Mkutano Mkuu wa 12 wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri Tanzania Bara (REDEOA) umeendelea kufanyika jijini Arusha kwa siku saba tangu ulipofunguliwa rasmi Machi 2, 2026 na Waziri wa Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Profesa Riziki Shemdoe.

Mkutano huo unawakutanisha Maafisa Elimu pamoja na wadau wa sekta hiyo kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha utendaji na kuongeza matokeo chanya katika sekta ya elimu nchini.

Akiwasilisha mada kuhusu Itifaki na Tabia Njema, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dk. Maulid J. Maulid, amesema viongozi wanapaswa kuishi kwa kuzingatia misingi ya nidhamu, tabia njema na utii kwa sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utendaji wa shughuli za kisekta.

Amesema kuzingatia itifaki na maadili mema kutaimarisha mahusiano kati ya wadau na wasimamizi wa sekta ya elimu na kusaidia kufanikisha malengo ya kisera yaliyowekwa na Serikali.

“Taswira njema ya utumishi wa umma hujengwa katika misingi ya nidhamu, tabia njema na uwajibikaji,” amesema Dk. Maulid.

Aidha, amesisitiza kuwa uimarishaji wa itifaki utaongeza weledi na uwajibikaji miongoni mwa viongozi wa elimu, hali itakayochangia kuleta ufanisi zaidi katika taasisi wanazozisimamia.

Amehitimisha kwa kuwataka viongozi hao kuwa mabalozi wazuri wa maadili na utaratibu katika maeneo yao ya kazi ili kuongeza tija na kuchochea maendeleo ya sekta ya elimu na Taifa kwa ujumla.







Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk.Dorothy Gwajima amewatoa rai kwa wanawake watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wawe vinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Dk.Gwajima ametoa rai hiyo leo Machi 4,2026 wakati wa kongamano la wanawake wa TANESCO, ambapo amesema pia shirika hilo lina mchango mkubwa katika maendeleo endelevu ya taifa na ustawi wa wanawake, hasa kupitia upatikanaji wa umeme unaorahisisha maisha na kuinua uchumi wa familia.

Akieleza zaidi amesema ajenda ya nishati safi ya kupikia ni ya kitaifa na haiwezi kufanikiwa bila ushiriki wa sekta zote, akiwemo wanawake wa TANESCO.

“Bila umeme wa uhakika katika kaya nyingi, mwanamke ataendelea kubeba mzigo wa kutumia kuni na mkaa, hali inayohatarisha afya na kupoteza muda wa kushiriki shughuli za maendeleo.

“Takwimu za Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 zinaonesha asilimia 81 ya kaya nchini bado zinatumia kuni na mkaa kupikia.Asilimia 55 hutumia kuni na asilimia 26 mkaa,”amesema Dk.Gwajima na kuongeza hali hiyo ni changamoto kubwa inayohitaji mapinduzi ya haraka ya fikra na utekelezaji wa mikakati madhubuti.

Aidha amesema matumizi ya umeme kwa kupikia bado ni madogo, yakifikia takribani asilimia 4.3 tu, huku gesi ikitumiwa na asilimia 9.4 ya kaya. “Nitoe rai kwa TANESCO kushirikiana na wizara yetu na wadau wengine kuhakikisha takwimu hizo zinabadilika kabla ya mwaka 2034.”

Amewakumbusha Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, tayari alishazindua mkakati wa Taifa wa nishati safi ya kupikia wenye lengo la kufikisha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034.

Pamoja na hayo amesema zipo dhana potofu kwamba kupikia kwa umeme ni gharama kubwa, lakini ukweli teknolojia ya sasa imeleta majiko yanayotumia umeme kidogo na kwa gharama nafuu.

Katika hatua nyingine amesema wizara yake itashirikiana na maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata na vijiji kupeleka elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya umeme kupikia lengo likiwa ni kubadili mitazamo hasi na kuhamasisha jamii kukumbatia mabadiliko hayo.

Wanahabari wametakiwa kuwa daraja la kuifikisha kwa umma mikakati na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ili kuhakikisha kunakuwepo uelewa wa pamoja utakaowezesha ustawi wa pamoja wa Taifa kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.

Wito huo umetolewa na Mgeni Rasmi, Tausi M. Kida, ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais–Mipango na Uwekezaji, na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, wakati akifungua mafunzo maalumu ya wanahabari kuhusu Dira 2050.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Dkt. Kida amesisitiza kuwa mafanikio ya utekelezaji wa Dira 2050 yanategemea kwa kiasi kikubwa namna wananchi wanavyoielewa, kuikubali na kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.

Amesema wanahabari wana nafasi ya kipekee katika kufafanua sera, mikakati na vipaumbele vya maendeleo kwa lugha rahisi na inayoeleweka kwa umma.

Kaulimbiu ya mafunzo hayo, “Uelewa wa Pamoja kwa Ustawi wa Pamoja,” inasisitiza dhamira ya kuhakikisha kila Mtanzania anafahamu mwelekeo wa Taifa na nafasi yake katika kuifikisha Tanzania tunayoitaka ifikapo mwaka 2050.





Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), yatakiwa kuongeza kasi ya urasimishaji wa biashara na kuimarisha mifumo ya kidijitali ili kuchochea ufanisi na ukuaji wa uchumi kwani BRELA ni lango kuu la uwekezaji nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga (Mb), Machi 04, 2026, wakati akifungua Baraza la wafanyakazi la BRELA na kuhimiza uwekezaji kwenye rasilimali watu, akitaka watumishi wapewe mafunzo na stahiki zao kwani ustawi wa wafanyakazi ndio siri ya mafanikio ya taasisi, na kuwataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu, weledi, na uzalendo.

Waziri Kapinga amebainisha kuwa kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za wadau, zaidi ya 80% ya biashara nchini zipo sekta isiyo rasmi, hivyo BRELA lazima iwe kinara wa kuzirasimisha, hatua ambayo itawawezesha Wajasiriamali wadogo kupata mikopo, masoko, na ulinzi wa kisheria.

Aidha, ameagiza kuhuisha mifumo ya TEHAMA ili iwe rafiki itakayopunguza gharama pamoja na muda wa mteja kupata huduma na kusisitiza kuwa mifumo hiyo lazima iwe na usalama wa taarifa wa hali ya juu na itumike kupata mrejesho wa haraka kutoka kwa wateja ili kuboresha utendaji.

Aidha, ameipongeza BRELA kwa ongezeko la usajili na makusanyo, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyakazi na kuitaka taasisi hiyo kugeukia mfumo wa uwezeshaji badala ya udhibiti pekee ili kukuza sekta binafsi nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa BRELA Bw. Godfrey Nyaisa amebainisha kuwa BRELA imevuka lengo la mapato kwa asilimia 105 na kutekeleza malengo kwa asilimia 78 katika nusu mwaka wa 2025/26, ambapo taasisi hiyo imewasilisha Shilingi bilioni 3.1 kwa Msajili wa Hazina, na kusema mafanikio hayo yanayotokana na mshikamano, kujituma na bidii ya watumishi.

Vilevile, amewasilisha Mpango Mkakati wa 2026–2031 unaolenga kuboresha za usajili na miundombinu, ikiwemo ujenzi wa ofisi za Dodoma na Kinondoni na kubainisha kuwa uongozi unaendelea kuimarisha maslahi ya watumishi kupitia muundo mpya wa mishahara na motisha ili kutatua changamoto za uhaba wa wafanyakazi na kuongeza tija.






Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akizungumza na menejimenti ya Kiwanda cha Keds Tanzania Co. Ltd kinachozalisha bidhaa mbalimbali za usafi katika ziara ya kikazi Mkoani Pwani.

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Rahma Kisuo, ameziagiza menejimenti za viwanda Mkoani Pwani kuboresha mazingira ya kazi namaslahi ya wafanyakazi ili kuwa na uzalishaji endelevu na wenye tija.

Ametoa agizo hilo katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa sheria mbalimbali za kazi ikiwemo Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 katikamaeneo mbalimbali ya kazi Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika viwanda vilivyotembelewa, Naibu Waziri Kisuoamesema pamoja na viwanda hivyo kufanya kazi nzuri ya uzalishaji na kutekelezasheria za kazi, ziara yake imabaini dosari ndogo ndogo zinazopaswa kurekebishwa nawahusika.

“Tumetembelea baadhi ya maeneo katika viwanda hivi na kujionea hali ilivyo. Kimsingiwanafanya vizuri japokuwa kuna kasoro chache tulizozibaini ikiwemo baadhi yawafanyakazi kutokuwa na mikataba ya ajira pamoja na kutokidhi baadhi ya viwango vyausalama na afya mahali pa kazi,” amesema Naibu Waziri Kisuo.

Amewaagiza watendaji kutoka Ofisi yake na Mamlaka nyingine za udhibiti, kutengamuda maalum wa kufanya ukaguzi wa kina katika viwanda hivyo ili kutoa ushauri stahikiwa maboresho yanayohitajika kwa wawekezaji.

Aidha, amewapongeza wamiliki wa viwanda husika kwa uzalishaji wenye mchangomkubwa katika uchumi wa nchi kupitia kodi inayolipwa serikalini pamoja na kuzalishaajira nyingi kwa Watanzania.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, ambaye aliambatana na Naibu Waziri katika ziara hiyo, ameeleza baadhi yamapungufu yaliyobainika katika mifumo ya usalama na afya ya viwandavilivyotembelewa ikiwa ni pamoja na mazingira ya kazi yenye joto kali, vumbi la makaaya mawe kutapakaa katika mazingira, upungufu wa vifaa kinga na ukosefu wa alama za usalama.

Amemhakikishia Naibu Waziri kuwa watalaam wake watashirikiana na mamlakanyingine kufanya ukaguzi wa kina ambao utawezesha wawekezaji kupata ushauriunaohitajika ili kuboresha mazingira yao ya uzalishaji.

Kwa upande wao, viongozi wa viwanda vilivyotembelewa akiwemo Bw. Jacob Lerise, Msimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala katika Kiwanda cha uundaji magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd, wamemshukuru Naibu Waziri na watendaji wake na kuahidikutekeleza maagizo mbalimbali yaliyotolewa katika ziara hiyo.

Ziara hiyo ya siku mbili Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imefanyika katika kiwanda cha bidhaa za usafi cha Keds Tanzania Co. Ltd, Aluminium Trailers Ltd ambao ni waundajiwa trela za malori, kiwanda cha kuunda magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd pamojakiwanda cha sabuni na vipodozi cha Creative Intertraders Ltd.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akitembelea maeneo mbalimbali katika Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026. Alioambatana nao ni Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, Mkurugenziwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma na Watendaji wenginekatika Ofisi ya Waziri Mkuu.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akiongea na wafanyakazi wa Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakati waziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026. Alioambatana nao ni Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Watendajiwengine katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano).

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Watendaji wengine katika Ofisi yaWaziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) wakifuatilia maelekezo ya Naibu Waziri waNchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo (hayupopichani), wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akiangalia bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakatiwa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akiongea na wafanyakazi wa Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakati waziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026. Alioambatana nao ni Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Watendajiwengine katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

Wafanyakazi wa kiwanda cha bidhaa za usafi cha Keds Tanzania Co. Ltd wakimsikilizaNaibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani,Machi 2-3, 2026.

Wanawake wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dar es Salam  wametembelea Gereza la Segerea na kutoa misaada mbalimbali kwa wafungwa, ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8.

Ziara hiyo pia imekuwa muendelezo wa maadhimisho ya miaka 25 ya chuo hicho, ambapo taasisi imekuwa ikitekeleza shughuli za kurejesha kwa jamii kupitia matendo ya kijamii na misaada kwa makundi yenye uhitaji.

Akizungumza wakati wa kukabidhi misaada hiyo, Zena Hussein, Meneja wa Sehemu ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao TPSC, aliyemwakilisha Mkuu wa Chuo, amesema wanamshukuru Mkuu wa  chuo kwa kuwawezesha kutekeleza jukumu hilo la kijamii, akieleza kuwa lengo ni kuonyesha upendo na mshikamano kwa wafungwa kama sehemu ya jamii.

Amesema kuwa, kama wanawake wafanyakazi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, wameona umuhimu wa kutambua kundi hilo na kujitoa kwa moyo wa huruma wakiamini kuwa si kila aliyepo gerezani ni mkosaji wa kukusudia, bali baadhi yao wamejikuta katika mazingira magumu yasiyotegemewa. Ameongeza kuwa misingi ya dini, kwa Waislamu na Wakristo, inahimiza kusaidia wahitaji na kuwa watoaji, hivyo wameamua kupeleka kile walichoweza kumudu.

Miongoni mwa misaada iliyotolewa ni sukari, mchele, unga, maharage, maji, dawa za usafi, khanga, mashuka ya watoto, ndala, mifagio, dawa za meno, mafuta ya kupaka, pedi za wanawake, nepi za watoto, maziwa ya watoto, vitabu vya dini ikiwemo Qur’an na Biblia pamoja na nguo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Gereza la Wanawake Segerea, SSP Hamida Mussa Matimba, ameishukuru TPSC kwa msaada huo akisema vitabu vya dini vitakuwa nguzo muhimu katika kuwajenga wafungwa kiimani na kuwasaidia katika mchakato wa mabadiliko chanya.

Alieleza kuwa gereza hilo linaendesha programu mbalimbali za mafunzo ya ufundi stadi ikiwemo ushonaji, upishi, ufyatuaji wa matofali, ujenzi, ufundi magari na umeme, akisisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha kila anayeingia gerezani anatoka akiwa na mabadiliko chanya ya kiimani, kimaadili na kiujuzi ili aweze kujitegemea anaporejea uraiani.

Aidha, aliwahimiza wanawake kuwa na moyo wa kusamehe ili kupunguza migogoro inayoweza kuishia kwenye vyombo vya sheria, akitolea mfano wa migogoro ya madeni katika vikundi vya mikopo. Pia alitoa wito kwa wazazi kuwalea vijana, hususan mabinti, katika misingi ya maadili na kuwajenga kuridhika ili kuepuka tamaa zinazoweza kuwaingiza katika matatizo ya kisheria.

Kaulimbiu ya Siku ya Wanawake Duniani mwaka 2026 inasema: “Haki na usawa kwa wanawake na wasichana ni msingi jumuishi kufikia Dira 2050.” Ziara hiyo imeakisi dhamira ya wanawake wa TPSC ya kuadhimisha siku hiyo kwa vitendo vinavyogusa jamii moja kwa moja
Meneja wa Sehemu ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao TPSC,Zena Hussein (kushoto) akikabidhi
Meneja wa Sehemu ya Mafunzo kwa Njia ya Mtandao TPSC,Zena Hussein akizungmza wakati kukabidhi misaada huo.

Mkuu wa Gereza la Wanawake Segerea, SSP Hamida Mussa Matimba akizungumza  wakati wa kukabidhi misaada huo. 



Top News