Hi kaka michuzi,


naona jiji letu la dar es salaam linazidi kuimarishiwa ulinzihapa farasi ambao wanatumika kulinda jiji letu wakiwa wameizunguka gari moja yenye namba ya kenya usoni mwa duka la makoba karibu na haidary plaza.


haikujulikana mara moja sababu za kuizunguka lakini waliandika kijinote na kuwaachia ujumbe wenye gari hongereni jeshi la polisi


Mdau

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2008

    hapo ndipo utagunduwa ni kiasi gani farasi hao wamekuwa na hali mabya ya kimaisha hebu tuwangalie hata afya zao zinaonsha mlo ni mdogo

    ReplyDelete
  2. Binafsi sio mtaalam wa farasi labda ng'ombe ndio nipo nao vema.

    Nafikiri ingekuwa vema hao farasi wangevishwa viatu maalum(sivijui kitaalam) kwa ajili ya kuwapunguzia msuguano wa kwato zao na barabara zetu za lami.

    Wadau hii imekaaje

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 09, 2008

    Bwana Ndaki, ni vyema umeanza kwa kusema kuwa si mtaalam wa farasi.

    Jappokuwa hata mimi si mtaalam wa farasi, lakini nimewahi ona viatu vya farasi na jinsi anavyovikwa.

    Kwa kawaida farasi wanavikwa viatu kwa ajili ya pamoja na mengine ni hilo ulilosema "kupunguza msuguano". Ila si msuguano tu, pia hata kuteleza kwenye cement au lami nk.

    Jeshi letu la polisi lina wataalam waliosome utunzaji wa farasi, mbwa nk katika kazi zao za usalama. Hivyo kwa mantiki rahisi tu nategemea hao farasi wetu wamevishwa viatu.

    Ila kwa kuangalia picha, au hata kwa kumwangalia farasi haraka haraka huwezi jua kuwa amevishwa viatu. Hii ni kutokana na kuwa viatu vya farasi si kama vyetu wanadamu. Farasi viatu vyao ni vipande vya chuma vyenye shepu ya U hivi (umbo sawa na kwato zao kwa chini). Na wanavalishwa kwa kubandikwa hivyo vyuma chini ya kwato zao, ili wakanyagapo ni hivyo vyuma tu ndivyo vinagusa ardhi. Ndio maana mara nyingi farasi anapopita karibu yako unasikia msuguano wa vyuma na ardhi, cement nk.

    Nadhani nimetoa mchango kiasi. Asante.

    Mdau- Amsterdam

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 09, 2008

    Jamani hivyo viatu vya Farasi vinaitwa "VIATU FARASI" nakumbuka hata Shule ys msingi tulisoma kuhusu aina za smaku na mojawapo ilikuwa "Kiatu Farasi"

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 09, 2008

    Ahsante mdau Amsterdam kwa shule yako. Je, hivi viatu kama vikiwa vinamuumiza huyu Farasi (just like sisi viatu vikikubana vinavyoumiza) utajuaje?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 09, 2008

    ....jibu ni moja tu 'UTANDAWAZI'. Utandawazi umefanya mambo mengi katika maisha ya kila siku ya nchi za dunia ya 3 au 'zinazoendelea' (sina uhakika)yafanywe kwa kukurupuka tu bila kufanyika kama yalivyo kwa hao wenye kuyaanzisha.

    Wadau, siyo kwenye Farasi peke yake. Ukisema ufanye uchunguzi (research) hapo Bongo utaibuwa mambo ya ajabu ambayo mengine ni fedheha kuyaanika kama hivi. Lakini ndiyo hivyo tena...hii ni moja ya madhara ya utandawazi kwa watu ambao 'bongozz' zao hazijishughulishi sana na ubora kwao kitu muhimu ni kitu kiwepo, basi.

    Lakini mimi naona pia hali kama hii inaashiria kwamba 'amani' bongo iko 'maili mianane' sina uhakika kama inakuja au inatokomea!

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 09, 2008

    watu wengine bwana,mnaacha ku comment vitu vya maana kuhusiana na hio picha mmekazania ooh "viatu farasi",what a shame wabongo!!!!jadilini vitu muhimu kwenye picha sio viatu vya farasi.Kazi kwenu.Hapo nilitegemea comments kuhusiana na ulinzi makini wa jeshi letu la polisi na mengine mengine sio viatu vya farasi.
    Cha chandu - UK

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 09, 2008

    Heri mimi sijajadili!
    De

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 09, 2008

    Cha chandu you are emotionally bankruptcy

    Watu wanaangalia beyond the picture. Na sio cha kwako unachotaka watu wadiscuss.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 09, 2008

    tuendelee na mjadala wa farasi, sasa wewe chachandu, unasemaje unataka watu wajadili nini cha maana, na wewe huna la maana maana unajadili lisilo la maana, waungwana na wenye busara zilizovuka mipaka huwa wananajadili na wanaanzisha mjadala bila kuwalaumu wengine, kila mtu ana uhuru wake wa kuwaza na kutoa maaoni kile kwanza alichofikiria na alichokiona, naam ungwapa uliloliona nao wangejadili, hilo zuri lako.

    MIMI NAONA HAO FARASI WANATISHA WANANCHI AMBAO HAWAJAZOEA HALI HIYO,

    PILI NI HATARI KWAWAGENI HASA WATALII KUSHUKIWA NA KUPELELEZWA KASI HICHO KUNA MBINU NYINGI SANA ZA KUPELELEZA WAHALIFU BILA WAO KUJUA, HII NI UNYANYASAJI NA SIO UTU, SUPPOSE HUYO MTU SIYO MWALIFU, UNAKUWA UMESHA MDISTURB

    mdau
    canada

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 10, 2008

    I m with you Mr Cha Chandu koz people think they know more about horses hehehehehehehehe.
    Eti Farasi wavae viatu.......mara eti viatu vikibana watajuaje.....? or i like this "Watu wanaangalia beyond the picture". What is there to look?????? apart from increasing security in a different way.
    What a nonsense.
    Mdau T-Dot

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 11, 2008

    MASKINI WATU WAMESIMAMA BARABARANI WANASHANGAA.HAWAJAZOEA MAMBO HAYA...OOPS!MA MDOGO UK.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 12, 2008

    Mkuuu michuzi yaani hamna siku niliyocheka kama leo maana hii mada ya FARASI imetia nanga sio mchezo yaani hapa nitakuwa nakuja kusoma kila siku maana wengine wanaongelea farasi wengine wanataka kuongelea ulinzi hahaha nimefurahi sana hata mimi hapa sina comment.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...