
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, leo Aprili 17, 2026 ameipokea Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyofanya ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu na taasisi mbalimbali za sekta ya afya Tanzania Bara.
Ziara hiyo imehusisha kutembelea Makao Makuu ya Wizara ya Afya, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na Bohari ya Dawa (MSD).
Akiongea mara baada yakuwapokea, Dkt. Samizi amesema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Amesema kuwa juhudi hizo zimejikita kuimarisha miundombinu ya afya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuboresha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi nchini.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Nasra Nassor, amesema ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wajumbe wa kamati kwani imewapa fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uendeshaji wa sekta ya afya.
Ameongeza kuwa maarifa waliyoyapata yatawasaidia kuboresha utoaji wa huduma za afya Zanzibar kwa kuzingatia mifumo na mbinu walizojifunza kutoka Tanzania Bara.
Akizungumza na watumishi hao, Waziri alielekeza changamoto mbalimbali za kiutendaji zinazokabili shughuli za uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za taasisi zitatuliwe. Vilevile, ametoa maelekezo ya namna bora ya kushughulikia na kuzitatua changamoto hizo kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.
Kwenye kikao hicho Mhe. Dkt. Kijaji aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas na Mkurugenzi wa Wanyamapori Dkt. Alexander Lobora huku akipokelewa na mwenyeji wake Kamishna wa Uhifadhi TANAPA CPA Musa Nassoro Kuji.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameendelea kuwasisitiza Watanzania waendelee kudumisha amani nchini kwa sababu inawawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
“Tuwe makini na watu wanaohamasisha uvunjifu wa amani kwa kuwa wengine walipwa kwa vitendo hivyo. Kama wao wamechagua maisha hayo wasiiuze nchi yetu. “Lazima tulinde amani ya nchi yetu.”
Amesema wanufaika wa kwanza wa amani ni wale wanaoishi katika eneo husika, hivyo hawana budi kuendelea kulinda amani na umoja wa kitaifa ili waendeleze shughuli mbalimbali za maendeleo.
Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Aprili 17, 2026) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kona ya Mbauda akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.
Waziri Mkuu amesisitiza hayo mara baada ya kukagua barabara ya Kilombero-Mbauda-Kisongo na Mbauda Losinyai zinazojengwa kwa njia nne pamoja na kuwekewa taa.
Ujenzi wa barabara hizo zenye jumla ya urefu wa kilomita 13 ni miongoni mwa maandalizi ya Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Mataifa ya Afrika (AFCON), 2027 ambapo Tanzania ni mwenyeji.
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema kuwa ujenzi wa barabara hizo unakwenda kuwasaidia wananchi wa Arusha pamoja na Watanzania kwa ujumla.
Waziri Ulega amesema mbali na kurahisisha usafiri na usafirishaji wa watu na mizigo, barabara hizo zinakwenda kuondoa tatizo la mafuriko katika baadhi ya maeneo baada ya kujengwa mitaro mikubwa.
Pia, Waziri Ulega amesema kila baada ya kilomita moja ya barabara kutawekwa taa ambazo zitawawezesha wananchi wa maeneo hayo kuendelea na shughuli za kiuchumi usiku na mchana.
Amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha shilingi bilioni 27 ambapo kati yake bilioni 17 kwa ajili ya mkandarasi na bilioni 10 fidia kwa waliopisha mradi huo.
Naye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kutokana na miradi ya maendeleo ya wananchi inayotekelezwa katika jiji hilo.
Waziri Makonda ambaye ni mbunge wa Arusha Mjini ametaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa barabara za njia nne na uwekaji wa taa ambazo zinakwenda kurahisisha ufanyaji wa biashara.
Ajali hiyo ilitokea Aprili 16, 2026, ambapo basi lenye namba za usajili T 289 EAG lililokuwa likiendeshwa na mtuhumiwa huyo liliacha njia na kupinduka kutokana na mwendo wa hatari.
Basi hilo lilikuwa likitoka Ifakara kuelekea Dar es Salaam likiwa na jumla ya abiria 57.
Kutokana na ajali hiyo, abiria 13 walijeruhiwa na kupatiwa matibabu katika vituo vya afya vilivyo karibu.
Jeshi la Polisi limetoa wito kwa madereva wote kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuzuia ajali zinazoweza kuepukika.
Imeandaliwa na Farida Mangube.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewataka Watanzania kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini akisisitiza kuwa mazingira ya amani ndiyo msingi muhimu unaowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kukuza uchumi wa taifa.
Amesema ni muhimu kwa wananchi kuwa makini na watu wanaohamasisha uvunjifu wa amani, akibainisha kuwa baadhi yao hufanya hivyo kwa maslahi binafsi. Alionya kuwa watu hao wasiruhusiwe kuihatarisha nchi, akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kulinda amani iliyopo.
Dkt. Nchemba ameeleza kuwa wanufaika wakuu wa amani ni wananchi wenyewe, hivyo wanapaswa kuilinda kwa nguvu zote ili kuendeleza shughuli zao za kila siku, ikiwa ni pamoja na biashara, kilimo na uwekezaji unaochangia maendeleo ya jamii.
Ameyasema hayo leo Ijumaa, Aprili 17, 2026, alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kona ya Mbauda mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ambapo pia alikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara muhimu jijini humo.
Aidha, ameeleza kuwa ujenzi wa barabara za Kilombero–Mbauda–Kisongo na Mbauda–Losinyai zenye urefu wa kilomita 13 ni sehemu ya maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027, huku Serikali ikiendelea kuboresha miundombinu ili kurahisisha usafiri, kukuza biashara na kuhakikisha wananchi wananufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na miradi hiyo.
.jpeg)











.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)





















.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)