The members of the Selection Committee of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE met on April 17, 2026, in Abidjan, Côte d’Ivoire, as part of the 2026 Inaugural Conference, to designate the laureate of the Super Prize Great Builder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

This year, the central theme of the proceedings was: “Investing in roads, investing in transport: for prosperity in Africa.”

During this annual meeting, the Selection Committee meticulously assessed the quality of investments in the road and transport sectors across the continent, drawing on the 2026 report of the Media Network for Infrastructure and Finance in Africa (MIFA), as well as publicly available reports in these fields.

Following deliberations, the Committee proceeded with the designation of the laureate of the Super Prize GreatBuilder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

Accordingly, His Excellency General Mamadi Doumbouya, President of the Republic of Guinea, has been designated Laureate of the Super Prize GreatBuilder – Babacar NDIAYE Trophy 2026.

He has been recognized for his personal leadership as well as for the investment efforts undertaken under the Simandou Vision 2040 program. This program indeed represents one of the “largest logistical transformations ever carried out in Africa.”

The Selection Committee particularly commended his commitment to integrated and sustainable development, as well as his vision to build outstanding infrastructure in the road and transport sectors for his country.

The Selection Committee congratulates His Excellency General Mamadi Doumbouya on this distinction and solemnly invites him to receive his trophy on May 27, 2026, in Brazzaville, Republic of Congo, during the Final Conference, which will be held on the sidelines of the Annual Meetings of the African Development Bank (AfDB).

Under the Builder Trophy

The Selection Committee thanks all speakers of the 2026 Inaugural Conference and is pleased to announce the laureates of the Builder Trophy for the year 2026:

 

- Road Maintenance Fund of the Republic of Guinea

- National Road Fund of Liberia

- AGEROUTE, Côte d’Ivoire

- PMUA Project, Côte d’Ivoire

- Road Transport Regulatory Authority (ARTI), Côte d’Ivoire

- National Bureau of Technical Studies and Development (BNETD), Côte d’Ivoire

All these laureates are also invited to receive their trophies during the Final Conference on May 27, 2026, in Brazzaville.

The Selection Committee extends its gratitude to His Excellency João Lourenço, President of the Republic of Angola, Laureate of the Super Prize Great Builder – Babacar NDIAYE Trophy 2025 and High Patron of the 2026 edition, as well as to his Special Representative at the 2026 Inaugural Conference, His Excellency Victor Hugo Guilherme, Minister of Planning.

The Selection Committee expresses its deep gratitude to Côte d’Ivoire and its highest authorities for their hospitality. It extends its sincere thanks, particularly to the Minister of Transport and Maritime Affairs and to the Minister of Planning and Development, for their distinguished contributions to the success of the 2026 Inaugural Conference.

The Selection Committee also thanks the United Arab Emirates, the regular host of the Inaugural Conference over the past three years, which, despite the relocation of the event due to the current situation in the Middle East, have remained committed to supporting this development initiative led by African journalists.


It joins the General Commission in expressing its deep gratitude to His Excellency Ali Youssef Alnuaimi, Ambassador of the United Arab Emirates to Côte d’Ivoire, for his advice, his effective presence at the Inaugural Conference, and the messages of cooperation and development he conveyed.

The Selection Committee thanks all its members across Africa, as well as all participants and partners of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE , 2026 edition.

The Selection Committee honors the memory of Dr. Babacar Ndiaye, inspirer of The Africa Road Builders – Trophée Babacar NDIAYE, and thanks the Babacar Ndiaye family for their remarkable contribution.

Finally, the Selection Committee thanks the African Development Bank and its President, Dr. Sidi Ould Tah, for their patronage and continued support for this organization.

For the Selection Committee
Mr. Kimwanga Bakari
Journalist, Spokesperson (Tanzania)





WADAU  wa sekta binafsi wamehimizwa kutumia kikamilifu fursa za uwekezaji kupitia miradi ya ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) ili kuchochea kasi ya maendeleo nchini. Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam katika mafunzo maalum yaliyolenga kuongeza uelewa na uwezo wa wadau kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Kituo cha PPP na Jukwaa la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), yamekuja wakati ambapo Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji kupitia maboresho ya sheria na miongozo ya ubia. Hatua hiyo inalenga kuvutia ushiriki mpana zaidi wa sekta binafsi katika miradi ya maendeleo.

Washiriki walipata fursa ya kujifunza kwa kina kuhusu mfumo wa PPP, ikiwemo taratibu za kuibua, kuandaa na kutekeleza miradi, sambamba na namna ya kutathmini hatari na faida zake. Aidha, walielekezwa jinsi ya kutumia taarifa za orodha ya miradi (pipeline) ili kubaini maeneo yenye fursa za uwekezaji.

Kupitia majadiliano ya kitaalamu na uzoefu wa wataalam, ilibainika kuwa sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kusaidia Serikali kufanikisha malengo ya muda mrefu ya maendeleo, ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Wadau walisisitizwa kuwa ubia si ubinafsishaji, bali ni ushirikiano unaolenga kuongeza ufanisi na tija.

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameibua mwamko mpya kwa wadau wa sekta binafsi kuona umuhimu wa kushiriki katika miradi ya ubia, huku yakitoa mwanga wa namna bora ya kunufaika na fursa zilizopo na kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa taifa.



Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), David Kafulila, ameeleza kwa kina dhana ya ubia (PPP) akisisitiza kuwa si ubinafsishaji, bali ni mfumo wa ushirikiano unaolenga kuongeza ufanisi na tija katika miradi ya maendeleo ya umma.

Akizungumza na wadau wa sekta binafsi jijini Dar es Salaam, Kafulila alisema mkanganyiko uliopo miongoni mwa wananchi unatokana na kufananisha PPP na ubinafsishaji, huku akifafanua kuwa katika ubia, Serikali hubaki na umiliki wa rasilimali zake huku sekta binafsi ikishiriki katika uwekezaji na uendeshaji.

Alieleza kuwa kuanzishwa kwa sera ya PPP mwaka 2009 na sheria ya mwaka 2010 kulilenga kurekebisha changamoto za mikataba ya nyuma, na kuhakikisha kuwa pande zote Serikali na wawekezaji—zinanufaika kwa usawa na kwa uwazi.

Kwa mujibu wa Kafulila, sababu kuu tatu zinazoifanya Serikali kuingia ubia ni pamoja na kutumia mtaji wa sekta binafsi badala ya kutegemea kodi za wananchi pekee, kupata teknolojia ya kisasa, na kuongeza ufanisi wa usimamizi wa miradi.

Aidha, alitofautisha kati ya mkandarasi wa kawaida na mwekezaji wa PPP, akieleza kuwa mkandarasi hulipwa baada ya kukamilisha kazi, wakati mwekezaji wa PPP huwekeza fedha zake na kurejesha gharama kupitia uendeshaji wa mradi kwa muda maalum.

Alisisitiza kuwa Kituo cha PPP kina jukumu la kuhakikisha mikataba yote inazingatia uwazi, ushindani na maslahi ya Taifa, akihitimisha kuwa ubia ni nyenzo muhimu ya maendeleo na si njia ya kupoteza mali za umma.




Picha za Pamoja.

 Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, leo Aprili 17, 2026 ameipokea Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyofanya ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu na taasisi mbalimbali za sekta ya afya Tanzania Bara.

Ziara hiyo imehusisha kutembelea Makao Makuu ya Wizara ya Afya, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na Bohari ya Dawa (MSD).

Akiongea mara baada yakuwapokea, Dkt. Samizi amesema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Amesema kuwa juhudi hizo zimejikita kuimarisha miundombinu ya afya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuboresha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi nchini.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Nasra Nassor, amesema ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wajumbe wa kamati kwani imewapa fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uendeshaji wa sekta ya afya.

Ameongeza kuwa maarifa waliyoyapata yatawasaidia kuboresha utoaji wa huduma za afya Zanzibar kwa kuzingatia mifumo na mbinu walizojifunza kutoka Tanzania Bara.




Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) leo tarehe 17, Aprili 2026 amefanya kikao kazi na maafisa na askari wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Makao Makuu jijini Arusha katika ukumbi wa Phase II.

Akizungumza na watumishi hao, Waziri alielekeza changamoto mbalimbali za kiutendaji zinazokabili shughuli za uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za taasisi zitatuliwe. Vilevile, ametoa maelekezo ya namna bora ya kushughulikia na kuzitatua changamoto hizo kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Kwenye kikao hicho Mhe. Dkt. Kijaji aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Wanyamapori Dkt. Alexander Lobora huku akipokelewa na mwenyeji wake Kamishna wa Uhifadhi TANAPA CPA Musa Nassoro Kuji.













 

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameendelea kuwasisitiza Watanzania waendelee kudumisha amani nchini kwa sababu inawawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

“Tuwe makini na watu wanaohamasisha uvunjifu wa amani kwa kuwa wengine walipwa kwa vitendo hivyo. Kama wao wamechagua maisha hayo wasiiuze nchi yetu. “Lazima tulinde amani ya nchi yetu.”

 Amesema wanufaika wa kwanza wa amani ni wale wanaoishi katika eneo husika, hivyo hawana budi kuendelea kulinda amani na umoja wa kitaifa ili waendeleze shughuli mbalimbali za maendeleo.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Aprili 17, 2026) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kona ya Mbauda akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Waziri Mkuu amesisitiza hayo mara baada ya kukagua barabara ya Kilombero-Mbauda-Kisongo na Mbauda Losinyai zinazojengwa kwa njia nne pamoja na kuwekewa taa.

Ujenzi wa barabara hizo zenye jumla ya urefu wa kilomita 13 ni miongoni mwa maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Mataifa ya Afrika (AFCON), 2027 ambapo Tanzania ni mwenyeji.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema kuwa ujenzi wa barabara hizo unakwenda kuwasaidia wananchi wa Arusha pamoja na Watanzania kwa ujumla.

Waziri Ulega amesema mbali na kurahisisha usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo, barabara hizo zinakwenda kuondoa tatizo la mafuriko katika baadhi ya maeneo baada ya kujengwa mitaro mikubwa.

 Pia, Waziri Ulega amesema kila baada ya kilomita moja ya barabara kutawekwa taa ambazo zitawawezesha wananchi wa maeneo hayo kuendelea na shughuli za kiuchumi usiku na mchana.

 Amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha shilingi bilioni 27 ambapo kati yake bilioni 17 kwa ajili ya mkandarasi na bilioni 10 fidia kwa waliopisha mradi huo.

Naye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kutokana na miradi ya maendeleo ya wananchi inayotekelezwa katika jiji hilo.

 Waziri Makonda ambaye ni mbunge wa Arusha Mjini ametaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa barabara za njia nne na uwekaji wa taa ambazo zinakwenda kurahisisha ufanyaji wa biashara.








Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Charles Hirali Msangi (34) kwa tuhuma za kusababisha ajali iliyosababisha abiria 57 kunusurika kifo katika eneo la Mikumi, kando ya barabara kuu ya Mikumi–Ifakara.

Ajali hiyo ilitokea Aprili 16, 2026, ambapo basi lenye namba za usajili T 289 EAG lililokuwa likiendeshwa na mtuhumiwa huyo liliacha njia na kupinduka kutokana na mwendo wa hatari.

Basi hilo lilikuwa likitoka Ifakara kuelekea Dar es Salaam likiwa na jumla ya abiria 57.

Kutokana na ajali hiyo, abiria 13 walijeruhiwa na kupatiwa matibabu katika vituo vya afya vilivyo karibu.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa madereva wote kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika.

Imeandaliwa na Farida Mangube.


VIWANDA vitatu vya bidhaa za Twyford vinavyofanya kazi chini ya KEDA (T) Ceramics Co. Ltd, vinavyojumuisha uzalishaji wa vigae na kioo, vinaendelea kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya viwanda nchini Tanzania. Kiwanda cha vigae kipo Chalinze, huku viwanda viwili vya kioo vikiwa Mkuranga. Kwa pamoja, viwanda hivi vinaajiri zaidi ya wafanyakazi 3,000 wa Kitanzania. Kupitia matumizi ya teknolojia ya kisasa ya uzalishaji wa kiotomatiki, viwanda hivi vinazalisha bidhaa bora, imara na za kudumu.

Mbali na kuboresha maisha ya wafanyakazi kupitia ajira na fursa za kiuchumi, viwanda hivi pia vinachangia maendeleo ya jamii zinazovizunguka. Aidha, bidhaa zinazozalishwa zina mchango mkubwa katika kubadilisha sekta ya ujenzi kwa kutoa vifaa vya viwango vya juu vinavyoimarisha uimara na kuongeza mvuto wa majengo, hivyo kuboresha mandhari ya mazingira kwa ujumla. Hayo yamebainishwa na Manager: Biashara na Miradi wa kampuni hiyo John Chimwejo, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii, mjini Mkuranga, mkoani Pwani, hivi karibuni.
Muonekano kwa juu (Overview) ya kiwanda cha vioo (glass) cha kampuni ya KEDA (T) Ceramics Co. Ltd kinachozalisha vioo vya Twyford Glass kilichopo eneo la Msufini, Kidete Mbezi, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.

Bwana Chimwejo amesema kuwa ushahidi wa mandhari nzuri ya majengo yaliyopendeza kwa vigae na vioo vya Twyford unaonekana wazi ukitembelea maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Katika hospitali, shule, pamoja na majengo ya serikali, taasisi za umma na binafsi, majengo mengi ya kisasa yamepambwa na vigae na vioo vya Twyford vinavyoboresha muonekano wake kwa kiasi kikubwa.

Kabla ya uwepo wa viwanda hivi nchini, vifaa vingi vya ujenzi kama vigae na vioo kwa majengo makubwa vilikuwa vikiagizwa kutoka nje ya nchi. Hata hivyo, kwa sasa vinazalishwa ndani ya Tanzania kupitia viwanda vya Twyford, hatua ambayo imechangia kupunguza gharama za ujenzi kwa kiasi kikubwa. Aidha, uzalishaji wa ndani umefanya vifaa hivi kupatikana kwa gharama nafuu huku ubora ukiendelea kuwa wa hali ya juu. Wafanyakazi wa kiwanda cha vioo (glass) cha kampuni ya KEDA (T) Ceramics Co. Ltd kinachozalisha vioo (float glass) vya Twyford kilichopo eneo la Msufini, Kidete Mbezi, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani. Ajira pia inazingatia usawa wa kijinsia, hakuna kazi ya kiume, wala kazi ya kike, kwao kazi ni kazi.



Bwana Chimwejo ametolea mfano wa Wodi ya Watoto Wachanga katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ambayo sakafu safi na ang’avu zilizowekwa vigae vya ubora wa juu vya Twyford. Hata katika Hospitali ya Rabininsia iliyopo Tegeta, vigae vinavyotumika ni vya Twyford. Aidha, vigae vya Twyford vimewekwa katika Jengo la Halmashauri ya Mji wa Mbinga Kusini, na kulifanya jengo hilo la ofisi ya serikali kuwa na muonekano wa kisasa na wa kuvutia.

Chimwejo ametaja Eneo la Viwanda la Chalinze, lililopo kilomita 70 kutoka jijini Dar es Salaam, ndipo kilipo kiwanda cha kisasa cha vioo na vigae vya Twyford kinachofanya kazi kwa saa 24, kikizalisha vigae kwa ajili ya soko la Tanzania na soko la nchi za Afrika.



Mbali na kiwanda kilichopo Chalinze, viwanda vingine viwili vya kioo vipo umbali wa takribani kilomita 100 kutoka Dar es Salaam katika maeneo ya Mbezi, Kidete Msufini na Mkiu, Nyamato, Wilaya ya Mkuranga, ambapo viwanda hivyo vikubwa vya kioo vinafanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Viwanda hivi vinatumia tanuru zenye joto la zaidi ya nyuzi joto 1,000 za Selsiasi, ambapo kioo kilichoyeyushwa huundwa kuwa mabamba ya maumbo mbalimbali kupitia mitambo ya kisasa inayojiendesha kwa mfumo wa otomatiki unaodhibitiwa na kompyuta. Bidhaa za Twyford Glass hazitumiki tu katika miradi ya ujenzi ndani ya Tanzania, bali pia husafirishwa kwenda masoko mbalimbali ya nje ya nchi.

Akizungumzia historia ya viwanda hivyo, Manager: Biashara na Miradi wa kampuni hiyo John Chimwejo, amesema kiwanda cha uzalishaji wa vigae vya Twyford nchini Tanzania kilianza uzalishaji mwaka 2017, na kuongeza uwekezaji kwa kasi, ndani ya miaka michache tu, kimeanzisha vituo vya uzalishaji vinavyohusisha sekta zote mbili za kauri na kioo, sio tuu kwa matumizi ya soko la Tanzania pekee, bali soko la Afrika Mashariki, Afrika nzima na nje ya Afrika.

Mtaalamu wa Kichina na wataamu wazalendo wa Kitanzania, wakiwa kwenye chumba cha kuendeshea mitambo ya uzalishaji vioo (Control room) inayojiendesha yenyewe ki atomatikali (automated) kwa kutumia compyuta kuzalisha vioo (float glass) kwenye kiwanda cha KEDA (T) Ceramics Co. Ltd kilichopo eneo la Mbezi wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.



Viwanda hivi vitatu vya kisasa vya vifaa vya ujenzi, vimejenga msingi muhimu kwa sekta ya ujenzi, kwa upatikanaji wa vifaa bora, imara na vya gharama nafuu kwa Tanzania na nchi za Afrika ambapo, zamani vifaa hivi viliagizwa kutoka nje ya nchi. Bidhaa hizi husambazwa si tu kwa soko la ndani la Tanzania lakini pia husafirishwa kwenda nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na Madagaska, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda, Uganda, Malawi, Sudan Kusini, Afrika Kusini, na Mauritius, na kuifanya chapa ya Twyford, kuwa ni chapa yenye ushawishi mkubwa wa vigae na vioo kwa Tanzania, Afrika Mashariki na kwingine Afrika.

Leo, Twyford Tanzania inaendesha viwanda vitatu vya uzalishaji nchini Tanzania, ikiwa na kiwanda kimoja cha vigae na viwanda viwili vya kioo. Kiwanda cha uzalishaji wa vigae kilichopo Chalinze kina ukubwa wa takribani hekta 93 na kimeajiri karibu wafanyakazi 1,000. Kiwanda hiki kimewekewa mitambo ya kisasa ya uzalishaji inayojiendesha kwa mfumo wa otomatiki, inayowezesha uzalishaji wa kiwango kikubwa kwa muda mfupi. Mchakato wa uzalishaji huanzia usindikaji wa malighafi, ukandamizaji, uchomaji hadi ufungashaji wa bidhaa.



Viwanda viwili vya uzalishaji wa vioo vya Twyford Tanzania vilivyopo Mbezi na Nyamato, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, vina ukubwa wa takribani hekta 120 kwa pamoja na vimeajiri zaidi ya wafanyakazi 2,000. Viwanda hivi huzalisha vioo vya ubora wa hali ya juu, vyenye uwezo wa kuyeyusha zaidi ya tani 1,100 za malighafi ya kioo kila siku. Vinazalisha aina mbalimbali za vioo vya ujenzi kwa unene na maumbo tofauti kuanzia milimita 3 hadi 12, ikiwa ni pamoja na kioo cha kawaida (clear glass), kioo chenye rangi, kioo kinachoakisi mwanga, pamoja na aina nyingine za vioo vya matumizi mbalimbali.

Kutokana na ubora wa bidhaa na uwezo mkubwa wa uzalishaji, Vioo vya Twyford husafirishwa kwenda zaidi ya nchi na maeneo 43 duniani, yakiwemo Afrika Mashariki, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Mashariki ya Kati, Amerika na Ulaya.

Ndani ya Tanzania, Twyford Tanzania imeanzisha mtandao wa mauzo wa kitaifa, kuanzia Dar es Salaam, Dodoma hadi mikoa mingine, ikifikia miji, maeneo ya vijijini, na hata visiwa vya Zanziba na Pemba. Kampuni hiyo inafanya yote haya ili kuhakikisha kwamba vifaa bora vya ujenzi vinapatikana kwa urahisi zaidi kuwahudumia watumiaji wa ndani na nje ya nchi. Twyford Tanzania pia imetoa faida kubwa za kiuchumi kwa Tanzania. Kwa upande mmoja, biashara hiyo inachangia mapato makubwa ya kodi kwa serikali kila mwaka; kwa upande mwingine, inazalisha mapato muhimu ya fedha za kigeni kupitia mauzo ya bidhaa nje ya nchi.

Hii inayofanywa na viwanda vya vigae na vioo vya Twyford Tanzania inaweza kuonekana kwa jicho la kawaida kama ni uzalishaji wa vifaa vya ujenzi tu. Hata hivyo, kwa mtazamo mpana na wa kina, Twyford Tanzania haizalishi tu vifaa vya ujenzi, bali inachangia kwa kiasi kikubwa kubadilisha taswira ya uchumi wa Tanzania.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mkiu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea msaada wa madawati, viti na vitabu uliotolewa na KEDA (T) Ceramics Co. Ltd kwa lengo la kuboresha mazingira yao ya kujifunzia.

Kampuni hii inasaidia kuihamisha Tanzania kutoka kuwa nchi inayotegemea uagizaji wa bidhaa kutoka nje (import-dependent country) hadi kuwa nchi inayozalisha na kusafirisha bidhaa nje (export-oriented country), na hivyo kuwa kitovu cha uzalishaji wa vifaa vya ujenzi vinavyouzwa katika masoko ya kimataifa. Kupitia mabadiliko haya, taifa linapata ongezeko la mapato ya fedha za kigeni na kuimarisha uchumi wa nchi kwa ujumla.

Kwa miaka mingi, Twyford Tanzania imeendelea kuboresha teknolojia yake ya uzalishaji kupitia uboreshaji wa ubunifu wa michanganyiko ya malighafi na kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ubora. Hatua hizi zimechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ubora na ufanisi wa bidhaa zake. Wakati huohuo, kampuni imeongeza matumizi ya malighafi zinazopatikana ndani ya nchi, jambo ambalo limepunguza gharama za uzalishaji na kupunguza utegemezi wa uagizaji wa malighafi kutoka nje ya nchi. Hii ni faida kubwa kwa taifa, kwani inasaidia kuongeza uzalishaji wa ndani unaotegemea rasilimali za nchini.



Ukiondoa faida kwa Tanzania na Watanzania kutokana na upatikanaji wa bidhaa bora, zenye ubora wa juu na gharama nafuu kutoka viwanda vya Twyford Tanzania, uwepo wa viwanda hivi pia umechangia kwa kiasi kikubwa katika ajira kwa Watanzania waliopata ajira rasmi katika shughuli za uzalishaji.

Menejiment ya ya kiwanda cha KEDA (T) Ceramics Co. Ltd wakiwa na wajumbe wa serikali ya kijiji Gongoni , waalimu, wazazi na wanafunzi wa Shule ya Gongoni, wilayani Mkuranga, mkoani Pwani, baada ya kukabidhi vifaa vya shule na vigae kwa serikali ya kijiji hicho kusaidia ujenzi wa shyule ya sekondari ya Gongoni.

Aidha, mamia kwa maelfu ya Watanzania wananufaika kupitia mnyororo wa thamani ikiwemo usambazaji, uuzaji na ununuzi wa bidhaa hizo bora. Zaidi ya hayo, jamii zinazozunguka viwanda hivi zimeendelea kunufaika kupitia utekelezaji wa sera ya uwajibikaji kwa jamii (CSR), ambayo imekuwa ikiunga mkono maendeleo ya kijamii na kuboresha maisha ya wananchi wa maeneo husika.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewataka Watanzania kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini akisisitiza kuwa mazingira ya amani ndiyo msingi muhimu unaowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kukuza uchumi wa taifa.

Amesema ni muhimu kwa wananchi kuwa makini na watu wanaohamasisha uvunjifu wa amani, akibainisha kuwa baadhi yao hufanya hivyo kwa maslahi binafsi. Alionya kuwa watu hao wasiruhusiwe kuihatarisha nchi, akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kulinda amani iliyopo.

Dkt. Nchemba ameeleza kuwa wanufaika wakuu wa amani ni wananchi wenyewe, hivyo wanapaswa kuilinda kwa nguvu zote ili kuendeleza shughuli zao za kila siku, ikiwa ni pamoja na biashara, kilimo na uwekezaji unaochangia maendeleo ya jamii.

Ameyasema hayo leo Ijumaa, Aprili 17, 2026, alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kona ya Mbauda mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ambapo pia alikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara muhimu jijini humo.

Aidha, ameeleza kuwa ujenzi wa barabara za Kilombero–Mbauda–Kisongo na Mbauda–Losinyai zenye urefu wa kilomita 13 ni sehemu ya maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027, huku Serikali ikiendelea kuboresha miundombinu ili kurahisisha usafiri, kukuza biashara na kuhakikisha wananchi wananufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na miradi hiyo.


Top News