Wito huo umetolewa na Diwani wa Kata ya Kwembe katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Kawina Hadji Konde, alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya saba ya Shule ya Awali na Msingi ya Mwendo, iliyopo Kibamba kwa Mangi, wilayani Ubungo.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyowakutanisha wazazi, walimu, wanafunzi na wadau mbalimbali wa elimu, Bw. Konde alisema shule binafsi na zile za Serikali zina nafasi kubwa ya kujenga mifumo ya ushirikiano katika maeneo mbalimbali, ikiwemo elimu, michezo, sanaa, utamaduni na shughuli za kijamii, kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuinua viwango vya elimu kwa manufaa ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.
Alisema ushindani kati ya shule unapaswa kujengwa katika misingi chanya inayochochea ubunifu, ubora wa ufundishaji na ujifunzaji, badala ya kuwa kikwazo cha ushirikiano kati ya taasisi hizo.
“Kwenye hili niwapongeze sana uongozi wa Shule ya Mwendo kupitia Mkuu wa Shule, Mwalimu Adolf Nyabarimba, ambaye kwa kweli amekuwa mdau mkubwa na mzuri katika masuala mbalimbali yanayohusu Kata yetu ya Kwembe. Amekuwa akishiriki vikao na mikutano mbalimbali inayohusiana na kata yetu kila anapohitajika na amekuwa akitoa ushirikiano wakati wote. Huu ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wa shule nyingine, kwa sababu shule ni sehemu ya jamii,” alisema Bw. Konde.
Aidha, Bw. Konde aliwasisitiza wazazi kuongeza ushirikiano na walimu katika malezi ya watoto, akieleza kuwa elimu bora haiishii darasani pekee, bali inahitaji pia misingi imara ya maadili, uwajibikaji, uzalendo na malezi yenye mwelekeo chanya.
Aliwataka wazazi na walezi kuwa karibu zaidi na watoto wao, kuwafuatilia na kuwasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii zinazoweza kuathiri ustawi wao wa kimwili na kisaikolojia, huku akisisitiza umuhimu wa kujenga mazingira salama kwa watoto ndani na nje ya shule.
Kwa upande wake, uongozi wa Shule ya Mwendo ulieleza umuhimu wa ushirikiano kati ya shule, wazazi na jamii katika kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu inayowaandaa kuwa raia wenye maarifa, nidhamu, ubunifu na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
Mahafali hayo yalipambwa na burudani na maonesho mbalimbali yaliyoandaliwa na wanafunzi, yakiwemo muziki, sanaa, utamaduni, ukakamavu pamoja na maonesho ya kitaaluma, yaliyowapa wazazi na wageni fursa ya kushuhudia vipaji na uwezo wa wanafunzi nje ya masomo ya darasani.
Diwani wa Kata ya Kwembe, Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Kawina Hadji Konde (wa pili kulia), akimkabidhi Manal Salum, mwanafunzi wa darasa la saba, zawadi ya Mwanafunzi Bora wa Kike katika Shule ya Awali na Msingi ya Mwendo, iliyopo Kibamba kwa Mangi, Wilaya ya Ubungo, wakati wa hafla ya mahafali ya saba ya shule hiyo, yaliyofanyika mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia tukio hilo ni viongozi na walimu wa shule hiyo.
Diwani wa Kata ya Kwembe, Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Kawina Hadji Konde (wa tatu kulia), akimkabidhi Olivia Kassim, mwanafunzi wa elimu ya awali, cheti cha kuhitimu elimu hiyo katika Shule ya Awali na Msingi ya Mwendo, iliyopo Kibamba kwa Mangi, Wilaya ya Ubungo, wakati wa hafla ya mahafali ya saba ya shule hiyo, yaliyofanyika mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia tukio hilo ni viongozi na walimu wa shule hiyo.
Mahafali hayo yalipambwa na burudani na maonesho mbalimbali yaliyoandaliwa na wanafunzi, yakiwemo muziki, sanaa, utamaduni, ukakamavu pamoja na maonesho ya kitaaluma, yaliyowapa wazazi na wageni fursa ya kushuhudia vipaji na uwezo wa wanafunzi nje ya masomo ya darasani.
Katika mahafali hayo, walimu, wazazi na wanafunzi walipata wasaa wa kucheza pamoja ili kujipongeza kwa hatua hiyo muhimu.













.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)


