Na Karama Kenyunko Michuzi Tv

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imesema itaendelea kuimarisha mifumo ya huduma za afya kupitia tafiti mbalimbali ili kuhakikisha wagonjwa wenye magonjwa adimu wanapata huduma stahiki na kwa wakati.

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amesema hayo leo Machi 4, 2026 wakati akifungua Kongamano la 16 la kusambaza matokeo ya tafiti za magonjwa adimu lililoanfaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kwa kushirikiana na AKRDF foundation jijini Dar es Salaam.

Pia Dkt.Magembe, amesema serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za chuo hicho kuwa kitovu cha ubora, ubunifu na utafiti kwa maendeleo ya taifa na ukanda wa Afrika Mashariki.

Amesema Serikali inayapa uzito stahiki magonjwa haya adimu, ili yaweze kushughulikiwa kwa kina na upana wake, kwa kushirikiana na Taasisi kama Ali Kimara, mashirika na sekta binafsi hivyo kuùwafikia watoto wengi zaidi," amesema Dkt. Magembe.

Ameeleza kuwa MUHAS ina wajibu wa kuongoza tafiti na kuzalisha wataalamu mahiri katika sekta ya afya. Aidha, amebainisha kuwa serikali itaendelea kuboresha huduma za rufaa na kuimarisha mifumo ya matunzo inayounganisha huduma za msingi na za kibingwa.

Kwa mujibu wa Dkt. Magembe, duniani kuna zaidi ya magonjwa adimu 7,000 yanayoathiri takribani watu milioni 400. Asilimia 80 ya magonjwa hayo husababishwa na vinasaba, na wastani wa mtu mmoja kati ya 2,000 huathirika.

Amesema kuwa nchini Tanzania, inakadiriwa kuwa asilimia sita ya wananchi wanaweza kuwa na aina fulani ya ugonjwa adimu.

"Miongoni mwa magonjwa adimu yanayoonekana zaidi ni selimundu, hemofilia, tawahudi, lupus erythematosus na Gaucher.

Aidha, Dkt. Magembe amesema hadi kufikia Desemba mwaka 2025 zaidi ya wataalamu wa afya 200 katika vituo 14 walikuwa wamepatiwa mafunzo ya kuanzisha vitengo vya tiba ya magonjwa adimu ikiwemo 'hemofilia' kuanzia ngazi ya msingi.

"Serikali imeshachukua hatua za kujenga uwezo wa maabara yetu ya Taifa, mafunzo kwa wataalamu wa Afya na kuanzisha vitengo maalum vya matibabu ya magonjwa adimu kuanzia ngazi ya msingi (Zahanati, kituo cha afya na hospitali za wilaya), tulianza na Seli mundu (Sickle cell) na sasa Hemofilia ambapo tayari wagonjwa 500 wamegundulika na wanaendelea na tiba,” amesema Dkt. Magembe.

Kwa upande wake, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS , Profesa Emmanuel Balandya, amesema MUHAS inatambua jukumu lake katika utoaji wa elimu, utafiti na huduma zinazohusu magonjwa adimu.

Ametaja changamoto zilizopo kuwa ni pamoja na uhaba wa vipimo vya vinasaba, gharama kubwa za uchunguzi na utegemezi wa maabara za nje ya nchi.

Ameongeza kuwa kupitia tafiti, ubunifu na ushirikiano na wadau, chuo kinaendelea kutafuta suluhisho endelevu yatakayotekelezwa ndani ya mfumo wa afya nchini.

“Kongamano hili, limeandaliwa kama jukwaa la kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kuibua mapendekezo yatakayobooresha utambuzi, matibabu na ubora wa maisha ya wagonjwa. Pia litatumika kusikiliza maoni ya wagonjwa na familia zao na kujadili namna bora ya kuimarisha rufaa kuanzia ngazi ya msingi hadi huduma za juu’ amesema Profesa Balandya.

Naye Mwenyekiti wa AKRDF, Sharifa Mbaraka, amesema matokeo ya tafiti yanatarajiwa kuleta maboresho chanya kwa watoto na jamii kwa ujumla, hasa yatakapoingizwa katika sera za afya.

Ameeleza kuwa makubaliano na MUHAS yanalenga kuanzisha tafiti mahususi, akibainisha kuwa kwa sasa watoto wenye magonjwa adimu hawatambuliwi ipasavyo katika mifumo ya bima ya afya, hivyo wanahitaji msaada zaidi.

Kaulimbiu ya mwaka huu, “Magonjwa Adimu: Ni Zaidi ya Tunavyoweza Kufikiria,” inalenga kuhamasisha jamii kutambua suala hilo kama ajenda ya kijamii, kielimu, kiutafiti na kisera inayohitaji ushirikiano wa wadau wote.

Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe akizungumza leo Machi 4, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa akifungua  Kongamano la Magonjwa Adimu 2026 lililoandaliwa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kwa Kushirikiana na Taasisi ya  Ali Kimara Rare Disease Foundation (AKRDF)
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS , Profesa Emmanuel Balandya, akizungumza leo Machi 4, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Magonjwa Adimu 2026 lililoandaliwa na  MUHAS kwa Kushirikiana na AKRDF.
Mwenyekiti wa AKRDF,  Sharifa Mbaraka akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa Kongamano la Magonjwa Adimu 2026.
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS , Profesa Emmanuel Balandya (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa AKRDF,  Sharifa Mbaraka wakisaini mkataba wa makubaliano kwa ajili ya kufanya tafiti kuhusu magonjwa adimu leo Machi 4, 2026 jijini Dar es Salaam




Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe (katikati), Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS , Profesa Emmanuel Balandya wakiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki Kongamano Magonjwa Adimu 2026.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ametembelea banda la Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) katika maonesho ya mafanikio ya siku 100 za uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na utatuzi wa kero za wananchi.

Maonesho hayo ya siku tatu yamefunguliwa leo machi 5, katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, yakishirikisha taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo TEMESA, ambapo imewasilisha mafanikio yao katika utoaji wa huduma kwa wananchi na kutoa elimu kuhusu majukumu yao.

Akiwa katika banda la TEMESA, Mhe. Senyamule alipata maelezo kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na TEMESA pamoja na mafanikio ya Wakala kutoka kwa Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma, Bi. Martha Joachim.


Akitoa ufafanuzi huo, Bi. Martha amesema TEMESA imepiga hatua katika kuboresha utoaji wa huduma za kiufundi kwa taasisi za Serikali kupitia matumizi ya mifumo ya kisasa na ya kidijitali.

Ameeleza kuwa miongoni mwa mafanikio hayo ni matumizi ya Mfumo wa Usimamizi wa Kazi za Matengenezo (MUM), unaosaidia na kurahisisha ufuatiliaji wa shughuli za matengenezo kwa ufanisi zaidi.



“Mfumo huu umeongeza uwazi, ufanisi na kasi katika utoaji wa huduma za matengenezo, na kusaidia taasisi za Serikali kupata huduma bora zinazopelekea kuwahudumia wananchi kwa ufanisi,” amesema.

Aidha, Bi. Martha ameongeza kuwa TEMESA inaendelea kuboresha utendaji kazi wake, hasa katika huduma za matengenezo ya magari ya Serikali, usimamizi wa vivuko pamoja na miundombinu ya umeme katika taasisi mbalimbali za Umma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule ameipongeza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuendesha zoezi la Samia Ardhi Kliniki linalofanyika nchi nzima.

Mhe. Senyamule ametoa pongezi hizo leo Machi 5, 2026 alipotembelea kliniki hiyo inayoendelea katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Dodoma.

“Nimekaa sijawahi kuona ubunifu wa jambo hili, na nimeambiwa linafanyika nchi nzima ya Tanzania. Hiki ni kitu cha pekee sana,” amesema Senyamule.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa mkoa wa Dodoma, awali aliposikia kuhusu kliniki hiyo alijiuliza kama kutapatikana wanawake wa kutosha kwenda kutatuliwa kero zao za ardhi, lakini hali imekuwa tofauti.

“Nilijiuliza kama wanawake watapatikana kwa wingi, lakini leo nimeshangaa kuona na kushuhudia kuwa sasa wanawake wengi wanamiliki ardhi,” amesema Senyamule.

Aidha, amesema kuwa kama jambo hilo lingefanyika miaka kumi au ishirini iliyopita, isingekuwa rahisi kupata wanawake wengi kwa sababu wengi hawakuwa na uelewa wa haki yao ya kumiliki ardhi.

“Kama ungelifanya jambo hili miaka kumi au ishirini iliyopita na kusema wanawake waje washughulikie kero zao za ardhi na kupata hati, usingewapata wengi kwa sababu wakati huo hatukuwa na uelewa kuwa sisi pia tunastahili kumiliki ardhi,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Mhe. Senyamule amewaasa wanawake kutunza vizuri hati zao za ardhi, akieleza kuwa ardhi ya Dodoma ina thamani kubwa inayoongezeka kila siku.

“Ukishapata hati yako, itunze vizuri kwa sababu ardhi ya Dodoma ina thamani kubwa na thamani yake inaendelea kuongezeka kila siku,” amesema.

Sambamba na hilo, Mhe. Senyamule pia amekabidhi hati miliki kwa baadhi ya wanawake waliofika katika kliniki hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Dodoma.

Samia Ardhi Kliniki ilianza rasmi tarehe 2 Machi 2026 katika mikoa yote nchini na inatarajiwa kuhitimishwa tarehe 7 Machi 2026 yenye Kauli Mbiu, Mwanamke; Haki Yako, Miliki Ardhi sasa.


-Yatoa elimu ya umuhimu wa Hifadhi ya Jamii na utunzaji wa mazingira

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepanda miti 600 katika shule mbili za Wilaya ya Ilemela, mkoani Mwanza, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8.

Zoezi hilo limefanyika Machi 4, 2026 katika Shule ya Msingi Chasubi na Nyakabonga pamoja na Shule ya Sekondari Kayenze, likiwa na lengo la kuhamasisha utunzaji wa mazingira pamoja na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Hifadhi ya Jamii kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Kupitia baadhi ya wafanyakazi wake wanawake, NSSF imesema kuwa hatua hiyo inalenga kujenga uelewa wa mapema kwa vijana kuhusu umuhimu wa kujiwekea akiba kwa ajili ya maisha ya uzeeni na kunufaika na mifumo rasmi ya Hifadhi ya Jamii.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Meneja wa Wananchi Waliojiajiri wa NSSF, Bi. Rehema Chuma, amesema upandaji miti unaashiria dhamira ya Mfuko huo katika kuchangia ustawi wa jamii, uyuchumi pamoja na kuhifadhi mazingira.

Ameeleza kuwa wanachama wanaojiunga na kuchangia NSSF hunufaika na mafao mbalimbali kwa mujibu wa sheria, yakiwemo mafao ya matibabu, uzeeni, ulemavu na mengineyo.

Kwa upande wake, Meneja wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Bw. Emmanuel Kahensa, amesema zoezi hilo limefanikiwa kwa ushirikiano na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), ambao walitoa miche bora ya miti kwa ajili ya kupandwa katika shule hizo.

Amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaimarisha juhudi za Serikali na taasisi zake katika kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Naye, Muhifadhi kutoka TFS, Bi. Maija Mkomwa, amesema upandaji wa miti katika taasisi za elimu ni hatua muhimu katika kujenga kizazi chenye utamaduni wa kutunza mazingira.

Walimu wakuu wa shule hizo wameishukuru NSSF kwa kushirikiana nao katika zoezi hilo, wakisema litawasaidia wanafunzi kujenga tabia ya kupenda na kulinda mazingira. Wanafunzi kwa upande wao wameahidi kuitunza miti hiyo ili iweze kuleta manufaa kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa mujibu wa NSSF, mpango huo ni sehemu ya mikakati yake ya uwajibikaji kwa jamii (CSR), sambamba na kuendeleza kauli mbiu yake ya kuwajengea wanachama maisha bora ya sasa na baadaye.
































 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam Kuna ushindi wa kupiga picha na kuonyesha watu. Halafu kuna ushindi wa aina nyingine. Ule unaokupa mwendo mpya kwenye maisha.

Daniel Deogratus Sambo, mjasiriamali wa Kigoma Mjini, amesema amepata mwendo huo baada ya kushinda pikipiki aina ya TVS kupitia kampeni ya #ShindaBoda ya PigaBet. Kwa Sambo, boda hii si zawadi ya kuitazama tu. Ni mchongo wa kufanya kazi zisogee na kipato kiongezeke.

“Nilianza kucheza muda mrefu, lakini leo nimebahatika kushinda pikipiki. Hii itanisaidia sana katika biashara zangu za kila siku,” alisema Sambo.

Kwa lugha ya Bongo, Sambo anasema hii ni kama kupewa mchongo wa kusukuma mambo. Inarahisisha shughuli, inaokoa muda, na inapunguza stress za usafiri. Hapo ndipo kauli ya #ShindaBoda inapokaa vizuri. Kuwa boss si lazima uwe na ofisi. Kuwa boss ni pale unapopata namna ya kujisimamia na kuongeza kipato.

Katika tukio hilo, mshindi mwingine Doreen Massawe naye alisema ushindi wake unaenda kubeba uzito wa kazi. Doreen, anayejihusisha na kilimo, amesema boda hiyo itamsaidia kurahisisha shughuli zake na kuongeza ufanisi wa kila siku.

“Ninajihusisha na kilimo, hivyo pikipiki hii itanisaidia sana kwenye shughuli zangu,” alisema.

Akizungumzia kampeni hiyo, Afisa Masoko wa PigaBet Tanzania, Hemed Msonge, alisema #ShindaBoda inatoa pikipiki mbili kila wiki kwa muda wa wiki sita. Alisisitiza kuwa ushiriki unapaswa kuwa wa uwajibikaji.

“Tunahimiza Watanzania kuendelea kushiriki kwa uwajibikaji. Droo zinaendelea kila wiki hadi mwisho wa kampeni,” alisema.
Kwa Sambo, ujumbe ni mmoja. Kuna zawadi, na kuna mchongo. Na hii ni mchongo wa kusukuma maisha.

18+ | Cheza kwa uwajibikaji.


















 

Dar es salaam – 05/03/2026

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir, ametoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kutumia fursa ya huduma za ardhi zinazotolewa kupitia Samia Ardhi Kliniki, akisisitiza umuhimu wa wanawake kumiliki ardhi kama njia ya kujikomboa kiuchumi.

Mufti Zubeir alitoa kauli hiyo baada ya kufika katika Kliniki ya Ardhi inayofanyika katika Ofisi za Ardhi za Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo alipata hati ya ardhi huku akishuhudia namna wananchi wanavyohudumiwa katika kliniki hiyo ambayo inaendelea nchi nzima.
Akizungumza mara baada ya kupata huduma hiyo, Mufti Zubeir alisema hatua ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuandaa Samia Ardhi Kliniki yenye kulenga kuwapa kipaumbele wanawake ni jambo muhimu linalosaidia kuongeza usawa katika umiliki wa rasilimali muhimu kama ardhi.

Alisema wanawake wanapaswa kutumia kikamilifu fursa hiyo ili waweze kupata hati za ardhi na kujiimarisha kiuchumi.

“Wanawake wana haki ya kumiliki mali mbalimbali ikiwemo magari na mali nyingine, hivyo hakuna sababu ya kuwanyima nafasi ya kumiliki ardhi. Ni muhimu jamii, hususan wanaume, kuachana na mila kandamizi zinazowazuia wanawake kumiliki rasilimali,” alisema Mufti Zubeir.

Aidha, aliwataka wanaume kuwapa nafasi wanawake kumiliki ardhi ili kuongeza idadi ya wanawake wenye umiliki rasmi wa ardhi nchini, jambo ambalo litasaidia kuimarisha ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Mufti Zubeir alipongeza maandalizi mazuri yaliyofanywa na Ofisi ya Mkoa wa Dar es Salaam katika uendeshaji wa kliniki hiyo, kuanzia mapokezi hadi utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema namna wateja wanavyohudumiwa kwa ufanisi ni jambo jema lenye manufaa kwa jamii na lina thawabu kubwa mbele za Mwenyezi Mungu, hususan katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Mufti Zubeir pia aliwaombea heri watumishi wanaotoa huduma katika kliniki hiyo ili waendelee kuwahudumia wananchi kwa uadilifu na bidii.

Samia Ardhi Kliniki zinaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za ardhi, hususan kwa wanawake, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa Machi 8 kila mwaka.



 

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda (kushoto) akipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware (katikati) muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2025 kwa ajili ya ziara yake ya kikazi.

**********************

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda amelipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa mikakati iliyojiwekea kutekeleza malengo ya nguzo ya tatu ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Mhe. Luvanda amesema hayo leo Alhamisi Machi 05, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kujitambulisha na kuzungumza na Menejimenti ya Baraza hilo sambamba na kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Ofisi hiyo.

Mhe. Luvanda amesema NEMC imebeba maono na matarajio makubwa ya nchi katika kufikiamalengo ya dira ya maendeleo ya taifa 2050 hususani utelekelezaji wa nguzo ya tatu inayoakisi masuala ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi.

“Kwa taarifa nilizoona nimeridhishwa na utayari wenu katika utekelezaji wa dira 2050…..Hatuna budi kutambua kuwa tumebeba matumaini ya Viongozi wakuu wa kitaifa katika kufanikisha utekelezaji wa Dira 2050 katika upande wa mazingira” amesema Mhe Balozi Luvanda.

Aidha Mhe. Balozi Luvanda amesema suala la elimu kwa umma halina budi kupewa kipaumbele na msukumo wa pekee ili kuhakikisha inapatiwa uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wakutunza na kuhifadhi mazingira kwa ajili ya mustabali endelevu wa taifa.

Balozi Luvanda pia ameishauri Menejmenti ya NEMC kuweka msukumo wa kujitangaza kwa jamii na wadau mbalimbali kwa kuwa misingi ya utekelezaji wa jukumu hilo limeanishwa katika sheria na kanuni zinazosimamia majukumu ya taasisi hiyo.

Mhe. Balozi Luvanda amesema NEMC ni taasisi muhimu yenye mchango mkubwa katika kuharakisha kasi ya ukuaji wa sekta za maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini na hivyo ana imani na watendaji wa ofisi hiyo katika kutekeleza jukumu hilo muhimu kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware amemshukuru Mhe. Balozi Luvanda kwa ziara hiyo ya kikazi katika ofisi za baraza hilo na kuwa ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano ili kuwezesha na kufanikisha dhamira na maono ya Serikali.

“Sisi kama Watumishi wa NEMC tunakukaribisha Mhe. Balozi Luvanda tutambua majukumu uliyonayo yanaakisi shughuli zinazotelekezwa na NEMC, hivyo tupo tayari kupokea maelekezo na kufanyia kazi” amesema Dkt. Sware.

Mhe. Balozi Baraka Luvanda aliteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais akichukua nafasi ya Prof. Peter Msoffe aliyehamishiwa Wizara ya Kilimo.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akipokea shada la maua kutoka Bi. Florida Kavure Afisa Mazingira waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akisalimiana na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026 kuanza ziara yake ya kikazi. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Baadhi ya Watendaji Waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakifuatilia kikao baina ya Ofisi hiyo na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea Ofisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Kemilembe Mutasa (kushoto) akifuatilia kikao baina ya Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Baadhi ya Watendaji Waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakifuatilia kikao baina ya Ofisi hiyo na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea Ofisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akifuatilia Makala mjongeo inayoelezea majukumu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Immaculate Sware akitoa taarifa ya utekelezaji wa Baraza hilo kwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Balozi Baraka Luvanda aliyefanya ziara ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akizungumza na Viongozi na Watendaji waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakiongozwa na Makurugenzi Mkuu, Dkt. Immaculate Sware (kulia) wakati wa ziara yake aliyoifanya katika ofisi hiyo Jijini Dar es Salaam leo Jijini Machi 05, 2026.

Naibu Katibu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware wakati wa ziara yake aliyoifanya katika Ofisi za Baraza hilo leo Jijini Dar es Salaam leo Machi 05, 2026.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware (kulia) na Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Kemilembe Mutasa (kushoto) pamoja na watendaji wengine wa Baraza hilo muda mfupi baada ya kumaliza ziara yake aliyoifanya katika Ofisi zas Baraza hilo leo Alhamisi Machi 05, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware muda mfupi baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi ya kutembelea ofisi za baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.

(NA MPIGAPICHA WETU)


Top News