Mkurugenzi wa TAWA TZ Engineering and Heaters Limited, Tawaqal Hassan, amesema kampuni hiyo imeshiriki Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini (LCCF 2026) linalofanyika jijini Mwanza kutokana na ubora wa bidhaa zake, hususan hita zinazotumika katika uchenjuaji wa madini.
Akizungumza na waandishi wa habari Julai 22, 2026, alisema vifaa hivyo vina mchango mkubwa katika kuongeza ufanisi wa upatikanaji wa dhahabu wakati wa uchenjuaji wa madini, huku akieleza ubora wa hita zinazozalishwa na kampuni hiyo unapimwa kwa kuzingatia viwango, voltage inayozalishwa, pamoja na uimara wa bidhaa hizo na wamekuwa wakipokea maoni chanya kutoka kwa wateja na wadau wanaotumia bidhaa zao.
Kwa mujibu wa Hassan, TAWA TZ Engineering and Heaters Limited inajihusisha na utengenezaji wa hita kwa matumizi ya migodini, viwandani, mahoteli, Bekari, viwanda vinavyohitaji joto katika uzalishaji, pamoja na vifaa vya kuyeyusha lami, amesema bidhaa hizo zimetengenezwa kwa kuzingatia mahitaji ya soko na kutoa suluhisho la kudumu kwa watumiaji.
Aidha, amesema serikali imewawezesha wao Kama vijana kupitia utoaji wa vibali vya kutengeneza bidhaa hizo nchini, hatua ambayo imewapa fursa ya kuonyesha uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji, ameongeza kuwa kampuni ipo tayari kuhudumia wateja wote wanaohitaji bidhaa hizo na inaendelea kujivunia kuwa miongoni mwa kampuni ya kwanza ya Kitanzania kutengeneza hita za aina hiyo kwa viwango vya ubora.
Hassan amesema wateja wakuu wa kampuni hiyo ni sekta ya madini, huku akieleza kuwa ushiriki wao katika LCCF 2026 utawapa nafasi ya kujenga ushirikiano na wadau kutoka ndani na nje ya nchi, pia ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini ili kuunga mkono juhudi za wazawa, kukuza viwanda vya ndani na kuchochea maendeleo ya uchumi.




.jpeg)





.jpeg)








.jpeg)


.jpg)







.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)




.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)


.jpeg)
