-Wizara ya Madini na CRDB waingia makubaliano ya utekelezaji wa programu

-Wachimbaji wadogo kukopeshwa Mitambo ya Uchenjuaji (CIP), Vifaa vya Kuchimba na Fedha za Uendeshaji

-Kikundi cha SAZA GOLD FAMILY wakaribia kuanza kunufaika kupitia leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na BAFEX

-Ni leseni aliyoelekeza Rais Samia kwa wachimbaji wadogo

Dodoma

Ikiwa ni mkakati wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kimitaji, Wizara ya Madini imeingia makubaliano na Benki ya CRDB kupitia programu maalum kwa ajili ya kuwasadia wachimbaji wadogo kwa kuwapatia mikopo kwa ajili ya ununuzi wa mitambo ya uchenjuaji (CIP), vifaa na gharama za uendeshaji.

Akizungumza kwenye kikao cha kujadili mapendekezo ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini katika utoaji wa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini, Waziri Mavunde amesema kupitia makubaliano haya, wachimbaji wadogo wenye leseni za madini wataweza kuomba na kupatiwa mikopo na benki hiyo na kuwezesha uzalishaji wao kuwa wenye tija na mchango wao kuendelea kukua kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali.

Akielezea moja ya wanufaika wa programu hiyo Waziri Mavunde amesema kuwa ni pamoja na kikundi cha SAZA GOLD FAMILY ambapo Benki ya CRDB ipo mbioni kutoa mkopo wa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ununuzi wa mtambo wa kuchenjua madini ya dhahabu na vifaa vya uchimbaji kwa kikundi hicho kinachoendesha shughuli zake katika eneo la Saza mkoani Songwe.

Ameendelea kusema kuwa awali, kupitia ziara ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu katika eneo la Saza, kikundi cha wachimbaji wadogo kupitia Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mulugo waliomba kupatiwa leseni ya uchimbaji wa madini, ambapo Rais Samia alielekeza kikundi hicho kupatiwa leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na Kampuni ya BAFEX.

Amesema ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kikundi cha SAZA GOLD FAMILY kilipewa leseni na kuanza kuchimba madini na kuomba mkopo kwa ajili ya mtambo wa uchenjuaji wa madini na vifaa ambapo mchakato wake ulianza mara moja kupitia Benki ya CRDB.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ameitaka Tume ya Madini na Benki ya CRDB kukamilisha Makubaliano ya Awali (MoU) ifikapo Jumatano ijayo ili taratibu za utoaji wa mkopo zikamilike mapema.

Ameeleza manufaa ya mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini kuwa ni pamoja na uzalishaji kuongezeka na mchango wao kuongezeka kwenye ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali hasa ikizingatiwa kwa sasa wanachangia asilimia 40.

Wakati huohuo, Mhe. Mavunde amezitaka Taasisi za Fedha nchini kuwaamini wachimbaji wadogo wa madini kwa kuweka mazingira rafiki ya mikopo kwani wana utajiri mkubwa wa rasilimali za madini.

“Ninaomba Taasisi za Fedha kuwaamini wachimbaji wa madini kwa kuwa wenyewe kwa wenyewe wana uwezo wa kukopeshana hadi shilingi bilioni tano kwa kuaminiana, mkiweka mazingira mazuri na kuwakopesha mtapata faida kubwa sana kupitia Sekta ya Madini na kukuza mitaji yenu,” amesisitiza Waziri Mavunde.

Naye Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mlugo akizungumza kwenye kikao hicho amempongeza Waziri Mavunde kwa kuwa mlezi wa wachimbaji wadogo wa madini nchini sambamba na kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa lengo la kuhakikisha wanatajirika kupitia Sekta ya Madini.

“Ninampongeza sana Waziri Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kuwapambania wachimbaji wadogo wa madini kuanzia kwenye upatikanaji wa leseni za madini, kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa ajili ya upatikanaji wa mikopo na kutatua changamoto mbalimbali,” amesema Mulugo.

Katika hatua nyingine ameitaka Benki ya CRDB kuajiri wataalam wa madini ili kuwa na uelewa wa Sekta ya Madini hali itakayowawezesha kutoa mikopo kwa urahisi zaidi na kuweka mazingira mazuri ya ukopeshaji.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa sambamba na kupongeza Benki ya CRDB kwa nia yake ya kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini amewataka kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini kuhusu masuala ya fedha ili waweze kukopa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba ameshauri Benki ya CRDB kuendelea kuweka mazingira mazuri ya utoaji wa mikopo kwa kuangalia historia ya uzalishaji kwa wachimbaji wadogo wa madini ili waweze kukopesheka.

Wakati huohuo akizungumza kwenye kikao hicho, Mwenyekiti wa Songwe Gold Family, Simon Ndaki ameshukuru sana kwa msaada wa Serikali kwa kuwaunganisha na Benki ya CRDB na kufanikisha hatua za awali za maombi ya mkopo huo.

“Tunamshukuru sana Waziri wa Madini na timu yake kwa kutupatia leseni ya madini na kusimamia kikamilifu hatua zote za awali za maombi ya mkopo kwenye kikundi chetu chenye wanachama 264, tunaamini kupitia uzalishaji wetu kwa kutumia vifaa vya kisasa mchango wetu unakwenda kuwa mkubwa kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali,” amesema Ndaki.











Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kaloleni na Shule ya Sekondari ya Msasani zinazozunguka Mlima wa Kilimanjaro walioshiriki zoezi la kupanda miti na kupata mitungi ya gesi , kutoka kampuni ya Taifa gas kwenye programu ya utunzaji wa mazingira ya 'Guardians of the Peak 2026'

Meneja Masoko wa Kampuni ya Taifa gas , Oscar Shelukindo akigawa mtungi wa gesi kwa mmoja wa washiriki wa programu ya uhifadhi wa mazingira ‘Guardians of the Peak 2026’ iliyofanyika Mkoani Kilimanjaro

Wanafunzi wa sekondari ya Msasani ya Manispaa ya Moshi wakiwa kwenye zoezi la upandaji wa miti na kujifunza utunzaji wa mazingira katika programu ya ‘Guardians of the Peak 2026’ iliyodhaminiwa na kampuni ya Taifa gas

Meneja Masoko wa Kampuni ya Taifa gas wa tatu kushoto , Oscar Shelukindo baada ya zoezi la kupanda miti na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali kwenye programu ya ‘Guardian of the Peak 2026’ iliyofanyika Mkoani Kilimanjaro

Wanafunzi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya zoezi la upandaji wa miti na kujifunza kuhusu nishati safi ya kupikia kwenye kilele cha programu ya ‘Guardians of the Peak 2026’ iliyofanyika Mkoani Kilimanjaro

Meneja Masoko wa Taifa Gas , Oscar Shelukindo akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi baada ya kushiriki zoezi la kupanda miti na uhifadhi ya mazingira katika programu’ Guardians of the Peak 2026’ Mkoani Kilimanjaro.


**
Kampuni ya usambazaji wa gesi nchini, Taifa Gas imedhamini programu ya kutangaza vivutio vya utalii nchini duniani na uhifadhi wa mazingira kupitia kupanda mlima Kilimanjaro ijulikanayo kama Guardians of the Peak msimu wa pili itakayofanyika kuanzia Januari 20-31, 2026 yenye kauli mbiu “Embrace Clean Energy, Protect Tomorrow”.


Kupitia programu hii mbali na washiriki kupanda Mlima Kilimanjaro pia watashiriki katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na utunzaji wa mazingira ikiwemo upandaji miti, kupatiwa elimu juu ya mabadiliko ya tabia nchi na uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ya gesi ili kupunguza uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya ukataji kuni na mkaa.


Akiongelea udhamini wa programu hii, Meneja wa Taifa Gas, Davis Deogratius amesema udhamini huu ni mwendelezo wa kampuni ya Taifa Gas kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kuepukana na matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira kwa ajili ya kulinda mazingira na afya za wananchi.


“Kupitia programu hii,Taifa Gas tumedhamini wanafunzi na baadhi ya wafanyakazi wetu kushiriki kupanda mlima Kilimanjaro vilevile kushiriki zoezi la kupanda miti katika sehemu mbalimbali za halmashauri ya mji wa Moshi,kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa vikundi vya wanawake wajasiriamali na kuwagawia mitungi ya gesi”, amesema Deogratius.


Amesema Taifa Gas imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono jitihada za Serikali kulinda mazingira kupitia uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia na usambazaji wa gesi katika makundi mbalimbali ya jamii katika sehemu za mijini na vijijini nchini kote na imekuwa ikitunukiwa tuzo mbalimbali za heshima za utunzaji mazingira kutoka Serikali na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi.


Taifa Gas imedhamini programu hii ya vijana ya Guardians of the Peak katika hatua za kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kupikia na kutangaza vivutio vya utalii hapa nchini.


Guardians of the Peak msimu wa pili inajumuisha wadau mbalimbali wa mazingira na utalii na wataalamu wa kuandaa makala za utalii (Documentary) zitakazotumika kutangaza vivutio vya utalii katika soko la China na duniani kote sambamba na uhamasishaji wa utunzaji wa mlima Kilimanjaro na kuhamasisha utali wa ndani.

Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amekabidhi jumla ya vifaa vya TEHAMA 1,429 vyenye thamani ya Shilingi Bilioni 5.2 kwa ajili ya Ofisi za Ardhi katika halmashauri 184 nchini, pamoja na ofisi za Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa.



Makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 23 Januari, 2026, jijini Dodoma, wakati wa kikao kazi kati ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wale wa taasisi zilizo chini ya Wizara.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni juhudi ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuhakikisha huduma katika sekta ya ardhi zinaimarishwa na kuboreshwa kwa ofisi za ardhi kupatiwa vifaa ili kurahisisha utendaji kazi wao katika kuwahudumia wananchi.

Vifaa vya TEHAMA vilivyokabidhiwa ni Kompyuta za kawaida 424, Kompyuta zenye uwezo mkubwa kwa ajili ya kazi za ardhi (GIS computer) 250, Skrini za Kusomea Ramani (GIS display) 391, Skana 41, Printa 44, Simu za Mezani zinazotumia Mtandao wa Taasisi bila kulipia (IP phones) 82, pamoja na UPS 197.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amesema Wizara yake imefanya maboresho mbalimbali ya kisera na kiutendaji, ikiwemo mifumo kidijiti ya utoaji wa huduma za sekta ya ardhi.

Amesisitiza kuwa, Wizara yake haitavumilia ucheleweshaji wowote wa utoaji huduma kwa wananchi kwa visingizio vya kukosa vitendea kazi.

Hata hivyo, amewataka watendaji hao wa sekta ya ardhi nchini, kuhakikisha vifaa hivyo vinatunzwa sambamba na kuzingatia matumizi ya mifumo ya TEHAMA iliyopo kwa lengo la kuhakikisha huduma zinatolewa kwa ufanisi.

Moja ya vipaumbele vya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika Bajeti ya Mwaka 2025/2026 ni kuimarisha mifumo ya TEHAMA katika utunzaji wa kumbukumbu, utoaji wa huduma, ukusanyaji wa maduhuli, na upatikanaji wa taarifa za ardhi na uthamini.Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimkabidhi vifaa vya TEHAMA kwa ajili ya kazi za sekta ya Ardhi Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mtwara Bw. Fredrick Mrema wakati wa Kikao Kazi kati ya Waziri wa Ardhi na Watumishi wa Sekta ya Ardhi tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma.Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya akimkabidhi vifaa vya TEHAMA Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Lindi Geofrey Martin wakati wa Kikao Kazi kati ya Waziri wa Ardhi na Watumishi wa Sekta ya Ardhi tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma.Sehemu ya vifaa vya TEHAMA vilivyokabidhiwa kwa ajili ya Ofisi za Ardhi katika halmashauri na ofisi za mikoa kuboresha utendaji kazi (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)











Na Munir Shemweta, WANMM

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amezielekeza Ofisi za Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa nchini kuhakikisha zinachukua hatua kwa wadaiwa wote wa kodi ya pango la ardhi.

Mhe. Dkt. Akwilapo ametoa kauli hiyo leo, tarehe 23 Januari, 2026, wakati wa kikao chake na watumishi wa Sekta ya Ardhi kilichofanyika jijini Dodoma.

Amesema Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ina jukumu la kukusanya mapato yatokanayo na Sekta ya Ardhi, hadi sasa imekusanya asilimia 37 ya lengo lake la kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 290.

"Ninatambua kuwa kila mkoa umepewa lengo la kukusanya maduhuli; hivyo, kila mmoja wetu atapimwa utendaji wake katika kufikia malengo ya makusanyo yaliyowekwa na mfanye bidii na uonekane unafanya vinginevyo tutakuita na kukuliza kama unatosha hapo ulipo," amesema.

Ikumbukwe kuwa tarehe 23 Desemba, 2025, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alitoa taarifa kwa umma ya kuwataka wamiliki wote wa ardhi kulipa kodi ya pango la ardhi kufikia Desemba, 2025, kabla Wizara haijaanza kuchukua hatua za kisheria.

Hatua zinazoweza kuchukuliwa kwa wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kufutiwa umiliki wa ardhi. Hatua hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi, Sura ya 113, fungu la 48(1), 50, 51 na 52.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya amewataka Makamishina wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa kuyapitia upya maombi yote ya wananchi waliokamilisha taratibu zote za kuomba hati milki za ardhi.

Ameagiza orodha kamili ya waombaji hao ivutwe kutoka kwenye Mfumo wa e-Ardhi na kuwasilishwa ofisini kwake kufikia Jumanne, tarehe 27 Januari 2026 ambapo amesisitiza kuwa, ucheleweshaji wowote hautavumiliwa na hatua zitachukuliwa kwa watakaokiuka maagizo hayo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga amewataka watumishi wa Sekta ya Ardhi kufanya kazi kwa kuzingatia utu na weledi. Aidha, amesisitiza watumishi hao kutatua changamoto za sekta ya ardhi kwa wakati huku wakihakikisha wananchi wanatatuliwa migogoro yao katika eneo husika kwa kupata majibu stahiki.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akizungumza na watumishi wa sekta ya ardhi wakati Kikao Kazi kati ya Waziri wa Ardhi na Watumishi hao tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma.





Sehemu ya Watumishi wa Sekta ya Ardhi wakiwa katika kikao kazi na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya akizungumza wakati Kikao Kazi kati ya Waziri wa Ardhi na Watumishi wa sekta ya ardhi tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza katika Kikao Kazi cha Waziri wa Ardhi na Watumishi wa sekta ya ardhi tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dodoma.

Katibu wa TUGHE tawi la Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Sili Mrisho akizungumza katika kikao kazi cha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo tarehe 23 Januari 2026 (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, amezindua rasmi Kitita cha Huduma Muhimu ya Bima ya Afya kwa Wote, kinachotarajiwa kuanza kutumika Januari 26 mwaka huu, sambamba na kuanza kwa usajili wa wananchi awamu ya kwanza katika mfumo wa Bima ya Afya kwa Wote.

Akizungumza leo Januari 24 jijini Dodoma wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, kilichowakutanisha Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya, Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Tanzania Bara pamoja na watumishi walio chini ya Wizara hiyo, kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji mzuri wa mpango huo.

Mchengerwa amesema kitita hicho kitagharimu shilingi 150,000 kwa familia yenye watu wasiozidi sita, Ameeleza kuwa utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote utazingatia wananchi wasio na uwezo wakiwemo wazee, watoto, wanawake wajawazito na watu wenye ulemavu, ambao watagharamiwa na Serikali.

Waziri Mchengerwa amesema Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, Sura ya 161, Kifungu cha 13, imeanzisha kitita cha mafao ya huduma muhimu, na kwamba Kanuni ya 31(4) ya Kanuni za Bima ya Afya kwa Wote (T.S. Na. 809 za mwaka 2024) zinampa Waziri wa Afya mamlaka ya kutangaza kwa umma kitita hicho.

Kwa mujibu wa Waziri Mchengerwa, kitita cha huduma muhimu kwa awamu ya kwanza kitawahusisha mchangiaji, mwenza wa mchangiaji na wategemezi wanne ambao ni mzazi wa mwanachama au wa mwenza wake, mtoto wa kumzaa, kuasili au wa kambo, pamoja na ndugu wa mwanachama aliye chini ya umri wa miaka 21.

Kwa upande wake, Mratibu wa Bima ya Afya kwa wote Kitaifa, Tumainieli Macha, amesema dhana ya Bima ya Afya kwa Wote inalenga malipo ya kabla ya huduma, uchangiaji wa pamoja, uwajibikaji wa pamoja, usawa, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wote.

Ameongeza kuwa jumla ya wananchi 3,695,465, sawa na kaya 931,693, wametambuliwa kuwa ni wasio na uwezo, wakiwemo wanawake wajawazito na watu wenye ulemavu. Aidha, wapo wazee 229 na watoto 267 wanaohudumiwa katika vituo maalum chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Amesema Katika awamu ya kwanza ya utekelezaji, jumla ya wananchi 1,457,602, sawa na kaya 276,004, wakiwemo wazee 229 na watoto 267, watasajiliwa na kugharamiwa na Serikali kupitia Halmashauri zote nchini.

Kwa ujumla, uzinduzi wa Kitita cha Huduma Muhimu ya Bima ya Afya kwa Wote unaashiria hatua muhimu ya Serikali katika kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha. 

Serikali imesisitiza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau wote ili kuhakikisha utekelezaji wa mpango huo unakuwa endelevu, jumuishi na wenye tija kwa maendeleo ya afya ya jamii na taifa kwa ujumla.





 

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Judith Kapinga amefanya ziara katika kiwanda cha ALAF Limited, kinachoongoza katika suluhisho mbalimbali za ujenzi Tanzania na kusema ameridhishwa na viwango vya uzalishaji kiwandani hapo.

Kapinga aliyekuwa ameongozana na viongozi wengine kutoka idara mbalimbali za wizara hiyo, alisema ALAF ni miongini mwa viwanda vya kuigwa kwani kimeonesha mfano halisi wa Tanzania yenye viwanda.

“Ubora wa bidhaa niliouona leo unathibitisha kuwa tunaweza kwani bidhaa hizi zinaweza kuuzwa hata nje ya nchi na kukidhi viwango vinavyotakiwa,” alisema na kuongeza kuwa serikali itaendelea kulinda viwanda vya ndani ili vizalishe kwa faida. 

Amefafanua uamuzi wa ALAF kuwekeza katika mtambo wa kuzalisha mabati ya rangi ambayo uzalishaji wake ulianza mwaka jana, ulikuwa sahihi kwani sasa watanzania wanaweza kuipata bidhaa hiyo kwa urahisi.

“Hapo awali nafahamu kuwa tulikuwa tunaagiza mabati haya kutoka nje ya nchi lakini sasa tunapata hapa hapa ALAF kwa urahisi na kwa haraka,” amesema na kuongeza kuwa uwepo wa mtambo huu umeongeza ajira kwa watanzania.

Amesema  serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote katika sekta hii ili kuhakikisha uzalishaji haukwami kwa namna yoyote kwa kushugulikia changamoto mbalimbali zinazoibuka kwa haraka ili pamoja na mambo mengine kuvutia uwekezaji zaidi.

“Milango yetu ikoa wazi kabisa na tunawahimiza mje tujadiliane pale ambapo mnapata changamoto ili tuzishugulikie kwa haraka kwa pamoja,” amesisitiza.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa ALAF Limited Bibhu Nanda amemshukuru Waziri Kapinga kwa kufanya ziara hiyo na kuahidi kuwa ALAF itaendelea kushirikiana na serikali kwa karibu ili malengo ya pande zote mbili yafikiwe kikamilifu.

“Lengo letu kuu ni kuendelea kuwa namba moja katika uzalishaji wa mabati na bidhaa nyingine za ujenzi kwani ndio kampuni kongwe ya mabati ambayo mwaka huu inaadhimisha miaka 63 tangu kuanzishwa kwake,” amesema.

Ametoa mwito kwa watanzania wajivunie bidhaa zinazozalishwa ndani hususani na kampuni ya ALAF.

ALAF Limited ni kampuni inayoongoza nchini Tanzania kwa kutengeneza mabati ya kuezekea nyumba. Ni kampuni iliyoanzishwa mwaka 1960, na inaendelea kuwa mdau muhimu katika maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini.

ALAF imeunganisha kikamilifu operesheni, si tu kwa kutengeneza mabati, lakini pia kwa kuzalisha vifaa vinavyotumika katika shughuli mbalimbali za uezekaji wa nyumba. ALAF Limited hutengeneza vifaa mbalimbali vya metali kwa matumizi mbalimbali ya uezekaji wa nyumba.


 Mwisho




 

▪️Wizara ya Madini na CRDB waingia makubaliano ya utekelezaji wa programu

▪️Wachimbaji wadogo kukopeshwa Mitambo ya Uchenjuaji (CIP), Vifaa vya Kuchimba na Fedha za Uendeshaji

▪️Kikundi cha SAZA GOLD FAMILY wakaribia kuanza kunufaika kupitia leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na BAFEX

▪️Ni leseni aliyoelekeza Rais Samia kwa wachimbaji wadogo

Dodoma.

Ikiwa ni mkakati wa kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kimitaji, Wizara ya Madini imeingia makubaliano na Benki ya CRDB kupitia programu maalum kwa ajili ya kuwasadia wachimbaji wadogo kwa kuwapatia mikopo kwa ajili ya ununuzi wa mitambo ya uchenjuaji (CIP), vifaa na gharama za uendeshaji.

Akizungumza kwenye kikao cha kujadili mapendekezo ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na Tume ya Madini katika utoaji wa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini, Waziri Mavunde amesema kupitia makubaliano haya, wachimbaji wadogo wenye leseni za madini wataweza kuomba na kupatiwa mikopo na benki hiyo na kuwezesha uzalishaji wao kuwa wenye tija na mchango wao kuendelea kukua kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali.

Akielezea moja ya wanufaika wa programu hiyo Waziri Mavunde amesema kuwa ni pamoja na kikundi cha SAZA GOLD FAMILY ambapo Benki ya CRDB ipo mbioni kutoa mkopo wa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ununuzi wa mtambo wa kuchenjua madini ya dhahabu na vifaa vya uchimbaji  kwa kikundi hicho kinachoendesha shughuli zake katika eneo la Saza mkoani Songwe.

Ameendelea kusema kuwa awali, kupitia ziara ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu katika eneo la Saza, kikundi cha wachimbaji wadogo kupitia Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mulugo waliomba kupatiwa leseni ya uchimbaji wa madini, ambapo Rais Samia alielekeza kikundi hicho kupatiwa leseni ya uchimbaji iliyokuwa inamilikiwa na Kampuni ya  BAFEX.

Amesema ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini kikundi cha SAZA GOLD FAMILY  kilipewa leseni na kuanza kuchimba madini na kuomba mkopo kwa ajili ya mtambo wa uchenjuaji wa madini na vifaa ambapo mchakato wake ulianza mara moja kupitia Benki ya CRDB.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde ameitaka Tume ya Madini na Benki ya CRDB kukamilisha Makubaliano ya Awali (MoU) ifikapo Jumatano ijayo ili taratibu za utoaji wa mkopo zikamilike mapema.

Ameeleza manufaa ya mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini kuwa ni pamoja na uzalishaji kuongezeka na mchango wao kuongezeka kwenye ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali hasa ikizingatiwa kwa sasa wanachangia asilimia 40.

Wakati huohuo, Mhe. Mavunde amezitaka Taasisi za Fedha nchini kuwaamini wachimbaji wadogo wa madini kwa kuweka mazingira rafiki ya mikopo kwani wana utajiri mkubwa wa rasilimali za madini.

“Ninaomba Taasisi za Fedha kuwaamini wachimbaji wa madini kwa kuwa wenyewe kwa wenyewe wana uwezo wa kukopeshana hadi shilingi bilioni tano kwa kuaminiana, mkiweka mazingira mazuri na kuwakopesha mtapata faida kubwa sana kupitia Sekta ya Madini na kukuza mitaji yenu,” amesisitiza Waziri Mavunde.

Naye Mbunge wa Songwe, Mhe. Philipo Mlugo akizungumza kwenye kikao hicho amempongeza Waziri Mavunde kwa kuwa mlezi wa wachimbaji wadogo wa madini nchini sambamba na kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa lengo la kuhakikisha wanatajirika kupitia Sekta ya Madini.

“Ninampongeza sana Waziri Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kuwapambania wachimbaji wadogo wa madini kuanzia kwenye upatikanaji wa leseni za madini, kuwaunganisha na Taasisi za Fedha kwa ajili ya upatikanaji wa mikopo na kutatua changamoto mbalimbali,” amesema Mulugo.

Katika hatua nyingine ameitaka Benki ya CRDB kuajiri wataalam wa madini ili kuwa na uelewa wa Sekta ya Madini hali itakayowawezesha kutoa mikopo kwa urahisi zaidi na kuweka mazingira mazuri ya ukopeshaji.

Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa sambamba na kupongeza Benki ya CRDB kwa nia yake ya kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo wa madini amewataka kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini kuhusu masuala ya fedha ili waweze kukopa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba ameshauri Benki ya CRDB kuendelea kuweka mazingira mazuri ya utoaji wa mikopo kwa kuangalia historia ya uzalishaji kwa wachimbaji wadogo wa madini ili waweze kukopesheka.

Wakati huohuo akizungumza kwenye kikao hicho, Mwenyekiti wa Songwe Gold Family, Simon Ndaki ameshukuru sana kwa msaada wa Serikali kwa kuwaunganisha na Benki ya CRDB na kufanikisha hatua za awali za maombi ya mkopo huo.

“Tunamshukuru sana Waziri wa Madini na timu yake kwa kutupatia leseni ya madini na kusimamia kikamilifu hatua zote za awali za maombi ya mkopo kwenye kikundi chetu chenye wanachama 264, tunaamini kupitia uzalishaji wetu kwa kutumia vifaa vya kisasa mchango wetu unakwenda kuwa mkubwa kwenye makusanyo ya maduhuli ya Serikali,” amesema Ndaki.





 

 

Msajili wa Baraza la Ushindani (FCT), Mhe. Mbegu Kaskasi,akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha ya kuwajengea uwezo kuhusu matumizi ya mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing).

ARUSHA:

Baraza la Ushindani (FCT) limewahimiza wadau na wafanyabiashara mkoani Arusha kutumia kikamilifu mfumo wa usajili wa mashauri kwa njia ya kielektroniki (e-filing), lengo likiwa ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama katika uwasilishaji wa mashauri.

Akizungumza katika mafunzo hayo Msajili wa Baraza hilo, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema mfumo huo wa kisasa umeundwa ili kurahisisha usajili wa mashauri na rufaa bila wadau kulazimika kufika katika ofisi za FCT, hatua ambayo itaokoa muda na kuongeza ufanisi.

“Mfumo huu utaimarisha uwazi, kasi ya utoaji haki na kupunguza usumbufu kwa wadau,” alisema Mhe. Kaskasi, akibainisha kuwa hatua hiyo inakwenda sambamba na msukumo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma."amesema Mhe.Kaskasi

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Moses Pesha, amelipongeza Baraza kwa kuendelea kutoa elimu kwa wanaohusika na wananchi kwa ujumla, akisema hatua hiyo imeongeza uelewa na kuimarisha imani ya wananchi katika mifumo ya utoaji haki.

Naye Afisa TEHAMA wa FCT, Ndg. Athumani Kanyegezi, amesema mfumo wa e-filing unaimarisha usalama wa taarifa na kuongeza urahisi wa kuzifikia ndani ya muda mfupi, tofauti na mfumo wa zamani wa kuhifadhi mafaili kwa mikono.

Katika upande wa wadau, mfanyabiashara wa jijini Arusha, Bi. Jonia Karumuna, ameipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara, kwa kuwezesha taasisi kama Baraza la Ushindani kuendelea kulinda haki za wafanyabiashara na kusikiliza rufaa zinazotokana na migogoro kutoka Tume ya Ushindani (FCC) na mamlaka mbalimbali za udhibiti ikiwemo EWURA, LATRA, TCRA, TCAA na PURA.

Amesema uwepo wa Baraza hilo umeongeza imani kwa wafanyabiashara kutokana na mchango wake katika kuhakikisha haki inatolewa kwa wakati na kwa kuzingatia misingi ya ushindani wa haki nchini.


Top News