📍 Bilioni 15 kukamilisha ujenzi akademia ya michezo Malya


NA Mashaka Mhando, Iringa

SERIKALI imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 15 katika mwaka wa fedha 2026/2027 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Akademia ya Taifa ya Michezo iliyopo Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya.

Hatua hiyo ya kiserikali inalenga kuweka mfumo thabiti na wa kudumu wa kuibua, kulelea, na kukuza vipaji vinavyopatikana kupitia mashindano ya shule za msingi na sekondari (UMITASHUMTA na UMISSETA).

Hayo yamebainishwa jana, Juni 17, 2026, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), wakati akifunga rasmi mashindano ya UMITASHUMTA yaliyokuwa yakifanyika mkoani Iringa.

Mhe. Mwinjuma alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza kwa nguvu kubwa katika sekta ya michezo na sanaa, ikitambua mchango wake katika kuzalisha ajira, kujenga afya, na kuongeza ushindani wa Taifa kimataifa.

Malya Academy na Matunda ya Serengeti Boys

Akifafanua kuhusu matumizi ya Akademia hiyo ya Malya, Mhe. Mwinjuma alisema kituo hicho kitakuwa na uwezo mkubwa wa kupokea na kuendeleza vipaji vinavyogunduliwa kwenye mashindano ya shule, ili kuandaa kizazi cha dhahabu kitakachowakilisha Taifa.

Kuthibitisha ubora wa mashindano hayo, Naibu Waziri aliweka wazi matokeo chanya yaliyoonekana hivi karibuni kupitia Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).

"Mafanikio ya Serengeti Boys yameonyesha umuhimu wa kuendelea kuwekeza kwenye michezo ya shule. Wachezaji wasiopungua watano wa kikosi hicho, akiwemo golikipa namba moja, ni zao halisi lililotokana na mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA," alibainisha Mhe. Mwinjuma.

Maandalizi ya FEASSSA Morogoro

Aidha, Mhe. Mwinjuma alihitimisha kwa kueleza kuwa mashindano yaliyofungwa Iringa ni msingi muhimu wa kuandaa wawakilishi wa Tanzania watakaoshiriki Mashindano ya Michezo ya Shule kwa Nchi za Afrika Mashariki (FEASSSA).

Mashindano hayo makubwa ya kikanda yanatarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu mkoani Morogoro, ambapo Naibu Waziri amewataka wanamichezo wote waliochaguliwa kuunda timu ya Taifa kambi kufanya maandalizi kabambe ili kuitangaza vyema Tanzania na kubakiza makombe nyumbani.













Na Mwandishi Wetu

Serikali imesema Tanzania bado haina mgonjwa wa Ebola na imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ulinzi dhidi ya ugonjwa huo pamoja na kusaidia juhudi za kikanda za kudhibiti maambukizi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, amesema Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha nchi inabaki salama dhidi ya tishio la ugonjwa huo unaoendelea kuripotiwa katika baadhi ya nchi jirani.

Amesema miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni kuhakikisha upatikanaji wa kutosha wa vifaa kinga katika bohari za dawa, kusimika maabara mbili za ziada kwa ajili ya uchunguzi na upimaji wa wagonjwa wanaoshukiwa kuwa na Ebola, pamoja na kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na uchunguzi katika maeneo yote ya mipakani na vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, zaidi ya watu 45,000 wamefikiwa na mafunzo kuhusu njia za kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Ebola, hatua inayolenga kuongeza uelewa wa jamii na kuimarisha utayari wa taifa kukabiliana na mlipuko wowote utakaoweza kujitokeza.

Waziri Mchengerwa amesema Tanzania imeendelea kushiriki kikamilifu katika juhudi za kikanda za kupambana na Ebola, akisisitiza kuwa usalama wa afya wa nchi jirani ni sehemu muhimu ya usalama wa afya wa Tanzania.

Amesema kupitia uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania imeendelea kutoa ushirikiano kwa nchi jirani zilizoathirika na ugonjwa huo, ambapo tayari vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 500 vimetolewa kusaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Uganda katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Pamoja na hatua hizo, Serikali imefafanua kuwa haijafunga mipaka yake, bali imeimarisha mifumo ya udhibiti, uchunguzi na ufuatiliaji katika maeneo yote ya kuingilia na kutoka nchini ili kuzuia kuingia kwa maambukizi.

Aidha, Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa mafanikio katika mapambano dhidi ya Ebola yanahitaji ushirikishwaji wa wadau wote, ikiwemo sekta binafsi, mashirika mbalimbali na wananchi kwa ujumla, kwani jukumu la kudhibiti ugonjwa huo haliwezi kubebwa na Serikali pekee.





-Awataka watendaji kuacha mazoea katika utekelezaji wa majukumu.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wa Wizara ya Maji pamoja na Wakuu wa Mikoa wasimamie vizuri mitambo ya uchimbaji visima ili iweze kufanya kazi iliyokusudiwa.

Amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alinunua mitambo ya uchimbaji wa visima hivyo watendaji wachukue hatua na waache kufanya kazi kwa mazoea.

"Nielekeze Wakuu wa Mikoa yote pamoja na wizara, kusimamia ili mitambo ile iweze kufanya kazi iliyokusudiwa, ni kweli kuna baadhi ya maeneo ya tunaendelea endelea na ile tabia ya business as usual, sasa ili kufikia matokeo ya Dira 2050, ni lazima tufanye kazi business unusual, tuache kufanya kazi kwa kuchukulia vitu kimazoea mazoea", Ameelekeza Waziri Mkuu.

Dkt. Mwigulu ametoa maelekezo hayo leo (Alhamisi Juni 18, 2026) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Kwimba, Cosmas Bullala.

Mbunge huyo alitaka kujua kauli ya Serikali kuhusu ufanisi wa mitambo hiyo, ambapo Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema mitambo hiyo inaendelea kuchimba visima katika maeneo mbalimbali nchini. Ambapo kwa sasa unatekelezwa mpango wa uchimbaji visima 900.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Mwigulu amesema Serikali inatarajia kuanza kuwalipa kifuta jasho askari waliojitolea katika vita dhidi ya Idd Amin wa Uganda mwaka 1978-79.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Njombe, Deodatus Mwanyika aliyetaka kujua ni lini Serikali itawalipa kifuta jasho askari hao, ambapo Waziri Mkuu Mwigulu amesema tayari Serikali imefanya mabadiliko ya Sheria ambapo sasa askari hao wanatambulika kisheria kutokana na hapo mwanzo kutotambuliwa.

“Mheshimiwa Spika, Sheria za zamani zilikuwa haziwatambui wapiganaji wale, hasa hasa wapiganaji waliopata mafunzo ya muda mfupi, hivi tunavyoongea, kupitia tangazo la Serikali la mwezi wa 6, mwaka 2025, kuhusu mabadiliko ya Sheria ya mafao ya veterani, sasa imeshawatambua wapiganaji hao”, Amesema Dkt. Mwigulu.

“Mheshimiwa Spika, wapiganaji hao wataanza kulipwa na watalipwa kwa kuwa sasa hakuna kikwazo cha kisheria ambacho kilikuwa kinawakwamisha, na kile cha uhakiki, kwani wapiganaji hao wameshahakikiwa”, Amesisitiza Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu.



Na Byera Deus Bukoba

Walimu walioko kazini pamoja na vijana ambao hawakufanikiwa kuendelea na elimu ya juu wametakiwa kutumia fursa zinazotolewa na vyuo vya elimu ya ujuzi vinavyotoa mafunzo kwa njia ya masafa ili kujiendeleza na kupata maarifa mapya yatakayowasaidia kukabiliana na mtaala mpya wa elimu.

Wito huo umetolewa wakati wa mahafali ya nne ya wahitimu wa DC Polytechnic Education Institute College kilichopo Halmashauri ya Bukoba mkoani Kagera, ambapo jumla ya wanafunzi 908 walihitimu katika ngazi za shahada na astashahada katika fani mbalimbali zikiwemo ualimu, utawala, uongozi, mawasiliano, teknolojia na ufundi.

Akizungumza katika Kongamano la Wahitimu (Convocation) la chuo hicho, Mkurugenzi wa Huduma za Jamii kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Elieth Lulu Niwagila, alisema Tanzania kwa muda mrefu imekuwa ikitekeleza mfumo wa elimu uliolenga zaidi utoaji wa maarifa ya darasani, lakini kwa sasa serikali imefanya maboresho makubwa ya mtaala ili kuzalisha wahitimu wenye umahiri, ubunifu na uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali za jamii.

Alisema wataalamu wa elimu wamejiridhisha na mabadiliko hayo ya mtaala na kwamba walimu walioko kazini wanapaswa kujiendeleza ili kuendana na mahitaji ya mfumo mpya wa elimu.

“Niseme kwamba sisi kama wataalamu wa masuala ya elimu tumevutiwa sana na mabadiliko haya. Dunia imebadilika sana na kinachohitajika sasa ni ujuzi. Serikali imeamua kutoa elimu ya ujuzi kwa miaka 10; baada ya hapo mtoto akiona hawezi kuendelea, anaweza kujiajiri, na anayeendelea hadi chuo kikuu anaweza kuendelea na fani hiyo ya ufundi,” alisema Dkt. Niwagila.

Kwa upande wake, Meneja wa DC Polytechnic Education Institute College, Jackson Kailanga, alisema chuo hicho kinaendelea kutoa elimu katika fani mbalimbali kwa kuzingatia maboresho ya mtaala wa elimu yanayotekelezwa kupitia Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 pamoja na maboresho yake ya mwaka 2023.

Alisema maboresho hayo yanaweka mkazo katika elimu inayozingatia stadi za kazi, vitendo na mahitaji ya dunia ya sasa.

Kailanga alisema chuo hicho kinatoa fursa kwa watu walioko kazini ambao hawakupata nafasi ya kuendelea na elimu ya juu kwa kuwajengea uwezo na kuwapatia maarifa yanayowawezesha kuendana na mahitaji ya elimu ya sasa.

Aliongeza kuwa walimu walioko mikoani huunganishwa katika vituo maalumu vya mafunzo ambapo hupatiwa wataalamu wa kuwafundisha hadi wanapohitimu masomo yao.

Aidha, alisema chuo hicho kinawakaribisha vijana waliomaliza darasa la saba hadi kidato cha nne kujiunga na mafunzo ya ufundi katika nyanja mbalimbali ikiwemo ufundi wa magari, umeme na taaluma nyingine za kiufundi. Alisema wataalamu kutoka vyuo vya ufundi stadi vya VETA hushiriki katika kuwajengea uwezo wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho.

Alitoa wito kwa vijana kutokata tamaa kwani zipo fursa nyingi za kujiajiri kupitia ujuzi na ubunifu. Pia aliwataka walimu walioko kazini kuendelea kujifunza na kupokea maarifa mapya ili kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea katika sekta ya elimu.

Naye Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) Kanda ya Ziwa, Godfrey Michael, alisema mhitimu bora ni yule anayeweza kutumia maarifa aliyoyapata kuijenga jamii yake na kuharakisha maendeleo.

Aliwataka wahitimu kutumia elimu waliyoipata kama nyenzo ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii, kuongeza ujuzi unaohitajika kwa sasa, kuepuka vitendo vya rushwa na udanganyifu, na kuchangia utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu nchini.



Na Mwandishi wetu - Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Stella Mwaiswaga pamoja na Watumishi wengine kutoka Ofisi hiyo wameshiriki ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi tarehe 17 Juni, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi ni moja ya matukio katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kaulimbiu moja na kufanya maonesho ya kazi mbalimbali kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma ambapo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni.

Kwa mwaka huu Maadhimisho hayo yamebeba kaulimbiu isemayo; “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi wa Huduma Endelevu”.

 SAmbamba na hilo Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu inashiriki maonesho hayo huku ikitoa elimu mbalimbali kwa umma kuhusiana na shughuli za Wakala Serikali wa uchapishaji Tanzania, elimu kuhusu masuala ya Menejimenti ya Maafa, Watu wenye Ulemavu, Ufuatiliaji na Tathimini pamoja na Masuala ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.









Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma


Serikali ya Tanzania imefafanua uamuzi wake wa kuweka akiba ya fedha za kigeni ikiwemo dola za Marekani na dhahabu, ikieleza kuwa hatua hiyo inatokana na mabadiliko ya kiuchumi yanayoendelea kuikumba dunia.

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Dodoma na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, aliyetaka ufafanuzi kuhusu sera ya serikali ya ununuzi na uuzaji wa dhahabu pamoja na maslahi mapana ya taifa.

Dkt. Mwigulu amesema kuwa dhahabu sasa imejumuishwa rasmi katika mfumo wa akiba ya fedha za kigeni, kama ilivyo kwa dola za Marekani, na si bidhaa ya biashara ya kawaida inayotumika kwa matumizi ya kila siku ya kiuchumi.

Amefafanua kuwa mpango wa ununuzi wa dhahabu umeendelea vizuri na hadi sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na takribani tani 27 za dhahabu kama sehemu ya akiba yake ya taifa.

Aidha, Waziri Mkuu huyo amesisitiza kuwa dhahabu ya taifa haiuzwi kiholela, na akabainisha kuwa utaratibu wa uuzaji wake, pale inapobidi, hufanywa kupitia taasisi rasmi za fedha au kwa tangazo la umma kupitia magazeti ya serikali, si kwa watu binafsi.

Dkt. Mwigulu amewahakikishia wabunge kuwa hakuna uuzaji holela wa dhahabu unaofanyika, bali mfumo uliowekwa unalenga kulinda maslahi ya taifa na kuimarisha uthabiti wa uchumi wa nchi.





Na Mwandishi Wetu-DODOMA

Wizara ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji.

Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla.

“Tunatumia jukwaa hili kuwafikia wananchi moja kwa moja, kuwaeleza huduma tunazotoa na kuwahamasisha kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa kwa ujumla,” amesema Msabimana.

Katika maonesho hayo, taasisi zilizo chini ya wizara hiyo zimeendelea kutoa huduma mbalimbali, ikiwemo huduma za usajili wa biashara kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni Tanzania (BRELA), ambapo wananchi wamewezeshwa kupata huduma za usajili wa kampuni, majina ya biashara na alama za biashara kwa njia ya kidijitali.

Kwa upande wa Mamlaka ya Usajili wa Maghala Tanzania (ZAGARA), wananchi wanaomiliki au wanaotarajia kuendesha maghala wamepata elimu na huduma za usajili pamoja na leseni zinazotakiwa kisheria.

Aidha, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE ) kimetumia maonesho hayo kutoa taarifa za udahili na programu mbalimbali za masomo zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu na wajasiriamali wenye ushindani sokoni.

Vilevile, Wakala wa Vipimo umeendelea kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo katika biashara ili kulinda haki za walaji na kuimarisha uaminifu katika shughuli za kibiashara nchini.

Msabimana amesema kupitia maonesho hayo, zaidi ya wananchi 365 wamepata huduma za kuboresha mifumo ya biashara zao pamoja na taratibu za usajili wa lebo za bidhaa, hatua inayosaidia kuongeza ubora na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa upande mwingine, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), limeendelea kutoa taarifa kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Liganga, Mchuchuma na Soda Ash, inayotarajiwa kuwa kichocheo cha mapinduzi ya viwanda, ajira na ukuaji wa uchumi.

Msabimana amewahimiza wananchi kutembelea mabanda ya wizara hiyo katika maonesho hayo ili kupata huduma, elimu na taarifa sahihi zitakazowawezesha kuboresha maisha yao na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi shindani wa Tanzania.
Na Janeth Raphael MichuziTv

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itazindua rasmi Awamu ya Pili ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC II) ikiwa ni hatua muhimu ya kuendelea kusogeza huduma za msaada wa kisheria, elimu ya sheria na upatikanaji wa haki karibu na wananchi wote nchini bila ubaguzi. 

Kampeni hiyo ni utekelezaji wa maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, yanayolenga kuhakikisha kila mwananchi anapata haki kwa wakati, uelewa wa sheria na uwezo wa kutatua changamoto za kisheria zinazomkabili katika maisha ya kila siku.

Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria, Juma Zuberi Homera amesema Awamu ya Pili ya kampeni hiyo imejengwa juu ya mafanikio ya awali yaliyopatikana katika Awamu ya Kwanza iliyotekelezwa kuanzia Aprili 2023 hadi Juni 2025 katika mikoa yote 31 ya Tanzania.

 Alieleza kuwa kupitia kampeni hiyo wananchi wengi walifikishiwa huduma mbalimbali za kisheria zikiwemo elimu ya sheria, ushauri wa kisheria na usuluhishi wa migogoro, hatua iliyosaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza uelewa wa jamii kuhusu haki na wajibu wao.

Kwa upande wa Zanzibar, kampeni ya awali ilitekelezwa katika mikoa yote mitano ya Unguja na Pemba ambapo jumla ya wananchi 422,908 walinufaika na huduma hizo. Kati yao, wanaume walikuwa 213,723 na wanawake 209,185. 

Mafanikio hayo yameelezwa kuwa ni ishara ya umuhimu wa huduma za msaada wa kisheria katika kuimarisha amani, kupunguza migogoro na kuongeza uelewa wa sheria katika jamii.

Kutokana na mafanikio hayo, Serikali imeamua kuendelea na Awamu ya Pili ya kampeni hii ambayo inalenga kuwafikia wananchi wengi zaidi, hususan walioko maeneo ya pembezoni na vijijini ambako upatikanaji wa huduma za kisheria bado ni changamoto.

Kupitia awamu hii mpya, wananchi watanufaika na huduma mbalimbali ikiwemo masuala ya ndoa na talaka, mirathi na wosia, migogoro ya ardhi, haki za watoto, ukatili wa kijinsia, haki za wafanyakazi, usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala pamoja na huduma za usajili wa matukio muhimu ya maisha na upatikanaji wa nyaraka muhimu za utambulisho.

Uzinduzi wa kitaifa wa Awamu ya Pili ya MSLAC unatarajiwa kufanyika tarehe 20 Juni 2026 katika Viwanja vya Maonesho Dole vilivyopo Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Samia suluhu hasani na pia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi atakuwepo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali, taasisi za umma na binafsi, mashirika ya kiraia na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar.

Serikali imesema zaidi ya washiriki 15,000 wanatarajiwa kuhudhuria uzinduzi huo mkubwa, ambao pia utahusisha utoaji wa huduma kupitia mabanda maalumu katika wilaya za Mjini, Magharibi A na Magharibi B. Aidha, timu za wataalamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Kamisheni ya Ardhi, Jeshi la Polisi Zanzibar pamoja na Jumuiya ya Mawakili Zanzibar zitapita katika shehia mbalimbali kutoa elimu ya sheria, usuluhishi wa migogoro na huduma nyingine za kisheria kwa wananchi moja kwa moja.

Serikali imewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uzinduzi huo na kunufaika na huduma zitakazotolewa, ikielezwa kuwa kampeni hiyo ni fursa muhimu ya kuongeza uelewa wa sheria, kupunguza migogoro ya kijamii na kuimarisha amani na utulivu nchini. 

Aidha, imeelezwa kuwa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia inaendelea kuwa mfano wa ushirikiano imara kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha haki inawafikia wananchi wote kwa usawa.


Serikali ilitenga takribani shilingi bilioni 3 katika mwaka wa fedha 2025/2026 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya na uboreshaji wa miondombinu katika Wilaya ya Mbogwe, Mkoa wa Geita.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe, Edwin Bayona, ameyasema hayo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigela, kukagua miradi ya maendeleo wilayani humo.

Bayona ameeleza kuwa fedha hizo zimetumika kujenga shule mpya ya msingi, kuongeza mabweni kwa wanafunzi wa kike, pamoja na matundu ya vyoo.

Aidha, Mkoa wa Geita umepokea takribani walimu wapya 1000. Wilaya ya Mbogwe imepata walimu 115 wa shule za msingi na sekondari ili kuongeza kasi ya ufundishaji katika miradi inayoendelea.

Mkuu wa Mkoa, Martin Shigela, amesema ziara hiyo ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mkoa huo huku akiwapongeza wananchi wanaoendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika ujenzi wa miundombinu katika sekta ya elimu.




Nyuki wameonekana kuwa na umuhimu mkubwa mbali na uzalishaji wa asali, baada ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kueleza kuwa sumu ya mdudu huyo imekuwa ikitumika katika huduma ya udungishaji wa nyuki inayolenga kusaidia afya ya mwili, huku wananchi wakipatiwa elimu kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa nyuki.

Akizungumza katika wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea kufanyika Jijini Dodoma, Afisa Nyuki kutoka TFS, Brenda Mwakipesile, amesema ushiriki wao katika maonesho hayo umelenga kuwafikia wananchi kwa kuwapa elimu kuhusu nyuki, uhifadhi wao pamoja na huduma mbalimbali zinazohusiana na mdudu huyo.

Amesema huduma ya udungishaji wa nyuki imekuwa ikipata mwitikio kutoka kwa wananchi kutokana na uelewa unaoongezeka kuhusu matumizi ya sumu ya nyuki, ambapo tafiti zilizofanyika zimeonesha kuwa sumu hiyo ina mchango katika kuboresha afya ya mwili na kusaidia kuua bakteria, fangasi na virusi.

Mwakipesile amesema baadhi ya watu wenye changamoto za maumivu ya viungo, maumivu ya muda mrefu pamoja na uvimbe wamekuwa wakinufaika na huduma hiyo, huku TFS ikiendelea kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa uhifadhi wa nyuki.

Ameeleza kuwa huduma ya udungishaji wa nyuki imekuwa ikitolewa na TFS kwa kipindi cha miaka minne na wamekuwa wakipokea mrejesho kutoka kwa wananchi waliopata huduma hiyo, akitolea mfano mtu aliyekuwa akisumbuliwa na goita ambaye alipata huduma mwaka 2024 na kutoa mrejesho mzuri.

Amesema mbali na faida ya kupata asali, nyuki wana mchango mkubwa katika mazingira na afya, hivyo wananchi wanapaswa kuwa na uelewa mpana kuhusu umuhimu wa kuwahifadhi na kutumia fursa zinazotokana na mdudu huyo.

Ameendelea kuwaalika wananchi kutembelea banda la TFS katika Wiki ya Utumishi wa Umma ili kupata elimu kuhusu nyuki na huduma mbalimbali zinazotolewa na wakala huo, huku akibainisha kuwa huduma ya udungishaji wa nyuki itaendelea kupatikana katika Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Vikindu baada ya maonesho hayo.



Benki ya Absa Tanzania jana imeandaa semina ya ngazi ya juu kwa wawekezaji wa taasisi, ikiwakutanisha wadau muhimu kutoka kampuni za bima, taasisi za fedha ndogo, wasimamizi wa mifuko ya uwekezaji, madalali wa masoko ya fedha na mifuko ya hifadhi ya jamii kujadili mwelekeo wa uchumi wa Tanzania pamoja na mwenendo unaojitokeza katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Warsha hiyo, iliyowavutia wawakilishi kutoka taasisi zisizo za kibenki za huduma za kifedha, wadhibiti wa sekta na viongozi wa tasnia mbalimbali, ililenga kuwapatia wawekezaji maarifa ya vitendo kuhusu namna ya kukabiliana na mazingira ya uchumi wa dunia yanayozidi kuwa magumu kutokana na mabadiliko ya viwango vya riba, kuyumba kwa thamani za sarafu pamoja na hali ya kutokuwa na uhakika wa kisiasa na kiuchumi duniani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira, alisisitiza umuhimu wa maandalizi na kufanya maamuzi ya kimkakati katika mazingira ya masoko yanayobadilika kwa kasi.

“Mafanikio katika mazingira ya sasa hayategemei uwezo wa kutabiri kila mabadiliko ya soko. Kinachohitajika ni kuwa tayari, kulindwa na kuwa katika nafasi nzuri wakati mabadiliko yanapotokea,” alisema.

Bi. Irene alisema kuwa licha ya mabadiliko yanayoendelea katika uchumi wa dunia na wa ndani ya nchi, bado kuna fursa kwa wawekezaji watakaokuwa na taarifa sahihi pamoja na mikakati madhubuti ya usimamizi wa hatari.

Alisisitiza tena dhamira ya Absa ya kuendelea kuwasaidia wateja wake wa taasisi kupitia utaalamu wa masoko, suluhisho bunifu za kifedha na ushauri wa kimkakati.

“Jukumu letu kama mshirika wenu katika Masoko ya Kimataifa ni kuwasaidia kukabiliana na hali ya kutokuwa na uhakika, kusimamia hatari kwa ufanisi na kutumia fursa zilizopo kwa kujiamini na kwa usahihi,” alisema.

Warsha hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano na Shirika la Tanzania Reinsurance Corporation (Tan Re), ambapo mchango wake katika kuimarisha sekta ya bima na huduma za kifedha nchini kupitia usimamizi madhubuti wa hatari ulitambuliwa wakati wa hafla hiyo.

Mtaalamu huyo wa Masoko ya Fedha Kimataifa kutoka Absa pia alizipongeza taasisi za udhibiti, zikiwemo Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwa mchango wao endelevu katika kujenga imani ya washiriki wa soko na kuunga mkono ukuaji endelevu wa sekta ya fedha.

Tukio hilo pia lilinufaika na ushiriki wa wataalamu wa Absa kutoka masoko mbalimbali barani Afrika, waliohudhuria ana kwa ana na kwa njia ya mtandao, jambo lililoonyesha kuongezeka kwa muunganiko wa masoko ya fedha barani humo pamoja na umuhimu wa kubadilishana maarifa.

Wakati wa semina hiyo, washiriki walipatiwa mawasilisho kuhusu mwenendo wa uchumi mpana unaoathiri Tanzania na dunia kwa ujumla, mikakati ya kusimamia hatari zinazotokana na mabadiliko ya viwango vya ubadilishaji fedha za kigeni na viwango vya riba, pamoja na suluhisho za uwekezaji zinazolenga kuongeza faida ya uwekezaji huku zikizingatia viwango vya hatari vinavyokubalika kwa taasisi husika.

Kwa mujibu wa Absa, kikao hicho ni sehemu ya dhamira pana ya benki hiyo ya kuwawezesha wawekezaji kupitia taarifa na uchambuzi wa masoko unaoweza kutumika moja kwa moja katika kufanya maamuzi, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu na wateja wake wa taasisi.

Kikiwa kimeandaliwa chini ya Lengo la Benki ya Absa la “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, pamoja... Hatua moja baada ya nyingine,” semina hiyo ililenga kuwapatia wawekezaji maarifa na nyenzo zinazohitajika kufanya maamuzi sahihi katika mazingira ya soko yanayobadilika na kutumia fursa mpya zinazojitokeza ndani na nje ya Tanzania.

Mmoja wa washiriki katika semina hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ushauri wa Kifedha ya Exodus Advisory, Bw. Ramadhan Kagwandi alishauri kutokana na Athari za kiuchumi zinazotokana na majanga ya kidunia hususani suala la kupanda kwa bei ya mafuta akisema juhudi hazina budi kufanyika katika kufanya uwekezaji mkubwa katika matumizi ya nishati mbadala wa mafuta, hususani matumizi ya gesi.

“La pili serikali inapaswa kuangalia namna nchi yetu inaweza kuwa na akiba ya kutosha ya mafuta endapo tutahitai kuendelea kutumia nishati hiyo, lakini lingine likiwa ni suluhisho la muda mrefu kama nchi ni kuwa na Uchumi unaojitegemea, na hili naona serikali imeshalifanyia kazi katika Bajeti ya 2026/2026 ikionesha kuwa asilimia karibu 75 ya bajeti inategemea vyanzo vya ndani,” alisemwa Bw. Kagwandi.

Kwa upande wake mshiriki mwingine, Bw. Beatus Mlingi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Diamond Global Securities alitoa shukurani kwa Benki ya Absa kwa kuwa na ubunifu katika kuandaa semina hiyo, kwani imewasaidia kupata masuluhisho mengine ya jinsi ya kuweza kufanya biashara zao kwa ufanisi licha changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira (kulia), na Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Biashara kutoka Absa Group, Bw. Gerald Nana (kushoto) wakizungumza na baadhi ya washiriki kutoka taasisi kubwa za uwekezaji wakati ya warsha ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo ili kutoa mwelekeo wa kiuchumi wa ndani na nchi nyingine mbalimbali duniani, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.



Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira akizungumza na baadhi ya washiriki kutoka taasisi kubwa za uwekezaji, wakati akifungua rasmi warsha ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo ili kutoa mwelekeo wa kiuchumi wa ndani na nchi nyingine mbalimbali duniani, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Biashara kutoka Absa Group, Bw. Kabelo Bogopa akizungumza na baadhi ya washiriki kutoka taasisi kubwa za uwekezaji wakati ya warsha ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo ili kutoa mwelekeo wa kiuchumi wa ndani na nchi nyingine mbalimbali duniani, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

 Mkuu wa Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Elisia Temu (kulia) akizungumza na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Exodus Advisory, Bw. Ramadhani Kagwandi wakati ya warsha ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo ili kutoa mwelekeo wa kiuchumi wa ndani na nchi nyingine mbalimbali duniani, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.




Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira (katikati) akipiga picha ya pamoja na washiriki kutoka taasisi kubwa za uwekezaji na wafanyakazi kutoka benki hiyo hiyo, wakati ya warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Benki ya Absa, ili kutoa mwelekeo wa kiuchumi wa ndani na nchi nyingine mbalimbali duniani, iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Dar es Salaam, Juni 17, 2026 – Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), imewahimiza waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuendelea kuwasilisha kazi zao za kuwania Tuzo za Samia Kalamu 2026 kabla ya kufungwa kwa dirisha la maombi mwishoni mwa mwezi huu.

Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa hadi Juni 15, 2026, jumla ya kazi 624 zilikuwa zimewasilishwa kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, huku vyombo vya habari mtandaoni vikiongoza kwa idadi kubwa ya kazi zilizowasilishwa.

Takwimu zinaonyesha kuwa vyombo vya habari mtandaoni vimewasilisha kazi 276, sawa na asilimia 44 ya kazi zote zilizopokelewa. Magazeti yamewasilisha kazi 178 (asilimia 29), televisheni kazi 102 (asilimia 16), redio kazi 60 (asilimia 10), huku majarida yakichangia kazi nane pekee, sawa na asilimia moja ya jumla ya mawasilisho.

Waandaaji wa tuzo hizo wameeleza kuwa Samia Kalamu Awards zinalenga kuhamasisha ubora, weledi na uwajibikaji katika uandishi wa habari za maendeleo, kwa kutambua mchango wa wanahabari katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu masuala ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kazi zinazostahili kushindanishwa ni zile zilizochapishwa au kurushwa katika vyombo vya habari kati ya Julai 1, 2025 na Juni 30, 2026.

Aidha, waandishi na taasisi za habari zimekumbushwa kuwa dirisha la kuwasilisha kazi litafungwa rasmi Juni 30, 2026 saa 5:59 usiku, hivyo zinapaswa kutumia muda uliobaki kuhakikisha kazi zao zinawasilishwa kwa wakati kupitia tovuti rasmi ya tuzo hizo.

Tuzo za Samia Kalamu zilianzishwa mwaka 2025 na zimekuwa jukwaa muhimu la kutambua na kuenzi mchango wa waandishi wa habari katika kuendeleza taifa kupitia kaulimbiu ya “Kalamu kwa Maendeleo.”

Kwa mujibu wa waandaaji, waandishi na vyombo vya habari vinakaribishwa kuendelea kushiriki ili kuhamasisha uandishi wenye tija kwa maendeleo ya Tanzania.
 By Muhidin Issa Michuzi


IMAGINE a vibrant hub teeming with life, that is the essence of Mnazi Mmoja Garden, once the cornerstone of community life in Dar es Salaam, a place where gatherings flourished, nurturing camaraderie and social interaction.

Just take a stroll through the garden one day, and it will unveil to you its historical weight: monuments and statues narrating Tanzania’s struggle for independence, and the ground where national heroes held crucial political rallies. 

It will be a living history lesson, that is, if you are lucky enough to be allowed in.

Mnazi Mmoja Garden hosted the inaugural gathering of TANU, forerunner of the ruling CCM, in 1954, a meeting that helped fuel the fight for statehood. In 1961, the Uhuru Torch was first ignited here, symbolising the struggle for freedom. From 1969, the garden hosted Mashujaa Day, honouring national heroes each July 25th, until the ceremony moved to Dodoma in 2016. 


The Arusha Declaration, too, was launched from this spot in 1967, charting Tanzania’s path toward socialism and self-reliance.

But ask the people who grew up around its gates, and the garden’s story takes a more intimate turn, one of swings rusted into silence, ponds gone dry, and gates that no longer open for the public they were built to serve.

Shaaban Scotto, a Kariakoo businessman who came of age in the 1960s and 70s, remembers a Mnazi Mmoja that doubled as a child’s entire world. Afternoons spent on its swings, free to wander without a single locked gate in sight. It is a freedom, he says, that today’s children in the neighbourhood will never know.

For Omary Popat, a TAZARA train driver born and raised in Kariakoo, the puzzle is more procedural than nostalgic. He cannot understand why the entire southern section of the garden remains under lock and key year-round, sealed off from a community living within walking distance of it. A public garden the public cannot enter, he says, is a contradiction nobody in authority has bothered to explain.

Yussuf Issa, known around Kariakoo as “Jesse,” built a different relationship with the garden, one of music and light. As a younger man, he made a habit of photographing the fishpond, drawn back by its stillness, and rarely missed a concert held on its grounds. For him, Mnazi Mmoja was a living cultural venue, and its slow closure has meant the quiet disappearance of a stage that once brought the city together.

Siwazuri Kibwana, born and bred in Kariakoo, takes the most practical view. If littering and vandalism are the real concern, he asks, why not simply post mgambo (city militia) to guard the grounds, rather than locking the public out altogether? It is, in her telling, a problem of enforcement, not access.





Beyond its serene façade, the garden holds the secrets of a bygone era when it served as a symbolic demarcation line during colonial rule, separating Indian inhabitants to the east from Africans and Arabs to the west, and as a clandestine meeting ground for freedom-seeking forefathers. Under colonial laws banning political assemblies, those forefathers turned to traditional dances as cover for secret meetings, strategising for the future while escaping the watchful eye of the authorities. The famous drummer statue standing amid the garden’s fishpond endures as a symbol of that resilience and unity.

And yet, as Scotto, Popat, Jesse, and Kibwana all attest in their own way, the garden’s significance has been allowed to recede into the past tense.

Start with the Uhuru Torch Monument at the centre of the park, on the spot where, legend holds, a single coconut tree once stood, giving the garden its Swahili name, Mnazi Mmoja, “one coconut tree.” This monument, later the venue for National Heroes Day, is today inaccessible to the very public it was built to inspire. Even after the ceremonies moved to Dodoma, the entire middle and southern end of the garden remains off-limits, gates closed every day, leaving residents like Popat with more questions than answers.

The garden’s significance extends beyond politics. In 1952, Greek entrepreneur George Anautoglou established the Anautoglou Hall, an entertainment complex that heightened its cultural standing, the very kind of cultural life that drew a young Jesse to its concerts decades later. That hall is now the seat of the Ilala District Council. Nearby stands the Amtulabhai Clinic, commissioned by the Karimjee family, alongside the Mnazi Mmoja dispensary, now elevated to hospital status, together a quiet legacy of public service.


A stone’s throw from the dispensary’s gates sits a police post that, while helping maintain order, has inadvertently contributed to neglect of the nearby Independence Stream. The monument there, adorned with the national coat of arms, once delighted visitors with a hissing jet of water for every coin tossed into its pond, perhaps the very pond that once drew Jesse’s camera. Today, it too is a no-go area.

The disparity runs deeper still. A significant portion of the park’s northern end, once a verdant oasis, has been repurposed for celebratory gatherings, becoming a cacophony of exhibition booths and tents that trample the foliage. A VIP stand was even built facing east, leaving dignitaries to bear the full glare of the sun, a puzzling choice next to the well-placed stand on the southern side.

This speaks to Kibwana’s point: the issue may be less about whether the garden should be open, and more about how it is managed when it is.

As the garden grapples with these complexities, it stands as a microcosm of challenges facing public spaces nationwide, where history and modernity often find themselves at odds. For Scotto, Popat, Jesse, and Kibwana, that tension is not abstract; it is the swing once played on, the locked gate passed daily, the concert no longer attended, the simple question of why guards could not solve what a fence has not.

A comprehensive strategy is imperative to genuinely honour the garden’s heritage and unlock its potential, one that prioritises accessibility, sustainability, and a return to its original purpose.

Dear city fathers, are you reading this?


 

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupitia Idara ya Mambo ya Ndani (INAD), leo Juni 17, 2026 imeandaa Kongamano la Maadili lililowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali kujadili nafasi ya maadili katika kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kujenga utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari. Kongamano hilo ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya TRA yatakayofanyika Julai 1, 2026.

Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa TRA, Naibu Kamishna wa TRA, Bw. Mcha Hassan Mcha, amesema kuwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, taasisi hiyo imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato, huku maadili yakiendelea kuwa nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yake.

Bw. Mcha amesema TRA inaendelea kuwekeza katika mifumo na mikakati mbalimbali ya kuimarisha maadili kwa watumishi wake na walipakodi ili kujenga uaminifu, uwajibikaji na kuongeza kiwango cha ulipaji kodi kwa hiari.

“Maadili hujenga imani, na imani hujenga ulipaji wa kodi kwa hiari,” alisema Bw. Mcha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum, ameipongeza TRA kwa kuandaa kongamano hilo na kueleza kuwa maadili ni msingi muhimu wa maendeleo ya jamii na taifa. Amesema mafundisho ya dini yanasisitiza uadilifu, uwajibikaji na kufanya mema, huku ulipaji wa kodi ukiwa sehemu ya wajibu unaochangia ustawi wa wananchi na maendeleo ya nchi.

Naye Mkuu wa Evangelical Fellowship Church Tanzania, Askofu Charles Asher Howard, amesema maandiko matakatifu yanaelekeza waumini kutimiza wajibu wao kwa mamlaka halali, ikiwemo kulipa kodi. Amebainisha kuwa maendeleo ya Tanzania yanategemea mchango wa kila mwananchi, hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la pamoja linalopaswa kutekelezwa kwa uaminifu na uzalendo.

Viongozi hao wa dini wamepongeza hatua ya TRA ya kuwashirikisha katika mijadala ya maadili na ukusanyaji wa mapato, wakisisitiza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za umma na viongozi wa dini una nafasi muhimu katika kuhamasisha wananchi kulipa kodi kwa hiari na kujenga taifa lenye uwajibikaji, uadilifu na maendeleo endelevu.


Top News