Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.
Na.Mwandishi Wetu-DODOMA
WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umeanzisha utaratibu mpya wa kupima utendaji wa madiwani kwa kuzingatia uwezo wao wa kuchochea ukuaji wa biashara katika kata zao hatua hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji na kuinua uchumi wa wananchi katika ngazi ya chini.
Hayo yamesemwa leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma ambapo amesema mfumo huo utazingatia idadi ya biashara mpya zinazoanzishwa pamoja na uwepo wa mazingira rafiki yanayowezesha wafanyabiashara kukua.
Amesema kupitia utaratibu huo, madiwani watahamasika zaidi kusimamia maendeleo ya biashara katika maeneo yao na kuhakikisha maafisa biashara wa halmashauri wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Aidha, Nyaisa amesisitiza kuwa ni wajibu wa madiwani kusimamia utekelezaji wa sheria za biashara, huku akionya dhidi ya uwepo wa shughuli haramu kama uzalishaji wa pombe bandia katika maeneo yao.
"BRELA inalenga kukuza biashara ndogondogo ili ziweze kurasimishwa, hatua itakayowawezesha wafanyabiashara kupata mikopo, kupanua shughuli zao na kufikia masoko mapana zaidi ndani na nje ya nchi."amesema Bw.Nyaisa
Nyaisa ameongeza kuwa vijana ndio kundi kubwa la wafanyabiashara nchini, hivyo kuna umuhimu wa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutumia ujuzi na elimu yao kujiajiri kupitia biashara endelevu.
Kwa mujibu wa takwimu za BRELA, kumekuwa na ongezeko kubwa la biashara katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, hali inayoashiria kuimarika kwa uchumi wa nchi.
Hata hivyo, amewahimiza wafanyabiashara kurasimisha shughuli zao ili kuongeza uwezekano wa kupata mikopo na kuepuka changamoto zinazotokana na mitaji isiyo rasmi.
Vilevile, amewashauri wamiliki wa biashara za kifamilia kuhakikisha wanawaorodhesha wanahisa wote wakati wa usajili ili kuepusha migogoro ya baadaye.
Katika hatua nyingine, Nyaisa amesema taasisi hiyo imeanza kufuatilia na kusajili bunifu zinazotokana na taasisi za elimu kuanzia ngazi ya chini hadi vyuo vikuu, hususan zile zinazolenga kuboresha shughuli za kibiashara.
Kwa upande wake, Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira, amesema mafunzo yaliyotolewa kwa madiwani yamewajengea uwezo wa kuelewa vyema taratibu za usajili wa biashara pamoja na aina mbalimbali za leseni.
"Madiwani sasa wana nafasi nzuri ya kuwaongoza wananchi kwa usahihi wanapohitaji kusajili biashara zao, hatua itakayosaidia kupunguza changamoto zilizokuwapo awali."amesema
Aidha, amefafanua kuwa leseni za biashara kundi “B” hutumika kwa biashara zinazofanyika ndani ya halmashauri moja, wakati leseni za biashara kundi “A” humruhusu mfanyabiashara kuendesha shughuli zake hadi ngazi ya kimataifa bila kutozwa tozo ya ziada za leseni za biashara kundi B.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma