Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) kwa niaba ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) kimezindua rasmi mafunzo ya Vihatarishi katika Usafiri wa Anga (Risk Management Course) tarehe 20 Aprili 2026 jijini Dar es Salaam. Mafunzo haya ya siku tano yanawakutanisha washiriki 20 kutoka Tanzania, Uganda na Eswatini wakiwawakilisha mamlaka za viwanja vya ndege na mashirika ya ndege.
Na Vero Ignatus
BENY Israel Mwaisaka, mchungaji wa kanisa la FPCT Komwale lililopo nje kidogo ya mji wa Handeni, wilaya ya Handeni mkoani Tanga anasema kuwa ninatambua na kuthamini Amani ambayo imekwepo tangu nchi ipate uhuru imekuwa msingi mkubwa wa maendeleo limewezesha wananchi kuishi kwa utulivu na kufanya shughuli zao bila hofu.
Kupitia amani hii, Watanzania wameweza kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi kwa uhuru mkubwa. Michezo, biashara, elimu na ibada vimekuwa vikifanyika kwa utulivu mkubwa,vilevile Vijana wamepata nafasi ya kusoma na kujiendeleza, huku watu wa dini mbalimbali wakifanya ibada zao kwa uhuru.
Haya yote ni matokeo ya juhudi za waasisi wa taifa letu ambao waliweka msingi wa umoja, mshikamano na upendo miongoni mwa Watanzania.
Mch.Mwaisaka anasema Amani ikikosekana hali hiyo huleta hofu kwa wananchi na kuhatarisha maendeleo katika sekta mbalimbali kama vile elimu, uchumi na hata uhuru wa kuabudu hivyo Ni muhimu kutambua kuwa amani si jambo la kudumu bila jitihada, bali inahitaji kulindwa na kila mmoja wetu kwa nguvu zote.
Katika mazungumzo mbalimbali ya kijamii, ndugu Hendry Lema, ambaye ni mzee mstaafu wa kanisa la KKKT Usharika wa Engarenaro Arusha, amekuwa akisisitiza umuhimu wa amani kwa maendeleo ya taifa. Anasema kuwa amani ndiyo nguzo kuu inayowezesha jamii kustawi, na bila amani hakuna maendeleo ya kweli yanayoweza kupatikana.
"Mimi ni baba na Kichwa cha familia pia ni mlezi wa kiroho na mshauri wa jamii, nahimiza watu kurejea katika misingi ya upendo, heshima na kuvumiliana,
Ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha kuwa tunadumisha misingi hii ya upendo na mshikamano. Kama alivyotuasa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, upendo ni silaha kubwa inayoweza kuondoa chuki, ubaguzi na migogoro.
Tukizingatia hilo, tutaweza kujenga taifa lenye umoja na lenye kuheshimiana kati ya wananchi na viongozi wao, tutangulize utu ili kuepusha migongano isiyo ya lazima.
Mwisho, nitoe wito kwa Watanzania wote bila kujali dini au imani zao, kuendelea kuliombea taifa letu na kumtanguliza Mungu katika kila jambo. Tukiwa na moyo wa toba na unyenyekevu,
Mungu atatusaidia kulinda amani yetu na kutujalia haki ya kweli. Kama ilivyoandikwa katika Mithali 14:34, “Haki huinua taifa; bali dhambi ni aibu ya watu wote.” Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki Watanzania.
BENY Israel Mwaisaka, mchungaji wa kanisa la FPCT Komwale lililopo nje kidogo ya mji wa Handeni mkoani Tanga

Serikali imesisitiza umuhimu wa michezo kwa wafanyakazi kama sehemu muhimu ya kuimarisha afya na kuongeza ufanisi mahali pa kazi.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe.Rahma Kisuo, wakati akifungua rasmi Michezo ya Mei Mosi Kitaifa 2026 iliyofanyika Aprili 20, 2026 katika viwanja vya Sabasaba mkoani Njombe.
Amesema kuwa afya ya mfanyakazi ni mtaji mkubwa unaochangia maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla, hivyo michezo inapaswa kupewa kipaumbele.
Aidha, Mhe.Kisuo amehimiza wafanyakazi kote nchini kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara badala ya kusubiri vipindi vya mashindano pekee. Amesisitiza kuwa mazoezi yawe sehemu ya maisha ya kila siku ili kuboresha afya na kuongeza tija kazini, huku akizitaka taasisi zote za umma na binafsi kuhakikisha zinatoa nafasi kwa wafanyakazi kushiriki shughuli za michezo.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Njombe Dkt. Stephane Nindi akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa, kufanyika kwa Maadhimisho ya Meimosi Njombe kumetoa fursa za kibiashara kwa wananchi wa mkoa huo.
Katika hatua nyingine, amewapongeza washiriki wa Michezo ya Mei Mosi na kuwataka kudumisha nidhamu, mshikamano na ushindani wa haki.
Amesisitiza kuwa michezo iwe chachu ya kuimarisha udugu na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi badala ya kuwa chanzo cha migogoro.
Kwa mwaka 2026, michezo hiyo inaongozwa na kauli mbiu isemayo, “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050,” huku watumishi na wachezaji wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) wakiwa miongoni mwa washiriki wa ufunguzi huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Uongozi wa Mtandao wa Wanawake Viongozi Afrika (AWLN) uliongozwa na Mlezi wake Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Liberia Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Aprili, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Uongozi wa Mtandao wa Wanawake Viongozi Afrika (AWLN), uliongozwa na Mlezi wake Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Liberia Mhe. Ellen Johnson Sirleaf pamoja na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia la Ethiopia Mhe. Sahle - Worke Zewde, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Aprili, 2026.



.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




















.jpeg)












