Na Victor Masangu, Bagamoyo

Baraza la michezo la Taifa (BMT) limeipongeza kwa dhati Taasisi ya Shajar inayomiliki shule ya Baobab kwa kuweza mipango madhubutti katika kukuza sekta ya michezo mbali mbali kwa wanafunzi na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiana na sapoti ya hali na mali katika kuendeleza maono waliyonayo katika kukuza vijapi vya watoto hasa wakiwa mashuleni.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa michezo mwandamizi wa (BMT) Charles Maguzu wakati wa sherehe za miaka 20 ya Baobab ambayo iliambatana na utoaji wa zawadi mbali mbali kwa washindi walioweza kuibuka kidedea katika michezo mbali mbali ikiwemo, mchezo wa soka, riadha, pete, pamoja na michezo mingine ambapo washindi walizawadiwa vikombe pamoja na medali.

Mwandamizi huyo amesema kwamba wao kama serikali kupitia baraza hilo wataendelea kushirikiana bega kwa bega na uongozi wa shule hiyo katika kukuza vipaji mbali mbali walivyonavyo wanafunzi wa shule hiyo kwani kwa lengo la kuweza kuwaendeleza zaidi kufika mbali.

Kadhalika Maguzu amewahiimiza walimu, na wazazi wanaendelea kuhakikisha wanalinda suala la watoto wao kuwa na malezi bora pamoja na kuwa wazalendo na nchi yao ikiwa pamoja na upendo ambao utawezza kuwafanya kufanya vizuri zaidi katika suala la elimu pamoja na mambo ya michezo mbali mbali.

"Kwa kweli nawapongeza kwa dhati uongozi mzima wa shule ya Baobab kwa kuwewza kunialika katika siku hii ambayo ni muhimu sana na kitu kingine niwapongeze kwa kuweka mikakakti madhubuti ya kuwaendeleza wanafunzi wenu katika nyanja ya michezo sambamba na masomo hii ni hatua nzuri sana na sisis kama serikali tutakuwa nanyi bega kwa bega katika kutimia malengo yenu", Maguzu

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Shajar Shani Swai ambayo ndiyo inayimiliki shule hiyo ya Baobab amebainisha kwamba wanaishukuru serikali kwa kuweza kuendelea kutoa sapoti ya hali na mali katika suala zima la kuboresha elimu pamoja na kushirikiana nao katika nyanja ya kukuza michezzo na vipaji kwa wanafunzi.

Maadhimisho ya miakaa 20 ya Taasisi hiyo ya Shajar yamekwenda sambamba na kufanyika kwa michezo mbali mbali pamoja na mbio za Marathon ambazo ziliandaliwa maalumu kwa ajiloi ya kuweza kuwasaidia watoto yatima na wenye mahitaji maalumu huku viongozi wa serikal viongozi wa dini, wakuu wa shule,taasisi wezeshi, wakuu wa Wilaya, wabunge pamoja na mawaziri walihudhulia kwa nyakati tofauti katika maadhimisho hayo.




▪️︎ Ataka kazi ifanyike usiku na mchana inapowezekana;

▪️︎ Asisitiza mashindano hayo ni fursa kubwa ya kiuchumi kwa Tanzania;

▪️︎ Awataka wakandarasi kukamilisha mikataba ya wafanyakazi na kushughulikia stahiki zao ndani ya wiki moja.


WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza kuongezwa kasi ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ili vikamilike kwa wakati na kukidhi viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Amesema kazi hiyo inapaswa kufanyika kwa kasi, ikiwemo kuongeza muda wa kufanya kazi pale inapobidi, ili viwanja vikamilike kwa wakati na Tanzania iwe tayari kabla ya ukaguzi wa maandalizi unaotarajiwa kufanywa na CAF.

Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo leo (Ijumaa, Agosti 21, 2026) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa viwanja vya mazoezi vya Farasi na Leaders Club jijini Dar es Salaam, ambavyo ni miongoni mwa viwanja vitakavyotumika katika maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027 yatakayofanyika kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda.

Amesema Tanzania haipaswi kusubiri hadi dakika za mwisho kukamilisha maandalizi yake kwa sababu CAF inahitaji kujiridhisha mapema kuwa miundombinu inayohitajika iko tayari.

“Twendeni tufanye kazi usiku na mchana tumalizie asilimia iliyosalia. Wenzetu wanaosimamia mashindano hawawezi kurisk tu kwamba tuko tayari, wanataka wajionee kwamba tuko tayari kukiwa bado kuna muda wa kutosha,” amesema.

Dkt. Mwigulu amesema mashindano ya AFCON hayapaswi kutazamwa kama tukio la michezo pekee, bali ni fursa kubwa ya kiuchumi ambayo Tanzania inapaswa kujiandaa kuitumia kikamilifu.

“Hii si michezo tu, bali pana uchumi ndani yake,” amesema na kuongeza kuwa baada ya kukamilisha miundombinu, nchi inapaswa kuelekeza nguvu katika kujiandaa kimkakati ili kunufaika na fursa za kiuchumi zitakazoambatana na mashindano hayo.

Katika ukaguzi huo, Waziri Mkuu pia ametoa maelekezo ya kushughulikia malalamiko ya wafanyakazi wanaoshiriki ujenzi wa viwanja hivyo, hususan kuhusu mikataba ya ajira, malipo ya muda wa ziada na stahiki nyingine.

Ameagiza Wizara yenye dhamana, wasimamizi wa miradi na wadau wengine kuhakikisha wafanyakazi wanapatiwa mikataba yao ndani ya wiki moja, huku hesabu za mishahara, malipo ya muda wa ziada na stahiki nyingine zikihakikiwa kwa kuzingatia makubaliano yaliyofikiwa.

“Suala la mikataba lishughulikiwe haraka, lakini pia wazingatie hizi hesabu walizozisema wafanyakazi. Hoja yao inaeleweka,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua uzalendo uliooneshwa na wafanyakazi hao kwa kuendelea na kazi licha ya changamoto walizozieleza, hivyo akaagiza masuala yao yashughulikiwe kwa mujibu wa sheria na makubaliano yaliyopo.

Aidha, amesisitiza kuwa mikataba hiyo izingatie kipindi ambacho wafanyakazi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwenye miradi hiyo.

Katika uwanja wa Leaders Club, Waziri Mkuu amewapongeza wafanyakazi kwa kuendelea kuchapa kazi na kuwataka waongeze juhudi ili miradi ikamilike ndani ya muda uliopangwa.

Amesema Serikali itaendelea kusimamia changamoto za wafanyakazi sambamba na kuhakikisha kasi ya ujenzi wa miundombinu inaongezeka, kutokana na umuhimu wa AFCON kwa uchumi, michezo na maendeleo ya nchi.

“Tusimwangushe Mheshimiwa Rais. Amejitoa sana kuhakikisha nchi yetu inakuwa mwenyeji wa mashindano haya. Twendeni tukamilishe kwa wakati,” amesema.

Awali, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, alisema viwanja vya Farasi na Leaders Club ni sehemu ya miundombinu inayojengwa ili kukidhi mahitaji ya CAF kwa ajili ya AFCON 2027.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Gerson Msigwa, amesema Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa karibu, sambamba na kushughulikia masuala ya wafanyakazi kwa kushirikiana na taasisi zinazohusika na masuala ya ajira na hifadhi ya jamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya wataalamu, ujenzi wa uwanja wa Farasi ulikuwa umefikia asilimia 74 na unatarajiwa kufikia zaidi ya asilimia 80 ifikapo mwisho wa mwezi huu, wakati ujenzi wa uwanja wa Leaders Club ukiendelea kwa kasi kuelekea hatua zinazotakiwa katika ratiba ya maandalizi.

Uwanja wa Farasi unajengwa kama uwanja wa mazoezi wenye vyumba vya kubadilishia nguo, vyumba vya waamuzi, madaktari na huduma nyingine muhimu, pamoja na mfumo wa kisasa wa kuondoa maji uwanjani.

Kwa upande wa Leaders Club, pamoja na huduma hizo, uwanja huo utakuwa na jukwaa lenye uwezo wa kuchukua takribani watazamaji 2,500.










Wafanyabiashara Tisa wa Mtaa wa Lumumba jijini Mwanza wamepata nafasi ya kujenga upya biashara zao baada ya NMB Bank, kwa kushirikiana na Reliance Insurance, kuwalipa fidia ya Sh1.072 bilioni kufuatia moto ulioteketeza maduka na mali zao Julai 3, 2026.

Meneja wa Madai ya Bima wa NMB Bank, Madoro Max, alisema wataalamu walitumwa kufanya tathmini ya uharibifu mara baada ya taarifa za moto kupokelewa. Tathmini hiyo ilithibitisha madai ya Sh1,072,554,090 kwa wafanyabiashara tisa waliokuwa na bima.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, aliwataka wafanyabiashara kulinda biashara na mali zao kwa bima. Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Faraja Ng’ingo, alisema malipo hayo yatawasaidia waathirika kurejesha biashara na vyanzo vya mapato.

Reliance Insurance ilisema wafanyabiashara tisa pekee kati ya zaidi ya 60 walioathiriwa walikuwa na bima. Mmoja wa wanufaika, Zablon Deogratius, alisema fidia ya NMB itawasaidia kuanza upya baada ya kupoteza mali na mitaji yao.












Na George Maziku, Mbogwe

MJUMBE wa Kamati ya Siasa ya wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita Pius Lukaga amemsifu na kumpongeza diwani wa kata ya N’homolwa, wilayani Mbogwe, mkoa wa Geita Pili Njile baada ya Diwani huyo kukamilisha ujenzi wa zahanati yake aliyoijenga katika kijiji anachotoka cha Nyanhwiga.

Lukaga ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za uzinduzi wa zahanati hiyo iliyopewa jina la PNS, alisema kuwa alichofanya diwani huyo ni utekelezaji Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), 2025-2030 kwa vitendo ambapo ilani hiyo inasisitiza serikali kushirikisha sekta binafsi kuwasogezea karibu wananchi huduma za jamii ikiwemo huduma za afya.

“Huyu Diwani pale wilayani chama tumtambua kama shujaa kutokana na kazi anazofanya za kutekeleza ilani ya chama, tunamshukuru sana kwa kazi anazofanya”, alisema Lukaga.

Aliongeza, “Huyu ni kiongozi mwenye utu na upendo mkubwa, kwasababu alikuwa na uwezo wa kumchukua mme wake kwenda kutalii na kula raha sehemu mbalimbali kama vile Dar es Salaam, Mbeya, lakini aliamua kuwekeza kwenye huduma hii muhimu kwa maisha ya wananchi wake, huu ni upendo mkubwa”, alibainisha kiongozi huyo wa CCM.

Lukaga aliwasihi wananchi wa kata ya N’homolwa kuendelea kumuunga mkono Diwani Njile na kamwe wasimwache kwani viongozi wa aina yake hawapatikani kila mahali na hawapatikani kila wakati.

“Nawaomba sana wananchi wa kata ya N’homolwa msimwache Diwani wenu, mtunzeni sana kama mboni ya jicho kwasababu viongozi wa aina hii hawapatikani kila mahali na hawapatikani wakati wote”, alisisitiza mjumbe huyo wa kamati ya siasa ya wilaya.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, mmiliki wa zahanati ya PNS ambaye pia ni diwani wa kata ya N’homolwa Njile, alieleza huduma zitakazotolewa na zahanati yake kuwa ni huduma za wagonjwa wa nje, upimaji, kliniki ya baba, mama na mtoto, huduma za dharura, na huduma za uzazi wa mpango.

Nae mfamasia wa wilaya ya Mbogwe Salum Mdimu aliyezungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Mbogwe, aliwahakikishia wananchi wa kata ya N’homolwa kuwa zahanati hiyo imekidhi vigezo vyote vya kisheria vya kutoa huduma za afya kwa watanzania hivyo wasihofu kwenda kutibiwa.

Nao wananchi wa kijiji cha Nyanhwiga waliotoa maoni kwa nyakati tofauti walimpongeza diwani Njile kwa kuwasogezea huduma za afya karibu, na kuwaondolea adha ya kufuata huduma hizo mbali na makazi yao.

“Nimefurahi sana kwa kufunguliwa zahanati hii na diwani wetu ambayo imetupunguzia usumbufu wa kwenda mbali, kabla ya zahanati hii tulisafiri mpaka Masumbwe kwani kuna baadhi ya huduma kama vile za vipimo hazikupatikana kwenye zahanati ya serikali iliyopo hapa kijijini kwetu, lakini sasa tutazipata huduma hizo kwenye zahanati ya diwani ya PNS”, alifafanua Colletha Lenard (31), mkazi wa kijiji cha Nyanhwiga.

“Kwa upande wangu nimefurahi sana kwasababu bado naendelea kuzaa, hii zahanati itakuwa msaada mkubwa kwangu kutokana na maelezo tuliyopewa na diwani wetu kwamba itakuwa na vipimo vyote kwa wazazi, zamani baadhi ya vipimo tulivifuata hospitali za mbali”, alibainisha Agnes Lucas (23), mkazi wa kijiji cha Nyanhwiga.





Na George Maziku, Bukombe

VITENDO  vya utoroshaji madini nchini kwa sehemu kubwa vinatokana na hatua ya serikali kuweka tozo lukuki kwa wachimbaji, Michuzi Blog imeelezwa.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa Chama cha wachimbaji wadogo wilaya ya Bukombe, mkoani Geita (GEREMA), Daniel Lusinge alipozungumza na vyombo mbalimbali vya habari ofisini kwake mjini Ushirombo.

Katika siku za karibuni kuliripotiwa matukio ya watu kukamatwa wakitorosha madini mbalimbali kinyume cha sheria, katika miji mbalimbali ikiwemo jijini Dar es Salaam ambako pia kuligundulika soko bandia la madini.

Lusinge ambaye pia ni Mwenyekiti wa soko la madini wilaya ya Bukombe aliwaambia wanahabari kuwa wachimbaji wanalipa tozo kuanzia mgodini baada ya kutoa mawe au mchanga kwenye maduara mpaka kwenye hatua ya mwisho wakati madini yanapofikishwa sokoni, jambo ambalo alisema linawakera na kuwakatisha tamaa wachimbaji. 

“Ukiacha watu wenye hulka ya kutenda maovu ambao wapo katika kila sekta, utoroshaji wa madini unachangiwa na uwepo wa tozo nyingi kwenye madini ambapo wachimbaji wanaanza kubanwa kwa tozo kuanzia mgodini, kwenye uchenjuaji mpaka sokoni, mambo hayo yanawakera wachimbaji wengi kwasababu wanabeba mzigo mkubwa wa gharama, wanaona kama wanaifanyia kazi serikali, maana watu wote wanataka faida hata serikali yenyewe inataka faida”,  alisema Lusinge.

Aliongeza, “Serikali inapaswa kupunguza tozo ili kuwashawishi wachimbaji wasitoroshe madini badala yake waende kuuza kwenye masoko yaliyowekwa na serikali ambayo yapo kila mahali nchini”, alifafanua katibu huyo wa GEREMA.

Kiongozi huyo wa wachimbaji wilayani Bukombe alishauri serikali kuboresha masoko ya madini nchini, huku akishauri utaratibu wa ukusanyaji mapato ya serikali kufanyika soko la madini.

Aidha, Mwenyekiti huyo wa soko la madini ameishauri serikali kuendelea kuwasaka na kuwaadhibu watu wote wanaojihusisha na biashara haramu ya utoroshaji madini nchini ili kukomesha uhalifu huo na hatimaye kuleta tija kwenye sekta ya madini na uchumi wa taifa kwa ujumla.

Wakati huo huo Lusinge ameiomba serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa kuwaletea mitambo ya utafiti na kuwauzia kwa bei nafuu ili kuwawezesha wachimbaji wengi wadogo kumudu na hatimaye kuchimba kwa uhakika.

“Tunaiomba serikali yetu kuisaidia sekta ya madini kwa kuleta mitambo ya kisasa ya utafiti wa madini ili tuweze kuchimba kwa uhakika. Pia tunaiomba serikali kutatua kwa haraka changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya madini ili kukuza sekta na kuifanya kuwa mhimili wa uchumi wa nchi yetu”, alisisitiza Lusinge.



Tanzania imejipanga kuanza kuzalisha umeme wa nyuklia ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuongeza vyanzo vya nishati na kukidhi mahitaji yanayoongezeka nchini, Mpango huo unalenga kuhakikisha Tanzania inaanza kutumia nishati ya nyuklia katika uzalishaji wa umeme, huku maandalizi na uwekezaji katika eneo hilo ukiendelea kuimarishwa na kukamilika ifikapo 2050.

Mtafiti Mwandamizi wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC), Eng. Christina Paul Nyakyi, amesema hayo jijini Tanga wakati akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu Kitaifa, amesema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Tanzania kuendeleza matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Eng. Nyakyi amesema lengo la mwaka 2030 ni Tanzania kuwa imeanza kuzalisha umeme wa nyuklia kupitia mtambo wa kwanza wa kuzalisha nishati hiyo, hii ina maana kuwa mwaka huo unatarajiwa kuwa mwanzo wa uzalishaji wa umeme wa nyuklia nchini, na si kwamba Tanzania itakuwa tayari imefikia kiwango kikubwa cha uzalishaji wa nishati hiyo bali ni hatua kwa hatua na kukamilika mwaka 2050.

Ameeleza kuwa uwekezaji huo ni muhimu kwa uchumi wa Tanzania kwa kuwa upatikanaji wa nishati ya uhakika ni msingi wa shughuli za viwanda, biashara na huduma mbalimbali, Kwa kuongeza vyanzo vya uhakika vya uzalishaji wa umeme, ikiwemo nishati ya nyuklia, Tanzania inaweza kuongeza uwezo wake wa kukidhi mahitaji ya umeme na kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana na upungufu wa nishati.

Katika sekta ya afya, Eng. Nyakyi amesema teknolojia ya nyuklia ina matumizi mbalimbali katika uchunguzi na matibabu ya magonjwa, ikiwemo saratani, amesema matumizi hayo yanaifanya teknolojia ya nyuklia kuwa na umuhimu mkubwa katika kuboresha huduma za afya na kusaidia wataalamu kupata njia bora zaidi za kugundua na kutibu baadhi ya magonjwa.

Amesema katika sekta ya kilimo, teknolojia ya nyuklia inaweza kutumika katika kuboresha uzalishaji wa mazao yanayoweza kustahimili mazingira mbalimbali, ambapo teknolojia hiyo inaweza kutumika katika juhudi za kudhibiti mbu wanaoeneza magonjwa, hatua ambayo inaweza kusaidia katika kukabiliana na changamoto za kiafya zinazohusiana na wadudu hao.

Aidha, ameeleza teknolojia ya nyuklia hutumika katika sekta ya ujenzi kupitia mfumo wa Non-Destructive Testing (NDT) unaowezesha wataalamu kukagua ubora, uimara na hali ya miundombinu bila kuharibu sehemu inayofanyiwa uchunguzi, ameongeza kuwa TAEC itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama na yenye manufaa ya teknolojia ya nyuklia ili kuongeza uelewa na kuondoa mitazamo hasi kuhusu teknolojia hiyo.

Kwa ujumla, mpango huo unaweka msingi wa Tanzania kutumia teknolojia ya nyuklia si kwa ajili ya umeme pekee, bali pia kuchochea maendeleo ya uchumi, afya, kilimo na miundombinu kupitia matumizi salama na yenye tija ya teknolojia hiyo.



Equity Group Holdings Plc imetangaza matokeo imara ya nusuya kwanza ya mwaka 2026, ikirekodi ongezeko la asilimia 32 la faida baada ya kodi kufikia TZS bilioni 841.75, kutoka TZS bilioni 640.1 zilizorekodiwa katika kipindi kama hicho mwakauliopita. Nchini Tanzania, Equity Bank Tanzania pia imeonyeshaukuaji imara baada ya kufikisha faida kabla ya kodi ya TZS bilioni 55.5, huku faida baada ya kodi ikikua kwa asilimia 82, ishara ya kuonesha kasi ya biashara, utekelezaji wenye nidhamuna kuongezeka kwa imani ya wateja katika soko.

Matokeo haya yanaonesha uimara wa Equity, uwezo wake wakukua katika mazingira ya biashara yanayobadilika namafanikio ya mkakati wake wa kutumia teknolojia kuboreshahuduma za kifedha. Ukuaji huu umechangiwa na kuimarika kwamapato, ufanisi wa uendeshaji, usimamizi thabiti wa viashiriavihatarishi na uwekezaji endelevu katika huduma za kifedhazinazoendeshwa na teknolojia, ambazo zinabadilisha namnawateja wanavyopata na kutumia huduma za benki.

Katika ngazi ya Equity Group , ukuaji huu unaakisi mafanikioya mageuzi ya muda mrefu ya taasisi hiyo kuelekea kuwa mtoahuduma za kifedha mwenye mifumo mbalimbali, ambaye nguzoyake kuu inajengwa kwenye teknolojia na uhusiano wa karibuna wateja. Equity inaendelea kuimarisha namnainavyowahudumia wateja kupitia mifumo ya kidijitali, matawi, mawakala na njia za malipo kwa wafanyabiashara.

Kwa Equity Bank Tanzania, matokeo ya nusu ya kwanza yamwaka yanaimarisha nafasi ya Benki katika kusaidia watubinafsi, wajasiriamali, Wafanyabiashara wadogo na wa kati, makampuni na taasisi za sekta ya umma. Matokeo hayayanaonyesha pia kuongezeka kwa imani ya wateja katika uwezowa Benki kutoa suluhisho za kifedha zinazogusa mahitaji halisiya kila siku, ikiwemo ukuaji wa biashara, malipo, akiba, mikopona usimamizi wa fedha.

Teknolojia imeendelea kuwa kichocheo muhimu cha matokeohaya. Katika Equity Group, asilimia 98.3 ya miamala yote ilifanyika nje ya matawi, huku asilimia 89.7 ya miamalaikichakatwa kupitia mifumo ya kidijitali. Mwenendo huuunaonyesha jinsi wateja wanavyozidi kuchagua huduma rahisi, salama na zinazopatikana kwa wakati wowote, na unaonyeshanafasi muhimu ya teknolojia katika kuongeza ufanisi, kuboreshahuduma na kurahisisha maisha ya wateja.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo hayo, MkurugenziMtendaji wa Equity Group, Dkt. James Mwangi, alisemamatokeo ya nusu ya kwanza ya mwaka 2026 yanaonyeshamafanikio ya safari ya muda mrefu ya Equity kujijenga kamataasisi ya kifedha ya kikanda, yenye huduma mbalimbali nainayowezeshwa na teknolojia.

“Matokeo yetu ya nusu ya kwanza ya 2026 yanaonyeshamafanikio ya mageuzi yetu ya makusudi kuelekea kuwa kundi la huduma za kifedha lenye huduma mbalimbali, linalowezeshwana teknolojia. Tunajenga taasisi iliyo tayari kwa siku zijazo, yenye uwezo wa kukua, iliyo salama na yenye kuleta matokeo, ikijengwa juu ya uwezo wa kidijitali, kuongeza ujuzi wawafanyakazi na utamaduni wa utekelezaji wenye nidhamu,” alisema.

Dkt. Mwangi aliongeza kuwa Equity inaendelea kujibadilishakutoka benki ya kawaida na kuwa taasisi jumuishi ya kifedhainayowezeshwa na teknolojia, yenye uwezo wa kukusanyamtaji, kuunganisha mifumo ya biashara na kuchochea ustawijumuishi na endelevu barani Afrika.

Kwa Equity Bank Tanzania, matokeo haya yanaweka msingiimara wa kuongeza kasi katika nusu ya pili ya mwaka 2026. Kipaumbele cha Benki kitakuwa kubadilisha kasi hii Ili kuwa nathamani kubwa zaidi kwa wateja, hususan kupitia suluhisho za malipo kwa wafanyabiashara zinazorahisisha makusanyo, kuongeza ufanisi wa biashara na kupunguza utegemezi wa fedhataslimu.
Miongoni mwa maeneo muhimu ya kimkakati ni Equity Lipa Namba, suluhisho linalowawezesha wafanyabiashara kupokeamalipo papo hapo, bila makato, kutoka benki yoyote au mtandaowowote wa simu, na kupata fedha zao wakati wowote. Kwa wafanyabiashara wadogo, wa kati na makampuni, hiiinamaanisha makusanyo ya haraka, mtiririko bora wa fedha, kupunguza hatari za kushughulika na fedha taslimu na kuwapawateja njia rahisi zaidi ya kulipa.

Kupitia Equity Lipa Namba, Benki inaendeleza ajenda yake yamageuzi ya kidijitali kwa kuwapa wafanyabiashara suluhisho la malipo linaloendana na mahitaji ya biashara za kila siku. Huduma hii inasaidia mauzo ya kila siku, makusanyo yawafanyabiashara na matumizi ya akaunti, huku ikichocheaukuaji wa amana, ukuaji wa biashara na matumizi mapana yamalipo ya kidijitali nchini Tanzania.

Pamoja na hilo, Equity Bank Tanzania itaendelea kuhamasishamatumizi ya Equity Mobile, huduma inayowawezesha watejakusimamia fedha zao kwa urahisi, kufanya miamala, kulipa bilina kupata huduma za benki mahali popote walipo. Benki pia itaendelea kuwekeza katika ulinzi kupitia bima, ili kuwasaidiawatu binafsi, wafanyabiashara na biashara kulinda kilewanachokijenga, kudhibiti vihatarishi na kukua kwa kujiaminizaidi.

Kuangalia mbele, Equity Bank Tanzania itaendelea kuwekamteja mbele, kuunga mkono ukuaji wa biashara na kuchangiamaendeleo ya uchumi wa Tanzania. Matokeo imara ya nusu yakwanza ya mwaka yanaimarisha dhamira ya Benki ya kutoasuluhisho za kifedha zilizo rahisi, za kidijitali na zenye ulinzi, ambazo zinaongeza thamani kwa wateja, wafanyabiashara, jamii, wanahisa na taifa kwa ujumla.

 Vodacom Tanzania Plc imeendelea kuonyesha ukuaji imara na kuzalisha thamani kwa wanahisa, wateja na jamii katika mwaka wa fedha uliomalizika Machi 31, 2026, mafanikio yaliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na uwekezaji endelevu katika miundombinu ya mawasiliano, huduma za kidijitali na huduma jumuishi za kifedha.


Matokeo haya yamebainishwa leo wakati wa Mkutano Mkuu wa 10 wa Mwaka wa Wanahisa wa Kampuni, ambapo wanahisa walijadili na kuidhinisha maazimio muhimu yanayohusiana na utendaji wa Kampuni kwa mwaka wa fedha 2026, malipo ya gawio, muundo wa Bodi, utawala bora pamoja na mwelekeo wa biashara kwa siku zijazo.

Katika mwaka wa fedha 2026, mapato ya huduma yaliongezeka kwa asilimia 21.8 hadi kufikia Shilingi trilioni 1.8, wakati faida kabla ya kutoa gharama za riba, kodi, uchakavu na upunguzaji thamani (EBITDA) iliongezeka kwa asilimia 38.8 hadi kufikia Shilingi bilioni 684.9.

Faida baada ya kodi iliongezeka kwa asilimia 18.4 hadi Shilingi bilioni 107.1, huku ukuaji wa faida halisi baada ya kodi ukifikia asilimia 125.5. Aidha Kampuni pia iliongeza idadi ya wateja wake hadi milioni 27.7, sawa na ongezeko la asilimia 22.3, ikichagizwa na ongezeko la asilimia 22.5 la wateja wa intaneti na asilimia 22.6 la wateja wa M-Pesa.

Matokeo haya yalitokana na uwekezaji mkubwa katika mtandao na majukwaa ya kidijitali ya Kampuni. Uwekezaji wa mitaji uliongezeka kwa asilimia 85.1 hadi kufikia Shilingi bilioni 323.9, ukiwezesha kuongezwa kwa vituo vipya 444 vya 4G na 25 vya 5G, sambamba na uwekezaji mkubwa katika mifumo ya TEHAMA na uboreshaji wa mtandao.

Kutokana na uwekezaji huo, wigo wa mtandao wa 4G ulifikia 76.3%, ikiwa ni ongezeko la asilimia 3.8, huku idadi ya watumiaji wa simu janja ikiongezeka kwa 31.5%. Tangu mwaka 2013, Vodacom Tanzania pia imejenga vituo 466 katika maeneo ya vijijini kupitia mpango wa Serikali wa kuimarisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini.

Utendaji huu mzuri wa Kampuni umewezesha pia kuongeza thamani kwa wanahisa. Mkutano Mkuu wa Mwaka umeidhinisha gawio la mwisho la shilingi 23.91 kwa kila hisa ya kawaida kwa mwaka wa fedha 2026, ambalo litalipwa ifikapo au kabla ya tarehe 15 Oktoba 2026 kwa wanahisa waliokuwa kwenye orodha ya wanahisa kufikia mwisho wa biashara tarehe 19 Agosti 2026.

Jumla ya gawio linalopendekezwa kwa mwaka huu wa fedha ni Shilingi bilioni 53.6, sawa na ongezeko la asilimia 18.4 ikilinganishwa na mwaka uliopita, hali inayoakisi sera ya Kampuni kuhusu gawio na dhamira yake ya kuweka uwiano kati ya kutoa thamani endelevu kwa wanahisa na kuendelea kuwekeza katika ukuaji wa biashara.

Mbali na thamani inayotokana moja kwa moja kwa wanahisa, Vodacom Tanzania imeendelea kutoa mchango mkubwa katika uchumi wa nchi. Katika mwaka wa fedha 2026, Kampuni ilichangia Shilingi bilioni 848 katika mapato ya Serikali kupitia kodi, tozo, ada za masafa ya mawasiliano na ada za udhibiti, huku ikitumia Shilingi bilioni 839 kwa wazabuni na washirika wa ndani wapatao 400. Kampuni pia iliwekeza Shilingi bilioni 6.9 katika mipango ya kijamii na kuwezesha ajira zisizo za moja kwa moja kwa zaidi ya Watanzania 320,000, wakiwemo wafanyakazi huru na mawakala wa M-Pesa.

Akizungumzia utendaji huo, Mkurugenzi wa Fedha wa Vodacom Tanzania Plc, Bi. Hilda Bujiku, alisema:

“Matokeo yetu ya mwaka wa fedha 2026 yanadhihirisha usimamizi makini wa fedha na mtazamo wenye uwiano katika matumizi ya mtaji. Tumeendelea kuimarisha biashara huku tukiwekeza kwa kiasi kikubwa katika mtandao, teknolojia na majukwaa yetu ya kidijitali, na kwa kufanya hivyo, kuzalisha thamani kubwa zaidi kwa wanahisa.


Mwelekeo huu unatuweka katika nafasi nzuri ya kuendeleza ukuaji, kudumisha uimara wa kifedha na kunufaika na fursa zijazo katika uchumi wa kidijitali unaoendelea kukua nchini Tanzania.”

Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania Plc, Philip Besiimire, alisema:

“Matokeo haya yanaonyesha thamani ya kuwa na mtazamo wa muda mrefu katika uwekezaji na ukuaji. Imani ya wanahisa wetu imetuwezesha kuendelea kuwekeza katika mtandao wetu, teknolojia na huduma za kifedha za kidijitali, huku tukizidi kuboresha utendaji wa biashara na kutoa thamani endelevu kwa wanahisa. Tunapoangalia mbele, tunaendelea kujielekeza katika kujenga biashara imara zaidi, yenye uwezo wa kuhimili changamoto na iliyo tayari kwa siku zijazo, inayozalisha thamani ya kudumu kwa wanahisa, wateja na jamii zetu.”

Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Tanzania Plc, David Tarimo, alisema:

“Imani na uungwaji mkono unaoendelea kutolewa na wanahisa wetu ni msingi muhimu wa uwezo wetu wa kujenga thamani endelevu kwa muda mrefu. Tutaendelea kujizatiti katika uwekezaji wenye nidhamu, utawala bora na usimamizi wenye uwajibikaji wa mitaji ya wanahisa. Mafanikio yaliyopatikana katika mwaka wa fedha 2026 yanaweka msingi imara wa ukuaji unaoendelea na mchango zaidi katika mustakabali wa uchumi wa kidijitali nchini Tanzania.”

Katika kipindi kijacho, Vodacom Tanzania itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya mtandao, huduma za kifedha za kidijitali, teknolojia, kuboresha uzoefu wa wateja na ubunifu, huku ikiimarisha ushirikiano unaolenga kuchochea maendeleo ya kidijitali na kiuchumi nchini Tanzania.

Kampuni itaendelea kuelekeza uwekezaji wake katika matokeo yanayodumu, kuimarisha utendaji wa biashara, kuboresha huduma kwa wateja, kutoa thamani kwa wanahisa na kuongeza mchango chanya kwa jamii.
Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Tanzania Plc, David Tarimo (katikati), akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mkutano Mkuu wa 10 wa Mwaka wa Wanahisa wa Kampuni ya Vodacom, uliojadili na kuidhinisha maazimio muhimu kuhusu utendaji wa mwaka wa fedha 2026, ikiwemo malipo ya gawio na mwelekeo wa biashara. Mkutano huo uliidhinisha gawio la mwisho la Shilingi 23.91 kwa kila hisa, sawa na jumla ya Shilingi bilioni 53.6 kwa mwaka wa fedha 2026. Mkutano huo ulifanyika Agosti 20, 2026 katika makao makuu ya Vodacom jijini Dar es Salaam. Wengine ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom Tanzania Plc, Philip Besiimire (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Fedha wa Vodacom Tanzania Plc, Bi. Hilda Bujiku (kushoto), na wajumbe wa bodi, Margret Ikongo (wa pili kulia), na Joyce Nkini-Iwisi (kulia).






Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), imefanya ziara ya ukaguzi katika mradi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko, kwa lengo la kujionea hatua ya utekelezaji wa mradi, kukagua miundombinu na maandalizi yaliyofanyika kuelekea kuanza kwa matumizi ya bandari hiyo, pamoja na kutathmini fursa zitakazotokana na uwekezaji huo katika shughuli za uvuvi na uchumi wa buluu.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 20 Agosti 2026, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof. Yunus D. Mgaya, ambapo Bodi hiyo imepata fursa ya kukagua maeneo mbalimbali ya bandari na kupata maelezo kuhusu hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya kuanza kwa shughuli zake.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Prof. Mgaya, amesema ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo, akieleza kuwa kukamilika na kuanza kufanya kazi kwa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko kutakuwa hatua muhimu katika kuimarisha sekta ya uvuvi nchini.

"Bandari hii ina nafasi kubwa katika kuongeza ufanisi wa shughuli za uvuvi, kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, pamoja na kutoa fursa za ajira na biashara. Nawahimize wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kutumia fursa zilizopo katika Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko kwa kuwekeza katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na sekta ya uvuvi," aliongeza Prof. Mgaya

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa TAFICO, Dkt. Suleiman Kiula, ndc , amesema Shirika hilo linaendelea na mchakato wa kushirikisha sekta binafsi pamoja na wadau mbalimbali kuhakikisha bandari hiyo inaendeshwa kwa ufanisi, kwa kutoa huduma wezeshi kwa viwango bora na nafuu ili kuvutia Meli nyingi kutumia bandari hiyo ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Dkt. Kiula amesema TAFICO inaendelea kutekeleza mikakati ya kushiriki kikamilifu katika kuendeleza shughuli za uvuvi wa kisasa na ukuzaji viumbe maji, ikiwemo uwekezaji katika Meli za uvuvi wa bahari kuu, uanzishaji wa mashamba ya kufuga samaki, miundombinu wezeshi, pamoja na kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi.

"Kuanza kwa shughuli za Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko kutafungua fursa mbalimbali kwa wavuvi, wafanyabiashara na wawekezaji, huku kukiwa na matarajio ya kuongeza ajira na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Kilwa na maeneo mengine nchini," alieleza Dkt. Kiula.

Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko ni mradi wa kimkakati unaolenga kuimarisha shughuli za uvuvi nchini. Miundombinu ya bandari hiyo inajumuisha gati lenye urefu wa mita 315 la kuhudumia meli za uvuvi zaidi ya kumi kwa wakati mmoja, eneo la kuhifadhi samaki, mtambo wa kizalisha barafu na eneo la matengenezo ya meli, hatua inayolenga kuongeza ufanisi katika shughuli za uvuvi na mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi.




























Na Janeth Raphael – MichuziTv 

Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) umeendelea kuimarishwa kwa kuunganishwa na zaidi ya mifumo 30 ya taasisi mbalimbali, hatua inayolenga kurahisisha mchakato wa zabuni za umma, kuongeza ufanisi na kuimarisha uhakiki wa taarifa za wazabuni.

Hatua hiyo pia imeongeza uwezo wa Serikali kudhibiti matumizi ya nyaraka zisizo halali katika mchakato wa ununuzi wa umma, huku wazabuni wakipata unafuu wa kuwasilisha taarifa na nyaraka zinazohitajika wakati wa kushiriki zabuni.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Dennis Simba, amesema maboresho hayo yanaendana na maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mifumo ya Serikali inaunganishwa na kusomana ili kuwezesha kubadilishana taarifa kwa ufanisi.

Simba ameyasema hayo leo, Agosti 20, 2026, jijini Dodoma wakati akieleza utekelezaji wa bajeti ya PPRA kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2026/2027.

Kwa mujibu wa Simba, NeST kwa sasa imeunganishwa na mifumo zaidi ya 30 inayohusisha maeneo mbalimbali muhimu katika uthibitishaji wa taarifa za wazabuni. Mifumo hiyo inajumuisha mifumo ya kibenki na malipo, hifadhi za jamii, bodi za usajili wa wataalamu pamoja na mifumo inayohusiana na utoaji wa leseni.

Amesema kuunganishwa kwa mifumo hiyo kumeboresha kwa kiasi kikubwa namna taarifa za wazabuni zinavyothibitishwa, kwani taarifa muhimu zinaweza kupatikana na kuhakikiwa moja kwa moja kupitia mifumo husika.

Simba amesema hatua hiyo pia imepunguza uwezekano wa kuwasilishwa kwa nyaraka za kughushi katika mfumo wa NeST, kwa kuwa taarifa na nyaraka mbalimbali zinaweza kufanyiwa uhakiki kupitia mifumo iliyounganishwa.

Aidha, amesema mfumo huo umeendelea kupunguza mzigo kwa wazabuni ambao hapo awali walilazimika kuandaa na kuwasilisha rundo la nyaraka katika hatua mbalimbali za mchakato wa zabuni.

“Ndiyo maana tunasema ununuzi wa umma sasa umerahisishwa na unaweza kutumia muda mchache kwa sababu rundo la nyaraka tayari lipo ndani ya mfumo,” amesema Simba.

Amesema matumizi ya teknolojia katika ununuzi wa umma siyo tu yanalenga kurahisisha taratibu, bali pia kuongeza uwazi, ufanisi na uaminifu katika mchakato mzima wa zabuni.

Kwa hatua hiyo, NeST imeendelea kuwa nyenzo muhimu katika utekelezaji wa ununuzi wa umma kwa njia ya kielektroniki, huku kuunganishwa kwake na mifumo mingine ya Serikali na taasisi mbalimbali kukitarajiwa kuongeza zaidi ufanisi wa huduma na kuimarisha udhibiti wa taarifa katika sekta ya ununuzi wa umma.



 

Na.Mwandishi Wetu- Dodoma

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake na kuitaka kuharakisha matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS) katika zao la parachichi ili kuongeza tija kwa wakulima.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Deodatus Mwanyika, ametoa pongezi hizo leo Agosti 20, 2026 jijini Dodoma baada ya Kamati hiyo kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya WRRB kwa mwaka 2025/26.

Mhe. Mwanyika amesema Kamati imeridhishwa na utendaji kazi wa WRRB, hasa katika kushughulikia changamoto za wananchi, na kuitaka Bodi hiyo iongeze kasi katika utoaji elimu ili kuchochea matumizi ya mfumo huo katika maeneo mengine.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wajumbe, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Kamati hiyo na kuihakikishia kuwa ataendelea kulinda majukumu ya taasisi zilizo chini yake kwa mujibu wa sheria.

Awali, akiwasilisha taarifa kwa Kamati hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema kwa mwaka 2025/26, WRRB imetoa leseni kwa waendesha ghala 235, kusajili ghala 951, wanunuzi 390, waweka mali 2,667 na kutoa stakabadhi za ghala 214,170.


Top News