.jpeg)
.jpeg)
CHIEF WA KIBONDO MWAMVUA RAJAB RUHAGA NYAMALIZA AFARIKI DUNIA GHALFA AKIWA MSIBANI MALINYI, MOROGORO

.jpg)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amesema Ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya maendeleo ya Afrika (AfDB), katika miradi ya kimkakati unaendelea kuimarika jambo linawezesha nchi kukua kiuchumi.
Ameyasema hayo Machi 25, 2026 alipokuwa anapokea nakala za hati za utambulisho za Mwakilishi Mkazi mpya wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania Bi. Mary Manneko Monyau, katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Mhe. Kombo amesema miradi hiyo imejikita zaidi katika sekta za miundombinu, usafirishaji, na nishati ambazo ni uti wa mgongo wa mabadiliko ya kiuchumi nchini. Ameongeza kuwa kwa sasa Benki hiyo inafadhili miradi 27 ikiwemo Barabara ya Mzunguko wa Nje ya Dodoma, Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) na Mradi wa nyaya za umeme za chini ya bahari unaounganisha visiwa vya Zanzibar, Pemba, na Mafia.
Aidha amempongeza Bi. Monyau kwa uteuzi wake na kueleza kuwa Serikali ina imani kubwa na uzoefu wake, hususan kutokana na mafanikio aliyoyaonesha alipokuwa Mwakilishi Mkazi nchini Sudan.
Kwa Upande wake Bi. Monyau amesisitiza kuwa AfDB itajikita zaidi katika kuoanisha mipango yake na Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050 ambapo imepania kuongeza upatikanaji wa mitaji na kusaidia miradi inayoinua uhuru wa kifedha wa Tanzania, huku ikizingatia kukuza ajira kwa vijana na miundombinu wezeshi itakayochochea ukuaji wa viwanda na biashara kanda nzima.
.jpeg)
Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Machi 24.2026 jijini Dar es Salaam Mwenda amesema miongoni mwa hatua zilizoanza kuchukuliwa ni pamoja na kuunda kamati ndogo ya wataalam inayohusisha Wizara ya Kilimo kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko, maofisa wa Forodha na waagizaji wa mafuta kwaajili ya kuweka utaratibu utakaoanza kutumika kuingiza mafuta hayo hivi karibuni.
Amesema utaratibu huo mpya unalenga kuwezesha biashara ya Mafuta baina ya Tanzania Bara na Zanzibar na kuchangamsha biashara katika Bandari za Bagamoyo, Mbweni na Kunduchi ambazo ndiyo hutumika kuingiza mafuta hayo.
"Tutatoa punguzo kwa mafuta yanayoingia Tanzania Bara kutoka Zanzibar ili kuwawezesha wanaoingiza mafuta hayo kupata faida, Serikali kupata kodi na pia kulinda viwanda vya ndani" amesema Mwenda.
Aidha Kamishna Mwenda amewaonya wafanyabiashara wa bidhaa hiyo watakaojihusisha na magendo baada ya kuanza kutumika kwa utaratibu huo kuwa Serikali haitasita kuwachukuli hatua kwa mujibu wa sheria.
Katika hatua nyingine Kamishna Mkuu amesema TRA itaendelea kutoa elimu ya kodi kwa wananchi wote na kuwezesha biashara baina ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa kuhakikisha kila anayestahili kulipa kodi analipa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Mhe. Ali Suleiman Ameir imeipongeza TRA kwa uwajibikaji na kuahidi kuwa wataendelea kushirikiana nayo katika kuieleza jamii umuhimu wa kulipa kodi.
Akizungumza katika kikao hicho, Ameir kazi inayofanywa na TRA imekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa hususan kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo hatua ambayo kwa kiasi kikubwa inachochea ukuaji wa uchumi.
Aidha amesema wamefanya ziara hiyo mahususi kwaajili ya kujifunza namna mfumo wa usimamizi wa kodi za ndani (IDRAS) unavyofanya kazi na kuipongeza TRA kwa kuanza kutumia mfumo huo ambao umeweza kuokoa muda wa walipakodi kwa kupata huduma popote walipo huku ukipunguza kwa kiasi kikubwa watumishi wa TRA kuonana na Walipakodi.
Wajumbe wengine wa Kamati ya Bunge ya Baraza la wawakilishi waliohudhuria kikao hicho wamepongeza juhudi za udhibiti wa magendo zinazofanywa na TRA huku wakiahidi kusimamia vizuri matumizi ya kodi zinazokusaywa.





TanTrade inaongoza mageuzi ya sekta ya biashara nchini Tanzania kupitia Mpango wa CART.IS, unaolenga kuimarisha biashara ya kidijitali kwa urahisi na ufanisi zaidi.
Kupitia ujumuishaji wa mifumo ya taasisi mbalimbali na matumizi ya taratibu zisizohitaji karatasi, CART.IS inapunguza urasimu, inaokoa muda na gharama, na kurahisisha huduma kwa wafanyabiashara.
TanTrade ikiwa ni mdau muhimu wa mpango huu chini ya Mkurugenzi Mkuu Dkt. Latifa Mohamed Khamis, amebainisha kuwa kupitia Mpango huu, Tanzania inaongeza ushindani wake katika soko la kimataifa kwa kutoa huduma za haraka za kisasa na zenye kuaminika.
Makamu wa Rais amesema hayo, wakati akifungua Kongamano la Kimataifa kuhusu maboresho ya sera ya elimu na mitaala nchini, linalofanyika katikaUkumbi wa Maktaba Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais, amesema suala la utekelezaji wa mabadiliko na maboresho yaliyofanyika kwenye Sera yetu ya Elimu na Mafunzo, na Mitaala kuanzia Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari hadi Elimu ya Juu, linataka Watanzania wote kutafsiri vema maono ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya mfumo wa elimu unaozingatia kutoa ujuzi na maarifa ili kumwezesha mhitimu kumudu mazingira yake, na kumudu ushindani kwenye ulimwengu wa kazi.
Aidha, Makamu wa Rais amesema suala la elimu jumuishi inayozingatia usawa ni miongoni mwa vipaumbele, ambapo Serikali imeweka msisitizo katika uwepo wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia pamoja na miundombinu rafiki kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesema kongamano hilo la kimataifa kuhusu maboresho ya sera naelimu na mitaala ni fursa nzuri ya ushirikishwaji wa watalaam na wachambuzi kuangalia jinsi ambavyo utekelezaji huo unaendelea.
Amesema kongamano hilo litaangazia zaidi namna bora na ufanisi yakutekeleza mageuzi ya elimu nchini.
Awali akitoa Taarifa kuhusu Kongamano hilo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. William Anangisye amesema malengo ya kongamano hilo ni kutafakari na kujenga uelewa wa pamoja miongoni mwa wadau mbalimbali kuhusu sera ya sasa ya elimu na mafunzo na marekebisho ya mitaala na athari zake kwa maendeleo endelevu.
Pia, amesema lengo lingine ni kuibua mijadala ya kitaaluma kuhusu mitaala yaelimu ya msingi, sekondari na elimu ya juu, kutafakari juu ya maendeleo yakitaaluma na nafasi ya elimu ya ualimu kulingana na maboresho ya sera yaelimu na mafunzo, kubadilishana uzoefu wa kimataifa na kikanda jinsimaboresho ya elimu yanavyoweza kuchangia ukuaji jumuishi na mustakbaliwa maendeleo endelevu.
Maboresho yaliyofanywa na serikali kwenye baadhi ya maeneo ya Sera ya Elimu na Mafunzo, yamefanyika ili kuondoa changamoto mbalimbali zilizokuwa zikiikabili elimu ya Tanzania, zikiwemo, kujikita zaidi kwenye elimu ya nadharia badala ya vitendo na pia, kutokuwepo kwa fursa za elimu na mafunzo zinazozingatia mahitaji ya soko la ajira.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa kuhusu maboresho ya Sera ya Elimu na Mitaala nchini, linalofanyika katika Ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tarehe 25 Machi 2026.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa kuhusu maboresho ya Sera ya Elimu na Mitaala nchini, linalofanyika katika Ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tarehe 25 Machi 2026.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. William Anangisye akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa kuhusu maboresho ya Sera ya Elimu na Mitaala nchini, linalofanyika katika Ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tarehe 25 Machi 2026.
Akifungua kikao hicho, Dkt. Maulid mesema kuwa watumishi wanapaswa kuwajibika kikamilifu katika nafasi zao huku wakidumisha mshikamano ili kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi.
“Tunapaswa kuwajibika kwa nafasi zetu kwa kuwa wamoja na wenye mshikamano ili kuleta tija katika utimizaji wa malengo ya taasisi,” amesema Dkt. Maulid.
Katika kikao hicho, watumishi wapya waliojiunga na ADEM kutoka taasisi mbalimbali walipata fursa ya kujitambulisha, ambapo waliaswa kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kujituma ili kuchangia maendeleo ya taasisi hiyo.
Kwa upande wake, Dkt. Lucas Mzelelela amesisitiza umuhimu wa watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma kwa kufanya kazi kwa bidii na nidhamu wakati wote wawapo kazini.
“Kila mtumishi anapaswa kutumikia kiapo chake cha utumishi wa umma kwa kuwajibika ipasavyo na kuwa na nidhamu ya kazi kwa muda wote wawapo kazini,” amesema Dkt. Mzelelela.
Kikao hicho kililenga kufanya mapitio ya mipango ya taasisi kwa mwaka wa fedha unaoendelea, kukumbushana majukumu ya kazi pamoja na kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi na taasisi kwa ujumla.


































.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)








