Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imetembelewa na Kamati ya Bunge ya Miundombunu na kupongezwa kwa jitihada zake za kuisimamia na kuiendeleza sekta ya usafiri wa anga nchini.

Kamati hiyo ya Bunge ya Miundombinu ilifanya ziara hiyo mnamo Februari 16, 2026 katika Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ziara hiyo iliongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Mhandisi Johnston Mutasingwa, kwa niaba ya Mwenyekiti Selemani Kakoso.

Ziara hiyo ya kikazi ilikuwa na lengo la kujua shughuli zinazofanywa na Mamlaka katika utekelezaji wa majukumu yake ya ki udhibiti .

Kamati hiyo iliihimiza TCAA kuendelea kumsimamia kikamilifu mkandarasi anayetekeleza Mradi wa ujenzi wa Majengo ya Kisasa ya Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vilivyokubalika.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile aliyeongozana na kamati hiyo, alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejikita katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga kupitia ujenzi, ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya anga pamoja na kuimarisha mifumo ya usimamizi. Alisema jitihada hizo zinategemea nguvu kazi yenye ujuzi mkubwa, na kwamba CATC, kwa kushirikiana na TCAA, ni nguzo muhimu katika kuzalisha wataalamu watakaoiwezesha sekta ya usafiri wa anga kukua kwa kasi na kwa usalama.

Kwa upande wa TCAA kamati hiyo ilipokewa na Mwenyekiti wa Bodi wa TCAA Dkt. Hamisi Mwinyimvua na kisha kupokea taarifa ya utendaji kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Bw. Salim Msangi.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Mhandisi Johnston Mutasingwa akizungumza akizungumza na menejimenti na watumishi wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipotembelea Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile akizungumza kuhusu Serikali ya Awamu ya Sita imejikita katika kuboresha sekta ya usafiri wa anga wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombunu aliyotembelea Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa TCAA Dkt. Hamisi Mwinyimvua akizungumza jambo wakatiwa  ziara ya Kamati ya Bunge ya Miundombunu aliyotembelea Makao Makuu ya TCAA.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Salim Msangi akitoa taarifa kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka hiyo kwa  Kamati ya Bunge ya Miundombunu ilipotembelea Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakiuliza maswali pamoja na kuchangia hoja mara baada ya kuwasilisha taarifa ya kazi zinazofanywa na TCAA


Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Miundombinu, menejimenti na watumishi wa TCAA wakiwa kwenye kikao kilichofanyika  Makao Makuu ya TCAA yaliyopo Banana-Ukonga.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bi. Mtumwa Khatib Ameir akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipotembelea ofisi za TCAA zilizopo Banana-Ukonga. jijini Dar es Salaam.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Shirikisho ya Somalia wamesaini Hati ya Makubaliano kuhusu masuala ya kiuhamiaji.

Hati hiyo ya Makubaliano imelenga kuondoleana hitaji la visa kwa Pasipoti za kidiplomasia na za kiutumishi pamoja na mashirikiano katika masuala ya uhamiaji baina ya nchi hizo mbili.

Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Serikali ya Somalia,Jenerali Abdullahi Sheikh Ismail Fartaag.

Akizungumza baada ya kusaini Hati ya Makubaliano , Waziri Katambi ametambua ushirikiano uliopo kati ya nchi hizo pamoja na mashirikiano yaliyopo katika masuala ya usalama wa raia na kuhamisha wafungwa.

Vilevile Waziri Katambi ameeleza kuwa  Tanzania itaendeleza ushirikiano na nchi zilizopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha usalama na Amani vinatawala katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tukio hilo pia limehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Ayoub Mohamed Mahmoud na Katibu Mkuu,Ally Senga Gugu.







-Pia awasilisha Salamu za Pole za Rais Dkt. Samia kwa waliofariki kwenye Machimbo, Korogwe.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amehani msiba wa Idrissa Zubeir Bin Ali (58) ambaye ni mdogo wake Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dkt. Abubakary Zubeiry bin Ally ambae amefariki Februari 15, 2026 katika Hospitali ya Muhimbili Dar Es salaam.

Akiwa Msibani hapo kuhani msiba huo, Mhe. Dkt. Mwigulu amewasilisha salamu za pole kwa wanakorogwe kutoka kwa Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vifo watu watano vilivyotokea Februari 15, 2026 katika Machimbo ya Mchanga ya BOLBIT kijiji cha Makuyuni, Tarafa ya Mombo.

“Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anawapa pole na kuwaombea moyo wa subira ndugu, Jamaa na wafiwa na Mwenyezi Mungu awape Pumziko la Amani marehemu wote”.





-Ni wa vifaa vya ujenzi jengo la Halmashauri ya Wilaya

-Zimo nondo 700, Marine boards 500 na matofali 2,000

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza wajumbe wa Kamati Mapokezi na Kamati za Ujenzi za mradi wa ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakamatwe na kuhojiwa mara moja ili watoe taarifa juu ya upotevu wa vifaa vya mradi huo.

“Kuna nondo 700, Marine boards 500 na matofali 2,000... hivi vifaa havijulikani viko wapi. Wahusika kila siku mnaripoti kazini, na mishahara mnalipwa wakati ujenzi umesimama na hakuna hatua zinazochukuliwa,” amesema wakati akimhoji Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Dkt. Jumaa Mhina.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Februari 16, 2026) wakati akizungumza na wananchi wa Lusanga, kata ya Mgomeni, wilayani Muheza waliofika kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi la ofisi hiyo itakayokuwa na ghorofa moja pindi ikikamilika.

“Kamanda wa TAKUKURU ninahitaji hii taarifa kwa kina kabla sijamaliza ziara yangu mkoani Tanga. OCD fuatilieni kwa kina ushiriki wa watumishi wa hii Halmashauri. Kila mmoja ahojiwe hadi tujue vifaa vilipoteaje.”

Amesema kuwa anazo taarifa kwamba timu ya manunuzi imenunua vifaa ambavyo vimewekwa stoo wakati hatua yake ya ujenzi haijafikiwa. “Nimeambiwa vifaa vingine vimekuja lakini vimekaa stoo tu. Ni kwa nini mmenunua vifaa hivyo wakati hamjamaliza hatua ya kwanza? Mshauri mwelekezi wa mradi yupo lakini hamsikilizi ushauri anaotoa,” alisema.

Jengo hilo ndiyo limemalizika kujengwa ghorofa ya chini, na linasubiri kuanza kuwekewa linta kwenye ghorofa ya kwanza.

Waziri Mkuu amekemea tabia ya kutochukua hatua masuala kama hayo yanapojitokeza hasa ikizingatiwa kwamba Halmashauri nyingine ambazo walipewa fedha kwa wakati mmoja wao wameshakamilisha kazi ya ujenzi.

Mapema, akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Kaimu Mkuu wa Idara ya Miundombinu na Maendeleo Mijini na Vijijini, Mhandisi Abdalla Jaha alisema mradi huo ambao umefikia asilimia 68, ulianza kujengwa Septemba 29, 2023 na wanatarajia ifikapo mwishoni mwa Juni, 2026 sakafu ya chini ianze kutumika.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa pongezi kwa kiwanda cha vifungashio cha Yogi PolyPack ambacho kiko Pongwe, nje kidogo ya Manispaa ya Tanga.

Akizungumza na viongozi na watumishi wa kiwanda hicho, Waziri Mkuu amesema uwekezaji uliofanywa ni mkubwa na kwamba serikali itaendelea kuhakikisha inatengeneza mazingira mazuri ya uzalishaji.

“Nimetembelea kiwanda, nimeona kazi nzuri ikiendelea na inatumia teknolojia ya kisasa. Haya ndiyo mambo Mheshimiwa Rais anataka kuyaona. Unatengeneza ajira, unazalisha bidhaa ambazo ni malighafi kwa viwanda vyetu hapa nchini na unatoa kipato kwa wafanyakazi wako,” amesema.

Mapema leo, Waziri Mkuu alitembelea bandari ya Tanga na kukagua shughuli za bandari hiyo na kisha kuzungumza na watumishi.

Akiwa bandarini hapo, alipokea maelezo ya uboreshaji wa bandari hiyo kisha akatembelea eneo ambalo zitajengwa gati mbili mpya, katika bandari ya Tanga ikiwa ni mkakati wa Serikali ya kuiongezea uwezo bandari ya Tanga wa kutoa huduma shindani na za ufanisi.

Akizungumza na watumishi wa bandari ya Tanga, Waziri Mkuu aliahidi kwamba Serikali itahakikisha inaendelea kufanyia kazi changamoto zote za kiutumishi zinazowahusu watumishi hao.

“Serikali itaendelea kufanya maboresho katika bandari hii ili iweze kuhudumia idadi ya meli nyingi kwa kadiri inavyowezekana. Tunatambua ushindani wa kibiashara uliopo lakini tutaendelea kufanya maboresho ili tunufaike na nafasi ya kijiografia ya mkoa wetu,” alisema.

Pia ameiagiza Mamlaka ya Bandari ifanyie kazi changamoto ya uhaba wa vifaa vya kupakulia mizigo ili kuendana sambamba na maboresho hayo.






MKUTANO wa Waandishi wa Habari kuhusu Ziara za Kikazi alizofanya Rais Mhe. Dkt. Samia, Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia pamoja na Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bw. Bakari Machumu akizungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Februari, 2026 kuhusu Ziara za Kikazi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizofanya Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 12-15 Februari, 2026 pamoja na Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 2-6 Februari, 2026.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahamoud Thabit Kombo akizungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Februari, 2026 kuhusu mafanikio ya Ziara ya Kikazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyofanya Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 12-15 Februari, 2026. Waziri Mhe. Balozi Kombo alielezea kwa kina ushiriki wa Tanzania katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika mkutano huo.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria Mkutano wa Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Februari, 2026 kuhusu Ziara za Kikazi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizofanya Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 12-15 Februari, 2026 pamoja na Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 2-6 Februari, 2026.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Februari, 2026 kuhusu mafanikio ya Ziara ya Kikazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyofanya Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 12-15 Februari, 2026.




Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya Habari wakiwa kwenye Mkutano kuhusu Ziara za Kikazi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizofanya Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia tarehe 12-15 Februari, 2026 pamoja na Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 2-6 Februari, 2026.



Na Saidi Lufune, Dodoma
NAIBU  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amehimiza Idara ya Maliakale kuongeza ubunifu katika kutangaza vivutio vya maliakale na makumbusho ya kihistoria ili kuvutia watalii wengi wa ndani na nje ya nchini.

Mhe. Chande amebainisha hayo jijini Dodoma katika kikao kazi na Idara ya Malikale ambapo amefafanua kuwa sekta ya maliakale nchini inapaswa kuwa juu na kuwa sehemu ya kuchangia ukuaji wa mapato katika ukuaji wa uchumi wa Taifa hususan katika kufufua maeneo mapya ya utalii wa malikale na makumbusho ya kihistoria

Aidha, ameiagiza idara hiyo kuongeza mashirikiano yenye tija na Wizara ya Utalii na Mambo ya Malikale ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ili kuongeza nguvu katika kutangaza mazao mapya ya vivutio vya Maliakale huku akisisitiza uhifadhi wa makumbusho ya nyimbo zitokananazo na matukio ya historia ya Taifa wakati na baada ya ukombozi wa Tangangika na Zanzibar.

Awali akiwasilisha taarifa za idara hiyo, Mkurugenzi wa Idara ya Malikale Dkt. Christowaja Ntandu amebainisha kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Idara ya Maliakale itaendelea kuhamasisha Mamlaka za Serikali za Mitaa kufungua maeneo na vivutio vipya vya Malikale; kuendelea kutangaza na kuhamasisha jamii kupitia maonesho, matamasha na warsha juu ya umuhimu wa kuwekeza na kutumia rasilimali za utamaduni kama zao mojawapo la utalii hapa nchini.







Top News