Benki ya NMB imetunukiwa cheti cha hadhi ya  Superbrand Afrika Mashariki kwa kipindi cha 2026–2028 baada ya kupata kura nyingi zaidi za watumiaji katika kundi la benki, kwa mujibu wa Baraza la Superbrands.

Utambuzi huo umetokana na tathmini iliyohusisha Baraza la Superbrands na watumiaji katika ukanda wa Afrika Mashariki. Miongoni mwa vigezo vilivyotumika ni ubora wa bidhaa na huduma, utofauti wa chapa pamoja na uwezo wa kutoa huduma kwa kiwango kinachofanana kwa muda.

Mjumbe wa Baraza la Superbrands, Dorine Bangapi, alisema hadhi hiyo haiwezi kununuliwa, kwa kuwa uteuzi hutokana na maoni na kura za watumiaji. Alisema NMB ilipata kura nyingi zaidi katika kundi la benki.

Cheti hicho kilipokelewa kwa niaba ya NMB na Mkuu wa Idara ya Masoko, Rahma Mwapachu. Benki hiyo imesema utambuzi huo unaongeza wajibu wa kuendelea kuboresha huduma na kulinda imani ya wateja wake.










Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka amesema IAA itaendelea kuimarisha miundombinu na mazingira ya kujifunzia ili kandaa watalaam mahiri na kuendana na mahitaji ya programu za kisasa hususani programu zinazohusisha matumizi makubwa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

Prof. Sedoyeka amesema hayo Agosti 24, 2026 katika hafla ya uzinduzi wa utoaji wa programu za Shahada ya Uhasibu na Teknolojia ya Habari (Bachelor Degree in Accountancy with IT) na Shahada ya Sayansi ya Kompyuta (Bachelor Degree in Computer Science) katika Kampasi ya Babati iliyofanyika Waangw’aray Mjini Babati.

“Tunaishukuru Serikali kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) imetoa jumla ya shilingi bilioni 13.7 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala, mkataba na maabara ya TEHAMA katika Kampasi ya Babati. Sisi pia tumewekeza katika teknolojia na mkakati wetu ni madarasa yetu yote yawe ‘smart classes’ madarasa janja” amesema.

Prof. Sedoyeka ameongeza kuwa dhamira ya IAA ni wanafunzi kujifunza katika mazingira yanayowapa nafasi ya kupata maarifa, kufanya mazoezi, kubuni, kujiandaa kwa mahitaji halisi ya dunia ya kazi na kuwa kutumia maarifa kutatua changamoto halisi.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Daniel Sillo amesema , taasisi za umma na binafsi zinatumia mifumo ya kidijitali katika kusimamia taarifa za fedha, kufanya ukaguzi, kuhifadhi kumbukumbu, kufanya uchambuzi wa taarifa na kutoa maamuzi, hivyo Taifa linahitaji wataalam walioandaliwa vema ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya dunia.

Mbunge wa Babati Mjini, Mhe. Emmanuel Khambay amepongeza Uongozi wa IAA kwa ubunifu huku akieleza umuhimu wa uwepo wa IAA mkoani Manyara kuwa utaongeza fursa za elimu na uchumi kwa Mkoa wa Manyara na mikoa jirani.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo IAA, Dkt. Mwamini Tulli amesema ,”IAA itahakikisha kuwa upanuzi wa huduma za elimu unaendana na ubora wa miundombinu, programu za masomo, teknolojia, rasilimali watu na huduma kwa wanafunzi.”
Dar es Salaam, Tanzania, 2026.
VIONGOZI wa Serikali, sekta sekta binafsi na wadau wa teknolojia wametoa wito wa kuongeza uwekezaji kwa vijana katika ubunifu na ujuzi wa kidijitali ili kuiwezesha Afrika kutoka katika utegemezi wa teknolojia na kuwa mzalishaji wa suluhu za kidijitali zinazoendana na changamoto za maendeleo ya bara husika.

Wito huo ulitolewa katika mkutano wa teknolojia na fintech uliyofanyika Dar es Salaam, ukiwakutanisha wadau mbalimbali kujadili nafasi ya teknolojia, ubunifu na teknolojia ya kifedha katika kukuza uchumi na kuibua fursa mpya kwa vijana ambao wanaendelea kuwa sehemu kubwa ya idadi ya watu barani Afrika.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki; Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Financial Technology Conference, Deogratius Kilawe; Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Nkundwe Moses; na Mkurugenzi wa Airtel Money Tanzania, Andrew Rugamba, pamoja na wadau wengine.

Serikali: Vijana wawe wabunifu wa teknolojia
Akizungumza katika mkutano wa teknolojia na fintech, Mhe. Angellah Kairuki, alisisitiza umuhimu wa vijana kubadili mtazamo na kutumia teknolojia kama nyenzo ya kutengeneza suluhu za changamoto zinazowakabili wao na jamii zao.

Alisema vijana hawapaswi kubaki kuwa watumiaji wa teknolojia zinazotengenezwa katika nchi nyingine, bali wanapaswa kuwezeshwa kupata maarifa na ujuzi utakaowawezesha kubuni na kutengeneza suluhisho zao wenyewe za kidijitali.

Waziri Kairuki pia alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa teknolojia katika kujenga kizazi cha vijana kinachoshiriki kikamilifu katika uzalishaji wa teknolojia na ubunifu.

Teknolojia na ubunifu vinafungua fursa

Majadiliano katika mkutano wa teknolojia na fintech yalibainisha kuwa ushiriki wa vijana katika teknolojia na ubunifu unaweza kuongeza fursa za ajira na ujasiriamali, kusaidia kutatua changamoto za jamii na kuimarisha uwezo wa Afrika kutengeneza bidhaa na huduma za kidijitali zinazoendana na mahitaji yake.

Wadau walisisitiza kuwa vijana wabunifu wanahitaji kupata maarifa, ujuzi wa vitendo, teknolojia na mazingira rafiki ya kuwawezesha kubadilisha mawazo yao kuwa suluhisho zenye matokeo halisi katika jamii na uchumi.

COSTECH na wadau waimarisha mazingira ya ubunifu

Ushiriki wa COSTECH, pamoja na Serikali, sekta binafsi na wadau wa teknolojia, uliweka mkazo katika umuhimu wa kujenga mfumo imara unaosaidia utafiti, ubunifu na maendeleo ya suluhisho za kiteknolojia zinazotengenezwa ndani ya nchi.

Ushirikiano mkubwa kati ya sekta mbalimbali unaweza kuongeza fursa kwa vijana wabunifu kuendeleza mawazo yao kutoka hatua ya ubunifu hadi utekelezaji na hatimaye kuchangia katika mabadiliko ya kidijitali nchini Tanzania na barani Afrika.

Airtel Tanzania yaunga mkono fursa za kidijitali

Katika kuendeleza juhudi za kuimarisha mabadiliko ya kidijitali, Airtel Tanzania ilishiriki na kuonyesha nia yake ya kusaidia ukuaji wa teknolojia, ubunifu na fursa zinazotokana na huduma za kifedha za kidijitali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Airtel Money Tanzania, Andrew Rugamba, aliiwakilisha Airtel katika majadiliano kuhusu mabadiliko yanayoendelea katika sekta ya teknolojia na huduma za kifedha za kidijitali.

Ushiriki wa Airtel Tanzania unaendana na dhamira ya kampuni ya kuunga mkono mipango inayopanua upatikanaji wa fursa za kidijitali na kuchochea ubunifu, ujasiriamali na ujumuishi wa kifedha.

Hafla hiyo pia iliangazia umuhimu unaoongezeka wa teknolojia ya kifedha katika maendeleo ya uchumi wa Afrika. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Financial Technology Conference, Deogratius Kilawe, ushiriki wa wadau kutoka zaidi ya nchi 83 unaonyesha kuongezeka kwa hamu ya kimataifa katika mfumo wa teknolojia ya kifedha barani Afrika na uwezo wake wa kuchangia ukuaji wa uchumi.

Kujenga mustakabali wa kidijitali wa Afrika kwa pamoja

Mkutano wa teknolojia na fintech ulisisitiza kuwa Serikali, sekta binafsi, taasisi za teknolojia na wabunifu wana jukumu la pamoja katika kujenga mazingira yatakayowawezesha vijana kupata ujuzi, teknolojia na fursa wanazohitaji ili kutengeneza suluhisho za kukabiliana na changamoto za sasa na za baadaye.

Kwa Airtel Tanzania, kuunga mkono majukwaa yanayowakutanisha watunga sera, wabunifu, taasisi za teknolojia na sekta binafsi ni sehemu ya dhamira yake ya kuwawezesha watu wengi zaidi kushiriki katika uchumi wa kidijitali.
MASHABIKI wa burudani za michezo ya kasino wana sababu nyingine ya kuongeza kasi, baada ya Wild 4th Fruits, mchezo mpya kutoka Xpanse, kuingia kwenye orodha ya michezo inayowapa wachezaji wa Meridianbet burudani yenye ladha ya kipekee. Mchezo huu umejengwa kwa mtindo rahisi, mwepesi na unaovutia, huku ukiunganisha mandhari ya matunda yenye rangi angavu na msisimko unaoongezeka kila unapocheza. Kwa wachezaji wanaopenda burudani isiyo na mambo mengi lakini yenye uwezo wa kuleta ushindi kwa kila hatua, Wild 4th Fruits imekua chaguo sahihi.

Ukiingia kwenye ulimwengu wa Wild 4th Fruits, kinachokukuta ni mandhari yenye uhai na mvuto unaokufanya utake kuendelea kuchunguza. Mchezo huu umebeba ladha ya michezo ya matunda ya zamani, lakini umeongezewa muonekano wa kisasa unaoufanya uwe rahisi kucheza na kufurahisha zaidi. Kila raundi inakuja na nafasi ya kuona matokeo mapya, huku muundo wake ukiweka mkazo kwenye burudani iliyo nyepesi na inayoweza kuchezwa bila usumbufu.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kinachoongeza mvuto wa Wild 4th Fruits ni kasi yake tulivu inayomruhusu mchezaji kufurahia safari bila haraka. Wakati mwingine, burudani bora si ile inayokulazimisha kukimbia, bali inayokupa nafasi ya kufurahia kila sekunde. Ndiyo falsafa inayojitokeza kwenye mchezo huu, ambapo kila raundi inaweza kuleta ushindi mpya na kuendeleza hamasa.

Wild 4th Fruits pia imeanza kujenga jina lake miongoni mwa wachezaji wa Meridianbet kutokana na simulizi ya ushindi inayozunguka mchezo huu. Furahia uzoefu wa mchezo na kuingia kwenye orodha ya washindi ukiwa na matarajio ya burudani. Hivyo, iwe unapenda michezo yenye muonekano wa kawaida wa matunda au unatafuta kitu kipya cha kujaribu, Wild 4th Fruits inakupa sababu ya kuingia na kuona kile ambacho Expanse imeandaa.

Kama burudani yako inapenda mchanganyiko wa matunda, rangi, urahisi na msisimko wa kila raundi, Wild 4th Fruits iko tayari kukupa safari mpya ndani ya Meridianbet. Ni mchezo unaokuja na mtindo rahisi lakini unaovutia, ukiweka kila mzunguko kama mwanzo wa tukio jipya.

 


MERIDIANBET imeongeza gia nyingine kwenye burudani kwa kuileta Non-Stop Blasts & Races, kampeni yenye zawadi zenye thamani ya hadi TZS 75,000,000,000. Hii ni kampeni inayowaleta pamoja wachezaji, mashindano na zawadi katika safari inayoendelea kupitia michezo iliyochaguliwa ya Playson. Kama unapenda kuona nafasi mpya zikifunguka mara kwa mara, basi hii ni ya kufuatilia.

Kwenye Power Blasts, kila mchezo unaweza kuwa na zawadi yake. Wachezaji wanaoshiriki kwenye michezo inayokidhi vigezo wanaweza kupata smart drops za bahati wakati wanacheza. Zawadi hizo zinaweza kujumuisha fedha taslimu, mizunguko ya bure na vizidishi.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Halafu tunahamia kwenye Grand Races, ambako ushindani unakuwa wa muda mrefu zaidi. Wachezaji hukusanya pointi kupitia michezo inayostahili na kupambana kwa nafasi kwenye msimamo. Kila pointi inaweza kuwa muhimu katika safari ya kupanda viwango, huku kila mshiriki akijaribu kumaliza akiwa juu zaidi ya wengine. Hii ni sehemu inayowapa nafasi wachezaji wanaopenda ushindani wenye mwendelezo.

Kwa upande wa kasi, Turbo Races zinaingia moja kwa moja kwenye tukio. Hizi ni mbio fupi zenye ushindani wa haraka na nafasi za mara kwa mara za kuingia kwenye kinyang'anyiro. Msimamo unapowekwa upya, wachezaji wanapata nafasi nyingine ya kupanda juu.

Uzuri wa kampeni hii ni kwamba Non-Stop maana yake tukio linaendelea katika awamu mbalimbali. Michezo inayoshiriki, zawadi, prize pools, na ratiba za mbio zinaweza kutofautiana kulingana na awamu ya promosheni. Kwa hiyo, fuatilia michezo inayoshiriki, angalia mbio zinazoendelea na uwe tayari kwa zawadi.

SHEFFIELD Wednesday na Wolverhampton Wanderers watakutana leo Jumanne, Agosti 25, 2026, katika mechi ya raundi ya pili ya Carabao Cup (EFL Cup). Mechi hii itachezwa uwanjani Hillsborough kuanzia saa 21:45.

Hali ya timu hizi mbili kwa sasa ni tofauti kabisa. Sheffield Wednesday, ambao msimu huu wanacheza League One baada ya kushushwa daraja kutoka Championship kwa sababu ya matatizo ya kifedha na uongozi, walipata mwanzo mzuri msimu huu wa 2026-27 wakiwa chini ya umiliki mpya baada ya kuimarisha kikosi chao kilichokuwa dhaifu msimu uliopita.

Hata hivyo, hivi karibuni walipata pigo baada ya kufungwa bao 1-0 nyumbani na Bradford City siku ya Ijumaa, jambo lililoacha wachezaji wakiwa na hamu ya kurejea vizuri.

Kwa upande wa Wolves, ambao wanacheza Championship, hali inaonekana bora zaidi. Timu hiyo tayari imepitisha hatua ya awali baada ya kuifunga Port Vale, na tangu hapo wameanza msimu wa ligi bila kufungwa.

Aidha, mchezo wao wa hivi karibuni dhidi ya Preston North End ulionesha maboresho makubwa chini ya kocha Cesar Peixoto, jambo linaloipa Wolves imani ya kuingia kwenye mechi hii wakiwa na ari ya juu.

Kuhusu wachezaji watakaoshiriki, Sheffield Wednesday hawana mchezaji yeyote aliye nje ya kikosi kwa sababu ya majeraha au adhabu, jambo linalompa kocha Henrik Pedersen uhuru wa kuchagua kikosi bora zaidi kinachopatikana.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema. Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kihistoria, mechi hii ina umuhimu maalum kwa Sheffield Wednesday, timu ambayo imekuwa na rekodi nzuri katika Carabao Cup miaka ya nyuma dhidi ya timu za daraja la juu, hivyo mashabiki hawapaswi kuwapuuza Owls licha ya changamoto walizopitia msimu huu.

Wolves, kwa upande wao, watakuwa wakitafuta kuendeleza msimamo wao thabiti na kuepuka mshangao dhidi ya timu ndogo, Kwa ujumla, mchezo huu unaahidi kuwa na msisimko mkubwa Sheffield Wednesday wakitafuta kujirekebisha nyumbani, na Wolves wakiwa na dhamira ya kuendeleza mwendo wao mzuri kuelekea raundi ya tatu ya Carabao Cup.

A new FANTA® flavour is adding a burst of deliciousness to the brand’s portfolio in Tanzania with the launch of FANTA® Berry.

This bolder, fruitier tasting beverage brings a splash of playfulness, fun, and refreshing enjoyment to fans across the country. 

Inspired by the vibrant energy of Tanzanian youth culture and the fast-rising Singeli movement, FANTA® Berry is set to tantalise taste buds with its vibrant twist. 

The new flavour is now available in selected retail outlets, supermarkets, universities, kiosks, and trade outlets across Tanzania.

“We’re thrilled to bring even more variety to Tanzanians with this vibrant addition to the FANTA® family. FANTA® Berry embodies our commitment to creating fun, fruity twists filled with deliciousness that cater to people’s evolving tastes,” said Kabula Nshimo, Senior Marketing Manager for Coca-Cola Tanzania. 

The launch campaign will come alive through the energetic “Kipapli” platform, designed to connect directly with Tanzania’s youth through music, dance, fashion, creator culture, and on-ground experiences across universities and high-traffic areas in Dar es Salaam.

As part of the experience, FANTA® Berry will bring the excitement to consumers through immersive commuter activations, influencer engagements and taste-test challenges.

 Coca-Cola Kwanza today embarked on a vibrant convoy journey, starting at the Mikocheni plant and making stops across Ubungo, Mabibo, Buguruni and Temeke before culminating in Mbagala. 

At each stop, consumers will enjoy FANTA® Berry tasting experiences, interactive entertainment and fun activities designed to create memorable brand experiences.

FANTA® Berry will roll creator challenges aimed at empowering young people to create content, grow their influence, and participate in the rapidly expanding digital creator economy.

 The activations will also include university engagements, trade market “Berrification” moments, influencer collaborations, and the #KipapliChallenge social media campaign.

With iconic favourites like FANTA® Orange and now FANTA® Berry, the brand continues to inspire a passion for life and unforgettable moments of deliciousness.

 Whether you're hanging out with friends, creating content, commuting across the city, or simply enjoying a playful moment, FANTA® Berry is the perfect companion.

 “Our diverse beverage portfolio reflects our dedication to meeting the preferences of Tanzanians. We’re proud to offer products that bring people together, spark joy, and add flavour and deliciousness to everyday moments,” said David Chait, General Manager at Coca-Cola Kwanza Ltd.

Get your FANTA® Berry fix today and bring on the fun and deliciousness!

Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (right), the Company’s Regional Trade Marketing Manager, Ms. Rukia Sakibu (left), and the firm’s Revenue Growth & Trade Marketing Director, Mr. Arthur Kyara (centre), showcase the newly launched Fanta Berry flavour bottles during an introductory event held in Dar es Salaam over the weekend.
Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (left) poses for a group photo with some Dar es Salaam residents who attended the official launch of the new Fanta Berry flavour in Dar es Salaam over the weekend.

Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (left) takes a selfie with some Dar es Salaam residents during the celebrations, marking the official launch of the new Fanta Berry flavour, in Dar es Salaam over the weekend.



Na Mwandishi Wetu
ZAIDI ya wanafunzi 95 wa Kitanzania wameondoka nchini kuelekea India kuanza masomo ya elimu ya juu katika vyuo mbalimbali, ikiwa ni kundi la kwanza kati ya wanafunzi 198 wanaotarajiwa kwenda kusoma nchini humo kupitia Global Education Link mwaka 2026.

Wanafunzi hao wamechagua programu zinazohusiana na sayansi, teknolojia na taaluma zinazohitajika katika dunia ya sasa, zikiwemo Computer Engineering, Cyber Security, Artificial Intelligence, Civil Engineering, afya, sheria na biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Meneja wa Tawi la Dar es Salaam, Micky Musa, amesema kuondoka kwa wanafunzi hao ni sehemu ya mpango wa kuwaunganisha vijana wa Tanzania na fursa za elimu ya kimataifa.

“Zaidi ya wanafunzi 95 wanaondoka katika kundi hili la kwanza kuelekea India, lakini kwa mwaka huu tunatarajia wanafunzi 198 kwenda kusoma nchini India. Hili si kundi la mwisho kwa sababu bado tuna wanafunzi wengine wanaoendelea kukamilisha taratibu zao,” amesema Musa.

Amesema Global Education Link pia inaendelea kuwaandaa wanafunzi wapatao 185 wanaotarajiwa kuelekea China, huku wengine wakiwa katika maandalizi ya kwenda Malaysia, Marekani na Uingereza.

Musa amewataka vijana wenye ndoto ya kusoma nje ya nchi kufika katika ofisi za Global Education Link zilizopo Dar es Salaam, Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha kupata ushauri kuhusu uchaguzi wa vyuo, programu za masomo, udahili, visa na maandalizi ya safari.

Miongoni mwa wanafunzi walioondoka ni Alvin Andrew Munda, mwenye umri wa miaka 17, anayeelekea Lovely Professional University nchini India kusomea Computer Science, akilenga baadaye kujikita katika Cyber Security.

“Napenda mfumo wenye practical zaidi kuliko kusoma theory na kuandika mitihani pekee. Nataka nitumie elimu nitakayoipata kutengeneza suluhisho na baadaye nijikite katika Cyber Security kwa sababu usalama wa mtandao ni muhimu sana katika dunia ya sasa,” amesema.

Munda amesema Global Education Link imemsaidia katika mchakato mzima, kuanzia kupata chuo hadi kukamilisha maandalizi ya safari.

Naye mwanafunzi mwingine anayekwenda kusomea Computer Science na Artificial Intelligence amesema anatarajia kuwa mtaalamu wa data na teknolojia, akieleza kuwa AI imeanza kuwa sehemu muhimu katika benki, hospitali, biashara, serikali na sekta nyingine.

Kwa upande mwingine, mwanafunzi anayekwenda kusomea Bachelor of Business Administration na Bachelor of Laws amesema ana ndoto ya kuwa mwanasheria na mfanyabiashara mwenye mafanikio, huku akipongeza Global Education Link kwa kumsaidia katika visa processing, kupata chuo na maandalizi ya safari.

Wazazi waliowasindikiza watoto wao Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wameipongeza Global Education Link kwa kusimamia mchakato wa watoto wao kuanzia hatua za awali hadi siku ya safari.

Donald Kito, mzazi wa Isaac Donald Kito anayekwenda Lovely Professional University kusomea Diploma ya Civil Engineering, amesema familia yake ilifahamu huduma za Global Education Link kupitia matangazo na baada ya kuwasiliana nao walipata maelezo yaliyowapa imani ya kuendelea na mchakato.
Na Mwandishi Wetu
MSANII maarufu wa muziki Christian Bella akiwa sambamba na bendi yake ya Malaika wanatarajiwa kukonga nyoyo za wananchi wa Dar es Salaam siku ya Ijumaa tarehe 28 katika ukumbi wa The Embassy Mbezi Kimara kwa Msuguri.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Edwin Bagenyi ambaye ni Meneja wa Embassy Hall alisema maandalizi yote yamekamilika na wananchi watakaofika watapata burudani ya kutosha kutoka kwa mwanamuziki huyo. Alisema kwa muda mrefu wananchi wa Kimara Mbezi na maeneo mengine ya jijini Dar es Salaam wamekuwa na shauku ya kumwona msanii huyo akitumbuiza maeneo hayo.

“Kwa muda mrefu tumepokea maombi ya wananchi wakitaka kumwona Christian Bella akitumbuiza kwenye ukumbi wetu wa kisasa kabisa wa Embassy, kwa hiyo tumeona tusiwanyime raha wateja wetu, tumeona aje tushirikiane kupendezesha siku hiyo,” alisema.

“Tumejiandaa vya kutosha watu watapata burudani ambayo wameililia kwa muda mrefu sana. Tunawaahidi wateja wetu kuwa burudani wanayoitarajia wataipata siku hiyo ya Ijumaa tarehe 28 hapa Embassy Hall,” alisema.

Christian Bella, ambaye amejijengea jina kubwa kupitia uwezo wake wa kuimba, kucheza na kuwasilisha burudani yenye mvuto jukwaani, anatarajiwa kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki watakaofika katika ukumbi huo. Uwepo wake unatajwa kuwa kivutio kikubwa kutokana na historia yake katika muziki na umahiri wake wa kuwasilisha nyimbo zinazopendwa na mashabiki wa rika mbalimbali.

Katika tukio hilo, mashabiki watapata fursa ya kusikiliza na kufurahia nyimbo mbalimbali za Christian Bella, zikiwemo zile zilizompa umaarufu katika safari yake ya muziki. Msanii huyo amekuwa akitambulika kwa sauti yake ya kipekee, uwezo wa kuimba muziki wa dansi na kushirikisha mashabiki wakati wa maonyesho yake.

Ukumbi wa Embassy Kimara unatarajiwa kuwa sehemu ya kukutana kwa wapenzi wa burudani watakaotaka kutumia muda wao wakifurahia muziki wa moja kwa moja. Tukio hilo pia linatarajiwa kutoa nafasi kwa mashabiki kujumuika, kucheza na kufurahia burudani katika mazingira ya ukumbi.

Waandaaji wa tukio hilo wanawahimiza mashabiki kujiandaa mapema ili kupata nafasi ya kushuhudia burudani hiyo. Aidha, tukio linatarajiwa kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sanaa na burudani, huku likitoa mchango katika kuendeleza muziki wa dansi na burudani nchini. Kwa wapenzi wa muziki wa dansi, usiku huo unatarajiwa kuwa wa burudani, muziki na kumbukumbu nzuri.

Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akizungumza jambo alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.


WAZIRI wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb), ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mipya ya Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) kinachojengwa eneo la Banana, jijini Dar es Salaam, na kueleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo.

Hadi Julai 19, 2026, mradi huo ulikuwa umefikia asilimia 23.9 ya utekelezaji baada ya miezi 11 tangu kuanza kwa ujenzi.

Katika ziara hiyo, Mhe. Prof. Mbarawa alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, pamoja na Menejimenti ya TCAA, ambapo alipatiwa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi na hatua mbalimbali zilizofikiwa.

Mradi huo wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 78 unalenga kujenga miundombinu ya kisasa ya mafunzo ya usafiri wa anga, kuongeza uwezo wa Tanzania kuzalisha wataalamu wa sekta hiyo na kuimarisha nafasi ya nchi kuwa kitovu cha mafunzo ya usafiri wa anga barani Afrika.

Mhe. Prof. Mbarawa ameipongeza TCAA kwa usimamizi wa mradi huo, huku akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati, kwa kuzingatia viwango vya ubora pamoja na thamani ya fedha.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuimarisha uwezo wa Tanzania katika kutoa mafunzo ya wataalamu wa usafiri wa anga na kuchangia maendeleo ya sekta hiyo nchini na barani Afrika.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Dkt. Jabiri K. Bakari (katikati) akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa(kushoto) kuhusu mradi mradi wa ujenzi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akitembelea na kukagua maendeleo ya  mradi wa  ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya majengo yaliofikia kwenye mradi wa  ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na taasisi zake kuhakikisha bunifu zinazozalishwa na Watanzania haziishii kuonyeshwa kwenye maonesho, bali zinaendelezwa, zinalindwa na kupelekwa sokoni ili zitoe suluhisho kwa changamoto mbalimbali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo, Jumatatu, Agosti 24, 2026, jijini Tanga wakati akihitimisha Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, akisisitiza umuhimu wa kujenga mfumo unaowawezesha wabunifu kubadilisha mawazo yao kuwa bidhaa na huduma zenye tija.

Amesema Tanzania ina wabunifu wenye uwezo mkubwa katika maeneo mbalimbali, hivyo hatua inayohitajika sasa ni kuhakikisha ubunifu huo unavuka hatua ya kuoneshwa kwenye maonesho na kufikia hatua ya kutumika, kuzalishwa kwa wingi na kuuzwa sokoni.

“Ni lazima tuvuke kwenye maonesho, twende kwenye uhalisia wa maisha kwamba hivi vitu ambavyo tunavionyesha kwenye maadhimisho kama haya sasa viende kwenye utaratibu wa kila siku wa maisha, tuvitengeneze vya kutosha, vitumike na viingie sokoni,” amesema Dkt. Mwigulu.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika sayansi, ujuzi na ubunifu kwa lengo la kuyageuza maeneo hayo kuwa nguzo muhimu za uchumi wa Taifa na kuchochea maendeleo kupitia matumizi ya tafiti na teknolojia.

“Hatutaweza kuendelea bila kuwa na sayansi, teknolojia na tafiti na tukatumia matokeo ya tafiti hizo. Hatutapata tija bila kutumia matokeo ya tafiti hizo,” amesema.

Dkt. Mwigulu pia amesema Serikali haitakubali kushusha viwango vya elimu, akisisitiza umuhimu wa taasisi zinazosimamia ubora wa elimu kuendelea kusimamia misingi ya kitaaluma katika kuandaa wataalamu wenye uwezo unaokubalika.

“Tusitengeneze mazingira yawe rahisi ya kujifunza, yawe na alama kubwa kubwa, lakini kazini kuwe na zero kubwa kubwa. Hiyo hapana. Lazima tusimamie misingi ya elimu,” amesema.

Amesisitiza kuwa katika sekta nyeti kama afya, uhandisi na elimu, ubora wa mafunzo haupaswi kuchezewa.

“Hatuwezi kucheza na afya za Watanzania… Hatuwezi tukaandaa wataalamu kwa namna duni duni hivi, tutaharibu sekta yote. Tunataka walimu walio bora, maengineia walio bora; wakijenga daraja, wakijenga jengo, liwe jengo kweli kweli,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameagiza mipango ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Tanga iangalie mahitaji ya kiuchumi na kijamii ya mkoa huo kwa kipindi cha miaka 25 ijayo, ili miundombinu inayojengwa sasa iendane na ukuaji wa uchumi, biashara, uwekezaji na ongezeko la matumizi ya usafiri wa anga.

“Lazima tunapojenga tuwaze mbele, tusijenge kwa ajili ya leo. Tuwaze mbele miaka 20 mbele, 25 mbele, kama ambavyo Dira yetu inatuambia,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema uwanja huo unapaswa kujengwa kwa hadhi ya Tanga kama lango muhimu la shughuli za kiuchumi kutokana na miradi mikubwa inayotekelezwa katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema maonesho hayo yanaakisi jitihada za Serikali katika kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha elimu inayounganisha nadharia na vitendo, ili kuandaa wahitimu wenye ujuzi wa kujiajiri na kuingia kwa ufanisi katika soko la ajira.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Caroline Nombo amesema jumla ya taasisi 91 za umma na binafsi zimeshiriki katika maadhimisho hayo, ambayo yamehusisha maonesho ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu, mashindano ya kitaifa ya ujuzi na ubunifu pamoja na makongamano yaliyolenga kujadili mchango wa elimu, ujuzi na teknolojia katika kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe Husna Sekiboko amesema Bunge litaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuendeleza elimu, ujuzi na ubunifu kupitia bajeti, sera na miongozo inayolenga kuwawezesha watafiti na wabunifu wa ndani kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa. Amesema kuna umuhimu wa kuzipa kipaumbele bidhaa na teknolojia zinazozalishwa nchini, zikiwemo katika taasisi za Serikali, ili kuongeza matumizi ya bunifu za Watanzania na kuchochea ukuaji wa wabunifu hao.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Buriani amesema uwekezaji wa Serikali katika sekta ya elimu umeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia mkoani humo, kuongeza miundombinu na kuchochea mafanikio ya wanafunzi, huku akipongeza maonesho hayo kwa kuibua na kuonesha uwezo mkubwa wa Watanzania katika sayansi, teknolojia na ubunifu.

Kaulimbiu ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu mwaka 2026 ni “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”









Na Janeth Raphael - MichuziTv 

Imani kwamba haki inaweza kufuatiliwa na kupatikana bila kujali hali ya mtu imeongezeka kwa familia moja kutoka Meru mkoani Arusha, baada ya kupata msaada kupitia Programu ya “Sema na Waziri” ya Wizara ya Katiba na Sheria.

Familia hiyo ilikuwa imekumbwa na changamoto baada ya kuacha kazi ya ualimu katika shule ya msingi ambako walikuwa wakijitolea kufundisha, huku ikiwa bado inadai stahiki zake. Changamoto hiyo iliwasilishwa kupitia programu hiyo na kuanza kufanyiwa kazi na watumishi wa Wizara.

Ufuatiliaji uliofanywa na Wizara kwa kuwasiliana na wahusika umefanikisha familia hiyo kupata stahiki zilizokuwa zikidaiwa, hatua ambayo imeelezwa kuwa imewapa matumaini mapya kuhusu upatikanaji wa haki.

Akizungumza katika programu hiyo, Lidya Ernest kutoka Meru, Arusha, amesema awali alikuwa na mtazamo kwamba haki ilikuwa rahisi kupatikana zaidi kwa watu wenye uwezo, lakini uzoefu walioupata umebadili mtazamo huo.

“Nitumie nafasi hii kumshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka Programu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa ajili ya kutusaidia Watanzania wote bila kuangalia matabaka wala nyadhifa, wala hali ya mtu. Hata sisi watu wa huku chini nasi tumefikiwa,” amesema Lidya.

Kwa mujibu wa Lidya, hatua hiyo imewapa yeye na mume wake ujasiri wa kuendelea kufuatilia haki zao kupitia njia sahihi, huku wakitambua umuhimu wa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali.

Katika hatua nyingine, Wizara ya Katiba na Sheria imewakabidhi Lidya na mume wake Sh milioni 1.5, fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha shughuli za ujasiriamali na kujikwamua kiuchumi.

Msaada huo unalenga kuwapa fursa ya kutumia fedha hizo kama mtaji wa shughuli za uzalishaji, hatua inayotarajiwa kusaidia familia hiyo kujenga chanzo cha kipato na kuimarisha maisha yao.

Tukio hilo limeonyesha pia nafasi ya Programu ya “Sema na Waziri” katika kuwapa wananchi jukwaa la kuwasilisha changamoto zao za kisheria na kupata ufuatiliaji kutoka kwa Wizara.

Kwa familia hiyo kutoka Meru, msaada walioupata haujaishia katika kurejeshewa stahiki walizokuwa wakidai, bali umeenda sambamba na kupata mtaji wa kuanza shughuli za ujasiriamali, jambo ambalo wameeleza kuwa limewapa matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi.

Hatua hiyo pia inaendelea kuimarisha ujumbe kwamba upatikanaji wa haki haupaswi kuwa fursa ya wachache, bali huduma inayopaswa kuwafikia wananchi wote bila kujali uwezo wao, hadhi au nafasi zao katika jamii.


 






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Taasisi ya Maendeleo ya Diaspora wa Kiafrika (ADDI) Balozi Dkt. Arikana Chihombori-Quao, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 24 Agosti, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Taasisi ya Maendeleo ya Diaspora wa Kiafrika (ADDI) Balozi Dkt. Arikana Chihombori-Quao baada ya mazungumzo, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 24 Agosti, 2026.





Top News