Na Janeth Raphael MichuziTv – Dodoma
Mashirika yasiyo ya kiserikali (AZAKI) yameiomba Serikali kupitia Bunge kuhakikisha asilimia tatu ya mapato ya halmashauri nchini zinatengwa mahsusi kwa ajili ya huduma za ulinzi na usalama wa mtoto, hatua inayolenga kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia na malezi yasiyo salama kwa watoto.
Wito huo umetolewa katika warsha ya wabunge kuhusu masuala ya ulinzi wa mtoto iliyoandaliwa na Shirika la World Vision Tanzania, ambapo Kamati za Kudumu za Bunge za PAC, LAAC pamoja na Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii zilishiriki kupokea mapendekezo kutoka kwa asasi za kiraia ili kuyafikisha bungeni.
Akizungumza katika warsha hiyo, mwakilishi wa asasi za kiraia, Ombeni Kimaro, alisema bado kuna ongezeko la vitendo vya ukatili dhidi ya watoto katika maeneo mbalimbali nchini, hali inayohitaji hatua za haraka za kisera na kifedha ili kukabiliana nayo.
Amesema ipo haja ya Serikali kuhakikisha fedha hizo zinaingizwa katika bajeti za taifa pamoja na halmashauri ili kuwezesha utekelezaji wa mipango ya ulinzi wa mtoto na huduma za kijamii zinazohusiana na ustawi wa watoto.
“Tunataka kuona suala la ulinzi wa mtoto linapewa uzito wa kitaifa. Halmashauri zitenge fedha maalum kusaidia mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia na kuhakikisha watoto wanakuwa katika mazingira salama,” alisema Kimaro.
Aidha, alisema kupungua kwa misaada kutoka kwa wafadhili wa kimataifa kwa mashirika yanayojihusisha na ulinzi wa mtoto kunapaswa kuwa chachu kwa Serikali kuongeza uwekezaji wa ndani katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Kwa mujibu wa Kimaro, kutotengwa kwa fedha hizo kunaweza kuchangia kuongezeka kwa changamoto za malezi, maadili na usalama wa watoto pamoja na vijana nchini.
“Bila kufanya hivyo tunaweza kujikuta tunazalisha kizazi kisicho salama na kisicho na maadili. Ulinzi wa mtoto ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa taifa la baadaye,” alisisitiza.
Akizungumza kwa niaba ya wabunge, Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Devotha Minja, alisema kamati hiyo ipo tayari kulisemea suala hilo bungeni ili kuhakikisha mapendekezo hayo yanafanyiwa kazi na fedha zinatengwa katika halmashauri zote nchini.
Kwa upande wake, mwakilishi wa Kamati ya LAAC, Josephine Kapone, alisema kamati hiyo itashirikiana na kamati nyingine kuhakikisha suala la ulinzi wa mtoto linapata usimamizi na utekelezaji unaostahili.
Naye mwakilishi wa Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Kafti Kafti, alisema kamati yao itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mapendekezo hayo kwa kuwa ndiyo yenye dhamana ya moja kwa moja katika masuala ya ustawi wa mtoto.
Mtafiti na mchambuzi kutoka HakiElimu, Joshua Mwakalikamo, alisema tafiti mbalimbali zimekuwa zikionesha umuhimu wa kuwekeza katika ulinzi wa mtoto ili kujenga jamii salama na yenye maadili bora.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mipango na Udhibiti Ubora wa World Vision Tanzania, AZAKI ZAITAKA SERIKALI KUTENGA 3% KWA ULINZI WA MTOTO.




.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)






.jpeg)























.jpeg)






.jpeg)

