Farida Mangube Morogoro
Lori la mizigo lenye namba za usajili T729 BBT pamoja na tela namba T677 BTY limeteketea kwa moto katika eneo la Lugono, karibu na Nyama Choma Barabara Kuu ya Iringa–Morogoro.
Tukio hilo la Lori kuwaka moto limetokea usiku wa kuamkia March 19 katika mazingira ambayo bado hayajafahamika wazi ambapo limeathiri vibaya sehemu ya mbele ya gari hiyo.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifika katika eneo la tukio na kufanikiwa kuudhibiti moto huo kabla haujasambaa zaidi, licha ya uharibifu mkubwa uliokwisha kutokea
Mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, akiwemo mwandishi wa Michuzi Blog, walishuhudia lori hilo likiwa limeteketea huku juhudi za uokoaji zikiendelea.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, mtu mmoja anasadikika kupoteza maisha kufuatia tukio hilo. Inadaiwa kuwa mwili wa mtu huyo uliungua vibaya kiasi cha kufanya utambuzi kuwa mgumu, huku mabaki yanayoaminika kuwa ya binadamu yakionekana katika eneo la tukio, ingawa utambuzi rasmi bado unasubiri uthibitisho wa mamlaka husika.
Wakati huo huo, jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro zinaendelea ili kutoa taarifa rasmi kuhusu chanzo cha ajali hiyo, kuthibitisha idadi ya waathirika pamoja na kueleza hatua zinazochukuliwa.
Aendelea kutufuatilia Michuzi Blog na Michuzi Tv ili kupata taarifa zaidi





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...