Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb), Ridhiwani Kikwete, amezitaka shule za msingi na sekondari kuwa na karakana zitakazokuwa chemchemi za ubunifu kwa vijana, huku akisisitiza kazi zitakazobuniwa zisajiliwe ili wabunifu wanufaike nazo.

Ridhiwani amesema usajili huo utawasaidia vijana kumiliki kazi zao na kuzitumia kama fursa za kiuchumi, badala ya watu wengine kuchukua mawazo yao na kujinufaisha huku wabunifu wakibaki bila manufaa.

Amesema hayo akimwakilisha Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Baobab, iliyopo Mapinga, Bagamoyo mkoani Pwani.

Mkurugenzi wa Baobab, Shani Swai, amesema kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi na wanafunzi 3,270 wamehitimu kidato cha nne ambapo asilimia 95 wameendelea na sekondari na vyuo vya ufundi. 

Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda .

Makamu wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (wa tatu kushoto), akiongoza washiriki wa Mashindano ya CRDB Bank International Marathon leo katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam. Kijitonyama, Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam. Mashindano ya CRDB Bank International Marathon yamegeuka kutoka kuwa tukio la michezo na kuwa mpango mkubwa wa kuleta athari chanya katika jamii, baada ya kukusanya zaidi ya Sh5 bilioni tangu yalipoanzishwa mwaka 2020, fedha ambazo zimeelekezwa katika kuboresha huduma za afya, kuwawezesha vijana na maendeleo ya jamii nchini Tanzania.

Athari hizo zilibainika. wakati toleo la saba la marathon hiyo lilipohitimishwa katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam, likiwakutanisha washiriki takribani 17,000 chini ya kaulimbiu “Kasi Isambazayo Tabasamu.”
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la CRDB Bank, Dk Abdulmajid Nsekela, alisema fedha zilizopatikana kupitia marathon hiyo zimeleta msaada unaoonekana kwa makundi yenye uhitaji, hususan watoto wenye matatizo ya moyo na wanawake wenye mimba hatarishi.

Alisema zaidi ya watoto 400 wenye matatizo ya moyo wamefanyiwa upasuaji, huku zaidi ya wanawake 240 wenye mimba hatarishi wakipatiwa huduma za afya na kujifungua salama.

“Kila mchango unawakilisha mtoto aliyepewa nafasi nyingine ya kuishi, mama aliyepata huduma salama zaidi wakati wa kujifungua na familia ambazo maisha yao yamebadilika,” alisema Dk Nsekela.
Athari katika sekta ya afya pia imepanuliwa kupitia ushirikiano na taasisi mbalimbali. Zaidi ya watoto 1,000 wamepatiwa matibabu ya moyo kupitia msaada uliowasilishwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), huku wanawake zaidi ya 450 wenye mimba hatarishi wakinufaika kupitia CCBRT.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road nayo imenufaika kupitia ujenzi wa kituo cha huduma kwa wateja kwa njia ya simu, hatua iliyosaidia kuboresha upatikanaji wa msaada kwa wagonjwa wa saratani.

Kwa upande wake, akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu Dk Mwigulu Lameck Nchemba, Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, alisema marathon hiyo imevuka mipaka ya michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi.

“CRDB Bank International Marathon imevuka kuwa tukio la michezo na kuwa harakati ya kitaifa inayochangia afya, ustawi wa jamii, uwezeshaji vijana na maendeleo ya kiuchumi, alisema Abdulla.

Alisema mpango huo unaonyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wananchi katika kukabiliana na changamoto za kijamii.

Abdulla aliipongeza CRDB Bank Foundation kwa kutumia michezo kukusanya rasilimali kwa ajili ya shughuli za kijamii, huku ikiendelea kupanua programu zake za vijana katika ujasiriamali, ubunifu, mazingira na maendeleo ya vipaji.

Kupitia programu zake kwa ujumla, taasisi hiyo inasema imewafikia zaidi ya wajasiriamali milioni tatu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kutoa zaidi ya Sh30 bilioni kama mtaji wa kuwawezesha.
Hatua hizo ni pamoja na zaidi ya Sh4.2 bilioni zilizotolewa kupitia mpango wa mikopo wa asilimia 10 wa halmashauri katika awamu yake ya kwanza kwa halmashauri tano, huku zaidi ya Sh3.5 bilioni zikitolewa kwa vijana kupitia changamoto ya Vijana Uchumi.

Mfuko wa Samia Commercialization Fund, unaotekelezwa kwa ushirikiano na COSTECH, pia umepokea Sh4.6 bilioni kusaidia vijana wabunifu kubadili mawazo yao kuwa biashara zinazoweza kujiendesha.

Aidha, Sh8 bilioni zimetengwa kupitia SIDO na TIRDO kwa ajili ya elimu ya fedha, mafunzo ya ujasiriamali, maendeleo ya biashara, huduma za ushauri wa kitaalamu na mtaji.

Sh5 bilioni nyingine zimetengwa kupitia programu za Go Green na IMBEJU kuwawezesha vijana na wanawake wanaoendesha biashara zinazozingatia mazingira, huku zaidi ya wanufaika 1,000 tayari wakiwa wamechaguliwa.
Abdulla alisema programu kama FursaHub, Imbeju UDSM Start-Up Challenge, Imbeju Ndondo Cup na Imbeju Zuchu MasterClass zimeendelea kupanua fursa kwa vijana wa Tanzania.

Pia aliipongeza taasisi hiyo kwa kuunganisha marathon na tamasha la IMBEJU Sauti Moja Concert, lililofanyika Dar es Salaam Ijumaa na kuvutia zaidi ya watu 15,000.

Tamasha hilo lilishirikisha wasanii wa kimataifa akiwemo mwimbaji wa R&B kutoka Marekani, Trey Songz, msanii wa Nigeria BNXN na DJ wa Afrika Kusini Kabza De Small, pamoja na wasanii wa Tanzania. Sehemu ya mapato ya tamasha hilo itaelekezwa katika kuwawezesha vijana, hususan katika sekta ya ubunifu.

Abdulla alisema mchanganyiko wa michezo na burudani unaweza kusaidia Tanzania kujenga kalenda pana ya matukio makubwa, huku ukitengeneza ajira, kukuza utalii na kuzalisha fursa za uwekezaji.
Alisema michezo si burudani pekee bali ni sehemu muhimu ya uchumi, akitaja maandalizi ya Tanzania kuandaa kwa pamoja Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 na Kenya na Uganda.

Pia alisisitiza umuhimu wa Imbeju Ndondo Cup katika kugundua na kukuza vipaji vya soka, akiwataka waandaaji kuendelea kulinda dhima yake ya msingi katika ngazi za chini huku wakiimarisha mifumo ya maendeleo ya vipaji.

Abdulla alisema Serikali imetenga Sh519.6 bilioni kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika mwaka wa fedha 2026/27, huku vipaumbele vikijumuisha miundombinu ya michezo, maandalizi ya AFCON 2027, maendeleo ya vipaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi.
Aliwahakikishia wadau wa sekta binafsi kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili Watanzania wanufaike na fursa zilizopo katika michezo na sekta ya ubunifu.

Kwa zaidi ya Sh5 bilioni zilizokusanywa kupitia marathon hiyo na programu nyingine za CRDB Foundation zinazohusisha mabilioni ya shilingi, tukio hilo linazidi kuwa nyenzo ya kubadili ushiriki katika michezo kuwa matokeo yanayopimika katika jamii na uchumi.

Abdulla aliwapongeza viongozi wa CRDB Bank, akiwemo Mwenyekiti wa Bodi Prof Neema Mori, Dk Nsekela, Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank Foundation CPA (T) Oswald Urassa na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation, Tully Esther Mwambapa, kwa mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Wakenya watawala CRDB Marathon

Wanariadha kutoka Kenya walitawala CRDB Marathon 2026 baada ya kushinda nafasi nyingi za juu katika mashindano makuu.

Katika mbio za kilomita 42 kwa wanaume, Abraham Kiptum alishika nafasi ya kwanza kwa muda wa saa 2:15:33, akifuatiwa na Mkenya mwenzake James Mwangi aliyemaliza kwa saa 2:16:11. Mtanzania Marco Sylvester alishika nafasi ya tatu kwa saa 2:16:33.

Kwa upande wa wanawake katika kilomita 42, Joyce Kemuma alishinda kwa saa 2:35:26, huku Mkenya Jacinta Chepkoech akimaliza wa pili kwa saa 2:36:57 na Mkenya mwingine Jane Chelagant akishika nafasi ya tatu kwa saa 2:39:18.
Washindi wa kilomita 42 kwa wanaume na wanawake walipata Sh12 milioni kila mmoja, washindi wa pili Sh5 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh2 milioni.

Katika nusu marathon, Mkenya Simon Kelenzyoki alishinda mbio za wanaume kwa saa 1:15:33, akifuatiwa na Mtanzania Ebei Francis aliyemaliza kwa saa 1:15:52, huku Mtanzania mwingine Boay Dawi akiwa wa tatu kwa saa 1:16:07.

Kwa wanawake, Mkenya Rebecca Chepkwemoi alishinda nusu marathon kwa saa 1:12:42, akifuatiwa na Mtanzania Failuna Matanga aliyemaliza kwa saa 1:13:21 na Mkenya Irine Mkungu aliyeshika nafasi ya tatu kwa saa 1:13:23.
Washindi wa nusu marathon walipata Sh6 milioni, washindi wa pili Sh2 milioni na waliomaliza nafasi ya tatu Sh1 milioni.

Wanariadha wa Tanzania walitawala mbio za kilomita 10 kwa wanaume, huku Jumanne Ngoya akishinda kwa muda wa dakika 29:53. Benard Geay alimaliza wa pili kwa dakika 29:58, huku Shedrack Hasani akiwa wa tatu kwa dakika 30:06.

Tanzania pia ilitwaa nafasi zote tatu za juu katika mbio za wanawake za kilomita 10, ambapo Transfora Mussa alishinda kwa dakika 34:00, Anna Dolomongo akimaliza wa pili kwa dakika 34:18 na Agnes Mwanghui akiwa wa tatu kwa dakika 34:45.

Washindi wa kilomita 10 walipata Sh2 milioni, washindi wa pili Sh500,000 na waliomaliza nafasi ya tatu Sh300,000.














Wahadzabe ni kabila linalopatikana mkabala na ziwa Eyasi pembezoni mwa hifadhi ya Ngorongoro na habari za maisha yao zimehifadhiwa katika makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu Mkoani Arusha.

Pamoja na mabadiliko ya ulimwengu na elimu kutolewa lakini kabila hili bado haliamini katika tohara kwa kijana wa kiume, kwao hiyo ni mwiko wakiamini binadamu anastahili kuwa kama alivyozaliwa.

Sababu kubwa ya kutokutahiriwa ni kuwa ukitahiriwa unapunguza nyama ya binadamu na kuizika wakati binadamu huyo akiwa hai, imani ni kwamba huwezi kata sehemu yoyote ya mwili wa binadamu aliye hai

Vilevile kabila  hili linaamini kwamba mwanaume akitahiriwa hupunguza ukubwa na utaalam wa mambo na kufanya  mwili wako kuwa na mapungufu hata wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Katika kuhakikisha kwamba mwanaume anakuwa na nguvu za kutosha wakati wa kushiriki tendo la ndoa hulazimika kula mizizi inayopatikana porini , matunda, asali ikiwa fresh na nyama pori ambayo inachomwa au kuchemshwa supu.

Kutokana na kutokutahiriwa Wahadzabe wanaamini kwamba miili yao huwa na nguvu ya kupambana na mnyama yoyote porini na hiyo ndiyo heshima ya mwanaume kamili ambaye hata anapochumbia kutaka kuoa hupimwa kwa uwezo wa kuwinda na kuleta chakula cha familia.

Hii ni sehemu ya maajabu ya maisha makabila wanaunda Ngorongoro Global Geopark ambapo licha ya Wahadzabe kuendelea kuishi katika ukanda huo lakini taarifa zao zinapatikana katika makumbusho ya Urithi Geopark.

Karibu Nyumbani Ngorongoro upate mshangao wa maajabu na uzoefu usiosahaulika.






Na Victor Masangu,Bagamoyo

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete, amewataka walimu wa shule za msingi na sekondari kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na weledi lengo ikiwa ni kuweza kuzalisha wanafunzi wenye ujuzi na maarifa ambao watalisaidia Taifa katika nyanja mbali mbali.

Ridhiwani ameyabainisha hayo alipokuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Shajar ambayo inamiliki shule ya Baobab iliyopo Wilaya ya Bagamoyo.

Amesema kwamba katika Taifa la Tanzania walimu wa shule za msingi na sekondari wana mchango mkubwa sana hivyo wanapaswa kufanya kazi zao katika misingi imara ambayo itaweza kusaidia kupata wataalamu bora.

Pia Ridhiwani amesema ameridhishwa na ubunifu unaofanywa na wanafunzi wa shule hiyo na kusisitiza kuwa kazi zao wanazozifanya kulindwa na kusajiliwa.

Amesema kwamba uongozi wa Taasisi hiyo wanapaswa kuwa daraja linalowavusha vijana kutoka kwenye vipaji kwenda kwenye uzalishaji, huku wanafunzi wakifundishwa ufundi pamoja na ujasiriamali, usimamizi wa fedha.

Katika maadhimisho hayo, Ridhiwani pia amezindua Baobab Institute of Tanzania (BIT), akisema taasisi hiyo haipaswi kuwa chuo kinachofuata mabadiliko ya dunia pekee, bali iwe taasisi inayotafsiri mahitaji ya Tanzania ya leo na kesho pamoja na Afrika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Shajar ambayo pia ndio wamiliki wa shule ya Bao Shani Swai,

amebainisha kwamba kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi.

Shani ameeleza Taasisi hiyo ina miliki kituo cha kulea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, hospitali inayotoa huduma za afya pamoja na shule za awali, msingi, sekondari na ufundi stadi.

Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda watoto na kuhakikisha wanakua katika mazingira ambayo ni rafiki na salama

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga ameipongeza Taasisi hiyo kwa kuweza kushirikiana bega kwa bega na serikali katika nyanja zote ikiwemo suala la kudumisha hali ya ulinzi na usalama na shughuli za kimaendeleo.

Maadhimisho ya kilele cha sherehe za miaka 20 ya Baobab yamehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali,vingozi wa tasisisi wezeshi,vingozi wa dini,wasanii pamoja na wageni wengine kutoka maeneo mbali mbali.






Top News