mdau john kitime katuletea tangazo hili ambalo lilitoka magazetini mwaka 1981 wakati makassy alipopata vyombo vipya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Michuzi natumia blog yako kufikisha ujumbe kwa Bw.John Kitime kama anaweza atengeneze cd ya nyimbo zake za kinyalukolo. Zilinikosha sana 95 alipozipiga pale National Museum kwenye maonyesho ya picha za marehemu Konga. Twisuka mgoyo.
    Mdau Mnyalukolo

    ReplyDelete
  2. Namuona Remmy ongala kwa chini kulia.

    ReplyDelete
  3. Kumbe John Kitime naye!alikuwa mojawapo wa wapambe nuksi wa mzee Makasy enzi zile?halafu tunasikia vile vyombo vipya alikopeshwa kupitia shirika la Utalii la taifa,na deni mpaka leo hajalipa!!!

    ReplyDelete
  4. issa hebu fanya mambo tupate kikosi kamili cha huyo mzee wakati ule ,namkumbuka jamaa mmoja alikuwa anaitwa Malik star sijui kama alikuwa na huyu babu?

    ReplyDelete
  5. Michu akhsante sana kwa picha hii...Hapa makassy ilitamba sana na kina Assossa na vibao vyao vya Binadamu hatosheki pamoja na Mambo bado. Huu muziki ulikuwa mtamu sana ila kwa sasa Flava ndio inaua kabisa vipaji vya wanamuziki wetu.

    ReplyDelete
  6. Dah wadau kama mnasoma kweli msaada tutani nawapenda sana wahenga nadhani walikuwa na akili ya kufa mtu hasa kwa usemi wa YA KALE NI DHAHABU hakuna Vibao vinavyonikuna kama siku ya kufa DR remmy na Makassy Orchestra, na kuna kibao makassy alipiga na jamaa anaitwa Mossesengo FAN FAN kinaitwa Namolema kama sijakosea kweli huundo ulikuwa mziki sasa hivi tunasikiliza nadhani ni kama vile kula kuku wa kisasa na kumwacha wa kienyeji ambaye ana ladha halisi, inanikumbusha sana nikiwa Sumbawanga Jamani . Tena kwa taarifa yenu wadau ule mziki wa Mambo bado ulishawahi HIT chart za uingereza na Kushika namba moja kwa wiki kadhaa, lkn mzee makassy hajafaidika na pesa za mauzo mpaka leo hajui ni nani alichukua mauzo hayo km mnabisha mtafuteni Masoud Masoud atawaambia ukweli

    ReplyDelete
  7. Siku hizi Makassy kaokoka anaimba kwaya kanisani alishaachana na huo ushetani wa kuimba miziki kwenye kumbi za walevi kama nyie washabiki wa miziki ya kidunia.

    Siku hizi ukiongea na Makassy kila baada ya maneno mawili lazima Aseme Bwana Yesu asifiwe.

    Na nyie waosha vinywa kwenye hii blog inabidi muokoke kama Makassy lakini kama hamtaki basi Michuzi na wanablog wenye vinywa vichafu inabidi wapelekwe kwa nguvu kwa mtumishi wa Mungu Makassy aende akawaatoe pepo wachafu waliowajaa na wanaowafanya wawe wanatukana watu hovyo kwenye hii blog.

    Naamini pepo wachafu wakiwatoka kwa Jina la Yesu kupitia Mtumishi mtakatifu wa Mungu Makassy kutakuwa na watakatifu wengi kwenye hii blog.Tupumzike kusikia matusi.Na Michuzi naye tusishangae akawa mtakatifu na akajiunga na Mtumishi wa Mungu Makassy kama mwimbisha Pambio za sifa na kuabudu na akaacha kuruhusu waosha vinywa waliojaa dhambi hadi matakoni kuvurumisha matusi kwenye hii blog.

    ReplyDelete
  8. JAMANI MZEE MAKASSY HIVI YUPO HAI?NAWAKUMBUKA WATOTO WAKE NILISOMA NAO WAKINA CLAIRE MAKASSY NA POLITA MAKASSY ENZI HIZO UNASOMA NA WATOTO WA MWANAMUZIKI ILIKUWA KAMA NJOZI BWANA MICHUZI...MDAU

    ReplyDelete
  9. Anon April 26, 2008 9:32 AM, umeokoka kweli? Sijui kama Michuzi kaisoma hii comment yako

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...