-Atoa maagizo lukuki ya kuboresha Mkoa huo kuelekea AFCON 2027.


-Ataka muonekano mzuri wa Jiji kwa kufanya usafi wa mazingira na kuondoa kabisa gereji bubu barabarani.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ametoa muda wa mwezi mmoja kwa wamiliki wa gereji na mafundi seremala kuondoa vyuma chakavu na samani chakavu maeneo ya barabarani ili jiji liwe nadhifu huku akiwataka Madiwani, wenyeviti wa mitaa,watendaji wa kata na mitaa pamoja na wakuu wa wilaya zote tano kushiriki kikamilifu katika ulinzi na usalama wa maeneo yao na Mkoa huo kwa ujumla ikiwemo kuanzisha vikundi vya sungusungu

Akizungumza katika katika kikao kazi maalum kilichokutanisha Madiwani, wenyeviti wa mitaa,watendaji wa Kata na Mitaa pamoja na wakuu wa wilaya zote tano za Mkoa huo Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila amesema vyuma hivyo chakavu kwenye maeneo ya barabara vimekuwa vikiharibu muonekano wa jiji huku pia akisisitiza serikali mkoani humo haitokuwa tayari kuona amani ya mkoa huo inavurugwa kwa kuwa mkoa huo ndio kitovu cha masuala ya kidiplomasia na uchumi

Aidha amezungumzia taarifa zinazosambaa mitandaoni juu ya uwepo wa watu wanaofikiria kufanya maandamano ambapo amewataka viongozi na mitaa na kata kuendelea kusimamia amani kwenye mitaa na kata zao

Sanjari na hayo Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amewataka viongozi wa wangazi za mitaa na kata kuimarisha usafi wa mazingira ili kuepukana na maradhi ya mlipuko na watambue kuwa Tanzania imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa mashindano ya AFCON,hivyo haitokuwa vyema kuona heshima hiyo ambayo Taifa imepata inaharibiwa kutokana na uzembe kwenye suala la usafi na amewataka wakurugenzi kusimamia vyema sheria na kanuni za usafi wa mazingira ili kuimarisha usafi na kudhibiti tabia ya utupaji taka hovyo huku akisisitiza majengo ya barabarani kupaka rangi nyumba zao

Akizungumzia suala la mchakato wa uendeshaji wa dampo la pugu kinyamwezi kwa ubia na kampuni binafsi Chalamila ametoa muda wa hadi julai 30 kwa mchakato huo kuanza kwa mpango huo na amehimiza Halmashauri zote za jiji hilo kuwa na dampo la kutupia taka sanjari na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kujua kutrndanisha taka na amepiga marufuku suala la ubandikaji wa picha za matangazo kwenue maeneo ya jiji hilo na amewstaka wakurugenzi kutotoa vibali vya bar kwenye makazi ya watu ikiwemo Masaki na Oystabay

Awali Katibu Tawala Mkoa wa Dar es salaam Ndg Abdul Mhinte amesisitiza suala la anuani za makazi kutumika vyema kutambua watu na makazi yao ili kusaidia kuimarisha Amani.







Na Janeth Raphael MichuziTv


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake Mhe. Devotha Minja, imekutana na uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya kupokea, kupitia na kuchambua taarifa ya hesabu za taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2025, zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Katika kikao hicho, PAC imeielekeza TRA kuchukua hatua za haraka kurekebisha mapungufu yote yaliyoibuliwa na CAG, hususan katika maeneo ya ukusanyaji wa kodi na usimamizi wa mapato ya serikali.

Kamati hiyo pia imeitaka TRA kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa kodi kwa kuongeza ufanisi katika ukaguzi, uhakiki wa taarifa za walipakodi, pamoja na kuboresha mifumo ya ufuatiliaji wa mapato ili kuhakikisha hakuna upotevu wa fedha za umma.

Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, amesema taasisi hiyo imepokea maelekezo yote ya PAC na kuyapa kipaumbele, huku akiahidi kuwa mapungufu yaliyobainishwa yatashughulikiwa ndani ya muda uliopangwa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TRA, Uledi Mussa, amesema kikao hicho kimekuwa fursa muhimu ya kujifunza na kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa zaidi ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi na walipakodi.

Ameongeza kuwa lengo la TRA ni kuwa taasisi inayoaminika na wananchi, huku ikiendelea kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari kama njia ya kuongeza mapato ya ndani na kuchochea maendeleo ya taifa.

Pia ameiomba PAC kuendelea kuwa mabalozi wa kuelimisha na kuhamasisha wananchi kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari ili kuunga mkono maendeleo ya nchi.








Na Oscar Assenga, Tanga

Mkoa wa Tanga unatarajia kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni 17, mwaka huu, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 27.7.

Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk. Batilda Burian, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.

Dk. Burian alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro, kabla ya kukimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 katika halmashauri zote za mkoa huo.

Alisema Juni 28, mwaka huu, Mwenge huo utakabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, huku miradi 11 ya vijana na miradi miwili ya sekta ya maji ikikaguliwa.

Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni kutoka kwa wahisani.

Akizungumzia kaulimbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.

“Tumewaandaa viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru,” alisema.

Aliongeza kuwa wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa unaosisitizwa katika kaulimbiu ya mwaka huu.

Mbali na kuhamasisha maendeleo, alisema Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya na umuhimu wa lishe bora.

Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru.

“Mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi mbalimbali vya sanaa katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha,” alisema.

Alisema kwa ujumla maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2026 yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha na mkoa uko tayari kwa shughuli zote za mbio hizo.

Na.Ashura Mohamed - Arusha

Katika kuhakikisha kuwa Uchumi wa wakazi wa mkoa wa Arusha unaimarika wananchi wa mkoa huo hususani Vijana wametakiwa kuhakikisha kuwa wanachangamkia fursa mbali mbali za kiuchumi ili kunufaika na ujio wa mashindano ya kimataifa ya Afcon 2027.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini bw.Jospeh Mkude,wakati wa Kongamano la Vijana la Engutoto Youth Summit kuhusu Mashindano ya AFCON 2027,Wakili Irene Ndosi ambaye ni Katibu Tarafa Suye amesema kuwa ujio wa Afcon ni neema kubwa kwa wakazi wa mkoa wa Arusha ambapo mbali na kupata burudani ya mpira wa miguu lakini pia ni fursa kwa makundi yote kuongeza uchumi wao.

"Fursa zitaanzia kuanzia watu wa chini kabisa boda boda,watu wa usafirishaji mpaka wanawake watengeneza shanga,kila mtu achukue nafasi hiyo kuleta mabadiliko chanya kwenye uchumi wake binafsi na familia yake na mkoa kwa ujumla,pia tuwe tayari kujaza eneo la uwanja wa Afcon kwasababu mashindano haya ni yakipekee na yanashirika nchi tatu ambazo ni Tanzania,Kenya na Uganda."Amesitiza Ndosi

Aidha Hamza Juma Njiku ni Diwani wa Kata ya Engutoto amesema kuwa kongamano hilo ni muhimu kwa kuwa limewakutananisha vijana na wadau mbal8 mbali katika kuonyesha fursa zilizopo kuelekea mashindano hayo ya Afcon.

"Sisi katika kata yetu fursa za Afcon zimetugusa moja kwa moja kwa kuwa tunajengewa Uwanja mkubwa mzuri wa Mazoezi kwaajili ya mashindano hayo ambapo utakuwa na uwezo wa kuchukuwa watu 5000 waliokaa,maegesho ya magari 500 na mabasi mawili kwaajili ya zile timu ambazo zitaingia kufanya mazoezi,ila uwanja ukikamilika na mashindano kumalizika utatumika kwaajili ya ligi kuu na michuano mbali mbali."Amesema Diwani Njiku

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM),Kata ya Engutoto ambaye ndio muandaaji wa Kongamano Engutoto Youth Summit,bw.Ibzan Michael Ruheta amesema kuwa kongamano hili si jukwaa la kisiasa bali ni jukwaa linalokutanisha watu wote kujadili fursa za AFCON kuelekea mwaka 2027.

Bw.Ruheta amesema kuwa Mashindano ya AFCON hayatahuishwa na Tanzania peke yake bali ushirikiano na mataifa mengine wakiwemo Kenya pamoja na Uganda,hivyo kama Watanzania ni wajibu wao kuamka na kuhakikisha tunaitumia nafasi hiyo ipasavyo.

"Ndugu mgeni rasmi, kama unavyojua nchi yetu imepata fursa ya kuandaa mashindano haya ya AFCON,hivyo kama viongozi mliopo katika nafasi za maamuzi, ni vizuri kujipanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali na taasisi mbalimbali zilizopo nchi yetu kwa kikisha fursa hizi tunazipata kwa wakati, vijana waheshimiwe, wasikilizwe na kero zao zitatuliwe ili nchi yetu inufaike."Amefafanua Mwenyekiti huyo

Kongamano la Engutoto Youth Summit lenye kauli mbiu ya "Unlocking 2027 AFCON Opportunity" limeandaliwa na Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Kata ya Engutoto,na limekusudia kuwajengea vijana uwezo wa kunufaika na fursa za michezo hiyo kubwa ya kimataifa ambapo limefanyika katika Chuo cha Uhasibu Arusha(IAA) na kukutanisha Vijana Zaidi ya 1000 ili kuonesha nyanja mbali mbali ambazo vijana wanaweza kunuifa nazo.
Picha ya Viongozi Mbali Mbali wa Chama na Serikali walioshiriki Kutoa Mada  katika Kongamano la Engutoto Youth Summit kupelekea Mashindano ya AFCON 2027.
Mgeni rasmi Wakili Irene Ndossi ambaye ni katibu Tarafa ya Suye akimwakilisha mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini akizungumza na Vijana ambao hawapo pichani
Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Engutoto mwenye Tisheti Nyeupe Bw.Ibzan Ruheta akiwa katika picha ya Pamoja na Wadau Mbali mbali
Safu ya Viongozi wa Chuo kutoka Chuo Cha Arusha Technical(ATC) ikiongizwa na Raisi wa Serikali ya wanafunzi  Bw.Magolosa Mosses mwenye  Suti nyeusi Kulia,mara baada ya kumalizika kwa Kongamano hilo katika Chuo Cha Uhasibu Arusha.

Na Farida Mangube Morogoro

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Michael Mwang’onda, amewataka wananchi walio karibu na vyanzo vya Maji kulinda vyanzo hivyo pamoja na miundombinu ya huduma hiyo.

Ametoa wito wakati akizindua mradi wa maji wa uhifadhi wa chanzo Cha mto Ruvu kupitia ujenzi wa miondombinu ya usambazaji Maji wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unaotarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa vijiji vya Dakawa na Mngazi Halmashauri ya Morogoro.

Amesema Serikali imeendelea kuwekeza fedha nyingi katika sekta ya maji kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi, hivyo ni wajibu wa jamii kuhakikisha miundombinu hiyo inalindwa na kutunzwa ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu.

Mradi huo wenye thamani ya Sh bilioni 3.18 unahusisha uchimbaji wa visima viwili vyenye uwezo wa kuzalisha lita 248,000 za maji kwa saa, ujenzi wa mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita 26, vituo 34 vya kuchotea maji pamoja na matenki mawili yenye uwezo wa kuhifadhi lita 160,000 za maji.

Aidha, mradi huo umejumuisha uwekaji wa pampu za kusukuma maji zenye uwezo wa lita 30,000 kwa saa katika Kijiji cha Mngazi na lita 50,000 kwa saa katika Kijiji cha Dakawa, hatua inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji kwa uhakika.

Katika kuimarisha matumizi bora ya rasilimali za maji, mradi huo pia umejenga birika la kunyweshea mifugo katika Kitongoji cha Lukenze, Kijiji cha Dakawa, ambalo linatarajiwa kusaidia kupunguza migogoro ya matumizi ya maji kati ya wakulima na wafugaji.

Kwa sasa mradi huo unawanufaisha wananchi 6,453 wa vijiji vya Dakawa na Mngazi, huku idadi ya wanufaika ikitarajiwa kuongezeka na kufikia watu 11,550 ifikapo mwaka 2043.

Mwang’onda alieleza kuridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kushiriki katika uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Baadhi ya wakazi wa vijiji vya Mngazi na Dakawa, akiwemo Kibua Haji na Maua Bunga, walieleza kufurahishwa na utekelezaji wa mradi huo wakisema umesaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa maji iliyokuwa ikiwalazimu kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi na salama.

Wananchi hao waliipongeza Serikali kupitia Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huo na kuomba huduma hiyo kuendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi katika maeneo mengine ya wilaya hiyo.






Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdalla Hamid, ameendelea na ziara yake ya kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Mtwara.

Akiwa katika shughuli za ubanguaji korosho, Ndugu Rabia amesema CCM itaendelea kusimamia na kulinda maslahi ya wakulima wa korosho, akibainisha kuwa zao hilo lina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi na Taifa.

Aidha, ameelekeza kuchimbwa kwa kisima cha maji katika eneo la Mtwanya Juu ili kusaidia shughuli za Kiwanda cha Ubanguaji Korosho.

“Serikali ya CCM haitorudi nyuma katika kulinda maslahi ya mkulima wa korosho. Mkulima anapostawi, Taifa linastawi. Tuendelee kuzalisha kwa wingi na kwa ubora zaidi ili kuongeza tija na manufaa kwa wakulima,” amesema Rabia.











The Office of Former President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr Jakaya Mrisho Kikwete, categorically refutes the false and misleading report currently circulating online, claiming that Dr Kikwete is associated with an alleged investment programme promising Tanzanians guaranteed income through an AI-powered financial platform.

The report claims that thousands of Tanzanians have already benefited from the programme after investing TSh 653,000, with promises of earning more than TSh 9,200,000 per month. These claims are entirely false.

The Office of the Former President wishes to make it absolutely clear that H.E. Dr Jakaya Mrisho Kikwete has never been involved in, endorsed, promoted, or supported any such financial scheme. His office has not authorised the use of his name, image, or reputation in connection with this alleged programme, and it will not engage in such activities.

Members of the public are strongly advised to ignore this false report and to exercise great caution against such fraudulent and illegal schemes. Anyone who comes across similar misleading information should treat it as fake news and avoid sharing, registering, or sending money to any person or platform linked to it.



Mwandishi Wetu, Ngorongoro
SERIKALI itaendelea kuongeza nguvu katika uhifadhi wa wanyamapori aina ya Faru ambao wapo haratini kutoweka kwa kuimarisha Mradi wa Kimkakati wa Uhifadhi wa Faru weupe ili kuongeza chachu ya ongezeko la uhifadhi na utafiti wa wanyamapori waliopo nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hasaan Chande wakati wa hafla maalumu ya kuwaachilia huru Faru weupe 17 waliopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ikiwa ni mradi maalumu uliofadhiliwa kupitia Shirika la Andbeyond kwa ushirikiano na Serikali ya Afrika Kusini

“Kwa kweli mmebuni kitu kizuri ambacho kinaleta tija na ufanisi na kuleta lmaendeleo kwa nchi yoyote, lengo kuu ikiwa ni kuongeza utafiti, uhifadhi na kupata elimu.

"Wako wengi Duniani watakuja kujifunza kupitia Faru hawa weile wakiwa ama ni wanafunzi, au wakufunzi," alisema Mhe. Chande.

Amempongeza na Kumshukuru Mhifadhi namba moja nchini katika uhifadhi na muongoza watalii, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utayari na utashi wake katika uhifadhi huku akiishukuru pia Serikali ya Afrika Kusini kwa ushirikiano mzuri na Tanzania kwa ufadhili wa Faru hao.

Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Alexander Lobora amesema hatua ya kuwaachia huru Faru hao kutoka kwenye uzio imesaidia katika kuongeza wigo wa kupata eneo kubwa zaidi la kujitafutia malisho huku wakihakikishiwa ulinzi kutokana na miundombinu ya ufuatiliaji wa wanyama ndani ya hifadhi

“Kwa niaba ya Sekta ya Utalii kwa ujumla serikali ipo tayari kupokea Faru zaidi kwa awamu ya pili kwa sababu tayari tumejifunza mengi kwa awamu ya kwanza na lengo la Faru hawa kubwa ni uhifadhi kama tulivyosaini Mikataba ya Kimataifa kama nchi kuhusu wanyamapori ambao wapo hatarini kutoweka,” alisema Dkt. Lobora.

Kwa upande wake Kamishina wa Uhifadhi wa Mamalaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw.. Abdul-Razaq Badru amesema, NCAA itaendelea kuimarisha ulinzi mkali kwa kutumia mitambo ya kisasa katika kuwalinda na kuwahifadhi wanyama hao walio hatarini kutoweka kwa ajili ya manufaa ya Taifa na kuongeza mwitikio wa uhifadhi na utafiti kwa kizazi hiki na kijacho.

Naye Mtendaji Mkuu wa Shirika la Anbeyond Bw. Mussa Mathayo amesema awali ulifanya utafiti wa eneo la kuishi Faru hao ili kuwa na afya njema na kujitafutia malisho na kubainisha kuwa shirika hilo lipo tayari kuongeza idadi ya Faru waliosalia ili kufikisha Faru 36 kama ilivyokuwa kwenye mkataba.







Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Energies Tanzania imezindua kituo kipya cha mafuta eneo la Wazo jijini Dar es Salaam huku mkakati wake wake ukiwa ni kuendelea kusogeza huduma za nishati za mafuta na gesi karibu na wananchi.

Akizungumza leo Juni 15,2026 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kituo hicho,Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Energies Tanzania Iman Mtafya amesema mazingira bora ya uwekezaji yanayofanywa na Serikali katika sekta ya nishati ya mafuta na gesi imewezesha Oryx kuendelea kusogeza upatikanaji wa nishati hizo.

“Oryx ndio tunaongoza kwenye mtandao wa vituo vya mafuta na usambazaji wa gesi na tutaendelea kuiunga mkono serikali katika kuhamasisha matumizi ya nishati na uzinduzi  wa kituo hiki ni mkakati wetu wa kuendelea kusogeza huduma zetu.

“Kwahiyo tunaendelea kuwekeza maeneo mbalimbali na tumeanza hapa Wazo na hivi karibuni tutafungua kituo kingine Dodoma ambacho kitakuwa umbali wa kilometa 40 kutoka Dodoma Mjini.Lengo ni kuonesha kama kampuni tunaendelea kuwafikia wateja kokote walipo, hata vijijini.”

Akieleza zaidi kampuni ya Oryx inajali usalama na katika kituo hicho wametumia teknolojia ya juu  huku akisisitiza pia wanazingatia ubora wa bidhaa zao na Oryx ndio kampuni pekee yenye maabara ya kupima ubora wa bidhaa zao ili kuhakikishia wateja wanapoweka mafuta katika vyombo vya moto yanakuwa yamezingatia ubora.

Mtafya amesema pia kama Serikali inavyoendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji ndio maana unaona na wao wanaendelea kukua kwa panua huduma na sio Dar es Salaam tu bali na mikoani. 

“Mazingira yaliyowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Nishati wawekezaji tunapata msaada mkubwa wa kupanua wigo wa kusogeza huduma karibu na wananchi, katika sekta ya nishati tunaona Waziri wa Nishati anavyoendelea kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya nishati .

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa CDT Oil na CDT Energies Boniphace Nasibu ambaye ndio msimamizi wa kituo hicho katika biashara ya mafuta,vilainishi pamoja na gesi amesema wameangalia jamii inayozunguka eneo hilo na kuona kuna kila sababu ya kusogeza huduma.

“Kituo chetu kipo karibu Madale ambako kuna mashamba ya jeshi,kiwanda cha saruji cha Wazo pamoja na watu wa eneo la Wazo na kwa ujumla tumejiridhisha hapa ni sehemu sahihi ya kuwahakikishia wananchi kupata mafuta na gesi ya kupikia.”

Amewahakikishia wateja wao watapata huduma zote zinazostahili ili wafurahie huduma za Oryx zinazopatikana huku akiishukuru oryx kwa kufanikisha uwepo wa kituo hicho.

Wakati huo huo akizungumza kwa niaba ya wananchi wa eneo la Wazo Sheikh Amani Hamis amesema kufunguliwa kwa kituo hicho mbali ya kusogeza huduma za nishati ya mafuta pamoja na gesi pia imewezesha vijana wa eneo hilo kupata ajira kupitia kituo hicho.

Amesema pia anaishukuru Serikali kwa kutoa fursa kwa wawekezaji kuja kuwekeza nchini na hivyo wawekezaji hao kuwezesha wananchi wa Watanzania kunufaika na uwekezaji huo.


Balozi wa Tanzania nchini China, Dkt. Suleiman Haji Suleiman, ameendelea na ziara yake inayolenga kukutana na wakuu wa vyuo vikuu mbalimbali nchini China ikiwemo Chuo cha Hong Kong Polytechnic University (HKPU) ambapo amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa chuo hicho, Prof Daniel Shek.

Aidha, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa shule za Biashara, Sayansi na Uhandisi na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa kitaaluma kati ya Chuo cha Hong kong polytechnic na Chuo Kikuu cha Sayansi cha Nelson Mandela (NM-AIST) cha jijini Arusha nchini Tanzania.

Balozi Dkt. Haji amesema kupitia ushirikiano huo, HKPU imeonesha utayari wa kusaidia wanafunzi wa Tanzania kupata maarifa na uzoefu wa kimataifa katika maeneo ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), Sayansi, Utafiti, Teknolojia na Uhandisi ambayo ndiyo nguzo muhimu za maendeleo katika dunia ya sasa pamoja na kutoa mafunzo kwa vitendo (Internship) kwa kipindi cha miezi sita hadi mwaka mmoja.

"Pamoja na mambo mengine, ushirikiano huu wa Tanzania na China katika Sekta ya Elimu, utahusisha programu maalumu za kukuza vipaji vya wanafunzi katika nyanja za Sayansi na Teknolojia, Uhandisi na Hisabati, hatua ambayo itasaidia kuandaa kizazi chenye uwezo wa kushindana katika uchumi wa maarifa na ajira za kimataifa," amesema.








Na Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma

Serikali imeagiza Jeshi la Polisi pamoja na Madawati ya Jinsia nchini kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria, ikiwa ni pamoja na ushoga, ukahaba na uendeshaji wa madanguro.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, alipokuwa akizungumza Bungeni, ambapo amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16, inayobainisha makosa mbalimbali ya jinai yanayohusiana na makosa ya kijinsia na uendeshaji wa biashara haramu za ngono.

Amesema vifungu vya 139 hadi 147 vya sheria hiyo vinaeleza wazi makosa yanayohusiana na vitendo hivyo, na kwamba mamlaka husika zitaendelea kuchukua hatua mara pale ushahidi wa kutosha utakapopatikana.

Aidha, Waziri Katambi ametoa onyo kwa watu wanaojihusisha na uendeshaji wa madanguro na shughuli za ukahaba, akibainisha kuwa sheria inakataza kumiliki au kunufaika na mapato yatokanayo na biashara hiyo pamoja na kushiriki kwa namna yoyote ile.

Kwa upande wake, Mbunge wa Katavi, Thomas Maganga, alihoji kauli ya Serikali kuhusu kuongezeka kwa matukio ya vitendo vya ushoga katika baadhi ya maeneo ya makazi, akidai kuwa hali hiyo imeanza kujitokeza katika baadhi ya kata na mitaa licha ya uwepo wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, alieleza kuwa vitendo vya ushoga ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za Tanzania, na wahusika wanapaswa kuchukuliwa hatua stahiki za kisheria.

Amesema mchakato wa kushughulikia makosa hayo unahusisha uthibitishaji wa tuhuma, uchunguzi wa kina, upelelezi wa kina wa vyombo vya dola, na hatimaye kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa taratibu za sheria.

KATAMBI amesitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa wahalifu wote wanaobainika kutenda makosa ya jinai wanachukuliwa hatua sawa na wengine wote bila upendeleo, kwa mujibu wa sheria za nchi.



Top News