Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh. Kanali Mstaafu Enos Mfuru (shoto) akiongea na wanakamati ya kusaidia elimu mkoa wa kagera leo hapa dar baada ya kuongea na waandishi wa habari kushukuru wadau wa mkoa huo kwa kujitolea hali na mali kufanikisha zoezi hilo. chini ni jedwali la mchakato mzima wa michango ambapo mkoa huo umevunja rekodi kwa kuchangisha bilioni 1.4 ambazo ziko mkononi. infawkti mwenye brifkesi ndiye mtunza hazina anic kashasha ambaye amefanya a vere gud job kumekishua kila kitu kinaenda akoding to plani katika mambo ya pesa. habari kamili na za maendeleo ya kagera nenda www.kagerayetu




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Haya! hongereni wana kagera ila msifanye ufisadi ili kupata pesa za kuchangia.
    Wengine nao wajifunze hasa ndugu zangu wa Pwani

    ReplyDelete
  2. bora safari hii wameamua kufanya la maana kidogo,sio kuishia kwenye majigambo tu ya kwenye michango ya harusi na sendoff alafu mji wao hawauendelezi,jitahidi wakina rwekiza,buberwa,kaishozi,mutabaji n.k ili kagera iwe jiji

    ReplyDelete
  3. haya ndio mambo tunatakiwa kuyaona nchi nzima, citizens taking matters at their own hands na sio kusubiri ufadhili. Mpaka lini tutategemea misaada kutoka nje? Watanzania inabidi tutilie umuhimu swala la elimu na sio mashuleni tu, hata 'after school hours' vipindi vya Televisheni viwe na mwelekeo wa kielimu kuchangamsha ubongo wa vijana wetu na kuinua 'exposure', na sio kuwa na ushabiki ktk masuala ya 'muziki, na udaku' ktk vipindi vya TV na magazeti. Kijana wa form 6 unaweza kumuuliza Global warming ni nini na akashindwa kukujibu. We need to create future minds; inventors and innovators. We have to be serious and stop meaningless ushabiki ktk masuala ya udaku.

    Dr. Rutachunzibwa,
    Okinawa Institute of Science and Technology, Japan

    ReplyDelete
  4. mkoa wa kagera huwa hauna matatizo ya madawati hata kidogo labda vijijini
    mi nimeanzia kusoma bukoba- rumuli na sikujua kama kuna matatizo ya madawati tz mpaka nilipohamia mkoa mwingine
    nshomile wanajitahidi nawapa hiyo kwenye madawati na ubora wa shule

    ReplyDelete
  5. Naungana na wanaopongeza juhudi hizi,tena naomba liwe ni jambo endelevu,yamkini si wote waliotarajiwa kushiriki uchangiaji wameweza kufanya hivyo kwa sababu mbali mbali,ikiwa ni pamoja na kukosa taarifa za kuwepo kwa uchangiaji huu,hivyo wapewe fursa tafadhali.
    Natumaini jitihada hizi zitalenga pia kuhuisha THE UNIVERSITY OF BUKOBA,pengine si ajabu akina Dr... mlioko Japan,mkarejea kufanya kazi katika chuo hicho.

    Mdau,
    Finland

    ReplyDelete
  6. bado mji uko nyuma sana na ndo maana kina nshomile wamehamia mwanza. kwa michango hii wanaweza kuleta ahueni.

    msifanye hili mara moja. iwe mara kwa mara. majigambo yasiishie mdomoni. mnajisifu nshomile wakati hata vyuo hakuna. sijui mlisoma wapi na mnataka watoto wenu waende wapi.

    ReplyDelete
  7. Dr. Rutachunzibwa! Unatisha mzee!

    ReplyDelete
  8. Aroo mimi Prof. Rwechungura wa university of Angani sikupewa taarifa? kwa nini wamenibypass? Sasa kwa jeuri nitachanga dola milioni 1 na nitazipitisha kwa bwana michuzi ili aziwasilishe kwa wahusika. siku nyingine tupeanane tarifa wote akina nshomile kwani kwetu pesa siyo tatizo

    ReplyDelete
  9. One gets frustrated kurudi kwani serikali yenyewe haina mfuko madhubuti wa kuchangia scientific research katika vyuo vyake. Jitihada za harambee kama hizi nadhani baadaye zikiwa'channeled vizuri zitaweza kusaidia kuwapatia 'grants' wanasayansi waTZ kufanya au kuanzisha research in natural sciences kwa mf. Tatizo pesa zitolewazo na serikali ni kwa ajili ya research za demographics/population studies, social health care issues, utandawazi nk. We need our own solutions to our own problems, we can't afford to import every bit of technology without us contributing to our own. Innovation drives development. Why can't we build our own pharmaceutical industries, processing industries, diamond cutting industries etc. Inabidi serikali iingilie kati na kusaidia hasa hasa scientific development na sio kupoteza fedha za umma ktk safari na semina kibao bila kuleta results. Pump money into biofuel research, wireless technology, molecular cell biology na vitu kama hivyo ndipo tutarudi. Lakini jitihada za wananchi zinanitia moyo, hasa hasa kuinua elimu ya kati (sekondari) kwani mpaka sasa kila mwaka asilimia 75% ya Form 4 graduates wanapata divisheni 4 na 0. Ni nchi gani tunatengeneza? Wazazi pia tuhimize watoto wetu ktk after school studies (si maanishi tuition), tuwahimize vijana wetu wawe members ktk maktaba, wasome literature, philosophy na vitu kama hivyo na sio kuwapa pesa kununua magazeti ya udaku (Ijumaa, Uwazi nk) au kushabikia eti Bongo Star search, big brother, urembo. Hamna nchi inayoendelea kutokana na hayo mambo. Ilinishangaza kuona Waziri akiwa kwenye VX akisoma gazeti la udaku.
    E Byarugaba, PhD

    ReplyDelete
  10. Infact kagera tunaweza leta maendeleo makubwa sana kama walioko ng'ambo wakichangia zahid,nshomile wengi tunaish na kuleta maendeleo nchi za watu wengine,umefika wakat wa kukumbuka nyumban.
    Hongera wote waliochangia.
    Mdau
    Chicago
    United States Of America

    ReplyDelete
  11. inashangaza sana mkoa wa kagera una wasomi wengi sana kulinganisha na mikoa mingine!ila cha ajabu katika huu mkoa maendeleo ni ziro!nshomile mnafanya nini ndugu zangu!MUNGU amewapa nafasi nzuri ila hamuendelezi mkoa wenu!
    Mdau!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...