wadau wa duka la vipodozi la aris lililoko sinza wanakukaribisha kwa shopingi maalumu ya valentine ambapo utaweza kujipatia pafyumu na losheni babu kubwa toka marekani kwa bei poa kabisa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Big up hilo duka lina bidhaa nzuri kweli me mwenyewe juzi nimeenda kununua zawadi ya mupenzi valentine dei.LOL

    ReplyDelete
  2. Naomba utuletee picha ya hilo duka basi ...

    ReplyDelete
  3. zawadi ni zawadi tuu!!hata mafuta ya nazi ni zawadi nzuri tuu...mkorogo pia ni zawadi nzuri tuu...

    ReplyDelete
  4. Hivi kutangaza duka ni lililopo Tanzania,tena Sinza ni lazima muweke picha za kina dada wazungu jamani?

    ReplyDelete
  5. Ndio ni lazima ehee! Kwani hujui kuwa ili uwe mzuri ni lazima ufanane na mzungu? Basi ndio hivyo lazima picha ya mzungu iwekwe ili watu wawe wazuri kama wazungu.

    Lol kina dada poleni mwenzenu mafuta yangu ya nazi na liwa poa ngozi yangu mororo sihitaji losheni wala nini.

    Mwenye duka hana makosa asipoweka hiyo picha ya njungu watu hawataenda wataona bidhaa ni za kiswahili/kibantu

    ReplyDelete
  6. hivi bado kuna watu wanathamini wazungu jamani!!mbona wazungu wengi choka mbaya tuu kama sie...kuwa mzuri sio lazima uwe kama mzungu..wazungu wanalala kwenye jua kupata ngozi nyeusi...cheusi dawa dada

    ReplyDelete
  7. Wajasirimali wa bongo...muhimu kuwa na online store siku hizi...Tupatie online store hiyo wengi tuna wapenzi wetu bongo. Ukimtumia mtu hela anunue perfume will never happen. Ukiamua kumnunulia frome hre umtumie siku hizi na mafuta haya yamepanda mwee hela ya kutuma express ni nyingi mno na ukituma kawaida huko ushuru wanachargiwa kama sana tu.

    Wekeni basi online store tunanunua halafu mwenye zawadi anakuja tu kuchukua huku kweli.
    Tunawachumba bongo lazima tuwajibike.

    ReplyDelete
  8. Michuzi, naomba utoe hili tangazo haraka sana kabla hujawatafutia wenzio balaa. Products za victoria secret huwezi na wala hauruhusiwi kuzinunua then kwenda kuziuza(re-sell), Mimi nafanya kazi the Limited Company, ndio tunatengeneza hizo products. Kwahiyo hii ikijulikana hilo duka watafunguliwa mashtaka mahakamani (being sued)na pesa watakayo daiwa ni kubwa sana. Kuuza products hizi nje ya maduka yetu inabidi uingie ubia(franchise) na the limited company. Otherwise hiyo ni sooo.kama huamini uliza mtu yoyote anayefanya kazi The Limited au duka lolote la Victoria Secret huku kwa wabeba mabox. Don't say I never warned you guys............

    ReplyDelete
  9. ehee duka ni kiboko jamani ni safi sana na kuna kila kitu nilikwenda leo jamani ni mambo kibao nimekuta si mchezo zawadi za wapendanao zipo.tena za kumwaga.tushindwe wenyewe

    ReplyDelete
  10. Arise ni duka sio la kibaguzi, linauza bizaa kwa watu wote wa rangi zote na jinsia zote. Nyie mnaomaindi na kuchambua picha zilizotumika mnaonesha ni jinsi gani hamjiamini. Mjasilimali wa arise usiwasikiliza vidudu mtu hao kwa mana hakuna kitu kitawarizisha hata ukiwafanyia nini!

    ReplyDelete
  11. MICHUZI. Hawa ni wengine au ni walewale Jamaa waliokosa AIBU kutuchafulia Blog yetu ya kijamii na bidhaa zao za CHINA NEW YORK.

    ReplyDelete
  12. wewe 8:12 acha zako...siye hapa hapa USA tunazinunua na kuziuza kwenye ebay...kila kwenye sell nipo na cupon zote nazujua. na nunua na kuziuza kwenye ebay hapa hapa USA and nobody ever sued me waachie wenzako riziki yao kwanza huko africa who cares

    ReplyDelete
  13. picha iliyowekwa si ya mzungu peke yake, ni, mzungu na black ila ina kuonyesha jinsi wanugu (black) wanavyojua kujiremba

    ReplyDelete
  14. Jamani kwa wale wenzangu wapenzi wa vidole juu(taarab) kuna muimbaji mmoja mzuri sana kwa uimbaji, mashuhuri sana alishawahi kuimba wimbo mmoja na mzee yusufu, anaelewa hasa jinsi ya kughani sauti yake na kufatisha vitendo wakati anaimba kwa madaha ya hali ya juu napenda sana jinsi anavyosimama kutuma ujumbe, ila kitu kimoja nimekiona kwa dada huyo kimemuangusha kwenye wimbo wake wa mwisho aloimba baada ya kujifungua, ameuimba bomba sanaaa ila poda aliyoipaka usoni sidhani kama kuna mtu akiangalia ataacha kugundua kasoro ambayo imetoa dosari kidogo kwa sisi watazamaji na washabiki wake katika album hiyo wakati tunaangalia,

    ombi langu fupi muwe munawashauri wateja wenu na muwaeleweshe namna ya upakaji unaanza na nini unamalizia na nini unapaka kiasi gani ili isiwawie vigumu katika kusoma maelekezo labda kwa lugha tofauti iliyoandikwa , hasa hao waimbaji maarufu wakati wanapanda kwenye stage waangalie namna wanavyojipodoa na aina ya vipodozi ubora wake wasiweke kasoro kubwa kama hiyo ya poda iwe inaenda na rangi yake wakati tunaangalia tusikarahike.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...