Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kusogeza nishati safi ya kupikia kwa wananchi baada ya kuzindua duka maalum la kuuza mitungi ya gesi ya Oryx na majiko yake katika Wilaya ya Chato mkoani Geita.

Uzinduzi huo umefanyikq eneo la Kabwanga wilayani Chato na kuhudhuriwa na wadau wa nishati safi akiwemo mgeni rasmi ambaye ni Ofisa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Nishati na Maji(EWURA) Mkoa wa Geita Bwanawadi Omari pamoja na wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Ofisa Huduma kwa Wateja EWERA Mkoa wa Geita Bwanawadi Omar amesema hatua hiyo ni muhimu katika kupunguza utegemezi wa nishati zisizo rafiki kwa mazingira kama kuni na mkaa ambazo zimekuwa zikichangia uharibifu wa misitu na athari nyingine za kiafya kwa wananchi hasa Wanawake na watoto.

“Watalaam wanatuambia ili kupata mkaa itabidi mti ambao utautumia kwa ajili ya kutengeneza mkaa inabidi uusubiri kwa miaka mitano na inategemea kati ya mti mmoja kwenda mti mwingine lakini tunaposema nishati safi ya kupikia tunamaanisha teknolojia ambayo ni rafiki wa mazingira.

“Pia ni gharama nafuu kwa namna moja ama nyingine lakini pia hazalishi sumu yaani kwa mfano sumu inayoweza kuzalishwa kutokana na mkaa ni nyingi zaidi wakati nishati safi ya kupikia haina sumu.Tunakumbuka miaka ya nyuma bibi zetu na mama zetu waliotumia kuni na mkaa kwa muda mrefu walikuwa na macho mekundu na kuwaita wachawi.”

Amesema uamuzi wa Oryx Gas kuweka duka la kuuza mitungi ya gesi ni hatua nzuri na ya kupongezwa kwani wananchi watapata nishati safi ya kupikia katika maeneo yao huku akisisitiza kupika kwa nishati safi ni rafiki wa mazingira.

Awali Meneja Mauzo wa Oryx Gas Tanzania Alex Wambi amesema uzinduzi wa duka hiyo wilayani Chato ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuunga mkono jitihada za Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

“Oryx Gas katika Mkoa huu wa Geita tunayo maduka 11 na tutaendelea kufungua maduka mengine zaidi kwani tunatamani mpaka mwaka unaisha tuwe na maduka yasiyopungua 20.Tunafanya hivi ili kushiriki kikamilifu sera hii ya nishati safi inafanikiwa.

“Ndio maana tunakuja na mpango wa mkakati wa kusogeza huduma kwa wateja wetu kwa kupitia maduka haya ambapo tunalenga pia kusogeza huduma kwa wananchi kupata mtungi wa gesi hasa ile ambayo ni ya bei rahisi kupitia maduka yetu,”amesema Wambi na kuongeza maduka hayo yanatumika kutoa elimu ya matumizi sahihi ya nishati safi ya kupikia.

Aidha amesisitiza mpango mkakati wa Oryx Gas kwa sasa ni kuhakikisha kila Mwananchi katika maeneo yote anatumia nishati safi ya kupikia na ndio maaana wameamua kuwa na maduka ya kuuza gesi hata maeneo ya pembezoni ili Mwananchi apate gesi kirahisi.


























Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imepitisha Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa mwaka wa fedha 2026/2027 inayolenga kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zitakazochochea ukuaji wa Uchumi wa Kidijitali.

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Kamati, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) aliiomba Kamati kuidhinisha matumizi ya Shilingi 222, 589,452,000/- huku akitaja vipaumbele saba (7) vya Bajeti hiyo kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 kuwa ni pamoja na Kutunga, Kuhuisha na kusimamia utekelezaji wa Miongozo inayosimamia Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, na Kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano ya Simu na Posta kote Nchini.

Vipaumbele vingine ni pamoja na Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kukuza na kuimarisha Biashara Mtandao Nchini, Kuimarisha miundombinu itakayowezesha utekelezaji wa Uchumi wa Kidijitali, Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Anga ya Mtandao, Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kuchochea ubunifu na kuimarisha ustawi wa Kampuni Changa za TEHAMA (ICT Startups), na Kuimarisha utekelezaji wa Programu ya Anga za Juu.

Akizungumza wakati wa Kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe, Selemani Kakoso ameipongeza Wizara kwa usimamizi mzuri wa Taasisi zilizo chini yake hali iliyopelekea Taasisi hizo kutoa Huduma za Mawasiliano zilizo bora na za Uhakika kwa Wananchi.

Mhe. Kakoso ameitaka Serikali kuendelea kuzisimamia Taasisi hizo huku akisisitiza kuongeza kasi ya uwekezaji katika Kituo cha Kuhifadhia Data (Data Centre), Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kuliwezesha Shirika la Posta Tanzania na kuhakikisha miradi yote inayosimamiwa na wizara inakamilika kwa wakati.

Naye Waziri Kairuki aliishukuru kamati kwa ushirikiano na ushauri wake uliowezesha kuiongoza Wizara kuongeza kasi ya kutekeleza majukumu yake ya kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini.





Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imepitisha Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa mwaka wa fedha 2026/2027 inayolenga kuongeza kasi ya utoaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zitakazochochea ukuaji wa Uchumi wa Kidijitali.   

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Kamati, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb) aliiomba Kamati kuidhinisha matumizi ya Shilingi 222, 589,452,000/- huku akitaja vipaumbele saba (7) vya Bajeti hiyo kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 kuwa ni pamoja na Kutunga, Kuhuisha na kusimamia utekelezaji wa Miongozo inayosimamia Sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, na Kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano ya Simu na Posta kote Nchini.

Vipaumbele vingine ni pamoja na Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kukuza na kuimarisha Biashara Mtandao Nchini, Kuimarisha miundombinu itakayowezesha utekelezaji wa Uchumi wa Kidijitali, Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Anga ya Mtandao, Kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kuchochea ubunifu na kuimarisha ustawi wa Kampuni Changa za TEHAMA (ICT Startups), na Kuimarisha utekelezaji wa Programu ya Anga za Juu. 

Akizungumza wakati wa Kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe, Selemani Kakoso ameipongeza Wizara kwa usimamizi mzuri wa Taasisi zilizo chini yake hali iliyopelekea Taasisi hizo kutoa Huduma za Mawasiliano zilizo bora na za Uhakika kwa Wananchi. 

Mhe. Kakoso ameitaka Serikali kuendelea kuzisimamia Taasisi hizo huku akisisitiza kuongeza kasi ya uwekezaji katika Kituo cha Kuhifadhia Data (Data Centre), Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, kuliwezesha Shirika la Posta Tanzania na kuhakikisha miradi yote inayosimamiwa na wizara inakamilika kwa wakati.

Naye Waziri Kairuki aliishukuru kamati kwa ushirikiano na ushauri wake uliowezesha kuiongoza Wizara kuongeza kasi ya kutekeleza majukumu yake ya kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa Huduma za Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini.





Mkuu wa Wilaya ya Rorya Dkt. Khalfany Haule  akizungumza na maafisa wa TASAC waliotembelea Ofisi ya Mkoa wa Mara hawapo pichani.
Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija akitoa elimu ya usalama majinI kwa   Wavuvi wa Wilaya ya Rorya.


*Jaketi Okozi ni Uhai na sio mzigo kwa msafirishaji

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Wilaya ya Rorya imetoa wito kwa wavuvi na wamiliki wa mitumbwi kuacha kupuuza matumizi ya vifaa vya kuokoa maisha majini.

Hayo ameyasema Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Mhe. Dkt. Khalfany Haule wakati maafisa Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC) walipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kutoa elimu ya Usalama wa vyombo vya majini.

Dkt. Haule alionya dhidi ya mtazamo potofu kwamba maboya ni mzigo wa gharama na kikwazo cha kazi ya uvuvi

Amesema kwa takwimu za mwaka uliopita, zaidi ya wavuvi 20 walipoteza maisha kutokana na mitumbwi kuzama, licha ya kuwa na maboya ndani ya vyombo lakini bila kuyavaa.

"Kupoteza maisha ni pigo kubwa kwa familia na inapunguza nguvu kazi ya taifa” amesema Mhe.Dkt.Haule

Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija, aliongeza kuwa wavuvi wengi hujiamini kupita kiasi kwa kudhani ujuzi wa kuogelea unatosha, jambo linalowaweka hatarini. Kwa sasa ni msimu wa upepo mkali, mawimbi makubwa na mvua zinazoendelea kunyesha zimeongeza hatari ya ajali majini.

Kwa kukabiliana na hilo, TASAC imeanzisha kampeni ya kutoa elimu kwa wamiliki wa vyombo vidogo, wavuvi, vyama vya wamiliki na wananchi ili kuondoa mitazamo potofu, tabia ya kupuuza na kuimarisha usalama wa usafiri majini.

Mhandisi Lusangija aliongeza kuwa wavuvi na wasafirishaji wajenge utamaduni wa kufuatilia utabili wa hali hewa kuliko kutumia utaalam wa asili, watumie mialo rasmi na kuwa na maboya.

Hata hivyo, baadhi ya wamiliki wa mitumbwi, akiwemo Hamza Kisuki, wamelalamikia tabia ya wavuvi kuvua maboya mara wanapofika majini na kuyageuza kuwa mito ya kulalia, wakijiamini kuwa uwezowao wa kuogelea unatosha.

Elimu hii imeanza kutolewa katika mwalo wa Esegere na Nyang’ombe, na itaendelea katika mialo ya Kinesi, Sota, Luhu, Busanga na Kilongwe. Walengwa ni viongozi wa Serikali za Mitaa, BMU, wavuvi, wamiliki wa mitumbwi na wananchi kwa ujumla.
Afisa Mfawidhi wa TASAC mkoa wa Mara Mhandisi Hezron Lusangija akitoa elimu kwa mvuvi namna ya kuvaa jaketi Okozi wakati wa dharula ya hatari.
Wavuvi na wamiliki wa Mitumbwi wakipata elimu ya usalama majini kutoka kwa maafisa wa TASAC hawapo pichani.




Na Elimu ya Afya kwa Umma
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imewahimiza Watanzania kurejea katika matumizi ya vyakula vya asili kama sehemu muhimu ya kujenga afya bora, kuzuia magonjwa, na kusaidia matibabu kwa njia salama na endelevu.

Akizungumza jijini Dodoma katika Mkutano wa Waziri wa Afya na wataalam wa tiba asili, Mkurugenzi wa Huduma za Uhamasishaji wa Afya (Elimu ya Afya kwa Umma), Dkt. Rahma Ahmed Hingora, amesema vyakula vya asili vina mchango mkubwa katika kuimarisha afya ya mwili na vinaweza kutumika kama sehemu ya kinga na tiba iwapo vitatumika kwa usahihi.

“Tunapaswa kurudisha utamaduni wa kula vyakula vya asili kama maboga, ubuyu na vyakula vingine vinavyopatikana katika mazingira yetu. Hivi ni vyakula vyenye virutubishi muhimu vinavyosaidia kuimarisha kinga ya mwili na afya kwa ujumla,” amesema Dkt. Hingora.

Amebainisha kuwa kumekuwa na mabadiliko ya mtindo wa maisha ambapo jamii imekuwa ikipuuza vyakula vya asili na kuelekea zaidi katika matumizi ya vyakula vilivyosindikwa, ambavyo mara nyingi hupoteza virutubisho muhimu na vinaweza kuongeza hatari ya magonjwa yasiyoambukiza.

“Ni muhimu kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya kemikali na virutubisho bandia kwenye vyakula. Turejee kula vyakula katika hali yake ya asili. Kula chakula kama dawa, na usisubiri kula dawa kama chakula,” amesisitiza.

Aidha, Dkt. Hingora amesema Serikali itaendelea kuimarisha utoaji wa elimu ya afya kwa wananchi kupitia vyombo mbalimbali vya habari, majukwaa ya kidijitali, pamoja na Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii, ili kuhakikisha jamii inapata uelewa sahihi kuhusu lishe bora na matumizi salama ya vyakula vya asili.

Katika mkutano huo, Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, alisisitiza umuhimu wa kuunganisha maarifa ya tiba asili na tiba ya kisasa, huku akihimiza wataalam kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa jamii kuhusu mchango wa vyakula vya asili katika afya.

Serikali inaamini kuwa matumizi sahihi ya vyakula vya asili yanaweza kusaidia kupunguza hatari ya magonjwa, kuimarisha kinga ya mwili, na kuchangia ustawi wa afya ya wananchi kwa ujumla.

 
Waziri wa Fedha wa Tanzania, Khamis Mussa Omar umza wakati wa mkutano huo uliofanyika leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam wakati kujadiliana juu ya uwekezaji na biashara yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 7.8 nchini Tanzania katika mkutano wa Bodi ya taasisi hiyo.



Na Mwandishi Wetu

AFRICAN Trade & Investment Development Insurance (ATIDI) imejadili uwekezaji na biashara yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 7.8 nchini Tanzania katika mkutano wa Bodi ya taasisi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam, hatua inayolenga kuimarisha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji wenye mitaji mikubwa.

Akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika leo Machi 26, 2026 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha wa Tanzania, Khamis Mussa Omar amesema kufungua uwezo kamili wa uchumi wa Tanzania kunahitaji ushirikiano imara unaoweza kuhamasisha mitaji mikubwa ya uwekezaji.

Amesema ATIDI imekuwa mshirika muhimu katika kupunguza hatari za uwekezaji, hali inayosaidia kuvutia mitaji ya sekta binafsi na kuwezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.

Pembeni mwa mkutano huo, uongozi wa ATIDI ulikutana na maafisa wa serikali, taasisi za kifedha, washirika wa maendeleo pamoja na wadau wa sekta binafsi kujadili namna ya kuimarisha zaidi mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Majadiliano hayo yaliambatana na warsha ya wadau wa ngazi ya juu iliyopewa jina la “Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji Tanzania,” iliyolenga kuboresha mfumo wa kifedha na kuongeza upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Washiriki wa mkutano huo walisisitiza umuhimu wa kupata suluhisho la pamoja katika kuongeza mtiririko wa mitaji kutoka sekta binafsi ili kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa gharama nafuu katika sekta muhimu za uchumi na kukuza biashara za kikanda.

Tanzania ina nafasi ya kipekee katika historia ya ATIDI ikiwa ni miongoni mwa nchi wanachama waanzilishi tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo mwaka 2001 kwa msaada wa Common Market for Eastern and Southern Africa (COMESA) na World Bank.

Kwa mujibu wa takwimu za taasisi hiyo, kwa kipindi cha miaka 25 iliyopita ATIDI imewezesha uwekezaji na biashara za mipakani barani Afrika zenye thamani ya zaidi ya dola za Marekani bilioni 93 kupitia huduma zake za bima ya mikopo ya biashara na uwekezaji.

Nchini Tanzania pekee, taasisi hiyo imesaidia zaidi ya sera 200 za bima, hatua iliyowezesha biashara na uwekezaji wenye thamani ya dola bilioni 7.8 huku kiwango cha hatari kinachodhibitiwa kikiwa karibu dola bilioni 1.8.

Uwekezaji huo umeelekezwa katika sekta muhimu za maendeleo ikiwemo miundombinu, nishati, mawasiliano na makazi nafuu.

Miongoni mwa miradi mikubwa iliyoungwa mkono ni reli ya kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) Tanzania ambayo imeendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha biashara na usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa ATIDI, Manuel Moses amesema changamoto kubwa kwa Afrika si ukosefu wa fursa bali ni hatari zinazohusiana na uwekezaji.

Naye Mtaalamu Mkazi wa Bima wa ATIDI, Tusekile Kibonde amesema taasisi hiyo inaendelea kutoa suluhisho za kupunguza hatari zinazowezesha upatikanaji wa fedha kwa miradi mikubwa barani Afrika huku akibainisha kuwa ushirikiano huo unasaidia kubadilisha fursa za uwekezaji kuwa ukuaji endelevu wa uchumi.







Top News