Na Mwandishi wa OMH

Dar es Salaam. Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa Kati wa Benki ya NMB wa mwaka 2026 hadi 2030 (Agenda 2030).

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo unaolenga kuboresha utendaji kazi wa benki hiyo, Bw. Mchechu aliupongeza uongozi wa NMB na Bodi ya Wakurugenzi kwa kuifanya benki hiyo kuwa miongoni mwa benki bora zinazochangia kwa kasi ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano, Serikali, inayomiliki asilimia 31.8 ya hisa za NMB, imepata Sh670 bilioni kutokana na uwekezaji wake katika benki hiyo, ambapo kati ya kiasi hicho, Sh224 bilioni ni gawio.

Sanjari na hilo, aliipongeza Benki ya NMB kwa kuoanisha vipaumbele vyake na maono ya Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, hususan katika maeneo ya afya, elimu, ujasiriamali na mazingira.

Katika kusisitiza umuhimu wa mwelekeo huo wa maendeleo, Bw. Mchechu alisema anatamani kuona taasisi zote nchini, ikiwemo za sekta binafsi, zikioanisha mikakati yao na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Alitaja Benki ya NMB kuwa mfano wa taasisi inayotekeleza mwelekeo huo kupitia utendaji wake wa kifedha na usimamizi makini wa mikopo.

“Benki ambayo imekuwa ikitoa wastani wa mikopo ya Sh5.6 trilioni kwa mwaka halafu inakuwa na wastani wa mikopo chechefu wa asilimia 2.5 ni kitu cha ajabu sana, hongereni sana NMB,” alisema.

Aidha, aliwataka wateja na wawekezaji kuendelea kuiamini na kupata huduma kutoka Benki ya NMB, akisisitiza kuwa ni sehemu salama kwa kuwekeza fedha zao.






-Rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri ipo Tayari : Dkt. Kiruswa

Na Wizara ya Madini, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Madini inaendelea na mchakato wa kuanzisha Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania (Tanzania Geoscientists Registration Board – TGRB), ambapo kwa sasa ipo katika hatua ya kukusanya maoni na mapendekezo ya wadau kabla ya kuanzishwa rasmi kwa bodi hiyo.

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amesema hayo leo Januari 28, 2026, Bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukene, Mhe. Stephano Luhende, aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanzisha bodi hiyo ili kuongeza ufanisi katika sekta ya madini nchini.

Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa baadhi ya taratibu tayari zimekwisha tekelezwa, ikiwemo uandaaji wa rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri kuhusu kuanzishwa kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.

Amefafanua kuwa kwa sasa Wizara ya Madini inaendelea na zoezi la kukusanya na kuchambua maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu masuala yatakayowezesha bodi hiyo kuanzishwa na kujiendesha kwa ufanisi, ikiwemo masuala ya uendeshaji na vyanzo vya fedha.

Ameongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukusanyaji na uchambuzi wa maoni, Wizara itawasilisha waraka huo katika ngazi za maamuzi za Serikali, ambazo ni kikao cha kitaalamu cha Makatibu Wakuu na kikao cha Baraza la Mawaziri, kwa ajili ya kujadiliwa na kupata ridhaa ya kuanzishwa rasmi kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania.



Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro imepokea tuzo ya uongozi bora wa kukuza na kuwezesha mazingira bora ya Biashara, baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika tathmini ya mazingira ya biashara iliyofanyika mkoani humo.

Tuzo hiyo, inayojulikana kama Kilimanjaro Award for Pro-Business Environment, imetolewa wakati wa kikao cha Baraza la Biashara la mkoa wa Kilimanjaro lililofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Moshi, kilichowakutanisha viongozi wa serikali, wafanyabiashara pamoja na wadau mbalimbali wa sekta binafsi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, alisema kuwa serikali itaendelea kuweka na kuboresha mazingira rafiki ya biashara ili kuwawezesha wafanyabiashara kuendesha shughuli zao kwa uhuru na ufanisi, kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo.

Babu alisisitiza kuwa mamlaka za ukusanyaji wa mapato, ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na halmashauri, hazipaswi kufunga biashara za wafanyabiashara pale wanapokuwa na madeni, bali zinapaswa kufanya mazungumzo na kufikia makubaliano ya namna bora ya ulipaji wa madeni hayo.

Alieleza kuwa hatua hiyo itawawezesha wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao huku wakitekeleza wajibu wao wa kulipa madeni kwa utaratibu uliokubaliwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, ameishukuru serikali ya mkoa kwa kutambua juhudi zinazofanywa na wilaya hiyo katika kuboresha mazingira ya biashara.

Amesema kuwa tuzo hiyo ni chachu ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kudumisha na kuimarisha mazingira rafiki kwa wafanyabiashara.




OFISA Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana(CMSA) CPA.Nicodemus Mkama amesema Mfuko wa Utekelezaji wa Pamoja wa Kampuni ya iTRUST Finance Limited uitwao  iTrust EAC Large Cap ETF unakuwa mfuko wa kwanza wenye uwekezaji wa Kikanda unaowekeza kwenye kampuni zenye mitaji mikubwa na zenye utendaji mzuri zaidi kuorodheshwa kwenye Soko la Hisa nchini Tanzania.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuorodheshwa kwa Mfuko wa iTRUST EAC LARGE CAP ETF, katika Soko la Hisa la Dar es Salaam leo Januari 28,2026 CPA.Mkama amesema Mfuko wa iTrust EAC Large Cap ETF ni mfuko unaowekeza katika hisa za kampuni zilizoorodheshwa katika masoko ya hisa ya nchi za Afrika Mashariki, ambazo zina mitaji mikubwa na zenye utendaji mzuri zaidi.

"Nawapongeza Bodi na Menejimenti ya iTrust Finance Limited kwa kuwezesha kuweka alama hii kubwa kwenye historia ya Masoko ya Mitaji  katika ukanda wa Afrika Mashariki."

Amesema pia Mfuko huu unaendeshwa na kampuni ya iTrust Finance Limited ambaye ni Meneja wa Mfuko (Fund Manager) na Benki ya NBC (NBC Bank Limited) ambaye ni Mtunza Dhamana wa Mfuko (Custodian); na umeidhinishwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

Amefafanua CMSA ina jukumu la kuendeleza na kusimamia masoko ya mitaji hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa shughuli katika masoko ya mitaji zinafanyika kwa kufuata sheria, taratibu na miongozo ili kuleta uwazi na haki kwa washiriki wote.

 "Katika kutekeleza jukumu la kuendeleza na kusimamia masoko ya mitaji hapa nchini, CMSA huidhinisha uanzishwaji wa bidhaa mpya katika masoko ya mitaji, ikiwa ni pamoja na Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja, ambapo katika kutekeleza jukumu hili, Mfuko wa iTrust EAC Large Cap ETF umepata idhini ya CMSA baada ya kukidhi matakwa ya sheria, taratibu na miongozo. 

"Mauzo ya vipande vya mfuko wa iTrust EAC Large Cap ETF yamepata mafanikio ya asilimia 540, ambapo kiasi cha Sh. billioni 54.03 kimepatikana, ikilinganishwa na lengo la Sh. bilioni 10,"amesema.

Aidha, asilimia 99.44 ya wawekezaji ni wawekezaji mmoja mmoja yaani Retail Investors na asilimia 0.56 ni wawekezaji ambao Kampuni na Taasisi yaani Institutional investors.Pia amesema asilimia 99.75 ya wawekezaji ni wawekezaji wa ndani na asilimia 0.25 ni wawekezaji wa kigeni.

CPA.Mkama amesema mafanikio hayo  yametokana na imani waliyoyano wawekezaji wa ndani na kimataifa kwenye masoko ya mitaji Tanzania na utendaji mzuri wa Kampuni ya iTrust Finance Limited.

Pia ni uthibitisho wa mazingira wezeshi ya kisera, kisheria na kiutendaji yanayotolewa na Serikali kupitia Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA). Mazingira yaliyowezesha matokeo mazuri ya kihistoria ya Mfuko wa iTrust EAC Large Cap ETF ni pamoja na:

Pamoja na hayo amesema uwekezaji wa Mfuko huo unajumuisha hisa za kampuni za CRDB Bank PLC, NMB Bank PLC, Tanzania Portland Cement Company (Twiga Cement), Tanga Cement PLC.

Nyingine ni Tanzania Cigarette Company Ltd (TCC), Vodacom Tanzania PLC, Safaricom PLC, Equity Group Holdings PLC, KCB Group PLC, British American Tobacco (BAT) Kenya, MTN Uganda Ltd, Stanbic Bank Uganda na Benk ya Kigali. Hatua hii imekuwa kivutio kikubwa kwa wawekezaji, kwani utendaji wa hisa hizi una ukwasi na ongezeko la thamani katika masoko husika.





Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi  Francis Kasambala akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti ngazi ya Jamii leo Januari 28,2026 huko Bahi Mkoani Dodoma, mwenye T-shirt nyeusi ni Mku wa Idara ya Mafunzo wa INADES-Formation Tanzania Michael Kihwele. Katika kampeni hiyo, jumla ya miti 2000 kati ya 6000 imepandwa ambapo jumla ya miche 20,000 inatarajiwa kupandwa katika vijiji mbalimbali vya wilaya hiyo.





Na Mwandishi Wetu Michuzi TV, Dodoma.
KATIKA kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za utunzaji wa mazingira na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, wananchi wa Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wamezindua kampeni ya upandaji miti ngazi ya jamii, ambapo jumla ya miche 20,000 inatarajiwa kupandwa katika vijiji mbalimbali vya wilaya hiyo.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika leo Januari 28, 2029 katika Shule ya Sekondari Mchingu iliyopo Bahi, ambapo wananchi kutoka vijiji vya Mndemu, Kisima cha Ndege, Chilungilu na Mkondai kwa pamoja walipanda miche 2,000 kati ya jumla ya miti 6,000 inayotarajiwa kupandwa katika awamu ya kwanza ya kampeni hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Francis Kasambala, aliyemwakilisha Mgeni Rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi na kuchukua hatua za vitendo katika uhifadhi wa mazingira.

Alisema kampeni hiyo ni kielelezo cha mshikamano wa jamii katika kulinda rasilimali za asili na kuongeza ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi.

Kasambala alisisitiza kuwa upandaji miti si tukio la siku moja, bali ni mchakato unaohitaji uangalizi na uwajibikaji wa pamoja ili kuhakikisha miche yote inakua na kuleta tija kwa jamii, ikiwemo kuboresha rutuba ya udongo, kuhifadhi vyanzo vya maji na kuimarisha usalama wa chakula.

Akizungumza kwa niaba ya Shirika la INADES-Formation Tanzania, Mkuu wa Idara ya Mafunzo, Michael Kihwele, aliyemwakilisha Mkurugenzi wa shirika hilo, Jacqueline Nicodemus, alisema kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa miaka mitatu unaofadhiliwa na shirika la Bread for the World.

Mradi huo unalenga kuwawezesha wanajamii wa vijijini katika Halmashauri za Bahi, Chemba na Kondoa kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Aliongeza kuwa kupitia kampeni hiyo, jamii itaendelea kupata elimu ya mazingira, mafunzo ya vitendo na ushirikiano wa karibu na Serikali za Mitaa pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), huku shughuli za upandaji na ufuatiliaji wa miti zikiendelea hadi msimu wa mvua utakapokamilika.

Kampeni hiyo inaendeshwa chini ya kaulimbiu isemayo “Panda Mti, Tuilinde Kesho”, ikilenga kuhamasisha jamii kuchukua jukumu la kulinda mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.


Na Saidi Lufune, Dodoma
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb.), amesema kuwa Serikali inatarajia kulipa Shilingi Milioni 524.1 kwa wananchi 1,603 wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Mkoani Mara kwa ajili ya malipo ya kifuta jasho na machozi kufuatia athari zinazotokana na wanyamapori wakali na waharibifu.

Mhe. Chande amebainisha hayo Bungeni jijini Dodoma akijibu swali la Mhe. Boniphace Mwita Getere (Mb), aliyetaka kufahamu, ni lini wananchi walioharibiwa mazao yao na tembo katika vijiji 9 vya Jimbo la Bunda vijijini watalipwa kifuta jasho.

“Kwa sasa Wizara inakamilisha taratibu za malipo hayo ili wananchi husika walipwe stahiki yao kwa mujibu wa Kanuni kupitia mfumo wa kieletroniki wa Problem Animal Information System (PAIS). Sambamba na mfumo huu mpya, kwa sasa Serikali itaendelea kulipa wananchi ambao hawana akaunti namba za benki au namba za simu kwa kutumia utaratibu wa awali ambapo wataalam hufika uwandani kufanya malipo hayo.” Alisema Mhe. Chande

Awali Mhe. Chande alieleza kuwa, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Wizara ililipa kifuta jasho na machozi jumla ya Shilingi 312,360,000/= kwa wananchi 1,115 wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.




Na Mwandishi Wetu Michuzi TV, Dodoma.

KATIKA kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za utunzaji wa mazingira na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, wananchi wa Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wamezindua kampeni ya upandaji miti ngazi ya jamii, ambapo jumla ya miche 20,000 inatarajiwa kupandwa katika vijiji mbalimbali vya wilaya hiyo.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika leo Januari 28, 2029 katika Shule ya Sekondari Mchingu iliyopo Bahi, ambapo wananchi kutoka vijiji vya Mndemu, Kisima cha Ndege, Chilungilu na Mkondai kwa pamoja walipanda miche 2,000 kati ya jumla ya miti 6,000 inayotarajiwa kupandwa katika awamu ya kwanza ya kampeni hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Francis Kasambala, aliyemwakilisha Mgeni Rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi na kuchukua hatua za vitendo katika uhifadhi wa mazingira.

Alisema kampeni hiyo ni kielelezo cha mshikamano wa jamii katika kulinda rasilimali za asili na kuongeza ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi.

Kasambala alisisitiza kuwa upandaji miti si tukio la siku moja, bali ni mchakato unaohitaji uangalizi na uwajibikaji wa pamoja ili kuhakikisha miche yote inakua na kuleta tija kwa jamii, ikiwemo kuboresha rutuba ya udongo, kuhifadhi vyanzo vya maji na kuimarisha usalama wa chakula.

Akizungumza kwa niaba ya Shirika la INADES-Formation Tanzania, Mkuu wa Idara ya Mafunzo, Michael Kihwele, aliyemwakilisha Mkurugenzi wa shirika hilo, Jacqueline Nicodemus, alisema kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa miaka mitatu unaofadhiliwa na shirika la Bread for the World.

Mradi huo unalenga kuwawezesha wanajamii wa vijijini katika Halmashauri za Bahi, Chemba na Kondoa kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Aliongeza kuwa kupitia kampeni hiyo, jamii itaendelea kupata elimu ya mazingira, mafunzo ya vitendo na ushirikiano wa karibu na Serikali za Mitaa pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), huku shughuli za upandaji na ufuatiliaji wa miti zikiendelea hadi msimu wa mvua utakapokamilika.

Kampeni hiyo inaendeshwa chini ya kaulimbiu isemayo “Panda Mti, Tuilinde Kesho”, ikilenga kuhamasisha jamii kuchukua jukumu la kulinda mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi  Francis Kasambala akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti ngazi ya Jamii leo Januari 28,2026 huko Bahi Mkoani Dodoma, mwenye T-shirt nyeusi ni Mku wa Idara ya Mafunzo wa INADES-Formation Tanzania Michael Kihwele. Katika kampeni hiyo, jumla ya miti 2000 kati ya 6000 imepandwa ambapo jumla ya miche 20,000 inatarajiwa kupandwa katika vijiji mbalimbali vya wilaya hiyo.




Tanzania na Oman zimeendelea kuonyesha dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira ili kuongeza ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kukuza uchumi wa mataifa yote mawili.

Hayo yamebainishwa wakati wa kikao cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu na Waziri wa Kazi wa Oman, Dkt. Mahad bin Said bin Ali Baawain walipokutana katika Mkutano wa Mawaziri wa Kazi Duniani (Global Labour Market Conference) uliofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Aidha, katika kikao hicho Waziri Sangu alielezea umuhimu wa kukamilishwa na kutiwa saini kwa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano wa masuala ya Kazi na Ajira (MoU) kati ya nchi hizo mbili, ili kuweka mfumo rasmi na endelevu wa usimamizi wa masuala ya ajira, ulinzi wa haki za wafanyakazi na utatuzi wa changamoto za kiutendaji zinazojitokeza.

Vilevile, Waziri Sangu ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa fursa za ajira kwa Watanzania katika sekta mbalimbali. Pia, amesema idadi ya Watanzania wanaofanya kazi nchini Oman imeendelea kuongezeka , jambo linaloonesha kuimarika kwa mahusiano ya ajira kati ya mataifa hayo mawili.

Kwa upande mwingine, nchi hizo zimekubaliana kuendeleza ushirikiano kwa kuendelea kupanua wigo wa ajira zenye staha, kulinda haki za wafanyakazi na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kijamii kati ya mataifa yetu mawili.








Na Said Mwishehe,Michuzi Blog

KAMPUNI ya Dorkin Organic Farming Co. Ltd ambayo imekuwa ikijihusika na tiba lishe kwa kutumia vyakula asili imezindua rasmi mgahawa wa chakula asili katika eneo la Gongolamboto wilayani Ilala Jijini Dar es Salaam.

Katika mgawa huo kutakuwa kunauzwa juisi,supu, ugali unaotokana na mahindi ya asili ambayo mbegu zake zimekuwepo tangu mwaka 1570 pamoja na uji wa maajabu unatokana na ndizi kitarasa na katika uji huo kuna faida mbalimbali ikiwemo ya madini muhimu yanayohitajika mwilini.

Pamoja na hayo imeelezwa uzinduzi wa mgahawa huo ni wa matumaini mapya ya afya, uchumi wa kilimo hai, na heshima ya Taifa la Tanzania katika sayansi ya chakula uponyaji.

Akizungumza leo Januari 28,2026 wakati wa uzinduzi wa Mgahawa huo wa chakula asili ,Mgeni rasmi ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Amana jijini Dar es Salaam Dk.Brayson Haule amesema kuna umuhimu mkubwa kwa wananchi kula vyakula vya asili ili kuhakikisha wanakuwa na afya bora.

“Tunatoa rai wananchi wale vyakula vya asili ambavyo havina gharama kubwa na vinapatikana kwa urahisi hata kwa kulima wenyewe.Vyakula vya asili vinachangia kwa kiasi kikubwa pia ongezeko la damu mwilini kwani hivi sasa kumekuwa na changamoto kubwa ya upungufu wa damu kwa akina mama wajawazito,watoto na wazee .

Katika uzinduzi wa mgahawa huo wa vyakula vya asili,Dk.Haule amempongeza Profesa Dorcas Kibona kupitia kampuni yake ya Dorkin Organic Farming Co. Ltd kwa kuanzisha mgahawa wa vyakula vya asili katika eneo la Gongolamboto.

Aidha amesema Serikali inatambua umuhimu wa tiba asili na kwa sasa imeshaweka milango wazi kati ya sekta ya afya na tiba asili huku akitoa mfano kuna hospitali tano zimeteuliwa kuwa na vyakula na dawa asili na miongoni mwa hospitali hizo ni hospitali ya Temeke ambako kuna duka maalum kwa ajili ya vyakula na dawa asili ambazo zimethibishwa.

“Na kwa sasa Serikali inahamasisha matokeo na matumizi ya tafiti ambazo zimefanyika nchini, hivyo tunampongeza Profesa Dorcas kwa kuwa mfano wa kuigwa na maprofesa wengine kwani ameweza kufanya tafiti katika mazingira yetu na akaiweka vitendo.”

Kwa upande wake Profesa Dorcas Kibona ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Dorkin Organic Farming Co. Ltd inayojihusisha na utafiti wa vyakula vya asili vyenye uwezo wa kuponya na kuimarisha afya ya binadamu ametoa rai kwa Wizara ya Afya kuona haja ya kuendelea kutenga maeneo katika hospitali za umma kuwa na maeneo ambayo vyakula asili vitapatikana.

Aidha amesema “Tuko hapa kwa ajili ya afya na naomba nirudi nyuma kidogo kwenye kitabu cha Biblia tena Mwanzo Moja katika mstari wa 1-12 kuna mambo matano nataka nikupitishe pale kwanini ninafanya haya,cha kwanza nimeangalia aridhi , udongo,maji ,mbegu na mwisho nikaangalia afya

“Mungu wakati anaumba Dunia alimuumba mwanadamu lakini mwanadamu aliumbwa siku ya sita ya uumbaji .Vitu vyote viliumbwa mwanzo kabisa,Adam aliumbwa siku ya sita lakini baada ya kuumbwa alipewa bustani ambapo agizo alililopewa na Mungu ailinde na kuitunza na baada ya kuitunza atakutana na kila kitu kinachogitajiwa katika maisha yake

“Sasa sisi leo tumeikuta dunia imechupushwa katika njia yake katika eneo la kulima,kutunza. Lakini Dorkin Organic kwa kuangalia hilo tukachagua mambo matano.Kwanini magonjwa yamekuwa mengi,kwanini watu wanakufa kwa umri mdogo,nikajua shida ni afya na afya haitoki mbali inatoka kwenye aridhi

“Aridhi lazima iwe na udongo lakini tumeikuta haina rotuba kwani udongo umechoka sana, kuna kemikamili za viwandani zinachosha udongo na asili ya udongo kuna madini ya chokaa na yameshachukuliwa yote na dawa za viwandani.

“Dorkin Organic kwa kutambua tukafanya utafiti tukaona shida sio chakula kiwandani,shida sio chakula kwenye hotel,shida sio chakula kwa mama anayepika.Shida ni kule shambani tukajidhatiti vizuri tukaanza shambani

“Nimekuwa mtanzania wa kwanza kupima chakula cha kiasili katika maabara ya India nikiongozwa na Serikali yangu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Nadharia inasema homoni ya Iswilini inapatikana kwa wanyama peke yake ambao ni Kima na Nguruwe sasa mimi nakuja na homoni ya Iswilini kutoka kwenye tunda la ndizi kitarasa.”

Hata hivyo ameeema kuzinduliwa kwa mgahawa wa vyakula asilia ni muendelezo wa kuhakikisha jamii ya Watanzania inapata vyakula ambavyo vitawaepusha na magonjwa na mgahawa huo utakuwa wazi muda wote ili watu wapate uji wa maajabu, juisi ya maajaabu na supu ya maajabu inayotokana na vyakula vya asili.




















Top News