FARIDA MANGUBE, MOROGORO
ZIARA ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba katika kata za Kidete na Tindika imekuwa faraja kubwa baada ya Serikali kutoa shilingi milioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji itakayoboresha maisha ya wakazi wa maeneo hayo

Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Sospeter Lutonja, amesema kwa Kata ya Kidete vitachimbwa visima 6 vyenye thamani ya shilingi milioni 360, ambavyo vinatarajiwa kunufaisha zaidi ya wakazi 15,000.

Kwa upande wa Kata ya Tindika, serikali imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya usambazaji wa maji katika vijiji vya Tindiga A, Tindiga B, na Maluwi ambapo awali wakazi wa maeneo hayo walikuwa wakitumia visima vya mkono maarufu kama “visima vya mdundiko,” ambavyo havikutosha kukidhi mahitaji ya kila siku.

Ziara ya Waziri Mkuu inaonesha wazi jinsi serikali inavyolenga kuhakikisha huduma za maji zinawafikia wananchi, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko na uhaba wa maji safi.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina.

Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee.

Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana

Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badala ya utaratibu wa maelekezo kutoka juu kwenda chini.

Alitumia pia kikao hicho kutoa rai kwa viongozi na wana CCM kuzingatia utaratibu wa kutoa maoni kuanzia ngazi ya chini kwenda juu.

“Nitoe wito kwa viongozi wetu tusifanye utaratibu wa kutoa amri kutoka juu kushuka chini maana uongozi mzuri ni lazima uanzie chini kwenda juu, yale tunayoyapata kutoka kwenye mashina, matawi ndio yatapanda juu kwa lengo la kukiimarisha chama chetu, alisema Dkt.Migiro.

Aidha, siku iliyofuata katika ziara yake, akizungumza na viongozi wa mashina na matawi wa Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Katibu Mkuu huyo wa CCM, alisema Chama Cha Mapinduzi hakijengwi katika majukwaa, bali hujengwa kuanzia ngazi ya mashina na matawi, huku akibainisha majukwaa hutumika zaidi kwa ajili ya kutoa hamasa.

“Mashina ndiyo moyo wa CCM kwa kuwa ndiyo yanayokutanisha chama na wananchi moja kwa moja kupitia vikao na shughuli mbalimbali za kijamii na kisiasa, amesisitiza Dk.Migiro, anayeendelea na ziara yake mkolani Dar es salaam yenye kauli mbiu ShinaLakoLinakuita.


NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WAKALA wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), imekamilisha matengenezo ya kivuko cha MV Kazi ambacho kilileta hitirafu mwanzoni mwa mwezi huu, kinatarajiwa kuanza kazi hapo kesho Januari 13, 2026 mchana.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari, Kaimu Mtendaji Mkuu TEMESA, Mosses Mabamba, amesema ukarabati wa kivuko hicho umechukua siku nne na kugharimu jumla ya shilingi milioni 30.

Ameeleza kuwa kazi hiyo imelenga kuhakikisha usalama na ufanisi wa huduma kwa wananchi wanaotegemea kivuko hicho.

"Majaribio ya kivuko hiki (MV Kazi) yatafanyika kesho asubuhi, na kuanzia majira ya saa nane mchana, kitaanza rasmi kutoa huduma kwa wananchi wa eneo la Feri na Kigamboni na kuweza kupunguza changamoto". Amesema

Aidha, Mabamba amebainisha kuwa kwa sasa kivuko cha MV Kazi kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 20 kwa safari moja, hatua inayolenga kupunguza msongamano na kurejesha hali ya kawaida ya usafiri katika eneo hilo.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wanaotumia kivuko hicho wamesema kurejea kwa huduma ya MV Kazi ni faraja kubwa kwani itarahisisha shughuli zao za kila siku, ikiwemo kwenda kazini, shuleni na katika shughuli za kibiashara.

Hata hivyo, wameitaka Serikali kuendelea kuboresha huduma za vivuko ili kuepuka adha zinazojirudia.

Wakati huo huo, Serikali imeweka mpango wa muda mrefu wa kuboresha usafiri wa majini kwa kuendelea na ukarabati wa kivuko cha MV Magogoni, kinachotarajiwa kuanza kutoa huduma mwezi Aprili.

Kivuko hicho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 2,000 na magari 60 kwa safari moja, hatua inayotajwa kuonesha dhamira ya Serikali katika kuboresha miundombinu ya usafiri wa majini na kuhakikisha wananchi wanapata huduma salama, ya uhakika na endelevu.




Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akiongea na wadau mbalimbali wa kongani ya Buzwagi wakati wa ziara hiyo

Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi akiongea wakati wa ziara hiyo.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya (Kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda (katikati) na Meneja wa ufungaji mgodi wa Barrick Buzwagi-Mhandisi Zonnastraal Mumbi.

Mkuu wa wilaya ya Kahama,Frank Nkinda akiongea wakati wa ziara hiyo.


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya akitembezwa katika maeneo mbalimbali ya Kongani ya Buzwagi.
**


#Yaipongeza Barrick kwa kufunga mgodi kwa viwango bora


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Dkt. Pius Stephen Chaya, amesema kuwa Kongani ya Viwanda ya Buzwagi Special Economic Zone inatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa Mkoa wa Shinyanga na Taifa kwa ujumla, kutokana na mpango wake unaotoa fursa mbalimbali za uwekezaji.


Dkt. Chaya ameyasema hayo baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kutembelea kongani hiyo iliyopo katika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga ambapo pia ameipongeza kampuni ya Barrick kwa ufungaji wa mgodi wa Buzwagi kitaalamu na kufanya eneo hilo kuwa la kuvutia kwa wawekezaji.


“Nimefurahi kusikia kuwa eneo hili limetengwa miongoni mwa maeneo sita ya uwekezaji, ambapo mnapanga kujenga vyuo vya ufundi, makazi, viwanda na miundombinu mingine muhimu. Hivyo basi, Buzwagi ni eneo sahihi kabisa kwa uwekezaji na limepangiliwa vizuri na wadau wote wanaosimamia eneo hili ikiwemo kampuni ya Barrick,” amesema Dkt. Chaya.


Ameongeza kuwa azma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kuhakikisha Watanzania wanakuwa na maisha bora na amewataka wananchi kuchangamkia fursa hii ya kongani kubadilisha maisha yao.


“Serikali inapenda kuona Wananchi wa Kahama na Tanzania katika sekta zote ikiwemo , akina mama lishe, wasomi na hata wasiokuwa wasomi wanapata ajira na fursa za kipato kupitia uwekezaji huu mkubwa katika kanda hii ya ziwa”, amesisitiza.


Dkt. Chaya amewataka viongozi pamoja na wadau wote wa maendeleo kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja ili kutimiza dhamira na maono ya Mheshimiwa Rais.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda aliyekuwa katika ziara hiyo ameeleza kuwa Kongani ya Viwanda ya Buzwagi ina vigezo vyote vinavyohitajika kuwavutia wawekezaji, ikiwemo mazingira rafiki ya uwekezaji, eneo kubwa pamoja na uwepo wa uwanja wa ndege unaorahisisha usafiri.


“Serikali inaendelea kufungua wigo kwa ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini na kuongeza manufaa ya rasilimali madini kwa kutenga eneo hili maalum la uwekezaji la ulipokuwa Mgodi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu la Barrick Buzwagi lenye ukubwa wa ekari 1331, ni kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa za migodini na tayari viwanda sita vimekwisha jengwa huku wamiliki wa viwanda 15 wakionesha nia ya kujenga viwanda katika eneo hilo”, ameeleza.


Ametoa wito kwa watanzania kuchangamkia fursa zilizopo katika kongani hiyo ili kukabiliana na changamoto za ajira kwa manufaa ya mtu mmoja mmoja na manufaa ya taifa.


Awali Akieleza Utekelezaji wa Mchakato wa kikamilisha Kongani hiyo Meneja Ufungaji wa Mgodi wa Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi, amesema kwa sasa kuna mwitikio mkubwa kwa wawekezaji kuhitaji kuwekeza katika Kongani hiyo kutokana na kukidhi vigezo vyote vinavyovutia wawekezaji.

Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt. Tumaini Msowoya, amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Iringa kuwa makini na maisha ya chuoni kwa kujiepusha na ndoa za rejareja, makundi yasiyo na tija pamoja na tabia zinazoweza kuwavuruga kimasomo, huku akisisitiza umuhimu wa uzalendo na nidhamu binafsi.

Akizungumza wakati wa sherehe za kuwapokea wanafunzi wa mwaka wa kwanza, Dkt. Msowoya alisema licha ya wanafunzi kuwa na umri wa zaidi ya miaka 18 kisheria, bado wanapaswa kujiuliza iwapo ndoa au mahusiano ya kuishi pamoja ndiyo yamewaleta chuoni, au ni dhamira ya kutimiza ndoto zao za kielimu.

“Najua mna umri wa zaidi ya miaka 18 hivyo si watoto kwa mujibu wa sheria, lakini jiulizeni: je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wenu wanajua mmeoa au mmeolewa mkiwa hapa?” alihoji Dkt. Msowoya.

Aliongeza kuwa tafiti alizowahi kufanya kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu zimebaini kuwa wanafunzi wengi huishi na wenza wao kwa siri bila familia zao kufahamu, jambo alilolitaja kuwa ni hatari na linaloweza kuathiri mwenendo wa masomo na maisha ya baadaye.

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka kujiingiza katika makundi yasiyo na mwelekeo chanya, akisisitiza kuwa wasomi ndio tegemeo la maendeleo ya taifa.

Katika hafla hiyo, Dkt. Msowoya alimwakilisha Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa ambaye alikuwa mgeni rasmi. Mwipopo aliwapongeza wanafunzi hao na kuchangia shilingi milioni 2,000,000 kwa ajili ya kuwasaidia katika safari yao ya masomo.

Amesisitiza kuwa nidhamu, maamuzi sahihi na uzalendo ni misingi muhimu kwa mwanafunzi yeyote anayelenga kufanikiwa chuoni na katika maisha kwa ujumla.



 


NAFASI ya ushindi hii hapa na wakali wa Meridianbet ambapo kupitia promosheni ya Beti Online unaweza ukaondoka na Samsung A26. Weka dau lako kuanzia 5000 na ubashiri hapa.

Meridianbet inaendelea kuwa kinara katika kutoa promosheni zenye thamani halisi kwa wachezaji wake. Kupitia kampeni yake mpya, kampuni hii inaleta fursa murua kwa mashabiki wa mpira kushiriki bashiri za mechi za Ligi kwa dau la kuanzia shilingi 5,000 tu na kuingia kwenye droo ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A26. Hii ni ofa inayochochea ushindani, msisimko na thamani kwa kila mchezaji anayejiunga.

Meridianbet wanasema kuwa ili ujiweke kwenye nafasi ya kuondoka na simu janja hii hapa na uwe wa Kidigitali kabisa ni vyema ukabashiri mara nyingi zaidi kwani kufanya hivyo kunakuweka karibu na ushindi leo hii wa Samsung A26.

Ukiachana na promosheni hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kampeni hii inalenga kuongeza hamasa kwa mashabiki kufurahia mechi za Ligi wakiwa na matumaini makubwa. Kila ubashiri unaowekwa si tu unaleta msisimko wa kutafuta ushindi wa dau, bali pia msisimko wa kusubiri droo ya kujua kama wewe ndio mteule wa kupata simu mpya. Huku mashindano yakiendelea kila wiki, kila mchezaji anapata nafasi nyingi kadri anavyobashiri mara kwa mara.

Washindi wa promosheni hii watatangazwa kila Ijumaa ambapo ndio siku ambayo simu hutolewa hivyo usikae mbali na fursa hii kwani inakupa nafasi ya wewe kumiliki simu kali ambayo itakufanya uweze kuperuzi.

Kumbuka kuwa unapoingia kwenye mashindano haya ya kuwania Samsung A26, hutakiwi Kuturbo Mkeka wako au CASH OUT kwa namna nyingine haitahusika kwani inatakiwa usubiri jamvi lako limalizike.

Na kufanya hivyo kutakufanya ujiondoe kwenye mashindano kwani tiketi yako itahesabika kama batili. Hivyo subiri hadi mechi zote zikamilike ndipo uweze kuingia kwenye wachezaji ambao sio batili.



Takribani wanafunzi 600 katika kata ya Kalangalala wenye Hali ya chini wanakadiliwa kupata madaftari kwa ajili ya kuanza nayo msimu mpya wa masomo 2026.

Kata ya kalangalala Ina jumla ya shule za msingi 9 na shule za sekondari mbili  ambapo jumla ya wanafunzi 1640 katika kata hiyo wameandikishwa kuanza darasa la kwanza.

Muitikio huo wa uandikiashwaji umemuibua diwani wa kata ya Kalangalala Ruben Sagayika kugawa madaftari pamoja na kalamu kwa Wanafunzi wanaotarajiwa kufungua shule Januari 13.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo amesema zoezi la ugawaji wa madaftari litakuwa endelevu katika kata hiyo ili kuhakikisha Kila mtoto anafika shuleni akiwa na vifaa vya shule.

"Tutakuwa pia tunapitia kwenye mashule tunaangalia watoto ambao hawana sare za shule na kuwashika mkono ili Hawa watoto waweze kupata elimu Bora" alisema Sagayika.

Kaimu afisa Elimu kata ya Kalangalala Regina Kitau amesema kuwa zoezi la ugawaji madaftari litatoa motisha kwa watoto kufika shule.

Kwa upande wao wazazi wameshukuru uwepo wa zoezi kwani wameweza kupunguza mzigo wa maandalizi ya vifaa vya shule inayotarajiwa kufunguliwa kesho.









 


KARIBU kwenye dunia ya msisimko wa Super Heli. Meridianbet inakualika ujiunge na burudani isiyokoma huku ukichunguza nafasi zako za ushindi. Wiki mbili tu zimebaki hadi kilele cha promosheni hii, na kila sekunde inayopita inaongeza shauku na fursa zako za kushinda. Hii ni nafasi yako ya kupaa juu, kushinda, na kujipatia zawadi zisizopimika.

Super Heli ni mchezo unaokupa changamoto ya ujasiri na maamuzi ya haraka. Kila Jumatatu, mshindi mmoja huondoka na Samsung A26 mpya kabisa. Kila raundi unayoicheza ni nafasi ya kujiweka mbele na kushika nafasi hiyo ya mwisho.

Meridianbet haikuachi nyuma, kuna michezo mbalimbali ya kasino mtandaoni pamoja na mechi za kimataifa za kubashiri zenye odds bomba zinazokuongezea nafasi ya kuongeza kipato chako kila siku. Kujiunga ni rahisi! Tembelea meridianbet.co.tz au piga *149*10#.

Kadri unavyoendelea kwenye Super Heli, odds zinapanda na msisimko unakua. Wachezaji hodari wanajua siri ya ushindi, kucheza kwa ustadi na kwa wakati mwafaka. Kila mzunguko ni tiketi yako ya kuzipa nafasi zako za Samsung A26. Hii si tu mchezo ila ni safari ya ushindi inayokuletea msisimko wa kweli.

Ukiwa na akaunti ya Meridianbet, kila mchezo ni fursa. Cheza mara nyingi, ongeza nafasi zako za kushinda, na ujiunge na wale watakaotembea na Samsung A26 mpya. Super Heli ni mchanganyiko wa teknolojia, msisimko, na zawadi zisizo na kifani. Tembelea Meridianbet.co.tz sasa, chukua nafasi yako, na uweke jina lako kwenye historia ya ushindi.

NA WILLIUM PAUL, SAME. 

MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni amewataka wahandisi wa Halmashauri kuacha tabia ya kukaa ofisini na badala yake kushuka moja kwa moja kwenye miradi ya kimaendeleo, akisisitiza kuwaacha walimu wakuu wa shule na mafundi peke yao kusimamia na kujenga ni hatari kwa ubora wa ujenzi wa miradi na husababisha miradi kujengwa chini ya viwango.

Kasilda ameyasema hayo jana wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu katika Shule ya Msingi Hedaru.

Alisisitiza kuwa ni wajibu wa wahandisi wa ujenzi kushiriki kikamilifu katika kila hatua ya utekelezaji wa miradi ili kuepusha kasoro zinazoweza kujitokeza endapo mafundi na kamati za ujenzi wataachwa kufanya kazi bila usimamizi wa karibu wa wataalam.

“Niwasisitize sana wahandisi wa ujenzi wa Halmashauri kuhakikisha mnafika kwenye miradi inayotekelezwa mara kwa mara, msiwaachie mafundi na kamati za ujenzi peke yao, tunahitaji kila hatua ya ujenzi isimamiwe na wataalam, kwa kushirikiana na TAKUKURU, ili ushauri na marekebisho yafanyike mapema kabla mradi haujafikia hatua kubwa zaidi,” alisema Kasilda.





 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina.

Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee.

Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana

Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badala ya utaratibu wa maelekezo kutoka juu kwenda chini.

Alitumia pia kikao hicho kutoa rai kwa viongozi na wana CCM kuzingatia utaratibu wa kutoa maoni kuanzia ngazi ya chini kwenda juu.

“Nitoe wito kwa viongozi wetu tusifanye utaratibu wa kutoa amri kutoka juu kushuka chini maana uongozi mzuri ni lazima uanzie chini kwenda juu, yale tunayoyapata kutoka kwenye mashina, matawi ndio yatapanda juu kwa lengo la kukiimarisha chama chetu, alisema Dkt.Migiro.

Aidha, siku iliyofuata katika ziara yake, akizungumza na viongozi wa mashina na matawi wa Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Katibu Mkuu huyo wa CCM, alisema Chama Cha Mapinduzi hakijengwi katika majukwaa, bali hujengwa kuanzia ngazi ya mashina na matawi, huku akibainisha majukwaa hutumika zaidi kwa ajili ya kutoa hamasa.

“Mashina ndiyo moyo wa CCM kwa kuwa ndiyo yanayokutanisha chama na wananchi moja kwa moja kupitia vikao na shughuli mbalimbali za kijamii na kisiasa, amesisitiza Dk.Migiro, anayeendelea na ziara yake mkolani Dar es salaam yenye kauli mbiu 'ShinaLakoLinakuita'.



 

Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Kilimo Hai Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo (TOAM) linaratarajia kufanya Mkutano MKuu wa Nne Machi 3hadi Machi 5 ,2026 jijini Dodoma kwa ajili ya kujadili na wadau kuhusiana na kilmo hai nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Bakari Mongo amesema mkutano huo ulitakiwa kufanyika Januari mwaka huu lakini waliahirisha kutokana sababu mbalimbali na kuahidi malengo waliotaka yatafikiwa katika mkutano huo wa mwezi machi.

Amesema wadau wajitokeze katika kufanikisha mkutano huo kwa kutoa udhamini katika kukidhi matarajio ya kilamo hai nchini.

Mongo amesema Mkutano Mkuu huo unatarajia kuwa wadau 400 wakiwemo wakulima ,Watunga Sera,Watafiti ,Wasomi,Sekta Binafsi ,Vyama vya Kiraia pamoja na Wabia wa Maendeleo.

Mongo amesema kuwa mkutano huo ni fursa ya kubadilisha maarifa na uzoefu ili kuboresha mifumo endelevu ya uzalishaji wa chakula cha kutosha ,kulinda mazingira na kuongeza mazao kwa wakulima nchini.

Aidha amesema katika mkutano huo wataangalia maudhui ya Usalama wa Chakula na Lishe Mbinu na Teknolojia za Kilimo Ikolojia Hai na Ustamilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi ,Manufaa ya Kiuchumi ya Kilimo Ikolojia Hai kwa Wakulima ,Maendeleo ya Kiteknolojia na Mfumo ya Uzalishaji wa Chakula pamoja na Mazingiea ya Kisera na Mifumo katika kuendeleza Kilimo Ikolojia Hai.
Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI  wa kituo cha wanahabari watetezi wa rasilimali na taarifa – MECIRA, Habibu Mchange, amewataka Watanzania kuziangalia kwa macho makali kampeni za upotoshaji zinazofanywa mitandaoni zinazopelekea baadhi ya watu kutiwa hofu kiasi cha kukaribia kuamini uwongo unaosambazwa, ambao mara nyingi huendeshwa na akaunti bandia ni watanzania ambao wako ndani ya nchi na wengine wako nje nchi.

Akizungumza katika kipindi cha Kipima Joto kinachorushwa na ITV Ijumaa tarehe 9 Januari, 2026, Mchange alisema kuwa ukiingia mitandaoni utakachokiona na kinachoendelea unaweza ukafikiri nchi haipo au ina mapambano makali, wakati hali ilivyo mtaani na unayoyasoma ni vitu viwili tofauti kabisa akisisitiza kuwa kwa sasa wanasiasa wameacha kuweka nguvu katika kuwafikia wananchi ana kwa ana na badala yake wamehamishia nguvu zao mitandaoni.

Mchange alisema kuna watu hawalimi, hawafugi, hawafanyi kazi yoyote, lakini kutwa kucha wako mitandaoni kutukana, hao ndio wanaoonekana sana mitandaoni, wanapiga kelele, wanatukana na kushambulia, lakini hawaakisi hata kidogo uhalisia wa maisha ya Watanzania walio wengi.

Aliongeza kuwa mtaani hali ni tofauti kabisa, kwani watu wanakimbizana na maisha, wanatafuta riziki zao kwa amani, furaha na utulivu.

“Watu wanajibidiisha kila kukicha, kuhakikisha wanapata mkate wao wa siku, bila muda wa kupoteza kwenye makelele ya mitandaoni”. Amesema

Mchange anabainisha kuwepo kwa mkakati wa makusudi wa kutumia matusi ya mtandaoni kama mbinu ya siasa kupitia kaulimbiu ya “kupiga spana”, akieleza kuwa kaulimbiu hiyo imetumika kuhalalisha kutukana, kubeza na kushambulia watu wenye mawazo kinzani, huku wahusika wakidhani wanajenga ushawishi wa kisiasa.

Mchange aliisema michezo hiyo inaratibiwa kwa pamoja na wanamitandao ambao wamefungiwa Nairobi na nchi nyingine, wakilishwa, wakilipiwa makazi na familia zao kuhudumiwa ili kazi yao kubwa iwe ni kutengeneza hofu kwa jamii ya Watanzania waliopo ndani ya nchi kupitia uwongo na propaganda zinazosambazwa mitandaoni pamoja na wenzao waliopo ndani ya nchi

Amebainisha kuwa kelele nyingi za mitandaoni hazina uhusiano na maisha halisi ya wananchi, na kwamba mitandao imejaa sauti za watu wachache wasiokuwa kwenye uhalisia wa nchi wanayoizungumzia akisisitiza kuwa mitandao ya kijamii si kioo cha maisha ya Watanzania, na kwamba uhalisia wa maisha uko mtaani, mashambani na kwenye shughuli halali za kila siku za wananchi, si kwenye akaunti bandia, matusi na makelele yanayoendeshwa kwa maslahi ya watu wachache.
Na Mwandishi wetu, Mirerani
WAKAZI wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, kwa zaidi ya wiki moja wamelalamikia kutopata huduma ya maji ya kunywa, baada ya malori yanayouza maji hayo kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kudaiwa kuzuiwa.

Kwa zaidi ya miaka 20 wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wanatumia maji ya kunywa yanayouzwa na malori kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe.

Hivi sasa, baadhi ya wakazi wengine wa mji huo wanatumia maji ya visima vifupi na virefu na maji ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jiji la Arusha (AUWSA) Mirerani, kwa ajili ya matumizi mengine ikiwemo kunywa.

Baadhi ya wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, wakizungumza juu ya changamoto hiyo wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo kwani wanatumia gharama kubwa kupata maji ya kunywa

Mmoja kati ya wakazi hao, Andrew John amesema kwa zaidi ya miaka 20 walikuwa wanatumia maji ya kunywa yanayotoka Hai ila wanasikitishwa hivi sasa kupata zuio hilo.

"Tulikuwa tunategemea malori ya kina 'Rumba Kali' kwa ajili ya kununua maji ya kunywa ila wanadai wamezuiwa kuleta maji Mirerani bila sababu ya msingi," amesema.

Amesema maji ya Hai yamewasaidia kwa muda mrefu kwani ya kisima na mengine hayakati kiu yana chumvi na maji ya chupa ni gharama kutumia na familia.

"Hivi sasa kuna baadhi ya malori machache yamefanikiwa kuleta maji Mirerani ila ndoo moja ya lita 20 ya maji ya kunywa tunauziwa Sh2,000 badala ya Sh1,000 kama awali," amesema.

Mmoja kati ya wauza maji wa eneo hilo, Abdi Soka amesema watu wengi wameathirika kwa ukosefu wa maji kutokana na zuio la mkuu wa wilaya ya Hai, Hassan Bomboko.

"Wanaoleta maji na kutuuzia kupitia malori kutoka mji mdogo wa Boma ng'ombe wamedai kuwa DC wa Hai, Hassan Bomboko amezua malori hayo yasilete maji mji mdogo wa Mirerani," amesema Soka.

Meneja wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira jiji la Arusha (AUWSA) Mirerani, Fidelis Shayo ameeleza kwamba hata yeye amesikia changamoto ya maji hayo kutopatikana.

Shayo amesema AUWSA aihusiki kuzuia huduma ya maji kutoka maeneo mengine japokuwa mradi wao wa maji wa Mirerani unaendelea kutoa huduma kwa uhakika maeneo hayo yakiwa safi na salama.

"Maji ya AUWSA Mirerani ni safi na salama kwani yametibiwa kwa dawa, tunaendelea kuwasihi watu wa eneo hilo waendelee kutumia hata kwa kunywa ndiyo sababu serikali imetenga Sh4.3 bilioni kwa ajili ya mradi wa maji Mirerani," amesema Shayo.

Hata hivyo, mkuu wa wilaya ya Hai, Hassan Bomboko alipoulizwa kwa njia ya simu juu ya suala hilo alikataa kulizungumzia.

"Kama upo huko Mirerani waulize viongozi wa huko juu ya suala hilo," amejibu DC Bomboko na kukata simu.

Kwa upande wake, ofisi mtendaji wa mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani (TEO) Isack Mgaya amesema kwa sababu suala hilo lipo nje ya wilaya ya Simanjiro wameshindwa kuingilia kati.

"Tulipata taarifa kuwa uongozi wa Hai ulizuia maji hayo kwa madai kuwa ni machache ila tumefikisha suala hilo kwa mkuu wa wilaya ya Simanjiro Fakii Lulandala ili azungumze na uongozi wa Hai," amesema Mgaya.
NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

Mwanamke mmoja amefariki dunia baada ya gari aina ya roli lenye namba ya usajili T696 CLY kuacha njia na kumgonga mwanamke huyo katika maeneo ya mataa ya Mbezi kwa Msuguli Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mashahidi gari hilo liliacha njia likijarabu kuwakwepa madereva pikipiki ambao walikuwa maeneo hayo na kusababisha kumgonga mtu huyo na kufariki hapo hapo.









Top News