Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Rukwa Albert Kipele amewataka viongozi na vijana wa umoja huo kuanzia ngazi ya kata, wilaya kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhusiana na kilele cha mwenge wa uhuru Kitaifa mkoani Rukwa.
Akizungumza na vijana wa hamasa na viongozi wa kata wa jumuiya hiyo wilaya ya Sumbawanga mjini leo, ikiwa ni maandalizi ya kuukaribisha mwenge wa uhuru ambapo kilele chake kitahitimishwa mkoani Rukwa.
Kipele amesema vijana wana jukumu la kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhakikisha makundi hayo yanakuwa na uelewa wa pamoja kuhusiana na mbio za mwenge wa uhuru kitaifa.
" Twendeni tukatoe elimu kwenye kata zetu,wilaya zetu tukiwaeleza wananchi frusa zitakazopatikana wakati wa kilele cha mwenge wa uhuru twendeni tukawahamasishe boda boda,mama na baba ntilie,wajasiliamari,machinga tuwashirikishe kushiriki uzimaji wa mwenge wa uhuru kitaifa".
"Nchi yetu ni kubwa sana tukumbuke mwenge huu uliwashwa visiwani Pemba na sasa utazimwa mkoani kwetu na uwenda sisi wote hapa hatukuwepo huko nyuma na hatujawahi kushuhudia unavyowashwa na kuzima,sasa leo tutashuhudia uzimaji wa mwenge wetu wa uhuru"amesema Kipele.
Pia amesema Jumuiya ya vijana ndiyo nguvu ya chama na kuwa ushirikiano ni muhimu ili kujenga jumuiya hiyo na kufanikisha jambo hilo.
"mshikamano ndiyo msingi wa kufanikisha jambo ambalo lipo mbele yetu,niwaombe vijana tujenge uaminifu na wakati huu ni wakushikamana ili jambo la kilele cha mwenge wa uhuru tufanikishe kwa pamoja"amesema Kipele.
Aidha amewataka vijana kuwa na umoja na kuepuka makundi yanayowagawa vijana hao bali kujenga umoja na mshikamano ambao ni msingi wa chama hicho.
Pia aliwataka viongozi UVCCM kata na wilaya mkoani Rukwa kufuata miongozo ya chama na kuwa na mipaka ya utendaji wao wa kazi ili kuondoa sintofahamu kwa viongozi wa ngazi za juu.
Kwa upande wao vijao wa hamasa pamoja na viongozi wamekishukuru chama cha mapinduzi CCM kwa kuendelea kuwatumia vijana katika shughuli za serikali na chama na kuwa watashirikiana kwa pamoja kuhakikisha elimu na hamasa inatolewa kwa makundi yote ya kijamii.
Wamesema wamefurahia ujio wa mwenge wa uhuru na kuwa historia inakwenda kuandikwa na kushuhudiwa katika kilele cha mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa zitakazo hitimishwa mkoani Rukwa Okt 14 mwaka huu.
