MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA MAJI WA SH BILIONI 3.18 MOROGORO, WANANCHI WATAKIWA KULINDA VYANZO
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda, amewataka wananchi walio karibu na vyanzo vya Maji kulinda vyanzo hivyo pamoja na miundombinu ya huduma hiyo.
Ametoa wito wakati akizindua mradi wa maji wa uhifadhi wa chanzo Cha mto Ruvu kupitia ujenzi wa miondombinu ya usambazaji Maji wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unaotarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa vijiji vya Dakawa na Mngazi Halmashauri ya Morogoro.
Amesema Serikali imeendelea kuwekeza fedha nyingi katika sekta ya maji kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi, hivyo ni wajibu wa jamii kuhakikisha miundombinu hiyo inalindwa na kutunzwa ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu.
Mradi huo wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unahusisha uchimbaji wa visima viwili vyenye uwezo wa kuzalisha lita 248,000 za maji kwa saa, ujenzi wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 26, vituo 34 vya kuchotea maji pamoja na matenki mawili yenye uwezo wa kuhifadhi lita 160,000 za maji.
Aidha, mradi huo umejumuisha uwekaji wa pampu za kusukuma maji zenye uwezo wa lita 30,000 kwa saa katika Kijiji cha Mngazi na lita 50,000 kwa saa katika Kijiji cha Dakawa, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kwa uhakika.
Katika kuimarisha matumizi bora ya rasilimali za maji, mradi huo pia umejenga birika la kunyweshea mifugo katika Kitongoji cha Lukenze, Kijiji cha Dakawa, ambalo linatarajiwa kusaidia kupunguza migogoro ya matumizi ya maji kati ya wakulima na wafugaji.
Kwa sasa mradi huo unawanufaisha wananchi 6,453 wa vijiji vya Dakawa na Mngazi, huku idadi ya wanufaika ikitarajiwa kuongezeka na kufikia watu 11,550 ifikapo mwaka 2043.
Mwang’onda alieleza kuridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kushiriki katika uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Baadhi ya wakazi wa vijiji vya Mngazi na Dakawa, akiwemo Kibua Haji na Maua Bunga, walieleza kufurahishwa na utekelezaji wa mradi huo wakisema umesaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa maji iliyokuwa ikiwalazimu kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi na salama.
Wananchi hao waliipongeza Serikali kupitia Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huo na kuomba huduma hiyo kuendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi katika maeneo mengine ya wilaya hiyo.


.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
