Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 28 Juni, 2026.

 

WAZIRI MKUU Dkt.  Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania waendelee kuhimizana kuhusu ulinzi wa Taifa na kamwe wasipuuze viashiria vya uvunjifu wa amani.

"Tuendelee kuhimizana kuhusu suala la ulinzi wa Taifa letu. Ulinzi wa Taifa letu ni wa kila Mtanzania na amani yetu ni ya kila Mtanzania."

"Sasa hivi hatupaswi kupuuzia viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Hatutakiwi kuvipuuza kwa sababu vimetuachia doa," amesema.

Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumapili, Juni 28, 2026) katika ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye usharika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida. 

Harambee hiyo ambayo ni ya nne kufanyika, ililenga kukusanya sh. bilioni 1.4 kwa ajili ya kuboresha vituo vya huduma za afya, kuimarisha vituo vya huduma za elimu, utumishi na uinjilisti vya Dayosisi hiyo ambavyo vinapaswa kukamilika ifikapo Desemba, mwaka huu.

Jumla ya sh. bilioni 1.331 zilikusanywa zikiwa ni fedha taslimu na ahadi.  Waziri Mkuu amesema sh. milioni 69 zilizobakia, zitakamilishwa ndani ya wiki ijayo kutokana na ahadi zilizotolewa na watu mbalimbali na timu aliyoiunda yeye ili isimamie kukamilishwa kwa ahadi hiyo.

Mapema, akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo, Mkuu wa Kanisa la KKKT, Askofu Dkt. Alex Gehazi Malasusa alisema kupitia harambee hiyo, washarika wamepewa nafasi ya kumrudishia Mungu shukrani kwa ukarimu aliowatendea maishani mwao.

"Kila tunachokifanya kinapaswa kimtukuze Mungu, mali na fedha zetu ziwe za halali, zisitokane na kuwakanyaga wengine. Mali na fedha zetu zitawaliwe na Mungu," alisisitiza. 

Naye, Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kati, Dkt. Cyprian Hilinti alisema kanisa hilo linaendelea kutekeleza jukumu la kuwaombea viongozi wa nchi kila Jumapili ikiwemo kuombea amani baina ya kabila na kabila, wakulima na wafugaji na vyama kwa vyama. 

"Tunatamani kuona msamaha ukipatikana katika nyanja tofauti. Msamaha ni dawa," alisema.

Alisema tangu waanze harambee hiyo miaka minne iliyopita, majimbo nane yamezaliwa, sharika mpya 27 zimezaliwa, wamepata washarika wapya 17,364 na wachungaji wapya 65.

Kwa upande wa huduma za jamii, Askofu Hilinti alisema wamefanikiwa kusajili shule mpya mbili za sekondari, shule moja ya msingi inayofundisha kwa Kiingereza (English medium) na akatumia fursa hiyo kuwashukuru washarika wote wa Dayosisi hiyo kwa kujitoa kwao katika kipindi chote hicho.
















Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma imeendesha zoezi la upandaji miti katika Shule ya Sekondari Miyuji B, iliyopo eneo la Mpamaa jijini Dodoma Juni 28,   2026, ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuelekea maadhimisho ya miaka 30 ya TRA pamoja na Tuzo za Rais kwa Walipakodi Bora. Zoezi hilo linalenga kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Meneja wa TRA Mkoa wa Dodoma, Pendolake Elinisafi, amesema katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA, Mamlaka imepata mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma kwa walipakodi kupitia maboresho ya mifumo ya kidijitali, ikiwemo Mfumo wa IDRAS, ambao umerahisisha ulipaji wa kodi, kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Elinisafi amesema mafanikio hayo yametokana na maboresho ya mifumo ya utoaji huduma, matumizi ya teknolojia pamoja na kujituma kwa watumishi wa TRA katika kuwahudumia walipakodi kwa weledi na ufanisi.

Aidha, amewapongeza watumishi wa TRA kwa mchango wao mkubwa katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, akieleza kuwa fedha zinazokusanywa kupitia kodi zimeendelea kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini, ikiwemo uboreshaji wa huduma za elimu, afya, ujenzi wa barabara na miundombinu mingine muhimu inayowanufaisha wananchi.

Amesema maadhimisho ya miaka 30 ya TRA yanatoa fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo mwaka 1996, huku yakichochea dhamira ya kuendelea kuboresha huduma kwa walipakodi na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo ya Taifa.

Akizungumzia zoezi la upandaji miti, amesema TRA imeamua kuhusisha maadhimisho hayo na shughuli za uhifadhi wa mazingira ili kuhamasisha jamii kutunza mazingira na kuchangia juhudi za kitaifa za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Pia amewahimiza Watanzania kuendelea kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa kwa kudai risiti za kielektroniki wanaponunua bidhaa au huduma na kutoa risiti wanapouza bidhaa au huduma, akisisitiza kuwa ulipaji wa kodi ni msingi wa maendeleo na utoaji wa huduma bora za kijamii kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Miyuji B, Mwalimu Joshua Nashari, ameishukuru TRA Mkoa wa Dodoma kwa kuichagua shule hiyo kwa zoezi la upandaji miti, akieleza kuwa miti hiyo itachangia kuboresha mazingira ya shule na kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kutunza mazingira.

Baadhi ya wazazi waliohudhuria shughuli hiyo, wameahidi kuwa wataendelea kushirikiana na walimu pamoja na wanafunzi kuitunza miti hiyo ili ikue na kuendelea kutoa manufaa kwa shule na jamii kwa ujumla kwa miaka mingi ijayo.







Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma


Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amewapongeza waandishi wa habari nchini kwa kazi wanayoifanya ya kuhabarisha umma, akieleza kuwa wao ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi.

Msigwa ameyazungumza hayo leo katika Mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma ambapo amesema Serikali inatambua mchango mkubwa wa waandishi wa habari katika kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi, akisisitiza kuwa bila vyombo vya habari na waandishi wake, mawasiliano kati ya Serikali na wananchi yasingekuwa na ufanisi unaostahili.

"Mnafanya kazi nzuri sana na ya kizalendo kwa maslahi ya Tanzania. Serikali inatambua jukumu lenu na itaendelea kushirikiana nanyi wakati wote mtakapohitaji ushirikiano," amesema Msigwa.

Amesema Serikali itaendelea kuipa ushirikiano sekta ya habari kwa kuwa inaamini waandishi wa habari ni wadau muhimu katika kujenga jamii yenye taarifa sahihi, uwajibikaji na maendeleo.

Hata hivyo, Msigwa amesema bado wapo watu wanaotamani kuona waandishi wa habari wakitumiwa kusambaza maudhui yanayoweza kuleta madhara kwa jamii na taifa, ikiwemo taarifa za uongo, chuki, uchonganishi, udhalilishaji pamoja na maudhui yanayolenga kuidhalilisha Tanzania.

Kwa mujibu wa Msigwa, hatua ya waandishi wengi wa habari kuendelea kusimamia misingi ya taaluma yao na kutokubali kutumiwa vibaya ni jambo la kupongezwa kwani limeendelea kulinda maslahi ya taifa na kuimarisha amani na mshikamano wa Watanzania.

Akizungumza kwa nafasi yake kama Msemaji Mkuu wa Serikali na msimamizi wa sekta ya habari nchini, Msigwa ametoa wito kwa waandishi wa habari kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kuzingatia maadili ya taaluma pamoja na sheria za nchi, huku wakitanguliza maslahi ya Watanzania katika kazi zao.

"Endeleeni kutumia kalamu zenu kwa manufaa ya Watanzania na maendeleo ya Taifa, si kwa maslahi ya watu wachache waliojipa jukumu la kuvuruga amani, umoja na mshikamano wa nchi," amesisitiza.

Kauli hiyo inaakisi msimamo wa Serikali wa kuendelea kushirikiana na sekta ya habari katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, zenye kujenga umoja wa kitaifa na kuchochea maendeleo ya Tanzania.


Mwanza.

‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), kupitia mradi wa RISE imehitimisha mafunzo ya Wakufunzi Wasaidizi (Training of Trainers – ToTs) yaliyowashirikisha wataalamu wa TARURA pamoja na Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa matengenezo ya kawaida ya barabara kupitia vikundi vya kijamii.

‎‎Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Mhandisi Richard Missa kutoka TARURA alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo maafisa na wadau watakaosimamia utekelezaji wa mradi ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika matengenezo ya barabara huku wakinufaika kiuchumi kupitia ajira na shughuli za matengenezo ya mara kwa mara.

‎"Lengo letu ni kuhakikisha wananchi wanakuwa sehemu ya utunzaji wa miundombinu ya barabara huku wakiongeza kipato chao. Zoezi hili ni endelevu na linahitaji ushirikiano wa kila mmoja wetu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa", amesema Mhandisi Missa.

‎Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya mradi wa RISE kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhandisi Emmanuel Mhiliwa, amesema serikali ina imani kuwa wataalamu wote waliopata mafunzo hayo watakwenda kuyatumia kwa ufanisi katika maeneo yao ya kazi na kuhakikisha vikundi vya kijamii vinafanya kazi kwa weledi.

‎‎"Kuna mawazo ya wananchi kuwa barabara ni mali ya TARURA au TANROADS pekee, wakati ukweli ni kwamba barabara ni mali ya wananchi wote, ndiyo maana tunaunda vikundi hivi vya kijamii ili wananchi washiriki moja kwa moja katika kutunza barabara. Hii itawajengea hisia ya umiliki wa miradi, kuongeza ajira, kulinda miundombinu hiyo na kuhakikisha inadumu kwa manufaa yao", amesema.








Na Janeth Raphael MichuziTv


Benki ya CRDB imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuwekeza katika ustawi wa wafanyakazi kwa kuendesha programu ya Wellness Day jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha wafanyakazi wanakuwa na afya bora ya mwili, akili na hisia ili kuongeza ufanisi kazini na kuboresha huduma kwa wateja.

Programu hiyo, ambayo imekuwa ikiadhimishwa kwa miaka sita mfululizo, imewakutanisha mamia ya wafanyakazi wa benki hiyo katika viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlin, ambapo walishiriki mazoezi ya viungo, michezo mbalimbali, vipimo vya afya pamoja na semina za lishe, afya ya akili na usimamizi wa mtindo bora wa maisha.

Akizungumza baada ya kuwaongoza wafanyakazi katika mazoezi ya viungo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Edward Mpina, amesema afya ya mfanyakazi ndiyo msingi wa utendaji bora wa taasisi, akisisitiza kuwa wafanyakazi wenye afya njema na utulivu wa akili huchangia kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma bora kwa wateja.

Amesema benki imeendelea kuweka ustawi wa wafanyakazi wake katika ajenda za kipaumbele kwa kuwa mafanikio ya taasisi yanategemea nguvu kazi yenye afya, motisha na uwezo wa kutekeleza majukumu kwa ufanisi.

“Tumekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wateja wetu wanapata huduma bora wakati wote. Hata hivyo, hilo haliwezi kufikiwa bila kuwa na wafanyakazi wenye afya njema ya mwili na akili. Wellness Day ni sehemu ya mkakati wetu wa kuwapa nafasi ya kupima afya, kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu lishe na mtindo wa maisha pamoja na kutatua changamoto zinazoweza kuathiri utendaji wao,” amesema Mpina.

Amebainisha kuwa kufuatia mafanikio ya programu hiyo katika maeneo mbalimbali, Benki ya CRDB itaendelea kuifikisha katika kanda zote nchini na nje ya Tanzania ambako benki hiyo inatoa huduma, ili kuhakikisha kila mfanyakazi ananufaika na mpango huo wa ustawi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Masoud Matange, amesema mazingira ya kazi ya sasa yanaweza kuwafanya wafanyakazi kutumia muda mwingi ofisini na kusahau kujali afya zao, jambo linaloweza kuongeza hatari ya magonjwa yasiyoambukiza pamoja na msongo wa mawazo.

Amesema kupitia Wellness Day, wafanyakazi wanakumbushwa umuhimu wa kufanya mazoezi mara kwa mara, kupata usingizi wa kutosha, kula lishe bora, kufanya vipimo vya afya kwa wakati na kutafuta ushauri wa kitaalamu kuhusu afya ya akili.

“Mafanikio ya Benki ya CRDB yanatokana na mchango wa kila mfanyakazi. Ndiyo maana tunaendelea kuwekeza katika afya na ustawi wao ili waweze kuendelea kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu kwa wateja wetu,” alisema Matange.

Mbali na mazoezi ya viungo na michezo, washiriki walipata huduma za uchunguzi wa afya pamoja na ushauri kutoka kwa madaktari na wataalamu wa afya kuhusu saikolojia, mahusiano, lishe, kinga dhidi ya magonjwa na namna ya kudhibiti msongo wa mawazo.

Programu hiyo ni mwendelezo wa kampeni ya Wellness Day ya mwaka 2026 ambayo ilizinduliwa jijini Mwanza kabla ya kuendelea katika kanda mbalimbali ikiwemo Burundi, Dar es Salaam, Pwani na sasa Kanda ya Kati yenye makao yake Dodoma.

Kupitia mpango huo, Benki ya CRDB inalenga kuwafikia wafanyakazi wake wote katika kanda nane za shughuli zake ndani na nje ya Tanzania, ikiwa na lengo la kujenga nguvu kazi yenye afya, weledi na uwezo wa kutoa huduma bora zinazokidhi matarajio ya wateja.











Na Victor Masangu, Pwani

Vijana wapatao kumi kutoka baadhi ya mikoa mbali mbali wamefanikiwa kutinga katika kinyang'anyiro cha shindano la Vijana uchumi Challenge kwa mwaka wa 2026 ambalo kilele chake kinatarajiwa kufanyika Julai 6 mwaka huu katika ukumbi Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa halfa ya kufunga kambi rasmi ya vijana wapatao 100 ambao walikuwa wameweka kambi ya siku nne katika shule yaa uongozi wa Mwalimu Julias Nyerere iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani.

Katibu Oomolo amesema kwamba kambi hiyo ilikuwa na vijana wapatao 100 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania bara na visiwani ambapo wameweza kufanyiwa usahili na kufanyiwa mchujo kutoka kwa majaji mahiri wapatao saba ambaao waliweza kuzingatia vigezo mbali mbali katika kufanya maamuzi na kuangalia mawazo ambayo yaliwasilishwa na vijana hao.

"Nimefaarijika sana kuwa mgeni rasmi katika kufunga kambi hii rasmi ya vijana wapatao 100 na wametoka sehemu mbali mbali na vijana hao wameweza kufanyiwa mchujo naa kubakia vijana 100 kati ya 100 ambao walikuwa kambi na kwamba watakwenda sasa katika fainali ambayo itafanyika katika ukumbi Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam,"amebaisha Omolo.

Kadhalika ameongeza kwamba mshindi wa kwanza katika shindano hilo la Vijana Uchumi Challenge atajinyakulia kitita cha kiasi cha shilingi milioni 50, ambapo mshindi wa pili atajisshindia shilingi elfu 30 na mshindi wa tatu anaondoka naa kiasi cha shilingi milioni 20 huku washindi wengine watapata kifuta jasho.

Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita itaendelea kuwapa sapoti kubwa na ushirikiano katika kuwawezesha vijana wote 100 waliofika hatua ya kambi ili kuhakikisha mawazo yao yanageuzwa kuwa miradi yenye tija.

Alifafanua Vijana Uchumi Challenge si shindano pekee, bali ni jukwaa la kuibua fikra za vijana, kulea ubunifu, kujenga ujasiri na kuthibitisha kuwa vijana wana nafasi kubwa ya kubuni suluhisho za changamoto za kiuchumi.

Omolo alibainisha kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Tanzania Bara ina vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35 wapatao milioni 20.6, sawa na asilimia 34.4 idadi inayoonesha kuwa taifa lina nguvu kazi kubwa ambayo ikitumia vipaji na kuendelezwa ipasavyo inaweza kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi.

Aliwataka vijana kutumia simu janja kama nyenzo ya kujiongezea kipato kwa kutumia teknolojia, pamoja na kunufaika na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na fursa nyingine zinazotolewa na Serikali.

Pia ametaja fursa nyingine kuwa ni mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kupitia mapato ya ndani, asilimia 30 ya zabuni zinazotengwa kwa makundi maalumu kupitia sheria ya manunuzi ya umma, pamoja na fursa zilizopo katika sekta za viwanda, uzalishaji na mnyororo wa thamani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Vijana Uchumi Challenge, Joseph Malekela, alieleza mashindano hayo yalizinduliwa Aprili 10, 2026, na baada ya kupokea na kuchambua maombi 7,852, vijana 100 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, walichaguliwa kuingia kambini.

Akisoma risala kwa niaba ya washiriki, Raiyan Juma Amour kutoka Zanzibar aliiomba Serikali kufanya tathmini ya kimkakati ya mawazo yote 100 yaliyowasilishwa ili yaweze kutumika katika sekta mbalimbali na kuchangia kuleta mageuzi ya kiuchumi na kutatua changamoto zinazoikabili nchi.

Katika kilele cha fainali za shindano hilo la Vijana Uchumi challenge kwa mwaka 2026 ambalo linatarajiwa kufanyika Julai 6 mwaka katika ukumbi Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.






Top News