Vodacom Tanzania PLC kwa kushirikiana na Chama cha Mpira wa Kikapu Dar es Salaam (BDL) waliandaa hafla ya tuzo maalum jijini Dar es Salaam, ikiwa ni kilele cha msimu wa Ligi ya Mpira wa Kikapu ya Dar es Salaam (BDL) 2025.

 Hafla hiyo ilikusudia kusherehekea mafanikio ya wachezaji, timu na wadau walioshiriki msimu mzima, huku ikiangazia athari chanya za uwekezaji wa Vodacom katika kukuza michezo na vijana nchini.Ligi ya mwaka huu ilihusisha jumla ya timu 277, kwa upande wa wanawake na wanaume  zilizoshiriki katika mashindano yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Don Bosco Oysterbay, ambao umekarabatiwa na Vodacom kama sehemu ya dhamira yake ya kukuza vipaji na kuinua ari ya vijana kupitia michezo. 

Tuzo na zawadi zilitolewa kwa mabingwa wa msimu huu pamoja na wachezaji bora wa kike na wa kiume, waliodhihirisha nidhamu na ubunifu uwanjani.

Akizungumza katika halfa hiyo Mkuu wa Idara ya bei za vifurushi na makundi maalum ya wateja, Gemma Kamara Alisema “Kwa Vodacom, ushirikiano huu na BD ni zaidi ya udhamini wa michezo. Ni njia ya kushirikiana na jamii katika kuwawezesha vijana kutambua uwezo wao. Tumejifunza mengi kupitia ligi hii, kuona vijana wakikua, wakijiamini, na kutumia michezo kama nguzo ya maendeleo binafsi na kijamii. 

Vodacom itaendelea kuwa mstari wa mbele kuwawezesha vijana kupitia michezo, elimu, na teknolojia kama nguzo kuu za kuwasaidia kufikia ndoto zaoKwa upande wake, Mpoki Mwakipake, Katibu wa Shirikisho la Mpira wa kikapu, aliishukuru Vodacom kwa mchango wake mkubwa katika kuendeleza mchezo wa mpira wa kikapu nchini. “Ushirikiano kati ya BD na Vodacom umeleta mabadiliko makubwa katika mchezo huu. 

Tumeshuhudia ongezeko la ari, nidhamu na ushindani wa kweli. Ni heshima kubwa kuona vijana wetu wakifikia viwango vya juu zaidi” alisema Mpoki Mwakipale, Katibu wa Shirikisho la Mpira wa kikapu,“Moja ya changamoto kubwa tunayokutana nayo kama wachezaji ni ukosefu wa miundombinu bora ya michezo,” alisema Nadia Samir, mchezaji wa Don Bosco Troncatti. 

“Lakini mwaka huu tumefarijika kuona mabadiliko makubwa uwanja wa Don Bosco umeboreshwa kwa udhamini wa Vodacom, ligi imekuwa ya ushindani zaidi.

 Tungependa kuona wadhamini wengine wakijitokeza ili kuendelea kuboresha mpira wa kikapu nchini Tanzania.”Kwa upande wa wanaume, Dar City Basketball Team waliibuka mabingwa baada ya ushindani mkali katika michezo ya fainali dhidi ya wapinzani wao JKT, wakijinyakulia zawadi ya shilingi milioni 10 kutoka Vodacom. 

Kwa upande wa wanawake, DB Lioness Basketball Team walitawala uwanjani na kutwaa taji la ubingwa wa BDL 2025, nao wakipokea zawadi ya shilingi milioni 10 kama sehemu ya kutambua jitihada na mafanikio yao.

Kupitia miradi kama hii, Vodacom inaendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuwa mshirika wa maendeleo kwa vijana wa Kitanzania ikitumia michezo, elimu na teknolojia kama nyenzo za kujenga kizazi kinachojiamini, chenye dira na matumaini ya kesho iliyo bora.

Hafla ya utoaji tuzo ilihudhuriwa na Vodacom, BD, wadau wa michezo, familia za wachezaji na waandishi wa habari. Usiku huo ulipambwa na muziki, furaha na shangwe za vijana waliotimiza ndoto zao kupitia mchezo wa mpira wa kikapu.


Rais wa Chama cha Mpira wa Kikapu Dar es Salaam (BD) Bw. Shendu Hamis Mwagalla, akikabidhi cheti cha kutambua mchango wa udhamini kwa Bi. Gemma Kamara, Mkuu wa Idara ya Bei za vifurushi na makundi maalumu ya wteja kutoka Vodacom Tanzania PLC, kama ishara ya kuthamini mchango wa kampuni hiyo katika kuendeleza mchezo wa mpira wa kikapu nchini. Kupitia udhamini huo, Vodacom imeboresha uwanja wa Don Bosco Oysterbay, kudhamini zawadi za washindi wa kwanza, pili na tatu, na kuendeleza programu za kuwawezesha vijana kupitia michezo. Tukio hilo limefanyika katika hafla ya utoaji tuzo za Ligi ya Mpira wa Kikapu ya Dar es Salaam (BDL) 2025, mwanzoni mwa wiki hii jijini Dar es Salaam.









Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema kuwa utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu miradi inayotarajiwa kutekelezwa ni miongoni mwa masuala muhimu ya kuzingatia ili kufanikisha utekelezaji wa miradi hiyo kwa ufanisi.

PURA imesema hayo Oktoba 15, 2025 katika Kijiji cha Ruvula Mkoani Mtwara, wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya mradi wa uchimbaji wa visima vitatu vya gesi asilia unaotarajiwa kutekelezwa katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani humo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mjiolojia Mwandamizi kutoka PURA Bw. Ebeneza Mollel amesema kuwa, pamoja na kudhibiti shughuli za kitalaamu, PURA pia inahakikisha wananchi wanajengewa uelewa wa miradi kabla ya kuanza utekelezaji.

“Sisi kama Mamlaka tunahakikisha kuwa, jamii zinazoishi au zinazozunguka maeneo ambayo miradi ya mkondo wa juu wa petroli inatekelezwa, zinashirikishwa kikamilifu katika miradi hiyo na kujengewa uelewa wa kina kuhusiana na mradi” alisema Mollel.

Sambamba na hilo, Bw. Mollel alisema kuwa, PURA inafuatilia kwa karibu hatua zote za utekelezaji wa mradi wa uchimbaji wa visima vya gesi asilia na kuwakumbusha watekelezaji wa mradi umuhimu wa utoaji wa uelewa wa mradi kwa wananchi.

Zoezi la utoaji wa uelewa wa mradi wa uchimbaji wa visima vya gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay linafanywa katika vijiji vitatu ambavyo ni Ruvula, Msimbati na Mtandi vilivyopo katika Kata ya Msimbati, Mtwara.

Mradi huo unaohusisha uchimbaji wa visima viwili vya uzalishaji na kisima kimoja cha utafiti unatarajiwa kugharimu zaidi ya Dola za Marekani milioni 80.2 unatekelezwa na Kampuni ya Maurel et Prom Tanzania kwa kushirikiana na TPDC.

Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza Desemba 2025 ambapo utawezesha, pamoja na mambo mengine, ongezeko la uzalishaji wa gesi asilia kwa wastani wa futi za ujazo milioni 30 kwa siku.

Ongezeko hilo litasaidia upatikanaji wa gesi asilia kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kuzalisha umeme, kwenye viwanda, majumbani na kwenye vyombo vya usafiri (magari na bajaji).
Mjiolojia Mwandamizi kutoka PURA, Bw. Ebeneza Mollel akizungumza na sehemu ya wadau kutoka Kijiji cha Ruvula wakati wa kikao cha kuwajengea wananchi uelewa kuhusiana na mradi wa uchimbaji wa visima vya gesi asilia katika Kitalu cha Mnazi Bay Mkoani Mtwara. Kikao hicho kimefanyika Oktoba 15, 2025.




Na. Vero Ignatus Michuzi Blog Arusha

Mkutano Mkuu wa  6 wa Mwaka wa AQRB 2025, umefanyika Jijini Arusha na kukutanisha taasisi za udhibiti kama AQRB, ERB, CRB,OSHA, NEMC, FIRE & RESCUE, EWURA NA TAMISEMI , Lengo kuu ni kukaa kwa pamoja na kuweza kubadilishana uzoefu katika udhibiti wa sekta ya ujenzi. 

Akifungua mkutano huo wa 6 wa mwaka Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi anayeshughulikia miundombinu Rogatius Mativila ameiagiza Bodi hiyo kuboresha Mifumo ya usajili na kuhakikisha miradi yote ya Umma inasimamiwa na wataalam waliosajiliwa ili kuepusha utapeli 

Ametahadharisha Bodi hiyo kuwa makini  na kampuni zisizokuwa na ubora zinazojihusisha na ujenzi kudhibitiwa, kwani ubunifu mkubwa kuzingatiwa   kwani yanahitajika Majengo yanayohimili mabadiliko ya tabianchi miradi ya kijani matumizi ya kisasa, Mifumo ya kidigitali katika usanifu na katika ukadiriaji wa miradi. 

"Kupitia ubunifu tutaweza kujenga majengo Bora salama rafiki kwa mazingira inayoendana na ndoto ya Tanzania ya viwanda na uchumi wa kidigitali" Alisema Mativila

Amewataja wakadieiaji na wasanifu Majengo kuwa ni moyo wa katika usalama wa Majengo yanayobeba maelfu ya wa Tanzania kutokana na ubora wa Majengo yanayoonyesha taswira nzuri ya nchi. 

Awali akitoa salamu za Bodi hiyo  Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Dkt.Daniel Matondo, amesema Bodi hiyo inasimamia uadilifu ubora na maadili ya wataalam  hadi kufikia tarehe 30 Septemba 2025 wamesajili wataalam 1170 makampuni 507 kati ya januari- septemba wamefanikiwa kufanya ukaguzi wa Majengo na majenzi yaliyosajiliwa awali pamoja na yale yanayojengwa kwa sasa 4598 miradi 1276 iliyokidhi matakwa ya kisheria, aidha waendelezaji zaidi ya 103 wamefikishwa mahakamani kwa kutokufuata taratibu za kisheria. 

Dkt.Matondo ameainisha  mada ndogo zinazojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na  Taarifa za Udhibiti na Taratibu za Udhibiti wa Miradi, kuangalia mchakato wa kupata vibali na idhini kutoka Bodi na vyombo vingine vinavyohusiana na udhibiti wa miradi ya ujenzi,Mifumo ya Usalama na Afya Kazini,kuhakikisha usalama wa wafanyakazi na watekelezaji wa miradi, na ufuatiliaji wa viwango vya afya kazini.

 Pia watajadili Usalama wa Moto katika Miradi ya Ujenzi, kuzingatia kanuni za kujikinga na moto katika majengo na miradi ya umma na ya watu binafsi, Uendelevu wa Mazingira,Tathmini na Athari zake, kuhakikisha miradi ya ujenzi inazingatia masuala ya kimazingira na usalama wa rasilimali za taifa,Udhibiti wa Maadili na Sheria,maadili ya kitaaluma, na usajili wa wataalamu katika kuhakikisha uwajibikaji na ufanisi wa sekta,Ufuatiliaji na Ripoti za Uzingatiaji Mahiri kuangalia mbinu na zana za kuhakikisha utekelezaji sahihi wa taratibu na udhibiti katika miradi ya ujenzi. 103 wamefikishwa mahakamani kwa kushindwa kufuata taratibu za kisheria.

Vilevile, Bodi ilifanya mikutano 3 ya kinidhamu na mashauriano nawataalamu pamoja na makampuni kwa lengo la kudhibiti uadilifu na uwajibikajikatika utoaji wa huduma.Kuhusu kutoa ushauri kwa Wananchi Bodi imeshirikikatika maonesho mbalimbali yanayojumuisha wananchi kamaSabasaba,nanenane .

Aidha katika juhudi za kuongeza uelewa kwawananchi wa taaluma hizi Bodi imeendesha mashindano ya insha kwawanafunzi wa shule za msingi na Sekondari na inaanza kutoa zawadi kwawaliofanya vizuri mwishoni mwa mwezi Oktoba 2025 .

Pia Bodi imepanua wigowa matangazo kwa umma kupitia wanahabari na mitandao ya kijamii navyombo vya usafri kama SGR, Bajaj na hata katika Barua pepe za Serikali y aani GMS. AlisemaPamoja na hatua kubwa zilizopigwa katika utekelezaji wa majukumu yake,

Aidha Dkt. Matondo amesema Bodi hiyo inakabiliwa na changamoto ikiwemo: Kutokamilika kwa Sheria Majengo, jambo linalochelewesha baadhi ya taratibu muhimu za usimamizi na udhibiti katika sekta ya ujenzi  Ufinyu wa bajeti ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi chini ya mpango wa AQIP, hali inayopunguza wigo wa kuwajengea uzoefu wakiutendaji wanafunzi na wahitimu Mwingiliano wa kisheria na taasisi nyingine za umma, mfano Barazal a Sanaa Tanzania (BASATA) na wadau wengine, unaohitaji uratibu . 

Amesema changamoto nyingine ni pamoja na Uelewa mdogo wa Sheria ya Bodi miongoni mwa wananchi, taasisib inafsi na hata baadhi ya taasisi za umma, jambo linalosababisha changamoto katika utii na utekelezaji wa masharti yake.

Hata hivyo, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi inaendelea kutekeleza hatua za makusudi za kutatua changamoto hizi, ikiwemo kukamilisha mchakato wa Sheria ya Majengo, kuongeza ushirikiano baina ya taasisi, kuimarisha uratibu wa mafunzo kwa vitendo na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu Sheria ya Bodi.

Mkutano huo wa Sita unaongozwa na Kaulimbiu isemayo: “Uzingatiaji Mahiri: Kuwawezesha Wataalamu katika Mazingira Yenye Udhibiti wa Kisheria.” Yaani kwa kiingerez Smart Compliance: Empowering Professionals in a Regulated Environment.”

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi anayeshughulikia miundombinu Rogatius Mativila
Dkt.Daniel Matondo, Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB)




Na Pamela Mollel, Arusha

Shirika lisilo la kiserikali Dyslexia Tanzania limeandaa mbio maalumu zijulikanazo kama “Dyslexia Awareness Run”, zenye lengo la kuelimisha jamii kuhusu watoto wanaojifunza kwa njia tofauti na mfumo wa kawaida unaotumika mashuleni.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, mwanzilishi wa shirika hilo Caudence Ayoti alisema kuwa tafiti zinaonesha kati ya watu watano, mmoja hukumbwa na changamoto ya kujifunza, jambo linaloonyesha umuhimu wa kuelimisha jamii mapema kuhusu hali hiyo.

Ayoti aliongeza kuwa serikali kupitia mtaala mpya wa CB (Competence Based Curriculum) imeanza kuangalia uwezo halisi wa mtoto badala ya mfumo wa zamani uliokuwa ukihimiza kukariri, akisema ni hatua chanya inayofungua nafasi kwa watoto wenye Dyslexia kuonekana na kuthaminiwa.

“Kazi kubwa tunayofanya ni kutoa elimu kwa jamii kuacha kuwaita watoto hawa ‘mazombi’ au kuwadharau. Tunataka jamii iwaoneshe upendo, uelewa na ukaribu,” alisema Ayoti akisisitiza dhamira ya taasisi yake kuendelea na warsha mashuleni na kampeni kupitia mitandao ya kijamii.

Aidha, alibainisha kuwa kupitia mbio hizi, taasisi yake inalenga kuongeza uelewa mpana zaidi, huku akifichua kuwa msukumo wa kuanzisha Dyslexia Tanzania ulitokana na uzoefu binafsi wa kulea mtoto mwenye changamoto hiyo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Dyslexia Tanzania, Snape Mwasyoke, alisema mbio hizo zitafanyika tarehe 19 Oktoba 2025 katika viwanja vya Mgambo jijini Arusha kuanzia saa kumi na mbili asubuhi, chini ya kauli mbiu “Tupaze Sauti Zetu”, zikilenga kuhamasisha ushiriki mpana wa jamii.

Naye Mwenyekiti wa Riadha Mkoa wa Arusha, Gerald Babu, alisema mbio hizo hazitaishia kwenye uelewa pekee bali pia zitasaidia kuibua vipaji vipya kwa watoto, huku Mkurugenzi wa DEMI Tours, John S. Rashidi, akiongeza kuwa kampuni yake imetenga asilimia 20 ya mapato kusaidia watoto wanaokabiliwa na changamoto za kujifunza kutokana na uelewa mdogo uliopo kwa jamii.






*Ni kupitia muendelezo wa Awamu ya Pili wa Kampeni ya NSSF Staa wa Mchezo Paka rangi

Na MWANDISHI WETU,

Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Beno Malisa, amewataka waajiri wa sekta binafsi kuhakikisha wanatimiza takwa la kisheria la kuwasilisha michango ya wanachama wao kwa wakati katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), ili kuendelea kuboresha ustawi wa wafanyakazi wao na kuimarisha huduma za hifadhi ya jamii nchini.

Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa majiko ya gesi kwa baadhi ya mama na baba lishe, wanachama wachangiaji wa mpango wa hiari na wastaafu wa Mkoa wa Mbeya, yaliyotolewa na NSSF.

Mhe. Malisa alisema hatua ya kuwasilisha michango kwa wakati ni muhimu kwa ustawi wa wafanyakazi. Alisisitiza kuwa kufanya hivyo ni kutekeleza wajibu wa kisheria na ni sehemu ya kuwajali wafanyakazi, kama wanavyosema NSSF kwamba “wanapaka rangi ustaa wao” kupitia mafao wanayonufaika nayo.

Aidha, Mhe. Malisa aliwahimiza wananchi waliojiajiri, wakiwemo vijana na wajasiriamali wadogo, kujiunga na kuchangia katika mpango wa hifadhi ya jamii wa NSSF ili kunufaika na mafao mbalimbali yakiwemo mafao mbalimbali yakiwemo ya matibabu, uzazi, uzee na mirathi.

Pamoja na hayo, Mhe. Malisa aliupongeza Mfuko wa NSSF kwa kuunga mkono ajenda ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya matumizi ya nishati safi, akieleza kuwa hatua hiyo ni ushahidi wa dhahiri wa dhamira ya Mfuko kugusa maisha ya wananchi kwa vitendo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema utoaji wa majiko hayo ya gesi ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya Mfuko ya kurudisha kwa jamii (CSR), ambayo inalenga kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kulinda mazingira, kuboresha afya za wananchi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Bw. Mshomba aliongeza kuwa tukio hilo limeenda sambamba na kampeni ya “NSSF Staa wa Mchezo Paka Rangi”, inayolenga kuhamasisha wananchi, hususan waliojiajiri, kujiunga na mpango wa kuchangia kwa hiari, waajiri kuwasilisha michango ya wanachama wao pamoja na matumizi ya mifuko ya TEHEMA.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Tunda, aliishukuru NSSF kwa mchango wake mkubwa katika kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa makundi mbalimbali ya wananchi, hasa wajasiriamali wadogo.

Awali, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Bw. Omary Mziya, alisema Mfuko utaendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na kuchangia, ili kuhakikisha kila Mtanzania “anapaka rangi ustaa wake” kupitia NSSF.






















Na Mwandishi Wetu, WMTH, Songwe.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohammed Khamis Abdulla, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha watanzania wote, hususan wanaoishi vijijini na maeneo ya mipakani, wanapata huduma za mawasiliano ya uhakika ili kuboresha maisha yao na kukuza uchumi wa Taifa.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua hali ya mawasiliano mkoani Songwe katika vijiji vya Kapele, Iyendwe, Mpande Kati, na kituo cha forodha cha mpaka wa Tunduma aliyoifanya Oktoba 15, 2025, Bw. Abdulla alisema ni wajibu wa Wizara hiyo ni kuhakikisha changamoto zote za upatikanaji wa mtandao zinatatuliwa kwa haraka ili wananchi waweze kunufaika na fursa za kidijitali.

Ameeleza kuwa, pamoja na changamoto ndogo zilizopo, Tanzania kwa sasa haina tatizo kubwa la mawasiliano kwa sababu maeneo mengi yana minara ya mawasiliano, na kuwaelekeza watoa huduma wote wa simu kushirikiana kutumia minara iliyopo ili kuwezesha mitandao yote kupatikana kwa urahisi katika vijiji vyote.

Ameeleza kuwa Wizara hiyo inaangalia uwezekano wa kuboresha sheria na sera ili kuwezesha mfumo wa “National Roaming”, ambapo mtumiaji wa laini ya mtandao mmoja ataweza kutumia mnara wa mtandao mwingine akiwa ndani ya mipaka ya Tanzania, jambo litakalosaidia kuboresha upatikanaji wa mawasiliano vijijini na maeneo ya pembezoni.

Kwa upande wake, Mhandisi Peter Mwasalyanda, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), alisema mfuko huo unatekeleza mradi mkubwa wa minara 758 unaofadhiliwa na Serikali na ambao umefikia asilimia 98 ya utekelezaji wake.

Amesema UCSAF pia imepanga kuanzisha miradi mipya katika maeneo ya mipakani, mbuga za wanyama na njia kuu za reli za SGR na TAZARA, lengo likiwa ni kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana hata katika maeneo yenye umuhimu wa kimkakati kwa maendeleo ya Taifa.

Naye Bw. Nsajigwa Mwambegele, Meneja Msaidizi wa Forodha Mkoa wa Songwe, alisema huduma bora ya mtandao inayotolewa na TTCL katika mpaka wa Tunduma imechangia kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, ambapo mwaka 2024/25 makusanyo yalifikia Bilioni 204 dhidi ya lengo la Bilioni 182, huku robo ya kwanza ya mwaka 2025/26 ikionesha ufanisi wa asilimia 120 kutokana na uwepo wa mtandao imara na wa kasi.







 

HANDENI-TC

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Handeni, mkoani Tanga, Esther Herman, ametoa wito kwa wananchi kuzingatia ulaji wa chakula bora kinachojumuisha makundi sita muhimu ili kuepuka magonjwa yatokanayo na lishe duni.

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Chakula Duniani yanayofanyika kitaifa jijini Tanga, chini ya kaulimbiu “Tuungane pamoja kupata chakula bora kwa maisha bora ya baadaye”, Esther ametaja makundi hayo ni wanga, protini, mboga za majani, matunda, mafuta pamoja na maji.

Amesema kila kundi lina umuhimu wake mwilini, na ulaji usio sahihi unaweza kusababisha udhaifu wa kinga ya mwili, utapiamlo, au uzito uliopitiliza.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa elimu ya lishe kuanzia ngazi ya kaya, akibainisha kuwa jamii nyingi bado hazina uelewa sahihi kuhusu mlo kamili, jambo linalochangia changamoto za afya kwa watoto na watu wazima.


Top News