Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imekamilisha ujenzi wa shule ya kisasa ya wasichana Mwanza ambayo imejengwa katika Wilaya ya Magu.

Shule hiyo imejengwa kupitia Mradi wa kuboresha Ubora wa Elimu Sekondari (SEQUIP) kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.1 huku ikiwa na miundombinu toshelevu.

Miundombinu iliyojengwa ni pamoja na maabara nne za (Kemia, Fizikia, Baiolojia na Jografia), vyumba 22 vya madarasa na ofisi 6, Vyoo matundu 23, mabweni 9, nyumba 5 za walimu, Jengo la utawala, Bwalo, Jengo 1 la TEHAMA, Mashimo ya maji taka pamoja na fensi.

Pia serikali kupitia mradi huo wa SEQUIP imetoa jumla ya Shilingi Bilioni 1.6 na tayari ipo katika hatua za ukamilishaji wa ujenzi wa shule mpya ya Amali katika kijiji cha Mhungwe kilichopo katika Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Ujenzi wa shule hiyo mpya unahusisha ujenzi wa Madarasa 8 na ofisi 2, Maktaba, Jengo la Utawala, Maabara 2 za Kemia na Baiolojia, Jengo la TEHAMA, Mabweni 4, Bwalo la chakula, Karakana 2 za ufundi Umeme na Uashi, Nyumba ya mwalimu, na Matundu 8 ya vyoo.





 

Na Mwandishi wetu, Prishtina

Ujumbe kutoka Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) ukiongozwa na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Rufani, Jaji Mstaafu Mhe. Awadh Bawazir umewasili Jijini Prishtina nchini Kosovo kwa ziara ya kikazi ya siku tano kuanzia tarehe 14 – 18 Julai, 2025.

Katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Mamlaka ya Rufani ameambatana na Wajumbe wa Mamlaka ya Rufani, Kamishna wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Dkt. Frederick Mwakibinga, Mkurugenzi wa Mipango Wizara ya Fedha, Bw. Moses Dulle pamoja na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya PPAA.

Mwenyekiti wa Ujumbe huo, Jaji Mstaafu Mhe. Awadh Bawazir ameeleza lengo la ziara hiyo ni kujifunza na kupata uzoefu wa Taasisi zinazosimamia Ununuzi wa Umma na mnyororo wa ununuzi wa umma hususan katika masuala ya ununuzi wa umma, uwasilishaji na ushughulikiaji wa malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroni nchini Kosovo.

Baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Prishtina, ujumbe wa Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma ulipokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kosovo Bw. Ilir Muçaj.

Ujumbe huo ukiwa nchini Kosovo unategemea kutembelea Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PRD), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRC), Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAO), pamoja na Idara ya Uratibu wa Ukaguzi wa Ndani (CHDIA). 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Kosovo Bw. Ilir Muçaj akizungumza na ujumbe kutoka Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) unaoongozwa na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Rufani, Jaji Mstaafu Mhe. Awadh Bawazir baada ya kuwasili Jijini Prishtina nchini Kosovo kwa ziara ya kikazi ya siku tano kuanzia tarehe 14 – 18 Julai, 2025

Na Mwandishi Wetu

WAZAZI ambao watoto wao wanakwenda kusoma nje ya nchi kwa mwaka wa masomo wa 2025/2026 wametakiwa kufuatilia kwa karibu mwenendo wa watoto wao kitaaluma na tabia.

Wito huo ulitolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Elimu Nje ya Nchi, Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel alipokutana na wazazi na wanafunzi hao siku ya Jumapili kwenye ofisi za GEL jijini Dar es Salaam ambapo wazazi na wanafunzi hao walipewa taratibu za mambo ya kuzingatia kabla, wakati na baada ya kufika nchi wanazokwenda.

Katika mkutano huo, ambao ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka vyuo vikuu mbalimbali duniani, wanafunzi wengi walikabidhiwa viza zao tayari kwa ajili ya safari ya kuelekea vyuoni, huku wazazi wakipata fursa ya kuzungumza ana kwa ana na baadhi ya wawakilishi wa vyuo hivyo.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel, alisema wazazi wanalipolipa ada wasidhani kwamba wamemaliza jukumu lao na badala yaake bado wanakuwa na wajibu wa kuwafuatilia.

Alisema ni muhimu sana kila mzazi akafanya hivyo ili kujua maendeleo ya mtoto wake kitaluma na tabia anapokuwa chuoni kwani baadhi yao wamekuwa wakibadilika na kufanya mambo yasiyostahili na kushindwa kuhitimu.

“Mzazi ukiona mtoto wako ana nyendo ambazo hazieleweki eleweki mwite nchini ukae naye uzungumze naye ujue shida yake kwasababu unaweza kukuta ameshaacha shule anafanyabiashara,” alisema Mollel

“Cha msingi kinachowapeleka kule nje ya nchi ni masomo siyo biashara, mkifika kule na kuanza kufanyabiashara mnaweza kushindwa kuhitimu kwa hiyo wazazi mnapaswa kuwa karibu sana ukiona mtoto wao kila akikupigia simu hana mazungumzo zaidi ya kuomba hela hapo anza kushtuka na kumfuatilia,” alisema

Mollel alisema ataendelea kutekeleza wajibu wake kuhakikisha kila mwanafunzi aliyekamilisha taratibu anafanikisha safari yake ya kwenda kuanza masomo katika vyuo walivyodahiliwa kwa wakati.

Alisisitiza kuwa maslahi ya mwanafunzi ndiyo kipaumbele cha kwanza na kwamba hatakubali kuona chuo chochote kinashindwa kutimiza wajibu wake.

Aidha, Mollel aliwakumbusha wazazi na vyuo husika kuhusu majukumu yao ya msingi katika kuhakikisha mafanikio ya safari ya kielimu ya watoto wao.

Katika mkutano huo, baadhi ya wazazi na wanafunzi waliotoa ushuhuda, wameeleza kufurahishwa na jinsi ambavyo Global Education Link imekuwa msaada mkubwa katika kutimiza ndoto zao.

Frank John alisema kama si kampuni hiyo, watoto wao wangeweza kujikuta mikononi mwa mawakala wa elimu ambao siyo waaminifu na kuwatapeli.

“Tunashukuru kuona GEL inasimamia kila kitu kuanzia Dar es Salaam hadi mwanafunzi anapofika chuoni na kizuri zaidi ni kwamba hata akifika chuo hawaishii hapo, wanafuatilia maendeleo yake ya kitaaluma kuhakikisha anatimu na kama anachangamoto yoyote wanaitatua,” alisema

Miongoni mwa wanafunzi waliopata nafasi ni wale waliodahiliwa katika chuo cha Dalian Neusoft University of Information (DNUI) cha China.

Wanafunzi hao wamedahiliwa kwa programu ya Bachelor of Computer Science miaka minne na Bachelor of Engineering in IT .

Hiyo ni moja ya programu bora zinazochanganya masomo ya kompyuta na uhandisi wa teknolojia ya habari.

“Hii ni fursa adhimu ya kielimu inayompa mwanafunzi uzoefu wa kimataifa na kazi kwa vitendo kupitia (Optional Practical Training) OPT katika kampuni za teknolojia nchini China,” alisema mzazi Emmanuel Mbaso.

Katika tukio hilo, wazazi na wanafunzi walitumia nafasi hiyo kuipongeza Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwa kutoa matokeo na Result Slips kwa wakati.

Mzazi Juma Kassim alisema kutoa matokeo mapema kumewezesha wanafunzi kukamilisha nyaraka za udahili kwa vyuo vikuu vya kimataifa kwa ufanisi mkubwa.

Mkutano huo ulitumika pia kuyajibu maswali muhimu kutoka kwa wazazi na wanafunzi na wanafunzi wengi tayari wamekamilisha hatua muhimu kama upatikanaji wa VIS na muda wowote kuanzia mwezi Agosti, wataanza safari ya kuelekea katika vyuo mbalimbali duniani.



Na Seif Mangwangi, Arusha

WAKATI Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango akitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa pili wa Mabaraza ya Habari Afrika (Nimca), kesho Julai 15, 2025, Umoja wa Mataifa (UN), umesema uanzishaji wa vyombo vya habari vya kujitegemea ni muhimu kwa maendeleo na uendelevu wa Demokrasia katika Taifa lolote Duniani.

Akizungumza katika siku ya kwanza ya mkutano huo ulioanza leo 14Julai 2025, Mkurugenzi msaidizi wa mawasiliano ya Habari kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni(UNESCO) Dkt. Tawfik Jelassi amesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari katika kuzingatia haki za binadamu, jinsia na watu wenye ulemavu sanjari na kuhakikisha matumizi ya akili mnemba.

Amesema uaminifu katika vyombo vya habari unajaribiwa kama maendeleo katika teknolojia ambayo hubadilisha jinsi habari inavyotengenezwa, kuhaririwa, kusambazwa na kutumika kwa walaji ambao husoma na kuelewa zaidi mambo mbalimbali yanavyokwenda.

"Uhuru wa kujieleza na ufikiaji wa habari unakabiliwa na shinikizo linalokua ulimwenguni hivyo katika muktadha huo ni lazima Azimio la Windhoek la mwaka 1991 likumbukwe ambalo linasisitiza kuanzishwa, kutunza na kukuza vyombo vya habari vya kujitegemea kwa maendeleo na uendelevu wa demokrasia katika taifa," amesema.

Dkt.Jelassi alisisitiza kwamba katika miongo mitatu iliyopita, nchi zote barani Afrika zimefanya maendeleo makubwa katika kukuza sekta ya vyombo vya habari inayoendeshwa na juhudi za ndani na za kitaifa ikiwemo kuunda mazingira ya kuwezesha mfumo wa kisheria na sera ambao huruhusu uandishi huru.

"Misingi hii inawezesha uandishi wa habari kufanikiwa na kupata uaminifu wa watu wanaofuatilia hata katika changamoto zinazoendelea na zinazoibukia," amesema

Amesema mkutano huo unatoa nafasi muhimu ya kudhibitisha ahadi ya pamoja kwamba ubora wa uandishi wa habari ni msingi wa demokrasia, haki za binadamu na maendeleo barani Afrika.

Aidha Dkt Jasisi amesisitiza juu ya kasi ya kiteknolojia, kuwa vyombo vya habari na kanuni za mawasiliano zinapaswa kushika kasi na maendeleo ya haraka ya kiteknolojia wakati wa kulinda uadilifu wa habari,uhuru wa kujieleza na ufikiaji wa ulimwengu kwa habari za kuaminika wakati huo huo uwekezaji katika akili bandia .

Awali Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), na Mwenyekiti wa Mtandao wa Mabaraza Huru ya Vyombo vya Habari Afrika (NIMCA),Ernest Sungura amesema mkutano huo unatarajia kufunguliwa na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango ikiwa ni kwa niaba ya Rais Samia Hassan Suluhu.

Amesema mkutano huo utawawezesha kuchukua hatua mbalimbali, ili kuhakikisha vyombo vya habari barani Afrika vinakuza ushirikiano na uvumbuzi zaidi katika habari.

"Ubora wa vyombo vya habari barani Afrika, unaangazia kujitolea kwao katika kuongeza ubora na uadilifu wa uandishi wa habari, "amesema.

Amesema mkutano huo wa kimataifa pia unaambatana na maonyesho ya kazi za kihabari na maadhimisho ya miaka 30 ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), NIMCA na Mabaraza Huru ya Habari Afrika Mashariki (EAPC) huku mada mbalimbali zikijadiliwa ikiwemo matumizi ya akili mnemba (AI) sera za usawa wa kijinsia hususan kwa watu wenye ulemavu na mada nyingine zitatolewa.

Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo akimwakilisha Mkurugenzi wa Habari Maelezo, Rodney Thadeus amesisitiza idara hiyo kuendelea kushirikiana na Baraza la Habari ( MCT), katika kuhakikisha sekta hiyo inaimarika zaidi nchini ikiwemo jitihada zake za kuhakikisha waandishi wa habari wanafuata maadili.

Mkutano huo umeshirikisha waandishi wa habari wakongwe, na wadau mbalimbali wa habari zaidi ya 500 kutoka nchi mbalimbali za Afrika.


Kassim Nyaki, NCAA.

Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) inatumia fursa ya mkutano wa pili wa mabaraza huru ya Habari Afrika unaofanyika jijini Arusha kunadi vivutio vya utalii vilivyopo Ngorongoro ili kuendelea kuwavutia wageni wengi zaidi.

Mkutano huo unaofanyika Jijini Arusha kuanzia tarehe 14- 17 Julai 2025 unawakutanisha wadau mbalimbali wa Sekta ya Habari kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika ambapo washiriki zaidi ya 200 wanahudhuria mkutano huo.

Afisa Utalii Mkuu NCAA Peter Makutian ameeleza kuwa ushiriki wa NCAA katika mkutano huo unalenga kuwafikia wajumbe wa mkutano huo na kuwaelezea vivutio vya utalii vilivyopo Ngorongoro ambayo ni kivutio Bora cha Utalii Afrika kwa mwaka  2023 na mwaka 2025.

"Kama mnavyojua Ngorongoro ni kivutio Bora cha utalii Afrika hivyo wageni wanahamasika na kuwa na shauku ya kujua vivutio vilivyopo,  fursa za uwekezaji na shughuli za utalii, kwa siku zote za mkutano huu tutahakikisha tunawafikia na kuendelea kutangaza eneo letu" alisema  Makutian.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni;  "Kuendeleza kanuni za vyombo vya habari na mawasiliano kwa ubora wa uandishi wa habari barani Afrika"



















Farida Mangube, Morogoro
MKEMIA Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelis Mafuniko, amesema mchango wa wadau katika utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Kemikali za Viwandani (Sura ya 182) umeendelea kuimarika, na kuonyesha kuongezeka kwa uelewa, uwazi na uwajibikaji katika kulinda afya ya jamii na mazingira nchini.

Dkt. Mafuniko alitoa kauli hiyo mjini Morogoro katika kikao kazi cha mwaka cha Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) kilichowakutanisha wadau zaidi ya 110 kutoka kanda zote sita zinazofanya kazi na mamlaka hiyo.

Alisema utekelezaji wa sheria hiyo umekuwa wa mafanikio zaidi kutokana na ushirikiano wa karibu kutoka kwa taasisi za serikali, sekta binafsi, na wadau wengine waliopo katika mnyororo wa kemikali, hatua inayosaidia taifa kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi holela au yasiyo salama ya kemikali hatarishi.

GCLA ilitumia fursa hiyo kuwatambua wadau waliotekeleza vizuri sheria na taratibu za usimamizi wa kemikali kwa mwaka 2023/2024, kwa kuwapatia vyeti vya pongezi na ngao za heshima.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa GCLA, Christopher Kadio, alisema wadau wote wa kemikali nchini wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya mamlaka hiyo ili kulinda afya za wananchi na mazingira ya nchi kwa ujumla.

Kadio aliongeza kuwa bado kuna haja ya kuongeza nguvu katika usimamizi wa kemikali kwa kuhakikisha kuwa hata kwenye maeneo madogo ya uzalishaji na usambazaji, taratibu zote za usalama na uhifadhi zinafuatwa ipasavyo.

Katika hafla hiyo Kanda ya Mashariki imeibuka mshindi wa jumla katika utekelezaji wa sheria kwa mwaka 2023/2024, ikifuatiwa na kanda nyingine ambazo pia zilitambuliwa kwa jitihada zao.

Wadau walioibuka vinara katika utekelezaji wa sheria hiyo walitunukiwa vyeti na ngao ikiwa ni sehemu ya motisha ya kuendelea kushirikiana na serikali katika kulinda jamii dhidi ya athari za kemikali.

Akizungumza kwa niaba ya wadau waliopata zawadi, Wilson Mchunguzi kutoka kampuni ya Oryx Gas Tanzania, alisema kutambuliwa kwa juhudi zao kumewapa ari mpya ya kuendelea kuboresha mifumo yao ya usimamizi wa kemikali na kuimarisha ushirikiano na GCLA.

“Kupokea zawadi hii ni heshima kubwa kwetu. Imetupa motisha ya kuongeza juhudi zaidi kuhakikisha tunazingatia kikamilifu matumizi salama ya kemikali katika shughuli zetu za kila siku,” alisema Mchunguzi.




Farida Mangube, Morogoro
JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia James Lugembe (55), mkazi wa Kitongoji cha Manzese B, Kata ya Mkwatani, Wilaya ya Kilosa, kwa tuhuma za kumuua mke wake, Restuta Walela (50), kwa kumkata kwa kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Alex Mkama, amesema tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamkia Julai 13, 2025.

Kamanda Mkama amesema baada ya kutekeleza tukio hilo, mtuhumiwa alijaribu kujiua kwa kunywa sumu, na kwa sasa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.

Amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni mvutano wa kifamilia, ambapo marehemu alilalamikia mumewe kwa kushindwa kutimiza majukumu ya kifamilia, huku mume akimtuhumu mkewe kwa ulevi na kuchelewa kurudi nyumbani mara kwa mara.

"Uchunguzi wa tukio hili unaendelea kwa kushirikiana na wadau wa haki jinai, na mara utakapokamilika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa," amesema Kamanda Mkama.

Aidha, Kamanda huyo ametoa onyo kali kwa wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu, akisisitiza kuwa hakuna mtu atakayekwepa mkono wa sheria.

Jeshi la Polisi limeendelea kuhimiza jamii kutatua migogoro ya kifamilia kwa njia ya mazungumzo na kuomba msaada wa kitaalamu ili kuepusha matukio ya kikatili kama hilo.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akiongoza kikao cha kawaida cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, leo Julai 14, 2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM (White House) mkoani Dodoma.

Kikao hicho, kinachotarajiwa kuendelea hadi Julai 16, kimeitishwa kufuatia kukamilika kwa zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kuwania uteuzi wa nafasi za uwakilishi katika vyombo vya dola. Nafasi hizo zinahusisha ubunge wa majimbo, ujumbe wa Baraza la Wawakilishi, viti maalum vya ubunge na Baraza la Wawakilishi, pamoja na udiwani wa kata na viti maalum.



Mshindi akioneshwa kiwanngo cha fedha alizoshinda katika fainali ya mchezo wa kurusha ndege Aviantor Legend
Wachezaji Nane walioshiriki mchezo wa kurusha ndege (Vindege) na Betway wakiwa katika picha ya pamoja.
Mshindi wa Milioni 57,500,000 Abdulrazak Ngoroge akizungumza kuhusiana na ushindi wake mara baada ya kuwashinda watu saba katika fainali ya mwezi mmoja.
Meneja wa Masoko wa Betway Calvin Mhina akizungumza kuhusiana na kupatikana mshindi wa milioni 57,500,000.
Baadhi ya majaj wakiwa katila kutazama wachezaji wa mchezo wa vindege na Betway

*Mshindi Aahidi Kuifanya Mambo ya Msingi

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Bet way imemkabidhi mshindi wa mchezo wa kurusha ndege Abdulrazak Ngoroge Sh.Milioni 57,500,000 baada ya kuwashinda wenzake saba.

Akizungumza mara ya mshindi kupatikana Meneja Masoko wa Betway Calvin Mhina amesema kuwa mchezo huo umeanza Juni na Kuhitimimisha Julai 12 ambapo wachezaji Nane walipatikana na kucheza kwa ajili ya kupata mshindi.

Amesema Kampuni nyingi zinazo huo mchezo lakini Betway ndio imeweza kutoa kiasi kubwa cha fedha ambayo mshindi anaweza kufanya maamuzi yake katika kuwekeza.

Mhina amesema kuwa wachezaji wote wameonesha umahiri wao lakini alihitajika mshindi mmoja wa kushinda sh.milioni 5,750,0000.

Aidha amesema kuwa wadau wa mchezo wa kubahatisha waendelee kucheza kistaarabu na kupata ushindi na Betway.

Mshindi wa Pili alipata sh.5750000 na Mshindi wa Tatu sh.Milioni 2.8 ambapo kampuni iliona kuna haja ya kuwazawadia kifuta jasho washindi wawili.

Mshindi Ngoroge amesema kuwa fedha hiyo aliopata anahitaji kutulia katika kupanga kitu chenye manufaa kwa sasa na baadae.

Amesema kuwa fedha bila ya kutuliza akili inaweza kuisha ndani ya siku mbili na kuanza kusema fedha mwanaharamu.

Hata hivyo amesema kuwa mchezo wa kubahatisha lazima kichwa kitulie ili kuendelea kushinda.

-Wasira akabidhi kwa niaba ya Rais Samia


RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ametoa sh. milioni 50 kuchaia ujenzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Nyalikungu wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu.

Akiwasilisha mchango kwa niaba ya Rais Samia, wilayani Maswa, jana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira alisema Dk. Samia anatambua mchango wa viongozi wa dini katika kuimarisha umoja na amani ya nchi.

"Sasa nawapa salamu za Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Rais Dk. Samia na kwa sababu nilimwambia nimealikwa mahali hapa kuwa mgeni rasmi kwa ajili ya mchango wa Kanisa na yeye ni mchamungu akaniambia na yeye atachangia sh. milioni 50," amesema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha, aliwaomba viongozi wa kanisa kuendelea kuiombea nchi hususan katika mwaka huu wa uchaguzi mkuu ufanyika kwa uhuru na amani.

"Naamini kabisa kwamba mnafahamu mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi, tunaliomba kanisa, tunawaomba viongozi wetu wa kanisa, tunawaomba waumini wote tuliombee taifa letu tunapopita katika uchaguzi huu kukawe na uchaguzi wa amani uchaguzi ulio huru lakini zaidi uchaguzi utakaotupatia viongozi watakaoendelea kuliongoza taifa hili," aliomba.

Akitoa salamu za shukrani Paroko wa Parokia hiyo, Padri Deogratius Ntindiko, alimshukuru Rais Samia kwa kuguswa na ujenzi huo na kuchangia kiasi hicho cha fedha.

"Kupitia nafasi yako (Wasira) tunamshukuru sana Rais Dk. Samia amegusa nyoyo zetu amegusa matarajio yetu kwa mchango wake wa sh. milioni 50, sisi wana Nyalukungu tunamuombea," alisema.











Hospitali ya Taifa Muhimbili [Upanga & Mloganzila] imeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la watoa huduma za afya katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam [Saba Saba] yaliyohitimishwa leo Julai 13, 2025.

Akizungumza katika sherehe za kufunga Maonesho hayo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amezipongeza taasisi zote zilizoshiriki maonesho hayo na kuzitaka kuongeza juhudi ili kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.

Aidha akikabidhi Tuzo hiyo Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Suleiman Jaffo ameipongeza Hospitali hiyo kwa huduma bora na za kibingwa zinazotolewa kwa wananchi.

Tuzo hiyo imetokana na ubora na utendaji kazi wa wataalam wake waliokuwa wakitoa huduma za kibingwa ambapo wananchi walipata fursa ya kupata elimu, ushauri, uchunguzi na matibabu ndani ya viwanja vya sabasaba.

Kwa upande wa wananchi waliotembelea banda la hospitali hiyo wameishukuru na kuipongeza Muhimbili kwa kuleta hospitali ndani ya maonesho na kusogeza huduma karibu yso kupitia maonesho ya sabasaba.

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imetambulisha msimu wa pili wa kampeni yake ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ mkoa wa Ruvuma ikilenga kuchochea kasi ya uzalishaji wa zao la kahawa mkoani humo hususani wilaya za Mbinga na Nyasa kupitia huduma mahususi na zenye upendeleo kwa wakulima wa zao hilo.

Ikitambulishwa kwa mara ya pili mkoani humo, kampeni hiyo inakwenda sambamba na mafunzo ya huduma mbalimbali zinazotolewa na benki ya NBC kwa wadau wa kilimo ikiwemo huduma ya bima ya mazao na bima ya afya, uwakala, huduma za kidigitali, mikopo ya zana za kilimo na pembejeo, ujenzi wa maghala pamoja na kuwasaidia wakulima shughuli mbalimbali zinazohusiana na maandalizi ya msimu wa uzalishaji na masoko ya mazao yao.

Hafla ya utambulisho wa kampeni hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga, ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw Kisare Makori huku ikihudhuriwa na viongozi wengine waandamizi wa wilaya hiyo pamoja na wadau mbalimbali wa zao la kahawa wakiwemo viongozi vya ushirika na wakulima. 

Wakati wa hafla hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mikakati wa Benki NBC, Bw Msafiri Shayo aliwaongoza maofisa wengine wa benki hiyo akiwemo Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun na Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa .

Akizungumzia kampeni hiyo, DC Makori pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa kutoa kipaumbele kwa wakulima nchini kupitia huduma zake, alisema ujio wa kampeni hiyo wilayani mwake ni ukombozi muhimu kwa wakulima wa kahawa wanaohitaji upendeleo maalum wa huduma za kifedha na kwamba serikali imejipanga kuhakikisha dhamira ya benki hiyo inafanikiwa.

“Zaidi nimefurahi kusikia kupitia kampeni hii wakulima wanaweza kupata mikopo ya vitendea kazi muhimu kama vile matrekta na zana nyingine za kisasa za kilimo, pembejeo za kilimo na mikopo ya malipo ya awali kwa wakulima.’’

“Pia huduma za bima za afya na kilimo zinazotolewa na NBC ni muhimu sana kwa wakulima, hasa katika kukabiliana na changamoto za kiafya kwao binafsi na familia zao na kujilinda dhidi ya hasara zitokanazo na majanga ya asili ambayo yamekuwa yakiathiri mazao yao,’’ alisema.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Bw Msafiri alisema kampeni hiyo ni sehemu ya muitikio wa benki ya NBC kufuatia wito wa Serikali wa kuchangia katika kufanikisha agenda 10/30 ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kutoka asilimia 5 hadi 10 ifikapo mwaka 2030.

“Sambamba na uzinduzi wa kampeni hii kwa wakulima wa zao la kahawa wilayani mbinga, pia tunatoa huduma mbali mbali kwao ikiwemo, ufunguaji wa akaunti za wakulima, ambazo hazina makato ya mwezi, huduma za mikopo kwa mkulima mmoja mmoja kwa ajili ya zana za kilimo kama matrekta na mikopo kwa vyama vya ushrika (AMCOS/Union) kwa ajili ya pembejeo zao.’’ Alitaja.

Kupitia kampeni hiyo benki ya NBC inatoa huduma za bima ya afya kwa wakulima na huduma za bima ya kilimo inayotoa fursa kwao kulipwa fidia pindi mazao yao yatakapoathiriwa na majanga mbalimbali yakiwemo yale ya asili.

Akifafanua zaidi kuhusu kampeni hiyo Bw Urassa alisema inawalenga wakulima wote wakiwemo mmoja mmoja, vyama vikuu vya ushirika na vyama vya msingi (AMCOS) ambavyo vitapitisha fedha za mauzo kwenye akaunti za NBC Shambani.

“Kupitia kampeni hii ambayo kwa mwaka huu tunaizindua kwa mara ya pili hapa mkoani Ruvuma mahususi kwa wilaya za Mbinga na Nyasa, wakulima wataweza kujishindia vitendea kazi mbali mbali kama vile ‘spray pumps’ ( pampu ya kupulizia dawa) na piki piki. Upande wa AMCOS na UNION watapata fursa ya kujishindia maguta kwa ajili ya usafirishaji wa mazao yao.’’ Alitangaza.

Wakizungumza kwa niaba wakulima hao, Mwenyekiti wa AMCOS ya Kibandai Bi Vestina Nombo pamoja nae Katibu wa Kipowolo AMCOS Bw Matius Kapinga pamoja na kuishukuru na kuipongeza benki hiyo kwa kampeni hiyo muhimu, walionyesha kuvutiwa na huduma za bima za afya na bima za kilimo kutokana na hitaji kubwa walilonalo wakulima hao kwenye masuala huduma bora za kiafya kwa ajili yao na familia zao huku pia wakiitaja huduma ya bima ya kilimo kama suluhisho sahihi dhidi ya athari zitokanazo na majanga mbalimbali yanayoathiri mazao yao.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Bw Kisare Makori (Katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga. Wengine ni pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mikakati wa Benki NBC, Msafiri Shayo (wa nne kulia), Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (wa tatu kushoto) maofisa wengine wa benki hiyo pamoja na wadau wa kilimo mkoani Ruvuma wakiwemo wakulima.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Bw Kisare Makori (alieshika mic) akizunguza na wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma na maofisa wa benki ya NBC wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Bw Kisare Makori (alievaa tai) akiwa kwenye picha ya pamoja na wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma na maofisa wa benki ya NBC wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.

Mkuu wa Kitengo cha Mikakati wa Benki NBC, Bw Msafiri Shayo (alieshika mic) akizungumza na wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.

Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (alieshika mic) akizungumza na wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.

Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (alieshika mic) akizungumza na wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.


Maofisa mbalimbali wa benki ya NBC wakielezea kuhusu huduma mbalimbali za benki hiyo mahususi kwa wakulima mbele ya wageni waalikwa wakiwemo wadau wa sekta ya kilimo mkoani Ruvuma wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako na NBC Shambani’ inayoratibiwa na benki ya NBC mahususi kwa wakulima wa zao la kahawa wilaya za Mbinga na Nyasa mkoa wa Ruvuma. Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki wilayani Mbinga.


Wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi huo wakulima walipata wasaa wa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki ya NBC kwa ajili yao.



Muonekano wa baadhi ya zawadi zitakazotolewa kwa washindi mbalimbali wa kampeni hiyo.


Top News