Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya ALAF Tanzania imezindua rasmi Tuzo ya Kiswahili ya Safal ya Fasihi ya Afrika kwa mwaka wa 2025, ambapo wanaotarajiwa kushiriki shindano hilo wametakiwa kuwasilisha kazi zao kwa ajili ya kupitiwa na majaji.

Hiyo ni tuzo ya 10 tangu kuanzishwa kwake 2015 na inafadhiliwa na kampuni ya ALAF Limited ya Tanzania na Mabati Rolling Mills ya Kenya (kampuni tanzu za Safal Investments Mauritius Limited).

Akizungumza jijini Dar es Salaam Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa ALAF Limited Tanzania, Hawa Bayumi amesema tuzo hiyo inaendelea kukua mwaka hadi mwaka huku ikivutia washiriki wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani.

“Hadi leo hii, zaidi ya kazi 3000 zimeshawasilishwa katika shindano hilo na washindi 29 wameshapokea zawadi zao ndani ya miaka hii 10. Miswada 22 kati ya iliyoshinda imeshachapishwa na Mkuki na Nyota Publishers na iliyobakia ipo kwenye mchakato wa kuchapishwa,” ameeleza.

Kuhusu zawadi alisema katika kipengele cha Riwaya mshindi wa kwanza atazawadiwa Dola 5,000 na Mshindi wa pili Dola 2,500, katika kipengele cha ushairi mshindi wa kwanza ataondoka na Zawadi ya Dola 5,000 na Mshindi wa pili Dola 2,500 wakati katika kipengele kipya cha hadithi fupi kutakuwa na mshindi mmoja tu atakayepokea Dola 2500.

Miswada itaanza kuwasilishwa kuanzia leo hii tarehe 28 Januari hadi tarehe 31 Machi 2026 ambapo zoezi hilo litafungwa rasmi ili kuwapa majaji nafasi ya kupitia miswada husika. Hafla ya utoaji tuzo inatarajiwa kufanyika Julai 2026 ambapo washindi watatangazwa.

“Tunatoa rai kwa waandishi duniani kote watumie fursa hii kujitangaza, wachapishe kazi zao ili wachangie katika kukuza lugha adhimu ya Kiswahili,” amesisitiza Bi. Bayumi.

Amebainisha kampuni ya ALAF inajivunia na itaendelea kutoa mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kama chachu ya maendeleo ya kiuchumi, taaluma na utamaduni nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI), Dk.Ramadhani Kadallah ameipongeza ALAF Kwa jitihada zake ze Mukunza Lugha ya Kiswahili."Tutaendelea kushirikiana na waandaaji kwani tuna maslahi makubwa na jambo hili.”

Mmoja wa washindi wa mwaka jana, Bashiru Abdallah alitoa Rai Kwa watunzi kutumia fursa hii kujitangaza na kuhakikisha wanaiandaa kazi zao vizuri ili wawe katika nafasi nzuri ya kushinda. "Ukiachia kushinda, tukio hili ni sehemu nzuri yakukutana na watu mbalimbali na kubadilishana uzoefu," alisisitiza.

Tuzo hiyo, iliyoanzishwa mwaka wa 2014 na Dkt. Lizzy Attree (Mkurugenzi wa Tuzo ya Caine) na Dkt. Mukoma Wa Ngugi (Chuo Kikuu cha Cornell), lengo kuu likiwa ni kutambua kazi nzuri za uandishi kwa lugha za Kiafrika sambamba na kuhimiza kazi za tafsiri kutoka lugha moja hadi nyingine miongoni mwa lugha za Kiafrika.

Safal Investments Mauritius Limited na matawi yake (Mabati Rolling Mills Limited ya Kenya na ALAF Limited nchini Tanzania) kwa pamoja yanajulikana kama The Safal Group. Safal Group ndiyo mzalishaji mkubwa wa bidhaa za kuezekea Barani Afrika ambapo kampuni hiyo inafanya jumla ya shughuli za uwekezaji 36 katika mataifa 11 Barani Afrika.



Mbunge wa Jimbo la Kibamba, Mheshimiwa Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki, ametembelea Kivuko cha Mabrouk na Kivuko cha Matembezi vilivyopo Mtaa wa Kibamba, Kata ya Kibamba, kwa lengo la kujionea hali halisi ya miundombinu ya vivuko hivyo na kubaini changamoto zinazowakabili wananchi wanaovitumia katika shughuli zao za kila siku.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Kairuki amesema amechukua hatua ya kugharamia kiasi cha shilingi 2,745,000 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kivuko cha Mabrouk ili kiweze kupitika kwa usalama na waenda kwa miguu.

Hatua hiyo inalenga kupunguza adha kwa wananchi pamoja na kuzuia matukio ya vifo vilivyokuwa vikijitokeza mara kwa mara, hususan nyakati za mvua kubwa ambapo baadhi ya wananchi walikuwa wakisombwa na maji.

Kwa upande wa Kivuko cha Matembezi, ambacho kimekuwa kwenye mipango kwa zaidi ya miaka 15 bila kutekelezwa, Mheshimiwa Angellah Kairuki aliwahakikishia wananchi wa Mtaa wa Kibamba kuwa atalifuatilia kwa karibu na kuhakikisha linapatiwa ufumbuzi wa kudumu ili kuondoa changamoto hiyo ya muda mrefu.

Wananchi wa Kibamba wamepongeza jitihada za Mbunge wao, wakieleza kuwa hatua hizo zinaonesha dhamira ya dhati ya kiongozi wao katika kusikiliza, kushughulikia na kutatua changamoto za msingi zinazowagusa moja kwa moja katika maisha yao ya kila siku.






Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA, Wolta Kirita amewataka Mameneja wa Mikoa na Wilaya katika mikoa yote 25 inayohudumiwa na taasisi hiyo kuelekeza nguvu zaidi za kiutendaji katika kuvisimamia na kuvijengea uwezo Vyombo vya Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) ili viimarishe utoaji wa huduma hiyo kwa wananchi waishio vijijini na kuchangia uchumi wa nchi.

Mkurugenzi Mkuu Kirita ametoa maelekezo hayo Januari 26, 2026 wakati akizungumza na watumishi wa RUWASA mkoa wa Mara ambako ameanza ziara ya kukagua shughuli za CBWSO na hali ya utoaji huduma ya maji vijijini katika mikoa ya Mara na Mwanza.

Ziara hiyo ni muendelezo wa zoezi la kukagua kazi za vyombo katika kuwahudumia wananchi ambapo Menejimenti ya RUWASA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu huyo inapita mikoani kutambua na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizopo katika kuwahudumia maji safi ya bomba wananchi wa vijijini.

Akizungumza na watumishi hao wakiongozwa na Meneja wa RUWASA mkoa wa Mara Mha. Charles Pambe na Mameneja wa wilaya za mkoa huo, Mkurugenzi Mkuu Kirita aliwataka kuweka na mpango wa kudumu wa mara kwa mara kuzitembelea CBWSO na kuzisadia pale zinapohitaji msaada wa kiufundi na kitaalamu ili kuzijengea uwezo wa kujua na kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria na kuondoa changamoto ndogondogo katika kuwahudumia wananchi.

Alisema tangu kuanzishwa kwake mwaka 2019, RUWASA imeshajenga miradi zaidi ya 3,000 ya maji vijijini na kwamba sasa ni wakati muafaka wa kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu na unahudumia wananchi maji kwa ufanisi.

Awali, akitoa taarifa ya hali ya huduma ya maji vijijini katika mkoa wa Mara kwa Mkugugenzi Mkuu aliyeambatana na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti, Meneja wa mkoa huo Mha. Pambe alisema wastani wa utoaji wa huduma umefikia asilimia 75 na kwamba ipo miradi inayoendelea kujengwa na itainua zaidi hali ya huduma.

Katika siku ya kwanza ya zoezi la ukaguzi wa CBWSO, Mkurugenzi Mkuu Kirita aliongoza ukaguzi huo katika CBWSO ya Bulisumakwi wilayani Musoma na Kokwe wilayani Rorya.








Na Mwandishi Wetu Michuzi Tv

VIJANA nchini wameungana kuadhimisha Siku ya Kumbukizi ya kuzaliwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakisema kuwa ni kiongozi mlezi wa vijana na chachu ya maendeleo ya taifa kwa vitendo.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika leo Januari 27,2026 Mratibu wa Taasisi ya Together for Samia ambaye pia ni Muandaaji wa shaghuli hiyo, Gulatone Masiga amesema tukio hilo limeandaliwa na vijana kwa hiari yao kama ishara ya upendo, heshima na kuthamini mchango wa Rais Samia katika kuwekeza maendeleo ya vijana na taifa kwa ujumla.

“Tuliona tufanye shughuli itakayotuleta pamoja, ikiwa ni nafasi ya sisi vijana kuonyesha upendo wetu kwa Rais wetu mama na mlezi wa vijana, ambaye ametujali na kuwekeza kwa vitendo katika maendeleo yetu,” amesema Masiga

Amesema vijana wengi waliokuwepo ni wa kizazi kipya ambacho kimenufaika kwa kiasi kikubwa na uongozi wa Rais Samia katika kipindi cha takribani miaka mitano, hususan kupitia ujenzi wa vyuo vya ufundi na ujuzi katika zaidi ya wilaya 62 nchini, hatua iliyowezesha vijana kupata maarifa na ujuzi wa kujiajiri.

Masiga ameongeza kuwa mageuzi katika sekta ya elimu kupitia mtaala unaozingatia maarifa (knowledge-based curriculum) umehakikisha wahitimu wa elimu ya msingi na sekondari wanapata vyeti vya elimu ya kawaida sambamba na vyeti vya ufundi (VETA), hali inayowawezesha kuingia kwenye soko la ajira au kujiajiri.

Katika sekta ya nishati, amesema uwekezaji mkubwa wa serikali, ikiwemo mradi wa zaidi ya shilingi trilioni moja wa kupeleka umeme katika vitongoji 99 nchi nzima, umefungua fursa nyingi za kiuchumi kwa vijana, wakiwemo mafundi seremala, welders, wajasiriamali wa saluni, car wash na shughuli nyingine za uzalishaji.

“Tunaona wazi kwamba uwekezaji huu ni fursa ya moja kwa moja kwa vijana,” amesema.

Ameeleza pia kuwa miradi mikubwa ya miundombinu ikiwemo reli ya kisasa (SGR) inayounganisha mikoa mbalimbali nchini itakapokamilika, vijana watakuwa miongoni mwa wanufaika wakuu kupitia ajira na shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa sekta ya afya, vijana hao wamepongeza ujenzi wa vituo vya afya hadi ngazi ya kata pamoja na kuanza kwa mpango wa bima ya afya kwa wote, ambapo kaya zitalipia kiasi cha shilingi 150,000 kwa familia yenye watu sita, huku makundi maalum yakigharamiwa na serikali.

Mmoja wa vijana walioshiriki hafla hiyo, Dorcas Mshiu ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa muanzilishi wa Vijana Innovation, amesema Rais Samia amefungua fursa nyingi za kiuchumi kwa vijana, ikiwemo urahisishaji wa usajili wa biashara na kuvutia wawekezaji nchini.

“Mama yetu hajatuacha.

Amesema kuwa Rais Samia ametengeneza mazingira rafiki kwa vijana kujiajiri, ikiwemo mikopo ya asilimia mbili na nne kupitia halmashauri. Hii ni serikali inayowaamini vijana,” amesema Doras.

Vijana hao wamesema sababu ya kuadhimisha siku hiyo ni kutambua uongozi wa Rais Samia unaojengwa juu ya misingi ya maridhiano, amani na umoja wa kitaifa, wakiahidi kuendelea kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya taifa.





Mbunge wa Jimbo la Kibamba, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo (DC) pamoja na watendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wamekutana katika kikao kazi kilicholenga kutafuta suluhisho la changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika jimbo la Kibamba.

Akizungumza katika kikao hicho, Mbunge wa Kibamba, Mheshimiwa Angella Kairuki, amesema changamoto ya maji imekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Jimbo hilo, hali inayohitaji hatua za haraka na za kudumu ili kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo.

Amesema kuna umuhimu wa kuwa na chanzo zaidi ya kimoja katika Jimbo hili, hivyo kazi ya kutambua na kupata maeneo ya uchimbaji wa visima vya maji inabidi ifanyike ikiwa ni mkakati wa kuongeza vyanzo vya maji na kupunguza utegemezi wa miundombinu ya sasa.

“Kipaumbele chetu ni kutambua maeneo sahihi ya kuchimba visima vya maji ili kuongeza vyanzo vya maji na kupunguza adha kwa wananchi, kwa sababu tutakapokuwa na vyanzo vingine vya huduma ni vigumu sana wananchi kulalamika kwa muda mrefu juu ya ukosefu wa maji,” amesema Mheshimiwa Kairuki.

Mheshimiwa Mbunge amesema utekelezaji wa mpango wa uchimbaji wa visima vya maji, sambamba na maboresho ya mtandao wa usambazaji wa maji, utawezesha wananchi kupata huduma ya maji kwa uhakika, hasa katika maeneo yenye changamoto kubwa.

“Nawaomba watendaji wa DAWASA kuhakikisha maeneo ya uchimbaji wa visima yanapatikana kwa haraka ili utekelezaji wake uanze na kuondoa adha hii kwa wananchi,” amesema Mheshimiwa Kairuki ambaye pia ni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na DAWASA ili kuhakikisha changamoto ya huduma ya maji katika Jimbo la Kibamba inapatiwa ufumbuzi wa kudumu na inaunga mkono juhudi zote za kitaalamu zitakazolenga kuboresha upatikanaji wa maji kwa wananchi.

Kwa niaba ya watendaji wa DAWASA katika jimbo la Kibamba, Ndugu Tumaini Mhondwa amesema tayari wanafanya tathmini ya kitaalamu ya maeneo mbalimbali kwa lengo la kubaini vyanzo vipya vya maji, ikiwemo uchimbaji wa visima, pamoja na kuboresha miundombinu ya usambazaji wa maji ili kuimarisha huduma ya maji katika jimbo hilo.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa( Mb.) amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TABD) na kufanya mazungumzo na yanayolenga kuendeleza ushirikiano kati ya wizara na benki hiyo na kuitaka kuendeleza miradi ya sekta za mifugo na uvuvi.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo 27 Januari 2026 katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo iliyopo Kambarage Tower Jijini Dodoma, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TADB alifika kujitambulisha kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi na kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara hiyo na Benki ya TADB katika kuendeleza sekta za Mifugo na Uvuvi.

Katika Mazungumzo hayo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameipongeza Benki ya TADB kwa jinsi inavyoshirikiana na wizara na kuiagiza kupanua wigo wa kuwasaidia wafugaji wadogo kupata mikopo nafuu ili waweze kuendeleza miradi yao, pamoja na kuongeza ushiriki wa Taasisi za kifedha kupitia TADB katika kutoa mikopo kwenye Sekta ya Mifugo na Uvuvi.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bw. Frank Nyabundege amempongeza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kwa kuteuliwa kuwa Mbunge na Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kuahidi kuongeza kasi ya utoaji mikopo kwenye Sekta ya Mifugo na Uvuvi hasa kwenye miradi inayowalenga vijana na wanawake.

Aidha, Bw. Nyabundege aliwasilisha taarifa fupi kuhusu ushiriki wa TADB katika Maendeleo ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi nchini ambapo kupitia TADB kama Benki ya Kisera inashirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuleta maendeleo katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi ikiwemo Benki kutoa mikopo ya mradi wa boti, ufugaji samaki kwa njia ya vizimba na mikopo ya vijana kupitia Programu ya BBT mifugo.

Kupitia mikopo ya miradi ya boti na vizimba TADB ilipokea kiasi cha Shilingi Bilioni 34.9 kwa ajili ya kutekeleza mradi ambapo hadi sasa kiasi cha Shilingi Bilioni 29.83 kimetolewa kwa wanufaika 5,932 katika mikoa 16 hapa nchini.

Aidha, TADB kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanikiwa kutoa jumla ya boti 219 na vizimba 536 kwa wanufaika wa miradi. Aidha, kwa kupitia mradi wa vijana wa BBT Mifugo, kiasi cha Shilingi Milioni 847.3 kimetolewa kwa wanufaika 106 kwa miradi ya mikopo isiyo na riba.

Bw. Nyabundege aliongezea kuwa TADB imewasilisha ushiriki wake katika kutoa mikopo katika Sekta ndogo ya Maziwa nchini kupitia Mradi wake wa TI3P ambapo kiasi cha Shilingi 40bn kimetolewa kwa wafugaji na wasindikaji wa maziwa nchini.

 Aidha, kupitia mradi wa TI3P TADB imefanikiwa kurekebisha na kujenga vituo 23 vya kukusanya maziwa vyenye thamani ya Shilingi 1.1bn kwa kushirikiana wafugaji,Wizara, Halmashauri na wasindikaji wa maziwa.

 

Miti imekuwa muhimili muhimu katika ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara kwani kupitia miti, viwanda hupata malighafi, biashara hukua, na uchumi huimarika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb.), Januari 27, 2026, akiwa ameambatana na Naibu Waziri,Mhe. Dennis Londo pamoja na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Needpeace Wambuya kushiriki zoezi la kupanda miti katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma. 

Zoezi hilo ni sehemu ya kusherehekea kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Mwanamazingira namba moja hapa nchini, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye aliazimisha siku yake 27 Januari, 1960 kwa kupanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026.

Aidha, Waziri Kapinga wakati akiongea na Watumishi wa Wizara hiyo baada ya kupanda mti, Altria rai kwa watumishi wa wizara kuhakikisha kila mmoja anashiriki kikamilifu katika upandaji miti ili kusaidia uhifadhi wa mazingira na kuibadili Dodoma kuwa ya kijani.

Uhifadhi na utunzaji wa miti unachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ndogo ya uchakataji wa mazao ya misitu, hususan utengenezaji wa mbao na samani, ambayo ni moja ya nyanja muhimu katika kukuza maendeleo endelevu ya sekta ya viwanda na biashara nchini

Farida Mangube, Morogoro 

Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) leo Januari 27, 2026 imeshiriki Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti #27Yakijani kwa kupanda miti ya asili aina ya Mkongo (Afzelia quanzensis), kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira na kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Zoezi hilo liliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI, Dkt. Revocatus Mushumbusi, kwa kushirikiana na Watumishi wa Taasisi hiyo kutoka Makao Makuu na Vituo vya Utafiti, na kufanyika katika moja ya maeneo ya shamba la miti la Taasisi. 

Akizungumza na Waandishi wa habari, Dkt. Mushumbusi alisema upandaji wa miti ya Mkongo unalenga kurejesha miti ya asili yenye thamani kubwa na iliyo hatarini kutoweka, sambamba na kuimarisha uhifadhi wake.

Aliongeza kuwa ushiriki wa TAFORI katika kampeni hiyo ni sehemu ya kutimiza wajibu wa kitaasisi wa kufanya utafiti, kuratibu na kusambaza matokeo ya utafiti wa misitu na ufugaji nyuki, kwa lengo kuu la kuendeleza uhifadhi miti ya asili na mingineyo, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuonesha mfano wa namna sahihi ya upandaji wa miti katika maeneo husika.

Zoezi la 27Yakijani linaongozwa na kaulimbiu “Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti”, kaulimbiu inayoakisi dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendeleza ajenda ya Taifa ya uhifadhi wa mazingira, ikiwemo upandaji miti, ulinzi wa vyanzo vya maji, kuimarisha uoto wa asili na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Kadhalika, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda mti wa muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, kama Kiongozi na mdau wa mfano katika kulinda na kutunza mazingira.








📍Atimiza ndoto yake ya siku nyingi ya kuitembelea Tanzania
WAZIRI  wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amempokea shabiki mashuhuri wa klabu ya Manchester City ya Uingereza Braydon Bent ambaye ametimiza ndoto yake ya siku nyingi ya kuitembelea Tanzania na kujionea vivutio mbalimbali ikiwemo Serengeti na Mlima Kilimanjaro.

Ni kama safari iliyochukua karne hivi ya kutoka tu Etihad Stdium hadi Serengeti! Shabiki huyo mtopezi wa Manchester City anasifika kwa kurekodi video akiongea Kiswahili na alipata kuahidiwa kuja Tanzania tangu mwaka 2020.

Leo, hatimaye, Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbasi wametimiza ndoto ya shabiki huyo ambaye amepata pia kuwahoji mastaa kama Neymar, Aguero, Kocha Pep Guadiola na sasa akiwa mtangazaji wa mechi za Man City na pia akiwa na vipindi Sky News.

“Ilikuwa ndoto yangu kubwa kufika nchi hii nzuri. Kwa mapokezi haya naona kabisa tayari safari yangu imeanza vyema kabisa,” alisema Braydon akiwa ameambatana na Bw. Mark Bent, baba yake mzazi.
Karibu kwenye nchi bora kwa Utalii wa safari duniani.




Top News