Na Mwandishi Wetu

ALN Tanzania, kampuni inayojishughulisha katika huduma za kisheria na ushauri wa biashara, imezitaka biashara za kifamilia nchini kuondokana na mifumo isiyo rasmi iliyowasaidia katika hatua za awali za ukuaji, na badala yake kukumbatia mifumo thabiti ya utawala bora.

Hatua hiyo itawezesha kulinda utajiri wa vizazi, kuhakikisha ustawi wa muda mrefu na kuvutia uwekezaji kutoka nje.

Wito huo ulitolewa wakati wa hitimisho la mfululizo wa semina za mafundisho ya kusimamia biashara za kifamilia katika mfumo sahihi ( Family Business Resilience & Growth Knowledge Series), zilizoandaliwa na ALN Tanzania kwa ushirikiano na International Finance Corporation (IFC) jijini Dar es Salaam wiki hii. Mfululizo huo semina hizo tatu ulijadili misingi ya utawala wa kifamilia, muundo wa bodi na katiba za familia katika awamu zilizopita, huku kikao cha mwisho kikijikita katika urithishaji na mpito wa uongozi.

Akizungumza katika semina hiyo, Shemane Amin, Mshirika wa ALN hapa nchini , alisisitiza kuwa mwendelezo wa biashara za kifamilia hauji kwa mazoea bali unapaswa kupangwa kwa makusudi.

“Biashara nyingi za kifamilia hukua kwa mafanikio katika miaka ya mwanzo kwa kutegemea imani na maamuzi yasiyo rasmi,” alisema. “Hata hivyo, kadri biashara zinavyopanuka na vizazi vinavyoongezeka kushiriki, kuweka mifumo rasmi kunakuwa muhimu kulinda biashara yenyewe na umoja wa familia.”

Alieleza kuwa kampuni hiyo ilianzisha mfululizo huo wa semina ili kuwapatia wamiliki wa biashara za kifamilia mifumo ya vitendo kuhusu utawala bora, upangaji wa urithishaji na uwazi wa uongozi mambo ambayo mara nyingi huamua iwapo biashara itaendelea baada ya kizazi cha mwanzilishi wa biashara (Founder) katika familia husika.

Kwa upande wake, Edward Williams, Mkurugenzi wa ALN Tanzania, alisisitiza umuhimu wa kuanza mapema kupanga urithishaji na kuonya dhidi ya mabadiliko ya uongozi yanayofanyika kwa dharura.

“Moja ya dhana potofu iliyoenea katika biashara za kifamilia ni kwamba urithishaji huanza pale mwanzilishi anapokuwa tayari kustaafu,” alisema. “Kwa uhalisia, urithishaji huanza mapema zaidi.

Mabadiliko yenye mafanikio ni yale ambayo ukuzaji wa uongozi, miundo ya wanahisa na mifumo ya utawala inakuwa tayari imewekwa tangu awali.”, alisema.

Alibainisha kuwa kadri biashara za Kitanzania zinavyokua kwa thamani na kuwa tata zaidi, mikataba rasmi ya wanahisa, katiba za familia, majukumu yaliyoainishwa wazi kwa watendaji wakuu na mifumo huru ya usimamizi vinakuwa muhimu katika kulinda thamani ya muda mrefu.

Naye Mona Doshi, Mshirika wa ALN kutoka Mombasa nchini Kenya, alizungumzia umuhimu wa sera rasmi za ajira kwa wanafamilia katika kuimarisha uimara wa biashara.

“Kadri familia zinavyopanuka kizazi hadi kizazi, kuwa na mwongozo wa uwazi kuhusu vigezo vya kuajiriwa, viwango vya utendaji na uwajibikaji husaidia kuzuia migogoro ya ndani na kuimarisha uongozi unaozingatia sifa,” alieleza.

Aliwahimiza wamiliki wa biashara kuweka mifumo rasmi ya utawala inayolinda urithi wa familia huku ikizingatia weledi, ili kuhakikisha mabadiliko ya uongozi yanategemea maandalizi na uwezo wa mtu badala ya kuchaguliwa kuongoza tu kwa sababu ni sehemu ya familia.

Akizungumza kwa niaba ya IFC, Rose Lumumba alisisitiza kuwa utawala bora uliowekwa kwa mifumo rasmi unahusishwa moja kwa moja na utayari wa kupokea uwekezaji na ustawi wa muda mrefu.

“Biashara za kifamilia zinazoweka mifumo ya utawala mapema huwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuvutia mitaji, kupanuka kwa uwajibikaji na kustahimili mabadiliko ya vizazi,” alisema.

Washiriki walikubaliana kuwa biashara za kifamilia zina mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania, na kwamba uwezo wake wa kuweka mifumo rasmi ya uongozi na utawala utaathiri uimara wa sekta binafsi kwa ujumla.

Tafiti za kimataifa zinaonesha kuwa ingawa biashara za kifamilia zinachangia zaidi ya asilimia 60 ya shughuli za sekta binafsi duniani, ni takriban asilimia 30 tu zinazofanikiwa kuvuka hadi kizazi cha pili, na chini ya asilimia 15 hufikia kizazi cha tatu. Wataalamu wa sekta hiyo wanaeleza kuwa upangaji madhubuti wa urithishaji na nidhamu ya utawala bora huongeza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa mafanikio ya mpito huo.

ALN Tanzania hutoa ushauri kwa biashara za kifamilia kuhusu uundaji wa mifumo ya utawala, mipango ya urithishaji, makubaliano ya wanahisa na suluhisho za usimamizi wa utajiri wa kuvuka mipaka, ikiwawezesha kubadilika kutoka biashara zinazoongozwa na waanzilishi hadi taasisi imara za kudumu.
Bi. Shemane Amin, Mshirika wa ALN Tanzania (kulia), akiendesha mazungumzo na Bw. Vineet Verma, Meneja Mkuu wa Kioo Limited, wakati wa hitimisho la mfululizo wa Uendeshaji kimfumo wa biashara za kifamilia ( Family Business Resilience & Growth Knowledge Series), ulioandaliwa kwa ushirikiano kati ya ALN na International Finance Corporation (IFC) jijini Dar es Salaam wiki hii.
Bw. Edward Williams, Mkurugenzi wa ALN Tanzania, akiongea wakati wa hitimisho la mfululizo wa kongamano la mafunzo ya uendeshaji kimfumo wa biashara za kifamilia (Family Business Resilience & Growth Knowledge Series), ulioandaliwa kwa ushirikiano kati ya ALN na International Finance Corporation (IFC) jijini Dar es Salaam wiki hii.

Baadhi ya washiriki wa hitimisho la mfululizo wa kongamano la mafunzo ya uendeshaji bora wa biashara za kifamilia ( Family Business Resilience & Growth Knowledge Series), ulioandaliwa na ALN Tanzania kwa ushirikiano na International Finance Corporation (IFC) jijini Dar es Salaam wiki hii.

📍Yataja utendaji wake kama kiungo muhimu kwenye chama na serikali

*NA MWANDISHI WETU, MBEYA

Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Vijijini, imemtunukia Tuzo maalum ya Heshima na Shukrani Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Solomon Itunda, kwa kutambua mchango wake mkubwa wa kuunganisha Serikali na Chama katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020-2025.

Tuzo hiyo imekabidhiwa jana tarehe 26 Februari 2026, wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya Wilaya kilichopokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 2025.

Akisoma maelekezo ya Kamati ya Siasa mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Hakimu Mwalupimbi, amemuelezea DC Itunda kama "Kiungo" madhubuti ambaye amekuwa akipatikana wakati wote kushughulikia kero za wananchi na mahitaji ya Chama bila kujali muda.

"DC Itunda umekuwa kiungo kikubwa baina ya Chama na Serikali. Iwe usiku wa manene, asubuhi au mchana, umekuwa ukipokea simu na pale unapokuwa na majukumu mengine unajibu kwa ujumbe mfupi na baadaye unapiga simu kufuatilia. Hiyo ni ishara ya kiongozi aliyelelewa na kukomaa ndani ya Chama," alisema Mwenyekiti huyo.

Mwenyekiti aliongeza kuwa uzoefu wa DC Itunda uliotukuka—kuanzia nafasi ya Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya hadi ngazi ya Taifa—umechangia kwa kiasi kikubwa utulivu na mafanikio yanayoonekana sasa wilayani humo.

 Alisisitiza kuwa tuzo hiyo ni ishara ya upendo na shukrani kutoka kwa wana-CCM ili kumtia moyo aendelee kukibeba Chama, hususan katika nyakati hizi za kuelekea majukumu mazito ya kitaifa.

Akizungumza kwa unyenyekevu baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amekishukuru Chama Cha Mapinduzi kwa malezi yaliyomfikisha katika nafasi hiyo ya utumishi wa umma.

Kamati ya Siasa ya Wilaya imebainisha kuwa utaratibu huo wa kutambua na kupongeza watendaji wanaofanya vizuri utakuwa endelevu ili kuongeza ari ya utumishi ndani ya Wilaya ya Mbeya.







 

📌Yasema mradi umesimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi

📌Yasisitiza ni kichocheo muhimu katika za fursa za kiuchumi na kijamii

Kamati ya Uongozi wa Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), tarehe 26 Februari 2026, imekagua maendeleo ya uzalishaji wa umeme katika mradi huo na kueleza kuridhishwa na usimamizi pamoja na utekelezaji wake, uliokidhi viwango vya ubora vinavyoendana na thamani ya fedha iliyowekezwa na Serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. Jim Yonazi , amesema kamati imefurahishwa na namna bwawa hilo linavyochochea ukuaji wa uchumi kwa kuongeza uzalishaji wa umeme unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini, hatua inayochangia kuimarika kwa upatikanaji wa nishati ya umeme.

“Tumeridhishwa na jinsi mradi huu ulivyosimamiwa na kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

 Ukilinganisha na miradi mingine barani Afrika, mradi huu umejengwa kwa ubora wa hali ya juu na umeleta unafuu katika huduma ya umeme nchini. Haya ni mafanikio makubwa kwa Taifa,” alieleza Dkt. Yonazi.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Bw. Petro Lyatuu, amesema mradi huo umekamilika  kwa asilimia 100 na mchango wake tayari umeanza kuonekana. 

Amefafanua kuwa mwaka 2021, gridi ya taifa ilikuwa na jumla ya megawati 1,600, lakini kwa sasa uwezo wa uzalishaji umefikia zaidi ya megawati 4,000, zaidi ya mara mbili ya kiwango cha awali.

“Kwa sasa bwawa linazalisha umeme na tija yake imeonekana wazi. Kuongezeka kwa uzalishaji kumeimarisha gridi ya taifa na tunaendelea kuongeza nguvu katika sekta ya nishati kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi,” alisisitiza Bw. Lyatuu.

Aidha kwa hatua nyingine Kamati hiyo ilitembelea kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze, kinachopokea umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere na kusambaza katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji, Mhandisi Antony Mbushi, amesema kituo hicho kimekamilika na tayari kinafanya kazi.

Ameongeza kuwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma umefikia asilimia 71.58, huku mradi wa kusafirisha umeme kutoka Chalinze kupitia Kinyerezi hadi Mkuranga umefikia asilimia 59.76.

‘’Kamati imeridhishwa na maendeleo ya miradi hiyo na kusisitiza kuwa mpango uliopo ni kuendelea kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha nishati ya umeme inakuwa ya uhakika na endelevu’,’Aliongeza Mha. Mbushi

Katika hitimisho la ziara hiyo, Kamati imeeleza kuwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya umeme unaifanya Tanzania kuwa kivutio cha uwekezaji na kitovu cha usambazaji wa umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati na Kusini.











 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni(kushoto) akiteta jambo na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla kabla ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026.


Na Mwandishi Wetu

Unguja:

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefungua semina yaWabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar na kusisitizaumuhimu wa kuimarisha usimamizi na uwajibikaji katika utekelezaji wa Mfuko wa KuchocheaMaendeleo ya Jimbo.

Semina hiyo imefanyika Unguja, Zanzibar Februari 26, 2026 akieleza kuwa Mfuko wa Jimboumechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji wa maji safina salama, umeme, elimu, barabara na kukuza shughuli za biashara katika jamii.

Amesema mfuko huo ulianzishwa kwa lengo la kuwashirikisha wananchi katika kubuni nakutekeleza miradi ya maendeleo inayogusa mahitaji halisi ya majimbo yao, hivyo ni wajibu wawabunge kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kikamilifu ili miradi iwe na tija na uendelevu.

“Serikali inalenga kuwezesha utekelezaji wa miradi ya haraka yenye manufaa kwa wananchi, kuimarisha uwajibikaji na ushiriki wa jamii katika kupanga na kusimamia maendeleo pamoja nakupunguza pengo la maendeleo kati ya maeneo mbalimbali,” amesema Mhe. Abdulla.

Ameeleza licha ya kuwepo kwa sheria na miongozo ya matumizi ya fedha za mfuko huo, badokuna changamoto za usimamizi katika baadhi ya halmashauri zilizosababisha kuibuka kwa hoja za ukaguzi.

Kutokana na changamoto hiyo amewataka watendaji wa halmashauri kusimamia ipasavyo fedhahizo ili kuepuka dosari na kuhakikisha thamani ya fedha inapatikana.

Aidha amezungumzia umuhimu wa kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya marekebisho yaSheria ya Mfuko wa Jimbo ya mwaka 2009, kufuatia maelekezo yaliyotolewa baada yakuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa mfuko kwa mwaka 2023/24 katika Kamati yaKudumu ya Bunge ya TAMISEMI.

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais imeombwa kuratibu upatikanaji wa maoni kutoka upandewa Zanzibar, hivyo akawahimiza wabunge kutumia semina hiyo kama jukwaa la majadiliano yawazi na kitaalamu kwa lengo la kuboresha mfumo wa mfuko huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema semina hiyo ni hatua muhimu katika kuimarishauelewa wa wabunge kuhusu utekelezaji na usimamizi wa Mfuko wa Jimbo.

Amesema maboresho yanayopendekezwa yanalenga kuhakikisha sheria na miongozo ya mfukoinaendana na hali halisi ya utekelezaji na kuongeza uwazi pamoja na ufanisi katika matumizi yafedha za umma.

Semina hiyo imewakutanisha wabunge kutoka majimbo 50 ya Zanzibar pamoja na viongozi nawatendaji kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, kwa lengo la kujadili kwa kina namna bora ya kuboresha utekelezaji wa Mfuko wa Kuchochea Maendeleo yaJimbo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauniakizungumza wakati wa Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla.
Baadhi ya Wabunge wakiwa kwenye Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. HemedSuleiman Abdulla.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni(katikati) akimkabidhi zawadi Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla mara baada ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026. Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Kundi la Vijana Kanda ya Pemba Mhe Zainab Abdallah.
Mbunge wa Kundi la Vijana Kanda ya Pemba Mhe Zainab Abdallah (wa kwanza kushoto) akimkabidhi zawadi Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla (kulia) mara baada ya kufungua Semina kwa Wabunge wa Jamhuri ya Muungano waTanzania kutoka Zanzibar kuhusu Mfuko wa Jimbo, iliyofanyika Zanzibar, Februari 26, 2026. Wa katikati ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Serikali imesema inatilia mkazo katika ulinzi na usalama wa kidijital ili kulinda miundombinu dhidi ya vitisho vya kimtandao ambavyo vinaweza kutumiwa na wahalifu wa ndani na nje ya nchi na kuhatarisha usalama wa wananchi na mali zao.

Akizungumza jijini Dodoma leo Februari 26, 2026 Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Angella Jasmine Mbelwa Kairuki wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kati ya wizara na sekta binafsi zilizoko chini ya wizara hiyo wakiwemo TCRA na TTCL,

Waziri Kairuki amesema serikali imeamua kuweka mazingira ya kisera, kisheria na miongozo mbalimbali katika ulinzi na usalama wa Huduma za mtandao kwa kuweka sera nzuri ya uwekezaji, akitolea mfano TCRA na TTCL, na kuwa Wajenzi wa minara ya mashirika hiyo ni wakandalasi wa hapa nchini na kuongeza kuwa mamlaka ya mawasiliano Tanzania na taarifa zao zinasaidia kuvutia uwekezaji utakao kuwa wa tija kwa Taifa.

Mheshimiwa Kairuki ameyaasa mashirika yaliyoko chini ya wizara hiyo kukamilisha na kutekeleza mipango kabambe kwa mifumo ya Tehama kwa awamu na hasa sehemu zenye pengo kubwa, kuendeleza kukuza uwekezaji wa sekta binafsi kwa kutoa motisha kuweka sheria nzuri na kuwepo na uwazi wa upatikanaji wa ardhi na leseni,kuimarisha usalama wa kidigiti kupitia sera mafunzo na uwekezaji katika vituo vya ulinzi wa kimtandao na upatikanaji wa watoa huduma kwa makundi dhaifu ili kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika uchumi wa kidijitali.

Kwa upande wake Mchumi mkuu wa Tume ya Taifa Mipango Bwana Jordan Matonya masema kuwa Dira inatoa mwongozo mzuri Kitaifa kwa kupanga na kutekeleza na kuleta muundo na maudhui ya Dira ya 2050 na kuwa na uchumi imara, na kuwa na mpango wa miaka mitano mitano huanzia mwaka huu Julai 2026.

Utakaorahisisha upatikanaji wa taarifa wa maeneo muhimu ya kiuwekezaji.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa,akizungumza na waandishi wa habari katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar  Es Salaam leo Februari 26, 2026.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
SERIKALI imesema kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya usafiri wa anga na reli umeongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa ubebaji wa mizigo nchini, huku kila sekta ikiwa na nafasi na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, wakati akifafanua mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati chini ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Februari 26, 2026 kuhusu usafiri wa anga, Msigwa amesema kuwa uwekezaji uliofanywa kupitia Kampuni ya Ndege Tanzania, Air Tanzania Company Limited, umeongeza kwa kasi uwezo wa kubeba mizigo ya kimataifa na kikanda.

Ameeleza kuwa ununuzi wa ndege ya mizigo aina ya Boeing 767-300F pamoja na upanuzi wa safari za kimataifa umewezesha kuongezeka kwa mizigo kutoka tani 2,567 mwaka 2021/22 hadi tani 6,919 mwaka 2024/25.

“Ongezeko hili limechangiwa na upanuzi wa safari za kimataifa, hali iliyorahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo, mifugo, mbogamboga na matunda kwenda masoko ya nje kwa haraka zaidi,” amesema Msigwa, akibainisha kuwa usafiri wa anga una faida ya kasi na unafuu kwa mizigo inayohitaji kuwahi sokoni au inayoharibika haraka.
Kwa upande wa reli, Msigwa amesema kuwa uwekezaji kupitia Shirika la Reli Tanzania umeongeza uwezo mkubwa wa kubeba mizigo kwa wingi na kwa gharama nafuu zaidi. Tangu kuanza kwa huduma za Reli ya Kisasa (SGR), zaidi ya tani 52,305 za mizigo zimesafirishwa hadi Desemba 2025, huku maboresho ya reli ya zamani (MGR) yakiongeza uwezo wa kubeba mizigo mizito kwa kuongeza kiwango cha ekseli kutoka tani 13.5 hadi 18.5.
Amefafanua kuwa tofauti na ATCL inayolenga zaidi mizigo ya thamani kubwa au inayohitaji kufikishwa kwa haraka, reli inalenga mizigo mikubwa na mizito kama saruji, makaa ya mawe, nafaka na bidhaa za viwandani, hususan katika safari za ndani na nchi jirani.

Hata hivyo, Msigwa amesisitiza kuwa sekta hizo mbili zinakamilishana badala ya kushindana.

“ATCL na TRC zinafanya kazi kwa mfumo unaosaidiana. Ndege zinasaidia kufungua masoko ya mbali kwa haraka, wakati reli inahakikisha mizigo inasafirishwa kwa wingi kutoka uzalishaji hadi bandarini au nchi jirani kwa gharama nafuu,” amesema.

Kwa mujibu wa Serikali, wakati ATCL imeongeza mapato ya fedha za kigeni kupitia safari za kimataifa, TRC imeimarisha mnyororo wa thamani wa ndani kwa kuunganisha maeneo ya uzalishaji na bandari, hatua inayochochea biashara ya kikanda na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania.

Kwa ujumla, Msigwa amesema mafanikio hayo yanaakisi mkakati wa Serikali wa kujenga mfumo jumuishi wa usafiri unaounganisha anga, reli na bandari, kwa lengo la kuongeza ufanisi wa ubebaji wa mizigo, kupunguza gharama za usafirishaji na kukuza uchumi wa taifa.



Na Khadija Kalili, Mlandizi
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Abuu Jumaa leo tarehe 25 Februari 2026 amekutana na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi katika mkutano maalumu wa kutoa shukran zake za dhati kwao kwa kumchagua kuwaongoza Jimboni humo.

Mhe.Mbunge Hamoud amesema hayo leo tarehe 25 kwenye mkutano uliofanyika Malandizi Stendi, Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani ambao umehudhuriwa na viongozi kutoka kata sita za Mlandizi Mjini.

"Baada ya miezi mitatu kupita ya uchaguzi leo nimekuja hapa ili niwashkuru kwa kusimama nami kwenyw uchaguzi na kunichagua kuwa mwakilishi wenu kwa mara nyingine tena nasema mimi siyo mjanja sana bali ni Mwenyeezi Mungu Mungu amepanga iwe hivi" amesema Jumaa.

"Nawashukuru sana kwa kunichagua kuwa Mbunge wenu, Wabunge wawili wa Viti Maalumu Asha Baraka na Hawa Mchafu pamoja na Madiwani 14wa kuchaguliwa na wa Viti Maalumu watano haya ni mafanikio makubwa kwa sababu nikiangalia safu yote ni majembe huvyo tupeane muda" amesisitiza Mhe.Jumaa.

Amesema kuwa anawashukuru pia kwa kumchagua Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan pia amewaomba wana CCM kumpa ushirikiano Mhe.Rais Dkt Samia hasa katika kipindi hiki ambacho anakwenda kumalizia ngwe yake ili aweze kutekeleza mambo mengi makubwa katika nchi yetu" amesema Mhe. Jumaa.

"Tunatakiwa wote kwa pamoja tumsaidie Mhe.Rais Dkt. Samia ili tuweze kuifikia Tanzania yenye mafanikio na kicheko kwa wote" amesema Mhe.Mbunge Jumaa.

Aidha Mh.Jumaa ameanza kwa kukutana na Kata sita ambazo ni Mlandizi ,Mtambani,Kawawa,
Mtongani,Janga na Kilangalanga.

Wakati huohuo ametoa ahadi lukuki ikiwa ni pamoja na kujenga maduka makubwa na ya kisasa Shopping Mall,Machinjio, Shule mpya kata ya Janga, atajenga Zahanati Kata ya Kawawa.

Mhe.Jumaa ameongeza kwa kusema kuwa wamekusudia kujenga jengo la Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akisisitiza kwa kusema kuwa Mungu akimjaalia atajenga kwa fedha zake mwenyewe.

"Baadaye tutapita katika ofisi zote za Kata kuangalia changamoto walizo nazo na tutazitatua.

Akizungumza kuhusu uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 2027 amewasisitiza Viongozi wote ambao wanajiona hawana uwezo wa kuongoza wajiengue mapema na kuatafuta warithi wao ikiwa pamoja na kuwaandaa vijana wenye wito ambao wana uwezona watakaowavusha katika uchaguzi huo ujao.
Katika kikao hicho cha Halmashauri Kuu Cha Sita cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kibaha Vijijini kimeongizwa na Mwenyekiti wake Mkali Kanusu ambaye amesisitiza kuwa mwakani atagombea tena katika nafasi hiyo.

"CCM ni Chama kizurikinatulea kinatuheshimisha pia runadhaminika hivyo tunendelee kukijenga kwa makundi kwa maslahi ya Chama chetu hivyo wote kwa sasa tukubaliane kufanya kazi na kushirikiana kwa pamoja.

Mimi ndiyo mwakilishi wa Mhe.Rais Dkt Samia hivyo hata kama hunipendi hunitaki wewe njoo tuzungumze kwa maslahi ya Chama chetu ili wote kwa pamoja tulete maendeleo.

"Nimedhamiria kupambana kupandisha Mamlaka ya Mji ,na jambo linakwenda vizuri katika ngazi za juu ikiwamo Wilaya na Mkoa.
Endapo tutapandishwa hadhi tutapata faida ya Mji kupangika kisasa ,kupata ongezeko katika ruzuku barabara zitajengwa katika kiwango cha lami ,pia ikumbukwe kuwa 2025-26 tumeongoza kwa nchi nzima kwa kukusanya mapato hili ni jambo la kujivunia ,tutamaliza ujenzi wa soko ,stendi ya mabasi tutajenga hoteli kubwa na ya kisasa maegesho ya magari.

Aidha Mhe.Jumaa amezitaja baadhi ya barabara ambazo ziko katika mpango wa kujengwa katika kiwango cha lami ni Chalinze Gwata, Utete, Rufiji na Makofia Mlandizi Mzenga.

Mbunge wa Jimbo la Kisarawe mkoani Pwani, Selemani Jafo, ameonesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Nyani, Kata ya Mafizi, akieleza kuwa hatua iliyofikiwa inaleta matumaini mapya kwa wananchi.

Mradi huo unaotekelezwa na kampuni ya BROADWAYS ENGINEERING CO LTD una thamani ya shilingi milioni 402.8 na hadi sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji, jambo linaloashiria kuwa upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo si wa muda mrefu tena.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji, mradi unahusisha ujenzi wa mnara wa tanki la maji lenye urefu wa mita 12 na uwezo wa kuhifadhi lita 50,000, pamoja na ujenzi wa vituo vitano vya kuchotea maji na ulazaji wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilometa 16.167.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Dkt. Jafo alimpongeza mkandarasi kwa kufanya kazi kwa kasi na weledi mkubwa, akibainisha kuwa kampuni hiyo imeendelea na kazi hata kabla ya kupokea malipo yoyote, jambo alilolitaja kuwa ni uzalendo na kujitolea kwa maendeleo ya wananchi.

Kutokana na kasi hiyo, Jafo ameiiomba Wizara ya Maji kulipa kiasi cha shilingi milioni 279.1 kwa kazi zilizokamilika ili kumwezesha mkandarasi huyo kuendelea na hatua zilizobaki na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Mbali na mkandarasi, mbunge huyo pia amempongeza Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kisarawe, Mhandisi Evangelista Kahwili, kwa usimamizi makini wa miradi ya maji ndani ya jimbo hilo, akisema nidhamu na ufuatiliaji wa karibu umechangia mafanikio yanayoonekana.

Wananchi wa Nyani na maeneo ya jirani wanatarajia kunufaika na mradi huo mara utakapokamilika, huku wakieleza kuwa utapunguza adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji na kuboresha afya pamoja na shughuli za kiuchumi katika eneo hilo.



▪️Ataka hatua za kinidhamu zichukuliwe licha ya fedha hizo kurejeshwa.

▪️Asisitiza hakuna kufanya ustaarabu kwa wezi wa mali za umma.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amemtaka Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Bahati Haule, kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa ya kila mmoja aliyehusika kuchukua fedha za mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa pamoja na kurejeshwa kwa fedha hizo, ni lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wote waliohusika na mpango huo ili kuimarisha uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma..

Amesema hayo leo Alhamisi (Februari 26, 2026) baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto. Ofisi hiyo itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.85 hadi kukamilika kwake, na ujenzi wake umefikia asilimia 85.

“Kamanda wa TAKUKURU, ninataka uniletee taarifa hii kabla sijamaliza ziara yangu katika Mkoa wa Manyara. Ninahitaji taarifa za mtu mmoja mmoja kwa wote waliohusika kuchukua fedha hizo. Hatukutumwa kuja kuchukua fedha za umma, hatua za kinidhamu lazima zichukuliwe,” amesisitiza.

Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa mbali na taarifa hiyo, anataka pia kuwasilishwa taarifa za mapato ya ndani, ikiwemo mapato yatokanayo na minada, zikionyesha namna yanavyokusanywa na kutumika. “Hakuna kuvumilia ubadhirifu wa mali ya umma. Tunataka kila mtu aheshimu fedha za utekelezaji wa miradi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana dhamira ya dhati ya kutatua changamoto za Watanzania, akisisitiza kuwa lengo lake ni kuona maendeleo endelevu yanapatikana nchini.






IKIWA taarifa na elimu ni nyenzo muhimu ya kukabiliana na changamoto za afya ripoti inaeleza waandishi wa habari za afya wanakumbwa na hali inayofanya wasitekeleze wajibu wao unaosaidia ustawi sekta hiyo barani Afrika.

Hayo yameelezwa kwenye ripoti ya mwelekeo wa Vyombo vya Habari vya Afya Afrika 2026, iliyozinduliwa Leo Februari 26, Feb na FINN Partners.

Pia ripoti hiyo inaangazia mwelekeo mpya unaokua wa uandishi wa habari unaozingatia suluhisho na unaoongozwa na Waafrika, ambao unaweza kubadilisha namna masuala ya afya yanavyoripotiwa barani humo.

Ripoti hiyo inatokana na maoni ya waandishi wa habari, wahariri na watetezi kutoka nchi 11 za Afrika, na inatoa taswira halisi ya jinsi habari za afya zinavyoripotiwa pamoja na mahitaji muhimu ya kuimarisha mchango wa vyombo vya habari katika kuboresha matokeo ya afya ya umma.

Waandishi wa habari za afya kwa sasa wanakabiliana na changamoto kadhaa, ikiwemo kupungua kwa ufadhili wa wafadhili, kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza kama saratani, kisukari na matatizo ya afya ya akili, milipuko ya mara kwa mara ya magonjwa ya kuambukiza, pamoja na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa afya. Wakati huo huo, vyumba vya habari vinafanya kazi kwa rasilimali chache, kupungua kwa madawati maalum ya afya, na upatikanaji mdogo wa takwimu sahihi na za wakati.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo Peter FINN, Mwanzilishi Mshirika na Mtendaji Mkuu wa FINN Partners amesema kuwa uandishi wa habari za afya ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha hali ya afya za Waafrika.

“Tuko katika wakati muhimu sana kwa mawasiliano ya afya barani Afrika. Uandishi wa habari unapokosa rasilimali za kutosha, afya ya umma huathirika. Mifumo imara ya afya inahitaji mifumo imara ya vyombo vya habari, na hiyo inamaanisha kuwachukulia waandishi wa habari kama washirika muhimu, si wasambazaji wa taarifa tu.”

Ripoti hiyo pia inaonesha kuwa mabadiliko katika ufadhili wa afya duniani yamekuwa mada kuu katika vyombo vya habari, yakizisukuma nchi kufikiria upya uhuru wa sekta ya afya, ufadhili wa ndani na uzalishaji wa ndani. Wakati huo huo, waandishi wa habari wanajitahidi kutafsiri mabadiliko hayo ya sera na kuyaonesha kwa namna yanavyoathiri maisha halisi ya wananchi.

“Namna masuala ya afya yanavyoripotiwa huathiri imani ya umma, vipaumbele vya sera na hatimaye uimara wa mifumo ya afya,” alisema Maryam Bigdeli, Mtaalamu wa Mifumo ya Afya na aliyewahi kuwa Mwakilishi wa World Health Organization nchini Morocco.

Maryam aliongeza kuwa “Katika kipindi hiki cha mabadiliko ya vipaumbele vya afya duniani na vikwazo vya ufadhili, nchi za Afrika zinapaswa kujikita katika kujenga mifumo imara inayotegemea huduma bora za afya ya msingi, ufadhili endelevu na utawala unaowajibika. Ripoti hii inaonesha umuhimu wa suluhisho za ndani na mjadala unaotegemea ushahidi ili kuhakikisha usawa na uimara wa mifumo ya afya kwa muda mrefu.”

Licha ya changamoto hizo, ripoti imebaini mwelekeo chanya ambapo waandishi wa habari wanazidi kuzingatia uandishi unaotumia takwimu na unaolenga suluhisho, huku ukitoa nafasi kubwa kwa wataalamu na muktadha wa Kiafrika. Waandishi wa habari wanatoa wito kwa wataalamu, watafiti na watendaji wa Kiafrika kunukuliwa zaidi kama vyanzo vikuu vya taarifa, na hivyo kubadilisha taswira ya Afrika kutoka kuwa mhanga wa matatizo hadi kuwa sehemu ya suluhisho.

“Matokeo ya ripoti hii yanaakisi hali halisi tuliyonayo,” alisema Sheriff Bojang, mwandishi wa The Africa Report. “Waandishi wa habari wana hamu kubwa ya kusimulia hadithi zenye athari, lakini wanakabiliwa na ukosefu wa rasilimali na upatikanaji mdogo wa wataalamu wa ndani wanaoaminika. Sasa tunahama kutoka kunukuu tafiti za Magharibi pekee na kuelekea katika kuwasilisha habari za afya kwa muktadha wa ndani. Ripoti hii inatoa mwongozo muhimu kwa mashirika ya afya kusaidia vyombo vya habari ili kuhakikisha taarifa sahihi zinawafikia wananchi.”

Ripoti hiyo inahitimisha kwa kutoa wito kwa serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, wafadhili na sekta binafsi kuwekeza katika uandishi wa habari wa ndani, kuboresha upatikanaji wa takwimu na wataalamu wa Kiafrika, pamoja na kujenga ushirikiano wa muda mrefu unaojengwa juu ya uaminifu ili kuimarisha afya ya umma barani Afrika.



Top News