PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Serikali ya Awamu ya Sita pamoja na mambo mengine imeimarisha zaidi ushirikiano wakimataifa na kutoa mchango mkubwa katika masuala ya kikanda na kimataifa yanayohusumazingira na mabadiliko ya Tabianchi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ameyasemahayo wakati akiongea na Waandishi wa Habari Unguja, Zanzibar Machi 3, 2026 wakati akitoakauli ya Serikali katika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Afrika inayoadhimishwa kila mwakaMachi 3.
Amesema kupitia ushawishi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. SamiaSuluhu Hassan katika medani ya kimataifa, Tanzania imepata fursa za kuongoza masualambalimbali ya kikanda ambayo ni pamoja na kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Nishati wa Wakuuwa Nchi za Afrika - Misheni 300 uliofanyika Januari 27 hadi 28 Januari, 2025 jijini Dar es Salaam.
Pia Tanzania ilifanikiwa kuwa mjumbe wa kudumu wa Kamati ya Umoja wa Afrika ya Wakuuwa Nchi na Serikali kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu waRais, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni kuwa Makamu Mwenyekiti wa Mkutano wa Nane waBaraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEA - 8) kuanzia Desemba 2025 hadi Desemba2027.
Amesema Maendeleo na ukuaji wa taifa lolote duniani pamoja na ustawi wa watu wake vimefungamana na hali na ubora wa mazingira. Hali ya mazingira ikiwa imara ukuaji wa uchumina ustawi wa watu pia huwa imara.
“Tarehe 3 Machi ya Kila mwaka, Bara la Afrika huadhimisha Siku ya Mazingira Afrika, siku hiiadhimu iliasisiwa mwaka 2002 na Baraza la Mawaziri la Umoja wa Afrika ikiwa ni moja yamaazimio muhimu ya Umoja wa Afrika katika kuhimiza nchi wanachama na Bara la Afrika kutunza na kuhifadhi mazingira,
“Kauli mbiu ya siku hii kwa mwaka huu ni ‘Assuring Sustainable Water Availability and Safe Sanitation Systems to Achieve the Goals of Agenda 2063". Ambayo tafsiri yake ni: "Uhakikawa upatikanaji Endelevu wa Maji na Mifumo Salama ya Usafi wa mazingira ili kufikiaMalengo ya Ajenda 2063,” amesema Mhe. Masauni.
Amesema, kauli mbiu ya siku ya Mazingira kwa Afrika mwaka huu inahusu Uhakika waupatikanaji Endelevu wa Maji na Mifumo Salama ya Usafi wa mazingira kwa maendeleoendelevu inatukumbusha umuhimu wa kutekeleza mipango shirikishi ambapo mtu na taasisi nimuhimu kushiriki ipasavyo kwa faida ya nchi.
“Kwa kutambua uhalisia huu, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imedhamiria kufungamanishakwa vitendo masuala ya mazingira, mabadiliko ya tabianchi na maendeleo endelevu”.
Ameongeza kuwa Dira 2050 imeweka nguzo adhimu inayohusu Uhifadhi wa Mazingira naustahimilivu dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi. Vile vile, Ilani ya CCM imeweka masuala yamazingira na mabadiliko ya Tabianchi kama mojawapo ya masuala muhimu yatakayozingatiwakatika kipindi cha mwaka 2025 – 2030.
Mhe. Masauni amesema Dunia inapitia katika changamoto kuu tatu za Mazingira ambazo ni: Upotevu wa Bioanuai; uchafuzi wa Mazingira kutokana na vyanzo mbalimbali pamoja naMabadiliko ya Tabianchi.
Amesema, uhalisia huu unakumbusha umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika kuimarishauhifadhi wa mazingira pamoja na ufumbuzi wa pamoja wa changamoto za mazingira, ni kwamuktadha huu, Tanzania ni nchi mwanachama wa mikataba mbalimbali inayohusu hifadhi nausimamizi wa mazingira.


PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Na Diana Deus- Kagera.
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), kwa kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imezindua rasmi vituo 23 vya kukusanyia maziwa (Milk Collection Centers – MCCs) vilivyojengwa na kuboreshwa kupitia Mradi Shirikishi wa Wasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa Tanzania (TI3P).
Waziri wa Uvuvi na Mifugo, Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, alisema mradi wa TI3P unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika mnyororo wa thamani wa maziwa nchini kwa kuongeza uzalishaji, kuboresha ubora wa maziwa na kupanua masoko kwa wafugaji wadogo, wa kati na wakubwa. Alisisitiza kuwa vituo vya kukusanyia maziwa si majengo tu, bali ni miundombinu ya kimkakati inayochochea mapinduzi ya kiuchumi kwa wafugaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza ajira vijijini.
Alisema Mkoa wa Kagera uliwahi kupiga hatua kubwa kwa kujikita katika masuala ya ushirika kabla ya kudorora, na kufufua ushirika kupitia sekta ya ufugaji ni njia muhimu ya kuinua uchumi wa kaya na kuurudishia mkoa hadhi yake ya kiuchumi kama ilivyokuwa miaka iliyopita.
Aidha, aliwashauri wafadhili wa mradi wa TI3P ambao ni Gates Foundation pamoja na watekelezaji ambao ni TADB kwa kushirikiana na Heifer International Tanzania na Land O’Lakes Venture 37 kuendelea kuimarisha ushirikiano huo wenye lengo la kuwaunganisha wazalishaji na wasindikaji ili kukuza sekta ya maziwa kwa njia jumuishi na endelevu kupitia mpango wa “Kopa Ng’ombe, Lipa Maziwa.”
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi, Mkurugenzi Mwendeshaji wa TADB, Frank Nyabundege, alisema hadi sasa zaidi ya Shilingi bilioni 41 zimetolewa kama mikopo kwa wadau katika mnyororo wa thamani wa maziwa.
Mradi umewezesha ununuzi wa mitamba 3,254 yenye thamani ya Shilingi bilioni 10.8 kwa lengo la kuongeza uzalishaji, pamoja na ufadhili wa viwanda 15 vya usindikaji maziwa kwa Shilingi bilioni 22.
Zaidi ya wafugaji 92,831 watafikiwa moja kwa moja kupitia huduma za kifedha, mafunzo na ugani. Ruzuku fungamanifu ya Shilingi bilioni 1.448 imetolewa kwa wafugaji na wasindikaji wa maziwa, huku Vyama vya Wazalishaji wa Maziwa (FPOs) 45 vikianzishwa na kuimarishwa, vikikusanya wastani wa lita 19,047 kwa siku.
Vituo 23 vya kukusanyia maziwa vimejengwa na kuboreshwa katika Kanda ya Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Zanzibar, vyenye uwezo wa kukusanya lita 45,500 kwa siku na kuhudumia wafugaji 4,016 katika mikoa nane na wilaya 18, kwa uwekezaji wa zaidi ya Shilingi bilioni 1.157.
Katika ziara yake mkoani Kagera, Waziri alitembelea Chama cha Ushirika cha Maruku, Bukoba Mjini, na kushuhudia utekelezaji wa mpango wa “Kopa Ng’ombe, Lipa Maziwa” unaolenga kuongeza kipato kwa vijana na wanawake kupitia ufugaji wa kisasa wa ng’ombe wa maziwa.
Chama hicho chenye wanachama 118, kati yao asilimia 26 ni wanawake, kimewanufaisha wanachama 24 waliopatiwa mitamba 24 yenye mimba. Pia wamepata ruzuku ya Shilingi milioni 18 kupunguza marejesho ya mikopo, ukarabati wa MCC wa Shilingi milioni 10.4 na tanki la kuhifadhia maziwa la lita 2,000. Wanachama hao wamepatiwa pia mbegu bora za malisho aina ya Juncao na mafunzo ya ufugaji bora kutoka Heifer International Tanzania.
Katika Kituo cha Nshamba chenye wanachama 541, kati yao wanawake 83, TADB imewezesha uanzishwaji wa MCC yenye uwezo wa kukusanya lita 2,000 kwa siku pamoja na jenereta ya dharura. Wanachama 143 wako katika mchakato wa kunufaika na mpango huo kwa kupatiwa mitamba 45 yenye mimba.
Aidha, katika Ushirika wa UWAWAMA, Kayanga wilayani Karagwe, wanachama 76 wamenufaika na mpango huo kwa kupatiwa mitamba 110 yenye mimba na ruzuku ya Shilingi milioni 85 ya kupunguza marejesho ya mikopo.
Kwa upande wa usindikaji, Mkurugenzi wa Kahama Fresh, Josam Ntangeki, alisema TADB imeendelea kushirikiana na Kahama Fresh Limited tangu Oktoba 2021 kwa kuwezesha ujenzi wa kiwanda na ununuzi wa mitambo ya kisasa yenye uwezo wa kusindika lita 20,000 za maziwa kwa siku pamoja na magari maalum ya kukusanya na kusambaza maziwa.
Alisema mwaka 2024, kupitia mpango wa “Kopa Ng’ombe, Lipa Maziwa,” benki iliwezesha upatikanaji wa mitamba bora kutoka Kenya na Uganda, hatua inayolenga kuwasaidia wafugaji wadogo kupata ng’ombe bora kwa mkopo wenye masharti nafuu.
MKUU wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amewakaribisha Watanzania hasa wanariadha kushiriki Kitulo Garden Marathon inayotarajia kufanyika Mei 2 mwaka huu.
Amesema anaamini mbio za Kitulo Garden Marathon zinakwenda kufanyika katika mwezi mzuri kwani mkoa huo utakuwa na wageni wengi ambao watakwenda kwenye sherehe za Mei Mosi hivyo kupitia mbio hizo washiriki wa ndani na nje watapata nafasi ya kutembelea hifadhi ya Kitulo ambayo ni maarufu kwa bustani ya maua na ndege
Akizungumza kuhusu maandalizi ya mbio hizo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka ametumia pia nafasi hiyo kuelezea Kitulo Garden Marathon zitasaidia kutangaza hifadhi ya Kitulo.
“Marathon ni mchezo ambao unasifa tofauti na michezo mingine kwani huleta wanariadha kutoka maeneo yote ya dunia hivyo maana yake itatuletea washiriki wa pande zote za nchi na pande zote za dunia.
“Watu wataifahamu Njombe kupitia Kitulo Garden Marathon ambayo pia ni sehemu sahihi kwa kufanya utalii wa ndani na utalii mwingine kama ambavyo watalii wamekuwa wakija kutalii katika utalii wa nchi yetu.”
Pia Mtaka amesema hifadhi ya Kitulo inabeba bustani ya maua ambayo hayapatikani sehemu kubwa ya nchi yetu kwani inautofauti wa maua na hali nzuri ya hewa ya Kitulo,Makete na Njombe
“Kwahiyo itakuwa na upekee kwani Watanzania wengi wanajua Njombe ni lenye ubaridi mkubwa kwa nchi yetu na ndio maana sisi kama Mkoa ni ziro malaria.Anayekuja Kitulo Garden Marathon ana nafasi nzuri ya kupata mandhari nzuri na hali ya hewa.
Pia amesema Kitulo Garden Marathon inaenda kuongeza sauti katika kuutangaza Mkoa wa Njombe,kuongeza sauti katika kutangaza fursa za Mkoa wa Njombe.”
Amewakaribisha Watanzania hususani wanariadha wanaojiandaa na mashindano mbalimbali kwenda katika marathoni hiyo kwa ajili ya kupima muda wao. kabla hawajaenda katika mashindano mbalimbali duniani.
Kwa upande wake Mwanariadha wa kimataifa na Mshindi wa kwanza wa mbio ndefu zilizofanyika nchini Uingereza mwaka 2022 akitokea mkoa wa Njombe Transfora Ngimbuchi amesema ameendelea na maandalizi ya Kitulo Garden Marathon huku akitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wanariadhaa wengine kushiriki.
“Riadha ni miguu yako mwenyewe unalala umasikini leo na kesho unamka tajiri hivyo napambana kushiriki mbio mbalimbali zilizopo nje na hata sasa najua kuna marathon itakayofanyika Poland Aprili mwaka huu ambapo pia nitashiriki.Napambana ili nipate sifa za kushiriki mashindano ya Olimpic
“Ninawakaribisha wanariadha wote wa kitaifa na kimataifa waje washiriki Kitulo Garden Marathon lakini sitakubali namba moja iende kwa mshiriki yeyote zaidi ya mzawa mwenyewe.”

Serikali kuendelea kuweka mazingira salama kwa wenye Viwanda vinavyofanya kazi na kutatua changamoto kwa wakati ili kuendelea kulinda ajira za Watanzania na kuongeza mzunguko wa fedha kwa jamii na wananchi kwa ujumla.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb) wakati wa ziara ya kikazi Machi 2, 2026 mkoani Morogoro.
Londo amemshauri Katibu Tawala mkoani Morogoro kuweka utaratibu kwa mikopo ya asilimia 10 kuwafikia walengwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) ili kuleta maana ya utoaji wa mikopo kwa jamii nchini.
Londo ametembelea viwanda vinne katika Manispaa ya Morogoro ikiwemo SIDO, Mkwawa, Cotex na Mazava katika ziara yake ya siku moja mkoani hapa.
Pia amesema ikiwa wajasiliamali hao watapata mikopo wakiwa hapo ambako wamezungukwa na aina mbalimbali za ujasiriamali itawasaidia kupata namna ya kujengwa na kuwa wajasiriamali wazuri na hivyo kuwa na uhakika wa kurejesha mikopo hiyo.
Uwepo wa gundi inayozalishwa kwenye viwanda hivyo vidogo vilivyopo kwenye eneo la viwanda SIDO Morogoro ambapo ameiomba serikali ya mkoa kusimamia uzalishaji huo na kufanya masoko makubwa ya gundi kuanzia ndani ya mkoa na kisha nje ya mkoa Taifa hadi nje ya nchi.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa SIDO, Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji anasema wanajipanga kuhakikisha wanaboresha eneo la viwanda la SIDO Morogoro ili kufanya wajasiriamali kulitumia kama kongani la viwanda na kuleta maana
Hata hivyo, Meneja wa SIDO Morogoro, Bi.Joan Nangawe anasema wametengeneza ajira zaidi ya 115 baada ya kutoa elimu, kuwakusanya wajasiriamali kwenye eneo la viwanda na kutoa mikopo ya shilingi Milioni 62.5.
Anasema katika siku 100 za Rais Samia Suluhu Hassan jumla ya wajasiriamali ambao ni vijana wanatarajia kupata mikopo ya shilingi Milioni 250 kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.
Mmoja wa wajasiriamali anayetengeneza Gundi kwenye eneo la viwanda SIDO Marry Hassan anasema licha ya kuwa na uhakika wa soko la ndani kwa mikoa ya Morogoro na Dar es salaam lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko ya nje ambayo yanaweza kuwapa nafasi kubwa katika kuongeza uzalishaji na kukua kiuchumi.

Fikiria unaingia tu getini, umbali wa nusu kilomita upande wako wa kushoto unashuhudia mti mkubwa umepambwa na mnyama adimu sana kuonekana nyakati za mchana, huyu si mwingine ni Anko Chui.
Sasa wakati Unamshangaa Chui inakulazimu ukimbizane na muda maana Big Five wengine kama Simba, Tembo, Faru na Nyati wanakusubiri Kasoko ya Ngorongoro wakiwa wamezungungukwa na makundi ya Pundamilia, swala, Pofu, viboko, Kasongo ndege aina Falamingo, Yangeyange, ndege karani na wengine wengi.
Ngorongoro ni hifadhi ya maajabu yenye Hadhi ya kimataifa, Destination ya maajabu, Bustani ya Eden, Nyayo za Laetoli, Tamaduni hai, Bonde la Olduvai na Mazalia ya Nyumbu.
SAME.
WAFUGAJI wanaoishi nje ya wilaya ya Same ambao walikuwa wameingiza mifugo yao ndani ya wilaya hiyo katika vijiji vilivyopo kata ya Vumari bila kuwa na kibali wameanza kutii agizo la Mkuu wa wilaya hiyo, Kasilda Mgeni la kuondoa mifugo yao ndani ya wilaya hiyo.
Kwa mujibu Mkuu wa Jeshi la Polisi wilayani Same, wafugaji hao walioingia kwa wingi bila kufuata taratibu za uhamasishaji wa mifugo na kusababisha mgogoro mkubwa kati ya wakulima na wafugaji kutokana na mifugo kulisha mazao na baadhi wakulima kupigwa sasa wameondoka kabisa.
Mnamo Februari 21 mwaka huu, Kasilda Mgeni alifika Kata ya Vumari na kutoa maagizo hayo rasmi ya kuwaondoa mifugo ndani ya siku saba, yaani kuanzia Februari 22 mwaka huu ambapo mifugo hiyo imeshaondolewa kwa hiari kabla ya operesheni maalum kufanyika.
Kasilda alionya kuwa endapo wafugaji hawatachukua hatua za kufuata agizo, vyombo vya ulinzi na usalama viko tayari kufanya operesheni maalum ya kuwaondoa mifugo hiyo, na hasara yoyote itakayotokea kwa mifugo hiyo haitakuwa jukumu la serikali kwa kuwa walishapewa taarifa na maagizo wazi.
Hadi leo, Machi 2, 2026, hali imerejea kuwa ya kawaida na utulivu wa hali ya juu huku Wakulima na wafugaji wanaoishi kihalali katika Kata ya Vumari wanaendelea na shughuli zao za kila siku kwa amani na utulivu mkubwa.

Akizungumza wakati wa zoezi la kugawa tende hizo, Mbunge Wambura amesema amefanya hivyo kama sehemu ya sadaka yake kwa waumini wa Kiislamu, akitambua kuwa futari ni sehemu muhimu ya ibada katika kipindi hiki cha Ramadhani. Amesema lengo lake ni kushiriki na wananchi wake katika ibada hiyo pamoja na kuomba baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Kwa upande wake, Sheikh wa Mkoa wa Geita, Alhadi Yusufu Kabaju, amemshukuru Mbunge huyo kwa kushirikiana na waumini wa Kiislamu katika kipindi hiki muhimu cha kiimani.
Amesema msaada huo unaonesha mshikamano, upendo na ushirikiano kati ya viongozi na wananchi bila kujali tofauti za dini.
Nao baadhi ya waumini na viongozi wa dini hiyo wameelezea umuhimu wa kuendelea kuombea amani Nchi pamoja na kuomea amani kwa mataifa ambayo kwa sasa yanamachafuko katika mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani
Hatua hiyo imepokelewa kwa furaha na waumini wa Kiislamu katika jimbo hilo huku wakieleza kuwa itasaidia kurahisisha futari katika kipindi hiki cha Ramadhani.
Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe Rosemary Senyalume ametoa wito kwa Wananchi wote wa Mkoa Dodoma kujitokeza kutumia fursa ya kutoa kero zao na kupata utatuzi katika siku 3 zilizoandaliwa kuanzia tarehe 4 hadi 6 Machi 2026 katika viwanja vya Nyerere Square kwani Taasisi zote za Umma zitakuwepo hapo kwaajili ya jambo hilo.Mhe Senyamule ameyasema hayo leo Jijini Dodoma Machi 2,2026 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu jambo waliloandaa la utatuzi wa kero mbalimbali za wananchi wa Dodoma kama ambavyo yamekuwa ni maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya vitendo ya Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba na maelekezo mahsusi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Prof.Riziki Shemdoe ambayo yamekuwa yakisisitiza utatuzi wa kero za Wananchi.
"Taasiisi zote za Umma zilizopo katika Mkoa wa Dodoma zitakuwepo pale Nyerere Square kwa siku tatu kusikiliza nakutatua kero za wananchi,kwahiyo ni wito wangu kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma kujitoleza kuja kutumia fursa hii adhimu ambayo tumeiweka ili kuwarahishia kwani Taasisi zitakuwepo pale kutoka upande wa afya,maji na hata miundombinu".
Aidha Mkuu wa Mkoa huyo ameainisha huduma tatu muhimu zitakazotolewa katika viwanja hivyo kwa siku hizo 3, kuwa ni kusikiliza kero za wananchi ambapo Taasisi zote za Umma zitashiriki kazi hii Pia kutoa Taarifa kwa Umma wa Wana Dodoma na Taifa kwa ujumla juu ya kazi iliyofanywa katika siku 100 za Dkt Samia akiwa madarakani katika awamu ya sita na muhula wake pili.
Ambapo tatu ni utoaji wa huduma bure kwa wananchi kama vile upimaji wa magonjwa ikiwemo sukari na presha pamoja na kuwepo kwa huduma za ki hiari za kutoa damu kwa watakaopenda ambapo huduma hizi zimeunganiswa ili kuwa fursa kwa wananchi wakati wa utatuzi wa kero zao.
Pamoja na hayo pia ametoa wito kwa Taasisi za Umma na Watumishi wake katika Mkoa wa Dodoma kuhakikisha kwamba kila mmoja anawajibika kusikiliza kero za wananchi kwani kama Mkoa wanategemea kutengeneza mfumo kuanzia ngazi za chini za Vitongoji mpaka ngazi ya Mkoa, mfumo wa kupata Taarifa za kero zinazosikilizwa na utatuzi wake katika ngazi zote na kuzitolea Taarifa kila mwezi.
Maelekezo hayo ameyatoa Machi 2, 2026 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 12 wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri Tanzania Bara unaofanyika katika Ukumbi wa Lush Garden Hotel jijini Arusha, ambapo amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri na Timu ya Usimamizi wa Halmashauri (CMT) kuwa karibu na wananchi na kusikiliza kero zao mapema badala ya kusubiri ziibuliwe wakati wa ziara za viongozi wakuu wa kitaifa.
Amesema kukosekana kwa utaratibu wa kuwasikiliza wananchi katika ngazi ya halmashauri kumesababisha wananchi wengi kujitokeza na malalamiko wakati wa ziara za viongozi wa kitaifa, hususan ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini.
Aidha, Prof. Shemdoe amewaelekeza Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri kusimamia kikamilifu changamoto ya mmomonyoko wa maadili katika jamii, akisisitiza kuwa mwalimu ni kioo cha jamii na ana jukumu la kutoa malezi na mafundisho yatakayojenga maadili mema kwa wanafunzi.
Ameongeza kuwa katika kipindi hiki cha ukuaji wa kasi wa sayansi na teknolojia, walimu wanapaswa kuwafundisha wanafunzi matumizi sahihi ya TEHAMA, hususan katika mitandao ya kijamii, ili teknolojia iwe chachu ya kuimarisha maadili na si kuyadhoofisha.
Wakati huo huo, Prof. Shemdoe amewasisitiza Maafisa hao kuhakikisha kuwa wanafuatilia kwq karibu na kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ya kuhakikisha ndani ya miezi sita kila shule nchini kunakuwa na vyoo vya kutosha vya wanafunzi na walimu.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Atupele Mwambene, amesema Mkutano Mkuu huo wa 12 umebeba kaulimbiu isemayo “Matumizi ya TEHAMA ni Nguzo Muhimu ya Uboreshaji wa Elimu Tanzania” na unalenga kufanya majadiliano yenye tija yatakayoboresha na kuimarisha sekta ya elimu nchini.
Na WAF-Korogwe
Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt. Japhet Simeyo amesema kikao kazi cha tathmini ya matukio na athari za kiafya kitawajengea uwezo wataalam kwenye mkoa huo ili wawe tayari kuzuia na kukabiliana na majanga yatokanayo na dharura.
Dkt. Simeyo ameyasema hayo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga leo Machi 02, 2026 katika kikao kazi cha tathmini ya matukio na athari za kiafya katika mkoa wa Tanga, kilichoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na asasi isiyo ya kiserikali ya PATH& CIHEB.
"Mkoa wa Tanga umekuwa na Majanga mbalimbali yanayotokea ikiwa ni pamoja na moto, ajali za barabarani, Magonjwa ya Milipuko na mabadiliko ya Tabianchi" amesema Dkt.Simeyo na kuongeza
"Mafunzo haya yamekuja kwa wakati muafaka kwani yatawajengea uwezo baina ya sekta mtambuka kwa kupitia za majanga yaliyowahi kutokea na kuimarisha afua za udhibiti wa majanga hayo kabla hayajatokea" amesema Dkt Simeyo
Kwa upande wake Mratibu-Udhibiti Athari za Majanga Wizara ya Afya, Dkt Saumu Nungu amesema kuwa kikao kazi hicho kinalenga kuainisha athari ambazo zinaweza kusababisha majanga na dharura katika mkoa wa Tanga na kuandaa mpango kazi ambao utasaidia mkoa kujiandaa vizuri.
"Pamoja na hilo kikao kupitia kikao hiki tutandaa kalenda itakayokuwa inaonyesha wakati ambao majanga yanaweza kutokea yaani Tanga Region Health Profile Risk and Calendar" amesema Dkt Saumu
Amefafanua kuwa kupitia kalenda ya matukio, timu za kukaliana na majanga ya dharura zitaweza kujiandaa mapema kabla ya kipindi ambacho athari hizo zina uwezekano wa kutokea, hivyo kuleta tija na kulinda afya za wananchi dhidi ya athari za majanga hayo.
Naye Dkt. Said Sheuya kutoka PATH&CIHEB amesema kuwa, Taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Afya katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na mapambano ya magonjwa ya mlipuko na ufuatiliaji wa magonjwa, ushirikiano wa mfumo wa Afya Moja, kuhakikisha uwepo wa mifumo ya afya inayosomana katika utoaji wa taarifa za magonjwa, na kufanya mafunzo kwa timu za kupambana na dharura katika mikoa.













.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)




.jpeg)









.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)

