Mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Peramiho kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Lazaro Komba Bunungu, amechukua rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge katika jimbo hilo lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Dkt. Bunungu amesema amejiandaa kikamilifu kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Peramiho endapo atapewa ridhaa hiyo na wananchi.

 Ameeleza kuwa dhamira yake ni kushirikiana na wananchi katika kuwaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kupitia sera na mwelekeo wa Chama Cha Mapinduzi.

Aidha, amewashukuru wananchi wa Peramiho kwa sapoti na ushirikiano wao, huku akiwataka kuendelea kudumisha mshikamano na umoja wakati wa mchakato wa uchaguzi.

 Vilevile, amekishukuru Chama Cha Mapinduzi Taifa kwa imani waliyoonesha kwake kwa kumpa ridhaa kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mdogo Peramiho

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Songea Vijijini, Juma Nambaila, amewashukuru viongozi wa CCM kutoka kata zote 16 za jimbo hilo kwa mshikamano wao, akisema hali hiyo ni ishara ya ushindi wa chama hicho katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari.

Naye Mwenyekiti wa CCM Songea Vijijini, Thomas Masolwa, amempongeza Dkt. Bunungu kwa kuchukua fomu hiyo, akisema CCM imemuamini kuwa msimamizi wa masuala ya maji, umeme na barabara, pamoja na kuwa sauti ya wananchi wa Peramiho.













 

Waziri wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb.), ameielekeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuelekeza mipango na mikakati yake zaidi katika kuendeleza kilimo cha mazao ya chakula na biashara yenye thamani kubwa katika soko la kimataifa, ili kuongeza kipato cha wakulima, wafugaji na wavuvi pamoja na kukuza mchango wa sekta hizo katika uchumi wa taifa.

Aidha, Waziri huyo amesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika mazao ya misitu ikiwemo ufugaji wa nyuki, akieleza kuwa sekta hiyo ina fursa kubwa ya kiuchumi na mchango katika uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu.

Ushauri huo umetolewa leo, Februari 1, 2026, Jijini Dodoma, wakati Waziri wa Fedha alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania ulioongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Frank Nyabundege, ambapo pia alipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Benki hiyo.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Omar ameahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na TADB katika utekelezaji wa mikakati yake ya muda wa kati, kwa lengo la kuongeza tija na mchango wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi katika maendeleo ya kiuchumi ya nchi.

Pamoja na hayo, Waziri wa Fedha ameipongeza TADB kwa ufanisi wake wa kiutendaji na mchango wake mkubwa katika kuchochea maendeleo jumuishi na endelevu, hususan katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi pamoja na viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Frank Nyabundege, amesema Benki hiyo imeendelea kukua kwa kasi kifedha, ambapo mizania yake imeongezeka kutoka shilingi bilioni 362.8 mwaka 2021 hadi kufikia shilingi trilioni 1.3 mwaka 2025.

Bw. Nyabundege amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa Benki hiyo mwaka 2015, TADB imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.3 kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, hatua iliyochangia kuimarisha uzalishaji na kuongeza thamani katika mnyororo wa sekta ya kilimo nchini.

Ametoa shukrani kwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha kwa kuiwezesha Benki hiyo kwa mtaji, akieleza kuwa hatua hiyo inaonesha dhamira na utashi wa kisiasa wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuikuza na kuiendeleza sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji huyo ameiomba Serikali kuendelea kuiwezesha TADB kimtaji kupitia bajeti kuu ya Serikali pamoja na kuidhamini Benki hiyo ili iweze kufikia masoko ya kimataifa ya mitaji, kwa lengo la kuongeza uwezo wa kutoa mikopo kwa wakulima na wadau wengine wa sekta ya kilimo.
  











Na Mwandishi wetu- Dodom.

Waziri wa Uchukuzi Prof Makame Mbarawa amesema Wizara imekamilisha taratibu za kuanza upanuzi mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam wenye lengo la kujenga magati 10 pamoja na matenki 15 ya mafuta.

 Ujenzi wa magati mawili (2) ya awali yenye urefu wa mita 500 utaanza mwezi Juni, 2026 na huku ujenzi wa matenki ukiendelea kutekelezwa kwa mafanikio makubwa. 

Prof Mbarawa ameyabainisha hayo leo jijini Dodoma kwenye  Mkutano na Waandishi wa habari akieleza utekelezaji wa siku 100 za Serikali ya awamu ya sita kipindi Cha pili.

"Uboreshaji huu utaongeza uwezo wa Bandari ya Dar es Salaam kuhudumia shehena hadi tani milioni 50 kwa mwaka ndani ya kipindi kifupi, kutoka takribani tani milioni 32 za sasa"

Amesema  kuanza kwa maandalizi ya ujenzi wa Bandari kubwa na ya kisasa ya Bagamoyo, Awamu ya Kwanza ya mradi huo itahusisha ujenzi wa gati lenye urefu wa kilometa 1.32 kwa ajili ya kuhudumia meli kubwa za kisasa (Mega Max). 

Bandari hiyo ni ya kimkakati katika kupunguza msongamano wa Bandari ya Dar es Salaam na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji wa baharini katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Aidh Prof Mbarawa amesema katika hatua nyingine za kuendeleza huduma za bandari nchini, Serikali imeanza utekelezaji wa Mradi wa Kurasini Logistics Terminal, unaolenga kupunguza msongamano wa shehena katika Bandari ya Dar es Salaam na kuongeza miundombinu muhimu ya kuhudumia shehena inayoharibika haraka (perishables). 

Hat hivyo Prof Mbarawa amesema Mradi huo unahusisha ujenzi wa kituo cha kisasa cha kuhifadhi makasha kwa muda katika eneo la mita za mraba 210,000, chenye uwezo wa kuhifadhi hadi makasha 700,000.

Aidha  Prof Mbarawa ameelez kuwa kwa sasa, Awamu ya Kwanza ya ujenzi katika eneo la mita za mraba 81,000 inaendelea; 

Wizara imekamilisha maboresho ya Bandari za Kemondo na Bukoba katika Ziwa Victoria na bandari hizi zinatarajiwa kuwa kitovu muhimu cha usafirishaji kati ya Bukoba, Mwanza na bandari za Uganda.

"Hatua hii itaongeza biashara ya kikanda na kupunguza gharama za usafiri kwa njia ya maji;

Katika hatua nyingine, Serikali kupitia TPA inaendelea na ujenzi wa  bandari ya Kisiwa Mgao  Mtwara mradi ambao ni maalum kwa ajili ya kuhudumia shehena ya mzigo mchafu (Dirty Cargo) kama vile Makaa ya Mawe na Saruji. Kwa sasa, Mkandarasi anaendelea na utekelezaji wa mradi huu ambao hadi sasa umefikia asilimia 18 ya utekelezaji"

Hata hivyo amesema mukamilika kwa mradi huo kutaongeza ufanisi katika utendaji wa Bandari ya Mtwara na vile vile uimarishaji na utunzaji wa mizigo katika Ziwa Nyasa, Serikali kupitia TPA inaendelea kutekekeza mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay unaohusisha ujenzi wa gati ya kuhudumia shehena ya magari (RO-RO) na meli, jengo la Utawala, Uzio, Barabara, Jengo la Kuhifadhia Mizigo pamoja na Jengo la Abiria. Mradi huu kwa sasa umefikia asilimia 46 ya utekelezaji wake.




 

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Simba imelazimishwa sare 2-2 na Esperance de Tunis katika mchezo wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa Afrika.

Katika mchezo huo Simba Sc ilifanikiwa kuongoza kwa mabao 2-0 kipindi cha kwanza kupitia kwa Shomari Kapombe na Yusuf Kagoma na kwenda mapumziko wa wakiwa mbele.

Kipindi cha pili Esperance de Tunis waliingia wakilisaka lango la Simba sc nakufanikiwa kupata bao la kwanza baada ya Lassane Kante kutoa basi ambayo ilimpata mpinzani na kwenda kufunga bao ambalo liliwapa matumaini na kufanikiwa kupata bao la pili.

Kwenye mchezo huo pia Esperance de Tunis walipata penati dakika ya za mwisho wa mchezo lakini penati hiyo hawakuweza kupata bao.



Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (katikati) akikata utepe ishara ya kuzindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga - Picha na Kadama Malunde


Waziri wa Madini, Anthony Mavunde akipata maelezo wakati akizindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga

Helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde na viongozi ,mbalimbali wakishuhudia helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick ikiruka angani kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga

Helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick ikiwa angani

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde akizungumza wakati akizindua helikopta ya kisasa ya Kampuni ya Barrick kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga
Meneja wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa hafla hiyo.
**



Kampuni ya Barrick ambayo inaendesha shughuli zake kwa ubia na serikali kupitia Twiga Minerals leo imezindua helikopta ya kisasa kwa ajili ya kufanya utafiti wa kijiolojia wa anga wenye kupunguza athari za kimazingira na kuboresha shughuli za utafutaji wa madini nchini.



Akizungumza kwenye uzinduzi wa utafiti huo wa kutumia helikopta , Wilayani Kahama , Mkoani Shinyanga, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema kwamba hatua hii ni muhimu katika kuimarisha sekta ya madini ya nchini na kufungua milango ya tafiti kwa kutumia nyenzo za kisasa zaidi.

Waziri Mavunde amesema uwekezaji wa teknolojia ya kisasa ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa sera ya madini ya Taifa , inayolenga kuimarisha utafiti wa rasiliamali madini, kuongeza thamani ya sekta ya madini katika uchumi wa taifa, na kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa ufanisi zaidi.

“Moja ya hatua kubwa kwa kampuni ya Barrick nchini kwa kushirikiana na kampuni ya Twiga Minerals ya serikali katika kufanya tafiti zaidi kwa njia ya kisayansi zaidi kwa lengo la kupanua wigo wa maeneo mapya ya utafiti na uwekezaji kwenye sekta ya madini nchini,”ameongeza Mavunde.

Ameongeza kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria katika kufanya tafiti kwa njia ya helikopta kwa sababu utafiti wa madini ni sayansi inahitaji uwekezaji mkubwa.

"Kupitia Dira ya Madini 2030: Madini ni Maisha na Utajiri, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuelekeza kuhakikisha tunaongeza eneo la utafiti wa kina wa madini kupitia uwekezaji wa Serikali na Sekta binafsi"



"Tunachokifanya leo hapa ni kiashiria tosha kwamba maono hayo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yanakwenda kufikiwa ipasavyo. Tunaishukuru Kampuni ya Barrick kwa kuamua kuunga mkono juhudi hizi za Serikali kwa vitendo", ameeleza Mhe. Mavunde.

Amefafanua Kampuni ya Barrick imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye tafiti na baada ya uzinduzi wa helikopta utafiti wake utagusa maeneo ya Nzega, Igunga , Msalala na Nyangh’wale katika Mkoa wa Shinyanga.

“Naipongeza Barrick kwa kuendelea kuwekeza kwenye eneo la tafiti kwa sababu dunia ya leo huwezi kukwepa utafiti katika shughuli za utafutaji wa madini ,” amesema Mavunde.



Akiongea katika hafla hiyo, Meneja wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido amesema kwamba ni hatua kubwa kwa kampuni hiyo kwa kushirikiana na serikali katika uzinduzi wa helikopta ya kisasa ya utafiti wa kijiolojia wa anga, itakayosaidia shughuli za utafutaji wa madini kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu.

Ameongeza kwamba kampuni ya Barrick inatarajiwa kufanya tafiti ya kijiolojia wa kutumia teknolojia ya hali ya juu na kisasa zaidi (high-resolution airborne geophysical surveys) ambayo huongeza usahihi wa upatikanaji wa taarifa za miamba iliyo chini ya ardhi, kupunguza athari za kimazingira na kuboresha ufanisi wa shughuli za utafutaji wa madini.

Ngido amesema uzinduzi wa tafiti hiyo ambayo itatumia helikopta , unaakisi dhamira ya kampuni ya Barrick kuendeleza kuwekeza nchini na kutafuta maeneo yatakayofaa kuanzia mgodi mkubwa ili kuleta mchango wa muda mrefu kwa maendeleo ya taifa.

Aidha, amefafanua kwamba mchango wa Barrick katika utafutaji wa madini nchini , umeonekana kwa vitendo kupitia ushirikiano wake na serikali chini ya Wizara ya Madini na Taasisi zake, Barrick imekuwa mdau mkubwa katika shughuli za utafiti za kijiolojia , kutoa ushauri wa kitaalamu, na kuwezeha upatikanaji wa taarifa za kimsingi za madini.

Pamoja na mambo mengine , Dkt. Ngido ameongeza kuwa kwa taarifa za tafiti zisizofaa kwa uchimbaji mkubwa , serikali imekuwa inazitumia taarifa hizo kugawa maeneo kwa ajili wachimbaji wadogo na kuboresha ufanisi wao , sambamba na malengo ya serikali ya kurasimisha na kuendeleza sekta ya uchimbaji mdogo , mfano wa maeneo ambayo tafiti za Barrick zimetumiwa na wachimbaji wadogo , ni Majimoto , Komarera na Golden Ridge ambapo shughuli za wachimbaji wadogo zimekuwa na tija.

“Kwa kipindi cha miaka mitano tayari tumewekeza Shilingi bilioni 100 katika kufanya utafiti wa kisayansi ili kuweza kugundua maeneo mapya kwa ajili ya uwekezaji mkubwa,” amesema Dkt. Ngido.

Kwa upande wake , Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga , Mboni Mhita amesisitiza kuwa serikali ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji ili waendelee kufanya kazi zao kwa ufanisi ili serikali iendelee kukusanya mapato.

Uzinduzi huo ni sehemu ya uwekezaji endelevu wa Barrick na Twiga katika kuboresha mbinu za utafiti na ugunduzi wa madini , kwa lengo la kupanua wigo wa rasilimali za madini na kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Tanzania kwa kizazi cha sasa na kijacho.












Top News