Waziri Katambi amezindua Programu hiyo leo,jijini Dar es Salam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo akizungumza na mamia ya wafanyabiashara,machinga,madereva bodaboda,mamalishe na babalishe amesema suala la amani na usalama ni jukumu la kikatiba la serikali iliyochaguliwa na wananchi.
Amesisitiza kuwa kipaumbele cha Rais Samia ni Nchi Kwanza, Wananchi kwanza na Uchumi kwanza.
“Wizara hii ina dhamana ya masuala ya Ulinzi na Usalama, ina dhamana ya ulinzi wa kila raia, ina dhamana ya ulinzi wa kila mali ya raia, ina dhamana ya ulinzi wa Rasilimali za Taifa pamoja na mali za Taifa zinazomilikiwa na Umma" alisema Katambi
“Taarifa yoyote,maelezo yoyote,kauli yoyote,uchochezi wa aina yoyote unaolenga kuhatarisha amani ya mtu mmoja ambae ni raia wa Tanzania,sisi kama Serikali kwa mujibu wa katiba ya mwaka 1977 Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao na rasilimali za nchi ni jukumu la Serikali kwa kuhakikisha wananchi wanakua salama kwenye mazingira ya uzalishaji na shughuli za maendeleo”aliongeza Waziri Katambi
Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa wafanyabiashara,bodaboda,machinga,babalishe na mamalishe walisema wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwawekea mazingira sahihi ya kufanya shughuli zao huku wakiweka wazi nia yao ya kutotumika na kikundi cha watu wachache wanaotaka kuchafua amani ya nchi.
Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Ayoub Mohammed Mahmoud,Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Edward Mpogolo,Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,SACP William Mkonda,Viongozi wa Wafanyabiashara,Bodaboda,Wamachinga,Mamalishe na Babalishe pamoja na wananchi.










.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)




















.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)




