NAIBU Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Rueben Kwagilwa akizungumza na vyombo vya habari Julai 2,2026 Jijini Tanga kuhusu tamko la Serikali kuhusiana na maandalizi ya Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12) unaotarajiwa kufanyika Kuanzia Octoba 6 hadi 9 Mwaka huu
Serikali imezitaka Wizara, Taasisi za Umma, Sekta Binafsi, Watafiti na Mashirika ya Kiraia kuchangamkia fursa ya Tanzania kuwa mwenyeji wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP 12).

Hayo yamesemwa leo Julai 2, 2026 Jijini Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu maandalizi ya Tanzania kuelekea Mkutano huo unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian akionesha kitabu chenye taarifa ya utafiti kuhusu masuala ya mazingira mkoani humo wakati wa mkutano wa Naibu Waziri Ofisi ya Makau a Rais (Muungano na Mazingira )Mhe Rueben Kwagilwa na waandishi wa habarai Julai 2 mwaka huu kuhusu tamko la Serikali kuhusu maandalizi ya mkutano wa 12 wa nchi wanachama wa mkataba awa Nairobi (COP 12) unaotarajiwa kufanyika nchini kuanzia Octoba 6-9 mwaka huu


Naibu Waziri Kwagilwa amesema katika Mkutano wa 11 wa Nchi Wanachama uliofanyika nchini Madagasca mwaka 2024, Tanzania ilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Mkataba wa Nairobi kwa kipindi cha miaka miwili hadi Disemba Mwaka 2026 pamoja na kuteuliwa kuwa mwenyeji wa COP12.


“Mkutano wa COP12 utajadili utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mkataba kwa kipindi cha mwaka 2024–2026 pamoja na kujadili masuala muhimu ikiwemo hifadhi na urejeshwaji wa mifumo ikolojia ya bahari kama mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari” amesema Mhe. Kwagilwa.

Baadhi ya watendaji waandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais wakifuatilia tamko la Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira ) Mhe.Rueben Kwagilwa wakati alipozungumza na waandishi wa habari Jijini Tanga kuhusu maandalizi ya mkutano wa 12 wa nchi wanachama wa mkataba awa Nairobi (COP 12) unaotarajiwa kufanyika nchini kuanzia Octoba 6-9 mwaka huu

Ameongeza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuipa kipaumbele sekta ya mazingira na uhifadhi wa rasilimali za bahari ili kuimarisha uhifadhi wa rasilimali za bahari, mito, maziwa, maji chini ya ardhi na maeneo oevu.

Wadau wa Mazingira na Wananchi wa Mkoa wa Tanga wakifuatilia tamko la Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Reuben Kwagilwa wakati alipozungumza na waandishi wa habari Jijini Tanga kuhusu maandalizi ya mkutano wa 12 wa nchi wanachama wa mkataba awa Nairobi (COP 12) unaotarajiwa kufanyika nchini kuanzia Octoba 6-9 mwaka huu

Kwa mujibu wa Naibu Waziri Kwagilwa, amesema Dira 2050 imeitambua sekta ya uchumi wa Buluu kuwa miongoni mwa sekta za kimkakati zinazokusudia kuleta mageuzi ya maendeleo endelevu na kuchangia ukuaji wa kijamii, kiuchumi na kiikolojia.


Amesema kuwa Tanzania ni nchi ya pwani yenye fursa kubwa ya kunufaika na sekta ya uchumi wa buluu kupitia uvuvi, nishati, usafirishaji, utalii, madini, mazingira na viwanda, hivyo mkutano huo utaliwezesha taifa kuwa katika nafasi bora ya kufikia maendeleo endelevu.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amesema matokeo ya utafiti uliofanyika mkoani humo yanaonyesha athari za mabadiliko ya tabianchi zimeanza kuathiri kwa kiwango kikubwa shughuli za uvuvi na ukuzaji wa viumbe maji, hususan kilimo cha mwani.

Amesema utafiti uliofanyika kati ya mwaka 2021 na 2025 umebaini kuwa joto la bahari limeongezeka kutoka nyuzi joto 25.6 mwaka 2021 hadi kufikia nyuzi joto 28.39 mwaka 2024, hali inayobadili mfumo wa ikolojia wa bahari na kuathiri uzalishaji katika sekta ya uvuvi.


"Tumeshuhudia ongezeko la karibu nyuzi joto tatu baharini, huku siku za wavuvi kwenda kuvua zikishuka kutoka siku 221 mwaka 2021 hadi siku 170 kutokana na upepo mkali na hatari ya usalama baharini. Pia mavuno ya samaki yamepungua kwa wastani wa asilimia 25 hadi 30," amesema Dkt. Burian.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Balozi Baraka Luvanda amesema mkutano wa COP 12 utahusisha washiriki takribani 500-600 ikiwemo viongozi wa nchi, wataalamu na wadau mbalimbali.

Ameongeza kuwa lengo la tamko hilo la Serikali ni kuweka msingi wa maandalizi ya kina, ikiwa ni pamoja na kubainisha vipaumbele vya Taifa, na kupanga mikakati ya ushiriki ili kuhakikisha maandalizi yanafanyika kwa ufanisi na kwa wakati.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa Mkataba wa Nairobi unaohusu Hifadhi, Usimamizi na Uendelezaji wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi.

Mkataba huu ulisainiwa tarehe 21 Juni 1985 na unatekelezwa chini ya usimamizi wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).




Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, amewataka waendesha maghala kuzingatia uadilifu, uwajibikaji na utoaji wa huduma bora ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Akifungua kikao maalumu cha waendesha maghala kilichofanyika mjini Morogoro Julai 1, 2026, Bangu, amesema waendesha ghala wanapaswa kuendana na wakati kwa kuwa waadilifu, kutoa huduma zenye viwango vya juu na kuhakikisha mfumo wa stakabadhi za ghala unaendelea kuwa na tija kwa wakulima, wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Waendesha ghala Tanzania, Abdulikarim amesema kikao hicho kimeandaliwa kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu masuala mbalimbali ya kiutendaji, kujadili changamoto zinazowakabili pamoja na kutafuta suluhisho la kuboresha maslahi ya waendesha ghala kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na uendeshaji wa shughuli zao.

Ameongeza kuwa maazimio na maelekezo yaliyotolewa katika kikao hicho yatawasaidia waendesha ghala kuongeza ufanisi wa kazi zao na kuendelea kutoa huduma bora kwa wadau wote wa sekta ya kilimo.
Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Bw. Asangye Bangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Afisa Biashara kutoka Ubalozi wa Misri nchini Tanzania, Bw. Wael Aref, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kupanua masoko ya mazao na mifugo kati ya nchi hizo mbili.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo Julai 2, 2026 jijini Dar es Salaam ambapo Bw. Bangu ameelezea majukumu ya WRRB pamoja na namna Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unavyowawezesha wakulima na wazalishaji kupata masoko yenye ushindani, kuongeza thamani ya mazao yao, na kuunganishwa moja kwa moja na wanunuzi wa ndani na nje ya nchi.

Amesema mfumo huo umeendelea kuwa nyenzo muhimu katika sekta ya kilimo kwa kuweka mazingira ya uwazi, kuongeza ushindani wa bei, na kuhakikisha wazalishaji wanapata uhakika wa masoko yao.

Aidha, viongozi hao wamejadili pia uwezekano wa kupanua wigo wa ushirikiano huo kwa kuingiza mifugo hai katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kuongeza aina ya bidhaa zinazoweza kuuzwa kupitia mfumo huo na kufungua fursa mpya za biashara kati ya Tanzania na Misri.
-Asema mijadala iko huru kwa wabunge wa vyama vyote, aeleza wapinzani wanavyopewa nafasi

-Pia azungumzia maandalizi kuelekea historia miaka 100 ya Bunge la Jamhuri ya Muungano




Na Said Mwishehe,Michuzi TV


SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, amevunja ukimya huku akiwazodoa wale wanadai Bunge ni dhaifu na halina meno.

Kutokana na hali hiyo, amesema kuwa Bunge lililopo na yake yaliyopita hakuna lililo dhaifu kwani kazi kubwa inayofanyika ni kuisimamia Serikali pamoja na kuwawakilisha wananchi ikiwamo kutunga sheria mbalimbali pamoja na kusimamia ustawi wa jamii.

Akizungumza katika kikao kati yake na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu miaka 100 ya historia ya Bunge, ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa nyakati zote likiwamo Bunge analoliongoza bado anatoa uwanja sawa kwa wabunge wa upinzani picha ya uchache wao.

Aidha amesema na kuhoji kuwa mjadala wa Bunge kuonekana dhaifu lakini nyakati zote bado wabunge wa upinzani wamekuwa wakipewa haki sawa kama takwa la kidemokrasia linavyotaka.

“Ndugu zangu kuna mambo yanaendelea na kuibuliwa na baadhi ya vyama vya upinzani. Kumbukeni mwaka 2015 Katiba ilikuwa ileile ambapo wabunge wa upinzani walikuwa 102 ambapo kati ya hao Chadema walikuwa 69.

“Tena wakati wanashinda Tume ya Uchaguzi kwa wakati ule haikuwa na maboresho na kambi rasmi ya upinzani ikatambulika.

“… kwanini Bunge lile lilikuwa na nguvu, lakini nini maana yake mjadala hapa chama kimoja (hakutaja jina) chama kimoja kilipata mgombea toka CCM katika uchaguzi wa mwaka 2015 jambo lililowasaidia kuimarika zaidi na kupata wabunge wengi. Sasa wapo wapinzani lakini hawajaimarika.

“Hapa Dar es Salaam wapinzani waliweza kuongoza Halmashauri za Kinondoni, Ubungo na hata Ilala pia ambazo zilikuwa upinzani na hata kufikia baadhi yao kusema wapewe nafasi ili tuongoze,” amesema Spika Bunge

Ameongeza kazi ya Bunge ambayo inafanyika kwa miaka yote kwanza kuisimamia ustawi wa wananchi, kuisimamia Serikali pamoja na kitunga sheria jambo ambalo linaendelea kufanyika hadi sasa.

Katika kujenga hoja yake kuhusu Bunge analoliongoza alisisitiza kuwa hakuna Bunge dhaifu au Bunge imara kwani Bunge lolote kazi zake zinajulikana kusimamia ustawi wa jamii.


KAMATI SAA 72 BUNGENI


Spika Zungu amesema kutokana na kutoa haki kwa wabunge na wananchi baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 vyama vyote vya upinzani vimeweza kupata wabunge tisa wakati hata ukitoa hoja ili uungwe mkono lazima muwe wabunge 10 lakini upinzani wakisimama wanakuwa tisa.

“Zipo hoja nzuri huyu hapa Ado (Mbunge wa Tunduru ACT) hata akitoa hoja wanakuwa tisa wakati kanuni inataka wawe 10,” amesema.

Amefafanua licha ya hali hiyo na takwa la kikanuni lakini bado Rais Samia aliagiza kamati za Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Serikali za Mitaa (LAAC) ziongozwe na wapinzani licha ya uchache wao kama njia ya kuimarisha demokrasia.

“Ni nani asiyejua kwamba Rais Dkt Samia ndio amewarudisha nchini wapinzani wengine waliokimbia nchi kwa kuwataka warudi ili tujenge Taifa letu, haya ni mapenzi makubwa ya Rais Samia.

“Hata mnaposikia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali lakini kamati ambayo kwenye Mpira tunaita kamati ya saa 72 Kwa maana PAC na LAAC ndio wajibu wa kumwita kila aliyetajwa,” amesema.



MIAKA 100 YA BUNGE


Amesema kwa sasa Bunge lipo kwenye maandalizi ya kusheherekea miaka 100 tangu kilipoanzishwa chombo hicho wakati wa utawala wa ukoloni hadi ilipozaliwa Tanzania.

“Wapo wengine watahoji kwa nini tunawataja wakoloni lazima tuwataje ili tuone tulipotoka, tulipo na tunapokwenda.

“Kauli mbiu yetu katika kutimiza miaka 100 ya Bunge ni Historia yetu,Dira yetu,” amesema Spika Zungu.













Top News