushindi, Wilder Icy Fruits umeingia kama nyongeza inayoweza kufanya kila mzunguko kuwa wa kusisimua zaidi.

Kinachoufanya mchezo huu kuvutia zaidi ni safari yake yenye mchanganyiko wa matunda ya barafu na sapraizi zinazoweza kujitokeza unapocheza. Kila hatua inakupa nafasi ya kufuatilia michanganyiko mbalimbali ya matunda huku ukifurahia muonekano wake wa kuvutia na mazingira yenye ladha ya ubaridi. Hapa hakuna nafasi ya kuchoshwa, kwani kila mzunguko unaweza kuleta tukio jipya na kukufanya utake kuona kinachofuata.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Wilder Icy Fruits inaleta furaha huku ukifuatilia uwezekano wa kupata mfululizo mzuri wa ushindi kutokana na uchezaji wako. Wachezaji wanapata nafasi ya kujaribu bahati zao kwa kufuatilia michanganyiko mbalimbali na kuona umbali ambao wanaweza kufika. Kwa kifupi, ni mchezo unaochanganya barafu, matunda, rangi na mshangao katika kifurushi kimoja cha burudani, huku kila mzunguko ukiwa na uwezo wa kuleta msisimko mpya.

Kwa sasa, wilder icy fruits inapatikana Meridianbet, hivyo wapenzi wa kasino mtandaoni wanaweza kujiunga na safari hii mpya ya matunda ya barafu. Unachohitaji ni kujisajili Meridianbet, kuingia kwenye mchezo na kuanza kufurahia burudani inayokuja na kila mzunguko. Iwe unapenda michezo mipya au unatafuta kitu tofauti cha kuongeza kwenye orodha yako ya burudani, Wilder Icy Fruits inakupa sababu ya kujaribu ladha yake mpya.

Usibaki nyuma wakati msisimko mpya ukiendelea. Wilder Icy Fruits umefika na umeleta upepo mpya wa burudani wenye matunda ya kuvutia, mandhari ya barafu na ushindi wa kila wakati. Jisajili Meridianbet sasa, ingia kwenye mchezo na uanze safari ya mfululizo wa ushindi.

Top News