leo nimebahatika kutembelea hospitali ya bugando na kukaribishwa na mdau mwansasu ambaye namshukuru kwa ukarimu wake. niulifarijika kukuta hapa pia pana wadau kibao wanaobukua na kula mzigo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Aisee mimi nilivyokuwa naisikia hosp ya bugando na ninavyoiona tofauti

    ReplyDelete
  2. michuzi tuwekee na vitu vya bukoba tuna hamu navyo hasa bukoba sec shool nimesoma pale nina miaka 11 hivi sasa sijaenda.nyumbani kutamu.samahani kwa usumbufu

    ReplyDelete
  3. Ahsante Michuzi, nimezaliwa hapo in the 70's. Lakini toka niondoke mwanza nikiwa hardly a year old, sijawahi kwenda na wala sijawahi kuiona bugando kwenye picha

    ReplyDelete
  4. Kaka Michuzi unajua kupiga picha ila wewe mwenyewe kupozi kwenye picha hujui kabisaaaaaaaaa!

    ReplyDelete
  5. Wee Muchunguzi yaani unakaa huko ughaibuni miaka 11 hujaenda nyumbani, aisee ni sikitiko. Yaani ukirudi wale watoto wa mzee Rwegasira, Rutashobya, Rweyemamu, Rugaimukamu, Rweyengeza, Rutachera, Rwegoshora na Rutechura utakuta wameishazeeka na hawatakukumbuka kama ulisoma nao pale Bukoba sec. Kwa kweli wee jitahidi tu uje usalimie.

    ReplyDelete
  6. mazokaaaa upo baba hapo BMC, kipingu,wapi ulitishiwa kurogwa na yule bro wa jamaa uliyemzidi class

    ReplyDelete
  7. michuzi hapo pembeni ya bugando kulikuwa na nyumba ya bibi fisi ilikuwa imejengwa katikati ya barabara gari zinapita pembeni kama bado uko mazoo icheki basi

    ReplyDelete
  8. anon ambae hujaenda nyumbani kwenu miaka 11 ndo umeshajilipua au nini!!

    yani umekuwa mkimbizi wa kisomali au kinyarwanda so kurudi home ndo sahau kabisa, masikini nakuonea huruma, mwisho wako utajikuta umerudishwa elitrea, kongo au ethiopia.

    ReplyDelete
  9. Hey mwacheni Mishuzi...Mganga hajigangi... Mmeshaona hata photographer yeyote upande mwingine wa picha si afadhali hata yeye anajua kuwapa watu camera yake wamchukue picha za kumbukumbu zake. Ukiwa na camera na unapiga picha ujue sura yako kuonekana kwenye hizo picha ni majaliwa. I know that because I like to take pictures for funny. Nina picha nyingi sana za matukio mbalimbali tu lakini unaweza ukamaliza siku nzima kutafuta sura yangu.

    ReplyDelete
  10. Michuzi, ulizia basi, yule bibi kizee hapo Bugando ambaye walishindwa kung'oa kijumba chake wakati wa ujenzi wa hospitali bado yupo? Nyumba yake ya nyasi ilikuwa inabadilika na kuwa mlima mkali na magreda kupinduka wakitaka kuing'oa. nasikia Nyerere akawaambia wamuache aendelee kuishi. Mwaka 1996 nilipokuwa Mwanza alikuwepo na nilimuona. Na aliendelea kupata mgao wa chakula toka hospitali kwa ajili ya "watu wake" aliokuwa nao mle ndani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...