📍Wamwangukia DPP amuachie Lissu
Na Mashaka Mhando, Tanga
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ngazi ya majimbo mkoani Tanga, wamemtaka Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Bara), John Heche, kujiuzulu au kukaa pembeni kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha zinazomkabili.
Sambamba na shinikizo hilo la ndani ya chama, viongozi hao wameiomba Serikali kupitia Mwanasheria Mkuu na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kufuta kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wao wa Taifa, Tundu Lissu, na kumuachia huru.
Msimamo huo umetolewa Julai 20 na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Handeni Mjini, Kombo Mohamed Maturu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akiwa ameambatana na viongozi wa majimbo mbalimbali na wanachama.
Taharuki na Tuhuma Dhidi ya Heche
Katibu huyo alieleza kuwa wamelazimika kuita waandishi kutokana na taharuki kubwa inayoendelea ndani ya chama chao inayotokana na misigano kati ya viongozi na wanachama, jambo linalokosesha chama afya. Alifichua kuwa awali walipanga kufanya maandamano makubwa kufikisha kilio chao.
"Kwanini Heche asizijibu hizi tuhuma au asitupishe akae pembeni ili tuchunguze tuhuma zake? Badala yake anakuja kujibu kwa kuwasema vibaya watu ambao tunawategemea kama wawakilishi... chama kipo chini kwa wanachama," alisema Matumla.
Maturu alimshutumu Heche kwa kutumia lugha isiyo ya kiungwana dhidi ya wawakilishi wao kwa kuwaita ‘mbwa’ badala ya kujibu hoja zinazoelekezwa kwake, huku akimtaka aache kugombana na Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema.
"Haya ni masikitiko yetu makubwa. Makamu Mwenyekiti wetu anatuhumiwa kufanya ubadhirifu halafu anajifanya mbabe. Tunataka ajibu tuhuma hizi au ajiuzulu mara moja. Hiki si chama cha mtu binafsi, ni taasisi ya watu. Tunampenda sana Heche, lakini atupishe hata wiki moja tufanye uchunguzi," alisisitiza.
Madai ya Meli ya Mafuta na Wito kwa Msajili
Katika madai mazito zaidi, Maturu alidai kuwa chama hicho kimekosa ujasiri wa kulalamikia upandaji wa bei za mafuta nchini kutokana na madai kuwa kiongozi wao wa juu anashirikiana na wafanyabiashara wa mafuta. Alihusisha hilo na tukio la hivi karibuni la kukamatwa kwa meli ya mafuta huko Yemen iliyokuwa inapeperusha bendera ya Tanzania.
Kutokana na mzozo huo, viongozi hao wamemwomba Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, kuunda tume ya kuchunguza madai hayo na asifanye mzaha na kauli za viongozi kuitana 'mbwa'. Pia, wamemtaka Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuingilia kati mgogoro huo ili kunusuru chama.
Kilio kwa Tundu Lissu
Kuhusu hali ya kisiasa, Maturu alisema licha ya kutokubaliana na ushindi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilio chao kikubwa kwa sasa ni kutaka Lissu aachiwe huru.
"Tunaomba Serikali iwe na huruma. Hii kesi ya Lissu ni ya kisiasa, haiwezekani mwaka wa pili sasa aendelee kushikiliwa kizuizini. Nchi inaingia kwenye migogoro na mataifa ya Ulaya na tunazuiwa misaada. Tunamuomba DPP aifute hii kesi, hakuna faida kuendelea kumshikilia," aliomba Maturu.
Msimamo wa BAVICHA na BAWACHA
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) Jimbo la Lushoto, Mambo Nassor Mkuya, aliunga mkono uamuzi wa viongozi hao wa Tanga wa kumtaka Heche apishe uchunguzi kwa kuwa chama ni cha wanachama na tuhuma hizo haziwezi kuachwa zipite. Mkuya alisisitiza kuwa kama Lissu angekuwepo, ubadhirifu huo usingetokea.
Naye Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Lushoto ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA wilayani humo, Jerida Ramadhani Mosha, alisema kuendelea kubaki ofisini kwa Heche kunaleta mgogoro. Aidha, alimuomba DPP "kuvaa viatu vya Lissu" na kujiona kama sehemu ya familia inayopata uchungu wa kiongozi huyo kukaa ndani kwa miaka miwili.
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Afrika inapaswa kutumia mabadiliko yanayoendelea katika siasa, uchumi na usalama duniani kama fursa ya kuharakisha maendeleo yake.
Amesema inapaswa kufanya hivyo kwa kuimarisha uongozi wa kimkakati, kuongeza thamani ya rasilimali zake na kujenga taasisi imara zitakazolinda maslahi ya wananchi wake na kuharakisha maendeleo ya Bara la Afrika.
"Afrika isiendelee kuwa uwanja wa ushindani wa mataifa makubwa. Tunapaswa kutumia nafasi yetu ya kimkakati, rasilimali tulizonazo na nguvu ya watu wetu kujiletea maendeleo yenye manufaa kwa wananchi wetu," amesema.
Waziri Mkuu alisema hayo leo (Jumanne, Julai 21, 2026) alipokuwa Mzungumzaji Mkuu katika Mkutano wa Pili wa Wahitimu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania (National Defence College – Tanzania) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.
Alisema dunia inaendelea kushuhudia mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kiusalama yanayochochewa na ushindani wa mataifa makubwa, maendeleo ya teknolojia, mabadiliko ya nishati na ushindani wa rasilimali muhimu, hali inayozitaka nchi za Afrika kuwa na viongozi wenye uwezo wa kufanya maamuzi ya kimkakati kwa manufaa ya Bara.
Alisisitiza Afrika ina takribani asilimia 30 ya madini muhimu yanayohitajika katika mapinduzi ya teknolojia na nishati safi duniani, hivyo Bara hilo linapaswa kutumia nafasi hiyo kujenga uchumi imara kupitia kuongeza thamani ya rasilimali zake badala ya kuendelea kuuza malighafi na kutegemea mataifa mengine.
"Afrika lazima iache kuwa uwanja wa ushindani wa mataifa makubwa. Tunapaswa kujenga uwezo wa kuongeza thamani ya rasilimali zetu, kuimarisha biashara ndani ya Bara na kutumia fursa zilizopo kujenga uchumi shindani na endelevu," alisisitiza.
Aidha, Waziri Mkuu amesema viongozi wa Afrika wanapaswa kujenga taasisi zenye uwezo wa kusimamia maendeleo, kulinda maslahi ya wananchi na kuhakikisha rasilimali za Bara zinatumika kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Akizungumzia hali ya usalama duniani, Waziri Mkuu alisema migogoro ya kimataifa imeendelea kuathiri uchumi wa Afrika kupitia kupanda kwa gharama za nishati, usafirishaji, bidhaa na huduma, hali inayosisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kujenga uchumi unaostahimili misukosuko ya nje, kuimarisha biashara baina ya nchi za Afrika na kuongeza ushirikiano wa kikanda.
Alisema changamoto hizo zinapaswa kuwa chachu ya Afrika kuwekeza zaidi katika viwanda vinavyoongeza thamani ya malighafi, teknolojia, utafiti na ubunifu ili kujenga uchumi imara na unaojitegemea.
Dkt Mwigulu pia aliwataka washiriki wa mkutano huo, ambao ni viongozi waandamizi kutoka sekta mbalimbali, kutumia jukwaa hilo kujadili na kutoa mapendekezo yatakayosaidia Afrika kubadili changamoto za kisiasa, kiuchumi na kiusalama kuwa fursa za maendeleo endelevu.
Awali, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Balozi Meja Jenerali Wilbert Ibuge, alisema mkutano huo unalenga kuwakutanisha wahitimu wa chuo hicho ili kubadilishana uzoefu, kuimarisha mtandao wa viongozi wa kimkakati na kujadili masuala muhimu yanayohusu siasa, uchumi, uongozi na usalama kwa maendeleo ya Afrika.
Naye, Kansela wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Dkt. Abdulhamid Mzee, alisema mkutano huo ni jukwaa muhimu la kitaaluma linalowakutanisha wahitimu, wataalamu na viongozi mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto na fursa zinazolikabili Bara la Afrika katika mazingira ya sasa ya dunia.
Baada ya mzungumzaji mkuu kuwasilisha mada yake, mkutano uliendelea kwa mjadala wa kitaalamu kuhusu mwenendo wa siasa, uongozi, uchumi na usalama katika karne ya 21 pamoja na athari zake kwa maendeleo ya Afrika, uliowashirikisha wataalamu na viongozi mbalimbali akiwemo Profesa Rwekaza Mukandala, Balozi Ombeni Sefue, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, Kamanda wa Jeshi la Kenya na mhitimu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Luteni Jenerali David Kipkemboi Ketter, na Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu).
Zoezi hilo liliongozwa na Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Stephen Chaula, akiwa pamoja na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ulanga, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Challe Deogratius ambao waliongoza zoezi la uchangiaji wa damu na kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa wagonjwa na wahitaji waliolazwa hospitalini hapo.
Wakizungumza hospitalini hapo wakati wa shughuli hiyo, kwa pamoja wameupongeza huo Mtandao wa Polisi Wanawake (TPF-Net) Wilaya ya Ulanga kwa kuratibu zoezi hilo, huku wakibainisha kuwa zoezi hilo haliimarishi tu uhusiano kati ya Jeshi la Polisi na jamii bali ni tendo lenye thawabu mbele za Mwenyezi Mungu.
Aidha, walieleza kuwa damu iliyochangwa itasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo, hususan wajawazito na akina mama waliojifungua, watoto pamoja na wagonjwa wengine wanaokabiliwa na upungufu wa damu.
Jeshi la Polisi limeendelea kuhimiza wananchi na taasisi mbalimbali kushiriki katika shughuli za kujitolea, ikiwemo uchangiaji wa damu, ili kuokoa maisha ya Watanzania na kuimarisha mshikamano wa kijamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametuma salamu za pole kwa Amir wa Qatar, Serikali na wananchi wa Qatar kufuatia kifo cha Amir wa zamani wa Taifa hilo, Hayati Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa salamu hizo za pole leo, tarehe 21 Julai 2026, alipofika katika Ubalozi wa Qatar nchini Tanzania, uliopo Oysterbay, jijini Dar es Salaam, na kusaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha kiongozi huyo.
Akiwa ubalozini hapo, Rais Dkt. Mwinyi, kupitia kwa Balozi wa Qatar nchini Tanzania, Mhe. Fahad Rashid Al-Muraikhi, ametoa salamu za pole kwa Amir wa Qatar, Mhe. Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, familia ya kifalme, Serikali na wananchi wa Qatar kutokana na msiba huo mkubwa.
Amesema Hayati Sheikh Hamad ataendelea kukumbukwa kwa uongozi wake wenye maono, mchango wake katika maendeleo ya Qatar na juhudi zake za kuimarisha elimu, uchumi, ustawi wa wananchi na nafasi ya Taifa hilo katika masuala ya kimataifa.
Hayati Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani alifariki dunia tarehe 12 Julai 2026, akiwa na umri wa miaka 74.
Rais Dkt. Mwinyi amesaini Kitabu cha Maombolezo muda mfupi baada ya kuwasili nchini akitokea India, alikohitimisha ziara yake ya kikazi nchini India.
Waziri wa Madini, Antony Mavunde ameshangazwa na uwekezaji mkubwa wa bilioni 4.8 uliofanywa na vijana katika kituo cha uchenjuaji wa madini Wilayani Chato.
Ametembelea kituo cha TAMPMED Mining Ltd ambacho kinatoa huduma za kisasa za uongezaji thamani ya madini kwa njia ya CIP na Elution huduma za maabara pamoja na usambazaji wa kemikali za uchimbaji wa dhahabu.
Kwa sasa kituo hicho kina plant 3 zenye uwezo wa kuchakata tani 750 za udongo na shughuli za vat leaching zimeshaanza.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, *lBw. Ramadhani Tampela amesema changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni ulipaji wa fidia kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yenye leseni za kampuni.
Amesisitiza kuwa kampuni haiwezi kukamilika bila kuwa na maeneo ya uchimbaji.
Kwa upande wake Waziri Mavunde amesema Serikali itaendelea kufuta leseni za watu wasio na nia ili kuwapa fursa wawekezaji wenye nia ya kufanya kazi.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amezitaka nchi za Afrika kuacha kutegemea matamko na ahadi zisizoambatana na utekelezaji, badala yake ziongeze uwekezaji wa ndani, uwajibikaji na matumizi ya ubunifu ili kuimarisha mifumo ya afya barani humo.
Dk. Kikwete alitoa kauli hiyo Julai 20, 2026, wakati akizungumza katika Mjadala wa Ngazi ya Juu wa Sera uliofanyika katika Hoteli ya Kempinski jijini Accra, Ghana, pembezoni mwa Mkutano Maalumu wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya.
Mjadala huo uliwakutanisha mawaziri, watunga sera, taasisi za kikanda, washirika wa maendeleo, viongozi wa sekta binafsi na wataalamu wa afya kutoka mataifa mbalimbali, ukiandaliwa kwa ushirikiano kati ya African Renaissance Trust, Wakfu wa Jakaya Mrisho Kikwete, Tume ya Umoja wa Afrika na wadau wengine.
Akizungumza katika mkutano huo, Dk. Kikwete alisema utegemezi wa muda mrefu wa misaada ya nje katika kugharamia sekta ya afya hauwezi kuendelea kuwa msingi wa mifumo ya afya ya Afrika, hasa wakati misaada ya maendeleo inapopungua na mahitaji ya huduma bora za afya yakiongezeka.
Alisema bara hilo linapaswa kuongeza uwezo wa kugharamia huduma zake za afya kupitia mapato ya ndani, matumizi yenye ufanisi wa rasilimali na uwajibikaji katika matumizi ya fedha za umma.
“Ujumbe kutoka Eswatini hadi Accra ni mmoja; Afrika lazima igharamie, izalishe na ilinde mustakabali wake wa afya,” alisema.
Dk. Kikwete alikumbusha kuwa ni miaka 25 sasa tangu kupitishwa kwa Azimio la Abuja la mwaka 2001 lililozitaka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kutenga angalau asilimia 15 ya bajeti zao kwa sekta ya afya, lakini nchi nyingi bado hazijafikia lengo hilo.
Alisema hali hiyo imeendelea kuchangia mzigo mkubwa wa magonjwa kama UKIMWI, kifua kikuu, malaria, pamoja na vifo vinavyoweza kuzuilika vya wajawazito na watoto wachanga.
Katika hotuba yake, Dk. Kikwete alieleza kuwa usalama wa afya ya mama na mtoto unapaswa kuwa kipaumbele kikuu, akibainisha kuwa takribani wanawake 260,000 hufariki kila mwaka duniani kutokana na matatizo yanayohusiana na ujauzito na kujifungua, huku karibu asilimia 70 ya vifo hivyo vikirekodiwa barani Afrika.
Alisisitiza kuwa changamoto si ukosefu wa maarifa, dawa au teknolojia, bali ni kushindwa kuzifikisha huduma hizo kwa wananchi wanaozihitaji.
“Mama anaporudi nyumbani salama, ni kwa sababu fedha, ushahidi wa kisayansi na utoaji wa huduma vimefanikiwa kukutana,” alisema.
Akitoa mfano wa Tanzania, Dk. Kikwete alisema ushirikiano kati ya Wakfu wa Jakaya Mrisho Kikwete, Wizara ya Afya na taasisi za utafiti umechangia kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto kupitia tafiti na mikutano ya kisayansi inayofanyika kila baada ya miaka miwili.
Alisema juhudi hizo zimechangia kupungua kwa vifo vya wajawazito kutoka zaidi ya vifo 550 kwa kila watoto 100,000 wanaozaliwa hai hadi vifo 104, hatua inayoiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kufikia lengo la Maendeleo Endelevu la kupunguza vifo hivyo hadi 70 ifikapo mwaka 2030.
Aidha, alisema mafanikio ya sekta ya afya hayapaswi kupimwa kwa kiwango cha fedha kinachotengwa pekee, bali kwa matokeo yanayowafikia wananchi.
“Swali si tunatumia kiasi gani katika afya. Swali ni kama uwekezaji wetu unawafikia wananchi wanaouhitaji zaidi,” alisema.
Katika mkutano huo pia ulizinduliwa mfumo wa African Renaissance Health Financing Insights Dashboard, utakaosaidia serikali kufuatilia ahadi za kifedha, matumizi ya bajeti, mapungufu ya fedha pamoja na matokeo ya uwekezaji katika sekta ya afya.
Dk. Kikwete alisema mfumo huo utasaidia kuimarisha uwajibikaji na ushirikiano kati ya wizara za afya na wizara za fedha ili kuhakikisha fedha zinazotengwa zinaleta matokeo yanayotarajiwa.
Pia alihimiza Afrika kupunguza utegemezi wa dawa na chanjo kutoka nje kwa kuwekeza katika uzalishaji wa ndani, kuimarisha Wakala wa Dawa wa Afrika na kutumia fursa za biashara ya kikanda kuimarisha usalama wa afya.
Katika mapendekezo yake, Dk. Kikwete aliwasilisha vipaumbele vitano ambavyo ni kuifanya afya kuwa uwekezaji wa kimkakati, kuongeza mapato ya ndani kupitia bima na kodi bunifu, kulinda huduma muhimu wakati misaada inapopungua, kuimarisha uwajibikaji na kuongeza ushirikiano wa kikanda.
Kwa upande wake, Kamishna wa Umoja wa Afrika anayeshughulikia Afya, Masuala ya Kibinadamu na Maendeleo ya Jamii, Balozi Amma Twum-Amoah, alisema mafanikio ya sera za afya yanapaswa kupimwa kwa maboresho yanayoonekana katika maisha ya wananchi.
Akihitimisha hotuba yake, Dk. Kikwete alisema Afrika haina upungufu wa mikakati wala ubunifu, bali changamoto iliyopo ni utekelezaji wa maamuzi yaliyokwishafikiwa.
“Tuondoke Accra tukiwa na dhamira ya kubadili ahadi kuwa bajeti, bajeti kuwa programu, programu kuwa matokeo yanayopimika, na matokeo kuwa maisha marefu, yenye afya na uzalishaji zaidi kwa wananchi tunaowahudumia,” alisema.
📍MWANZA
Mwenyekiti wa Kamati ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini kutoka Tume ya Madini, Dkt. Theresia Numbi, amesema Jukwaa la Tano la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini (LCCF 2026) ni jukwaa muhimu la kuwawezesha Watanzania kuongeza ushiriki wao katika uchumi wa madini kwa kuwajengea uelewa kuhusu fursa, sheria na taratibu za utoaji wa bidhaa na huduma migodini.
Dkt. Numbi ameyasema hayo leo, Julai 21, 2026, alipokuwa akizungumza mubashara kupitia kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV, akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki.
Amesema LCCF 2026 inatoa nafasi kwa wadau kujifunza, kujenga mitandao na kuchangamkia fursa zinazopatikana katika sekta ya madini, hususan katika eneo la ushirikishwaji wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.
Dkt. Numbi amesema utekelezaji wa sera ya ushirikishwaji wa Watanzania ni muhimu katika kuhakikisha wazawa wanashiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi zinazotokana na sekta ya madini, huku akibainisha kuwa tathmini ya utekelezaji wake ni takwa la kisheria linalofanyika kila baada ya miezi mitatu.
Amesema tathmini hiyo inalenga kuhakikisha sheria, kanuni na miongozo inazingatiwa, pamoja na kuongeza ushiriki wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini.
Kwa mujibu wa Dkt. Numbi, Tume ya Madini inaendelea kutoa huduma kwa wananchi kupitia mikoa yote 30 ya kimadini nchini, ikiwemo kutoa elimu na ushauri pamoja na kusimamia utekelezaji wa sheria na taratibu zinazohusu utoaji wa bidhaa na huduma migodini.
Amewataka watoa huduma wanaotarajia kufanya kazi na migodi kuhakikisha wanafahamu na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Tume ya Madini ili waweze kushiriki kikamilifu katika fursa zinazotokana na sekta hiyo.
Kwa upande wake, CPA Kasiki amesema kumekuwa na mwamko mkubwa miongoni mwa Watanzania wa kuchangamkia fursa zinazopatikana katika sekta ya madini, akibainisha kuwa kwa sasa kuna takribani aina 20 za bidhaa na huduma zinazotolewa na wazawa kupitia mpango wa ushirikishwaji wa Watanzania.
Amesema zaidi ya kampuni 20 tayari zimewasilisha maombi ya kuanzisha huduma kwa ajili ya kuhudumia shughuli za migodi katika eneo la Buzwagi, hatua aliyoieleza kuwa ni ishara ya kuongezeka kwa ushiriki wa Watanzania katika utoaji wa bidhaa na huduma katika sekta ya madini.
LCCF 2026, inayofanyika kuanzia Julai 22 hadi 24, 2026 katika Ukumbi wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza, inatarajiwa kuwaunganisha wadau mbalimbali wa sekta ya madini chini ya ugeni rasmi wa Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony P. Mavunde (Mb.).
Jukwaa hilo linaloandaliwa na Tume ya Madini linatarajiwa kuwakutanisha kampuni za uchimbaji wa madini, watoa huduma migodini, wafanyabiashara wa madini, wawekezaji, taasisi za umma na binafsi pamoja na wananchi kwa lengo la kujadili namna bora ya kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za kiuchumi zinazotokana na sekta hiyo.
Washiriki watapata fursa ya kujifunza kupitia mawasilisho ya kitaalamu, midahalo, mafunzo na maonesho yatakayowawezesha kuongeza uelewa kuhusu utekelezaji wa sera ya ushirikishwaji wa Watanzania na kunufaika na fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zinazopatikana katika sekta ya madini.
Aidha, jukwaa hilo litatoa nafasi kwa wadau kujenga mitandao ya kibiashara, kubadilishana uzoefu, kuanzisha ushirikiano wa kimkakati na kujadili mbinu za kuongeza ushiriki wa wazawa katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya madini.
Shughuli za jukwaa zitafanyika kwa siku tatu mfululizo kuanzia saa 2:00 kamili asubuhi kila siku.
Tume ya Madini imewahimiza wadau wa sekta ya madini na wananchi kwa ujumla kushiriki katika LCCF 2026 ili kupata uelewa mpana wa fursa zilizopo na namna ya kushiriki kikamilifu katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.
Jukwaa hilo limeendelea kuwa miongoni mwa majukwaa muhimu nchini yanayochochea ushirikishwaji wa Watanzania katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini, kukuza biashara na uwekezaji, pamoja na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa taifa.
Mtendaji Mkuu wa Kitengo Cha Wateja wa Makampuni (CIB), wa Absa Group kutoka Afrika Kusini, Bw. Zaid Moola (wa pili kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa makampuni (CIB), katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa kitengo cha CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mtendaji Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Makampuni (CIB), wa Absa Group Kutoka Afrika Kusini, Bw. Zaid Moola (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Wateja wa Makampuni wa Kanda ya Afrika, Bw. Sola Adegbesan, wakifurahi katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa jijini Dar es Salaam leo kwa wateja wa makampuni, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji hao kutoka absa group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia), akimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance, Bw. Muhammad Shah Newaj, katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushirikiano wa kibiashara baina yao. Kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi. Katikati ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Rwegalulira.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Masoko ya Fedha za Kigeni wa benki hiyo, Bi. Irene Rwegalulira, wakati wa hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja wa Makampuni wa Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga na Mkuu wa Kitengo cha Shughuli za kibenki wa benki hiy, Bw. Alred Urasa.
Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga akizungumza katika hafla waliyowaandaliwa wateja wa makampuni (CIB), jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. kikao hicho pia kiliwakutanisha wateja hao na watendaji wakuu wa kitengo cha CIB kutoka Absa Group, waliopo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Wateja wa Absa Group, Bw. Clive Potter (kushoto), akizungumza na baadhi ya wateja wa makampuni (CIB), katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kama sehemu ya kudumisha ushikiriano wa kibiashara baina yao. Katikati ni Mkurugenzi wa Fedha wa Amref Health Africa, Bw. Damas Nugashe na Mkurugenzi Mtendaji wa Savanna Fibre Tanzania, Bw. Thomas Wenanga.

Mtendaji Mkuu wa Wateja wa Makampuni (CIB) wa Absa Group, Bw. Zaid Moola, baadhi ya watendaji wakuu kutoka Absa Group, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, baadhi ya wafanyakazi na wateja wa CIB, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho jijini Dar es Salaam leo.
-WANANCHI KUNUFAIKA KIUCHUMI
Mbinga, Ruvuma
Wananchi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wanatarajia kunufaika na ujenzi wa barabara ya Utiri–Mahande yenye urefu wa kilomita 14 inayojengwa kwa kiwango cha lami, mradi unaotarajiwa kuimarisha usafirishaji wa mazao, kurahisisha huduma za kijamii na kuchochea ukuaji wa uchumi wa eneo hilo.
Mradi huo umefikia asilimia 85.31 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti mwaka huu hali inayowapa matumaini wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za usafiri hususan wakati wa mvua.
Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Ukaguzi ya TARURA, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bw. Henry Kaywanga amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea maendeleo ya mradi huo na kuhakikisha unatekelezwa kwa viwango vinavyokusudiwa ili kutoa manufaa yaliyotarajiwa kwa wananchi.
"Kamati hupokea taarifa za utekelezaji wa miradi mbalimbali lakini pia hutenga muda wa kutembelea maeneo ya kazi ili kujiridhisha na maendeleo yake pamoja na kutoa ushauri utakaosaidia miradi hiyo kukamilika kwa wakati na kutoa huduma bora kwa wananchi", amesema Bw. Kaywanga.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Barabara TARURA, Mhandisi Venant Komba amesema barabara hiyo inajengwa kupitia mradi wa Agri-Connect unaofadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya ukiwa na lengo la kuboresha miundombinu inayorahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka mashambani hadi sokoni hususan kahawa.
Ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutapunguza gharama na muda wa usafirishaji wa mazao, kuongeza fursa za biashara na kuinua kipato cha wakulima pamoja na wananchi wa Wilaya ya Mbinga kwa ujumla.
"Mradi huu utachochea ukuaji wa uchumi wa wananchi kwa kuhakikisha mazao yanasafirishwa kwa urahisi na kwa wakati tofauti na ilivyokuwa hapo awali", amesema Mhandisi Komba.
Naye, mkazi wa Mbinga Bw. Joseph Mbilinyi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya barabara akisema ujenzi wa barabara hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi.
Amesema pamoja na kurahisisha usafiri na usafirishaji wa mazao, barabara hiyo itaongeza upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii na kufungua fursa mpya za maendeleo kwa wakazi wa eneo hilo.
Kamati ya Ukaguzi ya TARURA chini ya Kaimu Mwenyekiti wake Bw. Henry Kaywanga inaendelea na ziara za kukagua miradi mbalimbali nchini ili kuhakikisha inatekelezwa kwa ufanisi, ubora unaotakiwa na kuleta matokeo chanya kwa wananchi.
For the Saitoti family, the relocation from Nainokanoka ward in Ngorongoro conservation area to Msomera Handeni Tanga represented far more than a geographical transition; it marked the commencement of a new chapter of new better future.
That chapter is now distinguished by profound joy.
On July 18, 2026, Evaline Saitoti, a young Maasai woman who resettled in Msomera with her family, solemnized her marriage and was welcomed into an American family currently residing in Zanzibar. The union constitutes not only a significant personal milestone but also exemplifies the emerging opportunities that have followed the family's voluntary relocation.
“Unlike Ngorongoro, Our life in Msomera has been characterized by opportunity, good life status surrounded by social services like schools, health centers, electricity, street road network, communication facilities and practice our traditional culture peacefully and safe” stated her elder brother, Emmanuel Saitoti.
“We have established a new home, and today we commemorate one of the most momentous occasions in our family’s history. Witnessing my sister establish her own family here is a blessing for which we are deeply grateful for what Tanzania Government did for us .”
Saitoti further noted that the family has fully integrated into their new community and maintains an optimistic outlook for the future.
“Msomera has afforded us the liberty to develop, to work, and to construct our lives with hope. Our hearts are replete with happiness today, for this place has truly become our home.”
As relatives, friends, and community members convened to honor Evaline’s wedding, the event transcended the bounds of a traditional marriage ceremony. It served as a testament to resilience, renewal, and the conviction that, through hope and determination, a new location can evolve into a place of opportunity, belonging, and enduring fulfillment.



.jpeg)
.jpeg)








.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)








.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

