Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Ali Munde (Mb), kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayoshughulikia Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano, pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati ya Mawaziri wa Biashara, Utalii, Viwanda na Madini.
Mkutano huo wa kimkakati ulioanza rasmi tarehe 24 Julai 2026 jijini Abidjan, Côte d’Ivoire, unalenga kuweka misingi imara ya ushirikiano wa kiuchumi barani Afrika.
Mkutano huo umejadili kwa kina umuhimu wa nchi za Afrika kuharakisha juhudi za kuendeleza sekta ya viwanda kwa kuongeza thamani ya malighafi za ndani badala ya kusafirishwa zikiwa ghafi, kuimarisha minyororo ya thamani ya kikanda, pamoja na kuweka mazingira bora na wezeshi yatakayovutia uwekezaji wenye tija kiuchumi.
Wajumbe wa mkutano huo walibainisha kuwa, kutokana na Bara la Afrika kuwa na rasilimali nyingi za asili, ardhi kubwa yenye rutuba kwa ajili ya kilimo, madini ya kimkakati na idadi kubwa ya vijana ambao ndio nguvu kazi kubwa katika uzalishaji, kuna umuhimu kwa Afrika kuwa kama kitovu cha uzalishaji na biashara duniani.
Aidha, mkutano huo umehimiza umuhimu wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani, kuboresha usimamizi wa rasilimali za asili, na kupambana na ukwepaji kodi ili kukabiliana na pengo kubwa la ufadhili wa maendeleo ya miundombinu ya kisekta.
Mawaziri na wataalamu hao walikubaliana kwa pamoja kuwa maendeleo ya viwanda hayawezi kufikiwa bila uwepo wa mfumo imara wa kifedha utakaowezesha upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu, kupunguza gharama za mikopo, na kuvutia sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akifuatilia mada zilizokuwa zikijadiliwa katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati) Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kulia) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kushoto), wakifuatilia mijadala katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama (wa pili kulia), na Kamishna Msaidizi Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. James Msina (kushoto), wakimsikiliza Afisa Usimamizi Fedha Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Glory Sindilo, akifafanua jambo katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kushoto) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), (katikati), Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Lemomo Kiruswa (kushoto) na Naibu Waziri wa Viwanda, Mhe. Dennis L. Londo (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufunguliwa kwa Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Mtendaji, Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, na kulia ni Naibu Gavana wa Sera za Kiuchumi na Fedha, Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Yamungu Kayandabila.

Naibu Waziri wa Fedha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akiteta jambo na Waziri wa Fedha wa Eswatini Mhe. Neal Rijkenberg, katika Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri (STC) ya Umoja wa Afrika inayosimamia masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano wa 5 wa Kamati Maalum ya Mawaziri inayosimamia masuala ya Biashara, Utalii, Viwanda na Madini, jijini Abidjan, nchini Côte d’Ivoire. Katikati ni Katibu wa Naibu Waziri wa Fedha, Bw. Yambi Kinyaki.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Abidjan, Côte d’Ivoire.)

NA MWANDISHI WETU, DAR
Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Maduka ya Biashara ya Maria Nyerere (Maria Nyerere Shopping Mall) ulio chini Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), amehimizwa kuongeza kasi ya ujenzi ili mradi huo ukamilike kwa wakati.
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda, Julai 22, 2026, Jijini Dar es Salaam, katika ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT Taifa, kukagua uhai wa Chama na miradi ya Jumuiya hiyo.
Chatanda amesema, ipo haja ya mkandarasi huyo kuongeza kasi ya ujenzi, huku akimshauri kuongeza wakandarasi wengine ili kumsaidia baadhi ya kazi na kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi huo.
"Mradi unakwenda vizuri, isipokuwa kwa mwenendo unavyokwenda na kwa muda tuliokubaliana huenda asikamilishe kwa wakati. Mkandarasi tunachomuhitaji aukamilishe mradi kwa mujibu wa tulivyokubaliana na kama kuna maeneo yeye hana uwezo wa kufanya, akabidhi kwa wakandarasi wengine (sub contractors) ili kazi ikamilike kwa wakati," amesema Chatanda.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti UWT Taifa, Zainabu Shomari, amesema mradi huo ni utekelezaji wa maagizo ya Chama wa kuzitaka Jumuiya zake kuwa na vitega uchumi.
"Chama kimeelekeza Jumuiya zake kujitegemea kiuchumi, kwahiyo, mradi huu ni utekelezaji wa maagizo na Chama na kwa hakika UWT tutafanikiwa kujitegemea," amesema Shomari.
Ikumbukwe kuwa, mradi wa Maria Nyerere Shopping Mall unatekelezwa eneo la Gerezani Jijini Dar es Salaam, ambapo unategemewa kuongeza mapato ili Jumuiya hiyo iwe na uwezo wa kuendesha shughuli zake bila kutegemea uwezeshwaji kutoka Chama ngazi ya Taifa.
Pamoja na mradi huo, Kamati hiyo, ilipata fursa ya kukagua eneo lake lenye ukubwa wa hekta 8.2, lililopo mtaa wa Zogo, kata ya Zingiziwa, wilayani Ilala, ambapo linategemewa kuongeza uwekezaji wa Jumuiya hiyo.

Na Mashaka Mhando, Muheza.
MBUNGE wa Jimbo la Muheza ambaye pia ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma 'MwanaFA', amewataka wajumbe wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo kutopepesa macho wala kubabaika linapokuja suala la kumchagua Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga katika uchaguzi mkuu wa chama hicho mwakani.
MwanaFA ametoa kauli hiyo Leo Julai 23 wakati akizungumza na Wana-CCM wa kata za Kwakifua na Tingeni, ambapo ametumia jukwaa hilo kumpigia debe zito Mwenyekiti wa sasa wa mkoa huo, Ustadh Rajab Abdallah, akieleza kuwa rekodi ya kazi zake za kukijenga chama haijawahi kufikiwa na kiongozi yeyote nchini.
Rekodi Zilizompa Kiki Ustadh Rajab
Akijenga hoja ya kwanini wajumbe hawapaswi kufanya makosa, Mhe. Mwinjuma aliwataka wanachama hao kutaja mwenyekiti yeyote nchini aliyewahi kujenga nyumba za watumishi wa chama kila wilaya, ambapo wajumbe walijibu "hakuna."
"Hebu nitajieni Mwenyekiti yeyote aliyejenga nyumba za watumishi wa chama mkoa wowote hapa nchini? Alihakikisha nyumba hizo zinakwisha kila wilaya. Wabunge tulikuwa tukichanga lakini Mwenyekiti alichanga zaidi. Hapa Muheza amehakikisha tunajenga ofisi ya wilaya ya kisasa ya ghorofa, huyu hapaswi kukosa kura hata moja ya Wana-Muheza," alisema MwanaFA.
Aliongeza kuwa kazi zinazofanywa na Mwenyekiti huyo zimerahisisha sana utekelezaji wa majukumu ya chama na kuwaondolea mzigo wabunge, hivyo kuwapa nafasi nzuri ya kubaki na jukumu moja tu la kuwahudumia wananchi.
"Nyumba za watumishi zimekamilika, jengo letu linakwenda kwa kasi, na juzi tena Mwenyekiti huyo huyo katoa Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa mwingine wa chama. Hatuwezi kupata mwenyekiti kama Ustadh Rajab. Huyu ni mtu wa kumshikilia na kwenda naye katika uchaguzi," alisisitiza.
"Hili Siyo Suala la Messi na Ronaldo, ni suala la uhai wa Chama chetu
Katika kusisitiza uzito wa jambo hilo, MwanaFA alitumia lugha ya kimichezo kuonya wajumbe wasichukulie uchaguzi huo kama ushabiki usio na tija.
"Tunatakiwa watu wote tujijue tutamuunga mkono nani. Hili siyo suala la kubishania nani mkali kati ya Messi na Ronaldo; hili ni suala linalogusa maisha yetu, uhai wa chama chetu na mustakabali wake kwa kuwa na mtu muhimu kama yeye.
"Kwa hiyo watu wote tuhakikishe tunamlinda, Mungu akimpa uhai Mwenyekiti wetu, tuhakikishe tunaendelea naye atuongozee chama ngazi ya mkoa tunamchagua tena," alionya MwanaFA.
Dua kwa Rais Samia
Mwisho, Mbunge huyo aliwaomba wananchi wa Muheza kuendelea kumsomea dua na kumuombea afya njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Alisema Rais Samia ameutendea haki Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Muheza kwa kupeleka fedha nyingi zilizowezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Samia, miradi mikubwa ya maji, elimu, na miundombinu ya barabara.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, leo Julai 23, 2026, ametembelea Pori la Akiba la Pande jijini Dar es Salaam na kukagua maendeleo ya miradi ya kuboresha miundombinu na huduma za utalii inayotekelezwa katika eneo hilo.
Miradi inayotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa bwawa la kuogelea (swimming pool), bwawa la watoto (Kids Playing Grounds), uwanja mdogo wa mpira wa miguu na uwanja wa beach volleyball, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea wageni na mashabiki wa AFCON 2027, ambayo Tanzania itaandaa kwa ushirikiano na Kenya na Uganda.
Dkt. Abbasi amesisitiza miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyotarajiwa ili kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata fursa ya kutembelea na kufurahia vivutio vya utalii vilivyopo Pori la Akiba la Pande.
Pori la Akiba la Pande linapatikana takribani kilomita 45 kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam na linaendelea kuimarishwa kuwa moja ya vivutio muhimu vya utalii wa asili nchini.



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)



.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

