Na Janeth Raphael MichuziTv 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amesema maridhiano ya kisiasa hayapaswi kutafsiriwa kama udhaifu, bali ni ishara ya ukomavu wa kisiasa unaoweka msingi imara wa umoja, amani na kuheshimiana katika jamii.

Akihutubia katika hafla ya utiaji saini wa Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar iliyofanyika visiwani Zanzibar leo, Alhamisi Julai 9, 2026, Rais Samia alisema viongozi wanaweza kuwa na mitazamo tofauti, lakini wakaunganishwa na dhamira ya kulinda maslahi ya taifa na ustawi wa wananchi.

Ameeleza kuwa maridhiano yanaonyesha uwezo wa viongozi kujadili hoja zinazowatofautisha kwa hekima, huku wakikubaliana katika masuala ya msingi yanayohusu uongozi na maendeleo ya nchi.

Rais Samia alisema hatua hiyo inafungua ukurasa mpya wa kuimarisha umoja, mshikamano, utulivu na amani kwa wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla, akisisitiza kuwa jitihada hizo zinapaswa kuendelezwa na kuenziwa.

“Hakika jitihada hizi zinahitaji kuendelezwa na kuenziwa. Nimesema jambo hili la kiungwana kwa kuwa uungwana unatufunza siasa za kushindana kwa hekima na si kwa kupaza sauti bila mantiki,” amesema Rais Samia.

Aidha, ametoa wito kwa viongozi na wadau wa siasa kuendelea kujenga utamaduni wa mazungumzo, kuheshimiana na kuweka mbele maslahi ya taifa ili kudumisha amani na kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya uwasilishaji wa Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar tarehe 09 Julai, 2026.







Na Mwandishi Wetu
USHIRIKIANO kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Japani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japani (JICA) umefungua fursa mpya za maendeleo katika sekta ya kilimo baada ya kutolewa kwa mkopo wa masharti nafuu wenye thamani ya zaidi ya Shilingi trilioni 3.5 kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB).

Fedha hizo zinatolewa kupitia Wizara ya Fedha chini ya mradi wa Two Step Loan, unaolenga kuongeza upatikanaji wa mitaji kwa sekta ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima binafsi, vikundi vya wakulima pamoja na wakulima wadogo na wa kati kupata mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kuongeza uwekezaji na uzalishaji.

Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa Biashara wa TADB anayesimamia miradi ya benki hiyo, Elias Misana, alisema mradi huo unalenga kuchochea ukuaji wa sekta ya kilimo kupitia ufadhili wa mazao matano ya kimkakati ambayo ni mahindi, mpunga, ngano, alizeti na mazao ya bustani.

Alieleza kuwa kupitia mpango huo, mkulima mmoja mmoja ataweza kupata mkopo wa hadi Shilingi milioni 200, huku vikundi vya wakulima na kampuni zinazojihusisha na shughuli za kilimo zikiweza kukopa hadi Shilingi bilioni tatu kwa masharti nafuu.

Misana alisema mpango huo pia umeweka kipaumbele kwa wanawake na vijana wanaojishughulisha na kilimo cha bustani, ambao watanufaika na viwango vya chini vya riba pamoja na muda mrefu na rafiki wa marejesho ya mikopo.

Kwa upande wake, Mratibu Mkuu wa JICA, Veronica Barua, alisema mradi wa Two Step Loan ni matokeo ya ushirikiano wa muda mrefu kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Japani unaolenga kuwawezesha wakulima wadogo na wa kati kupata mitaji ya uwekezaji, hususan wale waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya kupata mikopo kutoka taasisi za kifedha.

Alisema upatikanaji wa mitaji hiyo unatarajiwa kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao, kuboresha kipato cha wakulima na kuimarisha mchango wa sekta ya kilimo katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Mradi wa Two Step Loan ulianza kutekelezwa rasmi mwezi Juni mwaka 2025 na unatarajiwa kuendelea hadi mwaka 2029. Kupitia matawi ya TADB na benki washirika nchini kote, maelfu ya wakulima wanatarajiwa kunufaika na mpango huo, hatua itakayochochea usalama wa chakula, kuongeza uzalishaji na kuimarisha maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Albert Chalamila akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Yas, Pierre Canton Bacara kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) mara baada ya kutembelea banda hilo, Banda la Yas limekusanya suluhisho mbalimbali zinazolenga kuboresha maisha ya Watanzania, ikiwemo huduma ya uchunguzi wa macho bure, mpango wa kumiliki simu janja na rauta za 5G kwa mkopo, huduma za intaneti majumbani na kwa wajasiriamali kupitia Yas Fiber, suluhisho kwa wafanyabiashara na taasisi kupitia Yas Business, pamoja na huduma na suluhisho mbalimbali za kifedha kupitia Mixx.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila akizungumza katika  kwenye Banda la Yas katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) wakati alipotembelea Banda hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila akizungumza Mtoto aliyefika na mzazi wake kupata huduma ya Macho katika Banda la Yas  kwenye Banda la Yas katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) wakati Mkuu wa Mkoa huyo  alipotembelea Banda hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila akizungumza na mwananchi   kwenye Banda la Yas katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (SABASABA) wakati alipotembelea Banda hilo.


Na Mwandishi Wetu
KAMISHNA wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Aretas James Lyimo, ameipongeza Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kwa mchango wake mkubwa katika kulinda afya ya wananchi kupitia usimamizi madhubuti wa ubora, usalama na ufanisi wa dawa pamoja na bidhaa nyingine za afya.

Kamishna Lyimo alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la TMDA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, ambako alipata fursa ya kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na mamlaka hiyo pamoja na elimu inayotolewa kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya dawa na bidhaa za afya.

Katika ziara hiyo, Kamishna Lyimo alipokelewa na Meneja wa Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa TMDA, Gaudensia Simwanza, ambaye alimueleza kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo ya kusimamia ubora, usalama na ufanisi wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi pamoja na bidhaa nyingine za afya kabla ya kufikishwa kwa watumiaji.

Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Kamishna Lyimo alisema TMDA imeendelea kutekeleza wajibu wake kwa weledi, hatua inayochangia kuhakikisha Watanzania wanapata bidhaa za afya zilizo salama na zenye viwango vinavyokubalika.

Alisema usimamizi huo ni nguzo muhimu katika kulinda afya ya jamii na kuimarisha mapambano dhidi ya matumizi holela ya dawa pamoja na bidhaa nyingine zinazoweza kuhatarisha afya ya wananchi.

"TMDA ina jukumu kubwa katika kuhakikisha bidhaa za afya zinazowafikia wananchi zinakidhi viwango vya ubora, usalama na ufanisi. Hili ni jambo muhimu katika kulinda afya ya Watanzania na kuzuia matumizi yasiyo sahihi ya dawa," alisema.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya TMDA na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ili kuongeza ufanisi katika kudhibiti matumizi mabaya ya dawa na bidhaa nyingine zinazoweza kutumika kinyume cha sheria.

Kamishna Lyimo pia aliipongeza TMDA kwa kutumia Maonesho ya Sabasaba kama jukwaa la kuwafikia wananchi wengi kwa kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya dawa, umuhimu wa kutumia bidhaa za afya zilizosajiliwa pamoja na tahadhari dhidi ya bidhaa zisizokidhi viwango.

Alieleza kuwa elimu hiyo ni nyenzo muhimu katika kujenga jamii yenye uelewa wa masuala ya afya, kupunguza madhara yatokanayo na matumizi yasiyo sahihi ya dawa na kuongeza ushiriki wa wananchi katika kulinda afya zao.

Kwa upande wake, TMDA imeendelea kutumia maonesho hayo kutoa huduma na elimu kwa umma kuhusu usalama wa dawa, vifaa tiba na bidhaa nyingine za afya, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa zilizosajiliwa na zinazokidhi viwango vya ubora kwa ajili ya kulinda afya na ustawi wa jamii.







Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha utafiti kuhusu maboresho ya kisasa ya mnyororo wa thamani wa kilimo uliofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Maendeleo ya Canada (IDRC-CRDI) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Tuzo hiyo imekabidhiwa leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, na Meneja wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa Bodi hiyo, Bw. Elfaraja Kintingu.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Bangu amesema heshima hiyo ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya WRRB katika kuimarisha sekta ya kilimo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, ambao umeendelea kuongeza ufanisi wa biashara ya mazao, uwazi wa masoko na ushindani wa bei katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema WRRB itaendelea kushirikiana na taasisi za utafiti na wadau mbalimbali katika kuendeleza ubunifu na maboresho yanayochochea maendeleo ya mnyororo wa thamani wa kilimo kwa manufaa ya wakulima na uchumi wa Taifa.

Awali, akielezea kuhusu tuzo hiyo, Bw. Kintingu amesema imetolewa kwa kutambua ushirikiano na mchango wa WRRB katika kufanikisha utafiti huo, ambapo watafiti walitembelea ghala mbalimbali nchini ili kujionea utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na mchango wake katika kuimarisha biashara ya mazao, kuongeza uwazi wa masoko na kuboresha mnyororo wa thamani wa kilimo.

Wanawake na mabinti nchini wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kujiunga na kozi za ubaharia na fani nyingine zinazohusiana na uchumi wa bluu ili kunufaika na fursa nyingi za ajira na maendeleo zinazopatikana katika sekta hiyo.

Rai hiyo imetolewa na Mkufunzi Msaidizi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Winifrida Winsislaus Ngalu, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Julai 8, 2026.

Amesema bado kuna dhana potofu miongoni mwa jamii kwamba fani za ubaharia ni za wanaume pekee, jambo ambalo si sahihi kwani wanawake wengi tayari wameingia katika sekta hiyo na wanaendelea kufanya vizuri katika nafasi mbalimbali.

Ngalu amesema Chuo cha Bahari Dar es Salaam kinashiriki maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu fursa zinazopatikana kupitia kozi mbalimbali zinazotolewa chuoni hapo, pamoja na kuwahamasisha wananchi kujiunga na masomo yanayohusiana na uchumi wa bluu.

Aidha, amesema Serikali imeendelea kutoa kipaumbele kwa kozi zinazotolewa na chuo hicho, ambapo wanafunzi wanaojiunga kuanzia ngazi ya cheti wanaweza kupata mikopo hadi  elimu ya juu, hatua inayolenga kuongeza idadi ya wataalamu katika sekta hiyo muhimu.

Pia ameeleza kuwa chuo kinaendelea kupokea maombi ya wanafunzi wanaotaka kujiunga na programu za cheti na shahada za uzamili (Master’s Degree) pamoja na kozi za umahiri,  dirisha la maombi kwa awamu ya kwanza litafungwa Julai 10, 2026 na dirisha la ngazi ya Shahada yaani Digrii litafunguliwa Julai 15.

Ngalu ametoa wito kwa wanawake, mabinti na vijana kwa ujumla kutumia fursa hiyo kujiendeleza kielimu na kitaaluma, akisisitiza kuwa uchumi wa bluu una nafasi kubwa ya kuchangia ajira, ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa.










Geneva, Julai 2026

Tanzania imelitaka Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) kujenga mfumo wa kimataifa wa miliki bunifu unaowezesha nchi zinazoendelea kunufaika na maendeleo ya akili mnemba (Artificial Intelligence–AI), huku ikisisitiza umuhimu wa kuhamasisha matumizi ya teknolojia na kujengea watu uwezo.

Akiwasilisha taarifa ya nchi kwa niaba ya Mhe Balozi Possi katika Mkutano wa 68 wa Nchi Wanachama wa Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) ulioanza tarehe 7 Julai, 2026 na kufanyika Geneva Uswisi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Hoyce Temu, alisema miliki ubunifu imekuwa nyenzo muhimu ya kukuza ubunifu, viwanda na maendeleo ya uchumi.

"Tanzania inatambua miliki ubunifu kama kichocheo cha kimkakati cha ubunifu, uvumbuzi wa teknolojia, maendeleo ya viwanda na maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi," alisema.

Alisema Tanzania inaendelea kujenga uchumi unaotegemea maarifa na inaiona akili mnemba kama fursa ya kuongeza kasi ya ubunifu na ukuaji wa uchumi.

"Tunaamini kuwa mifumo jumuishi ya miliki bunifu, ujenzi wa uwezo na uhamishaji wa teknolojia ni muhimu ili kuwezesha nchi zinazoendelea kunufaika kikamilifu na akili mnemba pamoja na teknolojia nyingine zinazoibuka," alisema.

Kauli hiyo inakuja wakati mataifa duniani yanaendelea kujadili namna mfumo wa miliki ubunifu utakavyoweza kuendana na kasi ya maendeleo ya akili mnemba. Nchi nyingi zinazoendelea zimekuwa zikitaka ushirikiano mkubwa zaidi katika uhamishaji wa teknolojia na maarifa ili kupunguza pengo la kidijitali.

Balozi Temu alisema Tanzania inaendelea kuimarisha mfumo wake wa miliki bunifu kupitia mageuzi ya sheria, kuboresha utoaji wa huduma, kuimarisha utekelezaji wa sheria, kujenga uwezo wa taasisi na kuongeza uelewa wa umma.

Aliishukuru WIPO kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania kupitia programu mbalimbali za kiufundi na ujenzi wa uwezo, ikiwemo kliniki za usimamizi wa haki miliki kwa biashara ndogo na za kati pamoja na kampuni changa, miradi ya uhamishaji wa teknolojia kupitia vyuo vikuu na taasisi za utafiti, mafunzo ya uchunguzi wa hataza na uwekaji wa mfumo wa kidijitali wa usimamizi wa haki miliki.

"Tunaendelea kujizatiti kuimarisha mfumo wa haki miliki ili uchangie zaidi katika ubunifu, uwekezaji, ujasiriamali, ajira na ukuaji endelevu wa uchumi," alisema.

Balozi Temu alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na WIPO pamoja na nchi nyingine wanachama kujenga mfumo wa haki miliki unaojumuisha wote, unaozingatia usawa na unaoweza kukidhi mahitaji ya teknolojia za sasa na zijazo.











Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeanza kupokea wageni waliojumuika katika ofa maalumu ya Sabasaba kwa kutembelea vivutio vya utalii vinavyosimamiwa na wakala huo. Safari ya kwanza imewapeleka wageni hao katika Magofu ya Kaole yaliyopo wilayani Bagamoyo.

Wageni hao, wakiwemo Watanzania na raia wa kigeni, walipata fursa ya kutembelea eneo hilo la kihistoria na kujifunza kuhusu historia ya ustaarabu wa pwani ya Afrika Mashariki pamoja na urithi wa kihistoria wa Tanzania.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhifadhi Mambo Kale Daraja la II, Veronica Kombe, aliwahamasisha wananchi kutumia ofa ya Sabasaba kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vinavyosimamiwa na TFS. Alibainisha kuwa safari inayofuata itafanyika Julai 11 kuelekea Msitu wa Asili wa Pugu–Kazimzumbwi.

Baadhi ya wageni walioshiriki ziara hiyo walieleza kufurahishwa na uzoefu walioupata, wakisema wamefanikiwa kujionea kwa karibu maeneo ambayo kwa muda mrefu walikuwa wakiyasikia kupitia simulizi na kusoma kwenye vitabu.

Kupitia ofa hiyo ya Sabasaba, TFS inalenga kuwapa wananchi fursa ya kutembelea vivutio vya utalii kwa gharama nafuu, kujifunza historia, kuhamasisha utalii wa ndani, na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kuhifadhi urithi wa asili na kihistoria wa Tanzania.







Meridianbet imekuja kivingine tena kwa kuleta zawadi mpya inayotikisa anga la kasino mtandaoni. Candy Treasures 3 Reels, mchezo mpya kutoka Oryx, umeingia rasmi ukiwapa wachezaji wa Meridianbet nafasi ya kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kabisa duniani kuufurahia. Ukiwa umejengwa katika mandhari ya pipi za kuvutia, rangi zenye kung'aa na mfumo wa kisasa wa ushindi, mchezo huu unafungua ukurasa mpya wa burudani kwa kizazi kinachopenda changamoto na zawadi kubwa.

Kinachoipa Candy Treasures 3 Reels utofauti na michezo mingine ya sloti ni uwezo wake wa kuunganisha urahisi wa kucheza na msisimko wa ushindi unaoendelea. Wakati alama zinazofanana zinapokutana, mfumo wa Cascade huanza kufanya kazi, ambapo alama zilizoshinda hulipuka na kutoa nafasi kwa alama mpya kuingia. Hii ina maana kwamba ushindi mmoja unaweza kuzaa ushindi mwingine bila hata kuzungusha tena mchezo. Kwa wanaopenda burudani yenye kasi na matokeo yasiyotabirika, mfumo huu unaleta hisia za kusisimua ambazo huongeza hamasa kila sekunde.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Lakini si Cascade pekee inayovutia macho ya wachezaji. Candy Treasures 3 Reels imejaa vizidishi vingi sana vinavyoweza kuongeza thamani ya ushindi wako kwa kiwango kikubwa. Zaidi ya hayo, alama za Wild huingia kusaidia kukamilisha mchanganyiko wa ushindi, huku alama za Cash collect zikiongeza mlipuko wa furaha na ushindi wakati wowote. Kila mzunguko unakuwa safari mpya yenye matumaini, matarajio na nafasi ya kushinda zaidi.

Kwa wale wanaopenda teknolojia, burudani za kidijitali na ushindi wa haraka, Meridianbet inaendelea kuonyesha kwa nini ni jukwaa linaloongoza katika sekta hii. Kupitia Candy Treasures 3 Reels, kampuni hii imeleta ubunifu, urahisi wa matumizi na burudani ya kiwango cha kimataifa. Muonekano wake wa kuvutia, uchezaji usio na usumbufu na uwezekano wa ushindi wa kusisimua vinaufanya mchezo huu kuwa gumzo kwa mashabiki wa kasino.

Iwapo umekuwa ukisubiri nafasi ya kujaribu kitu kipya, cha kisasa na chenye utamu wa ushindi, basi huu ndio wakati wako. Ingia Meridianbet kasino leo na uwe miongoni mwa watu wa kwanza kufungua hazina zilizojificha ndani ya Candy Treasures 3 Reels. Katika ulimwengu huu wa pipi na milipuko ya ushindi, kila raundi inaweza kuwa mwanzo wa hadithi yako kubwa ya mafanikio.


Mechi hii kubwa itachezwa Alhamisi tarehe 9 Julai 2026 katika uwanja wa Gillette Stadium (unaojulikana pia kama Boston Stadium), mjini Foxborough, karibu na Boston, Marekani. Mchezo utaanza saa 20:00 kwa muda wa GMT, sawa na saa 23:00 usiku kwa muda wa Afrika Mashariki (na saa 22:00 mjini Paris, saa 21:00 Rabat). Huu ni mchezo wa robo fainali ya michuano ya Dunia, na si mchezo wa hatua ya makundi.

Safari ya timu hizi mbili kufikia hatua hii imekuwa ya kuvutia. Morocco walianza siku hiyo kwa ushindi mkubwa wa 3-0 dhidi ya mwenyeji mwenza Canada, ambapo Azzedine Ounahi alifunga mabao mawili na Soufiane Rahimi akaongeza la tatu wakati wa nyongeza. Upande wa France, timu ya Didier Deschamps ilishinda kwa shida dhidi ya Paraguay bao 1-0, likifungwa na Kylian Mbappe kutoka penati baada ya VAR kuthibitisha kosa dhidi ya Desire Doue.

Mechi hii ni marudio ya mchezo wa nusu fainali wa Kombe la Dunia la Qatar 2022, ambapo France waliishinda Morocco kwa mabao 2-0 na baadaye kufika fainali. Sasa timu zote mbili zinaingia kwenye mchezo huu zikiwa na matarajio makubwa zaidi ya ya mwaka 2022 si tu kufika nusu fainali, bali kutwaa kombe lenyewe.

Morocco wana uwezekano mdogo wa kushinda ukizingatia mtindo wao wa mashambulizi ya kurudi haraka (counter-attack) na historia yao ya kufika robo fainali mfululizo, ingawa wana changamoto ya kuumia kwa mshambuliaji wao muhimu Ismael Saibari. ikionesha jinsi mechi hii inavyotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa wa kimbinu.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Uwanja wa Gillette Stadium, ambao ni nyumbani kwa timu ya American football ya New England Patriots, unatarajiwa kujaa watazamaji wapatao 65,878 kwa mchezo huu. Hii itakuwa moja ya mechi kubwa zaidi za robo fainali za msimu huu, ikiwa na historia nzito kati ya timu hizi mbili tangu mkutano wao wa mwisho wa ushindani mwaka 2022. Mshindi wa mchezo huu atapata nafasi ya nusu fainali, hatua moja tu kabla ya fainali ya mashindano ya Dunia 2026.

Na Pamela Mollel,Arusha 

Maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Arusha yamekamilika kwa asilimia 100, huku wananchi wakihimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika shughuli za Mbio za Mwenge, kutembelea miradi ya maendeleo na kuhudhuria mkesha mkubwa wa burudani utakaofanyika Viwanja vya FFU Mworombo jijini Arusha 

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, anasema maandalizi yote yamekamilika na wilaya ipo tayari kuupokea Mwenge wa Uhuru, huku akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu

Anasema Mwenge wa Uhuru utatembelea na kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha maendeleo na kuhakikisha miradi hiyo inaleta tija kwa wananchi

Mkude anasema mbali na miradi ya maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika mapambano dhidi ya UKIMWI, malaria, rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na utunzaji wa mazingira kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo, "Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo."

Aliongeza kuwa baada ya shughuli za mchana kukamilika, kutafanyika mkesha wa Mwenge wa Uhuru katika Viwanja vya FFU Mworombo, ambapo wananchi watapata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wakiongozwa na Ali Kiba na Juma Nature

Aidha, aliwataka wakazi wa Arusha na maeneo ya jirani kutumia fursa hiyo kushuhudia Mbio za Mwenge wa Uhuru, kutembelea miradi ya maendeleo pamoja na kushiriki mkesha huo utakaokuwa na burudani na ujumbe wa uzalendo

Mkude alisema matarajio ya Wilaya ya Arusha ni kuona wananchi wakijitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wa Uhuru na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa jamii.



Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA Makyei Ntiro alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto) akipokea zawadi alipotembelea banda la Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)Happiness Mwamwembe alipotembelea banda la NBAA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la NBAA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Spika wa Bunge Mstaafu, Bi. Anne Makinda (kushoto) akizungumza na watumishi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) alipotembelea banda la Bodi hiyo lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Deogratius Luswetula (MB) (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBAA, CPA. Prof. Sylvia Temu (kulia) alipotembelea banda la Bodi NBAA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBAA, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisikiliza maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa NBAA Naimani Fute alipotembelea banda la NBAA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.(Sabasaba)
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBAA, CPA Dkt. Mwamini Tulli akisaini kitabu alipotembelea banda la NBAA alipotembelea banda la NBAA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la NBAA katika Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Dennis Simba kwenye picha ya pamoja na watumishi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi hiyo katika Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
CPA Kulwa Emmanuel Malendeja, Mkurugenzi wa Huduma za Shirika Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)  akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Bodi hiyo katika Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam..

Na Mwandishi wetu

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesema itaendelea kuweka msukumo katika kuendeleza sayansi na teknolojia kwani ndiyo msingi wa kukuza uchumi kupitia maarifa na kuboresha huduma katika sekta mbalimbali.

Akizungumza  Julai 8, 2026, baada ya kutembelea Taasisi ya Afya na Utafiti ya Ifakara (Ifakara Health Institute-IHI), tawi la Bagamoyo mkoani Pwani, Prof. Mkenda amesema taasisi hiyo ni ya mfano katika tafiti za kisayansi ambazo zinasaidia maendeleo ya sekta ya afya.

Amepongeza kazi za Taasisi hiyo akitolea mfano utafiti chanjo za malaria, majaribio ya dawa (clinical trials) na teknolojia za kisasa zinazotumika  katika utafiti.

Mkenda amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa IHI na vyuo vikuu vya ndani na vya kimataifa ili kuijengea Tanzania yenye uwezo wa kufanya tafiti zenye viwango vya kimataifa, kuzalisha maarifa na bidhaa zenye manufaa kwa wananchi.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa serikali inataka kuona dawa za asili zikifanyiwa utafiti, majaribio ya awali (pre-clinical) na clinical trials ili kuthibitisha ubora na usalama wake  hapa hapa nchini, hatua itakayowezesha Tanzania kuzalisha dawa zilizotokana na gunduzi za ndani na  kunufaika na matokeo yake  kwa kuwa na haki miliki.

Aidha, amesema wizara inaendelea kupitia sera ya Sayansi na Teknolojia ili kuhakikisha inakuwa shirikishi, inatekelezeka na inapimika, sambamba na kuvitaka vyuo vikuu nchini kuweka uzito sawa katika ufundishaji na utafiti.

Akizungumza kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Afya na Utafiti ya Ifakara (Ifakara Health Institute-IHI), tawi la Bagamoyo Dkt Ally Olotu amesema taasisi hiyo immejikita katika kuleta mabadiliko katika mifumo ya afya nchini na nje ya mipaka, kufanya tafiti za chanjo mbalimbali na tabia za jamii kuhusiana na Afya. 










Top News