Akifunga rasmi mafunzo ya wiki mbili ya kuwajengea uwezo maafisa hao katika masuala ya usimamizi wa vyama, Mrajisi Msaidizi anayeshughulikia Uhamasishaji, Masoko na Uwekezaji amesema mafunzo hayo yamekuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha ufanisi wa vyama vya ushirika, hususan katika ngazi za mikoa na kusisitiza kuwa mafunzo hayo yamewapa washiriki mbinu za kisasa za uongozi, usimamizi na ushirikishaji wanachama, hatua itakayosaidia kuongeza tija, uwazi na ushindani katika soko.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Isaiah Kapakala, alisema mafunzo hayo yalilenga pia kuwajengea washiriki uelewa mpana juu ya matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), akibainisha kuwa matumizi ya teknolojia ni nguzo muhimu katika kuongeza ufanisi na uwajibikaji wa taasisi za ushirika katika zama za sasa.
Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Sophia Kagimbo, amesema mafunzo hayo yamewapa msukumo mpya wa kufanya kazi kwa ubunifu, weledi na kujituma zaidi, akiahidi kuwa watatumia maarifa waliyoyapata kuhakikisha vyama vya ushirika vinapiga hatua kubwa za maendeleo kote nchini.
Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha sekta ya ushirika nchini ili iwe injini ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

























.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)