Airtel Tanzania, kampuni inayoongoza huduma za mawasiliano nchini, imezindua maduka mapya 17 ya Airtel Smart Shops jijini Dar es Salaam. Maduka haya ni sehemu ya mtandao wa maduka 31 nchini kote, ukiwa na lengo la kupanua huduma za kidijitali na kuongeza ujumuishaji wa kifedha kwa wananchi.
Uzinduzi huo uliofanyika Machi 12, 2026, ulihudhuriwa na Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, pamoja na viongozi wa serikali, wajasiriamali, na vyombo vya habari.
Waziri Kairuki alieleza kuwa uwekezaji huu ni ishara ya nia ya dhati kwa Airtel kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya mawasiliano na kuonyesha imani yake katika mazingira ya biashara Tanzania chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
“Maduka haya mapya yanaonyesha dhati ya Airtel katika kuleta huduma karibu na wananchi huku yakiboresha uzoefu wa wateja. Pia unaashiria imani thabiti katika mazingira ya biashara Tanzania,” alisema Waziri Kairuki.
Kwa upande wake, Charles Kamoto, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, alisema maduka haya hayako tu kama maduka ya rejareja. Yameundwa kama vituo vya kisasa vya huduma za kidijitali, vinavyotoa usajili wa SIM, intaneti ya kasi, huduma za kifedha kupitia Airtel Money, mauzo ya simu, na suluhisho za kibiashara kwa SMEs.
Maduka haya yamewekwa katika maeneo yenye shughuli nyingi jijini Dar es Salaam, ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wakazi na wajasiriamali. Uzinduzi huu ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa “Airtel Kila Kona”, unaolenga kufanikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano hata katika maeneo ya vijijini.
Kampuni pia imewekeza katika kupanua mtandao wake wa 4G, kuanzisha teknolojia ya 5G, na kuongeza uunganishaji wa kimataifa kupitia mfumo wa nyaya za chini ya bahari wa 2Africa Submarine Cable System.
Adriana Lyamba, Mkurugenzi wa Uzoefu wa Wateja Airtel Tanzania, alisema maduka haya yameundwa kutoa huduma haraka, bila karatasi, na kwa ufanisi. Maduka haya yanatarajiwa pia kuunda ajira na kusaidia SMEs na wajasiriamali wa ndani kwa kuwapatia zana za kifedha za kidijitali na huduma za mawasiliano za kisasa.
Na Maandishi Wetu
MKURUGENZI Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amesema Wananchi hususan wanaoishi vijijini wana matumaini na Serikali kupitia REA katika kuwaboreshea hali ya maisha na amewataka Watumishi wa Wakala kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kutimiza malengo ya Serikali kuhudumia wananchi wake.
Ametoa rai hiyo Machi 12, 2026 mkoani Morogoro wakati wa kufungua Kikao cha Tatu cha Baraza la Pili la Wafanyakazi wa REA lenye ajenda kuu ya kupitia na kujadili mapato na matumizi kwa Mwaka 2026/2027.
"Watumishi wenzangu mnafanya kazi nzuri, tuendelee kuhakikisha tunawatumikia wananchi, matumaini yao kwetu ni makubwa na leo hii tupo hapa kujadili Mapato na Matumizi katika kutekeleza na kukamilisha miradi na kwa bajeti ya REA imezingatia vipaumbele vya Serikali ikiwemo kuharakisha kupeleka umeme vitongojini, kuongeza idadi ya wateja na kutanua wigo upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia,” amesema Mhandisi Saidy.
Amesema makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti kwa Mwaka 2026/2027 yanayojadiliwa katika Baraza hilo yamelenga kuboresha mazingira ya kazi na uwezo wa Taasisi katika kutekeleza majukumu yake sambamba na maslahi ya Watumishi.
Akizungumzia mafanikio yaliyofikiwa ndani ya kipindi cha miezi 12 (kutoka kikao cha Baraza kilichopita cha Mwezi Machi, 2025 hadi kikao cha sasa Machi, 2026), Mha. Saidy amesema REA imefanikiwa kusambaza umeme kwenye vitongoji 3,532 ambayo ni sawa na wastani wa vitongoji 10 kwa siku.
"Ndani ya kipindi cha miezi 12 tumefanikiwa kusambaza mitungi 400,000, majiko banifu 300,000, kujenga mifumo ya kisasa ya kupikia kwa Taasisi 452 zinazohudumia zaidi ya Watu 100, tumeanza kutekeleza Mradi wa kupeleka Umeme - Jua kwa kaya takriban 20,000 katika visiwa 143 na ndani ya kipindi hiki miradi takriban mitatu ya kusambaza ùmeme imekamilika,” amesema Mkurugenzi Mkuu wa REA.
Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Hery Mkunda ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na uzalendo.
“REA mnafanya kazi kubwa sana, mmefanikisha azma ya Serikali ya kubadilisha na kuboresha maisha ya wananchi wa maeneo ya vijijini, kwa hili kila mwananchi anaetoka kijijini ni shahidi,” amepongeza Mkunda.
Kikao cha Tatu cha Baraza la Pili la Wafanyakazi wa REA kilihudhuriwa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Wilson Nyamanga, Mwakilishi wa Msajili wa HAZINA, Gerald Nzalalila pamoja na Katibu Mkuu wa TUGHE mkoa wa Dodoma, Samwel Nyangwa ambao walipata fursa ya kuzungumza na Watumishi.


.jpeg)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amefanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini Tanzania Mhe. Yordenis Despaigne Vera, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma, leo tarehe 12 Machi 2026.
Mazungumzo hayo, yamelenga kuimarisha uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Cuba, ambao unatimiza miaka 64. Cuba na Tanzania zimekuwa zikishirikiana katika Sekta mbalimbali za kimkakati kama vile Elimu, Afya, Utalii pamoja na Kilimo.
Tanzania na Cuba kwa miaka mingi zimeendelea kuwa na mahusiano na maelewano ya kiuchumi, kisiasa na kidiplomasia katika ngazi ya nchi mbili, kikanda na kimataifa. Tanzania na Cuba zilianzisha uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1962 mara tu baada ya Tanzania kupata uhuru mwaka 1961.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewapongeza wenyeviti na wajumbe wa tume zilizoundwa kutathmini matumizi ya ardhi katika eneo la Ngorongoro Conservation Area kwa kazi kubwa na ya kizalendo waliyoifanya katika kukamilisha majukumu yao.
Rais Samia amesema hayo leo Machi 12, 2026 katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma wakati akipokea ripoti za tume hizo, akisema jukumu walilopewa lilikuwa zito kutokana na kuhusisha maoni ya wadau wengi wenye mitazamo tofauti.
Amesema licha ya changamoto hizo, wenyeviti na wajumbe wa tume walitekeleza kazi yao kwa bidii, uadilifu na weledi mkubwa, hali iliyowezesha kukusanywa kwa taarifa muhimu zitakazosaidia kufanya maamuzi sahihi kwa manufaa ya taifa.
Rais Samia amesema baada ya kusikiliza kwa kina taarifa za tume hizo pamoja na kutazama makala ya video iliyoonesha hali halisi ya maeneo yaliyotembelewa, imebainika umuhimu wa kulinda mfumo wa ikolojia unaounganisha maeneo ya Ngorongoro Conservation Area, Pololeti Game Reserve na Lake Natron.
Amesema mfumo huo wa ikolojia ni wa kipekee na una umuhimu mkubwa kwa uhifadhi endelevu wa mazingira pamoja na rasilimali za taifa.
Aidha, Rais Samia amesema taarifa hizo pia zimeonesha uwepo wa rasilimali mbalimbali ikiwemo madini yanayotafutwa duniani ambayo yanapatikana katika maeneo hayo, hivyo kusisitiza umuhimu wa kuyahifadhi kwa manufaa ya taifa na dunia kwa ujumla.
Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema taarifa za tume pia zimeonesha changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa zoezi la uhamaji wa hiari kwa wakazi wa eneo la Ngorongoro kwenda maeneo ya Msomera, Saunyi na maeneo mengine.
Amesema Serikali ilianza zoezi hilo kwa nia njema, lakini imebaini kuwa kulikuwa na mapungufu katika baadhi ya maeneo, hivyo ni muhimu kuyatafakari na kuyarekebisha kabla ya kuendelea na hatua zinazofuata.
Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea na zoezi hilo la uhamaji wa hiari, lakini kwa kufanya maboresho yatakayozingatia changamoto zilizobainishwa ili kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa bora na wenye manufaa kwa wananchi pamoja na taifa.













.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)






.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)






.jpeg)
