Na Joseph Mahumi, WF


Serikali ya Tanzania imeendelea kung’ara katika jukwaa la kimataifa baada ya kuibuka mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.

Ushindi huo mkubwa unatokana na juhudi za Serikali katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa deni la umma, ikiwemo kuunganisha vyema mifumo ya kifedha ya Serikali na kuboresha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya maendeleo, ambapo Jopo huru la wataalamu lililochambua mawasilisho kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya ya Madola lilizingatia vigezo vya ubunifu, uimara na uendelevu katika kutoa tuzo hizo.

Akifungua hafla ya utoaji tuzo hizo, Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal, alisisitiza umuhimu wa nchi wanachama kuendelea kubuni mbinu madhubuti za kusimamia deni la umma ili kulinda uchumi dhidi ya misukosuko ya kifedha duniani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, Bi. Ruth Kattumuri, aliipongeza Tanzania kwa mageuzi makubwa iliyoyafanya katika kuimarisha usimamizi wa deni la umma.

Alieleza kuwa mafanikio hayo ni kielelezo cha dhamira ya dhati ya nchi katika kujenga uchumi imara na unaostahimili mishtuko ya kiuchumi.

Aidha, Bi. Kattumuri, alisema kuwa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola itaendelea kuisaidia Tanzania katika juhudi zake za kuboresha sera na mifumo ya usimamizi wa deni, sambamba na utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha 72 cha Kundi la Mawaziri wa Jumuiya ya Madola.

Mkutano huo wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola uliofanyika kwa muda wa wiki moja uliwakutanisha wataalamu wa usimamizi wa deni kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza na kujadili mbinu bora za kukopa, kusimamia na kulipa deni la umma, na umeandaliwa ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Jumuiya ya Madola wa Deni Imara, Bunifu na Endelevu, ambapo Tanzania imejitokeza kama kinara na mfano wa kuigwa barani Afrika na katika Jumuiya nzima ya Madola.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) akiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bw. Tanmaya Lal (kushoto) na  Mkurugenzi Mkuu Mwandamizi wa Idara ya Uchumi, Maendeleo, Biashara na Uwekezaji wa Sekretarieti ya Jumuiya hiyo, Bi. Ruth Kattumuri.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, akionesha tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza.
Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (Katikati) Aakiwa ameshika tuzo mbili ambazo Tanzania imepata kwa kuibuka Mshindi wa jumla wa mwaka katika Tuzo za Usimamizi wa Deni la Umma za Jumuiya ya Madola na Tuzo ya Ofisi Bora Kanda ya Afrika kupitia Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha (Debt Management Division), ambazo zilitangazwa tarehe 26 Machi 2026 wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Jumuiya ya Madola kuhusu Usimamizi wa Deni la Umma, uliofanyika jijini London, nchini Uingereza. Wengine katika picha ni washindi wenngine wa tuzo hizo kutoka nchi ya Barbados ambayo iliibuka mshindi wa Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Caribbean na Sri Lanka Msimamizi bora wa deni katika ukanda wa nchi za Asia.

Na Mwandishi Wetu

MFUKO wa Maendeleo ya jamii(TASAF)umeunga mkono juhudi za Serikali katika huduma ya afya kwa kutoa msaada muhimu katika Taasisi ya Saratani Ocean Road jijini Dar es Salaam.

Msaada huo umekabidhiwa leo hospitalini hapo na Meneja rasilimali watu wa mfuko huo Mariam Al- Jabiri kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Shedrack Mziray.

Al-Jabiri ambaye ameambatana na baadhi ya wafanyakazi wa Tasaf amesema Serikali imewekeza nguvu kubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini.

“Msaada huu umelenga kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini,”amesema huku akiwatakia uponyaji wa haraka wagonjwa wote wanaopata matibabu katika taasisi hiyo.

Aidha baadhi wa Wafanyakazi hao wa TASAF wakiongozwa na Meneja huyo wamepata nafasi ya kuwajulia hali wagonjwa hospitalini hapo huku wakiwafariji kwa kuwatia moyo na kufanya sala fupi kuwaombea uponyaji wa haraka.

Kwa upande wake Mwakalishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Ocean Road Dk.Diwani Msemo ameushukuru mfuko wa maendeleo ya jamii kwa msaada huo.









 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwaongoza Watanzania kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na wenye Ulemavu), Hayati William Vangimembe Lukuvi, tarehe 28 Machi, 2026.














Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.




Mheshimiwa Dkt. Kikwete ameambatana na mkewe Mama Salma Kikwete ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mchinga.


Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mama Anna Mkapa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabuJaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa George Masaju akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tano Mama Janeth Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Katibu Mkuu Kiongozi Mheshimiwa Balozi Moses Kusiluka akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.


 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Geita imefanikiwa kuzuia upotevu wa zaidi ya Sh milioni 94.21 zilizokuwa zimefujwa kupitia miradi ya maendeleo na malipo haramu.

Akizungumza na waandishi wa habari kuelezea utendaji wa taasisi hiyo kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka (Oktoba hadi Desemba 2026), Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Geita, Alex Mpemba, ameanika madudu yaliyokuwa yakifanyika kwenye miradi ya maendeleo na mifumo ya bima ya afya.

Moja ya mafanikio makubwa yaliyotajwa ni kurejeshwa kwa kiasi cha Shilingi milioni 32 zilizokuwa zimeidhinishwa kimakosa kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). 

Mpemba amefafanua kuwa fedha hizo zilikuwa zikitumika kumpatia matibabu mtu asiyestahili baada ya mtuhumiwa mmoja (jina limehifadhiwa) kumuingiza mnufaika hewa kwenye mfumo huo kinyume cha sheria.

Vilevile, TAKUKURU imefanikiwa kurejesha Shilingi milioni 20 kwenye akaunti ya AMCOS IDOSELOMWALO. Fedha hizi ni sehemu ya mkopo mkubwa wa Shilingi milioni 245 uliotolewa na benki ya CRDB, ambapo usimamizi mbovu ulipelekea kusuasua kwa marejesho hayo mpaka taasisi hiyo ilipoingilia kati.

Katika hatua nyingine, uchunguzi wa TAKUKURU umebaini ujanja uliokuwa ukifanywa na wakusanya mapato wa halmashauri kwa kutumia mashine za kielektroniki za POS. Badala ya kuwasilisha fedha benki, baadhi ya watumishi wasio waaminifu walikuwa wakizifuja.

Kufuatia msako huo, kiasi cha Shilingi milioni 8.14 kimepelekwa kwenye akaunti ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Geita, huku Shilingi 154,100 zikipelekwa Nyang’hwale.

 Aidha, Halmashauri ya Chato imepata jumla ya Shilingi milioni 5.6 (kutoka TANROADS na RUWASA) kama kodi ya huduma (Service Levy) ambayo ilikuwa haijawasilishwa ipasavyo.

Katika barabara ya Nzera-Nkome, mkandarasi alijaribu kufanya ujanja kwa kutumia kifusi cha mfinyanzi badala ya moramu iliyopo kwenye mkataba (BoQ). TAKUKURU ilizuia malipo ya Shilingi milioni 25.2 mpaka mkandarasi huyo alipolazimika kurudia kazi hiyo kwa viwango vinavyotakiwa.

Hali kadhalika, kiasi cha Shilingi milioni 300 zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa kompyuta katika Kituo cha Afya Nyabirezi-Chato kimeokolewa. 

Hatua hii ilikuja baada ya kubainika kuwa kompyuta hizo hazikuwasilishwa kama ilivyopangwa, jambo lililopelekea fedha hizo kurejeshwa ili zitumike kama ilivyokusudiwa.

Dkt. Edith Rwiza Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akiongea na Wajumbe wa Baraza la Tatu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania wakati alipokuwa anazindua baraza hilo mjini Morogoro.

******************

Na Mwandishi wetu

MOROGORO: Watumishi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wameagizwa kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kushiriki kikamilifu katika mijadala ya kikazi, kutoa ushauri wenye tija na kuchangia mawazo yatakayochochea maboresho ya utendaji wa taasisi hiyo pamoja na Serikali kwa ujumla. Wito huo unalenga kuimarisha ushirikishwaji, uwajibikaji na kuongeza matokeo chanya katika sekta ya elimu nchini.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Edith Rwiza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Tatu la Wafanyakazi wa TEA uliofanyika mkoani Morogoro, ambapo alikuwa Mgeni Rasmi akimuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Rwiza alisisitiza kuwa TEA ina jukumu muhimu katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini ili kuhakikisha upatikanaji wa elimu bora kwa wote. Alieleza kuwa juhudi hizo zinaenda sambamba na utekelezaji wa mtaala mpya unaolenga kukuza umahiri, ubunifu na matumizi ya teknolojia, hivyo kuwahimiza watumishi kuwa wabunifu na wenye kujituma katika maeneo yao ya kazi.

Aidha, alibainisha kuwa kuundwa kwa Baraza la Wafanyakazi ni kielelezo cha ushirikiano mzuri kati ya Menejimenti ya TEA na chama cha wafanyakazi pamoja na uzingatiaji wa sheria za kazi. Alisisitiza kuwa, mabaraza ya wafanyakazi ni vyombo muhimu vya kisheria vinavyotoa fursa kwa watumishi kushiriki katika maamuzi ya kimkakati ya taasisi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TEA Dkt. Erasmus Kipesha akiwasilisha taarifa ya mamlaka mbele ya mgeni rasmi alisema kuwa, miongoni mwa majukumu ya Baraza hilo ni kushiriki katika maandalizi ya bajeti, kupokea na kuchambua taarifa za utekelezaji, pamoja na kutoa mapendekezo ya maboresho. Aliongeza kuwa hatua hiyo inasaidia kuwajengea watumishi uelewa mpana kuhusu mwelekeo wa taasisi.

Dkt. Kipesha alieleza kuwa, TEA imeendelea kupata mafanikio makubwa ikiwemo kuimarisha ushirikiano na wadau wa maendeleo. Katika miaka ya fedha 2023/2024 na 2024/2025, mamlaka imetekeleza miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 2.15 kwa kushirikiana na wadau wake UNICEF Tanzania, huku katika mwaka wa fedha 2025/2026 miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 8.37 ikiendelea kutekelezwa, hususan katika maeneo ya STEM (Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati).

Naye mjumbe kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu Taifa Dkt. Nickson Mkiramweni alisisitiza kuwa, jukumu la kuijenga taasisi ni la wafanyakazi wote hivyo kila mmoja anapaswa kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na uzalendo. Alipongeza utendaji wa Baraza la Wafanyakazi la TEA akibainisha kuwa, linaendeshwa kwa misingi ya demokrasia na uwazi hasa katika masuala yanayohusu shughuli za mamlaka hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Dkt. Erasmus Kipesha (Kushoto) akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Baraza la Tatu la wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, mjini Morogoro.Kulia ni Mgeni Rasmi Dkt. Edith Rwiza.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Tatu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania wakifuatilia hotuba kutoka kwa mgeni rasmi Dkt. Edith Rwiza (hayuko pichani) alipokuwa anazindua baraza hilo mkoani Morogoro.

Mjumbe kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu Taifa Dkt. Nickson Mkiramweni akitoa salamu kutoka makao makuu ya chama hicho wakati wa uzinduzi wa Baraza la Tatu la wafanyakazi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania, mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi Mamlaka ya Elimu Tanzania CPA. Mwanahamis Chambega akieleza jambo wakati wa uzinduzi wa Baraza la Tatu la wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, mjini Morogoro. Kushoto ni Mkaguzi wa Ndani CPA. Richard Mazinge






Dar es Salaam, Tanzania
 

Zaidi ya wanafunzi 62,000 kote Tanzania sasa wananufaika na majiko salama na safi zaidi kufuatia usakinishaji wa zaidi ya majiko ya kisasa 170 ya nishati safi ya kupikia katika shule na taasisi za umma zaidi ya 45. Hatua hii muhimu iliadhimishwa katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, ikionesha mchango wa mpango huu katika kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na hivyo kukabiliana na ukataji wa miti.

Mpango huu unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) kupitia programu ya CookFund.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba alisema:
“Mapinduzi haya kuelekea matumizi ya nishati safi ya kupikia ni kipaumbele cha kimkakati cha taifa kinachochangia kulinda mazingira, kuboresha afya ya umma na kuongeza ufanisi wa kiuchumi. Kwa kuzipatia shule na taasisi za umma teknolojia za kisasa za kupikia, tunalenga kulinda misitu yetu, kupunguza hewa chafuzi, na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa kuzingatia Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034).”

Jitihada za nishati safi ya kupikia nchini zinaongozwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wizara na taasisi nyingine za Serikali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, pamoja na taasisi nyingine za umma. Hadi sasa, msaada huu kwa taasisi za umma, hususan shule, unalenga taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa wakati mmoja ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Hatua hizi zinaendana na vipaumbele vya kitaifa vya kupunguza ukataji wa miti, kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma. Matumizi ya kuni na mkaa huzalisha chembechembe hatarishi zinazoweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya mfumo wa upumuaji kama pumu na saratani ya mapafu.

Kupitia programu ya CookFund, inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, hatua hizi zinalenga kupunguza matumizi ya nishati za kuni na mkaa kwenda kwenye teknolojia bora na zenye ufanisi zaidi kama majiko yanayotumia mkaa mbadala, majiko ya umeme (electric pressure cookers), biyoethano, majiko banifu, pamoja na gesi. Teknolojia hizi zinatarajiwa kupunguza shinikizo kwa rasilimali za misitu, kuboresha ubora wa hewa jikoni, na kuongeza afya na usalama wa wanafunzi na watumishi. Hadi sasa, taasisi 45 zimeboresha mifumo yao ya upishi, nyingi zikiwa ni shule za msingi na sekondari.

Aidha, kupitia CookFund, UNCDF inatoa msaada wa kifedha na kiufundi kwa makampuni na wajasiriamali wanaokidhi vigezo ili kuongeza usambazaji wa nishati safi ya kupikia. Msaada huu unajumuisha uwekezaji wa mtaji na mtaji wa uendeshaji kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa biashara zinazojihusisha na uzalishaji, uagizaji, usambazaji na uuzaji wa majiko, mafuta na bidhaa au huduma zinazohusiana na nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Marc Stalmans, alisema:
“Umoja wa Ulaya umejikita kikamilifu katika kuendeleza hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi duniani, na Tanzania siyo tofauti. Mpango huu ni sehemu ya juhudi zetu za kusaidia mpito kuelekea nishati safi. Kupitia msaada wa Umoja wa Ulaya, jamii zinazingatia mbinu endelevu zinazolinda mazingira, huku zikichochea ukuaji wa uchumi, kukuza ajira, na kuboresha upatikanaji wa nishati mashuleni, kwenye biashara pamoja na kaya.”

Naye Mshauri Mkuu Maswala Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, alibainisha kuwa pamoja na msaada uliotolewa kwa taasisi 45 katika wilaya 14 za Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma na Mwanza, programu hiyo imewekeza dola milioni 10.1 katika biashara ndogo na za kati 102.

“Nishati safi ya kupikia inapunguza utegemezi wa kuni na mkaa huku ikiboresha usalama, afya na ufanisi wa majiko shuleni,” alisema Bw. Malika. “CookFund inaonesha wazi kuwa teknolojia za kisasa za nishati zinaweza kuleta mageuzi makubwa katika taasisi za umma na kuboresha moja kwa moja mazingira ya kujifunzia kwa maelfu ya wanafunzi.”

Kwa ujumla, programu hii imeleta matokeo chanya na yenye mageuzi makubwa, ikichangia uundaji wa ajira 27,005 (za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja), jumla ya biashara 4,933 katika mnyororo wa thamani wa nishati safi ya kupikia, kufikia kaya zaidi ya 482,089, na kupunguza zaidi ya tani 3,911,450 za uzalishaji wa hewa ukaa. Mafanikio haya yanaonesha mchango mkubwa wa programu hii katika maendeleo endelevu, ustawi wa jamii na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania.Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa pili kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, akitoa hotuba yake wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni.Mkuu wa Ushirikiano wa Ujumbe wa EU nchini Tanzania, Bw. Marc Stalmans, akihutubia hadhira wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan shule. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa tatu kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (kushoto), anapika wali akitumia jiko linalotumia nishati salama ya kupikia, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na kwa usimamizi wa programu kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuendeleza Mitaji (UNCDF), inatekeleza Mpango wa CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito cha matumizi ya upishi safi katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Kutoka kulia ni Bw. Marc Stalmans, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Tanzania, akiwa pamoja na Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika.


Top News