Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro ikiongozwa na makamu Mwenyekiti Dkt. Harriet Mtae jana tarehe 11 julai, 2026 imekagua uboreshaji wa miundombinu ya utalii eneo la Nyayo za Laetoli lililopo hifadhi ya Ngorongoro 

Wakiwa Laetoli Wakurugenzi hao wamekagua uhifadhi wa Nyayo zilizogundulika katika eneo hilo miaka zaidi ya milioni 3.6 iliyopita na kuangalia hatua za utekelezaji wa mradi wa Geopark unaohusisha ujenzi wa jengo la kupokelea wageni, jengo la kupumzika wageni, jengo lililojengwa kwa ajili ya kuhifadhi Nyayo sambamba na miundombinu mingine.

Naibu Kamishna wa Uhifadhi Joas Makwati anayesimamia uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii ameeleza kuwa ziara hiyo imelenga kutathmini utekelezaji wa miradi inayofanywa na mamlaka kwa lengo la kuimarisha shughuli za uhifadhi, kuboresha huduma za utalii na kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro.

Pamoja na kukagua miundombinu ya utalii wakurugenzi hao wamepokea taarifa ya hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na mipango ya kuendelea kuboresha mazingira ya utalii na shughuli za uhifadhi.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NCAA, Dkt. Harieth Mtae, alisema miradi hiyo inaakisi dhamira ya mamlaka ya kuendelea kuwekeza katika uboreshaji wa vivutio vya utalii na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wageni.

Ameongeza kuwa maboresho hayo yanatarajiwa kuongeza thamani ya vivutio vya utalii, kuvutia watalii zaidi na kuendelea kuitangaza Hifadhi ya Ngorongoro kama moja ya vivutio vinavyoongoza duniani.







Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Wasafi Media, Nasib Abdul maarufu Diamond Platnumz, amesema utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari unaweka mazingira bora ya kukuza uwekezaji katika sekta ya habari kwa kuhakikisha vyombo vya habari vinaendeshwa kwa kuzingatia sheria, weledi na viwango vya taaluma.

Diamond alitoa kauli hiyo tarehe 11 Juni, 2026 alipotembelea Banda la Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), kufuatia mwaliko wa Bodi hiyo ili kujionea huduma na elimu inayotolewa kwa waandishi wa habari pamoja na wananchi.

Alisema uwekezaji katika sekta ya habari unahitaji nidhamu, maono, subira na uongozi unaozingatia sheria, akibainisha kuwa usimamizi unaofanywa na JAB unasaidia wawekezaji kuelewa matakwa ya kisheria na namna ya kuyazingatia bila kuhisi kuwa biashara zao zinakwamishwa.

"Utekelezaji na usimamizi wa Sheria ya Huduma za Habari unaonesha ni kwa kiwango gani Serikali inaunga mkono uwekezaji wa vijana katika sekta ya habari. Kazi ya Bodi si kuzuia watu kufanya biashara, bali kuwaelekeza kufuata matakwa ya sheria na kuwahamasisha kuongeza elimu na kukidhi vigezo vinavyotakiwa," alisema Diamond.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa sheria unahitaji busara, maarifa na uwezo wa kuwaelimisha wadau ili waelewe mabadiliko ya taratibu bila kujenga hofu au kuona kuwa wanawekewa vikwazo.

"Kazi hii inahitaji busara na maarifa ya kuwafundisha watu, kuwaelekeza na kuwafanya waelewe taratibu mpya pasipo kuona kwamba wameharibiwa biashara zao. Nimeona Bodi ina timu nzuri inayounga mkono maono ya uongozi wake katika kusimamia sekta hii," alisema Diamond.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alimpongeza Diamond kwa uwekezaji wake katika sekta ya habari na kwa Wasafi Media kuendelea kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari.

Alisema JAB itaendelea kushirikiana na wamiliki wa vyombo vya habari na wadau wengine kuhakikisha sheria inatekelezwa kwa njia inayokuza weledi, uwajibikaji na maendeleo ya sekta ya habari, huku ikitoa elimu na ushauri unaowawezesha wadau kutekeleza matakwa ya sheria kwa ufanisi.

Ziara ya Diamond katika Banda la JAB ilikuwa sehemu ya maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika ndani ya Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, ambapo Bodi imekuwa ikitoa huduma za ithibati, elimu kuhusu Sheria ya Huduma za Habari na ushauri kwa waandishi wa habari, wamiliki wa vyombo vya habari na wananchi.

Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Kisheria wa Utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa Waandishi wa Habari Wakongwe, hatua inayolenga kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari waliolitumikia Taifa kwa muda mrefu na kwa utumishi uliotukuka katika maendeleo ya sekta ya habari nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 11, 2026, wakati wa maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika katika Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Kupitia hotuba yake iliyosomwa na Dkt. Egbert Mkoko, Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Bw. Tido Mhando, alisema mwongozo huo umeandaliwa kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa Bodi chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 pamoja na Kanuni zake, ili kuweka utaratibu wa utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa waandishi wa habari wakongwe waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya taaluma hiyo.

Alisema mwongozo huo unawahusu waandishi wa habari ambao wakati Sheria ya Huduma za Habari ilipoanza kutumika mwaka 2016 walikuwa na umri wa miaka 50 au zaidi na walikuwa tayari wametoa mchango mkubwa katika sekta ya habari, lakini hawakupata fursa ya kujiendeleza hadi kufikia sifa za kitaaluma zinazohitajika kwa mujibu wa sheria.

"Mwongozo huu unalenga kuhifadhi historia ya tasnia ya habari, kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe na kuhakikisha uzoefu wao unaendelea kuwa sehemu ya urithi wa taaluma ya uandishi wa habari nchini," ilieleza sehemu ya hotuba ya Mwenyekiti.

Bw. Mhando alisisitiza kuwa mwongozo huo hauondoi wala haupunguzi masharti ya msingi yaliyowekwa na Sheria ya Huduma za Habari kuhusu sifa za kupata ithibati kwa waandishi wa habari, bali unaweka utaratibu wa kutekeleza mamlaka ambayo sheria imeipa Bodi kuhusu utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa watu wenye utumishi uliotukuka na waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya sekta ya habari.

Aidha, aliipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuendelea kuiwezesha Bodi kutekeleza majukumu yake na kuimarisha ushirikiano unaolenga kukuza weledi, uwajibikaji na maadili katika taaluma ya uandishi wa habari.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alisema uzinduzi wa mwongozo huo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari na unaonesha dhamira ya Bodi ya kuimarisha viwango vya taaluma huku ikitambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe waliolitumikia Taifa kwa uaminifu, uzalendo na weledi.

Sambamba na uzinduzi huo, JAB iliendesha mdahalo uliowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchini, utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari pamoja na mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika mwaka mmoja wa utekelezaji wa mfumo wa utoaji wa ithibati kwa waandishi wa habari waliokidhi vigezo vya sheria.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, amesema thamani ya fedha itaendelea kuwa imara kuelekea kipindi cha mavuno ili kuwawezesha wakulima kupata thamani stahiki ya mazao yao kulingana na shughuli za kiuchumi wanazozifanya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Julai 10, 2026, Tutuba amesema kiwango cha riba ya Benki Kuu cha asilimia 6.25 kinalenga kuhakikisha kunakuwa na utulivu wa bei na mfumuko wa bei unaendelea kubaki kati ya asilimia 3 hadi 5.

Amesema kiwango hicho pia kitawezesha Mabenki kuwa na ukwasi wa kutosha kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, hivyo kusaidia shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara nchini.

Tutuba amesema wakulima wanapoanza kuvuna mazao yao, thamani imara ya fedha itasaidia kuhakikisha wanapata malipo yanayolingana na thamani halisi ya mazao yao sokoni.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa nje ya nchi pia watanufaika kwa kupata fedha za kigeni kulingana na thamani ya fedha walizotumia katika uzalishaji, huku tathmini ikionyesha kiwango cha riba cha asilimia 6.25 kinatosha kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.

Aidha, amesema BoT hutumia Maonesho ya Sabasaba kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kiwango cha riba ya Benki Kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza ukwasi katika mzunguko wa uchumi na kuwezesha upatikanaji wa fedha kwenye mabenki ya biashara.

Tutuba amesema maonesho hayo pia ni fursa kwa Watanzania kujifunza, kupata bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na mbinu mpya za kufanya shughuli za kiuchumi zinazochangia ukuaji wa uchumi wa nchi.






Na Mwandishi Wetu

MECHI kati ya timu ya soka ya Chuo cha Future World na timu ya Chanika Veteran umemalizika kwa sare 1-1 huku ujumbe mkubwa katika mechi hiyo ni kuhamasisha vijana kujiunga na Chuo hicho kupata ujuzi.

Katika mechi hiyo iliyochezwa leo Julai 11,2026 katika uwanja wa VODP uliopo Chanika kata ya zingiziwa wilayani Ilala jijini Dar es Salaam umeshuhudiwa na mamia ya wananchi wa Chanika na viunga vyake.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mechi hiyo Ofisa Masoko kutoka chuo Cha Future World Vocational David Msumba amesema lengo la mechi hiyo ni kukitambulisha chuo kwa wananchi hasa katika kata za Chanika na Zingiziwa

“Tumecheza mechi kati yetu Future World na Chanika Veterani na lengo kuu ni kuhamasisha wananchi kujiunga na chuo chetu ili kupata ujuzi kupitia kozi mbalimbali tunazitoa.”

Ametaja kozi zinazotolewa na chuo hicho ni ufundi wa magari na pikipiki, umeme wa majumbani,ulezi wa watoto wadogo,mafunzo ya urembo na ususi,Hotel Management pamoja na Computer Applications.

“Future World ni chuo chenye uzoefu wa karibu miaka 30 sasa, tangu kilipoanzishwa kwenye utoaji wa Mafunzo ya ufundi stadi katika fani mbalimbali.

“Hivi Karibuni, chuo hiki kimefungua tawi lake jipya eneo la Chanika kwa Ndevu eneo ambalo lina mandhari bora kabisa kwa utoaji wa elimu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa hosteli nzuri za wanafunzi.

“Vijana hasa wahitimu wa kidato cha nne mnakaribishwa chuoni au kuingia kwenye Tovuti ya chuo na kupata fomu ya kujiunga na mafunzo uyapendayo, au kwa mawasiliano 0715 015778 ”amesema Msumba




















Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa Kusikiliza makundi mbalimbali ya kijamii, leo tarehe 11/07/2026 amesikiliza makundi ya kijamii 52 ndani ya Mkoa wa Songwe.

Aidha, Ndg Rabia Abdalla Hamid amesema kuwa ameridhishwa na utendaji kazi wa viongozi wa Serikali ndani ya Mkoa wa Songwe baada ya wananchi katika makundi mbalimbali ya kijamii, makundi 52 kuuliza maswali, ushauri, maoni, changamoto, kero na baadae kujibiwa kwa usahihi na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe Jabir Makame aliyeambatana na Viongozi mbalimbali wa Serikali kwa ajili ya kujibu hoja za wananchi.

#KaziNaUtuTunasongaMbele

#CCMKimbilioLaWananchi

#CCMTabasamuLaWatanzania










Bonanza la kimichezo lililohusisha vyombo vya ulinzi na Usalama na watumishi wa halmashauri katika Wilaya ya Ulanga Mkoa wa Morogoro lafana huku likiwaleta karibu vyombo hivyo na watumilishi wa halmashauri wilayani humo.

Mgeni rasmi katika bonanza hilo alikuwa ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ulanga Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Deogratius Challe, ambapo alifungua bonanza hilo huku akiwataka watumishi hao na maafisa wa vyombo hivyo kutumia michezo hiyo kama sehemu ya kuimarisha afya zao pamoja na kujenga udugu utakaosadia kudumisha ushirikiano pamoja na kukomesha vitendo vya kiharifu Wilayani humo.

Ameongeza kuwa mafanikio katika utendaji wa kazi yanategemea mshikamano na ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali pamoja na wananchi ili kuifanya Wilaya hiyo iendele kuwa shwari muda wote.

Kwa Upande wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nalolikatumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu kinga na namna ya kukabiliana na majanga ya moto, huku maafisa wa Jeshi hilo wakitoa elimu kuwa moto una manufaa katika maisha ya kila siku, lakini unaweza kuwa hatari usipotumika au kudhibitiwa kwa usahihi na kwa wakati.

Nao idara ya Uhamiaji Wilayani humo ikatoa elimu kuhusu masuala ya uhamiaji, ikiwemo taratibu za utoaji wa hati za kusafiria na umuhimu wa wageni wote wanaoingia na kutoka nchini kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.

Sambamba na hilo afisa Utamaduni wa Wilaya ya Ulanga George Kayora, alieleza kufurahishwa na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Halmashauri na vyombo vya ulinzi na usalama huku akiweka wazi kuwa bonanza hilo limeimarisha mahusiano, mshikamano na afya za washiriki kupitia michezo hiyo.

Timu shiriki katika Bonanza hilo zilikuwa ni vyombo vya ulinzi na usalama vya Wilaya ya Ulanga dhidi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, ambapo Katika bonanza hilo, Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha Polisi Jamii kilitoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kubaini,kuzuia, na kutanzua uhalifu, pamoja na kutoa taarifa kwa wakati kuhusu vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa jamii.

Michezo iliyowakutanisha watumishi hao ni Mpira wa miguu, pete, bao, karata huku matokeo katika mpira miguu timu ya vyombo vya ulinzi ikiichapa goli tatu kwa mbili timu ya halmashauri.










 
 

Mr Walter Makundi (in blue shirt), a Tanzanian Civil and Structural Engineer who has lived in Singapore with his family since 1994, has described his recent meeting with senior government officials from several African countries as a great honour.


The engagement, organised by the Chandler Academy of Governance, brought together delegates from Rwanda, Kenya, Uganda, Mauritius, Malawi, Somalia, Zambia, Tanzania and South Africa.


“I am sincerely grateful to the Chandler Academy of Governance for allowing me to share my personal reflections on Singapore’s remarkable transformation,” Mr Makundi said.


He noted that during his more than three decades in Singapore, he had witnessed first-hand how visionary leadership, long-term planning, strong institutions and disciplined implementation had helped transform the country into one of the world’s most advanced and prosperous nations.


“It was a privilege to exchange ideas with such distinguished government leaders and to reflect on lessons that may be useful to African countries,” he said.


Mr Makundi expressed hope that Singapore’s development journey would continue to inspire African nations as they pursue sustainable growth, modern infrastructure, stronger institutions and improved governance.


He thanked the Chandler Academy of Governance and all participating delegates for the thoughtful discussions, warm fellowship and memorable experience.


The Chandler Governance Group (CGG) is an international non-profit organisation headquartered in Singapore. It works with governments to build capabilities through training, hands-on projects, partnerships, and knowledge creation and sharing.


CGG founder Richard F. Chandler established CGG in 2019 as the Chandler Institute of Governance (CIG), with the support of a group of seasoned former government leaders from several countries. He saw the value of an independent institute that would work with governments in highly practical ways. We are a practitioner-focused organisation, focusing on the “how” rather than just the “what” and “why”.

CIG rebranded in 2026 as CGG.


The Chandler Academy of Governance (CAG) is the Learning and Development division of CGG. We design and deliver training programmes for public sector leaders, equipping them with the skills to deliver high-performance government, with its signature programmes anchored in proprietary curriculum, practitioner-focused, and contextualised to local needs. 


It utilises a range of teaching techniques, including seminars, expert-led discussions, and site visits. We also work with clients to design customised programmes for public servants, tailored to the country context, objectives, and participant profiles.

.








BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya Kiswahili inaendelea kukua na kuenea duniani ambapo sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni 200 katika nchi 14 duniani na kutumika rasmi katika jumuiya kadhaa za kikanda barani Afrika na kimataifa.

Balozi Matinyi aliyasema hayo kwenye sherehe za Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani zilizoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Algeria na kufanyika jijini Algiers tarehe 9 Julai zikihudhuriwa na mabalozi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, taasisi za umma na binafsi, wanazuoni na waandishi wa habari walioongozwa na Katibu Mnadhimu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni na Sanaa ya Algeria, Bibi Nacera Ayaïchia.

“Mbali ya Tanzania, Kiswahili pia ni lugha ya taifa nchini Kenya, Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),” alisema Balozi Matinyi kwenye hotuba yake aliyoitoa kwa lugha ya Kiswahili na nakala yake katika tafsiri ya lugha za Kiarabu, Kifaransa na Kiingereza kusambazwa kwa wageni waalikwa waliopewa fursa ya kuifuatilia kwa sauti na maandishi kwenye skrini kubwa.

Sherehe hiyo ilinogeshwa na filamu fupi ya dakika kumi iliyoonesha marais wa zamani na wa sasa wa Tanzania na baadhi wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wakihutubia kwa lugha ya Kiswahili katika nyakati tofauti.

Filamu hiyo pia inamwonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwa lugha ya Kiswahili nchini Komoro mwaka 2025 kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru wa taifa hilo.

Balozi Matinyi aliongeza pia kwamba Kiswahili ni lugha rasmi ya Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Kadhalika, Balozi Matinyi aliitaja mifano ya redio za nchi za Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japan, China, Iran, India na wakati fulani Marekani ambazo hutumia lugha ya Kiswahili katika matangazo yake ya kila siku.

Akirejea kauli mbiu ya mwaka huu ya siku hiyo ya “Kiswahili kwa Amani, Mshikamano na Diplomasia ya Uchumi Duniani”, Balozi Matinyi alisema Kiswahili ni lugha ya kujivunia ambayo imetumika katika mapambano ya ukombozi barani Afrika na inaendelea kutumika kulinda amani, kuleta mshikamano na kujenga uchumi barani Afrika.

Sherehe hiyo iliyotumia lugha nne zikiongozwa na Kiswahili, ilipambwa pia na vinywaji vya chai na kahawa ya Tanzania, vyakula vya mapishi ya Kiswahili, maonesho ya mavazi ya wakaazi wa pwani ya Tanzania kama khanga, baibui, kanzu, vikoi na vitenge yaliyooneshwa na wanafunzi wa Tanzania.

Wanafunzi hao wa Tanzania wanaosoma kwenye vyuo vikuu nchini Algeria, walicheza pia ngoma mbili za makabila ya Tanzania ya Kimasai na Kihaya na kuimba shairi la Kiswahili.

Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani huadhimishwa mwezi Julai tangu mwaka 2022 kufuatia uamuzi wa UNESCO wa mwaka 2021 wa kuitangaza tarehe 7 Julai kuwa siku ya maadhimisho ya lugha hii pekee barani Afrika kuwahi kupewa hadhi hii kimataifa.


Top News