Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akijionea shughuli za uvuvi katika maeneo ya kazi ya wavuvi katika Soko la Kimataifa la Samaki Kirumba jijini Mwanza, ambapo pia alishiriki kuvua samaki akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba.















Na Karama Kenyunko Michuzi Tv

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameielekeza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kuendelea kusimamia ubora wa elimu inayotolewa na kuzuia madhara yanayohatarisha usalama wa watu na uchumi wa nchi.

Akizindua bodi mpya ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), leo Machi 6,2026, Dar es Salaam, Profesa Mkenda amesema katika kusimamia taasisi za utoaji elimu ya vyuo vya juu, tume inapaswa ifanye kazi ya kuwezesha na kusaidia wawekezaji wanaotaka kuanzisha vyuo Vikuu Tanzania kufikia ubora na viwango viwango vinavyotakiwa.

Pia amewataka Makamishna kuimarisha ubora wa elimu ya chuo kikuu nchini.

Usinduzi wa Bodi hiyo unaashiria mwanzo wa muhula mpya wa uongozi wa Bodi hiyo ambayo Mwenyekiti ni Prof. Makenya Maboko.

Akizungumza katika uzinduzi huo Profesa Mkenda amesema kuna wakati wanalaumiwa kwa kusimamia ubora, lakini wasiposimamia madhara yake ni makubwa kwa mfano vyuo vya madaktari kuna utaratibu wanapotoa shahada za udaktari, wanahitaji wanafunzi wangapi, maabara ngapi, walimu na madaktari wa aina gani.

"Tume imebeba jukumu kubwa la kulinda ubora wa elimu ya juu pamoja na imani ya umma katika vyuo vikuu, vyetu” amesema Prof. Mkenda.

Ameeleza kazi hizo hazifanywi na tume pekee bali hushirikisha na mabaraza ya madaktari na vigezo vingine vya Afrika Mashariki.

Ameongeza iwapo mwekezaji akitaka kukiuka ili kupata faida, matokeo yake ni kupata wahitimu ambao wataumiza watu katika kutibu.

Amesisitiza vigezo vya utoaji tiba nchini ni rahisi kuliko vilivyowekwa na Afrika Mashariki na kwamba hawapaswi kuvilegeza zaidi na badala yake kufikia vigenzo vya jumuiya hiyo.

"Tume hii ihakikishe inaufanisi wa kujibu malalamiko na kuwatembelea wadau wao ili kuzuia madhara yatokanayo na kutozingatia vigezo vya ubora ikiwemo uchumi wa nchi, usalama wa watu," amesisitiza.

Halikadhalika, Waziri Mkenda amesema kuwa vyuo vikuu vinapaswa kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia mifumo ya utawala bora sambamba na taratibu za uthibiti wa ubora wa elimu ili kupata wahitimu wenye elimu, maarifa, ujuzi na uwezo wa kustahimili ushindani kitaifa, kikanda na kimataifa.

Pia ameitaka tume hiyo kuongeza ufanisi katika mawasiliano, kuhimizana kutembelea maeneo ambayo wawekezaji wanataka kuanzisha vyuo vikuu na wawape ushauri

Akizungumza kwa niaba ya Tume, Prof. Maboko ameishukuru Serikali kwa imani iliyoiweka kwa Tume hiyo. Amesema kuwa Bodi itashirikiana kwa karibu na Sekretarieti ya Tume katika kuimarisha mifumo ya ndani ya uthibiti wa ubora wa elimu ya chuo kikuu pamoja na uzingatiaji wa sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa vyuo vikuu ili kuimarisha ukuaji na maendeleo endelevu ya elimu ya chuo kikuu nchini.

“Jukumu letu si la kiutawala pekee,” amebainisha Prof. Maboko. “Ni wajibu wa kimkakati kuhakikisha elimu ya chuo kikuu nchini inabaki kuwa yenye kuaminika, yenye ushindani na inayokidhi mahitaji ya soko la kitaifa, kikanda na kimataifa.”

Hafla ya uzinduzi huo, ilitanguliwa na warsha ya Makamishna wa TCU iliyofanyika tarehe 5 hadi 6 Machi 2026. Warsha hiyo ya kimkakati ilijikita katika kutathmini hali ya elimu ya chuo kikuu nchini kwa kulinganisha mfumo wa elimu ya juu wa Tanzania na mifumo ya elimu ya juu katika nchi za Afrika ikiwemo Mauritius, Afrika Kusini na Kenya.









 CHAMA cha Umoja wa Makandarasi na Watoa Huduma Shirikishi Tanzania (TUCASA) kimeiomba Serikali kuanzisha sheria maalum ya malipo katika sekta ya ujenzi ili kusaidia kuimarisha mazingira ya kazi kwa makandarasi wa ndani na kuhakikisha wanapata malipo kwa wakati wanapotekeleza miradi ya maendeleo ya umma.



Chama hicho kimesema kuwa uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuweka utaratibu wa wazi wa malipo na kupunguza changamoto ya ucheleweshaji wa fedha, hali ambayo kwa sasa inaathiri uwezo wa kifedha wa makandarasi wengi wa ndani.


Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 06, 2026 Mwenyekiti wa TUCASA, Qs Samuel Marwa amesema sheria hiyo inayojulikana kimataifa kama Security of Payment Act inaweza kusaidia kuweka mfumo wa kisheria unaolazimisha malipo ya kazi za ujenzi kufanyika ndani ya muda maalum pamoja na kuweka utaratibu wa haraka wa kutatua migogoro ya malipo.


Ameeleza kuwa ucheleweshaji wa malipo ya kazi zilizokamilika na kuthibitishwa umekuwa changamoto kubwa inayokwamisha ukuaji wa makandarasi wa ndani na kupunguza uwezo wao wa kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.


Marwa amefafanua kuwa kutokana na hali hiyo, wakandarasi wengi hulazimika kukopa fedha katika taasisi za kifedha kwa riba kubwa ili kuendelea na utekelezaji wa miradi waliyopewa na taasisi za umma.


Kwa mujibu wa Marwa, hali hiyo huongeza gharama za miradi na wakati mwingine husababisha baadhi ya kampuni kushindwa kuendelea na shughuli zao au hata kufilisika kutokana na mzigo wa madeni unaotokana na kuchelewa kwa malipo.


Aidha, TUCASA imeeleza kuwa uzoefu wa kimataifa unaonyesha kuwa uwepo wa sheria kama hiyo husaidia kuimarisha mtiririko wa fedha katika sekta ya ujenzi na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi.


Amebainisha kuwa sheria kama hiyo tayari inatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo Australia, Uingereza, Singapore na Malaysia ambapo imechangia kuimarisha sekta ya ujenzi na kulinda maslahi ya wakandarasi.


Chama hicho pia kimeipongeza Serikali chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuimarisha ushiriki wa makandarasi wa ndani katika miradi mikubwa ya maendeleo ya miundombinu nchini.


Pia kimetambua kauli ya Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba aliyoitoa Februari 15, 2026 mkoani Tanga alipokuwa akizungumza na wadau wa mradi wa bomba la mafuta la Afrika Mashariki (EACOP), ambapo alisisitiza umuhimu wa kulinda fursa za makandarasi wa ndani.


Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alionya dhidi ya baadhi ya makampuni ya kigeni yanayotumia majina ya Watanzania kusajili kampuni ili kupata zabuni za Serikali kinyume na taratibu.


Hata hivyo, TUCASA imesisitiza kuwa kuanzishwa kwa sheria ya malipo pamoja na maboresho ya mifumo ya manunuzi ya umma kutasaidia kujenga sekta imara ya ujenzi, kuongeza ushindani wa haki na kuhakikisha makandarasi wa ndani wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya miundombinu na uchumi wa taifa.CHAMA cha Umoja wa Makandarasi na Watoa Huduma Shirikishi Tanzania (TUCASA) kimeiomba Serikali kuanzisha sheria maalum ya malipo katika sekta ya ujenzi ili kusaidia kuimarisha mazingira ya kazi kwa makandarasi wa ndani na kuhakikisha wanapata malipo kwa wakati wanapotekeleza miradi ya maendeleo ya umma.


Chama hicho kimesema kuwa uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuweka utaratibu wa wazi wa malipo na kupunguza changamoto ya ucheleweshaji wa fedha, hali ambayo kwa sasa inaathiri uwezo wa kifedha wa makandarasi wengi wa ndani.


Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 06, 2026 Mwenyekiti wa TUCASA, Qs Samuel Marwa amesema sheria hiyo inayojulikana kimataifa kama Security of Payment Act inaweza kusaidia kuweka mfumo wa kisheria unaolazimisha malipo ya kazi za ujenzi kufanyika ndani ya muda maalum pamoja na kuweka utaratibu wa haraka wa kutatua migogoro ya malipo.


Ameeleza kuwa ucheleweshaji wa malipo ya kazi zilizokamilika na kuthibitishwa umekuwa changamoto kubwa inayokwamisha ukuaji wa makandarasi wa ndani na kupunguza uwezo wao wa kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.


Marwa amefafanua kuwa kutokana na hali hiyo, wakandarasi wengi hulazimika kukopa fedha katika taasisi za kifedha kwa riba kubwa ili kuendelea na utekelezaji wa miradi waliyopewa na taasisi za umma.


Kwa mujibu wa Marwa, hali hiyo huongeza gharama za miradi na wakati mwingine husababisha baadhi ya kampuni kushindwa kuendelea na shughuli zao au hata kufilisika kutokana na mzigo wa madeni unaotokana na kuchelewa kwa malipo.


Aidha, TUCASA imeeleza kuwa uzoefu wa kimataifa unaonyesha kuwa uwepo wa sheria kama hiyo husaidia kuimarisha mtiririko wa fedha katika sekta ya ujenzi na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi.


Amebainisha kuwa sheria kama hiyo tayari inatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo Australia, Uingereza, Singapore na Malaysia ambapo imechangia kuimarisha sekta ya ujenzi na kulinda maslahi ya wakandarasi.


Chama hicho pia kimeipongeza Serikali chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuimarisha ushiriki wa makandarasi wa ndani katika miradi mikubwa ya maendeleo ya miundombinu nchini.


Pia kimetambua kauli ya Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba aliyoitoa Februari 15, 2026 mkoani Tanga alipokuwa akizungumza na wadau wa mradi wa bomba la mafuta la Afrika Mashariki (EACOP), ambapo alisisitiza umuhimu wa kulinda fursa za makandarasi wa ndani.


Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alionya dhidi ya baadhi ya makampuni ya kigeni yanayotumia majina ya Watanzania kusajili kampuni ili kupata zabuni za Serikali kinyume na taratibu.


Hata hivyo, TUCASA imesisitiza kuwa kuanzishwa kwa sheria ya malipo pamoja na maboresho ya mifumo ya manunuzi ya umma kutasaidia kujenga sekta imara ya ujenzi, kuongeza ushindani wa haki na kuhakikisha makandarasi wa ndani wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya miundombinu na uchumi wa taifa.

Na Mwandishi Wetu 

USHIRIKIwa Tanzania katika maonesho makubwa ya utalii duniani ITB Berlin nchini Ujerumani, umeelezwa kuwa wa mafanikio makubwa, huku ukitoa fursa pana ya kuitangaza nchi kama kitovu cha utalii barani Afrika na kufungua milango mipya ya biashara na uwekezaji katika sekta hiyo muhimu ya uchumi.

Mafanikio hayo  yanatokana maonesho ambayo yanafanyika kila mwaka katika jiji la  Berlinhukutanisha wadau wa utalii kutoka zaidi ya nchi 180 duniani, yakiwemo mashirika ya utalii, wawekezaji, kampuni za safari na mahoteli pamoja na taasisi za serikali zinazohusika na maendeleo ya sekta ya utalii.

Ushiriki wa Tanzania umeongozwa na Bodi ya Utalii ya Tanzania (TTB) ukiwa na lengo la kuitangaza nchi kama Destination Tanzania Unforgettable na kuongeza fursa za biashara, uwekezaji na ushirikiano katika sekta ya utalii.

Katika maonesho hayo, zaidi ya kampuni 70 za utalii kutoka Tanzania pamoja na washiriki zaidi ya 169 wameungana chini ya banda la Tanzania kuonesha vivutio vya kipekee vya nchi, ikiwemo hifadhi za taifa, utajiri wa wanyamapori, fukwe za kuvutia za visiwa vya Bahari ya Hindi pamoja na utamaduni, historia na ukarimu wa Watanzania.

Siku ya tatu ya maonesho hayo iliadhimishwa kama Tanzania Day, ambapo wageni waliotembelea banda la Tanzania walipata nafasi ya kufurahia ladha ya vyakula vya Kitanzania, muziki na utamaduni wa Tanzania, sambamba na kupokea zawadi mbalimbali zilizotolewa na wadau wa sekta ya utalii. Tukio hilo lilivutia wageni wengi na kuifanya Tanzania kuwa moja ya vibanda vilivyovutia zaidi ndani ya maonesho hayo.

Kupitia ushiriki huo, Tanzania imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama World Leading Safari Destination, huku TTB,  ikiendelea kutekeleza jukumu lake la kuitangaza Tanzania kimataifa, kuvutia watalii wengi zaidi na kufungua masoko mapya ya utalii duniani.












Kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, Machi 8, wanawake wa Wilaya ya Chato mkoani Geita wameamua kuadhimisha siku hiyo kwa namna ya pekee kwa kutoa misaada na neno la faraja kwa makundi yenye uhitaji.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Chato, Christina Robert, amesema wanawake wa halmashauri hiyo wameguswa kuwafikia wanawake walioko katika Gereza la Wilaya ya Chato pamoja na wagonjwa hospitalini ili kuwapa moyo.

Mbali na neno la faraja, wametoa misaada ya vifaa muhimu vya kibinadamu kwa ajili ya wanawake wafungwa. Kwa upande wake, msimamizi wa wafungwa wanawake gerezani hapo ametoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuwakumbuka wafungwa wa kike ili kupunguza changamoto ndogondogo zinazowakabili.

Katika jitihada za kuhakikisha mtoto wa kike anasoma kwa uhuru, wanawake hao wametembelea shule mbalimbali na kutoa msaada wa taulo za kike (Pads).

Katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Jikomboe, jumla ya box 25 za taulo za kike zimekabidhiwa kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wenye uhitaji kubaki shuleni kwa amani wakati wanapokuwa katika mzunguko wao wa hedhi.

Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Chato, Diana Kaiza, amewataka wanafunzi wa kike kuzingatia maadili kama msingi wa mafanikio yao ya baadaye

"Inatakiwa muwe na maadili; Elimu bila maadili ni sawa na taa bila mwanga. Unapokuwa na maadili kuanzia nyumbani, basi hata shuleni utafanya vizuri na kuwa kiongozi bora," alisisitiza Kaiza.

Maadhimisho hayo yamehusisha pia kutembelea wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato, ambapo wanawake hao walishiriki kuwafariji na "kuwashika mkono" wagonjwa mbalimbali kama sehemu ya upendo na mshikamano kuelekea siku yao ya kihistoria.







  


Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake, wanawake kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wametembelea Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam na kutoa msaada wa vifaa na mahitaji mbalimbali kwa ajili ya kuwafariji wafungwa wanawake na watoto wanaoishi gerezani hapo.

Katika ziara hiyo, wanawake hao walikabidhi mahitaji muhimu kwa uongozi wa gereza ikiwemo vyakula, mavazi, taulo za kike, maziwa ya watoto pamoja na vifaa vya usafi, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za kuboresha ustawi wa wafungwa wanawake na watoto waliopo gerezani.

Kwa niaba ya Mkuu wa Gereza, Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Ngajebule Mbuguru, aliishukuru TCAA kwa msaada huo akibainisha kuwa unaleta faraja kwa wafungwa na kuwakumbusha kuwa bado ni sehemu ya jamii inayowajali.

Aliongeza kuwa vifaa na mahitaji yaliyotolewa vitasaidia kukidhi baadhi ya mahitaji muhimu ya kila siku ya wafungwa wanawake na watoto waliopo gerezani, huku Jeshi la Magereza likiendelea kutoa mafunzo ya ujuzi mbalimbali kwa wafungwa ili kuwaandaa kujitegemea pindi watakaporejea katika jamii.

Kwa niaba ya uongozi wa TCAA, Afisa Rasilimali Mkuu, Grace Kiunsi, alisema hatua hiyo ni sehemu ya utamaduni wa Mamlaka kushiriki katika shughuli za kijamii na kuendelea kuunga mkono makundi yenye uhitaji maalum katika jamii.

Alisema TCAA inaamini kuwa kuwatia moyo na kuwasaidia wanawake walioko katika mazingira mbalimbali ni sehemu ya kuchangia ujenzi wa jamii yenye mshikamano, utu na kujali.

Hatua hiyo imetajwa kuwa mchango muhimu katika kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuendeleza jamii yenye usawa na huruma kwa wote, hususan katika kipindi hiki cha kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake.
Wafanyakazi wanawake wa TCAA wakiongozwa na Afisa Rasilimali Mkuu, Grace Kiunsi wakikabidhi msaada wa vifaa na mahitaji mbalimbali Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Ngajebule Mbuguru kwa niaba ya Mkuu wa Gereza kwa ajili ya kuwafariji wafungwa wanawake na watoto wanaoishi gerezani hapo.
Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Ngajebule Mbuguru akiishukuru Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwa kuwafaraji kwa wafungwa na kuwakumbusha kuwa bado ni sehemu ya jamii inayowajali.
Afisa Rasilimali Mkuu, Grace Kiunsi akizungumza kuhusu Mamlaka inavyoshiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii na kuendelea kuunga mkono makundi yenye uhitaji maalum katika jamii.
Baadhi ya misaada iliyotolewa na TCAA katika gereza la Segerea

Top News