TCB Chief Executive Officer and Managing Director 
Adam Charles Mihayo



By Issa Michuzi


The Tanzania Commercial Bank (TCB) is again footing the bill for the annual gathering of board chairpersons and chief executives from public bodies, signing on as principal sponsor for the third year in a row.


The event, hosted by the Office of the Treasury Registrar, will take place in Arusha from 28 to 30 September.


TCB Chief Executive Officer and Managing Director Adam Charles Mihayo confirmed the support today, 9 September 2026, at a breakfast briefing with news editors at the Hyatt Kilimanjaro in Dar es Salaam. 


The bank, he said, is “honoured to participate in the important gathering and proud to serve as its principal sponsor for the third consecutive time.” 


He added, “We greatly appreciate the honour extended to us by the Office of the Treasury Registrar to participate in this important meeting.”


For Mihayo, the forum is no mere ceremony. Over three days, leaders from public institutions and corporations will swap experiences, audit their own performance, and hunt for workable ways to improve service delivery and deepen their contribution to national development.


He also pulled the media into that mission. 


When coverage is steady and clear, he said, Tanzanians can track the work of the Treasury Registrar and the bodies it oversees. “Better public understanding keeps those institutions moving toward greater transparency and accountability”, he added.


TCB’s lineage reaches back to 1925, when it opened as the Tanganyika Post Office Savings Bank. 


Today it is a full commercial bank, the government holding the majority stake, with other public institutions owning the rest. 


The bank offers retail, SME, corporate, treasury, and digital banking, and says its focus remains on innovative financial solutions and wider financial inclusion.


Renewing the sponsorship, the TCB chief adds, is one part of its broader promise to back efforts that strengthen public institutions and push Tanzania’s development agenda forward.


By Issa Michuzi

 More than 700 board chairpersons and chief executives from state institutions and corporations will gather in Arusha from 28 to 30 September to review their performance and strengthen their role in delivering Tanzania Development Vision 2050.

 

Acting Treasury Registrar Ms Lightness Mauki (pictured) outlined the agenda today, 9 September 2026, during a breakfast briefing with news editors at the Hyatt Kilimanjaro hotel in Dar es Salaam.

 

The briefing highlighted the growing role of public institutions in advancing national development and set the tone for the upcoming high-level forum.

 

She said the Arusha gathering will be guided by a theme centred on three priorities: high performance, inclusiveness and resilience.

 

The goal is to build public institutions capable of driving Vision 2050 while remaining responsive to changing circumstances.

 

Beyond translating the Vision into day-to-day action, Ms Mauki said the forum will give leaders under the Treasury Registrar’s oversight an opportunity to exchange lessons and make better use of existing experience.

 

She noted that the gathering is going to be more than a routine meeting, but a platform to align experience, resources, policy papers and government directives with faster and more efficient delivery.

 

Ms Mauki, who also serves as the Treasury Registrar’s Director of Planning, Research and Business Development, said government investment in the institutions has risen by 75 per cent in three years to Sh92 trillion.

 

Revenue performance has also improved, she said.

 

“In the financial year ending 2026, the entities remitted Sh1.307 trillion, up seven per cent from Sh1.208 trillion collected in the previous year,” she said.

 

She described the figure as the highest amount collected since the Office of the Treasury Registrar was established.

 

The Office of the Treasury Registrar of Tanzania was established on 13 November 1959 through Treasury Registrar Ordinance No. 35 of 1959 to acquire, hold and manage government investments. The legislation is now known as the Treasury Registrar (Powers and Functions) Act, Chapter 370.

 

“Numbers like these show that our institutions are ready to play their full part in Tanzania Development Vision 2050, whose implementation formally began in July,” she said.

 

“As leaders in government and public institutions, we have a duty to translate our responsibilities into practical action and deliver the expected results,” she said.

 

“I encourage Tanzanians to follow our activities and the discussions that will take place during the meeting of board chairpersons and chief executives,” she said.

 

“Above all, I invite everyone to join us in celebrating the achievements recorded so far, while renewing our commitment to discharging our responsibilities efficiently, patriotically and with dedication,” Ms Mauki said.


Na Karama Kenyunko Michuzi Tv


SHAHIDI wa tano wa utetezi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, John Heche, ameieleza Mahakama namna matukio mbalimbali aliyodai kuyashuhudia katika chaguzi yalivyosababisha chama hicho kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election” (Bila Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi).

Heche, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, ametoa ushahidi huo leo Septemba 9, 2026, katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, mbele ya Jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dustun Ndunguru.

Akijibu maswali ya Lissu, Heche amesema Desemba 2, 2024, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikaa na kujadili masuala mbalimbali yaliyohusu chaguzi, ikiwemo ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, kuenguliwa kwa wagombea wa chama hicho na matukio ya mauaji yaliyohusishwa na chaguzi.

Heche amesema kutokana na hali hiyo, hususani uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na chaguzi nyingine alizoshiriki na kuzishuhudia, chama hicho kiliona kuwa hazikuwa chaguzi za kawaida bali “uchafuzi”, jambo lililopelekea Kamati Kuu chini ya Mwenyekiti wa wakati huo, Freeman Mbowe, kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election.”

Amesema mabadiliko yaliyokuwa yakihitajika yalihusisha marekebisho makubwa ya Katiba na sheria, pamoja na kuondoa madaraka makubwa ya Rais katika uundaji wa Tume ya Uchaguzi na uteuzi wa watendaji wa uchaguzi.

“Kamati Kuu iliazimia mabadiliko makubwa ya kikatiba na ya kisheria,” amesema Heche.

Amedai chama hicho kilitaka Tume Huru ya Uchaguzi ambayo ingekuwa huru na isiyo na upendeleo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mwingine.

Heche amesema Aprili 3, 2025, CHADEMA ilikutana na watia nia waliokuwa wakitarajia kugombea kupitia chama hicho katika makao makuu ya chama, Mikocheni, Dar es Salaam, na kuwaeleza sababu za kuendelea na msimamo wa “No Reforms, No Election” uliokuwa umechukuliwa tangu Desemba 2024.

Akieleza matukio aliyodai kuyashuhudia katika chaguzi mbalimbali, Heche amesema ameshiriki chaguzi akiwa mgombea na kiongozi wa chama, ikiwemo uchaguzi wa Arumeru, Busanda, Igunga, Kinondoni pamoja na chaguzi za mwaka 2015 na 2020.

Amedai chaguzi hizo ziliambatana na matukio mbalimbali, ikiwemo mauaji ya wanachama, kuenguliwa kwa wagombea wa CHADEMA, kunyimwa fomu za viapo vya mawakala, mawakala kuondolewa vituoni wakati zoezi likiendelea, polisi kupiga watu na kuvuruga mikutano ya kampeni ya chama hicho.

Amedai pia kuwa wagombea wa chama hicho walinyimwa fomu za matokeo, huku akidai kulikuwa na kura za uongo kuingizwa na baadhi ya watu kubeba vibegi vya kura feki.

Akijibu maswali ya Lissu kuhusu matukio ya mauaji aliyoyakumbuka katika chaguzi hizo, Heche ameeleza tukio la uchaguzi wa mwaka 2015 katika Jimbo la Busanda, ambapo amesema kiongozi wa CHADEMA na mgombea wa ubunge, Alphonce Mawazo, aliuawa.

Amesema Mawazo alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita na Mjumbe wa Baraza Kuu la chama hicho.

Alipoulizwa kama kuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya waliohusika na mauaji ya Mawazo, Heche amesema hakumbuki vizuri mwisho wa kesi hiyo hivyo hawezi kueleza kwa usahihi.

Katika tukio lingine, Heche amesema wakati wa uchaguzi wa mwaka 2020, alipokuwa akifunga kampeni Nyamongo, Kata ya Matongo, alivamiwa na kushambuliwa kwa risasi, ambapo watu wawili waliuawa na wengine kujeruhiwa.

Lissu pia amemuuliza Heche kuhusu tukio jingine la mauaji katika jimbo lake.

Heche amesema polisi walimuua mdogo wake, Suguta Heche, ambaye alidai alikuwa amefungwa pingu mikono yote na kuchomwa kisu.

Alipoulizwa kuhusu hatua zilizochukuliwa, Heche amesema Kamanda wa Polisi wa wakati huo alitoa taarifa kuthibitisha kuwa Suguta aliuawa na polisi na kwamba hatua zingechukuliwa dhidi ya waliohusika.

Hata hivyo, amesema polisi huyo aliachiwa na mpaka sasa ni mtumishi wa Jeshi la Polisi.

Ushahidi huo umetolewa wakati Heche akiendelea kujibu maswali ya Lissu katika hatua ya utetezi wa kesi hiyo.

Shauri hilo limeahirishwa hadi kesho, ambapo Heche ataendelea kutoa ushahidi wake, huku Majaji wakitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu mashahidi wengine waliowekewa pingamizi.

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba nchini TMDA imefanikiwa kunasa shehena mbili kubwa za dawa na vifaa tiba zisizo sajiliwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere JNIA Terminal 3. Thamani ya jumla ya mizigo hiyo inakadiriwa kufikia zaidi ya shilingi milioni 360.Akizungumza na vyombo vya habari leo, Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo amesema shehena ya kwanza ilikamatwa tarehe 7 Septemba 2026 wakati wakaguzi wao wakifanya ukaguzi wa kawaida kupitia mfumo wao wa udhibiti.


"Wakaguzi wetu wamefanikiwa kukamata mabegi 20 yaliyokuja kutoka India. Yalikuwa na dawa nyingi sana zenye thamani ya shilingi milioni 310. Hapakuwa na nguo wala vyakula. Tatizo kubwa ni kwamba dawa hizo zote hazikuwa na usajili wala vibali vyovyote vya TMDA," amesema Dkt. Fimbo.
Dkt. Fimbo ameongeza kuwa tarehe 9 Septemba 2026, wamefanikiwa tena kunasa shehena nyingine yenye thamani ya shilingi milioni 50. Ndani ya shehena hiyo kulikuwa na sindano za lignocaine, bupivacaine, adrenaline na vitamini.

Pia kulikuwa na dawa za kutibu magonjwa ya saratani, kifafa, shinikizo la damu na kisukari. Miongoni mwa dawa hizo ni OZEMPIC na GLP-1 ambazo ni sindano maarufu sasa hivi mitandaoni zinazotumika kupunguza unene. Shehena hiyo pia ilikuwa na vifaa tiba vya meno bandia.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, dawa zisizosajiliwa ni hatari kubwa kwa afya ya wananchi kwani ubora, usalama na ufanisi wake haujathibitishwa na TMDA. Matumizi yake yanaweza kusababisha madhara kama kuchelewa kupona, usugu wa dawa, ulemavu na hata vifo.

Dkt. Fimbo amebainisha kuwa mpaka sasa watu watano wameshakamatwa na vyombo vya usalama na bado wanaendelea na uchunguzi zaidi. Amesisitiza kuwa dawa zote zilizokamatwa zitaenda kuteketezwa mara tu uchunguzi utakapokamilika.

TMDA imetoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuzingatia sheria na taratibu za uingizaji na usambazaji wa dawa na vifaa tiba nchini. Amesema ni marufuku kuingiza bidhaa za tiba bila kupata kibali cha TMDA na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahusika wote.




 

Dar es Salaam, Septemba 8, 2026  

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kimeanzisha programu mbili mpya za Shahada katika Kampasi ya Tabora na kuongeza programu ya Shahada ya Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Kampasi ya Dar es Salaam kwa Mwaka wa Masomo 2026/2027.

Kampasi ya Tabora imeanza kutoa Shahada ya Usimamizi wa Kumbukumbu, Nyaraka na Taarifa (Bachelor Degree in Records, Archives and Information Management) pamoja na Shahada ya Uhazili na Utawala (Bachelor Degree in Secretarial Duties and Administration). Hatua hiyo inaifanya Kampasi ya Tabora kuanza kutoa elimu ya ngazi ya Shahada katika maeneo hayo kwa mwaka huu wa masomo.

Kwa upande wa Dar es Salaam, TPSC imeongeza Shahada ya Usimamizi wa Rasilimali Watu (Bachelor Degree in Human Resource Management) katika programu zinazotolewa na Kampasi hiyo. Programu hiyo inalenga eneo la usimamizi wa rasilimali watu, ambalo ni miongoni mwa maeneo muhimu katika uendeshaji wa taasisi za umma na binafsi.

Kwa mujibu wa TPSC, mabadiliko hayo yanaendana na jukumu la Chuo la kutoa elimu na mafunzo yanayokidhi mahitaji ya Utumishi wa Umma pamoja na mabadiliko ya mazingira ya kazi na mahitaji ya wataalamu katika taasisi mbalimbali.

Akizungumzia kuanzishwa kwa programu hizo, Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho, amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Chuo kuongeza programu za elimu ya juu katika maeneo yanayohusiana na mahitaji ya kitaaluma na kiutendaji.

“Kuanzishwa kwa programu hizi za Shahada ni hatua muhimu katika juhudi za TPSC za kupanua fursa za elimu ya juu kwa Watanzania. Tunataka kuhakikisha kwamba wananchi wanapata fursa ya kujenga taaluma katika maeneo ambayo ni muhimu kwa ufanisi wa taasisi na maendeleo ya Utumishi wa Umma,” amesema Dkt. Mabonesho.

Kuongezeka kwa programu hizo kunatoa nafasi kwa wanafunzi na watumishi wanaotaka kuendeleza elimu yao katika fani za usimamizi wa rasilimali watu, usimamizi wa kumbukumbu na taarifa, pamoja na uhazili na utawala.

Hatua hiyo pia inaongeza idadi na mchanganuo wa programu za elimu ya juu zinazotolewa na TPSC katika kampasi zake, huku ikizingatia maeneo ya kitaaluma yanayohusiana moja kwa moja na utendaji wa taasisi na utoaji wa huduma.

Programu hizo zinapatikana katika Mwaka wa Masomo 2026/2027, ambapo TPSC inaendelea na mchakato wa udahili kwa waombaji wanaokidhi vigezo vilivyowekwa.

 







DODOMA, TANZANIA — September 8, 2026.

Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.

Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.

The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.

After the group discussions, the students came together for presentations.

Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.

Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.

It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.

Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.

Na Mwandishi wetu, Mirerani

MWENYEKITI wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara, (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi amewaasa wanasiasa wenye agenda nyepesi kuwaacha wachimbaji madini wafanye kazi zao na kutowachafua kuwa wanatorosha madini.

Mwenyekiti huyo wa MAREMA Elisha ameeleza hayo katika mkutano wa wachimbaji madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani, wakati wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Elisha amesema wachimbaji wasiwakubali kamwe wanasiasa wenye agenda nyepesi za kuwachafua kwani wengine wapo kwa ajili ya kuangalia maslahi yao pekee.

Amesema wachimbaji hawataki vikwazo wanataka wafanye kazi kwa saa 24 kila siku ili wapate madini kwani hivi sasa madini ya Tanzanite hayapatikani kwa wingi ila baadhi ya wanasiasa wanawakwamisha.

"Wachimbaji wanaposemwa vibaya naumia mno, tunapokuchagua kiongozi utuongoze siyo fimbo ya kutuchapia, agenda za kutuchafua wachimbaji tusikubali kamwe," amesema Elisha.

Amewaasa wachimbaji madini wawe wanachuja wanasiasa wakuchaguliwa pindi wakati ukifika kwenye uchaguzi ili wasiachiwe bomu.

""Tunapozungumzia uchumi wa Mirerani wasilete utani au kuwasingizia uongo wachimbaji na mwanasiasa mwenye agenda nyepesi atupishe, tuwe tunawauliza kwanza unatoka wapi, tumjue balozi wake," amesema Elisha.

Katibu mkuu wa MAREMA, Tariq Kibwe amesema kiwa wao wachimbaji siyo wanasiasa na wanajibana na kujinyima katika kuchimba madini ili wafanikiwe.

Kibwe amesema wachimbaji wapo sambamba na Mwenyekiti wa MAREMA Elisha katika kuwasemea na kuwatetea kwenye changamoto zao zinazowakabili.

"Baadhi ya wanasiasa wanatulalamikia kuwa wachimbaji tunawachangia viongozi wa juu, jamani wanapaswa kuelewa sisi hatukuchangia mtu tulichangia chama," amesema Kibwe.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameitaka Afrika kujenga uwezo wake wa ndani wa kugharamia, kusimamia na kuzalisha mahitaji muhimu ya huduma za afya, badala ya kutegemea misaada na mifumo ya nje kwa muda mrefu.

Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo, Jumatano Septemba 09, 2026, wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi unaofanyika jijini Arusha, ukiwakutanisha zaidi ya washiriki 2,700 kutoka mataifa 27.

Amesema Afrika inapaswa kubadili namna inavyoelewa na kutekeleza dhana ya kujenga uwezo, akisisitiza kuwa haipaswi kuishia katika miradi midogo isiyojenga uwezo wa kudumu, bali iwekeze katika uzalishaji wa dawa, vifaa tiba, teknolojia na wataalamu.

“Enzi zile nikiwa Waziri wa Fedha nilikuwa nawaambia nchi za Afrika zimeshashuhudia muda mrefu sasa wa maisha ya misaada na misaada inayoelekezwa pengine katika maeneo ambayo yanatofautiana na malengo ya ndani ya nchi kwa jina la capacity building. Capacity building. Capacity building. Na ndio tunaishia chapati, mandazi, sambusa. Hatuwekezi kitu kitakachodumu na kikawa endelevu.”

Dkt. Mwigulu amesema malengo ya ndani ya nchi yanayokwenda sambamba na malengo ya maendeleo endelevu yanapaswa kuheshimiwa na washirika wa maendeleo, ili misaada na uwekezaji viweze kuacha matokeo ya kudumu katika maisha ya Waafrika.

Amesema Tanzania inaendelea kuweka nguvu katika kuimarisha huduma za afya, ikiwemo kuongeza miundombinu, rasilimali watu na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, ambayo Serikali imeanza kutekeleza mwaka 2026.

“Tunapozungumza kuhusu afya ya msingi, tusizungumzie tu kujenga vituo vya afya. Tujenge pia uwezo wa nchi zetu kugharamia huduma hizo, kuzalisha mahitaji yake na kutumia teknolojia zetu wenyewe,” amesema.

Aidha, amesema Tanzania imeanza kuwekeza katika uwezo wa ndani wa uzalishaji wa dawa ili kupunguza utegemezi wa misaada na kuhakikisha upatikanaji wa dawa unaendelea kuwa wa uhakika hata wakati dunia inapokumbwa na changamoto zinazoathiri minyororo ya usambazaji.

Amesema Serikali pia itaendelea kuboresha mazingira ya watumishi wa afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za watumishi na kuongeza ajira katika sekta hiyo.

Dkt. Mwigulu amesema mkutano huo unapaswa kuzaa hatua mahsusi zinazoweza kutekelezwa na kupimwa, badala ya kuishia katika mijadala na maazimio.

Kwa upande wake,Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya, amesema Afrika ya mwaka 2026 si Afrika ya mwaka 1960 na kwamba wakati umefika kwa washirika wa maendeleo kubadili namna wanavyoshirikiana na serikali za Afrika.

Dkt. Kaseya amesema serikali za Afrika zinapaswa kuwa na umiliki na uelewa wa rasilimali zinazotolewa kwa ajili ya afya, huku fedha za washirika zikiendana na mipango ya kitaifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa WHO, Profesa Mohammed Janabi, amesema changamoto kubwa si kukosa suluhisho, bali ni kukosa ujasiri wa kuyafadhili, nidhamu ya kuyatekeleza na uwajibikaji wa kuyadumisha.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, amesema Serikali itaendelea kuongeza uwekezaji katika afya ya msingi kwa kuwa ndiyo ngazi inayohudumia wananchi wengi zaidi.

Amesema asilimia 95.6 ya wajawazito wanaojifungua nchini wanapata huduma katika ngazi ya afya ya msingi, huku asilimia 86 ya mahudhurio ya wagonjwa wa nje katika vituo vya umma yakihudumiwa katika ngazi hiyo.

Profesa Shemdoe amesema kati ya vituo 8,288 vya afya vinavyomilikiwa na Serikali, vituo 7,946 sawa na asilimia 95.8 ni vya ngazi ya afya ya msingi, hivyo uwekezaji katika ngazi hiyo ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa wananchi wengi.

Mkutano huo wa siku tatu unajadili namna ya kuimarisha huduma za afya ya msingi kuelekea upatikanaji wa huduma za afya kwa wote, kupitia ufadhili endelevu, ufanisi, ubora wa huduma, ubunifu, ushirikiano wa kikanda na kujenga mifumo ya afya inayostahimili majanga.







Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Rukwa Albert Kipele amewataka viongozi na vijana wa umoja huo kuanzia ngazi ya kata, wilaya kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhusiana na kilele cha mwenge wa uhuru Kitaifa mkoani Rukwa.

Akizungumza na vijana wa hamasa na viongozi wa kata wa jumuiya hiyo wilaya ya Sumbawanga mjini leo, ikiwa ni maandalizi ya kuukaribisha mwenge wa uhuru ambapo kilele chake kitahitimishwa mkoani Rukwa.

Kipele amesema vijana wana jukumu la kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhakikisha makundi hayo yanakuwa na uelewa wa pamoja kuhusiana na mbio za mwenge wa uhuru kitaifa.

" Twendeni tukatoe elimu kwenye kata zetu,wilaya zetu tukiwaeleza wananchi frusa zitakazopatikana wakati wa kilele cha mwenge wa uhuru twendeni tukawahamasishe boda boda,mama na baba ntilie,wajasiliamari,machinga tuwashirikishe kushiriki uzimaji wa mwenge wa uhuru kitaifa".

"Nchi yetu ni kubwa sana tukumbuke mwenge huu uliwashwa visiwani Pemba na sasa utazimwa mkoani kwetu na uwenda sisi wote hapa hatukuwepo huko nyuma na hatujawahi kushuhudia unavyowashwa na kuzima,sasa leo tutashuhudia uzimaji wa mwenge wetu wa uhuru"amesema Kipele.

Pia amesema Jumuiya ya vijana ndiyo nguvu ya chama na kuwa ushirikiano ni muhimu ili kujenga jumuiya hiyo na kufanikisha jambo hilo.

 "mshikamano ndiyo msingi wa kufanikisha jambo ambalo lipo mbele yetu,niwaombe vijana tujenge uaminifu na wakati huu ni wakushikamana ili jambo la kilele cha mwenge wa uhuru tufanikishe kwa pamoja"amesema Kipele.

Aidha amewataka vijana kuwa na umoja na kuepuka makundi yanayowagawa vijana hao bali kujenga umoja na mshikamano ambao ni msingi wa chama hicho.

Pia aliwataka viongozi UVCCM kata na wilaya mkoani Rukwa kufuata miongozo ya chama na kuwa na mipaka ya utendaji wao wa kazi ili kuondoa sintofahamu kwa viongozi wa ngazi za juu.

Kwa upande wao vijao wa hamasa pamoja na viongozi wamekishukuru chama cha mapinduzi CCM kwa kuendelea kuwatumia vijana katika shughuli za serikali na chama na kuwa watashirikiana kwa pamoja kuhakikisha elimu na hamasa inatolewa kwa makundi yote ya kijamii.

Wamesema wamefurahia ujio wa mwenge wa uhuru na kuwa historia inakwenda kuandikwa na kushuhudiwa katika kilele cha mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa zitakazo hitimishwa mkoani Rukwa Okt 14 mwaka huu.




JESHI la polisi mkoani Rukwa linamshikilia Maiko Sosolo Kazikulima (35) mkazi wa Kijiji Cha Mashete kata ya Mashete wilayani Nkasi mkoan Rukwa kwa tuhuma za kumuua mkewe  Victoria Mputa  (32) kwa kumpiga kichwani  akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine.

‎Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi mkoa Rukwa SACP Shadrack Masija amesema tukio hilo limetokea Jana J,Nne September 8,2026 majira ya saa 3 usiku wakati wakitoka kilabuni pamoja, ndipo ulipozuka ugomvi miongoni mwao uliohusishwa na wivu wa kimapenzi na kusababisha kuuawa kwa mwanamke huyo.

‎Amefafanua kuwa mtuhumiwa ambaye alikua mume wa marehemu wakiwa njiani kabla hawajafika nyumbani mzozo mkubwa kati Yao uliibuka huku Mume akiendelea  kumtuhumu mkewe kwa kuwa na mahusiano mengine na Wanaume wengine kiasi Cha kuchukua maamuzi ya kuanza kumpiga na rungu kichwani  kinyume Cha Sheria.

‎Kamanda Masija amesema mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na Polisi na kuwa upelelezi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.

‎‎Sambamba na hilo amewataka Wananchi kuendelea Kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi katika kuwabaini wahalifu na kuwa katika kipindi hiki wamekua wakipata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa Wananchi kitu kilichopelekea wahalifu wengi kunaswa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.



Wanakijiji wa Kinyamwenda, Kata ya Itaja, Wilaya ya Singida, wamepongeza ujenzi wa birika la kunyweshea punda na mifugo lililojengwa na INADES-Formation Tanzania kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Singida na wananchi, kwa ufadhili wa Brooke East Africa.

Birika hilo lilizinduliwa leo na Nathalia Mosha, Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, ambaye alisema linatarajiwa kuwahudumia takribani punda 720 na zaidi ya mifugo 9,000 kutoka Kinyamwenda na vijiji jirani vya Mipilo, Mwighanji na Itaja.

Mosha aliipongeza INADES-Formation Tanzania kwa kuleta mradi wa kuboresha maisha ya jamii kupitia ustawi wa mnyama kazi pundakatika vijiji vya Kinyamwenda, Ghata na Endesh, akisisitiza kuwa kuboresha ustawi wa punda kuna mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya jamii zinazowategemea.

Aliwataka wananchi waliopatiwa mafunzo kuhusu ustawi wa punda kuendelea kutoa elimu kwa wengine, hususan kuhusu matumizi sahihi ya tandiko na nira, ili kuwalinda punda dhidi ya majeraha na maumivu yasiyo ya lazima.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa INADES-Formation Tanzania, Jacqueline Nicodemus, Mkuu wa Idara ya Mafunzo, Michael Kihwele, aliwapongeza wananchi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha ujenzi wa birika hilo “Punda anapoboreka, nayo maisha ya jamii yataboreka kupitia mradi huo,” alisema Kihwele.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Utetezi na Ustawi wa Punda Wilaya ya Singida, Wilfred Mande, alisema birika hilo litapunguza umbali mrefu ambao mifugo imekuwa ikitembea kutafuta maji, hivyo kuimarisha ustawi wa punda na mifugo mingine.

Mande pia alieleza kuwa mradi huo umechangia kupungua kwa ukatili dhidi ya punda, kuimarika kwa huduma za afya kupitia kliniki za punda, kuanzishwa kwa klabu za ustawi wa punda shuleni, pamoja na kuwawezesha vikundi vya wananchi katika ujasiriamali, kuweka na kukopa.

Alisema vikundi pia vimeanza kutenga fedha kwa ajili ya kliniki za punda zinazofanyika kila baada ya miezi mitatu, hatua inayosaidia kuhakikisha punda wanapata matibabu na kutambuliwa kama wanyama wenye mchango mkubwa katika maisha ya jamii.






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameagwa rasmi na Menejimenti ya Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zilizo chini yake katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Kambarage Treasury Square, Dodoma. Jumatano Septemba 09, 2026.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughukia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, Menejimenti ya Wizara na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amewaasa Viongozi na Watendaji hao kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wasaidizi wake ili waendelee kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia Watanzania.

Aidha, Makamu wa Rais amewataka Viongozi na Watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uzalendo ili kutimiza matarajio ya wananchi kwa Serikali.













Uongozi wa Kata ya Mnadani umeanza kuchukua hatua za tahadhari kwa kukagua maeneo hatarishi yanayoweza kuathiriwa na mvua za El Nino.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge, alisema kuwa ukaguzi huo unafanyika kwa kushirikiana na Kamati ya Maendeleo ya Kata pamoja na viongozi wa Kanda Namba Sita, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Nino.

“Tumeanza kukagua maeneo ambayo tunaona yanaweza kuwa na changamoto wakati wa mvua, hasa sehemu zinazotuamisha maji na mitaro ambayo inahitaji kufunguliwa na kusafishwa,” alisema Kerenge.

Aidha aliongeza kuwa ufunguaji na usafishaji wa mitaro ni miongoni mwa hatua muhimu zinazotekelezwa ili kuhakikisha maji yanapata njia ya kupita na hivyo kupunguza uwezekano wa mafuriko na madhara mengine.

Aliwataka wananchi kushirikiana na viongozi kwa kuhakikisha mitaro na njia za maji zinakuwa wazi, pamoja na kutoa taarifa kuhusu maeneo yanayoweza kuwa hatarishi ili hatua zichukuliwe kwa wakati kwani zoezi la ukaguzi ni endelevu

Ziara hiyo ilishirikisha viongozi wa Kanda Namba Sita kubaini maeneo yanayoweza kukumbwa na changamoto za maji, ikiwemo maeneo yanayotuamisha maji pamoja na mitaro inayohitaji kufunguliwa na kusafishwa ili kurahisisha mtiririko wa maji wakati wa mvua.







Top News