FYI: The committee formed by the President Jakaya Mrisho Kikwete to investigate further on the BOT and linked scandals has just started receiving information from the public. If you have credible information that may help the committee in its investigation contact the following through their mobile numbers:


IGP Mwema: 0787 444433
DCI Manumba: 0754 206326
PCCB Director Hosea: 0754 763741
Deputy PCCB Director Mashaka 0754 336116

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Slaa anyaka skendo lingine

    2008-01-24 17:22:18
    Na Job Ndomba, Jijini


    Yule mbunge maarufu wa kulipua maskendo, Dokta Wilbroad Slaa (CHADEMA-Karatu) amenyaka skendo jingine bab`kubwa linalohusisha ulaji wa mabilioni kibao ya pesa za walalahoi.

    Akizungumza na Alasiri leo asubuhi, Dk.Slaa amesema pesa hizo zilizoliwa na vigogo ni kutoka katika mfuko wa Import Support uliokuwa ukifadhiliwa na Serikali ya Japan.

    Amesema mfuko huo uliokuwa na mabilioni kibao ulilenga kuwasaidia wafanyabiashara wadogo, lakini mapesa hayo yakaliwa hivi hivi na vigogo baada ya kukopeshana na kushindwa kulipa.

    Kwa mujibu wa Dk. Slaa, mfuko huo sasa umefutwa baada ya kugundulika umetumiwa vibaya na vigogo hao anaodai, wengi wao walifungua makampuni hewa kwa ajili ya kukamilisha ulaji wao.

    ``Vita dhidi ya ufisadi haijaisha, kwani baada ya hili la BoT najiandaa kulipua hili la upotevu wa mabilioni, kutoka katika mfuko wa Import Support,`` akasema Dk. Slaa.

    Amesema nchi hii ina maskendo mengi sana yanayofanywa na vigogo na hivyo lazima wachache wajitolee kuwashitaki kwa wananchi kwa ajili kuokoa uchumi wa taifa.

    ``Unajua tunapowataja mafisadi hawa, wananchi wanatakiwa watuunge mkono kwa kuwa kuna mapesa kibao yameibwa na vigogo,`` akaongeza.

    Amesema mfuko wa Import Support ulianzishwa kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, lakini wakapigwa changa la macho na mapesa hayo kuwafaidisha vigogo wachache.

    Hata hivyo Dk. Slaa hakutaka kutaja ni lini atalipua bomu hilo, lakini amesisitiza kuwa yuko katika hatua za mwisho mwisho kukamilisha uchunguzi wake.

    ``Kwa sasa siwezi kukuambia ni lini nitalipua ila wakati ukifika, nitawasilisha madai yangu mahali husika kama ilivyokuwa kwa lile skendo ya BoT, licha ya kwamba baadhi ya watu walianza kunibeza,`` akasema.

    Dk. Slaa ndiye aliyeibua skendo la BoT Julai mwaka jana, katika kikao cha Bunge wakati Waziri wa Fedha Bi.Zakhia Meghji akiwasilisha ripoti ya mapato na matumizi ya wizara hiyo.

    Hata hivyo baada ya kuibua hilo, Dk. Slaa alitakiwa kutoa hoja binafsi ambapo pia aliamua kushitaki kwa wananchi kwenye mkutano wa hadhara pale Mwembeyanga, Jijini Dar es Salaam.

    Baadhi ya matokeo ya skendo la Benki Kuu ni kubainika kwa ulaji wa zaidi ya shilingi bilioni 133 na kutimuliwa kazi kwa aliyekuwa gavana wa taasisi hiyo, Dk. Daud Balali.

    ReplyDelete
  2. INFORMATION FROM WHICH PUBLIC, CCM MEMBERS ONLY OR ALL TANZANIANS, EVERYBODY INCLUDING FOREIGNERS AND IT DOESN'T SAY IF OPPOSITION MEMBERS ARE ALSO WELCOME TO CONTRIBUTE AS THEY ARE ALWAYS NOT WELCOME. THE WHOLE THING SOUNDS LIKE ZE COMEDY, FIRST YOU SAY NO, THEN YOU SAY, YOU ARE TOO NOISY BUT YOUR NOISE WON'T LET ME SLEEP THEN YOU SAY YES BUT MOST OF ALL TOU SAY I DO NOT KNOW WHERE HE IS. THIS IS ABRACADABRA! I AM SORRY, I AM GOING TO SLEEP WHEN I WAKEUP NEXT 90 YEARS THE WHOLE THING WILL BE GONE WITH THE WIND.

    ReplyDelete
  3. I'm having such a hard time understanding WHY we are having the committee members be the point of contact. If someone has credible information, need to call the IGP/DCI/PCCB and Deputy Director PCCB. Let be serious about this, These four gentlemen are the heads of the most important agents in the country and I don't see how we putting them to task of collecting Data through phone calls or sms. I think we can do better than this. Lets build a better system to help getting to the bottom of this instead of having these important people taking calls from citizens. Its an unwise to my standards.

    ReplyDelete
  4. michuzi na swali, kuna madai fulani kuhusu hosea yaliwai kutolewa na waasaia fulani ughaibuni, kweli tue makini na baadhi yao, kwani ni hatari, naomba uweke hii, maana sijui walitoa madai wapi???

    ReplyDelete
  5. michuzi na mimi niliwahi kuyaona hayo madai, hivi nani aliwaruhusu kupublish bila ushahidi, maana ni jambo zito, waliyatoa wapi?? naomab uweke hii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...