ze comedy wanazidi kutesa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Kaka Michuzi...hivi kwa nini waTZ wanapenda vitu vya kijinga namna hii?

    Nakuuliza hivyo kwani nilipokuja Bongo mwezi uliopita ndugu zangu na marafiki zao waliofurika pale nyumbani siku ile wengi wao walikuwa wanasubiri hiki kipindi cha Ze Comedy. Haki ya nani, hawa jamaa hata kuchekesha hawajui na acting yao ni ya kitoto kabisa lakini utashangaa watu jinsi wanavyo-anguka chini kucheka. Kweli Bongo bado tuna safari ndefu sana ya ku-act.

    ReplyDelete
  2. ETI MITHUPU NASIKIA MWAMPAMBA MWISHO ANATAFUTWA, IS IT TRUE? HEBU CHEKI NA MWAIPAJA KWENYE BLOGU YAKE, THEN TUPE NEWS, SASA HASEMI ANATAFUTWA NA NANI, AU LABDA MSHKAJI ANATAK KUMPA KIDOGODOGO AU VIPI, TUPE NEWS, SORY KWA KUINGIZA HII COMENT AMBAYO HAIUSIKI HAPA, NAJUA LAZMA WADAU WENGI WATACHEKI COMMENTS ZA KINA MWANAWANE . THANKS

    ReplyDelete
  3. Jamani kama wewe uchekeshwi na hao watu waachie wenzio wacheke wenye kicheko halafu ni kweli kwamba umejijibu mwenyewe watanzania bado tunasafari ndefu lakini tunajitahidi appreciate maendeleo ya watu sio kuwakandamiza

    ReplyDelete
  4. Watu wengine sijui Wehu (Nilinde Michuzi hili si tusi ni kisifa) Unaposema vitu vya kijinga na we Kutoa macho kwa Mr Cooper inamaana we mjinga wa Kidhungu sio?

    ReplyDelete
  5. Wewe Mbwiga wa kwanza kabisa hapo juu inaelekea hujui saikoloji ya vichekesho.

    Vichekesho siku zote vinaendana na matukio ya jamii husika. Kama utaongea kitu ambacho watu hawakijui hata kama kinachekesha vipi watu hakitawachekesha, na wakicheka ni kwamba wanafuata mkumbo tu kama ilivyokuwa kwa Mr. Cooper.

    Sasa hawa jamaa wa Ze Comedy NI VICHWA KINOMA maana wanatumia matukio ya kawaida kabisa katika maisha ya kila siku ya Watanzania kutengeneza vichekesho.

    Kwa hiyo vichekesho vyao ni kwa ajili ya Watanzania. Kama wewe sio Mtanzania kwa kweli ni lazima vichekesho vyao vitakupinga chenga na utabaki unashangaa tu kwa nini watu wanacheka.

    ReplyDelete
  6. HAhaha Pope umenifurahisha sana MJINGA WA KIDHUNGUU!!!!! Huyu jamaa kweli mwehu acha umpe kisifa chake maana hicho ni kiambishi nafsi, hehehehe umenikumbusha mbali sana
    Kwa michuzi ukiingia umenuna lazima utacheka so kaka usibane comments acha tucheke turudi "kubeba box
    "

    ReplyDelete
  7. kaka salama?
    nilikuwa nyumbani bongo karibuni na nimefurahishwa sana na hawa jamaa kiasi kwamba kila ifikapo alhamisi huwa napiga simu wanieleze home kipindi kilikwendaje.tunaomba ukiwa kama mwakilishi wa wadau jaribu kutuwakilishia ili kama kuna mdau anweza akwa anatupostia on line vipindi vilivyopita nasi tuweze faidi uhondo huo wa nyumbani kwetu wenyewe.naomba fanyia kazi hili kaka.
    mdau paul sifa,greece

    ReplyDelete
  8. Huyo annony wa kwanza alosema hauni kichekesho inaonekana dhahiri kuwa bandama yake haifanyi kazi vizuri au ana kabisa hiyo bandama ya kumsapoti acheke.....atajiju, watanzania tunasonga MBELEEEEEE

    ReplyDelete
  9. Wewe annony wa kwanza umenichefua...Nina uhakika kuwa huna bandama kabisa ya kukusapoti ucheke! Utajiju, Watanzania HAOOOOOOO tunayeya, wewe lea vibabu na vibibi vizee huko ulaya...

    ReplyDelete
  10. Huyo jamaa hapo juu mbali na ushamba ni limbukeni anayejifanya kushadadia mambo ya UZUNGU na kukandya ya kwao. The Comedy iko full mzukx. Wewe ushindwe na ulegee. Nyie ndio huwa hamrudi kwenu wala hampaendelezi mpaka mletwe mkiwa mmekufa.

    ReplyDelete
  11. Dah Mdau umenichekesha sana kwamba jamaa hana bandama nafikiria jamaa kama hana bandama na ukamchekesha kitakachotokea....lol

    ReplyDelete
  12. kweli bongo watu wanapenda tu kuchekacheka, hata mi sikuona bali tu ujinga kwenye tv nikaamua kukata show katikati kwenda grocery kula ndovu
    ujinga tu bado sana yaani

    ReplyDelete
  13. Jamani anony mwingine kanichefua ni huyu hapa Wednesday, November 21, 2007 4:09:00 AM EAT Hebu jiunge na anony wa kwanza asiye na BANDAMA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...