Home
Unlabelled
jaji mkuu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MichuziBlogV2Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Zaidi ya wafugaji 1,500 wa kabila la Kimasai wamelazimika kukimbia makazi yao wakihofia kuangukiwa na mawe na majabali, baada ya Mlima Oldonyo Lengai uliopo wilayani Ngorongoro wenye volkano hai kulipuka na unaendelea kutoa moshi.
ReplyDeleteVolkano hiyo imekuja baada ya eneo hilo kukumbwa na matetemeko ya ardhi mfululizo katika siku za karibuni.
Imeelezwa kuwa mlima huo ulianza kutoa moshi na moto, kwa muda wa siku sita sasa na kusababisha uongozi wa vijiji vilivyoko jirani na mlima huo kuwataka waongoza watalii kutowapeleka wageni karibu na mlima huo kwani hali si shwari.
Muongoza watalii wa kupanda mlima huo, Bw. Peter Sule, aliliambia shirika la habari la PST kuwa kwa sasa shughuli za kupanda na wageni juu ya mlima huo zimesimama hadi hali itakapokuwa shwari.
Bw. Sule alisema mlipuko wa sasa wa volkano katika mlima huo ni mkubwa kuliko uliyowahi kutokea, ambapo uliambatana na moshi na moto, hasa nyakati za usiku.
``Kwa kweli hali ya aina hii sijawahi kuiona. Nimeongoza watalii kwa miaka 12 kupanda mlima huo na matukio ya kulipuka kwa volkano yaliyotokea hayakuwa makubwa kiasi hiki,`` alisema Sule.
Aliongeza kwamba nyakati za mchana moshi unakuwa mdogo huku usiku kukiwa na moshi mkubwa ulioambatana na mngurumo.
``Nyakati za usiku ingawa tunaishi mbali na mlima lakini bado tunashindwa kulala kutokana na mtikisiko ambao unatokea mara kwa mara, hii si hali ya kawaida. Hatujui yatakayotokea wakati wowote `` alisema Bw. Sule.
Aidha kiongozi wa ukoo kutoka kwa wafugaji waliokimbia makazi yao karibu na mlima huo, Bw. Loibanguti Kisioki aliiambia PST kuwa katika historia ya maisha yao karibu na mlima huo matukio yasiyokuwa ya kawaida yameanza kutokea katika siku za hivi karibuni.
``Mambo haya ya ajabu ajabu yalianza kutokea miaka michache iliyopita ambapo mwaka jana mlipuko wa volkano ulikuwa mkubwa na umekuwa ukijirudia mara kwa mara,`` alisema Kisioki.
Alisema jamii hiyo imekuwa ikitumia mlima huo kufanya matambiko ya kimila, ``lakini kwa sasa kuna hofu kubwa. Tunahisi Mungu wetu amekasirika ndiyo maana haya yanatokea.``
Aliongeza kuwa wanatarajia kufanya mkutano wa kimila namna ya kumuomba Mungu wao aitwaye Engai Narok awanusuru na balaa linaloweza kusababishwa na tetemeko la mlima huo.``
Wakati huo huo, tetemeko lingine la ardhi lilitikisa Kenya jana.
Kutokana na tetemeko hilo, wakazi mbalimbali nchini humo walipatwa na mshtuko mkubwa kufuatia tetemeko la ardhi ambalo lilitokea kwa nyakati mbili tofauti na wengine kukimbia makazi yao.
Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), tetemeko hilo lilitokea majira ya saa 3.30 na saa 9.30, usiku wa kuamkia jana.
Shirika la BBC liliwakariri maofisa wa hali ya hewa wa Kenya wakisema kwamba tetemeko hilo liliyakumba maeneo yaliyopo katika bonde la ufa.
Hata hivyo, imeelezwa kwamba hadi jana hakuna taarifa za maafa au majeruhi.
Katika siku za karibuni, mikoa ya Arusha na Kilimanjaro imekuwa ikikumbwa na heka heka kutokana na tetemeko la ardhi. Maeneo ambayo yamepitiwa na tetemeko ni pamoja na Same, Moshi, Longido na Oldonyo Lengai.
Barani Afrika, tukio la volkano linalokumbukwa sana ni lile lilitokea nchini Kongo (DRC) mwaka 1994 baada ya volkano kulipuka katika mlima wa Nyiragongo na kuleta maafa makubwa kwenye mji wa Goma, ulioko umbali wa kilometa 18 kutoka katika kilele cha mlima huo. Mlima huo unapitiwa na Bonde la Ufa la Afrika Mashariki.
Watalaamu wanasema kuwa volkano hulipuka pale kunapotokea nyufa katika uso wa ardhi na kuruhusu miamba ya ndani ya ardhi iliyoujiuji na yenye moto mkali (molten rock), majivu na gesi kuruka nje.
Ujiuji huo wa moto ukiganda juu ya uso wa dunia unasababisha miamba na shimo linalobakia husababisha ziwa.
Na kuhusu tetemeko la ardhi, watalaamu wanasema linasababishwa na ardhi kuruhusu kwa ghafla nguvu kubwa (stored energy) iliyohifadhiwa ardhini ambayo husababisha mawimbi yaitwayo seismiki.
Wanafafanua kuwa wakati mwingine ni matokeo ya matabaka ya ardhi (tectonic plates) mbayo hutembea na kusababisha mgandamizo mkubwa kwenye ardhi yanaposigishana. Mgandamizo huo unapokuwa mkubwa, husababisha miamba kuvunjika.
Halikadhalika watalaalamu wanasema kwamba wakati matetemeko mengine ya ardhi yanaweza kusababishwa na shughuli za kila siku za banadamu kama vile kupasua miamba, mengine yanatokana na milipuko ya volkano.