Na Mwandishi Wetu, Tanga

CHAMA cha National League for Democracy (NLD), kimeitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kutosita kuvifuta au kuvifungia vyama vyote vya siasa vinavyokiuka sheria na kuhatarisha amani ya nchi, kikitaka wanasiasa wanaoshindwa kufuata sheria wajitoe na kuwa wanaharakati.

Wito huo umetolewa Leo mei 25 jijini Tanga na Katibu Mkuu wa NLD, Doyo Hassan Doyo, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya kisiasa nchini, kufuatia hatua ya CHADEMA kuitisha maandamano ya nchi nzima kushinikiza kuachiwa kwa Mwenyekiti wao, Tundu Lissu.

Doyo alisema Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2019, na kuwataka Watanzania kuacha tabia ya kulalamika na kuishutumu mamlaka hiyo kuwa inaegemea upande mmoja pale inapochukua hatua za kisheria.

"Msajili haipendelei chama chochote, kila chama kinaonywa na kuadhibiwa kadiri kinavyofanya makosa. Baada ya CHADEMA kutoa kauli zinazoashiria uvunjifu wa amani, waliandikiwa barua ya kujieleza, lakini hata CCM nao waliandikiwa barua kufuatia kauli ya Mwenyekiti wa UWT, Mary Chatanda, aliyesema angekuwa Rais kwa dakika moja angekifuta CHADEMA. Hii inathibitisha msajili haangalii uso wa mtu," alisema Doyo.

Katibu Mkuu huyo alisisitiza kuwa vyama vyote vimesajiliwa kisheria, hivyo vinapaswa kuendesha shughuli zake ndani ya kanuni zilizowekwa na sio kujiendesha kama makundi ya harakati mitaani.

Aliongeza kuwa, pamoja na kelele na maneno mengi ya kisiasa, CHADEMA wametekeleza takwa la kisheria kwa kujibu barua ya msajili, na sasa ni jukumu la Ofisi ya Msajili kuweka wazi kwa umma kile ambacho chama hicho kimekijibu ili kuondoa sintofahamu.

"Kama kuna chama kinataka kujiendesha tofauti na sheria, wajitoe rasmi tujue ni wanaharakati. Kulinda amani ya nchi hii sio jukumu la Chama Tawala (CCM) pekee, ni jukumu letu sote wanasiasa kufanya siasa za kisheria, alieleza.

Doyo alirejea kumpongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayofanya ya kuleta umoja na utulivu kupitia falsafa yake ya maridhiano, ambayo imetoa uwanja mpana kwa vyama vyote kufanya siasa za kistaarabu.

Akizungumzia ziara yake mkoani Tanga, Doyo alisema mara ya mwisho kufika mkoani hapa ilikuwa ni wakati wa kuzindua kampeni za Urais mwaka 2025, na sasa amerejea maeneo hayo kwa ajili ya kuimarisha na kukisuka chama chake kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa NLD unaotarajiwa kufanyika mwakani (2027).




WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika miradi ya barabara nchini kwa kuwa ndiyo msingi wa kufungua uchumi, kurahisisha usafirishaji wa mazao na kuchochea maendeleo ya wananchi vijijini na mijini.

“Hizi kilomita 17 zilizobaki kuelekea Dabaga ni eneo muhimu sana la uzalishaji, hivyo Serikali itaendelea kuweka mkazo kuhakikisha eneo hilo linafunguliwa kwa kiwango cha lami,” amesema Dkt. Mwigulu.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumapili, Mei 24, 2026 alipokagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya Iringa (Ipogolo) – Kilolo yenye urefu wa kilomita 33.61 kwa kiwango cha lami chini ya Programu ya RISE (Barabara kwa Maendeleo na Fursa za Kiuchumi na Kijamii) katika Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ya miundombinu kwa lengo la kuimarisha shughuli za kiuchumi na kuboresha huduma za usafiri kwa wananchi.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali imekubaliana kuhakikisha miradi yote iliyoanza inakamilishwa kwanza sambamba na kuendelea kutoa fedha za utekelezaji kwa miradi iliyosainiwa mikataba lakini haikupata malipo ya awali.

“Tunahakikisha kwanza tunakamilisha miradi ambayo ilikuwa imeanza, iliyosainiwa lakini haikupata malipo ya awali na ile ambayo wakandarasi walishapatikana ili wananchi waanze kunufaika na miradi hiyo,” amesema.

Kadhalika, amesema Serikali imeongeza kasi ya utekelezaji wa miradi mingine baada ya kukamilisha baadhi ya miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Bwawa la Julius Nyerere, reli ya kisasa ya SGR pamoja na Daraja la Kigongo – Busisi.

“Tuliamua kwanza tumalize miradi mikubwa iliyokuwa imefikia hatua nzuri ili ianze kusaidia uchumi wa nchi. Sasa tunaongeza nguvu kwenye miradi mingine iliyokuwa imepunguza kasi ya utekelezaji wake,” amesema.

Amesema mradi huo wa barabara una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Kilolo kutokana na eneo hilo kuwa miongoni mwa maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya kilimo mkoani Iringa.

Kwa upande wake, Mbunge wa Kilolo, Rita Kabati amesema wananchi wa Kilolo wameendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa wa Serikali katika sekta ya miundombinu huku akiishukuru Serikali kwa kuendelea kutatua changamoto za usafiri katika wilaya hiyo.

“Uchumi wa Kilolo unategemea barabara. Maeneo mengi hayapitiki wakati wa mvua na suluhisho lake ni barabara za lami,” amesema Rita Kabati.

Naye Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Iringa, Mhandisi Hosea Machaka amesema mradi huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 60.14 umefikia asilimia 96 ya utekelezaji na tayari umekabidhiwa kwa matumizi.

Amesema mradi huo umehusisha ujenzi wa daraja la Ndiwili lenye urefu wa mita 40, makalavati makubwa 13, makalavati madogo 54 pamoja na njia za watembea kwa miguu na waendesha baiskeli kwa lengo la kuimarisha usalama wa watumiaji wa barabara.

Aidha, amesema wananchi 596 waliopitiwa na mradi huo walilipwa fidia ya zaidi ya shilingi bilioni 2.54 huku ajira 393 zikizalishwa ambapo asilimia 95 ya ajira hizo zilitolewa kwa wananchi wa eneo husika.








Na Janeth Raphael MichuziTv - Iringa


WAZIRI Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wananchi nchini kuacha kufanya mambo kwa mazoea na kuaminiana pekee, hasa katika masuala ya ardhi na mali, akisema kupungua kwa uaminifu katika jamii kunachochea migogoro mikubwa ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

Dkt. Mwigulu ametoa kauli hiyo leo wilayani Kilolo mkoani Iringa wakati akihutubia wananchi katika mwendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani humo, ambapo amesisitiza umuhimu wa wananchi kufuata taratibu rasmi za kisheria katika umiliki, uazimishaji na makubaliano mbalimbali ya mali.

Amesema kuwa wananchi wengi wamekuwa wakifanya makubaliano ya ardhi kwa mazoea bila kuyaweka kisheria, hali ambayo imekuwa chanzo kikubwa cha migogoro pindi mmoja wa wahusika anapofariki dunia au kutokea sintofahamu ndani ya familia.

“Mtu anaazimisha shamba kutoka kwa familia fulani, lakini wakabaki wanaaminiana tu bila kuandika makubaliano yoyote. Sasa mwenye shamba anapofariki au aliyekodishwa akitaka kubaki na eneo hilo, migogoro inaanza. Mkifika mahakamani inakuwa vigumu kushinda kwa sababu hakuna nyaraka wala utaratibu wa kisheria uliofuatwa,” amesema Dkt. Mwigulu.

Ameeleza kuwa mabadiliko ya maisha na kupungua kwa uaminifu katika baadhi ya maeneo ya jamii yanapaswa kuwa somo kwa wananchi kuona umuhimu wa kuweka kumbukumbu rasmi za kila makubaliano yanayohusu ardhi au mali nyingine muhimu.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kusimamia na kufuatilia migogoro ya ardhi nchini kwa karibu ili kuhakikisha wananchi wanapata haki zao pamoja na suluhisho la kudumu la migogoro hiyo.

Amesisitiza kuwa kufuata sheria na taratibu kutasaidia kupunguza kesi nyingi mahakamani, kuimarisha amani ndani ya familia na kulinda haki za pande zote zinazohusika katika umiliki wa mali.

Dkt. Mwigulu pia amewahimiza viongozi wa serikali za mitaa pamoja na wataalamu wa ardhi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuandikisha mikataba na kumiliki ardhi kwa mujibu wa sheria ili kuepusha migogoro inayoweza kuzuilika.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wamepongeza kauli ya Waziri Mkuu wakisema changamoto za migogoro ya ardhi zimekuwa zikisababisha migawanyiko ndani ya familia na hata kuchelewesha maendeleo katika jamii.

Ziara ya Dkt. Mwigulu mkoani Iringa inaendelea ambapo pamoja na mambo mengine anatarajiwa kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi kuhusu utekelezaji wa shughuli za Serikali katika maeneo tofauti ya mkoa huo.






*Kijana Gideon amshukuru kurejeshewa fedha za mtaji wa dagaa


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wa Serikali waache kufanya ubosi kwenye kazi za watu na pia waziheshimu kazi zao.

"Lazima tuheshimu kazi za watu, tuheshimu jitihada za kila mmoja na tusifanye ubosi kwenye kazi za watu," alisema.

Waziri Mkuu alitoa wito huo jana jioni (Jumamosi, Mei 23, 2026) wakati akizungumza na wakazi wa Iringa mjini katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kichangani, Kihesa, nje kidogo ya Manispaa ya Iringa.

Sambamba na wito huo, Waziri Mkuu alimwelekeza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Heri James awape maelekezo watumishi waliopo kwenye Halmashauri zote za mkoa huo na kuwataka waache kukamata vitendea kazi vya wananchi.

"Mkuu wa Mkoa watangazie viongozi wa Halmashauri zote za mkoa wako wasikamate vitendea kazi vya wananchi. Sitaki kusikia sahani wala bakuli ya mama lishe imekamatwa," alisema na kuonya kuwa endapo vitendea kazi hivyo vimehusika na kazi za uhalifu kama ujambazi, ubakaji, dawa za kulevya au meno ya tembo ndipo vinaweza kuchukuliwa kama vidhibiti kwani hayo ni makosa ya jinai.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amefanikisha kurejeshwa sh. 600,000 kwa Bw. Gideon Sebastian Yona ambazo zilikuwa ni za mtaji wa biashara yake ya dagaa. Akielezea kero yake mbele ya Waziri Mkuu, Bw. Yona alisema kuwa Februari 26, mwaka huu alipofika soko la Mlandege, Iringa alikuta magunia yake ya dagaa yameibiwa na akaripoti kwa mwenyekiti wa soko lakini hadi leo hajarudishiwa dagaa wala fedha yoyote.

Alipoulizwa kama analifahamu suala hilo, Mwenyekiti wa soko hilo, Kessy Michael Ndandu, alikiri kulitambua na kwamba siku hiyohiyo ya tukio alitoa taarifa kwa Afisa Biashara wa Manispaa, Bw. Mahenge Misinzo. Alisema alichukua hatua hiyo kwa sababu walinzi wa soko ni waajiriwa wa Halmashauri.

Alipoulizwa na Waziri Mkuu kama analitambua suala hilo, Afisa Biashara huyo, alidai kwamba amepata taarifa jana yake (Ijumaa, Mei 22, 2026) ndipo Waziri Mkuu alipokemea tabia ya kuzoea matatizo ya wananchi na kumuamuru yeye na wasaidizi wake wachange hiyo hela na wamlipe hapohapo sh. 600,000 zake.

Alipopewa fedha hiyo, Bw. Yona huku akiwa na tabasamu la nguvu, alirudi kumshukuru Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kumsaidia arejeshewe mtaji wake.

Waziri Mkuu alisikiliza kero mbalimbali zilizohusu ajira, ardhi, mafao, fidia na madeni ya wazabuni, ambazo baadhi alizitolea maamuzi, nyingine alizielekeza kwa mawaziri wa kisekta waliokuwepo na nyingine kwa viongozi wa Mkoa wa Iringa.

Mapema, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile alisema kuwa katika kuimarisha mawasiliano ya Kanda ya Kusini, Serikali imeidhinisha kiasi cha shilingi trilioni 3.3 kwa ajili ukarabati wa reli ya TAZARA ili kuboresha usafirishaji wa mazao na madini kutoka kwenye mikoa mbalimbali.

“Reli ya TAZARA ni ya kihistoria lakini imesuasua kwa miaka mingi. Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliridhia na zimeidhinishwa dola za Marekani bilioni 1.4 sawa na shilingi trilioni 3.3 ili kufanya maboresho ya reli hiyo yenye urefu km. 1,860 kutoka Dar es Salaam hadi Zambia. Ikikamilika, itasaidia kubeba mizigo kutoka mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Mbeya na Songwe,” alisema na kuongeza kuwa mbali na mazao ya chakula, mizigo mingine itakuwa ni ya madini, maparachichi na mahindi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba alisema mkoa wa Iringa umepokea sh. bilioni 124 ili kuhakikisha nishati ya umeme inapatikana mkoani humo. Hata hivyo, alikiri uwepo wa changamoto za wananchi waishio maeneo ya vijijini lakini wanaonekana kuwa wako maeneo ya mijini na hivyo kushindwa kumudu gharama za kuunganisha umeme.

“Nimepata taarifa kuwa mitaa ya Ugele na Mkoga ni ya pembezoni, kata zake zinaonekana ziko mjini lakini wananchi wake wanaishi kijijini na kiuhalisia hawawezi kumudu gharama ya sh. 320,000 ya kuunganisha umeme. Kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, tumewaingiza kwenye bajeti ya mwaka ujao, kwa hiyo tutawaunganishia umeme kwa sh.27,000/-,” alisema.

Naye, Mbunge wa Iringa, Fadhili Ngajilo alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa sh. bilioni 4.4 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la halmashauri ambalo kazi ya ujenzi imeshaanza.

Aliomba kupatiwa barabara za lami walau km. 50 ili kuboresha miundombinu ya mawasiliano ndani ya manispaa ya Iringa. Pia aliomba ijengwe barabara ya kutoka Iringa hadi Manyoni kupitia Pawaga ili kuwapunguza safari watu wanaosafiri kutoka mikoa ya Kusini kwenda mikoa ya Kanda ya Ziwa wasilazimike kuzungukia Dodoma.


 Kampuni inayotoa huduma za fedha kidigitali, Mixx kwa kushirikiana na kampuni ya Hisense, leo wametambulisha kampeni ya kitaifa itakayowawezesha Watanzania kujishindia zawadi mbalimbali kupitia matumizi ya huduma za Mixx.

Kampeni hiyo iliyopewa jina la ‘Jimixx FIFA World Cup 2026 na Hisense’ yenye kauli mbiu isemayo ‘Kila Muamala Ni Bao la Ushindi’ inaanza rasmi Mei hadi mwisho wa Julai 2026 ikiwa na lengo la kusheherekea Kombe la Dunia na wapenzi wa mchezo wa mpira wa miguu sambamba na kuhamasisha matumizi ya fedha kidijitali.

Kupitia kampeni hii, wateja watapata nafasi ya kujishindia fedha taslimu kiasi cha Shilingi milioni 1 kila siku, vifaa vya kisasa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kutoka Hisense vikijumuisha runinga za inchi 50, spika aina ya PartyBox pamoja na friji za milango miwili. Aidha, washindi watano watajishindia safari ya kwenda Mexico kushuhudia mechi za Kombe la Dunia mubashara na kulipiwa gharama zote.

Mbali na zawadi hizo, mshindi mmoja wa droo kuu ataibuka na ushindi wa shilingi milioni 50.

Wateja watakaotumia huduma za Mixx ikiwemo Lipa Kwa Simu, kutuma fedha Mixx kwenda Mixx, kulipia bili mbalimbali kama LUKU na visimbuzi, malipo ya michezo ya kubashiri, uwekezaji kwenye soko la hisa (DSE) pamoja na miamala yote itakayofanyika kupitia Mixx Super App, wataingia moja kwa moja kwenye droo ya kampeni hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mixx, Bi. Angelica Pesha alisema kampeni hiyo ni dhamira ya Mixx kuunganisha watanzania kupitia michezo huku ikihamasisha ujumuishaji wa huduma za kifedha kidijitali nchini.

“Mchezo wa Mpira wa miguu ni kitu ambacho kinachowaunganisha watanzania wengi na dunia nzima kwa ujumla. Kupitia kampeni hii tunataka wateja wetu wafurahie mapenzi yao ya soka huku wakinufaika na urahisi wa huduma za fedha kidijitali. Tunafurahia kuwapa wateja wetu uzoefu wa kipekee na zawadi zinazoweza kubadilisha maisha yao kupitia Mixx,” alisema Angelica Pesha.

Katika kipindi chote cha kampeni, Mixx na Hisense wataendesha shughuli mbalimbali za uhamasishaji nchini, kukabidhi zawadi kwa washindi kila wiki.

Akizungumza kwa niaba ya Hisense Bi. Tahera Karim, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Mars Communications Ltd (wauzaji na wasambazaji wa vifaa vya kieletroniki vya Kampuni ya Hisense) alisema ushirikiano huo unalenga kuwaletea Watanzania msisimko wa kusheherekea Kombe la dunia kupitia zawadi mbalimbali.

“Kombe la dunia ni moja ya matukio makubwa zaidi ya michezo duniani, na tunafurahia kushirikiana na Mixx kuwapa Watanzania nafasi ya kuwa sehemu ya uzoefu huu wa kipekee. Kupitia kampeni hii, wateja hawatajishindia zawadi pekee bali pia wataendelea kusherehekea mapenzi yao ya mpira wa miguu,” alisema Bi. Tahera

Mbali na zawadi na burudani ya soka, kampeni hiyo pia inalenga kuhamasisha Watanzania pamoja na wafanyabiashara wadogo kutumia zaidi huduma za malipo ya kidijitali kama Lipa Kwa Simu kwa miamala salama, rahisi na haraka zaidi.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mixx, Bi. Angelica Pesha, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya “Jimixx FIFA World Cup 2026 na Hisense” iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Bi. Tahera Karim, Afisa Mkuu wa Uendeshaji - Mars Communications Limited (wauzaji na wasambazaji rasmi wa vifaa vya kielektroniki vya Kampuni ya Hisense). Kampeni hiyo ambayo imezinduliwa kwa ushirikiano na Hisense, itawawezesha wateja kujishindia zawadi za fedha taslimu za kila siku zenye thamani ya Sh milioni 1, vifaa vya majumbani ikiwemo televisheni, friji na spika za PartyBox, pia kuna safari ya bure kwenda Mexico kwa washindi watano na mshindi wa jumla ambaye ataondoka na zawadi kuu ya Sh milioni 50 mwishoni mwa kampeni.





Absa Bank Tanzania has reaffirmed its commitment to nurturing local talent and strengthening leadership development in Tanzania through its partnership with the Fanisi Platform.

Speaking during the Fanisi Platform’s fifth anniversary celebration in Dar es Salaam, Absa Bank Tanzania Director of Human Capital and Culture, Mr. Patrick Foya, said the bank was proud to be associated with an initiative that continues to shape a new generation of leaders across the country.


Addressing guests, partners, alumni, and participants of the platform, Mr. Foya praised the vision of Fanisi founder Ms. Sarah Majengo, and said, the platform has, over the past five years, transformed mid-level professionals into confident corporate leaders by bridging talent gaps and redefining modern leadership in the region.

He noted that Absa’s partnership with Fanisi aligns with the bank’s purpose of empowering Africa’s future through investing in people and leadership development.

“At Absa, our purpose is to empower Africa’s tomorrow, together one story at a time, and for us that really starts with our people,” he said. “We are intentional about building leaders from within. We call it growing our own number, which simply means investing in our people and helping them grow into confident leaders.”

Mr. Foya revealed that since partnering with Fanisi in 2024, the bank has already seen about 40 employees graduate through the platform, while 28 others are currently enrolled in the latest cohort.

“As sponsors, our decision to invest in Fanisi was simple; we believe that empowering local talent is the single most effective way to drive sustainable economic growth,” he said.

Earlier, Fanisi Platform Founder, Ms. Sarah Majengo said the learning platform was established to bridge the gap between Tanzania’s national ambitions and the country’s human capital development needs.

She said, small and medium-sized enterprises (SMEs) account for more than 90 percent of businesses in Tanzania, employ over five million people and contribute significantly to the country’s Gross Domestic Product (GDP).

“However, many businesses continue to face challenges in accessing disciplined and competent professionals despite growing educational attainment. Findings from the World Bank says academic certificates alone are increasingly no longer considered reliable indicators of competence, with many companies struggling to find skilled and capable personnel,” she said.

Linking the issue to Tanzania’s broader development aspirations under the national Vision 2050 agenda, which targets the creation of a one‑trillion‑dollar economy driven by productivity and innovation, Ms. Sarah noted that many discussions surrounding Vision 2050 focus on whether Tanzania can develop its people quickly enough to sustain that ambition. He emphasized that the gap between Tanzania’s ambition and its human capital is precisely the gap that Fanisi exists to address.

She said the Fanisi has, over the past five years, implemented programs benefiting both young people and adults, while continuously refining its mission as a catalyst for people development.

“As for us at Fanisi, we are more committed than ever to ensuring more people have the opportunity to reach their full potential,” she added.

Fanisi is a learning platform and an invested partner in talent development for growth-focused companies and individuals, providing tailored training, networking opportunities and strategic placement.
Absa Bank Tanzania Director of Human Capital and Culture, Mr. Patrick Foya (fifth left), receives a sponsorship appreciation award from Fanisi Platform Founder, Ms. Sarah Majengo, during Fanisi’s 5th anniversary celebrations in Dar es Salaam over the weekend. Also pictured (third from right) is Tanzania Investment and Special Economic Zones (TISEZA) Director General, Mr. Gilead Teri, together with Absa Bank officials.

Absa Bank Tanzania Director of Human Capital and Culture, Mr. Patrick Foya (left), addresses participants during the Fanisi Platform 5th anniversary celebrations, sponsored by Absa Bank, in Dar es Salaam over the weekend.

 Absa Bank Tanzania Director of Human Capital and Culture, Mr. Patrick Foya (right), exchanges views with attendees during the Fanisi Platform 5th anniversary celebrations, sponsored by Absa Bank, in Dar es Salaam over the weekend.



Absa Bank Tanzania Director of Human Capital and Culture, Mr. Patrick Foya (left), greets attendees during the Fanisi Platform 5th anniversary celebrations, sponsored by Absa Bank, in Dar es Salaam over the weekend. In the middle are Mr. Christopher Shayo and Mr. Rwebu Mutahaba.


Fanisi Platform Founder, Ms. Sarah Majengo (left), addresses participants during the Fanisi Platform 5th anniversary celebrations, sponsored by Absa Bank, in Dar es Salaam over the weekend.







Tanzania Investment and Special Economic Zones (TISEZA) Director General, Mr. Gilead Teri (centre), together with Fanisi Platform Founder, Ms. Sarah Majengo (on his right), poses for a memento photograph with the platform’s partners, alumni, and stakeholders during the Fanisi Platform 5th anniversary celebrations, sponsored by Absa Bank, in Dar es Salaam over the weekend.


Na Karama Kenyunko, Michuzi TV
KATIKA ghala moja la kuhifadhi mazao nchini Tanzania, mfumo wa kielektroniki unapiga kengele. Dakika chache baadaye, ujumbe unaingia kwenye simu ya msimamizi wa ghala ukionya kuwa kiwango cha joto na unyevunyevu kimeanza kufikia mazingira yanayoweza kuzalisha sumu kuvu kwenye mahindi yaliyohifadhiwa.

Onyo hilo halihusu moto wala uvamizi wa wahalifu. Linaashiria uwepo wa mazingira yanayoweza kuchochea kuzalishwa kwa sumu kuvu kwenye mazao ya chakula.

Ingawa mazao kama mahindi, mtama na karanga ni sehemu ya chakula cha kila siku kwa mamilioni ya Watanzania, si wananchi wote wanaofahamu kuwa yanaweza kuwa chanzo cha hatari kubwa kiafya yanapoathiriwa na sumu kuvu.

Unapuzungumzia sumu kuvu katika mazao kama vile mtama, mahindi, na karanga, siyo Wananchi wote wanafamu kuwa sumu kuvu inaweza kuleta madhara kwa binadamu na mifugo na hatimaye kusababisha kansa ya ini.

Sumu kuvu ni aina ya sumu inayotengenezwa na kuvu au fangasi wanaoota kwenye mazao mbalimbali hasa nafaka kama vile mahindi, mtama, ngano, mchele na ulezi. Kuvu hao wanapoota huonekana kama ukungu. Mahindi ndiyo nafaka inayoshambuliwa zaidi na uchafuzi wa sumu kuvu ikilinganishwa na nafaka nyingine.

Mazao mengine yanayoweza kushambuliwa na fangasi hawa ni pamoja na mbegu za mafuta kama karanga, pamba, alizeti na korosho; mihogo mikavu; viungo vya chakula mfano iliki na mdalasini; mboga za majani pamoja na matunda yaliyokaushwa.

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula Duniani (FAO), sumu kuvu huharibu karibu asilimia 25 au zaidi ya chakula kinachozalishwa duniani kila mwaka.

Kutokana na madhara hayo, Idara ya Teknolojia na Sayansi ya Vyakula, Ndaki ya Kilimo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, imetengeneza teknolojia mpya ya mfumo wa kidigitali wa kudhibiti vigezo vinavyosababisha uzalishaji wa sumu kuvu (aflatoxins) ili kugundua viatarishi vinavyosababisha sumu kuvu katika mazao.

Hii si teknolojia kutoka nje ya nchi. Ni ubunifu uliotengenezwa Tanzania na timu ya watafiti wakiongozwa na Profesa Mshiriki Lilian Kaale kutoka Idara ya Teknolojia na Sayansi ya Vyakula, Ndaki ya Kilimo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Profesa Kaale ambaye pia ni Mkurugenzi wa Ubunifu na Ujasiriamali chuoni hapo anasema ubunifu huo unalenga kudhibiti sumu kuvu kabla haijazalishwa kwenye mazao yaliyohifadhiwa maghalani.

Anaeleza kwamba safari ya utafiti huo ilianza mwaka 2018 baada ya kupata ufadhili wa takribani Sh milioni 100 kutoka UNESCO.

“Niliona tatizo la sumu kuvu ni kubwa sana Tanzania. Mbali na kuharibu mazao, mazao yaliyoingiliwa na sumu hii yanaathiri afya za binadamu kwa kiwango kikubwa hususan kuchangia saratani ya ini,” anasema.

Baadaye aliomba ufadhili kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ambapo alipata shilingi milioni 120 ili kuendeleza tafiti zaidi kuhusu namna ya kutumia teknolojia ya kidigitali kugundua na kuzuia mazingira yanayochochea uzalishaji wa sumu kuvu.

Kwa mujibu wa Kaale, sumu hiyo huzalishwa na fangasi aina ya aspergillus pale mazingira fulani yanapokuwepo, hasa joto na unyevunyevu mkubwa.

“Vimelea hivi vinaweza kuwepo kwenye mazao lakini visizalishe sumu kuvu mpaka mazingira yanayowawezesha kufanya hivyo yatokee,” anasema.

Anataja mahindi, karanga na mtama kuwa miongoni mwa mazao yanayoathirika zaidi.

Anasema ubunifu huo umetengenezwa kwa kutumia vifaa vinavyopima kiwango cha unyevunyevu, joto na hali ya hewa ndani ya ghala.

Mfumo huo unapogundua mazingira yanaanza kufikia kiwango hatarishi cha kuzalisha sumu kuvu, kengele huanza kulia na ujumbe hutumwa moja kwa moja kwa msimamizi wa ghala kupitia simu.

“Ukidhibiti mazingira hayo mapema, fangasi hawawezi kuzalisha sumu kuvu,” anasema Profesa Kaale.

Anaeleza kwamba mfumo huo umeunganishwa na simu za wasimamizi wa maghala kuwawezesha kuwasha feni au kufungua milango ili kupunguza joto na unyevunyevu kabla hali haijafikia kiwango hatari.
Kwa mujibu wake, mazao baada ya kuvunwa hubaki hai na huendelea kuzalisha joto na unyevunyevu, hali hiyo huongeza uwezekano wa kuzalishwa kwa sumu kuvu wakati wa uhifadhi.

“Tafiti zinaonesha upotevu mkubwa wa mazao hutokea baada ya kuvuna, hasa kipindi cha uhifadhi,” anasema.

Anafafanua kuwa kwa sasa teknolojia hiyo imefungwa katika ghala lililopo Chemba mkoani Dodoma chini ya usimamizi wa Wizara ya Kilimo na wadau wengine wa serikali kama mfano wa majaribio tangu Agosti mwaka jana.

Kwa sababu ya gharama zake, Profesa Kaale anasema mkulima mmoja mmoja hawezi kuimudu kwa sasa na kwamba inalenga zaidi maghala makubwa ya serikali na wafanyabiashara wakubwa.

"Tumeshirikiana na serikali kwa sababu athari za sumu kuvu ni za taifa. Mfanyabiashara binafsi anaweza kupata mfumo huo kwa gharama ya takribani Sh milioni 30 ili kuusimika kwenye ghala lake," anasema.

Kwa mujibu wa Profesa Kaale, sumu kuvu ina madhara makubwa kwa ini na imehusishwa pia na magonjwa yasiyoambukiza pamoja na udumavu kwa watoto.

Anasema tatizo hilo linaweza kuathiri mamilioni ya Watanzania kwa sababu zaidi ya watu milioni 50 hutumia mahindi na karanga kama chakula cha kila siku.

“Ukilisha wanyama pumba zenye sumu kuvu, madhara yanaweza kurudi kwa binadamu kupitia mnyororo wa chakula,” anasema.

Anakumbusha tukio la mwaka 2015 mkoani Dodoma ambapo watu walifariki baada ya kula chakula kilichoathiriwa na sumu kuvu.

Kwa upande wake, Ibrahim Kinyoro ambaye ni mwanafunzi wa PhD anayesimamiwa na Profesa Kaale, anasema anakubaliana na teknolojia hiyo kwa kiasi kikubwa katika kukabiliana na sumu kuvu nchini.

Anasema teknolojia mbalimbali zimetumiwa na mtafiti huyo ikiwemo mifumo ya kengele "alarm" ya kutambua uwepo wa sumu kuvu.

"Teknolojia nzuri na nyingi zipo tayari na zimetoa matokeo isipokuwa uwekezaji na uendelevu wa teknolojia hizo kutumiwa na wakulima una gharama kubwa," anaeleza.

Kinyolo anasema ni wakati wa serikali, watunga sera na sekta binafsi kushirikiana kuwekeza katika teknolojia na kuwakomboa wakulima kukabiliana na sumu kuvu.

Anaeleza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na namna wanavyozalisha mazao yao, kuvu wataendelea kukua.

Kinyoro anasema sumu kuvu ikishaingia kwenye mahindi au karanga kuna baadhi ya hatua zikifanywa hupunguza kwa asilimia kidogo uwepo wake ikiwemo kuyachagua moja moja, kupepeta au kukoboa.

"Hizi ni njia za asili zinazotumika kuondoa sumu kuvu lakini mazao haya yakishambuliwa kwa wingi, zile unazozitoa kwa macho ndiyo ambazo zimeshambuliwa kwa kiwango kikubwa na zipo nyingine huwezi kuziona kwa macho."

Kwa upande wake, Mshauri wa Sera wa taasisi ya GRAIN, Leticia William, anasema sumu kuvu ni hatari sana ikiingia mwilini mwa binadamu au mnyama kwani inaua kimyakimya na inaweza kusababisha saratani.

Anasema ongezeko la uchafuzi wa sumu kuvu kwenye mazao ya chakula na chakula cha mifugo linaendelea kuwa tishio kubwa kwa afya ya binadamu na wanyama nchini Tanzania.

“Kutokana na hali hiyo, watu, watoto, ng’ombe, kuku, nguruwe na wanyama wengine wako kwenye hatari kubwa kutokana na matumizi ya mazao yaliyoathirika,” anasema.

Naye Mchumi Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Deogratius Lwezaura, anasema utafiti uliofanywa kati ya mwaka 2012 na 2014 katika kanda saba za kilimo ulithibitisha kuwa sumu kuvu inaweza kusababisha saratani ya ini, mzio, kudumaa kwa watoto pamoja na kuathiri ukuaji wa akili.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Profesa Martin Kimanya kwa kushirikiana na watafiti wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela mwaka 2016, Tanzania ilipoteza zaidi ya Sh bilioni 550 kila mwaka kutokana na athari za kiafya na kiuchumi zinazosababishwa na sumu kuvu kwenye mazao ya chakula.

Hasara hiyo inajumuisha mazao yanayokataliwa katika masoko ya ndani na nje pamoja na gharama za matibabu ya magonjwa kama saratani ya ini.

Ripoti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pia ilieleza kuwa bara la Afrika hupoteza wastani wa Dola za Marekani milioni 670 kila mwaka kutokana na bidhaa za kilimo kukataliwa katika masoko ya nje kwa sababu ya uchafuzi wa sumu kuvu.

Katika taifa linalotegemea kilimo, vita dhidi ya sumu kuvu si suala la maabara pekee. Ni suala la afya, usalama wa chakula na mustakabali wa uchumi wa taifa.

-Ni dawa zilizokamatwa ndani ya jahazi la Al Arab lililokuwa na raia saba wa Iran Bahari ya Hind

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza kilogramu 504.36 za dawa za kulevya aina ya heroin katika kiwanda cha saruji cha Dangote kilichopo mkoani Mtwara.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo kwa vyombo vya habari imeeleza kuwa uteketezaji huo umefanyika kutokana na amri ya Mahakama Kuu Masijala Ndogo ya Mtwara baada ya kukamilika kwa hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa waliohusika na dawa hizo.

Dawa hizo zilikamatwa ndani ya jahazi la Al Arab lililokuwa na raia saba wa Iran katika Bahari ya Hindi ndani ya eneo la kiuchumi la Tanzania.

Uteketezaji huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Sura ya 95 inayoruhusu kuteketezwa kwa vielelezo vya dawa za kulevya baada ya taratibu za kisheria kukamilika au wakati shauri linaendelea kwa idhini ya mahakama.

Katika hatua nyingine Mamlaka imeendelea kusisitiza umuhimu wa kuimarisha huduma za tiba na utengemao kwa watu wenye uraibu wa dawa za kulevya hususan katika ukanda wa kusini mwa Tanzania.

Katika kutekeleza azma hiyo, DCEA itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuwezesha upatikanaji wa huduma za MAT pamoja na kuanzishwa kwa nyumba za upataji nafuu (sober houses) ili kusaidia waraibu kupata huduma stahiki na kurejea katika maisha yenye tija kwa jamii.

Aidha imesema itaendelea kushirikiana na vyombo vya dola, wadau mbalimbali pamoja na wananchi katika kuzuia usafirishaji, biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

“Mamlaka itaendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma kuhusu madhara ya dawa za kulevya na umuhimu wa ushiriki wa jamii katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.”






▪️Aonya dhidi ya vitendo vya uchochezi, kujiteka na propaganda zinazolenga kuwagombanisha Watanzania

▪️Asema Serikali imejikita kusikiliza wananchi na kutatua kero zao badala ya mijadala ya uchaguzi

▪️Awataka wananchi kuendelea kulinda mshikamano na utulivu wa Taifa


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuendelea kuwa macho dhidi ya vitendo vinavyolenga kuvuruga amani ya nchi huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia usalama wa wananchi na mali zao.

“Kuweni macho na njama za aina hii, shughulikeni na waovu wa aina hii. Mliweza lile la Kibiti, mliweza lile la Amboni na mambo mengine mengi mmeweza. Kuweni macho kuhakikisha michezo ya aina hiyo haifanikiwi huku mkihakikisha usalama wa raia wetu na mali zao unaendelea kulindwa,” amesema Dkt. Mwigulu.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumamosi, Mei 23, 2026 alipozungumza na wananchi wa Manispaa ya Iringa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Kichangani mkoani Iringa.

Amesema amani ni msingi wa maendeleo ya Taifa na kwamba Watanzania wanapaswa kuendelea kulinda mshikamano wa kitaifa na kukataa vitendo vya uchochezi vinavyoweza kusababisha migawanyiko ya kisiasa, kidini au kijamii.

“Amani ni msingi wa maendeleo ya taifa letu. Kila mwananchi ana wajibu wa kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa salama na yenye mshikamano,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema zipo njama mbalimbali zinazolenga kuwagombanisha Watanzania kupitia siasa, dini na taarifa za upotoshaji huku akiwataka wananchi kuwa makini na watu wanaowachochea kufanya vitendo vinavyohatarisha usalama wa nchi.

“Tupuuze na wala tusiwe na ushirika na mtu anayekutuma kuvunja amani wakati yeye hayupo hapo na anajua yeye hataathirika,” amesema.

Kadhalika, Dkt. Mwigulu amesema baadhi ya matukio yanayoendelea kujitokeza nchini yakiwemo madai ya watu kujiteka au kushambuliwa yanapaswa kutazamwa kwa umakini mkubwa kwa kuwa baadhi yake yanaweza kuwa sehemu ya njama za kuwagawa Watanzania na kuichonganisha Serikali na wananchi wake.

“Hizi ni ajenda maalum. Hii ni michezo ambayo inalenga kutengeneza hasira na kuwafanya watu wachukiane,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali imejikita zaidi katika kutatua changamoto za wananchi na kusukuma maendeleo badala ya kuendelea kujadili siasa za uchaguzi muda mfupi baada ya uchaguzi mkuu kumalizika.

“Taifa linapotakiwa kupiga hatua, tujadili namna ya kutatua kero za wananchi badala ya kutumia muda mwingi kujadili uchaguzi,” amesema.

Amesema yeye binafsi ameendelea kufanya ziara mbalimbali za kusikiliza wananchi, kupokea changamoto zao na kuhakikisha Serikali inazitatua kwa wakati ili wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo.

“Watu wanahitaji kusikilizwa, wanahitaji kutatuliwa changamoto zao na wanahitaji maendeleo. Hiyo ndiyo kazi ambayo Serikali imepewa na wananchi,” amesema.

Aidha, Dkt. Mwigulu amesema Tanzania imeendelea kuwa mfano wa mshikamano na uvumilivu wa kidini na kijamii barani Afrika kutokana na misingi iliyoasisiwa na viongozi waasisi wa Taifa.

“Hii ndiyo nchi ambayo Mungu ametupatia na Baba wa Taifa ameturithisha. Tukatae vibaraka wanaotaka kuligawa Taifa letu,” amesema.

Waziri Mkuu pia amewaomba viongozi wa dini, wazee wa mila, viongozi wa kisiasa na wananchi kwa ujumla kuendelea kuhubiri amani, mshikamano na uzalendo ili taifa liendelee kuwa salama na lenye umoja.










▪️Asema mradi huo utafungua fursa mpya za uchumi na kupunguza msongamano wa magari mjini Iringa

▪️Aagiza wakandarasi kuwalipa kwa wakati wadaiwa wao

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ya miundombinu ili kuboresha usafiri, kuongeza ufanisi wa uchukuzi na kufungua fursa mpya za maendeleo ya kiuchumi nchini.

“Barabara hii ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla. Itasaidia kupunguza msongamano wa magari, kuongeza biashara na kuchochea ukuaji wa mji wa Iringa,” amesema Dkt. Nchemba.

Amesema hayo leo Jumamosi, Mei 23, 2026 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Mchepuo ya Mji wa Iringa (Iringa Municipal Bypass) yenye urefu wa kilomita 7.3 inayojengwa kwa kiwango cha lami mkoani Iringa.

Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya SINOHYDRO Corporation Limited kwa usimamizi wa TANROADS kupitia kitengo chake cha TECU, unagharimu shilingi bilioni 41.6.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza miradi mikubwa ya barabara nchini kwa lengo la kuimarisha uchumi na kurahisisha huduma za usafiri na uchukuzi.

Amesema barabara hiyo itakuwa suluhisho la kudumu la msongamano wa magari katika mji wa Iringa hususan katika eneo la mlima wa Ipogoro ambalo limekuwa likikumbwa na ajali na changamoto za usafiri kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu, magari na vyombo vingine vya usafiri.

“Ndugu zangu wana Iringa, Mheshimiwa Rais amejipambanua kuwa ni Rais wa matokeo. Akisema jambo analitekeleza, na ndiyo maana mnaendelea kuona miradi mikubwa ya barabara ikitekelezwa karibu kila kona ya nchi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya Serikali kuhakikisha wanawalipa kwa wakati wakandarasi wadogo, mafundi na vibarua wanaoshiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kadri wanavyopata fedha, wawalipe wale wanaotekeleza mradi pamoja nao. Sio vizuri mradi ukamilike wakati wengine waliotoa huduma wanadai malipo yao,” amesema.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa Serikali wa kujenga barabara za mchepuo katika miji mikubwa ili kupunguza msongamano wa magari na kuongeza ufanisi wa usafiri wa mizigo nchini.

Amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza miradi mingine ya barabara za mchepuo katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Dodoma, Mbeya, Morogoro, Mwanza, Arusha na Tanga.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Iringa, Mhandisi Hosea Machaka amesema utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 38.5 huku kazi mbalimbali zikiendelea ikiwemo ulipuaji wa miamba, ujazaji wa kifusi, ujenzi wa makalavati pamoja na ujenzi wa njia za mchepuo.

Amesema wananchi 186 walioathiriwa na mradi huo wamelipwa fidia yote yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 4.6, hatua iliyosaidia kuondoa changamoto za upatikanaji wa eneo la mradi.

Naye Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo amesema wananchi wa Iringa wameupokea mradi huo kwa matumaini makubwa kutokana na mchango wake katika kuboresha usafiri na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika mji huo.













MTAA mzima unaongelea Gates of Arabia kutoka Meridianbet na sababu ni moja tu, mchezo huu imebuniwa ukijumuisha burudani na hamasa za ushindi mkubwa. Kila raundi inaleta presha ya kusubiri kuona kama jackpot itatua upande wako. Hapa ni mwendo wa burudani na mkwanja kwenda sambamba.

Unaweka dau lako, mchezo unaanza kuzunguka na hapo ndipo picha linaanza rasmi. Ndani ya Gates of Arabia unaweza kushinda hadi mara 5,000 ya hela uliyoeka. Dakika moja unaweza kuwa kawaida tu, dakika inayofuata ukaanza kutuma meseji za leo nimepiga kitu.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya MERIDIANBET au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mizunguko ya bure pamoja na jackpot zinazotoka muda wowote zimeufanya mchezo huu kuwa gumzo kwa vijana wengi. Kila mzunguko wa mchezo una nafasi mpya ya kutoboa na hakuna anayejua bahati itatua kwa nani. Hii ndiyo maana watu wanarudi tena na tena kucheza.

Pia kuna ushindani wa hali ya juu ndani ya mchezo huu. Kila mmoja anataka awe kinara na kuonyesha kwamba bahati yake imemuwakia kwelikweli kuliko wengine. Ushindi mmoja tu unaweza kubadilisha furaha yako yote ya siku.

Usikae nje wakati wengine wanakusanya mkwanja. Ingia sasa Meridianbet, fungua Gates of Arabia na ujaribu bahati yako leo.

Mkoa wa Ruvuma umeendelea kujizolea umaarufu katika sekta ya madini baada ya makaa ya mawe yanayochimbwa katika wilaya za Mbinga, Songea na Nyasa kufungua masoko katika nchi mbalimbali za Afrika na Asia, huku zaidi ya tani milioni 3.6 zikizalishwa mwaka 2024/2025 na kuchochea ajira, biashara na matumizi ya nishati safi.

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi amesema shughuli za utafiti, uchimbaji na uchakataji wa makaa ya mawe zinazofanywa na makampuni pamoja na wadau mbalimbali zimekuwa na mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Amesema makaa hayo yenye ubora wa hali ya juu yanatumika katika viwanda vya saruji, usafishaji wa vyuma na shughuli nyingine za viwandani, huku sehemu ya uzalishaji ikipelekwa katika masoko ya Kenya, Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

“Migodi ya makaa ya mawe ya Ruvuma imeendelea kuvutia wawekezaji kutokana na ubora wa madini hayo, hali iliyosaidia kufungua masoko mapya katika baadhi ya nchi za Asia na Ulaya,” amesema Mhandisi Bikulamchi.

Ameeleza kuwa ukuaji wa sekta hiyo umechangiwa na kuongezeka kwa uwekezaji pamoja na mahitaji ya nishati duniani tangu mwaka 2019/2020, jambo lililoongeza mchango wa sekta ya madini katika mapato ya Serikali na maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma.

Katika hatua nyingine, wadau wa makaa ya mawe mkoani humo wameendelea kuunga mkono agenda ya matumizi ya nishati safi kupitia uzalishaji wa mkaa mbadala unaotokana na makaa ya mawe, wakiwemo Mgodi wa Jitegemee uliopo Wilaya ya Mbinga na Kampuni ya Suzlon ya Wilaya ya Songea.

Migodi hiyo imeendelea kuzalisha mkaa wa nishati safi unaotajwa kusaidia kupunguza matumizi ya mkaa wa kawaida unaotokana na ukataji miti, hatua inayochangia uhifadhi wa mazingira na kupunguza uharibifu wa misitu.

Msimamizi wa Mauzo na Uendeshaji wa Mgodi wa Jitegemee, Mark Tarimo amesema kampuni hiyo imetoa zaidi ya ajira 500 kupitia nafasi za kudumu na mikataba ya mwaka mmoja, huku bidhaa zake zikisafirishwa katika nchi za Afrika Mashariki na Falme za Kiarabu (UAE).

Tarimo amesema kampuni hiyo pia imetekeleza miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo ujenzi wa shule katika Kijiji cha Ruanda, zahanati katika Kijiji cha Luhagara pamoja na usambazaji wa majiko ya nishati safi kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Mgodi wa Suzlon, Jigar Chandarana amesema mkaa wa nishati safi unaozalishwa na kampuni hiyo ni mbadala wa mkaa wa kawaida kwa kuwa hudumu kwa muda mrefu, ni nafuu kwa matumizi ya nyumbani na husaidia kulinda mazingira dhidi ya uharibifu wa misitu.

Aidha, Mhandisi Bikulamchi amewataka wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa zilizopo katika sekta ya madini mkoani Ruvuma, huku akiwahimiza vijana kushiriki katika shughuli za uchimbaji, usafirishaji na utoaji wa huduma zinazohusiana na sekta hiyo.










Top News