Na Asia Singano na Josephine Majura, WF, Mwanza.
SERIKALI imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia sera na mipango mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), katika Mahafali ya 20 ya Shule ya Sekondari ya Thaqaafa, wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.

Alieleza kuwa, Serikari inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kupitia Sera na mipango mbalimbali ya kiuchumi na kijamii ili kuhakikisha kuwa vijana wanapata fursa za kuendeleza vipaji vyao na kuchangia kikamilifu maendeleo ya taifa.

‘’Dunia ya sasa inahitaji vijana wanaoweza kutatua changamoto kwa ubunifu, hasa katika nyanja za uchumi, teknolojia na ujasiriamali ‘’ Alisema Mhe. Munde (Mb).

Amewaasa vijana kuendelea kuwa na nidhamu na uadilifu kwakuwa Taifa linahitaji vijana wenye misingi imara ya maadili, wanaoweza kusimamia rasilimali za nchi kwa uwajibikaji na weledi.

Kwa upande wake Meneja wa Shule ya Thaqaafa, Bw. Idrisa Hayeshi, amewasisitiza wazazi kuendelea kushirikiana na walimu na Uongozi wa shule kufuatilia maendeleo ya wanafunzi ili kujua mwenendo wa tabia ambazo zina athari katika masomo yao.

“Shule imejipanga kutoa elimu bora ikiwa na matokeo mazuri kwa kila mwaka, tunavyofanya mawasiliano na mzazi ni kwamba atoe ushirikiano ili mtoto apate kitu kinachostahili’’ alisema Bw. Hayeshi.

Shule ya Sekondari Thaqaafa imeadhimisha Mahafali ya 20 ya Kidato cha Sita ambayo yalihudhuriwa na wahitimu (50).
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akipokea picha yake iliyochorwa wakati wa uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo uliofanyikakatika katika ukumbi wa Nkurumah.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akipokea tuzo kutoka kwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Joyce Juliasi Semkuyu, katika ukumbi wa Nkrumah. Tuzo hii ni ishara ya kutambua mchango wake katika jamii na juhudi zake za kuhamasisha maendeleo, hususan kwa wanawake.

Na Mwandishi Wetu WMJWM- Dar Es Salaam
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka watoto wa kike kujipambanua katika kuhakikisha wanatumia muda wao kufanya mambo yatakayowasaidia katika ustawi wa maisha yao.

Waziri Dkt. Gwajima ameyasema hayo tarehe 18 Aprili, 2026 wakati akizindua Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo.

Waziri Gwajima amesema jina la Binti Jasiri lina maana kubwa sana likiwakilisha ujasiri wa kusimama, kuota ndoto kubwa na kushinda changamoto hivyo katika ulimwengu wa leo, kunahitajika kuwa na mabinti ambao hawataogopa kushika nafasi za uongozi, kuanzisha biashara, wala kuchangia katika maamuzi makubwa ya kijamii na kiuchumi.

Ameeleza kuwa mpango huo umejengwa katika msingi imara unaoendana na dira ya maendeleo ya taifa yaani Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025, pamoja na malengo ya kimataifa ya maendeleo endelevu, hasa Elimu Bora (SDG 4) na Usawa wa Kijinsia (SDG 5).

“Binti Jasiri si tukio la siku moja bali ni mwanzo wa harakati endelevu na ni mwanzo wa kizazi kipya cha wanawake; Wenye maono, ujasiri na uwezo wa kubadilisha dunia.” Ameafafnua Waziri Dkt Gwajima.

Aidha amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana, bado mabinti wengi wanakutana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mentorship, fursa za uongozi na rasilimali za kujiendeleza hivyo kupitia Binti Jasiri, inaunda mazingira yatakayowawezesha mabinti kujifunza uongozi, kuunganishwa na wale waliowatangulia na kujenga ujasiri wa kujitegemea na hatimaye kuwa suluhisho la changamoto za jamii.

“Nitoe wito kwa Mabinti wangu wapendwa, nataka muondoke hapa leo mkiwa na jambo moja moyoni ambalo ni uwezo, thamani kwani unaweza kufika mbali zaidi ya unavyodhani pia usiruhusu hofu, maneno ya watu au mazingira yakuzuie kwani Dunia inahitaji sauti yako, mchango wako na uongozi wako basi chukua nafasi Jitokeze na Jiamini.” Amesisitiza Waziri Gwajima

Pia amewataka wadau wote wanaotokea serikalini, sekta binafsi, taasisi na washirika kusisitiza kuwa kuwekeza kwa mwanamke kwani ni uwekezaji kwa taifa na kumuinua msichana mmoja ni kuinua familia, jamii na uchumi mzima hivyo amewahimiza kuendelea kuunga mkono mipango kama hiyo kutoa mentorship na kufungua milango ya fursa kwa vijana wa kike.

Kwa upande wake Makamu wa rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Joyce Juliasi Senkuli amesema Jukwaa hilo limeanzishwa kwa lengo la kumkomboa binti kifikra, kihisia, kielimu na kiuchumi, kwa kutambua kuwa bado wapo mabinti wengi wanaopitia changamoto mbalimbali katika safari ya maisha na elimu.

Naye Mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Paulina Mabuga ameahidi kuwaunga mkono Mabinti hao ili waweze kufikia malengo yao katika kampeni walioianzisha ya kuwafanya Watoto wa kike kuinuka katika masuala mbalimbali katika jamii.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akizungumza katika uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah. .
Baadhi ya Washiriki katika uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM ulkofanywa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima katika ukumbi wa Nkurumah.

Na Khadija Kalili, Bagamoyo
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ambao umepokelewa asubuhi tarehe 18 Aprili 2026 kutoka Jijini Dar es Salaam utakagua miradi 68 ambapo kati ya miradi hiyo miradi 23 itawekwa mawe ya msingi, miradi 21 itazinduliwa na miradi 24 itakaguliwa.

RC Kunenge amesema kuwa miradi yote inathamani ya jumla ya Shilingi za Kitanzania Tsh.Bilioni 263,061,799, 595.55.

"Miradi yote hii imefanikiwa kutokana na ushirikiano mzuri uliopo baina ya viongozi wa serikali, wananchi na wadau wa maendeleo" amesema Kunenge.

Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha itaupokea mwenge huo tarehe 20 Aprili 2026 katika shule ya Msingi Gumba kata ya Gwata na kukimbizwa katika Miradi ya Maendeleo na kuhitimishwa kwa mkesha Mkubwa kiwanja cha Shule ya Msingi Mtongani.

Ujumbe mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 , unalenga katika ujenzi wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa chini ya kaulimbiu isemayo 'Tanzania yetu sote , tushikamane kwa kuleta pamoja maendeleo ' kauli mbiu hii inalenga kujenga na kuimarisha umoja wa Kitaifa na kuutumikia Mwenge wa Uhuru kuwaenzi na kuwatia moyo wazalendo wa kweli na makundi mbalimbali yenye mchango mkubwa katika kulinda amani, umoja na mshikamano kitaifa katika kujenga Tanzania imara kimaadili,kidiplomasia na kiuchumi ndani na nje ya mipaka yetu ikiwa ni pamoja na na kurejesha falsafa hii ya Mwenge wa Uhuru kwa wananchi wa Tanzania.

Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Wilaya saba na Halmashauri tisa kwa umbali wa Kilomita 1,065.9

The confrontation of the United States and Israel with Iran has moved from covert operations to open war, igniting a conflict that defies containment. What began as calculated strikes has become a multi-domain struggle involving air, sea, cyber, and proxy arenas, shifting power dynamics, exposing vulnerabilities, and pulling the world toward an uncertain edge where escalation moves faster than control and outcomes grow more unpredictable by the hour.


1. Introduction.

Wars begin when you will but they do not end when you please, Niccolò Machiavelli wisely noted, a thought that carries chilling clarity over the events of February 28, 2026, when the United States and Israel launched coordinated strikes against Iran, which opened open war and collapsed the fragile illusion that diplomacy was still holding. Only days earlier, indirect nuclear negotiations held in Geneva had ended without reaching any agreement, yet both sides still held a cautious belief that continued discussions might reduce tensions and narrow the gap between their demands and concerns, even though deep mistrust remained unchanged.

In that fragile atmosphere, the brief expectation of further diplomatic engagement quickly dissolved as the situation shifted from stalled talks into full military confrontation. Under the operation names “Operation Roar of the Lion” and “Operation Epic Fury,” coordinated strikes hit Tehran and other strategic locations, targeting nuclear facilities, ballistic missile infrastructure, and key political and military command structures.

Behind this sudden escalation, the foundations of the war stretch deep into history, tracing back to the turning point of 1979 and decades of hostility built on sanctions, proxy confrontations, and the unresolved nuclear question. Agreements collapsed, trust eroded, and by 2025, diplomacy had become little more than ritual performed but no longer believed.

From this long buildup, the months leading to February 2026 saw rising sanctions pressure, military buildups across the Gulf, and a persistent movement toward inevitability. What emerged was not a sudden conflict but a planned break and what can be understood as a preemptive decapitation strategy, aimed not simply at deterrence but at destabilizing Iran’s governing structure and strategic stability.

1.1. The Inferno.

With the conflict now fully ignited, the immediate consequences were as devastating as they were decisive. Within hours, Iranian state media confirmed the deaths of Supreme Leader Ali Khamenei, Defense Minister Aziz Nasirzadeh, and Chief of Staff Abdolrahim Mousavi, a blow that effectively removed Iran’s military leadership in a single stroke. Civilian casualties mounted alongside these high profile killings, which made clear the brutal reality that even the most advanced “precision” warfare cannot contain its human cost.

As the scale of destruction became clear, what had been conceived as a rapid, overwhelming strike to neutralize threats instead ignited a wider inferno. Iran responded with fury, launching hundreds of ballistic missiles and over a thousand drones, extending the theater of war across Israel and deep into the Gulf, including Bahrain, Qatar, Kuwait, the United Arab Emirates, and Saudi Arabia, turning a targeted operation into a regional conflagration within 24 hours.

Beyond this immediate exchange of force, a deeper and more unsettling reality emerges that this is not a single war but multiple wars taking place at the same time, each governed by its own tempo and logic. The air war moves at supersonic speed, measured in minutes as jets and missiles cross borders. The naval war progresses slowly but with severe consequences, as Iran moves to close the Strait of Hormuz, threatening a fifth of global oil supply.

Within this battlefield, the cyber war operates in silence while retaliatory strikes target American and Israeli systems. At the same time, the proxy war spreads outward, as Hezbollah, Iraqi militias, and Yemeni Houthis have entered the conflict, bringing new fronts into play. Together, these layers form a multi layered structure of violence in which each strike generates another strike, and no decisive victory appears possible.

1.2. No Control Point.

In the days and weeks that followed, the human, infrastructure, and economic toll of the war revealed its most haunting dimensions. Beyond the elimination of Iran’s leadership, civilian suffering surged into global consciousness, with pain and loss felt deeply on both sides of the conflict as families faced destruction, displacement, and grief.

The conflict escalated according to a relentless logic of escalation. Iranian retaliation struck United States military installations and allied facilities across Gulf states, while Israel intensified its campaign by targeting critical infrastructure such as the South Pars gas field, sending shockwaves through global energy markets and pushing oil prices higher. Escalation has become a paradoxical strategy propelled not by control but by the inability to avoid it, as each move intended to contain the conflict instead stretched it into a cycle with no clear endpoint. Machiavelli’s warning still stands not as philosophy but as lived reality.

Now, the question that haunts every capital including Washington, Tel Aviv, and Tehran is not how the war began but how it ends. A fragile ceasefire brokered in early April 2026 offers only a temporary pause in a conflict that continues to move beneath the surface. Intelligence assessments suggest Iran still retains the capacity to strike back in meaningful ways, even after sustained pressure, while external actors, including global powers, edge closer to involvement.

2. War in Motion.

This conflict rests on the operational coordination between the United States and Israel, who have adopted a doctrine built on dominant air superiority, where the sky itself becomes both shield and sword. Their strategy relies on precision strikes designed to dismantle Iran’s military architecture by targeting command centers, leadership networks, and communication systems in order to fracture coordination and impose strategic paralysis. Rather than engaging in prolonged territorial warfare, the objective is to control tempo from above, forcing Iran into reactive patterns of defense in several directions.

Alongside this aerial dominance, the United States and Israel extend pressure through maritime and regional strategic influence, where critical sea routes and energy corridors become extensions of the battlefield. In this structure, naval power is used to secure, monitor, and in some cases restrict movement through key chokepoints, especially the Strait of Hormuz. The security and stability of global shipping lanes in this region are therefore directly tied to operational outcomes on land, in the air, and at sea, transforming economic infrastructure into a strategic instrument of pressure. As a result, military operations and economic power function together as a single integrated system of influence, where control over movement and supply becomes as decisive as control over territory or airspace.

In contrast, Iran’s response relies on dispersion rather than concentration, following a doctrine of asymmetry and unpredictability. The war plays out as an interconnected system of pressure points across land, air, sea, cyber, and proxy fronts. Instead of matching conventional airpower, Iran stretches the battlefield through swarms of drones, ballistic and cruise missile strikes, and coordinated activity with allied non-state actors such as Hezbollah and other regional partners. This produces a wide and fragmented theater of war stretching from Lebanon to the Gulf, including maritime corridors and covert operational spaces. Proxy warfare becomes a main instrument, allowing Iran to extend its reach far beyond its borders while complicating containment and escalation control.

Technology intensifies this confrontation on all sides. Drone systems are used to saturate defenses through volume and unpredictability, while advanced missile interception networks operate under continuous pressure. At the same time, cyber operations introduce an invisible layer of warfare, targeting intelligence systems, communications infrastructure, and critical services. The result is a battlespace where physical destruction and digital disruption merge, compressing response time and increasing the complexity of every operational decision.

3. Fire and Whisper.

The path to the first wave of strikes was set in motion not by a sudden collapse of diplomatic reason, but by the slow, agonizing death of the Joint Comprehensive Plan of Action (JCPOA) nuclear agreement, now reduced to a ghost of its original form. For years, the JCPOA revival talks in Vienna had become a graveyard of good intentions, where every technical negotiation crumbled under the weight of maximalist demands.

From this prolonged stagnation, the failure of diplomacy became impossible to ignore. As detailed in the pre-war diplomacy failure, the collapse of these nuclear negotiations did not happen overnight but instead unfolded as a predictable funeral, with the United States insisting on dismantlement far beyond the original accord while Iran cloaked its positions in sovereign inviolability. The ghost of the deal haunted every empty chair at the table, and by the time the first bunker-buster hit its target, diplomacy had already been declared a casualty, even if no one had yet signed the death certificate.

Out of that diplomatic collapse, war did not replace negotiation entirely but rather forced it into a different form. Yet even as the bombs fell, diplomacy refused to die because it simply mutated into a desperate, parallel existence alongside the warfare. The Islamabad Talks became the clearest symbol of the deadlock, with conflicting demands hardening into absolute positions, as the United States and Israel demanded full nuclear dismantlement while Iran refused to surrender what it called an inalienable right to enrichment.

As those rigid positions intensified, even attempts to pause the violence proved fragile and temporary. At the same time, Europe began distancing itself from the military escalation because it feared a regional inferno, while Russia and China used their UN Security Council vetoes to shield Tehran, turning the Axis of Resistance diplomacy into a geopolitical shield. The underlying argument of this war is simple because it happened as deterrence failed, not because diplomacy was untried. From this point, a more unsettling truth about the nature of diplomacy in modern conflict begins to emerge. The main insight remains unsettling because diplomacy has not disappeared, but it is no longer aiming for peace and instead is only managing the catastrophe.

3.1. Voices Against the War.

Opposition to the war has emerged across multiple layers of the international system, combining political resistance, public protest, and moral condemnation. Several governments and international actors have either openly criticized or quietly distanced themselves from the escalation, warning that the conflict risks widening into a regional catastrophe with global consequences. Beyond state actors, widespread protests have taken place across different countries, reflecting a growing perception that the war is not only strategically dangerous but also legally and morally contested.

Within this growing opposition, the most visible and morally forceful resistance has come from Pope Leo XIV, who has consistently denounced the war as unjust and dangerous. He has warned that the world is being pushed by leaders who misuse power and even religion to justify violence, while insisting that “God does not bless any conflict” and calling the war a form of madness. His position has not been isolated, as other religious figures including the Archbishop of Canterbury have supported his call for peace, bringing attention to the human cost and the moral failure of continued escalation.

At the same time, the conflict has revealed a growing concern over the use of moral and religious language in political and military decisions to legitimize war, raising questions over how far such narratives influence public understanding of the war. Pope Leo XIV has warned that the world is “being ravaged by a handful of tyrants” who prioritize destruction over human welfare. He condemned those who manipulate “the very name of God” for military, economic, and political gain, arguing that this distorts both faith and responsibility. The danger in this confrontation is not only diplomatic but conceptual, because once war is framed in religious terms, it becomes harder to limit, harder to negotiate, and far more likely to escalate beyond political control.

4. Fractured World.

What began as a calibrated show of force has turned into a conflict that refuses containment, spilling across borders with a pace that outstrips diplomacy. The war’s geography now stretches from Israel and Lebanon across to the Gulf, with Hezbollah pulling Lebanon into sustained confrontation, while Gulf states, once peripheral, find themselves within the growing blast radius of retaliatory strikes and strategic intimidation. Missile trajectories and drone swarms no longer respect traditional frontlines, blurring the line between battle zones and areas once assumed to be secure as civilian infrastructure comes under repeated disruption.

Yet the deeper tremor is economic, felt far beyond the battlefield. The closure and contestation of the Strait of Hormuz, through which a fifth of the world’s oil flows, has turned energy markets into instruments of war, driving prices upward and injecting volatility into an already fragile global economy. The International Monetary Fund’s downgraded growth forecasts reflect this strain, pointing to a growing crisis in which inflation rises, supply chains tighten, and vulnerable economies, particularly energy importers, bear disproportionate pain.

If the battlefield exposes the mechanics of destruction, diplomacy reveals the fractures of the international system itself. The refusal of key NATO members such as the United Kingdom and France to fully support Washington’s escalation points to a clear strategic divide within the Western alliance. At the same time, a countervailing axis, operating in support of Iran through Russia’s intelligence assistance, China’s economic and technical links, and North Korea’s missile cooperation, has come together not as a formal bloc but as a shadow coalition working to reduce the United States’ influence. This is no longer a bipolar confrontation. It is a tri polar world in motion, where power is diffused, contested, and increasingly transactional.

5. Conclusion.

Now we know what a modern war looks like. It is a war that begins without clear authorization and proceeds without a consistent legal or moral framework. The strikes launched on 28 February 2026 by the United States and Israel against Iran did not receive approval from the United Nations Security Council, nor were they preceded by a direct Iranian attack on either state. In that sense, the conflict exposes a clear reality that the international system lacks the power to prevent or meaningfully constrain wars initiated by major powers. What emerges is not simply a failure of diplomacy, but a deeper erosion of the rules that once defined legitimacy in war, leaving smaller states and global stability increasingly vulnerable in a system where power acts first and justification follows later.

The war raises unresolved political and strategic questions that extend far beyond the battlefield. First, there is a lack of clear objectives and outcomes, with no visible endgame directing the course of the conflict. Second, rather than eliminating the threat of weapons of mass destruction, the conflict brings back the logic of deterrence in which Iran’s pursuit of nuclear capability gains renewed justification as the ultimate guarantee of security. Third, the political side of the war is becoming impossible to ignore. In the United States, the November 3, 2026 midterm elections stand as an important test of public opinion on foreign policy and military engagement, while in Israel the 27 October 2026 elections are increasingly tied to debates over leadership, security, and national direction. Whether the war ends before these electoral moments or instead influences them remains uncertain.

What this conflict has revealed most clearly is the limitation of military power in determining political reality. The United States and Israel have demonstrated their capacity to destroy targets and project power within this conflict, yet the war has also shown that destruction does not translate into control, nor does it guarantee favorable outcomes. Analysts increasingly point to the gap between tactical success and strategic ambiguity, where escalation produces no clear victory and no stable resolution. As scholars such as Stephen Walt have argued, the United States remains powerful, but its current policies risk weakening that power over time. In this environment, battlefield success is no longer enough to secure political outcomes, and the absence of a clear strategy continues to leave the conflict without a decisive direction.

In the end, the war appears to pause, but nothing truly ends. The Strait of Hormuz briefly reopened only to be closed again hours later. Oil prices fall, markets rise, and relief spreads across financial centers, yet these movements remain reactions, not resolutions. A ceasefire stretches across Iran and Lebanon, but it carries no clear victory, no decisive achievement, and no lasting settlement, only the quiet admission that force has reached its limits. The world has faced an energy shock on a scale not seen since the 1970s, and recovery will take years. What remains is a deeper uncertainty, because the conflict has not resolved the tensions that produced it, it has only exposed them. Power has proven capable of disruption, but not resolution, and stability, once broken, does not return with the same speed as markets. The war may pause, the strait may open and close, and the numbers may recover, but the future remains unsettled, and for now, no one truly knows what tomorrow will bring.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396


— The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.


Tume ya Madini kwa ushirikiano wa Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) pamoja na Taasisi ya kuendeleza Uchimbaji Mdogo (FADev) wameendelea kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo katika Mkoa wa Morogoro ikiwa ni Mkakati wa Serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo Mradi unaofadhiliwa na UNDP

Akizungumza na Wachimbaji wa madini ujenzi katika Mkoa wa Morogoro Afisa Program kutoka FADev Bi. Rehema Mkuli amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga wachimbaji wadogo wanaojihusisha na madini ya ujenzi na viwanda, hususani madini ya kokoto kwa lengo la kuboresha uelewa wao wa kitaalamu na kuhamasisha mbinu salama na zenye tija katika shughuli za uchimbaji.

Pia, Bi Rehema amesema wachimbaji hao wanajifunza juu ya mbinu za Msingi za Uchoraji wa Ramani za Kijiolojia (Basic Geological Mapping), Usanifu salama na bora wa mashimo (Safe and Efficient Pit Design)

Aidha, kwa upande wa wakufunzi kutoka ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro Mjiolojia Asifiwe Waksoni Ngala amewalezea wachimbaji juu ya Uchoraji wa ramani za kijiolojia, na kuwataka wachimbaji kujifunza zaidi juu ya utambuzi wa aina mbalimbali za miamba na kuelewa madini yanayopatikana ndani yake.

Ujuzi huo unasaidia kuongeza ufanisi katika utambuzi wa rasilimali, kupunguza uchimbaji wa kubahatisha, na kuongeza tija katika shughuli za uchimbaji.

Mafunzo haya yamelengwa kufanyika katika mikoa minne kati ya mikoa nane iliyofanyiwa utafiti wa Madini ya Maendeleo (Development Minerals). Mikoa hiyo ni Singida, Dodoma, Morogoro na Tanga.











Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) akipeana mkono wa shukrani na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (kushoto) wakipongezana na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.
Muonekano wa Trekta iliyotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.

Viongozi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale wakipeana vifaa kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri hiyo.

Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena akizungumza kwenye halfa hiyo ya makabidhiano ya trekta kwa halmashauri ya Nyang’wale

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (Katikati) na kulia kwake ni Senkondo Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena wakiwa kwenye utiaji wa saini katika halfa ya makabidhiano ya trekta kwa ajli ya kusomba taka na ufanyaji wa usafi kwenye halmashauri hiyo

Wafanyakazi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale wakiwa kwenye picha ya pamoja
*


Mgodi wa Barrick Bulyanhulu umeendelea kutekeleza sera yake ya mkakati endelevu wa kusaidia jamii baada ya kukabidhi trekta ya kusomba taka yenye thamani ya shilingi milioni 66 pamoja na vifaa vya kufanyia usafi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale kupitia fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) katika juhudi zake za kutunza mazingira nchini.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano ya trekta hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya Nyang'wale , Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, John Isack alisema msaada huo umekuja kwa wakati katika juhudi za kulinda na kutunza mazingira kwa maslahi ya wakazi wa wilaya hiyo na vitongoji vyake.

“Tunashukuru Barrick Bulyanhulu kwa msaada huu wa trekta , tunaamini sasa hali ya usafi katika Wilaya yetu itakuwa nzuri kwa kiasi kikubwa kwani hii ni trekta ya pili wametupatia, matarajio yetu ni kuongeza kasi ya kuondoa taka kutoka hapo awali ya kutoa mara mbili kwa wiki, awali tulikuwa tunazoa taka katika siku za Alhamisi na Jumatatu hivyo tutaongeza siku pia tunatarajia kuongeza huduma kwa maeneo ya miji inayokuwa kwa kasi kibiashara kama vile Bosolwa, Nyijundu, Bukwimba na maeneo ya migodini",alisema.

Isack aliongeza kuwa kampuni ya Barrick Bulyanhulu kupitia uwekezaji wake imefanikisha miradi mingi ya kijamii na utunzaji wa mazingira wilayani humo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi.

“Leo tumepokea Trekta ambalo limenunuliwa na kampuni ya Barrick Bulyanhulu kwa gharama ya Shilingi Milioni 66 , Trekta hili ni maalum kwa kazi ya kuzoa uchafu na kupeleka dampo kwa kweli ni msaada mkubwa kwa wilaya yetu kwani kwa miaka mingi sana tumekuwa na changamoto juu ya uzoaji wa taka katika mitaa yetu ukichukulia kwamba mji wetu unakua kwa kasi na kupelekea uzalishaji wa taka kuongezeka kwa kasi, na ni matarajio yangu sasa mazingira ya Wilaya yetu yatakuwa safi, nichukue fursa hii kuwaomba wananchi kufanya usafi kila siku kwani tayari kwa sasa tunalo trekta ambalo litakuwa linasomba taka mara kwa mara”, alisema.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo alitoa shukrani kwa viongozi wa serikali na wananchi kwa kuwa na uhusiano mzuri na Kampuni hiyo na kuongeza kuwa msaada wa trekta lililokabidhiwa ni kwa ajili ya kufanya usafi na utunzaji wa mazingira.

“Niwaombe ndugu zangu usafi ni jukumu letu sote,trekta hili tulitunze ili liweze kuboresha mazingira yetu ipasavyo ,milioni 66 ni pesa nyingi hivyo naamini tutakuwa tumefungua njia ya kuboresha mazingira ya usafi wilayani Nyang’hwale, haswa ikizingatia kampuni ya Barrick Bulyanhulu ni wadau wakubwa wa utunzaji wa mazingira”, alisisitiza Zuwena.






Mkaguzi wa Kata ya Milola, Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (A/INSP) Aloyce Andrew, kwa kushirikiana na wananchi wa kata hiyo, wamefanikiwa kumuua nyoka aliyekuwa akifugwa ambaye alisababisha taharuki kwa wakazi wa eneo la Mavimba, njia panda ya mnadani na wananchi wengine kushindwa kuendelea na shughuli zao kutokana na hofu.

Hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wananchi waliomuarifu mkaguzi huyo kuhusu uwepo wa mwananchi anayefuga nyoka, bila kufahamika anamtumia kwa madhumuni gani, jambo lililozua hofu kubwa miongoni mwao huku wengjne wakishindwa kuendelea na shughuli zao za kiuchumi.

Katika tukio hilo Mkaguzi huyo amewataka wananchi kuepuka kujihusisha na imani potofu ambazo mara nyingi zimekuwa chanzo cha kuvuruga amani na utulivu katika jamii huku akimtaka mwananchi huyo kuacha mara moja vitendo hivyo ambavyo vinaleta taharuki katika jamii.

Aidha, amesisitiza kuwa imani hizo potofu huchangia kudidimiza maendeleo, akitoa mfano wa tukio hilo ambapo ufugaji wa nyoka ulisababisha hofu kwa wananchi wanaojishughulisha na shughuli zao za kiuchumi.

Vilevile, amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa kuhusu vitendo vya uhalifu au viashiria vyake, ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa wakati.







KWENYE maisha ya sasa, si kila mtu anasubiri bahati imuangukie, kuna wale wanaojitengenezea nafasi zao wenyewe. Mtaa umejaa stori za watu waliogeuza dau dogo kuwa pesa ya maana, na sasa macho yote yako kwenye Big Bounty Challenge ya Meridianbet. Hapa ni kucheza kwa akili na kupanda ngazi hadi kileleni unapopatikana mkwanja wa maana.

Kila ukiweka dau lako, unaingia moja kwa moja kwenye vita ya nafasi ndani ya jedwali la uongozi la Games Global. Hii siyo mchezo wa kawaida, ni ligi ya wakali ambapo kila mmoja anapambana kuhakikisha jina lake linaonekana juu.

Vilevile, Michezo mingi zaidi ya kubashiri inaendelea kupatikana ndani ya Meridianbet ikiwa na ODDS kubwa na machaguo mengi zaidi. Kushiriki ni vyepesi kupitia tovuti ya MERIDIANBET au kwa kupiga *149*10#.

Usijali kama unaanza na kidogo, maana Meridianbet wamefanya mchezo uwe wazi kwa kila mtu. Kwa Tsh. 300 tu, tayari unakuwa sehemu ya mashindano ya kila wiki yenye zawadi nono ya Tsh. 30,000,000.

Mtaani hakuna anayependa kuangalia wengine wakila bata peke yao. Huu ndio muda wa kuchukua hatua na kujaribu bahati yako kwa juhudi zako mwenyewe. Kila dau linaweza kuwa mwanzo wa safari ya kubadilisha siku yako kuwa ya furaha, na labda hata maisha yako kabisa.

Meridianbet wameweka jukwaa, wamewasha taa, na wamefungua milango ya mamilioni. Sasa ni wewe kuamua kama utabaki pembeni au utaingia uwanjani kupambana. Big Bounty Challenge ni uhalisia unaosubiri uamue kuucheza. Cheza sasa na chukua chako.

LIGI Kuu ya Uingereza (EPL) inarudi na mechi ya kusisimua leo tarehe 19 kwenye uwanja wa Villa Park, ambapo Aston Villa itakuwa mwenyeji wa Sunderland kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza utakaopigwa saa 16:00 kwa muda wa Afrika Mashariki.

Aston Villa wanakwenda kwenye mchezo huu wakiwa na matumaini makubwa ya kuhakikisha nafasi yao ya kumaliza kwenye nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo, huku takwimu zao msimu huu wakishika nafasi ya 4 wakiwa na alama 55 nafasi inayowapa tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya endapo watamaliza msimu kwenye nafasi hiyo.

Kwa upande mwingine, Sunderland wanaongozwa na kocha Regis Le Bris na wamekuwa na kiwango kizuri msimu huu, wakiwa wameshinda mechi tatu kati ya nne zilizopita, na wanatarajiwa kumaliza msimu kwenye nafasi ya 10 kwa alama 46.

Katika mchezo wa kwanza wa msimu kati ya timu hizi, uliopigwa Septemba 21, 2025 kwenye uwanja wa Stadium of Light, ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 huku Matty Cash akiwa amefunga bao la Aston Villa huku William Isidor akifunga la Sunderland.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Aston Villa wamekuwa na rekodi nzuri wanapocheza kwenye uwanja wao wa Villa Park msimu huu, wakishinda mechi 10 kati ya 16 na kufunga mabao 23, huku Sunderland wakipata shida ugenini wakiwa wameshinda mechi 4 tu kati ya 16 na kufunga mabao 10 pekee. Jisajili sasa

Jiunge kwenye familia yenye Odds kubwa uweze kuvuna maokoto

Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni, Aston Villa wameibuka na ushindi mara 13 kati ya mechi 34 za Ligi Kuu, Sunderland wakiibuka na ushindi mara 7 huku sare zikiwa 14, na katika mechi za hivi karibuni za Villa Park, Aston Villa wamekuwa wakiibuka na ushindi mara 6, sare 2 na kushindwa mara 2 tu.

Mchezo huu unaahidi kuwa wa kuvutia kwa kuwa Aston Villa wanatafuta uhakika wa kushiriki michuano ya Ulaya, huku Sunderland wakiwa na ndoto za kufuzu kwa michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu.

Na Benny Mwaipaja, Washington D.C


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, ameishauri Benki ya Dunia kuangalia namna ya kuiwezesha sekta binafsi katika nchi za Afrika ili iweze kuwa imara na kuchangia kukuza uchumi wa nchi hizo.

Mhe. Balozi Omar, ametoa wito huo wakati akichangia mada katika mkutano wa Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika, wanachama wa Benki ya Dunia (Africa Group 1 Constituency), uliofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo, Jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Alisema kuwa wakati nchi za Afrika zinatakiwa kuongeza ufanisi katika kukusanya mapato yake ya ndani, sekta binafsi za nchi wanachama wa Benki ya Dunia ikiwezeshwa kikamilifu, inaweza kuvutia mitaji ya ndani sawa na mitaji ya nje.

Mhe. Balozi Omar alieleza kuwa nchi nyingi za Afrika zinakabiliwa na madeni yanayofikia ukomo wa kuendelea kukopa zaidi, hivyo njia ya kujikwamua na changamoto hiyo ni kuongeza makusanyo ya mapato yao ya ndani kwa kutoza kodi kubwa ambazo kwa namna moja au nyingine zinaathiri kundi kubwa la wananchi masikini.

Alishauri Benki ya Dunia kutumia mbinu za Mpango wa Marshall (Marshall Plan) kuzisaidia nchi za Afrika, mpango ulioanzishwa na Marekani mwaka 1947 ili kuziwezesha nchi za ulaya kukabiliana na athari za vita ya pili ya dunia, hatua iliyosaidia nchi hizo kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa, kupata usaidizi wa teknolojia, kukuza biashara na kusaidia kukuza uchumi wa nchi hizo.

Akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa majukumu ya Benki ya Dunia kwa Kundi la kwanza la Kanda ya Afrika, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dkt. Zarau Wendelin Kibwe, alisema kuwa Benki ya Dunia inatarajia kukusanya na kutumia dola za Marekani bilioni 100 kuziwezesha nchi wanachama kukabiliana na changamoto za kiuchumi pamoja na kukuza sekta binafsi.

Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza ujumuishaji kwa kupanua fursa za ajira kwa wanawake, vijana, na jamii zisizopewa kipaumbele huku ikiimarisha ulinzi wa kijamii na ustahimilivu kutokana na mabadiliko ya kiuchumi.

Aidha, Dkt. Kibwe alisema kuwa juhudi hizo kwa pamoja hazilengi tu kuunda ajira, bali pia kuhakikisha ajira hizo ni za uzalishaji, endelevu, na zinapatikana kwa wote kupitia Ajenda ya Ajira katika kubuni miradi (Agri-Connect, Nishati, Afya, na Madini) na kuweka kipaumbele kwenye sekta zinazozaa ajira kwa lengo la kuunda fursa zaidi za ajira kwa vijana.

Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika wanachama wa Benki ya Dunia (Africa Group 1 Constituency) limeundwa na nchi 22 kutoka Ukanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ambazo ni Tanzania, Botswana, Burundi, Eritrea, Eswatini, Ethiopia, Gambia, Kenya, Lesotho, Liberia, Malawi, Msumbiji, Namibia, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Somalia, Sudan Kusini, Sudan, Uganda, Zambia, na Zimbabwe.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza katika Mkutano wa Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency) wanachama wa Benki ya Dunia, uliofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Benki hiyo, jijini Washington D.C nchini Marekani, wakati wa Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia) na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, wakifuatilia mada mbalimbali katika Mkutano wa Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency) wanachama wa Benki ya Dunia, uliofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Benki hiyo, jijini Washington D.C nchini Marekani, wakati wa Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Washington D.C. Marekani)














-Ampongeza Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa uchapakazi

-Asisitiza Tanzania itavuka salama Kipindi hiki kigumu cha tatizo la mafuta 


Na Mwandishi Wetu.

"KAMA ambavyo imejaaliwa kuwa na aina mbalimbali ya vivutio vya Utalii,Mali asili,  yakiwemo madini na vinginevyo, pia hivyo Taifa la Tanzania limejaaliwa kuwa na viongozi hodari tangu ilipopata uhuru wake Mwaka 1961"

"Ukiacha viongozi wengine waliotangulia na kuliongoza Taifa hili,kwa sasa tunaye Mama yetu Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye kwa hakika watanzania wengi tunajivunia uongozi wake imara tangu aliposhika madaraka kutuongoza" ameanza kwa kusema hivyo Dkt.Sajad Habib Rai

Dkt.Sajad anayehudumu kama Meneja wa nchi katika Bohari ya kuhifadhia mafuta Jamii ya Petroli 'MOIL Energies' , anasema kupitia utawala wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kila jambo ndani ya nchi linakwenda sawa likiweko suala zima la nafasi kwa wawekezaji kufanya uwekezaji nchini.

"Hakika kwa hili Rais Samia anastahili pongezi, ameifanya Tanzania kuwa kimbilio la watu kutoka Mataifa ya nje kuja na kuwekeza, fursa hiyo haipo katika kila Taifa, hapa ndipo unaona uhodari wa Kiongozi huyu" anasema Dkt.Sajad

Kimsingi mtaalamu huyu katika fani za Ununuzi na Ugavi, usafirishaji, biashara katika Tasnia ya nishati ya mafuta akiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 20, kwake ni fahari kutekeleza majukumu yake chini ya utawala wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan 

"Kiongozi bora ni yule anayejulikana kwa kujenga timu zenye mshikamano, kuendesha ufanisi wa utendaji kazi, na kukuza utamaduni wa utendakazi na uwajibikaji, hakika Dkt.Samia amejitolea kufanya kazi kwa ubora, pamoja na mambo mengine hilo ni jambo pekee linalotufanya tufurahie uongozi wake" amesisitiza Dkt Sajad.

Dkt.Sajad kama mmoja wa viongozi wanaotoa mchango mkubwa katika sekta ya mafuta nchini, kupitia nafasi yake ya usimamizi wa bohari ya mafuta, ameonyesha uwezo mkubwa wa kuunganisha maslahi ya wafanyakazi, wawekezaji na Serikali kwa ujumla.

Uongozi wake umeendelea kuonekana kuwa wa vitendo siyo tu kwa timu yake anayoiongoza katika eneo lake la kazi, bali hata maeneo mengine ikiwemo Serikalini, kwani hivi karibuni kupitia mchango wake wa mawazo umesaidia kuleta tija katika eneo la kodi na ushuhuru kipitia biashara ya mafuta.

Kupitia mawazo yake ya kudhibiti vitendo vya ukwepaji kodi kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara wa mafuta akitoa wazo  kuwa kila muagizaji wa mafuta anapaswa kukadiriwa  kodi kulingana na kiasi Cha mafuta alichoagiza kabla ya mafuta hayo kuingia sokoni, kwa kiasi kikubwa kumesaidi kuleta tija.

Anasema wazo hilo ambalo kabla ya kulitoa kulisababisha kuwepo kwa 'ujanja ujanja' kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepo kodi kumesaidia kuiongezea mwanya Mamlaka ya Mapato ( TRA) kukusanya kodi yake kwa ufasaha hali ambayo pia imesaidia kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.

Anasema siku zote katika mazingira ya biashara ya mafuta ambayo yanahitaji umakini mkubwa, nidhamu pamoja na uwajibikaji, ameendelea na ataendelea kusimamia utendaji wa kazi kwa weledi mkubwa.

Moja ya mambo yanayomtofautisha ni namna anavyoweka mbele ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za Serikali, akionesha wazi kuunga mkono mifumo mipya ya usimamizi wa mafuta, ikiwemo ulipaji wa kodi kabla ya mafuta kuingia sokoni. 

Mfumo huu umechangia kupunguza mianya ya ukwepaji kodi sambamba na kuongeza mapato ya Serikali kwa kuleta ushindani wa haki kwa wafanyabiashara wanaofuata sheria.

Mchango wa Dkt Sajad kwa upande wa Serikali  unaonekana katika kuongeza mapato kupitia kodi, kudhibiti upotevu wa mafuta, kuimarisha usalama wa nishati na kusaidia uchumi wa taifa tukielewa pia kuwa Sekta ya mafuta ni mhimili mkubwa wa maendeleo ya nchi, hivyo viongozi wenye maono kama Dkt Sajad wanakuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya taifa.

Aidha akizungumzia changamoto ya mafuta inayoikumba Dunia kwa Sasa, Dkt Sajad anasema hali hiyo siyo kwa Tanzania pekee bali hata upande wa mataifa mengine Duniani ikichangiwa na mzozo unaendelea Mashariki ya Kati ingawa kwa Tanzania bado Kuna akiba ya kutosha ya mafuta.

Kwa ujumla, Dkt Sajad Habib Rai ni mfano wa kiongozi anayejali maendeleo ya wafanyakazi na Taifa kwa pamoja. Utendaji wake umeonyesha kuwa mafanikio siyo kwa taasisi yake tu, bali pia taasisi yoyote inayotegemea uongozi bora, uwajibikaji na uwezo wa kuendana na mabadiliko ya kisasa katika sekta husika, kupitia juhudi zake, sekta ya mafuta inaendelea kuwa na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Tanzania.




Na Byera Deus ,Bukoba

MBUNGE wa Jimbo la Bukoba Mjini Mhandisi Johnston Mtasingwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Dini  wameungana na wananchi wa Kata ya Kibeta katika mtaa wa Anyama   kushiriki Ibada  ya kuaga miili ya watoto wawili kati ya Wanne wa familia mbili waliofariki kutokana na Mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia Aprili 17,2026   katika Manispaa ya Bukoba, mkoani Kagera, ambayo ilisababisha vifo vya watoto wanne

Majina ya  watoto waliofariki ni  Eliza Edmund(13), mwanafunzi wa shule ya msingi Kashabo,Darasa la sita,Edwini Edmund(10), mwanafunzi wa darasa la nne Kashabo, Munihadi Mickidadi(13) aliyekuwa anasoma darasa la nne shule ya msingi Pamoja na Jamia  Mickidad(5).

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya watoto hao Mhandisi Mtasingwa  ambaye ni Mbunge wa Bukoba Mjini amesema  licha ya kuwa na majukumu ya vikao vya Bunge alipata taarifa saa 12 asubuhi.

Ambapo  alituma msaada wa awali na mara baada ya kuuliza swali lake Bungeni alianza safari ya kurudi jimboni na  alifika saa 6 usiku kuungana na familia hizo.

Amesema amesikitishwa na vifo vya watoto hao ambapo ametoa ombi kwa TANROAD na TARURA kuzibua mitaro hasa kipindi hiki cha mvua huku akiwataka wananchi kukagua nyumba zao mara kwa mara  katika msimu huu wa mvua  

Ametumia fursa hiyo kutoa pole kwa wananchi waliopoteza mifungo na makazi  na kuomba waendelee kuchukua tahadhari kwani mvua Bado ni nyingi na nitaendelea kunyesha na kuomba wananchi kuendelea kushirikiana pale matatizo yanapojitokeza

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Sima watoto wengine wawili  ambao wamefariki katika tukio hilo tayari wamezikwa kata ya Maruku  Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.

“Nimesikitishwa kuwa na vifo hivyo ambavyo vimekatiza ndoto za watoto wadogo ambao walikuwa na malengo makubwa ya badae.Mvua hizo ambazo zimenyesha baadhi ya wanchi wamepoteza mifungo yao hasa kuku wengi wamesombwa.

“Wengine wamepoteza makazi hivyo nitoe mwito kwa wananchi  wanaoishi mabondeni na kando kando ya Ziwa Victoria kuchukua tahadhari kabla ya vifo havijaongezeka.”

Ibada ya kuaga miili hiyo imeongozwa na Mchungaji Ediso Rugemeleza  Mchungaji  wa Usharika wa kanisaa kuu La Kiinjili la  Kilutheri KKKT Dayosisi Kasikazini Magaribi

Ambapo ametumia fursa hiyo kwa kuzishukuru taasisi za serikali kufanya uokozi  na wananchi Kujitolea ambao anadai kuwa hiyo ndio misingi ya utu. Vifo hivyo vimetokea baada ya ukuta wa hotel ya Perfect kuzidiwa na  maji na kuangukia nyumba za majirani na kusababisha vifo vya watoto hao.








Na Mwandishi Wetu

WAKATI Chama Cha Mapinduzi  (CCM) kikifungua dirisha  kwa makada wake kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki leo,Kada wa Chama

hicho ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga amechukua fomu kuwania nafasi hiyo.

Mtatiro ambaye ni miongoni mwa makada vijana na wasomi katika Taifa la Tanzania amechukua fomu hiyo ya kuwania Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki leo Aprili 18,2026  katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, zilizopo Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Amekabidhiwa na fomu hiyo  na Ofisa wa Chama Idara ya Organaizesheni, Raymond Mosi.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu Mtatiro amesema  ameamua kujitosa katika kinyang'anyiro hicho kutumia  haki  yake ya msingi katika kuliwakilisha taifa katika Bunge la Afrika Mashariki kwa maslahi mapana ya taifa.




Top News