Zaidi ya wakulima 2,000 wa kahawa, mbaazi na mazao mengine katika mikoa ya Arusha na Manyara wamenufaika na huduma za kifedha kidijitali za Mixx, zinazowawezesha kupokea malipo ya mazao, kupata mikopo na huduma za bima bila kulazimika kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za kifedha.

Meneja wa Biashara wa Mixx by Yas Kanda ya Kaskazini, Eric Sosthenes, amesema matumizi ya huduma hizo yanawapa wakulima njia salama na rahisi zaidi ya kusimamia fedha zao, huku yakiwapunguzia muda na gharama zilizokuwa zikitumika kufuata huduma za kifedha.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Arusha, Sosthenes alisema kupitia huduma ya Mixx Kilimo, wakulima wanaweza kupokea malipo ya mazao moja kwa moja kwa njia ya kidijitali pamoja na kupata huduma nyingine za kifedha zinazolenga kusaidia shughuli zao za kilimo.

“Tunataka mkulima awe na uwezo wa kupokea fedha zake kwa usalama na kwa wakati bila kulazimika kusafiri umbali mrefu. Kupitia Mixx Kilimo, tunarahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha zinazomsaidia mkulima kuendesha shughuli zake na kujiendeleza,” alisema.

Alisema huduma hiyo ni sehemu ya jitihada za Mixx kuongeza ujumuishaji wa kifedha miongoni mwa wakulima, hasa wale waliopo maeneo ambayo upatikanaji wa huduma za kawaida za kifedha umekuwa ukihitaji muda na gharama zaidi.

Baadhi ya wakulima wanaotumia huduma hiyo, akiwemo Ezekiel Mlingi na Baraka Emmanuel, walisema matumizi ya huduma za kidijitali yamewapunguzia changamoto ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za kifedha.

Walisema uwezo wa kupokea na kufanya miamala kupitia simu umewarahisishia kusimamia fedha zao na kutumia muda zaidi katika shughuli za uzalishaji.

Mixx imesema itaendelea kutumia huduma ya Mixx Kilimo kuwafikia wakulima wengi zaidi na kuwawezesha kupata huduma za kifedha kwa njia salama na rahisi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kutumia teknolojia kuboresha shughuli za kilimo na maisha ya wakulima.

Eric Sosthenes - Meneja wa Biashara Mixx - Kanda ya Kaskazini





Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (kushoto), akizungumza na watendaji kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) jijini Dar es Salaam Agosti 8, 2026.

.Baadhi ya Watendaji kutoka Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano za PSSSF, NSSF na OSHA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, akizungumza na watendaji kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) jijini Dar es Salaam Agosti 8, 2026.



Dar es salaam, Agosti 8, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu (Mb) leo (Jumamosi, Agosti 8, 2026) amefanya vikao kazi jijini Dar es salaam na Menejimenti za taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utendaji.

Katika vikao kazi hivyo, Waziri Sangu, kwa nyakati tofauti amekutana na Menejimenti za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Mashirika ya Umma (PSSSF); Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF); Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF); na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA).

Waziri Sangu amepokea taarifa za utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo kutoka kwa watendaji wake wakuu na kuelekeza taasisi hizo kuendelea kuongeza ufanisi hususan katika matumizi ya teknolojia ya Habari na mawasiliano (TEHAMA) katika utendaji na utoaji huduma kwa wananchi.

“Nawaelekeza kuongeza utoaji wa elimu ya matumizi ya kidijitali katika mifumo yetu ili kuwawezesha wale wasio na elimu ya kidijitali kupata huduma zetu kwa urahisi na haraka,” amesema Waziri Sangu.

Vikao hivyo vilihudhuriwa na Mkurugenzi wa Hifadhi ya Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Festo Fute, Wakurugenzi Wakuu wa PSSSF, NSSF, WCF na OSHA pamoja na wajumbe wa Menejimenti za taasisi hizo.

Mhe. Sangu ameendesha vikao kazi hivyo baada ya jana kukamilisha ziara yake ya siku saba katika wilaya zote za mkoa wa Lindi iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali mkoani humo.

Waswahili husema Chanda chema huvikwa pete msemo ambao umedhihirika siku ya mnyama “Simba Day “ baada ya klabu hiyo kumtunuku tuzo Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Abdul-Razaq Badru kutokana na mchango wake mkubwa wa kuunganisha utalii na michezo.

Kamishna Badru amekabidhiwa tuzo hiyo kutokana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kukubali na kushiriki kikamilifu maadhimisho ya wiki ya simba ambapo mamlaka ilitumia fursa hiyo kutangaza shughuli zake za uhifadhi na utalii na kukaribisha wadau mbalimbali kurudi nyumbani Ngorongoro

Dhamira ya Kamishna Badru ni kuhakikisha kuwa utalii wa Ngorongoro na michezo unafungamanishwa  sambamba ambapo tarehe 13 Julai,2026 mamlaka hiyo na klabu ya Simba ziliafikiana kushirikiana  katika tukio hilo lenye mamilioni ya watazamaji ndani na nje ya nchi ambalo uzinduzi wake ulifanyika tarehe 1 agosti, 2026 ndani ya Kasoko ya Ngorongoro.

“Chapa hizi mbili kubwa kimataifa zinaafikiana katika jambo hili kwa kuwa tunataka kutangaza utalii wa vivutio vilivyopo Ngongoro ndani na nje ya nchi na tuna uhakika tutafanikiwa kutokana na ukubwa wake  na kusaidia dhamira ya Serikali kuongeza wageni wengi zaidi wanaotembelea Ngorongoro ambayo ni kivutio namba moja Afrika kwa mwaka 2023 na 2025 ”.alisema Kamishna Badru.

Kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Klabu ya Simba kukamilisha tukio hilo jana tarehe 8, Agosti 2026 ni kama wamepiga bao la kusigino kutokana na maelfu ya watu kushiriki na kuridhika kwa mafanikio ya “Simba Day”.






Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Katikati), akipewa maelezo kuhusu huduma mbalimbali za kibenki zinazotolewa na Benki ya Absa Tanzania, alipotembelea banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, yaliyohitimishwa jana kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma.
Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Mwilongo Msungu (wa pili kushoto), akitoa maelezo kuhusu huduma za kibenki zinazotolewa na benki hiyo kwa mkazi wa Dodoma, Pius Killo, alipofika katika banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, yaliyomalizika jana kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma. Kushoto ni Meneja wa benki hiyo Mkoani Dodoma, Bw. Deogratias Luena na wa tatu kushoto ni Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi.
Meneja wa Benki ya Absa Mkoani Dodoma, Bw. Deogratias Luena (katikati), akitoa maelezo kuhusu huduma za kibenki zinazotolewa na benki hiyo kwa baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, yaliyomalizika jana, kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma.



Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya Absa Mkoani Dodoma, Bw. Emmanuel Basharasha, akitoa maelezo kuhusu huduma za kibenki zinazotolewa na benki hiyo kwa baadhi ya watembeleaji katika banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma jana.


Ofisa Mauzo wa Benki ya Absa Tawi la Dodoma, Bw. Gabriel Mlaga (kulia), akimpiga picha kwa ajili ya kufungua akaunti mpya ya mmoja ya wateja waliofika katika banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma jana.




Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Mwilongo Msungu (wa pili kulia), akitoa maelezo kuhusu huduma na bidhaa zinazotokewa na benki hiyo kwa Ofisa Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), Dk. John Joseph (wa pili kushoto), alipotembelea banda la benki hiyo, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane yaliyohitimishwa jana kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma.

Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Mwilongo Msungu (katikati), Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa benki hiyo, Bi. Abigail Lukuvi (wa pili kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa Absa tawi la Dodoma, wakipiga picha ya pamoja katika banda lao benki, wakati wa maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Wakulima ya Nane Nane, kwenye Viwanja vya Dk. John Samuel Malecela, Mkoani Dodoma.





- Yaendelea kukabidhi Malori kwa Vyama vya Ushirika

Kufuatia hatua ya Serikali kukabidhi Shilingi bilioni 300 kwa taasisi saba za kifedha, ikiwemo Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), kwa ajili ya kuwawezesha wanawake na vijana katika mnyororo wa thamani wa kilimo, benki hiyo imesisitiza utayari wake wa kutekeleza mpango huo kupitia suluhisho za kifedha bunifu na zinazokidhi mahitaji ya wakulima.

Akihitimisha Maadhimisho ya Maonesho ya Kilimo Nanenane 2026 yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma mwishoni mwa wiki, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi bilioni 300 kwa wakurugenzi wa taasisi hizo saba za kifedha, akisisitiza umuhimu wa kuongeza fursa za kifedha kwa makundi hayo ya kijamii ili yaweze kushiriki kikamilifu na kunufaika zaidi na fursa zinazotokana na sekta ya kilimo.

Akizungumzia utayari wa benki hiyo kutekeleza mpango huo, Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa NBC, Bw. Jacob Nangi, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Bw. Theobald Sabi, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuiamini NBC katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya uwezeshaji, hususan inayolenga vijana, wanawake na sekta ya kilimo.

Alisema NBC tayari imejipanga kutekeleza dhamira hiyo kwa kuendelea kubuni bidhaa na suluhisho za kifedha zinazokwenda sambamba na mahitaji ya makundi hayo.

“Pamoja na kuipongeza Serikali na Mheshimiwa Rais kwa hatua hiyo na kuona NBC inastahili kuwa mmoja wa wadau muhimu katika kufanikisha mpango huu, nisisitize utayari wetu wa kufanikisha mpango huu kulingana na malengo ya Serikali ya kuwasaidia vijana na wanawake nchini kushiriki na kunufaika kikamilifu na fursa mbalimbali zinazotokana na mnyororo mzima wa sekta ya kilimo,” alisema Bw. Nangi.

Akieleza hatua zinazochukuliwa na NBC kuthibitisha dhamira yake ya kuiwezesha sekta ya kilimo, Bw. Nangi alisema benki hiyo imeendelea kwenda hatua moja zaidi ya utoaji wa huduma za kawaida za kibenki kwa wakulima, kwa kubuni suluhisho zinazolenga changamoto na mahitaji mbalimbali yanayojitokeza katika mnyororo mzima wa thamani.

Katika kilele cha Maonesho hayo, NBC ilikabidhi rasmi malori 13 kwa Vyama Vikuu vya Ushirika vya RUNALI na Lindi Mwambao vya mkoani Lindi, na hivyo kufanya idadi ya malori yaliyotolewa na benki hiyo kwa vyama vya ushirika kufikia 28, baada ya kukabidhi malori mengine 15 kwa vyama vya TANECU na KACU mapema wiki iliyopita. Hatua hiyo inalenga kuongeza uwezo wa vyama hivyo kusafirisha mazao ya wakulima kwa ufanisi zaidi.

Benki hiyo pia ilikabidhi mkopo wa uboreshaji wa makazi kwa Bw. Emmanuel Nyambi Masanja, mkulima na mwanachama wa AMCOS ya Kasandalala, iliyopo Ushetu wilayani Kahama. Bw. Masanja ni miongoni mwa wakulima 57 waliowezeshwa na NBC kupitia mpango wa mikopo ya uboreshaji wa makazi kwa wakulima.

“Jitihada zote hizi zinaakisi mkakati wa NBC wa kwenda hatua moja zaidi ya utoaji wa huduma za kawaida za kibenki kwa wakulima. Tunataka kutoa suluhisho zinazogusa mahitaji muhimu katika mnyororo mzima wa thamani—kuanzia uzalishaji, upatikanaji wa mitaji, usafirishaji na uhifadhi wa mazao hadi kuboresha maisha na makazi ya wakulima,” aliongeza Bw. Nangi.

Akifafanua kuhusu uwezeshaji huo, Mkuu wa Idara ya Kilimo wa NBC, Bw. Raymond Urassa, alisema kati ya malori 13 yaliyokabidhiwa kwenye kilele hicho, 10 yamekwenda kwa RUNALI na matatu kwa Lindi Mwambao.

Alisema uwezeshaji huo unalenga kuongeza uwezo wa vyama hivyo kusafirisha mazao kwa ufanisi, kupunguza changamoto za usafirishaji na hatimaye kuongeza thamani inayobaki kwa wakulima.

“Tofauti na mkopo wa malori 15 mengine tuliyokabidhi kwa Chama Kikuu cha Ushirika cha Tandahimba na Newala (TANECU) na Chama Kikuu cha Ushirika Kahama (KACU) hivi karibuni, mkopo huu kwa RUNALI na Lindi Mwambao una thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 1.5, na unatarajiwa kuboresha ufanisi wa shughuli za ushirika na kuongeza uwezo wa wakulima kufikisha mazao yao kwenye masoko,” alisema Bw. Urassa.

Hafla ya makabidhiano hayo ilishuhudiwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, ambaye alisema uwezeshaji huo unaendana na msisitizo wa Serikali wa kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za fedha na vyama vya ushirika kama njia muhimu ya kuwafikia wakulima wengi zaidi.

Dkt. Ndiege alisema ushirika una nafasi muhimu katika kuwaunganisha wakulima na taasisi rasmi za kifedha, hivyo kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi rasmi na kupata huduma zinazokidhi mahitaji yao.

“Hatua hii inaonyesha upanuzi wa mtazamo wa huduma za kifedha kwa wakulima, ambapo mkulima haonekani tu kama mzalishaji wa mazao, bali pia kama mteja mwenye mahitaji ya kifedha yanayogusa ustawi wa familia yake na maisha yake kwa ujumla,” alisema.

Alisema ameguswa pia na mpango wa NBC wa mikopo ya uboreshaji wa makazi ya wakulima, akieleza kuwa mpango huo unaweza kusaidia kubadilisha mtazamo wa muda mrefu wa kutolipa kipaumbele suala la makazi bora kwa wakulima.

“Zaidi, kupitia mpango huu wa mikopo ya uboreshaji wa makazi, wakulima wengi watashawishika kuingia kwenye ushirika ili wanufaike na fursa hii. Pia watahakikishiwa maboresho ya makazi yao kwa sababu huduma inatangulia, kisha malipo yanafanyika baada ya mkulima kuuza mazao yake. Nawashukuru na kuwapongeza sana NBC kwa kubuni mpango huu,” alisema Dkt. Ndiege.

Kwa upande wao, viongozi wa vyama vya ushirika vilivyonufaika na uwezeshaji huo pamoja na mkulima aliyepokea mkopo wa uboreshaji wa makazi waliipongeza NBC kwa kuendelea kubuni bidhaa zinazolenga mahitaji halisi ya wakulima.

Mwenyekiti wa Lindi Mwambao, Bw. Ismail Nalinga, Mwenyekiti wa RUNALI, Bw. Odas Odas Mpunga, na mkulima Emmanuel Nyambi Masanja, walisema mfumo wa mauzo ya mazao kupitia vyama vya ushirika umeendelea kuimarika na hivyo kuvifanya vyama hivyo kuwa daraja muhimu kati ya wakulima na taasisi rasmi za fedha.

Bw. Mpunga alisema maboresho katika mfumo wa mauzo ya mazao kupitia vyama vya ushirika yameongeza uaminifu na kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wakulima.

“Mfumo wa mauzo ya mazao kupitia vyama hivi vya ushirika umeziwezesha benki kama NBC kuwa na msingi unaotuwezesha kunufaika na huduma zao, hususani mikopo, kwa usahihi zaidi. Kwa msingi huo, sisi kama wakulima kwa sasa tumekaribiwa na taasisi za fedha kuliko wakati mwingine wowote,” alisema.

Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa Benki ya NBC, Bw. Jacob Nangi (kushoto) akikabidhi picha ya inayosadifu muonekano wa nyumba iliyofanyiwa maboresho kwa Bw. Emmanuel Nyambi Masanja (kulia), mkulima na mwanachama wa AMCOS ya Kasandalala, iliyopo Ushetu wilayani Kahama ambae ni miongoni mwa wakulima 57 waliowezeshwa na NBC kupitia mpango wa mikopo ya uboreshaji wa makazi kwa wakulima. Tukio hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye Maadhimisho ya Maonesho ya Kilimo Nanenane 2026 yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege pamoja na maofisa wengine wa benki ya NBC.

Akihitimisha Maadhimisho ya Maonesho ya Kilimo Nanenane 2026 yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma mwishoni mwa wiki, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) alikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi bilioni 300 kwa wakurugenzi wa taasisi saba za kifedha ikiwemo NBC akilenga kuongeza fursa za kifedha kwa wanawake na vijana waweze kushiriki kikamilifu na kunufaika zaidi na fursa zinazotokana na sekta ya kilimo.

Mkuu wa Idara ya Kilimo wa NBC, Bw. Raymond Urassa (wa pili kulia) akifafanua kuhusu huduma mbalimbali za benki hiyo mahususi kwa wakulima mbele Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege pamoja na wadau wengine.

Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa Benki ya NBC, Bw. Jacob Nangi (wa pili kushoto) akimkabidhi mfano wa ufunguo wa gari Mwenyekiti wa chama cha ushirika cha Lindi Mwambao, Bw. Ismail Nalinga (wa pili), ikiwa ni ishara ya makabidhiano rasmi ya malori matatu (3) yaliyowezeshwa kupitia mkopo wenye riba nafuu kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC). Malori hayo yanalenga kuboresha usafirishaji wa mazao, kuongeza ufanisi wa shughuli za ushirika na kuimarisha kipato cha wakulima. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkuu wa Idara ya Kilimo wa NBC, Bw. Raymond Urassa (kulia) na Meneja wa Benki ya NBC tawi la Dodoma Bi Happyness Kizigira (kushoto)

Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa Benki ya NBC, Bw. Jacob Nangi (wa pili kushoto) akimkabidhi mfano wa ufunguo wa gari Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha RUNALI, Bw. Odas Odas Mpunga (wa pili), ikiwa ni ishara ya makabidhiano rasmi ya malori kumi (10) yaliyowezeshwa kupitia mkopo wenye riba nafuu kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC). Malori hayo yanalenga kuboresha usafirishaji wa mazao, kuongeza ufanisi wa shughuli za ushirika na kuimarisha kipato cha wakulima. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkuu wa Idara ya Kilimo wa NBC, Bw. Raymond Urassa (kulia) na Meneja wa Benki ya NBC tawi la Dodoma Bi Happyness Kizigira (kushoto)

Mkurugenzi wa Huduma za Biashara wa Benki ya NBC, Bw. Jacob Nangi (katikati) akionyesha cheti cha kutambua ushiriki na udhamini wa benki hiyo kwenye Maonesho ya Kilimo Nanenane2026 yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. Wengine wanaoonesha ishara ya ‘Tunakuona mbali’ ni maofisa waandamizi wa benki hiyo.

Tunakuona mbali mkulima

Viongozi mbalimbali wa serikali waliapata wasaa wa kutembelea banda la NBC lilikuwepo kwenye Maonesho ya Kilimo Nanenane2026 yaliyohitimishwa katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.


Wakulima wa Kanda ya Kati wanaotumia huduma za kifedha za Mixx by Yas kupitia vyama vya ushirika wameendelea kunufaika na malipo ya kidijitali na zawadi mbalimbali, hatua inayotajwa kuongeza usalama wa fedha, kuharakisha malipo na kuhamasisha uzalishaji wa mazao.

Akizungumza katika hafla ya Vuna na Mixx iliyofanyika wakati wa Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC), Dkt. Benson Ndiege, alisema ushirikiano kati ya Tume na Mixx umeleta mageuzi katika mfumo wa malipo kwa wakulima wanaouza mazao kupitia stakabadhi za ghala.

Alisema matumizi ya malipo ya kidijitali yameondoa changamoto zilizokuwa zikitokana na matumizi ya fedha taslimu, ikiwemo ucheleweshaji wa malipo na upotevu wa fedha, huku wakulima wakipokea fedha zao kwa usalama na kwa wakati.

"Malipo yanapowafikia wakulima kwa wakati yanawapa motisha ya kuongeza uzalishaji. Tumeona mabadiliko makubwa katika mfumo wa ushirika na ongezeko la mazao kutokana na kuimarika kwa huduma hizi," alisema Dkt. Ndiege.

Aliwataka wakulima wanaonufaika na mfumo huo kuwa mabalozi wa matumizi ya huduma za kidijitali ili kuwahamasisha wenzao kujiunga na mfumo huo, huku akiwapongeza maafisa ushirika na viongozi wa AMCOS kwa kuendelea kutoa elimu inayowasaidia wakulima kutumia huduma hizo kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Meneja wa Biashara wa Mixx Kanda ya Kati, Bw. Charles Gasper, alisema kampuni hiyo imeendelea kushirikiana na Serikali na vyama vya ushirika kuhakikisha wakulima wanapata huduma za kifedha zilizo salama, rahisi na za haraka.

Alisema katika hafla hiyo Mixx iliwatunuku zawadi wakulima zaidi ya 25 kutoka Kanda ya Kati waliotumia huduma zake kupitia vyama vya ushirika, zikiwemo pikipiki, maguta na baiskeli, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika matumizi ya huduma za kifedha kidijitali.

"Tunaamini tukimwezesha mkulima, tunachangia ukuaji wa familia yake, jamii na uchumi wa taifa. Hivyo tutaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo kuhakikisha wakulima wengi zaidi wananufaika na huduma za Mixx," alisema Bw. Gasper.
Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Vyama vya Ushirika (TCDC), Dkt. Benson Ndiege (aliyevaa suti nyeusi), akikabidhi funguo za pikipiki ya kubebea mizigo, almaarufu  'Guta', kwa Bw. Imani Ndelias Mwampashe kutoka Chama cha Ushirika cha Mlowa kilichopo Mkoa wa Iringa. Chama hicho kiliibuka mshindi wa jumla wa kampeni ya Mixx by Yas ya “Vuna na Mixx” kwa Kanda ya Kati. Makabidhiano ya zawadi hiyo yamefanyika hivi karibuni katika Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane jijini Dodoma.


Wakulima katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wameendelea kunufaika na huduma za malipo ya kidijitali zinazotolewa na Mixx by Yas, zinazowawezesha kupokea fedha za mazao moja kwa moja kupitia simu zao na kupunguza ulazima wa kusafiri umbali mrefu kufuatilia malipo.

Huduma hizo zimekuwa na umuhimu zaidi kwa wakulima waliopo maeneo ya vijijini na mbali na taasisi za kifedha, kwa kuwapa njia rahisi na salama ya kupokea na kufuatilia fedha zao baada ya kuuza mazao.

Akizungumza wakati wa kilele cha Maonesho ya Kilimo ya Nanenane katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, Meneja wa Biashara wa Mixx by Yas Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Charles Gardner, alisema matumizi ya mifumo ya malipo ya kidijitali yanaendelea kuondoa baadhi ya changamoto ambazo wakulima wamekuwa wakikumbana nazo katika kupokea fedha za mazao.

Gardner alisema kupitia Mixx, mkulima anaweza kupokea malipo moja kwa moja kwenye simu yake bila kulazimika kusafiri kwenda kufuata fedha, hali inayookoa muda na gharama huku ikipunguza utegemezi wa fedha taslimu.

“Tunataka mkulima aweze kupokea fedha za mazao yake kwa urahisi popote alipo. Badala ya kutumia muda na gharama kusafiri kufuatilia malipo, fedha zinaweza kumfikia moja kwa moja kupitia simu yake na akazitumia kulingana na mahitaji yake,” alisema Gardner.

Alisema Mixx by Yas inaendelea kutumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wakulima kuhusu matumizi ya huduma za kifedha za kidijitali na namna zinavyoweza kurahisisha shughuli zao za kila siku.

Baadhi ya wakulima wanaotumia huduma hizo wamesema malipo kupitia simu yamepunguza muda waliokuwa wakitumia kusubiri au kufuatilia fedha baada ya kuuza mazao yao.

Joyce Mube, mkulima kutoka Tunduma, alisema mfumo huo umemrahisishia kupokea na kufuatilia malipo ya mazao yake bila kulazimika kusafiri kwenda kufuata fedha.

“Unapopokea fedha kupitia simu unakuwa na uhakika wa malipo yako na unaweza kuyafuatilia kwa urahisi. Pia inapunguza muda na gharama ambazo tungetumia kwenda kufuata fedha,” alisema Mube.

Wakati huohuo, Meneja wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Roodny Alananga, amewataka wakulima na wajasiriamali kuzingatia ubora na viwango vya bidhaa zao ili kuongeza ushindani na kupata fursa katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Alananga alisema elimu inayotolewa na TBS inalenga kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kuboresha bidhaa zao na kuhakikisha zinakidhi viwango vinavyohitajika katika masoko mbalimbali.

Maonesho ya Nanenane yameendelea kuwa jukwaa muhimu kwa wakulima kukutana na wadau wa sekta ya kilimo na kupata taarifa kuhusu teknolojia, huduma za kifedha, masoko na viwango vya bidhaa zinazoweza kusaidia kuongeza tija na kipato.
Meneja wa Biashara wa Mixx - Kanda ya Nyanda za Juu Kusini,Charles Gardner



Na Mwandishi Wetu, Dodoma
CHUO cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimesema kimejipanga kuendelea kutoa elimu inayokwenda sambamba na mahitaji ya sasa ya teknolojia, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wahitimu wanakuwa na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira na uchumi wa kidijitali.

IFM imesema hayo wakati ikishiriki Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo na Ufugaji Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma ,Mwanza pamoja na Simiyu mbapo imeeleza kuwa ushiriki wake ni sehemu ya kusogeza huduma za elimu karibu na wananchi.

Kwa mujibu wa chuo hicho, ushiriki katika maonesho hayo ya kitaifa na ya kanda pia unalenga kuwafikia wananchi wanaozunguka kampasi zake na kuwapatia elimu pamoja na taarifa kuhusu fursa zinazopatikana kupitia programu mbalimbali za IFM.

IFM imeeleza kuwa maonesho hayo yamejikita katika kuongeza thamani ya mazao na bidhaa ili ziweze kupata masoko yenye tija, ambapo ujuzi wa usimamizi wa fedha ni muhimu katika kuhakikisha mnyororo mzima wa thamani unakuwa na tija kwa wazalishaji.

Chuo hicho kimesema pale mazao yanapoingia sokoni, masuala ya usimamizi wa fedha huwa muhimu katika kuhakikisha wakulima wanapata mapato yanayoendana na thamani ya uzalishaji wao, huku wakijengewa uwezo wa kutumia fedha hizo kwa ufanisi.

Aidha, IFM imeeleza kuwa elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia ni muhimu kwa wakulima na wafanyabiashara katika kuboresha utunzaji wa kumbukumbu za kifedha, kufanya maamuzi sahihi ya biashara na kuongeza tija katika shughuli zao za kiuchumi.











Matukio katika Picha Chuo cha  IFM  katika maonesho ya Kitaifa na Kanda.
Na Benny Mwaipaja, Mbeya

Serikali imetangaza kuendelea kuongeza uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, huku ikizitaka jamii za Nyanda za Juu Kusini kutumia fursa za soko, teknolojia na miundombinu ili kuongeza tija na kuharakisha utekelezaji wa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kauli hiyo ilitolewa mkoani Mbeya na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati wa kilele cha Maonesho na Sherehe za Wakulima Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, yaliyofanyika katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya.

Akizungumza mbele ya viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo, wakulima, wafugaji na wavuvi, Mhe. Balozi Omar alisema kaulimbiu ya Nanenane ya mwaka huu, “Tambua soko: Ongeza tija kutekeleza Dira ya 2050,” inapaswa kuwa chachu ya kuongeza uzalishaji wenye tija kuanzia shambani hadi kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Alisema uchumi wa Taifa umeendelea kuimarika, ambapo pato ghafi la Taifa lilifikia shilingi trilioni 234.1 mwaka 2025, kutoka shilingi trilioni 211.97 mwaka 2024, sawa na ukuaji wa asilimia 5.9 na Sekta ya kilimo nayo imeendelea kuonesha mafanikio makubwa, ikikua kwa asilimia 5.5 mwaka 2025 ikilinganishwa na asilimia 3.7 mwaka 2021, huku ikichangia asilimia 24.3 ya uchumi wa Taifa.

Kwa upande wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Mhe. Balozi Omar alisema eneo hilo limeendelea kuwa mhimili mkubwa wa uzalishaji na uchumi wa nchi. Alieleza kuwa pato la kanda hiyo lilifikia shilingi trilioni 32.8 mwaka 2024, sawa na asilimia 15.8 ya pato la Taifa, likiongezeka kutoka shilingi trilioni 29.6 mwaka 2023. Mkoa wa Mbeya uliongoza kwa pato la shilingi trilioni 11.6, ukifuatiwa na Iringa, Rukwa, Songwe, Njombe na Katavi.

Katika hatua ya kuimarisha sekta za uzalishaji, Mhe. Balozi Omar, alisema Serikali imeongeza bajeti ya sekta ya kilimo kutoka shilingi bilioni 276.72 mwaka 2021/22 hadi shilingi bilioni 1,132.36 mwaka 2026/27. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 698.99 zitaelekezwa Wizara ya Kilimo na shilingi bilioni 433.38 Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Alisema pia kuwa Serikali imeidhinisha shilingi bilioni 384.29 kwa mwaka 2026/27 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji nchini, hatua ambayo imechangia kuongezeka kwa eneo la umwagiliaji hadi hekta 983,466.1 mwaka 2025 kutoka hekta 727,280.6 mwaka 2022.

Akizungumzia hali ya chakula, Mhe. Balozi Omar alisema mikoa ya Nyanda za Juu Kusini imeendelea kufanya vizuri kwa kuwa na wastani wa uwezo wa kujitosheleza kwa chakula wa asilimia 219, juu zaidi ya kiwango cha chini kinachohitajika cha asilimia 120 na wastani wa Taifa wa asilimia 129.

Katika sekta ya mifugo na uvuvi, alisema Serikali imeendelea kuwekeza katika chanjo, masoko, mialo, boti za doria na usimamizi wa rasilimali za maji katika maziwa ya Nyasa, Rukwa na Tanganyika.

Aliongeza kuwa katika mikoa hiyo, jumla ya malambo 50 na mabwawa ya samaki 5,695 yamejengwa katika vipindi tofauti ili kuongeza uzalishaji na kipato kwa wananchi.

Kwa upande wa vijana, Mhe. Balozi Omar alisema Serikali imetenga shilingi bilioni 23 kupitia dirisha la mifugo na uvuvi kwa ajili ya kuwezesha miradi mbalimbali ya vijana, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kukuza uchumi wa sekta hizo.

Aliwataka viongozi wa mikoa na wilaya kusimamia amani, lishe, uhifadhi wa mazingira, pamoja na uanzishwaji wa vituo vya taarifa na teknolojia za kilimo katika kila kata ili kuwafikishia wakulima huduma na ubunifu unaooneshwa akisisitiza kuwa mafanikio ya sekta hizo yatategemea zaidi uzalishaji wenye tija, uhifadhi wa chakula, na matumizi bora ya fursa za soko.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akimkabidhi Funguo za Trekta kama Mkopo kutoka Benki ya CRDB, Mkazi wa Jiji la Mbeya, Bi. Christina Levi Mgaya (Katikati), kwa ajili ya kumwezesha katika shughuli zake za kuendeleza kilimo, wakati alipotembelea Mabanda ya Maonesho katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya kwa ajili ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Jijini Mbeya.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akisikiliza maelezo ya Afisa Maliasili Mkoa wa Mbeya, Bw. Petro Haule, kuhusu aina mbalimbali ya mavazi ya kale ambayo yalitokana na Ngozi, wakati alipotembelea Banda la Maliasili la Mkoa wa Mbeya, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla yakuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, jijini Mbeya. 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akisikiliza maelezo ya Meneja Utafiti wa Kiwanda cha Mbolea cha INTRACOM, Dkt. Tulole Buchoyeke, kuhusu tafiti za mbolea wanazozalisha, wakati alipotembelea Mabanda ya maonesho, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikuwa Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani- Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya. 

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto) akiangalia moja ya bidhaa ya Siagi ya Karanga inayozalishwa na Mjasiliamali Mdogo kupitia Kampuni yake ya Swahigo Enterprises, Bw. Albert Thomas (kulia), wakati alipotembelea Mabanda ya Maonesho, katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikua Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani – Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (katikati) akiteta jambo na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge (kushoto), wakati wakitembelea mabanda mbalimbali katika Viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya ambapo alikua Mgeni Rasmi katika hafla ya kuhitimisha kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Duniani – Nane Nane, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jijini Mbeya. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe.. Beno Malisa.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Mbeya)

Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, amehitimisha ziara yake nchini Tanzania na kuagwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Jukwaa hilo la siku mbili lililofunguliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, liliipatia Tanzania fursa ya kusaini hati tatu za makubaliano ikiwemo hati ya makubaliano ya kujenga kituo kipya cha huduma za usafishaji wa figo, mradi wa kuchakata gesi asilia kuwa gesi kimiminika na makubaliano kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Africa50 ya kuendeleza miundombinu ya usafirishaji wa umeme.

Aidha, Mikutano hiyo iliyokutanisha washiriki wapatao 1,200, imeipatia Tanzania fursa ya kutangaza vivutio vya utalii, uwekezaji na miradi ya kimkakati kwa lengo la kuvutia mitaji na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika maendeleo ya miundombinu na hivyo kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Kitaifa wa Miaka Mitano (FYDP IV) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiagana na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiongozwa kuelekea kupakia ndege na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kulia), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, akiongozwa na na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.










Picha za matukio mbalimbali wakati Rais wa Benki ya Maendeleo ya AfriKa (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah, alipoagana na Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Laurent Luswetula (Mb) (kushoto), katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa taasisi ya Africa50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Africa50 General Shareholders' Meeting - GSM and Infra for Africa Forum) iliyofanyika tarehe 5 na 6 Agosti, 2026, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)



Top News