.jpeg)
.jpeg)
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Neema Peter Majule, ameibana Serikali akiitaka kueleza mkakati wake wa kuwasaidia wahitimu wa vyuo vikuu kutumia vyeti vyao vya taaluma kama dhamana ya kupata mikopo kwa ajili ya kuanzisha biashara na miradi ya uwekezaji.
Akizungumza bungeni Jijini Dodoma Mei 21, wakati akiuliza swali namba 409 kwa Wizara ya Fedha, Dkt. Majule alisema kuwa sera ya elimu ya juu kwa sasa inalenga kuzalisha wahitimu wanaoweza kujiajiri na pia kuajiri wengine kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alieleza kuwa vyuo vikuu vingi Duniani vimeanzisha idara za Career Development kwa lengo la kuwaandaa vijana hao kuingia kwenye ulimwengu wa biashara na uwekezaji mkubwa.
Katika swali lake la kwanza, Dkt. Majule alihoji kama Serikali ipo tayari kuwabaini wahitimu wenye ubunifu na uwezo wa kuanzisha miradi mikubwa, na kuwapatia mikopo mikubwa ili waweze kufungua biashara zitakazosaidia kutoa ajira kwa Watanzania wengine.
Aidha katika swali lake la pili, mbunge huyo alihoji kama Serikali ipo tayari kutoa mitaji mikubwa kwa wahitimu watakaotumia vyeti vyao vya taaluma kama dhamana ya mikopo, au kama bado watahitajika kuwa na dhamana nyingine za ziada ili kupata fedha hizo.
Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Luswetula, amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira rafiki ya kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia programu mbalimbali ya mikopo yenye masharti nafuu, na tayari Serikali imetoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya kuwawezesha vijana kujiajiri na kuanzisha shughuli za kiuchumi.
Hata hivyo, ameeleza kuwa changamoto kubwa iliyopo ni kwamba wahitimu wengi wa vyuo vikuu bado hawana uzoefu wa kutosha katika kuendesha biashara kubwa na uwekezaji wa kiwango kikubwa.
Amesema Serikali inaamini vijana wanapaswa kuanza na biashara ndogo huku wakijengewa uwezo wa ujasiriamali, usimamizi wa biashara na uwekezaji kabla ya kufikia hatua ya kupata mikopo mikubwa.
📍Njombe
Mradi mkubwa wa uzalishaji wa kokoto uliopo mtaa wa Kambarage kata ya Njombe Mjini, unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa kokoto na kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza mapato ya Serikali katika Mkoa wa Njombe.
Mradi huo unaomilikiwa na mchimbaji mdogo wa madini ya ujenzi, Isaya Boniface, umefungwa mtambo mkubwa wa kusaga kokoto wenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 1,000 kwa siku kwa kushirikiana na kampuni ya India ya Shree Sonal Earth Ltd iliyotoa usaidizi wa kitaalam katika utekelezaji wake.
Akizungumza kuhusu mradi huo, Boniface amesema uwekezaji huo utamaliza changamoto ya upatikanaji wa kokoto ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikisafirishwa kutoka mikoa ya Iringa, Dodoma na Pwani, hususan Lugoba, kwa matumizi ya miradi mbalimbali ya ujenzi mkoani Njombe.
Amesema mradi huo utasaidia kupunguza gharama za ujenzi, kuongeza ajira kwa wananchi, kukuza mzunguko wa fedha pamoja na kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayohitaji kokoto kwa kiwango kikubwa.
Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi Lucas Mlekwa, amesema mradi huo ni miongoni mwa uwekezaji muhimu unaotarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kupitia madini ujenzi.
Amesema kutokana na uwezo wa uzalishaji wa tani 1,000 za kokoto kwa siku, Serikali inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi milioni 2.3 kwa siku kupitia tozo za mrahaba na ada ya ukaguzi, huku makadirio ya mapato ya mwaka yakifikia kati ya shilingi milioni 400 hadi 600.
“Mkoa wa Njombe unaendelea kushuhudia ukuaji mkubwa wa sekta ya ujenzi wa miundombinu, makazi na miradi ya Serikali, hivyo uwepo wa mradi huu utaongeza upatikanaji wa malighafi muhimu kwa utekelezaji wa miradi hiyo,” amesema Mhandisi Mlekwa.
Aidha, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo kwa kushirikiana na taasisi za kifedha ili kuwawezesha kupata mikopo na vifaa vya uzalishaji.
Mhandisi Mlekwa ameongeza kuwa miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa mkoani Njombe, ikiwemo mradi wa kiwanda cha chuma, itaongeza mahitaji ya kokoto na kufungua zaidi fursa za uwekezaji katika sekta ya madini ya ujenzi.
NA FARIDA MANGUBE, MOROGORO
Katika kipindi hiki cha kasi ya maendeleo ya teknolojia na mabadiliko makubwa ya mifumo ya mawasiliano duniani, waandishi wa habari hususan wanawake wametakiwa kuongeza juhudi katika kujiendeleza kielimu na kujikita kwenye taaluma za ubobezi ili kuendana na ushindani wa sekta ya habari na kuchangia maendeleo ya jamii.
Wito huo umetolewa mkoani Morogoro wakati wa Mahafali ya 47 ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ambapo baadhi ya wahitimu wa fani mbalimbali, akiwemo mwanahabari Kelvin Gwabala na Sophia Makame, walizungumza kuhusu umuhimu wa wanahabari kuendelea kujifunza na kuongeza ujuzi wa kitaaluma.
Akizungumza mara baada ya kuhitimu, Kelvin Gwabala amesema maendeleo ya teknolojia yamebadilisha mfumo wa utoaji habari, hivyo wanahabari wanapaswa kujifunza mbinu mpya za uandishi na matumizi ya teknolojia ili kubaki na ushindani katika tasnia hiyo.
Kwa upande wake, Sophia Makame amesisitiza umuhimu wa wanawake waliopo kwenye sekta ya habari kujiamini na kutumia fursa za elimu kujijengea uwezo wa kitaaluma, akieleza kuwa elimu ndiyo msingi wa mafanikio katika kazi za habari.
Profesa Raphael Chibunda ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), amesema chuo hicho kinaendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia pamoja na kuongeza programu mbalimbali zinazolenga kuwaandaa wahitimu wenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji ya soko la ajira la sasa.
Aidha, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Andrew Massawe, amesema SUA imeendelea kupata mafanikio katika sekta za elimu, utafiti na ubunifu, huku akibainisha kuwa chuo hicho kitaendelea kuwekeza katika kukuza taaluma zinazochochea maendeleo ya taifa.
Mbunge wa Jimbo la Katoro, Mhe. Mhandisi Kija Limbu Ntemi, ameiomba Wizara ya Ujenzi kuanza ujenzi wa barabara ya Ushirombo–Katoro yenye urefu wa km 47 kwa kutokea upande wa Katoro, ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo.
Akichangia wakati wa uwasishwaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi Bungeni, Mhe. Ntemi amesema ujenzi wa barabara hiyo tayari umeanza kwa kutokea Ushirombo, lakini wananchi wa Katoro hususan eneo la Stamico-CCM bado wanateseka sana na vumbi.
“Namuomba Mhe. Waziri achakate ili barabara hii ianze kujengwa pia kwa kutokea Katoro. Wananchi wangu wamechoka na vumbi, hasa pale Stamico-CCM,” alisema Mhe. Ntemi.
Aidha, mbunge huyo ameishukuru Wizara kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Chibingo–Chigunga, akisema hatua hiyo itarahisisha shughuli za kiuchumi na usafirishaji kwa wakazi wa maeneo hayo.
Mhe. Ntemi ameitaka Wizara kuhakikisha inawapata wakandarasi waliobobea na wenye rekodi nzuri ili kuepusha ujenzi wa barabara zisizodumu. Alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya wakandarasi kufanya kazi zisizo na kiwango, na kusababisha barabara kuharibika mara kwa mara.
Katika kueleza umuhimu wa ubora, alitolea mfano barabara ya Kahama–Masumbwe–Ushirombo–Runzewe ambayo amesema imebaki kuwa bora hadi leo licha ya kupitishwa na magari makubwa ya mizigo. “Waziri amtafute huyo mkandarasi aliyejenga barabara hii, ndiye afae kupewa kazi za kujenga barabara za nchi hii,” alishauri.
Vilevile, Mhe. Ntemi alimshukuru Rais wa Awamu ya Sita kwa namna anavyoendelea kufungua barabara mbalimbali nchini, akisema hatua hiyo inachochea maendeleo na kuunganisha mikoa na wilaya kwa urahisi.
Barabara ya Ushirombo–Katoro ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotarajiwa kufungua fursa za kiuchumi kwa wakazi wa Jimbo la Katoro na maeneo jirani pindi itakapokamilika.
.png)
.png)

Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali za maendeleo zilizotekelezwa katika Mkoa wa Kigoma, akisema zimekuwa faraja kubwa kwa wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za muda mrefu za miundombinu.
Mbunge huyo pia alimpongeza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kwa juhudi zake katika kusimamia utekelezaji wa miradi ya ujenzi na maboresho ya barabara nchini.
Akichangia hoja ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/27 leo Mei 21, 2026, bungeni jijini Dodoma, Baba Levo alisema wananchi wa Kigoma Mjini wamepitia mateso makubwa kwa muda mrefu kutokana na changamoto za miundombinu, lakini sasa wameanza kuona matumaini kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya serikali.
Amesema maendeleo yanayoendelea kufanyika Kigoma yamefuta machozi ya wananchi wengi ambao kwa miaka mingi walikuwa wakihitaji maboresho ya barabara na huduma nyingine muhimu za usafiri.
“Wananchi wa Kigoma Mjini wameteseka sana kwa muda mrefu, lakini leo hii serikali imefuta machozi yao kutokana na kazi kubwa inayofanyika. Tunamshukuru Rais Samia pamoja na Waziri Ulega kwa kusikiliza kilio cha wananchi,” alisema Baba Levo.
Katika mchango wake, mbunge huyo pia alimuomba Waziri Ulega kuyachukua maoni na changamoto zilizotolewa na wabunge mbalimbali kama sehemu ya kuongeza kasi ya utatuzi wa kero za wananchi.
Aidha, Baba Levo aliendelea kuishauri Wizara ya Ujenzi kuangalia uwezekano wa kujenga daraja la juu (flyover) katika moja ya maeneo hatarishi ya Kigoma Mjini ambako wananchi wamekuwa wakigongwa mara kwa mara kutokana na msongamano na changamoto za miundombinu ya barabara.
“Naomba nipate heshima ya kuwa na barabara za juu Kigoma Mjini. Tumeomba daraja kama lile la Manzese kwa sababu kuna eneo wananchi wanagongwa sana, hivyo tunahitaji suluhisho la kudumu,” alisema.
Kauli hiyo imeibua mjadala bungeni huku wabunge wengine wakisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya kisasa ili kuimarisha usalama wa wananchi na kukuza uchumi wa maeneo mbalimbali nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Mzinga, Mhe. Balozi Luteni Jenerali (Mstaafu), Charles Lawrence Makakala, amesema utekelezaji wa mpango huo utakuwa msaada mkubwa kwa wanawake wa vijijini ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikumbana na changamoto ya kutafuta nishati kwa ajili ya kupikia.
“Akina mama wa vijijini wanapata adha kubwa kutafuta nishati ya kupikia. Madhara ya kiafya wanayoyapata wao pamoja na watoto wao ni makubwa kwa sababu watoto pia hushiriki katika shughuli za maandalizi ya chakula. Hatua hii itasaidia utekelezaji wa sera ya nishati safi lakini pia kuinua ustawi wa jamii na uchumi endelevu,” amesema Makakala.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu, amesema ushirikiano huo utaongeza uzalishaji wa mkaa mbadala utokanao na mabaki ya mimea pamoja na uzalishaji wa majiko banifu kwa bei nafuu zaidi na hivyo kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, amesema makubaliano hayo pia yanakwenda kuongeza aina za nishati safi za kutumika zenye gharama nafuu zaidi lengo likiwa kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Mhandisi Saidy amesema kuwa kati ya Watanzania wanne, ni mmmoja tu ndo anatumia nishati safi ya kupikia. Hivyo kupitia ushirikiano huo unaokwenda kuongeza uzalishaji wa mkaa mbadala pamoja na majiko banifu, idadi ya Watanzania wanaotumia nishati safi ya kupikia itakwenda kuongezeka.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mzinga, Brigedia Jenerali Mhandisi Seif Athuman Hamisi, amesema makubaliano hayo yatahusisha maeneo mbalimbali ikiwemo kufanya tafiti za kuboresha matumizi ya majiko na mkaa safi ili kuhakikisha teknolojia hizo zinakidhi mahitaji ya wananchi.
Jamii imetakiwa kuendelea kuwajali watoto wenye mahitaji maalum na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapa upendo, msaada na ukaribu ili kuwajengea matumaini ya maisha bora.
Wito huo umetolewa leo, Mei 21, 2026, na Afisa Ushirika wa Wilaya ya Mvomero, Aidan Emily Nyamweru, wakati wa ziara ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Wilaya ya Mvomero katika Kituo cha Kulelea Watoto Wenye Mahitaji Maalum cha Amani, ambapo walifanya matendo ya huruma ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Jukwaa la Ushirika la Wilaya pamoja na maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani.
Katika ziara hiyo, tume hiyo imekabidhi mifuko miwili ya unga, sukari, daftari, rimu na kalamu kwa ajili ya watoto wa kituo hicho.
Afisa Ushirika huyo amesema kuwa kabla ya kufanyika kwa jukwaa la ushirika wilaya, wamekuwa na utaratibu wa kurejesha kwa jamii kupitia matendo ya huruma ili wananchi waelewe mchango wa ushirika katika jamii.
Amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa msingi wa saba wa ushirika unaosisitiza umuhimu wa kujali jamii.
Kwa upande wake, Mwalimu wa Shule ya Msingi Amani Mvomero, Athuman Shambani, ameushukuru Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa msaada huo huku akiomba wadau wengine kuendelea kusaidia vituo vya kulelea watoto yatima na wenye mahitaji maalum.
“Watoto hawa wanahitaji ukaribu, upendo na msaada kutoka kwa jamii ili wajione kuwa ni sehemu ya jamii,” alisema Athuman.
MAKAMU WA Rais Dkt Emmanuel Nchimbi amewataka waandishi waendesha ofisi kuongeza jitihada katika kutekeleza majukumu yao bila woga na kwamba Serikali inatambua mchango wao mkubwa kwa kazi wanayoifanya na ndio sababu Rais Dkt Samia amekubali kuwa mlezi wa chama hicho.
Aidha amewataka kutoa ushauri mzuri Kwa viongozi wao Kwa kutumia uzoefu waliokuwa nao pale yanapotokea mazingira ya kutoa ushauri katika taasisi hizo kwa kuwa itawajengea heshima na kufanya kuaminika.
Dkt Nchimbi akizungumza Leo Mei21, 2026 kwenye mkutano mkuu wa chama hicho unaendelea katika kituo cha Mikutano cha Tanzania Convention Center Ngurdoto Arusha, amesema waendesha ofisi ni watu muhimu na hawapaswi kubezwa Kwa namna yoyote Ile.
" Taasisi yenu inaaminika na ndio sababu Rais amekubali kuwa mlezi wenu, niwaombe tu kuendelea kuwa waaminifu na mfanye kazi Kwa uadilifu wakati wote wa utekelezajibwa majukumu yenu," amesema.
Akisoma risala ya chama hicho Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi waendesha ofisi Tanzania (TAPSEA),Bi.Zuhura Songambele Maganga amekemea tabia ya udhalilishaji inayoendelea kufanywa kupitia mitandao ya kijamii kuhusu kada ya Waandishi waendesha ofisi.
" Sisi kama waandishi waendesha ofisi maarufu kama Makatibu Muhtasi tunasikitishwa na tabia ya baadhi ya udhalilishaji inayoendelea huko mitandaoni, hii ni kada inayojiheshimu na watendaji wamekuwa na maadili na wanafuata miongozo ya Serikali," amesema.
Amesema kada hiyo ya waandishi waendesha ofisi isidhalilishwe kama inavyofanyika kwenye mitandao ya kijamii na majukwaani na kwamba ni taasisi inayoheshimika na miongoni mwao wako wake wa viongozi serikalini hivyo hawawezi kufanya mambo machafu ofisini kwao.
Amesema tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kukubali kuwa maezi wa chama hicho, wamekuwa na ujasiri wa kutekeleza majukumu yao na kujiamini.
Aidha Bi.Zuhura amemuomba Rais Samia kuwaongezea mshahara endapo uchumi utaruhusu kutokana na majukumu mengi ambayo wamekuwa wakiyatekeleza kama waandishi waendesha ofisi.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa umma, Ridhiwani kikwete, amesema katika mwaka 2026/2027, Serikali imepanga kuongeza ajira mpya 45,000 ikiwemo kada ya Waandishi waendesha ofisi Ili kuboresha na kurahisisha utumishi wa umma nchini.
Mgeni rasmi
-Yazingumzia pia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika hospitali hiyo,idadi ya wagonjwa waliohudumiwa
Na Said Mwishehe,Michuzi TV
UONGOZI wa Hospitali ya Benjamin Mkapa umeanza rasmi maandalizi ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, sambamba na uzinduzi wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwa na Mfuko maalum utakaowezesha huduma za matibabu ya upandikizaji uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu pamoja na huduma za upandikizaji figo.
Akizungumza leo katika kikao na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi, amesema hospitali hiyo imeendelea kuwa tegemeo kubwa kwa wananchi kwa kuhudumia takribani watu milioni 10 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na wagonjwa kutoka nje ya nchi.
Amesema kwamba Julai 15, 2026, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 10 ya hospitali hiyo, wanatarajia kufanya harambee yenye lengo la kupanua huduma za kibingwa, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kutokana na hali hiyo, Prof. Makubi amesema pia hospitali hiyo imekuwa moja ya vituo muhimu vya tiba utalii nchini huku akifafanua kupitia harambee hiyo, hospitali inalenga kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 7 ndani ya kipindi cha miaka miwili, fedha zitakazosaidia kugharamia matibabu kwa wagonjwa 100.
“Kati yao, watoto 50 wanatarajiwa kufaidika na matibabu ya selimundu kupitia upandikizaji uloto, huku wagonjwa wengine 50 wakipatiwa huduma ya upandikizaji figo,” amesema Prof. Makubi na kuongeza tayari Sh.bilioni zimeshapatikana hivyo wanaendelea kuziomba taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi kuchangia kwa hiyari katika mfuko huo.
Hata hivyo, Prof. Makubi aliishukuru Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na taasisi zake ambazo, kwa kushirikiana na wadau wengine, zimefanikiwa kuchangia kiasi cha Shilingi bilioni 4 hadi sasa.
“Kama mnavyofahamu, gharama za matibabu ni kubwa sana kwa wagonjwa. Tuna kila sababu ya kuendelea kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alichangia Shilingi bilioni moja nje ya bajeti kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa mbalimbali.
“Mchango huo ulisaidia wagonjwa waliokuwa hawana uwezo wa kugharamia matibabu yao, ambapo yeye alilipia gharama zote. Jambo hilo lilirejesha furaha kwa watoto, familia zao pamoja na wagonjwa wa figo waliopatiwa matibabu.”
Kuhusu mafanikio ya hospitali hiyo amesema kwa sasa ina watumishi 1,073, wakiwamo madaktari bingwa 100 sambamba na kuwa na vitanda 450 kwa ajili ya huduma za wagonjwa.
Pia amesema kwa sasa inatoa huduma za kibingwa 20, zikiwamo huduma za kibingwa za juu 18. Baadhi ya huduma hizo ni upandikizaji uloto, upasuaji wa moyo kwa kufungua kifua, uchunguzi wa moyo, kuzibua mishipa ya damu, upasuaji wa uti wa mgongo, upasuaji kwa kutumia matundu madogo pamoja na ubadilishaji wa nyonga na magoti.
“Hospitali imepata mafanikio makubwa kutokana na uwekezaji wa Serikali kuanzia awamu ya nne hadi ya sita, ambapo kiasi cha Shilingi bilioni 283 kimewekezwa katika majengo na vifaa tiba.
“Hivyo, unaweza kuona namna hospitali ilivyojidhatiti katika kuimarisha na kuboresha huduma za afya,” amesema huku akisisitiza hospitali hiyo imeendelea kutoa huduma za tiba utalii kwa raia kutoka nje ya nchi, ambapo baadhi yao huja moja kwa moja kufuata huduma hospitalini hapo.
“Kwa mfano, mwaka jana tuliwahudumia wagonjwa 2,897 kutoka Burundi. Pia wapo wagonjwa wanaokuja moja kwa moja kutoka nchini humo pamoja na wengine kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.”
Ametaja mafanikio mengine ni kufanyika kwa maboresho makubwa ya mifumo ya TEHAMA ambayo imerahisisha utoaji wa huduma bora kuanzia usajili wa wagonjwa. Pia wameanza makundi matano ya huduma huru yanayowezesha mawasiliano ya moja kwa moja na wagonjwa.


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)








.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


