Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na wadau wa maafa nchini katika Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS) tarehe 19 Juni, 2026 Jijini Dodoma.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Nandi-Ndaitwah alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali. Katika mapokezi hayo pia alikuwepo Balozi wa Jamhuri ya Namibia nchini Tanzania, Mhe. Gabriel Sinimbo.
Ziara hiyo inafanyika katika kipindi ambacho Tanzania na Namibia zinaendelea kuimarisha uhusiano wao wa kihistoria uliojengwa katika misingi ya mshikamano wa harakati za ukombozi wa Afrika, urafiki wa muda mrefu na ushirikiano wa karibu katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Akiwa nchini, Mhe. Rais Nandi-Ndaitwah anatarajiwa kufanya mazungumzo ya uwili na mwenyeji wake, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano katika sekta mbalimbali zenye manufaa kwa wananchi wa Tanzania na Namibia. Viongozi hao pia wanatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Ziara hii ya kwanza ya Kitaifa ya Rais Nandi-Ndaitwah nchini Tanzania tangu alipoingia madarakani inaashiria dhamira ya pamoja ya Tanzania na Namibia ya kuendeleza ushirikiano wa kimkakati, kuimarisha diplomasia ya uchumi, pamoja na kukuza biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili.
Ziara hii pia inatarajiwa kutoa fursa ya kuenzi historia ya ushirikiano wa ukombozi kati ya Tanzania na Namibia, huku ikifungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika nyanja mbalimbali za maendeleo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho cha wananchi wa mataifa hayo mawili.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa MSI Tanzania, Dkt. Stephen Mutegeki, amesema utekelezaji wa Programu ya Scaling Up Family Planning (SuFP) umeonyesha kuwa maendeleo makubwa yanawezekana pale wadau mbalimbali wanaposhirikiana katika kufikia malengo ya pamoja.
Akizungumza katika kongamano la kujifunza na kutathmini mafanikio ya programu hiyo lililofanyika jijini Dodoma, Dkt. Mutegeki alisema MSI Tanzania itaendelea kushirikiana na serikali na wadau wengine kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelezwa na kwamba huduma bora na zenye usawa za afya ya uzazi zinaendelea kuwafikia wananchi wote.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo wa Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania, Will Guest, alisema Serikali ya Uingereza itaendelea kuunga mkono juhudi za kuboresha afya ya uzazi na haki za wanawake na wasichana.
Alisema kupitia SuFP, zaidi ya wanawake na wasichana milioni 5.2 walifikia huduma za uzazi wa mpango, hatua iliyosaidia kuzuia zaidi ya vifo vya wajawazito 6,500 na mimba zisizotarajiwa milioni 8.3.
Akizungumza kwa niaba ya washirika wa utekelezaji, Mwakilishi Mkazi wa UNFPA nchini, Mark Bryan Schreiner, alisema mafanikio ya programu hiyo yamethibitisha kuwa maendeleo makubwa yanawezekana pale serikali, watoa huduma, washirika wa maendeleo na jamii wanaposhirikiana.
Kwa mujibu wa washirika hao, mafanikio yaliyopatikana kupitia SuFP yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na wadau mbalimbali, wakiwemo MSI Tanzania, UNFPA, Serikali ya Uingereza kupitia FCDO, EngenderHealth na Pathfinder International.
Programu ya SuFP iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2017 hadi 2026 kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia FCDO, ilitekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na taasisi za EngenderHealth, UNFPA, MSI Tanzania na Pathfinder International.
SERIKALI imeahidi kuendelea kuimarisha na kutekeleza huduma za uzazi wa mpango pamoja na afya ya uzazi, mama, mtoto na vijana ili kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana kupitia Mradi wa Scaling Up Family Planning (SuFP) yanaendelea kudumu hata baada ya mradi huo kufikia tamati.
Kauli hiyo imetolewa mkoani Dodoma na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe, kwa niaba ya Waziri wa Afya, wakati wa kongamano la kujifunza na kutathmini mafanikio ya Mradi wa SuFP lililofanyika jijini Dodoma baada ya utekelezaji wa miaka tisa.
Dkt. Magembe amesema serikali imejipanga kuhakikisha huduma hizo zinaendelea kutolewa kwa ubora katika ngazi zote za utoaji huduma kwa kuwa wananchi wanaendelea kuzihitaji bila kujali kama mradi umefungwa au la.
“Tunapozungumzia kufungwa kwa mradi, haimaanishi kufungwa kwa huduma. Watu wanaohitaji huduma bado wapo, hivyo jukumu letu kama serikali na wadau ni kuhakikisha huduma zinaendelea kutolewa kwa ufanisi na ubora uleule,” amesema.
Ameeleza kuwa serikali tayari imeonyesha dhamira yake kwa kuongeza mchango katika ununuzi wa bidhaa za uzazi wa mpango sambamba na kuzijumuisha katika mipango na bajeti za afya ili kuhakikisha upatikanaji wake unaendelea bila kukwama.
Katika hatua nyingine, Dkt. Magembe amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa (RMOs), Waganga Wakuu wa Wilaya (DMOs) na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha huduma za afya ya uzazi na uzazi wa mpango zinaendelea kupewa kipaumbele katika mipango na bajeti za maendeleo.
Ameonya kuwa kutoweka kipaumbele kwa huduma hizo kunaweza kusababisha kuongezeka kwa mimba za utotoni, vifo vya uzazi, kuacha shule kwa wanafunzi na changamoto nyingine za afya ya uzazi.
“Wananchi hawajui kama mradi umeisha au kuna changamoto za fedha. Wanachojua ni kwenda katika kituo cha afya na kupata huduma bora. Hilo ndilo jukumu letu sote kuhakikisha linatimia,” amesema.
Pia amepongeza juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ni Bingwa wa Umoja wa Afrika katika Afya ya Mama, Mtoto na Mchanga, akisema mafanikio yaliyopatikana nchini yanapaswa kutumika kama mfano kwa mataifa mengine barani Afrika.
WAZIRI Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wafugaji nchini kuanzisha mashamba ya malisho na kutumia teknolojia za kisasa za ufugaji ili kuongeza tija na kupata suluhisho la kudumu la migogoro kati ya wakulima na wafugaji inayochangiwa na ongezeko la matumizi ya ardhi.
Akifungua Maonesho ya Tri-Nations Livestock Expo yaliyofanyika Ubena Zomozi, Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani, Ijumaa Juni 19, 2026, Dkt. Mwigulu amesema ongezeko la idadi ya watu na matumizi ya ardhi linaifanya nchi kutafuta mbinu endelevu za kuhakikisha shughuli za ufugaji zinaendelea kwa tija bila kuibua migogoro.
"Hata tusingependa kufanya hivyo, hatuna njia nyingine kwa sababu ongezeko la matumizi ya ardhi linalosababishwa na ongezeko la idadi ya watu, huku ardhi ikiwa haiongezeki, linatulazimu kutafuta suluhisho endelevu," amesema Dkt. Mwigulu.
Amesema changamoto ya upatikanaji wa malisho inapaswa kwenda sambamba na matumizi ya mbegu bora za mifugo na malisho ili kuwawezesha wafugaji kupata maziwa mengi na nyama nyingi hata kwa kuwa na mifugo michache.
Aidha, Dkt. Mwigulu amewataka wafugaji wa Kitanzania kuyatumia maonesho hayo kama shamba darasa la kujifunza ufugaji bora, wa kisasa na wenye tija ili kuongeza uzalishaji na mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa Taifa.
Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa wadau wa sekta ya mifugo nchini kuchangamkia fursa za matumizi ya teknolojia za kisasa za ufugaji ili kuongeza uzalishaji na kukuza uchumi.
"Maonesho hayo yanapaswa kutumika kama darasa la teknolojia na jukwaa muhimu la kununua na kuuza mifugo bora kupitia minada inayoambatana na matukio hayo," amesema.
Pia, amewataka wazalishaji kuacha utamaduni wa kuandaa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu kwa ajili ya maonesho pekee na badala yake waufanye ubora huo kuwa utaratibu wa maisha yao ya kila siku ya kibiashara.
"Ninachokisema ni nini? Tulichokiona katika maonesho haya ndio uwe utaratibu wa maisha. Tusiwe na bidhaa tu kwa ajili ya maonesho; bidhaa za aina hii ndio ziwe bidhaa za kila siku katika maisha yetu," amesisitiza Dkt. Mwigulu.
Kwa upande mwingine, Dkt. Mwigulu amepongeza mchango wa sekta binafsi katika kuleta maendeleo na mageuzi ya kiuchumi katika sekta ya mifugo, akitaja Mbogo Ranch kuwa mfano wa kuigwa.
Vilevile, amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameondoa zaidi ya kodi 300 zilizokuwa zikigusa sekta mbalimbali za uzalishaji kwa lengo la kuendeleza sekta hizo, ikiwemo sekta ya mifugo na sekta nyingine zinazohusiana na uzalishaji.
Kwa Upande wake Waziri wa Mifugo Dkt. Bashiri Kakurwa amempongeza Rais Dkt.Samia Suluhu Haasan kwa jitihada zake za kuhakikisha anaikuza na kuiendeleza sekta ya mifugo nchini
Aidha, Amsemea kuwa lengo kuu la maonesho hayo ni kujenga mfungo imara wa biashara wa mifugo na mazao yake kwa kuwakutanisha wafugaji na wafanyabiashara na wadau wote katika mnyororo wa thamani wa sekta ya mifugo ili kubadlishana uzoefu na kujifunza mbinu za kisasa za ufugaji pamoja na kupanua fursa za masoko nchini
Naye Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye, amesema sekta ya mifugo ni muhimu sana katika uchumi wa nchi na inahitaji kusimamiwa vizuri ili iweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika maendeleo ya Taifa.















.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
