Ajali mbaya imetokea leo asubuhi katika eneo la Inyali, nje kidogo ya Jiji la Mbeya wakati basi la abiria la SABCO lililokuwa likitoka Tunduma (Mpakani mwa Tanzania na Zambia) kupitia Mbeya kwenda Dar es salaam lilipogonga roli kwa nyuma mteremkoni ambapo dereva alipotaka kulipita alikutana na pikap ikabidi arudi na kugonga roli kwa nyuma na kuua watu wawili papo hapo huku mmoja wa tatu ambaye alikuwa askari wa Usalama Barabarani akisindikiza basi hilo akifia Hospitali na kufanya jumla ya waliofariki mpaka sasa kufikia watatu.


Abiria kadhaa wamejeruhiwa, 15 wakiwa na hali mbaya sana.

Aziz.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 21, 2007

    Speed contol sheria na serikali iko wapi. yaani ajali zinaua kila siku na watu wala hawachukuliwi sheria yeyote.
    maisha ya watu yanateketea tu. Wenye magari wanatakiwa wachukuliwe seheria ili wakiajiri madereva wawe wanaajiri madereva wenye usjuzi.

    Mimi nilishapata ajali ya basi hapo TZ na I know how it feels na how much familia iligo through all that I don't even want to remember ...lakini kama ndio hivi ....inasikitisha sana...kila siku ni kuovertake....

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 22, 2007

    Kwa mtindo huu madereva wa public vehicles mnatupeleka wapi?This is unprofessional kabisa na kutokuonyesha kujali maisha ya abiria wanaotegemewa na watu lukuki.polisi barabarani wanachangia kwenye hili pia kwani manasi yanayokwenda kasi zaidi wanayajua but wakishapewa chao basi tena haliwahusu.Nikiwa Bongo nimewahi kuwa ferried kwa basi dogo ili tuvuke mizani na baada yakuvuka tukarudi kwenye basi lililozidi uzito safari ikaendelea though niliprotest kitendo hicho sikupata support ya abiria wenzangu na askari wa barabarani wanalijua hilo.Okoeni maisha ya watu madereva na si kukimbia ovyo ili kupata sifa kwa tajiri na madereva wengine.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...