Farida Mangube Morogoro 

Serikali imewataka watanzania   kuitumia vizuri fursa  ya Tanzania kuwa mwenyeji  wa  mashindano ya AFCON 2027 kwa kutangaza   tamaduni za makabila mbalimbali  kama sehemu ya vivitio adimu vinavyopatikananchini humo  sambamba na  kufanya vizuri kwenye michezo hiyo.

Kauli hiyo Imetolewa na  Mkuu wa Mkoa  Morogoro,Adam Malima  wakati akifungua Tamasha la Nne la Kitaifa la Utamaduni linalofanyika mjini Morogoro  ambapo jumla ya wahiriki 150,000 kutoka mikoa mbalimbali wanaonyesha  tamaduni.zao.

Amesema katika michuano hiyo  licha ya Tanzania kushiriki nchi zingine ni Kenya na Uganda ambazo  zinaendelea na maandalizi ya michezo  hiyo ambapo kwa Tanzania itafanyika Arusha,Dar es salaam na Zanzibar.

Aidha amewataka watanzania kuendelea kuheshimu utamadani kwani bila kuwepo Kwa  utamaduni huwezi kuwa na  heshima.

Naye  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema tamasha Hilo la Kitaifa la Utamaduni lilianzia Mkoani Dar Salaam,likaenda Songwe na Ruvuma na Mwaka huu linafanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumzia kuhusu  michuano ya AFCON  Msigwa amewataka watanzania watanzania  kuachiana  maneno yanaenezwa na baadhi ya watu wasioitakia mema   kwa kueneza uongo kuwa  michuano ya AFCON inayotarajiwa kufanyika mwakani kwa nchi tatu za Tanzania,Kenya na Uganda kuwa Kwa Tanzania imehamishwa sio taarifa za kweli.







Na Janeth Raphael – MichuziTv

Mwalimu wa Shule ya Awali DCT Canon Andrea Mwaka, Rose Isaka, aliyewahi kumfundisha Makamu wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, mwaka 1986, amemuelezea kiongozi huyo kuwa tangu akiwa mtoto alikuwa na tabia ya furaha, ucheshi, upole na kujali watu waliomzunguka.

Akizungumza kuhusu kumbukumbu zake za kipindi hicho, Rose amesema Ndejembi alikuwa mwanafunzi mwenye nidhamu na tabia njema, aliyependa kushirikiana na wenzake pamoja na kushiriki katika michezo, hususan mpira wa miguu.

“Alikuwa mwanafunzi mzuri sana, mcheshi na mwenye furaha wakati wote. Nimefurahi sana kwa sababu alikuwa ni mwanafunzi wangu,” amesema.

Amesema moja ya matukio ambayo yameendelea kubaki kwenye kumbukumbu yake ni pale Ndejembi alipomsaidia mwanafunzi mwenzake aliyeanguka na kuumia wakati wa michezo.

Kwa mujibu wa Rose, baada ya kuona mwanafunzi huyo ameumia, Ndejembi alimfuata na kumsaidia, jambo ambalo aliliona kama ishara ya kujali na kuwathamini wenzake tangu akiwa katika umri mdogo.

“Alikuwa hana matukio mabaya ya kutisha, hapana. Tukio ninalolikumbuka ni siku ambayo mwanafunzi mwenzake alianguka na kuumia, Ndejembi akaenda kumsaidia na kumhudumia vizuri sana. Hicho ndicho ninachokumbuka mpaka leo,” amesema.

Rose amesema tukio hilo lilimfanya kumtambua Ndejembi kama mtoto mwenye moyo wa kuwajali wengine, akieleza kuwa hulka ya kusaidia na kushirikiana na watu ilionekana wazi tangu utotoni.

Amesema anaamini tabia hizo njema alizokuwa nazo akiwa mtoto zimeendelea kuwa sehemu ya maisha yake hadi sasa, huku akimtakia mafanikio na kumwombea aendelee kuwa kiongozi mwenye moyo wa kuwasaidia wengine.

“Ninamwombea baraka kibao. Ninamwombea kwa Mungu aendelee kuwa mwema. Mungu azidi kumbariki sana na aendelee na tabia yake ileile ya kusaidia watu wote kama alivyokuwa utotoni,” amesema Rose.


Na MWANDISHI WETU


Watoto 1,337,079, wanatarajiwa kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio mkoani Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa mkoa huo, Abdul Mhite, alipozindua kampeni ya chanjo hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam, Albert Chalamila leo.

Mhite amesema kampeni hiyo itamalizika Agosti 30 mwaka huu na inalengakuwafiia watoto wote walio chini ya umri wa miaka 10.

Amesema , chanjo hiyo itahusisha watoto ambao pia waliwahi kupata chanjo hiyo awali.

“Tunawataka wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo hii hata kama awali mtoto aliwahi kuchanjwa. Chanjo itatolewa kwa mfumo wa matone,”amesema.

Ameeleza serikali imeandaa kampeni hiyo kwa lengo la kuongeza na kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya ugonjwa wa polio kwa kuhakikishawatoto wote walengwa wanafikiwa.

Mhite amebainisha chanjo hiyo itatolewa nyumbakwa nyumba, mtaa kwa mtaa, shuleni, vituo vya afya, zahanati, hospitali , sehemu za ibada, stendi, katika vituo vya kulea watoto, viwanja vya michezo na maeneo mbalimbali katika jamii.

“Nawaomba wazazi na walezi mshirikiae na timu za chanjo zinapofika katika maeneo yenu.Pia muwaruhusu watoto kupata matone ya chanjo hii,”ameeleza Mhite.

Katibu Tawala huyo, ametoa wito kwa viongozi wa halmashauri, serikali za mitaa, viongozi wa dini, walimu , wahamasishaji wa jamii na wadau wote kushiriki kikamilifu katikakampeni hyo ili kufikialengo.

Awali Ofisa wa Wizara ya Afya Mpango wa Chanjo Salama, Zainab Nyamgumi, alisema chanjo hiyo ni muhimu kwa Watoto hata kama waliwahi kuchanjwa awali.

Amesema chanjo hiyo ni muhimu na inaelekezwa na Shiria la Afya Duniani (WHO) kwa nchi kuitumia.

“Hii chanjo inatolewa kama nchi inaonekana inahatari ya mlipuko wa ugonjwa wapolio. Ni chanjo ambayo kwenye ratiba ya kawaida ya utoaji wa chanjo haipo.

Ndiyo mana tunasema hatakama mtoto amekamilisha chanjo lazima na hii chanjo apewe,”amesema Zainab.Alibainisha ni chanjo maalumu ambayo WHO inaelekeza nchi kuitumia pindi kunapo kuwa na hatari hiyo.

“Kwa hiyo hata mtoto ambaye amekamilisha chanjo bado anahatari kama hatapewa hii chanjo iliyopendekezwa na Shirikala Afya Duniani,”amebainisha.

Mganga Mkuu wa Mkoawa Dar es Salaam, Mohamed Mang’una, amehamasisha wazazi, walezi na wananchi. Kuhakikisha Watoto walengwa wanafikiwa na kupata huduma hiyo itakayo tolewa bila malipo.






 



Na Lusungu Helela, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Mhe. Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi Jama Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho, Mhe.Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.










Na Mwandishi Wetu, Pwani
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Forodha na Ushuru wa Bidhaa, imetoa elimu kwa wadau wa Forodha mkoani Pwani kuhusu mabadiliko ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2026, huku wazalishaji wakihimizwa kutumia fursa za unafuu wa ushuru wa forodha katika malighafi za uzalishaji.

Elimu hiyo imewaleta pamoja wawekezaji wa viwanda, mawakala wa Forodha na watumishi wa TRA, ikiwa na lengo la kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko hayo na namna yanavyoweza kutumika kuongeza uzalishaji wa bidhaa za ndani.

Akifungua mafunzo hayo, Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani, Peter Eliyona, amesema mabadiliko hayo ni muhimu katika kuboresha utendaji kazi na kuongeza uzalishaji wa bidhaa za ndani, huku akiwataka wawekezaji kutumia fursa za unafuu wa kodi kuongeza uzalishaji na ajira.

Mafunzo hayo yameendeshwa na Afisa Forodha Mkuu, Allan Maduhu, ambaye amesema mabadiliko hayo yamelenga kulinda viwanda vya ndani na kutoa unafuu wa ushuru wa forodha kupitia utaratibu wa Duty Remission kwa malighafi zinazotumika kuzalisha bidhaa nchini.

Amesema hatua hiyo inalenga kupunguza gharama za uzalishaji, kuhamasisha uwekezaji, kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa nchini pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa muhimu kupitia mpango wa Import Substitution.

Kwa mujibu wa Maduhu, Serikali imetoa unafuu wa ushuru wa forodha kwa malighafi za kuzalisha bidhaa mbalimbali, zikiwemo sabuni, nguzo za umeme za zege, nyaya za umeme, misumari na bidhaa za chuma.

Malighafi nyingine zinazonufaika na unafuu huo ni za kutengeneza vifungashio vya maboksi, vifungashio vya kuhifadhi chai na kahawa iliyochakatwa, vifungashio vya mbegu za kilimo pamoja na vifungashio vya maziwa.

Naye mwakilishi wa JFAWM Motors, Farida Ngwekerwa, amepongeza mabadiliko hayo akisema yatasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kurahisisha upatikanaji wa bidhaa kwa wananchi.

TRA imewataka watumishi na wawekezaji kuendelea kuzingatia mabadiliko ya sheria na kutumia fursa zilizopo, hatua ambayo itasaidia kukuza uzalishaji wa ndani, kuongeza ajira na kuimarisha mchango wa sekta ya viwanda katika uchumi wa Taifa








-Aomba Watanzania wafanye tathmini kwenye maeneo wanayoishi

-Ampongeza Mhe. Ndejembi kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imejipanga vema kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza wakati wa mvua kubwa za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi ujao hasa katika maeneo yanayopata mvua nyingi.

Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma, leo (Alhamisi, Agosti 27, 2026) wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukoba Mjini, Mha. Johnston Mutasingwa, kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kukabiliana na changamoto ya uharibifu wa miundombinu ya barabara na makazi ya wananchi kulingana na tahadhari ambayo imetolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) juu ya uwepo wa El-Nino yenye nguvu.

“Ni kweli tumepata tahadhari kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini juu ya uwepo wa mvua kubwa za El-Nino na hasa kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa ambako mvua hizo zinatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Septemba ama Oktoba mwanzoni. Serikali imejipanga kwa kuandaa mifereji katika maeneo hayo ili kuondoa uwezekano wa maji kurundikana.” 

Waziri Mkuu amesema Serikali imeelekeza TANROADS na TARURA zifanye ukaguzi wa barabara, madaraja, makalavati na mifereji ya maji ili kubaini mapema maeneo korofi yanayoweza kuathiriwa ili kuhakikisha wananchi hawakosi miundombinu kutokana na mafuriko.

“Bunge lako tukufu lilielekeza fedha za mifuko ya barabara ziwe zinakwenda moja kwa moja kwenye mifuko ya barabara badala ya Serikali kuu. Nimpongeze Waziri wa Fedha pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kuanza kutekeleza uamuzi huo ambapo kwa mwezi zaidi ya sh. bilioni 320 zinaenda moja kwa moja kweye mifuko na kuiwezesha kukabiliana na mambo kama haya,” amesema.

Amewataka Watanzania wachukue tahadhari kwa kila mmoja kufanya tathmini ya mahali wanapoishi kwa kuangalia mazingira ya mahali walipo kwani wanajua ni wapi maji huwa yanapita au yanatuama. “Tuendelee kuchukua hizo tahadhari ili maafa yasitokee ilhali tumeshatahadharishwa,” amesisitiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amempongeza Deogratius John Ndejembi kwa kuaminiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu ya CCM na kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dkt. Mwigulu ameitumia nafasi hiyo pia kumpongeza Rais Samia kwa kuwa na jicho la kipekee hadi akamuona Mheshimiwa Ndejembi. Amesema kiongozi huyo anazo sifa zinazomfanya astahili kupewa dhamana hiyo kubwa ya kitaifa.

“Mheshimiwa Naibu Spika, Deogratius Ndejembi ni kiongozi mahiri sana, ni kiongozi makini, ni kiongozi mchapakazi anayefanya kazi bila kuchoka ili Watanzania waweze kupata manufaa. Ndejembi pia ana sifa za unyenyekevu na upole, ni mtu rahimu asiye na hiana ndani yake,” amesema.

Waziri Mkuu amemhakikishia Mheshimiwa Ndejembi kuwa yeye pamoja na mawaziri wenzake wako tayari kushirikiana naye wakati akitekeleza majukumu yake mapya katika kuijenga Tanzania.



Na Janeth Raphael - MichuziTv


MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Udhibiti wa Visumbufu Tanzania (TPHPA) imesema hatua za kudhibiti visumbufu na magonjwa ya mimea zimewezesha kuokoa mazao kwa kiwango kikubwa na kuimarisha uwezo wa Tanzania kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru, amesema hayo jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mamlaka kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na mipango ya mwaka 2026/27.

Amesema katika kipindi hicho, TPHPA iliweka nguvu katika kuimarisha afya ya mimea, kudhibiti visumbufu na magonjwa, kuboresha huduma za maabara, kutumia teknolojia za kisasa na kuhakikisha mazao yanayozalishwa nchini yanakidhi viwango vinavyohitajika katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wa udhibiti wa ndege waharibifu, Prof. Ndunguru amesema hatua zilizochukuliwa na Mamlaka zimefanikisha kuokoa takribani tani milioni moja za mazao, yakiwemo nafaka, mahindi, ngano na mpunga.

Katika kukabiliana na viwavi jeshi, TPHPA ilifanya udhibiti katika maeneo yaliyoathirika kwa kushirikiana na wakulima pamoja na kampuni zinazozalisha viuatilifu.

Juhudi hizo zilifanyika katika eneo la takribani ekari 228,525 na kusaidia kuokoa takribani tani 342,737 za mazao mbalimbali, huku mahindi yakiwa miongoni mwa mazao yaliyonufaika.

Aidha, TPHPA ilichukua hatua za kudhibiti changamoto ya balae fanya katika maeneo yaliyoathirika, hatua iliyosaidia kulinda takribani ekari 70,136 za mazao.

Prof. Ndunguru amesema mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha uzalishaji wa mazao nchini unaendelea kuwa salama na wenye tija, huku Tanzania ikiimarisha uwezo wa kuuza mazao yake katika masoko ya kimataifa.

Kwa mwaka wa fedha 2026/27, Mamlaka inalenga kuendeleza udhibiti wa visumbufu na magonjwa ya mimea, kuimarisha mifumo ya afya ya mimea na kuongeza matumizi ya teknolojia ili kulinda uzalishaji na ushindani wa mazao ya Tanzania katika masoko ya kimataifa.




Serikali imejipanga kuhakikisha watoto wanapatiwa chanjo ya Polio ili kuendelea kuilinda Tanzania dhidi ya ugonjwa huo, licha ya nchi kutokuwa na mgonjwa wa Polio kwa sasa.

Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika hafla fupi ya ufunguzi wa kampeni ya utoaji chanjo ya Polio iliyofanyika katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Alhaj Shekimweri alisema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha afya za watoto nchini, akieleza kuwa watoto wamekuwa sehemu muhimu ya programu mbalimbali za afya zinazotekelezwa na serikali.

Aliongeza kuwa kama Wilaya ya Dodoma imepewea lengo la kuwafikia watoto 207,096 katika zoezi hilo, ikiwa ni sehemu ya jumla ya watoto 1,003,061 katika Mkoa wa Dodoma wanaolengwa katika maeneo husika.

“Viongozi, watendaji wa serikali, shule, kamati na bodi za shule wamehamasishwa kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo, ikiwamo kuwafikishia wazazi ujumbe kuhusu umuhimu wa kuwapeleka watoto kupata chanjo ingawa hatuna changamoto ya mgonjwa wa Polio nchini, ni muhimu kujihami kwa kuwakinga watoto wetu,” alisema Alhaj Shekimweri.

Kwa upande wake, mkazi wa Dodoma, Rosmith Mkoko aliishukuru serikali kwa kuwezesha upatikanaji wa chanjo hiyo, akiwataka wazazi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo.

“Chanjo ni muhimu katika kuwalinda watoto dhidi ya magonjwa na kwamba wazazi wanapaswa kutumia fursa hii kuhakikisha watoto wao wanapata kinga. Nawashauri wazazi wawalete watoto wapate chanjo hizi ili ziweze kuwalinda,” alisema Mkoko.

Zoezi hilo linatarajiwa kuendelea hadi tarehe 30 Agosti, 2026 kwa kushirikisha jamii, hususani wazazi na walezi, ili kuhakikisha watoto wote waliolengwa wanapata chanjo kwa wakati.




HALMASHAURI ya wilaya ya Siha inatarajia kutoa chanjo ya ugonjwa wa Polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka 10 wapatao 42049 ambapo wazazi na walezi wametakiwa kuhakikisha zoezi hilo linawafikia watoto wote walengwa ili kukabiliana na ugonjwa wa Polio.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Mkuu wa wilaya hiyo, Dkt. Christophe Timbuka wakati wa uzinduzi uliofanyika katika shule ya msingi Wiri ambapo kampeni hiyo itafanyika kwa siku nne na kudai kuwa,  serikali imeendelea kuweka mkazo katika kuimarisha na kulinda afya za wananchi hususan afyavna usalama wa watoto.

Dkt. Timbuka alisema kuwa, ugonjwa wa Polio ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Polio ambapo huathiri mfumo wa fahamu na kusababisha kupooza kwa viungo na hivyo kupelekea ulemavu wa kudumu.

"Jambo la msingi mnalopaswa kuelewa ni kwamba Polio inazuilika kwa chanjo na ndio maana Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuhakikisha watoto wote walio katika kundi lengwa la umri chini ya miaka kumi wanapatiwa chanjo kwa wakati" alisema Dkt. Timbuka.

 Alisema kuwa, Tanzania imeendelea kulinda mafanikio yake katika mapambano dhidi ya Polio, lakini bado tunapaswa kuwa waangalifu kutokana na uwepo na mzunguko wa virusi vya Polio katika baadhi ya maeneo ya Afrika na duniani. 

Aliongeza kuwa, Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe inasisitiza  kuwa, kampeni ya chanjo kwa watoto chini ya miaka 10 ni sehemu ya juhudi za kuongeza kinga ya jamii na kuzuia uwezekano wa maambukizi kwa hiyo, kampeni hiyo siyo jambo la kawaida la utoaji wa huduma za afya, bali ni juhudi ya kitaifa ya kulinda kizazi cha sasa na kijacho dhidi ya ugonjwa unaoweza kusababisha ulemavu wa kudumu na kupoteza nguvu kazi ya taifa letu.

Alibainisha kuwa, chanjo hiyo itatolewa katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha watoto wote wanafikiwa na  timu ya wataalamu wa afya pamoja na wahamasishaji waliopata mafunzo watatoa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya, Shule za Awali na Msingi, vituo vya malezi ya Watoto (Daycare), Makao ya Watoto,  Maeneo ya mikusanyiko ya jamii, huduma za nyumba kwa nyumba na Maeneo mengine yatakayobainishwa katika mpango kazi wa Halmashauri za vijiji.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga mkuu wa wilaya ya Siha, Dkt. Nsubili Mwakapeje alisema kuwa, maandalizi yote ya utoaji chanjo yamekamilika kama serikali ilivyoelekeza  ambapo timu za wataalam zipo tayari kuingia katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Siha kuwafikia watoto walengwa.

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Siha, Dancan Urrasa alitumia nafasi hiyo kuwasihi Madiwani kutoa ushirikiano kwa wataalam hao wa afya kwa kuwaelimisha wananchi kuwatoa watoto waweze kupatiwa chanjo hiyo.

"Natambua sisi Madiwani ndio tupo karibu na wananchi wetu sasa tushirikiane na wataalam wetu wa afya kuwaelimisha wananchi wetu kutambua umuhimu wa chanjo hii ili waweze kuwatoa watoto wote walengwa wapatiwe chanjo kwa hizi siku nne za kampeni hii" alisema Urrasa.






Miaka tisa baada ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza, mtangazaji wa redio Willy Nkya amepanda tena mlima huo, safari hii akiwa na jukumu la kuripoti matukio kila siku akiwa katika kilele cha mlima huo.

Nkya, ambaye alipanda mlima Kilimanjaro kwa mara ya kwanza mwaka 2017 muda mfupi baada ya kumaliza chuo, anasema safari yake ya mwaka huu imekuwa ya tofauti kwa namna kadhaa. Amepanda mlima akiwa na uzoefu zaidi akiwa na maandalizi ya kutosha ya mwili na uelewa mzuri wa namna ya kukabiliana na uchovu, baridi na mabadiliko ya hali ya hewa kadri anavyopanda.

Tofauti nyingine kubwa ilikuwa mawasiliano; safari hii ameweza kuwasiliana na kutekeleza majukumu yake ya kikazi katika maeneo mengi ya mlima.

Akiwa katika safari hiyo, alitakiwa kurekodi na kutuma video, sauti, picha na taarifa mbalimbali kwa ajili ya matangazo ya redio na mitandao ya kijamii.

Anasema mtandao wa Viwango wa Yas ulimwezesha kuendelea kutekeleza majukumu yake katika maeneo mengi aliyopita kuelekea kileleni, huku pia akiendelea kuwasiliana na familia na marafiki.

“Tofauti na mwaka 2017 ambapo mawasiliano yalikua ni ya shida, safari hii mambo yalikua ni tofauti, nimeweza kutuma video, picha, sauti na kuwasiliana bila matatizo na watu wangu wa karibu,” anasema Nkya.

“Kupanda mlima Kilimanjaro si mchezo. Kuna wakati unahisi kabisa uko kwenye dunia nyingine. Mtandao wa viwango wa Yas ambao unapatikana vizuri kabisa katika maeneo mengi ya mlima tuliyopita umenisaidia kuendelea kutimiza majukumu ya kazi zangu bila shida.” anasema.

Nkya aliendelea na safari hiyo hadi kufika Uhuru Peak, mita 5,895 kutoka usawa wa bahari, kilele cha juu zaidi barani Afrika.

Anasema safari yake ya mwaka huu imempa picha tofauti na ile ya miaka tisa iliyopita, hasa kwa namna ambavyo mawasiliano yalivyorahisisha mambo mengi katika mazingira ya mlima huo wenye changamoto nyingi.

“Kwangu hii ndiyo maana ya Mtandao wa Viwango, mtandao unaokuwezesha kuendelea kufanya kile unachotaka kufanya hata ukiwa katika safari yenye changamoto. Nimepanda na Yas hadi Uhuru Peak na nimeendelea kuwasiliana na dunia,” anasema.

Kwa Nkya, kufika Uhuru Peak hakukuwa mwisho wa safari pekee, bali pia ujumbe kwamba kila mtu ana kilele anachotamani kukifikia.

“Kila mmoja wetu ana kilele anachopanda katika maisha yake. Cha kwangu safari hii kilikuwa Uhuru Peak.”




Na WMA - Mwanza 

Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Mwanza umezitaka kampuni zinazojihusisha na uzalishaji wa mabati kuhakikisha zinazingatia matakwa ya sheria ya vipimo na viwango vya ubora vilivyowekwa, ili kulinda haki na fedha za wananchi.

Akizungumza mapema leo Agosti 27, 2026 mara baada ya zoezi la ukaguzi wa kushtukiza katika baadhi ya viwanda vya uzalishaji wa mabati mkoani Mwanza, Meneja wa Mkoa wa Wakala huo, Karim Zuberi, amesema kupitia kaguzi na taarifa zinazotolewa na wananchi, ndani ya kipindi cha mwaka huu, tayari wamebaini na kuchukua hatua dhidi ya wazalishaji watano waliobainika kuzalisha mabati yasiyokuwa na vipimo sahihi.

Zuberi amesema wananchi wanapaswa kuwa makini wanaponunua mabati na kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapohisi kuuziwa bidhaa zisizokuwa na vipimo sahihi, akiwataka pia wafanyabiashara kuacha tabia ya kuwapotosha wateja kuhusu vipimo vya unene wa mabati.

Amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakitoa taarifa zisizo sahihi kwa wateja kwa kuwafanya waamini kuwa kadri namba ya 'Gauge' inavyokuwa kubwa ndivyo bati linavyokuwa bora, wakati kinyume chake ndicho sahihi, ambapo bati lenye namba ndogo ya "Gauge' huwa na unene mkubwa zaidi.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu viwango vya bidhaa wanazonunua ili kuepuka udanganyifu unaoweza kusababisha hasara, hususan katika ujenzi wa makazi na miundombinu mingine.

Kwa upande wake, Biyolelo Ndaisaba, mmoja wa viongozi wa kampuni inayojihusisha na uzalishaji wa bidhaa hizo mkoani Mwanza, amesema udanganyifu katika vipimo vya mabati ni sawa na kuhujumu jasho la wananchi wanaotumia fedha zao kujenga makazi na kuendeleza shughuli nyingine.

Amesema kampuni yao imeendelea kuwa kinara katika kuzingatia usahihi wa vipimo vinavyotakiwa kisheria, akisisitiza kuwa wazalishaji wote wana wajibu wa kuhakikisha bidhaa wanazozipeleka sokoni zinakidhi viwango kwa manufaa ya walaji

Wakala wa Vipimo Mkoa wa Mwanza unaendelea na zoezi la ukaguzi wa bidhaa mbalimbali, linalofanyika kwa utaratibu wa kawaida pamoja na ukaguzi wa kushtukiza, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wananchi wanalindwa dhidi ya bidhaa zisizokidhi vipimo sahihi.





Na Janeth Raphael - MichuziTv - Bungeni Dodoma

Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kumwona Deogratius Ndejembi kuwa miongoni mwa viongozi wanaoweza kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu ya kitaifa, akielezwa kuwa msaidizi wake mpya katika nafasi ya Makamu wa Rais.

Dkt Mwigulu ametoa pongezi hizo leo Alhamisi, Agosti 27, 2026, wakati akijibu maswali ya papo kwa papo katika Bunge jijini Dodoma, akianza kwa kumpongeza Ndejembi ambaye amependekezwa kushika nafasi hiyo.

Ndejembi, ambaye ni Mbunge wa Chamwino mkoani Dodoma, alipendekezwa jana Jumatano, Agosti 26, 2026, na vikao vya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pendekezo hilo limekuja baada ya Dk Emmanuel Nchimbi kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais, hatua iliyokubaliwa na Rais Samia.

Kabla ya kupewa nafasi hiyo, Ndejembi alikuwa Waziri wa Nishati, nafasi aliyohudumu akisimamia masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati nchini.

Akizungumza Bungeni, Dkt. Mwigulu amemtakia Ndejembi mafanikio katika jukumu hilo jipya, huku akimpongeza Rais Samia kwa kumuamini na kumteua kuwa sehemu muhimu ya uongozi wa Serikali.

Uteuzi wa Ndejembi sasa unafungua ukurasa mpya katika uongozi wa Serikali, huku akitarajiwa kuendelea na majukumu ya kitaifa kwa nafasi yake mpya baada ya taratibu za kikatiba kukamilika.







Top News