Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akichangia mada katika mkutano ulioangazia umuhimu wa sekta ya maji katika maendeleo ya watu na uchumi wa dunia, chini ya kauli mbiu “usalama wa maji kwa mustakabali wa bara la Afrika: mtazamo wa mbele” ulioandaliwa na Benki ya Dunia, pembezoni mwa mikutano ya majira ya Kipupwe ya Benki hiyo na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, uliofanyika jijini Washington D.C, nchini Marekani.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Washington D.C, Marekani)

Na Benny Mwaipaja, Washington D.C
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kuweka mipango ya kuhakikisha kuwa maji salama yanapatikana kwa ajili ya matumizi ya binadamu na shughuli za kiuchumi lakini pia kulinda vyanzo vya maji.

Mhe. Balozi Omar alisema hayo wakati akichangia mada katika mkutano ulioangazia umuhimu wa sekta ya maji katika maendeleo ya watu na uchumi wa dunia, chini ya kauli mbiu “usalama wa maji kwa mustakabali wa bara la Afrika: mtazamo wa mbele” ulioandaliwa na Benki ya Dunia, pembezoni mwa mikutano ya majira ya Kipupwe ya Benki hiyo na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, uliofanyika jijini Washington D.C, nchini Marekani.

Akijibu swali la namna rasilimali za maji zinavyoweza kulindwa na kutumika kama rasilimali za kiuchumi, Mhe. Balozi Omar alisema ni muhimu ieleweke kwamba maji ni rasilimali muhimu hivyo ni lazima kufanya utafiti wa kutambua vyanzo vya maji vilivyopo ikiwemo mito na maziwa na kuweka utekelezaji wake kwenye mipango ya kitaifa ya maendeleo ya muda mfupi, wa kati na muda mrefu.

“Pia ni muhimu kuvifuatilia na kuvilinda vyanzo hivyo na kuzitumia rasilimali hizo kwa uangalifu mkubwa ili tuendelee kuwa na maji safi, kuvilinda vyanzo hivyo dhidi ya uvamizi na uchafuzi wa maji, pamoja na kuondoa upotevu wa maji.” Alisema Mhe. Balozi Omar

Alitahadharisha kuwa idadi ya watu inaendelea kuongeza kwa kasi barani Afrika hatua iliyosababisha kuwa na uhitaji mkubwa wa maji na kushauri kuwepo kwa ushirikiano madhubuti kati ya sekta binafsi na wadau wengine wa maendeleo kama Benki ya Dunia ili kuwezesha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili kutekeleza mira ya maji.

Mkutano huo wa maji uliwashirikisha Mawaziri wa Fedha na wadau wengine kutoka nchi wanachama wa Benki ya Dunia kutoka baadhi ya nchi za Bara la Afrika ambapo walijadili namna sera, uwekezaji, mabadiliko ya kimfumo wa kitaasisi unavyoweza kuboresha na kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama barani Afrika.



Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze, Aprili 19, 2026
MWENGE wa Uhuru umetambua mchango wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, kufuatia kuandika kitabu(andiko) kinachoelezea falsafa ya Mwenge wa Uhuru tangu kuanzishwa kwake mwaka 1961.

Imeelezwa Juhudi hizo za Ridhiwani, amezifanya wakati alipokuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, kuandika andiko hilo rasmi Kiserikali.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda, alitambua mchango huo kuwa sehemu ya historia ya Taifa wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yaliyofanyika Aprili 19, 2026 katika Shule ya Msingi Kiwangwa, Halmashauri ya Chalinze, ukitokea Halmashauri ya Bagamoyo.

Mbali ya hilo, Ridhiwani ametajwa kuwa miongoni mwa wananchi wawili wa wilayani Bagamoyo waliotoa mchango wa kipekee kwa jamii, ambapo mmoja alijitolea kuvusha watoto darajani kwenda shule, huku mwingine akitoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa shule.

Mwang'onda alieleza, Mwenge wa Uhuru ni moja ya tunu kubwa za Taifa, ukiwa kichocheo muhimu cha maendeleo, hususan katika kupambana na ujinga, maradhi na umaskini.

Awali, akipokea Mwenge huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze, Ramadhan Possi, alieleza jumla ya miradi saba yenye thamani ya sh. bilioni 34.179 inapitiwa, ambapo miradi mitatu imezinduliwa, mitatu imekaguliwa na mmoja umetembelewa.

Wakati huohuo, Mwang’onda ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika Kituo cha Afya Kiwangwa uliogharimu shilingi milioni 20.583.

Pia Mwenge wa Uhuru umetembelea ujenzi wa boksi kalvati katika barabara ya Mwinyi–Kudiembe, Kata ya Bwilingu, uliotekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 67.3 kupitia TARURA; na kutembelea kiwanda cha Starlinkgulf Trading Co. Ltd (Wallput) kilichojengwa kwa gharama ya zaidi ya sh bilioni 34.

*Awataka wahakikishe miradi inasimamiwa na kuleta tija iliyokusudiwa

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema watendaji wa Serikali wanajukumu la kuhakikisha miradi ya maendeleo inayotokelezwa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo ya maji, umeme, afya, miundombinu na elimu inasimamiwa ipasavyo ili Watanzania waweze kupata tija iliyokusudiwa.

Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka jitihada kubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hivyo ni lazima itekelezwe kama ilivyokusudiwa.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili, Aprili 19, 2026) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Msanga, Chamwino mkoani Dodoma baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa maji akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema jukumu kubwa walilonalo watendaji ni kusimamia ipasavyo miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao na kuhakikisha wananchi wananufaika kama ilivyokusudiwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha Watanzania wote wananufaika na rasilimali za Taifa kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao. “…Watanzania waweze kunufaika na matunda ya Taifa lao.”

Pia, Waziri Mkuu amewaasa Watanzania kujiepusha na watu wanaotumia kivuli cha imani za dini kufanya siasa za majukwaani, huku wakiwa na lengo ovu la kuwagawa watanzania kwa chuki za kiiimani na itikadi za kisiasa. “Ndugu zangu Watanzani tuendelee kulinda umoja na amani yetu. Kuna watu sasa wanatafuta namna ya kutumia siasa na dini ili kutugawa, tujihadhari na watu wa namna hiyo” amesisitiza.

Awali,Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la mradi wa Maji wa Miji 28 wilayani Chamwino, ambapo alitumia fursa hiyo kumshukuru Mheshimwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa mradi huo akisema ni wa kimkakati unaokwenda kumaliza tatizo la maji katika maeneo hayo.

Kwa upande wake, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso alisema Wizara ya Maji itahakikisha mradi huo mkubwa unakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika. “Kupitia Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA), Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka fedha nyingi na tayari vijiji 10,758 vimeshafikiwa na huduma ya maji safi na salama na vimebakia vijiji 1,575.”

Akitoa taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Usambazaji wa Maji Mijini kutoka Wizara ya Maji, Mhandisi Charles Mafie alisema kwamba mkataba wa mradi huo unatarajiwa kukamilika Agosti 10, 2026 ukiwa na thamani ya shilingi Bilioni 17.2 na umefikia asilimia 70.2 ya utekelezaji.

Mradi huo unatarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 60,000 katika kata za Msanga, Buigiri, Chamwino na Mtumba na kuongeza upatikanaji wa maji safi kutoka asilimia 91 hadi 100 pamoja na kuimarisha uzalishaji wa maji kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadae.

Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba, ametoa onyo kali kwa watu wanaodaiwa kuwa na njama za kuvuruga amani ya nchi, akiwataka Watanzania wote kuendelea kuwa walinzi wa kwanza wa utulivu na mshikamano wa taifa. Amesema kuwa amani ya Tanzania si jambo la kubahatisha, bali ni tunu inayopaswa kulindwa kwa nguvu zote na kila mwananchi.

Akizungumza jijini Dodoma, katika wilaya ya Chamwino, Dkt Mwigulu alionyesha msimamo thabiti wa serikali katika kuhakikisha hakuna mtu au kundi litakaloruhusiwa kuchezea amani ya nchi. Amesisitiza kuwa vyombo vya dola viko macho na vitachukua hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika kuhatarisha usalama na utulivu wa taifa.

Mbali na hilo, Waziri Mkuu ameelekeza ujumbe kwa viongozi wa umma, akiwataka kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na uwajibikaji wa hali ya juu. Amekemea vikali vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka, akisisitiza kuwa serikali haitamvumilia kiongozi yeyote atakayekiuka maadili ya utumishi wa umma.

Amefafanua kuwa anafuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo nchini ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana kwa wananchi. “Kila mradi ninaangalia, kila hatua inafuatiliwa. Atakayekwenda kinyume, hatabaki salama kwenye nafasi yake,” alisisitiza, akionyesha dhamira ya serikali kusimamia rasilimali za umma kwa umakini mkubwa.

Dkt Mwigulu amegusia pia suala la haki kwa wananchi, akionya kuwa hatasita kuwachukulia hatua wale wote wanaowaonea wengine au kukandamiza haki za wananchi. Kauli yake ya, “Wale wanaowaonea wengine nitashughulika nao, msiwe na mashaka — upele umepata mkunaji,” ilizua hisia za matumaini kwa wananchi kuhusu hatua madhubuti zitakazochukuliwa dhidi ya vitendo vya dhuluma.

Aidha, amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na serikali katika kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha maendeleo yanawafikia wote kwa usawa. Amesisitiza kuwa maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa amani, nidhamu na uwajibikaji wa pamoja.

Kauli hizo zinakuja wakati serikali ikiendelea kuimarisha misingi ya utawala bora, kupambana na rushwa, na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo kwa lengo la kujenga taifa lenye uchumi imara na ustawi wa wananchi wake.













Na Pamela Mollel,Arusha

Mashindano ya Tanfom Marathon yamefanyika kwa mafanikio makubwa jijini Arusha, yakiambatana na maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwake, tukio ambalo limeendelea kuipa heshima Tanzania katika sekta ya michezo na kuvutia wanariadha kutoka ndani na nje ya nchi.

Akizungumza katika mashindano hayo, Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania, Rogath John, amesema mashindano hayo yameonesha kiwango kikubwa cha ushindani na maandalizi bora kutoka kwa wanariadha, jambo linaloonesha maendeleo ya riadha nchini.

Amesema Tanfom Marathon ni sehemu muhimu ya maandalizi ya wanariadha kuelekea mashindano ya kimataifa, akibainisha kuwa lengo la shirikisho ni kuona Tanzania inazidi kuongeza ushindani na kupata medali zaidi katika mashindano makubwa duniani.

Kwa upande wa wadhamini, Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa CRDB Bank, Cosmas Sadat, amesema benki hiyo itaendelea kuunga mkono matukio ya michezo na kijamii kama sehemu ya kurudisha kwa jamii.

Amesema uwekezaji katika michezo unachochea afya bora, mshikamano wa jamii na pia kukuza fursa za kiuchumi kupitia michezo na utalii wa michezo.

Mashindano hayo ya kilomita 42 yamehusisha wanariadha kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda na Uholanzi, hali iliyoongeza ushindani na hadhi ya kimataifa ya tukio hilo lililofanyika Arusha.

Wanariadha wa ndani na nje walionesha kiwango kikubwa cha ushindani, hali iliyoifanya Tanfom Marathon kuendelea kuwa moja ya mashindano yenye hadhi kubwa nchini.

Kwa upande wa wanaume, Modest Petro Kalist ameibuka mshindi wa kwanza baada ya kuonesha kiwango cha juu cha mbio na uthabiti mkubwa. Kalist amesema ushindi huo umetokana na mazoezi ya muda mrefu na uzoefu wa mashindano ya awali, yaliyomsaidia kukabiliana na ushindani mkali kutoka kwa wanariadha wa kimataifa.

Kwa upande wa wanawake, Vaileth Adam ameibuka mshindi wa kwanza wa kilomita 42, akionesha nidhamu, uvumilivu na maandalizi mazuri yaliyomuwezesha kufanikiwa. Amesema ushindani wa kimataifa ulimpa motisha zaidi ya kuongeza juhudi na kuwahimiza vijana kuendelea kujituma katika michezo.

Katika mashindano hayo, washindi wamepatiwa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu, ambapo mshindi wa kwanza amepata shilingi milioni 6, huku washiriki wengine wakipatiwa zawadi tofauti ikiwemo magodoro kama sehemu ya kutambua juhudi zao.

Wadau wa michezo wamesema Tanfom Marathon imeendelea kuwa moja ya mashindano makubwa yenye mchango mkubwa katika kukuza riadha, kuimarisha afya za wananchi na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia michezo.

Kwa ujumla, maadhimisho ya miaka 60 ya Tanfom Marathon yameacha historia kubwa jijini Arusha, yakionesha ukuaji wa riadha nchini na kuimarika kwa ushiriki wa kimataifa.








Na Asia Singano na Josephine Majura, WF, Mwanza.
SERIKALI imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia sera na mipango mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), katika Mahafali ya 20 ya Shule ya Sekondari ya Thaqaafa, wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.

Alieleza kuwa, Serikari inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kupitia Sera na mipango mbalimbali ya kiuchumi na kijamii ili kuhakikisha kuwa vijana wanapata fursa za kuendeleza vipaji vyao na kuchangia kikamilifu maendeleo ya taifa.

‘’Dunia ya sasa inahitaji vijana wanaoweza kutatua changamoto kwa ubunifu, hasa katika nyanja za uchumi, teknolojia na ujasiriamali ‘’ Alisema Mhe. Munde (Mb).

Amewaasa vijana kuendelea kuwa na nidhamu na uadilifu kwakuwa Taifa linahitaji vijana wenye misingi imara ya maadili, wanaoweza kusimamia rasilimali za nchi kwa uwajibikaji na weledi.

Kwa upande wake Meneja wa Shule ya Thaqaafa, Bw. Idrisa Hayeshi, amewasisitiza wazazi kuendelea kushirikiana na walimu na Uongozi wa shule kufuatilia maendeleo ya wanafunzi ili kujua mwenendo wa tabia ambazo zina athari katika masomo yao.

“Shule imejipanga kutoa elimu bora ikiwa na matokeo mazuri kwa kila mwaka, tunavyofanya mawasiliano na mzazi ni kwamba atoe ushirikiano ili mtoto apate kitu kinachostahili’’ alisema Bw. Hayeshi.

Shule ya Sekondari Thaqaafa imeadhimisha Mahafali ya 20 ya Kidato cha Sita ambayo yalihudhuriwa na wahitimu (50).
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akipokea picha yake iliyochorwa wakati wa uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo uliofanyikakatika katika ukumbi wa Nkurumah.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akipokea tuzo kutoka kwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Joyce Juliasi Semkuyu, katika ukumbi wa Nkrumah. Tuzo hii ni ishara ya kutambua mchango wake katika jamii na juhudi zake za kuhamasisha maendeleo, hususan kwa wanawake.

Na Mwandishi Wetu WMJWM- Dar Es Salaam
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka watoto wa kike kujipambanua katika kuhakikisha wanatumia muda wao kufanya mambo yatakayowasaidia katika ustawi wa maisha yao.

Waziri Dkt. Gwajima ameyasema hayo tarehe 18 Aprili, 2026 wakati akizindua Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo.

Waziri Gwajima amesema jina la Binti Jasiri lina maana kubwa sana likiwakilisha ujasiri wa kusimama, kuota ndoto kubwa na kushinda changamoto hivyo katika ulimwengu wa leo, kunahitajika kuwa na mabinti ambao hawataogopa kushika nafasi za uongozi, kuanzisha biashara, wala kuchangia katika maamuzi makubwa ya kijamii na kiuchumi.

Ameeleza kuwa mpango huo umejengwa katika msingi imara unaoendana na dira ya maendeleo ya taifa yaani Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025, pamoja na malengo ya kimataifa ya maendeleo endelevu, hasa Elimu Bora (SDG 4) na Usawa wa Kijinsia (SDG 5).

“Binti Jasiri si tukio la siku moja bali ni mwanzo wa harakati endelevu na ni mwanzo wa kizazi kipya cha wanawake; Wenye maono, ujasiri na uwezo wa kubadilisha dunia.” Ameafafnua Waziri Dkt Gwajima.

Aidha amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana, bado mabinti wengi wanakutana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mentorship, fursa za uongozi na rasilimali za kujiendeleza hivyo kupitia Binti Jasiri, inaunda mazingira yatakayowawezesha mabinti kujifunza uongozi, kuunganishwa na wale waliowatangulia na kujenga ujasiri wa kujitegemea na hatimaye kuwa suluhisho la changamoto za jamii.

“Nitoe wito kwa Mabinti wangu wapendwa, nataka muondoke hapa leo mkiwa na jambo moja moyoni ambalo ni uwezo, thamani kwani unaweza kufika mbali zaidi ya unavyodhani pia usiruhusu hofu, maneno ya watu au mazingira yakuzuie kwani Dunia inahitaji sauti yako, mchango wako na uongozi wako basi chukua nafasi Jitokeze na Jiamini.” Amesisitiza Waziri Gwajima

Pia amewataka wadau wote wanaotokea serikalini, sekta binafsi, taasisi na washirika kusisitiza kuwa kuwekeza kwa mwanamke kwani ni uwekezaji kwa taifa na kumuinua msichana mmoja ni kuinua familia, jamii na uchumi mzima hivyo amewahimiza kuendelea kuunga mkono mipango kama hiyo kutoa mentorship na kufungua milango ya fursa kwa vijana wa kike.

Kwa upande wake Makamu wa rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Joyce Juliasi Senkuli amesema Jukwaa hilo limeanzishwa kwa lengo la kumkomboa binti kifikra, kihisia, kielimu na kiuchumi, kwa kutambua kuwa bado wapo mabinti wengi wanaopitia changamoto mbalimbali katika safari ya maisha na elimu.

Naye Mwakilishi wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Paulina Mabuga ameahidi kuwaunga mkono Mabinti hao ili waweze kufikia malengo yao katika kampeni walioianzisha ya kuwafanya Watoto wa kike kuinuka katika masuala mbalimbali katika jamii.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akizungumza katika uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM inayoongozwa na kaulimbiu isemayo Weka Malengo, Piga Hatua Timiza Malengo uliofanyika katika ukumbi wa Nkurumah. .
Baadhi ya Washiriki katika uzinduzi wa Binti Jasiri UDSM ulkofanywa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima katika ukumbi wa Nkurumah.

Na Khadija Kalili, Bagamoyo
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ambao umepokelewa asubuhi tarehe 18 Aprili 2026 kutoka Jijini Dar es Salaam utakagua miradi 68 ambapo kati ya miradi hiyo miradi 23 itawekwa mawe ya msingi, miradi 21 itazinduliwa na miradi 24 itakaguliwa.

RC Kunenge amesema kuwa miradi yote inathamani ya jumla ya Shilingi za Kitanzania Tsh.Bilioni 263,061,799, 595.55.

"Miradi yote hii imefanikiwa kutokana na ushirikiano mzuri uliopo baina ya viongozi wa serikali, wananchi na wadau wa maendeleo" amesema Kunenge.

Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha itaupokea mwenge huo tarehe 20 Aprili 2026 katika shule ya Msingi Gumba kata ya Gwata na kukimbizwa katika Miradi ya Maendeleo na kuhitimishwa kwa mkesha Mkubwa kiwanja cha Shule ya Msingi Mtongani.

Ujumbe mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 , unalenga katika ujenzi wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa chini ya kaulimbiu isemayo 'Tanzania yetu sote , tushikamane kwa kuleta pamoja maendeleo ' kauli mbiu hii inalenga kujenga na kuimarisha umoja wa Kitaifa na kuutumikia Mwenge wa Uhuru kuwaenzi na kuwatia moyo wazalendo wa kweli na makundi mbalimbali yenye mchango mkubwa katika kulinda amani, umoja na mshikamano kitaifa katika kujenga Tanzania imara kimaadili,kidiplomasia na kiuchumi ndani na nje ya mipaka yetu ikiwa ni pamoja na na kurejesha falsafa hii ya Mwenge wa Uhuru kwa wananchi wa Tanzania.

Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Wilaya saba na Halmashauri tisa kwa umbali wa Kilomita 1,065.9



WANANCHI wa Kijiji cha Daluni Kisiwani na vijiji vya jirani, wilayani Mkinga mkoani Tanga, wameanza kunufaika na huduma bora za mawasiliano kufuatia uzinduzi wa mnara wa 4G uliojengwa na Airtel Tanzania, hatua inayochochea mabadiliko ya kijamii na kiuchumi katika eneo hilo la mpakani.

Kwa miaka mingi, kijiji hicho kilikabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa mawasiliano ya uhakika, hali iliyokuwa ikiathiri shughuli za kiuchumi pamoja na mahusiano ya kijamii ndani ya familia na jamii kwa ujumla. Upatikanaji wa mtandao wa kasi sasa unaanza kufungua ukurasa mpya wa maendeleo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Afisa Masoko wa Airtel Mkoa wa Tanga, Nassor Laizer, alisema kampuni hiyo inaendelea kupanua huduma zake vijijini ili kuhakikisha hakuna Mtanzania anayeachwa nyuma katika mapinduzi ya kidijitali.

“Nia yetu ni kufikisha mawasiliano katika maeneo ya vijijini kama Daluni Kisiwani ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali. Mawasiliano si anasa tena, ni hitaji muhimu kwa maendeleo,” alisema Laizer.

Kauli hiyo inaakisi mwelekeo mpana wa sekta ya mawasiliano nchini, ambapo kampuni nyingi sasa zinaelekeza uwekezaji wao katika maeneo ambayo hapo awali hayakuwa na huduma za kutosha.

Kwa wakazi wa eneo hilo, manufaa ya mnara huo yanaonekana moja kwa moja katika maisha ya kila siku. Wakazi Kassim Kumba na Fatuma Hozza walisema changamoto ya mtandao ilikuwa ikisababisha hata migogoro ndani ya familia kutokana na kushindwa kuwasiliana kwa wakati.

“Kulikuwa na wakati huwezi kumpata ndugu yako kwa siku kadhaa. Hali hii ilisababisha kutoelewana na wakati mwingine migogoro ndani ya familia,” alisema Kumba.

“Sasa tunaweza kuwasiliana kwa urahisi. Inaleta utulivu na kuimarisha mahusiano,” aliongeza Hozza.

Maelezo yao yanaonyesha athari za moja kwa moja za ukosefu wa mawasiliano, si tu katika uchumi bali pia katika mshikamano wa kijamii.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge wa Mkinga, Kiroboto S. Kiroboto aliwataka wananchi kutumia fursa ya huduma hiyo mpya kwa maendeleo yao.

“Huu ni wakati sahihi kwa wananchi kutumia mtandao huu kwa shughuli za kiuchumi na kijamii, ikiwemo kutafuta masoko na fursa mbalimbali za kidijitali ambazo awali hazikuwepo,” alisema.

Uwekezaji wa miundombinu ya mawasiliano una mchango mkubwa katika kuchochea uchumi wa vijijini. Upatikanaji wa mtandao unawezesha huduma za kifedha za simu, biashara mtandaoni, elimu ya kidijitali na hata huduma za serikali kwa njia ya mtandao.

Uzinduzi wa mnara huo pia unaendana na juhudi za Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan za kupunguza pengo la kidijitali kati ya mijini na vijijini, kupitia ushirikiano na sekta binafsi pamoja na miradi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).

Kwa sasa, Daluni Kisiwani inaanza kushuhudia mabadiliko chanya, ambapo mawasiliano rahisi yanakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, na kuunganisha jamii ambayo kwa muda mrefu ilikuwa nyuma kimaendeleo.


The confrontation of the United States and Israel with Iran has moved from covert operations to open war, igniting a conflict that defies containment. What began as calculated strikes has become a multi-domain struggle involving air, sea, cyber, and proxy arenas, shifting power dynamics, exposing vulnerabilities, and pulling the world toward an uncertain edge where escalation moves faster than control and outcomes grow more unpredictable by the hour.


1. Introduction.

Wars begin when you will but they do not end when you please, Niccolò Machiavelli wisely noted, a thought that carries chilling clarity over the events of February 28, 2026, when the United States and Israel launched coordinated strikes against Iran, which opened open war and collapsed the fragile illusion that diplomacy was still holding. Only days earlier, indirect nuclear negotiations held in Geneva had ended without reaching any agreement, yet both sides still held a cautious belief that continued discussions might reduce tensions and narrow the gap between their demands and concerns, even though deep mistrust remained unchanged.

In that fragile atmosphere, the brief expectation of further diplomatic engagement quickly dissolved as the situation shifted from stalled talks into full military confrontation. Under the operation names “Operation Roar of the Lion” and “Operation Epic Fury,” coordinated strikes hit Tehran and other strategic locations, targeting nuclear facilities, ballistic missile infrastructure, and key political and military command structures.

Behind this sudden escalation, the foundations of the war stretch deep into history, tracing back to the turning point of 1979 and decades of hostility built on sanctions, proxy confrontations, and the unresolved nuclear question. Agreements collapsed, trust eroded, and by 2025, diplomacy had become little more than ritual performed but no longer believed.

From this long buildup, the months leading to February 2026 saw rising sanctions pressure, military buildups across the Gulf, and a persistent movement toward inevitability. What emerged was not a sudden conflict but a planned break and what can be understood as a preemptive decapitation strategy, aimed not simply at deterrence but at destabilizing Iran’s governing structure and strategic stability.

1.1. The Inferno.

With the conflict now fully ignited, the immediate consequences were as devastating as they were decisive. Within hours, Iranian state media confirmed the deaths of Supreme Leader Ali Khamenei, Defense Minister Aziz Nasirzadeh, and Chief of Staff Abdolrahim Mousavi, a blow that effectively removed Iran’s military leadership in a single stroke. Civilian casualties mounted alongside these high profile killings, which made clear the brutal reality that even the most advanced “precision” warfare cannot contain its human cost.

As the scale of destruction became clear, what had been conceived as a rapid, overwhelming strike to neutralize threats instead ignited a wider inferno. Iran responded with fury, launching hundreds of ballistic missiles and over a thousand drones, extending the theater of war across Israel and deep into the Gulf, including Bahrain, Qatar, Kuwait, the United Arab Emirates, and Saudi Arabia, turning a targeted operation into a regional conflagration within 24 hours.

Beyond this immediate exchange of force, a deeper and more unsettling reality emerges that this is not a single war but multiple wars taking place at the same time, each governed by its own tempo and logic. The air war moves at supersonic speed, measured in minutes as jets and missiles cross borders. The naval war progresses slowly but with severe consequences, as Iran moves to close the Strait of Hormuz, threatening a fifth of global oil supply.

Within this battlefield, the cyber war operates in silence while retaliatory strikes target American and Israeli systems. At the same time, the proxy war spreads outward, as Hezbollah, Iraqi militias, and Yemeni Houthis have entered the conflict, bringing new fronts into play. Together, these layers form a multi layered structure of violence in which each strike generates another strike, and no decisive victory appears possible.

1.2. No Control Point.

In the days and weeks that followed, the human, infrastructure, and economic toll of the war revealed its most haunting dimensions. Beyond the elimination of Iran’s leadership, civilian suffering surged into global consciousness, with pain and loss felt deeply on both sides of the conflict as families faced destruction, displacement, and grief.

The conflict escalated according to a relentless logic of escalation. Iranian retaliation struck United States military installations and allied facilities across Gulf states, while Israel intensified its campaign by targeting critical infrastructure such as the South Pars gas field, sending shockwaves through global energy markets and pushing oil prices higher. Escalation has become a paradoxical strategy propelled not by control but by the inability to avoid it, as each move intended to contain the conflict instead stretched it into a cycle with no clear endpoint. Machiavelli’s warning still stands not as philosophy but as lived reality.

Now, the question that haunts every capital including Washington, Tel Aviv, and Tehran is not how the war began but how it ends. A fragile ceasefire brokered in early April 2026 offers only a temporary pause in a conflict that continues to move beneath the surface. Intelligence assessments suggest Iran still retains the capacity to strike back in meaningful ways, even after sustained pressure, while external actors, including global powers, edge closer to involvement.

2. War in Motion.

This conflict rests on the operational coordination between the United States and Israel, who have adopted a doctrine built on dominant air superiority, where the sky itself becomes both shield and sword. Their strategy relies on precision strikes designed to dismantle Iran’s military architecture by targeting command centers, leadership networks, and communication systems in order to fracture coordination and impose strategic paralysis. Rather than engaging in prolonged territorial warfare, the objective is to control tempo from above, forcing Iran into reactive patterns of defense in several directions.

Alongside this aerial dominance, the United States and Israel extend pressure through maritime and regional strategic influence, where critical sea routes and energy corridors become extensions of the battlefield. In this structure, naval power is used to secure, monitor, and in some cases restrict movement through key chokepoints, especially the Strait of Hormuz. The security and stability of global shipping lanes in this region are therefore directly tied to operational outcomes on land, in the air, and at sea, transforming economic infrastructure into a strategic instrument of pressure. As a result, military operations and economic power function together as a single integrated system of influence, where control over movement and supply becomes as decisive as control over territory or airspace.

In contrast, Iran’s response relies on dispersion rather than concentration, following a doctrine of asymmetry and unpredictability. The war plays out as an interconnected system of pressure points across land, air, sea, cyber, and proxy fronts. Instead of matching conventional airpower, Iran stretches the battlefield through swarms of drones, ballistic and cruise missile strikes, and coordinated activity with allied non-state actors such as Hezbollah and other regional partners. This produces a wide and fragmented theater of war stretching from Lebanon to the Gulf, including maritime corridors and covert operational spaces. Proxy warfare becomes a main instrument, allowing Iran to extend its reach far beyond its borders while complicating containment and escalation control.

Technology intensifies this confrontation on all sides. Drone systems are used to saturate defenses through volume and unpredictability, while advanced missile interception networks operate under continuous pressure. At the same time, cyber operations introduce an invisible layer of warfare, targeting intelligence systems, communications infrastructure, and critical services. The result is a battlespace where physical destruction and digital disruption merge, compressing response time and increasing the complexity of every operational decision.

3. Fire and Whisper.

The path to the first wave of strikes was set in motion not by a sudden collapse of diplomatic reason, but by the slow, agonizing death of the Joint Comprehensive Plan of Action (JCPOA) nuclear agreement, now reduced to a ghost of its original form. For years, the JCPOA revival talks in Vienna had become a graveyard of good intentions, where every technical negotiation crumbled under the weight of maximalist demands.

From this prolonged stagnation, the failure of diplomacy became impossible to ignore. As detailed in the pre-war diplomacy failure, the collapse of these nuclear negotiations did not happen overnight but instead unfolded as a predictable funeral, with the United States insisting on dismantlement far beyond the original accord while Iran cloaked its positions in sovereign inviolability. The ghost of the deal haunted every empty chair at the table, and by the time the first bunker-buster hit its target, diplomacy had already been declared a casualty, even if no one had yet signed the death certificate.

Out of that diplomatic collapse, war did not replace negotiation entirely but rather forced it into a different form. Yet even as the bombs fell, diplomacy refused to die because it simply mutated into a desperate, parallel existence alongside the warfare. The Islamabad Talks became the clearest symbol of the deadlock, with conflicting demands hardening into absolute positions, as the United States and Israel demanded full nuclear dismantlement while Iran refused to surrender what it called an inalienable right to enrichment.

As those rigid positions intensified, even attempts to pause the violence proved fragile and temporary. At the same time, Europe began distancing itself from the military escalation because it feared a regional inferno, while Russia and China used their UN Security Council vetoes to shield Tehran, turning the Axis of Resistance diplomacy into a geopolitical shield. The underlying argument of this war is simple because it happened as deterrence failed, not because diplomacy was untried. From this point, a more unsettling truth about the nature of diplomacy in modern conflict begins to emerge. The main insight remains unsettling because diplomacy has not disappeared, but it is no longer aiming for peace and instead is only managing the catastrophe.

3.1. Voices Against the War.

Opposition to the war has emerged across multiple layers of the international system, combining political resistance, public protest, and moral condemnation. Several governments and international actors have either openly criticized or quietly distanced themselves from the escalation, warning that the conflict risks widening into a regional catastrophe with global consequences. Beyond state actors, widespread protests have taken place across different countries, reflecting a growing perception that the war is not only strategically dangerous but also legally and morally contested.

Within this growing opposition, the most visible and morally forceful resistance has come from Pope Leo XIV, who has consistently denounced the war as unjust and dangerous. He has warned that the world is being pushed by leaders who misuse power and even religion to justify violence, while insisting that “God does not bless any conflict” and calling the war a form of madness. His position has not been isolated, as other religious figures including the Archbishop of Canterbury have supported his call for peace, bringing attention to the human cost and the moral failure of continued escalation.

At the same time, the conflict has revealed a growing concern over the use of moral and religious language in political and military decisions to legitimize war, raising questions over how far such narratives influence public understanding of the war. Pope Leo XIV has warned that the world is “being ravaged by a handful of tyrants” who prioritize destruction over human welfare. He condemned those who manipulate “the very name of God” for military, economic, and political gain, arguing that this distorts both faith and responsibility. The danger in this confrontation is not only diplomatic but conceptual, because once war is framed in religious terms, it becomes harder to limit, harder to negotiate, and far more likely to escalate beyond political control.

4. Fractured World.

What began as a calibrated show of force has turned into a conflict that refuses containment, spilling across borders with a pace that outstrips diplomacy. The war’s geography now stretches from Israel and Lebanon across to the Gulf, with Hezbollah pulling Lebanon into sustained confrontation, while Gulf states, once peripheral, find themselves within the growing blast radius of retaliatory strikes and strategic intimidation. Missile trajectories and drone swarms no longer respect traditional frontlines, blurring the line between battle zones and areas once assumed to be secure as civilian infrastructure comes under repeated disruption.

Yet the deeper tremor is economic, felt far beyond the battlefield. The closure and contestation of the Strait of Hormuz, through which a fifth of the world’s oil flows, has turned energy markets into instruments of war, driving prices upward and injecting volatility into an already fragile global economy. The International Monetary Fund’s downgraded growth forecasts reflect this strain, pointing to a growing crisis in which inflation rises, supply chains tighten, and vulnerable economies, particularly energy importers, bear disproportionate pain.

If the battlefield exposes the mechanics of destruction, diplomacy reveals the fractures of the international system itself. The refusal of key NATO members such as the United Kingdom and France to fully support Washington’s escalation points to a clear strategic divide within the Western alliance. At the same time, a countervailing axis, operating in support of Iran through Russia’s intelligence assistance, China’s economic and technical links, and North Korea’s missile cooperation, has come together not as a formal bloc but as a shadow coalition working to reduce the United States’ influence. This is no longer a bipolar confrontation. It is a tri polar world in motion, where power is diffused, contested, and increasingly transactional.

5. Conclusion.

Now we know what a modern war looks like. It is a war that begins without clear authorization and proceeds without a consistent legal or moral framework. The strikes launched on 28 February 2026 by the United States and Israel against Iran did not receive approval from the United Nations Security Council, nor were they preceded by a direct Iranian attack on either state. In that sense, the conflict exposes a clear reality that the international system lacks the power to prevent or meaningfully constrain wars initiated by major powers. What emerges is not simply a failure of diplomacy, but a deeper erosion of the rules that once defined legitimacy in war, leaving smaller states and global stability increasingly vulnerable in a system where power acts first and justification follows later.

The war raises unresolved political and strategic questions that extend far beyond the battlefield. First, there is a lack of clear objectives and outcomes, with no visible endgame directing the course of the conflict. Second, rather than eliminating the threat of weapons of mass destruction, the conflict brings back the logic of deterrence in which Iran’s pursuit of nuclear capability gains renewed justification as the ultimate guarantee of security. Third, the political side of the war is becoming impossible to ignore. In the United States, the November 3, 2026 midterm elections stand as an important test of public opinion on foreign policy and military engagement, while in Israel the 27 October 2026 elections are increasingly tied to debates over leadership, security, and national direction. Whether the war ends before these electoral moments or instead influences them remains uncertain.

What this conflict has revealed most clearly is the limitation of military power in determining political reality. The United States and Israel have demonstrated their capacity to destroy targets and project power within this conflict, yet the war has also shown that destruction does not translate into control, nor does it guarantee favorable outcomes. Analysts increasingly point to the gap between tactical success and strategic ambiguity, where escalation produces no clear victory and no stable resolution. As scholars such as Stephen Walt have argued, the United States remains powerful, but its current policies risk weakening that power over time. In this environment, battlefield success is no longer enough to secure political outcomes, and the absence of a clear strategy continues to leave the conflict without a decisive direction.

In the end, the war appears to pause, but nothing truly ends. The Strait of Hormuz briefly reopened only to be closed again hours later. Oil prices fall, markets rise, and relief spreads across financial centers, yet these movements remain reactions, not resolutions. A ceasefire stretches across Iran and Lebanon, but it carries no clear victory, no decisive achievement, and no lasting settlement, only the quiet admission that force has reached its limits. The world has faced an energy shock on a scale not seen since the 1970s, and recovery will take years. What remains is a deeper uncertainty, because the conflict has not resolved the tensions that produced it, it has only exposed them. Power has proven capable of disruption, but not resolution, and stability, once broken, does not return with the same speed as markets. The war may pause, the strait may open and close, and the numbers may recover, but the future remains unsettled, and for now, no one truly knows what tomorrow will bring.

Thank you.

Written by Christopher Makwaia
Tel: +255 789 242 396


— The writer, is a University of West London graduate (formerly Thames Valley University) and an expert in Management, Leadership, International Business, Foreign Affairs, Global Marketing, Diplomacy, International Relations, Conflict Resolution, Negotiations, Security, Arms Control, Political Scientist, and a self-taught Computer Programmer and Web Developer.


Tume ya Madini kwa ushirikiano wa Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) pamoja na Taasisi ya kuendeleza Uchimbaji Mdogo (FADev) wameendelea kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo katika Mkoa wa Morogoro ikiwa ni Mkakati wa Serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo Mradi unaofadhiliwa na UNDP

Akizungumza na Wachimbaji wa madini ujenzi katika Mkoa wa Morogoro Afisa Program kutoka FADev Bi. Rehema Mkuli amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga wachimbaji wadogo wanaojihusisha na madini ya ujenzi na viwanda, hususani madini ya kokoto kwa lengo la kuboresha uelewa wao wa kitaalamu na kuhamasisha mbinu salama na zenye tija katika shughuli za uchimbaji.

Pia, Bi Rehema amesema wachimbaji hao wanajifunza juu ya mbinu za Msingi za Uchoraji wa Ramani za Kijiolojia (Basic Geological Mapping), Usanifu salama na bora wa mashimo (Safe and Efficient Pit Design)

Aidha, kwa upande wa wakufunzi kutoka ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro Mjiolojia Asifiwe Waksoni Ngala amewalezea wachimbaji juu ya Uchoraji wa ramani za kijiolojia, na kuwataka wachimbaji kujifunza zaidi juu ya utambuzi wa aina mbalimbali za miamba na kuelewa madini yanayopatikana ndani yake.

Ujuzi huo unasaidia kuongeza ufanisi katika utambuzi wa rasilimali, kupunguza uchimbaji wa kubahatisha, na kuongeza tija katika shughuli za uchimbaji.

Mafunzo haya yamelengwa kufanyika katika mikoa minne kati ya mikoa nane iliyofanyiwa utafiti wa Madini ya Maendeleo (Development Minerals). Mikoa hiyo ni Singida, Dodoma, Morogoro na Tanga.











Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) akipeana mkono wa shukrani na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (kushoto) wakipongezana na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.
Muonekano wa Trekta iliyotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.

Viongozi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale wakipeana vifaa kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri hiyo.

Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena akizungumza kwenye halfa hiyo ya makabidhiano ya trekta kwa halmashauri ya Nyang’wale

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (Katikati) na kulia kwake ni Senkondo Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena wakiwa kwenye utiaji wa saini katika halfa ya makabidhiano ya trekta kwa ajli ya kusomba taka na ufanyaji wa usafi kwenye halmashauri hiyo

Wafanyakazi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale wakiwa kwenye picha ya pamoja
*


Mgodi wa Barrick Bulyanhulu umeendelea kutekeleza sera yake ya mkakati endelevu wa kusaidia jamii baada ya kukabidhi trekta ya kusomba taka yenye thamani ya shilingi milioni 66 pamoja na vifaa vya kufanyia usafi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale kupitia fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) katika juhudi zake za kutunza mazingira nchini.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano ya trekta hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya Nyang'wale , Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, John Isack alisema msaada huo umekuja kwa wakati katika juhudi za kulinda na kutunza mazingira kwa maslahi ya wakazi wa wilaya hiyo na vitongoji vyake.

“Tunashukuru Barrick Bulyanhulu kwa msaada huu wa trekta , tunaamini sasa hali ya usafi katika Wilaya yetu itakuwa nzuri kwa kiasi kikubwa kwani hii ni trekta ya pili wametupatia, matarajio yetu ni kuongeza kasi ya kuondoa taka kutoka hapo awali ya kutoa mara mbili kwa wiki, awali tulikuwa tunazoa taka katika siku za Alhamisi na Jumatatu hivyo tutaongeza siku pia tunatarajia kuongeza huduma kwa maeneo ya miji inayokuwa kwa kasi kibiashara kama vile Bosolwa, Nyijundu, Bukwimba na maeneo ya migodini",alisema.

Isack aliongeza kuwa kampuni ya Barrick Bulyanhulu kupitia uwekezaji wake imefanikisha miradi mingi ya kijamii na utunzaji wa mazingira wilayani humo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi.

“Leo tumepokea Trekta ambalo limenunuliwa na kampuni ya Barrick Bulyanhulu kwa gharama ya Shilingi Milioni 66 , Trekta hili ni maalum kwa kazi ya kuzoa uchafu na kupeleka dampo kwa kweli ni msaada mkubwa kwa wilaya yetu kwani kwa miaka mingi sana tumekuwa na changamoto juu ya uzoaji wa taka katika mitaa yetu ukichukulia kwamba mji wetu unakua kwa kasi na kupelekea uzalishaji wa taka kuongezeka kwa kasi, na ni matarajio yangu sasa mazingira ya Wilaya yetu yatakuwa safi, nichukue fursa hii kuwaomba wananchi kufanya usafi kila siku kwani tayari kwa sasa tunalo trekta ambalo litakuwa linasomba taka mara kwa mara”, alisema.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo alitoa shukrani kwa viongozi wa serikali na wananchi kwa kuwa na uhusiano mzuri na Kampuni hiyo na kuongeza kuwa msaada wa trekta lililokabidhiwa ni kwa ajili ya kufanya usafi na utunzaji wa mazingira.

“Niwaombe ndugu zangu usafi ni jukumu letu sote,trekta hili tulitunze ili liweze kuboresha mazingira yetu ipasavyo ,milioni 66 ni pesa nyingi hivyo naamini tutakuwa tumefungua njia ya kuboresha mazingira ya usafi wilayani Nyang’hwale, haswa ikizingatia kampuni ya Barrick Bulyanhulu ni wadau wakubwa wa utunzaji wa mazingira”, alisisitiza Zuwena.







Top News