Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb), amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kisera, kifedha na kitaasisi ili kuchochea uvumbuzi unaojenga ajira na kujitegemea kwa Taifa.
Waziri Kairuki alitoa kauli hiyo Januari 19, 2026, akifungua Kongamano la 9 la Mwaka la TEHAMA (TAIC 2026), jijini Dar es Salaam. Na kuelezea furaha yake kuona jukwaa hili likitenga siku ya hii kwa ajili ya wanawake katika TEHAMA. Huku akisema kuwa hatua hii ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya kuhakikisha Wanawake na Wasichana wanashiriki kikamilifu katika mabadiliko ya kidijitali na uvumbuzi wa kiteknolojia.
“Wanawake wana mchango mkubwa katika kuendeleza TEHAMA, kuanzisha bunifu, kuongoza taasisi za kidijitali, na kubuni suluhisho zenye athari chanya za kijamii,” alisisitiza Mhe. Kairuki.
Waziri Kairuki pia alisisitiza umuhimu wa vijana katika mabadiliko ya kidijitali, huku akieleza kuwa kupitia kampuni changa za TEHAMA (ICT Startups), vijana wetu wana fursa kubwa ya kujiajiri badala ya kuajiriwa.
“Ni malengo ya Serikali kuwa kundi hili litambulike, liendelezwe na liungwe mkono kwenye kuboresha ubunifu wao,” alisema Waziri Kairuki.
Waziri Kairuki alieleza hatua za kimkakati zinazochukuliwa na Serikali ili kuhakikisha mabadiliko ya kidijitali yanatekelezwa kwa ufanisi. Aliiagiza Tume ya TEHAMA kuimarisha usajili na uendelezaji wa wataalam wa TEHAMA pamoja na kuimarisha mifumo ya kusimamia na kusaidia kampuni changa bunifu za TEHAMA ili bidhaa na huduma zao ziweze kuingia sokoni kwa ufanisi. Aidha, alizitaka Taasisi za Umma na Sekta Binafsi kuhakikisha zinawasilisha taarifa kuhusu mifumo yao ya TEHAMA kwa Wizara, na kuhakikisha mifumo hiyo inavyosomana na mifumo mingine.
Waziri Kairuki alisisitiza pia umuhimu wa wabunifu na waandaaji wa maudhui (“Content Creators”) kuhakikisha wanazingatia matumizi sahihi ya mifumo na teknolojia zinazoibukia, kama vile Akili Unde (AI), ili kuepuka matumizi yanayokiuka maadili ya nchini.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar ameishauri Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB) kuongeza ubunifu katika kushirikiana na Serikali pamoja na Sekta binafsi ili kuchangia katika maendeleo ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Ametoa ushauri huo jijini Dodoma alipokutana na kuzungumza na uongozi wa benki hiyo kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na fursa za ushirikiano kati ya Serikali na benki hiyo, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square.
Mhe. Balozi Omar alisema kuwa benki hiyo ni muhimu katika maendeleo ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na ikitumika vizuri inaweza kuufanya Ukanda huo kuwa mfano wa ukuaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii barani Afrika.
“Kasi ya maendeleo yanayotokana na benki hiyo ikionekana vizuri tutakuwa wa mfano na kuiwezesha jumuiya nyengine kama Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuja kujifunza kwetu”, alibainisha Mhe. Balozi Omar.
Aidha alisema kuwa ni muhimu pia kwa benki hiyo kuchangia katika kupunguza umaskini ikiwa ni pamoja na kujenga ujuzi na ustadi unaoendana na mahitaji ya kiuchumi, na mipango ya maendeleo ya muda mfupi na mrefu.
Aliishauri pia benki hiyo kujitangaza ili kuwawezesha wananchi hususan Sekta Binafsi waweze kutambua fursa mbalimbali zinazo patikana katika benki hiyo.
“ Jukumu lenu ni kuhakikisha wateja wanaifahamu zaidi benki pamoja na fursa zake”, alisisitiza Mhe. Balozi Omar.
Aidha, aliipongeza benki hiyo kwa mipango na michango mbalimbali ambayo imekuwa ikichangia katika maendeleo ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki hasa Tanzania.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Dkt. Charles Mwamwaja, alisema benki hiyo ilianzishwa mwaka 1967 kwa lengo la kuchangia katika kukuza maendeleo ya kiuchumi na wananchi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Alisema benki hiyo imeandaa mkakati madhubuti wa kuwawezesha wadau kufahamu fursa mbalimbali zinazopatikana katika benki hiyo kwa kuwa benki hiyo haifanyi kazi na Serikali pekee bali hata sekta ninafsi katika kuleta maendeleo.
Aidha, aliahidi kuyafanyia kazi kikamilifu maaelekezo na ushauri uliotokewa na Mhe. Waziri ili kuwezesha nchi kukamilisha mipango yake na kufikia maendeleo ya kiuchumi na ustawi wa wananchi.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bw. Benard Mono, alisema kuwa benki hiyo ipo tayari kuendeleza ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika miradi ya maendeleo ili kuzalisha ajira na kuongeza thamani katika sekta mbalimbali za uzalishaji.
Bw. Mono aliongeza kuwa wapo tayari kutoa mikopo katika sekta za umma pamoja na sekta binafsi kwa kuzingatia vigezo vya mkopeshwaji kwa lengo la kujenga Uchumi imara kwa nchi za Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania, kama lilivyo lengo la benki hiyo kuanzishwa la kuchochea maendeleo.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje, Bw. Rished Bade, Meneja Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bw. Stephen Wambura na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa kikao na Uongozi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), ambacho kilizungumzia mambo mbalimbali kuhusu benki hiyo pamoja na kujadili fursa za ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo hasa katika fursa za mikopo kwa taasisi za umma na sekta binafsi, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Dkt. Charles Mwamwaja ambaye aliongoza ujumbe wa benki ya EADB, akitoa maelezo ya awali ya benki hiyo kwa Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), walipomtembelea ofisi kwake Treasury Square, jijini Dodoma, ambapo walizungumza mambo mbalimbali kuhusu benki hiyo pamoja na kujadili fursa za ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo hasa katika fursa za mikopo kwa taasisi za umma na sekta binafsi.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bw. Benard Mono akifafanua jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (hayupo pichani) na uongozi wa benki hiyo, kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza kikao kati yake na Uongozi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB) ambapo walizungumza mambo mbalimbali kuhusu benki hiyo pamoja na kujadili fursa za ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo, Treasury Square, jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)
Diwani wa kata ya Butobela Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe Pascal Mapung’o amewataka wasimamizi wa miradi ya maendeleo jimboni Geita kuzingatia maelekezo ya utekelezaji wa miradi yanayotolewa na Halmashauri.
Mhe Mapung’o ameyasema hayo katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo iliyofanyika Januari 19,2026 katika jimbo la Geita ambalo Mbunge wake ni Mhe Joseph Musukuma.
Aidha katika ziara hiyo Mhe Pascal Mapung’o amewataka Wahandisi wa Halmashauri kuhakikisha wanashughulikia kasoro zote ambazo zimeonekana kwenye miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutumika.
“Kasoro zote ambazo tumeziona kwenye miradi zifanyiwe kazi kwa wakati ili miradi ikamilike kwa wakati na kuanza kutumika” Amesema Mhe Mapung’o
Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji Bi Sarah Yohana ambaye pia ni Afisa Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Geita amewataka mafundi ujenzi wanaotekeleza miradi hiyo kuongeza kasi ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati.
“Niwatake mafundi kuongeza kasi ya ujenzi ikiwa ni pamoja na wasimamizi wa miradi hii kuwalipa mafundi ujenzi kwa wakati” Amesema Bi Sarah
Vilevile Bi Sarah ametoa wito kwa Wasimamizi wa miradi kuwashirikisha wananchi katika maeneo yao utekelezaji wa miradi na kuwajulisha wananchi fedha za miradi zinapoingia ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu miradi ya maendeleo.
Kamati hiyo ikiwa na wataalam kutoka Halmashauri, imetembelea miradi ya ujenzi wa shule, ukarabati wa miundombinu ya madarasa,ujenzi wa nyumba za watumishi Pamoja na uzio katika nyumba hizo miradi ambayo thamani yake ni kiasi cha Shilingi Bilioni 2.1. fedha hizo zikiwa ni ni Mapato ya ndani, BOOST na wajibu wa Kampuni ya mgodi wa dhahabu wa Geita kwa jamii (CSR-GGML)
Ziara hiyo ni sehemu ya kuimarisha usimamizi wa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita ili ikamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa jamii.
Vilevile, Katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa malisho inayowakabili wafugaji wengi nchini, kituo hicho kimebuni teknolojia ya kuchakata mabua ya mahindi na magunzi kwa ajili ya kutengeneza chakula cha mifugo ili kunusuru mifugo dhidi ya athari za ukame, ambao umekuwa ukisababisha hasara kubwa ya kiuchumi kwa wafugaji kutokana na vifo na kupungua kwa tija ya mifugo yao.
Hayo yamesemwa Januari 19, 2026 na Naibu Waziri Dennis Londo alipotembelea kituo hicho na kukiagiza kuongeza kasi ya ubunifu ili kumwondoa mkulima katika matumizi ya jembe la mkono na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050.
Aidha, alisema pamoja na Mafanikio kilichonacho ni muhimu kwa kituo hicho kutafuta wabia katika halmashauri mbalimbali nchini ili kuhakikisha zana hizo zinazalishwa kwa wingi na kuwafikia wananchi vijijini na kuibadili sekta ya kilimo kuwa fursa ya kibiashara
Waziri Londo pia aliongeza kuwa ukosefu wa teknolojia rafiki unasababisha matumizi ya ardhi kubwa kuzalisha mazao machache, hivyo CAMARTEC inapaswa kuhakikisha teknolojia zao zinawafikia wakulima ili wajikwamue kiuchumi.
Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CAMARTEC, Mhandisi Godfrey Mwinama, alieleza kuwa kituo kimeanzisha mashamba darasa ili kuwawezesha wakulima kujifunza kwa vitendo matumizi ya zana bora kama mashine za kuchanjua mahindi, matrekta ya kisasa, na teknolojia za usindikaji zinazorahisisha kazi za shambani.
Aidha, CAMARTEC imeweka nguvu kubwa katika uzalishaji wa mitambo ya kubangua korosho kwa ajili ya wakulima wa mikoa ya Lindi, Mtwara, na maeneo mengine yanayozalisha zao hilo ili kuongeza thamani katika mnyororo wa zao la korosho na kuwasaidia wakulima kupata soko la uhakika na bei nzuri zaidi kuliko kuuza zao ghafi.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango, Audax Bahweitama, alihimiza kituo hicho kuhakikisha kuwa zana zote zinazobuniwa zinauzwa kwa bei nafuu na inayohimilika kwa mkulima mdogo. Alieleza kuwa upatikanaji wa zana hizo maeneo ya vijijini utachochea ukuaji wa uchumi wa taifa na kuongeza mapato ya serikali kupitia mnyororo wa thamani unaoanzia shambani hadi viwandani.
SHIRIKA la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO) limebuni, kusanifu na kutengeneza mtambo wa kuchakata zao la miwa ili kupata sukari kwa kiwango cha mjasiriamali wa kati, ikiwa ni jitihada za kupunguza uhaba wa sukari nchini pamoja na kuwaongezea wakulima wa miwa soko la uhakika.
Hayo yalisemwa Januari 19, 2026 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb.), wakati wa Ziara yake TEMDO jijini Arusha ambapo amelishauri Shirika hilo kuzalisha mitambo hiyo ya Sukari pamoja na mitambo mingine katika kanda zote nchini kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za ndani ikiwemo TAMISEMI na nje ya nchi, ili kufikia Malengo yanayotarajiwa.
Aidha, aliiagiza TEMDO kuzalisha mitambo inayoendana na kasi ya teknolojia ili kuhakikisha teknolojia zinazozalishwa zinaingia sokoni na kutoa fursa zaidi za kiuchumi na kuondokana na umaskini kwa Wajasiliamali na Wananchi kwa ujumla.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TEMDO, Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia, alisema Shirika hilo linaendelea kuweka mikakati madhubuti ya mageuzi ya viwanda kwa kuzalisha mitambo itakayotatua changamoto za wakulima na kuwawezesha kupata masoko ya uhakika ili kuongeza uzalishaji viwandani na kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.
Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Profesa Frederick Kahimba alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kupunguza pengo la uzalishaji wa sukari nchini sambamba na kuongeza thamani ya zao la miwa kwa wakulima wadogo na wa kati ambapo hadi sasa Shirika hilo limepokea maombi sita kutoka kwa Wajasiliamali wa kati wanaotaka kufungiwa mitambo hiyo ya Sukari kutoka Dodoma, Same, Manyara, Busega, Kilosa na Morogoro.
Temdo inazalisha bidhaa zaidi ya 16 ikiwemo vifaa tiba vya hospitali kama majokofu ya kuhifadhia maiti, vichomea taka hatarishi, vitanda vya aina mbalimbali vinavyohitaji kufika soko la Zanzibar ili kuongeza pato la Taifa, kukuza uchumi na kupunguza uagizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ya nchi. Alifafanua Kahimba.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango wa wizara hiyo, Audax Bahweitama akimwalikilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo alisema Serikali improvises Sera na Sheria mbalimbali zinazohusu Maendeleo ya Viwanda ili kufikia uchumi jumuishi kupitia viwanda kwa kuzalisha bidhaa zenye ushindani na ubora sokoni, kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.


Kaimu Katibu Mkuu , Wizara ya Maji Bwn. Henry Chisute amesema akifungua Warsha ya uhakiki na Kujenga Uwezo, iliyofanyika Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.
Amesema Tanzania imepiga hatua nzuri katika eneo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama pamoja na usafi wa mazingira.
Amesema ongezeko la idadi ya watu, kasi ya miji kukua, na athari zinazoongezeka za mabadiliko ya tabianchi zinaendelea kuongeza shinikizo katika mifumo ya maji na usafi wa mazingira. Hivyo inalazimu kuendelea kuboresha na kuimarisha mbinu za kufikisha huduma kwa wananchi.
Ameainisha jitihada za serikali pekee hazitoshi kufikia ukubwa wa malengo hivyo ni muhimu sekta binafsi ishiriki kwa nguvu zaidi, kwa mpangilio mzuri na kwa ubunifu katika utoaji wa huduma, uwekezaji na uendelevu.
Ameongeza lengo la Serikali si kuhamisha jukumu kutoka taasisi za umma, bali ni kujenga mfumo imara zaidi ambapo wadau wa umma na binafsi wanajumuishwa katika kutoa huduma ya maji na usafi wa mazingira.
Warsha imehudhuriwa na wawakilishi kutoka Wizara, Idara na Taasisi za Serikali , Sekta binafsi na washirika wa maendeleo ikiwemo Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika, UNICEF, GIZ, AFD na KfW.
Alitoa rai hiyo leo Jumatatu January 19 baada ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Singida Vijijini, iliyopo Ilongero, mradi unaogharimu Tsh. bilioni 3.7 katika siku ya pili ya ziara yake ya siku tano mkoani Singida.
Komredi Kihongosi alimpigia simu Waziri wa Afya Mhe. Mohamedy Mchengerwa na kuigiza wizara hiyo kuhakikisha gari hilo linafika kwa wakati.
Gari hili litarahisisha usafiri wa haraka kwa wagonjwa kutoka tarafa tatu zinazotegemea huduma kutoka hospitali hiyo, na hivyo kuondoa usumbufu mkubwa wa huduma ya afya kwa wakazi wa vijiji vilivyombali.




.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)







.jpeg)








.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)

