Mwaka 1976, Mtafiti wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey aligundua nyayo za zamadamu eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano iliyolipuka kwenye milima ya Ngorongoro zaidi ya miaka milion 3.6 iliyopita. Wataalamu wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale waitwao Australopithecus Afarensis.

Nyayo za Zamadamu Laetoli Ngorongoro ni ushahidi usiopingika kuwa zamadamu (Hominin) wa umri wa miaka milioni 3.66 iliyopita walitembea wima kwa miguu miwili eneo la Laetoli Tanzania.

Kutembea wima kwa miguu miwili kunatutofautisha wanadamu na wanyama kama Sokwe na Nyani waliotokana na babu/bibi mmoja miaka takribani millioni 7 iliyopita.

Uwepo wa Nyayo na masalia ya binadamu, ndege na wanyama, urithi wa utamaduni, mambo kale, mimea, maji, matunda na kila kitu kinachomfanya binadamu kuishi ni kiashiria kuwa pengine bustani ya Eden ni Ngorongoro ni mahali ambapo tunda la mti wa katikati lililiwa.



NA. MWANDISHI WETU – Dar es Salaam

KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mradi wa DART amesema Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha inamaliza changamoto ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam, ili wananchi waweze kupata huduma bora, ya haraka na yenye uhakika.

Akizungumza mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miundombinu ya usafirishaji jijini humo, Dkt. Yonazi amesema Serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuboresha sekta ya usafiri wa umma.

Alisema katika ziara hiyo, kamati ilitembelea Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART) pamoja na Kampuni ya Uendeshaji wa Mabasi Yaendayo Haraka (UDART) na kujionea maendeleo ya uwekezaji uliofanywa.

“Ni dhamira ya Serikali kuhakikisha usafiri wa Dar es Salaam unakuwa bora, wa kisasa na unaokidhi mahitaji ya wananchi. Tumejionea miundombinu iliyowekwa na jitihada zinazoendelea kuboresha huduma,” alisema.

Dkt. Yonazi alibainisha kuwa tayari kampuni zimeanza kuleta mabasi mapya, hatua itakayoliwezesha jiji hilo kuwa miongoni mwa majiji yenye usafiri wa kisasa barani Afrika. Aliongeza kuwa mabasi mengi yatatumia gesi asilia, huku Serikali ikiwa imejenga miundombinu ya vituo vya gesi ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kwa urahisi.

Aidha, alisema Serikali imewekeza katika mifumo ya TEHAMA itakayomwezesha mwananchi kutumia kadi maalumu kulipia nauli bila kulazimika kupanga foleni, jambo litakaloongeza ufanisi na kupunguza usumbufu.

Katika hatua nyingine, aliwahakikishia wananchi kuwa mabasi yote yaliyoharibika yatafanyiwa ukarabati na kurejea barabarani ili kuimarisha upatikanaji wa huduma.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Bw. Said Tunda alisema lengo kuu ni kurejesha furaha kwa wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwapatia usafiri wa uhakika.

Pia aliwataka waendesha daladala kuendelea kutoa huduma huku Serikali ikiendelea kufanya mazungumzo nao ili kupata utaratibu bora wa ushirikiano, hususan kwa zile zilizopewa kibali cha kutumia barabara ya mwendokasi.

Hatua hizo zinaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha maisha ya wananchi kupitia miundombinu imara na huduma bora za kijamii.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) anayemaliza muda wake, Bi. Veronica Nduva, tarehe 28 Februari, 2026 Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na masuala mengine, Katibu Mkuu ambaye anamaliza muda wake alimshukuru Mheshimiwa Rais na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi chote cha kuhudumu kama Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.




 

Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, ameanika hadharani kile kinachoonekana kuwa ni ukaidi na kusuasua kwa utendaji kazi ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Same, baada ya maelekezo ya mfululizo ya serikali kuhusu usalama wa umma kupuuzwa kwa takriban nusu mwaka.

Katika hali inayoashiria kuvurugika kwa nidhamu ya kazi na mnyororo wa amri (chain of command), Mhe. Kasilda amewapa viongozi na watendaji wa halmashauri hiyo makataa ya saa 72 kueleza kwa maandishi sababu za kushindwa kutekeleza agizo la kuvunja jengo la Soko Kuu la Same ambalo ni hatarishi.

Akizungumza kwa ukali mara baada ya kutembelea soko hilo, Mkuu huyo wa Wilaya alishangazwa na ukimya wa watendaji hao huku jengo hilo likiwa na nyufa kubwa zinazotishia maisha ya wananchi.

Alibainisha kuwa mkwamo huo si wa rasilimali, bali ni wa kinidhamu.

"Huu ni ukaidi wa wazi. Nimeshatoa maelekezo zaidi ya mara tatu kuhusu kuvunjwa kwa jengo hili, lakini hakuna utekelezaji.

Inasikitisha zaidi kuona hata barua rasmi ya Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) iliyoandikwa tangu Agosti 2025 imepuuzwa kwa miezi sita sasa," alisema Mhe. Kasilda.

Kauli hiyo ya DC Kasilda inaibua maswali mazito juu ya namna watendaji wa chini wanavyochelewesha maamuzi ya viongozi wa juu, hali inayoweza kuhatarisha usalama wa wananchi wanaotumia jengo hilo lililodumu kwa zaidi ya miongo mitano.

Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza kuwa serikali haiwezi kuvumilia utamaduni wa kufanya kazi kwa mazoea, hasa unahusisha hatari ya maafa.

Amewataka wahusika wote waliohusika kukwamisha agizo hilo kutoa utetezi wao kabla ya hatua kali za kinidhamu hazijachukuliwa dhidi yao.

" Nataka maelezo ya maandishi ofisini kwangu kueleza kwanini maelekezo ya serikali yanadharauliwa.

Hatua za kinidhamu zitafuata kwa kila aliyeshiriki kukwamisha jambo hili," alionya DC Kasilda.

Tukio hili linatathminiwa na wadau wa utawala bora kama fundisho kwa watendaji wa umma wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao kwa wakati, huku likionyesha dhamira ya Mkuu huyo wa Wilaya katika kusimamia uwajibikaji bila muhali.


Na Mwandishi Wetu,Kwimba

WATUMISHI wa idara ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza wamepatiwa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia sambamba ba kuelezea kwa kina madhara yanayotokana na matumizi ya kuni na mkaa kiafya.

Mafunzo hayo yametolewa na Kampuni ya Oryx Gas Tanzania ambapo lengo kuu ni kuiwezesha kada hiyo ya sekta ya afya kuwa na uelewa mpana kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia ya gesi na kisha watumishi hao wawe mabalozi kwa wananchi wengine wakiwemo wagonjwa.

Akizungumza Februari 27,2027 wakati wa utolewaji wa mafunzo hayo kwa watumishi wa sekta ya afya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza Mkuu wa Mafunzo wa Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Peter Ndomba amesema hatua hiyo ni katika muendelezo ule ule wa jitihada za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia

Tumeamua kuchukua kundi la idara ya afya katika Wilaya hiyo.

“Oryx Gas tumeamua kutoa mafunzo haya kwa watumishi wa afya wa Wilaya ya Kwimba kwasababu tunajua wananchi wanapopata matatizo ya kiafya wanakuja hospitali kwahiyo wale ndio wanakuwa watu wa kwanza kukutana na wananchi wenye matatizo.

“Kwahiyo tumeamua kuwapa mafunzo ya ndani kabisa kuhusu matumizi sahihi ya gesi,usalama na kila kitu kuanzia athari ya kimazingira pamoja na athari za kiafya.Kwahiyo tumekuwa na kundi kubwa la watumishi wote wa sekta ya afya zaidi ya 267 wakiwemo wa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba na wamepata mafunzo haya kwa siku mbili kuhusu nishati safi ya kupikia

“Tunafurahi mwitikio ni mkubwa na mafunzo haya ni mwanzo tu kwani tutakwenda katika taasisi zote,shule mbalimbali na kila jukwaa tutaweza kufika ili sasa muendelezo mzima wa matumizi ya nishati safi uweze kufikia watu wote”

Aidha Ndomba ametoa shukrani uongozi mzima wa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba, DMO pamoja na Mganga Mfawidhi kwa kuwapatia nafasi ya kukutana na Madaktari na wauguzi kuwapa elimu ya gesi ambayo watu wengi hawaijui.

“Tumegundua kuna haja ya kupeleka elimu hii kwao ili wawe mabalozi wanapokutana na wananchi,wagonjwa hasa wamama wanaokuja hospitali kwa matatizo mbalimbali na kuwafafanulia kwamba matumizi ya nishati ndio jambo muhimu na itasaidia kupunguza matatizo mengi yanayotokea kutokana na matumizi ya kuni na mkaa,”amesema Ndomba.

Kwa upande wao watumishi wa sekta ya afya katika Wilaya hiyo wameishukuru kwa kupatiwa mafunzo hayo ambapo wengine wamekiri wamekuwa wakitumia gesi ya kupikia kwa muda mrefu lakini hawakuwa wanajua faida na hasara zake lakini kupitia mafunzo hayo sasa watakuwa mabalozi kwa wengine.

Kwa upande wake Christian Mvula amesema ambaye Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba amesema wanashukuru Oryx kwa kuwapatia mafunzo ya matumizi sahihi ya gesi sambamba na kuachana na mkaa na kuni na kuingia katika matumizi ya gesi.

“Ukweli tumepata elimu sahihi ya kutumia gesi ya kupikia kama nishati ya kupikia majumbani na sisi watumishi tunafufahi kupata huduma hiyo na kimsingi tulikuwa tunateseka kutumia kuni na mkaa ambayo wakati mwingine ni ngumu kupatikana hasa kipindi hiki cha mvua.

“Lakini baada ya mafunzo haya tumeelewa matumizi ya gesi iliyosalama kama nishati ya kupikia na kwetu imekuwa nafuu kwani awali tulikuwa na uelewa tofauti, kulikuwa na nadharia nyingi mtaani kuhusu gesi ikiwemo usalama na gharama.Pia tumeelimishwa jinsi ya kutunza gesi ,kuikagua kila siku ili kuepusha changamoto na tumeelimishwa kuhusu madhara ya kuni na mkaa.”

Wakati huo huo Ofisa Muuguzi Salome Malale amesema ametumia gesi kwa miaka 15 lakini hakujua faida na hasara za gesi na yeye kama muuguzi kuna changamoto nyingi zimetokea kwa mfano jamii nyingi zinatumia kuni na mkaa.

“Ninavyojua walikuwa wanapata matatizo ya mapafu wengine macho na walikuwa wanakuja kutibiwa hospitalini, sasa kwa elimu ambayo nimeipata naweza kutoa elimu kwa jamii kutumia gesi na tuachane kutumia kuni au mkaa.

Kwa upande wake Robert Mayombya ambaye ni mtumishi wa hospitali ya Wilaya ya Kwimba amesema amefurahi kupata elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.”Nimejifunza matumizi mazuri ya gesi badala ya kutumia kuni na mkaa na nina imani nitatoa elimu kuanzia familia hadi majirani ili waachane na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake tutumie gesi.”

















On August noon in forty-four, beneath Tanganyika’s sky,
In Mwazye’s quiet parish land, a child began to cry.
The sixth of nine, yet heaven-marked before the world could see,
A shepherd chosen long before he bent his first small knee.

His sister saw the spark in him and made a solemn vow,
To guard his dream with sacrifice, though trials pressed her brow.
Her youth she gave, her wages too, his schooling to defend,
So he might serve the Lord of Life until his journey’s end.

Through Karema’s halls and Kaengesa’s rising gleam,
Through Kipalapala’s sacred books and nights of ceaseless stream,
His mind grew luminous, his spirit ardent, his purpose living beam,
A leader formed by discipline, by prayer, by sacred theme.

Ordained a priest in seventy-one, still humble, still afraid,
Yet faithful to the call of God, whatever price was paid.
In Rome he drank from ancient wells of moral truth and grace,
Then hastened home to serve his land, not seek a higher place.

A bishop young in Nachingwea, in Tunduru he stood,
To build where little yet was formed, to plant where none yet could.
Though fear would knock upon his heart whenever roles were new,
His answer was obedience, God’s will he would pursue.

In Dar he rose to guide the flock where giants once had been,
A Cardinal in scarlet red, yet simple still within.
He asked, “Why beg for distant grain when ours can fill the bowl?”
And taught the Church to stand upright in dignity of soul.

From twenty parishes he dreamed of one hundred in their place,
They doubted such a vision vast could ever run that race.
But when he laid the crozier down and passed the charge along,
One hundred eighteen stood in faith, his vision proved them wrong.

For death to him was not defeat, nor darkness, nor despair,
But simply door to promised glory beyond all earthly care.
The pilgrim laid his labors down where saints and angels sing,
And entered joy no mortal tongue could fully name or bring.

Though on 19 February he left this earthly state,
On 28 February, in solemn farewell we congregate.
Not stripped of honor, nor lost to sight,
But clothed in dignity, in hallowed rite.

A priest for decades he faithfully stood,
A guide in truth, in strength, in good.
A bishop, archbishop, cardinal upright,
A conscience steady in nation’s sight.

Eternal rest, O Lord, bestow,
Let endless light upon him glow.
May he who led with faithful hand
Now dwell within God’s promised land.

And when the final trumpet rings,
And time surrenders all its kings,
May the shepherd, his flock, and the Church above,
Rejoice in resurrected love.

His spirit whispers still,
Through every heart he touched, through every faithful will.
Though tears may fall, his love will never fade,
A shepherd, father, guide, forever ours to aid.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396


- The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mjasiriamali na mfugaji wa kuku kutoka Mapinga, Bagamoyo, Raphael Emmanuel, amejishindia pikipiki kupitia promosheni ya “Shinda Boda” inayoendeshwa na kampuni ya michezo ya kubashiri ya PigaBet.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya zawadi hiyo yaliyofanyika katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam, Raphael alimshukuru Mungu pamoja na PigaBet kwa kumpatia fursa hiyo akisema ushindi huo utamsaidia kupunguza changamoto za usafiri na kufungua milango ya mafanikio katika shughuli zake za kiuchumi.

“Pikipiki hii itanirahisishia maisha, hasa katika usafiri wa kila siku. Nimekuwa nikitumia gharama kubwa kusafiri, hivyo zawadi hii ni msaada mkubwa kwangu,” alisema Raphael, ambaye anaishi Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Afisa Masoko wa PigaBet, Hemed Msonge, alisema kampuni hiyo imeanza rasmi mpango wa kuwainua Watanzania kiuchumi kupitia zawadi za pikipiki mbili zitakazotolewa kila wiki kwa muda wa wiki sita mfululizo.

Alisema promosheni hiyo inalenga kuwapa washiriki fursa ya kujiongezea kipato kupitia shughuli za usafiri wa bodaboda, huku akisisitiza umuhimu wa kushiriki michezo kwa uwajibikaji.

Msonge aliwahimiza Watanzania wengi zaidi kushiriki promosheni hiyo, akieleza kuwa droo zitaendelea kufanyika kila wiki hadi mwisho wa kampeni, huku akisisitiza kaulimbiu ya kampeni hiyo kuwa ni “Cheza, shinda bodaboda na ubadilishe maisha yako.”


 

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetangaza kuanza kwa kampeni maalum ijulikanayo kama “Samia Ardhi Kliniki” itakayofanyika katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kuanzia tarehe 2 hadi 7 Machi 2026, kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayoadhimishwa tarehe 8 Machi 2026.Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Lucy Kabyemera, amesema kliniki hiyo itaendeshwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi za Ardhi za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.


“Kupitia Samia Ardhi Kliniki tunalenga kuwafikia wanawake wengi zaidi kwa kuwapatia elimu kuhusu haki zao za umiliki wa ardhi, kuwasaidia kitaalamu na kutoa hati miliki kwa waliokamilisha taratibu,” amesema Kabyemera.

Ameongeza kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Samia Suluhu Hassan ya kuwataka watumishi wa umma kuwafuata wananchi na kuwapatia huduma bora kwa kuzingatia utu. “Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi Sasa,’ na tunawahimiza wanawake wote kujitokeza kutumia fursa hii muhimu,” amesisitiza.
Kwa mujibu wa Kabyemera, serikali inalenga kuongeza idadi ya wanawake wanaomiliki ardhi kwani kwa sasa ni takribani asilimia 28 tu ya wanawake nchini ndio wanamiliki. “Tunaamini kumwezesha mwanamke kumiliki ardhi ni kuimarisha familia na Taifa kwa ujumla,” amesema.


 

 



SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) limeendelea kupata mafanikio makubwa kupitia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano.

Hadi kufikia sasa, shirika limefanikiwa kuwa na jumla ya ndege 16 baada ya kuwasili kwa Boeing 787-8 Dreamliner mwezi Agosti 2024. Ndege hizi zinajumuisha ndege za masafa marefu, kati, mafupi, na ndege moja ya mizigo.

Ukuaji wa idadi ya ndege umeiwezesha ATCL kupanua mtandao wake wa safari kutoka vituo 23 mwaka 2020/21 hadi vituo 33 mwaka 2025/26. Safari mpya za kimataifa zimezinduliwa kuelekea Lagos, Kinshasa, Accra, na miji mingine mikubwa barani Afrika. Hii imesaidia kuunganisha Tanzania na masoko makuu ya kikanda na kimataifa.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akielezea mafanikio ya siku 100 za Rais Samia Suluhusu Haasan akizungumza na waandishi wa habari katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere(JNIA) Februari 26,2026

Katika upande wa abiria, ATCL imeshuhudia ongezeko kubwa kutoka abiria 822,232 mwaka 2021/22 hadi milioni 1.17 mwaka 2024/25. Takwimu za nusu mwaka ya 2025 zinaonyesha tayari abiria zaidi ya 700,000 wamesafirishwa. Mafanikio haya yameongeza mapato ya shirika kwa asilimia 87.88, yakifikia Dola za Marekani milioni 157.69.

Sekta ya mizigo nayo imepata mapinduzi, ambapo tani za mizigo zilizosafirishwa zimeongezeka kutoka 2,567 hadi 6,919. Ununuzi wa ndege maalum ya mizigo umerahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo na mbogamboga kwenda masoko ya nje. Hii imetoa fursa mpya kwa wakulima na wafanyabiashara wa Tanzania kupata fedha za kigeni.

Serikali haina mpango wa kuishia hapo, kwani tayari mchakato wa kununua ndege nyingine nane uko katika hatua mbalimbali. Lengo ni kufikisha jumla ya ndege 28 katika kipindi kijacho ili kuimarisha zaidi utoaji wa huduma. Mipango ipo pia kuanzisha safari za Seychelles, Muscat, na Jeddah kabla ya Juni 2026.

Shirika pia limekuwa chanzo cha ajira, ambapo idadi ya watumishi imeongezeka kutoka 826 hadi 1,031. Watumishi 356 wamepatiwa mafunzo maalum katika fani za urubani na uhandisi wa ndege ili kuongeza tija. Uwekezaji huu katika rasilimali watu unalenga kuhakikisha huduma zinatolewa kwa weledi na usalama.

Kupitia kodi na tozo, ATCL imechangia shilingi bilioni 52.35 serikalini katika mwaka wa fedha 2024/25. Mafanikio haya yanathibitisha kuwa shirika linazidi kujiimarisha kibiashara na kupunguza utegemezi. ATCL sasa ni kiungo muhimu katika kukuza utalii na biashara ya kimataifa kwa Tanzania.
KATIKA kuadhimisha kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali imewasilisha mafanikio makubwa katika sekta ya uchukuzi na uwekezaji.

Sekta ya uchukuzi imeendelea kukua na kuongeza mchango wake katika Pato la Taifa kutoka asilimia 7.1 mwaka 2021 hadi asilimia 7.5 mwaka 2024. Hii ni matokeo ya falsafa ya "Kazi na Utu" katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.

Moja ya mafanikio makubwa ni kuimarisha mazingira ya uwekezaji kupitia uboreshaji wa miundombinu ya kimkakati. Serikali imekamilisha ujenzi wa Jengo la Viongozi Mashuhuri (VIP) katika uwanja wa JNIA ili kuongeza hadhi ya kidiplomasia. Aidha, miradi yenye thamani ya shilingi trilioni 1.154 imekuwa ikitekelezwa kukuza uwezo wa viwanja vya ndege.

Katika kipindi hiki, Rais amefanikiwa kuvutia wawekezaji wakubwa kupitia diplomasia ya kiuchumi. Matumizi ya fedha yameelekezwa katika miradi inayogusa wananchi moja kwa moja kama ujenzi wa meli na reli. Matokeo ya uwekezaji huu yameanza kuonekana kupitia ongezeko la mapato na ajira kwa vijana.

Ufanisi wa uongozi umejitokeza pia katika kuanza kwa safari za SGR ambazo zimekuwa kivutio kwa wasafiri wa ndani na nje. Hadi sasa, zaidi ya Watanzania 200,000 wamefaidika na ajira zilizotokana na mradi wa reli pekee. Hii inaonyesha jinsi uwekezaji wa serikali unavyorudi kwa wananchi kupitia fursa za kiuchumi.

Mafanikio mengine ni kufufua shirika la TAZARA ambalo lilikuwa likikabiliwa na changamoto za kiutendaji kwa muda mrefu. Mkataba wa uboreshaji ulisainiwa mwezi Septemba 2025, hatua ambayo itafungua zaidi biashara na nchi za SADC. Rais amehakikisha miradi yote ya kimkakati inapata fedha na kusimamiwa kwa karibu.

Msemaji Mkuu wa Serikali alisisitiza kuwa mafanikio haya ni mwanzo tu wa safari ya kufanya Tanzania kuwa kitovu cha uchumi. Mipango ya baadaye inahusisha ujenzi wa reli za mijini katika majiji ya Dar es Salaam na Dodoma. Pia, ujenzi wa kituo cha Logistics cha Kurasini unalenga kuimarisha uhifadhi wa mizigo ya abiria na wafanyabiashara.

Dhamira ya dhati ya Rais Samia imeonekana katika kuimarisha usalama wa usafiri wa majini kupitia ujenzi wa vituo vya uokoaji (MRCC). Kituo hiki kilichojengwa Mwanza kitasaidia kuratibu operesheni za dharura katika Ziwa Victoria. Kwa ujumla, siku hizi zimeacha alama ya mageuzi ya kifikra na kiutendaji katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Februari 27,2026 ameandaa Iftar maalum kwa wakazi wa Mkoa huo hafla ambayo imefanyika katika ukimbi wa Diamond Jubilee.

Katika hafla hiyo viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali pamoja na wananchi kutoka maeneo tofauti ya Jiji la Dar es Salaam wamehudhuria.

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Mufti Mkuu wa Tanzania Dkt Abubakar Zubeir bin Ally ambaye aliwaongoza waumini katika dua ya kuiombea nchi amani, mshikamano na maendeleo endelevu.

Akizungumza katika hafla hiyo RC Chalamila aliwataka wakazi wa Dar es Salaam kuendeleza umoja na upendo miongoni mwao, akisistiza kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya kuimarisha mshikamano wa kijamii na kusaidiana. Alieleza Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana na Viongozi wa Dini katika kudumisha amani na utulivu.Kwa upande wa Mufti Mkuu aliishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuandaa Iftar hiyo, akieleza kuwa matukio ya aina hiyo huimarisha uhusiano kati ya Serikali na Jamii ambapo ametoa wito kwa watanzania kuendelea kuiombea nchi na kuzingatia maadili katika kipindi hiki cha Ramadhani.

Hafla hiyo ilihitimishwa kwa futari ya pamoja iliyoambatana na mawaidha mafupi ya kidini huku washiriki wakionyesha furaha na mshikamano mkubwa





UJENZI wa Reli ya Kisasa (SGR) umepiga hatua kubwa, ambapo hadi Desemba 2025 utandazaji wa reli umefikia kilomita 747, sawa na asilimia 61 ya lengo.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwwa wakati akizungumza na waandishi wa habari akijibu hoja ya kusuasua kwa ujenzi.

Alisema hakuna kusuasua kwa ujenzi kwani vipande vya Dar es Salaam hadi Morogoro na Morogoro hadi Makutupora vimekaribia kukamilika kwa zaidi ya asilimia 98. Huduma tayari zimeanza kati ya Dar es Salaam na Dodoma, zikipunguza muda wa safari kwa kiasi kikubwa.

Uendeshaji wa SGR umeleta tija kubwa, ambapo abiria milioni 4.6 na tani 52,305 za mizigo zimesafirishwa hadi mwishoni mwa 2025. Mradi huu pia umezalisha ajira zaidi ya 200,000 kwa Watanzania katika nyanja mbalimbali. Shirika la Reli (TRC) sasa limeanza kujiendesha bila ruzuku ya mishahara kutoka serikalini, jambo ambalo ni mafanikio ya kipekee.

Sambamba na reli, Serikali imewekeza katika upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam ili kuongeza uwezo wa kuhudumia tani milioni 50 kwa mwaka. Mradi huu unahusisha ujenzi wa magati 10 mapya na matenki makubwa ya mafuta. Maboresho haya yanalenga kupunguza muda wa meli kukaa bandarini na kuongeza ufanisi wa kikanda.
Aidha, ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo umeanza kwa ajili ya kuhudumia meli kubwa za kisasa (Mega Max). Bandari hii itasaidia kupunguza msongamano katika Bandari ya Dar es Salaam na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji Afrika Mashariki. Hii ni sehemu ya mkakati wa kufanya sekta ya maji kuchangia zaidi katika uchumi.

Katika maziwa makuu, Serikali imekamilisha ujenzi wa meli mpya kama MV New Mwanza yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200. Pia, meli mbili mpya za mizigo zimejengwa katika Ziwa Tanganyika ili kuchochea biashara na nchi ya DRC. Meli ya MT Sangara nayo imekarabatiwa na kuanza safari za kusafirisha mafuta.

Mapato ya bandari yameongezeka kwa kiasi kikubwa baada ya maboresho na mikataba mipya ya uendeshaji. Takwimu za TRA zinaonyesha mapato ya forodha yamefikia shilingi trilioni 8.256, likiwa ni ongezeko la trilioni 1.17 ikilinganishwa na mwaka uliopita. Ukuaji huu unatokana na kuongezeka kwa ufanisi katika kuhudumia shehena.

Uunganishaji wa SGR na bandari ni mkakati wa kihistoria wa kuimarisha biashara na nchi zisizo na bandari. Reli ya TAZARA nayo inafanyiwa maboresho makubwa kwa kushirikiana na serikali ya Zambia na kampuni ya CCECC. Miradi hii kwa pamoja inaiweka Tanzania katika nafasi bora ya ushindani wa kibiashara kimataifa.
SEKTA ya utalii nchini Tanzania imeendelea kushuhudia ukuaji mkubwa na wa kihistoria, ikichochewa na jitihada za makusudi za Serikali ya Awamu ya Sita.

Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa idadi ya watalii wa nje imeongezeka kutoka 2,141,895 mwaka 2024 hadi kufikia 2,294,495 mwaka 2025. Hali kadhalika, utamaduni wa utalii wa ndani umeimarika, ambapo idadi ya watalii wazalendo imepanda kutoka milioni 3.2 hadi milioni 3.6 katika kipindi hicho.

Mafanikio haya yamepelekea kuongezeka kwa mapato ya fedha za kigeni, ambapo sekta hiyo imeingiza Dola za Marekani milioni 3.9 mwaka 2024 ikilinganishwa na milioni 1.3 mwaka 2021. Juhudi hizi zimepata msukumo mkubwa kupitia filamu za kimkakati za "Tanzania: The Royal Tour" na "Amazing Tanzania". Filamu hizi zimeongeza utambulisho wa nchi duniani na kuvutia wimbi jipya la wawekezaji na watalii.

Takwimu hizo zimetolewa na Msemaji Mkuu wa serikali Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa habari Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere Dar es salaam Februari 26, mwaka huu.

Alisema kutokana na uboreshaji wa vivutio, Tanzania imeshinda tuzo mbalimbali za kimataifa kupitia World Travel Awards (WTA) mwaka 2024 na 2025. Hifadhi ya Taifa ya Serengeti imeendelea kutambulika kama Hifadhi Bora ya Taifa Duniani kwa miaka sita mfululizo kuanzia 2019 hadi 2024. Mlima Kilimanjaro nao umetawala kama kivutio bora cha utalii barani Afrika.

Aidha, Tanzania imetangazwa kuwa kivutio bora zaidi cha safari za nyikani (Safari Destination) duniani kwa mwaka 2024 na 2025. Mafanikio haya yameimarisha imani ya watalii wa kimataifa na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha utalii barani Afrika. Serikali inaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya anga, reli, na barabara ili kurahisisha ufikiaji wa vivutio hivi.

Ukuaji huu si tu unaongeza mapato, bali pia unachochea sekta nyingine kama hoteli, usafirishaji, na biashara ndogo ndogo. Serikali inalenga kuendeleza kasi hii ili sekta ya utalii iendelee kuwa mhimili mkuu wa uchumi wa taifa. Kwa ujumla, sekta hii sasa inachangia kwa kiasi kikubwa katika kutengeneza ajira kwa Watanzania.

SERIKALI imetoa kauli ya usalama na uthabiti wa miundombinu ya viwanja vya ndege nchini huku ikisema maboresho makubwa ya kiteknolojia yaliyofanyika yanawezesha safari za anga kuwa salama.

Katika kuhakikisha viwango vya kimataifa vinazingatiwa, Tanzania imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO).

Msemaji amebainisha kuwa ukaguzi wa hivi karibuni wa ICAO umeonesha kuwa usalama wa anga nchini Tanzania umefikia asilimia 86, kiwango ambacho ni cha juu na cha kuridhisha kimataifa. Alama hizi zinajumuisha uwezo wa viwanja vyetu kuhimili changamoto za kimazingira na kiufundi wakati wote wa mwaka.

Serikali imewekeza shilingi trilioni 1.154 katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kwa ajili ya miradi ya kimkakati kwenye viwanja vya ndege. Sehemu ya fedha hizi imeelekezwa katika mifumo ya mifereji ya maji, ukarabati wa barabara za kuruka na kutua (runways), na usimikaji wa taa za kuongozea ndege (AGL) ambazo zinawezesha ndege kutua hata kukiwa na hali mbaya ya hewa au giza.

Aidha amewataka waandishi wa habari wanapokuwa na masuala ya kitaalamu katika masuala ya anga wahoji wahusika ili wapate majibu badala ya kukurupuka.

Alisema hayo akizungumzia tukio la mwanahabari mmoja kuandika kitu bila weledi na kusababisha taharuki kuhusiana na suala la ndege ya ATCL kushindwa kutua Mwanza na kulazimika kutua kwa dharura uwanja wa ndege wa Kilimanjaro.

Msemaji huyo pia aligusia ukarabati unaoendelea katika viwanja vingine kama Moshi na Shinyanga, ambapo ujenzi unahusisha barabara za kuruka na kutua kwa kiwango cha lami na mifumo imara ya mifereji. Kwa mfano, mradi wa uwanja wa Moshi unahusisha ujenzi wa barabara za mzunguko na uzio wa usalama ili kuzuia muingiliano usio wa lazima wakati wa hali ya hewa duni. Hatua hizi zote ni sehemu ya mpango kabambe wa TAA wa kuhakikisha viwanja vyote 61 nchini vinakuwa na usalama wa asilimia 100.

Serikali imewahakikishia wasafiri na mashirika ya ndege kuwa miundombinu ya anga nchini ipo imara na salama. Tuzo za kimataifa za ubora na usalama ambazo JNIA na KIA zimezipokea ni uthibitisho tosha kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kudhibiti vihatarishi vya usalama wa anga.

SUALA  la gharama za usafiri wa anga nchini limechukua sura mpya baada ya Serikali kukiri kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu bei kubwa za tiketi ambazo zimekuwa zikionekana kama mzigo kwa Mtanzania wa kawaida.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amebainisha kuwa, licha ya uwekezaji mkubwa unaofanywa katika ujenzi wa viwanja vya ndege nchini, nia kuu ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona miundombinu hiyo inamnufaisha mwananchi wa hali ya chini.

Amesema Serikali inatambua kuwa usafiri wa anga haupaswi kuwa anasa ya watu wachache wenye uwezo mkubwa wa kifedha pekee, bali uwe ni huduma inayofikika na kila mmoja ili kuchochea biashara na maendeleo.

Katika hatua ya kwanza ya utatuzi, Msemaji wa Serikali amefafanua kuwa wataalamu kutoka wizara husika tayari wameanza kufanyia kazi uchambuzi wa kina wa tozo, kodi, na ada mbalimbali ambazo zinachangia kupanda kwa bei za tiketi.

Amesema Zoezi hili linalenga kuona ni maeneo gani yanaweza kupunguzwa bila kuathiri uendeshaji wa viwanja vya ndege na mashirika. Huu ni mchakato wa kimkakati unaolenga kuleta uwiano kati ya gharama za uendeshaji na uwezo wa kifedha wa abiria wa ndani.

Amesema akijibu swali katika mkutano wake na waandishi wa habari Februari 26, Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere kwamba wananchi wasubiri nini kitafanyika wakati wa bajeti Juni mwaka huu, ambapo bajeti mpya ya Serikali inatarajiwa kusomwa bungeni.

Msemaji amewahakikishia Watanzania kuwa wakati wa mchakato huo wa bajeti, kila kitu kitakuwa wazi na maamuzi yatakayochukuliwa yatalenga kutoa unafuu wa moja kwa moja kwa wasafiri. Hii itakuwa ni habari njema kwa wale wanaotegemea usafiri huo kwa shughuli za dharura na biashara za haraka.

Uwekezaji ambao Serikali imefanya, ikiwemo ununuzi wa ndege mpya 16 za ATCL na ukarabati wa viwanja vya mikoani kama Tabora, Kigoma, na Shinyanga, unalenga kutanua wigo wa huduma hizi. Hata hivyo, uwekezaji huo hautakuwa na tija kamili kama ndege zitakuwa zinaruka bila abiria wa kutosha kutokana na gharama kubwa za nauli.

Aidha, serikali imeeleza kuwa ongezeko la mashirika ya ndege ya kimataifa yaliyovutiwa kuanza safari nchini, kama vile Air France na Saudi Arabia, ni ishara ya kukua kwa soko. Ushindani huu unapaswa kwenda sambamba na mazingira wezesha ya kodi ndani ya nchi ili kutoa fursa kwa mashirika ya ndani pia kukua na kutoa huduma kwa bei nafuu. Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa sekta ya uchukuzi inachangia zaidi katika pato la taifa kwa kuwafanya watu wengi zaidi wasafiri kwa anga.

Wananchi sasa wanasubiri kwa hamu mwezi Juni ili kuona ni kwa kiasi gani nauli hizo zitashuka. Matarajio ni kwamba kupungua kwa tozo kutaongeza mzunguko wa fedha na kuchochea utalii wa ndani, ambao tayari umeshuhudia ongezeko la kufikia watalii milioni 3.6 mwaka 2025. Hii itakuwa ni hatua kubwa katika kuleta mapinduzi ya usafirishaji nchini Tanzania.

Top News