Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa ALAF Limited, Hawa Bayumi (katikati) akitangaza orodha fupi ya waandishi waliofanikiwa kutinga fainali ya Tuzo ya Kiswahili ya Safal ya Fasihi ya Afrika 2025. Wengine kutoka kushoto ni Afisa Huduma kwa Wateja Tito Maliyalabu, Meneja Msaidizi wa kitengo cha Rasilimali watu Nyamizi Malatu, Meneja Mauzo ya Miradi, Tom Mwita na Afisa Uhusiano kwa Wateja, Grace Gabriel.

TUZO ya Kiswahili ya Safal ya Fasihi ya Afrika imetangaza orodha fupi ya miswada saba katika vipengele vitatu — riwaya, ushairi, na makusanyo ya hadithi fupi — ikiwa ni utangulizi wa hafla ya utoaji tuzo hizo kwa msimu wa 10, inayotarajiwa kufanyika Julai 24, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Tuzo hiyo inadhaminiwa na kampuni ya Safal Group, kupitia kampuni zake tanzu za Mabati Rolling Mills ya Kenya na ALAF iliyoko nchini Tanzania.

Tuzo ya Kiswahili ya Safal ya Fasihi ya Afrika ilianzishwa mwaka 2014 na Dkt. Lizzy Attree na Dkt. Mukoma wa Ngũgĩ ili kutambua kazi za uandishi katika lugha za Kiafrika sambamba na kuhamasisha kazi za utafsiri kwa lugha adhimu za asili ya Kiafrika.

Tuzo hiyo, ambayo kwa mwaka huu inaadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2015, imekuwa ikitolewa kila mwaka isipokuwa mwaka wa 2020, kutokana na kuweko janga la Covid 19 duniani kote.

Akizungumza wakati wa kutangaza orodha fupi ya waandishi waliofanikiwa kutinga fainali, Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa ALAF Limited, Bi Hawa Bayumi alisema “Tunapotangaza orodha hii fupi, tunayo furaha kuadhimisha miaka 10 ya tuzo hii . Hii ni hatua kubwa sana iliyopigwa na Safal Group kupitia kampuni zake tanzu yaani ALAF Limited ya Tanzania na Mabati Rollings Mills ya Kenya.

“Tunawashukuru wadau wetu wote ambao mmekuwa na sisi katika safari hii. Ni matumaini yetu kuwa mtaendelea kushirikiana na sisi huku Kiswahili kikiendelea kukua duniani,” aliongeza.

Washindi watapata zawadi kama ifuatavyo:
1. Riwaya Mshindi wa kwanza 5,000 USD
2. Riwaya Mshindi wa pili 2500 USD
3. Ushairi mshindi wa kwanza 5000 USD
4. Ushairi mshindi wa pili 2500 USD
5. Mshindi hadithi fupi 2500 USD
Alieleza kuwa washindi watapata fursa ya kazi zao kuchapishwa na kampuni ya Mkuki na Nyota Publishers.

"Tayari tumeshatoa zaidi ya dola 150,000 kwa waandishi zaidi ya 40 mchango ambao umewawezesha kuchapisha zaidi ya vitabu 20 hii ikiwa ni hatua kubwa katika kutangaza lugha ya Kiswahili duniani,” alisema Bi Bayumi.

Akitangaza uamuzi wa Majaji kuhusiana na tuzo hizo, Mwenyekiti wa jopo la majaji wa tuzo kwa mwaka huu, Profesa Rayya Timammy kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi, alisema kuwa ushindani wa Tuzo ya Kiswahili ya Safal ya 2025 ya Fasihi ya Afrika ulikuwa mkubwa sana.

Profesa Timammy aliongeza, “Hali hiyo imesababishwa na idadi kubwa ya mawasilisho yaliyopokelewa kuwa na vipaji vya hali ya juu na kipekee vilivyoonyeshwa na waandishi waliowasilisha kazi zao hizo.”

Majaji wengine walioungana na Prof. Rayya Timammy katika kusoma na kuteua machapisho ambayo yatashiriki shindano la tuzo kwa mwaka wa 2025 walikuwa ni pamoja na Dkt. Masoud Mohammed wa Chuo Kikuu cha Zanzibar na aliyewahi kuwa mfanyakazi wa chuo kikuu cha Makerere Prof. Austin Bukenya.

Miswada iliyochaguliwa katika orodha fupi pamoja na waandishi ni Pamoja na:

Riwaya:
Ziaka Imetoboka - Mathew Theuri Maina (Kenya)
Mwanamkasi Ndio Basi - Salim Hussein Ng'anzi (Tanzania)
Shamba la Mawe - Dickson Damas Mtalaze (Tanzania)

Ushairi:
Diwani ya Vizikwa Vya Kale - Ali Hilal Ali (Tanzania)
Zigo la Kichwa - Maimuna Hashim Maalim (Tanzania)
Rima la Miiko na Balaa - Lenard Barnaba Mtesigwa (Tanzania)

Mikusanyiko ya Hadithi Fupi:
Mbunge Mtarajiwa na Hadithi Nyingine - Dominic Maina Oigo (Kenya)
Koti la Karani na Hadithi Nyingine - Stallone Joyfully (Tanzania)
Siri ya Mama na Hadithi Nyingine - Sophia Said Puta (Tanzania)

Washindi wa jumla watatangazwa katika sherehe ya tuzo iliyopangwa kufanyika tarehe 24 Julai, 2026, katika ukumbi wa maktaba mpya ya Chuo Kikuu Dar es Salaam.

Vigezo vya Tuzo ya Kiswahili:
Tuzo hiyo itatolewa kwa kazi ambazo hazijachapishwa au kitabu bora ambacho kilichochapishwa ndani ya miaka miwili ya mwaka wa tuzo husika katika kipengele cha hadithi za kubuni (riwaya na makusanyo ya hadithi fupi), ushairi, kumbukumbu na riwaya za michoro.

Jumla ya tuzo zilizopendekezwa za dola 15,000 za Marekani zitagawanywa kama ifuatavyo:

Mbali na zawadi hizo, machapisho yaliyoshinda pia yatapata fursa ya kuchapishwa kwa Kiswahili na kampuni ya uchapishaji ya Mkuki na Nyota iliyoko nchini Tanzania, ambapo mashairi yaliyoshinda yatatafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza na kuchapishwa na Mfuko wa Vitabu vya Ushairi wa Kiafrika (APBF).

Kwa mwaka huu, jumla ya kazi 230 kutoka mataifa saba ziliwasilishwa kwa ajili ya kuwania tuzo hizo.


Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Polisi Wilaya ya Musoma mkoani Mara, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Edson Mwamafupa aliwaongoza Maafisa, Wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali katika zoezi la utoaji msaada kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Zoezi hilo la kibinadamu limefanyika katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Jipe Moyo kilichopo Manispaa ya Musoma, likiwa ni sehemu ya kuonyesha ukaribu na upendo wa jeshi hilo kwa jamii inayowazunguka.

Akikabidhi msaada huo wa vitu mbalimbali kwa msimamizi wa kituo hicho, Sister Maria Faustine, SSP Mwamafupa aliwataka watoto hao kutambua kuwa Jeshi la Polisi lipo pamoja nao wakati wote.

Aidha aliwasisitiza kuendelea kuzingatia masomo yao kwa bidii, wasaidiane na kupendana wao kwa wao, akibainisha kuwa tabasamu lao ndiyo furaha kuu ya jamii inayowazunguka.

Kwa niaba ya uongozi wa kituo na watoto wote, Sister Maria Faustine Alieleza kuwa ujio wa Jeshi la Polisi wilaya ya Musoma na msaada walioutoa si tu kwamba unasaidia kukidhi mahitaji ya watoto hao, bali pia unawapa faraja kubwa na kuwathibitishia kuwa jamii na vyombo vya ulinzi vinawajali na kuwalinda, huku akihitimisha kwa kuwaombea baraka za Mungu katika majukumu yao ya kila siku ya kulinda usalama wa raia na mali zao.






Na Mwandishi Wetu
TANZANIA imesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya nchi za Afrika katika kuimarisha matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia hususan kwenye vifaa visivyotumika kwa uchunguzi wa kitabibu, ili kuongeza ufanisi wa matumizi ya teknolojia hiyo katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Hayo ameyasema Mjumbe wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk, Amos Nungu, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC), wakati wa mkutano wa kujadili masuala ya usalama wa mionzi ya nyuklia kwenye vifaa visivyo vya uchunguzi wa kimatibabu uliowakutanisha washiriki i 35 kutoka nchi 25 za Afrika.

Dkt. Nungu amesema mafunzo hayo ya wiki nzima yameandaliwa na Shirika la Kimataifa la ya Atomu (IAEA) na yamekuwa fursa muhimu kwa nchi za Afrika kujifunza kutoka kwa wataalamu wa kimataifa pamoja na kubadilishana uzoefu kutokana na hatua mbalimbali za maendeleo ambazo kila nchi imefikia katika matumizi ya teknolojia ya nyuklia nje ya sekta ya tiba.

Dkt.Nungu amesema kuwa washiriki wanapata nafasi ya kusikiliza mawasilisho kutoka kwa kila nchi kuhusu mafanikio, changamoto na mikakati yao, jambo linalowezesha kujifunza kutoka kwa wenzao na kufanya tathmini ya maendeleo yao. Aidha, aliwataka washiriki wa Tanzania kutumia vyema fursa hiyo kwa kujifunza kutoka kwa wataalamu waliotoka mataifa yenye uzoefu mkubwa, ikiwemo Ureno, pamoja na wenzao wa Afrika.

Dkt. Nungu ameongeza kuwa ushirikiano huo utaisaidia Tanzania na nchi nyingine za Afrika kuimarisha usalama wa mionzi ya nyuklia, kuboresha mifumo ya udhibiti na kuongeza matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali za maendeleo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya usalama.

Nae Mtafiti na Mkaguzi wa Usalama wa Mionzi wa TAEC Elisha Edmund Amesema mafunzo hayo yamelenga kuimarisha uelewa na uwezo wa wataalamu katika usimamizi salama wa matumizi ya teknolojia hiyo.

Amesema mafunzo yataisaidia shughuli za ufuatiliaji na kukabiliana na uwezekano wa kuwepo kwa vifaa au nyenzo za mionzi ambazo zinaweza kuhatarisha usalama.

Edmund amesema mafunzo hayo watajadili changamoto mbalimbali ili kulinda wafanyakazi, wananchi na mazingira.




Na Mwandishi Wetu ,Korea
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Dkt. Juma Zuberi Homera (Mb.), ameipongeza Jamhuri ya Korea kwa kufanikiwa kuwa mwenyeji wa Kikao cha 48 cha Kamati ya Urithi wa Dunia ya UNESCO (48th Session of the World Heritage Committee), kinachofanyika katika Jiji la Busan kuanzia tarehe 19 hadi 29 Julai 2026.

Akichangia katika mjadala wa Kamati hiyo, Mheshimiwa Homera aliishukuru UNESCO kupitia Kituo cha Urithi wa Dunia (World Heritage Centre) kwa kuendelea kutoa usaidizi wa kitaalamu kwa nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, licha ya changamoto za kifedha zinazoikabili taasisi hiyo.

Aidha, alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kikamilifu na UNESCO katika kipindi chake cha uanachama wa Kamati ya Urithi wa Dunia ili kuhakikisha malengo na misingi ya Mkataba wa Urithi wa Dunia wa mwaka 1972 yanaendelezwa na kutekelezwa kwa ufanisi.

Katika mjadala kuhusu ushirikishwaji wa Watu wa Asili katika utekelezaji wa Mkataba wa Urithi wa Dunia wa mwaka 1972, Mheshimiwa Homera alieleza kuwa Tanzania inatambua kuwepo kwa Azimio la Umoja wa Mataifa la mwaka 2007 kuhusu Haki za Watu wa Asili (United Nations Declaration on the Rights of Indigenous Peoples – UNDRIP). Hata hivyo, alibainisha kuwa azimio hilo halina nguvu ya kisheria inayowafunga wanachama wa Umoja wa Mataifa. Vilevile, alieleza kuwa Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani (ILO Convention No. 169), ambao unahusu Watu wa Asili na wa Kabila, umeridhiwa na idadi ndogo ya nchi duniani.

Kutokana na hali hiyo, Tanzania iliomba ufafanuzi kuhusu msingi wa kisheria na namna ambavyo UNESCO inapendekeza kujumuisha ushirikishwaji wa Watu wa Asili katika utekelezaji wa Mkataba wa Urithi wa Dunia wa mwaka 1972, hususan pale ambapo hakuna wajibu wa kisheria unaotokana na vyombo husika vya kimataifa.

Kikao hicho kinaendelea hadi tarehe 29 Julai 2026. Katika kipindi cha mkutano huo, tarehe 27 Julai 2026, Tanzania inatarajiwa kuandaa mkutano wa pembeni (Side Event) utakaotoa fursa ya kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu uhifadhi, usimamizi na maendeleo endelevu ya Urithi wa Dunia.

Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imezindua "bulldozer" lenye thamani ya Shilingi milioni 450 katika Ranchi ya NARCO Ruvu, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa Ranchi hiyo, na kuongeza upatikanaji wa malisho, maji pamoja na kukuza uzalishaji wa mifugo nchini.

Akizungumza Leo Julai 20, 2026 Mkoani  Pwani, wakati wa hafla ya uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NARCO, Balozi Dkt. Aziz Ponary Mlima, amesema ununuzi wa "bulldozer" hilo ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya DIRA ya Taifa ya 2050, huku akibainisha kuwa litasaidia kukabiliana na changamoto za malisho na maji ambazo zinawakabili wafugaji nchini.

"Bulldozer hili litatumika kuchimba visima vya maji, kuondoa vichaka vinavyozuia ukuaji wa malisho na kutengeneza mipaka ya Ranchi ili kudhibiti uvamizi, na Ranchi hii ya NARCO Ruvu ndiyo ya kwanza kunufaika na matumizi ya mashine hii ambayo pia itasaidia kuboresha mazingira ya uwekezaji ndani ya ranchi za taifa." Amesema Dkt. Mlima

Balozi Dkt. Mlima ameongeza kuwa NARCO itaendelea kuwawezesha wawekezaji waliopo ndani ya Ranchi kwa kuwapatia huduma mbalimbali ikiwemo ukodishaji wa mitambo, hatua itakayoongeza tija ya uzalishaji na kuchangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali. 

Pia, Dkt. Mlima amewahimiza wafugaji kuwekeza katika mbegu bora za mifugo, madume bora, teknolojia ya uhimilishaji na matumizi ya viini tete ili kuongeza uzalishaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Mohamedi Zuberi Mbwana, amesema malengo makuu ya ununuzi wa "bulldozer" hilo ni kuongeza na kuboresha nyanda za malisho, kukuza uzalishaji wa nyama kwa ajili ya masoko ya ndani na nje ya nchi pamoja na kusaidia wafugaji kukabiliana na changamoto za malisho wakati wa kiangazi.

Aidha Mkurugenzi Mbwana, ametoa Rai Kwa wafugaji na wawekezaji kutumia "Bulldozer" hilo la NARCO ili waweze kubadili mfumo wao wa ufugaji Kwa kupanda malisho na kuondoa  vichaka. Vilevile Serikali imeazimia kuongeza tani za uuzaji wa nyama nje ya nchi kutoka tani 14000 Kwa sasa mpaka tani 50000 ifikapo mwaka 2030, NARCO inajukumu la kuongeza uuzaji huo wa nyama nje ya nchi.

Naye, mmoja wa wawekezaji katika Ranchi ya NARCO Ruvu, Bw. Mbambile Kisanjo, ameipongeza Serikali kwa kuleta "bulldozer" hilo akisema litasaidia kuboresha upatikanaji wa malisho, kutatua changamoto za mipaka, kuondoa vichaka na kuongeza upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo, mambo ambayo yataongeza tija kwa wawekezaji na wafugaji wanaotumia ranchi hiyo.

Uzinduzi wa "bulldozer" hilo unaonyesha dhamira ya Serikali kupitia NARCO katika kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya kisasa ya ufugaji ili kuongeza tija, uzalishaji na mchango wa sekta ya mifugo katika ukuaji wa uchumi wa taifa, sambamba na kufanikisha malengo ya DIRA ya Taifa ya 2050.







 What people often miss on CPI day is that the number itself isn't what moves the market. The common reaction is to check whether 3.4% number is high or low. But it's all priced in advance. The real driver of EUR/USD is the gap between the actual number and what the market was positioned for.

Even a 3.4% reading can cause the dollar to weaken if traders expect higher inflation. And the opposite scenario – weaker numbers that beat consensus expectations may drive the dollar’s strength. According to Federal Reserve research, the price driver here is a surprise component rather than the headline.


Why the Expectation Gap Is More Important Than the Level

Forex is driven by expectations for interest rate decisions. And inflation plays its role by impacting expectations for future central bank policy. This is the reason why identical numbers may cause opposite reactions at different times. It depends on how they compare to market positioning.

Main factors:

●      Monthly CPI and core CPI

●      Core services inflation

●      Revisions to the previous period data

●      Central bank policy pricing

Year-over-year data is less important in terms of price impact than monthly and core data.


How to Calculate Surprise

Start with the simplest metric: Surprise = Actual CPI − Consensus CPI. 

Consensus comes from the economic calendar's forecast and reflects the market positioning. And then you need to check the market reaction through rates. The sequence typically runs: CPI surprise → change in front-end yields → USD movement → the sentiment adjustment.


Traders frequently employ this methodology in combination with the JustMarkets Economic Calendar to track high-impact releases in real time.


What the Intraday Move Actually Looks Like

CPI reactions usually happen in three stages. The first one is a headline shock with the potential algorithms' reaction within a few seconds. Then comes the interpretation stage, with a time frame of 15-60 minutes and analysis of core numbers and yield confirmation. And then either continuation or reversal happens.

Approaches to Trading CPI Day

There are two common approaches to CPI.

●      The momentum approach requires the consistency of headlines and core surprises with yields' confirmation. Most traders wait until the first minute's candle is closed to avoid false signals.

●      The fade approach requires dislocations like the absence of yield confirmation to FX movement or dislocations between headlines and core numbers. In this case, traders wait 10−20 minutes for exhaustion of the initial move and reversal setup search.

Risk management is crucial. Most traders limit their position size to 0.25%-0.50% of their equity because of widening spreads and slippage. Sometimes the decision to trade off is more optimal during extreme volatility than forced entry.

One Way to Prepare for the Next CPI Day Release

A simple way to get ready is to monitor EUR/USD, GBP/USD, and USD/JPY pairs and an economic calendar with events' importance. The workflow is simple: Economic calendar → release → Trading platform.

The final step brings traders to the execution platform. Many turn to JustMarkets, which offers CFDs on these currency pairs, with execution stability and fast market access that make it well suited for high-volatility macro events.


Disclaimer: For informational purposes only. Trading financial instruments involves significant risk and may not be suitable for all investors. Ensure you understand the risks involved and trade responsibly.

 

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Plasduce Mbossa akitoa maelezo kuhusu ujenzi na ukarabati wa meli kabla ya uzinduzi uliofanyika katika bandari ya Kigoma mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Meli 4 za mizigo zitakazo hudumu katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, tarehe 20 Julai.



Matukio mbalimbali katika uzinduzi wa Meli 4 za mizigo zitakazo hudumu katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, tarehe 20 Julai, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kigoma, tarehe 20 Julai, 2026.
 

-Yalenga kurejesha mawasiliano ya barabara kwa muda mfupi wakati wa dharura

‎Dar es Salaam

‎Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wake kwa kuwapatia mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya kisasa ya mabomba ya "Weholite" yanayotumika kujenga makalavati ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza ufanisi wa kurejesha mawasiliano ya barabara yanapokatika kutokana na mvua kubwa.

‎Mafunzo hayo yamefanyika kwa ushirikiano na kampuni ya Mega Pipes Solutions Ltd na kuwashirikisha Mameneja wa TARURA kutoka mikoa yote 26 pamoja na wahandisi waliobobea katika usanifu wa madaraja.

‎‎Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mhandisi Mshauri wa TARURA Makao Makuu, Pharles Ngeleja amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wahandisi na mameneja wa TARURA kutumia teknolojia ya "Weholite" katika kurejesha mawasiliano ya barabara kwa haraka hususan wakati wa mvua kubwa zinazosababisha kukatika kwa miundombinu.

‎Amesema washiriki wamepatiwa elimu kuhusu hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ikiwemo upembuzi yakinifu, usanifu na uandaaji wa makadirio ya gharama (BOQ) jambo litakaloongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu nchini.

‎"Teknolojia hii inatuwezesha kurejesha mawasiliano ya barabara ndani ya muda mfupi pindi yanapokatika. Tayari tumeitumia katika maeneo mbalimbali ikiwemo mikoa ya Kilimanjaro na Dar es Salaam ambapo imesaidia wananchi kuendelea kupata huduma za kijamii na shughuli za kiuchumi bila usumbufu", amesema Ngeleja.

‎‎Kwa upande wake, Meneja wa TARURA mkoa wa Arusha Mhandisi Nicholas Francis amesema mafunzo hayo yataongeza uwezo wa wahandisi kutumia teknolojia hiyo yenye gharama nafuu na  inayorahisisha ujenzi wa makalavati na miundombinu mingine ya kuvusha maji.

‎"Paipu Kalavati hizi zinapatikana katika ukubwa tofauti zikiwemo zenye kipenyo cha hadi mita 3 ambazo zinaweza kutumika kujenga makalavati au madaraja madogo ya mita 4 hadi 5 na unaweza kujenga ndani ya siku 30 na kuruhusu barabara kupitika kwa haraka",  amesema.

‎Ameongeza kuwa teknolojia hiyo tayari imetumika katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwenye mifereji ya maji ya mvua ambapo imeonyesha ufanisi mkubwa na inakadiriwa kudumu kwa zaidi ya miaka 100 bila kushambuliwa na kutu au kuharibika.

‎Naye, Mhandisi wa Mauzo kutoka kampuni ya Mega Pipes Solutions Ltd, Mafikiri Mushi ameishukuru TARURA kwa kuendelea kuamini teknolojia hiyo na kushirikiana na kampuni hiyo katika kuimarisha miundombinu ya barabara.

‎‎Amesema ana matumaini kuwa baada ya mafunzo hayo wahandisi wa TARURA wataongeza matumizi ya paipu kalavati za "Weholite" katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini hatua itakayochochea ujenzi wa miundombinu imara, kisasa na yenye gharama nafuu kwa manufaa ya wananchi.









Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro inaendelea kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo ndani na nje ya Ngorongoro ili kuidhihirishia dunia kuwa eneo hilo ni hazina ya ulimwengu.

Akitoa maelezo kwa kaimu mkurugenzi wa idara ya Afrika kutoka wizara ya mambo ya nje ya Sweden bwana Dario Jovic, Afisa Mhifadhi mkuu wa Ngorongoro anayeshughulikia Masoko bwana Michael Makombe amesema pamoja na kreta ya Ngorongoro hifadhi hiyo ina mapango ya tembo na maporomoko ya maji ambayo mtalii akifika katika eneo hilo huondoa msongo wa mawazo.

Amevitaja vivutio vingine kuwa ni pamoja na kreta za Empakai na Olmoti,mchanga unaohama, mlima Lolmalsin, tambarare za mazalia ya Nyumbu Ndutu, mapango ya Amboni,kimondo cha Mbozi na magofu ya Engaruka.

Akitoa sifa ya moja ya kivutio bwana Makombe amesema kuna kivutio cha mchanga unaohama kwa kati ya mita 15-17 kwa mwaka ukiwa na umbo la nusu mwezi bila kuachana ambapo watalii wengi hufika kuona maajabu hayo.

Ameeleza jamii katika eneo hilo huamini mchanga wa eneo hilo ni tiba kwa mahusiano yaliyolegalega na kuwataka wasweden kutembelea Tanzania ili kujionea maajabu hayo.

Hifadhi ya Ngorongoro pia imepambwa na utamaduni wa kihistoria ambapo eneo la jiopaki ya Ngorongoro Lengai kuna makabila ya wahadzabe na wadatoga ambapo makabila hayo bado yanaheshimu mila na utamaduni wao bila kuathiriwa na mila nyingine.


Na Mwandishi Wetu 

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania(TRAMEPRO Tanzania ) limetoa mwitokwa Watanzania, Waafrika na jumuiya ya kimataifa kuendelea kujenga jamii inayoheshimu utu wa kila mtu, kuwekeza katika elimu, afya, sayansi, mazingira na amani.

TRAMEPRO imetoa mwito huo leo Julai 18,2026 katika kukimbizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela aliyekuwa Rais wa nchi ya Afrika Kusini. 

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu TRAMEPRO Tanzania  Boniventura Mwalongo amesema wanaungana na mataifa ya Afrika na dunia kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela mmoja wa viongozi mashuhuri waliobadilisha historia ya dunia kwa kupigania uhuru, usawa, haki za binadamu na maridhiano.

Pia amesema mambo ya kujifunza kupitia kutoka kwa Nelson Mandela ni kwamba elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ya kubadilisha dunia, msamaha ni nguvu, si udhaifu; hujenga taifa lenye umoja.

Mengine ni uvumilivu na subira vinaweza kushinda hata changamoto kubwa,  Uongozi ni huduma, si nafasi ya kutawala wengine, haki  na usawa ni msingi wa maendeleo endelevu.

"Mandela anatufundisha pia umoja wa Waafrika na kuheshimiana ni nguzo ya maendeleo ya bara letu. Afya, mazingira na maendeleo vinapaswa kwenda pamoja kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, " amesema Mwalongo. 

Akieleza zaidi amesema kwa waratibu asili Asili,TRAMEPRO Tanzania inaona mafunzo makubwa kutoka kwa Mandela katika kujenga umoja wa sekta, kuzingatia maadili ya taaluma, kuendeleza utafiti, kuhifadhi mimea tiba, kulinda mazingira na kushirikiana na taasisi za kisayansi ili tiba asili ichangie kikamilifu afya na maendeleo ya jamii.

Kuhusu historia ya Nelson Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji cha Mvezo, Mkoa wa Eastern Cape, Afrika Kusini. Jina lake la asili, Rolihlahla, katika lugha ya Kixhosa humaanisha mtu anayetikisa tawi la mti, na kwa maana ya kawaida huashiria mtu mwenye kuhoji au kupinga hali iliyopo.

Alipoanza shule ya msingi, mwalimu wake alimpa jina la Nelson, kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo katika shule nyingi za kikoloni.

Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme ya kabila la Thembu. Baba yake aliitwa Gadla Henry Mphakanyiswa Mandela, aliyekuwa mshauri wa mfalme wa Thembu, na mama yake aliitwa Nosekeni Fanny Mandela.

 Kutoka kwa wazazi wake alijifunza heshima, uwajibikaji, uongozi na umuhimu wa kuitumikia jamii.

Katika elimu, Mandela alianza masomo katika shule za wamisionari, akaendelea katika Chuo cha Healdtown, kisha akasoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare. 

Baadaye alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, ambako alijiandaa kuwa mwanasheria na mtetezi wa haki za wanyonge. Elimu yake ilimpa msingi wa kuelewa sheria na kuitumia kutetea usawa na utu wa binadamu.

Mandela aliongoza mapambano dhidi ya mfumo wa ubaguzi wa rangi (Apartheid). Kutokana na msimamo wake, alifungwa gerezani kwa miaka 27, lakini hakukata tamaa wala kuacha kuamini kuwa amani na maridhiano vinaweza kushinda chuki. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990, aliongoza mazungumzo yaliyoweka msingi wa Afrika Kusini mpya yenye demokrasia.


Mwaka 1994, Nelson Mandela aliingia katika historia kwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini aliyechaguliwa kidemokrasia. Uongozi wake ulijengwa juu ya maridhiano, msamaha na umoja wa kitaifa. Mwaka 1993, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mchango wake katika kumaliza Apartheid kwa njia ya amani.

Katika kipindi cha tarehe 01 hadi 15 Julai, mchezo wa kasino wa Monopoly Big Baller umeibuka kama mfalme wa malipo kwa wachezaji ndani ya Meridianbet. Zaidi ya Tsh. 11,700,000/= zimetolewa kwa washindi, jambo linalothibitisha kuwa huu si mchezo wa kawaida bali ni chanzo cha furaha na ushindi halisi.

Wachezaji wengi wamekuwa wakishuhudia ndoto zao zikigeuka kuwa halisi kupitia mchezo huu. Ni kama bahari ya ushindi ambapo kila tiketi ya kucheza inafungua mlango wa matumaini mapya. Ushindi huu mkubwa unazidi kuimarisha imani ya wachezaji kwamba Meridianbet si tu jukwaa la michezo ya kubahatisha, bali ni uwanja wa ndoto zinazotimia.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Monopoly Big Baller imekuwa gumzo mitaani, ikitajwa kama mchezo wa dhahabu kwa sababu ya malipo yake makubwa na ya mara kwa mara. Kila droo inapoendelea, wachezaji wanahisi msisimko wa kipekee, wakisubiri mpira wa bahati kuangukia nafasi yao ya ushindi.

Kwa wachezaji wapya, huu ni mwaliko wa kujiunga na familia ya washindi. Kwa wale waliokwishaonja ladha ya ushindi, ni uthibitisho kwamba bahati haichoshi. Ushindi wa zaidi ya milioni 11.7 ni ushahidi wa wazi kwamba Meridianbet inatoa thamani ya kweli kwa wachezaji wake.

Kwa hivyo, kama unatafuta mchezo unaolipa, unaosisimua na unaoleta furaha, basi Monopoly Big Baller ndiyo chaguo sahihi. Meridianbet imeweka historia, na sasa ni wakati wako kuandika ukurasa wako wa ushindi.
Usiku wa leo Sporting CP watakutana na klabu ya Kifaransa RC Strasbourg katika mechi ya kirafiki ya maandalizi ya msimu mpya wa 2026/27. Mechi hii itachezwa katika Uwanja wa Estádio do Algarve, na itakuwa ni hatua ya mwisho ya kambi ya mafunzo ya Sporting huko Algarve, ambayo ilianza tarehe 11 Julai. Mechi hii inakamilisha kambi hiyo ya mafunzo, baada ya Sporting kucheza dhidi ya mabingwa wa Scotland, Celtic, tarehe 14 Julai.

Kwa upande wa Sporting CP, wako katika hali nzuri ya maandalizi. Mechi yao ya hivi karibuni ilikuwa dhidi ya Celtic ambapo walishinda kwa mabao 4-1, hali inayoonyesha timu ina hamasa na ufanisi mzuri wa mbele ya golini kabla ya msimu mpya kuanza. Kocha atatumia mechi hii kuendelea kupima muundo wa timu, hasa wachezaji wapya na vijana wanaotafuta nafasi katika kikosi kikuu.

Strasbourg nao wanakuja mechini hii wakiwa na kasi kubwa ya mabao. Mechi yao ya mwisho kabla ya hii ilikuwa dhidi ya AS Monaco katika Ligue 1, ambapo walishinda kwa mabao mengi ya 5-4 matokeo yanayoonyesha ulinzi wao bado unahitaji kuimarika ijapokuwa mashambulizi yao ni hatari.

Msimu uliopita, klabu hiyo ya Kifaransa ilimaliza nafasi ya nane katika Ligue 1 na kufuzu kushiriki mashindano ya Ulaya, jambo linaloonyesha ni timu inayoendelea kukua kimuundo chini ya usimamizi wao wa sasa. Kitakwimu, Strasbourg ni timu inayopenda mabao mengi.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Msimu huu wanaoumaliza, waliungana kufunga mabao 92 katika mechi 53, wastani wa mabao 1.74 kwa mechi, huku asilimia 62 ya mechi zao zikiwa na jumla ya mabao zaidi ya 2.5. Wachezaji kama Joaquín Panichelli wamekuwa chanzo kikuu cha mabao msimu uliopita, hivyo ulinzi wa Sporting utahitajika kuwa makini sana dhidi ya mstari wa mbele wa Wafaransa hao.

Kwa ujumla, mechi hii ni fursa nzuri kwa mashabiki kuona jinsi timu zote mbili zilivyojiandaa kabla ya misimu yao kuanza Sporting wakielekea Liga ya Ureno na Strasbourg wakielekea Ligue 1. Ikizingatiwa mtindo wa mabao mengi wa pande zote mbili, kuna uwezekano mkubwa wa kuona mechi yenye mabao ingawa kwa vile ni mechi ya kirafiki, makocha wote wawili wanaweza kubadilisha wachezaji wengi ili kuwapa nafasi vijana na wachezaji wapya.

The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi, has thanked the Government of India for its continued efforts to strengthen cooperation with Tanzania in the sectors of education, health, trade, investment, water, science and technology.

President Dr. Mwinyi made the remarks today, July 19, 2026, when he met with India's Minister of External Affairs, Hon. Dr. S. Jaishankar, at a conference hall at the Taj Palace Hotel in New Delhi, India.

During the discussions, President Dr. Mwinyi asked India to increase the number of scholarship and training opportunities for students and professionals from Zanzibar, as well as to strengthen the IIT Madras Zanzibar campus by introducing more academic programmes and supporting the construction of its permanent campus.

President Dr. Mwinyi also handed over to Minister Jaishankar the Master Plan for the construction of the permanent IIT Madras Zanzibar campus, aimed at making Zanzibar a hub for higher education, research, innovation and technology for the African region.

For his part, Minister Dr. Jaishankar commended the progress made by IIT Madras Zanzibar and reaffirmed the Indian Government's commitment to continuing to strengthen cooperation with Tanzania across various development sectors.

President Dr. Mwinyi continues his visit to India, where he is meeting with various leaders with the aim of strengthening development cooperation between Zanzibar, Tanzania and India.









Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amewataka wakaguzi wa shule kutenda haki kwa shule binafsi na kuziona kama mshirika wa maendeleo badala ya mshindani.

Kadhalika, Profesa Tibaijuka ameipongeza shule ya St Anne Marie Academy kwa kuendelea kusomesha bure wanafunzi wanaofiwa na wazazi wao ikiwa shule pekee ya binafsi inayofanya hivyo kwa sasa nchini.

Alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa shule hiyo Julai 18, mwaka 2001.

Aliwataka wakaguzi wa elimu nchini kuacha kuziwekea vikwazo shule binafsi kwa kuziona kama washindani kwenye sekta ya elimu na badala yake wanatakiwa kuwaona kama washirika muhimu kwenye kutoa huduma hiyo.

”Unakuta wanawawekea wenye shule binafsi viwango vya kusadikika tofauti kabisa na shule za umma, sisemi kwama muwawekee viwango hafifu, hapana mimi nataka uwiano wa haki baina ya shule za umma na shule binafsi,” alisema

Alisema shule zingine zinapaswa kuiga mfano huo kwani elimu ni huduma na siyo biashara hivyo wanatakiwa kuwaacha waendelee na masomo baada ya wazazi wao wanaowalipia ada kufariki dunia.

Kadhalika, Profesa Tibaijuka alisema serikali imebadili mitaala ya zamani na kuingiza mitaala ya ufundi ambayo inamwezesha mwanafunzi kuchagua na hivyo kupata ujuzi utakaowawezesha kupata ajira au kujiajiri mapema wanapomaliza masomo yao.

Alisema wakati huu wa teknolojia ya kisasa shule zinapaswa kwenda na wakati kwa kuhakikisha zinakwenda sanjari na dunia ya sasa kwa kuwa na mafunzo ya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA.

Alisema shule bora ni ile yenye uwezo wa kufaulisha mwanafunzi ambaye alikuwa na matokeo ya kawaida kwani kuna baadhi ya shule ambazo zimekuwa zikichuja wanafunzi na kuchukua wale waliofaulu vizuri pekee.

“Kama mwanafunzi amefaulu kwa daraja la kwanza ili tujue hiyo ni shule bora lazima tujue aliingia akiwa na daraja la ngapi, kuna wanafunzi wengine kwa uwezo wao mkubwa hawahitaji hata mwalimu sasa ukichukua mwanafunzi bora akafaulu huwezi kujisifu,” alisema

“Nawapongeza St Anne Marie Academy kwani wao wamekuwa wakichukua wanafunzi wa kawaida na kuwatengeneza kufaulu kwa wastani wa daraja la kwanza na daraja la pili, nimemsikia Mkurugenzi akitaja mafanikio ya shule imekuwa ikiingiza wanafunzi bora kitaifa kila mwaka nawapongeza sana,” alisema

Mkurugenzi wa shule hiyo, Dkt. Jasson Rweikiza shule hiyo iliwahi kupata mwanafunzi bora kitaifa kwenye somo la hisabati kidato cha nne mwaka 2013, shule hiyo iliingia 10 bora kitaifa kwa miaka mine mfululizo na kwamba mwaka 2021 shule hiyo ilipata mwanafunzi bora kitaifa kwenye masomo yote.


Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
SERIKALI imesema itaendelea kuimarisha huduma za afya ya uzazi nchini ili kupunguza vifo vya kina mama vinavyotokana na utoaji mimba usio salama.

Naibu Waziri wa Afya, Dk Florence Samizi alisema bungeni kuwa asilimia 10 ya vifo vya wajawazito nchini vinahusishwa na utoaji mimba usio salama, hali inayoonyesha umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika kinga, elimu na huduma za matibabu kwa wanawake.

Alisema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeboresha miundombinu ya sekta ya afya na kuendelea kutoa huduma jumuishi baada ya utoaji mimba (CPAC) bila malipo katika vituo vya kutolea huduma za afya.

"Tunawapatia wanawake huduma baada ya kuharibikiwa na mimba, ikiwemo matibabu, dawa, ushauri nasaha na elimu ya uzazi wa mpango ili kupunguza hatari ya kupata mimba nyingine isiyotarajiwa na kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza," alisema Dk Samizi.

Aliongeza kuwa serikali inaendelea kuimarisha huduma rafiki kwa vijana kwa kutoa elimu ya afya ya uzazi, kujikinga dhidi ya mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa, pamoja na kuhakikisha manusura wa ukatili wa kijinsia na matukio mengine wanapata huduma stahiki kwa wakati.

Kauli hiyo imekuja wakati wadau mbalimbali wakiendelea kujadili utekelezaji wa Itifaki ya Maputo, ambayo Tanzania iliiridhia.

Mjadala umejikita zaidi kwenye Ibara ya 14(2)(c) ya itifaki hiyo, inayozitaka nchi wanachama kuchukua hatua zinazofaa kuruhusu utoaji mimba kwa njia ya tiba katika mazingira maalumu, ikiwemo pale ujauzito umetokana na ubakaji, unyanyasaji wa kingono, ndugu wa damu (incest), au endapo kuendelea kwa ujauzito kunaweka maisha au afya ya mama katika hatari, au maisha ya kijusi yako hatarini. Utekelezaji wa masharti hayo unafanyika kwa kuzingatia sheria za ndani za kila nchi.

Nchini Tanzania, utoaji mimba kwa hiari bado unadhibitiwa na sheria, isipokuwa katika mazingira yanayotambuliwa na sheria husika.

Hata hivyo, Serikali imeendelea kusisitiza kuwa wanawake wanaopata madhara baada ya utoaji mimba wanapaswa kufika katika vituo vya afya ili wapate matibabu, ushauri nasaha na huduma nyingine muhimu bila kuchelewa.

Wataalamu wa afya wanasema utoaji wa huduma hizo, sambamba na elimu ya afya ya uzazi na upatikanaji wa huduma kwa wakati, ni miongoni mwa hatua muhimu zinazoweza kupunguza vifo vya kina mama na kuboresha afya ya uzazi nchini.

Top News