Hayo yameelezwa leo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (Tanzania International Arbitration Centre – TIAC), ndugu Godson Nyange wakakti akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbu wa Wakili House, Dar es Salaam ili kuhabarisha umma kuhusu matukio hayo ambayo yamepangwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 jijini Dar es Salaam
Ndugu Nyange amesema kuwa kongamano hilo litafanyika tarehe 27 Machi, 2026 na litaongozwa na kauli mbiu isemayo, “Kutoka Majadiliano hadi Hatua: Kuendeleza Ushirikishwaji wa Wanawake katika Utatuzi wa Migogoro kwa Njia Mbadala (“From Dialogue to Action: Advancing Women’s Inclusion in Alternative Dispute Resolution (ADR).”) Kongamano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Wakili House jijini Dar es Salaam na litawaleta pamoja wataalamu wa sheria, watunga sera, wanataaluma, viongozi wa biashara, wataalamu wa ADR pamoja na wataalamu kutoka kada mbalimbali ili kuzitathimini kwa kina hatua za kuongeza ushiriki wa wanawake katika utatuzi wa migogoro.
Pia, ameongeza kuwa kongamano hilo litatanguliwa na mafunzo yatakayofanyika tarehe 24 hadi 26 Machi, 2026 na yatafanyika kwenye ukumbi wa Wakili House jijini Dar es Saalam ambapo mafunzo hayo yataongozwa na mada isemayo, “Kujenga Uwezo na Kujiamini kwa Wanawake katika Utatuzi Mbadala wa Migogoro (ADR).”
“Kihistoria, Sekta ya Utatuzi wa Migogoro kwa Njia Mbadala (ADR) imekuwa ikitawaliwa zaidi na wanaume, huku wanawake wakiwa wachache katika nafasi za usuluhishi (arbitration), upatanishi (mediation) na majukumu mengine ya ADR hasa katika nafasi za juu za kufanya maamuzi. Hali hii imeonekana duniani kote na barani Afrika ambapo tafiti zinaonyesha kuwa takribani asilimia 72 ya wasuluhishi katika kesi zinazohusiana na Afrika ni wanaume, wakati asilimia 28 tu ni wanawake. Vilevile, wanawake wanawakilisha takribani asilimia 29 hadi 34 ya uteuzi wa wasuluhishi katika taasisi kubwa za kimataifa za usuluhishi,” amefafanua ndugu Nyange.
Akizungumza kwa niaba ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OWMS), Bi. Mercy Kyamba, Mkurugenzi Msaidizi – Sehemu ya Udhibiti Ubora wa Ofisi hiyo amesema kuwa OWMS inashirikiana na TIAC kuendesha mafunzo na kufanya kongamano hilo kwa kuwa OWMS pamoja na majukumu mengine, imekasimiwa na kupewa dhamana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusimamia na kuendesha mashauri ya usuluhishi ndani na nje ya nchi kwa niaba ya Serikali.
Bi. Kyamba amesema kuwa uwepo wa mafunzo hayo na kongamano hilo ni dhamira ya pamoja ya TIAC na OWMS ya kuimarisha nafasi ya wanawake katika usuluhishi (arbitration), upatanishi (mediation) na mifumo mingine ya ADR. Mafunzo hayo yataendeshwa na wataalam wabobezi wa ndani na nje ya nchi na yamelenga kuwapatia wanawake maarifa, ujuzi wa vitendo na kujiamini kunakohitajika ili kushiriki kikamilifu katika michakato ya ADR.
Pia, Bi. Kyamba ameongeza kuwa maeneo muhimu yatajadiliwa kwenye mafunzo hayo yanahusu misingi ya usuluhishi (arbitration) na upatanishi (mediation); ujuzi wa vitendo katika majadiliano na usimamizi wa migogoro; viwango vya maadili na wajibu wa kitaaluma katika ADR; njia za kujenga taaluma na kupata ithibati katika ADR; na mikakati ya kujenga kujiamini na uwepo wa kitaaluma katika mashauri ya utatuzi wa migogoro.
Aidha, amesema kuwa kwa upande wa Kongamano, linatarajiwa kuwa jukwaa la kiwango cha juu la kujadili namna ya kuongeza ushiriki wa wanawake katika ADR ambapo majadiliano ya jopo la wataalamu yatawakutanisha wadau mashuhuri ili kuchambua masuala muhimu yakiwemo nafasi ya wanawake katika kuimarisha mifumo ya ADR; msaada wa taasisi katika kukuza wanawake katika usuluhishi na upatanishi; kujenga mitandao ya kitaaluma na fursa za ulezi (mentorship) kwa wataalamu wapya wa ADR; na athari pana ya utofauti wa kijinsia katika utoaji haki na imani ya kibiashara.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TIAC, Bi, Magreth Magoma amesema kuwa mafunzo na kongamano hilo ni sehemu ya juhudi pana za TIAC za kukuza matumizi na maendeleo ya utatuzi mbadala wa migogoro nchini Tanzania na katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki na kutachangia katika kujenga mfumo madhubuti na unaoaminika wa utatuzi wa migogoro unaosaidia upatikanaji wa haki, uhakika wa biashara na kuimarisha uwekezaji.
Bi. Magoma ameongeza kuwa kupitia uwepo wa Sheria ya Usuluhishi nchini ya mwaka 2020 ambayo inaelekeza kuwa mtu yeyote anayetaka kufanya usuluhishi lazima apate ithibati kutoka Wizara ya Katiba na Sheria. “Sheria hii ilianza utekelezaji wake mwaka 2021 ambapo hadi sasa Wizara imewapatia ithibati na kuwathibitisha jumla ya wanaume 444 katika eneo la usuluhishi na wanawake 89; majadiliano wanaume 162 na wanawake 38; wapatanishi wanaume 142 na wanawake 56; na upatanishi wanaume 77 na wanawake 14,” amefafanua Bi. Magoma.
Mafunzo na kongamano hilo litaangazia umuhimu wa uwiano wa kijinsia katika utatuzi wa migogoro, kujadili mikakati ya kuongeza uelewa na ushiriki na uongozi wa wanawake katika ADR ili kuwawezesha wanawake katika ADR na kuimarisha taaluma zao, kuchangia mfumo wa utatuzi wa migogoro ulio na uwiano, unaojumuisha wadau wote na unaoaminika zaidi.
Ndugu Godson Nyange, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam..jpeg)
Bi. Mercy Kyamba, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Udhibiti Ubora wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali akizungumzia ushirikiano uliopo kati ya Ofisi hiyo na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Bi. Magreth Magoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania (TIAC) wakimsikiliza ndugu Godson Nyange (hayupo pichani) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi Tanzania wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafunzo na kongamano la ushirikishwaji wa wanawake kwenye utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala yanayotarajiwa kufanyika tarehe 24 hadi 27 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.


.jpeg)


.jpeg)



















.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akibadilishana mawazo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa, Bi. Sekela Mwasubila, kuhusu utekelezaji wa mradi wa Huduma ya Mtandao inayotolewa kwa shule 5 na ofisi 5 za Kata.
Miundombinu ya teknolojia ya mawasiliano ya mawimbi ya microwave inayotolewa na kampuni ya Airtel, ikisambaza huduma ya intaneti yenye kasi ya Mbps 20, kupitia Mradi unaofadhiliwa na UNICEF.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Bukulu, Mwl. Joseph Paul, akieleza namna huduma ya mrandao inavyorahisisha ujifunzaji katika maabara ya kompyuta shuleni hapo.
Mkuu wa Shule ya Msingi Isabe, Mwl. Jackline Richard, akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi wa kusambaza huduma ya mtandao kwa shule na jamii.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume kuhusu fursa za kujifunza kidijitali, wakati wakikagua huduma ya mtandao imavyofanya kazi shuleni hapo na kusaidia wanafunzi kujifunza.
Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, wakikagua matumizi ya huduma mtandao darasani kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Amani Abeid Karume iliyopo WIlayani Kondoa.
Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akitoa maelezo kuhusu utendaji wa teknolojia ya intaneti katika moja ya vituo vilivyonufaika na mradi huo, Chama cha Ushirika cha Mawasiliano.






