malkia wa taarabu na unyago bi kidude angali anaendeleza libeneke sauti za busara na ni kivutio kikubwa kwa kila mtu hata kama hayuko jukwani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Bibi yangu mpenzi hebu pumzika tena, inatosha, maana hata sauti inakukataa, huna mvuto tena unatisha, umeanza kusaha lakini bado unangangania tu, cha maana hebu anza kusali na kuvuta uradi wa toba, kama hujapata mpaka leo basi hupati tena, na kama umepata basi ni wakati wako wa kutumia, ndio maana hata wazungu wanaita(kuritaya) pumzika bi mkubwa inatosha.

    ReplyDelete
  2. Wallahi wapig apicha nyie majasiri, maana huyu bibi kweny lenzi ya kamera si mtu unaweza kufikiria unatizama senema ya kutisha!!! Kama alivyosema anon hapo Juu, Bi mkubwa unatakiwa kupumzika na "kuvuta uradi wa toba" hii mambo ya kujianika na sura za kutisha namna hii si yake tena!!! Wanaotaka kufanya senema ya Science fiction na wanataka sura za kutisha natural wamkodi huyu bibi!!! (Nimechema)

    ReplyDelete
  3. na mie nakuunga mkono jamaa yangu,,huyu bibi kukata viuno jukwaani inatosha..sasa akimpata kijana akamwambia vipi atakataaa?maana huyu bibi kwa viuno kajaaliwa

    ReplyDelete
  4. Please leave this bibi alone, to do what she does best SINGING Mungu amemjalia sauti na umri, we kinakuuma nini? eti akapumzike, apumzike ili iweje ili afe? bibi songa mbele i wish you 50 years of gracing this stage, not sure if some of us will live that long........

    ReplyDelete
  5. Nyie wakichaa hapo juu mnaosema amekwisha na aache, sijui anatisha!

    Nikutokana na ufinyu wa elimu yenu ndio mnasema hivyo.

    Kama tungefuatilia hio fomula yenyu yakusema vya zamani havina samani basi tusingekua na mji mkongwe wa Zanzibar ambao tunajivunia hasa sisi wa unguja.

    Kama tungefuata fikra zenu nyie hapo juu basi kizazi kipya kisingejua asili ya Taarab na baada yake kuwa na hili rumba lenu la Jahazi Modern Taarab, na jahazi kama mnavyolijua sasa ni jahazi la rumba[ndombolo].

    Wasiompenda na wasimpende lakini sisi waunguja Bi Kidude ni Living Legend na kama ana uwezo wa kuwa jukwaani tutaendelea kuwa washabiki wake.

    ReplyDelete
  6. we muunguja hapo juu labda huna nguvu za kufanya kazi na unategemea bibi yako akulishe, ushauri ulio tolewa sio wa kupoteza mila zetu, bali bibi yako apumzike sasa, na wajukuu zake walithi kazi yake, na yeye avune matunda aliyo yapanda ujanani kwake, waunguja acheni kuwategea bibi zenu, fanyeni kazi nao wapumzike, mpaka afie jukwaani?

    ReplyDelete
  7. Ni kweli bibi angeritaya labda kangefungua shule ya unyago,akawafundisha wanawari kukatika, sio kunanga kama dagaa kauzu sokoni.

    ReplyDelete
  8. Mimi sio mzanzibari, napenda sana bi kidude,lakini kwa sasa mmmmmmmmmm aliimba siku moja muhogo wa jagombe nilitamani nikimbie, nikaona kweli kila kitu kina mwisho bibi yangu ni kweli pumzika sasa, achana na hao wajukuu zako wanao bonyeza kizenji na kula urojo tuuuuuu.

    ReplyDelete
  9. Kidude,please retire baby!!!tutamwambia Mkapa akugawie hisani ya migodi ya mkaa anayoimiliki hapo kwetu Mbeya...

    ReplyDelete
  10. http://www.youtube.com/watch?=iHVm41pYJCk

    Kama kazi yao nikula urojo tu basi waunguja waingekua na mifereji kwenye nyumba zao. Huko kwenu Dar mji mkuu walio na maji safi nyumbani kwao ni wangapi? Dar jiji lakini mpaka leo watu wanakunywa maji ya visima!? akha tuachieni Unguja yetu na Bi Kidude wetu

    ReplyDelete
  11. Nawaunga mkono anony hapo juu, siongelei urojo wala mifereji, nampenda bi Kidude sana, ishu ni kwamba kiafta hata kama ana Doc amshauri kupumzika, angalia kina Tina Tana, Diana Rose, na wengine wengi wameachia ngazi wanatumia mapesa yao sasa. Punzika sasa mpenzi wote tunakupenda na tunakukubali.

    ReplyDelete
  12. bibi yetu mpendwa haya mambo inabidi uyawache fanya urudi kwa mola wako hali ya kuwa bado moyo unadunda

    ReplyDelete
  13. Anayesema Tina Turner na Diana Rose wameachia ngazi anaishi dunia ya wapi?

    Tina juzi alitangaza kwamba anafaya duet na Beyonce.

    Diana Rose alikua Amsterdam mwaka wa jana Mei.

    Au unaongelea Diana na Tina mwingine?

    ReplyDelete
  14. Nyie watu mnaozungumza kwamba Bi Kidude apumzike mnashindwa kuelewa kuwa Bongo mambo ni tofauti! Eti mnatoa mifano ya kina Tina Turner na Diana Rose, huyu mzee anajua kuwa akipumzika ndio itakuwa mwanzo wa kifo chake, maana hatoweza kujikimu tena! hapo halipo hana akiba yeyote ya maana ambayo inaweza ikamsaidia kuendesha maisha yake pindi atakapo staafu. Ni bora sasa anajishughulisha na muzik ambao ni mazoezi tosha kwake kujiweka fit na kuendelea kupambana na maradhi tegemezi ambayo mengu hutokana na kuishi maisha ya kigogoi. Na kubaliana na wote wanaosema kuwa huyu mzee Kidude inabidi aanze kuvuta "uradi wa toba" lakini lazima mkumbuke kuwa maisha ni magumu mno bongo, kwahiyo watu wanalazimika kujishughulisha mpaka siku ya kufa!
    Kidume, USA

    ReplyDelete
  15. SHE IS THE LIVING LEGEND.....

    ReplyDelete
  16. Nyie acheni ushamba badala ya kujivunia utamaduni na kuomba michuzi awatumie picha za huyu bibi na nyimbo zake mnatazama sura yake na kuona kachoka. Mnadhani atafanana na Beyounce? Bibi yetu huyo tena kapendeza sana. Ahsante sana Michuzi picha kama hizi ni rare na ni Dhahabu kwa watu kama sisi tunaojua nini maana ya kujivunia utamaduni wako. Nakumbukia
    Chura punguza vituko na huo uhayawani umezeua sokomoko na watu hawaelewani. Akaja dada Rukia na ndooye nkononi chura ukajing`atua na kujitosa pembeni.....
    E bwana sio utani napenda sana hii kitu na pia nilishawaona kina Snoopy Dogg, Busta Rhymes, Fiddy Cents,M & M Slim Shaggy, Mary J Blige,Eve,na wanamuziki wengine kibao live huku Marekani. Wote hao ni poa lakini nadhani ningefurahia zaidi kumuona huyu Bibi kuliko hawa jamaa sababu ya utamaduni unaonihusu. Jay Z kaja Bongo kutembea vijana mmejazana lakini huko China Wamemkatalia kwenda hamna maadili na mafunzo ndani ya nyimbo zake kwa wachina. Vivyohivyo sisi tutabaki hatuna cha kujivunia kwa kuwa hatujua kupreserve na kusupport utamaduni na vipaji vya watu watu. Napenda sana kina Saida Karoli, Shaaban Robert, Agoro Anduru, Bulicheka, na Kipanya. Mzee michuzi endelea kutupa mavituuz ya home tumechoka na MTV na BET wewe ni burudani zaidi ya matV ya ughaibuni. Nakuombea mema na ufanikiwe zaidi katika shughuli na biashara zako.

    Michuzi oyeeeeeeeee. Cheka na michuzi pata habari na michouzy.

    ReplyDelete
  17. Bimkubwa pumzika dada wajukuu zako wanakutosa,

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...