Na: OWM (KAM) – Bungeni, Dodoma
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kwa lengo la kuhakikisha ustawi wa wananchi, pamoja na kuhakikisha utoaji wa pensheni kwa wakati.
Pongezi hizo zimetolewa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu, leo Aprili 15, 2026 wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.
Aidha, Mhe. Sangu amesema thamani ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeendelea kuongezeka ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) thamani yake imeongezeka kutoka Shilingi Trilioni 4.36 hadi Shilingi Trilioni 10.3. Mfuko wa PSSSF thamani yake iliongezeka kutoka Shilingi Trilioni 5.74 hadi Shilingi Trilioni 12.96.
Waziri Sangu amefafanua kuwa deni la Serikali katika mfuko wa PSSSF ilikuwa Trilioni 4.46, mwaka 2022/2023 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa hati fungani ya shilingi trilioni 2.17 kwa ajili ya kuulipa mfuko wa PSSSF deni lililodumu kwa muda mrefu la shilingi trilioni 4.6 la michango kabla ya 1999. Pia, Serikali imeendelea kulipa Trilioni 2.09 ambayo imesaidia thamani ya Serikali kulipa mfuko huo wa PSSSF kufikia asilimia 95.
Vilevile, Mhe. Sangu amesema kuwa kutokana na mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa himilivu imepelekea kwa sasa watumishi wa umma wanaostafu wanalipwa mafao yao ndani ya siku ishirini na tano huku kiwango cha kima cha chini cha pesheni kuongezeka toka shilingi 100,000 hadi kufikia shilingi 250,000 kwa wastaafu.
Kadhalika, Waziri Sangu amesema Mifuko ya hifadhi ya jamii imeendelea kuwekeza katika miradi yenye tija kwa lengo la kuongeza thamani ya michango ya wanachama na kukuza uchumi pamoja na kuongeza ajira kwa wananchi.
Akihitimisha mchango wake, Mheshimiwa Sangu aliwahakikishia wabunge kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano itaendelea kusimamia utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ufanisi, ili kuleta manufaa kwa Watanzania katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.
Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azan Zungu, amewapongeza wabunge kwa kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kusisitiza umuhimu wa wizara na taasisi husika kusimamia utekelezaji wake ili kuchochea maendeleo ya wananchi.
Na. Jacob Kasiri - Moshi.
“Dhamira ya kuurejesha Mlima Kilimanjaro katika usafi wake wa asili imejadiliwa leo Aprili 15, 2026 mjini Moshi katika kikao cha pamoja kilichowahusisha wawakilishi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, TANAPA na wamiliki wa Kampuni za utalii.
Uzalishaji wa taka ngumu na laini mlimani na baadae kuzishusha katika malango ya kushukia watalii imeonekana kama ndoto. Lakini ndoto hii itakuwa na matokeo chanya endapo, wenye makampuni ya utalii, waongoza wageni, Watalii na Wapagazi (wagumu) wataungana kwa pamoja kukusanya na kushusha ili kulinda mazingira na mandhari ya mlima huu unaoingiza takribani watalii elfu 65 kwa mwaka.
Akiongea namna ya kudhibiti uchafu, Mwenyekiti wa kikao hicho Bw. Michael Kilawila Mmiliki wa Kampuni ya “Coming to Africa” alisema;
“Sisi wenye Makampuni ndio tunaozalisha uchafu mlimani, hivyo ni jukumu letu kwa kushirikiana na mamlaka (KINAPA) kushusha taka hizo kwa kuwa mlima huo ni ofisi yetu. Hivyo sio vizuri kuichafua ofisi inayotuingizia kipato.”
Aidha, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro - Kamishna Msaidizi Mwandamizi Angela Nyaki alisema kuwa jitihada mbalimbali za serikali kudhibiti uchafu mlimani zinaendelea kila siku lakini bado uchafu unazalishwa mwingine.
“Ni wajibu wetu kuungana kuhakikisha uchafu tuonazalisha, tushuke nao ili kuufanya mlima wetu uwe safi, pia kumbukeni Mlima Kilimanjaro ni chanzo cha maji yanayotumika katika mji wa Moshi. Hivyo tunapochafua mlima tutambue madhara makubwa wanayapata wananchi wetu wanaotumia maji hayo.”
Sanjari na hilo pia Kamishna Nyaki aliwaomba wenye makampuni ya utalii wanapounadi mlima Kilimanjaro wauze vilele vitatu ambavyo ni Kibo, Shira na Mawenzi tofauti na sasa hivi wanauza kilele cha Kibo tu chenye urefu wa mita 5895 kutoka usawa wa bahari.
Naye, Simbo Natai - Mkurugenzi wa Kampuni ya “African Scenic” alisema; “Suala la uchafu tusiruhusu kuwa janga kwa sehemu tunayojipatia riziki, hivyo katika kikao hiki nashauri kabla ya kuanza kwa msimu wa utalii mwanzoni mwa mwezi mei, 2026 twende mlimani tukakusanye taka hizo na kuzishusha.”
David Mshana Mkurugenzi wa Kampuni ya “Enjoy Kili Ltd”, alishauri kuwa waongoza watalii(Guides) wapya kabla hawajapewa leseni ya kuongoza watalii wapandishwe mlimani kukusanya taka na kushuka nazo ili anapoongoza wageni pamoja na wapagazi awe ni mlinzi wa timu yake kuhakikisha hawatupi uchafu na kuharibu mazingira.
Mbali na mada ya taka mlimani pia agenda kama uokoaji wa wageni mlimani, waongoza watali na wapagazi kuwa na Kanzi Data na mapendekezo ya utoaji vyeti kwa watalii waliofika kileleni kwa njia ya kielektroniki zilijadiliwa na kupewa kipaumbele.

-Ataka watanzania waache tabia ya kujidogosha.
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema katika kipindi kifupi cha uongozi wake, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika historia ambayo kwa namna yoyote haiwezi kufutika kutokana na magaeuzi makubwa aliyoyafanya.
Amesema historia hiyo inaandikwa kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa, uandishi wa dira mpya ya Taifa ya 2025, kubadilisha mfumo wa elimu, kujenga madarasa mengi na shule za elimu ya amali, kuanzisha Bima ya Afya kwa Wote, kupandisha bajeti ya kilimo na kuongeza upatikanaji wa huduma za umeme na maji kwa wananchi vijijini.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo jioni (Jumatano, Aprili 15, 2026) Bungeni jijini Dodoma, wakati akitoa hoja ya kuhitimisha mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.
“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingia katika historia ya viongozi wachache wa Taifa letu waliopata heshima na bahati ya kuandika Dira ya Taifa 2050 pamoja na nyaraka nyingine muhimu za utekelezaji wa dira ikiwemo mpango wa maendeleao wa muda mrefu.”
Akielezea mafanikio kwenye sekta ya kilimo, Waziri Mkuu amesema: “Ili kuwezesha mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha kuongezeka kwa bajeti ya Wizara ya kilimo mara tano kutoka shilingi bilioni 270 mwaka 2020/2021 hadi shilingi trillioni 1.23 mwaka 2025/2026. Tumeshuhudia upatikanaji wa pembejeo za kilimo na ongezeko la matumizi ya mbolea.”
Kuhusu nishati, Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameingia katika rekodi kwa utekelezaji mkubwa wa mradi wa bwawa la umeme ambapo kwa sasa nchini kuna ziada ya umeme. “Alipokea huu mradi ukiwa katika asilimia 27 kwenda 30 ya utekelezaji. Amekamilisha mradi huo na sasa tuna ziada ya megawati zaidi ya 2,000. Tanzania ni nchi ambayo sasa ina ziada ya umeme.”
Amesema Mheshimiwa ametoa zaidi ya trilioni 1.2 za kujenga Mradi wa Gridi Imara ili kuondoa tatizo la kukatikatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.
Amesema kuwa Tanzania imesifiwa kwa weledi katika utafutaji wa rasilmali kwenye utekelezaji wa miradi mikubwa. “Juzi imetolewa tuzo kwa kwa nchi yetu ya kufanya vizuri katika kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi. Tanzania ni nchi ya mfano kwenye kutafuta rasilimali kwenye kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati.”
Waziri Mkuu amesema kutokana na hayo, katika mradi wa kimkakati wa reli ya kisasa tayari kipande cha tatu na cha nne kimepata fedha za kuanza ujenzi. “Vilevile, kipande cha tano nacho tayari kimepata fedha na utekelezaji wake unategemea certificates za mtekelezaji kadiri anavyokamilisha.”
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Watanzania waache kujidogosha kwani Tanzania imepiga hatua kubwa za kimaendeleo ikilinganishwa na nchi nyingine barani Afrika.
“Hapa Tanzania tunapenda kujidogosha hasa tusipojilinganisha na nchi nyingine. Tuache kujidogosha. Kwenye suala la umeme, hapa Afrika kuna nchi wameunganisha mikoa na mikoa tu lakini sisi kila kijiji umeme umeshafika. Na kwenye vitongoji 68,000, nusu yake umeme umeshafika na vitongoji zaidi ya 9,000 mikataba imeshasainiwa. Kwingine huko, ni mtu na solar yake au jenereta lake. Tunapaswa tujivunie kuwa tuko kwenye nchi ambayo viongozi wake maisha ya kila mtu na kuhakikisha keki ya Taifa inamfikia kila mtu,” ameongeza.
Kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Bunge limeidhinisha sh. trilioni 12.5 ambapo kati ya fedha hizo, sh. trilioni 8.73 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. trilioni 3.76 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo kwa Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake.
Vilevile, Bunge limeidhinisha sh. bilioni 225 kwa ajili ya Mfuko wa Bunge ambapo kati ya fedha hizo, sh. bilioni 207.99 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. bilioni 17.02 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
amepokea ujumbe maalum kutoka kwa Katibu Mkuu w a Jumuiya y a Madola, Bi. Shirley Ayorkor Botchwey, uliowasilishwa kwake n a Mjumbe Maalum, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Ujumbe huo pia umeainisha maeneo y a kipaumbele yanayofuatiliwa n a Jumuiya y a Madola, ikijumuisha uwazi n a ushirikiano katika tathmini ya matukio yaliyojitokeza wakati na baada y a Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, pamoja n a kupanua ushiriki wa kisiasa, kuendeleza majadiliano y a vyama n a kuimarisha uwajibikaji w a taasisi.
Katika ujumbe wake, Katibu Mkuu Botchwey amesisitiza dhamira ya Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana n a Tanzania katika kuimarisha misingi y a demokrasia, utawala bora n a maridhiano y a kitaifa kufuatia matukio yaliyojitokeza wakati n a baada y aUchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025.
Ameeleza kuwa Jumuiya y a Madola inaunga mkono juhudi zinazoendelea nchini na iko tayari kusaidia kujenga mazingira y a kisiasa yenye utulivu, ushirikishwaji n a kuaminiana kupitia mazungumzo na mageuzi ya taasisi.
Akizungumza wakati wa kupokea ujumbe huo, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania
inaendelea kushughulikia hali hiyo kupitia taasisi zake, akizitaja hatua mbalimbali
zilizochukuliwa n a Serikali, ikiwemo kuunda Tume Huru ya Uchunguzi, kwa lengo la
kurejesha utulivu, na kuimarisha uwajibikaji nchini.
Amebainisha kuwa matokeo ya Tume hiyo yataongoza hatua zinazofuata, ikiwemo
uwajibikaji, maridhiano na mageuzi y a taasisi, huku Serikali ikiendelea kusimamia
mchakato wa maridhiano ikiwemo majadiliano kupitia majukwaa yaliyopo kisheria na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.
Kwa upande wake, Mhe. Chakwera ameeleza utayari wa Jumuiya ya Madola kuendelea kushirikiana n a Tanzania katika juhudi za kuimarisha utawala w a sheria, ushirikiano wa kisiasa na mshikamano w a kitaifa.
Rais Mstaafu Chakwera amehitimisha ziara yake ya kikazi nchini kama Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya kisiasa na mchakato w a maridhiano, ambapo tayari amekwishakutana n a wadau mbalimbali wa kisiasa na kitaasisi nchini.

.jpeg)




Naibu waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt Ngwaru Maghembe (Mb.) amewasili nchini Brazil kwa ziara ya kikazi. Mhe. Naibu Waziri Dkt. Maghembe amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Dr. John Stephen simbachawene katika Ofisi ya Ubalozi. Mhe Naibu waziri alipata nafasi ya kukutana na kujadiliana masuala mbalimbali na Watumishi wa Ubalozi na kusisitiza umuhimu wa utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa kuvutia uwekezaji kutoka Brazili.
Katika ziara hiyo Mhe.Dkt Ngwaru Maghembe (Mb.) ataongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Mashauriano ya kisiasa kati ya Tanzania na Brazil. Mkutano huo unalenga kukuza uhusiano wa Kidiplomasia na Ushirikiano baina ya Tanzania na Brazili katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, Uwekezaji, Kilimo, Mifugo na Utalii
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeanza kuweka utaratibu wa kutumia hazina ya maarifa na uzoefu kutoka kwa Mabalozi Wastaafu ili kuimarisha utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kuimarisha diplomasia ya nchi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo , amebainisha utaratibu huo leo Aprili 15, 2026, jijini Dar es Salaam wakati anafungua kikao cha mashauriano kati ya uongozi wa Wizara na Mabalozi Wastafu.
"Wizara tumeanzisha utaratibu wa kuwa na vikao vya mara kwa mara na Mabalozi Wastaafu ili kuvuna maarifa na uzoefu wao kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia ili ulete nanufaa katika nyanja mbalimbali kama vile, siasa, ulinzi na usalama, uchumi, biashara, uwekezaji na utalii". Balozi Kombo alisema.
Balozi Kombo ametaja mifano ya maeneo ambayo angependa Mabalozi Wastaafu wachangie maarifa na uzoefu walio kuwa nao ili maeneo hayo yaendelee kuwa na manufaa zaidi kwenye nchi.
Maeneo hayo ni pamoja na mwenendo wa ufanyaji wa biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine, hususan zilizopo barani Afrika.
Amesema utekelezaji wa Dira 2050 ambayo inalenga uchumi wa dola bilioni moja, ni eneo lingine muhimu ambalo maarifa ya Mabalozi Wastaafu yanahitajika ili kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa wa ufanisi.
Waziri Kombo ameongeza kuwa mabadiliko yanayoendelea Duniani hususan, maendeleo ya kidigitali yanahitaji mikakati thabiti ili nchi iweze kunufaika na kuwa na mipango madhubuti ya kukabiliana na athari zake. Haya yote yanahitaji mawazo ya pamoja ili kuyaendeea kwa ufanisi.
Eneo lingine ambalo Waziri Kombo alisisitiza umuhimu wa kupata uzoefu wa Mabalozi Wastaafu ni siasa za ulimwengu ambazo zimekuwa hazitabiriki na zinasababisha madhara mbalimbali, hususan katika nchi zinazoendelea kama Tanzania.
Aidha, uzoefu wa Mabalozi Wastaafu unahitajika katika kuendeleza na kuimarisha taswira nzuri ya nchi na hasa nchi inapopewa dhamana ya majukumu ya kimataifa. Balozi Kombo alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika mwaka 2028 na hivyo maarifa yao ni muhimu ili kuhakikisha nchi inatekeleza jukumu hilo kwa ufanisi.
Awali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo alisema Wizara inaangalia uwezekano wa kuanzisha utaratibu rasmi kupitia Ofisi ya Rais-UTUMISHI ili ushirikishwaji wa Mabalozi Wastaafu uwe unatambulika rasmi.













.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)



.jpg)
.jpg)
.jpg)




.jpeg)
