Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma, tarehe 10 Agosti, 2026.
Katibu NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Kenani Kihongosi amesisitiza kuwa Vijana ndio walinda Nchi hivyo wanatakiwa kuilinda amani ya nchi ili waweze kufanya shughuli za uzalishaji kwa maendeleo ya Taifa na familia zao.
Ndugu Kenani ameyasema hayo leo tarehe 10 Agosti 2026 wakati akitoa mada kwenye Mafunzo ya Uongozi wa Seneti za Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Chuo cha Mafunzo Ihemi mkoani Iringa.
Pia, ametumia jukwaa hilo kukemea lugha chafu zinazotolewa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mitandao ya kijamii na kuwasihi vijana kuwa mstari wa mbele kumtetea Rais na wasikae kimya.
Aidha ametoa wito kwa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ndani na nje ya Tanzania kulipa Ada ya uanachama akieleza uhai wa Chama cha Mapinduzi (CCM) unatokana na wanachama kulipia ada.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wawake (UWT) Wilaya ya Kibahaa mjini Elina Mgonja Katika kuuunga juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwakomboa wanawake kiuchumi ameamua kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vitendo kwa wanawake wapatao 400 wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuondokana na wimbi la umasikini.
Akizungumza katika ziara yake maaalumu ya kikazi yenye lengo la kuwatembelea wanawake wa (UWT) katika kata mbali mbali kwa ajili ya kuwapa maarifa na ujuzi na kujifunza jinsi ya kutengeneza bidhaa za aina tofauti ambazo zitawapa fursa ya kujiajiri wao wenyewe na kuondokana na kuwa tegemezi kila kukicha.
Elina amebainisha kuwa amefanya ziara hiyo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake ambayo aliitoa ya kuwasaidia wanawake wa UWT kutoka kata zote 14 zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kwamba mafunzo hayo ambayo ameamua kuyatoa bure bila malipo yoyote yatakuwa ni mkombozi mkubwa katika kujikwamua kiuchumi,
Nao baadhi ya wanawake ambao wamepata mafunzo hayo akiwemo Mwajuma Makuka wamesema kwamba maffunnzo hayo yataweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kuondokana na kuwa tegemezi na kwamba watakwenda kuyafanyia kazi kwa hali na mali kwa lengo la kuweza kuondokana na wimbi la umasikini.
"Kwa kweli tunapenda kumshukuru kwa dhati Mwenyekiti wetu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonjwa kwa kuweza kufanya ziara hii na kuja kutupa elimu na mafunzo ya ujasiliamali na tumeweza kujifunza mambo mbali mbali ikiwemo kutengeneza bidhaa kama vile kutengeneza batiki, sabuni za kufulia, sabuni za kuogea pamoja na kupata ujuzi ambao tutakwenda kuufanyia kazi katika kutekeleza majukumu yetu,"amebainisha Mwajuma.
Mwenyekiti huyo wa UWT anaendelea na ziara yake ya kikazi ambapo hadi sasa ameshatembelea kata 7 ambazo ni Msangani, Mkuza, Tumbi, Maili moja, Kongowe, Kibaha pamoja na Kata ya Misususugu ambapo jumla ya wanawake 400 wameweza kunufaika na mafunzo hayo ya ujasiriamali kwa vitendo.
Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani Ocean Road imeanza kutekeleza zoezi la utoaji wa elimu kuhusu saratani pamoja na vipimo vya uchunguzi wa awali wa saratani kwa watumishi wa Wizara hiyo ili kuongeza uelewa wa namna ya kujikinga, kutambua dalili za awali na kuchukua hatua stahiki kukabiliana na ugonjwa huo.
Zoezi hilo litakalohusisha utoaji wa elimu kuhusu saratani mbalimbali, ikiwemo saratani ya matiti, tezi dume na shingo ya kizazi, pamoja na vipimo vya awali linatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 10 hadi 14 Agosti 2026, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Mtumba, jijini Dodoma.
Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, alisema ni muhimu kwa watumishi kufuatilia elimu ya afya ya saratani ili kuwa na uelewa wa kutosha kukabiliana na ugonjwa huo.
‘‘Ni muhimu kuwa na uelewa sahihi kuhusu saratani, hususan kwa kuzingatia kwamba utambuzi wa ugonjwa huo katika hatua za awali una nafasi kubwa katika matibabu na kuokoa maisha’’’ Alisema Bw. Sendo.
Aliwasisitiza watumishi wa Wizara hiyo kutumia fursa hiyo kupata elimu pamoja na kufanya vipimo vya awali vinavyotolewa ili kufahamu hali zao za afya.
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Saratani, Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Frank Ruta, aliwahimiza watumishi hao kutopuuza mabadiliko au dalili zisizo za kawaida katika miili yao na kufika katika vituo vya afya kwa ajili ya uchunguzi na ushauri wa kitaalamu.
Alisema utambuzi wa saratani katika hatua za awali unaongeza nafasi ya mafanikio ya matibabu, hivyo jamii inapaswa kujenga utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara na kuchukua hatua za mapema katika kuzuia na kukabiliana na saratani.
Dkt. Ruta alisemna elimu hiyo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uelewa wa watumishi na jamii kwa ujumla kuhusu afya na kuwahamasisha kuchukua hatua za mapema katika kuzuia na kukabiliana na saratani.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akizungumza katika zoezi la utoaji wa elimu kuhusu saratani pamoja na vipimo vya uchunguzi wa awali wa saratani kwa watumishi wa wizara hiyo, linalofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Mtumba, jijini Dodoma, kuanzia tarehe 10 hadi 14 Agosti 2026.

Afisa Utumishi Mwandamizi, Wizara ya Fedha, Bw. Salum Said, akifafanua jambo katika zoezi la utoaji wa elimu kuhusu saratani pamoja na vipimo vya uchunguzi wa awali wa saratani kwa watumishi wa Wizara hiyo, linalofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Mtumba, jijini Dodoma, kuanzia tarehe 10 hadi 14 Agosti 2026.


Daktari Bingwa wa Saratani kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Frank Ruta, akitoa elimu kuhusu kinga, utambuzi na matibabu ya saratani kwa watumishi wa Wizara ya Fedha, katika zoezi linalofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Mtumba, jijini Dodoma, kuanzia tarehe 10 hadi 14 Agosti 2026.


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakifuatilia elimu iliyokuwa inatolewa na wataalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road, kuhusu namna ya kujikinga, kutambua dalili za awali na kuchukua hatua stahiki katika kukabiliana na ugonjwa wa saratani, katika zoezi linalofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Mtumba, jijini Dodoma, kuanzia tarehe 10 hadi 14 Agosti 2026.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)
Na. Josephine Majura na Asia Singano, WF – Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema Serikali itaendelea kuimarisha mifumo ya bajeti na usimamizi wa fedha za umma kwa kuzingatia usawa wa kijinsia, hatua inayolenga kuhakikisha rasilimali za Serikali zinatumika kwa ufanisi katika kuchochea maendeleo jumuishi.
Mhe. Balozi Omar (Mb), aliyasema hayo jijini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, Bi. Julia Broussard, katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square jijini Dodoma.
Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya Wizara ya Fedha na UN Women, hususani katika utekelezaji wa Bajeti inayozingatia Masuala ya Kijinsia (Gender-Responsive Budgeting – GRB).
‘’Serikali ya Tanzania, inatambua umuhimu wa kuzingatia masuala ya kijinsia katika sera za fedha, mchakato wa uandaaji wa bajeti, ugawaji wa rasilimali na ufuatiliaji wa utekelezaji wa programu za Serikali ili kuhakikisha mipango ya kitaifa inachangia katika kujenga uchumi jumuishi na wenye usawa’’ alisema Mhe. Balozi Omar (Mb).
Alisema Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027, imezingatia usawa wa jinsia huku Serikali ikiona umuhimu wa kuandaa Taarifa Maalum ya Bajeti inayozingatia Masuala ya Kijinsia (Gender Budget Statement) kama sehemu ya mfumo rasmi wa usimamizi wa fedha za umma.
Alibainisha kuwa hatua hiyo inaweka msingi wa kuimarisha Mfumo wa Uandaaji wa Bajeti Unaozingatia Masuala ya Kijinsia (GRB), utakaosaidia kuhakikisha masuala ya kijinsia yanaingizwa kikamilifu katika mipango, uandaaji wa bajeti, ugawaji wa rasilimali na ufuatiliaji wa utekelezaji wa programu za umma.
“Muhimu siyo tu kuangalia kiasi cha fedha kilichotengwa au kutumika, bali pia matokeo yanayopatikana kutokana na rasilimali hizo na kupima matokeo ya matumizi ya fedha za umma’’. Alisema Mhe. Balozi Omar (Mb).
Aliongeza kuwa, katika kuhakikisha rasilimali zinazotengwa kwa ajili ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake zinafuatiliwa kwa ufanisi, mfumo wa Gender Budget Tagging unaopangwa kuanzishwa utakuwa nyenzo muhimu ya kubaini, kufuatilia na kuchambua matumizi ya bajeti yanayolenga masuala hayo.
Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, Bi. Julia Broussard alisema Wizara ya Fedha ina nafasi muhimu katika kuhakikisha Tanzania inapata na kutoa taarifa zinazohitajika kuhusu Kiashiria cha 5.c.1 cha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG 5), kinachopima uwepo wa mifumo ya kufuatilia na kuweka wazi mgao na matumizi ya rasilimali za umma kwa ajili ya kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.
Alisema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Wizara ya Fedha, katika kuimarisha mifumo na uwezo wa kitaasisi unaohitajika ili kuhakikisha masuala ya kijinsia yanaingizwa kikamilifu katika mipango, bajeti na usimamizi wa rasilimali za umma.
Ushirikiano huo unalenga kuimarisha matumizi ya takwimu na taarifa za bajeti katika kufanya maamuzi, kufuatilia rasilimali zinazotengwa kwa masuala ya kijinsia na hatimaye kuhakikisha matumizi ya fedha za umma yanaongeza matokeo chanya kwa wananchi, hususan katika kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.
Kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi Mbalimbali wa Wizara ya Fedha, akiwemo Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Bw. Melckzedek Mbise, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, Bw. Andambike Mololo pamoja na Wataalamu wengine wa Wizara ya Fedha.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiongoza Kikao chake na Ujumbe kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), Ukiongozwa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, Bi. Julia Broussard, ulipomtembelea Ofisini kwake, Treasury Square jijini Dodoma.
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, Bi. Julia Broussard, akizungumza wakati wa kikao na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), hayupo pichani, alipomtembelea Ofisini kwake, Treasury Square jijini Dodoma.
Kikao cha Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Treasury Square jijini Dodoma.
Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Bw. Melckzedek Mbise, (wakwanza kushoto), Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, Bw. Andambike Mololo, (wapili kushoto) pamoja na Wataalamu wengine wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia kikao cha Mhe. Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), hayupo pichani, na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri, Treasury Square jijini Dpodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (watano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (UN Women), nchini Tanzania, Bi. Julia Broussard, (watano kushoto), Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Bw. Melckzedek Mbise, (watatu kulia), Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali, Bw. Andambike Mololo (wa kwanza kulia), Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha, pamoja na wajumbe kutoka UN Women, baada ya kumalizika kikao cha Mhe. Balozi Omar (Mb) na Ujumbe huo.
(Picha na Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini, WF - Dodoma)
MANISPAA ya Iringa imepokea rasmi magari mawili yenye thamani ya Sh milioni 240.6 kwa ajili ya kurahisisha usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji (TACTIC) inayotekelezwa katika manispaa hiyo.
Makabidhiano hayo yamefanyika katika hafla fupi iliyohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamini Sitta, Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Zaina Mlawa, wataalamu wa Manispaa, TARURA pamoja na wadau wanaohusika na utekelezaji wa mradi huo katika viwanja vya manispaa.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Sitta amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa kwa juhudi za kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, huku akiwataka wataalamu kuhakikisha miradi inayotekelezwa kupitia TACTIC inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.
Sitta amesema magari hayo yamenunuliwa na mkandarasi kwa ajili ya shughuli za usimamizi wa mradi na yamekabidhiwa kwa Mhandisi Msimamizi ili kurahisisha ufuatiliaji wa kazi katika maeneo mbalimbali ya mradi.
Amesema baada ya kukamilika kwa mradi, magari hayo yatabaki kuwa mali ya Serikali na kutumika katika shughuli nyingine za Serikali, hivyo akasisitiza umuhimu wa kuyatunza na kuyatumia kwa malengo yaliyokusudiwa.
“Magari haya tunawakabidhi yakiwa mazuri na hali nzuri, yakiwa mapya kwa matumizi tunaomba yawe mazuri ili magari haya yaje kuwa na tija zaidi katika kazi zingine za Serikali,” alisema Sitta.
Aidha Sitta amemtaka Mshauri Elekezi wa mradi kusimamia kwa karibu kazi za mkandarasi ili kuhakikisha Serikali inapata thamani ya fedha na miradi inayokidhi viwango vilivyowekwa.
Mradi wa TACTIC katika Manispaa ya Iringa unahusisha ujenzi wa Soko la Kihesa, Ofisi ya Wahandisi pamoja na uboreshaji wa barabara za Mkimbizi-Bima, Mtwivila, Viziwi na Bontank zenye urefu wa jumla ya kilomita 5.26.
Kwa upande wake Mhandisi wa Manispaa ya Iringa, Rajabu Msangi alisema mradi huo ulianza Novemba 20, 2025 na unatarajiwa kukamilika Februari 11, 2027. Hadi sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 20.5.
Alisema gharama ya kazi zinazofanywa na mkandarasi ni Sh bilioni 20.258, huku gharama ya Mshauri Elekezi ikiwa dola za Marekani 550,397.50.
Katika utekelezaji wa mradi huo, ujenzi wa barabara unahusisha ujenzi wa makalavati sita, ambapo matatu tayari yamekamilika, ujenzi wa mifereji, uwekaji wa lami, taa na alama za barabarani,ujenzi wa Ofisi ya Wahandisi unaendelea, huku katika Soko la Kihesa kazi ikiwa imefikia hatua ya ujenzi wa kuta.
Msangi alisema mradi huo umekumbana na changamoto kadhaa, ikiwemo mvua za Desemba hadi Machi 2026 zilizoathiri baadhi ya kazi za udongo na tabaka za barabara, pamoja na kuchelewa kupatikana kwa baadhi ya wataalamu na kutokuwapo kwa mitambo ya kutosha.
Hata hivyo, amesema mkandarasi amechukua hatua za kukabiliana na changamoto hizo kwa kupanga upya ratiba ya kazi na kuongeza kasi ya utekelezaji ili kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya muda uliopangwa.
Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Zaina Mlawa, amesema utekelezaji wa miradi hiyo ni sehemu ya juhudi za kuboresha huduma na miundombinu katika Manispaa ya Iringa, akiwataka wadau wote kushirikiana kuhakikisha malengo ya mradi yanafikiwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika makazi yake, Kawe Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 10 Agosti 2026.













.jpeg)






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)









.jpg)



.jpeg)





.jpeg)
