Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma


Bunge la 13 limeunda jumla ya Kamati 17 huku wanawake wengi wakichomoza kuongoza kamati hizo, Wabunge wa upinzani wa Chaumma na ACT Wazalendo nao wapenya.

Majina ya vigogo yamechomoza kwenye Kamati hizo huku baadhi ya wabunge wakongwe wakirejea katika uongozi wa Kamati walizoongoza Bunge la 12.

Kamati zilizopewa wapinzani ni Hesabu za Serikali (PAC) ambayo amekabidhiwa Devotha Minja na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ambayo itaongozwa na Mbunge Tunduru Kaskazini Ado Shaibu.

Hii ni mara ya kwanza wapinzani kutoka vyama viwili tofauti wanaongoza Kamati hizo ambazo kwa kipindi kirefu zilikuwa chini ya Wabunge kutoka Chadema.

Katika taarifa ya Bunge, Devotha Minja atasaidiana Khalifan Aeshi ambaye amechaguliwa kuwa Makamu huku Kamati ya (LAAC) Makamu wake ni Abdallah Chikota.

Katika Bunge la 12 Kamati ya PAC iliongozwa na Naghenjwa Kaboyoka wakati Kamati ya LAAC Mwenyekiti wake alikuwa Halima Mdee wote wakitokea Chadema licha ya kuingia kwenye msukosuko wa kutimuliwa na chama chao.

Minja na Ado Shaibu wamepewa Kamati hizo ambazo zimekuwa na hoja nzito kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambapo mara nyingi Mashirika na Halmashauri yametajwa kuwa na mapungufu ya mifumo ya kimanunuzi na kupelekea upotevu mkubwa wa fedha.

Kamati zingine zilizoundwa ni Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambayo Mwenyekiti wake ni Anne Kilango Malecela na Makamu wake ni Christina Mndeme huku Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Mwenyekiti ni Masanja Kadogosa na Makamu wake Dougras Masaburi.

Kamati ya Sheria ndogo itaongozwa na Cecilia Pareso na Makamu wake ni Yahya Zuberi lakini Kamati ya Utawala,Katiba na Sheria wamepewa wabobezi wa Sheria ambapo Mwenyekiti ni Dk Damas Ndumbaro na Makamu wake Edwin Swale.

Kamati ya Sheria ndogo itaongozwa na Cecilia Pareso na Makamu wake ni Yahya Zuberi lakini Kamati ya Utawala,Katiba na Sheria wamepewa wabobezi wa Sheria ambapo Mwenyekiti ni Dk Damas Ndumbaro na Makamu wake Edwin Swale.

Mashimba Ndaki ameendelea kuongoza Kamati ya Bajeti na Makamu wake ni Ally Hassan King.

Naibu Waziri wa Nishati wa zamani Subira Mgalu amechaguliwa Kamati ya Nishati na Madini akisaidiwa na Simoni Lusengekile.

Mbunge Mpanda Seleman Kakoso amerudi kwenye nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu akisaidiana na Abubakari Asenga huku Kamati ya Afya na Masuala ya Ukimwi wamechaguliwa Dk Johannes Lukumay kuwa Mwenyekiti na Zeyana Abdallah Hamid ndiye Makamu.

Mbunge mwingine aliyerudia nafasi yake ni Timotheo Mzava ambaye ameendelea kuwa Mwenyekiti Kamati ya Ardhi,Maliasili na Utalii Makamu wake ni Mary Masanja na Kamati ya Elimu, Utamaduni na Michezo Husna Sekiboko atasaidiana na Cornel Magembe.

Kamati zingine ni Maji na Mazingira iliyorudi tena kwa Jackson Kiswaga nafasi ya Makamu ikienda kwa Profesa Pius Yanda na Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii itaongozwa na Hawa Machafu Makamu ni Regina Malima.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge la 12 Nagma Giga safari hii amepewa kuongoza Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Makamu ni Mbunge wa Dodoma Paschal Chinyele, Viwanda, Biashara, Biashara na Kilimo ameendelea Deodatus Mwanyika na Makamu wake amerudi Mariam Ditopile.

Kwenye Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) amechaguliwa Florence Kyombo atasaidiana na Jafari Chege.

Na. Joseph Mahumi na Saidina Msangi, WF, Dodoma.


Tanzania na Indonesia zimekubaliana kuendeleza zaidi ushirikiano wa kimaendeleo katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo na nishati kwa faida ya nchi hizo mbili.

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma, baada ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omary (Mb), kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Tri Yogo Jatmiko Avetisyan.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Balozi Omar, ameishukuru Serikali ya Indonesia kwa mchango wake mkubwa katika kusaidia sekta mbalimbali za uchumi wa Tanzania ikiwemo sekta za madini, kilimo na mifugo tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1964.

“Mwaka huu ni maadhimisho ya miaka 62 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Indonesia, na uhusiano wetu umeendelea kuimarika zaidi kadiri miaka inavyosonga mbele, na pia tumeona ziara kati ya viongozi wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipotembelea Indonesia, na Mhe. Prabowo Subianto Rais wa Indonesia alipokuja Tanzania, hii ni ishara ya uhusiano thabiti unaojengwa juu ya heshima na ushirikiano wa kweli,” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, dhamira ya Indonesia katika kukuza maendeleo endelevu na kupunguza umasikini imechangia kubadilisha kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania kupitia misaada ya kifedha, ushauri wa kitaalamu, na programu za kujenga uwezo.

Aidha Mhe. Balozi Omary aliwaalika wawekezaji kutoka Indonesia kuja kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo, uongezaji thamani wa mazao, madini, viwanda, nishati, miundombinu, afya, elimu na utalii.

Kwa upande wake, Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa nchi hizo zinadumisha ushirikiano zaidi ya Watanzania 170 wamepata manufaa kupitia programu hizo za kujenga uwezo katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, mifugo, nishati, madini, uvuvi na fedha.

“Tutahakikisha tunaimarisha zaidi uhusiano huu kwa kuongeza kuwajengea uwezo wataalmu wa Tanzania ili maeneo yote tuliyokubaliana kushirikiana yanaleta tija na ustawi mpana wa uhusiano wa nchi hizi mbili,” alisema Mhe. Balozi Avetisyan.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Bi. Tiba Kisonga na maafisa wengine waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na ubalozi wa Indonesia nchini.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akimkabidhi Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, zawadi iliyokuwa na bidhaa zinazozalishwa nchini Tanzania ikiwemo korosho na kahawa, baada kikao walipokutana na kufanya mazungumzo, katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akisalimiana na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, walipokutana na kufanya mazungumzo, katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.




Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa kikao na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, alipofika kwa ajili ya mazungumzo, katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao cha mazungumzo na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, ambaye alifika kwa ajili ya mazungumzo, katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, akizungumza katika kikao na Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), walipokutana na kufanya mazungumzo, katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (wa nne kulia), na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko Avetisyan (wa tano kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha, Tume ya Mipango na Ubalozi wa Indonesia, baada ya kikao cha mazungumzo kilichofanyika katika ukumbi wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma. Kutoka kushoto Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Bi. Tiba Kisonga, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban na Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade. Kutoka kulia ni Katibu wa Balozi wa Indonesia Bw. Antidius Karoli Kalisa, Mkuu wa Idara ya Utamaduni, siasa na Mambo ya Kijamii Bw. Michael Bastian Supit na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama,



(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)

Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma.

Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amewataka wadau wote wanaosimamia ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Msalato kushirikiana ili ujenzi huo ukamilike ifikapo Mwezi Mei mwaka huu.

Akizungumza jijini Dodoma, Januari 14, 2026 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo, Prof. Mbarawa amesema hatua ya ukamilishaji wa ujenzi (finishing), inahitaji umakini, kujali thamani ya fedha na ubora wa vifaa unaoendana na mahitaji.

"Mameneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mamalaka ya Viwanja vya ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) pamoja na Zimamoto na Uhamimiaji shirikianeni kikamilifu ili vifaa na mifumo ya uendeshaji isomane na kurahisisha utendaji wa kazi kiwanjani hapo", amesisitiza Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS mkoa wa Dodoma Eng. Zuhura Amani amesema wamejipanga kumsimamia kikamilifu mkandarasi anaejenga kiwanja hicho ili kikamilike kwa wakati.

Nae, Mkurugenzi wa Kiwanja kiwanja hicho, Clemence Mbaruck amesema watahakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango na tayari watumishi 170 tayari wameshahamishiwa Dodoma kwaajili ya kuanza kazi kwenye kiwanja hicho mara baada ya kufunguliwa rasmi.

Zaidi ya shillingi bilioni 370 zinatumika kwaajili wa ujenzi huo na kukamilika kwake kutachochea ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Dodoma kwani kutaruhusu ndege aina mbalimbali za kitaifa na kimataifa kutua Kiwanjani hapo.





WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yoichi Mikami na kujadiliana naye masuala ya uchumi, miradi ya maendeleo na uwekezaji.

Akizungumza na Balozi huyo leo (Jumatano, Januari 14, 2026) ofisini kwake Mlimwa jijini Dodoma, Waziri Mkuu ameishukuru nchi hiyo kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali kama vile barabara ya Arusha hadi Holili, bandari ya Kigoma, miradi ya kilimo na upatikanaji wa vifaa tiba vya huduma za afya ya mama na mtoto.

“Serikali itahakikisha kuwa miradi hii inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na inakamilishwa kama ilivyopangwa,” amesema Dkt. Mwigulu 

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kutuma salamu za pongezi kwa Waziri Mkuu wa Japan, Bibi Sanae Takaichi kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo tangu Oktoba, 2025 na kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo nchini humo. “Tanzania inasisitiza kuendeleza ushirikiano wa karibu na Japan kwa manufaa ya pande zote mbili,” amesema.

Kwa upande wake, Balozi Mikami alimweleza Waziri Mkuu kwamba amefurahishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya kijamii 79 ambayo awali ilikuwa inasuasua na kwamba tangu Septemba, 2024 hadi sasa, imebakia miradi 16 tu.

Alisema nchi yake itaendeleza ushirikiano na Tanzania ambao umedumu kwa miaka zaidi ya 60. 







WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka wizara zinazohusika na masuala ya ajira zisimamie kikamilifu utekelezaji wa sheria zinazotaka kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania zisifanywe na wageni isipokuwa zile zinazohitaji utaalamu ambao nchi inaupungufu.

 Vilevile, Waziri Mkuu amekemea tabia ya baadhi ya wenye nyumba kumpangisha raia mmoja wa kigeni na kumruhusu mpangaji huyo apangishe watu wengine ndani ya nyumba hiyo jambo ambalo ni hatari kwa usalama na pia halina tija kibiashara.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Jumatano, Januari 14, 2026 alipofungua Kikao cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Wizara za Kisekta kujadili fursa za ajira ndani na nje ya nchi.

Agizo hilo linalenga kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania kufuatia kuwepo kwa wimbi kubwa la wageni kufanya kazi au biashara ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania na kuliwezesha Taifa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa ajira.

“…Kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania ziachwe wafanye, si kuruhusu wageni wafanye. Tusioneane aibu kama tumefungua milango au kulegeza wataalamu wafuatilie. Wageni wafanye kazi za kitaalamu ambazo nchi ina uhaba wa wataalamu.”

 Amesema kuwa ni lazima wataalamu wa ndani wasimamie sheria ipasavyo na kama kuna maeneo yanayokwamisha wayabainishe na yafanyiwe marekebisho. “Hatuwezi kuleta watu wanaokuja kufanya kazi ambazo Watazania wanaziweza.” 

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuwa na wivu na nchi yao kwa kutoruhusu baadhi ya vitu kufanyika, ambapo alitolea mfano suala la wenye nyumba kumpangisha raia moja wa kigeni ambaye naye analeta wenzake wengi katika nyumba hiyo hiyo.

“Watanzania tuwe na wivu na nchi yetu, mfano mtu anamkodishia nyumba mgeni kwa dola 5,000 kwa mwaka na kisha mgeni huyo anawaleta wenzake 60 na anawakodisha dola 500 hapo Mtanzania anapata hasara, hii si sawa hata kwa usalama.”

Waziri Mkuu amewaagiza wahusika wafuatilie suala hilo la makazi ili wakae katika utaratibu ulio rasmi. “Eneo hili liangaliwe wageni wanalundikana na kufanya kazi ambazo Watanzania wangeweza kufanya, hatuwezi kuruhusu hili tunataka wawekezaji.”

Hivyo, Waziri Mkuu ameziagiza wizara zinazohusika zifuatilie suala hilo, pamoja na kuwasisitiza wasimamie utekelezwaji wa sheria kwa sababu kila nchi ina sheria zake na Tanzania inatekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria.

Amesema sheria zimetungwa ili kusaidia kujenga kampuni za Watanzania na kuzikuza, hivyo wizara zinazohusika zihakikishe hazisajili kampuni za kigeni kabla ya kuzifanyia uchunguzi wa kina kwa sababu baadhi ya taarifa zinazowasilishwa si sahihi.







Kasoko ya Empakaai ni mojawapo ya Kasoko za volkano ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, ikiwa na kingo za juu na ziwa zuri linalofunika zaidi ya asilimia 75 ya sakafu ya Kreta/Kasoko. Kivutio kikubwa ndani ya kreta hii ni idadi kubwa ya ndege heroe (flamingo) wanaoonekana kando ya ufukwe wa ziwa, Ndege wanapokuwa wengi hufanya ziwa hilo kuwa na rangi ya pinki.

Kreta hii katika nyanda za juu za Ngorongoro imezungukwa na kuta za misitu yenye mteremko mkali wa takribani mita 300 kwa urefu, zikiwa na uoto wa asili wa kijani kibichi, wanyamapori na aina mbalimbali ya ndege. Eneo lake lina upana wa takribani kilomita 8, huku karibu nusu ya sakafu yake ikifunikwa na ziwa la lenye magadi na kina kirefu, makazi ya heroe (flamingo) na ndege wengine wa majini. 

Kutoka juu ya ukingo wa kreta ya Empakai, wageni wanaweza kuona Mlima Oldoinyo Lengai, Bonde la Ufa na Ziwa Natron kwa mandhari ya kuvutia. Pia wanaweza kufurahia matembezi ya asili kutoka juu ya mlima au kushuka hadi sakafuni kushuhudia vivutio vilivyopo.

Empakaai ina kimo cha takribani mita 3,200 kutoka juu ya usawa wa bahari upande wa magharibi na mita 2,590 upande wa mashariki. Mara nyingi hufunikwa na ukungu kutokana na mwinuko wake ambapo ziwa huonekana la kijani kibichi au buluu ya kina.

Kreta/Kasoko  ya Empakaai ni maarufu kwa safari za kutembea kwa miguu, ambapo watalii hutembea kwa takribani saa mbili na nusu kwenda na kurudi kutegemea na uwezo wa mwili. Wageni wanaweza kuona kwa ukaribu ziwa na msitu mnene uliopo ndani na kuzunguka sakafu ya Kasoko.

 Kivutio cha Empakaai kinaweza kutembelewa wakati wowote wa majira ya mwaka, lakini inapendelewa zaidi kuanzia mwezi Juni hadi Desemba (msimu wa kiangazi).

 _Karibu Ngorongoro 

Tumerithishwa, tuwarithishe_ 








Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Mikami Yoichi, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, leo tarehe 14 Januari 2025.

Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha zaidi ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Japan.





 

MERIDIANBET imeleta upepo mpya katika tasnia ya michezo ya kasino mtandaoni kwa kutambulisha kampeni ya Non-Stop Win&Go Drop. Tofauti na promosheni za kawaida, mpango huu umebuniwa kuleta mtiririko endelevu wa fursa za ushindi, ukilenga kuongeza burudani na mvuto wa michezo ya bahati nasibu kwa wachezaji.

Kupitia mpango huu, wachezaji wanapewa nafasi ya kupata tiketi nyingi za bure kila siku, zikiwawezesha kushiriki bila kutumia fedha zao binafsi. Hii ni njia ya kipekee ya kufungua uzoefu wa mchezo, ambapo bahati huja bila shinikizo la hasara, na kila tiketi huwa kama mwaliko wa kujaribu fursa mpya.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi. Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Win&Go ni mchezo wa kisasa unaochanganya urahisi na kasi. Wachezaji huchagua seti ya namba kutoka kwenye mkusanyiko mkubwa, kisha matokeo hutolewa kwa muda mfupi unaorudiwa mara kwa mara. Mfumo huu umeundwa kuwapa washiriki msisimko wa papo kwa papo na matokeo yanayopatikana haraka.

Kilichoifanya Non-Stop Win&Go Drop kujitofautisha ni kuondoa vizuizi vinavyowazuia wengi kujaribu michezo ya kasino. Tiketi za bure zinawawezesha wachezaji kufurahia mchezo, kujifunza mifumo yake na kushiriki kwenye ushindi bila hatari ya moja kwa moja ya kifedha.

Non-Stop Win&Go Drop ni mfano wa jinsi ubunifu unavyoweza kubadilisha burudani ya mtandaoni kuwa safari ya kusisimua, inayolenga uwajibikaji na burudani salama kwa wachezaji wote wanaostahili kisheria.


Dar es Salaam, Januari 2026.
KAMPUNI ya Airtel Tanzania leo imezindua kampeni ya Wese ni Bure ambayo inatokana na kampeni mama Inayoitwa Mwaka umenyooka na My airtel money app, Kampeni hii inalenga kuhamasisha matumizi ya miamala ya kidigital kupitia huduma ya Lipa namba kila unapoweka mafuta kwenye vituo vya mafuta zaidi ya 62 kote nchini ambavyo ni Mount Mero, ACER, Zebra Station na Bavuai.

Kampeni ya Wese ni Bure ni sehemu ya juhudi endelevu za Airtel Tanzania za kuwazawadia wateja wake, ikithibitisha dhamira ya kampuni ya kurahisisha malipo ya kila siku kwa njia salama na rahisi. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara wa Airtel Money, Bw. Emmanuel Moshi, alisisitiza umuhimu wa malipo ya kidijitali katika maisha ya kila siku akisema: “Kwa kuunganisha Airtel Lipa Namba kwenye malipo ya mafuta, tunaongeza thamani ya huduma za fedha kidijitali kwenye huduma moja muhimu sana ya kila siku, huku tukiwazawadia wateja wetu kwa kuchagua miamala salama na rahisi isiyotumia fedha taslimu.”

Akisisitiza dhamira hiyo kwa ngazi ya jamii, Meneja wa Malipo kwa Wafanyabiashara wa Airtel Money, Bw. Ismail Simanga, alieleza manufaa ya moja kwa moja ya kampeni ya Mwaka Umenyooka na My Airtel Money kwa wateja akisema: “Kampeni hii inaleta thamani halisi kwa wateja wetu kwa kubadilisha ununuzi wa kawaida wa mafuta kuwa fursa ya kupata zawadi, huku ikichochea matumizi ya malipo salama, ya haraka na rahisi ya kidijitali”

Kupitia kampeni hii, wateja watakaonunua mafuta katika vituo hivyo na kulipia kupitia Airtel Lipa Namba watapata nafasi ya kushinda lita 10 za mafuta bure kila wiki katika kipindi cha mwezi mmoja. Ili kushiriki, mteja anatakiwa kununua mafuta yenye thamani ya Shilingi 10,000 au zaidi na kulipa kupitia Airtel Lipa Namba, ambapo ataingizwa moja kwa moja kwenye droo ya kila wiki. Washindi watatangazwa kila wiki katika kipindi chote cha kampeni. Airtel Tanzania inaendelea kuonesha namna suluhisho za kifedha kupitia simu zinavyoweza kuongeza urahisi, ufanisi na ujumuishaji wa kifedha kwa kuziunganisha na mahitaji ya kila siku ya wateja.


WAKALI wa ubashiri Tanzania, Meridianbet wanakwambia kuwa siku ya leo ipo kwaajili yako wewe kupiga pesa. Hivyo ingia kwenye akaunti yako na uanze safari ya kijanja ya kutengeneza pesa.

BUNDESLIGA kule Ujerumani inatarajiwa kuendelea kwa mechi kibao ambapo Wolfsburg atakipiga dhidi ya S.T Pauli ambapo mara ya mwisho kukutana kwenye mechi zao mbili walitoa sare yaani hakuna mabaye aliondoka na pointi 3. Je leo hii nani kuondoka na ushindi?. Bashiri hapa.

Pia bingwa mtetezi wa ligi hii FC Bayern Munich atakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya FC Cologne ambao wapo nafasi ya 11 hadi sasa. Vijana wa Kompany wanahitaji ushindi mnono kwenye mechi hii kuendelea kujiweka kileleni. Je mwenyeji anaweza kumzuia bingwa kuchukua pointi 3?. Tandika jamvi hapa.

Naye RB Leipzig atakuwa nyumbani kusaka ushindi mkubwa dhidi ya Freiburg ambao hawapewi nafasi kubwa pale Meridianbet kuondoka na pointi 3 muhimu kabisa. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 9 pekee. Pesa kubwa ipo kwenye mtanange huu na Meridianbet. Jisajili hapa.

Pesa ipo kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kule Uingereza kuna mechi kali ya CARABAO CUP hatua ya Nusu Fainali ambapo Chelsea atakipiga dhidi ya Arsenal na hii itakuwa ni London Derby. Mechi ya mwisho kukutana ilikuwa kwenye ligi ambapo walitoa sare. Ikumbukwe kuwa mara ya mwisho The Blues kupata ushindi mbele ya The Gunners ilikuwa ni mwaka 2021. Je nani kusonga mbele kwenye Fainali?. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Suka jamvi hapa.

Vilevile unaweza ukapiga pesa kwenye SERIE A kule Italia ambapo Napoli atakuwa nyumbnai kusaka ushindi dhidi ya Parma ambao wapo nafasi ya 15 huku wageni wao wakiwa nafasi ya 3 kwenye ligi. Meridianbet wameipa mechi hii machaguo zaidi ya 1000. Bashiri hapa.

Wakati kinara wa ligi, Inter Milan yeye atakuwa pia atakuwa nyumbani kupepetana dhidi ya US Lecce ambao wanashika nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi. Msimu uliopita wawili hawa walipokutana Milan waliondoka na ushindi mechi zote mbili. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Jisajili hapa.

Kule SAUDI PROFESSIONAL pia itaendelea ambapo Al Qadsiah atamenyana vikali dhidi ya Al Feiha ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 15. Mara ya mwisho kukutana hawa wawili, kila mtu aliondoka na pointi 3 mechi za mbili msimu uliopita. Tandika jamvi lako hapa.

Al Ahli ataumana dhidi ya Al Taawon ambao wapo nafasi ya 3 huku wenyeji woa wakiwa nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi. Meridianbet wameipa mechi hii ODDS KUBWA lakini pia ina machaguo zaidi ya 1000. Je wewe unampa nani nafasi ya kuondoka na mkwanja wa maana?. Beti hapa.

Na Mwandishi wetu, Simanjiro


WAKUU wa shule za sekondari na msingi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule kutokana na kasi ya ukuaji na kuongezeka kwa matumizi ya sayansi na teknolojia ulimwenguni.

Wakuu wa shule 23 za sekondari, 110 wa msingi wa shule za serikali na binafsi wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa wake kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu.

Afisa elimu ya awali na msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Darius Daudi Limandola amesema walimu hao wamepata mafunzo hayo ya uandaaji wa taarifa za shule kwenye vituo vitatu vya Orkesumet, Terrat na Mirerani.

Limandola ameeleza kwamba mafunzo hayo ya mfumo wa utoaji wa taarifa za kielimu kupitia mfumo wa kidigitali (School Information System) una lengo la kurahisisha utoaji na upatikanaji wa taarifa za shule husika kwa wakati.

Ameeleza kwamba mfumo huo unafanyakazi katika kutoa taarifa za kielimu za shule husika kila siku ikiwemo hali ya miundombinu ya shule, utekelezaji wa lishe kwa wanafunzi, hali ya watumishi na upatikaji wa huduma nyingine za kijamii hususani maji na umeme.

Amesema wanufaika wa mafunzo hayo ni wakuu 23 wa shule za sekondari, walimu wakuu 110 wa shule za msingi, maafisa elimu kata, walimu wa taaluma na takwimu na maafisa elimu ngazi ya wilaya.

Amewataka walimu wakuu na wakuu wa shule kusimamia utekelezaji wa mfumo huo mara moja baada ya shule kufunguliwa Januari 13, 2026 ambapo utairahisishia serikali kufanya maboresho na maamuzi sahihi katika shule husika kwa wakati.

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo, afisa elimu vifaa na takwimu wa halmashauri ya wilaya hiyo, Abdalah Hamis amesema walimu hao wamejengewa uwezo kwa muda wa siku mbili na kisha watakwenda kuwaelekeza walimu waliobaki katika shule zao.

"Mafunzo yamefanyika katika vituo vitatu vya Orkesumet shule ya sekondari Simanjiro, shule ya sekondari Terrat na shule ya awali na msingi Glisten Mirerani, ambayo yameanza juu kwa wachache watakaokwenda kuwafundisha wengi," amesema Hamis.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, mkuu wa shule ya sekondari Tanzanite, Jude Samwel Mziray amesema mfumo huo ni mzuri kwani wanaaachana na mtindo wa kuingiza taarifa kwenye makaratasi na kuweka katika mfumo wa kiteknolojia.

"Mfumo huo unarahisisha kwani unatoa taarifa ya shule hadi ngazi ya kata, kisha wilaya hadi ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) tofauti na tulivyozoea mwanzo kujaza katika makaratasi," amesema Mziray.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Naepo, kata ya Naisinyai, Simon Isack Magembe amesema mafunzo hayo yanawajengea uwezo zaidi wa kuboresha taarifa kwa matumizi sahihi.

Mwalimu Magembe amesema ujuzi walioupata wa kuandaa taarifa za mfumo huo umewarahisishia utendaji kazi wao tofauti na awali.



 Yas imeendelea na dhamira yake ya kuwekeza kwenye sekta ya elimu na kukuza vipaji vya vijana wa Kitanzania kupitia udhamini wa wanafunzi kumi mahiri waliochaguliwa kushiriki Kambi Maalum ya Mafunzo ya Hisabati Kigali, Rwanda kuanzia Januari 6 hadi 22, 2026.

Kambi hiyo ya kitaaluma, inayoandaliwa na African Olympiad Academy (AOA) kwa ushirikiano na MIT–Africa, inalenga kuwaandaa wanafunzi wenye vipaji kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika kwa ajili ya Mashindano ya Pan-African Mathematics Olympiad (PAMO) yanayotarajiwa kufanyika Juni mwaka huu.

Kupitia taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari, Afisa Mkuu wa Udhibiti Yas, Bi. Sylvia Balwire, alisema udhamini huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kampuni katika kuendeleza elimu, ubunifu na teknolojia nchini.

“Kupitia udhamini huu, tunaonyesha msimamo wetu wa muda mrefu wa kukuza elimu na kutengeneza kizazi kijacho cha watafiti, wavumbuzi na viongozi wa teknolojia. Somo la Hisabati ndiyo injini ya uchumi wa kidijitali, ubunifu na utatuzi wa changamoto za kisasa. Kwa kuwaunga mkono wanafunzi hawa, tunawekeza moja kwa moja kwenye mustakabali wa taifa letu,” alisema Bi. Balwire.

Aliwapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa, akibainisha kuwa uteuzi wao unaakisi uwezo, nidhamu na kujituma kwa kiwango cha juu katika somo la hisabati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa AOA, Arun Shanmuganathan, alieleza kufurahishwa kwake na ushiriki wa wanafunzi kutoka Tanzania ambao wamepata nafasi ya kuungana na wenzao mahiri kutoka Rwanda, Uganda, Kenya, Botswana, Namibia, Afrika Kusini na Nigeria ambao tayari wanasoma katika taasisi hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa MIT–Africa, Ari Jacobovits, alisema uwezo mkubwa ulioonekana kwa wanafunzi hao ndio sababu ya MIT kuwekeza kwa kina katika maendeleo yao, popote pale safari yao ya baadaye itakapowapeleka.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Chama cha Hisabati Tanzania (CHAHITA), Dkt. Said Sima, alitoa shukrani kwa Yas kwa mchango wake endelevu katika kukuza vipaji vya vijana na kuinua taaluma ya hisabati nchini.

Wanafunzi hao 10, ambao tayari wamesafiri kuelekea Rwanda kwa maandalizi haya muhimu ya kitaaluma na kimashindano, wanatoka maeneo mbalimbali ya Tanzania na wanawakilisha shule tofauti ikiwemo Ilboru Arusha, St. Francis Mbeya, Feza, Marian, Mahina, St. Monica Arusha na Mbeya Secondary.






Na Said Mwishehe,Michuzi TV

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Dk.Asha-Rose Migiro ametoa mwito kwa viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo Wabunge na Mawaziri kushiriki katika vikao vya mashina na matawi vinavyoitishwa katika maeneo yao.

Akizungumza leo Januari 13 wakati akihitimisha ziara yake ya mkoa wa Dar es Salaam kwa kufanya kikao kazi na viongozi wa CCM katika ngazi ya mashina pamoja na mabalozi Wilaya ya Ilala ameendelea kusisitiza umuhimu wa viongozi wa kitaifa wa Chama hicho kushiriki mikutano ya ngazi ya mashina na matawi.


 “Tumesema  mabalozi wetu mnafanya kazi nzuri  kwani mnaitisha mikutano katika mashina yenu ,hivyo tunapenda kutoa mwito mikutano hii isiwe kwa watu ambao wako katika ngazi ya mashina peke yake au ngazi ya tawi peke.


 “Viongozi wa kitaifa tunao wabunge katika mashina yetu , tunao mawaziri katika mashina yetu yetu.Nitoe mwito kwamba wawe sehemu ya mikutano  hii kwasababu kwa hakika hakuna anayeanzia juu wote tunaanzia kwenye mashina yetu.

“Kwahiyo iwe ni mfano kwa viongozi wetu kuwa sehemu mikutano ile ambayo inaitishwa na mabalozi wetu kwa maana hiyo tutakwenda kadri tunavyoendelea baada ya kupata taarifa ,kupata muhatasari wa yale yanayoendelea tupate kujua ni namna gani tujiimarishe zaidi.

Amesisitiza viongozi wanaposhiriki kwenye vikao ndipo wanapata nafasi ya kutazama changamoto zinazowakabili kama chama lakini na changamoto zinazoikabili jamii yetu na Chama Cha Mapinduzi kina wajibu wa kuzichukua changamoto hizo na kuzifikisha kwenye ngazi za juu.

“Ili  kwa pamoja na kwa kushirikiana nanyi mabalozi kwa kupata ushauri wenu kwa kupata nasaha zenu tuweze kuwapatia wananchi majibu ya changamoto zinazowakabili kwani wametupa dhamana ya uongozi

Kwa upande mwingine Dk.Migiro amezungumzia muelekeo wa Chama Cha Mapinduzi kimkakati katika kuendelea kuimarisha uhai wa chama hicho ambapo amefafanua mabalozi pamoja na kufanya kikao pia waendelee kuweka kumbukumbu za wanachama wao.

“Tumeambiwa hapa mashina ni sehemu muhimu sana ya usalama wa jamii yetu na usalama wa Taifa letu hivyo tutakuwa na wajibu wa kuhakikisha watu ambao tunaishi nao tunajua wanafanya nini na tunajua yale wanayoyafanya yanakuwa salama kwa Taifa letu 

“Tunajua pia hivi sasa balozi wa shina anaweza kuwa na nyumba nyingi sana hivyo kupitia vikao vyetu tutaangalia ni namna gani balozi wa shina apate mzigo ambao anaweza kuubeba ili twende kwa pamoja kuhakikisha chama chetu kinaendelea kuwa chama kiongozi na kinaendelea kushika dola kwa manufaa ya taifa letu.”
























Top News