Na Said Mwishehe,Michuzi TV

BARAZA la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam limesema limejipanga kutekeleza mambo yote muhimu yaliyowasilishwa na kamati za baraza hilo kwa lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi wa Jiji hilo lenye idadi kubwa ya watu nchini.

Kupitia kikao cha Baraza la Halmashauri hilo kilichofanyika Februari 24,2025 chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Nurdin Bilali kimetoa muelekeo wa yale ambayo yanakwenda kufanyika katika kata zote 36 kupitia maazimio yaliyopitishwa na kikao hicho.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa kikao hicho ambacho kulikuwa na ajenda mbalimbali ikiwemo ya kupokea taarifa ya robo ya pili ya mwaka kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025 ,Meya Bilali maarufu kwa jina la Shetta amesema baraza hilo limekutana katika kikao cha kawaida lakini amewahakikishia wananchi kuwa kuna mambo ya msingi wameazimia kuyatekeleza kwa maendeleo ya Jiji hilo.

“Mabaraza  kama hayo ni ya kawaida kwa lengo la kuhakikisha ajenda zinapitishwa haswa kwa kutambua tumetoka katika vikao vya bajeti.Kimsingi mabaraza hayo yanasaidia katika utekelezaji,  pia kurahisishia watendaji na madiwani kwenda kusimamia ambayo wamekubaliana katika baraza.”

Meya Bilali amesema matarajio ya wananchi ni makubwa katika baraza hilo ambalo ni wazi viongozi wote hasa madiwani wamekuwa na shauku ya kusimamia na kuleta maendeleo ndani ya kata zao 36.

“Niwahakikishie wananchi wa Jiji la Dar es Salaam tunakwenda kusimama nanyi katika kuhakikisha tunatekeleza mambo mbalimbali yanayokwenda kutekelezwa katika jiji hilo.Wananchi tegemeeni mambo mazuri katika jiji la Dar es Salaam.”

Pamoja na hayo Meya Bilali amefurahishwa na ushiriki wa vyama vya upinzani vya ACT-Wazalendo na CHAUMA katika kikao cha baraza hilo ambapo amesema uwepo wa vyama hivyo ni chachu kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kufanya vizuri

Awali wa kamati wa kikao cha baraza hilo kamati mbalimbali za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam zimewaslisha taarifa zao za kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025 sambamba na kutoa maazimio kadhaa.

Kwa upande wa Kamati ya Mipango Miji nq Mazingira ambayo Mwenyekiti wake ni Diwani wa Kata ya Kariakoo Haji Manara pamoja na mambo mengine imetoa maazimio kuwa katika Jiji hilo ziwe na mifereji ya kupitisha maji ili kusaidia barabara hizo kudumu kwa miaka mingi.

Azımio lingine kamati hiyo ni kwamba miradi ya ujenzi iwe shirikishi katika kata husika kwani hivi sasa unaweza kukuta kibali cha ujenzi kimetolewa lakini kata haina taarifa.Hivyo yeyote ambaye atakuwa na kibali cha ujenzi ahakikishe nakala ya kibali hicho inapelekwa eneo husika .

Wakati Kamati ya Utawala na Fedha nayo umewasilisha taarifa yake ya utekelezaji katika kikao cha baraza hilo sambamba na kutoa maazimio kadhaa likiwemo la fedha zinazotengwa katika miradi ya miundombinu hasa barabara iongezeke kutoka asilimia 10 mpaka asilimia 15.








Na Karama Kenyunko, Michuzi TV
KATIKA kukabiliana na changamoto ya uhaba wa vitabu vya tiba na ugumu wa lugha kwa wanafunzi, Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS) kwa kushirikiana na Mhadhiri wa chuo hicho, Profesa David Ngasapa, wamechapisha vitabu vya anatomia ili kuongeza uelewa wa wanafunzi na kufanya rejea wawapo katika kliniki.

Akizungumza na waandishi wa habari Februari 25, 2026 jijini Dar es Salaam, Profesa Ngasapa ambaye ni mwandishi wa vitabu hivyo, alisema anatomia ni somo la msingi kwa daktari kwani ndipo anaufahamu mwili wa binadamu unavyofanya kazi.

Alisema ameamua kuandika vitabu vinavyozingatia mfumo wa elimu unaolenga umahiri (Competence-Based Education), ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa udaktari hapa nchini.

“Moja ya sababu kuu iliyonisukuma kuandika vitabu hivi ni upatikanaji mdogo wa vitabu vya rejea, hali inayowalazimu wanafunzi kutegemea ‘notisi’ za walimu ambazo hutofautiana kutoka mwalimu mmoja hadi mwingine,” alisema Profesa Ngasapa.

Alieleza kuwa vitabu vingi vya zamani viliandikwa kwa lugha ngumu ya Kiingereza na waandishi ambao Kiingereza ni lugha yao ya kwanza, tofauti na wanafunzi wa Tanzania ambao kwao ni lugha ya tatu.

Amesema moja ya vitabu kinaangalia mimba inavyotungwa hadi mtoto anavyozaliwa na mabadiliko ya mwili wa binadamu yanavyotokea, vyanzo na sababu zake.

Alisema zamani kulikuwa na upungufu wa vitabu vya somo hilo nchini lakini kwa sasa havipatikani kabisa, na kwamba chuoni hapo kulikuwa na kitabu kimoja cha anatomia ambacho wanafunzi walitumia kutoa nakala.

“Mbali na uhaba wa vitabu hivi, sababu nyingine iliyonisukuma kuandika vitabu hivi ni kutumia lugha rahisi na yenye kueleweka ya Kiingereza, kuendana na mtaala wa sasa wa umahiri na kuhimiza wanafunzi kuelewa badala ya kukariri,” alieleza.

Alifafanua kuwa wanafunzi wanahangaika kuelewa lugha kabla hata ya kufahamu dhana, huku mifano inayotolewa katika baadhi ya vitabu vya zamani ikiendelea kuwatatanisha.

“Wanafunzi wanahangaika kuelewa lugha yenyewe kabla hata ya kufahamu dhana. Pia mifano inayotolewa inazidi kuwatatanisha. Mfano, wanaeleza mfuko wa nyongo una umbo la ‘pear’, lakini pears za Ulaya ni tofauti na za Njombe au Iringa. Hivyo mwanafunzi anashindwa kupata picha halisi,” alisema.

Alisema vitabu vipya vimeandikwa kwa lugha rahisi na mifano inayoendana na mazingira ya wanafunzi wa Afrika Mashariki ili kusaidia uelewa badala ya kukariri.

Alibainisha kuwa vitabu hivyo vimeandaliwa kwa kuzingatia mfumo wa elimu unaolenga umahiri, tofauti na mfumo wa zamani uliokuwa unahamasisha kukariri.

“Mitaala yetu sasa inazingatia umahiri. Lakini unakuta mitaala inasema hivi, vitabu vinasema kitu kingine. Sisi tumeandaa vitabu vinavyoendana moja kwa moja na mfumo wa sasa, ili mwanafunzi aelewe na aweze kutumia maarifa yake kliniki,” alisema.

Alisisitiza kuwa lengo ni kuzalisha madaktari bora zaidi, kwa kuwa anatomia ni somo la msingi linalomjengea mwanafunzi uelewa wa mwili wa binadamu kabla ya kuingia kwenye mafunzo ya kliniki.

Akizungumzia muda wa kuandaa vitabu hivyo, Profesa Ngasapa alisema mchakato wa kuandika moja kwa moja ulichukua takribani miaka mitatu, huku maandalizi, utafiti na uzoefu wa zaidi ya miaka 20 ya kufundisha vikichangia kukamilika kwa kazi hiyo.

Alikiri kuwa changamoto kubwa ilikuwa kuandika wakati akiendelea na majukumu ya kufundisha na kufanya utafiti, pamoja na kuandaa michoro ya kitaalamu inayohitajika katika somo la anatomia.

“Ni somo gumu, linahitaji michoro mingi na maandalizi makubwa. Kutayarisha michoro ilikuwa kazi ngumu sana,” alisema.

Alifafanua kuwa gharama za uchapishaji kwa vitabu viwili vya awali zilifikia takribani shilingi milioni 29, zikigharamiwa na MUHAS. Hata hivyo, chuo kitapanga bei itakayoongeza kiasi kidogo juu ya gharama za uzalishaji ili kuhakikisha mradi unakuwa endelevu.

“Hatutaki kila wakati kuomba fedha chuoni. Fedha zitokanazo na mauzo zitatumika kuchapisha nakala nyingine kwa wanafunzi wanaokuja,” alisema.

Aidha, alibainisha kuwa kuna mpango wa kuvitoa vitabu hivyo katika mfumo wa kidijitali siku zijazo, sambamba na mwelekeo wa dunia kuelekea kwenye teknolojia.

Alisema tayari chuo kimechapisha zaidi ya nakala 400 na wamepokea maombi kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Zambia, Zimbabwe na taasisi moja kutoka India iliyoonesha nia ya kununua vitabu hivyo.

Alieleza kuwa tatizo la uhaba wa vitabu vya tiba si la Tanzania pekee, bali linazikumba pia nchi jirani za Afrika Mashariki. Hata hivyo, alikiri kuwa vitabu vya kitaaluma havina faida kubwa kifedha kutokana na idadi ndogo ya wanafunzi, akitoa mfano fani ya udaktari wa meno inayochukua wanafunzi takribani 60 kwa mwaka.

Kuhusu uendelevu wa taaluma hiyo, alisema tayari ameanza kuwaandaa wahadhiri vijana watakaobeba jukumu hilo siku zijazo, akiwemo Mkuu wa Idara, madaktari na wahadhiri wanaoendelea na masomo ya uzamivu (PhD).

“Hawa ndio watakaokuja kuendeleza kazi hii. Tumewapa uzoefu na tunafanya nao kazi kwa karibu,” alisema.
Naye, Kaimu Rasi wa Ndaki ya Tiba, Profesa Agricola Joachim, alisema wanajivunia kupata vitabu hivyo ambavyo ni muhimu kwa ajili ya kutumiwa na wanafunzi na kupata elimu wanayoihitaji.

“Tunampongeza kwa kujitoa, jukumu letu ni kufundisha na kufanya tafiti na yeye ametoa muda wake kuandika na chuo kimempa sapoti kuchapisha vitabu kurahisisha ufundishaji na ujifunzaji,” alisisitiza.

Alihimiza walimu wengine kuandika vitabu vitakavyowasaidia Watanzania.

Profesa Ngasapa alimaliza kwa kuwasihi wanafunzi na jamii kwa ujumla kutumia vitabu hivyo kikamilifu, akisisitiza kuwa vitawasaidia kupata elimu yenye kuzingatia umahiri na kuwafanya wawe wataalamu bora zaidi katika sekta ya afya.





RAIS Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, leo ameweka saini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es Salaam, marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuweka saini, Dkt Kikwete alimpa mkono wa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Thaddaeus S. Ruwa’ichi, na kueleza kuwa marehemu Kardinali Pengo atakumbukwa daima kwa mchango wake mkubwa kwa Kanisa na Taifa pamoja na moyo wake wa upendo kwa wananchi na kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema Kardinali Pengo alikuwa rafiki wa wengi na kiongozi aliyegusa maisha ya watu wengi kupitia huduma yake ya kiroho na kijamii.

Aidha, Dkt Kikwete alitoa pole kwa Askofu Mkuu Ruwa’ichi, viongozi na waumini wa Kanisa Katoliki, akiwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi huku akiungana nao kumuombea marehemu apumzike kwa amani.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoa pole, Rais huyo Mstaafu alisema yeye na marehemu Kardinali Pengo walifahamiana kwa muda mrefu tangu alipokuwa akihudumu wilayani Nachingwea katika kituo chake cha kwanza cha kazi, wakati marehemu akiwa Askofu Mkuu aliyesimamia maeneo ya Tunduru na Lindi.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Thaddaeus S. Ruwa’ichi, alitangaza msiba huo tarehe 19 Februari 2026 saa 04:00 kwa masikitiko makubwa, akieleza kuwa mpendwa baba yetu, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa ratiba rasmi ya mazishi, shughuli za kuaga mwili wa marehemu zitaanza siku ya Jumamosi tarehe 28 Februari 2026 kwa kuwasili kwa mwili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu saa 03:00 asubuhi.

Kuanzia saa 03:15 asubuhi hadi saa 10:00 jioni waombolezaji watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu.

Saa 10:00 jioni kutakuwa na Misa Takatifu ya kumuombea marehemu itakayofuatiwa na mkesha wa sala na maombolezo utakaoshirikisha makundi mbalimbali ya kijimbo, wakiwemo watawa, walei pamoja na vyama vya kitume.

Siku inayofuata, yaani Jumamosi, mwili wa marehemu utaondoka Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu saa 12:00 asubuhi kuelekea Kituo cha Hija Pugu, na unatarajiwa kuwasili saa 12:45 asubuhi chini ya usimamizi wa Kamati ya Mazishi.

Kuanzia saa 01:00 hadi saa 03:45 asubuhi waombolezaji watapata tena fursa ya kutoa heshima za mwisho katika Kituo cha Hija Pugu.

Misa ya Mazishi itaanza saa 04:00 asubuhi katika Kituo cha Hija Pugu, ikihitimisha rasmi shughuli za mazishi.

Waumini na wananchi wote wanaombwa kushiriki katika ibada na sala hizi kwa utulivu na heshima inayostahili.

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alizaliwa tarehe 5 Agosti 1944 na kupadrishwa mwaka 1971.

Alisoma Teolojia ya Maadili katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Lateran mjini Roma, ambako alipata shahada ya uzamivu mwaka 1977. Baadaye alifundisha katika Seminari ya Kipalapala na kuwa Rektor wa kwanza wa Seminari ya Segerea hadi mwaka 1983.

Aliteuliwa kuwa Askofu wa Nachingwea mwaka 1983 na baadaye Askofu wa Jimbo la Tunduru–Masasi mwaka 1985. Mwaka 1990 aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu Msaidizi wa Dar es Salaam na mwaka 1992 akawa Askofu Mkuu kamili wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Mwaka 1998 alitangazwa kuwa Kardinali na Papa Yohane Paulo II, na alishiriki katika mikutano ya kumchagua Papa mwaka 2005 na 2013.

Kardinali Pengo alihudumu pia katika idara mbalimbali za Kanisa Katoliki la Roma na kuongoza Baraza la Makanisa Katoliki Afrika (SECAM) tangu mwaka 2007. Alistaafu mwaka 2019, akiacha alama ya uongozi thabiti na imani isiyotetereka.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dkt. Omary Sukari (aliesimama) akiongoza majadiliano wakati wa kikao kazi kilichokutana jijini Mwanza kupanga mikakati itakayotumika kufikisha huduma za VVU na UKIMWI kwa wachimbaji wadogo mkoani Geita.

Na Mwandishi Wetu
WADAU mbalimbali wamekutana jijini Mwanza katika kikao kazi maalum chenye lengo la kuimarisha mwitikio wa VVU miongoni mwa wachimbaji wadogo mkoani Geita, hatua inayolenga kuongeza kasi ya kufikia malengo ya kitaifa na kimataifa ya kudhibiti maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Kikao hicho kimefanyika katika kipindi muhimu, ikizingatiwa kuwa Mkoa wa Geita unakadiriwa kuwa na takriban asilimia 10 ya jumla ya wachimbaji wadogo milioni nne waliopo nchini Tanzania, wanaofanya kazi katika zaidi ya maeneo 100 ya uchimbaji. Licha ya kiwango cha maambukizi ya VVU mkoani Geita kwa ujumla kuwa asilimia 4.9, tafiti zinaonesha kuwa katika jamii za wachimbaji wadogo kiwango hicho kinakisiwa kufikia asilimia 9.3, karibu mara mbili ya wastani wa mkoa.

Aidha, mkoa huo kwa sasa umefikia kati ya asilimia 60 hadi 70 tu ya lengo la kwanza la 95 chini ya mfumo wa kimataifa wa 95–95–95, unaolenga kuhakikisha asilimia 95 ya watu wanaoishi na VVU wanajua hali zao, asilimia 95 ya wanaojua hali zao wanaanza matibabu, na asilimia 95 ya wanaopata matibabu wanafikia udhibiti wa virusi. Hii ina maana kuwa bado kuna idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU ambao hawajui hali zao.

Kikao hicho kiliwakutanisha wawakilishi kutoka Geita Gold Mining Limited (GGML), GGML Kilimanjaro Challenge Against HIV/AIDS Trust, Tanzania Commission for AIDS (TACAIDS), mamlaka za Serikali ya Mkoa na Serikali za Mitaa, waratibu wa VVU na UKIMWI pamoja na washirika wengine wa maendeleo. Lengo kuu lilikuwa kubuni afua mahsusi zenye matokeo makubwa na zinazolingana na mazingira halisi ya wachimbaji wadogo wa Geita.

Kupitia Kili Grants Portfolio ya mwaka 2024/2025, Trust imetenga shilingi milioni 100 kusaidia utekelezaji wa afua zitakazotekelezwa kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Machi 1, 2026.

Washiriki walibaini changamoto kadhaa zinazoathiri mwitikio wa VVU katika jamii za wachimbaji, ikiwemo uelewa mdogo kuhusu kinga, upimaji na matibabu; ushiriki mdogo katika huduma za upimaji; uhamaji mkubwa wa wachimbaji unaoathiri ufuatiliaji na mwendelezo wa matibabu; pamoja na unyanyapaa, imani potofu na uwepo wa jumbe zisizo thabiti katika maeneo ya uchimbaji.

Akizungumza katika kikao hicho, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita, Dkt. Omar Sukari, alisema hatua ya kwanza itakuwa kutoa elimu ya kina kwa jamii, hasa wale wanaofanya kazi katika migodi midogo inayozunguka mgodi wa GGM, ili kuwapatia maarifa sahihi kuhusu VVU na kuwahamasisha kujitokeza kupima.

Kwa mujibu wa mpango huo, huduma za upimaji wa VVU kupitia vituo vinavyohama zitaifikia moja kwa moja jamii za wachimbaji katika maeneo yao ya kazi. Lengo ni kuwafikia zaidi ya wachimbaji wadogo 5,000 na kuhakikisha wanaopatikana na maambukizi wanaunganishwa haraka katika Kliniki za Huduma na Matibabu (CTC) kwa ajili ya kuanza tiba.

Mratibu wa VVU na UKIMWI Mkoa wa Geita, Dkt. Yohane Kiaga, alisema mkoa unaliona zoezi hilo kuwa fursa muhimu kwa kuwa fedha zinazotumika zinatokana na juhudi za Watanzania wenyewe kupitia Kili Challenge. Aliongeza kuwa pamoja na kuwafikia wachimbaji, mpango huo pia utahusisha takriban shule 15 zilizopo katika maeneo ya uchimbaji ili kuimarisha elimu ya kinga kwa vijana balehe.

Mbali na huduma za upimaji, mpango huo utatumia vifaa vya mawasiliano ya mabadiliko ya tabia (IEC) vyenye ubunifu na vinavyodumu, ikiwemo michoro ya ukutani, mabango na vipeperushi vitakavyowekwa katika maeneo ya uchimbaji kama vikumbusho vya kudumu hata baada ya shughuli za uhamasishaji kukamilika.

Katika kipindi cha utekelezaji, wadau watabaini na kuchora ramani ya maeneo muhimu ya uchimbaji, kuratibu na mamlaka za mitaa pamoja na vituo vya afya, kufanya kampeni za uhamasishaji na upimaji, na kufuatilia idadi ya watu waliopimwa pamoja na wale waliounganishwa kwenye huduma za matibabu. Mafanikio ya mpango yatapimwa kwa kuangalia idadi ya waliopatikana, waliopimwa na waliounganishwa kwenye tiba.

Matokeo yanayotarajiwa ni kuongezeka kwa uelewa wa VVU miongoni mwa wachimbaji wadogo, zaidi ya watu 5,000 kupimwa, kuimarika kwa kasi ya kufikia lengo la kwanza la 95, kupungua kwa unyanyapaa katika jamii za uchimbaji na kuimarika kwa uratibu wa wadau mbalimbali.

Mpango huu unaakisi dhamira endelevu ya GGML Kilimanjaro Challenge Against HIV/AIDS Trust ya kupunguza athari za VVU na UKIMWI nchini Tanzania kwa kuwekeza rasilimali moja kwa moja katika jamii zilizo hatarini zaidi. Utekelezaji utakapoanza Machi 1, 2026, mshikamano uliooneshwa na wadau unatarajiwa kuweka msingi imara wa kuharakisha mafanikio katika mapambano dhidi ya VVU miongoni mwa wachimbaji wadogo wa Mkoa wa Geita.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe uliopangwa kufanyika Februari 26, 2026. Riasala hiyo amesoma akiwa Songea Mkoani Ruvuma leo Februari 25,2026. (Picha na INEC).

Na Mwandishi wetu, Ruvuma
WAPIGA Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika.

“Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele.

Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya siasa 15 vimesimamisha wagombea na kwa upande wa uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Shiwinga vyama vya siasa nane (08) vimesimamisha wagombea.

“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Februari 26, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.

Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.

Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.

“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.

Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).

MERIDIANBET inawapa wapenzi wa michezo nafasi ya kipekee ya kushinda kila wiki. Ukiwa mchezaji wa Super Heli, sasa unaweza kujishindia simu mpya ya kisasa ya Samsung A26, huku ukiendelea kufurahia msisimko wa michezo ya kasino mtandaoni. Hii ni fursa ya kipekee ya kuunganisha burudani na ushindi wa kweli, moja kwa moja kutoka Meridianbet.

Kila Jumatatu, mshindi mmoja atachaguliwa kushinda Samsung A26, na kwa majuma manne, jumla ya washindi wanne watapata zawadi hizi. Hii inamaanisha kuwa kila wiki unaanza kwa furaha na mwendo wa ushindi. Picha ya ushindi huu ni wazi, na inatoa mwamko wa kipekee wa kucheza na kushinda, ikikuinua kuwa mchezaji hodari na mwenye bahati.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi, Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kushiriki ni rahisi sana. Wachezaji wanapaswa kuingia kwenye akaunti yao ya Meridianbet kupitia tovuti rasmi au app ya Meridianbet, na kila unapocheza Super Heli nafasi zako za kushinda zinapanda. Kadri unavyocheza zaidi, ndivyo unavyoongezeka uwezekano wa kuwa mshindi wa Samsung A26. Hii ni njia bora ya Meridianbet kuongeza burudani yako na nafasi za ushindi kila wakati.

Meridianbet inajali wateja wake na inatambua jitihada za wachezaji wake. Kupitia promosheni hii, unaweza kushinda simu mpya bila gharama yoyote, huku ukiendelea kufurahia mchezo unaopenda. Ni fursa isiyo na kifani ya kuanza wiki yako kwa nguvu, furaha, na msisimko wa ushindi, huku ukiwa sehemu ya familia ya Meridianbet.

Usichelewe. Jisajili, cheza Super Heli, na uwe mmoja wa washindi wa Samsung A26. Meridianbet inakuletea ushindi, burudani, na zawadi za kipekee kila wiki. Huu ni wakati wako wa kushinda, kufurahia, na kuwa sehemu ya kampuni nambari moja ya kasino mtandaoni Tanzania.


Kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd imeungana na Chama cha Wachimbaji Madini Wadogo Tanzania (FEMATA) katika safari ya kwenda nchini Canada kushiriki maonesho ya teknolojia ya madini.

GF, ambao ni wadau na walezi wa wachimbaji hao, wametoa pongezi na mkono wa baraka kufuatia mwaliko huo wa kushiriki maonyesho makubwa ya kimataifa. Ushiriki huo unatarajiwa kufungua fursa ya kujifunza teknolojia za kisasa zitakazosaidia kuongeza thamani ya madini ya Tanzania, hususan madini ya lithium na cobalt yanayotumika kutengeneza betri za magari ya umeme.

Kupitia mafunzo na uzoefu watakaoupata, wachimbaji hao wanatarajia kuchangia upatikanaji wa malighafi za uhakika kwa viwanda vya ndani, ikiwemo sekta ya uunganishaji wa magari, jambo litakalosaidia kukuza uchumi wa nchi na kuongeza ajira.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kuwaaga washiriki wa safari hiyo, Katibu Mkuu wa FEMATA, Rogers Micheal Sezero, aliishukuru GF kwa kuendelea kuwashika mkono wachimbaji wadogo. Alisema ushirikiano huo umechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa wachimbaji siku hadi siku.

Alieleza kuwa GF imekuwa na mpango maalum wa kuwakopesha wachimbaji wadogo vitendea kazi badala ya fedha taslimu, hatua iliyowezesha wengi wao kumiliki mitambo na magari ya kazi kwa urahisi zaidi. Mpango huo rafiki umesaidia kuongeza tija na ufanisi katika shughuli zao za uchimbaji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa safari hiyo na mmoja wa wachimbaji, Dkt. Bernard Joseph, alisema licha ya kuwepo kwa makampuni mengi yanayofanya biashara na wachimbaji, GF imekuwa mstari wa mbele kuwasaidia wanapohitaji msaada.

“Tunapoenda kuitangaza FEMATA nchini Canada, GF wametupatia mahitaji muhimu ya safari na hawajawahi kutuacha tunapowahitaji kwa jambo dogo au kubwa. Kupitia programu zao za mafunzo kwa wachimbaji na madereva, nami ni mmoja wa wanufaika. Safari hii itanisaidia kuongeza ujuzi zaidi,” alisema Dkt. Joseph.

Naye Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa GF, Salman Karmali, alisema katika kuadhimisha miaka 19 ya kampuni hiyo, wameona ni vyema kurejesha kwa jamii kwa kuwawezesha FEMATA kushiriki maonyesho hayo ya teknolojia ya madini nchini Canada.

Aliongeza kuwa kabla ya safari hiyo, GF imekuwa ikiendesha semina na mafunzo katika maeneo mbalimbali yenye shughuli za madini kama Geita, Mwanza, Songwe na Lindi. Kupitia semina hizo, zaidi ya madereva na waendesha mitambo 1,000 kutoka makampuni tofauti wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya teknolojia za kisasa, hasa ikizingatiwa kuwa magari na mitambo ya sasa yanatumia teknolojia inayobadilika kwa kasi.

GF ni wauzaji wa magari ya mizigo ya FAW na mitambo ya XCMG, na wanajivunia kuadhimisha miaka 19 tangu kuanzishwa kwake. Kampuni hiyo pia inamiliki kiwanda cha kuunganisha magari kilichopo Kibaha, mkoani Pwani, ikiwa ni miongoni mwa viwanda vya kwanza vya aina hiyo nchini.
Mkuu wa kitengo cha mauzo wa kampuni ya GF Trucks & Equipment's  kanda ya ziwa, Poul Msuku akizungumza na viongozi wa chama cha wachimbaji wadogo (FEMATA)  wakati wa hafla ya kuwaaga kwa ajili ya safari ya wachimbaji wadogo nchini Canada kushiriki  maonesho na mafunzo ya teknolojia ya madini jijini Dar es salaam.Kulia ni Mkurugenzi wa asoko na mawasiliano wa  GF ,Salman Karmal
Mwenyekiti wa Safari ya wachimbaji wadogo nchini Canada ,Benard Joseph akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kuwaaga na kukabidhiwa vifaa na kampuni ya GF iliyofanyika jijini Dar es salaam
Mkurugeni wa masoko na mwasiliano wa kampuni ya GF,Salman Karmali(wa pili kushoto) akiwa na viongozi wa chama cha wachimbaji wadogo akiwakabidhi vitendendea kazi wakati wa hafla ya kuwaaga kabla ya kuanza safari ya nchini Canada kushiriki maonesho ya Madini hafla iliyofanyioka jijini Dar es salaam
Wananchi wa wilaya ya Bukombe mkoani Geita sasa wanaweza kupumua kwa amani baada ya Serikali ya Awamu ya Sita kukamilisha ahadi yake ya kuimarisha huduma za uokoaji na zimamoto wilayani humo.

Katika hafla iliyopambwa na matumaini makubwa, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela, amekabidhi magari ya msaada wa zimamoto ambayo yatakuwa mkombozi mkubwa katika kukabiliana na majanga ya moto na ajali za barabarani.

Mkuu wa Mkoa amebainisha kuwa gari hilo si kwa ajili ya kuzima moto tu, bali lina uwezo wa:

Kukata vyuma kwa urahisi,Hii itasaidia sana kuokoa watu walionaswa kwenye magari baada ya ajali,.Kubeba maji lita 400 Pamoja na foam compound lita 40 maalum kwa ajili ya kuzima moto wa mafuta (flammable liquids).

Sambamba na gari la zimamoto, Bukombe imepokea gari la kubebea wagonjwa (Ambulance). Gari hili limetengwa maalum kwa ajili ya kuwahi eneo la tukio pindi ajali zinapotokea ili kuokoa maisha ya wananchi kwa haraka zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Geita, Kenneth Mwakasitu, amewataka wakazi wa Bukombe kuwa na utamaduni wa kuheshimu king’ora.

"Natoa wito kwa wananchi kuzingatia sheria za barabarani na kupisha gari hili linapokuwa katika dharura. Hii itatuwezesha kufanya kazi yetu kwa ufanisi na kuokoa maisha kwa wakati," alisema Mwakasitu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Paskasi Muragiri, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutekeleza ahadi hiyo muhimu. Ameeleza kuwa ujio wa vifaa hivi unamaliza kipindi cha hofu na wasiwasi miongoni mwa wana-Bukombe pindi majanga yanapotokea.








Na Mwandishi Wetu, WMTH – Mtumba, Dodoma

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Switbert Zacharia Mkama (Mb.), amewatak Watumishi wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuimarisha ushirikiano kati ya wafanyakazi na Menejimenti ili kuhakikisha haki, motisha na tija vinatimizwa.

Amebainisha hayo tarehe 24 Februari, 2026 wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Kwanza la Wafanyakazi wa Wizara kwa mwaka wa fedha 2025/2026 lililofanyika jijini Dodoma. Aliongeza kuwa Baraza la Wafanyakazi ni kiungo muhimu kati ya Menejimenti na watumishi, likiwa na jukumu la kutoa ushauri kuhusu utendaji, kusimamia maslahi ya wafanyakazi, na kupitisha mipango ya mapato na matumizi ya Wizara.

Alisisitiza kuwa “hakuna haki bila wajibu,” na kwamba wafanyakazi wanapaswa kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha Wizara inatoa huduma bora kwa wananchi. Aidha, Naibu Waziri Mkama alitoa pongezi kwa watumishi wa wizara kwa bidii yao mwaka jana na kuhimiza motisha na mafunzo yanayolenga kuboresha ufanisi kazini.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara, Bw. Mohammed Khamis Abdulla, alieleza kuwa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi ni utekelezaji wa Agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Waraka Na. 1 wa Mwaka 1970 linalolenga kuanzisha mabaraza ya wafanyakazi katika taasisi za umma ili kuimarisha ushirikishwaji wa wafanyakazi mahala pa kazi, pamoja na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utawala bora.

Bw. Abdulla pia alieleza mafanikio ya Wizara katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, ikiwemo: kukamilika kwa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano kama ilivyopangwa; utekelezaji wa Mradi wa Minara 636 ya Mawasiliano Vijijini kufikia asilimia 71 ifikapo Desemba 2025; kuongezeka kwa uwezo wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kutoka 200 Gbps hadi 2,000 Gbps kwenye njia kuu, pamoja na kuimarishwa kwa maunganisho ya mipakani; na mtandao kuongezeka hadi kufikia kilometa 15,066 na kuunganisha wilaya 119 kati ya 139 zilizopangwa.

Aidha, Bw. Abdulla alibainisha miradi mingine inayoendelea kutekelezwa ikiwemo uratibu wa Mradi wa Satelaiti Ndogo ya Mafunzo (KIBOCUBE), maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Dodoma na Zanzibar, utekelezaji wa Mkakati wa Uchumi wa Kidijitali 2024–2034, ujenzi wa Chuo Mahiri cha TEHAMA (DTI) katika eneo la Nala, pamoja na uandaaji wa nyaraka za kitaifa za usimamizi wa TEHAMA.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Baraza la Wafanyakazi Taifa kwa Mkoa wa Dodoma, Bw. Maulid Kipeneku, aliwafikishia wajumbe salamu za Baraza na kuwashukuru wafanyakazi kwa ushirikiano wao, akisisitiza umuhimu wa kushirikiana na viongozi wa Wizara katika kuleta maendeleo endelevu ya sekta ya mawasiliano na teknolojia ya habari nchini.











Na. Vero Ignatus, Arusha.

Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba  ameitaka wizara ya maji kuchukua hatua za kisheria kwa yeyote atakayebainika kuchezea vyanzo na miundombinu ya kwani ni sawa na kuchezea na uhai.

Ameyasema hayo jana wakati akifungua mafunzo ya siku tatu  ya Mkutano wa Bodi za wakurugenzi wa Mamlaka za maji safi na Usafi wa mazingira nchini kilichofanyika Mkoani Arusha katika hotel ya Ngurdoto ambapo amesisitiza utumiaji mzuri wa maji ili kuepusha malalamiko.

"Jana nimepata taarifa ya watukukata mabomba ya maji na kutengeneza urembo chukueni hatua Kali za kisheria , pia nisisitize sitaki kuona mwanafunzi amebeba Kidumu cha maji, Shule za misingi, Secondary, Hospitali, Vituo vy Afya, zahanati zote ziwe na visiima vya maji" Alisema Dkr Mwigulu. 

 Waziri Mkuu anesema Jambo hilo  la kutunza vyanzo na miundombinu ya maji siyo kazi ya Wizara ya Maliasili na Utalii pekee bali ni kwa watanzana wote, kwani ni mihimu kuzingatia matumizi sahihi ya maji, "Fungulia unapotumia funga unapomaliza kutumia

Awali akitoa salami za Wizara Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia katika kipindi cha miaka 4 zaidi ya trilion 3 zimeongezwa katika miradi ya maji mjini na vijijini ambapo vijijini imefika asilimia 85.2% kwa eneo la mjini asilimia 92.5 ,ipo miradi ya miezi 28 inayoendelea  kuvuka lengo la asilimia 95℅ kwa mjini wana miradi zaidi ya 878  inaendelea  

Amesema mpaka sasa wana vijiji takribani 12333 kupitia wakala wa maji vijijini RUWASA wameshafikia vijiji 10,758 wamebakisha vijiji 1575 hadi kufikia 2030 vyote vitakuwa vimepata huduma ya maji safi na salama 

"Tumeanzisha Bodi za Mamlaka za maji majukumu lake ni kusimamia Mamlaka. hizo zilete ufanisi na kuhakikisha huduma mwananchi ataipata inakuwa bora na haina malalamiko ya aina yeyote Sisi katika Wizara hii tunakuhakikishia kwenda kufanya kazi zenye matokeo"

Amemuomba Waziri mkuu kuangakia ongezeko la bajeti ya Wizara ya maji huku akitilia mkazo  Wizara hiyo imejiwekea malengo makuu 3 ikiwemo kuleta matokeo chanya katika utendaji, mifumo na teknolojia kwa kushirikiana na chup cha maji ili kuleta ufanisi katika taasisi mageuzi makubwa, pamoja na teknolojiaa  italayotumika kuleta mageuzi chanya kwenye sekta za maji.

"Ni aibu Leo hii mwananchi alalamike amebambikiwa bili za maji hapana,haya ni maelekezo ya Rais kwamba tunakwenda kwenye mita janja muta kama luku ya umeme ili kuhakikisha tunaondokana na malalamiko" Alisema

Dkt James Andilile ni mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) amesema maisha ya kila siku ya mtanzania yanaanza na maji hivyo wanalo jukumu la. Kuhakikisha uwekezaji mkubwa ambao umefanywa na serikali unaleta tija kwa huduma ya maji safi na salama. 

"Tunaendelea kufuatilia na kuhakikisha kwamba Mamlaka za maji zinatoa huduma kama inavyotakiwa pia zinatekeleza na lengo namadhumuni ya serikali"

Sambamba na hilo Dkt. Mwigulu akizindua Mfumo wa kuunganisha maji kwa njia ya mtandao,( b) Uzinduzi wa mkakati wa kuanzishwa ufungaji wa mita za maji ya malipo ya kabla, (c) mkakati , aidha ufungaji wa mita za maji za malipo ya kabla kwa mwaka 2024 ziliungwa mita13528 hadi kufikia 2026 januari zimefungwa mita 23156









 

Na Seif Mangwangi , Michuzi TV, Arusha.

Mahakama ya Afrika ya Haki za  Binadamu na Watu (AfCHPR) imemchagua Jaji Blaise Tchikaya wa Serikali ya Jamhuri ya watu wa Kongo (Brazzaville) kuwa Rais mpya wa Mahakama hiyo akichukua nafasi ya Jaji Dkt. Modibo Sacko aliyemaliza muda wake.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Kwa vyombo vya habari na Mahakama hiyo Jaji Tchikaya amechaguliwa katika kikao cha majaji kilichofanyika Februari 23, 2026.

Taarifa hiyo imesema Rais mpya   atahudumu kwa kipindi kilichosalia cha muhula wa Rais anayeondoka, ambaye alichaguliwa tarehe 2 Juni 2025 kwa kipindi cha miaka miwili huku, Jaji Sacko akiendelea kusalia katika benchi la Mahakama kama Jaji.

Katika hotuba yake ya kuaga, Jaji Sacko alitoa shukrani za dhati kwa Majaji wenzake, Msajili, wafanyakazi na wadau wote wa Mahakama kwa ushirikiano na uungwaji mkono waliompa wakati wa uongozi wake.

Katika hotuba yake baada ya kuchaguliwa Rais mpya Jaji Tchikaya amesema amepokea jukumu hilo kwa heshima kubwa na dhamira ya kuendeleza misingi ya Mahakama akisisitiza kuwa wakati Mahakama ikijiandaa kuadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake, ni muhimu kutafakari mafanikio yaliyopatikana na kukabiliana na changamoto zilizopo ili kuimarisha zaidi ulinzi wa haki za binadamu barani Afrika.

Kwa niaba ya Mahakama, alitoa pongezi na shukrani kwa Jaji Sacko kwa uongozi wake thabiti na mchango wake katika kuimarisha taasisi hiyo muhimu ya Umoja wa Afrika.

Kufuatia uchaguzi huo, ofisi mpya ya uongozi sasa inaundwa na Jaji Blaise Tchikaya kama Rais na Jaji Bensaoula Chafika wa Algeria kama Makamu wa Rais.

*Wasifu wa Rais Jaji Blaise Tchikaya*

Rais Jaji Blaise Tchikaya ni Profesa wa sheria za umma za kimataifa na haki za binadamu mwenye uzoefu mpana wa kitaaluma.

Alichaguliwa kuwa Jaji wa Mahakama hiyo Julai 2018 kwa muhula wa miaka sita na aliwahi kuwa Makamu wa Rais wa Mahakama hiyo kuanzia Juni 2021 hadi Julai 2023.

Kwa upande wake Makamu wa Rais Jaji Bensaoula Chafika ana Shahada ya Uzamivu katika Sheria ya Umma na amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za juu katika mahakama na utawala nchini Algeria pamoja na kuwa mhadhiri na mshauri wa masuala ya sheria.

Alichaguliwa kuwa Jaji wa Mahakama hiyo mwaka 2017 na kuchaguliwa tena mwaka 2023 kwa muhula wa pili na Juni 2, 2025 alichaguliwa tena kwa muhula wa miaka miwili.

Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ni chombo cha Umoja wa Afrika kilichoanzishwa na Nchi Wanachama wake kwa lengo la kulinda na kuimarisha haki za binadamu na watu barani Afrika.

Mahakama hiyo inaundwa na Majaji 11 wanaochaguliwa kwa uwezo wao binafsi na hukutana mara nne kwa mwaka katika vikao vya kawaida pamoja na vikao vya ziada pindi inapohitajika.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Mashariki imewakumbusha wafanyabiashara na wadau wa gesi ya kupikia (LPG) kuzingatia usalama, afya na utunzaji wa mazingira, wakati wa kusafirisha, kuhifadhi na kuuza bidhaa hizo kwa wateja.

Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu, akizungumza wakati wa semina ya wadau hao iliyofanyika mkoani Pwani, 24 Februari 2026 aliwasisitiza wafanyabiashara wa jumla wa LPG kuwa na mikataba na wasambazaji wao na wauzaji wa rejareja wa bidhaa hiyo ili kukidhi matakwa ya kisheria na kiusalama.

Mhandisi Long’idu aliwahimiza pia wadau hao kuwaelimisha wasambazji na wauzaji wa rejareja wa LPG kuhusu usalama na umuhimu wa kutumka mizani iliyohakikiwa na Wakala wa Vipimo wakati wa kutoa huduma ili wananchi wapate huduma bora.

\

 

Na, Seif Mangwangi, Michuzi TV, Arusha

Waziri mkuu  Dkt.Mwigulu Nchemba amewataka wakandarasi wanaojenga miradi mbalimbali nchini kulipa stahiki za wafanyakazi wao kama walivyokubaliana kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo linalojengwa soko la kisasa la  kilombero baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa stendi na soko la Kilombero,  leo Februari 23, 2026, Waziri Mkuu Dkt Nchemba amesema wakandarasi wengii wamekuwa kero kwa wafanyakazi nchini.

DKT. Nchemba pia  ameagiza wakandarasi wanaolipwa nyongeza ya madai yao baada ya kucheleweshewa malipo na wao wawalipe wafanyakazi wao nyongeza ya fedha Kwa muda waliokaa kusubiri malipo yao.

“ Kumekuwa na kero ya wafanyakazi kwenye miradi ya ujenzi kucheleweshewa malipo yao na pengine wameshalipwa pesa zote ila wao wakicheleweshewa fedha wanadai na fidia ya kucheleweshewa, Sasa naagiza mkishalipwa pesa zenu na wafanyakazi wenu pia muwalipe nyongeza Kwa kuwasubiria,” amesema.

Akizungumza na wananchi wa Jiji la Arusha, Dkt.Nchemba amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa Jijini Arusha.

Akiwa katika ziara yake unapotekelezwa mradi wa ujenzi wa stendi kuu ya mabasi eneo la Bondeni city iliyopo kata ya Olasiti ameelekeza ujenzi  wa barabara njia nne na kuelekeza kuanza matumizi ya  magari ya mwendokaai yanayotumia gesi na umeme ili kusapoti matumizi ya nishati safi.

"Miradi inayotekelezwa katika nchi italeta heshima kwa taifa letu na inadhihirisha ile kauli ya kazi na utu,  kwa sasa kila mmoja anaona mageuzi makubwa katika sekta ya afya hospitali za wilaya zimejengwa 119 na kufungwa vifaa vyote, vituo vya afya 649, zahanati zaidi ya 2700, vifaa vya kibingwa katika hospitali zote za mikoa na rufaa, si hivyo tu bali hata umeme imebaki historia nzuri kwamba umeme haukatiki tena na mengine mengi ikiwemo sekta ya elimu ambayo imekuwa na mageuzi makubwa".

Kuhusu soko la Kilombero, Dkt Nchemba ameagiza wafanyabiashara waliokuwa wakitumia eneo Hilo ndio wapewe kipaumbele na kwamba ni marufuku Kwa mfanyakazi wa Serikali kukodishiwa visimba katika soko Hilo.

Kwa upande wake Waziri wa habari michezo sanaa na utamaduni Paul Makonda amempongeza Waziri mkuu kwa kuendelea kusikiliza kero za wananchi nchini na kuzipatia ufumbuzi.

Waziri Makonda amesema jiji la Arusha lina miradi 52  inayotekelezwa na inazingatia ilani ya chama cha mapinduzi (CCM).

"Waziri mkuu ndio msimamizi wa TAMISEMI hivyo kila kinachotamkwa kitatendeka ikiwemo kukamilisha barabara za ndani zenye urefu wa kilometa 13 zinazojengwa 

 kwa kiwango cha lami ili kurahisisha mawasiliano kuelekea mashindano AFCON.

Mkuu wa mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla amepongeza juhudi za wakandarasi wanaotekeleza miradi ya maendeleo katka mkoa wa arusha.

Ameahidi kushirikiana  na wadau mbalimbali kuhakikisha miradi hiyo  inakamilika kwa wakati kama ilivyoelekezwa na kuonya juu ya migogoro isiyo ya lazima baina ya wafanya biashara na baadhi ya watumishi wasio waadilifu.









Top News