Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunga mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.
...
Waandaji wa ratiba za masomo nchini wamehimiza umuhimu wa kuandaa na kuzingatia ratiba zenye uwiano sahihi kati ya masomo ya nadharia na vitendo, wakisema hatua hiyo ni muhimu katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi stahiki, wenye tija kazini na wanaochangia maendeleo ya Taifa.
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,wakati akifungua mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.
Dkt. Nchimbi amesema kuwa ratiba ya masomo siyo tu mpangilio wa vipindi darasani, bali ni nyenzo muhimu inayochangia moja kwa moja ubora wa elimu na uwezo wa wahitimu kuhimili ushindani katika soko la ajira
"Ili kupata matokeo chanya, ni lazima ratiba zizingatie kwa uzito sawa masomo ya kinadharia na mafunzo ya vitendo, ambayo ndiyo yanawajengea wanafunzi ujuzi halisi unaohitajika kazini."amesema Dkt.Nchimbi
Aidha, ameeleza kuwa ratiba bora zinapaswa pia kuzingatia shughuli nyingine muhimu zinazochangia malezi na makuzi ya mwanafunzi, ikiwemo michezo, ubunifu na maendeleo ya vipaji, ili kuandaa wahitimu waliokamilika katika nyanja zote.
“Hatupaswi kuangalia masomo pekee, bali pia tunapaswa kuandaa mazingira yanayomjenga mwanafunzi kitaaluma, kijamii na kimaadili,” amesisitiza.
Aidha amesema hivi sasa kuwekuwepo na kilio kikubwa kutoka kwa ajiri kuwa wahitimu wanaomba ajira katika taasisi zao wengi wao hawana ujuzi hivyo kushindwa kukidhi mahitaji yao.
“Kumekuwapo na kilio kutoka kwa ajiri wengi kuwa vyuo vyetu vinatoa wahitimu wasiokuwa na ujuzi lakini hii inaanzia kwenye sula la uandaji wa ratiba za masomo ambao hauzingatii wanafunzi kujifunza kwa vitendo.
“Hivyo basi kama tunatakaa kutoka hapa tulipo, lazima kuanza kuweka mkazo kwenye uandaaji wa ratiba za masomo ambazo zinazaingatia kujifunza kwa nadharia na vitendo ili kupata mahitimu watakao kidhi mahitaji ya soko la ajira na kuondoa malalamiko yaliyopo hivi sasa,”amesema
Amesema, ratiba ni nyenzo muhimu katika kuboresha ufundishaji kwakuwa inaweza kuwa msaada katika kudhibiti matumizki ya fedha na rasimali watu zilizopo.
“Kama unakuwa na ratiba nzuri unaweza kudhibiti matumizi ya fedha na rasamalli watu iliyopo ikatumika kikamilifu kuhudumia idadi kubwa ya watu,”amesema
Amesema kuwa yapo maeneo ambayo yamekuwa na malalamiko ya vipindi kugongana ama wanafunzi kukosa muda wa kushiriki mambo mengine kutokana na upangaji mbovu wa ratiba.
Kuhusu mafunzo hayo amesema kuwa lengo ni kuwajengea uwezo waandaji wa ratiba katika taasisi elimu nchini ili kuboresha utendaji kazi wao na kusaidia kupata mahitimu wenye ujuzi.
“Mafunzo haya tulianza kwa mara ya kwanza mwaka 2022, ambapo tuliona ipo haja kuwa na mafunzo kama ilivyo kwa tasnia nyingine, kwani kazi yetu inachangamoto nyingi sana hivyo ni vizuri tukutane na kuongezeana maalifa ili kuboresha upangaji wa ratiba katika taasisi zetu za elimu,”amesema
Kwa upande wake Mratibu wa mafunzo hayo Vicktoria Kessy, amesema kuwa moja ya lengo la mafunzo hayo ni kusaidia kupunguza malalamiko ya wajiri kupata wahitimu wasiokuwa na ujuzi.
“Tunawafundisha wataalam hawa wa uandaaji wa ratiba za masomo katika taasisi za elimu nchini ili kuboresha upangaji wa ratiba unaozingatia uwepo wa mafunzo ya nadharia na vitendo ili kutoa wahitimu wenye ujuzi tofauti na ilivyo sasa,”amesema
Naye Katibu wa Jukwaa hilo, Deusdedith Youze, amesema kuwa hivi sasa serikali imefanya marekebisho ya mitaala ya elimu ili kuwezesha wanafunzi kupata mafunzo ya amali hivyo suala la ratiba inayozingatia mafunzo kwa vitendo ni muhimu.
“Tunashukuru tumepata washiriki kutoka katika vyuo Zaidi ya 15 ambao wanahusika katika uandaaji wa ratiba za masomo lengo ni kuwaongezea mbinu ambazo zitawasaidia kuaandaa ratiba ikiwamo matumizi ya teknolojia za kisasa,”amesema

Mwenyekiti Mtendaji wa Jukwaa la Waratibu wa Ratiba za Elimu na Mafunzo Tanzania, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Alfred John Nchimbi,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.

Mratibu wa mafunzo Bi.Vicktoria Kessy,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungwa kwa mafunzo maalum kwa waandaji wa ratiba kutoka taasisi mbalimbali za elimu yaliyofanyika jijini Dodoma.





.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)



.jpeg)










.jpeg)



