What people often miss on CPI day is that the number itself isn't what moves the market. The common reaction is to check whether 3.4% number is high or low. But it's all priced in advance. The real driver of EUR/USD is the gap between the actual number and what the market was positioned for.

Even a 3.4% reading can cause the dollar to weaken if traders expect higher inflation. And the opposite scenario – weaker numbers that beat consensus expectations may drive the dollar’s strength. According to Federal Reserve research, the price driver here is a surprise component rather than the headline.


Why the Expectation Gap Is More Important Than the Level

Forex is driven by expectations for interest rate decisions. And inflation plays its role by impacting expectations for future central bank policy. This is the reason why identical numbers may cause opposite reactions at different times. It depends on how they compare to market positioning.

Main factors:

●      Monthly CPI and core CPI

●      Core services inflation

●      Revisions to the previous period data

●      Central bank policy pricing

Year-over-year data is less important in terms of price impact than monthly and core data.


How to Calculate Surprise

Start with the simplest metric: Surprise = Actual CPI − Consensus CPI. 

Consensus comes from the economic calendar's forecast and reflects the market positioning. And then you need to check the market reaction through rates. The sequence typically runs: CPI surprise → change in front-end yields → USD movement → the sentiment adjustment.


Traders frequently employ this methodology in combination with the JustMarkets Economic Calendar to track high-impact releases in real time.


What the Intraday Move Actually Looks Like

CPI reactions usually happen in three stages. The first one is a headline shock with the potential algorithms' reaction within a few seconds. Then comes the interpretation stage, with a time frame of 15-60 minutes and analysis of core numbers and yield confirmation. And then either continuation or reversal happens.

Approaches to Trading CPI Day

There are two common approaches to CPI.

●      The momentum approach requires the consistency of headlines and core surprises with yields' confirmation. Most traders wait until the first minute's candle is closed to avoid false signals.

●      The fade approach requires dislocations like the absence of yield confirmation to FX movement or dislocations between headlines and core numbers. In this case, traders wait 10−20 minutes for exhaustion of the initial move and reversal setup search.

Risk management is crucial. Most traders limit their position size to 0.25%-0.50% of their equity because of widening spreads and slippage. Sometimes the decision to trade off is more optimal during extreme volatility than forced entry.

One Way to Prepare for the Next CPI Day Release

A simple way to get ready is to monitor EUR/USD, GBP/USD, and USD/JPY pairs and an economic calendar with events' importance. The workflow is simple: Economic calendar → release → Trading platform.

The final step brings traders to the execution platform. Many turn to JustMarkets, which offers CFDs on these currency pairs, with execution stability and fast market access that make it well suited for high-volatility macro events.


Disclaimer: For informational purposes only. Trading financial instruments involves significant risk and may not be suitable for all investors. Ensure you understand the risks involved and trade responsibly.

 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Plasduce Mbossa akitoa maelezo kuhusu ujenzi na ukarabati wa meli kabla ya uzinduzi uliofanyika katika bandari ya Kigoma mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Meli 4 za mizigo zitakazo hudumu katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, tarehe 20 Julai.



Matukio mbalimbali katika uzinduzi wa Meli 4 za mizigo zitakazo hudumu katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, tarehe 20 Julai, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kigoma, tarehe 20 Julai, 2026.
 

-Yalenga kurejesha mawasiliano ya barabara kwa muda mfupi wakati wa dharura

‎Dar es Salaam

‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wake kwa kuwapatia mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya kisasa ya mabomba ya "Weholite" yanayotumika kujenga makalavati ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza ufanisi wa kurejesha mawasiliano ya barabara yanapokatika kutokana na mvua kubwa.

‎Mafunzo hayo yamefanyika kwa ushirikiano na kampuni ya Mega Pipes Solutions Ltd na kuwashirikisha Mameneja wa TARURA kutoka mikoa yote 26 pamoja na wahandisi waliobobea katika usanifu wa madaraja.

‎‎Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mhandisi Mshauri wa TARURA Makao Makuu, Pharles Ngeleja amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wahandisi na mameneja wa TARURA kutumia teknolojia ya "Weholite" katika kurejesha mawasiliano ya barabara kwa haraka hususan wakati wa mvua kubwa zinazosababisha kukatika kwa miundombinu.

‎Amesema washiriki wamepatiwa elimu kuhusu hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ikiwemo upembuzi yakinifu, usanifu na uandaaji wa makadirio ya gharama (BOQ) jambo litakaloongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

‎"Teknolojia hii inatuwezesha kurejesha mawasiliano ya barabara ndani ya muda mfupi pindi yanapokatika. Tayari tumeitumia katika maeneo mbalimbali ikiwemo mikoa ya Kilimanjaro na Dar es Salaam ambapo imesaidia wananchi kuendelea kupata huduma za kijamii na shughuli za kiuchumi bila usumbufu", amesema Ngeleja.

‎‎Kwa upande wake, Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha Mhandisi Nicholas Francis amesema mafunzo hayo yataongeza uwezo wa wahandisi kutumia teknolojia hiyo yenye gharama nafuu na  inayorahisisha ujenzi wa makalavati na miundombinu mingine ya kuvusha maji.

‎"Paipu Kalavati hizi zinapatikana katika ukubwa tofauti zikiwemo zenye kipenyo cha hadi mita 3 ambazo zinaweza kutumika kujenga makalavati au madaraja madogo ya mita 4 hadi 5 na unaweza kujenga ndani ya siku 30 na kuruhusu barabara kupitika kwa haraka",  amesema.

‎Ameongeza kuwa teknolojia hiyo tayari imetumika katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwenye mifereji ya maji ya mvua ambapo imeonyesha ufanisi mkubwa na inakadiriwa kudumu kwa zaidi ya miaka 100 bila kushambuliwa na kutu au kuharibika.

‎Naye, Mhandisi wa Mauzo kutoka kampuni ya Mega Pipes Solutions Ltd, Mafikiri Mushi ameishukuru TARURA kwa kuendelea kuamini teknolojia hiyo na kushirikiana na kampuni hiyo katika kuimarisha miundombinu ya barabara.

‎‎Amesema ana matumaini kuwa baada ya mafunzo hayo wahandisi wa TARURA wataongeza matumizi ya paipu kalavati za "Weholite" katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini hatua itakayochochea ujenzi wa miundombinu imara, kisasa na yenye gharama nafuu kwa manufaa ya wananchi.









Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro inaendelea kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo ndani na nje ya Ngorongoro ili kuidhihirishia dunia kuwa eneo hilo ni hazina ya ulimwengu.

Akitoa maelezo kwa kaimu mkurugenzi wa idara ya Afrika kutoka wizara ya mambo ya nje ya Sweden bwana Dario Jovic, Afisa Mhifadhi mkuu wa Ngorongoro anayeshughulikia Masoko bwana Michael Makombe amesema pamoja na kreta ya Ngorongoro hifadhi hiyo ina mapango ya tembo na maporomoko ya maji ambayo mtalii akifika katika eneo hilo huondoa msongo wa mawazo.

Amevitaja vivutio vingine kuwa ni pamoja na kreta za Empakai na Olmoti,mchanga unaohama, mlima Lolmalsin, tambarare za mazalia ya Nyumbu Ndutu, mapango ya Amboni,kimondo cha Mbozi na magofu ya Engaruka.

Akitoa sifa ya moja ya kivutio bwana Makombe amesema kuna kivutio cha mchanga unaohama kwa kati ya mita 15-17 kwa mwaka ukiwa na umbo la nusu mwezi bila kuachana ambapo watalii wengi hufika kuona maajabu hayo.

Ameeleza jamii katika eneo hilo huamini mchanga wa eneo hilo ni tiba kwa mahusiano yaliyolegalega na kuwataka wasweden kutembelea Tanzania ili kujionea maajabu hayo.

Hifadhi ya Ngorongoro pia imepambwa na utamaduni wa kihistoria ambapo eneo la jiopaki ya Ngorongoro Lengai kuna makabila ya wahadzabe na wadatoga ambapo makabila hayo bado yanaheshimu mila na utamaduni wao bila kuathiriwa na mila nyingine.


Na Mwandishi Wetu 

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania(TRAMEPRO Tanzania ) limetoa mwitokwa Watanzania, Waafrika na jumuiya ya kimataifa kuendelea kujenga jamii inayoheshimu utu wa kila mtu, kuwekeza katika elimu, afya, sayansi, mazingira na amani.

TRAMEPRO imetoa mwito huo leo Julai 18,2026 katika kukimbizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela aliyekuwa Rais wa nchi ya Afrika Kusini. 

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu TRAMEPRO Tanzania  Boniventura Mwalongo amesema wanaungana na mataifa ya Afrika na dunia kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela mmoja wa viongozi mashuhuri waliobadilisha historia ya dunia kwa kupigania uhuru, usawa, haki za binadamu na maridhiano.

Pia amesema mambo ya kujifunza kupitia kutoka kwa Nelson Mandela ni kwamba elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ya kubadilisha dunia, msamaha ni nguvu, si udhaifu; hujenga taifa lenye umoja.

Mengine ni uvumilivu na subira vinaweza kushinda hata changamoto kubwa,  Uongozi ni huduma, si nafasi ya kutawala wengine, haki  na usawa ni msingi wa maendeleo endelevu.

"Mandela anatufundisha pia umoja wa Waafrika na kuheshimiana ni nguzo ya maendeleo ya bara letu. Afya, mazingira na maendeleo vinapaswa kwenda pamoja kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, " amesema Mwalongo. 

Akieleza zaidi amesema kwa waratibu asili Asili,TRAMEPRO Tanzania inaona mafunzo makubwa kutoka kwa Mandela katika kujenga umoja wa sekta, kuzingatia maadili ya taaluma, kuendeleza utafiti, kuhifadhi mimea tiba, kulinda mazingira na kushirikiana na taasisi za kisayansi ili tiba asili ichangie kikamilifu afya na maendeleo ya jamii.

Kuhusu historia ya Nelson Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji cha Mvezo, Mkoa wa Eastern Cape, Afrika Kusini. Jina lake la asili, Rolihlahla, katika lugha ya Kixhosa humaanisha mtu anayetikisa tawi la mti, na kwa maana ya kawaida huashiria mtu mwenye kuhoji au kupinga hali iliyopo.

Alipoanza shule ya msingi, mwalimu wake alimpa jina la Nelson, kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo katika shule nyingi za kikoloni.

Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme ya kabila la Thembu. Baba yake aliitwa Gadla Henry Mphakanyiswa Mandela, aliyekuwa mshauri wa mfalme wa Thembu, na mama yake aliitwa Nosekeni Fanny Mandela.

 Kutoka kwa wazazi wake alijifunza heshima, uwajibikaji, uongozi na umuhimu wa kuitumikia jamii.

Katika elimu, Mandela alianza masomo katika shule za wamisionari, akaendelea katika Chuo cha Healdtown, kisha akasoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare. 

Baadaye alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, ambako alijiandaa kuwa mwanasheria na mtetezi wa haki za wanyonge. Elimu yake ilimpa msingi wa kuelewa sheria na kuitumia kutetea usawa na utu wa binadamu.

Mandela aliongoza mapambano dhidi ya mfumo wa ubaguzi wa rangi (Apartheid). Kutokana na msimamo wake, alifungwa gerezani kwa miaka 27, lakini hakukata tamaa wala kuacha kuamini kuwa amani na maridhiano vinaweza kushinda chuki. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990, aliongoza mazungumzo yaliyoweka msingi wa Afrika Kusini mpya yenye demokrasia.


Mwaka 1994, Nelson Mandela aliingia katika historia kwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini aliyechaguliwa kidemokrasia. Uongozi wake ulijengwa juu ya maridhiano, msamaha na umoja wa kitaifa. Mwaka 1993, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mchango wake katika kumaliza Apartheid kwa njia ya amani.

The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi, has thanked the Government of India for its continued efforts to strengthen cooperation with Tanzania in the sectors of education, health, trade, investment, water, science and technology.

President Dr. Mwinyi made the remarks today, July 19, 2026, when he met with India's Minister of External Affairs, Hon. Dr. S. Jaishankar, at a conference hall at the Taj Palace Hotel in New Delhi, India.

During the discussions, President Dr. Mwinyi asked India to increase the number of scholarship and training opportunities for students and professionals from Zanzibar, as well as to strengthen the IIT Madras Zanzibar campus by introducing more academic programmes and supporting the construction of its permanent campus.

President Dr. Mwinyi also handed over to Minister Jaishankar the Master Plan for the construction of the permanent IIT Madras Zanzibar campus, aimed at making Zanzibar a hub for higher education, research, innovation and technology for the African region.

For his part, Minister Dr. Jaishankar commended the progress made by IIT Madras Zanzibar and reaffirmed the Indian Government's commitment to continuing to strengthen cooperation with Tanzania across various development sectors.

President Dr. Mwinyi continues his visit to India, where he is meeting with various leaders with the aim of strengthening development cooperation between Zanzibar, Tanzania and India.









Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amewataka wakaguzi wa shule kutenda haki kwa shule binafsi na kuziona kama mshirika wa maendeleo badala ya mshindani.

Kadhalika, Profesa Tibaijuka ameipongeza shule ya St Anne Marie Academy kwa kuendelea kusomesha bure wanafunzi wanaofiwa na wazazi wao ikiwa shule pekee ya binafsi inayofanya hivyo kwa sasa nchini.

Alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa shule hiyo Julai 18, mwaka 2001.

Aliwataka wakaguzi wa elimu nchini kuacha kuziwekea vikwazo shule binafsi kwa kuziona kama washindani kwenye sekta ya elimu na badala yake wanatakiwa kuwaona kama washirika muhimu kwenye kutoa huduma hiyo.

”Unakuta wanawawekea wenye shule binafsi viwango vya kusadikika tofauti kabisa na shule za umma, sisemi kwama muwawekee viwango hafifu, hapana mimi nataka uwiano wa haki baina ya shule za umma na shule binafsi,” alisema

Alisema shule zingine zinapaswa kuiga mfano huo kwani elimu ni huduma na siyo biashara hivyo wanatakiwa kuwaacha waendelee na masomo baada ya wazazi wao wanaowalipia ada kufariki dunia.

Kadhalika, Profesa Tibaijuka alisema serikali imebadili mitaala ya zamani na kuingiza mitaala ya ufundi ambayo inamwezesha mwanafunzi kuchagua na hivyo kupata ujuzi utakaowawezesha kupata ajira au kujiajiri mapema wanapomaliza masomo yao.

Alisema wakati huu wa teknolojia ya kisasa shule zinapaswa kwenda na wakati kwa kuhakikisha zinakwenda sanjari na dunia ya sasa kwa kuwa na mafunzo ya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA.

Alisema shule bora ni ile yenye uwezo wa kufaulisha mwanafunzi ambaye alikuwa na matokeo ya kawaida kwani kuna baadhi ya shule ambazo zimekuwa zikichuja wanafunzi na kuchukua wale waliofaulu vizuri pekee.

“Kama mwanafunzi amefaulu kwa daraja la kwanza ili tujue hiyo ni shule bora lazima tujue aliingia akiwa na daraja la ngapi, kuna wanafunzi wengine kwa uwezo wao mkubwa hawahitaji hata mwalimu sasa ukichukua mwanafunzi bora akafaulu huwezi kujisifu,” alisema

“Nawapongeza St Anne Marie Academy kwani wao wamekuwa wakichukua wanafunzi wa kawaida na kuwatengeneza kufaulu kwa wastani wa daraja la kwanza na daraja la pili, nimemsikia Mkurugenzi akitaja mafanikio ya shule imekuwa ikiingiza wanafunzi bora kitaifa kila mwaka nawapongeza sana,” alisema

Mkurugenzi wa shule hiyo, Dkt. Jasson Rweikiza shule hiyo iliwahi kupata mwanafunzi bora kitaifa kwenye somo la hisabati kidato cha nne mwaka 2013, shule hiyo iliingia 10 bora kitaifa kwa miaka mine mfululizo na kwamba mwaka 2021 shule hiyo ilipata mwanafunzi bora kitaifa kwenye masomo yote.


Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
SERIKALI imesema itaendelea kuimarisha huduma za afya ya uzazi nchini ili kupunguza vifo vya kina mama vinavyotokana na utoaji mimba usio salama.

Naibu Waziri wa Afya, Dk Florence Samizi alisema bungeni kuwa asilimia 10 ya vifo vya wajawazito nchini vinahusishwa na utoaji mimba usio salama, hali inayoonyesha umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika kinga, elimu na huduma za matibabu kwa wanawake.

Alisema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeboresha miundombinu ya sekta ya afya na kuendelea kutoa huduma jumuishi baada ya utoaji mimba (CPAC) bila malipo katika vituo vya kutolea huduma za afya.

"Tunawapatia wanawake huduma baada ya kuharibikiwa na mimba, ikiwemo matibabu, dawa, ushauri nasaha na elimu ya uzazi wa mpango ili kupunguza hatari ya kupata mimba nyingine isiyotarajiwa na kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza," alisema Dk Samizi.

Aliongeza kuwa serikali inaendelea kuimarisha huduma rafiki kwa vijana kwa kutoa elimu ya afya ya uzazi, kujikinga dhidi ya mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa, pamoja na kuhakikisha manusura wa ukatili wa kijinsia na matukio mengine wanapata huduma stahiki kwa wakati.

Kauli hiyo imekuja wakati wadau mbalimbali wakiendelea kujadili utekelezaji wa Itifaki ya Maputo, ambayo Tanzania iliiridhia.

Mjadala umejikita zaidi kwenye Ibara ya 14(2)(c) ya itifaki hiyo, inayozitaka nchi wanachama kuchukua hatua zinazofaa kuruhusu utoaji mimba kwa njia ya tiba katika mazingira maalumu, ikiwemo pale ujauzito umetokana na ubakaji, unyanyasaji wa kingono, ndugu wa damu (incest), au endapo kuendelea kwa ujauzito kunaweka maisha au afya ya mama katika hatari, au maisha ya kijusi yako hatarini. Utekelezaji wa masharti hayo unafanyika kwa kuzingatia sheria za ndani za kila nchi.

Nchini Tanzania, utoaji mimba kwa hiari bado unadhibitiwa na sheria, isipokuwa katika mazingira yanayotambuliwa na sheria husika.

Hata hivyo, Serikali imeendelea kusisitiza kuwa wanawake wanaopata madhara baada ya utoaji mimba wanapaswa kufika katika vituo vya afya ili wapate matibabu, ushauri nasaha na huduma nyingine muhimu bila kuchelewa.

Wataalamu wa afya wanasema utoaji wa huduma hizo, sambamba na elimu ya afya ya uzazi na upatikanaji wa huduma kwa wakati, ni miongoni mwa hatua muhimu zinazoweza kupunguza vifo vya kina mama na kuboresha afya ya uzazi nchini.
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Makonda, ameridhishwa na maboresho yanayoendelea katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center inayotoa huduma kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, ALMC–JKCI Arusha.

Maboresho hayo yanafanyika kwa uwezeshaji wa Global Medicare, kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma za afya, kuboresha mazingira ya matibabu, kuimarisha utalii tiba na kuiandaa hospitali kutoa huduma zinazokidhi viwango vya kimataifa kuelekea mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2027.

“Lengo kubwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kabisa na katika mazingira mazuri. Vilevile tunataka kuimarisha utalii tiba na kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya AFCON 2027,” alisema Makonda.

Makonda pia alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya afya na kuruhusu taasisi za kibingwa kama JKCI kupanua huduma zake hadi mikoani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa JKCI ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Peter Kisenge, alisema maboresho yanayoendelea yanalenga kuibadilisha ALMC–JKCI kuwa kituo cha kisasa cha huduma za kibingwa chenye mazingira rafiki kwa wagonjwa.

Dkt. Kisenge alisema lengo ni kuhakikisha mgonjwa anapofika hospitalini anakutana na mazingira yenye usafi, utulivu, faraja na huduma zinazofanana na zinazopatikana katika hospitali kubwa za kimataifa.

“Tunataka mgonjwa anapokuja hapa asiingie katika mazingira yanayomwongezea hofu. Tunataka akute hospitali yenye mazingira mazuri, tulivu na yenye huduma zinazompa faraja,” alisema Dkt. Kisenge.

Kwa mujibu wake, skrini moja itaonyesha taarifa za wagonjwa waliopo wodini, ikiwemo mapigo ya moyo, kiwango cha oksijeni kwenye damu, shinikizo la damu na viashiria vingine muhimu vya afya.

Skrini nyingine itaunganishwa na mfumo wa Dozee, teknolojia inayowezesha mgonjwa kuendelea kufuatiliwa hata baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

Alisema mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji, upasuaji wa kujifungua au matibabu mengine yanayohitaji uangalizi wa siku kadhaa ataweza kufuatiliwa akiwa nyumbani, huku wauguzi na madaktari wakipokea taarifa za afya yake kwa wakati.

Dkt. Kisenge alisema mfumo huo utasaidia kugundua mapema mabadiliko ya hali ya mgonjwa na kuwawezesha wataalamu wa afya kuchukua hatua kabla hali haijawa mbaya.

Alisema vyumba vya wagonjwa vitawekewa vifaa vya kisasa vya ufuatiliaji, televisheni na mifumo ya kidijitali ya kuhifadhi historia ya mgonjwa, uchunguzi, dawa na matibabu yote anayopatiwa.

Dkt. Kisenge alisema hospitali pia inaandaa wodi maalumu ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu baada ya kutoka katika chumba cha wagonjwa mahututi, inayojulikana kama High Dependency Unit.

Dkt. Kisenge alisema mashine ya Cath Lab yenye thamani ya takribani shilingi bilioni tatu inatarajiwa kuwekwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya matatizo ya mishipa ya moyo.

Mkurugenzi wa Huduma za Kliniki wa ALMC–JKCI Arusha, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Sakeh Mwishete, alisema uongozi wa hospitali umeweka mkakati wa kuhakikisha wagonjwa wenye mahitaji tofauti wanapata huduma zinazowafaa.

Dkt. Mwishete alieleza kuwa vyumba vya VIP vimewekewa vifaa vinavyowezesha kubadilishwa haraka kuwa vyumba vya uangalizi maalumu au ICU endapo hali ya mgonjwa itabadilika.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mji

“Hiki ni chumba cha VIP, lakini kimewekewa vifaa maalumu. Endapo hali ya mgonjwa itabadilika, kinaweza kupandishwa hadhi na kutoa huduma za dharura au huduma zinazohitajika katika ICU bila kuchelewa,” alisema Dkt. Mwishete.

Naye, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura katika ALMC–JKCI Arusha, Dkt. Farida Abdallah, alisema kitengo cha dharura kinaendelea kupokea wagonjwa kutoka Arusha, Manyara, Singida na maeneo mengine ya Kanda ya Kaskazini.

“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha mgonjwa wa dharura anapata huduma kwa wakati ili kuzuia madhara ya kudumu au kupoteza maisha. Mimi pamoja na timu yangu tunafanya kazi saa 24 kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma za haraka,” alisema Dkt. Farida.


Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kuimarisha utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola kwa kuendesha mafunzo kwa vitendo kwa wataalamu wa afya, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kuimarisha uwezo wa mfumo wa afya katika kuzuia, kugundua na kutoa mwitikio wa haraka dhidi ya magonjwa ya mlipuko.

Hayo yamesemwa Julai 17,2026, na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dkt. Ibrahim Isack, wakati wa zoezi la usimamizi shirikishi na mafunzo kwa vitendo ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko, amesema kuwa maandalizi ya kutosha ndiyo msingi wa kudhibiti athari za milipuko kwa wananchi.

“Ebola ni ugonjwa unaohitaji umakini mkubwa na hatua za haraka. Wataalamu wa afya wanapaswa kuwa na uwezo wa kutambua viashiria vya awali, kutoa taarifa kwa wakati na kuanzisha hatua za awali za udhibiti ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi,” amesema Dkt. Isack.

Amesema usimamizi shirikisishi na mafunzo kwa vitendo hutoa nafasi ya kutathmini utendaji wa huduma za afya katika mazingira yanayofanana na hali halisi, jambo linalosaidia kubaini mapungufu yaliyopo na kuweka mikakati ya kuyafanyia kazi kabla ya kutokea kwa dharura.

Aidha, Dkt. Isack amesema mafanikio katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanategemea ushirikiano wa karibu kati ya wataalamu wa afya, viongozi wa sekta ya afya na taasisi mbalimbali, ili kuhakikisha kila ngazi inatimiza wajibu wake kwa wakati na kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura kutoka wizara ya afya, Dkt. Michael Kiremeji amesema mafunzo hayo yanalenga kuendelea kujenga umahiri wa wataalamu wa afya katika kutoa huduma salama na kufuata taratibu za kitaalamu wakati wa kukabiliana na magonjwa ya mlipuko, hatua inayochangia kuimarisha usalama wa wagonjwa na wahudumu wa afya.

Ameongeza kuwa Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuendesha mafunzo na usimamizi shirikishi katika maeneo mbalimbali nchini, kwa lengo la kuimarisha mfumo wa afya, kuongeza utayari wa kukabiliana na dharura za afya ya umma na kulinda afya za wananchi.









KUTOKA VUNJO

MBUNGE wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, Enock amewahimiza vijana kuendelea kumcha Mungu, kuzingatia maadili mema na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha maisha na mustakabali wao.

Koola alitoa kauli hiyo leo wakati wa ufunguzi wa bonanza la michezo la vijana wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kilimanjaro mashariki lililofanyika Marangu mashariki lililowakutanisha vijana 500 kutoka maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.

Koola aliwasisitiza vijana kujiepusha na makundi ya kihalifu, kuwa wazalendo na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya jamii na taifa.

Bonanza hilo linalenga kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa vijana kupitia ibada, maombi, kujifunza Neno la Mungu na kushiriki michezo mbalimbali inayokuza afya, nidhamu na maendeleo ya kijamii.

Alieleza kuwa, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Vunjo imeendelea kutekeleza programu mbalimbali zinazolenga kuwawezesha vijana kiuchumi ambapo  zinajumuisha mafunzo ya ufugaji wa kuku wa kibiashara, ufugaji wa ng'ombe wa maziwa, ufugaji wa samaki, kilimo cha kisasa na ujasiriamali, kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kujiajiri na kuongeza kipato.

Alisema kuwa, ofisi yake imewaajiri vijana mahsusi ili kuwasaidia wenzao kuunda vikundi vya kiuchumi, kuandaa katiba za vikundi, kukamilisha nyaraka za maombi ya mikopo ya Halmashauri isiyo na riba, pamoja na kuwaunganisha na taasisi za kifedha zinazotoa mikopo yenye masharti nafuu.

Alisisitiza kuwa uwekezaji kwa vijana ni msingi wa maendeleo endelevu ya Jimbo la Vunjo na Taifa kwa ujumla na kuahidi kuendelea kushirikiana na taasisi za dini na wadau mbalimbali katika kuwawezesha vijana kupata elimu, stadi za maisha na fursa za kiuchumi zitakazowasaidia kujenga maisha bora na kuchangia maendeleo ya nchi.







Top News