Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Kilimo Hai Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo (TOAM) linaratarajia kufanya Mkutano MKuu wa Nne Machi 3hadi Machi 5 ,2026 jijini Dodoma kwa ajili ya kujadili na wadau kuhusiana na kilmo hai nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Bakari Mongo amesema mkutano huo ulitakiwa kufanyika Januari mwaka huu lakini waliahirisha kutokana sababu mbalimbali na kuahidi malengo waliotaka yatafikiwa katika mkutano huo wa mwezi machi.

Amesema wadau wajitokeze katika kufanikisha mkutano huo kwa kutoa udhamini katika kukidhi matarajio ya kilamo hai nchini.

Mongo amesema Mkutano Mkuu huo unatarajia kuwa wadau 400 wakiwemo wakulima ,Watunga Sera,Watafiti ,Wasomi,Sekta Binafsi ,Vyama vya Kiraia pamoja na Wabia wa Maendeleo.

Mongo amesema kuwa mkutano huo ni fursa ya kubadilisha maarifa na uzoefu ili kuboresha mifumo endelevu ya uzalishaji wa chakula cha kutosha ,kulinda mazingira na kuongeza mazao kwa wakulima nchini.

Aidha amesema katika mkutano huo wataangalia maudhui ya Usalama wa Chakula na Lishe Mbinu na Teknolojia za Kilimo Ikolojia Hai na Ustamilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi ,Manufaa ya Kiuchumi ya Kilimo Ikolojia Hai kwa Wakulima ,Maendeleo ya Kiteknolojia na Mfumo ya Uzalishaji wa Chakula pamoja na Mazingiea ya Kisera na Mifumo katika kuendeleza Kilimo Ikolojia Hai.
Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI  wa kituo cha wanahabari watetezi wa rasilimali na taarifa – MECIRA, Habibu Mchange, amewataka Watanzania kuziangalia kwa macho makali kampeni za upotoshaji zinazofanywa mitandaoni zinazopelekea baadhi ya watu kutiwa hofu kiasi cha kukaribia kuamini uwongo unaosambazwa, ambao mara nyingi huendeshwa na akaunti bandia ni watanzania ambao wako ndani ya nchi na wengine wako nje nchi.

Akizungumza katika kipindi cha Kipima Joto kinachorushwa na ITV Ijumaa tarehe 9 Januari, 2026, Mchange alisema kuwa ukiingia mitandaoni utakachokiona na kinachoendelea unaweza ukafikiri nchi haipo au ina mapambano makali, wakati hali ilivyo mtaani na unayoyasoma ni vitu viwili tofauti kabisa akisisitiza kuwa kwa sasa wanasiasa wameacha kuweka nguvu katika kuwafikia wananchi ana kwa ana na badala yake wamehamishia nguvu zao mitandaoni.

Mchange alisema kuna watu hawalimi, hawafugi, hawafanyi kazi yoyote, lakini kutwa kucha wako mitandaoni kutukana, hao ndio wanaoonekana sana mitandaoni, wanapiga kelele, wanatukana na kushambulia, lakini hawaakisi hata kidogo uhalisia wa maisha ya Watanzania walio wengi.

Aliongeza kuwa mtaani hali ni tofauti kabisa, kwani watu wanakimbizana na maisha, wanatafuta riziki zao kwa amani, furaha na utulivu.

“Watu wanajibidiisha kila kukicha, kuhakikisha wanapata mkate wao wa siku, bila muda wa kupoteza kwenye makelele ya mitandaoni”. Amesema

Mchange anabainisha kuwepo kwa mkakati wa makusudi wa kutumia matusi ya mtandaoni kama mbinu ya siasa kupitia kaulimbiu ya “kupiga spana”, akieleza kuwa kaulimbiu hiyo imetumika kuhalalisha kutukana, kubeza na kushambulia watu wenye mawazo kinzani, huku wahusika wakidhani wanajenga ushawishi wa kisiasa.

Mchange aliisema michezo hiyo inaratibiwa kwa pamoja na wanamitandao ambao wamefungiwa Nairobi na nchi nyingine, wakilishwa, wakilipiwa makazi na familia zao kuhudumiwa ili kazi yao kubwa iwe ni kutengeneza hofu kwa jamii ya Watanzania waliopo ndani ya nchi kupitia uwongo na propaganda zinazosambazwa mitandaoni pamoja na wenzao waliopo ndani ya nchi

Amebainisha kuwa kelele nyingi za mitandaoni hazina uhusiano na maisha halisi ya wananchi, na kwamba mitandao imejaa sauti za watu wachache wasiokuwa kwenye uhalisia wa nchi wanayoizungumzia akisisitiza kuwa mitandao ya kijamii si kioo cha maisha ya Watanzania, na kwamba uhalisia wa maisha uko mtaani, mashambani na kwenye shughuli halali za kila siku za wananchi, si kwenye akaunti bandia, matusi na makelele yanayoendeshwa kwa maslahi ya watu wachache.
Na Mwandishi wetu, Mirerani
WAKAZI wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, kwa zaidi ya wiki moja wamelalamikia kutopata huduma ya maji ya kunywa, baada ya malori yanayouza maji hayo kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kudaiwa kuzuiwa.

Kwa zaidi ya miaka 20 wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wanatumia maji ya kunywa yanayouzwa na malori kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe.

Hivi sasa, baadhi ya wakazi wengine wa mji huo wanatumia maji ya visima vifupi na virefu na maji ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jiji la Arusha (AUWSA) Mirerani, kwa ajili ya matumizi mengine ikiwemo kunywa.

Baadhi ya wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wakizungumza juu ya changamoto hiyo wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo kwani wanatumia gharama kubwa kupata maji ya kunywa

Mmoja kati ya wakazi hao, Andrew John amesema kwa zaidi ya miaka 20 walikuwa wanatumia maji ya kunywa yanayotoka Hai ila wanasikitishwa hivi sasa kupata zuio hilo.

"Tulikuwa tunategemea malori ya kina 'Rumba Kali' kwa ajili ya kununua maji ya kunywa ila wanadai wamezuiwa kuleta maji Mirerani bila sababu ya msingi," amesema.

Amesema maji ya Hai yamewasaidia kwa muda mrefu kwani ya kisima na mengine hayakati kiu yana chumvi na maji ya chupa ni gharama kutumia na familia.

"Hivi sasa kuna baadhi ya malori machache yamefanikiwa kuleta maji Mirerani ila ndoo moja ya lita 20 ya maji ya kunywa tunauziwa Sh2,000 badala ya Sh1,000 kama awali," amesema.

Mmoja kati ya wauza maji wa eneo hilo, Abdi Soka amesema watu wengi wameathirika kwa ukosefu wa maji kutokana na zuio la mkuu wa wilaya ya Hai, Hassan Bomboko.

"Wanaoleta maji na kutuuzia kupitia malori kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe wamedai kuwa DC wa Hai, Hassan Bomboko amezua malori hayo yasilete maji mji mdogo wa Mirerani," amesema Soka.

Meneja wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira jiji la Arusha (AUWSA) Mirerani, Fidelis Shayo ameeleza kwamba hata yeye amesikia changamoto ya maji hayo kutopatikana.

Shayo amesema AUWSA aihusiki kuzuia huduma ya maji kutoka maeneo mengine japokuwa mradi wao wa maji wa Mirerani unaendelea kutoa huduma kwa uhakika maeneo hayo yakiwa safi na salama.

"Maji ya AUWSA Mirerani ni safi na salama kwani yametibiwa kwa dawa, tunaendelea kuwasihi watu wa eneo hilo waendelee kutumia hata kwa kunywa ndiyo sababu serikali imetenga Sh4.3 bilioni kwa ajili ya mradi wa maji Mirerani," amesema Shayo.

Hata hivyo, mkuu wa wilaya ya Hai, Hassan Bomboko alipoulizwa kwa njia ya simu juu ya suala hilo alikataa kulizungumzia.

"Kama upo huko Mirerani waulize viongozi wa huko juu ya suala hilo," amejibu DC Bomboko na kukata simu.

Kwa upande wake, ofisi mtendaji wa mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani (TEO) Isack Mgaya amesema kwa sababu suala hilo lipo nje ya wilaya ya Simanjiro wameshindwa kuingilia kati.

"Tulipata taarifa kuwa uongozi wa Hai ulizuia maji hayo kwa madai kuwa ni machache ila tumefikisha suala hilo kwa mkuu wa wilaya ya Simanjiro Fakii Lulandala ili azungumze na uongozi wa Hai," amesema Mgaya.
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Mwanamke mmoja amefariki dunia baada ya gari aina ya roli lenye namba ya usajili T696 CLY kuacha njia na kumgonga mwanamke huyo katika maeneo ya mataa ya Mbezi kwa Msuguli Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mashahidi gari hilo liliacha njia likijarabu kuwakwepa madereva pikipiki ambao walikuwa maeneo hayo na kusababisha kumgonga mtu huyo na kufariki hapo hapo.








Na. Jacob Kasiri - Zanzibar.

TANAPA kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZCT) watia nanga eneo la Forodhani leo Januari 11, 2026 kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii pamoja na fursa za uwekezaji.

Eneo la Forodhani ni maarufu sana Zanzibar kwa kuwa na wageni kedekede kutoka mataifa mbalimbali kuja kushuhudia shughuli za utalii zinazotekelezwa katika eneo hilo, pia eneo hilo limepokea meli kubwa ya kitalii ya M/S Azamara (Cruise ship) iliyotokea Mauritania ikiwa na watalii 668 na crews 368.

Hivyo uwepo wa TANAPA, TTB sanjari na Kamisheni ya Utalii Zanzibar kama mwenyeji wa eneo hilo ni fursa adhimu na mjarabu ya kunadi vivutio vya utalii kama vile utalii wa wanyamapori na fursa za utalii.

TANAPA wapo Kisiwani Unguja katika Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Dimani - Fumba, Zanzibar, aidha pia shirika hilo linatarajia kushiriki shamra shamra za Sikukuu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar leo usiku kwa kushuhudi urushwaji wa “FASH FASH” itakapotimu saa 6:00 usiku wa leo Januari 11, 2026.










WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameshiriki ibada ya Jumapili, leo, tarehe 11 Januari 2026, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Usharika wa Azania Front, jijini Dar es Salaam.

Ibada hiyo iliongozwa na Msaidizi wa Askofu wa KKKT DMP, Chediel Lwiza, kwa kushirikiana na mchungaji Victor Makundi. 






Naibu waziri wa maji Eng.Kundo Mathew amemuelekeza katibu mkuu wizara ya maji Kumfatilia mkandarasi aliyekabidhiwa mradi wa kuondosha maji taka uliopo katika kata ya Katende halmashauri ya wilaya ya Chato mkoani Geita na kuhakikisha anaondolewa kabisa katika mikataba ya wizara hiyo.

Ni wakati alipotembelea ujenzi wa mradi wa kuondosha maji taka na kukuta umetelekezwa na mkandarasi huyo ambaye hakuepo eneo la kazi.

Mradi wa kuondosha maji taka katika wilaya ya chato unaghalimu kiasi cha takribani shilingi bilioni 1.5 ambapo mpaka sasa mkandarasi ameshakabidhiwa takribani shilingi milioni 800 na kuutelekeza mradi huo.

Wilaya ya chato ina uhitaji mkubwa na mradi huo hususani kipindi cha mvua kutokana na kusambaa kwa maji taka katika maeneo mengi hivyo kuwaibua viongozi katika wilaya hiyo kumuangukia naibu waziri juu ya kukamilika kwa mradi huo.

Diwani wa kata ya Bungila Batromeo Christian amesema kuwa mradi huo ulinzishwa mnamo mwaka 2022 lakini mpaka sasa bado unasuasua huku mkandarasi akiwa ameshakula fedha nyingi.






NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekabidhi jumla ya vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa Taasisi ya Kusimamia Ufundishaji wa Elimu ya Dini ya Kiislamu (TISTA), ikiwa ni hatua ya kuimarisha ufundishaji wa somo hilo katika shule za sekondari nchini.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Januari 11, 2026 katika Ofisi za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) jijini Dar es Salaam, ambapo Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mhe. Abubakar Zuberi, ameupokea mzigo huo wa vitabu kwa niaba ya TISTA akiongozana na viongozi wengine wa taasisi hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda, amesema wamekabidhi nakala 5,000 za vitabu vya kiada vya somo la Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa kidato cha pili vyenye thamani ya shilingi milioni 16, pamoja na nakala 1,000 za vitabu vya mwongozo wa mwalimu vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2, na kufanya jumla ya vitabu vyenye thamani ya shilingi milioni 17.2.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuchapa na kusambaza vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa kidato cha sita pamoja na vile vya kidato cha tatu na cha nne mara tu vitakapokamilika, na kuzipa nakala kadhaa BAKWATA kwa ajili ya kusambaza katika shule zisizo za Serikali Tanzania Bara na Zanzibar.

Aidha, ametoa shukrani kwa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikiana kwa karibu na TISTA na kufanikisha zoezi la uandishi pamoja na uidhinishaji wa vitabu hivyo.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na madhehebu yote ya dini ili kuhakikisha Elimu ya Dini inafundishwa ipasavyo na kuchangia katika kujenga Mtanzania mwenye maadili mema.

Kwa upande wake, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mhe. Abubakar Zuberi, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano uliowezesha uandaaji wa maudhui ya vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha malezi na maadili kwa wanafunzi nchini.














Na Mwandishi Wetu

PEMBA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Pemba ina vivutio vingi vya utalii hivyo ujenzi wa Bandari yaMkoani, Pemba itafungua zaidi milango katika sekta mbalimbali.

Mhe. Masauni amesema, Bandari ya Mkoani ni kiunganishi na muhimili wa maisha ya kila siku ya wananchi wa Pemba, ni lango la biashara, elimu, afya, utalii na mshikamano wa kijamii katiya Pemba, Unguja na Tanzania Bara.

Ameyasema hayo Januari 10, 2026 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la kisasa la abiria katika bandari hiyo ambapo jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiriazaidi ya 1,500 na kuinua huduma za bandari kwa viwango vya kimataifa, ikiwa ni shamrasharakuelekea miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Amesema takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 90 ya abiria wanaosafiri kwenda nakutoka Kisiwa cha Pemba hutumia usafiri wa baharini, hali inayoifanya bandari hiyo kuwa naumuhimu kwa ajili ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

“Usafiri wa baharini si mbadala, bali ni mahitaji muhimu ya maisha ya wananchi wetu, ndiyomaana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeona umuhimu wa kuwekeza katika miundombinu yakisasa, salama kwa abiria,” amesema Mhe. Masauni.

Amesema ujenzi wa jengo hilo unatokana na mkataba wa uwekezaji kati ya Shirika la Bandari nawawekezaji wa Fumba Port, akibainisha kuwa ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya Serikali nasekta binafsi katika kuharakisha maendeleo ya miundombinu ya kimkakati.

“Ushirikiano huu unapunguza mzigo kwa Serikali, unaongeza ubora na ufanisi wa huduma, nakuchochea uchumi kupitia ajira kwa vijana na wananchi kwa ujumla,” amesema.

Amewata watoa huduma wa bandari, waendeshaji wa vyombo vya usafiri wa majini pamoja naabiria kuitumia miundombinu hiyo kwa nidhamu, uadilifu na kuitunza ili idumu kwa mudamrefu kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo, wakandarasi na wasimamizi wa mradikuhakikisha ujenzi unatekelezwa kwa ubora unaostahili, kwa wakati na kwa kuzingatia thamaniya fedha.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar, Akif Ali Khamis, amesemakukamilika kwa mradi huo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na changamoto yaupatikanaji wa usafiri wa uhakika kwa abiria wanaosafiri kati ya Pemba, Unguja na Tanzania Bara.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani, Pemba Mhe. Miza Hassan Faki, amesemauwepo wa bandari hiyo umechangia ongezeko la meli zinazotia nanga katika eneo hilo, akisemakuwa awali bandari ilikuwa inapokea abiria 60,000 kwa mwezi lakini kwa sasa inapokea zaidi yaabiria 100,000.

Ameongeza kuwa bandari hiyo imechangia pia kuongeza ajira kwa wananchi wa maeneo yajirani, hususan vijana ikiwa pamoja na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa mafuta ambapoawali uwezo wa kuhifadhi mafuta ulikuwa lita 100,000, lakini kwa sasa umeongezeka hadikufikia lita milioni mbili.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la kisasa la abiria katika Bandari ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, Januari 10, 2026.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (wa kwanza kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar, Akif Ali Khamis kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la kisasa la abiria katika Bandari ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, Januari 10, 2026.
 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo jipya la kisasa la abiria katika Bandari ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, Januari 10, 2026.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Na Mwandishi Wetu, Karatu.

NAIBU Waziri wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Regina Qwaray, ameonyesha kuridhishwa na utekelezaji wa miradi iliyojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii ( TASAF) kupitia mradi wa OPEC,ikiwemo wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Laja,wilayani Karatu.

Ametoa pongezi hizo jana wilayani humo alipotembelea Shule hiyo iliyojengwa katika Kijiji cha Laja,Karatu mkoani Arusha ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake mkoani humo.

Amesema ujenzi wa shule hiyo umeleta matokeo mazuri kwa jamii ikiwemo kuondoa adha ya wanafunzi waliokuwa wakitembea umbali mrefu kutokana na kijiji hicho kutokuwa na shule.

"Wanafunzi wengi walikuwa hawafiki shule,wengi walikuwa watoro lakini kupitia mradi huu ambapo hadi mabweni yamejengwa umesaidia kuondoa changamoto hiyo,"amesema

"Niwapongeze wananchi kwa kujitoa kwenu na kuona thamani ya elimu kwani mmeshiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuchangia mradi huu,tutunze mradi huu,"

Pia amewataka wazazi kutambua umuhimu wa kusomesha watoto na kuwa elimu ni hazina kwa vijana na inasaidia kuongeza wasomi na kuongeza kasi ya mabadiliko.

Awali Kaimu Mratibu wa TASAF Wilaya ya Karatu, Athanasi Sarwatt,amesema mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Laja umegharimu zaidi ya Sh.milioni 774.9 ambapo TASAF kupitia OPEC awamu ya nne walitoa Sh.milioni 659.5 huku zaidi ya Sh.milioni 115 zikiwa ni michango ya wananchi ikiwemo mchanga,kokoto,mawe,maji na nguvu kazi.

Amesema mradi huo umesaidia kuondoa utoro kwa wanafunzi kwani awali walikuwa wanasafiri umbali mrefu zaidi ya kilomita nane kwenda shule na kuwa mpango umesaidia kuongeza mahudhurio ya wanafunzi shuleni hasa wanaotoka kaya maskini sana.

Amesema shule hiyo ilisajiliwa Novemba 2023 na kuanza rasmi mwaka 2024 kwa kupokea wanafunzi 26 wa kidato cha kwanza na kwa sasa shule ina jumla ya wanafunzi 63 ambao ni kidato cha kwanza na pili na wote wanakaa bweni.

Kwa upande wake Mratibu wa TASAF mkoa wa Arusha,Richard Nkini,amesema kwa kipindi cha miaka miwili mkoa huo umepokea zaidi ya Sh 23 Bilioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo imeleta tija na mabadiliko katika jamii.

Wakati huo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Juma Hokororo, ameshukuru TASAF kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali hasa ya elimu na kuwa imesaidia kuinua elimu.

Amesema katika kipindi ambacho Shule zinakaribia kufunguliwa,halmashauri hiyo imeweka mikakati kuhakikisha watoto wote ambao wana umri wa kwenda shule wanaandikishwa  na kuripoti shule pamoja na wale waliofaulu wanaotakiwa kujiunga Kidato cha kwanza.











Top News