Na Mwandishi Wetu, Dodoma
CHUO cha Uhasibu na Usimamizi wa Fedha (IFM) kimesema kimejipanga kuendelea kutoa elimu inayokwenda sambamba na mahitaji ya sasa ya teknolojia, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wahitimu wanakuwa na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira na uchumi wa kidijitali.

IFM imesema hayo wakati ikishiriki Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo na Ufugaji Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma ,Mwanza pamoja na Simiyu mbapo imeeleza kuwa ushiriki wake ni sehemu ya kusogeza huduma za elimu karibu na wananchi.

Kwa mujibu wa chuo hicho, ushiriki katika maonesho hayo ya kitaifa na ya kanda pia unalenga kuwafikia wananchi wanaozunguka kampasi zake na kuwapatia elimu pamoja na taarifa kuhusu fursa zinazopatikana kupitia programu mbalimbali za IFM.

IFM imeeleza kuwa maonesho hayo yamejikita katika kuongeza thamani ya mazao na bidhaa ili ziweze kupata masoko yenye tija, ambapo ujuzi wa usimamizi wa fedha ni muhimu katika kuhakikisha mnyororo mzima wa thamani unakuwa na tija kwa wazalishaji.

Chuo hicho kimesema pale mazao yanapoingia sokoni, masuala ya usimamizi wa fedha huwa muhimu katika kuhakikisha wakulima wanapata mapato yanayoendana na thamani ya uzalishaji wao, huku wakijengewa uwezo wa kutumia fedha hizo kwa ufanisi.

Aidha, IFM imeeleza kuwa elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia ni muhimu kwa wakulima na wafanyabiashara katika kuboresha utunzaji wa kumbukumbu za kifedha, kufanya maamuzi sahihi ya biashara na kuongeza tija katika shughuli zao za kiuchumi.











Matukio katika Picha Chuo cha  IFM  katika maonesho ya Kitaifa na Kanda.
Na Benny Mwaipaja, Mbeya

Serikali imetangaza kuendelea kuongeza uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, huku ikizitaka jamii za Nyanda za Juu Kusini kutumia fursa za soko, teknolojia na miundombinu ili kuongeza tija na kuharakisha utekelezaji wa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kauli hiyo ilitolewa mkoani Mbeya na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati wa kilele cha Maonesho na Sherehe za Wakulima Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, yaliyofanyika katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya.

Akizungumza mbele ya viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo, wakulima, wafugaji na wavuvi, Mhe. Balozi Omar alisema kaulimbiu ya Nanenane ya mwaka huu, “Tambua soko: Ongeza tija kutekeleza Dira ya 2050,” inapaswa kuwa chachu ya kuongeza uzalishaji wenye tija kuanzia shambani hadi kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Alisema uchumi wa Taifa umeendelea kuimarika, ambapo pato ghafi la Taifa lilifikia shilingi trilioni 234.1 mwaka 2025, kutoka shilingi trilioni 211.97 mwaka 2024, sawa na ukuaji wa asilimia 5.9 na Sekta ya kilimo nayo imeendelea kuonesha mafanikio makubwa, ikikua kwa asilimia 5.5 mwaka 2025 ikilinganishwa na asilimia 3.7 mwaka 2021, huku ikichangia asilimia 24.3 ya uchumi wa Taifa.

Kwa upande wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mhe. Balozi Omar alisema eneo hilo limeendelea kuwa mhimili mkubwa wa uzalishaji na uchumi wa nchi. Alieleza kuwa pato la kanda hiyo lilifikia shilingi trilioni 32.8 mwaka 2024, sawa na asilimia 15.8 ya pato la Taifa, likiongezeka kutoka shilingi trilioni 29.6 mwaka 2023. Mkoa wa Mbeya uliongoza kwa pato la shilingi trilioni 11.6, ukifuatiwa na Iringa, Rukwa, Songwe, Njombe na Katavi.

Katika hatua ya kuimarisha sekta za uzalishaji, Mhe. Balozi Omar, alisema Serikali imeongeza bajeti ya sekta ya kilimo kutoka shilingi bilioni 276.72 mwaka 2021/22 hadi shilingi bilioni 1,132.36 mwaka 2026/27. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 698.99 zitaelekezwa Wizara ya Kilimo na shilingi bilioni 433.38 Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Alisema pia kuwa Serikali imeidhinisha shilingi bilioni 384.29 kwa mwaka 2026/27 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji nchini, hatua ambayo imechangia kuongezeka kwa eneo la umwagiliaji hadi hekta 983,466.1 mwaka 2025 kutoka hekta 727,280.6 mwaka 2022.

Akizungumzia hali ya chakula, Mhe. Balozi Omar alisema mikoa ya Nyanda za Juu Kusini imeendelea kufanya vizuri kwa kuwa na wastani wa uwezo wa kujitosheleza kwa chakula wa asilimia 219, juu zaidi ya kiwango cha chini kinachohitajika cha asilimia 120 na wastani wa Taifa wa asilimia 129.

Katika sekta ya mifugo na uvuvi, alisema Serikali imeendelea kuwekeza katika chanjo, masoko, mialo, boti za doria na usimamizi wa rasilimali za maji katika maziwa ya Nyasa, Rukwa na Tanganyika.

Aliongeza kuwa katika mikoa hiyo, jumla ya malambo 50 na mabwawa ya samaki 5,695 yamejengwa katika vipindi tofauti ili kuongeza uzalishaji na kipato kwa wananchi.

Kwa upande wa vijana, Mhe. Balozi Omar alisema Serikali imetenga shilingi bilioni 23 kupitia dirisha la mifugo na uvuvi kwa ajili ya kuwezesha miradi mbalimbali ya vijana, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kukuza uchumi wa sekta hizo.

Aliwataka viongozi wa mikoa na wilaya kusimamia amani, lishe, uhifadhi wa mazingira, pamoja na uanzishwaji wa vituo vya taarifa na teknolojia za kilimo katika kila kata ili kuwafikishia wakulima huduma na ubunifu unaooneshwa akisisitiza kuwa mafanikio ya sekta hizo yatategemea zaidi uzalishaji wenye tija, uhifadhi wa chakula, na matumizi bora ya fursa za soko.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akimkabidhi Funguo za Trekta kama Mkopo kutoka Benki ya CRDB, Mkazi wa Jiji la Mbeya, Bi. Christina Levi Mgaya (Katikati), kwa ajili ya kumwezesha katika shughuli zake za kuendeleza kilimo, wakati alipotembelea Mabanda ya Maonesho katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya kwa ajili ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Jijini Mbeya.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akisikiliza maelezo ya Afisa Maliasili Mkoa wa Mbeya, Bw. Petro Haule, kuhusu aina mbalimbali ya mavazi ya kale ambayo yalitokana na Ngozi, wakati alipotembelea Banda la Maliasili la Mkoa wa Mbeya, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla yakuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, jijini Mbeya. 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akisikiliza maelezo ya Meneja Utafiti wa Kiwanda cha Mbolea cha INTRACOM, Dkt. Tulole Buchoyeke, kuhusu tafiti za mbolea wanazozalisha, wakati alipotembelea Mabanda ya maonesho, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya. 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto) akiangalia moja ya bidhaa ya Siagi ya Karanga inayozalishwa na Mjasiliamali Mdogo kupitia Kampuni yake ya Swahigo Enterprises, Bw. Albert Thomas (kulia), wakati alipotembelea Mabanda ya Maonesho, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikua Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani – Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (katikati) akiteta jambo na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge (kushoto), wakati wakitembelea mabanda mbalimbali katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikua Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani – Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe.. Beno Malisa.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Mbeya)

Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, amehitimisha ziara yake nchini Tanzania na kuagwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Jukwaa hilo la siku mbili lililofunguliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, liliipatia Tanzania fursa ya kusaini hati tatu za makubaliano ikiwemo hati ya makubaliano ya kujenga kituo kipya cha huduma za usafishaji wa figo, mradi wa kuchakata gesi asilia kuwa gesi kimiminika na makubaliano kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Africa50 ya kuendeleza miundombinu ya usafirishaji wa umeme.

Aidha, Mikutano hiyo iliyokutanisha washiriki wapatao 1,200, imeipatia Tanzania fursa ya kutangaza vivutio vya utalii, uwekezaji na miradi ya kimkakati kwa lengo la kuvutia mitaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika maendeleo ya miundombinu na hivyo kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Kitaifa wa Miaka Mitano (FYDP IV) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiagana na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiongozwa kuelekea kupakia ndege na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kulia), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiongozwa na na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.










Picha za matukio mbalimbali wakati Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, alipoagana na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)




Na Mwandishi Wetu, Dodoma
SERIKALI imesema inaendelea kuimarisha sekta za kilimo, ufugaji pamoja na uvuvi kwa kuongeza thamani ya bidhaa ili ziweze kushindana katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, wakati akizungumza katika mjadala kuhusu Kilimo, Ufugaji na Uvuvi ulioandaliwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na kufanyika katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nane Nane yanayoendelea jijini Dodoma.

Mjadala huo uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka serikalini, sekta binafsi na taasisi zinazohusika na maendeleo ya sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Londo alisema Serikali imekuwa ikiratibu shughuli mbalimbali zinazolenga kuongeza uzalishaji na thamani ya bidhaa za kilimo, ufugaji na uvuvi ili kuongeza ushindani wa bidhaa hizo katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Alisema miongoni mwa hatua zinazochukuliwa ni kufanya tafiti katika maeneo mbalimbali yanayohusiana na kilimo, ufugaji na uvuvi, kwa lengo la kupata taarifa na teknolojia zitakazosaidia kuongeza tija na ubora wa bidhaa.

“Serikali inaendelea kuratibu shughuli mbalimbali, ikiwemo kufanya tafiti katika maeneo ya kilimo, ufugaji na uvuvi, kwa lengo la kuongeza uzalishaji unaoendana na kuongeza thamani ya bidhaa ili ziweze kupata masoko ndani na nje ya nchi,” alisema.

Aliongeza kuwa kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za mifugo na uvuvi ni hatua muhimu katika kuwawezesha wazalishaji kupata kipato zaidi, kuongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

FAO YAWEKA MKAZO MNYORORO WA THAMANI
Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Tanzania, Dkt.Nyabenyi Tipo, katika mijadala na wadau mbalimbali kuhusu uimarishaji wa mnyororo wa thamani wa kilimo chenye tija.

Alisema mjadala huo unalenga kuongeza tija katika kilimo, kupunguza upotevu wa mazao na kuhakikisha wakulima wanaongeza kipato kutokana na shughuli zao.

Tipo alisema FAO inalenga kuhakikisha mnyororo mzima wa uzalishaji, kuanzia shambani hadi sokoni, unaimarishwa ili mkulima,Mfugaji na pamoja Mvuvi waweze kunufaika zaidi na shughuli za kilimo.

Alisema katika kuimarisha mnyororo huo, ni muhimu kuweka mikakati ya kupunguza upotevu wa mazao unaotokea baada ya kuvuna, hususan katika hatua za usindikaji, uhifadhi na usafirishaji.

Aidha, alisema ni muhimu kuwaunganisha wadau mbalimbali katika sekta ya kilimo, wakiwemo wakulima, wafanyabiashara, wasindikaji, taasisi za fedha, watafiti na Serikali, ili kujenga mfumo unaowezesha kila mdau kunufaika na mnyororo wa thamani.

Tipo pia alisisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia na data katika kuendeleza kilimo cha kisasa kinachozingatia mahitaji ya soko pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa.

Alisema matumizi ya teknolojia yanaweza kuwasaidia wakulima kupata taarifa sahihi kuhusu masoko, uzalishaji na hali ya hewa, jambo litakalosaidia kuongeza ufanisi na kupunguza changamoto zinazowakabili katika uzalishaji.

Alisema FAO Tanzania imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Kilimo, taasisi za utafiti, mashirika ya kiraia na sekta binafsi katika kujadili na kubuni mikakati ya kuimarisha mifumo ya chakula nchini.

Alisema ushirikiano huo unalenga kujenga mnyororo wa thamani wa kilimo ulio imara na wenye tija, ambao utaongeza thamani ya mazao, kuboresha kipato cha wakulima na kuchochea ukuaji wa uchumi.



Na Khadija Kalili
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Singida Fatuma Mganga amesema tunafahamu suala la kilimo huwezi kulitenganisha na TARI na huwezi ukatengamisha uchumi wa nchi yetu na kilimo.

RAS Mganga amesema hayo alipokuwa mgeni rasmi siku ya korosho wakati wa maonesho ya wakulima nanenane Kitaifa Jiji Dodoma pamoja na maadhimisho ya miaka kumi ya TARI.

Amesema kwa sababu karibu yetu wananchi wengi waanjishughulisha na kilimo na tunapoongelea kilimo wakati huu tunaongelea kilimo biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Hamidu Mbwana amesema kilimo cha korosho kimetuletea tija sana kwenye upande wa uzalishaji kutoka tani 210,000 msimu wa 2021 -22 mpaka msimu wa 2025-26 tumeweza kuzalisha tani 618,000 tukiwa na lengo la kuzalisha tani Mil.1 ifikapo 2030.

Kwa sababu ya mafanikio tuliyopata upande wa uzalishaji tumeamua kuongeza thamani ya zao hili na kimsingi pamoja na kwamba zao hili linaleta tija sana kwa kuongeza pato kwa wakulima na kuongeza mapato kwa serikali .

Mkurugenzi Mkuu wa TARI Dkt.Thomas Bwana amesema Dira 2050 inataka tufikie uchumi wa mkubwa wa juu katika uchumi hatuwezi fikia huko bila nchi kukua sisi tunategemea ongezeko la tija hili litaongezeka tu kama tutatumia teknolojia sahihi zinatoka wapi zinatoka kwenye tafiti kwa hiyo ukiangalia utafiti ndiyo roho ya Dira.


Na. Asia Singano na Josephine Majura, WF - Dodoma

Serikali imezitaka taasisi zote za umma nchini kuimarisha usimamizi wa mali za Serikali kwa kuhakikisha taarifa zote za mali zinaingizwa na kutunzwa katika Mfumo wa Serikali wa Usimamizi wa Mali (GAMIS), ili kuongeza uwajibikaji, kuimarisha matumizi ya rasilimali za umma na kupunguza hoja za ukaguzi.

Maagizo hayo yalitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nanenane), yaliyofanyika katika Uwanja wa Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Alisema Serikali imetumia fedha nyingi kuwekeza katika miradi ikiwemo ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere -JNHPP (takribani sh. trilioni 6), ujenzi wa Reli ya kisasa-SGR (takribani sh. trilioni 10.6), ununuzi wa ndege, ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi (takribani sh. bilioni 716.3) pamoja na utekelezaji wa miradi ya maji mijini na vijijini (takribani sh. bilioni 457.4), huku akisisitiza umuhimu wa miradi hiyo.

“Mali za umma ni rasilimali muhimu zinazowezesha Serikali kutoa huduma kwa wananchi na kutekeleza miradi ya maendeleo, huku wastani wa asilimia 70 ya bajeti za taasisi za umma ukitumika katika ununuzi unaozalisha mali hizo, usimamizi wake unapaswa kuzingatia uwajibikaji, ufanisi na utii wa sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa’’ alisema Bw. Sendo.

Alisisitiza kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa na wingi wa rasilimali nchini ni muhimu kuwa na mikakati madhubuti ya kuzisimamia mali hizo ili ziweze kutumika kwa matumizi yaliyokusudiwa na kuiwezesha Serikali kupata manufaa ya uwekezaji uliokusudiwa kwa kipindi kirefu.

‘’Kwa upande wa Wizara ya Fedha ikiwa na dhamana ya Usimamizi wa Mali za umma nchini imefanya jitihada mbalimbali katika kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa Mali za umma nchini kwa Kusimika na kuwezesha matumizi ya mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Mali za Serikali

“Government Assets Management Information Systems - (GAMIS) ambao unatumika kutunza na kuchakata taarifa za mali za Taasisi zote za Umma hapa nchini’’, alisema Bw. Sendo.

Aliongeza kuwa, Wizara ya Fedha imefanya maboresho katika Sheria ya Fedha za Umma sura 348 pamoja na kuandaa Kanuni mahususi za Usimamizi wa Mali za Umma za mwaka 2024 ikiwa ni utekelezaji wa azma ya kuimarisha Mifumo ya Usimamizi wa Mali za Umma nchini.

Alisisitiza Maafisa Masuuli kuwa na mifumo thabiti ya uwajibikaji na kuwa mfano bora kwa wengine kwa kuzingatia misingi ya uadilifu, uwajibikaji, uwazi, na ufanisi katika kuonyesha kwamba mali za umma ni amana ambayo wamekabidhiwa kwa niaba ya Watanzania wote.

Aidha, taasisi hizo zimetakiwa kuhakikisha mali chakavu, sinzia, ziada na zilizokwisha muda wa matumizi zinaondoshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo ili kuimarisha ufanisi wa matumizi ya mali za umma.

Katika hatua nyingine Bw. Sendo amezitaka taasisi za umma kuwasilisha taarifa za ajali, hasara na upotevu wa mali kwa Mlipaji Mkuu wa Serikali ndani ya siku 30 tangu tukio litokee na mali zilizopata ajali au uharibifu zifanyiwe matengenezo mara baada ya kupata kibali husika.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akizungumza na Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha, alipowatembelea katika Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nanenane), yaliyofanyika katika Uwanja wa Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.



Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akiagana na Afisa Habari Mwandamizi, Wizara ya Fedha, Bw. Ramadhani Kissimba, mara baada ya kutembelea Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nanenane), yaliyofanyika katika Uwanja wa Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.(Picha na Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini, WF- Dodoma)


Na Janeth Raphael - MichuziTv

Serikali imesema Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi ‘Nanenane’ yamefungua fursa mpya za masoko ya nje kwa wakulima wa Tanzania, baada ya baadhi ya mazao ya kilimo kuanza kupata nafasi ya kuuzwa moja kwa moja katika soko la Sudan Kusini.

Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, amesema mafanikio hayo ni matokeo ya kuongezeka kwa ushiriki wa wadau wa ndani na nje ya nchi katika Maonesho ya Nanenane, ambayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwaunganisha wazalishaji na wanunuzi kutoka masoko mbalimbali.

“Maonesho haya yamekuwa jukwaa muhimu la kuwaunganisha wakulima na masoko. Ushiriki wa nchi mbalimbali umeleta manufaa makubwa na tayari mazao yetu yataweza kuuzwa moja kwa moja katika soko la Sudan Kusini,” alisema Chongolo.

Ameema Serikali imekuwa ikisisitiza maonesho hayo kufanyika kwa mtazamo wa kimataifa ili yaweze kuwasaidia wazalishaji wa Tanzania kupata masoko mapya, kuongeza mauzo ya bidhaa nje ya nchi na hatimaye kuongeza kipato cha wakulima.

Kwa mujibu wa Chongolo, jumla ya washiriki 1,668 kutoka ndani na nje ya nchi walishiriki katika Maonesho ya Nanenane mwaka huu, huku nchi zilizoshiriki zikijumuisha China, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Kenya, Urusi, Rwanda, Sudan Kusini, Burundi, Israel na Marekani.

Amesema pia wakulima, wavuvi na wadau wengine 286 waliokuwa waoneshaji walipata fursa ya kuonyesha bidhaa, ubunifu na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuongeza tija katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Chongolo amesema Serikali inaendelea kuboresha huduma za ugani kwa wakulima kupitia Wakala wa Taifa wa Huduma za Ugani, unaoshirikiana na sekretarieti za mikoa hadi ngazi ya vijiji ili kuhakikisha wakulima wanapata elimu na ushauri wa kitaalamu unaohitajika kuongeza uzalishaji na ubora wa mazao.

Katika kuwawezesha vijana kushiriki zaidi katika kilimo, alisema mpango wa Building a Better Tomorrow (BBT) umeendelea kutoa fursa kwa vijana kuingia katika shughuli za uzalishaji, ambapo ekari 126,180 zimeandaliwa katika halmashauri mbalimbali nchini kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumzia uzalishaji wa mazao ya mafuta, Chongolo alisema Serikali imeweka mkakati wa kuongeza uzalishaji wa ndani ili kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi. Alisema Tanzania kwa sasa huzalisha takribani tani 300,000 kwa mwaka, wakati mahitaji ya ndani yanafikia tani 700,000, hivyo nchi hulazimika kuagiza nje takribani tani 400,000 kwa mwaka.

Amesema hali hiyo inaifanya Tanzania kutumia zaidi ya dola milioni 200 kwa mwaka kuagiza mafuta kutoka nje, jambo lililosababisha Serikali kuweka mkakati maalumu wa kuongeza uzalishaji wa ndani na kuongeza kipato kwa wakulima.

Kwa kuanzia, Serikali imetambua Ruvuma, Njombe, Songwe na Rukwa kuwa miongoni mwa maeneo muhimu katika utekelezaji wa mkakati huo. Chongolo alisema hatua hiyo itaenda sambamba na ujenzi wa maghala ya kuhifadhi mazao ili kupunguza upotevu baada ya mavuno na kuwawezesha wakulima kupata thamani zaidi ya mazao yao.

Aidha, Serikali inaendelea kushirikiana na taasisi za fedha kuwawezesha vijana na wanawake wanaojihusisha na kilimo kupata mikopo pamoja na elimu ya kilimo na biashara kupitia mpango wa BBT.

Chongolo amesema Shilingi bilioni 300 zitatolewa kupitia benki mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wanawake wanaojihusisha na kilimo kupata mikopo. Benki hizo ni pamoja na CRDB, Stanbic Bank, NBC, TCB, Azania Bank, Benki ya Ushirika na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), ambayo ni mdhamini mkuu wa Maonesho ya Nanenane.

Kuhusu uendelezaji wa Maonesho ya Nanenane, Chongolo alisema Serikali inapendekeza maonesho hayo yaendelee kufanyika katika viwanja hivyo kutokana na uwezo wake wa kuhudumia washiriki na wananchi wengi, huku uzinduzi wake ukifanyika kwa kuzunguka katika kanda mbalimbali nchini.

Amesema utaratibu huo utasaidia kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapa fursa ya kushiriki katika maonesho hayo, huku wakulima na wadau wengine wakipata nafasi pana zaidi ya kuonyesha bidhaa zao, kutafuta masoko na kuunganika na fursa za biashara ndani na nje ya nchi.


Na Mwandishi Wetu

JAMII ya Wandondi na Wandwewe, imetoa mwito wa kitaifa na kimataifa kwa watu wote wenye nia njema kuungana katika Dua Maalum kwa ajili ya Amani, Umoja, Maridhiano, Mshikamano na Ulinzi wa Maisha ya Binadamu.

Dua hiyo ni mwito wa pamoja unaolenga kuwakutanisha watu wa imani, mila, tamaduni na mitazamo mbalimbali katika kusimama kwa pamoja kutetea amani, utu, uhai, mshikamano na heshima kwa mwanadamu, bila kujali tofauti za dini, kabila, rangi, taifa, utamaduni, itikadi au hali ya kijamii.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Chifu Felix G. L. Mfunda, kwa niaba ya jamii ya Wandondi na Wandwewe amesema dua hiyo itafanyika  Agosti 12, 2026,  ambapo Misa Maalumu ya Kikatoliki itafanyika katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Mhangazi, Parokia ya Kitanda, Namtumbo, Ruvuma. huku akitoa  mwito wa amani na maridhiano.

Aidha, kuanzia jioni ya Agosti 13 hadi mchana wa Agosti 14, 2026, kutafanyika dua, na shughuli za jadi zitakazoambatana na ngoma na sanaa mbalimbali za asili za Wandwele na Wandondi.

Jamii mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma, zikiwemo Makumbo, Lizombe na Makiwa, zinatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo zinazolenga kuenzi urithi wa tamaduni, kuimarisha undugu na mshikamano, pamoja na kukuza amani kati ya jamii.

Mfululizo huo utakamilishwa Agosti 16, 2026, kwa Dua Maalumu ya Kiislamu itakayofanyika jioni kwa ajili ya kuiombea Tanzania, Afrika na dunia nzima.
Ambapo  amesema Dunia ya leo inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo migogoro, vita, chuki, migawanyiko ya kijamii, changamoto za kiuchumi, ukosefu wa usawa na athari za mabadiliko ya tabianchi.

“Katika mazingira haya, tunapaswa kutambua kwamba amani si wajibu wa Serikali pekee; ni wajibu wa kila mwanadamu.Tunatoa mwito kwa viongozi wa kitaifa na kimataifa, viongozi wa dini, viongozi wa kimila, wasomi, vijana, wanawake, mashirika ya kiraia na wananchi wote kutumia nafasi zao kujenga madaraja ya maelewano badala ya kuta za migawanyiko.

“Tunasisitiza umuhimu wa mazungumzo, kusikilizana, kusameheana, kuheshimiana na kutafuta suluhu za amani katika kila tofauti inayojitokeza.”

Aidha amesema ulinzi wa maisha ni wajibu wa pamoja akifafanua maisha ya mwanadamu ni tunu kubwa na hayapaswi kuwekwa rehani kwa sababu ya tofauti za kisiasa, kidini, kikabila, kiuchumi, kijamii au kiitikadi.

Ameongeza kwa msingi huo, wanatoa mwito wa kuheshimiwa kwa utu wa binadamu, haki ya kuishi, usalama wa raia na ulinzi wa watoto, wanawake, wazee na makundi yote yaliyo katika mazingira hatarishi.

“Tunasisitiza tofauti zetu zisigeuke kuwa sababu ya kupoteza maisha ya watu.Kila jamii ina wajibu wa kulinda maisha na kujenga mazingira ambayo kila mwanadamu anaweza kuishi kwa usalama.

Pia amesema kuhusu amani, afya na ulinzi wa mazingira ni kwamba amani ya kweli haiwezi kutenganishwa na afya ya jamii, usalama wa chakula, maji safi, mazingira salama na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

“Uharibifu wa mazingira, ukataji wa misitu, uharibifu wa vyanzo vya maji, upotevu wa bayoanuai na athari za mabadiliko ya tabianchi vinaweza kuongeza changamoto za kijamii na kiuchumi na kuhatarisha maisha ya watu.

“Kwa hiyo, tunatoa mwito wa kuunganisha juhudi za amani, afya, mazingira na maendeleo endelevu kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Akieleza zaidi amesema katika dua kwa Watanzania ,Afrika na Dunia amefafanua Tanzania iendelee kuwa taifa la amani, umoja, mshikamano na utulivu na kwa Afrika ipate amani na utulivu wa kudumu.

Pia migogoro na vita duniani zipungue na hatimaye kumalizika na kuongeza viongozi wapate hekima, busara, uadilifu na moyo wa kuhudumia watu.Vijana wapate fursa za elimu, ajira, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo.

Kwa watoto walindwe dhidi ya ukatili, unyanyasaji na mazingira yanayohatarisha maisha yao. Wanawake, wazee na makundi yaliyo katika mazingira magumu walindwe na kuheshimiwa.Wagonjwa na wote wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali wapate faraja, matumaini na huduma stahiki na mazingira.

Kuhusu ujumbe kwa Watanzania amesema wanawakumbusha Umoja wetu ni nguvu yetu, amani yetu ni utajiri wetu, na maisha ya kila Mtanzania ni sehemu ya thamani ya Taifa letu.

“Tunapaswa kukataa chuki, uchochezi, ubaguzi, vurugu na lugha zinazogawa jamii. Badala yake, tujenge utamaduni wa kusikilizana, kuheshimiana, kusameheana, kusaidiana na kutatua tofauti zetu kwa njia za amani.

“Tanzania yenye amani na mshikamano ni msingi muhimu wa maendeleo ya watu wake na mchango mkubwa kwa amani ya Afrika na dunia.”

 


Na Munir Shemweta, Itilima


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameitaka mikoa na wilaya nchini kuhakikisha zinatenga na kuandaa maeneo maalumu yatakayotumika kwa ajili ya kuanzisha kongani za viwanda.

Amesema upangaji mzuri wa matumizi ya ardhi ni muhimu katika kuvutia wawekezaji kwa kuwa mwekezaji anahitaji eneo lililotengwa na kutambuliwa kwa matumizi husika kabla ya kuanzisha shughuli zake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati alikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa shule ya awali na msingi katika Kitongoji cha Mwankola, Kata ya Lagangabilili pamoja na kusikiliza kero za wananchi katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026 Dkt.  Akwilapo amesema hatua hiyo pia inalenga kuzuia migogoro ya matumizi ya ardhi kati ya makazi, shughuli za kilimo, viwanda na matumizi mengine yanayohitaji maeneo maalumu.

Aidha, Waziri huyo wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameeleza kuwa,  Wizara yake   imejipanga kuimarisha usimamizi wa sekta hiyo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na maeneo yao yanasimamiwa kwa kuzingatia sheria.

Amewataka wananchi wa Itilima kufuata sheria, kanuni na taratibu zinazohusu umiliki na matumizi ya ardhi ili kupunguza migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na migogoro ya ardhi.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha ameeleza kuwa, mkoa wa Simiyu hususan wilaya ya Itilima wanatambua umuhimu wa ardhi hasa katika kumilikisha wananchi, taasisi na vijiji lengo likiwa kuepuka migogoro ya ardhi.

Wakiwasilisha kero yao mbele ya Waziri wa Ardhi, wananchi wa Itilima wameiomba serikali kuwawekea uzio utakaowasaidia kuepukana na uvamizi wa mara kwa mara wa tembo wanaotoka hifadhini kwenda katika maeneo yao.

‘’Tunashukuru kwa ahadi ya kuwekewa uzio wa umeme kwa ajili ya kuzuia tembo kuvamia maeneo yetu ila tunaomba ahadi hiyo iwe ya kweli’. Amesema mkazi wa Itilima’

Hata hivyo, Mkuu wa mkoa wa Simiyu amewaambia wananchi hao kuwa serikali tayari imejipanga kuhakikisha inajenga uzio wa umeme kwa ajili ya kuzuia tembo kuingia katika maeneo ya wananchi.

‘’Niwaase wananchi kutoenda katika maeneo ya hifadhi kwa ajili ya kufanya uharibifu na mtoe ushirikiano wa kulinda uzio wa umeme pale utakaojengwa’’. Amesema

Mkuu wa wilaya ya Itilima Bi. Anna Gidarya amesema halmashauri ya wilaya ya Itilima ina lengo la kuandaa hati milki za viwanja vyote 1,604 vilivyopangwa ambapo hadi kufikia juni 2026 jumla ya hati milki 506 zimeandaliwa na kusajiliwa.

‘’Hati za viwanja vilivyosalia havijamilkishwa kwa vile wamiliki hawajalipia gharama za uandaaji wa milki hizo’’. Amesema Bi. Gidarya.

Katika hatua nyingine, Dkt. Akwilapo amewataka wananchi wa Wilaya ya Itilima kuendelea kulinda amani na utulivu uliopo nchini kwa kuwa ndiyo msingi wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

Amesema, hakuna uwekezaji unaoweza kufanyika kwa ufanisi katika mazingira yasiyo na amani, hivyo ni jukumu la wananchi kuendelea kuthamini na kulinda utulivu uliopo Tanzania.

Ameeleza kuwa maendeleo katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu, viwanda, biashara na miundombinu, yanahitaji mazingira tulivu yanayowawezesha wananchi na wawekezaji kufanya shughuli zao bila hofu.

“Uwekezaji wowote unategemea amani na utulivu na maendeleo yatakayopatikana yatatokana na amani. Hivyo amani inaiweka nchi katika nafasi nzuri ya kupokea wawekezaji,” amesema Dkt. Akwilapo.

Amesema uwepo wa amani unaifanya nchi kuwa na mazingira yanayovutia miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo baadaye inaweza kutoa ajira, kuongeza mapato na kuboresha maisha ya wananchi.

Ziara ya Dkt Akwilapo wilayani Simiyu ni sehemu ya mpango wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuwapeleka mawaziri katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali iliyoahidiwa kwa wananchi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akiomba kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akilakiwa na wananchi wa Itilima alipowasili Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani itilima mkoa wa Simiyu kusikiliza kero za wananchi wakati wa ziara yake mkoani humo.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akikabidhiwa Zawadi ya kuku na wananchi wa Kijiji cha Simiyu kata ya Migato mara baada ya kuzungumza nao wilayani Itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akipata maelezo ya mradi wa ujenzi wa Daraja katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilaya ya Itilima mara baada ya kusikiliza kero za wananchi tarehe 7 Agosti 2026. Kulia kwa Dkt Akwilapo ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu mhe. Anamringi Macha na kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Itilima Bi. Anna Gidarya.

Sehemu ya wananchi wa Itilima waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo uliofanyika katika Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilayani Itilima mkoa wa Simiyu tarehe 7 Agosti 2026.
Muonekano wa Daraja lililopo Kijiji cha Simiyu kata ya Migato wilaya ya Itilima.(PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI) 






Rais Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan ahutubia kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nanenane Kitaifa katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma









Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea banda la Kampuni ya pembejeo za kilimo ya Betaren ya Urusi katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.










Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Trekta baada ya uzinduzi wa magari kwa ajili ya Wakala ya Taifa ya Huduma za Ugani (NAESA) na Matrekta ya vyama vya Ushirika kwenye Maonesho ya Kilimo ya Nanenane, Kitaifa katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Kilimo Mhe. Daniel Chongolo wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Nanenane ambayo Kitaifa yanafanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.





















Top News