

MichuziBlogV2
Most read Swahili blog on earth
Bonyeza play kuangalia Michuzi TV LiVE
BONYEZA PLAY KUANGALIA AZAM TV LIVE
BONYEZA KUANGALIA CHANNEL TEN LIVE















Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt. Tumaini Msowoya, amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Iringa kuwa makini na maisha ya chuoni kwa kujiepusha na ndoa za rejareja, makundi yasiyo na tija pamoja na tabia zinazoweza kuwavuruga kimasomo, huku akisisitiza umuhimu wa uzalendo na nidhamu binafsi.
Akizungumza wakati wa sherehe za kuwapokea wanafunzi wa mwaka wa kwanza, Dkt. Msowoya alisema licha ya wanafunzi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18 kisheria, bado wanapaswa kujiuliza iwapo ndoa au mahusiano ya kuishi pamoja ndiyo yamewaleta chuoni, au ni dhamira ya kutimiza ndoto zao za kielimu.
“Najua mna umri wa zaidi ya miaka 18 hivyo si watoto kwa mujibu wa sheria, lakini jiulizeni: je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wenu wanajua mmeoa au mmeolewa mkiwa hapa?” alihoji Dkt. Msowoya.
Aliongeza kuwa tafiti alizowahi kufanya kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu zimebaini kuwa wanafunzi wengi huishi na wenza wao kwa siri bila familia zao kufahamu, jambo alilolitaja kuwa ni hatari na linaloweza kuathiri mwenendo wa masomo na maisha ya baadaye.
Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka kujiingiza katika makundi yasiyo na mwelekeo chanya, akisisitiza kuwa wasomi ndio tegemeo la maendeleo ya taifa.
Katika hafla hiyo, Dkt. Msowoya alimwakilisha Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa ambaye alikuwa mgeni rasmi. Mwipopo aliwapongeza wanafunzi hao na kuchangia shilingi milioni 2,000,000 kwa ajili ya kuwasaidia katika safari yao ya masomo.
Amesisitiza kuwa nidhamu, maamuzi sahihi na uzalendo ni misingi muhimu kwa mwanafunzi yeyote anayelenga kufanikiwa chuoni na katika maisha kwa ujumla.


NA WILLIUM PAUL, SAME.
MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni amewataka wahandisi wa Halmashauri kuacha tabia ya kukaa ofisini na badala yake kushuka moja kwa moja kwenye miradi ya kimaendeleo, akisisitiza kuwaacha walimu wakuu wa shule na mafundi peke yao kusimamia na kujenga ni hatari kwa ubora wa ujenzi wa miradi na husababisha miradi kujengwa chini ya viwango.
Kasilda ameyasema hayo jana wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu katika Shule ya Msingi Hedaru.
Alisisitiza kuwa ni wajibu wa wahandisi wa ujenzi kushiriki kikamilifu katika kila hatua ya utekelezaji wa miradi ili kuepusha kasoro zinazoweza kujitokeza endapo mafundi na kamati za ujenzi wataachwa kufanya kazi bila usimamizi wa karibu wa wataalam.
“Niwasisitize sana wahandisi wa ujenzi wa Halmashauri kuhakikisha mnafika kwenye miradi inayotekelezwa mara kwa mara, msiwaachie mafundi na kamati za ujenzi peke yao, tunahitaji kila hatua ya ujenzi isimamiwe na wataalam, kwa kushirikiana na TAKUKURU, ili ushauri na marekebisho yafanyike mapema kabla mradi haujafikia hatua kubwa zaidi,” alisema Kasilda.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina.
Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee.
Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana
Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badala ya utaratibu wa maelekezo kutoka juu kwenda chini.
Alitumia pia kikao hicho kutoa rai kwa viongozi na wana CCM kuzingatia utaratibu wa kutoa maoni kuanzia ngazi ya chini kwenda juu.
“Nitoe wito kwa viongozi wetu tusifanye utaratibu wa kutoa amri kutoka juu kushuka chini maana uongozi mzuri ni lazima uanzie chini kwenda juu, yale tunayoyapata kutoka kwenye mashina, matawi ndio yatapanda juu kwa lengo la kukiimarisha chama chetu, alisema Dkt.Migiro.
Aidha, siku iliyofuata katika ziara yake, akizungumza na viongozi wa mashina na matawi wa Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Katibu Mkuu huyo wa CCM, alisema Chama Cha Mapinduzi hakijengwi katika majukwaa, bali hujengwa kuanzia ngazi ya mashina na matawi, huku akibainisha majukwaa hutumika zaidi kwa ajili ya kutoa hamasa.
“Mashina ndiyo moyo wa CCM kwa kuwa ndiyo yanayokutanisha chama na wananchi moja kwa moja kupitia vikao na shughuli mbalimbali za kijamii na kisiasa, amesisitiza Dk.Migiro, anayeendelea na ziara yake mkolani Dar es salaam yenye kauli mbiu 'ShinaLakoLinakuita'.











