Katibu Mkuu wa chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato nchini (TAREWU) Dkt. Michael Marere na Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali wakionesha hati ya makubaliano baada ya kukubalino.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali Brighton Kinemo pamoja na Katibu Mkuu wa chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato Tanzania (TAREWU) wakisaini hati ya makubaliano ya TIB kutoa elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanachama wa (TAREWU).
Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Rasilimali , Brighton Kinemo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu makubaliano kati ya Taasisi yao na Chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato (TAREWU) kushoto ni Katibu wa Chama hicho Dkt. Michael Marere.

WAKATI kukiwa kuna ombwe la elimu ya fedha na uwekezaji nchini. Chama cha Wafanyakazi wa Wakusanya Mapato (TAREWU), na TIB Rasilimali zimesaini makubaliano ya ushirikiano katika elimu ya fedha na uwekezaji.

Makubaliano hayo yamekiwa leo Septemba 14, 2026 jijini Dar es Salaam, ambapo imeeelezwa kuwa makubaliano hayo ni mwanzo wa utekelezaji.

Brighton Kinemo, Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, wakati wa makubaliano hayo amesema kuwa utekelezaji wa mkataba huo utawawezesha wafanyakazi wa TAREWU kupata elimu ya fedha na uwekezaji itakayowawezesha kujimarisha kiuchumi kabla na baada ya kustaafu.

"Mtu anaweza kufanya kazi kwa miaka mingi lakini suala la msingi una elimu gani ya fedha na uwekezaji,".

"Kustaafu kunaandaliwa mapema. Makubaliano tunayokubaliana leo sio mwisho ni mwanzo wa utekelezaji,"

Naye Dkt. Michael Marere, Katibu Mkuu wa TAREWU amesema kuwa elimu ya fedha na uwekezaji kwa wanachama wake kupitia TIB itawawezesha wanachama wake kupaya elimu hiyo.

“Ustawi wa mwanachama hauishii katika masuala ya maslahi ya kikazi pekee. Tunaamini kwamba mwanachama anayekuwa na maarifa sahihi ya fedha, uwezo wa kupanga na kusimamia kipato chake, pamoja na kufanya maamuzi sahihi ya kifedha, anakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kujenga maisha yenye ustawi na usalama wa kiuchumi.”

Dkt. Marere ameongeza:“Hii ndiyo sababu TAREWU imeweka elimu ya fedha na ustawi wa kiuchumi kuwa miongoni mwa vipaumbele muhimu katika Mpango Mkakati wetu wa Pili wa 2026–2030. Ushirikiano wetu na TIB Rasilimali ni hatua ya kimkakati ya kuhakikisha kwamba azma hii inatekelezwa kwa vitendo na kuleta manufaa yanayoonekana katika maisha ya wanachama wetu.”

Aidha, Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa TAREWU inalenga kujenga utamaduni wa “mwanachama mwenye maarifa, mwenye uwezo wa kifedha na mwenye ustawi”, akieleza kuwa elimu ya fedha inapaswa kuwa sehemu ya uwezeshaji endelevu wa wanachama katika hatua mbalimbali za maisha yao.

“Tunataka kuondoka kwenye mtazamo wa elimu ya fedha kama tukio la mara moja na badala yake kuijenga kama utamaduni endelevu ndani ya TAREWU. Lengo letu ni kuwawezesha wanachama kuelewa fedha zao, kuzipangia malengo, kujenga akiba, kuwekeza kwa uelewa na kufanya maamuzi yanayolinda ustawi wao wa sasa na wa baadaye.”

Wakati huo huo Dkt. Marere amesema TAREWU hivi karibuni itazindua mfuko wa pamoja na uwezeshaji kwa wanachama wake.

NMB Foundation imetoa wito kwa wahitimu wa Kidato cha Sita mwaka 2026 wenye sifa kuwasilisha maombi ya Nuru Yangu Scholarship and Mentorship kabla ya dirisha kufungwa Ijumaa, Septemba 18, 2026.

Awamu hii imetengewa Sh bilioni 1 kufadhili vijana 50 wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza wa pointi tatu hadi tano, wanaotoka familia zenye uwezo mdogo na wanaojiunga na taasisi za elimu ya juu nchini.

Ufadhili utajumuisha ada na tozo za chuo, fedha za kujikimu, gharama za mafunzo kwa vitendo pamoja na kompyuta mpakato. Wanufaika pia watapata malezi elekezi na maandalizi ya kuingia katika soko la ajira.

Maombi yote yanaendelea kupokewa kupitia tovuti ya NMB Foundation, foundation.nmbbank.co.tz, hadi tarehe 18 Septemba 2026. Wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii wameombwa kuwafikishia taarifa vijana wenye sifa, hasa walioko vijijini.




MASHABIKI wa michezo ya kasino mtandaoni sasa wana sababu nyingine ya kuongeza presha ya ushindani, baada ya Expanse Cash Rush Challenge kuingia kazini ikiwa na zawadi nono zinazofikia jumla ya TZS 6,000,000. Mashindano haya yanayofanyika hadi Septemba 22, 2026, yanawapa wachezaji nafasi ya kuingia kwenye mbio za ushindi kupitia michezo 20 ya kusisimua kutoka Expanse ndani ya Meridianbet.

Katika ushindani huu, kila mchezaji ana nafasi ya kuchagua kati ya michezo 20 ya Expanse slot, huku dau la kuanzia likiwa ni TZS 1,000 pekee. Hii maana yake ni kwamba safari ya kuwania nafasi kwenye orodha ya washindi inaanza kwa dau dogo, lakini ushindani wenyewe unaweza kuwa mkubwa kadri siku zinavyosonga. Kila mzunguko unaweza kuongeza msisimko na kuifanya mbio ya Cash Rush kuwa tamu zaidi.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kivutio kikubwa zaidi ni hazina ya zawadi inayofikia TZS 6,000,000, ambayo imegawanywa kwa washindi 20 watakaofanya vizuri kwenye shindano hilo. Hivyo, si suala la kucheza tu, bali ni kuweka jumla ya dau zako katika mbio na kuhakikisha unajenga nafasi nzuri ya kuelekea kileleni. Kadri unavyoshiriki, ndivyo unavyoendelea kujitengenezea nafasi katika mashindano haya ya muda maalum.

Kwa wachezaji wanaopenda sloti zenye kasi, ushindani na nafasi ya kushinda zawadi za fedha, Cash Rush Challenge inakuja kama uwanja mwingine wa kuonyesha mbinu na uvumilivu. Kuanzia sasa hadi 22 Septemba, macho yanaelekezwa kwenye orodha ya washiriki huku kila mmoja akilenga kuandika jina lake miongoni mwa washindi 20 watakaogawana keki hiyo ya TZS 6 milioni.

Sasa ni wakati wa kuingia kwenye mbio, kuchagua mchezo unaoupenda kati ya michezo 20 ya Expanse na kuanza mbio kwa dau la chini la TZS 1,000. Usikubali mbio zipite bila wewe kushiriki. Expanse Cash Rush Challenge imewasha taa za ushindani, na zawadi ya TZS 6,000,000 ipo mezani kwa washindi.


ILE siku ya kutengeneza pesa ndefu na wakali wa ubashiri imefika, timu kibao kushuka dimbani kusaka ushindi. Je wewe unasaka ushindi wako wapi?. Ingia Meridianbet na ubeti sasa.

Yale mashindano ya Carabao Cup Raundi ya 3 kule Uingereza yataendelea ambapo mechi zipo kibao za kukufanya uwe mshindi, Ipswich atamenyana dhidi ya Arsenal ambao ni mabingwa watetezi wa ligi na vinara wa ligi hadi sasa huku nafasi ya kuondoka na mpunga ikiwa nje kabisa.

Mechi hii inakutanisha timu mbili zenye uwezo tofauti ambapo vijana wa Arteta wako kwenye kiwango bora sana si kwenye ligi tuu, bali kwenye mashindano yote ambapo wenyeji wao kwenye ligi hadi sasa wamekusanya pointi 6 kwenye mechi 4 huku wakiwa wameshinda mechi mbili na kupoteza mbili pia.

Huku Arsenal wao wameshinda mechi zote nne ambazo wamecheza huku wakiwa wameruhusu bao moja hadi sasa, na ni moja ya timu ambazo zinasifika kwa kujilinda zaidi hivyo ni ngumu mpinzani kupata goli.

Pesa kubwa ipo kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mechi nyingine ni hii ya Liverpool dhidi ya Tottenham Spurs ambao wameanza msimu vibaya sana wakiwa hawajashinda mechi yoyote hadi sasa , lakini pia bila kufunga bao lolote.

Kocha huyo wa Liver Iraola bado inajitafuta kwani imekuwa haina matokeo ya kushawishi sana tena hawa baada ya kutoa suluhu kwenye mechi yao wakiwa Anfield. Hii ni mechi ambayo Jogoo anahitaji kushinda ili kuthibitisha kwa mashabiki zao kuwa mpia una matokeo matatu.

Spurs licha ya kufanya usajili mkubwa msimu huu timu bado haipati matokeo mzuri, ambapo De Zerbi sasa ana kibarua kizito cha kufanya kipindi ambacho bado mechi hazijachanganya.

Mara ya mwisho kukutana timu hizi mbili, walitoa sare huku nafasi kubwa ya kupata ushindi pale Meridianbet anapewa Liver. Je wewe unampa nani nafasi kubwa ya kupata ushindi?. Suka jamvi hapa.

LALIGA kule Hispania ni mto juu ya moto Elche atamleta kwake Real Madrid ambapo kila timu inahitaji ushindi wa pointi 3 ili kuendelea kujiweka sawa kwenye msimamo wa ligi kuu.

Timu hiyo mpaka sasa kwenye mechi tano ambazo amecheza ameambulia pointi 2 pekee huku wenyeji wao wakiondoka na ppointi 12 kwenye msimamo wa ligi baada ya kupata ushindi mnono kwenye mechi yao iliyopita. Nani kushinda leo?. Jisajili hapa.

Madrid chini ya kocha mkuu Jose Mourinho wanahitaji kupambania taji la ligi kuu ambalo hawajalipata kwa muda sasa huku wakiwa wamewekeza kwenye usajili wa wachezaji wenye uwezo mkubwa ambao kwa pamoja wanaweza kuisaidia timu kufika malengo yao.

Hii sio mara ya kwanza wawili hawa kukutana, msimu uliopita kwenye mechi mbili za ligi walipokutana, Real aliondoka na pointi 4 ambapo mechi ya kwanza walitoa sare na ya pili wakashinda. Je leo hii nani unampa beti yako ya ushindi?. Suka jamvi hapa.

Meridianbet wao wanampa nafasi ya ushindi Mourinho na vijana wake, lakini pia mechi hii imepewa machaguo zaidi ya 1000. Beti sasa
NGORONGORO | SEPTEMBA 14, 2026

Watumishi wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa wamefanya ziara ya utalii wa ndani katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Bonde la Olduvai Gorge, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha utalii wa ndani, kuimarisha mshikamano na kuongeza ari ya utendaji kazi.

Katika ziara hiyo, watumishi wamepata fursa ya kujifunza kuhusu historia ya binadamu na masalia ya viumbe wa kale yanayopatikana Olduvai Gorge, eneo lenye umuhimu mkubwa katika tafiti za historia na maendeleo ya mwanadamu.

Aidha, wametembelea maeneo mbalimbali ya Hifadhi ya Ngorongoro na kushuhudia vivutio vya asili pamoja na wanyamapori mbalimbali, wakiwemo tembo, simba, faru, nyati, pundamilia, nyumbu, mbweha, swala, mbuni, viboko, ngiri na aina mbalimbali za ndege.

Ziara hiyo pia imelenga kuwahamasisha watumishi wengine na wananchi kwa ujumla kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini, sambamba na kukuza utamaduni wa utalii wa ndani, kubadilishana uzoefu na kuimarisha mahusiano miongoni mwa watumishi.











Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Serbia, mwenye makazi yake Roma, Italia, Mhe. Mbarouk Nassor Mbarouk, amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Serbia, Mhe. Aleksandar Vučić, katika Ikulu ya nchi hiyo jijini Belgrade tarehe 14 Septemba 2026.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya Hati hizo, Balozi Mbarouk amewasilisha salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa Rais Mhe. Aleksandar Vučić, Serikali na wananchi wa Serbia, na kusisitiza dhamira ya Tanzania ya kuendeleza uhusiano wa kirafiki na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Balozi Mbarouk ameeleza vipaumbele vya kipindi chake cha uwakilishi, akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, hususan katika maeneo ya biashara, kilimo, uwekezaji na elimu. Aidha Mheshimiwa Mbarouk ameeleza dhamira ya kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Serbia na wadau mbalimbali katika kuendeleza maeneo hayo kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizo mbili.

Kwa upande wake, Rais Vučić amempongeza Balozi Mbarouk kwa kuteuliwa kwake na kumtakia mafanikio katika utekelezaji wa majukumu yake ya kidiplomasia nchini Serbia, huku akiahidi kumpa ushirikiano katika kipindi chake cha uwakilishi.



MRATIBU wa Jukwaa la Kimataifa la Biashara na Uwekezaji la Kilimo na HortiLogistica Africa, Loveness Adolf, amewakaribisha wakulima, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau wengine wa sekta ya kilimo kujisajili mapema kushiriki HortiLogistica Africa 2026, itakayofanyika Novemba 8 hadi 10, 2026 katika Hoteli ya Ngurdoto, Arusha.

Amesema jukwaa hilo lenye kaulimbiu “Kuunganisha Masoko, Kukuza Ustawi” linatarajiwa kuwa na zaidi ya waonyeshaji 500 na kuvutia wageni kati ya 10,000 na 12,000, likilenga kuwaunganisha wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo na biashara.

Loveness amesema tukio hilo litatoa nafasi kwa washiriki kuonyesha bidhaa na huduma zao, kujenga mahusiano ya kibiashara na kutafuta fursa mpya katika masoko ya ndani na kimataifa.
Akizungumzia nafasi ya kilimo hai katika uchumi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Bakari Mongo, amesema kilimo hicho kina uwezo wa kuongeza uzalishaji, thamani ya mazao na ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko mbalimbali.

Amesema Tanzania ina fursa kubwa katika uzalishaji wa viungo, mazao ya asili na bidhaa nyingine zinazoweza kuongezewa thamani kupitia uchakataji, hivyo wakulima na wajasiriamali wanapaswa kutumia fursa hizo kukuza biashara zao.

Mongo amesema ushirikiano kati ya wakulima, vikundi vya wazalishaji, wasindikaji, wafanyabiashara na wadau wa uwekezaji ni muhimu katika kuhakikisha bidhaa za kilimo hai zinafikia masoko yenye tija.

Wakati huo huo Loveness amesema Jukwaa hilo litakuwa na shughuli mbalimbali zitakazowapa washiriki nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kufurahia mazingira ya Arusha wakati wa mkutano huo.

Amesema miongoni mwa shughuli zitakazofanyika ni camping, wellness ikiwemo huduma za massage, food fun run kutoka Mbuga kuelekea Arusha National Park, pamoja na programu ya ‘African Invite’ itakayolenga kuonyesha vyakula, utamaduni na burudani mbalimbali za Afrika.

Amesema pia kutakuwa na maonesho yanayoangazia mwelekeo wa sekta ya kilimo na utalii kwa miaka ijayo, yakiwemo maendeleo ya uzalishaji na uuzaji wa mazao kama parachichi, ili kuwawezesha washiriki kupata taswira ya fursa zinazoweza kujitokeza katika sekta hizo.

Kilimo hai chatajwa kuwa fursa ya kukuza biashara na masoko ya kimataifa
Mwanachama wa Taasisi Mwavuli ya Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Charles Bupamba, amesema wadau wa sekta ya kilimo wanatakiwa kutumia fursa zinazotokana na kilimo hai na kilimo ikolojia kuongeza uzalishaji wa bidhaa bora, salama na zenye ushindani katika masoko ya ndani na kimataifa. 

Bupamba amesema kilimo hai na kilimo ikolojia si jambo la kupuuzwa, kwani Tanzania ina wakulima na wazalishaji wanaojihusisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, ikiwamo viungo, mazao ya asili na bidhaa nyingine ambazo zinaweza kusindikwa, kuongezwa thamani na kuuzwa katika masoko mbalimbali.

Amesema kilimo hai na kilimo ikolojia ni miongoni mwa suluhisho muhimu kwa maendeleo ya sekta ya kilimo, huku kikitoa fursa kwa wakulima, vikundi vya wazalishaji, wasindikaji, biashara ndogo na za kati pamoja na vijana kuongeza thamani ya mazao na kukuza biashara zao.

Amesisitiza kuwa ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wakulima, wazalishaji na wafanyabiashara, akieleza kuwa majukwaa ya kimataifa yanatoa fursa kwa wadau kuonyesha bidhaa zao, kukutana na wanunuzi kutoka maeneo mbalimbali duniani, kujenga ushirikiano na wataalamu, kubadilishana uzoefu na maarifa, pamoja na kutafuta masoko mapya. Amesema pia majukwaa hayo yanawezesha wadau kujifunza teknolojia mpya katika kilimo, usindikaji na mifumo ya mnyororo wa thamani, hivyo kuongeza tija na ushindani wa bidhaa za Tanzania.

Na Janeth Raphael - MichuziTv

Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imewataka wataalamu wote waliosajiliwa ambao hawajalipa ada zao za mwaka kukamilisha malipo ya madeni yote ndani ya siku 30, ikionya kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo wanaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria, ikiwemo kufutiwa usajili na majina yao kuchapishwa rasmi.

Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, Godfred Mbanyi, ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa wajibu wa wataalamu waliosajiliwa na Bodi. Amesema hatua hizo zinalenga kuhakikisha wataalamu wanatimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazosimamia taaluma ya ununuzi na ugavi nchini.

PSPTB ni taasisi ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Fedha, iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi, Sura ya 179 ya Sheria za Tanzania. Bodi ina jukumu la kusimamia na kudhibiti viwango, mwenendo na maadili ya taaluma hiyo, huku ikiwa na mamlaka ya kusajili watu wanaokidhi vigezo na kuwapa uhalali wa kufanya kazi za kitaaluma katika eneo hilo.

Bodi imekumbusha kuwa ulipaji wa ada ya mwaka ni wajibu wa kisheria kwa kila mtaalamu aliyesajiliwa, kwa mujibu wa kanuni zake, ikiwemo Tangazo la Serikali Na. 364 la mwaka 2009. Mtaalamu anayeshindwa kulipa ada hiyo kwa kipindi cha miezi 24 mfululizo anaweza kupoteza hadhi ya usajili na jina lake kuondolewa kwenye daftari rasmi la PSPTB.

Aidha, PSPTB imeonya kuwa mtu anayeendelea kufanya kazi, kujitambulisha au kujihusisha na taaluma ya ununuzi na ugavi bila kuwa amesajiliwa na Bodi anafanya kosa la jinai na anaweza kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. Kwa mujibu wa Kifungu cha 46(2) na (3) cha Sheria ya PSPTB, Bodi ina mamlaka ya kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu dhidi ya wanaokiuka masharti hayo.

Kwa hatua hiyo, PSPTB imewataka wataalamu wote wenye madeni ya ada ya mwaka kuhakikisha wamelipa madeni yao yote ndani ya siku 30 kuanzia tarehe ya tangazo hilo. Bodi imesisitiza kuwa watakaokaidi watachukuliwa hatua, ikiwemo kufutiwa usajili, kuchapishwa kwa majina yao na, pale inapobidi, kufunguliwa mashitaka kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Bodi.



*Pia atoa maelekezo kwa TANROAD,Wakandarasi, wamiliki wa majengo 


Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MKUU wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Edward Mpogolo ametoa maelekezo kwa wafanyabishara katika maeneo ya Kariakoo katika kila meza tatu kunakuwa na chombo cha kuhifadhia taka huku pia wakandarasi nao wakitakiwa kuweka vyombo vikubwa Vya taka katika mitaa.

Mpogolo ametoa maelekezo hayo jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa shughuli za kufanya usafi katika mitaa mbalimbali ya Kariakoo likiwemo kwanza eneo pia la Soko Kuu la Kariakoo.

Akieleza mbele ya wananchi na wafanyabiashara wa Kariakoo Mpogolo amesema katika kuhakikisha Kariakoo inakuwa safi ni wajibu wa kila mfanyabiashara kuwa sehemu ya kuunga mkono jitihada zinazoendelea ili mazingira kuwa safi wakati wote.

“Kwa wafanyabiashara hakikisheni mnakuwa na chombo cha kuhifadhia taka, na Maelezo haya sio ombi ni lazima, kila baada ya baada ya meza tatu kuwe na chombo cha taka.Kwa wafanyabiashara ambao katika meza zao kutakuwa na taka watatozwa faini na meza itaondolewa kwa wiki moja.

“Na kwa wakandari katika kila mtaa wa Kariakoo kuwe na chombo kikubwa cha kuhifadhi taka.Kukiwa na vyombo vikubwa kwa ajili ya kuhifadhia taka maana yake wafanyabishara vyombo vyao vinapokuwa vimejaa watapeleka katika vyombo vikubwa vilivyopo katika mitaa ya Kariakoo.”

Kuhusu mitaro ya maji kuziba katika mitaa mbalimbali ya Kariakoo,Mpogolo ametoa maelekezo kwa Wakala wa Barabara Tanzania(TANROAD) kuhakikisha wanaanza kazi ya kusafisha mitaro hiyo ili maji yatiririke.

Kwa upande wa taa za barabarani Mpogolo amesema Wilaya hiyo imejipanga vema na kusisitiza taa za barabarani zitawekwa katika maeneo yote yaliyokusudiwa huku pia akitoa rai kwa wamiliki wa majengo Kariakoo kuhakikisha nao wanafunga taa.

Pia ametoa onyo kwa wamiliki wa majengo yanayoendelea kujengwa Kariakoo kuacha tabia ya kuweka matofali,mchanga na kokoto kwa muda mrefu katika barabara za mtaani.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kariakoo jijini Dar es Salaam Haji Manara amesema siasa za Kariakoo ni usafi wa mazingira pamoja na utulivu kwa wafanyabiashara wakubwa na wadogo, hivyo usafi ndio kipaumbele kwao.

“Mkuu wa Wilaya ya Ilala jitihada zako kuhusu usafi tunaziona lakini pia tumekuwa na vikao vya mara kwa mara kuzungumzia na kuweka mikakati ya usafi.Pia tunajua dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Usafi kwa Jiji la Dar es Salaam.”

Manara amesema pamoja na usafi unaoendelea lakini bado kuna baadhi ya mitaa uchafu ni changamoto kutokana na mitaro mingi kuziba, pia kuna mitaa ambayo haipitiki kabisa hivyo ametoa ombi kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala kufungua mitaa hiyo,ombi ambalo limekubaliwa.



 

Benki ya NMB imeorodheshwa katika nafasi ya tisa duniani ndani ya Daraja la Sita la benki zenye mali ya kati ya Dola za Marekani bilioni 3 na bilioni 10. NMB ni miongoni mwa benki 500 kutoka nchi 89 zilizojumuishwa katika orodha ya Forbes ya World’s Top Performing Banks 2026.

Forbes na Statista zilifanya tathmini hiyo kwa kuzingatia uwezo wa kupata faida, ukuaji na ubora wa mapato, uimara wa mtaji na vyanzo vya fedha, pamoja na ubora wa mali na ufanisi wa uendeshaji. Mwaka 2025, NMB iliripoti faida baada ya kodi ya takribani Sh760 bilioni na mali ya Sh17.6 trilioni.

Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna, amesema utambuzi huo unaakisi mageuzi ya muda mrefu ya benki na uwezo wa sekta ya benki Tanzania kushindana kimataifa.

Zaipuna amesema NMB itaendelea kutumia ukubwa wake, teknolojia, ushirikiano na uwezo wa kifedha kupanua upatikanaji wa mitaji katika kilimo, viwanda, biashara, miundombinu na uchumi wa kidijitali, ikiwa ni sehemu ya kusaidia utekelezaji wa Dira 2050.


Na. Jeshi la Polisi Dar es Salaam.

Katika kuhakikisha Jeshi la Polisi linaaendelea kujiimarisha katika Mafunzo na kutoa huduma Bora kwa Wananchi limeendelea kutoa mafunzo ndani na nje ya Tanzania kwa lengo la kuwajengea uwezo askari katika kutekeleza majukum kwa weledi na usasa ili kufanikisha adhima ya kutoa huduma bora kwa wananchi wanaolitegemea Jeshi hilo kwa ulinzi wao na mali.

Akiwaaga kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Camillus Wambura Mkuu wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Dkt Lazaro Mambosasa  amewataka Maafisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali wanaokwenda kuhudhuria mafunzo nchini Indonesia, kutumia vyema fursa hiyo kwa kuzingatia masomo watakayopatiwa na kuhakikisha maarifa na ujuzi watakaoupata unakuwa chachu ya kuleta tija, ufanisi na usasa katika utendaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, hususani katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Ameongeza kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi amesisitiza  washiriki hao wanatakiwa kuzingatia nidhamu, weledi na maadili ya Jeshi la Polisi wakati wote watakapokuwa nchini Indonesia huku akiwataka kuwakilisha vyema Tanzania na Jeshi la Polisi kwa kuhakikisha wanakuwa na mwenendo unaotoa taswira nzuri ya nchi yetu.

Aidha amewataka washiriki hao kutumia fursa hiyo kuitangaza Tanzania kwa kuonyesha sifa njema ya nchi yetu katika kudumisha amani, usalama na utulivu, pamoja na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ambapo pia amewataka kutangaza maeneo ya kipekee yenye umuhimu wa kihistoria na kiutalii, ikiwemo Bonde la Ngorongoro, ambalo ni miongoni mwa maeneo ya urithi wa dunia.

Dkt Mambosasa amebainisha kuwa Mafunzo hayo yanatarajiwa kujikita katika maeneo mbalimbali muhimu, yakiwemo, Uongozi na Maendeleo ya Kitaaluma (Professional Development and Leadership), Ushirikishwaji wa Jamii katika Ulinzi na Usalama (Community Policing) Teknolojia Zinazochipukia (Emerging Technologies), ikiwemo Akili Bandia (AI) Matukio Makubwa na Mbinu za Uchunguzi wa Jinai (High-Profile Incidents and Criminal Investigative Techniques) Mbinu Bora za Utendaji na Ubunifu (Best Practices and Innovations).

Sambamba na hayo ameweka wazi kuwa Masomo hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko na maboresho katika utendaji wa kazi za kila siku wa Jeshi la Polisi Tanzania, kwa kuwawezesha washiriki kupata maarifa, ujuzi na uzoefu mpya utakaosaidia kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukum ya Jeshi la Polisi.

Mafunzo hayo ya shirikisho la askari wa kike duniani na wasimamizi wa sheria IAWP yatahusisha nchi washiriki zaidi ya 64.





Na Farida Said Mkinga Tanga

Uwekezaji mkubwa unaotekelezwa na Chuo Kikuu Mzumbe kupitia ujenzi wa Kampasi ya Tanga, iliyopo Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, unatarajiwa kuwa chachu ya mageuzi ya kielimu, kijamii na kiuchumi katika eneo hilo.

Kampasi hiyo inatarajiwa kufungua fursa mbalimbali kwa wananchi wa Mkinga na maeneo jirani, ikiwemo upatikanaji wa elimu ya juu, huduma za afya, ajira, biashara pamoja na kuvutia uwekezaji katika maeneo mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Chuo hicho ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti Mstaafu wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara katika eneo la ujenzi wa Kampasi hiyo lililopo Kata ya Gombero, Wilaya ya Mkinga.

Ziara hiyo imelenga kujionea maendeleo ya ujenzi wa Kampasi hiyo pamoja na kusisitiza umuhimu wa kukamilisha miundombinu iliyosalia ili Kampasi hiyo ianze kutoa huduma zilizokusudiwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Shein amesema uwekezaji huo ni sehemu ya maono ya muda mrefu yenye manufaa mapana kwa jamii, akibainisha kuwa ubora wa majengo na miundombinu unaoonekana katika eneo hilo unaonesha dhamira ya Chuo Kikuu Mzumbe katika kujenga miundombinu endelevu itakayohudumia vizazi mbalimbali.

“Tunachokijenga hapa si kwa ajili yetu tu. Watakaokuja kunufaika zaidi ni watoto wetu, wajukuu zetu na vizazi vinavyofuata,” amesema Dkt. Shein.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amesema Kampasi hiyo ipo katika hatua za mwisho kuelekea kuanza kutoa huduma.

Amesema kazi kubwa iliyosalia ni ukamilishaji wa maeneo mbalimbali ya Kampasi, ambapo mkandarasi anaendelea na kazi hizo kabla ya miundombinu hiyo kuwa tayari kwa matumizi.

Kwa mujibu wa Prof. Mwegoha, kukamilika kwa ujenzi huo kutawezesha Kampasi kuanza kutekeleza majukumu yake na kutoa huduma mbalimbali zilizokusudiwa kwa jamii na wadau wengine.

Akizungumzia fursa zinazotokana na uwekezaji huo, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe, Balozi Modest Jonathan Mero, amesema uwepo wa Kampasi hiyo Mkinga ni fursa mpya ya maendeleo kwa jamii.

Amesema Kampasi hiyo itakuwa na mchango mkubwa katika sekta za elimu, afya, biashara na uwekezaji, huku mwingiliano kati ya wanafunzi, wataalamu na jamii ukiwa na nafasi muhimu katika kuchochea maendeleo ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Mhe. Gilbert Kalima, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Chuo Kikuu Mzumbe pamoja na wadau wengine kuhakikisha changamoto zinazoweza kuchelewesha matumizi ya Kampasi hiyo zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Aidha, Mhe. Kalima ametambua na kupongeza mchango wa viongozi wa vijiji waliowezesha upatikanaji wa eneo lenye ukubwa wa takribani ekari 300 kwa ajili ya ujenzi wa Kampasi hiyo.

Amesema upatikanaji wa eneo hilo umeweka msingi muhimu wa utekelezaji wa uwekezaji huo mkubwa, ambao unatarajiwa kuwa na manufaa ya muda mrefu kwa wananchi wa Mkinga na maeneo jirani.








Na mwandishi wetu

DODOMA. Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Profesa Dos Santos Silayo, amewataka watumishi wapya 328 kutumia mafunzo ya kijeshi na ukakamavu waliyopitia kujenga nidhamu, uadilifu na weledi katika kulinda rasilimali za misitu na nyuki nchini.

Profesa Silayo amesema hayo leo, Jumatatu, Septemba 14, 2026, wakati akifungua mafunzo elekezi kwa watumishi hao katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP-Mipango), Dodoma.

Watumishi hao wamepitia mafunzo ya awali ya kijeshi na ukakamavu katika Kituo cha Mafunzo cha TFS, Mlele kwa miezi sita, kabla ya kuanza majukumu katika vituo mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Profesa Silayo amesema mafunzo hayo hayakuwa mepesi, lakini yamewajengea nidhamu na ukakamavu unaohitajika katika kutekeleza majukumu yao kama askari wa uhifadhi.

Amewataka kufanya kazi kwa bidii, ubora na utu, huku wakiepuka rushwa, tamaa, uzembe na matumizi mabaya ya madaraka.

“Tufanye kazi hii kwa bidii, tuifanye kwa ubora wa hali ya juu, lakini tufanye kwa utu,” amesema.

Amesema watumishi hao wana taaluma mbalimbali, zikiwamo uhandisi, afya, manunuzi, uhasibu, misitu na nyuki, lakini wameunganishwa na dhamira moja ya kulinda na kuendeleza rasilimali za misitu na nyuki.

Pia amewataka kuheshimu viongozi na mfumo wa uongozi, kujifunza kutoka kwa watumishi waliowatangulia na kutumia taaluma zao kwa manufaa ya TFS na Taifa.

Baada ya kukamilisha mafunzo hayo elekezi, watumishi hao wanatarajiwa kupangiwa vituo mbalimbali vya kazi nchini.







Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu Stephen Wasira, amewasili leo mkoani Iringa, ambapo amepokelewa na viongozi wa Chama na Serikali wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Komredi Daudi Yasin.

Ndugu Wasira amepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Nduli, mkoani Iringa, alipowasili kwa ajili ya shughuli mbalimbali za Chama.

Akiwa mkoani humo, pamoja na shughuli nyingine, Ndugu Wasira anatarajiwa kufungua Mafunzo ya Wakufunzi wa Chama yatakayofanyika katika Chuo cha Mafunzo cha Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).






Top News