.jpeg)
.jpeg)
Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha utafiti kuhusu maboresho ya kisasa ya mnyororo wa thamani wa kilimo uliofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Maendeleo ya Canada (IDRC-CRDI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Tuzo hiyo imekabidhiwa leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, na Meneja wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Bodi hiyo, Bw. Elfaraja Kintingu.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Bangu amesema heshima hiyo ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya WRRB katika kuimarisha sekta ya kilimo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, ambao umeendelea kuongeza ufanisi wa biashara ya mazao, uwazi wa masoko na ushindani wa bei katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Amesema WRRB itaendelea kushirikiana na taasisi za utafiti na wadau mbalimbali katika kuendeleza ubunifu na maboresho yanayochochea maendeleo ya mnyororo wa thamani wa kilimo kwa manufaa ya wakulima na uchumi wa Taifa.
Awali, akielezea kuhusu tuzo hiyo, Bw. Kintingu amesema imetolewa kwa kutambua ushirikiano na mchango wa WRRB katika kufanikisha utafiti huo, ambapo watafiti walitembelea ghala mbalimbali nchini ili kujionea utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na mchango wake katika kuimarisha biashara ya mazao, kuongeza uwazi wa masoko na kuboresha mnyororo wa thamani wa kilimo.

Wanawake na mabinti nchini wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kujiunga na kozi za ubaharia na fani nyingine zinazohusiana na uchumi wa bluu ili kunufaika na fursa nyingi za ajira na maendeleo zinazopatikana katika sekta hiyo.
Rai hiyo imetolewa na Mkufunzi Msaidizi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Winifrida Winsislaus Ngalu, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Julai 8, 2026.
Amesema bado kuna dhana potofu miongoni mwa jamii kwamba fani za ubaharia ni za wanaume pekee, jambo ambalo si sahihi kwani wanawake wengi tayari wameingia katika sekta hiyo na wanaendelea kufanya vizuri katika nafasi mbalimbali.
Ngalu amesema Chuo cha Bahari Dar es Salaam kinashiriki maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu fursa zinazopatikana kupitia kozi mbalimbali zinazotolewa chuoni hapo, pamoja na kuwahamasisha wananchi kujiunga na masomo yanayohusiana na uchumi wa bluu.
Aidha, amesema Serikali imeendelea kutoa kipaumbele kwa kozi zinazotolewa na chuo hicho, ambapo wanafunzi wanaojiunga kuanzia ngazi ya cheti wanaweza kupata mikopo hadi elimu ya juu, hatua inayolenga kuongeza idadi ya wataalamu katika sekta hiyo muhimu.
Pia ameeleza kuwa chuo kinaendelea kupokea maombi ya wanafunzi wanaotaka kujiunga na programu za cheti na shahada za uzamili (Master’s Degree) pamoja na kozi za umahiri, dirisha la maombi kwa awamu ya kwanza litafungwa Julai 10, 2026 na dirisha la ngazi ya Shahada yaani Digrii litafunguliwa Julai 15.
Ngalu ametoa wito kwa wanawake, mabinti na vijana kwa ujumla kutumia fursa hiyo kujiendeleza kielimu na kitaaluma, akisisitiza kuwa uchumi wa bluu una nafasi kubwa ya kuchangia ajira, ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa.
Geneva, Julai 2026
Tanzania imelitaka Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) kujenga mfumo wa kimataifa wa miliki bunifu unaowezesha nchi zinazoendelea kunufaika na maendeleo ya akili mnemba (Artificial Intelligence–AI), huku ikisisitiza umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya teknolojia na kujengea watu uwezo.
Akiwasilisha taarifa ya nchi kwa niaba ya Mhe Balozi Possi katika Mkutano wa 68 wa Nchi Wanachama wa Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) ulioanza tarehe 7 Julai, 2026 na kufanyika Geneva Uswisi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Hoyce Temu, alisema miliki ubunifu imekuwa nyenzo muhimu ya kukuza ubunifu, viwanda na maendeleo ya uchumi.
"Tanzania inatambua miliki ubunifu kama kichocheo cha kimkakati cha ubunifu, uvumbuzi wa teknolojia, maendeleo ya viwanda na maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi," alisema.
Alisema Tanzania inaendelea kujenga uchumi unaotegemea maarifa na inaiona akili mnemba kama fursa ya kuongeza kasi ya ubunifu na ukuaji wa uchumi.
"Tunaamini kuwa mifumo jumuishi ya miliki bunifu, ujenzi wa uwezo na uhamishaji wa teknolojia ni muhimu ili kuwezesha nchi zinazoendelea kunufaika kikamilifu na akili mnemba pamoja na teknolojia nyingine zinazoibuka," alisema.
Kauli hiyo inakuja wakati mataifa duniani yanaendelea kujadili namna mfumo wa miliki ubunifu utakavyoweza kuendana na kasi ya maendeleo ya akili mnemba. Nchi nyingi zinazoendelea zimekuwa zikitaka ushirikiano mkubwa zaidi katika uhamishaji wa teknolojia na maarifa ili kupunguza pengo la kidijitali.
Balozi Temu alisema Tanzania inaendelea kuimarisha mfumo wake wa miliki bunifu kupitia mageuzi ya sheria, kuboresha utoaji wa huduma, kuimarisha utekelezaji wa sheria, kujenga uwezo wa taasisi na kuongeza uelewa wa umma.
Aliishukuru WIPO kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania kupitia programu mbalimbali za kiufundi na ujenzi wa uwezo, ikiwemo kliniki za usimamizi wa haki miliki kwa biashara ndogo na za kati pamoja na kampuni changa, miradi ya uhamishaji wa teknolojia kupitia vyuo vikuu na taasisi za utafiti, mafunzo ya uchunguzi wa hataza na uwekaji wa mfumo wa kidijitali wa usimamizi wa haki miliki.
"Tunaendelea kujizatiti kuimarisha mfumo wa haki miliki ili uchangie zaidi katika ubunifu, uwekezaji, ujasiriamali, ajira na ukuaji endelevu wa uchumi," alisema.
Balozi Temu alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na WIPO pamoja na nchi nyingine wanachama kujenga mfumo wa haki miliki unaojumuisha wote, unaozingatia usawa na unaoweza kukidhi mahitaji ya teknolojia za sasa na zijazo.

.jpg.jpeg)


Wageni hao, wakiwemo Watanzania na raia wa kigeni, walipata fursa ya kutembelea eneo hilo la kihistoria na kujifunza kuhusu historia ya ustaarabu wa pwani ya Afrika Mashariki pamoja na urithi wa kihistoria wa Tanzania.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhifadhi Mambo Kale Daraja la II, Veronica Kombe, aliwahamasisha wananchi kutumia ofa ya Sabasaba kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vinavyosimamiwa na TFS. Alibainisha kuwa safari inayofuata itafanyika Julai 11 kuelekea Msitu wa Asili wa Pugu–Kazimzumbwi.
Baadhi ya wageni walioshiriki ziara hiyo walieleza kufurahishwa na uzoefu walioupata, wakisema wamefanikiwa kujionea kwa karibu maeneo ambayo kwa muda mrefu walikuwa wakiyasikia kupitia simulizi na kusoma kwenye vitabu.
Kupitia ofa hiyo ya Sabasaba, TFS inalenga kuwapa wananchi fursa ya kutembelea vivutio vya utalii kwa gharama nafuu, kujifunza historia, kuhamasisha utalii wa ndani, na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kuhifadhi urithi wa asili na kihistoria wa Tanzania.
Na Pamela Mollel,Arusha
Maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Arusha yamekamilika kwa asilimia 100, huku wananchi wakihimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika shughuli za Mbio za Mwenge, kutembelea miradi ya maendeleo na kuhudhuria mkesha mkubwa wa burudani utakaofanyika Viwanja vya FFU Mworombo jijini Arusha
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, anasema maandalizi yote yamekamilika na wilaya ipo tayari kuupokea Mwenge wa Uhuru, huku akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu
Anasema Mwenge wa Uhuru utatembelea na kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha maendeleo na kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa wananchi
Mkude anasema mbali na miradi ya maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika mapambano dhidi ya UKIMWI, malaria, rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na utunzaji wa mazingira kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo, "Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo."
Aliongeza kuwa baada ya shughuli za mchana kukamilika, kutafanyika mkesha wa Mwenge wa Uhuru katika Viwanja vya FFU Mworombo, ambapo wananchi watapata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiongozwa na Ali Kiba na Juma Nature
Aidha, aliwataka wakazi wa Arusha na maeneo ya jirani kutumia fursa hiyo kushuhudia Mbio za Mwenge wa Uhuru, kutembelea miradi ya maendeleo pamoja na kushiriki mkesha huo utakaokuwa na burudani na ujumbe wa uzalendo
Mkude alisema matarajio ya Wilaya ya Arusha ni kuona wananchi wakijitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wa Uhuru na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa jamii.
Na Mwandishi wetu
Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesema itaendelea kuweka msukumo katika kuendeleza sayansi na teknolojia kwani ndiyo msingi wa kukuza uchumi kupitia maarifa na kuboresha huduma katika sekta mbalimbali.
Akizungumza Julai 8, 2026, baada ya kutembelea Taasisi ya Afya na Utafiti ya Ifakara (Ifakara Health Institute-IHI), tawi la Bagamoyo mkoani Pwani, Prof. Mkenda amesema taasisi hiyo ni ya mfano katika tafiti za kisayansi ambazo zinasaidia maendeleo ya sekta ya afya.
Amepongeza kazi za Taasisi hiyo akitolea mfano utafiti chanjo za malaria, majaribio ya dawa (clinical trials) na teknolojia za kisasa zinazotumika katika utafiti.
Mkenda amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa IHI na vyuo vikuu vya ndani na vya kimataifa ili kuijengea Tanzania yenye uwezo wa kufanya tafiti zenye viwango vya kimataifa, kuzalisha maarifa na bidhaa zenye manufaa kwa wananchi.
Prof. Mkenda ameongeza kuwa serikali inataka kuona dawa za asili zikifanyiwa utafiti, majaribio ya awali (pre-clinical) na clinical trials ili kuthibitisha ubora na usalama wake hapa hapa nchini, hatua itakayowezesha Tanzania kuzalisha dawa zilizotokana na gunduzi za ndani na kunufaika na matokeo yake kwa kuwa na haki miliki.
Aidha, amesema wizara inaendelea kupitia sera ya Sayansi na Teknolojia ili kuhakikisha inakuwa shirikishi, inatekelezeka na inapimika, sambamba na kuvitaka vyuo vikuu nchini kuweka uzito sawa katika ufundishaji na utafiti.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Afya na Utafiti ya Ifakara (Ifakara Health Institute-IHI), tawi la Bagamoyo Dkt Ally Olotu amesema taasisi hiyo immejikita katika kuleta mabadiliko katika mifumo ya afya nchini na nje ya mipaka, kufanya tafiti za chanjo mbalimbali na tabia za jamii kuhusiana na Afya.
Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa, ameipongeza Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa mageuzi inayoendelea kuyasimamia katika taasisi za umma, huku akiitaka kuendeleza juhudi hizo ili kuongeza tija ya uwekezaji wa Serikali.
Msigwa, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alitoa pongezi hizo leo, Julai 8, 2026, alipotembelea banda la OTR katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
"Hongereni sana kwa mageuzi mnayofanya ambayo yamewezesha kuongezeka kwa gawio na michango mingine kutoka kwa taasisi za umma na kampuni ambazo serikali ina hisa chache. Endeleeni kufanya kazi hiyo kwa bidii zaidi.”
Kwa mwaka wa fedha 2025/26, OTR imekusanya jumla ya Sh1.327 trilioni kutoka katika mashirika ya umma na kampuni ambazo Serikali ina umiliki wa hisa chache.
Kiasi hicho ni ongezeko la takribani Sh300 bilioni ikilinganishwa na Sh1.028 trilioni zilizokusanywa mwaka wa fedha 2024/25, sawa na ukuaji wa asilimia 30.
Aidha, Msigwa aliitaka OTR kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uwekezaji wa Serikali wenye thamani ya Sh92.3 trilioni unaosimamiwa na Ofisi hiyo, uliowekezwa katika mashirika ya umma na kampuni ambazo Serikali ina hisa chache.
“Wananchi wanapaswa kujua kuwa uwekezaji huu ni mali yao. Hivyo, ni muhimu wauelewe na waulinde kwa maslahi ya Taifa”.
Aliongeza kuwa uelewa wa wananchi kuhusu uwekezaji wa Serikali utasaidia kuongeza uwajibikaji na kuthamini mchango wa taasisi za umma katika maendeleo ya nchi.
Gawio na michango mingine inayokusanywa kutoka kwa mashirika ya umma na kampuni ambazo Serikali ina hisa chache huwasilishwa katika Mfuko Mkuu wa Serikali, ambako hutumika kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na utoaji wa huduma muhimu za kijamii, ikiwemo afya na elimu.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka Watanzania kuendelea kutembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), akisema maonesho ya mwaka huu 2026 yameonesha mafanikio makubwa ya maendeleo ya viwanda, ubunifu wa teknolojia na ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini.
Akizungumza Julai 08, 2026 baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho hayo, Kapinga amesema mwitikio wa wananchi ni mkubwa kiasi kwamba Serikali inatafakari kuongeza siku moja ya maonesho ili kutoa nafasi kwa wananchi wengi zaidi kushiriki na wafanyabiashara kuendelea kufanya biashara.
Amesema ukubwa wa maonesho hayo unamlazimu kuyatembelea mara kwa mara kwa kuwa haiwezekani kuona mabanda yote kwa siku moja, huku akieleza kuridhishwa na namna waoneshaji walivyojiandaa na ubora wa bidhaa zinazooneshwa.
Waziri Kapinga amesema maonesho ya mwaka 2026 yamebeba teknolojia mbalimbali za kisasa, ikiwemo magari yanayotumia umeme, magari ya mseto (hybrid), magari yanayotumia gesi asilia (CNG) kwa asilimia 100 pamoja na mitambo ya kisasa inayotumia umeme, hatua inayoonesha ukuaji wa sekta ya viwanda na matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira.
Aidha, amesema bidhaa za ndani zimeendelea kuongezeka ubora, hususan katika thamani na vifungashio, jambo linalodhihirisha mafanikio ya uwekezaji wa Serikali katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kukuza uzalishaji wa ndani.
"Wananchi waendelee kujitokeza kutembelea Sabasaba. Fursa zilizopo mwaka huu ni nyingi zaidi, hivyo ni wakati mzuri wa kujifunza, kufanya biashara na kuona maendeleo ya viwanda vya Tanzania," amesema Kapinga.
Ameongeza kuwa iwapo uamuzi wa kuongeza siku moja ya maonesho utapitishwa, utalenga kuwapa wananchi, hasa wanaokuwa kazini siku za kawaida, nafasi zaidi ya kutembelea maonesho hayo na kunufaika na fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji.




.jpeg)
.jpeg)







.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
