Wananchi  wakipata elimu katika Banda la VETA  aliyetembelea banda la kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Wananchi  wakipata elimu katika Banda la VETA  aliyetembelea banda la kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Korogwe Mkondo wa Amali Katika Fani ya Upishi  wakiwa na Bidhaa zao walizitengeneza katika Banda la TEA  kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano Bi.Julitha Mlay akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano Bi.Julitha Mlay akizungumza na Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Unesco  Bi.Julitha Mlay akiwaonesha namna ya  fursa za Tume hiyo kwa Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Unesco  Bi.Julitha Mlay akiwa katika picha  ya pamoja na  Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Usagara  wakati walipotembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Umma na Mawasiliano  Bi.Julitha Mlay akizungumza na mwananchi aliyetembelea banda la Tume ya Taifa ya UNESCO kwenye maonesho ya wiki ya elimu MAKISATU yanayoendelea katika viwanja vya shule ya Sekondari Usagara jijini Tanga.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimkabidhi Tuzo pamoja na Cheti, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Deogratius Kwiyukwa, kama Ishara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kushiriki kukuza na kuchochea shughuli za uchuki jumuishi na shukrani kwa ushiriki na kuwa tayari kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kwa kumtengenezea mazingira bora ya uwajibikaji kwa Taifa lake, katika Kilele cha Tamasha la Kizimkazi 2026, lililohitimishwa mwishoni wa Juma lililopita.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha, Kizimkazi, Zanzibar)

Na Benny Mwaipaja, Kizimkazi-Zanzibar
SAFARI ya mageuzi ya kiuchumi kuelekea Dira ya Taifa 2050 imeanza kushika kasi, huku mijadala kuhusu vichocheo vya uchumi ikiendelea kupewa uzito mkubwa nchini.

Miongoni mwa matukio yaliyoibua mjadala huo ni Tamasha la Kizimkazi 2026, lililofanyika kusini mwa Unguja na kukutanisha viongozi wakuu wa serikali, taasisi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Tamasha hilo lilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel John Nchimbi, pamoja na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, sambamba na viongozi wengine wa serikali akiwemo Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), vyama vya siasa, taasisi za umma na binafsi, pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mbali na kuwa jukwaa la kukutanisha wadau, tamasha hilo pia lilikuwa sehemu muhimu ya mdahalo wa kitaifa kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, ambapo viongozi waandamizi walitoa maoni yao kuhusu umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi kama sehemu ya maendeleo endelevu ya taifa.

Ajenda ya nishati safi inaenda sambamba na nguzo ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, ambayo ni sehemu ya msingi ya Dira 2050.

Kupitia nguzo hiyo, Tanzania inalenga kuwa kinara wa kimataifa katika uhifadhi wa mazingira kwa kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali za asili na kuimarisha uwezo wa taifa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Miongoni mwa taasisi zilizojitokeza kwa nguvu katika tamasha hilo ni Benki ya Maendeleo TIB, iliyoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Bw. Deogratius Kwiyukwa. TIB ni benki ya maendeleo ya Serikali iliyoanzishwa mahsusi kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini kupitia utafutaji wa mitaji, uandaaji wa miradi ili iweze kuvutia uwekezaji, pamoja na usimamizi wa mifuko ya maendeleo kwa niaba ya serikali na sekta binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari kando ya tamasha hilo, Bw. Kwiyukwa alisema
Benki ya Maendeleo ya Tanzania TIB, imejipanga kuongeza ufadhili wa miradi ya nishati safi nchini, kama sehemu ya jitihada za Taifa za kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Amesema benki hiyo imetenga fedha maalum za kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa miradi ya nishati mbadala ikiwemo ya jua, upepo, gesi asilia na nishati ya maji.

“Tunafahamu kuwa nishati safi ndio mkombozi wa viwanda, kilimo na nyumba za Watanzania. Kupitia ufadhili huu tunalenga kupunguza utegemezi wa nishati chafu na kuchochea uchumi wa kijani,” amesema Bw. Kwiyukwa.

Kwa mujibu wa TIB, hatua hii pia inalenga kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kushiriki katika miradi mikubwa ya miundombinu ya nishati, ambayo itasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ajira kwa vijana.

“Benki ya Maendeleo ya TIB imekuwa na mchango mkubwa hapa nchini katika kuleta mabadiliko chanya katika ukuaji wa sekta mbalimbali. Kupitia tamasha hili la Kizimkazi, tunaungana na Mheshimiwa Rais na wadau wengine kupambanua na kuonesha mchango wa sekta zote kufikia malengo ya Dira,” alisema.

Alieleza kuwa benki hiyo imejikita katika sekta mbalimbali muhimu ikiwemo miundombinu, nishati, utalii, uchumi wa buluu, vijana na wanawake, pamoja na utunzaji wa mazingira.

Kwa mujibu wa Bw. Kwiyukwa, TIB pia inasimamia mifuko mbalimbali ya maendeleo kwa niaba ya serikali na taasisi nyingine, ikiwemo mifuko ya maji, umeme vijijini, na nishati safi, katika Tanzania Bara na Zanzibar.

Alisema dhamira kuu ni kufikisha maendeleo kwa wananchi na kupunguza vihatarishi katika maeneo ambayo benki za biashara hushindwa kuyafikia.

Katika hatua nyingine, TIB kupitia kampuni yake tanzu ya TIB Rasilimali, imeendelea kufungua njia mbadala za upatikanaji na ukuzaji wa mitaji. Kampuni hiyo ni miongoni mwa mawakala wakubwa wa soko la hisa la Dar es Salaam, ikiwa na jukumu la kuuza na kununua hisa kwa niaba ya taasisi na watu binafsi. Pia hutoa huduma za elimu ya fedha, uwekezaji, pamoja na uwakala wa bima.

Bw. Kwiyukwa alisema kupitia TIB Rasilimali, taasisi na wananchi wamekuwa wakihamasishwa kutambua njia mbadala za kukuza mitaji yao bila kutegemea fedha za Serikali pekee.

Alibainisha kuwa Ofisi za Dar es Salaam na majukwaa ya mitandaoni zimekuwa zikiendesha madarasa maalumu ya kila wiki, hasa kwa vijana, ili kuwapa uelewa kuhusu njia salama na za uhakika za uwekezaji.

“Jitihada hizo zinaunga mkono malengo makubwa ya Dira 2050, yanayolenga kujenga uchumi wa thamani ya dola trilioni moja, kuongeza wastani wa kipato cha Mtanzania hadi dola 7,000 kwa mwaka, pamoja na kuhakikisha sekta binafsi inachangia kwa kiwango kikubwa zaidi katika ukuaji wa uchumi wa Taifa” alisema Bw. Kwiyukwa.

Sambamba na ushiriki wake katika tamasha hilo, Benki ya Maendeleo TIB pia ilitunukiwa tuzo na cheti kutoka kwa Mheshimiwa Rais kama ishara ya kutambua mchango wake na utayari wake wa kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kiuchumi kupitia maendeleo jumuishi.

Akihitimisha, Bw. Kwiyukwa aliipongeza Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuandaa Tamasha la Kizimkazi, akieleza kuwa limefungua fursa pana kwa Watanzania kujadili masuala muhimu ya maendeleo. Pia aliahidi kuwa TIB itaendelea kushiriki katika matamasha na majukwaa mengine yenye lengo la kuchochea maendeleo ya Taifa.

Sambamba na hayo, katika Tamasha hilo la Kizimkazi 2026, Benki ya Maendeleo TIB ilitunikiwa tuzo pamoja na cheti na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama Ishara ya kutambua mchango wa benki hiyo katika kushiriki kukuza na kuchochea shughuli za uchuki jumuishi na shukrani kwa ushiriki na kuwa tayari kuchochea maono ya Taifa ya kumkomboa mwananchi kwa kumtengenezea mazingira bora ya uwajibikaji kwa taifa lake.

Kwa ujumla, ushiriki wa TIB katika Tamasha la Kizimkazi 2026 umeonesha wazi nafasi ya taasisi za maendeleo katika kusukuma mbele ajenda ya nishati safi, uhifadhi wa mazingira na uwezeshaji wa kiuchumi, yote ikiwa ni sehemu ya safari ya Tanzania kuelekea Dira 2050.

Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb), Ridhiwani Kikwete, amezitaka shule za msingi na sekondari kuwa na karakana zitakazokuwa chemchemi za ubunifu kwa vijana, huku akisisitiza kazi zitakazobuniwa zisajiliwe ili wabunifu wanufaike nazo.

Ridhiwani amesema usajili huo utawasaidia vijana kumiliki kazi zao na kuzitumia kama fursa za kiuchumi, badala ya watu wengine kuchukua mawazo yao na kujinufaisha huku wabunifu wakibaki bila manufaa.

Amesema hayo akimwakilisha Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Baobab, iliyopo Mapinga, Bagamoyo mkoani Pwani.

Mkurugenzi wa Baobab, Shani Swai, amesema kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi na wanafunzi 3,270 wamehitimu kidato cha nne ambapo asilimia 95 wameendelea na sekondari na vyuo vya ufundi. 

Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda .

Makamu wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (wa tatu kushoto), akiongoza washiriki wa Mashindano ya CRDB Bank International Marathon leo katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam. Kijitonyama, Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam. Mashindano ya CRDB Bank International Marathon yamegeuka kutoka kuwa tukio la michezo na kuwa mpango mkubwa wa kuleta athari chanya katika jamii, baada ya kukusanya zaidi ya Sh5 bilioni tangu yalipoanzishwa mwaka 2020, fedha ambazo zimeelekezwa katika kuboresha huduma za afya, kuwawezesha vijana na maendeleo ya jamii nchini Tanzania.

Athari hizo zilibainika. wakati toleo la saba la marathon hiyo lilipohitimishwa katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam, likiwakutanisha washiriki takribani 17,000 chini ya kaulimbiu “Kasi Isambazayo Tabasamu.”
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la CRDB Bank, Dk Abdulmajid Nsekela, alisema fedha zilizopatikana kupitia marathon hiyo zimeleta msaada unaoonekana kwa makundi yenye uhitaji, hususan watoto wenye matatizo ya moyo na wanawake wenye mimba hatarishi.

Alisema zaidi ya watoto 400 wenye matatizo ya moyo wamefanyiwa upasuaji, huku zaidi ya wanawake 240 wenye mimba hatarishi wakipatiwa huduma za afya na kujifungua salama.

“Kila mchango unawakilisha mtoto aliyepewa nafasi nyingine ya kuishi, mama aliyepata huduma salama zaidi wakati wa kujifungua na familia ambazo maisha yao yamebadilika,” alisema Dk Nsekela.
Athari katika sekta ya afya pia imepanuliwa kupitia ushirikiano na taasisi mbalimbali. Zaidi ya watoto 1,000 wamepatiwa matibabu ya moyo kupitia msaada uliowasilishwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), huku wanawake zaidi ya 450 wenye mimba hatarishi wakinufaika kupitia CCBRT.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road nayo imenufaika kupitia ujenzi wa kituo cha huduma kwa wateja kwa njia ya simu, hatua iliyosaidia kuboresha upatikanaji wa msaada kwa wagonjwa wa saratani.

Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu Dk Mwigulu Lameck Nchemba, Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, alisema marathon hiyo imevuka mipaka ya michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi.

“CRDB Bank International Marathon imevuka kuwa tukio la michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi, alisema Abdulla.

Alisema mpango huo unaonyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wananchi katika kukabiliana na changamoto za kijamii.

Abdulla aliipongeza CRDB Bank Foundation kwa kutumia michezo kukusanya rasilimali kwa ajili ya shughuli za kijamii, huku ikiendelea kupanua programu zake za vijana katika ujasiriamali, ubunifu, mazingira na maendeleo ya vipaji.

Kupitia programu zake kwa ujumla, taasisi hiyo inasema imewafikia zaidi ya wajasiriamali milioni tatu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kutoa zaidi ya Sh30 bilioni kama mtaji wa kuwawezesha.
Hatua hizo ni pamoja na zaidi ya Sh4.2 bilioni zilizotolewa kupitia mpango wa mikopo wa asilimia 10 wa halmashauri katika awamu yake ya kwanza kwa halmashauri tano, huku zaidi ya Sh3.5 bilioni zikitolewa kwa vijana kupitia changamoto ya Vijana Uchumi.

Mfuko wa Samia Commercialization Fund, unaotekelezwa kwa ushirikiano na COSTECH, pia umepokea Sh4.6 bilioni kusaidia vijana wabunifu kubadili mawazo yao kuwa biashara zinazoweza kujiendesha.

Aidha, Sh8 bilioni zimetengwa kupitia SIDO na TIRDO kwa ajili ya elimu ya fedha, mafunzo ya ujasiriamali, maendeleo ya biashara, huduma za ushauri wa kitaalamu na mtaji.

Sh5 bilioni nyingine zimetengwa kupitia programu za Go Green na IMBEJU kuwawezesha vijana na wanawake wanaoendesha biashara zinazozingatia mazingira, huku zaidi ya wanufaika 1,000 tayari wakiwa wamechaguliwa.
Abdulla alisema programu kama FursaHub, Imbeju UDSM Start-Up Challenge, Imbeju Ndondo Cup na Imbeju Zuchu MasterClass zimeendelea kupanua fursa kwa vijana wa Tanzania.

Pia aliipongeza taasisi hiyo kwa kuunganisha marathon na tamasha la IMBEJU Sauti Moja Concert, lililofanyika Dar es Salaam Ijumaa na kuvutia zaidi ya watu 15,000.

Tamasha hilo lilishirikisha wasanii wa kimataifa akiwemo mwimbaji wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, msanii wa Nigeria BNXN na DJ wa Afrika Kusini Kabza De Small, pamoja na wasanii wa Tanzania. Sehemu ya mapato ya tamasha hilo itaelekezwa katika kuwawezesha vijana, hususan katika sekta ya ubunifu.

Abdulla alisema mchanganyiko wa michezo na burudani unaweza kusaidia Tanzania kujenga kalenda pana ya matukio makubwa, huku ukitengeneza ajira, kukuza utalii na kuzalisha fursa za uwekezaji.
Alisema michezo si burudani pekee bali ni sehemu muhimu ya uchumi, akitaja maandalizi ya Tanzania kuandaa kwa pamoja Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 na Kenya na Uganda.

Pia alisisitiza umuhimu wa Imbeju Ndondo Cup katika kugundua na kukuza vipaji vya soka, akiwataka waandaaji kuendelea kulinda dhima yake ya msingi katika ngazi za chini huku wakiimarisha mifumo ya maendeleo ya vipaji.

Abdulla alisema Serikali imetenga Sh519.6 bilioni kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika mwaka wa fedha 2026/27, huku vipaumbele vikijumuisha miundombinu ya michezo, maandalizi ya AFCON 2027, maendeleo ya vipaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi.
Aliwahakikishia wadau wa sekta binafsi kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili Watanzania wanufaike na fursa zilizopo katika michezo na sekta ya ubunifu.

Kwa zaidi ya Sh5 bilioni zilizokusanywa kupitia marathon hiyo na programu nyingine za CRDB Foundation zinazohusisha mabilioni ya shilingi, tukio hilo linazidi kuwa nyenzo ya kubadili ushiriki katika michezo kuwa matokeo yanayopimika katika jamii na uchumi.

Abdulla aliwapongeza viongozi wa CRDB Bank, akiwemo Mwenyekiti wa Bodi Prof Neema Mori, Dk Nsekela, Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank Foundation CPA (T) Oswald Urassa na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation, Tully Esther Mwambapa, kwa mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Wakenya watawala CRDB Marathon

Wanariadha kutoka Kenya walitawala CRDB Marathon 2026 baada ya kushinda nafasi nyingi za juu katika mashindano makuu.

Katika mbio za kilomita 42 kwa wanaume, Abraham Kiptum alishika nafasi ya kwanza kwa muda wa saa 2:15:33, akifuatiwa na Mkenya mwenzake James Mwangi aliyemaliza kwa saa 2:16:11. Mtanzania Marco Sylvester alishika nafasi ya tatu kwa saa 2:16:33.

Kwa upande wa wanawake katika kilomita 42, Joyce Kemuma alishinda kwa saa 2:35:26, huku Mkenya Jacinta Chepkoech akimaliza wa pili kwa saa 2:36:57 na Mkenya mwingine Jane Chelagant akishika nafasi ya tatu kwa saa 2:39:18.
Washindi wa kilomita 42 kwa wanaume na wanawake walipata Sh12 milioni kila mmoja, washindi wa pili Sh5 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh2 milioni.

Katika nusu marathon, Mkenya Simon Kelenzyoki alishinda mbio za wanaume kwa saa 1:15:33, akifuatiwa na Mtanzania Ebei Francis aliyemaliza kwa saa 1:15:52, huku Mtanzania mwingine Boay Dawi akiwa wa tatu kwa saa 1:16:07.

Kwa wanawake, Mkenya Rebecca Chepkwemoi alishinda nusu marathon kwa saa 1:12:42, akifuatiwa na Mtanzania Failuna Matanga aliyemaliza kwa saa 1:13:21 na Mkenya Irine Mkungu aliyeshika nafasi ya tatu kwa saa 1:13:23.
Washindi wa nusu marathon walipata Sh6 milioni, washindi wa pili Sh2 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh1 milioni.

Wanariadha wa Tanzania walitawala mbio za kilomita 10 kwa wanaume, huku Jumanne Ngoya akishinda kwa muda wa dakika 29:53. Benard Geay alimaliza wa pili kwa dakika 29:58, huku Shedrack Hasani akiwa wa tatu kwa dakika 30:06.

Tanzania pia ilitwaa nafasi zote tatu za juu katika mbio za wanawake za kilomita 10, ambapo Transfora Mussa alishinda kwa dakika 34:00, Anna Dolomongo akimaliza wa pili kwa dakika 34:18 na Agnes Mwanghui akiwa wa tatu kwa dakika 34:45.

Washindi wa kilomita 10 walipata Sh2 milioni, washindi wa pili Sh500,000 na waliomaliza nafasi ya tatu Sh300,000.














Top News