Na George Maziku, Kahama
 
DIWANI wa Kata ya Majengo, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, wilayani Kahama, mkoa wa Shinyanga Shida Zacharia Soko amechangia chakula chenye thamani ya zaidi ya milioni 6 kwa ajili ya wanafunzi wanaosoma kwenye shule tatu zilizopo kwenye kata yake.
 
Chakula hicho amekitoa juzi katika mkutano wa wazazi wa wanafunzi wanaosoma katikà shule tatu za Mama Samia Sekondari, shule ya msingi Anderson Msumba na shule ya msingi Majengo.
 
Mkutano huo aliuitisha yeye mwenyewe kwa lengo la kuwahasisha wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Frank Nkinda. 
 
Diwani huyo alitoa gunia 45 za mahindi yenye thamani ya milioni 2925000, maharage kilogramu 600 zenye thamani ya Sh. milioni 1200000, Mchele kilogramu 600 zenye thamani ya 12000, na sukari kilogramu 600  zenye thamani ya Sh. 1200000.

Akitoa mchanganuo wa mchango huo wakati akiukabidhi kwa Mkuu wa Wilaya, diwani Soko alisema kila shule itapata gunia 15 za mahindi, kilogramu 200 za maharage, kilogramu 200 za mchele na kilogramu 75 za sukari.

"Mheshimiwa mkuu wetu wa wilaya hapa mbele yako kuna pakeji (package) tatu ya chakula kwa ajili ya watoto wa shule ya sekondari ya Mama Samia, mimi ni mzee wa pakeji tu, hayo ndio mapigo yangu. Pakeji kama hii nimetoa kwa shule mbili za msingi za Anderson Msumba na Majengo", alifafanua Soko.

Akipokea mchango huo, mkuu wa wilaya Nkinda alimpongeza diwani  Soko kwa moyo wake wa kujitolea na kumtaka aendelee na moyo huo wa huruma na kujali wanyonge.

"Nakupongeza sana mheshimiwa diwani kwa moyo wako wa kutoa kwa wanyonge, wewe unaweza kufikiri haya unayofanya kuwa mambo madogo lakini nataka nikuambie kuwa haya ni mambo makubwa sana, ninakuomba uendelee na moyo huo na Mungu atakulipa", alisema mkuu wa wilaya Nkinda.

Aliongeza kuwa, " Nami nakuunga mkono kwa kuchangia kilogramu 500 za mahindi ambazo nitazitoa leo hii baada ya zoezi hili la kupokea mchango wako", alibainisha Nkinda.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa wito kwa wazazi na wadau wengine wa maendeleo kuunga mkono juhudi za diwani Soko kwa kuchangia kwa wingi chakula cha watoto wao wanaosoma katikà shule hizo.

Diwani Soko amekuwa na utaratibu wa kuchangia chakula kwa wanafunzi wanaosoma katika shule tatu za kata yake tangu achaguliwe kushika wadhifa huo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, 2025.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wazazi waliohudhuria mkutano huo waliunga mkono mpango wa kuchangia chakula cha wanafunzi ili kuwasaidia watoto kufuatilia vizuri masomo kutoka kwa walimu wao.
" Ni jambo zuri sana kwasababu itawasaidia watoto wetu kusoma kwa utulivu na kuelewa wanachofundishwa na walimu wao. Mimi nitachangia na ninawashauri wazazi wenzangu kuchangia kwa ajili ya ustawi wa watoto wetu", alisema Zuhura Rashid Salum ambaye ni mzazi wa mwanafunzi anaesoma shule ya msingi Majengo.

Naye Diana James aliyejitambulisha kuwa mzazi wa mwanafunzi anaesoma shule ya msingi Anderson Msumba alikubaliana na Mpango huo na kuahidi kuchangia.

"Mpango huu ni mzuri na muhimu sana kwasababu njaa ni mbaya, mtoto mwenye njaa hawezi kuzingatia kikamilifu masomo yake, hata sisi watu wazima hatuwezi kufanya kazi tukiwa na njaa, Mimi nipo tayari kuchangia chakula kwa mtoto wangu", alisema mzazi huyo.

Mkuu Wa Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga Frank Nkinda akiwa katikà mkutano wa  hadhara wa wazazi ulioitishwa na diwani Wa Kata ya Majengo Zacharia shida Soko
Magunia 15 ya Mahindi yaliyotolewa na diwani Soko kwaajili ya Chakula katikà shule ya Sekondari Samia iliyopo Kata ya Majengo Manispaa ya kahama

Wazazi Wa wanafunzi Wa shule tatu zilizopo katikà Kata ya Majengo
Diwani Wa kata ya Majengo Zacharia SOKO akifuatilia hotuba ya mkuu Wa wilaya
 



Na Mwandishi Wetu
TAASISI ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua mfumo wa kidijitali wa usajili wa wagonjwa na teknolojia mpya ya kisasa ya Dozee ya kufuatilia hali ya mgonjwa hata kiwa nyumbani.

Uzinduzi huo ulifanyika jana jijini Arushwa ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini,Paul Makonda.

Alisema uwekezaji huo unaifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoendelea kupiga hatua barani Afrika katika matumizi ya ubunifu wa kidijitali kuboresha huduma za matibabu na kutekeleza malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Makonda alisema matumizi ya teknolojia katika usajili wa wagonjwa, utunzaji wa kumbukumbu za kitabibu na ufuatiliaji wa wagonjwa baada ya matibabu ni sehemu ya maono ya Serikali ya kujenga taifa lenye uchumi unaotegemea maarifa, sayansi na teknolojia.

Katika kambi hiyo, Taasisi ya Moyo Mfumo wa teknolojia unaojulikana kitaalamu kama Dozee, una uwezo wa kufuatilia hali ya mgonjwa kwa wakati halisi akiwa amelazwa hospitalini au baada ya kuruhusiwa kurejea nyumbani.

Dozee ni mfumo unaotumia kifaa maalumu kinachowekwa chini ya godoro la mgonjwa na kufuatilia viashiria muhimu vya afya bila kulazimika kuunganisha vifaa vingi moja kwa moja kwenye mwili wake.

Dkt. Kisenge alisema mfumo huo una uwezo wa kufuatilia viashiria muhimu vya afya vya mgonjwa, vinavyojulikana kitaalamu kama vital signs, ikiwemo mapigo ya moyo, kiwango cha oksijeni kwenye damu na shinikizo la damu.

Alisema taarifa zinazokusanywa kupitia mfumo huo zinaweza kumfikia daktari kwa njia ya kidijitali, ikiwemo kupitia simu ya mkononi, hivyo kumwezesha kufuatilia mwenendo wa afya ya mgonjwa hata akiwa nje ya hospitali au anaendelea na shughuli nyingine.

Alifafanua kuwa teknolojia hiyo imelenga kusaidia kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika, hususan vinavyotokea baada ya hali ya mgonjwa kubadilika ghafla akiwa nyumbani baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

“Mara nyingi wagonjwa wanaporuhusiwa kwenda nyumbani, hali zao zinaweza kubadilika ghafla. Shinikizo la damu linaweza kushuka, mapigo ya moyo yanaweza kwenda kwa kasi sana au kiwango cha oksijeni kwenye damu kikapungua. Kupitia teknolojia hii, daktari anaweza kupata taarifa kwa wakati na kuchukua hatua mapema kabla hali ya mgonjwa haijawa mbaya,” alisema Dkt. Kisenge.

Alisema mfumo huo hautawanufaisha wagonjwa wa moyo na waliopata huduma za upasuaji pekee, bali unaweza pia kutumika kuwafuatilia wagonjwa wenye matatizo mengine ya kiafya.

Alitolea mfano wagonjwa wenye malaria kali, ambao wanaweza kupata mabadiliko ya ghafla ya mapigo ya moyo, shinikizo la damu na kiwango cha oksijeni kwenye damu.

Kwa mujibu wa Dkt. Kisenge, kufuatiliwa kwa viashiria hivyo kwa wakati kunaweza kuwasaidia wataalamu wa afya kubaini hatari mapema, kumfuata mgonjwa alipo, kumrudisha hospitalini inapohitajika na kumpatia matibabu sahihi.

Alisema uwekezaji katika mfumo huo unaifanya JKCI kuwa miongoni mwa taasisi zinazoongoza katika matumizi ya teknolojia za kisasa za kufuatilia wagonjwa, huku akieleza kuwa teknolojia ya aina hiyo inatumika pia katika nchi zikiwemo India na Marekani.

Dkt. Kisenge alisema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha huduma za afya za kibingwa na ubingwa bobezi nchini.


By TBN Staff Writer, London


Swahili Ambassador for Africa and former First Lady of Tanzania, Her Excellency Salma Kikwete, has underscored the vital role of the Kiswahili language in promoting unity, preserving culture and advancing social and economic development across Africa and the wider world.


She said Kiswahili has evolved far beyond its East African roots to become a language of regional integration and international dialogue, bringing together people from diverse cultures, backgrounds and nations. According to her, the language continues to serve as a powerful tool for fostering mutual understanding, strengthening cooperation and encouraging peaceful coexistence among communities.


Mrs Kikwete further noted that the growing use of Kiswahili on international platforms is clear evidence of its expanding global significance. She said its increasing adoption by international organisations, educational institutions and diplomatic forums demonstrates the language’s unique ability to bridge cultures while showcasing Africa’s rich linguistic and cultural heritage.


She made the remarks during a special celebration marking World Kiswahili Language Day, held at the House of Lords in London. The event was hosted following an invitation from Lord Paul Boateng, a Member of the House of Lords and a long-time supporter of stronger relations between the United Kingdom and Africa.


The celebration brought together diplomats, parliamentarians, academics, cultural leaders and members of the African diaspora to recognise the remarkable growth of Kiswahili from a regional lingua franca into one of the world’s fastest-growing international languages. Discussions focused on its contribution to education, diplomacy, trade, literature, media and cultural exchange, as well as opportunities to further expand its teaching and use worldwide.


Mrs Kikwete called upon governments, universities and cultural institutions to continue investing in the promotion of Kiswahili, describing it as an important vehicle for advancing African identity and strengthening international partnerships. She observed that as Africa assumes an increasingly influential role in global affairs, Kiswahili is well positioned to become a leading language of diplomacy, commerce, innovation and intercultural communication.


She also commended initiatives aimed at encouraging young people, both across Africa and within the diaspora, to embrace and preserve the language for future generations, saying such efforts are essential in safeguarding one of the continent’s greatest cultural assets.


The event at the House of Lords further reflected the growing international recognition of Kiswahili since UNESCO established World Kiswahili Language Day, celebrated annually on 7 July, making it the first African language to be officially recognised with a dedicated international day by the United Nations system.










 

Na Vero Ignatus, Michuzi TV-Arusha

Serikali imeeleza kuwa ina matarajio makubwa kwa Mawakili wa Serikali katika kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayolenga kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,

Matarajio hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya Mawakili wa Serikali yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia Julai 15 hadi 17, 2026.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Katimba amewataka Mawakili wa Serikali kuyatumia mafunzo hayo kuboresha utendaji wao wa kazi, ikiwemo kutoa ushauri wa kisheria, kuandaa na kupitia mikataba, kusimamia majadiliano ya kimkakati pamoja na kushughulikia mashauri kwa weledi na ufanisi.

Amesema Serikali inahitaji Mawakili wa Serikali wenye uwezo wa kuona mbali, kufikiri kimkakati na kutumia sheria kama nyenzo ya maendeleo ili kuhakikisha kila uamuzi wa Serikali unalinda maslahi ya Taifa, unakuza uchumi na kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Imani yangu kwenu ni kubwa kuwa ninyi mliohudhuria mafunzo haya mtakuwa sehemu ya kizazi cha Mawakili wa Serikali kitakachoiwezesha Taifa kufikia matarajio makubwa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050," amesisitiza Mhe. Katimba.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samwel M. Maneno, alisema mafunzo hayo yamewapa washiriki fursa ya kujadili na kujifunza masuala mbalimbali ya kimkakati yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi, ubunifu na ufanisi zaidi katika kulinda na kutetea maslahi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Maneno alieleza kuwa mafunzo hayo yalijikita katika usimamizi wa majadiliano na mikataba ya kimkakati, usuluhishi wa migogoro, ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP), usimamizi wa vihatarishi vya kisheria (Legal Risk Management), pamoja na matumizi ya Akili Unde (AI) katika taaluma ya sheria.

Aidha, aliwataka Mawakili wa Serikali kuendelea kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali (TPBA) 2026. 

Pia aliwasisitiza kusoma na kutafakari kwa kina kitabu cha Mama Samia Doctrine of Law ili kuelewa falsafa ya uongozi wa Rais na kuongeza kasi pamoja na ubora katika uchakataji wa masuala ya kisheria, hususan upekuzi na uandaaji wa mikataba kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maslahi ya Taifa.

Mafunzo hayo ya Bespoke 2026 yalifanyika chini ya kaulimbiu "Repositioning State Attorneys for Strategic Legal Leadership in Realizing Tanzania Development Vision 2050," yakihusisha Mawakili wa Serikali kutoka Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa (RS na LGAs) kwa lengo la kuimarisha uongozi wa kisheria katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.








Na Seif Mangwangi, Michuzi TV Arusha

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesema ina mikakati ya kuleta madereva kutoka visiwani humo kuja katika chuo cha ufundi Arusha (ATC), kujifunza ujuzi wa kuendesha magari tofauti ikiwemo ya viongozi na kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa wizara ya ujenzi na uchukuzi Zanzibar, Badria Atai Masoud, Julai16, 2026 alipofanya ziara katika chuo cha ufundi Arusha na kujionea mitambo mbalimbali inayotumika kufundishia wanafunzi chuoni hapo ikiwemo karakana ya magari.

Amesema katika ziara hiyo amegundua chuo cha ufundi Arusha kina ujuzi na uwezo mkubwa wa teknolojia ikiwemo matumizi ya umeme jua kuendeshea mitambo hivyo wataona namna ya kufanya ushirikiano na chuo hicho Ili kutoa msaada kwa madereva visiwani humo.

Aidha amesema amefurahishwa na ushirikiano unaoendelea kati ya chuo cha ufundi Arusha (ATC), na kampuni ya usafirishaji ya Abnan Transport and Logistic Ltd ambapo chuo hicho kinafundisha walimu wa madereva kupitia kampuni hiyo.

“ Zanzibar tumekuwa na ongezeko la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na ulemavu kwa watu wengi, tunaamini ushirikiano huu unaoendelea na ule ambao tutaufanya hapo baadae utasaidia kuepusha ajali,” amesema.

Wakati huo huo, Naibu Waziri Badria amesema Serikali visiwani humo  imeanza mchakato wa kuondoa matumizi ya magari ya mafuta ndani ya Serikali yake na  kuanza kutumia magari ya umeme.

Amesema Serikali ya Zanzibar imeanza kubadilisha mfumo wa injinia za magari yake na kutumia umeme, na kwamba mfumo huo umeanzia kwenye magari ya umma ya usafirishaji na baadae wataendelea kwa magari ndani ya Serikali.

“ Chini ya Rais Dkt Hussein Alli Mwinyi, tumeanza kutumia magari ya umeme hasa kwa magari ya usafiri wa umma, na tutaendelea hadi kwenye magari ndani ya Serikali, naamini tutawatumia sana chuo hiki,” amesema.

Awali Mkuu wa Chuo cha ufundi Arusha, Profesa Mussa Chacha alisema chuo chake kimeingia ushirikiano na taasisi ya Abnan Transport and Logistic Limited ambapo walimu kutoka ATC wako visiwani humo wakiwafundisha walimu na madereva kozinya udereva.

Profesa Chacha amesema chuo cha ufundi ATC kimeshaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 Kwa kuanzisha vitengo vitakavyotumiwa na wanafunzi kujifunza ujuzi mbalimbali kutokana na bunifu wanazozifanya chuoni hapo.

“ Tumeshaanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050, hivi sasa tunajenga karakana ambayo itatumika kutengeneza vipuri vya magari na mitambo na hapa wanafunzi wetu ndio watakuwa wakitumia mitambo hiyo kuzalisha, pia jengo hilo litakuwa na karakana ya kutengeneza fenicha mbalimbali, tutakuwa tunatengeneza na kuuza,” amesema na kuongeza:

“ Pia tunakamilisha jengo la hospitali ambalo mbali ya kutoa huduma Kwa wagonjwa wanafunzi na wengine kutoka, nje pia wale wanafunzi wanaotengeneza bidhaa za hospital watatumia nafasi hiyo kujifunza badala ya kusubiri Hadi waendesha field,” .





Sajenti wa Polisi (SGT) Noela Pallangyo, kutoka Jeshi la Polisi Nchini Tanzania ambaye kwa sasa anahudumu katika Misheni ya Kulinda Amani nchini Sudan Kusini chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), ametunukiwa Barua ya Pongezi kwa kutambua utendaji wake wa kipekee, weledi na mchango wake katika utekelezaji wa majukumu ya kulinda amani.

Amebainisha kuwa baada ya kupokea pongezi hiyo, SGT Noela ameweka wazi kuwa tuzo hiyo ni heshima kwake binafsi Pamoja na nchi yake na Jeshi la Polisi Tanzania huku akiwashukuru viongozi wake na askari wenzake kwa ushirikiano uliomwezesha , kufikia hatua hiyo ya kutunukiwa Barua hiyo.

Barua hiyo ya pongezi imetolewa kwa kutambua huduma yake ya mfano kwa kazi yake chini ya mwamvuli huo wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), ambapo aliweza pia kutekeleza majukumu yake kama Afisa wa Rasilimali Watu (Personnel Officer) katika Makao Makuu ya Mission Headquarters – (MHQ).

Katika barua hiyo, kutoka Umoja huo (UNMISS) imeeleza kuwa SGT Noela amehudumu kwa umahiri, bidii na weledi wa hali ya juu, huku akionyesha kiwango kikubwa cha ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake huku Misheni hiyo pia ikitambua mchango wake na umuhimu katika kufanikisha utekelezaji wa mamlaka ya (UNMISS) ya kulinda amani nchini Sudan Kusini.






Na Janeth Raphael - MichuziTv 

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) inaendelea kuthibitisha ubora wake kama moja ya vituo vinavyoongoza kutoa huduma za kibingwa barani Afrika, baada ya kufanikiwa kuwapatia matibabu ya upasuaji wa moyo watoto kutoka Nchini Burundi, ambao kwa sasa wanaendelea vizuri na wanatarajiwa kurejea nyumbani katika siku chache zijazo.

Mafanikio hayo yalidhihirika kupitia ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Gelasius Byakanwa, na Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Leontine Nzeyimana, waliotembelea hospitalini hapo kuwajulia hali watoto hao pamoja na wazazi wao, huku wakishuhudia kwa karibu ubora wa huduma za kibingwa zinazotolewa na Hospitali ya Benjamin Mkapa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, iliyofanyika leo  Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi, amesema hospitali hiyo imeendelea kujijengea heshima ndani na nje ya Tanzania kwa kutoa huduma za kibingwa zinazowanufaisha wananchi wa Tanzania pamoja na mataifa jirani.

Profesa Makubi ameeleza kuwa mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta ya afya pamoja na juhudi za wataalamu wa hospitali hiyo.

Aidha, alikumbusha kuwa mwaka jana timu ya madaktari wa Hospitali ya Benjamin Mkapa ilifanya kambi maalum ya matibabu nchini Burundi, ambapo ilitoa huduma kwa wananchi zaidi ya 2,000 na kufanikisha upasuaji kwa wagonjwa zaidi ya 50, hatua iliyozidi kuimarisha ushirikiano wa afya kati ya Tanzania na Burundi.

"Tunafurahi kuwaona Mabalozi wa Tanzania na Burundi mmetenga muda kuja kuwajulia hali watoto hawa. Watoto wote watatu waliofanyiwa upasuaji wanaendelea vizuri na wanatarajiwa kurejea nyumbani katika siku chache zijazo," alisema Profesa Makubi.

Pia alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya afya na kuziwezesha hospitali za nchini kutoa huduma za kibingwa zinazokidhi viwango vya kimataifa.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Gelasius Byakanwa, amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Burundi umeendelea kuimarika, huku sekta ya afya ikiwa miongoni mwa maeneo yanayoonyesha mafanikio makubwa.

Ameeleza kuwa Serikali za nchi hizo mbili zilishirikiana kuhakikisha watoto hao pamoja na wazazi wao wanapatiwa nyaraka za kusafiria kwa haraka, ambapo pasi za kusafiria zilipatikana ndani ya saa 24 ili kurahisisha safari ya matibabu.

Kwa upande wake Balozi wa Burundi Nchini Tanzania Leontine Nzeyimana, ameishukuru SerikalI ya Tanzania kwa kuwapatia matibabu watoto hao toka Burundi na ameomba ushirikiano huo uzidi kuendelea.




Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba amekagua maandalizi ya siku ya mashujaa yaliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali Mtumba Mkoa wa Dodoma.

Akizungumza mara maada ya kushuhudia majaribio ambayo yamefanywa na vikosi vya ulinzi na usalama amesema kuwa mpaka sasa mambo yanaenda vizuri na kupongeza maandalizi hayo.

"Nimekuja kujionea hatua ya maandalizi yanayoendelea kabla ya tukio letu kubwa na la kihistoria ambalo litafanyika tarehe 25/7/2026,, nikiri nimeridhishwa na maandalizi kufuatia taarifa ambayo tumepokea na kile ambacho tumejionea,,,.

Hapo awali Waziri wa Mambo ya Ndani kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi Mhe,Patrobas Katambi akisoma taarifa ya maandalizi amesema katika ya siku ya mashujaa tayari vipo vikundi mbalilimbali kutoka katika vyombo vya ulinzi na usalama.

Ameongeza kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya ulinzi na Usalama Mhe.Dkt Samia Hassan kwa maelekezo yake mahususi kwa ajiri ya kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi.

" Tunawahakikishia Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wako salama na kwa wageni wanaokuja kwa kufuata utaratibu nao wako salama,,.

Katika tukio hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule na wakuu wa vyombo ulinzi na Usalama wa Mkoa huu.









Na Mwandishi Wetu, Tabora

Wananchi wa mikoa ya Tabora na Katavi wameanza kushuhudia matokeo ya Mradi Shirikishi wa Uhifadhi wa Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame, huku shughuli za uhifadhi zikigeuka kuwa chanzo cha kipato, ajira na matumizi endelevu ya rasilimali za misitu.

Mafanikio hayo yamebainika wakati Kamati ya Wataalamu ya mradi ilipofanya ziara ya Julai 15 na 16, 2026 kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika maeneo ya mradi na kujionea namna zinavyowanufaisha wananchi.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi mbele ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora kabla ya ziara hiyo, Kaimu Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Dk. Zainabu Bungwa, alisema mradi umeanza kuleta mabadiliko yanayoonekana katika uhifadhi wa misitu na ustawi wa jamii kupitia uwekezaji kwenye shughuli za uzalishaji na maendeleo.

Alisema mradi umewezesha uanzishwaji wa vikundi vya wananchi vinavyojishughulisha na shughuli za kiuchumi, ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa magari na pikipiki kwa ajili ya usimamizi wa rasilimali za misitu, ujenzi wa maghala ya kuhifadhi mbegu za miti, mashamba darasa ya kilimo mseto cha misitu, ufugaji wa nyuki, maeneo ya malisho ya mifugo pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

“Tunaanza kuona matokeo chanya ya mradi katika maeneo mengi. Wananchi wanashiriki kikamilifu kwenye shughuli za uhifadhi huku wakiongeza kipato kupitia fursa zinazotokana na matumizi endelevu ya misitu,” alisema Dk. Bungwa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, John Gharuth Mboya, alisema mafanikio ya mradi yanapaswa kuambatana na uelewa wa pamoja wa viongozi wa mikoa na wilaya ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wake.

Alisema kuna umuhimu wa kuandaliwa taarifa ya kina itakayowasilishwa kwa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa na wilaya husika ili kuzijengea uelewa kuhusu malengo, mafanikio na mchango wa mradi katika maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Afisa Misitu wa Mkoa huo, Augustine Hildagadess, aliwataka wananchi kutenga maeneo rasmi ya malisho ya mifugo ili kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi na kuimarisha uhifadhi wa misitu.

Akizungumza baada ya kutembelea vijiji vya Mtakuja na Legezamwili wilayani Mlele, alisema wataalamu wa mradi wataendelea kushirikiana na vijiji kupanga matumizi bora ya ardhi yatakayolinda mazingira na wakati huo huo kukuza uzalishaji.

Katika ziara hiyo, Kamati ya Wataalamu iligawanyika katika makundi mawili. Kundi la kwanza lilikagua shughuli za mradi wilayani Sikonge, Kituo cha Ulinzi na Kituo cha Ufugaji Nyuki cha TFS Mlele pamoja na ofisi za viongozi wa Mkoa wa Katavi na Wilaya ya Mlele, huku kundi la pili likitembelea shughuli zinazotekelezwa katika wilaya za Urambo na Kaliua.

Mradi Shirikishi wa Uhifadhi wa Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame unafadhiliwa na Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa ushirikiano na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Mradi huo wenye thamani ya dola za Marekani 6,785,882 unatekelezwa kuanzia mwaka 2023 hadi 2027 ukiwa na lengo la kurejesha takribani hekta 34,000 za misitu ya miombo iliyoharibiwa, kuboresha maisha ya wananchi wanaoizunguka misitu na kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu.

Mbali na TFS na FAO, utekelezaji wa mradi unahusisha Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ICRAF, TARI, Wizara ya Maji, Wizara ya Mifugo, TAMISEMI pamoja na vikundi vya kijamii vinavyoshiriki katika shughuli za uhifadhi na maendeleo kwenye maeneo ya mradi.











Top News