By Hamis Shimye
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameonyesha ni mwanasiasa wa kidemokrasia mwenye kufuata taratibu za demokrasia kwa dhamira yake ya muhimu ya kukutana na wagombea wa urais walioshiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 kutoka vyama vya upinzani Ikulu, jijini Dar es Salaam Machi 31, 2026.
Tukio hilo limefanyika katika mazingira ya ushirikiano na uwazi wa kisiasa, huku likilenga kuimarisha ushirikiano kati ya vyama vya siasa na utulivu wa taifa.
Katika mazungumzo hayo, wagombea wa upinzani walipewa fursa ya kuwasilisha maoni na hoja zao, na Rais Samia akajibu kwa uwazi, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, heshima kwa sheria, na haki za raia.
Hatua hii ni ishara kwamba demokrasia nchini Tanzania inaendelea kukua kwa misingi ya ustaarabu na maadili ya kisiasa. Pia, imetoa tafsiri pana kuwa uongozi unaojumuisha pande zote ni chachu ya imani ya wananchi katika mfumo wa kidemokrasia.
Aidha, hatua hii inaonyesha wazi juu ya uongozi wa kiuwajibikaji na heshima kwa jamii aliyokuwa nayo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwatumikia Watanzania kwa ufanisi na uweledi mkubwa.
Kikao cha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wa upinzani kimeonyesha mfano wa ushirikiano kwa wagombea wote katika mchakato wa kisiasa na kuthibitisha kwamba uongozi wake unajali usawa, haki, na ustaarabu wa kisiasa ambao ni asili ya Tanzania.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa mstari wa mbele katika kufuata taratibu za kidemokrasia kwa kushirikisha wadau wa kisiasa, ikiwemo upinzani. Ameonyesha uwajibikaji na ustaarabu katika maamuzi ya kisiasa.
Kwa maneno mengine, siasa kwake sio tu uongozi wa serikali, bali pia ni mtindo wa kuunganisha mshikamano, maendeleo, na amani ya kisiasa huku akisukumwa na falsafa zake nne ambazo ni Maridhiano, Ustahamilivu, Mageuzi, na Kujenga upya.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amejitambulisha kama mwanasiasa wa kidemokrasia, ambaye anaamini kwa dhati katika ujenzi na ustawi wa taifa bora kupitia maridhiano na mshikamano wa kitaifa.
Uongozi wake umeendelea kuongozwa na imani kwamba maendeleo endelevu yanapatikana kwa kushirikisha wadau wote wa kisiasa, ikiwemo vyama vya upinzani, na kwa kuzingatia uwajibikaji, uwazi, na ustaarabu katika maamuzi ya serikali.
Mtazamo huo wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan unathibitisha kwamba siasa za kidemokrasia haziishii tu katika taratibu za kisheria, bali ni mtindo wa kuunganisha wananchi, kuendeleza mshikamano wa kitaifa, na kufanikisha maendeleo ya taifa.
Rais Samia anaendelea kuonyesha mfano wa kiongozi anayejali maridhiano, ustawi wa taifa, na maendeleo ya kila mwananchi, akithibitisha kuwa siasa za kidemokrasia ni msingi wa amani na maendeleo endelevu.
Hii inatokana na mfumo wa siasa zake hazishughulishi tu uongozi wa serikali, bali ni mtindo wa kuunganisha mshikamano, maendeleo, na amani ya kisiasa yenye kuonyesha maridhiano ya kweli ndio chachu ya amani na maendeleo.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuwa kielelezo cha uongozi wa kidemokrasia, akionyesha kwa vitendo siasa zenye uwajibikaji, ushirikishwaji na ustaarabu zinaweza kuendesha taifa kwa amani na maendeleo endelevu.
Kikao cha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na viongozi wa upinzani kimeonyesha ushirikiano wa vyama vyote uliopo Tanzania na imeonyesha kwamba serikali haiji kwa nguvu pekee, bali inashirikisha upinzani katika maamuzi muhimu ya kitaifa.
Pia, kikao hicho kinakwenda kupunguza mvutano au mkwamo wa kisiasa na kimekuwa sehemu ya juhudi binafsi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuondosha migongano ya kisiasa na kuleta maridhiano, utulivu wa kisiasa.
Kikao hicho ni ishara ya uimarishaji wa imani ya wananchi na kuwapa heshima viongozi wa upinzani jambo linaloongeza kuaminiana kati ya serikali, wananchi na vyama vya upinzani.
Huu ni mwendelezo wa ustaarabu wa kisiasa nchini Tanzania. Tukio hili linatuma ujumbe kwamba mazungumzo na kuheshimiana ni sehemu ya utawala na asili ya utamaduni wa Taifa la Tanzania.
Kuonyesha mtazamo wa kidemokrasia ambao unatoa ishara kwamba viongozi wanaweza kushirikiana bila kuchukua upande au kuchukiana bila sababu za msingi kwa kuwa taifa lina usawa wa kisiasa.
Hivyo, tukio hili lina tafsiri ya ushirikiano wa kweli, uwazi, na siasa za kidemokrasia zilizojengwa na waasisi wetu akiwemo Hayati Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amaan Karume. Hongera viongozi na wagombea wa Urais kutoka vyama 16 vya siasa nchini vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma
Serikali imelenga kuimarisha uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma, sambamba na kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa, huduma na kazi za ujenzi unazingatia ubora unaotakiwa, kwa wakati na kwa thamani halisi ya fedha (Value for Money).
Hayo yameelezwa na Kaimu Kamishina wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma kutoka Wizara ya Fedha, Alex Haraba, wakati akitoa taarifa kwa umma kuelekea uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya mwaka 2025.
Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Aprili 8, 2026 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Akizungumzia umuhimu wa sera hiyo, Haraba amesema ni hatua ya kimkakati inayolenga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za umma pamoja na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za Serikali kupitia mnyororo wa ugavi.
Amefafanua kuwa sera hiyo inalenga kufungamanisha shughuli zote za mnyororo wa ugavi ili kuimarisha utaratibu na usimamizi jumuishi, kuboresha matumizi ya rasilimali za umma, na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali.
Kwa mujibu wa Haraba, kwa muda mrefu shughuli za mnyororo wa ugavi zimekuwa zikitekelezwa kupitia sheria, kanuni na mifumo mbalimbali bila kuwepo kwa mwongozo mmoja wa kisera unaounganisha hatua zote kwa mtazamo jumuishi.
Amesisitiza kuwa kutokana na sehemu kubwa ya matumizi ya Serikali kupita katika ununuzi wa umma, mnyororo wa ugavi ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha rasilimali za umma zinasimamiwa kwa uwazi, ufanisi na uwajibikaji, hali itakayochochea ukuaji wa uchumi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Aidha, sera hiyo inaweka mkazo katika kuimarisha utawala bora, matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa mnyororo wa ugavi, pamoja na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii. Hatua hii inalenga kupanua fursa za kiuchumi na ajira kwa Watanzania, pamoja na kuhamasisha matumizi ya rasilimali na malighafi za ndani ili kuongeza thamani katika uzalishaji wa bidhaa na huduma.
Haraba ameongeza kuwa sera hiyo imeandaliwa kuweka mfumo jumuishi wa kimkakati wa kusimamia shughuli zote za mnyororo wa ugavi katika sekta ya umma. Mfumo huo unahusisha hatua mbalimbali kuanzia upangaji wa mahitaji, ununuzi wa umma, ugomboaji na uondoshaji wa mizigo ya Serikali, upokeaji na ukaguzi wa bidhaa, uhifadhi, matumizi na usambazaji, hadi uondoshaji wa mali za umma.
Uzinduzi wa sera hiyo unatarajiwa kuwa chachu ya maboresho makubwa katika usimamizi wa rasilimali za umma na kuongeza tija katika utoaji wa huduma za Serikali.
.png)
OWM-TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM– TAMISEMI) anayeshughulikia masuala ya Afya, Mhe. Dkt. Jafari Seif, amesema kuwa hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya katika ngazi ya huduma za afya ya msingi nchini imeendelea kuimarika na kufikia kiwango cha kuridhisha ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Akizungumza Aprili 2, 2026 jijini Dar es Salaam, katika kikao kazi kilichoongozwa na Waziri wa Afya, Mhe.Mohamed Mchengerwa, pamoja na wadau wa sekta ya afya, katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD), Mhe. Dkt. Seif amesema kuwa tathmini ya mwaka 2026 inaonesha hali ya upatikanaji wa dawa imefikia asilimia 89 katika hospitali, asilimia 88 katika vituo vya afya, na asilimia 88 katika zahanati.
Ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2024/25, vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi vilikusanya takribani Shilingi Bilioni 108, huku makusanyo hayo yakitarajiwa kuongezeka hadi kufikia Shilingi Bilioni 192 katika mwaka 2025/26.
Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu wa wizara hiyo kushirikiana kwa karibu na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kuandaa na kusimamia miongozo, taratibu na miundo ya usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya. Lengo la hatua hiyo ni kuhakikisha kuwa wafamasia kote nchini wanakuwa sehemu muhimu ya timu za menejimenti katika vituo hivyo, ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya.
Na Benny Mwaipaja, Tangier-Morocco
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, ametoa wito kwa nchi za Afrika kuwa na mtazamo wa pamoja katika kubuni na kutekeleza mikakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu, ambayo ni endelevu na jumuishi, itakayopunguza utegemezi na kuimarisha uthabiti wa uchumi wa Bara la Afrika ili kukabiliana na majanga na migogoro ya vita inayoendelea duniani.
Mhe. Balozi Omar alitoa wito huo jijini Tangier nchini Morocco, katika Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika, wakati akichangia mjadala kufuatia taarifa ya Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), inayochambua athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika.
Alibainisha kuwa baadhi ya nchi za Afrika, hususan zile zinazotegemea sekta ya utalii, zinaweza kuathirika zaidi na Mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati.
Kwa upande wa Tanzania, alibainisha kuwa Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa mgogoro huo kupitia ushirikiano katika Wizara za Kisekta na Taasisi zake, ili kubaini hatua stahiki za kisera zitakazolinda ustawi wa uchumi na maslahi ya wananchi.
Vilivile, alieleza kuwa pamoja na kwamba mgogoro huo umeathiri mtiririko wa biashara kwa kuwa ukanda wa Mashariki ya Kati ni lango muhimu la biashara kati ya Afrika na masoko ya kimataifa. Hivyo, ni muda muafaka wa Afrika kuona umuhimu wa kuwa na njia mbadala ya kufanya biashara hususan miongoni mwa nchi wanachama.
Mheshimiwa Balozi Omar alisisitiza kuwa kwa muda mrefu Afrika imekuwa ikijadili umuhimu wa kutumia rasilimali zake ipasavyo, na kwamba hali ya sasa inatoa fursa ya kuchukua hatua madhubuti za kujitegemea kwa kutumia rasilimali zake.
Alifafanua kuwa Bara la Afrika lina rasilimali za kutosha, ikiwemo mafuta na mbolea, ambazo zinaweza kuzalishwa na kupatikana ndani ya Bara kupitia ushirikiano, hususan Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA).
Mhe. Balozi Omar alieleza kuhusu umuhimu wa kuendelea na majadiliano chini ya uratibu wa UNECA kuhusu mageuzi katika mifumo inayosimamia maamuzi na sera za kifedha duniani (Global Financial Architecture), ili Afrika iweze kuwa na sauti moja yenye nguvu katika upatikanaji wa rasilimali za kifedha kwa gharama nafuu kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Alisisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi hayo yatategemea mshikamano na ushirikiano thabiti wa nchi za Afrika.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano huo, walieleza kuwa ili kukabiliana na mizozo hiyo nchi za Afrika zinahitaji kuweka sera na mikakati ya kuondoa vikwazo vya ufanyaji biashara na upitishaji wa bidhaa kwa kufungua mipaka yake.
Aidha, walishauri kuwa umefika wakati wa nchi za Afrika kuzalisha mafuta yake na kutumia vyanzo vingine mbadala vya nishati ili kukabiliana na uhaba wa mafuta na kupanda kwa bidhaa hiyo muhimu katika uzalishaji na uchumi wa mataifa hayo.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akichangia mjadala kufuatia taarifa ya Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), iliyochambua athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika na namna ya kukabiliana nazo, katika Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika, unaofanyika jijini Tangier nchini Morocco.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akishiriki Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), unaofanyika jijini Tangier nchini Morocco, ambao pamoja na mambo mengine unajadili athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika na namna ya kukabiliana nazo. Mkutano huo umewashirikisha pia Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji Mhe. Dkt. Pius Chaya na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba.Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akichangia mjadala kufuatia taarifa ya Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), iliyochambua athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika na namna ya kukabiliana nazo, katika Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika, unaofanyika jijini Tangier nchini Morocco.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kulinda na kudumisha amani, umoja na mshikamano nchini, akihimiza wananchi kuondoa ubaguzi na kuimarisha upendo katika jamii.
Amesema umoja wa wananchi ni msingi muhimu wa utulivu wa Taifa, na kila mmoja ana wajibu wa kulinda tunu hizo kwa vitendo.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, Aprili 03, 2026, baada ya kushiriki Sala ya Ijumaa iliyoambatana na Dua Maalum ya kuiombea nchi, viongozi na marehemu, iliyofanyika Msikiti wa Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mangapwani.
Dua hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kushirikiana na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil, na imefanyika katika Msikiti wa Mzee Ali Hassan Mwinyi uliopo Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Aidha, amewataka waumini kuepuka makundi yenye viashiria vya chuki na migawanyiko, akisisitiza kuwa dini inahimiza amani na uvumilivu.
Dua hiyo imehudhuriwa na Mke wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Mama Mariam Mwinyi, viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, viongozi wa dini pamoja na ndugu, jamaa na marafiki.
Sambamba na hayo, Rais Dkt.Mwinyi, akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali na waumini, walizuru kaburi la Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kumuombea dua maalum.
Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) imetoa utaratibu rasmi wa uombaji wa vibali vya kusimika mabango kando ya barabara, ikiwa ni hatua ya kukabiliana na matapeli wanaojifanya watumishi wa taasisi hiyo na kuwahadaa wafanyabiashara.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wananchi wanaotaka kuweka mabango wanapaswa kuwasilisha maombi yao kwa njia ya barua rasmi kwa wakala, wakieleza kwa kina ujumbe wa tangazo, ukubwa wa bango (kwa mita za mraba), pamoja na namba ya simu ya mawasiliano.
Hatua inayofuata itahusisha ukaguzi wa eneo lililopendekezwa kufungwa bango, ambapo maafisa wa TANROADS watathibitisha kama eneo hilo linakidhi vigezo vinavyotakiwa, Endapo mwombaji atakidhi vigezo, atapewa barua ya malipo yenye namba ya kumbukumbu (control number) kwa ajili ya kukamilisha malipo husika.
Baada ya kufanya malipo, mwombaji atapatiwa kibali rasmi cha kusimika bango, ambacho kitakuwa halali kwa kipindi cha mwaka mmoja, TANROADS imefafanua kuwa baada ya muda huo kuisha, mmiliki wa bango atalazimika kulipia upya ili kuhuisha kibali chake na kuendelea kutumia eneo hilo.
Wakala huo umewataka wananchi kuwa makini na watu wanaojitambulisha kama watumishi wake bila uthibitisho rasmi, na kusisitiza kuwa taratibu zote za maombi na malipo zinapaswa kufanywa kupitia njia rasmi zilizoainishwa.




.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.png)



















