Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Komredi Kenani Labani Kihongosi,ametembelea Shina Namba 7 la CCM katika Tawi la Manyoni Mjini, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kimkakati ya kuimarisha uhai wa Chama kuanzia ngazi ya mashina mkoani Singida.

Akiwa katika shina hilo lenye wanachama 150, Ndugu Kihongosi aliwashukuru wanachama na uongozi wa Shina Namba 7 kwa mshikamano, nidhamu na uongozi wao thabiti. Alisisitiza kuwa huo ndiyo utofauti wa CCM na vyama vingine, kwa kuzingatia muundo imara wa Chama, Katiba yake na uongozi madhubuti kuanzia ngazi ya taifa hadi mashinani.

Aidha, aliwasilisha salamu za Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kueleza kuwa hata yeye ameendelea kujifunza misingi ya uongozi bora kutoka kwa viongozi wa mashina, akitaja Shina Namba 7 kama mfano wa uongozi wa karibu na wananchi.

Amewahakikishia wananchi na wanachama wa shina hilo kuwa CCM itaendelea kuleta maendeleo.

Kazi na Utu tunasongambele.












Na Mwandishi wetu, Babati


MBUNGE wa Jimbo la Babati Mjini, Mkoani Manyara, Emmanuel Khambay amewataka maofisa ardhi wa Halmashauri ya Mji huo kufanya kliniki ya ardhi kwenye kata ili kuondoa migogoro ya ardhi inayowakabili baadhi ya wananchi.

Khambay ametoa agizo hilo kwenye kata ya Maisaka katika ziara ya kushukuru kwa kuchaguliwa na kusikiliza kero, malalamiko na changamoto zinazowakabili wakazi wa eneo hilo.

Ameeleza kwamba miongoni mwa malalamiko, kero na changamoto alizozipata katika jamii ni migogoro ya ardhi kwenye kata ya Maisaka hivyo maofisa ardhi waanzishe kliniki katika eeo hilo.

"Maofisa ardhi wa halmashauri anzisheni kliniki ya ardhi na kukutana na wakazi wa kata ya Maisaka, msikilize changamoto zao na kuwapatia majawabu," amesema Khambay.

"Lengo la ziara hii ni kuwashukuru na kusema asante kwa kunichagua na kusikiliza kero mbalimbali na miongoni mwa changamoto nilizozisikia ni migogoro ya ardhi," amesema Khambay.

Amesema tiba ya migogoro ya ardhi ni kuanzisha kliniki ya ardhi kwa maofisa ardhi kutoka ofisini na kwenda kwa watu kusikiliza matatizo yao na kueleza namna ya kuyatatua.

Hata hivyo, amewaahidi wakazi wa eneo hilo, kuendelea kushirikiana nao kufanikisha maendeleo na kutoa huduma bora bila upendeleo wowote ule.

Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Babati mjini, Elizabeth Malley amempongeza Khambay kwa kushika nafasi hiyo na kujitoa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wa mjini Babati.

Malley anewaomba wakazi wa Babati mjini wampe ushirikiano wa kutosha mbunge wao ili aweze kuwatumikia ipasavyo kwani uchaguzi umeshafanyika na kilichobaki ni kufanyika maendeleo.

Mmoja kati ya wakazi wa kata ya Maisaka, Rose John amepongeza hatua hiyo ya kufanyika kwa kliniki ya ardhi itakayofanywa na maofisa ardhi wa halmashauri hiyo.

Amesema kupitia kliniki hiyo itakayofanywa wataweza kumaliza migogoro ya ardhi ambayo kwa namna moja au nyingine inazorotesha maendeleo.



Manyoni, Singida, Januari 18, 2026

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Kenani Labani Kihongosi, ameanza rasmi ziara yake ya kimkakati leo tarehe 18 Januari 2026 mkoani Singida, ambapo ameanzia Wilaya ya Manyoni.

Ziara hii ni ziara maalum ya Chama Cha Mapinduzi inayolenga kuhakikisha Chama kinawafikia wanachama wote nchini sambamba na kusikiliza kero za wananchi, kuzifanyia kazi na kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Akizungumza na wanachama walio jitokeza, Ndugu Kihongosi aliwasilisha salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisisitiza umuhimu wa umoja, mshikamano na upendo.






Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden umeratibu na kushiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Matka yanayofanyika jijini Helsinki, Finland, kuanzia tarehe 14-18 Januari, 2026, huku ukitangaza vivutio vya utalii vya Tanzania pamoja na filamu ya Tanzania: The Royal Tour.

Maonesho hayo ni miongoni mwa maonesho makubwa barani Ulaya yakijumuisha kampuni 950 za utalii, usafiri wa ndege, vyombo vya habari, na ushauri elekezi wa utalii kutoka duniani kote ambapo katika siku ya kwanza yalipokea washiriki 56,000 wakiwemo watalii watarajiwa.

Kampuni binafsi za Lifestyle Safaris & Holidays na Lifetime Safaris za Tanzania nazo zinashiriki katika maonesho hayo zikiwa na timu ya Ubalozi wa Tanzania. Nchi zingine za Afrika zinazoshiriki ni Uganda, Kenya, Ushelisheli, Namibia, Afrika Kusini, Senegal, Moroko, Tunisia na Misri.

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, anayeiwakilishia pia Tanzania katika nchi za Nodiki, Baltiki na Ukraina, alitumia jukwaa kuelezea namna Tanzania ilivyopata heshima kubwa ya kushinda Tuzo za Utalii za Dunia tarehe 6 Desemba 2025, nchini Bahrain, ikiwa ni mwaka wa tatu mfululizo.

Balozi Matinyi alielezea pia namna Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, alivyoshiriki na kuigiza katika filamu ya kuitangaza Tanzania ya dakika 57 iitwayo Tanzania: The Royal Tour akiwa na mwandishi wa Marekani mshindi wa Tuzo ya Emmy, Peter Greenberg, mwaka 2022.

Balozi Matinyi aliiambia hadhira kwamba Tanzania ina vivutio vitatu kati ya Maajabu Saba ya Asili ya Afrika na pia maeneo saba yanayotambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kama Urithi wa Dunia, akiutaja mathalani Mlima Kilimanjaro, uhamaji mkubwa wa wanyamapori hifadhini Serengeti na bonde la Ngorongoro. Mbali ya hifadhi za taifa 22, Balozi Matinyi pia alitaja utajiri wa utamaduni wa makabila 126 ya Tanzania, hifadhi za historia ya kale kama michoro ya mapangoni ya Kondoa, Mji Mkongwe wa Zanzibar na miji ya Bagamoyo na Kilwa.

Balozi Matinyi pia alitumia maonesho hayo kufanya mazungumzo na wadau mbalimbali wakiwemo Afisa Mtendaji Mkuu wa Atlantic Link, Bi. Karin Gert Nielsen na Mwakilishi wa Danish Travel Show, zote za Denmark, Bw. Johnny Frandsen; Meneja wa kampuni ya Flygresor ya Sweden, Bw. Peter Hallgren; na kwa kampuni za Finland Mwanzilishi na Mkurugenzi Mwendeshaji wa GapEdu, Bw. Jyrki Nilson; Mkurugenzi Mwendeshaji wa Amanihoiva Limited, Bw. Juha Valtanen na Mwakilishi wa Matka Travel Fair, Inkeri Vainik. Mazungumzo hayo yalilenga namna ya kushirikiana katika kuutangaza zaidi utalii wa Tanzania barani Ulaya.


Imetolewa na:
Ubalozi wa Tanzani nchini Sweden,
17 Januari, 2025.








Na Oscar Assenga, MKINGA

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Maji Mkinga – Horohoro kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana kuukamilisha kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Aweso aliyasema hayo leo wakati wa halfa ya Mapokezi ya Vitendea kazi (Mabomba) vitakavyotumika katika utekelezaji wa Mradi wa Maji Mkinga-Horohoro ambao unagharimu kiasi cha Bilioni 35.



Halfa hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Tanga Uwasa,Dkt Ally Fungo,Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly,Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo pamoja na watumishi wa Tanga Uwasa,Ruwasa,Viongozi wa CCM na wananchi wa eneo la Manza.

Alisema kutokana na kwamba mradi huo ni muhimu kwa wananchi ambao wanakabiliwa na changamoto ya maji hivyo wahakikishe unakamalika kwa wakati na ujenzi wake uwe tofauti uende na maji katika maeneo yanayolazwa mabomba nao wapate maji.



“Tunajua tuna miradi mingi sana lakini nikuombe Katibu Mkuu utoe fedha ili mradi huo ukamilike kwa wakati ili wana Mkinga waweze kupata huduma ya maji safi na salama”Alisema



“Kama mnakumbuka tulimleta Rais Dkt Samia Suluhu aliweke kuweka jiwe la msingi kukamilika kwake tumuombe Rais aje kuzindua mradi huu wa Mkinga sababu ndio muasisi na ndio aliyweka jiwe la msingi”Alisema

Waziri Aweso aliwataka wafanye kazi hiyo kwa uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha hiyo kazi inakamilika na wana Mkinga waweze kupata maji safi na salama



Hata hivyo Waziri huyo alimuahidi Mbunge wa Jimbo la Mkinga Twaha Mwakiojakwamba watafanya kazi kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kutokana na kwamba wapo baadhi ya watumishi wanaishi Tanga kutokana na changamoto ya maji wakikamilisha mradi huo watapata maendeleo makubwa.


Alisema maendeleo hayo yatapatikana kwa wana Mkinga na wawekezaji mbalimbali watakwenda kuwekeza hiyo kazi wameibeba na kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Gilbert Kailima alisema wanaishukuru Serikali kutokana na kwamba mradi huo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya ya Mkinga na utaondoa adha kubwa ya Maji.


Alisema wanamshukuru Rais kwa kutoa kipaumbele sana katika mradi huo na ndio maana alikuja kuweka jiwe la Msingi katika mradi huo na kuhaidi watajitahidi kusimamia mradi huo kwa karibu kwa kushirikiana na Tanga Uwasa ili utekelezwe kwa wakati ili uanze kufanya kazi kama Rais anavyotamani iwe pamoja nawe.

Aidha alisema katika wilaya hiyo wana miradi mengine mikubwa iliyopo wilayani humo ikiwemo wa Gombero, Mapatano, Muhinduro na Bamba Mwarongo yote ni mikubwa ambayo Serikali chini ya Wizara ya Maji inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wake na ipo katika hatua mbalimbali.


“Kutokana na kwamba umefika leo tunaomba nayo hii miradi waone namna gani inaweza kuisha kwa wakati kama ambavyo wananchi wa Mkinga wanatamani iwe tunaimani sana na utendaji wako na katibu mkuu wa wizara ya Maji “Alisema.


Alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kutoa ushirikiano kwa mkaandarasi ambaye atatoa huduma ya usambazaji wa maji katika mradi huo na kuhakikisha vifaa vyake havihujumiwi badala yake wawe walinzi ili kufanya kazi yake vizuri.

Naye kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mkinga (CCM) Twaha Mwakioja alisema kwamba katika taifiti iliyofanywa changamoto kubnwa inawakabili zaidi ya wananchi asilimia 80 wamelalamikia hali ya upatikanaji wa maji.



Alisema kwamba mradi huo kabla ya kuanza kutekelezwa wastani wa upatikanaji wa maji katika wilaya ya Mkinga ni asilimia 60 mpaka 69 hivyo wana imani mradi huo utakapokamilika upatinaji wa maji utafika zaidi ya asilimia 88 mradi huo ni mkombozi mkubwa kwao.

Aidha alisema kwamba mradi huo utakakamilika zaidi ya vijiji 37 vinakwenda kupata maji safi na salama ya uhakika na Serikali imeweka fedha nyingi ili kuhakikisha unakamilika ili wananchi waweze kuondokana na adha ya maji.

“Mhe Waziri tunaomba mradi huu kwa maana umesuasua kwa mude mrefu kama unavyotambua upo nyuma zaidi ya miaka miwili na ifikapo julai mradi uwe umekamilika hivyo tunashukuru na wananchi wana mategemeo makubwa sana “Alisema

Mwisho


*Absa Ghana yashika nafasi ya kwanza kama Mwajiri Bora katika soko lake

Kwa mwaka wa tano mfululizo, Absa imetambuliwa kama Mwajiri Bora (Top Employer) kwa mwaka 2026 na Taasisi ya Top Employers (TEI), kufuatia tathmini huru ya mbinu zake za usimamizi wa rasilimali watu katika nchi sita za Afrika ambazo ni Botswana, Ghana, Kenya, Afrika Kusini, Zambia na Mauritius. Katika mafanikio ya kipekee, Absa Ghana pia imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kama Mwajiri Bora katika soko lake.

Kwa ujumla, Absa imepata alama ya asilimia 93.66% katika ngazi ya kundi, ikiongezeka kutoka asilimia 90.15% mwaka 2025 na kuzidi kwa kiasi kikubwa kiwango cha kimataifa cha asilimia 85.9%. Masoko yote yalipata alama za jumla zilizo juu ya asilimia 87, huku Absa Bank Botswana ikirekodi ongezeko kubwa zaidi la mwaka hadi mwaka la asilimia 5.53. Ghana iliongoza kwa kupata alama ya juu zaidi ya jumla ya asilimia 97.38%, huku maboresho makubwa pia yakishuhudiwa nchini Kenya na Afrika Kusini, kila moja ikiongezeka kwa asilimia 4.94. Absa Bank Zambia nayo iliongeza alama zake kwa zaidi ya asilimia 4, ikidhihirisha dhamira thabiti ya Absa katika sera na mifumo inayomlenga mfanyakazi.

Kupata ithibati hii katika masoko yote sita kunathibitisha ufanisi wa mbinu ya Absa katika usimamizi wa rasilimali watu ndani ya sekta ya huduma za kifedha barani Afrika, kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Afisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Kundi la Absa, Jeanett Modise, alisema mabadiliko makubwa yanaendelea katika namna watu wanavyoutazama kazi, hali inayobadilisha uhusiano kati ya waajiri na wafanyakazi. “Mashirika lazima yawe wazi na makusudi kuhusu thamani wanayotoa—kuanzia dhamira na utamaduni wa kazi hadi fursa za ukuaji na unyumbufu—wakati huohuo yakieleza kwa uwazi viwango, uwajibikaji na utendaji yanayotarajiwa. Uwazi huu ni muhimu katika kujenga imani, kuvutia vipaji bora na kuunda mazingira ya kazi ambayo watu wanaweza kustawi kikamilifu,” alisema Modise.

Aliongeza kuwa Absa imejikita katika kuboresha namna inavyofafanua na kuwasilisha pendekezo lake la thamani kwa wafanyakazi, ili liendane na uhalisia wa jinsi watu wanavyotaka kufanya kazi na kujenga taaluma zao. “Kutambuliwa kama Mwajiri Bora kwa mwaka wa tano mfululizo ni uthibitisho huru kwamba mkabala huu unawagusa wafanyakazi wetu na unatekelezwa kwa uthabiti katika masoko yetu yote.”

Kwa upande wake, Charles Russon, Mtendaji Mkuu wa Absa anayesimamia Kanda ya Afrika, alisema kuongezeka kwa idadi ya masoko ya Absa yanayopata ithibati ya Mwajiri Bora ni ushahidi mkubwa wa mkakati wake wa kumweka mtu kwanza kazini. “Tunajivunia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya Absa Ghana kama Mwajiri Bora namba moja katika soko lake. Hili linaonyesha kina cha uwezo wetu wa uongozi, nguvu ya utamaduni wetu wa kazi, na uwekezaji wetu wa makusudi kwa watu wetu kote katika kanda, ili kuwahudumia vyema wateja wetu,” alisema.

Moja ya matokeo muhimu ya tathmini hiyo ni Absa kupata alama kamili ya asilimia 100 katika maeneo ya Mkakati wa Biashara, Uongozi na Utendaji, jambo linaloonyesha uthabiti mkubwa katika jinsi mkakati unavyotekelezwa kupitia uongozi na utendaji wa shirika. Absa pia ilifanya vyema katika Maadili na Uadilifu, ikipata alama ya asilimia 99.49%, juu ya kiwango cha kimataifa kwa asilimia 1.45 na karibu asilimia 2 juu ya kiwango cha sekta. Alama ya Mazingira ya Kazi ilipanda hadi asilimia 98.41%, zaidi ya asilimia 10 juu ya wastani wa kimataifa na karibu asilimia 8 juu ya kiwango cha sekta.

Maboresho makubwa zaidi ya mwaka hadi mwaka yalirekodiwa katika michakato ya kuondoka kazini (+18%), utofauti, usawa na ujumuishi (+11.34%), zawadi na utambuzi (+8.78%), uendelevu (+7.35%), pamoja na chapa ya mwajiri (+5.28%).

TEI ni mamlaka ya kimataifa katika kutambua ubora wa mbinu za usimamizi wa rasilimali watu. Kupitia Mpango wake wa Ithibati unaotambulika duniani kote na unaotumia uchambuzi wa takwimu, TEI husaidia kampuni kuboresha mikakati yao ya kuvutia, kukuza, kuhusisha na kubakiza vipaji.

Maendeleo yaliyoshuhudiwa katika tathmini ya mwaka huu yamechangiwa na mkabala makini zaidi unaotumia takwimu katika kuelewa uzoefu wa wafanyakazi. Absa imeendelea kuimarisha mifumo yake ya kusikiliza maoni ya wafanyakazi, kwa kuanzisha vigezo bora zaidi vya kulinganisha na uchambuzi wa kina unaotoa mwanga juu ya viwango vya imani na ushiriki ndani ya shirika. Hatua hizi zimewezesha kuingilia kati kwa ufanisi zaidi pale panapohitajika, kuboresha uzoefu wa mfanyakazi katika hatua zote za ajira, na kuimarisha utamaduni wa uwazi na uwajibikaji.

Aidha, Absa imeongeza uwekezaji katika maendeleo ya uongozi kupitia mifumo iliyoboreshwa na mbinu za ufundishaji, jambo lililoimarisha uthabiti katika utekelezaji wa mkakati. Wakati huohuo, kundi limeendeleza juhudi zake katika ujumuishi, maendeleo ya ujuzi na mbinu za kubakiza vipaji kwa kutumia takwimu, kuhakikisha kuwa uwezo muhimu unajengwa na kudumishwa kwa muda mrefu. Hatua hizi kwa pamoja zimechangia maboresho ya jumla yaliyoonekana katika masoko yote na kuimarisha utendaji wa Absa katika tathmini hiyo.

“Kutambuliwa kwa mwaka wa tano mfululizo kunatupa mtazamo wazi wa jinsi utamaduni wetu na mbinu zetu za rasilimali watu zimekua kwa muda,” alisema Modise. “Tukiwa tumejipanga kulingana na mkakati wa kundi, tunaendelea kujitahidi kuwa karibu zaidi na wateja wetu, kwa kuwawezesha wafanyakazi wetu kutoa huduma bora. Tumekuwa makusudi katika kuimarisha pendekezo letu la thamani kwa wafanyakazi, tukilenga ubora wa kazi, uongozi, fursa za kujifunza na kukua, pamoja na ustawi wao.”

Alimalizia kwa kusema, “Msingi huu unaendelea kuunda aina ya mazingira ya kazi tunayojenga kwa ajili ya siku zijazo, mazingira yanayokidhi mahitaji ya dunia inayobadilika ya kazi na yanayoweza kuvutia na kukuza vipaji ambavyo shirika letu linavitegemea, vipaji vinavyotekeleza kusudi letu la kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine.”





*Absa Ghana yashika nafasi ya kwanza kama Mwajiri Bora katika soko lake

Kwa mwaka wa tano mfululizo, Absa imetambuliwa kama Mwajiri Bora (Top Employer) kwa mwaka 2026 na Taasisi ya Top Employers (TEI), kufuatia tathmini huru ya mbinu zake za usimamizi wa rasilimali watu katika nchi sita za Afrika ambazo ni Botswana, Ghana, Kenya, Afrika Kusini, Zambia na Mauritius. Katika mafanikio ya kipekee, Absa Ghana pia imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kama Mwajiri Bora katika soko lake.

Kwa ujumla, Absa imepata alama ya asilimia 93.66% katika ngazi ya kundi, ikiongezeka kutoka asilimia 90.15% mwaka 2025 na kuzidi kwa kiasi kikubwa kiwango cha kimataifa cha asilimia 85.9%. Masoko yote yalipata alama za jumla zilizo juu ya asilimia 87, huku Absa Bank Botswana ikirekodi ongezeko kubwa zaidi la mwaka hadi mwaka la asilimia 5.53. Ghana iliongoza kwa kupata alama ya juu zaidi ya jumla ya asilimia 97.38%, huku maboresho makubwa pia yakishuhudiwa nchini Kenya na Afrika Kusini, kila moja ikiongezeka kwa asilimia 4.94. Absa Bank Zambia nayo iliongeza alama zake kwa zaidi ya asilimia 4, ikidhihirisha dhamira thabiti ya Absa katika sera na mifumo inayomlenga mfanyakazi.

Kupata ithibati hii katika masoko yote sita kunathibitisha ufanisi wa mbinu ya Absa katika usimamizi wa rasilimali watu ndani ya sekta ya huduma za kifedha barani Afrika, kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Afisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Kundi la Absa, Jeanett Modise, alisema mabadiliko makubwa yanaendelea katika namna watu wanavyoutazama kazi, hali inayobadilisha uhusiano kati ya waajiri na wafanyakazi. “Mashirika lazima yawe wazi na makusudi kuhusu thamani wanayotoa—kuanzia dhamira na utamaduni wa kazi hadi fursa za ukuaji na unyumbufu—wakati huohuo yakieleza kwa uwazi viwango, uwajibikaji na utendaji yanayotarajiwa. Uwazi huu ni muhimu katika kujenga imani, kuvutia vipaji bora na kuunda mazingira ya kazi ambayo watu wanaweza kustawi kikamilifu,” alisema Modise.

Aliongeza kuwa Absa imejikita katika kuboresha namna inavyofafanua na kuwasilisha pendekezo lake la thamani kwa wafanyakazi, ili liendane na uhalisia wa jinsi watu wanavyotaka kufanya kazi na kujenga taaluma zao. “Kutambuliwa kama Mwajiri Bora kwa mwaka wa tano mfululizo ni uthibitisho huru kwamba mkabala huu unawagusa wafanyakazi wetu na unatekelezwa kwa uthabiti katika masoko yetu yote.”

Kwa upande wake, Charles Russon, Mtendaji Mkuu wa Absa anayesimamia Kanda ya Afrika, alisema kuongezeka kwa idadi ya masoko ya Absa yanayopata ithibati ya Mwajiri Bora ni ushahidi mkubwa wa mkakati wake wa kumweka mtu kwanza kazini. “Tunajivunia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya Absa Ghana kama Mwajiri Bora namba moja katika soko lake. Hili linaonyesha kina cha uwezo wetu wa uongozi, nguvu ya utamaduni wetu wa kazi, na uwekezaji wetu wa makusudi kwa watu wetu kote katika kanda, ili kuwahudumia vyema wateja wetu,” alisema.

Moja ya matokeo muhimu ya tathmini hiyo ni Absa kupata alama kamili ya asilimia 100 katika maeneo ya Mkakati wa Biashara, Uongozi na Utendaji, jambo linaloonyesha uthabiti mkubwa katika jinsi mkakati unavyotekelezwa kupitia uongozi na utendaji wa shirika. Absa pia ilifanya vyema katika Maadili na Uadilifu, ikipata alama ya asilimia 99.49%, juu ya kiwango cha kimataifa kwa asilimia 1.45 na karibu asilimia 2 juu ya kiwango cha sekta. Alama ya Mazingira ya Kazi ilipanda hadi asilimia 98.41%, zaidi ya asilimia 10 juu ya wastani wa kimataifa na karibu asilimia 8 juu ya kiwango cha sekta.

Maboresho makubwa zaidi ya mwaka hadi mwaka yalirekodiwa katika michakato ya kuondoka kazini (+18%), utofauti, usawa na ujumuishi (+11.34%), zawadi na utambuzi (+8.78%), uendelevu (+7.35%), pamoja na chapa ya mwajiri (+5.28%).

TEI ni mamlaka ya kimataifa katika kutambua ubora wa mbinu za usimamizi wa rasilimali watu. Kupitia Mpango wake wa Ithibati unaotambulika duniani kote na unaotumia uchambuzi wa takwimu, TEI husaidia kampuni kuboresha mikakati yao ya kuvutia, kukuza, kuhusisha na kubakiza vipaji.

Maendeleo yaliyoshuhudiwa katika tathmini ya mwaka huu yamechangiwa na mkabala makini zaidi unaotumia takwimu katika kuelewa uzoefu wa wafanyakazi. Absa imeendelea kuimarisha mifumo yake ya kusikiliza maoni ya wafanyakazi, kwa kuanzisha vigezo bora zaidi vya kulinganisha na uchambuzi wa kina unaotoa mwanga juu ya viwango vya imani na ushiriki ndani ya shirika. Hatua hizi zimewezesha kuingilia kati kwa ufanisi zaidi pale panapohitajika, kuboresha uzoefu wa mfanyakazi katika hatua zote za ajira, na kuimarisha utamaduni wa uwazi na uwajibikaji.

Aidha, Absa imeongeza uwekezaji katika maendeleo ya uongozi kupitia mifumo iliyoboreshwa na mbinu za ufundishaji, jambo lililoimarisha uthabiti katika utekelezaji wa mkakati. Wakati huohuo, kundi limeendeleza juhudi zake katika ujumuishi, maendeleo ya ujuzi na mbinu za kubakiza vipaji kwa kutumia takwimu, kuhakikisha kuwa uwezo muhimu unajengwa na kudumishwa kwa muda mrefu. Hatua hizi kwa pamoja zimechangia maboresho ya jumla yaliyoonekana katika masoko yote na kuimarisha utendaji wa Absa katika tathmini hiyo.

“Kutambuliwa kwa mwaka wa tano mfululizo kunatupa mtazamo wazi wa jinsi utamaduni wetu na mbinu zetu za rasilimali watu zimekua kwa muda,” alisema Modise. “Tukiwa tumejipanga kulingana na mkakati wa kundi, tunaendelea kujitahidi kuwa karibu zaidi na wateja wetu, kwa kuwawezesha wafanyakazi wetu kutoa huduma bora. Tumekuwa makusudi katika kuimarisha pendekezo letu la thamani kwa wafanyakazi, tukilenga ubora wa kazi, uongozi, fursa za kujifunza na kukua, pamoja na ustawi wao.”

Alimalizia kwa kusema, “Msingi huu unaendelea kuunda aina ya mazingira ya kazi tunayojenga kwa ajili ya siku zijazo, mazingira yanayokidhi mahitaji ya dunia inayobadilika ya kazi na yanayoweza kuvutia na kukuza vipaji ambavyo shirika letu linavitegemea, vipaji vinavyotekeleza kusudi letu la kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine.”




Na Mwandishi wa OMH

Kibaha, Pwani. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), imeendesha mafunzo ya siku nne kwa watumishi wapya 20 walioajiriwa katika ofisi hiyo, kwa lengo la kuwajengea uwezo maalumu wa kiutendaji katika utumishi wa umma.

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, kuanzia Januari 13 hadi 16, 2026.

Mafunzo hayo yaliendeshwa na Mkurugenzi wa Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu kutoka ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Chacha Marigiri, wakufunzi kutoka TPSC, wataalamu kutoka Hospitali ya Mnazi mmoja Pamoja na wataalaamu wa fedha na uwekezaji kutoka Mfuko wa Uwekezaji wa UTT AMIS.

Bw. Marigiri alitoa mafunzo kuhusu matumizi sahihi ya muda, akisisitiza umuhimu wa kuweka uwiano kati ya kazi na maisha binafsi ili kuepusha changamoto zinazoweza kumfanya mtumishi wa umma kushindwa kutekeleza majukumu yake.

“Watumishi wengi hushindwa kufanya kazi kwa ufanisi kwa sababu ya kukosa matumizi sahihi ya muda na kutoweka vipaumbele katika shughuli zao,” alisisitiza.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa TPSC, Bw. Hosea George ambaye ni mhadhiri kutoka chuo hicho alisema mafunzo hayo ni muhimu na mahususi kwa watumishi wapya ili kuwajengea uwezo wa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

“Mafunzo haya yanalenga kuchochea maendeleo ya serikali, pamoja na taasisi na mashirika ya umma yanayosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina,” alisema Bw. George.

Miongoni mwa mada zilizofundishwa ni pamoja na maadili na utendaji katika utumishi wa umma, Muundo wa serikali ya jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na uendeshaji wa shughuli zake kwa Tanzania bara na Zanzibar, mapitio ya sheria mbalimbali za utumishi wa umma, elimu ya afya ya ukimwi na magonjwa yasiyoambukizwa, afya ya akili, kupima utenda kazi wa watumishi pamoja na elimu ya fedha na kuweka akiba.

Akizungumza wakati wa kutoa mada ya afya, Dkt. Frank Mlaguzi kutoka Hospitali ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam aliwataka watumishi wa umma kuzingatia utunzaji wa afya zao dhidi ya magonjwa ya kuambukiza na yasiyoambukiza kama kisukari, shinikizo la damu, homa ya ini pamoja na changamoto za afya ya akili, akieleza kuwa magonjwa hayo huathiri kwa kiasi kikubwa utendaji kazi.

Bw. Chacha Marigiri aliwatunuku vyeti wahitimu wa mafunzo hayo na kukipongeza Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kwa kutoa mafunzo yenye tija, akibainisha kuwa mafunzo hayo yatasaidia kujenga watumishi wenye maadili, bidii na weledi.

Naye Goodluck Mtebene, mtumishi mpya wa umma katika Ofisi ya Msajili wa Hazina, Kurugenzi ya Fedha na Uhasibu, aliishukuru Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na TPSC kwa kuandaa mafunzo hayo.

“Mafunzo haya yamekuwa mwongozo muhimu katika kuufahamu vyema utumishi wa umma. Tunaahidi kuyazingatia maadili yote tuliyofundishwa katika utekelezaji wa majukumu yetu,” alihitimisha.





 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa utendaji kazi mzuri, maendeleo na mabadiliko makubwa yanayoonekana katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa , katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), baada ya Kamati kupokea Taarifa ya Muundo na Majukumu ya BRELA iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa.

Mhe. Mwanyika amesema kuwa, licha ya kazi nzuri inayoendelea kufanywa na BRELA, bado kuna changamoto ya wafanyabiashara na wamiliki wa kampuni wengi kutohuisha taarifa za kampuni zao kupitia mfumo wa BRELA. Ameeleza kuwa tatizo hilo ni kubwa, lakini wananchi wengi hawalitambui ipasavyo.

“Hili tatizo ni kubwa lakini wengi hawalielewi; wengi wana kampuni lakini hawajahuisha taarifa za kampuni hizo,” amesema Mhe. Mwanyika.

Kutokana na hali hiyo, Mhe. Mwanyika ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara kufanya utafiti na kutathmini namna ya kuboresha mfumo wa uhuishaji wa taarifa za biashara na kampuni, ili kuja na mfumo wezeshi, unaoongeza ufanisi na kuharakisha utoaji wa huduma.

Aidha, Mwenyekiti huyo amesisitiza umuhimu wa kuhuisha taarifa za biashara na kampuni, akitoa wito kwa wafanyabiashara kuchukua hatua hiyo kwa hiari na kwa wakati.

“Kuhuisha taarifa ni jambo jema, na ni muhimu tukalifanye,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa, amesema kuwa Wakala itaendelea kutoa elimu kwa Waheshimiwa Wabunge kupitia Kamati hiyo ili kuwajengea uelewa mpana kuhusu majukumu ya BRELA pamoja na mifumo ya kidijitali inayotumika katika utoaji wa huduma.

Bw. Nyaisa ameeleza kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu matumizi ya mifumo ya kidijitali bado ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha urasimishaji wa biashara na utoaji wa leseni.

Amefafanua kuwa mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo kumwezesha mwananchi kujisajili moja kwa moja bila usumbufu.

“Mfumo wa BRELA ni rafiki kwa mtumiaji na unajieleza wenyewe, hivyo humwezesha mtu kuingia moja kwa moja na kusajili kampuni yake bila usumbufu,” amesema Bw. Nyaisa.

Ameongeza kuwa BRELA inaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuwahamasisha kufahamu kuwa mchakato wa usajili wa biashara, kampuni na utoaji wa leseni si mgumu kama inavyodhaniwa.

Amebainisha kuwa katika mapitio ya sheria yanayoendelea, BRELA inapendekeza kutambuliwa rasmi kwa Mawakala wa Usajili wa Kampuni, ili kusaidia wananchi wanaokutana na changamoto wakati wa usajili.

“Lengo ni kuhakikisha mwananchi akikwama, anapata msaada kutoka kwa watu wanaotambulika na kuaminika,” amesisitiza Bw. Nyaisa.


Top News