WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametimiza ahadi yake ya kutoa pikipiki 10 kwa vikundi vya waendesha bodaboda wilayani Rungwe, mkoani Mbeya, ikiwa ni jitihada za kuwawezesha vijana kiuchumi.
Ahadi hiyo ilitolewa Desemba 18, 2025, wakati Waziri Mkuu alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Kiwira, alipokuwa akitoka wilayani Kyela katika ziara ya kikazi. Katika mkutano huo, Furaha Zuberi Mwakyusa aliwasilisha ombi la kupatiwa pikipiki kwa ajili ya vijana wa bodaboda, ambapo Waziri Mkuu aliridhia na kuahidi kutoa pikipiki 10.
Pikipiki hizo zimekabidhiwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Jaffar Haniu, kwa niaba ya Waziri Mkuu, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Tukuyu.
Katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya pia alikabidhi pikipiki ya magurudumu matatu (bajaji) kwa Richard Mgongo, Mtendaji wa Kata ya Kiwira mwenye mahitaji maalum, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi nyingine ya Waziri Mkuu aliyoitoa siku hiyo hiyo.
Akizungumza wakati wa makabidhiano, Haniu aliwataka waendesha bodaboda kuuenzi ukarimu huo kwa kudumisha amani na mshikamano, sambamba na kaulimbiu ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar inayosisitiza Amani na Mshikamano kwa Maendeleo Endelevu.
Aidha, aliwasisitiza kuzingatia sheria za usalama barabarani na kuzitunza pikipiki walizokabidhiwa ili ziweze kuwa chachu ya maendeleo yao badala ya kuwa chanzo cha ajali au vurugu.
“Tufuate sheria na taratibu zilizowekwa ili pikipiki hizi ziweze kutusaidia,” alisisitiza Haniu.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Benjamin Kuzaga, alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillius Wambura, amewaagiza makamanda wa polisi mikoa yote kuhakikisha madereva wa vyombo vya moto wanapatiwa mafunzo ili kupunguza ajali zinazosababishwa na uelewa mdogo.
Naye Richard Mgongo, mnufaika wa bajaji hiyo, aliishukuru Serikali kwa kumuwezesha kupata chombo hicho ambacho kitamsaidia kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Kwa niaba ya waendesha bodaboda, Furaha Zuberi Mwakyusa alitoa shukrani kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ushirikiano uliowezesha kupatikana kwa pikipiki hizo, akisisitiza kuwa wataendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu za usalama barabarani.



.jpeg)



.jpeg)















.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)