SERIKALI ya Tanzania na Chuo Kikuu cha Limerick cha nchini Ireland wamesaini hati ya makubaliano ya utekelezaji wa ufadhili wa Samia Scholarship Extended, utakaosomesha wanafunzi 32 kwenye chuo hicho.

Makubaliano hayo yamefanyika leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Adolf Mkenda pamoja na ujumbe kutoka ubalozi wa Ireland nchini Tanzania na kutoka chuo cha Limerick.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa hati hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa ufadhili huo ni sehemu ya ahadi ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa mwaka jana wakati wa kuzindua Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuimarisha elimu nchini kwa kuzalisha wataalamu watakaosomea sayansi na teknolojia ili kuendana na matakwa ya dunia.

Amesema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka, wakati Tanzania ikiendelea kuwekeza katika uchumi unaotegemea maarifa na ubunifu.

Pia alisema unaonesha dhamira ya pamoja ya kuwawezesha vijana kupitia elimu bora, uzoefu wa kimataifa na ujuzi wa kisasa kwa ajili ya baadaye, kwani chuo hicho kinatoa punguzo la ada kwa asilimia 50 kwa wanafunzi.

Alisema Serikali inaendelea kutekeleza Mpango wa Samia Scholarship katika Sayansi ya Data, Akili Unde (AI) na taaluma zinazohusiana na mpango wa kimkakati unaolenga kuwajengea vijana maarifa na ujuzi katika teknolojia mpya.

“Tumewapeleka wanafunzi 34 waliofanya vizuri kwenye mitihani yao ya kidato cha sita nchini Ireland ambapo wanafunzi 32 wamepata ufadhili kwenye chuo kikuu cha Limerick, chuo kinachoongoza kwa teknolojia na mafunzo ya vitendo, na wengine wawili tumewapeleka kwenye chuo cha Cork nchini Ireland,” amesema Profesa Mkenda.

Prof. Mkenda amesema kuwa wanafunzi hao ni sehemu ya ufadhili wa ‘Samia Scholarship’ kwa wanafunzi 50 waliofanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha sita ambapo tayari wanafunzi 16 wameshajiunga na chuo kikuu cha Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Prof. Mkenda amesema kuwa wizara hiyo inatekeleza agizo la Rais Samia kwa vitendo, “Mwaka huu tutawapeleka wanafunzi 50 katika vyuo vikuu mbalimbali vya nje, mwakani tutafanya zaidi.”

Waziri Mkenda amesema kuwa fursa hiyo inafungua mlango kwa watoto wa masikini kusoma kwenye vyuo vikuu vya nje bure. “Sisi Serikali tunagharamia nauli za kwenda na kurejea katika nchi husika na vyuo vinawasomesha bure. Hii fursa itawasaidia watoto wa wakulima, wafugaji au hata wamachinga.”

Kwa upande wake, Balozi wa Ireland nchini, Nicola Brennan amehimiza Serikali kuzingatia maono ya maendeleo ya muda mrefu, ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 na 2050 kwa kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika elimu bora ili vijana waweze kupata ajira na kuchangia katika maendeleo ya nchi.

Alisema Tanzania ina msingi mzuri wa rasilimali watu, utulivu wa nchi unaendelea kuimarika na idadi kubwa ya vijana huku kukiwa na fursa kubwa ya kukuza uwezo wao.

“Ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu Tanzania inatarajiwa kuongezeka maradufu kutoka takribani milioni 67 hadi zaidi ya milioni 130. Hili ni changamoto kubwa kuhakikisha vijana wanapata ajira,” alisema Nicola.

Aliongeza kuwa ni muhimu kuhakikisha vijana wanapata elimu bora na ujuzi unaowawezesha kupata ajira na kuchangia katika maendeleo ya nchi, akisisitiza elimu ni jambo la msingi sana.

Alisema kwa Ireland, uwekezaji katika elimu ni moja ya sababu kubwa zilizoifanya kufikia mafanikio makubwa kiuchumi, ukuaji na maendeleo na kuifanya kuwa ni nchi iliyoelimika zaidi duniani.

Alihimiza Serikali kuzingatia maono ya maendeleo ya muda mrefu, ikiwemo Dira 2050, kwa kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika elimu bora ili vijana waweze kupata ajira na kuchangia katika maendeleo ya nchi.

Alisema kuwa Chuo Kikuu cha Limerick ni chuo chenye kufundisha sayansi na teknolojia inayoendana na mahitaji ya wakati.

“Kwa sasa dunia ipo kwenye uvumbuzi wa kisayansi na teknolojia mpya ikiwa pamoja na akili unde (Artificial Intelligence).”

Naye, Profesa Colin Fitzpatrick, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Limerick amesema kuwa chuo hicho kinasifika katika ufundishaji wa vitendo pamoja na kuwapeleka wanafunzi wake kwenye kampuni zilizofanikiwa duniani ili kuongeza uzoefu na kuona uhalisia wa kile walichojifunza.

Amesema kuwa Ireland ni taifa linaloongoza kwa kuwa na kampuni kubwa za kiteknolojia barani Ulaya, hivyo anatarajia wanafunzi hao kutoka Tanzania watapata tija ya kujifunza nadharia na vitendo.
















Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimfariji, Germina Lukuvi, mjane wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi alipokwenda nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma kuhani, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akimfariji, Germina Lukuvi (wa tatu kushoto), mjane wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi alipokwenda nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma kuhani, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi, Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiwafariji watoto wa aliyekua Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, Mossy Lukuvi (wa pili kulia na Brown Lukuvi (kulia) nyumbani kwa marehemu Area D jijini Dodoma alipokwenda kuhani, Machi 26, 2026. Kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, Naibu Spika Daniel Sillo (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, wakati alikokwenda kuhani msiba nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi, Area D jijini Dodoma, Machi 26, 2026. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi aliyefariki jana Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.

Akiongea kwa niaba ya Serikali nyumbani kwa marehemu Area D, jijini Dodoma leo, Alhamisi, Machi 26, 2026, Waziri Mkuu amesema: “Kwa niaba ya Serikali natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa. Jambo hili zito, gumu kulielewa, gumu kulipokea.”

…Lakini ndio limeshatufika na sote hatukutarajia maana Mheshimiwa Waziri alikuwa kazini. Tuendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu na kuifariji familia. Mwenyezi Mungu awaimarishe kwa sababu yeyé ndio mfariji mkuu,” amesisitiza.

Vilevile, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kuihakikishia familia kwamba Serikali itaendelea kuwa pamoja nayo katika kipindi hiki chote cha majonzi.

Viongozi wengine waliokuwepo msibani hapo ni pamoja na Naibu Spika, Daniel Siro, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumisi wa Umma na Utawala Bora), Ridhiwani Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila.




Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya ALAF Limited imeahidi kuendelea kuwekeza zaidi katika afya za wafanyakazi ikiwemo kuwekeza zaidi katika ushriki wao katika mbio za KIlimanjaro Premium Lager International Marathon ambazo zimemalizika hivi karibuni Mjini Moshi.

Meneja Rasilimali watu wa ALAF Limited Jumbe Onjero alisema hayo punde tu baada ya mgeni rasmi katika mbio hizo, Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Paul Makonda kutembelea banda la kampuni hiyo katika uwanja wa Chuo Kikiuu Cha Ushirika Moshi ambapo kampuni hiyo ilishiriki katika maonesho maalumu maarufu kama The People’s Expo yanayoandaliwa na Kilimanjaro Marathon kila mwaka.

Alisema ushiriki wa wafanyakazi katika matukio kama haya unasaidia kuimarisha afya ya mwili na akili ili kuzidisha ufanisi wao katika kazi. “Kili Marathon ni mbio kubwa sana kwa hivyo

tukaona pamoja na kuwaleta wafanyakazi kushiriki lakini na sisi kama kampuni tudhamini mbio hizi ili pia tutangaze shughuli zetu hasa ikizingatiwa tuna mpango wa kufungua show room kubwa hapa Moshi ambayo itawahudumia wateja wetu wa hapa na maeneo jirani,” alisisitiza.

Alisema walidhamini zaidi ya washiriki 50 katika mbio za mwaka huu na kwamba ushiriki wao umekuwa jambo zuri na la kukumbukwa, ambapo alisema wafanyakazi wa kampuni hiyo walishiriki katika vipengele vyote vya mbio hizo ambavyo ni kilomita 42.2 za Kilimanjaro Premium Lager, mbio za kilomita 21.1 maarufu kama YAS half marathon na mbio za kujifurahisha za kilomita 5 zinazodhaminiwa na CRDB Bank.

"Tutaendelea kuunga mkono mbio hizi kwa lengo la kuinua sekta ya michezo sambamba na kuhakikisha wafanyakazi wetu wanafanya mazoezi yatakayoimarisha afya zao kupitia mbio za Kilimanjaro International Marathon,” alisema.

Alisema mwaka jana ALAF ilizindua klabu yake ya jogging inayojumuisha wafanyakazi kutoka vitengo mbalimbali vya kampuni hiyo ambapo wafanyakazi wataendelea kufanya mazoezi kwa ajili ya kushiriki mbio mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager International Marathon pamoja na mbio nyingine.

“Tulianza kwa kushiriki tu kawaida mwaka jana lakini mwaka huu tunapoadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa kampuni yetu tukaamua kudhamini mbio hizi kwa ukubwa zaidi,” alieleza.

Kampuni ya ALAF Limited (ALAF) ni kampuni inayoongoza kwa utengenezaji wa vifaa vya chuma vyenye ubora wa hali ya juu ambavyo ni maalum kwa ajili kuezekea paa za nyumba.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka wa 1960, ALAF imeendelea kutoa mchango mkubwa katika sekta ya ujenzi hapa nchini.

Shughuli za ALAF hazihusiani na uzalishaji wa vifaa vya chuma za kuezekea tu bali pia ianjihusisha na uzalishaji wa koili za chuma zilionakshiwa kwa rangi kwa ajili ya matumizi mablimbali kwenye sekta ya ujenzi pamoja na mirija ya chuma na mabomba kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Ni muuza wa kuni, maji na viazi aliyeshinda boda boda ya PigaBet

Dar es Salaam — Kuna watu wanaotafuta kazi. Halafu kuna watu ambao kila siku wanajitengenezea kazi kutoka kila pembe ya maisha. Muhammad Mussa wa Mburahati Motomoto ni mmoja wao.

Akiwa na miaka 45, mke na watoto wawili, Muhammad si mtu wa kukaa. Ana bucha la kuni, anauza maji, na pia anasambaza viazi vya chipsi kwenye magenge na sehemu za kukaanga chipsi. Kwa kifupi, maisha yake yanatembea kwenye biashara zaidi ya moja. Tatizo lilikuwa moja tu: mwendo wa kuzifikisha hizo biashara kwa watu.
Kutoka jirani na Soko la Mabibo hadi kwa wateja wake, usafiri ulikuwa ukikata kasi ya kazi. Hapo ndipo ushindi wake wa boda boda kupitia kampeni ya #ShindaBoda ya PigaBet unapopata maana ya kweli.

Mohammed anasema boda hiyo itakuwa msaada mkubwa katika biashara zake za kila siku, hasa kwenye kubeba na kusambaza bidhaa zake kwa urahisi zaidi.

“Itanisaidia katika shughuli zangu za kibiashara. Nitaanza kuongeza kipato na kufanya biashara nyingine,” amesema Mohammed.

Kwa maelezo yake, boda hiyo itarahisisha kubeba magunia ya viazi kutoka soko la Mabibo na kuyapeleka kwenye sehemu za kukaanga chipsi, pamoja na kusambaza kuni kwenye maeneo mbalimbali.

Kwa mtu anayesimamia biashara zaidi ya moja, hiki si chombo cha kutembelea tu. Hiki ni kifaa cha kazi.

Mohammed anaamini ushindi huu utaongeza ufanisi wa biashara zake na kusaidia kuimarisha maisha ya familia yake. Kile alichoshinda si usafiri tu, bali ni nafasi ya kusogeza biashara zake mbele kwa mwendo mmoja.

Kwa Mohammed, huu si ushindi wa kutazamwa. Ni mwendo wa kusukuma maisha.
18+ | Cheza kwa uwajibikaji.

 




LEO hii kutakuwa na mechi ya kibabe kabisa ya kuwania nafasi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia 2026. Ni Uturuki dhidi ya Romania ambapo kwenye mechi hii unaweza ukaibuka bingwa na Meridianbet.

Usiku wa leo saa 2:00, dimba la Tupras, Uturuki litashuhudia pambano la kuamsha shauku za mashabiki wa soka, wakati Uturuki itakabiliana na Romania katika raundi ya pili ya kufuzu Kombe la Dunia 2026.

Katika hatua za makundi, Uturuki imeonyesha kiwango cha juu, ikishinda mechi nne aliibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Bulgaria, 4-1 dhidi ya Georgia, 6-1 dhidi ya Bulgaria, 3-2 dhidi ya Georgia. Pia, Uturuki imepata sare 2-2 dhidi ya Spain, huku ikikubali kufungwa 6-1 dhidi ya taifa hilo. Kocha Montella Vincenzo anatarajiwa kutumia wachezaji wake wenye kasi na uwezo wa ushambuliaji kuhakikisha wanachukua hatua ya mbele katika raundi hii.

Romania, upande mwingine, imeonyesha ufanisi mkubwa katika kundi H: Ushindi 7-1 dhidi ya San Marino, 1-0 dhidi ya Austria, 2-0 dhidi ya Cyprus na 5-1 dhidi ya San Marino. Walipata sare 2-2 dhidi ya Cyprus, na kupoteza 1-0 dhidi ya Bosnia, kabla ya kurejea na ushindi 2-1 dhidi ya Austria na 3-1 dhidi ya Bosnia. Kocha Licescu Mircea anatarajiwa kuongoza kikosi chenye mchanganyiko wa wachezaji wachanga na wenye uzoefu. Jisajili sasa

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# ubashiri bila Intaneti, kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mabingwa wa kutoa pesa, wamekuwekea odds kali katika mechi, unaachaje mkwanja ukupite hivihivi?

Mara ya mwisho mataifa haya kukutana ilikuwa mwaka 2017, wakati Romania ilipoibuka na ushindi wa 2-0 nyumbani dhidi ya Uturuki. Ushindi huo unaongeza msisimko wa mashabiki wa soka, huku timu zote zikitarajia kurudisha heshima na ushindi leo usiku.

Mchezo huu unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa kutokana na rekodi za mechi za makundi na historia ya michuano ya awali. Uturuki, ikiwa nyumbani, inatazamiwa kushambulia kwa kasi huku Romania ikitaka kuonyesha umahiri wake wa ushambuliaji na kutoachia mapengo nyuma. Chukua Mkwanja wako na Meridianbet.


RAIS Mstaafu Dkt, Jakaya Mrisho Kikwete ameteuliwa kuwa Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu, jukumu linalomrejesha katika mstari wa mbele wa diplomasia ya bara Afrika.

Uteuzi huo ulitangazwa na Mahmoud Ali Youssouf, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, ambaye alionesha imani kubwa katika uzoefu na uongozi wa Kikwete kushughulikia changamoto tata za kisiasa, amani na usalama katika ukanda huo.

Ukanda huo unaendelea kuwa na changamoto nyingi, kuanzia migogoro ya kisiasa hadi maslahi ya kimkakati ya kimataifa, hasa kutokana na umuhimu wa Bahari Nyekundu katika biashara ya dunia. 

Ni eneo ambalo si tu linahusu nchi za Afrika, bali pia lina mvuto wa nguvu za kimataifa.

Katika nafasi hiyo mpya, Kikwete anatarajiwa kusaidia Tume hiyo  kuimarisha juhudi za kuleta amani kupitia diplomasia ya kuzuia migogoro, kukuza mazungumzo jumuishi, na kujenga uaminifu miongoni mwa wadau mbalimbali.

Aidha, alikabidhiwa jukumu la kuratibu juhudi za taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Intergovernmental Authority on Development, East African Community, League of Arab States pamoja na United Nations, ili kuhakikisha juhudi za kuleta amani zinakuwa na mshikamano na ufanisi.

Hili linaonekana kuwa jukumu nyeti zaidi, kwani ukanda huo kwa muda mrefu umekuwa ukivutia maslahi yanayokinzana kutoka kwa mataifa na taasisi mbalimbali. Kuleta mwelekeo mmoja kunahitaji busara, uvumilivu na ustadi wa hali ya juu wa kidiplomasia.

Na wengi wanaamini kwamba  hapo ndipo nguvu ya Dkt. Kikwete ilipo.

Siku zote amejulikana kwa mtindo wa uongozi wa mazungumzo badala ya mabavu, ushawishi badala ya shinikizo. Katika ukanda ambao mara nyingi nguvu za kijeshi hazijaleta suluhu ya kudumu, mtazamo huu unaweza kuwa wa faida kubwa.

Kwa Tanzania, uteuzi huu uliibua hisia za fahari ya kimya. Kwa miaka mingi, nchi imejijengea sifa ya kuwa na mchango mkubwa katika diplomasia ya bara—kuanzia enzi za Mwalimu Nyerere hadi viongozi waliomfuata

Uteuzi wa  Dkt Kikwete umetajwa kuwa ni ukumbusho kwamba uongozi hauishii madarakani. Mara nyingi, viongozi wastaafu hupata nafasi ya kutumia uzoefu wao kwa uhuru zaidi katika jukwaa la kimataifa, na wakati mwingine kwa mafanikio makubwa zaidi.

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika alieleza imani yake kwamba hekima na uzoefu wa Kikwete vitachangia kwa kiasi kikubwa katika kutafuta suluhu za kudumu za amani na ustawi katika ukanda huo.

Kwa Pembe ya Afrika, safari bado ni ndefu na yenye changamoto. Lakini diplomasia ni mchakato wa hatua kwa hatua, na si wa matokeo ya haraka. Na kwa kumteua Jakaya Kikwete, Umoja wa Afrika unaonekana kuchagua si tu kiongozi mwenye uzoefu, bali pia mtazamo wa subira, mazungumzo na matumaini ya suluhu ya kudumu.



CHIFU wa Kibondo mkoani Kigoma Mama Mwamvua Rajab Ruhaga Nyamaliza amefariki dunia ghafla asubuhi ya tarehe 24 Machi 2026 akiwa msibani Malinyi, mkoani Morogoro.

Taarifa za kifamilia zinaeleza kuwa marehemu alikuwa amesafiri kwenda Malinyi kuhudhuria mazishi ya binti yake, Zubeda Juma Ruhaga, kabla ya kifo chake hicho cha kushtukiza kutokea.

Kifo hicho kimeacha simanzi kubwa kwa familia, ndugu, jamaa na wakazi wa Kibondo, ambako marehemu alikuwa akihudumu kama kiongozi wa kimila na mshauri muhimu wa jamii.

Kwa sasa, familia ipo katika maandalizi ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka Morogoro kuelekea Kibondo, Kigoma, kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika nyumbani kwake.

Taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi zinatarajiwa kutolewa na familia kadri mipango inavyoendelea.
Na Mwandishi Wetu
WATANZANIA wanatarajiwa kunufaika na huduma za afya za kimataifa kufuatia ushirikiano wa kimkakati kati ya AXA Health International, Alliance Insurance Corporation Limited na MIC Global Risk Tanzania Ltd, hatua inayolenga kupanua upatikanaji wa bima ya afya ya kimataifa pamoja na matibabu maalum nje ya nchi.

Kupitia ushirikiano huo, kampuni hizo tatu zimeunganisha utaalamu wao ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya za kiwango cha juu kwa watu binafsi, wafanyabiashara, wageni wanaoishi nchini pamoja na wataalamu wanaosafiri kimataifa. Mpango huo unawawezesha wateja kupata matibabu maalum katika hospitali za nje ya nchi pale inapohitajika kupitia bima ya afya ya kimataifa.

Hatua hiyo inakuja kufuatia ushirikiano wa AXA Health International na Executive Healthcare Solutions ulioanzishwa Oktoba 2025 kwa lengo la kuimarisha mfumo wa usambazaji wa huduma za bima ya afya ya kimataifa nchini Kenya na maeneo mengine ya Afrika. Nchini Tanzania, MIC Global Risk Tanzania Ltd imechaguliwa kuwa msambazaji wa kipekee wa huduma hizo katika soko la ndani kwa kushirikiana na Alliance Insurance Corporation Limited.

Kupitia mpango unaojulikana kama Global Executive Health Plan (GEHP), wateja watapata fursa ya kufikia mtandao mpana wa hospitali na wataalamu wa afya wanaotambulika kimataifa, pamoja na huduma za ziada kama uokoaji wa kimatibabu na uratibu wa matibabu yanayofanyika nje ya mipaka ya nchi.

Akizungumzia ushirikiano huo, Afisa Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa AXA Global Healthcare, Karim Idilby, amesema kuanzishwa kwa huduma hiyo nchini Tanzania ni hatua muhimu katika mkakati wa kampuni hiyo kupanua uwepo wake katika masoko yenye ukuaji wa haraka barani Afrika.

Amesema kadri Tanzania inavyoendelea kuwa kitovu cha uwekezaji, biashara na kubadilishana uzoefu wa kitaalamu, ndivyo mahitaji ya huduma za afya za kimataifa yanavyozidi kuongezeka, jambo linalofanya ushirikiano huo kuwa na umuhimu mkubwa kwa wateja wanaohitaji matibabu maalum nje ya nchi.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Alliance Insurance Corporation Limited, Rajiv Kumar, amesema ukuaji wa uchumi wa Tanzania na kuongezeka kwa watu wanaosafiri kimataifa kumeongeza mahitaji ya huduma za afya za kimataifa zilizo salama na zinazoaminika.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa MIC Global Risk Tanzania Ltd, Aly Maherali, amesema mpango wa GEHP unaunganisha uzoefu wa kimataifa wa AXA Global Healthcare na mfumo wa bima ya ndani unaosimamiwa na Alliance Insurance Corporation Limited, hatua inayowapa watu binafsi, makampuni na wataalamu nchini Tanzania fursa ya kupata ulinzi wa afya katika kiwango cha kimataifa.

Amesema kwa zaidi ya miaka 25 kampuni yake imekuwa mstari wa mbele katika utoaji wa bima ya afya ya kimataifa katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara, na ushirikiano huo unaimarisha dhamira ya kuendelea kuwahudumia wateja nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.












Matukio mbalimbali katika Picha.

Top News