AFISA Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa PSSSF Bw.Alex Bwanakunu (kulia) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea Banda la PSSSF kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika uwanja wa Nyamhongolo Jijini Mwanza Agosi 2,2026


Dodoma, Agosti 2, 2026

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unashiriki katika Maonesho ya Nanenane 2026 kwa kutoa huduma mbalimbali na elimu kuhusu Hifadhi ya Jamii kwa wanachama wake na wananchi kupitia mabanda yake yaliyopo katika kanda tano nchini, ikiwemo Zanzibar.

Msanii maarufu nchini ,Mrisho Mpoto (wa pili kushoto) akiwa ameshika mkanda ,moja ya bidhaa zinazozalishwa katika kiwanda cha KLICL,Kinachomilikiwa na PSSSF kwa ushirikiano na Jeshi la Magereza ,alipotembelea Banda la Mfuko wa PSSSF kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026,kushoto ni Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Mfuko wa PSSSF Bw.Abdul Njaidi na kulia ni Afisa Mauzo kiwanda cha KLICL ,Bi,Mary Muna

Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano Mkuu wa Mfuko wa PSSSF, Bw. Abdul Njaidi, PSSSF imeshiriki maonesho hayo katika Kanda ya Kati viwanja vya Nanenane mkoani Dodoma, ambako Maonesho ya Nanenane 2026 yanafanyika kitaifa na tayari yamezinduliwa na Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Agosti 1, 2026. Kaulimbiu ya mwaka huu ni ‘Tambua Soko; Ongeza Tija na Thamani ya Kuelekea Dira 2025’.

Wanachama wa Mfuko wa PSSSF wakihudumiwa kwenye Banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti2,2026

Katika maonesho ya mwaka huu, PSSSF inashiriki; Zanzibar katika viwanja vya Dole, Kanda ya Magharibi mkoani Tabora katika viwanja vya Ipuli Mnadani, Kanda ya Ziwa jijini Mwanza katika viwanja vya Nyamhungolo, Kanda ya Kusini mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini jijini Mbeya, viwanja vya Nanenane.


Afisa Matekelezo wa Mfuko wa PSSSF Bi.Esther Mpemba (kulia ) akimuunganisha Mwanachama wa PSSSF ,Bi.Maliasa Sajoho na Mfumo wa PSSSF Member Portal ambao unamuwezesha kupata huduma za mfuko Kidijitali,kwenye maonesho ya Nanenane Viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 2,2026

"Tunawakaribisha wanachama wetu na wananchi wote kutembelea mabanda ya PSSSF katika kanda hizo ili kupata huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu kuhusu mafao, kuhakiki taarifa zao na michango, pamoja na kuwaunganisha katika huduma zetu za kidijitali, huku tukiwahakikisha kesho ya uhakika wanachama wetu’" alisema Bw. Njaidi

Afisa Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa PSSSF ,Bi .Saluna Ally (kushoto) akimuhudumia Mstaafu anayepokea Pensheni PSSSF ,Bw.Mwakibete G.Kasilati,kwenye banda la mfuko huu katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwenye viwanja vya Nanenane Jijini Mbeya,Agosti 2,2026

Aidha, watakaotembelea kwenye mabanda ya PSSSF watapata nafasi ya kuona fursa za uwekezaji wa Mfuko ambazo ni pamoja na bidhaa za ngozi zinazotengenezwa na Kiwanda cha KLICL na nyama kutoka machinjio ya Kimataifa ya Nguru.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika viwanja vya Nzunguni Jijini Dodoma Agosti 1,2026



Meneja wa PSSSF Kanda ya Magharibi Bw.Eliadi Mndeme akitoa elimu kwa mwanachama wa PSSSF wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi ambayo yanafanyika viwanja vya Ipuli mkoani Tabora Agosti 2,2026
Benki ya Exim Tanzania na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) leo wamezindua rasmi ushirikiano wao wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026, wakithibitisha dhamira yao ya pamoja ya kuendelea kuandaa kizazi kijacho cha wabunifu, watafiti na watatuzi wa changamoto kupitia sayansi, teknolojia, ubunifu na utafiti.

Ushirikiano huu unafikisha mwaka wa sita mfululizo tangu Benki ya Exim Tanzania ilipoanza kuunga mkono Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), jambo linalodhihirisha dhamira ya Benki ya kuwekeza katika elimu, ubunifu na maendeleo ya vijana, huku ikichangia maendeleo ya muda mrefu ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania (Exim Tower) jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza, alisema ushirikiano huo unaakisi imani ya Benki kuwa kuwawezesha vijana ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye ubunifu, ushindani na maendeleo endelevu kupitia falsafa yao ya “Ubunifu ni maisha”.

"Exim Bank Tanzania tunaamini kuwa ubunifu huanza kwa kuwawezesha vijana. Ushirikiano wetu na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) unaonesha dhamira yetu ya kuwaunga mkono wanafunzi wenye udadisi, ubunifu na ari ya kutafuta suluhisho zinazoweza kubadilisha jamii na kuchangia maendeleo ya taifa”. alisema D'Souza.

"Kwa miaka sita sasa, YST imekuwa mshirika wetu muhimu katika kuwaibua na kuwawezesha vijana wenye fikra bunifu kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kutatua changamoto zinazoikabili jamii. Tunaamini kuwa kwa kuwekeza katika elimu, ubunifu na maendeleo ya vipaji vya vijana leo, tunajenga msingi imara wa maendeleo endelevu ya Tanzania”. Aliongeza D’Souza

Programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya kwa kupokea jumla ya mawasilisho 1,330 ya miradi kutoka shule 287 za sekondari zilizopo katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya mchakato wa tathmini na ulezi wa kitaalamu uliofanywa na washauri wa sayansi wa YST, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya taasisi ya wanasayansi chipukizi yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Ukumbi wa maktaba mpya, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumzia ushirikiano huo, Mwanzilishi Mwenza wa taasisi ya wanasayansi chipukizi Tanzania, Dkt. Gozbert Kamugisha, aliishukuru Benki ya Exim Tanzania kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu katika kuwawezesha vijana wabunifu nchini.

"Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Benki ya Exim Tanzania kwa msaada wake endelevu katika kipindi cha miaka sita iliyopita.Kilichoifanya programu ya mwaka huu kuwa ya kipekee ni kwamba Benki ya Exim Tanzania haijajikita tu katika kutoa udhamini wa kifedha, bali pia imekuwa sehemu ya utekelezaji wa programu. Kupitia wataalamu wake, Benki imeungana nasi kutembelea shule mbalimbali, kukutana na walimu na wanafunzi, pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu unaowasaidia kuboresha tafiti na ubunifu wao ili kupata suluhisho zenye tija kwa jamii," aliongeza Dkt. Kamugisha

Katika hatua nyingine, Dkt. Gozibert Kamugisha alibainisha baadhi ya changamoto zinazoikabili YST, ikiwemo uhaba wa rasilimali fedha unaozuia kuwafikia vijana wote wenye vipaji na mawazo bunifu, pamoja na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.

“Bado jamii haijaelewa vya kutosha kwamba kama taifa hatuwezi kufikia maendeleo tunayoyataka bila kuwekeza kwa dhati katika vijana wetu, hususan katika sayansi, teknolojia na ubunifu. Tukitazama mataifa yaliyopiga hatua, yamewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuwawezesha vijana kufanya utafiti, ubunifu na ugunduzi. Serikali imeweka sera na mazingira mazuri ya kuhamasisha ubunifu, sasa ni wajibu wetu kuungana na kuhakikisha vijana wetu wanapata fursa za kutimiza ndoto zao na kuchangia maendeleo ya Taifa.” Aliongeza Kamugisha

Kwa zaidi ya miaka 16, taasisi ya wanasayansi chipukizi Tanzania (YST) imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu kupitia programu za mafunzo na uhamasishaji, zikiwawezesha kutambua changamoto zinazozikabili jamii na kubuni suluhisho zinazotekelezeka na zenye kuendana na mazingira ya Tanzania.

Ushirikiano wa Exim Bank unaimarisha dhamira hiyo kwa kuwaunga mkono vijana wanaobuni suluhisho katika maeneo mbalimbali, ikiwemo akili unde (Artificial Intelligence), kilimo na mifugo, uhifadhi wa mazingira, afya, usalama wa chakula, mawasiliano na ubunifu wa kijamii.

Ikiongozwa na falsafa yake ya "Ubunifu ni maisha", benki ya Exim Tanzania inaendelea kuunga mkono mipango inayofungua fursa kwa vijana wa Kitanzania na kuhamasisha ubunifu wa ndani. Kupitia ushirikiano wa kimkakati na YST, kwa zaidi ya miaka sita sasa toka mwaka 2021, Benki hiyo inaendelea kuwasaidia vijana kutumia elimu na maarifa wanayopata darasani kubuni suluhisho za changamoto halisi zinazoikabili jamii, huku ikikuza utamaduni wa utafiti, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo ya teknolojia.

Wakati maandalizi ya Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya mwaka 2026 yakiendelea, Benki ya Exim Tanzania na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wanaendelea kushirikiana kuwawezesha vijana wabunifu ambao mawazo, tafiti na ugunduzi wao vitachangia kujenga Tanzania yenye ubunifu zaidi, ushirikishwaji na ustawi endelevu.
Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam.

 Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania (Ex


 

Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.

Na.Mwandishi Wetu-Tabora

Wakuu wa Wilaya za Tabora, Mh. Upendo Wella, na Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua, wameipongeza EWURA kwa usimamizi mzuri wa huduma za nishati na maji nchini. Wametoa pongezi hizo walipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02.08.2026.

Viongozi hao wameitaka EWURA kuongeza hamasa kwa wananchi ili kubadili mtazamo na kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ili azma ya kufikia 80% ya watumiaji ifikapo 2034 itimie.

Aidha, wameisisitiza EWURA kuendelea kuhamasisha uwekezaji wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini, wakieleza kuwa huduma hiyo inahitajika kutokana na kushamiri shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magharibi, Mha. Karim Ally, alitumia fursa hiyo kueleza nafasi ya EWURA ya kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi (LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, ambapo kwa sasa ni 19 pekee.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magaharibi, Mha. Karim Ally(kushoto) akitoa maelezo ya majukumu yanayotekelezwa na Mamlaka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mh. Dkt. Rashid Chuachua(kulia) ikiwemo utoaji wa leseni na vibali vya ujenzi wa vituo vya mafuta, vituo vya CNG, utatuzi wa migogoro na malalamiko na nafasi ya EWURA katika kuweka mazingira wezeshi ya kupata wasambazaji wakubwa wa gesi ya mitungi ( LPG) katika eneo la Kanda ya Magharibi linalohudumia mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma, wakati kuongozi huyo alipotembelea banda la EWURA katika maonesho ya NaneNane yanayoendelea viwanja vya Ipuli, Tabora, leo 02/08/2026.

Meneja wa EWURA Kanda ya Magahribi, Mha. Karim Ally(kulia) akimweleza Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mh. Upendo Wella (kushoto), Mamlaka inavyoendelea kutoa elimu na kuhamasisha ujenzi wa vituo maeneo ya vijijini ambapo uhitaji bado ni mkubwa hususan katika maeneo ya pembezoni na hivyo kuendelea kuwepo uuzaji holela wa bidhaa za petroli, ambao ni hatari kwa afya, mazingira na maisha ya watu, wakati kiongozi huyo alipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya NaneNane, viwanja vya Ipuli, Tabora, leo, 02/08/2026.




Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Needpeace Wambuya, amepongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), hususan hatua ya kuanzisha mpango wa kuuza mifugo kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Akizungumza alipotembelea banda la WRRB katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea viwanja vya John Malecela jijini Dodoma leo Agosti 2, 2026, Wambuya amesema "Niwapongeze sana, kwa kazi nzuri mnayofanya, nimeona mpango wenu kuingiza mifugo kwenye Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, natumai mpo hatua nzuri kwasasa."

Kwa upande wake, Ofisa Leseni wa WRRB, Nasri Khea, amesema maandalizi ya mnada wa kwanza wa mifugo kupitia Mfumo huu yamefikia hatua za mwisho, huku mnada huo ukitarajiwa kufanyika hivi karibuni katika Wilaya ya Mvomero.

Amesema pia mfumo huo unakwenda kuingiza kuwezesha biashara za bidhaa mbalimbali ikiwamo Mwani na mahindi.
*Wananchi wakumbushwa kuchukua Amana zao zilizokuwa Benki ya FBME

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewataka wananchi kutembelea Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane ili kupata elimu kuhusu ulinzi wa amana zao na taratibu za kufidiwa fedha wanazoweka katika benki na taasisi za fedha zilizopewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akizungumza katika maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa DIB, Isack Kihwili, amesema wananchi wanapaswa kuhakikisha wanaweka fedha zao katika benki na taasisi za fedha zilizosajiliwa na kupewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania.

Amesema kufanya hivyo ni muhimu kwa kuwa kuweka fedha katika taasisi zisizo rasmi kunaweza kuwanyima wananchi haki ya kupata fidia endapo taasisi hizo zitashindwa kutekeleza majukumu yake au kushindwa kurejesha fedha za wenye amana.

Kihwili pia amewataka wenye amana katika iliyokuwa Benki ya FBME ambao bado hawajachukua fedha zao kujitokeza haraka ili kukamilisha mchakato wa malipo, akisema fedha zao bado zinawasubiri.

Amesema DIB imefikia hatua kubwa katika kulipa madai ya wenye amana wa benki hiyo, huku akibainisha kuwa ni asilimia ndogo tu ya walengwa ambao bado hawajajitokeza kuchukua fedha zao.

Kwa mujibu wa Kihwili, madai ya wenye amana wa FBME kwa upande wa Tanzania yalifikia takribani Sh bilioni 35, ambapo hadi sasa zaidi ya asilimia 85 ya fedha hizo tayari zimelipwa kwa walengwa.

Amesema bado kuna takribani watu 428 ambao hawajajitokeza kuchukua fedha zao zenye thamani ya karibu Sh bilioni nne, licha ya fedha hizo kuwa tayari zimetengwa kwa ajili yao.

“Tunawasihi wale ambao bado hawajajitokeza kuchukua fedha zao wafanye hivyo haraka, kwa sababu fedha hizo zimetengwa na zipo tayari kwa ajili ya malipo,” amesema.

Amefafanua kuwa baada ya kundi hilo kujitokeza na kulipwa fedha zilizotengwa kwa ajili yao, hatua inayofuata itakuwa ni kulipa asilimia 15 iliyobaki ili kuhakikisha kila mwenye amana anayestahili fidia analipwa madai yake kwa asilimia 100, kwa kuzingatia taratibu zinazotumika.


Aidha, Kihwili amesema bado kuna kundi la wadai wengine, wakiwemo baadhi ya wafanyakazi waliokuwa na madai yaliyofikishwa mahakamani, ambao malipo yao hayajahusishwa katika awamu inayoendelea kutokana na mchakato wa kufuatilia na kuhakiki mali za benki hiyo.

Amesema DIB inaendelea kufuatilia mali zilizobaki za benki hiyo ili kuhakikisha fedha za kutosha zinapatikana na kuwezesha kukamilishwa kwa malipo ya wadai hao kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imesema Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane ni fursa muhimu kwa wakulima kupata elimu na taarifa zitakazowasaidia kujiandaa kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2026/2027.

Akizungumza katika Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti Ubora wa TFRA, Happiness Mbelle, amesema wakulima wanapaswa kuhakikisha taarifa zao zimesajiliwa na kuhuishwa kwa wakati ili kuepuka changamoto wakati wa usambazaji wa mbolea.

Amesema mbolea inapatikana kwa kiasi cha kutosha, huku akiwataka wakulima kushirikiana na maafisa ugani katika kupima udongo ili kubaini mahitaji sahihi ya mbolea kulingana na aina ya mazao na hali ya udongo.

“Mkulima anapaswa kushirikiana na maafisa ugani kupima udongo ili kubaini mahitaji ya mbolea. Hii itasaidia kutumia mbolea kwa usahihi na kuongeza tija katika uzalishaji,” amesema Mbelle.

Aidha, amesema maonesho hayo ni fursa kwa wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini kupata elimu kuhusu matumizi sahihi ya mbolea, pamoja na huduma na majukumu ya TFRA.

Amesema TFRA itaendelea kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwawezesha kuelewa majukumu ya mamlaka hiyo na kuhakikisha wanapata huduma bora zenye viwango.

Mbelle amewataka wakulima kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu na ushauri kutoka kwa wataalamu ili kuongeza ufanisi na tija katika shughuli za kilimo.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
BARAZA la Taifa la Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limesema Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane ni fursa muhimu ya kutoa elimu kwa wanafunzi na wahitimu wa vyuo vya kati vinavyotoa mafunzo katika fani za kilimo na mifugo kuhusu fursa za kujiajiri katika sekta hizo.

Akizungumza katika Maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, jijini Dodoma, Afisa Udhibiti Ubora wa NACTVET, Doris Chiwambo, amesema sekta ya kilimo ina fursa kubwa za ajira na kujiajiri, hivyo wahitimu wa fani za kilimo na mifugo wanapaswa kutumia ujuzi walioupata kuanzisha shughuli za uzalishaji.

Amesema wahitimu hao wanaweza kujiajiri kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji na utoaji wa elimu na huduma za kitaalamu katika sekta hizo.

“Sekta ya kilimo ina fursa nyingi za ajira na kujiajiri. Wahitimu wa fani za kilimo na mifugo wanaweza kutumia elimu na ujuzi walioupata kujiajiri katika kilimo, ufugaji na hata kutoa elimu kwa jamii,” amesema Chiwambo.

Aidha, amesema maonesho hayo ni fursa pia kwa wananchi wanaopanga kuanzisha vyuo vinavyotoa mafunzo ya kilimo, mifugo na uvuvi kupata elimu na maelekezo kuhusu taratibu na vigezo vya kuanzisha na kuendesha vyuo hivyo.

Chiwambo amesema NACTVET itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake, pamoja na kuhakikisha jamii inaelewa huduma zinazotolewa na baraza hilo ili kufanikisha lengo la kutoa elimu na mafunzo yenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Ameongeza kuwa ushiriki wa NACTVET katika maonesho hayo unalenga kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi, pamoja na fursa zinazopatikana kupitia taaluma za kilimo, mifugo na uvuvi.

 

MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 2,2026 kwenye banda la chuo hicho akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka,wakati wa Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela Nzuguni jijini Dodoma kwa niaba ya 

.....

MKUU wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha,Prof. Epaphra Manamba,amesema wanaendelea kuandaa wataalamu wenye ujuzi na uwezo wa kutumia teknolojia za kisasa katika uzalishaji, usimamizi na biashara ya mazao, hatua itakayochangia kuongeza tija, ushindani na thamani ya sekta ya kilimo nchini.

Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt.John Malecela Nzunguni jijini Dodoma, Mkuu wa Kampasi ya Dodoma wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Prof.Epaphra Manamba, akimwakilisha Mkuu wa Chuo, Profesa Eliamani Sedoyeka, amesema IAA imeamua kushiriki maonesho hayo ili kuwa karibu na wakulima, kutoa elimu na kuonesha mchango wa taaluma katika kuimarisha uzalishaji wa kilimo nchini.

Amesema sekta ya kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania kwa kuwa inategemewa na takribani asilimia 65 ya nguvu kazi ya Taifa, lakini bado mchango wake katika Pato la Taifa ni takribani asilimia 26 pekee, hali inayoonesha kuwa kuna nafasi kubwa ya kuongeza tija kupitia matumizi ya maarifa, teknolojia na usimamizi bora wa biashara.

"Kilimo kinahitaji nguvu kazi yenye ujuzi, ubunifu na maarifa ya kisasa. Ndiyo maana Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa programu mbalimbali za biashara, uchumi, fedha na teknolojia ili kuwajengea uwezo wataalamu watakaosaidia kuifanya sekta ya kilimo iwe yenye ushindani na yenye mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa," amesema Prof.Manamba.

Ameeleza kuwa pamoja na changamoto za mitaji zinazowakabili wakulima wengi pamoja na utegemezi wa zana duni za kilimo, bado kuna fursa kubwa ya kuongeza uzalishaji endapo wakulima wataunganishwa na taasisi za kifedha pamoja na huduma za kitaalamu zitakazowezesha upatikanaji wa mitaji na uwekezaji katika teknolojia za kisasa.

Prof.Manamba amesema IAA imejikita pia katika kufundisha teknolojia zinazoibukia ikiwemo Akili Unde (Artificial Intelligence - AI), ambapo wanafunzi wa chuo hicho tayari wamebuni mifumo inayotumia AI kuboresha uzalishaji wa mazao kama vitunguu kwa lengo la kuongeza tija, kupunguza gharama za uzalishaji na kuifanya kilimo kuwa biashara yenye faida zaidi.

"Hatutaki kuona kilimo kinabaki kwa ajili ya kujikimu pekee. Tunataka wakulima walime kwa mtazamo wa biashara, waongeze thamani ya mazao yao na kuongeza kipato cha familia zao pamoja na kuchangia zaidi katika uchumi wa Taifa," amsisitiza.

Akizungumzia kaulimbiu ya Nanenane ya mwaka huu isemayo "Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa 2050," Prof.Epaphra Manamba amesema dira hiyo inalenga kujenga nguvu kazi yenye ujuzi na maarifa inayoweza kuleta mapinduzi katika sekta mbalimbali za uchumi, hususan kilimo.

Amebainisha kuwa taasisi za elimu zina jukumu la kuhakikisha zinatoa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na mabadiliko ya teknolojia ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji na kuifanya Tanzania kufikia malengo ya maendeleo ya Dira ya Taifa 2050.

Amesema kupitia ushiriki wa Maonesho ya Nanenane, Chuo cha Uhasibu Arusha kinaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu programu zake mbalimbali na namna zinavyoweza kuwaandaa vijana kuwa wataalamu watakaochangia maendeleo ya kilimo, biashara na uchumi wa kidijitali nchini.

▪️Awataka watumishi kutimiza wajibu wao

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewahimiza watendaji wa Serikali kuwahudumia kikamilifu Watanzania ili miradi inayojengwa na Serikali itoe matokeo chanya.

“Tunachokijenga hapa, si jengo pekee, bali tunajenga mazingira bora ya utendaji wa mfuko. Kupitia uwekezaji huu tunachochea na tunaharakisha utekelezaji wa dhamira ya dhati aliyoionesha Mheshimiwa Rais kumsaidia mkulima mdogo kwa kuwezesha kupata mikopo.”

“Watumishi wote wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa bidii ili uwekezaji huu uwe na manufaa kwa Taifa. Tusiweke ofisi nzuri halafu huduma zikawa duni, tutakua hatujafikia malengo yaliyokusudiwa, ofisi nzuri lakini mwananchi akija kupata huduma anaambiwa njoo kesho, njoo kesho, majengo haya hayatakuwa na maana,” amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili Agosti 2, 2026) Iyumbu jijini Dodoma wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu ya ofisi za Mfuko wa Udhamini wa Pembejeo za Kilimo (AGITF).

Dkt. Mwigulu amesisitiza kuwa uwekezaji huo unaofanywa na Serikali katika utafiti wa kilimo ni mwelekeo sahihi wa mageuzi katika sekta ya kilimo. “Kuwekeza kwenye utafiti ni njia sahihi ya kufanya mageuzi katika sekta husika, tumetoka kufanya uzinduzi wa makao makuu ya taasisi yetu ya utafiti wa kilimo, na pembeni yake kuna jengo zuri la maabara ya kilimo, kuonesha jinsi Rais anamaanisha kwa dhati kufanya mageuzi katika kilimo.”

“Kwa nchi nyingine maabara ile ya kisasa ingekuwa kwenye moja ya chuo kikuu, lakini ile ni maabara ya wizara na ipo hapa makao makuu ya nchi,” ameongeza Waziri Mkuu.

Awali akiwa katika mji wa Serikali - Mtumba, kwenye halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi za makao makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Waziri Mkuu alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza uwekezaji jijini Dodoma hali iliyochochea ukuaji wa mkoa huo.

Dkt. Mwigulu ameongeza kuwa hatua hiyo ya Rais Samia imeenda sambamba na kuwaamini wakandarasi wazawa jambo lililowakuza wakandarasi hao.

“Mheshimiwa Rais aliweka imani kwao, akasema waacheni wajenge. Tumeona majengo na miradi ikimeremeta….nilipita katika miradi ya sekta nyingine, nikakuta madaraja yenye urefu wa ghorofa yamejengwa na wakandarasi wazawa, zaidi ya madaraja 81, sasa ukiangalia kwa jicho la kibinafsi utasema si ni yule mmoja tu ndiyo akapata mradi, lakini niwaambieni huo ni mzunguko wa uchumi wa ndani ya nchi, ndiyo maana mabenki yanapata wateja na yamepunguza mikopo chechefu,” amesisitiza Waziri Mkuu.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha wizara hiyo kupata bajeti ya kutosha kuendesha shughuli zake, ikiwemo kuwaongezea bajeti kila mwaka.














NA DENIS MLOWE - DAR ES SALAAM

VICTORIA Group (VG) imetangaza kuandaa mbio za afya za VG Fun Run zitakazofanyika Agosti 8, 2026 katika viwanja vya Victoria Park, Ununio jijini Dar es Salaam, zikiwa na lengo la kuhamasisha afya, kuimarisha mshikamano wa wanachama na kuwashirikisha wananchi katika mazoezi ya mwili.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati ya VG Fun Run, Isidori Msaki, alisema wazo la kuanzisha mbio hizo limetokana na ukweli kuwa Victoria Group imekuwa pamoja kwa zaidi ya miaka 26 na sasa wanachama wengi wamefikisha umri wa zaidi ya miaka 50, jambo lililowasukuma kuweka kipaumbele kwenye afya zao.

Alisema Victoria Group ina wanachama 113 ambao pamoja na familia zao wanafikia takribani watu 700, hivyo wameona ni muhimu kuanzisha shughuli ya pamoja itakayowahamasisha kufanya mazoezi na kuishi maisha yenye afya.

Msaki alisema mbio hizo zitahusisha kukimbia umbali wa kilomita 10 kuanzia saa 12:00 asubuhi, huku washiriki wote watakaomaliza wakitunukiwa medali na kuandaliwa huduma ya supu, wakati wadhamini wa tukio watapatiwa vyeti vya shukrani kwa mchango wao.

Alisema tukio hilo halitawahusu wanachama wa Victoria Group pekee, bali pia limefunguliwa kwa marafiki na wananchi wote wanaotaka kushiriki.

Msaki alisema washiriki kutoka nje ya Victoria Group watatakiwa kulipa shilingi 30,000 ambazo zitajumuisha fulana maalumu, namba ya ushiriki pamoja na medali baada ya kumaliza mbio.

Aliongeza kuwa kwa wale wasioweza kushiriki mbio za kilomita 10, waandaaji wameandaa programu maalumu ya mazoezi ya aerobics itakayofanyika katika Victoria Park chini ya wakufunzi wa mazoezi, sambamba na burudani ya muziki na shughuli nyingine za kijamii.

Msaki alisema hadi sasa zaidi ya washiriki 126 wamekwishajisajili, huku matarajio yakiwa kufikisha zaidi ya washiriki 200 kabla ya siku ya tukio.

Naye Mwenyekiti wa Victoria Group, Sabasaba Mushingi, alisema kikundi hicho kilianzishwa takribani miaka 26 iliyopita kwa lengo la kujenga mshikamano na kusaidiana katika nyakati za furaha na huzuni, lakini kadiri miaka ilivyokwenda wamepanua shughuli zao hadi kwenye uwekezaji wa kiuchumi.

Alisema kwa sasa Victoria Group inamiliki vitega uchumi mbalimbali ikiwemo Victoria Park yenye thamani inayokadiriwa kuzidi shilingi bilioni moja kwa tathmini ya sasa, pamoja na uwekezaji katika hati fungani za Serikali na hisa.
Mushingi alisema VG Fund Run ni mwanzo wa safari ya kulifanya tukio hilo kuwa moja ya mbio kubwa nchini, zitakazokuwa zikifanyika kila mwaka na kuvutia washiriki wengi zaidi kutoka ndani na nje ya Victoria Group.

Alieleza kuwa baada ya tathmini ya tukio la mwaka huu, uongozi unapanga kuliboresha zaidi ili katika miaka ijayo liwe na zawadi kubwa, washiriki wengi zaidi na pia liwe jukwaa la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia jamii kupitia miradi mbalimbali ya kijamii.

Aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi Agosti 8 katika Victoria Park, Ununio, kushiriki siku ya mazoezi, afya na burudani, akisisitiza kuwa lengo kuu la Victoria Group ni kujenga jamii yenye afya bora huku ikiendeleza mshikamano na utamaduni wa kusaidiana.







Top News