sanamu ya mwalimu kule mitongo, butiama

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Ni: Mwitongo
    Si: Mitongo

    ReplyDelete
  2. wewe uliyemkosoa michuzi hapo juu pia umekosea!

    SIO: MWITONGO
    NI : MWINTONGO

    MIMI NAISHI HAPA, SASA BISHA....

    ReplyDelete
  3. Nilitundika Saa Wednesday, October 11, 2006 6:15:59 PM. Nikaandika si Mwitogo bali ni Mwitongo. Mimi natoka huko huko. Sisi tunaita, Mwitongo. Nyerere si Mkurya ni Mzanaki. Wazanaki wanaita "mwitongo", kama waitavyo Wajita kwa maana kwamba ni mahali palipohamwa but relics zake bado zipo, kwa mfano, in terms of makaburi ya mababu, miti ya matunda, na mabaki ya nyumba. Case closed!

    ReplyDelete
  4. Mnabishania nini maana ya hilo jina ni kuwa ni sehemu ya watu waliojaa matongotongo.Kuitwe mwintongo au mwitongo kikurya au kizanaki hakubadilishi hali ya kutopenda kunawa uso asubuhi kuondoa tongotongo kwenye macho ya watu wa eneo hilo wawe wakurya au wazanaki asubuhi huwa hawanawi uso wala kupiga mswaki wanakurupuka tu kwenda kwenye shughuli zao.

    ReplyDelete
  5. Nyinyi watu wa Musoma Kwa ubishi msije mkaanza kushikiana ubishi hapa.Case Close!!

    ReplyDelete
  6. MBONA KAMA LINASOGEA KULIA TARATIBU LENYEWE?

    ReplyDelete
  7. Akikasirika mpaka leo kifimbo chake kinacheza na yeye anasogea, siku ya mwisho alikishika kulia, shauri yenu.

    ReplyDelete
  8. We Butiama,
    hata kama umezaliwa huko, lakini anavyosema Trio kaka ndivyo tulivyofundishwa shule kwenye history.
    Sasa wewe kama unataka kuchokonoa vile unavyojua wewe, inabidi ukabadilishe vitabu vyote na uitishe breaking news.

    ReplyDelete
  9. vitabu gani hivyo vya historia? historia ya mwafrika imeandikwa na mzungu.Mnaambiwa kuwa Mlima Kilimanjaro umegunduliwa na wazungu wakati wachaga walikuwa pale siku zote na nyie mnakubali.

    ReplyDelete
  10. RadioButiama,
    Tunajua Mwalimu Nyerere alikuwa Mzanaki, wewe hatuna hakika. Alivyoelezea kuhusu Mwitongo ni kama anavyokuambia Trio Kaka sasa hiyo unayojaribu kusema wewe labda baadaye itakuja kukubalika. Tafuta kama utaweza pata hotuba yake aliyotoa siku anakabidhiwa ile nyumba aliyojengewa na jeshi. Alielezea kuhusu Mwitongo. Anasema kuwa mwitongo ni mahame. Kuhama siyo mpaka lazima uende kilometa alfu hata mita kumi ni kuhama. Na walihama pale baada ya Chief Burito kufariki. Sasa kama Mwlm ni hakuwa anajua Kizanaki hilo mimi simo.

    ReplyDelete
  11. asante sana kuona mjadala wa Butiama umenoga.
    Mimi naitwa Manyerere Nyembereka, ingawa mara zote nimekuwa nikitumia jina la Jackton kama jina la baba yangu mzazi.

    Kwetu ni Muhunda, Butiama, jirani kabisa na Mwitongo mnayoijadili! Mwitongo maana yake ni mahameni. Si kweli kwamba Mwitongo ni mahali pa kuzikia. Mwitongo ni mahali popote ambako mtu/familia iliishi, kisha ikahamia mahali pengine. Hapo palipohamwa ndipo panapoitwa mwitongo. Kwa hiyo, wapo watu wanaodhani kuwa Mwitongo ni kijiji! Hapana. Mwitongo ni kijisehemu tu cha mahame. kwa kuwa siku hizi maeneo yamekuwa finyu, ni wazanaki wachache wana Mwitongo, maana wakitoka walipo, wataenda kuishi wapi? Kila mahali pana mwenyewe!

    Pia neno Mwitongo, hata Wanyarwanda-Watutsi na Wahutu, wanalitumia kwa maana hiyo hiyo ya mahameni! Kweli, inawezekana asili ya Wazanaki ni huko huko! Sina uhakika na hili.

    Mchangiaji mmoja kataja makabila yanayoshabihiana na Wazanaki. Ni kweli kabisa kuwa Wazanaki, wangoreme, wakurya na kadhalika, wanasikilizana sana. Mimi naweza kuzungumza Kizanati, mwingine akazungumza kikura, mwingine akatwanga Kingoreme, au Kiikizu, sote tutaelewana tu! Kimsingi, haya si makabila, bali ni 'clan', yaani koo! Lakini Wajaruo, Wanandi, Wamaragori na makabila mengine ya aina hiyo, hatusikilizani nao kwa lugha. Lakini ajabu ni kwamba Wakisii tunasikilizana barabara!

    asanteni,

    Manyerere

    +255 713 335 469

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...