

MERIDIANBET imeongeza gia nyingine kwenye burudani kwa kuileta Non-Stop Blasts & Races, kampeni yenye zawadi zenye thamani ya hadi TZS 75,000,000,000. Hii ni kampeni inayowaleta pamoja wachezaji, mashindano na zawadi katika safari inayoendelea kupitia michezo iliyochaguliwa ya Playson. Kama unapenda kuona nafasi mpya zikifunguka mara kwa mara, basi hii ni ya kufuatilia.
Kwenye Power Blasts, kila mchezo unaweza kuwa na zawadi yake. Wachezaji wanaoshiriki kwenye michezo inayokidhi vigezo wanaweza kupata smart drops za bahati wakati wanacheza. Zawadi hizo zinaweza kujumuisha fedha taslimu, mizunguko ya bure na vizidishi.
Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.
Halafu tunahamia kwenye Grand Races, ambako ushindani unakuwa wa muda mrefu zaidi. Wachezaji hukusanya pointi kupitia michezo inayostahili na kupambana kwa nafasi kwenye msimamo. Kila pointi inaweza kuwa muhimu katika safari ya kupanda viwango, huku kila mshiriki akijaribu kumaliza akiwa juu zaidi ya wengine. Hii ni sehemu inayowapa nafasi wachezaji wanaopenda ushindani wenye mwendelezo.
Kwa upande wa kasi, Turbo Races zinaingia moja kwa moja kwenye tukio. Hizi ni mbio fupi zenye ushindani wa haraka na nafasi za mara kwa mara za kuingia kwenye kinyang'anyiro. Msimamo unapowekwa upya, wachezaji wanapata nafasi nyingine ya kupanda juu.
Uzuri wa kampeni hii ni kwamba Non-Stop maana yake tukio linaendelea katika awamu mbalimbali. Michezo inayoshiriki, zawadi, prize pools, na ratiba za mbio zinaweza kutofautiana kulingana na awamu ya promosheni. Kwa hiyo, fuatilia michezo inayoshiriki, angalia mbio zinazoendelea na uwe tayari kwa zawadi.
A new FANTA® flavour is adding a burst of deliciousness to the brand’s portfolio in Tanzania with the launch of FANTA® Berry.
This bolder, fruitier tasting beverage brings a splash of playfulness, fun, and refreshing enjoyment to fans across the country.
Inspired by the vibrant energy of Tanzanian youth culture and the fast-rising Singeli movement, FANTA® Berry is set to tantalise taste buds with its vibrant twist.
The new flavour is now available in selected retail outlets, supermarkets, universities, kiosks, and trade outlets across Tanzania.
“We’re thrilled to bring even more variety to Tanzanians with this vibrant addition to the FANTA® family. FANTA® Berry embodies our commitment to creating fun, fruity twists filled with deliciousness that cater to people’s evolving tastes,” said Kabula Nshimo, Senior Marketing Manager for Coca-Cola Tanzania.
The launch campaign will come alive through the energetic “Kipapli” platform, designed to connect directly with Tanzania’s youth through music, dance, fashion, creator culture, and on-ground experiences across universities and high-traffic areas in Dar es Salaam.
As part of the experience, FANTA® Berry will bring the excitement to consumers through immersive commuter activations, influencer engagements and taste-test challenges.
Coca-Cola Kwanza today embarked on a vibrant convoy journey, starting at the Mikocheni plant and making stops across Ubungo, Mabibo, Buguruni and Temeke before culminating in Mbagala.
At each stop, consumers will enjoy FANTA® Berry tasting experiences, interactive entertainment and fun activities designed to create memorable brand experiences.
FANTA® Berry will roll creator challenges aimed at empowering young people to create content, grow their influence, and participate in the rapidly expanding digital creator economy.
The activations will also include university engagements, trade market “Berrification” moments, influencer collaborations, and the #KipapliChallenge social media campaign.
With iconic favourites like FANTA® Orange and now FANTA® Berry, the brand continues to inspire a passion for life and unforgettable moments of deliciousness.
Whether you're hanging out with friends, creating content, commuting across the city, or simply enjoying a playful moment, FANTA® Berry is the perfect companion.
“Our diverse beverage portfolio reflects our dedication to meeting the preferences of Tanzanians. We’re proud to offer products that bring people together, spark joy, and add flavour and deliciousness to everyday moments,” said David Chait, General Manager at Coca-Cola Kwanza Ltd.
Get your FANTA® Berry fix today and bring on the fun and deliciousness!
Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (left) takes a selfie with some Dar es Salaam residents during the celebrations, marking the official launch of the new Fanta Berry flavour, in Dar es Salaam over the weekend.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na taasisi zake kuhakikisha bunifu zinazozalishwa na Watanzania haziishii kuonyeshwa kwenye maonesho, bali zinaendelezwa, zinalindwa na kupelekwa sokoni ili zitoe suluhisho kwa changamoto mbalimbali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo, Jumatatu, Agosti 24, 2026, jijini Tanga wakati akihitimisha Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, akisisitiza umuhimu wa kujenga mfumo unaowawezesha wabunifu kubadilisha mawazo yao kuwa bidhaa na huduma zenye tija.
Amesema Tanzania ina wabunifu wenye uwezo mkubwa katika maeneo mbalimbali, hivyo hatua inayohitajika sasa ni kuhakikisha ubunifu huo unavuka hatua ya kuoneshwa kwenye maonesho na kufikia hatua ya kutumika, kuzalishwa kwa wingi na kuuzwa sokoni.
“Ni lazima tuvuke kwenye maonesho, twende kwenye uhalisia wa maisha kwamba hivi vitu ambavyo tunavionyesha kwenye maadhimisho kama haya sasa viende kwenye utaratibu wa kila siku wa maisha, tuvitengeneze vya kutosha, vitumike na viingie sokoni,” amesema Dkt. Mwigulu.
Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika sayansi, ujuzi na ubunifu kwa lengo la kuyageuza maeneo hayo kuwa nguzo muhimu za uchumi wa Taifa na kuchochea maendeleo kupitia matumizi ya tafiti na teknolojia.
“Hatutaweza kuendelea bila kuwa na sayansi, teknolojia na tafiti na tukatumia matokeo ya tafiti hizo. Hatutapata tija bila kutumia matokeo ya tafiti hizo,” amesema.
Dkt. Mwigulu pia amesema Serikali haitakubali kushusha viwango vya elimu, akisisitiza umuhimu wa taasisi zinazosimamia ubora wa elimu kuendelea kusimamia misingi ya kitaaluma katika kuandaa wataalamu wenye uwezo unaokubalika.
“Tusitengeneze mazingira yawe rahisi ya kujifunza, yawe na alama kubwa kubwa, lakini kazini kuwe na zero kubwa kubwa. Hiyo hapana. Lazima tusimamie misingi ya elimu,” amesema.
Amesisitiza kuwa katika sekta nyeti kama afya, uhandisi na elimu, ubora wa mafunzo haupaswi kuchezewa.
“Hatuwezi kucheza na afya za Watanzania… Hatuwezi tukaandaa wataalamu kwa namna duni duni hivi, tutaharibu sekta yote. Tunataka walimu walio bora, maengineia walio bora; wakijenga daraja, wakijenga jengo, liwe jengo kweli kweli,” amesema.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameagiza mipango ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Tanga iangalie mahitaji ya kiuchumi na kijamii ya mkoa huo kwa kipindi cha miaka 25 ijayo, ili miundombinu inayojengwa sasa iendane na ukuaji wa uchumi, biashara, uwekezaji na ongezeko la matumizi ya usafiri wa anga.
“Lazima tunapojenga tuwaze mbele, tusijenge kwa ajili ya leo. Tuwaze mbele miaka 20 mbele, 25 mbele, kama ambavyo Dira yetu inatuambia,” amesema Dkt. Mwigulu.
Amesema uwanja huo unapaswa kujengwa kwa hadhi ya Tanga kama lango muhimu la shughuli za kiuchumi kutokana na miradi mikubwa inayotekelezwa katika mkoa huo.
Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema maonesho hayo yanaakisi jitihada za Serikali katika kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha elimu inayounganisha nadharia na vitendo, ili kuandaa wahitimu wenye ujuzi wa kujiajiri na kuingia kwa ufanisi katika soko la ajira.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Caroline Nombo amesema jumla ya taasisi 91 za umma na binafsi zimeshiriki katika maadhimisho hayo, ambayo yamehusisha maonesho ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu, mashindano ya kitaifa ya ujuzi na ubunifu pamoja na makongamano yaliyolenga kujadili mchango wa elimu, ujuzi na teknolojia katika kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe Husna Sekiboko amesema Bunge litaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuendeleza elimu, ujuzi na ubunifu kupitia bajeti, sera na miongozo inayolenga kuwawezesha watafiti na wabunifu wa ndani kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa. Amesema kuna umuhimu wa kuzipa kipaumbele bidhaa na teknolojia zinazozalishwa nchini, zikiwemo katika taasisi za Serikali, ili kuongeza matumizi ya bunifu za Watanzania na kuchochea ukuaji wa wabunifu hao.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Buriani amesema uwekezaji wa Serikali katika sekta ya elimu umeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia mkoani humo, kuongeza miundombinu na kuchochea mafanikio ya wanafunzi, huku akipongeza maonesho hayo kwa kuibua na kuonesha uwezo mkubwa wa Watanzania katika sayansi, teknolojia na ubunifu.
Kaulimbiu ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu mwaka 2026 ni “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”
Na Janeth Raphael - MichuziTv
Imani kwamba haki inaweza kufuatiliwa na kupatikana bila kujali hali ya mtu imeongezeka kwa familia moja kutoka Meru mkoani Arusha, baada ya kupata msaada kupitia Programu ya “Sema na Waziri” ya Wizara ya Katiba na Sheria.
Familia hiyo ilikuwa imekumbwa na changamoto baada ya kuacha kazi ya ualimu katika shule ya msingi ambako walikuwa wakijitolea kufundisha, huku ikiwa bado inadai stahiki zake. Changamoto hiyo iliwasilishwa kupitia programu hiyo na kuanza kufanyiwa kazi na watumishi wa Wizara.
Ufuatiliaji uliofanywa na Wizara kwa kuwasiliana na wahusika umefanikisha familia hiyo kupata stahiki zilizokuwa zikidaiwa, hatua ambayo imeelezwa kuwa imewapa matumaini mapya kuhusu upatikanaji wa haki.
Akizungumza katika programu hiyo, Lidya Ernest kutoka Meru, Arusha, amesema awali alikuwa na mtazamo kwamba haki ilikuwa rahisi kupatikana zaidi kwa watu wenye uwezo, lakini uzoefu walioupata umebadili mtazamo huo.
“Nitumie nafasi hii kumshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka Programu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa ajili ya kutusaidia Watanzania wote bila kuangalia matabaka wala nyadhifa, wala hali ya mtu. Hata sisi watu wa huku chini nasi tumefikiwa,” amesema Lidya.
Kwa mujibu wa Lidya, hatua hiyo imewapa yeye na mume wake ujasiri wa kuendelea kufuatilia haki zao kupitia njia sahihi, huku wakitambua umuhimu wa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali.
Katika hatua nyingine, Wizara ya Katiba na Sheria imewakabidhi Lidya na mume wake Sh milioni 1.5, fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha shughuli za ujasiriamali na kujikwamua kiuchumi.
Msaada huo unalenga kuwapa fursa ya kutumia fedha hizo kama mtaji wa shughuli za uzalishaji, hatua inayotarajiwa kusaidia familia hiyo kujenga chanzo cha kipato na kuimarisha maisha yao.
Tukio hilo limeonyesha pia nafasi ya Programu ya “Sema na Waziri” katika kuwapa wananchi jukwaa la kuwasilisha changamoto zao za kisheria na kupata ufuatiliaji kutoka kwa Wizara.
Kwa familia hiyo kutoka Meru, msaada walioupata haujaishia katika kurejeshewa stahiki walizokuwa wakidai, bali umeenda sambamba na kupata mtaji wa kuanza shughuli za ujasiriamali, jambo ambalo wameeleza kuwa limewapa matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi.
Hatua hiyo pia inaendelea kuimarisha ujumbe kwamba upatikanaji wa haki haupaswi kuwa fursa ya wachache, bali huduma inayopaswa kuwafikia wananchi wote bila kujali uwezo wao, hadhi au nafasi zao katika jamii.
MKUU wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela, Agosti 24, 2026 amepokea rasmi Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Shinyanga.
Hafla ya mapokezi imefanyika katika Kijiji cha Nyang'holongo, Kata ya Nundu, Wilaya ya Nyang'hwale.
Akizungumza baada ya kupokea mwenge huo, Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa wa Geita kwa mwaka 2026 utakimbizwa katika Halmashauri 6.
Atanzia na Halmashauri ya Nyang'hwale hadi kumalizia katika Halmashauri ya Chato, kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa.
Ameeleza kuwa wakati wa ukimbizaji wa Mwenge Mkoani Geita, utakimbizwa kwa umbali wa Kilometa 698.2.
Katika kipindi hicho jumla ya miradi 42 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 168.74 itapitiwa. Miradi hiyo itazinduliwa, kuekwa mawe ya msingi, kukaguliwa na kutembelewa.




.jpeg)




.png)



.jpeg)



.jpeg)










.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

















