Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tamasha la Kizimkazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza utamaduni, utalii, biashara na fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar, sambamba na kuchochea maendeleo ya wananchi.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 12 Agosti 2026, alipokuwa akizindua rasmi Tamasha la Kizimkazi 2026 lenye kaulimbiu “KIZIMKAZI Kumenoga!” katika Mkoa wa Kusini Unguja.
Amepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono ya kuasisi Tamasha hilo, ambalo limekuwa likichangia kuhifadhi mila na utamaduni, kukuza utalii na kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutumia Tamasha hilo kutangaza fursa za uwekezaji katika utalii, uvuvi, mwani na Uchumi wa Buluu, huku Serikali ikiendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na miundombinu ya uzalishaji.
Amesema Tamasha la Kizimkazi linaunga mkono dhamira ya Serikali ya kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar kutoka 800,000 hadi milioni 1.5, kupitia matukio maalum ya utalii na utangazaji wa vivutio, utamaduni, vyakula na ukarimu wa Wazanzibari.
Rais Dkt. Mwinyi amewapongeza waandaaji, wadhamini, taasisi za Serikali, Sekta Binafsi, wajasiriamali, wasanii, wanamichezo na wananchi kwa kufanikisha Tamasha la Kizimkazi 2026, akihimiza kuendelea kulitumia kama jukwaa la kufungua fursa mpya za maendeleo.
Tamasha hilo linaendelea hadi tarehe 14 Agosti 2026, ambapo kilele chake kitafanyika katika Uwanja wa Mwehe, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja.
📌 Asema wajibu wa kila Mtanzania ni kuhakikisha mafanikio yanakuwa endelevu
KIZIMKAZI, ZANZIBAR
Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelea kuwa endelevu.
Dkt. Biteko amesema hayo wakati akishiriki mjadala kuhusu “Uongozi wa Kimkakati wa Tanzania katika Kuharakisha Mabadiliko ya Nishati Endelevu na Jumuishi”, uliofanyika katika Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF), Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Amesema uwepo wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuipa msukumo ajenda hiyo katika ngazi mbalimbali za uongozi wake na kuifikisha hadi katika majukwaa ya kimataifa.
Dkt. Biteko amesema umuhimu wa kuendelea kuipa kipaumbele ajenda hiyo unatokana na ukubwa wa athari za matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia, ikiwemo uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, ambapo takribani hekta 470,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini.
Aidha, amesema zaidi ya watu 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa wakati wa kupika, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza kasi ya mpito kuelekea matumizi ya nishati safi.
Ameongeza kuwa matumizi ya nishati isiyo safi yana athari za kijinsia, hususan kwa wanawake ambao hutumia muda mwingi kutafuta kuni badala ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.
Amesema athari hizo pia zinawagusa watoto, ambapo baadhi yao hukosa muda wa kutosha wa kuhudhuria masomo kutokana na kulazimika kusaidia familia zao kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.
Katika mjadala huo, Dkt. Biteko amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini za mara kwa mara ili kubaini kiwango cha uendelevu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan baada ya wananchi kuwezeshwa kupata teknolojia na miundombinu husika.
Amesema tathmini hizo zitasaidia Serikali na wadau kubaini changamoto zilizopo, kupima matokeo yaliyofikiwa na kuweka mikakati madhubuti zaidi ya kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Pia, Dkt. Biteko ameipongeza Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazochangia utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa miundombinu pamoja na kuendesha midahalo inayowakutanisha wadau kujadili namna bora ya kuharakisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu nchini.
Kodi ni chanzo muhimu cha mapato kinachoiwezesha serikali kufanikisha mipango na mikakati yake ya kimaendeleo kwa wananchi wake.
Wananchi wanahitaji huduma nzuri za kijamii kama elimu, afya, maji, umeme, barabara na masoko. Aidha, wanahitaji pia kuwezeshwa kiuchumi kwa kupatiwa mikopo nafuu ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha shughuli za kibiashara na za kiujasiriamali.
Ni kwamba, mambo haya mazuri na mengine mengi, hayawezi kufanikiwa endapo serikali haitakuwa na fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wao. Hapa ndipo umuhimu wa ulipaji kodi unapoonekana.
Kimsingi, pamoja na umuhimu wa ulipaji kodi kwa maendeleo, walipakodi wanazo changamoto ambazo wanahitaji kuziwasilisha serikalini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili ziweze kufanyiwa kazi.
Iko hivi: Ulipaji kodi unahusisha wadau wawili yaani TRA na walipakodi. Kutokana na hili, haitawezekana ulipaji kodi ukawa na ufanisi endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto zao kwa wakati.
Pia, kwa upande wa TRA, hawataweza kukusanya kodi kwa uendelevu mzuri ikiwa walipakodi wao wamesongwa na changamoto lukuki.
Ndiyo maana, kwa kutambua umuhimu wa pande zote kuwa na uhusiano mzuri na kufanikisha ulipaji kodi, TRA wameamua kuitenga siku ya Alhamisi ya kila wiki, nchi nzima, katika ofisi za wilaya na mikoa, kusikiliza kero za wafanyabiashara na walipakodi kwa ujumla.
Na hapa, Meneja Elimu Kwa Mlipakodi TRA, CPA Paul Walalaze, anasema, kutokana na umuhimu wa ulipaji kodi unaozingatia utu, siku ya Alhamisi imetengwa kwa upekee kabisa, kuhakikisha walipakodi wanawasilisha changamoto zao kwa uwazi ili kupata ufafanuzi na ufumbuzi wake.
"Hatuwezi kufanikiwa ukusanyaji kodi kama walipakodi wetu wamesongwa na changamoto. TRA imetenga siku hii ya Alhamisi, wafanyabiashara watoe changamoto zao, maoni na ushauri ili azma ya kukuza maendeleo nchini kwetu ifanikiwe," amesema.
Ameongeza kuwa, "Sasa, siku ya Alhamisi imekuwa jukwaa muhimu kwa walipakodi nchini. Ni siku ambayo walipakodi wanaonana na maofisa mapato kueleza changamoto zao, kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kikodi na kibiashara ili kuweza kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri zaidi".
Ikumbukwe kuwa, mwelekeo wa serikali ni kujitegemea kibajeti kwa asilimia kubwa. Mwelekeo huu umejengwa katika misingi kuwa, nchi inajengwa na wananchi wenyewe.
Pamoja na ukweli kuwa, serikali haitaacha kupokea misaada kutoka kwa wadau na wabia wa maendeleo, lakini misaada hiyo itukute tukiwa katika safari yetu ya kujisimamia na kujitegemea kibajeti kufanikisha miradi ya maendeleo na ya kimkakati.
Ukweli ni kwamba, hatutaweza kufikia dhamira hii njema, endapo walipakodi hawatatatuliwa changamoto zao, ikizingatiwa kuwa walipakodi ndiyo waliobeba hatma ya maendeleo ya nchi kupitia ulipaji kodi.
Kwa kusisitiza hili, CPA Walalaze amesema, "Ewe mlipakodi mwenye changamoto, itumie siku ya Alhamisi kuwasilisha changamoto yako ili ipatiwe ufumbuzi. Utatuzi wa kero za kikodi utawezesha ulipaji kodi kufanyika vizuri na kujenga uhusiano mzuri baina ya Mamlaka na walipakodi wao".
Kwahiyo, mlipakodi hana sababu ya kulalamika, analo jukwaa rasmi la kuwasilisha changamoto zake kwa ufumbuzi zaidi. Utatuzi wa changamoto za walipakodi, utarahisisha ulipaji kodi wa hiari na kuharakisha maendeleo ya wananchi.
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani kupitia GIZ imezindua awamu ya pili ya mpango wa Akili Bandia unaolenga kuwajengea uwezo wananchi kutumia teknolojia ya AI katika kutatua changamoto mbalimbali na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayesimamia Miundombinu, Uzalishaji, Jamii na Siasa, Mhe. Aguer Ariik Malueth, amesema mpango huo ni sehemu ya juhudi za Jumuiya kuwaandaa vijana, watafiti na wajasiriamali kutumia fursa zinazotokana na maendeleo ya teknolojia ya Akili Bandia
Amesema awamu hiyo inalenga kuwafikia zaidi ya wananchi 20,000 kutoka nchi wanachama wa EAC kupitia mafunzo ya AI, huku ikiweka mkazo katika kukuza vipaji, ubunifu na utafiti ili Afrika Mashariki iweze kujenga uwezo wa ndani na kushindana katika uchumi wa kidijitali duniani
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Afrika Mashariki na Kati katika BMZ, Joachim Schmitt, amesema Ujerumani inaona umuhimu wa nchi za EAC kuwa na mwelekeo wa pamoja katika maendeleo ya teknolojia ya AI, akibainisha kuwa uwekezaji mkubwa uliofanyika barani Afrika bado haujasambaa kwa usawa katika nchi zote
Naye Mkurugenzi wa Uvumbuzi na Teknolojia wa Kundi la Equity, Winnie Mangeni, amesema ushirikiano huo utatoa nafasi kwa wanafunzi, watafiti na wabunifu kutengeneza suluhisho zinazotumia AI katika sekta ya fedha na maeneo mengine yenye umuhimu kwa maisha ya wananchi wa Afrika Mashariki
Katika hatua nyingine, waandaaji wametenga Dola za Marekani 50,000 kwa ajili ya kuzisaidia timu zitakazofanya vizuri katika shindano hilo, huku mwaka huu kukiwa na kipengele maalum kinachowaalika wabunifu kutumia AI katika kusaidia kugundua, kuzuia na kukabiliana na milipuko ya magonjwa, ikiwemo Ebola
Mpango huo pia unalenga kuimarisha ufundishaji na utafiti katika vyuo vikuu, kuongeza ujuzi wa kidijitali na kusaidia nchi wanachama kujenga sera zinazofanana kuhusu matumizi ya Akili Bandia, huku ukizingatia usawa wa kijinsia na kuhakikisha teknolojia hiyo inawanufaisha wananchi kwa upana zaidi.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanachama wa Chama hicho katika Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.
Shamra shamra za Mapokezi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali itaendelea kutenga rasilimali za kutosha ili kuhakikisha skuli zote zinakuwa na miundombinu ya kisasa, walimu wenye sifa, na vifaa stahiki vya kufundishia na kujifunzia.
Makamu wa Rais amesema hayo, wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Jengo la Dakhalia katika Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame iliyopo Kibuteni Unguja, Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra ya Tamasha la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026). Amesema jitihada za Serikali katika kuimarisha miundombinu ya elimu ni endelevu ambazo zinajumuisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia, samani na upatikanaji wa walimu wenye sifa.
Makamu wa Rais amesema lengo la uwekezaji huo, ni kuandaa vijana wenye maarifa, ubunifu na ujuzi utakao wawezesha kujitegemea na kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa Taifa. Amewasihi kutunza Dakhali hiyo na miundombinu mingine ya elimu kwa umakini mkubwa. Ametoa rai kwa Wananchi, Wazazi na walezi wa eneo hilo kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuwahimiza vijana kusoma kwa bidi na kulinda miundombinu ya elimu ya eneo hilo.
Aidha, Makamu wa Rais amesema mageuzi makubwa yaliyofanyika katika sekta ya elimu Zanzibar na Tanzania kwa ujumla yamekuwa na matokeo mengi chanya, ikiwemo kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika ngazi mbalimbali za elimu, kuimarika kwa miundombinu ya ufundishaji na ujifunzaji, ambako kumesababisha kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya kitaifa.
Amesema Dakhalia hiyo iliyofunguliwa ni sehemu ya miradi lukuki inayotekelezwa Zanzibar yenye lengo la kukuza na kuendeleza sekta ya elimu na kuifanya kuwa ya mfano wa kuigwa kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu, na miundombinu ya kisasa kote visiwani.
Vilevile, Makamu wa Rais amesema ufunguzi wa dakhalia hiyo unakwenda kutatua moja ya changamoto kubwa iliyokuwa inawakabili wanafunzi ya kutembea umbali mrefu na kutumia muda mwingi kwenda na kurudi skuli. Pia mazingira mazuri yanayotokana na kuwepo kwa dakhalia hiyo yataongeza umakini, nidhamu, na ushirikiano wa karibu miongoni mwa wanafunzi, ambapo pia ni fursa nzuri kwa walimu kuwasimamia, kuwalea, na kuwasaidia kikamilifu katika masomo yao ya kila siku.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar Mhe. Lela Mussa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeendelea juhudi za kuboresha elimu ikiwemo kusudio la kuondoa utaratibu wa wanafunzi kusoma katika awamu mbili yaani mchana na jioni ambao umekuwa ukiwaathiri katika elimu zingine ikiwemo masuala ya kidini.
Amesema uwekezaji wa Serikali ya Awamu ya Nane katika elimu unajidhihirisha wazi ambapo bajeti ya elimu imetoka bilioni 256 hadi kufikia trilioni 1.1 ikiwa ni uwekezaji mkubwa wa serikali kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi ya kutekeleza malengo endelevu ya dunia katika nyanja ya elimu.
Ujerumani kupitia Shirika lake la Maendeleo (GIZ) imeahidi kutoa jumla ya Euro milioni 39.8 kwa ajili ya kuimarisha biashara ya kikanda na ushirikiano wa kiuchumi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya kukamilika kwa mazungumzo ya ushirikiano wa maendeleo kati ya pande hizo mbili
Akizungumza katika kikao na ujumbe wa Ujerumani, Katibu Mkuu wa EAC, Balozi Stephen P. Mbundi, ameipongeza Serikali ya Ujerumani kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa Jumuiya hiyo, akisema mchango wake umekuwa na nafasi kubwa katika kuimarisha mchakato wa ushirikiano na maendeleo ya kikanda
Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayesimamia Masuala ya Forodha, Biashara na Fedha, Annette Ssemuwemba, amesema msaada huo umefika wakati muhimu kwa Jumuiya hiyo ikiwa katika hatua za utekelezaji wa Mkakati wake wa Saba wa Maendeleo, unaolenga kuongeza biashara, uwekezaji na fursa za kiuchumi kwa nchi wanachama
Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Afrika Mashariki na Kati katika Wizara ya Shirikisho ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani (BMZ), Joachim Schmitt, Afrika Mashariki ni miongoni mwa maeneo yenye kasi kubwa ya ukuaji wa biashara, hali inayolifanya kuwa eneo lenye mvuto kwa wawekezaji kutoka Ujerumani na Ulaya
Schmitt amesema sehemu ya fedha hizo italenga kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa biashara ndogo na za kati katika EAC, kupitia ushirikiano wa benki ya maendeleo ya Ujerumani na Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, huku hatua nyingine zikilenga kukuza ushiriki wa sekta binafsi na maendeleo ya mnyororo wa thamani
Aidha, washirika hao wamekubaliana kuendeleza ushirikiano katika maeneo mbalimbali yakiwemo biashara, teknolojia na mabadiliko ya kidijitali, afya, usimamizi wa maji ya mipakani, asasi za kiraia na maendeleo endelevu ya kiuchumi, kwa kushirikisha nchi wanachama, Umoja wa Ulaya, sekta binafsi na washirika wengine wa maendeleo
Katika fedha hizo, Euro milioni 4.8 zimetengwa kwa ajili ya kuimarisha maandalizi na mwitikio dhidi ya mlipuko wa Ebola kupitia mradi wa EAC/GIZ wa Support to Pandemic Preparedness in the EAC Region (PanPrep). Fedha hizo zitatumika katika mafunzo ya wahudumu wa afya, vifaa vya kujikinga, maandalizi ya upatikanaji wa chanjo na dawa, pamoja na uhamasishaji wa jamii kuhusu kinga na chanjo, kwa ushirikiano na Sekretarieti ya EAC, nchi wanachama, Africa CDC na WHO.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), amefanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Shirika la Tanzania Automotive Technology Centre (TATC), maarufu kama NYUMBU, lililopo Kibaha, Mkoa wa Pwani, kwa lengo la kujionea utendaji na utekelezaji wa majukumu yake.
Katika ziara hiyo, alitembelea maeneo mbalimbali ya shirika hilo linalomilikiwa na JWTZ na kuzungumza na uongozi wake ukiongozwa na Mwenyekiti, Luteni Jenerali na Balozi mstaafu Paul Meela. Dkt. Nyansaho aliupongeza uongozi wa NYUMBU kwa kazi zinazofanyika na kusisitiza shirika hilo liendelee kuongeza mchango wake katika uchumi, maendeleo ya teknolojia na ustawi wa Taifa.
TATC (NYUMBU) ni shirika la umma chini ya Wizara ya Ulinzi na JKT linalojihusisha na utengenezaji, ukarabati na ubunifu wa teknolojia katika eneo la vyombo vya moto, vipuri na vifaa vya uhandisi.
Yanga Day at Uhuru Stadium shows how SportPesa backs football beyond matchday
Yanga Day at Uhuru Stadium shows how SportPesa backs football beyond matchday
On Sunday, August 9, 2026 thousands of Young Africans SC supporters filled Uhuru Stadium as the club marked its 91st anniversary and introduced its squad and technical team for the 2026/27 season. The celebration combined player presentations, speeches, music and fan activities before Yanga faced Les Aigles du Congo in an international friendly. For SportPesa Tanzania, Yanga’s main sponsor since 2017, the event provided a live demonstration of how long-term football support can extend beyond branding on a match shirt.
Tickets had been offered at TZS 20,000 for Mzunguko, TZS 100,000 for VIP and TZS 300,000 for Royal seating. Outside the stadium, SportPesa set up a truck and provided a free live screening of the match. Dancers entertained supporters, while free merchandise was distributed during the match. SportPesa director Abbas Tarimba also attended to represent the sponsor and support the club, making Yanga Day a direct meeting point between the brand, the team and its supporters.
Yanga Day as a season launch
Green and yellow colours covered the stadium and surrounding areas as supporters welcomed the new squad under the theme “Mwakani Tena”. One of the most anticipated introductions was Namibia international Peter Shalulile, whose arrival has increased expectations around Yanga’s attack. The pre-match programme also gave the occasion its festival atmosphere, with DJ Ally B and artists including Chid Benz, T.I.D, Madee, Chege, Q Chilla, Mr Blue, Dogo Paten and Click Master entertaining the crowd.
Yanga Day, also known as Mwananchi Day, has evolved into a major football and entertainment event in Tanzania’s sporting calendar. The previous edition marked the club’s 90th anniversary at Benjamin Mkapa Stadium and featured a friendly against Kenya’s Bandari FC. This year’s move to Uhuru Stadium preserved the event’s central purpose: bringing the team and its supporters together before the new campaign.
The result provided an early test for the new squad
Yanga began the friendly strongly and took the lead in the 27th minute when Shalulile converted a penalty on his debut. Les Aigles responded nine minutes later through Tonny Talasi after the hosts failed to clear the danger inside their penalty area. Talasi struck again in the second half to complete the visitors’ comeback and give the Congolese side a 2–1 victory.
Coach Manqoba Mngqithi made several changes after the interval as he assessed different combinations across the squad. Although the result disappointed the home crowd, it gave the technical team an immediate view of the defensive work required before competitive football begins. The match showed why a season launch must balance celebration with an honest test of readiness.
Five consecutive titles raise expectations
Yanga entered the event as five-time consecutive league champions after a 3–0 win over JKT Tanzania secured the latest title. The club finished with 75 points, only two ahead of Simba SC, underlining how narrow the margin for another championship could be. New players must now meet the standards behind that run, while the technical team must turn the energy of the season launch into results.
The SportPesa Yanga partnership adds further significance to that challenge. The new signings must uphold the standards that produced five consecutive titles, while the technical staff must demonstrate that the club’s hunger remains strong. For supporters who closely follow Yanga’s fixtures and results, the event offered the first collective view of the team preparing to carry that pressure into the new season.
A sponsorship beyond the shirt
The partnership between Yanga SC and SportPesa began in 2017 and entered a new phase through a three-year renewal valued at TZS 21.7 billion. The agreement supports the men’s first team, the women’s team and grassroots football within the club. SportPesa also awarded a TZS 262.5 million bonus after Yanga secured its fourth consecutive league title.
These details show why sustainable sponsorship is about more than visibility. Reliable resources, technical planning and clear development pathways allow a club competing domestically and across Africa to plan effectively and invest at multiple levels. At Uhuru Stadium, the truck screening, dancers, merchandise distribution and Tarimba’s attendance made that relationship tangible for supporters, including those who followed the match from outside the venue.
“Yanga Day is more than a seasonal launch. It is a celebration of the supporters, the players and the football structure that keeps the club moving forward. Our partnership with Yanga goes beyond matchday visibility because it supports the men’s team, women’s football, grassroots development and the wider growth of Tanzanian football,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.
Beyond Tanzanian football opportunities
Yanga’s recent achievements show why the occasion matters beyond domestic success. The club reached the CAF Confederation Cup final and narrowly lost the title to USM Alger on the away-goals rule after a 2–2 aggregate score. That run demonstrated the continental reach Tanzanian clubs can achieve when strong performance, passionate support and stable management work together.
Yanga Day gave SportPesa Tanzania a live platform to show that football sponsorship is not only about shirt branding. It is about supporters, visibility, development and long-term club ambition. The partnership gives Yanga a foundation stretching from the men’s first team to women’s football and grassroots programmes, turning the event into a bridge between past success and the demands of a new season.
Conclusion
Yanga Day at Uhuru Stadium brought together celebration, supporter engagement and an early sporting test. The 2–1 defeat offered Yanga lessons before the new campaign, while the entertainment, free screening and merchandise distribution showed how SportPesa’s role can extend beyond shirt visibility. By supporting the senior team, women’s football, grassroots development and fan experiences, SportPesa continues to connect Yanga’s recent success with the demands of its next season.