Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) kwa kushirikiana na Shirika la ADAP (Association for the Development of Protected Areas) imeongoza hatua za uanzishwaji wa Jukwaa la Wadau wa Uyoga nchini, hatua itakayowezesha wadau wa Sekta ya Uyoga kunufaika kiuchumi na kuongeza kipato kupitia maendeleo ya zao hilo.

Akizungumza leo Machi 13, 2026 katika Makao Makuu ya TAFORI, Morogoro, wakati wa mkutano wa Uanzishwaji wa Jukwaa la Wadau wa Uyoga Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI, Dkt. Revocatus Mushumbusi, alisema jukwaa hilo litaratibu juhudi za Wadau wa Sekta ya Uyoga nchini kwa kuwawezesha kubadilishana maarifa na uzoefu pamoja na kuendeleza sekta hiyo.

Alisema kuanzishwa kwa jukwaa hilo kunalenga kuchangia maendeleo ya ustawi wa uhifadhi wa misitu, uchumi wa wananchi na kuongeza mchango wa zao hili katika pato la Taifa.

Aidha, alisema jukwaa hili litakuwa chombo muhimu cha kutoa ushauri wa kisera, kuhamasisha uwekezaji na kuimarisha ushirikiano wa Kitaifa na Kimataifa.

“Ni matumaini yangu kuwa kupitia chombo hiki, Wadau wataibua mawazo mapya, kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati madhubuti itakayosaidia kuendeleza Sekta ya Uyoga, usalama wa chakula, maendeleo ya uchumi yanayoweza kumgusa Mwananchi moja kwa moja na uhifadhi wa mazingira,” alisema.

Dkt. Mushumbusi alisisitiza ni muhimu kuimarisha tafiti za Kisayansi kuhusu aina na thamani ya uyoga ili zao hili liweze kutoa mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa. Aliongeza kuwa hatua hiyo iende sambamba na kujenga uwezo wa jamii katika kutambua uyoga unaoliwa na wenye sumu, pamoja na kuendeleza teknolojia za uongezaji thamani na kuimarisha masoko ya bidhaa za uyoga.

Alisema uyoga una mchango katika utekelezaji wa Sera mbalimbali za Taifa, ikiwemo Sera za Taifa za Kilimo na Lishe kwa kuongeza upatikanaji wa chakula chenye virutubisho muhimu. Pia alieleza kuwa maendeleo ya zao hilo yanaweza kuchochea ukuaji wa viwanda vidogo na vya kati kupitia uongezaji thamani kama ukaushaji, usindikaji na ufungashaji wa uyoga, hali itakayosaidia kuongeza ajira na kipato kwa Wananachi na hasa makundi maalumu ya kijamii wakiwepo Wanawake na Vijana.

Hatua ya kuanzishwa kwa Jukwaa la Uyoga nchini imefuata baada ya kufanyika kwa Warsha ya Wadau wa Uyoga iliyofanyika Mkoa wa Tabora mwezi Februari, 2025.

Mkutano huo umehudhuriwa na Wadau kutoka Shirika la ADAP, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA), Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela(NM-AIST), Wizara ya Mambo ya Ndani, pamoja na Wakusanyaji na Wafanyabiashara wa Uyoga.


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imefanya ziara ya kikazi mkoani Geita kukagua miradi inayosimamiwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), ambapo imemwagiwa sifa kwa mapinduzi ya teknolojia kwa wachimbaji wadogo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo katika eneo la Katente, Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, ameeleza kuwa serikali kupitia STAMICO imejikita kuhakikisha wachimbaji wadogo wanajifunza kwa nadharia na vitendo.

Dkt. Kiruswa amebainisha kuwa kituo hicho kinahudumia zaidi ya wachimbaji wadogo 1,019, ambao sasa wana uwezo wa kuleta marudio yao (mbare) na kuondoka na dhahabu iliyo safi ndani ya muda mfupi kutokana na matumizi ya teknolojia ya kisasa ya CIP.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha vituo vya mfano vinavyowasogezea wataalam karibu na wachimbaji.

"Ni wakati sasa kwa STAMICO na Wizara ya Madini kuona namna ya kuongeza ukubwa wa vituo hivi ili kutoa huduma kwa wachimbaji wengi zaidi na kwa uharaka zaidi," alisisitiza Mhe. Mgalu.

Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO, Bw. Deusdedith Magala, ametoa shukrani kwa Kamati hiyo kwa kuridhishwa na uwekezaji wa shirika hilo. Amesema jitihada hizo zinalenga kuhakikisha huduma za serikali zinafika moja kwa moja kwa walengwa katika sekta ya madini.











Na: Mwandishi Wetu

Wanachama wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), tawi la China (Diaspora), limeandaa Kongamano la Siku ya Kimataifa ya Wanawake 2026 kwa njia ya mtandao (Google Meeting) ili kujadili masuala mbalimbali ya kimaendeleo yamuhusuyo mwanamke.

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika Machi 15, 2026, majira ya saa tisa kamili alasiri hadi saa kumi na mbili kamili jioni. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) na Mbunge wa Viti Maalum, Mary Chatanda, anatarajiwa kushiriki Kongamano hilo akiwa Mgeni Rasmi. 

"Nimefurahi kupata mwaliko huu ambao kama wanawake tutajadili masuala mbalimbali ya kumuinua mwanamke kimaendeleo na changamoto zinazomkabili mwanamke kama tunavyojua mwanamke ni nguzo na kiungo muhimu katika maendeleo kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa. Kwa kweli tunajivunia kuona mwanamke mwenzetu, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, akionyesha uwezo mkubwa wa kiuongozi," amesema Chatanda.

Viongozi wengine watakaoshiriki Kongamano hilo la Wanawake ni pamoja na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) anayeshughulikia Masuala ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa - SUKI, Rabia Hamid, Mbunge wa Viti Maalum Vijana, Timida Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Rebeca Nsemwa na Mkuu wa wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva.

Wanachama wa CCM waishio nchini China wameandaa kongamano hilo ikiwa ni njia ya kuenzi mchango wa mwanamke katika maendeleo ya nchi. Ikumbukwe Siku ya Kimataifa ya Wanawake huadhimishwa kila mwaka ifikapo Tarehe 08 Machi, ambapo kwa mwaka huu 2026, maadhimisho hayo yamechagizwa na kaulimbiu isemayo " Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi Kufikia Dira 2050."



Cameroon-born, LA-raised Afrofusion artist releases her most personal work yet — a mid-tempo empowerment anthem produced by acclaimed producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated mixing engineer Giggz

LOS ANGELES, CA — March 6, 2026 — Nella, the Cameroonian-born, Bamiléké Afrofusion artist raising from Los Angeles and Houston, today announces the release of her new single “LUKAKU,” available now on Spotify, Apple Music, Boomplay, Audiomack, and YouTube.

LUKAKU is Nella’s most fully realized statement to date — a mid-tempo empowerment anthem that flips the Afrobeats tradition of pursuit and longing on its head. Where much of the genre celebrates the chase, LUKAKU is the sound of a woman who has stopped running and stopped waiting. Built on a steady 4/4 groove, syncopated bass, plucked electric guitar, and textured percussion, the production balances dancefloor rhythm with emotional restraint — a minor-key progression that gives the record depth while layered harmonies and polished vocals place it firmly in modern Afrobeats.



“I no fi chase. I no be Lukaku,” she declares in West African Pidgin — a language spoken across Nigeria, Cameroon, Ghana and the diaspora, and one that gives the hook its communal, chantable power. The reference is to the striker known for dribbling defenders: Nella refuses to be dribbled, chased, or played. The song moves between English and Pidgin, and the production — crafted by acclaimed producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated engineer Giggz — is globally resonant and unmistakably hers. Sonically, it sits at the intersection of Wizkid’s rhythmic subtlety, the unshakeable cool of early Sade, and the melodic confidence of Tems and Ayra Starr.

LUKAKU offers something genuinely underrepresented in music: a mid-tempo groove that empowers without bitterness, detaches without drama, and lets women walk away without asking to be chased. “Now my feelings stuck on rewind” — not moving forward, not chasing, just pausing. It is the strange peace of not caring enough to fast-forward anymore — emotional intelligence delivered with the vulnerability of Jorja Smith and the cool self-possession of Rihanna’s ANTI era. Produced by acclaimed music producer Mystro Sugar and mixed by Grammy-nominated mixing engineer and producer Giggz, LUKAKU arrives as the emotional centrepiece of a catalog that has amassed over 1.5 million total streams and a devoted global following Nella calls the Moonbeams.

“I gave you all my good years, it blew away to the wind. Now I’m gone. Bye bye.”

— Nella, LUKAKU

The song sits at a specific emotional crossroads in Nella’s discography. Her previous single, No Visa — released October 2025 — is, in chronological terms, its prequel: the release that came before LUKAKU. But as a piece of storytelling, No Visa is the sequel. It depicts a woman who has already done the internal work — who now loves fully and without walls. LUKAKU is the earlier chapter: the reckoning of a woman who once did not love herself, named what she gave away, and chose to reclaim it.

LUKAKU will be released via OneRPM distribution and is accompanied by a content strategy rooted entirely in Nella’s authentic story. Her father dancing to the song became one of the most-shared moments of her release campaign. The “good girl turn bad” origin story behind the song’s key lyric generated the highest saves and shares of any post in her career to date.


ABOUT NELLA


Nella is a Bamiléké Afrofusion artist born in Yaoundé, Cameroon, raised between Los Angeles and Houston. A healthcare provider by training, she is the creator of a sound that belongs to no genre and speaks to everyone who has ever had to choose between who they were told to be and who they actually are.

Her father played guitar; her mother danced. These were not influences — they were architecture. Nella founded her high school’s first Hip-Hop club in California, set music aside to build a career in healthcare, and returned to the studio not as a luxury but as a lifeline. Her catalog moves through English, French, West African Pidgin, and Fèfè, fusing Makossa, Bikutsi, Afrobeats, Amapiano, and R&B into a style that is equally celebration and confession.

Inspired by Tems, Tiwa Savage, Charlotte Dipanda, Beyoncé, and Teyana Taylor, Nella has been featured by Fox 21, GQ South Africa, The Guardian, Soundcity, Chop Daily, and Not Just Okay. With over 1.5 million streams, a growing global audience, and a community of Moonbeams who do not just follow her but claim her — Nella is not a rising artist. She is an arrived one.



STREAM LUKAKU


Spotify: open.spotify.com/artist/1srgbcQlCI56byuqb1FphT

Apple Music: music.apple.com/us/artist/nella/1764690030

YouTube: youtube.com/watch?v=LpWPlN68DoI

Boomplay: boomplay.com/artists/101354562

Audiomack: audiomack.com/nella-355


FOLLOW NELLA


Instagram: instagram.com/nellaleen_/

TikTok: tiktok.com/@nellaleen — 358.4K followers

YouTube Channel: youtube.com/@nellaleen

Facebook: facebook.com/nellasongbird/


PRESS CONTACT


Kris Noulaheu

Press / PR — Songbirds Media

nellasongbird@gmail.com


© 2026 Nella Music · Songbirds Media · OneRPM Distribution · All Rights Reserved



-Akemea watumishi wanaowaelekeza wananchi kununua dawa nje ya hospitali

-Aonya utapeli wa ardhi za vijiji

-Akemea wakandarasi wanaolipwa fedha za miradi lakini hawawalipi mafundi


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu mfumo wa upatikanaji wa dawa katika hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Ametoa agizo hilo leo Jumapili (Machi 15, 2026) alipokuwa akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nsimbo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Songambele mkoani Katavi, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Amesema Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa katika hospitali na vituo vya afya, lakini bado baadhi ya wananchi wanapofika kutafuta huduma wanaelekezwa kwenda kununua dawa katika maduka binafsi nje ya hospitali.

“Takwimu zinaonesha tuna utoshelevu wa dawa lakini mwananchi akienda hospitalini anaelekezwa mtaani kwenda kununua dawa. Huu mchezo haukubaliki. Duka la mtaani linapata wapi dawa ambayo Serikali haiwezi ikapata?” amesema.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu amesema ni muhimu kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini namna fedha za ununuzi wa dawa zinavyotumika pamoja na mfumo wa upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu ameonya tabia ya baadhi ya viongozi kuuza ardhi ya vijiji kwa njia zisizo halali na kusababisha migogoro ya ardhi katika jamii.

“Hata tukigombana ardhi haiongezeki. Binadamu tunaongezeka lakini ardhi haiongezeki. Hata tukipigana ardhi haiongezeki, kwa hiyo tuepuke kuchukiana kwa misingi hiyo,” amesema.

Amesema Serikali haitavumilia vitendo vya utapeli wa ardhi vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wasiowaadilifu.

“Watu wa aina hii wakishagundulika wasidunde mtaani lazima wafike kwenye mkono wa sheria. Wanataka kuvunja undugu wetu kwa tamaa na ubinafsi,” amesema.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameonya wakandarasi wanaolipwa fedha za miradi ya Serikali lakini wanashindwa kuwalipa mafundi na wakandarasi wadogo waliotekeleza kazi hizo.

“Mkandarasi anapewa kazi anaajiri mafundi, anatoa subcontract kwa wengine, yeye analipwa fedha yote ya mradi lakini hawalipi wale waliofanya kazi. Watu wa aina hiyo wasakwe popote pale walipo na wasiwe huru mpaka wawalipe watu ambao wameshafanya kazi,” amesema.

Amesema vitendo hivyo vinawanyima haki wananchi waliotekeleza kazi kwa uaminifu na vinaweza kuifanya jamii kuilaumu Serikali wakati fedha za miradi tayari zimeshalipwa kwa wakandarasi.

“Hii kuchukua fedha Serikali imeshalipa halafu wananchi wetu ambao wamefanya kazi hawajalipwa ni kuwasababishia umaskini watu ambao wamefanya kazi kwa uaminifu,” amesema.

Katika mkutano huo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo sekta za afya, elimu na miundombinu.

Amesema katika kipindi cha miaka minne iliyopita Serikali imejenga hospitali za wilaya 119, vituo vya afya 649 pamoja na zahanati zaidi ya 2,700 nchini kote kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Aidha, amesema Serikali imejenga zaidi ya shule za sekondari 1,300 pamoja na shule za ufundi zaidi ya 103 ili kuwawezesha vijana kupata elimu na ujuzi unaowawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.







Maafisa wa kulinda walaji kutoka Tume ya Ushindani (FCC) wametoa elimu kwa wananchi wa Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani kuhusu haki na wajibu wa mlaji, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji duniani yanayotarajiwa kufanyika Machi 31, 2026.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wananchi uelewa kuhusu namna ya kutambua bidhaa na huduma zenye ubora, pamoja na hatua wanazopaswa kuchukua pale wanapokutana na udanganyifu au ukiukwaji wa haki zao kama walaji. Wananchi pia wamehimizwa kuhifadhi risiti za manunuzi na kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini vitendo vya biashara visivyozingatia sheria.

Maafisa hao wameeleza kuwa lengo la utoaji wa elimu hiyo ni kuhakikisha walaji wanakuwa na uelewa wa kutosha ili kujilinda dhidi ya bidhaa bandia, bei zisizo halali na huduma zisizokidhi viwango. Aidha, wamesisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda maslahi yao kwa kufahamu haki na wajibu wao wanapofanya manunuzi au kutumia huduma mbalimbali.

Maadhimisho ya Siku ya Kumlinda Mlaji hufanyika kila mwaka duniani kote kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji na kuhamasisha biashara kufuata misingi ya haki, uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa bidhaa na huduma. Serikali na taasisi mbalimbali nchini huendelea kutumia maadhimisho hayo kutoa elimu kwa jamii ili kujenga mazingira salama na yenye ushindani wa haki sokoni.






 

Kuna methali isemayo “Asiyejua maana haambiwi maana “ lakini Ngorongoro leo itakuambia maana ya Nyayo za Laetoli.

Nyayo hizi ni za kihistoria na ni sehemu pekee duniani ambayo mafundi Viatu ulimwenguni wanaweza kufika na kutengeneza Viatu vya kihistoria vinavyoweza kushinda nishani ya Nobel kutokana na Nyayo za Laetoli zilivyo.

Katika eneo la Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro, tarehe 24, Julai mwaka 1978, Mtafiti maarufu wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey na timu yake iliyomhusisha Dkt. Paul Abell waligundua nyayo za zamadamu katika eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano inayoaminika kuwa ililipuka katika mojawapo wa milima ya Ngorongoro miaka milion 3.6 iliyopita. 

Wataalamu hawa wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis.

Nyayo za Zamadamu katika eneo la Laetoli ni ushahidi wa pekee na wa bayana duniani kote usiopingika kwamba zamadamu (Hominin) kwa mara ya kwanza walianza kusimama wima na kutembea kwa miguu miwili katika eneo la Laetoli Ngorongoro Tanzania miaka milioni 3.6 iliyopita.

 Binadamu hawa waliotembea wima kwa miguu miwili wametokana na babu/bibi mmoja aliyeishi miaka takribani millioni 7 iliyopita. 

Mwanadamu aliyepo Tandahimba, Gamboshi kule Bariadi, Tandale kwa mtogole, Mbagala Zakiem na yule aliyepo Jerusalemu, Macca, Dubai, New York, London, Johannesburg, Tehran, Gaza, Misri hadi Sudan na Mumbai wametokana na babu na bibi mmoja.

Katika kuthibitisha uhai, Nyayo za zamadamu ndizo za kustaajabisha katika eneo la Laetoli, zipo nyayo za wanyama wengine wa kale kama vile nyayo za tembo, twiga, faru na wanyama ndogo kama sungura, kanga na aina za wadudu.

Kwa nyayo za Laetoli zilivyo, mafundi Viatu na wamiliki wa viwanda vya Viatu duniani wanaweza kufika katika Eneo  hilo ili kupata  ujuzi zaidi wa namna ya kutengeneza Viatu vya kihistoria.

 Karibu kwetu Ngorongoro ambapo kila ukilala kuna ndoto ya maajabu inakuita


Muonekano wa Nyayo za Laetoli zilizoachwa na jamii za watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amepongeza jitihada za Benki ya NBC za kuendelea kupanua wigo wa ujumuishi wa kifedha kupitia huduma yake ya kibenki isiyo na riba, La Riba (Islamic Banking), akisema huduma hiyo imewafungulia Waislamu milango mipya ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi bila kwenda kinyume na misingi ya imani yao.

Bi. Senyamule aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dodoma wakati akiongoza hafla ya futari iliyoandaliwa na NBC kwa ajili ya wateja wake wenye imani ya Kiislamu pamoja na wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini na serikali. Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi na maofisa wa benki hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bi. Senyamule alisema huduma za kifedha zinazozingatia misingi ya Kiislamu zimekuwa chachu muhimu ya kuwawezesha waumini wa dini hiyo kushiriki kikamilifu katika mfumo rasmi wa kifedha, hivyo kuongeza kasi ya shughuli za kiuchumi katika jamii.

“Huduma ya La Riba imewafungulia wenzetu wenye imani ya Kiislamu milango ya kushiriki kikamilifu katika huduma za kifedha bila hofu ya kwenda kinyume na misingi ya dini yao. Hii ni hatua muhimu sana katika kuimarisha ujumuishi wa kifedha na kuhamasisha maendeleo ya wananchi,” alisema Bi. Senyamule.

Alisema uwepo wa huduma kama hiyo unachochea wananchi wengi zaidi kutumia taasisi rasmi za kifedha katika kukuza biashara, kilimo na shughuli nyingine za kiuchumi, jambo linalochangia kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake, Bw. Foya alisema huduma ya La Riba imeendelea kupata mwitikio mkubwa kutoka kwa wateja wenye imani ya Kiislamu nchini, huku ikitoa fursa kwao kupata huduma za kifedha zinazozingatia misingi ya dini yao.

Alisema kupitia dirisha hilo, zaidi ya wateja 24,000 wanahudumiwa kwa sasa, wakiwa na amana zinazozidi shilingi bilioni 90, huku uwezeshaji wa kifedha uliotolewa kupitia mfumo huo ukizidi shilingi bilioni 48.

“Takwimu hizi zinaonesha wazi kuwa huduma za La Riba zimepokelewa vizuri na wateja wetu wenye imani ya Kiislamu. Tutaendelea kuimarisha huduma hizi ili kuwapa wateja wetu suluhisho za kifedha zinazolingana na mahitaji na imani zao,” alisema Bw. Foya.

Aliongeza kuwa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, benki hiyo inaona ni muhimu kuimarisha zaidi mahusiano yake na wateja pamoja na wadau kwa kushirikiana nao katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Bw. Foya alibainisha kuwa NBC imefanikiwa kubuni na kutoa huduma mbalimbali za kifedha zinazozingatia misingi ya Kiislamu, zikiwemo akaunti za akiba na biashara, akaunti za uwekezaji wa muda maalum (Fixed Investment Accounts), pamoja na huduma za uwezeshaji wa kifedha kupitia mfumo wa Murabaha.

Katika hatua nyingine, Bi. Senyamule aliipongeza NBC kwa mchango wake katika kuendeleza michezo na ustawi wa jamii kupitia tukio la NBC Dodoma Marathon, ambalo limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuchochea uchumi wa jiji la Dodoma.

Alisema mbio hizo ambazo mwaka uliopita zilivutia zaidi ya washiriki 12,000, zimekuwa zikichochea shughuli za kiuchumi katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, utalii na huduma, huku pia zikisaidia kukusanya fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.

Akizungumzia mbio hizo, Bw. Foya alisisitiza kuwa NBC itaendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo ya jamii kupitia miradi mbalimbali ya kijamii, ikiwemo kuendeleza mbio hizo ambazo mbali na kukuza michezo pia zinachangia kuokoa maisha kupitia miradi ya afya.




Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (kushoto) akipokea zawadi maalum ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan kutoka kwa Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (katikati) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Anaeshuhudia ni Mkuu wa Kanda ya Kati wa benki ya NBC, Bw Miraji Msuya. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (mbele) akiwaongoza wageni waalikwa kupata futari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (katikati) akifuatilia matukio tofauti wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (kulia) na Meneja wa NBC tawi la Dodoma Bi Happiness Kizigira. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Meneja Uhusiano wa Huduma za Kibenki zinazozingatia Sheria za Imani ya Kiislam (Islamic Banking) wa benki ya NBC Bw Ally Abdul (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.


Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya (pichani) akifuatilia matukio wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini.






Hafla hiyo ilihusisha utoaji wa zawadi mbalimbali za mwezi wa Ramadhan kutoka NBC.









Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wateja na maofisa wa benki ya NBC wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha uwepo wa wateja na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa serikali na dini. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Fedha wa NBC, Rayson Foya, Mkuu wa Benki ya NBC Kanda ya Pwani Bi Zubeider Haroun (kulia walioketi) na kulia kwake ni Mkuu wa Kanda ya Kati wa benki ya NBC, Bw Miraji Msuya na Mwakilishi wa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh Ahmed Saidi (kushoto walioketi)

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuhakikisha mita za umeme zinahakikiwa kikamilifu kabla ya kufungwa kwa ajili ya matumizi, kwa kuzingatia sheria zilizopo ili kulinda haki za watumiaji.

Aidha, Kamati hiyo imeipongeza WMA kwa jitihada za uhakiki na ukaguzi wa vipimo mbalimbali, ikiwemo mita za maji, huku ikiitaka Wakala hiyo kuendelea kusimamia kwa ukaribu vipimo katika sekta ya ujenzi ili kupunguza malalamiko ya wananchi yanayotokana na bidhaa hizo.

Hayo yameelezwa leo Machi 14, 2026, na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, wakati wa ziara ya kikazi katika Kituo cha WMA cha Uhakiki wa Vipimo Misugusugu mkoani Pwani kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kujionea shughuli za uhakiki wa vipimo zinavyotekelezwa kituoni hapo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, aliihakikishia Kamati kuwa wizara itatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa.

Alisisitiza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha WMA inasimamia matumizi ya vipimo sahihi katika uzalishaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali, pamoja na Uhakiki wa mita za umeme na maji, ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alibainisha kuwa uhakiki wa vipimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa huo. Alieleza kuwa kwa sasa Mkoa wa Pwani una jumla ya viwanda 1,688, vikiwemo viwanda vikubwa 199 na vidogo sana 1,017, hivyo uhakiki wa usahihi wa Vipimo ni nyenzo muhimu katika kuvutia uwekezaji zaidi.

Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, alisema kuwa ukaguzi na uhakiki wa vipimo una nafasi kubwa katika kuhakikisha haki na usawa baina ya pande mbili zinazofanya biashara.

Pia, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanatumia vipimo vilivyohakikiwa, huku akiwasihi watoa huduma kuzingatia uadilifu kwa kutoa huduma kupitia vipimo sahihi ili kuleta usawa na kuhakikisha bidhaa zinazonunuliwa zinaendana na thamani halisi ya fedha.


By Moses Ntandu, Dar es Salaam, Tanzania

On the land of Sudan, this month of Ramadan has not arrived with peace or hope. Instead, it has come to a country exhausted by war, torn apart by pain, and immersed in the grief of thousands of families who have lost their loved ones.

The capital city, Khartoum, once the heart of life and commerce, now bears the marks of bullets, destroyed buildings, and streets filled with memories of war. Despite the great sacrifices and relentless efforts made by patriotic Sudanese youth through the government army, led by the commander who carries the vision of the nation’s liberation, Abdel Fattah al-Burhan, to ensure that peace, safety, and stability return to every part of the country.

The fighting between the Sudanese Armed Forces and the rebel militia Rapid Support Forces has turned large parts of the country into a field of humanitarian disaster. The regions of Darfur, Kordofan, and Blue Nile State have become living proof of how war can destroy a nation within a short time.

But the most painful truth is this: most of those who have died in this war are not soldiers. They are civilians. They are children who had dreams of going to school. They are mothers who were preparing food for their families. They are elderly people who were praying for peace in their country.

The world can not pretend not to see this situation, while those responsible act as though they know nothing.

The war in Sudan is not merely an internal political conflict, but a crisis initiated and engineered from outside the country for specific purposes. Will the world remain silent as this nation collapses? Will political leaders and those who once legitimized or supported this war continue hiding behind political language?

History teaches us that wars do not continue because of bullets alone. They persist because there are people who celebrate them, legitimize them, or support them in various ways, whether through money, military supplies, propaganda, or deliberate silence. Every word that incites hatred, every aid package sent to fighters, and every piece of propaganda that justifies bloodshed increases the number of new graves of innocent civilians.

Now is the time for truth. Now is the time for moral accountability. All individuals, political groups, or international stakeholders who once supported or legitimized armed rebellion in Sudan should come forward publicly and apologize.

Countries such as the United Arab Emirates, by openly supporting this war, providing logistics and various forms of military assistance to the rebels; nations that hosted those rebels, such as Kenya leading to a major diplomatic dispute with Sudan and even neighboring Ethiopia, accused of establishing training camps for rebels and creating diplomatic tensions, should openly apologize to the people of Sudan and to the world for their contribution—whether direct or indirect—to this great catastrophe.

Apologizing is not a weakness; it is the courage to accept the truth, and it is the first step toward restoring human dignity.

Peace can not be built on hypocrisy. No nation can be rebuilt on foundations of hypocrisy, propaganda, and deliberate silence. Sudan will need many years to rebuild itself to reconstruct schools, hospitals, its economy, and above all to heal the hearts of its people.




But that rebuilding can not begin without truth. And the truth is this: the blood of Sudanese civilians should never become part of anyone’s political games, or the ambitions of any group or nation seeking selfish interests while disregarding the lives of innocent people—even worse when they pursue those interests inside Sudan itself.

To the international community, political leaders, activists, and everyone with a conscience seeking peace and global security: Sudan is not merely a statistic in news reports.

Sudan is a nation of real people with families, dreams, and hopes. If the world continues to remain silent in the face of this disaster, history will judge that silence as quiet participation in the suffering of the Sudanese people. Because in the end, one truth remains clear.

Wars may be started by a few, but their pain is carried by millions of innocent people. The blood of Sudanese the blood of children, women, and the elderly cannot and must never be ignored.

A small example of the pain of war has recently been felt in the UAE following tensions with Iran. They have only been slightly attacked, yet their outcry has been loud after experiencing just a small fraction of what resembles the suffering occurring in Sudan.

Clearly, what you do not wish to be done to you, you should not do to others, treat others as you wish to be treated, as reflected in the Arabic saying: “Kama tadinu tudan” (As you judge, so shall you be judged).

As we approach the final days of the holy month of Ramadan and the season of Lent, it would be appropriate for all those who know within their conscience that they have been involved in the ongoing disaster in Sudan the deaths of innocent civilians and the destruction of infrastructure, private property, and public property to return quickly to their Creator, repent for these sins, sincerely seek forgiveness, and publicly apologize to the people of Sudan and their government.

The government’s efforts have greatly helped restore peace in many cities, while stability and security are increasingly prevailing in the capital, Khartoum. Recently, the sounds of joy and celebration were heard at Khartoum International Airport after the landing of the second passenger plane, raising hope that peace may soon return to the country as it once was.

The conclusion of this analysis is simple: the truth can not be hidden forever.

Every drop of blood spilt on Sudanese soil is testimony to a pain the world cannot ignore—from the ruined streets of Khartoum to the burned villages across the country, including Darfur. The cries of the Sudanese people call for justice, accountability, and an end to the war.

History will not only record those who fought in the war, but also those who remained silent, those who supported it, and those who watched without speaking while a nation burned.

That is why the time for truth has come: the time to admit mistakes, apologize, and stand on the side of peace.

Because in the end, a nation can be rebuilt and buildings can be reconstructed—but lives that have been lost will never return. And for the children of Sudan, for the future of this nation, and for the dignity of the entire world, the blood of Sudan must mark the end of war not the beginning of a new silence.



Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.

Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.

Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.

Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter




Ramadan Kareem. 🌙


Top News