KAMPUNI ya Taifa Gas imetangaza kuwa haitapandisha bei ya gesi ya majumbani (LPG) licha ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo kwa takribani asilimia 43 katika soko la kimataifa, hatua inayolenga kulinda watumiaji dhidi ya athari za mabadiliko ya kiuchumi duniani.
Taarifa hiyo iliyotolewa leo Aprili 3, 2026 jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa ongezeko hilo la bei duniani limechangiwa na kupanda kwa gharama katika minyororo ya ugavi na usambazaji wa gesi ya kupikia katika wiki za hivi karibuni.
Akizungumza kupitia taarifa hiyo, Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Devis Deogratius, amesema licha ya changamoto hizo, kampuni imeamua kubeba gharama hizo ili kuhakikisha wateja wanaendelea kupata huduma kwa bei nafuu.
“Katika mazingira haya ya sasa, tunayo dhamira ya dhati ya kuwasaidia wateja wetu kwa kubeba athari za ongezeko la gharama ya nishati ya kupikia kwa kutokuongeza bei huku tukihakikisha upatikanaji endelevu wa gesi safi na ya kuaminika,” amesema Deogratius.
Amesisitiza kuwa uamuzi huo unalenga kusaidia shughuli za kiuchumi, hasa kwa kaya na biashara ndogo ndogo zinazotegemea gesi ya kupikia kama chanzo kikuu cha nishati.
Deogratius amebainisha kuwa Taifa Gas inaelewa umuhimu wa nishati hiyo kwa Watanzania wengi, hivyo itaendelea kuhakikisha inapatikana kwa bei nafuu bila kuathiri usambazaji wake.
Aidha, kampuni hiyo imehakikishia umma kuwa itaendelea kusambaza gesi yake kwa uhakika kupitia mtandao wake wa maghala 25 yaliyosambaa nchini, hatua inayolenga kufikia wateja wa mijini na vijijini.
"Uwekezaji uliofanywa katika miundombinu ya usambazaji unaiwezesha kampuni hii kuhudumia maeneo mbalimbali ya nchi kwa ufanisi zaidi na kuendelea kuunga mkono ajenda ya kitaifa na kimataifa ya nishati safi.
Aidha amesema wataendelea kufuatilia mwenendo wa soko la kimataifa na kufanya maamuzi yatakayolinda maslahi ya wateja huku ikidumisha ubora wa huduma zake.

Taarifa hiyo iliyotolewa leo Aprili 3, 2026 jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa ongezeko hilo la bei duniani limechangiwa na kupanda kwa gharama katika minyororo ya ugavi na usambazaji wa gesi ya kupikia katika wiki za hivi karibuni.
Akizungumza kupitia taarifa hiyo, Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Devis Deogratius, amesema licha ya changamoto hizo, kampuni imeamua kubeba gharama hizo ili kuhakikisha wateja wanaendelea kupata huduma kwa bei nafuu.
“Katika mazingira haya ya sasa, tunayo dhamira ya dhati ya kuwasaidia wateja wetu kwa kubeba athari za ongezeko la gharama ya nishati ya kupikia kwa kutokuongeza bei huku tukihakikisha upatikanaji endelevu wa gesi safi na ya kuaminika,” amesema Deogratius.
Amesisitiza kuwa uamuzi huo unalenga kusaidia shughuli za kiuchumi, hasa kwa kaya na biashara ndogo ndogo zinazotegemea gesi ya kupikia kama chanzo kikuu cha nishati.
Deogratius amebainisha kuwa Taifa Gas inaelewa umuhimu wa nishati hiyo kwa Watanzania wengi, hivyo itaendelea kuhakikisha inapatikana kwa bei nafuu bila kuathiri usambazaji wake.
Aidha, kampuni hiyo imehakikishia umma kuwa itaendelea kusambaza gesi yake kwa uhakika kupitia mtandao wake wa maghala 25 yaliyosambaa nchini, hatua inayolenga kufikia wateja wa mijini na vijijini.
"Uwekezaji uliofanywa katika miundombinu ya usambazaji unaiwezesha kampuni hii kuhudumia maeneo mbalimbali ya nchi kwa ufanisi zaidi na kuendelea kuunga mkono ajenda ya kitaifa na kimataifa ya nishati safi.
Aidha amesema wataendelea kufuatilia mwenendo wa soko la kimataifa na kufanya maamuzi yatakayolinda maslahi ya wateja huku ikidumisha ubora wa huduma zake.






















































