RAIS  mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) miaka 18 iliyopita.

Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika.

Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo.

Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki jijini Dar es salaam.

Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.

Dkt. Kikwete alimpongeza Catherine kwa kutimiza ndoto yake ya kusomea udaktari, jambo ambalo aliahidi kulifanya alipokuwa mtoto. Alisema amefurahishwa kumuona akiwa mwenye afya njema na akijiandaa kulitumikia taifa kupitia taaluma ya tiba.

Kwa upande wake, Catherine alisema anatamani kuwa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto kama aliyowahi kupitia yeye mwenyewe, akieleza kuwa hiyo itakuwa ni moja ya njia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha na afya njema.


Na Seif Mangwangi, Michuzi TV, Karatu

SERIKALI imesema itaendelea kuwalinda wawekezaji wa ndani pamoja na kuunga mkono uwekezaji wowote unaofanywa na wawekezaji hao kwa lengo la kutoa huduma za kijamii.

Hayo yameelezwa leo 29 Mei 2026 na Mkuu wa Wilaya ya Karatu Lameck Karanga katika hafla ya uzinduzi wa kituo kipya ya mafuta cha Orxy kitakachokuwa kikiendeshwa chini ya kampuni ya halyaz.

DC Karanga amesema ujenzi wa kituo hicho cha mafuta ni muendelezo wa maono ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuhakikisha wawekezaji wa ndani wanajengewa mazingira mazuri Ili waweze kufanya biashara.

Amesema Karatu ndio lango kuu la utalii hivyo ujio wa kituo hicho kutasaidia wasafirishaji kupata nishati ya mafuta kwa urahisi na uhakika kwa kuwa bidhaa za kampuni hiyo zinaaminika katika ukanda wa Afrika na duniani kote.

"Kwa niaba ya Wilaya niwapongeze sana kwa uwekezaji huu, mbali ya kutuletea kituo bora lakini mmeanza na kutengeneza mazingira hasa ya bustani nzuri hapo mbele ya kituo chenu, hii inaonyesha ni namna gani mmekuja Karatu Kwa faida," amesema na kuongeza:

"Orxy wameonyesha usafi wa mazingira nje ya kituo cha mafuta na niwaombe watu wa Benki na wenyewe waige mfano huu ni utalii mzuri na kuonyesha wilaya ya karatu ni safi na kuwa na mazingira mazuri," amesema.

Aidha DC Karanga amewataka wananchi wa mji wa Karatu kuiga mfano wa kampuni ya Halyaz kufungua taasisi kama hizo Ili kusaidia jamii kupata ajira lakini pia Serikali kupata kodi. 

Mkurugenzi wa kampuni ya Halyaz inayoendesha kituo hicho cha mafuta cha Orxy Karatu, Ally Abdulrazak amesema ujenzi wa kituo hicho ni matokeo ya maono kwamba karatu inastahili huduma bora za nishati.

Amesema aliamua kuingia ubia na kampuni ya Orxy kufungua kituo hicho cha mafuta kwa kuwa ndio kampuni ambayo imekuwa ikitoa  mafuta safi na salama kwa magari aina tofauti tofauti.

Abdulrazak amesema wateja watakaofika kupata huduma katika kituo hicho watapata huduma zenye ubora wa kimataifa kwa kuwa Wafanyakazi wake wanaujuzi wa hali ya juu lakini pia huduma zote zinaendeshwa kwa kuzingatia ubora.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Orxy Tanzania, Meneja wa fedha wa kampuni hiyo, Greyson Francis amesema uzinduzi wa kituo hicho cha mafuta cha Orxy Karatu ni sehemu ya ndoto za kampuni hiyo kuendelea kupanua huduma zake Kwa jamii.

Amesema kampuni ya Orxy imesambaa katika nchi 19 barani Afrika na hapa nchini imeshasambaa mikoa yote na hivi karibu itazindua vituo viwili vya mafuta Jijini Dar es Salaam.



 

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith  Kapinga (Mb), ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kushirikiana kikamilifu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Taasisi nyingine husika katika kushughulikia na kuondoa kero zote zinazosababishwa na mifumo ya utoaji vibali kwa shehena zinazoingia nchini.

Waziri Kapinga ametoa agizo hilo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum alipokutana na Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi na ujumbe wake Mei 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kufuatia kuibuka kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa kuunganisha mfumo wa TANeSW wa TRA na mfumo wa OAS wa TBS na kusababisha usumbufu kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Aidha, Waziri Kapinga amepongeza jitihada zinazoendelea kuchukuliwa baina ya TBS pamoja na TRA katika kuunganisha mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha taratibu na kuongeza ufanisi wa utoaji wa vibali kwa shehena za mizigo inayoingia nchini.

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali imetoa zawadi ya sh. milioni 500 kwa Timu ya Taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kwa kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano hayo na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo (Ijumaa, Mei 29, 2026) ofisini kwake Mlimwa, Dodoma wakati akitoa salamu za pongezi kwa timu hiyo kufuzu hatua ya fainali kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema Rais Samia amewapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wote wa timu kwa mafanikio hayo makubwa ambayo yameendelea kuandika historia mpya katika sekta ya michezo nchini.

“Mheshimiwa Rais amenielekeza nitoe pongezi hizi kwa vijana wetu wa Serengeti Boys kutokana na mafanikio makubwa ya kutinga fainali na kuiwakilisha vema Tanzania katika mashindano hayo,” amesema Dkt. Mwigulu.

Waziri Mkuu amesema Serikali itatuma ndege maalum kwa ajili ya kuwafuata vijana hao watakapomaliza mashindano hayo ili kurejea nchini pamoja na kombe endapo watafanikiwa kutwaa ubingwa. “Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa ndege kwa ajili ya kuwafuata vijana wetu watakapokuwa wamemaliza mashindano hayo na kurejea nao nyumbani,” amesema.

“Tunaamini huu ni mwanzo tu wa pongezi ambazo Mheshimiwa Rais ameanza kuzitoa. Tunaamini kwamba wakirejea na kombe hilo, kutakuwa na sababu zaidi ya kuwapongeza kwa mafanikio hayo makubwa.”

Waziri Mkuu amemwelekeza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Paul Makonda na wadau wanaohusika, waendelee na uratibu wa wa safari kwa watu watakaokwenda kuwaunga mkono vijana wetu.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mwigulu amesema endapo Serengeti Boys watatwaa ubingwa, Serikali itawapatia kila mchezaji kiwanja kimoja katika Mji wa Suluhu New City uliopo mkoani Morogoro ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika kuitangaza Tanzania kupitia michezo.

Waziri Mkuu pia amewahamasisha Watanzania, taasisi, mashirika na wadau mbalimbali wa michezo kuendelea kutoa msaada na motisha kwa timu hiyo kuelekea mchezo wa fainali.

“Shime shime vijana wetu, inawezekana. Tuleteeni kikombe kile, mleteeni Dkt. Samia Suluhu Hassan kikombe, tuleteeni Watanzania ushindi huo. Kwa kiwango mlichokionesha, tunaamini mna uwezo wa kutwaa ubingwa huo,” amesema.

Sambamba na hilo, Waziri Mkuu amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa kinara wa maendeleo ya michezo nchini na kuchochea mafanikio yanayoendelea kupatikana katika sekta hiyo.


-Yasema kwa mara ya kwanza Serikali ilikamata tani 29.52 za aina mpya ya dawa za kulevya aina ya Kratom

-Pia mali zenye thamani ya zaidi ya Sh.bilioni 3.3 zilizohusishwa na makosa ya dawa za kulevya zilitaifishwa.


Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Profesa Palamagamba Kabudi ameta taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2025 ambapo inaonesha namna Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilivyowekeza na kuweka nguvu kubwa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya. 

Akiwasilisha taarifa hiyo leo Mei 29,2029 Bungeni Mjini Dodoma ,Profesa Kabudi amesema uwasilishaji wa taarifa hiyo ni utekelezaji wa Kifungu cha 66 cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Na. 5 ya Mwaka 2015, inayoiagiza Serikali kuandaa na kuwasilisha bungeni taarifa hiyo kila mwaka.

“Lengo ni kuonesha uwajibikaji wa Serikali kwa wananchi kupitia Bunge, pamoja na kutoa tathmini ya utekelezaji wa mikakati ya udhibiti wa dawa hizo kwa mwaka husika.Pia, taarifa hii inatoa nafasi kwa Bunge kutoa ushauri kwa Serikali kuhusu namna bora ya kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya nchini.”

Amefafanua kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, vyombo vya ulinzi na usalama, wadau wa ndani na nje ya nchi pamoja na jamii kwa ujumla, serikali imepata mafanikio makubwa katika kudhibiti biashara na matumizi ya dawa za kulevya.Katika taarifa hiyo Profesa Kabudi amesema mwaka 2025, bangi iliendelea kuwa dawa ya kulevya iliyokamatwa kwa kiwango kikubwa zaidi ambapo jumla ya tani 1,017.26, zilikamatwa. 

Amefafanua hata hivyo, kiasi kilichokamatwa kilipungua kwa asilimia 55.97 ikilinganishwa na mwaka 2024.Hiyo ni kutokana na uteketezaji wa mashamba makubwa ya bangi uliofanyika mwaka 2024 na kuimarika kwa udhibiti ikiwemo utoaji elimu kwa jamii inayojihusisha na kilimo cha bangi kuhusu madhara ya kilimo cha zao hilo.

Ameongeza pia jumla ya tani 26.36 za mirungi zilikamatwa. Kiasi hicho kiliongezeka kwa asilimia 42.88 ikilinganishwa na mwaka 2024. Ongezeko hilo linaashiria kuimarika kwa operesheni za ufuatiliaji na udhibiti hususan katika maeneo ya mipaka na njia zinazotumika kusafirisha dawa hizo.

Kwa upande wa dawa za kulevya za viwandani, amesema Serikali ilifanikiwa kukamata methamphetamine kilogramu 907.18, heroin kilogramu 672.23, cocaine kilogramu 4.89, MDMA gramu 178 na MDA gramu 7.82.

Aidha, kwa mara ya kwanza, mwaka 2025 Serikali ilikamata tani 29.52 za aina mpya ya dawa za kulevya aina ya Kratom itokanayo na mmea unaoitwa Mitrogyna speciosa. “Dawa hii iliingizwa nchini kama mbolea, baada ya uchunguzi ilibainika kuwa ni dawa za kulevya.”

Amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na kazi kubwa iliyofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika kudhibiti mitandao na njia za usafirishaji wa dawa za kulevya kupitia Nchi kavu, anga na majini.

Aidha, Serikali iliendelea kuimarisha ukaguzi katika vituo vya forodha, vyombo vya usafiri, kampuni za usafirishaji vifurushi na kwenye kampuni zinazojihusisha na biashara ya kemikali bashirifu na dawa tiba zenye asili ya kulevya kwa lengo la kudhibiti uchepushwaji. 

“Kupitia ukaguzi huo, jumla ya tani 31.76 na lita 183.500 za kemikali bashirifu pamoja na kilogramu 2.36 na mililita 160 za dawa tiba zenye asili ya kulevya zilikamatwa.”

Kuhusu makosa ya dawa za kulevya, mwaka 2025,amesema  jumla ya mashauri 1,124 yalifunguliwa katika Mahakama mbalimbali nchini. Pamoja na mashauri yaliyokuwa yakiendelea katika Mahakama mbalimbali nchini, mashauri 1,373 yalitolewa hukumu na Jamhuri ilishinda mashauri 1,058.

Aidha mali zenye thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni 3.3 zilizohusishwa na makosa ya dawa za kulevya zilitaifishwa.Pia Serikali iliendelea kutoa huduma za tiba na utengamao kwa watu wenye uraibu wa dawa za kulevya. 

“Mwaka 2025, jumla ya watu 85,425 wenye uraibu wa dawa za kulevya walipata tiba kwenye vitengo vya afya ya akili katika hospitali za rufaa za mikoa na Kanda, kliniki za MAT na nyumba za upataji nafuu nchini.

“Elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya iliendelea kutolewa kwa Umma kupitia kampeni mbalimbali za uelimishaji katika jamii, taasisi za elimu na vyombo vya habari ili kuijengea jamii uelewa, maamuzi sahihi na uwezo wa kujilinda dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya.

“Katika kuimarisha ushirikiano wa kitaifa, kikanda na kimataifa, Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi katika kubadilishana taarifa za kiintelijensia, kujenga uwezo wa kitaasisi pamoja na kuendesha operesheni za pamoja dhidi ya mitandao ya usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.

“Matokeo chanya katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanatokana na dhamira thabiti, maono na uongozi mahiri wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwani chini ya uongozi wake amewekeza kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya Nchini.”

Pia ameipongeza Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama, wataalamu wa afya, wadau katika mapambano na wananchi kwa ushirikiano wao uliosaidia kuyafikia mafanikio aliyoyaeleza.

“Naomba wananchi waendelea kutoa taarifa pale wanapohisi au kushuhudia viashiria vya biashara au matumizi ya dawa za kulevya kwa vyombo husika ili kuifanya nchi yetu kuwa mahali salama na huru dhidi ya matumizi na biashara dawa za kulevya.”








Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji, tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kikao cha kupokea Taarifa ya Sensa ya Wanyamapori iliyofanyika nchi nzima mwaka 2024 – 2025 iliyowasilishwa na Waziri ya Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji kupitia Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), tarehe 29 Mei, 2026 Ikulu Dar es Salaam.






 


Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Serikali imesema imeendelea kupata mafanikio makubwa katika vita dhidi ya dawa za kulevya nchini kutokana na kuimarika kwa ushirikiano wa ndani na nje ya nchi pamoja na uwekezaji mkubwa unaofanywa katika sekta ya usalama, intelijensia na udhibiti wa biashara haramu ya dawa hizo.

Hayo yameelezwa leo na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, katika Mkutano na waandishi wa habari Bungeni Dodoma wakati akiwasilisha Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya nchini kwa mwaka 2025.

Prof. Kabudi amesema Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa kitaifa, kikanda na kimataifa katika kubadilishana taarifa za kiintelijensia, kuendesha operesheni maalum za pamoja pamoja na kujenga uwezo wa taasisi zinazoshughulikia mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Amesema hatua hizo zimeendelea kusaidia kuvunja mitandao ya usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya ambayo imekuwa ikihatarisha usalama wa jamii, afya za wananchi na nguvu kazi ya taifa.

Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mafanikio hayo yanatokana na dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuimarisha mifumo ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kuongeza uwekezaji katika vyombo vya ulinzi, usalama na taasisi za udhibiti.

Amesema Serikali imeendelea kuiwezesha Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na taasisi nyingine zinazoshiriki katika operesheni za kudhibiti biashara hiyo haramu ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Matokeo haya yanaonyesha namna ambavyo ushirikiano wa pamoja kati ya Serikali, vyombo vya dola, wataalamu wa afya, wadau wa maendeleo na wananchi unavyoendelea kuzaa matunda katika vita dhidi ya dawa za kulevya,” amesema Prof. Kabudi.

Aidha, amesisitiza kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya hayawezi kufanikiwa bila ushiriki wa wananchi, huku akitoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa kwa mamlaka husika kuhusu vitendo vinavyohusiana na usambazaji, matumizi au biashara ya dawa za kulevya.

Ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mikakati ya kinga, elimu kwa umma, tiba na operesheni maalum ili kuhakikisha taifa linaendelea kuwa salama dhidi ya athari za dawa za kulevya ambazo zimekuwa zikichangia mmomonyoko wa maadili, ongezeko la vitendo vya uhalifu pamoja na kuathiri maendeleo ya vijana na jamii kwa ujumla.

Prof. Kabudi pia amewapongeza wananchi kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa vyombo vya usalama na taasisi zinazopambana na dawa za kulevya, akieleza kuwa mchango wa jamii ni msingi muhimu wa ushindi katika mapambano hayo.

Kwa upande wa Kamishina Jenerali Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema tatizo la dawa za kulevya ni suala  mtambuka linalohusisha mitandao ya kihalifu iliyopo nchi mbalimballi Duniani, hivyo mapambano dhidi ya tatizo hilo yanahitaj ushirikiano na nguvu za pampja kuanzia ngazi ya Kitaifa, kikanfa bna Kimataifa.




MECHI ya mkondo wa pili wa kugombania kucheza ligi kuu za Ufaransa yaani LIGUE 1 ipo hapa. Ni Nice vs Saint Etienne ambapo kila timu inahitaji kushinda leo kucheza ligi kuu msimu ujao. Je nani kushinda leo?

Hii ni mechi ambayo ina presha ndani yake kwasababu kila mmoja ana malengo sawa na mwenzake. Nice wao walikuwa ligi kuu na kutokana na kutokufanya vizuri imewabidi sasa wapambane kutafuta nafasi nyingine ili waweze kubaki ligi kuu.

Huku kwa upande wa Saint Etienne wao kutokana na kutofshika nafasi ya kwanza wlaipokuwa kule Ligue 2 sasa wanalazimika wapambane kwa hali na mali ili waweze kupata nafasi ya kucheza kwenye ligi Kuu ya Ufaransa yaani LIGUE 1.

Mchezo wa kwanza ulimalizika kwa sare tasa ya 0-0, matokeo ambayo yameacha kila kitu wazi kabisa kabla ya pambano hili la mwisho. Hakuna timu iliyoweza kupata faida, hakuna aliyethibitisha ubora wake, na sasa kila kitu kinategemea dakika 90 zijazo. Hii si mechi ya kawaida; ni mchezo wa kuamua hatma, mchezo ambao unaweza kubadilisha historia ya klabu ndani ya usiku mmoja. Jisajili hapa na Meridianbet

Piga pesa leo kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Nice wakiwa nyumbani, wataingia uwanjani wakijua kuwa presha ipo mabegani mwao. Mashabiki wanatarajia ushindi, viongozi wa klabu wanahitaji kuona timu ikirudi au kubaki kwenye kiwango cha juu, na wachezaji wanajua kuwa nafasi kama hizi haziji mara nyingi.

Saint-Étienne nao wanaingia katika mchezo huu wakiwa na kiu kubwa ya kurejea kwenye hadhi yao ya zamani. Klabu hii ina historia kubwa ndani ya soka la Ufaransa, na mashabiki wake bado wanaamini kuwa nafasi yao halisi ni Ligue 1. Sare ya bila kufungana kwenye mchezo wa kwanza imewapa matumaini makubwa, hasa wakiamini kuwa wanaweza kufanya jambo maalum ugenini.

Kila kosa linaweza kuwa mwisho wa ndoto za msimu mzima. Mabeki hawataki kufanya makosa, washambuliaji wanabeba matumaini ya maelfu ya mashabiki, na makocha wanapaswa kufanya maamuzi sahihi ndani ya dakika chache.

Ikumbukwe kuwa wa mpira wa miguu ni dakika 90 hivyo lolote linaweza kutokea na yoyote yule anaweza akashinda. Mchezo wa mwanza uliisha bila kuwa na mbabe na huu wa pili kila timu itaingia kwaajili ya ushindi pekee. Je nani kucheza ligue 1?. Bashiri mechi hii sasa.

 

Mafunzo Elekezi kwa Watumishi Wapya wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) yameanza leo, Mei 28, 2026, ikiwa ni hatua muhimu ya kuandaa wataalamu wa mamlaka hiyo kwa kuzingatia misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali. Watumishi wapya 29 wanashiriki mafunzo haya .yanayotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bi. Anjela Tulumamanywa, alisema kuwa mafunzo elekezi ni nyenzo muhimu kwa wafanyakazi wapya kujifunza misingi ya utumishi wa umma kupitia miongozo mbalimbali ya serikali. 


"Tunatarajia kuwa baada ya mafunzo haya, mtakuwa watumishi wa umma wanaofuata maadili ya utumishi wa umma, wakiwasiliana kwa ufanisi na kuheshimu usiri wa taarifa na nyaraka za serikali, huku pia wakielewa haki na wajibu wao," amesema.

Kwa upande wake, Bi. Zena Hussein ambaye ni Meneja wa kituo cha mafunzo kwa njia ya Mtandao  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, amesema kuwa mafunzo haya ni muhimu na lazima kwa watumishi wapya katika utumishi wa umma. 
"Mafunzo haya yanalenga kuimarisha uelewa wa misingi ya utumishi wa umma na miongozo ya serikali, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kwa kuzingatia maadili ya kazi," amesisitiza.

Aidha amesema kuwa Mafunzo haya yanatarajiwa kuongeza uelewa wa watumishi wapya kuhusu misingi ya utumishi wa umma na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ndani ya TISEZA. Vilevile, mchakato huo unazingatia taratibu na miongozo ya serikali, kwa lengo la kuhakikisha majukumu yanatekelezwa kwa uwajibikaji, uadilifu, na ufanisi.
Mafunzo haya ni utekelezaji waraka wa Utumishi Na. 5 wa mwaka 2011, uno wataka waajiri kuhakikisha kuwa watumishi wapya wanapatiwa mafunzo elekezi ndani ya miezi sita tangu kuajiriwa,







 

Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana na kufunguliwa kwa udahili wa wanafunzi katika mwaka wa masomo 2026/2027.




Baadhi ya matukio katika picha wakati wa kutangazwa kwa dirisha la udahili mwaka wa masomo 2026/2027.

Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limefungua dirisha la Udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada katika kozi zote zinazosimamiwa na NACTVET.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Katibu Mtendaji wa NACTVET Dkt.Mwajuma Lingwanda amesema dirisha Hilo limefunguliwa rasmi Mei 28 2026.

Amesema maombi ya udahili kwa kozi za Afya na Sayansi Shirikishi -Tanzania Bara, yatafanyika kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) unaopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Dkt.Mwajuma amesema udahili umeanza Mei 28 hadi Julai 10 2026 kwa awamu ya kwanza.

Aidha amesema maombi ya kozi zisizo za Afya na Sayansi Shirikishi, na kozi za Afya na Sayansi Shirikishi zitolewazo katika vyuo vilivyoko Zanzibar yatumwe moja kwa moja kwenye vyuo husika kuanzia Mei 28 Mei hadi Julai 10 mwaka Hui kwa awamu ya kwanza.

Hata hivyo Baraza limetoa orodha ya kozi zote na vyuo vinavyotoa kozi hizo, inapatikana katika Kitabu cha Mwongozo wa Udahili kwa Mwaka wa Masomo 2026/2027 kinachopatikana katika tovuti ya Baraza (www.nactvet.go.tz).

Baraza hilo limesema kila mwombaji kuhusika mwenyewe katika zoezi zima la kuomba kudahiliwa, kuandika taarifa zake kwa usahihi na umakini, na kutunza kumbukumbu atakazopatiwa na Baraza kupitia namba yake ya simu, bila kumpatia mtu mwingine yeyote ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza katika zoezi zima la maombi ya kujiunga na kozi katika vyuo mbalimbali.

Mambo ya Kuzingatia kwa Wanaoomba Kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (Central Admission System – CAS) ni Mwombaji anaweza kuomba chuo zaidi ya kimoja na Kuchaguliwa katika chuo alichoomba kutategemea ushindani utakaokuwepo katika chuo hicho.

Aidha amesema mwombaji akishachaguliwa, atapokea ujumbe kutoka NACTVET kupitia namba yake ya simu aliyoweka kwenye mfumo wakati wa kufanya maombi ujumbe utamjulisha kuwa amechaguliwa kujiunga na chuo husika na utakuwa na msimbo (code) ambao atatakiwa kuutunza na kuuwasilisha kwa chuo alichochaguliwa siku atakapowasili chuoni kwa ajili ya kuanza masomo.

Dkt. Mwajuma amesema baada ya kuwasilisha msimbo huo chuoni, atasajiliwa na chuo, kisha atapokea ujumbe kutoka NACTVET ukimweleza kuwa amesajiliwa. Baada ya kusajiliwa, mwanafunzi aingie katika tovuti ya NACTVET (www.nactvet.go.tz), kisha ajiridhishe kuwa amesajiliwa kwa kuhakiki taarifa zake kwa kubonyeza “link” inayosomeka “student’s information verification”.


*Aahidi Kusimama Kidete Iwe Mamlaka

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba amezindua mfumo mpya wa kidijitali wa kufuatilia uchafuzi wa mazingira wa Baraza la Taifa la Hufadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

Amefanya uzinduzi huo leo Mei 28,2019 jijini Dar es Salaam alipokuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwa baraza hilo mwaka 1986.

Maadhimisho hayo ambayo yaliambatana na maonesho ya masuala ya mazingira yamewashirikisha wageni mbalimbali wa serikali na wadau wa sekta binafsi wanaojihusisha na uhifadhi wa mazingira.

Dkt Mwigulu alianza kwa kuipongeza NEMC kwa kazi kubwa ambayo wameifanya kwa miaka yake 40 ya kuhifadhi mazingira akisisitiza kuwa bila mazingira safi binadamu na viumbe wengine wako hatarini kutoweka.

Amesema kazi ya kupambana na waharibifu wa mazingira siyo nyepesi na ndiyo sababu yeye binafsi atasimama kidete kuhakikisha NEMC inakuwa mamlaka ili ipate nguvu ya kukabiliana na wahalibifu wa mazingira.

Aidha, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mwanamazingira namba moja hali ambayo ilifanya atunukiwe tuzo kama kinara wa mazingira duniani kwa kupigia chapuo uhifadhi wa mazingira nchini.

“Mwanamazingira namba moja Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amenituma niseme hapa kwamba anatambua mchango wenu na ataendelea kushirikiana nasisi wote kwenye ulinzi wa mazingira, mheshimiwa Rais amekuwa mstari wa mbele kutunza mazingira na ameahidi kuendelea kuwa mstari wa mbele,” amesema Dkt Mwigulu

Amesema ingawa kuna watu wanalichukulia kwa wepesi suala la mazingira lakini tumeanza kuona athari za uhalibifu wa mazingira dhahiri kwenye maeneo mbalimbali nchini.

“Hapo zamani tuliona kama hadithi tu lakini sasa madhara ya kutojali mazingira yameanza kuja kwetu. Hili jambo siyo nadharia na si la kulichukulia kimzaha mzaha hata kidogo na shughuli za binadamu zimeongezeka kwa kasi mno hali ambayo inahatarisha mazingira,” alisema

“Watu wanaamua tu kukata miti ambayo wala wakati mwingine hawana haja nayo baada ya hapo. Mnakata miti mnasababisha jangwa tunakosa maji, mvua hakuna na ushindani wa matumizi ya ardhi unaongezeka kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na za binadamu kwa hiyo lazima tukubali kubadilika hatuwezi kwenda na mtindo ule ule wa maisha,” amesema Waziri Mkuu na kuongeza

“Tusipokubali kubadilika tutalazimishwa na yatakayotokea baadae na kwa kuwa NEMC inatakiwa kuwa mamlaka mimi nitasimama kidete iwe mamlaka, mchakato wake utapita Baraza la kazi sasa huko mimi ndiye Mweyekiti nawaaahidi nitalisimamia NEMC iwe mamlaka,”

Aidha, Dkt Mwigulu amesema Rais Samia ameongeza bajeti ya kilimo zaidi ya mara 5 kuwezesha kilimo cha umwagiliaji ili kuondoa mazoea ya wakulima kufyeka mapori na kuharibu mazingira wanapoongeza mashamba.

“NEMC inahitaji kuongezewa meno ili kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mazingira na miaka 30 ijayo inakadiriwa kuwa watanzania tutafika milioni 100 na zaidi kwa hiyo lazima NEMC iwe na nguvu kukabiliana na ongezeko la shughuli za binadamu zinazohalibu mazingira,” amesema

“Pamoja na mafanikio tuliyoyapata bado kuna kazi kubwa kufanya mambo makubwa kwenye miaka 40 ijayo. NEMC endeleeeni kutoa elimu ya mazingira kuanzia ngazi ya familia watu wajue umuhimu wa kutunza mazingira,” amesema




Top News