Kikao hicho kilimshirikisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi , Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu , Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Regina Quarry na baadhi ya Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu pamoja, Watendaji wa Wizara hizo na baadhi ya Wakuu wa Mikoa.
Habari Za Hivi Punde Habari Za Hivi Punde
Soma zaidi Mbaraka Mwinshehe aliwahi kuimba akiisifia Morogoro na jinsi maji yanavyotiririka kutoka milimani.
Mwinshehe angekuwa hai pengine angefika maporomoko ya maji Endoro (Endoro Waterfalls) kushuhudia maajabu ya maporomoko hayo yaliyopambwa na msitu uliosheheni sauti za ndege na kupambwa na ulinzi wa Wanyamapori mbalimbali.
Mwinshehe angesema ama kweli Mungu anajua kuumba!!! haya ni maporomoko ya aina yake na hapa hupaswi kuwa na mtazamo wa wahenga kwamba Chema chajiuza na kibaya chajitembeza laah hashaa,
Maporomoko haya ya maji Endoro ni eneo zuri lililopo kusini ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, takribani kilomita 6.5 kutoka mji wa Karatu.
Njia ya kuelekea maporomoko haya hupitia msitu na Mapango ya Tembo (Elephants Caves), na huchukua takribani saa 2–3 za matembezi ya wastani.
Mto Endoro hutiririsha maji mwaka mzima kutoka kwenye kingo za korongo, ukilishwa na chemchem za asili kutoka nyanda za juu za Ngorongoro, na kuanguka kwa urefu wa zaidi ya mita 40.
Naaam, njia ya kuelekea kwenye maporomoko hayo inapita sehemu ya msitu wa nyanda za juu kaskazi katika hifadhi ya Ngorongoro ambapo wapenda ndege na wanyamapori wakubwa kama tembo, nyati na nguruwe pori, Simba na wanyama wengine watakapopanda watakuwa na kumbukumbu isiyosahaulika
Hayo ni maporomoko ya maji ya Endoro ukifika huko utatamani uoge maji hayo na hasa ukiyavulia nguo.
Karibu Ngorongoro,
Maajabu yasiyoisha yanakuita.
Tumerithishwa, Tuwarithishe
Mwinshehe angekuwa hai pengine angefika maporomoko ya maji Endoro (Endoro Waterfalls) kushuhudia maajabu ya maporomoko hayo yaliyopambwa na msitu uliosheheni sauti za ndege na kupambwa na ulinzi wa Wanyamapori mbalimbali.
Mwinshehe angesema ama kweli Mungu anajua kuumba!!! haya ni maporomoko ya aina yake na hapa hupaswi kuwa na mtazamo wa wahenga kwamba Chema chajiuza na kibaya chajitembeza laah hashaa,
Maporomoko haya ya maji Endoro ni eneo zuri lililopo kusini ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, takribani kilomita 6.5 kutoka mji wa Karatu.
Njia ya kuelekea maporomoko haya hupitia msitu na Mapango ya Tembo (Elephants Caves), na huchukua takribani saa 2–3 za matembezi ya wastani.
Mto Endoro hutiririsha maji mwaka mzima kutoka kwenye kingo za korongo, ukilishwa na chemchem za asili kutoka nyanda za juu za Ngorongoro, na kuanguka kwa urefu wa zaidi ya mita 40.
Naaam, njia ya kuelekea kwenye maporomoko hayo inapita sehemu ya msitu wa nyanda za juu kaskazi katika hifadhi ya Ngorongoro ambapo wapenda ndege na wanyamapori wakubwa kama tembo, nyati na nguruwe pori, Simba na wanyama wengine watakapopanda watakuwa na kumbukumbu isiyosahaulika
Hayo ni maporomoko ya maji ya Endoro ukifika huko utatamani uoge maji hayo na hasa ukiyavulia nguo.
Karibu Ngorongoro,
Maajabu yasiyoisha yanakuita.
Tumerithishwa, Tuwarithishe
Katibu wa Uenezi, Itikadi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi, anatarajiwa kuanza ziara yake ya kimkakati nchi nzima itakayozinduliwa rasmi Januari 18, 2026 Wilayani Manyoni mkoani Singida.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 17 jijini Dodoma, amesema ziara hiyo itahusisha kutembelea wilaya zote za Mkoa wa Singida na kufanya mikutano ya hadhara kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.
Amesema lengo kuu la ziara hiyo ni kuwafikia wananchi wa ngazi ya chini ili kutatua changamoto zao, kuisimamia serikali, kuimarisha uimara wa chama, pamoja na kuhakikisha maendeleo ya wananchi kwa kufuatilia utekelezaji wa ahadi za Rais alizozitoa kipindi cha kampeni, ikiwemo ahadi ya kutekelezwa ndani ya siku 100, ili kubaini utekelezaji wake umefikia wapi au matarajio ya lini zitatimia.
Ameeleza kuwa katika ziara hiyo ya nchi nzima, CCM itahakikisha inawakumbusha wananchi wapi nchi ilipotoka na ilipo sasa, akitolea mfano maendeleo katika sekta ya umeme ambapo kwa sasa vijiji vyote nchini vimefikiwa na huduma ya umeme, na sasa ni zamu ya vitongoji vyote kupata huduma hiyo.
Akigusia wajibu wa chama, amesema ni kusikiliza wananchi na kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi, akisisitiza kuwa watu wote ni sawa na hakuna aliye muhimu kuliko mwingine. Amesema ni jukumu la jamii kuangalia vyama vyenye ajenda ya umoja, mshikamano na amani.
Ameongeza kuwa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan itafanya kazi kwa karibu sana na wananchi, ambapo ziara hiyo itafika hadi ngazi za mashina, matawi na kata, pamoja na kukutana na mabalozi wa CCM ambao ni msingi imara wa chama katika kuwafikia wananchi wote kwenye maeneo yao.


-Yataka Waajiri Sekta Binafsi kuzingatia viwango vilivyowekwa
Na: OWM (KAM) – Dodoma
Serikali imetoa tamko kuhusu amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi na kuwataka waajiri na wafanyakazi wa sekta hiyo kuzingatia viwango vilivyowekwa katika utekelezaji wa amri hiyo.
Hayo yamebainishwa Januari 16, 2025 Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu wakati akitoa ufafanuzi kuhusu Amri ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi.
Mhe. Sangu amesema amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi imeanza kutumika kuanzia tarehe 1 Januari, 2026 na ilitangazwa kupitia Gazeti la Serikali la tarehe 13 Oktoba, 2025 ambapo kima cha chini cha Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 33.4.
Amesema, zoezi la mapitio ya kima cha chini cha Mshahara lilikuwa shirikishi ambapo Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi walikubaliana utekelezaji wake.
“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi pamoja na Vyama vayo ili kuhakikisha mazingira ya kazi na hali za wafanyakazi zinaboreshwa ili kukuza tija na ustawi wa wafanayakazi,” amesema
Vilevile, Waziri Sangu amewataka Maafisa Kazi pamoja na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutoa elimu na ushauri kwa waajiri na wafanyakazi kuhusu utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara.
Kwa upande mwengine, Mhe. Sangu amesema Ofisi ya Waziri Mkuu itafuatilia suala hilo katika maeneo yote ya kazi, hivyo Serikali itawachukulia hatua waajiri ambao hawatatekeleza agizo hilo. Pia, ametoa wito kwa Waajiri na Wafanyakazi wa Sekta Binafsi kuelewa viwango vya kima cha chini vilivyoainishwa katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, afya, mawasiliano, usafirishaji, hoteli, madini, biashara na viwanda, shule binafsi, huduma za ulinzi binafsi, nishati, uvuvi na huduma ya baharini, michezo na utamaduni pamoja na huduma nyingine.
“Hatutapenda kuona migogoro inatokea katika maeneo ya kazi kwa sababu ya ucheleweshaji wa utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara katika sekta binafsi,” amesema
Na: OWM (KAM) – Dodoma
Serikali imetoa tamko kuhusu amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi na kuwataka waajiri na wafanyakazi wa sekta hiyo kuzingatia viwango vilivyowekwa katika utekelezaji wa amri hiyo.
Hayo yamebainishwa Januari 16, 2025 Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu wakati akitoa ufafanuzi kuhusu Amri ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi.
Mhe. Sangu amesema amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi imeanza kutumika kuanzia tarehe 1 Januari, 2026 na ilitangazwa kupitia Gazeti la Serikali la tarehe 13 Oktoba, 2025 ambapo kima cha chini cha Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 33.4.
Amesema, zoezi la mapitio ya kima cha chini cha Mshahara lilikuwa shirikishi ambapo Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi walikubaliana utekelezaji wake.
“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi pamoja na Vyama vayo ili kuhakikisha mazingira ya kazi na hali za wafanyakazi zinaboreshwa ili kukuza tija na ustawi wa wafanayakazi,” amesema
Vilevile, Waziri Sangu amewataka Maafisa Kazi pamoja na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutoa elimu na ushauri kwa waajiri na wafanyakazi kuhusu utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara.
Kwa upande mwengine, Mhe. Sangu amesema Ofisi ya Waziri Mkuu itafuatilia suala hilo katika maeneo yote ya kazi, hivyo Serikali itawachukulia hatua waajiri ambao hawatatekeleza agizo hilo. Pia, ametoa wito kwa Waajiri na Wafanyakazi wa Sekta Binafsi kuelewa viwango vya kima cha chini vilivyoainishwa katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, afya, mawasiliano, usafirishaji, hoteli, madini, biashara na viwanda, shule binafsi, huduma za ulinzi binafsi, nishati, uvuvi na huduma ya baharini, michezo na utamaduni pamoja na huduma nyingine.
“Hatutapenda kuona migogoro inatokea katika maeneo ya kazi kwa sababu ya ucheleweshaji wa utekelezaji wa amri ya kima cha chini cha Mshahara katika sekta binafsi,” amesema

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania- TASAC Bw. Mohamed Salum leo tarehe 16 Januari, 2026 amehitimisha rasmi mafunzo kwa watumisi wapya 25 yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Wakati akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu amewaasa watumishi hao kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, nidhamu ya kazi, ushirikiano na ubunifu katika kazi.

“Ndugu watumishi, napenda kuwakumbusha na kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kuzingatia maadili katika utumishi wa umma, nidhamu kazini, ushirikiano na kuendelea kujifunza kwakuwa Sekta ya usafiri kwa njia ya maji inakuwa kwa kasi sana kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia” amesema Bw. Salumu.

Pia, amewasihi kuzingatia kanuni na miongozo katika kutekeleza majukumu yao.
“Napenda mtambue yakuwa mmepewa dhamana kubwa na serikali hivyo ni vema kuzingatia Kanuni, Sheria, Taratibu na Miongozo mbalimbali inayosimamia utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kutunza siri, nidhamu na utii kwa viongozi wa serikali, kuendeleza mashirikiano, kutoa huduma bora kwa wateja, kulinda mali za Shirika pamoja na kufuata sheria na miongozo inayoongoza utekelezaji wa majukumu ya TASAC.

Mwisho Mkurugenzi Mkuu aliwakaribisha watumishi wapya TASAC na kuwatakia utekelezaji mwema wa Majukumu yao.



Mafunzo yalikuwa ya siku 14 ambapo watumishi hao wali kabidhiwa vyeti vya ushiriki na kukaribishwa katika utumishi wa umma.

.jpg)





.jpg)



Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Prof.Peter Msofe amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri na Wataalam katika Wilaya nne zinazotekeleza mradi wa kuongoa ardhi na urejeshaji wa uoto wa asili wa IKI-FLR kusimamia kwa dhati na uadilifu mkubwa huku wakitoa ushirikiano wa kutosha ili kufikia malengo ya mradi huo unaotekelezwa na Shirila la WWF na Wadau wenza.
Sambamba na kuwataka kuendelea kuhamasisha wananchi wa Wilaya hizo nne za Mikoa miwili ya Tanga na Dodoma ili waweze kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mradi huo pamoja na lengo la kupanda miti milioni moja na nusu kila mwaka Wilaya zote kuendelea kufanyiwa kazi kama inavyoelekezwa.
Prof.Msofe ameyasema hayo Jijini Dodoma katika Uzinduzi wa mradi wa uongoaji wa ardhi na kurejesha uoto wa asili unaosimamiwa na wadau mbalimbali kufadhiliwa na Serikali ya Ujerumani.
Ambapo amesema Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais itakuwa mstari wa mbele kuunga mkono na kutoa ushirikiano kamili kuona mradi huu unaleta matokeo tarajiwa na hata zaidi ya pale inapowezekana.
"Wakurugenzi ambao ndio wasimamizi wa Halmashauri na wataalam wa zile Wilaya nne za mradi ,Niwaagize kwamba msimamie kwa dhati na kwa uadilifu mkubwa mradi huu huku mkitoa ushikiano wa kutosha kwa watekelezaji wa mradi ili kufanya shughuli zao kwa ustadi".
Aidha Prof Msofe ametoa Wito kwa wadau watekelezaji wa mradi huo WWF,WRI na IUCN kuhakikisha suala la uharibifu wa mazingira unadhibitiwa pamoja na kuhakikisha upotevu wa misitu unapungua kwa kiasi kikubwa.
"Nitoe Wito kwa wadau watekelezaji wa mradi huu WWF,WRI na IUCN hakikisheni suala la uharibifu wa mazingira unadhibitiwa na upotevu wa misitu unapungua kwa kiasi kikubwa kwani mmeshajipambanua Tanzania na Duniani kote kuwa ninyi ni Taasisi makini na madhubuti".
Awali akitoa salamu za Shirika la WWF Dkt. Lawrence Mbwambo amesema kuwa Shirika hilo lina miaka 60 tangu kuanzishwa kwake na katika kipindi chote hicho Serikali ya Tanzania imekuwa ikiwashika mkono katika utekelezaji wa majukumu yao ambayo imepelekea kudumu na mafanikio waliyonayo.
Naye Bwana Almas Kashindye akitoa Taarifa ya mradi amesema kuwa lengo la mradi huu ni kurejesha uoto wa asili katika maeneo ambayo yameharibiwa na shughuli mbalimbali za kibinadamu na za kiasili na pia wanataka kulinda na kuhifadhi bioanuwai ambayo itachangia kuboresha maisha ya wananchi wanaozunguka misitu.
Na kuongeza kuwa wameweka lengo la kurejesha uoto wa asili kwenye zaidi ya hekari elfu 40 za maeneo yaliyoharibiwa katika Wilaya 4 za mradi ambazo ni Tanga wilaya mbili ya Korogwe na Kilindi na Dodoma ni Mpwapwa na Chamwino.
Bwana David Kavishe akitoa salamu kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma amesema kuwa wao kama Taasisi ya Serikali ni washirika muhimu katika utekelezaji wa mradi na asili ya jambo hili inatoka mwaka 2018 ambapo Serikali ya Tanzania iliridhia azimio la Umoja wa Afrika wa kuongoa ardhi iliyoharibika ambapo Tanzania iliahidi kuongoa hekari milioni 5.2 ya ardhi iliyoharibika.
Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 5 na utagharimu kiasi cha Shilingi za Kitanzania Bilioni 5.4 katika Wilaya nne kwa Mpwapwa na Chamwino mkoa wa Dodoma na kwa Wilaya ya Korogwe na Kilindi Mkoa wa Tanga.





Mh. Magoti alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mheshimiwa Kunenge, katika hafla ya kufunga mafunzo hayo yaliyolenga kuwawezesha Madiwani kutambua na kutekeleza vyema majukumu yao ya uwakilishi wa wananchi katika kata zao.
KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Tanzania imewahakikishia wakazi wa Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, kuimarika kwa huduma za mawasiliano na intaneti baada ya kuzindua rasmi mnara mpya wa kisasa katika eneo hilo.
Uzinduzi huo uliopokelewa kwa shangwe na wananchi, viongozi wa serikali pamoja na vijana, ni sehemu ya mkakati wa Airtel wa kupanua wigo wa huduma zake na kuhakikisha maeneo ya pembezoni yanafikiwa na huduma bora za mawasiliano.
Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Kelvin Msumule, Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa pamoja na Maendeleo ya Vijana Wilaya ya Kongwa, amesema uzinduzi wa mnara huo ni hatua muhimu katika kuwawezesha vijana kiuchumi na kijamii kupitia matumizi ya teknolojia ya kidijitali.
“Upatikanaji wa mawasiliano bora ni nyenzo muhimu katika kukuza vipaji, biashara za vijana na ajira za kidijitali. Mnara huu unafungua fursa nyingi kwa wananchi wa Wilaya ya Kongwa,” amesema Bw. Msumule.
Kwa upande wake, Bw. Gibson Renatus, Meneja wa Airtel Kanda ya Gairo, amesema kampuni hiyo imeendelea kusikiliza mahitaji ya wateja wake na kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha huduma zinaimarika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa.
“Airtel imejipanga kuhakikisha Watanzania wanapata huduma za uhakika.
Mnara huu ni matokeo ya maoni na maombi ya wananchi wa Wilaya ya Kongwa, na ni suluhisho la kudumu kwa changamoto za mawasiliano zilizokuwepo,” amesema Bw. Renatus.
Naye Bi. Jeni Maduma, mkazi wa Morisheni Wilayani Kongwa, ameishukuru Airtel kwa uwekezaji huo akisema kuwa utarahisisha mawasiliano, biashara ndogondogo pamoja na upatikanaji wa huduma za kifedha kupitia simu.
“Hapo awali mtandao ulikuwa changamoto kubwa, lakini sasa tuna matumaini mapya. Huu ni mwanzo mzuri wa maendeleo,” amesema Bi. Maduma.
Kwa upande wake, Bw. Baltazary Mikindo, mkazi wa Morisheni Wilayani Kongwa, amewahimiza wananchi kuulinda mnara huo ili uendelee kutoa huduma bila vikwazo.
“Miundombinu hii ni mali ya jamii. Ni jukumu letu sote kuilinda dhidi ya hujuma ili tuendelee kunufaika na huduma hizi muhimu,” amesema Bw. Mikindo.
Uzinduzi wa mnara huo umeelezwa kuja katika wakati muafaka ambapo serikali inaendelea kusisitiza matumizi ya TEHAMA katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku Airtel ikionyesha dhamira ya dhati ya kuwaunganisha Watanzania kupitia huduma bora za mawasiliano.a
Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema watakuwa wakali kwa watumishi watakaokiuka taratibu za utendaji na kusababisha migogoro ya ardhi.
Dkt. Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Januari, 2026 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakati wa kikao cha Wizara ya Ardhi na Kamati kilichokuwa na lengo la kuifahamu wizara ya ardhi na taasisi zake.
"Niihadi kamati, wizara yangu haiko tayari kuzalisha migogoro mipya na tunaona aibu kuongoza taasisi yenye migogoro" amesema Dkt. Akwilapo.
Amesema, katika kutekeleza majukumu yake, wizara ya Ardhi itahakikisha inazingatia sheria, kanuni na taratibu ili kupunguza migogoro ya ardhi iliyopo na kutokuzalisha migogoro ya ardhi mipya nchini.
"Tunona aibu migogoro ya ardhi kupelekwa kwa Wakuu wa Wilaya wakati wizara inayohusika na masuala ya ardhi ipo" amesema.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya amewaambia wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii kuwa, Wizara ya Ardhi haina uhusiano na migogoro ya ardhi bali yapo malalamiko yanayohusiana na masuala ya ardhi.
Ameomba ushirikiano na wajumbe wa kamati katika kushughulikia migogoro ya ardhi huku akisisitizia wizara y ardhi kusimamia watumishi wa sekta ya ardhi kuwa na maadili sambamba na kutenda haki wakati wa kutekeleza majukumu yao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utali Mhe. Timotheo Mnzava ameeleza kuwa, pamoja na kazi kubwa inayofanya wizara ya Ardhi katika kushughulikia migogoro ya ardhi lakini bado wizara ina jukumu la kuongeza nguvu katika kushugulikia migogoro ya ardhi nchini.
Aidha, Kamati hiyo imeelekeza Wizara kuona namna bora ya kutumia ardhi kwa kujenga majengo yanayoendana na mahitaji ya sasa na baadae kwa kuzingatia kasi ya ongezeko la watu wakati ardhi haiongezeki inabakia ni ileile.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja ametaka sheria na kanuni zifuatwe wakati wa kushughulika na watumishi wanaokiuka taratibu na kusababisha migogoro ya ardhi.
"Hili suala la watumishi tujitahidi kusimamia sheria vizuri tunahurumiana sana, tufikirie kwenye sheria why mtumishi amegawa viwanja mara mbili , tukisimamia tutafanikiwa" amesema
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia taasisi zake za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), vyuo vya Ardhi Morogoro (ARIMO) na Tabora (ARITA), Bodi ya Usimamizi wa Wapima, Bodi ya Usajili wa Wathamini pamoja na Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji imeelezea Muundo, majukumu, mafanikio na mipango ya taasisi zake mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema watakuwa wakali kwa watumishi watakaokiuka taratibu za utendaji na kusababisha migogoro ya ardhi.
Dkt. Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Januari, 2026 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakati wa kikao cha Wizara ya Ardhi na Kamati kilichokuwa na lengo la kuifahamu wizara ya ardhi na taasisi zake.
"Niihadi kamati, wizara yangu haiko tayari kuzalisha migogoro mipya na tunaona aibu kuongoza taasisi yenye migogoro" amesema Dkt. Akwilapo.
Amesema, katika kutekeleza majukumu yake, wizara ya Ardhi itahakikisha inazingatia sheria, kanuni na taratibu ili kupunguza migogoro ya ardhi iliyopo na kutokuzalisha migogoro ya ardhi mipya nchini.
"Tunona aibu migogoro ya ardhi kupelekwa kwa Wakuu wa Wilaya wakati wizara inayohusika na masuala ya ardhi ipo" amesema.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya amewaambia wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii kuwa, Wizara ya Ardhi haina uhusiano na migogoro ya ardhi bali yapo malalamiko yanayohusiana na masuala ya ardhi.
Ameomba ushirikiano na wajumbe wa kamati katika kushughulikia migogoro ya ardhi huku akisisitizia wizara y ardhi kusimamia watumishi wa sekta ya ardhi kuwa na maadili sambamba na kutenda haki wakati wa kutekeleza majukumu yao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utali Mhe. Timotheo Mnzava ameeleza kuwa, pamoja na kazi kubwa inayofanya wizara ya Ardhi katika kushughulikia migogoro ya ardhi lakini bado wizara ina jukumu la kuongeza nguvu katika kushugulikia migogoro ya ardhi nchini.
Aidha, Kamati hiyo imeelekeza Wizara kuona namna bora ya kutumia ardhi kwa kujenga majengo yanayoendana na mahitaji ya sasa na baadae kwa kuzingatia kasi ya ongezeko la watu wakati ardhi haiongezeki inabakia ni ileile.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja ametaka sheria na kanuni zifuatwe wakati wa kushughulika na watumishi wanaokiuka taratibu na kusababisha migogoro ya ardhi.
"Hili suala la watumishi tujitahidi kusimamia sheria vizuri tunahurumiana sana, tufikirie kwenye sheria why mtumishi amegawa viwanja mara mbili , tukisimamia tutafanikiwa" amesema
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia taasisi zake za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), vyuo vya Ardhi Morogoro (ARIMO) na Tabora (ARITA), Bodi ya Usimamizi wa Wapima, Bodi ya Usajili wa Wathamini pamoja na Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipangomiji imeelezea Muundo, majukumu, mafanikio na mipango ya taasisi zake mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakati wa kikao cha Kamati na wizara yake kilichokuwa na lengo la kuifahamu wizara ya ardhi na taasisi zake tarehe 16 Januari, 2026, Kushoto ni Naibu Waziri Kaspar Mmuya na Kulia ni Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya akizungumza katika kikao cha Kamati na wizara kilichofanyika jijini Dodoma tarehe 16 Januari, 2026. Katikati ni Waziri wa Ardhi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo na Kulia ni Katibu Mkuu Mhandisi Anthony Sanga
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza wakati wa kikao cha kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kilichofanyika jijini Dodoma tarehe 16 Januari 2026


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakiwa katika kikao cha kamati na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kilichofanyika jijini Dodoma tarehe 16 Januari 2026
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakiwa katika kikao cha kamati na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kilichofanyika jijini Dodoma tarehe 16 Januari 2026
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Hamad Abdallah akiwasilisha Taarifa ya shirika lake mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakati wa kikao cha Kamati na Wizara ya Ardhi kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma tarehe 16 Januari, 2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Timotheo Mnzava akizungumza wakati wa Kikao cha Kamati yake na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kilichofanyika jijini Dodoma tarehe 16 Januari 2026
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Mary Francis Masanja akizungumza wakati wa kikao cha Kamati na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bungeni jijini Dodoma tarehe 16 Januari, 202 (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
Subscribe to:
Comments (Atom)







.jpeg)
















