*KAWASIHI KUACHANA NA MAGENDO YA VITENGE NA KUPITA NJIA ILIYO RASMI

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia kupitia idara Forodhaimee delea na zoezi la kutoa elimu kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi kwa wadau wa forodha mkoani Songwe, ikiwa ni sehemu ya kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko yaliyoanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa niaba ya Meneja msaidizi Forodha mkoa wa Songwe, Afisa Forodha Mfawidhi wa Kituo cha Tunduma, Zahoro Makame, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha wadau kuelewa mabadiliko ya sheria mpya za kodi zilizoanza kutekelezwa mwezi Julai mwaka huu.

Makame amesema elimu hiyo ni muhimu kwa wadau wa forodha, wakiwemo mawakala wa forodha, wasafirishaji, wafanyabiashara na watumishi wa forodha, kwa kuwa mabadiliko hayo yanaathiri moja kwa moja namna taratibu za uingizaji na upelekaji wa bidhaa nje ya nchi zinavyotekelezwa.

Akifafanua kuhusu mabadiliko hayo,mwezeshaji ambaye ni Afisa Forodha Mfawidhi wa Mkoa wa Dodoma, Hassan Minga, amesema mabadiliko ya kibajeti yaliyofanywa kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2026 yamesababisha marekebisho katika sheria mbalimbali zinazohusiana na kodi na maeneo mengine ya biashara.

Minga amesema kwa upande wa forodha, kuna sheria kumi pamoja na kanuni moja zilizokumnwa na mabadiliko hayo. mapitio ya sheria moja ambazo zimeguswa na mabadiliko hayo, hatua inayolenga kukuza uchumi.
Kwa upande wake, Afisa Forodha Mkuu kutoka Kitengo cha Uwezeshaji Biashara Dar es Salaam, Alan Maduhu, amesema miongoni mwa mabadiliko hayo kuna hatua zinazowapa wafanyabiashara unafuu wa kodi, ikiwemo kupunguzwa kwa kiwango cha kodi kinachotozwa kwenye bidhaa ya vitenge vivyoingizwa nchini.
Maduhu amesema kodi ya vitenge ambayo awali ilikuwa ikitozwa kwa kiwango cha asilimia 50, sasa imeshushwa hadi asilimia 35 kuanzia mwaka huu wa fedha, akieleza kuwa wafanyabiashara wanapaswa kufahamu mabadiliko hayo ili waweze kufanya biashara kwa kuzingatia sheria.

Akihitimisha mafunzo hayo, Maduhu amewataka mawakala wa Forodha na Wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa toka nje ya nchi hasa kupitia mpaka wa Tunduma kutumia utaratibu wa kutengeneza Kadhia kabla ya mzigo kufika (PAD) ili kuwezesha uondoshwaji wa mizigo kwa haraka na kuepusha msongamano wa magari ya mizigo.

Kwa upande wao Mawakala wa Forodha walioshiriki mafunzo hayo, wameishukuru serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania kuwasogezea elimu hiyo muhimu na kuahidi kuwa mabalozi wa mabadiliko hayo ili kukuza biashara kupitia mpaka wa Tunduma ambao ni lango la SADC.


SAME.

ZAIDI ya watu 20 wanahojiwa na Jeshi la Polisi wilayani Same mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kudaiwa kuendesha shughuli za uchimbaji haramu wa madini katika vyanzo vya maji ndani ya mita 60 kinyume cha sheria na kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.

Akizungumza kuhusu hatua zinazochukuliwa jana ofisini kwake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, alisema Kamati ya Usalama ya wilaya ilipata taarifa za siri kuhusu uchimbaji huo katika maeneo mbalimbali na kufika kujiridhisha, ambapo ilibaini kuwepo kwa shughuli hizo.

Alisema baada ya kubaini hali hiyo, Kamati iliunda timu ya kwanza ya wataalamu kutoka RUWASA, Bodi ya Maji Bonde la Pangani, Maafisa Mazingira na Maafisa Madini, iliyofanya uchunguzi katika maeneo yote na kubaini uchimbaji haramu katika kata saba pamoja na uharibifu mkubwa wa mazingira.

Kasilda alisema kuwa, iliundwa timu ya pili kutoka ndani ya Kamati ya Usalama kwa ajili ya kuwabaini wahusika waliotajwa katika taarifa za siri zilizotolewa na wananchi na baadhi ya madiwani wenye nia njema na wazalendo.

“Hadi sasa zaidi ya watu 20 wanaotuhumiwa kuhusika na uchimbaji huo pamoja na kupeleka mitambo wamehojiwa na Jeshi la Polisi, na wengine wanaendelea kuhojiwa kwa awamu ili kupata ushahidi na watakaobainika kuhusika watachukuliwa hatua za kisheria, na viongozi wa Serikali watakaobainika pia watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma,” alisema Kasilda.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema hali kama hiyo iliwahi kutokea mwaka 2023, ambapo Kamati ya Usalama ilitembelea maeneo hayo na kufanikiwa kuwakamata zaidi ya watu watano waliokuwa wakijihusisha na uchimbaji haramu pamoja na mitambo yao, hali iliyofanya shughuli hizo kusitishwa kwa muda hata hivyo, alisema uchimbaji huo umeibuka tena mwaka huu na hatua za kuwadhibiti zinaendelea.

Pia, wachimbaji hao wamebainika kufanya shughuli za uchimbaji bila kuwa na vibali wala leseni kutoka kwenye mamlaka husika huku, Kasilda akiwaonya watu wanaopanga kurejea katika maeneo hayo na kuendelea na uchimbaji haramu, akisisitiza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya watakaokiuka taratibu.

Kasilda alizitaka taasisi za Serikali zinazohusika na uhifadhi wa mazingira na ulinzi wa vyanzo vya maji kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na kuchukua hatua za kisheria.

Pia amewapongeza wananchi na baadhi ya madiwani waliotoa taarifa za siri na kusisitiza kuwa Serikali itawalinda.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, SACP Saimon Maigwa alisema kuwa, Jeshi hilo limeshafungua jalada na kwa sasa linaendelea na uchunguzi ili kubaini ukweli wa jambo hilo.






Na Mwandishi wetu, Babati


Mkoa wa Manyara umeweka mkakati wa kuhakikisha watoto 670,000 wenye umri chini ya miaka 10 wanafikiwa na kupata chanjo katika Kampeni ya Chanjo ya Polio ya Matone, huku maandalizi ya Uzinduzi wa Kitaifa wa Kampeni hiyoyakiendelea kufanyika mkoani humo.

Akizungumza baada ya kupata nafasi ya kuonana na Kaimu Meneja Mpango wa Taifa wa Chanjo Dkt Georgina Joachim kutoka Wizara ya Afya pamoja na Dkt Floriani Tinuga kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, amesema mkoa uko tayari kutekeleza zoezi hilo kwa ufanisi.

Mhe. Sendiga amesisitiza kuwa Serikali ya Mkoa imejipanga kuhakikisha hakuna mtoto atakayeachwa nyuma, na kwamba juhudi zote zitaelekezwa katika kuwafikia watoto wote 670,000 wanaolengwa kupata chanjo kuanzia tarehe 27 hadi 30 Agosti 2026.

Amesema ushirikiano kati ya Serikali, wataalamu wa afya, viongozi wa maeneo, wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ni muhimu katika kuhakikisha kampeni hiyo inafikia malengo yaliyowekwa.

Kampeni hiyo inalenga kuimarisha kinga dhidi ya ugonjwa wa Polio kwa watoto na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwapeleka watoto kupata chanjo kwa wakati.

Katika utekelezaji wa kampeni, timu za wataalamu wa afya zinatarajiwa kushirikiana na viongozi na jamii watapita nyumba kwa nyumba, mashuleni, kwenye minada, masoko, nyumba za Ibada na maendeo yenye mikusanyiko kuwatafuta na kuwapatia chajo walengwa wote wa zoezi hili.

Mkoa wa Manyara pia unaendelea na maandalizi kuelekea uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya Polio ya Matone Kitaifa tarehe 27 Agosti 2026, huku uongozi wa Mkoa ukisisitiza utayari wake wa kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa mafanikio.



MERIDIANBET kupitia programu zake za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), imekabidhi msaada wa viti maalum vya magurudumu, maarufu kama wheelchairs, kwa Hospitali ya Kigogo, katika hatua inayolenga kuboresha huduma kwa wagonjwa na watu wenye uhitaji maalum. Mchango huo ni sehemu ya jitihada za kampuni kuendelea kuwa karibu na jamii na kushirikiana na taasisi mbalimbali katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Makabidhiano hayo yamekuja kupitia ushirikiano mzuri kati ya Meridianbet na uongozi wa Hospitali ya Kigogo, huku lengo likiwa ni kuongeza upatikanaji wa huduma muhimu kwa watu wenye mahitaji maalum. Wheelchairs hizo zinatarajiwa kusaidia hasa kwa wagonjwa wanaohitaji msaada wa kutembea au kusafirishwa kutoka eneo moja kwenda jingine ndani ya hospitali. Meridianbet imeonyesha kupitia hatua hii kwamba kampuni inaweza kutumia nafasi yake kuleta athari chanya nje ya shughuli zake za kawaida.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano, mwakilishi wa Meridianbet, Nancy Ingram, alisisitiza umuhimu wa afya katika kujenga jamii yenye nguvu na maendeleo endelevu. Ujumbe huo unaenda sambamba na ukweli kwamba jamii yenye afya ina nafasi kubwa ya kusonga mbele katika elimu, michezo, ajira na shughuli nyingine za maendeleo. Kwa hiyo, uwekezaji katika afya si msaada wa muda mfupi pekee, bali ni sehemu ya kujenga msingi imara wa maisha bora kwa wananchi. Kupitia CSR, Meridianbet imeendelea kuangalia maeneo ambayo mchango wake unaweza kuleta tofauti, na sekta ya afya ikiwa miongoni mwa maeneo hayo.

Kwa upande wake, Hospitali ya Kigogo ilipokea msaada huo kwa furaha, ikieleza kuwa wheelchairs hizo zitasaidia kuongeza ubora wa huduma pamoja na kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi. Hii ni kwa sababu vifaa vya usaidizi vina nafasi muhimu katika kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma kwa usalama na urahisi. Wheelchair ni nyenzo inayoweza kuwapa uhuru zaidi wahitaji kufika kwenye huduma wanazohitaji. Ushirikiano kati ya Meridianbet na Hospitali ya Kigogo kwa hiyo unaonyesha nguvu iliyopo pale sekta binafsi na taasisi za huduma za jamii zinapoungana kwa lengo moja.

Meridianbet inaendelea kusimama kama mshirika wa maendeleo ya jamii, ikielekeza sehemu ya jitihada zake kwenye afya, elimu na miradi mbalimbali ya kijamii. Msaada wa wheelchairs kwa Hospitali ya Kigogo unaongeza sura nyingine katika safari hiyo, ukionyesha kuwa dhamira ya kampuni ni kushiriki katika kujenga jamii yenye fursa na mazingira bora zaidi kwa wote.

 
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa akisaini Kitabu wakati alipotembelea Banda la TIA katika Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa akipata maelezo kutoka Mkuu wa Sehemu - Ukuzaji na Uendelezaji wa wanafunzi kitaaluma na kitaalam wa TIA Imani  Matonya  kuhusiana na bunifu mbalimbali wa wanafunzi na wahitimu was TIA  walizoleta katika Maonesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu ,Ujuzi na Ubunifu  Kwakati Mkuu wa Chuo hicho  alipotembelea Banda la TIA katika Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.
Baadhi ya Wahitimu na Wanafunzi wa TIA  ambao wenye bunifu ambazo zimesimamiwa TIA kwenye maonesho ya Wiki ya Elimu Kitaifa ,Ujuzi na Ubunifu inayoendelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara,Jijini Tanga.



Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imetakiwa kuongeza uwekezaji katika tafiti na ubunifu unaofanywa na vyuo vya elimu ya juu nchini ili kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za jamii na kuongeza mapato ya taifa kupitia teknolojia zinazozalishwa na wataalamu wazawa.
 
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Husna Sekiboko, wakati alipotembelea Banda la Chuo Kikuu  Dodoma (UDOM) katika Maonesho ya Wiki ya Elimu Kitaifa, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika Viwanja vya Usagara, Tanga.
 
Sekiboko amesema tafiti na ubunifu unaofanywa na vyuo vya elimu ya juu nchini umefikia hatua kubwa na una uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali zinazolikabili taifa, hivyo unapaswa kupewa kipaumbele, bajeti na uwezeshaji wa kutosha. Amesema miongoni mwa teknolojia iliyomvutia ni mfumo wa ultrasound uliobuniwa na wataalamu wa UDOM, unaolenga kutoa huduma za uchunguzi wa afya kwa gharama nafuu ikilinganishwa na baadhi ya vifaa vinavyopatikana sokoni. Kwa mujibu wa Sekiboko, teknolojia hiyo inaweza kusaidia kufuatilia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni kuanzia wiki 12 za ujauzito, pamoja na kusaidia katika uchunguzi wa afya ya mama na mtoto.
 
Amesema ubunifu huo ni mfano wa teknolojia zinazopaswa kuendelezwa na kusambazwa katika vituo vya afya nchini kabla ya Tanzania kuanza kuzisafirisha katika nchi nyingine za Afrika.
 
“Tunatakiwa kuwekeza na kuendeleza ufumbuzi ambao umefanyika kwa teknolojia hii iweze kukua, lakini isambae na iweze kutumika kwenye vituo vya afya nchi nzima. Baadaye tuuze kwenye nchi za jirani,” amesema.
 
Amesema Tanzania kwa sasa inatumia teknolojia kutoka nchi mbalimbali, zikiwamo China na India, katika sekta za afya, kilimo na maeneo mengine, hivyo ni wakati muafaka kwa taifa kuanza kuzalisha na kuuza teknolojia zinazobuniwa na wataalamu wa ndani. Sekiboko amesema teknolojia ya ultrasound iliyobuniwa UDOM inaweza kuwa miongoni mwa bidhaa za “Made in Tanzania” zinazoweza kutumika ndani ya nchi na kuuzwa nje, hatua ambayo inaweza kuongeza mapato ya vyuo na taifa, pamoja na kutoa ajira kwa wataalamu watakaohusika katika uzalishaji na matumizi yake.
 
Amesema ubunifu unaofanywa na vyuo unahitaji bajeti, uwezeshaji na kuunganishwa na masoko ili bidhaa na teknolojia zinazozalishwa ziweze kutumika katika taasisi mbalimbali za Serikali. Ameshauri Serikali kuingia mikataba na vyuo vya ndani kwa ajili ya kupata bidhaa na teknolojia zinazohitajika badala ya kutegemea zaidi bidhaa kutoka nje.
 
“Serikali ichukue sasa vile ambavyo vinazalishwa kwenye vyuo, iwe ndio outsource yao, badala ya kwenda kununua mashine nyingine au kuingia mikataba na China na kwingineko, waingie mikataba na vyuo,” amesema Sekiboko. Amesema hatua hiyo itasaidia kuimarisha uwezo wa vyuo, kukuza tafiti na kuhakikisha wataalamu waliobuni teknolojia hizo wanapatikana kwa urahisi wakati wa matengenezo au kutatua changamoto zinazoweza kujitokeza.
 
Katika hatua nyingine, Sekiboko ametoa wito kwa wananchi wa Tanga na mikoa jirani, ikiwamo Pwani, Dar es Salaam, Morogoro, Kilimanjaro, Arusha na Manyara, kujitokeza kwa wingi kutembelea Maonesho ya Wiki ya Elimu Kitaifa, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika Usagara.
 
Amesema maonesho hayo ni ya kitaifa na yameshirikisha vyuo na taasisi mbalimbali kutoka maeneo tofauti ya Tanzania, hivyo wananchi wana fursa ya kujifunza kuhusu elimu, ujuzi, tafiti na ubunifu unaofanywa nchini. Amesema wananchi wenye mahitaji ya elimu ya juu, wanaotarajia kuwapeleka watoto wao vyuoni au wanaotaka kujifunza kuhusu fursa za ujuzi na teknolojia wanapaswa kutumia nafasi hiyo kutembelea mabanda yaliyopo katika maonesho hayo.
 
“Ni jambo la ajabu sana tukifunga haya maonyesho, bado kuna Watanga huko nyumbani hajaja kuji, kushughulikia nini kinaendelea hapa. Wajitokeze, waje watembelee haya mabanda,” amesema.
 
Amesema ushiriki wa wananchi utasaidia kuongeza uelewa kuhusu kazi zinazofanywa na wasomi, wataalamu na wabunifu nchini, pamoja na namna teknolojia hizo zinavyoweza kutumika kutatua changamoto mbalimbali katika jamii.
 
Amesisitiza kuwa wananchi wote wanapaswa kutumia fursa hiyo kufika Usagara na kujionea ubunifu na teknolojia mbalimbali zinazoonyeshwa katika maonesho hayo.







Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) Profesa Haruni Mapesa, amesema maonyesho ya elimu, ujuzi na ubunifu ni jukwaa muhimu kwa taasisi za elimu kuonyesha kazi zinazofanywa na wanafunzi pamoja na kuwafungulia vijana fursa mbalimbali za kujifunza na kuendeleza vipaji vyao.

Profesa Mapesa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu ushiriki wa chuo hicho katika maonyesho ya elimu, ujuzi na ubunifu yanayoendelea mkoani Tanga, akimpongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, pamoja na Wizara hiyo kwa kuendelea kusimamia maonyesho hayo na kuwa na mafanikio.

Amesema maonyesho hayo yamekuwa na umuhimu kwa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kuwa yanatoa nafasi ya kuonyesha programu zinazotolewa na chuoni ikiwemo mafunzo yanayohusiana na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), pamoja na kazi za ubunifu zinazofanywa na wanafunzi.

“Tunajivunia kupata fursa ya kuonyesha kazi za vijana wetu, ubunifu wao katika sayansi, teknolojia na maeneo mbalimbali. Ubunifu huu umekuwa na mguso mkubwa na tunaamini siku zijazo utakuwa na matokeo makubwa zaidi,” amesema Profesa Mapesa.

Amesema chuo kina mpango wa kuendeleza ubunifu wa wanafunzi kwa kuunganisha kazi hizo na watumiaji na wadau wakubwa ili zitumike zaidi katika shughuli za uzalishaji na kuchangia maendeleo ya uchumi.

Profesa Mapesa amesema maonyesho hayo pia yamekuwa fursa kwa vijana wanaotaka kujiunga na Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kupata taarifa kuhusu programu mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho, huku baadhi yao wakipata huduma za usajili na maelekezo ya kujiunga na programu hizo moja kwa moja katika banda la chuo.

Ameeleza kuwa chuo kinatoa programu za umahiri, shahada ya kwanza, pamoja na diploma, huku akiwataka wananchi wa Tanga kutembelea maonyesho hayo, hususan banda la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, ili kupata fursa ya kujifunza zaidi kuhusu huduma na programu zinazotolewa na taasisi hiyo.

Aidha, amesema chuo hicho kina nafasi ya kipekee katika kuhifadhi na kutangaza historia ya Muasisi wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kupitia machapisho, kumbukumbu na hotuba zake ambazo, amesema, zimekuwa na mchango mkubwa katika historia ya Tanzania na Afrika.

Profesa Mapesa amewashukuru waandaaji wa maonyesho hayo pamoja na vyombo vya habari kwa kuendelea kuhabarisha umma kuhusu shughuli za maonyesho na kazi zinazofanywa na taasisi za elimu. Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusisitiza umuhimu wa elimu, ujuzi na ubunifu katika maendeleo ya taifa.

Amesema uwekezaji unaoendelea katika elimu, ujuzi na ubunifu ni muhimu katika kujenga Taifa lenye vijana wenye uwezo wa kutumia maarifa na teknolojia kutatua changamoto na kuchangia maendeleo ya Tanzania.

 

Na Mwandishi Wetu.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewataka Waandishi wa Habari wa Crown Media kulinda imani ya umma kwa kuzingatia weledi, maadili, uadilifu na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wito huo umetolewa wakati wa mafunzo ya siku mbili yaliyotolewa na JAB kwa Waandishi wa Habari wa Crown Media, kuanzia Agosti 18 hadi 19, 2026, jijini Dar es Salaam yakilenga kuwaongezea maarifa na kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, maadili na viwango vya taaluma ya uandishi wa habari.

Akiwasilisha Mada kuhusu Msingi na Mfumo wa Kisheria unaosimamia Sekta ya Habari nchini Tanzania katika mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amewasihi Waandishi wa Habari kuthamini na kulinda taaluma yao kwa kuzingatia misingi inayowaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Waandishi wa Habari tunapaswa kuthamini na kulinda taaluma yetu wenyewe. Weledi, maadili na uadilifu ndiyo msingi wa kuaminika kwa mwandishi na sekta ya habari kwa ujumla,” amesema Wakili Kipangula. 

Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko amewataka Waandishi wa Habari kuzingatia maadili katika kila hatua ya kazi zao, akieleza kuwa maadili ndiyo msingi wa uandishi wa habari unaowajibika na wenye tija kwa jamii.

“Mwandishi wa Habari anapaswa kuzingatia maadili ya kazi katika kila hatua ya utekelezaji wa majukumu yake, kwa kuwa uadilifu na uwajibikaji ndiyo msingi wa taaluma hii,” amesema Dkt. Mkoko alipokuwa akifafanua mada Kuhusu Maadili ya Utangazaji na makosa ya kimaadili yanayofanywa mara kwa mara.

Naye Mjumbe wa JAB na Kaimu Meneja wa Huduma za Kiswahili wa Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN), Bw. Mgaya Kingoba, akiwasilisha mada kuhusu uzalendo, amewataka Waandishi wa Habari kutumia taarifa kwa usahihi na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maslahi ya umma.


 Wakizungumza wakati wa tathmini ya mafunzo hayo, baadhi ya Waandishi wa Habari wa Crown Media wamesema wamepata uelewa mpana kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, hali iliyowasaidia kuondokana na fikra potofu zilizotokana na tafsiri zisizo sahihi zinazotolewa katika jamii kuhusu Sheria hiyo. Pia wameomba mafunzo kama hayo kutolewa mara kwa mara ili kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari.

“Kwa kweli, changamoto tuliyonayo katika vyombo vyetu vya habari ni kushindwa kutofautisha maoni binafsi na uchambuzi wa kitaaluma, pamoja na kushindwa kutenganisha nafasi ya mtu binafsi na wajibu wake kama mwanataaluma. Pia kumekuwa na dhana kwamba Bodi ipo kwa ajili ya kuwadhibiti Waandishi wa Habari, pamoja na uelewa mdogo kuhusu ithibati, umuhimu wake na nafasi yake katika kulinda heshima ya taaluma,” amesema Imani Luvanga mmoja wa washiriki.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya JAB kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, yanayolenga kuimarisha weledi, uadilifu, uwajibikaji na tija katika taaluma ya uandishi wa habari.


LEO hii unaweza ukatengeneza pesa ndefu kwa kusuka jamvi lako la ushindi na Meridianbet. Timu kibao zenye Odds kubwa zipo kwaajili yako, ingia na usuke jamvi siku ya leo.

Kama kawaida ligi zinaendelea kuchanganya huku wewe ukichangamkia odds za kibabe, Yanga atakuwa nyumbani kumenyana dhidi ya Coastal Union kwenye Ligi kuu ya Tanzania, NBC PREMIER LEAGUE. Hii ni mechi ambayo ushindi ni muhimu kwa timu zote mbili.

Baada ya kushinda kule ugenini sasa Yanga watakuwa wakisaka ushindi wa pili, huku Wagosi wa Kaya wao wakipoteza mechi ya kwanza ya ligi wakiwa nyumbani kwao. Vijana wa Manqoba wao ni mabingwa watetezi wa ligi mara tano mfululizo huku wakihitaji ushindi kuendelea kutetea taji lao.

Yanga kuelekea msimu huu mpya wa ligi iliweza kufanya usajili mkubwa wa wachezaji wenye uwezo mkubwa akiwemo Peter Shalulile, Zakuone, Toure na wengine wengi ambao kwa pamoja wataisaidia klabu hiyo kufanya vyema. Lakini wamemrejesha Aziz Ki ambaye huenda akaonekana kwenye mchezo huu wa leo.

Mkwanja upo kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Coastal wao ni timu ambayo msimu uliopita halikuwa na msimu mzuri kwani ilinusurika kucheza play offs, hivyo wanaweza wakaingia kwenye mchezo huu kwenda kujilinda zaidi kuliko kushambulia. Nani kuondoka na ushindi leo?. Beti hapa.

Takwimu zinaonesha kuwa mechi tano za misho kukutana timu hizi mbili kwenye ligi, Yanga wameondoka na ushindi mechi zote, na mara ya mwisho Coastal kupata ushindi mbele ya vijana hawa wa Jangwani ilikuwa ni 2021. Jisajili hapa.

Vilevile ligi kuu ya Saudi Arabia, SAUDI PRO LEAGUE pia itaendelea ambapo utapigwa mchezo mmoja kati ya Al-Fahya dhidi ya Al Hilal ambao walianza vyema kampeni yao ya msimu huu kwa kupata ushindi kwenye mechi yao ya kwanza wakati wenyeji wao wakipoteza.

Al Hilal wanataka kupambania taji la ligi msimu huu baada ya msimu uliopita kukosa taji hilo mbele ya Al Nassr, hivyo hii ni mechi ambayo ina umuhimu mkubwa sana kwao kwani Waswahili husema biashara asubuhi, na jioni ni mahesabu.

Al Fahya ni timu ya daraja la kati ambayo pia kule kwa wakali wa ubashiri Meridianbet hapewi nafasi kubwa ya kushinda mechi hii kutokana na ubora wa timu ambayo anakutana nayo yenye wachezaji wenye ubora mkubwa akiwemo Karim Benzema.

Mechi hii pia imepewa machaguo zaidi ya 1000 ambayo mteja anaweza akataytumia kwa kufanya ubashiri na kuondoka na ushindi mkubwa, kama vile kona, faulo, 2UP, na mengine ambayo mteja anataka.

Hii ni mechi ambayo mwenyeji anahitaji kulipa kisasi kwa hali na mali au kumaliza uteja mbele ya timu hii kwani kwenye mechi zao 5 za misho kukutana Al Hilal ameondoka na ushindi mechi zote. Je wewe nafasi ya ushindi unaiweka wapi?. Suka jamvi hapa.



Na Avila Kakingo
CHUO Kikuu cha Aga Khan kupitia Taasisi ya Maendeleo ya Elimu Afrika Mashariki (IED, EA), kimewakutanisha waelimishaji wa walimu, watunga sera, watafiti, viongozi wa shule, washirika wa maendeleo, walimu wanafunzi na wataalamu wa elimu kutoka Afrika Mashariki na maeneo mengine kujadili mustakabali wa uandaaji wa walimu.

Mkutano huo wenye kaulimbiu “Kufikiria Upya Uandaaji wa Walimu: Mabadilishano ya Kujifunza Afrika Mashariki kuhusu Ubunifu na Utendaji”, unalenga kutoa jukwaa la kubadilishana uzoefu, kuchunguza mbinu bunifu na kuandaa kwa pamoja suluhisho la kuimarisha uandaaji wa walimu. Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa IED, EA, Profesa Jane Rarieya, amesema mustakabali wa elimu katika Afrika Mashariki hautegemei kuwa na walimu wa kutosha pekee, bali namna wanavyoandaliwa, kusaidiwa na kuwezeshwa katika taaluma zao.

Profesa Rarieya amesema mabadiliko ya elimu yanachochewa na matumizi ya teknolojia za kidijitali na akili bandia (AI), mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la utofauti na ujumuishi pamoja na mabadiliko ya matarajio kuhusu elimu. Amesema mkutano huo unatoa fursa kwa wadau kujifunza kutoka kwa kila mmoja, kuimarisha ushirikiano kati ya shule, vyuo vikuu, jamii na mifumo ya elimu, na kutafakari upya namna ya kuwaandaa walimu kukabiliana na mahitaji ya madarasa ya sasa.

Mabadilishano hayo yanafanyika kwa mtazamo wa kujifunza kwa vitendo na kushirikishana uzoefu, kupitia vikao vya kubadilishana uzoefu, maabara za utekelezaji, madarasa maalumu, mijadala ya pande zote na majadiliano ya paneli. Kupitia vikao hivyo, washiriki wanajadili changamoto zinazofanana, kujifunza kutokana na mazingira mbalimbali na kujenga ushirikiano wa kuimarisha mifumo ya elimu katika ukanda huo.

Eneo jingine linalopewa kipaumbele ni kuwawezesha walimu kuwa na uwezo na uhuru wa kitaaluma wa kushiriki katika mageuzi ya elimu. IED, EA imeeleza kuwa kadri nchi zinavyoendelea kutumia mitaala inayozingatia umahiri, walimu wanahitaji kuwa na uwezo wa kuelewa mahitaji ya wanafunzi, kufanya maamuzi sahihi ya kitaaluma, kutathmini ujifunzaji, kubadilisha mbinu za ufundishaji na kushirikiana na jamii wanazozihudumia.

Kwa mujibu wa IED, EA, mabadilishano hayo ni wito kwa walimu, serikali, vyuo vikuu, shule, jamii na washirika wa maendeleo kushirikiana katika kufikiria upya uandaaji wa walimu Afrika Mashariki. Hatua zinazopendekezwa ni pamoja na kuimarisha mafunzo ya vitendo na ulezi kwa walimu wanafunzi, kujenga jumuiya za kujifunza kitaaluma kwa walimu wanaoanza kazi na kuwapa walimu wenye uzoefu nafasi ya kuwa viongozi, walezi na washiriki katika ubunifu na tafiti za elimu.
Kwa upande wake, Mhadhiri wa Taasisi hiyo, Dkt. Nipael Mrutu, amesema kongamano hilo linalenga kutafakari aina ya mwalimu anayehitajika katika dunia inayobadilika kwa kasi.

Dkt.Mrutu amesema fursa hiyo inawawezesha wataalamu kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu mbalimbali za ufundishaji, kutathmini zilizofanikiwa na ambazo hazikutoa matokeo yaliyotarajiwa na kutafuta njia bora za kuboresha elimu.

Amesema ubunifu ni muhimu kwa mwalimu wa sasa kwa kuwa anapaswa kutumia mbinu zinazowawezesha wanafunzi kujifunza kwa ufanisi na kukabiliana na mahitaji yanayobadilika katika jamii na dunia.

Naye mwalimu wa Shule ya Sekondari Jangwani na kiongozi wa Chama cha Walimu wa Somo la Kiingereza Tanzania, Ayub Msuya, amesema walimu wanapaswa kubadilisha mtazamo wa kuwalaumu wanafunzi wanaposhindwa kuelewa na badala yake kutafuta mbinu mpya zinazolingana na mahitaji yao.

Msuya amesema walimu wa Afrika Mashariki wanapaswa kujifunza kutoka kwa wenzao na kubadilishana mbinu za ufundishaji, ikiwamo matumizi sahihi ya teknolojia.

Amesema kwa somo la Kiingereza, walimu wanapaswa kuzingatia mazingira ya lugha wanamoishi wanafunzi na kuwajengea uwezo wa kuelewa, kuchambua na kutumia maarifa wanayopata.

Ameongeza kuwa kongamano hilo limefika wakati mwafaka kwa kuwa linawawezesha walimu kujifunza kutoka kwa wenzao wa nchi nyingine za Afrika Mashariki na kupata mbinu zitakazosaidia kuandaa wanafunzi wenye uwezo wa kuwasiliana, kuchambua na kutumia maarifa katika maisha ya sasa na yajayo.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Maendeleo ya Elimu Afrika Mashariki, kongamano hilo pia linalenga kuimarisha ushirikiano kati ya walimu, serikali, vyuo vikuu, shule, jamii na washirika wa maendeleo katika kuboresha uandaaji wa walimu katika ukanda huo.

Kupitia mijadala ya vikundi, maabara za utekelezaji, madarasa maalumu, meza za majadiliano na mijadala ya pamoja, washiriki wanajadili namna ya kuimarisha mafunzo ya vitendo na malezi kwa walimu wanafunzi, kujenga jumuiya za kitaaluma kwa walimu wanaoanza kazi na kuwawezesha walimu wenye uzoefu kushiriki katika uongozi, utafiti na ubunifu wa elimu.



Matukio mbalimbali katika picha.
Picha ya pamoja


Na Mwandishi Wetu, Tanga
CHUO cha Kodi (ITA) kimeshiriki Maonesho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga, kwa kutoa elimu kuhusu majukumu ya Chuo hicho pamoja na fursa za mafunzo zinazotolewa.

Wanafunzi na wadau mbalimbali waliotembelea banda la ITA wamepata fursa ya kufahamu kwa kina kuhusu programu za mafunzo zinazotolewa na Chuo hicho, huku wakihamasishwa kujiunga na mafunzo hayo.

Maonesho hayo yaliyoanza Agosti 15, 2026, yamekuwa pia jukwaa kwa ITA kuwaelimisha wananchi kuhusu nafasi ya taaluma mbalimbali katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na maeneo mengine ya ajira.

Akizungumza na wanafunzi waliotembelea banda hilo, Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Umma wa ITA, Oliver Njunwa, amesema mwanafunzi anayelenga kufanya kazi TRA anapaswa kuzingatia masomo yote kwa kuwa Mamlaka hiyo inaajiri wataalamu wenye taaluma mbalimbali.

“TRA ina wafanyakazi wenye taaluma mbalimbali, hivyo mwanafunzi anatakiwa kuzingatia masomo yote na kufanya vizuri katika masomo yake,” amesema Njunwa.

Aidha, amewataka wanafunzi wanaotaka kusoma ITA kutokuwa na mtazamo wa kwamba mhitimu wa Chuo hicho anapaswa kufanya kazi TRA pekee, bali kuwa tayari kufanya kazi katika taasisi au maeneo mengine ambako taaluma zao zinahitajika.

“Mwanafunzi aliyesoma ITA anajengwa kufanya kazi sehemu yoyote ambayo taaluma aliyoisomea inahitajika pamoja na kujiajiri,” amesema.

Maonesho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanaendelea katika Viwanja vya Usagara jijini Tanga hadi Agosti 24, 2026.

Top News