Home
Unlabelled
mjadala
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MichuziBlogV2Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
wananchi wamepumzika kujadili BUZWAGI na MAFISADI!!??
ReplyDeleteHizo Simba na Yanga zitawasaidia nini lakini??
Ndugu Watanzania wenzangu,
ReplyDeleteYanga imo njiani kuuzwa. Bei ya yanga imeshapangwa ni shilingi bilioni 3 na wannunuzi wa Yanga washajulikana. nani anajua pengine kesho zamu ya Simba kuuzwa.
Cha msingi hapa si kuuzwa kwa timu tu. Cha msingi ni kwa nini timu inataka kuuzwa? jinsi gani timu inataka kuuzwa? na kwa faida ya nani?
Serikali na Bunge la Awamu ya Nne imeonyesha ushabiki wake katika fani ya michezo. Imeonyesha hivyo kwa Rais na watendaji wengine wa Serikali walivyoshiriki katika kuiimarisha timu ya taifa. Bunge limeonyesha jinsi linavyothamini kandanda kwa kuruhusu kwa mara ya kwanza timu kuingilia kikao cha Bunge. Pia kwa mchango wa mamilioni ya shilingi iliyochangwa na wabunge kama motisha kwa wachezaji wa timu ya taifa.
Yanga na Simba siyo tu ni timu za kandanda bali pia ni moja ya vitambulisho vya taifa letu. Yanga pia ni ina asili ya kisiasa ya Tanzania. Kama hili limesahaulika basi yapasa likumbukwe na kutiliwa maanani.
Muhidin na wengine wote ambao mna nafasi ya kuweza kuwafikia wenye nguvu ya kuweza kuisitisha nia hii dhalimu nawaombeni mfanye hivyo haraka kabla mambo hayajaharika. Namuomba Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Muheshimiwa Mohamed Seif Hatibu achukue hatua za haraka kusitisha mizengwe ya nia ya kuiuza timu ya Yanga.
Mtanzania mwenzenu katika michezo,
Fidelis M Tungaraza.
huyo yellow man tx kwa usishi hawezekani.
ReplyDeleteeti wambur!... maneno mengi sanaa ,ubabaishaji tu .
ReplyDeletenyie watoto wa mjini mnalala nini kuwaachia wageni kama hawa kutuchanganya ??
YANGA KUWA KAMPUNI: KWA MISINGI IPI NA MASLAHI YA NANI?
ReplyDeleteMgogoro wa Yanga ni moja ya mambo ambayo nimekuwa nikiyafuatilia kwa karibu sana tangu ulipoibuka wiki chache zilizopita. Sikuwa na sababu nyingine ya kufuatilia mgogoro huo, isipokuwa ni kuangalia kwa makini chanzo cha mgogoro huo hasa kwa kuwa ulikuwa ukimuhusisha Bw. Manji ambaye katika miaka ya karibuni amekuwa habari, mjadala, gumzo na soga kubwa katika vyombo vyetu vya habari.
Ikumbukwe kuwa Manji alisitisha ufadhili wake Septemba 20. Seke seke la mgogoro huo lilianza tarehe 8 Oktoba mwaka huu pale Bw. Yusuf Manji alipotangaza kuacha ufadhili wake Yanga kwa sababu kuu moja nayo ni kushauriwa na familia yake na marafiki zake. (Tanzania Daima, 11/10/2007)
La kushangaza hapa ni kuwa siku moja baada ya tamko lake Bw. Manji, Oktoba 9 alifunga safari mpaka kwenye makutano ya mtaa wa Twiga na Jangwani yalipo makao makuu ya klabu ya Yanga. Pengine hilo siyo tatizo kwani naye kama mwanachama mwingine yeyote wa Yanga ana haki ya kufika mahali hapo, tatizo ni Bw. Manji kuitisha mkutano wa wazee na kuanza kurusha shutuma dhidi ya uongozi na kubadilisha sababu mbali ya ile aliyouelezea UMMA awali kwa maandishi ikiwemo ucheleweshaji wa KATIBA mpya, na kutoa masharti ya nini kifanyike ili abadilishe maamuzi yake mojawapo ni kubadilisha timu kuwa kampuni, hili lilikuwa ni kosa. Pamoja na hilo, Bw. Manji kutoa dau la milioni 50, 10 kwa ajili ya 'wazee' (Ukipenda unaweza kuiita rushwa) na 40 kwa ajili ya maandalizi ya timu, huku akitoa sharti kuwa ni lazima ziwe chini ya katibu mkuu Bw. Kisasa bila ya kufuata utaratibu na katiba ya klabu na kanuni za masuala ya fedha za klabu, hili lilikuwa kosa jingine. Hali hii ndiyo iliyopelekea mmoja wa 'wazee' wa Yanga kuhoji uhalali wa Manji kuwapangia jinsi ya kuendesha klabu kama alivyonukuliwa "Manji hawezi kutuchagulia wanachama au viongozi anaowataka huku ni kuvuka mipaka, yeye mwisho wake ni ufadhili na siyo kuchagua viongozi". (Tanzania Daima, 12/10/2007)
Kwa mujibu wa uchambuzi, mgogoro mzima ni kati ya uongozi halali wa Bw. Madega na mfadhili wa timu Bw. Manji. Jambo linalovuta hisia zangu hapa ni kuwa wakati Bw. Manji anautuhumu uongozi kwa kuchelewesha "utekelezaji wa vitendo" juu ya rasimu ya muafaka ikiwemo katiba mpya ambayo ingepelekea Yanga kuwa kampuni; Bw. Madega anapinga wazo la Yanga kuwa kampuni bila ya kufanyia marekebisho kadhaa muhimu kwa kulinda maslahi ya wengi ambao ni wanachama wa klabu hiyo kongwe.
Kwa kuwa Bw. Madega alionyesha wasiwasi wake waziwazi kwa wahariri wa habari tarehe 11/10/2007 juu ya suala zima la ujio wa Bw. Manji Jangwani na uhamishaji wa timu ya Yanga kwenda kuwa kampuni, ambako kutapelekea moja kwa moja Bw. Manji kuwa ndiyo mmiliki mkuu. Nilitegemea magazeti mengi yangeonyesha umakini wa Bw. Madega na hoja zake za msingi kama alivyoainisha. Kinyume chake, ni gazeti moja tu la kila siku ambalo liliandika kwa kirefu hoja za msingi za uongozi kukataa masharti ya mfadhili Bw. Manji. Zaidi ya hapo vyombo vingi vya habari vilikuza zaidi kauli ya Madega kuwa wazee wa Yanga wanatumiwa kwa njaa zao.
Pengine suala la muhimu hapa ni kujadili wasiwasi wa Bw. Madega juu ya kuwekwa rehani kwa maslahi ya wanachama wengi, ambao pengine kwa kutojua sheria au kwa makusudi (Ikumbukwe Bw. Madega yeye ni mwanasheria na wa wakili wa mahakama kuu) Kwa mujibu wa Bw. Madega kupitisha rasimu na kuwa katiba bila maerekebisho ya msingi kungeweza kuhatarisha uhai wa klabu na maslahi ya wanachama wengi; ameahinisha haya kama alivyonukuliwa na Tanzania Daima la 11/10/2007 kama ifuatavyo:
(1) Katika kifungu cha 39(2) (d) cha Katiba ya Yanga kinauagiza Mkutano Mkuu wa Uchaguzi kuchagua wanachama wawili ambao si miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha masilahi ya klabu kwenye kampuni.
(2) Kamati iligundua kifungu hiki kina makosa makubwa mawili, kwanza makosa yameshafanyika kuwa wanachama wawili hawakuchaguliwa kwenye mkutano wa uchaguzi, hivyo bodi ya kampuni hata kama itaundwa basi wawakilishi wa wanachama ndani ya kampuni hawatakuwepo, hivyo bodi ya kampuni kuifanya iwe batili.
Lakini kubwa naloliona hapa, ni kukosekana kwa uwakilishi wa dhahiri wa klabu katika bodi ya kampuni, kwani hisa ni mali ya mwanahisa na siyo mali ya klabu. Hivyo basi hata mwanahisa aliyepoteza sifa za kuwa mwanachama wa Yanga, bado anaweza kuendelea kumiliki hisa zake kimsingi. Hili huenda likapelekea wanachama wawili watakaoingia kwenye bodi ya wakurugenzi, kuwakilisha maslahi yao kama wanahisa na siyo maslahi ya klabu.
Ikumbukwe kuwa hisa zinarithishwa, lakini haki ya uanachama inapotea pale mtu anapopoteza sifa za kuwa mwanachama, ikiwemo kifo. Katika hili, kama katiba itaenda jinsi ilivyo tusishangae siku moja mwenye hisa nyingi akawa tajiri asiyependa michezo kabisa, achilia mbali kutokuwa mwanachama hata wa klabu hiyo. Kuiepusha Yanga na vilabu vingine na balaa hili, maslahi ya klabu katika kampuni iwayo yoyote ile, ni lazima yasimamiwe na viongozi waliochaguliwa na kimsingi ndio wasimamizi wakuu wa mali zote za klabu, ikiwemo maslahi ya wanachama. Na hili ni lazima litamkwe waziwazi kwenye katiba ya klabu kampuni, ni jinsi gani viongozi wa kuchaguliwa watashirikishwa kwenye bodi ya kampuni.
Pamoja na hayo wasiwasi mwingine ambao Bw. Madega ameuelezea waziwazi bila kificho ni kuwa:
(3) Kifungu cha 39 (2) (f) cha katiba kinataka klabu na kampuni kuingia katika makubaliano ya kimaandishi ya uendeshaji wa timu na kwa niaba ya klabu makubaliano hayo yatasainiwa na Katibu Mkuu wa klabu.
Udhaifu wa kipengele hiki ni pale katibu mkuu pekee ndiye anayetakiwa kusaini makubaliano. Swali, je, ni kwa nini kwa taasisi kubwa kama Yanga mikataba yake isainiwe na katibu mkuu peke yake?
(4) Kifungu cha 39(2)(b) kinamtambua mfadhili wa klabu kwa mujibu wa rasimu ya muafaka wa Yanga uliofikiwa na wanaYanga tarehe 22/06/2006 na ukiangalia rasimu ya muafaka, mfadhili ametambuliwa kama Yusuph Manji na si kampuni.
Hapa pia kuna kasoro kubwa ya kikatiba kwani haipaswi kwa jina la mtu binafsi (natural person) kuingia katika katiba kwani katiba inaundwa ili iishi muda mrefu, hivyo unapotambua jina la mtu binafsi kwenye katiba, maana yake umetengeneza katiba ya kuishi chini ya saa moja, kwani wakati wowote mwanadamu anaweza kupoteza uhai.
(5) Kifungu cha (39)(2)(c) ni kuwa klabu itamiliki hisa zilizo sawa na asilimia hamsini na moja (51%). Kama ni kweli klabu inamiliki hisa 51%, maana yake klabu ndiyo yenye hisa kubwa ndani ya kampuni, hivyo ni wazi kuwa kiongozi wa kampuni anapaswa kuwa kiongozi wa klabu ili kulinda masilahi ya hisa zake nyingi.
(6) Tofauti na mfumo uliopo sasa, klabu haina mwakilishi kwenye bodi ya kampuni. Hivyo hapo mbele utakuja kuona si kweli kwamba klabu inamiliki hisa 51% za kampuni.
Hayo ndiyo mapungufu ambayo uongozi wa Yanga umeyaona kwenye katiba na hivyo kufanya utekelezaji wa suala zima kuwa linataka muda.
(a) Muafaka.
Baada ya kupitia hati ya muafaka kwa kina, kamati iligundua yafuatayo:
(1) Kampuni ya Yanga itakuwa na hisa ya sh 6,000,000 (milioni sita).
- Hisa moja itauzwa kwa sh 1,000 (elfu moja) tu, hivyo kufanya mtaji wa kampuni kuwa ni sh 6,000,000,000 (bilioni sita) endapo hisa zote zitauzwa.
- Kifungu cha 3.2.2 cha rasimu ya muafaka kinaipa klabu hisa saba tu kati ya hisa 6,000,000. Thamani ya hisa saba ni sawa na shilingi 7,000. Hii ndiyo thamani ya kampuni kwenye klabu.
Hisa 3,059,993 zenye thamani ya shilingi 3,09,993,000 zitatengwa pembeni, zitatakiwa klabu kuzinunua ndani ya miaka miwili na klabu ikishindwa, basi hisa hizo zitauzwa kwa watu wengine.
Hivi tujiulize, klabu itapata wapi shilingi bilioni tatu ndani ya miaka miwili ili iweze kununua hisa?
Na asilimia 51 ya hisa zote za kampuni bali itakuwa na hisa saba tu zenye thamani ya shilingi 7000. Rasimu ya muafaka inasema kwamba mfadhili atamnunulia kila mwanachama hisa 10 zenye thamani ya shilingi 10,000.
Kutokana na mgawanyiko wa hisa ulivyo kwenye rasimu (7) tu, wakati mwanachama ana hisa 10 zenye thamani ya shilingi 10,000 kwa maana hiyo mwanachama mmoja ana thamani kubwa ndani ya kampuni kuliko ndani ya klabu yenyewe, ambayo thamani yake ni shilingi 7,000 na ndiyo maana klabu haikutakiwa kuwa na mwakilishi kwenye bodi ya kampuni kwa kuwa haina hisa nyingi kwenye kampuni.
Tujaribu kuangalia lengo la kununulia wanachama hisa, je ni kuwa anawapenda?, kitendo cha kuwahamisha kutoka klabu kwenda kampuni pamoja na timu si kuiua klabu? hapa suala la kuzingatiwa ni kuwa hakutakuwa na demokrasia nyingine ya kura moja mtu mmoja bali ni HISA MOJA KURA MOJA.
Na hili likifanyika mwenye hisa nyingi ndio mwenye maamuzi yote...hivi huko ndiko wanachama wa Yanga wanakotaka kwenda?
Vyombo vya habari
Vyombo vya habari vina dhamana kubwa ya kuhabarisha umma juu ya nini kinajiri, kama wengi wanavyopenda kusema habari ni haki ya kila msomaji. Pamoja na majukumu makubwa na heshima iliyoshiba juu ya vyombo vyetu vya habari, lakini inasikitisha kuwa vyombo vya habari vingi (si vyote) vinapoamua kuuza haki hiyo kwa wenye 'dau' zito. Migogoro katika vilabu vyetu kwa kiasi kikubwa inachochewa na ubinafsi wa wananchama wanaoendekeza njaa zao lakini pia imekuwa ikishadidiwa kwa kiwango kikubwa na vyombo vyetu vya habari. Sikemei umuhimu wa vyombo vya habari kutangaza kauli za uchochezi kama zilivyo, la hasha! nalotaka kusema hapa ni kuwa viripoti kwa nia ya kuujulisha umma, kuuonesha nini kinafanyika na kuutahadharisha na sio kuunga mkono uchochezi huo.
Aidha vyombo vyetu vya habari havina ruhusa ya kutetea uozo, maovu na uvunjifu wa amani katika vilabu vya michezo. Kutoa habari nusu nusu sio tu kunamnyima msomaji haki yake ya msingi, lakini pia kunakuwa kumesaidia kuchochea fujo zisizo na msingi. Ni ombi langu kuwa wakati umefika, kuanza kuheshimu wasomaji wetu/wenu kwa kuwapa kile kinachojiri kukiwa na habari ambazo zina uwiano, badala ya kuangalia nani mwenye dau, au habari gani itauza.
Dennis Londo
Watu wengine wana dhambi jamani. Eti wanamsingiziaga huyo Wambura kuwa eti nae ni "muangilikana." Jamani! Si dhambi hii.
ReplyDelete