Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kulia), Mkuu wa Idara ya Biashara NMB, Deogratias Shirima (kushoto) wakifurahia tuzo za Benki Bora ya Huduma kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), zilizotolewa na Euromoney na Global Finance wakati wa hafla iliyowakutanisha NMB na Mtandao wa Wafanyabiashara Wakubwa Wanaohudumiwa na benki hiyo ‘NMB Business Executive Network’ iliyofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TTI, Leonard Shayo na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya High Quality, Selina Letara.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kulia), Mkuu wa Idara ya Biashara NMB, Deogratias Shirima (kushoto) wakifurahia tuzo za Benki Bora ya Huduma kwa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), zilizotolewa na Euromoney na Global Finance wakati wa hafla iliyowakutanisha NMB na Mtandao wa Wafanyabiashara Wakubwa Wanaohudumiwa na benki hiyo ‘NMB Business Executive Network’ iliyofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TTI, Leonard Shayo na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya High Quality, Selina Letara.WADAU wa mchezo wa uogeleaji Tanzania wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kiwango cha kimataifa kupitia programu ya wiki tatu iliyolenga kukuza vipaji vya waogeleaji vijana, kuimarisha uwezo wa makocha wa wazawa, pamoja na kuwaelimisha wazazi kuhusu namna bora ya kuwaunga mkono wanamichezo katika safari yao ya mafanikio.
Programu hiyo iliyopewa jina la Tanzania Performance Development Series 2026, imeandaliwa na RaceBetter kwa ushirikiano na Monti AquaForce, na itafanyika kuanzia Julai 28 hadi Agosti 14 katika Kampasi ya Mikocheni ya Shule ya Kimataifa ya Monti, jijini Dar es Salaam.
Mafunzo hayo yataongozwa na kocha mashuhuri wa kimataifa wa uogeleaji na mwanzilishi wa RaceBetter, Ben Lee, ambaye anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam Jumatatu kutokea nchini Marekani.
Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Shule ya Kimataifa ya Monti, Fatma Fernandes, alisema mpango huo unaashiria mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu unaolenga kuimarisha maendeleo ya mchezo wa uogeleaji nchini Tanzania kwa kuunganisha utaalamu wa kimataifa na uongozi wa ndani ili kujenga mfumo endelevu wa kukuza vipaji kuanzia ngazi ya msingi hadi ushindani wa kiwango cha juu.
Mfululizo wa mafunzo hayo utaanza kwa Warsha ya Maendeleo ya Makocha itakayofanyika Julai 28 hadi 30, ikiwakutanisha makocha wa uogeleaji, walimu na viongozi wa vilabu vya uogeleaji. Warsha hiyo inalenga kuboresha viwango vya ufundishaji huku ikiwapa makocha wa ndani fursa ya kujifunza na kufanya kazi bega kwa bega na Ben Lee katika kipindi chote cha kambi za mafunzo kwa wanamichezo.
Fatma alisema pia kutakuwa na kambi tatu za mafunzo kulingana na makundi ya umri wa washiri.
“Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 6 hadi 8, itafanyika kuanzia Julai 30 hadi Agosti 1. Itafuatiwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 9 hadi 12 kuanzia Agosti 3 hadi 7. Programu hiyo itahitimishwa na Kambi kwa waogeleaji wenye umri wa miaka 13 na kuendelea, itakayofanyika kuanzia Agosti 10 hadi 14.
“Aidha, kutakuwa na mfululizo wa mafunzo kwa wazazi, yatakayotolewa bila malipo sambamba na kambi hizo. Vipindi hivyo vitajikita katika lishe na urejeshaji wa nguvu kwa wanamichezo, kujenga kujiamini na ustahimilivu, pamoja na kuwasaidia wazazi kujenga utaratibu mzuri wa maisha unaowawezesha watoto wao kufanikiwa ndani na nje ya bwawa la kuogelea,” alisema.
Alisema programu hiyo itafanyika katika bwawa la kuogelea la mita 25 la Shule ya Kimataifa ya Monti, lenye viwango vya kimataifa kwa mashindano ya kozi fupi, na hivyo kuwapatia washiriki mazingira bora ya mafunzo.
Aliongeza kuwa idadi ya washiriki imewekewa ukomo ili kuhakikisha kila mshiriki anapata mafunzo ya karibu katika vikundi vidogo na ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa wakufunzi.
Akizungumza kuhusu programu hiyo, Ben Lee, ambaye ana uzoefu mkubwa wa kufundisha waogeleaji kuanzia ngazi ya maendeleo, vyuo vikuu hadi Olimpiki, alisema lengo kuu si kuwajengea waogeleaji kasi pekee, bali kuwajenga kama watu.
“Lengo letu si kuzalisha waogeleaji wenye kasi zaidi pekee. Tunataka kuwasaidia watu kuwa na uwezo zaidi, kujiamini zaidi na kuwa tayari kwa fursa na changamoto zitakazokuja mbele yao,” alisema.
Katika kipindi chake cha ukocha, Ben Lee amewafundisha wanamichezo wengi waliofanikiwa kujiunga na programu maarufu za NCAA nchini Marekani na kushiriki mashindano ya kimataifa. Pia amefanya kazi na vilabu vya uogeleaji, shule na mashirikisho ya kitaifa katika nchi mbalimbali duniani.
Na Victor Masangu, Kibaha
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Taifa Ndg. Fadhili Maganya amewaasa viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) ngazi za Wilaya pamoja na Mkoa wa Pwani kuhakikisha kwamba wanalivalia njuga suala la kero ya migogogoro ya ardhi sambamba na kusikiliza changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukijenga chama pamoja na kukagua uhai wake na kuimarisha jumuiya zake sambamba na kuangalia mwenendo mzima wa utekelezaji wa ilani ikiwemo kukagua na kutembelea baadhi ya miradi mbali mbali ya maendeleo.
Mwenyekiti huyo amebainisha kuwa katika ziara hiyo pia imelenga kukutana na viongozi mbali mbali wa serikali na kupokea taarifa zao zinazohusiana na suala zima la utekelezaji wa kazi zao ambazo wanazifanya katika maeneo yao kwenye nyanja mbali mbali za kimaendeleo.
"Nimeanza ziara yangu ya kikazi katika Wilaya ya Kibaha na lengo kubwa na kwamba ziara hii ni ya kikazi na lengo lake kubwa ni kuangalia uhai wa chama jinsi ilivyo, pamoja na jumuiya zake ikiwa sambamba na kuweza kuangalia na kutembelea miradi mbali mbali ya kimaendeleo na kuzungumza na wanachama," amebainisha Mwenyekiti huyo.
Pia Mwenyekiti huyo amewasihi wanachama na viongozi kuhakikisha kwamba wanaachana kabisa na tabia ya kuwasikiliza baadhi ya wanaharakati ambao wamekuwa wakibeza mambo mbali mbali ambayo yanatekelzwa na serikali ya awamu ya sita na badala yake wajikite zaidi katika kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambazo anazifanya.
Pia amewahimiza madiwani na viongozi wengine kuhakikisha wanaweka misingi imara ya kusimamia utoaji wa fursa za mikopo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na halmashauri kwa lengo la kuwasaidia wajasiriamali waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini .
Aidha Mwenyekiti huyo hakusita kumpongeza kwa dhati Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuchapa kazi kwa bidii pamoja na kuendelea kutekeleza ilani kwa vitendo katika suala zima la kusimamia fedha ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauru ya Manispaa ya Kibaha Dkt. Rogers Shemwelekwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge akitoa salama zake amesema kwamba Mkoa wa Pwani imeweza kuendelea kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu, afya, umeme, miundombinu ya barabara pamoja na ujenzi wa viwanda.
Naye Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Hamoud Jumaa amesema kwamba lengo lake kubwa ni kuendelea kushirikiana bega kwa bega katika kuhakikisha chama cha serikali kinaendelea kuwa na mahusiano mazuri ikiwemo sambamba na kutekeleza ilani ya chama.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amebainisha kuwa ni jukumu la wanachama kuendelea na kuweza kushikamana katika kukijenga chama ikiwa sambamba na kuiimarisha zaidi kwa vitendo jumuiya zake zote.
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka amempongeza kwa dhati Mwenyekiti huyo kwa kuamua kufanya ziara ambayo itaweza kuleta uhai wa chama pamoja na kuimarisha jumuiya zake ikiwa pamoja na kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo.
Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amempongeza Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Taifa kwa kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuweza kuona umuhimu wa kufanya ziara yake ya kikazi ambayo itaweza kuleta matokeo chanya katika suala zima la kukiimarisha chama pamoja na jumuiya zake kwa pamoja.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ameanza ziara yake rasmi ya kikazi katika Mkoa wa Pwani ambapo ameanza katika Wilaya ya Kibaha ambapo ameweza kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo katika Zahanati ya Kilimahewa iliyopo kata ya Tangini, Kituo cha afya mlandizi pamoja na kutembelea mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi Mlandizi.

Mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe. Joachim Thobias Nyingo amekabidhi gari jipya aina ya ‘Toyota Pickup’ kwa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa wilaya hiyo Mha. Hopeness Liundi huku akitoa wito wa kutumia vizuri kitendea kazi hicho kwa kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa tija ili kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwafikishia huduma ya Majisafi ya bomba wananchi wa wilaya hiyo.
Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Meneja RUWASA Mkoa wa Dodoma Julai 27, 2026 na kuhudhuriwa na Meneja wa Mkoa huo Mha. Beatrice Kasimbazi pamoja na watumishi wengine wa mkoa huo.
Akizungumza kabla ya kuzindua na kukabidhi gari hilo, Mhe. Nyingo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiwezesha RUWASA na kuboresha utendaji wao wa kazi ikionesha dhamira ya dhati ya serikali kuwafikishia wananchi huduma muhimu ya majisafi ya bomba.
Hivi karibuni, Serikali kupitia RUWASA ilinunua na kugawa magari 22 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha utendaji wa taasisi katika kusimamia na kufuatilia miradi na huduma ya maji katika maeneo ya vijijini.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa wilaya Nyingo amemkaribisha Meneja mpya wa RUWASA wa mkoa wa Dodoma Beatrice Kasimbazi ambaye amehamishiwa mkoani humo akitokea mkoa wa Pwani, huku akitoa wito kwa watumishi wa wilaya hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya serikali na kuwahudumia wananchi.









Na Mwandishi wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaapisha Naibu Makatibu Wakuu wawili na kushuhudia viongozi wanne wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, ushirikiano, uwajibikaji na kuzingatia maslahi ya wananchi.
Akizungumza katika hafla iliyofanyika Ikulu, Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema uteuzi wa viongozi hao unaonesha imani ambayo Serikali imewawekea, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora, kufanya kazi kwa weledi na kuleta matokeo yanayogusa maisha ya Watanzania.
Rais Samia ameielekeza Ofisi ya Makamu wa Rais kuendelea kuimarisha usimamizi wa masuala ya Muungano kwa kushughulikia changamoto zinazojitokeza kupitia ushirikiano, ili kuendelea kuulinda na kuuimarisha Muungano wa Tanzania. Pia amesisitiza umuhimu wa kusimamia kwa karibu programu za uhifadhi wa mazingira na hatua za kukabiliana na changamoto zinazotishia ustawi wa Taifa.
Aidha, ameagiza Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuendelea kuboresha usimamizi wa watumishi wa umma kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuongeza ubora wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Katika sekta ya uchukuzi, Rais Samia amesisitiza kuongezwa kasi ya utekelezaji wa miradi ya reli, barabara, bandari na meli, pamoja na kutathmini fursa za kupanua biashara ya anga ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ili kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi.
Kwa upande wa sekta ya sheria, ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuendelea kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi kupitia kampeni za msaada wa kisheria, ili huduma hizo ziweze kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati.
Vilevile, Rais Samia ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuongeza juhudi katika kukuza biashara na kuboresha usimamizi wa maonesho ya biashara nchini. Pia ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuimarisha ulinzi na usimamizi wa hifadhi za taifa na rasilimali za utalii, akieleza kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.
Kwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha nafasi yake kama chombo cha Serikali na sauti ya Taifa kwa kuongeza ubora wa maudhui, weledi wa watumishi na ufanisi katika utoaji wa huduma za habari.
Walioapishwa ni Dkt. Latifa Mohammed Khamis, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano, pamoja na Bi. Prisca Burton Lwangili, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Viongozi wengine walioapa Kiapo cha Uadilifu ni Bw. Ephraim Balozi Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE; Bw. Salum Nassor Mnuna, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA; Bw. Massana Gibril Mwishawa, Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA; na Bi. Asha Dachi Mbaruk, Mkurugenzi Mkuu wa TBC.
Na Janeth Raphael - MichuziTv
Serikali imepanga kuwaweka kambini wanafunzi 1,050 waliofanya vizuri zaidi katika Mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2026 na kuchaguliwa kunufaika na mpango wa Samia Scholarship, ambapo watapatiwa mafunzo maalumu ya kuwaandaa kabla ya kuanza masomo yao ya elimu ya juu.
Kambi hiyo itafanyika katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela African Institution of Science and Technology (NM-AIST) jijini Arusha, ambako wanafunzi hao watapata mafunzo mbalimbali yatakayowajengea uwezo wa kitaaluma, uongozi na ubunifu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema mpango huo unatekelezwa kwa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ukiwa na lengo la kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) ili kuzalisha wataalamu watakaochochea maendeleo ya taifa na uchumi wa kisasa.
Profesa Mkenda amesema kati ya wanafunzi hao, 1,000 watapatiwa ufadhili wa kusoma katika vyuo vikuu vya ndani ya nchi, huku wanafunzi 50 bora zaidi wakipewa fursa ya kuendelea na masomo katika vyuo vikuu vya nje ya nchi kwenye fani zinazohitajika katika uchumi wa kidijitali.
Ameeleza kuwa wanafunzi hao wametokana na tahasusi za PCM (Physics, Chemistry and Mathematics), PCB (Physics, Chemistry and Biology), CBG (Chemistry, Biology and Geography), PMG (Physics, Mathematics and Geography), CBA (Chemistry, Biology and Agriculture) pamoja na PMC (Physics, Mathematics and Computer Science).
Kwa mujibu wa Waziri huyo, wanufaika wa ufadhili wa ndani wanapaswa kuomba udahili katika vyuo vikuu vya Tanzania kusomea shahada za Hisabati, Sayansi, Uhandisi au Tiba. Baada ya kupata udahili, watajaza fomu za kujiunga rasmi na mpango wa Samia Scholarship, ambapo Serikali itagharamia asilimia 100 ya ada na gharama za masomo yao.
Aidha, amesema majina ya wanafunzi wote waliochaguliwa yamechapishwa kwenye tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, na kuwataka wahitimu wa Kidato cha Sita kuyakagua pamoja na kufuata taratibu zote zilizowekwa ili kukamilisha mchakato wa kupata ufadhili huo.
Akizungumzia wanafunzi 50 watakaopelekwa kusoma nje ya nchi, Profesa Mkenda amesema wameteuliwa kutoka katika tahasusi za PCM, PMG na PMC, ambazo zinahitaji uwezo mkubwa wa Hisabati ya Juu (Advanced Mathematics).
Amefafanua kuwa uteuzi huo umezingatia alama halisi za mtihani (raw scores) badala ya daraja la ufaulu pekee, akibainisha kuwa wanafunzi wengi wanaweza kupata daraja la "A", lakini wakatofautiana kwa idadi ya alama walizopata.
Profesa Mkenda amesisitiza kuwa Serikali imezingatia uwazi na uadilifu katika mchakato mzima wa uteuzi ili kulinda hadhi ya mpango wa Samia Scholarship.
Amesema mwanafunzi yeyote mwenye mashaka kuhusu kutokuwamo kwenye orodha anaweza kuwasiliana na Wizara ya Elimu kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa alama zake kupitia Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA).
Kwa upande mwingine, Waziri huyo amebainisha kuwa asilimia 58 ya wanafunzi waliochaguliwa wanatoka katika shule za serikali, huku asilimia 42 wakitoka katika shule zisizo za serikali, akisisitiza kuwa uteuzi umefanyika kwa kuzingatia vigezo vya ufaulu bila kujali aina ya shule aliyosoma mwanafunzi.
Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro Abdul-Razaq Badru ameuambia mkutano wa 48 wa kamati ya Urithi wa Dunia kuwa Ngorongoro ni sehemu pekee ambayo binadamu duniani kote wanaweza kupata ushahidi sahihi wa chimbuko la asili ya binadamu.
Akizungumza mjini Busan,Jamhuri ya Korea wakati akiongoza Mkutano wa pembeni (Side event) ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kupata uelewa wa pamoja kuhusu hali ya uhifadhi wa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni eneo la Urithi wa Dunia, Badru amesema Ngorongoro ina ushahidi uliohifadhiwa wa nyayo za binadamu na masalia ya kale katika eneo la Laetoli na Olduvai zinazothibitisha suala hilo.
“Ngorongoro si tu eneo la utalii bali pia ni mahali ambapo historia ya binadamu wote kisayansi ilianzia”, alisema kamishna Badru.
Katika kikao hicho ameeleza kuwa kila nyayo iliyohifadhiwa ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inawakumbusha kurudi nyumbani kuona historia hiyo.
Badru amefafanua kuwa Ngorongoro ni sehemu ambayo binadamu alianzia kutumia zana mbalimbali za mawe kama teknolojia ya awali ya shughuli za kibinadamu na ndipo alipoanza kufanya harakati za kimaisha.
Mkutano wa kamati ya Urithi wa Dunia una lengo la kufanya maamuzi kuhusu maeneo mapya yanayopendekezwa kuingizwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia na kuimarisha juhudi za pamoja za kulinda, kuhifadhi, na kusimamia kwa uendelevu maeneo yenye thamani kubwa ya kiutamaduni na asili duniani.
■ Waziri Mavunde ataka mnyororo wote wa utoroshaji wa madini hayo udhibitiwe,
■ Asikitishwa na upotevu wa mapato ya Serikali yatokanayo na vitendo hivyo,
■ Aelekeza wahusika wote wafutiwe leseni na kutoruhusiwa tena kufanya biashara ya madini,
■ Atoa rai kwa wananchi kufanya biashara ya madini kupitia mfumo rasmi
📍Dar es Salaam,
Kufuatia kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini unaofanywa na Wizara ya Madini kupitia Kikosi Kazi (Taskforce), madini aina ya dhahabu Gramu 4,402.20 yenye thamani ya 1,238,458,594.42 yamekatwa yakitoroshwa.
Hayo yamesemwa leo tarehe 27 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb) Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari.
"Serikali kupitia Wizara ya Madini iliunda Kikosi kazi ambacho kinahusisha vyombo vya dola ili kudhibiti biashara haramu ya madini na utoroshaji. Hii ni sehemu tu ya kazi ambazo zimeendelea kufanywa na Kikosi kazi hicho katika kuimarisha mfumo wa ufanyaji biashara ya madini"
"Ndugu zangu, dhahabu hii yenye zaidi ya thamani ya bilioni 1.2 haikupitia katika mfumo rasmi wa ufanyaji biashara ya madini na hivyo kupelekea Serikali kukosa mapato ambayo yangeisaidia kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi" Alisisitiza Mhe. Mavunde.
Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa dhahabu hiyo iliyokamatwa imetaifishwa kwa mujibu wa taratibu za Sheria na imehifadhiwa Benki Kuu ya Tanzania.
Vilevile, Mheshimiwa Mavunde amekielekeza Kikosi Kazi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola kumhoji vizuri mtuhumiwa aliyekamatwa na dhahabu hizo kufahamu alikotoka na alikuwa anapeleka wapi, ili kuweza kutibu kabisa mzizi wa vitendo hivyo na kuvunja mnyororo wa wote wa utoroshaji.
Mhe. Mavunde alisisitiza kuwa, iwapo mtuhumiwa aliyekamatwa alikuwa na leseni ya ufanyaji biashara ya madini kufutiwa leseni hiyo mara moja na kuingizwa kwenye orodha maalum ya wenye makosa (blacklisted) ili asiruhusiwe tena kufanya biashara ya madini nchini.
Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde alitoa rai kwa wananchi wote kuzingatia na kufuata sheria na mifumo ya ufanyaji biashara ya madini ambayo tumejiwekea kupitia masoko ya madini na vituo vya ununuzi ambavyo vimesambaa Nchi nzima.





.jpeg)
.jpeg)








.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)






.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)

