wadau nawakumbusha kwamba huko dallas kuna mbongo ambaye ana ngazi ya juu katika sanaa ya kujilinda kwa mkono mtupu aitwaye sesnsei rumadha fundi (kati) ambapo sasa ana dani 4 baada ya kufuzu katika staili ya goju kwai. yeye ni mmoja wa wanafunzi bora wa sensei nantambu camara bomani aliyekuwa anafundishia karate shule ya zanaki na hadi sasa dojo lake lipo pale.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. eeh bwana michuzi kipindi kile ulikuwa unakuja pale Dojo kupiga picha Sensei bomani akishuka toka unyamwezini. Hebu weka hapa bloguni zile picha basi. Sensei Kheri Kivuli bado yupoo? Nidondoshee picha za dojo hapo huku ughaibuni sijaendeleza dojo tena.

    ReplyDelete
  2. Eeh bwana michuzi nakumbuka kipindi kile Sensei Bomani akishuka toka unyamwezini basi wewe ulikuwa unakuja pale Dojo kupiga picha na story inatoka Sunday News..hebu tuwekee basi zile picha mie toka niingie ughaibuni Dojo basi tena. Hivi Sensei Kheri Kivuli bado yupo?

    ReplyDelete
  3. Sorry hapo juu isomeke kama "Sempai" na sio Sensei Kheri Kivuli. labda kama amekuwa sensei siku hizi ila nilimwacha akiwa "Sempai"

    ReplyDelete
  4. Hii sanaa siku hizi bongo naona imefifia kidogo, Enzi hizo michuzi pale TABORA kuna mtu alikuwa akiitwa WAMDAKI na mwingine MAGEMBE, hawa jamaa walikuwa wababe wa sanaa hiyo na kupiga Chuma, walikuwa wanaingia TABORA JAZZ pale RUMUMBA BAR MTAA WA RUFITA, na msururu wa wapambe nyuma. Yaani enzi hizo ukiwa unajua kuzipiga kavu kavu wewe unakuwa kama mfalme wapambe kibao ila siku hizi imehamia kwenye BONGO FLEVA, kila jambo na wakati wake. Nafikiri hawa jamaa ndio waliompa hamasa huyu kijana kuingia kwenye fani

    ReplyDelete
  5. Big up on the promotion to "4 dan"

    Shemeji huyo, kaoa kwetu Iringa!!

    ReplyDelete
  6. Hongera bwana Rumadha sasa ni zamu ya kugawaujuzi huo nafurahi hata mama nasikia naye ni mwanafunzi mzuri sana wa mitindo hiyo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...