KAMPUNI ya mawasiliano ya simu ya Airtel Tanzania na kampuni ya teknolojia ya Huawei zimethibitisha upya dhamira yao ya kuendelea kuimarisha huduma za mawasiliano nchini kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa na ubunifu vilivyojadiliwa katika Kongamano la Huawei Mini Mobile World Congress (Mini MWC).

Kampuni hizo zimesema ushirikiano wao unaendelea kulenga kuharakisha mageuzi ya kidijitali, kupanua huduma za mtandao na kuboresha uzoefu wa wateja kupitia suluhisho za kisasa za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa kongamano hilo lililofanyika Tanzania Mei 12, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Charles Kamoto, alisema ushirikiano huo unaendelea kuwa sehemu muhimu katika kusaidia ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.

“Ni furaha kubwa kushiriki nanyi leo tunapojadili mustakabali wa sekta ya mawasiliano, mageuzi ya kidijitali na fursa zinazoendelea kujitokeza ndani ya soko letu na ukanda mzima,” alisema.

Mkutano huo uliwakutanisha viongozi na wataalamu wa kiufundi kutoka kampuni zote mbili kujadili teknolojia za baadaye zinazolenga kuboresha utoaji wa huduma na kuimarisha miundombinu ya mawasiliano nchini Tanzania.

Miongoni mwa maeneo ya kimkakati yaliyojadiliwa ni pamoja na ukuaji wa huduma za intaneti ya simu na majumbani, matumizi ya mitandao msingi inayotumia Akili Unde (AI), maendeleo ya teknolojia ya microwave pamoja na mifumo ya kisasa ya usafirishaji wa taarifa kwa njia ya kidijitali.

Kupitia ushirikiano huo, Airtel Tanzania na Huawei pia walijadili matumizi ya teknolojia za kisasa za wireless na AI zinazolenga kuongeza upatikanaji wa huduma za mtandao, kuboresha uthabiti wa huduma, kuongeza uzoefu wa wateja na kupunguza matumizi ya nishati katika mifumo ya mawasiliano.

Kamoto alisema matumizi ya teknolojia za kizazi kijacho yataongeza matumizi ya data, kusaidia ukuaji endelevu wa biashara na kuiweka Airtel katika nafasi ya kuwa kampuni kinara wa mawasiliano ya kidijitali nchini.

“Tunaendelea kuwa na malengo makubwa na dhamira thabiti katika kusukuma mbele dira ya Airtel kupitia ubunifu na ujumuishaji,” alisema.

Kwa upande wake, Huawei ilisema ushirikiano wake na Airtel Tanzania utaendelea kuwa nguzo muhimu katika safari ya mageuzi ya kidijitali nchini Tanzania.

Kampuni hiyo pia iliipongeza menejimenti ya Airtel Tanzania kwa kushiriki katika majadiliano ya kimkakati yanayolenga kukuza sekta ya mawasiliano nchini na kuhamasisha matumizi ya teknolojia mpya zinazoibukia.

Mini MWC ni jukwaa maalum linaloandaliwa na Huawei Tanzania kwa ajili ya kuwapa wadau fursa ya kujionea teknolojia bunifu zinazooneshwa katika Kongamano la Kimataifa la Mobile World Congress linalofanyika kila mwaka mjini Barcelona, Hispania.

Jukwaa hilo pia linawawezesha wadau wa sekta ya mawasiliano kujadili mwenendo wa teknolojia mpya pamoja na matumizi yanayoongezeka ya Akili Unde (AI) katika kuboresha huduma za mawasiliano nchini.

Baadhi ya viongozi wa Huawei waliohudhuria kongamano hilo ni pamoja na Rais wa Idara ya Bharti Group Key Account, Jack Huang, pamoja na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mauzo wa Huawei Tanzania, Galving Gao.

Kongamano hilo limefanyika wakati ambapo sekta ya mawasiliano nchini Tanzania inaendelea kushuhudia ukuaji mkubwa wa huduma za intaneti, matumizi ya huduma za kidijitali na ongezeko la matumizi ya data kutokana na mahitaji yanayoongezeka ya huduma bora na nafuu za mtandao.
Na Mwandishi Wetu
CHUO Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) na Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL) wamesaini makubaliano ya ushirikiano yatakayolenga kuwatafutia wanafunzi wa chuo hicho fursa mbalimbali za kitaaluma.

Makubaliano hayo yalisainiwa jana jijini Dar es Salaam kati ya Mkurugenzi Mkuu wa GEL, Abdulmalik Mollel, na Kaimu Mkuu wa DUCE, Profesa Pendo Malangwa.

Akizungumza katika hafla hiyo, mgeni rasmi aliyemwakilisha Ofisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Geofrey Kituye, aliipongeza GEL na DUCE kwa kuona umuhimu wa kuunganisha nguvu katika kusaidia maendeleo ya elimu na kuwaandaa vijana kwa maisha ya kazi baada ya masomo.

“Nitumie fursa hii kuwapongeza sana DUCE pamoja na Global Education Link kwa kuona umuhimu wa kuunganisha nguvu katika kusaidia maendeleo ya elimu na maandalizi ya vijana wetu kwa maisha ya kazi baada ya hatua mbalimbali za masomo,” alisema Kituye.

Aidha, alisema Dar es Salaam ni mkoa wenye nafasi kubwa katika maendeleo ya taifa kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu, shule za msingi na sekondari za serikali na binafsi, vyuo vya elimu ya juu, hospitali za rufaa na binafsi pamoja na viwanda vikubwa na vya kati vinavyoendelea kukua kila siku.

Alisema ukuaji huo wa uchumi na miundombinu unaongeza wajibu kwa wadau wa elimu kuhakikisha vijana wanapata maarifa, ujuzi, maadili na uwezo wa kutumia fursa zinazozidi kuongezeka ndani ya mkoa huo na taifa kwa ujumla.

“Ndiyo maana suala la kunasihi vijana kuhusu ulimwengu wa kazi baada ya masomo lina umuhimu mkubwa sana katika kipindi hiki. Kimsingi, mwanafunzi wa leo anatakiwa kujitambua mapema, kuelewa uwezo wake, mahitaji yake, ndoto zake na fursa za kazi zilizopo mbele yake,” alisema.

Aliongeza kuwa vijana wanapaswa kusoma wakiwa wanajua wanachosoma, sababu za kusoma taaluma hizo na namna watakavyotumia maarifa na ujuzi wanaoupata katika maisha yao ya baadaye.

Kituye alisema bila mwongozo sahihi wa taaluma, vijana wengi huchagua masomo bila kuzingatia uwezo wao, ndoto zao na mahitaji ya soko la ajira au fursa zinazotarajiwa kujitokeza miaka ijayo.

“Kwa kuzingatia hilo, ni jambo la faraja kuona kuwa DUCE pamoja na Global Education Link wameamua kuunganisha nguvu katika eneo hili muhimu,” alisema.

“Kwa niaba ya Ofisi ya Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, napenda kuupongeza tena uongozi wa DUCE pamoja na Global Education Link kwa kuanzisha ushirikiano huu muhimu. Ni imani yangu kuwa hatua hii ni mwanzo wa mabadiliko makubwa katika namna tunavyowaandaa vijana wetu kwa elimu, ajira, ubunifu na maisha ya baadaye,” aliongeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel, alisema GEL imefikisha miaka 19 katika kazi ya kuwapa wanafunzi mwongozo wa taaluma mbalimbali za kusomea.

Alisema moja ya kazi kubwa zinazofanywa na taasisi hiyo ni kuwatafutia wanafunzi wa Tanzania fursa za kusoma nje ya nchi pamoja na kusaidia kujenga ushirikiano kati ya vyuo vikuu vya ndani na vya nje kwa lengo la kuleta teknolojia na maarifa mapya nchini.

Alisema nchi zilizoendelea zimefikia mafanikio hayo kutokana na uwekezaji mkubwa katika maarifa ya wananchi wake, hivyo GEL imeona umuhimu wa kusaidia kuleta maarifa hayo Tanzania.

Mollel alisema GEL tayari imesaini mikataba ya ushirikiano na vyuo vikuu mbalimbali ikiwemo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Mzumbe, Nelson Mandela, TIA na vinginevyo, huku kusaini makubaliano na DUCE ikiwa ni mwendelezo wa juhudi hizo.

“Kila chuo tunachosaini nacho makubaliano tunakuwa na malengo maalum. Leo tumesaini na DUCE kwa ajili ya kutoa mwongozo kwa wanafunzi, na hatuishii kwa wanafunzi pekee; hata wazazi wanaotaka kujiendeleza kielimu au walimu wanaotaka kuongeza elimu tunawapa mwongozo,” alisema Mollel.

Naye Kaimu Mkuu wa DUCE, Profesa Pendo Malangwa, alisema tukio hilo linaonesha dhamira ya dhati ya kuwaandaa vijana katika maisha ya taaluma na ajira za baadaye.

Alisema kupitia ushirikiano huo, wanafunzi wa DUCE watapata mwongozo wa kitaaluma na kufahamu fursa zilizopo ndani na nje ya nchi ili kuwawezesha kukabiliana na ushindani mkubwa wa soko la ajira duniani.

Profesa Malangwa alisema DUCE itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kutoa elimu bora, kufanya tafiti na kuandaa wataalamu, huku GEL ikitoa uzoefu wake katika kuwaunganisha vijana na kuwapa ushauri wa maendeleo ya kitaaluma.

Alisema ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza mwongozo wa kitaaluma, ushirikishwaji wa wanafunzi, kuwajengea uwezo pamoja na kuimarisha mawasiliano kupitia vyombo vya habari ili kusaidia vijana kuelewa taaluma mbalimbali na mahitaji ya soko la ajira.

“Sote ni mashahidi hapa kwamba vijana wengi wakimaliza kidato cha sita hawana uwezo wa kuchagua wanachotaka kusoma. Wengine wanachagua tu kwa sababu wamesikia kutoka kwa watu wengine. Kupitia ushirikiano huu tunataka vijana wachague taaluma wanazozielewa na zitakazowaletea tija katika maisha yao ya baadaye,” alisema Profesa Malangwa.


-Benki Yathibitisha faida ya Sh bilioni 206 robo ya kwanza 2026.

Na Ashura Mohamed, Arusha

Benki ya CRDB imeahidi kuendelea kulinda misingi bora iliyoiweka katika nafasi nzuri ya kifedha nchini, huku ikichukua hatua za kuongeza kasi ya ukuaji kwa kuunda vitengo maalum vya wataalamu kulenga sekta za kimkakati kama mafuta, gesi, kilimo na madini.

Akizungumza mkoani Arusha wakati wa Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa wa benki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, alisema lengo ni kuhakikisha benki inatoa huduma zote kwa wakati, kwa urahisi na kwa gharama nafuu, huku ikiendelea kujali mteja.

“Tumeunda vitengo maalum ndani ya benki yetu vyenye wataalamu. Lengo ni kuhakikisha tunafanya vizuri katika sekta hizo na kunasa fursa mpya zitakazojitokeza kwa uwekezaji. Tunachunguza nchi inapoelekea ili tushinde katika maeneo hayo,” alisema Dkt. Nsekela.

Aliongeza kuwa CRDB itaendelea kudumisha mtaji imara, ubora wa mikopo na nidhamu ya kibiashara, huku ikitafuta fursa mpya katika sekta mtambuka kulingana na mwelekeo wa uchumi wa nchi.

Dkt. Nsekela pia aliomba wanahisa kuwa miongoni mwa wateja wa kwanza wa benki yao kwa kutumia huduma mbalimbali za kibenki ili kuiwezesha CRDB kusonga mbele zaidi. Alishukuru Bodi ya Wakurugenzi kwa miongozo na sera ambazo zimekuwa dira ya mafanikio ya benki.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Fedha wa CRDB, Fredrick Nshekanabo, alisema benki imepata faida ya shilingi bilioni 206 baada ya kodi katika robo ya kwanza ya 2026.

Alisema rasilimali za benki zimekua kwa asilimia 35 hadi kufikia shilingi trilioni 23.9, ikilinganishwa na shilingi trilioni 17.6 zilizorekodiwa katika robo ya kwanza ya 2025.

“Ukuaji huu umechangiwa hasa na ukuaji wa mikopo ambao umeongezeka kwa asilimia 34 hadi kufikia shilingi trilioni 14.7. Tunaona ukuaji huo katika mikopo midogo, ya kati na ya kilimo, ambazo ni sekta muhimu kwetu kimkakati,” alisisitiza Nshekanabo.

Aliongeza kuwa Amana pia zimekua kwa asilimia 36 hadi kufikia shilingi trilioni 16.3, jambo linaloonesha kuongezeka kwa imani ya wateja kwa benki.
Mkurugenzi wa fedha wa benki ya CRBB Fredrick Nshekanabo akizungumza wakati wa mkutano mkuu
Mkurugenzi wa benki ya CRBB Dkt.Abdulmajid Nsekela akizungumza na Wanahisa Jijini Arusha

Chama kikuu cha Ushirika Tandahimba Newala Limited (TANECU) kimesema mfumo wa stakabadhi za ghala umeleta mafanikio makubwa kwa wakulima wa korosho pamoja na jamii za Wilaya za Tandahimba na Newala kupitia ongezeko la ushindani wa soko, ajira na ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao.

Akizungumza Mei 18, 2026 katika maonesho ya miaka 20 ya mfumo wa stakabadhi za ghala yanayofanyika Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Bodi wa TANECU, Karimu Hamisi Chipola amesema mfumo huo ulianza mwaka 2006 katika Mkoa wa Mtwara hususan kwenye zao la korosho ambapo mwanzoni wakulima hawakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu mfumo huo.

Amesema Serikali ilitoa elimu kwa wakulima huku TANECU ikipewa dhamana ya kusimamia mfumo huo kwa wakulima wa zao la korosho katika maeneo yao jambo ambalo limeleta mafanikio makubwa.

Chipola amesema kabla ya kuanzishwa kwa mfumo huo wakulima walikuwa wanauza mazao yao kupitia soko huria bila kuwepo ushindani wala usimamizi mzuri wa bei jambo lililosababisha wakulima wengi kupata hasara.

Amesema baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa stakabadhi za ghala, wakulima wamekuwa na uhakika wa soko pamoja na bei nzuri za mazao yao kutokana na ushindani ulioongezeka katika biashara ya korosho.

Aidha amesema mfumo huo umechangia kuongeza ajira katika maeneo yao kupitia shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye maghala ikiwemo watunza maghala, vibarua wa kubeba magunia pamoja na shughuli ndogondogo za biashara zinazofanywa na wananchi.

“Mfumo huu umeleta tija kubwa kwa wakulima na jamii kwa ujumla kwani umeongeza ushindani wa soko na kutoa uhakika wa masoko ya mazao,” amesema Chipola.

Ameongeza kuwa mfumo huo pia umeimarisha vyama vya ushirika ambapo TANECU imeendelea kusimamia ukusanyaji wa tozo mbalimbali za wadau kupitia mfumo huo.

Kwa mujibu wa Chipola, zaidi ya Shilingi Bilioni 6 zimekusanywa na Halmashauri kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala jambo lililosaidia kuongeza mapato ya Serikali za Mitaa.

Pia amesema TANECU imefanikiwa kujenga kiwanda cha kubangua korosho chenye thamani ya Shilingi Bilioni 3.6 ambacho kwa sasa kinatoa ajira kwa zaidi ya wananchi 300.

Amesema chama hicho kinaendelea na hatua za mwisho za kujenga kiwanda kingine Wilaya ya Tandahimba kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao na kuwapa wakulima ushindani zaidi kwenye soko.

Aidha amesema TANECU kwa sasa ina maghala manne na ipo kwenye mkakati wa kujenga maghala sita zaidi ili kuimarisha uhifadhi wa mazao na kuongeza ufanisi wa mfumo wa stakabadhi za ghala katika maeneo yao.



Jumuiya ya wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ya Metali Tanzania (TBMA) umesema umeanza kuona mafanikio katika kutatua changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo wa madini nchini ikiwemo masoko, viwanda vya uchenjuaji pamoja na kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta ya madini.

Akizungumza Mei 18, 2026 katika Mkutano Mkuu wa Pili wa wanachama wa TBMA uliofanyika Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Thobias Kente amesema wamefanikiwa kuimarisha umoja wa wachimbaji na kuwaunganisha na wenye viwanda vya uchenjuaji wa madini ili kuongeza thamani ya madini.

Kente amesema lengo kuu la jumuiya hiyo ni kuhakikisha utajiri wa madini unawanufaisha wananchi hususan wachimbaji wadogo kwa kuboresha maisha yao kupitia mapato yatokanayo na shughuli za uchimbaji na biashara ya madini.

Amesema kwa sasa wachimbaji wadogo wameanza kupata nafasi kubwa zaidi ya kushiriki katika uchumi wa nchi kupitia sekta ya madini kutokana na juhudi za Serikali na ushirikiano uliopo kati ya wadau wa sekta hiyo.

Kwa upande wake, Katibu wa TBMA, Nobert Kaijage amesema jumuiya hiyo ilisajiliwa mwaka 2024 kwa lengo la kuwa daraja kati ya Serikali na wachimbaji pamoja na kuongeza fursa za uwekezaji na ajira kwa wanachama wake.

Amesema TBMA imeendelea kutoa elimu na ushauri kuhusu uchimbaji salama wa madini huku ikiwa na mpango wa kuwawezesha wachimbaji kupata vifaa vya kisasa kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Kaijage amesema mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na ongezeko la wanachama hai kutoka 15 hadi 40 pamoja na kuongezeka kwa uelewa wa sheria, kanuni na miongozo ya sekta ya madini kwa wanachama wa jumuiya hiyo.

Aidha amesema mapato ya jumuiya yameongezeka kupitia michango na ada za wanachama huku TBMA ikiendelea kusaidia utatuzi wa changamoto na migogoro ya wachimbaji katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kagera, Dodoma na Lindi.

Amesema kupitia jumuiya hiyo wachimbaji wengi wameanza kupata taarifa muhimu kuhusu masoko ya madini, uwekezaji na taratibu za kisheria jambo ambalo limeongeza uelewa na ushiriki wao katika shughuli za madini.

Hata hivyo amesema wachimbaji bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ucheleweshaji wa vibali vya mazingira na kemikali kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na mabadiliko ya bei za madini bila taarifa rasmi.

Ameongeza kuwa baadhi ya wanachama wanashindwa kumudu gharama za utafiti wa madini huku baadhi ya viwanda vikishindwa kununua malighafi kwa bei rafiki jambo linaloathiri uzalishaji na biashara ya madini nchini.

Kaijage amesema ucheleweshaji wa majibu ya changamoto kutoka kwa mamlaka husika umekuwa ukiwasababishia hasara wachimbaji wadogo na kupunguza kasi ya maendeleo ya shughuli zao.

Aidha amesema TBMA inaendelea kuiomba Serikali kuweka mazingira bora zaidi yatakayorahisisha upatikanaji wa vibali na kuongeza ushirikiano kati ya wachimbaji na taasisi za Serikali.

Amesema mipango ya jumuiya hiyo ni kuongeza wanachama wapya kupitia ziara, semina na makongamano pamoja na kuwezesha uanzishwaji wa viwanda vya uchenjuaji wa madini ili kuongeza thamani ya madini yanayochimbwa nchini.

Kaijage amesema jumuiya hiyo itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali pamoja na wadau wengine wa sekta ya madini ili kuhakikisha wachimbaji wadogo wananufaika zaidi na rasilimali za madini zilizopo nchini.





 




DAR ES SALAAM, TANZANIA
KATIKA kuadhimisha miaka 78 ya Nakba (Janga la mwaka 1948), Ubalozi wa Dola ya Palestina nchini Tanzania jana tarehe 16 Mei 2026, uliandaa hafla maalum na ya kihistoria ya uonyeshaji wa filamu iliyoteuliwa kuwania tuzo za Oscar iitwayo "Palestine 36". Hafla hiyo kubwa ya kidiplomasia iliyofanyika jijini Dar es Salaam, iliongozwa na Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe, na kuhudhuriwa na Mawaziri, Maafisa wa Serikali, Wajumbe wa Kundi la Wanadiplomasia (Diplomatic Corps), Mashirika ya Kimataifa, viongozi wa dini mbalimbali pamoja na wadau wa kijamii na vyombo vya habari.

Akihutubia hadhara hiyo, Balozi wa Dola ya Palestina nchini Tanzania, Mheshimiwa *Salam Abu Sharar*, alibainisha kuwa filamu hiyo si sanaa ya burudani tu, bali ni ushuhuda hai na chombo cha mapambano ya kuhifadhi kumbukumbu za mateso ya kihistoria dhidi ya jitihada za kufuta utambulisho wa Wapalestina. Balozi Abu Sharar alikumbusha ulimwengu juu ya maumivu yaliyorithiwa tangu mwaka 1948, ikiwemo mauaji ya kinyama ya Deir Yassin na kufukuzwa kwa nguvu kwa Wapalestina zaidi ya 750,000 kutoka kwenye ardhi zao. Alitoa wito mzito kwa jamii ya kimataifa kusimama kidete kutetea utu, kukataa kuhalalishwa kwa mifumo ya viwango viwili (double standards), na kuhakikisha sheria za kimataifa zinatumika kwa usawa ili kuwapatia Wapalestina haki yao ya msingi ya kuishi kwa uhuru na amani bila ukaliaji wa mabavu wa Israel.

Ubalozi wa Palestina unatoa shukrani zake za dhati kwa mshikamano huo mkubwa wa kidiplomasia. Balozi Salam Abu Sharar alieleza shukrani za kipekee kwa Serikali, wananchi, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa msimamo wao thabiti na usioyeyuka katika kuunga mkono haki halisi za watu wa Palestina. Ubalozi ulisisitiza kuwa urafiki kati ya mataifa haya mawili si wa kiofisi tu, bali ni mwendelezo wa misingi imara ya kimaadili na ukombozi iliyoachwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye daima alisimama kidete dhidi ya ubeberu, ukoloni, na ubaguzi, akiamini kuwa uhuru na utu ni haki ya kila mwanadamu.




Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma .

Serikali imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuboresha sekta ya usafirishaji wa bodaboda nchini kwa kuagiza halmashauri zote kutenga bajeti maalum kwa ajili ya ujenzi wa vituo na maegesho ya madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda.

Hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira ya kazi kwa vijana wanaojishughulisha na huduma za usafirishaji pamoja na kuongeza ufanisi, usalama na utaratibu katika shughuli zao za kila siku.

Akijibu swali la Mbunge wa Bukoba Mjini, Eng. Johnston Johansen Mutasingwa, aliyehoji mpango wa Serikali wa kuwajengea vijana waendesha pikipiki maeneo rasmi ya maegesho, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema Serikali tayari imeanza kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha sekta hiyo muhimu ya ajira kwa vijana.

Dkt. Dugange amesema Serikali imezielekeza halmashauri zote nchini kuendelea kuwatambua madereva wa bodaboda na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vyao katika maeneo mbalimbali.

Amesema hadi sasa Serikali imetenga maeneo 662 yenye ukubwa wa mita za mraba 5,859,756.18 katika halmashauri 146 nchini kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo, wakiwemo madereva wa bodaboda.

Aidha, Serikali inaendelea na ujenzi wa ofisi za wafanyabiashara wadogo katika mikoa mbalimbali nchini ili kurahisisha usimamizi, mawasiliano na utekelezaji wa shughuli zao. Ofisi hizo pia zinatarajiwa kuwahusisha madereva wa bodaboda ili kuwapa mazingira bora ya kufanya kazi zao kwa uratibu zaidi.

Kwa mujibu wa Dkt. Dugange, kiasi cha shilingi milioni 260 tayari kimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo katika mikoa 13 nchini.

Ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa utambuzi wa maeneo hayo na utoaji wa namba rasmi, Serikali itaendelea na ujenzi wa maegesho ya bodaboda katika vituo mbalimbali nchini, ikiwemo katika Manispaa ya Bukoba.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji, huku ikiweka mazingira rafiki yatakayosaidia shughuli zao kufanyika kwa usalama, utaratibu na ufanisi zaidi.



KAMA unapenda michezo ya kasino yenye msisimko, basi Book of Eskimo kutoka Meridianbet imekuja kukupa burudani tofauti kabisa. Mchezo huu unakupeleka kwenye ulimwengu wa barafu na ushindi mkubwa kupitia bonasi kali zinazofanya kila mchezo kuwa na presha ya ushindi.

Book of Eskimo imebeba bonasi tatu tofauti ambazo zinaongeza nafasi ya kujishindia zaidi kila unapocheza. Kila mzunguko unaweza kubadilika kuwa nafasi ya kufungua zawadi kubwa na kufanya mchezo uwe wa kuvutia zaidi kwa vijana wanaopenda kasino.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kitu kinachofanya mchezo huu kuwa wa kipekee ni uwezo wa raundi ya mzunguko kujirudia na hii inaweza kubadilisha matokeo muda wowote. Hapo ndipo mchezo unaanza kuwa moto zaidi na kukupa hamasa ya kuendelea kucheza bila kuchoka.

Pia kuna mizunguko ya bure ambayo inaongeza nafasi ya kupata malipo makubwa zaidi. Kadri mchezo unavyoendelea, ndivyo nafasi za ushindi zinavyokuwa tamu zaidi na kufanya kila dakika kwenye mchezo kuwa ya kusisimua.

Kwa wale wanaopenda uthubutu, bonasi ya ubashiri ipo tayari kuongeza ushindi wako mara mbili kwa kuchagua kadi sahihi. Huu ndio muda wa kuingia kwenye safari mpya ya kasino, fungua Book of Eskimo kupitia Meridianbet na anza kuwinda ushindi wako sasa.

Serikali imesema bado kuna watu wanaopinga mfumo wa stakabadhi za ghala kwa sababu zamani walikuwa wakinufaika kwa kuwanyonya wakulima kupitia biashara ya mazao, huku ikisisitiza kuwa mfumo huo umewekwa kwa lengo la kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na faida halali ya mazao yao.

Hayo yameelezwa Mei 17, 2026 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, wakati akifungua uzinduzi wa maonesho ya maadhimisho ya miaka 20 ya mfumo wa stakabadhi za ghala yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa  mfumo huo umeendelea kuwa mkombozi kwa wakulima kwa kuwawezesha kuhifadhi mazao yao katika mazingira mazuri na kupata bei yenye ushindani tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo baadhi ya wafanyabiashara walinunua mazao ya wakulima kwa bei ya chini iliyowapa hasara wakulima hao.

Londo amesema Serikali imeweka mazingira rafiki na wezeshi kupitia mfumo huo ili kuwasaidia wakulima kunufaika zaidi na mazao yao, huku baadhi ya watu wanaoupinga wakitaka kurejesha mazingira ya zamani yaliyokuwa yakiwanyima wakulima haki zao.

Aidha amesema kuwa, kilimo kinaendelea kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa, hivyo Wizara ya Viwanda na Biashara imepewa jukumu la kuhakikisha wakulima wananufaika na mazao yao pamoja na kuongeza ushindani katika biashara ya mazao nchini.

Pia amesema katika kipindi cha uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali imeendelea kuimarisha mfumo wa stakabadhi za ghala ili kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo na kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 ya kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa juu.

Amesema kuwa ushiriki wa sekta binafsi unatarajiwa kuchangia asilimia 70 kwenye ukuaji wa uchumi, huku akieleza kuwa ushirikiano wa taasisi zilizo chini ya Wizara za Viwanda na Biashara, Kilimo pamoja na Fedha umeendelea kuimarisha mfumo huo.

Hata hivyo, amesema Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala imeendelea kuwa mshirika muhimu katika kuimarisha ushindani wa biashara ya mazao nchini kwa kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika shughuli za ununuzi, huku ikiwawezesha wakulima kupata masoko ya uhakika na bei nzuri za mazao yao kupitia mfumo unaolenga kuongeza uwazi, tija na manufaa kwa wakulima.

Kwa upande wake, Witness Temba Afisa udhibiti ubora kutoka Bodi ya Usimamizi wa stakabadhi za Ghala, amesema katika kipindi cha miaka 20, Bodi hiyo imeendelea kutoa leseni kwa wadau mbalimbali wa biashara ya mazao na kuboresha uhifadhi wa mazao, jambo lililosaidia kupunguza upotevu wa mazao na kukuza uchumi wa wakulima.

Aidha, washiriki wa maonesho hayo wametakiwa kutumia fursa hiyo kubadilishana uzoefu na mawazo yatakayochangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 pamoja na kukuza uchumi wa Taifa kupitia sekta ya kilimo na biashara.



 

MECHI hii inachezwa kwenye dimba la Emirates Stadium, London, na ni mechi ya mwisho ya Arsenal nyumbani kwa msimu huu . Katika msimamo wa Ligi Kuu Uingereza, Arsenal wanaongoza kwa pointi 79 baada ya mechi 36, wakiwa na pointi mbili tu mbele ya Manchester City ambao wamecheza mechi moja pungufu.

Kwa upande mwingine, Burnley wamekwishashuka daraja wakiwa na pointi 21 tu, wameshikilia nafasi ya 19 . Kwa hivyo, mechi hii ina umuhimu mkubwa kwa Arsenal iwapo watashinda, Arsenal watatwaa ubingwa wa EPL kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2004. Hata iwapo City watashinda, Arsenal wanaweza kubeba ubingwa siku ya mwisho (Mei 24) kwa kushinda Burnley na Crystal Palace.

Arsenal wamepata pigo kubwa la majeruhi wiki chache kabla ya mechi hii. Ben White amethibitishwa kuwa na jeraha kubwa la goti ambalo litamuweka nje ya uwanja hadi mwisho wa msimu, hivyo hatoweza kucheza dhidi ya Burnley na hata Fainali ya Ligi ya Mabingwa. Jurrien Timber bado ana shida ya paja na hajakuwepo uwanjani kwa zaidi ya mechi 11, ingawa kuna matumaini kuwa atarejea kwa ajili ya mechi hii dhidi ya Burnley. Riccardo Calafiori pia aliondoka mapema katika mechi ya mwisho kwa sababu ya wasiwasi wa jeraha, lakini jeraha lake haliwezekani kuwa kubwa.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa upande wa Burnley, hakuna taarifa kubwa za majeruhi; timu hiyo itakuja ikiwa imezoeana na mapambano licha ya kushuka daraja mapema.

Kwa mujibu wa takwimu, Arsenal nyumbani wana rekodi nzuri: wameshinda mechi 14 kati ya 18, wakitoa sare 2 na kupoteza 2, wakiwa na wastani wa kupachika mabao kwa kila mechi huku safu yao ya ulinzi ikiruhusu wastani wa mabao machache tu kwa mechi.

Burnley ugenini wanarekodi mbaya sana, wameshinda mechi 2 pekee katika mechi 18 za ugenini, wakitoa sare 3 na kupoteza 13, wakiwa na wastani wa kufungwa mabao kuanzia matatu kwa mechi .

Katika mechi 5 za mwisho, Arsenal wameshinda mechi 3 mfululizo (dhidi ya West Ham, Fulham, Newcastle) wakiwa na safu safi katika mechi zote tatu, na mabao waliyofunga ni 1-0, 3-0, na 1-0 . Burnley kwa upande wao hawajashinda katika mechi 10 za mwisho, na katika mechi 5 za mwisho wamepoteza mechi 4 na kutoa sare 1.

Arsenal wanategemea sana mfungaji wao hodari Viktor Gyokeres ambaye amefunga mabao 14 kwenye Ligi Kuu msimu huu. Uwepo wake mbele utakuwa ni tishio kubwa kwa ulinzi dhaifu wa Burnley ambao umeruhusu mabao 73 kwa msimu mzima. Bukayo Saka pia ni mchezaji muhimu, akiwa na mabao 7 na asisti 4, na ndiye pekee kwenye kikosi cha Arsenal aliyeunda nafasi kubwa za kufunga (10 big chances).

Viungo wengine kama Martin Odegaard, Declan Rice, na Kai Havertz wanatarajiwa kudhibiti mwelekeo wa mchezo. Kwa upande wa Burnley, Jaidon Anthony ndiye mfungaji bora wa timu akiwa na mabao 8, lakini atakuwa akikabiliwa na safu ya ulinzi imara ya Arsenal ambayo imeruhusu mabao 26 pekee katika mechi 36.Jisajili

Kampuni ya mawasiliano ya Yas Tanzania imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano na kifedha nchini baada ya kuzindua rasmi duka jipya la Yas Store katika eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo wa kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi na kuchochea maendeleo ya kidijitali kwa jamii.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika hivi karibuni, Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja na Uendeshaji wa Yas, Mwangaza Matotola, alisema kufunguliwa kwa duka hilo kutarahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za Yas na Mixx kwa wakazi wa Kunduchi na maeneo ya jirani, hususan katika kipindi ambacho matumizi ya teknolojia yanaendelea kuongezeka kwa kasi nchini.

Alisema Kunduchi ni moja ya maeneo yanayokua kwa kasi kiuchumi na kijamii, huku wananchi wengi wakitegemea huduma za mawasiliano na kifedha katika shughuli zao za kila siku ikiwemo biashara, elimu na ajira za kujitegemea.

“Tunatambua umuhimu wa kuwafikia wananchi pale walipo. Kupitia duka hili, wateja wetu wataweza kupata huduma zote sehemu moja kwa urahisi zaidi,” alisema Matotola.

Aliongeza kuwa uwekezaji wa Yas katika miundombinu ya mawasiliano unaendelea kuleta matokeo chanya kwa Watanzania wengi, ambapo kampuni hiyo imewekeza zaidi ya trilioni moja katika kuboresha mtandao wake kote nchini, ikiwemo ujenzi wa minara zaidi ya 4,800 na upanuzi wa mtandao wa 4G na 5G unaowahudumia zaidi ya wateja milioni 31 nchini.

Kwa mujibu wa Matotola, uwekezaji huo umeendelea kufungua fursa mpya kwa vijana, wafanyabiashara na wanafunzi kwa kuwawezesha kupata huduma za kidijitali kwa urahisi zaidi na hivyo kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku.

“Teknolojia si anasa tena, ni sehemu muhimu ya maisha ya kila siku. Tunapoimarisha huduma za mawasiliano, tunasaidia biashara kukua, vijana kujiajiri kupitia majukwaa ya kidijitali, wanafunzi kupata elimu kwa urahisi zaidi na familia kuendelea kuwasiliana bila vikwazo,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mixx, Arnold Ngarashi, alisema,

“Tunafahamu kuwa huduma za kifedha zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya wananchi wengi, kuanzia wafanyabiashara wadogo hadi vijana wanaojiajiri. Kupitia uwepo wa duka letu hapa Kunduchi, tumejipanga kurahisisha zaidi upatikanaji wa huduma za Mixx na kuwapa wananchi uwezo wa kufanya miamala yao kwa urahisi zaidi bila usumbufu,” alisema Ngarashi.

Aliongeza kuwa Mixx itaendelea kuhakikisha wananchi wanapata suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kukuza biashara zao, kuweka akiba, kufanya malipo na kutuma fedha kwa urahisi zaidi, sambamba na kuchochea ujumuishi wa kifedha nchini.

Sambamba na hilo, Yas imewahimiza wananchi kutumia applikesheni mpya ya Yas App ambayo imezinduliwa hivi karibuni kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kampuni hiyo kidijitali na kufurahia zawadi mbalimbali ndani ya App hiyo.

Wakazi wa Kunduchi waliohudhuria hafla hiyo walieleza kuwa ujio wa duka hilo utasaidia kupunguza changamoto ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za mawasiliano na kifedha, huku wakiamini kuwa hatua hiyo itachochea shughuli za biashara na kuongeza urahisi wa upatikanaji wa huduma muhimu katika eneo hilo.

Kupitia upanuzi huo wa huduma, Yas na Mixx zinaendelea kuonesha dhamira yao ya kutumia teknolojia kama nyenzo ya kubadilisha maisha ya Watanzania na kuharakisha safari ya taifa kuelekea uchumi wa kidijitali.


Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Yas Tanzania, Bi. Mwangaza Matotola (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi duka jipya la Yas lililopo Kunduchi, Dar es Salaam, hivi karibuni. Wanaoshuhudia tukio hilo ni, kulia ni Mkuu wa Maduka wa Yas Tanzania, Bi. Sarah Sonelo pamoja na Mkuu wa kitengo cha Uendeshaji wa Huduma kwa Wateja, Bw. Henry Mboya (kushoto). Duka hilo jipya linalenga kuongeza upatikanaji wa huduma za kidijitali kwa wakazi na wafanyabiashara wa Kunduchi na maeneo ya jirani.

Benki ya NMB Plc imepata ufadhili wa jumla ya Dola za Marekani milioni 180, sawa na takribani Sh bilioni 468.1 za Kitanzania, kutoka IFC, British International Investment na Norfund, kwa ajili ya kuongeza mikopo kwa biashara ndogo na za kati, sekta ya kilimo, wanawake wajasiriamali na biashara zinazoongozwa na vijana nchini Tanzania.

Ufadhili huo unajumuisha Dola milioni 100 kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa, IFC, sawa na takribani Sh bilioni 260; Dola milioni 50 kutoka British International Investment, BII, sawa na takribani Sh bilioni 130; na Dola milioni 30 kutoka Norfund, sawa na takribani Sh bilioni 78. Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Kigali, Rwanda, pembezoni mwa Mkutano wa Wakurugenzi Wakuu Afrika, Africa CEO Forum.

Akizungumza wakati wa utiaji saini, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna, alisema ufadhili huo ni ishara ya imani ya taasisi za kimataifa kwa mkakati wa NMB na nafasi yake katika kusaidia ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupitia sekta binafsi, kilimo, wanawake na vijana.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Kanda ya Afrika wa BII, Chris Chijiutomi, alisema uwekezaji huo unaendeleza ushirikiano wa muda mrefu kati ya BII na NMB, huku ukilenga kusaidia upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu kwa MSMEs na biashara za kilimo. NMB inatarajiwa kutumia fedha hizo kuongeza mikopo, kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo na kupanua fursa kwa wajasiriamali nchini.
Hiii apa boss tumia.. Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna (kushoto), na Makamu wa Rais wa IFC Kanda ya Afrika, Ethiopis Tafara, wakionesha hati baada ya kusaini makubaliano ya ufadhili wa Dola za Marekani milioni 100 pembezoni mwa Mkutano wa Wakurugenzi Wakuu Afrika jijini Kigali, Rwanda. Ufadhili huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa NMB kusaidia biashara ndogo na za kati, sekta ya kilimo na maeneo mengine muhimu ya uzalishaji nchini Tanzania.


Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna,Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Kanda ya Afrika wa BII, Chris Chijiutomi na Mkurugenzi wa Norfund Kanda ya Afrika Mashariki, William Nyaoke, wakibadilishana hati baada ya kusaini makubaliano ya ufadhili wa Dola za Marekani milioni 80 pembezoni mwa Mkutano wa Wakurugenzi Wakuu Afrika jijini Kigali, Rwanda. Ufadhili huo utasaidia kuongeza mikopo kwa SMEs, sekta ya kilimo na biashara ambazo hazijafikiwa kikamilifu nchini Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna,Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Kanda ya Afrika wa BII, Chris Chijiutomi na Mkurugenzi wa Norfund Kanda ya Afrika Mashariki, William Nyaoke, wakisaini hati za makubaliano ya ufadhili wa Dola za Marekani milioni 80 pembezoni mwa Mkutano wa Wakurugenzi Wakuu Afrika jijini Kigali, Rwanda. Ufadhili huo utasaidia kuongeza mikopo kwa SMEs, sekta ya kilimo na biashara ambazo hazijafikiwa kikamilifu nchini Tanzania.












 

Na Mwandishi wetu- MBEYA

Serikali imeendelea kuimarisha uwezo wa Kitaifa wa Kuzuia, Kujiandaa, Kukabiliana na Kurejesha hali baada ya maafa ili kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama ya  kuepuka madhara makubwa yatokanayo na maafa.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ofisi ya Mkoa wa Mbeya, Dkt. Noah Sikwese wakati akifunga mafunzo kwa Wajumbe Wateule wa Timu ya Kukabiliana na Dharura (RERT), Waatalamu wa Unendeshaji wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura (REOCC) katika Mkoa huo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa.

Dkt. Sikwese, amesema timu za kukabiliana na dharura zimejengewa msingi muhimu wa utendaji utakaowezesha Mkoa kuwa na uwezo wa kujiandaa na kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka  na ufanisi mkubwa .

“Timu hizi zitahusika katika kufanya tathmini za awali na za kina wakati wa maafa kubaini mahitaji halisi ya waathirika, pamoja na kuratibu upatikanaji wa rasilimali muhimu kwa ajili ya kukabiliana na athari za maafa,” alisema Dkt. Sikwese.

Pia, aliongeza kwamba mafunzo yamekuwa nyenzo muhimu katika kujenga na kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiutendaji kwa watumishi wanaohusika katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya dharura.

“Kuanzishwa kwa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Mkoa wa Mbeya ni hatua muhimu katika kuimarisha uratibu wa shughuli za usimamizi wa maafa. Kituo hiki kitawezesha ufuatiliaji wa matukio  kwa ukaribu, ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa kwa wakati, pamoja na kuimarisha mawasiliano miongoni mwa wadau,” alieleza.

Sambamba na hilo Dkt. Sikwese alifafanua kuwa, utekelezaji wa mafunzo hayo ulianza katika Mikoa a Mwanza, Arusha, Dodoma, ambapo hatua za kuanzisha Vituo vya Operesheni na Mawasiliano ya Dharura pamoja na kuimarisha Timu za kukabiliana  na maafa zilianza kutekelezwa.

“Ni matarajio yangu mafunzo haya yataongeza ufanisi, uwajibikaji, ustahimilivu dhidi ya majanga katika Mkoa wetu wa Mbeya,”aliongeza.

Aidha, alitoa wito kwa wataalamu wote waliopatiwa mafunzo kuendelea kuyafanyia kazi maarifa na stadi, kudumisha nidhamu ya kazi na kujenga utamaduani wa ushirikiano wa kitaalamu huku akiwasisitiza kuendelea kufanya mazoezi ya mara kwa mara ya uokoaji na  utoaji wa huduma ya kwanza kwa majeruhi au waliofikwa na maafa.

“Usimamizi wa maafa ni jukumu letu sote, kila mmoja ashiriki sasa na kuchukua hatua katika eneo lake ili kuokoa na kulinda maisha, mali na mazingira,” alisisitiza Dkt. Sikwese.

Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa yam waka 2004 (Toleo la 2025) pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 202 imeipa jukumu la kuratibu masuala yote ya usimamizi wa maafa nchini.




Top News