▪️︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inapanga kufanya maboresho katika mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima hususan gharama na usumbufu wa kufuata huduma za maghala yaliyo mbali na maeneo yao ya uzalishaji.
Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 16, 2026 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma katika mwendelezo wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
Waziri Mkuu amesema Serikali imepokea malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mfumo huo na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha mfumo huo unawanufaisha wakulima kama ilivyokusudiwa.
“Maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ni wananchi wasiyafuate maghala, maghala yawafuate wananchi pale walipo,” amesema.
Aidha, Waziri Mkuu amesema ataitisha kikao maalumu kitakachowahusisha wakuu wa mikoa pamoja na sekta zinazohusika kutoka maeneo yanayozalisha mazao yanayotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kufanya tathmini ya changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.
“Nitaitisha kikao cha wakuu wa mikoa ya maeneo haya yanayozalisha mazao ambayo wananchi wake wamekuwa wakipata changamoto ili tupate mpango kazi wa namna ya kumaliza tatizo hili,” amesema.
Ametaja baadhi ya mikoa inayohusika kuwa ni Dodoma, Singida, Simiyu, Tabora pamoja na baadhi ya mikoa ya Kusini inayozalisha mazao ya biashara ikiwemo ufuta na dengu.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza wanunuzi wa mazao kutumia taasisi za kifedha kupata mikopo badala ya kuwakopesha wakulima kabla ya mauzo ya mazao yao.
“Wenzetu wanaokwenda kununua haya mazao wasiwakope wakulima, wao wakakope benki. Benki ndiyo taasisi zinazotoa mikopo,” amesema.
Amesema Serikali itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mfumo huo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma kwa urahisi na kunufaika ipasavyo na mazao yao.
︎ Dkt. Mwigulu asema maghala yawafuate wakulima badala ya wakulima kufuata maghala
︎ Serikali kuitisha kikao maalumu cha mikoa inayozalisha mazao ya biashara
Mwakilishi Mkazi wa UNDP Shogeki Komatsubara akizungumza kuhusiana nafasi ya UNDP katika ushiriki wa mkutano wa kufungua fursa za uwekezaji katika mkutano utaofanyika Mjini Arusha Juni Mwaka huu.OFISA Maendeleo ya Jamii ambaye ni Mratibu wa Programu ya Kizazi chenye usawa, John Mapunda ameeleza kwamba Tanzania imechagua eneo la haki na usawa wa kiuchumi katika Programu ya Kizazi Chenye Usawa.
Amesema eneo hilo lina mchango mkubwa katika kutatua changamoto mbalimbali za kijinsia nchini huku akifafanua kinara wa utekelezaji ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mapunda ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi cha kujadili namna kusuma ajenda ya Kizazi chenye Usawa ,kilichoandaliwa na Shirika la UN Women na kuwashirikisha Wahariri wa vyombo vya habari, waandishi na vijana Generation.
“Katika lengo hilo Tanzania imejiwekea maeneo manne makubwa ya utekelezaji ambayo ni kuongeza huduma za jamii zinazolenga kumpunguzia mwanamke mzigo wa kazi zisizo na malipo, kukuza ajira na kazi zenye staha hususan kwa wanawake, kuongeza uwezo wa wanawake kumiliki rasilimali za uzalishaji ikiwemo ardhi na biashara pamoja na kuandaa bajeti zenye mrengo wa kijinsia.
“Programu ya Kizazi Chenye Usawa ilianza mwaka 2021 na inatarajiwa kukamilika mwaka 2026 .Programu hiyo inatekelezwa Tanzania Bara na Zanzibar chini ya uratibu wa wizara zenye dhamana ya jinsia kwa kushirikiana na UN Women.”
Kwa upande wake Mchambuzi wa Programu za Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kutoka UN Women, Jackline Chami amesema kwa mwaka huu programu hiyo itajikita katika maeneo saba muhimu.
Ameyataja maeneo hayo ni ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi, uchumi wa malezi, ujuzi, ujumuishaji wa kidijitali, bajeti na ufadhili wenye mrengo wa kijinsia, kizazi chenye usawa katika taasisi na uendelevu pamoja na ujumuishaji wa watu wenye ulemavu na mabadiliko ya kijinsia.
“Maeneo hayo yanalenga kuongeza ushiriki wa wanawake katika uchumi, teknolojia, maamuzi na kuhakikisha makundi yote yanapata fursa sawa katika maendeleo ya taifa,”amesema alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu programu hiyo.
Awali Mtaalamu wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kutoka UN Women, Lillian Mwamdanga amesema jukwaa hilo limewakutanisha serikali, mashirika ya kiraia, vijana, sekta binafsi, vyombo vya habari pamoja na washirika wa maendeleo kwa lengo la kugeuza ahadi za usawa wa kijinsia kuwa matokeo halisi kwa wanawake na wasichana.
“Kupitia Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa linaloongozwa kwa pamoja na UN Women na wadau mbalimbali duniani, nchi zimekuwa zikitoa ahadi za kifedha na utekelezaji wa programu zinazolenga kuimarisha haki na uwezeshaji wa wanawake na wasichana.
“Tanzania imeonesha uongozi mkubwa kwa kuwekeza katika haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake ambapo tangu mwaka 2021 serikali imekuwa ikitekeleza programu ya kitaifa chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum,”amesema.
Akizumgumzia baadhi ya mafanikio yaliyofikiwa kuwa ni pamoja na kuanzishwa kwa NMB Gender Bond, uwekezaji katika huduma za malezi ya watoto na matumizi ya nishati safi ya kupikia ambayo imesaidia kupunguza mzigo wa kazi kwa wanawake na kuwapa muda zaidi kushiriki shughuli za uzalishaji mali.
Pia amesema ahadi zaidi ya 200 zimepatikana kutoka serikalini, asasi za kiraia, sekta binafsi na taasisi za elimu huku majukwaa 10,000 ya uwezeshaji wanawake yakianzishwa nchini ili kuongeza upatikanaji wa taarifa, fursa za uongozi na mitandao ya kijamii kwa wanawake.
Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo Mei 15, 2026 katika Sherehe ya Tisa ya Mahafali ya Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika Mlimani City, Jijini Dar es salaam.Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mnzava, amewataka viongozi wa vyama vya ushirika wilayani humo kuhakikisha wanatumia rasilimali na mali za ushirika kwa njia sahihi na yenye uwajibikaji. Amesisitiza kuwa matumizi mabaya ya mali hizo ndiyo chanzo kikuu cha migogoro na manung’uniko yanayojitokeza mara kwa mara baina ya wanachama.
Kauli hiyo ameitoa wakati wa mkutano wa wadau wa vyama vya ushirika uliofanyika hivi karibuni wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro. Katika mkutano huo, Mnzava alisema kuwa vyama vya ushirika vinapaswa kuwa daraja la kuleta maendeleo kwa wanachama wake, si chanzo cha malumbano na kutokuaminiana.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya, matumizi sahihi ya rasilimali, pamoja na uwazi katika usimamizi wa fedha na mali, yatajenga imani baina ya viongozi na wanachama. Pia itapunguza malalamiko ambayo mara nyingi husababisha migogoro inayoathiri ukuaji wa vyama hivyo.
Aidha, Mnzava alisisitiza umuhimu wa ujumuishaji na ukuaji wa pamoja wa uchumi jumuishi. Alisema viongozi wanapaswa kuwashirikisha wanachama katika maamuzi yote makubwa na kuhakikisha kila mwanachama anapata fursa ya kunufaika na shughuli za ushirika.
Mwishoni, Mkuu wa Wilaya aliwaagiza viongozi wa vyama vya ushirika kushughulikia kwa haraka malalamiko na kero za wanachama zinapojitokeza. Alionya kuwa endapo kero hizo zitaachwa bila kushughulikiwa, zitaendelea kuchochea migogoro na kudidimiza ari ya wanachama katika shughuli za uzalishaji na kiuchumi.
.jpeg)













.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)



























