*Kambi maalum inaanza Jumatatu hadi Septemba 11
Na Mwandishi Wetu
HOSPITALI ya Shifaa Pan African ya Kinondoni jijini Dar es Salaam imeandaa kambi maalum kufanya upasuaji wa kupunguza uzito kwa kutumia matundu madogo kuanzia Agosti 31 mpaka Septemba 11.
Daktari bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo, Kassim Bahsan alisema jana kuwa kambi hiyo itafanyika katika hospitali hiyo kuanzia Agosti 31 mwezi huu hadi Septemba 11.
Alisema katika kambi hiyo wananchi watapata fursa ya kufanyiwa tathmini ya mwili na kupata ushauri wa kitaalamu wa upasuaji wa kupunguza uzito kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya matundu madogo.
“Kama umekuwa ukipambana na unene kupita kiasi na unatafuta njia salama na yenye ufanisi ya kuboresha afya yako hii ni fursa muhimu ya kuchukua hatua kuelekea maisha yenye afya bora,” alisema Dk Bahsan
Alisema tarehe 4 mwezi Septemba hospitali ya Shifaa itaendesha mdahalo wa elimu kwa umma ambapo wananchi wote wanalikwa kushiriki kupata uelewa wa upasuaji wa kupunguza uzito.
“Ni semina ya elimu ya kupunguza uzito, watafahamu ni kwanini na nani ni mnufaika wa upasuaji huu watu watajifunza na watasikia ushuhuda kwa watu waliofanyiwa upasuaji na kupungua uzito, wengine wameacha dozi za kisukari, maumivu ya nyonga yameisha,” alisema
Naye Mkuu wa Idara ya Upasuaji hospitalini hapo, Dk Murad Tarmohamed alisema hiyo ni fursa kwa watu wenye matatizo ya uzito uliopitiliza kwani wanaweza kurejea kwenye maisha yao ya kawaida baada ya upasuaji.
“Wananchi waitumie hii fursa kukutana na madaktari bingwa wabobezi kwenye upasuaji ambao watawashauri hatua za kuchukua kabla ya upasuaji ili wafanyiwe matibabu yatakayowarejesha kwenye maisha ya kawaida,” alisema
“Uzuri ni kwamba upasuaji huu unafanywa kwa njia ya matundu madogo ambao unamwezesha mtu aliyefanyiwa matibabu kupona haraka na kuendelea na shughuli zake za kila siku,” alisema
Aidha, alisema kuna ushuhuda wa baadhi ya watu waliofanyiwa upasuaji kwenye hospitali hiyo wakiwa na uzito wa hadi kilo 148 na kufanikiwa kurudi kwenye kilo 98 ambao kwa sasa wanaishi maisha bora wakiwa wameondokana na uzito uliopitiliza.
Hospitali hiyo imeshawafanyia upasuaji wa kupunguza uzito ambao umekuwa wa wenye mafanikio kwa kutumia tundu dogo watu 20 waliokuwa na uzito mkubwa.
Daktari bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo, Murad Tarmohamed, alisema hospitali hiyo imeweka wataalamu bobezi kwa ajili ya taaluma hiyo.
“Watu wengi wanadhani kuwa upasuaji huu ni kwaajili ya urembo hapana, unafaida nyingi sana kama kuepuka magonjwa ya sukari na wakishafanyiwa wakapona kabisa, kuna watu wanakosa pumzi sababu ya uzito mkubwa wakifanyiwa wanapona,” alisema
Alisema kuna watu ambao wanapata shida ya magoti na nyonga sababu ya maumivu wanayopata wanapotembea lakini wakifanyiwa upasuaji wanapona.
Alisema magonjwa kama ya moyo yanayotokana na uzito kuwa mkubwa yamekuwa yakiondoka kwa watu wanaofanyiwa huduma hiyo.
“Mtu anapofanyiwa upasuaji huu anakuwa na nguvu zaidi anarudi kwenye maisha ya kawaida, anaacha kuchoka mara kwa mara anakuwa anafanya shughuli zake kama zamani, tunasisitiza ni muhimu sana si kwa muonekano bali kwa ajili ya afya ya mhusika,” alisema
“Umuhimu wa upasuaji kama huu ni shida ambazo unaondokana nazo baaada ya upasuaji kama moyo, sukari, presha sukari, maumivu ya nyonga, magoti na kukosa pumzi ukiwa umelala,” alisema hiyo ni kambi ya tatu kufanya hospitali ya Shifaa
“Faida ya upasuaji huu ni kwamba mgonjwa hakai sana hospitalini, akifanyiwa leo kesho anatoka anakwenda nyumbani kuendelea na maisha yake kama kawaida,” alisema



.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)







.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)













