Dodoma
RAIS wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania, Wakili Boniventure Mwambaja, amesema anaiona Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuwa ni miongoni mwa taasisi bora za maendeleo ya miundombinu barani Afrika kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwake mwaka 2017.

Wakili Mwambaja ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la TARURA katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa katika uwanja wa Dkt. John Malecela mkoani Dodoma.

Akizungumza baada ya kupata maelezo kuhusu shughuli na mafanikio ya wakala huo, amesema TARURA imeonyesha maendeleo makubwa katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi na matengenezo ya barabara za vijijini na mijini hatua ambayo imechangia kuboresha huduma za usafiri na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

"Ni dhahiri kuwa TARURA imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa majukumu yake ya ujenzi na matengenezo ya barabara tangu kuanzishwa kwake. Vilevile, imefanikiwa kuwajengea uwezo watumishi wake wanaosimamia miradi mbalimbali jambo linalodhihirishwa na mrejesho chanya kutoka kwa wananchi", amesema Wakili Mwambaja.

Ameongeza kuwa ongezeko la mtandao wa barabara zinazopitika katika maeneo mbalimbali nchini pamoja na utatuzi wa haraka wa changamoto katika maeneo korofi ni ushahidi wa dhamira na ufanisi wa wakala huo katika kuwahudumia wananchi.

TARURA inaendelea kushiriki Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yenye kauli mbiu "Tambua Soko; Ongeza Tija kutekeleza Dira 2050" kwa kutoa elimu kuhusu majukumu yake, mafanikio yaliyofikiwa na huduma mbalimbali zinazolenga kuboresha miundombinu ya barabara za vijijini na mijini nchini.
 


Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule ameipongeza shule ya Green Acres ya jijini Dar es Salaam kwa kuwa ya kwanza kuanzisha klabu ya Uhamiaji.

Alitoa pongezi hizo akiwa shuleni hapo wakati akizindua klabu hiyo ambapo aliambatana na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Vicent Haule na Meya wa Kinondoni, Songoro Mnyonge.

Mtambule alisema Wilaya yake inashule Zaidi ya 200 hivyo watapita shule baada ya shule kushawishi kuhakikisha kila shule inakuwa na klabu ya uhamiaji kama moja ya mbinu ya kuwafanya watoto wakatae uhamiaji haramu tangu wakiwa wadogo.

“Tutapita kuhamasisha shule zianzishe utaratibu huo ili wanafunzi wote wajue masuala ya uhamiaji wakiwa wadogo, tunapenda wahamiaji lakini wanaofuata taratibu na sharia za nchi yetu kwa hiyo lazima tuwajenge watoto kuchukua wahamiaji haramu tangu huku chini,” alisema

“Hata mama nyumbani anapotengeneza keki anatengeneza ili watoto wake wale sasa wakija watoto wa jirani wakila ile keki watoto wako wakakosa haipendezi, lazima tuwatolee taarifa kwa viongozi watu tunaoona kwamba ukaazi wao hapa nchini unamashaka mashaka,” alisema

Alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ubungo itaibeba ajenda ya uhamiaji kama moja ya masuala nyeti kuhakikisha hakuna mtu anayeingia nchini na kukaa bila kufuata utaratibu kwenye wilaya hiyo.

“Kuna watu wanarubuniwa na vitu vidogo vidogo ili wawafiche hawa wahamiaji haramu, natoa wito tusithubutu kuwapa nafasi wahmiaji haramu kukaaa kwenye maeneo yetu kwasababu tukikubain umemficha tukamkamata nawewe utakakatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria,” alisema

DC alilishukuru Jeshi la Uhamiaji nchini chini ya Dk Anna Makakala kwa namna ambavyo limefanikiwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha linadhibiti wawhamiaji haramu.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge alisema kuanzishwa kwa klabu hiyo ni mafanikio makubwa sana kwani wanafunzi watakuwa na uwezo wa kufahamu madhara ya wahamiaji haramu tangu wakiwa wadogo.

“Nimuhimu sana kurithisha vijana hawa wadogo umuhimu wa kukataaa wahamiaji haramu kwasababu madhara yake yanajulikana, kuanzishwa kwa klabu hizi ni moja ya mambo ya msingi kabisa ya kupigiwa mfano,” alisema

“Nawapongeza Green Acres kwa uamuzi wa kukubali klabu hii kuzinduliwa hapa shuleni mmekuwa wa kwanza Mkoa wa Dar es Salaam, na kwa bahati nzuri shule hii iliasisiwa na mheshimiwa diwani wetu wa Magomeni Bujugo ambaye ametangulia mbele za haki lakini maono yake bado yanaishi,” alisema

Aidha, Meya Songoro alimpongeza Mkurugenzi wa shule ya Green Acres, Jackline Rushaigo kwa namna ambavyo amemudu kusimamia na kuendeleza maono ya baba yake kwa kuifanya shule hiyo kuendelea kuongoza kitaaluma.

Naye Mkurugenzi wa shule hiyo, Jackiline Rushaigo alilishukuru Jeshi la Uhamiani nchini kwa kuichagua shule hiyo kuwa ya kwanza kuanzisha klabu hiyo miongoni mwa maelfu ya shule zilizoko nchini.

“Mmeona namna tunavyolea vipaji vya wanafunzi wetu, tunajitahidi kuwalea kwenye maadili mem asana hata wanapokuwa nje ya shule wanakuwa watu wema sana na nawaahidi kuwa klabu hii itakuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu,” alisema

Alisema wameamua kuanzisha klabu hiyo hapo shuleni kama sehemu ya kuwajengea uzalendo wa kuipenda nchi yao na kukataa kuona watu wasio raia wakiishi nchini bila kufuata taratibu na sheria za nchi.





 
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda, ameshangazwa na kiwango cha ubunifu wa teknolojia zinazobuniwa na kuzalishwa na kampuni ya Mati Technologies baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Mhe. Pinda alitembelea banda hilo leo na kupokea maelezo kutoka kwa viongozi na wataalamu wa Mati Technologies kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo katika kubuni na kutengeneza teknolojia zinazolenga kuongeza tija katika sekta ya kilimo na maeneo mengine ya maendeleo.

Katika ziara hiyo, alikagua teknolojia mbalimbali zinazotengenezwa na kampuni hiyo, ikiwemo ndege nyuki zinazotumika kunyunyiza viuatilifu na mbolea mashambani kwa usahihi, haraka na ufanisi mkubwa, pamoja na mifumo mingine ya kisasa ya kiteknolojia inayolenga kuboresha uzalishaji wa kilimo.

Baada ya kushuhudia namna teknolojia hizo zinavyofanya kazi, Mhe. Pinda alisema ameridhishwa na hatua kubwa ya ubunifu iliyofikiwa na wataalamu wa Kitanzania.



“Ni jambo la kujivunia kuona Watanzania wakibuni na kuzalisha teknolojia za kisasa zinazotoa suluhisho kwa changamoto mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta ya kilimo,” alisema.

Alisema maendeleo hayo yanaonesha uwezo mkubwa wa wataalamu wa ndani katika kubuni teknolojia zinazokidhi mahitaji ya nchi na kuchangia kukuza uchumi kupitia sekta ya kilimo na viwanda.


Aidha, aliipongeza Mati Technologies kwa kuwekeza katika utafiti, ubunifu na uzalishaji wa teknolojia za ndani, akisisitiza kuwa juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono ili kuharakisha maendeleo ya taifa na kuongeza ushindani wa bidhaa za Kitanzania katika soko la ndani na kimataifa.

Kwa upande wake, uongozi wa Mati Technologies ulisema kampuni itaendelea kubuni na kuzalisha teknolojia zenye ubora wa hali ya juu zitakazorahisisha shughuli za uzalishaji, kuongeza tija kwa wakulima na kuchochea matumizi ya teknolojia katika sekta mbalimbali za uchumi.





Maonesho ya Nane Nane yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuonesha mafanikio ya sekta za kilimo, mifugo, uvuvi, viwanda na teknolojia, huku yakivutia maelfu ya wananchi, wakulima, wawekezaji, wanafunzi na wataalamu kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Kupitia ubunifu wa teknolojia zinazozalishwa hapa nchini, Mati Technologies inaendelea kujijengea sifa kama moja ya kampuni zinazochochea matumizi ya sayansi, teknolojia na utafiti katika kuongeza tija ya uzalishaji na kuchangia maendeleo endelevu ya Tanzania.








Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta akisaini Kitabu cha wageni, baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akimpigia makofi Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kusaini Kitabu cha wageni katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Mhe. Dkt. Musenero Masanza wa Uganda akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam,
tarehe 06 Agosti, 2026.





Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akutana na Kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu Jijini Dare es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa kati ya Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bw. Mussa Makame, Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bi. Proscovia Nabbanja pamoja na Kampuni ya Biashara ya Mafuta na Nishati ya Vitol ya Bahrain, chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Tom Baker.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuhitimisha ziara rasmi ambapo walishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli, amewapongeza Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa mchango wake mkubwa katika utoaji wa huduma za ujenzi na usimamizi wa majengo ya Serikali, akieleza kuwa taasisi hiyo imekuwa mshirika muhimu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya wizara.

Mweli ameyasema hayo Agosti 6, 2026, baada ya kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Kilimo Nanenane Kitaifa yanayoendelea jijini Dodoma, amesema Wizara ya Kilimo imefanya kazi nyingi kwa kushirikiana na TBA, ikiwemo usimamizi wa ujenzi wa maghala, usanifu wa jengo la wizara pamoja na usimamizi wa miradi hiyo kwa weledi na ubora wa hali ya juu.

Ameeleza kuwa TBA imeendelea kujidhihirisha kama taasisi yenye uwezo wa kutoa huduma za ujenzi na usimamizi wa majengo zinazokidhi viwango, si kwa taasisi za serikali pekee bali pia kwa sekta binafsi, jambo linalochangia kuimarisha miundombinu ya maendeleo nchini.

Mweli amewahimiza wananchi na wadau wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kuhakikisha wanapita katika banda la TBA lililopo eneo la Private Sector Pavilion, ili kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na wakala huo pamoja na kupata taarifa kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya ujenzi na usimamizi wa majengo.




Na Janeth Raphael -MichuziTv

Katika hatua ya kuimarisha ubora wa elimu nchini, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) umetangaza kuimarisha na kupanua mafunzo yanayolenga kuwajengea uwezo viongozi wa sekta ya elimu ili kuongeza ufanisi katika usimamizi wa shule na taasisi za elimu.

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 6, 2026, jijini Dodoma, Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid Maulid, amesema taasisi hiyo inaendelea kutekeleza mkakati wa kuwapa viongozi wa elimu maarifa na ujuzi wa kisasa unaowawezesha kukidhi mahitaji ya sekta ya elimu inayobadilika kwa kasi.

Amesema mafunzo hayo yanawahusisha wakuu wa shule, walimu wakuu, maafisa elimu wa kata, halmashauri na mikoa, pamoja na wathibiti ubora wa shule, kwa lengo la kuongeza uwajibikaji, kuimarisha utawala bora na kuboresha usimamizi wa rasilimali za elimu.

Kwa mujibu wa Dkt. Maulid, tangu kuanzishwa kwa programu ya Stashahada ya Uongozi, Usimamizi na Utawala katika Elimu (DELMA), wahitimu 8,599 wamehitimu kati ya mwaka 2002 na 2025. Aidha, wahitimu 2,263 wamekamilisha Stashahada ya Uthibiti Ubora wa Shule (DSQA) tangu mwaka 2016.

Katika mwaka wa masomo 2025/2026 pekee, ADEM ilidahili wanafunzi 2,016, huku wengi wao wakijiunga na programu ya DELMA, hatua inayoonesha kuongezeka kwa mahitaji ya mafunzo ya uongozi wa elimu nchini.

Dkt. Maulid amesema mafunzo hayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha utendaji wa viongozi wa elimu, kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika usimamizi wa shule na kuongeza uwajibikaji katika utoaji wa huduma za elimu.

Ameeleza kuwa kupitia Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Shule za Awali na Msingi (BOOST), ADEM imepokea zaidi ya shilingi bilioni 16 kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa elimu katika kipindi cha miaka mitano.

Kupitia mradi huo, zaidi ya walimu wakuu 17,817, waratibu elimu wa kata zaidi ya 3,900 pamoja na maafisa elimu wa wilaya na mikoa tayari wamenufaika na mafunzo hayo, yanayolenga kuboresha huduma za elimu katika shule za umma.

Mbali na mafunzo, ADEM inaendelea kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya sera za elimu, huku ikipanua ushirikiano na taasisi za ndani na nje ya nchi ili kuimarisha matumizi ya teknolojia na ubora wa mafunzo.

Kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ADEM imejipangia kuongeza udahili wa wanafunzi wa mafunzo ya muda mrefu hadi 3,500, kuanzisha programu mpya za mafunzo, kuboresha miundombinu ya kampasi zake za Bagamoyo, Mbeya na Mwanza pamoja na kupanua matumizi ya TEHAMA.

Hatua hizo zinatarajiwa kuongeza uwezo wa viongozi wa elimu kusimamia mageuzi ya sekta hiyo na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kujenga mfumo wa elimu wenye ushindani na unaokidhi mahitaji ya maendeleo ya taifa.







Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameupongeza Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kwa maboresho makubwa ya utoaji wa huduma, hususan matumizi ya teknolojia yanayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Msonde amesema hayo leo, Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la TEMESA katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.



Dkt.Msonde Amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofikiwa na TEMESA, akieleza kuwa uimarishaji wa huduma za kidijitali pamoja na ongezeko la ubora wa mafundi umeongeza ufanisi wa wakala huo.

“Kilichonifurahisha zaidi ni uimarishaji wa mafundi. Sasa wanafanya kazi kwa weledi mkubwa na wanatengeneza magari kwa ubora. Kwa kweli TEMESA mmenifurahisha sana,hongereni sana” amesema Dkt. Msonde.



Aidha, amesema Serikali na wananchi wanaiamini TEMESA kutokana na mchango wake katika kulinda usalama wa magari ya Serikali na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma. Amewataka viongozi na watumishi wa wakala huo kuendelea kubuni na kuboresha huduma kwa kutumia teknolojia.



Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma- TEMESA, Bi. Martha Joachim, amesema miongoni mwa maboresho yaliyofanywa ni kuhuisha huduma ya ukodishaji wa mitambo kupitia Mfumo wa TIMIS, ambapo wateja sasa wanaweza kuwasilisha maombi ya ukodishaji kwa njia ya kidijitali, hatua iliyopunguza urasimu na muda wa kupata huduma.



Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Tambua Soko, Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050”, yanatarajiwa kuadhimishwa tarehe 8 Agosti, 2026.






Top News