Na MWANDISHI WETU
MKUU wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, ametangaza operesheni kali dhidi ya wanaojihusisha na uvujaji wa mapato wilayani humo na kumwagiza Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Aidan Kitare, kuivunja Kikosi Kazi cha Mapato (KKM) kinacho husika na usimamizi wa mapato.
Aidha ametoa onya kali kwa baadhi ya madiwani watakao jaribu kulalamika baada ya kuondolewa au jamaa zao kuondolewa katika kamati hiyo kutokana na kubainika kushiriki katika kuhujumu mapato.Magoti, aliyasema hayo alipohutubia kikao cha Baraza la Madiwani la Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani.
Ameeleza kusikitishwa na uvujaji mkubwa wa mapato katika wilaya hiyo hali inayo kwamisha maendeleo."Watu wana kula kwelikweli. Wanakula vibaya mno halafu wanalalamika. Nataka niwaambie tumefahamiana kwa sababu ya kazi, tofauti na kazi sina udugu nanyie. Tufanye kazi , tumsaidie Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kutekeleza majukumu,"amesema Magoti.
Amesema, dhamira ni kujenga Kisarawe inayo heshimu mali na mapato ya serikali ambapo kama mianya ya uvujaji wa mapato itadhibitiwa wilaya hiyo inaweza kukusanya sh.bilioni 7 tofauti na sh. bilioni 4 inazo kusanya sasa.
"Unakwenda sehemu unakuta waliumu wana kaa chini. Hawana ofisi. Hii ni aibu. Mapato yanaliwa na watu wachache,"amebainisha Magoti.
Amesema ana faili maalumu la wahusika wanao jihusisha kuhujumu mapato pamoja na maeneo yote yanayo tumika."Ninafaili hili hapa. Wahusika wote wanaohujumu mapato. Diwani ukiwa na malalamiko yoyote fika ofisini kwa Mwenyekiti wa Halmashauri au kwa mkurugenzi akulete kwa mkuu wa wilaya na ukibainika unahusika au ndugu yako unaye mtetea anahusika tukakupa ushahidi tutakuchukulia hatua,"amedai Magoti.
Amesema anataarifa za kila mtu aliyeondolewa katika Kikosi Kazi cha Mapato ya halmashauri hiyo kupitia faili maalumu la wahujumu wa mapato.
"Diwani yoyote anaye jua kwamba ndugu yake alikula mapato taarifa zake ninazo humu katika falili.Diwani yoyote atakaye piga kelele nitamkamata,"ameonya Magoti.
Ameeleza, diwani kuwa na ndugu anaye kusanya mapato siyo dhabi bali dhambi ni kumtumia ndugu yake huyo kujipatia mapato na kuibia halmashauri.
"Kwa Mamlaka niliyo nayo ninakuelekeza mkurugenzi kuvunja kikosi hicho hadi kufikia pia ukae na Kamati ya Usalama ya wilaya kuunda kikosi kipya,"amesema
Magoto amesema kikosi hicho kikundwa kikiundwa, kipewe semina na kiingie kazini kutekeleza majukumu ya kukusanya mapato.
Aliongeza; "Na hiki mkurugenzi ndiyo kipimo chako cha kwanza cha kujua unatosha ama utoshoshi. Mimi ndiyo nina vyombo. Hakuna mtu yoyote mwenye vyombo katika wilaya hii. Mkurugenzi usiogope. Mimi ndiyo naweza kusema uwepo au usiwepo kwa hiyo fanya kazi,".
Aidha ameelekeza polisi wilayani humo kumsakama mmiliki mmoja wa jengo la ghorofa jirani na ofisi za halmashauri hiyo ambalo alisema lina husika katika vitendo vya kuhujumu mapato.
"Kuna kijengo cha ghorofa jirani na hapa halmashauri. Mwiteni mmiliki anieleze shughuli zinazofanyika pale hadi saa saba usiku na kuanza kesho usiku (leo) wote watao kuwa pale wakamatwe,"amesema.Ameeleza mmiliki wa jengo hilo ambaye ni mwanamke afikishwe mbele yake kabla ya saa 9:00 alasili jana kujieleza.
Katika hatua nyingine, Magoti alitangaza kufanya operesheni ya kuvunja nyumba zilizojengwa kinyume cha sheria katika eneo la serikali la Homboza na kwamba katika operesheni hiyo aliyo ibatiza jina la Kanyamazongo atawatia mbaloni mabalozi saba wanaopinga jitihada za serikali.
"Hatuhitaji watu wanao hujumu serikali.Pale halmashauri itaingiza shilingi bilioni 5.8. Kuna shule imejengwa pale halmashauri ili nunua eneo lake yenyewe.Ni vitu vya ajabu sana,"amesema .
Aidha Magoti alitaja vizuizi vinavyoongoza kwa kuiba mapato wilayani humo na kuyatorosha kuwa ni Homboza, Kwa Pinda, Kiluvya Kisokwa, Ikuruwi, Kauzeni, Msanga na Masaki.
" Kuna watu wanachukua fedha taslimu pale.Tunaorodha yao humu katika faili. Tutakamata baiskeli, pikipi, magari na kila muhusika,"ameeleza Magoti.
Kuhusu watu wanaouza kiholela maeneo hususan katika eneo la Cha Kenge, Magoti amesema Operesheni Kanyazongo itamkumba kila muhusika.
"Madiwani niwaombe nyie ndiyo viongozi wa kamati za maendeleo za kata kwa hiyo kama eneo lako linauza viwanja kinyume cha utaratibu tutakuhoji,"amesema

