MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imeamuru kutolewa kwa wito (summons) kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF) na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), ili kutoa ushahidi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu.

Uamuzi huo umetolewa leo na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dustan Ndunguru baada ya Mahakama kusikiliza hoja za upande wa mashtaka na utetezi kuhusu ombi la Lissu la kuwaita mashahidi hao pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Mahakama imesema, kwa kuzingatia kifungu cha 314 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), ina hiari ya kuruhusu mashahidi kuitwa kwa kuangalia umuhimu wa ushahidi wao katika shauri.

Katika uamuzi huo, Mahakama imesema imeridhika kuwa ushahidi wa IGP, CDF na DCI ni muhimu katika kesi hiyo, hivyo imeamuru summons zitolewe ili waje kutoa ushahidi upande wa utetezi.

Hata hivyo, Mahakama imekataa ombi la kuwaita baadhi ya mashahidi waliotajwa na Lissu, akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu wa zamani Kassim Majaliwa, ikisema ushahidi wao hauhusiani na kesi hiyo kwa upande wa utetezi.

Mahakama pia imekubaliana na hoja ya upande wa mashtaka kwamba mashahidi ambao hawakutajwa wakati wa committal proceedings hawawezi kutajwa baadaye wakati wa usikilizwaji wa hoja za awali (PH).

Jaji Ndunguru amesema kifungu cha 281 cha CPA kinaeleza kuwa msajili atatoa summons kwa mashahidi waliotajwa wakati wa committal proceedings, huku Mahakama ikibaini kuwa katika mwenendo wa kesi hiyo hakukuwa na orodha ya mashahidi waliotajwa.

Kuhusu hoja ya kumuita Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Mahakama imesema mfano wa kesi ya Khatibu Ghandi hauwezi kutumika moja kwa moja kwa kuwa katika kesi hiyo shahidi huyo aliitwa na upande wa mashtaka na pia sheria ya sasa ya Usalama wa Taifa haikuwepo wakati huo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho saa tatu asubuhi kwa ajili ya kuendelea na hatua ya utetezi.


Wadau wa kilimo-misitu nchini Tanzania wameanzisha jukwaa maalum (TASP), litakalowaunganisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kubadilishana uzoefu, taarifa na ubunifu, pamoja na kuimarisha ushirikiano katika kuendeleza kilimo-misitu na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Akifungua jukwaa hilo Septemba 10, 2026 jijini Dodoma, Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Nickson Kimaro, amesema kilimo-misitu ni agenda mtambuka inayohitaji ushirikiano wa Serikali, wakulima, taasisi za utafiti, sekta binafsi, asasi za kiraia, taasisi za fedha na washirika wa maendeleo.

Amesema TASP inapaswa kuwa mfumo endelevu wa uratibu utakaowezesha wadau kuoanisha jitihada zao, kubaini mapungufu na kutumia rasilimali kwa ufanisi, huku kilimo-misitu kikiwa na manufaa ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Mkurugenzi Mtendaji wa Civic Social Protection Foundation (CPS), Nemence Iriya, amesema jukwaa hilo litatoa nafasi kwa wadau kukutana na kujadili sera, mikakati, sheria na taratibu zinazohusu kilimo-misitu, pamoja na kuimarisha uratibu wa shughuli zao.

Amesema TASP pia itasaidia kuhakikisha matokeo ya tafiti na ubunifu unaofanywa na watafiti unawafikia wakulima moja kwa moja, pamoja na watunga sera na wafanya maamuzi, na kuhalikisha tafiti hizo zinatumika katika kuboresha mipango na mikakati ya kilimo-misitu.

Kwa upande wake, Afisa Utafutaji Rasilimali Fedha, Mawasiliano na Utetezi kutoka VI-Agroforestry, Khalid Ngassa, amesema jukwaa hilo litawawezesha wadau kukutana pamoja, kubadilishana maarifa na uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili ili kupata suluhisho kwa pamoja.

Kwa ujumla, kuanzishwa kwa jukwaa hilo, kunatoa fursa muhimu ya kuwaunganisha wadau wa kilimo-misitu na kujenga mshikamano katika kushughulikia changamoto zinazowakabili, huku mafanikio ya jukwaa hilo yakitegemea utekelezaji wa mijadala na maazimio yaliyowekwa ili kuleta matokeo yanayoonekana kwa wakulima, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na maendeleo ya sekta hiyo nchini.














Na Nasra Ismail, Geita

Shirika la Arusha Society for the Protection of Animals (ASPA) kwa kushirikiana na Brooke East Africa limeendelea kutoa elimu kwa wafugaji na waendesha punda katika Kata ya Magenge, Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Hii imechangia kuboresha ustawi wa mnyama kazi huyo katika maeneo hayo.

Kupitia elimu wanayopatiwa na mashirika hayo, wamiliki na waendesha punda wameanza kuona faida ya kumtunza mnyama huyo ambaye sasa ameanza kuwaingizia kipato tofauti na awali.

Wananchi wamesema sasa wana elimu ya kumtunza punda na namna sahihi ya kumfungia mkokoteni. Hii imesaidia kumpunguzia mnyama huyo vidonda na mateso, tofauti na kipindi kilichopita kabla ya kupata elimu hiyo.

Afisa Mifugo wa Kata ya Magenge, George Sebastianamesema kupitia elimu inayotolewa na ASPA, kwa kipindi kirefu sasa punda wameanza kuzaliana. Hii inaonesha kuwa punda sasa wanapata ustawi na wanaishi vizuri.

Kwa upande wake, Afisa Elimu ya Ustawi wa Wanyama kutoka ASPA, Diana Msemo amesema mnyama kazi punda anahitaji utulivu wa hali ya juu ili aweze kufanya kazi zake za kiasili na kuongeza uwezekano wa kupata ujauzito na kuongeza kizazi chake.

Msemo amebainisha baadhi ya mambo yanayompa utulivu mnyama huyo ni pamoja na kupata muda wa kupumzika, kupewa matibabu ya mara kwa mara na kupunguziwa mizigo ambayo haimudu.

 




MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imefanya Kikao Kazi cha Kwanza cha Jukwaa la Ushauri la Wadau wa TRA kuhusu Maadili, kinachofanyika mkoani Morogoro, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na wadau katika kukuza maadili katika usimamizi wa kodi na forodha.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyowekwa wakati wa uzinduzi wa Jukwaa hiloAprili 24, 2026, ambao ulikuwa mwanzo wa kujenga njia rasmi na endelevu ya kusikiliza maoni, changamoto na mapendekezo ya wadau kuhusu masuala ya maadili katika shughuli za TRA.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Ndani wa TRA, Shaibu Mmari, amesema maadili si suala la ndani ya TRA pekee, bali ni msingi muhimu wa kujenga uhusiano wa kuaminiana kati ya Mamlaka, walipakodi na jamii kwa ujumla.

Amesema ni muhimu walipakodi kutendewa kwa heshima, maamuzi kutolewa kwa misingi ya sheria na taratibu zinazoeleweka, pamoja na huduma kutolewa kwa wakati na kwa usawa, hatua ambazo zinaongeza imani ya walipakodi na kuimarisha ulipaji kodi kwa hiari.

Aidha, Mmari amewataka wajumbe wa Jukwaa hilo kuzungumza kwa uwazi na kutoa maoni kuhusu maeneo ambayo yanaweza kuwa na changamoto za kimaadili, ikiwemo ucheleweshaji wa huduma, matumizi mabaya ya mamlaka, changamoto katika mifumo ya kidijitali na njia za kutoa taarifa, huku akisisitiza umuhimu wa kutoa mapendekezo mahususi na yanayotekelezeka.

Kwa upande wake, Naibu Kadhi Mkuu, Sheikh Ali Khamis Ngeruko, amesema ni vyema watumishi wa TRA pamoja na walipakodi kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao ili kuhakikisha kodi zinalipwa kwa haki na kwa hiari. Aidha, amewataka watumishi na walipakodi kujiepusha na vitendo vya rushwa na kuzingatia uadilifu katika shughuli za kodi.

Kikao hicho kimewakutanisha wawakilishi kutoka vyama vya wafanyabiashara, walipakodi, washauri wa kodi, mawakala wa forodha, taasisi za Serikali, asasi za kiraia, taasisi za dini pamoja na viongozi na watendaji wa TRA, ambapo pamoja na kujadili masuala mbalimbali ya maadili, kikao hicho kinajadili pia rasimu ya Hadidu za Rejea za Jukwaa zitakazoweka msingi wa utekelezaji wa majukumu yake na ushirikiano endelevu na wadau.

 





Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, pamoja na Mawaziri, wakimfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nyumbani kwake Kizimkazi, Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 10 Septemba 2026, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 7 Septemba 2026.


















-Wananchi watakiwa kulinda daraja


‎Wananchi wa maeneo ya Chigongwe, Ngambala na Nguji kata ya Chigongwe wilayani Dodoma wameondokana na changamoto ya kukatika kwa mawasiliano wakati wa mvua baada ya kukamilika kwa ujenzi wa daraja la Chigongwe lenye urefu wa mita 36 katika barabara ya Chigongwe–Ngambala–Nguji.

‎Mradi huo umetekelezwa na Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia fedha za Mfuko wa Dharura (CERC) zilizotengwa kwa ajili ya kurejesha na kuboresha miundombinu iliyoathiriwa na mvua kubwa za mwaka 2024 hali iliyokuwa ikiathiri usafiri wa wananchi, usafirishaji wa mazao na upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.

‎Akizungumza wakati wa ukaguzi wa daraja hilo, Meneja wa TARURA wilaya ya Dodoma, Mhandisi Emmanuel Mfinanga amesema mradi huo uliogharimu shilingi milioni 606 umehusisha ujenzi wa daraja pamoja na uchongaji na uwekaji wa kifusi katika barabara kilomita 1 ambapo kwa sasa mradi umekamilika.

‎Mhandisi Mfinanga amewataka wananchi wanaotumia daraja hilo kulinda na kutunza ikiwemo kuzuia wizi wa vyuma vya ulinzi na kuepuka kufanya shughuli zinazoweza kuharibu daraja au kuzuia mtiririko wa maji.

‎Amesema ushirikiano wa wananchi katika kuitunza na kuilinda miundombinu ni muhimu ili kuhakikisha barabara, madaraja, makalavati na mifereji inaendelea kudumu kwa muda mrefu na kufanya kazi kwa ufanisi hususan wakati wa mvua kubwa.

‎Naye, Diwani wa kata ya Chigongwe Mhe. William Nado amesema ujenzi wa daraja hilo umeondoa changamoto iliyodumu kwa muda mrefu na kuwawezesha wananchi wa Mkombola na Ngambala kusafiri kwa urahisi wakati wote wa mwaka.

‎Amesema hapo awali mvua zilikuwa kikwazo cha usafiri ambapo wananchi walilazimika kuchangishana fedha na kurekebisha njia ili magari, pikipiki na watembea kwa miguu waweze kupita lakini sasa daraja hilo limeondoa kikwazo na wananchi wanasafiri bila shida.

‎Mhe. Nado amesema kukamilika kwa daraja hilo kumebadili hali ya usafiri kwani wananchi wanaweza kusafirisha mazao yao na mahitaji mengine kwa urahisi zaidi hasa kwa kutumia pikipiki na pia wanafunzi wanafika shuleni kwa urahisi.

‎Kwa upande wake, Mwenyekiti wa mtaa wa Ngambala Bw. Kenneth King’omah amesema daraja hilo limekuwa mkombozi kwa jamii hasa wajawazito, wazee na wagonjwa waliokuwa wakipata changamoto kufika katika vituo vya afya.

‎Amesema wananchi wamejipanga kushirikiana na TARURA na viongozi wa eneo hilo kuhakikisha daraja hilo linalindwa na kutunzwa ili liendelee kuwa kiungo muhimu cha huduma na shughuli za kiuchumi na kijamii.

‎Mkazi wa Ngambala na dereva wa bodaboda, Bw. Isaya Juma amesema ujenzi wa daraja hilo umeondoa adha kubwa iliyokuwa ikiwakabili waendesha pikipiki kwani awali walilazimika kushuka kwenye pikipiki na kupanda eneo hilo kwa shida wakati wa kuvusha abiria au mizigo jambo lililosababisha usumbufu na kuchelewesha safari.

‎Amesema kwa sasa hata ukiwa umepakia abiria watatu au wanne unapita bila shida ambapo ameishukuru serikali kwa daraja hilo kwasababu limeondoa changamoto iliyodumu kwa miaka mingi.












Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), kupitia Chuo cha VETA Mkoa wa Mbeya ikishirikiana na Jeshi la Magereza mkoani Mbeya imeanza mchakato wa kutambua, kutathmini na kurasimisha ujuzi wa ufundi stadi kwa wafungwa 100 walioupata wakati wakitumikia vifungo.

Mchakato huo ulioanza tarehe 27 Agosti 2026 unafanywa kwa ushirikiano na Chuo cha Ufundi cha Jeshi la Magereza Ruanda, jijini Mbeya, na unatarajiwa kukamilika Septemba 15, 2026.

Akizungumza kuhusu mchakato huo, Meneja wa Kanda ya Kusini Magharibi, Shomari Chololo waombaji waliojitokeza ni wamegawanyika katika stadi Ufundi Umeme (8), Ufundi Bomba (10), Ufundi Seremala (15), Ufundi Uashi (41), Uungaji na Uundaji Vyuma (12), Ushonaji (11), Huduma za Ndani na Usafi pamoja na Utengenezaji wa Sabuni (3).

Kupitia mchakato huo, wafungwa watakaokidhi vigezo wanatarajiwa kupata vyeti vinavyothibitisha ujuzi wao, hatua inayolenga kuwawezesha kutumia ujuzi huo kwa tija, ikiwemo kujiajiri, kuajiriwa au kuanzisha shughuli za uzalishaji baada ya kumaliza kutumikia vifungo vyao

Mchakato huo ni sehemu ya jitihada za kutambua na kuthibitisha ujuzi unaopatikana kupitia mafunzo na uzoefu wa vitendo, ili wahusika waweze kuwa na uthibitisho rasmi wa uwezo wao wa kiufundi na kuutumia katika maisha yao baada ya kumaliza vifungo.

VETA huendesha programu ya Utambuzi na Urasimishaji Ujuzi uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi wa Mafunzo (RPL) ambapo mafundi hufanyiwa tathmini ya ujuzi wao, kubaini upungufu walio nao katika stadi husika, kisha kuandaliwa mafunzo ya muda mfupi kuziba upungufu na hatimaye kutunukiwa vyeti vya urasimishaji ujuzi wao.


















Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.




Benki ya NMB imejiunga kwa mara ya kwanza kuwa mdhamini wa Mbio za Mbuzi za mwaka 2026, zinazolenga kukusanya Sh milioni 200 kwa ajili ya kusaidia vijana 150 kujiunga na vyuo vikuu na mafunzo ya ufundi. Tukio hilo litafanyika Septemba 19 katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Idara ya Wateja Maalum wa benki ya NMB , Getrude Mallya, amesema uamuzi huo umetokana na uzoefu wa benki hiyo kama mshiriki wa tukio la mwaka jana pamoja na ulinganifu uliopo kati ya malengo ya Rotary na uwekezaji wa NMB katika elimu.

NMB hutenga asilimia moja ya faida baada ya kodi kila mwaka kwa uwekezaji wa kijamii. Mwaka 2025, benki hiyo ilitoa madawati 6,365 kwa shule 124 nchini, hatua iliyonufaisha takribani wanafunzi 19,095.

Rais wa Rotary Club of Dar es Salaam Oysterbay, Paul Muhato, amesema Sh milioni 163 kati ya Sh milioni 167 zilizokusanywa mwaka jana zimesaidia wanafunzi 136, wakiwemo 100 waliojiunga na vyuo vikuu na 36 waliojiunga na mafunzo ya ufundi.








 


SportPesa XUP turns every football lead into an early payout moment

SportPesa XUP turns every football lead into an early payout moment 

The new European football season has already brought its share of familiar chaos. Favorites can dominate the game, take the lead, and then lose control due to a late set piece or a swift counterattack. These dramatic turnarounds are what make football so captivating, but they also reveal the difference between strong moments during the game and the final result. SportPesa Tanzania addresses this tension with an early-payout option that settles bets before the final whistle.

SportPesa XUP gives football fans a different way to read a match because a lead can matter before the final whistle. Through 1UP, 2UP and 3UP markets, eligible selections can be settled early when the chosen team reaches the required goal advantage during the match. On XUp, the selected team can trigger an early payout by reaching the required lead before full time, depending on the market selected. 

A lead now carries meaning before the final whistle

A typical match-winner bet depends on the score at full time. The new early-payout football feature, however, recognizes an earlier turning point. In the 1UP market, your bet wins as soon as the supported team takes a one-goal lead. Even if a late equalizer changes the score, it does not undo a bet that is already settled.

Imagine a team leading 1-0 but conceding late to end the match 1-1. Normally, a win bet would lose because the game finished as a draw. But with the SportPesa 1UP, 2UP and 3UP option, your bet would have already won when that initial goal gave the team the lead. This key difference highlights the product’s value as it puts a clear worth on taking the lead itself.

“1UP, 2UP and 3UP make every lead more meaningful because fans do not only wait for the final whistle. When a selected team reaches the required goal margin, the market can settle early, which adds another layer of excitement to eligible football fixtures,” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

Why early-payout bets have different odds

The three levels reflect different expectations in a match. A one-goal lead triggers the 1UP market, whether the score is 1-0, 2-1, or 3-2. The next level, 2UP, requires a two-goal cushion, while 3UP demands a three-goal advantage. Each level poses a distinct question, can the team get ahead, establish firm control, or dominate the game with a commanding lead.

According to SportPesa 1UP early-payout, these bets often come with shorter odds than traditional full-time markets because reaching a lead is usually easier than maintaining it until the final whistle. Higher thresholds like 2UP and 3UP happen less frequently, so they typically offer bigger payouts than the 1UP option. Choosing the right one depends on anticipating how the match is likely to unfold, not just picking the favorite.

The launch meets a season defined by shifting momentum

Timing is everything. The Premier League, La Liga, Serie A, and Bundesliga regularly showcase matches that shift after substitutions, tactical tweaks, or a late surge of pressure. A strong favorite might score early but then face a fierce comeback, while another may need most of the game to break through. By focusing on the moment a team reaches a set lead, this new market captures the drama fans are already watching.

SportPesa offers this feature on selected match fixtures, with each available threshold clearly shown alongside the match on its platform. This keeps football at the heart of the experience and ties the platform to the lively debates that fill group chats, radio shows, and fan conversations every weekend, about who starts fast, who controls the game, and who stays vulnerable after taking the lead.

XUP on singlebets and multibets

Settlement works differently depending on the bet type. For a single bet, once the selected team reaches the required lead, that bet is settled immediately. In a multibet, the qualifying leg is marked as won, but the entire bet slip remains open until the other selections are decided. This means an early win in one match resolves only part of the overall bet, leaving the rest to play out.

This distinction mirrors how modern football fans watch the game. They follow multiple matches simultaneously, switch between live scores and broadcasts, and expect digital platforms to react quickly to on-pitch events. SportPesa adds valuable context, while the early-settlement feature turns a key moment in the game into a clear, decisive outcome on the platform.

Conclusion

SportPesa XUP gives football fans a more exciting way to follow selected matches by making every lead matter before the final whistle. With 1UP, 2UP and 3UP, eligible bets can settle when the chosen team reaches a one-goal, two-goal or three-goal advantage, adding more meaning to match momentum. For players using SportPesa, the key is to understand how each market works, check availability before placing a bet and enjoy the experience responsibly.

TCB Chief Executive Officer and Managing Director 
Adam Charles Mihayo



By Issa Michuzi


The Tanzania Commercial Bank (TCB) is again footing the bill for the annual gathering of board chairpersons and chief executives from public bodies, signing on as principal sponsor for the third year in a row.


The event, hosted by the Office of the Treasury Registrar, will take place in Arusha from 28 to 30 September.


TCB Chief Executive Officer and Managing Director Adam Charles Mihayo confirmed the support today, 9 September 2026, at a breakfast briefing with news editors at the Hyatt Kilimanjaro in Dar es Salaam. 


The bank, he said, is “honoured to participate in the important gathering and proud to serve as its principal sponsor for the third consecutive time.” 


He added, “We greatly appreciate the honour extended to us by the Office of the Treasury Registrar to participate in this important meeting.”


For Mihayo, the forum is no mere ceremony. Over three days, leaders from public institutions and corporations will swap experiences, audit their own performance, and hunt for workable ways to improve service delivery and deepen their contribution to national development.


He also pulled the media into that mission. 


When coverage is steady and clear, he said, Tanzanians can track the work of the Treasury Registrar and the bodies it oversees. “Better public understanding keeps those institutions moving toward greater transparency and accountability”, he added.


TCB’s lineage reaches back to 1925, when it opened as the Tanganyika Post Office Savings Bank. 


Today it is a full commercial bank, the government holding the majority stake, with other public institutions owning the rest. 


The bank offers retail, SME, corporate, treasury, and digital banking, and says its focus remains on innovative financial solutions and wider financial inclusion.


Renewing the sponsorship, the TCB chief adds, is one part of its broader promise to back efforts that strengthen public institutions and push Tanzania’s development agenda forward.


By Issa Michuzi

 More than 700 board chairpersons and chief executives from state institutions and corporations will gather in Arusha from 28 to 30 September to review their performance and strengthen their role in delivering Tanzania Development Vision 2050.

 

Acting Treasury Registrar Ms Lightness Mauki (pictured) outlined the agenda today, 9 September 2026, during a breakfast briefing with news editors at the Hyatt Kilimanjaro hotel in Dar es Salaam.

 

The briefing highlighted the growing role of public institutions in advancing national development and set the tone for the upcoming high-level forum.

 

She said the Arusha gathering will be guided by a theme centred on three priorities: high performance, inclusiveness and resilience.

 

The goal is to build public institutions capable of driving Vision 2050 while remaining responsive to changing circumstances.

 

Beyond translating the Vision into day-to-day action, Ms Mauki said the forum will give leaders under the Treasury Registrar’s oversight an opportunity to exchange lessons and make better use of existing experience.

 

She noted that the gathering is going to be more than a routine meeting, but a platform to align experience, resources, policy papers and government directives with faster and more efficient delivery.

 

Ms Mauki, who also serves as the Treasury Registrar’s Director of Planning, Research and Business Development, said government investment in the institutions has risen by 75 per cent in three years to Sh92 trillion.

 

Revenue performance has also improved, she said.

 

“In the financial year ending 2026, the entities remitted Sh1.307 trillion, up seven per cent from Sh1.208 trillion collected in the previous year,” she said.

 

She described the figure as the highest amount collected since the Office of the Treasury Registrar was established.

 

The Office of the Treasury Registrar of Tanzania was established on 13 November 1959 through Treasury Registrar Ordinance No. 35 of 1959 to acquire, hold and manage government investments. The legislation is now known as the Treasury Registrar (Powers and Functions) Act, Chapter 370.

 

“Numbers like these show that our institutions are ready to play their full part in Tanzania Development Vision 2050, whose implementation formally began in July,” she said.

 

“As leaders in government and public institutions, we have a duty to translate our responsibilities into practical action and deliver the expected results,” she said.

 

“I encourage Tanzanians to follow our activities and the discussions that will take place during the meeting of board chairpersons and chief executives,” she said.

 

“Above all, I invite everyone to join us in celebrating the achievements recorded so far, while renewing our commitment to discharging our responsibilities efficiently, patriotically and with dedication,” Ms Mauki said.


Na Karama Kenyunko Michuzi Tv


SHAHIDI wa tano wa utetezi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, John Heche, ameieleza Mahakama namna matukio mbalimbali aliyodai kuyashuhudia katika chaguzi yalivyosababisha chama hicho kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election” (Bila Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi).

Heche, ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, ametoa ushahidi huo leo Septemba 9, 2026, katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, mbele ya Jopo la Majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dustun Ndunguru.

Akijibu maswali ya Lissu, Heche amesema Desemba 2, 2024, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikaa na kujadili masuala mbalimbali yaliyohusu chaguzi, ikiwemo ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, kuenguliwa kwa wagombea wa chama hicho na matukio ya mauaji yaliyohusishwa na chaguzi.

Heche amesema kutokana na hali hiyo, hususani uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 na chaguzi nyingine alizoshiriki na kuzishuhudia, chama hicho kiliona kuwa hazikuwa chaguzi za kawaida bali “uchafuzi”, jambo lililopelekea Kamati Kuu chini ya Mwenyekiti wa wakati huo, Freeman Mbowe, kufikia msimamo wa “No Reforms, No Election.”

Amesema mabadiliko yaliyokuwa yakihitajika yalihusisha marekebisho makubwa ya Katiba na sheria, pamoja na kuondoa madaraka makubwa ya Rais katika uundaji wa Tume ya Uchaguzi na uteuzi wa watendaji wa uchaguzi.

“Kamati Kuu iliazimia mabadiliko makubwa ya kikatiba na ya kisheria,” amesema Heche.

Amedai chama hicho kilitaka Tume Huru ya Uchaguzi ambayo ingekuwa huru na isiyo na upendeleo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mwingine.

Heche amesema Aprili 3, 2025, CHADEMA ilikutana na watia nia waliokuwa wakitarajia kugombea kupitia chama hicho katika makao makuu ya chama, Mikocheni, Dar es Salaam, na kuwaeleza sababu za kuendelea na msimamo wa “No Reforms, No Election” uliokuwa umechukuliwa tangu Desemba 2024.

Akieleza matukio aliyodai kuyashuhudia katika chaguzi mbalimbali, Heche amesema ameshiriki chaguzi akiwa mgombea na kiongozi wa chama, ikiwemo uchaguzi wa Arumeru, Busanda, Igunga, Kinondoni pamoja na chaguzi za mwaka 2015 na 2020.

Amedai chaguzi hizo ziliambatana na matukio mbalimbali, ikiwemo mauaji ya wanachama, kuenguliwa kwa wagombea wa CHADEMA, kunyimwa fomu za viapo vya mawakala, mawakala kuondolewa vituoni wakati zoezi likiendelea, polisi kupiga watu na kuvuruga mikutano ya kampeni ya chama hicho.

Amedai pia kuwa wagombea wa chama hicho walinyimwa fomu za matokeo, huku akidai kulikuwa na kura za uongo kuingizwa na baadhi ya watu kubeba vibegi vya kura feki.

Akijibu maswali ya Lissu kuhusu matukio ya mauaji aliyoyakumbuka katika chaguzi hizo, Heche ameeleza tukio la uchaguzi wa mwaka 2015 katika Jimbo la Busanda, ambapo amesema kiongozi wa CHADEMA na mgombea wa ubunge, Alphonce Mawazo, aliuawa.

Amesema Mawazo alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita na Mjumbe wa Baraza Kuu la chama hicho.

Alipoulizwa kama kuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya waliohusika na mauaji ya Mawazo, Heche amesema hakumbuki vizuri mwisho wa kesi hiyo hivyo hawezi kueleza kwa usahihi.

Katika tukio lingine, Heche amesema wakati wa uchaguzi wa mwaka 2020, alipokuwa akifunga kampeni Nyamongo, Kata ya Matongo, alivamiwa na kushambuliwa kwa risasi, ambapo watu wawili waliuawa na wengine kujeruhiwa.

Lissu pia amemuuliza Heche kuhusu tukio jingine la mauaji katika jimbo lake.

Heche amesema polisi walimuua mdogo wake, Suguta Heche, ambaye alidai alikuwa amefungwa pingu mikono yote na kuchomwa kisu.

Alipoulizwa kuhusu hatua zilizochukuliwa, Heche amesema Kamanda wa Polisi wa wakati huo alitoa taarifa kuthibitisha kuwa Suguta aliuawa na polisi na kwamba hatua zingechukuliwa dhidi ya waliohusika.

Hata hivyo, amesema polisi huyo aliachiwa na mpaka sasa ni mtumishi wa Jeshi la Polisi.

Ushahidi huo umetolewa wakati Heche akiendelea kujibu maswali ya Lissu katika hatua ya utetezi wa kesi hiyo.

Shauri hilo limeahirishwa hadi kesho, ambapo Heche ataendelea kutoa ushahidi wake, huku Majaji wakitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu mashahidi wengine waliowekewa pingamizi.


Top News