
.jpeg)
Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omary akizungumza katika Banda la Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omary akipata maelezo kutoka kwa Kamishina wa Sensa ,Spika Mstaafu Anna Makinda wakati Waziri huyo alipotembelea katika Banda la Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 50 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MIXX imewakutanisha wajasiriamali 18 katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwawezesha kutangaza bidhaa na huduma zao pamoja na kupanua masoko.
.jpeg)

Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam.
Kadri Maonesho ya 56 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) yanavyoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeendelea kuthibitisha kuwa teknolojia ya nyuklia siyo teknolojia ya kutumika kwenye uzalishaji wa nishati pekee, bali ni nyenzo muhimu inayochochea maendeleo ya kiuchumi, biashara, uwekezaji na ustawi wa jamii kupitia matumizi yake katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Leo ikiwa ni siku ya sita tangu kuanza kwa maonesho hayo yaliyofunguliwa rasmi tarehe 28 Juni na yanayotarajiwa kuhitimishwa tarehe 13 Julai 2026, banda la TAEC limeendelea kuwa moja ya maeneo yanayovutia idadi kubwa ya wananchi, wanafunzi, watafiti, wawekezaji, wafanyabiashara na wadau kutoka ndani na nje ya nchi wanaotaka kupata uelewa kuhusu nafasi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Tanzania.
Ushiriki wa TAEC katika maonesho haya unaendana na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu sahihi kuhusu matumizi salama ya mionzi na teknolojia ya nyuklia pamoja na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa kupitia uzalishaji wenye tija, huduma bora za afya, usalama wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti na uhifadhi wa mazingira.
Akizungumza katika banda la TAEC lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TAEC, Bwana Peter Ngamilo, amesema maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu linaloiwezesha TAEC kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali, kuwaelimisha kuhusu majukumu ya Tume pamoja na fursa zinazotokana na matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika maendeleo ya Taifa.
“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha wananchi wanafahamu kuwa teknolojia ya nyuklia ni nyenzo muhimu ya maendeleo. Kupitia maonesho haya tunaendelea kutoa elimu kuhusu matumizi salama ya mionzi, wajibu wa TAEC katika usimamizi na udhibiti wa matumizi ya mionzi nchini, pamoja na namna teknolojia hii inavyochangia kukuza biashara, kuongeza tija katika uzalishaji na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Bwana Ngamilo.
Ameeleza kuwa wananchi wengi wamekuwa wakitembelea banda la TAEC kwa lengo la kupata ufafanuzi kuhusu teknolojia ya nyuklia na matumizi yake katika sekta mbalimbali, hali inayoonyesha kuwa uelewa wa jamii kuhusu teknolojia hiyo unaendelea kuongezeka siku hadi siku.
Katika sekta ya afya, TAEC imekuwa ikiendelea kutoa elimu kuhusu matumizi ya mionzi katika uchunguzi wa magonjwa, tiba ya saratani, tiba za nyuklia na uchunguzi wa kitaalamu unaowezesha madaktari kutoa huduma zenye usahihi zaidi kwa wagonjwa. Matumizi haya yameendelea kuboresha ubora wa huduma za afya nchini na kuongeza uwezo wa taasisi za tiba kutumia teknolojia za kisasa katika kuokoa maisha ya wananchi.
Kwa upande wa kilimo, wananchi wanaelimishwa namna teknolojia ya nyuklia inavyosaidia kuboresha mbegu za mazao, kuongeza uzalishaji, kudhibiti wadudu waharibifu wa mazao, kuhifadhi chakula baada ya kuvunwa na kuongeza usalama wa chakula. Teknolojia hizi zinachangia kuongeza ushindani wa bidhaa za kilimo katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Katika sekta ya mifugo, TAEC inaendelea kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika utambuzi wa magonjwa ya mifugo, kuboresha uzalishaji wa mifugo, kuimarisha lishe ya wanyama na kusaidia programu za uzalishaji zinazoongeza tija kwa wafugaji.
Sekta ya viwanda nayo ni miongoni mwa maeneo yanayonufaika kwa kiwango kikubwa kupitia matumizi ya teknolojia ya nyuklia. Kupitia teknolojia za mionzi, viwanda vinaweza kufanya ukaguzi wa ubora wa bidhaa bila kuziharibu (Non-Destructive Testing), kupima unene wa bidhaa mbalimbali, kufanya vipimo vya ubora wa miundombinu, kutambua hitilafu katika mitambo na kuongeza usalama wa uzalishaji. Teknolojia hizi husaidia kupunguza gharama za uzalishaji, kuongeza ubora wa bidhaa na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.
Aidha, katika sekta ya nishati na utafiti, TAEC inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa kujenga uwezo wa matumizi ya teknolojia za nyuklia katika tafiti zinazolenga kutatua changamoto za maendeleo, usimamizi wa rasilimali za maji, ulinzi wa mazingira na matumizi bora ya maliasili.
Kwa mujibu wa Bwana Ngamilo, elimu inayotolewa katika maonesho haya pia inalenga kuondoa dhana potofu ambazo baadhi ya wananchi wamekuwa nazo kuhusu teknolojia ya nyuklia.
“Wananchi wengi walikuwa wakihusisha teknolojia ya nyuklia na silaha pekee, lakini wanapofika katika banda letu wanajionea ushahidi kuwa teknolojia hii inagusa maisha yao ya kila siku kupitia huduma za afya, uzalishaji wa chakula, maendeleo ya viwanda, utafiti, usimamizi wa mazingira na sekta nyingine nyingi zinazochochea maendeleo ya uchumi wa Taifa.”
Maonesho ya Sabasaba yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuunganisha taasisi za Serikali, sekta binafsi, wawekezaji na wananchi katika kuonesha bidhaa, huduma na ubunifu unaochochea biashara na maendeleo ya uchumi wa Tanzania. Ushiriki wa TAEC katika maonesho hayo unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha teknolojia ya nyuklia inatumika kwa amani, usalama na manufaa ya wananchi wote huku ikichangia utekelezaji wa dira ya maendeleo ya taifa kupitia sayansi, teknolojia na ubunifu.
TAEC inaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea banda lake lililopo ndani ya Banda Kubwa la China, Vyumba Na. 60 na 61, katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam, ili kujionea teknolojia mbalimbali zinazotumiwa nchini na kupata elimu kuhusu mchango wa teknolojia ya nyuklia katika kujenga uchumi imara, kuongeza ushindani wa biashara na kuharakisha maendeleo endelevu ya Tanzania.






Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dennis Londo, ametembelea banda la Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji katika maonesho ya Sabasaba 2026 na kupata maelezo kuhusiana na Majukumu na utendaji kazi wa Ofisi hiyo na kukabidhiwa Mfuko wenye ujumbe wa Dira 2050 Wekeza Tanzania.
Aidha, Naibu Waziri Dennis Londo amepongeza utendaji kazi wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuhamasisha uwekezaji na kuanza kwa utekelezaji wa Dira 2050 ikiwa ni injini ya kukuza uchumi wa Nchi.


Na Mwandishi wetu,
Wakulima wa zao la Korosho wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia pembejeo za kilimo licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali.
Wakulima hao ambao ni Wakulima wa Korosho wa mkoa wa Mtwara wameendelea kupokea pembejeo za kilimo ikiwemo dawa za maji na dawa ya unga ama Sulphur ambapo hawakusita kupaza sauti zao za pongezi.
"Sisi Wakulima tunatambua jitihada za Rais Samia kutupa pembejeo ambapo hatujaamini kama tungepata kutokana na namna Wakubwa huko Ulaya wanavyopigana vita na hivyo kupelekea uzalishaji kupungua na kupata huku dawa ni Maajabu ambayo Rais Samia ameonyesha namna anavyotupambania sisi Wakulima." alisema Mwananchi ambaye pia ni Mkulima Ndugu Rashid Hamid maarufu kwa jina la Mkapa mkazi wa Nansinji.
Hayo yamejili wakati wa ziara aliyofanya Ndugu Emmanuel Shilatu ambaye ni Afisa Tarafa kujiridhisha juu ya mwenendo wa ugawaji wa pembejeo ambapo zoezi limeendelea vyema.
"Kwa niaba ya Wananchi ningependa kuungana nao kumpongeza Mhe. Rais Samia kwa namna anavyowajali Wakulima kwa kuwapatia pembejeo za kilimo. Anayafanya hayo sanjali na kuwapatia Wataalamu wa kilimo, kuwapatia mbegu na kuwasimamia Wakulima kupata masoko ya mazao Yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani. Hauwezi kuongelea mafanikio ya Kilimo na Wakulima nchini pasipo kumtaja Rais Samia." Alisema Shilatu
Halikadhalika Mwenyekiti Kijiji Cha Kivukoni Ndugu Jackson Joseph Milanzi alishukuru kwa pembejeo na kuhaidi kutekeleza maelekezo ya Afisa Tarafa ya kuendelea kusimamia ugawaji wa pembejeo hizo kwa uwazi, haki na usawa kama zoezi linavyoendelea.
Wakulima wa Korosho nchini wameanza kupokea pembejeo za kilimo mapema sana kwa msimu huu tofauti na hapo awali na hivyo wanatarajia kuwa na msimu mzuri wa Korosho kwa mwaka huu na hivyo kupata tija ya uzalishaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Julai 3, 2026, Mhifadhi Mkuu wa TAWA, Steven Madenge, amesema wananchi wanaotembelea banda la mamlaka hiyo wanapata fursa ya kujionea wanyamapori mbalimbali wakiwemo twiga, simba, chui, fisi, pundamilia, tembo na mamba, hatua inayolenga kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa uhifadhi na kuwavutia kutembelea hifadhi za wanyamapori nchini.
Aidha, amewataarifu wananchi kuwa TAWA imeandaa programu mpya iitwayo Pande Marathon, inayotarajiwa kufanyika Agosti 1, 2026 katika Hifadhi ya Pande, jijini Dar es Salaam, amesema mbio hizo zinalenga kuimarisha afya pamoja na kuendelea kuunganisha wananchi na shughuli za utalii na uhifadhi nchini.




.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)











.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)



