Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
MSIMU wa mbio za Mac D Promotions ‘ Mac D Marathon’ kwa mwaka 2026 unatarajiwa kufanyika Julai 4 mwaka huu katika viwanja vya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC,) Kwa kauli mbiu ya ‘Go Green With Gas’ yenye kulenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kutunza misitu.
Akizungumza katika uzinduzi wa mbio hizo uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa Mac D Promotions Denzel Rweyunga amesema kuwa mbio hizo ambazo usajili wake umeanza rasmi leo zinatarajiwa kushirikisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 pamoja na mbio za watoto za Kilomita 2.
Amesema kuwa licha ya kuhamasisha utunzaji wa afya kwa kukimbia mbio hizo pia zimelenga kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutunza mazingira kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi.
“Tunategemea kuwa na washiriki 3500 katika mbio hizi na maandalizi yameanza mapema ili kuzipa hadhi na viwango vya juu, na tayari usajili umefunguliwa kupitia www.macdmarathon.com na baada ya kujisajili na kufanya malipo kupitia simu au benki washiriki wataweza kupata vifaa zikiwemo tisheti katika vituo mbalimbali vilivyoainishwa.” Amesema.
Akifafanua kuhusu huduma muhimu katika mbio hizo amesema; wamejipanga kwa kuwa na huduma ya kwanza, vituo vya maji safi na salama ya kunywa ya Kilimanjaro, matunda pamoja na ulinzi na washiriki wote watakaofanikiwa kumaliza mbio hizo watapatiwa medali.
“Mac D Marathon 2026 itarushwa mbashara siku hiyo kupitia vituo vya ITV pamoja na East Africa Televison na baada ya mbio kutakuwa na burudani katika FM Academia chini ya Patcho Mwamba, michezo ya watoto, chakula na vinywaji pamoja na mpira wa miguu kati ya IPP na Mac D promotions.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Amani Ngoka amesema kupitia mbio hizo ambazo zimelenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi, shirikisho litatumia fursa hiyo kusaka vipaji na wawakilishi wa kimataifa katika riadha.
Aidha amewasisitiza wazazi kushiriki mbio hizo na watoto ambao watakimbia Kilomita 2 ili waweze kutambua na kuendeleza vipaji vyao na kuwataka Mac D promotions kufanya mbio hizo kuwa za kimataifa kwa mwaka ujao.
Kwa taarifa zaidi za ushiriki wa mbio hizo pamoja na udhamini Mac D Promotions itapokea kupitia tovuti pamoja na mawasiliano ya simu 0791799848/0702562009 pamoja na barua pepe macdmarathon@gmail.com.
Mbio za Mac D kwa mwaka 2026 zimedhaminiwa na Shirika la Nyumba la Taifa ( NHC ) , Kilimanjaro Natural Mineral Water, Azania Bank, ITV, Eb Maritime Group, Mart Group Ltd kupitia vinywaji vyake pendwa Tanzanite RoyalGin na Tanzanite Crafted For Royalt, Kaluba, Radio One, EATV, Montage na Ayo Tv.
Mkurugenzi wa Mipango na Biashara wa Mac D Promotions Denzel Rweyunga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mac D Marathon mwaka 2026 na kusema kuwa mbio hizo ambazo usajili wake umeanza rasmi leo zinatarajiwa kushirikisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 pamoja na mbio za watoto za Kilomita 2. Leo jijini Dar es Salaam.








.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
