Families, architects, students and members of the public gathered at dawn on Saturday, 11 July 2026, for a memorial walk honouring the late Beda Amuli, one of Tanzania’s pioneering architects whose work helped shape Dar es Salaam’s built identity.

Organised by Amuli’s family in collaboration with the Architectural Association of Tanzania (AAT), the walk was held under the theme, “Designing Tanzania: Architecture for People, Place, and Purpose.”

The journey began at the Old Boma Building along Sokoine Drive before proceeding, under police and traffic escort, to selected landmarks associated with the city’s architectural history, including the Kilimanjaro Hotel, the Institute of Finance Management, the National Cooperative Building and Kariakoo Market.

AAT President Architect T’Chawi said Amuli did more than design buildings; he created civic spaces where Tanzanians could work, learn, trade and gather.

The walk concluded at Kariakoo Market with reflections, media engagement and closing remarks, followed by a memorial church service at St Alban’s Anglican Church.

Ten years after his passing, Beda Amuli’s legacy remains embedded in Dar es Salaam’s streets, institutions and public spaces, inspiring a new generation to appreciate architecture as national identity and public service.














 

Na. Mwandishi Wetu, Dar.

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe Mhe. Petro Magoti ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa namna ilivyofanya maboresho ya Mitaala ya Elimu nchini yenye lengo la kumfanya muhitimu kuweza kujiajiri au kuajiriwa mara anapomaliza masomo  yake.

Mhe. Magoti ameyasema hayo leo tarehe 12/7/2026 katika maonesho ya Sabasaba ambapo amesema kuwa TET inafanya kazi nzuri ya kuboresha elimu nchini.

"Kwa kweli nawapongeza kwa kazi nzuri ya kuboresha Elimu nchini hasa hivi karibuni katika maboresho ya mitaala yaliyofanyika, ni tumaini langu kwamba wanafunzi nchi nzima wataendelea kufanya vyema, " Amesema mhe. Magoti.

Pia ameeleza, anafurahia namna wanafunzi wanaendelea kupatiwa vitendea kazi kama vitabu vinavyowapelekea kuendele kufanya vyema wakati wa masomo yao na kuendelea kuipongeza TET kwa uratibu mzuri na upatikanaji wa vitabu  mashuleni.

TET inashiriki katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya  biashara maarufu kama Sabasaba  yaliyoanza tarehe 28, Juni ambapo yanatarajiwa kufungwa hapo kesho, Julai 13.









Dar es Salaam, Julai 12, 2026

Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. William Kafiti, amesema Hifadhi Skimu ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) imeendelea kuwa mkombozi kwa wananchi waliojiajiri kwa kuwapa fursa ya kujiwekea akiba kwa ajili ya maisha ya baadaye, huku akiipongeza NSSF kwa kuimarisha huduma kwa wanachama kupitia mifumo ya kidijitali na utoaji wa huduma wenye viwango vya juu.

Akizungumza baada ya kutembelea banda la NSSF katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Mhe. Kafiti alisema ameridhishwa na kiwango cha huduma kinachotolewa na Mfuko huo, akibainisha kuwa wananchi wanapokelewa na kuhudumiwa kwa weledi, haraka na kwa kutumia teknolojia ya kisasa inayorahisisha upatikanaji wa huduma.

"Nimefurahishwa sana na huduma nilizoziona hapa, kila mfanyakazi yuko tayari na ana ari ya kumhudumia mwananchi kwa weledi na kwa wakati. Hili linaonesha dhamira ya kweli ya NSSF ya kuwahudumia Watanzania kwa viwango vya hali ya juu," alisema Mhe. Kafiti.

Alisema mafanikio hayo yanaakisi jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuimarisha sekta ya hifadhi ya jamii na kupanua wigo wa huduma kwa wananchi wote, hususan waliojiajiri ambao kwa miaka mingi walikuwa nje ya mfumo rasmi wa hifadhi ya jamii.

Mhe. Kafiti alieleza kuwa kuanzishwa kwa Hifadhi Skimu kumefungua ukurasa mpya kwa makundi mbalimbali ya wananchi waliojiajiri, wakiwemo bodaboda, mama na baba lishe, wafanyabiashara wadogo, wavuvi, wachimbaji wadogo wa madini, mafundi na makundi mengine ya wajasiriamali, kwa kuwawezesha kujiwekea akiba itakayowawezesha kuwa na uhakika wa kipato wanapofikia uzee.

"Kila mmoja atazeeka. Kesho iliyo bora hujengwa na maamuzi ya leo. Kupitia Hifadhi Skimu, NSSF imewapa wananchi waliojiajiri fursa ya kujenga maisha yenye uhakika baada ya kipindi chao cha kufanya kazi. Huu ni mpango unaostahili kuungwa mkono na kila Mtanzania," alisisitiza.

Aidha, aliipongeza NSSF kwa maboresho makubwa ya mifumo ya kidijitali yanayowawezesha wanachama kupata taarifa za michango yao kwa urahisi kupitia simu za mkononi, hatua aliyoielezea kuwa ni mapinduzi makubwa katika utoaji wa huduma za hifadhi ya jamii.

Mhe. Kafiti aliongeza kuwa NSSF inaendelea kutekeleza kwa vitendo azma ya Serikali ya kujenga taifa lenye wananchi wanaojitegemea kiuchumi kwa kuwawezesha kuweka akiba wakiwa bado wana nguvu za kufanya kazi ili wanapostaafu waendelee kuishi kwa heshima kupitia mafao na pensheni wanazostahili.

Naye, Theonasy Ngunga, mmoja wa wananchi waliotembelea banda la NSSF alieleza kuridhishwa na huduma alizopata, akisema alipokelewa kwa heshima, akaelekezwa katika kila hatua na ndani ya muda mfupi akapatiwa elimu kuhusu Hifadhi Skimu na kukamilisha taratibu za kujiunga na NSSF Portal.

"Nilipoingia nilipokelewa vizuri na kupewa maelekezo katika kila hatua. Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimehudumiwa na kuelewa namna ya kuchangia kupitia mifumo popote nilipo," alisema.

Kupitia Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam, NSSF inaendelea kuwahamasisha wananchi, hususan waliojiajiri, kujiunga na Hifadhi Skimu ili kujenga akiba kwa ajili ya maisha ya baadaye. Juhudi hizo zinaendana na azma ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya hifadhi ya jamii na kujenga kesho yenye uhakika kupitia mfumo endelevu wa hifadhi ya jamii.















Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
















- Apokelewa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Makongoro Nyerere pamoja na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Jacqueline Mzindakaya


Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.

Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.












Top News