Ametoa maelekezo hayo wakati wa Kikao Maalum cha Baraza cha kusikiliza na kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali [CAG]kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 2026.
Halmashauri ya Bukombe imepongezwa kwa kufaulu kupata Hati Safi katika ukaguzi wa CAG. Hati hiyo ni alama ya juu zaidi inayothibitisha kuwa fedha za umma zimetumika kwa uwazi na kwa mujibu wa sheria.
Kwa mujibu wa ripoti ya CAG, jumla ya hoja 24 zilibuliwa kwa mwaka 2026. Kati yake, hoja 5 zimeshatekelezwa na hoja 19 zinaendelea kutekelezwa
Mkuu wa Mkoa amewataka Madiwani kuacha tabia ya "kutengeneza hoja" ili zijibiwe, na badala yake kuzuia mapungufu kabla hayajatokea ili kuitunza taswira ya Serikali.
Halmashauri hiyo imefanikiwa kukusanya Shilingi Bilioni 5 za mapato ya ndani, sawa na asilimia 136.3 ya lengo. Hatua hiyo imeipatia sifa Halmashauri hiyo kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Mohammed Gombat.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe, Mhe. Erick Kagoma, kwa niaba ya Madiwani, amesema amepokea na atatekeleza maelekezo ya kupunguza idadi ya hoja zinazoibuliwa na CAG katika miaka ijayo.



.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)








