Home
Unlabelled
mama
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Huyu spika mbabe kweli mbunge akimuuliza waziri maswali ya kipumbavu anajibu yeye kwa kumshushua, pia anatumia silaha hiyo kuwabana Wabunge wa upinzani wanapowabana Mawaziri wa Kikwete kwenye budget zao, unakuta Mbunge wa upinzani anamuuliza swali Waziri, na Waziri hatoi maelezo ya kueleweka au anajibu tofauti, Mbunge wa upinzani akitaka maelezo zaidi au akimtaka Waziri astiki kwenye swali aliloulizwa basi Spika anaingilia na kudai swali lilishajibiwana hapo hapo anamtaka akae na aleta hoja nyingine, yaani kwa kifupi ukitaka kuuliza swali jiandae kuumbuka, Bunge linaendeshwa kibabe mno. MUNGU IBARIKI TANZANIA
ReplyDeleteKuna wafugaji wenye jumla ya ng'ombe 600,000 wameambiwa wahame kwenye bonde la Usangu kwa sababu wanaharibu mazingira, sasa waziri kaulizwa na bwana mahera (Cheyo) kwamba hawa wafugaji waende wapi maana wameambiwa warudi kwao na wengi wanatoka umasaini na Usukumani, sasa kutoka Mbeya hadi huko kwao wataruka na helcopter? kibaya zaidi ni kwamba sasa hivi wako kwenye mashamba yaliyotoka kuvunwa sasa kilimo kikianza si itakuwa balaa na wakulima, Waziri akajibu eti wameunda tume chini Wizara tatu (ardhi, utalii na mifugo) ili kutatua tatizo hilo na wanasubiri majibu, Cheyo akauliza tena kwa sasa hivi ng'ombe wale na kunywa wapi maana hamna eneo walilotengewa na wafugaji wanaingiza ng'ombe kinyemela kwenye eneo walilokatwaza wakati wa usiku kwa ajili ya kunywesha maji mifugo yao, Spika akamwambia kwamba Waziri alishajibu kwamba imeundwa tume maalum kutatua tatizo hilo
ReplyDeleteHivi jamani huyu ni Sitta ambaye alikuwa kiboko zamani katika kutaka kutoa shilingi ama mwingine?kama ni yeye anazeeka vibaya, unajua angekuwa mnyamwezi asingekuwa hivi maana kwake yeye naona cheo hiki kinampa wazimu, nini bwana kuna minyamwezi inayoheshimika kama akina Chifu Fundikira, marehemu Balozi Tumbo, akina Mapalala na akina Kasela Bantu na akina Tambwe,. Ukoo wa Sita haujulikani kabisa hapa Tabora labda huko Urambo ndio maana anajitutumua akifikiri atajulikana, thubutu, hata akija hapa TBR hakuna anayemmind anapita tu kwenda huko Ulyankulu, asilete ubabe,Bungeni kunatakiwa busara na hekima na siyo kutegemea Uwana Mtandaoa.Tunaomba rais na waziri mkuu wamshughulikie mru wao huyu, asilete utemi katika Bunge, hatukumtuma alete vioja vyake.Alafu eti mage katimiza mika 60!hafai kufanyiwa birthday huyo!kasahau walimu wenzake waliomfanya ajulikane na wamefanya kazi kubwa sana ya kuipitisha kasi mpya ikulu, sasa amewasahaua, atashuka tu!
ReplyDeleteAlo wewe anoy wa hapo juu naona unanikumbusha mbali sana maana nilipokuwaa shule ya msingi niligoma kufanya kazi kwa mwalimu jamaa walikuwa wananiita Sitta maana ni wakati ule Sitta alipotoa shilingi mpaka Moringe(RIP)ama Cleopa (waziri mkuu wa wakati ule ni mmoja wa hao) ilibidi ambembeleze nakumbuka mpaka picha ilitoka ktk magazeti, sasa kumbe kabadilika hivi. Ni kweli anataka kujulikana kinguvu. Nilifika UK kwa shughuli zangu nilibahatika kukutana na Mheshimiwa mmoja wa chama cha LABOUR, mara moja akaniulizia mzee Malecela, alo anajulikna sana mzee huyu na naheshimika sana na jamaa wa Labour kama mwanasiasa mstahiki,wanashangaa kwanini hayupo juu katika nyanjab za siasa za TZ .Nilimwambia ni Makamu wa chama, akafurahi walau kusikia hilo, hivyo chema chajulikana hata bila kujikweza kama huyo spika wetu.Asubiri aingie katika wanazuoni atajulikana na siyo kuforce.
ReplyDeleteVipi huyu mama Mnyarwanda!naona anafanana sana na watu wa kule ama atahari za Ulyankuru!
ReplyDeleteEasy guys alipo tangaza hiyo bday ya mkewe hawakuangusha part ilikuwa ni kumpongeza wakati majadiliano na uchambuzi wa mambo unaendelea.
ReplyDeleteMsimsumbue mama wa watu umri wenyewe umekwenda
ReplyDelete