Na Mwandishi wetu,
WAKULIMA wanatarajia makubwa ya hakikisho la uwepo wa Chakula Cha kutosha na Cha akiba kutokana na mazao kustawi kwa wingi shambani na hivyo kutarajia kupata mavuno mengi.

Wakulima wameyasema hayo leo tarehe 16 Januari 2026 mbele ya Afisa Tarafa Lisekese Emmanuel Shilatu alipo watembelea Wakulima Mashambani maeneo ya Kijiji cha Lukuledi B Kata ya Lukuledi kujionea hali ya Kilimo na kusikiliza na kutatua changamoto zao.

"Sisi Wakulima hatuna mashaka, mazao yamestawi na tunatarajia kupata mavuno mengi sana mvua zikiendelea kunyesha yatakayo pelekea kuwa na Chakula kingi na Cha akiba pia. Kwa ujumla tunaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia pembejeo kama vile Dawa na Mbegu zinazotupa faraja na hakikisho la Kilimo." Alisema Mkulima Yonas Edwin.

Akizungumza na Wakulima mbalimbali Shilatu aliwapongeza Wakulima hao na kuwapa angalizo la kuhifadhi Chakula.

"Nimekuja kuwatembelea kama ilivyo desturi yangu, nawapongeza Wakulima wote wa Tarafa yangu kwa kazi nzuri ya kulima na jambo la kufurahisha Wakulima wengi ni Vijana mmeamua kuwekeza kwenye Kilimo, hongereni sana. Najua uhakika upo wa mavuno mazuri kwa ajili ya Chakula na biashara. Angalizo msisahau kuweka akiba ya Chakula". Alisema Shilatu.

Nae Afisa Kilimo Kata Bi. Kuruthum amebainisha bayana endapo mvua zitaendelea kunyesha Wakulima wanatarajia kupata mavuno mengi kwani hatua za awali mazao yametoa dalili njema.

Maeneo mbalimbali kumekuwa na mvua zilizonyesha na Wakulima wametumia mvua hizo kulima mazao ya muda mfupi kama vile Mahindi, Mbaazi, Alizeti, Ufuta na Karanga.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela, kwa pamoja wakizindua rasmi Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai. Hafla hiyo ilifanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela wakisalimiana na baadhi ya wawekezaji na wakuu wa taasisi kutoka Dubai na Falme za Kiarabu katika hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo akizungumza wakati wakiwasili katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wakiwasili katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil akizungumza wakati wakiwasili katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Balozi wa Tanzania katika Falme za Kiarabu, Mhe. Balozi Luteni Jenerali Mstaafu, Yacoub Mohammed akizungumza wakati wakiwasili katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (wapili kushoto), akiwa ameongozana na Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Juma Malik Akil (kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (wapili kulia) wakati wakiwasili katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela, Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB na kampuni zake tanzu, pamoja na baadhi wawekezaji waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai, iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Washiriki wakifuatilia hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB wakifuatilia onyesho la ndege zisizo na rubani ‘drone’ likionyesha nembo ya Benki hiyo katika Falme za Kiarabu iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.
Washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB iliyofanyika jana katika ukumbi wa hoteli ya InterContinental, Dubai.

Dubai, UAE, 20 Januari 2026 – Mahusiano ya kiuchumi kati ya Afrika na Falme za Kiarabu (UAE) yamefikia hatua muhimu leo kufuatia uzinduzi rasmi wa Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai katika Kituo cha Fedha cha Kimataifa cha Dubai (DIFC). Hii ni mara ya kwanza kwa benki ya Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kupanua wigo wa huduma zake katika moja ya vituo vya fedha vyenye ushawishi mkubwa zaidi duniani.

Hatua hii inaweka Tanzania, pamoja na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, uchumi wa pamoja unaokaribia dola za Marekani bilioni 800, moja kwa moja katika mfumo wa mitaji ya kimataifa, kupitia taasisi ya fedha ya Kiafrika iliyoasisiwa barani Afrika, ikifanya kazi kama daraja kati ya fursa za kikanda na za kimataifa.

Uzinduzi huo uliwakutanisha viongozi wakuu kutoka taasisi za fedha za kimataifa, wawekezaji kutoka kote duniani, makampuni makubwa ya kimataifa na washirika wa maendeleo ya kifedha. Ushiriki huu unaonyesha kuongezeka kwa hamasa ya kimataifa kuhusu Afrika kama eneo linalofuata kwa ukuaji mkubwa wa uchumi duniani.

Hafla ya uzinduzi rasmi wa Ofisi hiyo iliongozwa na Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza kwa niaba ya Rais, Waziri Kombo aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuendeleza dira ya uchumi ya Tanzania kupitia diplomasia ya uchumi, jitihada ambazo zimekuwa zikitekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita. Alisema kuingia kwa benki hiyo Dubai ni mkakati madhubuti, akitaja nafasi ya Dubai kama kitovu kikuu cha mitaji ya dunia pamoja na uwepo wa mfumo imara wa kifedha na udhibiti.

“Uwepo wa benki ya Tanzania nchini Dubai utaimarisha mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Falme za Kiarabu, ukichochea biashara ambayo tayari imefikia takribani dola za Marekani bilioni 2.5 kwa mwaka. Aidha, utaimarisha muunganiko wa Afrika Mashariki na Kati na masoko ya kimataifa,” alisema Waziri Kombo.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Juma Akili, alisema hatua hiyo inaashiria kukomaa kwa sekta ya fedha ya Tanzania.

“Hatua hii muhimu inaonyesha ukomavu na kuongezeka kwa umahiri wa sekta ya fedha ya Tanzania, pamoja na uwezo wa taasisi zetu za ndani kushindana katika masoko ya fedha ya kimataifa.”

Ikiwa na idadi ya watu zaidi ya milioni 60, Tanzania imeonyesha uthabiti mkubwa wa kiuchumi kwa zaidi ya miongo miwili, ikidumisha ukuaji wa Pato la Taifa wa wastani wa asilimia 6–7 na kudhibiti mfumuko wa bei katika viwango vya tarakimu moja. Uthabiti huu umeifanya Tanzania kujijengea nafasi ya kipekee kama lango la uchumi linalounganisha Bahari ya Hindi na masoko ya nchi zisizo na bandari za Afrika Mashariki na Kati.

Kwa kuzingatia nafasi hiyo ya kimkakati, Benki ya CRDB imekuwa miongoni mwa taasisi za kifedha zilizo mstari wa mbele kuchochea ukuaji wa uchumi wa kikanda. Tangu kuanzishwa kwake miaka 30 iliyopita, Benki imekua sambamba na uchumi wa Tanzania na ajenda ya muunganiko wa kikanda. Kwa sasa, Benki ya CRDB inahudumia zaidi ya wateja milioni sita katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na jumla ya mali inayozidi dola za Marekani bilioni 9, na uwepo katika Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Akizungumza katika hafla hiyo, Abdulmajid Nsekela, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kundi la Benki ya CRDB, alisema upanuzi wa benki kwenda Dubai ni hatua ya kimantiki katika mkakati wa kikanda unaotokana na jiografia ya uchumi wa Tanzania na ajenda ya muunganiko wa Afrika.

“Benki ya CRDB imejengwa katika misingi ya kufadhili ukuaji wa Tanzania. Jinsi ambavyo Tanzania imekuwa ikikua na kuwa lango la uchumi katika ukanda huu, ndivyo Benki nayo imekuwa ikikua kikanda,” alisema. “Dubai sasa inatuwezesha kuunganisha mitaji ya kimataifa, Tanzania, na Afrika Mashariki na Kati.”

Afrika Mashariki na Kati kwa pamoja zinawakilisha soko la karibu watu milioni 400, ikishuhudia kuongezeka kwa biashara ya ndani ya Afrika, upanuzi wa miundombinu, rasilimali kubwa za madini na nishati, pamoja na nguvu kazi changa zaidi duniani. Afrika kwa ujumla ina watu bilioni 1.4, uchumi nwenye thamani ya dola za Marekani trilioni 3.4, na inatarajiwa kuwa robo ya idadi ya watu duniani ifikapo mwaka 2050.

Licha ya ukubwa huu, upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu bado ni changamoto kubwa. Ofisi ya Uwakilishi ya Benki ya CRDB Dubai imeanzishwa kuziba pengo hili kwa kuanzisha miradi, kupanga miundo ya ufadhili na kuhamasisha mitaji ya kimataifa kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika ukanda huu. “Afrika haina uhaba wa fursa,” alibainisha Nsekela. “Mara nyingi kinachokosekana ni daraja kati ya mitaji na utekelezaji. Ofisi hii ndiyo daraja hilo.”

Kwa kuanzisha uwepo wa benki ya Tanzania katika Dubai, Benki ya CRDB inatarajiwa kuimarisha ufadhili wa biashara, kuvutia mitaji ya uwekezaji na ushirikiano na taasisi za kifedha za kimataifa kati ya Ghuba na Afrika, ikitumia Tanzania kama lango la Afrika Mashariki na Kati. Ofisi hiyo pia inaongeza ushiriki wa Tanzania na ukanda huu katika masoko ya fedha za Kiislamu, ambayo thamani yake duniani inazidi dola za Marekani trilioni 4.

Neema Mori, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, alisema hatua hiyo inaakisi kuongezeka kwa imani kwa Benki hiyo kufanya kazi kwa viwango vya juu zaidi duniani. “Hiki ni kielelezo ni kauli kuhusu utawala bora, uwezo na uaminifu wa Benki yetu kimataifa,” alisema. “Uwepo wa Benki ya CRDB Dubai unaonesha kuwa benki za Afrika zinaweza kuanzisha ushirikiano wa kimataifa huku zikiendelea kuzingatia vipaumbele vya maendeleo ya Afrika.”

Viongozi wa Mamlaka ya Huduma za Fedha ya Dubai (DFSA) wameikaribisha Benki ya CRDB katika Kituo cha Fedha cha Kimataifa Dubai (DIFC), wakibainisha kuwa uwepo wa benki ya Kiafrika yenye mizizi imara ya kikanda unaimarisha korido ya fedha kati ya Afrika na Mashariki ya Kati, na kuboresha mtiririko wa mitaji ya muda mrefu kuelekea masoko yanayochipukia.
JESHI  la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa watatu ambao ni Mseveni Menat, Mkazi wa Uyole, Fred Lulandala, Mkazi wa Mapelele na Joseph Ngelenge, Mkazi wa Uyole Jijini Mbeya kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya Bhangi yenye uzito wa Kilo 168.

Watuhumiwa walikamatwa Januari 21, 2026 baada ya kuingia katika Stendi Kuu ya Mabasi Jijini Mbeya wakiwa kwenye Bajaji yenye namba za usajili MC 850 EWN aina ya TVS Kings wakiwa na dawa hizo za kulevya zikiwa kwenye mabegi nane wakitaka kuzisafirisha kuelekea Jijini Arusha.

Watuhumiwa wameeleza kuingiza nchini dawa hizo kutoka nchini jirani na walitaka kuzisafirisha kwa njia ya Basi kuelekea Jijini Arusha. Upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

WATIWA MBARONI KWA WIZI WA PIKIPIKI YA MAGURUDUMU MATATU.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa watatu ambao ni Ajiri Mwapelele, Mkazi wa Iganzo, Evils Shabani, Mkazi wa Igodima Jijini Mbeya na Victor Paulo, Mkazi wa Igurusi Wilaya ya Mbarali kwa tuhuma ya wizi wa Pikipiki ya Magurudumu matatu maarufu Guta yenye namba za usajili MC 495 FFY aina ya Sinoray.

Watuhumiwa waliiba Pikipiki hiyo Januari 21, 2026 saa 9 usiku huko katika Kijiji cha Uhenga, Wilayani Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe kwa mtu aitwaye Haruna Shomari Mahagile, Mkazi wa Kijiji cha Uhenga na kisha kuisafirisha Pikipiki hiyo hadi Mkoani Mbeya kwa ajili ya kuiuza.

Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilianza ufuatiliaji na Januari 21, 2026 saa 5 asubuhi huko Iganzo, Jijini Mbeya lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa na mali hiyo ya wizi. Upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa baadhi ya wananchi ambao bado wanajihusisha na uingizaji, usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya kuacha mara moja kwani ni kinyume cha sheria n ani hatari kwa afya zao na za wengine hususani vijana. Pia, wakumbuke ukikamatwa na utakapopatikana na hatia adhabu yake ni kifungo na usafiri uliotumika kusafirishia utataifishwa kwa mujibu wa sheria. Aidha, linatoa wito kwa baadhi ya watu wenye tamaa ya kujipatia mali kwa njia zisizo halali kuacha mara moja na badala yake watafute shughuli halali ili kujipatia kipato halali kwani kwa mujibu wa sheria ni uhalifu na haulipi na hauna nafasi kwenye jamii. Lakini uhalifu wowote ule kijamii ni aibu kwako na una dhalilisha familia.
Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
WATUHUMIWA wawili, Amasha Iddi Mrisho (40), mkazi wa Buza, Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32), raia wa Msumbiji, Januari 22, 2026, wamefikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya skanka.

Akisoma maelezo ya awali ya shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mhe. Lukosi, Mwendesha Mashtaka wa Serikali Wakili Nicas Kihembe akisaidiana na Erick alidai kuwa washtakiwa hao walikamatwa tarehe 08 Desemba 2025 katika mtaa wa Wailes, Temeke, Dar es Salaam, na maofisa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, wakati wa operesheni hiyo, DCEA ilikamata pakiti 20 za Bangi aina ya skanka zenye uzito wa jumla wa kilogramu 20.03, ambazo zilikuwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba, kisha kufichwa katika basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili wa Msumbiji AAM 297 CA.

Ilielezwa zaidi kuwa, mashtaka yanayowakabili washtakiwa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 16(I) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, inayokataza umiliki, usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya nchini.

Upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa, shtaka hilo halina dhamana kutokana na uzito wa dawa za kulevya walizokutwa nazo washtakiwa

Aidha, kwa mujibu wa wakili wa Serikali, upelelezi wa shauri hilo namba 1535/2026 ya mwaka 2026 bado unaendelea na mashahidi wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo siku itakayopangwa.

Shauri hili lilihairishwa hadi tarehe 05 februari 2026, huku washtakiwa wakirejeshwa rumande.









MERIDIANBET haikuja na kelele, imekuja na mpango mkakati kwa ajili ya wateja wake. Imeileta promosheni maalumu kupitia mchezo wa Super Heli ikiwa ni promosheni inayompa mchezaji udhibiti wa safari yake ya ushindi. Kila unapocheza, unajenga nafasi yako mwenyewe ya kuondoka na Samsung A26 mpya. Hapa, mchezaji ndiye rubani wa helikopta yake.

Katika kipindi ambacho kumekua na promosheni nyingi zisizo na matokeo, Meridianbet imeweka msimamo tofauti. Kila Jumatatu, mshindi mmoja hupatikana na kuondoka na Samsung A26 mpya kabisa. Ndani ya mwezi mmoja, washindi wanne wanathibitisha kuwa huu si mkakati wa matangazo tu, bali ni ushindi unaoonekana na kila mshiriki ana nafasi sawa.

Super Heli imejengwa juu ya kanuni moja muhimu, cheza zaidi, songa mbele zaidi. Kadri unavyoshiriki mara nyingi, ndivyo alama zako zinavyoongezeka na nafasi zako kupanuka. Huu ni mchezo unaothamini uaminifu wa mchezaji, bidii, na uthubutu wa kuendelea. Kila raundi ni mchango wako binafsi kuelekea ushindi.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kupitia akaunti yako ya Meridianbet, kila kitu kinafanyika kwa uwazi na urahisi. Mfumo wa kisasa unakuwezesha kucheza bila usumbufu, kufuatilia maendeleo yako, na kushiriki promosheni bila vikwazo. Super Heli ni ushahidi kuwa Meridianbet inaelewa mchezaji wa kisasa anayehitaji burudani yenye thamani ya ziada.

Super Heli inaendelea, lakini muda hausimami. Kadri siku zinavyopita, ndivyo nafasi zinavyopungua na ushindani kuongezeka. Huu ni wakati wa kuchukua hatua, sio kusubiri. Tembelea Meridianbet.co.tz sasa, ingia kwenye Super Heli, na ujihakikishie nafasi yako kabla ushindi haujachukuliwa na mwingine.

Na.Vero Ignatus, Arusha 

Wakala wa vipimo mkoani Arusha WMA wametoa onyo Kali Kwa wauzaji wa vitunguu kuacha kutumia vipimo vya  Rumbesa badala yake watumie vipimo vya mizani ili kupata thamani ya pesa na ujazo kamili bila kumuumiza mkulima wa zao la kitunguu.

Hayo yameelezwa na Afisa kutoka Wakala wa  Vipimo mkoani hapa,Jassson Theonest  Wakati akitoa elimu Kwa wakulima wa vitunguu wa Bonde la Eyasi wilayani karatu,mkoani Arusha, amesema matumizi  sahihi ya mizani  ni msaada mkubwa kwa wakulima, kwani yanahakikisha kila kilo inafikishwa sokoni ipasavyo, kuongeza mapato yao na kuimarisha biashara zao.

Amesema kuwa endapo mtu yeyote atakiuka maagizo hayo hatua Kali za kisheria  zitachukuliwa na sambamba na akutozwa fain kuanzia milion Moja mpk milion 20 Kwa mujibu wa sheria.

Nasisitiza tena kwenu wakulima na mlitambue jambo hili kwamba matumizi sahihi ya mizan ni msaada mkubwa kwenu wakulima, kwani yanahakikisha kila kilo inafikishwa sokoni ipasavyo, kuongeza mapato yenu na kuimarisha biashara zenu"alisema.

Sambamba na hilo wakala ya Vipimo imefanya mafunzo kwa wakulima wa vitunguu katika maeneo ya Karatu na Mang’ola, yakilenga kuwafundisha kuepuka kutumia mizani batili na kuhakikisha wanapata kilo halisi za mazao yao.

Wakulima wa vitunguu Moshi Hitler na  Joyce Elia wamesema kwamba kutumia mizani isiyo sahihi iliwanyima haki zao, kwa kuwa mara nyingi walipoteza kiasi kikubwa cha mazao yao kwa kuuzwa chini ya kilo halisi, hali iliyosababisha kupoteza mapato na kushusha morali yao. Baadhi walisema walihisi kunyonywa na wakuu wa masoko ambao walitumia mizani batili kuwazidishia hasara.

Wakulima hao waliishukuru Mamlaka Hiyo kwa kutoa elimu hii muhimu na kuahidi kuanza kutumia mizani sahihi kila wanapouza vitunguu vyao.


 


NAFASI ya ushindi hii hapa na wakali wa Meridianbet ambapo kupitia promosheni ya Beti Online unaweza ukaondoka na Samsung A26. Weka dau lako kuanzia 5000 na ubashiri hapa.

Meridianbet inaendelea kuwa kinara katika kutoa promosheni zenye thamani halisi kwa wachezaji wake. Kupitia kampeni yake mpya, kampuni hii inaleta fursa murua kwa mashabiki wa mpira kushiriki bashiri za mechi za Ligi kwa dau la kuanzia shilingi 5,000 tu na kuingia kwenye droo ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A26. Hii ni ofa inayochochea ushindani, msisimko na thamani kwa kila mchezaji anayejiunga.

Meridianbet wanasema kuwa ili ujiweke kwenye nafasi ya kuondoka na simu janja hii hapa na uwe wa Kidigitali kabisa ni vyema ukabashiri mara nyingi zaidi kwani kufanya hivyo kunakuweka karibu na ushindi leo hii wa Samsung A26.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kampeni hii inalenga kuongeza hamasa kwa mashabiki kufurahia mechi za Ligi wakiwa na matumaini makubwa. Kila ubashiri unaowekwa si tu unaleta msisimko wa kutafuta ushindi wa dau, bali pia msisimko wa kusubiri droo ya kujua kama wewe ndio mteule wa kupata simu mpya. Huku mashindano yakiendelea kila wiki, kila mchezaji anapata nafasi nyingi kadri anavyobashiri mara kwa mara.

Washindi wa promosheni hii watatangazwa kila Ijumaa ambapo ndio siku ambayo simu hutolewa hivyo usikae mbali na fursa hii kwani inakupa nafasi ya wewe kumiliki simu kali ambayo itakufanya uweze kuperuzi.

Kumbuka kuwa unapoingia kwenye mashindano haya ya kuwania Samsung A26, hutakiwi Kuturbo Mkeka wako au CASH OUT kwa namna nyingine haitahusika kwani inatakiwa usubiri jamvi lako limalizike.

Na kufanya hivyo kutakufanya ujiondoe kwenye mashindano kwani tiketi yako itahesabika kama batili. Hivyo subiri hadi mechi zote zikamilike ndipo uweze kuingia kwenye wachezaji ambao sio batili.



Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja TANESCO Mkoa wa Ruvuma Alan Njiro, amewataka wananchi kuacha kabisa tabia ya kukata miti au kufanya shughuli zozote karibu na miundombinu ya umeme wakati umeme ukiwa unawaka ni hatari na inaweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo vifo, kwani TANESCO hulazimika kukata umeme kwanza kabla ya kufanya kazi yoyote kwenye nguzo au transfoma ili kuhakikisha usalama wa wafanyakazi na wananchi kwa ujumla.

Akizungumza na wakazi wa  Gumbiro, Halmashauri ya Madaba, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, Njiro amesisitiza kuwa umeme ni hatari na unahitaji tahadhari kubwa wakati wote, amesema ajali nyingi za umeme husababishwa na uzembe au uelewa mdogo wa wananchi juu ya matumizi salama ya umeme.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kutumia muda wao kuwakumbusha watoto kuwa umeme ni hatari na unaweza kuua, hivyo hawapaswi kuchezea nyaya za umeme, hasa zile zilizoanguka chini au nyaya za “stay” zinazochimbiwa ardhini, ameonya kuwa kuchezea miundombinu hiyo kunaweza kusababisha majanga yanayoweza kuepukika endapo tahadhari zitazingatiwa.

Njiro pia ametoa wito kwa wakulima ambao mashamba yao yana nguzo za umeme kuacha mazoea ya kulima karibu na nguzo hizo au kushika nyaya za umeme, amesema kufanya hivyo kunahatarisha maisha yao, na amesisitiza umuhimu wa kuchukua tahadhari ili kuhakikisha wanakuwa salama muda wote.

Ameongeza kuwa endapo mwananchi anahitaji kukata miti katika eneo lenye nguzo au nyaya za umeme, anapaswa kuwasiliana na TANESCO ili wataalamu wafike kushusha nyaya na kuzima umeme kabla ya zoezi hilo kufanyika, Kwa maeneo hatarishi zaidi, amesema TANESCO hulazimika kukata miti hiyo wenyewe ili kuzuia ajali na kulinda usalama wa wananchi.

Katika hatua nyingine, Njiro amewakumbusha wananchi kuwa maombi ya kuunganishiwa umeme ni bure, na gharama ya kupata umeme vijijini ni shilingi elfu 27 tu, amesisitiza kuwa malipo hayo hufanyika kupitia namba ya kumbukumbu ya malipo na si kumpa mtu fedha mkononi, akiwataka wananchi kuwa waangalifu ili kuepuka utapeli.

TANESCO Mkoa wa Ruvuma imewahimiza wananchi kuzingatia taratibu za usalama wanapohitaji kukata miti karibu na miundombinu ya umeme kwa kushirikiana na TANESCO, Ushirikiano huo utasaidia kulinda maisha ya wananchi, kuepusha majanga yasiyo ya lazima na kuhakikisha miundombinu ya umeme inalindwa kwa manufaa ya jamii nzima.



 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amefanikiwa kumaliza mgomo wa wafanyakazi zaidi ya 1,500 wa Kiwanda cha NAMERA kilichopo Gongolamboto, jijini Dar es Salaam, mgomo uliokuwa umeanza tarehe 16 Januari, 2026.

Mgomo huo ulitokana na madai ya mishahara, ambapo mshahara wa kima cha chini kwa sekta binafsi umewekwa kwa mujibu wa Tangazo na Amri ya Serikali Namba 605A ya tarehe 13 Oktoba, 2025, inayotoa ongezeko la wastani wa asilimia 33.4. Kutokana na ongezeko hilo, mshahara wa chini umeongezeka kutoka Shilingi 275,060 mwaka 2022 hadi Shilingi 358,222 mwaka 2025. Hivyo basi, hakuna mtu au taasisi yoyote inayoruhusiwa kulipa mshahara chini ya kiwango kilichobainishwa katika Amri hiyo ya Serikali, hata kwa kuwepo kwa makubaliano yoyote kati ya taasisi binafsi kupitia chama chao cha waajiri (ATE) au mifumo mingine ya ndani.

Akizungumza na wafanyakazi pamoja na uongozi wa kiwanda hicho, Mhe. Mpogolo amesisitiza kuwa Amri ya Serikali ni ya lazima kutekelezwa na kwamba hakuna kampuni, taasisi au mwajiri yeyote anayekubalika kushuka chini ya viwango vilivyowekwa kisheria. Ameeleza kuwa makubaliano yoyote hayawezi kwenda kinyume na Amri ya Serikali.

Mpogolo ametoa maelekezo muhimu kwa uongozi wa kiwanda na wafanyakazi, ikiwemo kuhakikisha malipo ya mishahara yanatolewa kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Na. 605A la mwaka 2025, huku akisisitiza kuwa hakuna mfanyakazi atakayefukuzwa kutokana na kushiriki mgomo, ili kuimarisha mahusiano bora kati ya mwajiri na waajiriwa. Aidha, ameitaka kiwanda kushirikiana na Chama cha Wafanyakazi (TUICO) na Afisa Kazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kufanyika uchaguzi wa viongozi wa wafanyakazi watakao kuwa kiungo madhubuti kati ya wafanyakazi na uongozi, pamoja na kupitia mikataba ya ajira kuhakikisha inakidhi sheria na kanuni zinazohitajika. Mpogolo pia amehimiza ujenzi wa mahusiano mazuri na kulinda kiwanda kutokana na mchango wake mkubwa katika uchumi wa taifa na nafasi zake muhimu za ajira kwa wananchi.

Kwa upande wao, wafanyakazi wa kiwanda hicho wameeleza kuridhishwa na hatua zilizochukuliwa na Mkuu wa Wilaya, wakisema kuwa zimeleta matumaini mapya na kurejesha amani kazini. Wameahidi kurejea kazini mara moja na kuendelea kutekeleza majukumu yao kama kawaida.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam (RPC), ACP Yustino Mgonja, amepongeza juhudi za Mhe. Mpogolo katika kushughulikia mgogoro huo kwa haraka na kwa busara. ACP Mgonja amesema hali ya usalama katika eneo la kiwanda ni shwari na amewahakikishia wafanyakazi kuwa wapo salama.

Kwa upande wake, mmiliki wa Kiwanda cha NAMERA amesema yupo tayari kutekeleza makubaliano yote yaliyofikiwa kati ya uongozi wa kiwanda na Serikali, huku akiahidi kuboresha mazingira ya kazi na kuimarisha ushirikiano kati ya waajiri na wafanyakazi kwa maslahi ya pamoja.

Dc. Mpogolo amesema kuwa kiwanda hicho ni muhimu sana, hasa katika upande wa ajira. Hivyo basi, migogoro inaweza kuharibu upatikanaji wa ajira na ukuaji wa uchumi, kwa hivyo migogoro si jambo zuri.

Kufuatia kumalizika kwa mgomo huo, shughuli za uzalishaji katika Kiwanda cha NAMERA zinatarajiwa kurejea kama kawaida, huku wafanyakazi wakirejea kazini wakiwa na ari mpya ya kufanya kazi.



Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, ameitaka Wakala wa Vipimo (WMA) nchini kuongeza uwajibikaji katika kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Sheria ya Vipimo ili kuwalinda walaji dhidi ya udanganyifu na kuhakikisha wanapata bidhaa na huduma kulingana na thamani halisi ya fedha zao.

Londo amesema usimamizi madhubuti wa vipimo ni msingi muhimu katika kujenga uchumi shindani, himilivu na jumuishi, sambamba na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Ameyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Vipimo katika Kituo cha Uhakiki wa Vipimo Misugusugu Mkoa wa Pwani, ambapo amesisitiza kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara imejipanga kuhakikisha kunakuwepo na mazingira wezeshi ya biashara huku ikijenga imani kwa walaji katika huduma na bidhaa wanazopata.

Naibu Waziri ameongeza kuwa kutokuwepo kwa usimamizi sahihi wa vipimo kunawanyima walaji haki zao za msingi na kudhoofisha ushindani wa haki katika biashara, jambo linaloweza kuathiri ukuaji wa uchumi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo Bw. Alban Kihulla amewasihi Wananchi kushirikiana na Wakala huo kwa kutoa taarifa pindi wanapobaini kupatiwa huduma kwa kutumia vipimo visivyo sahihi, akisema ushirikiano wa Wananchi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti vitendo vya udanganyifu na kuimarisha haki katika biashara.

Wakala wa Vipimo ina jukumu la kuhakikisha vipimo vinavyotumika katika biashara vinakuwa sahihi kwa mujibu wa Sheria, hatua inayolenga kulinda maslahi ya walaji na kukuza biashara nchini.






Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Muyungi muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi hizo Mjini Zanzibar leo Alhamisi Januari 22, 2026.

*********************

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimepanga kuimarisha mashirikiano ili kuhakikisha fursa za Muungano zinawanufaisha wananchi na kuakisi maono ya Waasisi.

Hayo yamesemwa leo Alhamisi (Januari 22, 2026) Mjini Zanzibar na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa ziara yake aliyoifanya kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.

Dkt. Muyungi amesema Serikali zote mbili zimekuwa mstari wa mbele katika kutatua hoja za Muungano hatua inayolenga katika kufungua fursa za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar.

“Waasisi wetu walikuwa na malengo ya kubainisha fursa za mashirikiano ziweze kuwanufaisha wananchi, hivyo wakati umefika sasa wa kuhakikisha fursa hizo zinakuwa agenda muhimu tunazopaswa kuzibeba kama Watendaji wa Serikali” amesema Dkt. Muyungi.

Ameeleza kuwa ni wakati mwafaka wa kuenzi kwa matendo maono ya viongozi na waasisi wa Muungano kwa kuhakikisha wananchi wa pande zote mbili wananufaika ipasavyo kwa kufanya hivyo kutafsiri nia na malengo ya waasisi.

“Hadi sasa hoja 22 za Muungano zimepatiwa ufumbuzi, tumebaki na hoja 3 sawa na mafanikio ya asilimia 99 ya utatuzi wa hoja….ni muhimu kuhakikisha kuwa utatuzi wa hoja hizo unaleta manufaa endelevu kwa wananchi” amesema Dkt. Muyungi.

Aidha Dkt. Muyungi ameshauri kurejeshwa kwa mashindano ya michezo ya pasaka ambayo hapo awali yalikuwa ni sehemu muhimu ya kuimarisha mahusiano na mashiriano baina ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Akifafanua zaidi Dkt. Muyungi amesema viongozi na watendaji wa serikali zote mbili wamekusudia kutangaza fursa za muungano kwa wananchi na kuwahimiza wataalamu kuchakata fursa hizo ili kuona njia bora ya kuwanufaisha wananchi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapnduzi Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum Ofisi hizo zimekuwa zikishirikiana kwa karibu katika kuimarisha uratibu wa masuala ya Muungano na hatua hiyo imeendelea kuwanufaisha wananchi wa pande zote mbili.

“Katika kikao baina yetu tumekubaliana kuimarisha mashirikiano kupitia vikao vya pamoja na tumepanga wataalamu wetu kuweza kukutana ili kuandaa maazimio na kuangalia namna bora zaidi ya kuimarisha Muungano wetu” amesema Dkt. Islam.


Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Hassan Mitawi akifuatila mazungumzo baina ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Dkt. Islam Seif Salum akizungumza wakati wa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa ziara yake ya kujitambulisha leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum (mbele kulia) akizungumza wakati wa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa kikao baina yao kilichofanyika Mjini Zanzibar leo Alhamisi Januari 22, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Hassan Mitawi (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Juma Mohammed Salum (katikati) wakifuatilia kikao bainaya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum.

Katbu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Muyungi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi akiongozana na Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Mitawi muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum.

(NA MPIGAPICHA WETU)





Na Oscar Assenga,TANGA


BENKI Kuu ya Tanzania (BOT) imesema kwamba taasisi ndogo zinazotoa huduma za kubadilisha fedha za kigeni nchini zinapaswa kusajiliwa ili ziweze kupata leseni ya kuendesha shughuli zao,kinyume na hapo ni kosa kisheria.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Afisa Mwandamizi Mkuu kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mwile Kauzeni wakati alipokuwa akizungumzia na Waandishi wa habari kwenye viwanja vya Usagara Jijini Tanga, eneo ambalo Maadhimisho ya Wiki ya fedha kitaifa yanafanyika mwaka huu.

Mwile alikuwa akijibu Swali la Wanahabari waliotaka kujua hatua ambazo zinachukuliwa na benki kuu ya Tanzania katika kudhibiti Watu wanaoendesha biashara ya kubadilisha fedha kiholela.

Ambapo badala yake aliwasihi kufuata Sheria hatua ambayo itawawezesha kupata inayoruhusu uendeshaji kazi hiyo.

Alisema kuwa, ili mtu kufanya biashara hiyo anapaswa kufuata taratibu za kisheria kwa vile kinyume chake atakuwa ametenda kosa la jinai ambapo amewataka wale wenye nia kuendesha shughuli hiyo kutembelea matawi yake.

Aidha alisema taasisi ndogo za huduma za fedha zinahitaji kusajiliwa ili kuweza kupata leseni BOT kutokana na kwamba kubadilisha fedha bila leseni ni kosa kisheria

Awali akizungumza Afisa Mchambuzi Masuala ya Fedha wa BOT Charles Kanuda alisema kwamba, Serikali imekuja na mfuko wa udhamini wa mikopo ambapo kwa mtanzania anayehitaji mkopo huku akiwa hana dhamana toshelevu atapata dhamana mpaka asilimia 75.

Kanuda alisema kwamba,watu wengi wamekuwa wakijaribu kwenda kukopa huku wakiombwa dhamana yenye thamani kubwa zaidi ya mikopo wanayohitaji na hivyo kushindwa kupata mikopo.

Amesema kwamba hali hiyo imewasababisha watanzania walio wengi kushindwa kuchukua mikopo au kuchukua kiasi kidogo jambo ambalo limeathiri ufanisi wa biashara zao wanazoziendesha.

Katika maadhimisho haya ya wiki ya fedha kitafa yenye kauli mbiu ya " elimu ya fedha , msingi wa Maendeleo ya kijamii na kiuchumi" Wadau mbalimbali walitembelea na kupatiwa elimu banda la BOT.

Mwajuma Kileo ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Mkwakwani Jijini Tanga, yeye alielezea kuridhishwa kwake na elimu aliyoipata baada ya kutembelea banda hilo la BOT.

Alisema kwamba, kwa kutembelea banda hilo alijifunza namna ya kutambua fedha bandia mambo ambayo pia walikuwa wakiwafundisha wanafunzi kupitia somo la uraia wanapokuwa Shule.

Adrus Mahmoud (12) mwanafunzi wa darasa la sita kwenye Shule hiyo ya Mkwakwani,alisema amefarijika kupatiwa elimu ya ziada juu ya kutambua alama za kificho zilizomo kwenye noti na hivyo kumsaidia kubaini zilizo za bandia.


Na OWM- TAMISEMI, Dodoma

Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25 imeonesha mafanikio makubwa, ambapo rangi ya kijani imetawala katika viashiria vingi vya utekelezaji, ikiwa ni ishara ya kufanya vizuri kwa mikoa na halmashauri nchini.

Hayo yamesemwa leo Januari 22,2026 jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, wakati akifungua mkutano wa tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25.

Prof. Shemdoe amesema Taifa limeendelea kupiga hatua kubwa katika kuboresha hali ya lishe kwa wananchi, hali inayochangia kuimarisha nguvu kazi yenye afya bora na kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

“Nawashukuru Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Maafisa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa pamoja na viongozi na watendaji wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mikoa na Halmashauri kwa kazi kubwa ya kusimamia, kuratibu na kutekeleza Mkataba wa Lishe,” amesema Prof. Shemdoe.

Amewahakikishia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI itaendelea kushirikiana na kuwapa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kupunguza na hatimaye kutokomeza kabisa matatizo ya lishe nchini inafikiwa.

Amebainisha  kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya utekelezaji wa usia wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyehimiza kuimarishwa kwa sekta za Elimu, Afya na Uchumi ili kupambana na maadui watatu wa Taifa ambao ni ujinga, maradhi na umasikini.

Prof. Shemdoe amesema uwekezaji katika lishe ni mkakati wa kiuchumi wenye tija kubwa, na kwamba Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 imeipa kipaumbele kujenga jamii yenye afya kwa kuzingatia lishe bora ili kila mwananchi astawi.

Aidha, amesema Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025/30, ibara ya 2.3.2 (xi), imetambua umuhimu wa lishe katika kulinda na kujenga afya za wananchi, ambapo CCM itaendelea kuhimiza na kusimamia upatikanaji wa lishe bora kwa wote.

Akizungumza kuhusu dhana ya lishe bora, Prof. Shemdoe amesema ni matokeo ya kutokuwepo kwa magonjwa mwilini pamoja na ulaji sahihi wa vyakula vyenye virutubishi vyote vinavyohitajika.

Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuanza utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hatua itakayosaidia kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma stahiki za afya na kushinda adui maradhi.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, amesema lishe ni suala la msingi katika ukuaji wa binadamu kiakili na kimwili, sambamba na kuongeza tija katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Naye,Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu  anayeshughulikia afya Prof.Tumaini Nagu amesema serikali itaendelea  kusimamia kwa karibu utoaji wa huduma za lishe katika Mikoa na Halmashauri zote nchini.









Top News