Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akizungumza wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, akisema JamiiAfrica inaamini kuwa bila taarifa sahihi hakuna maamuzi sahihi, ndiyo maana wanashirikiana na Ubalozi wa Uholanzi pamoja na UTPC kuhakikisha waandishi wa habari wanapatiwa mbinu bora za kuhakiki taarifa na kukabiliana na propaganda.

Picha ya kumbukumbu washiriki wa mafunzo

Na Mwandishi wetu - Geita

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi badala ya taarifa potofu, akisisitiza kuwa mapambano dhidi ya upotoshaji wa habari yanahitaji weledi, maadili na matumizi sahihi ya teknolojia.

Akifungua mafunzo maalum kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa Taarifa yaliyofanyika Jumatano, Februari 18, 2026 mjini Geita, Simbaya amesema katika dunia ya sasa yenye wingi wa taarifa, ni rahisi kwa jamii kupotoshwa iwapo waandishi hawatakuwa makini katika uchambuzi na uthibitishaji wa habari.

“Wananchi wanahitaji taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Jukumu la mwandishi ni kuhakikisha jamii inapata ukweli. Ndiyo maana tumeona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya. Nendeni mkatumie elimu hii kwa vitendo. Tunataka muandike habari zenye uwezo wa kubadili jamii na kujenga taifa,” amesema Simbaya.

Ameongeza kuwa UTPC inataka kuona waandishi wakiendelea kushikilia misingi ya maadili ya taaluma yao na kuandika habari zenye tija zisizopotosha umma.

Lengo kuu ni kuwajengea waandishi uwezo wa kukabiliana na changamoto za fake news, misinformation na disinformation ambazo zimekuwa tishio kubwa duniani.

Washiriki wamepatiwa mbinu mbalimbali za uthibitishaji wa habari, ikiwemo matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence – AI), kugundua asili ya picha na video, kulinganisha taarifa na vyanzo vinavyoaminika, pamoja na kusoma zaidi ya vichwa vya habari ili kuepuka kupotoshwa.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa “Ukweli Kwanza” unaolenga kuongeza weledi wa waandishi wa habari na kuimarisha uwezo wa wananchi kupambana na upotoshaji wa taarifa. Kupitia mradi huo, waandishi wanafundishwa mbinu za fact-checking, matumizi sahihi ya teknolojia na namna ya kutambua na kukabiliana na misinformation na disinformation.

Aidha, mradi huo unalenga kuwawezesha waandishi chipukizi, hususan wanawake, kuwa mstari wa mbele katika kulinda ukweli na kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari nchini.

Kupitia mafunzo haya, UTPC na wadau wake wanaamini kuwa waandishi wa habari wataendelea kuwa nguzo muhimu ya ukweli, uwazi na uwajibikaji katika jamii.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uholanzi.

UTPC pia imeshirikiana na taasisi ya JamiiAfrica katika kupata wataalamu wanaoweza kutoa mafunzo haya kwa weledi.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.

Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita




















Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) kimeiomba Serikali kurasimisha lugha ya alama ili iwe lugha rasmi ya mawasiliano Tanzania sambamba na Kiswahili na Kiingereza, kwa lengo la kuwawezesha watu wenye uziwi kuwasiliana na kupata huduma sawa na wananchi wengine.

 Mwenyekiti wa chama hicho Selina Edward, ametoa  ombi hilo wakati wa warsha ya pamoja katika ujumuishi wa watu wenye ulemavu, iliyofanyika Jijini Dodoma ikiwa na lengo la kutoa ushawishi kwa serikali kurasimisha lugha ya alama kuwa sehemu ya lugha kuu za mawasiliano.

Amesema lugha ya alama ndiyo njia kuu ya mawasiliano kwa watu wenye uziwi na kuwa urasimishaji wake utasaidia kuondoa changamoto za mawasiliano kati ya viziwi na wasio na uziwi, hivyo kuwawezesha kupata haki za msingi kama wananchi wengine.

“Tumehangaika miaka mingi kuomba lugha ya alama irasimishwe na itumike kama lugha nyingine rasmi nchini,” 

 Amesema pamoja na kuwepo kwa sera inayotaka asilimia 30 ya zabuni za umma kutolewa kwa makundi yenye mahitaji maalum, utekelezaji wake bado ni mdogo kutokana na watendaji wengi kutofahamu sheria na sera husika.

 Mbunge wa viti maalum anayewakilisha watu wenye ulemavu, Nassiriya Nassir Ali, alisema ataendelea kupigania urasimishaji wa lugha ya alama ili kuwezesha ushiriki sawa wa watu wenye uziwi katika jamii.

Naye mshauri wa kisiasa kutoka Chama cha Viziwi cha Norway, Adriana Fjellaker, alisema ushirikiano wao na CHAVITA unalenga kusaidia viziwi kufahamu haki zao na kukuza ujumuishwaji wa kijamii.

Warsha hiyo ilihusisha viongozi kutoka serikalini, wadau wa maendeleo na wanachama wa CHAVITA, ikilenga kujenga uelewa kuhusu haki za watu wenye uziwi, kuimarisha mawasiliano jumuishi na kukuza ushiriki wa watu wenye ulemavu katika shughuli za kiuchumi.




 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akipaka majivu katika Ibada ya Jumatano ya Majivu iliyofanyika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu, Paul wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki Dodoma leo tarehe 18 Februari 2026. Ibada ya Jumatano ya Majivu ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresma ambacho hutumika na waumini wa dini ya Kikristo kwaajili ya mfungo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akishiriki Ibada ya Jumatano ya Majivu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu, Paul wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki Dodoma leo tarehe 18 Februari 2026. Ibada ya Jumatano ya Majivu ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresma ambacho hutumika na waumini wa dini ya Kikristo kwaajili ya mfungo.


MAKAMU Nchimbi ameungana na waumini mbalimbali kushiriki Ibada ya Jumatano ya Majivu katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu, Paulo wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki Dodoma leo tarehe 18 Februari 2026. 


Ibada hiyo, imeongozwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Wilbroad Kibozi. 


Akitoa mahubiri katika Ibada hiyo, Askofu Kibozi, amewasihi waamini kutumia kipindi hiki cha mfungo wa Kwaresma, kujitoa kwaajili ya wahitaji pamoja na kuombea familia, vijana, watoto na Taifa kwa ujumla.


Pia amesema katika kipindi hiki ambacho waumini wa Dini ya Kikristo na Kiislamu wanakutana pamoja katika mfungo, ni vema kupendana, kuheshimiana na kujaliana. 


Askofu Kibozi amesema wafanyabiashara wanapaswa kuwa wema na wakarimu katika kipindi hiki na kutambua kipindi hiki sio cha upandishaji bei ya bidhaa za vyakula bali inapaswa bei za bidhaa kupunguzwa.


Ibada ya Jumatano ya Majivu ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresma ambacho hutumika na waumini wa Dini ya Kikristo kwaajili ya mfungo.

Dkt. Arnold Koresha,  Mratibu wa programu ya SafeCare, akizungumza katika hafla hiyo, leo Februari 18,2026 Dar es Salaam.
Rais wa  Jukwaa la afya Tanzania (Tanzania Healthy Summit ) Dkt Omary Chillo akihutubia wakati wa hafla fupi ya kukabidhi  cheti cha utoaji huduma Bora kwa hospitali ya Qualitas iliyopo Kigamboni Dar es salaam. Hafla ya kukabidhi cheti hicho imefanyila leo  Februari 18, 2026 hospitalini hapo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa hospitali hiyo Josephat Kibwana na kushoto ni mratibu wa programu ya SafeCare Dkt. Arnold  Koresha.

RAIS wa Taasisi ya Afya ya Tanzania Health Summit (THS), Dkt. Omary Chilo, ametoa wito kwa watoa huduma za afya nchini kufanya tathmini ili kubaini mapungufu waiyonayo na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kufikia viwango vya kimataifa.

Dkt Omary Chillo, ametoa wito huo leo Februari 18, 2025 wakati wa hafla ya kukabidhi cheti cha ubora cha SafeCare ngazi ya nne (Level 4) kwa Kituo cha Afya cha Qualitas kilichopo Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Amesema jukumu la taasisi hiyo ni kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya nchini, kufikia watoa huduma mbalimbali na kuhimiza taasisi hizo kuboresha huduma zao.

Akizungumzia utafiti walioufanya, Dkt. Chilo amesema wamebaini changamoto kubwa zilizopo katika utoaji huduma ni utawala, miundombinu ya kutolea huduma na utendaji wa wafanyakazi kuwa bado ni mbovu.

Amesisitiza kuwa umuhimu wa watoa huduma na vituo vya afya kufanya tathmini za mara kwa mara ni ili kubaini mapungufu yaliyopo na kuyafanyia kazi kwa lengo la kufikia viwango vinavyotakiwa.

Alieleza kuwa ubora unapaswa kuzingatiwa katika hospitali na vituo vyote vya afya, bila kujali tofauti ya huduma wanazotoa.

“Ubora unatakiwa uzingatiwe katika hospitali na vituo vyote vya afya. Siyo kwamba hospitali moja iwe bora zaidi kuliko nyingine, huduma zinaweza kutofautiana lakini ubora unapaswa kuwa uleule,” amesema Dkt Chillo.

“Tunatamani watu wote watoe huduma katika ubora wa juu zaidi. Natoa wito kila kituo kufanya tathmini ya huduma wanazozitoa ili kujua mapungufu waliyonayo,” alisema.

Amesema taasisi hiyo ipo katika sekta ya afya kwa ajili ya kutoa cheti cha ubora wa juu wa huduma za afya.

Aidha, alisema SafeCare ni programu inayofanya tathmini ya utoaji wa huduma za afya katika hospitali, zahanati na kliniki zinazotoa huduma hizo na kwamba programu hiyo ambayo inatekelezwa kimataifa ipo Tanzania kwa zaidi ya miaka 10 na imekuwa chachu ya kuimarisha huduma za afya nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya Qualitas, Dkt Jane Manyahi, amesema wanafurahia kupokea cheti cha ubora wa ngazi ya nne wakiwa na uhakika wa usalama kwa wagonjwa na watoa huduma.

Amesema huduma wanazozitoa ni rafiki na zinatolewa kwa wakati.

“Napendekeza hospitali binafsi kujiunga na huduma hizi za kupima ubora kwani inaonesha uwezo wao wa kutoa huduma, mapungufu na miongozo ya kuondoa changamoto hizo,” amesema.

Aidha amewashauri watoa huduma wa sekta binafsi kujiunga na mifumo ya kujipima ubora wa huduma wanazotoa. Pia aliishauri hospitali za umma na binafsi kuzingatia viwango vya kimataifa ili kutoa huduma salama na zenye ubora.

Amebainisha kuwa kufuata viwango hivyo kunasaidia watumishi kufanya kazi katika mazingira bora na salama, jambo linaloongeza uaminifu kwa wagonjwa na jamii kwa ujumla.

“Ni jambo jema kwani linaongeza imani kwa jamii inayowazunguka, wakijua kuwa huduma wanazopata ni salama na bora,” amesema Dkt. Manyahi.

Naye mkazi wa Kigamboni, Esther Medson, aliyefika hospitalini hapo kupata huduma, ameeleza kuridhishwa kwake na huduma alizopata na kuipongeza hospitali hiyo kwa kustahili cheti cha ubora wa ngazi ya juu.

Aidha, amezitaka taasisi za sekta ya afya kuendelea kuwahudumia wagonjwa kwa weledi na kutumia taaluma zao ipasavyo ili kuboresha zaidi huduma wanazotoa.
Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Qualitas iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam,  Dkt.Jane Manyahi akionesha cheti  cha ubora  ngazi ya nne (level 4) kilichotolewa na Tanzania Healthy Summit (THS) kupitia programu yake ya SafeCare.

Na MASHAKA MHANDO, Tanga

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa majonzi makubwa kifo cha nguli wa muziki wa dansi nchini, Hayati Stephen Hiza (80), aliyetunga na kuimba wimbo wa kitaifa wa uzalendo, "Tanzania Nchi ya Furaha."

Hayati Mzee Hiza amehifadhiwa leo, Februari 18, 2026, katika nyumba yake ya milele eneo la Mwanzange, jijini Tanga. Akiwa na historia iliyotukuka, Mzee Hiza atakumbukwa kwa utunzi wake uliotikisa Radio Tanzania (RTD) mwaka 1967 akiwa na bendi kongwe ya Atomic Jazz ya Tanga, akizalisha vibao vilivyodumu vizazi na vizazi kama "Leo Nakupasulia", "Hamida Wangu", na "Sitamani Kitu".

Alama ya Mwaka 1967 na Uzalendo

Wimbo uliompa heshima ya kipekee na kumfanya atambulike kama "Mzalendo Namba Moja" wa sanaa ni "Tanzania Nchi ya Furaha". Wimbo huu, uliotungwa miaka sita tu baada ya Uhuru, umekuwa utambulisho wa amani na furaha ya Watanzania, jambo ambalo Rais Samia amesema litaacha alama isiyofutika.


Salamu za Pole na Tuzo ya Rais

Akizungumza kwa niaba ya Rais, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), amesema Rais Dkt. Samia aliguswa na mchango wa Mzee Hiza kiasi cha kutoa zawadi ya Shilingi Milioni 50 pamoja na tuzo ya heshima kupitia Tanzania Music Awards (TMA) mwaka 2024.

"Mzee Hiza ni kielelezo cha wasanii waliotumia vipaji vyao kujenga taifa. Rais aliipokea kwa furaha ajenda ya kumtuza Mzee Hiza kwa sababu anaijua thamani ya kazi yake tangu enzi za Atomic Jazz," alisema MwanaFA.

MwanaFA na Ahadi ya Rekodi

MwanaFA amesimulia kwa masikitiko kuwa katika tamasha la 'Hale Festival' mwishoni mwa mwaka jana, Mzee Hiza alimweleza kuwa ana nyimbo mpya alizomtungia Rais na alikuwa na shauku ya kuzirekodi. "Niliahidi kumgharamia kurekodi kwa fedha zangu, lakini Mungu amempenda zaidi kabla ya kutekeleza dhamira hiyo," alisema Naibu Waziri huyo.

Rambirambi na Heshima za Mwisho

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, amethibitisha kuwa Rais Samia ametuma rambirambi ya Shilingi Milioni 20 kupitia kwa Msaidizi wake wa Kijamii, Tido Mhando

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu (MCC), Ustadh Rajab Abdalrahaman, pamoja na Meya wa Jiji la Tanga, Muhina Mustapha 'Seleboss', wameeleza kuwa pengo la Mzee Hiza halitazibika kwani alikuwa muumini wa muziki wa maadili na malezi kwa jamii.

Mzee Stephen Hiza amefariki akiwa na umri wa miaka 80, akiiacha Tanga na Tanzania katika simanzi, lakini akituachia urithi wa sauti yake ya dhahabu inayotuambia: "Tanzania, Tanzania, nchi yenye furaha...".
















Top News