Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Agosti 30, 2026, amewasili Mpanda mkoani Katavi kuwa Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 25 ya Jimbo Katoliki la Mpanda.

Maadhimisho hayo yanafanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari St. Mary, Mpanda, mkoani Katavi.







Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius John Ndejembi, pamoja na familia yake, wameungana na waumini mbalimbali kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya Jumapili, katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Paulo wa Msalaba, Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, leo Jumapili, Agosti 30, 2026.




Na Mwandishi Wetu

MKAZI wa mtaa wa Unyasini katika Kata ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam Yahaya Kizenga amemuomba Rais DK.Samia Suluhu Hassan kupitia kwa Mkuu wa mkoa huo Albart Chalamila kuwasaidia kupata haki ya eneo la aridhi ambalo kuna watu wamevamia wakitaka kuwadhulumu.

Kwa mujibu Kizenga amesema amekuwa katika eneo hiki tangu mwaka 1976 ambalo alipewa na Nyerere wakati wa operesheni ya Nguvu Kazi na anayo hati ya Kijiji lakini cha kushangaza kuna watu wamejitokeza na kudai eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kizinga ambaye ni askari mstaafu wa Jeshi la Polisi amesema alipata eneo wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza na amekuwa akiishi katika eneo hilo tangu mwaka huo wa 1976.

“Nimekuwa nikiishi hapa tangu mwaka 1976 na ninamiliki eneo hili nikiwa na hati ya Kijiji niliyopewa wakati huo. Mbali na kuwa na nyumba yangu lakini nimekuwa nimekuwa nikiliendeleza kwa shughuli za kilimo cha mbogamboga “

Akieleza zaidi kuhusu eneo hilo amesema cha ajabu alitokea mtu aliyekuwa anajulikana kwa jina la Juliana Lyimo ambaye alikuwa anamiliki kampuni ya Oliver beach Resorts akidai hili eneo ni lake.

“Baada ya kujitokeza kwa mtu yule mimi pamoja na majirani wenzangu wanne tuliamua kwenda Serikali ya Mtaa Kawe lakini hatukupata suluhu hivyo tukaenda Mahakamani na tunashukuru Mungu baada ya kuwasilisha vielelezo vyetu tulishinda kesi mwaka 2015.

“Baada ya kushinda kesi mahakamani tulikwenda kukazia hukumu lakini pia ilibidi na twende Wizara ya Aridhi kwasababu miaka ambayo nimekaa tangu tushinde kesi mwaka 2015 tulikaa mpaka 2021 na kila siku tukiuliza tunaambiwa kuna rufaa.

“Lakini nilishutuka kwanini kuna rufaa miaka yote,hivyo nikaamua kwenda Wizara ya Aridhi tena kuangalia na kukuta yule mmiliki ambaye tulimshinda mahakamani ndio amemilikishwa ,hiyo ilikuwa mwaka 2021.Na sasa tumeona watu wamekuja na kuanza kumwaga kifusi katika eneo hili lenye ukubwa wa heka moja na nusu.”

Kizenga amesema kutokana na umri wa utu uzima amekuwa akikabiliwa na maradhi yeye pamoja na mkewe na kutokana na uchumi duni umesababisha wajanja wachache wanataka kuwadhulumu eneo lao na kwamba wanaamini anayeweza kuwasaidia kupata haki yao ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ambaye tumeshuhudia akitenda haki hasa kwa wake wasiokuwa na uwezo.

“Tunamuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ,Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pamoja na Mamlaka zinazohusika na utatuzi wa migogoro ya aridhi watusidie kupata haki yetu,hapa ni kwetu na tuko kihalali lakini leo hii wanakuja watu wanataka kutuondoa sasa wanataka twende wapi?

“Mkuu wa Mkoa tunakuomba utusaidie tupate haki yetu, sisi ni wazee tusio na kitu tunadhulumiwa.Ombi langu kwa mamlaka na viongozi wote watusikie kilio chetu.Wanaotaka eneo langu ni watu ambao wanafanya kila aina ya hila na mbinu na wapo tayari kufanya lolote kudhulumu”

Kwa upande wake Mariam Kizenga ambaye ni mke wa Mzee Kizenga amemuomba Rais DK.Samia Suluhu Hassan kupitia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwasaidia ili eneo lao lisichukuliwe na watu ambao wameonekana wanafanya ujanja ili kuwadhulumu.

“Tunamuomba Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na viongozi wengine watusaidie kuna mtu amekuja hapa na kuanza kuweka kifusi cha mchanga,anataka kutudhulumu.Tuko hapa kwa miaka 50 tukidhulumiwa tunakwenda wapi? Na sisi hatuna uwezo wa kujenga na makazi yetu yako hapa kwa muda wote .Tunaomba Serikali itusaidie.”






Benki ya NMB imewataka wafanyabiashara wa Mwanza, Mara na Geita kutumia malipo ya kidijitali na akaunti mahsusi za biashara ili kufikia masoko mapya na kusimamia fedha zao kwa usahihi.

Akizungumza katika jukwaa la NMB Business Executive Network jijini Mwanza, Mkuu wa Idara ya Biashara wa NMB, Deogratius Shirima, alisema mabadiliko ya teknolojia na mahitaji ya wateja yanawalazimu wafanyabiashara kubadili namna wanavyopokea malipo na kuendesha shughuli zao.

Shirima alisema suluhisho za malipo ya mtandaoni za NMB pamoja na NMB SME World Business Credit Card zinalenga kurahisisha miamala ya ndani na nje ya nchi. Pia alisema NMB imeboresha huduma za Bank Guarantee, ambapo dhamana za zabuni zisizohitaji dhamana ya mali (Unsecured Bid Bonds) zinaweza kufikia hadi dola milioni 10 za Marekani bila kuweka dhamana ya mali.

Kwa upande wake Leah Mwakang’ata, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Biashara kwa Wateja Wadogo na wa Kati (SME) wa NMB, aliwahimiza wafanyabiashara kutenganisha fedha binafsi na fedha za biashara kupitia akaunti rasmi. Alisema hatua hiyo inawasaidia wafanyabiashara kufuatilia mapato na matumizi kwa usahihi, kujenga historia nzuri ya kifedha na kupata huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji ya biashara zao.

Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza, Gabriel Mugini, alisema mazingira ya biashara mkoani humo yanaendelea kuvutia wawekezaji. Aliwataka wafanyabiashara kutumia fursa za kifedha na kiteknolojia zinazopatikana ili kupanua shughuli zao.


MASHABIKI wa michezo ya kasino, huu ni wakati wa kuongeza msisimko na kujaribu bahati yako kwa namna ya kipekee. Meridianbet imekuja na Mystery Multiplier Drop, inayokupa nafasi ya kukutana na zawadi za vizidishi vya kushtukiza unapocheza michezo yote ya Wazdan. Kila dau linalokidhi vigezo vya kampeni linaweza kukufungulia nafasi ya kupata vizidishi kwa bahati nasibu na kuongeza ushindi wako kwa kiwango ambacho huenda usikitarajie.

Kinachofanya kampeni hii iwe na ladha tofauti ni siri iliyopo kwenye kila kizidishi. Wachezaji wanaweza kupata mara 10, 20, 75, 150 au hadi 250. Ndiyo, umesoma vizuri, mara 250. Hii ina maana kuwa dau linalostahili linaweza kupata kizidishi kikubwa kulingana na zawadi itakayotokea kwa bahati nasibu. Kwa mashabiki wanaopenda msisimko wa kutokujua kitakachofuata, kila mchezo unaweza kuwa mwanzo wa tukio jipya.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Fikiria ukiwa umeingia kwenye mchezo wa Wazdan, kila kitu kikiwa tayari, halafu ghafla vizidishi vinatokea. Inaweza kuwa x10, ikapanda hadi x20, au bahati ikakuchagua kwa x75, x150 au x250. Huo ndiyo uzuri wa Mystery Multiplier Drop, huwezi kujua utakutana na kipi kabla haujacheza. Kampeni hii inaleta ladha kwenye kila dau linalokidhi vigezo, na kufanya michezo ya Wazdan kuwa na msisimko zaidi kwa wale wanaotafuta nafasi ya kushinda zawadi kubwa.

Kwa hiyo, kama unataka kuingia kwenye ulimwengu wa Mystery Multiplier Drop, hatua ya kwanza ni kujisajili na Meridianbet. Baada ya hapo, unaweza kuanza kucheza michezo ya kasino ya Wazdan inayoshiriki katika kampeni na kuipa bahati yako nafasi ya kuzungumza. Kumbuka, vizidishi vinajitokeza wakati wowote, hivyo kila dau linalostahili linaweza kuwa mwanzo wa ushindi wenye kusisimua.

Jisajili Meridianbet leo, chagua mchezo wako wa Wazdan, ingia kwenye burudani na uone ni kizidishi kipi utakachokutana nacho. Je, itakuwa x10, x75, x150 au utapata ile jackpot ya x250 ya dau lako? Uamuzi wa kujaribu bahati yako ni wako.




Na Mwandishi Wetu

KUNDI lingine la mamia ya wanafunzi wa Kitanzania wameondoka nchini Jumamosi kuelekea vyuo vikuu mbalimbali kuanza masomo ya elimu ya juu.

Wanafunzi hao walioondoka kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Terminal 3, jijini Dar es Salaam, wengi wao wamechagua programu zinazohusiana na sayansi, teknolojia na taaluma zinazohitajika katika dunia ya sasa, zikiwemo Computer Engineering, Cyber Security, Artificial Intelligence, Civil Engineering, programu mbalimbali za afya, sheria na biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Meneja wa Tawi la Dar es Salaam, Micky Musa, amesema kuondoka kwa wanafunzi hao ni sehemu ya mpango mpana wa kuwaunganisha vijana wa Tanzania na fursa za elimu ya kimataifa.

Alisema mbali na India, Global Education Link inaendelea kuwaandaa wanafunzi wengine wanaotarajiwa kuelekea nchini China, huku wengine wakiwa katika hatua mbalimbali za maandalizi ya kwenda kusoma Malaysia, Marekani na Uingereza.

“Kadiri muda unavyokwenda Watanzania wataendelea kuona makundi mengine ya wanafunzi yakiondoka. Tunawaomba vijana wenye ndoto ya kusoma nje ya nchi wafike katika ofisi zetu zilizopo Dar es Salaam, Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha. Muda bado upo. Njoo na matokeo yako, nasi Global Education Link tupo tayari kukusaidia kuifanya ndoto yako kuwa uhalisia,” amesema.

Musa pia amewataka wazazi na walezi wenye vijana wanaotamani kupata elimu nje ya nchi kutumia ofisi za Global Education Link kupata ushauri kuhusu uchaguzi wa vyuo, programu za masomo, udahili, visa na maandalizi ya safari.

Miongoni mwa wanafunzi walioondoka ni vijana wanaokwenda kusomea Computer Science Engineering, Artificial Intelligence na Cyber Security, wakisema wamechagua taaluma hizo kutokana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia na umuhimu wake katika maendeleo ya uchumi wa kisasa.



MSIMU mpya unazidi kunoga huku mechi mbalimbali za pesa zikiendelea, Odds kubwa na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Je nani unampa nafasi ya ushindi siku ya leo?. Ingia na ubeti sasa.

Meridianbet wanaanza kuiangazia ligi kuu ya Uingereza yaani EPL, ambapo Chelsea atakuwa mwenyeji wa Brighton ambao walishinda kwa kishindo kwenye mtanange wa kwanza wa ligi, hivyo hii ni mechi ambayo kila timu inahitaji kupata ushindi mnono siku ya leo.

Vijana wa Darajani chini ya kocha mkuu Xabi Alonso watakuwa na kibarua kizito cha kukusanya pointi 3 dhidi ya timu hiyo ambayo inaonekana ni ngumu kukabiliana nayo kwani msimu uliopita The Blues walipigika mechi zote mbili walizokutana kwenye ligi.

Meridianbet wanakwambia kuwa hii ni nafasi ya kupiga pesa kwa kumpatia ushindi Chelsea aweze kulipa kisasi akiwa nyumbani au umpatie Brighton ushindi kuendeleza ubabe dhidi ya timu hiyo. Bashiri hapa.

Piga pesa kupitia michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Lakini pia kule kule kwa wakali waubashiri wanasema kuwa kwa wale ambao hawajajisajili huu ndio wakati wake, usingoje kupitwa na mtanange huu wa moto pale Uingereza. Suka jamvi hapa.

Mechi nyingine ya baadae ya wewe kuondoka na maokoto ni hii ya Manchester United dhidi ya Ipswich Town ambao wamepanda daraja msimu huu kutoka kule ligi daraja la kwaznza wakiwa na matumaini ya kufanya vyema kwenye ligi kuu.

Ikumbukwe kuwa United chini ya Carrick wameanza msimu vibaya sana baada ya kupoteza kwa mabao 2 kwa bili ugenini, hivyo hii mechi yao ya kwanza wakiwa katika dimba la Old Trafford wanahitaji kupata ushindi wao wa kwanza.

Kwa upande wa Ipswich wao walianza vyema ligi kwa kuandikisha ushindi wakiwa nyumbani na sasa watakuwa ugenini kujaribu kupata matokeo chanya mbele ya Mashetani Wekundu. Odds Kubwa zipo mechi hii, hivyo bashiri sasa.

Uwepo wa kikosi kipana cha Man United kinawafanya wapewe nafasi kubwa ya kuondoka na ushindi huku pia faida ya kuwa nyumbani inapelekea wao kuwa wateule wa ushindi kwenye mchezo wa leo. Je wataweza kujinyakulia pointi 3 siku ya leo?. Tengeneza mkeka wako wa ushindi pale Meridianbet.

Kule Italia, SERIE A nayo kama kawaida kitawaka haswa kati ya Napoli dhidi ya Como 1907 ambao kwenye mechi yao kwanza walitoa sare hivyo huu ni mchezo ambao kwa namna moja au nyingine wanautolea macho sana.

Vijana wa Allegri wao waliondoka na pointi 3 wakiwa ugenini hivyo sasa watarejea pale katika dimba la Armando Maradona kusaka ushindi mwingine mbele ya mashabiki zao ambao wanaamini timu hiyo msimu huu inaweza ikagombea taji la Scudetto.

Takwimu zinaonesha kuwa mara ya mwisho kuonana hawa wawili, hakuna ambaye alikuwa mbabe kati yao na kwenye hizo mechi mbili hakuna ambaye aliweza kuona lango la mwenzake.

Hivyo basi hii mechi ambayo pointi 3 ni muhimu sana kwa wote wawili kwani kama unahitaji uwe kwenye mbio za ubingwa ni vyema ukaanza kupata matokeo mazuri kwenye mechi za mwanzo kabisa. Beti yako unaiweka kwa nani?. Jisajili hapa.
Wajawazito wanaopata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, watanufaika na vifaa vya kujifungulia pamoja na vifaa tiba vilivyotolewa na wafanyakazi wa Yas Tanzania katika jitihada za kumshika mkono akina mama wajawazito.

Msaada huo umetolewa kupitia Kampeni ya Tumaini, ambao ni mpango ulioanzishwa na wafanyakazi wa Yas, umeanza na hospitali hiyo huku ukitarajiwa kuendelea katika maeneo mengine mbalimbali nchini.

Kupitia kampeni hiyo, Yas imekabidhi vifaa vya kujifungulia, khanga, vitanda vya uchunguzi kwa wajawazito, mashuka, aproni na viti mwendo.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Yas Tanzania, Caroline Kavishe, alisema kampeni hiyo ni wazo la wafanyakazi wa Yas ambao wameamua kutumia nguvu yao ya pamoja kufanya jambo lenye manufaa kwa jamii.

“Tumaini ni kampeni inayoendeshwa na wafanyakazi wetu. Wamechagua kusimama pamoja na akina mama wajawazito kwa kutambua ugumu wa nyakati ambazo wanapitia katika kumleta mtoto duniani. Tunataka wafanyakazi wetu wajivunie si tu kwa kazi wanayofanya, bali pia mchango chanya wanaoweza kuuleta katika jamii,” alisema Kavishe.

Kavishe alisema kampeni hiyo pia inatambua mchango mkubwa wa madaktari, wauguzi na watoa huduma wengine wa afya ambao kila siku wanahudumia wajawazito, akina mama na watoto wachanga.

Kwa upande wake Meneja wa Mahusiano ya Nje - Yas Tanzania, Bi. Rukia Mtingwa, alisema wazo la kampeni hiyo limetokana na kutambua umuhimu wa kusimama pamoja na akina mama katika kipindi muhimu cha ujauzito na kujifungua.

“Kila mama anayekwenda hospitali kujifungua anakwenda na tumaini la kujifungua salama, kumbeba mtoto wake mikononi na kurudi naye nyumbani. Tukajiuliza, katika safari hii muhimu ya mama na mtoto, sisi tunaweza kufanya nini? Ndiyo maana tumeunganisha nguvu zetu na kuanza hapa Ubungo,” alisema Bi. Mtingwa.

Akizungumzia dhamira ya Yas kwa jamii, Mtingwa alisema kampuni inaangalia wajibu wake kwa upana zaidi ya kutoa huduma za mawasiliano na teknolojia.

“Tunaposema Mtandao wa Viwango, kwetu si suala la simu, intaneti na teknolojia pekee. Vilevile, ni suala la viwango vya namna tunavyowajibika kwa jamii. Tunataka popote Yas ilipo, jamii ihisi uwepo wetu kupitia mambo yanayogusa maisha yao,” alisema.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Ubungo, Dkt. Chrispin Kayola, alisema vifaa hivyo vitaongeza uwezo wa hospitali katika kuwahudumia wajawazito na akina mama wanaofika kujifungua.

“Tunapokea wajawazito karibia 150 kwa mwezi kipindi kama hiki cha low season na nusu kati yao huhitaji huduma za upasuaji, hivyo vifaa hivi vina umuhimu mkubwa sana kwa hospitali yetu. Vitasaidia kuwaongezea watoa huduma wetu nyenzo wanazohitaji kuwahudumia akina mama,” alisema Dkt. Kayola.

Kampeni ya Tumaini inatarajiwa kuendelea katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwapa wafanyakazi wa Yas nafasi ya kushiriki moja kwa moja katika kusaidia jamii, huku wajawazito na akina mama wakiwa miongoni mwa walengwa wa kampeni hiyo.
Afisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Yas Tanzania, Caroline Kavishe (kushoto), akikabidhi vifaa tiba kwa Mkuu wa Kitengo cha Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Ubungo, Dkt. Olivia Donald Shirima, ikiwa ni sehemu ya Kampeni ya Tumaini inayoendeshwa na wafanyakazi wa Yas kwa lengo la kusaidia wajawazito na akina mama. Makabidhiano hayo yalifanyika hivi karibuni katika hospitali hiyo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Ubungo, Dkt. Chrispin Kayola.










*Kambi maalum inaanza Jumatatu hadi Septemba 11

Na Mwandishi Wetu
HOSPITALI ya Shifaa Pan African ya Kinondoni jijini Dar es Salaam imeandaa kambi maalum kufanya upasuaji wa kupunguza uzito kwa kutumia matundu madogo kuanzia Agosti 31 mpaka Septemba 11.

 Daktari bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo, Kassim Bahsan alisema jana kuwa kambi hiyo itafanyika katika hospitali hiyo kuanzia Agosti 31 mwezi huu hadi Septemba 11.

Alisema katika kambi hiyo wananchi watapata fursa ya kufanyiwa tathmini ya mwili na kupata ushauri wa kitaalamu wa upasuaji wa kupunguza uzito kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya matundu madogo.

“Kama umekuwa ukipambana na unene kupita kiasi na unatafuta njia salama na yenye ufanisi ya kuboresha afya yako hii ni fursa muhimu ya kuchukua hatua kuelekea maisha yenye afya bora,” alisema Dk Bahsan

Alisema tarehe 4 mwezi Septemba hospitali ya Shifaa itaendesha mdahalo wa elimu kwa umma ambapo wananchi wote wanalikwa kushiriki kupata uelewa wa upasuaji wa kupunguza uzito.


“Ni semina ya elimu ya kupunguza uzito, watafahamu ni kwanini na nani ni mnufaika wa upasuaji huu watu watajifunza na watasikia ushuhuda kwa watu waliofanyiwa upasuaji na kupungua uzito, wengine wameacha dozi za kisukari, maumivu ya nyonga yameisha,” alisema

Naye Mkuu wa Idara ya Upasuaji hospitalini hapo, Dk Murad Tarmohamed alisema hiyo ni fursa kwa watu wenye matatizo ya uzito uliopitiliza kwani wanaweza kurejea kwenye maisha yao ya kawaida baada ya upasuaji.

“Wananchi waitumie hii fursa kukutana na madaktari bingwa wabobezi kwenye upasuaji ambao watawashauri hatua za kuchukua kabla ya upasuaji ili wafanyiwe matibabu yatakayowarejesha kwenye maisha ya kawaida,” alisema

“Uzuri ni kwamba upasuaji huu unafanywa kwa njia ya matundu madogo ambao unamwezesha mtu aliyefanyiwa matibabu kupona haraka na kuendelea na shughuli zake za kila siku,” alisema

Aidha, alisema kuna ushuhuda wa baadhi ya watu waliofanyiwa upasuaji kwenye hospitali hiyo wakiwa na uzito wa hadi kilo 148 na kufanikiwa kurudi kwenye kilo 98 ambao kwa sasa wanaishi maisha bora wakiwa wameondokana na uzito uliopitiliza.

Hospitali hiyo imeshawafanyia upasuaji wa kupunguza uzito ambao umekuwa wa wenye mafanikio kwa kutumia tundu dogo watu 20 waliokuwa na uzito mkubwa.

Daktari bingwa wa upasuaji wa hospitali hiyo, Murad Tarmohamed, alisema hospitali hiyo imeweka wataalamu bobezi kwa ajili ya taaluma hiyo.

“Watu wengi wanadhani kuwa upasuaji huu ni kwaajili ya urembo hapana, unafaida nyingi sana kama kuepuka magonjwa ya sukari na wakishafanyiwa wakapona kabisa, kuna watu wanakosa pumzi sababu ya uzito mkubwa wakifanyiwa wanapona,” alisema

Alisema kuna watu ambao wanapata shida ya magoti na nyonga sababu ya maumivu wanayopata wanapotembea lakini wakifanyiwa upasuaji wanapona.

Alisema magonjwa kama ya moyo yanayotokana na uzito kuwa mkubwa yamekuwa yakiondoka kwa watu wanaofanyiwa huduma hiyo.

“Mtu anapofanyiwa upasuaji huu anakuwa na nguvu zaidi anarudi kwenye maisha ya kawaida, anaacha kuchoka mara kwa mara anakuwa anafanya shughuli zake kama zamani, tunasisitiza ni muhimu sana si kwa muonekano bali kwa ajili ya afya ya mhusika,” alisema

“Umuhimu wa upasuaji kama huu ni shida ambazo unaondokana nazo baaada ya upasuaji kama moyo, sukari, presha sukari, maumivu ya nyonga, magoti  na kukosa pumzi ukiwa umelala,” alisema hiyo ni kambi ya tatu kufanya hospitali ya Shifaa

“Faida ya upasuaji huu ni kwamba mgonjwa hakai sana hospitalini, akifanyiwa leo kesho anatoka anakwenda nyumbani kuendelea na maisha yake kama kawaida,” alisema

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Ndugu Wazo Michael Mwang’onda, leo tarehe 28 Agosti 2026 ametembelea na kuzungumza na wafanyabiashara katika Hoteli ya KER iliyopo Mtaa wa Butambala, Kata ya Igulwa Wilaya ya Bukombe.

Ziara hiyo ni sehemu ya Programu ya Nishati Safi na Salama ya Kupikia inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Lengo ni kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika hoteli na migahawa.

Akizungumza na wamiliki na wafanyakazi wa Hoteli ya KER, Mwang’onda amesema Serikali ina dhamira ya kuwawezesha wafanyabiashara wa vyakula kutumia nishati safi ili kupunguza gharama za uendeshaji na kuboresha mazingira ya kazi.

Amesema matumizi ya nishati safi kama gesi ni ya ufanisi zaidi, yanaokoa muda na yana afya kuliko kutumia kuni na mkaa. Hii inawasaidia mama lishe na baba lishe kuongeza kipato chao kwa sababu gharama zinapungua na huduma inakuwa ya haraka.

Mwang’onda pia amesisitiza umuhimu wa kulinda mazingira. Amesema kupunguza matumizi ya kuni na mkaa kutaokoa misitu na kusaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.

Ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe kwa kuwekeza katika kuhamasisha wananchi kuhamia nishati safi kupitia mapato yake ya ndani. Amesema hatua hiyo inaonyesha nia ya dhati ya Serikali ya Mitaa kuleta maendeleo.

Wafanyabiashara wa Hoteli ya KER wamemshukuru Kiongozi wa Mwenge kwa ziara hiyo na wameahidi kuzingatia matumizi ya nishati safi katika shughuli zao za kila siku. Wamesema wamepata elimu ya namna ya kupika kwa usalama na kwa haraka.

Mwishoni Mwang’onda amewataka wafanyabiashara wengine wilayani Bukombe kuiga mfano wa Hoteli ya KER na kuanza kutumia nishati safi. Amesema kwa kufanya hivyo Tanzania itakuwa imepiga hatua kubwa katika kuhifadhi mazingira na kuboresha afya ya wananchi.








 WANANCHI waliotembelea banda la Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) katika Maonesho ya Utamaduni, wameeleza kufurahishwa na elimu wanayoipata kuhusu majukumu ya Wakala katika kuratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Wananchi hao wamesema maonesho hayo yamekuwa fursa muhimu kwao kupata uelewa kuhusu Mfumo wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement System – BPS), namna mafuta yanavyoagizwa nchini na nafasi ya PBPA katika kuratibu mchakato huo.

Bi. Maria Ngilisho, mmoja wa waliotembelea banda hilo, alisema elimu hiyo imemsaidia kuelewa mchakato wa upatikanaji wa mafuta nchini, ambao awali hakuwa na ufahamu wa kutosha kuuhusu.

“Nimefurahi kupata elimu hii kwa sababu tumekuwa tukitumia mafuta kila siku, lakini hatukuwa tunafahamu mchakato unaofanyika hadi mafuta yanapofika nchini. Sasa nimeelewa kuwa kuna taasisi kama PBPA inayoratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja,” alisema Ngilisho.

Naye, Bw. Michael Maganga, alisema mawasiliano ya ana kwa ana na watumishi wa PBPA yamewapa wananchi nafasi ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa moja kwa moja kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mafuta.

“Elimu tunayopata hapa ni muhimu sana kwa sababu tunapata nafasi ya kuuliza maswali yanayotuhusu kama watumiaji wa mafuta na tunapata majibu kutoka kwa wataalamu. Ni vizuri PBPA kuendelea kutumia maonesho haya kuwafikia wananchi,” alisema Maganga.

Kwa mujibu wa PBPA, miongoni mwa majukumu ya Wakala ni kukusanya mahitaji ya mafuta kutoka kwa kampuni za uuzaji wa mafuta, kuendesha zabuni za kimataifa za ununuzi wa mafuta kwa wingi, pamoja na kuratibu upokeaji na uwasilishaji wa bidhaa hizo nchini. Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha

Ushiriki wa PBPA katika maonesho mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Wakala za kuwaelimisha wananchi kuhusu majukumu yake na nafasi yake katika sekta ya mafuta, huku ukitoa fursa kwa wananchi kupata ufafanuzi kuhusu mchakato wa uagizaji wa mafuta na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa hizo unaendelea kuwa wa uhakika nchini.
Naibu Spika wa Bunge, Daniel Baran Sillo, amesema Bunge lipo tayari kushirikiana na Serikali katika maandalizi ya AFCON PAMOJA 2027. Alitoa kauli hiyo wakati wa Bonanza la Bunge na NMB jijini Dodoma, lililoandaliwa na NMB Bank kwa kushirikiana na Bunge.

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema benki hiyo imeandaa bonanza hilo kwa sababu michezo ina mchango katika afya na tija ya viongozi na watumishi. “Tunataka michezo iwe sehemu ya utamaduni wa kazi na huduma kwa wananchi,” alisema.

Mwenyekiti wa Bonanza la Bunge na Mbunge wa Makete, Festo Sanga, alisema tukio hilo limewakutanisha wabunge, wizara na taasisi mbalimbali, huku likitumika kuhamasisha mazoezi na mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Machano Ali Machano, alisema mashindano ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yatakayofanyika Arusha Desemba 2026 yatakuwa hatua nyingine ya kuimarisha michezo na ushirikiano wa kikanda.





















Top News