-Wananchi kuvuna lita bilioni 21 za maji chini ya ardhi
Na Mwandishi wetu
UTAFITI uliofanywa na Bodi ya Maji ya Wami Ruvu (WRWB) umeonesha kuwepo wa maji lita bilioni 21 za maji chini ya ardhi zitakazotumika kama mbadala wakati wa kipindi cha ukosefu wa maji katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Hatua hiyo muhimu ya WRWB ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya kwanza katika kutafuta vyanzo vipya mbadala vya maji katika kukabiliana na ukosefu wa mji katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani.
Utekelezaji wa uchimbaji wa visima virefu vya maji
mbadala (back up) unatekelezwa na WRWB kwa awamu mbalimbali katika jiji la Dar es salaam na Mkoa wa Pwani kama mbadala wa maji hii ni kutokana na kuwepo kwa vipindi vya ukame jambo ambalo limekuwa likiathiri uvunaji maji katika bonde na kusababisha mgao wa maji katika maeneo ya Pwani na Dar es salaam
Aidha, uchimbaji wa awamu ya kwanza unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Juni 2026.
Kwa mujibu wa mtaalam wa haidrojia kutoka WRWB,Omary Kizulwa alisema bodi imeamua kuwatumia wataalamu wake ili kubaini vyanzo vipya vya maji ili kuondoa kero ya maji katika mikoa ya Pwani na Dar es Salam kwa kuchimba visima mbadala vya kuhifadhi maji katika maeneo mbalimbali.
“Kwa sasa hivi Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu tunafanya tafiti katika jiji la Dar es salaam na Pwani tafiti hizi zinatuwezesha kubaini maeneo ambayo yana vyanzo vya maji chini ya ardhi ili tuweze kuchimba visima” “Visima hivi vitakua kama back up (mbadala) kusaidia kipindi ambapo ukame unapotokea au ambapo hata ukame hamna viweze kutumika katika kutoa huduma ya maji” alisema“Zoezi la utafiti na uchimbaji linaendelea mpaka sasa tumeshafanya utafiti zaidi ya maeneo 40, Maeneo ya Ruvu Juu, Ruvu chini, Kigamboni , Chamazi, Ubungo, Kinondoni na Mburahati” alisema
“Tumeshafanya tafiti na tumeshaweka pointi na hivi sasa tunavyozungumza mitambo ipo site inaendelea na uchimbaji mpaka sasa zaidi ya visima 17 vimechimbwa na baadhi ya visima vimeonesha uwezo mkubwa kutoa maji na ni maji mazuri, mfano eneo la Mburahati tumechimba kisima kikubwa pale kina uwezo wa kutoa maji takribani lita elfu 50,000 mpaka 100,000 kwa saa na visima vingine kama Ilala na visima vya huku Chamazi vina karibia elfu 10,000 mpaka elfu 20,000 na kuendelea”
Aidha mtaalam huyo alisema kuwa Tanzania haina uhaba wa maji huku akibainisha kuwa maji chini ya ardhi ni lita bilioni 21 na maji juu ya ardhi ni lita bilioni 105
MRADI WA KIDUNDA
Aligusia pia mradi wa maji wa kimkakati wa Bwawa la Maji Kidunda unaotekelezwa kwa gharama ya sh.bilioni 336 kuwa utasaidia nao kuhifadhi maji ya juu ya ardhi kipindi ambapo kuna ukame
Kwa mujibu wa serikali Mradi wa Bwawa la Kidunda ni muhimu kwa kuwa utawezesha kukidhi mahitaji ya maji kwa wananchi wanaotarajiwa kuongezeka na kufikianidadi ya watu 11,387,753 ifikapo mwaka 2032, ambapo mahitaji ya maji yanakadiriwa kufikia zaidi ya lita bilioni
1.028 kwa siku. Mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi kutoka kampuni ya Sino Hydro Corporation ya nchini China.
Bwawa la Kidunda, litakalokuwa na ujazo wa lita bilioni 190, litawezesha mitambo ya Ruvu Juu na Ruvu Chini, yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya lita milioni 466 kwa siku, kufanya kazi katika majira yote ya mwaka na hivyo kuondoa upungufu wa maji wakati wa kiangazi.
Mitambo hiyo inahudumia zaidi ya asilimia 80 ya eneo lote la huduma la DAWASA.
Kwa upande wake wakati wa ziara ya kukagua mradi wa Kidunda msishoni mwa mwaka jana Waziri wa Maji Jumaa Aweso alisema nchi nyingi duniani kwa sasa zinakabiliwa na changamoto ya ukameinayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi, hali ambayo pia imeanza kuathiri Tanzania.
Kutokana na hali hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliielekeza Wizara ya Maji kuchukua hatua za haraka na za muda mrefu ili kukabiliana na changamoto hiyo.
“Wizara ya Maji tuliweka mkakati wa muda mfupi jijini Dar es Salaam kwa kuchimba visima vitanovilivyogharimu takribani Sh.bilioni 23.6, sanjari na mkakati wa muda mrefu wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda mkoani Morogoro pamoja na mpango wa kutumia maji ya Mto Rufiji mkoani Pwani ili kuongeza uzalishaji wa maji,” alisema
Alisema kwa sasa mahitaji ya maji kwa Jiji la Dar es Salaam ni takribani lita milioni 534 kwa siku, ilhali changamoto ya ukame ikiathiri kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma ya maji.


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

























.jpeg)



.jpeg)

.jpeg)









