
maria sarungi anazidi kutuhabarisha kinachojiri mexico
Hello!
Asanteni kwa ushirikiano wenu mzuri!
Jana (tarehe 24) warembo wamerekodi introduction zao wakiwa wamevaa vazi la taifa. Flavia kama mnavyoweza kuona ameva vazi lililobuniwa na Farouque Abdela wa Zanzibar na ameshika kibuyu. Vazi lake ni Maasai-insipiration kwani ina mshono wa kisasa lakini imechukua elements za Kimaasai. Kwa kweli mrembo wetu alipendeza sana!
Leo tarehe 25 alianza siku na interview ya waandishi wa habari wa kimataifa n ni kati ya warembo ambao wamefanyiwa interview kupita wengine wote! Yaani nimefurahi sana, kwani anamudu vyema interview, anajiamini na majibu yake ni mazuri. Waandishi wengi walimwuliza kuhusu nywele yaani kwa nini amekuja na nywele fupi. Flavia aliwaeleza waandishi kwamba mwanamke wa kiafrika asili yake ni nywele fupi za kusuka lakini nywele ndefu zilizonyooka mgongoni ni nywele zilizowekwa dawa au/na kuwekewa extension. Lakini yeye amekuja na uasili wake. PIa aliulizwa kuhusu Tanzania, nchi yake kwamba iko wapi na ina vivutio gani na pia aliulizwa kuhusu ushiriki wa Tanzania kwa mara ya kwanza. Flavia alieleza vivutio vya Tanzania akiwa anatumia makabrasha na taarifa alizopata kutoka Tanzania Tourist Board.
Kwa kweli Flavia amekuwa balozi mzuri sana wa nchi yetu na anazidi kuitangaza nchi yetu. Tuzidi kumwombea!
Asanteni
Keep it up Flava
ReplyDeleteMichuzi link nyingine ni hii watu wavote kama kawaida
ReplyDeletehttp://news.yahoo.com/photos/ss/events/en/051007missuniverse/im:/070525/ids_photos_en/r120841975.jpg;_ylt=Ahgwr8arvKxjx2ovPVQO1V3BaMYA?sp=3000&auto=yes
Nadhani iko clear ni ya reuters baada ya interviwe ya leo
Michuzi link nyingine hii
ReplyDeletehttp://news.yahoo.com/photos/ss/events/en/051007missuniverse/im:/070525/ids_photos_en/r3728023131.jpg;_ylt=AosP71fo3IQpdpJTHLXeOdd.KcMA
Hii ni kali zaidi
Jamani si kuna wambulu na wairaq wenye nywele ndefu za asili? au sio watanzania? ahahahah..just saying. In all I voted her and i will continue..she is great. Bwana awe nawe!
ReplyDeleteNilijua tuu! Nweyele fupi za asili + kujiamini kama muafrika bila kuiga= black is beautiful! Hata kama asiposhunda zaidi, yeye ni Alek Wek wa TZ.. atapata modelling contracts! Way to go girl!
ReplyDeleteMiss Tanzania, Flaviana Matata, an electrical technician whose country is participating for the first time, is also challenging stereotypes of beauty with her shaved head. "I never let anyone define me neither by hair nor clothing as I believe God made me perfect as a pure, natural African woman," she said.
ReplyDeleteNINGEPENDA KUONA COMMENTS KUTOKA KWA YULE MODEL WETU CINTHIA MASASI HAPA..NI UCHOKOZI TU..
ReplyDeletejamani shime tumpigie kura huyu mtoto anatutia moyo sana. Hivi sasa anaongoza kwenye kumi bora anafuatiwa na USA muwe makini hakikisheni adui yake mmarekani awe mbali naye kama tulivyofanya venezuela. Ana kura nyingi mungu anaweza kusaidia miujiza Tanzania mwaka huu. Mhamasishaji
ReplyDeleteHebu tujifunze vizuri kuhusu makabila yetu Tanzania. Sasa haya mambo ya kuchanganya watu hayafai. Misupu naomba kuwaelimisha watanzania kwamba hatuna kabila linaloitwa Wambulu!tuna Wairaqw. Wairaqw wanapatikana katika Mkoawa Manyara,katika Wilaya za Mbulu,Babati,Hanang'(Hanang'wakiishi kwa ukaribu na majirani zao Wadatoga)Karatu ambayo imebakia Arusha nayo ni moja kati ya wilaya wanakopatikana kwa wingi.Kwahiyo tuna wairaqw wa Mbulu, lakini si Wambulu kama kabila,ama sivyo utakuwa na wababati nk!
ReplyDelete