WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa wito kwa wazalishiaji mbalimbali nchini waboreshe bidhaa zao ili zimudu ushindani wa kimataifa na ziweze kushindana kila siku na siyo wakati wa maonesho tu.

“Bidhaa ambazo tuko nazo zisiwe kwa ajili ya maonesho, bali ndiyo iwe standard ya bidhaa zetu katika maisha yetu. Tukishafikia hatua hiyo, tutakuwa tumetatua mambo mengi kwa mpigo ikiwemo kujihakikishia kwamba bidhaa zetu zinapata soko, ni lazima tuendelee kuoanisha uzalishaji na vigezo vya kimataifa vya masoko,” amesema.

Waziri Mkuu amesema hayo leo (Jumamosi, Agosti Mosi, 2026) wakati akizungumza na mamia ya wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Wakulima (Nanenane), yaliyofunguliwa rasmi katika Viwanja vya Dkt. John John S. Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema kufanya hivyo kutawezesha bidhaa zinazozalishwa kupata masoko popote duniani kutokana na ubora utakaokuwa nazo. “Tutengeneze bidhaa zetu za kila siku kama vile za kwenda kwenye maonesho. Katika maeneo mengi, tatizo siyo soko bali ni viwango vinavyoweza kumsukuma mnunuzi kutamani kununua bidhaa husika. Tukiboresha viwango, bidhaa zitanunuliwa na kwa njia hiyo tutaongeza uzalishaji na hivyo kupata masoko na kuongeza uchumi wa mtu mmoja moja,” amesititiza.

Akielezea kuhusu utoshelevu wa chakula nchini, Waziri Mkuu amesema kuwa nchi ina utoshelevu kwa asilimia 130 na imeongeza mauzo nje ya nchi kwa asilimia 77 na kuwa moja ya chanzo cha uhakika cha fedha za kigeni.

“Haya ni mabadiliko yanayochangiwa na hatua za serikali ya awamu ya sita kwa kuweka mazingira wezeshi na uwekezaji wenye tija kwenye mnyororo mzima wa sekta ya kilimo. Tangu Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipoingia madarakani, wakulima wamewezeshwa ruzuku ya pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea, zaidi ya tani 700,000 yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.4,” amesema.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea mabanda mbalimbali ya maonesho na kupata maelezo kutoka kwa wajasiriamali wanaoshiriki maonesho hayo ambapo aliipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kuboresha huduma za kifedha na kuzisogeza karibu na wananchi hasa wakazi wa vijijini, vijana na wanawake.

Amesema amefurahishwa na jitihada za benki hiyo za kuwafikia wananchi kupitia huduma za kibenki zinazotolewa kwa kutumia magari maalumu pamoja na kuwafuata wafanyabiashara katika masoko na minada mbalimbali nchini.

“Hatua hizi zinaendana na kiu ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuona Watanzania wengi wanapata huduma za uchumi jumuishi wa kifedha (financial inclusion) na hii itasaidia nchi kuondoka kwenye cash economy, itafanya tufike mahali mtu popote alipo ana fedha yake, na hata akitaka mahitaji fedha anayo,” amesema.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuboresha mazingira ya sekta ya fedha, ikiwemo kupunguza gharama za miamala ya kifedha ili kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanapata huduma bora za kibenki na kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya uchumi.

Akitoa maelezo mbele ya Waziri Mkuu, Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali wa Benki ya NMB, Bibi Vicky Bishubo, alisema benki hiyo imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za kifedha kupitia mpango wa huduma za benki vijijini unaotumia magari maalumu ya huduma za kibenki (mobile branch operations) yanayofika katika vijiji mbalimbali nchini kutoa huduma za kifedha, elimu ya fedha pamoja na mikopo kwa wananchi hususan wanawake na vijana wajasiriamali.

Bibi Bishubo alisema pia Benki ya NMB inaendelea kushirikiana na Serikali kupitia Wizara yenye dhamana ya masuala ya vijana katika utekelezaji wa mpango wa mikopo wa sh. bilioni 200 ulioanzishwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuwawezesha vijana kiuchumi. Alisema benki hiyo imeweka mazingira rafiki na kupunguza vikwazo vinavyoweza kuwazuia vijana kunufaika na mikopo hiyo.

Aidha, alisema benki hiyo inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za elimu ya juu, ikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Dodoma kuandaa programu na mitaala inayolenga kuwaandaa vijana katika matumizi ya huduma za fedha za kidijitali na kuongeza uelewa wao kuhusu sekta ya fedha.

Maonesho hayo ya 33 ya Nanenane yenye hadhi ya Kitaifa na Kimataifa, yanaendeshwa kwa lengo la kukuza uchumi, kuongeza matumizi ya teknolojia bora na kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amelielekeza Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) kuendelea kusonga mbele katika kutekeleza dhamira ya Serikali ya kubadilisha sekta ya Uvuvi nchini kuwa ya kibiashara, akisisitiza kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali umeweka msingi imara wa kuiwezesha Tanzania kunufaika zaidi na rasilimali za uvuvi wa bahari kuu.

Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo Agosti 01, 2026, alipotembelea banda la TAFICO katika Maonesho ya Nanenane 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma, ambapo alipokea maelezo kuhusu shughuli na uwekezaji unaotekelezwa na Shirika kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TAFICO, CPA Shaibu Matessa.

Akizungumza mara baada ya kupokea maelezo hayo, Mhe. Dkt. Mwigulu alisema Serikali imeonesha kwa vitendo dhamira ya kuibadili sekta ya uvuvi kupitia uwekezaji wa kimkakati katika miundombinu na vitendea kazi.

"Kupitia uwekezaji huu wa vitendea kazi na miundombinu tunaiona dhamira ya Serikali kwa vitendo katika kuibadilisha sekta hii ya uvuvi iwe ya kibiashara basi niseme tuu Songeni mbele," alisema Waziri Mkuu.

Awali, CPA Matessa alimweleza Waziri Mkuu kuwa Serikali imeendelea kuandika historia katika sekta ya uvuvi kupitia uwekezaji mkubwa utakaoiwezesha TAFICO kupata meli za kisasa za uvuvi wa bahari kuu pamoja na ujenzi wa Bandari ya Uvuvi, ambayo itakuwa kitovu cha shughuli za uvuvi wa bahari kuu nchini.

"Mhe. Waziri Mkuu mpaka sasa Shirika lina meli moja ya uvuvi wa Bahari Kuu na uwepo wa bandari ya uvuvi ambao umekamilika hivi vyote ni vitendea kazi muhimu katika kuleta mapinduzi ya Sekta ya Uvuvi na kuwa ya kibiashara".Alisema CPA.Matessa

Mabadiliko haya ya kisekta yanalenga kuongeza mchango wake katika uzalishaji wa mazao ya uvuvi, uchakataji na kuimarisha mnyororo wa thamani kwa mazao ya uvuvi na kuongeza ajira kwa wanawake na vijana.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza na uongozi wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO)  alipotembelea banda la Shirika hilo katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba  akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TAFICO, CPA Shaibu Matessa alipotembelea banda la Shirika hilo katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe pamoja na Rais wa Jamhuri ya Angola Mheshimiwa João Manuel Gonçalves Lourenço kama ishara ya uzinduzi wa Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) iliyopo Kilamba, jijini Luanda, Angola, tarehe 01 Agosti, 2026. Kulia ni Mama Maria Nyerere, Mjane wa Baba wa Taifa akishuhudia tukio hilo. Hospitali hiyo imepewa jina la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kama heshima na ishara ya kutambua mchango wake katika harakati za ukombozi wa Bara la Afrika, hususan nchi za Kusini mwa Afrika, ikiwemo Angola.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Jamhuri ya Angola, Mheshimiwa João Manuel Gonçalves Lourenço, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na viongozi mbalimbali wakati wakifuatilia Makala Maalum ya Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) pamoja na Historia ya Baba wa Taifa kabla ya uzinduzi wa Hospitali hiyo iliyopo Kilamba, jijini Luanda, Angola, tarehe 01 Agosti, 2026.

Taswira ya Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) iliyopo Kilamba, jijini Luanda, nchini Angola.
Taswira ya Hospitali Kuu ya Rufaa ya Rais Julius Nyerere (Hospital dos Queimados Presidente Julius Nyerere) iliyopo Kilamba, jijini Luanda, nchini Angola.

Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Wakili na CPA Dkt.Michael Marere na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Dynamic Consulting (GDC)  Anne Massawe wakisaini hati za makubaliano katika hafla iliyofanyika Ofisi za GDC  jijini Dar es Salaam.
Mkuugenzi wa  Mtendaji wa Global Dynamic Consulting Anne Massawe akizungumza namna watavyoshirikiana na  TAREWU katika makubaliano ya usimamizi wa miradi ya maendeleo ya uongozi.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Dkt.Michael Marere akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana TAREWU kuingia makubaliano na Global Dynamic  Consulting  (GDC)  kwa ajili ya usimamizi wa miradi ya maendeleo na uongozi.

Baadhi ya matukio katika picha mara baada ya kusaini makubaliano
Na Mwandishi Wetu
CHAMA cha Wafanyakazi Wakusanya Mapato Tanzania (TAREWU) kimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) na Global Dynamics Consulting (GDC), kwa lengo la kuimarisha uwezo wa wanachama wake katika usimamizi wa miradi na maendeleo ya uongozi.

Ushirikiano huo unalenga kuwawezesha wafanyakazi na viongozi kupata ujuzi, maarifa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taasisi zao na taifa kwa ujumla.

Akizungumza mara baada ya kusaini hati hiyo, Katibu Mkuu wa TAREWU, Wakili na CPA Dkt. Michael Marere, amesema ushirikiano huo ni sehemu ya mkakati mpana wa chama wa kuwajengea wanachama uwezo na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kitaaluma na kiuchumi.

Amesema TAREWU itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha wanachama wanapata fursa za kuongeza ujuzi, kubadilishana uzoefu na kunufaika na programu zinazolenga kuimarisha uwezo wao.

Dkt. Marere amesema makubaliano hayo yatawezesha taasisi hizo mbili kuandaa na kutekeleza programu mbalimbali za mafunzo, semina na shughuli nyingine zinazolenga kuongeza uwezo wa wafanyakazi na viongozi katika maeneo mbalimbali.

Amesema ushirikiano na GDC pia utalenga kuandaa programu za kukuza uongozi wenye ufanisi, kuimarisha uwezo wa viongozi katika taasisi mbalimbali na kuwajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa mujibu wa TAREWU, upatikanaji wa viongozi wenye uwezo ni muhimu katika kuhakikisha taasisi zinafanya kazi kwa ufanisi na kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Chama hicho kimesema mazingira ya sasa yanahitaji viongozi wenye uwezo wa kufanya maamuzi sahihi, kusimamia rasilimali kwa ufanisi na kuongoza mabadiliko yanayolenga kuboresha utendaji wa taasisi.

Aidha, TAREWU imesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika mafunzo na maendeleo ya viongozi ili kuwawezesha kukabiliana na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Dynamics Consulting (GDC), Anne Massawe, amesema kampuni hiyo ina dhamira ya kuendelea kusaidia taasisi mbalimbali kuimarisha mifumo bora ya uongozi na kuongeza uwezo wa utekelezaji wa miradi.

Massawe amesema kusainiwa kwa hati hiyo ni hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo, huku akisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa manufaa ya wanachama na jamii kwa ujumla.

Chini ya makubaliano hayo, TAREWU na GDC zinatarajia kutekeleza programu za kujenga uwezo katika usimamizi wa miradi na uongozi, warsha na semina za mafunzo, programu za uelekezi na ushauri elekezi kwa wanachama, pamoja na mijadala ya kubadilishana maarifa.

Shughuli nyingine zitakazotekelezwa ni pamoja na kutoa fursa za kujenga mitandao ya kitaalamu, tafiti na ubunifu unaolenga kuongeza uelewa na kuboresha utendaji wa taasisi.

Taasisi hizo zimesema juhudi hizo zinalenga kuhakikisha viongozi wanakuwa na maarifa, ujuzi na mtazamo unaowawezesha kuleta matokeo chanya katika taasisi wanazoziongoza.

Na Mwandishi Wetu
CHUO cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma VETA Chang’ombe, Dar es Salaam, kimesema mafunzo ya ubunifu wa mavazi na mitindo yanaendelea kuwa chachu ya kuwawezesha vijana kujiajiri, kuajiri wengine na kuchangia katika kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Chuo cha VETA Chang’ombe, Abraham Richard Mbughuni, wakati wa onyesho la kazi za wanafunzi wa mwaka wa tatu wa kozi ya Diploma ya Ubunifu wa Mavazi na Mitindo, ambapo wanafunzi waliwasilisha kazi zao ikiwa ni sehemu ya mtihani wa mwisho.

Mbughuni alisema ubunifu ulioonyeshwa na wanafunzi hao ni kielelezo cha maarifa na ujuzi walioupata chuoni, huku akieleza kuwa unathibitisha jitihada za VETA katika kuzalisha wahitimu wenye uwezo wa kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Alisema Serikali imeendelea kuwekeza katika elimu ya ufundi na stadi kupitia VETA, hatua inayowawezesha vijana kupata ujuzi wa kujitegemea badala ya kutegemea ajira rasmi ambazo mahitaji yake ni makubwa kuliko nafasi zilizopo.

“Kila ubunifu na muundo wa vazi unaoonyeshwa ni msingi wa ajira za baadaye na unaweza kuwa nembo ya Tanzania katika sekta ya ubunifu. Wanafunzi hawa si wahitimu pekee, bali ni wajasiriamali na waajiri wa kesho,” alisema.

Mbughuni aliwataka wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono sekta ya ubunifu wa mavazi kwa kuweka mazingira bora yatakayowezesha sekta hiyo kukua.

Alisema iwapo vyuo vya VETA vitaendelea kuzalisha wabunifu wengi kila mwaka, Tanzania itaongeza uwezo wa kuzalisha mavazi yake yenyewe na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Textile and Fashion Design katika VETA Dar es Salaam, Josephat Maghina, alisema onyesho hilo lilikuwa sehemu ya mtihani wa mwisho wa wanafunzi, ambapo kila mwanafunzi alitakiwa kuandaa mkusanyiko wa mavazi matano yaliyobuniwa kutokana na wazo au msukumo aliouchagua.

Maghina alisema mafunzo ya sasa yanazingatia ubunifu wa kisasa unaoanzia katika utafiti, uchoraji wa michoro, maandalizi ya kazi hadi utengenezaji wa mavazi, tofauti na mtazamo wa zamani wa kushona bila kufuata mchakato wa kitaalamu.

Alisema kozi hiyo inawawezesha wahitimu kujiajiri, kuajiriwa katika taasisi mbalimbali na kuanzisha biashara zao, huku akiwahimiza vijana wenye sifa kujiunga na VETA ili kunufaika na fursa zinazopatikana katika sekta ya mitindo na mavazi.

“Mahitaji ya wabunifu wa mavazi yanaendelea kuongezeka kutokana na ukuaji wa tasnia hii. Wahitimu wetu wana uwezo wa kushiriki katika matukio makubwa ya kitaifa na kimataifa, ikiwemo kubuni mavazi kwa viongozi na mashindano mbalimbali,” alisema Maghina.

Mhitimu wa kozi hiyo, Andrea Johannes, alisema mafunzo aliyoyapata yamemjengea uwezo wa kuingia kwa kujiamini katika soko la ajira, akieleza kuwa lengo lake ni kujiajiri na baadaye kuajiri vijana wengine baada ya kuanzisha karakana yake ya ushonaji.

Naye mhitimu, Beatrice Richard Mahimbo, alisema ujuzi walioupata kutoka kwa wakufunzi wa VETA umewapa msingi wa kujitegemea kiuchumi, huku akiahidi kuwahamasisha vijana wengine kujiunga na kozi hiyo ili kuongeza idadi ya wabunifu wenye uwezo nchini.

Jumla ya wanafunzi 27 wamehitimu mafunzo ya Diploma ya Ubunifu wa Mavazi na Mitindo, huku uongozi wa chuo ukieleza kuwa una imani wahitimu hao watakuwa sehemu ya nguvu kazi itakayochochea maendeleo ya sekta ya mitindo, kuongeza ajira na kuunga mkono juhudi za Tanzania za kujenga tasnia imara ya mavazi








Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi, akizungumza wakati wa semina maalum ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.



*Mmoja atoa ushuhuda wa ‘Tunalipa Jana’

*Bunge: tunawashukuru PSSSF kwa elimu



Morogoro, Julai 31, 2026

Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.

Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.

“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Bi. Angelina Sanga.

Mtumishi kutoka Ofisi ya Bunge, Bi. Angelina Sanga (kushoto), akiwa na Afisa Matekelezo kutoka PSSSF, Bi. Upendo Chilewa, wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bi. Sanga alipokuwa akijisajili kaaika huduma ya mifumo ya kidijitali.

Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.

Katika semina hiyo Mtumishi Mstaafu wa Bunge Bw. Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto, akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge kwa ajili ya Makatibu wa Kamati za Bunge mjini Morogoro.

Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Bw. Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine

Mtumishi Mstaafu wa Bunge, Bw. Gerald Magili, akitoa ushuhuda wake wakati wa semina hiyo mjini Morogoro. Bw. Magili aliipongeza PSSSF kwa kulipa mafao yake kwa wakati

“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Bw. Hajji Moshi.

Kwa upande wake, Bw. Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajji Moshi (kushoto), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamati za Bunge, Bw. Michael Chikokoto (kulia), mara baada ya kuhitimishwa kwa semina ya kutoa elimu ya Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro.
Makatibu wa Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kwa umakini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Hajj Moshi (kulia), wakati wa semina ya kujenga uelewa wa Hifadhi ya Jamii iliyoandaliwa na Ofisi ya Bunge mjini Morogoro tarehe 31 Julai, 2026.
Benki ya NMB imekabidhi hundi ya udhamini kwa Wizara ya Kilimo kwa ajili ya Maonesho ya Nanenane 2026, ikiendeleza ushirikiano wake wa muda mrefu na Serikali katika kukuza sekta ya kilimo.

Makabidhiano yaliyofanyika jana jioni jijini Dodoma yamefikisha jumla ya udhamini wa NMB katika maonesho hayo hadi Sh572 milioni ndani ya miaka minane mfululizo, yakionyesha dhamira ya benki hiyo katika kusaidia maendeleo ya wakulima, wafugaji na wavuvi.

Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango, alisema Nanenane ni jukwaa muhimu la kuwafikisha wazalishaji kwenye maarifa, teknolojia na huduma za kifedha zinazoongeza tija na kufungua fursa mpya za biashara.

Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo aliipongeza NMB kwa kuendelea kuwa karibu na wakulima na kuitaka benki hiyo kuendeleza ushirikiano huo ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi kupitia elimu, teknolojia na huduma za kifedha.



Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo (wapili kushoto), akipokea mfano wa hundi ya udhamini kutoka kwa Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango (wapili kulia), wakati wa hafla iliyofanyika jana jioni jijini Dodoma kwa ajili ya Maonesho ya Nanenane 2026. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli, na kulia ni Meneja Mwandamizi wa Idara ya Biashara za Serikali wa NMB, Amanda Feruzi. Udhamini huo unaendeleza ushirikiano wa muda mrefu kati ya NMB na Serikali katika kukuza maendeleo ya sekta ya kilimo.

Ni suala la muda tu kabla ya Belgrade Arena kufurika shamrashamra za UFC Fight Night Belgrade, moja ya matukio yanayotarajiwa zaidi mwaka huu katika ulimwengu wa michezo ya mapigano. Siku imewadia, na kila saa inayopita inaongeza hamu ya mashabiki kushuhudia mapambano yatakayovuta hisia za dunia nzima. Kwa wapenda ubashiri, wakati huu ni ishara kwamba wakati wa kufanya maamuzi muhimu umefika. Meridianbet imefungua mlango wa msisimko kwa odds zenye ushindani na masoko mbalimbali yatakayowafanya mashabiki waishi kila sekunde ya pambano kwa namna ya kipekee.

Wakati wapiganaji wakikamilisha maandalizi yao ya mwisho kupanda ulingoni, mashabiki nao wamehamia kwenye uchambuzi wa kina. Nani ana nafasi kubwa ya kushinda? Je, pambano litaisha mapema au litafika mwisho wa raundi zote? Haya ni baadhi ya maswali yanayotawala mijadala ya mashabiki duniani kote. Meridianbet imejiandaa kuwapa wabashiri fursa ya kugeuza uchambuzi wao kuwa nafasi halisi ya ushindi kupitia masoko mengi yanayokidhi aina tofauti za wabashiri.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kwa Meridianbet, mapambano haya yana uzito wa kipekee kwani yanakwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 25 ya mafanikio duniani. Kwa robo karne, kampuni imeendelea kuwa mstari wa mbele katika ubunifu wa huduma za ubashiri na kushirikiana na matukio makubwa ya michezo duniani. Ushiriki wake katika UFC Fight Night Belgrade unathibitisha dhamira hiyo ya kuendelea kuwapa mashabiki burudani ya kiwango cha juu pamoja na uzoefu unaokwenda sambamba na hadhi ya matukio makubwa ya kimataifa.

Kadiri muda unavyoendelea kupungua, ndivyo nafasi ya kujiandaa inavyokuwa muhimu zaidi. Wabashiri wenye uzoefu wanajua kwamba maandalizi yanaweza kuwa silaha muhimu kabla ya pambano kuanza. Kuchunguza takwimu, kufuatilia taarifa za mwisho na kuchagua odds zinazofaa ni sehemu ya safari ya kuelekea usiku mkubwa wa UFC. Meridianbet imehakikisha kuwa kila shabiki anapata mazingira bora ya kushiriki kuanzia pambano la kwanza hadi pambano kuu.

Hatimaye, hesabu za siku zimekamilika. Dunia inasubiri kuona nani ataondoka Belgrade akiwa mshindi, lakini kwa mashabiki wa Meridianbet, ushindi unaweza kuanza hata kabla ya mpiganaji wa kwanza kupanda ulingoni. Jiandae mapema, weka ubashiri wako na uungane na mamilioni ya mashabiki wanaosubiri kwa hamu usiku ambao utaandika historia nyingine ya UFC Fight Night Belgrade.

Leo, Jumamosi Agosti 1, 2026, mabingwa wawili wa jiji la London, Chelsea na Tottenham Hotspur, watakutana katika uwanja wa Accor Stadium, jijini Sydney, Australia, katika mchezo wa kirafiki wa maandalizi ya msimu mpya.

Mchezo huu utaanza saa 12:45 (saa za Afrika Mashariki), Ingawa ni mchezo wa kirafiki, historia ndefu ya ushindani kati ya timu hizi mbili inafanya mechi hii kuwa na hamasa kubwa kuliko michezo mingine ya maandalizi.

Chelsea, chini ya uongozi wa kocha mpya Xabi Alonso, wameanza msimu wao wa maandalizi kwa mchezo wa kusisimua uliomalizika kwa bao 6-4, ambapo João Pedro alionesha kiwango bora kwa hat-trick pamoja na pasi moja ya mabao.

Timu ya Chelsea bado iko katika kipindi cha mabadiliko chini ya mwelekeo mpya wa Alonso, hivyo mchezo huu utakuwa fursa nzuri ya kuona jinsi mfumo wake unavyoshika kasi. Hata hivyo, Chelsea watakosa huduma za wachezaji kadhaa muhimu kama Mykhailo Mudryk (anayetumikia kusimamishwa), Roméo Lavia, Estêvão, na Jamie Bynoe-Gittens ambao wote wako majeruhi.

Kwa upande wa Tottenham, kocha Roberto De Zerbi anaendelea na kazi yake baada ya kuiokoa timu dhidi ya kushuka daraja msimu uliopita. Spurs wamekuwa na maandalizi mazuri, wakishinda Auckland FC kwa mabao 2-0 na hivi karibuni kuifunga Sydney FC kwa penati baada ya sare ya 1-1. Timu hii pia itakuwa na mapungufu ya wachezaji muhimu kama Xavi Simons, Wilson Odobert, Ben Davies, na Dejan Kulusevski, wote wakiwa majeruhi.

Kihistoria, Chelsea wanaongoza kwenye mkutano wa moja kwa moja kati ya timu hizi mbili, wakiwa na ushindi 24 dhidi ya ushindi 6 wa Tottenham, huku michezo 11 ikiishia sare. Rekodi hii inaonyesha ukuu wa jadi wa Chelsea dhidi ya jirani zao wa London, ingawa mechi za hivi karibuni zimekuwa na ushindani mkali zaidi kutokana na uboreshaji wa timu zote mbili katika miaka ya hivi karibuni.

Kwa jumla, mechi hii itakuwa jaribio zuri kwa makocha wote wawili kupima nguvu za timu zao kabla ya msimu wa Ligi Kuu ya England kuanza rasmi Agosti 21. Ni fursa ya kuwaangalia wachezaji vijana na wapya wakijaribu kujithibitisha, huku mashabiki wakisubiri kwa hamu kuona ni nani atakayeibuka mshindi katika mzozo huu wa jiji la London ukiwa umefanyika mbali kabisa, huko Australia.

Azindua boti mbili za kisasa kufanya doria baharini, maziwa makuu



Na Mwandishi Wetu 

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa siku 14 kwa wizara na taasisi zinazohusika na Kituo cha Kitaifa cha pamoja cha Oparesheni zipeleke wawakilishi ili kianze kufanya kazi mara moja.

"Wizara na taasisi zote zinazohusika na utekelezaji wa majukumu katika Kituo cha Kitaifa cha pamoja cha Oparesheni zipeleke wawakilishi wote wanaohitajika ndani ya siku 14 kuanzia leo. Kituo hiki kianze kazi mara moja ili kuleta tija inayokusudiwa," amesema Waziri Mkuu. 

Dkt. Mwigulu ametoa wito huo leo (Ijumaa, Julai 31, 2026) wakati akizungumza na washiriki wa hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa boti mbili za doria aina ya PB Sailfish 02 na PB Sailfish 03 iliyofanyika bandarini, jijini Dar es Salaam. Boti hizo zimenunuliwa kwa thamani ya dola za Marekani milioni 1.6. 

Amezitaka Wizara za Muungano zinazohusika na suala hilo zishirikiane ili kuziba chochoro zote ambazo zingetumiwa na wahalifu katika eneo hili tunalolilenga na hasa katika mipaka ya mwambao wa bahari.

Ili kuhakikisha boti hizo zinafanya kazi kama inavyotarajiwa, Waziri Mkuu ameziagiza wizara na taasisi zote za umma zinazohusika katika matumizi ya boti hizi za doria zitenge fedha kwa ajili ya kazi za boti hizi.

"Ninasisitiza suala la kutenga bajeti ili kazi za doria zisikwamishwe na ukosefu wa bajeti.  Nimekuwa nikikutana na kesi kama hizo mikoani ambapo Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alinunua ambulance za kisasa na nyingine zina ICU lakini zinashindwa kuhudumia wagonjwa kwa wakati kwa kukosa mafuta. Hili linakinzana na dhamira njema ya Mheshimiwa Rais ya kutaka kuokoa maisha ya Watanzania pindi wanahitaji huduma hizo," amefafanua.

Akielezea umuhimu wa boti hizo za doria, Waziri Mkuu amesema makabidhiano ya boti hizo ni tukio muhimu kiuchumi kwa sababu zinaenda kulinda mazao yatokanayo na uchumi wa bluu. Amesema uhitaji wa boti hizo umekuwa ni kilio cha muda mrefu tangu yeye akiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Amesema upatikanaji wa boti hizo mbili, utaimarisha ulinzi hasa ikizingatiwa kwamba Tanzania ni lango la nchi nyingi zikiwemo za Afrika Mashariki na za SADC lakini usalama utakaokuwepo unahusu Tanzania na wananchi wa hizo nchi jirani. "Wananchi kutoka nchi hizo watakuwa na uhakika wa usalama watakapotumia lango la bandari ya Dar es Salaam," amesisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Prof. Palamagamba Kabudi alisema ununuzi wa boti mbili za doria aina ya PB Sailfish 02 na PB Sailfish 03 ulifanyika baada ya kukamilika kwa taratibu zote za manunuzi ambapo mkataba wa ununuzi ulisainiwa Julai 29, 2025 kati ya Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini na Kampuni ya Yamaha Motors Co. Ltd.

“Ujenzi wa boti hizo ulifanyika nchini Japan kwa kuzingatia vipimo na viwango vya kimataifa vilivyokubaliwa na wataalamu wa Serikali. Hadi kukamilika kwake, ujumbe wa wataalamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, TASAC, UNDP na Chuo cha Mipango ulifanya ziara za ukaguzi ili kujiridhisha na ubora wa kazi iliyotekelezwa,” alisema.

Naye, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mikami Yoichi alisema kijiografia Tanzania na Japan ziko mbali lakini zinaunganishwa na bahari za Hindi na Pasifiki na kwamba uwepo wa usalama kwenye mipaka ya baharini, kuwahakikishia wananchi wake usalama wa maisha yao.

Alisema ana imani kwamba Serikali ya Tanzania itahakikisha boti hizo zinatumika kwa miaka mingi kwa faida ya vizazi vijavyo.






 

Na Mashaka Mhando, Mbeya

VIWANJA vya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Mbeya vilitikiswa na shangwe na nderemo kufuatia mkutano mkubwa uliowakutanisha maelfu ya madereva wa bodaboda na bajaji wa Jiji hilo ana kwa ana na Mkuu wao wa Wilaya, Mhe. Solomon Itunda kuzungumzia amani na utulivu.

Mkutano huo, ambao ulitawaliwa na hali ya kirafiki na maelewano, haukuwa tu wa kutoa maagizo, bali ulikuwa ni jukwaa la kimkakati la kuwakumbusha vijana hao nafasi yao nyeti katika uchumi na usalama wa Jiji la Mbeya.

Akizungumza huku akishangiliwa na umati huo, Mhe. Itunda aliwaeleza madereva hao ukweli usiofichika kuwa wao ni injini muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa mustakabali wa nchi.

Alisema kutokana na asili ya kazi yao ya kukutana na mamia ya wananchi kila siku, wana nguvu kubwa ya kujenga au kubomoa taswira ya jiji katika sekta ya usafiri kwa kuwaeleza tofauti na uhalisia wa nchi inavyoendeshwa.

Hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya, ambaye amekuwa akisifika na wananchi wa Mbeya kama 'Mzee wa busara', aliwasihi madereva hao wa bodaboda na bajaji kuendesha vyombo vyao kwa umakini mkubwa na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kunusuru maisha yao na ya abiria wao.

"Ndugu zangu wa bodaboda na bajaji, sisi ni watu wa Mbeya, tunapokuwa kazini tulinde amani yetu. Nyie mkiwa mabalozi, lakini pia ni vizuri mkalinda amani ya nchi kwa kuhubiri amani kwa abiria wenu," alisema Itunda.

Katika kile kilichoonyesha kutambua mazingira wezeshi ya biashara, Mkuu huyo wa Wilaya alitumia jukwaa hilo kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Itunda aliweka wazi kuwa msingi imara wa amani, utulivu, na uhuru wa kiuchumi uliojengwa na Rais Samia ndio unaowapa vijana wengi fursa ya kujitafutia kipato mitaani bila bughudha.

Akifafanua kuhusu fursa za kiuchumi, DC Itunda aliwafafanulia wananchi hao kuwa awali mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji haikuwa ikiwafikia walengwa, lakini Rais Samia ameweka utaratibu mpya unaohakikisha kila kijana aliyekuwa kwenye kikundi ananufaika.

Aliwataka vijana hao, kama miongoni mwa wanufaika, kulinda fedha za mikopo wanayopewa na kuirejesha kwa wakati, ili asilimia hiyo 10 iweze kuwanufaisha vijana wengi zaidi wa Jiji hilo baada ya maboresho hayo makubwa.

DC Itunda aliwataka bodaboda hao kuunga mkono juhudi hizo za Rais kwa vitendo, huku wakiweka maslahi ya Tanzania mbele, ili kuhakikisha makundi ya vijana, wanawake, na watu wenye ulemavu yanawezeshwa na kuifanya Tanzania yenye watu milioni 65 kupiga hatua kiuchumi.

Hata hivyo, kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mhe. Itunda hakusita kugusa mshipa wa usalama. Aliwapa onyo na kuwasihi vijana hao kutokubali kutumika kama daraja la uhalifu. Aliwaomba wawe walinzi wa kwanza wa Jiji kwa kutoa taarifa za siri kwa vyombo vya dola mara wanapobaini watu wasioeleweka.

"Jiepusheni na makundi yenye mwelekeo wa kuvunja sheria. Ushirikiano wenu na Serikali ndiyo nguzo pekee itakayotuhakikishia Mbeya inabaki kuwa salama kwa maendeleo endelevu," alisisitiza Mhe. Itunda.

Kauli hizo za DC ziliingia vizuri masikioni mwa madereva hao, ambao kwa upande wao hawakuwa na hiyana. Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, viongozi wa bodaboda waliipongeza Serikali kwa kuendelea kuwathamini na kutatua changamoto zao.

Kama ishara ya kukubaliana na mwongozo wa DC Itunda, madereva hao waliweka ahadi nzito mbele ya mamlaka kuwa kuanzia sasa watakuwa mabalozi wazuri wa usalama barabarani, watafichua wahalifu wote wanaochafua taswira ya kazi yao, na watalinda amani ya Mbeya kwa nguvu zao zote.








Na Mwandishi wetu, Mirerani

WADAU wa madini ya Tanzanite, mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro, Mkoani Manyara, wamechangia Sh23.6 milioni kwa ajili ya kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya watoto wachanga njiti.

Lengo ni kuunga mkono mkoa wa Manyara, ambao umeandaa mbio za hisani za kuchangia ujenzi wa jengo la mama na mtoto na kuboresha huduma za afya zitakazofanyika mjini Babati, Agosti 22, 2026 mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba.

Wadau hao wa madini ya Tanzanite, wamechangia kiasi hicho mbele ya Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Cuthbert Sendiga kwa nia ya kukusanya kiasi cha Sh1.6 bilioni cha kuanza ujenzi kwenye hospitali ya wilaya ya Hanang'.

Sendiga amewashukuru wadau hao wa madini ya Tanzanite kwa kuchangia fedha hizo ili kufanikisha ujenzi huo wa wodi ya watoto njiti.

"Mmefanya jambo kubwa mno kwani watoto njiti 3,000 kila mwaka kwenye mkoa wetu huwa wanazaliwa kwa hiyo tunataka tufanye jambo la baraka kwa watoto wanaozaliwa chini ya miezi tisa," amesema RC Sendiga.

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro, Fakii Lulandala ameeleza kwamba wadau wa madini ya Tanzanite watajitokeza kwa wingi kuunga mkono mbio hizo za kusaidia watoto njiti.

"Mimi binafsi nitakimbia kilomita tano na wana Simanjiro kwa umoja wetu tutashiriki  kwa wingi mbio hizo kuchangia matibabu ya watoto wetu," amesema Lulandala.

Mkurugenzi wa JS Magezi, William Magezi wanaochimba kitalu D extension kwa kushirikiana na Tanzanite Afrika, amesema wadau wanaochangia wanakuwa wanatoa sadaka ambayo pia inakuwa toba kwa makosa yaliyofanyika.

"Mkurugenzi mwenza wa Tanzanite Africa Will Mushi alichangia Sh2 milioni na mimi nachangia Sh2 milioni hivyo jumla tumetoa Sh4 milioni," amesema Magezi.

Mkurugenzi wa JN Mining Justin Nyari ambaye amechangia Sh2 milioni ameeleza kuwa wadau wa nyanja tofauti washirikishwe katika sadaka hiyo.

"Hili jambo ni zuri mno katika kuokoa maisha ya watoto wetu, ushauri wangu wote wapitiwe kwa kupitia viongozi wetu wa kata na vitongoji ili kila mmoja ashiriki vile alivyojaliwa," amesema Nyari.

Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara wa madini mkoa wa Manyara, Mokia Ole Mrefu amesema ili kuunga mkono tukio hilo, jumanne ijayo watafanya kikao na wafanyabiashara wa madini ya Tanzanite ili kwa umoja wao nao wachangie.

"Pia nikiwa hapa hapa mdau wa maendeleo wa mkoa wa Manyara,  Taiko Ole Kulunju, amechangia kwa kutuma Sh1 milioni na mimi binafsi nachangia Sh500,000 ili kumuunga mkono RC wetu Sendiga," amesema Ole Mrefu.

Mmiliki mwingine wa mgodi wa madini ya Tanzanite, Joseph Manga ambaye amechangia Sh1 milioni ametoa ombi la kurekebishwa changamoto ya bei ya kibali cha kununua zana za milipuko.

"Tunakuunga mkono RC wetu kwenye hili ila tunakuomba utuangalie suala la sisi wachimbaji kulipia Sh100,000 kwa kila kibali cha kununua milipuko siyo sawa, kibali kiwe kimoja kwa bei hiyo hiyo," amesema Manga.




Top News