Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel, Bi. Doris Mollel, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus, katika Makao Makuu ya Shirika hilo huko Geneva.

Mazungumzo yao yalihusu ushirikiano katika kufikia #AfyaKwaWote na kupunguza vifo vya watoto wachanga barani Afrika na duniani kote.

Katika mazungumzo hayo, Bi. Mollel alielezea jinsi ambavyo Taasisi ya Doris Mollel inafanya kazi nchini Tanzania, hasa katika kuboresha miundombinu ya utoaji huduma kwa watoto wachanga, hasa wale wanaozaliwa kabla ya wakati.

Kwa upande wake, Dr. Tedros aliipongeza Taasisi hiyo kwa juhudi zake katika mapambano hayo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano.



Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amevutiwa na huduma zinazotolewa na Wakala ya Maabala ya Veterinari Tanzania (TVLA) alipotembelea banda la TVLA siku ya kilele cha Maonesho na Mnada wa Mifugo 2024 yaliyofanyika kwenye shamba la Mkonge la Highland Estate Chalinze Ubena Zomozi Mkoa wa Pwani Juni 16, 2024.

Akiongea kwa niaba ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Malinda alisema kuwa majukumu makubwa ya TVLA ni pamoja na kufanya utafiti wa magonjwa ya wanyama, kufanya uchunguzi wa magonjwa ya wanyama, kuzalisha na kusambaza chanjo za magonjwa ya Mifugo ambapo hadi sasa TVLA inazalisha aina 7 za chanjo.

Sambamba na hayo Dkt. Malinda aliongeza kuwa, mkakati wa Wizara kwa kushirikiana na TVLA imepanga hadi kufikia mwaka 2030 itakuwa inazalisha Chanjo 13 za kipaumbele na hadi kufikia sasa TVLA tayari imeshanunua magari ya mfumo wa baridi ambayo yanasambaza chanjo ambazo zimeshaanza kuzalishwa ili kuwafikia wafugaji kote nchini.

Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 26 kwa ajili ya kuendesha kampeni ya chanjo kitaifa kwa lengo la kuhamasisha wafugaji kuchanja Mifugo yao ili kuzuia isishambuliwe na magonjwa kwani kuchanja Mifugo kutaongeza mazao ya Mifugo kukizi soko la nje ya nchi. Alisema Dkt. Malinda

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko aliongozana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexandar Mnyeti (MB), Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mhe. Riziwani Kikwete, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, Naibu katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Daniel Mushi pamoja na viongozi waandamizi wa Wizara
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko akipata maelezo kuhusiana na huduma zinazotolewa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Malinda kwenye kileie cha Maonesho na Mnada wa Mifugo 2024 yaliyofanyika Juni 16, 2024 kwenye shamba la Mkonge la Highland Estate Chalinze Ubena Zomozi Mkoa wa Pwani.
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi akifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (hayupo pichani) kwenye kilele cha Maonesho na Mnada wa Mifugo 2024 yaliyofanyika Juni 16, 2024 kwenye shamba la Mkonge la Highland Estate Chalinze Ubena Zomozi Mkoa wa Pwani.
Wataalamu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Afisa Utafiti Mifugo Bw. Msafiri Kalloka (wa kwanza kushoto) pamoja na Daktari Mtafiti wa Mifugo Dkt. Fredy Makoga wakitoa elimu kuhusiana na huduma zinazotolewa na TVLA kwa wadau wa Mifugo waliotembembela banda la TVLA kwenye kilele cha Maonesho na Mnada wa Mifugo 2024 yaliyofanyika Juni 16, 2024 kwenye shamba la Mkonge la Highland Estate Chalinze Ubena Zomozi Mkoa wa Pwani.

 


Kampeni ya Holela-Holea Itakukosti inasisitiza mbinu kamilifu ya “Afya Moja" kushughulikia tatizo la UVIDA na magonjwa ya zuonotiki.

Holela-Holela ilizinduliwa mwishoni mwa mwezi uliopita ikiwa ni ushirikiano ya Ofisi ya Waziri Mkuu Wizara ya Afya, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).

Dodoma Jumamosi 15 Juni 2024

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu leo amekutana na kufanyia mazungumzo na KIDO ambaye ni balozi wa kampeni ya Holela-Holela itakukosti. Kampeni ya Holela-Holela itakukosti inasisitiza mbinu kamilifu ya " Afya Moja" kushughulikia tatizo la  UVIDA na magonjwa ya zuonotiki na ilizinduliwa Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi uliopita kwa uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana Wizara ya Afya, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Mazingira huku ikifadhaliwa na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) kupitia mradi wa Breakthrough ACTION.

Akizungumza leo Jijini Dodoma baada ya kufanyia mazungumzo na balozi KIDO, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisisitiza juu ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA) na magonjwa ya kipaumbele ya zuonotiki (magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu) ambayo kampeini ya Holela-Holela Itakukosti imelenga. ‘Naomba nichukue fursa hii nitoe wito kwa jamii kuwa Mtanzania anaweza kufanya mambo machache tu kukabiliana na UVIDA, kama vile kupata na kufuata ushauri wa mtaalamu wa afya kabla ya kutumia dawa, kutumia dozi ya dawa kikamilifu kama unavyoshauriwa na mtaalam wa afya, kufuata maelekezo ya mtaalam wa mifugo/kilimo juu ya matumizi sahihi ya dawa kwa mifugo/mimea, na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na usafi wa mazingiria kwa ujumla’. 

Waziri Ummy aliongeza, ‘Suala la UVIDA ni tatizo kubwa sana, na athari zake ni kama vile ugonjwa kujirudia rudia na kuchukua muda mrefu kupona, kuenea na kusambaa kwa vimelea sugu vya magonjwa dhidi ya dawa, ulemavu na hata kifo. Mbali na hapo kuna athari za kiuchumi kama vile kutumia gharama kubwa kwenye matibabu, hivyo kupungua kwa pato binafsi, la familia na taifa’.

Waziri Ummy alisema kuwa Serikali inafanya jitihada kabambe za kukabiliana na UVIDA, ikiwemo kuzindua kampeni ya “Holela Holela itakukosti”, inayolenga kuongeza uelewa juu ya UVIDA na kuleta mabadiliko chanya ya tabia ili kukabiliana na UVIDA katika jamii. Pamoja na kampeni hiyo upo mpango kazi wa mapambano ya UVIDA (NAP AMR 2023-2028), na kamati ya Taifa ya Mapambano ya UVIDA (AMR MCC) inayofanya kazi chini ya mwamvuli wa Afya moja. Vilevile kuna miongozo mbalimbali ya Kisekta inayosaidia katika mapamabano ya UVIDA” 

Kwa Upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa USAID nchini Tanzania Alex Klaits alisisitiza umuhimu wa juhudi za pamoja, akisema, "Kampeni inaonyesha jukumu muhimu la ushirikiano katika kuleta athari chanya na kuhakikisha uendelevu wa muda mrefu, ikiwaleta pamoja wadau wa Afya moja kutoka sekta mbalimbali kupambana na UVIDA na magonjwa ya zuonotiki.Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akipokea Zawadi kutoka kwa KIDO ambaye ni balozi wa kampeini ya Holela-Holela itakukosti mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo leo Jijini Dodoma. Kampeni ya Holela- Holela Itakukosti inazingatia udhibiti kuhusu usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA) na magonjwa ya kipaumbele ya zuonotiki (magonjwa ambayo yanaweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa wanadamu) na inaratibiwa na ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).







Picha mbalimbali: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisherehekea Siku ya Mtoto wa Afrika akiwa pamoja na wajukuu, Ikulu jijini Dar es Salaam. Siku hii huadhimishwa Juni 16 ya kila mwaka.

Katika kuadhimisha siku hii, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa Serikali, familia na jamii kushirikiana kuhakikisha watoto wanapata malezi bora yenye maadili mema, na kuhakikisha usalama wa mtoto ni jukumu la jamii nzima na siyo mzazi tu, vilevile kuwapatia elimu na historia za kuwahimiza uzalendo kwa nchi yao tangu wakiwa wadogo.



















Cheza na mwanao kama unavyocheza na simu yako, kama unvyoipenda simu yako na pia mpende mwanao kama unavyoipenda simu yako kwani ulawiti na ubakaji unafanyika majumbani, mashulei na mitaani bila kujali anasoma shule gani na ukigundua anafanyiwa ukatili chukua hatua mara moja bila kujali hata kama ni ndugu yako aliyefanya ukatili na kufanya hivyo utakuwa umewalinda watoto na vitendo vya kikatili ili kutengeneza Taifa imara lenye kumjua Mungu.

Hayo yamesemwa Juni 16, 2024 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Theopista Mallya alipokuwa akizungumza na waumini wa Kanisa la Anglican DCT lililopo eneo

la Chadulu Dodoma na kuwataka kuongea na watoto ili kuweza kubaini changamoto za ukatili wanazokumbana nazo na kuweza kuzitolea taarifa.

Katika hatua nyingine Kamanda Mallya amekemea suala la ushoga na usagaji huku akinukuu vifungu vya biblia Mwanzo 1:28, Walawi 18:22 na Warumi I 24 vinavyokataza masuala hayo kwani hata sheri za nchi zinakataza pia masuala ya ushoga na usagaji hivyo kuendelea kushabikia vitendo hivyo ni kumkosea mwenyezi Mungu na sheria za nchi.

Aidha Kamanda Mallya amewasihi waumini hao kujiepusha na mikopo ya kausha damu na Vikoba yanayosababisha madeni yaliyopitiliza na kuwataka kukopa kiasi unachoweza kulipa huku akirejea kwenye kitabu cha Zaburi 37: 21 kimeelezea kuhusiana na madeni kwani dawa ya madeni ni kulipa huku akikemea vitendo vya rushwa ambaye ni adui wa haki na hata kitabu cha Zaburi 15:5 na Kutoka 10:17 na 23:8 kinakataza kutoa na kupoekea rushwa ambayo hugeuza ukweli kuwa uongo.


Toka Dawati la Habari Polisi Dodoma.





Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kigoma kwa kushirikiana na Mkandarasi STECOL kuhakikisha wanaweka alama za tahadhari na kukagua mara kwa mara eneo la Mlima Busunzu sehemu ilipotokea changamoto ya kuharibika kwa kipande cha barabara chenye urefu wa takriban mita 100, wakati wakisubiri utatuzi wa kudumu kwenye eneo hilo.

Kasekenya ameelekeza hayo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Kabingo- Kasulu- Manyovu (Km 260), sehemu ya Mvugwe - Nduta (Km 59.35) na kueleza kuwa mkandarasi bado yupo eneo la mradi na kwa sasa anasubiri timu ya wataalamu inayofanya utafiti kuhusu kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ili kuendelea na ujenzi katika kipande hicho.

"Hakikisheni mnaendelea kuliangalia eneo hili, hata barabara zinazopita katika eneo hili zikagueni mara kwa mara na muweke alama za tahadhari ili watu wanapopita hapa wapite kwa uangalifu," amesema Kasekenya.

Aidha, Kasekenya ameongeza kuwa Serikali inaendelea na Ujenzi wa barabara ya Manyovu - Mnanila - Kasulu ambapo zaidi ya Kilometa 26 za barabara hiyo zimewekwa lami na inatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba mwaka huu.

Kadhalika, Kasekenya ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuufungua Mkoa wa Kigoma na nchi kwa ujumla kupitia Miundombinu ya barabara na hivyo kurahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kati ya Mkoa huo na Mikoa jirani ya Geita, Mwanza pamoja na nchi jirani za Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kasekenya, amemuelekeza Meneja wa TANROADS Mkoa huo kuendelea kuwasimiamia wakandarasi wanaojenga barabara hizo kukamilisha kwa wakati na kwa ubora ili kusaidia wananchi kuondokana na changamoto wanazozipata hususan kipindi cha mvua.

Kwa upande Wake, Mhandisi, Hamisi Juma kutoka Kampuni ya Mhandisi Mshauri M/s Conseil Ingenierie Limited (CIRA SAS) amesema kwa sasa mradi umefika asilimia 81.49 ambapo tabaka la lami limeshawekwa mpaka mwisho wa mradi na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2024.

Mhandisi, Juma ameongeza kuwa ujenzi wa mradi huo umehusisha pia na Ujenzi wa daraja la Malagarasi lenye urefu wa mita 77 na madaraja mengine mawili ambayo yote yamekamilika kwa asilimia 100.

Mradi wa barabara ya Mvugwe- Nduta (Km 59.35) umefadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na unagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 84.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kigoma, Eng. Narcis Choma (Wapili kushoto mbele), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kabingo - Kasulu – Manyovu (Km 260) sehemu ya Mvugwe – Nduta (Km 59.35), mkoani humo.

Muonekano wa kipande cha barabara kilichoharibika chenye urefu wa takriban mita 100 eneo la mlima Busunzu, mkoani Kigoma. Mkandarasi STECOL anasubiri timu ya wataalam inayotafiti eneo hilo kupata utatuzi wa kudumu ili kuendelea na ujenzi katika kipande hicho.


Muonekano wa barabara Kabingo - Kasulu – Manyovu (Km 260) sehemu ya Mvugwe – Nduta (Km 59.35), mkoani Kigoma. Barabara hiyo inajengwa na mkandarasi STECOL kwa gharama ya shilingi Bilioni 84 na inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2024.

Muonekano wa daraja la Malagarasi lenye urefu wa mita 77, mkoani Kigoma. Daraja hilo limejengwa na mkandarasi STECOL na limekamilika kwa asilimia 100.

PICHA NA WU.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Klaus Chilima. Ibada ya Mazishi hayo imefanyika katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi.

Akitoa salamu za rambirambi, Makamu wa Rais amesema Tanzania inatoa salamu za pole na kuungana na waombolezaji wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki kigumu.

Makamu wa Rais amesema Hayati Chilima alikuwa kiongozi imara, mwanamajumui wa kweli wa Afrika ambaye wakati wote alitanguliza mbele maslahi ya wananchi anaowaongoza na Afrika kwa ujumla.

Pia Makamu wa Rais amemtaja Hayati Chilima kama kiongozi aliyesimamia umoja, amani na usalama, mageuzi ya kiuchumi ya Malawi na utawala wa kidemokrasia nchini humo.

Makamu wa Rais amesema wananchi wa Malawi na Ukanda wote kwa ujumla wanapaswa kumuenzi Hayati Chilima kwa kuendeleza yale aliyosimamia na kuendelea kumuombea apumzike kwa amani.

Katika kushiriki Mazishi hayo ya Kitaifa Makamu wa Rais ameambatana na Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Hamza Hassan Juma, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato pamoja na Balozi wa Tanzania Mhe. Agnes Kayola.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi kushiriki Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima leo tarehe 16 Juni 2024. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe. Agnes Kayola na Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Rais Mstaafu wa Malawi Mhe. Dkt. Joyce Banda mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi kushiriki Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima leo tarehe 16 Juni 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimfariji Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi kushiriki Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima leo tarehe 16 Juni 2024.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akitoa heshima za mwisho wakati akiaga mwili wa aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima katika Mazishi ya Kitaifa yaliyofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi leo tarehe 16 Juni 2024.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akishiriki katika Ibada ya Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi leo tarehe 16 Juni 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akitoa salamu za rambirambi wakati wa Mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Malawi Hayati Dkt. Saulos Chilima katika Uwanja wa Taifa wa Bingu uliopo Lilongwe nchini Malawi leo tarehe 16 Juni 2024.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa ameungana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kutoa salamu za pole kwa familia ya aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Marehemu Dkt. Shogo Mlozi tarehe 15 Juni, 2024 jijini Arusha.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa familia ya Marehemu Dkt. Shogo Mlozi tarehe 15 Juni, 2024 jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Vita Kawawa akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa familia ya Marehemu Dkt. Shogo Mlozi tarehe 15 Juni, 2024 jijini Arusha.

Balozi Mussa na Mhe. Kawawa wakimfariji Prof. Eliamani Sedoyoka ambaye ni mume wa aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Marehemu Dkt. Shogo Mlozi.

Balozi Mussa na Mhe. Kawawa wakitoa faraja kwa wazazi wa marehemu.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama walipoungana na waombolezaji wengine katika msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Marehemu Dkt. Shogo Mlozi tarehe 15 Juni, 2024 jijini Arusha.

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dkt. Hussein Mohamed Omar, amesema matarajio ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona sekta ya kilimo inaleta mageuzi ya kiuchumi nchini.

Amesema kutokana na hatua hiyo ni lazima kufanyia kazi changamoto zilizopo katika sekta ya umwagiliaji ili kuwa na matokeo hayo.

Dkt. Hussein ameyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa Kamati zinazohusika na mradi wa Uhimilivu wa Mifumo ya Chakula unaodhaminiwa na Benki ya Dunia (WB).

Akieleza zaidi amesisitiza iwapo serikali haitafanyia kazi mahitaji yaliyopo katika sekta hiyo ya Umwagiliaji hakutakuwa na matokeo katika mageuzi ya kiuchumi yanayotokana na sekta ya kilimo nchini na wizara inaamini utendaji na ufanisi wa Tume unaweza kusimamia na kufikia azma ya Rais ya sekta ya kilimo kuleta mageuzi ya kiuchumi.

"Mradi huu ni muhimu katika mabadiliko ya tabianchi ili kuwa na usalama wa chakula, hivyo Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inalo jukumu mahususi katika kuhakikisha kunakuwa na matokeo chanya katika mradi huu na kufikia maono ya Rais Dk. Samia sekta ya kilimo kuleta mageuzi ya kiuchumi,”amesema.

Kwa upande wake Mratibu wa mradi huo kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Uhakiki Ubora, Naomi Mcharo, akitoa ufafanuzi katika mkutano huo amesema mradi huo ni wa dola za Marekani milioni 300 na unahusisha Awamu mbili moja wapo ikiwa ni Matokeo Kwanza (P4R) ukiwa ni utekelezaji wa miaka mitano.

Aidha Tume imetengewa Dola milioni 70 kufanikisha mradi huo kipindi hicho na kufafanua katika usimamizi na maamuzi ya mradi kunahitaji kuwa na kikao cha wataalamu, Kamati ya watendaji wakuu wa Wizara ambao ni Makatibu Wakuu wa Wizara katika sekta ya kilimo na kikao cha pande mbili za Muungano.

Amesema lengo ni kuangalia, kushauri na kuelekeza utekelezaji wa mradi ili kuleta ufanisi."NIRC imejipanga kukarabati miundombinu ya umwagiliaji kupitia mradi huo, kuwawezesha na kuwaelimisha wakulima juu ya uendeshaji, matunzo na usimamizi wa skimu za umwagiliaji."




Baraza la Uwzeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limeyataka makundi ya kinamama, vijana na makundi maalumu kutambua kuwa Program ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) imeanzishwa ili kuongoza tija kwa wafanyabiahara na wajasiriamali wenye biashara zao na siyo kuwa imekuja kutoa fedha kwa makundi hayo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bi. Beng’i Issa wakati alipokuwa akizungumza na makundi hayo katika Mkoa wa Iringa kuwa program hiyo haijaanzishwa kwa ajili ya kutoa fedha kwa makundi hayo bali kuleta uwezeshaji kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wenye biashara zao.

“Program hii ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)inajieleza vizuri kuwa imekuja kuimarisha biashara zilizopo ili kuwa na tija,” Uwezeshaji huo ni kwa ajili ya biashara ambazo zinafanyika na siyo kutoa fedha, alifafanua, Bi. Beng’i.

Akitoa mafano alisema kwamba program hiyo itawaimarisha wafanyabiashara kwa kibiashara wanazofanya, wakulima katika kilimo wanachofanya, kadhalika katika uvuvi na ufugaji. Pia uwezeshaji huo utaangalia vipaumbele vilivyopo katika mkoa husika na kutoa vitendea kama mashine, viwanda na vilevile ujuzi.

Bi, Beng’I alisema kwamba suala la mitaji litaangaliwa lakini kipaumbele kikubwa cha program hiyo ni kutoa vitendea kazi kwa ajili ya kuimarisha shughuli hizo za biashara na ujasiriamali. Makundi hayo kwa Mkoa huo wengi wanafanya shughuli za kilimo na ufugaji na baraza limeona shughuli hizo na ndio zitakazokuwa za kipaumbele.

Pia alisema wafanyabiashara wengine katika mkoa huo wanafanya shughuli za kusindika mazao ya kilimo na mifugo, na baraza kupitia madawati yake ya wilaya na mikoa yatatoa elimu namna ya kutumia mitandao ya teknonolojia waweze kufanya manunuzi ya umma kupitia mitandao kwa lengo la kupata fursa zilizopo serikali,

Mshauri wa Rais Masuala ya Wanawake, Sophia, Mjema alisema serikali imejiwekeza katika kuhakikisha shughuli za kiuchumi zinawezeshwa na aliwataka makundi hayo kujiandikisha na kutambuliwa pamoja na biashara zao ili kuweza kupata uwezeshaji.

“ Kutokana na shughuli kubwa za kilimo kama cha maua, miti ya mbao tunahitaji hapa muwe na kiwanda kikubwa cha kuchakata mazao haya”, na aliwataka viongozi wa mkoa huo kuwapa kazi za shughuli ndogondogo za ujenzi wapewe makundi hayo ili wawe wakandarasi wadogo.

Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wilaya ya Mfindi, Bi.Pascazia Lutu alisema elimu waliyoipata wataenda kuitumia na kuelimisha wengi ili waweze kuwa na mabadiliko ya kiuchumi.

Naye Mwananchi kutokana Manispaa ya Iringa, Bi. Mahanga Mng’ong’o alipongeeza mpango wa serikali wa kuwezesha makundi ya akinamama na hiyo itasaidia kujiepusha na mikopo toka katika taasisi mbalimbali zikiwemo kausha damu.

“ Hapa nimeona pia kunamikopo katika Benki ikiwemo NMB na hata katika halmashauri hivyo tumenufaika na elimu ambayo tumeipata hapa,” kumwezesha mama ni kuiwezesha familia nzima, alisisitiza.

Katibu Mtendaji wa Baraza la UwezeshajiWananchi Kiuchumi (NEEC,Bi.Beng’I Issa akizungumza na makundi ya akinamama, vijana na makundi maalum Mkoani Iringa wakati baraza hilo lilopoifikisha programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)mkoani humo, kulia kwake ni Mshauri wa Rais Masuala ya wanawake, Bi. Sophia Mjema, wa kwanza kushoto ni Rais Mkoa wa Iringa Doris Kalasa.  Picha na Mwandishi Wetu Iringa.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi.Beng’I Issa wa pili kutoka kulia akifurahi pamoja na  makundi ya akinamama, vijana na makundi maalumu ambao hawako pichani Mkoani Iringa wakati baraza hilo lilipoifikisha programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)mkoani humo,  wa pili kutoka kulia ni Mshauri wa Rais Masuala ya wanawake, Bi. Sophia Mjema na wa kwanza kutoka kushoto ni Rais Mkoa wa Iringa,Bi,Doris Kalasa na wa kwanza kulia ni Bi. Rita Mlagala.  Picha na Mwandishi Wetu Iringa.

Mshauri wa Rais Masuala ya wanawake, Bi. Sophia Mjema wa pili kutoka kulia akifuatilia jambo kutoka kwa makundi ya akinamama, vijana na makundi maalumu hawako pichani Mkoani Iringa wakati Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilopoifikisha programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA)mkoani humo,  wa kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bi.Beng’I Issa, wa pili kutoka kushoto ni Rais Mkoa wa Iringa Doris Kalasa na wa kwanza kulia ni Bi. Rita Mlagala.  Picha na Mwandishi Wetu Iringa.


Mshauri wa Rais Masuala ya wanawake, Bi. Sophia Mjema katikati mwenye kilemba akifurahi na makundia ya kinamama wa Mkoa wa Iringa, wakati Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilipoifikisha Programa ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) mkoani humo.


Top News