Paris, Ufaransa

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, Mheshimiwa Saidi Othman Yakubu, amekutana na ujumbe wa viongozi wanawake 18 kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) waliopo nchini Ufaransa kwa ziara ya kitaaluma ya kujenga uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu uongozi, usimamizi wa taasisi za elimu ya juu na maendeleo ya wanawake katika nafasi za maamuzi.

Ujumbe huo unaongozwa na Dkt. Janeth Emanuel Kigoba, Mkuu wa Kitivo cha Elimu cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, ambaye pamoja na viongozi wengine wanashiriki programu mbalimbali za kujifunza na kutathmini mifumo bora ya uongozi na utawala katika taasisi za elimu ya juu.

Akizungumza na ujumbe huo katika Ubalozi wa Tanzania mjini Paris, Balozi Yakubu alisema imekuwa jambo la kutia moyo kuona kuwa sekta ya elimu ya juu, ambayo kwa miaka mingi imekuwa nyuma katika kufikia usawa wa kijinsia ikilinganishwa na baadhi ya sekta nyingine, sasa inaendelea kupiga hatua na kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi.

“Nimefarijika kuona idadi kubwa ya wanawake viongozi kutoka taasisi ya elimu ya juu wakishiriki katika programu za kujijengea uwezo. Elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya jamii, hivyo ni muhimu kuona wanawake wakichukua nafasi zao stahiki katika kuongoza taasisi hizi muhimu,” alisema Balozi Yakubu.

Aliongeza kuwa vyuo vikuu vina nafasi ya kipekee katika kuandaa viongozi, wataalamu na watunga sera wa kesho, hivyo kuwepo kwa usawa wa kijinsia katika sekta hiyo kuna mchango mkubwa katika kuharakisha maendeleo ya taifa na jamii kwa ujumla.

Balozi Yakubu aliwahimiza washiriki hao kuendelea kuwa vinara wa mabadiliko katika taasisi zao kwa kuhakikisha kuwa wanawake wengi zaidi wanapata fursa za kushiriki katika uongozi, utafiti na ufundishaji.

Kwa upande wake, Dkt. Janeth Emanuel Kigoba alimshukuru Balozi Yakubu na Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa kwa mapokezi na ushauri walioutoa kwa ujumbe huo, akisisitiza kuwa ziara hiyo imewapa washiriki fursa muhimu ya kujifunza uzoefu wa kimataifa unaoweza kusaidia kuimarisha utendaji na uongozi wa taasisi za elimu ya juu nchini Tanzania.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Chuo Kikuu Huria cha Tanzania za kuimarisha uwezo wa viongozi wanawake na kukuza ushiriki wao katika nafasi za juu za uongozi, sambamba na kuchochea maendeleo ya elimu ya juu na usawa wa kijinsia nchini.



Na Mwandishi wetu Dodoma

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma imefichua kasoro nzito katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa wilayani Kongwa, ambapo baadhi ya kazi zimeonekana kutotekelezwa kwa viwango vilivyokubaliwa kwenye mikataba ya Serikali.

Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari leo jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa shughuli za TAKUKURU kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma, Christopher Myava, amesema taasisi hiyo imebaini matumizi ya nyavu kwenye madirisha na sehemu za hewa za milango badala ya vioo vilivyotakiwa kuwekwa kwa mujibu wa ramani ya ujenzi.

Amesema uchunguzi uliofanywa na TAKUKURU umeonesha pia kuwa baadhi ya vyoo vya mabweni hayo havikuwekewa masinki kama ilivyoelekezwa kwenye michoro ya mradi, huku kuta zikikosa vigae vilivyopangwa kufungwa kwa mujibu wa makubaliano ya utekelezaji wa kazi hiyo.

“Tumebaini tofauti kubwa kati ya kazi iliyotekelezwa na maelekezo yaliyopo kwenye mkataba wa mradi. Haya ni mambo ambayo yanaathiri ubora wa miradi pamoja na thamani ya fedha za Serikali,” amesema Myava.

Mbali na dosari hizo, TAKUKURU imeeleza kuwa baadhi ya vitasa vilivyowekwa kwenye mabweni hayo havifanani na vile vilivyoainishwa kwenye mkataba, huku baadhi ya vifaa vya ujenzi ikiwemo matofali na mabati vikidaiwa kutowasilishwa maabara kwa ajili ya kupimwa ubora wake kabla ya kutumika kwenye mradi.

Katika hatua nyingine, Myava amesema taasisi hiyo imefanikiwa kubaini mapungufu katika jumla ya miradi 36 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 156.4 kupitia operesheni za ufuatiliaji zilizofanywa katika sekta mbalimbali mkoani Dodoma.

Amesema TAKUKURU itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo ili kuhakikisha fedha za umma zinaleta matokeo yaliyokusudiwa na wananchi wanapata huduma bora kutokana na uwekezaji wa Serikali.

“Lengo letu ni kuona miradi yote inakamilika kwa viwango vinavyostahili na kuhakikisha hakuna mianya ya ubadhirifu wa fedha za umma,” ameongeza.

Baada ya kubaini dosari hizo, wahusika wa miradi hiyo wamepewa maelekezo ya kurekebisha mapungufu yote yaliyojitokeza ili miradi hiyo iweze kukidhi viwango vya kitaalamu pamoja na thamani ya fedha zilizotumika.


NA DENIS MLOWE,NJOMBE.

MAANDALIZI ya mbio za Uchumi Parachichi Marathon yameanza kushika kasi katika mkoa wa Njombe, ikiwa ni tukio kubwa lenye lengo la kutangaza na kuhamasisha thamani ya zao la parachichi ambalo ni uti wa mgongo wa uchumi wa wakazi wa Nyanda za Juu Kusini.

Marathon hii, inayotarajiwa kufanyika tarehe 26 Julai 2026 katika viwanja vya Sabasaba Njombe Mjini, imeandaliwa kwa lengo mahususi la kuonyesha mchango wa zao la parachichi katika kujenga uchumi imara wa mkoa huo kupitia zao la Parachichi.

Kupitia mbio hizi, wakulima wadogo watapatiwa elimu kuhusu kilimo bora, namna ya kuongeza uzalishaji, pamoja na kuwezeshwa kupata pembejeo, mbolea na vifaa vya kisasa vya kilimo.

Akizungumza kuhusu maandalizi hayo, Mkurugenzi wa Speak Sports Games Promotion, Respicius Mtabingwa Kajura, ambaye pia ndiye msimamizi mkuu wa tukio hilo, amesema mbio hizo ni zaidi ya mashindano ya mbio ni jukwaa la uchumi, elimu na fursa kwa jamii.

Amesema kuwa tukio hili ni bonanza kubwa kuwahi kutokea katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na linatarajiwa kuvutia washiriki kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Kajura amesema kuwa mbio hizo zitakuwa na makundi tofauti ya washiriki wakiwemo wanaokimbia 42km, 21km, 10km na 5km. Aidha, kaulimbiu ya mwaka huu, Parachichi ni Uchumi wa Njombe na Lishe Bora ya Mwanao, inalenga kuhimiza matumizi ya parachichi kama zao la lishe na biashara.

Ametoa wito kwa wadau wa michezo, kilimo, afya na jamii kwa ujumla kuungana nao ili kufanikisha tukio hilo ambalo lina matarajio ya kuleta hamasa na utalii wa michezo katika mkoa wa Njombe.

Mkurugenzi Kajura amewakaribisha wananchi wote kutoa ushauri, mawazo na michango yao ili kuhakikisha Uchumi Parachichi Marathon inafanyika kwa ubora na mafanikio makubwa kama inavyotarajiwa.


📍Wanafunzi wafurahia, wampongeza mbunge 


Na Mwandishi Wetu, Muheza

MBUNGE wa Muheza, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), amekagua mradi wa kisima cha maji matamu katika Shule ya Sekondari ya Kwabastola.

Shule hiyo iliopo Kata ya Makole wilayani hapa, kisima kimegharimu Shilingi milioni 12 kupitia kampuni ya Mo Maji, ikiwa ni mwendelezo wa mikakati yake ya kusogeza huduma za kijamii karibu na wapiga kura wake tangu aingie madarakani mwaka 2020.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo Leo Mei 29, 2026, Mhe. Mwinjuma alionyesha kufurahishwa na kukamilika kwake, hasa baada ya kubainika kuwa maji hayo ni matamu na hayana chumvi, jambo linaloyafanya yafae kwa matumizi ya shule na wananchi wa jirani.

"Wakati wa kampeni zangu, miongoni mwa ahadi kubwa nilizotoa ni kuhakikisha natatua kero ya dharura ya maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo letu. Kupatikana kwa maji haya matamu hapa Kwabastola ni ushahidi kuwa tunatekeleza Ilani kwa vitendo ili kuwasaidia watoto wetu wasome kwa utulivu," alisema MwanaFA.


Mabweni na Vyoo vya Kisasa Kunusurika

Naye Ofisa Mtendaji wa Kata ya Makole,  Rose Maghembe, alimshukuru Mbunge huyo kwa uamuzi wake wa kuchimba  kisima hicho, akieleza kuwa shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na wakati mgumu kutokana na uwepo wa majengo mapya yasiyo na maji.

"Tunashukuru sana Mbunge wetu kwa kisima hiki. Shule yetu ina mabweni ya wasichana na wavulana ambayo yana vyoo vya kisasa vya ndani ambavyo kitalamu vilikuwa haviwezi kuishi au kutumika bila maji. Upatikanaji wa maji haya sasa unakwenda kuwasaidia wanafunzi na wananchi wa jirani na shule," alisema Mtendaji huyo.

Maandalizi ya Kidato cha Tano Julai

Akiwasilisha taarifa fupi ya shule kwa niaba ya Mkuu wa Shule hiyo, Juma Rashid Mdachi, Makamu Mkuu wa Shule, Lilian Godlisten Massawe, alisema miundombinu hiyo ya maji imekuja wakati muafaka kuelekea upokeaji wa wanafunzi wapya wa kidato cha tano.

Lilian alianika takwimu zinazoonyesha kuwa shule hiyo kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 283, wakiwemo wavulana 132 na wasichana 151 waliopo kidato cha tatu, wakisoma katika mikondo miwili kwa kila kidato chini ya usimamizi wa walimu 13.

Aliongeza kuwa, mwezi ujao wa Julai (Mwezi wa Saba), shule hiyo inatarajia kupokea kwa mara ya kwanza wanafunzi wapya wa gredi ya juu wa Kidato cha Tano (High School) kwa michepuo ya tahasusi za Sayansi (CBG) na Sanaa (HGfa), hivyo kisima hicho kitasaidia kuondoa changamoto kubwa ya ukosefu wa maji.







RAIS  mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) miaka 18 iliyopita.

Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika.

Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo.

Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki jijini Dar es salaam.

Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.

Dkt. Kikwete alimpongeza Catherine kwa kutimiza ndoto yake ya kusomea udaktari, jambo ambalo aliahidi kulifanya alipokuwa mtoto. Alisema amefurahishwa kumuona akiwa mwenye afya njema na akijiandaa kulitumikia taifa kupitia taaluma ya tiba.

Kwa upande wake, Catherine alisema anatamani kuwa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto kama aliyowahi kupitia yeye mwenyewe, akieleza kuwa hiyo itakuwa ni moja ya njia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha na afya njema.


Na Seif Mangwangi, Michuzi TV, Karatu

SERIKALI imesema itaendelea kuwalinda wawekezaji wa ndani pamoja na kuunga mkono uwekezaji wowote unaofanywa na wawekezaji hao kwa lengo la kutoa huduma za kijamii.

Hayo yameelezwa leo 29 Mei 2026 na Mkuu wa Wilaya ya Karatu Lameck Karanga katika hafla ya uzinduzi wa kituo kipya ya mafuta cha Orxy kitakachokuwa kikiendeshwa chini ya kampuni ya halyaz.

DC Karanga amesema ujenzi wa kituo hicho cha mafuta ni muendelezo wa maono ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuhakikisha wawekezaji wa ndani wanajengewa mazingira mazuri Ili waweze kufanya biashara.

Amesema Karatu ndio lango kuu la utalii hivyo ujio wa kituo hicho kutasaidia wasafirishaji kupata nishati ya mafuta kwa urahisi na uhakika kwa kuwa bidhaa za kampuni hiyo zinaaminika katika ukanda wa Afrika na duniani kote.

"Kwa niaba ya Wilaya niwapongeze sana kwa uwekezaji huu, mbali ya kutuletea kituo bora lakini mmeanza na kutengeneza mazingira hasa ya bustani nzuri hapo mbele ya kituo chenu, hii inaonyesha ni namna gani mmekuja Karatu Kwa faida," amesema na kuongeza:

"Orxy wameonyesha usafi wa mazingira nje ya kituo cha mafuta na niwaombe watu wa Benki na wenyewe waige mfano huu ni utalii mzuri na kuonyesha wilaya ya karatu ni safi na kuwa na mazingira mazuri," amesema.

Aidha DC Karanga amewataka wananchi wa mji wa Karatu kuiga mfano wa kampuni ya Halyaz kufungua taasisi kama hizo Ili kusaidia jamii kupata ajira lakini pia Serikali kupata kodi. 

Mkurugenzi wa kampuni ya Halyaz inayoendesha kituo hicho cha mafuta cha Orxy Karatu, Ally Abdulrazak amesema ujenzi wa kituo hicho ni matokeo ya maono kwamba karatu inastahili huduma bora za nishati.

Amesema aliamua kuingia ubia na kampuni ya Orxy kufungua kituo hicho cha mafuta kwa kuwa ndio kampuni ambayo imekuwa ikitoa  mafuta safi na salama kwa magari aina tofauti tofauti.

Abdulrazak amesema wateja watakaofika kupata huduma katika kituo hicho watapata huduma zenye ubora wa kimataifa kwa kuwa Wafanyakazi wake wanaujuzi wa hali ya juu lakini pia huduma zote zinaendeshwa kwa kuzingatia ubora.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Orxy Tanzania, Meneja wa fedha wa kampuni hiyo, Greyson Francis amesema uzinduzi wa kituo hicho cha mafuta cha Orxy Karatu ni sehemu ya ndoto za kampuni hiyo kuendelea kupanua huduma zake Kwa jamii.

Amesema kampuni ya Orxy imesambaa katika nchi 19 barani Afrika na hapa nchini imeshasambaa mikoa yote na hivi karibu itazindua vituo viwili vya mafuta Jijini Dar es Salaam.



 

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith  Kapinga (Mb), ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kushirikiana kikamilifu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Taasisi nyingine husika katika kushughulikia na kuondoa kero zote zinazosababishwa na mifumo ya utoaji vibali kwa shehena zinazoingia nchini.

Waziri Kapinga ametoa agizo hilo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na ujumbe wake Mei 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kufuatia kuibuka kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa kuunganisha mfumo wa TANeSW wa TRA na mfumo wa OAS wa TBS na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Aidha, Waziri Kapinga amepongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa baina ya TBS pamoja na TRA katika kuunganisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha taratibu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa vibali kwa shehena za mizigo inayoingia nchini.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imetoa zawadi ya sh. milioni 500 kwa Timu ya Taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kwa kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano hayo na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo (Ijumaa, Mei 29, 2026) ofisini kwake Mlimwa, Dodoma wakati akitoa salamu za pongezi kwa timu hiyo kufuzu hatua ya fainali kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema Rais Samia amewapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wote wa timu kwa mafanikio hayo makubwa ambayo yameendelea kuandika historia mpya katika sekta ya michezo nchini.

“Mheshimiwa Rais amenielekeza nitoe pongezi hizi kwa vijana wetu wa Serengeti Boys kutokana na mafanikio makubwa ya kutinga fainali na kuiwakilisha vema Tanzania katika mashindano hayo,” amesema Dkt. Mwigulu.

Waziri Mkuu amesema Serikali itatuma ndege maalum kwa ajili ya kuwafuata vijana hao watakapomaliza mashindano hayo ili kurejea nchini pamoja na kombe endapo watafanikiwa kutwaa ubingwa. “Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa ndege kwa ajili ya kuwafuata vijana wetu watakapokuwa wamemaliza mashindano hayo na kurejea nao nyumbani,” amesema.

“Tunaamini huu ni mwanzo tu wa pongezi ambazo Mheshimiwa Rais ameanza kuzitoa. Tunaamini kwamba wakirejea na kombe hilo, kutakuwa na sababu zaidi ya kuwapongeza kwa mafanikio hayo makubwa.”

Waziri Mkuu amemwelekeza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Paul Makonda na wadau wanaohusika, waendelee na uratibu wa wa safari kwa watu watakaokwenda kuwaunga mkono vijana wetu.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amesema endapo Serengeti Boys watatwaa ubingwa, Serikali itawapatia kila mchezaji kiwanja kimoja katika Mji wa Suluhu New City uliopo mkoani Morogoro ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika kuitangaza Tanzania kupitia michezo.

Waziri Mkuu pia amewahamasisha Watanzania, taasisi, mashirika na wadau mbalimbali wa michezo kuendelea kutoa msaada na motisha kwa timu hiyo kuelekea mchezo wa fainali.

“Shime shime vijana wetu, inawezekana. Tuleteeni kikombe kile, mleteeni Dkt. Samia Suluhu Hassan kikombe, tuleteeni Watanzania ushindi huo. Kwa kiwango mlichokionesha, tunaamini mna uwezo wa kutwaa ubingwa huo,” amesema.

Sambamba na hilo, Waziri Mkuu amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa kinara wa maendeleo ya michezo nchini na kuchochea mafanikio yanayoendelea kupatikana katika sekta hiyo.


-Yasema kwa mara ya kwanza Serikali ilikamata tani 29.52 za aina mpya ya dawa za kulevya aina ya Kratom

-Pia mali zenye thamani ya zaidi ya Sh.bilioni 3.3 zilizohusishwa na makosa ya dawa za kulevya zilitaifishwa.


Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Profesa Palamagamba Kabudi ameta taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025 ambapo inaonesha namna Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilivyowekeza na kuweka nguvu kubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya. 

Akiwasilisha taarifa hiyo leo Mei 29,2029 Bungeni Mjini Dodoma ,Profesa Kabudi amesema uwasilishaji wa taarifa hiyo ni utekelezaji wa Kifungu cha 66 cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Na. 5 ya Mwaka 2015, inayoiagiza Serikali kuandaa na kuwasilisha bungeni taarifa hiyo kila mwaka.

“Lengo ni kuonesha uwajibikaji wa Serikali kwa wananchi kupitia Bunge, pamoja na kutoa tathmini ya utekelezaji wa mikakati ya udhibiti wa dawa hizo kwa mwaka husika.Pia, taarifa hii inatoa nafasi kwa Bunge kutoa ushauri kwa Serikali kuhusu namna bora ya kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya nchini.”

Amefafanua kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, vyombo vya ulinzi na usalama, wadau wa ndani na nje ya nchi pamoja na jamii kwa ujumla, serikali imepata mafanikio makubwa katika kudhibiti biashara na matumizi ya dawa za kulevya.Katika taarifa hiyo Profesa Kabudi amesema mwaka 2025, bangi iliendelea kuwa dawa ya kulevya iliyokamatwa kwa kiwango kikubwa zaidi ambapo jumla ya tani 1,017.26, zilikamatwa. 

Amefafanua hata hivyo, kiasi kilichokamatwa kilipungua kwa asilimia 55.97 ikilinganishwa na mwaka 2024.Hiyo ni kutokana na uteketezaji wa mashamba makubwa ya bangi uliofanyika mwaka 2024 na kuimarika kwa udhibiti ikiwemo utoaji elimu kwa jamii inayojihusisha na kilimo cha bangi kuhusu madhara ya kilimo cha zao hilo.

Ameongeza pia jumla ya tani 26.36 za mirungi zilikamatwa. Kiasi hicho kiliongezeka kwa asilimia 42.88 ikilinganishwa na mwaka 2024. Ongezeko hilo linaashiria kuimarika kwa operesheni za ufuatiliaji na udhibiti hususan katika maeneo ya mipaka na njia zinazotumika kusafirisha dawa hizo.

Kwa upande wa dawa za kulevya za viwandani, amesema Serikali ilifanikiwa kukamata methamphetamine kilogramu 907.18, heroin kilogramu 672.23, cocaine kilogramu 4.89, MDMA gramu 178 na MDA gramu 7.82.

Aidha, kwa mara ya kwanza, mwaka 2025 Serikali ilikamata tani 29.52 za aina mpya ya dawa za kulevya aina ya Kratom itokanayo na mmea unaoitwa Mitrogyna speciosa. “Dawa hii iliingizwa nchini kama mbolea, baada ya uchunguzi ilibainika kuwa ni dawa za kulevya.”

Amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na kazi kubwa iliyofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika kudhibiti mitandao na njia za usafirishaji wa dawa za kulevya kupitia Nchi kavu, anga na majini.

Aidha, Serikali iliendelea kuimarisha ukaguzi katika vituo vya forodha, vyombo vya usafiri, kampuni za usafirishaji vifurushi na kwenye kampuni zinazojihusisha na biashara ya kemikali bashirifu na dawa tiba zenye asili ya kulevya kwa lengo la kudhibiti uchepushwaji. 

“Kupitia ukaguzi huo, jumla ya tani 31.76 na lita 183.500 za kemikali bashirifu pamoja na kilogramu 2.36 na mililita 160 za dawa tiba zenye asili ya kulevya zilikamatwa.”

Kuhusu makosa ya dawa za kulevya, mwaka 2025,amesema  jumla ya mashauri 1,124 yalifunguliwa katika Mahakama mbalimbali nchini. Pamoja na mashauri yaliyokuwa yakiendelea katika Mahakama mbalimbali nchini, mashauri 1,373 yalitolewa hukumu na Jamhuri ilishinda mashauri 1,058.

Aidha mali zenye thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni 3.3 zilizohusishwa na makosa ya dawa za kulevya zilitaifishwa.Pia Serikali iliendelea kutoa huduma za tiba na utengamao kwa watu wenye uraibu wa dawa za kulevya. 

“Mwaka 2025, jumla ya watu 85,425 wenye uraibu wa dawa za kulevya walipata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili katika hospitali za rufaa za mikoa na Kanda, kliniki za MAT na nyumba za upataji nafuu nchini.

“Elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya iliendelea kutolewa kwa Umma kupitia kampeni mbalimbali za uelimishaji katika jamii, taasisi za elimu na vyombo vya habari ili kuijengea jamii uelewa, maamuzi sahihi na uwezo wa kujilinda dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya.

“Katika kuimarisha ushirikiano wa kitaifa, kikanda na kimataifa, Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi katika kubadilishana taarifa za kiintelijensia, kujenga uwezo wa kitaasisi pamoja na kuendesha operesheni za pamoja dhidi ya mitandao ya usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.

“Matokeo chanya katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanatokana na dhamira thabiti, maono na uongozi mahiri wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwani chini ya uongozi wake amewekeza kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya Nchini.”

Pia ameipongeza Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama, wataalamu wa afya, wadau katika mapambano na wananchi kwa ushirikiano wao uliosaidia kuyafikia mafanikio aliyoyaeleza.

“Naomba wananchi waendelea kutoa taarifa pale wanapohisi au kushuhudia viashiria vya biashara au matumizi ya dawa za kulevya kwa vyombo husika ili kuifanya nchi yetu kuwa mahali salama na huru dhidi ya matumizi na biashara dawa za kulevya.”








Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji, tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri ya Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji kupitia Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.






 


Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Serikali imesema imeendelea kupata mafanikio makubwa katika vita dhidi ya dawa za kulevya nchini kutokana na kuimarika kwa ushirikiano wa ndani na nje ya nchi pamoja na uwekezaji mkubwa unaofanywa katika sekta ya usalama, intelijensia na udhibiti wa biashara haramu ya dawa hizo.

Hayo yameelezwa leo na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, katika Mkutano na waandishi wa habari Bungeni Dodoma wakati akiwasilisha Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya nchini kwa mwaka 2025.

Prof. Kabudi amesema Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa kitaifa, kikanda na kimataifa katika kubadilishana taarifa za kiintelijensia, kuendesha operesheni maalum za pamoja pamoja na kujenga uwezo wa taasisi zinazoshughulikia mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Amesema hatua hizo zimeendelea kusaidia kuvunja mitandao ya usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya ambayo imekuwa ikihatarisha usalama wa jamii, afya za wananchi na nguvu kazi ya taifa.

Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mafanikio hayo yanatokana na dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuimarisha mifumo ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kuongeza uwekezaji katika vyombo vya ulinzi, usalama na taasisi za udhibiti.

Amesema Serikali imeendelea kuiwezesha Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na taasisi nyingine zinazoshiriki katika operesheni za kudhibiti biashara hiyo haramu ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Matokeo haya yanaonyesha namna ambavyo ushirikiano wa pamoja kati ya Serikali, vyombo vya dola, wataalamu wa afya, wadau wa maendeleo na wananchi unavyoendelea kuzaa matunda katika vita dhidi ya dawa za kulevya,” amesema Prof. Kabudi.

Aidha, amesisitiza kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya hayawezi kufanikiwa bila ushiriki wa wananchi, huku akitoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa kwa mamlaka husika kuhusu vitendo vinavyohusiana na usambazaji, matumizi au biashara ya dawa za kulevya.

Ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mikakati ya kinga, elimu kwa umma, tiba na operesheni maalum ili kuhakikisha taifa linaendelea kuwa salama dhidi ya athari za dawa za kulevya ambazo zimekuwa zikichangia mmomonyoko wa maadili, ongezeko la vitendo vya uhalifu pamoja na kuathiri maendeleo ya vijana na jamii kwa ujumla.

Prof. Kabudi pia amewapongeza wananchi kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa vyombo vya usalama na taasisi zinazopambana na dawa za kulevya, akieleza kuwa mchango wa jamii ni msingi muhimu wa ushindi katika mapambano hayo.

Kwa upande wa Kamishina Jenerali Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema tatizo la dawa za kulevya ni suala  mtambuka linalohusisha mitandao ya kihalifu iliyopo nchi mbalimballi Duniani, hivyo mapambano dhidi ya tatizo hilo yanahitaj ushirikiano na nguvu za pampja kuanzia ngazi ya Kitaifa, kikanfa bna Kimataifa.




MECHI ya mkondo wa pili wa kugombania kucheza ligi kuu za Ufaransa yaani LIGUE 1 ipo hapa. Ni Nice vs Saint Etienne ambapo kila timu inahitaji kushinda leo kucheza ligi kuu msimu ujao. Je nani kushinda leo?

Hii ni mechi ambayo ina presha ndani yake kwasababu kila mmoja ana malengo sawa na mwenzake. Nice wao walikuwa ligi kuu na kutokana na kutokufanya vizuri imewabidi sasa wapambane kutafuta nafasi nyingine ili waweze kubaki ligi kuu.

Huku kwa upande wa Saint Etienne wao kutokana na kutofshika nafasi ya kwanza wlaipokuwa kule Ligue 2 sasa wanalazimika wapambane kwa hali na mali ili waweze kupata nafasi ya kucheza kwenye ligi Kuu ya Ufaransa yaani LIGUE 1.

Mchezo wa kwanza ulimalizika kwa sare tasa ya 0-0, matokeo ambayo yameacha kila kitu wazi kabisa kabla ya pambano hili la mwisho. Hakuna timu iliyoweza kupata faida, hakuna aliyethibitisha ubora wake, na sasa kila kitu kinategemea dakika 90 zijazo. Hii si mechi ya kawaida; ni mchezo wa kuamua hatma, mchezo ambao unaweza kubadilisha historia ya klabu ndani ya usiku mmoja. Jisajili hapa na Meridianbet

Piga pesa leo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Nice wakiwa nyumbani, wataingia uwanjani wakijua kuwa presha ipo mabegani mwao. Mashabiki wanatarajia ushindi, viongozi wa klabu wanahitaji kuona timu ikirudi au kubaki kwenye kiwango cha juu, na wachezaji wanajua kuwa nafasi kama hizi haziji mara nyingi.

Saint-Étienne nao wanaingia katika mchezo huu wakiwa na kiu kubwa ya kurejea kwenye hadhi yao ya zamani. Klabu hii ina historia kubwa ndani ya soka la Ufaransa, na mashabiki wake bado wanaamini kuwa nafasi yao halisi ni Ligue 1. Sare ya bila kufungana kwenye mchezo wa kwanza imewapa matumaini makubwa, hasa wakiamini kuwa wanaweza kufanya jambo maalum ugenini.

Kila kosa linaweza kuwa mwisho wa ndoto za msimu mzima. Mabeki hawataki kufanya makosa, washambuliaji wanabeba matumaini ya maelfu ya mashabiki, na makocha wanapaswa kufanya maamuzi sahihi ndani ya dakika chache.

Ikumbukwe kuwa wa mpira wa miguu ni dakika 90 hivyo lolote linaweza kutokea na yoyote yule anaweza akashinda. Mchezo wa mwanza uliisha bila kuwa na mbabe na huu wa pili kila timu itaingia kwaajili ya ushindi pekee. Je nani kucheza ligue 1?. Bashiri mechi hii sasa.

 

Mafunzo Elekezi kwa Watumishi Wapya wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) yameanza leo, Mei 28, 2026, ikiwa ni hatua muhimu ya kuandaa wataalamu wa mamlaka hiyo kwa kuzingatia misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali. Watumishi wapya 29 wanashiriki mafunzo haya .yanayotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. 


"Tunatarajia kuwa baada ya mafunzo haya, mtakuwa watumishi wa umma wanaofuata maadili ya utumishi wa umma, wakiwasiliana kwa ufanisi na kuheshimu usiri wa taarifa na nyaraka za serikali, huku pia wakielewa haki na wajibu wao," amesema.

Kwa upande wake, Bi. Zena Hussein ambaye ni Meneja wa kituo cha mafunzo kwa njia ya Mtandao  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, amesema kuwa mafunzo haya ni muhimu na lazima kwa watumishi wapya katika utumishi wa umma. 
"Mafunzo haya yanalenga kuimarisha uelewa wa misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi," amesisitiza.

Aidha amesema kuwa Mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza uelewa wa watumishi wapya kuhusu misingi ya utumishi wa umma na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ndani ya TISEZA. Vilevile, mchakato huo unazingatia taratibu na miongozo ya serikali, kwa lengo la kuhakikisha majukumu yanatekelezwa kwa uwajibikaji, uadilifu, na ufanisi.
Mafunzo haya ni utekelezaji waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2011, uno wataka waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wapya wanapatiwa mafunzo elekezi ndani ya miezi sita tangu kuajiriwa,







 

Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana na kufunguliwa kwa udahili wa wanafunzi katika mwaka wa masomo 2026/2027.




Baadhi ya matukio katika picha wakati wa kutangazwa kwa dirisha la udahili mwaka wa masomo 2026/2027.

Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limefungua dirisha la Udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada katika kozi zote zinazosimamiwa na NACTVET.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda amesema dirisha Hilo limefunguliwa rasmi Mei 28 2026.

Amesema maombi ya udahili kwa kozi za Afya na Sayansi Shirikishi -Tanzania Bara, yatafanyika kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) unaopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Dkt.Mwajuma amesema udahili umeanza Mei 28 hadi Julai 10 2026 kwa awamu ya kwanza.

Aidha amesema maombi ya kozi zisizo za Afya na Sayansi Shirikishi, na kozi za Afya na Sayansi Shirikishi zitolewazo katika vyuo vilivyoko Zanzibar yatumwe moja kwa moja kwenye vyuo husika kuanzia Mei 28 Mei hadi Julai 10 mwaka Hui kwa awamu ya kwanza.

Hata hivyo Baraza limetoa orodha ya kozi zote na vyuo vinavyotoa kozi hizo, inapatikana katika Kitabu cha Mwongozo wa Udahili kwa Mwaka wa Masomo 2026/2027 kinachopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Baraza hilo limesema kila mwombaji kuhusika mwenyewe katika zoezi zima la kuomba kudahiliwa, kuandika taarifa zake kwa usahihi na umakini, na kutunza kumbukumbu atakazopatiwa na Baraza kupitia namba yake ya simu, bila kumpatia mtu mwingine yeyote ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza katika zoezi zima la maombi ya kujiunga na kozi katika vyuo mbalimbali.

Mambo ya Kuzingatia kwa Wanaoomba Kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (Central Admission System – CAS) ni Mwombaji anaweza kuomba chuo zaidi ya kimoja na Kuchaguliwa katika chuo alichoomba kutategemea ushindani utakaokuwepo katika chuo hicho.

Aidha amesema mwombaji akishachaguliwa, atapokea ujumbe kutoka NACTVET kupitia namba yake ya simu aliyoweka kwenye mfumo wakati wa kufanya maombi ujumbe utamjulisha kuwa amechaguliwa kujiunga na chuo husika na utakuwa na msimbo (code) ambao atatakiwa kuutunza na kuuwasilisha kwa chuo alichochaguliwa siku atakapowasili chuoni kwa ajili ya kuanza masomo.

Dkt. Mwajuma amesema baada ya kuwasilisha msimbo huo chuoni, atasajiliwa na chuo, kisha atapokea ujumbe kutoka NACTVET ukimweleza kuwa amesajiliwa. Baada ya kusajiliwa, mwanafunzi aingie katika tovuti ya NACTVET (www.nactvet.go.tz), kisha ajiridhishe kuwa amesajiliwa kwa kuhakiki taarifa zake kwa kubonyeza “link” inayosomeka “student’s information verification”.

Top News