Vyama 12 Vimepongeza ripoti ya tume ya kuchunguza matukio ya tarehe 29 na baada ya uchaguzi iliyowasilishwa na Jaji Chande.

Katika mkutano huo Mhe Doyo alipongeza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kukubaliana na mapendekezo yote yaliyopendekezwa na tume hiyo, aidha Mhe.Doyo amesisitiza pendekezo namba nne na pendekezo namba tano mamlaka husika wayafanyie kazi haraka kuondoa mzozo uliopo wa kisiasa hapa nchini.









Na Pamela Mollel,Arusha .

Katika kuendeleza misingi ya uongozi na ushirikiano wa kikanda, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imefanya makabidhiano ya nafasi ya Katibu Mkuu, ambapo Veronica Nduva amekabidhi madaraka kwa mrithi wake Stephen Patrick Mbundi katika hafla iliyofanyika kwenye makao makuu ya jumuiya hiyo jijini Arusha.

Makabidhiano hayo yamehitimisha rasmi kipindi cha uongozi wa Nduva, aliyeliongoza taasisi hiyo kwa msisitizo wa kuimarisha mshikamano wa nchi wanachama na kusukuma mbele ajenda za maendeleo ya kikanda, hususan katika nyanja za uchumi na ushirikiano wa kimkakati.

Katika kipindi chake cha uongozi, hatua mbalimbali zimechukuliwa katika kuimarisha utekelezaji wa miradi ya pamoja, kukuza biashara ndani ya ukanda na kuweka mazingira rafiki ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Aidha, ameweka msisitizo mkubwa katika umuhimu wa kuendelezwa kwa mshikamano miongoni mwa nchi wanachama, akieleza kuwa mafanikio yaliyofikiwa yanahitaji kulindwa na kuendelezwa kupitia ushirikiano wa karibu wa wadau wote wa maendeleo ndani ya EAC.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu mpya Balozi Mbundi ameanza majukumu yake kwa kueleza dhamira ya kuharakisha utekelezaji wa ajenda kuu za jumuiya, akitaja vipaumbele vya kuimarisha soko la pamoja, kukuza biashara ya ndani ya ukanda na kuongeza ufanisi wa taasisi zake.

Ameeleza kuwa atahakikisha kunakuwepo usimamizi thabiti wa rasilimali, uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa majukumu ya jumuiya, huku akihimiza ushirikiano wa karibu kati ya nchi wanachama katika kukabiliana na changamoto zilizopo.

Mabadiliko hayo ya uongozi yanakuja katika kipindi ambacho EAC inaendelea kupanuka na kuimarisha nafasi yake kikanda na kimataifa, hali inayoweka matarajio makubwa kwa uongozi mpya katika kusukuma mbele ajenda ya ujumuishaji wa kikanda na ustawi wa wananchi wake.







Na Mwandishi Wetu


Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.

Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gesi, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.

Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.

“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gesi inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.

Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gesi, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.

Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gesi ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.

Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.

Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gesi, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.

Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gesi ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.

Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gesi ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.

MKURUGENZI wa Kituo Cha Ubia Kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) David Kafulila amesema Muungano wa Tanzania ni wa kipekee barani Afrika kwa kuwa umejengwa juu ya misingi ya watu, na si serikali pekee.

Kupitia ukurasa wake wa X, Kafulila amesema Tanzania inaadhimisha miaka 62 ya Muungano ambao ni wa mataifa mawili huru barani Afrika uliofanikiwa kudumu kwa zaidi ya miongo sita.

Alitolea mifano ya miungano mingine barani Afrika iliyovunjika ndani ya muda mfupi, ikiwemo ule wa Ethiopia na Eritrea (1952-1962), Ghana-Guinea-Mali (1958-1963), na Senegambia (1982-1989).

Siri ya Mafanikio: Udugu na Utamaduni
Kafulila alieleza kuwa tofauti na miungano mingi ya Ulaya kama Umoja wa Ulaya au ya Asia ambayo inategemea zaidi makubaliano ya kiuchumi na kibiashara, Muungano wa Tanzania ulijengwa juu ya misingi imara ya udugu wa damu, lugha ya Kiswahili, na historia ya pamoja ya kijamii.

Jambo hilo, alisema, linaoufanya Muungano wa Tanzania kuwa na umoja wa watu zaidi kuliko umoja wa serikali pekee.

Alimalizia ujumbe wake kwa kusema: Tutazidi kuwakumbuka Nyerere na Karume siku zote kama hii.

Ujumbe huo umechapishwa ikiwa ni siku ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa Aprili 26, 1964.

 

Na Mwandishi wetu, Dodoma

Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) kimeitaka Serikali kuimarisha utawala bora na mifumo ya kisheria ili kuhakikisha utekelezaji wenye mafanikio wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Hayo yameelezwa katika andiko la ushauri kuhusu siasa na sheria lililowasilishwa serikalini, likilenga kuchambua changamoto za kisiasa na kisheria zinazoweza kuathiri maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa THTU Taifa, Dk. Paul Loisulie, utawala bora ni msingi muhimu wa maendeleo endelevu na unapaswa kuimarishwa katika ngazi zote.

Alisema pamoja na Tanzania kuwa na mfumo mzuri wa kikatiba na kisheria, bado kuna changamoto ya utekelezaji wa sheria hizo kwa vitendo, hali inayodhoofisha uwajibikaji na ufanisi wa taasisi za umma.

“Ni muhimu kuziba pengo la utekelezaji wa sera na sheria ili kuhakikisha haki, uwazi na ushiriki wa wananchi vinaimarika,” alisema.

THTU imebainisha changamoto mbalimbali ikiwemo masuala ya haki za binadamu, uhuru wa taasisi, ushiriki mdogo wa wananchi na uwepo wa rushwa ya kimfumo.

Katika mapendekezo yake, chama hicho kimeitaka Serikali kufanya marekebisho ya kisheria na kisera, kuimarisha taasisi za umma, pamoja na kuongeza ushiriki wa wananchi katika maamuzi ya maendeleo.

Chama hicho kimesisitiza kuwa bila utawala bora, utekelezaji wa Dira 2050 hautaweza kufikiwa kwa ufanisi.

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anafanya ziara katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6

Pia Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.










WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameshiriki ibada ya Jumapili, leo, Aprili 26, 2026, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Usharika wa Azania Front, jijini Dar es Salaam.

Ibada hiyo iliongozwa na Katibu wa Umoja wa Utume wa Injili (United Evangelical Mission - UEM) Kanda ya Afrika, Dkt. Ernest Kadiva, kwa kushirikiana na Mchungaji Kiongozi wa KKKT Usharika wa Azania Front, Victor Makundi.










-ASISITIZA MALEZI BORA KWA WATOTO KWA MANUFAA YA TAIFA

-APONGEZA JUKWAA LA TUZO ZA MALKIA WA NGUVU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameiasa jamii kukemea na kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji vinavyofanywa kwa wanawake hususani katika mitandao ya kijamii.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa kilele cha Tuzo kwa wanawake waliofanya vizuri katika sekta mbalimbali maarufu “Malkia wa Nguvu” kanda ya kati, zilizofanyika katika Ukumbi wa Mabele mkoani Dodoma. Amesema udhalilishaji huo unapaswa kukemewa na kila Mtanzania ili kusimamia heshima ya mwanamke katika jamii.

Makamu wa Rais amesema ni vema watanzania wote kuona wajibu wa kuilinda heshima ya mwanamke na kuwapima wanawake kwa majukumu yao yanayoleta maendeleo kwa Taifa. Amewasihi kipekee wanawake, kuacha tabia ya kushangilia katika mitandao ya kijamii hususani anapodhalilishwa mwanamke mwenzao.

Halikadhalika, Makamu wa Rais ametoa rai kwa Wanawake nchini kwa kushirikiana na jamii kwa ujumla kuchukua hatua katika kukabiliana na mmomonyoko wa maadili kwa watoto. Amesema imekuwepo tabia ya watoto kujiingiza katika matumizi ya mitandao ya kijamii ambayo imekuwa ikiwekwa maudhui yasiyofaa hivyo kuharibu maadili na kuhatarisha kizazi cha sasa na kijacho.

Makamu wa Rais amesema Serikali itaendelea kusimamia mambo yatakayoleta mabadiliko kwa wanawake ikiwemo kuendeleza majukwaa ya uwezeshaji ikiwemo mpango wa 2022-2032 na kusimamia mfuko wa maendeleo ya wanawake ambao unahusika na ukopeshaji.

Pia amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga maendeleo ya nchi kuinua ajira na kutengeneza fursa pamoja na kuzingatia nafasi ya mwanamke katika ujenzi wa Taifa. Ametoa wito kwa Jukwaa la Malkia wa Nguvu kushiriki kikamilifu katika kutoa elimu na hamasa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Makamu wa Rais amewapongeza wanawake katika kuendelea kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Taifa na shughuli za maendeleo kwa ujumla. Amesema nia ya Serikali kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ni kujenga Taifa lenye nguvu kwa kujengea uwezo watu wake kwa kuzingatia usawa katika jamii.

Makamu wa Rais amelipongeza Jukwaa la Malkia wa Nguvu kwa kusimamia kwa kutimiza miaka kumi kwa mafanikio, ambapo limefanya jitihada za pekee kubainisha fursa kwaajili ya wanawake na kuwahamasisha kuzitumia fursa hizo.

Makamu wa Rais amesema Serikali inavutiwa na malengo ya Taasisi inayosimamia Jukwaa la Malkia wa Nguvu husuani lengo kuu la kumuinua wanawake na kuwafanya kuwa wajasiriamali, wabunifu na viongozi.

Katika Kilele cha Tamasha hilo la Malkia wa Nguvu kanda ya kati, wanawake mbalimbali wamepata tuzo kwa kutambua mchango wao katika sekta mbalimbali ikiwemo ujasiriamali, ubunifu, utumishi wa umma na uongozi.

















LEO Katika uwanja wa Estadio de Vallecas unaowaka moto kwa sauti za mashabiki, Rayo Vallecano wanaikaribisha Real Sociedad kwenye pambano lenye mwelekeo tofauti.

Kwa Rayo, kila pointi ni swala la kuukimbia ukanda wa kushuka daraja wamekwama kwenye matokeo machache na sasa wanatafuta ukombozi nyumbani.

Kwa upande mwingine, Real Sociedad wanaangalia juu kuelekea Uropa wakijua kuwa ushindi wa ugenini unaweza kuwafungulia mlango wa kuingia kwenye Kombe la UEFA.

Rayo wana silaha za kasi kama Álvaro García na Isi Palazón wanaweza kuwapasua ulinzi wowote kwa mbio za pembeni, lakini madhaifu yao yapo nyuma. Makosa ya mtu mmoja yanatosha kubadilisha mchezo mzima, na kipa wao hana ushupavu wa kutosha.

Kinyume chake, Sociedad chini ya Matarazzo Pellegrino ni timu inayojiamini Mikel Oyarzabal anaongoza mstari wa mbele, huku Soler Carlos akitawala kiungo kwa utulivu na usahihi wa pasi. Lakini safari zao ugenini si nzuri kila wakati, na majeruhi yamewanyima wachezaji muhimu kama Guedes Goncalo, Zubeldia Igor na Odriozola Alvaro

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Hakuna timu inayopendelewa kwenye dimba la Vallecas Rayo wamewahi kuwafunga Sociedad nyumbani kwa ushindi wa kusisimua. Leo, rekodi inaweza kuvunjika kwa uamuzi mmoja wa kimkakati au kwa kosa moja tu. Ikiwa Rayo watashambulia bila woga, tunaweza kupata mabao; lakini wakijiruhusu kuvutwa kwenye mpira wa kudhibitiwa na Sociedad, basi usiku utakuwa mrefu kwa wenyewe kwa wenyewe.

Mwisho, mechi hii ni zaidi ya pointi tatu—ni chungu cha kujithibitisha. Ushindi kwa Rayo utakuwa ni ukombozi na uthibitisho kuwa wanaweza kushindana na wakubwa. Kwa Sociedad, ushindi wa ugenini unawakaribisha tena kwenye ndoto za Ulaya. Jisajili
-Awatoa hofu Watanzania wanaohofia upungufu wa dawa kutokana na mzozo mashariki ya kati

Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MKURUGENZI Mkuu wa Bohari ya Dawa(MSD) Mavere Tukai amewahakikishia Watanzania kuwa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini uko imara kwani kuna akiba ya kutosha kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita, licha ya kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, ameyasema hayo katika kikao kazi kilichohusisha wahariri na waandishi wa habari walipokutana kujadili masuala mbalimbali katika sekta ya afya na hasa mchango wa MSD katika kuendeleza jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba unakuwa wa uhakika nchini.

Hivyo ametumia kikao hicho kuwatoa wasiwasi miongoni mwa wananchi kuhusu uwezekano wa kupungua kwa dawa na vifaa tiba, hasa kutokana na athari zinazoweza kusababishwa na mvutano wa kijeshi kati ya Marekani na Iran.

“MSD imejipanga vyema kuhakikisha upatikanaji endelevu wa bidhaa hizo muhimu na tayari kuna tathmini inayoendelea kufanywa na timu maalumu ya wataalamu ili kubaini hatari zinazoweza kujitokeza na kuweka mikakati madhubuti ya kukabiliana nazo.”

Mkurugenzi Mkuu ameongeza juhudi zinaendelea kuimarishwa, hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi hauathiriki na mabadiliko ya hali ya usalama na uchumi wa kimataifa.

“Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa hali hiyo ili kuhakikisha huduma za afya nchini haziathiriki na wananchi wanaendelea kupata huduma bora bila usumbufu.










Top News