Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Jengo la Tiba ya Mionzi kwa Wagonjwa wa Saratani katika Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC), hatua inayotarajiwa kuimarisha huduma za matibabu ya saratani na kupanua upatikanaji wa huduma za kibingwa nchini.
Uzinduzi huo uliofanyika katika hospitali hiyo iliyopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro umeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita za kuboresha sekta ya afya kwa kuwekeza katika miundombinu ya kisasa ya matibabu na teknolojia za huduma za kibingwa.
Jengo hilo jipya la tiba ya mionzi linatarajiwa kuongeza uwezo wa KCMC kutoa huduma za kisasa za uchunguzi na matibabu ya saratani, huku likipunguza changamoto ya wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo katika maeneo mengine ya nchi.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia amesisitiza dhamira ya serikali ya kuendelea kuboresha huduma za afya kwa wananchi kupitia uwekezaji katika vifaa tiba, miundombinu na rasilimali watu, ili kuhakikisha huduma bora zinapatikana karibu na wananchi.
Kukamilika kwa mradi huo kunatajwa kuwa hatua muhimu katika kuimarisha mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza, hususan saratani, ambayo imeendelea kuwa miongoni mwa changamoto kubwa za afya nchini.
Kwa kuanza kutumika kwa kituo hicho, wagonjwa kutoka Kanda ya Kaskazini na maeneo jirani wanatarajiwa kunufaika na huduma za tiba ya mionzi kwa urahisi zaidi, jambo litakalosaidia kuharakisha upatikanaji wa matibabu na kuongeza matumaini ya uponaji kwa wagonjwa wengi.










.jpeg)




































.jpeg)


.jpeg)