WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Mwigulu  Nchemba, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kukuza vipaji vya vijana kupitia uwekezaji katika sekta ya michezo na ujenzi wa miundombinu ya kisasa.

Akizungumza usiku wa kuamkia  leo,  Julai 31 2026 wakati  tamasha la mchezo wa Masumbwi “Knockout ya Mama Season 9” liliofanyika katika ukumbi wa The super Dome  Masaki jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu amesisitiza mpango wa  Serikali kujenga arena kubwa ya kisasa itakayokuwa kitovu cha matukio mbalimbali ya michezo na burudani nchini.

Amesema Rais  Samia Suluhu Hassan anaendelea kuunga mkono juhudi za vijana na wadau wa michezo nchini, huku Serikali ikiendelea kushirikiana kwa karibu na sekta binafsi katika kuimarisha maendeleo ya michezo na kuibua vipaji.




 KUNA wakati kama binafamu wenye akili timamu lazima tutafakari mambo yanayoendelea nchini na kwa siku ya leo tujadili kidogo kuhusu michango ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA).


Ndio lazima tujadili maana imekuwa gumzo kila kila kona, sio kwasababu michango inadaiwa kutafunwa na baadhi ya viongozi wa Chama hicho, hapana.Nazungumzia kuhusu kusuasusa kwa michango yenyewe.

Ni kama wachangiaji wameshutuka kwamba fedha wanazotoa zinaliwa na wajanja wachache lakini kubwa zaidi waliokuwa wanakichangia kwa muda mrefu wakiwemo wafanyabishara wameona chama hicho kimepoteza muelekeo,hakina mvuto.

Ile Kampeni ya Tonetone ya kuchangia CHADEMA imedoda kabisa .Na hivi karibuni tumesikia tuhuma za michango kutafunwa na wachache.

Hata hivyo katika hili la michango ya CHADEMA kuonekana inasuasua ni vema kwanza tukarudi mwanzo kule wakati Chama hicho kimeanza mwaka 1992 baada ya kuanza kwa Mfumo wa Vyama vingi nchini Tanzania.

Wakati chama hicho kinaanza waanzilishi wake walikuwa mchanganyiko wa wanasiasa, wanaharakati, watu maarufu na wa sekta binafsi waliotaka mfumo wa kisiasa unaoweka msisitizo katika uwajibikaji na uhuru wa kiuchumi.

Miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa wakatiCHADEMA inaanza walikuwepo akina Edwin Mtei(sasa marehemu)Mwanasheria mashuhuri Bob Makani na wengine wengi.Hata Ndesamburo naye ni miongoni mwao.

Ukweli watu hao wa mwanzo kabisa hawakuwa wanamapinduzi, bali walikuwa wanakapitalisti waliochoshwa na uendeshaji wa Serikali ya wakati huo.

Kutokana na mipango na mikakati ya CHADEMA kwa wakati ule ilishuhudiwa wafadhili wa awali wengi wao wakiwa ni wafanyabiashara na sekta binafsi.

Katika miaka ya mwanzo, CHADEMA ilivutia msaada wa watu wenye uwezo na wafanyabiashara waliotaka sera zinazorahisisha biashara na uwekezaji.

Michango hiyo mara nyingi haikuonekana hadharani; ilitolewa kwa njia za ndani au kwa msaada wa kimkakati ili kuimarisha miundombinu ya chama na kampeni za kukujenga chama mikoani. Kujiunga kwa viongozi wenye umaarufu kuliongeza mvuto wa chama kwa wafadhili na wafuasi.

Pia ilikuwa ni jambo la kawaida kusikia Mfanyabiashara maarufu Mustafa Jafari Sabodo (sasa marehemu) akitoa mamilioni ya fedha kwa Chama hicho na ndoto yake ilikuwa ni kuona Chama hicho kinakuwa na Ofisi yake.

Ndoto ya Sabodo haikutimia maana licha ya kutoa zaidi ya milioni 100 hazikutumika kujenga ofisi.Sijui zilitumika wapi? Zile fedha hazikujulikana zilikwenda wapi.CHADEMA bwana wajanja wajanja sana.

Ukweli katika miaka 1995 mpaka miaka ya 2010 CHADEMA ilikua kwa kasi kubwa na mwaka 2014 baada ya Edward Lowassa alipotangaza kujiunga na Chama hicho kikakua zaidi.Tukashuhudia gumzo kubwa kwa chama hicho na umaarufu mkubwa katika historia ya siasa za vyama vingi nchini Tanzania.

Kujiunga kwake Lowasa kulionyesha uwezo wa CHADEMA kuvutia viongozi wa ngazi ya juu kutoka upande wa pili wa kisiasa. Mabepari walifungua mikoba yao, wakimimina fedha nyingi kuunga mkono chama.

Hata hivyo, kila kitu kilibadilika baada ya kuingia kwa uongozi mpya wa Tundu Lissu. Uongozi wake na wa viongozi wenzake wa kisiasa uliashiria mabadiliko ya mkazo wa chama kuelekea masuala ya haki za kiraia, uwazi, na masuala ya kijamii.

Hiyo ilileta mabadiliko ya mtazamo wa chama ambayo baadhi ya wafadhili waliona hayakuwa ya kuendeleza maslahi ya kiuchumi.

Pamoja nayo hayo tangu CHADEMA ilipofanya mabadiliko ya uongozi wake wa ngazi za kuu tunashuhudia athari na changamoto za mabadiliko hayo.

Mabadiliko hayo ya mwelekeo wa chama yameathiri pia chanzo cha ufadhili kwa operesheni za CHADEMA kwenye nyanja kadhaa. Ni wazi CHADEMA imepoteza uaminifu wa wafadhili wa sekta binafsi.

Haswa kundi la wafanyabiashara wanaotaka sera za soko huria wamesita kuendelea kutoa michango baada ya chama kuoonyesha msimamo wakisoshalisti au kinachokosoa tu sekta binafsi bila kujaribukuelewa changamoto zao.

Upungufu wa rasilimali za kampeni umeonekana wazi, bila michango kubwa, chama kinakosa uwezo wa kuendesha kampeni za kitaifa, kulipa miundombinu ya chama, na kumudu gharama za kisheria na mahitaji ya wanachama.

Hizo ni baadhi ya atahari za madiliko yaliyotokana na chama kilijikita na wanaharakati ambao wanaamini"wafanyabiashara hawana shida." Mabadiliko ya mwelekeo bila mkakati wa kuunganisha tabaka tofauti za wafuasi(wafanyabiashara, wanaharakati, wanasiasa wa jadi) umeacaha pengo la utekelezaji.

CHADEMA sasa inahitaji sera zinazoonyesha jinsi masuala ya kijamii (kama kupunguza umaskini) yanavyoweza kuendana na sera za kukuza biashara ili kuwashirikishawafadhili na wafuasi kwa pamoja.

Wafanyabiashara na wawekezaji wanaotazama uongozi huo wanaona chama kinachobeza matatizo yao na kuwafanya kuwa maadui. Kwa nini mfanyabiashara awekeze kwenye chama kinachomtukana?

Kwanini awekeze kwenye Chama ambacho kinahubiri shari badala ya heri.Kwanini Mfanyabiashara awekeze katika chama ambacho kutwa kuchwa kiko barabarani kina uhubiri chuki na mipasuko katika jamii?


Na Mwandishi Wetu
MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP-CENTRE), David Kafulila, amesema kuwa mfumo wa ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) si jambo la hiari au la kufikirika tu, bali ni mkakati madhubuti wa kimfumo unaolenga kuikomboa nchi kiuchumi na kuongeza ufanisi wa utendaji katika sekta mbalimbali.

Kafulila alibainisha hayo Alhamisi, Julai 30, 2026, wakati akihutubia wataalamu, wasomi, na wadau wa usafirishaji katika Kongamano la Mwaka la Chama cha Wataalamu wa Lojistiki na Usafirishaji Tanzania (CILT), lililofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Mabibo jijini Dar es Salaam.

Akichambua umuhimu wa mfumo huo, Kafulila alieleza kuwa mataifa mengi duniani yanageukia mifumo ya ubia kwa sababu kuu tatu ambazo ni kuvuta mitaji kutoka sekta binafsi, kuingiza teknolojia ya kisasa, na kuimarisha ufanisi wa usimamizi (management efficiency).

Alisisitiza kuwa uchumi wa sasa unategemea zaidi maarifa na ujuzi kuliko rasilimali za asili pekee.

"Ushirikiano wa kiuchumi kati ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) si jambo la hiari au la kuota, bali ni mkakati wa makusudi na wa kimfumo wa kuikomboa nchi kiuchumi na kuongeza ufanisi wa utendaji,” alisema.

“Serikali haiwezi kujenga kila kitu kuanzia bandari, reli, barabara, masoko na stendi, na wakati huo huo ikawa na fedha za kujenga watu wenye ubora wa kushindana duniani," aliongea.

Alibainisha kuwa kupitia PPP, serikali inajipa nafasi ya kuachia sekta binafsi maeneo ya kibiashara ili kuokoa fedha ambazo zinatumika kwenye uwekezaji mkubwa wa rasilimali watu kupitia elimu bora.

Katika kongamano hilo, Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba, alijibu ombi la Mkuu wa Chuo cha NIT, Dk Prosper Mgaya, kuhusu changamoto ya ukosefu wa mikopo kwa wanafunzi wanaochukua kozi za muda mfupi za kiufundi.

Dk Nchemba aliwahakikishia washiriki kuwa serikali imepokea ombi hilo kwa uzito mkubwa, akisema kuwa utaalamu katika fani za lojistiki na ufundi ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

"Serikali imepokea kwa uzito changamoto hiyo. Kozi za ufundi na lojistiki zinahitaji utimamu wa akili na uwezo wa mwanafunzi bila kujali hali ya kiuchumi ya familia anayotoka,” alisema Dk Nchemba.

“Serikali itaangalia mbinu mbadala ya kuwatengenezea mfumo rafiki wanafunzi wa kozi hizo za ufundi ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo," alisisitia.
Dkt. Nchemba alitolea mfano wa mfumo wa Samia Scholarship ambao umekuwa ukizingatia ufaulu na uwezo wa kitaaluma badala ya kigezo cha umaskini pekee, akiahidi kuwa serikali itaendelea kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu ya ufundi nchini.

Kongamano hilo limeonekana kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha sekta ya usafirishaji na mikakati mipana ya kiuchumi ya nchi kwa miaka 25 ijayo.


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imeiagiza Wizara ya Uchukuzi kuharakisha taratibu za kuwasilisha Waraka wa Baraza la Mawaziri ili kuwezesha kuanzishwa kwa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Lojistiki na Usafirishaji, hatua inayolenga kuimarisha ubora, weledi na uwajibikaji wa wataalamu wa sekta hiyo nchini.

Akifungua Kongamano la Wataalamu wa Lojistiki na Usafirishaji katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jijini Dar es Salaam leo, Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imepokea mapendekezo ya wadau wa sekta hiyo na itaendelea kuyafanyia kazi, ikiwemo kushirikiana na Ofisi ya Rais–Utumishi na TAMISEMI kutathmini uanzishwaji wa vitengo maalumu vya maafisa wa lojistiki na usafirishaji katika taasisi za umma.

Dkt. Nchemba amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya uchukuzi na kuimarisha Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kwa kuongeza bajeti na kuhakikisha fedha zilizoidhinishwa zinatolewa kwa wakati. Pia amesema itaendelea kutathmini uwezekano wa kuwajumuisha wanafunzi wa programu maalumu za chuo hicho katika mfumo wa mikopo ya elimu ya juu kadri hali ya kifedha itakavyoruhusu.

Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, amesema mafanikio ya sekta ya uchukuzi yametokana na uwekezaji wa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika reli ya kisasa (SGR), bandari, viwanja vya ndege na vyuo vya mafunzo, hatua zilizoongeza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa na kuongeza uwezo wa bandari za Dar es Salaam, Tanga na Mtwara kuhudumia mizigo.

Kihenzile amesema mapato yatokanayo na maboresho hayo yamewezesha Serikali kuendelea kuimarisha NIT kwa kujenga mabweni, kununua vifaa vya kisasa vya kufundishia na kuboresha miundombinu ya mafunzo ya marubani, wahandisi wa ndege na wataalamu wengine wa lojistiki na usafirishaji.

Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Wataalamu wa Lojistiki na Usafirishaji Tanzania (TALTA), Alphonce Mwingila, ameiomba Serikali kuweka mkakati madhubuti wa kuboresha mfumo wa ukaguzi na matengenezo ya magari ya mafunzo ya udereva ili kupunguza gharama zinazowakabili wamiliki wa shule za udereva.

«"Kuna msemo wa Kiingereza unasema, If you fail to plan, you are planning to fail. Tunahitaji mipango mizuri katika eneo hili. Baadhi ya magari yanapotoka TEMESA baada ya kufanyiwa ukaguzi yanakuwa na matatizo mapya kabisa, hivyo mmiliki analazimika kurudi tena kuyafanyia matengenezo na gharama zinakuwa kubwa kuliko uhalisia," amesema Mwingila.»

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Dkt. Prosper Mgaya, amesema ziara ya Waziri Mkuu chuoni hapo imeandika historia kwa kuwa ni mara ya kwanza kwa Waziri Mkuu kutembelea taasisi hiyo tangu ilipoanzishwa. Amesema mafanikio hayo yametokana na uwekezaji wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ikiwemo kutenga takribani Sh bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Umahiri cha Mafunzo ya Usafiri wa Anga.

Dkt. Mgaya amesema NIT imeendelea kujiimarisha kwa kutoa mafunzo katika modi zote tano za usafiri na kuboresha mitaala yake ili kuzalisha wataalamu wenye ushindani ndani na nje ya nchi, huku baadhi ya wahitimu wake wakiajiriwa na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na Air Dubai.

Aidha, amesema mafunzo ya urubani yameimarika baada ya Serikali kununua ndege za mafunzo, ambapo hadi sasa wanafunzi wanne wamehitimu urubani na wanane wako katika hatua ya kuruka peke yao (solo). Ameongeza kuwa NIT itaendelea kushirikiana na TALTA kuboresha mitaala ili iendane na mahitaji ya soko la ajira.Nikiihariri zaidi, inaweza kufupishwa hadi mtindo wa habari ya gazeti wenye paragrafu 8 bila kupoteza hoja kuu.













 

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Dellilah Kimambo, kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za afya na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha mfumo wa malipo ya huduma ili kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa urahisi, haraka, kwa ufanisi na kuondoa malalamiko ya wananchi.

Katika kikao hicho, Dkt. Magembe amesisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma za afya, akimtaka Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha mifumo ya TEHAMA ya hospitali inaendelea kuimarishwa ili kurahisisha mchakato wa malipo ya huduma, kuongeza uwazi kwa wananchi, kupunguza usumbufu na muda wa kusubiri kwa wagonjwa, pamoja na kuondoa udanganyifu.

“Mwananchi apate taarifa za malipo anayotakiwa kufanya kiganjani mwake kupitia simu ili kabla ya kulipa ajihakikishie kama malipo hayo ni sahihi au hapana”, amesema Dr Grace. 
Amemwelekeza Mkurugenzi wa Muhimbili kuimarisha usimamizi wa huduma za afya kupitia viongozi walioko chini yake wakiwemo wakurugenzi, mameneja na wasimamizi wote na endapo kutakuwa na watumishi wowote wasiowajibika achukue hatua zilizo chini ya mamlaka yake na mengine yanayohitaji Wizara kufanyia kazi, ayawasilishe ili hatua stahiki zichukuliwe. 

Amepongeza maboresho yanayoendelea kufanyika ikiwemo watumishi wanaofanya kazi kwa kujituma na weledi mkubwa.


Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Julai 29, 2026

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza rasmi kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, yakilenga kuimarisha weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari wa Bongo FM jijini Dar es Salaam, redio dada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya JAB, Tido Mhando, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kuelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kwa kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji.

“Mafunzo haya ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari. Leo tumeanza rasmi na waandishi wa habari wa Bongo FM, tutaendelea kwa vyombo vingine pia kwa sababu, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu. Hivyo, mafunzo haya yawe fursa ya kujenga uwezo na kuweka msingi imara wa kukuza na kulinda taaluma ya uandishi wa habari kwa kuongeza maarifa na weledi,” amesema Wakili Kipangula.

Akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, historia na uanzishwaji wake, katika mafunzo hayo yaliyoanza leo tarehe 29 Julai, 2026 katika ukumbi wa Bodi, Wakili Kipangula amesema sheria hiyo imeweka msingi wa kuimarisha taaluma ya habari kwa kubainisha viwango vya weledi, maadili na uwajibikaji

Amesisitiza kuwa JAB itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa kuzingatia haki, uwazi na kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari, huku ikihakikisha taaluma ya habari inalinda maslahi ya umma..

Aidha, amewataka waandishi wa habari kuzingatia sheria na maadili katika kila hatua ya ukusanyaji, uchakataji na usambazaji wa habari ili kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukiukaji wa taaluma.

Amesema kuzingatia misingi hiyo kunajenga weledi, kunalinda heshima ya taaluma na kuimarisha imani ya jamii kwa vyombo vya habari.
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.

Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

"Mafunzo haya yametupatia maarifa muhimu yatakayotusaidia kutekeleza majukumu yetu kwa kuzingatia maadili, sheria na viwango vya taaluma ya uandishi wa habari. Tunaamini yatachangia kuboresha utendaji wetu na kuongeza uwajibikaji katika kuhabarisha umma," wamesema washiriki hao.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imewahimiza wazabuni na wadau wa ununuzi wa umma kutumia Moduli ya Kupokea na Kushughulikia Malalamiko na Rufaa katika mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) kuwasilisha malalamiko na rufaa zao PPAA pindi wanapoona hawakutendewa haki katika michakato ya ununuzi wa umma.

Akizungumza na waandishi wa Habari pembezoni mwa Kongamano la kumi la ununuzi wa Umma la mwaka 2026 linaloendelea Jijini Arusha kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma PPAA, Bw. Nelson Kessy amesema kuanza kwa matumizi ya Moduli hiyo kuna faida nyingi kama vile kuokoa muda na gharama.

“Faida nyingine za wazabuni na taasisi nunuzi kutumia moduli ni pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji pamoja na kuwezesha utunzaji wa kumbukumbu sahihi za malalamiko na rufaa zinazowasilishwa na wazabuni, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa uamuzi,” amesema Bw. Kessy
Bw. Kessy ameongeza kuwa Mamlaka ya Rufani inawaelekeza wazabuni wote wa ndani na nje ya nchi kutumia Moduli ya kuwasilisha Malalamiko na Rufaa kwa kuzingatia Sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kanuni zake pindi wanapoona hawakutendewa haki katika zabuni walizoomba.

Katika hatua nyingine, Bw. Kessy amesema kuwa PPAA inatoa huduma ya Mkutano kwa njia ya Mtandao “Video Conference” ambapo hutumika kusikiliza mashauri ya wazabuni walioshindwa kufika moja kwa moja katika Ofisi za PPAA kwa ajili ya kusikiliza mashauri yalilowasilishwa mbele yake.

Huduma ya Mkutano kwa njia ya Mtandao imetoa fursa ya kuwasikiliza wazabuni walioshindwa kufika PPAA kutokana na sababu mbalimbali na kuiwezesha Mamlaka ya Rufani kutekeleza jukumu lake la msingi la utatuzi wa migogoro itokanayo na michakato ya ununuzi wa Umma. 

“Tangu kuanza kwa matumizi ya ‘video conference’ tayari PPAA imewasikiliza wazabuni mbalimbali kutoka katika mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria, Poland, India na China,” amesema Bw. Kessy. 

Kadhalika, Mamlaka ya Rufani inatarajia kuunganisha Moduli ya Malalamiko na Rufaa na mfumo wa Mahakama ya Tanzania ili kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma ikiwa ni njia mojawapo ya kuimarisha matumizi ya teknolojia katika sekta ya ununuzi wa umma. 

Naye mzabuni Peter Sarungi kutoka makundi maalum alisisitiza sekta ya makundi maalum ipewe kipaumbele zaidi katika uombaji wa zabuni na kufuatilia taasisi zilizotangaza zabuni ili wapewe taarifa kama wamepata zabuni au la ili kuwawezesha kujikwamua kiuchumi ikiwemo kutumia Moduli ya PPAA. 

Matumizi rasmi ya moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST yalianza mwezi Februari, 2025.



 

 

 Na.Mwandishi Wetu-Babati, Manyara

 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kaskazini imeendesha semina ya kuwajengea uwezo Maafisa wa Huduma kwa Wateja, Mahusiano na Sheria kutoka TANESCO na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira za Kanda ya Kaskazini kuhusu huduma kwa wateja na uzingatiaji wa matakwa ya kisheria.

Akifungua semina hiyo katika Hoteli ya White Rose, Babati, Meneja wa EWURA Kanda ya Kaskazini, Bw. George Mhina, aliwasisitiza washiriki kuyafahamu vyema majukumu yao ili waweze kutoa majibu sahihi, ya wakati na yanayozingatia sheria, hivyo kuboresha huduma kwa wateja.

Kwa niaba ya washiriki, Bi. Devotha Mayala kutoka Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tanga na Bw. Samwel Mandari kutoka TANESCO waliishukuru EWURA kwa mafunzo hayo, wakieleza kuwa yamewaongezea uelewa na uwezo wa kuwahudumia wateja kwa weledi zaidi.

Semina hiyo ni sehemu ya juhudi za EWURA za kuimarisha uwezo wa watoa huduma na kulinda haki za watumiaji wa huduma za nishati na maji kupitia Udhibiti wa Haki kwa Matokeo Chanya.

Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Dodoma, Joseph Chitinka, ameviagiza Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) pamoja na Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Dodoma (DORECU) kuandaa mpango kabambe wa ununuzi wa mbegu bora za ufuta ifikapo Agosti 5, 2026, ili kuongeza ushindani wa mazao ya wakulima katika soko la kimataifa.

Akizungumza Julai 30, 2026, wakati wa kufunga mafunzo maalum ya siku tatu kwa viongozi wa AMCOS, wajumbe wa bodi na viongozi wa DORECU jijini Dodoma, Chitinka alisema Mkoa wa Dodoma umejipanga kuhamasisha uzalishaji wa ufuta mweupe wenye thamani kubwa sokoni badala ya kuendelea kutegemea aina za ufuta wa rangi zinazolimwa kwa wingi hivi sasa.

Aidha, aliwataka viongozi wa vyama vya ushirika kuhakikisha matumizi yote ya fedha yanaidhinishwa na maafisa ushirika pamoja na Ofisi ya Mrajisi, huku mikataba yote ya watoa huduma ikifuata taratibu za kisheria ili kuzuia vitendo vya udanganyifu na ubadhirifu wa fedha za wanachama.

Chitinka amesisitiza umuhimu wa kufuata sheria za manunuzi, kuandaa mipango ya kimkakati na kuhakikisha AMCOS zinafanya kazi mwaka mzima badala ya kuwa vyama vya msimu, amewahimiza viongozi kushirikiana na jamii kuongeza wanachama, kuimarisha uzalishaji wa mazao na kutumia kikamilifu mfumo wa stakabadhi za ghala.

Kuhusu uchaguzi wa viongozi wa ushirika, alisema ni wakati wa kutoa nafasi kwa viongozi wapya wenye sifa na kuacha mfumo wa viongozi kukaa madarakani kwa muda mrefu, ameeleza kuwa mchakato wa uchaguzi utaanza mwezi Agosti baada ya maadhimisho ya Nanenane.

Kwa upande wa usimamizi wa fedha, amesema matumizi yote ya fedha za mfumo wa stakabadhi za ghala yatapaswa kupitishwa kwenye bajeti za mwaka ili kuondoa mianya ya matumizi mabaya, amevitaka vyama vilivyoshiriki minada msimu uliopita kuhakikisha vinalipa tozo zote zinazodaiwa kwa wakati.

Naye Mrajisi Msaidizi kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Richard Izengo, amesema mafunzo hayo yamelenga kuimarisha usimamizi, ukaguzi na uwajibikaji wa vyama vya ushirika, amesisitiza umuhimu wa kuandaa hesabu na kuziwasilisha kwa mkaguzi wa nje ili kuongeza uwazi kwa wanachama.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa DORECU, David Mtimbi Mwaka, amesema mfumo wa stakabadhi za ghala Una matarajio ya mafanikio makubwa zaidi katika misimu ijayo, kufuatia kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti madalali wa mazao Mkoani Dodoma.





Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Dodoma (DORECU) kimefanikiwa kuuza zaidi ya tani 11,000 za ufuta na kuwalipa wakulima zaidi ya shilingi bilioni 25, huku kikitangaza kuwa kinajiandaa kuanza mauzo ya mazao ya pamba na dengu hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhitimisha mafunzo ya siku tatu kwa wanaushirika 80 kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Dodoma, Meneja Mkuu wa DORECU, Feruzi Hassan Mwindi, alisema mafunzo hayo yalilenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi za ghala kwa msimu uliopita, kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu na kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya ushirika katika usimamizi wa shughuli zao.

Mwindi alisema mafunzo hayo yatawanufaisha wakulima wengi ambao ni wageni katika matumizi ya mfumo wa stakabadhi za ghala, kwa kuwa yatawawezesha kuhifadhi kumbukumbu na takwimu kwa usahihi pamoja na kuendesha vyama vyao kwa ufanisi zaidi katika misimu ijayo.

Makamu Mwenyekiti wa DORECU, David Mtimbi Mwaka, alisema wanachama wa mkoa wa Dodoma wamenufaika na mfumo wa stakabadhi za ghala ambao umechangia kudhibiti madalali (aggregators), akieleza kuwa mafanikio yaliyopatikana yanatoa matumaini ya kufanya vizuri zaidi katika msimu ujao.

Naye Mrajisi Msaidizi anayesimamia vyama vya ushirika visivyo vya kifedha kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Richard Izengo, alisema mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa kila mwaka wa kuimarisha usimamizi na ukaguzi wa vyama vya ushirika.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuandaa na kuwasilisha hesabu kwa mkaguzi wa nje ili taarifa za utekelezaji wa shughuli za vyama ziwasilishwe kwenye mikutano mikuu ya mwaka na kuongeza uwajibikaji kwa viongozi na wanachama.







Top News