Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akipata maelezo kuhusu hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma kutoka kwa Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael (wa pili kulia). Ziara hiyo imefanyika Machi 09, 2026 Mtumba Dodoma.

************

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya Suma JKT kuongeza kasi ya ujenzi wa Jengo la Ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma.

Dkt. Muyungi amesema hayo Machi 09, 2026 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi hiyo ambapo aliongozana na Viongozi na Menejimenti kwa ajili ya kujionea na hatua iliyofikiwa katika mradi huo.

Amesema mkandarasi wa kampuni ya Suma JKT hana budi kufanya kazi masaa 24 ili kuwezesha maboresho na ukarabati wa baadhi ya maeneo ndani ya jengo ambayo hayajakamilika.

Ameongeza kuwa Ofisi yake haitongeza muda wa kukamilisha mradi huo kwa kuwa ilishafanya hivyo hapo awali na hivyo kumtaka mkandarasi hukakikisha anatumia vyema muda uliopo kuweza kukamilisha na kukabidhi jengo hilo.

“Kamati ya Bunge inatarajia kufanya ziara katika mradi wa jengo hili tarehe 18 Machi mwaka huu, hivyo nawasisitiza kuhakikisha mnakamilisha kazi hii kwa wakati kabla yatarehe hiyo kufika” amesema Dkt. Muyungi.

Aidha Dkt. Muyungi amesema Ofisi yake imetimiza mahitaji yote yaliyohitajika kwa ajili ya kukamilisha mradi wa ujenzi wa jengo hilo ikiwemo malipo ya fedha kwa mkandarasi na ununuzi wa samani mbalimbali.

Pia Dkt. Muyungi amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha anajenga miundombinu yenye mifumo ya kisasa ya uchakataji na usimamizi wa taka ngumu kuweza kutumiakatika jengo hilo pindi litakapokamilika hatua inayolenga kutunza mazingira.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael amesema kampuni itazingatia maelekezo yaliyotolewa na kuyafanyia kazi ili kuhakikisha mradi wa ujenzi wa jengo hilo unakamilika katika muda uliopangwa.

Katika ziara hiyo Dkt. Muyungi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu (Muungano), Bw. Abdallah Hassan Mitawi na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda pamoja na menejementi ya ofisi hiyo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara yake ya  kukagua ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma. Ziara hiyo imeifanya Machi 09, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara yake ya  kukagua ujenzi wa mradi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba Dodoma. Ziara hiyo imeifanya Machi 09, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Juma Mohamed Salum (kushoto) akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dkt. Richard Muyungi wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma Machi 09, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kushoto) akizungumza jambo kwa Mratibu wa Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi hiyo kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo Machi 9, 2026. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Mhe. Balozi Baraka Luvanda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akitazama samani mbalimbali zilizopo ndani ya mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa jengo hilo Machi 9, 2026. Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasimali Watu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Paul Masanja.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi akikagua mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi hiyo unaoendelea katika Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma Machi 9, 2026. Kushoto ni Mratibu wa Mradi kutoka Kampuni ya Suma JKT, Mhandisi Richard Raphael.

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime

Faida za kuwepo mwekezaji mwenye uwezo, teknolojia za kisasa na mahusiano mazuri na jamii umedhihirika kutokana na Kikosi cha Dharura na Uokoaji (ERT) kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara ambacho kimesaidia kuokoa watu 22 wakiwemo watoto - waliokuwa wamezingirwa na mafuriko na kukwama kwa siku mbili katika kijiji cha Matongo, wilayani Tarime.


Wananchi hao walizingirwa na maji ghafla kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kulazimika kupanda juu ya miti ili kunusuru maisha yao, kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele.


“Tulijitahidi kuokoa maisha yao wote waliokuwa wamezingirwa na maji na hakuna kifo wala majeruhi. Kwa hivyo, lazima tuwashukuru watu wa mgodi walifanya kazi kubwa kwa kushirikiana na timu ya uokoaji ya wilaya na mkoa,” Meja Gowele aliwambia waandishi wa habari.


Alifafanua kuwa kikosi cha uokoaji kutoka mgodi huo ambao unaendeshwa na kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals kilitangulia kwenye eneo la tukio mara baada ya kupata taarifa - kikiwa na boti, magari na vifaa vingine vya kisasa vya uokoaji.


Shughuli za uokoaji zilianza Jumamosi iliyopita saa moja asubuhi hadi saa 12 jioni katika eneo la Mashambani lenye makambi ya wakulima na wafugaji.


“Mimi mwenyewe nilikuwepo tangu mwanzo hadi mwisho na Kamati ya Usalama, pamoja na timu za uokoaji za wilaya na mkoa zikishirikiana na mgodi ambao walitusaidia kwa kutoa vifaa vya kisasa kwa ajili ya uokoaji. Kwa hivyo, tuna kila sababu ya kuwashukuru watu wa mgodi kwa kazi waliyofanya,” alisema Meja Gowele.


Baada ya kuokolewa, wananchi hao walipatiwa huduma ya kwanza na kusaidiwa kurejea kwenye makazi yao katika vijiji mbalimbali wilayani Tarime.


“Baada ya kuwatoa tuliwacheki kuona kama wanahitaji matibabu lakini wengi walikuwa wana njaa na niliagiza wakapata uji na maji,” alisema Mkuu wa Wilaya, Meja Gowele.


Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Matongo, Charles Ryoba, alimshukuru Mkuu wa Wilaya, Gowele na Mgodi wa Barrick North Mara kwa kuchukua hatua za haraka kuokoa watu hao baada ya kuwapa taarifa za tukio hilo.


“Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa Mgodi wa Barrick North Mara kwa namna walivyopokea jambo hii na kufika kwa muda muafaka, hii inadhirisha wazi kuwa mahusinao yetu na Barrick ni mazuri,” alisema Ryoba mara baada ya shughulli za uokoaji kukamilika.


Alizishukuru pia timu za uokoaji za wilaya ya Tarime na mkoa wa Mara kwa kujitokeza kushiriki kuokoa maisha ya wananchi hao bila kukata tamaa.

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime










Baraza la Taifa la Hifadhi la na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekifunga Kiwanda cha Mara Nile Ltd kilichopo Misugusugu Kibaha Mkoani Pwani kinachojihusisha na uzalishaji wa kemikali ya Extra Neutral Alcohol (Ethanol) na Carbon dioxide kwa kosa la kutiririsha majitaka yasiyotibiwa kwenye mazingira

Hatua hiyo imekuja mara baada ya NEMC kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu utiririshaji wa majitaka kwenye Mazingira hali iliyozua taharuki kwa afya za wananchi wanaozunguka eneo hilo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria (NEMC) Bi. Luhuvilo Mwamila amesema awali NEMC ilifanya ukaguzi na kubaini mtambo wa kutibu majitaka usiotumika badala yake, kiwanda kimekuwa kikitiririsha maji taka yasiyotibiwa moja kwa moja kwenye mazingira na kumwaga tope lenye kemikali hatarishi (sludge).

Uchunguzi zaidi umeonyesha kuwa kiwanda kimekuwa kikinyonya majitaka na kuyamwaga kwenye machimbo ya mchanga nje ya eneo lao, huku tope sumu wakilichoma katika maeneo hayo hayo.

Hali hii ni kinyume cha taratibu za mazingira na kuhatarisha afya ya jamii na usalama wa ikolojia. kutotii maelekezo ya mamlaka, hatua kali zimechukuliwa ili kulinda mazingira na afya ya wananchi.






Na Mwandishi Wetu


Tanzania iko katika hatua za awali za upembuzi wa kushiriki katika mradi wa Jumuiya ya Ulaya (EU P111) mradi wenye lengo la kuimarisha udhibiti wa mabaki hatarishi ya kemikali katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Hayo yamesemwa Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) ambaye pia ni mratibu wa kitaifa wa mpango wa kuzuia na kupambana na majanga ya kikemia, kibaolojia, kira diolojia na kinyuklia (CBRN) Prof. Najat Kassim Mohammed wakati wa kikao kati ya wawakilishi kutoka Jumuiya ya Ulaya na wajumbe wa kitaifa wa mpango wa kukabiliana na majanga ya kikemikali, kibaolojia, kiradiolojia na kinyuklia.

Prof. Najat ameongeza kuwa mradi huo umekuja wakati muafaka ili kuongeza uelewa wa wanachi na wadau mbalimbali wa kemikali, hasa katika kuwajengea uwezo katika kukabiliana na hatari zinazotokana na sumu za mabaki ya kemikali sambamba na kusaidia watendaji wa mipakanai  kudhibiti uingizwaji wa kemikali zenye sumu nchini sambamba na kujenga utamaduni wa kutumia kemikali kwa matumizi salama.

 Kwa upande wake kiongozi wa utekelezaji wa mradi namba 111 katika kuzuia na kupambana na majanga na madhara ya mabaki ya kemikali kupitia harakati za Jumuiya ya Ulaya (EU CBRN CoE) Bw. Pablo Taboada ametoa taarifa ya mradi huo kwa wajumbe wa kitaifa wa mpango wa kukabiliana na majanga ya kikemikali, kibaolojia, kiradiolojia na kinyuklia. 

Wajumbe wa Timu ya Taifa ya CBRN pamoja na wawakilishi wa mamlaka na za serikali na wadau wa kemikali wamekutana kujadili kwa kina fursa ambazo Tanzania inaweza kuzipata kupitia mradi huo. Katika kufafanua Bw. Pablo amesema mradi huo wa Umoja wa Ulaya una lengo la kusaidia nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati katika kupambana na hatari (sumu) zitokanazo na matumizi/mabaki ya kemikali ndani ya jamii.

Katika taarifa hiyo, Bw. Pablo ameongeza kuwa mradi huo namba (EU P111) umelenga nchi 11 ambazo ni Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ethiopia, Kenya, Ghana, Zambia, Uganda, Seychelles, Rwana na Malawi ambapo pamoja na taasisi zinazosimamia usalama kwa wananchi kujengewa uwezo mradi huo utaenda sambamba na kutoa mafunzo kwa shule za sekondari na vyuo vya kati na vyuo vikuu ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kutambua madhara ya sumu za kemikali ili waweze kujua na kujikinga, na kutoa elimu hiyo kwa jamii.

 Kwa upande wake Meneja wa usajili wa kemikali na maabara za kemia Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bwn. Musa Kuzumila amesema mradi huo utawasaidia katika utoaji wa elimu kwa makundi mbalimbali yanayohusika na usimamizi na udhibiti wa utumiaji wa kemikali hapa nchini.

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam, Machi 10, 2026. Tume ya Ushindani (FCC) imesema itaendelea kusimamia kwa karibu haki za walaji kwa taasisi na kampuni zinazotumia mikataba iliyoandaliwa kwa upande mmoja, ili kuhakikisha watumiaji wa huduma na bidhaa hawapati hasara kutokana na mikataba hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, alipokuwa akizungumza katika semina ya wadau kutoka taasisi na kampuni zinazotumia mikataba ya upande mmoja, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Ngasongwa alisema FCC inaendelea kufuatilia kwa karibu mikataba ya aina hiyo ili kuhakikisha haikiuki haki za walaji katika soko. Alifafanua kuwa mikataba ya upande mmoja hutumiwa sana na taasisi mbalimbali kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati, lakini ni muhimu iwe chini ya uangalizi ili kuepuka matumizi yanayoweza kuwa kinyume na sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.

Alisema semina hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa utoaji wa elimu kwa wadau kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani, yanayolenga kuongeza uelewa kuhusu haki na wajibu wa walaji pamoja na watoa huduma.

“Ninatambua kuwa mikataba inayoandaliwa kwa upande mmoja ina faida katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati. Hata hivyo, FCC ina jukumu la kuifuatilia kwa karibu, kwani bila uangalizi kunaweza kuwa na mambo yanayofanyika kinyume na maslahi ya walaji katika soko,” alisema Ngasongwa.

Aliongeza kuwa hata pale taasisi zinapotaka kuunganisha huduma au mikataba yao, ni muhimu kufanya tathmini ya kina ili kubaini kama kuna vipengele vinavyoweza kukiuka masharti ya ushindani au kuathiri ubora wa huduma kwa walaji.

Ngasongwa alisisitiza kuwa kila mtu ni mlaji kwa namna moja au nyingine, hivyo ni muhimu kuhakikisha thamani ya fedha inayotolewa na mteja inaendana na ubora wa huduma au bidhaa anayopata. Alisema hali hiyo pia husaidia kujenga uaminifu kati ya watoa huduma na walaji.

Aidha, alisema FCC itaendelea kukutana na makundi mbalimbali ya wadau kwa lengo la kuwapa uelewa mpana kuhusu majukumu ya taasisi hiyo na umuhimu wa kuzingatia sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Tusekelege Mwaikasu, alisema semina hiyo ni muhimu kwa taasisi za kifedha kwani itawasaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa walaji kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika.

Alisema benki, kupitia umoja wao, zimekuwa zikitekeleza kampeni ya “Niko Fiti”, inayolenga kuhakikisha huduma za kifedha zinatolewa kwa ubora na kwa kuzingatia mahitaji ya walaji.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindqni Ushindani Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa akizungumza wakati akifungua Semina kwa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa inayokatazwa na Sheria ya Ushindani FCC, Bi.Magdalena Utouh  akizunguza wakati wa kuhitimisha semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa na upande mmoja jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa FCC,Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusiana na Semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA ) Bi.Tusekelege Mwaikasu akitoa neno kwa niaba ya wadau katika mkutano na FCC ,jijini Dar es Salaam.































Mkutano ukiendelea







Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Mkuu wa FCC Khadija Ngasongwa akiwa katika matukio picha za za pamoja makundi mbalimbali.

Top News