Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Afya, Dk Florence Samizi amewataka watanzania kuwekeza kwenye miundombinu ya afya ili kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi.

Naibu Waziri ameipongeza hospitali ya E.M ya Kigamboni kwa uwekezaji mkubwa iliyofanya kwenye mtambo wa kisasa wa uchunguzi wa magonjwa CT SCAN na huduma za usafishaji wa damu (Dialysisi) ambao unasaidia kupunguza rufaa zisizo za lazima.

Alitoa pongezi hizo jana Dar es Salaam na wakati wa uzinduzi rasmi wa mashine ya kusafisha damu na mashine ya uchunguzi wa afya CT SCAT ya hospitali hiyo iliyoko kata ya Mjimwema Kigamboni.

Alisema uwekezaji kama huo unasaidia jitihada za serikali kupeleka huduma karibu na wananchi na kuepusha muda na gharama za wananchi kufuata huduma hizo maeneo ya mbali na maeneo wanakoishi.

“Kwaniaba ya Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa napenda kuwapongeza kwa dhati kabisa kwa uwekezaji huu, nilipofika pale nje nilimwambia msaizidi wangu kumbe kitu chenyewe ni kikubwa hivi, nawapongeza sana kwa uongozi mkubwa na kutimiza ndoto na kuwa na wataalamu wazuri maana ungewekeza bila wataalamu isingesaidia sana,” alisema

Alisema uwekezaji uliofanywa na hospitali ya E.M unaonyesha dhamira ya dhati ya kuokoa maisha ya watanzania kupata tiba sahihi na kwa wakati.

“Kama alivyosema Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hii uwekezaji huu umegharimu shilingi bilioni 10 si pesa kidogo ni uwekezaji mkubwa sana tena umefanywa na mtanzania mzawa kusaidia juhudi za serikali kuhudumia watanzania,nawapongeza wote kwa kutimiza haya maono,” alisema

Alisema ili mtu aweze kufanyakazi vizuri lazima awe na afya njema hivyo serikali itaendelea kuwekeza kwenye sekta ya afya kuhakikisha taifa lake linakuwa na wananchi wenye afya.

“Kwa dhati kabisa nampongeza Rais Samia kwa kuwekeza kwenye sekta ya afya, ndani ya miaka minne tu amewekeza zaidi ya trilioni sita ambazo zimeenda kwenye miradi ya ujenzi wa hospitali na zahanati, ameweza kujenga hospitali 119, vituo vya afya 649 na zahanati 2,700 na kuweka vifaa tiba vya kisasa na ameajiri watumishi wa afya,” alisema

“Huduma kama uchujaji wa damu ni muhimu sana kwa wananchi wanaosumbuliwa na figo hivyo huduma hiyo itawasaidia sana wananchi kuchuja damu na kuendelea na maisha yao, huduma hizi tumezoea kuzipata nje ya nchi sasa leo hii mzawa amezileta Kigamboni,” alisema

“Nasikia ni ya kwanza Kigamboni kutoa huduma hii napenda kuwaambia wananchi hakuna haja ya kwenda mbali kutafuta huduma mfike hapa E.M kupata huduma hizo badala ya kuhangaika kwenda mbali,” alisema

Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk Egna Makwabe alisema wamekuwa wakipata wagonjwa kutoka nchi za Congo DCR, Zambia, Malawi, Comoro, Burundi Rwanda, Benin, Ghana, Nigeria, Kenya, Urusi china na Marekani .

“Ujio wa wagonjwa kutoka nje ya nchi ulitushangaza sana tunakiuliza je wanakuja kwasababu ya eneo tulilopo au ninini hasa kimewavutia kuacha hospitali zote kuja kwetu tukagundua kuwa ni imani yao kutokana na huduma tunazotoa,” alisema

Alisema kwa sasa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje wastani wa 300 kwa siku na kwamba kwa sasa wanamadaktari bingwa bobezi wauguzi na wataalamu wa maabara.

Alisema E.M itashirikiana na serikali kuhakikisha bima ya afya kwa wote inawanufaisha wananchi wanapougua wasilazimike kutoa fedha kupata matibabu na kwamba walishiriki kutoa maoni kwenye uandaaji wa bima ya afya kwa wote.

Alisema wanatoa huduma za kuwaona wagonjwa wa nje, wanaolazwa, huduma za upasuaji, huduma za matibabu ya mgongo, mfumo wa fahamu na mifupa, huduma za maabara na geologia, huduma za uangalizi maalum na huduma za kibingwa za figo na saratani.

Alisema hospitali imewekeza kwenye huduma za kuchuja damu, mitambo ya kuchunguza magonjwa kama CT SCAN na upasuaji wa kisasa kwa njia ya matunda na karibuni wataanzisha huduma za macho .



Balozi wa Italia nchini Tanzania, Giuseppe Sean Coppola, amesema kuwa Italia inaadhimisha toleo la 10 la Siku ya Ubunifu wa Italia Duniani, tukio linalolenga kuonesha mchango wa nchi hiyo katika ubunifu wa kimataifa.

Amesema mpango huo umeanzishwa na Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Wizara ya Utamaduni ya Italia, ukiwa na lengo la kukuza ubunifu unaochangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi duniani.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Balozi Coppola alieleza kuwa Italia ni miongoni mwa mataifa vinara katika ubunifu wa bidhaa, akitaja mji wa Milan kuwa kitovu cha ubunifu barani Ulaya na duniani kwa ujumla.

Kwa mwaka huu, maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kubuni upya: kurejesha, kuboresha na kubadili mawazo, maeneo na mahusiano.”

Maonesho hayo yanafanyika katika ukumbi wa Rangy Gallery, yakihusisha mradi wa pamoja wa utengenezaji wa vioo kati ya Shanga uliopo Arusha na eneo la Murano nchini Italia.

Mradi huo unahusisha wataalamu wa vioo kutoka Murano waliokuja Tanzania kufundisha mbinu za kisasa za utengenezaji wa bidhaa za mikono. Bidhaa hizo hutengenezwa kwa kutumia taka (recycling), hatua inayochangia uhifadhi wa mazingira.

Aidha, Shanga ni taasisi inayowaajiri watu wenye ulemavu, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya kijamii na kuwainua kiuchumi.

Katika kuimarisha ubunifu huo, Balozi Coppola alibainisha kuwepo kwa ushirikiano na Nelson Mandela African Institution of Science and Technology, unaolenga kulinda haki miliki za wabunifu.

Maonesho hayo pia yanajumuisha bidhaa za vioo kutoka Venice, jiji lenye historia ya zaidi ya miaka 1,000 katika utengenezaji wa vioo, pamoja na taa za kisasa kutoka kampuni ya Potcerini.

Balozi huyo alisisitiza kuwa ubunifu wa Italia unalenga kuunganisha uzuri na matumizi bora (comfort), huku ukimweka mwanadamu katikati ya kila bidhaa inayobuniwa.

Amewahimiza Watanzania kutembelea maonesho hayo yanayoendelea mwezi mzima wa Aprili, pamoja na kuunga mkono bidhaa za ubunifu na miradi ya kijamii kama Shanga.

Akizungumzia mafanikio ya mradi huo, Balozi Coppola alisema kuwa mapokezi yake katika Murano yalikuwa chanya, huku mafundi wawili wabobezi wa utengenezaji vioo wakifika Tanzania kushiriki mafunzo na kubadilishana ujuzi.

Aliongeza kuwa wadau wa sekta ya ubunifu wameunga mkono mradi huo, wakiuona kama daraja muhimu la kuimarisha uhusiano wa watu kwa watu (people-to-people connection), wenye manufaa makubwa kijamii na kiuchumi.

Kwa ujumla, ushirikiano huo unaendelea kuleta matokeo chanya katika kukuza sanaa, ubunifu na kuimarisha mahusiano ya kimataifa kati ya Italia na Tanzania.













Na Janeth Raphael - MichuziTv

Rais Samia amesema Taifa litamkumbuka William Lukuvi kama kiongozi aliyegusa maisha ya wengi kwa moyo wake wa upendo, hekima, na kujitolea kwa dhati katika utumishi wa umma.

"Hayati Lukuvi atabaki katika kumbukumbu zetu si tu kwa nafasi alizoshika, bali kwa namna alivyoweza kujenga mahusiano mema na ya kudumu ndani ya jamii"

Pia Rais Samia amesema LUKUVI alikuwa kiongozi aliyesikiliza, aliyeshirikiana na makundi mbalimbali, na aliyethamini mchango wa kila mmoja katika kujenga taifa.

Katika kipindi hicho ambacho dunia inakumbwa na changamoto nyingi na mabadiliko yasiyotabirika, umuhimu wa kuwa na viongozi wenye uzoefu mpana na waliopitia ngazi mbalimbali za uongozi hauwezi kupuuzwa

"Tulimuhitaji sana ndugu Lukuvi leo—zaidi hata kuliko jana—ili kuendelea kutoa mwongozo na busara katika nyakati hizi ngumu"

Aida Rais Samia amesema Maisha na utumishi wa LUKUVI vinatufundisha somo muhimu sana: kwamba uongozi ni dhamana, si fursa ya kujinufaisha, n wajibu wa kuitumikia jamii kwa uaminifu, uwajibikaji, na moyo wa kujitolea bila kuchoka, Haya ndiyo maadili aliyoyaishi, na huu ndio urithi wake kwa taifa letu"

Hata hivyo Rais Samia amesema ni jukumu letu sasa kuuenzi na kuuendeleza urithi huo Tuige mfano wake kwa kuimarisha mshikamano, kuheshimiana, na kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya wote, kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumemuenzi kwa vitendo, na kuhakikisha kuwa mchango wake unaendelea kuzaa matunda kwa vizazi vijavyo.














 Na Joseph Mahumi, WF


Serikali ya Tanzania imeendelea kung’ara katika jukwaa la kimataifa baada ya kuibuka mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.

Ushindi huo mkubwa unatokana na juhudi za Serikali katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa deni la umma, ikiwemo kuunganisha vyema mifumo ya kifedha ya Serikali na kuboresha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya maendeleo, ambapo Jopo huru la wataalamu lililochambua mawasilisho kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Madola lilizingatia vigezo vya ubunifu, uimara na uendelevu katika kutoa tuzo hizo.

Akifungua hafla ya utoaji tuzo hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal, alisisitiza umuhimu wa nchi wanachama kuendelea kubuni mbinu madhubuti za kusimamia deni la umma ili kulinda uchumi dhidi ya misukosuko ya kifedha duniani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, Bi. Ruth Kattumuri, aliipongeza Tanzania kwa mageuzi makubwa iliyoyafanya katika kuimarisha usimamizi wa deni la umma.

Alieleza kuwa mafanikio hayo ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya nchi katika kujenga uchumi imara na unaostahimili mishtuko ya kiuchumi.

Aidha, Bi. Kattumuri, alisema kuwa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola itaendelea kuisaidia Tanzania katika juhudi zake za kuboresha sera na mifumo ya usimamizi wa deni, sambamba na utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha 72 cha Kundi la Mawaziri wa Jumuiya ya Madola.

Mkutano huo wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola uliofanyika kwa muda wa wiki moja uliwakutanisha wataalamu wa usimamizi wa deni kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza na kujadili mbinu bora za kukopa, kusimamia na kulipa deni la umma, na umeandaliwa ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Jumuiya ya Madola wa Deni Imara, Bunifu na Endelevu, ambapo Tanzania imejitokeza kama kinara na mfano wa kuigwa barani Afrika na katika Jumuiya nzima ya Madola.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) akiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal (kushoto) na  Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya hiyo, Bi. Ruth Kattumuri.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, akionesha tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) Aakiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni washindi wenngine wa tuzo hizo kutoka nchi ya Barbados ambayo iliibuka mshindi wa Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Caribbean na Sri Lanka Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Asia.

Na Mwandishi Wetu

MFUKO wa Maendeleo ya jamii(TASAF)umeunga mkono juhudi za Serikali katika huduma ya afya kwa kutoa msaada muhimu katika Taasisi ya Saratani Ocean Road jijini Dar es Salaam.

Msaada huo umekabidhiwa leo hospitalini hapo na Meneja rasilimali watu wa mfuko huo Mariam Al- Jabiri kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Shedrack Mziray.

Al-Jabiri ambaye ameambatana na baadhi ya wafanyakazi wa Tasaf amesema Serikali imewekeza nguvu kubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini.

“Msaada huu umelenga kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini,”amesema huku akiwatakia uponyaji wa haraka wagonjwa wote wanaopata matibabu katika taasisi hiyo.

Aidha baadhi wa Wafanyakazi hao wa TASAF wakiongozwa na Meneja huyo wamepata nafasi ya kuwajulia hali wagonjwa hospitalini hapo huku wakiwafariji kwa kuwatia moyo na kufanya sala fupi kuwaombea uponyaji wa haraka.

Kwa upande wake Mwakalishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Ocean Road Dk.Diwani Msemo ameushukuru mfuko wa maendeleo ya jamii kwa msaada huo.









Moshi ilichangamka kwa mara nyingine tena huku maelfu ya wakimbiaji, mashabiki, na watazamaji wakikusanyika kwa toleo la mwaka 2026 la Kilimanjaro Marathon.

Kilichoanza zaidi ya miongo miwili iliyopita kama mbio, kimekua na kuwa moja ya majukwaa yenye nguvu zaidi kitaifa nchini Tanzania, yakileta pamoja michezo, utalii, utamaduni, na jamii kwa namna ya kipekee.

Mbio za mwaka huu zilivutia ushiriki mkubwa kutoka kote Tanzania na duniani kwa ujumla, na kuimarisha nafasi yake kama tukio muhimu la utalii wa michezo.

Kuanzia wanariadha wa kiwango cha juu hadi wakimbiaji wa mara ya kwanza, tukio hili liliunda uzoefu wa pamoja uliovuka mstari wa mwisho wa mashindano. Haikuwa tu kuhusu ushindani, bali pia ushiriki, muunganiko, na fahari ya taifa.

Kiini cha mafanikio haya ya muda mrefu ni Tanzania Breweries Public Limited Company kupitia chapa yake kuu ya Kilimanjaro Lager, ambayo imekuwa ikiunga mkono mbio hizi kwa miaka mingi. Ushirikiano huu umechukua nafasi kubwa katika kuunda tukio hili kuwa jukwaa linalotoa thamani ya kijamii na kiuchumi.

Mbio hizi zinaendelea kuleta faida halisi kwa uchumi wa eneo husika. Hoteli zilijaa wageni, huduma za usafiri ziliongezeka, na wafanyabiashara wadogo walipata ongezeko la biashara kutokana na wageni waliokuja Moshi. Kwa biashara nyingi ndogo, wiki ya marathon ni mojawapo ya vipindi muhimu zaidi kwa mwaka.

Faida hii inaonesha mchango wa tukio hili katika kusaidia maisha ya watu na kuimarisha uchumi wa ndani.Zaidi ya shughuli za kiuchumi, marathon hii inaongeza mwonekano wa Tanzania kimataifa.

Washiriki wa kimataifa na vyombo vya habari vinaendelea kuiweka Tanzania kama kivutio kinachotoa si tu uzuri wa asili bali pia uzoefu wa kiwango cha kimataifa uliopangwa vizuri. Mkoa wa Kilimanjaro hasa unafaidika na mwonekano huu, ukithibitisha nafasi yake kama kitovu cha utalii na burudani za kipekee.

Kampeni ya mwaka huu, “The Best of Us - Vyakwetu Vizuri,” iliongeza maana ya kina kwa tukio hili. Ikitokana na misemo, methali, na lugha ya kila siku ya Watanzania, kampeni hii ilisherehekea utambulisho, uthabiti, na maadili kwa pamoja.

Iliunganisha chachu ya mbio na maisha halisi ya Watanzania, na kufanya marathon hii kuwa ya kibinafsi na ya kitaifa kwa wakati mmoja.

Afya na ustawi pia vinaendelea kuwa sehemu muhimu ya faida ya marathon hii. Kwa miaka mingi, tukio hili limechangia kujenga utamaduni wa kukimbia na kuishi maisha yenye afya nchini.

Watu wengi zaidi wanashiriki katika shughuli za mazoezi, na taasisi mbalimbali zinaanzisha majukwaa yanayohamasisha harakati na ustawi wa mwili. Marathon imekuwa mfano wa kile ambacho juhudi endelevu za afya ya jamii zinaweza kufanikisha nchini Tanzania.

Burudani haikuishia kwenye mbio pekee. Kili Dome kwa mara nyingine ilileta pamoja michezo, muziki, sherehe, na kuunda mazingira yenye hamasa ambapo washiriki na watazamaji waliweza kuungana na kujiburudisha.

Mchanganyiko huu wa michezo na maisha ya kijamii unaakisi nafasi pana ya marathon katika kuunda uzoefu wa pamoja.

Akizungumza baada ya tukio, Mkurugenzi Mtendaji Michelle Kilpin alieleza ukuaji na umuhimu unaoendelea wa marathon hii kama jukwaa la kitaifa.

“Marathon ya Kilimanjaro inaendelea kuwaleta watu pamoja kutoka asili mbalimbali kwa namna inayoakisi maana halisi ya Tanzania. Inaunga mkono utalii, inakuza afya, na inajenga mahusiano yenye maana katika jamii.


Tunajivunia kuona jinsi tukio hili linavyoendelea kukua na kutoa thamani zaidi ya mbio zenyewe.”Kadri toleo la mwaka 2026 linavyohitimishwa, Kilimanjaro Marathon inabaki kuwa zaidi ya tukio la kila mwaka la michezo.

Ni jukwaa linalochochea shughuli za kiuchumi, linaimarisha mshikamano wa jamii, linahamasisha maisha yenye afya, na linaonesha Tanzania kwa dunia.

Kupitia uungwaji mkono wake unaoendelea, Tanzania Breweries Plc kupitia Kilimanjaro Lager inaendeleza dhamira yake ya kusaidia mipango inayowaunganisha watu na kuchangia maendeleo ya muda mrefu ya taifa.

Mbio zinaweza kuishia kwenye mstari wa mwisho, lakini faida yake inaendelea kwa muda mrefu zaidi.










 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwaongoza Watanzania kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na wenye Ulemavu), Hayati William Vangimembe Lukuvi, tarehe 28 Machi, 2026.















Top News