Dar es Salaam, 23 Februari 2026 — Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amepongeza kwa ushirikiano wa kimkakati kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini, akieleza kuwa mpango maalum wa kifedha uliozinduliwa leo kwa ajili ya wachimbaji wadogo ni hatua ya kihistoria itakayobadili kabisa mfumo wa upatikanaji wa mitaji katika sekta ya madini nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma hizo na utiaji saini wa Mkataba wa Makubaliano (MOU) uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana, Waziri Mavunde alisema sekta ya madini imeendelea kukua kwa kasi, ikichangia asilimia 10 ya Pato la Taifa na zaidi ya asilimia 56 ya mapato ya fedha za kigeni kupitia mauzo ya nje yanayozidi dola za Marekani bilioni 5 kwa mwaka.
“Sekta ya madini sasa ni injini ya uchumi wetu. Tunachokishuhudia leo ni daraja linalounganisha maono ya Serikali na nguvu ya mtaji kutoka sekta ya fedha. Ushirikiano huu unaenda moja kwa moja kumgusa mchimbaji mdogo na kumwinua katika uchumi rasmi. Benki ya CRDB hakika mmeonyesha kuwa ni Benki kiongozi katika kuleta suluhisho stahiki kwa sekta mbalimbali. Tunawashukuru sana,” alisema Waziri Mavunde.

Alisisitiza kuwa chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imekuwa ikitekeleza mageuzi ya kisera, kiusimamizi na kisheria ili kuhakikisha sekta ya madini inawanufaisha Watanzania wengi zaidi, hususan wachimbaji wadogo. Alieleza kuwa azma ya Serikali ni kuona uchimbaji hauishii kwenye kuuza mawe ghafi, bali unapanuka hadi kwenye uchakataji na uongezaji thamani ndani ya nchi.
Mpango uliozinduliwa na Benki ya CRDB unaleta mageuzi makubwa katika mfumo wa dhamana kwa kutambua dhamana mbadala zinazotokana moja kwa moja na shughuli za uchimbaji. Kwa mara ya kwanza katika sekta ya benki nchini, leseni halali za uchimbaji, mikataba ya mauzo ya dhahabu, na akiba ya dhahabu iliyohifadhiwa katika viwanda vya kusafisha pamoja inatambuliwa kama dhamana zinazokubalika kwa ajili ya mikopo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema mpango huo ni mfumo kamili wa kifedha unaogusa mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya madini kuanzia uchimbaji, uchakataji, uhifadhi, usafirishaji hadi biashara na masoko ya ndani na nje ya nchi.
“Huu ni muundo mpya wa kifedha unaotambua uhalisia wa sekta ya madini. Tumekubali dhamana zinazotokana na shughuli halisi za wachimbaji badala ya mali zisizohusiana na sekta.

 Hii itafungua milango kwa maelfu ya wachimbaji wadogo waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa kifedha,” alisema Nsekela.
Alieleza kuwa mpango huo unajumuisha mikopo ya mtaji kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za uchimbaji, mikopo ya ununuzi wa mitambo na vifaa vya kisasa, mikopo inayodhaminiwa na dhahabu, huduma za bima za migodi na wafanyakazi kupitia CRDB Insurance, pamoja na akaunti maalum za miamala ya madini na dhahabu zitakazorahisisha ufuatiliaji na uwazi wa biashara.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Donald Mmari, alimweleza Waziri wa Madini kuwa Bodi imeweka miongozo ya kimkakati inayolenga kuhakikisha sekta ya madini inakua kwa kuzingatia misingi ya uendelevu, uwajibikaji na uchumi shirikishi.
“Tunataka kuona wachimbaji wadogo wanapanda ngazi kutoka uchimbaji wa jadi hadi kutumia teknolojia bora, kupata masoko rasmi na kushiriki katika uongezaji thamani. Ukuaji wa sekta ya madini lazima uwe endelevu na wenye manufaa kwa jamii,” alisema Dkt. Mmari.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa taasisi chache za kifedha zilizowekeza kwa kiwango kikubwa zaidi katika sekta ya madini nchini. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana, Benki hiyo imetoa mikopo yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 186 katika sekta ya madini, ambapo shilingi bilioni 136 zimetolewa kwa wachimbaji wakubwa na shilingi bilioni 50 kwa wachimbaji wadogo.  

Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji, Rais wa Chama cha Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA), John Bina alisema mpango huo umeleta matumaini mapya kwa wachimbaji wadogo waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya kukosa dhamana zinazokubalika na taasisi za fedha.
“Leo tunashuhudia mwanzo wa zama mpya. Wachimbaji wadogo tumepewa heshima ya kutambuliwa kama washirika halali wa maendeleo. Tunaishukuru sana Benki ya CRDB kwa kutuletea suluhisho hii, na tunawaahidi tutaendelea kushirikiana nao pamoja na Serikali kuhakikisha tunatumia fursa hii kwa uwajibikaji,” alisema.

Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya Benki CRDB na Tume ya Madini unatarajiwa kuimarisha urasimishaji wa wachimbaji, kuongeza upatikanaji wa mitaji nafuu, kukuza ajira kwa vijana na wanawake katika maeneo ya migodi, pamoja na kuongeza mapato ya Serikali kupitia uwazi wa miamala na ufuatiliaji wa kidijitali.

Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga

Elimu ni haki muhimu ya binadamu. Elimu ni nyenzo muhimu ya kumsaidia binadamu kumudu maisha yake. Kwa kutambua hilo, ndiyo maana wazazi na walezi wanapambana sana kusomesha watoto na vijana wao ili kuwawezesha kupata elimu bora ya kuwasaidia katika maisha yao na kutimiza ndoto zao za kimaendeleo walizonazo. 

Kazi kubwa na nzuri zimefanyika nchini katika kuboresha sekta ya elimu katika ngazi zote za elimu kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu Ili watoto na vijana wa Kitanzania waweze kupata elimu bora ya kuwasaidia maishani mwao. Mitaala ya ujifunzaji imeboreshwa ili kuwajengea wanafunzi umahiri wa kujitegemea pindi wanapohitimu ngazi mbalimbali za masomo yao.

Ikumbukwe kuwa mabadiliko haya mazuri ya mitaala yamekuja kipindi hiki ambacho wahitimu wengi wana changamoto ya kukosa stadi na ujuzi stahiki wa kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri katika sekta mbalimbali. Ndiyo maana wengi tunapongeza mabadiliko haya ya mitaala kwa ustawi mwema wa wahitimu. Katika elimu ya juu, serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inaratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wanafunzi huku wanufaika wa mikopo hiyo wakiwajibika kuirejesha mikopo hiyo baada ya kuhitimu na kuwa na kipato katika sekta rasmi au isiyo rasmi. 

Kwa kutambua changamoto iliyopo kwa baadhi ya wahitimu kukosa ujuzi na stadi mbalimbali, HESLB inashirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo taasisi ya kifedha katika kuhakikisha wanawajengea uwezo wahitimu ili waweze kuajiriwa au kujiajiri ambapo kufanikiwa kwao kunaiwezesha HESLB kukusanya fedha kutoka kwa wahitimu hao lakini pia nchi kupata wataalamu kwa maendeleo.

Mathalani, Februari 18, 2026, katika Ofisi za CRDB Makao Makuu Jijini Dar es Salaam, HESLB iliingia makubaliano ya kushirikiana na CRDB Bank Foundation na kampuni ya Basil Link ili kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vikuu kupata ujuzi wa kidigitali, elimu ya ujasiriamali na elimu ya fedha. 

Kwa hakika makubaliano haya ni mwelekeo mzuri katika kuwaandaa wanafunzi wa vyuo vikuu kujitegemea kutokana na mafunzo muhimu watakayoyapata kupitia uwezeshaji utakaofanywa hasa katika kuwa na jicho la kuona fursa za kiuchumi zilizopo. 

Kupitia programu hiyo lijulikanalo kwa jina la "Imbeju - SmartElite," wanafunzi wa vyuo watapata mafunzo ya ujasiriamali ili kuweza kujiajiri wenyewe. Aidha, watapata pia elimu ya fedha ambayo ni muhimu sana katika ulimwengu huu wa sasa. Sanjari na hilo, wanafunzi watapata mikopo nafuu na ushauri elekezi wa namna bora ya kuwekeza mikopo hiyo ili ilete tija kiuchumi. 

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Mwambapa alisema "Tunataka kuona vijana wanachangamkia fursa, wanabuni, wanaanzisha biashara na hata kuajiri wengine. Hii si tu kuwasaidia kumaliza chuo, bali kuwaandaa kuingia katika uchumi wa kidigitali wakiwa tayari na ujuzi pamoja na raslimali."

Kwa upande wa Dk. Peter Mmari ambaye ni Mkurugenzi na Upangaji Mikopo wa HESLB amesema "Kupitia mpango huu, wanafunzi wataongeza uwezo wa kutumia mifumo ya kidijitali na watapata fursa ya kujiajiri wakiwa vyuoni au baada ya kuhitimu. Tunaamini wataweza pia kutoa mchango katika kuwainua Watanzania wengine kielimu na kiuchumi."

Kimsingi, vijana wenye vipaji na mawazo bunifu watanufaika na mpango huu huku wakiwezeshwa mitaji na vitendea kazi kama kompyuta. Kwa hakika programu ya Imbeju - Smart Elite, ni mkombozi kwa vijana hasa katika ulimwengu wa uchumi wa kidijitali na biashara.







Na Diana Byera,Karagwe

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Kagera,  Devotha Daniel, ametoa msaada wa Sh.   1,000,000 kwa mtoto Grecseous Raphael mwenye umri wa miezi 4, mkazi wa Kata ya Kihanga, Wilaya ya Karagwe, anayesumbuliwa na uvimbe kichwani 

Lengo la msaada huo ni kumuwezesha mtoto huyo kupelekwa  Hospitali ya Kanda ya Bugando kwa ajili ya upasuaji.

Mbunge Devotha Daniel ametoa msaada huo ikiwa ni katika kipindi cha kuendelea kusambaza tabasamu kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo,  amesema alipata taarifa za mtoto huyo kupitia matangazo ya kituo cha redio ya jamii cha Fadeco Radio, ambapo mama wa mtoto alikuwa akiomba msaada kwa wasamaria wema.

 “Baada ya kusikia taarifa hizo, niliguswa na kuamua kufika moja kwa moja kwa familia ya mtoto kwa ajili ya kuona hali halisi na kutoa mchango wangu.”

Mbali na msaada huo wa fedha ameahidi kugharamia bima ya afya kwa familia nzima ya mtoto huyo, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na ulinzi wa matibabu.

Kwa upande wake, mama wa mtoto Swaumati Sijaji amemshukuru Mbunge huyo kwa kufika nyumbani kwao na kuwafariji pamoja na kutoa msaada huo ambao utasaidia kumpeleka mtoto waoHospitali ya Kanda ya Bugando kufanyiwa upasuaji wa uvimbe huo.

Hata hivyo familia ya mtoto huyo imesema msaada huo umewapa matumaini mapya ya kuona mtoto wao anapatiwa matibabu stahiki na kurejea katika hali ya kawaida.Hawakutarajia  kupata msaada kwa haraka kiasi hicho huku wakimuahidi kumuombea Mbunge huyo ili aendelee kuwahudumia wananchi kwa moyo wa huruma.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Karagwe Georgiana Mkapapa amesema kitendo hicho kinaonesha namna Mbunge huyo alivyo karibu na wananchi wake, na kuwataka wanawake na wananchi kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono na kumuamini katika jitihada zake za kuwatumikia na kuwaletea maendeleo.








KLABU ya FC Barcelona imeendelea kufanya vyema kwenye michuano yote msimu huu huku wakiwa na malengo ya kuchukua makombe yote msimu huu. Meridianbet wanakwambia kuwa bashiri mechi zote za Barca hapa.

Barcelona imekuwa katika safari yenye ushindani mkubwa msimu huu, ikishiriki mashindano yote makubwa kwa malengo ya kurejesha hadhi yake ya juu barani Ulaya. Ingawa jana timu ilipata matokeo yasiyotarajiwa na kupoteza mechi, hilo halifuti kazi kubwa ambayo imekuwa ikifanywa katika kipindi chote cha msimu.

Kwa mtazamo mpana, mwenendo wa Barcelona umeonyesha uthabiti, maendeleo ya kiufundi, na ari ya ushindani inayostahili pongezi.

Katika La Liga, Barcelona imekuwa miongoni mwa timu zinazowania nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi ambapo mpaka sasa wapo nafasi ya 2 kwenye msimamo baada ya kupoteza mechi ya jana.

Licha ya ushindani mkali kutoka kwa wapinzani wao wa jadi, Barcelona imeendelea kubaki kwenye nafasi nzuri ya kupigania taji hadi hatua za mwisho.

Chukua maokoto leo hii kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Katika Ligi ya Mabingwa Ulaya yaani (UEFA), timu imeonyesha dhamira ya kurejea katika ubora wake wa kimataifa. Mechi kadhaa zimeonyesha ukomavu wa kikosi, hasa kwa wachezaji ambao wamepewa nafasi na sasa wapo kwenye hatua ya 16 bora.

Msimu huu, Barcelona imeendelea na mbio zake katika Copa del Rey, ikiwa na azma ya kutetea au kudai taji hilo. Ushindi muhimu umepatikana dhidi ya wapinzani wenye nguvu, na kuonyesha kuwa kikosi kimejizatiti kuonyesha ushindi kila mechi. Lakini ina kibarua kizito baada ya kupoteza mechi ya kwanza kwa mabao 4-0.

Hadi sasa, Barcelona ipo miongoni mwa timu zinazojivunia uwiano wa ushindi na nafasi za juu kwenye mashindano yote, ikiwa imejipanga vizuri kwa kufikia malengo ya msimu. Timu ina nafasi nzuri ya kushika taji la La Liga, kufika mbali kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, na kudumisha hadhi yake kwenye mashindano ya taifa.

Chini ya kocha mkuu Hans Flick Barca wameendelea kuwa ni timu bora licha za kupata majeruhi ya wachezaji akiwemo Pedri, Gavi, Raphina na wengine wengi.





Na.Mwandishi Wetu

Taasisi ya Jafo Education Foundation imefadhili jumla ya vijana 51 kusoma katika Chuo cha FDC Kisarawe - Mzenga, kwa lengo la kuwawezesha kupata ujuzi wa fani mbalimbali za ufundi.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua miradi na kuzungumza na wananchi katika Kata ya Mzenga, Mbunge wa Jimbo la Kisarawe Mhe.Dkt. Selemani Jafo, amesema vijana hao 51 watatoka katika kata zote 17 za wilaya hiyo na taasisi hiyo itagharamia ada zao za masomo.

"Hii ni fursa muhimu kwa vijana wa Kisarawe kujipatia ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuajiriwa, hasa katika kipindi hiki ambacho soko la ajira linahitaji wataalamu wenye ujuzi wa vitendo."amesema Dkt. Jafo

Dkt.Jafo amesema kuwa Chuo cha FDC Kisarawe – Mzenga ni chuo kipya kilichojengwa wilayani humo na tayari kinatoa mafunzo katika fani mbalimbali zikiwemo ufundi magari, ushonaji, ujenzi, mapishi, umeme, kompyuta pamoja na mafunzo ya muda mfupi.

Aidha, Dkt. Jafo ameeleza kuwa tangu mwaka 2010 amefanikiwa kusaidia zaidi ya vijana 500 kutoka familia zenye changamoto kusoma katika ngazi mbalimbali, ikiwemo kidato cha tano, astashahada, stashahada na shahada.

Katika kuendeleza juhudi za kukuza elimu ya ufundi, tarehe 20 Februari, Dkt. Jafo kupitia taasisi yake amekabidhi msaada wa vyerehani vinne vya umeme katika chuo hicho, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa dhamira kuu ni kuwawezesha vijana katika fani za ufundi ili kujenga msingi imara wa ajira rasmi na zisizo rasmi, pamoja na kuongeza kasi ya maendeleo katika Wilaya ya Kisarawe.





Na Pamela Mollel, Arusha

Habari njema kwa wakazi wa Arusha! Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imependekeza bajeti ya shilingi bilioni 75.4 kwa mwaka wa fedha ujao, hatua inayotajwa kuwa chachu ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, miundombinu na huduma za kijamii.

Bajeti hiyo inatajwa kuwa na neema kubwa kwa wanafunzi wapya zaidi ya 20,000 wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwakani.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika juzi, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Baraka Simon, alisema bajeti hiyo imegawanyika katika sehemu kuu mbili.

Alifafanua kuwa kati ya bilioni 75.4 zilizopendekezwa, fedha hizo zimeelekezwa katika miradi ya maendeleo, huku mapato ya ndani yakitarajiwa kuwa shilingi bilioni 9.2.

“Bilioni 75.4 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo, lakini kwa upande wa mapato ya ndani ni bilioni 9.2. Tuna imani kubwa sana na bajeti hii na tunajua italeta mafanikio makubwa sana na itakuwa rafiki kwa wananchi,” alisema.

Katika hatua nyingine, alisema bajeti hiyo imelenga pia kuandaa vyumba zaidi ya 200 vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza watakaoanza masomo mwakani.

Alieleza kuwa mabadiliko yanayotarajiwa katika mfumo wa elimu yataongeza idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza, baada ya wanafunzi wa darasa la sita kuhitimu na kujiunga na ngazi hiyo sambamba na wenzao wengine.

“Mwakani kutakuwa na mabadiliko ya mfumo wa elimu. Wanafunzi wa darasa la sita wakimaliza watajiunga na kidato cha kwanza, lakini hata hao wengine nao wanatakiwa kuingia kidato cha kwanza. Tumejipanga vyema,” aliongeza.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mlangarini, Emanuel Mrema, alisema wanashukuru kwa bajeti hiyo kwani imegusa nyanja zote muhimu zinazohitajika katika jamii.

Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto katika baadhi ya kata, kupitia bajeti hiyo vijiji vyote vitanufaika na miradi ya maendeleo itakayotekelezwa katika mwaka wa fedha ujao.

Kwa ujumla, bajeti hiyo imeibua matumaini mapya kwa wananchi wa Wilaya ya Arusha, huku matarajio makubwa yakiwekwa katika utekelezaji wake ili kuleta matokeo chanya yanayokusudiwa.



 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkoa wa Geita, Menejimenti ya Mgodi wa Geita na watendaji wa Ofisi yake katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).

*************

Na Mwandishi Wetu

Wito umetolewa kwa makampuni makubwa ya uchimbaji madini nchini kuwekeza katikakuwawezesha wachimbaji wadogo katika nyanja mbalimbali ikiwemo teknolojia za kisasa na usimikaji wa mifumo ya usalama na afya mahali pa kazi ili kujenga uchumijumuishi unaotokana na sekta ya madini.

Wito huo umetolewa na serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, alipofanya ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria yaUsalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabuwa Geita (GGML).

Waziri Sangu ameipongeza menejimenti ya Mgodi huo kwa kuzalisha ajira nyingi kwaWatanzania ambapo GGML imeajiri jumla ya wafanyakazi 2,366 moja kwa moja na4,629 wameajiriwa kupitia wakandarasi mbalimbali wanatoa huduma katika Mgodi waGGML.

Sambamba na pongezi hizo, Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kazi ameutakaMgodi huo kuhakikisha kwamba shughuli zake zinakuwa na athari chanya katikauchumi wa jamii zinazowazunguka kwa kutoa fursa za kazi za muda mfupi ikiwemokuwezesha miradi mbalimbali ya kijamii.

Aidha, Waziri Sangu ameipongeza GGML kwa kuchagua suala la usalama na afya kwawafanyakazi kuwa tunu yao ya kwanza katika shughuli zao za uchimbaji na uchakatajiwa madini jambo ambalo limewafanya kujenga mifumo madhubuti ya kulinda afya nausalama wa wafanyakazi inayozingatia matumizi ya teknolojia za kisasa.

“Ninawapongeza kwa kuweka usalama na afya kama tunu yenu ya kwanza na hiiimejidhirisha katika wasilisho lenu mlilofanya hapa ambapo masuala ya usalama naafya yamechukua nafasi ya juu zaidi ya biashara mnayofanya,” ameeleza Waziri Sangu na kuongeza:

“Pongezi hizi inastahili pia Taasisi ya OSHA ambayo imekuwa ikiwaongoza katikakutekeleza hayo kupitia usimamizi mzuri wa Sheria Na.5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 na miongozo mbalimbali chini ya sheria hiyo ambayowamekuwa wakiitoa kupitia kaguzi zao za mara kwa mara.”

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita,Hashim Abdallah Komba, amesema OSHA ni miongoni mwa Taasisi zenye msaadamkubwa katika kuwezesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kufanyika kwa tija katikaMkoa wa Geita.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema ziara hiyo, inalenga kuona jinsi OSHA inavyoshirikiana na wadau wake kutekeleza Sheria yaUsalama na Afya mahali pa kazi ambayo dhima yake kuu ni kulinda nguvukazi ya Taifa dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi pamoja na kulinda uwekezaji kupitiakuzuia uharibifu wa mali.

Awali, menejimenti ya GGML iliwasilisha taarifa juu ya shughuli zao iliyoainisha jinsiafya na usalama wa wafanyakazi unavyozingatiwa katika shughuli husika. Miongonimwa masuala yaliyoelezwa katika taarifa hiyo ni pamoja na historia ya mgodi ambapoimeelezwa kuwa madini katika mgodi huo yaligunduliwa mnamo mwaka 1898 nauchimbaji rasmi kuanza mwaka 1999.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkoa wa Geita, Menejimenti ya Mgodi wa Geita na watendaji wa Ofisi yake katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita, Menejimenti ya Mgodi wa Geita na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwa ameambatana na watendaji katika Ofisi yake na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita, wakifuatilia wasilisho la taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi huo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwa ameambatana na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi.Khadija Mwenda, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita na watendaji wengine katika Ofisi yake wakitembelea baadhi ya maeneo ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi huo. Katika ziara hiyo, wafanyakazi wa GGML walionesha onesho la jinsi wanavyochukua tahadhari dhidi ya vihatarishi mbalimbali vya ajali na magonjwa katika shughuli zao za kila siku.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML), Bw. Ashraf Suryaningrat, mara baada ya kuhitimisha ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi huo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akifanya majumuisho mara baada ya kuhitimisha ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi.Khadija Mwenda akiwa na Meneja wa OSHA Kanda ya Ziwa, Lodgard Bishanga na Meneja Mwandamizi wa Usalama na Afya wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML), Dr. Kiva Mvungi katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi GGML iliyofanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu.


Na Mwandishi Wetu Wetu - DODOMA


Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) imetoa mafunzo ya vipimo kwa wanafunzi wa Dr. Samia Dodoma Secondary School, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi katika biashara na maisha ya kila siku.

Katika zoezi hilo, wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kuhusu dhima na majukumu ya Wakala huo, pamoja na namna unavyolinda maslahi ya watumiaji na wafanyabiashara kwa kuhakikisha vipimo vinakuwa sahihi na vya kuaminika.

Akizungumza baada ya mafunzo hayo, Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa WMA, Veronica Simba, amesema elimu ya vipimo itatolewa katika mikoa yote ya Tanzania Bara ili kuhakikisha wanafunzi wengi zaidi wanapata uelewa wa matumizi sahihi ya vipimo.

Amesema mpango huo unalenga kukuza uelewa wa masuala ya vipimo kwa vijana, sambamba na kuimarisha utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji katika sekta ya biashara nchini.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Dodoma, Said Ibrahim, amesema mafunzo hayo yanaenda sambamba na uanzishwaji wa Klabu za Vipimo mashuleni ili kuendelea kuandaa mabalozi mahiri watakaotoa elimu ya vipimo shuleni na katika jamii kwa ujumla.

“Kwa Dodoma tayari tumeshatoa mafunzo katika shule mbili ambazo ni Shule ya Msingi Mtemi Mazengo na leo tumetoa hapa katika Shule ya Sekondari ya Dkt. Samia Dodoma. Tunaamini mabadiliko katika matumizi ya vipimo sahihi yataongezeka,” amesema Said.

Naye , Mwalimu Mussa Madandi, ambaye pia ni mlezi wa Klabu ya Vipimo shuleni hapo, amesema elimu hiyo wamekuwa wakiifundisha darasani, lakini mafunzo yaliyotolewa na WMA yamewapa wanafunzi nafasi ya kujifunza kwa vitendo, jambo litakalosaidia kuongeza uelewa na kuimarisha matumizi ya vipimo sahihi.

“Vipimo ni somo tunalolifundisha karibu kila darasa, lakini leo wanafunzi wamepata mafunzo kwa vitendo kutoka kwa wataalamu wenyewe. Naamini hali hii itaongeza hamasa ya kuzingatia usahihi katika matumizi ya vipimo na kuwafanya wawe mabalozi wazuri kwa wazazi wao na jamii inayowazunguka,” amesema Mwalimu Madandi.

Mwanafunzi Itabangola Elias amesema elimu hiyo imewasaidia kuelewa namna ya kutambua vipimo sahihi na kujikinga dhidi ya udanganyifu unaoweza kujitokeza katika biashara.

Baada ya mafunzo hayo, wanafunzi walishiriki kujibu maswali mbalimbali kuhusiana na vipimo na shughuli za Wakala huo, ambapo waliofanya vizuri walipatiwa zawadi mbalimbali kama sehemu ya kuwahamasisha kuendelea kujifunza na kuwa mabalozi wa matumizi sahihi ya vipimo katika jamii.




JE unajua kuwa muda wako wa kuibuka bingwa umefika na Meridianbet?. Weka dau lako unalolitaka leo na ujiweke kwenye nafasi ya wale ambao wataibuka na ushindi siku ya leo.

Ligi pendwa Duniani, EPL inatarajiwa kuendelea ambapo Crystal Palace atamenyana dhidi ya Wolves ambao ni vibonde wa ligi hadi sasa wakiwa na pointi 9 kwenye mechi 26 ambazo wamecheza hadi sasa. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo ijiweke kwenye nafasi nzuri. ODDS KUBWA zipo pale Meridianbet. Bashiri hapa.

Pia kule City Ground kutakuwa na mechi ya kibabe kati ya Nottingham Forest vs Liverpool ambao wanataka kumaliza nafasi za nne kwenye msimamo wa ligi. Mara ya mwisho kukutana Slot na vijana wake walipokea kichapo kizito wakiwa nyumbani. Leo hii wanaweza kulipa kisasi?. Suka jamvi hapa.

London Derby safari hii ni Tottenham vs Arsenal ambao wapo kwenye mbio za ubingwa huku mechi hii ikiwa na umuhimu sana kwao. Presha inazidi kuwa kubwa baada ya kudondosha pointi kwenye michezo ya hivi karibuni. Meridianbet wanampa nafasi kubwa ya kushinda The Gunners. Je wewe unampa nani nafasi ya ushindi leo?. Tengeneza jamvi hapa.

Saka maokoto leo hii kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roulette,Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hispania, LALIGA nayo kama kawaida kuna mitanange ya kukata na shoka Getafe ataumana vikali dhidi ya Sevilla ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 3 pekee huku mechi ya mwisho kukutana, mwenyeji aliondoka na ushindi. ODDS KUBWA zinakungoja pale Meridianbet. Jisajili hapa.

Nao mabingwa watetezi wa ligi, FC Barcelona watakuwa nyumbani kumenyana dhidi ya Levante ambao wanashika nafasi ya 19 kwenye ligi. Vijana wa Hans Flick wanahitaji ushindi kwenye mechi hii ili waweze kutetea taji lao. Je wageni watawazuia?. Mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000 Meridianbet. Beti sasa.

Mechi ya usiku kabisa itakuwa ni hii ya Villarreal vs Valencia ambapo Nyambizi wa Njano yeye yupo nafasi ya 3 huku wageni wao wakiwa nafasi ya 15. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo. Je wewe unampa nani pesa yako akupatie mshindo?. Bashiri hapa.

Vilevile kule Italia, SERIE A itaendelea ambapo Atalanta atakipiga dhidi ya Napoli ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi. Tofauti yao hadi sasa ni pointi 8 huku Meridianbet wakiipa mechi hii ODDS KUBWA. Unangoja nini kutengeneza mkeka wako siku ya leo?. Beti sasa.

Pia AC Milan yeye atakuwa kibaruani kusaka ushindi dhidi ya Parma ambao wanashika nafasi ya 12 huku Milan wao wakiwa nafasi ya 2 kwenye msimamo wa ligi. Wenyeji wapo kwenye mbio za ubingwa huku ushindi wa leo ukiwa ni muhimu sana kwao. Je leo hii wanaweza kushinda?. Suka jamvi hapa.

AS Roma atakuwa nyumbani kukiwasha dhidi ya Cremonese ambao hawapewi nafasi ya kushinda mechi hii. Wageni wapo nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi hadi sasa wakiwa na pointi zao 24 huku wenyeji wao wakiwa na pointi 47. ODDS KUBWA zipo hapa hivyo beti sasa.


-Ammwagia sifa Rais Dkt Samia kwa Mapinduzi ya elimu


NA MWANDISHI WETU, MBEYA

MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amewataka wahitimu wa kidato cha sita nchini kuwa mabalozi wa nidhamu na uzalendo, huku akibainisha kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ni dhamira ya dhati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutengeneza taifa la wasomi wenye ushindani.

Mhe. Itunda ameyasema hayo jana wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya Sekondari Ivume yaliyofanyika jijini Mbeya.


Sifa kwa Rais Samia na Maboresho ya Miundombinu

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, DC Itunda amempongeza kwa dhati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumwaga mabilioni ya fedha mkoani Mbeya kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu ikiwemo madarasa, maabara za kisasa na mabweni.

"Chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Rais Samia, tumeshuhudia mabadiliko makubwa ya mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa wakati ili kuhakikisha watoto wetu wanasoma katika mazingira bora, jambo ambalo limeongeza morali kwa walimu na kuinua kiwango cha ufaulu," alisema Mhe. Itunda.

Wito wa Nidhamu na Uzalendo kwa Wahitimu

DC Itunda amewahimiza wahitimu hao wa Ivume Sekondari kutolewa macho na mafanikio ya muda mfupi, badala yake wazingatie nidhamu na uzalendo wanapoelekea kwenye ngazi za juu za elimu. Aliwasisitiza kuwa Serikali inawategemea kama nguvu kazi ya baadae ya Taifa.

"Nidhamu ndiyo dira ya mafanikio yenu kuanzia sasa. Tunatarajia muwe mabalozi wazuri wa Ivume na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla kule mwendako. Epukeni vitendo vinavyoweza kuharibu mustakabali wenu na wa Taifa lenu," aliongeza.

Maagizo kwa Waliobaki Shuleni

Kwa upande mwingine, Mhe. Itunda amewataka wanafunzi wanaoendelea na masomo kuongeza bidii na kuzingatia maadili mema, akionya kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo vya utovu wa nidhamu ambavyo vinakwamisha juhudi za kuinua taaluma.

Mapema, Uongozi wa Shule ya Sekondari Ivume uliishukuru Serikali ya Mkoa na Wilaya kwa ushirikiano wa karibu, ukiahidi kuendelea kusimamia taaluma na kulea vijana katika misingi ya uzalendo na uwajibikaji.






Top News