Katika mkutano huo Mhe Doyo alipongeza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kukubaliana na mapendekezo yote yaliyopendekezwa na tume hiyo, aidha Mhe.Doyo amesisitiza pendekezo namba nne na pendekezo namba tano mamlaka husika wayafanyie kazi haraka kuondoa mzozo uliopo wa kisiasa hapa nchini.
Katika mkutano huo Mhe Doyo alipongeza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kukubaliana na mapendekezo yote yaliyopendekezwa na tume hiyo, aidha Mhe.Doyo amesisitiza pendekezo namba nne na pendekezo namba tano mamlaka husika wayafanyie kazi haraka kuondoa mzozo uliopo wa kisiasa hapa nchini.
JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YAPATA KATIBU MKUU MPYA, STEPHEN MBUNDI ACHUKUA NAFASI YA VERONICA NDUVA
Na Pamela Mollel,Arusha .
Katika kuendeleza misingi ya uongozi na ushirikiano wa kikanda, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imefanya makabidhiano ya nafasi ya Katibu Mkuu, ambapo Veronica Nduva amekabidhi madaraka kwa mrithi wake Stephen Patrick Mbundi katika hafla iliyofanyika kwenye makao makuu ya jumuiya hiyo jijini Arusha.
Makabidhiano hayo yamehitimisha rasmi kipindi cha uongozi wa Nduva, aliyeliongoza taasisi hiyo kwa msisitizo wa kuimarisha mshikamano wa nchi wanachama na kusukuma mbele ajenda za maendeleo ya kikanda, hususan katika nyanja za uchumi na ushirikiano wa kimkakati.
Katika kipindi chake cha uongozi, hatua mbalimbali zimechukuliwa katika kuimarisha utekelezaji wa miradi ya pamoja, kukuza biashara ndani ya ukanda na kuweka mazingira rafiki ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo.
Aidha, ameweka msisitizo mkubwa katika umuhimu wa kuendelezwa kwa mshikamano miongoni mwa nchi wanachama, akieleza kuwa mafanikio yaliyofikiwa yanahitaji kulindwa na kuendelezwa kupitia ushirikiano wa karibu wa wadau wote wa maendeleo ndani ya EAC.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu mpya Balozi Mbundi ameanza majukumu yake kwa kueleza dhamira ya kuharakisha utekelezaji wa ajenda kuu za jumuiya, akitaja vipaumbele vya kuimarisha soko la pamoja, kukuza biashara ya ndani ya ukanda na kuongeza ufanisi wa taasisi zake.
Ameeleza kuwa atahakikisha kunakuwepo usimamizi thabiti wa rasilimali, uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa majukumu ya jumuiya, huku akihimiza ushirikiano wa karibu kati ya nchi wanachama katika kukabiliana na changamoto zilizopo.
Mabadiliko hayo ya uongozi yanakuja katika kipindi ambacho EAC inaendelea kupanuka na kuimarisha nafasi yake kikanda na kimataifa, hali inayoweka matarajio makubwa kwa uongozi mpya katika kusukuma mbele ajenda ya ujumuishaji wa kikanda na ustawi wa wananchi wake.
Na Mwandishi Wetu

Na Mwandishi wetu, Dodoma
Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) kimeitaka Serikali kuimarisha utawala bora na mifumo ya kisheria ili kuhakikisha utekelezaji wenye mafanikio wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Hayo yameelezwa katika andiko la ushauri kuhusu siasa na sheria lililowasilishwa serikalini, likilenga kuchambua changamoto za kisiasa na kisheria zinazoweza kuathiri maendeleo ya taifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa THTU Taifa, Dk. Paul Loisulie, utawala bora ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu na unapaswa kuimarishwa katika ngazi zote.
Alisema pamoja na Tanzania kuwa na mfumo mzuri wa kikatiba na kisheria, bado kuna changamoto ya utekelezaji wa sheria hizo kwa vitendo, hali inayodhoofisha uwajibikaji na ufanisi wa taasisi za umma.
“Ni muhimu kuziba pengo la utekelezaji wa sera na sheria ili kuhakikisha haki, uwazi na ushiriki wa wananchi vinaimarika,” alisema.
THTU imebainisha changamoto mbalimbali ikiwemo masuala ya haki za binadamu, uhuru wa taasisi, ushiriki mdogo wa wananchi na uwepo wa rushwa ya kimfumo.
Katika mapendekezo yake, chama hicho kimeitaka Serikali kufanya marekebisho ya kisheria na kisera, kuimarisha taasisi za umma, pamoja na kuongeza ushiriki wa wananchi katika maamuzi ya maendeleo.
Chama hicho kimesisitiza kuwa bila utawala bora, utekelezaji wa Dira 2050 hautaweza kufikiwa kwa ufanisi.
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anafanya ziara katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6
Pia Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.
.jpeg)
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameshiriki ibada ya Jumapili, leo, Aprili 26, 2026, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Usharika wa Azania Front, jijini Dar es Salaam.
Ibada hiyo iliongozwa na Katibu wa Umoja wa Utume wa Injili (United Evangelical Mission - UEM) Kanda ya Afrika, Dkt. Ernest Kadiva, kwa kushirikiana na Mchungaji Kiongozi wa KKKT Usharika wa Azania Front, Victor Makundi.
-ASISITIZA MALEZI BORA KWA WATOTO KWA MANUFAA YA TAIFA
-APONGEZA JUKWAA LA TUZO ZA MALKIA WA NGUVU
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameiasa jamii kukemea na kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji vinavyofanywa kwa wanawake hususani katika mitandao ya kijamii.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa kilele cha Tuzo kwa wanawake waliofanya vizuri katika sekta mbalimbali maarufu “Malkia wa Nguvu” kanda ya kati, zilizofanyika katika Ukumbi wa Mabele mkoani Dodoma. Amesema udhalilishaji huo unapaswa kukemewa na kila Mtanzania ili kusimamia heshima ya mwanamke katika jamii.
Makamu wa Rais amesema ni vema watanzania wote kuona wajibu wa kuilinda heshima ya mwanamke na kuwapima wanawake kwa majukumu yao yanayoleta maendeleo kwa Taifa. Amewasihi kipekee wanawake, kuacha tabia ya kushangilia katika mitandao ya kijamii hususani anapodhalilishwa mwanamke mwenzao.
Halikadhalika, Makamu wa Rais ametoa rai kwa Wanawake nchini kwa kushirikiana na jamii kwa ujumla kuchukua hatua katika kukabiliana na mmomonyoko wa maadili kwa watoto. Amesema imekuwepo tabia ya watoto kujiingiza katika matumizi ya mitandao ya kijamii ambayo imekuwa ikiwekwa maudhui yasiyofaa hivyo kuharibu maadili na kuhatarisha kizazi cha sasa na kijacho.
Makamu wa Rais amesema Serikali itaendelea kusimamia mambo yatakayoleta mabadiliko kwa wanawake ikiwemo kuendeleza majukwaa ya uwezeshaji ikiwemo mpango wa 2022-2032 na kusimamia mfuko wa maendeleo ya wanawake ambao unahusika na ukopeshaji.
Pia amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga maendeleo ya nchi kuinua ajira na kutengeneza fursa pamoja na kuzingatia nafasi ya mwanamke katika ujenzi wa Taifa. Ametoa wito kwa Jukwaa la Malkia wa Nguvu kushiriki kikamilifu katika kutoa elimu na hamasa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Makamu wa Rais amewapongeza wanawake katika kuendelea kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Taifa na shughuli za maendeleo kwa ujumla. Amesema nia ya Serikali kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ni kujenga Taifa lenye nguvu kwa kujengea uwezo watu wake kwa kuzingatia usawa katika jamii.
Makamu wa Rais amelipongeza Jukwaa la Malkia wa Nguvu kwa kusimamia kwa kutimiza miaka kumi kwa mafanikio, ambapo limefanya jitihada za pekee kubainisha fursa kwaajili ya wanawake na kuwahamasisha kuzitumia fursa hizo.
Makamu wa Rais amesema Serikali inavutiwa na malengo ya Taasisi inayosimamia Jukwaa la Malkia wa Nguvu husuani lengo kuu la kumuinua wanawake na kuwafanya kuwa wajasiriamali, wabunifu na viongozi.
Katika Kilele cha Tamasha hilo la Malkia wa Nguvu kanda ya kati, wanawake mbalimbali wamepata tuzo kwa kutambua mchango wao katika sekta mbalimbali ikiwemo ujasiriamali, ubunifu, utumishi wa umma na uongozi.

Na Said Mwishehe,Michuzi TV
MKURUGENZI Mkuu wa Bohari ya Dawa(MSD) Mavere Tukai amewahakikishia Watanzania kuwa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini uko imara kwani kuna akiba ya kutosha kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita, licha ya kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, ameyasema hayo katika kikao kazi kilichohusisha wahariri na waandishi wa habari walipokutana kujadili masuala mbalimbali katika sekta ya afya na hasa mchango wa MSD katika kuendeleza jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba unakuwa wa uhakika nchini.
Hivyo ametumia kikao hicho kuwatoa wasiwasi miongoni mwa wananchi kuhusu uwezekano wa kupungua kwa dawa na vifaa tiba, hasa kutokana na athari zinazoweza kusababishwa na mvutano wa kijeshi kati ya Marekani na Iran.
“MSD imejipanga vyema kuhakikisha upatikanaji endelevu wa bidhaa hizo muhimu na tayari kuna tathmini inayoendelea kufanywa na timu maalumu ya wataalamu ili kubaini hatari zinazoweza kujitokeza na kuweka mikakati madhubuti ya kukabiliana nazo.”
Mkurugenzi Mkuu ameongeza juhudi zinaendelea kuimarishwa, hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi hauathiriki na mabadiliko ya hali ya usalama na uchumi wa kimataifa.
“Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa hali hiyo ili kuhakikisha huduma za afya nchini haziathiriki na wananchi wanaendelea kupata huduma bora bila usumbufu.


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)









.jpeg)

.jpeg)






.jpeg)






.jpeg)






.jpeg)




.jpeg)