


.jpeg)











MichuziBlogV2
Most read Swahili blog on earth
Bonyeza play kuangalia Michuzi TV LiVE
BONYEZA PLAY KUANGALIA AZAM TV LIVE
BONYEZA KUANGALIA CHANNEL TEN LIVE



.jpeg)











CHAMA cha Umoja wa Makandarasi na Watoa Huduma Shirikishi Tanzania (TUCASA) kimeiomba Serikali kuanzisha sheria maalum ya malipo katika sekta ya ujenzi ili kusaidia kuimarisha mazingira ya kazi kwa makandarasi wa ndani na kuhakikisha wanapata malipo kwa wakati wanapotekeleza miradi ya maendeleo ya umma.
Chama hicho kimesema kuwa uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuweka utaratibu wa wazi wa malipo na kupunguza changamoto ya ucheleweshaji wa fedha, hali ambayo kwa sasa inaathiri uwezo wa kifedha wa makandarasi wengi wa ndani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 06, 2026 Mwenyekiti wa TUCASA, Qs Samuel Marwa amesema sheria hiyo inayojulikana kimataifa kama Security of Payment Act inaweza kusaidia kuweka mfumo wa kisheria unaolazimisha malipo ya kazi za ujenzi kufanyika ndani ya muda maalum pamoja na kuweka utaratibu wa haraka wa kutatua migogoro ya malipo.
Ameeleza kuwa ucheleweshaji wa malipo ya kazi zilizokamilika na kuthibitishwa umekuwa changamoto kubwa inayokwamisha ukuaji wa makandarasi wa ndani na kupunguza uwezo wao wa kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.
Marwa amefafanua kuwa kutokana na hali hiyo, wakandarasi wengi hulazimika kukopa fedha katika taasisi za kifedha kwa riba kubwa ili kuendelea na utekelezaji wa miradi waliyopewa na taasisi za umma.
Kwa mujibu wa Marwa, hali hiyo huongeza gharama za miradi na wakati mwingine husababisha baadhi ya kampuni kushindwa kuendelea na shughuli zao au hata kufilisika kutokana na mzigo wa madeni unaotokana na kuchelewa kwa malipo.
Aidha, TUCASA imeeleza kuwa uzoefu wa kimataifa unaonyesha kuwa uwepo wa sheria kama hiyo husaidia kuimarisha mtiririko wa fedha katika sekta ya ujenzi na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi.
Amebainisha kuwa sheria kama hiyo tayari inatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo Australia, Uingereza, Singapore na Malaysia ambapo imechangia kuimarisha sekta ya ujenzi na kulinda maslahi ya wakandarasi.
Chama hicho pia kimeipongeza Serikali chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuimarisha ushiriki wa makandarasi wa ndani katika miradi mikubwa ya maendeleo ya miundombinu nchini.
Pia kimetambua kauli ya Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba aliyoitoa Februari 15, 2026 mkoani Tanga alipokuwa akizungumza na wadau wa mradi wa bomba la mafuta la Afrika Mashariki (EACOP), ambapo alisisitiza umuhimu wa kulinda fursa za makandarasi wa ndani.
Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alionya dhidi ya baadhi ya makampuni ya kigeni yanayotumia majina ya Watanzania kusajili kampuni ili kupata zabuni za Serikali kinyume na taratibu.
Hata hivyo, TUCASA imesisitiza kuwa kuanzishwa kwa sheria ya malipo pamoja na maboresho ya mifumo ya manunuzi ya umma kutasaidia kujenga sekta imara ya ujenzi, kuongeza ushindani wa haki na kuhakikisha makandarasi wa ndani wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya miundombinu na uchumi wa taifa.CHAMA cha Umoja wa Makandarasi na Watoa Huduma Shirikishi Tanzania (TUCASA) kimeiomba Serikali kuanzisha sheria maalum ya malipo katika sekta ya ujenzi ili kusaidia kuimarisha mazingira ya kazi kwa makandarasi wa ndani na kuhakikisha wanapata malipo kwa wakati wanapotekeleza miradi ya maendeleo ya umma.
Chama hicho kimesema kuwa uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuweka utaratibu wa wazi wa malipo na kupunguza changamoto ya ucheleweshaji wa fedha, hali ambayo kwa sasa inaathiri uwezo wa kifedha wa makandarasi wengi wa ndani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 06, 2026 Mwenyekiti wa TUCASA, Qs Samuel Marwa amesema sheria hiyo inayojulikana kimataifa kama Security of Payment Act inaweza kusaidia kuweka mfumo wa kisheria unaolazimisha malipo ya kazi za ujenzi kufanyika ndani ya muda maalum pamoja na kuweka utaratibu wa haraka wa kutatua migogoro ya malipo.
Ameeleza kuwa ucheleweshaji wa malipo ya kazi zilizokamilika na kuthibitishwa umekuwa changamoto kubwa inayokwamisha ukuaji wa makandarasi wa ndani na kupunguza uwezo wao wa kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.
Marwa amefafanua kuwa kutokana na hali hiyo, wakandarasi wengi hulazimika kukopa fedha katika taasisi za kifedha kwa riba kubwa ili kuendelea na utekelezaji wa miradi waliyopewa na taasisi za umma.
Kwa mujibu wa Marwa, hali hiyo huongeza gharama za miradi na wakati mwingine husababisha baadhi ya kampuni kushindwa kuendelea na shughuli zao au hata kufilisika kutokana na mzigo wa madeni unaotokana na kuchelewa kwa malipo.
Aidha, TUCASA imeeleza kuwa uzoefu wa kimataifa unaonyesha kuwa uwepo wa sheria kama hiyo husaidia kuimarisha mtiririko wa fedha katika sekta ya ujenzi na kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi.
Amebainisha kuwa sheria kama hiyo tayari inatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo Australia, Uingereza, Singapore na Malaysia ambapo imechangia kuimarisha sekta ya ujenzi na kulinda maslahi ya wakandarasi.
Chama hicho pia kimeipongeza Serikali chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa kuimarisha ushiriki wa makandarasi wa ndani katika miradi mikubwa ya maendeleo ya miundombinu nchini.
Pia kimetambua kauli ya Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba aliyoitoa Februari 15, 2026 mkoani Tanga alipokuwa akizungumza na wadau wa mradi wa bomba la mafuta la Afrika Mashariki (EACOP), ambapo alisisitiza umuhimu wa kulinda fursa za makandarasi wa ndani.
Katika mkutano huo, Waziri Mkuu alionya dhidi ya baadhi ya makampuni ya kigeni yanayotumia majina ya Watanzania kusajili kampuni ili kupata zabuni za Serikali kinyume na taratibu.
Hata hivyo, TUCASA imesisitiza kuwa kuanzishwa kwa sheria ya malipo pamoja na maboresho ya mifumo ya manunuzi ya umma kutasaidia kujenga sekta imara ya ujenzi, kuongeza ushindani wa haki na kuhakikisha makandarasi wa ndani wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya miundombinu na uchumi wa taifa.
Na Mwandishi Wetu
USHIRIKIwa Tanzania katika maonesho makubwa ya utalii duniani ITB Berlin nchini Ujerumani, umeelezwa kuwa wa mafanikio makubwa, huku ukitoa fursa pana ya kuitangaza nchi kama kitovu cha utalii barani Afrika na kufungua milango mipya ya biashara na uwekezaji katika sekta hiyo muhimu ya uchumi.
Mafanikio hayo yanatokana maonesho ambayo yanafanyika kila mwaka katika jiji la Berlinhukutanisha wadau wa utalii kutoka zaidi ya nchi 180 duniani, yakiwemo mashirika ya utalii, wawekezaji, kampuni za safari na mahoteli pamoja na taasisi za serikali zinazohusika na maendeleo ya sekta ya utalii.
Ushiriki wa Tanzania umeongozwa na Bodi ya Utalii ya Tanzania (TTB) ukiwa na lengo la kuitangaza nchi kama Destination Tanzania Unforgettable na kuongeza fursa za biashara, uwekezaji na ushirikiano katika sekta ya utalii.
Katika maonesho hayo, zaidi ya kampuni 70 za utalii kutoka Tanzania pamoja na washiriki zaidi ya 169 wameungana chini ya banda la Tanzania kuonesha vivutio vya kipekee vya nchi, ikiwemo hifadhi za taifa, utajiri wa wanyamapori, fukwe za kuvutia za visiwa vya Bahari ya Hindi pamoja na utamaduni, historia na ukarimu wa Watanzania.
Siku ya tatu ya maonesho hayo iliadhimishwa kama Tanzania Day, ambapo wageni waliotembelea banda la Tanzania walipata nafasi ya kufurahia ladha ya vyakula vya Kitanzania, muziki na utamaduni wa Tanzania, sambamba na kupokea zawadi mbalimbali zilizotolewa na wadau wa sekta ya utalii. Tukio hilo lilivutia wageni wengi na kuifanya Tanzania kuwa moja ya vibanda vilivyovutia zaidi ndani ya maonesho hayo.
Kupitia ushiriki huo, Tanzania imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama World Leading Safari Destination, huku TTB, ikiendelea kutekeleza jukumu lake la kuitangaza Tanzania kimataifa, kuvutia watalii wengi zaidi na kufungua masoko mapya ya utalii duniani.
.jpeg)
