Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO mkoa wa Ruvuma, Alan Njiro, ametoa wito kwa wateja wa shirika hilo kuhakikisha wanatumia vifaa vya umeme vyenye ubora na vinavyokidhi viwango katika nyumba zao ili kuepuka changamoto na hatari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya vifaa visivyo na ubora au feki.
Njiro ametoa wito huo akiwa katika Mtaa wa Pambazuko, Kata ya Shule ya Tanga, Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, wakati akitoa elimu kwa wananchi waliopitiwa na Mradi wa REA Awamu ya Pili, amehimiza wananchi kununua vifaa vyenye alama za ubora na kutumia mafundi waliosajiliwa na wenye ujuzi wakati wa kusuka miundombinu ya umeme katika nyumba zao.
Kwa upande wake, Afisa Usalama wa TANESCO Mkoa wa Ruvuma, Paulo Maysoli, amewataka wananchi wa mkoa huo kutunza na kuilinda miundombinu ya umeme dhidi ya uharibifu na vitendo vya wizi, akisisitiza kuwa miundombinu hiyo ni mali ya umma na ni jukumu la kila mwananchi kuilinda na kuitunza.
Aidha, wananchi wa Mtaa wa Pambazuko wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa REA katika mtaa wao, wakieleza kuwa mradi huo utachangia kuboresha maisha yao na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
TANESCO Mkoa wa Ruvuma imewahimiza wananchi kushirikiana na taasisi husika kwa kuzingatia matumizi ya vifaa vya umeme vyenye ubora, kuzingatia ushauri wa kitaalamu na kulinda miundombinu ya umeme, ili kuhakikisha usalama, uendelevu wa huduma ya umeme na maendeleo endelevu katika jamii.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (MB), kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula, wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yaliyofanyika tarehe 21 Januari 2026 katika Viwanja vya Usagara mkoani Tanga.
Katika hotuba hiyo, Waziri wa Fedha amebainisha kuwa wananchi wengi wamekuwa wakipata athari mbalimbali kutokana na kukopa fedha katika taasisi zisizo rasmi, hivyo kusisitiza umuhimu wa wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu uhalali wa taasisi za kifedha kabla ya kukopa.
Amehimiza wananchi kusoma na kujiridhisha na mikataba ya mikopo wanayoingia ili kuepuka hasara zinazotokana na kusaini mikataba bila kuelewa masharti yake.
Kwa upande wake, Gavana wa BoT, Bw. Emmanuel Tutuba, kupitia hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Ustawi na Huduma Jumuishi za Fedha, Bw. Kennedy Komba, amesema kuwa katika kutekeleza sera za ujumuishi wa kifedha na kuongeza uwazi, ulinzi na ufikikaji wa huduma kwa watumiaji wa huduma za fedha, hususan kwa wale wenye malalamiko dhidi ya watoa huduma au wanaokosa taarifa kamili kuhusu gharama, tozo na utaratibu wa ukokotoaji wa riba na mikopo, BoT imeanzisha na kuimarisha mifumo mbalimbali.
Mifumo hiyo ni pamoja na mifumo ya uwasilishaji na usimamizi wa malalamiko (SEMA na BOT), kilinganishi cha bei, kikokotoo cha gharama za mikopo, pamoja na utaratibu wa usimamizi shirikishi kwa watoa huduma ndogo za fedha wa kundi la pili, hatua ambazo zimeongeza uwazi, ufanisi na ubora wa huduma za fedha zinazotolewa kwa wananchi kwa kuzingatia matakwa ya sheria na kanuni zilizopo.
Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayofanyika kuanzia tarehe 19 hadi 26 Januari 2026, yanalenga kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya fedha na matumizi ya huduma rasmi za fedha kwa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.





Kamishna wa Kodi za Ndani, Alfred Mlegi amesema hayo leo Januari, 21,2026 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa IDRAS) kwa wafanyabiashara na walipa kodi wote.
Mlegi amesema TRA imetoa mafunzo hayo kwa wafanyabiashara na walipa kodi kabla ya kuanza kutumika kwa mfumo huo ili kuwaongeza uelewa juu ya namna ya kuutumia na kuepuka changamoto.
“Tumelenga kuunganisha mfumo huu kwenye jumla ya taasisi 300, lakini kwa kuanzia tunaanza na hizi 60 ili ziendelee kutoa huduma ikiwemo kuwasiliana moja kwa moja bila mfanyabiashara au mlipa kodi kufika katika ofisi zetu,” amesema Mlega
Amesema mfumo huo una jumla ya moduli 17, lakini 15 zipo tayari kuanza kufanya kazi isipokuwa mbili za ukaguzi na uchunguzi ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi.
“Mfumo huu ni kwa ajili ya wananchi katika kuwasaidia katika suala la kulipa kodi, kutunza kumbukumbu za bidhaa zilizouzwa au kununuliwa, shughuli zote za mapingamizi pamoja na kukusanya taarifa zitakazotusaidia kufanya makadirio ya kodi na kuondoa malalamiko ya hisia za kubambikiwa kodi,” amesema.
Ameeleza kuwa awali kulikuwa na mifumo mingi iliyokuwa ikitumika kutoa huduma kwa wafanyabiashara hali iliyosababisha usumbufu, hivyo TRA imeamua kuja na mfumo mmoja utakaomsaidia mfanyabiashara kufanya shughuli zote za usimamizi wa kodi.
Ameongeza, “Hapo awali wafanyabiashara wengi walikuwa wakilalamika kuhusu kodi wanazokadiriwa kuwa si sahihi na wengine wakidai tulikuwa tunawabambikia kodi. Kutokana na hitaji la maboresho, tumekuja na mfumo huu kwa sababu unakusanya taarifa nyingi kutoka sehemu mbalimbali, hivyo itakuwa rahisi kufanya makadirio ya kila mfanyabiashara na mlipa kodi. Ndiyo maana leo tunatoa elimu kuhusu mfumo huu.”
Mlega amesema kulikuwepo na malalamiko juu ya matumizi ya mashine za EFD, lakini kupitia mfumo huo hakutakuwa na ulazima wa kuwa na mashine hiyo kwa kuwa mfumo utamwezesha mtumiaji kutoa risiti.
Kwa upande wake, mwakilishi wa Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Dar es Salaam, Pendo Lukas amesema wana imani na mfumo huo kwa sababu utaondoa kilio na malalamiko ya wafanyabiashara.
Pendo ametoa wito kwa wafanyabiashara kuukubali mfumo huo pamoja na kuendelea kuwaunga mkono TRA katika kile wanachokifanya cha kumsaidia mfanyabiashara, akisema wanatumia gharama nyingi na muda wao kuhakikisha kila mfanyabiashara anahudumiwa kwa ukaribu na kwa weledi.
“Tuna imani kwa sababu kupitia mafunzo haya kila mfanyabiashara ataweza kujihudumia yeye mwenyewe pamoja na uwazi wa malipo yake kwa kuzingatia ulichotumia ndicho ulipe,” amesema.
Ameishukuru TRA kwa kuboresha mifumo yao kwani imesaidia kodi kuwa rafiki kwa wafanyabiashara, na kwa sasa hawana migogoro wala hawakimbii mamlaka hiyo kama ilivyokuwa hapo awali.




Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, leo Januari 21, 2026 amewasilisha Taarifa ya Taasisi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini jijini Dodoma.
Kamati hiyo ilipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Nishati na utekelezaji wa Majukumu ya TANESCO




Kocha wa Timu ya Mpira ya Pete ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) akizungumza na wachezaji wa timu wakati wa kipindi cha mapumziko katika mchezo baina yao na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.

MKurugenzi Msaidizi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Hanifa Selengu akizungumza jambo na wachezaji wa Timu wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.
Sehemu ya wachezaji wa akiba na benchi la ufundi la Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakifuatilia maelekezo ya kocha wa timu hiyo Bw. Mafuru Buriro wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.(NA MPIGAPICHA WETU)
TIMU ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) imeendeleza wimbi la ushindi katika mashindano ya Ligi ya Muungano ya mchezo huo yanayoendelea katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar.
Katika matokeo ya mechi ya leo Jumatano Januari 21, 2026, Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais imeiadhibu vikali Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jumla ya magoli 45 dhidi ya 34 katika mchezo ambao Ofisi hiyo ilitawalawa maeneo yote ya mchezo.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo, Mchezaji wa Timu hiyo, Bi. Anna Akwilini amesema nidhamu, ushirikiano na kujitumu kwa wachezaji ndio siri kubwa ya mafanikio ya timu hiyo katika mashindano hayo.
“Benchi la ufundi kupitia Kocha amekuwa akiturekebisha kwa makosa madogo madogo na pia hamasa ya mashabiki katika majukwaa imekuwa ikitujengea hali ya kujiamini na kupata hamasa kubwa katika kila mchezo tunaocheza” amesema Akwilini.
Amesema wachezaji wa timu hiyo wamekusudia kuendelea kufanya vizuri zaidi katika michezo yote iliyosalia ili iweze kuibua na ushindi na hatimaye kunyakua ubingwa wa Ligi hiyo ambayo imekuwa na ushindani wa hali ya juu kutoka kwa timu zote.
“Ofisi itahakikisha itajipanga vyema zaidi kwa kufanya usajili wa wachezaji wakati wa Ligi ya mashindano ya mchezo kwa upande wa Tanzania Bara na baadaye kufanya vizuri zaidi katika mashindano ya Muungano” amesema Mwasamale.
Kwa upande wake Kocha wa Timu hiyo, Bw. Mafuru Buriro amesema mechi hiyo ilikuwa ngumu lakini kutokana uimara wa kikosi chake kimeweza kufanya vizuri na kuwa na imejipanga inapata matokeo mazuri katika michezo iliyosalia.
“JKT ni timu iliyokaa pamoja kwa muda mrefu wamezoeana na kupata muda mwingi wa kufanya mazoezi ya pamoja lakini tulitumia uzoefu na bidi ya wachezaji wetu katika kupata ushindi katika mchezo huu” amesema Buriro.
Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 15 Januari mwaka huu yameshirikisha jumla ya Timu 11 ikiwemo Timu 06 kutoka Tanzania Bara na Timu 05 kutoka Zanzibar ambapo yanatarajia kuhitimishwa rasmi tarehe 24 Januari mwaka huu.
Timu zinazoshiriki Ligi ya Mashindano hayo ni Ofisi ya Makamu wa Rais, JKT, JKU, Mafunzo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Kikosi cha Valantia Zanzibar (KVZ), Polisi Arusha, Dodoma Jiji, Zimamoto na Uhamiaji.

Jumla ya Wapiga Kura 38,151 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa marudio katika Kata za Malangali iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Mkoa wa Rukwa na Mzinga iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

************
Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) imeendeleza wimbi la ushindi katika mashindano ya Ligi ya Muungano ya mchezo huo yanayoendelea katika Uwanja wa Amani Complex, Zanzibar.
Katika matokeo ya mechi ya leo Jumatano Januari 21, 2026, Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais imeiadhibu vikali Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jumla ya magoli 45 dhidi ya 34 katika mchezo ambao Ofisi hiyo ilitawalawa maeneo yote ya mchezo.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo, Mchezaji wa Timu hiyo, Bi. AnnaAkwilini amesema nidhamu, ushirikiano na kujitumu kwa wachezaji ndio siri kubwa ya mafanikio ya timu hiyo katika mashindano hayo.
“Benchi la ufundi kupitia Kocha amekuwa akiturekebisha kwa makosa madogo madogo na pia hamasa ya mashabiki katika majukwaa imekuwa ikitujengea hali ya kujiamini na kupata hamasa kubwa katika kila mchezo tunaocheza” amesema Akwilini.
Amesema wachezaji wa timu hiyo wamekusudia kuendelea kufanya vizuri zaidi katika michezo yote iliyosalia ili iweze kuibua na ushindi na hatimaye kunyakua ubingwa wa Ligi hiyo ambayo imekuwa na ushindani wa hali ya juu kutoka kwa timu zote.
“Ofisi itahakikisha itajipanga vyema zaidi kwa kufanya usajili wa wachezaji wakati wa Ligi ya mashindano ya mchezo kwa upande wa Tanzania Bara na baadaye kufanya vizuri zaidi katika mashindano ya Muungano” amesema Mwasamale.
Kwa upande wake Kocha wa Timu hiyo, Bw. Mafuru Buriro amesema mechi hiyo ilikuwa ngumu lakini kutokana uimara wa kikosi chake kimeweza kufanya vizuri na kuwa na imejipanga inapata matokeo mazuri katika michezo iliyosalia.
“JKT ni timu iliyokaa pamoja kwa muda mrefu wamezoeana na kupata muda mwingi wa kufanya mazoezi ya pamoja lakini tulitumia uzoefu na bidi ya wachezaji wetu katika kupata ushindi katika mchezo huu” amesema Buriro.
Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 15 Januari mwaka huu yameshirikisha jumla ya Timu 11 ikiwemo Timu 06 kutoka Tanzania Bara na Timu 05 kutoka Zanzibar ambapo yanatarajia kuhitimishwa rasmi tarehe 24 Januari mwaka huu.
Timu zinazoshiriki Ligi ya Mashindano hayo ni Ofisi ya Makamu wa Rais, JKT, JKU, Mafunzo, Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Kikosi cha Valantia Zanzibar (KVZ), Polisi Arusha, Dodoma Jiji, Zimamoto na Uhamiaji.

Sehemu ya wachezaji wa akiba na benchi la ufundi la Timu ya Mpira wa Pete (Netiboli) ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) wakifuatilia maelekezo ya kocha watimu hiyo Bw. Mafuru Buriro wakati wa mchezo baina ya timu hiyo na Timu ya Jeshi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) uliofanyika katika Uwanja wa Amani Complezx, Zanzibar. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuibuka na Ushindi wa Magoli 45 kwa 34.

Accra, Ghana
Tume ya Madini Tanzania imefanya ziara ya kikazi kwa Bodi ya Dhahabu ya Ghana (Ghana Gold Board – GoldBod) jijini Accra, ikiwa na lengo la kujifunza kwa vitendo namna taasisi hiyo ya kipekee imefanikiwa kubadilisha taswira ya biashara ya dhahabu nchini Ghana na kuimarisha mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa.
Ziara hiyo ya mafunzo ya kubadilishana uzoefu (peer learning) imebaini kuwa GoldBod imeweka mifumo madhubuti ya kuwasimamia wachimbaji wadogo na kuwajumuisha katika mfumo rasmi wa biashara ya dhahabu.
Hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya udanganyifu na utoroshaji wa dhahabu, kuongeza mapato ya serikali na fedha za kigeni, pamoja na kuimarisha akiba ya dhahabu ya Benki ya Ghana.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa GoldBod, Profesa Richard Nunekpeku, amesema kwa kipindi kirefu wachimbaji wadogo walikuwa nje ya mfumo rasmi, hali iliyosababisha upotevu mkubwa wa mapatato kwa serikali.
Amesema kuanzishwa kwa GoldBod kumewezesha dhahabu yote inayozalishwa kukusanywa na kufanyiwa biashara kwa njia halali, hivyo kuchangia mapato ya taifa, kuongeza akiba ya dhahabu ya Benki ya Ghana na kudumisha uthabiti wa thamani ya fedha ya nchi hiyo.
Katika ziara hiyo, ujumbe wa Tume ya Madini pia umetembelea kitengo cha Gold Jewelry kilicho chini ya Ghana Gold Board, kinachoshughulikia utengenezaji, uthibitishaji, uwekaji alama za thamani na usafirishaji wa bidhaa za usonara.
Kitengo hicho kinatajwa kuwa ni hatua muhimu katika kuongeza thamani ya dhahabu nchini Ghana na kuimarisha ushirikiano wa wadau wote katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini.
Ziara hiyo ya kihistoria imeonesha umuhimu wa ushirikiano wa kikanda barani Afrika katika kusimamia rasilimali za madini. Kupitia uzoefu wa GoldBod—bodi pekee yenye mamlaka ya kununua, kuuza, kupima, kuhakiki, kutoa thamani na kusafirisha dhahabu pamoja na madini mengine ya thamani, Tanzania imepata mafunzo muhimu yatakayosaidia kuimarisha mifumo ya usimamizi wa biashara ya madini. Mfano wa Ghana unaonesha kuwa usimamizi thabiti na wa kitaasisi wa sekta ya madini unaweza kuleta manufaa makubwa kwa wananchi na maendeleo ya taifa kwa ujumla.













.jpg)
.jpeg)















.jpeg)
.jpeg)
