WAZIRI wa Kilimo, Mhe. Daniel Godfrey Chongolo (Mb) amefanya mazungumzo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Alexander Mkumbo (Mb) katika ofisi ndogo za Wizara hiyo tarehe 29 Desemba 2025, jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yamelenga kujadili maeneo ya kipaumbele katika Sekta ya Kilimo na dhana ya kilimo biashara katika kuleta tija zaidi kwa wakulima, ikiwemo uongezaji wa ubanguaji wa Korosho kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuhakikisha zaidi ya asilimia 50 ya Korosho zinazalishwa nchini zinabanguliwa ndani ya nchi ifikapo mwaka 2030.

Eneo lingine lililojadiliwa katika mazungumzo hayo ni kuweka msukumo kwenye uzalishaji wa mazao yanayochangia upatikanaji wa uhakika wa mafuta ya kula nchini kama vile Michikichi na Alizeti, ili kupunguza na hatimae kutokomeza utegemezi wa mafuta yanayotoka nje ya nchi.


Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara wa soko la Bunju B, Jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara na kukagua maendeleo ya ujenzi wa soko hilo pamoja na ujenzi wa Kituo cha Mabasi, leo Desemba 29, 2025.





 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Desemba 29,2025 amesoma risala maalum kuhusu uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Siha lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania Bara na Jimbo la Fuoni lililopo Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Tanzania Zanzibar unaotaraji kufanyika Desemba 30,2025.
 
Jaji Mwambegele amesema, uchaguzi mdogo huo utahusisha pia, kata tano za Tanzania Bara. Kata hizo ni;            Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mkoa wa Morogoro; Mbagala Kuu iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam; na Nyakasungwa iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, Mkoa wa Mwanza.
 
Nyingine ni Kata ya Masoko iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mkoa wa Mbeya; na kata ya Ndono iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Mkoa wa Tabora.
 
Aidha, amesema jumla ya wagombea 33 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi za ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja. Kati ya wagombea 33, wagombea 21 sawa na asilimia 63.64 ni wanaume na wagombea 12 sawa na asilimia 36.36 ni wanawake. Kwa namna ya pekee, Tume inavipongeza vyama vilivyoshiriki na wagombea waliojitokeza kushiriki.
 
Jaji Mwambegele amesema, jumla ya Wapiga Kura 218,024 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi huo na jumla ya vituo 556 vya Kupigia Kura vitatumika.
 
“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho tarehe 30 Desemba, 2025 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Majimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
 












-Asifu Kasi ya Makusanyo ya Maduhuli

-Mara yafanikiwa kukusanya Tsh bilioni 112.61, sawa na asilimia 107.25 ya lengo la kipindi husika

-Ahimiza Uzingatiaji Sheria, Taratibu na Misingi ya Utawala Bora

Mara

Katika kuendeleza dhamira ya Serikali ya kuimarisha utendaji kazi na uwajibikaji katika utumishi wa umma, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo amesisitiza kuwa Serikali iko macho na inaendelea kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika mazingira ya kazi ikiwemo kuendelea kuleta vitendea kazi vya kisasa ili kuboresha utendaji kazi wao na kutowakatisha tamaa.

Ameyasema hayo, leo tarehe 29 Desemba 2025 wakati akizungumza na watumishi wa Tume ya Madini Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa Mara na kuwatia moyo watumishi hao kuwa Serikali inaendelea kuboresha changamoto ndogondogo zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa shughuli zao.

Mbibo amewahakikishia watumishi hao kuwa Serikali ipo macho, inatambua changamoto zilizopo na tayari inaendelea kuzifanyia kazi hatua kwa hatua. Amesema uwepo wa vitendea kazi vipya, ikiwemo magari mapya, ni ushahidi wa dhahiri wa dhamira ya Serikali katika kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Aidha, Mbibo amewahimiza na kuwatia moyo watumishi hao katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kuwataka kuendeleza mshikamano, bidii na uvumilivu kazini, na kwamba changamoto hazipaswi kuwavunja moyo watumishi.

Sambamba na kukutana na watumishi hao kwa lengo la kuwasikiliza changamoto zao, Naibu Katibu Mkuu Mbibo pia amepata fursa ya kujionea kwa karibu mwenendo wa shughuli za kila siku, zinazotekelezwa na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa Mara.

Katika hatua nyingine, Mbibo ametoa pongezi kwa watumishi wa Ofisi hiyo kwa kazi nzuri ya makusanyo ya maduhuli inayoendelea kufanyika, akieleza kuwa matokeo hayo yanatokana na nidhamu, ushirikiano na uwajibikaji kazini na kuelekeza kuwa juhudi hizo ziendelezwe zaidi kwa kuzingatia sheria, taratibu na misingi ya utawala bora.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa Mara Mhandisi Hamad Kallaye amesema kuwa, kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Mkoa wa Mara umepangiwa lengo la kukusanya jumla ya shilingi bilioni 210.0. Hadi kufikia tarehe 28 Disemba, 2025, katika kipindi cha Julai hadi Disemba, Ofisi imefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 112.61, sawa na asilimia 107.25 ya lengo la kipindi husika na asilimia 53.62 ya lengo la mwaka mzima.

Ziara hiyo imeacha taswira chanya miongoni mwa watumishi, ambao wameeleza kufarijika na kutiwa moyo na ujumbe wa Serikali, wakiahidi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na uzalendo kwa maendeleo ya Sekta ya Madini katika Mkoa wa Mara na Taifa kwa ujumla.








Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 29, 2025 amekagua hali za uzalishaji na usambazaji wa maji eneo la Ruvu Chini, mkoani Pwani.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi, Serikali ilianza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

“Mipango hii ya ujenzi wa miradi inayolenga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji ilianza muda mrefu, Serikali iliona na ilianza kutafuta majawabu ya hali hii miaka mitatu iliyopita kwa kujenga miradi mikubwa itakayotoa matokeo chanya” Amesema Dkt. Mwigulu












Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, Daniel Sillo, akizungumza wakati akiongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Utatu Mtakatifu Masakta, Jimbo Katoliki la Mbulu, wilayani Hanang’ mkoani Manyara Desemba 28, 2025.

Na Dotto Mwaibale
NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, Daniel Sillo, Mungu ameendelea kumpa kibali cha kuongoza harambee za uchangiaji wa shughuli za kidini ambazo zimekuwa na mafanikio makubwa.

Desemba 28, 2025 Mhe. Sillo aliongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Utatu Mtakatifu Masakta, Jimbo Katoliki la Mbulu, wilayani Hanang’ mkoani Manyara ambapo jumla ya Sh.Milioni 37 zilipatikana.

Harambee hiyo inakuwa ya pili kuifanya tangu alipochaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya ile aliyoifanya Novemba 23, 2025 katika Kanisa la Tirano lililopo eneo la Galapo mkoani humo ambapo alichangisha Sh. Milioni 5.7 kwa ajili ya ununuzi wa vyombo vya muziki ambavyo vitatumika kuhubiri injili kwa njia ya uimbaji.

Jambo hilo katika imani siyo dogo linaonesha ni jinsi gani Mungu anavyompa kibali mtumishi wake huyo katika kufanya kazi yake ya kuwatumikia wananchi kwa namna tofauti.

Katika harambee zote hizo Mhe. Sillo amekuwa akisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika shughuli mbalimbali za maendeleo pamoja na ujenzi wa nyumba za ibada.

Aidha, jambo lingine ambalo amekuwa akilihimiza ni Watanzania kuendelea kuilinda na kudumisha amani na kueleza kuwa amani ndiyo inayowafanya watu waweze kukutana na kufanya shughuli za maendeleo na kuabudu ambapo alitumia nafasi hiyo kuwaomba viongozi wa dini kuendelea kumuombea Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wakiwemo wabunge.

Akizungumza katika harambee hiyo Paroko wa Parokia ya Utatu Mtakatifu Masakta, Padre Gabriel Mrina, alimshukuru Naibu Spika kwa kuitikia wito wa kuongoza tukio hilo la Baraka na kumtakia mafanikio zaidi katika kulitumikia Taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Parokia, Karoli Paulo, alisema kanisa hilo litaendelea kuhubiri amani amani na kuwakumbusha waumini wake kuendelea kuwa na maadili mema, upendo na kuheshimiana pasipo kumbagua mtu.

Katika harambee hiyo iliyohusisha michango ya waumini na wadau mbalimbali, jumla ya Sh. Milioni 37 zimepatikana na kiasi cha fedha zinazohitaji ili kukamilisha ujenzi huo ni Sh. Milioni 49.

Kanisa hilo lenye vigango saba, chini ya Mapadri wa Shirika la Utume wa Yesu, lilianza mwaka 2001 na limekuwa kitovu muhimu cha ibada na huduma za kijamii kwa waumini wa eneo la Masakta.

Baadhi ya waumini wa kanisa hilo, akiwemo Paul Andrew alisema kukamilika kwa ujenzi wa kanisa hilo kutakuwa na tija kubwa kwa wananchi wa eneo hilo la Masakta na wilaya ya Hanang’ kwa ujumla.
Naibu Spika Mhe. Sillo akiongoza harambee hiyo.Viongozi wa kanisa hilo wakiwa kwenye harambee hiyo.
Muonekano wa kanisa hilo ambalo ujenzi wake unaendelea.
Chanzo za habari ni WH- NEWS

Mwandishi Wetu, Unguja

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema ahadi iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya ujenzi wa kituo cha kumbukumbu na Nyaraka za Muungano (Makavazi) inaelekea ukingoni.

Mhe. Masauni amesema hayo Disemba 28, 2025 wakati wa Uwekaji wa Jiwe la Msingi Jengo la Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla kuelekea shamrashamra za miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Amesema Mhe. Dkt. Samia alipokuwa Mnazi Mmoja, Zanzibar kwenye kampeni ya uchaguzi moja ya ahadi alizotoa ndani ya miaka mitano atakayofanya ni pamoja na ujenzi wa Makavazi ya Muungano ambapo yatakuwepo Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar.

“Nichukue fursa hii Mgeni rasmi kuwaelezea wananchi kwamba ahadi hiyo ya Mhe. Rais ya ujenzi wa makavazi inaelekea ukingoni, na hivi karibuni nilipata nafasi ya kutembelea jengo lililopo pale Dodoma na kwa kuanzia tutaanza na Dar es Salaam kwa kutumia kwa muda ukumbi wa Karimjee kisha Zanzibar,” amesema Mhe. Masauni.

Ameongeza kuwa makavazi hayo yatasaidia vijana kupata elimu baada ya kugundua kuna vijana wengi bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu mambo yanayohusu Muungano na historia ya nchi.

Amesisitiza kuwa moja ya mkakati wa utoaji wa elimu kwa umma kuhusu mambo yanayohusu Muungano, Ofisi ya Makamu wa Rais itahakikisha matumizi sahihi ya makavazi hiyo.

Mh. Masauni amesema kwenye makavazi hayo kutakuwa na uhifadhi wa vitu mbalimbali ambapo wananchi watakuwa wanakwenda kuona na kujifunza, hivyo uwepo wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar na Makavazi itakuwa suluhisho kwa wengi kujua historia ya nchi.

Maeneo yaliyopendekezwa katika makavazi hiyo ni pamoja na sehemu ya kuhifadhi nyaraka, eneo la kupokelea nyaraka, eneo la uhifadhi nyaraka, eneo la kusomea, ukumbi wa mikutano, eneo la makumbusho na eneo la utawala.


Timu ya Vodacom Tanzania  kanda ya ziwa ikiendelea kusambaza upendo kwa wateja wake kwa kugawa Kapu la Vodacom ikiwa ni ishara ya kusherehekea msimu huu wa sikukuu pamoja na wateja wao na kuhitimisha sherehe za Miaka 25 ya utendaji wa kampuni hiyo hapa nchini. Hafla hii imefanyika katikati ya mwezi Disemba wilaya ya Karagwe, mkoani Kagera.


WAKALI wa ubashiri Tanzania, Meridianbet wanakwambia kuwa leo hii ipo kwaajili ya kuhakikisha hawakuachi patupu. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi za leo hivyo bashiri sasa.

Kama kawaida michuano ya AFCON itaendelea ambapo Comoros atakuwa kibaruani dhidi ya Mali moja ya timu ambazo ngumu na zenye wachezaji wenye ubora wa hali ya juu. Mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili, mwenyeji alipoteza hivyo leo hii ni siku ya wao kulipa kisasi. Je wanaweza kupata ushindi?. Bashiri hapa.

Mtanange mwingine ni huu wa Zambia dhidi ya Morocco ambao ni washindi wa 3 Kombe la Dunia 2022 kule Qatar. Pia timu hiyo ipo kwenye timu ambazo zinapewa nafasi kubwa ya kushinda taji hili. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Bashiri hapa.

Angola vs Egypt ni moja ya mechi kali kabisa kupigwa huku kila timu ikihitaji kushinda mechi hii. Ikumbukwe kuwa Mafarao ndio wenye mataji mengi kwenye michuano hii. Mara ya mwisho kukutana hawa wawili hakuna ambaye aliondoka na ushindi. Meridianbet inakwambia kuwa ODDS KUBWA zipo hapa. Jisajili hapa.

Pia naye Zimbabwe ataumana dhidi ya South Africa ambao mechi yao ya mwisho ya kwenye mashindano walipata ushindi, huku wenyeji wao walipoteza mechi yao ya mwisho. Je nani kuondoka na pointi 3 za uhakika pale Meridianbet?. Suka jamvi hapa.

Ondoka na ushindi haraka kwenye michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

CHAMPIONSHIP kule Uingereza itaendelea pia ambapo Conventry atakipiga dhidi ya Ipswich ambapo tofauti ya pointi kati yao ni 13 huku takwimu zikionesha kuwa mechi ya mwisho kukutana hawa wawili, mwenyeji alipasuka. Je loe hii ni siku ya mwenyeji kulipa kisasi akiwa kama kinara wa ligi?. Bashiri hapa.

Nao Leicester City ataumana dhidi ya Derby Country ambao mpaka sasa ana pointi 30 huku mwenyeji wake akiwa na pointi 31. Tofauti yao ni pointi 1 pekee huku kila timu ikihitaji ushindi kusogea juu kwenye msimamo wa ligi. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa leo. Beti sasa.

Piga pesa mechi hii ya Norwich City vs Watford huku tofauti yao hadi sasa kwenye msimamo wa ligi ikiwa ni 12. Nafasi ambayo yupo mwenyeji ni mbaya sana na anataka ashinde mechi hii atoke huko chini alipo. Lakini je anaweza kushinda mbele ya mgeni wake ambaye yupo nafasi ya 14. Suka jamvi hapa.

Pia West Bromwich atakuwa dimbani kukiwasha dhidi ya QPR ambao wanashika nafasi ya 9 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 16. Kila timu inahitaji ushindi leo hii iweze kujiweka nafasi nzuri kwenye ligi. Meridianbet wameweka machaguo zaidi ya 1000 kwenye mechi hii. Jisajili hapa.

MERIDIANBET imeamua kukubadilisha kabisa maana ya ushindi. Sasa, si suala la kufurahia mchezo pekee, ni kuhusu kuondoka na kifaa cha kisasa mkononi. Kupitia promosheni mpya kabisa, wachezaji wa Aviator wanapata nafasi ya kushinda simu mpya ya Samsung A26 kila wiki, bila presha wala masharti magumu.

Aviator si mchezo wa bahati nasibu wa kawaida. Ni mchezo wa maamuzi ya haraka, umakini wa hali ya juu na uwezo wa kusoma muda. Kadri ndege inavyopaa, ndivyo faida inavyoongezeka lakini mwenye ushindi ni yule anayejua ni lini achukue hatua ya kuitoa pesa yake kabla ya ndege kuanguka. Ni mchezo unaochanganya akili, hisia na msisimko wa sekunde chache zenye thamani kubwa.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Meridianbet imechukua msisimko huo na kuupa maana mpya kwa kuambatanisha ushindi wa kidijitali na zawadi halisi. Kupitia promosheni hii, mchezaji mmoja anachaguliwa kila Jumatatu na kuondoka na Samsung A26 mpya kabisa, zawadi inayothibitisha kuwa Aviator si mchezo wa kupatia tu pesa, ni fursa ya kuboresha maisha.

Kinachovutia zaidi ni urahisi wa kushiriki. Hakuna kiwango kikubwa cha dau la kuanzia, hakuna masharti ya baada ya ushindi. Unachotakiwa kufanya ni kucheza Aviator kama kawaida kupitia tovuti ya meridianbet.co.tz au programu ya Meridianbet, na tayari unakuwa ndani ya mbio za ushindi. Kila dau ni nafasi mpya.

Kwa yeyote aliyekuwa akisubiri ishara ya kuanza au kurejea kwenye ubashiri wa kisasa, huu ndio wakati. Aviator inapaa, Samsung A26 inangoja mshindi, na Meridianbet inaendelea kuthibitisha kwa vitendo kuwa ushindi wa kweli una ladha zaidi unapokuja bila jasho. Jiunge sasa meridianbet na ruhusu ushindi ukutafute.



Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, ameliagiza Jeshi la Polisi Wilaya ya Kipolisi Ilala, kupitia Kamanda wake ACP Yustino Mgonja, kuhakikisha linawakamata mara moja watu wote waliohusika na mauaji ya kikatili ya mwananchi Salehe Iddi Salehe.

Marehemu Salehe Iddi Salehe alivamiwa nyumbani kwake katika Mtaa wa Zavala, Kata ya Buyuni, Jijini Dar es Salaam, tarehe 04 Desemba, 2025, majira ya saa 11 alfajiri, na kundi la watu wasiojulikana wanaodaiwa kuwa wahalifu. Baada ya kushambuliwa kikatili, alifariki dunia siku hiyo hiyo akiwa njiani akipelekwa Hospitali ya Amana, majira ya saa 2 asubuhi.

Akizungumza katika mkutano wa wananchi wa Mtaa wa Zavala, DC Mpogolo alisema marehemu alikuwa mzalendo wa kweli aliyepigania kwa muda mrefu kulinda maeneo ya wazi ya Serikali, ikiwemo ardhi za shule, masoko na vituo vya afya, dhidi ya genge la wahalifu waliokuwa wakiyauza kinyume cha sheria.

Alifafanua kuwa maeneo hayo ni sehemu ya viwanja vilivyopimwa na Serikali kupitia Programu ya Viwanja 20,000 katika Kata ya Buyuni kati ya miaka 2003 hadi 2005, ambapo marehemu alikuwa mstari wa mbele kupinga uvamizi na uuzwaji wa maeneo ya umma.

Mpogolo aliongeza kuwa Jeshi la Polisi, chini ya uongozi wa ACP Mgonja, lina mifumo na nyenzo madhubuti za kiuchunguzi na ukamataji, hivyo aliwataka wananchi kuliamini Jeshi hilo ili kurejesha hali ya usalama na kuimarisha utawala wa sheria katika Wilaya ya Ilala.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alimwagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, kupitia Idara ya Mipango, kuendelea kubaini, kutambua na kurejesha maeneo yote ya wazi ya huduma za jamii yaliyotengwa na kulipiwa na Serikali.

Pia alisisitiza kuwepo kwa ushirikiano wa karibu kati ya Jiji la Dar es Salaam na Jeshi la Polisi ili kubaini na kuvunja genge la wahalifu wa ardhi wanaouza viwanja vya umma kwa wananchi wasio na uelewa wa kisheria.


Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya mwenendo wa Mvua Kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Imeeleza kuwa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini zimesababisha uharibifu wa miundombinu muhimu, ikiwemo reli, barabara na mifumo ya umeme, hali iliyoathiri shughuli za usafiri wa abiria na shehena katika baadhi ya maeneo.

Katika taarifa iliyotolewa na TMA leo Desemba 28, 2025 imeeleza kuwa mvua hizo zimeathiri reli ya zamani ya MGR baada ya madajara kuharibika katika eneo la Kidete wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro, pamoja na eneo la Gulwe wilayani Dodoma. Aidha, kumekuwepo na hitilafu za umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na umeme wa reli ya kisasa ya SGR, hali iliyosababisha usumbufu katika utoaji wa huduma za usafiri.

Pia imeeleza barabara kuu ya Morogoro–Iringa, hususani eneo la Mama Marashi hadi Mikumi, imeripotiwa kukumbwa na maporomoko ya mawe na tope yaliyorundikana barabarani, jambo lililosababisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara hiyo na kuchelewesha safari.

TMA imetoa ufafanuzi kuhusu hali hiyo kuwa ni sehemu ya vipindi vya mvua kubwa vilivyokuwa vimetolewa tahadhari kuanzia tarehe 26 hadi 29 Desemba 2025. Kwa mujibu wa TMA, mikoa iliyotabiriwa kuathirika ni pamoja na Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Dodoma, Singida, Songea, Morogoro, Lindi, Mtwara, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikiwemo Kisiwa cha Mafia) pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

"Hadi kufikia saa 3:00 asubuhi ya leo, vituo vya hali ya hewa vimerekodi viwango vikubwa vya mvua vilivyozidi milimita 50 ndani ya saa 24 katika maeneo ya Same (milimita 94.5), Morogoro (milimita 58.6) na Tabora (milimita 55.4). Vituo vingine vilivyopata mvua ni Hombolo (milimita 49.5), Kibaha (milimita 43.6), Dodoma (milimita 36.6) na Iringa (milimita 35.6)." imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

TMA imeeleza kuwa mifumo ya hali ya hewa inaonesha kuendelea kuimarika kwa ukanda wa mvua, hali itakayochangia kuendelea kwa vipindi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Mara, Simiyu, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Morogoro, Ruvuma, Lindi na Mtwara kesho tarehe 29 Desemba 2025.

Kwa upande wake, Serikali imesema inaendelea kuchukua hatua za haraka kurejesha hali ya kawaida katika miundombinu iliyoharibiwa ili kuhakikisha usalama wa wananchi na kuendelea kwa shughuli za kiuchumi huku wananchi wakitakiwa kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri wa hali ya hewa kutoka TMA na kuzingatia ushauri wa wataalam ili kujikinga na athari zinazoweza kujitokeza.




Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linaendelea kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati wa utafiti wa mafuta na gesi asilia katika kitalu cha Eyasi–Wembere, kinachojumuisha mikoa mitano ya Simiyu, Singida, Arusha, Shinyanga na Tabora, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na nafuu nchini.


Mradi huo unatekelezwa katika wilaya za Meatu (Simiyu), Iramba na Mkalama (Singida), Karatu na Ngorongoro (Arusha), Kishapu (Shinyanga) pamoja na Igunga (Tabora), ukiwa na lengo la kuongeza vyanzo vya nishati (energy mix) kwa ajili ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya wananchi.


Akizungumza na waandishi wa habari katika kambi ya Utafiti iliyoko katika kijiji cha Endesh, wilayani Karatu, Meneja Mradi, Mjiofizikia Sindi Maduhu, amesema utekelezaji wa mradi huo unatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Petroli ya mwaka 2015, inayoipa TPDC jukumu la kufanya utafutaji na uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia nchini.


Maduhu amesema kuwa katika awamu ya pili ya mradi, TPDC inaendelea na ukusanyaji wa taarifa za mitetemo (2D seismic data acquisition) kwa kutumia vilipuzi, hatua inayotokana na hali ya kijiografia ya maeneo yaliyosalia, yaliyoko katika ukanda wa ziwa Eyasi na kitangiri na maeneo oevu yanayohitaji mbinu maalum za kitaalamu.


“Awamu ya pili ya mradi ilianza rasmi mwezi July 2024 ambapo asilimia 47 tulitumia magari maalum ya mitetemo na kufikia juni 2025 tulianza maeneo yenye ziwa kwa kutumia vilipuzi. Hadi sasa imefikia takribani asilimia 69 ya utekelezaji, huku gharama za jumla zikifikia Shilingi bilioni 28,” amesema Maduhu.


Ameongeza kuwa mradi huo umeleta manufaa ya moja kwa moja kwa jamii zinazozunguka maeneo ya utekelezaji, ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa takribani vijana 1000 kutoka maeneo husika, sambamba na utekelezaji wa miradi ya uwajibikaji kwa jamii (CSR).


Miradi hiyo ya kijamii imejumuisha uchimbaji wa visima vya maji, ujenzi wa malambo ya mifugo pamoja na ugawaji wa vifaa vya michezo katika shule za msingi na sekondari, hatua inayolenga kuboresha huduma za kijamii na ustawi wa wananchi.


Hata hivyo, Maduhu amesema mradi huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi, ambapo maeneo yaliyotarajiwa kuwa na maji yamekauka na kusababisha vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya kutumika kwenye maeneo hayo kushindwa kufanya kazi , hali inayoongeza ugumu na gharama katika zoezi la ukusanyaji wa taarifa za utafiti.


Licha ya changamoto hizo, TPDC imeeleza kuwa itaendelea kutekeleza mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu, usalama na ulinzi wa mazingira, ili kuhakikisha malengo ya kitaifa ya utafiti na maendeleo ya sekta ya mafuta na gesi yanafikiwa kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.





















Top News