Families, architects, students and members of the public gathered at dawn on Saturday, 11 July 2026, for a memorial walk honouring the late Beda Amuli, one of Tanzania’s pioneering architects whose work helped shape Dar es Salaam’s built identity.

Organised by Amuli’s family in collaboration with the Architectural Association of Tanzania (AAT), the walk was held under the theme, “Designing Tanzania: Architecture for People, Place, and Purpose.”

The journey began at the Old Boma Building along Sokoine Drive before proceeding, under police and traffic escort, to selected landmarks associated with the city’s architectural history, including the Kilimanjaro Hotel, the Institute of Finance Management, the National Cooperative Building and Kariakoo Market.

AAT President Architect T’Chawi said Amuli did more than design buildings; he created civic spaces where Tanzanians could work, learn, trade and gather.

The walk concluded at Kariakoo Market with reflections, media engagement and closing remarks, followed by a memorial church service at St Alban’s Anglican Church.

Ten years after his passing, Beda Amuli’s legacy remains embedded in Dar es Salaam’s streets, institutions and public spaces, inspiring a new generation to appreciate architecture as national identity and public service.














 

Na. Mwandishi Wetu, Dar.

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe Mhe. Petro Magoti ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa namna ilivyofanya maboresho ya Mitaala ya Elimu nchini yenye lengo la kumfanya muhitimu kuweza kujiajiri au kuajiriwa mara anapomaliza masomo  yake.

Mhe. Magoti ameyasema hayo leo tarehe 12/7/2026 katika maonesho ya Sabasaba ambapo amesema kuwa TET inafanya kazi nzuri ya kuboresha elimu nchini.

"Kwa kweli nawapongeza kwa kazi nzuri ya kuboresha Elimu nchini hasa hivi karibuni katika maboresho ya mitaala yaliyofanyika, ni tumaini langu kwamba wanafunzi nchi nzima wataendelea kufanya vyema, " Amesema mhe. Magoti.

Pia ameeleza, anafurahia namna wanafunzi wanaendelea kupatiwa vitendea kazi kama vitabu vinavyowapelekea kuendele kufanya vyema wakati wa masomo yao na kuendelea kuipongeza TET kwa uratibu mzuri na upatikanaji wa vitabu  mashuleni.

TET inashiriki katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya  biashara maarufu kama Sabasaba  yaliyoanza tarehe 28, Juni ambapo yanatarajiwa kufungwa hapo kesho, Julai 13.









Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi  ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
















- Apokelewa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Makongoro Nyerere pamoja na Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Jacqueline Mzindakaya


Na OWM–TAMISEMI, Sumbawanga

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe, amewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya kumuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ufunguzi wa mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji na huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Mafunzo hayo yatafanyika kuanzia Julai 13 hadi 16, 2026 katika Manispaa ya Sumbawanga, yakiwa yameratibiwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacqueline Mzindakaya, kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Prof. Shemdoe alipokelewa katika Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Makongoro Nyerere akiambatana na Mhe. Mhe. Jacqueline Mzindakaya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali.

Kesho, Julai 13, 2026, Prof. Shemdoe atafungua rasmi mafunzo hayo katika Ukumbi wa Country Hotel, ambapo yanatarajiwa kuwakutanisha wananchi, wajasiriamali, vikundi vya wanawake na vijana, makundi yenye mahitaji maalum pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu fursa za mitaji, mikopo na huduma mbalimbali za uwezeshaji zinazotolewa na Serikali na taasisi zake, ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji, kukuza biashara, kuongeza ajira na kuinua kipato cha familia.

Mafunzo hayo pia yanatarajiwa kuwapa washiriki taarifa sahihi kuhusu namna ya kufikia huduma za kifedha na programu za uwezeshaji wa kiuchumi, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na kuharakisha maendeleo ya mkoa wa Rukwa kwa ujumla.











Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba, amesema thamani ya fedha itaendelea kuwa imara kuelekea kipindi cha mavuno ili kuwawezesha wakulima kupata thamani stahiki ya mazao yao kulingana na shughuli za kiuchumi wanazozifanya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) Julai 10, 2026, Tutuba amesema kiwango cha riba ya Benki Kuu cha asilimia 6.25 kinalenga kuhakikisha kunakuwa na utulivu wa bei na mfumuko wa bei unaendelea kubaki kati ya asilimia 3 hadi 5.

Amesema kiwango hicho pia kitawezesha Mabenki  kuwa na ukwasi wa kutosha kwa ajili ya utoaji wa mikopo kwa wananchi na wafanyabiashara, hivyo kusaidia shughuli mbalimbali za uzalishaji na biashara nchini.

Tutuba amesema wakulima wanapoanza kuvuna mazao yao, thamani imara ya fedha itasaidia kuhakikisha wanapata malipo yanayolingana na thamani halisi ya mazao yao sokoni.

Ameongeza kuwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa nje ya nchi pia watanufaika kwa kupata fedha za kigeni kulingana na thamani ya fedha walizotumia katika uzalishaji, huku tathmini ikionyesha kiwango cha riba cha asilimia 6.25 kinatosha kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.

Aidha, amesema BoT hutumia Maonesho ya Sabasaba kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kiwango cha riba ya Benki Kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei, kuongeza ukwasi katika mzunguko wa uchumi na kuwezesha upatikanaji wa fedha kwenye mabenki ya biashara.

Tutuba amesema maonesho hayo pia ni fursa kwa Watanzania kujifunza, kupata bidhaa na huduma mbalimbali pamoja na mbinu mpya za kufanya shughuli za kiuchumi zinazochangia ukuaji wa uchumi wa nchi.




Kituo cha Uzalishaji na Ukuzaji wa Viumbe Maji cha Lubambangwe kilichopo Chato Mkoa wa Geita, kimefikia asilimia 80 ya utekelezaji. Kituo hicho kiko chini ya Wizara ya Uvuvi na kinatarajiwa kuhudumia wafugaji wa samaki kutoka mikoa yote ya Kanda ya Ziwa.

Hayo yamebainishwa na Kamati ya Siasa na Utekelezaji ya CCM Mkoa wa Geita wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi ya maendeleo wilayani hapa.

Akitoa taarifa, Kaimu Ofisa Mfawidhi wa Kituo hicho Bilali Banali amesema kituo hicho kina uwezo wa kuzalisha zaidi ya samaki laki tatu kwa mwezi pamoja na kuzalisha vyakula vya samaki.

Amesema lengo la kituo hicho ni pia kukusanya zaidi ya shilingi milioni 180 kwa mwaka kupitia utoaji wa vibali vya viranga na vizimba kwa wafugaji.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Waridi Mngumi amewataka wananchi kulinda kituo hicho ili kiweze kuwanufaisha kiuchumi.

Amesema kituo hicho kimejengwa kwa kuzingatia Falsafa ya Uchumi wa Buluu kwani kitatoa pia mafunzo mafupi kwa wananchi kuhusu ufugaji wa samaki na uzalishaji wake.


















Top News