.jpeg)
.jpeg)
Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.
Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru ameongoza kikao cha kimkakati kilichojumuisha waheshimiwa Madiwani, Viongozi wa Mila, watendaji wa kata, wenyeviti wa Vijiji na watendaji wa vijiji kwa lengo la kudumisha mahusiano na uboreshaji wa huduma za kijamii na uboreshaji wa shughuli za Uhifadhi shirikishi.
Kamishna Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kikao hicho ni sehemu ya mkakati wa Mamlaka hiyo kukutana na makundi mbalimbali kujadili uboreshaji wa shughuli za kijamii na huduma za wananchi kama Maji, shule, Malisho, barabara, mawasiliano, afya na mengineyo.
"Viongozi na Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro ni wadau muhimu katika hifadhi, tunakutana nao kama sehemu ya kuboresha uhusiano na kuwaeleza mikakati ya Serikali dhidi yao.
kwa sasa tunaboresha miundombinu ya huduma za maji, ujenzi wa Barabara kwa tabaka gumu kutoka Loduare hadi Golini, kujenga minara mipya ya mawasiliano 9 ndani ya hifadhi ili kufikisha huduma kwa wananchi na wadau mbalimbali" amefafanua Kamishna Badru.
Kwa upande wa Viongozi waheshimiwa Madiwani, viongozi wa Mila wameiomba Serikali kupitia Mamlaka hiyo kuendelea kuboresha mahusiano, huduma za kijamii kama miundombinu ya Maji, barabara, ukarabati wa vituo vya afya na shule, mahitaji ya baraza la wafugaji, chunvi za mifugo na mpango wa malisho ya mifugo hawa wakati wa kiangazi.
Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma leo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000 tu, huku ada ya maombi ikiwa ni Sh10,000 pekee.Manyoni, Singida, Februari 12, 2026 — Ziara ya mafunzo ya wataalamu wa Idara ya Misitu Zanzibar imeingia siku ya pili leo kwa ujumbe huo kuanza rasmi mafunzo ya vitendo katika Shamba Darasa la Nyuki la TFS, wilayani Manyoni.
Mafunzo hayo yameanza kwa mada ya uanzishaji na usimamizi bora wa Hifadhi za Nyuki (Bee Reserves) iliyowasilishwa na Askari wa Uhifadhi – Ufugaji Nyuki Wilaya ya Manyoni, Jacline Leshabari, akieleza hatua za kisheria, kiutawala na kiikolojia zinazohitajika katika kuanzisha na kulinda maeneo maalum ya nyuki.
Akiwasilisha mada hiyo, Leshabari amesema hifadhi za nyuki zimekuwa nyenzo muhimu si tu katika kuongeza uzalishaji wa asali na mazao yatokanayo na nyuki, bali pia katika kulinda misitu na bioanuai. “Usimamizi madhubuti wa hifadhi hizi unahakikisha upatikanaji endelevu wa malighafi za nyuki huku ukihifadhi mfumo wa ikolojia,” amesema.
Kwa mujibu wa ratiba ya mafunzo, wataalamu hao kutoka Zanzibar wanatarajiwa pia kujionea kwa vitendo utambuzi wa maeneo ya hifadhi, uwekaji wa mizinga ya kisasa, pamoja na mbinu za kushirikisha jamii katika kulinda na kunufaika na rasilimali za nyuki.
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu Zanzibar, Said Juma Ali, amesema mafunzo ya siku ya pili yamewapa mwanga mpana juu ya namna TFS inavyounganisha uhifadhi na uchumi wa jamii kupitia sekta ya nyuki. Amesisitiza kuwa uzoefu huo utasaidia Zanzibar katika mpango wake wa kuanzisha hifadhi za nyuki na kuendeleza utalii wa nyuki.
Ziara hiyo ya siku tano inatarajiwa kuendelea kwa mafunzo zaidi kuhusu uchakataji wa asali, viwango vya ubora na masoko, huku ushirikiano kati ya TFS na Idara ya Misitu Zanzibar ukitajwa kuwa kichocheo cha mageuzi ya sekta ya nyuki nchini.
Dkt. Komba amesema hayo leo Februari 12, 2026 katika zoezi la ugawaji wa vitabu vya Amali kwa wakuu wa shule zote Tanzania Bara ambazo zinatoa Elimu ya Sekondari katika mkondo huo.
Amesema, mwaka 2024 Serikali ilianza kutekeleza Mtaala uliobereshwa ambao umegawanyika katika mkondo wa Amali na mkondo wa jumla, huku akisisitiza mkondo wa Amali lengo lake ni kujenga Elimu ujuzi kwa mwanafunzi.
Sambamba na ugawaji wa vitabu vya Amali, Dkt. Komba amesema, TET imetoa mafunzo kwa wakuu wa shule wote kuhusu maboresho yaliyofanyika kwenye Mtaala hasa katika mkondo wa Amali, pamoja na namna kutumia Maktaba mtandao ambapo vitabu vyote hupatikana.
Aidha, Dkt Komba amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizosaidia upatikanaji wa vitabu nchini, hasa vitabu vya Amali ambavyo vinagawiwa bure kwa shule zote nchini za Serikali na za binafsi.
Nae, Meneja uchapaji na usambazaji wa vitabu Taasisi ya Elimu Tanzania Bw. Emmanuel Stanslaus ametoa wito kwa walimu kuhakikisha wanatua vitabu hivyo kwa usahihi ili vilete tija kwa wanafunzi kulingana na fani wanazosoma.
Kwa upande wake Mkuu wa shule ya ufundi Nzega na Makamu Mwenyekiti wa wakuu wa shuke Tanzania Bara Mwl. Mwanakombo Juma Martin amesema vitabu hivyo vilivyotolewa bure kwa shule za Serikali na binafsi vitasaidia katika ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi hivyo kuleta tija katika utekelezaji wa Mtaala ulioboreshwa mkondo wa Amali.
Nae, Mkuu wa shule ya Ufundi ya wavulana Bwiru iliyopo Mkoani Mwanza Mwl. Thomas Werema amesema Elimu ya Amali inaenda kuwa Mkombozi kwa vijana wa Tanzania, kwani hutoa fursa kwa mw anafunzi kujiajiri, kuajiriwa au kuajiri wengine pindi amalizapo masomo yake, hivyo kusaidia kukabiliana na changamoto ya ajira nchini.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)














.jpeg)





.jpeg)










.jpeg)




