(Administrative Reviews) yamewasilishwa na kushughulikiwa na Taasisi Nunuzi kupitia Moduli jambo linaloonyesha mwitikio chanya kutoka kwa wazabuni na Taasisi Nunuzi katika kutumia mfumo kwa ajili ya kupokea, kuchambua na kutoa maamuzi kuhusu malalamiko yanayohusu michakato ya ununuzi wa Umma.
Jumla ya rufaa 26 zimewasilishwa na kushughulikiwa na Mamlaka ya Rufani kupitia moduli hiyo, hatua ambayo imeongeza ufanisi katika usimamizi wa rufaa, kupunguza muda wa kushughulikia mashauri, na kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa haki.
James Sando Katibu Mtendaji Mamlaka ya Rufani ya Wazabuni za Umma (PPAA) ameyabainisha hayo leo jijini Dodoma katika Makutano na Waandishi wa Habari akitangaza miradi ya maendeleo na fursa za vijana kwa mwaka 2025/20.
Sando amesema kwa ujumla, takwimu hizo zinaonesha mafanikio makubwa ya awali katika matumizi ya Moduli ya kushugulikia Malalamiko na Rufaa, zinaimarisha mifumo ya ununuzi wa umma nchini kwa kuhakikisha uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika mchakato wa Ununuzi.
Katika kuendeleza azma ya Serikali ya kuimarisha uwazi, uwajibikaji, na ufanisi katika sekta ya ununuzi wa umma hususan ushughulikiwaji wa malalamiko na rufaa zinazotokana na michakato ya ununuzi wa umma,
Mamlaka ya Rufani kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), imekamilisha ujenzi wa Moduli ya Kupokea na kushughulikia Malalamiko na Rufaa zinazotokana na michakato ya Ununuzi wa Umma (Complaints and Appeals Management Module).
"Moduli hii ipo katika Mfumo wa Ununuzi wa Umma kwa Njia ya Kielektroniki (NeST), na inatoa njia rahisi, ya haraka, na yenye uwazi kwa wadau wote kushiriki katika mchakato wa usulushi wa migogoro ya ununuzi"
Amesema inachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha utendaji na kuimarisha imani katika mfumo wa ununuzi wa umma.
Hata hivyo Sando amesema Serikali kupitia Wizara ya Fedha ilizindua rasmi matumizi ya moduli hiyo Februari 2025, Tangu uzinduzi huo, moduli imeleta mageuzi chanya katika namna taasisi za umma zinavyoshirikiana na Mamlaka ya Rufani kupokea, kusajili na kushughulikia malalamiko na rufaa kutoka kwa wazabuni walioshiriki katika michakato ya ununuzi wa umma na kwa sasa, malalamiko yote yanawasilishwa kupitia moduli ya Usimamizi wa Malalamiko na Rufaa katika mfumo wa NeST.
"Moduli hii imeendelea kutumika na wadau mbalimbali kwa madhumuni ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki, ikileta ufanisi mkubwa katika mchakato mzima.
Sando atoa wito kwa wazabuni wote nchini pamoja na wadau wa ununuzi wa umma kushiriki mafunzo ya matumizi ya moduli hiyo pale Mamlaka ya Rufani inapoyatangaza Mafunzo.
yatawawezesha kuelewa namna bora ya kutumia moduli hiyo pale wanapokabiliwa na changamoto katika michakato ya ununuzi wa umma.



.jpeg)


.jpeg)








