KUNA MDAU KANITUMIA WARAKA HUU NAMI NAUPOSTI KAMA ULIVYO:


Ndugu Michuzi,

Salamu.

Ninayo yangu matano : Kwanza, wewe ni mwandisi wa magazeti (mpigapicha). Sawa. Kuna kitu kinaitwa kwa lugha ya Kiingereza, "intellectual property", na kinalindwa sana kwa heshima na askari wa doria aitwaye, "copyrights". Kwa muda mrefu, umekuwa ukitundika, tundika mapicha mengi ambayo mengine ni copyrighted. Na baada ya kuyatundika, naona unayalinda na askari wa doria hao hao, kama copyrights yako. Pengine, sielewi. Lakini huu ni wizi mkubwa.

Pili, ki-journalism, kuna kitu kinaitwa “freedom of expressions”. Lakini wengine tunaamini kuwa uhuru wa kusema au kuandika kitu chochote, in the name of “freedom of speech” bila social nidhamu, ni wendawazimu mkubwa. Ndio maana una-threaten waandikaji wa maneno machafu, machafu kwenye blogu lako, ambao hujigamba kuwa ni uhuru wa kutoa maoni na kuwasiliana (kutuma na kupokea news, information and propaganda nzuri au mbaya - propaganda ambazo wakati mwingine wataalamu wa mambo ya communication huita “political and social propaganda”. Lakini kwa upande mwingine, we must be very informed when we attempt to trudge on this thin-cutting edge: censorship! For time may come when vya wale walio “high priests” tu ndivyo vitapokelewa na kutumwa ili visikike – a one-way information generation – na ku-control minds za walalahoi au walio nje ya mainstream.

Tatu, unapendelea sana u-paparazi wa vilivyo vizuri tu - monuments nzuri. Tuletee picha za walala hoi pia kwa wingi tuone the daunting Tanzanian condition, na tujaribu ku-contribute to resolve the obtaining ugly situation. Tuelemishe bila ya kutupaka na one-sided stories. You may not be feeding us with news, information or education but numbing propaganda, which may numb us to death! Nina uhakika kuwa wana-blog wana ability ya kupambanua na how to remain sane katika ulimwengu wa sasa in which we are bombarded with instantaneous information. If some cannot, let us educate them; they have the ability and capacity for such functionally informative education.

Nne, sina ubaya na yale uyafanyayo. Hii inatusaidia sana sisi Watanzania wa ughaibuni katika kuona yale yatokeayo nyumbani ki-picha. Na pia husaidia wa nyumbani kuona yale yatokeayo ughaibuni, hususani, safari za viongozi wetu na wawakilishaji wetu. Picha, bwana, huzungumza mara elfu moja kuliko maneno ya kuandika. Picha ni "gestalt" - inapenya moja kwa moja hadi kwenye kiini cha "psyche". Ndio maana ni rahisi kwa washiriki wa blogu hii kupenda sana kuandika, andika "comments" zao. Maneno ya kuandika, kwanza lazima ujue kusoma neno moja, moja. Halafu utunge sentenso na para kabla ya kuunda picha (kuelewa) kile usomacho. maneno ni "linear". Lazima kuyatunga moja, moja, kama shanga!

Mwisho, wewe ni mpigapicha wa Gazeti la Daily News (gazeti la serikali au la umma). Nielemishe, kama nimekosea. Sijui kama kila wakati unatumia kamera yako ama ya kazini na pia kupata picha ambazo wakati mwingine tunaziona kwenye blogu lako. Kutumia kamera ya kazini kwako na kwa kuwa wewe una uhuru wa kupata picha kutoka kwenye archive ya Daily News - picha ambazo mimi siwezi kuzipata kwa urahisi bila kibali na kuzitumia - huoni kuwa hapa kuna kile kiitwacho katika business transactin environment, "conflict of interest" au kujinufaisha?

Kwa kuwa haya niliyoandika yana uzito mkubwa ki-blogu, napenda sana yasomwe pia na waheshimiwa wana-blogu. Tuzidi kupanuana constructive mawazo; ni maarifa mazuri.

Rommel Mauma

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 41 mpaka sasa

  1. Maneno mazuri,yana mafunzo fulani fulani ndani yake.Kwanini mwandishi anachanganyachanganya lugha?Ni ili aonekane msomi zaidi au ni ulimbukeni tu?Inaonekana wazi kwamba kiswahili anakijua fika,anakiandika vizuri tu.
    Ndugu maneno yako mazuri yanapoteza uzito kwa uchanganyaji wa lugha.Tabia hii hata wabunge wetu wanayo,tabia mbaya sana hii.Chagua lugha moja,andika,utaeleweka.

    ReplyDelete
  2. ..sielewi point yake ni nini bado

    ReplyDelete
  3. Asante sana watanzania wenzangu kwa kumpa ukweli Michuzi maana nilikuwa nafikiria ni jinsi ya kuwasiliana nae ili nimuelimishe na mambo ambayo yanafanana na uwazi alioutoa Romel.
    Asante allie.

    ReplyDelete
  4. muchuzi, mwambie huyo romel anaweza kuanzisha blog yake kama hapendelewi na uendeshaji wako..
    Keep it up..
    Kutoka Ugaibuni..

    ReplyDelete
  5. Anony wa 3.15 asante sana! Jamani lugha hizi, hata kama mtu unataka kuchanganya kiingereza na kiswahili basi fanya hivyo kwa akili siyo unatuandikia 'ki-journalism' huo ni upuuzi gani?
    Michuzi anachanganya lugha ndiyo, lakini nia yake ni kuleta nakshi fulani, na vichekesho kwenye kazi yake, anapoandika mambo ya maana hafanyi upuuzi huo.
    Kuhusu maoni yako, kusema ukweli mie naungana na wale wanaosema Michuzi blog yake hii, wacha afanye apendavyo, na atoe picha apendazo...si mali yako wala ya serikali hii na ushukuru kuwa unapata kusoma mambo yaliyomo. Kama hafuati sheria zilizopo za haki miliki basi hana budi kuwajibika mwenyewe, lakini bado hilo ni tatizo lake mwenyewe, na ajirekebishe kwa faida yake mwenyewe.
    Na kwako Rommel (hivi hilo jina ulitoa wapi?) unapoandika kumkosoa mtu, andika kama mtu mwenye nia ya kusaidia siyo kukosoa. Tusisahau kuwa Michuzi amepiga hatua kubwa sana kuanzisha blog hii, na hata kuwezesha watu kutoa maoni na kadhalika. Ni vizuri kujenga, kuliko kubomoa, kukosoa si kubaya, ila tafuta njia nyingine ya kufikisha ujumbe vizuri, siye tumezoea malalamiko tu...

    ReplyDelete
  6. We fala utakuwa Mkwamba tu! Inaonyesha kwa jinsi gani ulivyo "simple minded person". Mi sijui tatizoliko wapi kama we hupendi we kamua. Unataka kutuletea Ugoloko wakohumu. Blog ziko kibao sio lazima uje humu hujalazimishwa. Mirost ameamua ku base katika anga hizi za wajanja kama wajanja.

    ReplyDelete
  7. Tatizo wabongo huwa tuko obsessed kuangalia what is wrong with other people na sio vitu gani positive hao watu walivyo navyo.Hii tabia ndio inaturudisha nyuma sana waafrika na inaonyesha ubinafsi wa hali ya juu miongoni mwetu.

    Huyu mwandishi hana tofauti na millions of nay-sayers ambao kila ukija na idea huwa wanatafuta vijisababu kibao kukuambia kwa nini huwezi kufanikiwa.Wao wako obsessed nakukukatisha tamaa na kutafuta kitu gani unafanya kibaya.

    Huyo mwandishi alianza kwa nia nzuri lakini ukisoma zaidi unaona anang'at ana kupuliza hapo hapo.Lugha anayoitumia Michuzi hapa ni nzuri na huwa inachangamsha audience wake.

    Brother Michuzi usikate tamaa kabisa na haya maneno yanayoandikwa.Nilisoma story yako kule kwa kaka Jeff Msangi kuhusu ulipoanza kazi y apigaji picha na ilinipa motisha sana.Ulielezea jinsi mtu alivyoandika article kuponda picha zako na ukamfuata boss wako na kulalamika.Lakini boss wako akakuambia kuwa ukiona mtu ananaidka hata kitu kibaya kuhusu picha zako ujue ameona kazi unayofanya.

    Hapa napo wembe ni ule ule.

    Mturutumbi.

    ReplyDelete
  8. Sina mengi ila namuambia mwandishi kwa herufi kubwa: BLOGI ZIKO NYINGI AU ANZHISHA YAKO. MICHUZI ANATUFANYIA OFA TU HALIPWI CHOCHOTE (NO COMMERCIALS INDEED). Bw. Michuzi ni gift from above. Hata Nyerere alipondwa hivi hivi alipong'atuka ndio watu wanamuona wa maana. Msimuudhi Michuzi aki-quit, tulio nje tutapata wapi habari.

    Maaaaaan, Mauma's comments suck. We lea mataahira na kufaidisha wazungu angalau mwenzio anatupa news za bongo na SAUMU kali bila kujali.

    BIG UPS MICHUZI. Mungu akuzidishie.

    ReplyDelete
  9. Huyu jamaa Romel kwanza jina lake halisi sio hilo. Huyu anaonekana haishi Ughaibuni. Yuko hapo hapo Dar Es Salaam. Wanamuonea wivu Michuzi.Hii blog ni private ya Issa Michuzi. Yeye mwenyewe ana uhuru wa kufanya lolote. Hata kama anatumia picha za Daily News, lakini kwa faida ya nani? Kwa faida yetu wote na hasa sie tulio Ughaibuni. Kwa kweli bahadhi yetu tulishapoteza radha na hamu ya Tanzania. Bwana Michuzi na mapicha yake amepiga pale pale tunapotaka watu wa ughaibuni. Michuzi hachana na huyo jamaa hana sera yoyote zaidi ya wivu wa kawaida wa wabongo.

    ReplyDelete
  10. Rommel, mawazo yako na mantiki ya mwelekeo wa hoja zako haviendani kabisa na suala zima la mtandao na blogs (samahani sijui ki-Swahili nasaha cha blog). Mtandao na mwelekeo mzima wa blog ni kujaribu kukwepa viunzi kama copyrights, conflict of interests, intellectual properties, etc. na kuwapa watu uwezo wa moja kwa moja kutoa na kupokea habari. Hivyo unavyotaka Michuzi afanye kwa kufuata ushauri wako ni mbinu ya kutawala mawazo (censorship) na kuhodhi habari. Hizo ndiyo sera za akina Mkapa za Ukweli na Uwazi wakati kila kitu ni siri ya serikali. Michuzi angeweza kutengeneza hela nzuri kwa kuuza uwezo wa kutembelea picha na habari zake (subscription) lakini pia angekuwa anawanyima akina siye uwezo wa kupata habari hizo.
    Michuzi, endelea na kazi yako nzuri. Tuko hapa ughaibuni na Mnyamwezi wa Karate.

    ReplyDelete
  11. wa moja ni wa moja tu, hata umpe kumi; atarudi na moja! We Rommel umeanza kumtembelea Michuzi lini? sisi tumeanza wakati bado ana "triple digits", Several times I've seen a photo with comment like, Kwa hisani kutoka..na kadhalika. This is a sort of source referencing and aknowledgement. Professional practise!!!. Otherwise nimeona picha za watoto wa shule wakisubiri mabasi, picha za makorongo barabarani, misururu ya magari, mlundikano wa nyumba, ombaomba na vingine vingi tu. Do you consider these: quoting "Monuments nzuri"? or cause you have not seen what you want to see?
    Talking about Conflict of Interest, serious, just because he is carring Daily News camera, he can not take a picture for himself?. Moreover these are agreement between employee and employer. You do not know, I do not know, let's just enjoy the Information delivered to us for free!!!. Wewe Romell unataka kuniambia you can/have not use Office pen for personal use? or it is too small. Michuzi is an artist at work 24*7. Michuzi is for Tanzanian and not Daily News only. By the way Michuzi, when is your birthday, we can come up with Michuzi day. I'm out!

    ReplyDelete
  12. Namuunga mkono huyo jamaa wa juu hapo na mwisho yote aliyo eleza huyu Rommel ni kama michuzi anazitumia hizo Camera na picha kwa manufaa yake Profit ,lakini hii kitu ni "FREE" copyrights, conflict of interests, intellectual properties, etc.Hazina Nafasi hapa

    ReplyDelete
  13. Michuzi unajua CYNTHIA MASASI ni binti mzuri sana lakini basi tu, Wabongo hawana shukrani wanamtukana sana wakati anamafanikio mazuri tu. Nilisikia ana taka ku act movie katika miji furani ya Tanzania na huku marekani itakayo elezea maisha yake halisi nadhani ataiita bongoland 2, vipi Michuzi unahabari zozote kuhusu hiyo movie? Michuzi narudia tena kama utapata muda wa kuisoma hii comment naomba maelekezo ni wapi tuta pata kalender zake? Pili tutaweza kweli kuona picha zake zote zilizo baki humu blogoni?Asante

    ReplyDelete
  14. Michuzi wewe ni mtu mzima vitu kama hivi ushakutana navyo sana kwenye maisha yako. si kila mtu anafurahia maendeleo yako pole sana na mungu akuzidishie huo moyo wa uvumilivu. Kama kuna mabadiliko unatakiwa kuyafanya tutakwambia sisi na sio mtu anaonekana siku ya kwanza tu na anataka mabadiiko, we tumia hata Camera ya ikulu sie shida yetu ni picha tu

    ReplyDelete
  15. Jamani wabongo vipi huyu Rommel sijui siametumia haki yake kutoa maoni kama ninyi mnavyo toa maoni kumu criticize yeye? Hana ubaya na MICHUZI ametoa maoni kama sisi wana blog hayatupendezi ni sawa tu ametoa maoni sioni kwa nini watu wote humu mmekalia huyo aanzishe ya kwake mara eti ana wivu sijui, hee dude it was just a comment Michuzi anaweza kuifata ama kuikataa that is it! mnaweza kumwona huyu chizi lakini nyinyi hapo ndiyo machizi, comments sikiliza ukiona haifai pinga siyo eti jamaa anakuonea wivu, mara wabongo hatupendani ama anzisha ya kwako? hayo ni maneno ya kitoto kabisa. Sidhani kama kuna haja ya kumtukana huyu bwana eti anawivu wakati alikuwa anatoa comment zake tu. Well done Rommel good comment and it is up to michuzi to think about it na wewe mtoa maoni unakalibishwa kutoa yakwako yatakayo jenga/fundisha wana blog wote ikiwa ni pamoja na owner mwenyewe Mr. MICHUZI

    ReplyDelete
  16. HIVI JAMANI KUMBE KUNA UPENDELEO KWENYE MISS WORLD,SIKUJUA KAMA HATA NANCY SUMARI ALIPENDELEWA ALIPO TWAA TAJI LA MISS WORLD AFRIKA?

    Miss World upendeleo mtupu - Wema

    2006-10-12 09:35:09
    By Somoe Ng?itu


    Wakati mrembo wa Tanzania, Wema Sepetu, akidai kuwa upendeleo umejaa katika mashindano ya urembo ya dunia, Kamati ya Miss Tanzania imesema kuwa haijakata tamaa kutokana na kutimiza malengo yake ya hapa nyumbani.

    Wema alisema kuwa alikwenda katika mashindano hayo kama mshindani na alijitahidi kushiriki katika mashindano yote ya awali katika kuhakikisha anajiweka katika nafasi nzuri lakini bahati haikuwa yake.

    Alisema kuwa hata mrembo wa Angola ambaye ndiye alitwaa taji la Malkia wa Afrika lililokuwa linashikiliwa na Nancy Sumary hakuwa na mvuto ila kilichomsaidia ni baadhi ya majaji walioshiriki walikuwa wanatoka Angola.

    ”Nilijitahidi kadri ya uwezo wangu, na sidhani kama nina mapungufu yoyote ila naamini kuwa katika mashindano yoyote kuna kushinda na kushindwa,” alisema Wema.

    Aliongeza kuwa pia alijitahidi kutangaza vivutio vya utalii na utamaduni wa Tanzania kwa kugawa bendera na fulana zenye bendera ya taifa na wanyama mbalimbali.

    ReplyDelete
  17. TO MICHUZI PLEASE....
    I didn`t intend to use your name michuzi as the one who post a comment. Very sorry MICHUZI I wrote your name by mistake it should read MIZZOU. Thank you

    ReplyDelete
  18. its true tunahitaji vitu vya maana kwenye blog mambo ya kinje this kinje that we dont like it. okay pili freedom of speech is allowed and we love constructive criticism kwahito fulani kaandika kingereza kiswahili it dont hel as long as you get the message wabongo hovyo kupigana madongo tuu hela watu hawana majungu millioni kumi its about time make money wake your minds up sio bwana. michuzi blog yako ni nzuri inatukutanisha at the same time we are coming from different backgrounds kuna watu wamezaliwa na mitusi you cant change them so tutasukumana nao hivyo hivyo tuu. tufanyaje kitu kidongo madongo hela zero ongeeeeni giza likiingia mtalala shauri zenu big up michuzii

    ReplyDelete
  19. ?????????????
    Freedom of speech jamani, tusiwe vihiyo basi jamaa alitoa mawazo yake,lakini tatizo ambalo mi naliona amechanganya hayo mawazo na ukosoaji kwa pamoja,lakini kama tunavyomuambia yeye ni haki yake kusema yalio moyoni mwake kama mnavyofanya nyie na mimi. Now kama unapungana nae attack point zake na sio ohh unatumia lugha mchanganyiko au anzisha yako sasa na wewe si usisome habari yake kama unakasirika basi. Anyway Michuzi asente kwa kutuwekea kitu kinachotuonyesha fikra za level tofauti.


    "In order 2 survive u got 2 learn 2 live with regreats"

    ReplyDelete
  20. Mimi sio mnajimu wa nyota au jinsia za zawtu lakini kwa umbile la jina la Maima, naamini ni mwanaume. Nimesoma maoni yako unayoyaita "uhuru wa kuandika" na nakupongeza kwa hilo ILA nasikitika hata wewe uko nje ya mstari. Naamini umeandika uliyoandika kwa kurupuka na sio kufikiria kwa kina kwa kuwa UNADHANI WEWE NI MSAFI.lo hakuna lolote. Angalialiboriti lako na usitake kujikweza. Usitake umaarufu kupitia Michuzi, jimwage nawe tukuchambue kama karanga. KAKA MICHUZI, UZI ULE ULE,USILEGEZE

    Pia nadhani, bwana Michuzi anabusara sana, maana kwa uzoefu wake wa kuifahamu jamii ilivyo na makasoro yake, kwanza amekusetiri kwa kutokujibu. HONGERA MICHUZI. Kwa kuwa yeye ni mtu mtanashati, bila kusema,ametuwekea uchafu waki bwana Maima ili tukueleze. SI AJABU WEWE NDIE MWANDIKA MATUSI KATIKA BLOG HII. SASA TUNAKUFAHAMU.

    Naungana na wengine kukuomba bwana maima ufungue blog yako na umuombe bwana michuzi akulete kwetu ili tuone wewe ni bigwa katika lipi. Usihofu, tumia uhuru wako wa kuandika UTULETEE KAZI YAKO/ZAKO nasi tutakujibu.

    Kaka michuzi, sisi wa ughaibuni tunafurahia kazi yako inayoonysha 1.unaenda na wakati..kuleta matukio kila yatokeapo 2.ni mwana histiria...na historia inatufudisha jana,leo na kesho..hivyo picha za matukio ya kihistoria ni muhimu.

    Natamka wazi kuwa, kupitia blog ya Michuzi wanangu wameanza kufahamu wawazi wao walikozaliwa.

    ASANTE KAKA MICHUZI, HONGERA. JINA LAKO KUBWAAAAAAAAA

    ReplyDelete
  21. Hii ni mara yangu ya kwanza kutoa mawazo yangu kwenye blogu hii lakini nimekua nikifuatilia kwa muda mrefu sasa.
    romel ametoa hoja nzuri sana lakini kuna mambo yanayotakiwa kuzingatiwa sana,kwanza mambo ya intellectual properties ni mambo ya kisheria na yanachanganya watu wengi sana lakini iko siku yatakuja kutumbukiza watu wengi pamoja na blogu kama hii shimoni,ni vema mtu akasema chanzo (acknowledge source) ya taarifa yoyote pale anapoipata,lakini la pili,tusipoiendeleza lugha yetu ya kiswahili na tunajua mwaka huu ni mwaka wa lugha za kiasili kwa umoja wa Afrika(AU) sasa sijui tunasubiri nani atusaidie,nilitegemea kwa mtu kama romel angetumia misamiati ya kiswahili ili watu wakae na waseme hivi hili neno maanake nini,ngoja nikalitafute kwenye kamusi.badala yake anakimbilia kiingereza,tafadhali tusiwe kama acolite wa kenya au wabunge wetu wanaochanganya lugha kila siku.
    la tatu,Michuzi wakati niko nyumbani nilikuwa sioni umuhimu mkubwa wa hii blogu lakini sasa nauona,ila nadhani ni kweli kuwa Tanzania si peponi kiasi hiko,kuna ufedhuli na uhayawani unaoendelea... hebu tupe picha za segerea,dampo,usafiri wa treni,barabara za mbezi,shule za primary za nje ya miji zenye walimu wawili bila choo,hospitali ya mwananyamala,wanafunzi vituo vya mabasi saa 12 jioni na mambo kama hayo as well,si mazuri tu yanayotakiwa kuwa kwenye eneo hili.asante

    ReplyDelete
  22. wewe hapo juu uliyeweka comment na kujita michuzi, sisi wana blog hii tunajua kwamba tunajua kwamba wewe sio michuzi, na mtu yoyote akisoma maoni yako tu ataona jinsi unavyojichanganya kwa sababu umejiita michuzi lakini unamuongelea michuzi kama mtu mwingine. kama huwezi tumia jina lako hapa unauhuru wa kuweka anonymous.

    ReplyDelete
  23. KUNA KAUKWELI NDANI YA MANENO YA BWANA ROMMMEL MAUMA
    1) HII BLOG NI BURE, LAKINI NAKUMBUKA KUWA KUNA PICHA MOJA BWANA MICHUZI ALIWEKA PICHA DUKA LAKE LA KUPIGA PICHA-SIO KWAMBA ANAFANYA MARA KWA MARA LAKINI BLOG INAWEZA KUTMIKA KUTANGAZA BISHARA YAKE. MFANO MIMI NILIKUWA SIJUI KAMA MICHUZI ANA BIASHARA YA KUPIGA PICHA, NIMEIJULIA HUMU HUMU.
    2) HAKUNA ANAYEPINGA KUWA HII BLOG NI MAENDELEO YA HALI YA JUU SANA. LAKINI INAONEKANA WAPIGA PICHA WENZAKE BWANA MICHUZI WANAIBIWA PICHA ZAO-HIVYO WANA HAKI YA KUNUNG'UNIKA
    3) NAKUPONGEZA BWANA MICHUZI KWA UJASIRI WA KUWEKA HAYA MAONI, MWINGINE ASINGEWEKA. HII INAONYESHA UKOMAVU WA FIKRA NA MTAZAMO WA MAMBO.
    4) MWISHO, NASHAURI KUWA UWE UNAWEKA PICHA AMBAZO NI ZA KWAKO, AMBAZO HAZITALETA UGOMVI NA WAPIGA PICHA WENZIO.

    ReplyDelete
  24. uliyeweka maoni ya 4:44pm juu tu kwamba michuzi halipwi kwa kazi hii, hivyo huwezi kudemand picha gani akuwekee.

    ReplyDelete
  25. MICHUZI hongera kwa habari motomoto unazotupatia nduguzo tulioko ng'ambo. Huyu anaejiita ROMELO ni limbukeni tu hana lolote. maoni yake yanachanganya kila mtu sababu anasema anataka habari za nyumbani na wakati huo huo analalamika kwanini habari zinatumwa-kama umesoma kipengele anachosema unapataje picha za kwenye archive ya Daily News inaonyesha waziwazi wivu na kitimanyongo alichonacho kwa MICHUZI na kwa wale wenye maendeleo kuliko yeye. Wivu wa watanzania baina ya wao wa wao ndio unaoturudisha nyuma kila siku.
    ROMELO hujalazimishwa kukodoa mimacho yako humu ndani hivo tuachie sisi haya mambo kama huyawezi. HONGERA SANA MICHUZI kwa kutuletea habari za nyumbani. GOD BLESS YOU BROTHA

    ReplyDelete
  26. http://ema.mtvbaseafrica.com/index.jhtml

    ReplyDelete
  27. mzee wa sumo:
    http://mpoki.blogspot.com/

    ReplyDelete
  28. Kwako Romel,
    Uchanganyaji wako wa lugha unatia Kinyaa hata kama kuna watu watakuunga mkono. Ukichanganya na habari yenyewe unavyorukia mambo ya copyright ndio kabisa unaoneka mchovu wa kutupwa. Ili ujifunze rejea post ya ghmm huko juu.
    Hupendiblog ya Michuzi tafuta utakayopenda au uanzishe yako uone kama hata utafikia hatua aliyofikia Michuzi.

    ReplyDelete
  29. Angalieni hawa kina Mazembe, hii imekuwa ndio advertisement media? Michuzi watu kama hawa ondoa postings zao. Wanataka kujivunia bila jasho. Find other means of advertising, sio kwenye blogu ya watu bure bure. Hawa ndio kina Romell. Jamani kama kuna mpiga picha anasema picha ni ya kwake, Ai-publish au ajitambulishe kwenye hii blogu kuwa picha ni ya kwake. Otherwise, shut up and go to bed. Michuzi Big up, kuna mtu ameuliza birthday yako, sema bwana watu tukupe zawadi, you deserve better. DO YOUR THING, WE GOT YOUR BACK!!

    ReplyDelete
  30. Michuzi siku hizi umekuwa mwanasiasa mnoo.Naiunga mkono paragraph ya tatu ya ROMMEL MAUNA. Kuhusu Michuzi kuonyesha matukio mazuri tu ya home na hasa ya yanayotokea kwenye majukwaa ya kisiasa kila siku TZ na kuyapa mgongo matukio kutoka mitaani wanapoishi watanzania halisi. Sio vibaya kuonyesha mambo mazuri lakini inafaa uonyeshe pia matukio ya kila siku ya watu wa kawaida mitaani mazuri na mabaya.Nakumbuka miaka ya 1980 ulikuwa unatoa picha mzuri sana za maisha watu wa kawaida mitaani, naamini picha hizo ndizo zilizokupa umaharufu miongoni mwa wapiga picha na waandishi wa habari wa TZ kwa kufuatilia maisha ya waTZ WA Kawaida,sasa umesahamu picha zilizokupa umaarufu na kuegemea kwenye siasa. Kumbuka wahenga walisema "usiache mbachao kwa msala upitao"

    ReplyDelete
  31. Hivi mnajua ule mwimbo wa "eeeh jamani eeh binadamu hatosheki, hata ukimpa nini eeh milele haridhiki."

    Ndio hichokinachoendelea hapa.Maana kila mtu anataka Michuzi alete picha anazotaka yeye.Michuzi akilet ahizo picha za walalahoi watu wengine watasema Michuzi mbona unaleta picha mbaya tu za Bongo kwani bongo hakuna vitu vizuri.

    Michuzi endelea na kazi yako na blog hii imepata umaarufu kwa wembe huo huo ulioutumia tokea mwanzao.Usibadilishe kwa ajili ya watu.Hao watu nao wanaweza kufungua blog zao vile vile na ku post hizo picha wanazotaka.

    ReplyDelete
  32. michuzi naona umeanza usanii wa katrina hapo juu.toa na acha mara moja

    ReplyDelete
  33. Wewe Michuzi Fala nini? Unaweka tangazo la kusaidia watu wa Bush wakati watu wako wanakufa na njaa, Kwa nini usiweke Tangazo la kuwasaidia wabongo wenzako?

    ReplyDelete
  34. Anatengeneza pesa na ads za google huyo.

    ReplyDelete
  35. Waswahili tuna tabu sana yani mtu ajitumikishe mwenyewe na bado mnamsumbua ooh mara hujui mara sijui nini kwanini hamfungui blog yenu au bora uwende hizo zenye matao ya juu hii ya michuzi mkatuachia sisi kina maimuna.

    ReplyDelete
  36. Huyo bwana romeni ni mshamba tu nadhani ni mtani wangu bwengo ishomile,ndio wenye tabia ya kuchanganya lugha,si unajua wahaya tena......

    ReplyDelete
  37. Web log au, kwa kifupi, blog, ni makala ya mara kwa mara inayoelezea msimamo wa mtu binafsi kimtandao katika kujieleza wazi, kufafanua na kuwasilisha fikira, imani, na msimamo wake kuhusu mada yeyote ile. Sio lazima mwana-blogu ajitambulishe yeye ni nani. Hii inawawezesha mwana-blogu na washiriki au wadau wake kubadilishana mawazo na kujihusisha katika malumbano, ambacho ni kiini hai cha uhuru wa kutangaza (kupeleka) au kupokea masuala mbalimbali. Ingawa teknologia hii ya blogu inanufaisha wachache tu wenye Mtandao, blogu inasaidia sana demokrasia ikue, inawili na itande bila ya sensa ya serikali au vikundi vya siasa, dini, mila, na mtu binafsi. Malumbano budi yaendeshwe kwa nidhamu safi; lakini mara nyingi huleta mabishano yaliyojaa lugha chafu na majidai binafsi yasiyo na msingi au mantiki yeyote. Kuelemishana ni maarifa; maarifa ni maisha bora.

    Kuna tofauti kati ya blogu na ukumbi"chatroom" (kwa lugha ya Kiingereza).

    ReplyDelete
  38. Kila mtu na staili yake kwa watu wake. Hata yule mzungu aliyekuja Bongo kupiga sinema ya Darwin Nightmare alipiga mambo mabaya matupu, tena akapiga kwa kujifichaficha! Si kwamba alikuwa hawezi kupiga kwa uwazi au kupiga mambo mazuri yaliyoko nchini, ila hiyo ndiyo staili aliyoamua kuitumia, akiamini kwamba ndiyo itaonyesha kwamba kile alichokipiga ni cha kweli. Hii ya Michuzi ni staili yake. Kama wewe hupendi fungua blogu ya mtu mwingine usome. Mimi napenda kila mtu awe na staili yake, hata huyu aliyezua mjadala huu, kaandika kwa staili yake, kachanganya kimombo na kiswahili, hiyo ni staili yake.

    ReplyDelete
  39. Bwana Michuzi, unafahamu kabisa kwamba kabla ya mafanikio kunakuwa na vizingiti mbali mbali. Nataka kukuambia kuwa huyu jamaa naye ni kizingiti kimoja wapo. pengine unahitaji watu kama hawa ili upate nguvu zaidi(be stronger)The more chalanges you go through the stronger you get. Keep it up Issa, we r with you..

    ReplyDelete
  40. Mimi ninaunga mkono wale wanaosema madai ya "Rommel" hayana msingi.

    Kila mtu ataendesha blogu yake kwa staili yake anayoona inafaa kulingana na interests zake.

    Mimi naona Michuzi analeta uwiano mzuri wa picha za burudani, siasa, kihistoria na vile vile mabandiko kama haya yasiyo na picha.

    Sasa wewe unataka alete "picha mbaya" ili iweje? Kwani sehemu mbaya za bongo huzijui? Zikibandikwa kwenye blogu ndio itakuwaje?

    Kama ni kusaidia we saidia tu, sio mpaka Michuzi abandike picha kwenye blogu.

    ReplyDelete
  41. Fisadi ni fisadi tu!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...