TUMBATU, ZANZIBAR — Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndugu Abdi Mahamoud Abdi, amekagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Tumbatu, akieleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutarahisisha upatikanaji wa huduma za afya, ikiwemo huduma za kibingwa, kwa wananchi wa Kisiwa cha Tumbatu.

Akitoa taarifa ya kitaalamu wakati wa ziara hiyo, msimamizi wa mradi amesema hospitali hiyo itatoa huduma mbalimbali za afya, zikiwemo huduma za afya ya jamii na huduma za kibingwa, hatua itakayosaidia kupunguza changamoto ya wananchi kusafiri nje ya kisiwa kufuata huduma hizo.

Wananchi wa Tumbatu wamempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuendelea kutekeleza ahadi za Serikali kwa vitendo, hususan katika kuimarisha huduma za kijamii na afya.

Kwa upande wake, Ndugu Abdi amempongeza Dkt. Mwinyi kwa hatua zinazoendelea kuchukuliwa katika kuimarisha huduma za afya katika Kisiwa cha Tumbatu, huku akisisitiza umuhimu wa kukamilisha miradi hiyo kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotarajiwa.

Aidha, amewataka madaktari na watumishi wa afya kuhakikisha wanatoa huduma bora, zenye weledi na zinazozingatia mahitaji ya wananchi, akisisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na kuimarisha ustawi wao.

📆 16 Septemba, 2026
📍 Tumbatu, Zanzibar.




 

Na. Asia Singano, WF – Dodoma.

Wizara ya Fedha imeendelea kuandaa na kuboresha miongozo mbalimbali inayolenga kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya ukaguzi na kuongeza ufanisi wa kazi hiyo, ili kuendelea kulinda fedha za umma na kukuza uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie, wakati akifungua Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Mhandisi Nindie alisema kuwa mwongozo huo unahusisha hatua mbalimbali za mchakato wa ukaguzi, na kwamba baadhi ya vipengele vyake vinapitia hatua ya uhakiki ili kuhakikisha vinaendana na mahitaji na viwango vinavyotakiwa.

“Tunachukua baadhi ya vipengele kwa ajili ya kuvithibitisha, ambapo ni muhimu kupitia na kuthibitisha miongozo hiyo kabla ya kuanza kutumika kikamilifu. alisema Mhandisi Nindie.

Alieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa miongozo inayotumika katika kazi za ukaguzi ina ubora, inaeleweka na inawasaidia watendaji kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa watumishi kuwa na vyeti vya kitaaluma (certification), kwakuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuongeza ufanisi na ubora wa utekelezaji wa majukumu yao.

“Suala la kuwa na vyeti vya kitaaluma limekuwa sehemu muhimu ya mipango ya kuimarisha uwezo wa watumishi. Natambua kuwa tangu mwaka 2021 kulikuwa na mpango uliolenga kuongeza idadi ya watumishi wenye vyeti hivyo,” alisema Mhandisi Nindie.

Alibainisha kuwa kuendelea kuwekeza katika ujuzi na taaluma za watumishi ni hatua muhimu katika kuboresha utendaji kazi na kuhakikisha majukumu ya taasisi yanatekelezwa kwa viwango vinavyohitajika.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara ya Fedha, kupitia Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali yakiwakutanisha Wakaguzi wa Ndani kutoka taasisi za umma na kutoka Wizara ya Fedha, ili kuwaongezea uelewa katika utekelezaji wa majukumu yao.


Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie, akizungumza wakati wa kufungua Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie (kushoto), akiagana na Mhasibu Mkuu wa Fungu 6 – Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Samwel Mangi, baada ya kumalizika kwa Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie (kushoto), akijadiliana jambo na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi, Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Paison Mwamnyasi, wakati wa Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Mkaguzi wa Ndani Mwandamizi, Idara ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bi. Vaileth Nyanga, akitoa wasilisho kuhusu muhtasari Mifumo ya Kuimarisha Ufanisi wa Kazi za Ukaguzi Serikalini, wakati wa program ya Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie, akigawa kitabu cha Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa, Mkaguzi wa Ndani kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC), Bw. Ernest Josephat, mmoja wa washiriki wa program ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo iliyowakutanisha wakaguzi wa ndani kutoka taasisi za umma ambayo yaliandaliwa na Wizara ya Fedha, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Mhandisi Kenneth Nindie (katikati, walioketi), na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi, Bw. Paison Mwamnyasi (wa tatu kushoto, walioketi), wakiwa katika picha ya pamoja na Wakaguzi wa Ndani baada ya Mafunzo ya Uelewa na Ugawaji wa Mwongozo wa Ukaguzi wa Mifumo ya Taarifa kwa Wakaguzi wa Ndani wa Serikali, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mabele jijini Dodoma.

(Picha na Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini, WF – Dodoma)





Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndugu Abdi Mahamoud Abdi, amewasili katika Kisiwa cha Tumbatu, Jimbo la Tumbatu, kuendelea na ziara yake ya kukagua na kuimarisha uhai wa Chama Cha Mapinduzi katika matawi.

Ziara hiyo inalenga kukutana na wanachama, kusikiliza changamoto zinazowakabili, pamoja na kuhimiza mshikamano, utekelezaji wa majukumu na uimarishaji wa Chama katika ngazi za chini.















WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ndani ya wiki moja, Serikali itachukua hatua ya kuhakikisha bei ya saruji inakuwa himilivu kwa wananchi, baada ya kubaini malalamiko ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Simiyu.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Septemba 15, 2026) wakati akizungumza na wananchi wa Bariadi Mjini, mkoani Simiyu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CCM Saba Saba.

“Serikali tumeliona hilo. Serikali sikivu tumesikia hilo. Nimewatuma wataalamu ndani ya wiki moja wawe wameshapata ufumbuzi. Tutatoa tamko la njia ya kushusha bei ya saruji ili kila Mtanzania aweze kumudu. Katika baadhi ya maeneo bei ya saruji imefikia zaidi ya sh. 26,000 na katika baadhi ya mikoa ya mipakani imefikia sh. 32,000,” amesema na kusisitiza kuwa Serikali inataka wananchi waweze kumudu gharama za ujenzi wa nyumba na miradi mingine ya maendeleo.

Kuhusu zao la pamba, Waziri Mkuu amesema ameielekeza Wizara ya Kilimo ikutane na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja na ifikapo Oktoba 15, 2026 apelekewe mapendekezo rasmi kuhusu bei na mfumo bora wa ununuzi wa zao hilo ili kuhakikisha wakulima wananufaika zaidi.

“Nimeipokea hoja hii. Nimeelekeza Wizara ya Kilimo ikae na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja. Ifikapo tarehe 15 mwezi wa 10, niwe nimeshapata mapendekezo rasmi yaliyorejea mifumo ambayo tumeshaitumia na kubaini upi ni mfumo bora ili tuweze kuhakikisha kwamba wakulima wananufaika,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema pia Serikali imebadilisha utaratibu wa kodi kwa wenye biashara mpya, ambapo mfanyabiashara anayeanzisha biashara atapewa muda wa kuimarisha biashara yake kabla ya kuanza kubeba mzigo wa kodi. “Zamani ilikuwa mtu akianzisha tu biashara, siku hiyo hiyo anaanza kudaiwa kodi. Sasa tumefuta, atasubiriwa mwaka mzima ili biashara yake iimarike,” amesema.

Amesema hatua hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kujenga uchumi shirikishi, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kutekeleza sehemu kubwa ya shughuli za maendeleo.

Mapema, akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Bariadi Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, amemshukuru Waziri Mkuu kwa ziara hiyo na kueleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo ikiwemo inayogusa sekta za maji, elimu, afya na barabara. 

Mhandisi Kundo amesema mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria wenye thamani ya sh. bilioni 440 unaendelea kutekelezwa mkoani humo, huku Serikali ikiwa imetoa sh. milioni 460 kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Majaida–Munambala katika Mto Ndoba.

Kuhusu ujenzi wa soko la kisasa la Bariadi mjini, Mhandisi Kumndo amesema ujenzi wake unaendelea, huku akiomba kasi ya mkandarasi iongezwe ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Akigusia barabara za Bariadi Mjini, Mhandisi Kundo amesema Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha kilomita zote 8.6 zilizotengewa ujenzi zinajengwa kwa awamu mbili, ambapo kilomita tano zitajengwa katika awamu ya kwanza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Said Mtanda, amesema Serikali ya Mkoa itasimamia na kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara hiyo na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Maagizo na maelekezo yako uliyoyatoa katika ziara yako hii tunayasimamia, tuyatekeleze, na kuleta ripoti ya utekelezaji katika ofisi yako ya Waziri Mkuu,” amesema.









NA MWANDISHI WETU

MAKAMU wa Rais Deogratius Ndejembi, amesisitiza umuhimu wa kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kijani kupitia upatikanaji wa ujuzi, teknolojia, mitaji na masoko na kwamba vijana wanapaswa kutambuliwa kama wabunifu, wajasiriamali, watafiti na viongozi wa uchumi wa kijani na si wanufaika pekee wa programu za tabianchi.

Aidha amesema vijana wanapaswa kugeuza changamoto za mabadiliko ya tabianchi kuwa fursa za uwekezaji, ajira, ubunifu na ukuaji wa uchumi wa kijani nchini Tanzania.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni kwa niaba ya Makamu wa Rais Ndejembi, katika hafla ya ufunguzi wa Jukwaa la Kimataifa la Tanzania Green Summit 2026 (TGS) Dar es Salaam, jana.

Masauni, amesema mabadiliko ya tabianchi hayapaswi kutazamwa kama changamoto ya kimazingira pekee, bali kama eneo lenye fursa kubwa za maendeleo ya kiuchumi.

Amebainisha, kaulimbiu ya jukwaa hilo inayosema 'Geuza hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kuwa fursa, inaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na mipango mbalimbali ya Serikali ya kukabiliana na mabadiliko hayo.

“Tanzania ina fursa kubwa katika nishati jadidifu, nishati safi ya kupikia, kilimo endelevu, usimamizi wa taka, uchumi wa mzunguko, utalii endelevu, uchumi wa buluu na suluhisho zinazotegemea mifumo ya asili,"amesema.

Aidha, Handisi Masauni, amesisitiza a umuhimu wa kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kijani kupitia upatikanaji wa ujuzi, teknolojia, mitaji na masoko.

Ameeleza, vijana wanapaswa kutambuliwa kama wabunifu, wajasiriamali, watafiti na viongozi wa uchumi wa kijani na si yo wanufaika pekee wa programu za tabianchi.

“Tanzania imechukua hatua mbalimbali katika agenda ya mazingira na tabianchi, ikiwemo kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa Kituo cha Afrika cha Vijana cha Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabianchi, pamoja na Ofisi ya Kikanda ya Santiago Network on Loss and Damage, hatua zinazolenga kuongeza uwezo wa nchi zinazoendelea kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi,”amesema.

Ameipongeza TGS, kwa kuandaa jukwaa hilo la siku mbili linalojumuisha washiriki zaidi ya 1000 kutoka mataifa zaidi ya 10 na wataalamu 30.

Amesema mkutano huo ambao ni wa pili kufanyika ni jukwaa muhimu la majadiliano kukuza ushirikiano wa kuchangia katika utekelezaji wa ajenda za Tanzania Kijani, kuhusu hifadhi ya mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Awali, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Richard Muyung, alisema Tanzania inaendelea kutumia fursa zinazotokana na mifuko ya kimataifa ya mazingira na tabianchi, huku akitaja pia uwepo wa miradi ya biashara ya kaboni inayoratibiwa kupitia Kiutuo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC).

Ameeleza, fursa hizo zinapaswa kuendelezwa kwa kuzingatia utunzaji wa mazingira, uongezaji thamani ndani ya nchi, uhamishaji wa teknolojia na uundaji wa ajira kwa Watanzania.

Naye Mwasisi wa TGS,Redemptus Caesar, amesema mikakati ya siku za usoni ni i kuanzisha jukwaa ambalo halitakuwa jukwaa la kukutana na kubadilishana mawazo pekee bali jukwaa la kuoneshana fursa.

"Ndiyo maana katika siku hizi mbili tutakazo kaa tutapata nafasi ya kufanya mazungumzo hali yanayoangazia fursa zinazopatikana katika sekta za mazingira,"amebainisha Caesar.

Pia amesema jukwaa hilo litawawezesha washiriki kuziona fursa za moja kwa moja, ambapo kutakuwa na chumba maalumu cha kuwakutanisha uso kwa uso wadau mbalimbali kuzungumza na kukubaliana kushirikiana katika fursa walizonazo.

"Aidha tunatazamia kuwa na mikutano ya pembezoni mwa jukwaa hili sita kwa kila siku zitafanyika tatu.Mdau atachagua fursa anayo iona ni muhimu kudhuria ili kunufaika na fursa iliyopo,"amesema .

Pia Caesar, amebainisha katika jukwaa hilo TGS itatambulisha jukwaa la Youth Evironmental Enterineurship Platform, litakalo husisha kusaidia kukuza shughuli za vijana za ujasiramali.















 

Na Farida Said KATESHI, MANYARA

Mamia ya watalii wa ndani walijitokeza Septemba 12–13, 2026 kushiriki Mount Hanang’ Nyama Choma Festival, lililofanyika kwa mara ya sita katika Msitu wa Mazingira Asilia wa Mlima Hanang’.

Tamasha hilo liliwakutanisha wananchi na wageni kwa mchanganyiko wa burudani na utalii wa mazingira, huku washiriki wakipata fursa ya kufurahia nyama choma, kufanya hiking, kupiga kambi na kujionea vivutio mbalimbali vya asili.

Miongoni mwa vivutio vilivyowavutia washiriki ni maporomoko ya maji, ndege wa aina mbalimbali na wanyama, pamoja na mandhari ya Mlima Hanang’ na utajiri wa ikolojia unaopatikana katika msitu huo.

Mmoja wa washiriki, Raphael Joel, amesema kuendelea kwa tamasha hilo kunachochea hamasa kwa Watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

“Matamasha kama haya yanaongeza hamasa kwa watalii wa ndani kutembelea vivutio vilivyopo nchini. Tunapata burudani, lakini pia tunajifunza umuhimu wa kuhifadhi mazingira,” amesema Joel.

Ameipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa kutumia matukio kama hayo kutangaza utalii wa ndani na kuhamasisha wananchi kuthamini na kushiriki katika uhifadhi wa mazingira.

Mhifadhi Mkuu wa Msitu wa Mazingira Asilia wa Mlima Hanang’, Abubakar Mpapa, amesema tamasha hilo linatoa fursa kwa wageni kufurahia nyama choma, kupiga kambi na kujionea vivutio vya asili vilivyopo katika eneo hilo.

Amesema TFS itaendelea kuhamasisha utalii wa ndani kupitia matukio mbalimbali, huku ikisisitiza matumizi endelevu ya misitu na ushiriki wa jamii katika uhifadhi wa mazingira.








  

Mwalimu wa Mbeya ashinda TZS milioni 246.6 kwenye Midweek Jackpot ya SportPesa Tanzania

Mwalimu kutoka Chunya amekuwa mmoja wa washindi wakubwa wa SportPesa Tanzania mwaka 2026 baada ya kugeuza tiketi ya TZS 1,000 ya Midweek Jackpot kuwa ushindi wa TZS 246,660,590. Magreth Muindi Njolowelo, mwenye umri wa miaka 50, alitabiri kwa usahihi matokeo ya mechi zote 13 na kukabidhiwa rasmi zawadi yake jijini Dar es Salaam tarehe 9 Septemba 2026. Ushindi wake unaongeza moja ya mwenendo mkubwa wa SportPesa Tanzania mwaka 2026, ambapo wanawake wamekuwa washindi wanne kati ya washindi watano wakubwa wa jackpot hadi sasa mwaka huu.

Ushindi wa Magreth umeleta simulizi kubwa kwenye Midweek Jackpot, zaidi ya thamani ya pesa pekee. Ushindi wake unavutia kwa sababu hauhusu tu ukubwa wa hundi aliyopokea. Ni simulizi ya uvumilivu, mipango ya familia na mwenendo wa mwaka 2026 ambapo wanawake wameendelea kuonekana zaidi kwenye orodha ya washindi wakubwa wa SportPesa Tanzania.

Ushauri wa rafiki wageuka kuwa ushindi wa TZS milioni 246.6

Safari ya Magreth na SportPesa ilianza mwaka 2024 baada ya kugundua jukwaa hilo kupitia utafutaji mtandaoni, kisha baadaye akatiwa moyo na rafiki yake kujaribu Midweek Jackpot ya TZS 1,000. Ingawa baadhi ya watu waliomzunguka walihoji kwa nini aliendelea kucheza, Magreth aliendelea kuwa mvumilivu na polepole akajenga kujiamini kupitia ushindi wa awali, ikiwemo ushindi mwingine wa TZS milioni 10 kabla ya ushindi wake huu mkubwa wa jackpot.

Safari hiyo inaufanya ushindi wake kuwa na uzito mkubwa zaidi wa kihisia. Kosa moja tu la utabiri lingeweza kumaliza safari yake ya jackpot, lakini Magreth alikamilisha kadi nzima ya mechi 13 kwa usahihi. SportPesa Tanzania ilisherehekea tukio hilo kwa makabidhiano rasmi, ikimweka Magreth, mipango yake ya familia na mafanikio yake makubwa katikati ya tangazo hilo.

Kutoka darasani Chunya hadi hundi ya TZS milioni 246.6

Magreth anaamini kuwa pesa hizo zinaweza kufungua fursa mpya kwa familia yake na amesema atakuwa makini katika kuzisimamia. Kauli yake ya busara inaendeleza simulizi hii zaidi ya tangazo la ushindi, na kuielekeza kwenye maamuzi yatakayosaidia kuunda mustakabali wa familia yake. Orodha ya washindi wa jackpot wa SportPesa inajumuisha wafanyabiashara, madereva na wafanyakazi wa hoteli kutoka Dar es Salaam, Iringa na Zanzibar. Ushindi wa Magreth sasa unaongeza mwalimu kutoka Chunya kwenye rekodi hiyo ya kitaifa.

Simulizi ya Magreth ni simulizi ya uvumilivu. Mstari wake wa ushindi ulimhitaji kupata kila mechi kwa usahihi, si matokeo moja pekee. Kadiri kila mechi ilivyokamilika, safari kutoka kwenye tiketi ya kawaida ya Midweek Jackpot hadi ushindi mkubwa iliendelea kuwa karibu zaidi. Kwa mashabiki wa soka, safari hii inaongeza msisimko na kuufanya ushindi wa mwisho kuwa wa kipekee zaidi.

Ushindi huu waongeza rekodi ya washindi wa SportPesa mwaka 2026

Ushindi wa Magreth unaweka wazi rekodi ya SportPesa mwaka 2026. “Simulizi ya Magreth ni maalum kwa sababu inamhusu mwalimu, mama na shabiki wa soka kutoka Chunya. Tiketi yake ya TZS 1,000 imefungua ukurasa mpya katika maisha yake, na tunajivunia kumsherehekea kama mmoja wa washindi wakubwa wa SportPesa Tanzania mwaka 2026,” alisema Mkuu wa Masoko wa SportPesa Tanzania, Tracy Humplick.

Takwimu hizi zinaweka ushindi wa Magreth kwenye muktadha mpana zaidi, si kama tangazo la mshindi mmoja pekee. Washindi wote watano wa Midweek Jackpot mwaka 2026 wamevuka hadhi ya mamilionea, huku wanawake wakiwa wanne dhidi ya mwanaume mmoja, jambo linaloupa mwaka huu sura ya kipekee. Humplick pia alithibitisha kuwa Magreth amejiunga na washindi wa SportPesa iliyojengwa katika historia ya kampuni, na kumpa mwalimu huyo kutoka Chunya nafasi kwenye rekodi hiyo.

Hitimisho

Ushindi wa Magreth Muindi Njolowelo wa TZS milioni 246.6 si matokeo mengine tu ya SportPesa Jackpot. Ni simulizi ya mwalimu kutoka Chunya ambaye tiketi yake ya TZS 1,000 ya Midweek Jackpot imekuwa moja ya matukio makubwa ya ushindi nchini Tanzania mwaka 2026. Ushindi huu una sifa zote zinazofanya simulizi ya kitaifa ikumbukwe: mshindi mwenye jina, mafanikio ya kutabiri mechi 13 kwa usahihi, kiasi halisi cha zawadi na mpango binafsi wa maisha. Hundi itavuta macho ya wengi, lakini simulizi ya Magreth ndiyo inaupa ushindi huu nguvu ya kukumbukwa.




 Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Africa Tourism Private Sector Alliance (ATPSA) Tourism Roadshow Tanzania 2026, jukwaa litakalowakutanisha wafanyabiashara wa utalii, wanunuzi na wadau kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika kwa ajili ya kukuza biashara na ushirikiano katika sekta hiyo.

Roadshow hiyo itafanyika Zanzibar Septemba 27, 2026, katika Hotel Verde Zanzibar, kabla ya kuhamia Arusha Septemba 30, 2026, katika Gran Meliá Arusha.

Tukio hilo linafanyika wakati Tanzania ikiendelea kuimarisha nafasi yake katika sekta ya utalii barani Afrika, baada ya kutambuliwa kuwa Africa’s Leading Destination 2026, huku Bodi ya Utalii Tanzania ikishinda tuzo ya Africa’s Leading Tourist Board 2026 kwa mwaka wa tano mfululizo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dr. Thereza Mugobi, amesema Roadshow hiyo ni fursa kwa Tanzania kutangaza vivutio vyake, lakini pia kushiriki katika kujenga soko la utalii la Afrika kwa Waafrika.

Kwa upande wake, Madam Devotha Mdachi, Mjumbe wa Bodi na Mwakilishi Rasmi wa Africa Tourism Partners (ATP) na Africa Tourism Private Sector Alliance (ATPSA) kwa ukanda wa Afrika Mashariki, amewataka wadau wa utalii nchini kutumia fursa hiyo kujenga masoko mapya na ushirikiano wa kibiashara.

Washiriki kutoka nchi mbalimbali zikiwemo Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Uganda, Namibia, Nigeria, Rwanda na Afrika Kusini, pamoja na India na Belgium, wanatarajiwa kushiriki katika mikutano hiyo.

Msingi wa Roadshow utakuwa ni mikutano ya biashara kwa biashara (B2B), ambapo washiriki watatumia mfumo wa ATPSA B2B Appointment Platform kupanga mikutano na washirika wao wa biashara. Kila mshiriki atapata nafasi ya kufanya hadi mikutano 15 iliyopangwa kabla.

Kaulimbiu ya Roadshow hiyo ni “Meet. Connect. Trade. Grow Africa.”, ikiwa na lengo la kuimarisha biashara ya utalii, ushirikiano wa sekta binafsi na kukuza utalii wa ndani ya Afrika.

ATPSA inaeleza kuwa mustakabali wa utalii barani Afrika unahitaji nchi, biashara na watu kuunganishwa zaidi ili kujenga soko imara la utalii ndani ya bara.











Top News