Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Wakati Tanzania ikiendelea kukabiliwa na changamoto ya ongezeko la taka ngumu mijini na vijijini, Serikali imezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha mapato yatokanayo na shughuli za usafi na udhibiti wa taka yanatumika moja kwa moja kuboresha huduma hizo pamoja na kuimarisha mazingira.

Hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa ukusanyaji na usimamizi wa taka huku Serikali ikihimiza jamii kuanza kuzitazama taka kama rasilimali yenye thamani ya kiuchumi badala ya mzigo wa mazingira.

Akizungumza leo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Udhibiti wa Taka Ngumu na Usafi wa Miji, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe amesema halmashauri zote zinapaswa kutenga na kurejesha asilimia 10 ya mapato yanayotokana na shughuli za udhibiti wa taka ili kuviwezesha vitengo vya usafi wa mazingira kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Mkutano huo umebeba kaulimbiu isemayo “Taka Ngumu ni Mali; Tumia, Rejeleza na Weka Miji Safi.”

Profesa Shemdoe amesema bado hali ya usimamizi wa taka nchini si ya kuridhisha kutokana na baadhi ya halmashauri kushindwa kuwa na maeneo rasmi ya kutupia taka.

Amesema kati ya halmashauri 184 zilizopo nchini, ni halmashauri 43 pekee zenye madampo rasmi, jambo ambalo linaathiri juhudi za usafi wa mazingira na kuongeza hatari ya uchafuzi wa mazingira pamoja na magonjwa ya mlipuko.

“Ni muhimu kuhakikisha taka zinakusanywa na kuhifadhiwa katika maeneo maalum ili kulinda afya za wananchi na kuweka mazingira safi katika miji na makazi yetu,” amesema.

Aidha, ameonya kuhusu tabia ya utupaji holela wa taka kwenye mitaro ya maji, akisema hali hiyo imekuwa chanzo kikubwa cha mafuriko wakati wa mvua kutokana na kuziba kwa mifumo ya maji.

Kwa mujibu wa Profesa Shemdoe, viongozi wa mikoa, wilaya pamoja na serikali za mitaa wanapaswa kuhakikisha suala la usafi wa mazingira linakuwa agenda ya kudumu katika vikao vya maamuzi ili kuongeza uwajibikaji katika jamii.

Katika hatua nyingine, Serikali imehimiza wananchi kuanza kutenganisha taka kuanzia zinakozalishwa ili kurahisisha shughuli za urejelezaji wa plastiki, vyuma, karatasi na taka nyingine zinazoweza kutumika tena.

Amesema mfumo huo utasaidia kuongeza thamani ya taka na kufungua fursa mpya za ajira na biashara kwa wananchi, hususan vijana na wanawake.

“Tunapaswa kubadili mtazamo kuhusu taka. Zinaweza kuwa chanzo kikubwa cha kipato kupitia shughuli za ukusanyaji, uchakataji na urejelezaji,” amesema.

Profesa Shemdoe pia amewataka vijana na wanawake kutumia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kuanzisha miradi ya ukusanyaji na uchakataji wa taka ngumu ili kujiongezea kipato huku wakichangia uhifadhi wa mazingira.

Amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Japan kutafuta teknolojia za kisasa za uteketezaji na urejelezaji wa taka kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu la usimamizi wa taka nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma umeongeza bajeti ya usafi wa mazingira kutoka Shilingi milioni 750 hadi Shilingi bilioni 3 kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema fedha hizo zitatumika kununua vifaa vya usafi, kuboresha ukusanyaji wa taka pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utunzaji wa mazingira.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Mabadiliko ya Tabianchi na Tathmini kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Kanizio Manyika amesema Tanzania huzalisha zaidi ya tani milioni 17 za taka ngumu kila mwaka huku asilimia 60 hadi 75 ya taka hizo zikibaki kwenye mazingira kutokana na kutokusanywa ipasavyo.

Ameonya kuwa hali hiyo ni tishio kwa afya za wananchi na mazingira na kusisitiza umuhimu wa kuwa na mifumo endelevu ya usimamizi wa taka.

Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Joseph Birango amesema takwimu zinaonyesha magonjwa sita kati ya 10 yanayoisumbua jamii yanachangiwa na uchafuzi wa mazingira pamoja na mifumo duni ya usimamizi wa taka.

Awali, Mwenyekiti wa Wakuu wa Vitengo vya Udhibiti wa Taka na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara, William Mpangala aliitaka Serikali kutoa maelekezo madhubuti zaidi kwa halmashauri ili kuhakikisha fedha zinazotokana na shughuli za udhibiti wa taka zinarejeshwa kikamilifu katika kuboresha huduma za usafi wa mazingira.







*Rais Macron atangaza uwekezaji wa dola bilioni 27 Barani Afrika

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 11, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Mkutano huo umewakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo umekuwa wa manufaa kwa Bara la Afrika na Ufaransa kwa pamoja kwani majadiliano yamegusa namna ya kuzifanya pande hizo mbili ziweze kunufaika na ushirikiano huo.

Amesema rasilimali zinazopatikana barani Afrika zinatosheleza ikiwa zitatumika vizuri katika kujenga uchumi wa Afrika.

“Lengo kubwa la jitihada hizi ni kupambana na umasikini lakini pia na kutengeneza ajira kwa makundi makubwa ikiwemo la vijana pamoja na wanawake,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa ni maeneo ambayo yamepewa umuhimu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

“Nguzo zote zilizoongelewa kwenye dira lakini pia na maeneo ya kipaumbele yameguswa katika mijadala ya leo,” amesema.

Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, alizitaka nchi za Afrika kutafakari upya mifumo ya kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali za ndani, uwekezaji pamoja na ushirikiano wa kikanda ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo ya muda mrefu.

Aidha, Rais Ruto amesema ni wakati wa Afrika kujiweka kama mdau katika uchumi wa kimataifa badala ya kuwa mnufaika wa misaada ya nje pekee.

“Afrika haiwezi tena kubaki kama mshiriki asiyekuwa na sauti katika mifumo ya kimataifa ambapo baadhi ya maamuzi muhimu hufanywa bila sauti ya usawa,” alisema.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, alisema Bara la Afrika linapiga hatua kubwa za maendeleo na ni bara ambalo halisubiri majawabu ya changamoto bali linatoa majawabu ya changamoto mbalimbali lilazokabiliana nazo.

Katika hatua nyingine, Rais Macron alitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika katika sekta za nishati, Akili Unde, uchumi wa bahari pamoja na kilimo.

“Mpango huu utasaidia kutengeneza takriban ajira 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa,” alisema.

Aidha, Rais Macron aliwataka wafanyabiashara wa Afrika kuona fursa zilizopo nchini Ufaransa na kwenda kuwekeza.

“Hatuko hapa tu kuja kuwekeza katika Bara la Afrika pamoja nanyi, tunawahitaji viongozi wakubwa wa biashara wa Afrika kuja kuwekeza nchini Ufaransa,” alisema.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema watu wa Bara la Afrika wanapaswa kuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara hilo.

“Bara hili limebarikiwa rasilimali nyingi, hapa wenyewe ndio wanapaswa wawe wa kwanza kunufaika,” alisema.

Dkt. Mwigulu amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano.


Na Mwandishi wetu, Simanjiro
JUMUIYA ya Wazazi wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, imesajili wanachama wapya 16,648 kwa njia ya kielekroniki.

Katibu wa jumuiya ya wazazi wa CCM wilaya ya Simanjiro, Sasi Mirumbe ameeleza hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya wazazi iliyofanyika kata ya Ruvu Remit.

Mirumbe amesema kuwa kati ya wanachama hao wapya 16,648 wanaume ni 7,319 na wanawake ni 9,165.

Ameeleza kwamba katika uhai wa jumuiya hiyo wamekuwa wakifanya vikao na ziara kwa mujibu wa kanuni na kusajili wanachama wapya.

Amesema kutokana na jumuiya ya wazazi kuhusika na mazingira, malezi ya vijana katika elimu afya na uchumi wa kujitegemea, jukumu ambalo wamekuwa wakilifanya mara kwa mara na vizuri sana.

"Tumekwenda mbali kama jumuiya ya wazazi Simanjiro kwa kutambua baadhi ya watu wazima wasiojua kusoma na kuandika tumekuja na mpango wa darasa mabomani," amesema Mirumbe.

Amesema darasa mabomani ni mpango wa kuwafundisha watu wazima kwenye vitongoji vyao majumbani ili wajue kusoma, kuhesabu na kuandika, kwa kutoa mchango wao wa elimu ya awali, msingi na sekondari kama wazazi.

Amesema ujenzi wa nyumba ya mtumishi, wamefanikiwa kuanza ujenzi ambayo hivi sasa ipo usawa wa madirisha.

"Mhe mgeni rasmi kukamilika kwa nyumba hii kutaendelea kuimarisha jumuiya yetu na chama chetu katika kuongeza rasilimali za kudumu na kupunguza adha kwa mtumishi kupanga pindi yakitokea mabadiliko ya kiutumishi, amesema.

Aidha, amesema nyumba hiyo imesimama kwa muda wa mwaka mmoja kwa kukosa matofali 1,000 ya thamani ya shilingi milioni 1.4 saruji mifuko 50 ya shilingi 900,000 nondo za mm12 shilingi milioni 1 nondo za mm6 za shilingi milioni 1.4 misumari ya shilingi 17,000 mbao shilingi 540,000 binding wire sh 70,000 fedha za fundi shilingi 1.6 jumla shilingi 5,747,500.

Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo James Ole Millya ameipongeza jumuiya hiyo kwa namna wanavyotekeleza wajibu wao ikiwemo kuyasema mema yanayofanywa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Ole Millya amechangia shilingi 500,000 za ujenzi wa nyumba ya mtumishi na kumuagiza mfanyabiashara maarufu Lesiangiki Mulla kushirikiana na wadau wa maendeleo kukamilisha jengo hilo.

Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Haiyo Yamat Mamasita amesema wamekuwa na utaratibu wa kufanya maadhimisho ya wiki ya wazazi katika kata mbalimbali.

Haiyo amesema kwa mwaka 2026 waliamua kupitia vikao kuwa kilele cha maadhimisho hayo yafanyike kata ya Ruvu Remit na mwaka 2027 yatafanyika katika kata nyingine.

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inatarajia kutoa vibali vya ajira mpya katika mwaka wa fedha 2026/27 kwa sekta ya afya pamoja na kada nyingine, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kupunguza uhaba wa madaktari na wauguzi nchini.
 Akizungumza Mei 12, 2026 katika Kongamano la Kwanza la Kisayansi la Wauguzi lililoambatana na Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika katika Hotel Verde Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi alisema Serikali itaendelea kuwekeza zaidi katika kuboresha huduma za afya ili kuhakikisha wananchi wanapata matibabu bora na ya kisasa.
 Alieleza kuwa Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya afya ikiwemo ujenzi wa Hospitali Mpya ya Mnazi Mmoja pamoja na Hospitali ya Saratani Binguni, sambamba na ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa na kuimarisha mafunzo kwa watumishi wa sekta hiyo.

 Rais Dkt. Mwinyi pia aliwataka wauguzi nchini kuendelea kufanya kazi kwa kujituma, huruma na kuzingatia maadili ya taaluma yao, akisisitiza kuwa wauguzi wana nafasi kubwa katika kuimarisha huduma za afya na kuokoa maisha ya wananchi.
 Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo, “Kuwawezesha Wauguzi ni Kuokoa Maisha” (Empowering Nurses, Saving Lives).


Na mwandishi wetu
WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, amewataka waandishi wa habari pamoja na jamii kwa ujumla kutambua wajibu wao katika kusimamia malezi na makuzi ya watoto ili kujenga familia imara na taifa lenye maadili mema.

Akizungumza katika semina ya malezi iliyoandaliwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii na Makundi Maalum Kairuki alisema mafanikio ya kibiashara, kiuongozi na kijamii hayawezi kuwa na maana endapo msingi wa familia katika malezi na makuzi haujajengwa vizuri.

“Tutambue hivyo, pamoja na yote utafanikiwa kibiashara, kiuongozi na mengine mengi lakini kama msingi wa familia yako katika malezi na makuzi haujakaa sawa utateteleka. Hata ukipata mafanikio yatakuwa ya muda mfupi na hutakuwa na faraja wala furaha, hivyo eneo hili ni la kusisitiza na kutilia mkazo,” alisema Kairuki.

Aidha, aliitaka jamii kuzingatia matumizi sahihi ya simu za mkononi pamoja na vyombo vingine vya teknolojia, akieleza kuwa watoto wengi wamejikuta wakitumia vibaya mitandao ya kijamii.

“Kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi, laini ya simu hutolewa kwa mtu mwenye umri wa miaka 18 kwenda juu. Sasa unabaki na maswali unapoambiwa watoto wetu wameona vitu vya hovyo, unajiuliza wanavionea wapi ilhali kanuni zinakataza,” alisema.

Kairuki alisisitiza kuwa mtoto hastahili kumiliki simu ya mkononi, huku akibainisha kuwa baadhi ya wazazi na walezi wamelegeza usimamizi wao jambo linalochangia watoto kuathirika na matumizi mabaya ya teknolojia.

“Ni muhimu kwa wazazi kutambua kuwa sheria za nchi haziruhusu jambo hilo, hivyo niwaombe sana kutambua kuwa ulinzi unaanza na sisi wenyewe majumbani mwetu kwa kufuatilia watoto wetu wanaangalia nini chini ya ulinzi wetu,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Kairuki alikemea tabia ya matusi, udhalilishaji na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, akisema vitendo hivyo ni kosa kisheria na vyombo vya dola vitaendelea kuchukua hatua dhidi ya wanaokiuka sheria.

“Vyombo vya ulinzi na usalama vitaendelea kusimamia suala hili ikiwemo kufunga akaunti mbalimbali za watu watakaokiuka sheria. Mitandao ina fursa nyingi chanya kwa maendeleo binafsi na jamii hivyo itumike kwa manufaa,” alisema.

Naye Daktari wa Saikolojia ya Jamii, Dkt. Garvin Kweka alisema wazazi wengi kwa sasa wanalea watoto wasioweza kuhimili changamoto za maisha pamoja na hisia zao.
“Ndiyo maana siku hizi watoto wameanza kujiua. Hii ni kutokana na kutengeneza kizazi kisichoweza kuhimili maumivu kabisa. Nina takwimu kuwa mtoto wa kwanza mwenye umri mdogo kujiua alikuwa na miaka sita kutoka Mkoa wa Katavi,” alisema.

Aliongeza kuwa jamii inapaswa kuwajengea watoto uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha badala ya kuwalea katika mazingira yanayowafanya washindwe kuvumilia misukosuko mbalimbali ya maisha.

▪️Dkt. Mwigulu asisitiza matumizi sahihi ya rasilimali ili kujenga uchumi wa Afrika

▪️Rais Macron atangaza uwekezaji wa dola bilioni 27 Barani Afrika
 
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 12, 2026 ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.
 
Mkutano huo umewakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.
 
Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo umekuwa wa manufaa kwa Bara la Afrika na Ufaransa kwa pamoja kwani majadiliano yamegusa namna ya kuzifanya pande hizo mbili ziweze kunufaika na ushirikiano huo.
 
Amesema rasilimali zinazopatikana barani Afrika zinatosheleza ikiwa zitatumika vizuri katika kujenga uchumi wa Afrika.
 
“Lengo kubwa la jitihada hizi ni kupambana na umasikini lakini pia na kutengeneza ajira kwa makundi makubwa ikiwemo la vijana pamoja na wanawake,” amesema.
 
Aidha, Waziri Mkuu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa ni maeneo ambayo yamepewa umuhimu katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
 
“Nguzo zote zilizoongelewa kwenye dira lakini pia na maeneo ya kipaumbele yameguswa katika mijadala ya leo,” amesema.
 
Akizungumza katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, alizitaka nchi za Afrika kutafakari upya mifumo ya kiuchumi kwa kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali za ndani, uwekezaji pamoja na ushirikiano wa kikanda ili kuhakikisha kunakuwa na maendeleo ya muda mrefu.
 
Aidha, Rais Ruto amesema ni wakati wa Afrika kujiweka kama mdau katika uchumi wa kimataifa badala ya kuwa mnufaika wa misaada ya nje pekee.
 
“Afrika haiwezi tena kubaki kama mshiriki asiyekuwa na sauti katika mifumo ya kimataifa ambapo baadhi ya maamuzi muhimu hufanywa bila sauti ya usawa,” alisema.
 
Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron, alisema Bara la Afrika linapiga hatua kubwa za maendeleo na ni bara ambalo halisubiri majawabu ya changamoto bali linatoa majawabu ya changamoto mbalimbali lilazokabiliana nazo.

Katika hatua nyingine, Rais Macron alitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika katika sekta za nishati, Akili Unde, uchumi wa bahari pamoja na kilimo.
 
“Mpango huu utasaidia kutengeneza takriban ajira 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa,” alisema.
 
Aidha, Rais Macron aliwataka wafanyabiashara wa Afrika kuona fursa zilizopo nchini Ufaransa na kwenda kuwekeza.
 
“Hatuko hapa tu kuja kuwekeza katika Bara la Afrika pamoja nanyi, tunawahitaji viongozi wakubwa wa biashara wa Afrika kuja kuwekeza nchini Ufaransa,” alisema.
 
Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema watu wa Bara la Afrika wanapaswa kuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara hilo.
 
“Bara hili limebarikiwa rasilimali nyingi, hapa wenyewe ndio wanapaswa wawe wa kwanza kunufaika,” alisema.

Dkt. Mwigulu amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano.









Na Mwandishi Wetu, BRUSSELS

KAMPUNI ya ndege ya Brussels Airlines ya nchini Ubelgiji imeandika historia mpya kwa kutangaza kuanza kwa safari za moja kwa moja kati ya Brussels nchini Belgium na Kilimanjaro International Airport kuanzia Juni 3, 2026.

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, safari hizo zitafanyika mara mbili kwa wiki, kila Jumatano na Jumamosi, hatua inayotajwa kuwa chachu mpya kwa sekta ya usafiri wa anga, biashara na utalii nchini Tanzania.

Uzinduzi wa safari hizi unaonekana kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Ubelgiji huku ukirahisisha usafiri kwa watalii, wafanyabiashara na wananchi wa pande zote mbili.

Kuanzishwa kwa safari hizi za moja kwa moja kunatarajiwa kuongeza ushindani wa huduma za usafiri wa anga kwa kupunguza muda wa safari na kutoa chaguo zaidi kwa abiria wanaosafiri kati ya Afrika Mashariki na Ulaya.

Aidha, hatua hiyo inatajwa kuwa muhimu katika kukuza biashara ya kimataifa, hasa kwa bidhaa zinazohitaji usafirishaji wa haraka kama matunda, mboga mboga, maua, minofu ya samaki pamoja na bidhaa nyingine zinazouzwa katika masoko ya Ubelgiji na nchi jirani za Ulaya.

Ubelgiji imeendelea kuwa miongoni mwa washirika muhimu wa Tanzania katika biashara ya bidhaa za kilimo na madini, huku ikiwa moja ya nchi chache za Ulaya ambapo thamani ya bidhaa zinazotoka Tanzania kwenda nchini humo ni kubwa kuliko bidhaa zinazoagizwa kutoka huko.

Katika sekta ya utalii, safari hizi mpya zinatarajiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka Ubelgiji na mataifa jirani ya Ulaya wanaotembelea vivutio maarufu vya Tanzania kama Serengeti National Park, Ngorongoro Conservation Area na Mount Kilimanjaro.

Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya watalii kutoka Ubelgiji imeongezeka kwa kasi kutoka takribani watalii 9,000 mwaka 2018 hadi zaidi ya 18,000 mwaka 2024, jambo linalodhihirisha kuimarika kwa mahusiano ya watu wa nchi hizo mbili pamoja na kuongezeka kwa hamasa ya kutembelea Tanzania.

Mafanikio haya yanaelezwa kuwa matokeo ya mahusiano ya muda mrefu na ya kirafiki kati ya Tanzania na Ubelgiji yaliyoendelea kuimarishwa chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia diplomasia ya uchumi, maboresho ya sera, uwekezaji katika miundombinu pamoja na mazingira ya amani na utulivu nchini.

Serikali imewataka wafanyabiashara na wadau wa sekta ya utalii kutumia kikamilifu fursa zinazotokana na safari hizi mpya ili kuongeza na kukuza biashara, uwekezaji na mapato yatokanayo na utalii pamoja na kuimarisha zaidi uhusiano wa Tanzania na mataifa ya Ulaya.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwenye hafla ya Uapisho wa Rais huyo iliyofanyika katika Viwanja vya Kololo, Kampala nchini humo tarehe 12 Mei, 2026.



Matukio mbalimbali wakati wa Sherehe za Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni zilizofanyika katika Viwanja vya Kololo, Kampala nchini humo, tarehe 12 Mei, 2026.

 

Na Saidi Saidi, WMJJWM – Iringa

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Felister Mdemu, amewataka wanawake kushirikiana katika kujikwamua kiuchumi huku wakiendelea kuthamini familia, malezi bora, kuwaheshimu waume zao na kuhakikisha watoto wanapata malezi yenye maadili mema.

Mdemu amesema hayo mkoani Iringa, wakati wa mafunzo ya mwongozo wa uanzishwaji na uwezeshaji wa majukwaa ya wanawake kiuchumi yaliyofanyika katika Kijiji cha Kipaduka, Kata ya Uhambingeto, wilayani Kilolo. Mafunzo hayo yalihusisha madiwani pamoja na viongozi wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi kutoka kata mbalimbali za mkoa huo.

Akizungumzia umuhimu wa majukwaa hayo, Mdemu amesema ni maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, yenye lengo la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia elimu ya fedha, ujasiriamali, matumizi ya teknolojia pamoja na upatikanaji wa mikopo na masoko.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa wanawake kupata taarifa sahihi, kuunganishwa katika vikundi na kushiriki kikamilifu katika majukwaa hayo ili wasiachwe nyuma kutokana na ukosefu wa taarifa au usimamizi hafifu. Pia amewataka madiwani kushirikiana na taasisi za fedha, sekta binafsi pamoja na wataalam ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wanawake katika maeneo yao.

Naye Diwani wa Viti Maalum kutoka Tarafa ya Kilolo, Mheshimiwa Julieth Mkolongo, akizungumza kwa niaba ya madiwani na viongozi wa majukwaa hayo, amesema wako tayari kutekeleza maelekezo yaliyotolewa ili kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kiuchumi kwa maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao, baadhi ya wanawake walioshiriki mafunzo hayo wamesema elimu waliyoipata itawasaidia kuendesha vikundi vyao kwa ufanisi, kuongeza kipato pamoja na kuimarisha ustawi wa familia zao.


JE unajua kuwa ukiwa na Meridianbet una nafasi ya kutengeneza pesa zaidi ya Mamilioni?. Tumia Bet Builder leo ambapo unaweza ukabashiri mechi moja ambayo ina machaguo zaidi ya mawili na kuendelea.

Je unajua kuwa ndani ya Meridianbet, burudani ya ubashiri imepewa kiwango kingine kabisa kupitia huduma ya BET BUILDER inayokupa uhuru wa kutengeneza jamvi lako mwenyewe kwa namna unayotaka.

Wale ambao ni wapenzi wa mpira wa miguu na unapenda ODDS KUBWA pamoja na ushindi mkubwa, basi huu ndio muda wako wa kuonyesha uwezo wa kutabiri mechi kwa akili na ubunifu zaidi kwai mechi 1 unaweza ukaibeti kwa machaguo mengi zaidi.

Chaguo hili la BET BUILDER linakuruhusu kuchanganya machaguo mbalimbali ndani ya mechi moja na kutengeneza ODDS zako binafsi. Unaweza kuchagua timu itakayoshinda, mchezaji atakayefunga, idadi ya mabao, kona, kadi na machaguo mengine mengi ndani ya dakika chache tu.

Mfano wikendi hii kwenye mechi ya Westham dhidi ya Arsenal unaweza ukachagua kona zianzie 9, magoli kuanzia 2, kadi zisizidi 7, timu zote zifungane, handcape nk. Na kwenye Bet Bulder pia mara nyingi Odds zake huwa ni kubwa zaidi kwahiyo unaweza ukawa na mechi zako 5 na ukawa na odds nyingi.

Tengeneza pesa leo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Unapotumia BET BUILDER kumbuka kuwa huwezi Kucash out mkeka wako kwahiyo inabidi usubiri mpaka mechi zote ambazo umechagua ziishe ndipo uweze kutoa pesa zako ndani ya Meridianbet. Lakini pia chaguo hili unaweza kulipata kwenye mechi ambazo zinaendelea yaani za LIVE.

Hili ni soko ambalo watu wengi wameanza kulitumia kwani linakupa nafasi nzuri ya kuchanganua vyema machaguo ambayo unayataka. Huu ni muda ambao hutakiwa kurudi nyuma bali unachotakiwa kufanya ni kuchangamkia fursa hii siku ya leo.

Na kikubwa unapotuma Bet Builder unaweza ukabashiri mechi za ligi yoyote au mashindano yote yaani kuanzia kule EPL, LALIGA, BUNDESLIGA, EUROPA pamoja na UEFA lakini pia unaweza ukaweka dau lako lolote unalilotaka ili ubashiri leo.

Ingia kwenye akaunti yako ndani ya Meridianbet leo, tumia BET BUILDER na uonyeshe ubingwa wako wa kutabiri mechi. Odds kubwa, burudani ya kiwango cha juu na nafasi ya kushinda pesa nyingi vinakusubiri sasa hivi.
Dar es Salaam, Tanzania — Women leaders, professionals and changemakers have been urged to embrace continuous learning and digital skills development in order to remain competitive in today’s rapidly evolving workplace shaped by artificial intelligence (AI) and digital transformation.

The call was made during this year’s Mother’s Day Dinner organized by Hold a Sister’s Hand (HASH), which brought together influential women from different sectors for high-level discussions under the theme “Reskilling While Caregiving.” The event focused on empowering mothers and caregivers to balance family responsibilities while adapting to the changing demands of the modern workforce.

The HASH Mother’s Day Dinner 2026 was sponsored by CRDB Bank Plc, Schweppes, Brutal Fruit, Ctrl Creative, Asilia African Honey, Serenity Beauty Bar and More With Mau, whose support contributed to the success of the event.

Held at Hyatt Regency Dar es Salaam, the event attracted more than 100 women including corporate executives, entrepreneurs, policymakers, technology experts, bankers and young professionals committed to advancing women’s economic empowerment and leadership in the digital age. 

 Speakers at the event emphasized that the rise of AI and digital technologies is transforming industries globally, creating both opportunities and challenges for women. They noted that many working mothers risk being left behind if they fail to upgrade their skills and embrace innovation-driven careers.

Founder and CEO of Bloom Wellness, Sophia Byanaku, who delivered the keynote address, encouraged women to prioritize both personal wellness and professional growth, stressing that resilience and adaptability are becoming essential skills in the future of work.

Cyber Security Expert and CEO of Serensic Africa, Esther Lugoe Mengi, challenged women to break barriers in technology and cybersecurity during her presentation on “Bridging the Digital Glass Ceiling.” She emphasized the need for greater female representation in emerging technologies and digital leadership spaces. 
 

Meanwhile, Founder and CEO of Unleashed Africa Social Enterprises, Khalila Mbowe, highlighted concerns over bias in artificial intelligence systems used in recruitment and promotions. She warned that unless ethical safeguards are introduced, AI could reinforce workplace inequalities instead of eliminating them.

The discussions explored critical issues affecting women in the digital era, including bridging the digital gender gap in AI adoption, ethical leadership, responsible use of technology, and addressing bias in AI-driven recruitment and promotions. Participants also highlighted the importance of adaptability, lifelong learning, networking and mentorship in helping women remain relevant in highly competitive environments.

Founder of HASH Tanzania, Vivian Temi, said the initiative aims to create a supportive community where women can openly discuss challenges facing mothers and caregivers in workplaces increasingly influenced by automation and digital systems.


“We want women to understand that caregiving should never limit their dreams, ambitions or leadership potential. Women deserve opportunities to grow, reskill and thrive while still taking care of their families,” she said.

A fireside discussion featuring Veronica Muumba, Head of Talent Management at CRDB Bank Plc, and moderated by Maureen Njeri, Head of Brand and Marketing at Settlo Technologies Limited, highlighted how institutions can create supportive environments for employees balancing caregiving and career advancement.

The discussion showcased how progressive workplace policies such as flexible working arrangements, mentorship programs, wellness initiatives and digital upskilling opportunities are helping women thrive professionally while maintaining family responsibilities.

Participants also took part in an interactive panel discussion moderated by Lucy Tomeka, featuring Shumbana Walwa of Equity Bank Tanzania, emotional intelligence counselor Ngianasia Marealle Minja and Kai Mollel of Stanbic Bank Tanzania. The panelists shared practical experiences on overcoming workplace barriers, adapting to technological shifts and building sustainable careers while caregiving.

Many attendees called for stronger workplace policies that support women through flexible work arrangements, access to digital training, affordable childcare services and inclusive leadership programs that promote gender equality in decision-making spaces.

The event concluded with a renewed call for governments, private sector institutions and development partners to invest more in women’s digital empowerment and skills development to ensure they fully participate in shaping the future economy.

Participants agreed that empowering women with technology, financial literacy and leadership skills is not only critical for gender equality, but also essential for sustainable social and economic development across Africa in the digital age.



Top News