Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Neema Mwigulu Nchemba, ametoa wito kwa viongozi na wadau wa Afrika kuweka kipaumbele katika ulinzi wa watoto dhidi ya ukatili wa kidijitali.

Akizungumza jijini Nairobi, Kenya Mei 12, 2026, katika Mkutano wa Wenza wa Mawaziri wakuu wa nchi za Afrika, uliofanyika Pembezoni mwa Mkutano wa “Africa-Forward Summit” ukilenga kujenga mazingira salama ya kidijitali kwa watoto wa Afrika katika ulimwengu unaoendeshwa na Akili Unde (AI). Bi.Nchemba alisisitiza kuwa mustakabali wa bara la Afrika hautategemea tu vigezo vya kiuchumi, bali uwezo wa watoto kujifunza na kuvumbua katika nafasi ya kidijitali bila hofu ya unyanyasaji.

Katika hotuba yake, alibainisha kuwa ingawa teknolojia ya Akili Bandia (AI) inatoa fursa kubwa katika sekta za elimu, afya, na ujasiriamali, imeleta pia hatari mpya na halisi. Alitaja changamoto kama vile uonevu mtandaoni, unyanyasaji wa kijinsia unaochochewa na AI, na ulaghai kama vitisho vinavyovuruga utu na maendeleo ya watoto barani Afrika.

Ameeleza hatua zilizopigwa na Tanzania, ikiwemo kufanya marekebisho ya Sheria ya Mtoto (Sura ya 13) na kuimarisha utekelezaji wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015. Aidha, alikumbusha Kampeni ya Kitaifa ya Ulinzi wa Watoto Mtandaoni iliyoanzishwa Februari 2024 na kuundwa kamati maalum ya wadau mbalimbali ili kuhakikisha mazingira salama kwa watoto.

Mkutano huo, uliandaliwa na Kuongozwa na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mama Rachel Ruto ambapo ulihitimishwa kwa wito wa dharura wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda na sheria madhubuti.















KAMPUNI ya utoaji wa huduma za bima ya afya kwa waajiri, Vitality Health International (Africa), imebadilisha rasmi jina na sasa itafahamika kama Discovery Health – Global Health Solutions, hatua inayolenga kuimarisha utoaji wa huduma za afya kwa waajiri na wafanyakazi wao nchini Tanzania na katika bara la Afrika kwa ujumla.

Mabadiliko hayo yameanza rasmi Januari 1, 2026, huku kampuni hiyo ikieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuendeleza huduma zake za afya kwa kuunganisha uzoefu wake wa muda mrefu na programu ya ustawi ya Vitality pamoja na teknolojia za kisasa za huduma za afya.

Akizungumza Johannesburg, Afrika Kusini, Mkurugenzi Mkuu wa Discovery Health – Global Health Solutions, Emma Knox, alisema licha ya kubadilika kwa jina la kampuni, dhamira yao ya kuhakikisha watu wanakuwa na afya bora na maisha yenye ustawi itaendelea kuwa ile ile.

“Ingawa jina letu linabadilika, ahadi yetu kwa wateja wetu na kusudi letu la msingi la kuwafanya watu wawe na afya njema na kulinda maisha yao vinaendelea kubaki vilevile,” alisema Knox.

Alieleza kuwa mabadiliko hayo yatawezesha kampuni hiyo kuimarisha ushirikiano wake na kampuni za bima za ndani barani Afrika pamoja na kuleta suluhisho mpya za afya zinazolenga mahitaji halisi ya waajiri na wafanyakazi wao.

Nchini Tanzania, kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na Strategis Insurance, ushirikiano ulioanza mwaka 2024, kwa lengo la kutoa huduma bora za afya zinazokidhi mazingira ya ndani ya huduma za afya na mahitaji ya waajiri wa Kitanzania.

Kwa mujibu wa Knox, ushirikiano huo umeiwezesha kampuni kupanua huduma zake nchini huku ikiendelea kutoa suluhisho za afya zenye kuzingatia mahitaji ya soko la ndani.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Strategis Insurance, Dk. Malav Manek, alisema wana matumaini makubwa ya kuendelea kuimarisha ushirikiano huo kupitia Discovery Health – Global Health Solutions.

“Tunaendelea kujizatiti kutoa bidhaa za kibunifu zinazolenga kukidhi mahitaji ya wateja huku tukihakikisha kiwango cha juu cha huduma kwa wateja wetu,” alisema Dk. Manek.

Kupitia mfumo wake mpya wa Global Health Solutions, kampuni hiyo itaendelea kutoa huduma za usimamizi wa afya na “managed care” kwa kutumia uzoefu wa zaidi ya miaka 34 wa Discovery Health katika sekta ya afya nchini Afrika Kusini.

Discovery Health pia imeeleza kuwa itaendelea kuweka mkazo katika usimamizi bora wa huduma za matibabu, udhibiti wa hatari pamoja na matumizi ya mifumo ya kisasa ya taarifa za afya ili kuhakikisha wateja wanapata huduma bora kwa gharama endelevu.


▪️︎ Asema Serikali inalenga kupunguza utegemezi wa kuagiza dawa kutoka nje

▪️︎ Aisisitiza Afrika kuongeza thamani ya malighafi na kuimarisha uhamishaji wa teknolojia


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania imeweka kipaumbele katika uwekezaji wa viwanda vya dawa nchini ili kupunguza utegemezi wa kuagiza dawa kutoka nje ya nchi.

Dkt. Mwigulu amesema hayo jijini Nairobi, Kenya alipokutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Christophe Lecourtier, kando ya Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward Summit).

“Tunaagiza kiasi kikubwa cha dawa kutoka nje ya nchi, lakini sasa tumeweka kipaumbele kuona jinsi tunavyoweza kuwekeza kwenye viwanda vya dawa ili tuzalishe hapa nchini,” amesema Dkt. Nchemba.

“Kupitia ofisi yako pamoja na wadau wengine, wanaweza kutumia fursa hii kubwa iliyopo kuja kuwekeza kwenye eneo hilo. Na kama unavyofahamu, kuwekeza Tanzania ni kuingia katika lango la ukanda wa Afrika Mashariki (EAC) pamoja na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).”

Aidha, Dkt. Mwigulu amepongeza dhamira ya AFD ya kuusaidia Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria Awamu ya Pili, akieleza kuwa mradi huo ni wa kimkakati katika kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kutoa kipaumbele katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo reli ya kisasa ya SGR, nishati, kilimo hususan umwagiliaji pamoja na sekta ya afya kupitia uwekezaji katika uzalishaji wa dawa nchini.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameishukuru AFD kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

“Tunathibitisha tena dhamira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea kufanya kazi kwa karibu na AFD kwa manufaa ya maendeleo ya wananchi wetu,” amesema.

Akizungumza katika mjadala kuhusu maendeleo ya sekta ya kilimo, Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa wadau wa maendeleo kuoanisha malengo ya Bara la Afrika ili kuchochea maendeleo endelevu.

“Tumekaa muda mrefu tukizungumzia kujenga uwezo badala ya kujenga miundombinu itakayowezesha bara letu na nchi zetu kuendesha ajenda zao ipasavyo,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika uhamishaji wa teknolojia na matumizi ya mifumo ya kisasa ya kilimo.

“Tunatarajia ushirikiano katika uhamishaji wa teknolojia ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa matumizi ya zana za kisasa za kilimo, utekelezaji wa huduma za ugani na mifumo ya kidijitali. Si muda sasa wa kusafirisha malighafi nje ya nchi, tunataka mwelekeo wetu uwe kwenye kuongeza thamani,” amesema.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa uliofanyika Mei 11 hadi 12, 2026 jijini Nairobi, Kenya. 








Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Wizara ya Uchukuzi imewasilisha ombi la kuidhinishiwa bajeti ya jumla ya Shilingi 2,872,738,082,000 kwa mwaka wa fedha 2026/27, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya kuimarisha na kuendeleza sekta ya uchukuzi nchini.

Kwa mujibu wa makadirio hayo, kati ya fedha hizo, Shilingi 126,041,236,000 zimetengwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida, huku Shilingi 2,746,696,846,000 zikielekezwa katika Miradi ya Maendeleo, ikilenga kuboresha miundombinu ya usafiri wa anga, reli, barabara na huduma nyingine za uchukuzi.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kuwa bajeti hiyo imelenga kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya sekta ya uchukuzi nchini, sambamba na kuongeza ufanisi wa huduma za usafiri.

Ameeleza kuwa pamoja na hotuba hiyo, wizara imeambatisha majedwali mbalimbali yenye takwimu na taarifa za kina ili kutoa uelewa mpana zaidi kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi kuhusu hali ya utekelezaji wa sekta hiyo.

Aidha, amesema majedwali hayo ni sehemu ya hotuba rasmi ya bajeti na yanapatikana pia kupitia tovuti ya Wizara ya Uchukuzi kwa ajili ya rejea ya umma kupitia www.uchukuzi.go.tz.

Wizara hiyo inaendelea kuweka mkazo katika kuboresha miundombinu ya uchukuzi ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa nchini.



Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Serikali imewataka vijana wa Kitanzania kujiepusha na ushawishi wa kujiingiza katika migogoro ya kivita ya kimataifa kwa lengo la kutafuta kipato, ikionya kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria na inaweza kuhatarisha maisha yao.

Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Maghembe wakati akijibu swali la Mbunge Jesca John Magufuli aliyehoji Serikali ina mkakati gani wa kujenga uelewa kwa vijana kuhusu athari za kushiriki katika migogoro ya kimataifa, ikiwemo vita kati ya Ukraine na Urusi.

Dkt. Maghembe amesema katika kipindi cha hivi karibuni kumekuwepo na mwenendo wa baadhi ya vijana, hususan kutoka Bara la Afrika, kuhamasishwa kujiunga na majeshi ya nchi zinazokabiliwa na migogoro ya kivita kwa ahadi ya ajira na kipato bora kutokana na changamoto za ukosefu wa ajira katika nchi zao.

Amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kutoa elimu ya uraia na kuongeza uelewa kwa vijana kuhusu madhara ya kujiingiza katika vita vya nje, ikisisitiza kuwa kushiriki katika migogoro hiyo bila utaratibu rasmi ni kinyume cha sheria za Tanzania pamoja na sheria za kimataifa.

“Vijana wanapaswa kuelewa kuwa migogoro ya kimataifa ina athari kubwa kiusalama, kijamii na kiuchumi, na kwa baadhi inaweza kusababisha vifo, majeraha makubwa au ulemavu wa kudumu,” amesema Dkt. Maghembe.

Ameeleza kuwa juhudi hizo zinaongozwa na miongozo mbalimbali ya kitaifa ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001 Toleo la 2024 pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambazo zinahimiza usalama, ustawi wa vijana na ushiriki wao katika shughuli halali za maendeleo.

Wakati huo huo, Serikali imeendelea kuratibu upatikanaji wa ajira salama kwa vijana nje ya nchi kupitia mikataba ya ushirikiano wa kikanda na kimataifa inayolenga kuhakikisha Watanzania wanapata fursa za kazi katika mazingira yanayolindwa kisheria.

Dkt. Maghembe amesema katika mwaka huu wa fedha, Serikali imefanikisha upatikanaji wa nafasi 1,500 za ajira kwa madereva nchini Qatar pamoja na nafasi nyingine 300 za wauguzi nchini Saudi Arabia.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kutekeleza programu mbalimbali za kuwawezesha vijana kiuchumi, ikiwemo kutenga shilingi bilioni 200 kwa ajili ya mikopo ya vijana sambamba na programu maalum za kisekta zinazolenga kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na ajira rasmi.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha vijana kutumia fursa halali za kiuchumi zilizopo ndani na nje ya nchi badala ya kujiingiza katika shughuli zinazoweza kuhatarisha usalama na mustakabali wao.




-Ni zilizoingizwa kinyume na utaratibu ili kwenda kutengeneza dawa za kulevya

-DCEA yaweka wazi jinsi walivyozikamata,magari yaliyokuwa yakizisafirisha yashikiliwa



Na Said Mwishehe,Michuzi TV


OPERESHENI maalum iliyofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya jijini Dar es Salaam imewezesha kukamatwa kwa lita 66,048 za kemikali bashirifu zilizoingizwa nchini kinyume na taratibu za kisheria.

Katika operesheni hiyo iliyofanyika Aprili mwaka huu,Mamlaka hiyo imeshirikiana na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA).

Akizungumza leo Mei 13,2025 jijini Dar es Salaam Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amezitaja kemikali zilizokamatwa ni Cyclohexanone zenye ujazo wa lita 16,048 na Extra Neutral Alcohol (ENA) zenye ujazo wa lita 50,000.

Aidha amesema magari mawili yaliyohusika kusafirisha kemikali hizo yanashikiliwa na watuhumiwa wawili wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

“Kutokana na udhibiti wa dawa za kulevya kuimarika duniani, mitandao ya kihalifu imekuwa ikitumia kemikali bashirifu kuzalisha dawa za kulevya katika maabara bubu.

“Kemikali hizo ni halali kwa matumizi ya viwandani, kitabibu, kilimo, ujenzi, madini pamoja na tafiti za kisayansi, lakini wahalifu huzitumia vibaya kwa kuzichepusha kutoka katika matumizi halali na kuzitumia kutengeneza dawa za kulevya.”

Ameongeza hali hiyo imeongeza changamoto katika mapambano didi ya dawa za kulevya duniani na kuifanya nchi yetu kuendelea kumarisha mifumo ya udhibiti wa kemikali bashirifu ili kuzuia uchepushwaji wake katika matumizi haramu.

Kamishina Jenerali Lyimo amesema uchunguzi ullofanyika umebaini kemikali aina ya Cyclohexanone zillingizwamnchini na kampuni ya Kinglion Investment Company LTD kinyume na mataka ya mitumo ya udhibiti ikivemo kibali kutoka Mamaka husika.

Adha, kemikali aina ya Extra Neutral Alcohol (ENA) zilikuwa zinasafirishwa kwa kutumia magari ya yanayotumika kubeba mafuta aina ya Petroli yaliyoandikwa Danay Petroleum 3YE 1203 aina ya Scania kwa utumia vibali wya kughushi.

“Magari mayo yalkuwa yakibeba kemikali kutoka kampuni ya Maranie Group Company Limited iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani.”

Amesema katika operesheni hiyo, Mamlaka imemkamata Bakira Abel Zacharia (44), mkazi wa Dar es Salaam, dereva wa gari namba T 794 BMB lenye tela tanki namba T 166 AHW lililokuwa limebeba lita 30,000 za kemikali hizo.

Pia, mamlaka imemkamata Vicent Stephen Rashid (26), mkazi wa Mbeya, dereva wa gari namba T 568 EQF lenye tela tanki namba T 640 EQN lililokuwa limebeba lita 20,000 za kemikali hizo.

“Mazingira ya uingizaji na usafirishaji wa kemikali hizo yanaashiria uwepo wa nia ovu ya kuzichepusha kwa matumizi haramu, ikiwemo utengenezaji wa dawa za kulevya.

“Kemikali aina ya Cyclohexanone ni miongoni mwa kemikali zilizothibitika kimataifa kutokana na taarifa za kutumika katika maabara bubu zinazozalisha dawa za kulevya aina ya Phencyclidine (PCP).”

Aidha, lita 16,048 za kemikali za Cyclohexanone zilizokamatwa kama zingechepushwa zingeweza kuzalisha tani 11.4 za dawa za kulevya aina ya Phencyclidine kwa kuwa kilo moja ya kemikali hizo huweza kuzalisha takribani gramu 750 za dawa za kulevya.

Amefafanua kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali za Viwandani na Majumbani sura 182, usafirishaji wa kemikali unahitaji taratibu maalumu ikiwemo vibali vya kuingiza na kusafrisha Kemikali.

“Matumizi ya vibali vya kughushi na utoaji wa taarifa za ongo kuhusu matumizi yaliyokusudiwa ya kemikali husika ni kosa kisheria,”amesisitiza.

Pia amesema usafrishaji wa kemikali kwa nja fiche hususani kwa kutumia magari ya kubeba petroli ni ukukwaji mkubwa wa taratibu za udhibiti wa kemikali na ni kiashiria cha uwepo wa jaribio la kuzichepusha kwa matumizi haramu.




Na Victor Masangu, Kibaha

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha katika kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta chachu ya maendeleo imeamua kutumia fursa ya makusanyo ya fedha za mapato yake ya ndani katika kuhakikisha inakabiliana na changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi ikiwemo suala la kuboresha  miundombinu ya  barabara za mitaa zilizopo katika kata zote 14.

Hayo yamebainishwa na Mstahiki meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr. Nicas Mawazo wakati wa kikao cha kikanuni cha  baraza la madiwani robo ya tatu  ya kuanzia mwezi januari mwaka huu wa 2026 hadi kufikia Machi ambapo amebaini lengo kubwa ni kuhakikisha wanawaletea mabadiliko chanya ya kimaenndeleo katika nyanja mbali mbali kupitia mapato ya ndani.

Mstahiki Meya amebainisha kwamba katika kikao hicho wamemeweza kupata fursa ya kupokea taarifa mbali mbali kutoka katika baadhi ya taasisi ikiwemo Dawasa, Tanesco, Bima ya afya, Tarura, pamoja na nyinginezo kwa lengo la kujadili mambo mbali mbali ambayo yataweza kuletaa tija zaidi katika kutatua changamoto mbali mbali za wananchi katika maeneo ambayo wanaishi.

"Tumefanya  kikao chetu cha kikanuni cha baraza letu la  madiwani   na kwamba tumejadili mambo mbali mbali ikiwemo suala la  upatikanaj  wa huduma ya maji safi na salama, kuboresha miooundombinu ya barabara za mitaa ambapo tumeweza kutenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa kila mtaa na hii itaweza kusaidia kwa kiais kikubwa katika kuboresha miundombinu ya barabara sekta ya elimu na afya ,"amebainisha  Dr. Nicas

Kwa upande  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt. Rogers Shemwelekwa amesema kwamba lengo kubwa niu kuzidi kuendelea kuongeza kasi zaidi katika suala zima  ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo pia yataweza  kusaidia  katika  kutekeleza  baadhi ya miradi mbali mbali ya maendeleo.

Shemwelekwa  ameahidi kuendelea kushirikiana bega kwa bega na viongozi pamoja na  madiwani kwa lengo la kuweza   kuleta dhana pana ya ushirikishwaji  ambayo   itaweza  kuleta matokeo chanya kataika suala zima la maendeleo.

Nao baadhi ya madiwani wa viti maalumu akiwemo Selina Wilson katika kupambana naa maambukizi mapya ya virusi vya ukimvi (VVU) hakusita kuwahimiza wakinababa kutumia kinga kwa lengo la kuweza kuepukana na maambukizi mapya na kwamba ni vema sasa kuwahimiza umuhimu wa kutumia kondomu katika tendo la ndoa na kuacha na ngono zembe.

Naye Diwani wa viti maalumu Shufaa Mshana pamoja na Sara  Uledi wamesema wameomba juhudi za makusudi zifanyika katika kuboresha sekta ya afya hasa kwa upande wa wakinamama wajawazito ambao wamekuwa wakitembea umbari mrefu katika baadhi ya maeneo kwa ajili ya kwenda  kupata huduma ya kujifungua.

Kikao cha kikanuni  cha baraza la madiwani robo ya tatu ya kuanzia Januari hadi machi mwaka huu kimeweza kujadili mambo mbali mbali ikiwemo suala la kuimarisha miundombinu ya barabara za mitaa, kuboresha huduma ya maji safi na salama, upatikanaji wa bima ya afya kwa wote, suala la afya, elimu  pamoja na mambo  mengine yaa msingi kwa ajili ya maslahi ya wananchi kwa ujumla.








Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO
Katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya ardhi nchini, Serikali imelenga kutekeleza mikakati ya kuongeza kasi ya uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi vijijini pamoja na kutumia mbinu jumuishi na shirikishi zinazowahusisha wananchi na wadau katika hatua za upangaji wa ardhi.

Mikakati hiyo inalenga kutekelezwa kwa kupanua programu za kitaifa za upangaji ardhi vijijini kwa kushirikiana na wadau wa maeneo husika, kutumia teknolojia za kisasa na ramani za kidigitali ili kuongeza ufanisi, pamoja na kuharakisha upimaji na utoaji wa hati za kimila, kwa lengo la kupunguza migogoro ya ardhi.

Akizungumza wakati wa kuzindua jukwaa la siku tatu la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, alisema mikakati hiyo pia inahusisha kuimarisha ushirikiano kati ya wizara, halmashauri, wadau na jamii kwa ujumla katika utekelezaji wa majukumu ya sekta hiyo.

Amesema serikali inahamasisha matumizi endelevu ya ardhi, ikiwemo kilimo hifadhi na ufugaji unaozingatia uwezo wa ardhi, ili kuhakikisha rasilimali hiyo inatumika kwa tija na kwa njia inayopunguza migogoro.

Kwa ujumla, Mhe. Dkt. Akwilapo ameeleza kuwa mikakati hiyo inalenga kuleta mabadiliko kutoka katika hatua ya kupanga mipango kwenda katika utekelezaji wake kwa vitendo, ili kuhakikisha ardhi inatumika kwa njia jumuishi inayozingatia maendeleo endelevu.

Ametoa rai kwa jamii kushiriki kuchangia gharama za uandaaji wa hati za hatimilki za kimila, kama ambavyo tayari imeanza kutekelezwa katika baadhi ya maeneo na kusisitiza kuwa, utaratibu huo utasaidia kuongeza kasi ya umilikishaji wa ardhi na kuwafanya wananchi kuwa na milki salama.

“Bila shaka, uchangiaji huu wa gharama utaongeza kasi ya umilikishwaji na hivyo kuwafanya wananchi kuwa na milki salama,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima, alisema mkoa wake umechukua hatua madhubuti katika kukabiliana na migogoro ya ardhi, hususan kati ya wakulima na wafugaji, kwa kufanya tathmini na utafiti wa kina kubaini chanzo cha changamoto hizo.

Amesema mkoa wa Morogoro umeweka utaratibu wa kujadili migogoro ya wakulima na wafugaji kama ajenda ya kudumu katika vikao vya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa vinavyofanyika kila mwezi.

“Tumefanya maamuzi ya makusudi ya kuhakikisha tunabaini tumetokea wapi. Katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, kila mwezi tumeweka ajenda ya migogoro ya wakulima na wafugaji,” alisema Mhe. Malima.

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi, Bw. Joseph Mafuru, alisema takwimu zinaonesha kuwa kati ya vijiji 12,333 nchini, ni vijiji 4,925 pekee, sawa na asilimia 39.9, ndivyo vilivyo na mipango ya matumizi ya ardhi, huku vijiji 7,408 bado havijapata mipango hiyo.

Bw. Mafuru alisema changamoto kuu zinazosababisha kasi ndogo ya uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ni ufinyu wa rasilimali fedha na matumizi hafifu ya teknolojia stahiki.

Ameeleza kuwa, licha ya kuongezewa bajeti kila mwaka, bado kuna haja ya wadau mbalimbali kukutana na kuweka mikakati ya pamoja itakayowezesha kukamilisha hatua zote za upangaji wa matumizi ya ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa kuzindua jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi lililofanyika mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026.

Sehemu ya washiriki wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Wa pili kushoto) na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) wakipata maelezo ya vitabu vinavyoelezea mipango ya matumizi ya ardhi kutoka kwa Afisa Mipango Miji Mkuu wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bw, John Chua wakati wa Jukwaa la wadau lililofanyika mkoani Morogoro tarehe 12 Mei 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam Malima akizungumza katika Jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi linaloendelea mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Tume ya Matumizi bora ya Ardhi Bw. Joseph Mafuru akizungumza wakati wa uzinduzi wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi lililofanyika mkoani Morogoro.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo (Wa pili kulia), Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kulia) na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi Bw. Joseph Mafuru (kulia) wakifuatilia michango ya wadau wakati wa uzinduzi wa jukwaa la wadau wanaohusika na uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi uliofanyika mkoani Morogoro.
( PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI).

Na Mwandishi Wetu
* Matumizi sahihi ya tiba asili na ulinzi wa mazingira.
SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO)limesema linatambua nafasi ya wanawake na akina mama katika: uhifadhi wa mimea dawa,malezi ya maadili ya jamii,

TRAMEPRO imeyasema hayo kupitia Katibu Mkuu wake Boniventura Mwalongo wakati wakitoa salamu katika Maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani.

Mwalongo amesema Shirika hilo linatoa salamu za heshima, upendo na pongezi kwa akina mama wote duniani katika maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa duniani kote kila Jumapili ya pili ya mwezi Mei.

Ameongeza lengo ni kuthamini mchango mkubwa wa mama katika malezi, ustawi wa familia, maadili ya jamii na maendeleo ya Taifa. Historia inaonyesha kuwa maadhimisho haya yalianzishwa kupitia juhudi za Anna Jarvis nchini Marekani mwanzoni mwa karne ya 20, kama njia ya kutambua upendo, kujitoa na nafasi ya mama katika maisha ya mwanadamu.

"Katika maadhimisho haya ya mwaka 2026, tunawakumbusha wananchi kuendelea kuwaheshimu, kuwathamini na kuwaenzi akina mama kwa mchango wao mkubwa katika jamii, afya, malezi, elimu, kilimo, mazingira na maendeleo ya kizazi cha sasa na kijacho."

Pia amesema TRAMEPRO inaamini kuwa jamii yenye kuwathamini wanawake na akina mama ndiyo msingi wa Taifa lenye maadili, afya njema na maendeleo endelevu.

Kauli ya kutafakari mwaka 2026: “Upendo wa Mama ni msingi wa familia imara na jamii yenye utu.”

" Mungu awabariki akina mama wote duniani.

Mungu ailaze roho ya marehemu mama yangu mzazi Ostela Sanga mahali pema peponi. Amina."

Airtel Tanzania imezindua mnara mpya wa mawasiliano wenye kasi ya 4G katika kata ya Kayenze, hatua inayolenga kuimarisha ubora wa mtandao na kuondoa changamoto ya mawasiliano hafifu iliyokuwa ikiwakabili wananchi kwa muda mrefu.

Uzinduzi huu ni sehemu ya mkakati wa Airtel Tanzania kusogeza karibu huduma bora za mawasiliano na kifedha kwa wananchi, hususan maeneo yanayokua kwa kasi kiuchumi na kijamii.

Akizungumza May 9, 2026 wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa Biashara wa Kanda ya Mwanza Mlaki Mchala alisema Airtel inatambua changamoto ya kipato kwa Watanzania wengi, hivyo inaendelea kuhakikisha huduma zinapatikana kwa gharama nafuu zaidi.

Alisema Airtel imeendelea kuimarisha ushindani katika huduma za Airtel Money kwa lengo la kupunguza gharama kwa wananchi katika matumizi ya kila siku, huku akieleza kuwa kampuni hiyo kwa sasa ni miongoni mwa zenye viwango vya chini vya makato nchini.

“Katika huduma za Lipa, awali wananchi walikuwa wakilalamikia makato makubwa, lakini sasa tumeondoa kabisa makato hayo kwa wateja. Tutaendelea kuboresha huduma hizi kadri mahitaji yanavyoendelea kuongezeka,” alisema.

Mchala alisisitiza kuwa kipaumbele cha Airtel ni kuboresha ubora wa mtandao, kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuhakikisha zinamudu gharama kwa wananchi wengi zaidi.

Kwa upande wake, Mektirida Jacob, makzi wa Kayenze alisema ujio wa mnara huo ni faraja kubwa kwa wakazi wa eneo hilo waliokuwa wakikumbana na changamoto ya kukatika kwa mawasiliano.

“Kwa sasa tutafaidika vizuri kwa sababu mnara upo karibu nasi. Zamani mtandao ulikuwa unakatika mara kwa mara, lakini sasa hali itakuwa bora zaidi,” alisema.

Aliongeza kuwa wananchi wanatarajia kuendelea kunufaika na maboresho ya huduma pamoja na ofa mbalimbali za mawasiliano kama vile muda wa maongezi, SMS na data.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Kayenze, Yasin Haruna alisema wananchi wa Kayenze wanatoa pongezi kwa Serikali na Airtel kwa kuwaletea huduma hiyo muhimu.

“Tunafurahi sana kuona wamefika hapa kwetu na kutujengea mnara wa mawasiliano. Tunaahidi kuulinda ili uendelee kutoa huduma kwa muda mrefu,” alisema.

Kayenze ni miongoni mwa kata zinazokua kwa kasi ndani ya Ilemela, ikiwa chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela. Kata hiyo ina mitaa mitano, kaya 4,187 na wakazi 17,201.

Eneo hilo lina shughuli mbalimbali za kiuchumi zikiwemo uvuvi kutokana na ukaribu na Ziwa Victoria, kilimo cha mbogamboga na biashara ndogondogo, ambazo zote zinategemea kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa mawasiliano ya uhakika.

Katika uzinduzi wa mnara huo, Diwani wa kata ya Kayenze, James Katoro aliwataka wananchi kushiriki katika kulinda miundombinu hiyo muhimu kwa maendeleo ya jamii.

“Miundombinu hii inagharimu fedha nyingi, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuilinda ili iendelee kutoa huduma kwa muda mrefu,” alisema.

Aliongeza kuwa Serikali chini ya uongozi wa Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi nchini.

KILA kona ni stori za ushindi, watu wakibishana nani alipiga pesa nyingi zaidi na nani bado anasubiri bahati imuangukie. Ni kupitia mchezo wa Magic Wheel kutoka Meridianbet ukiwa na burudani yenye msisimko wa kila sekunde.

Magic Wheel imekuja na mtindo wake tofauti kabisa. Mbele yako kuna gurudumu lenye nafasi 56 zinazozunguka kwa kasi huku kila mmoja akisubiri kuona litakaposimama. Ndani yake kuna namba 53 na nafasi 3 maalumu zinazoweza kubadilisha kila kitu kwa muda mfupi sana. Kila mzunguko ni nafasi mpya ya kushinda.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kuicheza ni rahisi sana. Unachagua namba zako kati ya 1, 2, 6 au 11, unaweka dau lako halafu unasubiri bahati yako iamue. Gurudumu likianza kuzunguka ndipo presha na msisimko vinaanza kupanda. Hapo ndipo utajua kwa nini vijana wengi wameukubali mchezo huu.

Na kama unataka moto zaidi, Box Bonus ipo kukupa nafasi nyingine ya kutoboa. Mabox matatu yanakuja na uchaguzi wa low, medium au high odds. Hakuna anayejua kilichojificha ndani mpaka uchague box lako mwenyewe. Ukipatia, unaweza kusepa na ushindi mkubwa bila kutarajia.

Meridianbet wameleta burudani inayochanganya bahati, msisimko na nafasi ya kushinda kwa pamoja. Kama unapenda changamoto na unataka kuonja ladha ya ushindi, huu ndio muda wako wa kuingia kwenye Magic Wheel. Zungusha gurudumu na uone kama leo bahati itasimama upande wako.

NA MWANDISHIWI WETU – MASVINGO – ZIMBABWE

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya (Mb), amewasili nchini Zimbabwe kushiriki Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi unaofanyika Masvingo, Zimbabwe kuanzia tarehe 11 haadi 14 Mei, 2026.

Mara baada ya kuwasili, Mhe. Mmuya amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Balozi Suzan S. Kaganda na kuipongeza Tanzania kushiriki katika mkutano huo unaolenga kujadili maendeleo yaliyopatikana katika utekelezaji wa programu za kikanda na masuala ya kimkakati katika utekelezaji wa afua mbalimbali katika Usimamizi wa maafa kwa nchi za SADC.

Masuala mengine yaliyoelezwa na Mheshimiwa Balozi Suzani ni  pamoja na Tanzania kuendelea kuzitangaza fursa zilizopo ikiwemo sekta ya utalii, uchukuzi pamoja na kilimo  huku akiahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Zimbabwe.

Sambamba na hayo, mkutano huo utahudhuriwa na wadau mbalimbali wa masuala ya Usimamizi wa Maafa kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo ni fursa kwa Tanzania kuendelea kujitangaza Kimataifa kwa kuwa na mifumo thabiti ya Usimamizi wa Maafa pamoja na  kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Menejimenti ya maafa.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoshiriki katika Mkutano huo wa siku Nne ambapo umekutanisha wadau wa  masuala ya maafa kutoka nchi kumi na sita wakiwemo wataalamu kutoka  katika ngazi za Kimataifa pamoja na Mashirika ya Umoja wa Kimataifa.








Na Janeth Raphael MichuziTv

Serikali imeendelea kuimarisha sekta ya afya nchini kwa kuongeza ajira za watumishi wa kada mbalimbali, hatua inayolenga kupunguza uhaba wa wataalamu katika hospitali, vituo vya afya na zahanati, hususan katika maeneo yenye upungufu mkubwa wa watumishi.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Dkt. Jafar Seif, amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/21 hadi 2025/26 Serikali imeajiri jumla ya watumishi 37,921 wa kada za afya na kuwapangia vituo vya kazi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.

Dkt. Seif ametoa kauli hiyo bungeni leo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Christina Solomon Mndeme, aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali wa kuongeza watumishi wa afya katika Mkoa wa Tabora ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Akizungumzia hali ya Mkoa wa Tabora, Dkt. Seif amesema mahitaji halisi ya wataalamu wa afya ni watumishi 8,121, lakini waliopo sasa ni 3,467 pekee, sawa na asilimia 43 ya mahitaji yote. Hivyo, mkoa huo bado unakabiliwa na upungufu wa watumishi 4,654, sawa na asilimia 57.

Amesema licha ya changamoto hiyo, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kupunguza pengo hilo ambapo kati ya mwaka wa fedha 2024/25 hadi 2025/26, jumla ya watumishi 856 wa kada mbalimbali za afya wameajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi katika halmashauri zote za Mkoa wa Tabora.

Aidha, Dkt. Seif amesema halmashauri nane za Mkoa wa Tabora zimeandaa mkakati maalum wa kuongeza nguvu kazi katika sekta ya afya kupitia mapato ya ndani. Kwa mwaka wa fedha 2026/27, halmashauri hizo zimetenga jumla ya shilingi milioni 413.8 kwa ajili ya kuajiri watumishi 87 wa afya kwa mfumo wa mikataba.

Kwa mujibu wa Serikali, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu na maeneo yao pamoja na kupunguza mzigo wa kazi kwa watumishi waliopo sasa katika vituo vya kutolea huduma.

Serikali imeendelea kusisitiza kuwa itaendelea kuboresha mazingira ya utoaji huduma za afya nchini kwa kuongeza ajira, kuimarisha miundombinu ya afya na kuhakikisha wataalamu wa kutosha wanapatikana katika maeneo yenye uhitaji mkubwa.





Viongozi mbalimbali wa Chama cha mapinduzi Mkoa na Wilayani wakiambatana na Viongozi wa Serikali mkoa wa Dodoma wameanza safari ya Kikazi kuelekea mkoani Mtwara kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Ushirika vya Msingi.

Viongozi hao wakingozana na Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma Ndg Joseph Chitinka na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Dodoma Bibi Theresia Nyoka wameanza ziara hiyo leo Mei 12, 2026 kutokea mkoani Dodoma kuelekea mkoani humo.

Mrajis Msaidizi wa mkoa wa Dodoma ameeleza lengo la ziara hiyo ni kuwajengea uwezo, kujifunza utekelezaji wa Mfumo wa stakabadhi za ghala na kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali kwenye Vyama Vikuu na Vyama vya Msingi Ushirika vya mkoa wa Mtwara na hivyo kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kiushirika ndani ya Mkoa wa Dodoma.

Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 13 hadi 14, 2026 na kuwahusisha Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa, Wenyeviti wa CCM Wilaya Mkoani Dodoma, Sekretariti ya Mkoa CCM, Baadhi ya Makatibu wa Chama wilaya na Wenezi,, Makatibu, Makatibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Viwanda na Biashara na Kilimo.


Top News