Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba amekagua maandalizi ya siku ya mashujaa yaliyofanyika katika uwanja wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali Mtumba Mkoa wa Dodoma.

Akizungumza mara maada ya kushuhudia majaribio ambayo yamefanywa na vikosi vya ulinzi na usalama amesema kuwa mpaka sasa mambo yanaenda vizuri na kupongeza maandalizi hayo.

"Nimekuja kujionea hatua ya maandalizi yanayoendelea kabla ya tukio letu kubwa na la kihistoria ambalo litafanyika tarehe 25/7/2026,, nikiri nimeridhishwa na maandalizi kufuatia taarifa ambayo tumepokea na kile ambacho tumejionea,,,.

Hapo awali Waziri wa Mambo ya Ndani kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi Mhe,Patrobas Katambi akisoma taarifa ya maandalizi amesema katika ya siku ya mashujaa tayari vipo vikundi mbalilimbali kutoka katika vyombo vya ulinzi na usalama.

Ameongeza kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya ulinzi na Usalama Mhe.Dkt Samia Hassan kwa maelekezo yake mahususi kwa ajiri ya kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi.

" Tunawahakikishia Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wako salama na kwa wageni wanaokuja kwa kufuata utaratibu nao wako salama,,.

Katika tukio hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule na wakuu wa vyombo ulinzi na Usalama wa Mkoa huu.









Na Mwandishi Wetu, Tabora

Wananchi wa mikoa ya Tabora na Katavi wameanza kushuhudia matokeo ya Mradi Shirikishi wa Uhifadhi wa Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame, huku shughuli za uhifadhi zikigeuka kuwa chanzo cha kipato, ajira na matumizi endelevu ya rasilimali za misitu.

Mafanikio hayo yamebainika wakati Kamati ya Wataalamu ya mradi ilipofanya ziara ya Julai 15 na 16, 2026 kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika maeneo ya mradi na kujionea namna zinavyowanufaisha wananchi.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi mbele ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora kabla ya ziara hiyo, Kaimu Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Dk. Zainabu Bungwa, alisema mradi umeanza kuleta mabadiliko yanayoonekana katika uhifadhi wa misitu na ustawi wa jamii kupitia uwekezaji kwenye shughuli za uzalishaji na maendeleo.

Alisema mradi umewezesha uanzishwaji wa vikundi vya wananchi vinavyojishughulisha na shughuli za kiuchumi, ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa magari na pikipiki kwa ajili ya usimamizi wa rasilimali za misitu, ujenzi wa maghala ya kuhifadhi mbegu za miti, mashamba darasa ya kilimo mseto cha misitu, ufugaji wa nyuki, maeneo ya malisho ya mifugo pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

“Tunaanza kuona matokeo chanya ya mradi katika maeneo mengi. Wananchi wanashiriki kikamilifu kwenye shughuli za uhifadhi huku wakiongeza kipato kupitia fursa zinazotokana na matumizi endelevu ya misitu,” alisema Dk. Bungwa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, John Gharuth Mboya, alisema mafanikio ya mradi yanapaswa kuambatana na uelewa wa pamoja wa viongozi wa mikoa na wilaya ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wake.

Alisema kuna umuhimu wa kuandaliwa taarifa ya kina itakayowasilishwa kwa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa na wilaya husika ili kuzijengea uelewa kuhusu malengo, mafanikio na mchango wa mradi katika maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Afisa Misitu wa Mkoa huo, Augustine Hildagadess, aliwataka wananchi kutenga maeneo rasmi ya malisho ya mifugo ili kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi na kuimarisha uhifadhi wa misitu.

Akizungumza baada ya kutembelea vijiji vya Mtakuja na Legezamwili wilayani Mlele, alisema wataalamu wa mradi wataendelea kushirikiana na vijiji kupanga matumizi bora ya ardhi yatakayolinda mazingira na wakati huo huo kukuza uzalishaji.

Katika ziara hiyo, Kamati ya Wataalamu iligawanyika katika makundi mawili. Kundi la kwanza lilikagua shughuli za mradi wilayani Sikonge, Kituo cha Ulinzi na Kituo cha Ufugaji Nyuki cha TFS Mlele pamoja na ofisi za viongozi wa Mkoa wa Katavi na Wilaya ya Mlele, huku kundi la pili likitembelea shughuli zinazotekelezwa katika wilaya za Urambo na Kaliua.

Mradi Shirikishi wa Uhifadhi wa Misitu ya Miombo ya Nyanda Kame unafadhiliwa na Mfuko wa Mazingira Duniani (GEF) kupitia Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa ushirikiano na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Mradi huo wenye thamani ya dola za Marekani 6,785,882 unatekelezwa kuanzia mwaka 2023 hadi 2027 ukiwa na lengo la kurejesha takribani hekta 34,000 za misitu ya miombo iliyoharibiwa, kuboresha maisha ya wananchi wanaoizunguka misitu na kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu.

Mbali na TFS na FAO, utekelezaji wa mradi unahusisha Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ICRAF, TARI, Wizara ya Maji, Wizara ya Mifugo, TAMISEMI pamoja na vikundi vya kijamii vinavyoshiriki katika shughuli za uhifadhi na maendeleo kwenye maeneo ya mradi.










Na Hamis Dambaya - Stockholm

Balozi wa Tanzania nchini Sweden mheshimiwa Swahiba Mndeme amesema miongoni mwa kazi kubwa waliyonayo katika Ubalozi huo ni kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania katika nchi ya Sweden, Finland, Norway, Denmark, Iceland, Latvia, Lithuania, Estonia na Ukraine ili kuongeza idadi ya watalii kutoka nchi hizo kutembelea Tanzania.

Balozi Mndeme ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na maafisa kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro waliotembelea ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Sweden kushiriki programu mbalimbali ikiwemo siku ya tamasha la Kiswahili kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii

“Maeneo ninayoyasimamia ya takriban nchi tisa ni ya kimkakati hivyo mimi na watumishi wenzangu katika ubalozi wetu, tunatumia fursa zilizopo katika nchi hizi kutangaza vivutio vyetu na ninaamini tukishirikiana kwa pamoja tutaibua soko jipya la utalii katika ukanda huu”,alisema balozi Mndeme.

Kwa upande wake Meneja mawasiliano na uhusiano kwa umma wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Hamis Dambaya amesema Mamlaka ina mkakati wa kuibua mazao mapya ya utalii ikiwemo ya malikale, urithi utamaduni na kuendeleza mazao yaliyopo ili kuyaongezea thamani kwa wageni wanaotembelea hifadhi ya Ngorongoro.

“Tuna kampeni mbalimbali tunazoziendesha ikiwemo kuhamasisha watu duniani kurudi nyumbani Ngorongoro ili kupata ukweli kuhusu historia ya binadamu wa kale aliyepatikana katika eneo la Ngorongoro”,alisema bwana Dambaya.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inatangaza shughuli zake za utalii nchini Sweden ambapo itashiriki katika tukio kubwa la maadhimisho ya siku ya kiswahili nchini humo.



Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Julai 17, 2026 amekagua na kupokea taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika Julai 25, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa, Mtumba, jijini Dodoma.

Katika ukaguzi huo, Waziri Mkuu ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuwataka wote wanaohusika kuendelea kukamilisha maandalizi yaliyobaki kwa wakati ili maadhimisho hayo yafanyike kwa utaratibu na hadhi inayostahili.

Maadhimisho hayo yataongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu.






Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya MiXX imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia kampeni ya "Kombe la Dunia ya Ikiingia Tu... Golii!", inayowapa nafasi ya kujishindia zawadi kwa kufanya malipo ya huduma mbalimbali kupitia MiXX Super App.

Katika wiki ya nane ya kampeni hiyo, washindi sita walitangazwa, ambapo wanne walikabidhiwa fedha taslimu za shilingi milioni moja kila mmoja, huku washindi wawili wakijishindia vifaa vya kisasa vya Hisense.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi hizo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Malipo ya Kidijitali wa MiXX, Mshamma Mshamma, alisema kampeni hiyo imeendelea kuwafikia Watanzania wengi, huku jumla ya washindi 80 wakinufaika tangu ilipoanza.

Alisema washindi wamekuwa wakijishindia fedha taslimu pamoja na vifaa mbalimbali vinavyotolewa kwa ushirikiano na kampuni ya Hisense, jambo linaloonyesha dhamira ya MiXX ya kuwazawadia wateja wake waaminifu.

Mshamma alisema kampeni bado inaendelea, akibainisha kuwa mshindi wa mwisho ataondoka na zawadi kubwa ya shilingi milioni 50.

Aliwahimiza wananchi kuendelea kutumia MiXX Super App kufanya malipo ya huduma mbalimbali za kifedha ili kuongeza nafasi ya kushinda zawadi hizo.

"MiXX Super App ni zaidi ya programu ya malipo. Ni jukwaa linalorahisisha huduma za kifedha huku likiwapa watumiaji nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali," alisema Mshamma.

Mmoja wa washindi, Ibrahim Mandoa, mkazi wa Kinondoni, alisema ushindi wake umempa imani kuwa kampeni hiyo ni ya kweli na inawanufaisha watumiaji wa MiXX Super App.

"Nimefurahi sana kushinda na hii ni mara yangu ya kwanza kupata zawadi kama hii, na ninawahimiza Watanzania kuipakua na kuitumia MiXX Super App mara kwa mara kufanya malipo mbalimbali ili nao wapate nafasi ya kushinda," alisema Mandoa


Dar es Salaam, Julai 17, 2026

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetangaza nafuu kwa waajiri wenye malimbikizo ya michango kwa kuwapatia fursa ya msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango, huku ukiwataka kuchangamkia fursa hiyo ili kupunguza mzigo wa madeni, kuimarisha uzingatiaji wa sheria na kulinda haki za wafanyakazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema kuwa msamaha huo, ulioanza kutekelezwa tarehe 1 Juni 2026, utaendelea hadi 31 Desemba 2026.

Bw. Mshomba alieleza kuwa tangu kuanza kwa msamaha huo, waajiri wameonyesha mwitikio chanya ambapo hadi sasa zaidi ya waajiri 6,000 wamejitokeza kutumia fursa hiyo na Mfuko umekwishakusanya zaidi ya shilingi bilioni 46 za michango tangu kuanza kwa msamaha huo tarehe 1 Juni 2026.

“Tunawasihi waajiri wote kutumia fursa hii mapema. Fedha ambazo wangezilipa kama tozo wanaweza kuzielekeza katika shughuli za uzalishaji, upanuzi wa biashara, kuongeza tija na kuboresha ustawi wa wafanyakazi,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema msamaha huo utaendelea hadi tarehe 31 Desemba 2026, ambapo waajiri watakaolipa malimbikizo yote ya michango ya msingi ifikapo tarehe 31 Agosti 2026 watanufaika na msamaha wa asilimia 100 ya tozo.

Alifafanua kuwa waajiri watakaokamilisha malipo yao kati ya Septemba na Oktoba 2026, watanufaika na msamaha wa asilimia 75, huku wale watakaolipa kati ya Novemba na Desemba 2026 wakipata msamaha wa asilimia 50.

Aidha, alisema waajiri ambao hawakuwa na malimbikizo ya michango hadi tarehe 31 Mei 2026 lakini walikuwa na tozo pekee, watanufaika na msamaha wa asilimia 100 endapo wataendelea kuwasilisha michango yao kwa wakati hadi mwezi Desemba 2026.

Bw. Mshomba alisema fursa hiyo imetolewa ili kuwapa waajiri nafasi ya kurekebisha hali ya ulipaji wa michango na kutumia fedha ambazo zingelipwa kama tozo katika shughuli za uzalishaji, kuongeza tija na kuboresha mazingira ya kazi.

“Fedha ambazo waajiri wamekuwa wakizilipa kwa ajili ya kufidia tozo zinaweza kuelekezwa katika kuboresha maeneo yao ya kazi, kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji.

Ndiyo maana fursa hii imetolewa ili waajiri wanufaike,” alisema.

Alisema ulipaji wa michango kwa wakati ni muhimu kwa kuwa unamwezesha mfanyakazi kupata haki zake za hifadhi ya jamii wakati anapopata majanga mbalimbali ikiwemo kustaafu.

NSSF YAENDELEA KUIMARIKA

Katika hatua nyingine, Bw. Mshomba alisema NSSF imeendelea kuimarika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, ambapo thamani ya Mfuko imeongezeka kutoka shilingi trilioni 4.8 mwezi Machi 2021 hadi kufikia zaidi ya shilingi trilioni 11.6 Juni 2026.

Alisema ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la wanachama na michango, uwekezaji wenye tija, mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma.

Alieleza kuwa kupitia mifumo ya TEHAMA, waajiri na wanachama sasa wanaweza kufuatilia na kuwasilisha michango, kufuatilia madai ya mafao na kupata huduma mbalimbali bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Kuhusu ulipaji wa mafao, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuboresha mifumo yake ambapo kwa sasa mafao mengi hulipwa ndani ya siku 20, tofauti na siku 60 zinazotakiwa kisheria.

“Lengo letu ni kuhakikisha mwanachama anapata stahiki zake kwa wakati. Endapo kuna ucheleweshaji mara nyingi chanzo huwa ni mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati,” alisema.

UWEKEZAJI WENYE TIJA, SKIMU YA HIFADHI KUONGEZA WANUFAIKA

Akizungumzia uwekezaji, alisema NSSF inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati inayochangia ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira, akitolea mfano Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kimeendelea kuongeza uzalishaji, kutoa ajira na kuwawezesha wakulima wanaokizunguka.

Kuhusu Skimu ya Hifadhi, Bw. Mshomba alisema mpango huo umewezesha wananchi waliojiajiri kujiunga na mfumo wa hifadhi ya jamii na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi pamoja na huduma za matibabu.

“Tunawahimiza waliojiajiri kujiunga kupitia Skimu ya Hifadhi kwa sababu mpango huu unabadilisha maisha yao na kuwapa uhakika wa kunufaika na mafao mbalimbali. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa Staa wa Mchezo katika kujilinda dhidi ya changamoto za maisha,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema NSSF itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha mfumo wa hifadhi ya jamii nchini na kuhakikisha unaleta manufaa kwa Watanzania wengi zaidi.
















Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Yas Tanzania imesema itaendelea kuenzi urithi wa Hayati Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, kwa kuwekeza katika teknolojia za kidijitali na kuimarisha ushirikiano unaolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa Watanzania.

Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha urithi wa Hayati Mkapa, mwakilishi wa Yas Afisa Mkuu wa fedha Innocent Rwetabura alisema kiongozi huyo aliamini kuwa nguvu ya taifa hupimwa kwa ustawi wa wananchi wake, huku akisisitiza umuhimu wa kujenga taasisi imara, mifumo endelevu na ushirikiano unaochochea maendeleo ya kizazi hadi kizazi.

Retabura alisema wakati Tanzania ikielekea kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, teknolojia imepewa nafasi muhimu katika kuimarisha sekta ya afya kupitia mifumo ya taarifa za afya, huduma za afya kidijitali na matumizi ya takwimu sahihi katika kufanya maamuzi.

Alieleza kuwa pamoja na kuendelea kuimarisha miundombinu ya afya, teknolojia sasa imekuwa nguzo muhimu katika kubadilisha namna huduma zinavyotolewa, ikiwemo tiba kwa njia ya mtandao (telemedicine), uchunguzi wa magonjwa kwa njia za kidijitali, mafunzo endelevu kwa wataalamu wa afya na huduma za dharura zinazowafikia wananchi kwa haraka.

Kwa mujibu wa Yas, mafanikio hayo yamechangiwa na uwekezaji mkubwa wa kampuni katika sekta ya mawasiliano, ambapo katika kipindi cha miaka minne iliyopita imewekeza zaidi ya shilingi trilioni 1.2 kupanua upatikanaji wa teknolojia za 4G na 5G nchini kote.

Aidha, kampuni hiyo ilieleza kuwa maendeleo ya teknolojia yamefungua fursa kwa vijana wabunifu, wahandisi na wajasiriamali wa kijamii kushiriki katika kutatua changamoto mbalimbali za afya kupitia ubunifu wa kidijitali.

"Hayati Rais Mkapa aliwahi kusema kuwa mustakabali wa nchi uko mikononi mwa vijana. Leo tunashuhudia kauli hiyo ikitimia kupitia matumizi ya teknolojia ambayo yanawapa vijana uwezo wa kubuni suluhisho za kuboresha huduma za afya," alisema.

Yas pia ilisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi, ikisema ndiyo msingi wa kuharakisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Kampuni hiyo ilitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa kwa ushirikiano na Serikali na wadau mbalimbali, ikiwemo mradi wa usajili wa vizazi kupitia RITA na UNICEF uliotumia teknolojia ya simu kuwezesha watoto chini ya miaka mitano kupata vyeti vya kuzaliwa kwa njia ya SMS, ambapo zaidi ya watoto milioni 13 wamesajiliwa.

Pia ilieleza kuwa imeshirikiana na Hospitali ya CCBRT katika matibabu ya watoto wenye tatizo la miguu ya kupinda (clubfoot), sambamba na kuendesha huduma za bure za uchunguzi na matibabu ya macho nchini Tanzania Bara na Zanzibar, ambazo hadi sasa zimewanufaisha zaidi ya Watanzania 23,000.

Katika hatua nyingine, Yas ilitangaza kuwa ipo katika mazungumzo na Taasisi ya Benjamin William Mkapa kwa lengo la kuanzisha ushirikiano wa kimkakati utakaotekeleza miradi endelevu ya afya na maendeleo kwa wanawake, watoto na vijana nchini.

Kampuni hiyo ilisisitiza kuwa itaendelea kuwekeza katika suluhisho bunifu za teknolojia ili kuimarisha mifumo ya afya, kupanua upatikanaji wa huduma bora na kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya sekta ya afya, ikiwa ni sehemu ya kuuenzi urithi wa Hayati Rais Benjamin William Mkapa.


 

Twenzetu Duniani na SportPesa passes 200 winners as World Cup excitement builds

Twenzetu Duniani na SportPesa passes 200 winners as World Cup excitement builds

SportPesa Tanzania has rewarded more than 200 winners in the first 2 weeks of Twenzetu Duniani na SportPesa, giving World Cup fans excitement in the tournament. The promotion gives customers a chance to win prizes for every qualifying bet they place during the tournament. Football fans across the country now have an extra reason to follow each matchday, on top of the World Cup itself. 

Twenzetu Duniani na SportPesa is giving Tanzanian fans more than matchday drama. It is giving them weekly chances to win. Every goal, prediction, and surprise result now carries extra excitement because active customers have weekly chances to win as the World Cup continues. 

How the promotion works 

Twenzetu Duniani na SportPesa works in a simple way. A player places a qualifying Sportsbook or Casino bet during the promotion period, and that bet gives them one entry into the draw. The campaign runs from 16 June 2026 to 19 July 2026, with weekly draws taking place during the campaign and the Grand Draw set for 20 July 2026.

The full promotion gives customers a chance to win from a TZS 100,000,000 prize pool. Weekly winners will share TZS 50,000,000 across the campaign period, while 10 Grand Draw winners will share another TZS 50,000,000 equally. The promotion is clear: customers follow the World Cup, place qualifying bets, and enter the draw. 

The prize money has grown fast 

The weekly prize pool has already grown quickly. Week 1 paid out TZS 5,000,000 to qualifying winners. Week 2 doubled that figure to TZS 10,000,000, reflecting how many more customers took part as the tournament progressed. 

SportPesa Tanzania expects the weekly rewards to keep climbing as the World Cup moves toward the knockout rounds. More matches, more qualifying bets, and a larger pool of entries for each draw. For fans, bigger prizes are still ahead. 

Weekly rewards keep the World Cup excitement going 

The weekly reward structure gives fans a fresh reason to stay connected as the World Cup continues. After the first two weeks, the campaign still has bigger prize moments ahead. The next phases will raise the weekly prize pool to TZS 15,000,000 and then TZS 20,000,000.

This progression keeps the promotion active beyond the opening weeks. Fans can follow fixtures, study match statistics, and enter the draws throughout the campaign period. By the end of the weekly phase, SportPesa Tanzania will have shared TZS 50,000,000 through weekly winners before the Grand Draw. 

Every World Cup match creates a new opportunity

The World Cup runs 104 matches from the group stage through the final, and each one gives fans a new reason to take part. Fans can track team form, injuries, and squad rotation before kickoff, then place a qualifying bet based on what they see. The tournament rewards fans who pay attention to these details. 

That daily interest in match conditions feeds directly into the weekly draws. A fan who follows Monday’s fixtures and places a qualifying bet has the same shot at that week’s draw as one who bets on the last match before it closes. The format ties football knowledge to a real chance of winning. 

A World Cup experience with more rewards 

The World Cup gives fans new emotions every matchday. Fans follow team news, discuss predictions, watch fixtures, and celebrate the moments that define the tournament. Twenzetu Duniani na SportPesa adds reward opportunities to that shared football experience. 

“More than 200 winners in two weeks shows that fans are not just watching the World Cup. They are actively taking part in the excitement with SportPesa. As the tournament moves forward, we expect even more customers to join the weekly draws and the Grand Draw,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

More prizes are still to come 

Twenzetu Duniani na SportPesa runs from 16 June 2026 to 19 July 2026, covering the full main World Cup campaign period Cup. On 20 July 2026, SportPesa Tanzania will hold a grand total prize pool of TZS 100,000,000. Ten grand draw winners will each receive TZS 5,000,000, for a combined TZS 50,000,000. 

The grand draw adds one more moment of reward before the World Cup and the promotion both close. It rewards customers for staying involved with SportPesa across the full tournament, from the opening group matches through the final. 

Conclusion 

Twenzetu Duniani na SportPesa runs until 19 July 2026, so fans still have time to enter both the weekly draws and the Grand Draw. As the World Cup moves into its knockout rounds, the matches, and the stakes, only get bigger. Fans can follow World Cup fixtures, place qualifying bets, and stay involved as the tournament continues. Customers must follow the official promotion terms and conditions. 

Bet responsibly

Jane Mwakyoma - Rukwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Missana Kwangura amehitimisha mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyofanyika wilayani humo mkoani Rukwa.

Kwangura aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga  Nyakia Chirukile kama mgeni rasmi amesema mafunzo hayo yanapaswa kuwa chachu ya maendeleo kwa washiriki na jamii kwa ujumla kwa kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha shughuli zao za kiuchumi.

"Kupitia mafunzo haya mliyoyapata, hakikisheni yanakuwa chachu ya maendeleo katika jamii. Tumiaeni maarifa haya kuongeza thamani ya shughuli zenu za kiuchumi, kujiongezea kipato na kuchangia maendeleo ya Taifa," alisema  Kwangura.

Aidha amesema programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi zina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi, kupunguza umaskini na kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa Jacqueline Chrisant Mzindakaya amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uwezo wa kutambua na kunufaika na fursa mbalimbali za mitaji ili waweze kuanzisha, kuendeleza na kupanua shughuli zao za kiuchumi.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Gwakisa Bapala amesema mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa NEEC wa kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwapatia elimu kuhusu fursa za mitaji, namna ya kuandaa miradi inayoweza kupata ufadhili pamoja na matumizi sahihi ya mikopo ili kukuza biashara.

Mafunzo hayo yamewakutanisha wadau mbalimbali wa uwezeshaji wananchi kiuchumi, wakiwemo SELF Microfinance Fund (SELF MF), Benki ya CRDB, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Agricultural Inputs Trust Fund (AGITF), Azania Bank pamoja na PASS Trust, ambao wametoa elimu kuhusu huduma na fursa za kifedha zinazopatikana kwa wananchi .





Pendekezo la Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Songea (SOUWASA) la kuongeza bei ya maji kwa matumizi ya nyumbani kutoka shilingi 1,730 hadi shilingi 2,700 kwa kila mita ya ujazo limejadiliwa katika mkutano wa wadau ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) uliofanyika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Mkutano huo umefanyika Julai 16, 2026, ukiwa na lengo la kukusanya maoni ya wananchi na wadau kuhusu ombi hilo la marekebisho ya bei za huduma za majisafi na uondoaji wa majitaka kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2026/27 hadi 2030/31.

Akifungua mkutano huo, Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa EWURA, Mhandisi Walter Christopher, amesema zoezi hilo ni sehemu ya utaratibu wa kisheria unaolenga kuhakikisha maamuzi ya bei yanafanywa kwa kuzingatia maoni ya wananchi pamoja na hali halisi ya utoaji wa huduma.

Mhandisi Christopher amesema SOUWASA imeomba marekebisho ya bei kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na matengenezo, upanuzi wa mtandao wa maji na majitaka pamoja na ukarabati wa miundombinu chakavu.

Ameeleza kuwa EWURA itachambua maoni yote yatakayopokelewa kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho, huku akisisitiza kuwa lengo ni kupata uwiano kati ya uwezo wa wananchi kumudu gharama za maji na uwezo wa mamlaka kuendelea kutoa huduma bora na endelevu.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amesema sekta ya maji ni msingi wa maendeleo ya jamii na uchumi, hivyo maamuzi kuhusu bei yanapaswa kufanyika kwa ushirikishwaji wa wananchi.

Kwa upande wake, Mhandisi Jafari Kinjalambaya wa SOUWASA amesema mapendekezo ya marekebisho ya bei yanalenga kuwezesha mamlaka kukarabati kilomita 32 za mabomba chakavu, kujenga vyanzo vipya vya maji, matenki na mtambo wa kutibu maji, kusambaza mabomba kwa urefu wa kilomita 194.7, kupanua mtandao wa majitaka kwa kilomita 14 pamoja na kufunga mita mpya za malipo ya awali na kubadilisha mita chakavu ili kuboresha ukusanyaji wa mapato na huduma kwa wateja.

Hata hivyo, wananchi na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano huo wametoa maoni tofauti kuhusu pendekezo hilo, wakitaka Serikali na EWURA kuzingatia uwezo wa wananchi wenye kipato cha chini kabla ya kuidhinisha ongezeko la bei.



Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, tarehe 7 Julai 2026 aliongoza Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili yaliyofanyika katika Bunge la Uingereza (House of Lords), jijini London.

Maadhimisho hayo yalifanyika kwa mwaliko maalum wa Mheshimiwa Lord Paul Boateng, Mjumbe wa Baraza la Juu la Bunge la Uingereza (House of Lords), na yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali, wanadiplomasia, wabunge, wadau wa elimu pamoja na wapenzi wa lugha ya Kiswahili kutoka mataifa mbalimbali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Salma Kikwete alisisitiza umuhimu wa Kiswahili kama chombo cha kuimarisha mshikamano, utamaduni na maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani Afrika na duniani kwa ujumla. Alieleza kuwa kuendelea kwa matumizi ya Kiswahili katika majukwaa ya kimataifa ni ushahidi wa nafasi yake kubwa katika kuunganisha watu wa tamaduni na mataifa mbalimbali.

Mheshimiwa Salma Kikwete, ambaye pia ni Balozi wa Heshima wa Kiswahili Barani Afrika, alibainisha kuwa lugha ya Kiswahili imeendelea kupata heshima na kutambulika duniani, hatua inayochangiwa na juhudi za viongozi, taasisi na wadau mbalimbali wanaoendelea kuikuza na kuieneza lugha hiyo katika nyanja za elimu, biashara, diplomasia na teknolojia.

Maadhimisho hayo pia yalihudhuriwa na Mabalozi wa nchi mbalimbali za Afrika nchini Uingereza wakiongozwa na Mheshimiwa Christiane Katsande, Balozi wa Zimbabwe nchini Uingereza na Amidi wa Mabalozi wa nchi za Afrika wanaowakilisha mataifa yao nchini humo. Ushiriki wa mabalozi hao uliakisi mshikamano wa Afrika katika kuendeleza na kuipa hadhi lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya mawasiliano na utangamano wa bara hilo.

Kwa upande mwingine, maadhimisho hayo yalipambwa pia na uwepo wa mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kanda Bongo Man, ambaye ni miongoni mwa wasanii wa Afrika waliotoa mchango mkubwa katika kueneza matumizi na umaarufu wa Kiswahili kupitia muziki wake uliovuka mipaka ya bara la Afrika na kufikia hadhira ya kimataifa.

Aidha, Mheshimiwa Salma Kikwete aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wadau wengine kwa juhudi zao za kuendeleza na kuhamasisha matumizi ya Kiswahili kimataifa, akisisitiza kuwa lugha hiyo ni sehemu muhimu ya urithi wa Afrika na nyenzo ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.

Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Bunge la Uingereza yameendelea kuonesha kukua kwa hadhi na ushawishi wa Kiswahili duniani, huku Tanzania ikiendelea kuwa kinara katika juhudi za kukuza na kueneza lugha hiyo katika ngazi ya kimataifa.










Top News