Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Spika wa Bunge, Mussa Azan Zungu, ametoa onyo dhidi ya tabia ya utoro miongoni mwa baadhi ya wabunge na viongozi wa Serikali, akisema hali hiyo imezidi na kuanza kudhoofisha nidhamu pamoja na ufanisi wa shughuli za Bunge.

Akizungumza leo Bungeni jijini Dodoma, Spika Zungu amesema baadhi ya wabunge wamekuwa wakifika asubuhi kusaini mahudhurio kisha kuondoka, na baadaye kurejea jioni kwa ajili ya kusaini tena bila kushiriki vikao vya Bunge.

Amesema pia kuna wabunge wanaosaini mahudhurio kwa niaba ya wenzao ambao hawapo kabisa Bungeni, jambo alilolitaja kuwa ni ukiukwaji wa taratibu za Bunge unaostahili kuchukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu.

“Kuna wanaokuja asubuhi, wanasaini na kuondoka. Jioni wanarudi kusaini tena. Wapo pia wanaowasainia wenzao ambao hawapo. Tunawafahamu wanaosaini na wanaosainiwa, na hatua za kibunge zinapaswa kuchukuliwa,” alisema Spika Zungu.

Aidha, amesema kuna kundi lingine la wabunge ambao hawaonekani kabisa katika shughuli za Bunge licha ya kutokuwa na sababu za msingi za kutokuwepo, hali aliyoeleza kuwa ni kudharau mamlaka ya Spika pamoja na wananchi waliowachagua.

Spika Zungu amesisitiza kuwa kuanzia Jumatatu ijayo hatarajii kuona tabia hizo zikiendelea, akibainisha kuwa Ofisi ya Katibu wa Bunge ina uwezo wa kufuatilia na kubaini mahali alipo kila mbunge wakati wa shughuli za Bunge.

Pia aliiagiza Wizara inayosimamia mawasiliano kushirikiana katika kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa mahudhurio ya wabunge ili kudhibiti utoro huo.

Katika hatua nyingine, Spika alimwelekeza Waziri Palamagamba Kabudi kulifanyia kazi suala hilo kwa kuwa liko chini ya usimamizi wa ofisi yake.

Vilevile, alikemea utaratibu wa baadhi ya mawaziri na manaibu wao kuwa safarini kwa wakati mmoja, akisema hali hiyo husababisha kukosekana kwa uwakilishi wa Serikali ndani ya Bunge.

“Haipendezi Waziri kuwa kwenye ziara huku Naibu Waziri naye akiwa kwenye ziara wakati huohuo. Wapeane zamu ili mmoja awepo Bungeni wakati mwingine akiwa kwenye majukumu ya nje,” alisisitiza.

Kauli ya Spika imekuja wakati Bunge likiendelea na shughuli zake jijini Dodoma, huku akitaka nidhamu ya mahudhurio irejee na kila kiongozi kutimiza wajibu wake kwa wananchi.



Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre), David Kafulila, amesema mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) una mchango mkubwa katika kuongeza ufanisi wa taasisi za umma na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Kafulila alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza katika mhadhara wa umma uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), akieleza kuwa mataifa mengi duniani yameendelea kuwekeza katika mfumo wa PPP kutokana na manufaa yake katika kuimarisha utendaji wa taasisi na kuongeza tija ya kiuchumi.

Alisema sababu kuu tatu zinazochochea matumizi ya mfumo huo duniani ni kuvutia mitaji ya sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi ya umma, kuongeza ufanisi wa taasisi za serikali na kukuza ubunifu.

“PPP siyo tu njia ya kupata fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo, bali ni nyenzo muhimu ya kuongeza ufanisi wa taasisi za umma na kuhamasisha ubunifu unaochangia maendeleo endelevu ya uchumi,” alisema Kafulila.

Alibainisha kuwa tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa katika baadhi ya nchi zilizoendelea, takribani asilimia 25 ya utajiri wa taifa unatokana na ufanisi wa taasisi zake, huku rasilimali za asili zikichangia karibu asilimia tano pekee.

Kwa mujibu wa Kafulila, mafanikio ya nchi hizo hayatokani na ukosefu wa rasilimali za asili, bali uwezo wa kujenga mifumo madhubuti inayowezesha matumizi bora ya rasilimali zilizopo.

Alitolea mfano nchi za China, Marekani na Urusi ambazo pamoja na kuwa na utajiri mkubwa wa rasilimali za asili, zimejikita zaidi katika kuimarisha rasilimali watu, ubunifu na taasisi zenye ufanisi mkubwa.

“China inazalisha dhahabu nyingi kuliko nchi yoyote Afrika, Marekani ina mafuta mengi kuliko mataifa mengi duniani na Urusi ina gesi nyingi kuliko nchi yoyote Afrika. Hata hivyo, msingi wa maendeleo yao ni nguvu ya taasisi, ubunifu na rasilimali watu,” alisema.

Kafulila alisisitiza kuwa Tanzania inaweza kunufaika zaidi na mfumo wa PPP kwa kutumia sekta binafsi kama mshirika wa maendeleo katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, huku ikiimarisha ufanisi wa taasisi za umma na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi.






Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kushirikiana na wananchi na wadau mbalimbali katika kuimarisha ulinzi na usalama wa maisha na mali kupitia doria, misako na oparesheni za kuzuia na kubaini uhalifu. Katika kipindi cha mwezi Mei 2026, jumla ya watuhumiwa 871 wa makosa mbalimbali ya jinai walikamatwa katika maeneo tofauti ya mkoa huo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, makosa yaliyohusika ni pamoja na mauaji, kujeruhi, ubakaji, kupatikana na silaha bila kibali, dawa za kulevya pamoja na wizi. Watuhumiwa waliokamilishiwa upelelezi walifikishwa mahakamani, ambapo baadhi yao wamekutikana na hatia na kuhukumiwa vifungo mbalimbali kwa mujibu wa sheria.

Katika matukio ya hivi karibuni, Polisi wanawashikilia watuhumiwa wawili, Baraka Mwakatobe (31) na Said Baraka (39) wakazi wa Dodoma, kwa tuhuma za kusafirisha vipodozi vyenye viambata sumu vilivyopigwa marufuku nchini. Watuhumiwa hao walikamatwa Mei 28, 2026 katika kizuizi cha Polisi Chimala wakiwa na shehena ya boksi 403 za vipodozi hivyo pamoja na bidhaa nyingine zisizo rasmi.

Aidha, Jeshi hilo linamshikilia Shaban Safari (48) mkazi wa Kyela kwa tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya aina ya heroin kete 27 pamoja na bangi. Inadaiwa mtuhumiwa huyo alikamatwa akiwa na dawa hizo zilizofichwa kwenye mfuko wa khaki, huku akituhumiwa kuwa muuzaji wa dawa hizo katika eneo hilo.

Kwa kipindi hicho hicho cha Mei 2026, Polisi wamesema pia waliwakamata watuhumiwa 20 wakiwa na bangi kilo 12.24, watuhumiwa wawili wakiwa na gongo lita 30 na wengine wawili wakiwa na silaha aina ya gobole, hatua inayoonesha kuendelea kudhibiti uhalifu na vitendo vya kihalifu mkoani humo. Aidha, kesi 224 zilifikishwa mahakamani ambapo 122 zilimalizika kwa hukumu za hatia na 73 bado zinaendelea.

Jeshi la Polisi limehimiza wananchi kuendelea kushirikiana kwa kutoa taarifa za uhalifu na kufika mahakamani kutoa ushahidi ili kusaidia haki kutendeka. Pia limetoa onyo kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu kuacha mara moja, likisisitiza kuwa uhalifu haulipi na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaobainika.


Na Mwandishi Wetu, Arusha
MKURUGENZI wa Mauzo wa Turaco Collection Tanzania, Florenso Kirambata, amesema kuwa maonesho ya Karibu-KiliFAIR 2026 ni jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania kimataifa, kubadilishana uzoefu na kujenga ushirikiano wa kibiashara katika sekta ya utalii inayokua kwa kasi duniani.

Akizungumza wakati akiwasilisha hoteli za Turaco Collection katika maonesho hayo yanayofanyika jijini Arusha, Florenso alisema tukio hilo linawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya utalii, ukarimu, safari na uwekezaji kutoka Tanzania na mataifa mengine duniani.

Maonesho ya Karibu-KiliFAIR 2026 yanafanyika kuanzia Juni 4 hadi 7, 2026 katika Viwanja vya Magereza, Arusha.

Florenso alisema Turaco Collection imeendelea kuimarisha uwepo wake nchini kupitia hoteli zake katika maeneo mbalimbali. Dar es Salaam kuna Element by Westin Dar es Salaam na Delta Hotels by Marriott Dar es Salaam, huku Kaskazini mwa Tanzania kukiwa na Turaco Ngorongoro Valley Lodge, Tribute Portfolio na Turaco Manyara View Lodge, Tribute Portfolio. Zanzibar, kampuni inamiliki Turaco Nungwi Resort, Tribute Portfolio, Turaco Spice Tree Stone Town, Tribute Portfolio pamoja na Beyt Al Salaam by Turaco.

Alieleza kuwa hoteli zote za Turaco Collection zinazobeba chapa za kimataifa zinaendeshwa kwa kuzingatia viwango vya Marriott International, jambo linalochangia kuimarisha ubora wa huduma, matumizi ya teknolojia za kisasa na utoaji wa uzoefu wa kiwango cha kimataifa kwa wageni wanaotembelea Tanzania.

Akizungumzia matumizi ya Akili Bandia (AI) katika sekta ya ukarimu, Florenso alisema Marriott International inaamini teknolojia hiyo inapaswa kuboresha uzoefu wa wageni kwa kuufanya kuwa wa kibinafsi zaidi, wenye ufanisi mkubwa na rahisi, huku ikidumisha misingi ya ukarimu unaozingatia mahusiano ya kibinadamu.

Alisema kampuni hiyo inaendelea kuwekeza katika teknolojia za AI ili kuboresha mifumo ya uwekaji nafasi za malazi, shughuli za uendeshaji wa hoteli, programu za uaminifu kwa wateja na huduma mbalimbali za wageni.

“Teknolojia haitachukua nafasi ya ukarimu wa kibinadamu, bali itaongeza uwezo wa wafanyakazi wetu kutoa huduma bora zaidi. Mwelekeo wa Marriott International ni kutumia AI kuifanya safari ya mgeni, kuanzia kupanga safari, kuweka nafasi, kuwasili hotelini hadi kuondoka, kuwa rahisi, ya haraka na yenye uzoefu wa kipekee,” alisema Florenso.

Aliongeza kuwa kupitia ushirikiano wake na Marriott International, Turaco Collection inaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya teknolojia katika sekta ya ukarimu ili kuhakikisha wageni wanaotembelea Tanzania wanapata huduma zinazokidhi viwango vya kisasa vya kimataifa.









Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo, ametembelea banda la Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika Maonesho ya Kimataifa ya Mbeya City Expo 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Uhindini, jijini Mbeya, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na taasisi hiyo katika kulinda maslahi ya walaji na kuimarisha ushindani wa biashara nchini.

Katika maonesho hayo, FCC imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusu haki za mlaji, namna ya kutambua na kuepuka bidhaa bandia pamoja na umuhimu wa ushindani wa haki katika shughuli za biashara.

Elimu hiyo imevutia mamia ya wananchi waliojitokeza kutembelea banda hilo na kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayohusu biashara, ushindani na ulinzi wa walaji.

Akizungumza wakati akifunga Maonesho hayo yaliyodumu kwa siku tisa Mei 30, 2026 jijini Mbeya, Naibu Waziri Londo alisisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya bidhaa bandia, akieleza kuwa bidhaa hizo zinaathiri afya za watumiaji, kudhoofisha biashara halali na kupunguza mapato ya Serikali.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kanda wa FCC - Nyanda za Juu Kusini Bw. Dickson Mbanga, amesema taasisi hiyo imejipanga kuendelea kuimarisha kampeni za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kutambua bidhaa halisi na kuepuka kununua au kutumia bidhaa zisizo na viwango vinavyotakiwa.

Mbanga alisema Maonesho ya Mbeya City Expo yamekuwa jukwaa muhimu la kuifikia jamii kwa karibu na kutoa elimu inayolenga kuongeza uelewa kuhusu sheria za ushindani na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wafanyabiashara wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa bandia.

“Tunatumia maonesho haya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu hatari za bidhaa bandia na kumlinda mlaji. Lengo letu ni kuhakikisha watumiaji wanakuwa na taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi bora wanaponunua bidhaa mbalimbali sokoni,” alisema Mbanga.

Aliongeza kuwa FCC itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa biashara na vyombo vya usalama katika kudhibiti bidhaa bandia zinazoingia sokoni, huku ikiendelea kuhamasisha wananchi kutoa taarifa wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazotiliwa shaka.

Maonesho ya Mbeya City Expo 2026 yamewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali za uchumi, biashara na uwekezaji, huku yakitoa fursa kwa taasisi za umma na binafsi kuonesha huduma, bidhaa na mafanikio yao kwa wananchi. Kupitia ushiriki wake, FCC imeendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya kulinda walaji na kujenga mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki kwa

Said Mwishehe,Michuzi TV


MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) zimeingia makubaliana ya kuwapa ujuzi waraibu waliopona matumizi ya dawa za kulevya ili waweze kujitegemea na kuepuka kurejea kwenye matumizi ya dawa hizo.

Akizungumza wakati wa utiaji saini makubaliano hayo ya ushirikiano leo Juni 4,2026 jijini Dar es Salaam Kamishina Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo amesema mamlaka hiyo imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kudhibiti na kupambana na tatizo la dawa za kulevya nchini, ikiwemo kuzuia biashara haramu ya dawa hizo, kutoa elimu kwa jamii pamoja na kuimarisha huduma za tiba na urejeshaji wa waraibu katika jamii.

“Ushirikiano na VETA umetokana na kutambua umuhimu wa kuwawezesha waraibu waliopona kupata ujuzi wa kujiajiri na kushiriki shughuli za uzalishaji. Pia ushirikiano huu ni mfano mzuri wa namna taasisi za serikali zinavyoweza kushirikiana katika kutatua changamoto za kijamii kwa manufaa ya taifa,”alisema.

Alifafanua waraibu wengi wanaopata nafuu hujikuta wakirejea kwenye matumizi ya dawa za kulevya endapo hawapati shughuli za kufanya au mbadala wa kuwawezesha kujipatia kipato. Hivyo, mafunzo ya ufundi stadi yatawasaidia kujenga maisha mapya na kuondokana na mazingira yanayoweza kuwarudisha kwenye uraibu.

Aidha baada ya kuhitimu mafunzo hayo, wahitimu watawezeshwa kwa vifaa vidogo vya kuanzia kazi kulingana na ujuzi walioupata ili waweze kuanzisha shughuli za uzalishaji na kujipatia kipato. Pia wataunganishwa na taasisi za fedha zinazotoa mikopo midogo midogo (microfinance) ili kupata mitaji ya kuanzisha biashara na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Katika hatua nyingine, Kamishina Lyimo alisema ushirikiano huo unaendana na mradi wa serikali wa ujenzi wa kituo kikubwa cha urejeshaji na mafunzo kwa waraibu katika Jiji la Dodoma. Kituo hicho kitatoa mafunzo mbalimbali kwa mfumo wa VETA kwa waraibu waliopata nafuu na kuthibitishwa kuwa wana uwezo wa kuendelea na masomo ya ufundi stadi.

Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, waraibu wanaopata matibabu katika kliniki, nyumba za uangalizi maalumu (Sober Houses), hospitali za rufaa na za kanda watapimwa maendeleo yao, na watakapobainika kuwa wamepona kwa kiwango kinachowaruhusu kujifunza, wataelekezwa katika kituo hicho cha Dodoma au kwenye vituo vingine vya VETA vilivyopo nchini.

“Ili kurahisisha mchakato huo, DCEA imeanzisha kitengo maalumu cha Social Welfare Recovery Response, ambacho jukumu lake ni kufuatilia ustawi wa waraibu waliopona, kuwaunganisha na jamii, kuwasaidia kupata mikopo na fursa za ujasiriamali pamoja na kusimamia matumizi ya mitaji wanayopata ili kuhakikisha inaleta tija na kurejeshwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.”

Mamlaka hiyo imeishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha DCEA na kuimarisha ushirikiano kati ya sekta mbalimbali za serikali. Ilisema hatua hiyo itasaidia kuhakikisha waraibu waliopona hawarejei tena kwenye matumizi ya dawa za kulevya, huku wakipata nafasi ya kurejesha heshima yao katika jamii kupitia elimu, ujuzi na ajira.

DCEA pia imebainisha mahitaji ya huduma za matibabu na urejeshaji kwa waraibu yanaendelea kuongezeka nchini, hivyo ushirikiano huo unatarajiwa kuwa chachu ya kuwasaidia wengi zaidi kujenga maisha mapya na kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa upande Mkurugenzi Mkuu VETA CPA.Athony Kasore alisema ushirikiano huo unalenga kuwapa nafasi waraibu waliopata nafuu na kuthibitishwa kuwa tayari kwa mafunzo, ili wapate ujuzi utakaowawezesha kujitegemea kiuchumi. Kwa mujibu wa taasisi hiyo, wahitimu watakuwa na uwezo wa kujiajiri, kuajiriwa au hata kuanzisha vikundi vya uzalishaji vitakavyotoa ajira kwa wengine.

Aidha, alisema kuwa makubaliano hayo yanakuja kuimarisha juhudi zilizokuwa zikifanyika awali za kuwapatia mafunzo baadhi ya waraibu waliorejeshwa kutoka DCEA. Kupitia mfumo huo rasmi, waraibu wote watakaopokelewa watapatiwa mafunzo, kutambuliwa kwa ujuzi wao na kupewa vyeti vitakavyowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kijamii.

Aliongeza kuwa vyeti vitakavyotolewa vitawasaidia wahitimu kupata fursa mbalimbali za mikopo kutoka serikalini na taasisi za kifedha, hatua itakayowawezesha kuanzisha miradi na biashara za kujiongezea kipato. VETA imeeleza kuwa uwekezaji katika ujuzi ni sehemu muhimu ya kuwawezesha vijana kujenga maisha bora na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

“Tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za umma ili kukabiliana na changamoto za kijamii. Pia imewataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kushiriki katika mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya na kuwahamasisha vijana kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi kama njia ya kujenga mustakabali wenye tija kwao na taifa.”








MKURUGENZI wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),  Moshi Kabengwe, amewataka viongozi wa taasisi hiyo kuzingatia afya ya akili kwa watumishi wanaowasimamia kwa kuwa karibu nao na kujenga mazingira bora ya kazi yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Kabengwe ametoa rai hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa kufungua mafunzo juu ya masuala ya afya ya akili na ushauri nasaha kwa viongozi wa TRA kwa mkoa wa Dar es Salaam 

Amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za TRA za kuendelea kujenga mazingira bora ya kazi ili watumishi waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuchangia kikamilifu katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

"Mapato ya kodi ndiyo yanayowezesha utoaji wa huduma mbalimbali za jamii, hivyo ni muhimu kila mmoja wetu awe na afya njema kimwili na kiakili ili aweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo," amesema Bw.Kabengwe.

Ameeleza kuwa kupitia mafunzo hayo, Kiongozi wanapatiwa maarifa ya kutambua dalili na viashiria vya msongo wa mawazo kwa watumishi, jambo litakalowasaidia kuchukua hatua za mapema kabla changamoto hizo hazijaathiri utendaji kazi.

Kabengwe amesema kiongozi anapaswa kuwa karibu na watumishi wake na kujenga mahusiano mazuri yatakayowafanya wajisikie huru, kuthaminiwa na kuwa na hamasa ya kufika kazini kila siku.

"Ukiona dalili kwamba mtumishi anaelekea kupata changamoto ya afya ya akili, ni muhimu kuanza kuchukua hatua za haraka za kumsaidia na kuweka mikakati ya muda mrefu ya kumwezesha kurejea katika hali yake ya kawaida," amesema.

Ameongeza kuwa viongozi wanapaswa kuwashauri watumishi wao na kuwaelekeza njia sahihi za kupata msaada wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali za kisaikolojia.

Amesisitiza kuwa afya ya akili ni suala muhimu katika kuongeza tija mahali pa kazi na kwamba viongozi wana wajibu wa kuhakikisha wanatengeneza mazingira salama, yenye ushirikiano na yanayowajali watumishi wote.


📍SONGWE

Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi imekagua na kupitia Mpango wa Ufungaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Shanta (New Luika Gold Mine) uliopo mkoani Songwe ili kuhakikisha mpango huo unazingatia matakwa ya Sheria ya Madini, Sura ya 123, pamoja na Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira za mwaka 2010.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi, Mhandisi Hamisi Kamando, amesema mapitio hayo yanalenga kuhakikisha mgodi una mpango madhubuti wa kurejesha mazingira katika hali salama baada ya shughuli za uchimbaji kukamilika, sambamba na kulinda afya na usalama wa wananchi wanaouzunguka mgodi huo.

Amesema kwa mujibu wa Sheria ya Madini na Kanuni ya 206 ya Kanuni za Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira za mwaka 2010, migodi yote ya kati na mikubwa inatakiwa kuandaa na kuwasilisha mipango ya ufungaji migodi kwa Mkaguzi Mkuu wa Migodi kwa ajili ya mapitio ya kitaalam kabla ya kuidhinishwa na Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi.

Mhandisi Kamando amefafanua kuwa jukumu la Kamati hiyo ni kupitia mipango ya ufungaji migodi na kutoa ushauri wa kitaalam ili kuhakikisha migodi inafungwa kwa kuzingatia viwango vya mazingira, usalama na afya, na siyo kusitisha shughuli za uzalishaji kabla ya migodi kumaliza rasilimali zake.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Shanta (New Luika Gold Mine), Mhandisi Exupery Lyimo, amesema mgodi huo unaendelea kutekeleza viwango vya usalama, afya na utunzaji wa mazingira na upo tayari kutekeleza maelekezo yote yatakayotolewa na Kamati ili kuboresha mpango wake wa ufungaji.

Kikao hicho kimewakutanisha wataalam kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Madini, Wizara ya Maji, Wizara ya Maliasili na Utalii, Tume ya Matumizi Endelevu ya Ardhi, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Tume ya Madini pamoja na viongozi wa Serikali wa ngazi ya wilaya.











MITAA imepata stori mpya ya ushindi kupitia Books of Egypt kutoka Meridianbet. Huu ni mchezo unaokupeleka moja kwa moja kwenye ulimwengu wa Misri ya kale, ambako siri za utajiri na mafanikio zinakutana. Kwa wanaopenda burudani, hapa ndipo sehemu sahihi.

Books of Egypt imeundwa kwa mtindo wa kipekee unaokupa nafasi ya kufurahia mchezo huku ukisaka ushindi mkubwa. Kila alama inaweza kuwa mwanzo wa safari mpya ya mafanikio. Kinachohitajika ni kufanya maamuzi sahihi, kuwa makini na kucheza kwa mbinu zako.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Moja ya vivutio vikubwa vya mchezo huu ni alama ya kitabu ambayo inaweza kubadilisha kila kitu ndani ya muda mfupi. Alama hii maalum hufanya kazi muhimu na ikitokea mara tatu au zaidi, inaweza kufungua mizunguko ya bure inayoongeza nafasi za kupata ushindi zaidi.

Mbali na hilo, mchezo huu una bonasi maalum inayoongezeka kadri unavyoendelea kucheza. Kipengele hiki kinaongeza hamasa na kuwapa wachezaji nafasi ya kuendelea kufuatilia ushindi wao kwa matumaini makubwa zaidi. Kila mzunguko unaweza kuwa nafasi mpya ya kubadilisha matokeo na kuandika historia yako mwenyewe.

Usikubali kubaki nyuma wakati wengine wanafurahia burudani hii ya kipekee. Tembelea Meridianbet leo, fungua Books of Egypt na ujionee mwenyewe kwa nini mchezo huu umevutia mashabiki wengi. Weka dau lako kwa umakini, furahia kila hatua ya mchezo na uanze safari yako ya kusaka ushindi mkubwa.




ZIMEBAKI siku chache sana kuelekea michuano mikubwa ya Kombe la Dunia 2026 ambayo inatarajiwa kuanza June 11 huku baadhi ya timu zikipewa nafasi kubwa ya kushinda taji hili. Je nafasi hii unampa nani?

Timu ya kwanza inayopewa nafasi ya kushinda Kombe la Dunia na Meridianbet ni Hispania ambayo mpaka sasa imepewa ODDS 5.50 kujipatia kombe hili. Chini ya kocha mkuu Luis de la Fuente, Hispania imekuwa ni timu yenye ubora wa hali ya juu. Kikosi kizru cha wachezaji wenye ubora akiwemo Lamine Yamal, Pedri, Gavi, Williums wamekuwa tishio kwa mabeki wa timu pinzani.

Changamoto yao kubwa itakuwa kutumia nafasi wanazotengeneza na kukabiliana na presha ya hatua za mtoano dhidi ya mataifa makubwa akiwemo bingwa mtetezi Argentina, Ufaransa, au Brazil

Je mabingwa hawa wa Kombe la Euro wanaweza kushinda taji hili?. Tengeneza pesa kwenye michuano hii ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kuanza siku chache zijazo.

Piga pesa leo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Nafasi ya pili ya kuchukua Kombe la Dunia inaenda kwa Ufaransa ambao pia ni wanafainali wa 2022. Hii ni timu ambayo imejengwa na ubora mkubwa chini ya kocha mkuu Didier Deschamps ambaye ana uzoefu mkubwa kabisa kweye mashindano haya baada ya kucheza fainali mbili mfululizo yaani 2018 na 2022. Suka jamvi hapa.

Timu hii ina mchanganyiko wa nyota wenye uzoefu na vipaji vya kizazi kipya. Wakiwa na wachezaji kama Kylian Mbappé, Ousmane Dembélé, Desire Doue, Aurélien Tchouaméni, William Saliba na wengine wengi kama kina Barcola ambao wanatarajiwa kukipa kikosi nguvu zaidi.

Ufaransa wana timu bora kabisa ambayo inaweza ikapambania Kombe hili kabisa kwani wana wachezaji wenye nguvu, kasi, kujituma na uthabiti. ODDS KUBWA ya 6.00 inakungoja hapa. Jisajili sasa.

Nao Uingereza ni Taifa lingine ambalo linapewa nafasi ya tatu na wakali wa ubashiri Tanzania Meridianbet kushinda taji hili kwa ODDS 7.00 kwani mpaka sasa chini ya kocha mkuu Thomas Tuchel timu hiyo imeimarika sana na inahitaji kukata ukame huo toka mwaka 1966.

Wakiwa na nyota kama Harry Kane, Bukayo Saka, Declan Rice, Eze na wengine inawapa nafasi ya kuwa moja ya timu za kushindania taji hili. Uingereza wana uwezo wa kushambulia kwa njia mbalimbali na kuamua mechi kupitia ubunifu wa viungo na ukali wa washambuliaji wao.

Lakini changamoto kubwa kwa timu hiyo imekuwa kutafsiri ubora wa kikosi kuwa mafanikio katika mechi za hatua za mwisho. Mara nyingi wamekuwa wakifika mbali kwenye mashindano makubwa lakini wakishindwa kuvuka kizingiti cha nusu fainali au fainali. Je unadhani kwa kikosi ambacho Tuchel amekiita anaweza akafika nacho Fainali?. Timu hii imepewa Odds 7.00 kushinda taji hili. Jisajili sasa.

Bingwa mtetezi wa Kombe hili Argentina naye yupo kwenye timu 5 ambazo zinapewa nafasi ya kushinda kombe hili. Ikumbukwe kuwa nguvu ya Argentina haipo tu kwenye majina makubwa ya wachezaji wao, bali pia katika umoja, nidhamu na uzoefu walioujenga kwa miaka kadhaa chini ya kocha Lionel Scaloni. Kikosi hiki kina mchanganyiko wa nyota wenye uzoefu kama Lionel Messi, Lautaro Martínez na Rodrigo De Paul pamoja na kizazi kipya chenye vipaji kinachoendelea kuchukua nafasi muhimu.

Je chini ya Lionel Scalon Messi na Argentina yek wanaweza kutetea taji lao msimu huu. Bashiri timu hii kuchukua ubingwa pale Meridianbet kwa Odds 9.00 na uwe mshindi wako leo.

Na timu ya 5 inayokamlisha zile Top 5 ni Brazil ambao mara ya mwisho kuchukua Kombe hili ilikuwa ni mwaka 2002 na kufanya wawe na makombe matano hadi sasa. Brazil bado ni taifa lenye historia kubwa zaidi kwenye mashindano haya, na nguvu yao kubwa ipo katika ubora wa wachezaji wa kushambulia.

Pia wana wachezaji wenye uwezo kama Neymar, Vinícius Júnior, Raphinha Marquinhos, Bruno Guimarães, na wengine wengi. Chini ya kocha mkuu Carlo Ancelotti wanatarajiwa kufanya vyema. Lakini je bado wana timu yenye uwezo wa kupambana na timu zenye ubora kwasasa. 9.00 ndio Odds za timu hii kubeba ubingwa. Beti sasa.


ALBINISM Sports Club yenye Makao Makuu yake jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TASACI), imeandaa mechi ya kirafiki kati ya timu ya Bunge.

Mechi hiyo ya kirafiki itakayofanyika Juni 6 2026 katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma na mtanange huo huo ni sehemu ya maandalizi kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kuongeza Uelewa kuhusu Ualbino, ambayo huadhimishwa duniani kote Juni 13 Juni kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha jamii kuhusu haki, usawa, heshima na ustawi wa watu wenye ualbino.

Taarifa iliyotolewa katika vyombo vya habari leo Juni 3,2026 na Abdallah Majiwa ambaye ni Mwenyekiti wa Albinism Sports Club amesema tukio hilo linatarajiwa kuwakutanisha pamoja Wabunge, watu wenye ualbino, wananchi wa Jiji la Dodoma na maeneo ya jirani na wadau mbalimbali wa masuala ya
haki za binadamu.

Amefafanua kuwa kaulimbiu ya mwaka huu ni: “Wezesha Watu Wenye Ualbino kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu.” Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo.

“Tunatoa mwito kwa wananchi wote wa Dodoma na maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki na kuunga mkono tukio hili muhimu lenye lengo la kujenga jamii yenye usawa, heshima na fursa
kwa wote.

“Mbali na burudani ya michezo, mechi hii inalenga kuhamasisha ushirikishwaji wa watu wenye ualbino katika nyanja zote za maendeleo, kuongeza uelewa wa jamii kuhusu changamoto na fursa zinazowakabili, na kuendeleza mjadala kuhusu haki, usawa na fursa kwa watu wenye ualbino nchini Tanzania.”

Ameongeza malengo mahsusi ya mechi hiyo ni kuwaleta pamoja Wabunge, watu wenye ualbino na wadau mbalimbali ili kujenga mshikamano na kutafakari kwa pamoja namna bora ya kuwalinda, kuwawezesha na kuwaendeleza watu wenye ualbino;

Pia kuunganisha juhudi za Bunge, Serikali na wadau wengine katika kupinga unyanyapaa,kuondoa imani potofu, na kukomesha vitendo vya ubaguzi na ukatili dhidi ya watu wenye ualbino,kuelimisha jamii kuhusu masuala ya afya yanayowahusu watu wenye ualbino hususan umuhimu wa kinga dhidi ya miale ya jua na utunzaji wa afya ya ngozi;

Katika siku hiyo pia shughuli mbalimbali siku ya mechi ya waheshimiwa wabunge na watu wenye ualbino, inayotarajiwa kuanza saa 11 jioni na itatanguliwa na matukio mbalimbali muhimu yatakayolenga kuelimisha, kuhamasisha na kukuza ushirikishwaji wa watu wenye ualbino katika jamii.

Amesema matukio hayo ni pamoja na semina kubwa kuhusu masuala ya afya, mazingira na haki za watu wenye ualbino, utoaji wa huduma za afya ya ngozi, uwasilishaji wa risala ya waandaaji, hotuba fupi kutoka kwa viongozi mbalimbali wakiwemo waheshimiwa wabunge na mgeni rasmi pamoja na uzinduzi rasmi wa Albinism International Marathon.

Kuhusu Historia ya Siku ya Kimataifa ya Kuongeza Uelewa Juu ya Ualbino (13 Juni)
inatokana na Azimio la umoja wa mataifa kuhusu kuanzishwa kwa Siku ya Kimataifa ya Kuongeza Uelewa kuhusu Ualbino (International Albinism Awareness Day) lilipitishwa Desemba 18 2014 kupitia Azimio Na. A/RES/69/170 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa

Aidha Juni 13 ilichaguliwa kuwa siku rasmi ya maadhimisho hayo kwa sababu ndio tarehe ambayo Umoja wa Mataifa ulipitisha Azimio lake la kwanza kuhusu haki za watu wenye ualbino mwaka 2013.

Kuhusu Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira amesema ni mdau muhimu katika maadhimisho haya kupitia shughuli mbalimbali za elimu, afya na uhifadhi wa mazingira.

Mchango wake unajumuisha kuelimisha jamii kuhusu afya ya ngozi, kinga dhidi ya madhara ya mionzi ya jua kwa watu wenye ualbino, pamoja na kupinga imani potofu zinazochochea unyanyapaa na ukatili.Pia kukuza matumizi sahihi na salama ya tiba asilia kwa mujibu wa Sheria Na. 23 ya mwaka 2002 ya Tiba Asili na Tiba Mbadala.

Pia kuhamasisha utunzaji na uhifadhi wa mazingira kama msingi wa afya bora ya jamii,kulinda mimea tiba na rasilimali nyingine za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho na kushirikiana katika kampeni za kupinga unyanyapaa, ubaguzi na ukatili dhidi ya watu wenye ualbino na watu wenye ulemavu kwa ujumla kupitia michezo na shughuli za kijamii.




Na Oscar Assenga, Tanga


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (MB), amesisitiza umuhimu wa taasisi za kifedha nchini kuendelea kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii kwa kuanzisha na kuunga mkono mipango inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.

Akizungumza jijini Tanga wakati wa uzinduzi rasmi wa ushirikiano kati ya Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) kupitia mpango wa “Cash Waqf”, Mwinjuma alisema ushirikiano huo ni hatua muhimu katika kuongeza upatikanaji wa rasilimali fedha za kufadhili elimu ya juu nchini.



Uzinduzi huo pia uliambatana na ufunguzi rasmi wa tawi la PBZ IKHLAS, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo wa kusogeza huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi.

“Ni muhimu taasisi za fedha nchini kuendelea kushiriki katika maendeleo ya jamii kwa kuunga mkono mipango itakayowanufaisha wananchi katika maeneo mbalimbali,” alisema Mwinjuma.



Aidha, aliipongeza PBZ kwa juhudi zake za kupanua huduma za kifedha katika maeneo tofauti nchini, akibainisha kuwa hatua hiyo inachangia kuongeza ujumuishaji wa kifedha na kukuza uchumi wa taifa.

Pia aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na benki hiyo, ikiwemo huduma za akaunti, uwekezaji na mikopo, ili kuimarisha shughuli zao za kiuchumi na kuboresha ustawi wa maisha yao.



Kwa upande wake, Mkurugenzi Mwendeshaji wa PBZ, CPA Fahad Hamid, alisema benki hiyo iliyoanzishwa Juni 30, 1966, inakaribia kutimiza miaka 60 ya kutoa huduma za kifedha kwa wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Alisema PBZ inaendelea kupanua wigo wa huduma zake nchini, ambapo kwa sasa imefanikiwa kufika katika mikoa minane ya Tanzania Bara, hatua inayolenga kuwafikia wananchi wengi zaidi.



Naye Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dkt. Bill Kiwia, alisema ushirikiano huo una lengo la kupanua vyanzo vya rasilimali fedha ili kuwawezesha vijana wengi zaidi kupata ufadhili wa masomo, hususan wanaojiunga na mafunzo ya amali kupitia vyuo vya kati.



Kwa mujibu wa Dkt. Kiwia, makubaliano hayo yataongeza uwezo wa HESLB kuwafikia wanafunzi wengi zaidi na kusaidia kuzalisha nguvu kazi yenye ujuzi unaohitajika katika viwanda na sekta nyingine za uzalishaji.



Akifafanua kuhusu mpango wa “Cash Waqf”, Meneja wa Uzingatiaji wa Shariah wa PBZ IKHLAS, Dkt. Issa Mohamed, alisema mpango huo unatoa fursa kwa watu binafsi, taasisi, wahisani na wawekezaji kuchangia au kuwekeza fedha zitakazosaidia kuongeza upatikanaji wa ufadhili wa elimu ya juu kwa vijana wa Kitanzania.



Alisema kupitia ushirikiano huo, PBZ na HESLB wanatarajia kuweka mfumo endelevu wa ukusanyaji na uwekezaji wa fedha kupitia mpango wa “Cash Waqf”, hatua itakayoongeza upatikanaji wa mikopo ya elimu ya juu na kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kutimiza ndoto zao za elimu.

Ushirikiano huo unatajwa kuwa miongoni mwa mikakati muhimu ya kuongeza fursa za elimu kwa vijana na kuchangia maendeleo ya rasilimali watu nchini.

Top News