Aidha, Dkt. Samia alisema: “Serikali imezindua skimu ya hifadhi ya jamii ili kuhakikisha wananchi waliojiajiri wanajumuishwa katika mfumo wa hifadhi ya jamii.”
.jpeg)

MichuziBlogV2
Most read Swahili blog on earth
Bonyeza play kuangalia Michuzi TV LiVE
BONYEZA PLAY KUANGALIA AZAM TV LIVE
BONYEZA KUANGALIA CHANNEL TEN LIVE
.jpeg)




Na Mwandishi Wetu.
WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameshiriki katika semina kuhusu Mpango Mkakati wa Gridi ya Maji ya Taifa.
Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa Bunge wa Msekwa,Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri katika mada yake amesema Gridi ya Maji ya Taifa ni mfumo wa kimkakati wa usambazaji maji kutoka kwenye vyanzo vya uhakika na kuyapeleka katika maeneo yenye uhaba wa maji nchini.
Ameongeza hadi sasa Wizara ya Maji imekamilisha vipande vya mtandao wa Taifa wa maji ikiwamo kutoa maji ziwa Victoria kwenda mikoa ya Shinyanga, Tabora na Shelui katika mkoa wa Singida.
Kwa upande wake Waziri wa Maji Jumaa Aweso akihitimisha mada amewaomba ushirikishwaji wa jamii na ushirikiano kwa wabunge wote ili kuhakikisha mpango mkakati wa Gridi ya Maji ya Taifa unafanikiwa ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ya majisafi na salama na kuchochea ukuaji wa uchumi ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo (DIRA 2050).
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Peter Majule, ameibua mjadala bungeni kuhusu uwazi na haki katika biashara ya kaboni, akitaka serikali kueleza mikakati iliyopo kuhakikisha wananchi wa chini, hususan wanawake na vijana, wananufaika ipasavyo.
Akizungumza Bungeni Jijini Dodoma, Dkt. Majule alitaka kujua ni viashiria gani na mfumo gani serikali imeweka kuhakikisha makisio ya mapato yanayotokana na misitu na ardhi ya wananchi yanazingatiwa kwa usahihi katika biashara hiyo inayohusisha wawekezaji.
Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Festo Dugange, alikiri kuwepo kwa changamoto za ukosefu wa uwazi katika vipimo na malipo ya biashara ya kaboni kutokana na ushirikiano kati ya wadau mbalimbali.
Dugange alieleza kuwa serikali imeanza hatua za makusudi za kuboresha mfumo huo kupitia uanzishwaji wa kituo maalum cha kuratibu biashara ya kaboni kilichopo Morogoro, ambacho kinatarajiwa kuhamishiwa Dodoma.
Alisema kituo hicho kitashirikiana na wadau na serikali kuhakikisha vipimo sahihi vya kaboni vinapatikana na wananchi wananufaika moja kwa moja kulingana na kiwango halisi cha kaboni kinachozalishwa katika maeneo yao.
KUNDI la Kimataifa la Vijana wa Amani (IPYG) limeendesha programu jumuishi ya amani na usalama katika eneo la Mwenge, jijini Dar es Salaam, Aprili 2026, chini ya kaulimbiu “Elimisha Amani, Hakikisha Usalama: Ibara ya 10 ya DPCW.” Mpango huo uliunganisha shughuli za uhifadhi wa mazingira na mafunzo ya vitendo ya usalama, ukiwa na lengo la kukuza utamaduni wa amani sambamba na kuimarisha ustahimilivu wa jamii
Azimio la Amani na Kusitishwa kwa Vita (DPCW) ni mfumo wa kimataifa unaobainisha misingi ya kumaliza vita na kuendeleza amani endelevu, ambapo Ibara ya 10 inasisitiza umuhimu wa kueneza utamaduni wa amani.
Kama sehemu ya programu hiyo, zoezi kubwa la plogging lilifanyika katika Makutano ya Mwenge na Kituo Kipya cha Mabasi cha Mwenge. Zaidi ya vijana 300 pamoja na wakazi wa eneo hilo walishiriki kukusanya na kuchambua taka, hatua iliyochangia kuboresha mazingira ya eneo hilo.
Sambamba na usafi huo, kulifanyika kampeni ya uhamasishaji wa umma inayozingatia Ibara ya 10 ya DPCW chini ya kaulimbiu “Elimisha Amani, Hakikisha Usalama.” Kampeni hiyo iliunganisha elimu ya amani na mafunzo ya vitendo ya usalama, ikihamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika kulinda jamii zao.
Kwa kushirikiana na Dingonet, shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na usimamizi wa majanga, programu hiyo ilijumuisha maonesho ya matumizi sahihi ya vizima moto na taratibu za kukabiliana na dharura. Washiriki walipata fursa ya kufanya mazoezi ya vitendo yaliyolenga kuimarisha uwezo wao wa kukabiliana na hali za dharura kwa ufanisi.
Programu hiyo ilitekelezwa kwa ushirikiano na mashirika mbalimbali ya ndani, ikiwemo Juhudi Mwenge Group, G4TC, British School, Kilimanjaro Institute, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, pamoja na WEO, No Limit Foundation, UDSM, Dingonet, TAYO na Sisi Tanzania. Kampuni ya Coca-Cola pia ilishiriki kwa kutoa vinywaji kwa washiriki kama sehemu ya msaada wake.
Mmoja wa washiriki alisema, “Kushiriki katika usafi wa mazingira na mafunzo ya usalama kumeongeza uelewa wangu kwamba amani inaweza kujengwa kupitia vitendo halisi katika jamii.”
Afisa mmoja wa IPYG alieleza kuwa shirika hilo litaendelea kupanua programu kama hizi kwa kushirikiana na wadau wa ndani ili kuimarisha ushiriki wa vijana katika ujenzi wa amani.