Na Pamela Mollel,Arusha

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Laban Kihongosi, anaanza ziara maalum ya siku tatu mkoani Arusha kuanzia Juni 4 hadi 6, 2026, kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi, kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuimarisha uhai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika ngazi zote

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Saipulani Ramsey, amesema ziara hiyo ni fursa adhimu kwa wananchi kufikisha changamoto zao moja kwa moja kwa viongozi wa chama na Serikali ili zipatiwe ufumbuzi wa haraka.

Ramsey amesema Kihongosi pamoja na ujumbe wake watatembelea na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujionea maendeleo yaliyofikiwa na kupokea maoni ya wananchi kuhusu ubora wa huduma zinazotolewa

Ameeleza kuwa sekta za elimu, afya, maji na miundombinu ni miongoni mwa maeneo yatakayopata kipaumbele katika ziara hiyo, huku viongozi wakitarajiwa kukusanya maoni na mapendekezo yatakayosaidia kuboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wananchi

Mbali na masuala ya maendeleo, ziara hiyo itahusisha tathmini ya uhai wa CCM kuanzia ngazi ya matawi hadi mkoa, pamoja na mikutano na wanachama na viongozi wa chama kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa maelekezo mbalimbali ya chama.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, Kihongosi ataanza ziara yake Wilaya ya Karatu Juni 4, kisha kuelekea Arumeru Juni 5, kabla ya kuhitimisha kwa mkutano mkubwa wa hadhara katika Jiji la Arusha Juni 6

Wakati huo huo, CCM Mkoa wa Arusha imesema imeendelea kuimarisha chama katika maeneo mbalimbali ambapo tayari imefikia kata 107 kati ya kata 161 kupitia ziara inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Thomas Ole Sabaya. Chama hicho kimesema mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa na umechangia kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo katika jamii.




Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imeshiriki kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa Viwango vya Kazi kinachoendelea jijini Geneva, Uswisi, ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Katika kikao hicho kilichifanyika leo Juni 2, 2026 ambapo wajumbe wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa viwango vya kazi, ikiwemo mjadala wa jumla kuhusu ripoti kuu ya Kamati ya Mkutano na maadhimisho ya miaka 100 ya ajenda ya Kazi zenye Staha, Tathmini ya Jumla, pamoja na wajibu wa nchi wanachama katika kuwasilisha taarifa na kutekeleza majukumu mengine yanayohusiana na viwango vya kazi.

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho ulijumuisha Jaji wa Mahakama ya Rufani Dkt. Yose Joseph Mlyambina, Kamishna wa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Kazini, Suzan Mkangwa, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Khadija Mwenda, pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Usekelege Mpulla

Tanzania, ambayo ni mwanachama wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) na mjumbe wa Bodi ya Magavana inayowakilisha nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki, inaendelea kushiriki Mkutano Mkuu wa 114 wa shirika hilo unaowakutanisha wawakilishi wa Serikali, Waajiri na Wafanyakazi kutoka nchi wanachama 187.





Na Mwandishi Wetu


MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19.

Katika hukumu iliyotolewa Juni 1, 2026, Jaji S.E. Kisanya alisema ushahidi wa upande wa mashtaka ulithibitisha pasipo shaka kuwa washtakiwa hao walikuwa na umiliki wa dawa hizo.

Mchambuzi wa Serikali kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Leonida Daniel Michael, aliithibitishia mahakama kuwa pakiti 16 zilizokamatwa zilikuwa na heroin yenye uzito wa kilo 15.19 baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kisayansi.

Mahakama ilibaini kuwa utetezi wa washtakiwa haukuweza kuibua shaka dhidi ya ushahidi wa mashahidi na vielelezo vilivyowasilishwa.

Mshtakiwa wa pili, Sharifa Selemani Bakari, aliachiliwa huru baada ya mahakama kubaini kuwa upande wa mashtaka haukuthibitisha ushiriki wake katika kosa hilo.

Mbali na kifungo hicho, mahakama imeagiza heroin yote iliyokamatwa pamoja na vifaa vya kufungashia kuteketezwa kwa mujibu wa sheria.




Na Mwandishi Wetu, DODOMA

Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026 umezindua mradi wa kusimika kamera za usalama wenye thamani ya shilingi 682,561,548.6, ukiwa na lengo la kuimarisha ulinzi na usalama wa raia, mali zao pamoja na miundombinu ya umma.

Mradi huo umetekelezwa kwa ushirikiano ambapo Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa kiasi cha shilingi 519,891,609.27, huku Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ukichangia shilingi 162,669,939.34 kupitia Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa ajili ya kuunganisha mfumo huo kupitia Mkongo wa Taifa.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo, Wazo Mwang’onda alisema ameridhishwa na mradi huo katika kuimarisha usalama wa Jiji la Dodoma na utasaidia kuvutia wawekezaji kutokana na mazingira salama yaliyopo.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewahakikishia wawekezaji usalama wao kwa kuonesha dhamira ya serikali kwa kutenga fedha nyingi kwa ajili ya kufunga kamera katika Jiji la Dodoma. 

Dodoma iko salama, na uhalifu wowote utakaojitokeza utashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za Jeshi la Polisi kwa haraka, kwa kuwa wahalifu wataweza kufuatiliwa kwa urahisi kupitia mfumo huu. Mwenge wa Uhuru umefurahishwa na ufungaji wa kamera hizi kwa ajili ya kuimarisha usalama” alisema Mwang’onda.

Akisoma taarifa ya mradi huo, Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA, Joseph Fungo alisema kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia 80, ukihusisha kusimika nguzo, kufunga kamera pamoja na vifaa katika chumba cha kuongozea. 

Alieleza kuwa hatua zinazofuata ni kuunganisha kamera zote ili ziweze kusomana na chumba cha kuongozea kupitia Mkongo wa Taifa, kuingiza umeme wa gridi katika vituo 33 vya kamera, kutoa mafunzo kwa watumiaji, na kuandaa mfumo wa usimamizi katika kipindi cha matazamio.

Nae, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisema kuwa wamejifunza kutoka nchi mbalimbali na kubaini kuwa usalama ni nguzo muhimu katika miji ya kisasa. Aliongeza kuwa kamera za ulinzi barabarani zitasaidia kudhibiti matukio ya uhalifu hali inayowapa wawekezaji uhakika zaidi wa mazingira salama.






Na Benny Mwaipaja, Dodoma.

Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi trilioni 21.3 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara hiyo pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27.

Akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango na Bajeti bungeni, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema fedha hizo zitatumika kugharamia matumizi ya kawaida na maendeleo katika mafungu manane ya Wizara, ambapo kati ya fedha hizo, shilingi trilioni 19.4 zitatumika kwa matumizi ya kawaida huku shilingi trilioni 1.8 zikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa katika Bajeti hiyo, Serikali imepanga kuendelea kusimamia uchumi kwa weledi ili kuhakikisha ukuaji wa uchumi unafikia asilimia 6.3 mwaka 2026 huku mfumuko wa bei ukidhibitiwa kubaki katika katika wigo wa wastani wa asilimia 3 hadi 5.

“Serikali pia inalenga kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za umma pamoja na kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, alibainisha kuwa Wizara imepanga kutenga shilingi bilioni 100 kila mwezi kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi, wakandarasi, wazabuni na watoa huduma ili kupunguza changamoto za malimbikizo ya madeni serikalini.

Kwa upande wa mapato, alisema kuwa Wizara ya Fedha imekadiriwa kukusanya jumla ya shilingi trilioni 55.2, ambapo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatarajiwa kukusanya zaidi ya shilingi trilioni 39.

Katika hatua nyingine, aliliomba Bunge kuiidhinishiwa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi shilingi bilioni 132.2 kwa ajili ya kuimarisha shughuli za ukaguzi wa matumizi ya fedha za umma pamoja na kuendelea na ujenzi wa ofisi zake katika baadhi ya mikoa nchini.

Mhe. Balozi Omar alieleza kuwa bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa pamoja na Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.


TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2025/26


Mhe. Balozi Omar alieleza kuwa jumla ya shilingi trilioni 20.18 ziliidhinishwa kwa ajili ya utekelezaji wa matumizi ya kawaida na maendeleo kwa mafungu manane ya wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2025/26.

Alisema kati ya fedha hizo, shilingi trilioni 19.43 zilitengwa kwa matumizi ya kawaida ikijumuisha mishahara ya shilingi trilioni 1.10 na matumizi mengineyo ya shilingi trilioni 18.33.

“Bajeti ya maendeleo ilikuwa shilingi bilioni 747.30, ambapo shilingi bilioni 601.70 zilikuwa fedha za ndani na shilingi bilioni 145.60 fedha za nje” Alisema Mhe. Balozi Omar.

Alisema kuwa wakati wa mapitio ya kati ya mwaka, bajeti ya wizara ilihuishwa na kupungua kutoka shilingi trilioni 20.18 hadi shilingi trilioni 19.94, ambapo kati ya kiasi hicho, shilingi trilioni 19.45 zilitengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi bilioni 485.99 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

“Hadi kufikia mwisho wa Aprili 2026, wizara ilikuwa imepokea jumla ya shilingi trilioni 14.08 sawa na asilimia 70.63 ya bajeti iliyohuishwa. Matumizi halisi yalifikia shilingi trilioni 14.05, sawa na asilimia 99.76 ya fedha zilizopokelewa” alifafanua Mhe. Balozi Omar.

Wizara pia ilieleza mafanikio yaliyopatikana katika ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa deni la Serikali pamoja na ukuaji wa uchumi ambapo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, Serikali ilifanikiwa kukusanya na kutafuta shilingi trilioni 41.37 kutoka vyanzo vya ndani na nje, sawa na ufanisi wa asilimia 82.4 ya lengo la mwaka.

Katika kipindi hicho, Serikali ilitumia shilingi trilioni 9.74 kuhudumia deni la Serikali, ambapo shilingi trilioni 4.45 zilielekezwa kwenye deni la nje na shilingi trilioni 5.29 kwa ajili ya deni la ndani na kwamba ulipaji wa madeni kwa wakati umeendelea kuijengea Tanzania imani katika masoko ya fedha ya kikanda na kimataifa.

“Nina furaha kulijulisha Bunge lako Tukufu kuwa Tanzania imeibuka mshindi wa jumla katika Tuzo ya Usimamizi wa Deni la Umma katika nchi za Jumuiya ya Madola, pamoja na tuzo ya Ofisi Bora ya Usimamizi wa Deni la Serikali katika Kanda ya Afrika” alisisitiza Mhe. Balozi Omar.

Kwa upande wa uchumi, Tanzania ilikua kwa wastani wa asilimia 5.9 mwaka 2025 ikilinganishwa na asilimia 5.5 mwaka 2024. Ukuaji huo umechangiwa na kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi, kuimarika kwa miundombinu, shughuli za kilimo, uchimbaji madini, ujenzi pamoja na utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Aidha, alieleza kuwa kiwango cha mfumuko wa bei kiliendelea kubaki katika wastani wa asilimia 3.4 huku akiba ya fedha za kigeni ikifikia dola za Marekani bilioni 5.723, kiasi kinachotosheleza uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje kwa zaidi ya miezi 4.4

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiwasilisha bungeni jijini Dodoma, Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na Mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka 2026/2027, ambapo ameliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi trilioni 21.3 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)
NALA - DODOMA

‎HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetekeleza ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 1.6 kutoka barabara kuu ya Bahi hadi Hospitali ya Jiji, hatua inayolenga kuboresha huduma za afya na kiuchumi kwa wananchi wa Kata ya Nala.

‎Akizungumza wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, Wazo Mwang’onda alipongeza mradi huo na kusema kuwa ni bora, umekidhi vigezo vyote muhimu kama taratibu za ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami zinavyotaka.

‎Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru umeridhishwa na ujenzi huo na upo tayari kuizindua. “Mwenge wa Uhuru umeridhishwa na ujenzi huu wa barabara ya Kilomita 1.6 ambayo imekamilika kwa ubora wa hali ya juu na sasa upo kwenye matazamio ya mwisho, umeridhishwa na namna barabara hii imejengwa. Tunaamini wakazi wa eneo hili watanufaika sana na uwepo wa barabara hii" alisema Mwang’onda.

‎Awali akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa barabara hiyo, Mhandisi wa Miradi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mha. Nicodemus Kileo alisema kuwa mradi huo ulitekelezwa na mkandarasi mzawa M/s. Kings Builders Limited kwa gharama ya shilingi bilioni 2.87 zilizotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, na upo tayari kuzinduliwa.

‎Nae, Mkazi wa Nala, Gervazi Sebastian alipongeza ujenzi wa barabara hiyo akieleza kuwa imeondoa adha ya usafiri kwa wakazi wa Nala. "Tunaishukuru sana serikali kwa kutujengea hii barabara, awali ilikuwa ngumu kupata usafiri wa nafuu kwasababu barabara ilikua mbovu. Kwakweli serikali imetuokoa hata huduma zingine zinapatikana kwa urahisi" alisema Sebastian.

‎Katika hatua nyingine, Mkazi wa Mtaa wa Segu Chini, Asia Omari alipongeza ujenzi wa barabara hiyo akisema kuwa imekuwa mkombozi kwa watumiaji hasa wanawake wajawazito wanaopita kwenda kupata matibabu katika Hospitali ya Jiji la Dodoma.

‎Mradi huo ni miongoni mwa miradi iliyozinduliwa na kuwekewa jiwe la msingi na Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026 uliobeba kaulimbiu isemayo “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo”.




Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Fedha imetangaza vipaumbele vinane (8) vya kimkakati kwa mwaka wa fedha 2026/27, vyenye lengo la kukuza uchumi, kuimarisha nidhamu ya matumizi ya rasilimali za umma, na kulipa madeni.

Vipaumbele hivyo vimewasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akisoma mapendekezo ya mpango na bajeti ya wizara hiyo.Sera na mikakati hiyo mikuu imegawanyika katika maeneo yafuatayo:

1. Ukuaji wa Uchumi na Kudhibiti Mfumuko wa BeiWizara imepanga kusimamia uchumi jumla ili ufikie ukuaji wa asilimia 6.3 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2026. Aidha, jitihada zitawekwa ili kudhibiti mfumuko wa bei ubaki kwenye viwango vya tarakimu moja (wastani wa asilimia 3.0 hadi 5.0), huku akiba ya fedha za kigeni ikitunzwa kukidhi uagizaji wa bidhaa na huduma kwa angalau miezi minne (4).

2. Nidhamu ya Matumizi na Ukusanyaji MapatoIli kuhakikisha thamani halisi ya fedha za umma inaonekana, serikali itaimarisha nidhamu ya bajeti (fiscal discipline). Hatua hii itahusisha usimamizi madhubuti wa ununuzi wa umma na kupunguza tabia ya kuhamisha fedha kutoka fungu moja kwenda jingine (reallocation between votes).

3. Kuvunja Rekodi ya Mapato (Tsh Bilioni 55,200.75)Katika bajeti kuu ya serikali ya jumla ya shilingi bilioni 62,334.19, Wizara ya Fedha inalenga kuboresha mifumo ya kodi, misaada, na mikopo ili kuchangia shilingi bilioni 55,200.75 kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina. Hii ni sawa na asilimia 88.6 ya bajeti yote.

4. Kulipa Madeni na Kuaminika KimataifaSerikali imetenga shilingi bilioni 15,102.80 kwa ajili ya kulipa kwa wakati riba na mitaji ya madeni yanayotarajiwa kuiva. Hatua hii inalenga kulinda mikataba na kuendelea kujenga imani kwa wawekezaji katika masoko ya fedha ya kikanda na kimataifa.

5. Mabilioni ya Kulipa Watumishi na WakandarasiHabari njema kwa wadau wa ndani ni kwamba serikali itakuwa ikitoa shilingi bilioni 100.00 kila mwezi. Fedha hizi zitasaidia kulipa madeni ya watumishi wa umma, wakandarasi, wazabuni, na watoa huduma mbalimbali ili kuchochea mzunguko wa fedha.

6. Usawa wa Mgawanyo wa Fedha kwa HalmashauriKutakuwa na maboresho makubwa kwenye ugawaji wa rasilimali fedha kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa (Halmashauri). Mgawanyo huo utazingatia tafiti za kitaalamu ili kuondoa urudufu wa majukumu na kuleta uwiano wa kimaendeleo nchini.

7. Mageuzi ya Mfumo wa Bajeti (PBB)Serikali itafanya tathmini ya kina ya usimamizi wa bajeti kwa kutumia Mfumo wa Programu (Programme Based Budgeting – PBB). Lengo ni kuwezesha maamuzi sahihi ya kimabadiliko katika upangaji wa bajeti unaoleta matokeo ya moja kwa moja kwa wananchi.

8. Matumizi ya Akili Unde (AI) na Utawala BoraKatika kwenda na wakati, wizara itajenga uwezo wa watumishi wake kuhusu masuala ya Mazingira, Jamii na Utawala Bora (ESG). Kubwa zaidi, serikali itaanza kuingiza matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) katika usimamizi wa fedha za umma na uchumi ili kuongeza ufanisi na uwazi.





Na Albano Midelo

Wakati wengi walidhani ajali ilizika ndoto zake milele, Deogratius Chami ameandika historia mpya Tanzania kwa kuwa mtu wa kwanza mwenye ulemavu wa kutumia kiti mwendo kufika kilele cha Mlima Kilimanjaro (Uhuru Peak, mita 5,895).

Chami, mzaliwa wa Moshi ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi wa Kilimanjaro Disability Royour Tour and Safaris, alifikia mafanikio ya kupanda mlima Kilimanjaro baada ya safari ya siku saba mwaka 2014, na kurudia tena mwaka 2023 kwa siku sita pekee.

Mrajisi wa Ushirika Mkoa wa Ruvuma Venance Msafiri akizungumza siku ya maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani ambayo yalifanyika wilayani Nyasa mkoani Ruvuma,amesema ushirika umechangia mafanikio ya mwenye ulemavu huyo baada ya kumpatia mkopo wa maendeleo wa shilingi milioni nane mwaka 2023, hivyo kufanikiwa kuanzisha kampuni hiyo ya utalii..

Amesema Kupitia kampuni hiyo Chami sio tu anautangaza utalii,bali pia anautangaza ushirika na kwamba wanatarajia kumualika mkoani Ruvuma ili aweze kuja kutembelea vivutio vya Mkoa wa Ruvuma hususani wilaya ya Nyasa ambayo ni kitovu cha utalii katika Mkoa.

Akiwa na miaka 13 darasa la sita shule ya msingi Kilimanjaro,Chami alipata ajali mbaya ilimlaza kwa karibu miaka miwili katika Hospitali ya KCMC Moshi. Ndoto zake za kuwa mwanajeshi na mchezaji wa mpira zilionekana kufutika.

Hata hivyo, ushauri wa mwalimu wake wa shule ya msingi ulimgeuza kutoka nafasi ya 129 darasani hadi kuwa miongoni mwa wanafunzi bora, hatua iliyomfikisha hadi Shahada ya Maendeleo ya Jamii na Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mwaka 2013.

Kwa mujibu wa WHO (2023), watu bilioni 1.3 duniani wanaishi na ulemavu, sawa na asilimia 16 ya idadi ya watu wote. Chami amethibitisha kuwa ulemavu si mwisho wa mafanikio bali mwanzo wa njia mpya ya ushindi.


Picha mbalimbali za Deogratias Chami mtanzania wa kwanza mwenye ulemavu kupanda mlima kilimanjaro hadi kileleni  kwa kutumia kiti mwendo ,Chami amepanda mlima kilimanjaro mara mbili mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2014 ambapo alitumia siku saba kufikia kileleni na mara ya pili mwaka 2023  akiwa na kampuni yake ya utalii alifanikiwa kupanda mlima kilimanjaro kwa kutumia siku sita hadi kileleni

PIRATES Power kutoka Meridianbet imekuandalia safari ya kipekee katikati ya bahari ya hazina yenye burudani na nafasi kubwa za ushindi. Huu ni mchezo unaokupa nafasi ya kuingia kwenye ulimwengu wa mabaharia jasiri wanaosaka utajiri mkubwa kila siku.

Ndani ya mchezo huu, kila mzunguko unaweza kuwa mwanzo wa ushindi mkubwa. Pirates Power inakupa nafasi ya kushinda hadi mara 5000 ya dau lako, jambo linalofanya kila mzunguko kuwa na msisimko wa kipekee na matumaini ya kubadilisha siku yako kwa sekunde chache tu.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mchezo huu umebeba mistari 20 ya ushindi pamoja na njia 6 tofauti za kushinda, hivyo kuongeza nafasi zako za kuondoka na tabasamu. Alama za Wild zina uwezo wa kuongeza ushindi wako mara mbili, huku alama za Scatter zikifungua milango ya bonasi zinazoweza kukuletea zawadi kubwa zaidi.

Kwa wapenzi wa jackpot, Pirates Power imejaa fursa za kutikisa akaunti yako. Unaweza kukutana na Mini, Major au Grand Jackpot ambazo zinasubiri baharia mwenye bahati kujinyakulia. Bonasi maalum nazo zinaongeza nafasi ya kuendelea kushinda bila kukata tamaa.

Usikose nafasi ya kujiunga na maelfu ya wachezaji wanaofurahia burudani na ushindi ndani ya Meridianbet. Panda jahazini leo, cheza Pirates Power na anza safari yako ya kuelekea kwenye hazina kubwa inayoweza kubadilisha mchezo wako kabisa.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini nchini kuimarisha maadili kwa jamii na kukuza maemdeleo.

Mhe. Sangu amesema hayo alipomwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika hafla ya kumsimika uaskofu mchungaji Daniely Liyaseke wa Kanisa la The Charismatic Episcopal Church of Tanzania, Dayosisi mpya ya Ukanda wa Tanzanite One, iliyofanyika Mei 31, 2026 Kijiji cha Terat, Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Sangu amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa makanisa katika kuimarisha maadili, mshikamano wa kijamii na maendeleo ya Taifa na itaendeleza ushirikiano huo. Ameongeza kuwa kauli mbiu ya kanisa hilo “Kwa neema ya Mungu, tunajenga Huduma kwa vizazi vya sasa na vijavyo” inaakisi dhamira ya kuwekeza kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Vile vile, Mhe. Sangu alisisitiza mambo matatu muhimu kwa Taasisi za dini ziendelee kuombea amani, mshikamano na afya njema kwa viongozi wakuu wa nchi akiwemo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kadhalika, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na tasasisi za dini katika malezi ya vijana ili kujenga Taifa lenye maadili, upendo na uwajibikaji, pia kuendeleza ushirikiano katika utoaji wa elimu na huduma za kijamii kwa kizazi chenye uzalendo na uwajibikaji.

Aidha, Mhe. Sangu aliongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa, Ofisi na ununuzi wa gari, ambapo katika harambee hiyo Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amechangia Shilingi Milioni 15 na Waziri Sangu amechangia Shilingi Milioni 5.

Naye, Askofu Daniely Liyaseke aliwashukuru viongozi wa Serikali, viongozi wa dini na waumini kwa mshikamano na ushirikiano, akisisitiza kuwa “ukiona kobe yupo juu ya mti, ujue kuna aliyempandisha.”

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Millya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mhe. Fakih Lulandala, walipongeza uongozi wa Askofu Liyaseke na kusisitiza kuwa uwepo wa Dayosisi hiyo ni nguzo ya mshikamano wa kijamii na maendeleo ya kiroho.


TIMU ya Taifa ya Wales itashuka dimbani leo Juni 2 kuikaribisha Ghana katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaochezwa saa 21:45 usiku kwenye Uwanja wa Cardiff City nchini Uingereza.

Mchezo huu unatajwa kuwa wa kihistoria kwani ni mara ya kwanza kwa Wales kucheza dhidi ya taifa la Afrika katika mchezo wa kimataifa wa wanaume, huku pia ukiwa mkutano wa kwanza kabisa kati ya mataifa haya mawili.

Wales chini ya kocha Craig Bellamy itaingia kwenye mchezo huo ikiwa na lengo la kuendelea kujenga kikosi chake kuelekea michuano ijayo ya UEFA Nations League. Bellamy amekuwa akisisitiza soka la kushambulia kwa kasi, presha kubwa kwa wapinzani na matumizi ya wachezaji wa pembeni, jambo ambalo linaweza kuipa Wales faida ya kucheza mbele ya mashabiki wake wa Cardiff.

Kwa upande wa Ghana, Black Stars wanautumia mchezo huu kama sehemu ya maandalizi ya Kombe la Dunia 2026. Kikosi hicho kinachonolewa na Carlos Queiroz kimewasili Wales na baadhi ya nyota wake wakubwa akiwemo Antoine Semenyo, Jordan Ayew, Thomas Partey pamoja na Iñaki Williams. Hata hivyo, kutokuwepo kwa Mohammed Kudus kutokana na majeraha kunaweza kupunguza ubunifu wao katika eneo la ushambuliaji.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kiufundi, mchezo huu unaweza kuwa wa ushindani mkubwa kutokana na tofauti za mitindo ya timu hizo. Wales wanapendelea kumiliki mpira na kufanya mashambulizi ya haraka kutoka pembeni, wakati Ghana hutegemea nguvu, kasi na mipira ya kushtukiza kupitia washambuliaji wake. Vita kubwa vinatarajiwa katikati ya uwanja ambapo Thomas Partey atakuwa na jukumu la kuzuia kasi ya viungo wa Wales.

Kwa ubora wa vikosi na maandalizi ya sasa, mchezo huu unaonekana kuwa wazi kwa timu zote mbili. Wales wana faida ya uwanja wa nyumbani na sapoti ya mashabiki wao, lakini Ghana wana wachezaji wengi wanaocheza ligi kubwa za Ulaya wenye uwezo wa kubadilisha matokeo wakati wowote. Jisajili

Benki ya NMB imetumia uzinduzi wa Tamasha la Twenzetu kwa Yesu kuwafikia vijana kwa ujumbe wa maadili, nidhamu ya fedha na matumizi sahihi ya huduma za kidijitali, katika jukwaa linalounganisha muziki wa injili, imani na mshikamano wa kijamii.

Akizungumza katika tamasha hilo, Meneja Mwandamizi Wateja Binafsi Benki ya NMB, Zuberi Bani, alisema ushiriki wa benki hiyo unalenga kuwa karibu na vijana na jamii kwa kuwapatia maarifa ya kifedha yanayoweza kuwasaidia kujenga tabia ya kuweka akiba, kupanga matumizi na kutumia huduma rasmi za kifedha kwa usalama. “Twenzetu kwa Yesu ni zaidi ya tamasha la muziki; ni nafasi ya kukutana na vijana, kuzungumza nao kuhusu maadili, nidhamu ya fedha na huduma zinazoweza kuwawezesha katika maisha yao ya kila siku,” alisema Bani.

Alisema NMB inaendelea kutoa suluhisho zinazogusa mahitaji ya vijana na familia, zikiwemo NMB Mtoto Account, Chipukizi na Mwanachuo, pamoja na huduma za kidijitali kama NMB Mkononi, Mshiko Fasta na NMB Pesa, zinazorahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha na kukuza utamaduni wa kuweka akiba.

Aidha, alisema huduma ya Kikundi Account sasa inapatikana kupitia App ya NMB Mkononi, hivyo kuondoa ulazima wa mteja kufika tawini. Kupitia Twenzetu kwa Yesu, NMB imesema itaendelea kushirikiana na wadau wa kijamii katika kukuza elimu ya fedha, huduma bunifu na mshikamano unaochangia maendeleo ya vijana na jamii kwa ujumla.






 

ATTRACTING pickleball players from more than seven countries, the Tanzania Pickleball Open 2026 tournament backed by Absa Bank Tanzania, underscoring the growing popularity of the sport and Tanzania’s ambitions to become a regional sports and tourism hub.

The five-day tournament, held at the Gymkhana Club grounds in Dar es Salaam, brought together elite pickleball players from Kenya, Uganda, Rwanda, South Africa, the Democratic Republic of Congo, India, Turkey and Dubai for one of East Africa’s largest pickleball competitions.

Organised through a partnership between the Tanzania Pickleball Association (TPA) and the East Africa Racket Sports Club (EARSC), the event featured a corporate prize pool of US$15,000 and premium playing equipment, attracting both international competitors and local spectators.

As the tournament’s title sponsor, Absa Bank Tanzania said its support reflects a broader commitment to youth development, community engagement and the promotion of emerging sports in the country.

Speaking during the closing ceremony, Absa Bank Tanzania Marketing and Communications Manager, Mr Beda Biswalo, said the tournament had demonstrated the growing potential of pickleball to unite communities and create opportunities for young people.

“We are inspired by the remarkable energy, discipline and international talent displayed throughout the tournament,” said Mr Biswalo. “Our partnership reflects a deeper purpose—championing a sport that unites communities while creating meaningful opportunities for young people.”

He encouraged more Tanzanians, particularly youth, to embrace the sport, noting that pickleball offers opportunities for recreation, fitness and professional development.

Sports stakeholders say the rapid growth of pickleball is creating new opportunities for athletes through international rankings, scholarships and participation in an expanding global professional circuit. The sport’s accessibility and relatively low cost have also contributed to its increasing popularity across different age groups.

The tournament's success aligns with Tanzania’s broader efforts to strengthen sports as a contributor to economic growth and tourism. Through support from government institutions and private-sector partners, the country has increasingly hosted regional and international sporting events aimed at showcasing Tanzania as a destination for sports tourism.

“Absa Bank investment in the tournament supports the Government’s agenda of developing sports infrastructure, nurturing local talent and positioning sports as a driver of economic activity. The initiative is in line with ongoing efforts by the National Sports Council (BMT) to expand opportunities for athletes and sports organisations”, Mr Biswalo added.

The bank also acknowledged the contributions of the Government of Tanzania, co-sponsors Pepsi and CBD Hotel, technology partner Courtly, tournament organisers and fans whose support contributed to the successful staging of the championship.

Following the success of the 2026 edition, Absa Bank remains committed to supporting the growth of pickleball and is optimistic that the Tanzania Pickleball Open will continue to attract increased international participation, help develop the next generation of Tanzanian athletes, and elevate the country's profile on the global sporting stage.

On his part, the President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Director, Kartik Kapor, stated that the Tanzania Pickleball Open 2026 was a resounding success and marked only the beginning of Tanzania’s journey toward becoming a global pickleball powerhouse.

During the finals Women’s Doubles, Rakshika/Agni won 1st place, Sally/Rinaaz won 2nd place and Edna/Ester, WON 3rd place. On men’s Double category, Yuvraj/Purvansh won 1st place, Fifi/Shane won 2nd place and Kartik/Dev won 3rd place.

On the Men’s Singles; Purvansh won 1st place, Fifi 2nd and Dev won 3rd place. International Mixed Doubles; Shaheed/Deandra won 1st place, Ahmad/Zainab 2nd and Lisa/Zuber won 3rd place. Open Women’s Singles; Agni won 1st place, Tamara won 2nd and Sally won 3rd place.

On Mix Doubles winners; Rakshika/Dev won 1st place, 2nd place went to Alikhan/Sally and Yuvraj/Agni won 3rd place.
President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Chairman, Kartik Kapor, shakes hands with Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), during the closing ceremony of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by the financial institution, at the Dar es Salaam Gymkhana Club.
Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (left), presents awards to winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.



Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), presents trophies to one of the winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank.
Pickleball players in action during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

A pickleball player showcases her skills during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.

Cheerful winners of the recently concluded Tanzania Pickleball Open 2026 pose during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank
Na Janeth Raphael MichuziTv Bungeni - Dodoma

Mbunge wa Viti Maalumu, Khadija Shaban Taya, amesema kuwa anawaheshimu wanaume kwa nafasi yao katika jamii kama baba na kaka, lakini ameeleza kuwa sehemu kubwa ya changamoto za mmomonyoko wa maadili inatokana na baadhi ya wanaume kushindwa kutekeleza ipasavyo majukumu yao ya kifamilia, hali inayosababisha wanawake kubeba mzigo mkubwa wa uangalizi wa familia.

Akichangia hoja hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya Maendeleo ya jamii Jinsia Wanawake na Makundi maalum Kwa mwaka wa fedha 2026/27 amesema kuwa pale wanaume wanaposhindwa kusimama katika majukumu yao ya malezi na uongozi wa familia, wanawake hujikuta wakilazimika kutoka na kujitafutia kipato ili kuhakikisha watoto wanapata mahitaji ya msingi.

Amefafanua kuwa hali hiyo imekuwa na athari za kijamii, ikiwemo kuongezeka kwa changamoto za malezi na kuporomoka kwa misingi ya maadili katika baadhi ya familia.

“Kwa hakika hakuna mwanamke mwenye akili timamu anayependa kumuumiza mwanaume anayempenda na kumheshimu. Wanawake wengi wanajikuta wakibeba majukumu makubwa kwa sababu ya mazingira yaliyopo,” amesema.

Aidha, Mbunge huyo ameeleza kuwa kuna baadhi ya wanaume wanaotelekeza familia zao, ikiwemo watoto wenye ulemavu, hali inayosababisha wanawake kuachwa peke yao katika mzigo wa malezi na matunzo.

Ameongeza kuwa katika baadhi ya familia, watoto wenye ulemavu wamekuwa wakikosa msaada wa baba zao, jambo linalosababisha changamoto kubwa kwa akina mama wanaojitahidi kuwalea na kuwahudumia bila msaada wa karibu wa kifamilia, wakati mwingine hata kukumbana na kutengwa na baadhi ya ndugu na jamii.

Katika wito wake kwa Serikali, Khadija Shaban Taya ameiomba kuangalia kwa karibu kundi la watoto wenye ulemavu na wazazi wao, ili kuhakikisha wanajumuishwa kikamilifu katika sera na mipango ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, ili kurahisisha upatikanaji wa huduma na utekelezaji wa haki zao.



Top News