Na Mwandishi Wetu, DSM.

Serikali kupitia Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) kwa kushirikiana na Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya huu (HESLB) imeanzisha mfuko wa Ngorongoro Scholarship Fund kwa lengo la kuwezesha wanafunzi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kupata fursa ya masomo ya elimu ya juu kupitia ufadhili Ngorongoro Fund.

Akizungumza wakati wa mkutano wa waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam kwa niaba ya kamishna wa Uhifadhi, Kamishna msaidizi mwandamizi wa uhifadhi anayesimamia idara ya Maendeleo ya Jamii Gloria Bideberi ameeleza kuwa Program hiyo inalenga kuboresha maisha ya jamii zinazoishi ndani ya hifadhi, ambapo kwa kushirikiana na bodi ya mikopo ya elimu ya juu watahakikisha kila mtoto anayeishi ndani ya hifadhi hiyo anayekidhi vigezo anapata nafasi ya kupata ufadhili wa elimu ya juu.

“Kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ufadhili huu utasaidia kuondoa malalamiko ya upendeleo, taratibu zote za ufadhili wa vijana wetu zitakuwa wazi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa tukitambua kuwa elimu ndiyo msingi wa kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi, kijamii na mazingira” amesema kamishna Bideberi.

Ameongeza kuwa Ngorongoro Fund inaongozwa na kauli mbiu isemayo "Elimu Endelevu kwa Maendeleo ya Jamii na Uhifadhi" itakwenda kufadhili watoto wa kitanzania waliodahiliwa katika vyuo vilivyopo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kunufaisha vijana watakaojikita katika masomo ya uhifadhi wa Wanyamapori na misitu, Malikale na utalii na hapo baadaye wigo utaendelea kutanuliwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Dkt. Bill Kiwia amesema kuanzia mwaka wa masomo 2026/2027, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwa kushirikiana Ngorongoro, itaanza kutoa ufadhili huo maalum kwa wanafunzi kutoka eneo la Hifadhi ya Ngorongoro watakaosoma fani zinazohusiana na uhifadhi wa maliasili, usimamizi wa wanyamapori, pamoja na taaluma nyingine zitakazoainishwa katika Mwongozo wa Utoaji wa Scholarship hiyo.

Dkt. Kiwia ameeleza kuwa hatua ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huu utaanza kwa kutoa ufadhili kwa wanafunzi 15, ambapo Ngorongoro imetenga shilingi milioni 99 kugharamia masomo ya ufadhili na kuwawezesha vijana hao kupata elimu ya juu, kujenga wataalamu watakaosaidia kuhifadhi rasilimali za Taifa, na kuchochea maendeleo endelevu ya jamii zinazozungukaHifadhi ya Ngorongoro.

Kwa ushirikiano wa karibu kati ya HESLB na NCAA, tayari tumekamilisha Mwongozo Maalum wa Utoaji wa Scholarship ya NCAA ambapo mwongozo huo umeweka vigezo, taratibu na masharti ya utoaji wa ufadhili huo kwa wanafunzi wanaotoka katika jamii zinazoishi ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kutambua programu mahususi zitakazopewa kipaumbele, hususan zile zinazohusiana na uhifadhi wa maliasili, usimamizi wa wanyamapori na taaluma nyingine zinazochangia maendeleo endelevu ya eneo la Ngorongoro na Taifa kwa ujumla.

Sambamba na mwongozo huo, HESLB imekamilisha maandalizi ya mfumo wa kidijitali wa kupokea na kuchakata maombi ya scholarship ambapo hii dirisha la kupokea maombi litafunguliwa tarehe 15 Agosti, 2026, kwa sasa Ngorongoro na bodi ya mikopo zinaendelea kutoa elimu na uhamasishaji kwa waombaji watarajiwa ili kuwawezesha kuelewa vigezo vya scholarship hii na kujaza maombi yao kwa usahihi na kwa wakati.

Kabla makubaliano haya ya leo, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ilikuwa ikitekeleza ufadhili huu kupitia Baraza la Wafugaji ambapo mpaka mwaka wa fedha uliopita 2025/2026 zaidi ya watu elfu kumi na tano kutoka ndani ya hifadhi wamepatiwa ufadhili katika nyanja mbalimbali ikiwemo ualimu, udaktari, uhandisi, uhasibu, wataalamu wa uhifadhi na kada nyingine nyingi zinazochangia maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.












Na Victor Masangu, Kibaha

Katika kupambana na wimbi la umasikini na kuachana na kuwa tegemezi kwa wanawake Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja ameamua kutoa darasa maalumu kwa ajili ya kufundisha mafunzo ya ujasiriamali na jinsi ya kutenghheneza bidhaa kwa wanawake mbali mbali kwa lengo la kuweza kuwasaidia kuachana na kuwa tegemezi ikiwa sambamba na kujikwamua kiuchumi

Hayo yamebaishwa wakati wa ziara yake maalumu yenye lengo la kuweza kukutana na baadhi ya makundi ya wanawake kwa ajili ya kutoa darasa la mafunzo mbali mbali ya ujasiliamali yenye lengo la kuwaongozea ujuzi na elimu ambayo itawasaidia katika kutengeneza biadha za aina tofauti.

Mwenyekiti huyo ametoa darasa la mafunzo hayo kwa wanawake wa jumuiya ya UWT katika kata mbili za Msangani na Kata ya Mkuza ambapo zaidi ya wanawake 100 wameweza kupatiwa mafunzo mbali mbali ya kutengeneza bidhaa mbali mbali ikiwemo kufundisha jinsi ya kutengeneza bidhaa za batiki, sabuni za kuogea, sabuni za chooni,shampuu kwa ajili ya nywele.

Mgonja amebainisha kwamba ametoa kutoa elimu hiyo ya darasa la mafunzo ya ujasiriamali bure bila malipo ikiwa ni utekelezaji wake wa ahadi ambayo aliitoa wakati akiwa katika ziara yake ya kuwashukuru wanawake hao ambao waliweza kukiheshimisha chama wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ambapo waliweza kupiga kura za kisdindo.

"Ahadi ni deni kwa hiyo mimi kama Mwenyekiti wa UWT nimekuja kuwapa elimu na mafunzo mbali mbali ya ujasiliamali bila malipo ya iana yoyote na kwamba mafunzo hayo ni moja ya ahadi yangu ambayo niliitoa wakati nikiwa katika ziara yangu ya kutoa shukrani kwa wanawake kukipigia chama cha mapinduzi kura nyingi za kishindo katika uchaguzi mkuu,"amebainisha Mwenyekiti Mgonja.

Kwa upande wake Katibu katibu wa UWT Cesilia Ndaru amewahimiza wanawake kuhakikisha kwamba wanatumia fursa mbali mbali za ujasiriamali na kuachana kabisa na tabia ya kuwa na majungu na kuzungumza maneno ambayo hayana faida yoyote na badala yake wajiunge katika vikundi vya ujasiriamali.

Naye mjumbe wa kamati ya utekeelzaji wa UWT Zainabu Gama amebainisha kwamba darasa la mafunzo hayo yataweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa wanawake hao katika kujiongezea kipato na kujikwamu kiuchumi.

Nao baadhi ya wanawake kutoka kata za Msangani na Mkuza ambao wameweza kupata fursa ya kupata elimu hiyo ya kutengeneza bidhaa mbali mbali wamesema wamempongeza Mwenyekiti wa UWT kwa kuwapatia darasa hilo la elimu ambayo itakwenda kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika kujikwamua na wimbi la umasikini na kujikwamua kiuchumi.

Ziara maalumu ya Mwenyekiti wa UWT Kibaha mjini ambayo imendaliwa mahususi kwa ajili ya kutekeleza ahadi yake ambayo aliitoa ya kuwa na darasa la kutoa elimu ya ujasiriamali na jinsi ya kutengeneza bidha bila malipo ambapo ameanza mafunzo hayo katika kata mbili za Msangani pamoja na Mkuza.







Na Mwandishi Wetu
MARAIS sita wa Afrika wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, wanatarajiwa kushiriki Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika utakaofanyika Agosti 5 na 6, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam. Viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria ni Rais wa Angola, João Lourenço, Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, Rais wa Msumbiji, Daniel Francisco Chapo, Rais wa Nigeria, Bola Ahmed Tinubu, Rais wa Kenya, Dkt. William Samoei Ruto na Rais wa Gabon, Brice Clotaire Oligui Nguema.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Agosti, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema Serikali imekamilisha maandalizi yote ya kuwa mwenyeji wa mkutano huo mkubwa wa kimataifa unaotarajiwa kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 1,200 kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika, wakiwemo viongozi wa taasisi za fedha za kimataifa, wanahisa wa Africa50, wawekezaji, viongozi wa sekta binafsi na washirika wa maendeleo.

Chalamila amesema mkutano huo ni miongoni mwa majukwaa makubwa zaidi ya mwaka 2026 yanayolenga kuharakisha maendeleo ya miundombinu barani Afrika kupitia ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), huku ukiipa Tanzania fursa ya kujitangaza kama kitovu cha biashara, uwekezaji na maendeleo ya miundombinu Afrika.

Amesema kupitia mkutano huo, Serikali itawasilisha miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), Bandari ya Dar es Salaam, miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme pamoja na miundombinu ya TEHAMA, kwa lengo la kuvutia uwekezaji wa kimataifa na kuharakisha utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (FYDP IV) pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Chalamila amewahakikishia wananchi na wageni wote kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika kwa ushirikiano wa wizara mbalimbali, taasisi za Serikali, vyombo vya ulinzi na usalama na wadau wengine ili kuhakikisha mkutano huo unafanyika katika mazingira salama, tulivu na yenye viwango vya kimataifa. Aliongeza kuwa Mkoa wa Dar es Salaam umejipanga kuhakikisha wageni wote wanapata huduma bora tangu wanapowasili hadi watakapoondoka nchini.

Aidha, amewataka wananchi kuwapokea wageni kwa ukarimu, kudumisha usafi wa mazingira na kuzingatia sheria na taratibu za nchi, huku akiwahimiza wafanyabiashara na watoa huduma kutumia fursa hiyo kutoa huduma bora, zenye weledi na uadilifu pamoja na kuepuka upandishaji wa bei usio halali ili kuendelea kuijengea Tanzania taswira nzuri mbele ya jumuiya ya kimataifa.

Chalamila amesema Serikali inaamini mafanikio ya mkutano huo yataongeza fursa za uwekezaji, kukuza uchumi, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa pamoja na kufungua ajira na fursa mpya za maendeleo kwa Watanzania.



Na Mwandishi Wetu
MKURUGENZI wa Sera na Mipango, Needpeace Wambuya, amevitaka Vyama vya Ushirika nchini kutumia teknolojia ya kisasa katika uzalishaji na uongezaji thamani wa bidhaa ili ziweze kukidhi viwango na mahitaji ya masoko ya ndani na nje ya nchi.

Wambuya ameyasema hayo katika Maonesho ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, alipokuwa akimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga.

Amesema Vyama vya Ushirika ni nguzo muhimu katika kukuza uchumi wa nchi kwa kuwa vinawakusanya wananchi pamoja, hususan wakulima na wafugaji, na kuwawezesha kushirikiana katika uzalishaji, utafutaji wa masoko na upatikanaji wa mitaji.

Wambuya amesema ameridhishwa na namna Vyama vya Ushirika vilivyojipanga katika kuunganisha nguvu za wanachama, kuongeza uzalishaji na kutafuta masoko ya uhakika kwa bidhaa zao, hatua ambayo alisema inasaidia kuongeza tija na kipato kwa wanachama.

“Vyama vya Ushirika vinapaswa kutumia teknolojia ya sasa ili kuongeza uzalishaji na kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa zinakuwa na ubora unaokidhi viwango vya masoko ya ndani na nje ya nchi,” amesema Wambuya.

Aidha, Wambuya amesema zao la kakao linalozalishwa mkoani Mbeya ni miongoni mwa mazao yenye ubora na kuwataka wazalishaji pamoja na Vyama vya Ushirika kuhakikisha bidhaa hiyo inawekewa nembo ya Tanzania ili kuongeza utambulisho wake na ushindani katika masoko ya kimataifa.

Amesema matumizi ya teknolojia, ubunifu na uongezaji thamani wa mazao ni muhimu katika kuwawezesha wakulima kupata tija zaidi, kuongeza thamani ya bidhaa na kuchangia kwa kiwango kikubwa katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Wakati huohuo, Wambuya amewataka Vyama vya Ushirika kuendelea kuimarisha mifumo ya uzalishaji na uongezaji thamani wa mazao ya kahawa na pamba ili kuhakikisha wakulima wanaendelea kunufaika na rasilimali hizo na kupata masoko yenye tija.

Amesema hatua hiyo itawezesha mazao hayo kuwa na ushindani zaidi katika masoko ya ndani na kimataifa, huku ikiongeza kipato cha wakulima na kuimarisha mchango wa sekta ya ushirika katika uchumi wa Taifa.



Na Belinda Joseph – Dodoma.

CHAMA Kikuu cha Ushirika wa Mazao Songea na Namtumbo (SONAMCU) mkoani Ruvuma kimesema mfumo wa Stakabadhi za Ghala umeendelea kuwanufaisha wakulima wake, huku kikijivunia kuwalipa wanachama kwa wakati bila kuwepo malalamiko yoyote.

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 3, 2026, katika Maonesho ya Kilimo Nanenane Kitaifa yanayoendelea jijini Dodoma, Mwenyekiti wa SONAMCU, Ally Hassan Chemka, amesema chama hicho kinaendelea kufanya vizuri katika usimamizi wa mazao kupitia mfumo wa Stakabadhi za Ghala, hali iliyochangia kuongeza imani ya wakulima na kuimarisha huduma kwa wanachama.

Chemka amesema sambamba na mafanikio hayo, SONAMCU inaendelea na ujenzi wa ofisi yake mpya katika mtaa wa Mahenge, Songea Mjini, ambapo ujenzi huo umefikia hatua za mwisho kukamilika, amesema ifikapo Oktoba mwaka huu, chama hicho kitaanza pia ujenzi wa ofisi ya tawi la SONAMCU Wilaya ya Namtumbo.

Ameeleza kuwa tayari chama kimejenga maghala mawili pamoja na nyumba ndogo ya watumishi, huku katika mwaka wa fedha 2026/2027 kikitarajia kujenga ofisi yenye ukumbi wa mikutano na maghala manne ya kuhifadhia mazao ili kuongeza uwezo wa kuhudumia wanachama.

Aidha amesema SONAMCU imejipanga kununua malori manne yatakayotumika kusafirisha pembejeo na mazao ya wanachama kwenda kwenye maghala ya kuhifadhia, pamoja na kununua gari la kisasa la chama litakalorahisisha shughuli za usafiri na uratibu wa mikutano katika mikoa yote inayohudumiwa na chama hicho.

Akizungumzia ushiriki wao katika Maonesho ya Nanenane, Chemka amesema maonesho hayo ni muhimu kwa kuwa yanawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, hivyo yamewapa fursa ya kujifunza mbinu mpya za uzalishaji wa mbegu bora, kupata uzoefu kutoka kwa vyama vingine vya ushirika na kutambua masoko mapya ya mazao.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa SONAMCU, Hajji H. Haule, amesema chama hicho kinawahudumia wakulima wa mazao ya tumbaku, mbaazi na ufuta, huku uzalishaji katika mwaka wa fedha 2025/2026 uzalishaji wa tumbaku uliongezeka kutoka tani 1,800 hadi tani 2,800, wakati uzalishaji wa mbaazi uliongezeka kutoka tani 4,000 hadi tani 11,000.

Amesema uzalishaji wa ufuta haukuwa mkubwa katika msimu uliopita kutokana na changamoto ya mvua na kwa msimu wa mwaka 2026/2027, SONAMCU imejipanga kuongeza uzalishaji wa mazao yote inayoyasimamia kupitia kuendelea kuwawezesha wakulima na kuboresha huduma zinazotolewa na chama hicho.







Na Mwandishi Wetu, Dodoma
TUME ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imejipanga kutoa fursa za ajira kwa maelfu ya vijana kupitia utekelezaji wa miradi ya uchimbaji wa visima na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji nchini.

Mpango huo unalenga kuongeza ajira kwa vijana wenye ujuzi wa uhandisi na ufundi, sambamba na kuongeza upatikanaji wa maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 32 ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa NIRC, Raymond Mndolwa, alisema Tume imejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya umwagiliaji ili kuwawezesha wakulima kuzalisha kwa tija na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Alisema katika kipindi cha miaka mitatu hadi minne iliyopita, Tume imefanikiwa kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji, ikiwamo uchimbaji wa visima na ujenzi wa miundombinu, huku wakandarasi 146 wakiendelea na kazi katika maeneo mbalimbali nchini na usanifu wa miradi 634 ukiendelea.

Mndolwa alisema katika mwaka wa fedha 2026/27, Tume inatarajia kuzindua zaidi ya miradi 30 ya umwagiliaji ambayo itasaidia kuongeza maeneo yanayolimwa kwa kutumia umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Aidha, alisema Tume imeanza kusambaza pampu za umwagiliaji katika mikoa saba, zoezi lililoanza Mkoa wa Katavi, ambapo vifaa hivyo vitawawezesha wakulima kutumia maji kutoka kwenye mito na mabonde kwa njia inayozingatia uhifadhi wa mazingira, hususan katika kilimo cha mboga na matunda.

Alisema Serikali pia imepokea zaidi ya pampu 1,000 zinazotumia nishati ya jua, ambazo zitagawiwa kwa wakulima katika maeneo ambayo hayajanufaika moja kwa moja na miradi ya umwagiliaji kutokana na jiografia ya maeneo hayo.

Kwa mujibu wa Mndolwa, pampu hizo zitasaidia wakulima kupata maji kwa urahisi na hivyo kuongeza uzalishaji wa kilimo cha umwagiliaji katika maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji.

Kuhusu uchimbaji wa visima, alisema hadi sasa visima 415 vimechimbwa, huku kazi hiyo ikiendelea katika wilaya mbalimbali nchini.

Alisema utekelezaji wa miradi hiyo utafungua fursa kubwa za ajira kwa vijana wenye taaluma za uhandisi na ufundi, ambao wataunda vikundi vitakavyowezeshwa kusimamia, kufunga na kufanya matengenezo ya miundombinu ya visima katika halmashauri 154 nchini.

Mndolwa aliwataka vijana wenye ujuzi katika fani hizo kujitokeza kutumia fursa zitakazotokana na miradi hiyo, akisema mpango huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuongeza ajira na kukuza ushiriki wa vijana katika sekta ya kilimo.

Alisema utekelezaji wa miradi hiyo pia unalenga kuchangia kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hasa katika kuongeza mchango wa sekta ya kilimo kwenye uchumi na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Aliongeza kuwa Tume imeweka mpango wa kuchimba jumla ya visima 67,000 ifikapo mwaka 2035, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji kwa ajili ya umwagiliaji na kuwezesha maeneo mengi zaidi nchini kufanya kilimo chenye tija.


Na Seif Mangwangi, Michuzi TV Arusha

MKUTANO wa 153 wa Jumuiya ya Mabunge Duniani (IPU),  unatarajiwa kufanyika nchini Tanzania huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan akitarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Mkutano huo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo 4 Agosti 2026, Jijini Arusha, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu amesema  mkutano huo utafanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) kuanzia Oktoba5 Hadi 9, 2026.

Amesema Tanzania iko tayari kupokea ujumbe wa wageni zaidi ya 2000 watakaohudhuria mkutano huo ikiwemo maspika wa Mabunge kutoka nchi 183 Duniani, Wabunge, Maafisa wa Bunge na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda, Wanadiplomasia, Washirika wa Maendeleo, Mashirika ya Kiraia, Taasisi za Elimu ya Juu pamoja na Vyombo vya Habari kutoka pande zote za dunia.

" Ni mkutano wa kihistoria kufanyika nchini kwetu na ni heshima kubwa sana tuliyopewa kama nchi, hivyo hi ni fursa adhimu sana ambayo inaonyesha namna dunia ina imani na nchi yetu katika kuendesha masuala ya utawala Bora," Amesema Spika Zungu.

Amesema masuala muhimu ya Kimataifa yatajadiliwa wakati wa Mkutano huo ikiwemo, Utawala wa Kidemokrasia, Amani na Usalama, Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Kidijitali, Akili Unde, Ushiriki wa Walemavu, Vijana na Wanawake, Ustahimilivu wa Kiuchumi na Malengo ya Maendeleo Endelevu.

" Tuna imani kubwa kuwa, pamoja na mambo mengine, majadiliano hayo yatatoa mchango mkubwa katika kutatua changamoto zinazoikabili dunia kwa sasa ikiwa ni pamoja na Mabadiliko ya Tabianchi, Migogoro ya Kimataifa na Ugumu wa Maisha," Amesema na kuongeza:.

"Hii itadhihirisha kuwa Diplomasia ya Kibunge ina umuhimu mkubwa katika kutatua changamoto tunazokabiliana nazo kupitia majadiliano, makubaliano na ushirikiano kati ya Mataifa,".

Amesema mkutano huo pia utaimarisha ushirikiano wa Kimataifa, kukuza ushirikiano wa kimkakati na kutoa fursa adhimu kwa Sekta za Utalii, Usafirishaji na Huduma nchini Tanzania na  zaidi, Mkutano huo utatoa fursa ya kuionesha dunia utajiri  uliokuwepo nchini wa utamaduni, fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii vinavyotambulika duniani.

Aidha Spika Zungu amesema katika mkutano huo, Rais wa Mabunge Duniani Dkt Tulia Ackson ambaye pia Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atastaafu nafasi hiyo baada ya kumaliza muda waje na kutoa fursa Kwa Spika mwingine kuchaguliwa.

"Ni jambo la kujivunia kuwa, Mtanzania mwenzetu, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb.) ndio Rais wa IPU kwa sasa, nafasi ambayo ameishika tangu Mwaka 2023 na kuitumikia vema katika kuhakikisha ufanikishaji wa Dira hiyo," amesema.

Inter-Parliamentary Union (IPU) ni Umoja wa Mabunge 183 Duniani ulioanzishwa Mwaka 1889.







Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imesema Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo na Ufugaji Nane Nane ni muhimu katika kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji kuhusu matumizi sahihi ya dawa za kilimo na mifugo.

Akizungumza katika Maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, Mkaguzi wa Dawa wa TMDA, Benedict Brashi, amesema matumizi yasiyo sahihi ya dawa za kilimo na mifugo yanaweza kusababisha madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.

Amesema dawa zinazotumika katika kilimo na ufugaji zinahitaji kuzingatia ushauri wa wataalamu pamoja na muda wa kusubiri baada ya matumizi, kabla ya mazao au bidhaa za mifugo kuanza kutumika au kuuzwa.

“Dawa zikitumika katika kilimo au ufugaji, ni muhimu kuzingatia ushauri wa wataalamu kwa muda wanaopewa ili Mazao au nyama vikiingizwa sokoni visiwe na madhara kwa afya ya mlaji,” amesema Brashi.

Aidha, amesema ulinzi dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi yasiyo sahihi ya dawa ni jukumu la kila mwananchi, huku akiwataka wananchi kutoa taarifa pindi wanapobaini matumizi yasiyo sahihi ya dawa ili hatua stahiki zichukuliwe.

Brashi pia amesisitiza kuwa dawa za kilimo, mifugo na binadamu zilizomaliza muda wake hazipaswi kutupwa kiholela, kwa kuwa zinaweza kusababisha madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.

Amesema dawa hizo zinapaswa kupelekwa katika hospitali, vituo vya afya au zahanati kwa ajili ya kushughulikiwa na kuteketezwa kwa utaratibu unaostahili.

Amesema TMDA inaendelea kutumia maonesho hayo kuwaelimisha wananchi kuhusu matumizi salama na sahihi ya dawa, hatua inayolenga kulinda afya ya jamii na kuhakikisha usalama wa chakula kinachozalishwa nchini.
Na Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50 Bw. Alain Ebobisse, amebainisha kuwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), ni fursa ya kuonesha mafanikio ambayo Tanzania imeyapata katika sekta ya miundombinu, kutangaza fursa zinazopatikana ikiwa ni ushahidi kuwa uwekezaji katika miundombinu ya Afrika una tija, unalipa na unaweza kufadhiliwa.

Bw. Ebobisse alisema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), katika kikao cha pamoja cha maandalizi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.

Bw. Ebobisse alibainisha kuwa ajenda kuu ya mkutano huo itakuwa ni ujenzi wa uchumi wa viwanda barani Afrika kupitia uongezaji thamani wa rasilimali za ndani, jambo linalotegemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa nishati ya uhakika huku akipongeza dira ya uongozi wa Tanzania katika kuvutia mtaji wa sekta binafsi.

"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono makubwa ya kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi katika sekta ya miundombinu nchini Tanzania. Sisi Africa50 ni mojawapo ya nyenzo zinazosaidia kutekeleza maono hayo kwa kushirikiana katika utekelezaji wa miradi, ambapo miundombinu mbalimbali ikiwemo nishati ni muhimu katika maendeleo ya viwanda na kutuma ujumbe kuwa Afrika iko tayari kwa uwekezaji," alisema Bw. Ebobisse.

Bw. Ebobisse aliongeza kuwa Africa50 imeweka kipaumbele kikubwa katika miundombinu ya gesi asilia ikiwemo mabomba na mitambo ya uchakataji ili kuelekeza gesi zaidi kwenye maeneo ya viwanda nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla ili kuongeza thamani ya rasilimali na kuimarisha uchumi wa Afrika.

Alisisitiza kuwa licha ya uwepo wa kundi kubwa la wawekezaji tayari wenye hamasa ya kushiriki, huo ulikuwa wakati muafaka wa kutuma ujumbe kwa Tanzania, Afrika na dunia nzima kwamba Bara la Afrika liko tayari na ni eneo salama na la kimkakati kwa uwekezaji wa miundombinu.

Naye Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi, Khamis Mussa Omar (MB), alisema kuwa Serikali imekamilisha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Miundombinu Afrika unaolenga kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi katika miundombinu ya kimkakati, ikiwemo gesi asilia, umeme na viwanda barani Afrika.

Alisema Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa Forum), utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Dar es Salaam unatarajiwa kufunguliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

"Tunatarajia kusaini hati tatu za mashirikiano katika afya hasa usafishaji wa damu (dialysis), tumefanya tathmini ya maendeleo ya miradi ya kimkakati ikiwemo mradi wa gesi asilia, miundombinu ya usafirishaji wa nishati, pamoja na masuala mengine ya nishati yanayolenga kuharakisha maendeleo ya uchumi wa viwanda, " alisema Mhe. Balozi Omar.

Balozi Omar alithibitisha kuwa Serikali imejiridhisha kuwa maandalizi yote muhimu ya mkutano huo unaotarajiwa kukutanisha viongozi wa kitaifa, marais wa taasisi za kifedha, na wawekezaji wakubwa wa kimataifa yako tayari ili kuhakikisha mkutano huo wa siku mbili unapata mafanikio makubwa na kufikia malengo yaliyokusudiwa.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kushoto), akiwa katika picha na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50, Bw. Alain Ebobissé, walipokutana na kufanya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili maandalizi ya mwisho ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC), Jijini Dar es Salaam, ukitarajiwa kuwaleta pamoja Washiriki wapatao 1,200 wakiwemo viongozi wa Serikali, wanahisa wa Africa50, taasisi za fedha, wawekezaji wa kimataifa na sekta binafsi.


Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), na Ujumbe wa Taasisi ya Africa50 ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Alain Ebobissé (kushoto), wakifanya kikao katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, kilichojadili maandalizi ya mwisho ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC), Jijini Dar es Salaam, ukiwaleta pamoja Washiriki wapatao 1,200 wakiwemo viongozi wa Serikali, wanahisa wa Africa50, taasisi za fedha, wawekezaji wa kimataifa na sekta binafsi.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa kikao chake na ujumbe wa Taasisi ya Africa50 ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Alain Ebobissé (hayupo pichani), walipokutana na kufanya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili maandalizi ya mwisho ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC), Jijini Dar es Salaam, ukiwaleta pamoja Washiriki wapatao 1,200 wakiwemo viongozi wa Serikali, wanahisa wa Africa50, taasisi za fedha, wawekezaji wa kimataifa na sekta binafsi.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi wa Africa50, Bw. Alain Ebobissé, akizungumza wakati wa kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), na ujumbe wa Taasisi ya Africa50 katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili maandalizi ya mwisho ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) utakaofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026 katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC), Jijini Dar es Salaam, ukiwaleta pamoja Washiriki wapatao 1,200 wakiwemo viongozi wa Serikali, wanahisa wa Africa50, taasisi za fedha, wawekezaji wa kimataifa na sekta binafsi.



(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WF, Dar es Salaam)











Na Mwandishi Wetu
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, ameitaka NIC Insurance kuendelea kutoa elimu ya bima kwa makundi mbalimbali ya wananchi, ikiwamo Mabaraza,Mabaraza ya Madiwani ya Mikoa, Mabaraza ya Wafanyakazi, wanafunzi wa vyuo, shule za msingi na sekondari, ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa bima.

Dkt. Fatuma amesema elimu hiyo pia inapaswa kuwafikia wakulima, hususan kuhusu Bima ya Kilimo, ili kuwasaidia kujikinga na hasara zinazoweza kusababishwa na majanga na kulinda uwekezaji wao katika shughuli za kilimo.

Amesema hayo alipotembelea Banda la NIC Insurance katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, akisisitiza kuwa bima ni muhimu katika kuwalinda wananchi na mali zao dhidi ya hasara zinazoweza kusababishwa na majanga mbalimbali.

Kwa mujibu wa Dkt. Fatuma, wananchi kwa sasa wamekuwa wakijikita zaidi katika kilimo cha biashara kinachohitaji uwekezaji mkubwa wa fedha, hivyo ni muhimu kwao kuchukua bima ili kulinda mitaji na uwekezaji wao dhidi ya majanga yanayoweza kujitokeza.

“Wananchi sasa wanawekeza fedha nyingi katika kilimo cha biashara, hivyo wanahitaji kuwa na bima ili kulinda uwekezaji wao dhidi ya majanga na hasara mbalimbali,” amesema.

Aidha, Dkt. Fatuma amesema Madiwani wana nafasi kubwa katika kuwafikishia wananchi elimu kuhusu bima kutokana na kuwa karibu na jamii wanazoongoza.

Amesema kupitia Mabaraza ya Madiwani na majukwaa mbalimbali wanayoshiriki, elimu kuhusu umuhimu wa bima inaweza kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwahamasisha kuchukua hatua za kulinda mali zao pamoja na shughuli zao za kiuchumi.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya kampuni za bima na viongozi wa Serikali za Mitaa ni muhimu katika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu bidhaa mbalimbali za bima, hususan zinazolenga kulinda shughuli za kilimo na uwekezaji wa wakulima.

[10:08 AM, 8/4/2026] Chalila Tg: Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt.Fatuma Mganga

akizungumza nkatika Banda la NIC Insurance kwenye maonesho ya Kilimo ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Dkt.John Samwel Malecela Jijini Dodoma
Na Mwandishi Wetu
MWANAFUNZI wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Paschal Sabuni Shija, amebuni mfumo wa kidijitali unaounganishwa na mizani ya kupimia pamba kwa lengo la kumwezesha mkulima kupata taarifa sahihi za uzito wa pamba yake na kurahisisha ufuatiliaji wa malipo.

Akizungumza katika Maonesho ya Kimataifa ya NaneNane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, jijini Dodoma, Shija amesema ubunifu wa mawazo ya Kiteknolojia utasaidia jamii kutatua changamoto zinazowakabili wananchi na kuibua fursa za ajira.

"Nimekuwa miongoni mwa wanafunzi wanaonufaika na mpango wa TIA wa kukuza, kuendeleza vipaji na taaluma jambo linalonisaidia kuendeleza wazo ili kutatua changamoto kwa jamii",amesema Shija.

" TIA imekuwa ikinisimamia kunipa mwongozo katika kuboresha ubunifu huu ili kutoa suluhisho la changamoto zinazowakabili wakulima wa pamba na mazao mengine",amesema Shija.

Mfumo huu utamsaidia mkulima anapopima pamba kupata taarifa ya uzito wa mazao hayo moja kwa moja kwenye simu yake ya mkononi, sambamba na kupatiwa stakabadhi yenye taarifa za muamala.

Shija alisema mfumo huo pia utasaidia kuongeza uwazi katika mchakato wa ununuzi wa pamba na kupunguza mianya ya udanganyifu ambayo imekuwa ikiwakatisha tamaa baadhi ya wakulima kuendelea na kilimo cha zao hilo.

Matumizi ya teknolojia katika sekta ya kilimo ni muhimu kwa kuwa yanamwezesha mkulima kupata taarifa kwa wakati, kufuatilia mazao yake na kuwa na ushahidi wa miamala inayohusiana na mauzo,Aliongeza Shija.

Aidha, Shija alisema mpango wa TIA wa kuendeleza mawazo na ubunifu wa wanafunzi una nafasi kubwa katika kuongeza fursa za ajira, hususani kwa vijana wanaohitimu masomo ya vyuo mbalimbali,kwani inaweza kuwa chanzo cha kujiajiri na suluhisho la changamoto zinazowakabili wananchi.

Alisema ubunifu unaotokana na wanafunzi unaweza kuwa chanzo cha kujiajiri na pia kutoa suluhisho la changamoto mbalimbali zinazolikabili Taifa.

"Ninatoa wito kwa vijana kutumia maarifa wanayopata vyuoni kubuni teknolojia zitakazokuwa na manufaa kwa jamii", amesema Shija.

Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Jijini Dodoma yaliyoanza tarehe 1 Agosti 2026 baada ya yakifunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba yameendelea kuvuta wageni wengi kutembelea banda la wizara ya Maliasili na utalii na kushuhudia vivutio mubashara kutoka Ngorongoro kupitia luninga kubwa iliyofungwa Katika viwanja hivyo.

Wageni waliotembelea banda hilo ni pamoja Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, Brigedia Jenerali Shija Lupi, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) na wananchi mbalimbali ambao wameelezwa vivutio mbalimbali vya wanyamapori, malikale na urithi wa utamaduni unaoelezea historia ya binadamu katika hifadhi ya Ngorongoro 

Mhe. Waziri Kijaji alipotembelea banda hilo ameeleza kuwa “Nawapongeza Ngorongoro kwa jitihada za kutumia mifumo ya kidigitali kutangaza vivutio vya utalii, tumeeleza uwepo wa vivutio mbalimbali vya wanyamapori, milima, uwepo wa Kreta tatu, mchanga unaohama, mazalia ya nyumbu, maporomoko ya maji na vingine vingi vinavyoashiria kuwa Ngorongoro ni Nyumbani kwa kila kivutio”

Kwa upande wake Brigedia Jenerali Shija Lupi amesema kuwa kuona vivutio mubashara vya utalii katika maonesho ya nanenane na kuelezwa hadithi za chimbuko la binadamu na gunduzi za visukuku mbalimbali, nyayo za Laetoli na ugunduzi wa Fuvu la Zinjanthropus vinaashiria kuwa kila binadamu asili yake ni Ngorongoro na kuonyesha umuhimu wa kutembelea hifadhi hiyo 

Brigedia Shija ameongeza kuwa kutumia teknolojia katika maeneo ya hifadhi ina mchango mkubwa wa kutangaza vivutio vya utalii duniani na kuimarisha ulinzi kwa rasilimali za nchi.








 



Na Oscar Assenga, TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Rashid Mchatta amefungua kikao kazi cha Wakurugenzi na Mameneja wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini huku akisisitiza matumizi teknolojia ya kisasa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao.

Wito huo umetolewa jijini Tanga na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, wakati akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Sekta ya Maji nchini.

Kikao hicho kinafanyika chini ya kaulimbiu “Huduma Janja: Matumizi ya Teknolojia kwa Huduma Bora kwa Wateja”, kikilenga kuwawezesha wakurugenzi na mameneja hao kubadilishana uzoefu na kujadili mbinu mbalimbali za kuboresha huduma kwa wananchi.

Mchatta aliipongeza Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini na kuiwezesha Wizara ya Maji kutekeleza miradi na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na huduma za usafi wa mazingira nchini.

Pia aliipongeza uongozi wa Wizara ya Maji unaoongozwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, Naibu Waziri, Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Rose Ambrose, kwa juhudi wanazofanya katika kusimamia utekelezaji wa majukumu ya wizara hiyo.

Alisema mafanikio yanayoonekana katika sekta ya maji, kuanzia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati hadi uboreshaji wa huduma kwa wananchi, yanaonesha kuwa uongozi wa wizara hiyo umejikita katika kuhakikisha huduma zinaboreshwa kila siku.

“Viongozi hawa wameonesha weledi, uzoefu na uthubutu katika kusimamia sekta ya maji. Ushirikiano wao umeendelea kuleta mafanikio yanayoonekana na wananchi wanaendelea kushuhudia mabadiliko katika huduma za maji na usafi wa mazingira,” alisema Mchatta.

Alisema kikao hicho ni fursa muhimu kwa wakurugenzi na mameneja wa huduma kwa wateja kujifunza, kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa Mchatta, mafunzo hayo pia yanahusu ufanisi wa biashara katika mamlaka za maji pamoja na mbinu za uwekezaji binafsi, ambapo wataalamu kutoka UTT-AMIS wanashiriki kutoa elimu kwa washiriki.

Aliwataka washiriki kutumia kikamilifu fursa hiyo kujifunza mbinu mpya, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma kwa wateja.

“Ninaamini mafunzo haya yatakuwa chachu ya kuboresha ufanisi mtakaporudi katika vituo vyenu vya kazi na hivyo kuongeza ubora wa huduma mnazozitoa kwa wananchi,” alisema.

JUKWAA LA WAKURUGENZI LAZIDI KUKUA

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka za Maji nchini, Alawi Ahmad, alisema jukwaa hilo ni sehemu muhimu ya uongozi katika sekta ya maji, kwa kuwa linawapa nafasi wakurugenzi na mameneja kukutana, kujadiliana na kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili katika utoaji wa huduma.

Alisema jukwaa hilo limekuwa likifanya vikao kila mwaka na kwa sasa lina takribani miaka 10 tangu kuanzishwa kwake.

“Jukwaa hili limekuwa likitusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utoaji wa huduma kwa wateja na pia limetumika kama sauti ya pamoja ya wakurugenzi wa huduma kwa wateja katika sekta ya maji,” alisema Ahmad.

Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi  Abbas Muslim Pyarali  alisema kikao hicho kinawakutanisha wakurugenzi wa mamlaka za maji wanaojikita katika utoaji wa huduma kwa wateja.

Abbas ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Maji alisema kikao hicho kitakachodumu kwa siku tatu kitawapa washiriki nafasi ya kupata mafunzo maalumu na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Wizara ya Maji za kuhakikisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira zinaendelea kuboreshwa nchini.








Top News