Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (Mb), Ridhiwani Kikwete, amezitaka shule za msingi na sekondari kuwa na karakana zitakazokuwa chemchemi za ubunifu kwa vijana, huku akisisitiza kazi zitakazobuniwa zisajiliwe ili wabunifu wanufaike nazo.Ridhiwani amesema usajili huo utawasaidia vijana kumiliki kazi zao na kuzitumia kama fursa za kiuchumi, badala ya watu wengine kuchukua mawazo yao na kujinufaisha huku wabunifu wakibaki bila manufaa.
Amesema hayo akimwakilisha Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Baobab, iliyopo Mapinga, Bagamoyo mkoani Pwani.
Mkurugenzi wa Baobab, Shani Swai, amesema kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi na wanafunzi 3,270 wamehitimu kidato cha nne ambapo asilimia 95 wameendelea na sekondari na vyuo vya ufundi.
Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda .

Alisema mpango huo unaonyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wananchi katika kukabiliana na changamoto za kijamii.

Wahadzabe ni kabila linalopatikana mkabala na ziwa Eyasi pembezoni mwa hifadhi ya Ngorongoro na habari za maisha yao zimehifadhiwa katika makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu Mkoani Arusha.
Pamoja na mabadiliko ya ulimwengu na elimu kutolewa lakini kabila hili bado haliamini katika tohara kwa kijana wa kiume, kwao hiyo ni mwiko wakiamini binadamu anastahili kuwa kama alivyozaliwa.
Sababu kubwa ya kutokutahiriwa ni kuwa ukitahiriwa unapunguza nyama ya binadamu na kuizika wakati binadamu huyo akiwa hai, imani ni kwamba huwezi kata sehemu yoyote ya mwili wa binadamu aliye hai
Vilevile kabila hili linaamini kwamba mwanaume akitahiriwa hupunguza ukubwa na utaalam wa mambo na kufanya mwili wako kuwa na mapungufu hata wakati wa kushiriki tendo la ndoa.
Katika kuhakikisha kwamba mwanaume anakuwa na nguvu za kutosha wakati wa kushiriki tendo la ndoa hulazimika kula mizizi inayopatikana porini , matunda, asali ikiwa fresh na nyama pori ambayo inachomwa au kuchemshwa supu.
Kutokana na kutokutahiriwa Wahadzabe wanaamini kwamba miili yao huwa na nguvu ya kupambana na mnyama yoyote porini na hiyo ndiyo heshima ya mwanaume kamili ambaye hata anapochumbia kutaka kuoa hupimwa kwa uwezo wa kuwinda na kuleta chakula cha familia.
Hii ni sehemu ya maajabu ya maisha makabila wanaunda Ngorongoro Global Geopark ambapo licha ya Wahadzabe kuendelea kuishi katika ukanda huo lakini taarifa zao zinapatikana katika makumbusho ya Urithi Geopark.
Karibu Nyumbani Ngorongoro upate mshangao wa maajabu na uzoefu usiosahaulika.
Na Victor Masangu,Bagamoyo
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais–Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete, amewataka walimu wa shule za msingi na sekondari kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na weledi lengo ikiwa ni kuweza kuzalisha wanafunzi wenye ujuzi na maarifa ambao watalisaidia Taifa katika nyanja mbali mbali.
Ridhiwani ameyabainisha hayo alipokuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Shajar ambayo inamiliki shule ya Baobab iliyopo Wilaya ya Bagamoyo.
Amesema kwamba katika Taifa la Tanzania walimu wa shule za msingi na sekondari wana mchango mkubwa sana hivyo wanapaswa kufanya kazi zao katika misingi imara ambayo itaweza kusaidia kupata wataalamu bora.
Pia Ridhiwani amesema ameridhishwa na ubunifu unaofanywa na wanafunzi wa shule hiyo na kusisitiza kuwa kazi zao wanazozifanya kulindwa na kusajiliwa.
Amesema kwamba uongozi wa Taasisi hiyo wanapaswa kuwa daraja linalowavusha vijana kutoka kwenye vipaji kwenda kwenye uzalishaji, huku wanafunzi wakifundishwa ufundi pamoja na ujasiriamali, usimamizi wa fedha.
Katika maadhimisho hayo, Ridhiwani pia amezindua Baobab Institute of Tanzania (BIT), akisema taasisi hiyo haipaswi kuwa chuo kinachofuata mabadiliko ya dunia pekee, bali iwe taasisi inayotafsiri mahitaji ya Tanzania ya leo na kesho pamoja na Afrika.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Shajar ambayo pia ndio wamiliki wa shule ya Bao Shani Swai,
amebainisha kwamba kwa sasa shule hiyo ina zaidi ya wanafunzi 1,000 na tangu mwaka 2007 hadi 2026, jumla ya wanafunzi wa 4,495 wa kidato cha sita wamehitimu, huku asilimia 98 wakiendelea na elimu ya vyuo vikuu ndani na nje ya nchi.
Shani ameeleza Taasisi hiyo ina miliki kituo cha kulea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, hospitali inayotoa huduma za afya pamoja na shule za awali, msingi, sekondari na ufundi stadi.
Naye Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amewataka Watanzania kushikamana katika kuwalinda watoto na kuhakikisha wanakua katika mazingira ambayo ni rafiki na salama
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga ameipongeza Taasisi hiyo kwa kuweza kushirikiana bega kwa bega na serikali katika nyanja zote ikiwemo suala la kudumisha hali ya ulinzi na usalama na shughuli za kimaendeleo.
Maadhimisho ya kilele cha sherehe za miaka 20 ya Baobab yamehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali,vingozi wa tasisisi wezeshi,vingozi wa dini,wasanii pamoja na wageni wengine kutoka maeneo mbali mbali.











.jpeg)






































