
DODOMA, TANZANIA — September 8, 2026.
Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.

Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.

The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.
After the group discussions, the students came together for presentations.

Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.

Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.

It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.

Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.


MWENYEKITI wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara, (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi amewaasa wanasiasa wenye agenda nyepesi kuwaacha wachimbaji madini wafanye kazi zao na kutowachafua kuwa wanatorosha madini.
Mwenyekiti huyo wa MAREMA Elisha ameeleza hayo katika mkutano wa wachimbaji madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani, wakati wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Elisha amesema wachimbaji wasiwakubali kamwe wanasiasa wenye agenda nyepesi za kuwachafua kwani wengine wapo kwa ajili ya kuangalia maslahi yao pekee.
Amesema wachimbaji hawataki vikwazo wanataka wafanye kazi kwa saa 24 kila siku ili wapate madini kwani hivi sasa madini ya Tanzanite hayapatikani kwa wingi ila baadhi ya wanasiasa wanawakwamisha.
"Wachimbaji wanaposemwa vibaya naumia mno, tunapokuchagua kiongozi utuongoze siyo fimbo ya kutuchapia, agenda za kutuchafua wachimbaji tusikubali kamwe," amesema Elisha.
Amewaasa wachimbaji madini wawe wanachuja wanasiasa wakuchaguliwa pindi wakati ukifika kwenye uchaguzi ili wasiachiwe bomu.
""Tunapozungumzia uchumi wa Mirerani wasilete utani au kuwasingizia uongo wachimbaji na mwanasiasa mwenye agenda nyepesi atupishe, tuwe tunawauliza kwanza unatoka wapi, tumjue balozi wake," amesema Elisha.
Katibu mkuu wa MAREMA, Tariq Kibwe amesema kiwa wao wachimbaji siyo wanasiasa na wanajibana na kujinyima katika kuchimba madini ili wafanikiwe.
Kibwe amesema wachimbaji wapo sambamba na Mwenyekiti wa MAREMA Elisha katika kuwasemea na kuwatetea kwenye changamoto zao zinazowakabili.
"Baadhi ya wanasiasa wanatulalamikia kuwa wachimbaji tunawachangia viongozi wa juu, jamani wanapaswa kuelewa sisi hatukuchangia mtu tulichangia chama," amesema Kibwe.
Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo, Jumatano Septemba 09, 2026, wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi unaofanyika jijini Arusha, ukiwakutanisha zaidi ya washiriki 2,700 kutoka mataifa 27.
Amesema Afrika inapaswa kubadili namna inavyoelewa na kutekeleza dhana ya kujenga uwezo, akisisitiza kuwa haipaswi kuishia katika miradi midogo isiyojenga uwezo wa kudumu, bali iwekeze katika uzalishaji wa dawa, vifaa tiba, teknolojia na wataalamu.
“Enzi zile nikiwa Waziri wa Fedha nilikuwa nawaambia nchi za Afrika zimeshashuhudia muda mrefu sasa wa maisha ya misaada na misaada inayoelekezwa pengine katika maeneo ambayo yanatofautiana na malengo ya ndani ya nchi kwa jina la capacity building. Capacity building. Capacity building. Na ndio tunaishia chapati, mandazi, sambusa. Hatuwekezi kitu kitakachodumu na kikawa endelevu.”
Dkt. Mwigulu amesema malengo ya ndani ya nchi yanayokwenda sambamba na malengo ya maendeleo endelevu yanapaswa kuheshimiwa na washirika wa maendeleo, ili misaada na uwekezaji viweze kuacha matokeo ya kudumu katika maisha ya Waafrika.
Amesema Tanzania inaendelea kuweka nguvu katika kuimarisha huduma za afya, ikiwemo kuongeza miundombinu, rasilimali watu na utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, ambayo Serikali imeanza kutekeleza mwaka 2026.
“Tunapozungumza kuhusu afya ya msingi, tusizungumzie tu kujenga vituo vya afya. Tujenge pia uwezo wa nchi zetu kugharamia huduma hizo, kuzalisha mahitaji yake na kutumia teknolojia zetu wenyewe,” amesema.
Aidha, amesema Tanzania imeanza kuwekeza katika uwezo wa ndani wa uzalishaji wa dawa ili kupunguza utegemezi wa misaada na kuhakikisha upatikanaji wa dawa unaendelea kuwa wa uhakika hata wakati dunia inapokumbwa na changamoto zinazoathiri minyororo ya usambazaji.
Amesema Serikali pia itaendelea kuboresha mazingira ya watumishi wa afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za watumishi na kuongeza ajira katika sekta hiyo.
Dkt. Mwigulu amesema mkutano huo unapaswa kuzaa hatua mahsusi zinazoweza kutekelezwa na kupimwa, badala ya kuishia katika mijadala na maazimio.
Kwa upande wake,Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya, amesema Afrika ya mwaka 2026 si Afrika ya mwaka 1960 na kwamba wakati umefika kwa washirika wa maendeleo kubadili namna wanavyoshirikiana na serikali za Afrika.
Dkt. Kaseya amesema serikali za Afrika zinapaswa kuwa na umiliki na uelewa wa rasilimali zinazotolewa kwa ajili ya afya, huku fedha za washirika zikiendana na mipango ya kitaifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa WHO, Profesa Mohammed Janabi, amesema changamoto kubwa si kukosa suluhisho, bali ni kukosa ujasiri wa kuyafadhili, nidhamu ya kuyatekeleza na uwajibikaji wa kuyadumisha.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe, amesema Serikali itaendelea kuongeza uwekezaji katika afya ya msingi kwa kuwa ndiyo ngazi inayohudumia wananchi wengi zaidi.
Amesema asilimia 95.6 ya wajawazito wanaojifungua nchini wanapata huduma katika ngazi ya afya ya msingi, huku asilimia 86 ya mahudhurio ya wagonjwa wa nje katika vituo vya umma yakihudumiwa katika ngazi hiyo.
Profesa Shemdoe amesema kati ya vituo 8,288 vya afya vinavyomilikiwa na Serikali, vituo 7,946 sawa na asilimia 95.8 ni vya ngazi ya afya ya msingi, hivyo uwekezaji katika ngazi hiyo ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa wananchi wengi.
Mkutano huo wa siku tatu unajadili namna ya kuimarisha huduma za afya ya msingi kuelekea upatikanaji wa huduma za afya kwa wote, kupitia ufadhili endelevu, ufanisi, ubora wa huduma, ubunifu, ushirikiano wa kikanda na kujenga mifumo ya afya inayostahimili majanga.
Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Rukwa Albert Kipele amewataka viongozi na vijana wa umoja huo kuanzia ngazi ya kata, wilaya kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhusiana na kilele cha mwenge wa uhuru Kitaifa mkoani Rukwa.
Akizungumza na vijana wa hamasa na viongozi wa kata wa jumuiya hiyo wilaya ya Sumbawanga mjini leo, ikiwa ni maandalizi ya kuukaribisha mwenge wa uhuru ambapo kilele chake kitahitimishwa mkoani Rukwa.
Kipele amesema vijana wana jukumu la kutoa elimu na kuhamasisha makundi mbalimbli ya kijamii kuhakikisha makundi hayo yanakuwa na uelewa wa pamoja kuhusiana na mbio za mwenge wa uhuru kitaifa.
" Twendeni tukatoe elimu kwenye kata zetu,wilaya zetu tukiwaeleza wananchi frusa zitakazopatikana wakati wa kilele cha mwenge wa uhuru twendeni tukawahamasishe boda boda,mama na baba ntilie,wajasiliamari,machinga tuwashirikishe kushiriki uzimaji wa mwenge wa uhuru kitaifa".
"Nchi yetu ni kubwa sana tukumbuke mwenge huu uliwashwa visiwani Pemba na sasa utazimwa mkoani kwetu na uwenda sisi wote hapa hatukuwepo huko nyuma na hatujawahi kushuhudia unavyowashwa na kuzima,sasa leo tutashuhudia uzimaji wa mwenge wetu wa uhuru"amesema Kipele.
Pia amesema Jumuiya ya vijana ndiyo nguvu ya chama na kuwa ushirikiano ni muhimu ili kujenga jumuiya hiyo na kufanikisha jambo hilo.
"mshikamano ndiyo msingi wa kufanikisha jambo ambalo lipo mbele yetu,niwaombe vijana tujenge uaminifu na wakati huu ni wakushikamana ili jambo la kilele cha mwenge wa uhuru tufanikishe kwa pamoja"amesema Kipele.
Aidha amewataka vijana kuwa na umoja na kuepuka makundi yanayowagawa vijana hao bali kujenga umoja na mshikamano ambao ni msingi wa chama hicho.
Pia aliwataka viongozi UVCCM kata na wilaya mkoani Rukwa kufuata miongozo ya chama na kuwa na mipaka ya utendaji wao wa kazi ili kuondoa sintofahamu kwa viongozi wa ngazi za juu.
Kwa upande wao vijao wa hamasa pamoja na viongozi wamekishukuru chama cha mapinduzi CCM kwa kuendelea kuwatumia vijana katika shughuli za serikali na chama na kuwa watashirikiana kwa pamoja kuhakikisha elimu na hamasa inatolewa kwa makundi yote ya kijamii.
Wamesema wamefurahia ujio wa mwenge wa uhuru na kuwa historia inakwenda kuandikwa na kushuhudiwa katika kilele cha mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa zitakazo hitimishwa mkoani Rukwa Okt 14 mwaka huu.
JESHI la polisi mkoani Rukwa linamshikilia Maiko Sosolo Kazikulima (35) mkazi wa Kijiji Cha Mashete kata ya Mashete wilayani Nkasi mkoan Rukwa kwa tuhuma za kumuua mkewe Victoria Mputa (32) kwa kumpiga kichwani akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi mkoa Rukwa SACP Shadrack Masija amesema tukio hilo limetokea Jana J,Nne September 8,2026 majira ya saa 3 usiku wakati wakitoka kilabuni pamoja, ndipo ulipozuka ugomvi miongoni mwao uliohusishwa na wivu wa kimapenzi na kusababisha kuuawa kwa mwanamke huyo.
Amefafanua kuwa mtuhumiwa ambaye alikua mume wa marehemu wakiwa njiani kabla hawajafika nyumbani mzozo mkubwa kati Yao uliibuka huku Mume akiendelea kumtuhumu mkewe kwa kuwa na mahusiano mengine na Wanaume wengine kiasi Cha kuchukua maamuzi ya kuanza kumpiga na rungu kichwani kinyume Cha Sheria.
Kamanda Masija amesema mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na Polisi na kuwa upelelezi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.
Sambamba na hilo amewataka Wananchi kuendelea Kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi katika kuwabaini wahalifu na kuwa katika kipindi hiki wamekua wakipata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa Wananchi kitu kilichopelekea wahalifu wengi kunaswa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
Birika hilo lilizinduliwa leo na Nathalia Mosha, Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, ambaye alisema linatarajiwa kuwahudumia takribani punda 720 na zaidi ya mifugo 9,000 kutoka Kinyamwenda na vijiji jirani vya Mipilo, Mwighanji na Itaja.
Mosha aliipongeza INADES-Formation Tanzania kwa kuleta mradi wa kuboresha maisha ya jamii kupitia ustawi wa mnyama kazi pundakatika vijiji vya Kinyamwenda, Ghata na Endesh, akisisitiza kuwa kuboresha ustawi wa punda kuna mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya jamii zinazowategemea.
Aliwataka wananchi waliopatiwa mafunzo kuhusu ustawi wa punda kuendelea kutoa elimu kwa wengine, hususan kuhusu matumizi sahihi ya tandiko na nira, ili kuwalinda punda dhidi ya majeraha na maumivu yasiyo ya lazima.
Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa INADES-Formation Tanzania, Jacqueline Nicodemus, Mkuu wa Idara ya Mafunzo, Michael Kihwele, aliwapongeza wananchi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha ujenzi wa birika hilo “Punda anapoboreka, nayo maisha ya jamii yataboreka kupitia mradi huo,” alisema Kihwele.
Mande pia alieleza kuwa mradi huo umechangia kupungua kwa ukatili dhidi ya punda, kuimarika kwa huduma za afya kupitia kliniki za punda, kuanzishwa kwa klabu za ustawi wa punda shuleni, pamoja na kuwawezesha vikundi vya wananchi katika ujasiriamali, kuweka na kukopa.
Alisema vikundi pia vimeanza kutenga fedha kwa ajili ya kliniki za punda zinazofanyika kila baada ya miezi mitatu, hatua inayosaidia kuhakikisha punda wanapata matibabu na kutambuliwa kama wanyama wenye mchango mkubwa katika maisha ya jamii.
Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughukia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, Menejimenti ya Wizara na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amewaasa Viongozi na Watendaji hao kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wasaidizi wake ili waendelee kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia Watanzania.
Aidha, Makamu wa Rais amewataka Viongozi na Watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uzalendo ili kutimiza matarajio ya wananchi kwa Serikali.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge, alisema kuwa ukaguzi huo unafanyika kwa kushirikiana na Kamati ya Maendeleo ya Kata pamoja na viongozi wa Kanda Namba Sita, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Nino.
“Tumeanza kukagua maeneo ambayo tunaona yanaweza kuwa na changamoto wakati wa mvua, hasa sehemu zinazotuamisha maji na mitaro ambayo inahitaji kufunguliwa na kusafishwa,” alisema Kerenge.
Aidha aliongeza kuwa ufunguaji na usafishaji wa mitaro ni miongoni mwa hatua muhimu zinazotekelezwa ili kuhakikisha maji yanapata njia ya kupita na hivyo kupunguza uwezekano wa mafuriko na madhara mengine.
Aliwataka wananchi kushirikiana na viongozi kwa kuhakikisha mitaro na njia za maji zinakuwa wazi, pamoja na kutoa taarifa kuhusu maeneo yanayoweza kuwa hatarishi ili hatua zichukuliwe kwa wakati kwani zoezi la ukaguzi ni endelevu
Ziara hiyo ilishirikisha viongozi wa Kanda Namba Sita kubaini maeneo yanayoweza kukumbwa na changamoto za maji, ikiwemo maeneo yanayotuamisha maji pamoja na mitaro inayohitaji kufunguliwa na kusafishwa ili kurahisisha mtiririko wa maji wakati wa mvua.
WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amesema Mkoa wa Pwani umewekwa kuwa kituo kikuu cha kuhifadhi vifaa vya dharura vitakavyotumika kukabiliana na athari za mvua za El Nino.
Amebainisha vituo vingine vimewekwa katika Kanda ya Kati-Dodoma, Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini, huku Pwani ikiwa kituo kikuu cha kuhifadhi vifaa hivyo.
Ulega ameeleza hayo alipowasili mkoani Pwani kwa ajili ya kutekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kujiandaa mapema kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo.
Amesema vifaa vilivyohifadhiwa Pwani, vikiwemo makaravati ya chuma, vikapu vya mawe na madaraja ya chuma, vinapaswa kuwa tayari kutumika wakati wowote, huku akisisitiza ukaguzi na usafishaji wa mitaro, makaravati na madaraja ili kuhakikisha maji yanapita kwa uhuru na kuzuia barabara kukatika.
Ulega ameiagiza Wakala wa Barabara Tanzania, TANROADS, na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini, TARURA, kuhakikisha wanakagua madaraja na mitaro yote nchini, kuzibua mitaro pamoja na makaravati ili kuruhusu maji kupita kwa urahisi.
Aidha, amezitaka TANROADS na TARURA kufanya tathmini za mara kwa mara katika maeneo hatarishi, akisisitiza tathmini hizo kufanyika kila wiki ili kuongeza nguvu katika maeneo ambayo yanaweza kuzidiwa na mvua na kuhakikisha hakuna barabara inayofungwa.
Katika hatua nyingine, amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani kusimamia wakandarasi ambao hawajalipwa, huku akiwataka wakandarasi kuendelea na utekelezaji wa majukumu yao na kutoa ushirikiano katika kipindi hiki cha maandalizi.
Meneja wa TANROADS Pwani, Mhandisi Joel Mwambungu, amesema wamejipanga katika mikoa yote 26 inayosimamiwa na TANROADS, ikiwemo kusafisha madaraja, mitaro na makaravati.
Ameeleza eneo la Ruvu Chini na Daraja la Mto Mpiji ni miongoni mwa maeneo yanayofanyiwa kazi, ambapo wanaendelea kusafisha kingo za mto ili kuruhusu maji kupita kwa kiwango kilichosanifiwa.
Mwambungu amesema vifaa vilivyopo ni pamoja na makaravati ya chuma yenye urefu wa mita 5,638, sawa na makaravati 568, pamoja na vikapu vipande 4,240, ambavyo vitatumika endapo barabara au madaraja yatapata hitilafu.
Amesema pia kuna madaraja makubwa saba, karavati za plastiki zenye urefu wa mita 1,200, sawa na karavati 120, pamoja na karavati za chuma zenye urefu wa mita 1,500, sawa na karavati 150.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, ametoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari katika maeneo wanayoishi, akiwataka wanaoishi mabondeni kuondoka ili kujikinga na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.











.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)





.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)








