


Akisoma maelezo ya awali ya shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mhe. Lukosi, Mwendesha Mashtaka wa Serikali Wakili Nicas Kihembe akisaidiana na Erick alidai kuwa washtakiwa hao walikamatwa tarehe 08 Desemba 2025 katika mtaa wa Wailes, Temeke, Dar es Salaam, na maofisa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, wakati wa operesheni hiyo, DCEA ilikamata pakiti 20 za Bangi aina ya skanka zenye uzito wa jumla wa kilogramu 20.03, ambazo zilikuwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba, kisha kufichwa katika basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili wa Msumbiji AAM 297 CA.
Ilielezwa zaidi kuwa, mashtaka yanayowakabili washtakiwa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 16(I) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, inayokataza umiliki, usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya nchini.
Upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa, shtaka hilo halina dhamana kutokana na uzito wa dawa za kulevya walizokutwa nazo washtakiwa
Aidha, kwa mujibu wa wakili wa Serikali, upelelezi wa shauri hilo namba 1535/2026 ya mwaka 2026 bado unaendelea na mashahidi wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo siku itakayopangwa.
Shauri hili lilihairishwa hadi tarehe 05 februari 2026, huku washtakiwa wakirejeshwa rumande.










Na.Vero Ignatus, Arusha
Wakala wa vipimo mkoani Arusha WMA wametoa onyo Kali Kwa wauzaji wa vitunguu kuacha kutumia vipimo vya Rumbesa badala yake watumie vipimo vya mizani ili kupata thamani ya pesa na ujazo kamili bila kumuumiza mkulima wa zao la kitunguu.
Hayo yameelezwa na Afisa kutoka Wakala wa Vipimo mkoani hapa,Jassson Theonest Wakati akitoa elimu Kwa wakulima wa vitunguu wa Bonde la Eyasi wilayani karatu,mkoani Arusha, amesema matumizi sahihi ya mizani ni msaada mkubwa kwa wakulima, kwani yanahakikisha kila kilo inafikishwa sokoni ipasavyo, kuongeza mapato yao na kuimarisha biashara zao.
Amesema kuwa endapo mtu yeyote atakiuka maagizo hayo hatua Kali za kisheria zitachukuliwa na sambamba na akutozwa fain kuanzia milion Moja mpk milion 20 Kwa mujibu wa sheria.
Nasisitiza tena kwenu wakulima na mlitambue jambo hili kwamba matumizi sahihi ya mizan ni msaada mkubwa kwenu wakulima, kwani yanahakikisha kila kilo inafikishwa sokoni ipasavyo, kuongeza mapato yenu na kuimarisha biashara zenu"alisema.
Sambamba na hilo wakala ya Vipimo imefanya mafunzo kwa wakulima wa vitunguu katika maeneo ya Karatu na Mang’ola, yakilenga kuwafundisha kuepuka kutumia mizani batili na kuhakikisha wanapata kilo halisi za mazao yao.
Wakulima wa vitunguu Moshi Hitler na Joyce Elia wamesema kwamba kutumia mizani isiyo sahihi iliwanyima haki zao, kwa kuwa mara nyingi walipoteza kiasi kikubwa cha mazao yao kwa kuuzwa chini ya kilo halisi, hali iliyosababisha kupoteza mapato na kushusha morali yao. Baadhi walisema walihisi kunyonywa na wakuu wa masoko ambao walitumia mizani batili kuwazidishia hasara.
Wakulima hao waliishukuru Mamlaka Hiyo kwa kutoa elimu hii muhimu na kuahidi kuanza kutumia mizani sahihi kila wanapouza vitunguu vyao.

Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja TANESCO Mkoa wa Ruvuma Alan Njiro, amewataka wananchi kuacha kabisa tabia ya kukata miti au kufanya shughuli zozote karibu na miundombinu ya umeme wakati umeme ukiwa unawaka ni hatari na inaweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo vifo, kwani TANESCO hulazimika kukata umeme kwanza kabla ya kufanya kazi yoyote kwenye nguzo au transfoma ili kuhakikisha usalama wa wafanyakazi na wananchi kwa ujumla.
Akizungumza na wakazi wa Gumbiro, Halmashauri ya Madaba, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, Njiro amesisitiza kuwa umeme ni hatari na unahitaji tahadhari kubwa wakati wote, amesema ajali nyingi za umeme husababishwa na uzembe au uelewa mdogo wa wananchi juu ya matumizi salama ya umeme.
Aidha, amewataka wazazi na walezi kutumia muda wao kuwakumbusha watoto kuwa umeme ni hatari na unaweza kuua, hivyo hawapaswi kuchezea nyaya za umeme, hasa zile zilizoanguka chini au nyaya za “stay” zinazochimbiwa ardhini, ameonya kuwa kuchezea miundombinu hiyo kunaweza kusababisha majanga yanayoweza kuepukika endapo tahadhari zitazingatiwa.
Njiro pia ametoa wito kwa wakulima ambao mashamba yao yana nguzo za umeme kuacha mazoea ya kulima karibu na nguzo hizo au kushika nyaya za umeme, amesema kufanya hivyo kunahatarisha maisha yao, na amesisitiza umuhimu wa kuchukua tahadhari ili kuhakikisha wanakuwa salama muda wote.
Ameongeza kuwa endapo mwananchi anahitaji kukata miti katika eneo lenye nguzo au nyaya za umeme, anapaswa kuwasiliana na TANESCO ili wataalamu wafike kushusha nyaya na kuzima umeme kabla ya zoezi hilo kufanyika, Kwa maeneo hatarishi zaidi, amesema TANESCO hulazimika kukata miti hiyo wenyewe ili kuzuia ajali na kulinda usalama wa wananchi.
Katika hatua nyingine, Njiro amewakumbusha wananchi kuwa maombi ya kuunganishiwa umeme ni bure, na gharama ya kupata umeme vijijini ni shilingi elfu 27 tu, amesisitiza kuwa malipo hayo hufanyika kupitia namba ya kumbukumbu ya malipo na si kumpa mtu fedha mkononi, akiwataka wananchi kuwa waangalifu ili kuepuka utapeli.
TANESCO Mkoa wa Ruvuma imewahimiza wananchi kuzingatia taratibu za usalama wanapohitaji kukata miti karibu na miundombinu ya umeme kwa kushirikiana na TANESCO, Ushirikiano huo utasaidia kulinda maisha ya wananchi, kuepusha majanga yasiyo ya lazima na kuhakikisha miundombinu ya umeme inalindwa kwa manufaa ya jamii nzima.
Mgomo huo ulitokana na madai ya mishahara, ambapo mshahara wa kima cha chini kwa sekta binafsi umewekwa kwa mujibu wa Tangazo na Amri ya Serikali Namba 605A ya tarehe 13 Oktoba, 2025, inayotoa ongezeko la wastani wa asilimia 33.4. Kutokana na ongezeko hilo, mshahara wa chini umeongezeka kutoka Shilingi 275,060 mwaka 2022 hadi Shilingi 358,222 mwaka 2025. Hivyo basi, hakuna mtu au taasisi yoyote inayoruhusiwa kulipa mshahara chini ya kiwango kilichobainishwa katika Amri hiyo ya Serikali, hata kwa kuwepo kwa makubaliano yoyote kati ya taasisi binafsi kupitia chama chao cha waajiri (ATE) au mifumo mingine ya ndani.
Akizungumza na wafanyakazi pamoja na uongozi wa kiwanda hicho, Mhe. Mpogolo amesisitiza kuwa Amri ya Serikali ni ya lazima kutekelezwa na kwamba hakuna kampuni, taasisi au mwajiri yeyote anayekubalika kushuka chini ya viwango vilivyowekwa kisheria. Ameeleza kuwa makubaliano yoyote hayawezi kwenda kinyume na Amri ya Serikali.
Mpogolo ametoa maelekezo muhimu kwa uongozi wa kiwanda na wafanyakazi, ikiwemo kuhakikisha malipo ya mishahara yanatolewa kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Na. 605A la mwaka 2025, huku akisisitiza kuwa hakuna mfanyakazi atakayefukuzwa kutokana na kushiriki mgomo, ili kuimarisha mahusiano bora kati ya mwajiri na waajiriwa. Aidha, ameitaka kiwanda kushirikiana na Chama cha Wafanyakazi (TUICO) na Afisa Kazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kufanyika uchaguzi wa viongozi wa wafanyakazi watakao kuwa kiungo madhubuti kati ya wafanyakazi na uongozi, pamoja na kupitia mikataba ya ajira kuhakikisha inakidhi sheria na kanuni zinazohitajika. Mpogolo pia amehimiza ujenzi wa mahusiano mazuri na kulinda kiwanda kutokana na mchango wake mkubwa katika uchumi wa taifa na nafasi zake muhimu za ajira kwa wananchi.
Kwa upande wao, wafanyakazi wa kiwanda hicho wameeleza kuridhishwa na hatua zilizochukuliwa na Mkuu wa Wilaya, wakisema kuwa zimeleta matumaini mapya na kurejesha amani kazini. Wameahidi kurejea kazini mara moja na kuendelea kutekeleza majukumu yao kama kawaida.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam (RPC), ACP Yustino Mgonja, amepongeza juhudi za Mhe. Mpogolo katika kushughulikia mgogoro huo kwa haraka na kwa busara. ACP Mgonja amesema hali ya usalama katika eneo la kiwanda ni shwari na amewahakikishia wafanyakazi kuwa wapo salama.
Kwa upande wake, mmiliki wa Kiwanda cha NAMERA amesema yupo tayari kutekeleza makubaliano yote yaliyofikiwa kati ya uongozi wa kiwanda na Serikali, huku akiahidi kuboresha mazingira ya kazi na kuimarisha ushirikiano kati ya waajiri na wafanyakazi kwa maslahi ya pamoja.
Dc. Mpogolo amesema kuwa kiwanda hicho ni muhimu sana, hasa katika upande wa ajira. Hivyo basi, migogoro inaweza kuharibu upatikanaji wa ajira na ukuaji wa uchumi, kwa hivyo migogoro si jambo zuri.
Kufuatia kumalizika kwa mgomo huo, shughuli za uzalishaji katika Kiwanda cha NAMERA zinatarajiwa kurejea kama kawaida, huku wafanyakazi wakirejea kazini wakiwa na ari mpya ya kufanya kazi.




Londo amesema usimamizi madhubuti wa vipimo ni msingi muhimu katika kujenga uchumi shindani, himilivu na jumuishi, sambamba na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Ameyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Vipimo katika Kituo cha Uhakiki wa Vipimo Misugusugu Mkoa wa Pwani, ambapo amesisitiza kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara imejipanga kuhakikisha kunakuwepo na mazingira wezeshi ya biashara huku ikijenga imani kwa walaji katika huduma na bidhaa wanazopata.
Naibu Waziri ameongeza kuwa kutokuwepo kwa usimamizi sahihi wa vipimo kunawanyima walaji haki zao za msingi na kudhoofisha ushindani wa haki katika biashara, jambo linaloweza kuathiri ukuaji wa uchumi kwa ujumla.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo Bw. Alban Kihulla amewasihi Wananchi kushirikiana na Wakala huo kwa kutoa taarifa pindi wanapobaini kupatiwa huduma kwa kutumia vipimo visivyo sahihi, akisema ushirikiano wa Wananchi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti vitendo vya udanganyifu na kuimarisha haki katika biashara.
Wakala wa Vipimo ina jukumu la kuhakikisha vipimo vinavyotumika katika biashara vinakuwa sahihi kwa mujibu wa Sheria, hatua inayolenga kulinda maslahi ya walaji na kukuza biashara nchini.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Muyungi muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi hizo Mjini Zanzibar leo Alhamisi Januari 22, 2026.
*********************
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimepanga kuimarisha mashirikiano ili kuhakikisha fursa za Muungano zinawanufaisha wananchi na kuakisi maono ya Waasisi.
Hayo yamesemwa leo Alhamisi (Januari 22, 2026) Mjini Zanzibar na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa ziara yake aliyoifanya kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.
Dkt. Muyungi amesema Serikali zote mbili zimekuwa mstari wa mbele katika kutatua hoja za Muungano hatua inayolenga katika kufungua fursa za kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar.
“Waasisi wetu walikuwa na malengo ya kubainisha fursa za mashirikiano ziweze kuwanufaisha wananchi, hivyo wakati umefika sasa wa kuhakikisha fursa hizo zinakuwa agenda muhimu tunazopaswa kuzibeba kama Watendaji wa Serikali” amesema Dkt. Muyungi.
Ameeleza kuwa ni wakati mwafaka wa kuenzi kwa matendo maono ya viongozi na waasisi wa Muungano kwa kuhakikisha wananchi wa pande zote mbili wananufaika ipasavyo kwa kufanya hivyo kutafsiri nia na malengo ya waasisi.
“Hadi sasa hoja 22 za Muungano zimepatiwa ufumbuzi, tumebaki na hoja 3 sawa na mafanikio ya asilimia 99 ya utatuzi wa hoja….ni muhimu kuhakikisha kuwa utatuzi wa hoja hizo unaleta manufaa endelevu kwa wananchi” amesema Dkt. Muyungi.
Aidha Dkt. Muyungi ameshauri kurejeshwa kwa mashindano ya michezo ya pasaka ambayo hapo awali yalikuwa ni sehemu muhimu ya kuimarisha mahusiano na mashiriano baina ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Akifafanua zaidi Dkt. Muyungi amesema viongozi na watendaji wa serikali zote mbili wamekusudia kutangaza fursa za muungano kwa wananchi na kuwahimiza wataalamu kuchakata fursa hizo ili kuona njia bora ya kuwanufaisha wananchi.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapnduzi Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum Ofisi hizo zimekuwa zikishirikiana kwa karibu katika kuimarisha uratibu wa masuala ya Muungano na hatua hiyo imeendelea kuwanufaisha wananchi wa pande zote mbili.
“Katika kikao baina yetu tumekubaliana kuimarisha mashirikiano kupitia vikao vya pamoja na tumepanga wataalamu wetu kuweza kukutana ili kuandaa maazimio na kuangalia namna bora zaidi ya kuimarisha Muungano wetu” amesema Dkt. Islam.

Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Hassan Mitawi akifuatila mazungumzo baina ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Dkt. Islam Seif Salum akizungumza wakati wa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa ziara yake ya kujitambulisha leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum (mbele kulia) akizungumza wakati wa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi wakati wa kikao baina yao kilichofanyika Mjini Zanzibar leo Alhamisi Januari 22, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Hassan Mitawi (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Juma Mohammed Salum (katikati) wakifuatilia kikao bainaya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum.

Katbu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Richard Muyungi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yao kilichofanyika leo Alhamisi Januari 22, 2026 Mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi akiongozana na Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Abdallah Mitawi muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao baina yake na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Dkt. Islam Seif Salum.
(NA MPIGAPICHA WETU)

Na Oscar Assenga,TANGA
BENKI Kuu ya Tanzania (BOT) imesema kwamba taasisi ndogo zinazotoa huduma za kubadilisha fedha za kigeni nchini zinapaswa kusajiliwa ili ziweze kupata leseni ya kuendesha shughuli zao,kinyume na hapo ni kosa kisheria.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Afisa Mwandamizi Mkuu kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mwile Kauzeni wakati alipokuwa akizungumzia na Waandishi wa habari kwenye viwanja vya Usagara Jijini Tanga, eneo ambalo Maadhimisho ya Wiki ya fedha kitaifa yanafanyika mwaka huu.
Mwile alikuwa akijibu Swali la Wanahabari waliotaka kujua hatua ambazo zinachukuliwa na benki kuu ya Tanzania katika kudhibiti Watu wanaoendesha biashara ya kubadilisha fedha kiholela.
Ambapo badala yake aliwasihi kufuata Sheria hatua ambayo itawawezesha kupata inayoruhusu uendeshaji kazi hiyo.
Alisema kuwa, ili mtu kufanya biashara hiyo anapaswa kufuata taratibu za kisheria kwa vile kinyume chake atakuwa ametenda kosa la jinai ambapo amewataka wale wenye nia kuendesha shughuli hiyo kutembelea matawi yake.
Aidha alisema taasisi ndogo za huduma za fedha zinahitaji kusajiliwa ili kuweza kupata leseni BOT kutokana na kwamba kubadilisha fedha bila leseni ni kosa kisheria
Awali akizungumza Afisa Mchambuzi Masuala ya Fedha wa BOT Charles Kanuda alisema kwamba, Serikali imekuja na mfuko wa udhamini wa mikopo ambapo kwa mtanzania anayehitaji mkopo huku akiwa hana dhamana toshelevu atapata dhamana mpaka asilimia 75.
Kanuda alisema kwamba,watu wengi wamekuwa wakijaribu kwenda kukopa huku wakiombwa dhamana yenye thamani kubwa zaidi ya mikopo wanayohitaji na hivyo kushindwa kupata mikopo.

Amesema kwamba hali hiyo imewasababisha watanzania walio wengi kushindwa kuchukua mikopo au kuchukua kiasi kidogo jambo ambalo limeathiri ufanisi wa biashara zao wanazoziendesha.
Katika maadhimisho haya ya wiki ya fedha kitafa yenye kauli mbiu ya " elimu ya fedha , msingi wa Maendeleo ya kijamii na kiuchumi" Wadau mbalimbali walitembelea na kupatiwa elimu banda la BOT.
Mwajuma Kileo ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Mkwakwani Jijini Tanga, yeye alielezea kuridhishwa kwake na elimu aliyoipata baada ya kutembelea banda hilo la BOT.
Alisema kwamba, kwa kutembelea banda hilo alijifunza namna ya kutambua fedha bandia mambo ambayo pia walikuwa wakiwafundisha wanafunzi kupitia somo la uraia wanapokuwa Shule.
Adrus Mahmoud (12) mwanafunzi wa darasa la sita kwenye Shule hiyo ya Mkwakwani,alisema amefarijika kupatiwa elimu ya ziada juu ya kutambua alama za kificho zilizomo kwenye noti na hivyo kumsaidia kubaini zilizo za bandia.
Na OWM- TAMISEMI, Dodoma
Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25 imeonesha mafanikio makubwa, ambapo rangi ya kijani imetawala katika viashiria vingi vya utekelezaji, ikiwa ni ishara ya kufanya vizuri kwa mikoa na halmashauri nchini.
Hayo yamesemwa leo Januari 22,2026 jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, wakati akifungua mkutano wa tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25.
Prof. Shemdoe amesema Taifa limeendelea kupiga hatua kubwa katika kuboresha hali ya lishe kwa wananchi, hali inayochangia kuimarisha nguvu kazi yenye afya bora na kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.
“Nawashukuru Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Maafisa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa pamoja na viongozi na watendaji wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mikoa na Halmashauri kwa kazi kubwa ya kusimamia, kuratibu na kutekeleza Mkataba wa Lishe,” amesema Prof. Shemdoe.
Amewahakikishia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI itaendelea kushirikiana na kuwapa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kupunguza na hatimaye kutokomeza kabisa matatizo ya lishe nchini inafikiwa.
Amebainisha kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya utekelezaji wa usia wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyehimiza kuimarishwa kwa sekta za Elimu, Afya na Uchumi ili kupambana na maadui watatu wa Taifa ambao ni ujinga, maradhi na umasikini.
Prof. Shemdoe amesema uwekezaji katika lishe ni mkakati wa kiuchumi wenye tija kubwa, na kwamba Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 imeipa kipaumbele kujenga jamii yenye afya kwa kuzingatia lishe bora ili kila mwananchi astawi.
Aidha, amesema Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025/30, ibara ya 2.3.2 (xi), imetambua umuhimu wa lishe katika kulinda na kujenga afya za wananchi, ambapo CCM itaendelea kuhimiza na kusimamia upatikanaji wa lishe bora kwa wote.
Akizungumza kuhusu dhana ya lishe bora, Prof. Shemdoe amesema ni matokeo ya kutokuwepo kwa magonjwa mwilini pamoja na ulaji sahihi wa vyakula vyenye virutubishi vyote vinavyohitajika.
Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuanza utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hatua itakayosaidia kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma stahiki za afya na kushinda adui maradhi.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, amesema lishe ni suala la msingi katika ukuaji wa binadamu kiakili na kimwili, sambamba na kuongeza tija katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Naye,Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia afya Prof.Tumaini Nagu amesema serikali itaendelea kusimamia kwa karibu utoaji wa huduma za lishe katika Mikoa na Halmashauri zote nchini.



.jpeg)



















.jpeg)


