Kuna methali isemayo “Asiyejua maana haambiwi maana “ lakini Ngorongoro leo itakuambia maana ya Nyayo za Laetoli.

Nyayo hizi ni za kihistoria na ni sehemu pekee duniani ambayo mafundi Viatu ulimwenguni wanaweza kufika na kutengeneza Viatu vya kihistoria vinavyoweza kushinda nishani ya Nobel kutokana na Nyayo za Laetoli zilivyo.

Katika eneo la Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro, tarehe 24, Julai mwaka 1978, Mtafiti maarufu wa masuala ya Akiolojia Dr. Mary Leakey na timu yake iliyomhusisha Dkt. Paul Abell waligundua nyayo za zamadamu katika eneo la Laetoli zilizohifadhika katika mwamba wa jivu la volcano inayoaminika kuwa ililipuka katika mojawapo wa milima ya Ngorongoro miaka milion 3.6 iliyopita. 

Wataalamu hawa wanaamini kuwa nyayo hizo ziliachwa na jamii ya watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis.

Nyayo za Zamadamu katika eneo la Laetoli ni ushahidi wa pekee na wa bayana duniani kote usiopingika kwamba zamadamu (Hominin) kwa mara ya kwanza walianza kusimama wima na kutembea kwa miguu miwili katika eneo la Laetoli Ngorongoro Tanzania miaka milioni 3.6 iliyopita.

 Binadamu hawa waliotembea wima kwa miguu miwili wametokana na babu/bibi mmoja aliyeishi miaka takribani millioni 7 iliyopita. 

Mwanadamu aliyepo Tandahimba, Gamboshi kule Bariadi, Tandale kwa mtogole, Mbagala Zakiem na yule aliyepo Jerusalemu, Macca, Dubai, New York, London, Johannesburg, Tehran, Gaza, Misri hadi Sudan na Mumbai wametokana na babu na bibi mmoja.

Katika kuthibitisha uhai, Nyayo za zamadamu ndizo za kustaajabisha katika eneo la Laetoli, zipo nyayo za wanyama wengine wa kale kama vile nyayo za tembo, twiga, faru na wanyama ndogo kama sungura, kanga na aina za wadudu.

Kwa nyayo za Laetoli zilivyo, mafundi Viatu na wamiliki wa viwanda vya Viatu duniani wanaweza kufika katika Eneo  hilo ili kupata  ujuzi zaidi wa namna ya kutengeneza Viatu vya kihistoria.

 Karibu kwetu Ngorongoro ambapo kila ukilala kuna ndoto ya maajabu inakuita


Muonekano wa Nyayo za Laetoli zilizoachwa na jamii za watu wa kale wanaofahamika kama Australopithecus Afarensis

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuhakikisha mita za umeme zinahakikiwa kikamilifu kabla ya kufungwa kwa ajili ya matumizi, kwa kuzingatia sheria zilizopo ili kulinda haki za watumiaji.

Aidha, Kamati hiyo imeipongeza WMA kwa jitihada za uhakiki na ukaguzi wa vipimo mbalimbali, ikiwemo mita za maji, huku ikiitaka Wakala hiyo kuendelea kusimamia kwa ukaribu vipimo katika sekta ya ujenzi ili kupunguza malalamiko ya wananchi yanayotokana na bidhaa hizo.

Hayo yameelezwa leo Machi 14, 2026, na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, wakati wa ziara ya kikazi katika Kituo cha WMA cha Uhakiki wa Vipimo Misugusugu mkoani Pwani kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kujionea shughuli za uhakiki wa vipimo zinavyotekelezwa kituoni hapo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, aliihakikishia Kamati kuwa wizara itatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa.

Alisisitiza kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha WMA inasimamia matumizi ya vipimo sahihi katika uzalishaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali, pamoja na Uhakiki wa mita za umeme na maji, ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, akitoa salamu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alibainisha kuwa uhakiki wa vipimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa mkoa huo. Alieleza kuwa kwa sasa Mkoa wa Pwani una jumla ya viwanda 1,688, vikiwemo viwanda vikubwa 199 na vidogo sana 1,017, hivyo uhakiki wa usahihi wa Vipimo ni nyenzo muhimu katika kuvutia uwekezaji zaidi.

Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa WMA, Bw. Alban Kihulla, alisema kuwa ukaguzi na uhakiki wa vipimo una nafasi kubwa katika kuhakikisha haki na usawa baina ya pande mbili zinazofanya biashara.

Pia, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanatumia vipimo vilivyohakikiwa, huku akiwasihi watoa huduma kuzingatia uadilifu kwa kutoa huduma kupitia vipimo sahihi ili kuleta usawa na kuhakikisha bidhaa zinazonunuliwa zinaendana na thamani halisi ya fedha.


By Moses Ntandu, Dar es Salaam, Tanzania

On the land of Sudan, this month of Ramadan has not arrived with peace or hope. Instead, it has come to a country exhausted by war, torn apart by pain, and immersed in the grief of thousands of families who have lost their loved ones.

The capital city, Khartoum, once the heart of life and commerce, now bears the marks of bullets, destroyed buildings, and streets filled with memories of war. Despite the great sacrifices and relentless efforts made by patriotic Sudanese youth through the government army, led by the commander who carries the vision of the nation’s liberation, Abdel Fattah al-Burhan, to ensure that peace, safety, and stability return to every part of the country.

The fighting between the Sudanese Armed Forces and the rebel militia Rapid Support Forces has turned large parts of the country into a field of humanitarian disaster. The regions of Darfur, Kordofan, and Blue Nile State have become living proof of how war can destroy a nation within a short time.

But the most painful truth is this: most of those who have died in this war are not soldiers. They are civilians. They are children who had dreams of going to school. They are mothers who were preparing food for their families. They are elderly people who were praying for peace in their country.

The world can not pretend not to see this situation, while those responsible act as though they know nothing.

The war in Sudan is not merely an internal political conflict, but a crisis initiated and engineered from outside the country for specific purposes. Will the world remain silent as this nation collapses? Will political leaders and those who once legitimized or supported this war continue hiding behind political language?

History teaches us that wars do not continue because of bullets alone. They persist because there are people who celebrate them, legitimize them, or support them in various ways, whether through money, military supplies, propaganda, or deliberate silence. Every word that incites hatred, every aid package sent to fighters, and every piece of propaganda that justifies bloodshed increases the number of new graves of innocent civilians.

Now is the time for truth. Now is the time for moral accountability. All individuals, political groups, or international stakeholders who once supported or legitimized armed rebellion in Sudan should come forward publicly and apologize.

Countries such as the United Arab Emirates, by openly supporting this war, providing logistics and various forms of military assistance to the rebels; nations that hosted those rebels, such as Kenya leading to a major diplomatic dispute with Sudan and even neighboring Ethiopia, accused of establishing training camps for rebels and creating diplomatic tensions, should openly apologize to the people of Sudan and to the world for their contribution—whether direct or indirect—to this great catastrophe.

Apologizing is not a weakness; it is the courage to accept the truth, and it is the first step toward restoring human dignity.

Peace can not be built on hypocrisy. No nation can be rebuilt on foundations of hypocrisy, propaganda, and deliberate silence. Sudan will need many years to rebuild itself to reconstruct schools, hospitals, its economy, and above all to heal the hearts of its people.




But that rebuilding can not begin without truth. And the truth is this: the blood of Sudanese civilians should never become part of anyone’s political games, or the ambitions of any group or nation seeking selfish interests while disregarding the lives of innocent people—even worse when they pursue those interests inside Sudan itself.

To the international community, political leaders, activists, and everyone with a conscience seeking peace and global security: Sudan is not merely a statistic in news reports.

Sudan is a nation of real people with families, dreams, and hopes. If the world continues to remain silent in the face of this disaster, history will judge that silence as quiet participation in the suffering of the Sudanese people. Because in the end, one truth remains clear.

Wars may be started by a few, but their pain is carried by millions of innocent people. The blood of Sudanese the blood of children, women, and the elderly cannot and must never be ignored.

A small example of the pain of war has recently been felt in the UAE following tensions with Iran. They have only been slightly attacked, yet their outcry has been loud after experiencing just a small fraction of what resembles the suffering occurring in Sudan.

Clearly, what you do not wish to be done to you, you should not do to others, treat others as you wish to be treated, as reflected in the Arabic saying: “Kama tadinu tudan” (As you judge, so shall you be judged).

As we approach the final days of the holy month of Ramadan and the season of Lent, it would be appropriate for all those who know within their conscience that they have been involved in the ongoing disaster in Sudan the deaths of innocent civilians and the destruction of infrastructure, private property, and public property to return quickly to their Creator, repent for these sins, sincerely seek forgiveness, and publicly apologize to the people of Sudan and their government.

The government’s efforts have greatly helped restore peace in many cities, while stability and security are increasingly prevailing in the capital, Khartoum. Recently, the sounds of joy and celebration were heard at Khartoum International Airport after the landing of the second passenger plane, raising hope that peace may soon return to the country as it once was.

The conclusion of this analysis is simple: the truth can not be hidden forever.

Every drop of blood spilt on Sudanese soil is testimony to a pain the world cannot ignore—from the ruined streets of Khartoum to the burned villages across the country, including Darfur. The cries of the Sudanese people call for justice, accountability, and an end to the war.

History will not only record those who fought in the war, but also those who remained silent, those who supported it, and those who watched without speaking while a nation burned.

That is why the time for truth has come: the time to admit mistakes, apologize, and stand on the side of peace.

Because in the end, a nation can be rebuilt and buildings can be reconstructed—but lives that have been lost will never return. And for the children of Sudan, for the future of this nation, and for the dignity of the entire world, the blood of Sudan must mark the end of war not the beginning of a new silence.



Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.

Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.

Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.

Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter




Ramadan Kareem. 🌙


-Asema taasisi za dini nguzo ya maadili na amani nchini

-Aonya migogoro ya ardhi inaweza kuvuruga mshikamano wa Taifa


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini nchini katika kulinda amani, kuimarisha maadili na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumapili (Machi 15, 2026) wakati akitoa salamu katika Ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Mpanda Mjini, Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, iliyoongozwa na Askofu Imani Ahobokile Chibona.

Amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za dini katika kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu, upendo, haki na uwajibikaji.

“Nimekuja pia na salamu za upendo kutoka kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kudumisha amani, maadili mema na mshikamano wa kitaifa,” amesema.

Waziri Mkuu amesema taasisi za dini zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi, hususan katika sekta za elimu, afya na malezi ya jamii.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuwekeza katika miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Katavi ikiwemo miradi ya maji, barabara na nishati kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi.

Akizungumzia sekta ya maji, Dkt. Mwigulu amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mradi wa Maji wa Miji 28 ambapo jana aliweka jiwe la msingi la mradi wa kusambaza maji kutoka Bwawa la Milala unaotarajiwa kuzalisha lita milioni 12 za maji kwa siku na kuhudumia wakazi wa Manispaa ya Mpanda.

Katika sekta ya miundombinu, amesema Serikali imekamilisha ujenzi wa barabara ya Mpanda – Tabora yenye urefu wa kilometa 352 kwa kiwango cha lami ambayo imekuwa kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi katika mkoa huo.

Aidha, amesema ujenzi wa barabara ya Mpanda – Uvinza – Kanyani unaendelea ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 15.7, huku ujenzi wa barabara ya Kagwira – Karema nao ukiendelea kwa lengo la kufungua fursa za kiuchumi katika ukanda wa Ziwa Tanganyika.

Waziri Mkuu pia amesema Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa nishati ya umeme katika Mkoa wa Katavi ambapo vijiji vyote 172 tayari vimeunganishwa na umeme huku vitongoji 534 kati ya 912 vikifikishiwa huduma hiyo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amewataka Watanzania kuendelea kulinda amani, umoja na mshikamano wa kitaifa akisisitiza kuwa amani ya nchi ni matokeo ya jitihada za pamoja za Serikali, taasisi za dini na wananchi.

“Taifa letu limeendelea kuwa kisiwa cha amani kwa sababu ya mshikamano wa Watanzania. Tuendelee kuwa mabalozi wa amani katika familia, maeneo ya kazi na katika jamii kwa ujumla,” amesema.

Akizungumzia umuhimu wa kudumisha amani, umoja na mshikamano, Mheshimiwa Waziri Mkuu amesema kuwa mnufaika namba moja wa amani ni mwananchi mwenyewe na Taifa kwa ujumla.

“Tunapaswa kuepuka migogoro isiyo ya lazima hususan ya ardhi. Hata tukigombana au kupigana ardhi haiongezeki. Kilicho muhimu ni kukaa pamoja, kuzungumza na kushirikishana ili kutumia ardhi yetu kwa manufaa ya wote,” amesema.

Amesema kuendelea kwa migogoro ya ardhi kunaweza kuliweka Taifa katika mazingira yasiyo mazuri na kupelekea chuki pamoja na kuvunjika kwa umoja wa kitaifa. Ameongeza kuwa msingi wa maendeleo ya Taifa lolote ni amani, umoja na mshikamano, hivyo ni muhimu kuendelea kuliombea Taifa lisipoteze tunu hizo.

Kwa upande wake, Askofu wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, Dkt. Imani Ahobokile Chibona, amesema Kanisa linaendelea kuhimiza waumini kudumisha amani, mshikamano na maadili mema katika jamii kwani amani ya Taifa inaanza na mtu mmoja mmoja katika familia na jamii.

Askofu Chibona pia ameitaka jamii kuendelea kuwaombea viongozi wa kitaifa ili Mungu awape hekima, nguvu na afya njema katika kuliongoza Taifa, huku akisisitiza kuwa Serikali imeendelea kufanya kazi kubwa ya kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta mbalimbali.










Taasisi ya Ramadhan Charity Programme 2026 imewataka Watanzania kutumia mwezi mtukufu wa Ramadhani kuwa wamoja, kusaidiana na kufanya kazi kwa pamoja katika kuwasaidia watu wenye uhitaji katika jamii.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Ramadhan Charity Programme 2026, Ahmed Misanga, wakati akikabidhi sadaka ya iftar katika kituo cha Jaamiul-Furouq, kilichopo wilayani Manyoni mkoani Singida.

Misanga amesema kuwa kutoa sadaka kunahitaji moyo wa kusaidia na si lazima mtu awe tajiri. Ameongeza kuwa watu wenye uwezo wajitokeze kushirikiana katika kuwasaidia wenye uhitaji, kwani wapo wengi hasa katika vituo vya kulea watoto yatima na watu wasiojiweza.

Aidha, Misanga amesisitiza kuwa kutoa sadaka na kutumia mali katika njia ya Allah ni miongoni mwa matendo mema na bora, kwani hufuta madhambi na makosa kama vile maji yanavyozima moto.

Katika hatua nyingine, amewahimiza vijana kusoma kwa bidii ili wawe watu wema katika jamii na baadaye waweze kusaidia wengine wenye uhitaji.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa kituo hicho Nawawi Salimu, ameishukuru Taasisi ya Ramadhan Charity Programme 2026 kwa kuendelea kutoa sadaka ya iftar katika kituo hicho kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Amesema msaada huo umekuwa na mchango mkubwa kwa wanafunzi wa kituo hicho, na amewahimiza wadau hao kuendelea na moyo huo wa kusaidia jamii, bila kuishia katika kituo hicho pekee bali kufikia pia vituo vingine vyenye uhitaji.

“Mimi pamoja na wanafunzi wangu hatuna cha kuwalipa, lakini tunaamini Mwenyezi Mungu ndiye atakayewalipa kwa wema huu mlioufanya,” amesema Nawawi.

Aidha, amewaomba wadau wengine kuiga mfano wa Ramadhan Charity Programme 2026 kwa kuwafikia walengwa na kutoa sadaka katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, kwani bado kuna uhitaji mkubwa.

Ameongeza kuwa katika kituo hicho kuna zaidi ya watoto 100 wanaopata elimu ya dini na malezi ya mazingira, huku akisema milango ya msaada bado ipo wazi kwa yeyote mwenye nia ya kusaidia.




Dar es Salaam. Uganda na Tanzania zimekubaliana kuondoa vikwazo vyote vya biashara kati ya nchi hizo mbili ifikapo mwezi Juni mwaka huu, hatua inayolenga kupunguza gharama za kufanya biashara, kuimarisha biashara ya pande mbili na kukuza ushirikiano wa kiuchumi.

Ahadi hiyo ilitangazwa wakati wa chakula cha jioni rasmi kilichoandaliwa na Ubalozi wa Uganda nchini Tanzania jijini Dar es Salaam Alhamisi jioni, kuelekea Kikao cha Tano cha Tume ya Kudumu ya Pamoja kati ya Uganda na Tanzania (JPC).

Kikao hicho kimefanyika kuanzia Machi 11 hadi Machi 13, 2026 katika Julius Nyerere International Convention Centre, na kimewakutanisha maafisa wa serikali kutoka nchi zote mbili kujadili na kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, uwekezaji na ushirikiano wa kikanda.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Fred Mwesigye, alisema nchi hizo mbili zina uhusiano wa kihistoria unaozidi urafiki wa kawaida na kufikia kiwango cha undugu wa karibu.

“Tungependa kuwaambia Watanzania na Waganda kwamba sisi si marafiki tu, bali ni ndugu. Kila tunachofanya tunakifanya kama ndugu—bila migogoro, bila vikwazo na bila changamoto zisizo za lazima,” alisema.

Kwa mujibu wa balozi huyo, lengo kuu la mazungumzo yanayoendelea kati ya serikali hizo mbili ni kuimarisha zaidi uhusiano wa kiuchumi na kuhakikisha wafanyabiashara wa pande zote wanafanya biashara bila vikwazo visivyo vya lazima.

“Tunapoelekea kwenye kikao cha tano cha JPC, tumekubaliana kuwa vikwazo vyote vilivyopo katika biashara vitaondolewa ifikapo mwezi Juni. Hii ina maana tunatarajia kuona nafaka zikiingia Uganda bila vizuizi, na wafanyabiashara wa Uganda wakifanya biashara Tanzania bila vikwazo,” alisema Balozi Mwesigye.

Alieleza kuwa baadhi ya tozo na gharama zinazohusiana na kodi zimekuwa miongoni mwa changamoto kubwa zinazoongeza gharama kwa wafanyabiashara kati ya nchi hizo mbili. Kuondolewa kwa vikwazo hivyo kutasaidia biashara kukua kwa kasi na kuimarisha ujumuishaji wa kiuchumi.

Balozi Mwesigye pia aliipongeza Tanzania kwa kuboresha miundombinu inayorahisisha biashara kati ya nchi hizo mbili.

Alitaja maendeleo ya barabara zinazounganisha Tanzania na Uganda, mipango ya kuufikisha Reli ya Kisasa (SGR) hadi Uganda pamoja na maboresho katika bandari zinazotumiwa na wafanyabiashara wa Uganda, ikiwemo Tanga, Mwanzana Dar es Salaam.

“Maboresho haya yatafanya usafirishaji wa bidhaa kati ya nchi zetu uwe rahisi zaidi. Mara tu gharama zilizobaki zitakaposhughulikiwa, biashara kati ya Uganda na Tanzania itakua kwa kasi zaidi,” alisema.

Balozi Mwesigye pia alizungumzia kile alichokiita kutokuwepo kwa uwiano katika uwekezaji kati ya nchi hizo mbili.

Alisema uwekezaji wa Watanzania nchini Uganda kwa sasa unazidi dola bilioni 2, huku uwekezaji wa Waganda nchini Tanzania ukiwa takribani dola milioni 200.

“Huo ni utofauti mkubwa. Lakini mara vikwazo vilivyosalia vitakapoondolewa, tunatarajia bidhaa za Uganda kama sukari kuingia Tanzania bila changamoto, huku bidhaa za Tanzania kama mchele zikifika kwa urahisi zaidi katika soko la Uganda,” aliongeza.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Uganda, Vincent Bagiire, aliwapongeza maafisa kutoka nchi zote mbili kwa mafanikio yaliyopatikana katika siku mbili za majadiliano kuelekea kikao cha JPC.

Alisema diplomasia ya kisasa inazidi kuelekeza nguvu katika masuala ya uchumi na biashara, huku majukwaa kama JPC yakisaidia kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi.

“Diplomasia ya sasa inalenga zaidi maslahi ya kiuchumi na kibiashara. Mifumo kama JPC ni nyenzo muhimu katika kutekeleza mtazamo huo na kusaidia kukuza uchumi wetu,” alisema.

Aidha alimpongeza Ubalozi wa Uganda jijini Dar es Salaam kwa juhudi zake katika kukuza ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili, ikiwemo mipango ya kuongeza mauzo ya bidhaa nje ya nchi.

Alitaja pia juhudi zinazoendelea za kuuza mabasi ya umeme yanayotengenezwa Uganda katika masoko ya kikanda ikiwemo Tanzania, akisema tayari kuna dalili kuwa mabasi hayo yanaweza kupata soko nchini Tanzania.

Waziri wa Nchi wa Mambo ya Nje wa Uganda anayeshughulikia Ushirikiano wa Kikanda, John Mulimba, alisema ushirikiano wa kikanda ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unaendelea kuwa msingi muhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi wanachama.

Alibainisha kuwa mageuzi ya hivi karibuni ndani ya jumuiya hiyo yanatarajiwa kuboresha maamuzi na kuimarisha taasisi za kikanda.

“Tumekutana hapa kwa ajili ya JPC ili kuthibitisha upya dhamira yetu ya kutekeleza Itifaki ya Soko la Pamoja na Umoja wa Forodha. Mifumo hii tayari inatoa mwongozo wa masuala mengi tunayojadili,” alisema.

Alisisitiza kuwa hatua inayofuata ni kuhakikisha makubaliano yaliyofikiwa yanatekelezwa kwa vitendo.

“Lazima tuondoke hapa tukiwa na ratiba na majukumu yaliyo wazi ili wizara, idara na taasisi ziweze kutekeleza tuliyokubaliana badala ya kuweka nyaraka makabatini,” alisema.

Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC) ni jukwaa muhimu la ushirikiano wa pande mbili ambapo Tanzania na Uganda hupitia na kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, miundombinu, usalama na ujumuishwaji wa kikanda.

Na Mwandishi Wetu

WANAWAKE watatu wamebahatika kupata fursa ya kupandikiza mimba bure katika kituo cha kupandikiza mimba cha Kairuki Green IVF (KGIVF), Kilichoko Bunju A Mianzini jijini Dar es Salaam.

Walipata fursa hiyo jana jioni wakati wa droo iliyochezeshwa na mgeni rasmi Jokate Mwegelo wakati wa sherehe za siku ya wanawake zilizoandaliwa na Mtandao wa Elimu ya Afya Kairuki (KHEN) jijini Dar es Salaam .

Wanawake hao ni miongoni mwa wanawake zaidi ya 137 wa mikoa mbalimbali walioomba kupata fursa hiyo ya bure lakini katika mchujo uliofanyika walibahatika wanawake hao watatu pekee.

Kwa wastani gharama za kupandikiza mimba kwa Tanzania ni kati ya shilingi milioni 18 mpaka 20.

Mkurugenzi wa KGIVF, Dk Clementina Kairuki alisema waliopata fursa hiyo watahudumiwa bure kuanzia hatua za awali hadi kupandikiza mimba kama sehemu ya kituo hicho kusaidia jamii.

Alisema wameamua kutoa huduma hiyo bure kama sehemu ya kusherehekea siku ya mwanamke duniani kuwapa furaha ya kupata familia wanawake ambao wamekuwa wakitamani kupata familia lakini wanashindwa kutokana na kukosa pesa.

Alisema KGIVF iliona wanawake wengi wamekuwa wakijitokeza kutaka kupandikizwa mimba kwenye kituo hicho lakini asilimia 30 hawawezi kumudu gharama za huduma hiyo.

“Kuna watu wengi wanapata shida wanatukanwa kwenye familia wanaachika kwenye ndoa kwasababu hawajabahatika kupata watoto, tafiti zinaonyesha kuwa kila ndoa sita moja inachangamoto ya kupata watoto ndiyo maana tukaona tutoe fursa hii,” alisema

Alisema KGIVF imekuwa ikitoa elimu kwa jamii kuhusu ukubwa wa tatizo hilo na namna bora ya kupata suluhu ya kulitatua kwa kupandikiza mimba.

“Tumetambua kuwa kuna watanzania wengi wenye tatizo hili lakini hawana uwezo wa kuja KGIVF kupandikiza mimba kwasababu ya uwezo wa kifedha ndiyo maana tumechagua wanawake watatu tuwape huduma hii bure kama sehemu ya kutoa elimu kwa jamii,” alisema

Mgeni rasmi kwenye hafla hiyo, Jokate Mwegelo alisema Mtandao wa Elimu ya Afya Kairuki (KHEN) ni mfano wa kuigwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutokana na mambo makubwa waliyofanya.

Alisema KHEN imefanya mambo makubwa ikiwemo kuanzisha Kituo cha kupandikiza mimba KGIVF, Kairuki Hospitali, Kiwanda cha kutengeneza dawa kilichoko Kibaha mkoani Pwani, Chuo Kikuu Kairuki na Kampasi ya chuo hicho iliyoko Boko.

“Mimi ni mdau mkubwa sana wa Kairuki, nimekuwa nikiwasemea sana na leo naomba nijirasimishe kuwa balozi wa Kairuki, nitawasemea vizuri popote nitakapokuwa kwasababu nyinyi mmeonyesha mfano wa kuigwa kwenye kusaidia jamii yetu,” alisema Jokate Mwegelo.

“Mimi nitakuwa balozi wa viwango kwasababu nimeona Kairuki ni taasisi ya viwango vya juu sana, siongei haya kumfurahisha mtu hapa nasema hili kutoka kwenye sakafu ya moyo wangu, katika taasisi zilizoasisiwa na watanzania wenzetu, Kairuki ni taasisi ya mfano Afrika Mashariki na Kati kwasababu imesimama na haitetereki,” alisema

“Wako watu walianzisha biashara hata miaka mitatu haijafika zikafa, lakini leo hii ukizungumzia Kairuki unazungumzia Hospitali, unazungumzia Kairuki Green IVF, unazungumzia kiwanda cha dawa Kibaha, chuo cha Kairuki ambacho kinawanafunzi zaidi ya 2,000 nani kama Kairuki,” alisema




















📌 Umeme umewashwa kwa mara ya kwanza katika vitongoji viwili

📌 Zaidi ya Shilingi bilioni 60 zatumika kusambaza umeme kwenye vitongoji vya mkoa wa Shinyanga


Kahama, Shinyanga📍

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeridhishwa na namna fedha za Bajeti ya Mwaka 2025/2026 zilizoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinavyotumika katika utekelezaji wa Miradi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati pamoja na zoezi la kuwasha umeme kwa mara ya kwanza katika kitongoji cha Mine, kata ya Mwakata, Jimbo la Msalala na kitongoji cha Mjimwema katika Jimbo la Kahama wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, amesema ziara ya kamati imelenga kukagua na kujionea utekelezaji wa Miradi ili kuhakikisha fedha zilizotengwa na Bunge zinatumika kwa ufanisi.

“Tumepewa dhamana na Bunge kuhakikisha fedha zilizotengwa zinatekeleza kusudi lililokusudiwa. Bunge lilitenga bajeti ya shilingi bilioni 400 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kwa ajili ya miradi ya kufikisha umeme vitongojini, na tumekuja kuona thamani ya fedha hizo kama imetumika ipasavyo. Kwa kweli tumeridhishwa na kazi inayofanywa na REA,” amesema Mhe. Mgalu.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo unaonesha mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma ya umeme.

Naye Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema ukaguzi wa miradi unaofanywa na Kamati ya Bunge ni sehemu muhimu ya utekelezaji wa Katiba, inayolenga kuhakikisha Bunge linasimamia ipasavyo matumizi ya fedha za umma katika miradi ya maendeleo.

Makamba amesema katika bajeti ya Wizara ya Nishati, ilipanga kuwa kila jimbo nchini litapatiwa vitongoji 15 vitakavyofikishiwa huduma ya umeme ili kuongeza kasi ya maendeleo kwa Wananchi.

Amesema Miradi hiyo inaendelea kubadilisha maisha ya Wananchi kwa kuchochea shughuli za kiuchumi pamoja na kuboresha huduma za kijamii na kuongeza fursa za maendeleo katika maeneo ya vijijini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, amesema mkoa wa Shinyanga una jumla ya vitongoji 2,704 ambapo kati ya hivyo vitongoji 1,180 tayari vimefikishiwa huduma ya umeme.

Amesema vitongoji 582 vipo katika Mradi wa HEP II (B); Mradi uliosainiwa Januari mwaka huu ambao unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

“Kuanzia mwaka wa fedha 2024/2025 hadi sasa REA imeidhinisha zaidi ya shilingi bilioni 61 kwa ajili ya kufikisha umeme katika vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Shinyanga,” amesema Mhandisi, Olotu.

Aidha ameahidi kuwa REA itaendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali na Bunge kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini vinafikiwa na huduma ya umeme.










Top News