Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda (kushoto) akipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware (katikati) muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2025 kwa ajili ya ziara yake ya kikazi.

**********************

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda amelipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa mikakati iliyojiwekea kutekeleza malengo ya nguzo ya tatu ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.

Mhe. Luvanda amesema hayo leo Alhamisi Machi 05, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kujitambulisha na kuzungumza na Menejimenti ya Baraza hilo sambamba na kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Ofisi hiyo.

Mhe. Luvanda amesema NEMC imebeba maono na matarajio makubwa ya nchi katika kufikiamalengo ya dira ya maendeleo ya taifa 2050 hususani utelekelezaji wa nguzo ya tatu inayoakisi masuala ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi.

“Kwa taarifa nilizoona nimeridhishwa na utayari wenu katika utekelezaji wa dira 2050…..Hatuna budi kutambua kuwa tumebeba matumaini ya Viongozi wakuu wa kitaifa katika kufanikisha utekelezaji wa Dira 2050 katika upande wa mazingira” amesema Mhe Balozi Luvanda.

Aidha Mhe. Balozi Luvanda amesema suala la elimu kwa umma halina budi kupewa kipaumbele na msukumo wa pekee ili kuhakikisha inapatiwa uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wakutunza na kuhifadhi mazingira kwa ajili ya mustabali endelevu wa taifa.

Balozi Luvanda pia ameishauri Menejmenti ya NEMC kuweka msukumo wa kujitangaza kwa jamii na wadau mbalimbali kwa kuwa misingi ya utekelezaji wa jukumu hilo limeanishwa katika sheria na kanuni zinazosimamia majukumu ya taasisi hiyo.

Mhe. Balozi Luvanda amesema NEMC ni taasisi muhimu yenye mchango mkubwa katika kuharakisha kasi ya ukuaji wa sekta za maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini na hivyo ana imani na watendaji wa ofisi hiyo katika kutekeleza jukumu hilo muhimu kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware amemshukuru Mhe. Balozi Luvanda kwa ziara hiyo ya kikazi katika ofisi za baraza hilo na kuwa ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano ili kuwezesha na kufanikisha dhamira na maono ya Serikali.

“Sisi kama Watumishi wa NEMC tunakukaribisha Mhe. Balozi Luvanda tutambua majukumu uliyonayo yanaakisi shughuli zinazotelekezwa na NEMC, hivyo tupo tayari kupokea maelekezo na kufanyia kazi” amesema Dkt. Sware.

Mhe. Balozi Baraka Luvanda aliteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais akichukua nafasi ya Prof. Peter Msoffe aliyehamishiwa Wizara ya Kilimo.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akipokea shada la maua kutoka Bi. Florida Kavure Afisa Mazingira waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akisalimiana na watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026 kuanza ziara yake ya kikazi. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Baadhi ya Watendaji Waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakifuatilia kikao baina ya Ofisi hiyo na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea Ofisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Kemilembe Mutasa (kushoto) akifuatilia kikao baina ya Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Baadhi ya Watendaji Waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakifuatilia kikao baina ya Ofisi hiyo na Naibu Katibu Mkuu (Mazingira), Mhe. Balozi Baraka Luvanda wakati wa ziara yake ya kikazi kutembelea Ofisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akifuatilia Makala mjongeo inayoelezea majukumu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakati wa ziara yake ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware.

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Immaculate Sware akitoa taarifa ya utekelezaji wa Baraza hilo kwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Balozi Baraka Luvanda aliyefanya ziara ya kutembelea Ofisi za Baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akizungumza na Viongozi na Watendaji waandamizi wa Baraza la Taifa la Hifadhin a Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakiongozwa na Makurugenzi Mkuu, Dkt. Immaculate Sware (kulia) wakati wa ziara yake aliyoifanya katika ofisi hiyo Jijini Dar es Salaam leo Jijini Machi 05, 2026.

Naibu Katibu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware wakati wa ziara yake aliyoifanya katika Ofisi za Baraza hilo leo Jijini Dar es Salaam leo Machi 05, 2026.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware (kulia) na Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Kemilembe Mutasa (kushoto) pamoja na watendaji wengine wa Baraza hilo muda mfupi baada ya kumaliza ziara yake aliyoifanya katika Ofisi zas Baraza hilo leo Alhamisi Machi 05, 2026.

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Balozi Baraka Luvanda akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Immaculate Sware muda mfupi baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi ya kutembelea ofisi za baraza hilo Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 05, 2026.

(NA MPIGAPICHA WETU)

Na Maandishi Wetu, Dodoma.

Tanzania inaendelea kuimarisha ushindani wa haki na udhibiti wa bidhaa bandia kupitia Tume ya Ushindani (FCC) pia Sheria ya Alama za Bidhaa, 1963 inalinda biashara halali na watumiaji dhidi ya udanganyifu.

FCC inaidhinisha miungano 4 katika sekta ya fedha, ikilenga kuimarisha mfumo wa malipo ya kidijitali na huduma za benki. Aidha, udhibiti wa bidhaa bandia unaendelea kulinda biashara halali na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC),  Khadija Ngasongwa, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo na fursa kwa vijana, leo Machi 05, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Khadija amesema Katika kipindi cha 2025/26, Tume ya Ushindani imeidhinisha miungano 4 katika sekta ya Fedha, Kuidhinishwa kwa miungano hii miwili (2) katika sekta ya fedha na malipo kunaweza kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania kwa kuimarisha mfumo wa kadi na malipo ya kidijitali kupitia uwekezaji wa Toppan Global Security Limited katika DZ Card (Africa) Limited, hivyo kuongeza usalama na ufanisi wa miamala ya kielektroniki.

Vilevile, muungano unaohusu kampuni ya Soren Investment Company Limited na Habib African Bank Limited unatarajiwa kuleta mtaji mpya na uwezo wa kibiashara ili kuimarisha huduma za benki, kutanua upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara na wananchi, na kuchochea ushindani katika sekta ya fedha ambao unaweza kupunguza gharama za huduma za kifedha na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na uwekezaji katika teknolojia za kifedha.

Aidha amesema Udhibiti wa Bidhaa Bandia FCC imeendelea kusimamia kikamilifu Sheria ya Alama za Bidhaa, 1963 ambayo jukumu muhimu katika kuzuia uingizaji, uuzaji, na usambazaji wa bidhaa bandia au zile zenye maelezo potofu. 

"Bidhaa bandia huzuia ushindani wa haki, kuathiri vibaya biashara halali, na kuhadaa watumiaji, hivyo kuunda uwanja usio sawa wa biashara. Sheria hii inahakikisha kuwa biashara zinapewa fursa ya kufanikiwa kutokana na ubora, ubunifu, na kufuata sheria, badala ya udanganyifu"

Hata hivyo amesema hiyo inakuza soko lenye ushindani wa haki na uwazi, likilinda imani ya watumiaji na kuwezesha makampuni kuwekeza kwa kujiamini katika ukuaji na ubunifu.

Kudhibiti bidhaa bandia kwa mujibu wa sheria hii pia kunachangia ukuaji wa uchumi. Biashara halali zinabaki na mapato yao, jambo linalochochea uwekezaji zaidi, kuongeza ajira, na kuendeleza ubunifu. Watumiaji wanalindwa dhidi ya bidhaa zisizo salama au zisizo halisi, na hivyo kupunguza hasara za kiuchumi zinazotokana na udanganyifu. 

Aidha, jitihada za kuzuia bidhaa bandia zinaboresha sifa ya biashara kitaifa na kimataifa, kuwavutia wawekezaji, na kuongeza mauzo ya nje, Kwa kuunganisha utekelezaji madhubuti, ushirikiano wa sekta, na uhamasishaji wa Umma, Sheria hiyo inahakikisha kuwa ushindani wa haki na uthabiti wa kisheria unachochea ukuaji wa uchumi endelevu wa nchi. 








Na Oscar Assenga, Tanga


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amefanya ziara ya kutembelea Jengo la Kitega Uchumi la Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) “Mkwakwani Plaza” ambalo litagharimu kiasi cha Bilioni 8.6 huku akiwapongeza kwa usimamizi imara na ubora mkubwa.


Akizungumza akiwa katika eneo la mradi huo RC Batilda alisema kwamba ubunifu ambao wameutumia shirika hilo kuanzia hatua ya ujenzi mpaka usimamizi wanafanya wenyewe kupitia wataalamu wao jambo ambalo litawezesha kuwepo kwa ubora.
Alisema kwamba kutokana na uwepo wa fursa hiyo watu wa Tanga wanapaswa kuichangamkia sasa na wasisubiri bali waanze sasa kujiitokeza kuchukua nyumba katika Jengo hilo la kitega Uchumi la NHC

“Nitumie fursa hii kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa zilizopo katika Jengo hili wale ambao wana fedha za mitaji waweze kuzungumza na Meneja wa NHC na leo tumekuja kwenye ziara hapa na kamati ya usalama ya mkoa kukagua ujenzi wa jengo hilo niendelee kuwapongeza NHC kazi inaendelea vizuri na ya viwango vya hali ya juu hongereni sana”Alisema
Aidha alimpongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kuendelea kusukuma mbela maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu na makazi

Awali akizungumza Menej awa Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) Mhandisi Mussa Kamendu alisema kwamba Jengo hilo litakuwa na maeneo ya maduka ,ofisi za kupangisha katika sehemu ya Biashara huku likiwa na Gorofa nne za makazi.



Alisema kwamba katika Jengo hilo eneo la makazi nyumba ya vyuma viwili itakuwa inauzwa kwa kiasi cha Milioni 178 na za vyumba vitatu zitauzwa kwa shilingi Milioni 240 bei zote zikijumuisha VAT.

Aidha alisema kwamba wanawakaribisha wananchi kuchangia fursa ya kuweza kununua vyumba hizo huku akiwashukuru ambao wamekwisha kujitokeza na wapangaji wamepata wengi.


Naye kwa upande wake Mhandisi wa Ujenzi huo Mhandisi Ephahim Fanuel Msigwa alisema kwamva jengo hilo lilianza mwaka 2025 na kwa mujibu wa mkataba wanatakiwa kumaliza mwezi Juni 2027.

Mhandisi Ephahim aliongeza kwamba kupitia mradi huo wametengeneza ajira za kazi 189 na wanawashukuru watu wa Tanga wamejitokeza kwa asilimia kubwa .

Mradi wa jengo hilo la Mkwakwani Plaza ni mradi wa Kisasa ambalo linajumisha sehemu za biashara na makazi na kwamba utajkapokamilika utaongeza thamani ya mji wa Tanga na kutoa fursa zaidi ya ajira na uwekezaji kwa wananchi.











 Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Tanzania), kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Chuo cha Indian Institute of Technology Madras Zanzibar (IIT Madras Zanzibar), limewakutanisha viongozi wa vyuo vikuu, watunga sera na wadau wa mifumo ya ubunifu kutoka Afrika Mashariki kuanzia Machi 4–6, 2026, katika Mpango wa Kihistoria wa Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma (Faculty Exchange Programme) unaolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa (startups) na kukuza ujasiriamali.


Ingawa Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki vinazalisha tafiti nyingi, vipaji na miliki bunifu (intellectual property), ni uvumbuzi mchache unaofanikiwa kuingia sokoni kama biashara endelevu na zenye uwezo wa kukua. Mpango huu unalenga kuziba pengo hili la kimfumo kwa kuimarisha mifumo ya taasisi, vivutio na ushirikiano unaowezesha uanzishaji wa biashara ndani ya taasisi za elimu ya juu.

Ukifanyika chini ya kaulimbiu “Vyuo Vikuu kama Injini za Ubunifu: Kujenga Njia Endelevu kutoka Maarifa mpaka Biashara,” mpango huu unaviweka vyuo vikuu kama nguzo muhimu za ubunifu, uendelezaji wa teknolojia na ukuaji wa biashara. Utekelezaji wake unafanyika kupitia Mradi wa Ubunifu wa FUNGUO, ambao ni mradi wa kimkakati unaofadhiliwa kwa pamoja na Serikali ya Uingereza (FCDO), na kutekelezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP Tanzania). Mpango huu unawakutanisha viongozi wa kitaaluma, watengenezaji wa mifumo ya ubunifu na watunga sera ili kuimarisha mifumo inayosukuma mawazo kutoka maabara za utafiti mpaka kuwa biashara zenye uwezo wa kukua.

Jukwaa hilo lilifunguliwa rasmi na Mheshimiwa Fatma Mabrouk Khamis, Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambaye katika hotuba yake kuu alisisitiza:

“Tunapofungua programu hii, ningependa kusisitiza kuhusu hatua kadhaa za kuchukua. Kwanza, ushirikiano huu uzalishe matokeo halisi ikiwemo tafiti za pamoja, programu za kubadilishana wahadhiri na miradi shirikishi ya ubunifu. Pili, ubadilishanaji wa maarifa uwe sehemu ya kudumu ndani ya mifumo ya vyuo vikuu na sera za kitaifa za ubunifu. Tatu, watunga sera waendelee kuimarisha mifumo ya udhibiti inayounga mkono ujasiriamali na ubunifu. Nne, ubunifu ubaki jumuishi ili kuhakikisha wanawake, vijana na taasisi changa wanapata fursa. Mwisho, mafanikio yapimwe kwa athari halisi — kwa idadi ya biashara bunifu zitakazoanzishwa na ajira zitakazozalishwa,” alisisitiza Mhe. Khamis.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Godfrey Nyamrunda, Mkuu wa Ofisi Ndogo ya UNDP Zanzibar, Tanzania, alisisitiza umuhimu wa kimkakati wa mpango huu katika vipaumbele vya maendeleo ya taifa:

“UNDP tunaona vyuo vikuu kama kiunganishi muhimu ndani ya mfumo wa ubunifu wa Tanzania. Kupitia mipango kama FUNGUO, tunawekeza katika mifumo, ushirikiano na nyenzo za kifedha zinazowezesha wabunifu vijana kupiga hatua kutoka wazo mpaka kuwa biashara. Mpango huu wa kubadilishana wahadhiri unaimarisha ajenda hiyo kwa kuviwezesha vyuo vikuu kuwa si wazalishaji wa maarifa tu, bali pia wajenzi wa biashara bunifu zinazoleta ukuaji endelevu na ajira zenye staha,” alisema Bw. Nyamrunda.

Akiutambulisha Mpango wa Ushirikiano huo katika Utafiti, Ubunifu na Ujasiriamali, Dkt. Jacqueline Owigo, Mshauri wa Utafiti na Ubunifu katika Kituo cha Utafiti na Ubunifu Afrika Mashariki, Ubalozi Mkuu wa Uingereza jijini Nairobi, alisisitiza umuhimu wa kujenga mifumo imara ya ubunifu kupitia ushirikiano wa kimataifa.

“Kote katika ukanda huu, tumejifunza kuwa mifumo hai ya biashara bunifu haijitokezi kwa bahati mbaya; hujengwa kwa makusudi. Vyuo vikuu vina nafasi ya msingi katika kulea vipaji vya ujasiriamali, kuimarisha njia za kukuza tafiti mpaka kuwa katika uendelezaji wa kibiashara, na kuwaunganisha wabunifu na sekta binafsi pamoja na wawekezaji. Kupitia ushirikiano wa Uingereza–India–Afrika Mashariki, tunajenga jukwaa la kujifunza kwa pamoja na kushirikiana linalowawezesha wabunifu vijana kubadilishana mawazo kuwa suluhisho za ubunifu kwa vitendo,” alisema Dkt. Owigo.

Katika hotuba yake ya utangulizi, Profesa Prabhu Rajagopal, Kaimu Mkurugenzi, Chuo cha IIT Madras – Kampasi ya Zanzibar, alisisitiza umuhimu wa Zanzibar kuwa mwenyeji wa tukio hilo:

“Kuandaa programu hii hapa Zanzibar kunaakisi dhamira yetu ya kujenga utamaduni wa ubunifu uliounganishwa kimataifa na unaojibu mahitaji ya ndani. Vyuo vikuu vinapaswa kubadilika kutoka kuwa wazalishaji wa maarifa mpaka kuwa waanzilishi wa biashara hai bunifu. Kwa kutumia motisha, kuimarisha mifumo ya uhamishaji wa teknolojia, na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, tunaweza kujenga njia endelevu kutoka utafiti mpaka biashara; tunatarajia kuona mbeleni wahitimu wanakuwa waajiri, na sio watafuta ajira pekee,” alisema Prof. Rajagopal.

Kutokana na mafanikio ya awamu ya kwanza, ilyiojulikana kama RISE 4.0. Awamu ya Pili ya mpango huu imeyaalika makundi tofauti ya wanafunzi yenye mifano ya bunifu zilizoanza kufanya kazi (prototypes) zinazoshughulikia changamoto za mabadiliko ya tabianchi kupitia teknolojia za Mapinduzi ya Nne ya Viwanda (Industry 4.0) kama vile akili bandia (AI), ujifunzaji wa mashine (machine learning), Mtandao wa Vitu (IoT), roboti, blockchain, uchakataji wa kidijitali wa hali ya juu na mifumo ya utabiri.

Programu hii ambayo ilifanyika kwa njia ya mtandaoni ilibuniwa kuyasaidia makundi tofuati ya wanafunzi kuboresha suluhisho zao walizobuni, kuthibitisha mahitaji ya soko na kuonyesha hatua ya utayari wa Bidhaa Inayokubalika Sokoni (Minimum Viable Product - MVP), ikiwa na njia thabiti ya kuelekea kuwa biashara kamili. Suluhisho bunifu zinatarajiwa kutoa ufumbuzi kwenye maeneo ya kipaumbele kama vile nishati safi na jadidifu, kilimo na mifumo ya chakula inayostahimili tabianchi, miji na miundombinu himilivu na mzunguko wa uchumi na urejelezaji taka.

Makundi yatakayofanya vizuri zaidi yatapatiwa mtaji wa awali, fursa ya kujumuishwa katika programu za mafunzo ya ukuaji kupitia taasisi washirika, na kuunganishwa katika mtandao mpana wa ubunifu ili kuimarisha utayari wao wa kupokea uwekezaji na kukuza biashara. Mbali na maboresho ya kiufundi, programu inasisitiza kukidhi soko, msaada wa taasisi na kuunganishwa kimfumo ili kuhakikisha mifano bunifu ya suluhisho bora inageuka kuwa biashara endelevu zenye athari chanya kwa tabianchi.

Sambamba na mafunzo ya siku nne kwa wanafunzi, Mpango wa Kubadilishana Uzoefu utakaofanyika wa siku tatu utawakutanisha viongozi wa kitaaluma kuchambua mifano hai kutoka nchi za kimataifa na kikanda ya uanzishaji wa biashara bunifu, ukijifunza kutoka taasisi kama Indian Institute of Technology Madras na Chuo Kikuu cha Leeds. Majadiliano yataangazia usimamizi wa ubunifu, usimamizi wa miliki bunifu, mifumo ya uhamishaji wa teknolojia, na ushirikiano kati ya vyuo vikuu na sekta binafsi, yakihitimishwa kwa Maonesho ya Ubunifu wa Wanafunzi na mpango kazi wa utekelezaji wa baadaye.

Kwa pamoja, vipengele vya mada hizi vinakusudia kuimarisha mitandao ya kikanda, kuongeza uwezo wa wahadhiri katika uendelezaji wa teknolojia kibiashara, na kuviweka vyuo vikuu vya Tanzania na Afrika Mashariki kama injini za ukuaji wa ujasiriamali unaochochewa na ajenda ya tabianchi.

– MWISHO –
Kuhusu FUNGUO

Mpango wa FUNGUO wa UNDP unachochea ubunifu nchini Tanzania kwa kukuza ukuaji wa uchumi kupitia kulea wajasiriamali, kuwezesha upatikanaji wa rasilimali za kifedha, na kuendeleza ushirikiano wenye kuleta matokeo. Mpango huu unafadhiliwa kwa pamoja na Umoja wa Ulaya, Serikali ya Uingereza, Serikali ya Finland na UNDP. FUNGUO inalenga kuondoa vikwazo ndani ya mfumo wa ubunifu wa Tanzania — kuanzia ufadhili mpaka ushauri elekezi — kwa kuyapa makampuni changa na biashara ndogo zana zinazohitajika kukua, kustawi na kuleta athari chanya endelevu.

Mhe. Fatma Mabrouk Khamis, Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akihutubia wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali. Semina hiyo inafanyika katika Chuo cha IIT Madras Zanzibar na kuandaliwa na UNDP Tanzania kupitia Mradi wake wa Ubunifu wa FUNGUO, kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo imewakutanisha viongozi wa vyuo vikuu, watunga sera na wadau wa mifumo ya ubunifu kutoka Afrika Mashariki kuanzia Machi 4–6, 2026.

Godfrey Nyamrunda, Mkuu wa Ofisi Ndogo ya UNDP Zanzibar, Tanzania, akizungumza wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali.

Profesa Prabhu Rajagopal, Kaimu Mkurugenzi, Chuo cha IIT Madras – Kampasi ya Zanzibar, akizungumza wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali.

Dkt. Jacqueline Owigo, Mshauri wa Utafiti na Ubunifu katika Kituo cha Utafiti na Ubunifu Afrika Mashariki, Ubalozi Mkuu wa Uingereza jijini Nairobi, akizungumza wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali.


Dkt. Kumar Praveen, Balozi Mdogo wa India Zanzibar akizungumza wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali.





Meneja Mradi wa Funguo wa UNDP Tanzania, Joseph Manirakiza, akizungumza wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa semina ya Kubadilishana Wataalamu wa Kitaaluma inayolenga kuvigeuza Vyuo Vikuu kuwa injini za kuanzisha biashara bunifu changa na kukuza ujasiriamali.




















Kufuatia tangazo la hivi karibuni kwamba Standard Chartered Bank Tanzania ilitoa mchango wa USD 11,500 kwa Challenges Worldwide Tanzania ili kuchochea ukuaji wa ujasiriamali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Benki hiyo katika utekelezaji wa mpango wa Standard Chartered Foundation wa RISE/E, mpango wa Wazo Bora Pitch umehitimishwa kwa mafanikio kwa kutoa jumla ya TZS 17,000,000 kama mtaji wa kuanzisha biashara kwa wajasiriamali waliobobea.

Wazo Bora Pitch ni kilele cha programu ya mafunzo ya kina iliyofadhiliwa kupitia msaada wa Benki na kutekelezwa na Challenges Worldwide Tanzania. Mpango huu ulianza Desemba 2025 kwa tangazo la mwezi mmoja la kupokea maombi, lililovutia kundi kubwa la wajasiriamali watarajiwa kutoka sekta mbalimbali.

Baada ya kufungwa kwa dirisha la maombi, washiriki 15 walichaguliwa kushiriki katika mafunzo maalum (bootcamp) yaliyolenga kuboresha mifumo ya biashara, kuimarisha usimamizi wa fedha, na kuongeza utayari wa kupokea uwekezaji. Baada ya kukamilisha mafunzo, washiriki saba walichaguliwa kuingia hatua ya mwisho ya mashindano ya uwasilishaji wa mawazo (pitch) yaliyofanyika wiki hii jijini Dar es Salaam.


Mwisho wa mashindano:


• Mshindi – Ng’oga Masheri Kaswahili – alitunukiwa TZS 10,000,000 kama mtaji wa kuanzisha au kukuza biashara.

• Mshindi wa Pili – Mohamed Muhidini – alipokea TZS 4,000,000.

• Mshindi wa Tatu – Nipaeii Mtana – alitunukiwa TZS 3,000,000.


Jumla ya TZS 17,000,000

zilizotolewa zitawezesha upanuzi wa biashara, uundaji wa ajira, na ukuaji wa masoko kwa biashara zilizoshinda.

Wazo Bora Pitch ni sehemu ya mpango mpana wa RISE/E ulioanzishwa mwaka 2024 kupitia Standard Chartered Foundation. Mpango huo wa miaka mitatu wenye thamani ya TZS bilioni 2.2 unalenga kusaidia moja kwa moja biashara ndogo 340 na kuunda ajira mpya 478 kote Tanzania, ukiweka mkazo maalum kwa wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu.

Mwakilishi wa Standard Chartered Bank Tanzania – George Binde – Afisa Mtendaji Mkuu alisema:

“Mnamo Desemba tulitangaza mchango wetu wa USD 11,500 kuunga mkono mpango huu kwa kushirikiana na Challenges Worldwide Tanzania. Leo tunaona matokeo halisi ya uwekezaji huo. Tunajivunia kuona washiriki wetu wakiimarisha biashara zao na washindi wetu wa mwisho wakionyesha ukuaji mkubwa, uwazi wa malengo na ustahimilivu. Tunafurahi pia kwamba mtaji huu wa kuanzisha biashara utasaidia kubadilisha fursa kuwa mafanikio yanayopimika.”

Hitimisho la Wazo Bora Pitch linaimarisha dhamira ya pamoja ya Standard Chartered Bank Tanzania na Challenges Worldwide Tanzania ya kukuza uchumi shirikishi na kuwawezesha wajasiriamali kujenga biashara imara zinazozalisha ajira.







Mkutano Mkuu wa 12 wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri Tanzania Bara (REDEOA) umeendelea kufanyika jijini Arusha kwa siku saba tangu ulipofunguliwa rasmi Machi 2, 2026 na Waziri wa Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Profesa Riziki Shemdoe.

Mkutano huo unawakutanisha Maafisa Elimu pamoja na wadau wa sekta hiyo kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha utendaji na kuongeza matokeo chanya katika sekta ya elimu nchini.

Akiwasilisha mada kuhusu Itifaki na Tabia Njema, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dk. Maulid J. Maulid, amesema viongozi wanapaswa kuishi kwa kuzingatia misingi ya nidhamu, tabia njema na utii kwa sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia utendaji wa shughuli za kisekta.

Amesema kuzingatia itifaki na maadili mema kutaimarisha mahusiano kati ya wadau na wasimamizi wa sekta ya elimu na kusaidia kufanikisha malengo ya kisera yaliyowekwa na Serikali.

“Taswira njema ya utumishi wa umma hujengwa katika misingi ya nidhamu, tabia njema na uwajibikaji,” amesema Dk. Maulid.

Aidha, amesisitiza kuwa uimarishaji wa itifaki utaongeza weledi na uwajibikaji miongoni mwa viongozi wa elimu, hali itakayochangia kuleta ufanisi zaidi katika taasisi wanazozisimamia.

Amehitimisha kwa kuwataka viongozi hao kuwa mabalozi wazuri wa maadili na utaratibu katika maeneo yao ya kazi ili kuongeza tija na kuchochea maendeleo ya sekta ya elimu na Taifa kwa ujumla.








Top News