TUME ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, Leo Februari 13 imekutana na Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali George Waitara.

Mahojiano hayo ya Tume na Waitara yamefanyika katika Ofisi za Tume hiyo zilizopo Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na namna Matukio haya yalivyoanza, yalivyoathiri wakazi wa Mkoa wa Arusha, Mali na Miundombinu yake. 

Hata hivyo Tume inaendelea na mahojiano na waathirika wa Matukio hayo kwa ajili ya hatua zaidi kama Taifa ili Matukio kama hayo yasijirudie tena.






 

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupata huduma za ushauri wa kisheria katika Kliniki ya Sheria bila malipo inayotarajiwa kufanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 16 hadi 22 Februari, 2026.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ametoa rai hiyo tarehe 13 Februari, 2026 wakati akizungumza na Vyombo vya Habari kuhusiana na Uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya pamoja na Kliniki ya Sheria bila malipo kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam, ambapo Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kuwa, lengo la Kliniki hizo ni kusogeza huduma za kisheria karibu zaidi na Wananchi.

“Lengo kuu la Kliniki hizi ni kusogeza huduma mbalimbali za kisheria kwa wananchi, ili wananchi wawe na utajiri wa huduma za kisheria”.Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha, Mhe. Johari amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake katika kulinda, utawala wa Sheria ambao ndiyo msingi wa maendeleo ya nchi.

“Napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mhe. Rais kwa Uongozi wake, na zaidi katika eneo la msaada wa kisheria kwa wananchi, na kufanya huduma hizi ziwe zinapatikana kwa urahisi kwa wananchi.” Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akizungumzia kuhusu Kamati za Ushauri wa Kisheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa Kamati hizo ni kutoa Ushauri wa Kisheria kwa Wananchi, Watumishi wa Umma na Viongozi wa umma ili kutatua changamoto za kisheria zinazojitokeza katika ngazi ya Mikoa na Wilaya.

Vilevile, Mhe. Johari ameeleza kuwa uwepo wa Kamati za Ushauri wa Kisheria, kutasaidia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali, malalamiko ya Kisheria kutoka kwa wananchi, vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu, pia kamati hizo zitakuwa zikitoa elimu ya Sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali katika maeneo yao.








Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akihitimisha mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewana OSHA kwa wajumbe wa Kamati hiyo Februari 12, 2026.

Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imesema majukumu yaWakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) yakitekelezwa ipasavyoyatalipunguzia Taifa mzigo wa kuhudumia wananchi wanaoweza kuumia au kupatamagonjwa yatokayo na kazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Hawa Chakoma, alipokuwaakihitimisha mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA kwawajumbe wa Kamati hiyo Februari 12, 2026.

Mafunzo hayo ya siku moja ambayo yamefanyika bungeni Jijini Dodoma ni utekelezajiwa maagizo yaliyotolewa na Kamati hiyo katika kikao cha Januari 19, 2026 OSHA ilipowasilisha taarifa kuhusu muundo na majukumu yake. Mafunzo hayo yanalengakuiwezesha Kamati hiyo kutekeleza ipasavyo jukumu lake la kuisimamia Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) na Taasisi chini yake ikiwemo OSHA.

Mheshimiwa Chakoma ameipongeza Taasisi ya OSHA kwa jitihada inazofanyakutekeleza majukumu yake ikiwemo kutoa mafunzo kwa waaajiri na wafanyakazi, kufanya ukaguzi wa mifumo ya usalama na afya ukiwemo uchunguzi wa afya za wafanyakazi katika hatua mbalimbali.

“Niendelee kuwapongeza pamoja na kuwashukuru kwa mafunzo haya ambayoyamewafungua wabunge wengi na kimsingi ni mafunzo mazuri ambayo ukiyaangaliakwa haraka haraka unaweza kudhani ni kwa ajili ya maeneo ya kazi tu lakini kiukweliunaweza kuyatumia hata katika mazingira ya nyumbani kwenye hatari tofauti tofauti,” ameeleza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii nakuongeza:

“Mafunzo haya ni kwa ajili ya kuimarisha afya za wafanyakazi na wananchi kwa ujumlana sote tunakuballiana kwamba OSHA ipo kwa ajili ya kuliokoa Taifa ambapo ikifanyakazi yake sawa sawa kwa mujibu wa utaratibu waliotueleza hapa ama hakika tutakuwatunaliokolea Taifa letu mzingo mzito wa kuwatibia wagonjwa ama kuwapa fidiawafanyakazi waliomia kazini.”

Sambamba na kuipongeza OSHA kwa kutoa mafunzo mazuri, Kamati hiyo imeitakaOSHA kuwashauri wamiliki wa sehemu za kazi kutumia teknolojia na mitambo ya kisasailiyosanifiwa katika namna inayopunguza athari nyingi za kiusalama na kiafya wakitoleamfano wa vipando (lift) zilizopo katika majengo marefu katika miji mbalimbali hapa nchini.

Aidha, Kamati hiyo imependekeza elimu ya masauala ya usalama na afya kutolewa kwawabunge wote pamoja na wanachi mbalimbali wakiwemo wakulima wadogo wadogohususan wanaojishughulisha na kilimo cha tumbaku mkoani Tabora.

“Tangu nilipoingia kwenye hii Kamati na kujua kazi zinazofanywa na OSHA natamanikuwaona kila mahali na kupitia mafunzo yetu ya leo OSHA wametoa elimu kubwa sana japo hatukuwa na muda wa kutosha,” amesema Katani Ahmad Katani, Mjumbe waKamati.

“Niwapongeze OSHA kwa mafunzo mazuri na niungane na wenzangu kusema kuwamafunzo haya ni muhimu sana na yanaweza kutusaidia sana katika maisha yetu ya kilasiku na niombe tuendelee kupatiwa mafunzo kama haya,” ameeleza Mariam Kisangiambaye ni Mjumbe wa Kamati.

OSHA ni miongoni mwa Taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusianoyenye jukumu la kusimamia utekelezaji wa Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Miongoni mwa majukumu ya msingi ya OSHA ni kutoamafunzo ya usalama na afya kwa waajiri, wafanyakazi na umma kwa ujumla.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sanguakitoa maelezo ya awali kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kuhusu mafunzo ya usalama na afya mahala pakazi yaliyoandaliwa na OSHA Kamati hiyo.

Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi. Khadija Mwenda, akitoa ufafanuzi wa masuala na hoja mbalimbali zilizoibuliwa na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo yaJamii baada ya mafunzo ya usalama na afya mahala pakazi,yaliyotolewa kwa Kamatihiyo Bungeni Jijini Dodoma.

Mkufunzi wa Huduma ya Kwanza Mahali pa Kazi kutoka OSHA, Bi. Moteswa Meda, akiwasilisha mada katika mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa kwaWajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Bungeni Jijini Dodoma.

Mkaguzi wa Mazingira ya Kazi na Afisa Mafunzo kutoka OSHA, Bw. Simon Lwaho, akiwasilisha mada kuhusu vihatarishi vya usalama na afya katika mafunzo ya usalamana afya mahali pa kazi yaliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi naMaendeleo ya Jamii Bungeni Jijini Dodoma.
Mkaguzi wa Afya kutoka OSHA, Dkt. Edwin Senguo, akiwasilisha mada kuhusumagonjwa yatokanayo na kazi katika mafunzo ya usalama na afya mahali pa kaziyaliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Bungeni Jijini Dodoma.
Afisa Sheria kutoka OSHA, Thomas Nsyengula, akiwasilisha mada kuhusu maudhui yaSheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 katika mafunzo yausalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge yaUstawi na Maendeleo ya Jamii Bungeni Jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii,wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mafunzo mafunzo ya usalama naafya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA kwa Kamati hiyo Bungeni Jijini Dodoma.

Na John Walter-Manyara

Wizara ya Maji imezindua mpango maalum wa uwekezaji katika maji safi, usafi wa mazingira na usafi binafsi wenye thamani ya shilingi bilioni 94.62, utakaotekelezwa wilayani Hanang’, mkoani Manyara.

Mpango huo wa miaka mitano unaotekelezwa kwa ushirikiano na Shirika la WaterAid Tanzania, umezinduliwa Februari 11, 2026 na Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, katika hafla iliyofanyika wilayani humo.

Lengo kuu la mpango huo ni kutatua changamoto ya ukosefu wa maji katika vijiji vya wilaya ya Hanang’ na kuboresha huduma za usafi wa mazingira na usafi binafsi kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhandisi Mathew amesema kuwa rasilimali zinazotarajiwa kupatikana kupitia vyanzo vya kawaida hadi mwaka 2030 ni shilingi bilioni 41.75, hali inayoacha pengo kubwa la kifedha.

Kutokana na hali hiyo, amesisitiza umuhimu wa mchango kutoka sekta binafsi na wadau wa maendeleo katika kufanikisha utekelezaji wa mpango huo.

Naibu Waziri ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuziba pengo hilo kwa maslahi ya wananchi, na kuhakikisha mpango huo unaingizwa kikamilifu katika mipango na bajeti za kila mwaka.

Pia amewahimiza wadau wa maendeleo na sekta binafsi kuuona mpango huo kama ramani na mwaliko rasmi wa kuwekeza katika Wilaya ya Hanang’.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Hanang’, Almish Hazal, amemshukuru Naibu Waziri kwa jitihada zinazofanywa na Serikali pamoja na wadau katika kuimarisha miradi ya maji.

Hata hivyo, ameeleza kuwa changamoto kubwa inayokabili miradi ya visima ni upatikanaji wa nishati, hususan majenereta, akibainisha kuwa matumizi ya sola bado ni tatizo kutokana na hali ya baridi katika wilaya hiyo.

Ameomba kuwepo kwa ushirikiano kati ya Tanesco na RUWASA ili kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika miradi ya maji, hatua itakayosaidia “kumtua mama ndoo kichwani kwa asilimia 100.”

Naye Mkurugenzi wa WaterAid Tanzania, Anna Mzinga, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo, huku akiiomba kutoa kipaumbele katika rasilimali zitakazohitajika wakati wa utekelezaji wa mpango huo.

“Leo hii tunapouweka mpango huu mezani, tunatoa mwaliko wa wazi kwa kila mmoja kushiriki. Tunaishukuru Serikali kwa ushirikiano wake, lakini tunaomba iendelee kuongoza kwa kutoa kipaumbele katika uwekezaji wa mpango huu, Washirika wa maendeleo na sekta binafsi waweke nguvu zao pale ambapo mpango wa Serikali unaelekeza,” amesema Mzinga.

Uzinduzi wa mpango huo unatarajiwa kuwa chachu ya maboresho makubwa ya huduma za maji na usafi wa mazingira katika Wilaya ya Hanang’, na kuchangia ustawi wa afya na maendeleo ya wananchi wake.





Na Seif Mangwangi, Michuzi TV, Arusha

Baraza Madiwani la Jiji la Arusha limejipanga kuwa Baraza la kwanza nchini kujiendesha kwa kutumia mapato ya ndani bila kutegemea ruzuku kutoka Serikali kuu.

Akifungua kikao cha pili cha robo mwaka cha Baraza la Madiwani wa Jiji hilo leo 13 Februari 2026, Meya wa Jiji la Arusha Maximilian Iranghe amesema mpango wa Jiji hilo kujiendesha kwa mapato yake ya ndani pia umepitishwa na kuridhiwa kwenye vikao vya vya Madiwani wa Chama cha Mapinduzi ndani ya Baraza hilo.

Amesema kwa mwaka Jiji linauwezo wa kukusanya zaidi ya bilioni 150 Kwa mwaka huku Bajeti ya matumizi ikiwa ni bilioni 130 Kwa mwaka.

“ Kwa mapato ya Bilioni 150 bado tutakuwa na ziada ya bilioni 20 ambayo tutairudisha Serikalini ili iende kusaidia Halmashauri zingine za pembezoni, Kikubwa hapa tunatakiwa kukusanya mapato na kuboresha na kubuni vyanzo vipya vya mapato,” amesema.

Amesema mapato hayo yatapatikana kwa Jiji hilo kuboresha machinjio yake ya nyama iliyoko katika Kata ya sakina, kujenga hoteli za kitalii, kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na stand Kwa kuingia ubia na watu binafsi kujenga jengo la biashara.

“Miaka 50 iliyopita Serikali ya china iliamua kuwekeza kwenye Serikali za mitaa katika miradi ya wananchi, ilikopa na hizo pesa inajenga miundo mbinu ya kutosha ndani ya mitaa, hivi sasa ni matajiri wakiwa,” amesema.

Aidha amewataka Madiwani kuwatangazia wananchi katika maeneo yao ya utawala kuchangamkia fursa ya mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Jiji hilo huku akiagiza Idara ya Maendeleo ya Jamii kufuatilia marejesho kwa watu waliokopa.

Amesema fedha zinazotengwa kwaajili ya mikopo zimekuwa zikirudishwa na kupangiwa matumizi mengine baada ya kukosa watu wa kukopa jambo ambalo linarudisha nyuma kusudio la kutengwa Kwa fedha hizo.

Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Dkt Maduhu Nindwa Kwa niaba ya Mkurugenzi John Kayombo amesema vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka Jana 2025 baada ya uchaguzi mkuu zimesababisha uharibifu wa miundo mbinu ya zaidi ya bilioni 1.8.

Kutokana na uharibifu huo, Mkurugenzi ameliomba Baraza la Madiwani kuridhia kutumika kwa kiwango hicho cha fedha Ili kurejesha miundombinu hiyo ikiwemo Barabara pamoja na ukarabati wa majengo kwenye hali yake ya kawaida.

Akizungumza kwenye Baraza hilo Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude amewataka Madiwani kutumia hekima, utii na busara katika kuwatumikia wananchi Ili kuweza kuwaletea maendeleo.

Amesema kila mmoja akiwa na kiu ya kutatua matatizo ya wananchi watafanikiwa, “naomba Madiwani tuwe na upendo kwa wote, tufuate kanuni na taratibu, upendo, utii na nidhamu vinaenda pamoja, tukiwa tunaingia kazini tuzingatie haya yote,” amesema na kuongeza:

“Rais amekuwa akisisitiza suala la mapato na pia Meya amesisitiza wakati wa kufungua mkutano huu. Tuwe tuna hakikisha tunasimamia vyema suala la ukusanyaji wa mapato kwenye vyanzo vilivyopo,kuna vyanzo vingi vya mapato ambavyo hazikusanywi kufikia asilimia 100,” amesema.





WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Mradi wa kupooza umeme uliopo Mkata mkoani Tanga ambao chenye uwezo wa 2X60MVA 132/33kV, pamoja na ujenzi wa njia za kusambaza umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 45 kutoka kituo cha Mkata kwenda kijiji cha Kwamsisi .

Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa gharama ya Shilingi Bilioni 44.14 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme na Shilingi Bilioni 5.75 kwa ajili ya ujenzi wa njia ya kusambaza umeme.

Mradi huo ni miongoni mwa miradi ya uimarishaji wa Gridi ya Taifa wenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Wilaya za Handeni na Kilindi pamoja na kuimairisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Migodi ya Graphite katika Kijiji cha Kwamsisi.










Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 13 Februari 2026, Dodoma.

Katika Mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amewahimiza watendaji DSE kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa wabunifu katika masuala ya masoko na kuendelea kuvutia uwekezaji.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, ameahidi kuendelea kushirikiana vema na Serikali katika kutafuta mitaji ili kuweza kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kufikia uchumi wa Dola za Marekani Trilioni Moja ifikapo 2050.

Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ni taasisi ya kimkakati ya Taifa inayowezesha ukusanyaji na usimamizi wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kufadhili maendeleo ya uchumi wa Tanzania. DSE ni jukwaa rasmi linalowawezesha wawekezaji wa ndani na wa kimataifa kufanya biashara ya hisa, hatifungani, na bidhaa nyingine za kifedha katika mazingira yenye uwazi na utawala bora.

Thamani ya Jumla ya Soko la Hisa la Dar es Salaam ni shilingi Trilioni 31.9, ikiwa na jumla ya wawekezaji waliosajiliwa 779,000

Soko la Hisa la Dar es Salaam ni Mwanachama wa Masoko ya hisa ya Dunia, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).






Zaidi ya wananchi 7000 wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kunufaika na huduma ya bima ya afya kwa wote kwa awamu hii ya uzinduzi.

Mpango wa bima ya afya kwa wote wazinduliwa katika kijiji cha Kising'a Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Februari 10, 2026.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Afisa tarafa wa tarafa ya Ismani Ndg. Benitho Kayugwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Iringa amesema serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania imeona wananchi wake wanavyopata tabu hasa katika sekta ya afya na wameanza na makundi maalumu ambao watapata kadi za bima ya afya ili kupata matibabu bure, huku akiwasisitiza wananchi wanufaika kuzitunza kadi hizo.

Aidha, Wananchi 7827 kutoka halmashauri ya wilaya ya Iringa yenye kata 28 wamashatambuliwa na wanatarajiwa kunufaika na mpango wa bima ya afya kwa wote awamu hii ya uzinduzi.

Kampeni hii inaendelea kwa kata zote za Halmashauri yenye lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu pasipo vikwazo vya kifedha.

Kwa upande wake mratibu wa bima ya afya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Dkt Renatha Kato amesema, Halmashauri ya Wilaya inaanza zoezi hilo kwa awamu ya na kaya zisizokuwa na uwezo, ambazo zitagharamiwa na Serikali.














Top News