Na Mwandishi Wetu, Manyara.

MKUU wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amepinga takwimu zinazoonesha kuwa upatikanaji wa huduma za dawa mkoani humo umefikia asilimia 93, akisema kuwa takwimu hizo haziakisi uhalisia wa hali iliyopo kutokana na wingi wa malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu ukosefu wa dawa na huduma muhimu za afya.

Sendiga ametoa kauli hiyo wakati wa kikao cha kuanza utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote (BAW) ngazi ya mkoa wa Manyara, kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kikihusisha wadau wa afya wakiwemo Mganga Mkuu wa Mkoa, waganga wakuu wa wilaya pamoja na kamati za afya za halmashauri.

Amesisitiza kuwa utekelezaji wa bima ya afya kwa wote hauwezi kufanikiwa endapo wananchi wataendelea kukumbana na kero za ukosefu wa dawa, vipimo na huduma nyingine muhimu katika vituo vya afya na hospitali. “Huduma bora za afya lazima ziende sambamba na bima ya afya kwa wote. Wananchi hawapaswi kulalamika,” amesema RC Sendiga.

Katika kuhakikisha mpango huo unafanikiwa, Mkuu huyo wa Mkoa amezielekeza halmashauri zote za Manyara kuhakikisha zinafikisha elimu ya Bima ya Afya kwa Wote hadi ngazi ya kaya, kwa kuwafikia wananchi wa makundi yote wakiwemo vijana wa bodaboda, bajaji, wazee na kaya masikini, ili waweze kuelewa faida na umuhimu wa kujiunga na bima hiyo.

Aidha, amewataka waganga wafawidhi chini ya usimamizi wa Mganga Mkuu wa Mkoa na waganga wakuu wa wilaya kuhakikisha huduma zote muhimu, ikiwemo dawa na vipimo, zinapatikana kwa wakati katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya, ili kuondoa malalamiko na kurejesha imani ya wananchi.

Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ulianza rasmi Januari 26, 2026, ukiwa na lengo la kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma za afya kwa uhakika, nafuu na kwa usawa, hatua ambayo Mkoa wa Manyara umeanza kuitekeleza kikamilifu kwa kuhamasisha wananchi na kusimamia ubora wa huduma za afya.

TANZANIA and Norway have reaffirmed their partnership in the agricultural sector, with a renewed focus on smart farming technologies aimed at boosting productivity and improving the livelihoods of small-scale farmers.

During a courtesy meeting on 29th January 2026 in Dodoma, Hon. Daniel Chongolo (MP) met with H.E. Tone Tinnes, Ambassador of Norway to Tanzania, to discuss new strategies for agricultural cooperation. Minister Chongolo highlighted the importance of zoning farmland to meet specific agricultural needs, noting that modern technology could help maximize yields while conserving land.

“With advanced farming methods, 200 acres can produce what 1,000 acres would under traditional practices. This allows us to intensify productivity while preserving the environment,” said Hon. Chongolo.

Ambassador Tinnes praised Tanzania’s leadership in agriculture, describing the country as a “food basket of the region.” She also reaffirmed Norway’s commitment to supporting Tanzania’s growth, citing ongoing collaborations with institutions such as the Sokoine University of Agriculture (SUA); Private Agricultural Sector Support (PASS); Tanzania Agricultural Research Institute (TARI); and the Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT/AGCOT).

On his part, Minister Chongolo welcomed Norway’s continued involvement, particularly in irrigation projects that enable farmers to cultivate three seasons annually. He also invited Norway to extend its support to the Mwalimu Julius K. Nyerere University of Agriculture and Technology (MJNUAT) in Mara Region, mirroring the assistance provided to SUA.

In essence, both sides emphasized that smart agriculture is not only about increasing profits but also about adding value, protecting the environment, and ensuring long-term sustainability for Tanzania’s farming endeavors.












NAIBU Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) amefanya kikao na wawakilishi kutoka Chama cha Wamiliki wa Viwanda Vidogo na Wazalishaji Wadogo Tanzania (TASSIM)  chenye makao makuu jijini Dar es Salaam, kujadili fursa za uwekezaji na kuboresha ushirikiano katika tasnia ya mbolea, mbegu pamoja na viuatilifu nchini.

Kikao kimefanyika tarehe 29 Januari 2026 katika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Mtumba jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa TASSIM, Bw. ELIA Joseph; Mhasibu wa TASSIM, Bw. Twaha Kitongo; Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao wa Wizara ya Kilimo, Bi. Yasinta Nzogela; pamoja na wawakilishi kutoka Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA); na Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC).

Pamoja na mambo mengine, Mhe. Silinde amewaeleza Wadau hao kuwa Wizara ya Kilimo itaendelea kushirikiana na wawekezaji katika masuala ya uzalishaji kwa kuwa mahitaji ya mbegu pamoja na mbolea yanazidi kuongezeka siku hadi siku kutokana na matumizi ya wakulima, hali inayofanya suala la uwekezaji kutokwepeka.  

Fursa mbali zilizopo katika uwekezaji ni pamoja na fursa katika uzalishaji wa ngano na mafuta ya kupikia ambazo zitaiwezesha Sekta ya Kilimo kufikia azma ya Serikali ya kukidhi mahitaji yaliyopo kupitia uzalishaji wa ndani.









Na Mwandishi wetu, Morogoro.

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imezindua mradi wezeshi wa “Ramani Zetu, Sauti Zetu”, unaolenga kuwajengea uwezo Wananchi wa Mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Pwani katika kukabiliana na Majanga.

Akizungumza katika Uzinduzi huo uliofanyika leo tarehe 29 Januari, 2026 Mkoani Morogoro Mkurugenzi Msaidizi wa Operesheni na Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Kanali Selestine Masalamado amesema, mradi huo umekuja wakati mufaka ambao jitihada kubwa zikiwa zinaendelea za kuzuia majanga ya asili maeneo mbalimbali ya nchi.

Aidha, ameeleza kuwa “tunahitaji uwepo wa data sahihi za wakati bila kusahau ushirikishwaji wa moja kwa moja wa jamii katika kuendelea kukabiliana na majanga ya asili na athari zake”.

“Mpango huu unaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kujenga Taifa lenye jamii imara yenye uwezo wa kutumia maarifa ya teknolojia katika kufanya maamuzi ya maendeleo” ameongeza Kanali Masalamado.

Naye, Mkurugenzi wa Taasisi ya OpenMap Development Tanzania (OMDTZ) Bw. Innocent Maholi, amesema Mradi huo unalenga kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema, ikiwa ni pamoja maandalizi na usimamizi wa maafa kwa kutumia teknolojia na ushiriki wa wananchi katika ukusanyaji wa taarifa muhimu za maeneo yao.

“Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi na hatua za usimamizi madhubuti wa maafa ambazo sehemu muhimu ya safari ya kuelekea maendeleo endelevu na uchumi imara wa wananchi,” amebainisha.









Viongozi kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) wakitembelea shule ya msingi Savannah iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga
Meneja wa Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani kutoka TISEZA, Felix John akizungumza baada ya kutembelea uwekezaji katika sekta ya elimu Shule ya Msingi na Sekondari Savannah Manispaa ya Shinyanga.

Na Mwandishi wetu _ Malunde 1 blog

Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imeendelea kuimarisha mkakati wa kuhamasisha uwekezaji wa ndani kwa kufanya ziara ya kikazi mkoani Shinyanga, ikisisitiza umuhimu wa miundombinu bora kama kichocheo kikuu cha kuvutia na kulinda uwekezaji.

Akizungumza leo Januari 29 2026 baada ya ukaguzi wa mradi wa uwekezaji katika sekta ya elimu uliofanyika katika Shule ya Msingi na Sekondari Savanah, Meneja wa Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani kutoka TISEZA, Felix John, amesema serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara ili kupunguza gharama na hatari kwa wawekezaji.

“Serikali inaweka mazingira rafiki kwa mwekezaji kwa kuimarisha miundombinu muhimu kama maji, umeme, barabara na mawasiliano katika maeneo yote yaliyotengwa kwa uwekezaji,” amesema John.

Ameeleza kuwa uwepo wa miundombinu hiyo huongeza tija ya miradi, kupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza ushindani wa Tanzania kama kitovu cha uwekezaji wa kikanda.



Uwekezaji wa Elimu Watajwa Kuwa Mfano wa Thamani ya Ndani

Katika ziara hiyo, TISEZA imekagua uwekezaji mkubwa wa sekta binafsi katika Shule ya Savannah, unaotajwa kuwa mfano wa uwekezaji wa kijamii wenye mchango wa moja kwa moja kiuchumi na kijamii katika mkoa huo.

Mkuu wa shule hiyo, Wema Kanyika, amesema taasisi hiyo inahudumia jumla ya wanafunzi 936 kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha sita.

“Tuna wanafunzi 512 wa elimu ya awali na msingi, pamoja na wanafunzi 424 wa sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Shule ina wafanyakazi 50 wanaoishi ndani ya eneo la shule,” amesema Kanyika.

Ameongeza kuwa uwekezaji huo unafanyika katika eneo la hekta 80, likiwa na miundombinu jumuishi ikiwemo Ufugaji wa ng’ombe kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa na nyama kwa matumizi ya shule, Visima vya maji kwa uhakika wa upatikanaji wa maji na Bustani za miti ya matunda kwa lishe na mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi.

Muundo huo unaonyesha mwelekeo wa uwekezaji unaojitegemea kwa sehemu katika mahitaji ya chakula na huduma muhimu, hali inayopunguza gharama za uendeshaji kwa muda mrefu.

Shinyanga Yajipanga Kuwa Kitovu cha Uwekezaji

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, amesema mkoa huo umejipanga kimkakati kupokea uwekezaji mkubwa zaidi kupitia maeneo maalum yaliyotengwa rasmi.



“Katika mkoa wa Shinyanga kuna maeneo mawili makubwa ya uwekezaji ambayo ni Buzwagi na Nyanshimbi. Maeneo haya yanaendelea kuboreshwa miundombinu ili kuhakikisha hakuna kikwazo kwa mwekezaji,” amesema Mhita.

Ameongeza kuwa uwepo wa bandari kavu (dry port) mkoani humo unatarajiwa kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo, kupunguza gharama za usafirishaji na kuifanya Shinyanga kuwa lango muhimu la biashara kwa ukanda wa Ziwa na nchi jirani.

Mtazamo wa Kiuchumi

Hatua za TISEZA kuunganisha uhamasishaji wa uwekezaji na uboreshaji wa miundombinu zinaonekana kulenga: Kuvutia wawekezaji wa ndani kabla ya kutegemea zaidi mitaji ya nje, Kukuza ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja na Kuchochea maendeleo ya mnyororo wa thamani katika sekta kama elimu, kilimo, ujenzi na huduma.

Shinyanga inaibuka kama moja ya mikoa inayolengwa kimkakati katika ramani ya uwekezaji wa ndani, huku miundombinu, ardhi iliyotengwa na miradi ya kimkakati kama bandari kavu vikionekana kuwa vivutio vikuu kwa wawekezaji wapya.

Mkuu wa shule ya Savannah Wema Kanyika akieleza uwekezaji katika sekta ya elimu

























Top News