Na Mwandishi Wetu Michuzi Tv

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imebainisha njia rasmi zinazotumika katika usambazaji wa taarifa za hali ya hewa nchini, huku ikiwasisitiza wananchi kuachana na matumizi ya taarifa zisizo rasmi zinazozagaa mitandaoni.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa TMA – Ofisi ya Zanzibar, Masoud Makame Faki, alipokuwa akizungumza na wananchi kupitia vyombo mbalimbali vya habari kwa lengo la kuwakaribisha kutembelea banda la TMA katika Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara Zanzibar (ZITF) yanayoendelea katika Viwanja vya Nyamanzi kuanzia Desemba 29, 2025 hadi Januari 16, 2026.

Faki amesema wananchi wanapaswa kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa kupitia njia rasmi zinazotumiwa na TMA, ikiwemo vyombo vya habari vilivyosajiliwa, blogu na tovuti ya Mamlaka (www.meteo.go.tz) pamoja na mitandao ya kijamii ya TMA ikiwemo YouTube, Instagram, Twitter (X), WhatsApp Channel na Facebook, ambazo akaunti zake zinapatikana kwenye ukurasa wa mwanzo wa tovuti ya Mamlaka.

“Ninawasisitiza wananchi kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa kupitia njia rasmi za TMA na kuachana na tabia ya kusambaza taarifa potofu wanazozikuta mitandaoni, kwani zinaweza kuathiri mipango ya maendeleo inayotekelezwa nchini,” amesema Faki.

Ameongeza kuwa kupitia maonesho hayo, TMA inaendelea kutoa elimu na ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya hali ya hewa, ikiwemo hali ya fukuto la joto inayoendelea kushuhudiwa visiwani Zanzibar.

Faki ameeleza kuwa kwa sasa Dunia ipo kwenye mzunguko unaoelekea katika kizio cha kusini, hali inayosababisha kuwepo kwa jua la utosi na kuongeza kiwango cha joto. Aidha, kutokana na Zanzibar kuzungukwa na maji, unyevu huongezeka angani na kusababisha wakazi kukumbwa na hali ya fukuto la joto.




Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), inahitaji shilingi bilioni 1.6 kwaajili ya kuwafanyia upasuaji wa moyo watoto 420 wanaougua maradhi ya moyo ambao wazazi wao hawana uwezo wa kugharamia matibabu yao.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Taasisi ya Heart Team Foundation Africa, Dk Naiz Majani, aliyezungumza kwa niaba ya JKCI wakati wa hafa ya kuupongeza mgodi wa madini wa Geita Gold Mine (GGM) kwa kusaidia upasuaji wa watoto 14 wanaougua moyo katika taasisi hiyo.

Alisema HTFA kwa kushirikiana na JKCI mwaka jana walifanya harambee kukusanya fedha za matibabu kwa wagonjwa wa moyo ambapo GGM ni miongoni mwa wadau wengi waliotoa fedha kugharamia matibabu hayo.

“Tulipowaomba GGM walichangia shilingi milioni 56, matibabu ya moyo ni gharama kubwa sana duniani kote na kwa hapa Tanzania asilimia 70 ya matibabu hayo gharama inakuwa kwa serikali na asilimia 30 kwa wazazi lakini bado asilimia 30 ni kubwa sana kwa mtanzania wa kawaida,” alisema

Alisema kwa mwaka 2025 HTAF ilifanikiwa kusaidia watoto 303 kupata matibabu ya moyo kwa upasuaji wa moyo na asilimia tano wamesaidiwa na GGM na maendeleo yao ni mazuri kwa kiwango cha asilimia 95.

Alisema watoto waliosaidiwa na kufanyiwa upasuaji kupitia fedha zilizotolewa na GGM wametoka mikoa 11 ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Iringa, Lindi, Kibosho, Mbeya, Singida, Handeni, Pwani na Mbeya.

Dk Naiz alisema katika kila watoto 100 wanaozaliwa wakiwa hai mmoja au wawili wanakuwa na tatizo la moyo na kuongeza kuwa takwimu za hapa nchini ni kwamba kila mwaka wanazaliwa watoto milioni mbili kwa hiyo kuna watoto 10,000 ambao kila mwaka wanazaliwa na matatizo ya moyo.

Makamu wa Rais wa GGM, Simon Shayo, alisema wanaona fahari kuwa sehemu ya jitihada za kusaidia kuokoa maisha ya watoto wanaougua moyo na alitoa wito kwa taasisi mbalimbali kuunga mkono jitihada zinazofanywa na JKCI kuokoa maisha ya watoto wanaougua moyo.

“GGM tunajisikia fahari kubwa sana kuwa sehemu ya juhudi hizi, hatujutii na tunaona ni wajibu wetu kuwasaidia watanzania katika sekta hii ya afya, napenda kuwaambia watu wa sekta binafsi kuwa biashara unayofanya itakuwa na faida tu pale itakapokuwa inasaidia kubadilisha ustawi wa watu,” alisema

“Hapa JKCI kuna kazi ya kuwaokoa watoto na kurejesha tabasamu kwao, sisi GGM tunaahidi kuendelea kushirikiana na JKCI, ingawa hatujapata maombi rasmi lakini naamini mkileta ombi tutaweka kwenye mpango wetu wa utekelezaji,” alisema

Mkurugenzi Mkuu wa Global Medicare, Abdulmalik Mollel aliishukuru GGM kwa namna ambavyo imekuwa mstari wa mbele kusaidia watoto wanaougua moyo kutibiwa katika taasisi ya JKCI.







Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imezindua siku ya Taaluma ya Uhasibu "Annual Accountancy Career Day" yenye lengo la kuimarisha na kukuza taaluma ya uhasibu nchini. Sambamba na hilo Bodi imefanya uzinduzi wa mfumo utakaowakutanisha pamoja waajiri, wanachama wa Uhasibu, Wanafunzi wa Vyuo mbalimbali kutoka (CBE, UDSM, NIT, IFM, TIA, Mzumbe, Chuo cha Kodi, Chuo Kikuu cha Ardhi nk.) pamoja na wanazuoni "NBAA Accountancy Hub".

Akifungua jukwaa hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA. Prof. Sylvia S. Temu, amesema kuwa wazo la kuandaa siku hiyo ya Taaluma ya Uhasibu "Annual Accountancy Career Day" lilitokana na jitihada za makusudi za Bodi kutafuta siku maalum ya kuwakutanisha wanafunzi wa Elimu ya juu, watahiniwa wa mitihani ya Bodi na waajiri ili wakae pamoja na kujadiliana mustakabali wa taaluma ya Uhasibu nchini.

CPA. Prof. Temu alisema Bodi inatarajia jukwaa hilo kuleta matokeo makubwa, akibainisha kuwa ni fursa ya kipekee inayokutanisha kizazi kipya cha wahasibu na wahasibu wabobezi pamoja na waajiri kutoka sekta mbalimbali. Alieleza kuwa jukwaa hilo linaweka mazingira bora ya kuchagiza maono, matarajio na matumaini ya wahasibu wa sasa na wa baadaye.

Aliongeza kuwa NBAA inapenda kusikia moja kwa moja mawazo, matarajio na changamoto zinazowakabili wanafunzi na watahiniwa wa Mitihani ya Bodi katika safari yao ya kitaaluma, ili Bodi na wadau wake waendelee kuijenga taaluma ya Uhasibu kwa kuzingatia uhalisia wa mazingira ya kazi.

Aidha, alisema jukwaa hilo linawakutanisha washiriki na taasisi za sekta binafsi na za umma, jambo linalowapa fursa ya kupata uzoefu na kuwaunganisha moja kwa moja na wahasibu wabobezi pamoja na waajiri, ili kuelewa mahitaji halisi ya soko la ajira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno, alisema kuwa "Annual Accountancy Career Day" ni nguzo muhimu katika maandalizi ya watahiniwa wa Mitihani ya Bodi na maisha ya kazi, kwa kujenga daraja kati ya elimu ya kitaaluma darasani na uhalisia wa taaluma ya Uhasibu.

Katika jukwaa hilo, kulikuwa na mabanda takribani 30 kutoka kwa waajiri na taasisi mbalimbali, zikiwemo Taasisi za Serikali, Taasisi za fedha, kampuni za Ukaguzi na Uhasibu,  ambapo washiriki walipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na waajiri.
Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA. Prof. Sylvia S. Temu akisoma hotuba ya ufunguzi wa siku ya Taaluma ya Uhasibu "Annual Accountancy Career Day" yenye lengo la kuimarisha na kukuza taaluma ya uhasibu nchini. Sambamba na hilo Bodi imefanya uzinduzi wa mfumo utakaowakutanisha pamoja waajiri, wanachama wa Uhasibu, Wanafunzi wa Vyuo pamoja na wanazuoni "NBAA Accountancy Hub". uliofanyika katika ofisi za NBAA jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno akizungumza kuhusu mchakato wa kuanzisha "Annual Accountancy Career Day" ili kuwakutanisha waajiri, wanachama wa Uhasibu na Ukaguzi, Wanafunzi wa Vyuo pamoja na wanazuoni ili kuendeleza taaluma ya Uhasibu nchini.
Mkurugenzi wa Huduma za Shirika kutoka NBAA CPA Kulwa Malendeja akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa "Annual Accountancy Career Day" uliofanyika katika ofisi za NBAA jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali (CBE, UDSM, NIT, IFM, TIA, Mzumbe, Chuo cha Kodi, Chuo Kikuu cha Ardhi nk.) pamoja na wadau wa Uhasibu wakifuatilia hotuba za ufunguzi wa "Annual Accountancy Career Day"  uliofanyika katika ofisi za NBAA jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA. Prof. Sylvia S. Temu akikabidhi vyeti pamoja na tuzo kwa kutambua mchango wa wadhamini wa "Annual Accountancy Career Day" iliyofanyika katika ofisi za NBAA, Mhasibu House jijini Dar es Salaam tarehe 13/01/2026.
Picha za pamoja za meza kuu, waajiri, wadhamini na washiriki wa siku ya taaluma ya Uhasibu
Vodacom Tanzania imeendeleza mpango wake wa Kapu la Vodacom kwa kuzindua msimu mwinginewa ‘Back to School’, hatua inayothibitisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni katika kusaidia jamii kupitia elimu. Kupitia kampeni hii, Vodacom inalenga kuwasaidia wazazi na wanafunzi kurejea shuleni kwa kuwapatia mamia ya makapu ya vifaa vya shule (Kapu la Shule) kwa familia na wanafunzi wanaohitaji msaada zaidi katika mikoa mbalimbali nchini.

Mpango wa Kapu la Vodacom ulianza kama jitihada za kusaidia jamii wakati wa msimu wa sikukuu, lakini sasa umebadilika na kuwa harakati kubwa ya mshikamano na kujali, ikihakikisha elimu inaendelea kuwa kipaumbele kwa kila mtoto. Kupitia mpango huu, Vodacom inasimama bega kwa bega na wazazi pamoja na wanafunzi katika maandalizi ya mwaka mpya wa masomo, huku ikisaidia kupunguza mzigo wa gharama ambao huwa ni mkubwa hasa mwezi wa Januari.

Akizungumza kuhusu mpango huu, Mkurugenzi wa M-Pesa Vodacom Tanzania, Epimack Mbeteni alisema kuwa elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. Alisema kuwa kuendeleza Kapu la Vodacom zaidi ya msimu wa sikukuu ni uwekezaji wa moja kwa moja katika mustakabali wa watoto na Taifa la Tanzania.

Aliongeza kuwa mpango wa “Kapu la Vodacom Back to School” hauhusiani tu na utoaji wa misaada, bali ni kuhusu kujenga mshikamano wa kijamii na kuhakikisha kila mtoto anapata nyenzo muhimu za kufanikisha masomo yake. Alisisitiza kuwa huu si msaada wa hisani, bali ni jitihada za pamoja za kujali na kusonga mbele kama jamii moja.

Vodacom imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuleta mabadiliko chanya na endelevu kupitia miradi inayowawezesha familia na kuimarisha mifumo ya elimu nchini. Kampeni ya Kapu la Vodacom ilizinduliwa rasmi mwishoni mwa Novemba mwaka jana, ikiwa na lengo la kusherehekea na kushirikiana na wateja wake kwa kuwapatia furaha na shukrani katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Kwa ujumla, mpango huu unalenga kuleta uzoefu wa kipekee kwa wateja, kuimarisha uhusiano kati ya Vodacom na jamii, pamoja na kudhihirisha dhamira ya kampuni ya kuendelea kuwa karibu na wateja na jamii zake wakati wote.



Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania Plc eneo la Kawe na Bagamoyo Naomi Kasera (kulia) akikabidhi Kapu kwa Mzazi Fransisca Mosha ( Kushoto) na Mwanafunzi wa shule ya msingi Bunju A, Njma Juma (katikati) katika muendelezo wa kampeni ya “Tupo Nawe Tena na Tena” ikilenga kugawa makapu yenye vifaa vya shule kwa wateja mbalimbali nchini. Kampeni hiyo imeendelea kugawa makapu katika shule tofauti hapa nchini, Hafla hii imefanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwaunga mkono wazazi katika msimu huu wa Watoto kurudi mashuleni kwa kutoa baadhi ya vifaaa vya shule vitakavyo wezesha Watoto kuendelea na masomo yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hakuna taifa linaloweza kufikia maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wake bila kuwepo kwa usimamizi mzuri wa haki unaosimamiwa na Mahakama huru, yenye uwezo na uadilifu.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Januari 13, 2025 jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA), unaoongozwa na kauli mbiu “Jukumu la Mahakama Huru Katika Utoaji Haki.”

Dkt. Samia amesema uwepo wa Mahakama huru ni nguzo muhimu ya utawala bora na ni msingi wa upatikanaji wa haki kwa wananchi, akisisitiza kuwa uhuru wa Mahakama lazima uende sambamba na uwajibikaji, uadilifu, nidhamu, utii wa sheria na uzalendo kwa taifa.

“Serikali itaendelea kuulinda na kuheshimu uhuru wa Mahakama, lakini uhuru huo hauna budi kuenda sambamba na uwajibikaji na maadili ya kazi."

Aidha, Rais Samia amesema Dira ya Taifa ya 2025–2050 imejengwa juu ya misingi ya utawala bora, amani, usalama na utulivu, akibainisha kuwa mhimili wa Mahakama una nafasi muhimu katika kujenga taifa lenye haki na ustawi wa kudumu.

Mkutano huo wa TMJA unawakutanisha majaji na mahakimu kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kujadili masuala ya uboreshaji wa utoaji haki na kuimarisha utendaji wa Mahakama.






 

Na Mwandishi Wetu

KATIBU wa Halmashauri Kuu(NEC)ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo Kenan Kihongosi amefanya kikao kazi na viongozi mbalimbali wa Chama hicho pamoja na wasanii wa Bendi ya TOT.

Kihongosi amefanya kikao kazi hicho leo katika Ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam ambapo katika kikao hicho ametumia nafasi hiyo kuelezea mipango na mikakati mbalimbali yenye lengo la kuiimarisha Chama hicho.

Aidha Kenan amewahakikishia viongozi walioshiriki kikao kazi hicho kwamba anatambua kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi Mkuu 2025 napia kwa lengo la kukifanya Chama Cha Mapinduzi kuendelea kuwatumikia wananchi ambao wamekuwa na matumaini makubwa na Chama hicho chini ya Mwenyekiti wao Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.









Top News