Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 20,2026 amefanya mazungumzo na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Emmanuel Tutuba, ofisini kwa Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma.


Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, amekutana na uongozi wa Chama cha Mabroka wa Madini Tanzania (CHAMMATA) jijini Dodoma kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili mabroka wa madini nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, pamoja na watendaji wengine kutoka Wizara ya Madini na Tume ya Madini, hatua inayoonesha dhamira ya Serikali kushirikiana kwa karibu na wadau wa sekta ya madini katika kuendeleza sekta hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wanachama wa CHAMMATA, Mwenyekiti wa chama hicho, Jeremia Kituyo, amewasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili mabroka wa madini, ambapo mara baada ya kusikiliza hoja na maoni yaliyowasilishwa, Naibu Katibu Mkuu Mbibo amewahakikishia viongozi wa CHAMMATA kuwa Serikali itayafanyia kazi mapendekezo hayo kwa kushirikiana na taasisi husika, ili kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Mbibo amesisitiza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Madini imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wadau wote wa sekta ya madini, wakiwemo wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini, wanafanya kazi katika mazingira rafiki, salama na yenye tija kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Ameongeza kuwa jitihada hizo zinalenga kuongeza uzalishaji, kuimarisha biashara ya madini kwa uwazi na ushindani, pamoja na kuhakikisha mchango wa sekta ya madini unaendelea kukua na kuchangia ipasavyo katika Pato la Taifa na maendeleo ya uchumi wa nchi kwa ujumla.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau wa sekta ya madini wameipongeza Wizara ya Madini kwa kuchukua hatua kubwa za kuwawezesha wananchi, ikiwemo utoaji wa leseni za madini kwa vikundi vya vijana, kuwarasimisha wadau wa madini na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za madini kwa mujibu wa sheria na kanuni za madini.

Aidha, wadau hao wameiomba Wizara ya Madini kuendelea kutoa msaada zaidi, hususan katika kuwaunganisha na Taasisi za Fedha ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo itakayowaongezea uwezo wa mitaji na kuchochea ukuaji wa biashara zao za madini nchini.



Na Mwandishi wetu Dodoma.

Brigedia Jenerali Hassan Mabena ambaye ni Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ametoa Rai kwa Vijana wa Kitanzania,Wazazi na Walezi kutorubuniwa na yeyote kutoa fedha kwaajili ya kununua nafasi au fursa ya kujiunga na nafasi za JKT zilizotangazwa leo hii.

Brigedia Jenerali Mabena ameyasema hayo leo Jijini Dodoma Januari 20,2026 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari akitoa Taarifa ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele ya kuwataarifu Vijana wote wa Tanzania Bara na Visiwani kuhusu nafasi za kjiunga na mafunzo ya JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2026 ambayo mchakato wake utaanza Januari 26,2026.

Na kuwasisitiza Vijana wa Kitanzania kwenda katika ngazi ya Halmashauri,Wilaya na Mikoa ambako ndiko mchakato unakofanyika kwa kushuka chini hadi ngazi ya Tarafa na Vijiji ili kupata fursa hiyo kwa wale ambao watakidhi vigezo na mahitajio kama ilivyoeleelezewa katika tovuti ya JKT. 

"Msisitizo wangu ni kwamba nafasi hizi haziuzwi kwahiyo pasije pakatokea mtu yeyote akataka kutumia fursa hii kwa kusema kwamba anaweza akampatia Mtanzania yeyote nafasi ya kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa kwa kuweza kutoa kiasi cha pesa iwe kwa kutumiwa ujumbe wa simu au ana kwa nana".

Aidha amesema kuwa utaratibu wa vijana kuomba nafasi hiyo na hatimaye kuchaguliwa kujiunga na mafunzo unaratibiwa na Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambako mwombaji anaishi hivyo ni vema kwenda huko ili kuepukana na utapeli wa mitandaoni.

Pamoja na kubainisha kuhitajika kwa vijana wenye taaluma za Diploma in Information Technology, Diploma in Business Information System, Diploma in Computer Science,Diploma in Information and Communication Technology (ICT) pamoja na taaluma zinginezo nyingi na mahitajio kama ilivyoanishwa katika tovuti ya Jeshi la Kujenga Taifa ya www.jkt.mil.tz.

"Utaratibu wa vijana kuomba na hatimaye kuchaguliwa kujiunga na mafunzo hayo unaratibiwa na Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambako mwombaji anaishi".

Jeshi la Kujenga Taifa huwa linaendesha mafunzo ya aina tatu kama vile mafunzo ya lazima,mafunzo ya kujitolea kama haya yaliyo tangazwa na pia mafunzo kwa makundi maalum pale inapohitajika kwa wale wanaofanya kazi na jamii.











📍Accra, Ghana

Tanzania is set to deepen domestic participation, industrial growth and value retention in its mining sector following the strengthening of institutional collaboration with Ghana on Local Content implementation.


The two countries are enhancing cooperation on policies and best practices aimed at increasing the participation of local citizens and firms across the mining value chain, strengthening domestic institutions and ensuring that a greater share of mineral wealth benefits national economies.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema Mabalozi wa Mashina ndiyo nguzo ya kukipambania Chama,Kwani ndiyo macho, masikio na daraja la kuunganisha Chama Cha Mapinduzi na kuendelea kulinda umoja wao kama nguvu ya kusonga mbele ili kuwatumikia wananchi.

Akizungumza leo Januari 20,2026 katika Mkutano wake na Mabalozi wa Mashina Mkoa wa Dodoma, Dkt Migiro amesema Mashina ni ngome ya ulinzi  wa chama  kwani yataendelea kuwa Walezi, na kuwaunganisha wananchi pamoja, kwani siasa Lazima iende sambamba na uchumi ndio maana Mashina yanatija kwa Chama.

Amesema ni mahala pa kuikusanya jamii pamoja, kutangaza kazi nzuri inayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, amewataka kufanya vikao vya mara kwa mara na kufikisha maadhimio ngazi za juu, ambapo kupitia Chama wanaweza kuishauri serikali iliyoko madarakani.

Dkt. Migiro ametoa wito kwa viongozi wa ngazi zote za Kitaifa, kuhakikisha wanahudhuria vikao vya Chama kwenye ngazi za Mashina, ili kujadili kwa pamoja na kutatua au kueleza  ahadi walizoahidi watakaposhika Dola zimefikia wapi utekelezaji wake, ili kulinda umoja wa Chama na kuwa nguvu ya kusonga mbele kuwatumikia wananchi.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Wabunge waliohudhuria mkutano huo, Mbunge wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde, amesema kuwa katika miaka mingi iliyopita hakuna kipindi ambacho Chama kimewaangalia Mabalozi vizuri kama awamu hii ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, akitoa rai kwa Mabalozi na viongozi wote kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Katibu Mkuu.














Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga, ametembelea Kata za Mkako na Kihangimahuka katika mwendelezo wa ziara yake ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi mkubwa waliompatia yeye na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lihale, Mhe. Kapinga aliahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Wilaya pamoja na taasisi husika ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, hususan katika sekta za miundombinu, maji na umeme.

“Serikali ipo pamoja nanyi, na mimi kama Mbunge wenu nitaendelea kushirikiana na viongozi wa wilaya na taasisi zote kuhakikisha changamoto zenu zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu".

Katika kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya elimu, Mhe. Kapinga alitoa msaada wa bati 50 za geji 28 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 1.7 pamoja na kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya ununuzi wa kenchi, kwa ajili ya ujenzi wa chumba kimoja cha darasa katika Shule ya Msingi Liale.

Aidha, alitembelea Shule ya Sekondari Kihangimahuka ambapo alikabidhi kompyuta moja yenye thamani ya shilingi milioni 2.5 pamoja na mifuko 50 ya saruji yenye thamani ya shilingi laki tisa, ikiwa ni jitihada za kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji. Vilevile, aliahidi kuipatia shule hiyo mashine ya fotokopi kabla ya kumalizika kwa mwezi Februari 2026.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Vijijini alisema Serikali itaendelea kuleta miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Mbinga Vijijini, hususan katika sekta ya afya, alieleza kuwa jumla ya wahudumu wa afya 100 wameanza kuwasili katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri, wakiwemo madaktari zaidi ya 10, manesi wenye shahada zaidi ya 30 pamoja na wataalamu wengine wa afya.

Aidha, alimpongeza Mhe. Kapinga kwa mchango wake katika kuboresha huduma za afya, ikiwemo kuwasaidia kupata gari la wagonjwa (ambulance) ambalo limekuwa likisaidia kwa kiasi kikubwa kusafirisha wagonjwa, pamoja na ahadi yake ya kukarabati jengo la kinamama katika Zahanati ya Lihale.

Kwa upande wa wananchi wa Kata za Mkako na Kihangimahuka walimpongeza na kumshukuru Mbunge wao kwa kuendelea kutoa michango yake binafsi katika miradi ya maendeleo, wakieleza kuwa hatua hizo zimeongeza mshikamano na ari ya wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii.

Ziara hiyo ni sehemu ya mkakati wa Mbunge huyo wa kuimarisha ushirikiano kati ya wananchi, viongozi na taasisi za serikali kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu katika Jimbo la Mbinga Vijijini.











Na Pamela Mollel,Arusha

Wawekezaji wazawa wadogo na wa kati wamepata fursa adhimu ya kuunganishwa moja kwa moja na vyanzo vya mitaji, masoko pamoja na vivutio mbalimbali vya uwekezaji, kupitia jukwaa maalum lililoandaliwa na Chemba ya Taifa ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TNCC), kwa kushirikiana na Mamlaka ya Uwekezaji Tanzania (TISEZA) pamoja na Baraza la Biashara Afrika Mashariki (EABC).

Jukwaa hilo, lililofanyika mkoani Arusha, liliwakutanisha wawekezaji wa ndani kwa lengo la kufungua fursa mpya za uwekezaji, kuwaunganisha na taasisi za kifedha, pamoja na kuwapatia mwongozo wa namna ya kupata mitaji kwa ajili ya kukuza mnyororo wa thamani wa bidhaa na huduma za ndani.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gerald Teri, aliwahimiza wawekezaji wazawa kusajili miradi yao ili kupata Vyeti vya Uwekezaji, akieleza kuwa vyeti hivyo vinatoa ulinzi wa kisheria pamoja na vivutio mbalimbali ikiwemo msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na ushuru wa forodha kwa mashine na vifaa vya uzalishaji.

Kwa upande wa upatikanaji wa mitaji, Benki ya Maendeleo ya Tanzania (TIB) ilieleza dhamira yake ya kusaidia wawekezaji wadogo na wa kati kupitia mikopo yenye masharti nafuu, hususan kwa miradi ya viwanda na biashara zinazoongeza thamani.

Akizungumza kwa niaba ya benki hiyo, Mkurugenzi wa Mipango wa TIB, Joseph Felix Chilambo, alisema benki hiyo inalenga kuhakikisha changamoto ya mtaji haiwi kikwazo kwa Watanzania wenye nia ya kuwekeza katika shughuli za uzalishaji.

Naye Rais wa TNCC, Vicent Minja, alisisitiza kuwa jukumu kuu la chemba hiyo ni kuwaunganisha wawekezaji wazawa na masoko ya ndani na ya kimataifa. Alibainisha kuwa kupitia mtandao mpana wa TNCC, mwekezaji mdogo kutoka Arusha anaweza kupata washirika wa kibiashara kutoka sehemu mbalimbali duniani, hali itakayochochea uhamishaji wa teknolojia, kuongeza ufanisi na kuimarisha ushindani katika uzalishaji.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji wa EABC, Iman Kajula, alisema jukwaa hilo ni muhimu kwa wawekezaji wengi wa Kitanzania, hususan wale wanaokabiliwa na changamoto ya kutambua na kufikia fursa mpya za uwekezaji. Aliongeza kuwa mkutano huo umefungua milango kwa wafanyabiashara kujifunza, kuunganishwa na wadau sahihi, pamoja na kuchukua hatua za vitendo kuanzisha au kupanua uwekezaji wao.

Jukwaa hilo lilidhaminiwa na Benki ya Maendeleo ya Tanzania (TIB) pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), likiwa ni sehemu ya jitihada za pamoja za kukuza uwekezaji wa wazawa na maendeleo ya uchumi wa Taifa.







Tanzania is set to deepen domestic participation, industrial growth and value retention in its mining sector following the strengthening of institutional collaboration with Ghana on Local Content implementation.


The two countries are enhancing cooperation on policies and best practices aimed at increasing the participation of local citizens and firms across the mining value chain, strengthening domestic institutions and ensuring that a greater share of mineral wealth benefits national economies.

This was underscored during an official experience-sharing visit by a delegation from Tanzania’s Mining Commission to Ghana’s Minerals Commission, which focused on exchanging knowledge, policy approaches and implementation frameworks for Local Content in the mining sector.

Speaking during the visit, Chairperson of the Local Content Committee from Tanzania, Dr Theresia C. Numbi, said Local Content is not merely a legal requirement but a strategic tool for national development, industrialisation and economic empowerment.

“Local Content in the mining sector forms a strong foundation for national development, industrial growth and economic empowerment in Tanzania. The 2009 Mineral Policy, the Mining Act (Cap. 123), and the Mining (Local Content) Regulations of 2018 mandate the Mining Commission to coordinate, supervise and ensure effective implementation of Local Content across the entire mineral value chain,” said Dr Numbi.

She noted that Tanzania has already recorded tangible gains from Local Content implementation, with employment of Tanzanians in the mining sector reaching 98 per cent, while procurement of local goods and services rose to 88 per cent by 2025.

According to Dr Numbi, collaboration with Ghana will further strengthen Tanzania’s capacity to consolidate these gains by refining regulatory frameworks, improving monitoring and compliance systems, and expanding opportunities for local suppliers, service providers and professionals.

She added that the partnership will support Tanzania’s efforts to accelerate skills development, technology transfer and the growth of local industries linked to mining, including manufacturing, engineering services and mineral value addition.

“The collaboration lays a foundation for a long-term and strategic partnership between the Mining Commission of Tanzania and the Minerals Commission of Ghana. It will also serve as a valuable reference for other African countries seeking to implement effective Local Content policies,” she said.

Dr Numbi emphasised that agreed areas of cooperation will be implemented through joint training programmes, exchange of experts, and the strengthening of legal and institutional systems to ensure that mining revenues and opportunities meaningfully benefit local communities.

On his part, the Chief Executive Officer of the Minerals Commission of Ghana, Mr Isaac Tandoh, welcomed the Tanzanian delegation and reaffirmed Ghana’s commitment to close cooperation in the mining sector.

He said the partnership aims to promote the exchange of knowledge, technology and regulatory experience in mineral exploration, extraction and trade, as part of broader efforts to advance sustainable development of Africa’s mining sector.

During the visit, experts from both countries discussed key issues including human capital development, technology transfer, knowledge succession planning, and robust monitoring and accountability mechanisms, with a view to addressing shared challenges such as limited mineral exploration and slow development of downstream value-addition industries.

The collaboration is expected to position Tanzania to further maximise the economic and social benefits of its mineral resources, while reinforcing Africa-led solutions for sustainable and inclusive mining development.










 


Top News