Na Mwandishi Wetu.

*DODOMA* : MAMLAKA ya Uteuzi imeridhia maombi ya muda wa ziada kwa Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 hivyo imeiongezea tena muda wa siku ishirini na moja (21) na kuitaka ikamilishe kazi kabla au ifikapo Aprili 24, 2026.

Mamlaka hiyo imeeleza sababu za kuongeza muda huo kwa Tume ni pamoja na kuiwezesha Tume kukamilisha uchambuzi wa ushahidi, taarifa na maoni yaliyopokelewa, kutoa fursa kwa wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi kufanyia kazi baadhi ya vielelezo vipya vilivyowasilishwa.

Sababu nyingine ni kuiwezesha Tume kukamilisha maandalizi ya Ripoti itakayowasilishwa kwa Rais na kutoa fursa kwa Tume kuandaa tafsiri ya Ripoti hiyo.

Tume hiyo ilianza kutekeleza majukumu yake Novemba 20, 2025 na kutarajiwa kukamilisha kazi yake ndani ya kipindi cha siku 90. Hata hivyo, kutokana na sababu mbalimbali, Tume iliongezewa muda wa kukamilisha kazi na kutakiwa kuwasilisha Ripoti kwa Rais kabla au ifikapo April 3, 2026.

Hivyo, kufuatia nyongeza ya muda, wananchi waliendelea kujitokeza kwa wingi tofauti na matarajio ya Tume. Hivyo, Tume iliendelea kupokea ushahidi, taarifa na maoni zaidi. 

Kwa sababu hiyo, Tume haikuweza kukamilisha kazi yake ndani ya muda wa nyongeza uliotolewa na hivyo kulazimika kuomba muda wa ziada ili kukamilisha kazi yake. 

Tume inaendelea kuwashukuru wananchi na wadau wote waliotoa ushirikiano kwa Tume wakati wa kufanya uchunguzi, ikiwemo wale waliofika mbele ya Tume kutoa ushahidi, taarifa na maoni, waliopiga simu na kutuma ujumbe, waliotuma ushahidi, taarifa na maoni kwa maandishi na waliowasiliana na Tume kwa njia za mitandao ya kijamii.


 


-Asema Serikali itatoa kauli baada ya uchunguzi

-Aagiza vibanda vipya vigawiwe kwa wafanyabiashara halisi


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza hatua za haraka kurejesha shughuli za biashara kufuatia ajali ya moto ulioteketeza Soko la Mawasiliano (Simu 2000) lililopo katika Kata ya Sinza, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Ameyasema hayo Aprili 6, 2026, alipofika kukagua madhara ya tukio hilo la moto lililotokea Aprili 4, 2026, ambapo takribani vibanda 500 vya wafanyabiashara wadogo viliteketea.

Akizungumza na wafanyabiashara hao, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu tukio hilo na itatoa kauli rasmi baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa kina ulioelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Mheshimiwa Rais amepata taarifa ya jambo hili, anawapa pole sana na ameelekeza uchunguzi wa kina ufanyike ili tujue chanzo cha tatizo hili. Na kazi hiyo imekwisha kuanza ili tuweze kupata undani wa chanzo cha jambo hili lililojitokeza,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu ameagiza eneo la soko hilo kusafishwa mara moja ili kuruhusu wafanyabiashara kuanza taratibu za kurejesha shughuli zao.

“Mkurugenzi, ukitoka hapa leo wakati unamalizia siku… kesho hapa pote pasafishwe. Hii kazi ya kusafisha kesho iishe,” amesema.

Amesema Serikali itashirikiana na taasisi za kifedha kusaidia wafanyabiashara wenye mikopo waliopoteza mitaji yao, pamoja na kuweka utaratibu wa kuwaongezea muda wa kurejesha mikopo hiyo na kuwezesha upatikanaji wa mikopo mipya yenye nafuu kupitia mamlaka za serikali za mitaa.

“Mkurugenzi sasa kwenye mikopo mipya nenda kaangalie una ukoko gani… tufanye kipaumbele kwa hawa ambao mtaji wao umeungua ili wapate haraka,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameagiza kuwepo kwa eneo la stendi katika mpango wa ujenzi wa soko hilo ili kurahisisha shughuli za biashara.

Kadhalika, amekemea vitendo vya ulanguzi wa vibanda katika masoko na kusisitiza kuwa vibanda vitolewe kwa wafanyabiashara halisi wanaofanya biashara.

Vilevile, amewataka wananchi kushirikiana katika kulinda amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa amani ni msingi wa shughuli zote za kiuchumi. “Ni lazima tuwe na amani kwenye nchi yetu. Kila Mtanzania awe mdau wa amani katika nchi yetu,” amesema.

Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa kuheshimu sekta binafsi katika kukuza uchumi wa nchi, akieleza kuwa ndiyo mhimili mkuu wa ajira kwa Watanzani











Na: Mwandishi Wetu, Pangani

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Bara na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Mussa Mwakitinya, amezindua rasmi mashindano ya mpira wa miguu yaliyopewa jina la "Aweso Vijana Cup," wilayani Pangani mkoani Tanga.

Uzinduzi huo umefanyika Aprili 4, 2026, katika uwanja wa Kata ya Mwera. Katika hotuba yake fupi ya ufunguzi, Mwakitinya ameupongeza uongozi wa UVCCM wa wilayani humo kufuatilia uratibu mzuri wa mashindano hayo huku akisisitiza  umuhimu wa vijana kushiriki kikamilifu ili kukuza vipaji vyao.

"Vijana wetu wana uwezo mkubwa, kupitia Aweso Vijana Cup tunafungua jukwaa la wao kuonyesha vipaji vyao na kujijengea mustakabali bora," amesema Mwakitinya.

Sambamba na hilo, Mwakitinya amesema serikali ipo pamoja na wadau wote wa michezo ili kuhakikisha sekta ya michezo inakua na inachangia maendeleo ya nchi.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Tanga, Ramadhani Omary, amesema vijana ni wadau muhimu kwa uhai wa Chama na maendeleo ya nchi, hivyo wanapaswa kutumia fursa zilizopo katika mazingira yao ikiwemo suala la michezo.

Katika mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo, timu ya Tungamaa ilipata ushindi wa (1-0) dhidi ya Mwera. Tungamaa ilipata goli la ushindi katika dakika 87, kupitia kwa mchezaji wake Said Mandera, na hivyo kuchukua alama tatu muhimu.

Mashindano hayo yanahusisha timu kutoka Kata zote 14 za wilaya ya Pangani huku mfadhili wa mashindano hayo akiwa ni Mbunge wa Jimbo la Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso.








Na Maiko Luoga Kibondo

Waumini wa Dayosisi ya Kibondo Kanisa Anglikana Tanzania, 6 aprili 2026, walijitokeza kwa wingi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Hilario – Kibondo, kushiriki Ibada ya Misa Takatifu maalumu ya Upatanisho na Msamaha.

Ibada hiyo maalumu iliongozwa na Askofu Daudi Ndahana, ili kuomba toba na msamaha kwa Mungu kufuatia mgogoro ulioibuka wakati wa uchaguzi wa kumpata Askofu wa pili wa Dayosisi hiyo, mwezi Septemba 2025 ambao uliwagawa waumini na baadhi kutengwa na Kanisa.

Askofu Ndahana alisema, mgogoro huo ulitengeneza hali ya tofauti kati ya waumini na Kanisa, hivyo uongozi ulifanya jitihada za kutafuta Suluhu kwa njia ya amani, kisha kuandaa Ibada ya upatanisho ambayo imetumika kuwapokea Wahudumu na waumini waliotengwa na huduma ya Kanisa.

“Tumekuja hapa ili kuomba Toba na Msamaha kwa Mungu, wakati wa mchakato wa uchaguzi wa uaskofu tulikosea, pia leo tumewarudisha kundini wenzetu waliotengwa na Kanisa” alisema Askofu Ndahana.

Kasisi Canon. Dkt. George Otieno Lawi, Katibu Mkuu Kanisa Anglikana Tanzania, alishiriki Ibada hiyo na kueleza kufurahishwa na hatua ya maridhiano iliyofikiwa na Dayosisi ya Kibondo ili kulinda afya ya Kanisa.

“Dayosisi ya Kibondo ilipita katika kipindi kigumu wakati wa mchakato wa kumpata Askofu wa pili, lakini Leo nina furaha kuona Kanisa limefikia hatua hii muhimu, Mungu awabariki sana” alisema Katibu Mkuu Lawi.

Wakizungumza kwa niaba ya waumini waliorudishwa kundini kuendelea na ushirika wa Kanisa katika Dayosisi ya Kibondo, James Ngomagi na Sedekia Ruduga, walisema, baada ya kutafakari kwa kina waliona ni vyema kujishusha ili kuliponya Kanisa la Mungu.

“Tulitofautiana na Kanisa la Mungu, baada ya kutafakari kwa kina Tukatafuta njia ya maridhiano Tunashukuru Mungu na Kanisa kutupokea” walisema.

Baadhi ya waumini walioshiriki Ibada hiyo akiwemo Bw. Zamoyoni Uzale, Lameck Kagina, Bi, Irene Ulimwengu na Jenipher Wilson walisema, Ibada hiyo imekuwa ya baraka na mafanikio kwa Kanisa la Mungu.

“Tumeshiriki Ibada ambayo imekuwa ya amani na furaha mbele za Mungu kwakuwa tumeona hatua ya upatanisho tunaamini haya ni mafanikio katika kukuza Injili ya Kristo” walisema waumini hao.

Ibada hiyo ilitanguliwa na zoezi la kuteketeza kwa moto fimbo na miti iliyotumiwa wakati wa vurugu za mchakato huo ili kuonesha kuwa jambo hilo limeisha na kuendelea kulitangaza jina la Mungu.






Na; Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amewataka wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu nchini na vijana kuendelea kulinda na kutetea misingi ya Muungano iliyoachwa na Waasisi.

Mhe. Mhandisi Masauni ameyasema hayo Aprili 06, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano maalum la kumuenzi aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Waziri Masauni amesema mwasisi huyo wa Muungano ameacha alama na historia ya kudumu kwa vizazi vya sasa na vijavyo, juhudi zilizotokana na mchango alioutoa katika kuwaunganisha Watanzania na kupambania maslahi ya wananchi wanyonge.

“Leo hii tunapomuenzi Sheikh Abeid Amani Karume tuna mengi ya kujifunza kutoka kwake kwani tumejionea jinsi alivyojali na kutetea maslahi ya wananchi wanyonge na zaidi ni juhudi zake katika kuasisi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964” amesema Mhandisi Masauni.

Aidha Mhe. Masauni amemtaja Sheikh Abeid Amani Karume Zanzibar kuwa ni kiongozi imara aliyesimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Zanzibar juhudi ambazo zimendelea kusimamiwa katika awamu mbalimbali za uongozi.

Amesema Sheikh Abeid Amani Karume ataendelea kukumbukwa na Watanzania kutokana na kuibua sera zilizogusa hisia za wananchi walio wengi ikiwemo ugawaji bure wa ardhi, utoaji wa elimu bure, matibabu ya bure na ujenzi wa makazi ya kisasa.

“Sheikh Karume aliishi ndoto ya muda mrefu ya uanamajumui wa kiafrika katika kuunganisha Bara zima la Afrika na kuunda Shirikisho la Afrika kwa vitendo na alifanya mambo mengi muhimu ambayo kamwe hayawezi kusahaulika” amesema Mhe. Mhandisi Masauni.

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi amesema kongamano hilo ni la kwanza kufanyika kwa upande wa Tanzania Bara ambalo linalenga kuhamasisha vijana kutambua mchango wa waasisi wa muungano ikiwemo Sheikh Abeid Amani Karume.

Amesema katika kuchagiza elimu ya Muungano, Ofisi hiyo imeandaa programu ya elimu kwa umma ambayo imekusudia kuelimisha wananchi wa makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo vijana na wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu nchini.

Kongamano hilo la siku moja limeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa kushirikiana na Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akifungua Kongamano la kumbukizi ya miaka 54 ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Aprili 6, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza wakati akifungua Kongamano la kumbukizi ya miaka 54 ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Aprili 6, 2026.


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la kumbukizi ya miaka 54 ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Aprili 6, 2026.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la kumbukizi ya miaka 54 ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, Aprili 6, 2026.





Baadhi ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu waliohudhuria Kongamano la kumbukiziya miaka 54 ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani katika Ukumbi wa Karimjee jijiniDar es Salaam, Aprili 6, 2026.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

-Atoa pole kwa wafanyabiashara wa Soko la Mawasiliano (Simu 2000) waliopata ajali ya moto

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Aprili 5, 2026, ameshiriki Tamasha la Pasaka la Mtoko na Christina Shusho lililofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika tamasha hilo, Waziri Mkuu amesema kuwa Pasaka ni kipindi muhimu kinachowakumbusha Watanzania kuishi kwa upendo, mshikamano na kudumisha amani katika jamii.

“Amani si kwa ajili ya faida ya Rais wala Serikali, bali ni kwa ajili ya kila mwananchi. Pasipo amani hata shughuli ndogo kama kujitafutia kipato haziwezi kufanyika.”

Ameeleza kuwa mnufaika wa kwanza wa amani ni mwananchi mwenyewe, kwani bila utulivu hata shughuli za kiuchumi, kijamii na ibada haziwezi kufanyika ipasavyo.

Aidha, amempongeza mwimbaji wa muziki wa Injili, Christina Shusho, kwa kuandaa tamasha hilo kubwa lililovuta maelfu ya waumini, akisema mafanikio yake yanaonesha kuwa lina kibali cha Mungu.

“Ukiona jambo linafanikiwa kiasi hiki, ujue lina kibali cha Mungu. Serikali haitakuwa kikwazo katika mipango ya kuendeleza huduma ya injili.”

Vilevile, Waziri Mkuu amewapa pole wafanyabiashara waliokumbwa na ajali ya moto ulioteketeza Soko la Mawasiliano (Simu 2000) lililopo katika Kata ya Sinza, Wilaya ya Ubungo, mkoani Dar es Salaam, iliyotokea Aprili 4, 2026, na kusema Serikali inafanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo cha tukio hilo na kuchukua hatua stahiki.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Patrobas Katambi, amesisitiza umuhimu wa wananchi kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kudumisha amani na utulivu wa nchi.

“Ulinzi na usalama wa nchi ni jukumu la kila Mtanzania. Ni muhimu wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kudumisha amani na utulivu wa nchi yetu.”

Tamasha hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, pamoja na waumini na wadau wa muziki wa Injili kutoka ndani na nje ya nchi.





Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO)limetoa ufafanuzi kuwa kwa mujibu wa taaluma ya afya na sayansi ya mwili wa binadamu, hakuna ushahidi wowote wa kitabibu unaothibitisha kuwa mwanaume anaweza kupoteza uume wake kwa kuguswa au kwa njia ya kichawi.

Ufafanuzi huo wa TRAMEPRO unakuja katika kipindi ambacho kumeibuka taarifa kuhusu kuongezeka kwa kasi kwa imani potofu, ushirikina na uzushi unaohusisha madai ya “kuguswa na kupoteza uume kwa wanaume” katika baadhi ya maeneo ya nchi.

Taarifa iliyotolewa leo Aprili 6,2026 na Katibu Mkuu Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) nchini Boniventura Mwalongo amesema kutokana na hali hiyo imeona ni vema ikatoa ufafanuzi katika hilo.

“Ukweli wa kisayansi na kitabibu kwa mujibu wa taaluma ya afya na sayansi ya mwili wa binadamu, hakuna ushahidi wowote wa kitabibu unaothibitisha kuwa mwanaume anaweza kupoteza uume wake kwa kuguswa au kwa njia ya kichawi.

“Matukio yanayoripotiwa mara nyingi huhusiana na hofu kali, mshtuko wa kisaikolojia na wasiwasi unaosababisha hisia zisizo sahihi mwilini.Mabadiliko ya muda mfupi ya mfumo wa fahamu au misuli.”

Amesema hivyo basi hiyo si tukio halisi la kimwili bali ni changamoto ya kisaikolojia inayohitaji uelewa sahihi na ushauri wa kitaalamu wa afya.

Hata hivyo amesema TRAMEPRO inaonya kuwa kuendelea kueneza taarifa zisizo na uthibitisho kunachochea hofu na taharuki katika jamii
Kunasababisha madhara kwa watu wasio na hatia.

“Kunadhoofisha juhudi za kukuza elimu ya afya na maendeleo ya jamii.Ni wajibu wa kila mwananchi kuepuka kusambaza uvumi na kuhakikisha taarifa zinathibitishwa kupitia vyanzo rasmi na sahihi.

Akifafanua zaidi amesema hatua hizo zinaendana na Kifungu cha (iii) cha Katiba ya TRAMEPRO kinachosema:

“(iii) Kupinga matumizi ya dawa asilia yanayopelekea na kuhamasisha vitendo vya jinai, mfano mauaji, wizi na vitendo vyote viovu.”

Pia amesema athari kwa jamii ni kuenea kwa imani hizo potofu kuna madhara makubwa, ikiwa ni pamoja na kuvuruga amani na mshikamano wa kijamii,kusababisha msongo wa mawazo na matatizo ya afya ya akili,kuwafanya wananchi kutumia rasilimali zao katika huduma zisizo sahihi pamoja na kuchelewesha upatikanaji wa huduma stahiki za afya.
Mwalongo amesema TRAMEPRO inatoa mwito kwa wananchi wote kutafuta huduma za afya katika vituo rasmi pindi wanapopata dalili zisizo za kawaida,kupuuza na kupinga imani potofu zisizo na msingi wa kisayansi.

Poa kudumisha amani, utulivu na mshikamano katika jamii na kutoa taarifa kwa mamlaka husika kuhusu vitendo vya utapeli au uchochezi wa uvunjifu wa amani

Wakati kwa vyombo vya habari vinahimizwa kutoa elimu sahihi kwa umma kwa kuzingatia weledi, ukweli na maadili ya taaluma ya habari,kuepuka kuripoti taarifa za uvumi bila uthibitisho pamoja na kushirikiana na wataalamu wa afya na taasisi husika katika utoaji wa taarifa sahihi.

Hata hivyo amesema TRAMEPRO inasisitiza mapambano dhidi ya imani potofu ni jukumu la wadau wote wa maendeleo na katika kuimarisha juhudi hizi iko tayari kushirikiana kwa karibu na
wadau mbambali ikiwemo Wizara ya Afya.

“Lengo ni kuhakikisha elimu sahihi kuhusu madhara ya uramali, urui, uzushi na ushirikina inawafikia wananchi wote, na vitendo hivi vinatambuliwa wazi kuwa ni hatari kwa ustawi wa jamii na vinapaswa kukemewa na kukomeshwa.”






NIRC Makambako.

Waziri wa Kilimo Mhe. Daniel Chongolo ametangaza neema kwa wakulima wa Idofi, Wilaya ya Makambako, ambapo Serikai inaenda kutekeleza mradi Mkubwa wa Umwagiliaji utakaonufaisha ekari zaidi ya 1.300.

Amesema, hatua hiyo itainua uchumi hivyo ni muhimu kuunga mkono mpango wa Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wa kutekeleza mradi huo wa ujenzi wa miundombinu ya Umwagiliaji katika skimu ya Idofi, utakaowezesha kilimo chenye tija na kufungua fursa mbalimbali za maendeleo katika eneo hilo.

Mhe. Chongolo amesema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi ya Idofi.

Amesema, Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wanatumia kikamilifu rasilimali zilizopo ili kujiletea maendeleo endelevu.

“Nimekuja mwenyewe kuwaambia ukweli wa kile kinachotakiwa kufanyika. Ni lazima tukae mkao wa watu tunaojua tunachokitaka,” amesisitiza Waziri Chongolo.

Mheshimiwa Chongolo, amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza fedha nyingi katika miradi ya kilimo, kwa lengo la kuinua uchumi wa wanachi.

Ameongeza kuwa, alibaini kuwa wananchi wengi hawalimi kwa tija licha ya kuwa na maeneo makubwa, kutokana na changamoto ya maji na miundombinu duni ya kilimo.

“Wataalamu walibaini kuwa eneo linalolimwa kwa sasa halifiki ekari 300, wakati eneo lote lina ukubwa wa ekari 1,300. Likiboreshwa, wananchi wataweza kulima eneo lote kwa tija na kuinua uchumi hii ni fursa kwetu wanachi wa Makambako,”alieleza.

Kwa mujibu wa tathmini ya awali ya wataalamu, mradi huo utahusisha ujenzi wa bwawa la Umwagiliaji na uwekaji wa miundombinu ya kisasa itakayowezesha uzalishaji wa mazao mwaka mzima.

Aidha Waziri Chongolo amewahakikishia wananchi kuwa hakuna mkulima atakayepoteza eneo lake kutokana na utekelezaji wa mradi huo.

“Eneo litakapoboreshwa, hakuna mkulima atakayeondolewa. Wanaolima sasa ndiyo watakaobaki, isipokuwa mtu aamue mwenyewe kuondoka au kuuza eneo lake,” amesisitiza.

Hata hivyo, amewahimiza wananchi kuwa tayari kushirikiana na Serikali kwa kutoa nafasi kwa muda mfupi ili kuruhusu utekelezaji wa mradi, kabla ya kurejeshwa katika maeneo yao kwa manufaa makubwa zaidi.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Makambako, Kenneth Haule, amewahimiza wananchi kujifunza kutoka katika maeneo ambayo tayari yamenufaika na miradi ya Umwagiliaji kama vile Igomelo, Pawaga na Itipingi, ambako uzalishaji umeongezeka kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Usanifu Mhandisi Sadati Kolowa kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji amebainisha kuwa ushirikishwaji wa wananchi ni kipaumbele katika miradi yote ya Umwagiliaji, kuanzia hatua za awali hadi utekelezaji wake, ili kuhakikisha kunakuwa na uelewa na maridhiano ya pamoja.

Naye Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Njombe, Machage Mwema, amesema wananchi watapewa umiliki wa maeneo yao ndani ya mradi huo na watakuwa na mamlaka ya kufanya maamuzi juu ya matumizi ya ardhi zao.

Mwema, ameongeza kuwa kwakuwa utekelezaji wa mradi utajumuisha maboresho mbali mbali ndani ya eneo hilo, shughuli zote za maboresho zitahusisha wananchi wenyemashamba ndani ya eneo la mradi na hakuna uharibifu wa mazao utakaofanyika na wala hakuna nguvu itakayotumika kuhamisha wanachi kwani watapanga na kuamua wao wenyewe

Kwa niaba ya wananchi, mkulima wa eneo hilo Erasto Mbuna, ameomba Serikali kupitia wataalamu kuhakikisha wanashirikishwa kikamilifu na kuzingatia maoni yao katika kila hatua ya utekelezaji wa mradi.

Mradi wa Umwagiliaji Idofi unatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa eneo hilo, ukiwa sehemu ya mkakati wa Serikali kwa kuhakikisha kilimo kinakuwa cha kisasa, chenye tija na kinachochangia kwa kasi ukuaji wa uchumi wa wa eneo hilo na Taifa kwa ujumla.  

MERIDIANBET imekuja tena, na sasa kiuwazi kabisa wanakwambia kwamba mali ipo shambani. Lakini si shamba la kawaida, hapa hupandi mahindi wala mihogo. Hapa unalima bahati yako, unalima bashiri zako, na mavuno ni ushindi mkubwa. Ukiingia shambani hapa, kila hatua ni nafasi ya kushika pesa nyingi zaidi ya unavyoweza kufikiria.

Usikose nafasi hii ya kipekee. Fortune Farm ya Meridianbet imejaa neema na zawadi zisizo na mwisho. Ukiweka bashiri zako, unapoanza kuzungusha gurudumu la bonasi, ndipo unapoanza kuona nguvu ya shamba. Hapa kuna viwango vitatu vya zawadi, 3 Wilds Level 1, 4 Wilds Level 2, na 5 Wilds Level 3. Kila kimoja kina vizidishi ambavyo vinaongeza zaidi kile ulichoweka.

Meridianbet wanakupa jukwaa pana la kubashiri, mechi kali za kimataifa hadi michezo ya kasino mtandaoni iliyojaa burudani. Ukiwa na odds zenye ushindani mkubwa, kila tiketi inakuwa na thamani zaidi. Jiunge sasa kupitia tovuti yao au piga *149*10#.

Kila ushindi wa bonasi utazidishwa kulingana na bashiri uliyoanza nayo, yaani kila mbegu unayopanda ni faida. Hivyo, ukiingia shambani, hakikisha unacheza kwa akili na unafuata mpangilio wa shamba la Meridianbet. Hapa, siyo tu unashinda mara moja, bali unazidisha kila bashiri unayoweka, huku ukiendelea kufurahia burudani ya Fortune Farm.

Hivyo basi, wabashiri wote, hii ni fursa isiyo ya kawaida. Shamba limefunikwa na mazao ya faida, yaani kila mzunguko ni nafasi ya kushinda ushindi. Karibu Fortune Farm ya Meridianbet, ambapo unalima bashiri zako na kuvuna pesa kubwa.

USHINDANI kati ya Napoli na AC Milan umekuwa ni mojawapo ya mechi zinazosubiriwa kwa hamu kubwa katika ligi kuu ya Italia, Serie A.Leo usiku, timu hizi mbili zinatarajiwa kupambana kwenye uwanja wa Diego Armando Maradona.

Historia yao ya moja kwa moja (Head to Head) inaonesha mchezooo wa kuvutia. Katika michezo 43 iliyopita, Napoli imefanikiwa kushinda mara 16, wakati AC Milan wamepata ushindi mara 13, na sare zimekua mara 14 . Hii inaonesha kwamba hakuna timu inayotawala kwa urahisi, na kila mchezo huwa ni vita ya pointi tatu.

Katika msimu huu, mechi ya mwisho kati ya timu hizi ilichezwa Septemba 2025, ambapo AC Milan waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 . Ushindi huo uliwaweka Wana Rossoneri katika nafasi nzuri, lakini Napoli wana nia ya kulipiza kisasi mbele ya mashabiki wao. Dimba la Maradona linajulikana kwa kuwa ngome kwa Napoli, na wanatumai kutumia fursa hiyu kuvunja historia ya usawa ili kuwafunga wageni wao.

Timu zote mbili zinaingia kwenye mechi hii ikiwa na rekodi tofauti. Napoli wamekuwa na matokeo mabaya kidogo nyumbani kwao msimu huu, mechi zao za nyumbani zikiwa na zaidi ya mabao mawili. Kwa upande mwingine, AC Milan wana rekodi nzuri ugenini, huku mechi zao za ugenini zikiwa na zaidi ya mabao mawili . Hii inatabiri mchezo ambao huenda ukawa wa kuvutia na mabao mengi. Jisajil sasa

Kwa kuzingatia historia, mechi za Napoli na Milan huwa hazina mshindi kabla ya kuanza. Sare imekuwa ikitokea mara nyingi, na ni muhimu kutambua kwamba katika mechi mbili za mwisho za makabiliano ya moja kwa moja, hakuna timu iliyofunga zaidi ya bao moja, Leo usiku, timu zote zitataka kubadilisha mtiririko huo kwa kushambulia kwa nguvu zaidi.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Katika takwimu za jumla, Napoli amefunga mabao 57 dhidi ya Milan waliofunga 53, ikionyesha kuwa timu ya nyumbani ina uwezo mdogo wa kufunga . Hata hivyo, mchezo wa leo si wa takwimu tu; ni suala la fahari na nafasi ya kukaa kwenye mbio za kutwaa ubingwa. Hii ni mechi ya pointi sita ambayo inaweza kubadilisha kabisa mwelekeo wa ligi.

Kwa ujumla, historia inaonesha kwamba mechi hii itakuwa ya usawa na yenye changamoto. AC Milan wanaweza kujisikia wazuri baada ya ushindi wao wa mwisho, lakini Napoli wana nguvu ya nyumbani na wanataka kuwaonesha wapenzi wao kwamba bado wapo kwenye mbio. Ni mchezo ambao hauwezi kutabirika kwa urahisi, na matokeo yake yataamuliwa na makosa madogo madogo.

Mwisho kabisa, uwanja wa Diego Armando Maradona utakuwa umejaa mashabiki wanaosubiri kuona kama Napoli wataweza kubadilisha historia ya usawa katika makabiliano haya. Kila timu itakuwa na lengo la kuchukua pointi zote, lakini historia inaonesha kwamba sare inawezekana. Itakuwa ni usiku wa kusisimua kwa wapenda soka wa Italia na duniani kote.

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania TCAA kupititiakwa mkurugenzi wake Ramadhani Msangi imempongeza Mkurugenzi wa kituo cha afya cha Aerospace Medical and Training Centre (AMTc) Kwa kutengeneza kitabu chenye muongozo wa kutoa huduma za afya kwenye ndege, akisema huo ni mwanzo mpya wa kusaidia huduma za anga nchini Tanzania.


Wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho jijini Dar es Salaam, Dkt. Nasra Nassor Omar amesema hiyo ilikuwa ni ndoto yake siku nyingi kusaidia sekta ya anga nchini.

Baadhi ya watu walio katika sekta hiyo wakiwemo Annamaria Rogatus Nzamba, Ramla Mshana na Lilian Felix Mlolere nao wametoa uzoefu wao kwa sekta hiyo.

Top News