Msaada huo umetolewa ikiwa ni sehemu ya juhudi za taasisi hiyo kuendeleza matendo ya kijamii na kuwafariji wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika hospitali hizo. Viongozi wa JAI wamesema lengo la msaada huo ni kuonesha mshikamano na kuwapa faraja wagonjwa pamoja na familia zao katika kipindi wanachopitia changamoto za kiafya.
Baadhi ya wagonjwa na ndugu waliopokea msaada huo wameishukuru taasisi hiyo kwa kuwajali na kuwasaidia katika kipindi kigumu, wakisema chakula hicho kitawapunguzia mzigo wa gharama za kila siku wakati wa matibabu.
Kwa upande wake, uongozi wa JAI umeeleza kuwa utaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za afya na jamii kwa ujumla ili kusaidia makundi yenye uhitaji na kuimarisha mshikamano wa kijamii








Akizungumza na Wanahabari Jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema msimu huu wa Sikukuu familia zinakuwa pamoja hivyo Kampeni hiyo itawapa nafasi ya kupata ofa kabambe ya kifurushi cha juu mara baada ya kulipia kifurushi chochote kile ikiwemo Nyota , Uhuru,Mambo ,Smart pamoja na Super.
Hata hivyo Malisa ameongeza kuwa ofa hiyo inawalenga watumiaji wa dishi na Antenna wataweza kuona maudhui yote.
Pia amesema katika ofa hiyo kuna Tamthilia mpya ya "ITS OK NOT TO BE OK" inayoruka saa mbili na nusu kupitia chaneli ya Novela plus pamoja na gangs of Manila Kuanzia Machi 28 kupitia Novela E plus.
Sanjari na Maudhui ya Kimichezo kwenye Ligi pendwa mbalimbali Ikiwemo Saudi pro league ya La Liga kupitia chaneli za Michezo kwa Lugha ya Kingereza na Kwa Lugha ya Kiswahili kupitia Tv3.
Hata hivyo ameongeza kuwa wikiendi hii kuna jambo kwenye Ligi ya Carabao (ARSENAL NA MAN CITY) fainali imefika "TOP TWO YA ENGLAND Wanakutana kwenye Bonge la Fainali ya Carabao cup na Mechi kubwa itarushwa na Tv3 kwa lugha ya Kiswahili ,hivyo Mteja wa Uhuru Lipia 23,000 upate siku Tani zaidi Bure Kabisa.


Na Mwandishi Wetu
Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari
Tanzania (TPA) inaendelea kufungua fursa za uwekezaji katika sekta ya meli ili kuimarisha usafirishaji wa mizigo ndani na nje ya nchi.
Katika juhudi hizo, TPA ilipokea maombi kutoka kampuni ya Gold Voyage Logistics Limited, tanzu ya Zijin Mining Group Co. Ltd, ya kukodisha eneo katika Bandari ya Karema kwa ajili ya ujenzi wa meli nne kubwa za mizigo. Mradi huu unalenga kuongeza kipato cha wananchi wa mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma inayopitiwa na Ziwa Tanganyika pamoja na kukuza uchumi wa taifa.
Ujenzi wa meli hizo ulianza Aprili 2025 na unatarajiwa kukamilika Julai 2026. Hadi sasa, mradi umefikia zaidi ya asilimia 95, huku meli zote tayari zikiwa majini zikisubiri hatua za mwisho za uhakiki kabla ya kuanza kutoa huduma.
Akizungumza jijini Mwanza, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema meli hizo zitakapoanza kazi zitaimarisha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi na Zambia. Pia zitachochea usafirishaji wa mizigo kupitia maeneo ya Manono, Bandari ya Kalemie, Kigoma, Dar es Salaam na Tanga.
Zaidi ya hayo, mradi huu utawanufaisha wakulima kwa kurahisisha usafirishaji wa mazao yao, pamoja na kuleta ajira kwa Watanzania hususan mabaharia, ambapo kila meli itahitaji angalau wafanyakazi 15. Shughuli za upakiaji, upakuaji, huduma bandarini na biashara ndogondogo pia zinatarajiwa kuongezeka kwa kasi.
Msigwa ameongeza kuwa meli hizi zitafungua fursa zaidi za kiuchumi kwa kuimarisha usafirishaji wa mizigo kupitia reli ya SGR, huku wamiliki wa malori wakinufaika kutokana na uwezo mkubwa wa kila meli kubeba tani kati ya 8,000 hadi 10,000 kwa safari moja.
WANARIADHA WA TANZANIA WAMEENDELEA KUNG’ARA MASHINDANO YA YAS KILI INTERNATIONAL HALF MARATHON 2026,
Kupitia matokea ya mbio hizo, kategori ya wanaume iliongozwa na Bw. Michael Geay aliyetwaa dhahabu baada ya kukimbia kwa 1:04:10, akifuatwa kwa karibu na Josephat Joshua Gisumo aliyemaliza kwa 1:04:14, huku mkimbiaji wa Kenya, James Kairiuki, akishika nafasi ya tatu kwa 1:04:30. Kwa upande wa wanawake, Hamida Musa aliongoza safu ya Watanzania, akifuatiwa na Failuna Matanga, huku Mkenya Veronika Wanjiku akimaliza wa tatu.
Akizungumza mara baada ya kukamilisha mbio, Geay alisema ushindani ulikuwa mkali lakini akasisitiza fahari yake ya kuiwakilisha nchi. Alieleza kuwa, “Nimefurahi sana kushinda. Haikuwa rahisi, kwani kila mmoja alikuwa analenga medali ya dhahabu.”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, aliwapongeza wanariadha kwa nidhamu, uzalendo na uthabiti wao. Alisoma pia salamu za pongezi kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ameahidi kuwa mgeni rasmi katika mbio za mwakani na kuongeza zawadi ya washindi kwa shilingi milioni 100.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Yas, Pierre Canton Bacara, alieleza kuwa kiwango cha ushindani kimeendelea kupanda na kusisitiza dhamira ya kampuni kuendeleza michezo, kuimarisha uhusiano na jamii na kuendeleza miradi ya mazingira, ikiwemo upandaji wa miti zaidi ya 50,000 katika maeneo yanayozunguka Mlima Kilimanjaro.
Bacara amesisitiza kuhusu kaulimbiu ya mwaka huu ya “Kila Kona, Kila Hatua Kasi zaidi,” kuwa inaakisi juhudi za kampuni kuhakikisha huduma za mawasiliano ya 4G na 5G zinawafikia Watanzania kote nchini.
Aliongeza kuwa, “Kwa mwaka wa tatu mfululizo, Kampuni hiyo imetambuliwa kimataifa na Ookla kama mtandao wenye kasi zaidi nchini. “Tunaendelea kuwekeza katika miundombinu ili kuhakikisha kila Mtanzania anafikiwa na mawasiliano ya uhakika-iwe ni biashara, elimu, kilimo au kusherehekea mafanikio ya ushindi wa mbio kama hizi za Yas Kili International Half Marathon mtandaoni.”
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu, aliipongeza Yas kwa kuendeleza urafiki wa muda mrefu na jamii ya mkoa huo na kusema mbio hizo zimekuwa kichocheo cha utalii, biashara na maendeleo ya jamii.
Katika mbio za Yas Kili Half Marathon kwa mwaka huu, maelfu ya Watanzania wamejitokeza kushiriki huku viwango vya ushindani vikipanda, na ushindi katika makundi mbalimbali ukitawaliwa na wanariadha wa ndani, jambo lililoleta hamasa kubwa miongoni mwa mashabiki.
Mbio za Yas Kili International Marathon kwa mwaka 2026 zimevutia umati mkubwa wa washiriki na watazamaji, likidhihirisha ukubwa wa mbio hizi katika kukuza uzalendo, kuhamasisha utalii na kuonesha hadhi ya Tanzania inavyozidi kuimarika katika mbio za masafa marefu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Austria anayeshughulikia masuala ya kisiasa, Mheshimiwa Balozi Dkt. Hannah Liko, amewasili nchini Machi 22, 2026 kwa ziara ya kikazi ya siku tatu inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, biashara na ushirikiano katika maeneo mbalimbali kati ya Tanzania na Austria.
Akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dkt. Liko amepokelewa na Balozi na Mwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Vienna, Mhe. Naimi S. Aziz, pamoja na Balozi wa Austria nchini, mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Dkt. Christian Fellner.
Wakati wa ziara hiyo, Dkt. Liko anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe (Mb.), pamoja na viongozi kutoka wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji), Wizara ya Fedha, Wizara ya Mambo ya Ndani na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Aidha, anatarajiwa kutembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika nyanja za kitaaluma na elimu ya juu. Ziara hiyo inatarajiwa kuhitimishwa Machi 25, 2026.
Majadiliano hayo yaligusia maeneo mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo, usimamizi wa majanga, huduma za afya, maendeleo ya rasilimali watu pamoja na sheria za kibinadamu (Humanitarian Law).
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, International Federation of Red Cross and Red Crescent Societies ndicho chombo kinachoongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya wanavoluntia, wanaofanya kazi kupitia matawi takribani 200,000 katika nchi 191 duniani.
Aidha, imeelezwa kuwa Red Cross Tanzania ilikuwepo hata kabla ya uhuru wa nchi, na baada ya Tanzania kupata uhuru ilianzishwa rasmi kwa Sheria Na. 71 ya mwaka 1962, kufuatia pia azimio la Umoja wa Mataifa la mwaka 1947. Kwa sasa, shirika hilo limeenea katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisafiri kwa Treni ya Kisasa ya Umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam kuelekea Morogoro leo tarehe 21 Machi 2026.
Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Maji, yatakayofanyika mkoani Morogoro, kesho tarehe 22 Machi 2026.

Viongozi mbalimbali pamoja na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.

Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally akizungumza kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waumini wa Dini ya Kiislamu, Viongozi, Wageni mbalimbali na Watanzania kwenye Baraza la Eid El Fitr Kitaifa lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Machi, 2026.





.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

















.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
