Arusha, Tanzania, Juni 27, 2026 – Maadhimisho ya Siku ya Bima yamehitimishwa kwa mafanikio kupitia mashindano ya gofu ya ICEA LION King of the Course, yaliyowakutanisha wataalamu wa sekta ya bima, viongozi wa biashara na wadau mbalimbali kwa siku ya ushindani, kujenga mahusiano na kubadilishana uzoefu.
Mashindano hayo, yaliyodhaminiwa na ICEA LION General Insurance, yalidhihirisha dhamira ya kampuni hiyo ya kuendelea kuunga mkono mipango inayokuza ushirikiano ndani ya sekta ya bima huku yakihamasisha ushindani wenye tija na kuimarisha mahusiano ya kitaaluma.
Karim Jamal aliibuka mshindi wa jumla na kutwaa taji la King of the Course (Mfalme wa Uwanja). Kutokana na ushindi huo, amejishindia safari yenye udhamini kamili ya kuiwakilisha Tanzania katika fainali za King of the Course, zitakazofanyika Mombasa, Kenya, mwezi Oktoba mwaka huu. Aidha, alikabidhiwa zawadi mbalimbali wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo.
Mashindano hayo yalihudhuriwa na viongozi wa ICEA LION Group, viongozi wa Taasisi ya Bima Tanzania (Insurance Institute of Tanzania – IIT) pamoja na wadau wengine kutoka sekta ya bima, wakionesha mshikamano na dhamira ya pamoja ya kuendeleza sekta hiyo nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Jared Awando, Mtendaji Mkuu wa ICEA LION General Insurance Tanzania, alisema kampuni hiyo itaendelea kuunga mkono mipango inayojenga ushirikiano na kuimarisha maendeleo ya sekta ya bima.
"Katika ICEA LION tunaamini kuwa mahusiano imara ni msingi wa kujenga sekta ya bima yenye uimara na uwezo wa kukidhi mahitaji ya wateja. Tunajivunia kuunga mkono mipango inayowaleta pamoja wataalamu wa sekta hii huku tukisherehekea ubora ndani na nje ya uwanja wa gofu," alisema.
Mashindano hayo yalihitimisha rasmi maadhimisho ya Siku ya Bima mwaka huu, yakionesha dhamira ya wadau wa sekta hiyo ya kuimarisha ushirikiano, taaluma na kuongeza uelewa wa umma kuhusu umuhimu wa bima katika kukuza ustahimilivu wa kiuchumi.
Kuhusu ICEA LION General Insurance
ICEA LION General Insurance imekuwa ikitoa huduma za bima nchini Tanzania tangu mwaka 1999. Kampuni hiyo hutoa huduma mbalimbali za bima, ikiwemo bima za magari, afya, mali na biashara, kwa lengo la kuwasaidia watu binafsi na taasisi kulinda mali na shughuli zao dhidi ya hatari mbalimbali.
Ikiendeshwa chini ya ahadi yake ya chapa ya Simba wa Bima, ICEA LION imejizatiti kutoa huduma za bima zenye ubunifu na zinazotegemewa, zinazowapa wateja ujasiri wa kusonga mbele kwa kujiamini. Kama sehemu ya ICEA LION Group, mojawapo ya makundi yanayoongoza kwa huduma za kifedha Afrika Mashariki, kampuni hiyo inaendelea kuhamasisha matumizi ya bima na kuimarisha ustahimilivu wa kifedha nchini Tanzania.
Bw. Jared Awando (wa tatu kutoka kushoto), Mtendaji Mkuu wa ICEA LION General Insurance Tanzania, akiwa pamoja na washindi wa mashindano ya gofu ya ICEA LION King of the Course na viongozi wa ICEA LION Group mara baada ya hafla ya utoaji wa tuzo iliyofanyika jijini Arusha. Mashindano hayo, yaliyofanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Bima, yalimshuhudia Karim Jamal akitwaa ubingwa wa jumla na kujishindia safari yenye udhamini kamili ya kuiwakilisha Tanzania katika fainali za King of the Course zitakazofanyika Mombasa, Kenya, mwezi Oktoba mwaka huu, pamoja na zawadi nyingine mbalimbali.


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

















































