NA DENIS MLOWE IRINGA

WANAFUNZI wa zamani (Alumni) wa Shule ya Sekondari Tosa Maganga wameungana kuchangisha Shilingi milioni 250 kwa ajili ya ununuzi wa basi la shule hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo.

Akizungumza kuhusu mpango huo, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Grayson Nyamoga, ambaye ni mmoja wa wanafunzi waliowahi kusoma katika Shule ya Sekondari Tosamaganga amesema Alumni wamekubaliana kushirikiana kuhakikisha shule hiyo inapata basi litakalosaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na shughuli mbalimbali za shule.

Nyamoga amesema mahitaji yaliyobainishwa na shule ni pamoja na ukarabati wa Bweni la Mandela, ukarabati wa Bweni la Mapinduzi, ununuzi wa samani kwa ajili ya ukumbi wa chakula (dining hall), pamoja na ununuzi wa basi ambalo linakadiriwa kugharimu Shilingi milioni 250.

Amesema Alumni wameamua kuanza na jukumu la kuchangia fedha za ununuzi wa basi hilo, wakiamini kuwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii na shule iliyowapa msingi wa elimu wanafunzi hao ambao sasa wako katika kada mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

“Tunawahamasisha wana Tosa na Alumni wote tushirikiane kuchangia fedha hizi, Shilingi milioni 250, ili tuweze kununua basi hilo na kuwakabidhi vijana wetu na wadogo zetu waliopo pale Shule ya Sekondari Tosa Maganga,” amesema Nyamoga.

Amesema basi hilo linatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa wanafunzi na shule kwa ujumla, hasa katika kurahisisha usafiri wa wanafunzi wakati wa shughuli za kielimu, michezo, ziara za kitaaluma na shughuli nyingine zinazohitaji usafiri.

Nyamoga amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Alumni kuhakikisha maadhimisho ya miaka 100 ya Shule ya Sekondari Tosa Maganga yanaacha alama ya kudumu kwa kizazi cha sasa na kijacho, badala ya kuwa sherehe pekee.

Maadhimisho ya miaka 100 ya Shule ya Sekondari Tosamaganga yanatarajiwa kufanyika kuanzia Oktoba 8 hadi 10, 2026, ambapo Alumni wanatarajiwa kushiriki katika shughuli mbalimbali zitakazolenga kuimarisha uhusiano kati ya shule na wanafunzi wake wa zamani.

Amesisitiza kuwa mchango wa kila mwana Tosa ni muhimu katika kufanikisha lengo hilo, akiwataka Alumni kutumia fursa hiyo kuunga mkono maendeleo ya shule yao na kuhakikisha wanafunzi waliopo sasa wanapata mazingira bora ya kusoma na kufanya vizuri kitaaluma.

Amesema lengo la mwisho ni kuona juhudi hizo zinasaidia kuboresha mazingira ya shule na kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira rafiki yatakayowapa nafasi kubwa ya kufaulu na kutimiza ndoto zao.





-AAHIDI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU, UTII NA UZALENDO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa dhamana ya kuwa msaidizi namba moja na kuahidi utii, uadilifu, uzalendo na uchapaji kazi.

Makamu wa Rais amesema hayo, wakati akiwasalimu wananchi wa Jimbo la Chamwino, waliojitokeza kumpokea kwa wingi nje ya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, mara baada ya kuapishwa kuwa Makamu wa Rais. Amesema ataendelea kufanya kazi ya kumsaidia Mhe. Rais kwa uadilifu na kuwatumikia watanzania wote ili kuharakisha maendeleo.

Aidha Makamu wa Rais amesema ataendelea kuwawakilisha vyema vijana hapa nchini na kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha Tanzania inazidi kusonga mbele katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Akitoa salamu zake kwa wananchi hao, Makamu wa Rais amewahakikishia kuendelea kutekeleza majukumu yake mapya kwa uadilifu, bidii na kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa.

“Wana sitawazingua, na Mama sitamzingua,” amesema Ndejembi, katika ujumbe uliosisitiza dhamira yake ya kutekeleza wajibu aliopewa na kuendelea kuwa mwaminifu na mwakilishi mwema wa vijana.

Makamu wa Rais amewasalimu wananchi wa Jimbo la Chamwino ikiwa ni
jimbo alilolitumikia kabla ya kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais.














Na TAEC Dodoma


Kila mwaka tarehe 29 Agosti, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Majaribio ya Nyuklia (International Day against Nuclear Tests), ikiwa ni fursa ya kutafakari madhara yaliyosababishwa na majaribio ya silaha za nyuklia na kuendelea kuhimiza juhudi za kujenga dunia yenye amani na usalama.

Siku hii ilianzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2009 kupitia Azimio Na. 64/35, kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu madhara ya majaribio ya silaha za nyuklia na umuhimu wa kuyasitisha. Tarehe 29 Agosti pia ina umuhimu wa kihistoria kutokana na kufungwa kwa eneo la majaribio ya nyuklia la Semipalatinsk nchini Kazakhstan mwaka 1991.

Tangu jaribio la kwanza la silaha ya nyuklia mwaka 1945, zaidi ya majaribio 2,000 yamefanyika duniani, yakiacha historia ya madhara kwa afya ya binadamu, mazingira na usalama wa dunia.

Katika kuadhimisha siku hii, Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) inaungana na jumuiya ya kimataifa kupinga majaribio ya silaha za nyuklia na kusisitiza matumizi salama, yenye uwajibikaji na ya amani ya sayansi na teknolojia ya nyuklia.

Ni muhimu kuelewa kuwa kupinga majaribio ya silaha za nyuklia si kupinga teknolojia ya nyuklia. Teknolojia hii inapotumika kwa madhumuni ya amani na chini ya mifumo madhubuti ya usalama na udhibiti, ina mchango mkubwa katika kuboresha maisha na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Nchini Tanzania, TAEC ina jukumu la kusimamia na kudhibiti matumizi salama ya vyanzo vya mionzi pamoja na kuhamasisha matumizi ya amani ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, kilimo, mifugo, viwanda, migodi, maji, utafiti, mazingira na nishati.

Katika afya, teknolojia ya mionzi inatumika katika uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali; katika kilimo na mifugo inachangia katika utafiti, uboreshaji wa uzalishaji na udhibiti wa baadhi ya wadudu na magonjwa. Mbinu za nyuklia pia zina matumizi muhimu katika tafiti za rasilimali za maji, viwanda, migodi na maeneo mengine ya maendeleo.

Kwa msingi huo, tunapaswa kutofautisha kati ya matumizi ya nyuklia kwa madhumuni ya kijeshi na matumizi yake kwa madhumuni ya amani. Hofu inayotokana na madhara ya silaha za nyuklia isiwe sababu ya kuiona teknolojia yote ya nyuklia kama tishio.

TAEC itaendelea kuhakikisha matumizi ya vyanzo vya mionzi nchini yanafanyika kwa kuzingatia sheria na viwango vya usalama ili kuwalinda wafanyakazi, wagonjwa, wananchi na mazingira. Tutaendelea pia kutoa elimu kwa umma ili kuondoa dhana potofu na kuongeza uelewa kuhusu manufaa ya matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia.

Tunapoadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kupinga Majaribio ya Nyuklia, tunatoa wito kwa wananchi kuendelea kupata taarifa sahihi na kuunga mkono matumizi salama na ya amani ya teknolojia ya nyuklia kwa manufaa ya Taifa na ustawi wa binadamu.

Ujumbe wetu ni wazi: HAPANA kwa majaribio ya silaha za nyuklia; NDIYO kwa matumizi salama na ya amani ya teknolojia ya nyuklia kwa maendeleo ya Taifa.

“Mionzi kwa Matumizi Salama na Teknolojia ya Nyuklia kwa Maendeleo ya Taifa.”

Na Janeth Raphael - MichuziTv -Ikulu Chamwino 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema uamuzi wa kumteua Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais ulizingatia sifa, uzoefu na uwezo wake wa kubeba dhamana kubwa ya uongozi wa taifa.

Rais Samia amesema nafasi hiyo imekabidhiwa tena kwa kijana, akimtaka Ndejembi kutumia fursa hiyo kujifunza, kukua kiakili na kutekeleza majukumu yake kwa weledi, utii na uaminifu kwa maslahi ya Watanzania.

Akizungumza leo, Agosti 29, 2026, katika hafla ya kumuapisha Ndejembi kuwa Makamu wa Rais iliyofanyika Ikulu Chamwino, Dodoma, Rais Samia amesema uamuzi wa kumrudisha kijana katika nafasi hiyo ulifanyika kwa kauli moja.

“Kwa kauli moja tuliamua kuirudisha nafasi ya Makamu wa Rais kwa vijana na tuendelee kulea. Imetoka kwa kijana na tumeirudisha kwa kijana. Tunakuomba kijana (Ndejembi) ukakue sio kwa umri bali ukakue kiakili, tumekupa majukumu makubwa ni imani yangu utaweza,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema Ndejembi alipata uungwaji mkono wa wabunge kwa kauli moja kutokana na sifa alizonazo zinazomfanya astahili kushika nafasi hiyo.

“Wabunge walimpitisha Deogratius Ndejembi kwa kauli moja kwa kuzingatia sifa za Makamu wetu wa Rais,” amesema.

Amesema kabla ya kufikia nafasi ya Makamu wa Rais, Ndejembi amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini na katika sekta binafsi, akieleza kuwa uzoefu huo utakuwa nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake mapya.

“Makamu wa Rais Deogratius Ndejembi, kabla ya wadhifa huu, ulishika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini na sekta binafsi. Sina shaka kwamba uzoefu huo utakusaidia kutekeleza majukumu ya dhamana hii uliyopewa,” amesema Rais Samia.

Kwa mujibu wa Rais Samia, hakuna shule maalumu inayomwandaa mtu kuwa Makamu wa Rais, bali uwezo wa kutekeleza majukumu hayo unajengwa kupitia sifa binafsi, bidii, weledi, nidhamu pamoja na utayari wa kujifunza na kusimamia utekelezaji wa majukumu.

Amesema sifa hizo zitamsaidia Ndejembi kutekeleza ipasavyo dhamana aliyopewa na taifa.

Rais Samia pia amesema uzoefu wa Ndejembi ndio uliowafanya viongozi kutokuwa na kusita katika kupitisha jina lake wakati wa kutafuta mtu wa kujaza nafasi hiyo.

“Kwa uzoefu huo ndio maana wakati tunatafuta mtu wa kujaza nafasi hii, hatukusita hata kidogo kupitisha jina lako. Hivyo ni matamanio na matarajio yetu sote Watanzania utalitumikia vyema, kwa utii, uaminifu, utu, busara, uzalendo, hekima, maarifa na uzoefu ulio nao, ukimtanguliza Mungu mbele na kwa maslahi ya taifa,” amesema.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amemtaka Ndejembi kwenda kuwatumikia Watanzania wote bila kujali tofauti zao, akisisitiza umuhimu wa kiongozi kuweka mbele maslahi ya taifa.

“Nenda ukawatumikie Watanzania bila kujali tofauti zao,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema serikali ina kazi kubwa ya kutekeleza ahadi zilizowekwa kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, sambamba na kuanza utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya miaka 25 ijayo.

Amesema dira hiyo imebeba matarajio makubwa ya maendeleo kwa wananchi, hivyo utekelezaji wake unahitaji umoja, mshikamano, ushirikiano, utulivu na uongozi bora.

“Ili tuweze kutekeleza haya yote kwa maslahi ya wananchi wetu na taifa kwa ujumla, tunahitaji umoja, mshikamano, ushirikiano, utulivu na uongozi bora,” amesema.

Uapisho wa Ndejembi unafungua rasmi ukurasa mpya katika safari yake ya uongozi wa kitaifa, huku akianza kutekeleza majukumu ya Makamu wa Rais chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan


















 


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema ni matamanio na matarajio ya Watanzania wote kwamba Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, ataitumikia vyema Tanzania kwa utii, uaminifu, utu, busara, hekima, uzalendo na maarifa

Rais Samia ameyasema hayo leo Jumamosi, Agosti 29, 2026, Ikulu ya Chamwino, Dodoma, mara baada ya kumuapisha Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema uteuzi wa Ndejembi umetokana na kuzingatia sifa na vigezo alivyo navyo, ikiwemo umri wake ambao, kwa mujibu wa Rais Samia, bado ni kijana mwenye nguvu, ari na kasi ya kujituma katika kutekeleza shughuli za Serikali.

“Nivishukuru vikao vya Chama cha Mapinduzi vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu kwa kupendekeza na kuridhia jina la Deogratius Ndejembi katika nafasi ya Makamu wa Rais,” amesema Rais Samia.

Amesema kwa kauli moja waliamua kuirudisha nafasi hiyo kwa vijana ili waendelee kulelewa katika uongozi, akimtaka Ndejembi akue kiakili kutokana na ukubwa wa majukumu aliyopewa.

Rais Samia amesema Ndejembi ana uzoefu wa uongozi serikalini na sekta binafsi, hivyo anaamini uzoefu huo utamsaidia kutekeleza majukumu ya dhamana hiyo.

“Cheo ni dhamana, cheo hiki tulichokupa sio ufalme ni dhamana. Ni dhamana uliyopewa na Watanzania kupitia Chama cha Mapinduzi lakini pia kupitia Bunge,” amesema.

Ametoa wito kwa Ndejembi kuwatumikia Watanzania bila kujali tofauti zao, huku akisisitiza umuhimu wa umoja, mshikamano, ushirikiano, utulivu na uongozi bora katika kutekeleza Ilani ya CCM ya 2025–2030 na Dira ya Maendeleo ya miaka 25 ijayo.

Rais Samia pia amewashukuru mabalozi na wakuu wa mashirika ya kimataifa waliohudhuria tukio hilo, akisema uwepo wao unaonesha urafiki, udugu na ushirikiano na Tanzania, pamoja na ushahidi wa uwezo wa nchi kubadilisha viongozi kwa amani na utulivu.




LEO Liverpool watapambana na Nottingham Forest kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Anfield, katika mechi itakayokuwa ya kwanza ya nyumbani kwa kocha mpya wa Liverpool, Andoni Iraola.

Hii itakuwa mechi ya kwanza ya msimu wa 2026-27 kwenye dimba la Anfield, huku Liverpool wakitaka kurejea baada ya sare waliyopata siku ya kwanza dhidi ya Newcastle. Iraola, aliyekuwa akiongoza Bournemouth msimu uliopita, sasa ana jukumu zito la kuwarudisha "The Reds" kwenye ushindani wa ubingwa.

Liverpool walianzaa msimu huu wakiwa na matokeo ya kusisimua dhidi ya Newcastle, ambapo walifunga mabao mara mbili baada ya kuwa nyuma, kwa mabao ya Cody Gakpo na penalti ya Dominik Szoboszlai dakika ya 99, hivyo kupata sare ya 2-2.

Kwa upande wa Forest, msimu wao ulianza vibaya zaidi chini ya kocha mpya Oliver Glasner, baada ya kufungwa 1-0 nyumbani na Leeds United, ambao walipata ushindi kwa freekick ya moja kwa moja ya Anton Stach. Kwenye msimamo wa ligi kwa sasa, Liverpool wako nafasi ya 10 na pointi 1, huku Forest wakiwa chini zaidi, nafasi ya 15 bila pointi.

Kuhusu majeraha, Liverpool watakosa wachezaji kadhaa muhimu. Watakuwa bila Conor Bradley, Hugo Ekitiké, Joe Gomez, Jayden Danns na Giovanni Leoni kutokana na majeraha, huku Curtis Jones akiwa na tatizo la kiuno linaloweza kumzuia kucheza.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema. Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hata hivyo, silaha kuu ya Liverpool bado ipo Florian Wirtz anabaki kuwa tishio kuu la mbele, akisaidiwa na Federico Chiesa na Alexander Isak. Kwa upande wa Forest, hali ni nzuri zaidi kwani Glasner ana karibu wachezaji wote wanaopatikana, isipokuwa Nicolo Savona na Ryan Yates, hivyo timu yake itakuwa na nguvu kamili ya mashambulizi kupitia Ola Aina, Morgan Gibbs-White na Igor Jesus.

Historia ya mechi hizi mbili inaonyesha ushindani mkubwa. Katika mechi tano za mwisho kati ya timu hizi, Liverpool wameshinda mara tatu, Forest mara moja, na mechi moja imeishia sare.

Hata hivyo, kumbukumbu za hivi karibuni si nzuri sana kwa Liverpool msimu uliopita Forest walishinda 3-0 dhidi ya Liverpool kwa bao la Morgan Gibbs-White, kabla ya Liverpool kulipiza kisasi Februari 2026 kwa ushindi wa 1-0 uwanjani kwa Forest. Hii inaonyesha kuwa Forest si timu ya kudharauliwa, hata dhidi ya mabingwa wa zamani wa Ulaya.

MASHINDANO ya Expanse: Big Wins Start Here yanaingia katika hatua za mwisho, huku wachezaji wakibakiza takribani wiki moja tu kabla ya pazia kushuka rasmi. Hii ni nafasi ya wapenzi wa michezo ya sloti kuingia kwenye ushindani na kuwania sehemu ya zawadi nono yenye jumla ya TZS 5,000,000 kupitia Meridianbet. Kama ulikuwa unasubiri muda sahihi wa kujaribu bahati yako, muda huo umefika.

Katika Expanse: Big Wins Start Here, washiriki watakuwa na nafasi ya kucheza jumla ya michezo 15 ya sloti za Expanse, huku dau la chini likiwa ni TZS 200 kwa kila raundi. Hii ina maana kuwa huhitaji kuanza na dau kubwa ili kuingia kwenye ushindani. Kila raundi ina nafasi ya kukuongezea safari kuelekea nafasi za juu, na kadiri mashindano yanavyokaribia mwisho, ndivyo presha ya kupanda kwenye msimamo inavyoongezeka.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Lakini usidanganyike na muda uliobaki, mashindano yanamalizika Septemba 5, 2026. Siku chache zilizobaki zinaweza kuwa na mabadiliko makubwa kwenye msimamo, kwani washiriki wanaweza kuendelea kusaka nafasi nzuri hadi dakika za mwisho. Kwa hiyo, kama tayari umeshaanza safari yako, huu ni wakati wa kuongeza kasi, na kama bado hujaingia, bado una nafasi ya kujiunga na kushuhudia burudani ya Expanse huku ukilenga sehemu ya zawadi ya TZS 5,000,000.

Ukiwa na michezo 15 ya kasino mtandaoni kuchagua, safari yako ya kutafuta ushindi haijafungwa kwenye mchezo mmoja pekee. Kinachobaki ni wewe kuingia uwanjani, kuchagua mchezo unaoupenda na kuanza kusaka nafasi yako kwenye mashindano haya maalum yanayopatikana Meridianbet pekee. Kumbuka, muda haukusubiri na tarehe ya mwisho inakaribia kwa kasi.

Ushindi unaanza hapa. Huo ndio ujumbe wa Expanse, na sasa ni wakati wa kugeuza mchezo wako kuwa ushindi. Jiandae, ingia kwenye mashindano, cheza kwa kuwajibika na ufuatilie nafasi yako kabla ya Septemba 5, 2026. Kwa wapenzi wa sloti wanaotafuta msisimko mpya, Expanse ni sehemu ambayo ushindi unaanza.

Na Lusungu Helela, Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini. 

Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu. 

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi. 

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete 

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo. 

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi. 

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete 

Kwa upande wake, Mhe. Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma. 

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao. 

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi. 

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi. 

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho, Mhe.Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia. 

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira. 

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Mji wa  Serikali Mtumba jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.














 


Top News