- Yabadilishana uzoefu katika masuala mazima ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira .

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekutana na kufanya mazungumzo na Wizara ya Mazingira, Maendeleo ya Miji na Mabadiliko ya Tabianchi, Taasisi ya Utafiti wa Udongo, Maji na Majanga, Idara ya Maji safi na Maji Taka, Taasisi ya Mradi wa Maendeleo ya Mji wa Konya na Kampuni ya Turko wakati wa maonesho ya zana bora na pembejeo za kilimo na kilimo hifadhi katika Mji wa Konya nchini Uturuki

Mazungumzo hayo yalilenga kubadilishana uzoefu katika masuala ya usimamizi na uhifadhi wa mazingira ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa na kujifunza mbinu bora zinazotumika katika kukabiliana na changamoto za kimazingira.

Akifafanua utekelezaji wa majukumu kutoka NEMC,wakati wa mazungumzo hayo Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi Bi Suzan Chawe amesema wajibu wa Baraza ni kushauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu masuala ya Mazingira na kusimamia Uhifadhi wa Mazingira kwa mujibu wa Sheria na kuainisha majukumu mengine ya Baraza iliyonayo kuwa ni kusimamia mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii, Utafiti wa Mazingira, Uzingatiaji na Utekelezaji Sheria na kutoa elimu ya Mazingira.

Mada zilizojadiliwa ni pamoja na matumizi ya zana zenye kuzingatia kilimo hifadhi, utafiti na utoaji taarifa za kimazingira kwa umma, ushirikishaji wa wadau katika utekelezaji wa Sheria za mazingira, utoaji wa elimu ya mazingira kwa jamii hususani mashuleni, pamoja na mikakati ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, wataalam wa Mazingira kutoka Konya walisisitiza umuhimu wa tafiti za kisayansi katika sekta mbalimbali ili kuboresha maamuzi ya kikanuni na kisheria na namna ya kudhibiti uchafuzi unaotokana na shughuli za viwanda.

Mbali na mazungumzo hayo, NEMC pia ilipata fursa ya kutembelea maonesho ya kilimo nchini humo yaliyolenga kuonesha zana zenye kukuza kilimo hifahi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha Maendeleo endelevu yenye kuzingatia usimamizi bora wa mazingira kwa kizazi kijacho.

Ujumbe wa NEMC kutoka Tanzania, ulioambatana na wawakilishi kutoka Wizara ya Kilimo pamoja na wadau wa mazingira , pia ulipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Mhe. Iddi Seif Bakari hatua iliyoonesha dhamira ya nchi katika kuimarisha diplomasia ya mazingira na ushirikiano wa kimataifa

Faida za ujio wa NEMC kwenye maonesho hayo pamoja na mazungumzo yaliyofanyika yanatarajia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya NEMC pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Uturuki katika sekta ya mazingira.










Na.Vero Ignatus, Arusha

Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na michezo imeendesha mafunzo kwa waandaa maudhui mtandaoni Mkoani Arusha yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo ili kuleta tija kwa kazi zao katika majukwaa mbalimbali ya mitandaoni

Akizungumza Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Utamaduni na sanaa CPA Nyakaho Mturi Mahemba Mafunzo amesema mafunzo hayo yalikuwepo na watoa mada mbalimbali kutoka kwa wabobevu ambapo mada hizo zitawasaidia kuzalisha maudhui mazuri yenye maadili katika jamii yanayothamini utu na nchango wa Mtanzania katika shughuli za kila siku.

Aidha amesema lengo la mfuko huo wa Utamaduni nia thabiti ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwapatia fursa vijana waaoandaa maudhui mtandaoni kwa kuwapatia mikopo wenye riba nafuu Kukuza, kuendeleza na kuimarisha sekta ya sanaa na utamaduni kwa manufaa ya kijamii na kiuchumi.

"Mfuko huu unalenga Kukuza ajira kupitia sanaa kwa vijana na wadau wa sekta Kuinua ubora wa kazi za sanaa ili ziweze kushindana ndani na nje ya nchi uchochea uchumi wa ubunifu una lengo la kusaidia sera za serikali katika kukuza sekta ya sanaa"

Mahemba amesema Vile vile katika mafunzo hayo wametoa Elimu ya fedha namna ya kuweka Akiba elimu ya urasimishaji, na uwekezaji ambapo itawasaidia waandaa maudhui kukopo kwa nidhamu nakusimamia mitaki yao vyema ili iweze kuwa na tija.

Mafunzo hayo yaneweza kushirikisha waandaa maudhui mtandaoni zaidi ya 450 ambapo waikuwepo na watoa mada mbalimbali wabobevu.

Baada ya kuwezeshwa mtaji tumieni vizuri katika maeneo mliyokusudia na mrudishe kwa wakati ili wengine nao waweze kunufaika rudisheni mikopo kwa wakati hiyo ili wengine nao wanufaike.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Kelvin Kanje amesema mafunzo hayo ya awamu ya kwanza kwa watengeneza Maudhui mtandaoni yalianzia mkoa wa Dar es salama, Mwanza ambapo wamehitimisha mkoani wa Arusha .

Aidha amesema mafunzo hayo ni ahadi aliyoutoa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia. Suluhu Hassan kwa kutangaza fursa kwa vijana kwa kutoa Bil 50 ambapo wengine wameshakopa n kuchukua fedha huku wengine wakiendelea kujipanga .

Kwa upande wake mtengeneza Maudhui Mtandaoni Fahad Fuad amesema wakati sahihi wa kutengeneza maudhui ameeleza kwa kina mbinu na mikakati ya kuchagua muda wenye tija ili kufikia hadhira kwa ufanisi zaidi.

Amefafanua umuhimu wa kuelewa tabia za watazamaji, sambamba na majukwaa yanayotumika pamoja na mzunguko wa matumizi ya mitandao ili kuongeza ushawishi na mwonekano wa maudhui

Aidha Mafunzo haya ya awamu ya kwanza jijini Arusha yanawaleta pamoja wabunifu wa maudhui ili kujifunza, kubadilishana uzoefu, na kuboresha ubora wa kazi zao. Hii ni hatua muhimu katika kukuza uchumi wa kidijitali na kuimarisha nafasi ya Tanzania kwenye ramani ya maudhui ya mtandaoni.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Utamaduni na sanaa  CPA Nyakaho Mturi Mahemba
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Kelvin Kanje akizungumza na waaandaaji mudhui mtandaoni Jijini Arusha





Washiriki wa mafunzo na waaandaaji maudhui mtandaoni

 

NA MWANDISHI WETU.

BENKI ya NMB imepuliza rasmi kipyenga cha matumizi ya Magari Maalum Yanayotoa Huduma za Kibenki (Matawi Yanayotembea – Bank on Wheels), huku wakazi wa Dar es Salaam wakiipongeza benki hiyo kwa kuiishi kwa vitendo kaulimbiu yake ya Karibu Yako.

Mapema mwaka huu, NMB iliyatambulisha rasmi magari nane yatakatotumika kama Matawi Yanayotembea, yakilenga kuwafikishia Huduma Jumuishi za Kibenki wakazi wa mijini na vijijini, hususani kwenye masoko, minada ya mifugo, biashara na machimbo ya madini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa utoaji huduma jijini Dar es Salaam Alhamisi Aprili 9, Mkuu wa Idara ya Mauzo na Mtandao wa Matawi ya NMB, Donatus Richard, alisema ‘Bank on Wheels’ ni sehemu ya mkakati wao wa usambazaji wa Huduma za Kibenki Vijijni ‘NMB Rural Banking Strategy.’

Alibainisha kuwa, magari hayo yatagawanywa katika kanda mbalimbali za beni hiyo, kuyaongezea nguvu yale waliyokuwa nayo awali, lengo likiwa ni kuwafikia wateja wao zaidi ya Mil. 10 na kuvutia wengine kufungua akaunti na kuwa sehemu ya benki hiyo ili kuharakisha ukuaji wao kiuchumi.

“Magari haya ni zaidi ya fursa kwa wateja wetu, wajasiriamali, wafanyabiashara kwenye masoko na minada na kwa wadau wa mnyororo wa thamani kilimo unaojumuisha kilimo chewe, ufugaji na uvuvi, kuwawezesha kupata huduma za kifedha, ushauri, bima, mikopo na elimu ya fedha.

“Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa taasisi nyingi za fedha hususani mabenki, yamejikita katika kuimarisha utoaji huduma mijini, lakini sisi NMB tunatambua ukubwa wa mzunguko wa fedha uliopo huko na ndio maana tumechagua kuwafuata huko kuwahudumia kwa ukaribu bila kuwapotezea muda.

“Leo tumeanza rasmi kutoa huduma kupitia magari haya yaliyozinduliwa wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Muda wa Kati wa Mwaka 2026 hadi 2030 (MTP Agenda 2030). Haya yanaenda kuungana na yale yaliyokuwepo awali na, lakini tutayaongeza kulingana na mahitaji,” alisema.

Donatus alibainisha kwamba watayagawa katika Kanda za Dar es Salaam, Zanzibar, Kanda ya Kati, Kanda ya Kusini, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Magharibi na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, ambako yatapangiwa ratiba ya kutoa huduma katika mikoa inayounda kanda hizo.

Aliwataka Watanzania kuhakikisha wanaendana na kasi ya benki yake katika kujenga Uchumi Jumuishi, tangu walipoanza na NMB Mkononi, kisha wakaja na mawakala ambao sasa wamefikia zaidi ya 73,000 kote nchini na sasa kuja na Matawi Yanayotembea, lengo likiwa kuharakisha ukuaji wao kiuchumi.

Hellen Mushi, ambaye ni mfanyabiashara wa Duka la Simu katika Jengo la Manzese Plaza, lililopo Manzese Bakhresa, alikiri kufurahishwa na namna NMB inavyowajali wateja wao kwa kuwasogezea huduma za kibenki mahali walipo na kwamba hiyo ndio maana halisi ya Karibu Yako.

“Binafsi hii imenivutia sana, nimekuwa mteja ninayetumia huduma za NMB kwa muda mrefu, lakini kila uchao wamekuwa na utamaduni wa kubuni bidhaa na huduma rafiki kwa wateja. Hii ‘Bank on Wheels’ ni kubwa na bora zaidi, kwa sababu inatupa uhuru sisi tusiopenda kupoteza muda matawini.

“Nawapongeza na kuwashukuru, huku nikiwataka Watanzania kuchangamkia fursa zilizomo katika huduma za benki hii, ambayo licha ya kuwa na matawi mengi karibu katika kila wilaya, lakini bado inaona umuhimu wa kuwafikia walioko vijijini, minadani na mashambani,” alisema Hellen.

Naye Mchungaji Elias Masangu Waburuba, Mkazi wa Kahama mkoani Shinyanga, aliyeshuhudia uzinduzi wa utoaji huduma wa ‘Bank on Wheels’ jijini Dar es Salaam, aliipongeza NMB kwa huduma bora, bunifu, rahisi, salama na nafuu kwa wateja wao wadogo, wa kati na wakubwa.

“Benki hii imekuwa rafiki kwa wateja wao na wananchi kwa ujumla, wakiwemo walioko mbali na miji, kwa sababu huduma zao zimesambaa mpaka vijijini sio tu kupitia matawi, bali mawakala wao, huku pia kukiwa na huduma za NMB Mkononi, ambayo ni rahisi kutumia ikiwa na fursa kibao.

“Ndio maana nakiri kwamba NMB ni benki iliyorahisisha sana huduma za kifedha kwa wananchi, binafsi naipongeza kwa huduma bora na kwa kuwa nimekuja Dar es Salaam kibiashara tu kutoka Kahama, basi naamini tutakutana tena huko vijijini na naahidi kuwa balozi mwema wa benki hii.

“Kule kwenye magulio na minada ya mifugo, mazao na madini, vihatarishi kwa watu wenye pesa taslimu mkononi ni vingi, ikiwemo wizi, uporaji, upotevu na mengineyo, kwa hiyo NMB kuja na Matawi Yanayotembea, ni kutusaidia sisi wadau wa biashara,” alisisitiza Mchungaji Elias.

Madereva wa malori, mama lishe, wauza mitumba na bidhaa zingine wanaozunguka eneo la Manzese Darajani, walioshuhudia uzinduzi wa utoaji huduma za kibenki kupitia Matawi Yanayotembea, waliipongeza NMB kwa kuwa mbele ya wakati kupitia huduma zao bunifu.
Mkuu wa Idara ya Mauzo na Mtandao wa Matawi ya Benki ya NMB, Donatus Richard (katikati), akimhudumia  Mwajuma Athumani Saidi aliyehudhuria uzinduzi rasmi wa utoaji huduma kupitia magari maalum (Matawi Yanayotembea - Bank on Wheels'), uliofanyika jijini Dar es Salaam. Magari hayo nane ni sehemu ya mkakati endelevu wa usambazaji Huduma za Kibenki Vijijini 'NMB Rural Banking Strategy. 
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam Seka Urio (kulia), akishuhudia mfanyakazi wa benki hiyo akimhudumia mmoja wa wateja ndani ya magari maalum ya kutoa huduma za kibenki (Matawi Yanayotembea - Bank on Wheels'), aliyehudhuria uzinduzi rasmi wa utoaji huduma wa magari hayo
uliofanyika jijini Dar es Salaam. Magari hayo nane ni sehemu ya mkakati endelevu wa usambazaji Huduma za Kibenki Vijijini 'NMB Rural Banking Strategy. 
Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Seka Urio (wa nne kushoto), akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo, wakati wa uzinduzi rasmi wa utoaji huduma kupitia magari maalum (Matawi Yanayotembea), uliofanyika jijini Dar es Salaam Alhamisi Magari hayo nane ni sehemu ya mkakati endelevu wa usambazaji Huduma za Kibenki Vijijini 'NMB Rural Banking Strategy. '

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekihakikishia Chama cha Mawakili Zanzibar kuwa Serikali inathamini na kuunga mkono kazi nzuri inayofanywa na taasisi hiyo ya kuwasaidia wananchi katika masuala ya kisheria.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 09 Aprili 2026, alipokutana na uongozi wa Chama cha Mawakili Zanzibar ulioongozwa na Rais wa chama hicho, Wakili Joseph Shaban Magazi, waliofika Ikulu, Zanzibar.

Hata hivyo, ameshauri uongozi wa chama hicho kulipatia ufumbuzi wa kudumu tatizo la wanafunzi wa ngazi ya digrii ya sheria wanaoshindwa kuendelea na masomo. 

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amepongeza uamuzi wa Chama cha Mawakili Afrika Mashariki kufanya mkutano mkuu wa mwaka hapa Zanzibar, na kwamba Serikali, kwa kushirikiana na wadau, itaunga mkono kufanikisha mkutano huo.

Naye Rais wa Chama cha Mawakili Zanzibar, Ndugu Joseph Shaban Magazi, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa uongozi wake na juhudi zake katika kuifungua Zanzibar na kuifanya kuwa kituo bora cha uwekezaji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati

Kwa upande mwingine,  Rais Dkt. Mwinyi ametumia fursa hiyo kuikabidhi gari taasisi hiyo, ambayo iliomba katika maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyopita, kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake.











Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetoa tuzo kwa washindi 10 wa shindano la insha la viwango la mwaka 2024/2025, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Viwango Afrika mwaka 2026. 

Washindi hao wametoka katika vyuo mbalimbali nchini, ambapo jumla ya washiriki walikuwa wanafunzi 522 wa elimu ya juu kati yao, wanawake walikuwa 230 na wanaume 292, huku shindano hilo likiratibiwa na Shirika la Viwango Afrika (ARSO).

Akizungumza leo Aprili 9, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria wa TBS, Dkt. Candida Shirima, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu, amesema taasisi hiyo inatambua mchango wa washiriki hao katika kuongeza uelewa wa viwango na kuelimisha jamii.

Amesema viwango vina mchango mkubwa katika kukuza biashara kwa kuongeza uaminifu kwa walaji, kuchochea biashara endelevu na kukuza uchumi wa taifa, huku akisisitiza umuhimu wa kuzingatia viwango kila siku.

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa shindano hilo, Dkt. Jalia Muna, amesema insha tano bora kutoka kwa washindi hao zitawasilishwa ARSO kwa ajili ya kushindanishwa barani Afrika, na maoni ya washindi yatasaidia kuboresha utendaji kazi wa TBS.
















Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Rhimo Nyansaho, tarehe 9 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo ya kikazi na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Guy Kabombo Muadiamvita, aliyekuwa katika ziara rasmi nchini Tanzania.


Mazungumzo hayo yamefanyika katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo jijini Dodoma, yakilenga kuimarisha ushirikiano wa kihistoria na kidiplomasia wa ulinzi kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katika kikao hicho, Dkt. Nyansaho alimhakikishia mgeni wake kuwa Serikali ya Tanzania, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, iko tayari kuendeleza ushirikiano na DRC katika sekta mbalimbali za ulinzi. Maeneo hayo ni pamoja na kubadilishana wataalamu, kutoa mafunzo ya kijeshi, pamoja na kushirikiana kukabiliana na changamoto za kiusalama kama uhalifu wa mtandaoni na ugaidi.

Aidha, Dkt. Nyansaho alieleza kuwa ziara ya Mhe. Kabombo ni ishara ya uhusiano imara uliopo kati ya nchi hizo mbili, na inaonesha dhamira ya pamoja ya kuendeleza urafiki, maelewano na ushirikiano wa muda mrefu. Alisisitiza kuwa mazungumzo ya mara kwa mara yamekuwa msingi muhimu katika kujenga ushirikiano madhubuti kati ya Tanzania na DRC.

“Nina imani kuwa kupitia ushirikiano wetu, tutaweza si tu kukabiliana na changamoto za pamoja, bali pia kutumia fursa zilizopo kukuza uchumi na ustawi wa wananchi wetu,” alisema Dkt. Nyansaho.

Kwa upande mwingine, alibainisha kuwa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na DRC una nafasi kubwa ya kuimarika zaidi, hususan kupitia matumizi ya Bandari ya Dar es Salaam katika usafirishaji wa mizigo, jambo litakalochochea maendeleo ya pande zote mbili.

Mwisho, Waziri Nyansaho alisisitiza dhamira ya Tanzania kuona DRC inaimarika kiusalama na kiuchumi, akieleza kuwa mafanikio ya nchi moja ni faida kwa ukanda mzima.









Top News