Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya NIC Insurance imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa Bima ya COMESA (COMESA Yellow Card), ikieleza kuwa huduma hiyo inarahisisha safari za kuvuka mipaka ya nchi wanachama wa Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) bila kulazimika kukata bima mpya ya lazima katika kila nchi.

Akizungumza katika Banda la NIC Insurance kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa Mwandamizi wa kampuni hiyo, Bi. Erika Nnko, amesema Bima ya COMESA ni mfumo wa kikanda wa bima ya vyombo vya moto unaowapa madereva uhuru wa kusafiri kwa usalama katika nchi wanachama wa COMESA huku wakitambuliwa kisheria kupitia kadi maalumu ya njano inayofahamika kama COMESA Yellow Card.

Amesema mmiliki wa chombo cha moto anapokata bima hiyo kupitia kampuni za bima zilizoidhinishwa nchini, hupatiwa Yellow Card ambayo hutambulika na mamlaka za nchi zote zinazoshiriki katika mfumo huo.

Erika amesema kadi hiyo hutoa kinga dhidi ya madai yanayotokana na majeraha kwa watu wengine au uharibifu wa mali za watu wengine unaoweza kusababishwa na chombo cha moto wakati wa safari katika nchi wanachama wa COMESA.

Ameeleza kuwa mfumo huo unarahisisha biashara na usafirishaji wa mizigo pamoja na safari za watu binafsi kwa kuondoa ulazima wa kukata bima mpya ya lazima ya mkataba wa tatu (Third Party) kila unapovuka mpaka wa nchi mwanachama.



Na Mwandishi Wetu
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, ameipongeza Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kwa juhudi zake za kuwawezesha vijana kujiajiri kupitia Kituo chake cha Kiatamizi cha IAA Business Start Up Centre, kinachowasaidia kubadili mawazo ya kibunifu kuwa biashara zenye mafanikio.

Tutuba alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la IAA katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema anafurahishwa na maendeleo ya kituo hicho, akieleza kuwa alishiriki katika hatua za mwanzo za kuanzishwa kwake na sasa anashuhudia matokeo chanya kupitia vijana wanaobuni na kuanzisha biashara zinazochangia maendeleo ya uchumi.

"Ninakumbuka tulipoanzisha kituo hiki. Leo ninafurahi kuona kinaendelea kuzalisha vijana wenye ubunifu na kuwageuza mawazo yao kuwa fursa za kiuchumi," alisema Tutuba.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa, Uhusiano na Masoko wa IAA, Sarah Goroi, alisema taasisi hiyo imeendelea kuwekeza katika kuwaandaa vijana kwa kujiajiri kupitia Kituo cha Kiatamizi, sambamba na kutoa elimu inayokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Alisema mbali na mafunzo ya darasani, IAA imeweka mazingira rafiki yanayowezesha wanafunzi kuanzisha biashara zao huku wakipata ushauri wa kitaalamu, mafunzo ya ujasiriamali na ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha mawazo yao yanakua na kuwa biashara endelevu.

Sarah alisema katika mwaka wa masomo 2024/2025 zaidi ya vijana 8,600 walinufaika na programu za ujasiriamali, huku vijana 1,520 wakiwasilisha mawazo mbalimbali ya biashara kupitia kituo hicho.

Aliongeza kuwa kati ya mawazo hayo, zaidi ya biashara 50 zilianzishwa na kampuni 12 zikafanikiwa kusajiliwa rasmi, zikijikita katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara, teknolojia, sanaa, uhifadhi wa mazingira na shughuli nyingine za kiuchumi.

Alisema kupitia Kituo cha Kiatamizi, wahitimu wengi wamefanikiwa kujiajiri na wengine kuanzisha kampuni zinazowaajiri vijana wenzao, hatua inayochangia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na ujasiriamali.









Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI  ya Mixx imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia kampeni ya Kombe la Dunia ya MiXX Super, ambapo washindi watatu wamekabidhiwa zawadi za shilingi milioni moja kila mmoja kwa kutumia aprication ya MiXX Super app kufanya malipo ya huduma mbalimbali.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi hizo katika banda la Yas kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Meneja wa Biashara Mixx Mkoa wa Dar es Salaam, Estony Venant, alisema kampeni hiyo imeendelea kuwagusa Watanzania wengi huku jumla ya washindi 48 wakinufaika hadi sasa.

Alisema kati ya washindi hao,zaidi ya washindi 20 wamejishindia vifaa mbalimbali kutoka kwa mshirika wa Mixx kampuni ya Hisense, huku washindi wengine zaidi ya 40 wakijishindia fedha taslimu za shilingi milioni moja kila mmoja.

Venant alisema kampeni hiyo bado inaendelea na kwamba mshindi wa mwisho atajishindia zawadi kubwa ya shilingi milioni 50, akiwahimiza wananchi kutumia Aprication ya MiXX Super app katika kufanya malipo ya huduma mbalimbali za kifedha ili kuongeza nafasi ya kushinda.

"MiXX Super ni zaidi ya Aprication malipo; ni jukwaa linalorahisisha huduma za kifedha huku likiwapa watumiaji nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali. Tunawahimiza wananchi kuipakua na kuitumia mara kwa mara," alisema Venant.



Ilipofika Juni 11, 2026, dunia ilishuhudia uzinduzi wa mashindano makubwa kuliko yote ya michuano ya Dunia mechi ya ufunguzi kati ya Mexico na Afrika Kusini ikizindua msimu wa timu 48, badala ya 32 za zamani. Tangu siku hiyo hadi sasa ambapo mashindano yamefikia hatua ya raundi ya 16, kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimfumo na pia matukio kadhaa yaliyoibua mijadala mikali kuhusu haki na uwazi wa maamuzi ya kiuchezaji.

Jambo la kwanza lililobadilisha sura ya mashindano ni sheria mpya zilizoletwa na IFAB kabla ya fainali kuanza. Badala ya kusubiri muda mrefu kwa mabadilishano ya wachezaji, sasa mchezaji anayetoka uwanjani ana sekunde kumi tu, la sivyo mbadala wake atalazimika kusubiri dakika moja. Vilevile, refa anaweza kuanzisha kaunti-daun ya sekunde tano kwa mirushano ya kando na migongo ya lango ili kuzuia kupoteza muda kimakusudi.

Mapumziko ya lazima ya kunywa maji ya dakika tatu kwa kila nusu ya mchezo pia yameletwa, ingawa baadhi ya watazamaji wamelalamikia kuwa mapumziko hayo yametumika zaidi kwa matangazo ya kibiashara kuliko ustawi wa wachezaji.

Mabadiliko mengine muhimu yamehusu matumizi ya VAR. Sasa mfumo huu unaruhusiwa kupitia upya maamuzi ya kona zisizo sahihi, kadi nyekundu zilizotokana na kadi ya pili ya njano, na hali za kumwadhibu mchezaji asiye sahihi.

Aidha, sheria mpya ya kutoa kadi nyekundu kwa mchezaji anayefunika mdomo wake wakati wa ugomvi na mpinzani imeanza kutumika, huku Miguel Almirón wa Paraguay akiwa mchezaji wa kwanza kufukuzwa chini ya sheria hiyo dhidi ya Uturuki. Teknolojia ya mstari wa nusu-otomatiki (semi-automated offside), inayotumia vitambuzi ndani ya mpira wa Adidas Trionda, nayo imeongeza usahihi wa maamuzi ya "off-side" kuliko wakati mwingine wowote.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hata hivyo, usahihi huo wa kiteknolojia haujaondoa utata. Katika hatua ya makundi, mabao ya Iran dhidi ya Misri na Brazil dhidi ya Scotland yalifutwa na VAR, hali iliyowafanya baadhi ya viongozi wa mashirikisho, akiwemo rais wa shirikisho la mpira la Brazil, kuandikia FIFA wakitaka uthabiti zaidi wa kanuni hizo.

Mvutano ulizidi wiki iliyopita pale Folarin Balogun wa Marekani alipopewa kadi nyekundu dhidi ya Bosnia kabla FIFA haijaigeuza baada ya kuombwa na Rais Trump, na hivi karibuni zaidi, bao la Misri lililofutwa dakika za mwisho za mechi dhidi ya Argentina huko Atlanta liliizua tena hisia za upendeleo miongoni mwa mashabiki na wachambuzi.

Nje ya viwanja, mashindano haya pia yamekumbwa na changamoto za kiusalama, kiuchumi na kisiasa kuanzia ukaguzi mkali usio wa kawaida uliokabili timu za Senegal na Uzbekistan walipowasili Marekani, mgomo wa wafanyakazi wa uwanja wa SoFi Stadium, hadi bei za tiketi zilizofika hadi dola 11,000 kwa fainali.

Kwa pamoja, matukio haya yanaonesha kwamba, ingawa sheria mpya na teknolojia zimefanikiwa kuongeza kasi na usahihi wa mchezo, bado kuna safari ndefu kuelekea kuaminika kikamilifu machoni pa mashabiki na timu shindani.
Kwa kizazi kinachopenda burudani yenye msisimko, Meridianbet imeleta promosheni inayobadilisha namna ya kufurahia michezo ya kasino. Golden Goal Rewards ni jukwaa linalokupa nafasi ya kushindania jumla ya TZS milioni 450 huku ukiendelea kufurahia michezo unayoipenda. Kila mzunguko wa mchezo unaweza kuwa hatua ya karibu zaidi kuelekea ushindi mkubwa ambao unaweza kubadilisha siku yako kuwa ya kipekee.

Baada ya kujiunga kwenye promosheni hii, safari ya ushindi inaanza mara moja. Unachohitaji ni kucheza michezo inayostahili na kutimiza masharti ya ushiriki. Kilicho cha kuvutia zaidi ni kwamba Meridianbet imeweka mfumo wa Prize Drops za ghafla, zawadi ambazo zinaweza kuingia moja kwa moja kwenye akaunti yako wakati wowote ukiwa katikati ya mchezo. Hapo msisimko wa kweli unazaliwa, kwa sababu huwezi kujua ni muda gani bahati yako itang’ara.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mbali na zawadi za papo hapo, Golden Goal Rewards imeundwa kuwapa wachezaji motisha ya kuendelea kushiriki. Kila mchezo unaoucheza unakusaidia kujikusanyia pointi ambazo zinakupandisha kwenye msimamo wa kila wiki. Kadri unavyokuwa hai kwenye promosheni, ndivyo nafasi yako ya kuingia kwenye orodha ya washindi inavyoongezeka. Hii inamaanisha kuwa kila wiki ni fursa mpya ya kuonyesha uwezo wako na kupanda juu ya msimamo.

Kwa walio wengi, michezo ya kasino ni sehemu ya burudani na mapumziko ya kila siku. Meridianbet imeelewa hilo na kuunda promosheni inayokupa furaha, ushindani na nafasi halisi ya kushinda. Golden Goal Rewards inaleta mazingira ambayo kila mshiriki anaweza kujisikia sehemu ya safari kubwa ya ushindi.

Huu ndio wakati wa kuchukua hatua. Ingia sasa ndani ya Meridianbet, jiunge na Golden Goal Rewards na ujionee jinsi ushindi unavyoweza kutokea wakati wowote. TZS milioni 450 zinasubiri washindi wenye ujasiri wa kucheza kwa kujiamini. Kila wiki inaleta mwanzo mpya, na kila mchezo unaweza kuwa mlango wa kuandika historia yako ya ushindi ndani ya Meridianbet.
Dar es Salaam, Julai 10, 2026

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umewahimiza wananchi waliojiajiri nchini kujiunga na kuchangia katika Mfuko huo ili kujijengea akiba, kupata kinga ya kijamii na kuwa na uhakika wa maisha ya sasa na baadaye.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala, Bw. Ekwabi Mujungu, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, wakati akifungua Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri iliyofanyika Julai 10, 2026 katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Bw. Mujungu alisema Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri ni sehemu ya mkakati wa NSSF wa kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa wananchi waliojiajiri, ambao ni sehemu muhimu ya ukuaji wa uchumi wa nchi.

"Wananchi wengi wanaojiajiri hupata kipato kupitia shughuli wanazozifanya, lakini bila kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba wanaweza kujikuta wakikabiliwa na changamoto wanapofikia uzee au wanapopoteza uwezo wa kufanya kazi. Kujiunga na NSSF ni hatua muhimu ya kujenga uhakika wa maisha ya sasa na ya baadaye," alisema Bw. Mujungu.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya kupanua wigo wa hifadhi ya jamii ili wananchi wote, bila kujali aina ya shughuli wanazofanya, wanufaike na huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii.

"Tunawahimiza wananchi wote waliojiajiri kutumia fursa hii kujiunga na kuchangia NSSF. Mtu anapoanza kuweka akiba mapema, anajijengea msingi imara wa kunufaika na mafao mbalimbali yatakayomsaidia yeye na familia yake pale yatakapohitajika," alisisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa NSSF Mkoa wa Kigamboni, Bw. Siraji Kisaka, alisema siku hiyo maalumu imeandaliwa mahsusi kuwafikia wananchi waliojiajiri kwa kuwapatia elimu kuhusu umuhimu wa kujiunga na kuchangia NSSF pamoja na kuwafahamisha mafao na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko.

"Lengo letu ni kuhakikisha wananchi waliojiajiri wanapata uelewa sahihi kuhusu hifadhi ya jamii na umuhimu wa kujiunga na kuchangia NSSF. Tunataka wajenge utamaduni wa kujiwekea akiba ili wawe na usalama wa maisha yao ya sasa na ya baadaye," alisema Bw. Kisaka.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Uwezeshaji Wanawake Tanzania (TAWEN), Florence Massunga, aliwataka wananchi waliojiajiri kuitumia fursa hiyo kujiunga na NSSF, akisema kufanya hivyo kutawasaidia kujenga usalama wa kifedha na kupunguza utegemezi wanapokumbwa na changamoto za maisha.

Baada ya ufunguzi wa shughuli hiyo, wananchi waliojiajiri walipewa elimu kuhusu mfumo wa hifadhi ya jamii, utaratibu wa kujiunga na kuchangia NSSF, mafao mbalimbali yanayotolewa na Mfuko pamoja na umuhimu wa kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba mapema ili kuwa na uhakika wa maisha ya sasa na baadaye.

Siku Maalumu ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri ni sehemu ya shughuli za NSSF katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, zenye lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi, kuongeza uelewa kuhusu hifadhi ya jamii na kuwahamasisha wananchi waliojiajiri kujiunga na kuchangia NSSF.





















Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid, leo Julai 20, 2026 akiwa mkoani Mbeya amekutana na kusikiliza changamoto, maoni na mapendekezo kutoka kwa makundi mbalimbali ya kijamii.

Makundi yaliyowasilisha hoja zao ni pamoja na wakulima, wafugaji, wachimba madini, wafanyabiashara, wavuvi, mama na baba lishe, machinga, waendesha usafirishaji, mafundi ujenzi, mafundi gereji, wanamichezo, walimu wazalendo, wazee wastaafu pamoja na vikundi mbalimbali vya kijamii.

Ndg. Rabia alipokea kero, ushauri na mapendekezo yaliyowasilishwa na wananchi hao, huku baadhi ya hoja zikijibiwa na nyingine kutolewa maelekezo kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi.

Baada ya kikao hicho, Ndg. Rabia aliwataka wananchi kuendelea kulinda amani ya Tanzania, akisisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo endelevu na kila Mtanzania ana wajibu wa kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama na yenye utulivu ili wananchi waendelee kufanya shughuli za uzalishaji kwa maendeleo ya taifa.








Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) leo tarehe 10 julai, 2026 amekutana na bodi ya wakurugenzi mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro katika ofisi za mamlaka hiyo zilizopo Karatu mkoani Arusha na kusisitiza umuhimu wa bodi hiyo kufuatilia kwa karibu shughuli zote za utendaji ili kuanza mwaka mpya wa fedha 2026/2027 kwa kasi na ufanisi.

Mhe. Kijaji amesema kuwa bajeti ya mwaka mpya wa fedha inaanza na utekelezaji wa dira ya taifa ya maendeleo ya mwaka 2050 hivyo vikao vyake na bodi za taasisi zilizopo chini ya wizara vina lengo la kuanza utekelezaji wa dira, bajeti na ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa pamoja.

Ameitaka bodi hiyo kuongeza nguvu katika kuimarisha uhifadhi, kutangaza utalii na kusimamia maendeleo ya jamii na kusisitiza kuwa jitihada hizo ziendane na kasi ya kukamilisha miundombinu wezeshi ikiwemo barabara kuu ya Loduare hadi Golini, kuimarisha mawasiliano ndani ya eneo lote la hifadhi, kukamilisha mradi wa fensi ya umeme ili kupunguza migongano kati ya wanyamapori na wananchi, kudhibiti ujangili na kuendelea kuimarisha mahusiano ya hifadhi na wananchi wanaoizunguka.

“Tulinde uhifadhi wa Ikolojia ya Ngorongoro kwa wivu mkubwa, tuendelee kubuni mazao mapya ya utalii na kuyatangaza, tujipange kikamilifu kuhakikisha Ngorongoro kama premium destination inawafikia na kuwashawishi wageni watakaohudhuria matukio ya AFCON, mkutano wa umoja wa Mabunge duniani, tuzo za dunia za utalii na shindano la Miss world ambapo matukio yote yatafanyika Tanzania kati ya mwezi oktoba 2026 na Julai mwaka 2027” amesisitiza Dkt. Kijaji.

Katibu wa Bodi, ambae ni kamishna wa Uhifadhi Ngorongoro Abdul-Razaq Badru amemueleza Mhe. waziri kuwa, Ngorongoro imepiga hatua ya kimageuzi kwenye mifumo ya kidijitali (ICT Transformation), uhifadhi endelevu kwa kuimarisha doria za kisasa, kuboresha miundombinu hasa barabara ya tabaka gumu kutoka geti la loduare hadi Seneto (km 29.5) kwa gharama ya TZS 80.3 bilioni

Badru ameongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2025/26 eneo la Ngorongoro idadi ya watalii ilifikia 1,061,620 na fedha shilingi 269.5 Bilioni zilikusanywa. Ngorongoro imeendelea na jitihada za kulinda hadhi tatu za kimataifa kutoka UNESCO ambazo ni Urithi wa Dunia (World Heritage Site), Hifadhi ya Biosphere (Man and Biosphere Reserve), na Geopark ya Dunia (Ngorongoro-Lengai Global Geopark) ili ziendelee kuinufaisha nchi yetu.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi Ngorongoro Dkt. Harriet Mtae amemueleza Mhe waziri kuwa, katika kipindi cha miezi sita (06) iliyopita bodi ya Ngorongoro imetekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria, kanuni pamoja na maelekezo ya Serikali ili kuhakikisha Mamlaka inatekeleza kikamilifu dhamana yake ya kuhifadhi maliasili za Wanyamapori, malikale na urithi wa dunia, kuendeleza utalii endelevu na kuboresha shughuli za maendeleo ya jamii.



Na Janeth Raphael MichuziTv

Vigogo wanane wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wameendelea kushikiliwa rumande baada ya upande wa Jamhuri kueleza kuwa upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi na rushwa inayowakabili bado haujakamilika.

Shauri hilo lilipotajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma jana, Julai 9, 2026, Wakili wa Serikali, Gothard Mwingira, aliiambia mahakama kuwa upelelezi umefikia hatua za mwisho, lakini bado haujakamilika. Alieleza kuwa upande wa mashtaka unasubiri kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kabla ya kuendelea na hatua zinazofuata za shauri hilo.

Kutokana na maelezo hayo, upande wa Jamhuri uliomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa kwa kesi hiyo wakati taratibu za upelelezi zikikamilishwa.

Washtakiwa katika shauri hilo ni aliyekuwa Rais wa CWT, Leah Ulaya, Rais wa sasa wa CWT, Suleiman Ikomba, aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maganga Japhet, Katibu Mkuu wa sasa, Joseph Misalaba, pamoja na Nashon Kidudu, Baraka Mbonalibha, Wambura Kihengu na Angelina Wambura. Pia kampuni ya Pyrite and Industries Company Limited inatajwa kama mshtakiwa katika kesi hiyo.

Viongozi hao walifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani Mei 25, 2026, ambapo walisomewa jumla ya mashtaka 14 yanayohusisha uhujumu uchumi na rushwa.

Hata hivyo, hawakutakiwa kujibu mashtaka hayo kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi haina mamlaka ya kusikiliza kesi zinazohusu uhujumu uchumi.

Shauri hilo litaendelea kutajwa mahakamani baada ya upande wa Jamhuri kukamilisha upelelezi na kupata kibali kinachohitajika kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka.





New York, Marekani


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeeleza hatua zake za kuanza kutekeleza Mpango wa Nne wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano, 2026/27–2030/31 (FYDP IV), ambao ni mpango wa kwanza wa muda wa kati wa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Hayo yamelezwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais–Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Mbaga Kida, wakati wa mkutano wa pembezoni mwa Jukwaa la Ngazi ya Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa linalosimamia Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (HLPF 2026), uliofanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, Marekani.

Mkutano huo, wenye mada “Driving Industrial and Inclusive Economic Transformation: Financing, Innovation and Sustainable Growth in Agricultural and Blue Economy Value Chains”, uliandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), pamoja na UNDP, UNIDO na washirika wengine.

Dkt. Kida alisema Tanzania inaingia katika awamu mpya ya utekelezaji wa maendeleo inayolenga kubadilisha mafanikio ya ukuaji wa uchumi na uwekezaji katika miundombinu kuwa ongezeko la uzalishaji, ajira zenye tija, mauzo ya nje, ongezeko la thamani ya bidhaa na ustawi mpana wa wananchi.

Dkt. Kida alisema uchumi wa Tanzania kwa sasa unakua kwa asilimia 5.9 na unatarajiwa kufikia asilimia 6.3 ifikapo mwisho wa mwaka huu. Ukuaji huo ulichangiwa na kuimarika kwa shughuli mbalimbali za uzalishaji na huduma, pamoja na kuendelea kwa uwekezaji katika miundombinu na miradi ya kimkakati.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa lengo si kasi ya ukuaji pekee, bali ukuaji unaogusa maisha ya wananchi wote. “Lengo letu si kuongeza ukubwa wa uchumi pekee. Tunataka ukuaji unaoongeza kipato cha wananchi, unaotengeneza ajira, unaopunguza umaskini na unaowezesha wanawake, vijana, wakulima wadogo na wajasiriamali kushiriki kikamilifu katika uchumi,” alisema Dkt. Kida.

Dkt. Kida alibainisha kuwa kilimo, misitu na uvuvi vinaendelea kuwa sehemu muhimu ya uchumi wa Tanzania, vikichangia asilimia 24.3 ya Pato la Taifa mwaka 2025. Alisema mchango wa uvuvi katika Pato la Taifa uliongezeka kutoka asilimia 1.9 mwaka 2020 hadi asilimia 2.2 mwaka 2025, hatua inayoonesha fursa zinazoongezeka katika uchumi wa buluu.

“Tunataka kuondoka katika uchumi unaouza malighafi na kuelekea uchumi unaosindika, unaoongeza thamani, unaotumia teknolojia na unaounganisha wazalishaji wa ndani na masoko ya kitaifa, kikanda na kimataifa,” alisema.

Dkt. Kida pia alisema Tanzania itawasilisha Mapitio ya Tatu ya Hiari ya Nchi ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu tarehe 14 Julai 2026.

Mapitio hayo yanaonesha maendeleo yaliyopatikana katika maji safi, nishati, miundombinu, afya, usafiri, teknolojia ya kidijitali na uimarishaji wa rasilimali za ndani.

Kwa upande wake, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York, Mhe. Togolani Edriss Mavura, alisema mageuzi ya viwanda barani Afrika yanapaswa kuwa jumuishi na kuwanufaisha wakulima wadogo, wanawake, vijana, wavuvi, wafugaji, biashara ndogo na washiriki wa sekta isiyo rasmi.

Alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika teknolojia, uwekezaji, masoko, ujuzi, fedha za maendeleo na ujenzi wa minyororo ya thamani inayounganisha nchi za Afrika.

Ofisa Mkuu wa Fedha wa UNCDF, Bw. Karen Vardanyan, aliitaja Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoonesha namna fedha bunifu zinavyoweza kutumika kuharakisha maendeleo katika ngazi ya taifa na mamlaka za serikali za mitaa.

Alieleza kuwa upatikanaji wa nishati safi ya kupikia umeongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 28.6 mwaka 2025. Maendeleo hayo yanaungwa mkono na utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia, uwekezaji wa sekta binafsi na juhudi za Serikali za kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa.

Bw. Vardanyan pia alitaja Tanga UWASA Green Revenue Bond, iliyokusanya dola za Marekani milioni 20.8 kwa ajili ya miundombinu ya maji inayohimili mabadiliko ya tabianchi. Hatifungani hiyo ilikuwa ya kwanza ya kijani katika ngazi ya mamlaka ya chini ya kitaifa Afrika Mashariki, huku wawekezaji wa ndani wakichangia asilimia 65 ya uwekezaji wote.

Mifano mingine iliyotajwa ni PesaTech Accelerator, inayosaidia ubunifu wa huduma za kifedha na biashara zinazoongozwa na vijana, pamoja na mfumo wa LoCAL unaowezesha mamlaka za serikali za mitaa kuongeza uwekezaji unaohimili athari za mabadiliko ya tabianchi.

Bw. Vardanyan alitoa wito kwa Serikali, taasisi za fedha, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kubadili ahadi za kimataifa kuwa miradi inayoweza kufadhiliwa na uwekezaji halisi katika kilimo, uchumi wa buluu, viwanda, maji, nishati na miundombinu.

Mkutano huo ulihitimisha kuwa utekelezaji wa Dira 2050 na FYDP IV utahitaji ushirikiano madhubuti kati ya Serikali, sekta binafsi, taasisi za fedha, Umoja wa Mataifa, washirika wa maendeleo, asasi za kiraia na jamii.

Dira 2050 inalenga kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye uchumi wa kipato cha kati cha juu, yenye Pato la Taifa la dola za Marekani trilioni moja, pato la wastani kwa mtu linalozidi dola 7,000 na kuondoa umaskini ifikapo mwaka 2050.











Top News