wabongo sita, wakiwemo mabondia wanne, inasemekana wametiwa mbaroni huko mauritius leo asubuhi kwa kile kilichoelezwa kukutwa na madawa ya kulevya. kwa mujibu wa tovuti ya http://www.defimedia.info/ watuhumiwa hao walikamatwa na kikosi cha kuzuia mihadarati na kwamba watafikishwa mahakama ya Mahébourg mchana huu na kustakiwa kwa kukutwa na mihadarati.
huo unaweza kuwa ndio mwisho wa safari ya timu ya taifa ya ndondi ambayo iko huko kwa ajili ya kushiriki kwenye ubingwa wa afrika, kwani timu yote pamoja na kocha wao imehusishwa katika kashfa hiyo.
pichani juu shoto ni bondia emilia patrick ambaye ndiye bondia pekee wa bongo ambaye anatakiwa atuwakilishe kwenye michuano ya olympic huko beijing. wa chini yake ni kocha nassoro michael na kulia chini ni petro mtagwa. majina ya wengine hayakupatikana mara moja.
Kwa mujibu wa waandaji wa michuano hiyo wamesema tukio hilo halitoathiri mashindano hayo, ila tanzania ndio imeshajitoa yenyewe..


Ni kweli,nimelisoma hilo gazeti(la kifaransa).Box nne wamedakwa nazo leo asubuhi.Jamani jamani aibu gani tena hii nyie wanamichezo yetu na bendera yetu??Na mnafungwa.
ReplyDeleteYana thamani ya Rs(?)millioni 40(Rand?)
ReplyDeletePoleni sana lakini kama ni kweli mmekutwa na hayo madawa ya kulevya mmefanya jambo baya ambalo pia limeibisha nchi pamoja na fani yenu. Nadhani tamaa zimewaponza kwa kutumiwa na watu ili mpate pesa lakini matokeo yake ndiyo hayo ni kuambulia mvua kadhaa jela. Huu ni uhalifu ambao hata tanzania haukubaliki kwani mnashiriki kuteteketeza hiki kizazi lakini pia kuongeza uhalifu na hili nadhani litakuwa funzo kwa wanamichezo wengine. Hapa nadhani mtaungana na timu ya Zombe na kasusura. Wizara inabidi ichunguze vipato vya wadhamini pamoja na mapromota hii michezo kwani wengi wao wanajificha kwa kivuli cha ufadhili
ReplyDeleteAMINA CHIFUPA UPOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO. MAMBO YAKO SIO MCHEZO NIMEYAKUBALI. KEEP IT UP
ReplyDeleteNaam,na kweli hao ndio wawakilishi halisi wa kibongo ughaibuni!!!au ndio wanachama wapya wa tawi la Livapuuu hapo kwetu!??
ReplyDeleteKama ni kweli basi ni aibu sana, ndugu zangu tutaacha lini tabia za kutaka kutajirika haraka haraka namna hii. watanzania wengi wako katika jela nying nchi za nje kwa makosa kama haya na bado hatujifunzi kutoka kwa wenzetu. Nawapa pole member wa familia zao. Jambo moja sasa basi wale jamaa wa kalamajuu wafanye fanye wachangishe pesa kuwapatia hawa ndugu zetu mawakili wazuri. kusema kweli hawa ni masikini zaidi ya yule mama alie huko.
ReplyDeleteMh! hii aibu sasa.
ReplyDeleteaibu kaka hiyo hebu fatilia kwa karibu hii habari utupatie up to date mara kwa mara ,.najiuliza hao mabondia waliondoka vp hapa bongo au ndio hatuna ulizi wa kutosha?? watu wa kitengo cha madawa vp walikuwa wamelala?? au ni zengwe wamefanyiwa?? MICHUZI TUAMBIE MZIGO SI KG NGAPI?? AU SAMANI YAKE??
ReplyDeleteAjali kazini
ReplyDeleteAIBU KWA TANZANIA.
ReplyDeletebraza michu,hii kali sana hawa jamaa tulidhani wanatuwakilisha watanzania kumbe wanatuaibisha!nimesoma link hiyo juu nimeshindwa kuelewa chenji 40m kulingana na dola kama ni kweli basi jamaa wanastahili kuwa huko.na kama wamechomekewa sina la kusema zaidi ya pole.
ReplyDeleteHiiiii!!! hiyo hisiwe mbinu maana kisiwa chenyewe ni maarufu kwa fitina kumejaa wadosi hisiwe ni mbinu ya kututaka tuwanunue mabondia wetu kwa fedha nyingi kama kitega uchumi!???hapo kidogo tua mashaka Martius wakenya wengi na wabongo wapo jela kwa makosa yakusingiziwa
ReplyDeleteHivi hawa wana kichaaa!!nani aliwadanganya wabebe madawa ya kulevya?hata ukiona sura zao zimekakakaaa ki ninja ninja tuu..jamani kila mtu aende shule akasome hilo ndio langu jambo...wasekwe ndani hao,wametutia aibu sana taifa letu
ReplyDeleteKaka Michu hii ni aiBU kubwa sana kwa Taifa letu. Yaani wawakilishi wa taifa wanakutwa na mihadarati tena wakiwa wamebeba bendera ya taifa!! Nadhani inanipa wasiwasi na kupata changamoto ya kufikiri kwamba inawezekana ndio ka machezo ketu haka,labda ndio arobaini imefikia kwa hawa jamaa. Labda hata timu zingine huwa wanabeba mihadarati na inawezekana kabisa ni biashara ya hawa wanaojiita wafadhili na ni lazima serikali itakuwa na taarifa kwa namna moja au nyingine. Afadhali imejulikana, shame on you timu ya ngumi na viongozi woote wa michezo hapa Tanzania!! Aibu sana!!
ReplyDeleteKaka Gee, Arusha.
bongo njaa kali
ReplyDeletewala sishangai, serikali haiwaangalii wao wanaangalia mpira wa miguu tu na mauritius soko zuri, kilo mpaka elfu 80 dollars kwanini wasijaribu, yote maisha, bahati haikuwa yenu tu.
ReplyDeleteSince I dont have anything nice to say let me.........Okei
ReplyDeleteHaaah!! Ama kweli Bongo hali ni mbaya ya kiuchumu, hii yote ni njaa maana mafisadi wamekula kila kitu kiasi kwamba hata wawakilishi wetu wanapopata fursa za michezo km hawa akilini wanafikiria dili tuu, na tena dili zenyewe za hatari, poleni sana, japo mmetuaibisha, lakini tunaelewa, sasa serikali ikawakamate wanaoleta uchumi mbovu na kuathiri ndugu zetu wengi, hao ni baadhi tu na wachache saana kati ya wengi wanaodumbukia katika misukosuko km hii japo hawatangazwi....Poleni saana, na tunaomba ubalozi wetu huko uwasimamie na kuwadhamini.
ReplyDeleteMungu ibariki Tanzania na walaani Mafisadi.
Presumed innocent until proven guilty.
ReplyDeleteMauritius imeamua kuilia dipu Tanzania mwaka huu, undava undava tu!!! Hapo wengine walienda haja hovyo kwenye uwanja wetu mpya.
Taifa Stars mtakapoenda huko inabidi mtoe kipondo cha mbwa mwizi, inaanza kuwa tabu sasa.
Huyo bondia ndio yule tulikuwa tunaombwa watanzania tumchangie aende kwenye olympic?Kazi kweli kweli
ReplyDeleteWenye udaga wako Bongo.Aibu tupu kwa taifa,vigogo, taifa stars,ndondi,scouts,wanariadha.Haya kazi ipo.
ReplyDeletehaya yote ni matikeo ya matatizo ya kiuchumi yanayosababisha njaa na tamaa kwa wabongo wengi, ila wameliabisha sana Taifa letu na sekta ya michezo kiujumla.
ReplyDeleteLily - DSM
Hi kaka Michuzi. Leo katika baadhi ya magazeti kuna habari ya Mbunge mmoja wa Bunge letu aliyekuwa anawanga Bungeni akimwaga uganga kwenye viti vya wenzie na kamera zikamkamata. Magazeti hayajasema ni nani laikini mimi kwa utafiti wangu nimegundua kwamba ni Bwana Vijisenti. Je habari hizi ni za kweli
ReplyDeletenimepokea kwa masikitiko makubwa sana hii habari kaka Michuzi,Tanzania inakwenda wapi hasa huyu kocha Nassoro Michael ni afisa mkubwa wa Jeshi kuingilia biashara ya ujinga kama hiyo kama ni kweli pia amliaibisha jeshi letu
ReplyDeleteHakuna cha njaa kali wala nini. Mshenzi ni mshenzi tu. Watu wanuza madawa marekani na ulaya na hawana njaa kali wala nini na wala hawatosheki kusema wataacha.
ReplyDeleteHawa ni watiwe jela for life. Wanatuharibia vijana wetu na madhar tunayapata wote. Kila kona ni mateja kwa kwenda mbele. Siwafagilii hata kidogo. Washenzi wakubwa.
Kama alivyo sema hapo mwenzangu, boiashara ya madawa ni tamaa ya pesa za haraka na nyingi.
ReplyDeleteTabia ya kubeba ma dawa kwa wana michezo haswa mabondia ni sio kitu kipya, nilisha wahi kutana na bondia aliye wahi kwenda Thailand kwenye shindano na aliniambia alibeba madawa so sidhani ni jambo jipya ni lipo na lina fanyika sana.
Nadhani uanze kuwa sikitikia hawa jamaa pale ambapo mtu wa karibu yako au hata mtoto wako awe ana tumia madawa ,ndio utajua uzuri wa madawa na nadhani uta wasikitikia sana hawa jama kwa kufanya kazi nzuri ya kuingiza madawa , ingawa hatuna cha kusema sababu hatujui mazingira halisi na bado hawaja kutwa na hatia mahakamani.
Jamani huyu wa kwanza na wa mwisho mbona wana fanana ? hizo pua mashavu naona zina fanana sana ni ndugu? kama ni ndugu what a loss!!!! yani two brothers.....oh gosh
ReplyDeleteReally saddening for many obvious reasons. In addition to that, I personally knew Nassor Michael having seeing him in the ring on several occassions in the mid and late eighties - twice or so he was up against mighty Cubans. I recall him winning one of those fierce encounters. Surely, this, if true, is an adverse addition to his otherwise brilliant CV...
ReplyDeleteA Kenyan woman in Mauritius has been arrested along with two Tanzanian boxers and four officials after they were busted trying to smuggle heroin worth a reported USD $1.8 million into Mauritius.
ReplyDeleteThe woman, whose name has not yet been released, appeared to be the contact in Mauritius for the Tanzanians who had just arrived in the island for the African boxing championships with the heroin. They were arrested as they attempted to hand over the drugs to the Kenyan woman by placing them outside near their hotel.
Source:http://breakingnewskenya. wordpress.com
Mdau
Port-Louis
dont be ridiculous you whiney people
ReplyDeletefirst of all wewe TUMAINI sasa unasema marehemu amina chifupa amefanya mambo yake for what purpose?
second mnaolia aibu aibu mnajua watu wangapi na raia wa wapi wanakamatwa na madawa kila siku.mnalia lia aibu ya nini.aibu kama ingekua baba yako.kila mtu anavuta mibangi siku izi,sijui mnabung'aa nini