Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametoa wito kwa Wakazi wa Dunga mkoa wa Kusini Unguja kuendelea kushirikiana na Idara ya Uhamiaji pamoja na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, katika kuhakikisha amani inaendelea kushamiri nchini.

Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Afisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kati mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar katika hafla iliyofanyika katika eneo Dunga. 

Amewasihi kushirikiana na Serikali kwa njia ya kutoa taarifa mbalimbali kuhusu wahamiaji haramu, watu wanaoishi nchini kinyume cha sheria, au wanaojihusisha na shughuli haramu zilizo kinyume na malengo ya ukaazi wao. Makamu wa Rais amesema amani na umoja ni Tunu za Taifa, ambayo kila mtanzania anapaswa kuilinda.  

 Makamu wa Rais amewasihi wananchi wote kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika kuiletea nchi maendeleo ili kwa pamoja kuweza kufikia malengo ya kuboresha maisha ya kila Mtanzania na kuiletea maendeleo nchi.

 Halikadhalika, Makamu wa Rais ametoa rai kwa Taasisi za Serikali kuendelea kuwaamini na kuwapa watanzania wazawa kazi za ujenzi ili waendelee kupata uwezo wa kiteknolojia na kifedha. 

Makamu wa Rais ameipongeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya uhamiaji kwa kutoa kandarasi kwa mtanzania mzawa katika ujenzi wa jengo la Afisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kati, Unguja.

 Aidha, Makamu wa Rais amesema Serikali imejikita katika kuimarisha huduma za uhamiaji kwa kuboresha vitendea kazi na miundombinu kwa ujumla. Ameongeza kwamba Ujenzi wa Afisi za Uhamiaji za Wilaya ni njia mojawapo ya jitihada za kufikia azma hiyo. 

Sambamba na uboreshwaji wa Miundombinu ya Majengo, Serikali imeweka mkazo katika utoaji wa Mafunzo kwa watumishi, kusimamia stahiki za Watumishi, na kufanya maboresho ya mara kwa mara ya Sheria na Kanuni za Uhamiaji nchini. 

Vilevile, Makamu wa Rais amesema huduma za Kiuhamiaji Zanzibar ni muhimu na ni chachu katika kukuza sekta ya biashara, uwekezaji na utalii, kwa kuzingatia ongezeko kubwa la Wageni wanaotembelea Zanzibar, hususan katika kipindi ambacho Serikali zote mbili zimejikita kukuza Sekta ya Utalii kufuatia uzinduzi wa Filamu maarufu ya Royal Tour.

Makamu wa Rais amesema Mapinduzi ya mwaka 1964 yaliyoongozwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume yana historia kubwa kwa Zanzibar na watu wake. 

Tangu wakati huo, Mapinduzi hayo yameijengea heshima kubwa Zanzibar na kuwapa Wazanzibari wigo mpana wa kufanya maamuzi kuhusu maisha yao wenyewe na kujiletea maendeleo.

 Amesema pia Muungano umeimarisha zaidi umoja, mshikamano na kudumisha amani na utulivu, na kuchochea maendeleo kwa wananchi wote. Amesema Baada ya Mapinduzi na Muungano, huduma mbalimbali za jamii kama vile afya na elimu zilifunguka kwa wananchi wote. 

Jengo hilo la Afisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kati limegharimu shilingi bilioni 2.1.










Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Mpango wa Maendeleo ya Jamii kupitia Mfuko wa TASAF umeendelea kuonesha mchango mkubwa katika kuboresha huduma za afya nchini, ambapo katika Kijiji cha Mgunga, Kata ya Msamalo wilayani Chamwino mkoani Dodoma, wananchi wameeleza kufurahishwa na hatua ya ujenzi wa Kituo cha Afya Msamalo huku wakitoa ombi la kukamilishwa kwa majengo muhimu ya huduma za upasuaji na mama na mtoto ili kuongeza ufanisi wa huduma.

Hali hiyo imebainishwa wakati wa ziara ya wataalamu na wawakilishi kutoka Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania waliotembelea eneo hilo kwa lengo la kukagua maendeleo ya utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango wa TASAF pamoja na kujionea namna mradi wa kituo hicho cha afya unavyoendelea kunufaisha jamii ya maeneo ya jirani.

Katika maelezo yao, wananchi wamesema uwepo wa kituo hicho umekuwa mkombozi mkubwa, lakini bado changamoto ya kukosekana kwa huduma za upasuaji na wodi ya mama na mtoto imeendelea kuwalazimu kusafiri umbali mrefu kufuata huduma katika hospitali za wilaya na rufaa, jambo linaloongeza gharama na wakati wa kupata matibabu.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mgunga, Simon Masagasi, amesema ujenzi wa kituo hicho umekuwa hatua muhimu kwa maendeleo ya afya ya jamii, lakini bado kuna hitaji kubwa la kukamilisha miundombinu iliyobaki ili kituo kiweze kutoa huduma zote muhimu kwa wakazi wa eneo hilo na vijiji jirani.

Alieleza kuwa kabla ya uwepo wa kituo hicho, wananchi, hususan wajawazito, walilazimika kutumia usafiri wa mbali na wakati mwingine usio salama kufuata huduma, hali iliyokuwa ikiweka maisha yao hatarini.

Mkazi wa eneo hilo, Mary Sabugo, amesema awali changamoto ya huduma za afya ilikuwa kubwa zaidi, kwani walilazimika kusafiri kwenda maeneo ya mbali hata kwa matatizo madogo ya kiafya, jambo lililokuwa likichelewesha matibabu na kuongeza hatari kwa wagonjwa.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Msamalo, Rebecca Kitundu, amesema kituo hicho kinahudumia zaidi ya wakazi 16,000 kutoka kata za Msamalo, Ikoa na Igandu, hivyo ongezeko la huduma linahitaji miundombinu imara zaidi ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Amefafanua kuwa kukamilika kwa majengo ya upasuaji na huduma za mama na mtoto kutasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa pamoja na kupunguza rufaa zisizo za lazima kwenda hospitali za mbali.

“Tunashukuru kwa hatua iliyofikiwa kupitia TASAF, lakini bado tunaiomba Serikali na wadau wa maendeleo kuhakikisha miundombinu iliyobaki inakamilishwa ili huduma ziwe bora zaidi,” alisema Kitundu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ukaguzi wa Ndani, Uswege Edward, aliipongeza Serikali kwa ushirikiano wake katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia TASAF, akisema umeleta mabadiliko chanya katika sekta mbalimbali ikiwemo afya.

Alibainisha kuwa awamu ya pili ya mpango huo imewezesha uboreshaji wa huduma za jamii katika maeneo mengi nchini, huku akishukuru pia wadau wa maendeleo wakiwemo Ubalozi wa Uswisi kwa kuendelea kufuatilia na kushirikiana katika miradi hiyo.

Aidha, aliwahimiza wananchi waliopitia katika mpango huo na kufikia hatua ya kujikwamua kiuchumi kuendelea kushiriki shughuli za uzalishaji mali ili kudumisha mafanikio yaliyopatikana kupitia programu hiyo ya kijamii.

Serikali imetangaza kuwa awamu ya tatu ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia TASAF inatarajiwa kuanza kutekelezwa hivi karibuni katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayotarajiwa kuongeza wigo wa miradi ya maendeleo na kuimarisha zaidi huduma za msingi kwa wananchi, hususan katika sekta za afya, elimu na miundombinu ya kijamii.










Wanamichezo wa TCDC Sports Club wameshiriki mashindano ya riadha (mbio) katika Michezo ya kitaifa Meimosi inayoendelea mkoani Njombe.

Wachezaji walioshiririki mbio hizo ni Mbaso John aliyekimbia Mita 100 na kuibuka mshindi wa tatu (3) katika round ya kwanza, na baadae kupoteza nafasi ya ushindi katika hatua ya nusu fainali.

Mchezaji mwingine ni William Valentine aliyeshiriki riadha mbio za Mita 800 na kutofaninikiwa kupata ushindi baada ya kuzidiwa na wanariadha kutoka Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya ndani.

Kwa upande wake Noel Steven ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCDC Sports Club ameshiriki mchezo wa Draft ambapo kwa mzunguko wa kwanza TCDC Sports Club ilishinda mechi mbili na mzunguko wa pili kupata draw na hivyo kutofanikiwa kuvuka hatua za makundi baada ya kuzidiwa kete na TRA na Wizara ya Kilimo.

Michezo hiyo yote imechezwa Aprili 21, 2026 katika viwanja vya Njombe Sekondari na Viwanja vya sabasaba (77) mkoani humo.

NuLife Advanced  Fertility Centre continues to establish itself as a leading provider of advanced fertility care in Tanzania, delivering world-class reproductive solutions supported by strong clinical outcomes and international expertise. 

Over the past four years,the clinic has performed a significant successful number of cycles (OPU +FET) ,resulting in  more than 400 babies delivered through A.R.T with an overall success rate of 65%. 

NuLife Advanced Fertility Centre offers a full range of services including IVF, IUI, PRP, and TESA/PESA procedures, alongside advanced genetic testing (PGT-A) and a cryopreservation program.

They are one stop solution to all gynecological issues like fibroids,cysts all the way  up to mild,moderate and severe endometriosis.

They specialize in surgical skills using  keyhole surgery. As part of its commitment to excellence, the clinic partners with internationally renowned fertility expert Dr. Nayana Patel, working alongside NuLife’s own leading specialist, Dr. Madhav. 

These ongoing collaborations include knowledge transfer,technology transfer and skill set up gradation. A representative from NuLife Fertility Centre stated: "We are committed to making high-quality fertility care accessible while maintaining international standards, combining advanced technology with compassionate, patient-centered care."



 

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Neema Peter Majule, ameishauri Serikali kuboresha utendaji wa Wakala wa usajili, Ufilisi na udhamini (RITA) ili kuondoa ucheleweshaji wa utoaji wa vyeti vya vifo, hali inayowaathiri kwa kiasi kikubwa wananchi hususan yatima na wajane.

Akichangia hoja wakati wa uwasilishaji wa bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Aprili 24, 2026, Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Majule amesema RITA ni taasisi nyeti inayogusa moja kwa moja ustawi wa jamii, hivyo kuna haja ya kuongeza ufanisi, kasi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma zake.

Ameeleza kuwa kuchelewa kupatikana kwa vyeti vya vifo kunakwamisha jitihada za yatima wanaotaka kujiendeleza kielimu pamoja na wajane wanaohitaji kukamilisha taratibu za mirathi, akisisitiza kuwa huduma hizo zinapaswa kutolewa kwa wakati ili kulinda haki za makundi hayo.

Katika mchango wake, mbunge huyo pia amepongeza jitihada za Serikali kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign, akisema imekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za huduma za kisheria.

Amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusukuma mbele upatikanaji wa haki kwa wananchi, pamoja na Waziri na Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria kwa juhudi zao katika kusogeza huduma za msaada wa kisheria karibu na wananchi.

Hata hivyo, amesisitiza haja ya kuboresha zaidi huduma hiyo kwa kuanzisha mfuko maalum utakaowezesha wanufaika wa msaada wa kisheria kupata msaada wa gharama za usafiri na pesa ya kujikimu wanapofuatilia kesi zao.

Aidha, ametoa wito kwa mahakama kuharakisha usikilizwaji wa kesi ili ziweze kumalizika kwa wakati, pamoja na kutumia mbinu za kitaalamu ikiwemo tathmini za kisaikolojia ili kubaini mapema kesi za kubambikiwa na kuhakikisha haki inatendeka bila kuchelewa.

 

 Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi (hayupo pichani) wakati akifunga   mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi (hayupo pichani) wakati akifunga   mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

 Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga  mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

 Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga  mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

...

Waandaji wa ratiba za masomo nchini wamehimiza umuhimu wa kuandaa na kuzingatia ratiba zenye uwiano sahihi kati ya masomo ya nadharia na vitendo, wakisema hatua hiyo ni muhimu katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi stahiki, wenye tija kazini na wanaochangia maendeleo ya Taifa.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,wakati akifungua mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Dkt. Nchimbi amesema kuwa  ratiba ya masomo siyo tu mpangilio wa vipindi darasani, bali ni nyenzo muhimu inayochangia moja kwa moja ubora wa elimu na uwezo wa wahitimu kuhimili ushindani katika soko la ajira

"Ili kupata matokeo chanya, ni lazima ratiba zizingatie kwa uzito sawa masomo ya kinadharia na mafunzo ya vitendo, ambayo ndiyo yanawajengea wanafunzi ujuzi halisi unaohitajika kazini."amesema Dkt.Nchimbi

Aidha, ameeleza kuwa ratiba bora zinapaswa pia kuzingatia shughuli nyingine muhimu zinazochangia malezi na makuzi ya mwanafunzi, ikiwemo michezo, ubunifu na maendeleo ya vipaji, ili kuandaa wahitimu waliokamilika katika nyanja zote.

“Hatupaswi kuangalia masomo pekee, bali pia tunapaswa kuandaa mazingira yanayomjenga mwanafunzi kitaaluma, kijamii na kimaadili,” amesisitiza.

Aidha amesema hivi sasa kuwekuwepo na kilio kikubwa kutoka kwa ajiri kuwa wahitimu wanaomba ajira katika taasisi zao wengi wao hawana ujuzi hivyo kushindwa kukidhi mahitaji yao.

“Kumekuwapo na kilio kutoka kwa ajiri wengi kuwa vyuo vyetu vinatoa wahitimu wasiokuwa na ujuzi lakini hii inaanzia kwenye sula la uandaji wa ratiba za masomo ambao hauzingatii wanafunzi kujifunza kwa vitendo.

“Hivyo basi kama tunatakaa kutoka hapa tulipo, lazima kuanza kuweka mkazo kwenye uandaaji wa ratiba za masomo ambazo zinazaingatia kujifunza kwa nadharia na vitendo ili kupata mahitimu watakao kidhi mahitaji ya soko la ajira na kuondoa malalamiko yaliyopo hivi sasa,”amesema

Amesema, ratiba ni nyenzo muhimu katika kuboresha ufundishaji kwakuwa inaweza kuwa msaada katika kudhibiti matumizki ya fedha na rasimali watu zilizopo.

“Kama unakuwa na ratiba nzuri unaweza kudhibiti matumizi ya fedha na rasamalli watu iliyopo ikatumika kikamilifu kuhudumia idadi kubwa ya watu,”amesema

Amesema  kuwa yapo maeneo ambayo yamekuwa na malalamiko ya vipindi kugongana ama wanafunzi kukosa muda wa kushiriki mambo mengine kutokana na upangaji mbovu wa ratiba.

Kuhusu mafunzo hayo amesema kuwa lengo ni kuwajengea uwezo waandaji wa ratiba katika taasisi elimu nchini ili kuboresha utendaji kazi wao na kusaidia kupata mahitimu wenye ujuzi.

“Mafunzo haya tulianza kwa mara ya kwanza mwaka 2022, ambapo tuliona ipo haja kuwa na mafunzo kama ilivyo kwa tasnia nyingine, kwani kazi yetu inachangamoto nyingi sana hivyo ni vizuri tukutane na kuongezeana maalifa ili kuboresha upangaji wa ratiba katika taasisi zetu za elimu,”amesema

Kwa upande wake  Mratibu wa mafunzo hayo Vicktoria Kessy, amesema kuwa moja ya lengo la mafunzo hayo ni kusaidia kupunguza malalamiko ya wajiri kupata wahitimu wasiokuwa na ujuzi.

“Tunawafundisha wataalam hawa wa uandaaji wa ratiba za masomo katika taasisi za elimu nchini ili kuboresha upangaji wa ratiba unaozingatia uwepo wa mafunzo ya nadharia na vitendo ili kutoa wahitimu wenye ujuzi tofauti na ilivyo sasa,”amesema

Naye Katibu wa Jukwaa hilo, Deusdedith Youze, amesema kuwa hivi sasa serikali imefanya marekebisho ya mitaala ya elimu ili kuwezesha wanafunzi kupata mafunzo ya amali hivyo suala la ratiba inayozingatia mafunzo kwa vitendo ni muhimu.

“Tunashukuru tumepata washiriki kutoka katika vyuo Zaidi ya 15 ambao wanahusika katika uandaaji wa ratiba za masomo lengo ni kuwaongezea mbinu ambazo zitawasaidia kuaandaa ratiba ikiwamo matumizi ya teknolojia za kisasa,”amesema

Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga  mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Mratibu wa mafunzo Bi.Vicktoria Kessy,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungwa kwa  mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewahimiza waumini wa dini ya Kiislamu kuitumia vema misikiti kwa ajili ya kujadiliana na kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizopo katika jamii.

Alhaj. Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 24 Aprili 2026, alipojumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa iliyoambatana na ufunguzi wa Msikiti Mpya wa Jamaa Nour uliopo Boshowa, Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Ameeleza kuwa zipo changamoto nyingi katika jamii zinazohitaji kupatiwa ufumbuzi, hususan zile wanazokabiliana nazo watu wa makundi maalumu, wakiwemo wajane, wazee wasiojiweza, watoto, watu wenye ulemavu na mayatima.

Aidha, Alhaj Dkt. Mwinyi amesema waumini wana wajibu mkubwa wa kuitumia misikiti kusomesha dini, hususan kwa watoto ili waijue vema dini yao, pamoja na kusali kwa bidii na kumcha Mwenyezi Mungu, kwani hiyo ndiyo sababu kuu ya kujengwa misikiti mikubwa na mizuri katika maeneo mbalimbali.

Vilevile, Alhaj Dkt. Mwinyi amewahimiza waumini kuutunza msikiti huo mpya ili ubaki katika haiba na mazingira bora wakati wote, kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuchangia, pamoja na kuwatunza maimamu na walimu wa madrasa, na kumshukuru mfadhili wa msikiti huo kwa uamuzi wake.










Top News