Kasoko ya Empakaai ni mojawapo ya Kasoko za volkano ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro, ikiwa na kingo za juu na ziwa zuri linalofunika zaidi ya asilimia 75 ya sakafu ya Kreta/Kasoko. Kivutio kikubwa ndani ya kreta hii ni idadi kubwa ya ndege heroe (flamingo) wanaoonekana kando ya ufukwe wa ziwa, Ndege wanapokuwa wengi hufanya ziwa hilo kuwa na rangi ya pinki.

Kreta hii katika nyanda za juu za Ngorongoro imezungukwa na kuta za misitu yenye mteremko mkali wa takribani mita 300 kwa urefu, zikiwa na uoto wa asili wa kijani kibichi, wanyamapori na aina mbalimbali ya ndege. Eneo lake lina upana wa takribani kilomita 8, huku karibu nusu ya sakafu yake ikifunikwa na ziwa la lenye magadi na kina kirefu, makazi ya heroe (flamingo) na ndege wengine wa majini. 

Kutoka juu ya ukingo wa kreta ya Empakai, wageni wanaweza kuona Mlima Oldoinyo Lengai, Bonde la Ufa na Ziwa Natron kwa mandhari ya kuvutia. Pia wanaweza kufurahia matembezi ya asili kutoka juu ya mlima au kushuka hadi sakafuni kushuhudia vivutio vilivyopo.

Empakaai ina kimo cha takribani mita 3,200 kutoka juu ya usawa wa bahari upande wa magharibi na mita 2,590 upande wa mashariki. Mara nyingi hufunikwa na ukungu kutokana na mwinuko wake ambapo ziwa huonekana la kijani kibichi au buluu ya kina.

Kreta/Kasoko  ya Empakaai ni maarufu kwa safari za kutembea kwa miguu, ambapo watalii hutembea kwa takribani saa mbili na nusu kwenda na kurudi kutegemea na uwezo wa mwili. Wageni wanaweza kuona kwa ukaribu ziwa na msitu mnene uliopo ndani na kuzunguka sakafu ya Kasoko.

 Kivutio cha Empakaai kinaweza kutembelewa wakati wowote wa majira ya mwaka, lakini inapendelewa zaidi kuanzia mwezi Juni hadi Desemba (msimu wa kiangazi).

 _Karibu Ngorongoro 

Tumerithishwa, tuwarithishe_ 







Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Bunge la 13 limeunda jumla ya Kamati 17 huku wanawake wengi wakichomoza kuongoza kamati hizo, Wabunge wa upinzani wa Chaumma na ACT Wazalendo nao wapenya.

Majina ya vigogo yamechomoza kwenye Kamati hizo huku baadhi ya wabunge wakongwe wakirejea katika uongozi wa Kamati walizoongoza Bunge la 12.

Kamati zilizopewa wapinzani ni Hesabu za Serikali (PAC) ambayo amekabidhiwa Devotha Minja na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ambayo itaongozwa na Mbunge Tunduru Kaskazini Ado Shaibu.

Hii ni mara ya kwanza wapinzani kutoka vyama viwili tofauti wanaongoza Kamati hizo ambazo kwa kipindi kirefu zilikuwa chini ya Wabunge kutoka Chadema.

Katika taarifa ya Bunge, Devotha Minja atasaidiana Khalifan Aeshi ambaye amechaguliwa kuwa Makamu huku Kamati ya (LAAC) Makamu wake ni Abdallah Chikota.

Katika Bunge la 12 Kamati ya PAC iliongozwa na Naghenjwa Kaboyoka wakati Kamati ya LAAC Mwenyekiti wake alikuwa Halima Mdee wote wakitokea Chadema licha ya kuingia kwenye msukosuko wa kutimuliwa na chama chao.

Minja na Ado Shaibu wamepewa Kamati hizo ambazo zimekuwa na hoja nzito kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambapo mara nyingi Mashirika na Halmashauri yametajwa kuwa na mapungufu ya mifumo ya kimanunuzi na kupelekea upotevu mkubwa wa fedha.

Kamati zingine zilizoundwa ni Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambayo Mwenyekiti wake ni Anne Kilango Malecela na Makamu wake ni Christina Mndeme huku Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Mwenyekiti ni Masanja Kadogosa na Makamu wake Dougras Masaburi.

Kamati ya Sheria ndogo itaongozwa na Cecilia Pareso na Makamu wake ni Yahya Zuberi lakini Kamati ya Utawala,Katiba na Sheria wamepewa wabobezi wa Sheria ambapo Mwenyekiti ni Dk Damas Ndumbaro na Makamu wake Edwin Swale.

Kamati ya Sheria ndogo itaongozwa na Cecilia Pareso na Makamu wake ni Yahya Zuberi lakini Kamati ya Utawala,Katiba na Sheria wamepewa wabobezi wa Sheria ambapo Mwenyekiti ni Dk Damas Ndumbaro na Makamu wake Edwin Swale.

Mashimba Ndaki ameendelea kuongoza Kamati ya Bajeti na Makamu wake ni Ally Hassan King.

Naibu Waziri wa Nishati wa zamani Subira Mgalu amechaguliwa Kamati ya Nishati na Madini akisaidiwa na Simoni Lusengekile.

Mbunge Mpanda Seleman Kakoso amerudi kwenye nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu akisaidiana na Abubakari Asenga huku Kamati ya Afya na Masuala ya Ukimwi wamechaguliwa Dk Johannes Lukumay kuwa Mwenyekiti na Zeyana Abdallah Hamid ndiye Makamu.

Mbunge mwingine aliyerudia nafasi yake ni Timotheo Mzava ambaye ameendelea kuwa Mwenyekiti Kamati ya Ardhi,Maliasili na Utalii Makamu wake ni Mary Masanja na Kamati ya Elimu, Utamaduni na Michezo Husna Sekiboko atasaidiana na Cornel Magembe.

Kamati zingine ni Maji na Mazingira iliyorudi tena kwa Jackson Kiswaga nafasi ya Makamu ikienda kwa Profesa Pius Yanda na Kamati ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii itaongozwa na Hawa Machafu Makamu ni Regina Malima.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge la 12 Nagma Giga safari hii amepewa kuongoza Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Makamu ni Mbunge wa Dodoma Paschal Chinyele, Viwanda, Biashara, Biashara na Kilimo ameendelea Deodatus Mwanyika na Makamu wake amerudi Mariam Ditopile.

Kwenye Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) amechaguliwa Florence Kyombo atasaidiana na Jafari Chege.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Mikami Yoichi, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, leo tarehe 14 Januari 2025.

Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha zaidi ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Japan.





 

Na Mwandishi wetu, Simanjiro


WAKUU wa shule za sekondari na msingi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule kutokana na kasi ya ukuaji na kuongezeka kwa matumizi ya sayansi na teknolojia ulimwenguni.

Wakuu wa shule 23 za sekondari, 110 wa msingi wa shule za serikali na binafsi wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa wake kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu.

Afisa elimu ya awali na msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Darius Daudi Limandola amesema walimu hao wamepata mafunzo hayo ya uandaaji wa taarifa za shule kwenye vituo vitatu vya Orkesumet, Terrat na Mirerani.

Limandola ameeleza kwamba mafunzo hayo ya mfumo wa utoaji wa taarifa za kielimu kupitia mfumo wa kidigitali (School Information System) una lengo la kurahisisha utoaji na upatikanaji wa taarifa za shule husika kwa wakati.

Ameeleza kwamba mfumo huo unafanyakazi katika kutoa taarifa za kielimu za shule husika kila siku ikiwemo hali ya miundombinu ya shule, utekelezaji wa lishe kwa wanafunzi, hali ya watumishi na upatikaji wa huduma nyingine za kijamii hususani maji na umeme.

Amesema wanufaika wa mafunzo hayo ni wakuu 23 wa shule za sekondari, walimu wakuu 110 wa shule za msingi, maafisa elimu kata, walimu wa taaluma na takwimu na maafisa elimu ngazi ya wilaya.

Amewataka walimu wakuu na wakuu wa shule kusimamia utekelezaji wa mfumo huo mara moja baada ya shule kufunguliwa Januari 13, 2026 ambapo utairahisishia serikali kufanya maboresho na maamuzi sahihi katika shule husika kwa wakati.

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo, afisa elimu vifaa na takwimu wa halmashauri ya wilaya hiyo, Abdalah Hamis amesema walimu hao wamejengewa uwezo kwa muda wa siku mbili na kisha watakwenda kuwaelekeza walimu waliobaki katika shule zao.

"Mafunzo yamefanyika katika vituo vitatu vya Orkesumet shule ya sekondari Simanjiro, shule ya sekondari Terrat na shule ya awali na msingi Glisten Mirerani, ambayo yameanza juu kwa wachache watakaokwenda kuwafundisha wengi," amesema Hamis.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, mkuu wa shule ya sekondari Tanzanite, Jude Samwel Mziray amesema mfumo huo ni mzuri kwani wanaaachana na mtindo wa kuingiza taarifa kwenye makaratasi na kuweka katika mfumo wa kiteknolojia.

"Mfumo huo unarahisisha kwani unatoa taarifa ya shule hadi ngazi ya kata, kisha wilaya hadi ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) tofauti na tulivyozoea mwanzo kujaza katika makaratasi," amesema Mziray.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Naepo, kata ya Naisinyai, Simon Isack Magembe amesema mafunzo hayo yanawajengea uwezo zaidi wa kuboresha taarifa kwa matumizi sahihi.

Mwalimu Magembe amesema ujuzi walioupata wa kuandaa taarifa za mfumo huo umewarahisishia utendaji kazi wao tofauti na awali.



 Yas imeendelea na dhamira yake ya kuwekeza kwenye sekta ya elimu na kukuza vipaji vya vijana wa Kitanzania kupitia udhamini wa wanafunzi kumi mahiri waliochaguliwa kushiriki Kambi Maalum ya Mafunzo ya Hisabati Kigali, Rwanda kuanzia Januari 6 hadi 22, 2026.

Kambi hiyo ya kitaaluma, inayoandaliwa na African Olympiad Academy (AOA) kwa ushirikiano na MIT–Africa, inalenga kuwaandaa wanafunzi wenye vipaji kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika kwa ajili ya Mashindano ya Pan-African Mathematics Olympiad (PAMO) yanayotarajiwa kufanyika Juni mwaka huu.

Kupitia taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari, Afisa Mkuu wa Udhibiti Yas, Bi. Sylvia Balwire, alisema udhamini huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kampuni katika kuendeleza elimu, ubunifu na teknolojia nchini.

“Kupitia udhamini huu, tunaonyesha msimamo wetu wa muda mrefu wa kukuza elimu na kutengeneza kizazi kijacho cha watafiti, wavumbuzi na viongozi wa teknolojia. Somo la Hisabati ndiyo injini ya uchumi wa kidijitali, ubunifu na utatuzi wa changamoto za kisasa. Kwa kuwaunga mkono wanafunzi hawa, tunawekeza moja kwa moja kwenye mustakabali wa taifa letu,” alisema Bi. Balwire.

Aliwapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa, akibainisha kuwa uteuzi wao unaakisi uwezo, nidhamu na kujituma kwa kiwango cha juu katika somo la hisabati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa AOA, Arun Shanmuganathan, alieleza kufurahishwa kwake na ushiriki wa wanafunzi kutoka Tanzania ambao wamepata nafasi ya kuungana na wenzao mahiri kutoka Rwanda, Uganda, Kenya, Botswana, Namibia, Afrika Kusini na Nigeria ambao tayari wanasoma katika taasisi hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa MIT–Africa, Ari Jacobovits, alisema uwezo mkubwa ulioonekana kwa wanafunzi hao ndio sababu ya MIT kuwekeza kwa kina katika maendeleo yao, popote pale safari yao ya baadaye itakapowapeleka.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Chama cha Hisabati Tanzania (CHAHITA), Dkt. Said Sima, alitoa shukrani kwa Yas kwa mchango wake endelevu katika kukuza vipaji vya vijana na kuinua taaluma ya hisabati nchini.

Wanafunzi hao 10, ambao tayari wamesafiri kuelekea Rwanda kwa maandalizi haya muhimu ya kitaaluma na kimashindano, wanatoka maeneo mbalimbali ya Tanzania na wanawakilisha shule tofauti ikiwemo Ilboru Arusha, St. Francis Mbeya, Feza, Marian, Mahina, St. Monica Arusha na Mbeya Secondary.






Na Said Mwishehe,Michuzi TV

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Dk.Asha-Rose Migiro ametoa mwito kwa viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo Wabunge na Mawaziri kushiriki katika vikao vya mashina na matawi vinavyoitishwa katika maeneo yao.

Akizungumza leo Januari 13 wakati akihitimisha ziara yake ya mkoa wa Dar es Salaam kwa kufanya kikao kazi na viongozi wa CCM katika ngazi ya mashina pamoja na mabalozi Wilaya ya Ilala ameendelea kusisitiza umuhimu wa viongozi wa kitaifa wa Chama hicho kushiriki mikutano ya ngazi ya mashina na matawi.


 “Tumesema  mabalozi wetu mnafanya kazi nzuri  kwani mnaitisha mikutano katika mashina yenu ,hivyo tunapenda kutoa mwito mikutano hii isiwe kwa watu ambao wako katika ngazi ya mashina peke yake au ngazi ya tawi peke.


 “Viongozi wa kitaifa tunao wabunge katika mashina yetu , tunao mawaziri katika mashina yetu yetu.Nitoe mwito kwamba wawe sehemu ya mikutano  hii kwasababu kwa hakika hakuna anayeanzia juu wote tunaanzia kwenye mashina yetu.

“Kwahiyo iwe ni mfano kwa viongozi wetu kuwa sehemu mikutano ile ambayo inaitishwa na mabalozi wetu kwa maana hiyo tutakwenda kadri tunavyoendelea baada ya kupata taarifa ,kupata muhatasari wa yale yanayoendelea tupate kujua ni namna gani tujiimarishe zaidi.

Amesisitiza viongozi wanaposhiriki kwenye vikao ndipo wanapata nafasi ya kutazama changamoto zinazowakabili kama chama lakini na changamoto zinazoikabili jamii yetu na Chama Cha Mapinduzi kina wajibu wa kuzichukua changamoto hizo na kuzifikisha kwenye ngazi za juu.

“Ili  kwa pamoja na kwa kushirikiana nanyi mabalozi kwa kupata ushauri wenu kwa kupata nasaha zenu tuweze kuwapatia wananchi majibu ya changamoto zinazowakabili kwani wametupa dhamana ya uongozi

Kwa upande mwingine Dk.Migiro amezungumzia muelekeo wa Chama Cha Mapinduzi kimkakati katika kuendelea kuimarisha uhai wa chama hicho ambapo amefafanua mabalozi pamoja na kufanya kikao pia waendelee kuweka kumbukumbu za wanachama wao.

“Tumeambiwa hapa mashina ni sehemu muhimu sana ya usalama wa jamii yetu na usalama wa Taifa letu hivyo tutakuwa na wajibu wa kuhakikisha watu ambao tunaishi nao tunajua wanafanya nini na tunajua yale wanayoyafanya yanakuwa salama kwa Taifa letu 

“Tunajua pia hivi sasa balozi wa shina anaweza kuwa na nyumba nyingi sana hivyo kupitia vikao vyetu tutaangalia ni namna gani balozi wa shina apate mzigo ambao anaweza kuubeba ili twende kwa pamoja kuhakikisha chama chetu kinaendelea kuwa chama kiongozi na kinaendelea kushika dola kwa manufaa ya taifa letu.”























-Asisitiza mabalozi kupandisha bendera za chama kwenye maeneo yao.

-Asema chama kinawajali na kuwathamini mabalozi.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amesema maendeleo ya kweli kwa wananchi huanzia katika mashina ya Chama hicho, akisisitiza kuwa jitihada zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi hupata nguvu kupitia uongozi wa ngazi za chini.

Dkt. Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke tangu chama hicho kianzishwe, amesema hayo katika mkutano wake na Mabalozi wa Mashina wa CCM katika Wilaya ya Ilala, ikiwa ni hitimisho la ziara yake katika Mkoa wa Dar es Salaam yenye lengo la kuimarisha uhai wa CCM kuanzia kwenye mashina Kwa kauli mbiu ya "Shina lako linakuita".

Akizungumza na Mabalozi hao amesema mashina ndiyo sehemu ya kwanza ya wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo, kwa kuwa ndiko wanakotoka wananchi wenyewe na ndiko changamoto zao halisi zinapojadiliwa.

Ameeleza kuwa mahusiano kati ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya kisiasa hayawezi kutenganishwa, kwa kuwa mashina imara huwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji, jambo linaloongeza imani ya wananchi kwa Chama.

Ameongeza kuwa viongozi wa mashina wana wajibu mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, akisema uangalizi wa karibu wa miradi hiyo ndio msingi wa maendeleo yenye tija kwa wananchi.

Aidha, Mwanadiplomasia huyo, amesema Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongeza kazi kubwa inayofanywa na mabalozi hao wa mashina na kwamba chama kitaendelea kuthamini mchango wao mkubwa kwenye mashina.
























Top News