Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
TAASISI zinazojihusisha na sekta ya ubaharia zimetakiwa kuimarisha ushirikiano ili kuwawezesha wanafunzi wanaohitimu masomo ya ubaharia kupata ajira kwenye meli mbalimbali na kuchangia ukuaji wa sekta hiyo nchini.

Wito huo umetolewa leo Julai 4, 2026 na Kiongozi wa Taasisi ya Mission for Seafarers, Father Johnson Lameck, wakati wa maadhimisho ya Siku Maalumu ya Kuwakumbuka na Kuwaombea Dua Mabaharia waliotangulia mbele za haki.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Father Lameck alisema Tanzania imejaliwa kuwa na bahari pamoja na fursa nyingi za uchumi wa buluu, hivyo kuna umuhimu wa taasisi zinazohusika na sekta ya ubaharia kushirikiana katika kuwaandaa wahitimu na kuwaunganisha na soko la ajira.

“Hapa nimesikia zipo taasisi mbalimbali. Tuone namna gani tunaweza kushirikiana na wanaosomesha mabaharia na kuwapatia vyeti. Kazi zao ni za meli na shughuli nyingine mbalimbali,” alisema.

Alisema kuna haja ya taasisi hizo kushirikiana na Chuo cha Mabaharia Dar es Salaam (DMI) ili wanafunzi wanaomaliza masomo wapate nafasi za ajira kwenye meli mbalimbali.

“Tuone namna gani tunaweza tukajikondesha na DMI ili wanafunzi hawa wanaomaliza waweze kupata ajira kwenye meli hizo. Hicho ndicho kilio chao kikubwa pale kwetu. Tunafahamu na tunaangalia namna gani tunaweza kusaidia wakapata ajira kwenye meli mbalimbali,” alisema.

Aidha, aliwataka viongozi wa taasisi mbalimbali kuweka mikakati ya pamoja ya kuwawezesha vijana kupitia miradi mbalimbali itakayochochea maendeleo yao na kuimarisha sekta ya ubaharia.

Pia alisisitiza kuwa sekta ya uchumi wa buluu ina fursa kubwa za ajira na maendeleo, akihimiza vijana kuzitumia rasilimali za bahari kujijengea uchumi na kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa upande mwingine, Father Lameck alitoa salamu za pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao baharini na kuwataka Watanzania kuendelea kuwaombea ili wapate faraja na nguvu wanapoendelea kuwakumbuka waliotangulia mbele za haki.

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka rekodi mpya katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya jumla ya Shilingi trilioni 37.96 katika mwaka wa fedha 2025/26, sawa na asilimia 105.24 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni 36.07.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, leo Julai 04, 2026 imeeleza kuwa mafanikio hayo katika makusanyo ya kodi ni sawa na ukuaji wa asilimia 17.61 ikilinganishwa na makusanyo ya Shilingi trilioni 32.27 yaliyopatikana katika mwaka wa fedha 2024/25.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na kuendelea kutumia mbinu za kisasa katika usimamizi wa kodi, kuimarisha uzingatiaji wa sheria za kodi pamoja na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Takwimu zinaonyesha kuwa katika miezi yote 12 ya mwaka wa fedha uliomalizika Juni 2026, TRA ilifanikiwa kuvuka malengo ya makusanyo ambapo kwa Mwezi Juni wameweka rekodi mpya kwa kukusanya Shilingi trilioni 4.01, sawa na ufanisi wa asilimia 107.98, huku Januari, Machi na Aprili pia zikifanya vizuri kwa kuvuka malengo yaliyowekwa.

Katika taarifa hiyo, TRA imeeleza kuwa mafanikio hayo yameiwezesha mamlaka hiyo kuweka rekodi mpya nne katika usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali nchini, hatua inayodhihirisha kuendelea kuimarika kwa mifumo ya kodi na usimamizi wa mapato.

Mamlaka hiyo imewahakikishia wananchi na wadau mbalimbali kuwa itaendelea kuboresha huduma kwa walipakodi, kuimarisha matumizi ya teknolojia na kuhakikisha mapato ya Serikali yanaongezeka kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma za kijamii.

Mafanikio ya TRA yanatarajiwa kuongeza uwezo wa Serikali kutekeleza bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27 kupitia mapato ya ndani, sambamba na kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo ya nje.

TRA yavunja rekodi ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo mbali na kuvuka malengo ya makusanyo kwa miaka miwili mfululizo, TRA pia imeweka rekodi mpya ya kukusanya mapato kwa miezi 24 mfululizo kuanzia Julai 2024 hadi Juni 2026, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mamlaka hiyo.

Katika kipindi hicho, wastani wa ufanisi wa makusanyo umefikia asilimia 104.64.

Aidha, mwezi Desemba 2025 uliweka historia mpya baada ya TRA kukusanya Shilingi trilioni 4.13 ndani ya mwezi mmoja, kiwango kilichovunja rekodi ya awali ya Shilingi trilioni 3.58 iliyowekwa Desemba 2024.

Kwa mwaka wa fedha 2025/26, wastani wa makusanyo ya kila mwezi umefikia Sh. trilioni 3.16, kutoka wastani wa Sh.trilioni 2.69 uliopatikana mwaka 2024/25.

Mafanikio hayo yameelezwa kuwa yametokana na uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kusimamia mageuzi ya ukusanyaji wa mapato kwa kusisitiza utii wa sheria za kodi, kuhamasisha ulipaji wa hiari, kupanua wigo wa walipakodi, kuimarisha matumizi ya mifumo ya TEHAMA na kuhakikisha kodi zinazokusanywa zinatumika katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika kipindi hicho, TRA imekamilisha ujenzi wa Mfumo wa Usimamizi wa Kodi za Ndani (IDRAS), ulioanza kutumika rasmi Februari 2026. Mfumo huo umeunganishwa na mifumo ya taasisi 52 za umma na taasisi 30 binafsi, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato na kurahisisha utoaji wa huduma kwa walipakodi.

Vilevile, kampeni za kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari zimeendelea kuzaa matunda, ambapo kiwango cha utii wa walipakodi kimeongezeka kutoka asilimia 77.48 mwaka 2020/21 hadi asilimia 85.71 mwaka 2024/25, huku pengo la kodi likipungua hadi asilimia 1.89.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, utekelezaji wa sera za kiuchumi zinazolenga kuhimili misukosuko ya uchumi duniani umechangia kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji na biashara nchini, hali iliyowezesha TRA kufikia ufanisi wa makusanyo wa wastani wa asilimia 105.24 katika mwaka wa fedha 2025/26, sambamba na ukuaji wa mapato wa asilimia 17.61.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi baada ya tafiti, kubadilishana uzoefu na stadi mbalimbali kutoka kwa Nchi zenye mbinu bora,teknolojia ya juu pamoja na uzoefu mkubwa wa kukabiliana na uhalifu,Amezindua Programu Maalumu ya Usalama,Maendeleo na Samia ambayo pia itashirikisha hatua za Mafunzo na Vifaa vya Kisasa kutoka nchi zilizoendelea Kiusalama lengo ikiwa ni kuimarisha na kuhusianisha Usalama na masuala ya Amani na Maendeleo Tanzania bara na visiwani .

Waziri Katambi amezindua Programu hiyo leo,jijini Dar es Salam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo akizungumza na mamia ya wafanyabiashara,machinga,madereva bodaboda,mamalishe na babalishe amesema suala la amani na usalama ni jukumu la kikatiba la serikali iliyochaguliwa na wananchi.

Amesisitiza kuwa kipaumbele cha Rais Samia ni Nchi Kwanza, Wananchi kwanza na Uchumi kwanza.

“Wizara hii ina dhamana ya masuala ya Ulinzi na Usalama, ina dhamana ya ulinzi wa kila raia, ina dhamana ya ulinzi wa kila mali ya raia, ina dhamana ya ulinzi wa Rasilimali za Taifa pamoja na mali za Taifa zinazomilikiwa na Umma" alisema Katambi

“Taarifa yoyote,maelezo yoyote,kauli yoyote,uchochezi wa aina yoyote unaolenga kuhatarisha amani ya mtu mmoja ambae ni raia wa Tanzania,sisi kama Serikali kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977 Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao na rasilimali za nchi ni jukumu la Serikali kwa kuhakikisha wananchi wanakua salama kwenye mazingira ya uzalishaji na shughuli za maendeleo”aliongeza Waziri Katambi

Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa wafanyabiashara,bodaboda,machinga,babalishe na mamalishe walisema wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwawekea mazingira sahihi ya kufanya shughuli zao huku wakiweka wazi nia yao ya kutotumika na kikundi cha watu wachache wanaotaka kuchafua amani ya nchi.

Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Ayoub Mohammed Mahmoud,Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo,Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,SACP William Mkonda,Viongozi wa Wafanyabiashara,Bodaboda,Wamachinga,Mamalishe na Babalishe pamoja na wananchi.


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itakamilisha mchakato wa kuunda Halmashauri ya Mwibara ili kusogeza huduma za Serikali karibu na wananchi na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za kijamii na maendeleo.

Ametoa kauli hiyo leo Julai 4, 2026, alipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Halmashauri ya Mji wa Bunda mkoani Mara, baada ya Mbunge wa Bunda Vijijini, Mhe. Boniface Mwita Getere, kuwasilisha ombi la wananchi la kuanzishwa kwa halmashauri hiyo.

Waziri Mkuu alisema Serikali imepokea hoja hiyo na kutambua umuhimu wake, akibainisha kuwa utaratibu wa kuanzisha halmashauri mpya utaendelea kufuatwa ili kuhakikisha huduma za Serikali zinawafikia wananchi kwa ufanisi zaidi.

"Nimeipokea hoja hii. Serikali ina utaratibu unaofuatwa katika kugawa maeneo ya kiutawala. Nimemuelekeza Mkuu wa Mkoa pamoja na Sekretarieti ya Mkoa kuendelea na mchakato huo ili Serikali iweze kupeleka mapendekezo kwenye mamlaka husika kwa hatua zinazostahili," alisema Waziri Mkuu.

Alisema Serikali imeendelea kutekeleza sera ya kusogeza huduma karibu na wananchi, ndiyo sababu imekuwa ikiendelea kuanzisha maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji wa kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma.

Katika kufafanua hatua za utekelezaji wa Serikali, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange, alisema Serikali itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma katika Wilaya ya Bunda kupitia uwekezaji katika sekta za afya, elimu na miundombinu, huku ikikamilisha hospitali, vituo vya afya na kuongeza watumishi wa sekta ya afya.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, alisema Serikali itaendelea na mpango wa kupanga matumizi bora ya ardhi na kupima vijiji, sambamba na kuimarisha mfumo wa usimamizi wa ardhi ili kudhibiti migogoro ya umiliki na kuhakikisha hati mbili hazitolewi katika eneo moja.

Naye Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, alisema Serikali itaendelea kukamilisha Mradi wa Maji wa Onyamswa pamoja na miradi mingine ya maji katika Bunda, akisisitiza kuwa kipaumbele ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kabla ya ujenzi wa miundombinu ya utawala.

Aidha, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, alisema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Mara, huku wananchi wa maeneo ya mijini yenye sifa za vijijini wakiendelea kunufaika na utaratibu wa kuunganishiwa umeme kwa gharama nafuu.

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha utawala bora na kusogeza huduma karibu na wananchi kupitia uanzishwaji wa maeneo mapya ya kiutawala pale inapobainika kuwa kuna uhitaji, sambamba na kuendelea kuwekeza katika sekta za afya, elimu, maji, nishati na miundombinu ya maendeleo.



Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) ni Bi. Bernadetta Ndunguru akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Baobab mkondo wa Amali Doreen Maki kuhusiana  Fani ya Umeme alivyojipanga katika kufikia malengo ya Uhandisi wa Umeme wakati Mwenyekiti Baraza hilo wakati alipotembelea banda la NACTVET katika maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) ni Bi. Bernadetta Ndunguru akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Bwiru mkoani Mwanza  mkondo wa Amali Daud Elias akipata kuhusiana  Fani ya Ujenzi wa Majengo  alivyojipanga katika kufikia malengo ya Uhandisi wa Uhandisi wa Majengo wakati Mwenyekiti Baraza hilo wakati alipotembelea banda la NACTVET katika maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET)  Bernadetta Ndunguru akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa NACTVET mara baada kutembelea Banda katika maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.


MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imezindua rasmi shughuli za Kijiji cha Bima katika Maadhimisho ya Miaka 50 ya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam maaraufu kama maonyesho ya Sabasaba.

Uzinduzi huo umeongozwa na Kamishna wa Bima, Dkt. Baghayo Saqware, na umehudhuriwa na viongozi wa kampuni za bima, madalali wa bima, watoa huduma na wadau mbalimbali wa sekta ya bima hapa nchini.

Kijiji cha Bima ni jukwaa la kila mwaka linaloratibiwa na TIRA kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya bima kwa lengo la kuwasogezea wananchi elimu ya bima, ushauri wa kitaalamu na huduma mbalimbali za bima katika eneo moja.

Kupitia jukwaa hilo, wananchi hupata fursa ya kujifunza umuhimu wa kuweka bima aina mbalimbali kwa lengo la kulinda maisha, afya, mali, biashara na uwekezaji wao kwa ujumla.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Dkt. Saqware, amesema kukua kwa sekta ya bima kunategemea sana uelewa wa wananchi kuhusiana na dhana nzima ya bima.

Amesema jambo hilo linahitaji ushirikiano mkubwa wa wadau wote katika kuhakikisha elimu na huduma za bima zinawafikia Watanzania wengi zaidi.

Aidha Ametoa wito kwa wananchi kutembelea Kijiji hicho cha Bima kilichozinduliwa ili kupata elimu sahihi inayohusiana na maswala yote ya bima pamoja na kuwa nafasi ya kuchagua aina ya bima ambazo watazihitaji.

Kwa upande wake, uongozi wa TIRA umeeleza kuwa ushiriki wake katika Maonesho ya Sabasaba unaendana na dhamira ya kuongeza uelewa wa umma kuhusu bima katika kukuza ujumuishi wa huduma za kifedha na kuimarisha mchango wa sekta ya bima katika maendeleo ya uchumi wa Taifa.

Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi huo katika kipindi chote cha maonesho, wananchi watapata huduma za ushauri, elimu ya bima, ufafanuzi wa bidhaa mbalimbali za bima pamoja na nafasi ya kukutana ana kwa ana na makampuni yanayojishughulisha na huduma za bima pamoja na wadau wengine walioko kwenye sekta hiyo.

Taarifa hiyo imeendelea kusema kuwa uongozi wa TIRA unaendelea kuhimiza wananchi kutumia huduma za bima kama nyenzo muhimu ya kudhibiti vihatarishi na kujenga ustahimilivu wa kifedha kwa watu binafsi, biashara na taasisi.

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) ni taasisi ya Serikali yenye jukumu la kusimamia, kuendeleza na kuhakikisha sekta ya bima inakuwa imara, shindani katika shughuli zinazohusiana na maswala ya bima kwa ujumla pamoja na inayolinda maslahi ya watumiaji wa huduma za bima.








Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MFUMO wa kufuatilia, kudhibiti na kukusanya taarifa za mafuta yanayoingia nchini kwa wakati halisi (Supervisory Control and Data Acquisition -SCADA) umeendelea kuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha usimamizi wa mafuta nchini kwa kuongeza uwazi, usahihi wa taarifa na ufanisi katika ushushwaji wa mafuta yanayoingia kupitia bandari zetu hadi kufika kwenye maghala ya kuhifadhia.

Kupitia mfumo huo, Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umefanikiwa kuimarisha udhibiti wa upotevu wa mafuta na kuongeza uhakika wa takwimu zinazotumika katika kufanya maamuzi ya kiutendaji.

Akizungumza katika mahojiano na gazeti la Uhuru kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Afisa Lojistiki wa Mafuta wa PBPA, Bi. Hilda Kowero, alisema mfumo wa SCADA umeleta maboresho makubwa katika usimamizi wa mafuta kwa kuwezesha ufuatiliaji wa shughuli zote muhimu kwa wakati halisi.

"Teknolojia hii inatuwezesha kupata taarifa sahihi kwa wakati kuhusu mwenendo wa mafuta yanayoingia nchini. Hivyo, tunakuwa na uwezo wa kufuatilia mnyororo mzima kwa usahihi na kuongeza uwajibikaji katika usimamizi wa mafuta," alisema Bi. Kowero.

Aliongeza kuwa pamoja na kuratibu uagizaji wa mafuta kupitia Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement System - BPS), PBPA pia ina jukumu la kuhakikisha nchi inakuwa na akiba na upatikanaji wa mafuta unaoaminika wakati wote hivyo kuimarisha usalama wa hali ya upatakinaji wa mafuta nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi akizungumza waandishi wa habari kuhusiana na JKT kuibuka mshindi wa Kwanza katika Bidhaa za Kilimo na Uvuvi kwenye Maonesho ya 50  Biashara ya Biashara Kimataifa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi, akiwa katika picha ya pamoja na maafande wa JKT  mara baada ya kushangilia ushindi wa ubunifu wa jeshi katika bidhaa za Kilimo na Uvuvi.

Na Mwandishi Wetu
JESHI  la Kujenga Taifa (JKT) limeibuka mshindi wa kwanza katika kundi la bidhaa za kilimo na uvuvi kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), mafanikio ambayo yameelezwa kuwa ni matokeo ya uzalishaji wenye ubora, ushirikiano na utekelezaji wa maelekezo ya viongozi wa jeshi hilo.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Sabasaba Kitaifa upande wa JKT, Brigedia Jenerali Shija Lupi, alisema ushindi huo unathibitisha kuwa bidhaa zinazozalishwa na JKT zinakidhi viwango vya ushindani na zimeendelea kutambulika nchini.

Alisema tuzo hiyo si ya kwanza kwa JKT, kwani taasisi hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika maonesho hayo kwa miaka iliyopita kupitia bidhaa zinazozalishwa na Shirika la SUMA JKT.

"Hata mwaka jana tulikuwa washindi wa kwanza kwa bidhaa za samani na mwaka huu tumeamua kushindana katika kundi la bidhaa za kilimo na uvuvi na tumefanikiwa kuibuka washindi wa kwanza. Hii inatupa hamasa ya kuendelea kuboresha bidhaa zetu ili tuendelee kufanya vizuri kila mwaka," alisema.

Alisema ushirikiano uliopo katika mnyororo mzima wa uzalishaji umeiwezesha JKT kuendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na ushindani mkubwa sokoni.

Akizungumzia mchango wa JKT katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Brigedia Jenerali Lupi alisema taasisi hiyo imekuwa mstari wa mbele katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuzalisha chakula na mazao ya biashara pamoja na kutoa mafunzo kwa wananchi.

Alieleza kuwa JKT inamiliki mashamba makubwa ya uzalishaji na ranchi mbalimbali, ikiwemo Ranchi za Misenyi, Orujoro na Mafinga, huku ikiendelea na ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha uzalishaji wa maziwa kitakachoongeza thamani ya bidhaa za mifugo.

Aidha, alisema kupitia kampuni zake, ikiwemo SUMA JKT, taasisi hiyo imeendelea kuzalisha bidhaa mbalimbali za viwandani pamoja na kutoa huduma za kitaalamu katika sekta ya kilimo na uvuvi.

Alitaja pia mchango wa kampuni ya SUMA Poni, inayojihusisha na ujenzi wa mabwawa ya kisasa ya ufugaji wa samaki na usimikaji wa mifumo ya uzalishaji, huku wataalamu wa JKT wakiendelea kutoa ushauri wa kitaalamu bila malipo kwa wananchi wanaohitaji kuwekeza katika kilimo, mifugo na uvuvi.

Brigedia Jenerali Lupi aliwataka wananchi kutembelea banda la JKT katika Maonesho ya Sabasaba ili kujionea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na taasisi hiyo pamoja na kupata elimu kuhusu fursa za uzalishaji na uwekezaji katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na viwanda.
Mgeni Rasmi Katika Ufunguzi Maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa   Rais wa Msumbiji Daniel Francisco Chapo akimkabidhi Mwakilishi wa Kampuni ya GF Truck Salman Karmal  Tuzo ya Mshindi wa Kwanza wa Banda Bora katika Maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa ,jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya GF Trucks imesema katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) imepata mafanikio ya kuaminika kwa ubora baada ya kutwaa tuzo ya banda bora kwa mwaka wa pili katika maonesho hayo

Mafanikio hayo yanaelezwa kutokana na kuendelea kuendelea katiika kuleta teknolojia bunifu na rafiki kwa mazingira nchini.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mwakilishi wa kampuni hiyo, Salman Karmali, amesema mafanikio hayo ni ishara ya imani ambayo kampuni imejijengea kwa wadau na wananchi kupitia ushiriki wake wa muda mrefu katika maonesho hayo.

Amesema GF Trucks and Equipment imekuwa mshiriki wa maonesho ya Sabasaba kwa miaka mingi na imeendelea kutumia jukwaa hilo kuwatambulisha Watanzania bidhaa na teknolojia mpya zinazolenga kuongeza ufanisi katika sekta Usafirishaji pamoja na mitambo.

Mwaka huu wa maadhimisho ya miaka 50 ya Sabasaba, GF Trucks and Equipment imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuleta suluhisho za kisasa katika sekta ya usafirishaji, ujenzi na uchimbaji, huku ikijikita katika matumizi ya teknolojia endelevu na rafiki kwa mazingira.


“Ni heshima kubwa kwetu kupata tuzo hii kwa mwaka wa pili mfululizo. Tunawashukuru viongozi wa TanTrade kwa kutupa heshima hii na kutuongezea hamasa ya kuendelea kuboresha huduma na bidhaa zetu,” amesema.

Amebainisha kuwa katika maonesho ya mwaka huu kampuni imewasilisha bidhaa mbalimbali zikiwemo magari madogo, malori, mitambo mizito pamoja na mashine za kisasa za utafiti na uchimbaji maji.

Amesema vivutio vikubwa katika banda lao ni mitambo pamoja na mashine za utafiti na uchimbaji zinazojulikana kama drilling rigs au exploration rigs, ambazo hutumika katika tafiti za vyanzo vya maji na shughuli nyingine za uchimbaji.

Amesema baadhi ya mitambo hiyo imebuniwa kwa kuzingatia mazingira na mahitaji ya Tanzania baada ya kufanyiwa tafiti za kina ili kuhakikisha inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Karmali amesema kampuni hiyo inaendelea kuunga mkono juhudi za kuhifadhi mazingira kwa kuleta teknolojia zinazopunguza matumizi ya mafuta na kupunguza athari kwa mazingira.

“Kwa sasa dunia inaelekea kwenye matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira. Sisi tumekuja na bidhaa zenye matumizi madogo ya mafuta na pia tumewaletea magari yanayotumia umeme ya chapa ya Hyundai, ambayo tayari yameanza kutambulishwa nchini,”amesema.

Ameongeza kuwa kampuni hiyo itaendelea kutoa ofa maalum kwa wateja wake hadi mwisho wa maonesho hayo na kuwahimiza wananchi pamoja na wadau wa sekta mbalimbali kutembelea banda lao ili kujionea teknolojia mpya zinazowasilishwa na kampuni hiyo.

Mwakilishi wa Kampuni GF Truck & Equipment akiwa katika ufunguzi wa maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa


Na Mwandishi Wetu
AFISA Mtendaji Mkuu wa MIXX, Angelica Pesha, amesema kampuni hiyo imejipanga kikamilifu kuwahudumia wananchi wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kuwapatia huduma mbalimbali za kifedha na mawasiliano kwa urahisi na usalama.

Pesha alitoa kauli hiyo alipotembelea banda la MIXX katika maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Alisema MIXX imeweka mazingira rafiki yatakayowawezesha wananchi kufanya miamala mbalimbali ya kifedha bila ulazima wa kubeba fedha taslimu, hatua ambayo inalenga kuongeza usalama na urahisi wa huduma kwa watumiaji.

"Hatuna sababu ya wananchi kutembea na fedha taslimu wakati huduma zetu zinapatikana hapa bandarini. Tunawahimiza wote wanaotembelea Sabasaba kufika banda la MIXX ili wapate huduma za kifedha kwa haraka na kwa usalama," alisema Pesha.

Aliongeza kuwa, pamoja na huduma za kifedha, MIXX pia inatoa huduma mbalimbali za mawasiliano, ikiwemo ununuzi wa bando na huduma nyingine zinazowarahisishia wateja kuendelea kuwasiliana popote walipo.

Pesha aliwataka wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kutembelea banda la MIXX ili kujionea huduma zinazotolewa na kupata elimu kuhusu suluhisho mbalimbali za kidijitali zinazorahisisha maisha ya kila siku.

Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yamewakutanisha taasisi za Serikali na sekta binafsi zikionyesha bidhaa, huduma na ubunifu mbalimbali unaochochea maendeleo ya biashara na uchumi nchini.

Afisa Mtendaji Mkuu wa MIXX Angelica Pesha akizungumza na waandishi wa habari walivyojipanga kuhudumia wananchi maonesho ya Sabasaba


NAIBU Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango - Biashara na Ubunifu, Dkt. Blandina Kilama amesema anaitegemea Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya maendeleo 2050 iliyoanza Julai Mosi mwaka huu.

Akizungumza katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa - Sabasaba katika banda la PURA Dkt Kilama amesema ana matumaini makubwa kwamba PURA itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha utekelezaji wa DIRA 2050 unakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Bw. Ebeneza Mollel kutoka PURA amesema kufuatia utekelezaji wa DIRA 2050 tayari PURA imehuisha Mpango Mkakati wa Taasisi kwa mwaka 2026/27 - 2030/31 ili kuendana na matakwa ya DIRA 2050.

Nishati ni moja ya kichocheo katika vichocheo vitano kufanikisha malengo ya DIRA 2050, ambapo PURA inaendelea kutoa elimu kuhusu utafutaji uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchini katika Maonyesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba.
-Yatwaa tuzo mbili ikiwemo mshindi wa tatu wa jumla

Rais Samia aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho hayo. Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Tukio hilo lilifanyika Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo wakipokea maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa maonesho hayo. Maonesho hayo yamefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo Julai 3, 2026, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili, ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo (kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire (kulia), kuhusu huduma ya simu mpya ya smati kitachi inayouzwa na kampuni hiyo ili kuwawezesha Watanzania kuingia katika ulimwengu wa kidijitali wakati Marais hao walipotembelea banda la Vodacom muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA). Katika hafla hiyo, Vodacom Tanzania ilitunukiwa tuzo mbili ikiwemo Tuzo ya Nafasi ya Tatu katika Kundi la Washindi wa Jumla wa Maonesho hayo na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni kutambua mchango mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo.

Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), wakifurahia ushindi baada ya kampuni yao kutunukiwa tuzo mbili: Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho yote na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni utambuzi wa mchango wake mkubwa kama mshirika muhimu wa Maonesho hayo. Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi Julai 3, 2026, na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, ambaye kabla ya hafla ya ufunguzi aliambatana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutembelea banda la Vodacom na kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitazama huduma mbalimbali zilizokuwepo ndani ya banda la Vodacom, wakati wa kutembelea banda hilo muda mfupi kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA), baada ya kupata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Philip Besiimire, kuhusu huduma zinazotolewa na kampuni hiyo.



Na Mwandishi Wetu, Shelisheli
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Chande (Mb.) ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 69 wa Shirika la Utalii Duniani Kamisheni ya Afrika uliofanyika mjini Mahe, Jamhuri ya Ushelisheli.

Mkutano huo ulifunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Ushelisheli, Mhe. Dkt. Patrick Herminie Julai 2, 2026 ukiwa na dhima ya "Kuimarisha Rasilimali Watu ili Kuchochea Ukuaji wa Utalii Barani Afrika.”

Pamoja na mambo mengine mkutano huo ulijadili hali ya Sekta ya Utalii Barani Afrika na Duniani kwa ujumla ikijumuisha mwenendo wa ukuaji wa watalii, changamoto na fursa zilizopo; pamoja na hatua zinazochukuliwa katika utekelezaji wa programu na mipango ya Shirika la Utalii la Umoja wa Mataifa (UN Tourism) katika ngazi ya Kimataifa na Kikanda; utalii endelevu; maendeleo ya rasilimali watu na elimu ya utalii; uwekezaji na ubunifu katika sekta; pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama na wadau mbalimbali.

Kupitia Mkutano huo Mkurugenzi wa Shirika la Utalii Kanda ya Afrika Bi. Elcia Grandcourt aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Afrika kwa kipindi cha Mwaka 2025/26 iliyosheheni shughuli zilizotekelezwa kwa kushirikiana na nchi wanachama na wadau mbalimbali, ikiwemo kuimarisha uwezo wa rasilimali watu, kukuza utalii endelevu, kuendeleza ubunifu na matumizi ya teknolojia, kuongeza uwekezaji na ushindani katika Sekta ya Utalii, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa Kikanda ili kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo jumuishi kupitia utalii.

Sambamba na taarifa hiyo Bi. Grandcourt, aliwasilisha matokeo ya Utafiti kuhusu Kukuza Upatikanaji wa Elimu ya Utalii na Maendeleo ya Rasilimali Watu Barani Afrika.

Aidha, nchi wanachama walijadili kwa kina kuhusiana na uwezeshaji wa usafiri ndani ya nchi za Afrika kuwa na muunganiko wa safari ya pamoja, kurahisisha upatikanaji wa Visa, sambamba na utoaji wa elimu na maendeleo ya rasilimali watu.






WENGE wa Uhuru umewasili wilaya Siha ukitokea Hai mkoani Kilinanjaro ambapo unatarajiwa kukimbizwa kilomita 144 katika wilayani humo na kutembelea miradi ya maendeleo saba.

Akizungumza katika mapokezi hayo, yakiyofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Ormelili, Mkuu wa wilaya ya Siha, Christophe Timbuka alisema kuwa, Mwenge huo utazindua, kuweka mawe ya msingi pamoja na kutembelea miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo.

Miradi itakayotembelewa ni uwekaji wa jiwe la msingi kituo cha afya Ormelili chenye thamani ya milioni 250, uzinduzi wa mradi wa maabara za kemia na fizikia katika shule ya sekondari ya Sikirari wenye thamani ya shilingi milioni 104.71.

Miradi mingine ni kutembelea mradi wa vijana kazi iendelee Lawate wenye thamani ya shilingi milioni 25, uwekaji wa jiwe la msingi daraja la upinde wa mawe Songu (milioni 153.7.), uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa maji Gararagua kwenda vijiji 8 (Bilioni 1.59).

Aidha Mwenge huo utaweka jiwe la msingi mradi wa upanuzi wa shamba la kuku wazazi la Tanbreed (Bilioni 9.71) na kuzindua shule mpya ya sekondari Mitimirefu (milioni 584.28).






Na Mwandishi Wetu


NCHI za Tanzania na Urusi zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya utalii, hatua inayolenga kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili na kuongeza fursa za utalii, biashara na uwekezaji.

Makubaliano hayo yanaenda sambamba na kuanza kwa safari za moja kwa moja za kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) zinazounganisha Moscow na Tanzania Bara pamoja na Zanzibar, hatua itakayorahisisha usafiri wa watalii na wafanyabiashara kati ya masoko hayo mawili.

Katika safari hiyo ya kihistoria ya kwanza, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji, aliongoza ujumbe wa Tanzania uliojumuisha Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na wadau zaidi ya kampuni 47 za utalii.

Ujumbe huo ulikutana na wadau wa sekta ya utalii kutoka Urusi kupitia mikutano ya biashara baina ya wafanyabiashara (B2B), iliyowapa fursa ya kujadiliana, kujenga ushirikiano mpya wa kibiashara na kutangaza vivutio vya kipekee vya utalii vya Tanzania kwa soko la Urusi.

Hatua hii inatarajiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka Urusi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya utalii, na kuchangia utekelezaji wa malengo ya Tanzania ya kukuza sekta ya utalii na uchumi wa nchi kupitia masoko mapya ya kimkakati.











Top News