Na Victor Masangu, Kibaha

Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwakomboa wanawake katika kujikwamua kiuchumi Azania bank imeamua kuja na mpango kabambe uliopewa jina la Fanikisha Mwanamke Hodari ambao utaweza kuwasaidia kupata mikopo yenye riba nafuu ambayo itawasaidia kiasi kikubwa kuendesha shughuli zao na kujiingizia kipato lengo ikiwa ni kuodokana na wimbi la umasikini na kujikwamua kiuchumi.

Hayo yamebainisha na Meneja wa Azania bank tawi la Kibaha mjini Anna Monyo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na baadhi ya wanawake kutoka kata mbali mbali za Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa lengo la kuweza kuwapatia elimu na mafunzo mbali mbali yanayohusiana na fursa zilizopo ikiwa pamoja na jinsi ya kutumia mkopo ambao wanautoa wenye riba nafuu ya asilimia 1 kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Meneja huyo amebainisha kwamba lengo kubwa na mikakati ambayo wamejiwekea ni kuhakikisha kwamba wanamwezesha mwanamke kwa kumpatia mikopo ili aweze kupiga hatua na kusonga mbele zaidi na kutimiza ndoto zake alizonazo katika suala zima la kuweza kujikwamua kiuchumi na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo.

"Tunashukuru sana kukutana na baadhi ya wanawake wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kitu kikubwa ambacho tumekifanya ni kuweza kuwasogezea huduma yetu kwa ukaribu kwani tumeweza kufungua tawi letu la Azania bank hapa Kibaha na kwamba mtu anaweza kukopa kuanzia kiasi cha shulingi laki mbali hadi kiasi cha milioni 5 kulingana na uwezo wake alionao.

Meneja huyo amebainisha kwamba katika kutambua umuhimu wa wanawake wameamua kuja na akaunti hiyo maalumu ambayo itaweza kuwa ni mkombozi mkubwa ya kuwainua kiuchumi wanawake ambao ni wajasiriamali na kupitia akaunti hiyo wataweza kutimiza ndoto zao walizojiwekea.

Kadhalika ametoa wito kwa wanawake hao kuhakikisha wanajiunga katika vikundi mbali mbali vya ujasiriamali ili kuweza kupata fursa ya mikopo hiyo kwa urahisi na kwamba endapo wakiwa na kikundi wataweza kupatiwa mikopo hiyo ambayo itaweza kuwasaidia kuondokana na kuwa tegemezi na kuondokana na wimbi la umasikini.

Nao baadhi ya wanawake ambao wameweza kupata fursa ya kupatiwa elimu mbali mbali wameushukuru uongozi mzima wa Azania Bank tawi la Kibaha chini ya Meneja wake kwa kuweza kuona umuhimu mkubwa wa kuwatembelea na kuwapa mwenendo mzima wa elimu ambayo itaweza kuwasaidia katika suala zima la utunzaji wa fedha na kutimia vizuri fursa za mikopo ambayo inatolewa kwa riba nafuu ya kiwango cha asilimia 1 kwa mwezi mmoja.







Na Oscar Assenga, TANGA

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara ,Dennis Londo amesema Serikali haitawavumilia wafanyabiashara wa mkonge wanaofanya udanganyifu katika masoko ya nje huku akiitaka Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) kuchukua hatua za haraka dhidi yao wanaodaiwa kuchukua fedha kutoka kwa wanunuzi wa nje bila kupeleka bidhaa walizoahidi, ikisema vitendo hivyo vinahatarisha uaminifu wa Tanzania katika masoko ya kimataifa.

Amesema tabia hiyo ya baadhi ya wafanyabiashara inachafua taswira ya nchi na kuwaweka katika mazingira magumu wafanyabiashara wengine wanaofuata taratibu na kufanya biashara kwa uaminifu.

Londo alitoa kauli hiyo jijini Tanga wakati wa kikao kazi kati ya TSB, Chama cha Wakulima wa Mkonge (SAT) na wafanyabiashara wa zao hilo.

Amesema Tanzania inaendesha uchumi wa soko huria, lakini uhuru huo haupaswi kutumiwa kama mwanya wa kufanya biashara kinyume cha sheria au kukiuka misingi ya uaminifu katika masoko ya kimataifa.




“Nimesikia hapa wafanyabiashara wakilalamika kwamba wakati mwingine wanataka kukamatwa kwa sababu kuna baadhi ya wafanyabiashara wamefanya udanganyifu kwenye soko. Mtu akifanya hivyo anashindwa kujua kwamba huku nje yeye anatambulika kama Tanzania na wala si kampuni yake,” amesema.

Amesema Serikali haiwezi kuvumilia vitendo vinavyoweza kuilazimisha nchi kutumia muda na rasilimali nyingi kurejesha uaminifu na taswira yake katika masoko ya kimataifa.

Kutokana na hali hiyo, Naibu Waziri ameiagiza TSB, kwa kushirikiana na wadau wengine wa zao hilo, kuchukua hatua mapema dhidi ya wafanyabiashara watakaobainika kufanya vitendo hivyo ili kulinda soko la mkonge na maslahi ya wafanyabiashara wanaofuata sheria.




“Pamoja na kwamba Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ya kibiashara, hatuwezi kuvumilia hilo,” amesema.
TSB: WACHUKUA FEDHA, HAWAPELEKI MIZIGO

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TSB, Saddy Kambona, amesema changamoto hiyo ni miongoni mwa mambo aliyokutana nayo katika ziara zake kwenye masoko ya mkonge duniani.

Amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakichukua fedha kutoka kwa wanunuzi wa nje, lakini baadaye kushindwa kupeleka mizigo, hali ambayo imeanza kuchafua jina la Tanzania katika masoko hayo.




“Kwenye ziara yangu nimekutana na malalamiko kwamba kuna wafanyabiashara wamechukua fedha halafu wameshindwa kupeleka mizigo. Watu wanafanya udanganyifu kwenye masoko ya nje,” amesema Kambona.

Amesema wafanyabiashara watakaobainika kufanya vitendo hivyo wanaweza kuchukuliwa hatua, ikiwamo kufutiwa usajili au leseni zao.

Kwa mujibu wa Kambona, hatua hizo zinalenga kulinda uaminifu wa biashara ya mkonge kutoka Tanzania na kuhakikisha wafanyabiashara wanaofanya biashara kwa kufuata taratibu hawaathiriwi na vitendo vya watu wachache.


UZALISHAJI MKONGE WAPANDA

Pamoja na changamoto hiyo, Kambona amesema uzalishaji wa mkonge nchini umeendelea kuongezeka, kutoka tani 36,000 mwaka 2020 hadi kufikia tani 75,000 mwaka 2025.

Amesema mwaka 2020 wakulima wakubwa walichangia asilimia 68 ya uzalishaji wa mkonge, huku wakulima wadogo wakichangia asilimia 32.

Hata hivyo, amesema hali hiyo imebadilika kutokana na juhudi za kuwawezesha wakulima wadogo, ambapo mwaka 2025 walichangia asilimia 55 ya uzalishaji, huku wakulima wakubwa wakichangia asilimia 45.


WAFANYABIASHARA: TUNABEBESHWA DHAMBI ZA WACHACHE

Wafanyabiashara wa mkonge walioshiriki kikao hicho wamesema vitendo vya wachache vimekuwa na madhara kwa wafanyabiashara waaminifu kutoka Tanzania, ambao wakati mwingine hujikuta wakihusishwa na tuhuma au kesi zinazotokana na biashara zisizofanyika kwa uaminifu.

Gasper Daudi wa Harvest Agritech Limited amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakisababisha matatizo katika masoko ya nje, hali inayowaathiri hata wale wanaofanya biashara kwa kufuata sheria.



Amesema ni muhimu Serikali na TSB kuweka mifumo madhubuti ya kuhakikisha wafanyabiashara wanaokiuka taratibu wanachukuliwa hatua mapema.



Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Aja Tanzania Limited, Happiness Nyiti, ameomba Wizara ya Viwanda na Biashara kuweka mpango maalumu wa kurejesha uaminifu katika masoko ambayo tayari yameathiriwa na vitendo vya baadhi ya wafanyabiashara.


“Vitendo hivi vinachafua taswira ya nchi yetu. Tunaomba Naibu Waziri atusaidie kuweka mpango mzuri wa kutengeneza taswira ya nchi yetu kwenye maeneo ambayo yanaonekana waziwazi kwamba imani ya wafanyabiashara wa zao hilo kutoka Tanzania imeshuka,” amesema Nyiti.



Amesema hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa Tanzania ina wafanyabiashara wengi wanaozingatia ubora na uaminifu, lakini juhudi zao zinaweza kuathiriwa na vitendo vya wachache.

Amesema kurejesha uaminifu katika masoko ya kimataifa kutasaidia kuongeza fursa za biashara na kuchochea zaidi uzalishaji wa mkonge nchini.

Dar es Salaam

Makandarasi wanaotekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara za kuingia viwanja vya mazoezi na uendelezaji wa barabara ya uwanja wa Taifa ambayo itatumika wakati wa michuano ya AFCON wametakiwa kufanyia kazi maelekezo yote wanayopatiwa na Wakala ya Barabara za Vijini na Mijini (TARURA) kabla ya kuanza kwa mvua za El Nino.

Msisitizo huo umetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TARURA Mhandisi Florian Kabaka wakati wa ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara hizo jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Kabaka amesema kwamba Makandarasi hawapaswi kuzungumza tu bali kutekeleza kwa kufanyia kazi yale yote wanayoshauriwa na kuelekezwa na Wakala huo ili mvua zitakavyoanza kunyesha iwakute wamemaliza ujenzi wa mitaro ya maji na hivyo kuepusha maeneo muhimu kutokupata changamoto za maji na kuathiri miundombinu mingine.

Aidha, Mwenyekiti huyo amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi unaoendelea na kuwapongeza kwa kufanya kazi usiku na mchana, pia kuwepo kwa wataalam, mitambo na vifaa vingine inatoa matumaini ya kufikia hatua nzuri hadi kufikia mwisho wa mwezi huu.

Amesema miradi yote inayotekelewa Dar es Salaam imefikia 50% na kuwasisitiza kuongeza kasi zaidi.
Pamoja na hayo, Mhandisi Kabaka aliwatoa hofu wananchi kwamba TARURA watahakikisha wanaboresha barabara zote muhimu wakati wa El Nino ili wananchi wasikwame katika kupata huduma muhimu.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff amesema miradi hiyo inaendelea vizuri na wao kama wasimamizi wataendelea kuwafuatilia kwa karibu ili kuhakikisha kazi zinamalizika kwa wakati ifikapo Desemba mwaka huu.

Pia amesema kwa hatua iliyofikiwa ana uhakika barabara zote zitakamilika kwa viwango na kufikiwa masharti yaliyowekwa.








 



Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa Malaigwanani ,wazee na kina mama maarufu wapatao 33 kutoka kata 11 za ndani ya eneo la hifadhi Ngorongoro ili kuwajengea uwezo wa kutambua fursa mpya za kiuchumi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kamishina Msaidizi Mwandamizi anayeshughulikia huduma za jamii bi Gloria Bideberi amesema lengo la semina hiyo ni kuhakikisha Malaigwanani na wazee hao wanapata elimu ya kutosha kuhusu ujasiriamali na namna ya kutumia fursa zinazopatikana katika maeneo yao.

Bi. Gloria alieleza kwamba elimu hiyo itakwenda sambamba na ziara za kujifunza kwa vitendo, ambapo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ikiwemo kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za maziwa Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga ili kujifunza namna bidhaa zinavyozalishwa, kuendelezwa na kufikishwa katika masoko.

“Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa wananchi hawa wanapata elimu ya kutosha na kuwawezesha kutembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ili kujifunza kwa vitendo zaidi,” alisema Gloria

Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika maendeleo endelevu ya eneo la Hifadhi Ngorongoro.












Na Mwandishi wetu – Dar es Salaam

Taasisi ya OpenMap Development Tanzania (OMDTZ) kwa kushirikiana na Serikali imeanza zoezi la kukabidhi Mipango ya Kata ya Kujiandaa na Kukabiliana na Mafuriko kwa jamii katika kata tano za Jiji la Dar es Salaam. 

Zoezi hilo la siku tano kuanzia tarehe 14 hadi 18 Septemba 2026 ambalo litaziwezesha Kata kupokea mpango na elimu kwa lengo la kuzijea uwezo wa kukabiliana na mafuriko endapo yatatokea katika maeneo yao.

Zoezi hilo linalotekelezwa kupitia Mradi wa “Ramani Zetu, Sauti Zetu”, unaofadhiliwa na Zayed Sustainability Prize, linahusisha Kata za Keko, Makurumila, Mabibo, Ubungo na Tabata, na linalenga kuwezesha jamii na viongozi kuwa na mipango na taarifa sahihi za maeneo yao kwa ajili ya maandalizi na mwitikio wa mafuriko.

Akifungua rasmi zoezi hilo katika Kata ya Keko, Diwani wa Kata hiyo Mheshimiwa Ismail Amanzi alieleza umuhimu wa mipango hiyo kutumika kama nyenzo ya vitendo katika kuimarisha maandalizi ya jamii na kupunguza athari za mafuriko.

“Zoezi hili limekuja wakati sahihi hivyo, ni vyema tukaitumia fursa hii kwa kuhakikisha elimu tunayopewa inafanyiwa kazi kwa vitendo ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa kwa kuzingatia athari za mafuriko katika maeneo yetu”, alisema mhe. Amanzi

Kwa upande wake Mkurugenzi wa OpenMap Development Tanzania, Bw. Innocent Maholi, amesema ushirikishwaji wa jamii katika kutambua maeneo hatarishi na kuweka taarifa hizo kwenye ramani ni hatua muhimu ya kuhakikisha wananchi wanakuwa sehemu ya kwanza ya maandalizi ya maafa.

“Lengo letu si kutengeneza ramani pekee, bali kuhakikisha taarifa hizo zinatumika na jamii katika kufanya maamuzi na kuchukua hatua kabla ya mafuriko kutokea,” amesema Maholi.

Alifafanua kuwa, kupitia mipango hiyo, wananchi wamewezeshwa kutambua maeneo hatarishi, njia salama za uhamishaji, maeneo ya mikusanyiko na hatua muhimu za kuchukua kabla na wakati wa mafuriko. Zoezi hilo pia linahusisha elimu kwa jamii kuhusu tahadhari za mapema, usafi wa mifereji na hatua za msingi za uokoaji.

Mradi wa “Ramani Zetu, Sauti Zetu” unalenga kuimarisha ustahimilivu wa jamii dhidi ya mafuriko kupitia ramani shirikishi, mipango ya maandalizi ya maafa na matumizi ya taarifa za ndani za jamii katika kuchukua hatua za kupunguza vihatarishi.

Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu yenye dhamana ya kuratibu shughuli za Serikali ikiwemo ya masuala ya maafa nchini imeendelea kusisitiza umuhimu wa maandalizi ya mapema na ushirikiano kati ya Serikali na jamii katika kupunguza madhara yatokanayo na majanga, hususan wakati wa misimu ya mvua hasa kipindi hiki cha mvua za El Nino.

AWALI

OpenMap Development Tanzania (OMDTZ) ni taasisi inayolenga kutumia teknolojia ya ramani, taarifa za kijiografia na ushirikishwaji wa jamii katika kutambua na kupunguza vihatarishi vya majanga. Kupitia Mradi wa “Ramani Zetu, Sauti Zetu”, OMDTZ inashirikiana na Serikali na wadau mbalimbali kuwezesha jamii kutambua maeneo hatarishi, njia salama na rasilimali muhimu, pamoja na kuandaa mipango ya maandalizi na kukabiliana na mafuriko ili kuimarisha ustahimilivu wa jamii.









Katibu Mkuu wa chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato nchini (TAREWU) Dkt. Michael Marere na Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali wakionesha hati ya makubaliano baada ya kukubalino.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali Brighton Kinemo pamoja na Katibu Mkuu wa chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato Tanzania (TAREWU) wakisaini hati ya makubaliano ya TIB kutoa elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanachama wa (TAREWU).
Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali , Brighton Kinemo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu makubaliano kati ya Taasisi yao na Chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato (TAREWU) kushoto ni Katibu wa Chama hicho Dkt. Michael Marere.

WAKATI kukiwa kuna ombwe la elimu ya fedha na uwekezaji nchini. Chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato (TAREWU), na TIB Rasilimali zimesaini makubaliano ya ushirikiano katika elimu ya fedha na uwekezaji.

Makubaliano hayo yamekiwa leo Septemba 14, 2026 jijini Dar es Salaam, ambapo imeeelezwa kuwa makubaliano hayo ni mwanzo wa utekelezaji.

Brighton Kinemo, Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, wakati wa makubaliano hayo amesema kuwa utekelezaji wa mkataba huo utawawezesha wafanyakazi wa TAREWU kupata elimu ya fedha na uwekezaji itakayowawezesha kujimarisha kiuchumi kabla na baada ya kustaafu.

"Mtu anaweza kufanya kazi kwa miaka mingi lakini suala la msingi una elimu gani ya fedha na uwekezaji,".

"Kustaafu kunaandaliwa mapema. Makubaliano tunayokubaliana leo sio mwisho ni mwanzo wa utekelezaji,"

Naye Dkt. Michael Marere, Katibu Mkuu wa TAREWU amesema kuwa elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanachama wake kupitia TIB itawawezesha wanachama wake kupaya elimu hiyo.

“Ustawi wa mwanachama hauishii katika masuala ya maslahi ya kikazi pekee. Tunaamini kwamba mwanachama anayekuwa na maarifa sahihi ya fedha, uwezo wa kupanga na kusimamia kipato chake, pamoja na kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, anakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujenga maisha yenye ustawi na usalama wa kiuchumi.”

Dkt. Marere ameongeza:“Hii ndiyo sababu TAREWU imeweka elimu ya fedha na ustawi wa kiuchumi kuwa miongoni mwa vipaumbele muhimu katika Mpango Mkakati wetu wa Pili wa 2026–2030. Ushirikiano wetu na TIB Rasilimali ni hatua ya kimkakati ya kuhakikisha kwamba azma hii inatekelezwa kwa vitendo na kuleta manufaa yanayoonekana katika maisha ya wanachama wetu.”

Aidha, Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa TAREWU inalenga kujenga utamaduni wa “mwanachama mwenye maarifa, mwenye uwezo wa kifedha na mwenye ustawi”, akieleza kuwa elimu ya fedha inapaswa kuwa sehemu ya uwezeshaji endelevu wa wanachama katika hatua mbalimbali za maisha yao.

“Tunataka kuondoka kwenye mtazamo wa elimu ya fedha kama tukio la mara moja na badala yake kuijenga kama utamaduni endelevu ndani ya TAREWU. Lengo letu ni kuwawezesha wanachama kuelewa fedha zao, kuzipangia malengo, kujenga akiba, kuwekeza kwa uelewa na kufanya maamuzi yanayolinda ustawi wao wa sasa na wa baadaye.”

Wakati huo huo Dkt. Marere amesema TAREWU hivi karibuni itazindua mfuko wa pamoja na uwezeshaji kwa wanachama wake.

NMB Foundation imetoa wito kwa wahitimu wa Kidato cha Sita mwaka 2026 wenye sifa kuwasilisha maombi ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship kabla ya dirisha kufungwa Ijumaa, Septemba 18, 2026.

Awamu hii imetengewa Sh bilioni 1 kufadhili vijana 50 wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza wa pointi tatu hadi tano, wanaotoka familia zenye uwezo mdogo na wanaojiunga na taasisi za elimu ya juu nchini.

Ufadhili utajumuisha ada na tozo za chuo, fedha za kujikimu, gharama za mafunzo kwa vitendo pamoja na kompyuta mpakato. Wanufaika pia watapata malezi elekezi na maandalizi ya kuingia katika soko la ajira.

Maombi yote yanaendelea kupokewa kupitia tovuti ya NMB Foundation, foundation.nmbbank.co.tz, hadi tarehe 18 Septemba 2026. Wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii wameombwa kuwafikishia taarifa vijana wenye sifa, hasa walioko vijijini.




MASHABIKI wa michezo ya kasino mtandaoni sasa wana sababu nyingine ya kuongeza presha ya ushindani, baada ya Expanse Cash Rush Challenge kuingia kazini ikiwa na zawadi nono zinazofikia jumla ya TZS 6,000,000. Mashindano haya yanayofanyika hadi Septemba 22, 2026, yanawapa wachezaji nafasi ya kuingia kwenye mbio za ushindi kupitia michezo 20 ya kusisimua kutoka Expanse ndani ya Meridianbet.

Katika ushindani huu, kila mchezaji ana nafasi ya kuchagua kati ya michezo 20 ya Expanse slot, huku dau la kuanzia likiwa ni TZS 1,000 pekee. Hii maana yake ni kwamba safari ya kuwania nafasi kwenye orodha ya washindi inaanza kwa dau dogo, lakini ushindani wenyewe unaweza kuwa mkubwa kadri siku zinavyosonga. Kila mzunguko unaweza kuongeza msisimko na kuifanya mbio ya Cash Rush kuwa tamu zaidi.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kivutio kikubwa zaidi ni hazina ya zawadi inayofikia TZS 6,000,000, ambayo imegawanywa kwa washindi 20 watakaofanya vizuri kwenye shindano hilo. Hivyo, si suala la kucheza tu, bali ni kuweka jumla ya dau zako katika mbio na kuhakikisha unajenga nafasi nzuri ya kuelekea kileleni. Kadri unavyoshiriki, ndivyo unavyoendelea kujitengenezea nafasi katika mashindano haya ya muda maalum.

Kwa wachezaji wanaopenda sloti zenye kasi, ushindani na nafasi ya kushinda zawadi za fedha, Cash Rush Challenge inakuja kama uwanja mwingine wa kuonyesha mbinu na uvumilivu. Kuanzia sasa hadi 22 Septemba, macho yanaelekezwa kwenye orodha ya washiriki huku kila mmoja akilenga kuandika jina lake miongoni mwa washindi 20 watakaogawana keki hiyo ya TZS 6 milioni.

Sasa ni wakati wa kuingia kwenye mbio, kuchagua mchezo unaoupenda kati ya michezo 20 ya Expanse na kuanza mbio kwa dau la chini la TZS 1,000. Usikubali mbio zipite bila wewe kushiriki. Expanse Cash Rush Challenge imewasha taa za ushindani, na zawadi ya TZS 6,000,000 ipo mezani kwa washindi.


ILE siku ya kutengeneza pesa ndefu na wakali wa ubashiri imefika, timu kibao kushuka dimbani kusaka ushindi. Je wewe unasaka ushindi wako wapi?. Ingia Meridianbet na ubeti sasa.

Yale mashindano ya Carabao Cup Raundi ya 3 kule Uingereza yataendelea ambapo mechi zipo kibao za kukufanya uwe mshindi, Ipswich atamenyana dhidi ya Arsenal ambao ni mabingwa watetezi wa ligi na vinara wa ligi hadi sasa huku nafasi ya kuondoka na mpunga ikiwa nje kabisa.

Mechi hii inakutanisha timu mbili zenye uwezo tofauti ambapo vijana wa Arteta wako kwenye kiwango bora sana si kwenye ligi tuu, bali kwenye mashindano yote ambapo wenyeji wao kwenye ligi hadi sasa wamekusanya pointi 6 kwenye mechi 4 huku wakiwa wameshinda mechi mbili na kupoteza mbili pia.

Huku Arsenal wao wameshinda mechi zote nne ambazo wamecheza huku wakiwa wameruhusu bao moja hadi sasa, na ni moja ya timu ambazo zinasifika kwa kujilinda zaidi hivyo ni ngumu mpinzani kupata goli.

Pesa kubwa ipo kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mechi nyingine ni hii ya Liverpool dhidi ya Tottenham Spurs ambao wameanza msimu vibaya sana wakiwa hawajashinda mechi yoyote hadi sasa , lakini pia bila kufunga bao lolote.

Kocha huyo wa Liver Iraola bado inajitafuta kwani imekuwa haina matokeo ya kushawishi sana tena hawa baada ya kutoa suluhu kwenye mechi yao wakiwa Anfield. Hii ni mechi ambayo Jogoo anahitaji kushinda ili kuthibitisha kwa mashabiki zao kuwa mpia una matokeo matatu.

Spurs licha ya kufanya usajili mkubwa msimu huu timu bado haipati matokeo mzuri, ambapo De Zerbi sasa ana kibarua kizito cha kufanya kipindi ambacho bado mechi hazijachanganya.

Mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili, walitoa sare huku nafasi kubwa ya kupata ushindi pale Meridianbet anapewa Liver. Je wewe unampa nani nafasi kubwa ya kupata ushindi?. Suka jamvi hapa.

LALIGA kule Hispania ni mto juu ya moto Elche atamleta kwake Real Madrid ambapo kila timu inahitaji ushindi wa pointi 3 ili kuendelea kujiweka sawa kwenye msimamo wa ligi kuu.

Timu hiyo mpaka sasa kwenye mechi tano ambazo amecheza ameambulia pointi 2 pekee huku wenyeji wao wakiondoka na ppointi 12 kwenye msimamo wa ligi baada ya kupata ushindi mnono kwenye mechi yao iliyopita. Nani kushinda leo?. Jisajili hapa.

Madrid chini ya kocha mkuu Jose Mourinho wanahitaji kupambania taji la ligi kuu ambalo hawajalipata kwa muda sasa huku wakiwa wamewekeza kwenye usajili wa wachezaji wenye uwezo mkubwa ambao kwa pamoja wanaweza kuisaidia timu kufika malengo yao.

Hii sio mara ya kwanza wawili hawa kukutana, msimu uliopita kwenye mechi mbili za ligi walipokutana, Real aliondoka na pointi 4 ambapo mechi ya kwanza walitoa sare na ya pili wakashinda. Je leo hii nani unampa beti yako ya ushindi?. Suka jamvi hapa.

Meridianbet wao wanampa nafasi ya ushindi Mourinho na vijana wake, lakini pia mechi hii imepewa machaguo zaidi ya 1000. Beti sasa
NGORONGORO | SEPTEMBA 14, 2026

Watumishi wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa wamefanya ziara ya utalii wa ndani katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Bonde la Olduvai Gorge, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani, kuimarisha mshikamano na kuongeza ari ya utendaji kazi.

Katika ziara hiyo, watumishi wamepata fursa ya kujifunza kuhusu historia ya binadamu na masalia ya viumbe wa kale yanayopatikana Olduvai Gorge, eneo lenye umuhimu mkubwa katika tafiti za historia na maendeleo ya mwanadamu.

Aidha, wametembelea maeneo mbalimbali ya Hifadhi ya Ngorongoro na kushuhudia vivutio vya asili pamoja na wanyamapori mbalimbali, wakiwemo tembo, simba, faru, nyati, pundamilia, nyumbu, mbweha, swala, mbuni, viboko, ngiri na aina mbalimbali za ndege.

Ziara hiyo pia imelenga kuwahamasisha watumishi wengine na wananchi kwa ujumla kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini, sambamba na kukuza utamaduni wa utalii wa ndani, kubadilishana uzoefu na kuimarisha mahusiano miongoni mwa watumishi.












Top News