baada ya handakizzzz sasa ni mashimozzzz ambapo kila uendako utayakuta baada ya wadau kujisaidia mifuniko ya chuma ambayo inasemekana wanaednda kuuza kama skrepa. huu ni mtaa wa somali maeneo ya gerezani, na ile nyumba mbele kushoto ilipopaki gari ndipo alipoishi jabari la muziki marehemu marijani raajabu 'dozza'

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. bro michu
    umenikumbushia zakale kwetu hisia zote leo ziko nyumbani kwenye mtaa wetu huu. Yani wachaa, unashukuriwa kwa sana natamani ningekuwa kadege ningeruka nikafika kwetu lakini ubavu sinao niko majuu utumwani..
    shukran sana bro kwa kuweka picha hii ubarikiwe daima na ramadhan kareem

    ReplyDelete
  2. FUNGA KABISA BUSTANI YA MNAZI MMOJA MPAKA WASTAARABU WATAPOTOKEA, LINI? SIJUI!
    HEBU ANGALIA MFUNIKO 'WASHENZI' WANAIBA? MI-ANONY MINGINE ITASEMA TUWEKE WANAUSALAMA KATIKA KILA MFUNIKO.

    ReplyDelete
  3. Doh! Umaskini jamani! Sasa serikali inabidi waingilie na kuonya hao wanaopokea hiyo scrap Metal kuwa wasipokee hiyo mifuniko la sivyo watafungwa! Kama hawatapokea watu hawataiba.

    Kukosa huo mfuniko hapo ni hatari kwa wapita njia na magari pia.

    ReplyDelete
  4. Nyumba Ya Marijani(Dozza) ni ya blue, sio ile iliopaki gari nje kama ulivyo eleza kwenye picha. Na huyo aloiba mfuniko namajua lazima atakuwa Iddi michuzi (wajina Wako):-). Bwana michuzi hicho ndio kijiji chetu cha Gerezani palipo unguwa shoka ukabakia mpini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...