Na Janeth Raphael - MichuziTv
Ikiwa taifa liko katika juhudi za kujenga jamii yenye maadili, amani, mshikamano na uwajibikaji, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limetakiwa kuendelea kutumia nafasi yake katika kuimarisha misingi hiyo na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rose Mary Senyamule, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT unaofanyika katika Ukumbi wa Chimwaga, jijini Dodoma.
Senyamule amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa KKKT katika maendeleo ya taifa, ikieleza kuwa kwa miaka mingi kanisa hilo limekuwa mshirika muhimu katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii.
Amesema huduma hizo ni pamoja na elimu, afya, malezi ya vijana, huduma kwa watu wenye mahitaji maalum pamoja na misaada ya kijamii na juhudi za kupambana na umaskini.
Senyamule amesema pamoja na huduma za kijamii, KKKT imeendelea kuwa mdau katika shughuli za kiuchumi na uwekezaji, huku viongozi wa dini wakiwa na nafasi ya kipekee katika kujenga maadili mema, kudumisha amani na kuimarisha umoja wa kitaifa.
“Viongozi wa dini tunatambua kuwa mnaaminika sana na wananchi kuliko taasisi na watu wengine. Kwa sababu hiyo, mafundisho na matendo yenu yanaweza kuleta mabadiliko makubwa katika familia, jumuiya na taifa kwa ujumla,” amesema.
Amesema taifa linahitaji viongozi wa dini wanaoweza kuwa sauti ya matumaini na faraja kwa wananchi, hususan wale wanaopitia changamoto mbalimbali za maisha.
Senyamule amewataka wachungaji na viongozi wa dini kwa ujumla kuendelea kuwa sauti ya faraja kwa wenye huzuni, matumaini kwa waliokata tamaa na msaada kwa watu walio katika mazingira magumu.
Katika eneo la malezi, amesema kuna umuhimu wa kuimarisha malezi ya kiroho na kimaadili, hasa kwa watoto na vijana, ili kuwaandaa kuwa kizazi chenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.
Aidha, amewataka wachungaji kuendelea kutoa elimu inayowajenga wananchi katika nyanja za kiroho, kijamii na kiuchumi, huku wakihimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, kutumia fursa zilizopo na kushiriki katika shughuli halali za maendeleo.
“Imani iendelee kusambaa sambamba na matendo yanayoleta ustawi wa mtu binafsi, jamii na taifa kwa ujumla,” amesema.
Mkutano Mkuu wa 6 wa Wachungaji wa KKKT umehusisha wachungaji kutoka Dayosisi 28 za KKKT na umefunguliwa na Mkuu wa KKKT, Askofu Alex Malalusa.
Mkutano huo unatarajiwa kuendelea hadi Septemba 17, 2025, ukiwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu huduma ya kanisa, malezi ya kiroho na nafasi ya kanisa katika jamii na maendeleo ya taifa.
Ndg. Abdi ameyasema hayo leo, Septemba 13, 2026, wakati akiendelea na ziara za kukagua uhai wa CCM katika Tawi la Pita na Zako, Jimbo la Kijini, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Amesema ziara hizo pia zinalenga kuhamasisha viongozi na wanachama wa CCM kuunga mkono juhudi zinazofanywa na viongozi wakuu wa Serikali katika kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi.
Amesema CCM itaendelea kuisimamia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha inatekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama, ikiwemo kuweka mazingira bora kwa wananchi, hususan wakulima wa mwani, kupata masoko ya uhakika yatakayowawezesha kuongeza kipato na kuboresha maisha yao.
Kwa upande wake, Katibu wa Idara ya Organisation wa CCM Zanzibar, Ndg. Omar Ibrahim Kilupi, amewataka wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kulinda amani na utulivu uliopo nchini, akisisitiza kuwa amani ni tunu kubwa waliyoachiwa na viongozi na mababu waliotangulia.
Viongozi wa Jimbo la Kijini, akiwemo Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo, wamemuahidi Naibu Katibu Mkuu huyo kuendelea kusimamia na kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo, sambamba na kuimarisha huduma za kijamii kwa wananchi.
Wamesema wataendelea kushughulikia maeneo muhimu kwa wananchi, ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama, kuboresha huduma za afya pamoja na kuendeleza michezo kwa vijana.
Katika ziara hiyo, Ndg. Abdi pia amepata fursa ya kumtembelea na kumjulia hali Ndg. Mwanakombo Mcha Mohammed, ambapo alimpa faraja na kumtakia afya njema.
Prof. Shivji ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza katika mkusanyiko wa kuonesha mshikamano na wananchi wa Palestina, hususan watoto wa Gaza wanaoendelea kukabiliwa na madhara ya vita na mashambulizi.
Amesema hakuna binadamu mwenye huruma anayeweza kubaki kimya anaposhuhudia mauaji na mateso dhidi ya watoto na raia, akisisitiza kuwa suala la Palestina si la Wapalestina pekee, bali ni suala linalopaswa kugusa dhamira ya wanadamu wote.
“Kama wewe ni binadamu, huwezi kukaa kimya wakati watoto wanauliwa, wakati watu wanauliwa na mauaji yanaendelea pale Gaza.”
Prof. Shivji pia amerejea historia ya Tanzania katika kupigania uhuru, kupinga ukoloni na ubaguzi, akisisitiza kuwa msimamo huo ulijengwa kwa kiasi kikubwa katika misingi iliyoasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Amesema Tanzania imekuwa na historia ya kuunga mkono harakati za ukombozi, ikiwemo harakati za Palestina, na imeendelea kuwa na uhusiano wa kidiplomasia na Palestina.
Kwa upande wake, Kassimu Hassan, mmoja wa viongozi wa Taasisi ya Friends of Palestine Tanzania, amesema mshikamano kati ya Tanzania na Palestina unapaswa kuendelea kuonyeshwa, hasa wakati watoto wa Palestina wanakabiliwa na mazingira magumu na kunyimwa haki ya kuishi na kucheza kwa amani kama watoto wa mataifa mengine.
Kassimu amesema jamii inapaswa kuendelea kupaza sauti katika kutetea haki, usalama na amani kwa watoto wa Palestina.
Pia amekumbusha msimamo wa kihistoria wa Tanzania katika kuunga mkono harakati za ukombozi wa Palestina, akisisitiza umuhimu wa kizazi cha sasa kuendeleza mshikamano huo.
“Uhuru wa Palestina ni uhuru wetu sote. Viva Palestina, Freedom for Palestine,” amesema Kassimu Hassan.
Naye Mwanasheria na mwanachama wa Friends of Palestine Tanzania, Tina Mfanga, amesema Watanzania waliolelewa katika misingi ya kupigania uhuru iliyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere wataendelea kuunga mkono haki ya Palestina.
Tina amesema ni muhimu utamaduni huo ukarithiwe na kizazi kijacho, ndiyo maana watoto walihusishwa katika tukio hilo ili kuwafundisha historia ya mshikamano kati ya Tanzania na Palestina na kuwafanya wafahamu hali wanayopitia watoto wenzao wa Gaza.
Amesema watoto wanapaswa kufahamu madhila yanayowakabili wenzao wa Palestina, huku akisisitiza kuwa jamii haipaswi kukaa kimya mbele ya vitendo vya ukatili na ukiukwaji wa haki za binadamu.
“Tutaendeleza mapambano haya na tutaendelea kuwarithisha watoto wetu. Ndiyo maana kwenye tukio la leo tuko na watoto kama sehemu ya kuwarithisha utamaduni huu na kuwafundisha historia hii,” amesema Tina Mfanga.
Ndg. Abdi ameyasema hayo leo, Septemba 13, 2026, alipowasili katika Tawi la CCM Kivunge A, Jimbo la Kijini, ambapo amefurahishwa na hali ya uhai, umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama wa CCM katika jimbo hilo.
Amesema hali hiyo ni ishara ya mshikamano wa wanachama, jambo alilolitaja kuwa ni msingi muhimu katika kukiimarisha Chama na kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake.
Kwa upande wake, Katibu wa NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi, Ndg. Khamis Mbeto Khamis, amesema ziara hiyo inalenga kukagua na kutathmini hali ya uhai wa CCM kuanzia ngazi ya matawi hadi jimbo.
Aidha, amewataka wanachama wa CCM kuelekea uchaguzi wa ndani wa Chama mwaka 2027 kutumia fursa hiyo kuchagua viongozi bora, wenye uwezo wa kukiongoza Chama na kukivusha kwa mafanikio kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030.
Katika ziara hiyo, Ndg. Abdi pia amemtembelea na kumjulia hali Ndg. Khamis Ali Khamis nyumbani kwake Kivunge B, hatua aliyosema inalenga kuendelea kuonesha thamani ya kuwajali, kuwathamini na kuwakumbuka wazee pamoja na wanachama waliokitumikia Chama Cha Mapinduzi.
Ndg. Abdi ameyasema hayo leo, Septemba 13, 2026, alipowasili katika Tawi la CCM Kivunge, Jimbo la Kijini, ambapo alizungumza na wanachama wa CCM pamoja na wajumbe wa Kamati za Siasa.
Amesema ushiriki wa wanachama katika vikao mbalimbali vya Chama ni muhimu katika kuimarisha umoja na mshikamano kati ya viongozi na wanachama, sambamba na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Chama.
Aidha, amesema Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, anaendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo, ikiwemo kuhakikisha wananchi wanapata ufumbuzi wa changamoto zinazohusu huduma za kijamii.
Amezitaja huduma hizo kuwa ni pamoja na elimu, afya, maji safi na salama, pamoja na ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya barabara.
Katika ziara hiyo, Ndg. Abdi pia alimtembelea na kumjulia hali Ndg. Fatima Mtwana Ame nyumbani kwake Kivunge, akisisitiza umuhimu wa kuendeleza mshikamano, upendo na kujali wanachama wa CCM.
Tanzania imesisitiza umuhimu wa kuimarisha huduma za afya ya msingi ili kufikia huduma bora za afya kwa wote huku ikiweka mkazo katika uwekezaji, upatikanaji wa fedha, matumizi ya teknolojia, na kuhakikisha usawa katika utoaji wa huduma hizo nchini.
Akifunga Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi (IPHC2026) kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI Prof. Shemdoe, Naibu Waziri Dkt. Festo Dugange amesema jitihada za Serikali katika kuimarisha afya ya msingi na hospitali za rufaa zimeiwezesha Tanzania kutambulika zaidi barani Afrika.
Dkt. Dugange ameeleza kuwa hatua hizo kubwa zimesaidia kupunguza vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 556 mwaka 2015/2016 hadi vifo 104 kwa kila vizazi hai laki moja,Aidha, nchi za Afrika zimehimizwa kujenga mifumo inayostahimili mabadiliko ya tabianchi na kuendeleza ajenda ya Three Zeros.
Aliongeza kuwa uwekezaji katika sekta ya afya lazima uambatane na mnyororo imara wa ugavi wa bidhaa, watumishi wenye ujuzi, dawa, vifaa tiba, na mifumo ya kidijitali. Hatua hii itasaidia taasisi za afya kubadilishana taarifa na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mkutano huo umefikia maazimio 10, yakiwemo kuzitaka Serikali za Afrika kuweka afya ya msingi kuwa kipaumbele kwenye bajeti zao. Lengo ni kuongeza fedha za ndani ili wananchi wapate huduma bora, nafuu, na kwa wakati bila kujali maeneo wanayotoka au uwezo wao kiuchumi.
Pia imesisitizwa kuwa kuimarisha afya ya msingi pamoja na hospitali za mikoa, kanda, na taifa utaongeza uwezo wa mfumo wa afya na kupunguza changamoto za huduma vijijini, ambapo washiriki wanetakiwa kuhakikisha maazimio yote yanatekelezwa kwa vitendo baada ya kurejea makwao.
Katika hatua nyingine, Dkt. Dugange amesisitiza kila mwananchi apate huduma bila ubaguzi wowote. Ametaka kuimarishwa kwa mifumo ya kidijitali ya taarifa za afya, bima, na ufuatiliaji wa magonjwa ili kuboresha utendaji kazi katika sekta hiyo.
Maazimio mengine ni pamoja na kuimarisha ufadhili unaozingatia utendaji (performance-based financing), kutekeleza ajenda ya Lusaka, kutumia tafiti kwenye maamuzi, kuendeleza watumishi wa afya, na kuwekeza kwenye malezi ya mtoto kupitia African Union Champion Roadmap on Nurturing Care.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndg. Abdi Mahmoud Abdi, amesema CCM itaendelea kuimarisha uhai na uimara wa chama, ikiwemo kujenga na kuimarisha matawi yake katika majimbo mbalimbali.
Ndg. Abdi ameyasema hayo alipowasili katika Tawi la CCM Kidagoni, Jimbo la Nungwi, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara zake za kukagua na kuimarisha uhai wa CCM kuanzia ngazi ya matawi hadi majimbo.
Amesema uhai na uimara wa chama unategemea kwa kiasi kikubwa ushiriki wa wanachama wake katika kutekeleza wajibu wao, hususan kulipa ada za uanachama kwa wakati, ambazo huchangia katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za chama, ikiwemo ujenzi na uimarishaji wa matawi.
Aidha, Ndg. Abdi amesema amezipokea changamoto zilizowasilishwa na viongozi pamoja na wanachama wa Tawi la CCM Kidagoni, zikiwemo ukosefu wa jengo la tawi kwa ajili ya shughuli za chama na changamoto ya miundombinu ya barabara.
Amesisitiza kuwa uongozi wa CCM utaendelea kuzifuatilia changamoto hizo kwa lengo la kuboresha mazingira ya utendaji wa chama na kuwawezesha viongozi na wanachama kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Katika ziara hiyo, Ndg. Abdi pia alipata fursa ya kumtembelea na kumjulia hali Ndg. Asiata Hamada Suleiman nyumbani kwake Kidagoni.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndg. Abdi Mahmoud Abdi, amewasili katika Tawi la CCM Kidoti, Jimbo la Nungwi, na kufanya mazungumzo na viongozi pamoja na wanachama wa chama hicho.
Ziara hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa ukaguzi wa uhai wa CCM unaofanyika kuanzia ngazi ya matawi hadi majimbo, kwa lengo la kuimarisha chama na kuhakikisha shughuli zake zinatekelezwa kwa ufanisi.
Akizungumza na wanaCCM hao, Ndg. Abdi amewataka wanachama kuendelea kulipa ada zao za uanachama kwa wakati, akisisitiza kuwa ulipaji wa ada ni miongoni mwa wajibu muhimu unaochangia kukifanya chama kuwa imara na hai.
Amesema ushiriki wa wanachama katika kutekeleza wajibu wao utasaidia kuongeza uwezo wa CCM kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho na kusimamia utekelezaji wa ahadi zake kwa wananchi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa viongozi na wanachama kuendelea kushirikiana, kusikilizana na kudumisha mshikamano ili kuongeza ufanisi wa shughuli za chama katika ngazi zote.
Kwa upande wake, Katibu wa Kamati Maalum wa Idara ya Oganaizesheni CCM Zanzibar, Ndg. Omar Ibrahim Kilupi, amewataka wanaCCM kuendelea kujiandikisha na kupata Kitambulisho cha Mzanzibari Mkazi, hatua itakayowawezesha kujiandaa kutimiza haki yao ya msingi ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030.
Ndg. Abdi anaendelea na ziara yake katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kukagua uhai wa CCM, huku akikutana na viongozi na wanachama kwa lengo la kusikiliza changamoto zao, kuimarisha mshikamano na kuongeza ufanisi wa shughuli za chama.
.jpeg)




































.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)








.jpeg)

