
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amewataka Maafisa Mazingira kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wanaokiuka Sheria Ndogo ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa kutupa taka ovyo ndani ya mifereji ya maji taka katika Soko Kuu la Jiji hilo.
Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo Mei 30, 2026 wakati alipoongoza viongozi, watendaji na wananchi Mkoa huo katika zoezi la usafi wa mazingira katika eneo la Soko Kuu la Jiji hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho kuelekea Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026.
Amesema baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wamejenga mazoea ya kutupa taka ovyo katika mifereji ya maji taka katika Soko hilo hali inayochangia kukithiri kwa uchafu na hivyo kuchochea kasi ya uharibifu wa mazingira.
“Natoa maelekezo kwa maafisa mazingira wa jiji na meneja wa soko kuhakikisha kunakuwa na utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usafi wa mazingira katika Soko hili na kila anayekiuka sheria hakikisheni anatozwa faini” amesema Mtanda.
Aidha Mhe. Mtanda amesema faini hizo zitakazolipwa na wafanyabiashara hao zitatumika katika kulipa gharama za huduma ya usafi inayotolewa na Halmashauri ya Jiji na hivyo kuhimiza watumiaji wa soko kuzingatia taratibu za usafi ili kulinda mazingira.
Mhe. Mtanda pia amewalekeza maafisa mazingira kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa wafanyabiashara waliopo ndani ya soko ili kuhakikisha wanatekeleza maelekezo, miongozo na ya sheria zilizopo ili huduma za soko hilo ziendelee kuwa endelevu kwa wananchi.
Amesema suala la usafi ni ustaarabu, hivyo ni wajibu wa jamii inayozunguka katika eneo hilo kuhakikisha wanajenga utamaduni wa kupenda na kuthamini usafi wa mazingira yanayowazunguka ili kulinda afya za watumiaji wa bidhaa na huduma zinazopatikana ndani soko hilo.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amewataka wananchi wa Mkoa huo kujenga utamaduni wa kupanda miti katika maeneo yao kwani kwa kufanya ni kutekeleza amri na maelekezo ya mwenyezi mungu aliyoyatoa katika vitabu takatifu.
Awali akitoa taarifa ya tathimini ya hali ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Afisa Mazingira wa Jiji hilo, Bw. Daudi Joseph amesema katika mwaka 2025/2026 Jiji hilo limefanikiwa kupanda miti 768,476 ambapo miti 176,750 imepandwa na wananchi na wadau wa mazingira.
Ameongeza pia katika kuchagiza suala la utunzaji na uhifadhi wa mazingira, Jiji hilo limeanzisha na kutekeleza kampeni mbalimbali ikiwemo Tunza Mazingira Ng’arisha Nyamagana na kusimamia shughuli za usafi wa mazingira kwa kushirikiana na viongozi wa Jiji hilo.
“Wilaya ya Nyamagana inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kushirikiana na wadau ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira katika Kata zote 18” amesema Joseph.
Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Afisa Misitu Mwandamizi Bw. Lucas Sabida ameupongeza Mkoa wa Mwanza kwa juhudi mbalimbali inazoendelea kuzifanya katika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kutunza mazingira.
Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa timu ya wataalamu wa Mazingira ya Mkoa huo na kuufanya kuwa ni miongoni mwa Mkoa ya mfano katika uhamasishaji wa jamii kuhusu umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira.
Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, 2026 yatafanyika Kitaifa Mkoani Dodoma yakiwa na kauli mbiu isemayo Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (kulia) akiongoza viongozi na watendaji wa Mkoa huo kufanya usafi katika eneo la Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 katika zoezi la usafi wa mazingira Mkoani humo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda (wa pili kushoto) akiwa pamoja na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo wakikagua maeneo mbalimbali ya Soko Kuu la Jiji la Mwanza Mei 30, 2026 wakati wa zoezi la usafi wa eneo hilo kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2026. Kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana, Bw. Thomas SalalaSerikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imeeleza kuendelea kuimarisha mifumo ya malezi, maadili na ustawi wa watoto na familia kama msingi muhimu wa kujenga Taifa lenye nguvu kazi yenye tija na maendeleo endelevu.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Dorothy Gwajima, wakati akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/27 bungeni, ambapo ameeleza kwa kina mikakati inayoendelea kutekelezwa na Serikali katika kuhakikisha watoto wa Tanzania wanalelewa katika misingi bora ya maadili, ulinzi na ustawi wa kijamii.
Dkt. Gwajima amesema Wizara yake ina jukumu la kuratibu na kusimamia masuala yote yanayohusu malezi, maadili, matunzo na ustawi wa watoto pamoja na familia, ambazo ni nguzo muhimu katika maendeleo ya Taifa.
Amefafanua kuwa malezi chanya ya watoto yanayoambatana na maadili mema ni msingi wa kujenga Taifa imara lenye jamii yenye nidhamu, mshikamano na uwezo wa kuchangia maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.
Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuratibu utoaji wa elimu ya malezi chanya kwa wazazi, walezi na vijana balehe ikiwa ni sehemu ya juhudi za pamoja za kupunguza na hatimaye kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto nchini.
Katika hotuba yake hiyo, Waziri Gwajima amesisitiza kuwa watoto ni rasilimali muhimu na mtaji wa Taifa, hivyo wanapaswa kulindwa, kupendwa na kuendelezwa katika misingi ya maadili na tamaduni za Kitanzania.
Amesema mazingira bora ya malezi yanapaswa kuanzia ndani ya familia ambayo ndiyo chimbuko la tabia, nidhamu na maadili ya mtoto, lakini amebainisha kuwa kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo umaskini wa kipato, migogoro ya kifamilia, ukatili na vifo vya wazazi au walezi, baadhi ya watoto hujikuta wakiishi katika mazingira hatarishi yanayowafanya kuhitaji huduma za malezi mbadala na ulinzi wa kijamii.
Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ya mwaka 2021/22 hadi 2025/26, ambayo inalenga kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa chini ya miaka minane anapata huduma jumuishi za malezi na makuzi ili kuongeza kiwango cha ukuaji timilifu kutoka asilimia 47 ya sasa hadi asilimia 90 ifikapo mwaka 2050 kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Amesema katika mwaka wa fedha unaoendelea, Wizara imeratibu uandaaji wa mfumo wa kitaifa wa kupima matokeo ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto unaojulikana kama Early Childhood Development Scorecard, ambao utasaidia kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa viashiria vya maendeleo ya mtoto nchini.
Aidha, Serikali imeanzisha mfumo wa kukusanya na kuchambua takwimu na taarifa za afua za malezi na makuzi ya awali ya mtoto kupitia mfumo wa ECD Dashboard, unaounganisha mifumo ya sekta mbalimbali za Serikali na taasisi zake.
Mfumo huo unalenga kubaini na kufuatilia utekelezaji wa nguzo tano muhimu za malezi na makuzi ya watoto wadogo ambazo ni afya bora, lishe toshelevu, uchangamshi na ujifunzaji wa awali, malezi yenye mwitikio pamoja na ulinzi na usalama wa watoto. Waziri Gwajima amesema nguzo hizo zina umuhimu sawa katika kuhakikisha mtoto anapata makuzi bora yatakayomwezesha kuwa raia mwenye mchango chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Katika hatua nyingine, Dkt. Gwajima amesema Wizara imetoa mafunzo kuhusu mifumo hiyo kwa maafisa 227 kutoka ngazi za mikoa na halmashauri zote nchini, ambapo kati yao maafisa 17 walitoka ngazi ya Wizara, 26 kutoka mikoa na 184 kutoka halmashauri, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali ya kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa afua za malezi na makuzi kwa karibu zaidi.
Amesema Serikali itaendelea kuhakikisha kila mtoto nchini analindwa, anapata malezi bora na analelewa katika mazingira salama yatakayomuwezesha kukuza vipaji na uwezo wake kikamilifu ili kuchangia maendeleo ya Taifa la kesho.
Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo, ameibua mjadala bungeni jijini Dodoma baada ya kutoa maoni yanayogusa namna sera na elimu ya kijinsia zinavyotekelezwa nchini, akisisitiza haja ya kuangaliwa kwa usawa wa pande zote mbili za kijinsia bila kuacha kundi lolote nyuma.
Mbunge huyo amezungumza hayo wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka wa fedha 2026/27 ambapo ameseleza kuwa maendeleo ya jamii hayawezi kufanikiwa ipasavyo endapo yatabaki yakilenga upande mmoja tu wa jamii.
Katika mchango wake, Baba Levo ameeleza kuwa kumekuwa na mitazamo inayojikita zaidi katika kumuwezesha mwanamke, jambo ambalo kwa mujibu wake ni muhimu, lakini akasisitiza kuwa wanaume nao wanapaswa kuingizwa kikamilifu katika mipango ya elimu na uelimishaji kuhusu masuala ya kijinsia na maendeleo ya familia.
Mbunge huyo pia amegusia changamoto zinazojitokeza ndani ya mahusiano na ndoa, akieleza kuwa baadhi ya migogoro ya kifamilia hutokana na kutoelewana, ukosefu wa uwazi na wakati mwingine madai yanayoibua hisia kali kati ya wanandoa.
Baba Levo amesitiza pia umuhimu wa elimu ya ukatili wa kijinsia kutolewa kwa uwiano, akisema kuwa ingawa wanawake wanapaswa kuendelea kulindwa na kupewa uelewa zaidi kutokana na changamoto wanazokumbana nazo, pia kuna haja ya kuwajengea wanaume uelewa wa namna ya kushughulikia changamoto za kifamilia na kuepuka migogoro inayoweza kusababisha matatizo makubwa katika jamii.
Kauli hizo zimeibua mjadala mpana miongoni mwa wabunge na wananchi, ambapo baadhi wameunga mkono wito wake wa kuangalia usawa wa kijinsia kwa pande zote, huku wengine wakisisitiza kuwa juhudi za sasa bado zinapaswa kuendelea zaidi katika kuwawezesha wanawake kutokana na historia ya changamoto walizopitia.
Na Atley Kuni, WAF-Dar es Salaam
Washiriki wa Maonesho ya Kimataifa ya Bidhaa za Kinywa na Meno Tanzania kutoka Mataifa mbalimbali duniani wameisifu Tanzania kwa ukarimu, mapokezi mazuri na ushirikiano wa hali ya juu walioupata katika kipindi chote cha maonesho hayo yaliyofanyika nchini.
Washiriki hao wamesema mazingira rafiki yaliyoandaliwa yamechangia mafanikio makubwa ya maonesho na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma na kibiashara kwa sekta ya afya ya kinywa na meno.
Akizungumza wakati wa kufunga maonesho hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya anayeshughulikia Dawa na Vifaa Tiba, Ndugu Emmanuel Tayari, amesema mafanikio ya maonesho hayo yanaonesha nafasi ya Tanzania kama kitovu muhimu cha uwekezaji, ubunifu na ushirikiano kwenye huduma za afya barani Afrika, akibainisha kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi yatakayochochea maendeleo ya sekta hiyo.
Washiriki kutoka nje ya nchi wameelezea Tanzania kuwa ni taifa lenye watu wenye upendo, heshima na wanaozingatia misingi ya kidiplomasia, jambo ambalo limewavutia wengi wa wageni hao,wengi wameahidi kurejea Tanzania kushiriki katika maonesho yajayo.
"Maonesho haya yametupatia fursa ya kubadilishana uzoefu na kujifunza teknolojia mpya zinazolenga kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno kwa wananchi" amesema Mshiriki Mmoja kutoka nchini Zambia.
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, afya bora ya kinywa na meno ni sehemu muhimu ya afya kwa ujumla kwani huchangia kuzuia magonjwa mbalimbali na kuboresha ustawi wa maisha ya jamii.
Naibu Katibu Mkuu Bw. Tayari amewahakikishia washiriki ushirikiano wa karibu kutoka Serikali kwa maandalizi ya maonesho yajayo yatakayofanyika kuanzia tarehe 27 hadi 29 Mei, 2027.
"Serikali itaendelea kurahisisha taratibu za uingizaji wa bidhaa za kinywa na meno zitakazotumika katika maonesho hayo ili kuhakikisha washiriki wanapata mazingira bora ya kushiriki na kuonesha ubunifu wao", amesema Tayari.
Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu Tayari amewataka, washiriki hao kuwa mabalozi wazuri wa Tanzania kwa kuwahamasisha watengenezaji na wadau wengine wa bidhaa za kinywa na meno kutoka mataifa mbalimbali kushiriki kwa wingi katika maonesho yajayo. Hatua inayo tarajiwa kuongeza uwekezaji, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na kuendelea kuboresha huduma za afya ya kinywa na meno kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na dunia kwa ujumla.
MANYARA: KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi amesema msingi mkuu wa Chama chao ni kusikiliza wananchi na kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi.
Kihongosi amesema hayo leo Juni Mosi, 2026 wakati akizungumza na wanachama na wananchi wa Shina Namba Moja, Tawi la Masakta, Kata ya Masakta wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika Kanda ya Kaskazini.
Amesema CCM imeendelea kuwa karibu na wananchi kwa sababu imejengwa katika misingi ya kusikiliza maoni yao, kutambua mahitaji yao na kuyafikisha katika mamlaka husika kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi.
“Kazi hizi zinafanywa na chama kwa sababu chama hiki ndicho kinaunda Serikali. Lakini msingi wa CCM ni kusikiliza watu, kutatua shida za watu na zile changamoto ambazo zinakuwa kubwa basi zipelekwe katika maeneo husika ili zipatiwe ufumbuzi,” amesema Kihongosi.
Katika hatua nyingine, Kihongosi amesema chama kitaendelea kufuatilia suala la kupandisha hadhi zahanati ya Masakta na kuwa kituo cha afya kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.
“Kama vigezo vitakuwa vimekidhi, niwahakikishie chama kitaendelea kusimamia kwa asilimia mia moja. Sote kwa pamoja tutashirikiana kuhakikisha jambo hili linapatiwa ufumbuzi wake,” amesema.
Kihongosi ameeleza hayo akujibu ombi la wananchi wa Kata hiyo ambalo lilihusu kupandishwa kwa hadhi ya Zahanati yao ya Kijiji kuwa Kituo cha Afya kutokana na ongezeko la idadi ya watu wanaohudumiwa katika zahanati hiyo na kuomba kuongeweza madaktari.
Awali akiwasilisha taarifa ya shina, Katibu wa Shina Namba Moja, Dismas Gwasima, aliiomba CCM na Serikali kuangalia uwezekano wa kupandisha hadhi zahanati ya Masakta na kuwa kituo cha afya kutokana na ongezeko la idadi ya wananchi wanaohudumiwa na kituo hicho.
Alisema zahanati hiyo imekuwa ikitoa huduma kwa zaidi ya miaka 20, lakini kwa sasa mahitaji ya huduma za afya yameongezeka sambamba na kukua kwa idadi ya watu, hali inayosababisha wananchi kukosa baadhi ya huduma muhimu zinazopatikana katika vituo vya afya.
Gwasima alisema wananchi wanahitaji kuongezewa huduma za mama na mtoto, huduma za upasuaji, watumishi wa afya pamoja na nyumba za watumishi ili kuboresha utoaji wa huduma katika eneo hilo.
.png)
SERIKALI YAFAFANUA JINSI WANAWAKE WA VIJIJINI WANAVYONUFAIKA NA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI
MCHEZO huu wa kirafiki utakaopigwa leo Juni 1 saa 00:00 usiku una umuhimu mkubwa kwa timu zote mbili zilizofuzu Kombe la Dunia linaloanza mwezi huu. Brazil, anayewemo kundi C, anautumia mchezo huu kujenga kasi na kuirekebisha safu yake ya mwisho kabla ya mashindano.






.jpeg)





.jpeg)




.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)









