DIWANI wa Kata Zingiziwa iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Salehe Kaniki ameendelea kugusa maisha ya makundi mbalimbali yenye uihitaji maalum.
Miongoni mwa makundi ambayo Diwani Kaniki ameyagusa na kuyafikia ni kundi la watu wenye mahitaji maalum ambapo leo Mei 22,2026 amekabidhi vitimwendo (baiskeli) viwili na viti vya kusukuma vitano na magongo kwa watu wenye ulemavu.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo Diwani Kaniki amesema amefanikisha kufikisha msaada huo kwa walengwa kupitia ushirikiano kati yake na wenyeviti wa Serikali za mtaa katika kata hiyo kwa kuorodhesha walengwa na leo wamekabidhi msaada huo.
“Tumekutana kwa dhumuni moja la kusaidia ndugu zetu wenye uhitaji maalum ambao hawawezi kutembea ,tumekabidhi baiskeli mbili na viti vya kusukuma vitano kwa ujumla wake tumewafikia watu saba lakini tumetoa na magongo ya kutembelea.
“Kwahiyo kuna magongo mengine tumeweka ya ziada lakini kuna wengine wamejitokeza na tumeandika majina yao ambao nao tutawapatia.Kwangu msaada huu pia ni sehemu ya sadaka katika jamii kwani mwezi kama huu wa tano nilimpoteza kaka yangu.
“Kwahiyo msaada niliotoa leo iwe ni sehemu ya sadaka kwake huko aliko na iwe dua nzuri na Mwenyezi Mungu ampunguzie adhabu za kaburini,”amesema huku akisisitiza waliopata baiskeli hizo zitawarahisishia katika safari na wale waliokuwa wanabebwa sasa waaachwe watumie baiskeli hizo.
Wakati huo huo Diwani Kaniki ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kupeleka miradi ya maendeleo kwani kwenye Kata hiyo ya Zingiziwa limejengwa bweni kwa ajili ya wenye uhitaji maalum ambalo ni la kisasa na hivi karibuni litazinduliwa.
“Kwahiyo kuna wengine wanafunzi wenye mahitaji maalum hasa wenye ulemavu wataingia katika mabweni hayo kwa ajili ya kuwawezesha kupata elimu kwa uzuri zaidi .Hivyo namshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na wakati huo huo namshukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwani fedha wanazotoa zinakwenda sehemu husika.”
Kwa upande wao baadhi ya waliopatiwa msaada huo akiwemo Pili Abdallah na Seif Mbedo wamemshukuru Diwani Kaniki kwa kuwapata msaada huo ambao unakwenda kutatua changamoto ya usafiri waliyokuwa wakiipata.



.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)


.jpg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)







