Balozi Mteule wa Tanzania nchini Oman, Mheshimiwa Maulidah Hassan, amefanya ziara ya kumuaga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Kombo amempongeza Balozi Maulidah kwa kuaminiwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mchango wake alioutoa alipokuwa Msaidizi Binafsi wa Rais katika masuala ya diplomasia.

Aidha, amemsisitiza kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Oman, hususan katika sekta za biashara, uwekezaji na utalii, pamoja na kulinda maslahi ya Watanzania wanaoishi nchini humo, huku akimhimiza kutumia uzoefu wake kuendeleza uhusiano huo.

Kwa upande wake, Balozi Maulidah amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa imani aliyompa na kuahidi kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu na weledi wa hali ya juu. Amesema pia kuwa amedhamiria kuendeleza diplomasia ya uchumi na kuimarisha uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Oman.


Na Farida Mangube, Morogoro

Wakati idadi kubwa ya vijana nchini ikiendelea kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ajira na mitaji, juhudi za makusudi zinaendelea kufanyika ili kuwawezesha kujiajiri na kufikia ndoto zao za kiuchumi.

Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali ya Tanzania kupitia Chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirikiana na Serikali ya Denmark inatekeleza mradi wa Crowdfunding for Youth Entrepreneurship in Tanzania (C4YET), unaowawezesha vijana kupata mitaji kwa njia ya ubunifu kupitia majukwaa ya mtandaoni, hatua inayolenga kuwainua kiuchumi na kuwawezesha kujiajiri.

Akizungumza katika hafla ya kuhitimisha mradi huo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Alen Mushi, amesema mradi huo umeleta mafanikio makubwa kwa kuwafikia vijana waliokuwa na mawazo ya biashara lakini walikosa mitaji ya kuanzisha au kuendeleza shughuli zao.

Amesema kupitia mfumo huo, vijana wanaweza kuwasilisha mawazo yao ya biashara mtandaoni na kuchangiwa fedha, kisha kupata mikopo yenye riba nafuu ya asilimia tatu bila kulazimika kuweka dhamana.

“Zaidi ya vijana 200 tayari wamepatiwa mitaji kwa urahisi bila masharti magumu, huku wengi wao wakiendesha miradi yao kwa mafanikio,” alisema Profesa Mushi.

Kwa upande wake, Mratibu wa mradi huo, Dkt. Nsubili Issaga, ameeleza kuwa mfumo huo unatoa mbadala wa mikopo yenye riba kubwa ambayo awali ilikuwa kikwazo kwa vijana wengi.

Naye Mratibu kutoka Denmark, Profesa Lars Bo Jeppesen, amewataka vijana kuchangamkia fursa hiyo kwa kuwa ni njia muhimu ya kupunguza ukosefu wa ajira na kukuza uchumi kupitia ujasiriamali.

Baadhi ya wanufaika wa mradi huo wamesema kuwa wamefanikiwa kukuza biashara zao na kuongeza mitaji, huku wengine wakipata fursa za masomo ya juu ikiwemo Shahada ya Uzamivu (PhD).

Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Tanzania ina zaidi ya watu milioni 61, ambapo zaidi ya milioni 20.6 ni vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35, kundi ambalo ndilo nguvu kazi ya taifa lakini linaendelea kukumbwa na changamoto ya ajira na mitaji.









Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kusogeza nishati safi ya kupikia kwa wananchi baada ya kuzindua duka maalum la kuuza mitungi ya gesi ya Oryx na majiko yake katika Wilaya ya Chato mkoani Geita.

Uzinduzi huo umefanyikq eneo la Kabwanga wilayani Chato na kuhudhuriwa na wadau wa nishati safi akiwemo mgeni rasmi ambaye ni Ofisa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Nishati na Maji(EWURA) Mkoa wa Geita Bwanawadi Omari pamoja na wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Ofisa Huduma kwa Wateja EWERA Mkoa wa Geita Bwanawadi Omar amesema hatua hiyo ni muhimu katika kupunguza utegemezi wa nishati zisizo rafiki kwa mazingira kama kuni na mkaa ambazo zimekuwa zikichangia uharibifu wa misitu na athari nyingine za kiafya kwa wananchi hasa Wanawake na watoto.

“Watalaam wanatuambia ili kupata mkaa itabidi mti ambao utautumia kwa ajili ya kutengeneza mkaa inabidi uusubiri kwa miaka mitano na inategemea kati ya mti mmoja kwenda mti mwingine lakini tunaposema nishati safi ya kupikia tunamaanisha teknolojia ambayo ni rafiki wa mazingira.

“Pia ni gharama nafuu kwa namna moja ama nyingine lakini pia hazalishi sumu yaani kwa mfano sumu inayoweza kuzalishwa kutokana na mkaa ni nyingi zaidi wakati nishati safi ya kupikia haina sumu.Tunakumbuka miaka ya nyuma bibi zetu na mama zetu waliotumia kuni na mkaa kwa muda mrefu walikuwa na macho mekundu na kuwaita wachawi.”

Amesema uamuzi wa Oryx Gas kuweka duka la kuuza mitungi ya gesi ni hatua nzuri na ya kupongezwa kwani wananchi watapata nishati safi ya kupikia katika maeneo yao huku akisisitiza kupika kwa nishati safi ni rafiki wa mazingira.

Awali Meneja Mauzo wa Oryx Gas Tanzania Alex Wambi amesema uzinduzi wa duka hiyo wilayani Chato ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuunga mkono jitihada za Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

“Oryx Gas katika Mkoa huu wa Geita tunayo maduka 11 na tutaendelea kufungua maduka mengine zaidi kwani tunatamani mpaka mwaka unaisha tuwe na maduka yasiyopungua 20.Tunafanya hivi ili kushiriki kikamilifu sera hii ya nishati safi inafanikiwa.

“Ndio maana tunakuja na mpango wa mkakati wa kusogeza huduma kwa wateja wetu kwa kupitia maduka haya ambapo tunalenga pia kusogeza huduma kwa wananchi kupata mtungi wa gesi hasa ile ambayo ni ya bei rahisi kupitia maduka yetu,”amesema Wambi na kuongeza maduka hayo yanatumika kutoa elimu ya matumizi sahihi ya nishati safi ya kupikia.

Aidha amesisitiza mpango mkakati wa Oryx Gas kwa sasa ni kuhakikisha kila Mwananchi katika maeneo yote anatumia nishati safi ya kupikia na ndio maaana wameamua kuwa na maduka ya kuuza gesi hata maeneo ya pembezoni ili Mwananchi apate gesi kirahisi.


























Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imepitisha Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa mwaka wa fedha 2026/2027 inayolenga kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zitakazochochea ukuaji wa Uchumi wa Kidijitali.

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Kamati, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) aliiomba Kamati kuidhinisha matumizi ya Shilingi 222, 589,452,000/- huku akitaja vipaumbele saba (7) vya Bajeti hiyo kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 kuwa ni pamoja na Kutunga, Kuhuisha na kusimamia utekelezaji wa Miongozo inayosimamia Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, na Kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano ya Simu na Posta kote Nchini.

Vipaumbele vingine ni pamoja na Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kukuza na kuimarisha Biashara Mtandao Nchini, Kuimarisha miundombinu itakayowezesha utekelezaji wa Uchumi wa Kidijitali, Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Anga ya Mtandao, Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kuchochea ubunifu na kuimarisha ustawi wa Kampuni Changa za TEHAMA (ICT Startups), na Kuimarisha utekelezaji wa Programu ya Anga za Juu.

Akizungumza wakati wa Kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe, Selemani Kakoso ameipongeza Wizara kwa usimamizi mzuri wa Taasisi zilizo chini yake hali iliyopelekea Taasisi hizo kutoa Huduma za Mawasiliano zilizo bora na za Uhakika kwa Wananchi.

Mhe. Kakoso ameitaka Serikali kuendelea kuzisimamia Taasisi hizo huku akisisitiza kuongeza kasi ya uwekezaji katika Kituo cha Kuhifadhia Data (Data Centre), Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kuliwezesha Shirika la Posta Tanzania na kuhakikisha miradi yote inayosimamiwa na wizara inakamilika kwa wakati.

Naye Waziri Kairuki aliishukuru kamati kwa ushirikiano na ushauri wake uliowezesha kuiongoza Wizara kuongeza kasi ya kutekeleza majukumu yake ya kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini.





Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imepitisha Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa mwaka wa fedha 2026/2027 inayolenga kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zitakazochochea ukuaji wa Uchumi wa Kidijitali.   

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Kamati, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) aliiomba Kamati kuidhinisha matumizi ya Shilingi 222, 589,452,000/- huku akitaja vipaumbele saba (7) vya Bajeti hiyo kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 kuwa ni pamoja na Kutunga, Kuhuisha na kusimamia utekelezaji wa Miongozo inayosimamia Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, na Kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano ya Simu na Posta kote Nchini.

Vipaumbele vingine ni pamoja na Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kukuza na kuimarisha Biashara Mtandao Nchini, Kuimarisha miundombinu itakayowezesha utekelezaji wa Uchumi wa Kidijitali, Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Anga ya Mtandao, Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kuchochea ubunifu na kuimarisha ustawi wa Kampuni Changa za TEHAMA (ICT Startups), na Kuimarisha utekelezaji wa Programu ya Anga za Juu. 

Akizungumza wakati wa Kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe, Selemani Kakoso ameipongeza Wizara kwa usimamizi mzuri wa Taasisi zilizo chini yake hali iliyopelekea Taasisi hizo kutoa Huduma za Mawasiliano zilizo bora na za Uhakika kwa Wananchi. 

Mhe. Kakoso ameitaka Serikali kuendelea kuzisimamia Taasisi hizo huku akisisitiza kuongeza kasi ya uwekezaji katika Kituo cha Kuhifadhia Data (Data Centre), Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kuliwezesha Shirika la Posta Tanzania na kuhakikisha miradi yote inayosimamiwa na wizara inakamilika kwa wakati.

Naye Waziri Kairuki aliishukuru kamati kwa ushirikiano na ushauri wake uliowezesha kuiongoza Wizara kuongeza kasi ya kutekeleza majukumu yake ya kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini.





Mkuu wa Wilaya ya Rorya Dkt. Khalfany Haule  akizungumza na maafisa wa TASAC waliotembelea Ofisi ya Mkoa wa Mara hawapo pichani.
Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija akitoa elimu ya usalama majinI kwa   Wavuvi wa Wilaya ya Rorya.


*Jaketi Okozi ni Uhai na sio mzigo kwa msafirishaji

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Wilaya ya Rorya imetoa wito kwa wavuvi na wamiliki wa mitumbwi kuacha kupuuza matumizi ya vifaa vya kuokoa maisha majini.

Hayo ameyasema Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Mhe. Dkt. Khalfany Haule wakati maafisa Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC) walipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kutoa elimu ya Usalama wa vyombo vya majini.

Dkt. Haule alionya dhidi ya mtazamo potofu kwamba maboya ni mzigo wa gharama na kikwazo cha kazi ya uvuvi

Amesema kwa takwimu za mwaka uliopita, zaidi ya wavuvi 20 walipoteza maisha kutokana na mitumbwi kuzama, licha ya kuwa na maboya ndani ya vyombo lakini bila kuyavaa.

"Kupoteza maisha ni pigo kubwa kwa familia na inapunguza nguvu kazi ya taifa” amesema Mhe.Dkt.Haule

Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija, aliongeza kuwa wavuvi wengi hujiamini kupita kiasi kwa kudhani ujuzi wa kuogelea unatosha, jambo linalowaweka hatarini. Kwa sasa ni msimu wa upepo mkali, mawimbi makubwa na mvua zinazoendelea kunyesha zimeongeza hatari ya ajali majini.

Kwa kukabiliana na hilo, TASAC imeanzisha kampeni ya kutoa elimu kwa wamiliki wa vyombo vidogo, wavuvi, vyama vya wamiliki na wananchi ili kuondoa mitazamo potofu, tabia ya kupuuza na kuimarisha usalama wa usafiri majini.

Mhandisi Lusangija aliongeza kuwa wavuvi na wasafirishaji wajenge utamaduni wa kufuatilia utabili wa hali hewa kuliko kutumia utaalam wa asili, watumie mialo rasmi na kuwa na maboya.

Hata hivyo, baadhi ya wamiliki wa mitumbwi, akiwemo Hamza Kisuki, wamelalamikia tabia ya wavuvi kuvua maboya mara wanapofika majini na kuyageuza kuwa mito ya kulalia, wakijiamini kuwa uwezowao wa kuogelea unatosha.

Elimu hii imeanza kutolewa katika mwalo wa Esegere na Nyang’ombe, na itaendelea katika mialo ya Kinesi, Sota, Luhu, Busanga na Kilongwe. Walengwa ni viongozi wa Serikali za Mitaa, BMU, wavuvi, wamiliki wa mitumbwi na wananchi kwa ujumla.
Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija akitoa elimu kwa mvuvi namna ya kuvaa jaketi Okozi wakati wa dharula ya hatari.
Wavuvi na wamiliki wa Mitumbwi wakipata elimu ya usalama majini kutoka kwa maafisa wa TASAC hawapo pichani.

Top News