Taasisi ya Saratani Ocean Road imeendelea kutoa elimu na huduma za uchunguzi wa saratani mbali mbali katika Maadhimisho ya Wiki ya Afya Kitaifa 2026.

Kilele cha maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Zimbwini, Kibiti Mkoa wa Pwani, ambapo mgeni rasmi ni Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, ambayo ni maaluku kwa chanjo, Bima Afya kwa wote na usafi wa mazingira.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Meneja wa Huduma za Uchunguzi wa Saratani na Elimu kwa Umma, DK. Maguha Stephano, amesema taasisi hiyo inaunga mkono juhudi za serikali kuhakikisha  wananchi wanapata elimu kuhusu saratani.

Maguha amesema pia wanahakikisha wananchi wanapata chanjo zinazozuia maambukizi ya virus I vinavyosababisha saratani za mlango wa kizazi, saratani ya  ini na huduma za uchunguzi wa saratani mbali mbali, zikiwemo mlango wa kizazi, matiti na tezi Dume kwa wanaume.

Amesema Saratani ya tezi Dume inafanyika kwa njia ya kipimo cha damu na huduma hizo zinatolewa bila malipo na taasisi hiyo.

Aidha Maguha amewaomba wananchi wa Mkoa wa Pwani katika katika Wilaya ya Kibiti kutumia fursa hiyo  kupata huduma hizo bure.




 Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

KATIKA Kuendelea kuboresha huduma kwa watanzania Shirika La Mawasiliano Tanzania (TTCL,) kupitia faida ya Shilingi Bilioni 22.98 iliyotengeneza kwa mwaka wa fedha 2024/2025 limenunua na kukabidhi idara ya ufundi magari saba aina ya Hilux yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.6 pamoja na bajaji 28 zenye thamani ya shilingi  milioni 291.2 na kuzielekeza idara na vitengo kutumia vitendea kazi hivyo kwa kuwafikia na kutoa huduma kwa wakati kwa wateja na kufikia malengo ya kuwaunganisha na huduma wateja milioni moja kwa kipindi cha miaka mitatu.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi magari na bajaji hizo kwa wakuu wa Idara na Vitengo vya Shirika hilo Mkurugenzi mkuu wa TTCL Moremi Marwa amesema, vitendea kazi hivyo vimelenga kuwafikia kwa wakati wateja wanaotumia huduma kutoka Shirika hilo ikiwemo watumiaji wa huduma ya Faiba Mlangoni kwako.

`` Magari pamoja na bajaji hizi zitatumiwa na mafundi na watumishi wanaohudumia wateja, pindi huduma zinapokatika au wateja kupata hitilafu katika utumiaji wa huduma mafundi wetu watawafikia kwa wakati na kutatua changamoto na kwa ufanisi zaidi. “Amefafanua.”

Aidha amesema; Shirika hilo pia limenunua magari matano aina ya Hiace ambayo yatapokelewa mwisho wa mwezi huu mahususi kwa ajili ya masoko na mauzo kwa kuwafikia wateja wao pamoja na kuwafikia wateja wapya na kufafanua kuwa vifaa hivyo ni sehemu ya faida iliyotengenezwa na Shirika hilo ili kuweza kuhudumia wateja wao kwa ufanisi zaidi na kupata mapato yatakayoendeleza Shirika na kutoa gawio kwa Serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa ufundi wa TTCL Mhandisi. Cecil Francis amemshukuru Mkurugenzi mkuu wa Shirika hilo kwa kusimamia maamuzi hayo ya kimkakati kwa kuhakikisha kunakuwa na vitendea kazi vitakavyorahisisha utoaji huduma na kuwafikia wateja wengi zaidi na kuwataka wafanyakazi wa Shirika hususani Idara ya ufundi kuvitumia vitendea kazi hivyo kwa madhumuni yaliyowekwa ili kuleta tija kwa Shirika na watumiaji wa huduma za TTCL.

Cecil ameeleza kuwa wamejidhatiti katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati pamoja na kuhakikisha wanafikia mikoa yote nchini na kuhakikisha azma ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya mawasiliano na kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia inatimia.

Mkurugenzi wa Shirika La Mawasiliano Tanzania (TTCL,) Moremi Marwa akizungumza wakati akikabidhi magari na bajaji hizo kwa Idara na Vitengo na kuwasisitiza kutumia vitendea kazi hivyo kwa malengo na kuleta matokeo chanya katika utoaji huduma. Leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Shirika La Mawasiliano Tanzania (TTCL,) Moremi Marwa (kulia,) akikabidhi mfano wa funguo kwa Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika hilo Vedastus Mwita (kushoto,) Leo jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi wa Shirika La Mawasiliano Tanzania (TTCL,) Moremi Marwa (kulia,) akikabidhi mfano wa funguo kwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirika hilo Mhandisi. Cecil Francis (kushoto,) Leo jijini Dar es Salaam.

SERIKALI imesema uzalishaji na uingizaji wa mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku umepungua kwa asilimia 95 hatua iliyochangia kupungua kwa uzalishaji wa taka za plastiki katika maeneo mbalimbali nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa bungeni jijini Dodoma leo Aprili 29, 2026, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Dkt. Catherine Joachim aliyetaka kujua Serikali imepata matokeo gani katika kupunguza uchafuzi wa mazingira tangu kuanza kwa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki mwaka 2019.

Akijibu swali hilo Mhe. Kwagilwa alibainisha kuwa baada ya katazo hilo kiwango cha uelewa wa wananchi kuhusu madhara ya plastiki kiliongezeka kutoka kutoka chini ya asilimia 40 mwaka 2018 hadi kufikia zaidi ya asilimia 85 mwaka 2026.

Kutokana na hatua hiyo, alitoa rai kwa wananchi kuendelea kuzingatia katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kwa ajili ya kulinda afya na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha, Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa taka za plastiki katika maeneo ya fukwe za bahari na maziwa zimepungua kwa takribani asilimia 60 hivyo kupunguza hatari kwa viumbe wa majini.

Halikadhalika, Mhe. Kwagilwa alieleza kuwa katazo la mifuko ya plastiki limesaidia kupungua kwa gharama za kuzibua mitaro ya maji machafu kwa wastani wa asilimia 30 hadi 40, kwani mifuko ya plastiki ilikuwa chanzo kikuu cha uzibaji wa miundombinu hiyo.

Akijibu maswali ya nyongeza, alibainisha kuwa Serikali imeweka jitihada madhubuti za kuhakikisha taka hususani zile za plastiki zinazozalishwa katika maeneo mbalimbali nchini zinarejelezwa na kuzalisha bidhaa.

Pia, alisema Serikali inahakikisha kwenye majiji kwa mfano Dar es Salaam, inajenga madampo makubwa yatakayoambatana na viwanda vitakavyofanya shughuli ya urejelezaji na kuchakata taka kuwa bidhaa, hatua itakayosaidia kudhibiti taka.

Ifahamike kuwa mifuko ya plastiki ni aina ya mifuko yenye mchanganyiko wa kemikali zisizooza hivyo kuleta athari kwenye mazingira pamoja na afya kwa binadamu na wanyama.

Aidha, kutokana na tafiti mbalimbali mifuko ya plastiki huchukua miaka 400 hadi 1000 kuoza ardhini na hivyo kuleta athari mbalimbali zikiwemo kuathiri mifumo ikolojia ya bahari ambapo inakadiriwa 100,000 viumbe bahari na ndege bahari millioni moja kila mwaka wanakufa kwa kula mifuko ya plastiki.

Athari zingine ni pamoja na kuchafua miji kutokana na kushindwa kuoza, kuathiri mifugo kutokana na kula mifuko ya plastiki, kuharibu miundombinu kwa kuziba kwenye mifereji na baadhi ya njia za maji, kubeba na kusambaza viumbe vamizi na bakteria na pia inapochomwa moshi wake una madhara na unaweza kusababisha maradhi ya kansa.



MAAFISA Usafirishaji maarufu kwa jina la Bodaboda wa Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya wahimizwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe Josephine Manase Aprili 28, 2026 wakati akifungua mashindano ya Mpira wa Miguu ya "Kyela Polisi Jamii Bodaboda Super Cup, 2026 yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa Polisi Kyela na kushirikisha Maafisa Usafirishaji wa Wilaya hiyo kutoka katika Kata 33.

Mhe Manase amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kuilinda Amani iliyopo kwa kuacha na kujiepusha kujihusisha na makundi yasiyofaa, vitendo visivyofaa katika jamii na badala yake washirikiane na Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi na usalama pamoja na kufichua wahalifu.

Aidha, Mhe Manase amepongeza mikakati thabiti ya Jeshi la Polisi Wilayani humo katika kuzuia uhalifu kupitia utekelezaji wa falsafa ya Polisi Jamii ambayo imekuwa ikishirikisha wananchi, kuwajengea uwezo na uelewa wa masuala ya usalama hali inayopelekea kupata mafanikio katika kuzuia uhalifu.

Mkuu wa kitengo cha ushirikishwaji wa Jamii, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Henry Mwaibambe kutoka Makao Makuu ya Polisi Dodoma amewasihi wananchi wa Kyela kuilinda Amani iliyopo na kuacha kusikiliza maneno yenye nia ya kuvuruga amani na utulivu uliopo kwani kwenye amani watakuwa huru kufanya kazi zao za uzalishaji mali.

Naye, Diwani wa Kata ya Mikoroshini Gwakisa Mwakipesile amesema kuwa mashindano hayo yamekuwa na faida kubwa kwa vijana hasa Bodaboda kwani yamerejesha imani kati ya Jeshi la Polisi na Wananchi wa Kyela ambapo ushirikiano huo ni ishara ya mahusiano mazuri katika kukabiliana na uhalifu.

Kwa upande wake, Joshua Mwaisumo, Mkazi wa Kyela amepongeza waandaaji wa mashindano hayo kwani yamesaidia kuisogeza jamii karibu na Jeshi la Polisi na kusaidia jamii kupata elimu, kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu na hatimaye Kyela kuwa salama.

Fainali ya mashindano hayo yalizikutanisha timu za Bodaboda Kata ya Ipinda dhidi ya Bodaboda Kata ya Serengeti na kushuhudia Bodaboda Kata ya Ipinda kuibuka mabingwa kwa changamoto za penati 5 kwa 3 na kuzawadi Ng'ombe, Jezi na Mpira. Mashindano hayo yalibeba ujumbe unaosema, "Amani, Utulivu na Mshikamano, kwa usalama na Maendeleo yetu"
 




WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amezindua makati wa Taifa wa Kukabiliana na Mmomonyoko wa Maadili wa mwaka 2026/27 hadi 2036/37, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mustakabali wa Taifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Makonda amesema mkakati huo unatekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa Septemba 24, 2024 mkoani Ruvuma wakati wa Tamasha la Tatu la Kitaifa la Utamaduni, ambapo alielekeza kuandaliwa mfumo wa pamoja wa kitaifa utakaounganisha nguvu za Serikali, familia na wadau wote kulinda utambulisho wa Watanzania.

Amesema maadili ni msingi mkuu wa maendeleo ya nchi yoyote, yakitoa mwelekeo wa fikra, mienendo na maamuzi ya jamii katika nyanja zote, huku akibainisha kuwa Katiba ya mwaka 1977 kupitia Ibara ya 9 inaweka misingi ya Utu, Umoja, Usawa, Utaifa na Uwajibikaji kama nguzo za maisha ya Mtanzania.

Makonda amesema licha ya fursa zinazotokana na maendeleo ya sayansi, teknolojia na utandawazi, bado kuna changamoto ya mmomonyoko wa maadili ikiwemo kupungua kwa uwajibikaji, kudhoofika kwa taasisi ya familia, matumizi yasiyofaa ya mitandao, kuongezeka kwa uhalifu, matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na makundi mbalimbali.

Kutokana na hali hiyo, Serikali imeandaa mkakati wa miaka 10 unaolenga kujenga jamii yenye maadili imara inayozingatia utu, uwajibikaji, uzalendo na mshikamano wa kitaifa". Amesema Makonda

Amesema kuwa mkakati huo umezingatia maeneo muhimu ikiwemo kuimarisha taasisi ya familia, kuboresha urithishaji wa maadili kupitia elimu, kuhamasisha matumizi sahihi ya teknolojia na mitandao, pamoja na kuimarisha usimamizi wa sheria na kanuni zinazolinda maadili ya jamii.

Amesema mkakati huo umeandaliwa kwa ushirikishwaji wa wadau mbalimbali kutoka Serikalini, sekta binafsi, taasisi za dini, wasanii, vijana na jamii kwa ujumla ili kuhakikisha unakuwa na uhalisia na umiliki wa pamoja.

Aidha, Makonda ametoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika kulinda na kuendeleza maadili, akisisitiza kuwa zaidi ya asilimia 42 ya Watanzania ni watoto na vijana wenye umri chini ya miaka 15, hivyo kuna wajibu wa pamoja kujenga msingi imara wa kimaadili kwa kundi hilo.

Amewataka wazazi na walezi kuwajibika katika malezi, viongozi wa dini na jamii kuhamasisha maadili, wasanii na wazalishaji wa maudhui kuzalisha kazi zinazojenga jamii, vyombo vya habari kuelimisha umma, na mamlaka za udhibiti kuimarisha utekelezaji wa sheria.

"Utekelezaji wa mkakati huu utaanzia ngazi ya familia hadi Taifa, Serikali inaahidi kuhakikisha wadau wote wanapata elimu na taarifa za mkakati huo kupitia majukwaa mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii kwani bila maadili imara, maendeleo endelevu hayawezi kufikiwa.



Arusha
SERIKALI  imesema haina mpango wa kusimamisha ama kuzuia shughuli za uwindaji wa kitalii na badala yake inaendelea kuandaa na kuboresha sera,sharia na miongozo itakayohakikisha uwindaji wa kitalii unafanyika kwa kuzingatia uhifadhi wa wanyamapori, kukuza mapato ya Taifa na kuchochea maendeleo ya jamii.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi kati ya chama cha wamiliki wa kampuni za uwindaji Tanzania, katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua na kuenzi sekta ya wanyamapori kwakuwa ni rasilimali ya kipekee yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa jamii na hivyo haina mpango wa kuisimamisha bali kuiendeleza.

Ameongeza kuwa ni matarajio ya mkutano huo kuwa utabainisha mikakati ya kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya uwindaji wa kitalii ili kujenga ustawi na kuongeza ushindani wa Tanzania katika soko la uwindaji wa kitalii kimataifa.

Amewataka wadau hao wa uwindaji wa kitalii kuilinda sekta hiyo kwa kuzingatia maadili na kuendeleza uhifadhi na kupmabana na ujangili, kutokukwepa kodi, kulipa kodi na stahiki za jumuiya au wananchi zinazozunguka maeneo ya ya uwindaji.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha Katibu Mkuu, Mkurugenzi wa Wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Alexander Lobora amesema mikutano ya aina hii imekuwa na tija kwa Serikali na wadau wa tasnia ya uwindaji wa kitalii katika kutafuta suluhu ya changamoto kubwa zinazoikabili tasnia hii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji Tanzania (TAHOA); Bw. Michel Mantheakis, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano inaoutoa kwa tasnia hiyo na kuongeza kuwa Chama hicho kitaendelea kutekeleza wajibu wake kwa kuzingatia sheria na taratibu kwa kuwa kushuka ama kusimama kwa uwindaji wa kitalii ni kukosekana ama kushusha mapato ya serikali lakini pia kudhorota kwa uhifadhi na hivyo kutokomea kwa uwindaji wa kitalii.





Na David KAFULILA, Aprili29,2026
JANA PPP CENTRE tulikuwa na kikao cha kawaida cha Baraza la wafanyakazi. Pamoja na kuwapongeza kwa mafanikio makubwa ya kufanya Agenda ya PPP kueleweka kwa kasi kwa umma na mfumo mzima wa Serikali kiasi Dira na Mpango wa muda mrefu( LTPP) na Mpango wa Nne wa miaka5( FYDPIV) kuonesha PPP kuwa nguzo muhimu kwa ufanikishaji, zaidi ni mafanikio bayana kwamba wakati awamu ya sita inaanza , miradi ya PPP ilikuwa ya thamani ya 1bn Dollar- 2.5Trilioni( Financing Strategy 2021/22 - 2025/26. ), ndani ya miaka4, thamani ya miradi ya Ubia imeongezeka kwa 8.5Trilion.

Hata hivyo niliwapa changamoto moja kuhusu namna Sheria ya Utumishi wa Umma inavyomlinda Mtumishi kwa gharama ya mlipa kodi. Niliwaeleza kuwa sheria iliwekwa kumlinda mtumishi dhidi ya matumizi mabaya ya viongozi wabaya ingawa sasa inaonekana kuwa mwiba kwa mlipa kodi kwani ugumu wa kumwondoa mtumishi asiyefaa ni mzigo kwa kumlipa kodi.

Niliwapa mfano wa nchi kama Botswana, wao mtumishi akiwa na utendaji mbovu kwa miaka miwili mfululizo anafukuzwa mara moja na endapo atakata rufaa , anakuwa nje ya Utumishi. wakati Tanzania utumishi unakoma baada ya rufaa zote kuamuliwa.

Mtumishi akifukuzwa Tanzania inachukua mpaka miezi22 kufukuzwa rasmi wakati Botswana hatua zote ni miezi3.

Kwa Mujibu wa Ripoti ya CAG ya Machi2024, inaonesha kwamba kati ya wafanyakazi 1124 waliothibitika kuwa na utendaji hafifu kwa miaka2 mfululizo katika kipindi cha mwaka 2022/23, Ni watendaji 138 tu waliofukuzwa sawa na asilimia 12%( mfumo wa rufaa unawapa ushindi).

Wakati Botswana kwa kipindi hicho 2022/23 , kati ya wafanyazi 241 waliothibitika kuwa na utendaji mbovu kwa miaka miwili mfululizo, 214 sawa na asilimia 88% walifukuzwa.

Watendaji wabovu wanagharimu pakubwa walipa kodi. Ndio maana nimependa kurejea uhusiano kati ya ufanisi wa Taasisi kwenye nafasi ya uchumi kwa kurejea Ripoti ya OxfordReview ya 2014, kwamba asilimia 25% ya uchumi wa mataifa13 makubwa zaidi kwa Uchumi Duniani, uchumi wao unatokana na ufanisi wa Taasisi ambao kwa kiasi kikubwa unategemea sana ubora wa rasilimali watu ikiwemo watumishi wa Umma..Ndio msingi wa hoja yangu kwetu wafanyakazi kuwa , Sheria inayotulinda dhidi ya uonevu isionee walipa kodi!
Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Samson Allute.
Mwezeshaji Mafunzo, Osiah Mwanyesya.

Na Mwandishi Wetu
WALIMU wanaofundisha masomo ya Sayansi na Hisabati nchini, wametakiwa kutumia teknolojia pamoja na mbinu bunifu za ufundishaji ili kuongeza uelewa kwa wanafunzi na kusaidia kuzalisha wataalamu wa sayansi watakaochangia maendeleo ya taifa kijamii na kiuchumi.

Wito huo umetolewa Aprili 29, 2026 na Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Samson Allute, wakati akifungua mafunzo ya siku tano kwa walimu wa Sayansi na Hisabati kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu.

Allute amesema matumizi ya teknolojia katika ufundishaji yatawawezesha walimu kufundisha kwa ufanisi zaidi huku yakichochea wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi na Hisabati tangu wakiwa mashuleni.

Amesema serikali inaendelea kuwekeza katika sekta ya elimu kupitia Mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP), unaolenga kuboresha miundombinu ya shule, kutoa mafunzo kazini kwa walimu pamoja na kuimarisha matumizi ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

“Mwalimu anapaswa kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kufikiri, kufanya ubunifu na kuwa wataalamu watakaosaidia maendeleo ya taifa,” amesema Allute.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea walimu uwezo wa kutumia teknolojia na mbinu shirikishi za ufundishaji ili kuboresha ufaulu wa wanafunzi katika masomo ya Sayansi na Hisabati.

Aidha, amewataka walimu kutumia maarifa watakayoyapata kuwasaidia wanafunzi kuondoa hofu ya masomo ya sayansi ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakionekana kuwa magumu kwa baadhi yao.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Happiness Goyi, mwalimu wa Kemia kutoka Shule ya Sekondari Mwakibuga mkoani Simiyu, amesema mafunzo hayo yatamsaidia kutumia mbinu za kisasa zitakazowawezesha wanafunzi kuelewa kwa urahisi masomo ya sayansi na kuyapenda zaidi.

Naye Daniel David, mwalimu wa Fizikia, amesema matumizi ya teknolojia katika ufundishaji yatawasaidia wanafunzi kuendana na mabadiliko ya dunia ya sasa yenye ushindani mkubwa wa sayansi na teknolojia.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuwajengea uwezo walimu 523 kutoka mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Tabora na Katavi kupitia mradi wa SEQUIP.


HII ni nafasi ya wazi kwa kila mwenye kiu na njaa ya mafanikio makubwa kwenye Dunia hii inayohitaji teknolojia ili kutoboa kiuchumi. Meridianbet kwa kutambua uhitaji mkubwa wa vijana kuwekeza kwenye masoko ya hisa huku wakihitaji mfumo mwepesi wa kuendesha uwekezaji wao basi wamekuletea Stock Trade.

Ndani ya Stock Trade, utakutana na soko linalobadilika muda wote. Bei zinapanda na kushuka kulingana na matukio mbalimbali, na hapa ndipo akili yako inahitajika zaidi. Kila uamuzi unaoufanya, iwe kununua au kuuza, unaweza kuwa hatua ya kukuingizia ushindi mkubwa. Hii ni kwa wote wanaopenda mafanikio.

Meridianbet wanakupa jukwaa pana la kubashiri, mechi kali za kimataifa hadi michezo ya kasino mtandaoni iliyojaa burudani. Ukiwa na odds zenye ushindani mkubwa, kila tiketi inakuwa na thamani zaidi. Jiunge sasa kupitia tovuti yao au piga *149*10#.

Cha kuvutia zaidi, unafanya biashara ya vitu vya kipekee kabisa kama madini yaliyopo angani na rasilimali za kwenye sayari nyingine. Ni kama umeingia kwenye dunia ya kisasa ya kidigitali ambapo kila kitu kina thamani yake. Ukishiriki, unaweza kugeuza nafasi ndogo kuwa mafanikio makubwa.

Tofauti na michezo mingine, Stock Trade inahitaji umakini wa hali ya juu na uwezo wa kufuatilia mabadiliko ya haraka yanayotokea. Hapa ni mipango, uchambuzi, na maamuzi ya haraka yanayokupa ushindi. Ndiyo maana vijana wengi wanaikimbilia kwa sababu inachanganya burudani na akili kwa kiwango cha juu.

Usibaki nyuma wakati wengine wanatumia fursa hii mpya. Jiunge na Meridianbet leo, fungua akaunti yako kwa urahisi, na anza safari yako ya kipekee ndani ya Stock Trade. Huu ndio muda wako wa kujaribu kitu kipya, kujifunza, na kushinda, anza sasa.


MPAMBANO mwingine wa kibabe umefika Jumatano hii katika dimba la Civitas Metropolitano kati ya Atletico Madrid dhidi ya Arsenal ambao ni vinara wa ligi kuu ya Uingereza.

Atletico Madrid na Arsenal hii ni moja za mechi ya kutazama katika mashindano ya UEFA Champions League inatarajiwa kuwa mechi ya kuvuta hisia za mashabiki wengi Duniani huku kila timu ikipewa nafasi ya kushinda mechi hii.

Kwa upande wa Atletico Madrid, timu hii inajulikana kwa mfumo wake wa kiulinzi uliokamilika chini ya mbinu za Diego Simeone. Atletico ni timu inayopenda kujenga msingi wake kwenye nidhamu, umakini na uwezo wa kuvumilia presha kubwa kutoka kwa wapinzani.

Hawapendi kucheza soka la kumiliki mpira muda mrefu, bali wanapendelea kusubiri nafasi na kushambulia kwa kasi pale mpinzani anapokuwa amezubaa. Wachezaji kama Antoine Griezmann, Koke, Solorth, Alvarez na wengine ni muhimu sana kwenye safu ya ushambuliaji siku ya leo.

Ukiachana mechi hiyo ya UEFA, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Arsenal kutoka kule Uingereza, chini ya Mikel Arteta wamejijengea sifa ya kucheza soka la kisasa linalotegemea umiliki wa mpira, kasi ya maamuzi na mzunguko wa pasi wa haraka na safu bora ya kuzuia huku wakiwa wameruhusu mabao machache kwenye michuano hii.

Martin Odegaard ndiye injini ya ubunifu katikati ya uwanja, akitoa pasi za mwisho na kuongoza tempo ya mchezo. Upande wa mashambulizi, Bukayo Saka ni tishio la mara kwa mara kutokana na kasi yake, dribbling na uwezo wa kufunga mabao katika nafasi ndogo.

Takwimu zinaonesha kuwa mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili, vijana wa Simeone walipoteza vibaya sana. Lakini sasa wanakutana kwenye Nusu Fainali moja ya mechi ambayo ni muhimu sana kwa wote wawili kwani kila timu haijawahi kushinda taji hili.

The Gunners mpaka sasa kutoka kwenye makombe 4 ambayo alikuwa anayawania, amebakiza mawili pekee huku nayo inabidi aongezee bidii ili aweze kuchukua. Kule EPL mpaka sasa licha ya kuwa anaongoza ligi bado presha ni kubwa kwani anayeshika nafasi ya pili ambayo ni City ana mchezo mmoja mkononi.

Huku kwenye UEFA ndio kadri michuano inavyozidi kusogea mbele, ndivyo ambavyo mechi zinazidi kuwa ngumu, hivyo Arteta akifanya mzaha anaweza kujikuta amekosa makombe yote tena na msimu huu.

Atletico yeye baada ya kukosa Kombe la Copa del Rey, sasa nguvu zote zimehamia kwenye UEFA ambapo sasa inabidi washinde mechi hii dhidi ya Arsenal huku nafasi ya kwenda hatua ya Fainali akipewa mwenyeji.

Na Farida Mangube Morogoro

Bodi ya Maji ya Bonde la Wami-Ruvu imewatoa hofu wakazi wa Manispaa ya Morogoro kuwa maji ya Bwawa la Mindu ni salama, kwani kemikali iliyomwagika haikufikia chanzo cha maji.

Wasiwasi huo ulizuka kufuatia ajali ya lori lililokuwa likisafirisha kemikali aina ya sulphur kuacha njia na kugonga miti mita 300 kutoka bwawa la Mindu mtaa wa mikoroshini Kata ya Mindu barabara kuu ya Morogoro–Iringa.

Mkurugenzi wa Bonde la Maji bonde la Wami-Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmasi, amesema hatua za haraka zilizochukuliwa na wataalamu zilisaidia kuzuia kemikali hiyo kusambaa hadi kwenye chanzo cha maji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA), CPA Sais Kyejo, amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa hakuna madhara yaliyobainika katika ubora wa maji yanayosambazwa.

“Wananchi waendelee kutumia maji bila hofu,” amesema Kyejo.

Naye Meneja wa Kanda ya Kati wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Bi Magdalena Mtenga, amesema hadi sasa hakuna madhara yaliyoripotiwa kwa wananchi, licha ya kemikali hiyo kuwa hatarishi endapo itashughulikiwa bila tahadhari.

Ameeleza kuwa sulphur ina sifa ya kuwaka na hata kulipuka, pamoja na kusababisha muwasho wa ngozi au koo, lakini hali hiyo haikutokea wakati wa operesheni ya kuiondoa katika eneo la ajali.

Taasisi mbalimbali zikiwemo Bonde la Wami-Ruvu, MORUWASA, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) pamoja na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji zilishiriki kuondoa kemikali hiyo kwa usalama.

Meneja wa NEMC Kanda ya Morogoro na Rufiji, Arnold Mapinduzi, amesema kemikali hiyo itateketezwa kwa mujibu wa sheria ili kulinda mazingira.

Ajali hiyo ni ya tatu ndani ya mwezi mmoja kuhusisha usafirishaji wa kemikali aina ya sulphur Barabara kuu ya Morogoro - Iringa hali inayochochea haja ya kuimarisha usalama wa usafirishaji wa kemikali hatarishi.





MHESHIMIWA Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameihakikishia Jamhuri ya Belarus kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano na nchini hiyo na kwamba amewaalika wawekezaji na wafanyabiashara kuja nchini  kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta za kilimo, uvuvi, elimu na afya.

 Kauli hiyo imetolewa leo (Jumanne, Aprili 28, 2026) na Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov, Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam.

Pia, Dkt. Mwigulu amepokea kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mwaliko wa ziara ya kikazi nchini Belarus wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Belarus, Mheshimiwa Alexander Lukashenko.

 Waziri Mkuu, amesema Serikali imeboresha mazingira ya uwekezaji na biashara, pia Tanzania kibiashara ipo katika eneo la kimkakati kijiografia kwa kuwa ni kitovu cha Mataifa ya Ukanda wa Afrika Mashariki na ya Kusini mwa Afrika.

“Ni kutokana na umuhimu huo, Tanzania kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 imejiwekea lengo la kuwa tegemeo la kanda hizo katika sekta ya kilimo sanjari na sekta ya afya ambayo Dira 2050 inataka Tanzania ijitosheleze katika uzalishaji wa dawa kufikia asilimia 80 ifikapo mwaka 2050.” Amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Belarus katika sekta hizo utakuwa na matokeo chanya na ya haraka kutokana na nchi ya Belarus kupiga hatua katika sekta hizo, hasa matumizi ya teknolojia kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya dawa na zana za kilimo. 

“Tutaangalia uwezekano wa kubadilishana wataalam kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo, ambapo Tanzania itatuma wataalam wa kilimo nchini Belarus ili wapate ujuzi, mfano katika teknolojia ya uundaji matrekta ya kisasa na zana nyingine za kilimo.” Ameongeza Waziri Mkuu.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov ameeleza kuwa Serikali ya Belarus ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, mifugo, uvuvi, elimu, sayansi na teknolojia.

“Nimefanya mazungumzo na mawaziri wa sekta muhimu hapa Tanzania, wakiwemo Waziri wa Elimu, Waziri wa Ulinzi na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, ambapo kwenye eneo la uvuvi tumeona fursa ya kuwa wananuzi wazuri wa mazao ya baharini kwani Tanzania yanapatikana kwa wingi.” 

Ameongeza kuwa Belarus na Tanzania zinatarajiwa kusaini mikataba ya makubaliano (MoU) kuhusu kuwa na Tume ya Pamoja ya Biashara kati ya Tanzania na Belarus.“Makubaliano hayo yatawawezesha wafanyabiashara wa Tanzania na wa Belarus kuendesha shughuli zao kirahisi na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi.”

Wakati akikabidhi ujumbe wa mwaliko wa ziara ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Belarus, Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov amesema pia Waziri Mkuu wa Belarus, Alexander Turchin anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini Tanzania hivi karibuni.










📌 Yapongeza REA na SUMA JKT kwa utekelezaji thabiti

📌 Bilioni 3.2 kukamilisha miradi Ludewa

Ludewa, Njombe📍

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeeleza kuridhishwa na kasi na ubora wa utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme katika maeneo ya mwambao wa Ziwa Nyasa yaliyopo katika Wilaya za Ludewa na Makete, ikipongeza juhudi za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na mkandarasi, Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT).

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara ya ukaguzi katika maeneo ya Nkanda na Lumbila, Mjumbe wa Bodi, Florian Haule, alisema Bodi imejionea maendeleo makubwa ya mradi huo unaolenga kusambaza umeme kwa wananchi waishio katika maeneo yenye changamoto za kijiografia wilayani Ludewa na Makete.

Alieleza kuwa pamoja na ugumu wa miundombinu katika ukanda huo wa Bonde la Ufa, utekelezaji wa mradi unaendelea kwa kasi ya kuridhisha, ambapo kazi ya usimikaji wa nguzo imefikia hatua kubwa na kinachoendelea sasa ni uvutaji wa nyaya.

“Tumefurahishwa na hatua iliyofikiwa. Vifaa vyote muhimu vimeshafikishwa na katika siku chache zijazo tutaanza kushuhudia ufungaji wa transfoma,” alisema Haule.

Kwa mujibu wa Haule, mkandarasi SUMA JKT ameihakikishia Bodi kukamilisha kazi hiyo ifikapo Julai, 2026; ahadi inayotoa matumaini kwa wananchi wenye uhitaji mkubwa wa huduma ya umeme katika maeneo hayo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Utafiti REA, Mhandisi Yusuph Ismail, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, alisema hatua inayofuata ni usimikaji wa transfoma na ujenzi wa njia za umeme za msongo mdogo (LV) ili kuanza kuunganisha wateja wa awali.

Alibainisha kuwa katika kitongoji cha Nkanda, kazi ya usimikaji wa nguzo kwa umbali wa takribani kilometa tisa imekamilika kwa kiwango kikubwa, huku matarajio yakiwa ni kuwasha umeme ifikapo Mei 25, mwaka huu.

“Tunawahimiza wananchi kufanya maandalizi ya ndani ya nyumba (wiring) ili waweze kuunganishiwa umeme mara moja pindi huduma itakapoanza,” alisisitiza Mhandisi Ismail.

Aliongeza kuwa upatikanaji wa umeme utakuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Ziwa Nyasa, hususan kwa shughuli za uvuvi, kwa kuwezesha matumizi ya teknolojia za kisasa za kuhifadhi samaki na kuongeza thamani ya mazao hayo.

Aidha, huduma za kijamii ikiwemo shule, vituo vya afya, nyumba za ibada na ofisi za vijiji zinatarajiwa kunufaika moja kwa moja na mradi huo, hali itakayoboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi Mwendeshaji wa kampuni ya umeme ya SUMA JKT, Meja James Mhame, ambaye pia ni Meneja wa Mradi huo, alisema utekelezaji unaendelea vizuri huku zaidi ya asilimia 80 ya kazi ya awamu ya kwanza ikiwa imekamilika.

“Hatua inayofuata ni uvutaji wa nyaya kwa kiwango kikubwa pamoja na ufungaji wa transfoma ili kuanza kusambaza umeme kwa wananchi wa Nkanda na Lumbila,” alisema Meja Mhame.

Kwa upande wake, Meneja Msimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, alisema Serikali imetenga shilingi bilioni 3.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo katika Wilaya ya Ludewa, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha vitongoji vyote vinafikiwa na huduma ya umeme.

Alifafanua kuwa changamoto za kijiografia katika ukanda huo, ikiwemo usafirishaji wa vifaa kwa njia ya maji na kupandishwa milimani, ndizo zilizosababisha REA kulichagua jeshi kutekeleza mradi huo.

“Maelekezo ya Bodi yametutaka kuhakikisha wananchi wote walio tayari wanaunganishwa na umeme kabla mkandarasi hajaondoka. Tumejipanga kuyatekeleza kikamilifu,” alisema Mhandisi Nagu.

Miradi hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia REA za kuhakikisha upatikanaji wa umeme unawafikia wananchi wote wa vijijini, hususan wale wanaoishi katika maeneo ya pembezoni kama ukanda wa Ziwa Nyasa.











Na Mwandishi wetu- DODOMA

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, amesema Ofisi yake ikishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Menejimenti ya Maafa ipo katika hatua ya kuanzisha Kituo cha Operasheni ya Dharura katika Mkoa ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2004.

Dkt. Kazungu ameyasema hayo leo tarehe 27 Aprili,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa Timu ya kukabiliana na dharura ya Mkoa ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa pamoja na uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa.


Aidha, Dkt. Kazungu ameshukuru ujio wa elimu hiyo ndani ya Mkoa wa Dodoma akisema itasaidia kuwajenga kielimu Maafisa wa Mkoa ili waweze kupeleka elimu katika ngazi za Wilaya.


"Elimu hii itasaidia kuongeza ujuzi na weledi kwa Maafisa wa Mkoa kwani majanga haya yamekuwa na madhara mengi kwa jamii," alisema Dkt. Kazungu.


Pia, alisisitiza ukusanyaji wa taarifa kwa wakati na kabla ya majanga ili kurahihisisha kuyakabili pamoja na kuboresha mawasiliano ya karibu baina ya wananchi na Maafisa wa Mkoa.


"Lazima kuwepo ushirikiano baina yetu na Wananchi ili tuweze kupambana na maafa ndani ya Mkoa wetu wa Dodoma," alisisitiza.

Awali Kaimu Mkurugezi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Selestine Masalamadu aliupongeza Mkoa wa Dodoma kwa kuwa tayari kupokea elimu ya maafa na majanga na kusema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara hiyo ina jukumu la kuratibu shughuli za Kuzuia, Kupunguza Athari, Kujiandaa, Kukabiliana na Kurejesha hali baada ya maafa.

Vilvile, alisema kuwa Ofisi inaendelea kuratibu uanzishaji na uendeshaji wa Vituo vya Operesheni na Mawasiliano ya Dharura vya Mikoa pamoja na Timu za kukabiliana na dharura , ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Usimamaizi wa Maafa ya Mwaka 2004, Sheria ya Usimamaizi wa maafa Na. 6 ya mwaka 2022 na kanuni zake.


“Lengo la mafunzo haya ni kuimarisha uwezo wa Mkoa kuratibu shughuli za usimamaizi wa maafa ili kupunguza madhara wakati wa dharura. Mafunzo haya yatawajengea uwezo washiriki katika maandalizi, uratibu wa taarifa, mwitikio wa haraka, usimamizi rasilimali na utoaji wa huduma kwa waathirika,” alifafanua Kanali Masalamadu.


Aidha, alibainisha kwamba kila Mkoa unatakiwa kuwa na chumba maalum kwa ajili ya kuratibu shughuli za maafa na dharura huku akihimiza kuharakishwa kwa upatikanaji wa chumba chenye sifa stahiki kuwezesha uanzishwaji kamili wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Mkoa wa Dodoma.


Top News