.jpg)
.jpg)
Na Mwandishi Wetu, Arusha
Arusha.
Tarehe 15 Mei 2026: Serikali imeipongeza Benki ya CRDB Bank Plc kwa
juhudi zake za kuhamasisha uwekezaji nchini kupitia elimu ya fedha,
uwekezaji wa hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kuwajenga vijana
kuwa wawekezaji wa baadaye.
Pongezi hizo zimetolewa jana jijini
Arusha na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Omar wakati akifungua Semina ya
Wanahisa wa Benki ya CRDB iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa 31 wa
mwaka wa benki hiyo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha
(AICC).
Semina hiyo ilikuwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na
Uwekezaji kwenye Hisa” na iliwakutanisha viongozi wa serikali, wanahisa,
wataalamu wa masoko ya mitaji pamoja na vijana kutoka maeneo mbalimbali
nchini.
Akizungumza katika semina hiyo, Waziri Omar alisema
vijana wanapaswa kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi kupitia
uwekezaji badala ya kutegemea ajira pekee.
“Kaulimbiu ya mwaka
huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa taifa letu. Vijana hawapaswi
kuishia kutafuta ajira pekee, bali wanastahili kushiriki katika umiliki
wa uchumi kupitia uwekezaji,” alisema Waziri Omar.
Aidha,
aliipongeza benki hiyo kwa hatua ya kufungua Ofisi ya Uwakilishi Dubai,
akisema hatua hiyo imeongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya fedha na
uwekezaji kimataifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema benki hiyo itaendelea
kuwawezesha vijana kupitia huduma za kifedha, ubunifu na programu za
maendeleo ya ujasiriamali.
Alisema kupitia CRDB Bank Foundation
na programu ya IMBEJU, maelfu ya vijana na wafanyabiashara wadogo
wamefikiwa kwa mafunzo, mitaji na ushauri wa biashara.
“Tunaamini
vijana wa leo si wateja tu wa benki yetu, bali ni wawekezaji, wabunifu
na viongozi wa uchumi wa kesho,” alisema Dkt. Nsekela.
Naye
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Neema Mori alisema
uwekezaji katika hisa ni njia muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa
muda mrefu kwa vijana na familia za Kitanzania.
Profesa Mori
alisema mafanikio ya Benki ya CRDB yanaonyesha namna uwekezaji wa muda
mrefu unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa wanahisa.
Alibainisha
kuwa ndani ya miaka mitatu iliyopita thamani ya hisa za benki hiyo
imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 253, huku bei ya hisa ikifikia wastani
wa Sh2,800 kutoka Sh460 mwaka 2023.
Aidha, alisema bodi ya
wakurugenzi inapendekeza gawio la Sh90 kwa kila hisa kutokana na matokeo
mazuri ya kifedha ya mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la asilimia 38
ikilinganishwa na mwaka uliopita.
Profesa Mori aliwahamasisha
wazazi kuanza kuwawekezea watoto wao hisa mapema ili kuwajengea msingi
imara wa maisha ya kifedha ya baadaye.
Benki ya CRDB ni miongoni
mwa taasisi kubwa za kifedha Afrika Mashariki na Kati, ikiwa na zaidi
ya wateja milioni sita katika nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo pamoja na ofisi ya uwakilishi Dubai, Falme za
Kiarabu..jpeg)
.jpeg)
Waziri
wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati
akifungua Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa 31
wa Wanahisa, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”,
semina inayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha
(AICC), ambapo alitoa wito kwa Taasisi za Fedha nchini kupunguza riba na
gharama nyingine za mikopo ili kuwawezesha wananchi wakiwemo vijana
kupata mitaji ya kuwekeza kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Abdulmajid Nsekela, akizungumza wakati
wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB katika
Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya “Vijana na
Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi
Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika Kituo cha
Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, akizungumza
wakati wa hafla ya ufunguzi wa Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB
katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa hao, uliobeba kauli mbiu ya
“Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa”, uliofunguliwa na Waziri wa Fedha,
Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), uliofanyika katika
Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).




.jpg)
.jpg)












.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)






