Unguja:
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefungua semina yaWabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar na kusisitizaumuhimu wa kuimarisha usimamizi na uwajibikaji katika utekelezaji wa Mfuko wa KuchocheaMaendeleo ya Jimbo.
Semina hiyo imefanyika Unguja, Zanzibar Februari 26, 2026 akieleza kuwa Mfuko wa Jimboumechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji wa maji safina salama, umeme, elimu, barabara na kukuza shughuli za biashara katika jamii.
Amesema mfuko huo ulianzishwa kwa lengo la kuwashirikisha wananchi katika kubuni nakutekeleza miradi ya maendeleo inayogusa mahitaji halisi ya majimbo yao, hivyo ni wajibu wawabunge kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kikamilifu ili miradi iwe na tija na uendelevu.
“Serikali inalenga kuwezesha utekelezaji wa miradi ya haraka yenye manufaa kwa wananchi, kuimarisha uwajibikaji na ushiriki wa jamii katika kupanga na kusimamia maendeleo pamoja nakupunguza pengo la maendeleo kati ya maeneo mbalimbali,” amesema Mhe. Abdulla.
Ameeleza licha ya kuwepo kwa sheria na miongozo ya matumizi ya fedha za mfuko huo, badokuna changamoto za usimamizi katika baadhi ya halmashauri zilizosababisha kuibuka kwa hoja za ukaguzi.
Kutokana na changamoto hiyo amewataka watendaji wa halmashauri kusimamia ipasavyo fedhahizo ili kuepuka dosari na kuhakikisha thamani ya fedha inapatikana.
Aidha amezungumzia umuhimu wa kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya marekebisho yaSheria ya Mfuko wa Jimbo ya mwaka 2009, kufuatia maelekezo yaliyotolewa baada yakuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa mfuko kwa mwaka 2023/24 katika Kamati yaKudumu ya Bunge ya TAMISEMI.
Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeombwa kuratibu upatikanaji wa maoni kutoka upandewa Zanzibar, hivyo akawahimiza wabunge kutumia semina hiyo kama jukwaa la majadiliano yawazi na kitaalamu kwa lengo la kuboresha mfumo wa mfuko huo.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema semina hiyo ni hatua muhimu katika kuimarishauelewa wa wabunge kuhusu utekelezaji na usimamizi wa Mfuko wa Jimbo.
Amesema maboresho yanayopendekezwa yanalenga kuhakikisha sheria na miongozo ya mfukoinaendana na hali halisi ya utekelezaji na kuongeza uwazi pamoja na ufanisi katika matumizi yafedha za umma.
Semina hiyo imewakutanisha wabunge kutoka majimbo 50 ya Zanzibar pamoja na viongozi nawatendaji kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, kwa lengo la kujadili kwa kina namna bora ya kuboresha utekelezaji wa Mfuko wa Kuchochea Maendeleo yaJimbo.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni(katikati) akimkabidhi zawadi Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla mara baada ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026. Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Kundi la Vijana Kanda ya Pemba Mhe Zainab Abdallah.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS







.jpeg)




.jpeg)


































