VUNJO. 

MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Enock Koola amewapongeza walimu wa madrasa kwa juhudi zao za malezi ya kiroho na maadili kwa watoto na vijana kupitia elimu ya dini. 

Koola ametoa kauli hiyo leo alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya kuhifadhi Qur'an yaliyofanyika mji wa mdogo wa Himo ambapo aliwapongeza washiriki wote kwa nidhamu, juhudi na kujituma katika mashindano hayo muhimu kwa ustawi wa jamii.

Mbunge aliwahimiza vijana kuendelea kushikamana na misingi ya imani, kuzingatia masomo yao darasani pamoja na kuepuka makundi yenye mienendo hatarishi ili kujenga jamii salama na Taifa lenye kizazi chenye maadili mema.

Katika kuhitimisha hafla hiyo, Koola alikabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano, vyeti kwa washiriki wote, pamoja na zawadi maalum kwa walimu na majaji waliowezesha kufanikisha mashindano hayo.






 

Na Mwandishi Wetu,Kwimba

WATUMISHI wa sekta ya afya katika Wilaya ya Kwimba wamepatiwa nishati safi ya kupikia ya mitungi mikubwa ya gesi ya Oryx na majiko yake pamoja na kupatiwa elimu ya matumizi sahihi na salama ya nishati hiyo.

Mitungi hiyo ya gesi ya Oryx kwa watumishi hao wa sekta ya afya Wilaya ya Kwimba Februari wamepatiwa jana Februari 28,2026 wakati wa uzinduzi wa jengo la kisasa la kuhudumia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Wilaya hiyo na jengo hilo ya limejengwa kwa ufadhili wa Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kushirikiana na Keep a Child Alive (KCA)

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Benoit Araman ,Meneja Mafunzo wa kampuni hiyo Peter Ndomba amesema wamegawa mitungi ya gesi kwa watumishi hao wa hospitali Wilaya ya Kwimba kama sehemu ya kuunga mkono jitihada hizo za kuhudumia watoto njiti lakini pia kuendelea kuhamasisha nishati safi ya kupikia nchini kwa kundi hilo muhimu.

“Oryx Gas Tanzania pamoja na Doris Mollel Foundation tayari tuna mkataba wa miaka minne katika kuunga mkono juhudi zake kwa mtoto njiti na leo tunatoa mitungi 167 kwa wafanyakazi wote wa idara ya afya hapa Kwimba

“Unajua kwanini tunafanya hivyo?Tunajua watu wa idara ya afya ndio wanakutana na wagonjwa kwa mara ya kwanza,wao ndio wasomi na ndio watalaam ambao wanaweza kuelekeza wagonjwa jinsi gani ya kujiepusha na madhara ya kuni na mkaa.

“Hivyo tumeona ni muhimu kundi hili kulisapoti na kupitia ubia wetu sisi na Dorris Mollel Foundation tutaendelea kufanyakazi ndani ya miaka minne ili kwa pamoja tujue tumefikia hatua gani kwa nchi nzima,”amesema Ndomba .

Kuhusu mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya nishati ya kupikia ya gesi ,Ndomba amesema Oryx Gas lengo pia ni kuiwezesha kada hiyo ya sekta ya afya kuwa na uelewa mpana kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia ya gesi kisha wawe mabalozi kwa wananchi wengine wakiwemo wagonjwa.

“Tumeamua kutoa mafunzo haya kwasababu tunajua wananchi wanapopata matatizo ya kiafya wanakuja hospitali kwahiyo wale ndio wanakuwa watu wa kwanza kukutana na wananchi wenye matatizo.

Kwa upande wao watumishi wa sekta ya afya katika Wilaya hiyo wameishukuru kwa kupatiwa mitungi ya gesi pamoja na elimu ya matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia kwani wanaamini watakuwa mabalozi waziri wa kuelezea faida za kutumia nishati hiyo ya kupikia ambayo ni salama kiafya.

Akizungumza baada ya kupatiwa mitungi hiyo Dk.Makore Maro ameishukuru kampuni hiyo kwa kuwapatia mitungi ya gesi ambayo kwao itakuwa na tija kubwa huku wakieleza kwa sasa kupitia majiko ya gesi waliyopatiwa watatumia muda mfupi kuandaa chakula na hivyo kuwa na muda mwingi wa kuhudumia wagonjwa.

Wakati huo huo Maria Sakimu ambaye ni Muuguzi na Msimamizi Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba amesema wanashukuru kupatiwa nishati safi ya kupikia huku akieleza watakuwa mabalozi kwa wengine kuelezea umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia ya badala ya kutumia nishati chafu ya kupikia ya kuni na mkaa .



















Na Mashaka Mhando, Tanga

JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga linafanya uchunguzi wa ajali mbaya ya barabarani iliyosababisha kifo cha mgonjwa mmoja na kujeruhi watu wengine wanne, baada ya gari la wagonjwa (Ambulance) kugongana uso kwa uso na lori la mizigo.

Tukio hilo limetokea leo Machi 1, 2026, majira ya saa 6:10 usiku katika eneo la Saruji, Wilaya ya Tanga, kwenye barabara kuu ya Tanga kuelekea Segera.

Chanzo cha Ajali

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, ilisema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa ajali hiyo imetokana na uzembe wa dereva wa gari la wagonjwa. 

Inadaiwa kuwa dereva huyo alikuwa katika mwendo kasi uliompelekea kushindwa kulimudu gari hilo na kuhama upande wake wa kushoto na kuingia upande wa kulia, kisha kugongana uso kwa uso na lori.

Waliohusika na Madhara

Gari la wagonjwa lenye namba za usajili STM 7202, mali ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, lilikuwa likitokea Mombo kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Bombo likiendeshwa na Alphonce Alfan. 

Gari hilo liligongana na lori aina ya Scania (T 628 DSG) lililokuwa likitokea Tanga kuelekea Arusha likiendeshwa na John Philipo.

Katika ajali hiyo, mgonjwa aliyekuwa akisafirishwa, Zaharia Abrahaman Mdoe (41), mkazi wa Goha – Korogwe, amepoteza maisha.

Watu wengine wanne waliojeruhiwa na kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa matibabu ni:

 Zainabu Abrahaman Mdoe

 Seleman Hassan Mdoe

 Naiman Msofe Mdoe Hatibu Deusi Hatibu (Muuguzi aliyekuwa akimsindikiza mgonjwa).

Onyo la Polisi

Jeshi la Polisi limetoa wito mkali kwa madereva wote nchini kuzingatia sheria za usalama barabarani na kuepuka mwendo kasi pamoja na maamuzi hatarishi wanapokuwa barabarani.

"Tunawakumbusha watumiaji wote wa barabara kuwa usalama ni jukumu la kila mmoja," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga. 

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa ajili ya uchunguzi wa kitatibu na taratibu nyingine za kifamilia.




RAIS  Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekabidhi Tuzo za Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026 katika Hafla iliyofanyika Accra, Ghana tarehe 28 Februari 2026.

Tuzo hizo zinatolewa na Jarida la Africa Leadership Magazine linaloandaliwa na Taasisi ya Uongozi Afrika (Africa Leadership Organisation) ambayo Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Bodi yake ya Ushauri.

Mshindi wa Jumla wa Tuzo hizo ni Rais John Dramani Mahama wa Ghana, ambaye ametunukiwa Tuzo ya Mwafrika wa Mwaka kwa Mwaka 2026 kwa kutambua mchango wake katika kukuza demokrasia na uchumi nchini Ghana pamoja na kuwa kinara katika kuimarisha utengamano wa kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA).

Akihutubia kabla ya kukabidhi Tuzo hiyo ya mshindi wa jumla, Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ameeleza kuwa "kila kizazi za uongozi hukutana na changamoto za kipekee za wakati wake na hivyo hulazimika kubuni njia za kipekee za kuzitatua". Akaongeza kuwa "kipimo mojawapo cha mafanikio katika uongozi ni kuweza kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuboresha hali ya jumla ya kimaisha kwa watu unaowaongoza kutoka hali ya chini kwenda hali ya juu zaidi".

Mbali na Rais Mahama, miongoni mwa watu mashuhuri waliiopata Tuzo hizo ni pamoja na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Lesotho, Samuel Matekane aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi nchini Lesotho pamoja na Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuliimarisha jeshi la Uganda na kukuza diplomasia ya kijeshi katika ukanda wa maziwa makuu.

Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah alipata Tuzo ya Kiongozi Bora wa Kisiasa Afrika huku Makamu wa Rais wa Angola Esperança da Costa, Makamu wa Rais wa Angola akioata Tuzo ya Kiongozi Bora Mwanamke barani Afrika.

Tuzo ya Rais Mahama ilipokelewa kwa niaba yake na Mwanasheria Mkuu wa Ghana, ambaye pia ni Waziri wa Sheria wa Ghana, Dominic Akuritinga Ayine wakati tuzo ya Jenerali Kainerugaba ilipokelewa na Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda, Kanali Chris Magezi.

Kila mwaka Jarida la Africa Leadership Magazine huratibu mchakato wa wazi unaojumuisha kupokea mapendekezo ya viongozi mbalimbali wenye sifa ambao hupigiwa kura kwa njia ya mtandao ili kupata washindi. Viongozi wa tasnia mbalimbali zikiwemo uongozi wa kisiasa, diplomasia, biashara na uwekezaji, ujasiriamali, habari, ulinzi na usalama, nk., wanaoshinda hupokea Tuzo hizo kwa kutambua mchango wao katika kusimamia vizuri tasnia zao pamoja na kulea na kuwaandaa vijana wanaowaongoza ili kuja kuwa viongozi bora wa baadaye.

Katika hafla hiyo, jumla ya Tuzo 36 zilitolewa.



CHAMA cha Waandishi wa Afrika (Pan African Writers Association – PAWA) kinatarajia kuzindua kitabu kipya kinachomuenzi aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Vitabu ya Conakry yatakayofanyika Aprili 2026 nchini Guinea Conakry. Chapisho hilo linaadhimisha maisha na uongozi wa Magufuli kufuatia kifo chake tarehe 17 Machi 2021, na linakusanya mitazamo mbalimbali ya Waafrika kuhusu mchango wake wa kisiasa na athari za uongozi wake.

Kitabu hicho ni mkusanyiko wa mashairi na insha zilizoandikwa kwa lugha za Kiingereza, Kifaransa na Kiswahili na waandishi 46 kutoka nchi 27 za Afrika pamoja na diaspora ya Kiafrika. Kimehaririwa na Rais wa PAWA, Profesa Bill Ndi wa Chuo Kikuu cha Tuskegee nchini Marekani, na ni kitabu cha tatu katika mfululizo wa machapisho ya PAWA yanayowaenzi viongozi mashuhuri wa Afrika. Machapisho yaliyotangulia yaliwahusu aliyekuwa Rais wa Ghana John Jerry Rawlings na mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi kutoka Nigeria, Profesa Wole Soyinka.

Kitabu hiki kinaangazia kupanda kwa Magufuli kisiasa na nafasi yake kama kiongozi na alama ya taifa, ambaye sera zake za mageuzi na mtindo wake thabiti wa uongozi viliacha alama kubwa katika maisha ya umma nchini Tanzania. Mashairi na insha zilizomo ndani yake zinachambua maono yake ya uongozi wenye nidhamu na kujitegemea, huku zikielezea falsafa ya kauli mbiu yake maarufu “Hapa Kazi Tu” kama ishara ya kujiamini kwa Waafrika na maendeleo yanayotokana na vipaumbele vya ndani.

Kupitia tafakuri za kifasihi na kitaaluma, kitabu kinamwelezea Magufuli kama kiongozi aliyepinga mifumo iliyokuwepo na kujaribu kuipa taifa mwelekeo mpya. PAWA inaweka urithi wake sambamba na viongozi mashuhuri wa Afrika kama Nyerere, Nkrumah na Mandela, huku uzinduzi wa Conakry ukiwa wa kwanza kabla ya uzinduzi mwingine katika nchi mbalimbali za Afrika baadaye mwaka huu.

Na Khadija Kalili, Kibaha
MKOA wa Pwani unaungana na Mikoa mingine nchini kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani tarehe 8 Machi 2026 maadhimisho hayo Kimkoa yatafanyika katika Uwanja wa Ujamaa wa Ujamaa, Kata ya Umwe, Tarafa ya Ikwiriri, Halmashauri ya Mji Rufiji.

Mratibu wa maadhimisho hayo Mkoa wa Pwani, Roseline Kimaro, amesema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge.

Kimaro amesema kuwa kaulimbiu ya mwaka huu inasema , “Haki kwa Wanawake na Wasichana: Msingi wa Maendeleo Jumuishi Dira 2050,” ambayo inalenga kusisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia na upatikanaji wa haki kama nguzo muhimu ya maendeleo endelevu ya taifa.

Amesema kuwa kuwa lengo kuu la maadhimisho hayo ni kutambua, kuthamini na kusherehekea mchango mkubwa wa wanawake katika nyanja mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi, sambamba na kuhimiza jamii kuendelea kusimamia na kulinda haki za wanawake na wasichana.

“Maadhimisho haya pia ni jukwaa la kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, pamoja na kuhamasisha ushiriki sawa wa wanawake katika fursa za maendeleo,” amesema Kimaro.

Kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa, maadhimisho yataanza rasmi Machi 1 hadi Machi 7 kwa kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii, zikiwemo utoaji wa elimu kwa umma, kampeni za uhamasishaji kuhusu usawa wa kijinsia, pamoja na shughuli za kijamii zitakazowahusisha wanawake na wadau wa maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo.

Kimaro ameongeza kwa kusema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri ili kuhakikisha kilele cha maadhimisho hayo kinafanyika kwa mafanikio na kufikisha ujumbe kwa jamii kwa upana zaidi.

Aidha amevitaka vyombo vya habari, taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho hayo, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za kuinua hadhi na kulinda haki za wanawake na wasichana katika Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, ijipange ipasavyo kuhakikisha kuwa inachangia upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 ambayo imeainisha kuwa na uwiano wa Pato la Taifa wa shilingi trilioni 1 ifikapo mwaka 2050.

Mhe. Balozi Omar alisema hayo alipokutana na kuzungumza na Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya TRA wakati wa ziara yake ya kikazi katika Mamlaka hiyo, ikiwa na mara yake ya kwanza Tangu ateuliwe na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya MUuungano wa Tanzania kushika wadhifa huo hivi karibuni.

Alisema kuwa Dira iliyomaliza muda wake iliitaka Tanzania kufikisha uwiano wa Pato la Taifa wa dola za Marekani bilioni 90 hadi kufikia mwaka 2025 lakini makadirio mapya yanataka kiwango hicho kifikie dola za Marekani trilioni 1 ambazo TRA inatakiwa kujipanga ipasavyo kufanikisha upatikanaji wa fedha hizo kwa kiwango cha asilimia 70 ili kutekeleza Dira hiyo ipasavyo.

Aidha, Mhe Balozi Khamis Mussa Omar, aliipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA kwa kuimarisha uhusiano wake na walipa kodi na kuitaka Manejimenti ya TRA kuhakikisha kuwa mchakato wa kudai kodi kwa hiari uendelee kuwa hivyo ili kuendeleza uhusiano na walipa kodu ambao wana mchango mkubwa wa kukuza Mapato.

Kuhusu udhibiti wa Walipakodi wasio waaminifu, Mhe. Balozi Omar, aliitaka TRA kuongeza jitihada za kudhibiti changamoto hiyo ikiwemo tabia ya baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kuingiza bishaa nchini wakidai zinaelekezwa nje ya nchi lakini zinachepushwa na kubakizwa nchini pamoja na udanyanyifu wa mauziano ya kibiashara (Price Transfer), hatua ambayo inakwaza maendeleo ya kiuchumi.

Kwa upande wao, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA, Bw. Yusuph Juma Mwenda na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, Bw. Uledi Abass Mussa, walimhakikishia Mhe. Waziri wa Fedha kwamba TRA imejipanga kuchangia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 kwa kuongeza ufanisi wa makusanyo ya forodha na kodi za ndani.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amehitisha ziara yake ya siku mbili ya kutembelea Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA jijini Dar es Salaam ambapo alitembelea na kujionea utendaji kazi wa Idara mbalimbali za Mamlaka hiyo pamoja na mifumo ya kidijiti inayotumika kurahisisha ulipaji kodi na taarifa kwa Walipakodi.





Meridianbet inakupa nafasi ya kubashiri mechi zako unazozitaka siku ya leo kwani nafasi ya wewe kuibuka ipo. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya kupiga pesa.

EPL kule Uingereza inatarajiwa kuendelea Fulham atakuwa nyumbani kucheza dhidi ya Tottenham Hot Spurs ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni mwneyeji aliondoka na ushindi hivyo siku ya leo ni nafasi kwa mgeni kulipa kisasi. ODDS KUBWA zipo mechi hii. Bashiri hapa.

Manchester United atamkaribisha kwake Crystal Palace ambao wanashika nafasi ya 13 huku vijana wa Carrick wakiwa nafasi ya 4. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kusogea juu kwenye msimamo wa ligi. Meridianbet imeweka machaguo zaidi ya 1000 kwenye mechi hii. Tandika jamvi hapa.

Mechi kali kabisa Uingereza itakuwa London Derby ya Arsenal vs Chelsea huku takwimu zikionesha kuwa The Blues mara ya mwisho kushinda mbele ya vinara hawa wa ligi ilikuwa ni 2021. Vijana wa Arteta wanahita ushindi kujiweka vyema kwenye mbio za ubingwa. Je nani kuondoka na pointi 3 hapa?. Beti sasa.

NB: Mbali na kubashiri mechi za kandanda, Meridianbet pia inakupa nafasi ya kucheza michezo ya kasino mtandaoni kama Aviator, Keno, Super Heli, ambapo unaweza kujishindia zawadi kama simu mpya aina ya Samsung A25. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Pia kule Hispania, LALIGA inatarajiwa kuendelea Valencia ataumana dhidi ya Osasuna ambapo tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni 7. Mechi ya mwisho kukutana kati yao mgeni aliondoka na pointi 3. Meridianbet wanakwambia kuwa hii ni nafasi ya wewe kuchukua mkwanja wako. Jisajili hapa.

Naye Real Betis atakiwasha dhidi ya Sevilla ambao wanashika nafasi ya 12 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo kujiweka sawa kwenye nafasi nzuri. Je beti yako wewe unaiweka wapi siku ya leo?. Tandika jamvi hapa.

Na mechi ya usiku kabisa itakuwa ni hii ya Girona dhidi ya Celta Vigo ambao wapo nafasi ya 6 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo. Je wewe unaiweka wapi beti yako siku ya leo?. Suka jamvi hapa.

Kule Ujerumani, BUNDESLIGA pia itaendelea VFB Stuttgart atamenyana vikali dhidi ya Wolfsburg huku tofauti yao hadi sasa ikiwa ni 23. Mwenyeji anahitaji ushindi leo ili aweze kuendelea kukaa nafasi 4 za juu kwenye msimamo wa ligi. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo kwenye mechi hii siku ya leo. Tandika jamvi hapa.

Halikadhalika naye Freiburg atakuwa ugenini dhidi ya Frankfurt ambao wanahitaji ushindi kwenye mechi hii siku ya leo. Mechi ya mwisho kukutana kati yao walitoa sare huku Meridianbet wakikupa nafasi kubwa ya kupiga pesa siku ya leo. Jisajili hapa.

Kwa upande wa RB Leipzig yeye atakuwa akisaka ushindi pia kule ugenini dhidi ya Humburger ambao leo hii wanataka kulipa kisasi baada ya kupoteza mechi ya mwisho walipokutana. ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo kwenye mechi hii siku ya leo. Suka jamvi hapa.

Kule SERIE A pia ligi kuu ya Italia kuna mechi za pesa Sassuolo atamenyana dhidi ya Atalanta huku tofauti ya pointi kati yao hadi sasa 10. Mgeni anaingia kwenye mchezo huu akiwa na kumbukumbu za kuchapika kwenye mechi yao ya kwanza kukutana kwenye ligi. Je anaweza akalipa kisasi siku ya leo?. Bashiri hapa.

Torino uso kwa uso dhidi ya Lazio ambao wapo nafasi ya 10 huku wenyeji wao wakiwa nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi. Kila timu inahitaji ushindi siku ya leo ili kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi. Nafasi ya kuondoka na ushindi ipo Meridianbet siku ya leo. Suka jamvi hapa.

Baada ya kupoteza mechi 5 kwenye mashindano yote, Juventus atakuwa ugenini kumenyana na AS Roma ambao wapo nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi. Wenyeji wana mwenendo mzuri kwenye ligi huku ushindi huu ukiwa ni muhimu sana kwao. ODDS KUBWA zipo kwenye mechi hii leo. Bashiri hapa.


Mkuu wa Idara ya Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience SOMG), Dkt. Emmanuel Kazimoto (wa pili kulia) akifungua mafunzo hayo ya siku ya pili ya kuwajengea uwezo wa wanafunzi wa mwaka wa nne wa chuo hicho kuhusu masuala ya madini na Jiolojia
Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

Mkufunzi wa kampuni ya Barrick, Dkt. Yann Mpaka akifundisha nadharia na vitendo mbalimbali ya jinsi ya kusoma ramani ya miamba kwenye mafunzo ya siku ya pili yaliyoratibiwa na Barrick kwa kushirikina na Shule ya Madini na Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mkufunzi kutoka Kampuni ya Barrick Dkt. Yann Mpaka akiwa kwenye mafunzo hayo ya weledi kwa wanafunzi wa Shule ya Madini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)



Mtaalamu kutoka Barrick, Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini

Mtaalamu kutoka Barrick , Ibrahim Kamage ambaye alihitimu katika shule hiyo mwaka 2023 akitoa mada kwenye mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na kampuni ya Barrick nchini

Baadhi ya wanafunzi wa mwaka wa nne wa Shule ya Madini na Sayansi ya Jiolojia (School of Mining and Geoscience) ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakifuatilia mafunzo kwenye semina hiyo ya kitaaluma iliyokuwa ikitolewa na watalaamu kutoka Kampuni ya Barrick nchini.


Sehemu ya wanafunzi wa mwaka wa nne wakifuatilia mafunzo hayo ya mambo ya madini na Jiolojia na hasa teknolojia inavyotumika kwenye migodi duniani , mafunzo hayo yalifadhiliwa na kampuni ya Barrick hapa nchini.

Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria masomo katika picha ya pamoja na wakufunzi.
**
#Yaja na programu ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa sekta ya madini UDSM


Kampuni ya Barrick nchini inaendelea kufanikisha dhamira yake ya kujenga kizazi kipya cha wataalamu wenye maarifa ya kisasa katika sekta ya madini kupitia Programu ya kuwapatia mafunzo wanafunzi wanaosoma shahada ya kwanza ya fani ya madini na jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kutumia wataalamu wabobezi na wenye uzoefu kutoka ndani ya kampuni.


Kupitia programu hiyo kwa kushirikiana na Shule ya Madini na Jiolojia (SOMG) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,wataalamu kutoka Barrick wameendesha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo katika tasnia ya madini na jiolojia wanafunzi wa mwaka wa mwisho kwenye shule ya madini.


Akizungumzia kuhusu mafunzo kupitia programu hii Mkuu wa Shule hiyo Profesa Elisante Mshiu, amesema yatakuwa ni endelevu kwa kubadilishana uzoefu na wataalamu katika tasnia kutoka Barrick kwa nia ya kuwapatia wanafunzi ujuzi , uelewa wa ndani na jinsi ya kukabiliana na changamoto katika sehemu za uchimbaji na utafiti wa madini kwenye miamba na chini ya ardhi.


Amesema progamu imelenga pia kuwaunganisha wanafunzi na wadau wakubwa katika tasnia ya madini kutoka sekta binafsi ili kuwajengea uwezo na kujiamini ili wanapomaliza masomo yao waweze kuhimili ushindani katika soko la ajira nchini na nje ya nchi na wengine kuweza kujiajiri kupitia taaluma walizosomea.


“Mafunzo haya zaidi yanawapa mwangaza wa aina ya kazi wanazotarajia kukutana nazo pindi wanapomaliza masomo yao , kujua ni kwa jinsi ya kufanya utafiti wa kujua kiasi cha madini kilichopo chini ya ardhi, miamba , namna bora ya kusoma ramani na kuwa na matarajio ya kitafiti na kisayansi zaidi kwenye fani ya Jiolojia,” ameongeza Profesa Mshiu.


Kwa upande wake , Mkuu wa Idara wa Shule hiyo ya Madini (SOMG) , Dkt Emmanuel Kazimoto amesema mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick ni fursa ya kipekee kwa wanafunzi wa mwaka wa nne katika shule hiyo katika kupanua uelewa wao kuhusu masuala ya madini , joto la ardhi na elimu ya miamba pamoja na matumizi ya teknolojia kwenye kufanya tafiti za madini chini ya ardhi.


Dkt. Kazimoto amesisitiza kuwa programu itaendelea kufungua milango zaidi wa wanafunzi wa chuo hapo kupenda zaidi masomo ya madini na Jiolojia kwa sababu ya kufundishwa na wadau ambapo wanatoka kweye makampuni makubwa ya uchimbaji madini hapa nchini kama vile Barrick.


“Muhimu ni kwamba wameshawaona wenzao ambapo wamepata kazi Barrick na wengine wamepata kazi nje ya nchini kwa hiyo ni muhimu waendelee kujifunza kwa vitendo zaidi jinsi ya kusoma ramani , ugunduzi wa kiasi ya hifadhi ya madini ambacho kipo chini ya ardhi , jinsi ya kupima joto chini ya ardhi na mambo mengine ya kitaalamu zaidi,” ameongeza Dkt. Kazimoto.


Amesema kwamba ni muhimu kuendelea kupanua wigo wa ushirikiano kati yao na wadau wa madini kama vile Barrick katika juhudi za kuifanya sekta hii ya madini si tu kwa ajili ya mapato ya nchini lakini pia kupanua mianya ya uelewa wa masomo haya kwa wanafunzi kutoka kizazi hadi kikazi kwa maslahi mapana ya nchini.


Mkufunzi wa mafunzo hayo, Dkt. Yann Waku Mpaka , Mjiolojia kutoka kampuni ya Barrick amesema umuhimu wa mafunzo yanayotolewa kupitia programu hii ni jinsi ya kubadilishana na kupeana uelewa , taarifa , ujuzi na uzoefu wa uchimbaji , utafutaji na utafiti kwenye sekta ya madini.


Dkt. Mpaka ameongeza kwamba kuna umuhimu wa kuwajengea uwezo wanafunzi kwenye maeneo ya utafiti , usomaji wa ramani za miamba na jinsi ya kujua joto la ardhi na namna bora ya kufanya shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini kwa njia ya kitaalam zaidi ambayo ni salama pia,na masuala mbalimbali yanayohusiana na tasnia ya madini.


Amesema kuna umuhimu wa kuendelea kuweka mkazo kwenye sayansi na teknolojia nadharia ya uchimbaji na tafiti za madini duniani zimebadilika, uwekezaji mkubwa kwenye vifaa na teknolojia vinawalazimu vijana kwenye sekta hii kujua hasa teknolojia ya kisasa kwenye tafiti na uchimbaji wa madini.


Ibrahim Kamage ambaye ni mtalaamu kutoka Barrick na ni mhitimu wa shule hiyo ya chuo kikuu ya Madini na Jiolojia mwaka 2023 alisema kwamba ni muhimu kwa wanafunzi hao kukuza uelewa wao wa mawasiliano na mahusiano kwa jamii.


“Katika fani Jiolojia ni muhimu kwa mtaalamu kujifunza jinsi ya kuwasiliana na watu mbalimbali kuanzia mafundi hadi wanakijiji kwenye maeneo ya uchimbaji ili kupunguza migogoro kwenye jamii na kuondoa dhana potofu kwamba sehemu za migodi ina migogoro na wananchi wanaozunguka migodi hiyo,” ameongeza Kamage.


Akizungumza kwa niaba ya wenzake , Paul Maghembe ambaye naye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne chuoni alisema kwamba mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa jinsi ya kusoma ramani za miamba , matumizi ya teknolojia na ukusanyaji wa data (takwimu) kwenye shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini.


Sarah Nestory Musembele ambaye anachukua shahada ya sayansi ya Jiolojia chuoni hapo alisema kwamba ni ndoto zake kwamba anataka kuwa na weledi na kuzingatia maadili ya kazi ya Jiolojia na kuleta mabadiliko kwenye sekta hiyo hapa nchini.

Top News