SHIRIKA la uvuvi Tanzania (TAFICO) limeelezea dhamira ya kuwa injini na nyenzo ya kimkakati katika utekelezaji wa Dira 2050, hususani kujenga uchumi wa buluu, kujenga ajira, kuleta mapato ya fedha za kigeni, kukuza viwanda vinavyotegemea rasilimali za maji na kuchochea kasi ya miundombinu ya uvuvi.
SHIRIKA la uvuvi Tanzania (TAFICO) limeelezea dhamira ya kuwa injini na nyenzo ya kimkakati katika utekelezaji wa Dira 2050, hususani kujenga uchumi wa buluu, kujenga ajira, kuleta mapato ya fedha za kigeni, kukuza viwanda vinavyotegemea rasilimali za maji na kuchochea kasi ya miundombinu ya uvuvi.Na Munir Shemweta, Dodoma
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imekutana leo tarehe 12 Agosti 2026 Bungeni jijini Dodoma kupokea na kujadili taarifa kuhusu utendaji wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, ikiwa ni sehemu ya jukumu la Bunge la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika sekta ya ardhi.
Katika kikao hicho, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeieleza Kamati hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kuboresha utendaji wa Mabaraza hayo, ambayo yako chini ya Wizara hiyo.
Miongoni mwa hatua zilizobainishwa ni kuongezeka kwa idadi ya Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, kupungua kwa mashauri na malalamiko, kuimarishwa kwa matumizi ya mifumo ya kidijiti pamoja na kuboreshwa kwa mfumo wa uendeshaji wa shughuli za madalali.
Pamoja na mafanikio hayo, Kamati imeelezwa kuwa bado zipo changamoto kadhaa zinazoathiri utendaji wa Mabaraza hayo na kwamba Wizara inaendelea kuzifanyia kazi ili kuongeza ufanisi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amewaeleza wajumbe wa Kamati kuwa, Serikali inaendelea kushughulikia changamoto zinazoyakabili Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, akieleza kuwa kutatuliwa kwa changamoto hizo kutasaidia kuyafanya Mabaraza kuwa bora zaidi na yenye manufaa makubwa kwa wananchi.
Awali, wajumbe wa Kamati wameitaka Wizara kuweka mkazo zaidi katika matumizi ya usuluhishi wakati wa kushughulikia migogoro ya ardhi badala ya kila shauri kulenga kupata mshindi na mshindwa.
Wamesema, usuluhishi unaweza kusaidia kupunguza migogoro, kuharakisha utatuzi wa mashauri na kujenga mahusiano mazuri miongoni mwa wananchi.
Wajumbe hao wameeleza kuwa, pamoja na mafanikio yanayoonekana katika utendaji wa Mabaraza, bado ipo haja ya Wizara kuchukua hatua za haraka kukabiliana na changamoto zilizopo ili Mabaraza hayo yaweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuendelea kujenga imani ya wananchi.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Timotheo Mzava, amesisitiza umuhimu wa Wizara kuongeza idadi ya wenyeviti wa Mabaraza, kupanua upatikanaji wa Mabaraza katika wilaya mbalimbali pamoja na kukamilisha mfumo wa kidijiti ili kuongeza ufanisi na kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
“Sisi kama Kamati tunaona umuhimu wa kuwa na Mabaraza kila Wilaya pamoja na kukamilika kwa mfumo wa kidijiti, kwa kuwa mtakapoboresha, kelele kuhusu Mabaraza zitapungua,” amesema Mhe. Mzava.
Kikao hicho kilichoongozwa na Mhe. Mzava pia kimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga, Naibu Katibu Mkuu Bi. Lucy Kabyemera, pamoja na viongozi na watendaji wengine wa Wizara.
Na George Maziku, Geita
HOSPITALI ya Gakala iliyopo kijiji cha Masumbwe, kata ya Bukandwe, wilaya ya Mbogwe inategemea kupokea jopo la madaktari bingwa watakaotoa huduma mbalimbali kuanzia tarehe 17 Agosti, mwaka huu mpaka tarehe 21.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa hospitali hiyo Bunga Dadu Gakala wakati alipozungumza na jopo la waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari ofisini kwake.
Alisema kuwa lengo la kuendesha kambi hiyo ni kuwapunguzia wananchi wa wilaya ya Mbogwe na wilaya zingine jirani, gharama za kufuata huduma za matibabu zinazotolewa na madaktari bingwa.
“Hospitali ya Gakala inawatangazia wakazi wa Masumbwe kuwa kutakuwa na madaktari bingwa kuanzia Jumatatu tarehe 17 mpaka 21, mwezi huu. Tutapokea madaktari bingwa 5 wa magonjwa ya kina mama, daktari bingwa wa watoto, daktari bingwa wa upasuaji, daktarin bingwa wa mifupa na daktari bingwa wa magonjwa ya ndani kama vile sukari, presha na magonjwa mengine yote ya ndani.
“Kwahiyo tunawakaribisha sana wananchi wote wa Masumbwe na maeneo mengine mbalimbali ya wilaya ya Mbogwe na hata wilaya za jirani, waje wapate huduma za mabingwa wa tiba”, alisema Gakala.
Amezitaja huduma zitakazotolewa na madaktari hao kwa kina mama kuwa ni afya ya uzazi, ushauri na vipimo kabla ya ujauzito, matatizo ya kutopata mtoto (Ugumba), uangalizi kipindi cha ujauzito, Ultrasound kwa wajawazito na wasio wajawazito na kutokwa uchafu au damu isiyo kawaida sehemu za siri.
“Pia madaktari hao watatoa matibabu ya uvimbe katika nyonga au tumbo, uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na matatizo yatokanayo na hedhi na ukomo wa hedhi”, alifafanua Gakala.
Mkurugenzi huyo amesema kuwa imekuwa kawaida kwa hospitali yake kupokea madaktari bingwa kwa lengo la kuwapatia wananchi wa Masumbwe fursa ya kupata huduma za matibabu karibu na makazi yao badala ya kusafiri mbali kutafuta huduma hizo.

.jpg)




Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, akiwa na Tuzo ya shukrani baada ya kukabidhiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhiwa
Zanzibar, Agosti 12, 2026
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameutunuku Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) tuzo ya kutambua mchango wake katika kuwezesha kufanyika kwa Mdahalo wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, usiku wa kuamkia leo, Agosti 12, 2026.
Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, kwa niaba ya Mfuko, ikiwa ni sehemu ya utambuzi kwa taasisi na wadau walioshiriki katika kuwezesha mdahalo huo, uliofuatiwa na Maonesho ya Picha za Tamasha la Kizimkazi.
Mdahalo huo umefanyika sambamba na Tamasha la 10 la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026), linalofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo tamasha hilo limeanza rasmi leo kwa matembezi pamoja na uzinduzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.
Ushiriki wa PSSSF katika mdahalo huo unaakisi dhamira ya Mfuko ya kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kuunga mkono mijadala yenye umuhimu kwa jamii, mazingira na maendeleo endelevu.
Aidha, PSSSF inawakaribisha wanachama na wananchi kutembelea banda la Mfuko katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoanza leo, Agosti 12, 2026, kwa ajili ya kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko, amesema Afisa Uhusiano Mkuu wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady.
Mwisho
Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya mazungumzo na kampuni ya Fitch Ratings Ltd ikiwa ni sehemu ya mapitio ya pili ya mwaka 2026 ya tathmini ya Fitch Ratings, katika mchakato unaohusisha taasisi mbalimbali za Serikali.
Mazungumzo hayo yanalenga kuwapa wachambuzi wa Fitch Ratings fursa ya kupata taarifa za kina kuhusu mwenendo wa uchumi wa Tanzania, utekelezaji wa sera za kibajeti na fedha, pamoja na mikakati ya Serikali katika usimamizi wa deni la Taifa.
Kwa upande wa OTR, mjadala ulijikita katika utendaji wa taasisi za umma, mageuzi yanayoendelea, vihatarishi vya kifedha, pamoja na mtiririko wa fedha kati ya Serikali na taasisi za Umma.
Mapema mwaka huu, Fitch Ratings iliendelea kuipa Tanzania daraja ‘B+’ kwa hadhi ya ulipaji wa madeni ya muda mrefu ya fedha za kigeni, ikitaja mwelekeo imara wa ukuaji wa uchumi na uwezo wa Serikali kukabiliana na changamoto za kifedha baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Fitch inakadiria kuwa uchumi wa Tanzania utakua kwa asilimia 6 kwa mwaka 2026, kiwango ambacho ni kikubwa zaidi ya wastani wa asilimia 4.5 kwa nchi zenye daraja la ‘B’.
Katika muktadha huo, Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, aliyeongoza timu ya OTR, aliieleza timu ya Fitch kuhusu mageuzi yanayolenga kuboresha utendaji na ufanisi wa taasisi za umma, kuimarisha utawala bora na uwajibikaji, pamoja na kupunguza utegemezi wa taasisi hizo kwa Serikali.
Alisema ajenda ya mageuzi ya OTR katika kipindi cha miaka miwili iliyopita imeweka mkazo zaidi katika uongozi, usimamizi wa utendaji na uwajibikaji, ikiwemo kuboresha ubora wa Bodi na timu za menejimenti na kuimarisha tathmini za Bodi ili kubaini mapungufu ya ujuzi.
Bw. Mchechu alisema matokeo ya mageuzi hayo yanaendelea kuonekana katika mchango wa kifedha wa taasisi za umma kwa Serikali.
Katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2026, taasisi zilizo chini ya Msajili wa Hazina zilichangia takribani Sh1.881 trilioni kwa Serikali kupitia gawio na michango mingine, ikilinganishwa na Sh1.028 trilioni katika mwaka wa fedha uliotangulia.
“Tunachokiona ni utayari wa taasisi kuanza kuchangia, au kuongeza mchango wao kwa Serikali,” alisema Bw. Mchechu.
Aliongeza kuwa taasisi zinazoendelea kuhitaji msaada wa Serikali zinatarajiwa kuonesha namna zinavyopunguza utegemezi huo.
Alisema hatua za urekebishaji na uwekezaji wa mtaji zilizochukuliwa katika taasisi kama Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) zimesaidia kupunguza majukumu hayo na kuimarisha hali ya kifedha ya taasisi hizo.
Timu ya Fitch pia iliomba taarifa kuhusu mipango ya kuorodhesha baadhi ya taasisi za umma katika soko la mitaji.
Bw. Mchechu alisema Benki ya Biashara Tanzania (TCB) ni miongoni mwa taasisi zinazotayarishwa kuorodheshwa katika soko la mitaji kupitia uuzaji wa hisa kwa umma kwa mara ya kwanza (IPO), huku Shirika la Taifa la Bima (NIC) likifanyiwa tathmini kwa ajili ya uwezekano wa kuorodheshwa katika soko hilo.
Lengo la muda mrefu ni kurekebisha, kuimarisha na kuorodhesha katika soko la mitaji taasisi kadhaa za umma zinazofaa kabla ya mwaka 2030.
Bw. Mchechu alisema pia OTR imezipa taasisi 58 za umma uhuru zaidi wa kiutendaji, unaoziruhusu kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa mamlaka walizopewa bila kuingiliwa katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alisema mageuzi hayo yameimarisha pia uwezo wa ndani wa OTR, hususan katika uchambuzi wa biashara, na hivyo kuiwezesha Ofisi kufanya uchambuzi wa kina zaidi wa bajeti, uwekezaji na mipango ya kimkakati ya taasisi za umma.
Msajili wa Hazina alisema ushirikiano kati ya OTR na Wizara zinazosimamia sekta mbalimbali umeimarika, huku uhusiano huo ukielekezwa zaidi katika kuhakikisha taasisi za umma zinatekeleza vipaumbele vya Serikali.
“Si suala tena la kusema ‘unapaswa kufanya hili na si lile’, bali ‘unafanyaje ili taasisi hii itekeleze kile ambacho Mhe. Rais anataka?’” alisema Bw. Mchechu.
Ujumbe wa Fitch uliongozwa na Bw. José Mantero, Mkurugenzi Mshirika na mchambuzi mkuu anayeshughulikia Tanzania, akifuatana na Bi. Gaimin Nonyane, Mkurugenzi wa Kitengo cha Sovereign and Supranational Group cha Fitch Ratings, na Bw. Gerard Arabian, Makamu wa Rais na Mshauri wa Masuala ya Serikali ‘Sovereign Advisor’ katika Kitengo cha Public Sector Group Corporate Banking.
Bw. Mantero alisema Fitch ililenga kupata uelewa mpana zaidi kuhusu ajenda ya mageuzi ya OTR katika mashirika ya umma, hususan juhudi za kuboresha utendaji wa taasisi na kusimamia madeni na mtiririko wa fedha kati ya Serikali na taasisi za umma.
Alisema mapitio hayo pia yanatathmini athari za maendeleo yanayoendelea katika Mashariki ya Kati kwa Tanzania, ikiwemo athari zinazoweza kujitokeza katika fedha za Serikali, urari wa malipo na mfumuko wa bei kutokana na mabadiliko ya bei za mafuta na mbolea.
Akizungumzia hali chanya ya kifedha ya Serikali inayotokana na uhusiano wake wa kifedha na taasisi za umma, Bw. Mantero alisema: “Hii ni habari njema sana kwa hali ya fedha za Serikali.”
Kwa upande wake, Bi. Nonyane alionekana kuvutiwa na kuongezeka kwa mchango wa mashirika ya umma, akibainisha kuwa mchango huo wa hivi karibuni ulikuwa sawa na takribani asilimia 0.8 ya Pato la Taifa.
Alitaka pia kufahamu namna hali hiyo ilivyobadilika kutoka kipindi ambacho baadhi ya mashirika ya umma nchini yalikuwa yakikabiliwa na changamoto za kifedha.
Mwelekeo huo unaongeza matumaini kwamba mageuzi yanayoendelea yataimarisha zaidi utendaji na uendelevu wa kifedha wa taasisi za umma, kuongeza mchango wao katika uchumi na mapato ya Serikali, pamoja na kuunga mkono juhudi pana za Tanzania za kudumisha uimara wa kifedha na kuboresha hadhi yake ya mikopo.
Taarifa zilizotolewa katika mazungumzo ya OTR na Fitch Ratings yatachangia katika tathmini pana ya kampuni hiyo kuhusu uwezo wa Tanzania wa kutimiza majukumu yake ya kifedha, ikiwa ni sehemu ya mapitio ya pili ya mwaka 2026 ya tathmini ya hadhi ya Tanzania ya ulipaji wa madeni ya Serikali.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetakiwa kuangalia namna ya kupeleka huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini Comoro kutokana na huduma hizo kutopatikana nchini humo.
Rai hiyo imetolewa leo na Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Dkt. Salim Hamad alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge kuona namna ambavyo huduma zinazotolewa na JKCI zinaweza kuwakomboa wananchi wa Comoro.
Dkt. Hamad alisema baada ya JKCI kuweka kambi maalumu ya matibabu ya moyo katika kisiwa cha Anjouan kilichopo nchini Comoro uongozi wa kisiwa hicho umeitaka JKCI kuingia mkataba nao wa kuendelea kufanya kambi za matibabu jambo ambalo linaonesha umahiri wa huduma zinazotolewa na wataalamu wa JKCI.
“Nilifurahi nilipokutana na uongozi wa kisiwa cha Anjouan na kuniomba niwajulishe kuwa wanataka tuingie nao mkataba wa kufanya kambi za matibabu, hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu katika kutoa huduma bingwa za matibabu ya moyo”, alisema Dkt. Hamad.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema uhitaji wa huduma za matibabu ya moyo nchini Comoro ni mkubwa kutokana na mwitikio uliokuwepo wakati wa kambi ya matibabu iliyofanyika mwezi Oktoba mwaka jana katika kisiwa cha Anjouan.
“Tunaandaa mkakati wa kuitangaza JKCI nchini Comoro ili tuweze kuwasaidia wananchi wa Comoro kufahamu zaidi huduma tunazozitoa na kuwapunguzia adha ya kuzifuata huduma hizi mbali na nchi ya Comoro”, alisema Dkt. Kisenge.
Jumuiya ya umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo wakiwemo Azania bank wameamua kuungana kwa pamoja na kuitoa darasa la mafunzo kwa wajasiriamali kutoka kata zote 14 kwa lengo la kuweza kuwapa ujuzi wa kutengeneza bidhaa mbali mbali ambazo zitawasaidia kujikwamua kiuchumi.
Akizungumza katika ziara maalumu ya kikazi yenye lengo la kuweza kutoa mafunzo hayo Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amebainisha kwamba ameamua kutoa darasa hilo ikiwa ni ahadi yake ambayo aliitoa wakati wa zira ya kushukuru wanawake kwa kuweza kuipigia CCM kura za kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mwenyekiti Mgonja amesema kwamba ametembelea wanawake hao na kutoa fursa za mafunzo ya ujarisiamali kwa kuwafundisha jinsi ya kutengeneza bidhaa za aina tofauti zikiwemo utengenezaji wa sabubi kwa ajili ya kufulia nguo , sabuni ya kuogea, na namna ya kutengeneza batiki pamoja na utengenezaji wa bidhaa nyingine.
"Nikiwa kama Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini nimeamua kutimiza ahadi yangu ya kuwapa mafunzo ya ujariamali bure wanawake kutoka kata zote 14 zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na mafunzo haya pia nimeshirikiana na wenzetu wa Azania bank ambao na wao wameweza kutoa elimu ya jinsi ya kutunza fedha na kujikwamua kiuchumi,"amebainisha Mwenyekiti Mgonja.
Kwa upande wake Afisa Mahusiano wa Azania Bank Happiness Lema amebainisha kwamba lengo lao kubwa la kushirikiana bega kwa bega na Jumuiya ya ya wanawake wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini kwa lengo la kuwasaidia kuwapa elimu ya kujikwamua kichumi ikiwemo pamoja na suala zima la utunzaji wa fedha.
"Sisi kama Azania bank tumeoana kuna umuhimu mkubwa wa kuweza kushirikiana na Jumujiya ya wanawake wa UWT Wila ya Kibaha mjini na tumeamua kutembea nao katika ziara yakeo yenye lengo la kutoa darasa maaalumu kwa ajili ya kuwafundisha jinsi ya kutengeneza bidhaa na sisi kama benki tumewafundisha namna bora ya kujikomboa kiuchumi pamoja na jinsi ya kutumia fursa za mikopo yenye liba nafuu,"amenainisha Happiness.
Ziara ya Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini ya kutoa mafunzo kwa wanawake wajasiriamali kwa sasa inaendelea kufanyika ambapo hadi sasa imeshapita katika kata tisa ambazo ni Msangani, Mkuza, Maili moja, Tumbi, Viziwaziwa, Kibaha, Kongowe, Misugususgu pamoja na Kata ya Visiga.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tamasha la Kizimkazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza utamaduni, utalii, biashara na fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar, sambamba na kuchochea maendeleo ya wananchi.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 12 Agosti 2026, alipokuwa akizindua rasmi Tamasha la Kizimkazi 2026 lenye kaulimbiu “KIZIMKAZI Kumenoga!” katika Mkoa wa Kusini Unguja.
Amepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono ya kuasisi Tamasha hilo, ambalo limekuwa likichangia kuhifadhi mila na utamaduni, kukuza utalii na kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutumia Tamasha hilo kutangaza fursa za uwekezaji katika utalii, uvuvi, mwani na Uchumi wa Buluu, huku Serikali ikiendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na miundombinu ya uzalishaji.
Amesema Tamasha la Kizimkazi linaunga mkono dhamira ya Serikali ya kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar kutoka 800,000 hadi milioni 1.5, kupitia matukio maalum ya utalii na utangazaji wa vivutio, utamaduni, vyakula na ukarimu wa Wazanzibari.
Rais Dkt. Mwinyi amewapongeza waandaaji, wadhamini, taasisi za Serikali, Sekta Binafsi, wajasiriamali, wasanii, wanamichezo na wananchi kwa kufanikisha Tamasha la Kizimkazi 2026, akihimiza kuendelea kulitumia kama jukwaa la kufungua fursa mpya za maendeleo.
Tamasha hilo linaendelea hadi tarehe 14 Agosti 2026, ambapo kilele chake kitafanyika katika Uwanja wa Mwehe, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja.




.jpeg)







.jpeg)


.jpeg)




.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

















