Dar es Salaam, 18 Julai 2025

Mwandishi wa vitabu vya kuelimisha watoto, Bi. Riziki Mohamed Juma, amezindua rasmi kitabu chake kipya kiitwacho “Saburi” katika hafla iliyofanyika katika Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam. 

Uzinduzi huu uliambatana na utambulisho wa vitabu vingine vya watoto, vikiwemo vya maandishi ya kawaida na vya nukta nundu kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Vitabu hivi vimetolewa kwa ushirikiano kati ya Mtalimbo Books na Dhahabu Publishers, na vinapatikana katika maduka ya vitabu na maktaba za jamii nchini.

Saburi ni hadithi ya kuvutia inayowasilisha ujumbe kuhusu athari za utoro shuleni kwa njia rahisi na ya kufundisha. Ni kitabu kinachofaa kwa watoto, wazazi, walezi na walimu.


Na Pamela Mollel, Arusha

Jiji la Arusha linajiandaa kupokea zaidi ya wataalamu 700 wa usimamizi wa rasilimaliwatu na utawala kutoka taasisi mbalimbali za umma nchini, kwa ajili ya kujadili mwelekeo mpya wa utendaji kazi unaolenga kuendana na kasi ya mageuzi ya teknolojia na mabadiliko ya mahitaji ya huduma kwa umma.

Mkutano huo mkubwa wa kitaifa unatarajiwa kuwapa nafasi wataalamu hao kuchambua kwa kina namna bora ya kuimarisha ufanisi katika taasisi za umma kupitia mifumo ya kisasa ya utawala na matumizi ya TEHAMA. Wataalamu hao watashiriki katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Jumuiya za Wataalamu wa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala katika Utumishi wa Umma (TAPA-HR), utakaofanyika kuanzia Julai 22 hadi 25, 2025, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora, chini ya kaulimbiu: "Mwelekeo mpya wa nafasi ya wataalamu wa usimamizi wa rasilimaliwatu na utawala: Kusukuma mabadiliko, kuendana na mageuzi ya teknolojia kwa ajili ya kuboresha huduma katika utumishi wa umma."

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 18, 2025 jijini Arusha, Mwenyekiti wa TAPA-HR, Grace Meshy, alisema mkutano huo ambao ni wa kwanza kufanyika nchini, utafunguliwa rasmi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora, Mheshimiwa George Simbachawene.

Meshy alisema kuwa mkutano huo ni sehemu muhimu ya mkakati wa kujiandaa kukabiliana na mazingira ya utendaji yanayobadilika kwa kasi, hasa katika nyanja za kidijitali, ili kuongeza ufanisi katika taasisi za umma.

“Kasi ya mabadiliko ya teknolojia inaonyesha wazi kuwa kuna uhitaji mkubwa wa wataalamu wa utawala na rasilimaliwatu wenye uwezo wa kuendana na mabadiliko hayo ili kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi,” alisema Meshy.

Aidha, alieleza kuwa mkutano huo utakuwa jukwaa la kipekee kwa wataalamu hao kujifunza, kubadilishana uzoefu, na kuimarisha uwezo wao wa kitaaluma kwa lengo la kuleta mageuzi chanya katika taasisi za umma.

Kwa mujibu wa Meshy, mkutano huo pia unatarajiwa kuwa hatua muhimu ya kuimarisha weledi, maadili, na mifumo ya kiutendaji miongoni mwa wataalamu wa kada ya rasilimaliwatu na utawala nchini.

Naye Katibu wa TAPA-HR, Prisca Lwangili, alisema mkutano huo utahusisha mada mbalimbali zenye lengo la kuboresha mbinu bora za kiutawala, kuimarisha uongozi, matumizi ya TEHAMA, na kukuza uwajibikaji katika sekta ya umma.

“Tunaomba waajiri kutoka wizara, mamlaka za serikali za mitaa, wakala wa serikali, mashirika ya umma, vyuo vikuu na taasisi nyingine za umma kuhakikisha wanawawezesha wataalamu wao kushiriki katika mkutano huu, kwani ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa maendeleo ya rasilimaliwatu na utawala bora,” alisema Prisca.







KILA mwaka Julai 18 dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela kwa kutenga angalau dakika 67 kufanya huduma ya kijamii, kama njia ya kumuenzi shujaa huyo wa Afrika Kusini aliyejitolea maisha yake kupigania haki za binadamu, amani, usawa na utu wa mwanadamu.

Katika kuadhimisha siku hii muhimu mwaka huu 2025, Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na Ubalozi wa Afrika Kusini waliungana kwa dakika 67 za huduma ya kijamii katika Makao ya Watoto wenye mahitaji maalumu kilichopo Kurasini, jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo limewakutanisha watumishi wa Umoja wa Mataifa, wawakilishi wa kidiplomasia, wadau wa maendeleo, na wanachama wa Jukwaa la Biashara kati ya Afrika Kusini na Tanzania.

Washiriki walijihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii zikiwemo kusafisha mazingira, kupanda mimea ya bustani na kusaidia kazi za jikoni, kama ishara ya mshikamano na moyo wa kujitolea aliouacha Mandela.

Jukwaa la Biashara la Afrika Kusini na Tanzania pia walichangia vifaa muhimu kwa ajili ya makao ya watoto wenye mahitaji Maalumu, hatua iliyodhihirisha mshikamano wa sekta binafsi na taasisi za kimataifa katika kusaidia jamii.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania,  Susan Namondo amesema;
“Leo tunamuenzi Madiba si kwa maneno bali kwa vitendo. Kila tendo la huduma—hata liwe dogo vipi, huchangia katika kujenga utu, heshima na matumaini. Ushirikiano wetu wa leo ni ushahidi wa nguvu ya umoja na mshikamano.”

Siku ya Nelson Mandela ni wito kwa kila mtu duniani kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya wengine. Kauli mbiu ya Mandela “It is in your hands” inakumbusha kuwa kila mtu anao uwezo wa kuleta mabadiliko, hasa kwa wale walio katika mazingira magumu.

"Kwa pamoja, Umoja wa Mataifa Tanzania, Ubalozi wa Afrika Kusini, na wadau wengine wamesimama kwa moyo mmoja kuendeleza urithi wa Mandela kupitia huduma, mshikamano na matumaini." Amesema





Mawaziri wa Mawasiliano kutoka Tanzania na Kenya wamezindua rasmi maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) wa Tanzania unaosimamiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), na mikongo ya baharini ya Mombasa kupitia Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (ICTA).

Uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidigitali wa Kenya, Injinia William Kabogo Gitau, pamoja na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mhe. Jerry Silaa.

Mawaziri hao wamesisitiza kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria, ikilenga kuimarisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya uhakika, pamoja na kupunguza changamoto za kukatika kwa mtandao.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Gitau amesema: “Jambo la msingi ni ushirikiano wa dhati kati ya nchi zetu mbili. Ni muhimu kuhakikisha tunatunza miundombinu hii ya kimkakati ili kuepuka uharibifu unaoweza kusababisha kukatika kwa umeme na mtandao. Pia tuendelee kuimarisha mahusiano yetu kwa manufaa ya pande zote.”

Kwa upande wake, Mhe. Jerry Silaa alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya pamoja ya mawasiliano kati ya nchi washirika ni wajibu wa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya kikanda.

“Kuna faida kubwa ya kuwa na maunganisho mengi ya mikongo ya mawasiliano. Hii husaidia kuwepo kwa mtandao wa uhakika, unaotegemewa hata wakati wa changamoto za kiufundi katika njia moja ya mawasiliano,” alisema Silaa.

Mkongo huo tayari umeanza kufanya kazi nchini Kenya, hatua inayowezesha huduma za intaneti na mawasiliano kusambaa kwa kasi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Uzinduzi huu unaashiria mafanikio makubwa katika juhudi za kuunganisha ukanda huu kidigitali na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.










Kamishna wa Uhifadhi - TANAPA, CPA Musa Nassoro Kuji, ameongoza hafla ya kumuapisha rasmi Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi - Cecilia Mtanga leo Julai 18, 2025 Makao Makuu ya Shirika hilo yaliyopo mtaa wa Majengo jijini Arusha. Uapisho huo ni baada ya Kamishna huyo kuteuliwa na Bodi ya Wadhamini - TANAPA katika kikao cha 210 kilichofanyika jijini Mwanza Mei, 2025.

Katika hafla hiyo Kamishna Kuji alimpongeza Kamishna Mtanga kwa uteuzi huo sanjari na kuwa Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu - TANAPA na kumtaka aendeleze juhudi za kulinda na kuhifadhi rasilimali za asili kwa weledi, uwajibikaji na moyo wa kizalendo. Aidha, amesisitiza mshikamano kwa watumishi wote katika kuhakikisha malengo ya TANAPA yanafikiwa kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wake, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi - Cecilia Mtanga aliishukuru Bodi ya Wadhamini - TANAPA kwa kumuamini na kumteua, hivyo ameahidi kutekeleza majukumu yake kwa bidii na kushirikiana na wenzake ili kuhakikisha urithi wa taifa unasimamiwa ipasavyo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.












NA WILLIUM PAUL, ROMBO.

SERIKALI imejipanga kikamilifu kutekeleza mikakati ya kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza darasa la saba (mtaala wa zamani) na wale wa darasa la sita (mtaala mpya) mwaka 2027 wanaendelea na masomo bila vikwazo.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda jana, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa kidijitali wa uthibiti ubora wa shule za msingi na sekondari wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, ambapo alisema Serikali itatumia mbinu mbalimbali kuhakikisha hakuna mwanafunzi atakayeachwa.

Profesa Mkenda, amesema mwaka 2027 utakuwa wa kipekee, kwani kutakuwa na mahafali ya wanafunzi kutoka madarasa mawili tofauti, darasa la saba kwa mtaala wa zamani na darasa la sita kwa mtaala mpya ambao wote watamaliza elimu ya msingi kwa pamoja.

"Tutatumia mikakati ya aina mbalimbali kuhakikisha tunalitekeleza hili la elimu 2027 tuna mikakati ya akiba, tunajenga VETA kila Wilaya, tunaweza kufanya VETA ziache kuchukua wanafunzi kwa muda kwamba darasa la Saba na la Sita wote wanahitimu wakati mmoja , VETA ikawa Sekondari wakasoma kule wakimaliza VETA ikarudi kwenye shughuli zake," alisema Profesa Mkenda

Alisema hatua nyingine ni kuzitumia baadhi ya shule za Sekondari za watu binafsi kupeleka watoto wa serikali, kwa kuwalipia ada endapo makubaliano ya ada yatakuwa ni mazuri ili wasome.


 Wadhamini wa mbio za NBC Dodoma Marathon Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania na Kampuni ya Bima ya Jubilee Allianz Tanzania wamesisitiza dhamira yao ya kuendelea kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ili kuhakikisha mbio hizo zinatimiza makusudi yake ya uwajibikaji kwa jamii huku pia zikitoa hamasa na furaha iliyokusudiwa kwa washiriki.

Dhamira za wadau hao wawili zimewekwa wazi leo jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya NBC Bw Rayson Foya waliotembelea makao makuu ya kampuni hizo wadhamini kwa lengo la kukabidhi jezi maalum na vifaa vitakazotumiwa na washiriki wa mbio hizo ikiwa ni ishara ya muaandaaji huyo kutambua na kuheshimu mchango wao katika kufanikisha msimu wa sita wa mbio hizo.

Mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma zinalenga kuendeleza mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi, kupanua ufadhili wa wakunga hadi kufikia wakunga 200 pamoja na kuanzisha mpango mpya wa kufadhili masomo ya wauguzi 100 kwa ajili ya watoto wenye changamoto za usonji (autism) nchini.

Mapema wakiwa makao makuu ya Jubilee Allianz Tanzania Bw Foya na ujumbe wake akiwemo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa benki ya NBC Bw Godwin Semunyu walipata wasaa wa kuzungumza na kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Bw Jaideep Goel, ziara ambayo pia iliendelea kwa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania na kupokelewa na maofisa waandamizi wa kampuni hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi wa Biashara Bw Nguvu Kamando.

Katika mazungumzo yake na wadau hao Bw Foya pamoja na kuwashukuru kwa udhamini wao muhimu katika mbio hizo alisisitiza kuhusu umuhimu ushirikiano baina ya taasisi mbalimbali hapa nchini katika kufanikisha nia ya pamoja ambayo ni kurejesha kwa jamii kupitia jitihada mbalimbali zinazolenga kupambana na changamoto zinazowagusa wanajamii hususani katika masuala yanayohusu afya.

“NBC Dodoma Marathon sio tu tukio la kimichezo bali pia ni jukwaa la matumaini ya maisha kwa watanzania. Ushiriki wa wadau hawa wakiwemo Vodacom Tanzania na Jubilee Allianz na wadau wengine wote tuliowatembelea na tutakaoendelea kuwatembelea umekuwa ni chachu muhimu katika kufanikisha kusudi letu hilo mihumu...tunawashukuru sana’’ alisema Bw Foya

Kwa upande wake Bw Kamando pamoja na kupongeza ubora na ubunifu wa jezi hizo, aliishukuru benki hiyo kwa namna inavyoandaa tukio hilo kwa weledi wa hali ya juu hatua ambayo imeongeza mvuto wake kiasi cha kuwavutia maelfu ya washiriki kutoka ndani na nje ya nchi.

“Zaidi tunawapongeza NBC kwa namna ambavyo wamekuwa wakilitumia tukio hilo kukusanya fedha kwa ajili ya kufanikisha makusudi muhimu ya mbio hizi. Ni kupitia kuridhishwa kwetu na nia pamoja na uratibu wa mbio hizo ndio imekuwa sababu ya Vodacom Tanzania kuendelea kuziunga mkono kama wadau muhimu huu ukiwa nim waka wa pili sasa na tunaahidi kuendelea kuziunga mkono zaidi katika misimu mingine ijayo,’’ alisema.

Usajili wa mbio hizo unaendelea kupitia tovuti ya www.events.nbc.co.tz ambapo washiriki wanatakiwa kuchangia kiasi cha TZS 45,000 kwa usajili wa mtu mmoja mmoja au 42,000 kwa usajili wa kikundi chenye idadi ya watu 30 au zaidi.





Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya NBC Bw Rayson Foya (kushoto), Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Bw Nguvu Kamando (katikati) sambamba na maofisa wengine waandamizi wa taasisi hizo akiwemo Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa benki ya NBC Bw Godwin Semunyu (kulia) wakionesha jezi maalum kwa ajili ya mbio za NBC Dodoma Marathon zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma wakati wa hafla ya makabidhiano ya jezi hizo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.






Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya NBC Bw Rayson Foya (katikati), Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Bima ya Jubilee Allianz Tanzania Bw Jaideep Goel (kulia) sambamba na maofisa wengine waandamizi wa taasisi hizo wakionesha jezi maalum kwa ajili ya mbio za NBC Dodoma Marathon zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma wakati wa hafla ya makabidhiano ya jezi hizo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.








Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Bima ya Jubilee Allianz Tanzania Bw Jaideep Goel (kushoto) akizungumza na wageni wake kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambao ni waandaaji wa mbio za NBC Dodoma Marathon wakiongozwa na Mkurugenzi wa Fedha wa benki hiyo Bw Rayson Foya ( wa tatu kulia) wakati maofisa hao walipotembelea makao makuu ya kampuni ya Bima ya Sanlam kwa ajili ya kumkabidhi jezi maalum kwa ajili ya mbio za NBC Dodoma Marathon zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.






Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa benki ya NBC Bw Godwin Semunyu (wa pili kulia) akizungumza na wenyeji wao maofisa kutoka Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania (waliopo upande wa kulia) wakati maofisa hao walipotembelea makao makuu ya kampuni ya Bima ya Sanlam kwa ajili ya kumkabidhi jezi maalum kwa ajili ya mbio za NBC Dodoma Marathon zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.







Maofisa wa Benki ya NBC wakiwasili makao makuu ya Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa ajili ya kukabidhi kwa viongozi wa kampuni hiyo jezi maalum kwa ajili ya mbio za NBC Dodoma Marathon zinazotarajiwa kufanyika Julai 27, mwaka huu jijini Dodoma. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.


MERIDIANBET wanazidi kumwaga zawadi kwa wateja wao kila kukicha. Hii ya sasa ni funga kazi kabisa. Mtu yeyote anayejisajili na meridianbet kisha kuweka muamala wake na kushiriki kwenye mchezo wowote ule, aidha michezo ya ubashiri ama kasino mtandaoni basi aanajiweka kwenye nafasi kubwa ya kujishindia simu mpya ya kisasa aina ya Samsung A25 mpaka mara tano kama pongezi ya yeye kutumia Meridianbet.

Baada ya kuja na bonus za kutosha kwenye michezo mbalimbali kama Superheli, expanse tournament, Wild White Whale na Aviator sasa nafasi imekuja kwako uliyekosa zawadi kwenye michezo hiyo ambapo sasa kwa kufanya kitu chepesi kama kuweka dau na kucheza mchezo wowote basi upo kwenye nafas kubwa ya ushindi. Meridianbet haimuachi nyuma mtu yeyote kwa sasa.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Bonus hii imekuja na urahisi wa kushiriki kwani unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha umejisajili na meridianbet kupitia tovuti ama application yao ya simu kisha weka dau lako na ucheze. Unavyozidi kucheza zaidi ndivyo unavyozidi kujiakikishia nafasi ya kushinda. Droo ya kutoa zawadi hizi za simu itafanyika tarehe 01-08-2025 na washindi watatangazwa siku hiyohiyo.

Promosheni hii iliyoanza tarehe 01-07-2025 inatarajiwa kuendelea kwa kipindi cha mwezi mzima na itatamatika tarehe 31-07-2025. Tiket za mfumo “system tickets” pamoja na zile za cash out hazitohesabiwa wakati wa droo, ni tiketi za kawaida pekee zitakazozingatiwa kwenye promosheni hii kali kabisa kutoka meridianbet.

Jisajili sasa na meridianbet kisha cheza michezo mbalimbali kwenye jukwaa hili la michezo ya kubashiri mara nyingi uwezavyo na uweze kuibuka bingwa wa simu kali na za kisasa aina ya Samsung A25.

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi Bilioni 19.6 kwa ajili ya Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari SEQUIP mkoani Njombe.

Kati ya fedha hizo jumla ya Shilingi Bilioni 4.360 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo majengo ya madarasa, maabara, mabweni, Bwalo la chakula Jengo la Utawala na nyumba za walimu katika shule ya Sekondari ya wasichana ya mkoa wa Njombe ambayo imekamilika.

Hayo yamebainishwa tarehe 17 Julai 2025 na Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Njombe Mwl Nelasi Mulungu ambapo amesema pia Bilioni 1.6 imetolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya Mkoa ya Amali ambayo inaendelea na ujenzi katika Wilaya ya Ludewa.

Mwl Mulungu amesema kuwa serikali imetoa zaidi ya Bilioni 12.638 kwa ajili ya ujenzi wa shule 20 za kata katika mkoa huo wa Njombe.

Pia amesema kuwa serikali imetoa zaidi ya Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mingine katika mkoa wa Njombe ikiwemo ujenzi wa Mabweni, Nyumba za walimu, na Matundu ya vyoo.



-Fursa za elimu ya juu kimataifa sasa kupatikana Dar

Na Mwandishi Wetu

WAKALA wa Elimu Nje ya nchi Global Education Link inatarajia kuwakutanisha wanafunzi wa Tanzania na vyuo vikuu zaidi ya 20 kutoka nchi mbalimbali duniani katika maonyesho jijini Dar es Salaam ambapo wanafunzi watapata fursa ya kujua fursa za kusomea kozi mbalimbali kwenye vyuo hivyo

Global Education Link imesema wanafunzi watakaotaka kusoma nje ya nchi watapata udahili wa papo hapo.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Global Education Link, Abdulmalik Mollel, wakati akizungumza kuhusu maonyesho hayo.

Alisema kwenye maonyesho hayo yatakayofanyika siku ya Jumanne Julai 22 kutakuwa na vyuo vikuu kutoka mataifa mbalimbali vikiwemo kutoka nchi za Cyprus, India China Malaysia, Uingereza, Canada, Marekani, Australia, Uturuki , Mauritius na Dubai

Alisema baadhi ya vyuo vikuu vitakavyoshiriki kwenye maonyesho hayo vitatoa ufadhili wa kuanzia asilimia 20 hadi 80 wakati vingine vitatoa ufadhili wa moja kwa moja.

Mollel alisema kwa wanafunzi wanaotaka kusomea Shahada za Uzamili na Uzamivu hasa kwenye masomo ya uhandisi watapewa ufadhili kwa asilimia 100.

“Ndani ya maonyesho hayo vyuo vikuu kutoka Cyprus, India China Malaysia, Uingereza,Canada Marekani, Australia, Uturuki , Mauritius Dubai vyuo vitatoa udahili wa papo kwa papo kwa hiyo wanafunzi waliomalisa sekondari wachangamkie fursa hii,” alisema .

Aliwahakikishia wazazi kuwa kuna uhakika wa kupata udahili ilimradi mwanafunzi awe amefaulu na kwamba watapata vyuo vikuu bora ambavyo vinatambulika na nchi zao na mamlaka za ithibaki ndani ya Tanzania.

“Wanafunzi watakaokuja watapata vyuo vya kimataifa kwenye kozi mbalimbali na gharama ni zile zile kama za vyuo vya ndani ya nchi,” alisema

“Tumezingatia vyuo vikuu ambavyo vinamalezi na usalama kwa wanafunzi na ambavyo vinauwezo wa kutoa nyaraka zitakazomwezesha mwafunzi kwenda chuo kikuu kwa wakati, vyuo vikuu vyenye malazi na ambavyo vimekidhi vigezo vya ithibati na ubora wa kozi wanazotoa,” alisema

“Njia za kushiriki kwenye maonyesho ziko tatu, kwa anayetamani kuja Serena hotel kuanzia asubuhi na ushiriki wa kufanya miadi kwa kupiga simu kutaka kujua chuo unachotaka kusoma na watu wa GEL watapokea simu na kukupa taarifa unazotaka,” alisema

“Unaweza ukaingia kwenye tovuti ya Global Education Link ukapata taarifa zote ukajaza taarifa zako na ukapata udahili wa haraka sana,” alisema

Alisema urithi wa mtoto ni elimu na GEL imeona umuhimu wa kutoa mchango wake kwa kuwaletea vyuo vikuu vya nje na kuwapa udahili wa hapo hapo wanafunzi wanaohitaji kusoma nje ya nchi.






Top News