kuna mdau kaniamuru nioneshe tena nondo zangu na pia nimburudishe kwa kile alichoita kukosa usingizi kutokana na kukesha kuangalia globu yetu hii. kwa kuwa mteja ni mfalme sina budi kumsujudia kwa picha hiyo nikimuonesha kaka charles kizigha na bernad rwebagira aliyeko masomoni berlin kwa sasa hizo nondo. kuhusu burudani mie naona mdau huyu apewe hii hapa chini ya Nyota Ndogo - Watu na Viatu - http://www.jambovideo.com/2007/06/11/nyota-ndogo-watu-na-viatu/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2007

    Duuh, hizo zana kambambe! Kweli mwezetu umejizatiti. Hongera.

    Na hilo shati lako nalo...ni kiboko, sito sema mengi ila kusema ukweli linanikumbusha enzi za Mobutu na kofia yake.. lol, SteveD.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2007

    Kusema ukweli sijaufili huu musiki wa mtu na kiatu. Lete vitu vya uhakika bwana.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2007

    michuzi nakupa saa 24 toka sasa uombe radhi na kurekebisha kauli yako ya kumsujudia huyo mdau la sivyo yatakayokupata mimi simo. hasujudiwi ila ALLAH.
    Engineer-Kilwa

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2007

    Michuzi itakuwa vizuri utengeneze tovuti ya snaps zako maana picha zako ni nzuri profeshno, au vipi!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2007

    Brother Michuzi naomba msalimie huyo Brother Benard,alikuwa jirani yangu pale kawe tanganyika packers,michuzi angalia jamaa huyo asije kukushusha kileleni kwa maana ni mbaya sana kwa picha na sasa kaenda kuongezea professionalism,hahahahha,tuwasiliane mkubwa mimi nipo Finland,email martinnako@yahoo.com.(nako)

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2007

    Michuzi umekamilika!! si mchezo,safi sana,lazima nifagilie..!! ukiamua kuingia kwenye kitengo lazima uwe kamili.
    Mimi huo wimbo huwa unanikuna sana tatizo huwa sielewi kwanini unaitwa watu na viatu! wadau naomba nisaidieni kwanini ametumia neno Viatu hapo..

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2007

    We Michuzi, hizo kemera ni zako binafsi au mwajiri wako (dele-nyuzi)???

    kama ni za kwako basi mimi sina wasi. ila kama ni za mwajiri wako basi unatakiwa kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya mali ya Umma. Dele-nyuzi ni kampuni ya uma, utumiaji mbaya wa vyombo vyake ni ubaridhifu wa mali ya uma.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 13, 2007

    Michuzi ulitakiwa kusema mwanzoni kabisa kamera hizo ni za mwajili wako au wewe binafsi. Sababu kama ni za mwajili wako, nasi tumelipa kodi za kununua hivyo vitu ingawa ulitumwa wewe ukanunua. Ni vizuri ukafanya acknowledgement kwa employer wako kuwa anakuweka up-2-date.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...