02: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Salaam Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe Xi Jinping iliyokabidhiwa kwake na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.

01: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian, Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.

03: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania ni Mhe. Chen Mingjian mara baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika Ikulu ya Tunguu, Zanzibar tarehe 28 Julai, 2026.



Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) itashiriki katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane Kitaifa 2026 yatakayofanyika kuanzia tarehe 1 Agosti 2026 kwenye viwanja vya Dkt. John Malecela, Dodoma, ikiwa na mpango maalumu wa kuwaunganisha wadau wa sekta ya nafaka na mazao mchanganyiko na fursa za masoko, biashara, teknolojia na uongezaji thamani.

Ushiriki wa COPRA unaendana na kaulimbiu ya Nanenane 2026, “Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050,” kwa kuweka msisitizo katika uzalishaji unaozingatia mahitaji ya soko, ubora wa mazao, biashara rasmi, uongezaji thamani na matumizi ya teknolojia ili kuongeza tija na ushindani wa mazao ya Tanzania.

Banda la COPRA litakuwa kitovu cha maarifa, huduma, biashara na ubunifu, ambapo wakulima, wafanyabiashara, wasindikaji, wawekezaji, vijana na wananchi kwa ujumla watapata elimu na ushauri wa kitaalamu kuhusu masoko ya ndani na kimataifa, viwango vya ubora, mifumo rasmi ya biashara, uongezaji thamani, teknolojia na huduma za kidijitali kupitia mfumo wa COPRAMIS.

Kipekee katika Nanenane 2026, COPRA itaandaa Warsha Maalumu ya Zao la Mahindi itakayofanyika tarehe 5 Agosti 2026. Warsha itakutanisha wadau kujadili uwekezaji kwenye uzalishaji, masoko, biashara, fedha na mitaji, uongezaji thamani na ushindani wa zao hilo. 

Aidha, tarehe 7 Agosti 2026, kutakuwa na siku ya watengeneza maudhui ya biashara ya mazao mtandaoni ‘Digital Agribusiness Influencers Day’, na kuwakutanisha na Mamlaka na kutoa fursa ya kupata ufahamu wa masoko na biashara rasmi ya nafaka na mazao mchanganyiko ili kuunganisha na kutumia nguvu ya mawasiliano katika kukuza taarifa za masoko, fursa za biashara, teknolojia na ubunifu.

Mkurugenzi Mkuu wa COPRA, Bi. Irene Madeje Mlola, amesema ushiriki wa Mamlaka mwaka huu umejikita katika kuhakikisha wadau wanapata maarifa, taarifa sahihi, uelewa huduma na fursa zinazowawezesha kufanya maamuzi bora katika uzalishaji na biashara ya nafaka na mazao mchanganyiko.

“Tunataka kila mdau anayefika Banda la COPRA aondoke akiwa na uelewa wa uzalishaji wenye tija, viwango, ubora, soko na fursa zinazoweza kumsaidia kuongeza tija na thamani ya mazao yake. 

Sambamba na kutafuta masoko ya nje, tunataka pia kuhamasisha matumizi na uongezaji thamani wa mazao yetu hapa nchini ili kujenga soko imara la ndani na kuongeza fursa kwa wakulima na wafanyabiashara,” amesema Bi. Mlola.

COPRA inawakaribisha wakulima, wafanyabiashara, wasindikaji, wawekezaji, vijana na wananchi kwa ujumla kutembelea Banda la COPRA kuanzia tarehe 1 Agosti 2026, kupata huduma na ushauri wa kitaalamu, kutambua fursa za masoko na biashara, kujifunza kuhusu matumizi na uongezaji thamani wa mazao, pamoja na kujenga mitandao ya biashara.

Pia, COPRA itakuwa na eneo maalumu la vyakula vya lishe vinavyotokana na mazao yanayosimamiwa na Mamlaka, likiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya mazao yanayozalishwa nchini, hususan mikunde kama choroko, dengu na mbaazi. 

Kupitia maonesho ya mapishi na vyakula mbalimbali, wageni watajifunza namna mazao hayo yanavyoweza kutumika katika mlo wa kila siku, huku yakifungua fursa za uongezaji thamani, biashara na kupanua soko la ndani kwa mazao ya wakulima.

Nanenane 2026: Tambua Soko; Ongeza Tija Kutekeleza Dira 2050.

Mkurugenzi Mkuu wa Copra, Bi Irene Madeje Mlola.

Balozi Mobhare Matinyi (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya ETDCO, ambayo ni kampuni tanzu ya TANESCO waliokuwa ziarani nchini Algeria. Kulia kwa Balozi Matinyi ni Mwenyekiti wa bodi hiyo, Bw. Raymond Mbilinyi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme nchini (ETDCO), Bw. Raymond Mbilinyi, ameahidi kushirikiana na Shirika la Umeme na Gesi la Algeria (SONELGAZ) katika teknolojia ya kisasa ya usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuboresha huduma hiyo nchini.

Akizungumza na Balozi Mobhare Matinyi katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania jijini Algiers tarehe 25 Julai, 2026, Bw. Mbilinyi alisema ziara yao ya wiki moja imewapatia mwanga kuhusu teknolojia ya kisasa ya usafirishaji na usambazaji wa umeme inayozingatia ubora wa huduma na utunzaji wa nishati.

Bw. Raymond alimfahamisha Balozi Matinyi kwamba kupitia ziara hii waliona fursa nyingi za ushirikiano na Sonelgaz kupitia kampuni yake ya Sonelgaz International ambayo inaendelea na miradi ya umeme nchini Msumbiji, Chad, Niger, Senegal, Cote d’Ivoire na Tunisia.

Kwa upande wake, Balozi Matinyi alilisitiza umuhimu wa taasisi za nishati nchini kuja Algeria kujifunza, kubadilishana uzoefu na kubuni mikakati ya ushirikiano katika maeneo ambayo Algeria imepiga hatua kubwa.

Akigusia maendeleo ya sekta ya nishati nchini Algeria, Balozi Matinyi alidokeza kwamba asilimia 99 ya nchi ya Algeria imeunganishwa na umeme na asilimia 70 imeunganishwa na mtandao wa gesi wakati Sonelgaz huzalisha megawati 26,000 za umeme.

Naye Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Usimamizi ya Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI) iliyopo Arusha, Profesa David Kalaba, aliushukuru Ubalozi kwa kushirikiana nayo katika kuratibu ziara hiyo iliyojumuisha kutembelea viwanda vya vifaa vya umeme vya kampuni ya GISB jijini Mostaganem.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
GLOBAL Education Link (GEL) imesema jumla ya wanafunzi, wazazi na walezi 1,113 wamefikiwa na kupatiwa huduma kupitia maonesho ya Global Education Fair 2026 yaliyofanyika Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam na leo Jumanne yanafanyika Four Point by Sheraton Arusha na tarehe 30 Rockcity Mall Mwanza.

Akizungumza baada ya kukamilika kwa maonesho yaliyofanyika Julai 25, 2026 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa GEL, Abdulmalik Mollel, alisema mwitikio huo unaonesha kuongezeka kwa uhitaji wa taarifa sahihi kuhusu fursa za kusoma nje ya nchi.

Alisema kupitia maonesho hayo, washiriki walipata ushauri kuhusu uchaguzi wa kozi, vyuo vikuu, scholarships, gharama za masomo, malazi, visa na maisha ya mwanafunzi katika mataifa mbalimbali.

“Mwitikio tulioupata Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam unaonesha kuwa wanafunzi na wazazi wanahitaji mwongozo sahihi kabla ya kufanya maamuzi kuhusu elimu ya juu,” alisema Bwana Mollel.

Alisema zaidi ya watu 700 walitembelea banda la GEL katika maonesho yaliyofanyika Viwanja vya Maisara, Zanzibar, watu 168 walihudhuria maonesho ya Dodoma na wengine 245 walishiriki maonesho ya Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Mollel, jumla ya maombi 209 ya udahili yaliwasilishwa kupitia maonesho hayo matatu.

Alisema Zanzibar ilipokea maombi 79 ya udahili katika vyuo vikuu vya China, India, Malaysia, Afrika Kusini na mataifa mengine, ambapo wanafunzi 30 walipata udahili papo kwa papo.

Kwa upande wa Dodoma, maombi 78 yaliwasilishwa, wanafunzi 50 wakapata udahili papo kwa hapo na wengine 40 wakafungua mafaili mapya kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kujiunga na vyuo.

Katika maonesho ya Dar es Salaam, watu 108 walionesha nia ya kuendelea na taratibu za udahili, maombi 52 yaliwasilishwa, barua 41 za udahili zilikuwa tayari na mafaili mapya 15 yalifunguliwa.

Alisema mafanikio hayo yametokana na kuwapa wanafunzi nafasi ya kukutana moja kwa moja na wawakilishi wa vyuo vikuu, kuuliza maswali na kupata ushauri unaozingatia matokeo yao ya kitaaluma, uwezo wa kifedha na malengo ya baadaye.

Mollel alisema Global Education Fair hailengi kuwasaidia wanafunzi kupata udahili pekee, bali pia kuwajengea uwezo wa kuchagua taaluma zenye fursa katika soko la ajira na zinazoweza kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Tunataka mwanafunzi achague kozi inayolingana na uwezo wake, mahitaji ya soko la ajira na mchango anaoweza kuutoa katika maendeleo ya Taifa, badala ya kuchagua kwa kufuata mkumbo,” alisema.

Alitaja baadhi ya maeneo yenye fursa kuwa ni sayansi za afya na tiba, uhandisi, teknolojia ya habari na mawasiliano, akili bandia, sayansi ya data, usalama wa mtandao, nishati, kilimo cha kisasa, biashara, fedha, usafirishaji, utalii, elimu na teknolojia za viwanda.

Katika maonesho ya Dar es Salaam, vyuo vilivyoshiriki ni pamoja na Lovely Professional University, Sharda University, SRM University–AP, Maharishi Markandeshwar (Deemed to be University)—MMU, Noida International University na Asia Pacific University of Technology and Innovation.

Pia kulikuwa na mabanda yaliyotoa taarifa kuhusu fursa za kusoma China, Malaysia, North Cyprus, Marekani, Canada, Uingereza, Uholanzi, Australia, Ireland, New Zealand na Dubai.

Mollel aliwaalika wakazi wa Kanda ya Kaskazini kushiriki maonesho yatakayofanyika Julai 28, 2026 katika Hoteli ya Four Points by Sheraton jijini Arusha.

Aidha, aliwaalika wakazi wa Kanda ya Ziwa kufika kwenye maonesho yatakayofanyika Julai 30, 2026 katika Rock City Mall jijini Mwanza, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.

Aliwataka wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne, Kidato cha Sita, stashahada, shahada na wale wanaotafuta nafasi za masomo ya uzamili kufika wakiwa na matokeo au vyeti vyao.

“Tunawaalika wanafunzi, wazazi na walezi wa Arusha, Mwanza na mikoa ya jirani kufika na kupata ushauri wa moja kwa moja kuhusu kozi, vyuo, udahili na scholarships,” alisema Mollel.

Alisema GEL itaendelea kuwaongoza wanafunzi kuanzia hatua ya kuchagua kozi na chuo, kuomba udahili, kupata visa na malazi hadi maandalizi ya safari ya kwenda kusoma nje ya nchi.






Kwa masikitiko makubwa, familia ya Mr. & Mrs. Boniventura Mwalongo wa Nsalaga, Mbeya, inatangaza kupotea kwa mdogo wao anayefahamika kwa jina la Faraja Nicodemu Mwalongo(33).


Faraja aliondoka nyumbani kwa dada yake, Enilita Ferdinand Mwalongo, eneo la Juhudi, Ilemi – Jiji la Mbeya, saa 2:15 usiku Julai 25, 2026, akieleza kuwa anaelekea Kanisa Katoliki la Roma, Mbeya Mjini. Tangu wakati huo hajarejea nyumbani na hajulikani alipo.

Faraja amekuwa na changamoto ya afya ya akili tangu alipohitimu masomo yake katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), hali iliyomfanya ahitaji uangalizi na msaada wa karibu.

Sifa za mavazi alipokuwa akiondoka:
- Gauni la rangi ya bluu na nyeupe.
- Sweta ya kaba shingo.
- Miguuni alikuwa amevaa mabotiboti.

Familia inaomba kwa dhati ushirikiano wa kila mwananchi katika juhudi za kumtafuta Faraja.
Kwa yeyote atakayemuona Faraja, una taarifa kuhusu alipo, au unadhani umekutana naye, tafadhali usisite kuwasiliana nasi mara moja kupitia namba zifuatazo:

📞 0782 728 605
📞 0756 147 487
📞 0676 003 969

Familia inaendelea kuwa na imani kwamba kwa ushirikiano wa jamii na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, Faraja Nicodemu Mwalongo atapatikana salama na kurejea nyumbani.

 

Na Victor Masangu, Kibaha

Mwenyekiti wa Jumuiya ya  Wazazi CCM Taifa Ndg Fadhili Maganya amempongeza Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Kibaha Dkt Rogers Shemwelekwa kwa kutekeleza ilani ya chama  kwa vitendo  kwa  kuweza kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo  kupitia mapato yake ya ndani.

Pongezi hizo amezitoa  wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha  yenye lengo la  kuweza  kuangalia uhai wa  chama cha mapinduzi (CCM) ikiwa sambamba  na  kuimarisha jumuiya zake  zote za vijana, wazazi, na wanawake na kufuatilia utekelezji wa Ilani  ya chama.

Katika ziara hiyo Mwenyekiti huyo ambaye pia ameweza kupata fursa ya kutembelea mradi wa Zahanati ya Kilimahewa ambapo ameridhishwa kuona ujenzi wa majengo yaliyopo yamejengwa katika kiwango kinachotakiwa na kwamba fedha  zaidi ya kiasi cha shilingi milioni 285 zimetokana na mapato ya ndani.

"Nampongeza kwa dhati Mkurrugenzi mtendaji wa Manispaa ya Kibaha mji Dkt. Rogers Shemwelekwa kwa kuweza kuchapa kazi kwa bidii katika  suala zima la utekelezaji wa ilani kwa vitendo kwani ameweza kutekeleza baadhi ya miradi kwa kutumia fedha za mapato ya ndani nampa hongera sana,"amebainisha Mwenyekiti wa Wazazi Taifa

Pia Mwenyekiti  huyo akiwa katika mkuitano wake wa ndani na viongozi wa CCM pamoja na jumuiya za ke ambao umeefanyika katika shule ya Uongozi  ya mwalimu Julias Nyerere amempongeza  Mkurugenzi huyo kwa uwajibikaji na  kusimamia vema   utoaji wa mikopo ya asilimia 10  ambayo inatolewa na Halmashauri.

"Nimeridhishwa na huduma mnayotoa, nimeona mna idadi nzuri ya watumishi pia vifaa tiba sambamba na maji jambo ambalo ni muhimu sana katika zahanati, naipongeza Manispaa na nampongeza Mkurugenzi kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kujenga Zahanati hii kwa kutumia mapato ya ndani," amesema Maganya.

 Maganya akizungumzia  suala la zima la utoaji wa fursa za  mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Manispaa, Maganya amesema pamoja na kazi kubwa waliyoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata mikopo hiyo isiyokuwa na riba bado kuna jukumu la kushuka chini zaidi ili kuwafikia wananchi wengi.

 "Kitu kikubwa  mkurugenzi pamoja na kufanya kazi nzuri sana katika mambo mbbali mnbali lakini  kwa sasa hakuna  budi kuwafikia wananchi wengi zaidi ili kupunguza malalamiko yanayotolewa na wananchi, nataka nione hii idadi uliyosema ya wajasiriamali 3000 vikundi 457 vinaongezeka na kuwa vingi zaidi"

Maganya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt Shemwelekwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kushirikiana na Viongozi wa CCM Wilaya ili kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri baina ya Chama  pamoja na  Serikali.

Kwa upande wa Mkuu wa  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt Shemwelekwa amesema katika kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 inafika kwa wananchi yeye pamoja na tilmu yake walienda kwenye Kata 7 za Manispaa kwa ajili ya kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na vikundi vya wajasiriamali ili kuweza kupata mikopo hiyo isiyokuwa na riba.

"Mimi na timu yangu tulifika katika Kata 7 za Manispaa, tukatoa elimu ya mikopo na hadi kufikia mwaka 2026, tumevifikia vikundi zaidi ya 457 sawa na wajasiriamali 3,000 waliokidhi vigezo na tumewapatia mikopo hiyo na wanairudisha kwa wakati ili wananchi wengine waendee kuchukua,"amesema Dkt Shemwelekwa.

Ameongeza kuwa, wamekuwa na utaratibu mzuri wa kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi katika matukio yote na hata kwenye utoaji wa mikopo hiyo wa vikundi wamekuwa bega kwa bega katika kuimarisha mahusiano ya Chama na Halmashauri kwa ujumla.

Kwa upande  wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe, Silvestry Koka amesema kwamba ataendelea kushirikiana bega kwa bega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa lengo la kuweza kuendelea kukusanya mapato kwa lengo la kupata fedha ambazo zitatumika katika miradi mbali mbali ya maendeleo.

"Mimi kama Mbunge wa Jimbo hili nitahakikisha naendelea kushirikiana kwa dhati na watendaji wengine pamoja na mkurugenzi na lengo kubwa ni ni kuendelea kuwaletea wananchi chachu kubwa ya kimaendeleo na mimi nampongeza sana Mkurugenzi wetu Dkt. Rogers Shemwelekwa kwa kazi nzuri ambayo anaifanya ya ukusanyaji wa mapato ya ndani," amebaainisha Mbunge Koka.

Naye Meya wa Manispaa ya Kibaha Mjini  Mhe. Dr Nicas Mawazo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazinkubwa anayoifanya na kuleta fedha kwa ajili ya maendeleo ya Manispaa ya Kibaha.

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha  kwa upande wa suala la utoaji wa fursa za  mikopo ya asilimia 10,  kwa makundi ya vijana, walemavu na wakinamama hadi kufika mwaka 2026 imefanikiwa kutoa kiasi   cha  jumla ya Shilingi bilioni 3.1 katika  vikundi   vipatavyo 457.



Na Mwandishi Wetu, 

TANZANIA  imepiga hatua nyingine katika juhudi za kuendeleza mchezo wa uogeleaji kufuatia kuwasili kwa kocha wa kimataifa, Ben Lee, ambaye atatoa mafunzo ya kiwango cha kimataifa kwa waogeleaji, makocha na wazazi kupitia programu maalumu iliyoandaliwa na Monti International School.

Ujio wa Ben Lee unaelezwa kuwa ni hatua muhimu katika safari ya kuinua viwango vya uogeleaji nchini kwa kuwaletea Watanzania utaalamu wa kimataifa bila kulazimika kusafiri nje ya nchi. Kocha huyo ana uzoefu mkubwa wa kuwafundisha waogeleaji walioshiriki mashindano ya NCAA na Olimpiki.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mapokezi ya kocha huyo jana jijini Dar es Salaam, Afisa Michezo wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Petro Gallos mbali na kupongeza ujio wake, amesema wakufunzi wa ndani wa mchezo huo wanapaswa kutumia mwanya huo adhimu kwa kuchota ujuzi wenye manufaa.

Naye Mkurugenzi wa Ufundi wa Chama cha Uogeleaji Tanzania (TSA), Amina Mfaume alisema; “mafunzo yatakayotolewa na kocha huyo yataongeza ufanisi wa makocha wetu na kutusaidia kuangalia maendeleo ya waogeleaji kwani wale watakaowashiriki wataona jinsi gani makocha wa kimataifa wanavyofanya mafunzo yao.”

Awali Mkurugenzi wa Monti International School, Fatma Fernandes, alisema ushirikiano kati ya RaceBetter na Monti si wa tukio la muda mfupi, bali ni mwanzo wa mpango wa muda mrefu unaolenga kuendeleza vipaji vya waogeleaji wa Tanzania na kuwajengea uwezo makocha wa ndani.

"Ujio wa Ben Lee nchini Tanzania ni hatua muhimu katika safari yetu ya kuijenga Tanzania kuwa kitovu cha maendeleo ya uogeleaji Afrika Mashariki. Kupitia ushirikiano huu, tunataka kuwajengea uwezo waogeleaji, makocha na wazazi, na kuweka msingi imara wa mafanikio ya muda mrefu katika mchezo wa uogeleaji," alisema Fatma Fernandes.

Kwa mujibu wa ratiba ya programu hiyo, mafunzo kwa makocha yatafanyika kuanzia Julai 28 hadi 30, yakifuatiwa na kambi za mafunzo kwa waogeleaji wa makundi mbalimbali ya umri, huku mafunzo ya juu yakihitimishwa Agosti 14.

Fernandez alisema mafunzo kwa makocha yatatolewa bure kwa makocha wote waliosajiliwa na Chama cha Uogeleaji Tanzania (TSA), licha ya gharama za kumleta kocha huyo wa kimataifa kugharamiwa kikamilifu na Shule ya Kimataifa ya Monti.

Aliongeza kuwa mafunzo hayo yatafanyika katika bwawa la kisasa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Monti, Mikocheni, kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 5:00 asubuhi kila siku.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuwasili nchini Tanzania, Ben Lee mbali nakushukuru kwa mapokezi makubwa, alisema ujio wake unalenga kusaidia kuendeleza vipaji vya wazawa kuanzia ngazi za chini na kuweka misingi kwa makocha na waogeleaji kupata mafanikio ya muda mrefu.



 

Na Mwandishi Wetu, Arusha
 
Benki ya NMB imekabidhi udhamini wa Sh10 milioni kwa mwanariadha wa Tanzania, Alphonce Simbu, ili kumsaidia katika maandalizi ya kushiriki mbio za TCS Sydney Marathon 2026 zitakazofanyika Agosti 30, 2026 jijini Sydney, Australia.

Udhamini huo unalenga kumpunguzia Simbu changamoto za kifedha wakati wa maandalizi, ili aweze kuelekeza nguvu zake zote kwenye mazoezi na kuiwakilisha Tanzania vyema katika mashindano hayo ya kimataifa.

Akimkabidhi Simbu hundi ya udhamini huo jijini Arusha, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, alisema benki hiyo imeamua kuwa sehemu ya safari ya mwanariadha huyo kutokana na rekodi yake ya kuendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Alisema NMB inaamini mchango huo utampa utulivu wa kufanya maandalizi yake bila vikwazo vya kifedha.

"Tunamwamini Simbu kwa sababu ameendelea kuiandikia Tanzania historia katika mchezo wa riadha. Tunaamini hata safari hii atafanya makubwa na kuendelea kulitangaza taifa letu," alisema Ladislaus.

Alimtakia Simbu maandalizi mema na mafanikio makubwa katika mashindano hayo.

Mbali na fedha hizo, NMB pia ilimkabidhi Simbu kadi ya benki pamoja na NMB Band, bangili ya malipo ya kidijitali inayotolewa kwa ushirikiano na Mastercard, ambayo itamwezesha kufanya malipo salama na kwa urahisi katika maeneo mbalimbali duniani yanayokubali Mastercard au Visa.

Kwa mujibu wa Ladislaus, huduma hiyo itarahisisha miamala ya kifedha ya mwanariadha huyo wakati wote wa safari na kipindi cha mashindano.

Akizungumza baada ya kupokea udhamini huo, Simbu alisema maandalizi yake yanaendelea vizuri na afya yake ipo katika hali nzuri huku akieleza kuwa analenga kutwaa medali ya dhahabu nchini Australia.

"Maandalizi yanaendelea vizuri na nina afya njema. Niko tayari kwa changamoto ya Sydney Marathon na nina imani kubwa ya kufanya vizuri. Lengo langu ni kurudi nyumbani na medali ya dhahabu," alisema Simbu.

Aliwataka Watanzania kuendelea kumuombea ili afanikiwe kutimiza ndoto hiyo na kuiletea nchi heshima.

Katika hatua nyingine, Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Rogath Steven, alisema maandalizi ya wanariadha yanaendelea vizuri chini ya usimamizi wa shirikisho.

Alisema Simbu pamoja na mwanariadha Magdalena Shauri wamekuwa wakifanya mazoezi katika eneo la Ilboru, Arusha, kutokana na mazingira na hali ya hewa inayofanana kwa kiasi kikubwa na ile ya Sydney.

"Maandalizi yanaendelea vizuri na tuna imani kubwa na wanariadha wetu. Tunaamini Tanzania ina nafasi nzuri ya kupigania medali ya dhahabu katika mashindano hayo," alisema Steven.

TCS Sydney Marathon ni miongoni mwa marathon kubwa duniani na mwaka huu inatarajiwa kushirikisha zaidi ya wakimbiaji 40,000 kutoka mataifa mbalimbali. Mbio za kilomita 42 zitaanzia Miller Street na kumalizikia katika eneo la Sydney Opera House Forecourt.


NAJUA wengi wetu tunamfahamu Mwanasheria maarufu nchini Fatma Karume ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Shangazi.

Shangazi ambaye pia ni mwanaharakati alikuwa mstari wa mbele katika kuikosoa Serikali ya Awamu ya Tano iliyokuwa inaongozwa na Hayati Dk.John Magufuli.

Staili ya Shangazi katika kuikosoa Serikali uliwakwaza baadhi ya viongozi na hali hiyo ilisababisha kuingia kwenye changamoto mbalimbali katika shughuli zake za kisheria na za uwanaharakati. 

Miongoni mwa changamoto ambazo Shangazi alizipitia ni pamoja na tukio la kupigwa bomu katika Ofisi za IMMMA Advocates ambapo Fatma Karume alikua Mshirika.

Wakati Fatma Karume a.k.a Shangazi anaendelea na harakati hizo alikuwa na Maria Sarungi na wawili hao walishiriki kufichua mengi ya Serikali ya Hayati John Magufuli. 

Ndio waliofichua tuhuma za upotevu wa fedha Sh. Trilioni 1.5 trillion ambao Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)profesa Mussa Asad aliuandika kupitia ripoti yake. 

Ripoti ya upotevu wa fedha hizo ukasababisha Profesa Asad kuondolewa kazini.Hivyo Dk.Magufuli akawa Rais wa kwanza tangu Uhuru kumfukuza CAG.

Fatma na Maria wakajipa kazi ya kuwa watetezi katika matukio yaliyokuwa yanatokea kwa mfano malalamiko ya watu kutekwa na wale waliokuwa wanaitwa wasiojulikana.

Waliotekwa kwa wakati ule walikuwepo pia kama kina Mo Dewji, Roma Mkatoliki, Mdude, Azory Gwanda.

Kwa wanaokumbuka vizuri baada ya Mama kuingia madarakani Shangazi aliamua kuwa mwanaharakati full time.Na wakati huo tayari Shangazi alikuwa amenyang’wanya kibali cha uwakili na IMMMA advocates walimtimua maana alikua hana muda wa kufanya kazi zao za uwakili.Kazi za uwanaharakati zilikua nyingi mno. 

Hivyo katika awamu ya mama (Rais Dk.Samia) Shangazi na Maria walikua wameingia mfumo wa kulipwa fedha na NGOs kufanya uwanaharakati (Ford Foundation ikiwa moja wapo). 

Hapo Fatma Karume alikubali hizo fedha lakini kumbuka alikua hana shida sana na hizo fedha kutokana na historia ya familia yake maana Babu yake Abeid Karume ndio aliyekuwa baba wa Taifa Zanzibar na baba yake akaja kuwa Rais wa Zanzibar.

Pia  Shangazi bado alikuwa anapokea fedha za pango kwenye Jengo la IMMMA advocates, na pango za apartments alizojenga mume wake wa zamani ambazo wakagawana .Hivyo Shangazi hakuwa na dhiki ya fedha kama ilivyo kwa Maria.Kwa Maria yeye biashara inayomuweka mjini ni Uanaharakati. 

Sasa Shangazi Fatma wakati nchi inaelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 akagundua biashara ya uanauharakati ina manufaa zaidi kwa watu ambao anawapigania kuliko manufaa yake. 

Kuna makundi yaliyokuwa yametokea ndani ya CCM kuutaka Urais tulipokuwa tunaelekea 2025. Majina yaliyokuwa katika makundi kwa sasa tunayahifadhi kwa ile staili Nguruwe pita mkuki sina.

Katika uchaguzi ule mwaka 2025 baadhi ya waliokuwa ndani ya makundi kuutaka Urais walipanga na safu katika ngazi mbalimbali na hata kwa wabunge. 

Harakati za hovyo na zisizo na tija kwa Taifa ndizo zilizosababisha na vurugu za Oktoba 29 mwaka 2025.Kupitia wanaharakati uchwara waliokuwa wanatumwa na wakubwa wao huko nje wakaja na Samia Must Go.

Hata hivyo wakati hayo yalipokuwa yakiendelea Shangazi aliona mwelekeo unavyoenda kuna damu zinakuja kumwajika kwenye uchaguzi wa mwaka 2025.Waliokuwa wanatoa fedha kufadhili hayo yote akili yao iko kwenye madini na gesi iliyoko Lindi na Mtwara.

Kwa Shangazi wakati wote alikuwa anawaza na kuangalia kama ndio Samia Must Go halafu nani  anachukua madaraka na kwa manufaa gani yeye mwenyewe akaogopa zaidi!!! 

Shangazi akajitafakari na kuona anayoyafanya hayana tija kwake wala kwa Taifa lake hivyo aliamua kwenda Hija na alivyorudi akaamua kuachana na Uwanaharakati  na mambo machafu yote ya Dunia.

Kwa sasa Shangazi ameamua kuishi maisha yqnayompendeza Mungu,amesimama katika misingi ya imani yake ya dini ya Kiislamu na anaendesha maisha katika utaratibu wenye utu, ubinadamu.Sio Shangazi yule aliyekuwa moto na page yake ilikuwa ya Faya.Leo amepoa Shangazi na maisha yanaendelea. 



Benki ya NMB imewahakikishia wafanyabiashara kuendelea kuwapatia masuluhisho ya kifedha yanayolenga mahitaji ya sekta mbalimbali za uchumi. Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki katika Jukwaa la NMB Business Executive Network 2026 lililowakutanisha zaidi ya wafanyabiashara 300 kutoka Dar es Salaam na Pwani.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema benki hiyo imeanzisha Madawati ya Kisekta ili kutoa huduma zinazolingana na mahitaji ya sekta kama madini, ujenzi, utalii, kilimo, afya na elimu. Alisema masuluhisho hayo yanajumuisha Asset Financing, Bid Bond, Advance Payment Guarantee na Performance Guarantee.

Katika jukwaa hilo, NMB pia ilitambulisha tuzo mbili za kimataifa ilizotunukiwa mwaka huu ambazo ni Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Euromoney na Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Global Finance, zikidhihirisha kutambuliwa kwake kimataifa kwa ubora wa huduma.

Jukwaa hilo lilitoa nafasi kwa wafanyabiashara na viongozi wa NMB kujadiliana kuhusu mahitaji ya sekta binafsi na namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano unaochochea ukuaji wa biashara na uchumi wa Tanzania.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kulia), Mkuu wa Idara ya Biashara NMB, Deogratias Shirima (kushoto) wakifurahia tuzo za Benki Bora ya Huduma kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), zilizotolewa na Euromoney na Global Finance wakati wa hafla iliyowakutanisha NMB na Mtandao wa Wafanyabiashara Wakubwa Wanaohudumiwa na benki hiyo ‘NMB Business Executive Network’ iliyofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TTI, Leonard Shayo na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya High Quality, Selina Letara.









Na Mwandishi Wetu

WADAU wa mchezo wa uogeleaji Tanzania wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kiwango cha kimataifa kupitia programu ya wiki tatu iliyolenga kukuza vipaji vya waogeleaji vijana, kuimarisha uwezo wa makocha wa wazawa, pamoja na kuwaelimisha wazazi kuhusu namna bora ya kuwaunga mkono wanamichezo katika safari yao ya mafanikio.

Programu hiyo iliyopewa jina la Tanzania Performance Development Series 2026, imeandaliwa na RaceBetter kwa ushirikiano na Monti AquaForce, na itafanyika kuanzia Julai 28 hadi Agosti 14 katika Kampasi ya Mikocheni ya Shule ya Kimataifa ya Monti, jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yataongozwa na kocha mashuhuri wa kimataifa wa uogeleaji na mwanzilishi wa RaceBetter, Ben Lee, ambaye anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam Jumatatu kutokea nchini Marekani.

Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Monti, Fatma Fernandes, alisema mpango huo unaashiria mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu unaolenga kuimarisha maendeleo ya mchezo wa uogeleaji nchini Tanzania kwa kuunganisha utaalamu wa kimataifa na uongozi wa ndani ili kujenga mfumo endelevu wa kukuza vipaji kuanzia ngazi ya msingi hadi ushindani wa kiwango cha juu.

Mfululizo wa mafunzo hayo utaanza kwa Warsha ya Maendeleo ya Makocha itakayofanyika Julai 28 hadi 30, ikiwakutanisha makocha wa uogeleaji, walimu na viongozi wa vilabu vya uogeleaji. Warsha hiyo inalenga kuboresha viwango vya ufundishaji huku ikiwapa makocha wa ndani fursa ya kujifunza na kufanya kazi bega kwa bega na Ben Lee katika kipindi chote cha kambi za mafunzo kwa wanamichezo.

Fatma alisema pia kutakuwa na kambi tatu za mafunzo kulingana na makundi ya umri wa washiri.

“Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 6 hadi 8, itafanyika kuanzia Julai 30 hadi Agosti 1. Itafuatiwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 9 hadi 12 kuanzia Agosti 3 hadi 7. Programu hiyo itahitimishwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 13 na kuendelea, itakayofanyika kuanzia Agosti 10 hadi 14.

“Aidha, kutakuwa na mfululizo wa mafunzo kwa wazazi, yatakayotolewa bila malipo sambamba na kambi hizo. Vipindi hivyo vitajikita katika lishe na urejeshaji wa nguvu kwa wanamichezo, kujenga kujiamini na ustahimilivu, pamoja na kuwasaidia wazazi kujenga utaratibu mzuri wa maisha unaowawezesha watoto wao kufanikiwa ndani na nje ya bwawa la kuogelea,” alisema.

Alisema programu hiyo itafanyika katika bwawa la kuogelea la mita 25 la Shule ya Kimataifa ya Monti, lenye viwango vya kimataifa kwa mashindano ya kozi fupi, na hivyo kuwapatia washiriki mazingira bora ya mafunzo.

Aliongeza kuwa idadi ya washiriki imewekewa ukomo ili kuhakikisha kila mshiriki anapata mafunzo ya karibu katika vikundi vidogo na ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa wakufunzi.

Akizungumza kuhusu programu hiyo, Ben Lee, ambaye ana uzoefu mkubwa wa kufundisha waogeleaji kuanzia ngazi ya maendeleo, vyuo vikuu hadi Olimpiki, alisema lengo kuu si kuwajengea waogeleaji kasi pekee, bali kuwajenga kama watu.

“Lengo letu si kuzalisha waogeleaji wenye kasi zaidi pekee. Tunataka kuwasaidia watu kuwa na uwezo zaidi, kujiamini zaidi na kuwa tayari kwa fursa na changamoto zitakazokuja mbele yao,” alisema.

Katika kipindi chake cha ukocha, Ben Lee amewafundisha wanamichezo wengi waliofanikiwa kujiunga na programu maarufu za NCAA nchini Marekani na kushiriki mashindano ya kimataifa. Pia amefanya kazi na vilabu vya uogeleaji, shule na mashirikisho ya kitaifa katika nchi mbalimbali duniani.



MASHABIKI wa UFC na burudani za mapambano, hesabu imeanza rasmi. Zimebaki siku tatu tu kabla ya historia kuandikwa wakati UFC Fight Night itakapofanyika kwa mara ya kwanza kabisa nchini Serbia usiku wa Agosti 1, 2026, katika ukumbi wa Belgrade Arena. Tukio hili linazidi kuvuta hisia duniani, huku Meridianbet ikiongoza msisimko huo kama mdhamini rasmi wa pambano hili la kihistoria linalosubiriwa kwa hamu na mamilioni ya mashabiki.

Kwa Meridianbet, udhamini huu ni hatua kubwa inayokwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 25 ya mafanikio ya kampuni hiyo katika sekta ya ubashiri duniani. Kwa robo karne, Meridianbet imeendelea kujenga sifa kupitia ubunifu, huduma bora na kuwaletea wateja uzoefu wa kisasa, jambo lililoifanya kuwa mshirika wa matukio makubwa ya michezo duniani.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kadri saa zinavyosogea kuelekea Fight Night, ndivyo presha na hamasa vinavyoongezeka. Belgrade inajiandaa kupokea wapiganaji watakaopanda ulingoni kuonyesha uwezo wao mbele ya mashabiki kutoka kila kona ya dunia. Kwa vijana wanaopenda UFC, hii si mechi ya kukosa, bali ni usiku ambao historia mpya ya mchezo huo itaandikwa huku kila pambano likiwa limejaa ushindani, mbinu na burudani ya kiwango cha juu.

Ili kuongeza msisimko huo, Meridianbet imeandaa mazingira bora kwa mashabiki kubashiri kwa karibu kupitia odds zenye ushindani mkubwa, machaguo mengi ya ubashiri na ofa maalum zitakazofanya Fight Night iwe na ladha ya kipekee. Lengo ni kuhakikisha kila shabiki anakuwa sehemu ya tukio hili kubwa na kupata burudani inayokwenda sambamba na nafasi ya ushindi.

Kama bado hujajiandaa, huu ndio wakati wako. Zimebaki siku tatu tu kabla ya kengele ya kwanza kupigwa Belgrade. Jiandae kushuhudia UFC ikiandika historia nchini Serbia, huku Meridianbet ikiendelea kuthibitisha kwa nini imekuwa moja ya chapa zinazoaminika zaidi duniani katika ulimwengu wa michezo na ubashiri.


Leo hii una nafasi kubwa ya kuishia maisha ya ndoto zako ukiweza kubashiri kwa usahihi mechi 13 za Jackpot ya Meridianbet. Hii ni nafasi ya wewe kuingia kwenye kinyang’anyiro cha kuwa mshindi kwnai hata bila intaneti unaweza ukabashiri mechi za mpira wa miguu.

Kwenye ulimwengu huu wa kizazi kipya fursa ni chache sana ambazo huja kwa urahisi lakini hubeba uwezo mkubwa wa kubadilisha hatima ya mtu. Kupitia Meridianbet, wachezaji sasa wana nafasi ya kipekee ya kujaribu bahati yao kupitia Jackpot ya mechi 13 yenye zawadi kubwa ya hadi TSh milioni 200, na yote haya yanapatikana kwa urahisi kupitia huduma ya USSD.

Bila kutumia Intaneti utumia, mchezaji anaweza kupiga USSD, kuchagua Jackpot, na kuanza safari yake ya kutabiri matokeo ya mechi 13. Hakuna haja ya intaneti, hakuna ucheleweshaji ni urahisi wa hali ya juu unaokupa nafasi ya kushiriki popote ulipo.

Pindi tiketi ikinunuliwa haiwezi kugharishwa au kurejeshewa pesa, na matokeo ya Jackpot ni ya mwisho na hakuna mjadala mwingine tena.

Jackpot hii inaleta changamoto ya kipekee ambayo inahitaji umakini na maamuzi sahihi. Kila mechi kati ya zile 13 ni hatua muhimu kuelekea ushindi wa mamilioni. Kadri unavyokaribia kupata majibu sahihi kwa kila mechi, ndivyo unavyosogea karibu zaidi na zawadi kubwa inayoweza kubadilisha maisha yako kwa kiwango kikubwa.

Ukiachana na Jackpot hiyo, Meridianbet inakwambia tengeneza mkwanja kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kinachofanya jackpot hii kuwa ya kuvutia zaidi ni ukubwa wa zawadi yake. Shilingi milioni 200 si tu pesa, bali ni fursa ya kufungua milango mipya ya maisha iwe ni kuanzisha biashara, kutimiza ndoto binafsi, au kuboresha maisha kwa ujumla.

Hii ndiyo sababu Meridianbet imeweka mkazo katika kutoa promosheni zinazogusa maisha halisi ya wachezaji wake.

Kwa kubonyeza *149*10# yaani mfumo wa USSD inahakikisha kuwa kila mtu ana nafasi sawa ya kushiriki. Hata bila simu ya kisasa, kila mchezaji anaweza kuingia kwenye mchezo na kujaribu bahati yake kwa hatua chache tu. Hii ni teknolojia rahisi lakini yenye nguvu inayounganisha wachezaji na fursa kubwa ya ushindi.

Na Victor Masangu, Kibaha

Mwenyekiti wa  Jumuiya ya wazazi Taifa Ndg. Fadhili Maganya amewaasa viongozi wa chama cha mapinduzi  (CCM)  ngazi  za Wilaya pamoja na   Mkoa wa Pwani  kuhakikisha kwamba  wanalivalia njuga  suala la kero  ya  migogogoro ya ardhi sambamba na kusikiliza   changamoto mbali mbali   zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake ya  kikazi yenye lengo la   kukijenga chama pamoja na kukagua uhai wake na kuimarisha jumuiya zake sambamba na kuangalia mwenendo mzima wa utekelezaji wa ilani  ikiwemo kukagua na kutembelea  baadhi ya miradi mbali mbali  ya maendeleo.

Mwenyekiti huyo  amebainisha kuwa katika ziara hiyo pia imelenga kukutana na viongozi mbali mbali wa serikali na kupokea taarifa zao  zinazohusiana  na suala zima la  utekelezaji wa kazi  zao  ambazo wanazifanya katika   maeneo yao  kwenye  nyanja mbali mbali za kimaendeleo.

"Nimeanza ziara yangu ya kikazi katika Wilaya ya Kibaha na lengo kubwa na kwamba ziara hii ni ya kikazi na lengo lake kubwa ni kuangalia uhai wa chama jinsi ilivyo, pamoja na jumuiya zake ikiwa sambamba na kuweza kuangalia na kutembelea miradi mbali mbali ya kimaendeleo na kuzungumza na wanachama," amebainisha Mwenyekiti huyo.

Pia Mwenyekiti huyo   amewasihi  wanachama  na viongozi kuhakikisha kwamba wanaachana  kabisa na tabia ya  kuwasikiliza baadhi ya  wanaharakati ambao  wamekuwa wakibeza mambo mbali mbali ambayo  yanatekelzwa  na serikali ya awamu ya sita  na badala yake  wajikite zaidi katika kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambazo anazifanya.

Pia amewahimiza madiwani na   viongozi wengine kuhakikisha wanaweka misingi imara ya  kusimamia  utoaji wa fursa za  mikopo ya asilimia 10  ambayo  inatolewa na halmashauri kwa lengo la kuwasaidia wajasiriamali waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini .

Aidha Mwenyekiti huyo hakusita kumpongeza kwa dhati Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwa  kuweza kuchapa kazi  kwa bidii pamoja na kuendelea kutekeleza ilani kwa vitendo katika suala zima la kusimamia fedha ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali  ya maendeleo pamoja na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauru ya Manispaa ya Kibaha Dkt. Rogers Shemwelekwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge akitoa salama zake amesema kwamba Mkoa wa Pwani imeweza kuendelea kutekeleza miradi mbali  mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu, afya, umeme, miundombinu ya barabara pamoja na ujenzi wa viwanda.

Naye Mjumbe wa halmashauri kuu ya   chama cha mapinduzi (CCM) Taifa   Hamoud Jumaa amesema kwamba lengo lake kubwa ni kuendelea kushirikiana bega kwa bega katika kuhakikisha  chama cha serikali kinaendelea kuwa na mahusiano mazuri ikiwemo sambamba na kutekeleza ilani ya chama.  

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amebainisha kuwa ni jukumu la wanachama kuendelea  na kuweza kushikamana katika kukijenga chama  ikiwa sambamba na kuiimarisha  zaidi kwa vitendo jumuiya zake zote.

 Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka  amempongeza kwa dhati Mwenyekiti huyo  kwa kuamua kufanya ziara ambayo itaweza kuleta uhai wa chama pamoja na kuimarisha jumuiya zake ikiwa pamoja na kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka  amempongeza Mwenyekiti wa jumuiya  ya wazazi Taifa kwa kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuweza kuona umuhimu wa kufanya ziara yake ya kikazi ambayo itaweza kuleta  matokeo chanya katika suala zima la kukiimarisha chama pamoja na jumuiya zake kwa pamoja.

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ameanza ziara yake rasmi ya kikazi katika Mkoa wa Pwani ambapo ameanza  katika Wilaya ya Kibaha ambapo ameweza kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo katika Zahanati ya Kilimahewa iliyopo kata ya Tangini, Kituo cha afya mlandizi pamoja na  kutembelea mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi Mlandizi.





                                

 


Mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe. Joachim Thobias Nyingo amekabidhi gari jipya aina ya ‘Toyota Pickup’ kwa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa wilaya hiyo Mha. Hopeness Liundi huku akitoa wito wa kutumia vizuri kitendea kazi hicho kwa kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa tija ili kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwafikishia huduma ya Majisafi ya bomba wananchi wa wilaya hiyo.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Meneja RUWASA Mkoa wa Dodoma Julai 27, 2026 na kuhudhuriwa na Meneja wa Mkoa huo Mha. Beatrice Kasimbazi pamoja na watumishi wengine wa mkoa huo.

Akizungumza kabla ya kuzindua na kukabidhi gari hilo, Mhe. Nyingo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiwezesha RUWASA na kuboresha utendaji wao wa kazi ikionesha dhamira ya dhati ya serikali kuwafikishia wananchi huduma muhimu ya majisafi ya bomba.

Hivi karibuni, Serikali kupitia RUWASA ilinunua na kugawa magari 22 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha utendaji wa taasisi katika kusimamia na kufuatilia miradi na huduma ya maji katika maeneo ya vijijini.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa wilaya Nyingo amemkaribisha Meneja mpya wa RUWASA wa mkoa wa Dodoma Beatrice Kasimbazi ambaye amehamishiwa mkoani humo akitokea mkoa wa Pwani, huku akitoa wito kwa watumishi wa wilaya hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya serikali na kuwahudumia wananchi.









Top News