Na Janeth Raphael - MichuziTv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema mawakili na maafisa wa sheria wa Serikali wana nafasi ya msingi katika kulinda rasilimali za taifa kwa maamuzi yote ya Serikali yanaongozwa na sheria, weledi na uzalendo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali uliofanyika jijini Arusha leo, Rais Samia amesema taaluma ya sheria ni nyenzo muhimu ya kuzuia hasara kwa Serikali kupitia ushauri wa kitaalamu unaotolewa kabla ya maamuzi makubwa kufanyika.

Ameeleza kuwa mwanasheria mwenye weledi anaweza kusaidia kulinda mikataba ya Serikali, kuimarisha uwajibikaji na kuhakikisha rasilimali za umma zinasimamiwa kwa manufaa ya wananchi. Kwa mujibu wake, jukumu hilo halihitaji nguvu za kijeshi, bali linahitaji uadilifu, uzalendo na uamuzi sahihi unaozingatia sheria.

Rais Samia pia amezitaka taasisi zote za umma kuimarisha mifumo ya kutambua mapema vihatarishi vya kisheria, hususan katika maeneo ya mikataba, manunuzi ya umma, ardhi, miradi ya maendeleo, TEHAMA, mazingira, ajira na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, amesema Serikali inaendelea na mchakato wa kutafsiri sheria kwa lugha ya Kiswahili ili kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu haki zao, wajibu wao na mipaka ya mamlaka ya Serikali, jambo litakalosaidia kuimarisha utawala wa sheria nchini.

Aidha, Rais amesema mawakili wa Serikali wana mchango mkubwa katika kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050, akibainisha kuwa maeneo kama uchumi wa kidijitali, ulinzi wa taarifa binafsi, usimamizi wa rasilimali, ubia kati ya sekta ya umma na binafsi pamoja na biashara za kikanda yanahitaji mifumo madhubuti ya sheria na taasisi zenye uwajibikaji.

Amehitimisha kwa kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda haki za binadamu kwa kuzingatia Katiba na sheria za nchi, huku akiwataka mawakili wa Serikali kuhakikisha sheria wanazosimamia zinaendelea kulinda haki za wananchi, kuimarisha utawala wa sheria na kuhifadhi maslahi ya taifa katika mazingira yanayoendelea kubadilika duniani.





Na Janeth Raphael - Michuzi Tv 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema mafanikio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yatategemea uwepo wa mfumo madhubuti wa sheria unaolinda maslahi ya nchi, kuimarisha utoaji wa haki na kuweka mazingira rafiki ya ukuaji wa uchumi unaoendeshwa na maarifa, ubunifu na uwekezaji.

Akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili wa Serikali uliofanyika jijini Arusha leo, Rais Samia amesema wataalamu wa sheria wana jukumu kubwa la kuhakikisha mfumo wa kisheria unaendana na kasi ya maendeleo na mahitaji mapya ya taifa katika kipindi cha miaka 25 ijayo.

Ameeleza kuwa Tanzania inapoelekea kutekeleza Dira ya 2050, maeneo kama uchumi wa kidijitali, ulinzi wa taarifa na data, usimamizi wa rasilimali za madini, ardhi na bandari, pamoja na biashara za kikanda na ubia kati ya sekta ya umma na binafsi, yanahitaji sheria bora, sera zinazotabirika na mikataba yenye tija ili kuongeza ushindani wa uchumi na kuvutia uwekezaji.

Rais Samia amesema mabadiliko yanayoendelea duniani katika nyanja za uchumi na siasa yanapaswa kuwa chachu kwa wataalamu wa sheria kuongeza umakini katika kulinda maslahi ya taifa, rasilimali zake na kuhakikisha mikataba yote inazingatia manufaa ya Watanzania.

Aidha, amewataka mawakili wa Serikali kuendelea kusimamia utungaji na utekelezaji wa sheria zinazolinda uhuru wa nchi, haki za wananchi na mali za umma, huku akizitaka taasisi za Serikali kuimarisha mifumo ya kutambua na kudhibiti vihatarishi vya kisheria katika mikataba, manunuzi ya umma, miradi ya maendeleo, ardhi, TEHAMA, mazingira na utoaji wa huduma.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema Serikali inaendelea na mchakato wa kutafsiri sheria mbalimbali kwa lugha ya Kiswahili ili kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu haki na wajibu wao, hatua aliyoeleza kuwa itasaidia kuimarisha utawala wa sheria, uwajibikaji na ushiriki mpana wa wananchi katika maendeleo ya taifa.

Amesisitiza kuwa mfumo imara wa sheria si msingi wa utoaji wa haki pekee, bali pia ni nguzo muhimu ya maendeleo endelevu, ustawi wa uchumi na ulinzi wa maslahi ya Tanzania kwa vizazi vya sasa na vijavyo.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi, Mawakili, wageni mbalimbali, kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Viongozi, wageni mbalimbali wakiwa kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya nakala ya Kitabu cha Falsafa ya Sheria ya Mama Samia (Mama Samia Doctrine of Law); kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Hamza Johari kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026. Kitabu hicho kinaelezea historia, falsafa na mafanikio ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia.
Picha namba 04. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Serikali Bw. Bavoo Anatoly Junus kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Heshima kutoka kwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Serikali Bw. Bavoo Anatoly Junus kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Mabanda ya maonesho ya masuala mbalimbali ya Sheria kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) Jijini Arusha, tarehe 13 Julai, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) kwa ajili ya kufungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) Jijini Arusha, tarehe 13 Julai, 2026.


NA: MWANDISHI WETU

Rai imetolewa kwa wadau mbalimbali kujitoa kwa hali na mali kuchangia fedha kwa ajili ya mfuko unaohudumia wagonjwa wa figo na upandikizaji uloto kwa watoto wenye selimundu (sickle cell) wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, Julai 13, 2026, jijini Dodoma.

Chatanda amesema, kutokana na gharama kubwa za matibabu ya magonjwa hayo, viongozi, taasisi binafsi, asasi za kiraia na wananchi kwa ujumla hawana budi kuunganisha nguvu ya pamoja, kuwezesha upatikanaji wa shilingi bilioni saba, ili wagonjwa wasio na uwezo, waweze kunufaika na mfuko huo na hatimaye kuokoa maisha yao.

"Wenzetu Hospitali ya Benjamin Mkapa, wamekuja na mpango kabambe wa kukusanya shilingi bilioni saba za kugharamia wagonjwa wa figo na selimundu, na UWT tuliposhirikishwa tuliona ni jambo jema kwani linagusa uhai wa watu, hivyo basi, niwaombe wadau na wananchi kwa ujumla kuchangia kuwezesha kuokoa maisha ya wagonjwa hao," amesema Chatanda.

Aidha, amesema upatikanaji wa fedha hizo utawezesha kuleta matumaini ya wagonjwa hao kuishi tena na ndiyo maana hafla hiyo imepewa jina la "Okoa Maisha Gala".

"Hata jina la tukio hili linajieleza wazi, yaani Okoa Maisha Gala, na sisi UWT tuko sambamba na serikali yetu ambayo imewekeza fedha nyingi katika uboreshaji wa sekta ya afya ili kuokoa maisha ya wananchi kwani wananchi wanapokuwa na afya njema, wanakuwa na uwezo wa kufanya shughuli zao za kujiingizia kipato na kujenga uchumi wa nchi," ameongeza.

Katika kuadhimisha miaka kumi ya utoaji huduma, BMH wameratibu hafla ya uchangiaji ili kupata fedha za kutibu wagonjwa wa figo na selimundu. Hafla hiyo inatarajiwa kuongozwa na Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, Julai 16, 2026, katika Ukumbi wa Mabeyo wa jijini Dodoma.



Vijana wa Tanzania wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya bahari, huku Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kikieleza kuwa wahitimu wake wanaendelea kupata ajira ndani na nje ya nchi, hususan katika mataifa ya Mashariki ya Kati kutokana na mahitaji makubwa ya wataalamu wa ubaharia.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 13, 2026, Nahodha na Mwalimu kwa Njia ya Vitendo Daraja la Pili wa DMI, Master Kelly Mwandambo, amesema ubaharia ni taaluma yenye fursa nyingi za ajira na kipato kizuri, hivyo vijana wanapaswa kuichagua kama taaluma ya ndoto zao.

Amesema bado jamii imekuwa na dhana potofu kuwa ubaharia ni fani ya wanaume au watu wahuni, jambo ambalo si la kweli, akisisitiza kuwa taaluma hiyo ni ya kitaaluma kama zilivyo taaluma nyingine na wanawake wana nafasi sawa ya kufanikiwa.

Mwandambo amesema mafunzo ya ubaharia yanafuata viwango vya kimataifa vinavyosimamiwa na Shirika la Kimataifa la Bahari, hali inayowafanya wahitimu wa DMI kuwa na uwezo wa kushindana katika soko la ajira duniani kwa kuwa wanapata mafunzo yanayolingana na yanayotolewa katika nchi nyingine ikiwemo Marekani.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kuwahamasisha watoto wao kujiunga na Chuo cha Bahari Dar es Salaam, akieleza kuwa taasisi hiyo inatoa mafunzo kuanzia ngazi ya cheti hadi Shahada za Uzamili (Masters), hatua inayowafungulia wahitimu fursa za ajira katika sekta ya bahari duniani.

Kwa upande wake, Mkufunzi Msaidizi wa DMI na Mhandisi wa Baharini, Winfrida Winsislaus Ngalu, amesema wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho wanapata fursa mbalimbali za ufadhili wa masomo, ikiwemo mikopo ya serikali kuanzia ngazi ya cheti, Samia Scholarship, mikopo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na MELT Fund kwa wanaosoma kozi zinazohusiana na ubaharia.

Amesema pamoja na ufadhili huo, wahitimu wa DMI wameendelea kuwa miongoni mwa wataalamu wanaohitajika zaidi katika soko la ajira la kimataifa, jambo linaloifanya sekta ya bahari kuwa moja ya maeneo yenye mustakabali mzuri kwa vijana wanaotafuta taaluma yenye ajira za uhakika na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa Taifa. 










Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed, amesema Zanzibar ina uwezo mkubwa wa kuimarisha uchumi kupitia biashara, utalii na utamaduni, huku akisisitiza umuhimu wa kuzalisha bidhaa na huduma zenye ubora wa kushindana katika masoko ya ndani na kimataifa.

Akizungumza alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Zanzibar ndani ya Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Ayoub alisema licha ya ukubwa mdogo wa kijiografia wa Zanzibar, visiwa hivyo vina historia, fursa na uwezo mkubwa wa kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji.

"Tukiri kwamba kwa ukubwa wa eneo Zanzibar ni ndogo, lakini kwa ubora wa bidhaa na huduma Zanzibar ni kubwa zaidi ya tunavyofikiria. Tuende tukashindane kwa ubora wa bidhaa, ubora wa vifungashio na ubora wa utoaji wa huduma," alisema.

Alieleza kuwa historia ya Zanzibar kama lango la biashara katika Bahari ya Hindi inapaswa kuendelea kutumika kuvutia wawekezaji na kufungua masoko mapya ya bidhaa na huduma zinazozalishwa visiwani.

Ayoub alisema maadhimisho ya miaka 50 ya Sabasaba yameendelea kudhihirisha mchango wa maonesho hayo katika kukuza biashara, uwekezaji na ushirikiano wa kiuchumi, huku Zanzibar ikinufaika kwa kutangaza bidhaa zake na ubunifu wa wananchi.

Aidha, alisema utamaduni wa Zanzibar ni rasilimali muhimu ya kiuchumi inayoweza kuongeza mapato kupitia sekta za utalii, sanaa na biashara. Alisisitiza umuhimu wa kuendeleza mavazi ya asili, muziki wa taarabu na mila mbalimbali kama vivutio vinavyoweza kuongeza thamani ya utalii wa Zanzibar.

Pia alihimiza kuendelea kukuza matumizi ya Kiswahili kama nyenzo ya biashara na utalii, akisema lugha hiyo imeendelea kufungua fursa za ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi ndani na nje ya nchi.

Katika hotuba yake, Ayoub alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake, akisema umeendelea kudumisha amani na usalama nchini, hali inayoweka mazingira wezeshi kwa biashara, uwekezaji na maendeleo.

Aliwataka wafanyabiashara na wawekezaji kutumia fursa zilizopo Zanzibar kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kuwekeza katika sekta mbalimbali kwa lengo la kukuza uchumi endelevu na kuongeza ustawi wa wananchi.


Na Mwandishi Wetu
WANANCHI wanaotembelea Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) wanaendelea kunufaika na huduma mbalimbali za mawasiliano na ofa maalum zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia banda lake lililopo katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere.

Katika banda hilo, maafisa wa TTCL wanatoa elimu kuhusu huduma na suluhisho mbalimbali za mawasiliano pamoja na teknolojia za kidijitali, huku wakiwawezesha wananchi kujionea uwezo wa intaneti ya kasi ya juu na huduma zinazolenga matumizi ya nyumbani, taasisi na biashara.

Mbali na elimu hiyo, TTCL imeandaa ofa maalum za Sabasaba zinazowawezesha wateja kupata vifaa vya mawasiliano kwa bei zilizopunguzwa pamoja na huduma mbalimbali za kidijitali zinazorahisisha mawasiliano na shughuli za kila siku.

Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Banda la TTCL, Bi. Janeth Maeda, alisema ushiriki wa shirika hilo katika Sabasaba 2026 unalenga kuwasogezea wananchi huduma karibu zaidi, kuongeza uelewa kuhusu bidhaa na huduma za TTCL, pamoja na kuimarisha mahusiano na wateja na wadau.

Alisema maonesho hayo pia yanatoa nafasi muhimu kwa TTCL kupokea maoni na mrejesho kutoka kwa wateja ili kuendelea kuboresha huduma zake na kuendana na mahitaji ya soko la mawasiliano linalokua kwa kasi.

Aidha, wananchi na wadau wanaotembelea banda hilo wanapata fursa ya kutumia huduma ya Public Wi-Fi bila malipo, hatua inayowawezesha kujionea ubora na kasi ya intaneti inayotolewa na TTCL.

TTCL imeendelea kuwahamasisha wananchi kutembelea banda lake katika kipindi chote cha maonesho ili kujionea teknolojia bunifu, kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu huduma za mawasiliano na kunufaika na ofa mbalimbali zilizoandaliwa mahsusi kwa maonesho ya Sabasaba 2026



Lusaka, Julai 8, 2026
AFISA Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel Africa, Sunil Taldar, ametangaza dhamira ya kuunganisha shule 5,000 na mtandao wa intaneti ifikapo mwaka 2027 katika nchi 14 barani Afrika ambapo kampuni hiyo inatoa huduma. Hatua hii inatekelezwa kupitia taasisi yake ya hisani, Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF).

Hadi sasa, mradi huo wa ushirikiano wenye thamani ya dola milioni 57 uliozinduliwa mwaka 2021, umefanikiwa kuunganisha shule 3,296 na kutoa fursa ya mtandao kwa zaidi ya wanafunzi milioni 2 na walimu takribani 40,000. Maeneo 64 ya kujifunzia kwa njia za mtaondao yameondolewa malipo (zero-rated), na kuwawezesha watumiaji zaidi ya milioni 11 kupata maudhui ya elimu bila gharama yoyote.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Shule ya Wasichana ya Mtakatifu Monika (St. Monica) mjini Lusaka, ambayo ni moja ya shule 300 zilizokwishaunganishwa na intaneti nchini Zambia, Afisa Mtendaji Mkuu huyo wa Airtel Africa alieleza kuwa mpango huo una mchango mkubwa katika kuboresha ubora wa elimu kwa kupanua fursa ya kupata rasilimali za kidijitali za kujifunzia kwa watoto wa Afrika, kwa kushirikiana na serikali husika.

Bw. Taldar aliongeza: "Wanafunzi wanapata elimu ya kiwango cha juu kutoka kwenye mtaala ulioandaliwa na UNICEF kwa kushirikiana na Wizara mbalimbali za Elimu, inayopatikana kupitia mtandao wa Airtel. Pia tunawajengea uwezo walimu ili waweze kutumia njia za kidijitali kwa ufanisi kutoa elimu. Lengo letu ni kuendelea kuimarisha upatikanaji wa mtandao wenye tija mashuleni kwa kutoa intaneti ya bure, majukwaa yasiyotozwa gharama za data, na kuwanoa walimu kote barani."

Akitoa shukrani zake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Wasichana ya Mtakatifu Monika (St. Monica), Sr. Matilda Soloko alisema: "Sisi ni miongoni mwa mwa shule za kwanza kabisa kuunganishwa katika awamu ya kwanza na wanafunzi wetu wameweza kusoma kwa kutumia njia za kidijitali kujifunzia na uelewa wao katika masomo umeimarika sana. Tunwashukuru sana Airtel na UNICEF."

Mwakilishi wa UNICEF nchini Zambia, Dkt. Saja Farooq Abdullah alisema: "Ushirikiano wet una Airtel Africa ni kuziba pengo la ujumuishi wa kidijitali. Tunataka kuhakikisha kwamba kila mtoto anaweza kujifunza sehemu yoyote alipo. Kwetu, jambo la kujivunia sana kuona wanafunzi hawa wasichana wanavyoweza kujifunza kwa wakati na kasi yao wenyewe, jinsi wanavyoweza kupitia upya masomo, na jinsi wanavyofanya kazi zao za nyumbani (homework) kwa urahisi."

Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari katika Wizara ya Elimu nchini Zambia, Yvonne Mwemba Chuulu, aliwapongeza UNICEF na Airtel kwa ushirikiano huo akisema: "Sisi kama Wizara ya Elimu hatuwezi kufanya haya peke yetu, na tunashukuru kwa ushirikiano tulio nao na wenzetu wa Airtel Africa na UNICEF. Watoto wetu wana uwezo wa kujifunza kwa mfumo mseto, ambapo tuna mwalimu ambaye pia anatumia vifaa vya kidijitali. Pia tumesikia kutoka kwa wanafunzi kwamba wana uwezo wa kuingia kwenye mifumo ya kidijitali wakiwa nyumbani, jambo ambalo ni zuri kwa sababu wanafunzi wetu wanaendelea kujifunza wakiwa katika mazingira ya majumbani mwao."

Mpango huu wa Kuunganisha Shule unatoa uwanja mpana kwa wanafunzi kujifunza kwa njia za kidijitali katika nchi 13: Chad, Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Gabon, Kenya, Madagascar, Malawi, Niger, Nigeria, Rwanda, Tanzania, Uganda, na Zambia. Kwa kuzipatia shule hizi huduma ya intaneti na kuwapatia walimu mafunzo ya matumizi ya zana za kidijitali, mpango huu unawapa watoto, hasa katika maeneo ya pembezoni mwa miji na ya vijijini, zana na ujuzi wa kidijitali wanaouhitaji ili kufanikiwa.

Taasisi ya Airtel Africa Foundation inaendelea kuboresha maendeleo jumuishi kupitia nguzo nne za kimkakati: Ujumuishi wa Kifedha, Elimu, Uendelevu wa Mazingira, na Ujumuishi wa Kidijitali. Ripoti ya Mwaka ya Airtel Africa Foundation ya 2025/26 inapatikana katika www.airtelafricafoundation.org.

Na. Mwandishi Wetu - Dar es Salaam

SERIKALI imewataka Watanzania kuendelea kulinda na kudumisha amani ya nchi kwa kutambua kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa, huku ikisisitiza kuwa jukumu hilo linamhusu kila mwananchi bila kujali dini, kabila au itikadi za kisiasa.

Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, profesa Palamagamba Kabudi, wakati wa Ibada ya Siku Maalumu ya Wanaume (AMO Big Day) iliyofanyika katika Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA), Mwenge, tarehe 11 Julai, 2026 jijini Dar es Salaam.

Dkt. Nchemba alisema ulinzi wa amani unapaswa kupewa kipaumbele na kuwa ajenda namba moja ya kitaifa kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, unaowezesha wananchi kuishi kwa utulivu, kufanya kazi kwa bidii na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.

Alisema kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda amani kwa kuheshimu sheria za nchi, kuimarisha mshikamano wa kitaifa na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama na utulivu wa nchi.

“Suala la ulinzi wa amani lipewe kipaumbele na kwa kila mmoja liwe ajenda namba moja ya kitaifa. Watanzania wote tutambue kuwa tunao wajibu wa kulinda amani yetu,” alisema.

Aidha, Dkt. Nchemba aliwataka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhamasisha wananchi kudumisha amani, upendo, mshikamano na maadili mema kupitia mafundisho yao.

Alisema viongozi wa dini wana nafasi muhimu katika kujenga jamii yenye umoja na mshikamano, hivyo wanapaswa kuendelea kuhubiri ujumbe wa amani na kuhimiza wananchi kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa taifa.

“Viongozi wa dini endeleeni kuhubiri kuhusu umuhimu wa kudumisha amani na upendo miongoni mwa wanajamii. Ninawasihi sana katika hili, shirikianeni na Serikali kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa na amani na utulivu. Suala la ulinzi wa amani halina mbadala; sote kwa pamoja tuendelee kuweka msisitizo katika kulinda amani ya nchi,” alisema.

Alisema Tanzania imeendelea kujijengea heshima ndani na nje ya nchi kutokana na historia yake ya amani, umoja na mshikamano, hali iliyowezesha kuvutia uwekezaji, kukuza biashara, kuboresha utoaji wa huduma za jamii na kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Nchemba aliwapongeza waumini wa Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA) Mwenge kwa kukamilisha ujenzi wa jengo la kisasa la ibada, akisema ni ushahidi wa imani yao, mshikamano na kujitoa katika kazi ya Mungu.

“Hili ni jambo la kujivunia. Ni alama ya imani yenu thabiti, mshikamano wenu wa kijamii na bidii yenu ya kujitoa kwa kazi ya Mungu,” alisema.








Kamati ya Siasa na Utekelezaji ya CCM Mkoa wa Geita imeridhishwa na mwendo wa ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe.

Jengo hilo lililokwama kwa muda mrefu baada ya mkandarasi kushindwa kumaliza mkataba, sasa linaendelezwa na Halmashauri kupitia force account na limefikia asilimia 68 ya ukamilishaji.

Pesa zilizopokelewa kwa ajili ya mradi huo ni takribani shilingi bilioni 1.8.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa mradi huo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nicholous Kasendamila ameipongeza Halmashauri kwa hatua madhubuti zilizochukuliwa kuhuisha mradi huo.

Amesema kwa sasa mwendo wa ujenzi ni wa kuridhisha.

Mwenyekiti Kasendamila amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kuwa tayari kupokea ushauri na maelekezo kutoka kwa viongozi ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati bila kusuasua.














Families, architects, students and members of the public gathered at dawn on Saturday, 11 July 2026, for a memorial walk honouring the late Beda Amuli, one of Tanzania’s pioneering architects whose work helped shape Dar es Salaam’s built identity.

Organised by Amuli’s family in collaboration with the Architectural Association of Tanzania (AAT), the walk was held under the theme, “Designing Tanzania: Architecture for People, Place, and Purpose.”

The journey began at the Old Boma Building along Sokoine Drive before proceeding, under police and traffic escort, to selected landmarks associated with the city’s architectural history, including the Kilimanjaro Hotel, the Institute of Finance Management, the National Cooperative Building and Kariakoo Market.

AAT President Architect T’Chawi said Amuli did more than design buildings; he created civic spaces where Tanzanians could work, learn, trade and gather.

The walk concluded at Kariakoo Market with reflections, media engagement and closing remarks, followed by a memorial church service at St Alban’s Anglican Church.

Ten years after his passing, Beda Amuli’s legacy remains embedded in Dar es Salaam’s streets, institutions and public spaces, inspiring a new generation to appreciate architecture as national identity and public service.














 


Top News