Na Said Mwishehe,Michuzi Blog
-MAMIA ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)ambao ni
Mabalozi wa mashina kutoka Wilaya za Temeke na Kigamboni jijini Dar es Salaam wamesema wanamatumamaini makubwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Dk.Asha-RoseMigiro
Wamesema Dk.Migiro ameweka historia ya kuwa Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke ndani ya chama hicho na kwa uwezo wake mkubwa katika siasa na uongozi ni wazi chama hicho kimepata Katibu mkuu sahihi.
Wakizungumza leo Januari 7,2026 katika ukumbi wa PTA uliopo Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam mabalozi hao wa shina ambao wamefika kwa ajili kushiriki kikao kazi kilichoandaliwa na Dk.Migoro wamesema wanaamini kupitia kikao hicho watapata maneno ya faraja kutoka kwake.
Balozi wa Shina kutoka Kibada wilayani Kigamboni Mwakibona Jumanne amesema wanamshukuru Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Dk.Migiro kuwa Katibu Mkuu katibu mkuu wa ccm
Aidha amesema wanashukuru Dk.Migiro kwa ujio wake leo kwani atawaambia neno la faraja wana CCM na Watanzania kwa ujumla.
Aidha amesema anaipongeza Serikali kwa kutuliza nchi na mpaka leo hali ni shwari na amani imetewala.”Ingekuwa nchi nyingine hali isingekuwa kama ilivyo na pengine ingeendelea kuharibika zaidi , hivyo tunaiomba Serikali iendelee kuwa na msimamo huo huo kusimamia amani ya nchi.
“Kwa utulivu na amani ndio tunaweza kufanya maendeleo ya nchi ,kijamii na kuhakikisha tunaendelea kupata maendeleo na Tanzania inasonga mbele.”
Kwa upande wake Asia Sadick ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM kutoka Kijiji cha Wavuvi Kata ya Mtoni amempongeza Mwenyekiti na Rais Dk.Samia kwa kumteua Dk.Migoro kuwa Katibu Mkuu kwani wanamatumaini na hawana shaka na uwezo wake katika uongozi na katika kikao cha leo wanatarajia kupewa ujumbe uliobeba matumaini kwa Taifa la Tanzania.
Katibu Mkuu Dk.Migoro leo anaanza ziara katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo leo Januari 7,2026 atakuwa na kikao kazi na viongozi mbalimbali wakiwemo mabalozi wa mashina katika Wilaya za Temeke na Kigamboni .Kikao hicho kinafanyika ukumbi wa PTA uliopo viwanja vya Sabasaba jiijini Dar es Salaam















.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)











.png)

000








