Na: Calvin Gwabara – Morogoro.

Wakulima wa kilimo cha mpunga kinachotegemea mvua nchini wamewashukuru watafiti wa Mradi wa Mpunga Himilivu kwa Mabadiliko ya Tabianchi na Rafiki kwa Mazingira barani Afrika (CERA) kwa jitihada walizozianzisha kuzalisha mbegu bora ya mpunga unaohimili changamoto za hali ya hewa ili kuinua kipato cha wakulima wa zao hilo Afrika.

Mtafiti mwandamizi kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Dkt. Atugonza Bilaro akifafanua jambo kwa wakulima wakati wa zoezi hilo Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.

Hayo yamebainishwa na wakulima kutoka mikoa ya Morogoro, Shinyanga na Songwe wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za awali na taarifa mbalimbali muhimu zitakazosaidia watafiti hao kuweza kujua changamoto wanazokabiliana nazo katika kilimo hicho ili kuweza kusaidia wao kuzalisha mbegu mpya zilizoboreshwa ambazo zitaweza kuhimili mabadiliko hayo ya tabia nchi.

Ukusanyaji huo wa takwimu umefanyika kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), katika vijiji nane ukishirikisha wakulima wapatao 258.

Akizungumza na watafiti hao mkulima Bwana Maroja Shana kutoka Kijiji cha Silela kata ya Shilela Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Mkoani Shinyanga amesema kuwa ujio wa mradi huo ni ukombozi kwa wakulima wengi wa mpunga nchini ambao wanalima kwa kutegemea mvua na hasa kwenye wilaya yao ambayo zao kubwa la bishara na chakula ni mpunga.

“Zamani tulikuwa tunategemea mvua za msimu ambazo zilikuwa zinanyesha kwa utaratibu unaotabirika, lakini sasa hali imebadilika kabisa maana mvua zinachelewa kuanza au zinanyesha kwa vipindi vifupi sana na kusababisha maji kukosekana mashambani. Hali hii imeathiri sana uzalishaji wangu wa mpunga kwa sababu zao hili linahitaji maji ya kutosha ili likue vizuri. Mara nyingi hulazimika kupanda mara kadhaa bila mafanikio, jambo linaloniongezea gharama na kunipunguzia kipato” alieleza Bwana Shana.

Aliongeza “kutokana na ukame huu wa mara kwa mara, maisha yangu na familia yangu yamekuwa magumu zaidi kwani mavuno yanapopungua, hata chakula cha nyumbani kinakuwa hakitoshi, na wakati mwingine nalazimika kununua chakula ambacho ningepaswa kukizalisha mwenyewe. Pia nashindwa kumudu gharama za pembejeo bora kama mbegu na mbolea, jambo linaloendelea kudidimiza uzalishaji wangu na hali hii inanifanya nitafakari njia mbadala za kilimo, lakini bado nahitaji msaada wa kitaalamu na mbegu bora ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuendelea kujikimu kupitia kilimo cha mpunga”.

Kwa upande wake Zilpa Simchimba, mkulima mwanamke wa mpunga kutoka Wilaya ya Momba Mkoani Songwe amesema kuwa mvua zimekuwa hazitabiriki. Wakati mwingine hazinyeshi kabisa au zinanyesha kwa muda mfupi usiotosha kukua kwa mpunga hali ambayo husababisha mashamba kukauka mapema na kuathiri ukuaji wa zao hilo linalotegemewa sana na familia yake kwa chakula na kipato.

“Nikiwa kama mama, changamoto hizi zinaniumiza zaidi kwa sababu nabeba jukumu la kuhakikisha familia inapata milo ya kila siku na ninapopata mavuno kidogo hulazimika kugawanya chakula kwa uangalifu au wakati mwingine kupunguza idadi ya milo kwa siku ili kukidhi mahitaji ya watoto wangu. Pia huwa nalazimika kuuza sehemu ya mazao kidogo ninayopata ili kukidhi mahitaji mengine muhimu kama ada za shule na huduma za afya, jambo linalozidi kupunguza akiba ya chakula nyumbani” alieleza Zilpa.

Aliongeza “ninaamini kuwa jitihada hizi za watafiti za kutafiti na kuzalisha mbegu za mpunga zinazoweza kuhimili ukame na mabadiliko ya tabia nchi, zinaweza kubadilisha maisha yetu na ya wakulima wengine wanawake, lakini nasisitiza pia tupewe elimu sahihi ya kupambana na changamoto hii wakati tukisubiria kazi hii kubwa waliyoianza watafiti wa mradi huu wa CERA”.

Akizungumza na wakulima wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro wakati wa zoezi la ukusanyaji wa taarifa za awali za utafiti, Mtafiti Mkuu wa Mradi huo wa CERA, Prof. Suzan Nchimbi Msolla kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), amesema kuwa mradi huo unalenga kuimarisha ustahimilivu wa zao la mpunga dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi, hususan ukame, kwa wakulima wa Tanzania na Kenya.

Mtafiti Mkuu wa Mradi huo wa CERA, Prof. Suzan Nchimbi Msolla kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) akizungumza malengo ya zoezi hilo na Mradi wa CERA kwa wakulima wa Mpunga Afrika.

Prof. Msolla ameeleza kuwa miongoni mwa malengo makuu ni pamoja na kupunguza pengo la kijinsia kwa kuwawezesha zaidi wakulima wanawake, hasa wanaoongoza kaya, kupitia uelewa wa mazingira yao na namna jamii zinavyokabiliana na ukame.

“Mradi huu utajikita pia katika kuendeleza mbegu bora za mpunga zinazoweza kuhimili ukame kwa kuingiza sifa za ustahimilivu kwenye mbegu zinazopendwa na wakulima na zinazokidhi mazingira ya ndani. Sambamba na hilo, watafiti watatekeleza mbinu bora za kilimo katika maeneo yenye ukame, ikiwemo matumizi ya upandaji wa moja kwa moja na kilimo cha mzunguko ili kupunguza matumizi ya maji na uzalishaji wa gesi chafuzi na kujenga uwezo wa taasisi za ndani kupitia mafunzo na uwekezaji katika miundombinu ya utafiti” Alifafanua Prof. Msolla.

Kwa mujibu wa Prof. Msolla, matokeo yanayotarajiwa ni pamoja na kuimarika kwa usalama wa chakula na kupungua kwa athari za ukame kwa wakulima, hasa kupitia matumizi ya mbegu zinazostahimili ukame na mbinu bora za kilimo.

Aidha amesema mradi huo utachangia kuongeza uzalishaji na kipato kwa wakulima, huku ukipunguza matumizi ya maji na kulinda mazingira. Pia, mradi utaimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika utafiti wa mpunga na kusaidia taasisi za ndani kuwa na uwezo endelevu wa kufanya tafiti na kuzalisha teknolojia zitakazowanufaisha wakulima kwa muda mrefu.

Mradi huu unatekelezwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mpunga (IRRI), Shirika la Utafiti wa Kilimo na Mifugo Kenya (KALRO), na Chuo Kikuu cha Copenhagen kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Denmark (DANIDA).

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA ZOEZI HILO LA UKUSANYAJI WA TAKWIMU

Mtafiti Mkuu Msaidizi wa mradi huo Dkt. Emanuel Malisa akizungumza na wakulima kuhusu zoezi hilo la ukusanyaji wa takwimu linavyofanyika.

Wakulima wa kilimo cha mpunga kinachotegemea Mvua wakifuatilia maelezo ya watafiti kabla ya kuanza zoezi la udodosaji.

Mtafiti kutoka SUA Bi. Rehema Mollel akizungumza na mkulima wa mpunga kwenye kijiji cha Madoto Wilayani Kilosa.

Mtafiti Mkuu wa Mradi wa CERA, Prof. Suzan Nchimbi Msolla, Mtafiti kutoka TARI Dkt. Atugonza Bilaro na Mtafiti Mkuu Msaidizi wa mradi huo Dkt. Emanuel Malisa wakiwa kwenye majadiliano na wakulima kupata taarifa.




 

 

DAR ES-SALAAM:


Hospitali ya kumbukumbu ya Dr Ole Lengine, Dr Ole Lengine Memorial Hospital iliyopo Kibamba jijini Dar EsSalaam imezindua gari maalumu la kisasa la kubebea wagonjwa(Ambulance) ili kutatua changamoto zinazowakabili wagonjwa wasiojiweza katika eneo hilo na maeneo ya jirani.

Awali akizungumza na waandishi wa habari, wageni na wananchi waliofika hospitalini hapo kushuhudia uzinduzi huo, Mchungaji Ezekiel Ngao amesema ujio wa gari hilo ni sehemu ya kuimarisha vita dhidi ya maradhi na afya kwa binadamu na kurejesha tumaini jipya kwa wale waliokata tamaa.

“wagonjwa wengi wanapoteza maisha kwa kukosa huduma stahiki ya dharura kabla ya kufika hospitalini na mara nyingi hutokana na kukosa gari maalum la wagonjwa lenye fifaa tiba, madawa na watoa huduma ya dharura ya kiafya” Mchungaji Ngao amesema hayo mara baada ya kuongoza zoezi zima la uzinduzi huku akitoa wito kwa serikali kuisaidia sekta binafsi wanaowekeza katika eneo la afya kwani wanachangia sana uzalishaji wa nguvu kazi ya taifa la sasa la kesho.

Dr Felister Kimolo ni mmoja kati wajumbe toka sekta ya afya waliohudhuria tukio la uzinduzi wa gari hilo ambapo amesema gari hilo litasaidia sio tu wagonjwa wanaofika hospitalini hapo bali pia wale wanaotoka katika vituo vya afaya vya jirani, wajumbani na wale wanaopata ajali katika mikoa ya jirani na kwingineko kulingana na mahitaji ya huduma hiyo kwa wakati huo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Dr Ole Memorial Hospital, Betha Emmanuel amesema ujio wa gari hilo ni sehemu ya kuiunga mkono serika katika jitihada zake za kusogeza karibu huduma za kiafya kwa wananchi na kwamba gari hilo litasaidia kutoa huduma ya dharura katika maeneo yanayopatwa na majanga mbalimbali kama moto, mafuriko na ajali.

Naye Mkurugenzi Mtendaji (CEO) wa hospitali hiyo Dr Emmanuel Ole Lengine amesema hospitali hiyo itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali kupitia sekta ya afya katika kuboresha huduma za afya ambapo baada ya gari hilo, ni mwanzo wa maandalizi ya uboreshaji wa huduma zingingine za dharura yaani Emergency service. Dr Emmanuel amesema hayo huku akielekeza msisitizo kwa wauguzi hususani wa kitengo cha huduma ya dharura (Emergency) kuwa sehemu ya matumaini kwa wagonjwa wanafika kupata huduma hiyo.
Mchungaji Ezekiel Ngao akikata utepe kuashiria kuzindulia rasmi kwa gari maalum la kisasa la kubebe wagonjwa katika hospitali ya kumbukumbu ya Dr Ole Lengine.

(Kushoto kwake ni CEO wa Hospitali hiyo Dr Emmanuel Ole Lengine, katikati ni Dr Felister Kimolo kutoka manispaa ya Ubungo na kulia ni Mkurugenzi wa Dr Ole Lengine Memorial Hospital, Bertha Emmanuel.
C.E.O wa Dr Ole Lengine Memorial Hospital Dr Emmanuel Ole Lengine katikati akiongea na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa gari maalum la kisasa la kubebea wagonjwa.

Kulia ni Dr Felister Kimolo kutoka manispaa ya ubungo na kushoto ni Mkurugenzi wa Dr Ole Lengine Memorial Hospital Bertha Emmanuel.

Dar es Salaam.

‎Zaidi ya Bilioni 517 zimeelekezwa kuboresha miundombinu ya barabara Mkoa wa Dar es Salaam kupitia Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) hatua inayolenga kuondoa changamoto ya usafiri na kukuza ukuaji wa uchumi.

Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi Geofrey Mkinga ameeleza kuwa mradi huo umekuwa na manufaa makubwa kwa kuwa  sehemu ya utatuzi wa changamoto ya miundombinu ya barabara mkoani humo.

‎‎Amesema kuwa serikali kupitia TARURA inaendelea na maboresho na matengenezo ya barabara zenye urefu wa Km 250 kwa kiwango cha lami katika wilaya zote tano (5) za mkoa wa Dar es Salaam ambazo zinagharimu shilingi Bilioni 516 ili kuchochea shughuli za kiuchumi na biashara ndani ya mkoa.

‎‎"TARURA mkoa wa Dar es Salaam tuna mtandao wa barabara Km 5057 kati ya hizo lami ni Km 677 sawa na asilimia 13 huku barabara za udongo zipo zaidi ya Km 2500 sawa na asilimia 50 ya mtandao wote, ujenzi wa barabara za lami zitapunguza barabara za udongo ili kuboresha huduma za usafiri na usafishaji, kupunguza foleni na changamoto za mafuriko, kuongeza ajira na kuchochea ukuaji wa biashara na uchumi", alisema. ‎

‎Aliongeza kuwa pamoja na changamoto ya mvua lakini kazi zinaendelea vizuri ili zikamilike kwa wakati ambapo utekelezaji umefikia zaidi ya asilimia 80 huku wanatarajia barabara nyingi zitakamilika na kuanza kutumika mwezi Agosti hadi Oktoba 2026 mpaka mwezi Aprili 2027.

‎  ‎"Barabara ya Banana hadi Kivule, barabara ya Mbezi Msumi zilikuwa na kilio kikubwa kutoka kwa wananchi mpaka ifikapo mwezi 8 mpaka wa 10 barabara hizi zitakamilika, katikati ya mji Kariakoo ambapo ni eneo la kibiashara barabara nyingi zilikuwa hazipitiki zina matope, maboresho yanaendelea na maeneo mengine mengi ndani ya mkoa wetu maboresho yanaendelea", alisema.

‎Amewaomba wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho ujenzi unaendelea na miundombinu hiyo itakapokamilka wananchi wawe walinzi na watunzaji wa miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

‎Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa mkoa huo wameishukuru serikali kwa kuboreshewa miundombinu ya barabara katika maeneo mbalimbali ambapo wamesema miundombinu hiyo ikikamilika itaboresha shughuli za usafiri na usafirishaji na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii.






Na Diana Byera,Bukoba.


SERIKALI imetoa Sh. 16 kwa ajili ya kufanya maboresho ya upanuzi na njia za kusambaza umeme kwenye kituo cha kupokea,kupoza na kusambaza umeme cha Kibeta wilayani Bukoba mkoani Kagera.

Kituo hicho kinahudumia wilaya ya Bukoba,Missenyi na Muleba kwa lengo la kuongeza ufanisi wa upatikanaji wa umeme katika mkoa wa Kagera

Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Kagera Mhandisi Tawakal Rwahila amesema mradi wa upanuzi wa kituo cha Kibeta umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 30 mwaka huu.

Amefafanua kituo hicho kilijengwa mwaka 1993 kikiwa na uwezo wa megawati 20, lakini kutokana na ongezeko kubwa la mahitaji ya umeme kwa wananchi na shughuli za kiuchumi, Serikali ilianza rasmi mradi wa upanuzi mwaka 2023 kwa lengo la kuongeza uwezo hadi kufikia megawati 120.

Akieleza maendeleo ya mradi huo, Mhandisi Rwahila amesema tayari vifaa muhimu vimewasili na vinaendelea kufungwa, ikiwa ni pamoja na vivunja umeme (circuit breakers) vya kisasa, njia ya ziada ya usambazaji (feeder), pamoja na transfoma inayopunguza msongo wa umeme kutoka kilovolti 33 hadi kilovolti 11.

“Kwasasa majaribio ya awali ya mfumo yanaendelea, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea kukamilika kwa mradi huo kwa wakati uliopangwa.”

Mradi huo unatekelezwa na mkandarasi TBEA kutoka nchini China, ambaye anaendelea na usimikaji wa miundombinu kwa viwango vinavyolenga kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye ya umeme katika mkoa wa Kagera.

Akieleza zaidi amesema kukamilika kwa kituo hicho kutaongeza uwezo wa usambazaji wa umeme pamoja na kupunguza changamoto ya ukatikaji wa umeme katika wilaya za Bukoba, Missenyi na Muleba huku akitaja kuwa hiyo ni Fursa ya kipekee kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika Fursa ya viwanda.

“Katika kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025, TANESCO imefanikiwa kusambaza umeme katika vijiji vyote 664 vya mkoa wa Kagera.Vitongoji 3,000 tayari vikiwa vimeunganishwa na huduma hiyo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha umeme unafika hadi ngazi ya vitongoji, na mradi wa Kibeta ni sehemu muhimu ya kufanikisha azma hiyo.”







Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Katika hotuba yake ya mapito na mwelekeo wa kazi za Serikali kwa mwaka 2026/27 iliyowasilishwa leo Bungeni, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesisitiza juhudi za Serikali za kuhakikisha upatikanaji wa nishati endelevu unasaidia ukuaji wa kiuchumi na kijamii nchini.

Dkt. Nchemba ameeleza kuwa nishati ya umeme ni kichocheo kikubwa cha maendeleo, hasa katika viwanda, teknolojia na matumizi ya nyumbani. Kutokana na mikakati ya Serikali, miradi mbalimbali ya uzalishaji wa umeme, ikiwemo ujenzi wa bwawa la Julius Nyerere kwa kutumia fedha za ndani, imekamilika na sasa nchi ina ziada ya umeme. 

Aidha, Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa umeme ili kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme na kuunganisha wilaya ambazo hazipo kwenye gridi ya Taifa.

Waziri Mkuu ameelekeza Wizara ya Nishati kuhakikisha upatikanaji wa umeme katika vitongoji, hospitali, vituo vya afya, zahanati, shule, taasisi za dini na visima vya maji. Vilevile, amesisitiza ushirikiano na Wizara ya Fedha kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa mradi wa Gridi Imara zinatolewa kwa wakati ili kuondoa tatizo la kukatika kwa umeme.

Mbali na umeme, Serikali imeongeza matumizi ya gesi asilia, ambapo kutoka Julai 2025 hadi Februari 2026, mtandao wa usambazaji wa gesi umeongezeka kutoka kilomita 184.8 mwaka 2024/25 hadi kilomita 243.6. Vituo 14 vya kujaza gesi asilia vilivyokamilika vinatoa huduma kwa viwanda, taasisi na nyumbani.

Dkt. Nchemba pia ameeleza kuwa licha ya changamoto za kiusalama kikanda na kimataifa, Serikali inaendelea kusimamia upatikanaji wa bidhaa za mafuta na kuhakikisha bei zao zinabaki himilivu. 

Serikali pia inaendeleza miradi ya kuongeza uwezo wa kuhifadhi mafuta, ikiwemo ghala lenye uwezo wa kupokea tani 308,110 katika Bandari ya Dar es Salaam, ambalo sasa limefikia asilimia 30 ya ujenzi, na kuongeza uwezo wa Bandari ya Mtwara kutoka tani 29,280 hadi tani 110,221.


-Kwa mwaka 2026/2027, Serikali itazingatia:

Kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kukidhi mahitaji ya nishati.

Kusambaza umeme katika vitongoji ambavyo havijapatiwa huduma.

Kuendeleza shughuli za kutafuta, kusafirisha, kuhifadhi na kusambaza mafuta na gesi asilia.

Kukamilisha mpango wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika taasisi.



Kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hata hivyo Dkt.WIGULU amesema kuwa jitihada hizo za Serikali zinalenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za nishati na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.





 Na Said Mwishehe,Michuzi TV

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limefanyika ziara ya kutembelea Kituo cha Kupoza Umeme cha Ifakara wilayani Kilombero mkoani Morogoro ambacho kimejengwa na Wakala wa Umeme Vijijini(REA) huku ikielezwa uwepo wa Kituo hicho umepeleka mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika ziara hiyo leo Machi 31,2026 , Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyoba, ameeleza kwamba  kituo hicho kimemaliza changamoto ya kukatika kwa umeme iliyokuwa ikizorotesha shughuli za uzalishaji na huduma za kijamii.

Ameongeza Serikali inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia REA imetoa Sh. bilioni 25 kugharamia ujenzi wa kituo hicho.Umeme unaozalishwa na kituo hicho ni megawati 18 na kati ya hizo saba ndio zinatimika.

Amefafanua umeme wa uhakika umefungua fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali ndani ya Wilaya hiyo.”Nitumie Jukwaa hili la Wahariri kuwakaribisha watu kuja kuwekeza.”

Kwa upande wakeMwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, amepongeza uwekezaji huo ambapo amefafanua unaonesha matumizi sahihi ya rasilimali za umma na mchango wa REA katika kusambaza umeme vijijini.

Amesisitiza REA wamefanya kazi kubwa ya kupeleka umeme vijijini na kwa sasa hakuna Mwananchi anayetoa rushwa kwa ajili ya kupatiwa nguzo TANESCO na hiyo imetokana na REA kuweka mikakati ya kuhakikisha nguzo za umeme zinapelekwa katika vijiji na sasa katika vitongoji.

Awali Meneja wa Usimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, amesema mradi huo umegharimu Sh.bilioni 25, ukihusisha pia ujenzi wa njia za kusafirisha umeme za msongo wa kilovolti 33 zenye urefu wa kilometa 70 pamoja na huduma za ushauri elekezi.

“Kituo hiki kimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Kilombero na Ulanga kwa kuondoa changamoto ya upatikanaji wa umeme na kuwezesha shughuli za kiuchumi kama kilimo na uchimbaji madini,” alisema.




Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Serikali imeweka wazi mwelekeo wake wa maendeleo kwa kusisitiza kuwa Mpango na Bajeti ya mwaka 2026/2027 ni hatua ya mwanzo katika utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/2027–2030/2031), unaolenga kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Waziri Mkuu Dkt MWIGULU Nchemba ameyabainisha hayo leo Bungeni Dodoma wakati akiwasilisha hotuba ya mapito na mwelekeo wa kazi za Serikali, Makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2026/27 ambapo amesema kuwa utekelezaji wa Dira 2050 unakusudia kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050, huku wastani wa pato la mtu mmoja mmoja ukitarajiwa kufikia dola 7,000 kwa mwaka.

Amesisitiza kuwa Dira 2050 ndiyo dira kuu ya maendeleo ya Taifa, hivyo mafanikio yake yanategemea ushiriki wa wadau wote. Waziri Mkuu aliwataka viongozi wa Serikali, taasisi za dini, sekta binafsi, asasi za kiraia pamoja na wadau wa maendeleo kuhakikisha mipango yao inaendana na vipaumbele vya Dira hiyo. Aidha, aliielekeza Tume ya Mipango kuendelea kutoa elimu kwa umma ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.

Katika hatua nyingine, Serikali imeendelea kuimarisha uchumi unaoongozwa na sekta binafsi. Katika mwaka 2025/2026, jumla ya miradi 927 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 11.08 ilisajiliwa, hali inayoashiria kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji na kuongezeka kwa imani ya wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wa kilimo, Serikali imefanikiwa kuimarisha uzalishaji wa chakula na kuhakikisha usalama wa chakula nchini. Taarifa zinaonesha kuwa tani 23,783,128 za mazao zilizalishwa katika msimu wa 2024/2025, kiwango kinachozidi mahitaji ya tani 18,279,054 kwa mwaka 2025/2026, hivyo kuifanya nchi kuwa na uhakika wa chakula kwa asilimia 130.

Ongezeko hilo limetokana na upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, hususan mbolea inayotolewa kwa ruzuku. Katika msimu wa kilimo wa 2025/2026, Serikali imetoa tani 1,098,990 za mbolea, sawa na asilimia 73.26 ya lengo. Kati ya hizo, tani 574,664.99 zenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.03 zimesambazwa kwa wakulima zaidi ya 526,000 kupitia mpango wa ruzuku, hatua iliyochochea matumizi ya pembejeo na kuongeza tija ya uzalishaji.

Kwa ujumla, Serikali inaonesha dhamira ya dhati ya kuijenga Tanzania yenye uchumi imara, unaojitegemea na unaotoa fursa kwa wananchi wake wote kupitia utekelezaji madhubuti wa Dira 2050.




LIGI kuu ya Hispania yaani LALIGA inazidi kupamba moto huku wakali wa ubashiri leo watakupatia uchambuzi wa Atletico Madrid ambao wameuwa na fomu nzuri msimu huu na uwezekano wa kuondoka na taji lolote msimu huu.

Timu huu ambayo ipo chini ya kocha mkuu Diego Simeone wamaeendelea kuwa moja ya timu zenye heshima kubwa barani Ulaya, lakini msimu wao wa sasa unaonyesha wazi kuwa wako kwenye kipindi cha mpito kati ya ubora wa zamani na ushindani wa kisasa.

Atletico Madrid imejijengea utambulisho wa uimara wa kujilinda na nidhamu ya hali ya juu, lakini changamoto zinazoikabili sasa zinaonyesha wazi kuwa mfumo huo unahitaji maboresho ili kuendana na kasi ya mpira wa leo.

Kwenye LaLiga, Atletico Madrid wamekuwa wakipambana kubaki kwenye nafasi za juu ambapo hadi sasa wapo nafasi ya 4 baada ya kukusanya pointi zao 57 kwenye michezo 29 ambayo wamecheza na wakiwa nyuma kwa pointi 16 kwa kinara wa ligi.

Wapo nyuma ya vigogo kama Real Madrid na Barcelona, jambo linaloonyesha pengo lililopo katika consistency. Mara nyingi wanapoteza pointi muhimu dhidi ya timu ndogo hili ndilo tatizo kubwa linalowafanya washindwe kusimama kama wagombea halisi wa taji. Ugenini wamekuwa wakionyesha udhaifu mkubwa, tofauti na uimara wao wanapocheza nyumbani.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Timu hiyo ina wachezaji wazuri sana ambao hufanya vyema kwenye mechi kubwa na safari hii imeongeza wachezaji kama Ademola Lookman ambaye ataenda kusaidiana na kina Solorth, Giuliano Simeone, Koke na wengine kibao.

Julian Alvarez ambaye pia alijiunga na timu hiyo amekuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi hicho, lakini pia ni mchezaji ambaye anahitaji sana na baadhi ya timu kutoka Uingereza ikiwemo, Chelsea, Arsenal na zingine. Lakini mpaka sasa bado mustakabali wake hujajulikana.

Kwa upande wa Antoine Griezman naye pia amekuwa na mchango mkubwa kalbuni hapo lakini anaondoka mwishoni mwa msimu huu na tayari amesaini mkataba wa kuitumikia Orlando City ya Marekani hivyo Madrid watajitaji kusaka mchezaji mwingine kuziba pengo hilo.

Simeone na vijana wake kwenye mashindano ya Copa del Rey wamefanikiwa kufika hatua ya Fainali baada ya kumtoa Barcelona na watakipiga dhidi ya Real Sociedad April 18, hili ni Kombe ambalo wanalitaka kwa hali na mali kutokana na ushindano uliopo kwenye mashindano mengine. Je Atletico watabeba Kombe hili?. ODDS KUBWA izpo Meridianbet ingia na ubeti sasa.

Atletico Madrid kwenye ligi ya Mabingwa Ulaya yaani UEFA Champions League, wameendelea kufanya vizuri ambapo mpaka sasa wapo hatua ya Robo Fainali na wamepangwa kucheza dhidi ya FC Barcelona hivyo badi Simeone ana kibarua kizito kabisa mbele ya vijana wa Hans Flick.

Ni mechi ngumu kabisa lakini pia kama wakichanga karata zao vizuri wanaweza wakaibuka na ushindi kwani hii si mara ya kwanza kukutana hawa wawili. Je unadhani Barca watakubali kutolewa kwenye UEFA?. Bashiri hapa.

Kwa ujumla, Atletico Madrid ni timu ambayo bado ina uwezo wa kushindana katika mashindano yote, lakini imekosa ule uthabiti wa kuwa mabingwa. Ili kurejea kileleni, wanahitaji kuongeza ubunifu katika safu ya ushambuliaji, kupunguza utegemezi kwa mchezaji mmoja, na kubadilika kimfumo ili kuendana na mahitaji ya soka la kisasa. Bila kufanya hivyo, wataendelea kubaki kwenye kundi la timu bora lakini si mabingwa wanaotawala.

 

Mabadiliko ya bei za mafuta nchini kwa mwezi Aprili 2026 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na vita inayoendelea kati ya Marekani kwa kushirikiana na Israeli dhidi ya Irani iliyoanza tarehe 28 Februari 2026, mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema jana.

“Kushambuliwa kwa visima vya mafuta, maghala ya kuhifadhi mafuta na viwanda vya kusafisha mafuta (refineries) pamoja na Irani kufunga Lango la Hormuz linalopitisha takriban asilimia 20 ya mafuta yanayosafirishwa kwenda kwenye masoko mbalimbali duniani, imeathiri hali ya uzalishaji mafuta kwenye nchi za Mashariki ya Kati ambako Tanzania inaagiza kwa kiasi kikubwa; imeongeza gharama za usafirishaji kutokana na kukosekana kwa meli za kusafirisha mizigo na imeongeza gharama za bima za meli za mizigo kutokana na vita,” imeeleza taarifa iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari jana.

Kwa mwezi Aprili 2026, gharama za kuagiza mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es Salaam zimeongezeka kwa wastani wa asilimia 15.3 kwa mafuta ya petroli na asilimia 10.8​ kwa mafuta ya dizeli na hakuna mabadiliko ya gharama kwa mafuta ya taa.

EWURA imesema ongezeko hilo ni janga la kidunia na Tanzania kama sehemu hiyo inachukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa upatikanaji wa mafuta nchini na bei himilivu ili kupunguza madhara ya kiuchumi na kijamii. Kutokana na hali hiyo, EWURA imewashauri wananchi kutumia mafuta kwa uangalifu na ufanisi mkubwa.


KWA wengi, Jumatano ni katikati ya wiki yenye pilikapilika za kawaida, lakini kwa Meridianbet, siku hii imebadilika kabisa na kuwa jukwaa la ndoto na zawadi. Kupitia kampeni maalum ya Jumatano ya Zawadi, kila mchezaji sasa ana sababu mpya ya kutazamia siku hii kwa hamu, kwani ushindi hauishii kwenye pesa pekee bali unaenda mbali zaidi.

Utaratibu wake ni mwepesi kueleweka na unavutia kujaribu. Unachotakiwa kufanya ni kubashiri tiketi yenye angalau mechi tatu kuanzia Jumatano hadi Jumanne ya wiki inayofuata, na hapo hapo unakuwa umeingia moja kwa moja kwenye droo ya kila wiki. Hakuna hatua za ziada wala masharti magumu, ni kubashiri tu kama kawaida na kusubiri bahati yako iangaze.

Meridianbet wanakupa jukwaa pana la kubashiri, mechi kali za kimataifa hadi michezo ya kasino mtandaoni iliyojaa burudani. Ukiwa na odds zenye ushindani mkubwa, kila tiketi inakuwa na thamani zaidi. Jiunge sasa kupitia tovuti yao au piga *149*10#.

Kivutio kikubwa zaidi ni zawadi zenyewe. Kila Jumatano, washindi wanapata nafasi ya kujinyakulia simu mpya kabisa ya Samsung A26, na jumla ya washindi wanne kila mwezi. Hii si tu zawadi ya kawaida, bali ni kifaa kitakachokupa kumbukumbu ya ushindi wako kila siku.

Kadri unavyoongeza idadi ya tiketi na kupanga mikeka yako kwa umakini, ndivyo unavyoongeza nafasi zako za kushinda. Hii inaifanya Jumatano ya Zawadi kuwa zaidi ya promosheni, ni fursa ya kimkakati kwa kila mchezaji mwenye ndoto ya kushinda. Meridianbet wameifanya Jumatano kuwa siku ya matumaini, furaha na zawadi kwa kila anayethubutu kujaribu bahati yake.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma, amesema kuwa ushirikiano kati ya WCF na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) utasaidia kupunguza ajali za barabarani na kulinda nguvu kazi ya Taifa.Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ushirikiano (MoU) iliyofanyika tarehe 31 Machi 2026 jijini Dar es Salaam, Dkt. Mduma alisema kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha usalama barabarani pamoja na kuongeza uelewa kwa madereva ambao ni wadau wakuu wa Mfuko huo.

“Ushirikiano huu utatuwezesha kuimarisha usalama barabarani na kuongeza uelewa kwa madereva, ambao ni sehemu muhimu ya wadau wetu,” alisema Dkt. Mduma.

Alieleza kuwa WCF ilianzishwa kwa lengo la kushughulikia fidia kwa wafanyakazi wanaopata ajali au magonjwa yatokanayo na kazi, lakini tathmini zinaonesha kuwa sehemu kubwa ya madai yanatokana na ajali za barabarani, hali inayohitaji juhudi za pamoja kupambana nayo.

“Sehemu kubwa ya madai tunayopokea yanatokana na ajali za barabarani, hivyo kuna umuhimu wa wadau kushirikiana kupunguza tatizo hili,” aliongeza.
Akizungumza zaidi, Dkt. Mduma alisema kuwa kupitia mkataba huo, taasisi hizo mbili zitashirikiana katika maeneo muhimu ikiwemo utoaji wa mafunzo na elimu kuhusu usalama wa usafirishaji, kufanya tafiti, kubadilishana taarifa pamoja na kujengeana uwezo wa kitaalamu.

“Makubaliano haya yatajikita katika mafunzo, tafiti, ubadilishanaji wa taarifa na kujengeana uwezo wa kitaalamu ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi,” alisema.

Aidha, alibainisha kuwa ushirikiano huo utaongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kila taasisi na kusaidia kufikia malengo ya pamoja ya kupunguza ajali pamoja na kuboresha ustawi wa wafanyakazi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Mhandisi Dkt. Prosper Mgaya, pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji waliokuwepo, walishuhudia utiaji saini wa makubaliano hayo ambayo yanatarajiwa kuleta mageuzi chanya katika sekta ya usafirishaji nchini.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo LATRA, Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani, TANROADS, TARURA, pamoja na vyama vya wamiliki wa mabasi na malori.



 

Mbeya- Jumanne, Machi 31, 2026


Katika kuadhimisha miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Kampasi ya Mbeya imefanya shughuli za kijamii, ikiwemo kutembelea na kutoa misaada kwa vituo viwili vya watoto yatima jijini Mbeya.

Shughuli hiyo imehusisha watumishi wa chuo hicho wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, pamoja na Mkurugenzi wa Kampasi ya Mbeya, Ndugu Saidy Nzagamba. Vituo vilivyotembelewa ni Kituo cha Watoto Yatima Iwambi kilichopo mtaa wa Iwambi na Kituo cha Bi Aisha Foundation kilichopo mtaa wa Soweto.

Katika ziara hiyo, TPSC Kampasi ya Mbeya imekabidhi mahitaji mbalimbali kwa ajili ya watoto hao, yakiwemo mchele, maharage, sabuni, juisi, mafuta ya kupikia, vitunguu, na mbuzi kwa ajili ya lishe na mahitaji ya kila siku.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Itunda, aliipongeza TPSC kwa maadhimisho yenye dhamira ya kugusa maisha ya watu. Alisema hatua hiyo inaonyesha utu na maadili ya utumishi wa umma yanayojengwa na chuo hicho.

"Chuo hiki kimeendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa taifa letu kwa kutoa watumishi bora. Kila kinachofanywa hapa kinaonyesha dhamira ya kweli ya kuwahudumia wananchi na kujenga jamii yenye mshikamano," alisema Mhe. Itanda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampasi ya Mbeya, Ndugu Saidy Nzagamba, alisema chuo hicho kimeamua kushiriki na kusaidia watoto yatima kama sehemu ya kuwajengea faraja na kuwahakikishia kuwa jamii inawajali.

"Tunatambua changamoto wanazokabiliana nazo watoto hawa, ndiyo maana tumeamua kuwa jirani nao na kuwagusa kwa upendo. Huu ni mwanzo wa dhamira yetu kuendelea kushiriki shughuli za kijamii katika siku zijazo," alisema Nzagamba.

Viongozi wa vituo vya Iwambi na Bi Aisha Foundation waliushukuru uongozi wa TPSC Kampasi ya Mbeya kwa upendo na michango iliyotolewa, wakisema misaada hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa katika malezi na ustawi wa watoto.





















Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) iliyopo jijini Dodoma, inatarajia kuhitimisha rasmi maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake kwa kufanya harambee maalum ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu ya upandikizaji uloto na figo kwa wananchi wenye uhitaji.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Abel Makubi, amesema kuwa maadhimisho hayo yalianza Oktoba 13, 2025, na yatahitimishwa Mei 8, 2026, baada ya kudumu kwa takribani miezi saba.

Prof. Makubi amesema kuwa lengo kuu la maadhimisho hayo ni kuhamasisha wadau kushiriki katika harambee itakayolenga kukusanya shilingi bilioni 7 ndani ya kipindi cha miaka miwili. Fedha hizo zitatumika kusaidia matibabu ya wagonjwa 100, ambapo 50 ni watoto wenye ugonjwa wa selimundu wanaohitaji upandikizaji wa uloto, na wengine 50 ni wagonjwa wa figo.

Ameeleza kuwa gharama za matibabu hayo ni kubwa, hivyo hospitali imeona umuhimu wa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) pamoja na taasisi nyingine ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hizo muhimu.

Kwa mujibu wa Prof. Makubi, hospitali hiyo kwa sasa inahudumia takribani wananchi milioni 10 kutoka mikoa nane ya Tanzania, na imeanza pia kupokea wagonjwa kutoka nje ya nchi kama sehemu ya kukuza utalii wa matibabu.

Ameongeza kuwa hospitali hiyo ina jumla ya watumishi 1,173, wakiwemo madaktari bingwa zaidi ya 100, na kwa sasa inatoa huduma 20 za kibingwa pamoja na huduma 18 za ubingwa bobezi.

Katika hatua nyingine, Prof. Makubi amesema BMH ina mipango ya kuanzisha miradi ya kimkakati ikiwemo vituo vya umahiri katika matibabu ya saratani, upanuzi wa huduma za upandikizaji uloto, pamoja na kuanzisha taasisi maalum za macho, moyo, na upasuaji wa ubongo na mifupa ndani ya miaka mitano ijayo.

Amesema lengo ni kuifanya hospitali hiyo kuwa kitovu cha utalii wa matibabu nchini na barani Afrika.

Katika kilele cha maadhimisho hayo, mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Sambamba na hilo, hospitali imepanga kufanya kongamano la kisayansi Mei 6, 2026, litakalowakutanisha wataalam wa afya, hususan katika masuala ya upandikizaji wa viungo.

Prof. Makubi ametoa wito kwa taasisi za afya, wadau wa maendeleo na wafadhili kujitokeza kwa wingi kuunga mkono juhudi hizo ili kusaidia kuokoa maisha ya wananchi wenye uhitaji wa matibabu hayo ghali.

BMH Kuadhimisha Miaka 10 kwa Harambee ya Bilioni 7 Kuboresha Huduma za Upandikizaji Uloto na Figo



 


Top News