Na Mwandishi Wetu

KATIBU wa Halmashauri Kuu(NEC)ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo Kenan Kihongosi amefanya kikao kazi na viongozi mbalimbali wa Chama hicho pamoja na wasanii wa Bendi ya TOT.

Kihongosi amefanya kikao kazi hicho leo katika Ofisi ndogo za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam ambapo katika kikao hicho ametumia nafasi hiyo kuelezea mipango na mikakati mbalimbali yenye lengo la kuiimarisha Chama hicho.

Aidha Kenan amewahakikishia viongozi walioshiriki kikao kazi hicho kwamba anatambua kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi Mkuu 2025 napia kwa lengo la kukifanya Chama Cha Mapinduzi kuendelea kuwatumikia wananchi ambao wamekuwa na matumaini makubwa na Chama hicho chini ya Mwenyekiti wao Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.









Mkuu wa Idara ya Masoko wa Benki ya Stanbic Tanzania, Neemarose Singo, mara baada ya kupokea tuzo ya Benki Bora ya Mwaka 2025 nchini Tanzania katika Tuzo za The Banker, zilizoandaliwa na jarida la Financial Times, kwenye hafla iliyofanyika jijini London, Uingereza hivi karibuni. Ameambatana na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo na waandaaji wa tuzo hizo

Benki ya Stanbic imetajwa kuwa Benki Bora Zaidi Tanzania kwa mwaka 2025 na jarida la The Banker, chapisho la kimataifa la masuala ya benki chini ya Financial Times.

 Tuzo hii inatambua utendaji mzuri wa kifedha wa Benki, ubunifu na mchango wake endelevu katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania.Tuzo hii inafuatia mchakato wa tathmini uliopima utendaji wa benki katika masoko ya Afrika. 

Hii ni mara ya nane kwa Stanbic kupokea heshima hii, jambo linaloimarisha nafasi yake kama moja ya taasisi za kifedha zinazoaminika na kudumisha viwango vya juu nchini Tanzania.

Katika soko lenye ushindani mkubwa, tuzo hii inatambua mchango mkubwa wa Stanbic katika sekta muhimu za uchumi wa Tanzania ikiwemo nishati na miundombinu, pamoja na kuendeleza ubunifu unaosaidia ukuaji wa biashara ndogo na za kati.

Katika kipindi cha hadi kufikia Juni 2025, Stanbic iliunga mkono ajenda ya viwanda ya Tanzania kwa kutoa zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 1 (takribani Shilingi trilioni 2.5), katika uwezeshaji wa maendeleo kwenye sekta za nishati, usafirishaji na zingine. 

Uwezeshaji huu uliwezesha utekelezaji wa miradi muhimu ya miundombinu ya kitaifa ikiwemo uboreshaji wa bandari, upanuzi wa gridi ya Taifa ya umeme na uwezeshaji katika mnyororo wa thamani wa gesi asilia.Jarida hilo la Uingereza pia lilitambua mchango wa Stanbic katika kuleta athari chanya kwa Watanzania. 

Kupitia uwekezaji wa kijamii katika elimu, afya, mazingira na elimu ya kifedha. Benki iliwanufaisha zaidi ya watu milioni 2 walioko sehemu mbali mbali nchini kwa mwaka 2025. 

Kiatamizi cha Stanbic Biashara Incubator kiliwafikia wajasiriamali takribani 5,000 kwa kuwapatia stadi za ujuzi wa vitendo uliowawezesha kuongeza uelewa wa kifedha, biashara, matumizi ya nishati safi na ushiriki katika fursa za biashara.

Akizungumza kuhusu tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, alisema kuwa tuzo hiyo inaakisi historia ya Benki na dira yake ya baadaye.

“Kama sehemu ya Standard Bank Group, tunajivunia kutajwa kuwa Benki Bora Tanzania kwa mwaka 2025. Tuzo hii inatambua safari yetu ya miaka 30 nchini Tanzania na inathibitisha dhamira yetu kwamba Tanzania ni nyumbani kwetu na tunachangia ukuaji wake. Katika mwaka uliopita, tuliwekeza mitaji katika miradi ya kimkakati katika sekta za nishati, biashara na miundombinu. 

Tukapanua wigo wa upatikanaji wa huduma za kifedha kupitia suluhisho za kidijitali na kuchochea uwekezaji katika biashara za kikanda. Tunaendelea kujizatiti kwa kubadili fursa kuwa matokeo chanya nchini Tanzania,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Masoko wa Stanbic Bank Tanzania, Neemarose Singo, alisema tuzo hiyo ni matokeo ya juhudi za wafanyakazi wa Benki na imani kubwa walokuwanayo wateja wao.“Tuzo ya Benki Bora ni uthibitisho wa kazi kubwa iliyofanywa na timu zetu kote nchini.

 Inatambua nidhamu yetu, ubunifu wetu na dhamira yetu ya kuwezesha biashara, familia na jamii kukua. Tunajivunia hatua hii na tunawashukuru wateja wetu kwa kuendelea kuchagua Stanbic kama mshirika wao,” alisema.

Bi Singo aliongeza kuwa mwaka 2025 ulikuwa mwaka wa kihistoria kwa Benki, ulioshuhudia ufunguzi wa matawi mapya, matumizi mapana ya huduma za kidijitali, shughuli imara za masoko ya mitaji na kuendelea kuunga mkono vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.

Katika mwaka huo, Stanbic iliendelea kupanua mtandao wake wa matawi, kuboresha huduma za kidijitali na kusaidia ukuaji wa biashara kupitia suluhisho za kifedha kama uwezeshaji wa wasambazaji, uwezeshaji wa mnyororo wa ugavi na mikopo mahsusi kwa biashara ndogo, za kati na za makampuni makubwa.

Utambuzi huu unaashiria hatua nyingine muhimu katika safari ya miaka 30 ya Stanbic nchini Tanzania na unaweka msingi wa vipaumbele vya Benki kwa mwaka 2026, ikiwemo upanuzi Zaidi wa mtandao wa matawi yetu, kuimarisha mahusiano na wateja na kuendelea kuwekeza katika teknolojia ya kidijitali na fedha endelevu.






Na WAF, Dodoma

Waziri wa afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo amekutana na wawekezaji wa vifaa tiba kutoka kampuni ya A to Z iliyopo nchini Tanzania waliojitokeza kwaajili ya kuunga mkono juhudi za serikali za kuinua sekta ya viwanda vya dawa nchini

Akizungumza jijini Dodoma Januari 12, 2026 Waziri Mchengerwa ameahidi kuwepo kwa ushirikiano mkubwa baina ya serikali na wawekezaji wa viwanda vya dawa nchini huku akisisitiza upatikanaji wa hati ya viwango kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa wenye nia ya kuwekeza

“Wawekezaji wamesema wapo tayari kushirikiana na serikali na wanafanya uwekezaji mkubwa ambao utatosheleza soko la ndani na sisi tumewapokea na tuko tayari kushirikiana nao lakini takwa la kwanza ni lazima wapate hati ya viwango kutoka WHO, lakini wamenithibitishi kwamba ndani ya mwaka mmoja watakuwa wamepata”

Amesema, Mpango wa serikali ni kuwa na viwanda kwa muda mrefu, huku akithibitisha kuanza kwa mchakato kwa wawekezaji hao wa kufuatilia hati za viwango za Good Manufacturing Practice (GMP) ambazo zinategemewa kupatikana ndani ya mwaka mmoja 

“Serikali ina mpango wa kuwa na viwanda vingi vyenye ubora vitakavyodumu kwa muda wa miaka 100, hatutaki kiwanda leo kipo, kesho imekuja seikali nyingine kimeshakufa, ndiyo maana tunashirikiana nao, tunawaunga mkono kwa ukaribu ili tujue palipo na changamorto tuzitatue”

Waziri Mchengerwa amewakaribisha A to Z na wawekezaji wengine kwenye Jukwaa la Uwekezaji katika Uzalishaji wa Dawa Tanzania lililoandaliwa na Wizara ya Afya kwa lengo la kuwakutanisha wawekezaji wa ndani na wa kimataifa katika sekta ya dawa, wazalishaji, washirika wa maendeleo pamoja na wadau muhimu kutoka sekta za afya na uwekezaji litakalofanyika Januari 19, 2026








 


Na Mwandishi wetu, Simanjiro
WAKUU wa shule za sekondari na msingi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule kutokana na kasi ya ukuaji na kuongezeka kwa matumizi ya sayansi na teknolojia ulimwenguni.

Wakuu wa shule 23 za sekondari, 110 wa msingi wa shule za serikali na binafsi wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa wake kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu.

Afisa elimu ya awali na msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Darius Daudi Limandola amesema walimu hao wamepata mafunzo hayo ya uandaaji wa taarifa za shule kwenye vituo vitatu vya Orkesumet, Terrat na Mirerani.

Limandola ameeleza kwamba mafunzo hayo ya mfumo wa utoaji wa taarifa za kielimu kupitia mfumo wa kidigitali (School Information System) una lengo la kurahisisha utoaji na upatikanaji wa taarifa za shule husika kwa wakati.

Ameeleza kwamba mfumo huo unafanyakazi katika kutoa taarifa za kielimu za shule husika kila siku ikiwemo hali ya miundombinu ya shule, utekelezaji wa lishe kwa wanafunzi, hali ya watumishi na upatikaji wa huduma nyingine za kijamii hususani maji na umeme.

Amesema wanufaika wa mafunzo hayo ni wakuu 23 wa shule za sekondari, walimu wakuu 110 wa shule za msingi, maafisa elimu kata, walimu wa taaluma na takwimu na maafisa elimu ngazi ya wilaya.

Amewataka walimu wakuu na wakuu wa shule kusimamia utekelezaji wa mfumo huo mara moja baada ya shule kufunguliwa Januari 13, 2026 ambapo utairahisishia serikali kufanya maboresho na maamuzi sahihi katika shule husika kwa wakati.

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo, afisa elimu vifaa na takwimu wa halmashauri ya wilaya hiyo, Abdalah Hamis amesema walimu hao wamejengewa uwezo kwa muda wa siku mbili na kisha watakwenda kuwaelekeza walimu waliobaki katika shule zao.

"Mafunzo yamefanyika katika vituo vitatu vya Orkesumet shule ya sekondari Simanjiro, shule ya sekondari Terrat na shule ya awali na msingi Glisten Mirerani, ambayo yameanza juu kwa wachache watakaokwenda kuwafundisha wengi," amesema Hamis.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, mkuu wa shule ya sekondari Tanzanite, Jude Samwel Mziray amesema mfumo huo ni mzuri kwani wanaaachana na mtindo wa kuingiza taarifa kwenye makaratasi na kuweka katika mfumo wa kiteknolojia.

"Mfumo huo unarahisisha kwani unatoa taarifa ya shule hadi ngazi ya kata, kisha wilaya hadi ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) tofauti na tulivyozoea mwanzo kujaza katika makaratasi," amesema Mziray.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Naepo, kata ya Naisinyai, Simon Isack Magembe amesema mafunzo hayo yanawajengea uwezo zaidi wa kuboresha taarifa kwa matumizi sahihi.

Mwalimu Magembe amesema ujuzi walioupata wa kuandaa taarifa za mfumo huo umewarahisishia utendaji kazi wao tofauti na awali.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akiongea na wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakati wa kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo katika chuo hicho.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakimaliza Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya wakati akitoa hotuba yake
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akikabidhi kiasi cha shilingi milioni mbili kwa uongozi wa chuo kikuu cha Iringa zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao.

Na Fredy Mgunda, Iringa.
WANAFUNZI wa vyuo vikuu wametakiwa kujiepusha na ndoa za rejareja,makundi ya hovyo yenye viashiria vya kuharibu masomo na maisha kwa wanafunzi wenye ndoto ya kuja kulitumikia taifa la Tanzania na nje ya Tanzania.

Akizungumza wakati kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuo kikuu cha Iringa,Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya alisema kuwa wanafunzi wanapaswa kuepukana na ndoa za rejareja, makundi ya hovyo na kuwa wazalendo kwa ajili ya maisha yao.

Dkt Msowoya amesema baadhi ya wanafunzi hujikuta wakitumbukia kwenye ndoa za rejareja na kusahau lengo la masomo kutokana na tamaa za kifedha na kuishi maisha mazuri chuo jambo ambalo limekuwa likipoteza dira ya masomo kwa wanafunzi wengi.

"Najua mna miaka zaidi ya 18 hivyo sio watoto Kwa mujibu wa kawaida lakini je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wako wanajua umeoa au kuolewa huku?" amesema na kuongeza, Dkt Msowoya

"Niliwahi kufanya utafiti kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu nikagundua wengi wanaishi na wenza ilhali familia zao hazijui. Hii ni hatari,"

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka makundi yenye viashiria hasi katika masomo na maisha kwa ujumla.
Katika hafla hiyo, alitoa mchango wa shilingi milioni mbili (2,000,000) zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao.
FARIDA MANGUBE, MOROGORO
ZIARA ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba katika kata za Kidete na Tindika imekuwa faraja kubwa baada ya Serikali kutoa shilingi milioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji itakayoboresha maisha ya wakazi wa maeneo hayo

Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Sospeter Lutonja, amesema kwa Kata ya Kidete vitachimbwa visima 6 vyenye thamani ya shilingi milioni 360, ambavyo vinatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakazi 15,000.

Kwa upande wa Kata ya Tindika, serikali imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya usambazaji wa maji katika vijiji vya Tindiga A, Tindiga B, na Maluwi ambapo awali wakazi wa maeneo hayo walikuwa wakitumia visima vya mkono maarufu kama “visima vya mdundiko,” ambavyo havikutosha kukidhi mahitaji ya kila siku.

Ziara ya Waziri Mkuu inaonesha wazi jinsi serikali inavyolenga kuhakikisha huduma za maji zinawafikia wananchi, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko na uhaba wa maji safi.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina.

Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee.

Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana

Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badala ya utaratibu wa maelekezo kutoka juu kwenda chini.

Alitumia pia kikao hicho kutoa rai kwa viongozi na wana CCM kuzingatia utaratibu wa kutoa maoni kuanzia ngazi ya chini kwenda juu.

“Nitoe wito kwa viongozi wetu tusifanye utaratibu wa kutoa amri kutoka juu kushuka chini maana uongozi mzuri ni lazima uanzie chini kwenda juu, yale tunayoyapata kutoka kwenye mashina, matawi ndio yatapanda juu kwa lengo la kukiimarisha chama chetu, alisema Dkt.Migiro.

Aidha, siku iliyofuata katika ziara yake, akizungumza na viongozi wa mashina na matawi wa Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Katibu Mkuu huyo wa CCM, alisema Chama Cha Mapinduzi hakijengwi katika majukwaa, bali hujengwa kuanzia ngazi ya mashina na matawi, huku akibainisha majukwaa hutumika zaidi kwa ajili ya kutoa hamasa.

“Mashina ndiyo moyo wa CCM kwa kuwa ndiyo yanayokutanisha chama na wananchi moja kwa moja kupitia vikao na shughuli mbalimbali za kijamii na kisiasa, amesisitiza Dk.Migiro, anayeendelea na ziara yake mkolani Dar es salaam yenye kauli mbiu ShinaLakoLinakuita.


NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WAKALA wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), imekamilisha matengenezo ya kivuko cha MV Kazi ambacho kilileta hitirafu mwanzoni mwa mwezi huu, kinatarajiwa kuanza kazi hapo kesho Januari 13, 2026 mchana.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari, Kaimu Mtendaji Mkuu TEMESA, Mosses Mabamba, amesema ukarabati wa kivuko hicho umechukua siku nne na kugharimu jumla ya shilingi milioni 30.

Ameeleza kuwa kazi hiyo imelenga kuhakikisha usalama na ufanisi wa huduma kwa wananchi wanaotegemea kivuko hicho.

"Majaribio ya kivuko hiki (MV Kazi) yatafanyika kesho asubuhi, na kuanzia majira ya saa nane mchana, kitaanza rasmi kutoa huduma kwa wananchi wa eneo la Feri na Kigamboni na kuweza kupunguza changamoto". Amesema

Aidha, Mabamba amebainisha kuwa kwa sasa kivuko cha MV Kazi kina uwezo wa kubeba abiria 800 na magari 20 kwa safari moja, hatua inayolenga kupunguza msongamano na kurejesha hali ya kawaida ya usafiri katika eneo hilo.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wanaotumia kivuko hicho wamesema kurejea kwa huduma ya MV Kazi ni faraja kubwa kwani itarahisisha shughuli zao za kila siku, ikiwemo kwenda kazini, shuleni na katika shughuli za kibiashara.

Hata hivyo, wameitaka Serikali kuendelea kuboresha huduma za vivuko ili kuepuka adha zinazojirudia.

Wakati huo huo, Serikali imeweka mpango wa muda mrefu wa kuboresha usafiri wa majini kwa kuendelea na ukarabati wa kivuko cha MV Magogoni, kinachotarajiwa kuanza kutoa huduma mwezi Aprili.

Kivuko hicho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 2,000 na magari 60 kwa safari moja, hatua inayotajwa kuonesha dhamira ya Serikali katika kuboresha miundombinu ya usafiri wa majini na kuhakikisha wananchi wanapata huduma salama, ya uhakika na endelevu.




Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akiongea na wadau mbalimbali wa kongani ya Buzwagi wakati wa ziara hiyo

Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi akiongea wakati wa ziara hiyo.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya (Kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda (katikati) na Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi.

Mkuu wa wilaya ya Kahama,Frank Nkinda akiongea wakati wa ziara hiyo.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akitembezwa katika maeneo mbalimbali ya Kongani ya Buzwagi.
**


#Yaipongeza Barrick kwa kufunga mgodi kwa viwango bora


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya, amesema kuwa Kongani ya Viwanda ya Buzwagi Special Economic Zone inatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa Mkoa wa Shinyanga na Taifa kwa ujumla, kutokana na mpango wake unaotoa fursa mbalimbali za uwekezaji.


Dkt. Chaya ameyasema hayo baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kutembelea kongani hiyo iliyopo katika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga ambapo pia ameipongeza kampuni ya Barrick kwa ufungaji wa mgodi wa Buzwagi kitaalamu na kufanya eneo hilo kuwa la kuvutia kwa wawekezaji.


“Nimefurahi kusikia kuwa eneo hili limetengwa miongoni mwa maeneo sita ya uwekezaji, ambapo mnapanga kujenga vyuo vya ufundi, makazi, viwanda na miundombinu mingine muhimu. Hivyo basi, Buzwagi ni eneo sahihi kabisa kwa uwekezaji na limepangiliwa vizuri na wadau wote wanaosimamia eneo hili ikiwemo kampuni ya Barrick,” amesema Dkt. Chaya.


Ameongeza kuwa azma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kuhakikisha Watanzania wanakuwa na maisha bora na amewataka wananchi kuchangamkia fursa hii ya kongani kubadilisha maisha yao.


“Serikali inapenda kuona Wananchi wa Kahama na Tanzania katika sekta zote ikiwemo , akina mama lishe, wasomi na hata wasiokuwa wasomi wanapata ajira na fursa za kipato kupitia uwekezaji huu mkubwa katika kanda hii ya ziwa”, amesisitiza.


Dkt. Chaya amewataka viongozi pamoja na wadau wote wa maendeleo kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja ili kutimiza dhamira na maono ya Mheshimiwa Rais.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda aliyekuwa katika ziara hiyo ameeleza kuwa Kongani ya Viwanda ya Buzwagi ina vigezo vyote vinavyohitajika kuwavutia wawekezaji, ikiwemo mazingira rafiki ya uwekezaji, eneo kubwa pamoja na uwepo wa uwanja wa ndege unaorahisisha usafiri.


“Serikali inaendelea kufungua wigo kwa ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini na kuongeza manufaa ya rasilimali madini kwa kutenga eneo hili maalum la uwekezaji la ulipokuwa Mgodi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu la Barrick Buzwagi lenye ukubwa wa ekari 1331, ni kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa za migodini na tayari viwanda sita vimekwisha jengwa huku wamiliki wa viwanda 15 wakionesha nia ya kujenga viwanda katika eneo hilo”, ameeleza.


Ametoa wito kwa watanzania kuchangamkia fursa zilizopo katika kongani hiyo ili kukabiliana na changamoto za ajira kwa manufaa ya mtu mmoja mmoja na manufaa ya taifa.


Awali Akieleza Utekelezaji wa Mchakato wa kikamilisha Kongani hiyo Meneja Ufungaji wa Mgodi wa Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi, amesema kwa sasa kuna mwitikio mkubwa kwa wawekezaji kuhitaji kuwekeza katika Kongani hiyo kutokana na kukidhi vigezo vyote vinavyovutia wawekezaji.

Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt. Tumaini Msowoya, amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Iringa kuwa makini na maisha ya chuoni kwa kujiepusha na ndoa za rejareja, makundi yasiyo na tija pamoja na tabia zinazoweza kuwavuruga kimasomo, huku akisisitiza umuhimu wa uzalendo na nidhamu binafsi.

Akizungumza wakati wa sherehe za kuwapokea wanafunzi wa mwaka wa kwanza, Dkt. Msowoya alisema licha ya wanafunzi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18 kisheria, bado wanapaswa kujiuliza iwapo ndoa au mahusiano ya kuishi pamoja ndiyo yamewaleta chuoni, au ni dhamira ya kutimiza ndoto zao za kielimu.

“Najua mna umri wa zaidi ya miaka 18 hivyo si watoto kwa mujibu wa sheria, lakini jiulizeni: je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wenu wanajua mmeoa au mmeolewa mkiwa hapa?” alihoji Dkt. Msowoya.

Aliongeza kuwa tafiti alizowahi kufanya kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu zimebaini kuwa wanafunzi wengi huishi na wenza wao kwa siri bila familia zao kufahamu, jambo alilolitaja kuwa ni hatari na linaloweza kuathiri mwenendo wa masomo na maisha ya baadaye.

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka kujiingiza katika makundi yasiyo na mwelekeo chanya, akisisitiza kuwa wasomi ndio tegemeo la maendeleo ya taifa.

Katika hafla hiyo, Dkt. Msowoya alimwakilisha Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa ambaye alikuwa mgeni rasmi. Mwipopo aliwapongeza wanafunzi hao na kuchangia shilingi milioni 2,000,000 kwa ajili ya kuwasaidia katika safari yao ya masomo.

Amesisitiza kuwa nidhamu, maamuzi sahihi na uzalendo ni misingi muhimu kwa mwanafunzi yeyote anayelenga kufanikiwa chuoni na katika maisha kwa ujumla.



 


NAFASI ya ushindi hii hapa na wakali wa Meridianbet ambapo kupitia promosheni ya Beti Online unaweza ukaondoka na Samsung A26. Weka dau lako kuanzia 5000 na ubashiri hapa.

Meridianbet inaendelea kuwa kinara katika kutoa promosheni zenye thamani halisi kwa wachezaji wake. Kupitia kampeni yake mpya, kampuni hii inaleta fursa murua kwa mashabiki wa mpira kushiriki bashiri za mechi za Ligi kwa dau la kuanzia shilingi 5,000 tu na kuingia kwenye droo ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A26. Hii ni ofa inayochochea ushindani, msisimko na thamani kwa kila mchezaji anayejiunga.

Meridianbet wanasema kuwa ili ujiweke kwenye nafasi ya kuondoka na simu janja hii hapa na uwe wa Kidigitali kabisa ni vyema ukabashiri mara nyingi zaidi kwani kufanya hivyo kunakuweka karibu na ushindi leo hii wa Samsung A26.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kampeni hii inalenga kuongeza hamasa kwa mashabiki kufurahia mechi za Ligi wakiwa na matumaini makubwa. Kila ubashiri unaowekwa si tu unaleta msisimko wa kutafuta ushindi wa dau, bali pia msisimko wa kusubiri droo ya kujua kama wewe ndio mteule wa kupata simu mpya. Huku mashindano yakiendelea kila wiki, kila mchezaji anapata nafasi nyingi kadri anavyobashiri mara kwa mara.

Washindi wa promosheni hii watatangazwa kila Ijumaa ambapo ndio siku ambayo simu hutolewa hivyo usikae mbali na fursa hii kwani inakupa nafasi ya wewe kumiliki simu kali ambayo itakufanya uweze kuperuzi.

Kumbuka kuwa unapoingia kwenye mashindano haya ya kuwania Samsung A26, hutakiwi Kuturbo Mkeka wako au CASH OUT kwa namna nyingine haitahusika kwani inatakiwa usubiri jamvi lako limalizike.

Na kufanya hivyo kutakufanya ujiondoe kwenye mashindano kwani tiketi yako itahesabika kama batili. Hivyo subiri hadi mechi zote zikamilike ndipo uweze kuingia kwenye wachezaji ambao sio batili.



Takribani wanafunzi 600 katika kata ya Kalangalala wenye Hali ya chini wanakadiliwa kupata madaftari kwa ajili ya kuanza nayo msimu mpya wa masomo 2026.

Kata ya kalangalala Ina jumla ya shule za msingi 9 na shule za sekondari mbili  ambapo jumla ya wanafunzi 1640 katika kata hiyo wameandikishwa kuanza darasa la kwanza.

Muitikio huo wa uandikiashwaji umemuibua diwani wa kata ya Kalangalala Ruben Sagayika kugawa madaftari pamoja na kalamu kwa Wanafunzi wanaotarajiwa kufungua shule Januari 13.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo amesema zoezi la ugawaji wa madaftari litakuwa endelevu katika kata hiyo ili kuhakikisha Kila mtoto anafika shuleni akiwa na vifaa vya shule.

"Tutakuwa pia tunapitia kwenye mashule tunaangalia watoto ambao hawana sare za shule na kuwashika mkono ili Hawa watoto waweze kupata elimu Bora" alisema Sagayika.

Kaimu afisa Elimu kata ya Kalangalala Regina Kitau amesema kuwa zoezi la ugawaji madaftari litatoa motisha kwa watoto kufika shule.

Kwa upande wao wazazi wameshukuru uwepo wa zoezi kwani wameweza kupunguza mzigo wa maandalizi ya vifaa vya shule inayotarajiwa kufunguliwa kesho.









 


Top News