A new FANTA® flavour is adding a burst of deliciousness to the brand’s portfolio in Tanzania with the launch of FANTA® Berry.

This bolder, fruitier tasting beverage brings a splash of playfulness, fun, and refreshing enjoyment to fans across the country. 

Inspired by the vibrant energy of Tanzanian youth culture and the fast-rising Singeli movement, FANTA® Berry is set to tantalise taste buds with its vibrant twist. 

The new flavour is now available in selected retail outlets, supermarkets, universities, kiosks, and trade outlets across Tanzania.

“We’re thrilled to bring even more variety to Tanzanians with this vibrant addition to the FANTA® family. FANTA® Berry embodies our commitment to creating fun, fruity twists filled with deliciousness that cater to people’s evolving tastes,” said Kabula Nshimo, Senior Marketing Manager for Coca-Cola Tanzania. 

The launch campaign will come alive through the energetic “Kipapli” platform, designed to connect directly with Tanzania’s youth through music, dance, fashion, creator culture, and on-ground experiences across universities and high-traffic areas in Dar es Salaam.

As part of the experience, FANTA® Berry will bring the excitement to consumers through immersive commuter activations, influencer engagements and taste-test challenges.

 Coca-Cola Kwanza today embarked on a vibrant convoy journey, starting at the Mikocheni plant and making stops across Ubungo, Mabibo, Buguruni and Temeke before culminating in Mbagala. 

At each stop, consumers will enjoy FANTA® Berry tasting experiences, interactive entertainment and fun activities designed to create memorable brand experiences.

FANTA® Berry will roll creator challenges aimed at empowering young people to create content, grow their influence, and participate in the rapidly expanding digital creator economy.

 The activations will also include university engagements, trade market “Berrification” moments, influencer collaborations, and the #KipapliChallenge social media campaign.

With iconic favourites like FANTA® Orange and now FANTA® Berry, the brand continues to inspire a passion for life and unforgettable moments of deliciousness.

 Whether you're hanging out with friends, creating content, commuting across the city, or simply enjoying a playful moment, FANTA® Berry is the perfect companion.

 “Our diverse beverage portfolio reflects our dedication to meeting the preferences of Tanzanians. We’re proud to offer products that bring people together, spark joy, and add flavour and deliciousness to everyday moments,” said David Chait, General Manager at Coca-Cola Kwanza Ltd.

Get your FANTA® Berry fix today and bring on the fun and deliciousness!

Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (right), the Company’s Regional Trade Marketing Manager, Ms. Rukia Sakibu (left), and the firm’s Revenue Growth & Trade Marketing Director, Mr. Arthur Kyara (centre), showcase the newly launched Fanta Berry flavour bottles during an introductory event held in Dar es Salaam over the weekend.
Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (left) poses for a group photo with some Dar es Salaam residents who attended the official launch of the new Fanta Berry flavour in Dar es Salaam over the weekend.

Coca-Cola Kwanza Ltd General Manager, Mr. David Chait (left) takes a selfie with some Dar es Salaam residents during the celebrations, marking the official launch of the new Fanta Berry flavour, in Dar es Salaam over the weekend.



Na Mwandishi Wetu
ZAIDI ya wanafunzi 95 wa Kitanzania wameondoka nchini kuelekea India kuanza masomo ya elimu ya juu katika vyuo mbalimbali, ikiwa ni kundi la kwanza kati ya wanafunzi 198 wanaotarajiwa kwenda kusoma nchini humo kupitia Global Education Link mwaka 2026.

Wanafunzi hao wamechagua programu zinazohusiana na sayansi, teknolojia na taaluma zinazohitajika katika dunia ya sasa, zikiwemo Computer Engineering, Cyber Security, Artificial Intelligence, Civil Engineering, afya, sheria na biashara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Meneja wa Tawi la Dar es Salaam, Micky Musa, amesema kuondoka kwa wanafunzi hao ni sehemu ya mpango wa kuwaunganisha vijana wa Tanzania na fursa za elimu ya kimataifa.

“Zaidi ya wanafunzi 95 wanaondoka katika kundi hili la kwanza kuelekea India, lakini kwa mwaka huu tunatarajia wanafunzi 198 kwenda kusoma nchini India. Hili si kundi la mwisho kwa sababu bado tuna wanafunzi wengine wanaoendelea kukamilisha taratibu zao,” amesema Musa.

Amesema Global Education Link pia inaendelea kuwaandaa wanafunzi wapatao 185 wanaotarajiwa kuelekea China, huku wengine wakiwa katika maandalizi ya kwenda Malaysia, Marekani na Uingereza.

Musa amewataka vijana wenye ndoto ya kusoma nje ya nchi kufika katika ofisi za Global Education Link zilizopo Dar es Salaam, Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha kupata ushauri kuhusu uchaguzi wa vyuo, programu za masomo, udahili, visa na maandalizi ya safari.

Miongoni mwa wanafunzi walioondoka ni Alvin Andrew Munda, mwenye umri wa miaka 17, anayeelekea Lovely Professional University nchini India kusomea Computer Science, akilenga baadaye kujikita katika Cyber Security.

“Napenda mfumo wenye practical zaidi kuliko kusoma theory na kuandika mitihani pekee. Nataka nitumie elimu nitakayoipata kutengeneza suluhisho na baadaye nijikite katika Cyber Security kwa sababu usalama wa mtandao ni muhimu sana katika dunia ya sasa,” amesema.

Munda amesema Global Education Link imemsaidia katika mchakato mzima, kuanzia kupata chuo hadi kukamilisha maandalizi ya safari.

Naye mwanafunzi mwingine anayekwenda kusomea Computer Science na Artificial Intelligence amesema anatarajia kuwa mtaalamu wa data na teknolojia, akieleza kuwa AI imeanza kuwa sehemu muhimu katika benki, hospitali, biashara, serikali na sekta nyingine.

Kwa upande mwingine, mwanafunzi anayekwenda kusomea Bachelor of Business Administration na Bachelor of Laws amesema ana ndoto ya kuwa mwanasheria na mfanyabiashara mwenye mafanikio, huku akipongeza Global Education Link kwa kumsaidia katika visa processing, kupata chuo na maandalizi ya safari.

Wazazi waliowasindikiza watoto wao Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wameipongeza Global Education Link kwa kusimamia mchakato wa watoto wao kuanzia hatua za awali hadi siku ya safari.

Donald Kito, mzazi wa Isaac Donald Kito anayekwenda Lovely Professional University kusomea Diploma ya Civil Engineering, amesema familia yake ilifahamu huduma za Global Education Link kupitia matangazo na baada ya kuwasiliana nao walipata maelezo yaliyowapa imani ya kuendelea na mchakato.
Na Mwandishi Wetu
MSANII maarufu wa muziki Christian Bella akiwa sambamba na bendi yake ya Malaika wanatarajiwa kukonga nyoyo za wananchi wa Dar es Salaam siku ya Ijumaa tarehe 28 katika ukumbi wa The Embassy Mbezi Kimara kwa Msuguri.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Edwin Bagenyi ambaye ni Meneja wa Embassy Hall alisema maandalizi yote yamekamilika na wananchi watakaofika watapata burudani ya kutosha kutoka kwa mwanamuziki huyo. Alisema kwa muda mrefu wananchi wa Kimara Mbezi na maeneo mengine ya jijini Dar es Salaam wamekuwa na shauku ya kumwona msanii huyo akitumbuiza maeneo hayo.

“Kwa muda mrefu tumepokea maombi ya wananchi wakitaka kumwona Christian Bella akitumbuiza kwenye ukumbi wetu wa kisasa kabisa wa Embassy, kwa hiyo tumeona tusiwanyime raha wateja wetu, tumeona aje tushirikiane kupendezesha siku hiyo,” alisema.

“Tumejiandaa vya kutosha watu watapata burudani ambayo wameililia kwa muda mrefu sana. Tunawaahidi wateja wetu kuwa burudani wanayoitarajia wataipata siku hiyo ya Ijumaa tarehe 28 hapa Embassy Hall,” alisema.

Christian Bella, ambaye amejijengea jina kubwa kupitia uwezo wake wa kuimba, kucheza na kuwasilisha burudani yenye mvuto jukwaani, anatarajiwa kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki watakaofika katika ukumbi huo. Uwepo wake unatajwa kuwa kivutio kikubwa kutokana na historia yake katika muziki na umahiri wake wa kuwasilisha nyimbo zinazopendwa na mashabiki wa rika mbalimbali.

Katika tukio hilo, mashabiki watapata fursa ya kusikiliza na kufurahia nyimbo mbalimbali za Christian Bella, zikiwemo zile zilizompa umaarufu katika safari yake ya muziki. Msanii huyo amekuwa akitambulika kwa sauti yake ya kipekee, uwezo wa kuimba muziki wa dansi na kushirikisha mashabiki wakati wa maonyesho yake.

Ukumbi wa Embassy Kimara unatarajiwa kuwa sehemu ya kukutana kwa wapenzi wa burudani watakaotaka kutumia muda wao wakifurahia muziki wa moja kwa moja. Tukio hilo pia linatarajiwa kutoa nafasi kwa mashabiki kujumuika, kucheza na kufurahia burudani katika mazingira ya ukumbi.

Waandaaji wa tukio hilo wanawahimiza mashabiki kujiandaa mapema ili kupata nafasi ya kushuhudia burudani hiyo. Aidha, tukio linatarajiwa kuwakutanisha wadau mbalimbali wa sanaa na burudani, huku likitoa mchango katika kuendeleza muziki wa dansi na burudani nchini. Kwa wapenzi wa muziki wa dansi, usiku huo unatarajiwa kuwa wa burudani, muziki na kumbukumbu nzuri.

Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akizungumza jambo alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.


WAZIRI wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb), ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mipya ya Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) kinachojengwa eneo la Banana, jijini Dar es Salaam, na kueleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo.

Hadi Julai 19, 2026, mradi huo ulikuwa umefikia asilimia 23.9 ya utekelezaji baada ya miezi 11 tangu kuanza kwa ujenzi.

Katika ziara hiyo, Mhe. Prof. Mbarawa alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, pamoja na Menejimenti ya TCAA, ambapo alipatiwa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi na hatua mbalimbali zilizofikiwa.

Mradi huo wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 78 unalenga kujenga miundombinu ya kisasa ya mafunzo ya usafiri wa anga, kuongeza uwezo wa Tanzania kuzalisha wataalamu wa sekta hiyo na kuimarisha nafasi ya nchi kuwa kitovu cha mafunzo ya usafiri wa anga barani Afrika.

Mhe. Prof. Mbarawa ameipongeza TCAA kwa usimamizi wa mradi huo, huku akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati, kwa kuzingatia viwango vya ubora pamoja na thamani ya fedha.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuimarisha uwezo wa Tanzania katika kutoa mafunzo ya wataalamu wa usafiri wa anga na kuchangia maendeleo ya sekta hiyo nchini na barani Afrika.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Dkt. Jabiri K. Bakari (katikati) akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa(kushoto) kuhusu mradi mradi wa ujenzi wa  Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akitembelea na kukagua maendeleo ya  mradi wa  ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya majengo yaliofikia kwenye mradi wa  ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) unaendelea katika eneo la Banana, jijini Dar es Salaam.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na taasisi zake kuhakikisha bunifu zinazozalishwa na Watanzania haziishii kuonyeshwa kwenye maonesho, bali zinaendelezwa, zinalindwa na kupelekwa sokoni ili zitoe suluhisho kwa changamoto mbalimbali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo, Jumatatu, Agosti 24, 2026, jijini Tanga wakati akihitimisha Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu, akisisitiza umuhimu wa kujenga mfumo unaowawezesha wabunifu kubadilisha mawazo yao kuwa bidhaa na huduma zenye tija.

Amesema Tanzania ina wabunifu wenye uwezo mkubwa katika maeneo mbalimbali, hivyo hatua inayohitajika sasa ni kuhakikisha ubunifu huo unavuka hatua ya kuoneshwa kwenye maonesho na kufikia hatua ya kutumika, kuzalishwa kwa wingi na kuuzwa sokoni.

“Ni lazima tuvuke kwenye maonesho, twende kwenye uhalisia wa maisha kwamba hivi vitu ambavyo tunavionyesha kwenye maadhimisho kama haya sasa viende kwenye utaratibu wa kila siku wa maisha, tuvitengeneze vya kutosha, vitumike na viingie sokoni,” amesema Dkt. Mwigulu.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika sayansi, ujuzi na ubunifu kwa lengo la kuyageuza maeneo hayo kuwa nguzo muhimu za uchumi wa Taifa na kuchochea maendeleo kupitia matumizi ya tafiti na teknolojia.

“Hatutaweza kuendelea bila kuwa na sayansi, teknolojia na tafiti na tukatumia matokeo ya tafiti hizo. Hatutapata tija bila kutumia matokeo ya tafiti hizo,” amesema.

Dkt. Mwigulu pia amesema Serikali haitakubali kushusha viwango vya elimu, akisisitiza umuhimu wa taasisi zinazosimamia ubora wa elimu kuendelea kusimamia misingi ya kitaaluma katika kuandaa wataalamu wenye uwezo unaokubalika.

“Tusitengeneze mazingira yawe rahisi ya kujifunza, yawe na alama kubwa kubwa, lakini kazini kuwe na zero kubwa kubwa. Hiyo hapana. Lazima tusimamie misingi ya elimu,” amesema.

Amesisitiza kuwa katika sekta nyeti kama afya, uhandisi na elimu, ubora wa mafunzo haupaswi kuchezewa.

“Hatuwezi kucheza na afya za Watanzania… Hatuwezi tukaandaa wataalamu kwa namna duni duni hivi, tutaharibu sekta yote. Tunataka walimu walio bora, maengineia walio bora; wakijenga daraja, wakijenga jengo, liwe jengo kweli kweli,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameagiza mipango ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Tanga iangalie mahitaji ya kiuchumi na kijamii ya mkoa huo kwa kipindi cha miaka 25 ijayo, ili miundombinu inayojengwa sasa iendane na ukuaji wa uchumi, biashara, uwekezaji na ongezeko la matumizi ya usafiri wa anga.

“Lazima tunapojenga tuwaze mbele, tusijenge kwa ajili ya leo. Tuwaze mbele miaka 20 mbele, 25 mbele, kama ambavyo Dira yetu inatuambia,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema uwanja huo unapaswa kujengwa kwa hadhi ya Tanga kama lango muhimu la shughuli za kiuchumi kutokana na miradi mikubwa inayotekelezwa katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema maonesho hayo yanaakisi jitihada za Serikali katika kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha elimu inayounganisha nadharia na vitendo, ili kuandaa wahitimu wenye ujuzi wa kujiajiri na kuingia kwa ufanisi katika soko la ajira.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Caroline Nombo amesema jumla ya taasisi 91 za umma na binafsi zimeshiriki katika maadhimisho hayo, ambayo yamehusisha maonesho ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu, mashindano ya kitaifa ya ujuzi na ubunifu pamoja na makongamano yaliyolenga kujadili mchango wa elimu, ujuzi na teknolojia katika kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe Husna Sekiboko amesema Bunge litaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kuendeleza elimu, ujuzi na ubunifu kupitia bajeti, sera na miongozo inayolenga kuwawezesha watafiti na wabunifu wa ndani kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa. Amesema kuna umuhimu wa kuzipa kipaumbele bidhaa na teknolojia zinazozalishwa nchini, zikiwemo katika taasisi za Serikali, ili kuongeza matumizi ya bunifu za Watanzania na kuchochea ukuaji wa wabunifu hao.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Buriani amesema uwekezaji wa Serikali katika sekta ya elimu umeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia mkoani humo, kuongeza miundombinu na kuchochea mafanikio ya wanafunzi, huku akipongeza maonesho hayo kwa kuibua na kuonesha uwezo mkubwa wa Watanzania katika sayansi, teknolojia na ubunifu.

Kaulimbiu ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu mwaka 2026 ni “Elimu, Ujuzi na Ubunifu: Njia ya Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.”









Na Janeth Raphael - MichuziTv 

Imani kwamba haki inaweza kufuatiliwa na kupatikana bila kujali hali ya mtu imeongezeka kwa familia moja kutoka Meru mkoani Arusha, baada ya kupata msaada kupitia Programu ya “Sema na Waziri” ya Wizara ya Katiba na Sheria.

Familia hiyo ilikuwa imekumbwa na changamoto baada ya kuacha kazi ya ualimu katika shule ya msingi ambako walikuwa wakijitolea kufundisha, huku ikiwa bado inadai stahiki zake. Changamoto hiyo iliwasilishwa kupitia programu hiyo na kuanza kufanyiwa kazi na watumishi wa Wizara.

Ufuatiliaji uliofanywa na Wizara kwa kuwasiliana na wahusika umefanikisha familia hiyo kupata stahiki zilizokuwa zikidaiwa, hatua ambayo imeelezwa kuwa imewapa matumaini mapya kuhusu upatikanaji wa haki.

Akizungumza katika programu hiyo, Lidya Ernest kutoka Meru, Arusha, amesema awali alikuwa na mtazamo kwamba haki ilikuwa rahisi kupatikana zaidi kwa watu wenye uwezo, lakini uzoefu walioupata umebadili mtazamo huo.

“Nitumie nafasi hii kumshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka Programu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa ajili ya kutusaidia Watanzania wote bila kuangalia matabaka wala nyadhifa, wala hali ya mtu. Hata sisi watu wa huku chini nasi tumefikiwa,” amesema Lidya.

Kwa mujibu wa Lidya, hatua hiyo imewapa yeye na mume wake ujasiri wa kuendelea kufuatilia haki zao kupitia njia sahihi, huku wakitambua umuhimu wa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali.

Katika hatua nyingine, Wizara ya Katiba na Sheria imewakabidhi Lidya na mume wake Sh milioni 1.5, fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha shughuli za ujasiriamali na kujikwamua kiuchumi.

Msaada huo unalenga kuwapa fursa ya kutumia fedha hizo kama mtaji wa shughuli za uzalishaji, hatua inayotarajiwa kusaidia familia hiyo kujenga chanzo cha kipato na kuimarisha maisha yao.

Tukio hilo limeonyesha pia nafasi ya Programu ya “Sema na Waziri” katika kuwapa wananchi jukwaa la kuwasilisha changamoto zao za kisheria na kupata ufuatiliaji kutoka kwa Wizara.

Kwa familia hiyo kutoka Meru, msaada walioupata haujaishia katika kurejeshewa stahiki walizokuwa wakidai, bali umeenda sambamba na kupata mtaji wa kuanza shughuli za ujasiriamali, jambo ambalo wameeleza kuwa limewapa matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi.

Hatua hiyo pia inaendelea kuimarisha ujumbe kwamba upatikanaji wa haki haupaswi kuwa fursa ya wachache, bali huduma inayopaswa kuwafikia wananchi wote bila kujali uwezo wao, hadhi au nafasi zao katika jamii.


 






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Taasisi ya Maendeleo ya Diaspora wa Kiafrika (ADDI) Balozi Dkt. Arikana Chihombori-Quao, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 24 Agosti, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Taasisi ya Maendeleo ya Diaspora wa Kiafrika (ADDI) Balozi Dkt. Arikana Chihombori-Quao baada ya mazungumzo, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 24 Agosti, 2026.




Jumla ya miradi 42 katika mkoa wa Geita, itakaguliwa, kuzinduliwa na kuwekwa mawe ya msingi na mwenge wa uhuru ambao umepokelewa Leo mkoani Geita.

MKUU wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela, Agosti 24, 2026 amepokea rasmi Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Shinyanga.

Hafla ya mapokezi imefanyika katika Kijiji cha Nyang'holongo, Kata ya Nundu, Wilaya ya Nyang'hwale.

Akizungumza baada ya kupokea mwenge huo, Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa wa Geita kwa mwaka 2026 utakimbizwa katika Halmashauri 6.

Atanzia na Halmashauri ya Nyang'hwale hadi kumalizia katika Halmashauri ya Chato, kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa.

Ameeleza kuwa wakati wa ukimbizaji wa Mwenge Mkoani Geita, utakimbizwa kwa umbali wa Kilometa 698.2.

Katika kipindi hicho jumla ya miradi 42 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 168.74 itapitiwa. Miradi hiyo itazinduliwa, kuekwa mawe ya msingi, kukaguliwa na kutembelewa.







CRDB Bank imeshiriki katika kilele cha Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, kinachofanyika Jijini Tanga, ikiwa ni sehemu ya ushiriki wa wadau mbalimbali kutoka sekta ya umma na binafsi katika maadhimisho hayo.

Ushiriki wa CRDB Bank unaendelea kuakisi nafasi ya sekta ya fedha katika kuchangia jitihada zinazolenga kuimarisha elimu, ujuzi na ubunifu kama nyenzo muhimu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini

John Mtani, Meneja Mwandamizi wa Biashara za Serikali, CRDB Bank, akishiriki katika kilele cha Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026 jijini Tanga, pamoja watumishi, viongozi mbalimbali na wananchi waliotembelea Banda la CRDB Benki.






JUMLA ya wazee 246 wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa matibabu hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee bila vikwazo vinavyotokana na ukosefu wa vitambulisho hivyo.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la wazee cha robo ya nne kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Afisa Ustawi wa Jamii wa Manispaa ya Sumbawanga Herry Sanga amesema wamefanikiwa kutoa vitambulisho vya msamaha wa matibabu ikiwa wanawake 138, wanaume 108 huku wazee 29 ambao hawakuwa na vitambulisho vya msamaha wa matibabu wamepewa msamaha wa muda wa matibabu.

Kwa upande wake katibu wa Baraza la wazee Manispaa ya Sumbawanga Moris Massanja amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu kwa wazee kuhusu haki zao pamoja na huduma zinazopatikana kwa ajili yao.

Utoaji wa vitambulisho vya msamaha wa matibabu kwa wazee unalenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wazee katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na kuhakikisha wazee wanapata huduma za matibabu kwa wakati na bila vikwazo vinavyotokana na ukosefu wa vitambulisho.




Top News