Mr Walter Makundi (in blue shirt), a Tanzanian Civil and Structural Engineer who has lived in Singapore with his family since 1994, has described his recent meeting with senior government officials from several African countries as a great honour.


The engagement, organised by the Chandler Academy of Governance, brought together delegates from Rwanda, Kenya, Uganda, Mauritius, Malawi, Somalia, Zambia, Tanzania and South Africa.


“I am sincerely grateful to the Chandler Academy of Governance for allowing me to share my personal reflections on Singapore’s remarkable transformation,” Mr Makundi said.


He noted that during his more than three decades in Singapore, he had witnessed first-hand how visionary leadership, long-term planning, strong institutions and disciplined implementation had helped transform the country into one of the world’s most advanced and prosperous nations.


“It was a privilege to exchange ideas with such distinguished government leaders and to reflect on lessons that may be useful to African countries,” he said.


Mr Makundi expressed hope that Singapore’s development journey would continue to inspire African nations as they pursue sustainable growth, modern infrastructure, stronger institutions and improved governance.


He thanked the Chandler Academy of Governance and all participating delegates for the thoughtful discussions, warm fellowship and memorable experience.


The Chandler Governance Group (CGG) is an international non-profit organisation headquartered in Singapore. It works with governments to build capabilities through training, hands-on projects, partnerships, and knowledge creation and sharing.


CGG founder Richard F. Chandler established CGG in 2019 as the Chandler Institute of Governance (CIG), with the support of a group of seasoned former government leaders from several countries. He saw the value of an independent institute that would work with governments in highly practical ways. We are a practitioner-focused organisation, focusing on the “how” rather than just the “what” and “why”.

CIG rebranded in 2026 as CGG.


The Chandler Academy of Governance (CAG) is the Learning and Development division of CGG. We design and deliver training programmes for public sector leaders, equipping them with the skills to deliver high-performance government, with its signature programmes anchored in proprietary curriculum, practitioner-focused, and contextualised to local needs. 


It utilises a range of teaching techniques, including seminars, expert-led discussions, and site visits. We also work with clients to design customised programmes for public servants, tailored to the country context, objectives, and participant profiles.

.








BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya Kiswahili inaendelea kukua na kuenea duniani ambapo sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni 200 katika nchi 14 duniani na kutumika rasmi katika jumuiya kadhaa za kikanda barani Afrika na kimataifa.

Balozi Matinyi aliyasema hayo kwenye sherehe za Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani zilizoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Algeria na kufanyika jijini Algiers tarehe 9 Julai zikihudhuriwa na mabalozi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, taasisi za umma na binafsi, wanazuoni na waandishi wa habari walioongozwa na Katibu Mnadhimu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni na Sanaa ya Algeria, Bibi Nacera Ayaïchia.

“Mbali ya Tanzania, Kiswahili pia ni lugha ya taifa nchini Kenya, Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),” alisema Balozi Matinyi kwenye hotuba yake aliyoitoa kwa lugha ya Kiswahili na nakala yake katika tafsiri ya lugha za Kiarabu, Kifaransa na Kiingereza kusambazwa kwa wageni waalikwa waliopewa fursa ya kuifuatilia kwa sauti na maandishi kwenye skrini kubwa.

Sherehe hiyo ilinogeshwa na filamu fupi ya dakika kumi iliyoonesha marais wa zamani na wa sasa wa Tanzania na baadhi wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wakihutubia kwa lugha ya Kiswahili katika nyakati tofauti.

Filamu hiyo pia inamwonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwa lugha ya Kiswahili nchini Komoro mwaka 2025 kwenye sherehe za miaka 50 ya uhuru wa taifa hilo.

Balozi Matinyi aliongeza pia kwamba Kiswahili ni lugha rasmi ya Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Kadhalika, Balozi Matinyi aliitaja mifano ya redio za nchi za Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Japan, China, Iran, India na wakati fulani Marekani ambazo hutumia lugha ya Kiswahili katika matangazo yake ya kila siku.

Akirejea kauli mbiu ya mwaka huu ya siku hiyo ya “Kiswahili kwa Amani, Mshikamano na Diplomasia ya Uchumi Duniani”, Balozi Matinyi alisema Kiswahili ni lugha ya kujivunia ambayo imetumika katika mapambano ya ukombozi barani Afrika na inaendelea kutumika kulinda amani, kuleta mshikamano na kujenga uchumi barani Afrika.

Sherehe hiyo iliyotumia lugha nne zikiongozwa na Kiswahili, ilipambwa pia na vinywaji vya chai na kahawa ya Tanzania, vyakula vya mapishi ya Kiswahili, maonesho ya mavazi ya wakaazi wa pwani ya Tanzania kama khanga, baibui, kanzu, vikoi na vitenge yaliyooneshwa na wanafunzi wa Tanzania.

Wanafunzi hao wa Tanzania wanaosoma kwenye vyuo vikuu nchini Algeria, walicheza pia ngoma mbili za makabila ya Tanzania ya Kimasai na Kihaya na kuimba shairi la Kiswahili.

Siku ya Lugha ya Kiswahili Duniani huadhimishwa mwezi Julai tangu mwaka 2022 kufuatia uamuzi wa UNESCO wa mwaka 2021 wa kuitangaza tarehe 7 Julai kuwa siku ya maadhimisho ya lugha hii pekee barani Afrika kuwahi kupewa hadhi hii kimataifa.


"....Mimi nikifa nitaaga siwezi kuondoka kimya kimya", Seif Kisauji amemwambia Ankal kwa utani wakati Mwanamuziki huyo maarufu kama Babu wa TikTok, akikanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa amefariki dunia.

Babu wa TikTok akiongea akiwa msikiti wa Maamur ulioko Upanga jijini Dar amekanusha taarifa hizo na kuwahakikishia mashabiki wake kuwa yuko hai na anaendelea vizuri.

Ameeleza kuwa chanzo cha mkanganyiko huo ni kifo cha mtoto wa familia yao, Mabrouk Kisauji, na si yeye, na kwamba wapo hapo Maamur kukamilisha mipango ya safari ya Tanga, na kwamba yeye na familia yake wanasafiri kuelekea huko leo kwa ajili ya kuhudhuria mazishi.

Kisauji kaongea haya yote baada ya kuona video yake akiimba kusambazwa mitandaoni ikiwa imeambatanishwa na madai ya uongo kwamba amefariki, jambo lililozua taharuki miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Amewasihi watumiaji wa mitandao kuwa makini na taarifa za upande mmoja kwani katika zama hizi za kila mtu kujifanya mwandishi wa habari, taarifa zisizo sahihi ni nyingi mno.

Pia amewataka walio wanahabari wasiwe na papara za kuchapisha taarifa ammbazo hazijathibitishwa kwa kuwa hiyo inawavunjia heshima kwa kuonekana ni waongo na wadaku.


Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya NIC Insurance imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa Bima ya COMESA (COMESA Yellow Card), ikieleza kuwa huduma hiyo inarahisisha safari za kuvuka mipaka ya nchi wanachama wa Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) bila kulazimika kukata bima mpya ya lazima katika kila nchi.

Akizungumza katika Banda la NIC Insurance kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa Mwandamizi wa kampuni hiyo, Bi. Erika Nnko, amesema Bima ya COMESA ni mfumo wa kikanda wa bima ya vyombo vya moto unaowapa madereva uhuru wa kusafiri kwa usalama katika nchi wanachama wa COMESA huku wakitambuliwa kisheria kupitia kadi maalumu ya njano inayofahamika kama COMESA Yellow Card.

Amesema mmiliki wa chombo cha moto anapokata bima hiyo kupitia kampuni za bima zilizoidhinishwa nchini, hupatiwa Yellow Card ambayo hutambulika na mamlaka za nchi zote zinazoshiriki katika mfumo huo.

Erika amesema kadi hiyo hutoa kinga dhidi ya madai yanayotokana na majeraha kwa watu wengine au uharibifu wa mali za watu wengine unaoweza kusababishwa na chombo cha moto wakati wa safari katika nchi wanachama wa COMESA.

Ameeleza kuwa mfumo huo unarahisisha biashara na usafirishaji wa mizigo pamoja na safari za watu binafsi kwa kuondoa ulazima wa kukata bima mpya ya lazima ya mkataba wa tatu (Third Party) kila unapovuka mpaka wa nchi mwanachama.



Na Mwandishi Wetu
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, ameipongeza Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa juhudi zake za kuwawezesha vijana kujiajiri kupitia Kituo chake cha Kiatamizi cha IAA Business Start Up Centre, kinachowasaidia kubadili mawazo ya kibunifu kuwa biashara zenye mafanikio.

Tutuba alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la IAA katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema anafurahishwa na maendeleo ya kituo hicho, akieleza kuwa alishiriki katika hatua za mwanzo za kuanzishwa kwake na sasa anashuhudia matokeo chanya kupitia vijana wanaobuni na kuanzisha biashara zinazochangia maendeleo ya uchumi.

"Ninakumbuka tulipoanzisha kituo hiki. Leo ninafurahi kuona kinaendelea kuzalisha vijana wenye ubunifu na kuwageuza mawazo yao kuwa fursa za kiuchumi," alisema Tutuba.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa, Uhusiano na Masoko wa IAA, Sarah Goroi, alisema taasisi hiyo imeendelea kuwekeza katika kuwaandaa vijana kwa kujiajiri kupitia Kituo cha Kiatamizi, sambamba na kutoa elimu inayokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Alisema mbali na mafunzo ya darasani, IAA imeweka mazingira rafiki yanayowezesha wanafunzi kuanzisha biashara zao huku wakipata ushauri wa kitaalamu, mafunzo ya ujasiriamali na ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha mawazo yao yanakua na kuwa biashara endelevu.

Sarah alisema katika mwaka wa masomo 2024/2025 zaidi ya vijana 8,600 walinufaika na programu za ujasiriamali, huku vijana 1,520 wakiwasilisha mawazo mbalimbali ya biashara kupitia kituo hicho.

Aliongeza kuwa kati ya mawazo hayo, zaidi ya biashara 50 zilianzishwa na kampuni 12 zikafanikiwa kusajiliwa rasmi, zikijikita katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, teknolojia, sanaa, uhifadhi wa mazingira na shughuli nyingine za kiuchumi.

Alisema kupitia Kituo cha Kiatamizi, wahitimu wengi wamefanikiwa kujiajiri na wengine kuanzisha kampuni zinazowaajiri vijana wenzao, hatua inayochangia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na ujasiriamali.









Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI  ya Mixx imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia kampeni ya Kombe la Dunia ya MiXX Super, ambapo washindi watatu wamekabidhiwa zawadi za shilingi milioni moja kila mmoja kwa kutumia aprication ya MiXX Super app kufanya malipo ya huduma mbalimbali.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi hizo katika banda la Yas kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Meneja wa Biashara Mixx Mkoa wa Dar es Salaam, Estony Venant, alisema kampeni hiyo imeendelea kuwagusa Watanzania wengi huku jumla ya washindi 48 wakinufaika hadi sasa.

Alisema kati ya washindi hao,zaidi ya washindi 20 wamejishindia vifaa mbalimbali kutoka kwa mshirika wa Mixx kampuni ya Hisense, huku washindi wengine zaidi ya 40 wakijishindia fedha taslimu za shilingi milioni moja kila mmoja.

Venant alisema kampeni hiyo bado inaendelea na kwamba mshindi wa mwisho atajishindia zawadi kubwa ya shilingi milioni 50, akiwahimiza wananchi kutumia Aprication ya MiXX Super app katika kufanya malipo ya huduma mbalimbali za kifedha ili kuongeza nafasi ya kushinda.

"MiXX Super ni zaidi ya Aprication malipo; ni jukwaa linalorahisisha huduma za kifedha huku likiwapa watumiaji nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali. Tunawahimiza wananchi kuipakua na kuitumia mara kwa mara," alisema Venant.



Ilipofika Juni 11, 2026, dunia ilishuhudia uzinduzi wa mashindano makubwa kuliko yote ya michuano ya Dunia mechi ya ufunguzi kati ya Mexico na Afrika Kusini ikizindua msimu wa timu 48, badala ya 32 za zamani. Tangu siku hiyo hadi sasa ambapo mashindano yamefikia hatua ya raundi ya 16, kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimfumo na pia matukio kadhaa yaliyoibua mijadala mikali kuhusu haki na uwazi wa maamuzi ya kiuchezaji.

Jambo la kwanza lililobadilisha sura ya mashindano ni sheria mpya zilizoletwa na IFAB kabla ya fainali kuanza. Badala ya kusubiri muda mrefu kwa mabadilishano ya wachezaji, sasa mchezaji anayetoka uwanjani ana sekunde kumi tu, la sivyo mbadala wake atalazimika kusubiri dakika moja. Vilevile, refa anaweza kuanzisha kaunti-daun ya sekunde tano kwa mirushano ya kando na migongo ya lango ili kuzuia kupoteza muda kimakusudi.

Mapumziko ya lazima ya kunywa maji ya dakika tatu kwa kila nusu ya mchezo pia yameletwa, ingawa baadhi ya watazamaji wamelalamikia kuwa mapumziko hayo yametumika zaidi kwa matangazo ya kibiashara kuliko ustawi wa wachezaji.

Mabadiliko mengine muhimu yamehusu matumizi ya VAR. Sasa mfumo huu unaruhusiwa kupitia upya maamuzi ya kona zisizo sahihi, kadi nyekundu zilizotokana na kadi ya pili ya njano, na hali za kumwadhibu mchezaji asiye sahihi.

Aidha, sheria mpya ya kutoa kadi nyekundu kwa mchezaji anayefunika mdomo wake wakati wa ugomvi na mpinzani imeanza kutumika, huku Miguel Almirón wa Paraguay akiwa mchezaji wa kwanza kufukuzwa chini ya sheria hiyo dhidi ya Uturuki. Teknolojia ya mstari wa nusu-otomatiki (semi-automated offside), inayotumia vitambuzi ndani ya mpira wa Adidas Trionda, nayo imeongeza usahihi wa maamuzi ya "off-side" kuliko wakati mwingine wowote.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hata hivyo, usahihi huo wa kiteknolojia haujaondoa utata. Katika hatua ya makundi, mabao ya Iran dhidi ya Misri na Brazil dhidi ya Scotland yalifutwa na VAR, hali iliyowafanya baadhi ya viongozi wa mashirikisho, akiwemo rais wa shirikisho la mpira la Brazil, kuandikia FIFA wakitaka uthabiti zaidi wa kanuni hizo.

Mvutano ulizidi wiki iliyopita pale Folarin Balogun wa Marekani alipopewa kadi nyekundu dhidi ya Bosnia kabla FIFA haijaigeuza baada ya kuombwa na Rais Trump, na hivi karibuni zaidi, bao la Misri lililofutwa dakika za mwisho za mechi dhidi ya Argentina huko Atlanta liliizua tena hisia za upendeleo miongoni mwa mashabiki na wachambuzi.

Nje ya viwanja, mashindano haya pia yamekumbwa na changamoto za kiusalama, kiuchumi na kisiasa kuanzia ukaguzi mkali usio wa kawaida uliokabili timu za Senegal na Uzbekistan walipowasili Marekani, mgomo wa wafanyakazi wa uwanja wa SoFi Stadium, hadi bei za tiketi zilizofika hadi dola 11,000 kwa fainali.

Kwa pamoja, matukio haya yanaonesha kwamba, ingawa sheria mpya na teknolojia zimefanikiwa kuongeza kasi na usahihi wa mchezo, bado kuna safari ndefu kuelekea kuaminika kikamilifu machoni pa mashabiki na timu shindani.
Kwa kizazi kinachopenda burudani yenye msisimko, Meridianbet imeleta promosheni inayobadilisha namna ya kufurahia michezo ya kasino. Golden Goal Rewards ni jukwaa linalokupa nafasi ya kushindania jumla ya TZS milioni 450 huku ukiendelea kufurahia michezo unayoipenda. Kila mzunguko wa mchezo unaweza kuwa hatua ya karibu zaidi kuelekea ushindi mkubwa ambao unaweza kubadilisha siku yako kuwa ya kipekee.

Baada ya kujiunga kwenye promosheni hii, safari ya ushindi inaanza mara moja. Unachohitaji ni kucheza michezo inayostahili na kutimiza masharti ya ushiriki. Kilicho cha kuvutia zaidi ni kwamba Meridianbet imeweka mfumo wa Prize Drops za ghafla, zawadi ambazo zinaweza kuingia moja kwa moja kwenye akaunti yako wakati wowote ukiwa katikati ya mchezo. Hapo msisimko wa kweli unazaliwa, kwa sababu huwezi kujua ni muda gani bahati yako itang’ara.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mbali na zawadi za papo hapo, Golden Goal Rewards imeundwa kuwapa wachezaji motisha ya kuendelea kushiriki. Kila mchezo unaoucheza unakusaidia kujikusanyia pointi ambazo zinakupandisha kwenye msimamo wa kila wiki. Kadri unavyokuwa hai kwenye promosheni, ndivyo nafasi yako ya kuingia kwenye orodha ya washindi inavyoongezeka. Hii inamaanisha kuwa kila wiki ni fursa mpya ya kuonyesha uwezo wako na kupanda juu ya msimamo.

Kwa walio wengi, michezo ya kasino ni sehemu ya burudani na mapumziko ya kila siku. Meridianbet imeelewa hilo na kuunda promosheni inayokupa furaha, ushindani na nafasi halisi ya kushinda. Golden Goal Rewards inaleta mazingira ambayo kila mshiriki anaweza kujisikia sehemu ya safari kubwa ya ushindi.

Huu ndio wakati wa kuchukua hatua. Ingia sasa ndani ya Meridianbet, jiunge na Golden Goal Rewards na ujionee jinsi ushindi unavyoweza kutokea wakati wowote. TZS milioni 450 zinasubiri washindi wenye ujasiri wa kucheza kwa kujiamini. Kila wiki inaleta mwanzo mpya, na kila mchezo unaweza kuwa mlango wa kuandika historia yako ya ushindi ndani ya Meridianbet.
Dar es Salaam, Julai 10, 2026

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umewahimiza wananchi waliojiajiri nchini kujiunga na kuchangia katika Mfuko huo ili kujijengea akiba, kupata kinga ya kijamii na kuwa na uhakika wa maisha ya sasa na baadaye.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala, Bw. Ekwabi Mujungu, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, wakati akifungua Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri iliyofanyika Julai 10, 2026 katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Bw. Mujungu alisema Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri ni sehemu ya mkakati wa NSSF wa kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa wananchi waliojiajiri, ambao ni sehemu muhimu ya ukuaji wa uchumi wa nchi.

"Wananchi wengi wanaojiajiri hupata kipato kupitia shughuli wanazozifanya, lakini bila kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba wanaweza kujikuta wakikabiliwa na changamoto wanapofikia uzee au wanapopoteza uwezo wa kufanya kazi. Kujiunga na NSSF ni hatua muhimu ya kujenga uhakika wa maisha ya sasa na ya baadaye," alisema Bw. Mujungu.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya kupanua wigo wa hifadhi ya jamii ili wananchi wote, bila kujali aina ya shughuli wanazofanya, wanufaike na huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii.

"Tunawahimiza wananchi wote waliojiajiri kutumia fursa hii kujiunga na kuchangia NSSF. Mtu anapoanza kuweka akiba mapema, anajijengea msingi imara wa kunufaika na mafao mbalimbali yatakayomsaidia yeye na familia yake pale yatakapohitajika," alisisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa NSSF Mkoa wa Kigamboni, Bw. Siraji Kisaka, alisema siku hiyo maalumu imeandaliwa mahsusi kuwafikia wananchi waliojiajiri kwa kuwapatia elimu kuhusu umuhimu wa kujiunga na kuchangia NSSF pamoja na kuwafahamisha mafao na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko.

"Lengo letu ni kuhakikisha wananchi waliojiajiri wanapata uelewa sahihi kuhusu hifadhi ya jamii na umuhimu wa kujiunga na kuchangia NSSF. Tunataka wajenge utamaduni wa kujiwekea akiba ili wawe na usalama wa maisha yao ya sasa na ya baadaye," alisema Bw. Kisaka.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Uwezeshaji Wanawake Tanzania (TAWEN), Florence Massunga, aliwataka wananchi waliojiajiri kuitumia fursa hiyo kujiunga na NSSF, akisema kufanya hivyo kutawasaidia kujenga usalama wa kifedha na kupunguza utegemezi wanapokumbwa na changamoto za maisha.

Baada ya ufunguzi wa shughuli hiyo, wananchi waliojiajiri walipewa elimu kuhusu mfumo wa hifadhi ya jamii, utaratibu wa kujiunga na kuchangia NSSF, mafao mbalimbali yanayotolewa na Mfuko pamoja na umuhimu wa kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba mapema ili kuwa na uhakika wa maisha ya sasa na baadaye.

Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri ni sehemu ya shughuli za NSSF katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, zenye lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi, kuongeza uelewa kuhusu hifadhi ya jamii na kuwahamasisha wananchi waliojiajiri kujiunga na kuchangia NSSF.





















Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid, leo Julai 20, 2026 akiwa mkoani Mbeya amekutana na kusikiliza changamoto, maoni na mapendekezo kutoka kwa makundi mbalimbali ya kijamii.

Makundi yaliyowasilisha hoja zao ni pamoja na wakulima, wafugaji, wachimba madini, wafanyabiashara, wavuvi, mama na baba lishe, machinga, waendesha usafirishaji, mafundi ujenzi, mafundi gereji, wanamichezo, walimu wazalendo, wazee wastaafu pamoja na vikundi mbalimbali vya kijamii.

Ndg. Rabia alipokea kero, ushauri na mapendekezo yaliyowasilishwa na wananchi hao, huku baadhi ya hoja zikijibiwa na nyingine kutolewa maelekezo kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi.

Baada ya kikao hicho, Ndg. Rabia aliwataka wananchi kuendelea kulinda amani ya Tanzania, akisisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo endelevu na kila Mtanzania ana wajibu wa kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama na yenye utulivu ili wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji kwa maendeleo ya taifa.









Top News