jk akiwa na mwanzilishi wa nyumba ya sanaa dar, sister jean pruitt na waziri wa habari, utamaduni na michezo mh. seif khatibu wakati wa tamasha la chuo cha sanaa bagamoyo. enzi zake nyumba ya sanaa palikuwa na vijana walemavu waliokuwa wakijifunza kazi za sanaa na pia wasanii mbali mbali walikuwa wanapatumia kuonesha na kuuza bidhaa zao. hivi sasa ni naiti kilabu na walemavu hawajulikani walipo. nasikia sister jean ameanza mchakato wa kurejesha hadhi ya nyumba ya sanaa kuwa nyumba ya sanaa na si vinginevyo. na pia hivi sasa anaendesha kituo cha watoto wa mitaani kiitwacho dogodogo senta mtaa wa mansfield. habari zake zaidi bofya hapa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Yaani suti ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeachia! Hebu angalieni mkono wa suti (sleeve) - aibu gani hii!!!!

    ReplyDelete
  2. Hivi anony hapo juu,unayesema suti ya rais 'imeachia' umeangalia vizuri kweli?+au we mwenzetu hujui aina ya suti.Aaahaha ahahha umenichekesha sana!Hii aina ya suti inafanana kabisa na kaunda suti,tofauti yake hizi zina mikono mirefu.Huvaliwa bila shati ndani,hapo mwisho wa mkono wa suti kuna kifungo...sasa huo ndo uwazi kama akifungua kifungo aweze kuivua kwa urahisi.Ndio style yake hiyo ndugu yangu,umeondoka bongo lini?Hata mimi sipo bongo lakini nazijua hizo.Poa,wakati mwingine uangalie kwa makini..halafu utoe maoni yako eeeh,umesikia????

    ReplyDelete
  3. Nashukuru mungu huyu Bibi amerudi maana manyang'au tayari walishageuza NYUMBA YA SANAA uwanja wa fisi. Kila siku nikipita pale roho inaniuma sana na zaidi ninaposikia serikali imetenga mabilioni kujenga JUMBA LA UTAMADUNI. Watanzania tumuunge mkono bibi huyu kukomboa NYUMBA YA SANAA.Wanautamaduni unganeni nyuma ya bibi huyu mlikomboe jumba lenu.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 06, 2008

    Kwa taarifa yenu
    huyu mama ndiye chanzo cha nyumba ya sanaa kufika hapo na katika makundi yote yanayoigombea nyumba ya sanaa hakuna hata moja linalijali manufaa ya msanii na mzalishaji wa tanzania

    Nyumba ya Snaa irudishwe kwa wasanii na si ktk mikono ya waliowahi kuwa pale

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...